Search This Blog

Friday 7 April 2023

I WAS WRONG | NILIKOSEA - 1

 


IMEANDIKWA NA : PATRICK CK

******************************************

Simulizi : I Was Wrong | Nilikosea 

Sehemu Ya Kwanza (1)


“ Mabibi na mabwana sasa ni wakati wa kufungua shampeni.Mbele yetu hapa tuna chupa tano za shampeni. Shampeni ya kwanza ni kwa ajili ya wazazi.Chupa ya pili ni kwa ajili ya maharusi wetu.Shampeni ya tatu ni kwa ajili ya wanafamilia.Shampeni ya nne ni kwa ajili ya wanakamati na shampeni ya tano ni kwa ajili ya wageni waalikwa wote mliohudhuria sherehe hii ya aina yake.Ningewaomba sasa wale wote waliowekwa maalum kwa ajili ya kutufungulia shampeni hizi wapite mbele mara moja ili tuweze kulianza zoezi letu” Mshereheshaji aliyekuwa amevalia nadhifu sana akiwa ndani ya suti nyeusi iliyomka vyema akawataarifu wageni waliokuwa wamefurika ukumbini wakiwa na nyuso zilizojaa tabasamu.

Watu waliokuwa wameandaliwa maalum kwa ajili ya kufungua shampeni zile wakapita mbele ya ukumbi na kila mmoja akakamata chupa yake na kuanza kuzitikisa kwa manjonjo.

“ Ndugu wageni waalikwa mabibi na mabwana shampeni yetu ya kwanza inayokwenda kufunguliwa ni kwa ajili ya wazazi.Tunaomba mfunguaji wa kwanza atufungulie shampeni tafadhali” akasema mshereheshaji na mwanadada mmoja aliyekuwa amevalia gauni refu lenye kumeremeta akazunguka na chupa ile huku akicheza kwa manjonjo na mara ukumbi wote ukalipuka kwa kelele za kushangilia.Shampeni kwa ajili ya wazazi ilikuwa imefunguliwa.Wazazi wa pande zote mbili wa mwanaume na mwanamke wakamiminiwa shampeni ile na kugongesheana glasi wakapongezana.

“ Mabibi na mabwana shampeni yetu ya pili ni kwa ajili ya maharusi wetu.Nawaomba maharusi wetu msimame toka hapo mahala mlipo na msogee hapa mbele.” Akasema mshereheshaji na maharusi wakasimama na kusonga mbele.

Mwanadada aliyekuwa ameandaliwa maalum kwa ajili ya kufungua shampeni ya maharusi akaanza kuitikisa chupa ile huku akicheza kwa madoido.Ghafla kikasikika kishindo kikubwa.Ukumbi wote ukashangilia kwa kudhani shampeni ile ilikuwa imefunguka kwa kishindo lakini ghafla ukumbi ukawa kimya kabisa baada ya kusikia sauti kubwa ikipiga yowe.Ilikuwa ni sauti ya Flaviana jumbo ,mwanamke mrembo ambaye mchana wa siku hiyo amefunga ndoa na kijana mtanahati sana Robinson Gregory.Robinson bwana harusi alikuwa amelala sakafuni akiwa hana fahamu huku damu nyingi ikimvuja.Pembeni ya pale alipokuwa amelala Robinson kulikuwa na vipande vya chupa.Kila mtu alikuwa anashangaa kilichokuwa kimetokea.Sandra mwanamke aliyefungua shampeni ya pili kwa ajili ya maharusi alikuwa amesimama akitetemeka mwili mzima.Hakuamini kitu kilichokuwa kimetokea.Hakuelewa ni kwa namna gani chupa ile ya shampeni iliweza kumponyoka toka mikononi mwake na kwenda kumpiga bwana harusi kichwani.Lilikuwa ni tukio la kushangaza sana,watu walibaki wanajiuliza namna lilivyotokea lakini hakuna aliyekuwa na jibu.

Haraka haraka Robinson akapakiwa garini na kukimbizwa hospitali .Akiwa njiani kueleka hospitali mara akaona kitu mfano wa jitu moja kubwa na lakutisha likimjia na kumtaka amfuate.Robinson akaogopa sana na kutetemeka.Jitu lile jeusi na lenye sauti nzito likamsogelea karibu zaidi na kutaka kumshika mkono lakini Robinson akauvuta mkono wake kwa nguvu ili jitu lile lisimguse.

Kutokana na kuuvuta mkono wake kwa nguvu ili usishikwe na lile jitu la kutisha akajikuta akiubamiza ukutani na mara akastuka.Kumbe alikuwa ndotoni.Jasho jingi lilikuwa linamtoka huku akihema kwa nguvu.

“ Ouh my gosh ! it’s a dream ..!! akasema Robinson.mwili wake ulikuwa unamtetemeka kwa uoga kutokana na ndoto ile mbaya na ya kutisha.Kwa takribani dakika tano alikuwa amekaa kitandani akiitafakari ndoto ile ya ajabu.

“ Sijawahi kuota ndoto mbaya na ya kutisha kama hii.” Akasema Robinson .Kelele za majogoo waliokuwa wakiwika kwa wingi zikamfanya aitupie jicho saa kubwa ya ukutani ili kujua mida hiyo ilikuwa ni saa ngapi.

“ Saa kumi na mbili kasorobo.Kumeku

cha !! akasema Robin na kuinuka akingia bafuni akaoga halafu akarejea chumbani akawasha runinga ili atazame taarifa ya habari ya asubuhi wakati akiendelea kujiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini.Habari ya kwanza katika taarifa ya habari toka shirika la utangazaji la taifa ilikuwa kuhusiana na kumbu kumbu za tukio la kigaidi la September 11 lililotokea mwaka 2001 nchini Marekani.Robin akastuka

“ Kumbe leo ni September 11.Ndiyo maana nimeota ndoto ile ya ajabu ajabu.Hii huwa ni siku yangu mbaya sana.” Akawaza halafu akaketi kitandani.Akazama katika mawazo ya ghafla.

“ Tarehe kama ya leo miaka mitano iliyopita mke wangu Flaviana aliniacha.Ni siku inayonikumbusha machungu mengi sana.Bado sijaweza kumsahau Flaviana mwanamke niliyempenda kwa moyo wangu wote na kujitolea kila nilivyoweza kwa ajili yake.Nilifanya kila niwezalo ili kumfanya awe ni mwanamke mwenye furaha lakini badala yake hakuyakumbuka hayo yote na akaniacha nisijue la kufanya.” Akawaza Robin halafu akainamisha kichwa.Akakumbuka maneno makalio aliyoambiwa na mke wake siku alipoondoka nyumbani.

“ Don’t fool yourself that I love you Robin.I’ve never loved you .I married you not for love.I just wanted to enjoy life but five years with you its been a hell to me.Robin sijawahi kuwa na furaha nikiwa nawe hata siku moja.Hujawahi kunipa furaha zaidi ya karaha” maneno haya yakamjia Robin kichwani.Akashika kichwa chake.

“ Mpaka leo sielewi Flaviana alitoa wapi ujasiri wa kunitamkia maneno haya makali ambayo kila nikiyakumbuka yanakitonesha kidonda ambacho kimeanza kupona.” Akawaza Robin

“Robin you are a worthless man I’ve ever seen in this world.Its better if you die because you have no any value in this world.Kosa kubwa nililolifanya ni kukuonyesha utupu wangu.Hukustahili kabisa kuuona utupu wangu mtu kama wewe.Nitakijutia kitendo hiki kwa miaka yangu yote hadi ninaingia kaburini.Ninaku

acha na kwenda zangu na mara tu nitakapokiacha hiki kibanda chako naomba usijaribu kunifuatilia .To me you are dead already so I’ll never think of you”

Maneno haya yakamuumiza mno Robin akavuta pumzi ndefu halafu akasimama akaenda dirishani akalifungua na kutazama nje.

“ Nilimpa Flaviana kila alichokihitaji katika maisha yake.gari zuri,vito vya thamani kubwa.Niliwathamini ndugu zake kuliko hata nilivyowathamini wa kwangu lakini pamoja na hayo yote bado aliniacha.Wanawake ..!!!..” akawaza Robin halafu akarejea na kukaa kitandani akajiangalia kidoleni

“ Kwa muda wa miaka mitano bado nimeivaa pete hii ya ndoa.nadhani ni wakati muafaka sasa wa kuivua.Flaviana hataweza kurudi tena kwangu ,amekwisha nisahau na hanihitaji tena na mimi pia simuhitaji tena.Ni wakati sasa wa kuyasahu maisha ya nyuma na kuuruhusu moyo wangu uanze maisha mapya.Kwa miaka mitano nimekuwa kifungoni ,natakiwa nijiweke huru sasa.Nimekwisha msahau Flaviana lakini siwezi kuisahau tarehe hii.” Akawaza Robin halafu taratibu akaanza kuilegeza pete ile ya ndoa kidoleni kwake kwa lengo la kuivua

“ Flaviana.tulivishana pete mbele ya madhabahu na mashahidi lakini leo hii ninaivua pete hii nikiwa peke yangu ,ninajuta kukufahamu na kuanzisha mahusiano nawe.Umenifanya niishi maisha magumu kwa kipindi kirefu lakini sasa ni wakati muafaka wa mimi kukusahau na kuyaanza tena maisha yangu mapya.Ninapoivua pete hii ninakutoa katika moyo na akili yangu.Sikutambui tena kama mke wangu wa ndoa .Kitu pekee ambacho ninakishukuru toka kwako ni kunizalia mtoto mrembo ambaye ameteseka kwa miaka hii yote mitano bila ya kumuona mama yake mzazi.Mimi nimekuwa ndiye baba na mama yake.Kwa heri Flaviana…” akasema Robin huku akiivua pete ile na kuitazama.Toka walipovishana pete ile kanisani siku ya ndoa yao hajawahi kuivua hadi siku hii ya leo.Akaifunga pete ile katika karatasi na kuitupa katika chombo cha takataka

“To me you never existed..” akasema Robin wakati akiitupa pete ile katika chombo cha taka.Mara mlango wake ukagongwa.Akaufungua na kukutana na sura yenye tabasamu ya mwanae Penny.

“ Hallow Penny” akasema Robin

“ Shikamoo baba” akasema Penny

“ marahaba hujambo Penny?

“ Sijambo baba.Sijakuona mezani nikaogopa pengine unaumwa nikaona nije nikuangalie” akasema penny.Robin akatabasamu

“ Ahsante Penny.Mimi siumwi lakini nimechelewa kidogo kuna kazi nilikuwa nafanya .Ninakuja mezani sasa hivi” akasema robin huku akitabasamu

“ Mungu hawezi kukunyima kila kitu.Nimekosa mke lakini nimebahatika kuwa na mtoto mwenye akili anayenipenda na kunijali sana.Nampenda sana mwanangu Penny na ndiyo maana ninafanya kila niwezalo ili aweze kusoma sana na vile vile kumjengea msingi mzuri wa maisha yake.Sifikirii hata kutafuta mwanamke mwingine ambaye anaweza akamlea na kumpatia ule upendo wa mama,lakini toka aliponitenda Flaviana nimewaogopa sana wanawake.” Akawaza Robin wakati akivaa koti.Akajitazama katika kioo na kuhakikisha amependeza vya kutosha kisha akachukua mkoba wake na kutoka mle chumbani akaelekea chumba cha chakula akaungana na binti yake Penny wakapata kifungua kinywa.Huwa wana kawaida ya kupata kifungua kinywa pamoja kila asubuhi kabla ya kuondoka ,Penny akaelekea shuleni na Robin akaeleka kazini kwake

“ baba leo naomba usije kunichukua katika ule muda wa kawaida wa kutoka.Nilimuomba mwalimu Lucy anisaidie kunifundisha hesabu Fulani ambazo sikuzielewa vizuri na akaniambia kwamba leo hii baada ya masomo atanifundisha.Nitakapokuwa tayari nitamwambia akutaarifu” akasema Penny

“ Usijali Penny.hata hivyo utakuwa umenisaidia sana kwani leo hii nina kikao na wageni muhimu sana.Ukimaliza mwambie mwalimu Lucy anipigie simu na endapo nitakuwa bado kikaoni nitamtuma dereva aje akuchukue

“ Baba leo sitaki dereva aje anichukue.nataka wewe mwenyewe uje unichukue “ akasema penny.Robin akatabasamu na kusema

“ haya mama ,nitakuja kukuchukua”

Baada ya kifungua kinywa wakaondoka na kumuacha Sofia mfanyakazi wa ndani akiendelea na shughuli zake.Robin alimpitisha kwanza Penny shuleni halafu yeye akaelekea kazini kwake.baada ya kufika kazini akasalimiana na wafanyakazi wake na kuingia moja kwa moja ofisini .Hakujisikia kufanya kazi yoyote siku hii. Alihisi uchovu na kichwa chake alikiona kizito sana .Aliegemea kiti chake huku akichezea kalamu.Alionekana ni mwingi wa mawazo .

“ Siwezi kuendelea kuteseka namna hii.Maisha yangu ni mazuri sasa hivi.Nina kampuni yangu ya utalii na ninajiweza kiuchumi.Nilichokosa ni kitu kimoja tu.Mwanamke wa maisha yangu.Naogopa kuanzisha mahusiano kwa sababu ya mwanangu Penny.Ninawafahamu wanawake walivyo kwa watoto wa wanawake wenzao.Sintavumilia kumpata mwanamke ambaye atamtesa mwanangu.Hili tu ndilo linanifanya nisite kuingia katika mahusiano mengine baada yakutengana na Flaviana.” Akawaza Robin halafu akaiwasha komyuta yake

“ Lakini nitaendelea na maisha haya hadi lini? Natakiwa nimpate mtu wa kuniliwaza,ambaye ana mapenzi ya kweli na ambaye atanipenda mimi na mwanangu Penny.Mwanamke huyo nitampata wapi? Sina hakika kama wanawake wa aina hiyo bado wanaishi katika sayari hii ya dunia.Wanawake wenye mapenzi ya aina hiyo ninayoitaka mimi waliishi enzi hizo za mitume na manabii .Kizazi hiki kinachoangaliwa ni uwezo wako wa kiuchumi.Sitaki mwanamke anipende kutokana na uwezo wangu wa kifedha bali nataka anipende kwa moyo wake wote na anipende mimi na si fedha zangu” akawaza Robin na mara mlango ukafunguliwa akaingia Neema katibu muhtasi wake

“Bosi wale wageni tayari wamekwisha fika” akasema neema

“ Ok .wakaribishe katika chumba cha mikutano ninakuja sasa hivi” akasema Robin.Neema akatoka.Robin akamuangalia wakati akitoka mle ofisini akatabasamu

“ Neema ni mwanamke aliyeumbika kiafrika haswa.Ana adabu na mchapa kazi mzuri. lakini niliwahi kusikia kwamba ana mabwana watatu. Huyu naye namuingiza katika kundi lile lile la akina Flaviana.” Akawaza Robin huku akiinuka kitini akavaa koti lake na kwenda kuonana na wageni wake.

********

David Mwauka alikuwa anakatiza katika mitaa ya jiji la Arusha huku akiwa na tabasamu usoni.Ni masaa mawili sasa amekuwa akizunguka na kulifurahia jiji hili lenye uzuri wa kipekee.Ni September 11 saa tatu za asubuhi alipomaliza kifungo chake cha miaka mitatu katika gereza jipya la Oltoreo lililoko nje kidogo ya jiji la Arusha na kuachiwa huru.Alifungwa gerezani kwa tuhuma za wizi wa mamilioni ya fedha.

Alikuwa amevaa suruali ya jeans rangi ya bluu na shati la rangi nyekundu.Chini alivaa viatu vya wazi.Alionekana ni kijana wa kawaida sana.Hakujua aelekee wapi na mfukoni hakuwa na pesa zaidi ya shilingi elfu moja na mia tano tu.Japokuwa alikuwa akizunguka na kulifurahia jiji hili la Arusha na viunga vyake ,moyoni David alikuwa na mawazo mengi sana akijiuliza nini kitafuata katika maisha yake.Hakujua angeanzia wapi au angeyaanza vipi maisha yake.

“ Mimi ni mwanaume nitapambana na nitaishi.Nitaishi hapa hapa Arusha.Nyumbani sintarejea kamwe.Nahisi hakuna anayenikumbuka tena hivi sasa.Itakuwa ni furaha yao kusikia kwamba nimekwisha fariki na siko tena duniani.Mungu ni mwema na bado ana malengo na mimi na atanisaidia nitayaanza maisha yangu mapya.” Akawaza David akiwa ameinamisha kichwa na ghafla akastushwa na kelele za akina mama wawili waliokuwa wamebeba vikapu vya ndizi.Akainua kichwa na kuliona gari moja lenye rangi nyeusi likiyumba na kupoteza uelekeo likielekea upande wa David.Kwa kasi david akaruka na kulishikilia tawi la mti na gari lile likaugonga ule mti .Kwa kuwa halikuwa katika mwendo mkali mti ule haukuweza kuvunjika. David akashuka mtini na kwa hasira huku akitokwa na jasho jingi akaelekea katika mlango wa gari lile na kugonga kwa nguvu.Alikuwa na hasira sana kwa kukoswakoswa kugongwa.Mara mlango ukafunguliwa na hasira zote alizokuwa nazo zikayeyuka

“ Ouh my God ! ..akasema David baada ya kuchungulia ndani ya gari.Mle garini alikuwemo mzee mmoja wa makamo ambaye alionekana kuwa mgonjwa sana,.

“ Nis..nisa..ni.sss..saaiiidiiiiieeee…….!!!!!! akasema kwa taabu yule mzee.Kwa kasi ya aina yake Dadid akamvuta Yule mzee na kumuweka katika kiti cha pembeni halafu akakaa katika kiti cha dereva.Akaufunga mlango na kulirudisha gari nyuma na kuondoka eneo lile na kuwaacha watu waliokuwa wameanza kujaa ili kushuhudia kilichokuwa kimetokea wakishangaa.

“ Nip..ele.ke..hosp…!! akasema kwa taabu Yule mzee.

“ Mzee usijali ninakupeleka hospitali.” Akasema Alois na moja kwa moja akakumbuka kwamba wakati akikata mita ya jiji hili aliiona hospitali moja kubwa inayomilikiwa na watu toka China.Alifika katika hospitali ile na kwa haraka Yule mzee akapokelewa na kuanza kupatiwa matibabu.Baada ya muda David akaitwa katika chumba cha daktari mkuu

“ habari yako kijana” akasema daktari Yule ambaye alikifahamu vyema Kiswahili

‘ Nzuri daktari.Anaendeleaje mgonjwa wangu? Akauliza David

“ Mgonjwa wako anasumbuliwa na shinikizo la damu lakini tunaendelea kumuhudumia na usiwe na wasi wasi.Ataendelea kulazwa hapa akiwa katika uangalizi wa madaktari.Kitu kinachohitajika kwa sasa chukua hii karatasi na uende katika dirisha la cashier yeye atakupigia hesabu ya gharama zote zinazohitajika za vipimo na dawa na kisha kulipa utapeleka risiti katika dirisha la dawa .Kuna dawa na vifaa ambavyo vinatakiwa vichukuliwe baada ya kulipiwa kwanza” akasema daktari Yule.David akastuka sana lakini hakutaka kuonyesha mstuko wake mbele ya Yule daktari.Kilichomstua zaidi ni wapi angepata pesa ya kulipa ? mfukoni alikuwa na shilingi elfu moja na mia tano tu.Akachukua karatasi ile iliyoandikwa kichina na kueleka katika dirisha lililoandikwa Cashier.Akaikabidhi karatasi ile na kupigiwa hesabu .Jumla alitakiwa kulipa kiasi cha shilingi laki nne na elfu ishirini na tatu na mia saba.Kijasho kikamtoka.Akaichukua karatasi ile na kutoka nje.

“ Nitafanya nini? Nitapata wapi pesa hizi nyingi? “ akawaza David na kuzama katika mawazo mengi.Alitamani kuondoka zake na kumuacha mzee Yule peke yake pale hospitali lakini kuna sauti ndani yake ilikuwa inamwambia kwamba asiondoke na kumuacha mzee Yule peke yake.Akainama na kufikiri kwa muda kisha akapata wazo Fulani,akainuka na kuelekea katika gari .Simu ya yule mzee ilikuwa mle garini na ilikuwa inaita.David akaichukua na kuishika mkononi.Alipoge

uza shingo Katika kiti cha nyuma kulikuwa na mkoba.Akauvuta mkoba ule na kuufungua.Mapigo ya moyo wake yakaanza kwenda kwa kasi kubwa.Kulikuwa na mabunda ya noti yaliyopangana.David akahisi kuchanganyikiwa.Picha mbali mbali za haraka haraka zikamjia kichwani kuhusiana na fedha zile nyingi.Hakuwa na fedha na alihitaji fedha ili aweze kuyaanza maisha yake mapya baada ya kutoka gerezani.Wazo la kuchuka fedha zile na kutokomea zake likamjia.Hakumj

ua mzee Yule kwa hiyo angeweza kuchukua fedha zile nyingi na kupotea kabisa na asingeonekana tena.Akatabasamu baada ya kulipata wazo lile lakini ghafla akasikia sauti ndani yake ikimwambia kwamba asifanye hivyo anavyotaka kufanya.

“ Ouh No ! Siwezi kufanya hivi ninavyofikiria kufanya.Si vizuri kumfanyia mwanadamu mwenzangu jambo kama hili.Natakiwa nitafute fedha kwa jasho langu mwenyewe na si kwa kukimbia na fedha za watu.Ee Mungu naomba unisaidie niweze kuwa mwaminifu kwa mzee huyu.Nataka kuishi maisha mazuri na ya haki.” Akawaza David halafu akachukua bunda moja akahesabu noti zile nyekundu .Bunda lile lilikuwa na shilingi millioni tano.Akachukua kiasi cha fedha zinazotakiwa kulipwa akaenda kulipa na kisha akaelekea katika chumba ambacho alilazwa Yule mzee.Hakuruhusi

wa kuingia mle chumbani kwa wakati huo bado Yule mzee alikuwa anaendelea kuhudumiwa.

“ Natakiwa nimsaidie mzee huyu kama baba yangu.Nadhani ni Mungu aliyemuongoza kwangu kwani ingekuwa ni mtu mwingine asingekubali kuyaacha mamilioni yale .Angetokomea nayo yote.Siwezi kufanya hivyo .Nimekaa gerezani nimejifunza namna ya kuwa mtu safi.Nilifungwa bila hatia lakini pamoja na hayo nimejifunza vitu vingi sana nikiwa gerezani.” Akawaza David

Akarudi nje na kuichunguza simu ya Yule mzee.Alikuwa akitafuta namba ya simu ya mke wake au mtu wake wa karibu ili aweze kuwataarifu kuhusiana na ugonjwa uliompata mzee wao.Katika kuyapekua majina katika simu ile akakutana na jina moja limeandikwa my princes Pauline.Akatabasamu.

“ Inawezekana huyu akawa ni mtu wa karibu wa huyu mzee.Ngoja nimpigie nimtaarifu” akasema David huku akibonyeza kitufe cha kupigia simu na simu ikaanza kuita.

***************************************

Pauline alikuwa ameketi sofani akitazama runinga.Siku hii ya leo hakutaka kutoka kwenda sehemu yoyote.Alikuwa mkimya na mwenye mawazo mengi.Mara simu yake ikaanza kuita.Akaangalia mpigaji Alikuwa ni baba yake

“Nimesahau kuizima simu yangu.Siku kama ya leo sitakiwi kupokea simu yoyote ile.Hii ni siku yangu mbaya sana.Kwanza alianza kufariki mdogo wangu tarehe kama ya leo na kuniacha nikiwa peke yangu,miaka miwili baadae siku kama ya leo nilipokea taarifa za kifo cha mama yangu.Mwaka jana mchumba wangu niliyempenda sana alipigwa risasi na majambazi waliotaka kupora benki na akafariki tarehe kama ya leo.No ! sipokei simu hii.Tena ngoja niizime kabisa “ akawaza Pauline na kushika simu yake ambayo bado iliendelea kuita

“ I’m sorry dady.Leo sintapokea simu yoyote hata simu yako” akasema Pauline na kupeleka kidole chake katika kitufe cha kuzimia simu lakini ghafla akabadili mawazo

“ Inawezekana baba akawa na jambo la muhimu analotaka kuniambia.Ngoja nimsikilize” akawaza Pauline halafu akabonyeza kituife cha kupokelea.

“ Hallow baba” akasema

“ Hallow “ ikasema sauti ya kiume tofauti na ile aliyoizoea ya baba yake.Pauline akastuka

“Hallow we ni nani? Akauliza Pauline kwa wasi wasi.Sauti yake ilianza kutetemeka

“ Naongea na Pauline? Ikauliza sauti ile

“ Ndiyo unaongea na Pauline.Wewe ni nani? Akauliza Pauline huku akitetemeka

“ Mimi naitwa David”

“ Mwenye simu hii yuko wapi? Umeipata wapi simu yake? Akauliza Pauline

“Naomba unisikilize Pauline.” Akasema David na kumfanya Pauline azidi kutetemeka

“ Uko wapi mida hii?

“ Niko hapa nyumbani Njiro”

“ Ok.sasa ni hvi naomba uje hapa katika hii hospitali ya wachina baba yako amelaza hapa amepatwa na tatizo kidogo.Utanikuta hapa” akasema David na kukata simu

“ Hallo Dav……!!!.” Akaita Pauline lakini tayari David alikwisha kata simu.Pauline akahisi kuchanganyikiwa.

“Ouh Mungu wangu kwa nini kila ikifika tarehe kama hii kila mwaka lazima niwe ni mtu mwenye huzuni? Kuna nini katika tarehe hii?Tafadhali naomba umponye baba yangu.Bado namuhitaji sana katika maisha yangu.yeye ndiye mtu pekee na wa muhimu kwangu kwa sasa.Please Lord save him” akaomba Pauline huku akiinuka na kuelekea chumbani kwake akavaa haraka haraka na kutoka kwa kasi.Alikuwa anatetemeka mwili.Alistushw

a sana na taarifa zile.Akapanda katika gari lake lakini mikono ilikuwa inamtetemeka bado.

“ I have to do this.I have to drive..!!” akasema Pauline halafu akavuta pumzi ndefu na kuliwasha gari akaondoka kuelekea hospitali




“ Ok.sasa ni hvi naomba uje hapa katika hii hospitali ya wachina baba yako amelaza hapa amepatwa na tatizo kidogo.Utanikuta hapa” akasema David na kukata simu

“ Hallo Dav……!!!.” Akaita Pauline lakini tayari David alikwisha kata simu.Pauline akahisi kuchanganyikiwa.

“Ouh Mungu wangu kwa nini kila ikifika tarehe kama hii kila mwaka lazima niwe ni mtu mwenye huzuni? Kuna nini katika tarehe hii?Tafadhali naomba umponye baba yangu.Bado namuhitaji sana katika maisha yangu.yeye ndiye mtu pekee na wa muhimu kwangu kwa sasa.Please Lord save him” akaomba Pauline huku akiinuka na kuelekea chumbani kwake akavaa haraka haraka na kutoka kwa kasi.Alikuwa anatetemeka mwili.Alistushw

a sana na taarifa zile.Akapanda katika gari lake lakini mikono ilikuwa inamtetemeka bado.

“ I have to do this.I have to drive..!!” akasema Pauline halafu akavuta pumzi ndefu na kuliwasha gari akaondoka kuelekea hospitali

ENDELEA………………………………………

Pauline alifika hospitali na moja kwa moja akaelekea mapokezi kuulizia kuhusu hali ya baba yake.Wahudumu waliokuwa mapokezi wakampa moyo na kwamba asiwe na wasi wasi baba yake alikuwa anaendelea vizuri.Pauline akaomba kuonana na daktari mkuu lakini akaombwa asuburi kwa sababu kwa muda huo mganga mkuu alikuwa anamuhudumia mtu mwingine.Akaenda kukaa katika viti vya kupumzikia huku ameinamisha kichwa.Kichwa chake kilijaa mawazo mengi.Alijiona ni mtu mwenye mkosi katika hii dunia.Aliichukia September 11.Kila mwaka huwa ni siku mbaya sana kwake.

“ Kuna nini katika tarehe hii? Kwa nini kila mwaka katika tarehe hii lazima nikumbwe na jambo baya? Kwanza alikuwa mdogo wangu,halafu mama yangu ,akafuata mchumba wangu na mwaka huu ni baba yangu.Nani atafuata mwaka ujao? Ouh gosh I’m tired of this..Maisha yangu yamegeuka na kuwa ya huzuni kubwa kutokana na tarehe kama ya leo. Lazima kuna jambo ambalo haliko sawa na ndiyo maana kila ikifika tarehe kama ya leo lazima kuna jambo baya linatokea.” Akawaza Pauline mara akahisi kama mkono wa mtu umeligusa bega lake.Akainua kichwa na kukutanisha macho na kijana mmoja mwenye uso uliopauka na mavazi kuukuu.Hakuwa na kumbu kumbu kama amewahi kumuona kijana Yule mahala kokote.Sura yake ilikuwa ngeni kabisa machoni pake

“nadhani wewe ndiye Pauline? Akauliza Yule kijana.Huku akisita Pauline akajibu

“ Ndiye mimi.wewe ni nani?

“ Mimi ni David.!!..”

Pauline akastuka na kushangaa .

“ Naomba unifuate huku nje ninahitaji kuongea nawe” akasema david.pauline akainuka na kumfuata kijana Yule.

“ Wewe ndiye uliyenipigia simu? Akauliza Pauline

“ Ndiye mimi” akajibu David

“ baba yangu anaendeleaje? Amepatwa na tatizo gani?

“ Usihofu Pauline .Baba yako anaendelea vizuri .Alipatwa na tatizo la shinikizo la damu akiwa barabarani na kupoteza mwelekeo.Kwa bahati nzuri hakuwa katika barabara yenye magari mengi na hakuwa katika mwendo mkali vinginevyo ingekuwa mbaya sana kwake.Nilifanikiwa kuliendesha gari lake na kumkimbiza hapa hospitali ambao amepokelewa na ameanza kuhudumiwa na madaktari wanasema kwamba hali yake inaendelea vizuri.” Akasema david

“ Ouh ahsante sana David.Ni kweli baba yangu huwa ana tatizo hilo la shinikizo la damu .Nashukuru sana kwa kumsaidia baba yangu.Mungu akubariki David “ akasema Pauline huku akifungua pochi lake na kutoa noti tatu za shilingi elfu kumi kumi akampatia David.

“ Ahsante sana Pauline lakini naomba uziweke fedha hzo utazitumia kwa matumizi mengine.Nimemsaidia baba yako kama ambavyo ningeweza kumsaidia mtu mwingine yeyote bila malipo.” Akasema David ingawa alizihitaji sana fedha zile ili ziweze kumsaidia katika wakati huu mgumu ambao anahitaji sana fedha ili aweze kuyaendesha masha yake.

“ david tafadhali naomba uzichukue fedha hizi kama ahsante yangu kwa kitendo chako cha kumsaidia baba yangu.Umefanya jambo kubwa sana na hii ni shukrani yangu na si kwamba ninakulipa.tafadhali naomba upokee David” Pauline akasisitiza

“ Ahsante sana Pauline lakini sintaweza kuzipokea fedha hizo.Nimefanya ninalotakiwa kufanya kama binadamu.” Akasema David na kumfanya Pauline atabasamu huku akizirejesha fedha zile katika mkoba wake.

“Pauline mbona uko peke yako? Mama yako yuko wapi? Ndugu zako wengine wana taarifa kuhusiana na ugonjwa wa baba yako? Akauliza david

“Mama mdogo yuko Morgoro na tayari nimekwisha mfahamisha na hivi sasa anafanya mipango ya usafiri ili aweze kurejea mara moja.Anaangalia uwezekano wa kupata ndege ya haraka.Ndugu wengine nao nimekwisha wataarifu ingawa wanaishi mbali na hapa Arusha.” Akasema Pauline na David akauliza tena

“ mama yako mzazi yuko wapi?

“ mama yangu alikwisha fariki dunia” akasema Pauline

“ Pole sana Pauline”

“ ahsante david.Haya ndiyo mambo ya dunia kwa hiyo hatuna budi kuyakubali na kuyazoea.Kifo ni sehemu ya maisha yetu wanadamu” akasema Pauline

“ Kwa hiyo hakuna ndugu wengine wa karibu ambao unaweza ukashirikiana nao katika kumuuguza baba yako?

“ Kwa hapa arusha baba hana ndugu zaidi ya marafiki .Ndugu zake wengi wako mikoani hususani Mbeya na wengine wako Ulaya.” Akasema Pauline.

“ sawa Pauline.Naomba basi nikukabidhi ufunguo wa gari la mzee na badhi ya vitu vyake.Hii ni simu yake na ndani ya gari kuna mkoba wenye fedha.Sifahamu kuna kiasi gani cha fedha katika mkoba ule lakini nimetoa hapo kiasi kilichokuwa kinatakiwa kulipwa hapa hospitalini na risiti ni hii hapa.Utanisamehe Pauline kwa kushika vitu vya baba yako bila ruhusa lakini sikuwa na namna nyingine kwani zilikuwa zinatakiwa fedha za haraka na mimi sikuwa na fedha hizo zilizokuwa zinatakiwa” akasema David.Pauline akavua miwani na kumuangalia David usoni.

“ Ni kweli leo baba alikuwa na safari ya kuelekea benki kupeleka fedha.Ahsante Mungu kwa kijana huyu wa ajabu kukutana na baba,wangekuwa ni vijana wengine kwanza wangeondoka na gari na fedha zote na kumtelekeza baba,lakini David ameweza kutunza uaminifu na nina imani hajachukua hata senti moja katika mamilioni ya fedha zile.” Akawaza Pauline

“ Pauline ahsante sana nadhani kwa sasa mimi naweza kuondoka” akasema david

“ nashukuru sana kwa msaada na uaminifu wako mkubwa David.Watu kama wewe ni nadra sana kuonekana katika dunia hii ya sasa.Ningekuomba David uendelee kubaki hapa hadi baba atakapopata nafuu ili aweze kumshuhudia kijana huyu wa aina yake ambaye ameyaokoa maisha yake “ akasema Pauline

“ Hata mimi ningefurahi sana kama ningeendelea kukaa hadi baba yako atakapopata nafuu lakini nasikitika Pauline nalazimika kuondoka.Kuna mambo ambayo natakiwa kuyashughulikia “ akasema david

“ david usijali kama ni kazi niko tayari kukulipa hata fedha ambazo ungepaswa kulipwa leo .Naomba uendelee kukaa nami hapa hospitali.Nahitaji mtu wa kunisaidia kumuuguza baba na kunipa nguvu.Nakuhitaji David.Tafadhali naomba tuendelee kuwa wote hapa hospitali.” Akasema Pauline.David akainama akawaza na kusema

“ Sawa Pauline nimekubali ,nitaendelea kukaa hapa hospitali.”

“ ahsante sana David.Usijali nitakulipa gharama zote za siku ya leo.Unafanya kazi wapi?

“Sina kazi? Akajibu David kwa ufupi.Pauline hakuonyesha kuridhishwa na jibu lile akauliza tena

“ Unaishi wapi david?

“ Kwa sasa sina mahala pa kuishi” akajibu David akiwa ameinamisha kichwa chini

“ Huna mahala pa kuishi? Unamaanisha nini unaposema hivyo? Pauline akashangaa

“ Pauline naomba nikueleze ukweli kwamba mimi si mwenyeji wa Arusha . siku hii ya leo nimemaliza kifungo changu katika gereza la Oltoreo na nimeachiwa huru.Kwa hivi sasa sijui nielekee wapi na wala nitaanzaje maisha yangu.hakuna mtu ninayemjua hapa Arusha na sijui nielekee wapi ndiyo maana nilihitaji kwenda kuendelea kutafuta namna nitakavyoweza kuimaliza siku ya leo .” akasema David

“ Ouh my gosh !!..akasema Pauline na kumtumbulia macho David kana kwamba amekutana na mzuka.

******************************

Kikao na wageni waliokuwa wamemtembelea kilimalizika ,Robin akaagana nao kisha akarejea ofisini kwake.Wakati akiufungua mlango kuingia ofisini ,Neema katibu wake muhtasi akamfahamisha kwamba wakati akiwa katika kikao na wageni wake kuna simu imepigwa toka shuleni kwa Penny wakimtaka afike mara moja kuna tatizo limetokea.Robin akastuka sana

“ Kuna tatizo gani? akauliza

“ Sifahamu bosi.Mwalimu aliyepiga amesema ufike pale mara moja mara baada ya kumaliza kikao chako”

“ Ouh my God ! Penny anaweza akawa amepatwa na tatizo gani? akajiuliza Robin na kwa haraka akaingia ofisini kwake akachukua mkoba wake na kutoka kwa kasi

“ Neema sitisha miadi yangu yote siku ya leo.Inawezekana Penny amepatwa na tatizo kubwa kwa hiyo sitegemei kurudi tena.” Akasema Robin na kuchomoka kwa kasi hadi katika gari lake na kuondoka kuelekea shuleni kwa Penny.

“ Ouh Mungu wangu naoba unisaidie mwanangu Penny asiwe amepatwa na jambo baya.nampenda sana mwanangu na sipendi kumuona akipatwa na matatizo.yeye ndiye kila kitu kwangu” akawaza Robin

Alifika shuleni anakosoma mwanae na kuelekea moja kwa moja katika ofisi ya mkuu wa shule.Jasho lilikuwa linamtiririka.

“ Karibu sana” Robin akakaribishwa na mwalimu mmoja wa kike mwenye sura nzuri sana,mrefu mwembamba na mwenye nywele ndefu.Alikuwa na suati laini sana huyu mwalimu

“ Ahsante mwalimu.Mimi naitwa Mr Robinson ni baba mzazi wa mwanafunzi anaitwa Penny.Nimepata ujumbe kwamba natakiwa shuleni haraka kuna jambo limetokea.Nomba unieleze mwalimu,mwanangu Penny amepatwa na tatizo gani? akauliza Robin kwa wasi wasi.Yule mwalimu mwenye uzuri wa kipekee akamuangalia Robin usoni na kusema

“ wewe ndiye baba yake Penny?

“ Ndiye mimi mwalimu.Mwanangu penny amepatwa na tatizo gani? akauliza Robin kwa wasi was.mwalimu Yule hakumueleza chochote akainuka na kumuomba Robin amfuate.

“ Mwalimu mbona huniambii mwanangu amepatwa na tatizo gani? akauliza Robin lakini mwalimu Yule ambaye alikuwa akitembea kwa haraka hakumjibu kitu.Wakayavuka majengo ya shule na kuelekea katika majengo yaliyoonekama kama nyumba za kuishi.Wakaelekea katika nyumba moja iliyokuwa na geti kubwa jekundu.Yule mwalimu akalifungua wakaingia ndani .

“ penny yuko huku? Anaumwa?? Akauliza Robin.Yule mwalimu hakumjibu kitu akaufungu mlango mkubwa wa kuingilia sebuleni wakaingia katika sebule kubwa

“ Surprise..!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!......” Sauti kubwa ikasikika mara tu Robin alipoingia pale sebuleni.Akastuka sana.Moyo ulikuwa unamwenda mbio.Penny mwanae akiwa na wanafunzi wenzake zaidi ya kumi walikuwa na nyuso zenye furaha kubwa .Walikuwa wamesimama wakiwa na maua mikononi.

“ Ouh my gosh ..Penny !!!!!.. akasema Robin kwa mshangao.Penny akamsogelea

“ Happy birthday dady” akasema Penny

Robin alishindwa kuyazuia machozi kumtoka .Akainama na kumkumbatia mwanae.Ilikuwa nisiku yake ya kuzaliwa lakini kutokana na mawazo mengi aliyokuwa nayo hakukumbuka kabisa kuhusu siku hii muhimu.

“ Ahsante sana Penny.Ahsante sana mwanangu” akasema Robin huku wanafunzi wakipiga makofi.Penny akamshika mkono na kumuongoza hadi katika meza ilikokuwa imeandaliwa keki nzuri yenye maandishi mazuri ya kumtakia yeye Robin heri ya siku yake ya kuzaliwa.Mishumaa ikawashwa halafu akaipuliza yote na kuizima ,wanafunzi wakapiga makofi.Robin alikuwa na furaha iliyopitiliza.

Wakati wanafunzi wakiwa jikoni wakiandaa chakula,mwalimu mkuu akamfuata Robin huku akitabasamu na kusema kwa sauti laini.

“ Happy birthday Mr Robin”

Robin akatabasamu na kushukuru.

“ Penny alinifuata na akaniomba kwamba anahitaji kumfanyia baba yake kitu muhimu katika siku yake ya kuzaliwa na akaniomba msaada wa mawazo nikampa wazo hili la kukufanyia sherehe ya kustukiza”

Robin akatabasamu na kusema

“ Ouh kumbe lilikuwa ni wazo lako..! Nashukuru sana mwalimu.Nashukuru sana.Sikuwa na kumbu kumbu yoyote kuhusiana na siku yangu ya kuzaliwa”

“ Ni kweli.Watu wengi huwa hawakumbuki siku zao za kuzaliwa na hasa kutokana na kutingwa na kazi nyingi au kutokuona umuhimu wa siku hii” akasema mwalimu halafu kikapita kimya cha muda ,Robin akauliza

“ Mwalimu utaniwia radhi kwani nilikuwa katika wasi wasi mwingi na sikukumbuka hata kuuliza jina lako.Sijui unaitwa mwalimu nani?

“ Naitwa mwalimu Lucy” akajibu

“ Ouh kumbe wewe ndiye mwalimu Lucy.!! Penny amekuwa akikutaja kila siku.Ninafurahi kukufahamu”

“Hata mimi nimefurahi kukufahamu.namp

enda sana Penny ni mwanafunzi wa pekee kabisa.Ana adabu,ana akili sana darasani,ni msafi anajituma katika kazi na ni binti mwenye uelewa wa hali ya juu kabisa.Nilikuwa natamani sana kukutana na wazazi wake siku moja kwani tabia hii njema na kila alichonacho kimetokana na malezi bora ya wazazi wake.Kwa bahati mbaya Penny aliniambia kwamba mama yake hayuko nanyi tena.Napenda kukusifu kwa malezi mazuri uliyompa mwanao.Si kazi rahisi kuwa baba na mama kwa wakati mmoja.Lakini wewe umemudu na kumfanya Penny awe hivi alivyo.Hongera sana..” Akasema mwalimu Lucy

“ nashukuru sana mwalimu Lucy.Kuhusu malezi ya Penny ni kwamba sote tumeshiriki kumlea na kumfikisha hapa.Sote tumetimiza wajibu wetu ipasavyo.Kama mzazi na kama mwalimu.naomba tuendelee kushirikiana katika malezi ya watotowetu hawa” akasema Robin.

