Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL - 5

  

Simulizi : The Football 

Sehemu Ya Tano (5)


alikuwa ni mtu muhimu katik 

auchunguzi wetu na nilitarajia 

sana kupata habari nyingi kutoka 

kwake lakini naomba maumivu 

haya yote yabaki ndani mwetu na 

jambo hili libaki siri yetu io ili 

uchunguzi endelee.Nathan 

amekuja Tanzania kimya kimya na 

apotee kimya kimya”akasema 

Mathew “Mathew umeongea mambo 

mengi lakini hakuna hata moja 

lililoingia kichwani 

mwangu.Nataka kusikia kitu 

kimoja tu.Wapi ulipo mwili wa 

Nathan? 

“Mheshimiwa rais mwili wa 

Nathan hautaweza kupatikana kwa 

sababu tayari umekwisha pelekwa 

mafichoni kwa hiyo hautaweza 

kuonekana.Suala hili litabaki kama 

lilivyo na hakuna atakayegundua 

kama Nathan amefariki.” 

“Umefanya nini Mathew? 

Akauliza Dr.Vivian 

“Mwili wa Nathan tayari 

umepelekwa kwenda kuzikwa 

mahala ambako hakuna atakayeweza kupafahamu” 

akasema mathew 

“Mathew nitakufunga miaka 

isiyo na idadi gerezani kama hili 

unalonieleza ni la kweli.Tafadhali 

naomba uni…………….” Mara simu 

ya Mathew ikaita ,akaitoa mfukoni 

na kutazama mpigaji alikuwa ni 

Meshack Jumbo.Haraka haraka 

akaipokea 

“Hallo mzee Meshack” 

akasema Mathew 

“Mathew I’m in trouble !! 

akasema Meshack Jumbo huku 

akihema kwa kasi 

“What trouble?! 

‘Mathew fanya haraka 

nitafutie msaada kama uko karibu 

na rais” “Mzee Meshack hebu tulia na 

unieleze nini kimetokea? 

“Nimevamiwa nyumbani 

kwangu na askari ambao wameua 

walinzi wangu na sasa wamevamia 

ndani wanapekua kila mahali” 

“Wewe uko wapi mzee Jumbo? 

“Nimewahi kutoka na mke 

wangu na msichana wetu wa kazi 

tumekuja kujificha huku 

shambani.Tulisikia milio ya risasi 

hivyo nikawahi kuitoa familia 

yangu haraka.Tafadhali naomba 

msaada wako.Niombee msaada 

kwa rais kwani watuhawa 

wnaonekana hawana nia njema” 

akasema Meshack Jumbo 

“Sawa Mzee.Endelea kujificha 

hapo hapo wakati naangalia kitu cha kufanya ,rais niko naye hapa 

karibu nitamueleza na msaada 

unakuja muda si mrefu” akasema 

Mathew na kukata simu 

akamgeukia Dr.Vivian 

“Meshack Jumbo yuko katika 

matatizo makubwa na anahitaji 

msaada wa haraka sana” akasema 

Mathew 

“Kuna nini kimetokea? 

Dr.Vivian akauliza 

“Meshack anasema kwamba 

amevamiwa na watu wenye mavazi 

ya askari polisi wameua walinzi 

wake na wameingia nyumbani 

kwake wanapekua kila kona ya 

nyumba yake.Anahitaji msaada wa 

haraka sana” akasema Mathew 

“Oh my God ! is he ok? “Yeye na familia yake 

wamefanikiwa kutoka kabla 

wavamizi hao hawajaingia ndani 

na wamejificha shambani.Msaada 

wa haraka unatakiwa ili kumsaidia 

kwani hatujui watu hao wana 

lengo gani na kuna uwezekano 

kama wakikosa wanachokitafuta 

watakwenda kuwatafuta shambani 

mahala walikojificha” 

“Jamani ! Mambo gani haya 

yanatokea? Akasema Dr.Vivian 

“Madam president msaada wa 

haraka mno unahitajika” akasema 

Mathew.Dr.Vivian akachukua simu 

na kumpigia mkuu wa jeshi la 

polisi na kumtaarifu kuhusiana na 

tukio lile la kuvamiwa nyumba ya 

Meshack Jumbo akamtaka atume askari waelekee hapo haraka sana 

kumuokoa Meshack na familia 

yake. 

“Mathew hao watu 

wanaotumia mavazi na sare za 

askari wetu ni akina nani?akauliza 

Dr.Vivian 

“Mheshimiwa rais hao watu 

lazima watafutwe haraka sana 

kwani hata sisi tulivamiwa na watu 

kama hao waliokuwa na sare na 

magari ya polisi.Naomba kwa sasa 

nielekee kwa Meshack Jumbo 

kutoa msaada.Nitakuja baada ya 

kutoka kwa Meshack Jumbo ili 

tuendelee na mjadala wetu” 

akasema Mathew na kutoka 

haraka akaingia katika gari na kuondoka ikulu kuelekea kwa 

Meshack Jumbo 

“Hawa watu wanaotumia 

mavazi ya askari ni akina nani? 

Kwanza walituvamia sisi na 

baadae wakatoweka baada ya 

askari wenzao kutokea.Meshack 

Jumbo anadai kwamba naye 

amevamiwa na watu wale wale 

wenye sare za askari polisi.Ni 

akina nani hawa? Wanatafuta 

nini?akajiuliza Mathew akiwa 

katika mwendo mkali kuelekea 

kwa Meshack Jumbo 

“Taratibu ninaanza 

kuwahusisha hawa watu hawa 

wanaotumia mavazi ya askari na 

mtandao wa siri ambao sifahamu 

lengo lake ni nini.Kama wangekuwa ni askari polisi wa 

kweli basi wasingekimbia baada 

ya wenzao kutokea.Halafu 

inaonekana walipewa taarifa ya 

ujio wa wale askari kwani niliona 

wanahimizana kuingia katika 

magari yao na kuondoka kwa kasi 

kubwa.Hili suala lazima 

nilifukuliwe na niufahamu huu 

mtandao wa askari wanaotumia 

sare na vifaa vya jeshi la polisi 

.Wanatafuta nini kwa Meshack 

Jumbo? Kwa nini wakamvamia 

usiku huu? Akajiuliza Mathew 

“Hili suala litafukua vitu vingi 

sana vilivyojificha kwani kila 

ninavyozidi kuchimbua ndivyo 

mambo mengi zaidi 

yanavyoendelea kuibuka.Alianza Fakrim,akaja Nathan na sasa 

limeibuka kundi la askari 

wanaovamia na kutoweka ambao 

nina uhakika mkubwa kwamba 

wanatumiwa kwa ajili ya kazi 

fulani.Nani anawatuma na kwa 

nini?Nikiweza kupata fununu 

kuhusiana na haa askari polisi 

hawa basi nitaweza kugundua 

jambo kubwa “ akawaza Mathew 

Alikaribia kufika nyumbani 

kwa Meshack Jumbo na kukuta 

mtaa ukiwa katika heka heka 

kubwa na watu walikuwa 

wameamka .Magari ya poilisi 

yaliwasha vimuli muli. 

“Mtaa umejaa 

watu,inaonekana kulitokea 

mtafaruku mkubwa nyumbani kwa Meshack.Nadhani askari polisi 

walifika kwa wakati kama 

walivyotakiwa na rais” akawaza 

Mathew akiendesha gari kwa 

tahadhari kuelekea nyumbani kwa 

Meshack Jumbo.Mita kadhaa 

akakuta kuna uzio wa askari 

akashuka garini na kujitambulisha 

kuwa anatoka ikulu na 

akaruhusiwa kupita .Kulikuwa na 

gari nne za zimamoto na 

wafanyakazi wa zimamoto 

walikuwa wanamalizia kuuzima 

moto uliokuwa unawaka.Jumba la 

Meshack Jumbo lilikuwa 

limeteketea kwa moto.Mathew 

akahisi kuchanganyikiwa 

“Oh my God ! akasimama nje 

ya gari akishuhudia shughuli iliyokuwa inafanywa na askari wa 

kikosi cha zimamoto.Eneo lote la 

kuzunguka nyumba ya Meshack 

Jumbo lilikuwa limezingirwa na 

askari polisi wenye silaha.Mathew 

akampigia simu Meshack Jumbo na 

kumjulisha kwamba tayari 

amekwisha fika na Meshack 

akamuelekeza mahala 

alipo,akamfuata 

“Pole sana mzee Jumbo.Wote 

wazima ? 

“Sote wazima Mathew.Ahsante 

sana kwa msaada wa haraka.Mara 

tu baada ya kukupigia simu 

hazikupita hata dakika kumi polisi 

wakafika hapa kwa bahati mbaya 

walikuta tayari nyumba imeanza 

kuwaka moto lakini nawashukuru pia kikosi cha zimamoto kwani nao 

walifika kwa wakati na kama 

unavyoona wanamalizia kuuzima 

moto” akasema Meshack 

“Pole sana mzee 

wangu.Kikubwa nashukuru wewe 

na familia yako mko salama.Mzee 

Meshack naomba tusogee kidogo 

pembeni tuzungumze” akasema 

Mathew 

“Mathew naomba unisubiri 

kama dakika kumi hivi nimalizane 

kwanza na kamanda wa polisi 

halafu tutazungumza” akasema 

Meshack Jumbo na kumuacha 

Mathew, akaenda kuzungumza na 

kamanda wa polisi aliyeongozana 

na kikosi kile cha askari waliofika 

pale nyumbani kwake. “Huu ni ukatili mkubwa 

sana.Ni akina nani hawa 

wanafanya mambo haya? Hawa si 

askari polisi.Hili ni genge la 

wahalifu ambao wanatumia sare 

na vifaa vya polisi na kujifanya 

askari ili kuweza kufanikisha 

mambo yao ya kihalifu.Ninaapa 

lazim….” Mathew akatolewa 

mawazoni na simu yake iliyoita 

alikuwa ni rais akaipokea haraka 

“Hallow mheshimiwa rais” 

“Umekwisha fika nyumbani 

kwa Meshack? 

“Ndiyo mheshimiwa rais 

nimekwisha fika hapa nyumbani 

kwa Meshack Jumbo.Yuko salama 

yeye na familia yake lakini nyumba 

yake imeteketezwa kwa moto na kikosi cha zimamoto wamejitahidi 

sana kufika kwa wakati na hivi 

sasa wanamalizia kuuzima moto 

huo.” 

“Dah ! akasema rais na kuvuta 

pumzi ndefu 

“Umefanikiwa kuonana na 

kuzungumza na Meshack Jumbo? 

Askari polisi walifika kwa wakati 

na kuwazuia hao askari wavamizi? 