Ilikuwa ni siku nzuri sana kwa Robin na mwanae Penny.Alihisi furaha ya aina yake ambayo aliikosa kwa muda mrefu.Baada ya sherehe ile ndogo wakaondoka na kurejea nyumbani kwao.

“ Penny nashukuru sana kwa tukio la leo.Umeikumbuka siku yangu ya kuzaliwa.Umenipa furaha sana Penny.Sikutegemea kabisa kama ungeweza kunifanyia jambo kama hili” akasema Robin wakiwa mezani wakipata chakula cha usiku

“ Baba,ni muda mrefu nimekuona huna furaha hata kidogo na huikumbuki tena siku yako ya kuzaliwa.Nikaongea na mwalimu Lucy akanipa wazo la kukufanyia sherehe ile ndogo ya kustukiza.” Akasema Penny halafu wakaendela kula kimya kimya

“ baba ,mama unawasiliana naye? Akauliza Penny na kumstua baba yake.Hakutegemea swali lile toka kwa mwanae.Ikamchukua muda kidogo kujibu

“ Hapana Penny.Mama yako toka alipoondoka sijawahi kuwasiliana naye tena.Kwa nini umeuliza?

“ Nilitaka tu kufahamu kama una mawasiliano naye kwa sababu imepita muda mrefu sana sijawahi kumuona na hata kuisikia sauti yake.Hatukumbuki tena.Amekwisha tusahau” akasema Penny.Maneno yale yakamuumiza sana Robin

“ Penny mwanangu naomba usiwaze mambo kama hayo.Mimi niko hapa na chochote utakachokitaka utakipata.Iko siku mama yako atatukumbuka na atakuja kukutembelea” akasema Robin.Penny akaacha kula akaweka kijiko mezani na kuonekana kuzama katika mawazo

“ Sina hakika kama siku moja atakuja tena.Ninashangaa sana roho aliyonayo mama yangu.hanikumbuki hata mimi mtoto wake ,na hataki hata kujua ninaendeleaje.Baba simpendi mama yangu na sitaki hata kumuona” akasema Penny

“ penny usiseme hivyo.Hata kama amekukosea kiasi gani lakini atabaki kuwa mama yako.Inakubidi umpende na usimchukie.Kitu tunachotakiwa kufanya ni kumuombea ili awe na maisha mazuri huko aliko” akasema Robin.Penny akainamisha kichwa na kufikiri kwa muda kisha akainua kichwa chake na kusema

“ Baba umemuona mwalimu Lucy? Akauliza Penny. Baba yake akatabasamu

“ ndiyo nimeonana naye leo.Amekumwagia sifa nyingi kwamba wewe ni mwanafunzi hodari mwenye bidii na nidhamu.”

“ Nampenda sana mwalimu Lucy.Ni mpole na mkarimu.Ananipenda sana.aliniomba siku moja aje afahamu mahala ninakoishi.Nimemwambia nitawasiliana nawe kwanza ili kama utakubali basi tumualike aje jumamosi ya wiki hii” akasema Penny.Baba yake akatabasamu na kusema

“Nadhani jumamosi ni siku nzuri.Mwambie tutamkaribisha siku ya jumamosi.” Akasema Robin na uso wa Penny ukapambwa na tabasamu pana sana.Sura ya mwalimu Lucy ikamjia Robin kichwani akatabasamu.

“ She’s so pretty.Ana uzuri wa kipekee kabisa.anaonekana ni mwenye roho nzuri na anapenda sana watoto” akawaza Robin huku akitabasamu na kuvuta pumzi ndefu.



ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Baba umemuona mwalimu Lucy? Akauliza Penny. Baba yake akatabasamu

“ ndiyo nimeonana naye leo.Amekumwagia sifa nyingi kwamba wewe ni mwanafunzi hodari mwenye bidii na nidhamu.”

“ Nampenda sana mwalimu Lucy.Ni mpole na mkarimu.Ananipenda sana.aliniomba siku moja aje afahamu mahala ninakoishi.Nimemwambia nitawasiliana nawe kwanza ili kama utakubali basi tumualike aje jumamosi ya wiki hii” akasema Penny.Baba yake akatabasamu na kusema

“Nadhani jumamosi ni siku nzuri.Mwambie tutamkaribisha siku ya jumamosi.” Akasema Robin na uso wa Penny ukapambwa na tabasamu pana sana.Sura ya mwalimu Lucy ikamjia Robin kichwani akatabasamu.

“ She’s so pretty.Ana uzuri wa kipekee kabisa.anaonekana ni mwenye roho nzuri na anapenda sana watoto” akawaza Robin huku akitabasamu na kuvuta pumzi ndefu.

ENDELEA…………………………………..

Baada ya kumaliza kula akamuacha mwanae akiendelea na kujisomea yeye akaelekea chumbani kwake akajilaza kitandani.Akavuta pumzi ndefu

“ Siku yangu ilianza vibaya kwa kuota ndoto mbaya lakini imeisha vizuri sana.Sikutegema kama siku hii ya leo ingeisha nikiwa na furaha kubwa namna hii.Penny amenifanya niwe na furaha.namshukur sana Mungu kwa kunipa mtoto huyu mwenye akili nyingi .Nina haki ya kujisifu kwa malezi niliyompa na kumfanya awe hivi alivyo.Namsikiotikia sana Flaviana kwa kitendo chake cha ukatili alichokifanya na kumsahau kabisa mwanae.Penny ameumizwa sana na kitendo hiki na kwa sasa anamchukia kabisa mama yake na hataki hata kumuona tena.Ana haki ya kumchukia lakini sitaki afanye hivyo.Yule ni mama yake na ataendela kuwa mma yake hata kama amemkose akiasiagani.” Akawaza Robin akiwa amejilaza kitandani.Mara picha ya mwalimu Lucy ikamjia tena kichwani akatabasamu

“ Penny na mwalimu Lucy wanapendana sana.Nilimsikia akimuongela mara nyingi na sikuwahi kumuona mwalimu Yule,lakini nilipoonana naye leo nilistujka kidogo.Japokuwa nmlkuwa na mstuko kutokana na taarifa zile za kuakiwa kufka kwa haraka shulenmi lakini nilisisimka kidogo baada ya kuiona sura yake.Dah ! ni mwanamke mzuri sana.Ni mzuri wa sura na umbo na ananekana ni mwanamke mwenye hekima na busara na anapenda sana watoto.Ninamshukuru kwa kuwa amekuwa karibuna Penny na amemsaidia kuupata ule upendo wa mama ambao ameukosa kw amiaka mingi.Nadhani anastahiliheshima ya kipekee kabisa .Itabidi siku hiyo atakapokuja hapa nyumbani apewe mapokezi ya kipekee kabisa ili kumuonyesha shukrani zetu na kumshukur kw akazi kubwa anayoifanyakwa mwnaangu Penny.” Akawaza Robin halafu akajgeuza upande wa pili

“Itanibidi nimtafutie na kijizawadi kidogo kama ahsante yangu kwake.Nitaongea na Penny aniambie mwalimu wake anapendelea vitu gani.” akawaza Robin.Sura ya mwalimuLucy bado iliendelea kumjia kichwani.Alikumbuka namna alivyokuwa akitabasamu

“ Naomba nikiri kwmaba nimevutiwa sana na Yule mwalimu.Sijui imenitokeaje lakini ghafla tu baada y akumuona nimejikuta nikivutiwa naye.lakini hata hivyo sitakiwi kuanza kuumiza kichwa changutena kwani mwanamke mzuri kama Yule hawezi kukosa mtu wake.tena inawezekana mwenzi wake akawa ni mtu mwenye uwezo mkubwa kiuchumi.Ngoja nijenge kwanza urafiki naye wa kawaida tu .Sitaki kutafuta matatizo tena kwa wakatyi huu japokuwa ninahuitaji sasa kutafuta mwanamke ambaye atanipenda na kumpenda mwanangu.” Akawaza Robin

****************************

Pauline bado aliendela kumuangalia David kwa macho makali .

“ Ouh gosh ! siamini kama maneno haya nayonieleza David ni ya kweli.Ametoka gerezani? Kwa ninialifungwa? Al;ifanya kosa gani kijana mwenye roho nzuri kama huyu? Hanyeshi kama ni kijana mhalifu au anayeweza kutenda kosa lolote la kijinai.Kuna kitu nimekigundua kwa kijana huyu .Kuna kitu kimejificha ndani yake “

“Pauline mbona unaniangalia namna hiyo? Samahani kama nimekustua kwa kukuambia ukweli wangu kwmaba nimetoka kifungoni.Lakinihuo ni ukweli halisi na endapo haujisikii vizuri au kama umeogopa kwa kudani labda ninaweza kuwa ni mhalifu,isikupe shaka mimi nitaondoka na nitarejea tena kesho kuja kumaugali mzee wako” akasema David

“ Hapana David ,si hivyo unavyowaza.Samahani kwa kukuangali namna hii.Ni kweli nimestushwa sana na kusikia kwamba ulikuwa umefungwa na hivi leo umemaliza kifungo chako.Nilikuwa najiuliza ni kosa gani ambalo limepelekea kijana mwema kama wewe ukaenda kule?

David akatabasamu na kusema

“ Umejuaje kama mimi ni mwema?

“Mtu mwema hana alama usoni lakini anajulikana kutokana na maneno na matendo yake.Kitendo ulichokifanya leo hii kwa mzee wangu kinadhihirisha hayo kwamba u kijana mwema na mweney roho ya ajabu sana.Ni mfano wa kuigwa”

“ ahsante sana Pauline kwa kulitambua hilo .Ahsnte kwa kuniamni pia kwa sababu zama iz ni nadra sana kwa mtu kuaminiwa kwa haraka namna hii.Siku hiz hata wazazi wanashidwa kuwaamini watoto wao. Dunia imebadilika sana.Upendo uaminifu vimetoweka.Ubin

afsi umetawala siku hizi na kila mmoja anajiangalia yeye pekee.Pamoja na hayo najaribu kuionyesha jamii kwamba tunahitaji kurejesha upendo miogoni mwetu.Tuhurumiane,tupendane na tusaidiane.” Akasema David.Pauline akazidi kuvutiwa na maeno yake

“ David una mneno ya busara sana.Nafurai kukutana na mtu kama wewe.Hata baba nina imani atafurahi sana kukuona kijana mwenye uaminifu wa aina yake kama wewe.Naomba nichukue nafasi hii kukukaribisha uishi nyumbani kwetu.Tuna nyumba kubwa tu hapa Arusha na tunaishi watu wachache,mimi baba na mama mdogo pamojana mfanyakazi wetu mmoja.Kwa kuw aka sasa huna sehemu ya kuihsi naomba ukubali kwenda kuishi nyumbani kwetu “

“ Paulne nashukru sana lakini naomba nisiwe mzigo kwa familai yenu kwa msaada huu niliomsaidia baba yako.”

“ Haoana David.Wewe umetoa msaada kwa baba yangu na kwa familai yanguna sisi kama ulivyofanya wewe tunakusaidia wewe.Umekiri kwamba huna sehemu ya kuishi kwa hiyo nakukaribisha nyumbani kwetu.Utaishi nasi pale hadi hapo maisha yako yatakapokua mazuri .”

“ Pauline familia yako itaweza kunikubali mtu kama mimi na hasa muonekano wanguna wakigundua kwamba nimetoka gerezani,wataniogopa na kudhani kwamba mimi ni mhalifu kama ilivyojengeka katika jamii kwamba kila mtu anayefungw agerezani ni mhalifu.”

“ David naomba unisikilize mimi.Muoneano wa mtu si tabia ya mtu.Wewe si mhalifu na ungekuwa na tabia hizo ungeondoka nay ale mamilioni ya bba yaliyokuw akatika mkoba.Unajua kulikuwa na kaisi gani katika ule mkoba? Kulikuwa na shlingi million themanini na saba.NI pesa nyingi ambazo ungeweza kwenda kuyaendesha maisha yako bila matatizo .Hicho ni kithibitisho tosha kwmaba wewe si mhalifu na kama ulifungwa basi ni kw amakosa mengne lakini si kwa uhalifu.Tafadhalinaomba ukubalikuja kuishi nasi.Usihofu kuhus muonekano.Hiki ni kituambacho kinawea kubadilishwa ndani ya dakika mbili.” Akasema Pauline.David alishindwa kukataa kwani alihitaji sana sehemu ya kuweza kuishi wkati akiyapanga maisha yake vizuri.

Kwa kuw amgonjwa ao alikuwa amelala kwa wakati huo ,Pauline akamuomba David waende wakapate chakula cha mchana .Wakaingia katika gari la Pauline na kuelekea katika hoteli moja kubwa .

“ Pauline umenileta katika hoteli hii ,naomba nisikutie aibu kutokana na muonekano wangu” akasema David na kumfanya Pauline acheke

Waliaguiza chakula na kuanza kula.Pauline alikuwa anamchunguza David kwa kuibia namna alivyokuwa anakula.

“ David anaonekana ni kijana ambaye anafahamu vitu vingi.Muonekano wake na matendo yake viko tofauti ana.” Akawaza Pauline

Wakati wakiendela kula mara Pauline akapigiwa simu akapokea na kuongea na mtu aliyempigia na alipomaliza akamgeukia David

“ Ni mama mdogo amenitaarifu kwamba amekosa ndege ya haraka kwa hiyo hataweza kuja leo .Atakuja kesho” akasema Pauline halafu akainama na kuzama katika mawazo.

“Pauline kuna tatizo lolote? Akauliza david

“ David ninasikitishwa sana na huyu mama yangu mdogo kwani amekuwa akimpa baba wakati mgumu sana.Toka mama yangu alipofariki dunia na baba akaamua kuoa mwanamke mwingine akitegemea kuwa na maisha yenye furaha lakini imekuwa tofauti sana.Maisha yake hayana furaha hata kidogo.Huyu mama amekuwa akimpa wakati mgumu sana” akasema Pauline

“ Matatizo katika ndoa ni kitu cha kawaida lakini kuna kitu kimoja ambacho unatakiwa ujiulize kwamba je huyo mama yako mdogo anampenda baba yako ?

Swali lile likampa Pauline ugumu wa kulijibu

“ Sifahamu David.Siwezi kujua kama anampenda baba yangu ama vipi lakini ninachofahamu ni kwamba yeye amekuwa ni chanzo cha matatizo mengi ya baba.Amekuwa na utumiaji mbaya sana wa fedha na hivyo kuifanya baadhi ya miradi ya baba kufungwa kitu ambacho kimekuwa kikimuumuza sana baba yangu na kumfanya awe na mawazo mengi”

David akastuka sana kwa maneno yale ya Pauline

“ Mbona umestuka Dadid?

“ Its nothing..” akajibu David na kumstua kidogo Pauline

“ Kumbe David anafahamu kiingereza vizuri !! Kuna mambo ambayo yamejificha ndani yake.Kuna haja ya kumfahamu kwa undani kijana huyu.Lakini itabidi kwenda naye taratibu kwani anaonekana hapendi kuyazungumzia maisha yake.” Akawaza Pauline.

Baba yake Paulne alikuwa anaendelea vizuri na madaktari wakawaomba Pauline na David waende wakapumzike na wasiwe na wasi wasi na afya ya mgonjwa wao kwani maendeleo yake yalikuwa mazuri.hawakuweza kuongea naye kwa jioni hiyo kwa kuwa alikuwa amelala.Wakaondoka pale hospitali na kuelekea nyumbani kwa akina Pauline maeneo ya Njiro.David alikuwa akimfuata Pauline akiendesha gari la baba yake Pauline na Pauline yeye akiendesha gari lake

Walifika nyumbani kwa akina Pauline David akakaribishwa ndani .Lilikuwa ni jumba kubwa na la kifahari.

“ Wow ! I’m back to life again” akawaza David huku akitabasamu




 Pauline alikuwa makini akimtazama 

David katika kila hatua kwa jicho la 

wizi.Alitaka kumfahamu kijana huyu ni 

kijana wa namna gani .David 

akakaribishwa sofani na baadae wakapata 

chakula cha usiku halafu akaenda 

kuonyeshwa chumba chake cha 

kulala.Kilikuwa ni chumba kikubwa 

chenye kitanda kikubwa kilichotandikwa 

mashuka mazuri yenye nakshi za kupendeza.Akaa juu ya kile kitanda 

akalibonyeza godoro lile na kutabasamu 

 “ Muda mrefu umepita toka nilipolala 

katika sehemu laini na ya kupendeza 

kama hii.Ama kweli maisha yana maajabu 

sana kwa sababu jana nilikuwa mfungwa 

lakini leo hii niko katika jumba hili la 

kifahari.Nina imani Mungu bado 

ananipenda na hatanitupa hata siku moja 

kwa sababu yeye mwenyewe anafahamu 

kwamba sikutenda kosa nililotuhumiwa 

kulitenda na nilifungwa pasipo na 

hatia.Yote haya nimemwachia yeye 

mwenyewe kwani ndiye tumaini langu 

kwa sasa.Sikuwa na sehemu ya kula wala 

kulala lakini kwa maongozi yake nimekula 

na nimepata sehemu ya kulala.” Akawaza 

David halafu akavua shati lake na kubaki 

na fulana ya ndani.Mara mlango 

ukagongwa.Akaenda kufungua na 

kukutana na sura yenye tabasamu ya 

Pauline. 

 “ Pauline karibu” akasema David 

 “ Ahsante David.Samahani kwa 

kukusumbua nimekuletea hizi nguo 

ambazo utabadilisha ukioga.Kesho 

tutakwenda kufanya manunuzi ya nguo zako za kuvaa.Naomba ujisikie amani na 

ujione kama uko nyumbani “ akasema 

Pauline na kumfanya David atabasamu 

 “ Ahsante sana Pauline.Sipati neno la 

kuelezea shukrani zangu kwako kwa 

wema wote ulionifanyia.” 

 “ Ouh David thats nothing.Haya usiku 

mwema kesho tutaamkia hospitali kujua 

hali ya baba” akasema Pauline na 

kuondoka.David akabaki amesimama pale 

mlangoni akimuangalia Pauline halafu 

akatabasamu akafunga mlango na 

kuziangalia nguo zile alizokuwa 

ameletewa. 

 “ Pauline ni msichana mwenye adabu 

sana na ni mkarimu mno.Amenikumbusha 

aliyewahi kuwa mpenzi wangu Dinah.Sijui 

yuko wapi sasa hivi na maisha yake 

yakoje.” David akatabasamu baada ya 

kulikumbuka jina lile 

 “ Maandiko yanatuambia kwamba 

tuwapende na kuwaombea maadui zetu 

waishi siku nyingi .Nitamuombea Dinah 

aishi maisha marefu ili ashuhudie namna 

maisha yangu yatakavyobadilika 

.Alinitenda kiasi ambacho mpaka leo hii 

ninaendelea kujiuliza kama ni kweli ni yeye ndiye aliyenifanyia vile au ni kivuli 

chake. Alikubali kurubuniwa na fedha na 

kuniangamiza.Hakunionea huruma kama 

ninakwenda kuteseka gerezani kwa kosa 

ambalo sikulitenda. Dah ! wanawake.Sina 

hamu nao tena.nayachukia mapenzi sana 

na sifikirii kabisa kuingia mapenzini 

tena.Nadhani maisha yangu yote 

yaliyobaki nitakuwa peke yangu.” 

Akawaza David halafu akachukua taulo na 

kuingia bafuni akajimwagia maji na 

kurejea chumbani akajilaza 

kitandani.Kabla ya kufumba macho 

akamshukuru sana Mungu kwa kuendelea 

kumpigania na kumuwezesha kuimaliza 

siku ile. 

 Kwa upande wake Pauline alikuwa 

bado amekaa katika sofa lililoko 

chumbani kwake akiangalia filamu. 

 “ Sijui kwa nini David ametokea 

kuniingia moyoni namna hii.Toka 

nilipomuona nimekuwa nikijisikia 

kumsaidia .Ni kijana mwenye moyo wa 

kipekee kabisa.Kitendo alichokifanya leo 

ndicho kimenifanya niwe na moyo wa 

kumsaidia.Nina hakika hata baba 

akikutana naye ataamua kumsaida.Lakini hata hivyo bado ninajiuliza ni kwa nini 

alifungwa? Alitenda kosa gani 

lililompeleka gerezani? Haoneani kama 

mhalifu, na kama angekuwa na tabia hiyo 

basi angeondoka na mamilioni yale ya 

baba yaliyokuwamo kwenye gari.Lakini 

kwa wema wake hakufanya 

hivyo.Maongezi yake yanaonyesha ni 

kijana mwenye upeo .Maongezi yake 

yamejaa busara na hekima.Ana ushauri 

mzuri sana.Ukikaa naye kwa muda mfupi 

utagundua kwamba mavazi na 

muonekano wake ni tofauti kabisa na 

undani wake. he looks so handsome” 

akawaza Pauline na kutabasamu 

 “ Kuna ulazima wa kumsaidia David 

.lakini hata hivyo bado kuna haja ya 

kumfahamu kiundani ni nani ,ametoka 

wapi na ni namna gani tunaweza 

kumsaidia.Kesho asubuhi baada ya kutoka 

hospitali nitamfanyia manunuzi ya nguo 

,viatu na vitu vingine vingine vya 

kumpendezesha” akawaza Pauline 



Saa kumi na mbii za asubuhi iliwakuta 

Pauline na David hospitali.Baba yake 

Pauline mzee Mwakabuka alikuwa 

anaendelea vizuri sana kwa sasa.Pauline 

akafurahi sana 

 “ Nashukuru Mungu kwa maendeleo 

haya mazuri.Sijaweza kulala usiku wa leo 

nikiwaza kuhusu hali yako” Pauline 

akamweleza baba yake 

 “ usihofu kitu mwanangu.Ninaendelea 

vizuri sana.Mama yako ulimtaarifu kama 

ninaumwa? Akauliza baba yake Pauline 

 “ mama nilimtaarifu kwamba unaumwa 

na akasema kwamba angejitahidi ili apate 

ndege ya jioni ya kuja Arusha lakini 

baadae akanipigia simu na kunitaarifu 

kwamba amekosa ndege kwa hiyo atarejea 

leo.Amenipigia simu leo asubuhi na 

kuniuliza maendeleo yako”akajibu 

Pauline 

 “Ahsane sana Pauline kwa 

kunijali.Usihofu chochote kuhusu 

mimi.Ninaendelea vizuri sana na kuna 

uwezekano leo hii nikaruhusiwa kurejea 

nyumbani” akasema mzee Zakaria. 

Pauline akatabasamu  “Nilikuona kama umeongozana na 

mtu.Yuko wapi? Akauliza mzee Zakaria 

.Pauiline akatoka nje ya kile chumba na 

kumkuta David amesimama katika maua 

 “ david mbona uko nje? 

 “Nimewaacha kwanza muongee 

kifamilia.Anaendeleaje baba? 

 “ anaendelea vizuri sana.tafadhali 

twende ndani ukamsalimu” akasema 

Pauline na kumshika mkono David 

wakaingia chumbani. 

 “ Shikamoo mzee” David akamsalimu 

mzee Zakaria 

 “ marahaba kijana” akajibu mzee 

Zakaria huku akimuangalia David kwa 

makini .Hakuwahi kumuona hata mara 

moja. 

 “ baba huyu anaitwa David ndiye 

aliyekuleta jana hapa hospitali.” Akasema 

Pauline.mzee Zakaria akastuka kidogo na 

kuinuka akakaa na kumtazama David 

 “ Kumbe huyu ndiye aliyenileta hapa? 

Nimekuwa nikiumiza kichwa kumjua mtu 

ambaye alinileta hapa na madaktari 

waliniambia kwamba ni dereva wangu 

lakini nikashangaa dereva wangu ni nani 

kwa sababu mimi sina dereva.Kumbe ni wewe kijana wangu.Ahsante sana kijana.” 

Akasema mzee Zakaria “ Nashukuru 

mzee.”akasema David. 

 “ Hebu nikumbushe ilikuaje hadi 

ukanifikisha hapa? Akauliza mzee Zakaria 

 “Nilikuwa nikitembea barabarani na 

mara nikaona gari lako likiyumba na 

kupoteza uelekeo na kisha likagonga mti 

na kusimama.Jambo zuri ni kwamba 

haukuwa katika mwendo mkali.Nilikukuta 

ukiwa katika hali mbaya na 

nikakuendesha hadi hapa.” Akasema 

David.mzee Zakaria akainama na 

kusikitika. 

 David akamnong’oneza Pauline 

kwamba anatoka nje .Mzee Zakaria 

alikuwa na mawazo mengi. 

 “ Baba unawaza nini? Akauliza Pauline 

 “Ninauwaza huu ugonjwa na mahala 

utakaponipeleka.” Akasema mzee Zakaria 

 “Baba hutakiwi kuwaza sana kwa 

sasa.Kitu cha msingi ni kujali afya yako 

kwanza .Kwa hivi sasa itakubidi upunguze 

baadhi ya kazi zako na kuutumia muda 

mwingi kwa ajili ya mapumziko na 

mazoezi.” Akasema Pauline  “Uko sahihi Pauline .natakiwa 

nipumzike sana kwa sasa.Lakini hata 

hivyo sina hakika kama mama yako 

anaweza akasimamia miradi yetu 

yote.Unafahamu kitu alichokifanya mama 

yako na kunisababishia matatizo 

haya.Nitaweza kupumzika tu kama 

utanihakikishia kwamba utakuwa tayari 

sasa kuiendesha miradi yetu.” 

 “ baba tutaongea masuala haya 

ukishatoka humu hospitali.Kwa sasa 

jitahidi usiwaze chochote kuhusiana na 

masuala haya” akasema Pauline.Kikapita 

kimya kifupi halafu mzee zakaria 

akamuita Pauline na kumnong’oneza kwa 

sauti ndogo 

 “ Pauline ndani ya gari kulikuwa na 

mkoba wenye fedha nilizokuwa 

nazipeleka benki. Kulikuwa na kiasi cha 

zaidi ya milioni themanini.Ulizipata fedha 

hizo? Moyo wangu umestuka sana baada 

ya kumuona kijana huyu .Anaonekana 

mjanja mjanja sana” akauliza mzee 

Zakaria 

 “ Baba huwezi kuamini ,fedha zote ziko 

salama.”  “ Ziko salama? Huyu kijana 

hakukwapua fedha? Ilikuaje hata 

ukaziwahi fedha hizo? Akashangaa mzee 

Zakaria 

 “ Baba hutakiwi kumtilia shaka 

David.Alipokufikisha hapa alinipigia simu 

kwa kutumia simu yako na nikafika hapa 

mara moja nikamkuta .Alinikabidhi 

funguo ya gari,simu na mkoba wenye 

fedha.Alitoa kiasi kidogo tu cha fedha 

kilichokuwa kinahitajika hapa hospitali 

na akanikabidhi risiti.” 

 Mzee Zakaria akaonyesha mshangao. 

 “ Unasema kweli Pauline? Huyu kijana 

ameweza kuziwasilisha fedha zote bila 

kukwapua hata kidogo? 

 “ Kweli kabisa baba .Hakuna hata 

shilingi yako moja iliyopotea.” 

 “ Ouh my God..! akasema mzee Zakaria 

 “ Huyu kijana anaishi wapi? Anafanya 

kazi gani? 

 “ Baba huyu kijana ana matatizo kidogo. 

Tutaongea nyumbani ukishatoka hapa 

hospitali lakini kwa sasa naomba tu 

ufahamu kwamba anaishi nyumbani 

kwetu”  “ Anaishi nyumbani kwangu? 

Akashangaa mzee Zakaria 

 “Ndiyo baba.Anashi nyumbani kwa 

sasa.Lakini utakapotoka tukakaa 

tutaongea na utamfahamu huyu kijana 

vizuri na utaamua wewe mwenyewe kama 

aendelee kukaa nyumbani au utaamua 

aondoke zake.Lakini kutokana na kitendo 

cha kiungwana alichokifanya jana 

niliazimia aje kuishi nasi nyumbani 

kwetu” 

 “ kwani ametokea wapi huyu kijana na 

alikuwa anaishi wapi hapa Arusha? Do you 

trust him? 

 “ Dady naomba usimuwaze sana huyu 

kijana .Utakapotoka tutaongea kwa 

undani.Kuhusu kumuamini ndiyo 

nimelazimika kumuamini kwa ajili ya 

kitendo chake cha jana.Angekuwa ni 

kijana mwenye sifa ya udokozi basi 

angeweza hata kuondoka na kila kitu na 

kukutelekeza hapa lakini kijana huyu 

hakufanya hivyo amekaa hapa na 

kuhakikisha kwamba ananikabidhi kila 

kitu chako.” 

 “ Kweli inanishangaza sana katika 

ulimwengu kama huu kijana kama huyu anafanya kitu cha kiungwana kama 

hiki.Kwa kweli huyu kijana anastahili 

pongezi na shukrani za kipekee 

kabisa.Hali yangu inaendelea vizuri na 

nitatoka leo nataka nimfahamu huyu 

kijana vizuri” akasema mzee Zakaria 

 ****************************************

******************* 

 Robin aliwahi sana kazini siku 

hii.Tofauti na siku iliyotangulia ,leo 

alikuwa na uso mchangamfu na wenye 

tabasamu.Aliianza siku yake vizuri. Toka 

ameamka asubuhi ya leo kuna sura moja 

tu ambayo imekuwa ikimjia kichwani 

kwake kila mara na kumfanya 

atabasmu.Ilikuwa ni sura ya mwalimu 

Lucy 

 “Sijui kwa nini toka nilipoonana na 

mwalimu Yule kila mara sura yake 

imekuwa ikinijia kichwani.Napenda nikiri 

kwamba mwalimu Yule ana uzuri wa 

kipekee kabisa.Zaidi ya yote ana vitu 

Fulani vya ziada vinavyomfanya azidi 

kuvutia.Ana heshima na anaonekana ni 

msikivu na kinachonifurahisha ni namna anavyompenda mwanangu 

Penny.Naisubiri kwa hamu sana siku hiyo 

ya Jumamosi tutakapomkaribisha 

nyumbani kwa ajili ya chakula kama 

alivyoomba Penny.Natakiwa kumtafutia 

kijizawadi kidogo ili kuendelea kuujenga 

urafiki mzuri baina yetu.Atanisaidia sana 

kwa upande wa Penny kwani 

anamuangalia kama mtoto wake.Kuna 

mambo ambayo yeye kama mtoto wa kike 

hawezi akaniambia mimi lakini kama 

atakuwa karibu na mwalimu Lucy basi 

anaweza akamweleza na akamsaidia.Tena 

ngoja nimpigie simu nimtaarifu kuhusiana 

na mwaliko wa jumamosi “akawaza Robin 

na kuchukua simu akapiga shuleni kwa 

akina Penny 

 “ hallow naongea na mwalimu mkuu ? 

akauliza Robin 

 “ Ndiyo unaongea na mwalimu mkuu 

hapa.Nani mwenzangu? 

 “ Mimi ni mzazi.wewe ni mwalimu 

Lucy? 

 “ Ndiye mimi “ 

 “ Mimi ni Robin babayake Penny” 

 “ Ouh Robin..habari yako? habari za 

toka jana? Nakusubiri uje hapa uanze darasa la awali” akasema mwalimu Lucy 

na kumtania Robin akimaanisha kwamba 

robin ni mtoto aliyezaliwa jana kwani 

alisherehekea siku yake ya 

kuzaliwa.Robin akacheka sana na kusema 

 “ bado ninanyonya na baada ya kuanza 

kutembea nitakuja kuanza darasa la 

awali” wote akacheka halafu Robin 

akasema 

 “ Mwalimu Lucy samahani kwa 

usumbufu mida hii, kuna ujumbe wowote 

ambao Penny amekuletea? 

 “ Hapana Mr Robin.sijaonana bado na 

Penny kwa sababu bado wako darasani 

.Ninaweza kuonana naye baadae wakati 

wa mapumziko.Ulimpa ujumbe aniletee 

mimi? 

 “ Ndiyo nilimpa ujumbe 

wako.Aliniambia kwamba ungependa ujue 

mahala anakoishi.Nimefurahi sana kwa 

hilo na tunakualika rasmi kwa chakla cha 

mchana nyumbani kwetu siku ya 

jumamosi” akasema Robin.Mwalimu Lucy 

akatabasamu 

 “ Ouh ahsante sana Mr Robin.Penny ni 

rafiki yangu na ninamlea kama mwanangu 

kwa hiyo nilihitaji kufahamu mahala anakoishi na akaniambia kwamba 

ataongea na wewe .Nashukuru kama 

umekubali niwatembelee siku hiyo ya 

jumammosi.” 

 “ Ahsante sana mwalimu 

Lucy.Nakutakia kazi njema,tutaonana siku 

hiyo ya jumamosi.Nitamtuma dereva aje 

akuchukue nyumbani kwako” 

 “ Ahsante sana Mr Robin.kazi njema” 

akasema mwalimu Lucy na kukata 

simu.Alibaki ameishikilia simu ile huku 

akitabasamu 

 “Nimefurahi sana kwenda kujua mahala 

anakoishi Penny.Ninampenda sana Yule 

mtoto na ninamlea kama mwanangu wa 

kumzaa mwenyewe.Namsikitikia 

mwanamke aliyemtelekeza mtoto kama 

huyu.” Akawaza Mwalimu Lucy. 

 “ Hata hivyo namsifu sana Robin baba 

yake Penny kwa malezi mazuri 

aliyompatia binti yake na kumfanya awe 

ni mfano wa kuigwa.Amemlea binti katika 

maadili mazuri sana.” Sura ya robin 

ikamjia kichwani akatabasamu 

 “He’s so handsome,charming and 

funny.Ni mwanaume mzuri sana na sijui 

kwa nini huyo mke wake aliamua kuondoka na kumuacha .Natamani niwe 

naye karibu kama marafiki anaonekna ni 

mtu mwenye busara na mwenye kujali” 

Mara wakaingia walimu wawili mle ofisini 

,akaachana na mawazo ya Robin 

 Robin alikuwa katika tabasamu zito 

baada ya kumaliza kuongea na mwalimu 

Lucy. 

 “Sijui kwa nini mwalimu Yule 

ameniingia katika akili yangu ghafla 

namna hii.Nahisi kuanza kuvutiwa 

naye.Lakini ngoja niachane na mawazo 

haya kwa sababu lazima atakuwa na 

mpenzi wake na mimi sitaku kuingilia 

mahusiano ya mtu yeyote kwani 

nayafahamu maumivu yake.Nitakuwa 

naye karibu kama rafiki na mwalimu wa 

mwanangu.lakini hata hivyo itanibidi 

nimtafutie kijizawadi Fulani kidogo 

ambacho nitampatia atakapokuja siku ya 

jumamosi.Sijui nitamtafutia zawadi gani? 

akawaza Robin halafu akaendelea na kazi 

zake 

******************************  Wakiwa bado hospitali ,simu ya Pauline 

ikaita.Alikuwa ni mama yake mdogo 

akaongea naye halafu akamgeukia David 

 “ Mama mdogo amekwisha tua uwanja 

wa ndege na yuko njiani anakuja 

hospitali” 

 “ Hizo ni habari nzuri “ akajibu David 

 David akaumuangalia Pauline 

aliyekuwa ameinamisha kichwa kwa 

makini na kumuuliza 

 “Pauline mbona umeonekana 

kubadilika ghafla? 

 “ David naomba nikwambie ukweli wa 

moyo wangu ,simpendi mama mdogo 

japokuwa sina ugomvi naye lakini moyo 

wangu haumpendi kabisa kutokana na 

vitendo vyake.kama nilivyokwambia jana 

kwamba yeye ndiye chanzo cha matatizo 

haya ya baba.Tatizo limekuwa kwa baba 

yangu ambaye amekuwa akimsikiliza na 

kumuacha mama mdogo afanye vile 

atakavyo.Hiyo ndiyo sababu iliyonifanya 

mimi niachane kabisa na miradi ya 

kifamilia na kuanza kushughulika na 

biashara zangu mwenyewe.” Akasema 

Pauline  “ Pole sana Pauline.Ninachoweza 

kukushauri kwa sasa ni kwamba jaribu 

kusimama imara na kuhakikisha kwamba 

miradi ya familia inasimamiwa 

ipasavyo.Usikubali kuacha miradi ya 

familia ikafa au kushindwa kujiendesha 

kutokana na kukosekana kwa 

fedha.Simama imara.” Akasema David 

Pauline akainama na kuonekana kuzama 

katika mawazo.Hakutaka kuongelea tena 

suala lile akabadili maongezi na wakaanza 

kuongelea masuala mengine kabisa ya 

mazingira. 

 Nusu saa baadae Victoria Sikongo 

mwanamke ambaye anasifika kwa 

kujipamba kwa vito vya thamani jijini 

Arusha akawasili hospitali ,akasalimiana 

na Pauline na kisha akataka kuelekea 

katika chumba cha mgonjwa lakini 

hakuruhusiwa kuingia ndani kwa wakati 

huo kwa sababu madaktari bado 

waliendelea na vipimo. 

 “ Hali ya mume wangu inaendeleaje? 

Akauliza Vicky wakati akisubiri 

kuruhusiwa kuingia katika chumba cha 

mgonjwa.  “ Anaendelea vizuri tofauti na jana.” 

Akajibu Pauline kwa kifupi halafu 

hawakuongea tena kitu chochote.Baada ya 

muda Pauline akainuka 

 “ Mama mdogo mimi natoka kidogo na 

David,tutarudi baada ya muda mfupi” 

akasema Pauline 

 “ na huyu ni nani? Akauliza Vicky 

 “ anaitwa David.Tunaishi naye 

nyumbani kwa sasa” akasema Pauline na 

kumstua sana Vicky lakini hakutaka 

kusema chochote 

 Pauline na David wakaingia garini na 

kuondoka 

 “ Mama yako ameridhia mimi niishi 

pale nyumbani kwenu? Naona kama 

hakufurahi ulipomwambia kwamba 

ninaishi pale kwenu” 

 “ David mimi ndiye niliyekukarbisha 

nyumbani kwa hiyo usimsikilze mtu 

mwingine yeyote.Apende asipende utaishi 

nyumbani kwetu” akasema Pauline huku 

akikanyaga mafuta.Walielekea katika 

maduka ya nguo alikoenda kumnunulia 

David mavazi. 

 Hatimaye Vick akaruhusiwa kuingia 

katika chumba cha mgonjwa baada ya madaktari kutoka.Akamkumbatia mume 

wake na kumbusu ,akampa pole nyingi 

 “ nashukuru Mungu ninaendelea vizuri 

kwa sasa” akasema mzee zakaria 

 “ Jana nimeshindwa kupata ndege ya 

haraka hivyo nikashindwa kuja kuungana 

nawe mume wangu.siku wa leo sijaweza 

kulala nikikuwaza wewe tu” akasema 

Vicky 

 Baada ya mongezi ya hapa na pale Vicky 

akamuuliza mumewe 

 “Nimemuona Pauline akiwa na kijana 

mmoja amevaa mavazi kuu kuu 

akaniambia kwamba anaishi nasi 

nyumbani kwetu.Ni kweli? katokea wapi 

Yule kijana? Anafanya kazi gani? akauliza 

Vicky 

 “ Hata mimi nimemuona leo hii na 

Pauline akanifahamisha kwamba 

amemchukua na kumpa hifadhi nyumbani 

kwetu” akasema mzee Zakaria 

 “ Hifadhi ?!!..Vicky akashangaa 

 “Kwani hana mahala pa kuishi? 

Akauliza Vicky 

 “ Mke wangu naomba tusiyaongelee 

hapa haya masuala.Tutajua kila kitu 

nikisha toka hospitali.Madaktari wamesema wanasubiri hadi saa saba za 

mchana waangalie hali yangu na kama 

hakutakuwa na mabadiliko basi 

nitaruhusiwa kurejea nyumbani.Jioni ya 

leo tutakaa naye na kumfahamu vizuri.” 

Akasema mzee Mwakabuka 

 “Sihitaji wageni katika nyumba 

yangu.Kijana Yule anaonekana muhuni na 

asiye na mwelekeo.Sintakubali aishi pale 

nyumbani kwangu.Nyumba yangu si 

kambi ya kufuga vibaka.Kijana mwenyewe 

ana macho kama mwizi mwizi hivi.” 

Akawaza Vicky.Tayari alikwisha anza 

kumchukia David 

************************ 

 Ni saa mbili za usiku familia nzima 

imekaa sebuleni.Mzee Zakaria amekwisha 

toka hospitali baada ya madaktari 

kuridhika na maendeleo yake.Pamoja nao 

sebuleni alikuwepo pia David ambaye 

alikuwa kimya sana. 

 “ David .! akaita mzee Zakaria na 

kumtazama David  “ Naam mzee” akaitika David na 

kuelekeza shingo yake alipokuwa amekaa 

mzee Zakaria 

 “Napenda kwa niaba ya familia yangu 

nikushukuru sana kwa msaada wako 

mkubwa.Uliyaokoa maisha yangu.Bila 

wewe sijui hivi saa ningekuwa katika hali 

gani.Nadhani ilikuwa ni kwa maongozi ya 

Mungu nipite njia ile ili nikutane 

nawe.Nasema ahsante sana” akasema 

mzee zakaria 

 “ Nashukuru mzee.Nilifanya jambo 

ambalo linapaswa kufanywa na mtu 

yeyote mwemye ubinadamu” akasema 

David 

 “ Jambo la pili ambalo nataka 

nikushukuru ni kwa uaminifu wako 

mkubwa.Ulinifikisha hospitali 

ukahakikisha nimepata 

matibabu,ukawasiliana na familia yangu 

na alipokuja Pauline ukamkabidhi kila 

kitu ukiwemo mkoba uliokuwa na fedha 

zaidi ya shilingi milioni themanini.Ni 

vigumu sana kuamini lakini ni kweli 

ulifanya jambo hili.Katika dunia ya sasa ni 

vigumu kuwapata watu wenye uaminifu 

kama wako.Nasema ahsante sana na ninakuomba uendelee na uaminifu huo si 

kwangu mimi tu hata kwa watu wengine 

.Ungeweza kuondoka na mkoba ule wenye 

mamilioni ya fedha pamoja na gari lakini 

hukufanya hivyo.Ahsante sana david” 

akasema mzee Zakaria na David hakujibu 

kitu akatabasamu.Vicky ambaye alikuwa 

amekaa pembeni ya mumewe akiwa na 

glasi iliyoja mvinyo akaweka glasi mezani 

na kuuliza 

 “ David nasikia ulikuwa umefungwa 

gerezani? 

 David akawaangalia wote kwa zamu 

halafu akasema 

 “Ni kweli nilikuwa nimefungwa na siku 

niliyokutana na mzee ni siku ambayo 

nilikuwa nimemaliza adhabu yangu na 

nikaachiwa huru” akasema David 

 “Pole sana david lakini tungependa 

kufahamu ulifungwa kwa kosa gani? 

akauliza tena Vicky.Mzee Zakaria na 

Pauline wote wakamuangalia lakini 

hakujali akayaelekeza macho yake kwa 

David 

 “Mama ni historia ndefu sana na 

samahani wkani sitaki kuyaongelea mambo ambayo yamepita.” Akasema 

david 

 “ jaribu kutueleza hata kidogo ili tupate 

walau picha ni kitu gani hasa kilisababisha 

ukapelekwa kule gerezani? Akauliza tena 

Vicky.David alionyesha kutokupendezwa 

na swali ile akainama chini na kuanza 

kufikiri. 

 “ Naomba David asiulizwe jambo lolote 

linalohusiana na matatizo 

yaliyomkuta.Naomba aachwe atulie na 

atatueleza yeye mwenyewe kama 

akipenda kutueleza pale atakapokuwa 

tayari kufanya hivyo”akasema mzee 

Zakaria.Mke wake akamtazma usoni na 

kuonyesha kutokuridhishwa na kauli ile 

ya mume wake 

 “ Honey ,sijamuuliza kwa ubaya , lengo 

langu ni kumfahamu David kiundani 

,ametoka wapi,na nini malengo yake ya 

usoni baada ya kutoka kifungoni” akasema 

Vicky 

 “ Naomba mjadala kuhusu David 

ufungwe rasmi na sitaki kusikia mtu 

yeyote akimuuliza kitu chochote kile 

kuhusiana na maisha yake au wapi 

ametoka.Atatueleza pale atakapokuwa tayari.” Akasema mzee Zakaria halafu 

akamgeukia david 

 “ David utakaa hapa nyumbani kwangu 

kwa muda wote utakaouhitaji wewe 

mwenyewe.Hapa ni nyumbani kwenu na 

usiwe na hofu yoyote.Nitakulea kama 

mmoja wa wanafamilia yangu kutokana na 

msaada wako mkubwa 

ulionisaidia.Endapo una tatizo lolote 

naomba usisite kunieleza mimi au mama 

yako hapa au mweleze Pauline lakini 

ningependa kama una tatzio lolote uje 

unione mimi mwenyewe.Sihitaji kufahamu 

umetoka wapi na ulifanya nini ukafungwa 

gerezani ila ninachofahamu nikwamba 

umenifanyia jambo ambalo sijawahi 

kufanyiwa katika maisha yangu na ambalo 

sioni kitu ninachoweza kukufanyia 

ambacho kinaweza kulingana na jambo 

ulilonifanyia.Jisikie amani hapa 

nyumbani.” Akasema mzee Zakaria.Vick 

akaingilia kati na kusema 

 “ Baba Pauline sioni kama unafanya 

sawa.Huyu ni mtu ambaye umekutana 

naye mtaani na hujui ametoka wapi,ndugu 

zake wako wapi.Itakuwaje iwapo atapatwa na matatizo akiwa nyumbani kwetu? 

Akauliza Vicky 

 “Nimekwisha sema kwamba David 

atakaa hapa nyumbani kama 

mwanafamilia na sitaki maswali juu yake 

yaendelee kuulizwa.Ndugu zake ni sisi 

hapa.Ndugu yake ni mimi hapa 

aliyenisaidia na kuniokoa.” Akasema mzee 

Zakaria akionyesha kukerwa na tabia ile 

ya mke wake.David aliyekuwa 

akiyashuhudia mabishano yale kati yam 

zee zakaria na mke wake akasimama na 

kusema 

 “ Samahani mzee wangu.Nashukuru 

sana kwa msaada wako mkubwa na 

kunisaidia niweze kuishi hapa nyumbani 

kwako. Ni kweli nilipotoka gerezani 

sikuwa na sehemu ya kula wala kulala na 

sikujua ningeelekea wapi.Sikuwa na 

mwelekeo wowote wa maisha lakini 

mlinipokea katika familia yenu.Mmenilea 

kama mwanafamilia yenu.Pamoja na hayo 

mzee wangu ningeomba nisiwe chanzo cha 

mvurugano katika familia 

yako.Ningeomba uniruhusu niondoke 

nikaendelee na maisha yangu mahala 

pengine.. “ akasema David  “ David nimekwisha sema kwamba 

wewe ni mmoja wa wanafamilia hii na 

utaishi hapa na kauli yangu ni ya 

mwisho.Hutakwenda sehemu yoyote 

ile.Utakaa hapa hapa” akasema mzee 

Zakaria kwa ukali kidogo halafu akainuka 

na kuelekea chumbani kwake na kisha 

mke wake naye akainuka na kumfuata 

 “ Pauline inaonekana mama yako 

hajapendezwa kabisa na mimi kuwepo 

hapa numbani.Sipendi niwe chanzo cha 

matatiz…………….” David hakumaliza 

sentensi yake Pauline akamkatisha 

 “ Shhhhhhhhhhhhhh..!! usiseme 

chochte David.Baba amekwisha sema na 

utaendelea kukaa hapa hapa kwetu.” 

Akasema Pauline na kimya kifupi kikapita 

halafu akasema 

 “ David kesho kuna mzigo nitaupokea 

dukani kwangu.Ningeomba uambatane 

nami ukanisaidie kuupakua” akasema 

Pauline 

 “ Pauline unafanya biashara gani? 

akauliza David 

 “ Nina fanya biashara ya nguo.Nina 

duka la nguo “ akasema Pauline kisha 

wakaendelea kuangalia filamu 



 Saa tatu za asubuhi siku iliyofuata 

David na Pauline wakaingia garini na 

kuelekea katika ofisi za kampuni moja ya 

usafirishaji ambayo walimsafirishia 

mizigo yake.Baada ya kulipa pesa 

aliyokuwa anatakiwa kuilipa,mizigo yake 

ikapakiwa katka gari la mizigo na 

kupelekwa dukani kwake ikashushwa na 

kuhifadhiwa katika chumba cha 

kuhifadhia mizigo.Baada ya kumaliza kazi 

ile ya kuhifadhi mizigo ile,Pauline 

akaendelea kuangalia hesabu za duka 

lake na baadae wakaelekea katika hoteli 

moja nzuri kwa ajili ya kupata chakula cha 

mchana. 

 “ Hongera Pauline,duka lako zuri 

sana.Lina nguo nzuri “ akasema David 

.Pauline akatabasamu na kusema 

 “ Ahsante sana David umenisaida mno 

siku ya leo.” 

 Wakaendelea kula kimya kimya halafu 

Pauline akauliza 

 “ David umewahi kufanya biashara? 

 David akatabasamu kidogo na kusema  “Nina shahada ya biashara na nina 

uzoefu katika masuala ya biashara” 

akasema david na kumfanya Pauline 

amshangae 

 “ kweli? Akauliza Pauilne 

 “ Kweli Pauline.Nina shahada ya 

biashara toka katika chuo kikuu cha dare s 

salaam na nina uzoefu katika biashara na 

masoko.” akasema David 

 “Wow ! basi ni maongozi ya Mungu 

amekuleta kwetu.Nadhani baba atafurahi 

sana akisikia kwamba una elimu ya 

biashara.Kwa muda mrefu amekuwa 

akitafuta mtu atakayemuamini wa 

kumsaidia katika biashara zake.” 

 “ baba yako anajishughulisha na 

biashara gani? 

 “ ana miradi mingi tu.Ana maduka 

,miradi ya mbao,vituo vya mafuta n.k 

 “ Ouh kumbe baba yako ni tajiri sana” 

akasema David 

 “ Siwezi kukataa kwamba baba yangu 

ana utajiri mkubwa lakini kwa siku za hivi 

karibuni ameingia katika mgogoro 

mkubwa wa kifedha baada ya kumuoa 

mama mdogo.Biashara zake zimekuwa 

zikiyumba sana na kuna biashara zake imemlazimu kuzifunga kutokana na 

kuendeshwa kihasara.” 

 “ Nini hasa tatizo la mama yako mdogo? 

 “ mama mdogo ana matatizo 

makubwa.Kwanza si muaminifu na ni 

mfujaji sana wa fedha na nina wasi wasi 

anaficha fedha kwa siri.Niliwahi 

kumueleza baba kuhusu jambo hili lakini 

likazua matatizo makubwa na nikaamua 

kuachana na biashara za familia 

nikaanzisha biashara yangu.Toka wakati 

huo baba amekosa mtu wa karibu wa 

kumuamini.Lakini kwa siku za karibuni 

ameanza kukubaliana na maneno yangu 

kuhusiana na mama mdogo.” Akasema 

Pauline 

 “Pauline nasikitika sana kwamba 

sintakubali kufanya kazi kwa baba yako 

na kukutana na mtu mwenye tabia kama 

za mama yako mdogo.Sitaki kuingia katika 

mgogoro mwingine hasa kwa wakati huu 

ambao nahitaji kuyajenga upya maisha 

yangu” akasema David 

 “David tafadhali naomba 

usikatae.Nitaongea na baba ili uweze 

kumsaidia na utakapomsaidia baba utakuwa umenisaidia na mimi vile vile.I’m 

your friend ..right? akasema Pauline 

 “ Ndiyo Pauline mimi nawe ni marafiki 

lakini najaribu kuyakwepa matatizo hasa 

kwa wakati huu ambao ninaanza 

kuyajenga upya maisha yangu.” 

 “ David tafadhali naomba 

usikatae.Kama huwezi kufanya kazi kwa 

baba do it for me.Nisaidie mimi.Familia 

yangu inakuhitaji sana na Mungu 

amekuelekeza kwetu ili uweze 

kutusaidia.Tafadhali naomba usiseme 

hapana.Baba kwa sasa anaumwa na 

anahitaji mtu wa kuweza kumsaidia 

katika kazi zake hasa kwa wakati huu 

ambao hana imani tena na mama mdogo 

kutokana na vitendo vya ufujaji wa fedha 

alivyovionyesha.Alinitaka mimi nirudi 

kuisimamia miradi ya familia ili kumpa 

yeye nafasi ya kupumzika lakini wakati 

nikitafakari nitawezaje kufanya hivyo 

umetokea wewe .David naomba usikatae 

kutusaidia” akasema Pauline.David 

akainama akaonekana kuzama katika 

mawazo mengi. 

 “ Nataka kujiingiza tena katika matatizo 

ambayo ninajaribu kuyakimbia lakini nahisi kushindwa kukataa kuwasaidia 

akina Pauline katika kuisimamia miradi 

yao.Ni watu wazuri wenye roho nzuri na 

moyo wa ukarimu.Wamenikaribisha 

nyumbani kwao na wananitunza kama 

mmoja wa wanafamilia.Mzee zakaria 

ameonyesha kuniamini lakini tatizo liko 

kwa mke wake.Anaonekana 

kutokufurahishwa na uwepo wangu pale 

katika familia yao na ndiyo maana jana 

usiku alikuwa akijaribu kutaka 

kuyachimba maisha yangu.Endapo mzee 

Zakaria ataridhika nami na kuniomba 

nimsaidie katika majukumu itanilazimu 

kukubali na pengine hii inaweza kuwa ni 

fursa yangu ya kuyatengeneza upya 

maisha yangu yaliyopoteza mwelekeo.” 

Akawaza David halafu akamtazama 

Pauline wote wakatabasamu 

 “ Toka nilipokutana naye niliamini 

kuna kitu ambacho kimejificha kwa 

david.Kumbe bi kijana msomi na ana 

shahada ya biashara !!..Kuna mambo 

mengi ambayo yamejificha nyuma yake 

ambayo hataki kuyaweka wazi.Kwa nini 

hataki kuiweka wazi historia yake? 

Ametoka wapi na famili yake iko wapi? Kwa nini alifungwa gerezani? Amekuwa 

akiyakwepa kabisa maswali haya.Kuna 

haja ya kumfahamu huyu kijana.Niliwahi 

kusoma katika simulizi mbali mbali 

kwamba kuna watu ambao hujiweka 

katika hali kama hii ya David kumbe ni 

wapelelezi .Nina wasi wasi sana na huyu 

kijana.Kuna nyakati ninaanza kuingiwa na 

wasi wasi naye lakini hata hivyo kuna 

ulazima wa kumfahamu undani wake na ili 

kumfahamu vizuri inabidi kujiwa naye 

karibu sana.” Akawaza Pauline 

 Wakati david na Pauline wakipata 

chakula cha mchana,Robin na mfanyakazi 

wake wa ndani walikuwa katika pilika 

pilika za kufanya manunuzi kwa ajili ya 

maandalizi ya ujio wa mwalimu Lucy 

nyumbani kwao siku itakayofuata yaani 

jumamosi.Walifanya manunuzi ya vitu 

vingi ambavyo waliona vingefaa kwa ajili 

ya siku muhimu kama ile.Baada ya 

kuridhika na manunuzi waliyoyafanya 

wakarejea nyumbani ambako maandalizi 

kabambe yalianza ikiwa ni katika kuiweka 

nyumba katika hali ya usafi na unadhifu 

wa kipekee kabisa.  *************************************** 

 Vicky alimuaga mumewe mzee Zakaria 

kwamba kuna mahala anakwenda na 

asingechelewa kurudi.Aliingia katika gari 

lake la kifahari na kuondoka na breki ya 

kwanza ilikuwa nyumbani kwa rafiki yake 

kipenzi Safia. 

 “Vicky umerudi lini ? si uliniambia 

umekwenda Morogoro na Yule kijana 

Danny? Imekuaje umerudi mapema 

namna hii? Akauliza Safia baada ya Vicky 

kuingia sebuleni kwake.Vicky akautupa 

mkoba wake sofani na kuketi halafu 

akavuta pumzi ndefu 

 “ Ouh Safia mimi sijui nina mkosi gani 

jamani..!! akalalama Vicky ambaye 

masikio,shingona vidole vyake 

vilipambwa kwa vito vya thamani kubwa 

 “Kwa nini unasema hivyo Vicky? 

Akauliza safia huku akimuita mfanyakazi 

wake wa ndani na kumuomba awaletee 

vinywaji 

 “Nilikuwa na Danny katika hifadhi ya 

Udzungwa tukila raha za dunia mara kila 

kitu kikatibuka” akasema Vicky “Ilikuaje Vicky? Nini kilitokea? Akauliza 

Safia 

 “Nilipigiwa simu na Pauline akaniambia 

kwamba Yule mzee amepatwa na 

shinikizo la damu na amelazwa 

hospitali.Ikanilazimu niahirishe kila kitu 

na kurudi mara moja.Nimerudi jana 

mchana .Nimechukia sana Safia kwa 

kukatishwa katika starehe zangu.Nilikuwa 

nikipata raha za dunia na Danny na 

sikupanga kama ningerejea mapema 

namna hii.Nimemchukia sana Yule 

mzee.Hanikuni nitakavyo lakini 

ninapompata mtu anayenikuna kisawasa 

kinaibuka kikwazo.Naona ingekuwa 

vyema kama angekufa tu ili niendelee na 

maisha yangu ya starehe.Nimechoshwa na 

maisha haya ya kufungwa ndani kama 

njiwa” akasema Vicky 

 “ Dah ! pole sana shoga.Kwa hiyo 

anaendeleaje mzee? Akauliza Safasi 

 “ Linaendelea vizuri tu..” akajibu Vicky 

huku akibetua midomo yake 

 “Pole sana shoga yangu.Usisikitike sana 

.Jaribu kupanga tena miadi na Danny ili 

mkutane tena na muendelee na mambo 

yenu.Nafahamu ugumu unaoupata kwayule mzee .Jitahidi usije ukazeeka shiga 

yangu.wewe bado mtoto mbichi kabisa” 

 “ Safia sijui kama nitaweza kumpata 

tena Danny hivi karibuni.tayari amerudi 

kazini kwake Botswana.Alikuja kwa 

dharura ya wiki mbili na kumuona tena 

itachukua muda mrefu.Sijui nitafanyaje 

mimi…!! Akalalama Vicky halafu kimya 

kikapita 

 “Ninavyokwambia mimi nina bahati 

mbaya ,nimerudi kwagu na kumkuta 

Pauline amemuokota muhuni mmoja na 

kumleta aishi pale nyumbani kwangu.” 

 “ Muhuni ..!!!? Safia akashangaa 

 “ Mzee Zakaria anaweza kweli kukubali 

kuishi na muhuni kwa ninavyomfahamu 

mzee Yule alivyo na sheria kali? 

 “ hata mimi sielewi imetokeaje.Yaani 

Yule mzee humuelezi kitu kuhusu huyo 

kijana. Kijana mwenywe ametoka gerezani 

na hajulikani hata kwao ni wapi ,ukitaka 

kumuuliza ametokea wapi hajibu na mzee 

Zakaria anakuwa mkali kama nini.Shoga 

yangu nimekereka sana kwa sababu kwa 

namna mzee anavyomuamini Yule kijana 

kama hirizi yake ,nina wasi wasi akizoea sana baadhi ya mambo yangu yanaweza 

yasiende sawa.” 

 “ Dah ! hili sasa ni janga “ akasema Safia 

 “ janga si kidogo shoga ! yaani akili 

yangu haifanyi kazi vizuri.Nataka nimalize 

nyumba yangu haraka haraka ili 

ikiwezekana niachane na Yule marehemu 

mtarajiwa.Unajua hata kama akifariki hivi 

sasa sintakuwa na changu pale kwa 

sababu sijazaa mtoto na Yule mzee na 

siwezi kuzaa naye mtoto hata iwe vipi” 

akasema Vicky 

 “Kwa hiyo umepanga nini shoga? 

Akauliza safia 

 “ Kuhusu nini safia? Akauliza Vicky 

 “Kuhusu huyo kijana. Utamuacha 

aendelee kukaa hapo nyumbani kwako? 

 “ Thubutu !!..labda siyo mimi Vicky 

madhahabu..” akasema Vicky na kisha 

wote kwa pamoja wakacheka kicheko 

kikubwa na kugonganisha mikono. 

 “ namvutia kasi kwanza ili nimsome 

vizuri nyendo zake kwa sababu kwanza 

anaonekana ni mzubavu na asiyefahamu 

chochote.Ukimuona ni kama aliwahi 

kuchukuliwa msukule” akasema Vickyhalafu wote wakacheka tena kicheko 

kikubwa sana 

 “ Lakini Vicky mimi nina wazo moja 

kuhusu huyo kijana” 

 “ wazo gani Safia? 

 “Huyo kijana usimfukuze.anaweza 

akawa ni mtaji mkubwa sana kwako.” 

 “ Kivipi? Akauliza Vicky 

 “Kama mzee zakaria anamuamini basi 

unachotakiwa kukifanya ni kumuweka 

karibu yako ili hata kama kuna jambo 

unalifanya basi lisimfikie mzee Zakaria au 

Pauline.Wakati mwingine wewe ni 

binadamu na una mahitaji na hali ya mzee 

ndiyo kama hivyo tena,unaweza 

ukamtumia huyo kijana akakuliwaza” 

akasema Safia halafu Vicky akacheka sana. 

 “ Ama kweli Safia umenichoka shoga 

yangu.Yaani mimi Vicky madhahabu nilale 

na Yule kinyago.!!? Hata kama nina hamu 

ya namna gani na mwanaume lakini siwezi 

kuthubutu kumvulia nguo Yule 

kijana.Nakwambia ukimuona utashangaa 

utafikiri ni msukule uliotoroka.Hana 

mbele wa nyuma.Lakini kuhusu hilo la 

kwanza ulilolisema kwamba naweza kuwa 

naye karibu nitalifikiria lakini sina hakika kama anaweza akakubali kushirikiana 

nami.” akasema Vicky 

 “ Vicky hakuna kitu kinachoshindikana 

hapa duniani.Pesa ndiyo inayowezesha 

kila kitu.Ukiwa na pesa utaweza kufanya 

lolote unalotaka.Hata huyo kijana endapo 

ataonja pesa atakuwa tayari kushirikiana 

nawe.Inawezekana huko alikotoka 

alikuwa kibaka kwa hiyo endapo ataonja 

maisha mazuri na ukampatia fungu la 

kutosha basi atakufanyia kila 

unachokitaka.Kuhusu kumtumia huyo 

kijana kingono sikuwa na maana mbaya 

na wala sikutaka kukushusha thamani 

shoga yangu lakini nilikuwa nakupa tu 

wazo kwamba endapo unaweza ukazidiwa 

na ukahitaji mtu wa kukupa raha basi 

unaweza mara moja moja ukamtumia 

huyo kijana tena ukiwa hapo hapo kwako 

bila hata ya kwenda mbali .Kuhusu 

muonekano wake isikupe 

shaka.Muonekano ni kitu ambacho 

kinaweza kubadilishwa wakati 

wowote.Huyo huyo unayemuona leo kama 

msukule akipata fedha na kujibadilisha 

ataitwa mheshimiwa.” Akasema Safia na 

Vicky akatabasamu na kusema  “ Ok Safia tuachane na hayo ya 

nyumbani kwangu, vipi kuhusu mafundi 

waliendelea na kuweka milango ? 

akauliza Vicky 

 “ Ndiyo na hata hivi sasa wako jengoni 

wanaendelea na kazi.” 

 “ Nashukuru sana shoga yangu kwa 

kunisaidia kusimamia nyumba 

yangu.Nataka iende haraka kwa sababu 

nina mipango mikubwa sana ndani ya 

muda mfupi ujao.” Akasema Vicky huku 

akilifungua pochi lake 

 “Mipango gani Vicky? Mbona 

hunishirikishi mimi shoga yako? Akauliza 

Safia 

 “ Usihofu safia.Wewe ni mtu wa kwanza 

ambaye nitakufahamisha lakini si sasa 

hivi hadi hapo kila kitu kitakapokuwa 

tayari.Kimya kingi kina mshindo 

mkuu.Nimekuwa kimya kwa muda mrefu 

sasa subiria kusikia mshindo wake.” 

Akasema Vicky huku akitabasamu na 

kutoa kitita cha dola za marekani na 

kuanza kuhesabu kiasi Fulani halafu 

akampatia Safia 

 “ kamata hizo shoga zitakusaidia kwa 

mambo madogo madogo” akasema Vicky  “Dah ! shoga ama kweli wewe si 

mwenzetu tena. Siku hizi hutumii tena 

haya madafu yetu.Ni mwendo wa madola 

tu” akasema Safia huku akitabasamu 

 “Toka nimezaliwa nilikuwa natumia 

shilingi.Kwa hivi sasa nataka nibadili 

maisha yangu na kuanza kutumia dola tu.” 

Akasema Vicky huku akiinuka sofani 

 “ Safia,mimi si mkaaji nimepita tu 

kukujulia hali na kukufahamisha kwamba 

nimesharudi.Nataka nielekee mjengoni 

nikaangale mafundi wanavyoendelea 

kisha nirejee nyumbani kwani lile zee 

lisiponiona linaweweseka kama linakata 

roho.Nitawasiliana nawe baadae shoga 

yangu” akasema Vicky huku akipiga hatua 

kuelekea katika gari lake akaondoka 

 “Safia amenipa wazo japo la kijinga 

lakini linaweza likawa na msaada 

kwangu.Natakiwa kumsoma Yule kijana 

na kumuweka upande wangu.Endapo 

nikimtia mkononi anaweza akanisaidia 

sana katika mipango yangu 

mbalimbali.Nina hakika atakapoonja 

fedha hatakuwa na kauli kwangu na 

nitampeleka nitakavyo.Hili ni wazo zuri 

sana.Lakini hili la kumtumia kingono Yule kijana mhhhh ! inataka moyo sana.Lakini 

safia yuko sahihi Yule kijana anaweza 

akanisaidia kuikata kiu yangu pale 

ninapokuwa na hamu.Nina kila kitu kwa 

sasa,maisha mazuri,nina fedha za kutosha 

na nilichokosa ni kuridhishwa tu kimwili 

na Yule mzee kwa sasa kutokana na hali 

yake hawezi akanikuna nitakavyo.Mimi ni 

mwanamke wa shoka nahitaji dozi ya 

maana ili niridhike kitu ambacho Yule 

mzee hakiwezi sasa hivi.Danny 

ananifikisha nitakapo lakini naye yuko 

mbali ,laiti kama angekuwa karibu 

ningekuwa nakwenda kwake kila siku 

kupata huduma .Natakiwa kutafuta namna 

ambayo nitakuwa nikijiridhisha.Ninaweza 

kumtumia yule kijana lakini mhh ! “ 

akawaza Vicky wakati akielekea mji 

mdogo wa Usa river anakojenga jumba 

lake la ghorofa mbili 

 “ Kijana mwenyewe mchafu mchafu 

namna ile ana thamani kweli ya kuweza 

kuuona utupu wangu? Lakini kama 

alivyosema Safia ninaweza nikambadili 

muonekano na akawa ni kijana nadhifu 

kabisa.Ngoja nianze kulifanyia kazi jambo 

hili.Sitaki mipango yanguivurugike.Nitafanya kila niwezalo ili kila 

kitu nilichokipanga kiende kinavyotakiwa 

“ akawaza Vicky 

 Baada ya kumaliza kula,Pauline na 

David wakaingia garini na kuelekea Rafiki 

classic moja ya duka kubwa na maarufu 

kwa kuuza nguo za kisasa za kiume jijini 

Arusha.Pauline hakutaka David achague 

chochote na akataka yeye ndiye 

amchagulie nguo zile ambazo angeona 

zinamfaa.Pauline alichagua nguo nyingi na 

za gei ghali.Kila nguo aliyoichagua ilimkaa 

vyema David. 

 “ Una umbo zuri sana david.Kila nguo 

inakukubali “ akasema Pauline na 

kumfanya David atabasamu.Baada ya 

kununua mavazi na vitu vingine wakatoka 

na kuelekea katika saluni kubwa ya kiume 

jijini Arusha ambako David alitengenezwa 

nywele,kucha na kuukarabati uso 

wake.Wakati haya yote yakifanyika 

Pauline alikuwa katika saluni ya kike 

iliyokuwa pembeni akiosha nywele 

zake.Baada ya kumaliza kuosha nywele 

akarejea kumtazama David na mara 

akapigwa na mshangao mkubwa.Akabaki 

anamtazama huku akitabasamu  “ Wow ! Its incredible…I knew you are 

handsome” akasema Pauline .David 

aliendelea kutabasamu.Alikuwa 

amependeza sana.Sasa alionekana kijana 

wa kisasa na nadhifu mno. 

 “ David sikufichi unafanana na wale 

waimbaji muziki mashuhuri wa huko 

Marekani.” Akasema Pauline na wote 

wakcheka. 

 “Pauline ahsante sana “ akasema David 

wakati wakielekea katika gari 

 “ Ouh David hupaswi kunishukuru 

,hakuna jambo lolote nililokufanyia 

ambalo unapaswa kunishukuru kwalo” 

akasema Pauline 

 “ Pauline ,ninaonekana mtu tena kwa 

sababu yako.Dakika chache zilizopita kila 

aliyeniona aliweza kudhani labda mimi ni 

mmoja wa wale vijana wanaotumia 

mihadarati kwa namna nilivyokuwa 

nimechakaa lakini umeweza kunitoa kule 

na kunirudisha tena katika dunia ya 

unadhifu.kwa sasa ninaonekana ni kijana 

mtanashati ,kijana wa kisasa.Ahsante sana 

Pauline” akasema David.pauline 

akatabasamu.  “ Unakumbuka nilikuambia kwamba 

muonekano wa mtu unaweza 

ukabadilishwa ndani ya dakika kadhaa 

tu.Angalia sasa umekuwa ni mtu mpya 

kabisa.Aliyekuona jana au juzi akikuona 

na leo hii lazima akupotee.Siku zote mtu 

hapimwi kwa sura yake bali kwa moyo na 

matendo yake.Kwa muonekano uliokuwa 

nao wakati umetoka gerezani ,ilikuwa 

vigumu sana kukubalika katika 

jamii.Lakini kilichokufanya ukaaminika 

hata na familia yetu pamoja na 

muonekano ule ni muonekano wako wa 

ndani.” Akasema Pauline 

 “ Ahsante sana Pauline.Umenifundisha 

kitu kikubwa mno katika maisha haya” 

Akasema David na kisha safari ya 

kuelekea nyumbani ikaanza 

 “ Kwa kweli maisha yana maajabu 

sana.Kilichotokea ninaona ni kama 

ndoto.Jana nilikuwa mtu ambaye 

sitazamiki lakini leo hii nimebadilika na 

sasa kila mtu anaweza akanitazama.Sijui 

nimemfanyia kitu gani Mungu kiasi cha 

kunipendelea namna hii.Namshukuru kwa 

kunikutanisha na familia hii iliyojaa 

upendo wa hali ya juu sana.wamenipokea na kulea kama mmoja wa wanafamilia 

yao.Sijui ni jambo gani ninaweza 

kuwafanyia kuwalipa wema huu mkubwa 

walionifanyia.Kama nisingejikuta 

mikononi mwa watu hawa sijui maisha 

yangu yangekuaje hivi sasa.Nadhani 

ningekuwa na maisha mabaya sana kwani 

sikuwa na msingi wowote wa kuniwezesha 

kuanza maisha yangu mapya.Kitu pekee 

ambacho ninaweza kukifanya kama 

shukrani yangu ya pekee kwa familia hii ni 

kuzidi kuwa muaminifu kwao.” Akawaza 

David wakati wakiendelea na safari ya 

kurejea nyumbani 

 “Toka nilipomuona kwa mara ya 

kwanza nilijua tu David ni kijana mwenye 

kuvutia sana. Nilikuwa sahihi.Muonekano 

wake wa sasa lazima utamstua kila mtu 

aliyemuona siku ya juzi au 

jana.Amebadilika mno na kunistua hata 

mimi mwenyewe ambaye niko naye 

karibu muda wote. Kwa sasa anaonekana 

ni kijana mtanashati.Ninahofu hivi 

vijisichana vya mjini vikimuona kijana 

mtanashati kama huyu basi lazima vianze 

kujipitisha kwake.Nitapambana na 

mwanamke yeyote ambaye atajipitisha kwake.Nitamuonya pia David kuhusu 

suala hilo kwa sasa.Ninawafahamu 

mabinti wa mjini huwa hawakawii 

kujitongozesha na hasa wakigundua 

kwamba kijana mwenyewe ni mgeni basi 

watamsumbua sana.David anatakiwa 

aanze kuyajenga maisha yake na 

sintakubali kuona kinyamkera yeyote 

anajipitisha pitisha” akawaza Pauline. 

 “ Endapo baba atakubali David afanye 

kazi kama msimamizi wa biashara zake 

nina hakika atazidi kupendeza na 

itanilazimu kumuonya kuhusiana na 

masuala ya starehe pia.Jiji hili la Arusha 

limejaa starehe za kila aina.Inanibidi niwe 

karibu naye sana ili kuweza kumchunga 

asipotee njia.najua yatasemwa mengi sana 

kwa mimi kuonekana karibu na David 

lakini watu wameumbwa kusema na 

waache tu waseme.Mimi nitazidi kuwa 

naye karibu na nitampa kila aina ya 

msaada anaouhitaji ili aweze kuyajenga 

maisha yake.Ni nadra sana katika dunia ya 

sasa kumpata kijana kama 

huyu,.Ninajivunia kumfahamu na nina 

hakika urafiki wetu utakwenda mbali na 

utadumu milele.” Akawaza Pauline na safari ikaendelea kimya kimya kila mmoja 

alikuwa na mawazo yake 

 Walifika nyumbani wakashuka garini 

na kueleka ghorofa ya juu alikokuwapo 

mzee Zakaria akipumzika.Alikuwa 

amekaa kibarazani akipunga upepo huku 

akisoma kitabu chake 

 “Halo dady..hauchoki kusoma tu? Ujana 

wako wote umesoma vitabu na hata 

uzeeni unaendelea kusoma? Akatania 

Pauline.Mzee Zakaria akakifunga kitabu 

chake akavua miwani ya kusomea na 

kugeuka kumtazma mwanae na mara 

akastuka na kumtazama David 

 “ Baba mbona unamtazama David 

namna hiyo? Akauliza Pauline 

 “Wow ! you are amazing ! you are like a 

hollywood superstar..” akasema mzee 

Zakaria akitabasamu baada ya kumuona 

David namna alivyokuwa amebadilika. 

 “ Unaendeleaje mzee? Akauliza David 

 “ Ninaendelea vizuri vijana wangu” 

akasema mzee Zakaria. 

 “ nashukuru mzee kama unaendelea 

vizuri.” Akasema David halafu akaaga 

kwamba anakwenda chumbani kwake.  “Wow.! Nimeshangaa sana.Kumbe 

David ni kijana mwenye muonekano 

mzuri namna hii.Its amazing” akasema 

mzee Zakaria baada ya Davidi kuondoka . 

 “Nilimpeleka kwenda kumtafutia 

mavazi na kisha nikampeleka saluni 

akatengenezwa na kuwa katika 

muonekano ule.He’s handsome right? 

Akasema Paulie.baba yake akatabasamu 

na kusema 

 “Yah ! David ni kijana mzuri ambaye 

kila mwanamke anawaza kuwa naye.” 

Akasema mzee Zakaria kauli ile Pauline 

hakuonyesha kuipenda 

 “ Baba , sina hakika kama David ni mtu 

wa namna hiyo.Anaonekana ni kijana 

mwenye kujiheshimu na mwenye malengo 

na maisha yake.Sina hakika sana lakini 

kwa namna ninavyomuona nina hakika 

hataweza kujitumbukiza katika mambo 

kama hayo ya wanawake” akasema 

Pauline baba yake akatabasamu 

 “ Ninafurahi kuona unavyomuamini 

David namna hiyo” akasema mzee Zakaria 

 “ Sijui imenitokeaje lakini nimejikuta 

nikimuamini sana David.Nadhani ni 

kutokana na tabia yake nzuri ndiyo maana sina wasi wasi naye hata kidogo” akasema 

Pauline mzee Zakaria 

akatabasamu.Pauline akameza mate na 

kusema 

 “baba kuna kitu kingine ambacho leo 

nimekigundua kuhusu David” 

 “ Kitu gani tena Pauline? 

 “nadhani kuna vitu vingi ambavyo 

hatuvifahamu bado kuhusiana na David 

kwa sababu ni kijana ambaye hapendi 

kuyaweka wazi maisha yake lakini leo 

amenitamkia kwamba ana shahada ya 

biashara na masoko toka chuo kikuu cha 

Dare s salaam.” Akasema Pauline 

 “ Are you sure? Akauliza mzee Zakaria 

kwa mshangao kidogo 

 “ yes dady.Japo sijakaa naye kwa muda 

mrefu na simfahamu vizuri lakini kwa 

muda huu mchache niliomfahamu David 

nimegundua kwamba si mtu wa 

kudanganya.Hapendi kusema uongo na 

ndiyo maana ninamuamini na ninaimani 

anasema ukweli kuhusu taaluma yake” 

 “ Ninakumini sana Pauline na kama ni 

kweli hayo unayoyasema basi Mungu 

atakuwa amemuongoza kijana huyu aje 

kwetu kwa sababu nilikuwa nahitaji sana kijana msomi na mwaminifu wa kuweza 

kunisaidia katika kusimamia biashara 

zetu.Kwa muda mrefu sasa tumekuwa 

tukiingizwa hasara na watu waliokuwa 

wakizisimamia biashara zetu. Wengi 

wametuibia na wametuacha katika 

madeni makubwa.David atakuwa ni 

msaada mkubwa sana kwetu.Ouh thank 

you God” akasema mzee Zakaria. 

 “Hata mimi baada ya kusikia hivyo 

nilishukuru sana na nikasema kwamba 

nitakueleza ili kama utakubali basi David 

awe ni msaidizi wako na hasa kwa wakati 

huu ambao unahitaji kupumzika.Mimi 

nitakuwa naye karibu ili kumuongoza na 

kwa pamoja tunaweza tukafanya mambo 

makubwa sana.Ninamuona ni kijana 

mwenye upeo mkubwa na mwenye akili 

nyingi”akasema Pauline 

 “ Pauline mimi sina neno hata kidogo 

kwani hata hivyo nilikua nikifikiria jambo 

kama hilo la kumfundisha biashara ili 

aweze kunisaidia katika miradi yangu 

mbali mbali lakini kama ulivyosema 

kwamba ana shahada ya biashara basi huu 

ni msaada mkubwa sana kwetu.Tutaanza 

kwanza kumuangalia kabla ya kumkabidhi rasmi azisimamie biashara 

zote.Kesho tutakwenda naye na atafanya 

kazi katika ofisi yangu na baada ya 

kuhakikisha kwamba tayari ameonyesha 

utendaji kazi mzuri basi i tutamkabidhi 

rasmi ofisi na atafanya kazi pembeni ya 

meza yangu” akasema mzee Zakaria 

 “ baba nashukuru sana kwa kukubali 

kumsaidia David.I’m so happy dady” 

akasema Pauline kwa furaha. 

 “ Pauline ningekuwa mtu wa ajabu sana 

kama ningeshindwa kumsaidia kijana 

kama yule ambaye ameniokoa na 

amenionyesha uaminifu mkubwa 

sana.Pamoja na hayo naomba 

unihakikishie jambo moja Pauline” 

 “ Jambo gani baba? 

 “Promise me that you want fall for 

him.He’s like your brother” akasema mzee 

David , Pauline akatabasamu na kabla 

hajajibu ikasikika sauti ya Vicky aliyeingia 

pale kwa ghafla. 

 “ Fall for whom? Akauliza Vicky na 

kuwasua Pauline na baba yake. 

 “ Ouh Darling you are back” akasema 

mzee Zakaria.Vicky akamsogelea na 

kumbusu.  “ Nimerudi 

darling.Umeshindaje?Unaendeleaje?akauli

za Vicky 

 “ Ninaendelea vizuri sana mke wangu.I 

missed you” 

 “I missed you too darling” akasema 

Vicky halafu akavuta kiti na kuketi karibu 

na mume wake. 

 “Darling wakati naingia nimesikia 

ukimueleza Pauline kwamba asithubutu 

kuanguka mapenzini ,is she in love? 

Akauliza Vicky 

 “ Hapana mke wangu nilikuwa 

namtahadharisha kwamba asithubutu 

kufikiria masuala ya kimapenzi kati yake 

na David.Unajua vijana wa kileo wakiwa 

karibu sana basi huwa hawakawii kujikuta 

wakiwa mapenzini.David na Pauline 

wametokea kuelewana sana na ndiyo 

maana nikawa namtahadharisha Pauline 

kwamba David ni kama kaka yake kwa 

hiyo wajitahidi kuishi kama kaka na dada 

na wasivukwe mipaka” akasema mzee 

Zakaria 

 “ ama kweli mzee zakaria umemchoka 

mwanao.Yaani huyu Pauline anayefanana 

na Beyonce aanguke kimapenzi kwa Yule kijana !! hahahaaaaaaa…haloooo !!! hizo ni 

ndoto za mchana.Hilo ni jambo 

lisilowezekana hata kidogo.Kijana 

mwenyewe Yule asiye na mbele wala 

nyuma.” Akasema Vicky. 

 “ Dah ! mke wangu ungebahatika 

kumuona namna David alivyobadilika basi 

usingesema kwamba ni kijana asiye na 

mbele wala nyuma.” Akasema mzee 

Zakaria 

 “ amebadilika? Akashangaa Vicky 

 “ Pauline amempeleka saluni na 

ukimuona hautaamini kama ndiye Yule 

unayesema hana mbele wala nyuma” 

akasema mzee Zakaria.Vicky akabetua 

midomo na kuguna 

 “ Mhhhh!!!..” kisha akainuka na 

kuelekea chumbani kwake. 

 “Pauline naomba usimjali mama 

yako.Nadhani unamfahamu tabia 

yake.Mchukulie kama alivyo “akasema 

mzee Zakaria 

 “ Usihofu baba.Mama mdogo 

ninamuelewa sana na hanipi shida” 

akasema Pauline 

 “ Sawa Pauline.Tutaongea zaidi jioni na 

kumfahamisha David kuhusiana na maamuzi haya.Ila tafadhali naomba 

uyazingatie hayo niliyokwambia” akasema 

mzee zakaria.Pauline akainuka na 

kuelekea chumbani kake 

 “baba kafikiria kitu gani hadi akanipa 

tahadhari ile? Akajiuliza Pauline wakati 

akielekea chumbani kwake 

 “ Ameona kitu gani kati yangu na 

David? Lakini naomba nikiri kwamba 

toka nilipomuona David nimebadilika 

sana.Kuna mabadiliko Fulani ambayo 

nimeanza kuyaona hata mimi .Nimekuwa 

ni mtu mwenye furaha sana tofauti 

nilivyokuwa kabla ya kukutana na 

David.Vile vile kila mara ninataka kuwa 

karibu na David.Toka alipofariki Frank 

mchumba wangu sijawahi kuwa na 

ukaribu na mvulana yeyote kama 

ilivyonitokea kwa David” akawaza Pauline 

halafu akaufungua mlango wa chumbani 

na kuingia chumbani kwake Akakaa 

kitandani 

 “I feel something different when I’m 

with him..naomba niwe wazi kwamba kwa 

siku hizi chache nilizomfahamu david 

nimebadilika sana na ndiyo maana hata 

baba ameanza kuwa na wasi wasi kuhusu mwelekeo wangu na David kwani 

ananifahamu vizuri mimi ni msichana 

ambaye sifahamu kushindwa.If I want 

something I go and get it. “ akawaza 

Pauline halafu akavua nguo zake na kuvaa 

nguo anazopenda kuvaa akiwa nyumbani 

 “ Jinsi ninavyojisikia nikiwa na 

David,ninavyofurahi nikiongea naye 

,vinaweza vikawa ni viashiria kwamba 

nimeanza kumpenda David? Akajiuliza 

Pauline halafu akajiangalia katika kioo na 

kutabasamu 

 “Yawezekana pengine nikawa nimeanza 

kuvutiwa na David na ndiyo maana nikiwa 

naye karibu lakini sijui kama nina hisia 

zozote za kimapenzi kwake .Hata hivyo 

kuna kitu ninakihisi kwake ambacho si 

cha kawaida.Natamani niwe naye muda 

wote.Natamani nimfuate hata chumbani 

kwake nikaongee naye.Nadhani ni ukaribu 

huu ndio uliomstua baba na kudhani 

kwamba ninaweza kujikuta mapenzini na 

David”akawaza Pauline halafu akaenda 

tena kukaa kitandani 

 “Kwa sasa ni mapema sana kusema 

kwamba kuna hisia zozote za kimapenzi 

kati yetu lakini endapo itatokea kwamba mimi na David tukapendana basi hakuna 

anayeweza kunizuia kumpenda kwani 

sioni kama kuna kosa lolote mimi 

kupendana naye.Halafu mama mdogo 

nitamuonya aache kabisa kumdharau 

David.Sintavumilai matusi au dharau 

zozote zile toka kwake akimdharau au 

kumtusi David” akawaza Pauline halafu 

akatoka na kwenda kuungana na 

mtumishi wao kuandaa chakula cha usiku.