Wamefanikiwa kumpata hata 

mmoja ili tuwafahamu ni akina 

nani?akauliza rais 

“Mheshimiwa rais 

nimefanikiwa kuonana na 

Meshack Jumbo lakini kwa hivi 

sasa bado anatoa maelezo kwa 

polisi na atakapomaliza nitapata 

nafasi nzuri ya kuweza kuzungumza naye kwa upana 

namna jambo hili lilivyotokea .Kwa 

ufupi tu aliniambia kwamba askari 

wale walifika kwa wakati sana ila 

bado hajaweka wazi kama 

walifanikiwa kuwapata wale 

askari 

wavamizi.Nitakapozungumza naye 

muda mfupi ujao nitalifahamu 

hilo.Mheshimwa rais ninakusihi 

usihofu hawa watu watafahamika 

tu.Mpaka hapa tunauhakika hawa 

si askari wetu bali watakuwa 

wanatumia sare na vifaa vya jeshi 

letu.Nakuahidi kuwasaka hadi 

kuwapata hawa watu” 

“Mathew hawa watu 

wanapaswa kutafutwa kwa udi na 

uvumba hadi wapatikane kwani wameanza kuleta hofu 

kubwa.Wanaonekana ni watu 

wenye kufahamu mambo 

mengi.Baada ya kutoka hapo 

nakuhitaji uje hapa ikulu pamoja 

na Meshack na familia 

yake.Nitawatafutia sehemu ya 

muda ya kuishi wakati 

tunashughulikia kuyajenga upya 

makazi yao.Halafu mimi na wewe 

bado tuna mazungumzo” akasema 

Dr.Vivian 

“Mheshimiwa rais kuna jambo 

nataka nikuombe” 

“Unataka nini Mathew? 

“Mapema uliniambia kwamba 

nisiendelee na uchunguzi wangu 

lakini nakuomba mheshimiwa rais 

niendelee na uchunguzi wangu kwani mambo mengi yameanza 

kuibuka likiwamo na hili kundi la 

askari polisi wavamizi.Niachie 

nimalizie uchunguzi wangu kwani 

nikiachia hapa utakua ni ushindi 

kwao mheshimiwa rais.Hatupaswi 

tuwape ushindi” 

“Mathew tutalizungumza hilo 

utakapokuja huku ikulu. Lakini 

naomba nikuweke wazi kwamba 

nimekwisha kifunga kitabu hicho 

kwa hiyo usitegemee nikifungue 

tena” akasema Dr.Vivian na kukata 

simu 

“Theresa alikosea sana 

kumuua Nathan.Nilifahamu 

mambo kama haya yangeweza 

kutokea na ndiyo maana nikataka 

kufanya uchunguzi wangu kwa siri bila Dr.Vivian kufahamu 

chochote.Sasa Dr.Vivian 

amefahamu na kila kitu 

kimesimama.Hataki niendelee 

tena na uchunguzi wangu .Huu si 

utani ni kweli hataki niendelee na 

uchunguzi kwani ni kawaida yake 

kutokurudi nyuma akishafanya 

maamuzi yake.Atakuwa amefanya 

kosa kubwa sana kuliacha suala 

hili kati kati.Nilikaribia sana 

kuanza kuupata mwanga “ 

akawaza 

“Lakini hapana siwezi kufanya 

anavyotaka rais.Siwezi kuachana 

na hili suala.Hata kama yeye 

hataki niendelee na uchunguzi 

wangu mimi nitaendelea 

kimyakimya bila ya kumshirikisha yeye na hadi niufahamu 

ukweli.Sijawahi hata mara moja 

kufanya uchunguzi na kuishia 

njiani.Ninapoanza uchunguzi 

wangu lazima nihakikishe 

nimefika mwisho na majibu 

yakapatikana na kama kuna 

wahalifu basi wanafikishwa mbele 

ya sheria.Lazima Tanzania 

tufahamu wanachokitafuta 

Marekani katika nchiyetu kwani 

suala hili limekwisha onyesha 

dalili kwamba limevuka mipaka ya 

nchi kwa hiyo siwezi kuliacha hivi 

hivi.Lazima nifahamu sababu ya 

Dr.Vivian kuchunguzwa na 

Marekani .Lazima ipo sababu ya 

kumchunguza.Hawawezi kupoteza 

muda wao kumchunguza kama hakuna jambo la msingi 

wanalolitaka” akawaza Mathew na 

Mzee Meshack akatokea 

“Samahani kwa kukuacha 

peke yako .Pilikapilika nyingi 

sana.Nakuomba tusogee huku 

pembeni” akasema Meshack 

Jumbo wakasogea pembeni 

“Siamini kilichotokea mzee 

Jumbo.Pole sana mzee 

wangu.Dakika chache zilizopita 

hapa palisimama jumba la kifahari 

lakini sasa limebaki gofu.Huu ni 

ukatili mkubwa.Pokea salamu 

nyingi za pole toka kwa rais na 

amenitaka tukitoka hapa 

tuongozane kuelekea ikulu wewe 

na familia yako” “Ahsante sana 

Mathew.Kikubwa 

ninachomshukuru Mungu ni 

kwamba mimi na familia yangu 

wote tuko salama 

kabisa.Nasikitika nimewapoteza 

walinzi wangu wote wawili 

.Imeniuma sana” akasema 

Meshack Jumbo na kuinamisha 

kichwa 

“Hebu nipe picha halisi ya 

kilichotokea mzee Jumbo lakini 

kabla hujanieleza chochote nataka 

kufahamu je lile begi nililoliacha 

hapa liko salama nalo ni mojawapo 

ya vitu vilivyoteketea? Akauliza 

Mathew 

“Lile begi liko salama.Ni kitu 

pekee nilichofanikiwa kuokoa kwani naamini lina umuhimu 

mkubwa sana” 

Mathew akashusha pumzi kwa 

jibu lile la Meshack Jumbo.Tayali 

aliamini lile begi lenye vifaa 

alivyotoa kwa Nathan liliteketea. 

“ Nikiwa maktaba nikiendelea 

na kazi zangu kwani niliamini 

baada ya kutoka kwa rais lazima 

ungerudi hapa hivyo sikutaka 

kulala mapema,nilisikia mbwa 

wangu wakibweka sana na mara 

nikasikia milio ya risasi.Nikazima 

taa zote ndani na kwenda 

kuangalia runinga 

iliyounganishwa na kamera za 

ulinzi na hakukuwa na picha 

zozote .Nikajua tayari kulikuwa na 

tatizo.Nikawaamsha haraka mke wangu na binti yetu wa kazi 

nikachukua kompyuta yangu 

ndogo na lilebegi ulilolileta 

tukaenda mafichoni.Hapa kwangu 

nina sehemu ya siri ya 

kujificha.Kuna njia ya chini kwa 

chini ya kwenda kutokea 

shambani.Niliitengeneza maalum 

kwa ajili ya nyakati kama 

hizi.Tulitoka mle ndani 

kimyakimya na kwenda kujificha 

shambani ndipo nikapata nafasi 

ya kukupigia simu kuomba 

msaada.Tukiwa tumejificha 

shambani nilifanikiwa kuwaona 

wale wavamizi wakiwa wamevaa 

sare za polisi wakiwa na silaha kali 

wakiwa wameizunguka nyumba 

yangu wakipekua kila sehemu Wakifunua kila mfuniko 

waliouona.Baada ya muda 

nikawaona askari wanne 

wakielekea mahala tulipokuwa 

tumejificha mmoja wao akiwa na 

kitu kama simu kubwa ambacho 

nahisi kilikuwa kinampa 

maelekezo.Alipofika karibu na 

pale tulipokuwa tumejificha 

wakasimama na nikaona 

wanaelekezana jambo.Mimi tayari 

nilikuwa na bastora nimejiandaa 

kwa lolote.Mara ghafa yule jamaa 

aliyekuwa na ile simu kubwa 

mithili ya tablet akapigiwa simu na 

kwa haraka sana wakaondoka 

huku wakikimbia na hazikupita 

dakika tatu jumba langu likaanza 

kuwaka moto. Niliwapigia simu jeshi la zimamoto na wakafika kwa 

haraka sana na hata polisi nao 

walifika kwa wakati kabisa lakini 

hakuna hata mmoja wao 

aliyekamatwa “ akasema Meshack 

Jumbo 

“Who are they? Akauliza 

Mathew 

“Swali hilo ni dogo lenye 

maneno matatu lakini majibu yake 

ni magumu kupatikana kwa 

haraka.Mathew wale watu siwezi 

kusema kwamba si askari 

polisi.Ninawafahamu askari na 

wale jamaa walisogea karibu 

kabisa na mahala nilipokuwa na 

nikawatazama japokuwa wao 

hawakuwa wananiona wale ni 

askari kabisa tena wenye mafunzo ya hali ya juu kwani utaona kabla 

ya kuingia ndani waliharibu 

kamera zote ili kusiweze kuwa na 

picha yoyote ya kuwafanya 

watambulike hii inaonyesha hawa 

si watu wa kawaida.Hata wewe 

ulisema kwamba ulizingirwa na 

askari waliokuwa wamejihami 

vilivyo na walipotea mara tu askari 

wenzao walipotokea .Hicho ndicho 

kilichotokea hapa.Inaonekana 

kuna watu ndani ya jeshi la polisi 

wanawajiulisha kwamba kuna 

askari wanakuja nao huondoka 

haraka” akasema Meshack 

“Ninaamini wale wale 

waliotuvamia usiku huu kule 

Uwazi Roadi ni hawa hawa 

waliokuja hapa kwako.Je walikuwa wananifuatilia mimi? Walijuaje 

kama niko hapa? Mathew akauliza 

“Sina hakika kama walikuwa 

wanakufuatilia wewe.Hawa kuna 

kitu walikuwa wanakitafuta kwani 

walikuwa na ile tablet iliyokuwa 

inawapa maelekezo na wao 

walikuwa wanaifuata hiyo ndiyo 

maana walikaribia sana kufika 

mahala nilipokuwa 

nimejificha.Kama si kupigiwa simu 

basi tungekuwa tunazunguma 

mambo mengine” akasema 

Meshack Jumbo.Mathew 

akainamisha kichwa akatafakari 

kidogo na kusema 

“Mzee Jumbo inabidi 

tuwaachie askari polisi suala hli 

walishughulikie na watatupa majibu ni nani hawa askari 

wanaotuvamia.Nadhani sasa 

tuondoke twende ikulu na askari 

polisi wataendelea kuwepo hapa 

hadi kesho utakapofanyika 

uchunguzi.” Akasema Mathew na 

mzee Jumbo akaenda kuzungumza 

na kamanda wa polisi aliyeongoza 

kikosi cha askari waliofika pale 

kwake na kumjulisha kwamba 

ameitwa na rais ikulu hivyo yeye 

na familia yake wanaondoka na 

watawaachia askari polisi 

waendelee na shughuli zao za 

uchunguzi.Mzee Jumbo akarejea 

akiwa ameongozana na mke wake 

pamoja na mtumishi wao wa ndani 

akamkabidhi Mathew mkoba wake 

wenye zile simu tatu pamoja na saa alivyovitoa kwa Nathan kisha 

wakoandoka kuelekea ikulu. 



Mzee Jumbo sipati neno zuri 

la kusema ila naomba wewe na 

familia yako mfahamu kwamba 

nimeguswa sana na hiki 

kilichotokea na kwa niaba yangu 

mwenyewe na watanzania wote 

itoshe kusema pole 

sana.Ninawaahidi kwamba hawa 

wote waliofanya kitendo hiki cha 

kikatili watatafutwa kokote waliko 

na watapatikana.Hakuna 

atakayesalia.”akasema Dr.Vivian 

baada ya Meshack Jumbo na 

familia yake kuwasili ikulu kuonana na rais kama alivyokuwa 

ameelekeza 

“Nashukuru sana rais na 

kikubwa tunachoshukuru kwamba 

sote ni wazima isipokuwa 

tumewapoteza walinzi wetu 

wawili.”akasema Meshack Jumbo 

“Poleni sana.” Akasema rais na 

kumuita mmoja wa walinzi wake 

akamuelekeza jambo halafu 

akawaelekea akina Meshack 

“Mzee Meshack ,mama na 

binti watakwenda kupumzika 

mahala nilikoandaa kwa ajili yenu 

kupumzika wakati tunawaandalia 

sehemu nzuri ya kuishi ili nyumba 

yenu iweze kufanyiwa ukarabati 

mkubwa.Meshack Jumbo wewe 

bado nahitaji uwepo hapa kuna mambo ya kujadili usiku huu” 

akasema rais na mke wa Meshack 

Jumbo na mtumihsi wao wa ndani 

wakachukuliwa wakapelekwa 

mahala alikoagiza rais paandaliwe 

kwa ajili yao.Sebuleni walibaki 

rais,Mathew,Meshack Jumbo na 

Theresa. 

“Mzee Jumbo narudia tena 

kwa mara nyingine kukupa pole 

kwa hili lililoikumba familia 

yako.Kwa kuwa wote tuko hapa 

nadhani ni wakati mzuri wa 

kuweza kulijadili hili jambo.Hawa 

watu ni akina nani ?Kweli ni askari 

wetu? Wanatumwa na nani? 

Akauliza Dr.Vivian “Mheshimiwa rais hawa watu 

ni askari wa jeshi letu la polisi” 

akasema Meshack Jumbo 

“Mheshimiwa rais,ili 

kuwafahamu watu hawa ni akina 

nani inabidi tuunganishe tukio 

lililotokea kwa Meshack Jumbo na 

lile lililotupata mimi na Theresa 

ambapo tulivamiwa na watu hao 

ambao walikuwa na sare na vifaa 

vya jeshi la polisi.Walikuwa na 

magari na silaha za kivita.Baada ya 

kukuomba msaada na ukatuma 

askari kutusaidia wale wavamizi 

wakakimbia.Kabla ya kuja hapa 

nilikwenda kwanza kwa Meshack 

Jumbo nikachukua gari lake na 

kuja hapa na muda mfupi baada ya 

mimi kuondoka nyumba yake imevamiwa na watu wale wale 

wenye sare za polisi na kama 

ilivyotokea kwetu watu wale 

waliondoka haraka kabla polisi 

hawajafika.Wale waliotuvamia 

mimi na Theresa ni hawa hawa 

waliomvamia Meshack Jumbo na 

ninahisi hawa jama walikuwa 

wananifuatilia mimi na 

walifahamu kwamba niko pale 

kwa Meshack Jumbo na ndiyo 

maana wakavamia na kufanya 

uharibifu ule mkubwa.Hawa kama 

alivyosema Meshack ni askari 

polisi lakini wanafanya matukio 

haya kwa siri na ndiyo maana 

hutoweka haraka baada ya 

kupewa taarifa kwamba askari wenzao wanakuja” akasema 

Mathew 

“Una maanisha kwamba kuna 

kikundi ndani ya jeshi la polisi 

wanaofanya maovu haya? Rais 

akauliza 

“Kwa namna inavyoonekana 

iko hivyo mheshimiwa rais” 

akasema Mathew 

“Kama ni hivyo lengo lao ni 

nini? Nani anawatuma? Akauliza 

rais 

“Hatuwezi kupata majibu ya 

maswali hayo mheshimiwa rais 

bila kufanya uchunguzi ndiyo 

maana ninakuomba uniruhusu 

niendelee kufanya uchunguzi wa 

suala hili.Kuna mambo mengi 

yamejificha katika jambo hili na kadiri tunavyoendelea kulichimba 

yazidi kuibuka na usiku wa leo 

tumegundua uwepo wa kikundi 

hiki cha askari polisi ambao 

hatujui nani anawatuma 

kutufuatilia na wanaonekana wana 

lengo baya na sisi” akasema 

Mathew 

“Mathew unachosema ni kweli 

kabisa kwamba tunahitaji sana 

kufahamu kuhusu hawa askari 

lakini utanisamehe kwani 

nimekwisha sema sitaki uendelee 

tena na uchunguzi wa suala 

hili”akasema rais 

“Madam preside…” 

“I’m sorry Mathew tayari 

nimekwisha fanya maamuzi” 

akasema rais “Mheshimiwa rais..” Mathew 

akataka kusema kitu lakini rais 

akamzuia 

“Mathew kama unataka 

kuliongelea suala hili tafadhali 

naomba usijisumbue kwani siwezi 

kubadilisha msimamo wangu.It’s 

over !! 

“Whats going on here? 

Akauliza Meshack Jumbo 

Dr.Vivian akawatazama 

Mathew na Theresa halafu 

akasema 

“Mzee Meshack nimeamua 

kusitisha ule uchunguzi aliokuwa 

anaufanya Mathew” 

“Umesitisha?!! Kwa nini 

mheshimiwa rais? Akauliza 

Meshack Jumbo “Nimeamua hivyo mzee wangu 

na atakueleza Mathew mwenyewe 

kwa nini nimeamua hivyo” 

akasema Dr.Vivian huku 

akimtazama Mathew kwa hasira 

“Madam president hili si suala 

jepesi na haliwezi kuachwa hivi 

hivi.Kuna tatizo lolote limetokea 

na kukufanya usitishe uchunguzi 

huu ambao tayari Mathew 

amekwisha piga hatua na sasa 

anaelekea kuzuri? Akauliza 

Meshack 

“Nimeamua hivyo mzee wangu 

kwa sababu toka nilipompa 

Meshack kazi hii hakuna kitu 

chochote cha maana ambacho 

amekifanya zaidi ya kuniongezea 

matatizo kila uchao.Nimeamua kuachana na kazi hii.Sitaki tena 

kutaka kuwajua watu waliomuua 

baba yangu” 

“Mheshimiwa rais tafadhali 

mwanangu naomba kama kuna 

tatizo limetokea litafutiwe 

ufumbuzi lakini si kusitisha 

uchunguzi huu ambao ni wa 

muhimu sana sana.Kwa zaidi ya 

miaka kumi sasa toka lilipotokea 

tukio hakuna hatua yoyote 

iliyowahi kupigwa katika 

kufahamu ni akina nani walifanya 

tukio lile lakini kwa siku hizi mbili 

Mathew amefanya uchunguzi wake 

na tayari kuna mwanga umeanza 

kuonekana.Haya yote yaliyotokea 

usiku wa leo ni matokea ya kazi 

nzuri anayoifanya Mathew.Tafadhali mheshimiwa 

rais usiliache suala hili njiani “ 

akasema Meshack Jumbo 

“Mzee Jumbo nakuheshimu 

mno lakini tayari nimekwisha 

fanya maamuzi yangu na siwezi 

kubadili nilichokiamua.Uchunguzi 

huu hautaendelea.Ninashukuru 

kwa namna Mathew alivyojitolea 

na kuifanya kazi hii na kwa kipindi 

kifupi imeweza kuleta mwanga 

lakini sihitaji aendelee zaidi ya 

hapa.Imetosha mzee Jumbo.” 

“Kuna nini madam president 

hadi ukaamua kusitisha uchunguzi 

huu muhimu? Akauliza Meshack 

“Meshack naomba 

tusiliongelee hilo kwani hakuna 

kauli inayoweza kubadilisha msimamo wangu.Nimeamua hivyo 

na itabaki hivyo.Naomba 

tusipoteze muda kulizungumzia 

hilo.Tuendelee na masuala 

mengine” 

“Madam president No ! 

Hatuwezi kuachana na suala hili 

kubwa ambalo linauweka hadi 

usalama wa taifa 

mashakani.Usalama wako uko 

mashakani pia.Hili ni suala nyeti 

sana hatuwezi kuliacha likaenda 

hivi hivi.Rais Anorld aliuawa ,baba 

yako aliuawa na hatua zimeanza 

kupigwa kuupata ukweli wa nani 

waliowaua kwa hiyo hatuwezi 

kuliacha jambo hili hewani kama 

lilivyoachwa miaka kumi 

iliyopita.Binafsi siko tayari kuliona jambo hili likiishia hapa.Nataka 

liendelee hadi lifike mwisho 

wake.Madam president nakuomba 

sana nafahamu wewe ni rais 

mwenye msimamo mkali na ni 

kawaida yako kusimama katika 

maamuzi yako lakini nakuomba 

kwa mara ya kwanza uende 

kinyume na maamuzi yako na 

uruhusu suala hili liendelee.” 

Akasema Meshack Jumbo na 

Dr.Vivian akasimama akiwa 

amefura hasira 

“Naomba tuelewane 

jamani.Mimi ndire rais wa 

jamhuroi ya muungano wa 

Tanzania.Mimi ndiye mwenye 

kuamua nini kifanyike na nani 

afanye.Kauli yangu ni ya mwisho.Nimekwisha amua 

kwamba suala hili halitaendelea 

tena na huo ndio msimamo wangu 

kwa nini mnakuwa wagumu 

kunielewa? Akauliza Dr.Vivian kwa 

hasira.Meshack Jumbo naye 

akasimama na kumtazama rais 

“ Is this because of Nathan’s 

death? Akauliza.Dr.Vivian 

hakujibu kitu alikuwa 

ameinamisha kichwa 

“Answer me madam president 

is it because of Nathan’s death? 