 Ni usiku wa saa mbili ,familia yote 

imekusanyika kwa ajili ya chakula cha 

usiku.David ndiye aliyekuwa wa mwisho 

kuingia katika chumba kile cha 

chakula.Mara tu alipoingia ,Vicky 

akaonyesha mstuko Fulani baada ya 

kumtazama lakini akajitahidi kuonyesha 

kwamba hakuwa amestuka.David 

akawasalimu wote kisha akavuta kiti na 

kuketi. 

 “ Wow ! amependeza sana.Kumbe ni 

kijana nayevutia namna hii.Dah 

nimestuka sana kwa mabadiliko haya ya 

ghafla.Anaonekana ni kijana wa kisasa na mtanashati sana.Ouh gosh ! Safia alikuwa 

sahihi kabisa kwamba kijana huyu 

anaweza akawa ni msaada mkubwa 

kwangu.Lazima nianze mikakati ya 

kumuweka karibu angali mapema kwani 

inaonekana Pauline tayari 

amekwishaanza kuonyesha dalili kwamba 

amevutiwa na huyu kijana” akawaza Vicky 

 “He’s so handsome.dah ! mpaka mwili 

wote umesisimka.Sikujua kama kijana 

huyu ni mzuri kiasi hiki.He’s amazing” 

akawaza Vicky huku akimtazama David 

kwa jicho la wizi. 

 Waliendelea kula na baada ya kula 

mzee Zakaria akamuomba David 

asiondoke walikuwa na maongezi naye 

 “ David,kuna jambo ambalo Pauline 

aliniambia.Ni kweli kwamba una shahada 

ya biashara? akauliza mzee Zakaria 

 “ Ni kweli mzee” akasema David huku 

akitazaam chini.Alionekana kuwa ni 

kijana mwenye aibu nyingi na hakupenda 

kumtazama mtu machoni 

 “Vizuri sana” akasema mzee Zakaria 

halafu kikapita kimya kifupi akaendelea 

 “Nadhani Pauline atakuwa amekwisha 

kudokeza kwamba mimi ninajishughulisha na biashara.Nina 

biashara mbali mbali hapa mjni na katika 

miji mingine mikubwa.Kwa muda sasa 

biashara zangu zimekuwa haziendi vizuri 

kutokana na kukosekana usimamizi 

makini.Pauline yeye ana biashara zake 

kwa hiyo hawezi akapata nafasi ya 

kuisimamia pia miradi yetu ya 

familia.Nimekuwa nikitafuta watu wa 

kunisaidia lakini wamekuwa ni chanzo cha 

miradi yetu mingi kufa kutokana na kuiba 

na kutuacha katika madeni makubwa.Kwa 

sasa hali yangu kiafya imekuwa si nzuri na 

Pauline ameniomba kwamba uwe msaidizi 

wangu na unisaidie kuzisimamia biashara 

hasa wakati huu ambao nahitaji 

mapumziko.David ninakuamini na 

ninakuomba unisaidie katika jambo 

hili.Kuja kwako katika familia yetu ni kwa 

maongozi ya Mungu kwani alijua 

tunahitaji mtu kama wewe.Je uko tayari 

kufanya kazi name kijana wangu? 

Akasema mzee Zakaria.David akafikiri 

kidogo na kusema 

 “ Mzee Siwezi kusema hapana hasa 

kutokana na wema mkubwa 

mlionitendea.Niko tayari kufanya kazi yoyote utakayonipatia ili mradi iwe ni kwa 

kukusaidia wewe” akasema David na sura 

ya mzee Zakaria ikapambwa na tabasamu 

pana 

 “ Ahsante sana David.Ninashukuru sana 

kwa kukubali kwako kufanya kazi 

hii.Kesho nitakwenda kukuonyesha 

sehemu yako ya kazi na kazi ambazo 

utakuwa ukizifanya.” Akasema mzee 

Zakaria.Vicky ambaye muda huo wote 

alikuwa kimya akaonyesha mstuko 

 “ Darling mbona mnafanya maamuzi 

bila kunishirikisha na mimi? Imekuaje 

ukamuamini huyu kijana haraka namna 

hiyo na kuamua kumpa biashara zako 

aziendeshe? Unafahamu mahala 

alikotoka? Unaaminije kama atakuwa 

muaminifu tofauti na wale woet 

waliotanulia na kusababisha madeni 

makubwa? Akauliza Vicky 

 “Usijali mke wangu ,David ni 

mwanafamilia yetu kwa sasa na hakuna 

tatizo katika kumuamini.Hata hivyo 

atafanya kazi hii akisaidiana na Pauline 

hadi hapo atakapoweza kuifanya yeye 

mwenyewe.Kwa sasa ninahitaji 

mapumziko ya kutosha kwa hiyo ninahitaji mtu wa kuweza kunisaidia 

katika kuziendesha biashara zangu.David 

ndiye kijana ambaye Mungu ametuelekeza 

kwetu “ akasema mzee Zakaria 

 “Pamoja na hayo ulitakiwa 

unishirikishe na mimi ili upate mawazo 

yangu.Au mimi sina nafasi katika familia 

hii? Akauliza Vicky kwa ukali 

 “Pauline na David kesho tutakwenda 

sote kumuonyesha David ofisi yake .Usiku 

mwema na mlale salama” akasema mzee 

zakaria kisha akainuka na kueleka 

chumbani kwake akimuacha Vicky mke 

wake amefura kwa hasira.Naye akainuka 

kwa hasira na kuelekea chumbani kwake. 

 “David naomba usikasirike wala kuhofu 

kuhusu mama mdogo.Ndivyo alivyo na 

unatakiwa umvumilie” akasema Pauline 

 “ Usihofu Pauline.Ninalifahamu hilo na 

ninafahamu wazi kwamba mama yako 

mdogo hapendezwi kabisa na uwepo 

wangu hapa .Najua nitakumbana na vikazo 

vingi lakini nitavumilia kwa sababu yako 

na mzee Zakaria.Mmekuwa ni watu wema 

sana kwangu kwa hiyo nitavumilia kila 

kitu kwa ajili yenu.Nitafanya kazi kwa 

mzee Zakaria na ninakuhakikishia nitatumia kila aina ya uwezo wangu na 

ndani ya kipindi kifupi your father’s name 

will be on top again.I promise you that” 

akasema David halafu wakaagana na kila 

mmoja akelekea chumbani kwake. 

******************************* 

 Kumepambazuka siku ya 

jumamosi.Toka asubuhi Robin alikuwa 

katika pilika pilika nyingi.Alisaidiana na 

mwanae Penny na mfanyakazi wao wa 

ndani katika kusafisha mazingira ya 

kuzunguka nyumba yao na yakawa 

safi.Jumamosi hii ni siku ambayo 

walitegemea kutembelewa na mgeni 

ambaye alionekana muhimu sana kwa 

Robin, Mgeni huyu alikuwa ni mwalimu 

Lucy mwalimu mkuu wa shule anayosoma 

Penny. 

 “ Mpaka hapa nadhani tumefikia 

asilimia sabini ya maandalizi ya mgeni 

wetu wa leo.Mtu yeyote anayetembelea 

nyumbani kwako kitu cha kwanza 

ambacho atakitazama ni mazingira.Kwa 

sasa mazingira yako safi na kilichobaki ni 

chakula na vinywaji” akawaza Robin halafu akaingia jikoni na kuanza 

maandalizi ya chakula akisaidiana na 

mtumishi wake wa ndani ambaye alikuwa 

akishangaa sana na kujiuliza kuhusiana na 

mgeni anayefanyiwa maandalizi makubwa 

namna ile. 

 “ Lazima atakuwa ni mgeni muhimu 

sana kwani sijawahi kuona bosi wangu 

akiwa makini namna hii na maandalizi” 

akawaza mfanyakazi wa ndani wa Robin 

 Saa sita za mchana akawasili dereva na 

kumchukua Penny wakaelekea nyumbani 

kwa mwalimu Lucy kwenda kumchukua 

kama Robin alivyokuwa amemuahidi. 

 Takribani dakika ishirini sasa 

zimekwisha pita mwalimu Lucy akiwa 

bado anajiangalia katika kioo kikubwa 

chumbani kwake.Alikuwa akijihakikisha 

kama amependeza vya kutosha kabla 

hatakutana na Robin.Siku hii alikuwa 

amependeza kupita maelezo.Alivaa gauni 

refu la rangi nyeusi lililomkaa vyema 

kutokana na umbo lake jembemba.Nywele 

zake ndefu zilikuwa zinang’aa na 

kuvutia.Kila ambaye angekutana na 

mwalimu huyu siku ya leo asingeshindwa kugeuka na kumtazama kwa namna 

alivyokuwa amependeza. 

 “ Nadhani nimependeza vya 

kutosha.Sijui kwa nini nimejiskia kutaka 

kupendeza sana siku ya leo.” Akawaza 

mwalimu Lucy na kutazama juu 

 “ Gosh.! Toka asubuhi ni sura ya Robin 

pekee ndiyo inayotawala kichwa 

changu.Sijui ni kwa nini ametokea 

kuniingia kichwani ghafla namna 

hii.Natamani kama ningekuwa naonana 

naye kila siku.Robin ana vitu Fulani 

ambavyo wanaume wengi hawana.” 

akawaza na kutabasamu 

 “Kwa zaidi ya miaka kumi sasa 

hatimaye ametokea mwanaume mmoja 

ambaye amenifanya nikauvunja mwiko 

wangu wa kutokuhitaji ukaribu wowote 

na mwanaume.Niliwachukia sana 

wanaume na hasa kwa mambo 

waliyonifanyia lakini nashangaa kwa 

Robin imekuwa tofauti .Nimejikuta 

nikikubali kiurahisi mwaliko wake.Ndiyo 

maana ninasema kwamba Robin ana vitu 

Fulani ambavyo wanaume wengi hawana.” 

Akawaza Pauline halafu akageuka na 

kujitazama kwa nyuma halafu kwa mbele akapindisha kichwa akaziangalia tena 

nywele zake na mara sura ya Robin 

ikamjia kichwani na kumfanya asisimke 

mwili na mara kengele ya mlangoni ikalia 

akatoka chumbani na kwenda kuufungua 

mlango akakukata na sura yenye 

tabasamu pevu ya Penny.Kwa furaha 

aliyokuwa nayo akajikuta akimkubatia 

 “ Mwalimu Lucy leo umependeza sana.” 

Akasema Penny 

 “ Ahsante sana Penny.baba hajambo? 

 “ Baba hajambo na ametutuma tuje 

tukuchuke “ akasema penny 

 Kwa kuwa tayari alikwisha jiandaa 

,mwalimu Lucy akaingia garini na safari ya 

kuelekea kwa Robin ikaanza. 

 Saa saba wakawasili numbani kwa 

Robin.Penny akaonyesha tabasamu 

akiyafurahia mazingira na maua mazuri 

yaliyopandwa kuizunguka nyumba yote 

 “ Karibu ndani mwalimu Lucy” akasema 

penny na kumkaribisha mwalimu Lucy 

ndani 

 Mara tu alipoingiandani akakutana na 

sura yenye tabasamu ya Robin ambaye 

alikuwa amevaa kofia na mavazi maalum 

ya wapishi.  “mwalimu Lucy karibu sana” akasema 

Robin kwa furaha huku 

akitabasamu.Mwalmu Lucy alipatwa na 

msisimko wa aina yake mara tu 

alipomuona Robin. 

 “ Ahsante sana Robin.” akajibu 

mwalimu Lucy huku akipeana mikono na 

Robin kisha akaketi sofani 

 “ Habari za toka majuzi? Akaanzisha 

maongezi Robin 

 “ habari nzuri Robin.Unaendeleaje? 

akauliza Lucy 

 “ Ninaendelea vizuri sana mwalimu 

Lucy” akajibu Robin 

 “ Ouh Robin naomba uniite Lucy 

inatosha ” akasema mwalimu Lucy , Robin 

akatabasamu 

 “Sikujua kama huwa unaingia jikoni “ 

akasema Lucy na kumfanya Robin acheke 

kidogo 

 “Huwa ninaingia jikoni mara kwa mara 

ninapokuwa na nafasi.Unajua kabla ya 

kuwa na kampuni yangu ya utalii nilikuwa 

na kazi ya kuwapikia watalii wa kizungu 

kwa hiyo ilinilazmu kusoma namna ya 

kupika vyakula vya mataifa mbali mbali 

.Nipatapo nafasi huwa napenda kuingia jikoni na kupika “ akasema Robin.Uso wa 

Lucy ukapambwa na tabasamu na vishimo 

vikajitokeza katika mashavu yake 

 “Kuna msaada wowote unaoweza 

ukauhitaji huko ikoni? Akauliza Lucy 

 “ Hapana Lucy.Wewe ni mgeni na 

hutakiwi kupewa kazi yoyote” 

 “ Ouh C’mon Robin.Jikoni ni kazi zetu na 

tumeshazizoea.tafadhali naomba kama 

kuna kazi yoyote ninaweza kukusaidia 

jikoni .Mara nyingi huwa ninapenda na 

mimi kusaidia baadhi ya kazi hata kama 

ni ndogo tu” akasema Lucy.Robin 

akatabasamu na kusema 

 “ hapana Lucy.Naomba upumzike na 

hata hivyo tumemaliza kila kitu” 

 “ Robin sintajisikia amani endapo 

nitaondoka katika nyumba hii bila kugusa 

kazi yoyote .Tafadhali naomba unipe kazi 

yoyote ile na mimi nisaidie.Let’s make this 

day so enjoyable and fun” akasema Lucy 

 “Kwa kuwa umesisitiza basi naomba 

unisaidie kukata kachumbari” akasema 

Robin kisha akamuongoza mwalimu Lucy 

kuelekea jikoni 

 “ Jiko lako zuri sana,nimelipenda” 

akasema Lucy  “ Ahsante sana Lucy..” akasema Robin 

halafu akawaacha Mwalimu Lucy Penny na 

mfanyakazi wa ndani wakiendelea na 

maandalizi ya mwisho na yeye akaelekea 

chumbani kwake kujiandaa.Alipoingia 

chumbani kwake akasimama na kuegemea 

mlango. 

 “Uuuphhh.,!!!!!!!..” akavuta pumzi ndefu 

na kutabasamu 

 “Dah ! mwili wangu wote umesisimka 

sana.Lucy ni mwanamke mzuri hakuna 

mfano.Anaupeleka mbio moyo wangu kwa 

uzuri wake.Ni mcheshi,mkarimu na 

alichonifurahisha zaidi amezoea haraka 

sana hapa kwangu kana kwamba ni 

sehemu ambayo amekuja mara kadhaa.” 

Akawaza Robin huku akatabasamu 

 “Ninahisi ninaanza kumpenda 

mwanamke huyu.Toka Flaviana 

aliponikimbia sijawahi kuwa na hisia za 

namna hii kwa mwanamke yeyote Yule 

lakini imenitokea hivi sasa kwa Lucy.Kila 

nikimuona mwili wangu unasisimka na 

mapigo ya moyo yanakwenda mbio.What 

am I going to do? Simfahamu kiundani na 

sifahamu kama ana mume au hana,kama 

ana mpenzi au hana.Sitaki kujiingiza katika matatizo kwa kuanguka mapenzini 

na mwanamke ambaye tayari yuko katika 

mahusiano.Ninayafahamu maumivu ya 

kuvunjiwa mahusiano kwa hiyo sitaki 

kuingilia uhusiano wake kama anao.” 

 Akawaza Robin na kuvua nguo akaingia 

bafuni kuoga.Bado sura ya mwalimu Lucy 

ilikuwa inamjia. 

 “ Ana midomo laini na mizuri,sauti 

tamu ambayo utapenda kuisikiliza muda 

wote,ana macho malegevu na nywele 

ndefu .Mwili wake laini kama malaika..ouh 

gosh..She’s driving me crazy…” akawaza 

Robin huku akiendelea kuoga. 

 “ Ngoja niziweke mbali kwanza hisia 

hizi zilizoanza za kumpenda Lucy hadi 

hapo nitakapomfahamu zaidi.Kwa sasa 

itanilazimu nijenge urafiki wa kawaida tu 

na kama kunaweza kutokea lolote basi ni 

huko mbeleni na si sasa hivi.” Akawaza 

Robn wakati akivaa nguo.Alijitazama 

katika kioo na kujiona nama alivyokuwa 

amependeza,akatoka mle chumbani na 

kuelekea katika chumba cha 

chakula.Tayari mwalimu Lucy akisaidiana 

na Penny na mtumishi wa ndani 

walikwisha andaa meza na aliyekuwa akisubiriwa ni Robin.Mwalimu Lucy 

alipomuona Robin namna alivyopendeza 

akatabasamu 

 “ bado ninajiuliza kwa nini huyu mke 

wa Robin aliamua kumkimbia mwanaume 

mzuri kama huyu? He’s so handsome.Ana 

kila sifa ya kijana mzuri ” akawaza Lucy 

 “Karibuni tujukumuike kwa chakula” 

akasema Robin na wote wakaketi vitini 

lakini kabla ya kula chakula ,Penny 

akaomba kwa niaba ya wote halafu 

chakula kikaanza kupakuliwa.Mezani 

kulikuwa na aina mbali mbali za vyakula. 

 “ Chakula kizuri sana Robin.Hongera 

wewe ni mpishi mzuri ” akasema Lucy 

akikifurahia chakula kile kitamu. 

 “ Ahsante sana Lucy…” akajibu Robin 

huku akitabasamu 

 “ Kuna wakati tuliwahi kuwa na 

mashindano ya kupika pale shuleni na 

Penny akaibuka mshindi sikufahamu siri 

yake nini hadi akajua kupika namna ile 

lakini leo nimemfahamu mwalimu wake” 

akasema Lucy na wote wakacheka.Ilikuwa 

ni furaha tupu pale mezani.mwalimu Lucy 

alikuwa ni mcheshi mno.Kila mtu pale 

mezani alimpenda  Baada ya kumaliza kula Robin na 

mwalimu Lucy wakaelekea sebuleni 

wakati Penny na mfanyakazi wao wa 

ndani wakisaidiana katika kuosha vyombo 

vilivyotumika kwa chakula. 

 “ Robin napenda nichukue nafasi hii 

kukushukuru sana kwa chakula 

kitamu.Sikutegemea kama unaweza 

ukawa ni mpishi mzuri kiasi hiki.Napenda 

nikiri kwamba ni muda mrefu sijaweza 

kula chakula kitamu kama hiki” akasema 

Lucy .Robin akatabasamu na kusema 

 “ Ahsante sana Lucy kwa kuyapenda 

mapishi yangu.Kupika ni kitu 

ninachokipenda na kama nilivyokwambia 

awali kwamba kabla sijawa na kampuni 

yangu mwenyewe nilikuwa nikifanya kazi 

ya kuwapikia watalii kwa hiyo ilinilazimu 

kujifunza namna ya kupika vyakula vya 

mataifa mbali mbali” akasema Robin 

 “Endapo ningekuwa na hoteli 

,ningekuajiri Robin..nadhani hoteli hiyo 

ingekuwa inafurika watu kila siku” 

akasema Lucy halafu wote wakacheka 

kicheko kikubwa. 

 “Lucy unatumia kinywaji gani? Robin 

akamuuliza mwalimu Lucy  “Hapa una kinywaji gani? akauliza Lucy 

 “ hapa kuna soda ,maji,na mvinyo” 

 Lucy akatabasmau na kusema 

 “ Naomba mvinyo….” 

 Robin akaleta chupa kubwa ya mvinyo 

na kuiweka mezani akamimina katika 

glasi mbili na wakaanza kunywa. 

 Robin ,Jumamosi ya leo ni moja kati ya 

siku zangu kubwa na zenye furaha sana 

kwa sababu nimekutana na familia iliyojaa 

upendo na furaha.Nimefurahi sana.” 

 “ Hata sisi tumefurahi sana 

umetutembelea Lucy..Binafsi nimefurahi 

kwanza kukufahamu.Penny alikuwa 

akinieleza kuhusiana na namna 

unavyomlea na nikawa na hamu ya 

kukuona na kukushukuru.Ahsante sana 

kwa kunisaidia kumlea mwanangu na 

kumuelekeza katika maadili mazuri” 

akasema Robin halafu akainuka na 

kueleka chumbani kwake akachukua 

albamu kubwa la picha na kurejea 

sebuleni akampatia mwalimu Lucy . 

 “ katika albamu hii kuna picha zote za 

Penny tangu akiwa mtoto mdogo.” 

Akasema Robin na huku akitabasamu mwalimu Lucy akalipokea na kuanza 

kulifungua lile albamu 

 “ Wow ! toka akiwa mdogo Penny 

alikuwa ni msichana mrembo sana.” 

Akasema mwalimu Lucy huku akiendelea 

kutazama picha .Mara macho yake 

yakagota katika picha moja ambayo 

aliitazama kwa makini halafu akainua 

kichwa na kumtazama Robin 

 “ Huyu ndiye mama yake Penny? 

Akauliza Lucy.Robin akatabasamu na 

kusema 

 “ .Anaitwa Flaviana.Ndiye mama mzazi 

wa Penny” 

 “she’s so pretty” akasema mwalimu 

Lucy huku akitabasamu 

 “Ni kweli alikuwa ni mwanamke mzuri 

sana kwa sura na umbo lakini moyo wake 

haufanani na uzuri wake.” Akasema Robin 

 “Kwa kweli hata mimi nashangazwa 

sana na kitendo alichokifanya cha 

kuondoka na kumtelekeza kabisa 

mwanae.Penny ananiambia kwamba ni 

miaka mingi hajawahi kumuona mama 

yake na wala hajui yuko wapi” 

 “ Ni tamaa za maisha ya starehe na 

anasa ndivyo vilivyompelekea akaamua kufanya vile alivyofanya.” Akasema 

Robin.Mwalimu Lucy akatikisa kichwa na 

kusema 

 “ Pamoja na kwamba mimi pia ni 

mwanamke naomba nikiri kwamba 

alifanya jambo baya sana kwako na kwa 

mtoto wake.” Akasema mwalimu Lucy 

 “ Kwa mzazi mwenye kuwa na uchungu 

na watoto wake lazima ataumia sana kwa 

kitendo cha Flaviana.Lakini sishangai sana 

kwa sababu kuna ule msemo unaosema 

kwamba not all women are born to be 

mothers..Sidhani kama Flaviana ni mmoja 

wa wanawake ambao wameumbwa 

mahususi kuwa mama.Hana sifa za kuwa 

mama.” Akasema Robin na kuinama chini. 

Akafikiri kwa muda halafu akasema 

 “ Lakini hata hivyo ninashukuru kwa 

kuwa Penny ameweza kumpata mbadala 

wa mama yake.Lucy nakushukuru sana 

kwa kuwa karibu na mwanangu.Ahsante 

kwa kujivika majukumu ambayo 

mwingine aliyakimbia.Umekuwa ni 

msaada mkubwa sana kwa Penny” 

akasema Robin 

 “ Usijali Robin.Ni jukumu langu kufanya 

hivyo ninavyofanya kwa Penny na kwa wanafunzi wengine wote kwanza kama 

mwalimu na pili kama mama.Lakini 

naomba nikiri kwamba sijui ni kwa nini 

nimetokea kuwa na ukaribu na Penny kwa 

namna hii kiasi kwamba watu wote 

wanafikiri labda ni mtoto wa mmoja wa 

ndugu zangu.Siku haiwezi kuisha bila 

kuonana naye tukaongea hata kwa muda 

mfupi nikafahamu maendeleo yake na 

kama ana tatizo lolote .Ninampenda sana 

Penny na ninamlea kwa misingi yote ya 

malezi bora kama mwanangu.Ni kwa 

sababu ya kutaka kuwa karibu naye zaidi 

ndiyo maana nimeanzisha mchakato wa 

kujenga shule ya sekondari pale pale 

katika eneo langu ili wanafunzi 

watakaomaliza elimu ya msingi basi 

waendelee na elimu ya sekondari pale 

pale.Wazo hili lilikuja baada ya kufikiria 

kutengana na Penny pindi atakapomaliza 

masomo yake ya elimu ya msingi.Penny ni 

binti wa kipekee,amekuwa akiniliwaza na 

kunifanya niwe na furaha kila mara 

nikiwa naye.Hongera sana Robin kwa 

Baraka hii ya mtoto huyu wa kipekee .” 

Akasema mwalimu Lucy. “ Ahsante sana Lucy..Hata mimi 

namshukuru sana Mungu kwa kumlea 

mwanangu vyema na katika maadili 

mazuri.Lakini sote tunastahili 

kupongezana kwani sote tumechangia 

katika malezi ya Penny” akasema Robin 

na mwalimu Lucy akatabasamu 

 “Lucy kuna kitu umekitamka hapa 

kwamba una mpango wa kuanzisha shule 

ya sekondari? 

 “ Ndiyo Robin.Ninataka kuanzisha 

sekondari.Hivi sasa niko katika mchakato 

huo na umefikia sehemu nzuri.Kuna 

wafadhili ambao wamejitolea kunisaidia 

na muda wowote kuanzia sasa ujenzi 

utaanza.” Akasema Lucy 

 “ Ina maana shule ile ni ya kwako? 

Akauliza Robin 

 “ Ndiyo Robin.Shule ile ni ya kwangu 

japo watu wengi hawalifahamu hilo.Mimi 

ndiye mmiliki wa shule ile “ akasema 

mwalimu Lucy 

 “ Hongera sana.Hata mimi sikujua kama 

shule ile ni yako.Unastahili pongezi Lucy 

kwa kuwa na shule nzuri na bora kama sebuleni. “ Ahsante sana Robin” akasema Lucy 

huku akitabasamu.Penny akajiunga nao 

na kisha maongezi na vicheko vikatawala 

pale sebuleni.

 Mzee Zakaria ,akiwa na Pauline na 

David waliwasili katika jengo moja kubwa 

la ghorofa nne lililopo maeneo ya Kijenge 

lililojulikana kama Arusha shopping 

mall.Lilikuwa ni jengo kubwa lenye 

maduka mengi na biashara mbali mbali . 

 “ David hili ni jengo langu na hapa pana 

ofisi yangu kuu na biashara zangu kadhaa 

ziko katika jengo hili” akasema mzee 

zakaria kabla hawajashuka garini. 

 “ Ouh ..umejitahidi sana mzee.” 

Akasema David halafu Pauline ambaye 

ndiye aliyekuwa akiendesha akaegesha 

gari wakashuka na kuelekea katika ofisi 

ya mzee Zakaria iliyopo katika ghorofa ya 

nne.Mzee huyu alionekana maarufu sana 

kwani watu wengi walikuwa 

wakimsalimia na kumpa pole kwa 

kuumwa.Walifika katika ofisi yake 

akasalimiana na sekretari wake kisha 

wakaingia ndani 

 “ David hii ndiyo ofisi yangu 

kuu.Shughuli zako zote utakuwa 

ukizifanyia katika ofisi hii.Utawekewa 

meza hapo pembeni na utakuwa ukifanya 

shughuli zote badala yangu kwa sababu 

sintakuwa nikifika hapa mara kwa 

mara”akasema mzee Zakaria David 

alionekana kushangaa sana na kushindwa 

kuamini kama mzee yule alikuwa na 

utajiri mkubwa namna ile 

 “David mimi ni mfanyabiashara 

mkubwa hapa Arusha.Nina miradi kadhaa 

mikubwa.Katika jengo hili kuna 

supermarket hapo ghorofa ya chini ..ni 

moja katiya supermarket kubwa hapa 

Arusha.Katika jengo hili pia nina duka la 

vifaa vya elektroniki kama vile simu ,redio 

na vitu vingine vingi.Kwa sasa duka hli 

linasimamiwa na mke wangu kwa sababu 

yeye ndiye aliyekuwa akisafiri mara kwa 

mara kwenda nchini China na kwingineko 

kufuatilia bidhaa.Ghorofa ya pili kuna 

duka la samani za ndani.Bidhaa nyingi za 

duka lile tunazitoa nje ya nchi .Ukiacha 

bashara hizo ninalo pia duka la vito na mapambo.Hili linasimamiwa na mke 

wangu.Vile vile nimeingia katika biashara 

ya kununua na kuuza madini aina ya 

Tanzanite japokuwa biashara ile bado 

haijaanza kuniingizia faida lakini na hiyo 

pia inasimamiwa na mke wangu.Nina 

vituo viwili vya mafuta na magari manne 

ya kubebea mafuta.Vile vile nina magari 

ya kubeba mchanga yapo sita.” Akasema 

mzee Zakaria. 

 “ Kuna miradi mingine ambayo ilikuwa 

inaniingizia hasara ikanibid kuifunga .Vile 

vile kuna miradi ambayo nimeikopea 

fedha nying I benki kama huu wa kununua 

na kuuza madini.Binafsi sikuafiki 

kuanzishwa kwa mradi huu lakini mama 

yenu alisisitiza sana hivyo ikanibidi 

kukubali lakini toka ulipoanzishwa 

umekuwa ukiingizaq hasara kubwa 

sana.Miradi mingi kwa hivi sasa hali yake 

kifedha si nzuri kutokana na kukosekana 

kwa usimamizi thabiti na madeni 

makubwa yaliyosababishwa na watumishi 

waliokuwa wakiiba na kukimbia na au 

miradi iliyokopewa fedha 

kutokujiendesha kifaida.” Akasema mzee 

Zakaria.  “ David ninakuweka kuwa msimamizi 

wa miradi hii yote.Wewe utasimamia 

mapato na matumizi yote ya fedha na 

kuhakikisha kwamba miradi yote 

inajiendesha kifaida.Nataka nitumie muda 

mwingi kupumzika kwa hiyo wewe 

ukisaidia na na Paulie mtasimamia 

biashara zote.” Akasema mzee Zakaria 

halafu wakatoka na kuanza kutembelea 

miradi yote pamoja na kutambulishwa 

kwa wafanyakazi kwamba David ndiye 

atakayekuwa msimamizi mkuu wa miradi 

yote . 

 “Bado simaini mzee huyu ameniamni 

kiasi gani hadi anipatie usimamizi wa 

miardi hii mikubwa.Hili ni jukumu zito na 

ni changamoto kubwa kwangu.Kwa 

uaminifu huu aliouonyesha kwangu 

nitajitahidi nisimuangushe.Nitafanya kazi 

hii kwa uadilifu mkubwa na yeye 

mwenyewe atafurahi.Nadhani ni maongozi 

ya Mungu yalinielekeza nifike hapa kwa 

mzee huyu kwani alikuwa anahitaji mtu 

kama mimi” akawaza David wakati 

wakilizungukia lile supermarket kubwa 

linalomilikiwa na mzee zakaria 




 Gari ya kifahari aina ya BMW inafunga 

breki nje ya Saluni moja kubwa ya kike 

jijini Arusha .Baada ya kama dakika mbili 

hivi mlango ukafunguliwa na akashuka 

mwanamke mmoja mrembo sana 

.Akafunga mlango wa gari kwa madaha na 

kisha kwa mwendo wa maringo akaanza 

kutembea kuingia ndani ya saluni ile.Watu 

wote waliokuwapo pale nje waligeuza 

shingo zao kumuangalia mwanamke yule 

aliyekuwa amevaa suruali ya bluu 

iliyomkaa vyema na shati dogo jeupe 

.Alikuwa ni mwanamke aliyeumbika 

hasa.Huyu alikuwa ni Vick. Ambye alikuwa 

maarufu sana kwa jina la Vicky 

madhahabu kutokana na kupenda kuvaa 

vito vingi vya dhahabu mwili 

mzima.Alikuwa na vipini viwili vya 

dhahabu juu ya jicho lake la kulia,masikio 

yake yote mawili yalikuwa yamejazwa na 

heleni za dhahabu.Puani alikuwa na kipini 

cha dhahabu .Shingoni alikuwa na cheni 

mbili za dhahabu na katka vidole vyote 

vya mikono alikuwa na pete za 

dhahabu..Katika miguu yake yote miwlili alikuwa anavaa cheni za dhahabu maarufu 

kama vikuku.Hii ndiyo sifa kubwa 

aliyokuwa nayo mwanamke huyu ambaye 

aliolewa na mzee zakaria mmoja wa 

matajiri wakubwa wa jiji hili la Arusha 

baada ya mke wake kufariki dunia. 

 Alitembea kwa mwendo wake ule wa 

kuringa kana kwamba hataki kukanyaga 

chini,halafu akaingia ndani ya salun ile. 

 “ Ouh ! Magold ,karibu sana” akasema 

safia shoga yake mkubwa na Vicky 

 “ Ahsante sana Safia.Habari za 

tokajana? 

 “ za toka jana nzuri tu.Anaendeleaje 

mzee Zakaria?akauliza Safia 

 “ Anaendelea vizuri tu..Anazidi kupata 

nafuu ” akasema Safia na kuketi kitini 

 “ Shoga mbona leo unaonekana 

umechoka sana..kulikoni? akauliza Safia 

 “ Safia nina matatizo makubwa 

mwenzio.” 

 “ tatizo gani tena Vicky? 

 “ Si yule kijana niliyekwambia jana? 

 “ kafanya nini? 

 “Yule kijana kumbe yuko tofauti na 

nilivyokuwa namfikiria.Jana nimerudi 

nyumbani nikakuta Pauline amempeleka saluni na kumtengeza.Dah ! nilistuka 

baada ya kumuona.Nakwambia shoga 

yangu nilimpotea yule kijana” akasema 

Vicky 

 “ Kwani alikuaje? Hebu nielezee shoga 

yangu” 

 ‘Amebadilika huyo kijana.Ukimuona 

utafikiri ni muimba muziki wa 

Marekani.Amependeza mno.Kumbe yule 

kijana ni mzuri sana.” Akasema Vicky 

 “ Nilikwambia shoga kwamba 

usimdaharau kwa sababu ya muonekano 

wake.Muonekano wa nje ni kitu ambacho 

kinaweza kubadilishwa dakika yoyote 

ile.” 

 “ Kweli kabisa Safia,kwa kweli kijana 

yule amenivutia ghafla hata mimi.Hivi 

nikwambiavyo usiku kucha wa leo sijalala 

ninamuwaza yeye tu.Safia kijana yule nina 

imani atanifaa sana .Kicwha changu 

kimechanganyikiwa siju hata nifanyeje 

shoga yangu” akasema Vicky 

 “ taratibu Vicky.Suala hili si la 

kuliendea haraka .Angalia usije ukaharibu 

mambo mapema.Unachotakiwa kufanya 

kwa sasa ni kuanza kujenga mazingira ya kuweza kumpata huyo kijana bila ya mtu 

yeyote kugundua.”akasema Safia 

 “ Nina wasi wasi Safia.Pauline tayari 

amekwisha anza kuoyesha kila dalili kuwa 

anampenda yule kijana.Na yule msichana 

huwa hashindwi kitu.Akitaka kitu fulani 

atakitafuta hadi atakipata.Kama 

amempenda David basi ni lazima 

atampata tu na kwa namna ninavyoona 

uelekeo wao kuna kila dalili ya mapenzi 

kati yao” akasema Vicky 

 “Usihofu kuhusu hilo Vicky.Hata kama 

akiwa na Pauline wewe si utakuwa 

unamtumia kwa kukuridhisha tu? Wewe 

tayari una mume wako na si kwamba 

unamtaka huyo kijana kwa ajili ya kuwa 

mpenzi wako bali ni kwa ajili ya 

kukusaidia kukata kiu yako ya mapenzi 

pale unapohitaji kukunwa.Kwa hiyo 

hakuna tatizo endapo huyo kijana 

atakuwa na Pauline” akasema Sa fia 

 “ Safia kitu kingine ambacho 

kinaniumiza kichwa n kwamba mzee 

Zakaria ameamua kumkabidhi miradi yote 

yule kijana.Yeye ndiye atakayekuwa 

akiisimamia.Tumelumbana sana usiku 

lakini amekataa kata kata kuniskiliza na hataki ushauri wowote kuhusiana na suala 

hili.Hivi tunavyoongea,ameambatana na 

mwanae Pauline wamekwenda 

kumkabidhi rasmi huyo kijana kazi ya 

kusimamia biashara zote za mzee 

Zakaria” akasema Vicky 

 “ Vicky usinitanie shoga yangu..Hiyo 

haiwezi kuwa kweli” 

 “ Sikutanii shoga yangu.Ni ukweli 

mtupu.Mzee zakaria ameamua hivyo na 

hakuna yeyote ambaye anaweza 

akamshauri vinginevyo kuhusiana na yule 

kijana.” 

 “ Sasa itakuaje? Ina maana hata 

biashara zako zote zitakuwa chini yake? 

 “ Ndiyo maana yake.Amemkabidhi kila 

kitu.Hata mimi niko chni yake .” 

 “ Huyu mzee ana wazimu ? akauliza 

safia kwa mshangao 

 “Sijui safia.Siju amefikiria kitu gani hadi 

akafanya maamuzi haya .Sifahamu 

ameona kitu gani.Kwa upande fulani 

ninaanza kumchukia yule kijana kwa 

sababu yeye atakuwa chanzo cha mimi 

kushindwa kufanya mambo 

yangu.Atakuwa ni kikwazo kikubwa sana 

kwangu.Kijana huyu anaonekana ni mtiifu sana na mwaminifu na endapo atagundua 

dosari yoyote katika biashara zangu 

lazima atamweleza mzee 

Zakaria.Ninaogopa jambo hilo lisitokee 

hasa kwa wakati huu ambao bado 

sijakamilisha mipango yangu” akasema 

Vicky 

“ Usihofu Vicky.Kijana huyo usifikire 

kumfanyia jambo lolote lile na wala 

usimchukie.Ukitaka mambo yako yote 

yaende safi basi mfanye awe rafiki 

yako.Kuwa muwazi kwake na 

mueleweshe kila kitu.Mfanyie yale mambo 

ambayo yatamfanya awe karibu yako 

zaidi.na ukifanikiwa katika hilo basi 

utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe 

moja.Utamtumia kukidhi haja zako na vile 

vile utamtuma katika kuendelea kuchuma 

mali kabla yule m zee hajafa .Mfundishe na 

muonyeshe upande wa pili wa maisha 

ulivyo.Muonyeshe maisha ya anasa na 

namna pesa inavyotumiwa.Nina imani 

akishanogewa na maisha hayo 

atakusikiliza kwa kila kitu shoga 

yangu.,Katika dunai hi hakuna asiyependa 

pesa.Pesa ndiyo kila kitu ,ilimuuza hata 

masihi.Nina imani hata huyo ijana akishaonja utamu wa fedha basi mtakuwa 

kitukimoja.” 

 “ hapo umenena jambo shoga yangu na 

ndiyo maana ninapenda unishauri 

ninapokuwa na matatizo.Nitajitahidi 

kumuweka karibu yule kijana na 

nitamfanyia mambo makubwa ambayo 

hajawahi kufanyiwa na mtu 

yeyote.Nitambeba hadi China 

nitakapokwenda kufunga bidhaa na huko 

nitamuonyesha raha za dunia zilivyo na 

kuanzia hapo nina hakika lazima atafanya 

kila nitakachokitaka.Nitampeleka 

nitakavyo mmi.Naomba Mungu nifanikiwa 

katika hili.” Akasema Vicky 

 “ Ninakufahamu vizuri Vicky.lazima 

utafanikiwa tu.” Akasema Safia 

 “ safia nashukuru sana kwa ushauri 

wako.Ngoja nielekee jengoni kwanza 

nikaangalie ujenzi unavyoendelea nataka 

katika mafundi waongeze kasi ili nyumba 

yangu iishe mapema Nina wasi wasi 

mambo yanaweza yakaharibika kabla 

sijamaliza hekalu langu.” akasema Vicky 

halafu akatoka akaingia garini na 

kuelekea Usa river katika nyumba yake. ************************** 

 “ Robin nakushukuru sana kwa 

kunikaribisha nyumbani kwako siku ya 

leo.Nimekuwa na siku njema sana na 

yenye furaha.Nimefurahi sana kufahamu 

Penny anaishi wapi,nimekula chakula 

kizuri mno .Kuwa ujumla siwezi kuelezea 

furaha yangu kwa siku ya leo” akasema 

mwalimu Lucy.Mida hiyo ilipata saa kumi 

na moja za jioni 

 “ hata mimi nashukuru sana Lucy kwa 

kufika hapa kwetu na kushinda pamoja 

nasi.Mimi na mwanangu Penny 

tumefurahi sana na ninakuomba huu 

usiwe mwisho wa kuja 

kututembelea.Unakaribishwa muda 

wowote hapa nyumbani.” Akasema Robin 

 “ Nashukuru Robin.Nitakuwa nikija 

mara kadhaa kuwatembelea.hata hivyo na 

mimi nina ombi kwenu.Nawakaribisheni 

kwangu wiki ijayo siku ya jumapili kwa 

chakula cha mchana na tushinde sote hadi 

jioni.Nitafurahi sana kama mtakubali 

mwaliko wangu” akasema mwalimu Lucy  “Usihofu Lucy.Tutakuja nyumbani 

kwako kama ulivyotualika hiyo jumapili” 

akasema Robin 

 “ nashukuru sana Robin.Nina imani 

itakuwa ni siku njema sana na yenye 

furaha kama hii ya leo” akasema Lucy na 

kujiandaa kutaka kuinuka lakini Robin 

akamuomba samahani na akaelekea 

chumbani kwake kisha akarejea na 

kiboksi kidogo kilichofungwa vizuri. 