Akauliza tena Meshack 

Jumbo.Dr.Vivian akainua uso wake 

ulikuwa umeloa 

machozi.Alishindwa kujiuzia 

akaangusha kilio.Mathew akamfuata akamshika mkono na 

kumketisha sofani. 

“I’m sorry madam president” 

akasema huku akimpiga piga 

mgongoni. 

“Let’s leave her alone for a 

while” akasema Mathew na wote 

wakatoka nje wakamuacha 

Dr.Vivian peke yake akilia. 

“Kwa namna yoyote ile zoezi 

hili la uchunguzi haliwezi kuishia 

hapa.Lazima uchunguzi 

uendelee.Hatua kubwa imekwisha 

pigwa kwa hiyo hatuwezi kuishia 

njiani.Lazima tutumie kila namna 

ya ushawishi kumfanya rais 

akubali uchunguzi huu uendelee.” 

Akasema Meshack Jumbo “Nilijua haya yote yatatokea 

na ndiyo maana nikawa sitaki 

uchunguzi huu ufanyike kwani 

ungeibua mambo mengi ya 

hatari.Hata hivyo kuna kitu 

nimekigundua hapa.Baba aliuawa 

na kikundi cha askari polisi ambao 

niliwashuhudia mwenyewe kwa 

macho yangu.Mambo yaliyotokea 

usiku wa leo yamenifanya niamini 

kwamba kuna mtandao mkubwa 

ndani ya serikali ambao unatumia 

kikundi cha askari polisi kwa ajili 

ya shughuli zao.Nina hakika kabisa 

wale askari waliotuvamia mimi na 

Mathew na hawa waliokwenda 

kuvamia na kuichoma nyumba ya 

Meshack Jumbo ni kitu kimoja na 

wale walimuua baba.Natamani nimueleze Mathew lakini naogopa 

nisije nikaongeza matatizo 

zaidi.Ngoja niliache suala hili kama 

lilivyo.” Akawaza Theresa 

“Nini hasa lengo la hawa 

jamaa? Akauliza Meshack Jumbo 

“Mzee Jumbo kama 

nilivyosema awali kwamba hawa 

jamaa lazima watakuwa 

wananifuatilia mimi kwani 

walituvamia njiani wakashindwa 

kunipata na baadae wakanifuata 

nyumbani kwako na waliamini 

lazima nitakuwa pale”akasema 

Mathew.Kukawa na ukimya kila 

mmoja akiwaza lake na mara Mzee 

Jumbo akasema 

“Wale watu walikuwa na kifaa 

walichokuwa wanakifuata kilichowaongoza hadi mahala 

nilipokuwa.Hili limenifanya 

nijiulize maswali mengi yasiyo na 

majibu kwamba waliwe…..” 

“Mr Jumbo wait” akasema 

Mathew 

“Kuna kitu nimekifikiria 

kutokana na hayo maelezo yako.” 

“Kitu gani Mathew? Akauliza 

Meshack 

“Unasema hao jamaa 

walikuwa na kifaa kilichokuwa 

kinawaelekeza na wakafika hadi 

eneo ulilokuwa umejificha na kwa 

bahati nzuri hawakuweza 

kuendelea baada ya kutaarifiwa 

kwamba kuna askari wanakuja 

kwako hivyo wakaondoka haraka 

sana.Hii inanifanya niamini kwamba kuna kitu walikuwa 

wanakitafuta.Katika mkoba ule 

niliouleta kwako kuna simu tatu za 

Nathan pamoja na saa ya 

mkononi.Ninahisi yawezekana 

kifaa hicho unachokisema 

walikuwa wanakifuatilia kilikuwa 

kinanasa mawimbi ya mojawapo 

ya kifaa na ndiyo maana waliweza 

kufika hadi nyumbani kwako na 

kama haitoshi wakakaribia hadi 

eneo ulilokuwa umejificha kwa 

msaada wa hicho kifaa 

chao.Ninahisi hivyo kwa sababu 

sioni sababu ya kuja kuvamiwa 

nyumbani kwako na kufanya 

uharibifu ule mkubwa.Kwa nini 

iwe leo usiku tena baada ya mimi 

kuuleta mkoba ule na kuondoka?Lazima walikuwa 

wanaufuatilia ule mkoba na kifaa 

hicho walichokuwa nacho kilikuwa 

kinanasa mawimbi ya mojawapo 

ya vitu vilivyokuwamo ndani ya 

mkoba” akasema Mathew 

“Mathew hiki unachokisema 

kinaweza kuwa na mashiko na 

hata mimi naweza kuamini 

hivyo.Nimejiuliza sana sababu ya 

kuvamiwa na sijaona kwa nini 

nivamiwe.Watu wale hawakuwa 

majambazi bali walivamia 

wakitafuta kitu fulani mahususi 

ambacho walikuwa na uhakika 

kitakuwemo mle ndani.Sasa 

nimepata picha kwamba 

yawezekana walikuwa 

wanalitafuta lile begi.Kile kifaa walichokuwa nacho kilikuwa 

kinawaelekeza mahala begi lile 

lilipo.Mwanga unaanza 

kupatikana” akasema Meshack 

Jumbo 

“Mwanga unaanza kupatikana 

lakini je hawa watu wana 

mahusiano gani na vifaa vya 

Nathan? Kwa nini wavitafute? 

Mathew akauliza 

“Hapo ndipo swali linapokuwa 

gumu na linahitaji majibu” 

akasema Meshack 

“Ninahisi yawezekana wale si 

askari bali ni kikundi cha watu 

wanaotumia sare na vifaa vya 

askari polisi kufanikisha mambo 

yao. Kama ni hivyo basi lazima 

kikundi hicho kina mashirikiano na Nathan na kama jibu ni ndiyo 

basi kuna mtandao mrefu tayari 

hapa nchini unaotumiwa na akina 

Nathan na kwa kuwa Nathan ni CIA 

basi lazima mtandao huo pia 

utakuwa chini ya CIA na kama jibu 

ni ndiyo basi lazima kuna jambo 

kubwa wanalolitafuta hapa 

Tanzania” akasema Mathew 

“Mathew mtiririko huu 

uliouelezea umenifanya niipate 

picha kamili ya hili 

jambo.Tukifahamu kuhusu 

kikundi hicho cha askari polisi hao 

wavamizi tutaweza kufahamu 

mambo mengi yaliyojificha” 

“Hilo litawezekana endapo tu 

rais atakuwa tayari uchunguzi 

uendelee.Kama ataendelea kuushikilia msimamo wake 

kwamba uchunguzi huu ufikie 

mwisho basi hakuna 

kitakachoweza kujulikana na 

atakuwa amefanya kosa kubwa 

sana kwani hatujui nini lengo la 

hawa jamaa.Wametengeneza 

mtandao ndani ya 

serikali,wanakusanya taarifa 

mbali mbali za rais na hatujui 

wana malengo gani” akasema 

Mathew 

“Mathew kwa namna yoyote 

ile hatuwezi kuliacha suala hili 

liishie hapa.Lazima tuhakikishe 

limefika mwisho.Lazima ukweli 

ujulikane.Lazima tuhakikishe 

tunamshawishi rais kwa namna 

yoyote ile akubali suala hili liendelee.Mathew tafadhali kijana 

wangu nakusihi usikatishwe tamaa 

na rais.Hata kama hataki suala hili 

liendelee sisi lazima tuliendeleze 

hata kwa siri bila ya yeye 

kufahamu.Lazima tukubaliane sote 

kwa pamoja kwamba suala hili 

litaendelea.Theresa are you with 

us?Mathew anakuhitaji sana kwa 

ajili ya kupata nyaraka mbali 

mbali muhimu” Akauliza Meshack 

Jumbo na Theresa hakujibu kitu 

akainamisha kichwa 

“C’mon Theresa .Don’t shut us 

down .We need you.Dada yako ana 

hasira kutokana na kile 

kilichotokea kwa Nathan lakini 

ukweli ni kwamba yuko katika 

hatari kubwa.Hatujui hawa watu ambao wamekuwa wakifuatilia 

taarifa zake wana lengo 

gani?Maamuzi tutakayoyachukua 

vijana wangu yatakuwa na msaada 

mkubwa kwa dada yako na kwa 

taifa.Tuwe kitu kimoja sote.Are 

you with us? Akauliza Meshack 

Jumbo na Theresa akabaki kimya 

“Kabla ya kufanya maamuzi 

yoyote Theresa” akasema Mathew 

“Lazima ufahamu kwamba hii 

ni operesheni hatari sana na wewe 

mwenyewe umeshuhudia hatari 

inayojitokeza kwa hiyo 

utakapoamua kuwa pamoja na sisi 

katika operesheni hii ujue kwamba 

tunapambana na watu hatari hivyo 

unatakiwa ukubali kutoka moyoni ” akasema Mathew na Theresa 

akafikiri kidogo na kusema 

“I’m with you” akasema 

Theresa. 

“Good.Sasa tunaingia tena 

ndani kumuona rais na 

tutamueleza kwamba sote 

tumekubaliana kwamba uchunguzi 

huu uendelee.” Akasema Meshack 

Jumbo na kuwaongoza akina 

Mathew wakaingia sebuleni kwa 

Dr.Vivian na wote wakasimama 

wakimtazama Dr Vivan, 

“What? Akauliza Dr.Vivian 

akishangaa namna walivyokuwa 

wamesimama wanamtazama 

“Mbona wote mnanitazama 

kama mmeona mzimu?akauliza 

Dr.Vivian “Madam president 

tunafahamu kwamba uko katika 

wakati mgumu kutokana na hiki 

kilichotokea leo.Umeumia na sote 

tumeumia vile vile.Hatukutegemea 

kama jambo hili litafika hapa 

lilipofika lakini kwa kuwa 

limetokea hatuna budi kulikabili 

na kuendelea mbele.Kutokana na 

hiki kilichotokea umezuia 

uchunguzi 

usiendelee.Tunaiheshimu sana 

kauli yako kama mkuu wetu wa 

nchi na hatuwezi kuipuuza lakini 

kutokana na uzito wa jambo hili 

mimi na wenzangu tumeamua 

kuendelea na uchunguzi hadi 

mwisho na tutakapomaliza 

operesheni hii mimi na Theresa tutajisalimisha mbele ya vyombo 

vya usalama kwa mauaji ya 

Nathan.Tunakuomba mheshimiwa 

rais uridhie ombi letu hili la 

kuendelea na uchunguzi wetu 

kwani hata ukikataa sisi 

tutaendelea na uchunguzi wetu 

hadi mwisho” akasema Mathew 

“Madam president 

tumejadiliana na vijana 

wangu,tumeona ni vyema 

uchunguzi uendelee.Madam 

president kuna jambo ambalo 

tumeligundua na unapaswa 

kulifahamu kuhusiana na hiki 

kinachoendelea.Mathew tell her” 

akasema Meshack Jumbo 

“Nilipokwenda katika chumba 

cha Nathan usiku wa leo nimechukua simu tatu ambazo 

niliziweka katika mkoba wangu 

pamoja na saa yake ya 

mkononi.Tulivamiwa na wale 

askari na wakafanikiwa kuondoka 

baada ya askari wenzao kutokea 

na baada ya kuondoka pale 

nilikwenda moja kwa moja kwa 

Meshack Jumbo nikamuachia begi 

lile lililokuwa na zile simu na ile 

saa ndipo nikaja hapa.Baada tu ya 

kuondoka nyumba ya Meshack 

ikavamiwa na kwa mujibu wa 

Meshack Jumbo baada ya nyumba 

yake kuvamiwa alitoka ndani kwa 

kutumia mlango wa siri na kwenda 

kujificha nje ya nyumba lakini 

mara wale wavamizi wakafika 

mpaka eneo alikuwa amejificha.Hawakuweza kumuona 

ila yeye aliweza kuwaona 

vyema.Walikuwa na kifaa fulani 

ambacho walikuwa wanakifuata 

kilichokuwa kinawaelekeza kitu 

fulani.Hii inatupa picha kwamba 

kifaa kile walichokuwa nacho 

kilikuwa kinanasa mawimbi ya 

moja wapo ya kifaa kilichokuwamo 

ndani ya lile begi.Kwa hiyo basi 

tunaamini Nathan alikuwa na 

mashirikiano na watu huku 

Tanzania na kama ndiyo basi 

lazima kuna mtandao mrefu wa 

watu ambao unaweza hata 

kutumia polisi wetu katika 

kufanikisha mambo yao. Na 

mtandao huu utakuwa umeundwa 

kwa kazi maalum hivyo tumeamua kuendelea na uchunguzi kufahamu 

nani walio katika huu mtandao na 

lengo lao nini” akasema Mathew na 

bada ya muda Dr.Vivian akasema 

“Mmetumia kila aina ya 

ushawishi hadi mmefanikiwa 

kunishawishi nikubaliane nanyi 

japokuwa bado moyo wangu 

unaumia sana kwa hiki 

mlichokifanya lakini kwa upande 

wa pili baada ya maelezo yako 

kuna kitu nimeanza kukiona 

hapa.Kuna uwezekano Nathan 

akawa anatumiwa kwa kazi 

maalum.Yawezekana nilikua 

kipofu wa mapenzi na sikuweza 

kugundua chochote na wala 

sikuwa na wasi wasi naye hata 

kidogo.Nadhani inabidi kwa mara ya kwanza katika maisha yangu 

nitengue msimamo wangu na 

kuruhusu uchunguzi 

uendelee.Mathew endelea 

kuchunguza jambo hili na 

tuufahamu mtandao huu 

unaoweza hata kutumia askari 

polisi au sare na vifaa vya jeshi letu 

kwa ajili ya kufanyia 

uhalifu.Chunguza ufahamu kama 

mtandao huo una mahusiano 

yoyote na CIA au serikaliya 

Marekani na chochote 

utakachohitaji nitakuwezesha 

lakini bado ninataka kujua kitu 

kimoja,mwili wa Nathan uko wapi? 

“Mheshimiwa rais mwili wa 

Nathan kwa sasa hautaweza 

kuonekana mheshimiwa rais utanisamehe kwa hilo.Mwili huu 

ukionekana ni hatari kubwa 

sana.Kwa kuwa alikuja Tanzania 

kwa siri hata kifo chake kinapaswa 

kuwa cha siri vile vile.” akasema 

Mathew 

“Hapo ndipo ninapotofautiana 

nawe Mathew.Kwa nini kifo chake 

kiwe siri?kwa nini isitafutwe 

namna ya kueleza labda alikufa 

kwa ajali au kitu kingine na halafu 

mwili wake ukabidhiwe kwao 

wauzike kwa heshima zote za 

familia?



Madam president 

anachokisema Mathew ni sahihi 

kabisa.Katika mambo kama haya 

ya uchunguzi kuna nyakati 

inawalazimu mfanye maamuzi magumu kama haa aliyoyafanya ya 

kuuficha mwiliwa Nathan 

usijulikane ili kumuwezesha yeye 

kuendelea na uchunguzi 

wake.Nathan alikuja Tanzania 

kimya kimya na hata kupotea 

kwake kunapaswa kuwa kimya 

kimya.Marekani wakigundua 

jambo hili utaibuka mzozo 

mwingine mkubwa kwa hiyo ili 

kuepusha hilo tunapaswa 

kuendelea na mambo yetu kimya 

kimya kama vile hakuna 

kilichotokea.Najua ni mtu wako wa 

muhimu japokuwa ulikuwa 

umekorofishana naye lakini 

hatujui moyoni mwako ulikuwa 

unampenda kiasi gani kwa hiyo 

itakulazimu ulie kimya kimya mheshimiwa rais kwani lazima 

ifanyike hivi.Tumeamua 

kulichuguza hili jambo ni gumu na 

mambo kama haya tutakutana 

nayo hivyo lazima tukubaliane 

nayo” akasema Meshack Jumbo 

“Mnajaribu sana kunishawishi 

nikubaliane nanyi lakini moyo 

wangu umeumia mno.Kutokana na 

hoja mlizozijenga sina budi 

kukubaliana nanyi uchunguzi 

uendelee ila naomba tafadhali 

kama huko mbeleni kutatokea 

jambo lenye kunihusu moja kwa 

moja mimi tafadhali naomba 

msilitolee maamuzi ya haraka bila 

ya kunishirikisha kwanza 

mimi.Sitaki mambo yaliyotokea 

kwa Nathan yajirudie tena.Tayari mmekwisha uumiza moyo wangu 

mno” akasema Dr.Vivian 

“Tumekuelewa madam 

president.Ila kuna jambo nataka 

nikuombe” 

“Jambo gani Mathew? 

“Naomba Theresa abaki na 

wewe hapa ikulu.Au kama 

hatapata nafasi ya kukaa nawe 

hapa basi ulinzi uimarishwe 

nyumbani kwake.Watu hawa kama 

wameweza kunifahamu mimi basi 

yawezekana kabisa kwamba hata 

Theresa tayari wamekwisha 

mfahamu kwani hatujui mtandao 

huu umesambaa kiasi gani ndani 

ya serikali.”akasema Mathew 

“Nafasi ipo kubwa sana hapa 

ikulu ila Theresa mwenyewe ndiye hataki kuishi hapa lakini kutokana 

na hali ya usalama kuwa tete kwa 

sasa atalazimika kuishi hapa hadi 

hapo nitakapokuwa na uhakika 

kwamba hali ya usalama huko nje 

ni shwari.Vipi kuhusu wewe 

Mathew unahitaji ulinzi nyumbani 

kwako?Hawa jamaa watakuwa 

wanakufuatilia kila mahala kwa 

hiyo nyumbani kwako kunatakiwa 

kuwa na ulinzi imara.Nitaagiza 

wapelekwe askari nyumbani 

kwako” 

“Ahsante mheshimiwa rais 

lakini sihitaji ulinzi wowote kwa 

sasa.Ninaweza kujilinda mimi 

mwenyewe lakini pale 

nitakapohitaji ulinzi nitakujulisha” 

akasema Mathew “Are you sure? 

“Ndiyo mheshimiwa rais” 

akasema Mathew 

“Meshack Jumbo wewe na 

familia yako yote mtaishi katika 

nyumba moja ya serikali wakati 

nyumba yako ikijengwa 

upya.Mtapata ulinzi mkali na wa 

kutosha kwa hiyo naomba ufanye 

kazi zako kwa uhuru kabisa bila 

hofu” akasema Dr.Vivian 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais” akasema Meshack 

“Muda umekwenda sana 

tayari ni usiku mwingi hivyo 

nahitaji kupumzika.Naomba na 

ninyi mkapumzike ili tuweze 

kuikabili kesho”akasema Dr.Vivian “Theresa wewe utabaki hapa 

ikulu hadi hapo tutakapokuwa na 

usalama kuhusu maisha yako” 

akasema Mathew 

“Hapana Mathew.Tutaondoka 

wote kama ni kufa niko tayari” 

akasema Theresa akionekana bado 

kuwa na hasira 

“Kama yeye mwenyewe 

anataka hivyo basi vizuri.Meshack 

Jumbo vijana wangu 

watakuchukua kukupeleka mahala 

utakapoishi na familia yako kwa 

muda.Nawatakia nyote usiku 

mwema” akasema Dr.Vivian na 

akina Mathew wakaondoka. 

“Mzee Jumbo usiku wa leo 

sintalala hadi nihakikishe 

nimeufahamau ule mtandao wa wale askari” akasema Mathew 

baada ya kutoka ofisini kwa 

Dr.Vivian 

“Huwezi kwenda peke yako 

huko tutakwenda sote.Sijazeeka 

kiasi ambacho siwezi 

kupambana.Kwa hiyo umepanga 

kufanya nini? Kuna sehemu yoyote 

ya kuanzia? 

“ Kama walikuwa wanafuatilia 

mojawapo ya vifaa vya Nathan basi 

itakuwa ni hii saa ambayo 

nilimvua mkononi ambayo ndiyo 

inafanya kazi lakini simu zake zote 

zimezimwa kwa hiyo hakuna 

mawimbi yanayosafiri.Hivyo 

naamini bado watakuwa 

wanaendelea kufuatilia kwa hiyo 

lazima tufanye mtego mdogo.Tunakwenda katika 

makaburi ya mkwajuni pale 

tutaifukia saa ya Nathan chini 

halafu tutasubiri pale kama 

watatokea ila naamini lazima 

watakuja.Kama wanacho kifaa 

wanachokitumia kufuatilia hii saa 

basi wataifuata” akasema Mathew. 