 “ hii ni zawadi yako Lucy kwa kuja 

kututembelea leo” akasema Robin 

 “ wow ! Robin ahsante 

sana..Ninashukuru sana.You are real 

wonderfull” akasema mwalimu Lucy kwa 

furaha. Halafu akainuka 

 “ Robin nadhani muda wangu wa 

kuondoa umefika.” Akasema mwalimu 

Lucy 

 “ Mwalimu kwa nini usikae hadi usiku? 

Baba atakurudisha nyumbani kwa gari” 

akasema penny na kumfanya mwalimu 

Lucy acheke kidogo 

 “Ahsante sana Penny,nitakaa siku 

nyingine lakini leo nahitaji kuwahi 

kuondoka kuna mahala nahitajika kwenda 

jioni hii” akasema mwalimu lucy Robin na Penny wakamsindikiza Lucy 

hadi nje ,Robin akamfungulia mlango wa 

gari akaingia garini.Dareva akageuza gari 

na kuanza kuondoka.Robin na Penny 

wakampungia mikono mwalimu Lucy na 

gari likaondoka 

****************************** 

 Ni usiku wa saa tatu,David akiwa 

chumbani kwake akijiandaa kulala.Alihisi 

uchovu kutokana na mizunguko mingi 

waliyoifanya siku hiyo..Walizungukia 

karibu miradi yote ya mzee zakaria 

 “ Nimekabidhiwa jukumu zito 

sana.Miradi ya mzee Zakaria ni mingi na 

inayohitaji usimamizi makini.Nitaifanya 

kazi hii kwa uaminifu mkubwa na kwa 

uwezo wangu wote na nitahakikisha 

kwamba biashara zote zinakwenda kwa 

faida na ile miradi yote iliyokufa 

inafufuliwa.Miradi ambayo haitakuwa na 

faida yoyote lazima tuifunge.Najua 

ninaingia katika mgogoro mzito na baadhi 

ya wafanyakazi wa mzee ambao 

wamekuwa si waaminifu kwa hiyo ujio 

wangu utakuwa ni kikwazo kwao katika kuendeleza wizi na ufujaji .Nitapambana 

nao na Mungu atanisaidia kwani 

anafahamu nia yangu ni njema.” Akawaza 

David halafu akajilaza kitandani 

 “ Mungu ni mwema 

sana.Amenikutanisha na familia hii tajiri 

,na wametokea kuniamini kupita 

kiasi.Akawaza David halafu akainuka 

kitandani akaenda kulifungua kabati 

akatoa pochi yake kuu kuu na toka ndani 

ya pochi ile akatoa pete fulani ya dhahabu 

iliyoandikwa neno moja V.Akaiweka pete 

ile katika kiganja chake akaitazama kwa 

muda 

 “Siku moja nitakupata tu na 

kukukabidhi pete hii ambayo nimeitunza 

kama mboni ya macho yangu.” Akawaza 

David halafu akairudisha pete ile katika 

pochi ile kuu kuu na kabla hajafunga 

kabati kengele ya mlango wa chumba 

chake inalia.Akalifunga haraka haraka 

kabati na kuvaa shati kisha akaelekea 

mlangoni akijua lazima atakua ni Pauline 

au mzee zakaria.baada ya kuufungua 

mlango akapigwa na butwaa baada ya 

kukutana na sura yenye tabasamu ya Vicky madhahabu mke wa mzee 

zakaria.Alistuka sana…. 

 “ Hallo David “ akasema Vicky huku 

akitabasamu.David alikuwa anamuangalia 

huku akiogopa.Hakutegemea kama Vick 

angekuja pale chumbani kwake mida ile 

na hasa akiwa katika nguo nyepesi za 

kulalia. 

 “ Mama..karibu” akasema David huku 

sauti yake ikionyesha uoga. 

 “ Vicky.!!..call me Vicky..”akasema Vicky 

huku akimkazia macho David ambaye 

alikuwa anatetemeka kwa ndani. 

 “ Mbona unatetemeka david? 

Hukutegemea kuniona hapa mida hii? Just 

relax mimi siyo mtu mbaya kama 

walivyokwamba Pauline na baba 

yake.Mimi ni mtu mzuri sana na 

rafiki.Nadhani unaniogopa kwa sababu 

hujanizoea lakini kwa kuwa bado 

tunaendelea kukaa wote humu ndani basi 

tutakuwa tunakutana mara kwa mara na 

utanizoea.” Akasema Vicky huku 

akirembua macho yake. 

 “ David nimekuletea hizi nguo ni za 

kulalia.Watu walioendelea kama sisi 

huvaa nguo hizi wakati wa kulala.” Akasema Vicky huku akimrushia david 

mfuko 

 “ Usiku mwema david” akasema Vicky 

na kuondoka.David akabaki anamuangalia 

hadi alipopotea kabisa ,akaufunga mlango 

wake na kukaa kitandani.Kijasho kilikuwa 

kinamtoka. 

 “ Sikutegemea kabisa kama huyu mama 

angekuja kunigongea mida hii wakati 

watu wote wamelala.Alikuwa ana lengo 

gani? Kwa nini asinipe hizi nguo kabla ya 

kuja kulala? Akajiuliza David lakini 

akashindwa kupata jibu. 

“ Mbona unatetemeka david? 

Hukutegemea kuniona hapa mida hii? Just 

relax mimi siyo mtu mbaya kama 

walivyokwamba Pauline na baba 

yake.Mimi ni mtu mzuri sana na 

rafiki.Nadhani unanogopa kwa sababu 

hujanizoea lakini kwa kuwa bado 

tunaendelea kukaa wote humu ndani basi 

tutakuwa tunakutana mara kwa mara na 

utanizoea.” 

maneno haya ya Vicky yakamrudia 

kichwani.  “nashindwa kumuelewa Yule mama 

alikuwa na lengo gani kuniambia maneno 

yale.Kwa nini anatafuta ukaribu na mimi 

wakati toka aliponiona alionyesha wazi 

kwamba hayuko tayari mimi niishi katika 

nyumba hii? Itanibidi kujihadhari sana na 

huyu mama kwani kwa mujibu wa Pauline 

ni kwamba huyu ndiye chanzo cha 

matatizo ya mzee Zakaria kutokana na 

ufujaji wa pesa kwa kupenda mno anasa 

na starehe.Natakiwa kujihadhari kwa 

sababu anaonekana si mtu mzuri hata 

kidogo” akawaza David halafu akaufungua 

ule mfuko uliokuwa na nguo akazitazama 

na kuzifungia kabatini 

 “ Sintazivaa nguo hizi ,tena ngoja 

niende nikazitupe katika pipa la 

takataka.” Akawaza David halafu 

akaubeba mfuko ule na kwenda hadi 

katika pipa la kutupia taka taka akazitupa 

nguo zile na kuanza kurejea chumbani 

kwake na mara akaisikia sauti ya Pauline 

ikimuita.Alikuwa amekaa kibarazani 

katika kona yenye mwanga hafifu 

 “Pauline,umenistua sana.Unafanya nini 

mida hii huku nje?  “ Nikuulize wewe unafanya nini huku 

nje usiku huu? Akauliza Pauline 

 “ Kuna taka taka nimetoka kuzitupa” 

akajibu Pauline 

 “ David kazi ya kutupa taka taka si kazi 

yako.Kama una taka taka za kutupa 

ungezihifadhi hadi kesho.Huu ni muda wa 

kupumzika” 

 “ usijali Pauline nitafanya hivyo siku 

nyingine.Vipi wewe mbona uko hapa mida 

hii? Akauliza David 

 “ Nimekosa usingizi ndiyo maana 

nimekaa hapa mida hii nikijaribu 

kuhesabu nyota.Mara nyingi nikiwa sina 

usingizi huja hapa na kukaa nikitazama 

angani hadi hapo usingizi 

utakaponichukua.” Akasema 

Pauline.David akamsogelea 

 “Pauline kitu gani kinakukosesha 

usingizi? 

 “ Nina mawazo mengi na ndiyo maana 

ninakosa usingizi” 

 “ Unawaza kitu gani hadi ukakosa 

usingizi? 

 “Ninawaza mambo mengi kuhusu 

maisha yangu ya mbele.Ninawaza kuhusu 

kuwa na familia na kuwa na watoto wawili..ninawaza mambo mengi 

sana,biashara nakadhalika” 

 “ Pole sana Pauline,hupaswi kuwa na 

mawazo mengi namna hiyo hadi ukakosa 

usingizi.Kitu cha muhimu ni kuwa na 

malengo na mipango ya kuweza kuyafikia 

malengo hayo.” 

 “David wewe una malengo gani kuhusu 

maisha yako ya mbele? 

 “ Kusema ukweli Pauline sina malengo 

yoyote kwa sasa kwa sababu maisha 

yangu yalibadilika na ndoto zangu zote 

zikapotea pale nilipokwenda 

gerezani.Kwa sasa ninachokifikiria katika 

akili yangu ni kumfanyia kazi mzee 

Zakaria na baada ya biashara zake 

kusimama na kuwa katika hali nzuri basi 

nitajua nini cha kufanya.” Akasema David 

 “ will you leave us? Akauliza 

Pauline.David akatabasamu na kusema 

 “ I don’t know,but I’m happy here.I feel 

like I’m home” akasema David na 

kumfanya Pauline atabasamu 

 “Pauline niambie kuhusu mama yako 

mdogo.Ni mtu mwenye tabia zipi? 

Akauliza David  “Mama mdogo ni mtu ambaye anapenda 

sana starehe.Anapenda maisha ya kifahari 

sana ,nadhani hata wewe mwenyewe 

umemuona.Anapenda kuvaa mavazi ya bei 

ghali na hata maisha yake anataka yawe ya 

namna hiyo.Ni kutokana na aina ya maisha 

anayoyataka ndiyo maana amekikuwa 

akitumia fedha nyingi sana kila siku ,na 

hivyo kusababisha biashara zetu 

kuyumba.Ni mtu ambaye anapenda sana 

kujilimbikizia mali na si mkweli.” 

Akasema Pauline 

 “ Umewezaje kuishi naye? Akaulzia 

David 

 “ Mimi nimeweza kuishi naye kwa 

sababu simfuatilii.I’m busy with my 

business.Hapo awali niliwahi kumuonya 

baba kuhusiana na tabia za ufujaji fedha 

za mama mdogo lakini hakunisikia ndipo 

nilipamua kuachana kabisa na kusimamia 

miradi ya familia nikaelekeza nguvu 

katika biashara zangu.Mama mdogo 

akautumia mwanya huo kuanza kufuja 

atakavyo hadi baba akapatwa na ugonjwa 

huu wa moyo kutokana na kuwa na 

mawazo mengi sana.Lakini haya yote yamesababishwa na kutotaka kunisikiliza” 

akasema Pauline 

 “ Pauline naomba unisikilze kwa 

makini’ akasema David 

 “ Nakusikiliza” 

 “Pauline mimi ni mgeni tu katika 

familia yenu na sifahamu baba yako 

amehangaika kiasi gani hadi akaipata mali 

hii aliyonayo leo.Mimi kama mtu ambaye 

ameniamini na kunikabidhi jukumu la 

kuzisimamia biashara zake nitaifanya kazi 

hii kwa juhudi kubwa na uaminifu wa hali 

ya juu sana.Lakini ili kufanikisha hayo 

yote ninahitaji sana sapoti yako.Mimi na 

wewe tunatakiwa tusimame imara katika 

hili.Mimi ni mtu baki na sina nguvu yoyote 

lakini endapo nitakuwa na wewe nitapata 

nguvu na kila kitu kitakwenda 

vizuri.Pauline usikubali hata kidogo mali 

alizohangaikia baba yako zipotee bure 

mikononi mwa watu.Mali hizi ni za kwako 

kwa hiyo unatakiwa usimame imara 

kuzilinda dhidi ya mfujaji yeyote Yule.” 

Akasema David 

 “ david mimi niko tayari kwa lolote na 

ninakuahidi kwamba nitafanya nawe kazi bega kwa bega na wala usihofu chochote” 

akasema Pauline huku akitabasamu 

 “Nafurahi kusikia hivyo.Kama 

alivyoelekeza mzee kazi ya kwanza 

ambayo natakiwa kuifanya ni kuanza 

kupitia biashara moja baada ya nyingine 

na kujua mwenendo wake na kama 

itaonekana haina faida basi nitamshauri 

mzee tuiondoe.Hakuna haja ya kuwa na 

biashara nyingi ambazo zinakuwa mzigo 

katika kuziendesha” 

 “ Hilo ni wazo zuri sana David.hata 

mimi niliwahi kumsahuri hivyo baba 

lakini akawa mkali na hakutaka 

kunisikia.Itakuwa vyema kama 

utamshauri tuzipunguze biashara ambazo 

hazina faida” akasema Pauline 

 “Pauline muda umekwenda sana ni 

wakati wa kwenda kupumzika “ akasema 

David na kisha kila mmoja akaelekea 

chumbani kwake 

*********************************** 

 Chumba kina mwanga hafifu wa bluu na 

muziki laini ulisikika kwa mbali.Ni saa nne 

za usiku Mwalimu Lucy akiwa chumbani kwake amejilaza kitandani.Toka amerejea 

nyumbani sura yake imekuwa ni yenye 

tabasamu muda wote 

 “ Robin umeifanya siku yangu kuwa ni 

yenye furaha sana.Sikutegea kama siku 

yangu ingeisha nikiwa na furaha ya ajabu 

namna hii.Ni muda mrefu sana sijawahi 

kuipata furaha ya namna hii” akawaza 

Lucy halafu akainuka kitandani na 

kwenda katika meza yake ndogo akaishika 

saa ndogo nzuri ya kike halafu 

akatabasamu 

 “Thank you so much Robin.Nimeipenda 

zawadi yako” akasema Lucy huku 

akitabasamu 

 “ Ee Mungu kwa nini nisiwe na mtu 

kama Robin katika maisha yangu? Ana kila 

sifa ya mwanaume niliyekuwa nikimuota. 

Nadhani ni wakati sasa wa kusahau 

mambo ya nyuma na kusonga 

mbele.Nitalegeza msimamo wangu kidogo 

na kujiweka karibu na Robin kwa sababu 

anaonekana kuwa ni mwanaume wa 

tofauti kidogo “ akawaza Mwalimu lucy 

***********************************  Saa nne za asubuhi siku ya jumapili 

Pauline na David waliwasili katika kanisa 

kuu la kiaskofu jijini Arusha kwa ajili ya 

kuhudhuria ibada.Ilikuwa ni furaha 

kubwa kwa Pauline baada ya kugundua 

kwamba David alikuwa ni muumini wa 

dhehebu la kikatoliki kama walivyokuwa 

wao 

 Ibada ilimalizika saa saba za mchana na 

baada ya kusalimiana na watu kadhaa 

anaofahamiana nao,Pauline akamuongoza 

David garini lakini kabla ya kuliondoa gari 

akasema 

 “ David nina wazo moja” 

 “ Wazo gani Pauline 

 “Ulipanga kwenda ofisini baada ya 

kutoka katika ibada “ 

 “ Ndiyo Pauline.Nimepanga nikaanze 

kupitia baadhi ya taarifa za miradi na 

kuifahamu vyema.Natafuta sehemu ya 

kuanzia kumshauri mzee kuhusu biashara 

zake kwa hiyo natakiwa kuifahamu vyema 

kila biashara namna inavyoendeshwa” 

akasema David 

 “That’s good.Lakini ninaonelea 

ingekuwa vyema kama kazi hii ungeianza 

siku ya kesho.Tuitumie siku ya leo kupumzika na kufurahi.Let’s go 

somewhere and have fun” akasema 

Pauline 

 “ Sawa Pauline hakuna tatizo” akajibu 

David kisha wakaondoka na kuelekea 

katika hoteli moja ya kitalii iliyoko 

Ngaramtoni.Ilikuwa ni hoteli yenye 

mandhari ya kupendeza na kuvutia 

mno.Walipokewa kwa bashasha na 

wahudumu wachangamfu wenye 

kuifahamu vyema kazi yao. 

 “ Huwa napenda sana kuja kupumzika 

huku kila mwisho wa wiki.Kuna hewa safi 

na utulivu wa kutosha na hata huduma zao 

ni nzuri sana” akasema Pauline wakati 

wakisubiri chakula walichoagiza kiwe 

tayari 

 “Ni sehemu nzuri hata mimi 

nimeipenda sana.Huwa unakuja 

mwenyewe? Akauliza David 

 “ Hupenda kuja mwenyewe lakini mara 

nyingi huja na rafiki zangu” 

 “ Pauline kuna kitu ninataka kukuuliza” 

akasema David 

 “ Uliza David usihofu” 

 “Ndugu zako wengine wako wapi? Toka 

nimefika pale kwenu sijawahi kumuona ndugu yako yeyote Yule na wala sijasikia 

mtu yeyote akizungumzia habari za ndugu 

zako.” Akasema David na pauline akavuta 

pumzi ndefu 

 “ wazazi wangu walibahatika kuwa na 

watoto wawili tu.Mimi na mdogo wangu 

Michael.Kwa bahati mbaya yeye 

amekwisha fariki” akasema Pauline na 

kuinama chini 

 “ dah ! pole sana Pauline” 

 “ ahsante David.Kwa hivi sasa mimi 

ndiye mtoto pekee niliyebaki wa mzee 

Zakaria” 

 “Ilikuaje hado akapoteza maisha? 

Akauliza David.Pauline akachukua glasi ya 

maji akanywa halafu akamtazama David 

usoni na kusema 

 “David ,dunia hii imejaa maajabu 

makubwa na kuna vitu ambavyo vinatokea 

na ni vigumu kuamini hadi uvishuhudie 

kwa macho yako.” Pauline akanyamaza 

kana kwamba kuna kitu anakikumbuka 

halafu akasema 

 “Michael alifariki kwa kuangukiwa na 

chuma cha mazoezi wakati akifanya 

mazoezi .Huwa ninaumia sana kila 

nikumbukapo tukio hili.Nilimpenda sana Michael na kifo chake kimeacha pengo 

kubwa kwangu” 

 “ Pole sana Pauline.samahani kama 

nimekukumbusha machungu ya kufiwa na 

ndugu yako” 

 “ Usijali David.Ninajitahidi kadiri 

niwezavyo kuizoea hali hii japokuwa kuna 

kitu kimoja ambacho kinaniumiza kichwa 

changu na kuyafanya maisha yangu yakose 

furaha” 

 “ Jambo gani hilo Pauline? Unaweza 

ukaniambia? 

 Pauline akafikiri kidogo na kusema 

 “ Ni kuhusu hii siku ya Septemba 11.” 

 “ Septemba kumi na moja?!!!!....David 

akauliza kwa mshangao 

 “ Ndiyo” akajibu Pauline huku 

akishangaa namna David alivyostuka 

.Mara simu yake ikaita 

 “ Hallow Genevive” akasema Pauline 

baada ya kupokea simu 

 “Pauline uko wapi we mtoto wa kike? 

Ikauliza sauti ya upande wa pili 

 “ Niko huku Songera hoteli.Wewe uko 

wapi? 

 “Niko hapa mjini kati na Tamia.Uko na 

nani?  “Niko na David.” 

 “ David !!!!!..David yupi tena? Genevive 

akashangaa 

 “Hauwezi kumfahamu .Njooni huku 

mtakuja kumfahamu akasema Pauline na 

kukata simu akaiweka mezani 

 “ Rafiki zangu Genevive na 

Tamia.Wanakuja hapa muda si 

mrefu.wanataka wakufahamu” akasema 

Pauline na kumfanya David atabasamu 

 “Pauline kabla hujapokea simu kuna 

kitu uliniambia kuhusiana na tarehe hii ya 

septemba kumi na moja” 

 “ Ndiyo David.Sifahamu imetokeaje 

lakini tarehe hii kila mwaka imekuwa ni 

siku ambayo naweza kusema ni mbaya 

kwa familia yangu.Sielewi kuna 

mahusiano gani kati ya tarehe hii na 

familia yangu japokuwa sina imani katika 

mambo ya kichawi na waganga lakini nina 

wasi wasi lazima kuna mahusiano fulani 

yasiyo ya kawaida kati ya tarehe hii na 

familia yangu.Ninasema hivyo kwa 

sababau katika tarehe kama hiyo mama 

yangu alifariki dunia baada ya kuanguka 

toka ghorofani.Mwaka uliofuata mchumba 

wangu ambaye nilitegemea kufunga naye ndoa alifariki dunia baada ya kupigwa 

risasi na majambazi waliovamia benki 

aliyokuwamo.Katika tarehe kama hiyo 

tena mdogo wangu alifariki dunia kwa 

kuangukiwa na chuma cha mazoezi na 

mwaka huu kama si wewe basi ninaamini 

hata baba yangu angefariki kwa ajali 

ambayo ingemtokea.Siku ile nilikuwa 

nimekaa ndani na sikutaka kwenda 

sehemu yoyote.Hata pale uliponipigia 

simu kwa kutumia simu ya baba nilisita 

kupokea nikihofia kuwa huenda kukawa 

na taarifa mbaya.Nusura nichanganyikiwe 

pale uliponiambia kwamba baba 

amelazwa hospitali.Toka nilipokuwa na 

umri wa miaka kumi na tano mambo haya 

yamekuwa yakijitokeza kila mwaka tarehe 

kama hiyo.yalianza kwanza matukio ya 

maduka kuungua ,magari kupata ajali 

lakini kwa miaka ya hivi karibuni 

yamefuatana matukio ya vifo .Sielewi nini 

kitatokea mwaka unaokuja katika tarehe 

hiyo. I don’t know who will be next.Hili ni 

jambo linalonifanya niishi kwa mashaka 

makubwa na kila mwaka unapofika 

mwezi septemba basi raha yote ya maisha 

hupotea kila nikiikumbuka tarehe hiyo.Mpaka leo hii hatujawahi kukaa kama 

familia na kuliongelea suala hili na kwa 

nini tarehe hii imekuwa ikituletea 

majanga kila mwaka.Ninatamamni 

kumuuliza baba lakini 

ninaogopa.Nimekwambia haya kwa 

sababu wewe ni mtu ninayekuamini na 

nina imani hutamweleza mtu yeyote 

kuhusiana na mambo haya yanayoendelea 

katika familia yetu kwa sababu ni mambo 

ya ndani ya kifamilia” akasema Pauline 

Uso wa David ulikuwa umeloa jasho na 

alionekana kubadilika sana. 

 “David whats wrong?Are you ok? 

Akauliza Pauline baada ya kuona namna 

David alivyoonyesha mabadiliko ya ghafla 

 “Samahani Pauline .Ninakuja sasa 

hivi,naelekea maliwatoni” akasema David 

na kuinuka akaelekea maliwatoni 

 “ Nini kimempata David? Mbona 

kabadilika ghafla baada ya kumweleza 

mambo yanayotokea katika familia yetu 

kila mwaka? Au ameingiwa na woga? 

Akawaza Pauline na mara kwa mbali 

akawaona rafiki zake Genevive na Tamia 

wakijongea huku nyuso zao zikiwa na 

tabasamu  David aliingia maliwato na kusimama 

katika kioo cha kujitazamia.Akachukua 

kitambaa na kujifuta jasho kisha akavuta 

pumzi ndefu 

 “Septemba kumi na moja..!!!!!!!” 

akasema taratibu na kwa sauti ndogo 

 Pauline amekitonesha kidonda 

kilichoanza kupona.Siku hii hata kwangu 

pia imekuwa ni ya majanga 

makubwa.Mama yangu alifariki katika 

tarehe hiyo.NI katika tarehe hiyop 

nilihukumiwa kifungo gerezani na katika 

tarehe kama hiyo nikaachiwa huru.tarehe 

kama hiyo nimejikuta katika familia ya 

akina Pauline ambayo nayo imekuwa 

ikiandamwa na majanga kila mwaka 

katika tarehe hiyo.Kuna nini katika tarehe 

hii? Kuna mahusiano gani kati yangu mimi 

na tarehe hii? “ akawaza David halafu 

akajifuta jasho 

 “lazima kuna kitu kilichojificha nyuma 

ya tarehe hii.Ni tarehe ambayo hata katika 

kalenda ya dunia imekuwa na matukio ya 

ajabu ajabu..I’m so confused” akawaza na 

mara akasikia vishindo vya mtu akija kule 

maliwatoni akajifuta jasho na kujiweka vizuri halafu akatoka na kurejea kule 

mezani alikomuacha Pauline 

 Mezani pale kuliongezeka wasichana 

wawili 

 “ Hi ladies” David akawasalimu na 

wakaitika kwa pamoja na kumfanya David 

atabasamu kutokana na sauti zao nyororo 

walikuwa ni mabinti warembo sana 

 “Ladies,huyu hapa ni David.Anaishi 

nyumbani kwetu na kuanzia sasa ndiye 

atakayekuwa meneja wetu mpya kwa hiyo 

ni mtu ambaye tutakuwa naye mara nyingi 

“ Pauline akafanya utambulisho 

 “Dvid hawa ni rafiki zangu 

wakubwa.Huyu hapa anaitwa genevive 

,anafanya kazi Exim bank na huyu hapa 

anaitwa Loveness lakini sisi tumezoea 

kumuita kwa jina la Tamia.Anafanya kazi 

katika shirika moja la ndege hapa 

Arusha.Ni watu ambao utazoea kuwaona 

mara wa mara.Muda mwingi huwa 

tunakuwa pamoja kama hivi” akasema 

Pauline.Huku akitabasamu David 

akainuka na kuwapa mikono akina 

Genevive 

 “ Nimefurahi sana kuwaona.” Akasema 

David  “Hata sisi tuemfurahi sana kukutana 

nawe.Sisi sote unaotuona hapa ni marafiki 

wa muda mrefu toka tukiwa shule ya 

msingi, sekondani na hadi sasa bado tuko 

pamoja.” Akasema tamia binti mfupi 

mweupe sana na mwenye umbo 

dogo.Alizipunguza nywele zake na 

kumfanya awe mrembo zaidi.Genevive 

yeye alikuwa ni mrefu wastani na 

mwembamba. 

 “ Pauline mbona hujatuweka wazi david 

ni nani wako? Ni ndugu yako? Tuweke 

wazi tufahamu” akasema Tamia ambaye 

kwa hulka yake ni muongeaji sana 

 “ Taratibu Tamia.Hayo mambo 

mengine unayotaka kuyafahamu 

hayakuhusu” akasema Pauline na wote 

wakacheka ,wakaendelea na vinywaji na 

maongezi.wakati maongezi yamekolea 

Tamia akamuita Pauline pembeni 

 “ Pauline naomba uniweke wazi shoga 

yangu,David ni nani wako? Niambie 

tafadhali” akasema Tamia 

 “Kwa nini unataka kufahamu Tamia? 

Nimekwishamtambulisha kwenu 

inatosha.” Akasema Pauline  “ Pauline naomba uniambie “ 

akaendelea kusisitiza Tamia 

 “ kwa nini unataka kumjua david? 

Akauliza Pauline 

 “ Pauline I‘m dying to know.Niweke 

wazi mna mahusiano gani ? 

 “Tamia sintakwambia hadi hapo 

utakaponieleza kwa nini unataka kumjua 

David” 

 “ He’s drivng me crazy.!!! Hapa nilipo 

miguu yangu yote inatetemeka kila 

nikimtazama.Ouh Pauline David is so 

handsome.I think I’m fallng in love with 

him” akasema tamia na kumstua pauline 

 “Stupid ..!! Falling in love? 

 “ Yes Pauline..dont yopu know about 

love at first sight?Nilipomuona tu David 

moyo wangu ulistuka nikasisimka mwili 

mzima.Pauline david is the man I’ve been 

waiting for.Pleas……………..” tamia 

hakumaliza alichotaka kukisema Pauline 

akamkatisha 

 “Stop Tamia..Tafadhali Usianze mchezo 

wako kwa David.Tamia hupitwi na 

mwanaume mzuri.!! Safari hii nakuonya 

chezea wanaume wengine wote lakini si 

David.Hauna mapenzi ya kweli and all you think is money” akasema Pauline kwa 

ukali kidogo. 

 “ Pauline this time its for real.I real feel 

love.Please understand me Pauline” 

akasema Tamia 

 “Tamia wewe ni rafki yangu kipenzi 

lakini usitake urafiki wetu ukaingia katika 

mgogoro kwa sababu ya David.Be careful” 

akasema Pauline na kuanza 

kuondoka.Tamia akamshika mkono 

 “ Niambie Pauline.Mna uhusiano wa 

kimapenzi na David.Tell me and I’ll 

understand” akasema tamia.Pauline 

akamtazama kwa macho makali na 

kusema 

 “Awe wangu ,asiwe wangu tafadhali 

sitaki upuuzi wako kwa david,umenisikia 

Tamia?Akasema kwa ukali pauline na 

kuondoka 

 “ Pauline hawezi kunizuia kufanya kitu 

ambacho moyo wangu 

unakipenda.Nimetokea kumpenda david 

ghafla na nitafanya kila niwezalo nimpate 

hata kama itanilazimu kuuvunja urafiki 

wetu niko tayari kwa hilo” akawaza Tamia 

na kurejea mezani  Saa moja za jioni wakarejea nyumbani 

wakamsalimu mzee Zakaria na baadae 

wote wakajumuika katika chakula cha 

usiku 

 “ David kesho unaanza kazi rasmi” 

akasema mzee Zakaria baada ya kumaliza 

kula 

 “ Ndiyo mzee .Kesho naanza rasmi 

majukumu yangu” akasema David 

 “nakutegemea sana David.” Akasema 

mzee Zakaria 

 “ Usihofu mzee,nitafanya kazi hii kwa 

uwezo wangu wote” 

 “nafurahi kusikia hivyo kijana 

wangu.kama nilivyokuelekeza kwamba 

uanze kuipitia miradi yote halafu ufanye 

ukaguzi wa kina na kisha unishauri nini 

tufanye” 

 “Nitafanya kama ulivyoniagiza mzee” 

akasema David halafu mzee zakaria 

akawatakia usiku mwema na yeye na 

mkewe wakaeleke chumbani kwao.David 

na Pauline nao kila mmoja akaelekea 

chumbani kwake. 

 Akiwa amejilaza kitandani akitafakari 

namna atakavyoianza siku ya kesho mara 

kengele ya mlango wake ikalia.Akainuka na kwenda kuufungua mlango .Alihisi 

miguu ikimtetemeka alipokutanisha 

macho na Vicky 

 “ You again !!!!..akasema David na mara 

mlango wa chumba cha Pauline nao 

ukafunguliwa .David kijasho kikamtoka. 

 Kama ilivyokuwa kwa David,Vicky naye 

akaonyesdha mstuko wa dhahiri baada ya 

kuusikia mlango wa chumba cha Pauline 

ukifunguliwa.Akageuka na kugonganisha 

macho na Pauline ambaye naye alikuwa 

anashangaa.Hakutegemea kumuona 

mama yake mdogo mahala pale mida ile. 

 “ Mama mdogo ! Mbona uko huku mida 

hii? Kuna tatizo gani? Hali ya baba 

imebadilika? Akauliza Pauline kwa wasi 

wasi 

 “Hapana Pauline .Baba yako anaendelea 

vizuri.Leo mchana katika pita pita zangu 

niliiona suti moja nzuri nikaona ni vyema 

kama nikimchukulia David.Nilisahau 

kumpatia wakati ule hivyo nimeona siwezi 

kulala bila kumletea ili aivae siku ya 

kesho.He’s our new manager so he have to 

look like a real manager on his first day.” 

Akasema Vicky halafu akamgeukia David  “David mzigo wako huu .Nina imani 

sijakosea vipimo .Usiku mwema” akasema 

Vicky huku akimpatia David mfuko 

uliokuwa na nguo na kuondoka.David na 

Pauline wakabaki wamesimama 

wakimsindikiza kwa macho hadi 

alipopotea kisha wakatazamana 

 “ Sorry David kwa usumbufu.Mama 

mdogo huwa yuko namna hiyo.Unatakiwa 

umfahamu na umzoee.” Akasema Pauline 

 “ Nitajitahidi Pauline” akajibu David 

 “ Haya David usiku mwema.Nenda 

kalale” akasema Pauline huku akipiga 

hatua kuelekea katika kibaraza ambacho 

hupenda kukaa nyakati za usiku na hasa 

anapokosa usingizi.David alifumbua 

mdomo na kutaka kusema neno lakini 

akaogopa akaufunga mlango na kuingia 

chumbani ,akautupa mfuko ule aliopewa 

na Vicky kitandani. 

 “ Huyu mama anatafuta kitu gani 

kwangu? Jana aliniletea nguo za kulalia na 

leo hii tena ameniletea suti.Mbona 

simuelewi ana lengo gani na 

mimi?Kinachonishangaza zaidi ni kwamba 

amekuwa anakuja kwa wakati ambao 

watu wote wamekwisha lala.Gosh ! I’m confused” akawaza David na kukaa 

kitandani 

 “ Itabidi nimweleze ukweli kwamba 

siipendi tabia yake hii ya kuja kunigongea 

usiku wakati watu wote wamelala.Kama 

kuna kitu anataka kunipatia basi anipatie 

wakati watu wote hawajalala na 

wakishuhudia.Tabia yake hii inaweza 

ikaleta udadisi kwa watu.Niliuona 

mshangao aliouonyesha Pauline.Hii si 

picha nzuri hata kidogo na sijaipenda” 

akawaza David halafu akaufungua mfuko 

ule na kutoa suti nzuri ya rangi ya kahawia 

akaijaribisha na kutabasamu 

 “hakukosea kabisa vipimo.Utadhani 

alinipima kwanza kabla ya kwenda 

kununua” akasema David kwa sauti ndogo 

huku akijitazama katika kioo 

 “Ni suti nzuri sana na ya gharama 

kubwa hata mimi nimeipenda.Tatizo 

linakuja je niivae au nisiivae hiyo kesho 

kama alivyosema? Akajiuliza David halafu 

akatazama juu akatafakari kwa muda 

 “ Ninawekwa katika majaribu 

makubwa.Endapo nisipoivaa huyu mama 

anaweza akakasirika na kuona kama 

nimemdharau.Yawezekana labda ana lengo zuri tu la kutaka nipendeze 

nionekane nadhifu.Itabidi niivae tu ili 

nimridhishe” akawaza David 

 Pauline alikuwa ameegemea nguzo ya 

kibaraza akitazama juu angani.Kitendo 

cha kumuona mama yake mdogo mlangoni 

kwa David kilimpa maswali mengi . 

 “ Bado simaini kama ile suti mama 

mdogo aliyomnunulia David ndiyo 

ilimfanya akamgongee mlango wakati 

watu wote wamelala.Kwa nini hakumpa 

mapema kama lengo lake lilikuwa 

zuri?Ninalazimika kuanza kuwa na wasi 

wasi kuhusiana na nyendo za mama 

mdogo na huu ukaribu anaoutafuta kwa 

David.Ninazifahamu tabia zake si nzuri 

hata kidogo na kuna tetesi niliwahi 

kuzisikia japo sijazithibitisha kwamba si 

mwaminifu katika ndoa yake na kwamba 

katika safari zake mbali mbali za kwenda 

nje ya nchi amekuwa akitoka nje ya ndoa 

yake.Amekuwa akitembea na vijana 

wadogo wadogo.kama tetesi hizi ni za 

kweli basi atakuwa anatafuta ukaribu na 

David ili aweze kuuendeleza uchafu 

wake.Nashawishika kuamini hivyo kwa 

sababu mwanzoni hakutaka kabisa kumona David hapa nyumbani lakini 

baada tu ya kumuona namna 

alivyobadilika na kupendeza ghafla 

anaanzisha ukaribu na kuanza 

kumnunulia hadi nguo.lazima kuna kitu 

anakitafuta lakini 

hatakipata.Nitapambana naye” akawaza 

Pauline halafu akarejea ndani.Alipofika 

usawa wa chumba cha david akasimama 

akautazama mlango ule kana kwamba 

anataka kugonga na mara akastuka 

 “ Gosh ! I’m going crazy.Nitaonekanaje 

iwapo nitakutwa nimesimama nje ya 

mlango wa David” akawaza Pauline na 

kupiga hatua kuelekea chumbani kwake 




Kumekucha siku ya jumatatu.Saa tatu 

za asubuhi tayari Pauline na David 

walikuwa ofisini.Ni siku ya kwanza ya 

David ofisini kama msimamizi mkuu wa 

biashara zote za mzee Zakaria.Siku hii 

alikuwa amependeza sana akiwa ndani ya 

suti nzuri ya gharama kubwa 

aliyonunuliwa na Vicky.  Kazi ya kwanza ambayo alianza nayo ni 

kupitia taarifa za fedha za miradi yote na 

kisha afanye ukaguzi wa mali yote iliyopo 

na thamani yake. 

 Alianza kwanza kwa kulipitia faili lenye 

taarifa za fedha za supermarket na wakati 

akiendelea na zoezi hilo Pauline 

akaondoka ,akaelekea katika biashara 

zake kwa ahadi ya kurejea mchana kwa 

ajili ya kwenda kupata chakula 

pamoja.Wakati David akiendelea kupitia 

taarifa zile za kifedha mara mlango 

ukafunguliwa,akafikiri ni sekretari 

ameingia lakini alipoinua kichwa 

akajikuta akipata mstuko baada ya 

kugonganisha macho na Vicky mke wa 

mzee Zakaria.Siku hii ya leo alivaa suruali 

nyekundu na shati jeupe .Alikuwa 

amesimama mbele ya David huku 

akitabasamu 

 “Hallow David “ akasema Vicky 

 “ mama ..!! karibu “ akasema David kwa 

kubabaika 

 “ Vicky..Call me Vicky..Usiniite mama 

labda tukiwa mbele za watu au mbele ya 

mzee Zakaria.Lakini tukiwa sisi wawili 

pakee just call me Vicky au madam Vicky.Mtaani ninajulikana kama Vicky 

madhahabu kwa hiyo nitafurahi nawe 

ukiinita kwa jina hilo au ukishindwa basi 

niite madam Vicky” akasema Vicky huku 

akisogea na kukaa juu ya meza 

 “ Wow ! umependeza sana David.You 

look like a manager” akasema Vicky huku 

akitabasamu lakini David hakujibu 

kitu.Kimya kikapita hapo ofisini wote 

wakiangaliana na Vicky akasema 

 “ David nafikiri Pauline na baba yake 

hawakukuonyesha ofisi yangu ilipo” 

 “ Ndiyo madam.Pauline aliniahidi 

kunipeleka siku yoyote ndani ya wiki hii” 

akajibu Pauline 

 “ Sawa David nimekuja kukuchukua 

ukaifahamu ofisi yangu na ujue namna 

biashara ya madini inavyofanyika.” 

Akasema Vicky.Davidi akaonyesha 

wasiwasi Fulani 

 “ madam kwa nini tusifanye iwe siku 

nyingine? Nina kazi nyingi sana za kufanya 

leo hii.Ni siku yangu ya kwanza hapa 

kazini” akasema David 

 “Ouh my dear David,usihofu kuhusu 

kazi.Hata hii nayo ni sehemu ya kazi.You 

are a manager now kwa hiyo unatakiwa ufahamu kila kitu 

unachokisimamia.Hatutachukua muda 

mrefu ninakwenda kukuonyesha mara 

moja na kukurudisha uendelee na kazi 

zako” akasema Vicky.Kwa shingo upande 

David akakubali kuongozana naye kwenda 

kulitazama duka lake.Waliingia katika 

gari la kifahari la Vick wakaondoka 

 “ Lazima utaingia katika mtego wangu 

tu na ukishaingia hautatoka kamwe.Mimi 

ndiyo Vicky madhahabu 

bwana.Nitakutumia 

nitakavyo.Utaniridhisha kila pale 

nitakapokuhitaji.Utanisaidia kuikamilisha 

mpango wangu mkubwa nilioupanga. 

Akawaza Vicky wakiwa garini wakieleka 

katika ofisi yake 

 Walifika ofisini kwa Vicky ,David 

akaonyeshwa namna shughuli za ununuzi 

na uuzaji wa madini 

zinavyofanyika.Ilikuwa ni ofisi nzuri sana 

na ya kuvutia. 

 “ David ni saa saba za mchana sasa .Its 

lunch time.Twende tukapate chakula 

kabla ya kurejea ofisini kwako.” Akasema 

Vicky.David akasita.  “ Mbona una wasi wasi David? Hutaki 

kwenda kula chakula na mimi? 

Unaniogopa? 

 “ Si hivyo Madam.Nilikuwa na miadi na 

Pauline kwamba anipitie mchana huu 

twende wote tukapate chakula.” 

 “Ouh kumbe ni hilo tu 

linalokusumbua.Usiogope David.Pauline 

ni mtu wako wa karibu na utakuwa naye 

muda mrefu tofauti na mimi ambaye 

hatutakuwa tukionana mara kwa 

mara.Kama meneja wetu mpya nahitaji 

kukufahamu japo kidogo tu kwa hiyo 

nitafurahi iwapo utakubali kwenda kupata 

nami chakula cha mchana leo hii.”akasema 

Vicky.David akashindwa kukataa na 

kuingia garini wakaelekea sehemu 

ambayo Vicky alitaka wakapate chakula 

 “ Taratbu tu utaingia mwenyewe katika 

ndoano yangu.” Akawaza Vicky wakiwa 

wamesimama katika mataa wakisubiri 

kuruhusiwa kuondoka.Mara simu ya 

David ikaanza kuita na kumstua Vicky 

ambaye aligeuza shingo na kumtazama. 