Walifika mkwajuni na 

kuegesha gari katika klabu moja 

ambako kulikuwa na onyesho la 

bendi ya muziki wa dansi 

“Ninyi mtabaki hapa mimi 

nitatembea kwa miguu.Kutoka 

hapa hadi makaburini si mbali.Kila 

kitakachojiri huko nitawajulisha” 

“Mathew huwezi kwenda huko 

peke yako .Nitaongozana nawe 

kwenda huko makaburini na Theresa atabaki hapa.” Akasema 

Meshack Jumbo 

“Theresa utabaki hapa mimi 

na Meshack Jumbo tunakwenda 

makaburini.Kitakachojiri huko 

tutakujulisha” akasema Mathew 

“Mathew I’m so 

scared.Tafadhali naomba niende 

nanyi.naogopa kubaki hapa peke 

yangu” akasema Theresa 

“Huko tuendako ni hatari 

Theresa na kunaweza kutokea 

hata mapigano .Si sehemu salama 

kwa wewe kuwepo” 

“Ni afadhali nikiwa karibu 

nanyi mtanilinda kuliko nivamiwe 

hapa nikiwa peke yangu na mimi 

sifahamu namna ya kujilinda” 

akasema Theresa “Ok twende wote” akasema 

Mathew wakashuka garini 

akaubeba ule mkoba wake wenye 

simu pamoja na ile saa ya Nathan 

wakaondoka kuelekea makaburi 

ya mkwajuni.Walitembea kwa 

miguu umbali wa kilometa tatu 

wakakunja kulia wakafuata njia 

inayoelekea makaburini.Kulikuwa 

kimya na sauti za ndege bundi 

zilikuwa zinasikika.Theresa 

aliogopa sana hakuwahi kufika 

maeneo kama yale usiku.Kadiri 

walivyozidi kwenda ndivyo giza 

lilivyozidi kuongezeka na 

wakajikuta wakaiingia katika 

vichaka na miti miti.Kulitisha sana 

“Tutafute sehemu nzuri 

ambayo tutaweza kuifukia hii saa na halafu tupate sehemu nzuri ya 

kujificha na kuwaona wale 

watakaokuja” akasema 

Mathew.Walichimba shimo katika 

kaburi ambalo lilizikwa karibuni 

wakaifukia ile saa ya Nathan halafu 

wakaenda kujificha mbali 

kidogo.Wakiwa wamejificha mara 

ghafla majani yakasikika 

yakitikisika.Mathew ambaye 

alikuwa anaangaza kama bundi 

akajiweka tayari . 

“Kuna mtu atakuwa anakuja 

nasikia majani yanatikisika” 

akasema Meshack Jumbo. 

“Jiweke tayari yawezekana ni 

wale jamaa wanakuja” akasema 

Mathew na kutokea pale mahala 

walipokuwa wamekaa waliweza kuwaona watu watatu wakiwa 

wamebeba mfuko mkubwa 

wakauweka juu ya moja la kaburi 

wakamwaga vitu vilivyokuwamo 

ndani na kuanza kugawana 

“Hawa ni wezi wametoka 

kuiba na huku ndiko sehemu 

wanayotumia kugawana mali 

walizoiba.Tuwaache wafanye 

shughuli zao na wakimaliza 

wataondoka wenyewe ” akasema 

Mathew wakiendelea kuwatazama 

wezi wale wakigawana na kutaka 

kupigana wenyewe kwa wenyewe 

baada ya mmoja wao kuonekana 

kutaka kuchukua mali nyingi zaidi 

ya wenzake.Mara ghafla wote 

wakatulia. “Nasikia kuna nyayo za mtu” 

akasema moja wao 

“Hao wanga tu.Nani anaweza 

kuja huku usiku huu? Akasema 

moja wao 

“Hebu tulieni.Kuna watu 

wanakuja huku” akasema na wote 

wakakaa katika tahadhari kubwa 

na mara wakatimua mbio 

wakaacha kila kitu walichoiba juu 

ya kaburi.Kitendo kile 

kiliwashangaza kidogo akina 

Mathew 

“Mbona wanakimbia kuna 

nini? Akauliza Meshack Jumbo na 

kabla Mathew hajajibu kitu mara 

wakaonekana watu wanne wakiwa 

na mavazi ya polisi na bunduki wakielekea mahala ambako 

Mathew alifukia ile saa ya Nathan 

“Meshack it’s 

them.Wamekuja.”akasema Mathew 

kwa kunong’ona 

“Kwa hiyo tunafanya nini? 

Akauliza 

“Jiweke tayari.Nikitoa 

maelekezo tutaanza 

mashambulizi.Lazima tuwafahamu 

ni akina nani hawa” akasema 

Mathew. 

“Lakini tutawaweza hawa 

wako wanne na hatujui kama kuna 

wengine wako nao na halafu wana 

silaha kali sisi tuna bastora mbili 

tu” akasema Meshack Jumbo. “Usiogope Meshack lazima 

tupambane nao.Get ready” 

akasema Mathew . 

Wale askari polisi wakiwa na 

kifaa fulani mithili ya simu 

walifika hadi katika lile kaburi 

Mathew alikofukia saa ya 

Nathan.Wakaanza kufukua mahala 

pale huku wale wawili wenye 

bunduki wakiwa katika tahadhari 

kubwa wakitazama huku na huko 

“Umewaona wale wawili 

wenye bunduki ,tutaanza 

nao.Mchukue wa kushoto mimi 

nitamchukua wa kulia.Make sure 

you don’t miss.Hakikisha 

umemlenga kichwani kwani 

mwilini wamejikinga kwa fulana za 

kuzuia risasi.” Akasema Mathew “Usihofu Mathew.Let’ do this” 

akasema Meshack Jumbo 

“On my count ,three ,two,one” 

Wale jamaa wawili waliokuwa 

wanachimba wakashangaa baada 

ya wenzao kuanguka ghafla.Wote 

wakaacha kazi waliyokuwa 

wanaifanya na kusimama 

kushuhudia kile 

kilichotokea.Kufumba na 

kufumbua wakajikuta wakichezea 

risasi zilizotoka katika bastora 

zenye viwambo vya sauti kutoka 

kwa akina Mathew. 

“Good Job.I hope they’re all 

dead.Mimi ninakwenda kuwaona 

,cover me” akasema Mathew na 

kutoka kwa tahadhari akaelekea 

mahala walipokuwa wale

 askari.Wote walikuwa 

wameanguka chini na hawakuwa 

na uhai kwani risasi zile zililengwa 

katika vichwa vyao.Haraka haraka 

akitoa ile saa ya Nathan akaiweka 

mfukoni halafu akaanza 

kuwapekua wale 

jamaa.Hakuwakuta na kitu kingine 

zaidi ya kile kifaa mithili ya simu 

walichokuwa wanakitumia 

kufuatilia ilipo saa ya Nathan. 

Wakati anakitazama kifaa kile 

mara akasikia vishindo vya watu 

wakielekea mahala pale.Haraka 

haraka akalala chini na mara 

wakatokea watu watano wote 

wakiwa na mavazi ya askari na 

wakiwa na silaha. “Tonny” akaita mmoja 

wao.Mathew akaishika bunduki 

moja ya wale jamaa waliowaua 

aina ya SMG na kujiweka 

tayari.Wale jamaa walikuwa 

wamesimama wakiangaza kila 

kona 

“Tonny”akaita tena mmoja 

wao.Mathew akapiga mluzi wale 

jamaa wakaanza kuelekea kule 

mahala ilikotokea sauti ile ya 

mluzi.Ghafla Mathew akasimama 

na wale jamaa wakakutana na 

mvua ya risasi kutoka katika 

bunduki ile aliyokuwa ameishika 

Mathew.Wale jamaa hawakuwa 

wamejiandaa kwa shambulio 

lolote kutokea hivyo hawakuweza 

kupata muda wa kuachia risasi hata moja na wote wakafa.Mathew 

akaitupa ile bunduki akachukua 

nyingine mbili toka kwa wale 

jamaa na kumfuata Meshack 

Jumbo.Alimkuta akiwa ameloa 

jasho.Theresa alikuwa 

anatetemeka kwa woga 

“Mzee Jumbo nakuomba 

mchukue Theresa muondoke eneo 

hili mshuke bondeni kwani 

naamini hawa jamaa bado wako 

wengi na milio ile ya risasi 

imewastua na watakuja hapa muda 

si mrefu kwa hiyo ni hatari sana 

kwenu kuwepo eneo hili.Wasiliana 

na rais mueleze kwamba tunahitaji 

msaada wa polisi haraka sana 

wafike hapa ili kuwadhibiti hawa 

jamaa” akasema Mathew na bila ubishi Meshack Jumbo akamshika 

mkono Theresa wakaanza 

kuondoka kwa tahadhari kubwa 

wakimuacha Mathew peke yake. 

Kabla Mathew hajaamua nini 

cha kufanya likatokea kundi 

lingine la watu saba wote wakiwa 

na silaha wakiwa katika tahadhari 

kubwa.Mathew akiwa katika kile 

kichaka walichokitumia kujificha 

aliweza kuwaona vyema lakini wao 

hawakuweza kumuona.Hakutaka 

kuwapa nafasi akaanza 

kuvurumisha risasi.Kwa bahati 

mbaya ile bunduki aliyokuwa nayo 

haikuwa na risasi za kutosha 

akaitupa haraka ili achukue 

nyingine lakini wale jamaa ambao 

mara tu risasi zilipoanza kuvuma walilala chini, walikwisha fahamu 

mahala risasi zilikokuwa 

zinatokea hivyo wote wakasimama 

kwa haraka na kuanza 

kuvurumisha risasi kuelekea 

upande ule aliokuwako Mathew 

ambaye tayari alikwisha wasoma 

na aliwahi kuondoka eneo lile 

kabla ya wao hawajaanza 

kushambulia.Ghafla wakajikuta 

wakimiminiwa risasi kutokea kwa 

nyuma yao.Mathew alikuwa 

amejilaza juu ya kaburi moja 

aliwaona vizuri na kuwaondoa 

mmoja baada ya 

mwingine.Kilichokuwa kinatokea 

hapa usiku huu pale makaburini ni 

kama katika filamu.Mathew 

aliendelea kubana pale pale juu ya kaburi akisubiri kama kuna 

wengine watajitokeza.Kwa dakika 

tatu hakukuwa na mtu yeyote 

aliyejitokeza.Mathew akawafuata 

wale jamaa aliowaua mwanzo 

akawapiga picha kwa kutumia 

simu yake. 

“Hawako peke yao.Lazima 

kuna wengine bado wapo.Hawa 

jamaa wamejiandaa vilivyo.” 

Akawaza mathew na mara kwa 

mbali akasikia ving’ora vya magari 

ya polisi akajua tayari msaada 

umefika,akaenda kujificha katika 

kichaka kimoja kwani hakuwa na 

imani kama yupi ni askari wa 

kweli na yupi siye.Kundi la askari 

polisi zaidi ya kumi na tano 

wakatokea wakiwa na tochi kubwa wakimulika kila sehemu na 

wakafanikiwa kuiona ile miili ya 

askari waliouawa na Mathew. 

“Haraka ipakieni garini kabla 

hawajafika hapa kwani watafika 

hapa muda wowote toka sasa” 

akasema mmoja wao aliyeonekana 

kiongozi 

“Beka,Stanley na Jacob 

imarisheni ulinzi mahala hapa 

kwani hatujui hao jamaa wako 

wangapi na wamejificha 

wapi.Yeyote atakayejitokeza 

mkate pumzi haraka sana” 

akasema yule jamaa kiongozi 

wao.Mathew akastuka 

“Hawa ni askari polisi wa 

kweli au nao ni kundi moja na 

hawa jamaa?akajiuliza “Ngoja niendelee kujificha 

nisijitokeze hadi hapo 

nitakapokuwa na uhakika kama 

hawa kweli ni askari au ni 

mtandao wa wale wavamizi.” 

Akawaza Mathew 

Wale askari walimaliza 

kuibeba ile miili haraka haraka na 

kuondoka.Mathew akasikia 

muungurumo wa magari 

yakiondoka.Aliendelea kujificha 

pale kwa muda akisubiri kuona 

kama kuna chochote kitakachojiri 

lakini kuliendelea kuwa kimya 

kabisa.Akachukua simu na 

kumpigia Meshack Jumbo 

“Mzee mko wapi? “Tumeshuka huku chini 

tumejificha .Tumesikia milio mingi 

ya risasi uko salama? 

“Niko salama mzee. Twendeni 

tuondoke eneo hili.Kuna mambo 

yametokea hapa ambayo si ya 

kawaida lakini nimekwisha pata 

picha halisi” akasema Mathew na 

kuwasubiri akina Meshack na 

Theresa 

“Hawa waliochukua miili ya 

wale jamaa niliowamaliza ni 

wenzao.Hawa jamaa ni askari na 

wanafahamu mbinu zote za 

kupambana.Kwa bahati nzuri mimi 

ni mjuzi zaidi yao ndiyo maana 

nimefanikiwa kuwaondoa 

vinginevyo si rahisi kuwaondoa 

wale jamaa waliokuwa wamejihami vilivyo” akawaza 

Mathew 

“Nilifanya jambo zuri 

kuwapiga picha kabla 

hawajachukuliwa.Kupitia picha 

hizo tutaweza kuwafahamu ni 

akina nani.Swali 

ninalojiul………………” Mathew 

akatoka mawazoni baada ya 

kusikia majani yakitikisika na 

vishindo vya nyayo za mtu 

zikisikika.Akajiweka sawa na mara 

simu yake ikaita alikuwa ni 

Meshack Jumbo.Mathew akaipokea 

na kuongea kwa sauti ya chini 

Meshack akamtaarifu kwamba 

tayari amekwisha fika mahala 

walipokuwa wamejificha mwanzo 

na Mathew akawafuata. “Pole sana Mathew.Haikuwa 

kazi nyepesi kupambana na hawa 

jamaa” akasema Meshack Jumbo 

“Mzee hatuna muda wa 

kuendelea kukaa hapa 

tumekwisha pata uhakika sasa wa 

kile tulichokuwa 

tunakitafuta.Tuondokeni haraka 

eneo hili” akasema Mathew 

akitangulia mbele na akina 

Meshack wakimfuata 

nyuma.Walipoondoka maeneo yale 

ya makaburi Mathew akaitupa 

kichakani silaha ile aliyokuwa 

ameibeba aliyoichukua kutoka 

kwa wale askari 

waliokufa.walitembea kimya 

kimya hadi katika gari lao 

wakaondoka.Dakika chache baada ya kuondoka wakakutana na 

msafara wa magari ya polisi 

ukielekea kule makaburini 

“Hawa wanakwenda wapi? 

Muda wote hawakuwa wamepewa 

taarifa hadi wavamizi 

wakaondoka? Akauliza Meshack 

Jumbo 

“Mzee Jumbo nimegundua 

kuna watu ndani ya jeshi la polisi 

wanashirikiana au wanatumiwa na 

watu wanaoshirikiana na akina 

Nathan.Ulipopiga simu kwa rais 

kuomba msaada kilikuja haraka 

kikosi cha askari polisi ambao 

waliichukua ile miili ya wale jamaa 

waliouawa na kuondoka 

haraka.Hawakuwa mbali nami na 

niliwachunguza vizuri ni askari polisi waliokuwa na mafunzo yote 

ya kipolisi.Hiki kinachokwenda 

huko sasa hivi ni kikosi cha pili” 

akasema Mathew na kumshangaza 

Meshack Jumbo 

“Kuna kikosi cha kwanza 

kimekuja tayari na kuiondosha ile 

miili ya wale askari waliouawa? 

Akauliza Meshack kwa mshangao 

“Ndiyo mzee .Ile miili yote 

iliondolewa na kikosi kilichofika 

mwanzo.Nilifanikiwa kupata picha 

za wale jamaa niliowamaliza kabla 

wenzao hawajafika halafu ninacho 

kifaa kile ambacho wamekuwa 

wanakitumia katika uchunguzi” 

“Ulifanya jambo zuri sana 

kuwapiga picha .Akili yako inafanya kazi haraka haraka” 

akasema Meshack. 

“Kitu kikubwa cha kufahamu 

ni mahusiano yaliyopo kati yao na 

Nathan. Kipaumbele kwa sasa ni 

kuwasaka na kuwafahamu 

viongozi wa huu mtandao ni akina 

nani.Inaonekana ni watu waliomo 

ndani ya serikali.Mpigie tena simu 

rais mwambie tunakwenda 

kumuona sasa hivi” Akasema 

Mathew 

“Ni saa kumi alfajiri sasa 

atakubali kuonana nasi muda 

huu?akauliza Meshack Jumbo 

baada ya kutazama saa yake 

“Lazima akubali kuonana 

nasi.Jambo hili ni la muhimu 

sana.Call her” akasema Mathew na Meshack Jumbo akampigia simu 

rais akamjulisha kwamba 

wanakwenda kwake kuonana 

naye. 

“Natamani nikimbie 

nikajifiche mbali na hapa ambako 

hakuna kashikashi kama hizi 

zinazoendelea hapa 

nyumbani.Nimeogopeshwa sana na 

haya mambo yanayoendelea.Kwa 

haya mambo ninayoyaona 

simuamini mtu yeyote zaidi ya 

Mathew.Huu mtandao wa hawa 

askari polisi umenitisha sana .Ni 

hawa ndio waliomuua baba.Ni 

watu hatari na hawana 

huruma.Sitaki kukaa mbali na 

Mathew hata kidogo.Ni yeye pekee 

ninayeamini anaweza akanilinda kwa wakati huu” akaendelea 

kuwaza Theresa huku safari 

ikiendelea kimya kimya 

Waliwasili ikulu na rais 

akawapokea wakaelekea katika 

chumba cha mazungumzo 



Mheshimiwa rais samahani 

sana kwa kukusumbua alfajiri 

namna hii” akasema Mathew 

“Bila samahani karibuni 

sana.Nafahamu msingeweza kuja 

alfajiri yote hii kama kusingekuwa 

na kitu cha maana cha kunijulisha” 

akasema Dr.Vivian 

“Ni kweli mheshimiwa rais 

kuna jambo ambalo tunataka 

kukujulisha” Akasema Mathew 

“Karibuni” akasema Dr.Vivian “Mheshimiwa rais baada ya 

kuondoka hapa hatukwenda kulala 

bali tuliendelea na kazi.Tulitaka 

kufahamu hawa askari 

waliotuvamia mimi na Theresa na 

baadae kuvamia nyumbani kwa 

Meshack Jumbo ni akina nani? 

Tukaamua kuweka mtego kwa 

kwenda kuificha mahala saa ile ya 

Nathan ambayo ndiyo tuliyokuwa 

na uhakika kwamba walikuwa 

wanaifuatilia.Tuliweka mtego 

wetu katika makaburi ya 

Mkwajuni na kama tulivyokuwa 

tumetegemea wale jamaa walifika 

hadi pale makaburini.Ni wale wale 

jamaa waliokuwa wamevaa mavazi 

ya jeshi la polisi na walijihami kwa 

silaha za kivita.Wote walikuwa na SMG.Tulipambana nao na 

kufanikiwa kuwaua wapatao tisa 

ingawa haikuwa rahisi kwani ni 

watu wenye mafunzo na uzoefu 

namna ya kupambana na 

kujihami.Baada ya hapo mzee 

Meshack alikupigia simu na 

kukuomba msaada” 

“Ndiyo alinipigia simu na 

kunijulisha kwamba mko katika 

makaburi ya mkwajuni na 

mnahitaji msaada ingawa 

hakunieleza nini kilichokuwa 

kinaendelea huko.Nilimpigia simu 

Inspekta jenerali wa polisi mara 

moja na kumtaka atoe maelekezo 

kiende kikosi cha askari polisi 

waliojihami kwa silaha kali haraka 

sana katika makaburi ya

 Mkwajuni.Poleni sana kwa 

kilichotokea huko” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais kwa msaada wako mkubwa 

lakini kitu cha kushangaza kikosi 

cha kwanza cha askari waliofika 

pale hakikuwa kikosi cha kuja 

kutoa msaada kwetu bali walikuja 

kuondoa miili ya wale askari 

waliokufa” 

“What ?! Dr.Vivian akashangaa 

“Walifika askari kwa haraka 

sana lakini walichokuja kukifanya 

ni kuchukua miili ya wale askari 

waliokufa na kuondoka haraka na 

niliwasikiwa kwa masikio yangu 

kiongozi wao akiwaharakisha 

kuipakia miili katika magari kabla 

askari hawajafika.Dakika zaidi ya kumi na tano baadae wakati na sisi 

tukiondoka tukakutana na kikosi 

cha askari wakielekea huko.Kwa 

hiyo mheshmiwa rais unaweza 

kuona ni kitu gani kinachoendelea 

hapa.Kuna watu wako ndani ya 

jeshi la polisi au wana mawasiliano 

na watu wakubwa waliomo ndani 

ya jeshi la polisi ambao 

wanashirikiana na hawa jamaa 

ambao hatujui kama ni askari 

polisi au ni akina nani.Tunahitaji 

kuufahamu ni akina nani 

wanaoendesha mtandao huu na 

watu wale kama ni askari au 

siyo.Nilifanikiwa kupiga picha 

miili ya baadhi ya wale niliokuwa 

nimewaua pamoja na silaha 

zao.Nitakuachia picha hizo ili viongozi wa polisi waweze 

kuwatambua kama ni askari 

wao.Tukiwafahamu ni akina nani 

na wanatoka kituo gani cha polisi 

tutaweza kuwafahamu viongozi 

wao.Hao viongozi wao lazima wana 

mahusiano na akina Nathan na 

ndio wanaotekeleza mipango 

miovu ya Marekani kwa nchio 

yetu.Tukiwapata hao viongozi wao 

tutafahamu mambo mengi toka 

kwao.Mheshimiwa rais hicho 

ndicho kilichotokea usiku wa leo” 