 “Pauline huyu ananitafuta” akasema 

David  “Usipokee simu.Iache iite na ikikata 

izime kabisa.Nitaongea naye mimi na 

kumfahamisha kila kitu” akasema 

Vicky.Simu ikaita hakuipokea na 

ilipokatika David akaizima simu yake 

kama alivyoelekezwa na Vicky 

 “Sikujua kama una simu David” 

akasema Vicky 

 “ Pauline alininunulia kwa ajili ya 

mawasiliano” 

 “Vizuri sana.Niandikie namba zako za 

simu katika simu yangu” akasema Vicky 

huku akimpa David simu yake amuandikie 

namba 

*********************************** 

 Saa saba za mchana Pauline akafika 

ofisini kwa baba yake ambako ndiko David 

anafanyia kazi.Walikuwa wamekubaliana 

kwamba ampitie mchana huo kwa ajili ya 

kwenda kupata chakula cha mchana.Kitu 

cha kushangaza Pauline hakumkuta David 

ofisini. 

 “ David kaelekea wapi? Akamuuliza 

sekretari wa ofisi ile  “Hakuniambia ni wapi anaelekea lakini 

alitoka hapa akiongozana na madam 

Vicky.” 

 “ Vicky ..!!? akashangaa Pauline 

 “ Ndiyo.Madam Vicky alikuja hapa na 

akaondoka na David” 

 “ Wameelekea wapi? Kwa nini David 

asinifahamishe kama kuna mahala 

amekwenda kwa dharura?Mama mdogo 

anatafuta nini kwa David. Akawaza 

Pauline halafu akatoa simu yake na 

kumpigia David.Simu ilita bila 

kupokelewa na alipojaribu kupiga kwa 

mara ya pili haikuwa ikipatikana tena. 

 “ whats wrong with him? Akajiuliza 

Pauline halafu akazitafuta namba za simu 

za mama yake mdogo akampigia.Simu 

ikaita lakini haikupokelewa.Akapiga mara 

ya pili na ya tatu lakini simu 

haikupokelewa.Pauline akahisi kama 

nguvu zinaanza kumuisha na kwa mbali 

machozi yakaanza kumlenga. 

 “ David na mama mdogo wako wapi? 

Kwa nini hawataki kupokea simu ? 

akajiuliza lakini hakupata jibu. 

*****************************  Bango kubwa lenye maandisi makubwa 

CHINESE RESTAURANT katika geti la 

kuingilia yalimuashiri a David kwamba 

walikuwa wakielekea hapo katika hoteli 

ya kichina 

 “ David umewahi kula chakula cha 

kichina? Akauliza Vicky 

 “ Hapana Madam.” Akajibu David 

 “Leo nataka ujaribu kuonja kidogo uone 

ladha yake.” Akasema Vicky wakati 

akiegesha gari.Sura zilizoonekana hapa ni 

za watu toka bara asia na watu wenye asili 

ya afrika walikuwa wawili tu David na 

Vicky. 

 “ Huwa ninasafiri sana kwenda nchini 

China kununua bidhaa kwa hiyo 

ikanilazimu kujifunza kula chakula cha 

kichina.” Akasema Vicky .Muhudumu 

akafika mara moja akaagiza Chinese 

Chicken salad kwa wote wawili. 

 “ David nimekuleta hapa ili tupate 

chakula pamoja na kuzoeana.Najua mpaka 

hivi sasa utakuwa na mitazamo mingi 

kuhusiana na mimi na ndiyo maana 

umekuwa ukiniogopa .Naomba usisikie 

maneno ya mtu yeyote atakayekwambia kwamba mimi ni mtu mbaya na 

katili.Mimi ni mtu mzuri sana kwa Yule 

mtu anayeendana na mimi lakini kwa Yule 

ambaye hatuendi sawa lazima ataniona ni 

mtu mbaya.Utanifahamu vizuri na 

utakubaliana na haya nikwambiayo” 

akasema Vicky ,akala kidogo na kisha 

akamtazama David 

 “ David sifahamu mahala ulikotoka na 

kwa nini ulipata matatizo yale ya 

kufungwa gerezani lakini kwa 

kukutazama unaonekana ni kijana 

mwenye kiu ya mafanikio 

makubwa.Ninasema uongo? Akauliza 

Vicky.Huku akitabasamu David akasema 

 “ Ni kweli Madam.Hakuna mtu yeyote 

katika dunia hii asiyependa mafanikio.” 

 “ Sawa kabisa.Kijana kama wewe 

unatakiwa uwe na maisha yako 

mazuri,uwe na nyumba nzuri ,gari zuri la 

kutembelea,fedha ya kutosha 

nakadhalika.Nina damira ya kukusaidia 

David ili uweze kuyafikia hayo yote kama 

unayahitaji.” 

 “ real ? akauliza David ambaye 

alionyesha kuanza kuvutiwa na maongezi 

yale ya Vicky  “Kweli kabisa David.wewe si kijana wa 

kwanza mimi kumsaidia kufikia mafanikio 

anayoyahitaji.Nimewasaidia vijana wengi 

kama wewe na kwa sasa kila mmoja ana 

miradi yake na wanaishi maisha mazuri 

sana.Hata wewe nitakusaidia lakini 

nitafanya hivyo iwapo tutakubaliana kwa 

mambo flani flani” akasema Vicky 

 “Madam una maanisha nini unaposema 

mambo Fulani Fulani? Ni mambo gani 

hayo ambayo unataka kukubaliana na 

mimi? 

 “usiwe na haraka David utafahamu kila 

kitu ila naomba ufahamu kwamba nina nia 

ya dhati ya kutaka kukusadia ili uweze 

kuwa na maisha mazuri na ujitegemee 

wewe mwenyewe na si kuendelea kufanya 

kazi kwa watu kama hivi unavyofanya kwa 

mzee Zakaria na kusubiri kulipwa 

mshahara mwisho wa mwezi.Vijana wengi 

waliokuwa wakifanya kazi kwa mzee 

Zakaria ni mimi ndiye nilyewafumbua 

macho na kuwasaidia.Hivi sasa ni watu 

matajiri huko waliko.Mzee Zakaria ni mtu 

ambaye hapendi kuona mafanikio ya watu 

wengine na hupenda kujinufaisha kwa 

jasho la wengine.Utamfanyia kazi kubwa lakini mwisho wa siku anaweza 

akakufukuza kama mbwa na usiambulie 

chochote.Hii ni sababu ambayo ilimfanya 

hata mwanae Pauline aamue kuanzisha 

biashara zake mwenyewe.Kama kijana 

unayeonekana msomi na mwenye kiu ya 

maendeleo nataka nikufumbue macho ili 

usizubae na kufa masikini.Wakati ndio 

huu wa kuyatengeza maisha yako” 

akasema Vicky 

 “ Taratibu nimeanza kukuelewa 

Madam” akasema David 

 “ Good.! Napenda vijana waelewa kama 

wewe.Sasa ni hivi ninataka kukufundisha 

mambo mengi ,namna ya kufanya 

biashara,namna ya kutengeneza 

mamilioni ya fedha ndani ya muda 

mfupi,nitakufundisha biashara za 

kimataifa.You’ll be a great man 

David.Nitakufanyia hayo yote kama 

utakubaliana nami jambo moja tu dogo 

sana” akasema Vicky halafu akala chakula 

kidogo na kumgeukia tena David 

 ”David umetoka gerezani na unatakiwa 

kuyajenga maisha yako upya.Muda 

unasonga mbele na haurudi 

nyuma.Niamini nikwambiacho na siku moja utanishukuru kwa msaada 

wangu.Mimi tayari nina maisha mazuri 

,ninapata kila ninachokihitaji,ninauwezo 

wa kwenda kokote nitakapo.Kwa ujumla 

ninaishi yale maisha ninayoyahitaji 

mimi.Lengo langu ni kuwasaidia na 

wengine kama wewe ili waweze kufikia 

malengo yao.Nitakusaidia David lakini 

kwa gharama ndogo sana” 

 David aliyekuwa ameacha kula 

akimsikiliza Vicky akatabasamu na 

kusema 

 “Uko sahihi madam.Ni kweli ninahitaji 

kuyajenga maisha yangu upya.Ninahitaji 

maisha mazuri .Nitashukuru kama 

utanisaidia ili niwe na maisha mazuri 

kama unavyoniahidi” 

 “ nafurahi sana kusikia hivyo 

David.Kwa hiyo uko tayari kukubaliana 

nami kwa kile ninachokitaka? 

 “ Nitaangalia Madam kama ni kitu 

kilicho ndani ya uwezo wangu.” 

 “ Usiogope David.Si kitu kikubwa 

sana.Its just a silence” 

 “ Silence !!..David akashangaa.Vicky 

akatabasamu 

 “ yes I need your silence.”  “ Bado sijakuelewa madam 

unamaanisha nini? 

 “ Iko hivi .Najua umeanza kufanya 

ukaguzi katika miradi yote kama 

ulivyoelekezwa na mzee Zakaria.Kuna 

miradi ambayo nataka usiiguse kabisa 

katika ukaguzi wako.Duka la vito na 

mapambo na ofisi yangu ya kuuza na 

kununua madini ya Tanzanie.Katika ripoti 

yako utaonyesha kwamba kila kitu katika 

miradi hii kinakwenda vizuri na hakuna 

tatizo lolote” 

 David akashusha pumzi na wote 

wakatazamana 

 ‘Can yuou do that for me David? 

Akauliza Vicky 

 “Ninakosa neno la kukuambia Madam” 

akasema David 

 “C’mon David you can do it.A real men 

never scared so be a man.Hi ni fursa yako 

umeipata ya kurekebisha maisha 

yako.Kumbuka hii ni nafasi ya dhahabu na 

siku zote nafasi za dhahabu kama hizi 

huwa haziji mara mbili” akasema Vicky 

 “ Madam umenipa mtihani mgumu 

sana.Naomba unipe muda nifikiri kuhusu 

suala hili halafu nitakujibu”  “ David suala halihitaji muda wa 

kwenda kufikiria.Ni jambo ambalo 

tunatakiwa tulimalize hivi sasa.Ni muhimu 

sana kwangu” akasema Vicky 

 “David akamtazama kwa makini usoni 

na kusema 

 “Kwa nini jambo hili ni muhimu sana 

kwako? Kama nitakubali kusema uongo 

kwa mzee zakaria nahitaji kufahamu kwa 

nini nifanye hivyo unavyotaka nifanye.” 

 “Ouh David you want to know much.Any 

way kwa vile umetaka kujua nitakwambia 

ukweli.Lakini naomba nikutahadharishe 

kwamba ukithubutu kumweleza mtu 

yeyote mambo nitakayokuambia I will kill 

you” akaonya Vicky halafu akaendelea 

 “ Mimi ni mwaname mwenye ndoto na 

malengo.Ni mrembo kama unavyoniona na 

bado umri wangu haujaenda.Mume wangu 

mzee Zakaria umri wake umekwenda sana 

na muda wowote anaweza akafariki dunia 

kwa hiyo yanibidi nifanye mapema 

maandalizi ya maisha yangu ya 

mbele.Ndani ya biashara zile mbili kuna 

manufaa yangu ambayo Zakaria na 

Pauline hawafahamu na ndiyo maana 

sitaki miradi ili iguswe na mtu yeyote.Once they find out what I’m 

doing,I’m finished and all my hard work 

will be for nothing.Hii ndiyo sababu pekee 

inayonifanya nikuombe ufanye hvyo.I 

swear in heaven and earth nitafanya 

maisha yako yawe ya kifahari.A handsome 

guy like you,needs to be a boss in his own 

company” akasema Vicky.David akainama 

akafikiri halafu akasema 

 “ Ok ! Madam.Nitafanya unavyotaka 

lakini tafadhali naomba usiende nje ya 

ahadi zako.Nahitaji unifanyie hayo 

uliyoyasema utanifanyia.Nahitaji kujenga 

maisha yangu na kuishi maisha mazuri 

kama uliyoniahidi.Papo hapo naomba 

utambue kwamba mzee Zakaria 

ameniamini sana na kitendo 

nitakachokifanya ni cha udanganyifu na 

kupoteza uaminifu wangu kwake na 

Pauline na kwa hiyo basi na mimi 

nitakuwa na maombi yangu kwako .Wote 

lazima tunufaike na jambo hili” akasema 

David.Vicky akatabasamu 

 “ Usihofu kuhusu kufaidika 

David.Nimekwisha kuahidi mambo mengi 

mazuri nitakayokufanyia.Nitakufundisha 

namna ya kutengeneza pesa na ndani ya kipindi kifupi utakuwa 

milionea.Nitakufundisha biashara ya 

kimataiafa.Tutakwenda wote hadi China 

na Hong Kong utafahamu namna 

tunavyonunua bidhaa.Mambo mengi 

nitakufanyia na si lazima yote nikwambie 

leo.Mengine yatakuja kama surprise lakini 

naomba tu ufahamu kwamba ndani ya 

kipindi kifupi kijacho you’ll be a 

millionaire” akasema Vicky 

 “ Nafurahi kusikia hivyo 

Madam.Ninaamini kwamba utatimiza 

ahadi zako lakini pamoja na hayo kuna 

mambo ambayo na mimi nitayahitaji toka 

kwako” akasema David .Vicky 

akatabasamu na kuuliza 

 “Ni mambo gani unayohitaji David? 

 “ Nitakwambia lakini si sasa.Kwa sasa 

tuendelee na awamu ya kwanza ya 

makubaliano yetu” akasema David 

 “ so it’s a deal ….!!” Akasema Vicky 

 David akamuangalia na kusema 

 “ Deal ….” 

*******************************************

******  Baada ya kumkosa David ,Pauline 

hakuwa tena na hamu ya kula akaamua 

kurejea dukani kwake.Kichwa chake 

kilijaa mawazo mengi kuhusiana na 

kitendo cha David kuondoka na mama 

yake mdogo bila kumtaarifu.Alishindwa 

kufanya kazi yake akaegemea kiti akiwa 

na mawazo mengi 

 “ David na mama mdogo wamekwenda 

wapi? Kwa nini aamue kuizima kabisa 

simu yake na mama mdogo hapokei simu? 

Huu ukaribu wao umetokeaje? 

Nakumbuka ni mama mdogo aliyekuwa 

akipinga kwa nguvu zote David asiishi 

pale nyumbani.Nashangaa mambo 

yalivyobadilika na kwa ghafla ukaribu huu 

umetokea.Nafahamu ni kitu gani 

anachokihitaji mama mdogo kwa 

David.Endapo nikigundua kwamba 

anataka kumtumia David kwa starehe 

zake basi kutakuwa na vita kati yangu 

naye.Mimi ndiye niliyembadilisha David 

na kumuweka katika hali ile aliyokuwa 

nayo sasa ambayo kila mmoja 

anamtamani” akawaza Pauline  “lakini kwa nini moyo wangu uumie 

kwa ajili ya David? Mtu ambaye sina 

mahusiano naye yoyote.Lazima niidhibiti 

hali hii.Sitakiwi kuumia bila sababu za 

msingi.I’m so stupid.Naumia moyo wangu 

kwa ajili ya mtu nisiyemfahamu hata 

mahala alikotoka.I have to stop this” 

akainua kichwa na kuinamia kompyuta 

yake. 

 “ No ! I cant stop thinking about 

him.He’s already in my nerves and every 

where that’s why I’m so jealousy. kila 

nikiwa naye nahisi furaha kubwa na ya 

ajabu mno.Nahisi ninaanza kumpenda na 

ndiyo maana sitaki mwanamke yeyote 

amkaribie.Sielewi imetokeaje lakini nina 

uhakika mkubwa kwamba ninampenda 

David na hizi hisia ni za kweli.Pamoja na 

hayo itabidi niendelee kujizuia 

nisionyeshe chochote kwamba tayari 

nimeanguka mapenzini mpaka hapo 

nitakapokuwa na uhakika kwamba David 

naye ameonyesha kuvutiwa nami.Kwa 

sasa itaendelea kubaki siri yangu wakati 

nikimchunguza na kumfahamu 

vizuri.Kuna kitu nimekumbuka .Jana 

tukiwa Ngaramtoni nilimweleza David kuhusiana na tarehe kumi na moja 

Septemba na namna inavyoambatana na 

matukio ya ajabu kwa familia yetu kila 

mwaka.Alistuka sana na kijasho kikaanza 

kumtoka akainuka na kwenda 

maliwatoni.Kitu gani kilimstua ? Kuna nini 

anakifahamu kuhusiana na tarehe hii? 

Mstuko ule haukuwa wa bure.Lazima kuna 

kitu anakifahamu kuhusiana na suala hili 

.Kuna mambo mengi siyajui kuhusiana na 

David.Historia yake ,wapi ametoka ,familia 

yake na mambo yote yanayohusiana 

naye.Ili kumjua vizuri lazima niwe naye 

karibu.Ikiwezekana …..” Pauline 

akastuliwa toka mawazoni na mtu 

aliyeingia na kusimama mbele yake 

 “ Tamia …!!!” akasema Pauline 

 “ Hi Pauline..” akasema Tamia huku 

akitabasamu 

 “Umenistua sana.habari za toka jana? 

Mbona leo umetoka mapema? 

 “Nimeomba ruhusa” akajibu Tamia 

 “Karibu Tamia ,have a seat” akasema 

Pauline na Tamia akavuta kiti akakaa 

 “Pauline are you ok? Unaonekana una 

mawazo mengi.Nini kinakusumbua? 

akauliza tamia  “ Ni mambo ya kawaida tu .Kuna 

mambo yananiumiza kichwa changu” 

 “ Pole Pauline .Can you share with me? 

 “ Usihofu Tamia ni mambo ya kawaida 

tu.” Akasema Pauline 

 “Sawa kama ni hivyo lakini muda 

wowote ukiwa tayari kuniambia chochote 

kinachokusumbua usisite kufanya hivyo” 

 “ Ahsante sana Tamia” 

 “ Pauline nina wazo moja .Kwa nini 

tusiende Plasco tukale Ice cream? 

Akasema Tamia 

 “ May be that’s the best Idea for 

now.Lets go” 

 Pauline akainuka kitini akamshika 

mkono Tamia wakaingia katika gari la 

tamia na kuanza safari ya kwenda Plasco 

sehemu maarufu kwa kuuza Ice cream. 

 Wakiwa garini simu ya Pauline 

ikaita.Akatazama mpigaji alikuwa ni David 

 “ Hallow David” akasema Pauline na 

kumstua Tamia aliyekuwa akiendesha 

gari 

 “hallow Pauline” akajibu David 

 “Uko wapi David? 

 “ Niko hapa ofisini”  “ Ok Nakuja sasa hivi” akasema Pauline 

na kukata simu 

 “ twende tupite kwanza ofisini kwa 

baba” akasema Pauline 

 “Was that David” akauliza Tamia 

 “ Yah “ akajibuPauline kwa ufupi 

 “ Kwa nini Pauline hataki kusikia au 

kuona mtu akiwa karibu na David?Kuna 

nini kati yao?Je wana mahusiano ya 

kimapenzi na hataki tujue?lakini sina 

hakika kama wana mahusiano hayo 

vinginevyo asingekuwa anakaa pale 

kwao.Inawezekana wakawa na undugu 

japokuwa Pauline hataki kuweka 

wazi.Nitafanya utafiri hadi nijue david na 

akina Pauline wana mahusiano 

gani.Nimetokea kumpenda David na 

nitafanya kila linalowezekana hadi awe 

wangu.This time its for real.I feel love” 

akawaza Tamia huku wakiendelea na 

safari 

 Walifika katika jengo kubwa la Arusha 

shopping mall wakashuka na kuelekea 

katika ofisi ya mzee Zakaria 

 “ Hallow David” akasema Pauline baada 

ya kuingia ofisini  “ Hi Pauline” akasema David huku uso 

wake ukionyesha wasi wasi fulani lakini 

ghafla ukabadilika na kutabasamu baada 

ya kuiona sura yenye tabasamu ya Tamia. 

 “ Hallow david” akasema Tamia kwa 

sauti nyororo huku akimpa mkono 

wakasalimiana 

 “ Hello tamia Habari za toka jana? 

 “habari nzuri David” akajibu Tamia 

 “Nafurahi kukuona tena.karibu sana “ 

akasema david 

 “ Ahsante David”akajibu Tamia halafu 

akatoka mle ofisini na kumuacha Pauline 

na David peke yao 

 “ Nilikupitia twende lunch nikakukosa “ 

akasema Pauline 

 “mama mdogo alipita hapa 

akanichukua akanipeleka kunionyesha 

ofisi yake na namna wanavyofanya 

biashara ya madini.Kwa kuwa tayari muda 

wa chakula ulikwishafika akaniomba 

tukapate wote chakula cha 

mchana.Uliponipigia simu kwa bahati 

mbaya haikuwa na chaji ya kutosha 

ikazima” akasema David  “ Sawa David ,hakuna tatizo.Nilitaka tu 

kufahamu ulikuwa wapi.kazi 

inakwendaje? 

 “ Kazi inakwenda vizuri.Bado 

ninaendelea kupitia taarifa za kifedha za 

miradi yote kabla sijaanza ukaguzi 

rasmi.baada ya wiki moja nitatoa taarifa 

yangu na mapendekezo kama alivyoagiza 

mzee Zakaria.” Akasema David 

 “Good.halafu kuna kitu 

nimekumbuka.Nimewahi kumueleza baba 

kwamba hii biashara ya kununua na kuuza 

madini imekuwa inatuingizia hasara 

kubwa na madeni lakini hakukubaliana 

nami.Hali yetu kifedha imeyumba baada 

ya biashara hii ya madini na ile ya kuuza 

vito kuanzishwa.Biashara hizi 

zimegharimu fedha nyingi mno lakini 

hakuna faida yoyote inayopatikana mpaka 

sasa.Kwa kuwa baba amekuamini na 

amekuwa nafasi ya kumshauri chochote 

kuhusiana na bashara hizi ni wakati 

muafaka sasa wa kuzifunga biashara hizi 

mbili.Katika ripoti yako utakayoitoa 

naomba ueleze wazi namna biashara hizi 

zinavyoingiza hasara na mwisho ushauri 

kwamba zifungwe kabisa.Sitaki tena mama mdogo ajishughulishe na masuala 

yoyote yanayohusiana na biashara 

zetu.Please David do that for me” 

akasema Pauline.David akashusha pumzi 

 “ David nitakupitia jioni wakati wa 

kurejea nyumbani kwa sasa kuna mahala 

ninakwenda na Tamia” akasema Pauline 

na kutoka mle ofisini.Mara tu alipotoka 

Tamia akaingia na kumrushia David kadi 

ndogo yenye mawasiliano yake 

 “Call me later” akasema kwa sauti 

ndogo na kutoka nje kwa kasi.David 

kijasho kilikuwa kinamtiririka 

 “ Nimejiingiza katika matatizo 

makubwa” akawaza 

 “ I’m confused and I don’t now what to 

do anymore.tayari nimemkubalia madam 

Vicky matakwa yake na wakati huo 

Pauline naye ameleta ombi lake.Nisimame 

upande upi? Nimsikilize nani? I’m 

confused” David alihisi kuchanganyikiwa 

na hakujua afanye nini.Akainamisha 

kchwa akawaza halafu akaendelea na kazi 

zake. 

 Hakukuwa na maongezi mengi baada ya 

chakula cha usiku.Kila mmoja akaelekea 

chumbani kwake.Ilikuwa ni siku ngumu sana kwa David.Alichoka mwili na 

akili.Hakuwa amepata ufumbuzi wowote 

kuhusiana na ombi la Pauline kwamba 

ashauri biashara zinazosimamiwa na 

Vicky zifungwe kutokana na kuendeshwa 

kwa hasara.Akajitupa kitandani na kuanza 

kukumbuka maongezi yake na Vicky 

mchana 

 “Nitakufundisha namna ya kutengeneza 

pesa na ndani ya kipindi kifupi utakuwa 

milionea.Nitakufundisha biashara ya 

kimataiafa.Tutakwenda wote hadi China 

na Hong Kong utafahamu namna 

tunavyonunua bidhaa.Mambo mengi 

nitakufanyia na si lazima yote nikwambie 

leo.Mengine yatakuja kama surprise” 

 Akakakumbuka maneno haya ya Vicky 

halafu akainuka na kukaa 

 “ Madam Vicky hakuonyesha kuwa 

anatania kwa yale aliyokuwa 

anayasema.Inaonekana anafaidika sana 

kutokana na biashara zile na ndiyo maana 

ameniahidi kunifanyia mambo mengi ili 

niweze kuuficha uovu wake na kuzinusuru 

biashara zake zisifungwe.Ni kitu gani huwa anakifanya katika biashara hizo 

ambacho hataki Pauline na baba yake 

wakifahamu?I need to find out” akawaza 

David na kuinuka kitandani akaenda 

kukaa sofani. 

 “ I swear in heaven and earth 

,nitayafanya maisha yako yawe ya 

kifahari.You are a handsome guy.You need 

to own your company and be a boss” 

 Maneno haya ya Vicky yakaendelea 

kujirudia kichwani kwa 

David,akatabasamu 

 “ Swali ninalotakiwa kujiuliza ni kweli 

ninahitaji hivi vitu alivyoniahidi Madam 

Vicky? Akajiuliza halafu akainuka na 

kwenda kusimama katika kioo kikubwa 

cha kujiangalia 

 “ May be yes .I need them” akasema kwa 

sauti ndogo 

 “ Lakini vipi kuhusu Pauline? Ni kweli 

kabisa inaonyesha biashara zile mbili 

zinazosimamiwa na Madam Vicky 

zimekuwa zikiendeshwa kwa hasara 

kubwa na Pauline yuko sahihi kwamba ni 

wakati sasa wa kuzifunga biashara hizo.Je nilipuuze ombi lake? Atajisikiaje 

nitakapolipuuza ombi lake? Lazima 

nifanye maamuzi yenye busara.” Akawaza 

David na mara akakumbuka kitu 

 “ Tamia aliniachia kadi yenye namna 

zake za simu na kuniomba nimpigie.Ngoja 

niwasiliane naye.Ni msichana mrembo na 

mcheshi sana.Napenda tabasamu lake ana 

sauti nyororo,umbo zuri.Amebarikiwa 

uzuri wa kipekee .” akawaza David huku 

akiufungua mkoba wake na kutoa kadi 

aliyopewa na Tamia akaandika namba za 

simu zilizo kuwa katika ile kadi na kupiga 

 “Hallow “ sauti nyororo ikasikika 

upande wa pili wa simu baada ya kupokea 

 “Hallow naongea na nani? Akauliza 

David 

 “Mimi ni Tamia ,wewe ni nani? Akauliza 

Tamia kwa sauti ya kubembeleza 

 “Mimi ni David.” 

 “ Ouh David .!!...” akasema Tamia kwa 

furaha 

 “ Nafurahi umenipigia simu 

David.Nilikuwa naisubiria kwa hamu 

sana simu yako.Unaendeleaje? 

 “ Naendelea vizuri sana 

Tamia.Nimekumbuka mida hii kwamba ulinipatia kadi nikaona ni vyema kama 

nikakupigia kabla sijalala.” 

 “ David nashukuru sana kwa 

kunipigia.Nimefurahi kuisikia sauti 

yako usiku huu” 

 “ Hata mimi nimefurahi sana kukusikia 

Tamia.Una sauti nzuri sana” 

 “ Ouh ahsante David.Nimefurahi 

sana.Tutazidi kuwasiliana” 

 “ Haya Tamia.nakutakia usiku mwema” 

 “ Ahsante sana David.Usiku mwema 

nawe.Ulale salama .Ahsante kwa 

kunipigia” akasema Tamia na David 

akakata simu.Uso wake ulijenga 

tabasamu kubwa 

 “ Tamia amebarikiwa sauti laini sana 

yenye kubembeleza.Utatamani 

uendelee kuisikia muda wote.Naomba 

nikiri kwamba Mwenyezi Mungu 

alimpendelea uzuri binti huyu.” 

Akawaza David na mara ujumbe mfupi 

wa simu ukaingia,ulitoka kwa Tamia 

 “ David hivi wewe na mzee Zakaria mna 

mahusiano gani? Ni ndugu? 

 David akatabasamu baada ya kuusoma 

ujumbe ule halafu akaandika ujumbe 

wa majibu  “Hatuna mahusiano ya kindugu lakini 

ninamheshimu mzee Zakaria kama 

baba yangu” 

 Baada ya dakika moja ukaingia ujumbe 

mwingine toka kwa Tamia 

 “Nashukuru kusikia hivyo.Sweet 

dreams David” ndivyo ulivyosomeka 

ujumbe ule wa Tamia 

 “ Tamia ni msichana mrembo ,ni 

mcheshi na mwenye maneno mengi.Ni 

mwepesi sana kumzoea mtu kama 

alivyonizoea mimi.Tofauti na 

Tamia,Genevive yeye ni mpole sana na 

mwenye aibu nyingi.Nafurahi kukutana 

na mabinti hawa warembo” akawaza 

David 



 Ni wiki ambayo ilikwenda kwa kasi 

kubwa na hatimaye siku ya Jumapili 

imewadia.Nisiku ambayo Robin na 

familia yake walialikwa kwa chakula 

cha mchana nyumbani kwa mwalimu 

Lucy.Ni siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa 

hamu kubwa na Robin aliyetaka 

kuonana tena na mwalimu Lucy ambaye tayari amekwisha anza kuingia 

katika fikra zake.Toka alipoonana naye 

kwa mara ya kwanza ,sura ya mwalimu 

huyu mwenye uzuri wa kipekee 

imekuwa ikimjia akilini kila 

mara.Hakutaka kupingana na akili yake 

kwamba tayari alikwisha anza kuzama 

mapenzini na mwalimu huyu lakini 

alitaka kwanza amfahamu vyema kabla 

ya jambo lolote 

 “ Leo nitaonana tena na mwalimu 

Lucy.Nina hamu kubwa ya kuiona tena 

sura ile yenye kunisisimua mwili 

mzima.Leo lazima nipate ukweli wa 

masuala ambayo ninataka kuyafahamu 

kuhusiana na Lucy.Penny aliniambia 

kwamba hajawahi kumuona mtoto 

yeyote wa mwalimu Lucy.Mume na 

familia yake wako wapi?Mwanamke 

mzuri kama Yule hawezi kukosa mume 

na watoto.Yote haya nitayafahamu Leo 

na kisha nitaamua nini cha kufanya.” 

Akawaza Robin akiwa katika kioo 

kikubwa cha kujitazamia.Alikuwa 

anajiandaa kwa safari ya kuelekea 

nyumbani kwa mwalimu Lucy Saa sita na nusu za mchana Robin 

Penny na mtumishi wao wa ndani 

waliingia garini na kuanza safari ya 

kuelekea katika mualiko nyumbani kwa 

mwalimu Lucy 

 Toka kulipopambazuka 

asubuhi,mwalimu Lucy alikuwa katika 

heka heka kubwa ya kufanya maandalizi 

kwa ajili ya ugeni alioutegemea.Hakuwa 

na mtu wa kumsaidia hivyo ilimlazimu 

kufanya kazi zote peke yake.Uso wake 

ulipambwa na tabasamu baada ya 

kumaliza kazi zote kabla ya saa saba za 

mchana 

 “ Ouh Thanx God ! .Kila kitu 

kimekamilika kwa wakati.Nilikuwa na 

wasi wasi pengine wageni wangeweza 

kufika kabla ya kukamilisha maandalizi” 

akawaza Lucy huku akionja mchuzi wa 

samaki na kutabasamu 

 “ wow ! Its perfect.Kwa mujibu wa 

Penny,Robin anapenda mno Samaki 

aliyeungwa na nazi.Nina imani atakipenda 

chakula nilichomuandalia leo” akawaza 

Lucy halafu akaelekea chumbani kwake 

kwa ajili ya kujiandaa kwani mida ya 

kuwasili wageni wake ilikaribia  Saa saba na dakika ishirini na nne 

kengele ya mlangoni ikalia.Moyo wa 

mwalimu Lucy ukalipuka kwa furaha 

 “ They are here.!! Akasema taratibu na 

kutoka chumbani akaelekea 

mlangoni.Alikuwa amependeza kupita 

kiasi.Alivaa suruali ya jeans ya rangu ya 

bluu na shati jekundu 

 “ wow ! karibuni sana” akasema kwa 

furaha mwalimu Lucy baada ya kufungua 

mlango na kukutana na Robin na familia 

yake.Kwa furaha alikumbatiana na Penny 

 “ Hi Robin “ akasema mwalimu Lucy 

huku wakipeana mikono 

 “Hallo Lucy” akajibu Robin 

 “Nafurahi sana mmekuja.Karibuni 

sana.Karibuni ndani” akasema mwalimu 

Lucy.Wageni wake wakaingia ndani 

akawakirimu kwa vinywaji 

 “ Habari za toka jumamosi iliyopita? 

Akauliza mwalimu Lucy 

 “ habari ni nzuri.namshukuru Mungu 

tuko wazima na tunaendelea vizuri.Vipi 

wewe unaendeleaje? 

 “ hata mimi ninamshukuru Mungu 

ninaendelea vizuri.Wiki yangu ilikuwa 

nzuri sana”  “ Nafurahi kusikia hivyo” akasema 

Robin halafu wakaendelea na maongezi 

kidogo na kisha wakahamia katika 

chumba cha chakula ambako tayari meza 

ilikwisha andaliwa.Kabla ya kula ,Penny 

akaongoza sala ya kuombea chakula 

halafu Lucy akawakaribisha wote 

kujumuika pamoja 

 “Lucy naomba nikusifu kwa namna 

ulivyokiandaa chakula hiki.Umekiandaa 

kwa ustadi mkubwa sana.naomba nikiri 

kwamba sijawahi kula samaki mtamu 

kama huyu uliyemuandaa leo” akasema 

Robin na kuufanya sura ya mwalimu Lucy 

ichanue kwa tabasamu. 

 “ Nilijua unapenda sana Samaki ndiyo 

maana nikamuaanda maalum kwa ajili 

yako” akasema Mwalimu Lucy 

 “Ulijuaje kama ninapenda Samaki? 

Akauliza Robin.Mwalimu Lucy na Penny 

wakaangaliana. 

 “ Nilimwambia mimi” akasema Penny 

halafu wote wakacheka na kuendelea 

kupata chakula.Baada ya kumaliza kula 

Penny na mtumishi wao wa kazi za ndani 

wakafanya usafi,Robin na mwalimu Lucy 

wakaelekea sebuleni.Saa tisa za alasiri mwalimu Lucy na Robin wakawaacha 

Penny na Deborah mtumishi wao wa ndani 

wakiangalia filamu wao wakelekea 

bustanini 

 “ Lucy nashukuru sana kwa 

makaribisho mazuri na chakula 

kitamu.Hongera sana,wewe ni mmoja wa 

wapishi hodari kabisa hapa nchini.” 

Akasema Robin wakati wakiendelea na 

vinywaji bustanini 

 “ Nashukuru sana kwa kufika kwenu 

Robin.Nimefurahi sana .mmeifanya siku 

yangu iwe ya furaha kubwa” akasema Lucy 

 “ Lucy kuna kitu ninataka kukuuliza 

samahani lakini kama nitakuwa 

nimeingilia mambo yako ya ndani” 

 “ Usijali Robin,uliza chochote” akasema 

mwalimu Lucy.Robin akanywa funda la 

mvinyo na kuuliza 

 “Sijaona familia yako toka tumefika 

hapa,wako wapi? 

 Swali lile likamfanya mwalimu Lucy 

acheke kicheko kikubwa . 

 ‘ Robin wewe ni mchunguzi 

sana.Kusema ukweli sina familia” Robin 

naye akacheka kwa jibu lile la mwalimu 

Lucy  “You are jocking Lucy” akasema Robin 

 “ sikutanii Robin.Ni kweli sina familia” 

 “ Unaanisha kwamba familia yako haiko 

hapa au huna kabisa? Akauliza Robin 

 “ sina kabisa familia” 

 “ kwa hiyo unaishi mwenyewe? 

 “Ndiyo ninaishi mwenyewe.Mbona 

umeonyesha kushangaa Robin?” akauliza 

mwalimu Lucy 

 “Ni kweli nimeshangaa na ni vigumu 

kuamini kwamba mwanamke kama wewe 

hauna familia,nikimaanisna mume na 

watoto.Hujawahi kuolewa? 

 “Si kitu cha ajabu kukosa familia 

Robin.Ni maamuzi tu ya mtu.Kuhusu 

kuolewa sijawahi kuolewa” akasema 

mwalimu Lucy 

 “Ni kweli ni maamuzi ya mtu lakini 

inastusha sana hasa kwa mwanamke kama 

wewe kuamua kutokuwa na familia” 

 “ Kwani mimi nina kitu gani cha tofauti 

cha kukustua Robin? Akauliza mwalimu 

Lucy huku akitabasamu 

 “Uko tofauti Lucy na ninaweza kusema 

kwamba maamuzi hayo ya kuishi bila 

familia si sahihi kwako japokuwa 

sifahamu sababu iliyokupelekea ukaamua hivyo lakini wewe ni mwanamke ambaye 

unafaa sana kuwa mama bora.” 

 “ Una uhakika huo Robin? 

 “Nina uhakika Lucy.Mfano dhahiri ni 

namna unavyomlea mwanangu Penny 

akiwa shuleni.Penny anajisikia furaha ya 

ajabu kwa kuwa uko karibu naye na 

unamlea kama mtoto wake” 

 “ Ahsante sana Robin kama umeliona 

hilo lakini kwa bahati mbaya si wanawake 

wote wanauwezo wa kuanzisha familia” 

akasema mwalimu Lucy huku akiinamisha 

kichwa chake 

 “ Kwa ufahamu wangu,mwanamke 

hujisikia fahari kubwa na ukamilifu pale 

tu anapokuwa na familia yake yaani mama 

wa familia.Ikitokea mwanamke mwenye 

sifa za kuwa mama kama wewe ukaamua 

kuishi bila familia lazima kutakuwa na 

sababu nzito na kubwa.” Akasema Robin 

.Mwalimu Lucy aliinamisha kichwa halafu 

akatoa kitambaa akafuta machozi.Robin 

alikiona kitendo kile akaingiwa na wasi 

wasi 

 “ Lucy ! whats wrong? Akauliza Robin 

kwa wasi wasi.Mwalimu Lucy akainua kichwa na kujilazimisha kutabasamu 

akasema 

 “ Its ok Robin.Dont mind about me .” 

 “ Samahani Lucy kama nimekuuliza kitu 

ambacho hukupenda kuulizwa.” 

 “ Usijali Robin.Just forget about 

that.Lets talk about something 

else.Unapenda kufuga? 

 “Napenda sana kufuga na hasa bata .” 

Akasema Robin 

 “ Twende nikutembeze ukaangalie 

baadhi ya mifugo yangu.Ukiacha kazi ya 

kufundisha mimi ni mfugaji pia” akasema 

Mwalimu Lucy. 

 Wakainuka na kwenda sehemu ya pili 

ya bustani ile ambako kulikuwa na mto 

mdogo uliokatisha na pembeni ya mto huo 

kulikuwa na majani mafupi yenye ukijani 

uliokolea.Ilikuwa ni mandhari ya kuvutia 

sana.Bata weupe zaidi ya kumi walikuwa 

wanaogelea katika mto ule 

 “ Wow ! I love this place” akasema 

Robin kwa furaha 

 Walitoka eneo hilo na kwenda katika 

mabanda ya mifugo .Kulikuwa na ng’ombe 

wa maziwa,mbuzi,nguruwe na 

kuku.Ilikuwa ni siku nzuri sana kwa Robin na familia yake pamoja na mwalimu Lucy 

pia.Waliongea mambo mengi ikiwa ni 

kufahamiana zaidi na saa kumi na mbili za 

jioni Robin na familia yake wakaingia 

garini wakaondoka kurejea nyumbani 

kwao. 

 “Siku yangu ilikuwa nzuri sana.Toka 

nilipoanza kuwa karibu na Robin 

nimejiona ni mtu mwenye utofauti 

nimekuwa ni mwenye furaha sana tofauti 

na huko awali.Natamani ukaribu huu 

uendelee zaidi na zaidi” akawaza 

mwalimu Lucy akiwa kitandani.Picha ya 

siku nzima ikamjia akatabasamu 

 “ Ilibaki kidogo furaha yangu yote 

ipotee pale nilipoanza kukumbuka maisha 

yangu ya nyuma.Nilikitonesha kidonda 

ambacho kilianza kupona.Ee Mungu 

naomba unisaidie niweze kuyasahau 

maisha yale niliyoishi huko nyuma ili 

moyo wangu uweze kuwa na 

amani.Ninajitahidi sana kuyasahau lakini 

ninashindwa.Nataka kuufungua moyo 

wangu tena na kuanza maisha mapya 

lakini historia yangu ya nyuma inanitesa 

na ninashindwa kuwa na furaha katika 

maisha yangu.Sitaki kuendelea kuumizwa na yale yaliyotokea huko nyuma.Nataka 

kupenda tena na tayari ninahisi moyo 

wangu umeanguka mapenzini lakini 

historia ile bado inaniandama kila 

niendapo.What am I going to do now? 

Akawaza mwalimu Lucy.Akainuka 

akafungua kabati na kutoa faili moja 

kubwa lenye makaratasi 

yaliyochakaa.Aliisoma karatasi ya kwanza 

na ya pili akashindwa kuendelea 

akalifunga faili na kulitupa 

pembeni,macho yake yalijaa 

machozi.Akajilaza kitandani na kuanza 

kukumbuka historia nzima ya maisha 

yake. 

************************************* 

 Ni saa tisa alasiri,Lucy amekwisha 

maliza kuosha vyombo vilivyotumika 

katika mlo wa mchana na sasa alikuwa 

akifanya usafi wa nyumba.Alikuwa 

akifagia chumba kimoja baada ya 

kingine.Alipokifikia chumba cha Jackson 

akasimama na kutega sikio lake mlangoni 

ili asikie kama kulikuwa na mtu yeyote 

mle ndani.  “Mbona kuko kimya namna hii? Nadhani 

Jackson hatakuwepo humu 

chumbani.Mara nyingi akiwepo 

utatambua kutokana na sauti ya juu ya 

muziki .” Akawaza Lucy akiwa amesimama 

mbele ya ule mlango na ufagio wake 

mkononi. 

 “ni siku ya pili leo sijafanya usafi 

chumbani kwa kaka Jack.Ngoja nifanye 

usafi haraka haraka kabla 

hajarudi.Akikuta sijafanya usafi na leo 

,anaweza akanishitaki kwa mama.” 

Akawaza Lucy huku akikinyonga kitasa 

cha mlango,akaufungua na kujitoma 

ndani.Mara tu baada ya kuingia mle 

chumbani jicho lake likatua katika 

luninga.Akastuka na kuushika mdomo 

wake kwa alichokiona.Alisisimka mwili 

mzima.Kwa sekunde kadhaa alibaki 

ameduwaa .Alihisi kama vile amepigwa na 

shoti ya umeme.Hakujua atoke nje au 

aendelee kutazama filamu ile. 

 “Lucy mbona unaingia bila hodi? Sauti ya 

Jackson ikamstua Lucy.Wakati akiingia 

mle chumbani,hakuwa amemuona Jackson 

aliyekuwa amejilaza kitandani huku 

amevaa spika za masikioni ili sauti ya filamu aliyokuwa akiitazama isiweze 

kusikika kwa watu wengine.Huku 

akitetemeka Lucy akajibu. 

 “Samahani kaka jack sikujua kama uko 

ndani.Nilihitaji kufanya usafi,nikaona 

kimya nikajua haupo ndani.Naomba 

unisaheme kaka sirudii tena.” Lucy 

akasema kwa kutetemeka huku akipiga 

hatua taratibu kutoka mle chumbani.Jack 

akazima ile Luninga na kuamka pale 

kitandani alipokuwa amejilaza. 

 “Lucy,njoo uendelee na usafi.ila siku 

nyingine kabla ya kuingia uwe unabisha 

hodi.Mara nyingine unaweza ukakutana 

na vitu visivyokufaa” Jackson akasema 

huku akitabasamu 

 “Ndiyo kaka Jack” Lucy akajibu kwa 

adabu huku akimpisha Jackson mlangoni. 

 “Akiniuliza mtu mwambie nimekwenda 

kucheza Basketball” jack akasema 

 “Sawa kaka jack” 

 Lucy akaingia mle chumbani na 

kusimama kuuegemea ukuta akapumua 

kwa nguvu.Mwili wote ulikuwa 

ukimtetemeka.hakujua hali ile ilitokana 

na uoga au ni kutokana na kile alichokiona 

mle ndani muda mfupi uliopita.  “Uuuuphhh !” Lucy akapumua kwa nguvu. 

 “ Ni mara yangu ya kwanza kuona filamu 

ya watu wakifanya mapenzi.Sijawahi 

kuona mambo haya toka nizaliwe.Sijui 

hata huwa wanafanyaje.” Akawaza Lucy 

huku akielekea katika meza ya Luninga 

akasimama mbele yake akiikodolea 

macho Luninga ile. 

 “Laiti ningejua mahala alikoiweka ile cd 

ningeiangalia kabla kaka jack 

hajarudi.Picha zile zimenisisimua 

sana.”Dakika mbili zilimalizika Lucy akiwa 

amesimama akiikodolea macho luninga 

ile. 

 “Ngoja niendelee na usafi kabla Jack 

hajarudi” Lucy akainama na kuendelea na 

kazi ya kufanya usafi katika chumba cha 

Jackson,alipomaliza akafunga na 

kuendelea na kazi nyingine. 

 Ni mwaka wa nne sasa toka Lucy aanze 

kufanya kazi za ndani katika familia hii ya 

bwana na bibi Simon ndukalyo ambao 

walikuwa na mtoto mmoja tu aliyeitwa 

Jackson.Familia hii ni moja ya familia 

zenye kuishi kwa amani na upendo 

mkubwa.Ni familia ya watu wacha Mungu 

na wenye upendo mkubwa kwa ndugu jamaa na marafiki. Toka amefika hapa 

Lucy amekuwa akiishi kwa furaha kubwa 

kama yuko kwao.Alijiona ni mmoja kati ya 

wafanyakazi wachache wa ndani ambao 

wamebahatika kufanya kazi katika familia 

zinazowathamini,kuwajali na kuwafanya 

ni sehemu yao.Lucy amekuwa 

akithaminiwa na kupendwa kama mtoto 

wa familia hii.Kwa wageni waliokuwa 

wakifika pale nyumbani hakuna 

aliyegundua kama Lucy ni mfanyakazi wa 

ndani.Wengi walimchukulia kama ni 

mmoja wa watoto wa Bw na Bi Simon.Kwa 

kuwa muda mwingi mtoto wao Jackson 

amekuwa akiutumia akiwa shuleni ,bwana 

na bibi Ndukalyo wamekuwa 

wakiliwazwa kwa uwepo wa Lucy na hivyo 

kumchukulia kama ni mtoto wao.Kwa sasa 

ni wiki ya pili imekatika toka Jackson 

arejee nyumbani kwa likizo ya mwezi 

mmoja baada ya shule kufungwa.Jackson 

amekuwa akimuheshimu Lucy kama dada 

yake. 

 “lazima niitafute cd ile aliyokuwa 

akiiangalia Jackson.Nitasubiri kesho 

wakati Jack hayupo nitaitafuta na kwenda 

kuitazama.Nina hamu sana ya kuona huwa wanafanya vipi.Nina miaka kumi na sita 

sasa na sijawahi kufanya mambo hayo na 

wala sijawahi kuona .Kesho lazima 

niangalie huwa wanafanyaje.Nina hamu ya 

kujaribu.Nasikia kuna raha ya 

ajabu.Lakini hata nikisema nijaribu 

kufanya hivyo nitampata wapi mwanaume 

wa kufanya naye? Inanibidi kwa sasa 

nianze kutafuta mwanaume ambaye siku 

moja atakuwa mume wangu.japokuwa 

baba na mama wananikataza kila siku 

lakini nitajaribu kufanya kwa siri .Siku 

moja natakiwa kuwa na nyumba yangu na 

watoto wangu.natakiwa kuanza kujifunza 

mambo haya angali bado mapema.” Lucy 

akawaza.Ulikuwa ni usiku mrefu sana 

kwake.Hakuwahi kusisimkwa mwili kama 

ilivyomtokea leo.Kila alipojitahidi 

kufumba macho picha ya mwanamke na 

mwanaume wakifanya mapenzi aliyoiona 

katika filamu ile ikawa inamjia 

.Alishindwa kupata usingizi. 

 ********************** 

 Asubuhi na mapema siku iliyofuata Lucyakaamka na kufanya kazi zote kama ilivyo 

kawaida yake.Hadi inatimu saa mbili za 

asubuhi alibakiwa na kazi moja tu ya 

kufua nguo.Alijitahidi kumaliza kazi zake 

mapema ili aweze kupata nafasi ya 

kuangalia cd ile aliyoiona jana chumbani 

kwa Jackson.Saa nne za asubuhi,baada ya 

kuoga na kupata stafstahi Jackson 

akamuaga Lucy kwamba anatoka kwenda 

kwa rafiki zake. 

 Baada ya kuhakikisha kwamba Jack 

ameondoka,Lucy akasuuza nguo zake 

haraka haraka na kumaliza zote kisha 

akaenda chumbani kwa Jackson ambaye 

hakuwa na kawaida ya kuufunga mlango 

wake kwa funguo.Baada ya kuingia 

chumbani mle moja kwa moja akaelekea 

katika kabati ambamo Jack huwa 

akihifadhi cd zake.Akapekua moja baada 

ya nyingine na kukutana na ile aliyokuwa 

akiitafuta.Kasha la cd ile lilikuwa na picha 

za watu wakiwa watupu na wengine 

wakifanya mapenzi. 

 “Ndiyo hii hii” akawaza Lucy huku 

akilifungua lile kasha na kuangalia kama 

cd ilikuwemo ndani.Taratibu akatoka na 

kuelekea sebuleni ,akawasha luninga kubwa ya sebuleni halafu akawasha na 

deki ya dvd.Kabla hajaiweka cd ile katika 

deki akahakikisha mlango wa nje 

umefungwa vizuri kiasi kwamba hakuna 

mtu ambaye angeweza kuufungua.Akarudi 

sebuleni akikimbia na kuanza kuitazama 

filamu ile 

 Joto lilizidi kumpanda kila dakika 

ilivyosonga.Mambo aliyoyaona katika cd 

ile yalikuwa makubwa na hakuwahi 

kuyaona toka azaliwe.Hakuwahi kuona 

watu wakifanya mapenzi na leo hii ilikuwa 

ni mara yake ya kwanza.Alihisi mwili wote 

ukimsisimka .Jasho jembamba lilikuwa 

likimtiririka.Ilipomalizika akaitoa na 

kuirudisha mahala alikoitoa chumbani 

kwa Jackson na kisha akaenda chumbani 

kwake akajitupa kitandani. 

 “Yule mwanamke alionekana anapata 

raha ya aina yake.Alikuwa akilia lakini 

hakuwa akitoa machozi.Nilidhani labda 

yule jamaa alikuwa akimuumiza lakini 

walipomaliza wote wakaanza 

kucheka.Halafu kabla hawajamaliza yule 

mwanaume alifumba macho na kukunja 

sura nilidhani naye alikuwa ameumia 

lakini baada ya muda mfupi nikaona ametoa vitu Fulani hivi.sijui ni vitu gani 

vile halafu wote wakaanza 

kucheka.Kumbe ninakosa mambo mengi 

sana mazuri.Nakumbuka wakati bado niko 

msichana mdogo kule kijijini kwetu 

nilikuwa nikiwasikia wasichana wakubwa 

wakiongelea raha walizokuwa wakizipata 

toka kwa wanaume wao.Nahitaji na mimi 

nimpate mwanaume ambaye atanifanya 

nizipate raha hizo kama wale wasichana 

wa kwenye ile filamu.” Akawaza Lucy. 

 Ni wazi Lucy bado alikuwa mgeni kabisa 

katika masuala mazima ya 

mapenzi.Hakujua mapenzi ni kitu 

gani.Baada tu ya kuangalia ile cd aliyoitoa 

kwa Jackson amepatwa na hamu ya kutaka 

kujaribu . 

 “ Laiti kama ningekuwa na muda wa 

kutoka na kwenda huko nje ningeweza 

walau kutafuta mwanaume mmoja wa 

kunipa raha.lakini baba na mama ni 

wakali na siruhusiwi hata kutoka nje…” 

dakika mbili zikapita akiwa amejilaza 

kitandani kwake akiwaza. 

 “Nimekumbuka kitu.Kuna yule kaka 

ambaye huwa anatumwa kuleta nyama ya 

mbwa kila siku.Yule kaka kila akija amekuwa akipenda kunitania sana,mara 

aniite mchumba wake.Kuna siku aliwahi 

kunitamkia kwamba analipenda umbo 

langu na halali akiniwaza,nakumbuka 

nilimjibu vibaya.Kumbe nilifanya 

makosa.Sikutakiwa kumjibu vibaya Toka 

nimemjibu vibaya amekuwa hataki tena 

mazoea na mimi.Itanibidi nianzishe tena 

ukaribu kati yangu naye.lakini 

atanichukuliaje? Atanionaje ? Lucy 

akajishika kichwa akiwaza 

 “Potelea mbali,vyovyote 

atakavyonichukulia lakini mimi nahitaji 

mwanaume wa kujaribu naye na kama 

akikubali,tutakuwa tukikutana mchana 

aletapo nyama ya mbwa .Muda huo huwa 

hakuna mtu nyumbani hivyo hakuna mtu 

atakayeweza kugundua chochote.” Lucy 

akawaza na kwa mbali akasikia kama 

kengele ya geti inalia.Akakurupuka na 

kuelekea getini.Akafungua haraka haraka 

na mara akakutanisha macho na 

Elisha,kijana mwenye tenda ya kuleta 

nyama za mbwa kila siku.Lucy 

akamtazama kana kwamba ilikuwa ni 

mara yake ya kwanza kumuona.Elisha 

akastuka kumuona Lucy katika hali ile  “Lucy vipi mbona leo unaniangalia 

namna hiyo.Kuna tatizo? Elisha akauliza 

tena. 

 Lucy akajaribu kuongea lakini akajikuta 

akishindwa. 

 “Lucy una tatizo gani leo? Elisha akauliza 

 “hakuna tatizo lolote Elisha.” Lucy 

akasema huku akikipokea kifurushi kile 

cha nyama ,kisha akafunga geti.Elisha 

akaondoka akishangaa . 

 “Mungu wangu kwa nini nimeshindwa 

kumwambia ukweli? Akajilaumu huku 

ameliegemea geti. 

 “Nimefanya ujinga mkubwa.Nimeshindwa 

kumshawishi Elisha.sasa nitafanya na 

nani? Nahitaji mwanaume lakini sijui 

nitampata wapi manake humu ndani ni 

kama niko kifungoni.Siruhusiwi hata 

kutoka na kwenda kutembea.Kesho akija 

tena nitabuni namna ya kumfanya aingie 

ndani” Lucy akawaza halafu akachukua 

furushi lile la nyama na kuelekea 

ndani.Aliendelea na kazi zake za mchana 

lakini mawazo yote yakawa katika ile 

filamu aliyoitazama. 

 “Wanawake wenye wanaume wao 

wanafaidi sana.Nahitaji na mimi nipate mwanaume wa kuweza kunipa raha katika 

maisha yangu.” Akawaza Lucy na mara 

kengele ya getini ikalia kuashiria kwamba 

kuna mtu.Akaacha kazi aliyokuwa 

akiifanya na kwenda kufungua.Lilikuwa ni 

gari dogo lenye vioo vyeusi ,likaingia 

ndani na kisha akafunga geti.Toka ndani 

ya lile gari akashuka Jackson na 

kulizunguka gari kisha akaufungua 

mlango mwingine wa gari na akashuka 

binti mmoja mwenye uzuri wa 

kustaajabisha.Alikuwa ni binti mfupi 

mwenye umbo zuri na mwenye sura ya 

kupendeza.Lucy akabaki ameduwaaa 

akimshangaa binti yule aliyekuja na Jack. 

 “Lucy wazee hawajarudi bado? Jackson 

akauliza 

 “Bado kaka Jack” Lucy akajibu kwa 

adabu. 

 Jack na yule msichana wakashikana 

mikono na kuelekea moja kwa moja 

chumbani kwa Jack.Lucy alibaki 

amesimama akiwakodolea macho. 

 “Msichana mrembo sana yule.Ndiye 

mpenzi wa Jack au vipi? “ Lucy akawaza 

huku akiegemea meza ya jikoni. 

 “wanakwenda kufanya nini chumbani? Nahisi labda watakuwa wanakwenda 

kufanya mapenzi.Jamani mbona 

wasichana wenzangu wanafaidi sana 

tofauti na mimi? Lini na mimi nitapata 

raha kama wazipatazo wasichana 

wenzangu? Akawaza Lucy kisha 

akakiweka chini kisu alichokuwa akikatia 

nyama. 

 “Ngoja nikasikie wanafanya nini mle 

chumbani.” Lucy akatoka mle jikoni na 

kwa hatua za kunyata akaelekea mahali 

kilipo chumba cha Jackson.Akanyata hadi 

mlangoni.Akatega sikio lakini hakuweza 

kusikia kilichokuwa kikiongelewa mle 

chumbani zaidi ya sauti kubwa ya muziki. 

Taratibu akaondoka pale mlangoni na 

kuelekea chumbani kwake akajitupa 

kitandani. 

 “Najua lazima watakuwa wakifanya yale 

mambo.Napata hamu ya kujaribu.Sijui 

kwa nini niliangalia ile filamu .Kabla ya 

kuitazama sikuwa na mawazo kama 

haya.Lakini hata hivyo mimi ni msichana 

mkubwa sasa hivi ninatakiwa kuyafahamu 

mambo haya.Ninatakiwa niufurahie 

usichana wangu.Kuna kitu 

nimejifunza.Natakiwa kuanza kujipamba ili nivutie kama yule dada.” Lucy akainuka 

na kwenda katika kioo kikubwa ambacho 

aliwekewa chumbani kwake baada ya 

kuvunjika katika chumba cha 

Jackson.Akajiangalia usoni. 

 “Nina sura nzuri inayoweza kumvutia 

kila mwanaume.Natakiwa kuanza 

kujifunza kuifanya sura yangu ing’ae na 

kuwa na mvuto zaidi.Akavua fulana 

aliyokuwa ameivaa na kukitazama kifua 

chake kisha akatabasamu. 

 “Nina kifua kizuri sana.Matiti yangu 

yamesimama na yanavutia.” Akawaza 

huku akitabasamu kisha akavua na sketi 

aliyokuwa ameivaa.Akajitazama katika 

kioo jinsi mwili wake ulivyo 

akatabasamu.Akageuka na nyuma na 

kujitazama kisha akawaza. 

 “Nimebarikiwa kuwa na mwili mzuri 

sana.Nahitaji kuwa mwanamke wa 

kisasa.Nianze kuvaa mavazi 

yanayokwenda na wakati kama wasichana 

wengine wanavyovaa.Nadhani kila 

mwanaume atataka kuwa nami” Lucy 

akastuliwa katika mawazo na sauti ya 

Jackson akimuita.akavaa haraka haraka 

na kutoka mle chumbani. “Ulikuwa wapi Lucy? Jackson akauliza. 

 “Nilikuwa chumbani kwangu napanga 

nguo.” Lucy akajitetea 

 “Ok Lucy naomba umtengenezee mgeni 

wangu juice ya maembe” 

 “Sawa kaka Jack” Lucy akasema na 

kugeuka kuelekea jikoni. 

 “Lucy “ jack akaita na kumfanya Lucy 

ageuke ghafla na kuanza kurudi pale 

alipokuwa amesimama Jackson 

 “Funga vifungo vya fulana yako” Jack 

akasema huku akitabasamu na kuelekea 

chumbani kwake.Lucy akageuka kwa aibu 

na kupiga hatua kuelekea jikoni huku 

akifunga vifungo vya fulana yake. 

 “Sikujua kama fulana yangu ilikuwa 

wazi.Jack atanielewaje? Anaweza 

akadhani nilifanya vile makusudi? 

 Baada ya dakika tano juice ikawa tayari 

Lucy akaiweka katika sinia pamoja na 

glasi mbili akaelekea chumbani kwa 

Jackson.Alikuwa na wasiwasi 

mwingi.Alipofika mlangoni akagonga 

mlango na kisha jacksona akamruhusu 

aingie ndani.Alipoingia mle chumbani 

akaviweka vinywaji juu ya meza na 

kuwakaribisha jack na yule rafiki yake.Kabla hajatoka Jack akakumbuka 

jambo 

 “Lucy nilisahau kukutambulisha .Huyu ni 

rafiki yangu,namaanisha mchumba wangu 

anaitwa Salha..Salha huyu ni dada yangu 

anaitwa Lucy .Usimuogope huyu ni 

mzungu hana tabu” 

 “Nafurahi kukufahamu Lucy” Salha 

akasema kwa sauti laini na kumfanya Lucy 

atabasamu na kutoka mle chumbani 

akaelekea jikoni. 

 “Jamani yule dada ni mzuri 

sana.Anapendeza mno.Anaonekana ni 

msomi na hata mavazi yake yanaonekana 

ni ya bei ya juu .Nataka kuwa kama 

yeye.Hata kama sina elimu ya kutosha 

lakini kama msichana nahitaji kujipenda 

na kuwa na mvuto.” Akawaza Lucy. 

 Baada ya chakula cha usiku ,wazazi wa 

Jackson wakondoka na kuelekea 

chumbani kwao wakamuacha Jack 

sebuleni akitazama mchezo wa mpira wa 

miguu..Lucy alikuwa jikoni akimalizia 

kufanya usafi wa vyombo na alipomaliza 

akaelekea sebuleni ili kutazama filamu za 

kiswahili kama afanyavyo kila 

siku.Hakuwa akijua kama Jack alikuwapo pale sebuleni akitazama mechi ya mpira 

wa miguu.Haikuwa kawaida yake kuwapo 

pale sebuleni mida kama ile.Mara nyingi 

baada ya chakula cha usiku huwa 

anakwenda kujifungia chumbani kwake 

na kutazama filamu




Haikuwa kawaida yake kuwapo 

pale sebuleni mida kama ile.Mara nyingi 

baada ya chakula cha usiku huwa 

anakwenda kujifungia chumbani kwake 

na kutazama filamu. 

 “kaka jack ! “ Lucy akasema kwa kustuka 

baada ya kumkuta jack mle sebuleni. 

 “Sikujua kama uko hapa” Lucy akasema 

 “Kuna mechi kali sana leo ya mpira wa 

miguu kati ya Brazil na Hispania ndiyo 

imeniweka hapa hadi saa hizi” jack 

akasema na kumfanya Lucy atabasamu 

 “Hizo timu unazoziongelea siifahamu 

hata moja” Lucy akasesma huku 

akitabasau. 

 “nakufahamu wewe unapenda filamu za 

kiswahili.”

 “Ndiyo kaka jack napenda filamu za 

kiswahili kwa sababu sifahamu 

kiingereza” 

 “sawa Lucy ngoja nitazame tazame kidogo 

halafu nitakuacha utazame filamu zako za 

kiswahili” Jackson akasema 

 “usijali kaka Jack wewe endelea 

kutazama mpira mimi nakwenda 

chumbani.Nitatazama kesho” Lucy akasema 

 “Kulala mapema namna hii?Kaa bwana 

tuongee ongee kidogo” akasema jack 

akiwa ameelekeza macho yake katika 

Luninga kubwa iliyokuwamo mle sebuleni 

 Lucy akaketi sofani akijaribu kutazama 

kilichokuwa kikiendelea katika 

Luninga.Muda mfupi baadae ikawa ni 

mapumziko.jack akamgeukia Lucy 

 “ Lucy mama hajakuuliza kitu chochote 

kuhusu mgeni aliyekuja hapa leo? 

 “hapana kaka Jack ,hajaniuliza kitu 

chochote.Sidhani kama anajua kama kuna 

mgeni alifika hapa leo” 

 “Tafadhali usimwambie kama nilikuja na 

mtu hapa nyumbani.Yatakuwa matatizo” 

 “Sintamwambia kaka Jack.”Lucy akasema 

na kutabasamu. 

 “Mbona unatabasamu? 

 “basi nimefurahi tu.Salha ni mzuri sana” 

Lucy akasema na kumfanya Jackson atoke 

kicheko kidogo. 

 “Umemuona eenh “ 

 “Ndiyo kaka Jack.Anakufaa sana” jack 

akacheka tena kicheko kikubwa. 

 “halafu kaka jack nina shida.” 

 “Shida gani tena Lucy ?” 

 “Salha alikuwa amevaa yale mavazi yake 

yamempendeza sana.Unaweza ukanisaidia 

kumuuliza alinunua wapi ili na mimi 

nimpatie fedha akaninunulie? 

 Jack akatabasamu na kusema 

 “Ouh unataka kuwa mrembo kama Salha? 

Jack akauliza huku akicheka kichini chini 

 “Sitaki kuwa kama yeye lakini amenivutia 

sana.Inaonekana ni mtu anayejua 

kupangilia mavazi.Nataka na mimi niwe 

na mavazi ya kisasa” 

 “Nafurahi kama umelitambua hilo Lucy 

.Siku nyingi nimekuwa nataka kukueleza 

juu ya mavazi yako ambayo hayakufanyi 

uonekane wa kisasa.Lucy una umbo zuri 

sana lakini mavazi yako unayovaa 

yanakufanya uonekane kama mtumishi wa 

kanisa.Hebu badili mavazi .Kwa hilo umbo 

lako kama ukipata mavazi yanayokukaa 

,nakwambia magari yanaweza 

yakagongana barabarani” 

 Wote wakajikuta wakiangua kicheko.kwa 

maneno yale ya Jack 

 “Kaka Jack nawe yaani magari yagongane 

kwa ajili yangu? Lucy akauliza huku 

akiendelea kucheka 

 “Hivi Lucy wewe hujioni jinsi ulivyoumbika? Nashangaa unavyojizeesha 

wakati unauwezo wa kumfanya hata 

mkurugenzi akakupa funguo ya benzi” 

Jack akasema na kumfanya Lucy acheke 

kicheko kikubwa. 

 “Usidhani nakutania Lucy.una umbo zuri 

sana.hata Salha alikusifia kwamba u 

mwanamke mrembo sana kama 

hujajitambua.” 

 “nashukuru kama alisema hivyo lakini 

mimi najiona wa kawaida tu” 

 “Usijidangaye Lucy.Wewe ni mrembo 

sana.Ngoja nitaongea na Salha akufanyie 

mpango wa mavazi na kisha upelekwe 

saluni ukatengenezwe na ukitoka hapo 

nakuapia lazima utasababisha ajali “ Lucy 

akacheka tena kwa maneno yale ya Jack 

 “Halafu Lucy sijawahi kukuona hata simu 

moja uko na shemeji.Huwa unamficha 

wapi? Jack akauliza swali la kichokozi 

 “Shemeji gani tena unamuongelea? Lucy 

akauliza 

 “aahh ! Lucy usijifanye huelewi bwana.Ina 

maana wewe huna bwana? Jack akasema 

kwa utani huku akikodolea macho 

Luningani ambako timu zilianza kurejea 

uwanjani.  “hahahaaaa kaka jack bwana mimi sina 

bwana.Nani atanitaka mtu kama mimi? 

Hata kama ningekuwa naye kwa geti 

lililoko hapa nyumbani unadhani 

ningethubutu kumleta? 

 “Usinidanganye Lucy.Huko 

unakokwenda magengeni ndiko huwa 

mnakutana mnamalizana huko huko” 

 “Si kweli kaka jack.Mimi sina mambo 

hayo na wala huo muda wa kwenda 

gengeni sina.hata kusuka nywele msusi 

anakuja hapa hapa ndani.Nikitoka hapa 

labda jumapili kwenda kanisani napo 

huwa nimeongozana na mama.” 

 “Nawafahamu nyie wanawake huwa ni 

wajanja sana.hata kanisani unaweza 

ukachoropoka halafu kabla ibada 

haijakwisha unarejea” Jack akatania 

 “hapana kaka Jack.Mimi kwanza mambo 

hayo siyafahamu hata kidogo.Mimi bado 

mshamba” Lucy akajibu huku akicheka 

 “unataka kuniambia hujawahi kuwa na 

mwanaume toka umezaliwa? 

 “kweli kaka Jack.Sijawahi kuwa na 

mwanaume yoyote na wala sifahamu 

lolote kuhusiana na mambo hayo” Jibu lile 

likamfanya Jack ageuze shingo na kumtazama Lucy kwa mshangao. 

 “Mbona unanitazama hivyo? Lucy 

akauliza 

 “Ninashangaa kwa sababu ni nadra sana 

kwa miaka hii kumkuta binti wa umri 

wako akiwa hayafahamu haya mambo.” 

 “kweli ninavyokwambia kaka Jack.Mimi 

sijui chochote kuhusiana na mambo haya.” 

Lucy akasema huku akiona aibu na 

kuinama chini. 

 “Kaka jack ninaenda kulala,tutaonana 

kesho” Lucy akasema huku akiinuka 

 “H..haya..usiku mwema” Jack akajibu 

huku sauti yake ikionekana kukwama 

kwama. 

Alimkodolea macho Lucy akitembea 

kutoka mle sebuleni 

 “Wallah mtoto ni mzuri huyu lakini tatizo 

bado hajajitambua.Pamoja na uzuri wote 

huu bado anasema hajawahi kukutana na 

mwanaume yeyote.Du ! .” Jack akawaza. 

 “Ngoja nifanye mpango wa 

kumpendezesha.Nina uhakika lazima 

ataleta gumzo kutokana na umbo 

lake.Wasichana wengine wamebarikiwa 

sana kuwa na mvuto wa ajabu mmoja wao 

ni huyu Lucy.” Jack akastuliwa toka katika mawazo mengi za sauti za watu 

wakishangilia goli lililofungwa .Mawazo 

kuhusu Lucy yakapotea. 

Asubuhi na mapema Lucy akaamka kama 

ilivyo kawaida yake na kuendelea na kazi 

zake za ndani.Mpaka muda ambao wazazi 

wa Jack wanaamka ili kujiandaa kuelekea 

makazini yeye tayari alikwisha maliza kazi 

zote anazopaswa kufanya asubuhi.Uso 

wake ulionekana kuwa na nuru na 

alionekana mwingi wa furaha..Alitamani 

muda uende kwa kasi ili aweze kuonana 

na Elisha .Bado alikuwa na hamu ya 

kutaka kujaribu kufanya tendo la 

ndoa.Kila avutapo picha za filamu ya 

ngono aliyoiona ,mwili wote ulimsisimka 

na damu kumchemka. 

 “Siwezi kuendelea na hali hii.Kila 

niwazapo kuhusu ile filamu mwili wote 

unanisisimka.lazima niondokane na hali 

hii.Nitaondokana na hali hii mara tu 

nitakapopata mwanaume wa kunitimizia 

haja zangu..Inanibidi nianze kujenga 

mazoea na Elisha.Nikishajenga mazoea ya 

kutosha naye nadhani nitaweza 

kumshawishi hata kwa fedha .Kitu kingine 

kinachoweza kuniaidia kupata mwanaume ni kaka kaka Jack alivyosema 

kwamba natakiwa kubadili mwonekano 

wangu na kuwa kma wasichana wengine 

wanaokwenda na wakati.Aliniahidi 

atanitafutia mavazi mazuri ya kisasa 

ambayo yatanifanya nipendeze na 

kuoeneka kama msichana 

mrembo.Nikish………………..” 

 Hakuendelea na mawazo yake mara 

akastuliwa na Jack. 

 “Unawaza nini Lucy?” .Lucy akastuka sana 

,hakujua kama Jack alikuwepo nyuma 

yake akimuangalia. 

 “Siwazi kitu kaka Jack.” Lucy akasema 

 “baba na mama wamekwisha ondoka? 

 “Ndiyo jack .Wamekwisha ondoka muda 

mwingi.” Lucy akajibu 

 “Ok sasa nitatoka kidogo nitaenda dukani 

kwa Salha kama nilivyokuwa nimekuahidi 

jana kwamba nitakwenda kwake 

kuangalia mavazi ambayo yatakufaa” 

 “Ouh Kaka Jack ahsante sana.Ngoja 

nikakuletee pesa” Lucy akasema huku 

akiweka beseni alilokuwa amelishika 

chini 

 “hapana Lucy.Huna haja ya kunipa 

pesa.Nimejitolea kukununulia mavazi hayo bila malipo.” 

 “Ahsante sana kaka Jack.Sijui hata 

nikushukuruje” Lucy akasema 

 “ Ok mi natoka nitarudi muda si mrefu” 

Jack akasema huku akiondoka. 

Lucy akaelekea chumbani kwake akakaa 

kitandani. 

 “Sipati picha muonekano wangu ndani ya 

mavazi mapya kama yale aliyokuwa 

ameyavaa Salha.Itanibii nimuombe mama 

ruhusa walau jumapili moja niende 

nikatembee kwa sababu nimekuwa 

nikijifungia humu ndani kila siku.Hii ni 

sababu inayonifanya nishindwe hata kuwa 

na marafiki.” Akawaza Lucy huku 

akijitazama katika kioo halafu akatoka na 

kwenda kuoga,akajiweka safi na 

kuendelea na shughuli nyingine. 

 Masaa mawili yalipita Jackson akarejea 

akiwa amebeba mifuko mitatu.Lucy 

akamkimbilia na kwenda kumpokea. 

 “kaka Jack hizi ndizo zawadi zangu? Lucy 

akauliza huku akichanua tabasamu pana 

sana 

 “ndiyo Lucy.Vitu hivi vyote ni vyako.” Jack 

akasema na wote wakaingia sebuleni 

kisha Jack akaanza kufungua mfuko mmoja mmoja na kutoa vilivyokuwa ndani 

yake.Zilikuwa ni nguo nzuri na za thamani 

.Lucy alibaki ameushika mdomo wake 

asiamini kama mavazi yale yalikuwa yake. 

 “Sasa nenda kaanze kujaribisha vazi moja 

moja halafu uje hapa nikuangalie namna 

ulivyopendeza.” Jack akamwambia Lucy 

ambaye alikusanya nguo zote na viatu 

akaelekea chumbani kwake. 

 “Mungu wangu bado siamini kama 

mavazi haya ni yangu.Sijui atakuwa 

amenunua kiasi gani kwa sababu 

yanaonenaka ni mavazi ya gharama 

kubwa.” Lucy akawaza kisha akaanza 

kujaribisha vazi moja moja. 

 “Utafikiri alinipima manake kila nguo 

imenikaa vyema” Lucy akawaza halafu 

akatoka mle chumbani na kwenda 

sebuleni alikokuwa amekaa Jack 

akitazama televisheni.Jack akastuka 

alipomuona. 

 “Wow ! nilijua tu.Nilijua tu mara 

utakapokuwa ndani ya mavazi haya ni 

lazima utabadilika.You are so amazing” 

jack akasema huku amesimama akiwa na 

tabasamu la mshangao 

 “Nenda kavae na zile nyingine nione” Jack akamwambia Lucy ambaye akarudi 

chumbani kwake akiwa mwingiwa furaha 

kwa sifa alizopewa na Jack .Akavaa vazi 

jingine,akarudi tena sebuleni kukaguliwa 

na jack.Vazi la mwisho lilikuwa ni gauni 

jekundu refu ambalo lilimkaa na 

kumpendeza Lucy kupita nguo zote. 

 “Kwa vazi hili,Lucy umependeza.Sipati 

picha siku umevaa vazi hili huko mtaani 

itakuwaje.” Jack akasema huku akimkagua 

Lucy kwa makini.Akamsogelea karibu. 

 “Lakini hapa kifuani hapatakiwi pawe 

namna hii.Unatakiwa upate nguo ya ndani 

ambayo itaendana na rangi ya vazi” jack 

akasema huku akimsogelea Lucy karibu 

na kuirekebisha nguo ile katika maeneo ya 

kifua na ghafla Lucy akastuka kama mtu 

aliyepitiwa na chaji za umeme. 

 “Mbona umestuka ,kulikoni? Jack 

akauliza kwa mshangao 

 “Umenigusa shingoni nikastuka sana” 

Lucy akasema huku akitazama chini.Jack 

akatabasamu na mara kengele ya 

mlangoni ikalia kuashiria kwamba kuna 

mtu getini. 

“ngoja nikatazame ni nani.Nisubiri hapa nakuja” Jack akasema na kutoka kuelekea 

getini. 

 “Jack amenigusa shingo nikastuka 

sana.Nini kimenitokea? Nimesikia 

msisimko wa ajabu sana.” Lucy akawaza 

huku akiupeleka mkono kifuani pake na 

kushika mahala ulipo moyo.Mapigo ya 

moyo wake yalikuwa yakienda kwa kasi . 

 Wakati akielekea getini Jack naye 

alikuwa ameinamisha kichwa chini 

akiwaza 

 “Kwa nini Lucy alistuka nilipomgusa 

shingo? Du ! alistuka sana mpaka 

nikaogopa..Nakumbuka jana usiku 

aliniambia kwamba hajawahi kuguswa na 

mwanaume yoyote yule.Nadhani hii ndiyo 

sababu nilipomgusa akastuka.Lucy ni binti 

anayevutia mno.Hata mimi tayari 

ameshaanza kunishawishi.Ana umbo 

linalotamanisha mno….” 

 Jack akafika getini na kulifungua 

akakutana na Elisha. 

 “hallo Elisha ,karibu sana” Jack 

akamkaribisha Elisha 

 “Ahsante sana jack.Nimeleta huu 

mzigo.Chakula cha mbwa” Akasema Elisha 

na kumkabidhi jack mfuko ule wa nyama akaondoka zake. 

 “ Kwani kuna tatizo lolote nikitembea na 

Lucy? Yule ni msichana wa ndani tu na 

wala hatuna uhusiano wowote wa 

kindugu.Lucy anahitaji kupata mtu wa 

kumfundisha na kumpatia raha za dunia 

hii.Kama ni kweli alivyokuwa akinieleza 

kwamba hajawahi kuguswa na mwanaume 

yoyote kwa nini basi mimi nisiwe wa 

kwanza? Pale alipo tayari mwili 

umeshaanza kupata msisimko na ndiyo 

maana alistuka mara tu nilipomgusa 

shingoni.Hapana leo simuachi.……..” Jack 

akawaza huku akitembea kwa kasi 

kuelekea sebuleni alikomuacha 

Lucy.hakukumbuka kufunga tena 

geti.Mawazo yake yote yalikuwa kwa Lucy 

 “Ni Elisha ndiye aliyekuwa 

akigonga.Ameleta nyama ya mbwa” Jack 

akamwambia Lucy. 

 “Elisha ? Ameshaondoka? Lucy akauliza. 

 “Ndiyo ameshaondoka.Vipi kuna tatizo 

lolote? Jack akauliza 

 “hapana jack hakuna tatizo lolote” Lucy 

akasema huku moyoni akijilaumu sana 

kwa Elisha kuondoka kwani alitamani 

kama angeonana naye.  “Ok Hebu geuka nyuma nikutazame 

ulivyopendeza.” Jack akamwambia Lucy 

ambaye aligeuka huku akitabasamu 

 “Jamani huyu mtoto ni balaa tupu.Liwalo 

na liwe lakini leo simuachi.Mtoto 

ameyaamsha mashetani yangu.” 

 Jack akawaza kisha taratibu akasogea na 

kuyashika mabega ya Lucy. 

 “Kilichobaki hapa ni mkufu wa dhahabu 

ambao utashuka mpaka hapa” Jack 

akasema huku akiupeleka mkono kifuani 

.Lucy akabaki amesimama kama vile 

amepitiwa na umeme.Alihisi mstuko 

mkubwa mara Jack alipokigusa kifua 

chake..Jack aliligundua hilo akaushusha 

mkono chini kidogo ya pale alipokuwa 

amepagusa ,akausimamisha katika titi la 

kulia.Lucy akatoa mguno hafifu na kuvuta 

pumzi kwa kasi.Akataka kugeuka lakini 

tayari Jack alikwisha mdhibiti ipasavyo. 

 “kaka Jack mimi sitaki,niache niende.” 

Lucy akasema kwa taabu 

 “Shhhhhhhhh!!!….tulia Lucy nikufundishe 

mchezo mzuri .Tulia nikupe raha” 

Lucy akajaribu kufanya purukushani ili 

achomoke mikononi mwa Jack lakini 

tayari Jack alikuwa amemkamata kwa nguvu. 

Pamoja na kwamba alikuwa akiogopa , 

kwa upande wa pili alihisi msisimko wa 

ajabu kila pale Jack alipokuwa 

akimgusa.Kadiri muda ulivyokuwa 

ukienda alihisi kuishiwa nguvu.Jack 

aliendelea kuupeleka mkono wake wa 

kulia katika kila kiungo alichoamini 

kingeweza kumsisimua Lucy.Kwa sasa 

Lucy alikuwa akihema mfululizo huku 

akitoa mguno kutokana na raha alizokuwa 

akisikia.Alikuwa hajiwezi.Alihisi raha ya 

aina yake.Jack akamketisha sofani.Lucy 

alihisi macho mazito kufunguka.Katika 

umri wake wa miaka kumi na tisa 

hakuwahi hata mara moja kuhisi raha ya 

namna ile.Ilikuwa ni mara yake ya kwanza 

 “ja…a…aaac.k….Lucy akajaribu kuongea 

lakini sauti yake ilikuwa ikikwama.Jack 

alikwisha pandisha mzuka na kwa haraka 

akalivua lile gauni alilovaa 

Lucy,akabakiwa na nguo za ndani.Jack 

mapigo ya moyo yakabadilika na kuanza 

kwenda kwa kasi .Udenda ulimtoka baada 

ya kuushuhudia mwili mwororo wa Lucy 

mwili ambao haujawahi kuchezewa na 

mwanaume yeyote .Akazidisha manjonjo na kuzidi kumpagawisha Lucy na 

kumfanya azidi kutoa sauti za miguno kwa 

raha alizokuwa akizisikia. 

 Dakika chache baadae Jack alikuwa juu ya 

mwili wa Lucy ambaye alikuwa 

akilalamika kwa maumivu 

aliyoyasikia.Tayari Lucy alipoteza 

usichana wake.Jack aliendelea 

kushughulika bila kujali kelele alizokuwa 

akizitoa Lucy na mara ghafla akastuliwa 

na sauti kali ya mtu aliyesimama 

mlangoni.Alikuwa ni mama yake Jack 

aliyerudi nyumbani kwa dharura.Jack 

alitamani ardhi ipasuke aingie ndani.Kwa 

kasi ya aina yake akaruka toka pale sofani 

akanyakua nguo zake na kukimbia 

kuelekea chumbani kwake na kumuacha 

Lucy pale sofani.Lucy alistushwa na 

kitendo cha Jack kuinuka ghafla na 

kutimua mbio.Hakuwa amesikia sauti ya 

mama yake Jack aliyekuwa amesimama 

mlangoni asiamini kile 

alichokiona.Akainuka pale sofani na kitu 

cha kwanza kukiona ni damu iliyokuwa 

imemtoka na maumivu makali sehemu za 

siri.Ghafla akasikia kama hatua za mtu 

akitembea akageuza shingo kutazama akakutanisha macho na mama yake 

Jack.Akahisi mwili kufa ganzi.Akashindwa 

afanye nini. 

 Mwili wote ulikuwa ukimtetemeka 

kwa uoga.Sura ya mama Jack ilikuwa 

imebadilika na kuwa kama mbogo 

majeruhi.Alikuwa amefura kwa 

hasira.Huku akitetemeka na machozi 

kumtoka Lucy akapiga magoti. 

 “mama naomba unisamehe kwa kosa hili 

sintarudia tena.Hatujawahi kufanya hivi 

leo ni mara yangu ya kwanza.Mama 

naomba unisamehe sintarudia tena 

kufanya kitendo kama hiki” 

 Mama Jack akamtazama Lucy aliyekuwa 

amepiga magoti kwa macho makali halafu 

akayaelekeza macho katika damu 

iliyokuwa sofani akauma meno kwa hasira 

na kusema. 

 “Lucy inuka vaa nguo zako haraka.Halafu 

ninaingia chumbani nikitoka nikute 

umeshaondoa uchafu wote hapa sebuleni.” 