akasema Mathew 

“Nimekosa neno la kusema ila 

poleni sana na hongereni kwa kazi 

nzuri mliyoifanya.Sasa naamini 

kweli kutakuwa na mtandao wa 

watu ndani ya serikali yangu ambao wanashirikiana na 

Marekani.Nathan anafanya kazi 

kwa niaba ya serikali ya Marekani 

na kama kuna mtu ndani ya 

serikali yangu anashirikiana na 

Nathan basi anashirikiana moja 

kwa moja na serikali ya 

Marekani.Lazima tuwatafute hawa 

wote tuwapate na wapate stahili 

yao.Wakati huu ambao tuko vitani 

tunapigania uchumi wetu 

hatupaswi kuwa na watu kama 

hawa.Inawezekana hata katika 

watu wanaonizunguka kuna watu 

wanaoshirikiana na Marekani 

kunihujumu.Kuna kitu kilitokea 

Marekani ambacho mpaka sasa 

najiuliza kilitokeaje lakini 

sijaweza kupata jibu.Nilikutana na wale wawakilishi wa wafanya 

biashara wa China na yule mjumbe 

wa rais wa Korea Kaskazini kwa 

siri lakini kesho yake rais wa 

Marekani alikuwa na taarifa zote 

za yale yote tuliyoongea na 

wajumbe wale na hapo ndipo 

mgogoro kati yangu na Marekani 

ulipoanzia.Mathew unadhani 

Nathan anaweza akahusika 

chochote na jambo hili? Unadhani 

hii ni mojawapo ya kazi 

anazozifanya Nathan za kupata 

taarifa zangu?Akauliza Dr.Vivian 

“ Kuna uwezekano mkubwa 

wa hilo jambo mheshimiwa 

rais.Naomba kwanza kuuliza je 

Nathan kuna kitu chochote aliwahi 

kukupa unakivaa aidha mkufu,bangili au saa? Akauliza 

Mathew 

“Mathew alinipa mkufu wa 

thamani kubwa sana wenye kidani 

chenye madini ya Tanzanite ambao 

huwa ninauvaa mara chache 

ingawa Nathan amekuwa 

ananisisitiza kwamba niuvae mara 

nyingi.Hupenda kuniona nikiwa 

nimeuvaa” akasema Dr.Vivian 

“Uliuvaa ulipokwenda 

Marekani?Wakati unazungumza na 

hao jamaa ulikuwa umeuvaa? 

“Ndiyo nilikuwa 

nimeuvaa.Nathan alikwisha 

nitaarifu kwamba tutaonana New 

york na kila mara anionapo 

hupenda kuniona nikiwa 

nimeuvaa mkufu huu alionipatia wenye kidani cha thamani kubwa 

chenye alama ya V alama ya jina 

langu.” 

“Unaweza ukanipa huo mkufu 

kama hutajali? Akasema Mathew 

na Dr.Vivian akaenda chumbani 

kwake akarejea na kiboksi kidogo 

chenye nakshi za kupendeza na 

toka ndani ya kiboksi kile akatoa 

mkufu mzuri wa gharama kubwa 

sana akampatia Mathew. 

“Dah ! mkufu wa gharama 

kubwa sana huu.Gharama yake ni 

kiasi gani? 

“Milioni mia moja na hamsini” 

akasema Dr.Vivian na wote 

wakatazamana.Mathew 

akauchukua mkufu ule 

akautazama kwa makini sana na kutoa kitu fulani katika mkoba 

wake na kuchomoa kitu fulani 

kama msumeno mdogo akaikata 

sehemu ya nyuma ya kile kidani na 

kisha akatoa kitu fulani ndani yake 

akakitazama na kumuonyesha 

Dr.Vivian. 

“Kama nilivyokueleza awali 

kwamba Nathan hakuwa na 

mapenzi yoyote kwako bali 

alikuwa karibu yako akikuonyesha 

mapenzi makubwa ili kukupofusha 

bali alikuwa na kazi maalum na 

hiki ndicho alichokuwa 

anakifanya.Alikuwa na kazi ya 

kukusanya taarifa zako.Ndani ya 

mkufu huu wa thamani kubwa 

kumewekwa kifaa hiki kidogo 

ambacho hukusanya taarifa zako zote.Kila unapouvaa mkufu huu 

kuna kitu cha kuweza kuhisi joto la 

mwili na hivyo vifaa vilivyofungwa 

humu huanza kufanya kazi na 

hurekodi kila kitu unachokiongea 

wakati umeuvaa huu mkufu ndiyo 

maana Nathan alikuomba uuvae 

mara kwa mara ili waweze 

kuyafahamu mambo yako 

mengi.Kama ulikuwa umeuvaa 

mkufu huu wakati ukizungumza na 

hao jamaa basi waliweza kunasa 

maongezi yako yote na ndiyo 

sababu ya rais wa Marekani 

kufahamu kuhusu mazungumzo 

yako na mjumbe maalum wa rais 

wa Korea Kaskazini.” 

Dr.Vivian alitaka kusema kitu 

midomo ikabaki inamtetemeka. “I hope he’s in hell right 

now.Kumbe amekuwa 

ananidanganya kwa muda mrefu 

bila ya mimi kufahamu.Nilikuwa 

mjinga sana kwa kukubali 

kupofushwa na penzi lake la 

bandia.Kama ni hivi kuna mambo 

mengi sana watakuwa 

wameyapata kutoka kwangu 

kwani nimekuwa na mkufu huu 

kwa muda mrefu.Kuna kitu gani 

hasa wanakitafuta kutoka 

kwangu?!! Akauliza Dr.Vivian 

“Hilo ndilo jambo 

tunalopaswa kulichunguza 

mheshimiwa rais.Lazima kuna 

jambo ambalo wanalichunguza 

kwako” akasema Mathew “Mathew tafadhali naomba 

ufanye kila uwezalo kuhakikisha 

suala hili linafika 

mwisho.Samahani kuhusu maneno 

niliyoyazungumza 

awali.Nakuomba hakikisha 

unachunguza na kuwafahamu wote 

waliomo katika mtandao huu wa 

hapa Tanzania ambao 

wanashirikiana na serikali ya 

marekani” 

“Nitajitahidi mheshimiwa rais 

lakini kwa kuanzia kuufahamu 

mtandao huu tunaomba utusaide 

tuweze kuwafahamu hawa askari 

waliouawa usiku wa leo kule 

mkwajuni kama ni askari wa jeshi 

letu na tutawafahamu watu 

waliowatuma.Picha zao utabaki nazo na utazikabidhi kwa mkuu wa 

jeshi la polisi ili ziweze kufanyiwa 

kazi haraka sana na kuwafahamu 

watu wale kama ni askari wetu” 

akasema Mathew 

“Kesho asubuhi kitu cha 

kwanza kitakuwa hicho,nitakutana 

na wakuu wa jeshi la polisi na 

nitatoa maelekezo ya kuwatafuta 

hawa jamaa na kufahamu ni akina 

nani na kama ni askari wetu na 

kama siyo wanatoa wapi sare na 

vifaa vya jeshi la polisi” akasema 

Dr.Vivian 

“Ahsante Dr.Vivian,hiyo 

itakuwa ni sehemu nzuri ya 

kuanzia kuufahamu mtandao 

huu.Vile vile naomba 

nikukumbushe kwamba Camilla Snow anawasili asubuhi ya leo 

akitokea Havana kwa hiyo kama 

nilivyokuomba kwamba apate 

kuruhusiwa kuingia nchini kwani 

atanisaidia sana katika uchunguzi 

wangu” akasema Mathew 

“Nitalifanyia kazi hilo usijali” 

akasema Dr.Vivian 

“Ahsante Dr.Vivian .Sisi ngoja 

tukapumzike walau kidogo kwani 

usiku mzima tumekesha macho” 

akasema Mathew na kumrushia 

Dr.Vivian picha zile za wale watu 

waliouawa makaburini katika 

simu yake halafu akaiacha pia ile 

saa ya Nathan ili rais 

aitunze,wakaagana na Meshack 

Jumbo akachukuliwa na walinzi wa 

rais akapelekwa mahala walikoandaliwa nyumba,Mathew 

na Theresa wao wakatumia gari la 

Meshack Jumbo wakaondoka. 

“Mathew sitaki unipeleke 

nyumbani kwangu.Ninaogopa sana 

wale jamaa wanaweza wakanifuata 

nyumbani.Nataka twende wote 

nyumbani kwako kama hutajali” 

akasema Theresa 

“Hakuna tatizo kuhusu hilo” 

akasema Mathew kwa ufupi 

“Nimesikia unamwambia dada 

kuhusiana na huyo mtu anaitwa 

Camilla Snow.Ni nani huyo? 

“Camilla anatoka Marekani na 

anakuja kwa lengo la kusaidiana 

nami katika shughuli hii kama 

ujuavyo kwamba suala hili tayari limekwisha vuka mipaka ya 

nchi.”akasema Mathew. 

“Mathew ahsante sana kwa 

kile ulichokifanya leo.Nimeamini 

wewe ni maalum kabisa na 

unaweza ukalifumbua fumbo 

hili.Sikutegemea kama kwa muda 

mfupi namna hii ungeweza kupiga 

hatua kubwa namna hii” akasema 

Theresa 

“Ahsante lakini haya yote 

yasingewezakana bila ya 

ushirikiano wako.Umefanya kazi 

kubwa sana.Endapo 

usingemmaliza Nathan haya yote 

tusingeyafahamu.Tusingejua kama 

kuna mtandao wenye mahusiano 

naye” akasema Mathew na safari 

ikaendelea 

WASHINGTON DC - MAREKANI 

 Saa tatu za usiku jijini 

Washington DC kikao cha siri 

kinafanyika katika ikulu ya 

Marekani ambacho 

kiliwakutanisha wakuu wa shirika 

la kijasusi la Marekani CIA na rais 

Mike straw. 

“Karibuni sana.Willy 

uliponiambia kwamba unahitaji 

kuja kuniona jioni ya leo 

nimelazimika kuahirisha shughuli 

zangu nyingine ili 

tukutane.Naamini kuna jambo la 

msingi sana unalokuja kunieleza” 

akasema rais Mike straw 

“Mheshimiwa 

rais,nimelazimika kuja kukuona ili kukupa taarifa za muhimu.Kuna 

matatizo yametokea Tanzania.” 

Akasema Willy Gadner 

mkurugenzi wa CIA 

“Nini kimetokea 

Tanzania?Kwa wakati huu hii ni 

taarifa ambayo sitaki kuisikia 

kabisa.Macho yetu yote 

tumeyaelekeza 

Tanzania.Tukiruhusu kosa lolote 

hata dogo tutatoa mwanya kwa 

Korea Kaskazini 

kujimarisha.Tunapaswa kufanya 

kila tuwezalo