Mama Jack akasema kwa hasira huku 

akipiga hatua kwa kasi kuelekea 

chumbani kwake.Lucy akainuka na kuvaa nguo zake kisha akachukua chombo na 

kufanya usafi pale sebuleni kusafisha 

damu zilizokuwa sofani.Bado mwili 

ulikuwa ukimtetemeka kutokana na uoga 

uliompata baada ya kukutwa sebuleni 

wakifanya kiendo kile. 

 “Siku yangu ya kwanza imekuwa na 

mkosi namna hii.Sijui ni kwa nini 

nilimkubalia Jack tufanye vile.Najutia 

maamuzi yangu.Sijui mama 

atanichukuliaje.Nimemuona amekasirika 

sana.Sijawahi kumuona akiwa 

amekasirika kiasi kile.” Lucy akawaza 

huku akidondosha machozi 

 Baada ya kumaliza kufanya usafi pale 

sebuleni akaelekea chumbani kwake 

akajifungia akilia.Kwanza alikuwa akilia 

kutokana na maumivu aliyokuwa 

akiyasikia na pili alikuwa akilia kwa 

sababu hakujua hatima yake baada ya 

kufumwa wakifanya tendo lile sebuleni. 

 “Ngoja nikamuombe mama 

msamaha.Kama si ushawishi wa Jack 

nisingefanya hivi.Ni kweli nilikuwa 

nahitaji kujaribisha kufanya mapenzi ili 

niisikie hiyo raha wanayosema watu 

wanaipata wakifanya mapenzi lakini sikutaka kufanyia pale sebuleni.Ni Jack 

ndiye aliyenishawishi tukafanyia pale hadi 

mama alipotukuta.Itanibidi nimueleze 

mama ukweli ili anisamehe.” Lucy 

akawaza kisha akachukua nguo yake 

akafuta machozi halafu akasimama .Kila 

alipotaka kupiga hatua kutoka mle 

chumbani akasita.Alihisi miguu inakuwa 

mizito kunyanyuka.Mwioshowe akajikaza 

na kuamua kwenda kuonana na mama 

Jack.Mara tu alipofungua mlango 

akakutanisha macho na mama Jack 

aliyekuwa akielekea kule chumbani kwa 

kasi huku bado amevimba kwa 

hasira.Lucy akaogopa sana akabaki 

amesimama mlangoni asijue la kufanya 

 *********** 

 Baada ya kutoka mbio pale sebuleni 

Jackson akaelekea chumbani kwake 

akaufunga mlango wake kwa 

funguo.Alikuwa akihema kwa nguvu. 

 “Sijui nitauweka wapi uso 

wangu.Sikutegemea kama mama 

angetokea mida hii.Nimefanya kosa kubwa 

sana.Mama alikuwa akiniamini mno kwamba ni mtoto niliyetulia lakini kwa 

kitendo alichokishuhudia leo kimevunja 

kabisa uaminifu huo kwa mama.I’m so 

stupid.” Jack akakipiga kichwa chake kwa 

mkono wake wa kulia.Akavaa nguo na 

kuketi sofani. 

 “Nimefanya jambo la aibu mno.Kibaya 

zaidi nimemsababishia hatari Lucy.Kwa 

jinsi ninavyomfahamu mama yangu 

sidhani kwama Lucy atakuwa na 

usalama.Sina hakika kama atakubali 

kuendelea kuishi naye baada ya 

kukishuhudia kitendo kile.Lucy hakuwa 

tayari kufanya vile ni mimi ndiye 

niliyemshawishi na kumsababishia balaa 

hili lote.No ! lazima nikamtetee Lucy kwa 

mama.Ninayepaswa kulaumiwa na 

kuadhibiwa ni mimi na si Lucy.” Akawaza 

Jack,akainuka na kuvaa fulana . 

 “Naogopa kuonana na Mama lakini ngoja 

niwe jasiri nikaonane naye nijaribu 

kumtetea Lucy halafu nimuombe mama 

msamaha ili mambo haya yasimfikie 

baba.Du ! endapo atafahamu kuhusu 

jambo hili nitakuwa nimejisababishia 

balaa kubwa” Jack akawaza akavuta umzi 

ndefu na kukishika kitasa akaufungua mlango.Kabla hajapiga hatua moja 

akasikia mama yake akiongea kwa 

ukali.Akaogopa kutoka akatega sikio lake 

kusikiliza. 

 “tayari mambo yameanza.Ni muda mrefu 

sijamsikia akifoka na mama huwa 

akiongea kwa sauti kali namna ile ujue 

kuna kitu kimemkasirisha kupita 

kiasi.Masikini Lucy ‘Jack akawaza lakini 

hakuwa na lakufanya.Hakuwa na ujasiri 

wa kuweza kuonana na mama yake kwa 

wakati ule.Akabaki amejibanza pale 

mlangoni akisikiliza mama yake akifoka 

kwa sauti ya juu. 

 ************* 

Lucy alibaki ameganda pale mlangoni 

kama sanamu alipomuona mama yake 

Jack akielekea kule chumbani 

kwake.Jasho lilikuwa likimtoka na 

machozi yaliendelea kumchuruzika bila 

kukauka.Alikijutia kitendo alichokifanya. 

Mama jack alizidi kuja kwa mwendo wa 

kasi akiwa amevimba kwa hasira.Toka 

ameanza kufanya kazi katika nyumba hii 

kama mtumishi wa ndani Lucy ahajawahi hata mara moja kumshuhudia mama huyu 

mwenye tabasamu lisilokauka akiwa 

katika hali hii.Akaogopa sana. 

 “mama naomba unisamehe sintarudia 

tena kufanya kitendo kile.” Lucy akapiga 

magoti a kuomba msamaha baada ya 

mama jack kumkaribia.Kitendo kile ni 

kama kiliongeza hasira za mama 

Jack.Akamfuata Lucy pale chini na 

kumuinua kwa nguvu 

 “Inuka haraka mnafiki mkubwa 

wewe.Siku zote nimekuthamini na 

kukuchukulia kama mwanangu 

.Nimekulea na kukutunza ,siku zote 

nimekuwa nikikufunza maadili mema 

nawe ukakiri kwamba umenielewa kumbe 

nikitoka unafanya huu ushenzi 

wako.Umeniudhi sana Lucy.Nimechukia 

sana.Tena bila aibu unafanya mapenzi na 

mtoto wangu sebuleni katika kiti ambacho 

wanakaa wazazi wenu na bila hata wasi 

wasi mnafanya mambo yenu kwa uhuru 

mkubwa na hata mlango 

hamjafunga.Natamani sijui nikumeze kwa 

hasira nilizonazo.Imekuwa ni bahati 

nimewakuta mimi,ingekuwaje kama 

mngekutwa na mgeni ?Tungezificha wapi nyuso zetu kwa aibu hii kubwa? 

 Mama jack alikuwa akiongea kwa ukali 

na kwa hasira alizokuwa nazo machozi 

yalikuwa yakimtoka.Lucy akaogopa sana 

akaamua kufumbua mdomo na kujitetea. 

 “Mama ni leo tu 

nimefan…………………………….” Kabla 

hajamaliza kuongea mama Jack akaongea 

kwa sauti ya ukali 

 “kelele fisi wewe !.Tena usithubutu 

kuongea wakati ninaongea .Kibaya zaidi 

Jackson ni sawa na kaka yako.Umedriki 

kumshawishi hadi akashawishika na 

uchafu wako.Nimemlea Jack katika 

maadili makubwa na ninaamini kwamba 

ni wewe ndiye uliyemshawishi hadi 

akakubali kufanya uchafu ule.Kama leo 

umediriki kufanya na Jack mchana 

kweupe vipi siku ambazo huwa hakuna 

mtu hapa nyumbani? Inaonekana 

wanaume huwa wanapishana kama timu 

ya mpira.Inaonekana umeigeuza nyumba 

yangu danguro la kufanyia uchafu 

wako.Nasema ahsante sana kwa sababu 

hizi ndizo fadhila unazonilipa baada ya 

mema yote niliyokufanyia.” Mama jack 

akazidi kuwa mkali.Lucy akapiga magoti na kumshika miguu akajaribu kuomba 

msamaha. 

 “Mama nimefanya leo tu na Jack.naomba 

unisamehe sintarudia tena” Lucy akaomba 

msamaha huku akilia . 

 “tafadhali usinishike miguu.Huna faida 

kwangu hata kidogo.Kwa kuwa 

umeonyesha dharau sasa naomba 

unisikilize kwa makini.Nenda chumbani 

kwako,funga kila kilicho chako .Sitaki 

kukuona tena hapa nyumbani 

kwangu.Chukua hizi hapa shilingi laki 

tano zitakusaidia kuanzia 

maisha.Nimekupa kiasi hicho cha fedha 

kwa sababu ninakupenda na sitaki upate 

shida huko uendako.Siaki uendele 

kunililia .Inuka na ukafunge mizigo yako 

na uondoke hapa mara moja.” Mama jack 

hakuwa na masihara tena.Alikuwa na 

hasira zisizomithilika.Akamuacha Lucy 

akiwa ameinama akilia akatembea kwa 

kasi kuelekea chumbani kwa 

Jackson.Akakiminya kitasa kwa nguvu 

lakini mlango ulikuwa umefungwa kwa 

funguo 

 “hata ukifunga mlango,labda uchimbe 

handaki utokeze kwa nje lakini kama si hivyo lazima tupambane.Umenisikitisha 

sana Jack.Sikutegemea hata siku moja 

kama ungeweza kufaya kitendo cha aibu 

namna ile.Kama ni uchafu wenu ingekuwa 

vyema mngeenda kujificha huko vichakani 

mkafanya tani yenu lakini si kufanyia 

sebuleni.Hii ni dharau kubwa sana na 

kamwe sintavumilia vitendo vya dharau 

nyumbani kwangu.Ingekuwaje kama ni 

mgeni amekuja na kuwakuta mkifanya 

uchafu ule? Jack umeniudhi sana leo na 

kwa hili ni lazima nimweleze baba yako na 

unafahamu jinsi baba yako alivyo.lazima 

mtapigana ngumi.” Mama Jack akasema 

huku akiugonga mlango wa chumba cha 

Jack kwa nguvu.Jack alikuwa amejifungua 

ndani akiogopa.Aliposikia kauli ya 

kwamba habari zile zitamfikia baba yake 

aliogopa sana ikamlazimu afungue mlango 

ili amuombe msamaha mama yake mambo 

yale yaishe na yasimfikie baba yake. 

 Baada tu ya kufungua mlango alikutana 

na sura iliyojaa hasira ya mama yake na 

bila maelezo akamvaa na kuanza 

kumvurumishia makofi makali mfululizo. 

 “mama nisamehe nimekosa sintarudia 

tena” Jack akajaribu kujitetea.Mama yake hakusema chochote akaendelea 

kumtandika makofi.Alipotosheka 

akamsukumia ndani. 

 “Na kuanzia sasa wewe ndiye 

utakayekuwa ukifanya kazi zote za humu 

ndani kwa sababu huyu mke wako sitaki 

kumuona tena katika nyumba yangu” 

akasema mama Jack huku akihema kwa 

nguvu.Jack alikuwa amesimama mlangoni 

hana la kufanya uso wake ukiwa 

umevimba kwa makofi aliyotandikwa na 

mama yake. 

 Mama Jack akaondoka kwa kasi na 

kuelekea chumbani kwa 

Lucy.Akausukuma mlango na kuingia kwa 

nguvu 

 “Bado hujafungasha mizigo 

yako?Akauliza kwa ukali. 

 “Ninafunga mama” Lucy akasema huku 

akimwaga machozi.Mpaka hapa aliamini 

hakukuwa na namna nyingine ya kuweza 

kumshawishi mama Jack abadili msimamo 

wake.Kilichobaki ilikuwa kufunga mizigo 

na kuondoka nyumbani kabla mambo 

hayajaharibika.Mama Jack alitoka mle 

ndani kwa kasi na kuelekea chumbani 

kwake na baada ya muda mfupi akarudi na sanduku kubwa lisilokuwa na kitu 

ndani akaliweka kitandani na kuanza 

kupakia nguo na vitu mbali mbali vya 

Lucy.Baada ya kuhakikisha vitu vyote 

vimeingia ndaniya lile sanduku 

akamtazama Lucy usoni. 

 “Kuna chochote kilichobakia? 

 “Hakuna mama” Lucy akasema 

 “Kuna hela au kitu chochote unachonidai? 

 “hakuna mama” Lucy akasema 

 “Ok kama hakuna basi nakutakia safari 

njema na maisha mema huko 

uendako.Umeshakuwa mtu mzima sasa 

kwa hiyo unahitaji uwe na nyumba yako.” 

Mama Jack akasema huku akiufungua 

mlango na kumruhusu Lucy atoke.Bado 

machozi yakiendelea kumdondoka Lucy 

akalikokota lile sanduku kubwa alilopewa 

na mama Jack na kuanza kutoka mle 

chumbani.Ghafla akakutanisha macho na 

Jack,akapandwa na hasira baada ya 

kumuona mtu ambaye alisababisha yale 

yote yatokee. 

 “Lucy mbona umesimama? Tafadhali 

naomba uendelee na safari” mama Jack 

akafoka na kisha Lucy akaendelea 

kulikoota sanduku lake na kutoka nje.  “kwa heri ya kuonana “ mama jack 

akasema huku akilifunga geti baada ya 

Lucy kutoka . 

Kwa haraka akarudi ndani na kumkuta 

jack amesimama katika mlango wa sebule. 

 “mama naomba unisikilize.Lucy hakuwa 

na makosa,ni mimi ndiye niliy………..” 

kabla hajamaliza kuongea mama yake 

akasema kwa ukali 

 “Jack nimesema sitaki kusikia lolote 

kutoka kwako.kama hujaridhika na 

unaona mkeo ameonewa na wewe funga 

mizigo yako na uondoke hapa haraka sana 

mfuate mkaanze maisha” Kauli ile ya 

mama yake ikamnyong’onyeza Jack na 

taratibu akaondoka huku ameinamisha kichwa.




Mita mia mbili toka aliache geti la 

nyumba aliyoizoea na kuiona kama ni 

nyumbani kwao,Lucy akasimama 

akageuka na kuitazama nyumba ile 

iliyokuwa ikionekana bati la kijani,akafuta 

machozi yaliyokuwa yakimdondoka. 

 “Sikutegemea kama mambo yangekuwa 

hivi.Lakini yote haya ameyasababisha Jack 

kwani ni yeye ndiye aliyenishawishi 

kufanya mapenzi palesebuleni.Nilikuwa 

mjinga sana kumkubalia kiurahisi namna 

ile.Shauku yangu ya kutaka kujaribu 

mambo imenitokea puani.Kwa sasa sina 

mahala pa kwenda na sijui nianzie 

wapi.Sina ndugu yeyote hapa mjini na 

wala sina rafiki.Nitafanya nini? “ Lucy 

akawaza halafu akaliinua sanduku lake na 

kuendelea na safari. 

 “Mama amenipa shilingi laki tano na pesa 

yangu niliyokuwa nikilipwa mshahara 

niliyokuwa nikiitunza ni shilingi laki saba 

na thelathini.kwa jumla nina shilingi 

milioni moja na zaidi.Hizi zinaweza kabisa 

kunisaidia kuanzisha maisha 

yangu.Ninaweza kununua kitanda na 

kupanga chumba ,halafu nikapata na 

vyombo kidogo vya kuanzia maisha na 

zitakazobaki ninaweza kubuni biashara 

yoyote ya kufanya.” Lucy akatabasamu 

baada ya kupata wazo lile. 

 “Kuna siku niliwahi kusikia mtu akiongea 

kwamba kila jambo hutokea kwa 

sababu.nadhani hata huku kufukuzwa 

kwangu nyumbani kuna sababu maalum 

ya kunifanya nikajifunze maisha halisi 

yakoje.Ningeishi katika jumba lile 

nikifungiwa hadi lini? Sitakiwi kuendelea kulia wala kujilaumu.Niko huru sasa 

kufanya jambo lolote.lakini katika vitu 

vyote nayachukia mapenzi 

sana.Nilitegemea ningesikia raha na 

badala yake ni karaha na 

maumivu.Nitaishi mwenyewe.Sihitaji tena 

mwanaume.Siku yangu ya kwanza kufanya 

mapenzi mwanaume wangu wa kwanza 

imekuwa na balaa .Sitaki mwanaume 

mwingine tena.Nitaishi mwenyewe.” Lucy 

akawaza huku akiendelea na safari 

kuelekea kituo cha basi.hakujua anataka 

kwenda wapi lakini alikuwa akielekea 

kituo cha dala dala. 

 “Sasa ninataka kwenda wapi? Akawaza 

akiwa amesimama katika kituo cha 

dalaladala 

 “Nimekumbuka kitu.Ni kwa nini nisiende 

kwa Pendo yule dada ambaye ndiye 

aliyenitoa Singida na kunileta huku kuja 

kunitafutia kazi.Hili ni wazo zuri.Nina 

imani bado ananikumbuka japokuwa ni 

muda mrefu sijakwenda hata 

kumtembelea.Nitamuomba nikae kwake 

kwa muda wa siku chache wakati 

nikijipanga kuanza maisha yangu 

mwenyewe.Halafu kwa kuwa yeye anafahamika hapa mjini itakuwa rahisi 

kunitafutia chumba cha kuishi na hata 

kunisaidia kubuni biashara ya 

kufanya.Ngoja nielekee kwake.Iwapo 

nitamkosa basi nitajua namna nyingine ya 

kufanya” Lucy akapanda dala dala 

lililokuwa likielekea Kijenge 

mwanama.Njiani alikuwa akitabasamu 

kila alipowaona wasichana wenzake 

walivyokuwa wamejipamba na kuonekana 

nadhifu. 

 “hata mimi siku moja nina imani 

nitakuwa na maisha kama yo.Nitakuwa na 

maisha mazuri,nitakuwa mrembo.” 

Akawaza. 

 Baada ya kushuka katika dala dala Lucy 

akalibeba sanduku lake na kuanza 

kutembea kuelekea katika nyumba 

anayoishi Pendo,mtu pekee ambaye 

anamfahamu mjini Arusha.Hakuwa mgeni 

wa meneo yale ya kijenge kwa sababu 

kabla hajapata kazi kwa akina Jack aliishi 

na Pendo kwa miezi takribani minne. 

 Geti la nyumba ya Pendo lilikuwa wazi 

akaingia na kuelekea moja kwa moja 

mlango wa sebuleni akagonga.Sauti ya 

muziki iliyokuwa ikitoka mle ndani ilimuhakikishia kwamba Pendo 

atakuwepo.Mara mlango ukafunguliwa na 

dada mmoja mweupe aliyejipamba 

akapambika akajitokeza. 

 “karibu mgeni” akasema Pendo huku 

akimtazama Lucy kwa makini. 

 “Ahsante dada Pendo.Mimi ni Lucy yule 

msichana uliyemtafutia kazi kwa mama 

Jack.Unanikumbuka? 

 Pendo akapatwa na mshangao 

 “Ni wewe Lucy? ..Ouh gosh ! ndiyo 

umekuwa hivi? Umenenepa halafu 

umependeza.Umekuwa msichana mkubwa 

tofauti na kipindi kile ulikuwa bado katoto 

kadogo” Pendo akasema huku akilichukua 

begi la Lucy na kuliingiza ndani. 

 “karibu Lucy.habari za huko” Pendo 

akasema huku akimfungulia Lucy soda 

 “habari za huko nzuri” 

 “hawajambo mabosi wako? 

 “hawajambo wanakupa salamu nyingi” 

Lucy akasema 

 “Enhee ! Ni kwa nini muda wote huo 

umekaa bila hata kuja kunisalimia ? 

 “dada Pendo kazi zilikuwa nyingi halafu 

pale ni geti kali sikuruhusiwa kutoka” 

 “Ok .Kwa hiyo leo ndiyo wamekupa likizo?  “si likzo dada Pendo .Nimeamua kuacha 

kazi nataka kuanza maisha yangu”Lucy 

akasema na kumfanya Pendo astuke 

kidogo. 

 “Unataka kuanza maisha yako Kivipi? 

Akauliza pendo. 

 “nataka kuishi maisha 

yakujitegemea.nataka kupanga chumba 

changu na kuanzisha japo kibiashara 

kidogo.” 

 “sasa mdogo wangu kupanga chumba na 

kuanzisha biashara vyote vinahitaji kuwa 

na pesa..wewe una pesa za kutosha 

kufanya hivyo? 

 “Ndiyo dada Pendo nina kiasi cha kutosha 

kuniwezesha kuanza maisha.” 

 “Una shilingi ngapi” 

 “Nina shilingi milioni moja na zaidi.Si 

ninawea kabisa kuishi na kufanya 

biashara yangu ndogo? Nimekuja kwako 

ili unisaidie nipate chumba cha kuishi na 

vile vile unisaidie kubuni biashara ndogo 

ya kuniwezesha kuishi hapa mjini” Lucy 

akasema 

 “wow ! mdogo wangu umenikuna 

sana.Umewezaje kuwa na kiasi kikubwa 

hivyo cha pesa? Kweli mdogo wangu nimeamini una akili.Sasa sikiliza.Hapa ni 

nyumbani kwako.Utakaa hapa na mimi 

nitakusaidia kukutafutia chumba na hata 

kukusaidia kuanzisha biashara 

nzuri.Nimefurahi sana kuona ni namna 

gani ulivyokuwa na akili mdogo 

wangu.lakini kabla hujaanza kujitegemea 

ninaomba msaada wako.” 

 “msaada upi dada Pendo” 

 “Nimefungua grosari la kuuza 

vinywaji.Mpaka sasa hivi bado sijapata 

mtu wa kunisaidia kuuza.Ninaomba 

wakati bado ninahangaika kukutafutia 

chumba na kukubunia biashara,unisaidie 

kuuza grosari langu na mimi nitakulipa 

mwisho wa mwezi.Unasemaje kuhusu 

hilo? 

 “Hakuna shaka dada Pendo.Nimefurahi 

sana kwa sababu itanisaidia hata mimi 

kujifunza namna ya kufanya biashara.” 

 “Ahsante sana mdogo wangu.Nimefurahi 

sana.Ninaona ni kama Mungu alikuleta ili 

uje tukae pamoja na tufanye 

biashara.Nitahakikisha maisha 

yanakunyookea hadi wewe mwenyewe 

utashangaa.Kwa sasa leta hizo pesa zako 

nikakuwekee benki ili mpaka utakapoamua kuanza maisha yako 

mwenywe ujikute una pesa za kutosha ” 

 Pendo akasema huku akitabasamu na 

kwa furaha Lucy akalifungua sanduku lake 

na kumkabidhi Pendo pesa yote aliyotoka 

nayo kwa akina Jack. 

 “Lucy hapa ni nyumbani kwako,jisikie 

huru.Mimi natoka tutaonana baadae.” 

Pendo akasema na kuondoka akimuacha 

Lucy ameketi sofani 

akitabasamu.Hakuamaini kama mambo 

yameanza kumwendea vizuri namna ile. 

 “Siku yangu ya kwanza kufanya 

mapenzi,Mara yangu ya kwanza 

kukamata kiasi kikubwa hivi cha pesa, na 

ni mara yangu ya kwanza kuwa huru 

badaa ya kuwa nafungiwa ndani kama 

mifugo.Siku hii ya kwanza inaonekana 

kuwa na nuru japokuwa ilianza kwa balaa 

lakini inaisha kwa nuru.Pamoja na yote 

siku hii sintaweza kuisahau maishani .” 

Lucy akawaza akachukua maji na 

kuelekea bafuni kuoga. 

 Lucy akafungua ukurasa mpya wa maisha 

yake.Akaanza kufanya kazi ya kuuza 

vinywaji katika grosari ya Pendo. 

Mwanzoni ilimuwia vigumu kwa sababu bado hakuwa amezoea kuchangamana na 

watu hususan walevi.Kutokana na jinsi 

umbo lake lilivyokuwa zuri na la kuvutia 

watu wengi walikuwa wakivutiwa naye na 

kumtaka kimapenzi.Alikumbana na 

vikwazo vingi vya wanaume wakimtaka 

kimapenzi.Uzuri wake ulipelekea kila siku 

watu wafurike katika grosari ile 

aliyokuwa akiuza.Wengi wa waliokuwa 

wakija kunywa hapa walisikia uzuri wa 

Lucy na jinsi alivyojua kuhudumia wateja 

wake na wengi wakataka kuja kujaribu 

bahati yao.Pamoja na wakati mgumu Lucy 

aliokuwa nao kutoka kwa wanaume 

wakware,hata siku moja hakuthubutu 

kumkubalia mwanaume yeyote yule 

kutoka naye kimapenzi.Kila 

alipokumbuka kilichomtokea nyumbani 

kwa akina Jack aliumia sana na hakutaka 

tena kujihusisha na masuala ya 

mapenzi.Siku moja akiwa kazini Lucy 

akahisi kizungu zungu ikamlazimu 

kufunga grosari na kurejea nyumbani 

kupumzika.Akampigia simu Pendo na 

kumtaarifu kwamba anarejea nyumbani 

kupumzika baada ya kushindwa kufanya 

kazi kwa siku hiyo kutokana na hali yake kubadilika.Alipofika nyumbani akameza 

vidonge na kulala mpaka jioni.Saa moja za 

jioni Pendo akarejea na kumkuta Lucy 

akiendelea vizuri.Wakiwa wamekaa 

sebuleni wakiongea baada ya mlo wa 

usiku Lucy akamwambia Pendo 

 “Dada Pendo kuna jambo nataka 

kukueleza.” 

 “jambo gani hilo mdogo wangu? Pendo 

akauliza 

 “Dada Pendo nataka niache kazi” 

 “Unataka uache kazi !! Pendo akauliza 

kwa mshangao 

 “Ndiyo dada Pendo” 

 “kwa nini unataka uache kazi? 

 “dada nimechoka na usumbufu 

ninaoupata toka kwa 

wateja.Ninasumbuliwa sana kila 

siku.Wanaume wananitaka kimapenzi na 

mimi siko tayari kwa hilo.Kinachoniudhi 

ni kwamba kwa nini wanashindwa 

kuheshimu kazi yangu? Kazi ya uhudumu 

ni kazi kama zilivyo kazi nyingine lakini 

kila muhudumu wa baa wanamhesabu ni 

Malaya.Mimi ninajiheshimi sana na ndiyo 

maana toka nimeanza kazi sijamkubalia 

hata mmoja wao.Ili kuepuka usumbufu huu nimeona itakuwa vyema kama 

nikiacha kazi “ akasema Lucy.Pendo 

akamuangalia kwa makini,akamsogelea 

na kusema. 

 “Mdogo wangu naomba tafadhali usiache 

kazi kwa sasa.Nafahamu ni usumbufu wa 

namna gani unaoupata kutoka kwa 

wateja.Yote hii ni kutokana na umbo lako 

zuri. Lucy wewe ni msichana mzuri sana 

na ndiyo maana unawatoa udenda 

wanaume kila upitapo.Lucy mdogo wangu 

naomba nikueleze kwamba uzuri huu 

ulionao ni mtaji tosha wa kuweza 

kukufanya wewe ukaishi maisha mazuri 

na yenye furaha kuliko hata mimi.Laiti 

kama uzuri huu ulionao ningekuwa nao 

mimi ,ningekuwa ni mwanamke tajiri sana 

.Vigogo wote wa mji huu 

ningewakamata.Sikufundishi tabia mbaya 

mdogo wangu lakini kwa sasa umekwisha 

kuwa msichana mkubwa na kwa hiyo 

unatakiwa uanze kujenga maisha 

yako.Unatakiwa uutumie vyema uzuri 

wako.Usisubiri hadi wakati umeshazeeka 

ndipo ukastuka.Wakati ni huu.Mimi 

nakushauri kwamba tafuta mtu mmoja 

ambaye utatulia naye ambaye atakugharamia,atakutunza ,atakuwezesha 

kimasha.Unaona hapa nilipo mimi ni kwa 

sababu nilikuwa na mwanaume mmoja 

ambaye anafanya biashara ya 

madini.Huyo ndiye aliyenijengea 

nyumba,akaninunulia gari,na hata mtaji 

wa kuanzisha biashara ile ya grosari 

amenipa yeye.Nakushauri hata wewe 

tafuta mtu mmoja ambaye anaweza 

akakutoa kimaisha.Nimekuwa 

nikisumbuliwa na wanaume wengi 

wakinitaka niwaunganishe kwako.Mimi 

nimekuwa nikiogopa kufanya hivyo bila ya 

ridhaa yako mwenyewe.Kama utakuwa 

tayari,kuna mzee mmoja anafanya kazi 

mamlaka ya mapato ana fedha za 

kutupa.Mzee huyu amekuwa akikutaka 

mara nyingi lakini siku zote nimekuwa 

nikimzungusha na kumwambia kwamba 

bado haujanipa jibu.Kama utamkubali 

mzee huyu ,nakuhakikishia kwamba 

maisha yako yatabadilika na kuwa mazuri 

kuliko hata ya kwangu.Mzee yule ni mtu 

wa heshima zake kwa hiyo hana mambo 

ya kitoto.Japokuwa ana mke wake lakini 

hiyo si sababu kwani kama akiwa nawe 

atakufanya mke wake mdogo na utapata kila kitu unachokihitaji katika maisha 

haya.Mdogo wangu hii ni nafasi 

umeipata.Naomba usiiache.Itumie angali 

bado mapema ujenge maisha yako” Pendo 

akasema na kumtazama Lucy aliyekuwa 

ameweka mkono shavuni akisikiliza kwa 

makini. 

 “Dada Pendo mimi nimekusikiliza kwa 

makini lakini naomba nikwambie kwamba 

siko tayari kufanya hivyo unavyotaka 

nifanye.Msimamo wangu utabaki pale pale 

kwamba nitajiweka mbali kabisa na 

wanaume na kama ikitokea nikahitaji 

mwanaume basi si katika kipindi 

hiki.Nahitaji kujenga kwanza maisha 

yangu na ndipo nifikirie masuala 

mengine.Dada mimi nimekuwa 

mfanyakazi wa ndani kwa miaka mingi na 

nimeshapata manyanyaso mengi kwa hiyo 

sitaki kuendelea kunyanyasika 

tena..Nataka nitumie nguvu zangu 

kuyajenga maisha yangu mwenyewe 

.Nataka nisome ili niwe na walau elimu ya 

kunisaidia kuelewa ulimwengu huu 

unavyokwenda.Iwapo nikianza 

kujishughulisha na masuala ya wanaume 

kwa sasa malengo yangu yote yataharibika.Kingine kinachonifanya 

nikatae ushauri wako ni kwamba 

ninawachukia wanaume sana.” Lucy 

akasema. 

 “Kwa nini unawachukia wanaume ? Pendo 

akauliza 

 “Sifahamu ni kwa nini lakini 

ninawachukia wanaume kupita kiasi” 

 Kimya kifupi kikapita Pendo akainuka 

akachukua kinywaji chake akanywa na 

kisha akasema 

 “Si kwamba nakulazimisha kufanya hivyo 

lakini nilikuwa najaribu kukushauri ni 

kwa namna gani unaweza ukaishi maisha 

mazuri hapa mjini kwa kutumia huo uzuri 

wako.Kama umeona kwamba ushauri 

wangu mimi haufai hakuna tatizo .lakini 

ninachokusihi kwamba usiache kazi kwa 

sasa .Subiri kwanza nijitahidi kumpata 

mtu wa kuweza kunisaidia kufanya kazi 

ile .Ok Lucy mimi nakwenda kulala 

tutaonana kesho ila usisahau kesho 

kwenda hospitali kupima kama una 

Malaria ”Pendo akasema na kuingia 

chumbani kwake. 

 “Toka mwanzo nilifahamu kitu kama hiki 

ni lazima kingejitokeza.Ni kweli mimi ni masikini nisiye na mbele wala nyuma 

lakini hii si sababu ya kunifanya 

niudhalilishe utu wangu kwa tamaa ya 

fedha.Nimekwisha weka mikakati ya 

kuishi na kujitegemea mwenyewe .Sitaki 

kuishi maisha ya kumtegemea 

mwanaume.Sitaki mtu anitumie atakavyo 

eti kwa sababu ya fedha zake” akawaza 

Lucy akiwa amejilaza sofani. 

 “Nikikumbuka maumivu niliyoyapata siku 

ya kwanza nimefanya mapenzi na Jack 

sitaki kurudia tena mchezo ule.Namuomba 

Mungu anisaidie ili niweze kulisahau tukio 

lile .Kila nikilikumbuka nahisi kama 

kichwa kinaniuma sana.Tena 

nimekumbuka kwa siku za hivi karibuni 

nimekuwa nikiumwa na kichwa,halafu 

nausikia mwili mchovu sana.Pengine 

ninaweza kuwa na Malaria.Wiki ya pili 

sasa nimekuwa nikijiskia hovyo sana kila 

asubuhi .Kama dada Pendo alivyosema 

kesho kabla ya kwenda kazini nitapita 

kwanza zahanati nikapate dawa na 

kuangalai malaria.” Akawaza Lucy 

akachukua glasi ya maji akanywa na 

kuelekea chumbani kwake kulala. 

Saa tatu za asubuhi siku iliyofuata ilimkuta Lucy katika dawati la wagongwa 

wanaosubiri kumuona daktari .Zamu yake 

ilipofika akaingia na kumueleza daktari 

jinsi anavyojisikia .Daktari akamuhoji 

maswali kadhaa kuhusiana na ugonjwa 

wake na kisha akaandika karatasi na 

kumpatia ili aelekee maabara kwa ajili ya 

vipimo.Nusu saa baadae vipimo vyote 

alivyoandikiwa na daktari vikawa tayari 

na hivyo akaitwa tena kwa daktari 

kwenda kupokea majibu yake. 

 “Lucy tumekupima malaria lakini hauna 

maambukizi ya Malaria,hauna ugonjwa 

mwingine wowote tuliofikiri unaweza 

kuwa nao.Lakini kuna swali ningeomba 

nikuulize” 

 “Uliza tu daktari” Lucy akasema 

 “Lucy wewe una elimu gani? 

 “Mimi nilisoma hadi darasa la nne 

nikaacha shule” 

 “Hapa Arusha unaishi na wazazi wako? 

 “Hapana.Ninaishi na dada “ 

 “Unafanya kazi gani? 

 “Nilikuwa mfanyakazi wa ndani na kwa 

sasa ninamsadia dada katika biashara ya 

kuuza vinywaji” 

 “Basi hii ndiyo sababu” Dokta akasema taratibu huku akimuangalia Lucy 

 “Sababu ya nini daktari? Lucy akauliza 

kwa wasi wasi 

 “Lucy tumegundua kwamba una ujauzito 

wa mwezi mmoja na wiki mbili “ 

 “Unasemaje !! Lucy akastuka na 

kusimama.Daktari akamsihi aketi kitini 

 “Tumekupima na tumegundua kwamba 

una ujauzito wa mwezi mmoja na wiki 

mbili.Nimekuuliza maswali haya ili nione 

kama una ufahamu wowote kuhusiana na 

masuala ya ujauzito kwa sababu 

inaonekana hukuwa ukijua kama u 

mjamzito.Ninachokushauri kuanzia sasa 

ni kuanza kuhudhuria kliniki ili waweze 

kukuelekeza njia bora zaidi za kuweza 

kujitunza kipindi hiki cha kulea mimba na 

hadi pale utakapojifungua” akasema 

daktari 

 Lucy aliinama kwa dakika zipatazo tatu 

na alipouinua uso wake macho yake 

yalijaa machozi. 

 “Mbona unaliza Lucy” Daktari akauliza 

 “Ninalia daktari kwa sababu sikutegemea 

kuwa na mtoto kwa sasa.Bado 

sijayatengeneza maisha yangu ,nitaishije 

na mtoto huyu? Nitamtunza vipi? Lucyakasema kwa uchungu 

 “Usilie Lucy.mambo kama haya huwa 

yanatokea sana na hasa pale unapofanya 

mapenzi bila kujikinga na mimba za bila 

mpangilio.Wasichana wengi ambao bado 

hawana elimu juu ya masuala ya uzazi na 

ngono salama wanajikuta wakipata mimba 

wasizozitarajia.Jambo limeshatokea ila 

ninachoweza kukushauri ni kwamba 

ongea na dada yako na umueleze hali 

halisi ili afahamu vile vile jadiliana na mtu 

unayedhani ndiye aliyekupa mimba hii na 

mpange mipango mizuri ya kumlea 

mwanenu atakapozaliwa. .Kingine 

ninachokuomba ni kwamba usifikirie 

kuitoa mimba hiyo.Nafahamu, wasichana 

wengi ambao huwa wanapata mimba 

ambazo hawakuzitarajia huwa 

wanakimbiilia kuzitoa mimba 

hizo.Nakuomba tafadhali usijaribu 

kufanya hivyo.Kufanya hivyo ni kosa 

mbele za Mungu na ni hatari kwa maisha 

yako.Jitahidi uanze kuhudhuria kliniki 

mara kwa mara na upate malekezo ya 

namna ya kujitunza katika kipindi hiki cha 

ujauzito na jinsi utakavyomlea mwanao 

baada ya kujifungua.”  Lucy akainuka na kumuaga daktari 

akaondoka .Kichwa kilikuwa kizito sana 

na alihisi kama amebeba kitu kikubwa 

mno kichwani.Alitembea taratibu akiwa 

na mawazo mengi.Hakuwa na hamu hata 

ya kufanya kazi siku hivyo akarejea 

nyumbani na kujitupa kitandani kwake 

 “Nina uhakika mimba hii itakuwa ya Jack 

kwa sababu sijawahi kufanya mapenzi na 

mwanaume mwingine zaidi yake.Lazima 

ni yeye.Lakini iwapo nikimwambia 

atakubali ? Sina hakika kama 

atakubali.Hata wazazi wake hawawezi 

kukubali kama mimba hii ni ya mtoto 

wao.Nitafanya nini mimi? Dada Pendo 

naye atakuwa tayari kunilea mimi na 

mimba yangu? Ninachokiona hapa 

atanishauri nikaitoe.Siwezi kukubali 

kamwe kwenda kuitoa mimba hii.Nahisi 

kuchanganyikiwa kabisa.Sielewi nitafanya 

nini.Naona kama maisha yangu 

yametawaliwa na mikosi mingi.” Lucy 

akawaza ,akachukua vidonge vya kutuliza 

maumivu ya kichwa akameza na kwenda 

chumbani kwake kujipumzisha.Hii ilikuwa 

ni siku ngumu sana katika maisha yake. 

 “Itanibidi nimwambie dada Pendo anipatie zile fedha zangu ili nikaanze 

maisha yangu mwenyewe.Sitaki kuwa 

kero kwa mtu mwingine.Sina hakika kama 

atakubali kunitunza nikiwa mjamzito na 

hadi pale nitakapojifungua.” Akawaza 

Lucy. 

 Siku nzima alishinda chumbani 

kwake.Jioni Pendo akarejea na kitu cha 

kwanza kutaka kukifahamu ni kwa nini 

Lucy hakufungua biashara. 

 :”Dada sikuwa najisikia vizuri.Nilitoka 

zahanati nikarudi nyumbani kupumzika” 

 “Lucy mdogo wangu naelewa kwamba 

hujisikii vizuri lakini biashara ile ndiyo 

inayotufanya mimi na wewe tuishi 

mjini.Kama tukifunga biashara ile kamwe 

hatutaweza kuishi.Jitahidi kesho ujivute 

vute ukafungue biashara.” 

 “Nitajitahidi kesho nikafungue dada 

Pendo” Lucy akajibu 

 “Huko hospitali wamesema 

unasumbuliwa na nini? Malaria? Pendo 

akauliza. 

 Lucy akakaa kimya 

 “Lucy huko hospitali ulikoenda kupima 

wamekwambia unasumbuliwa na nini? 

Pendo akauliza tena  “dada Pendo wamesema…..” Lucy 

akashindwa kuendelea akaanza kutoa 

machozi 

 Pendo akahisi kuna jambo kubwa 

linamsumbua Lucy akamsogelea na kukaa 

karibu naye. 

 “Niambie mdogo wangu ,wamekupa 

majibu gani? Usiogope kuniambia mimi ni 

dada yako.Niambie wamesemaje? 

 “dada wamesema nina mimba” Lucy 

akasema na kumfanya Pendo kustuka 

 “hapana hawajapima vizuri” Pendo 

akasema kwa mshangao 

 “Wamepima vizuri dada na wamenikuta 

kweli nina mimba ya mwezi mmoja na 

wiki mbili” 

 Pendo akazama katika mawazo ya 

ghafla.Akatazama juu kwa sekunde kdhaa 

halafu akamgeukia Lucy na kusema 

 “Kama ni kweli, mimba hiyo umeipata 

wapi? Jana uliniambia kwamba hutaki 

wanaume sasa hiyo mimba umeipataje? 

 Lucy akakaa kimya 

 “Ninakuuliza Lucy.Ni nani mwenye hiyo 

mimba? Niambie nijue nikamtafute ili 

aweze kutimiza majukumu yake” Pendo 

akauliza na sauti yake ilionyesha hakuwa na utani hata kidogo 

 “Mbona hunijibu Lucy? Kama hutaki 

kunijibu basi kesho mimi na wewe mguu 

kwa mguu tunakwenda kwa daktari na 

kuitoa mimba hiyo” 

 Huku akilia Lucy akasema 

 “dada mimi sitaki kutoa mimba 

hii.Nitailea mimi mwenyewe” 

 “Utailea vipi hiyo mimba Lucy? Hebu 

nieleze utaileaje? Angalia maisha yako 

hata kitanda huna unategemea utaishi 

vipi? Kama hutamtaja mtu aliyekupa 

mimba hiyo basi hakuna mjadala tena 

kesho tunaongozana na kwenda kuitoa 

hiyo mimba.Tumeelewana? Pendo 

akasema 

 “Dada Pendo naomba tafadhali 

usinipeleke nikaitoe hii mimba kwa 

sbaabu daktari amenionya kwamba ni 

hatari kwa afya yangu.” Lucy akaomba 

huku machozi yakimtoka 

 “Kama hutaki kwenda kutoa hiyo mimba 

nitajie ni nani aliyekupa hiyo mimba.” 

 Huku akitetemeka Lucy akasema 

 “Ni Jackson mtoto wa yule mama 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog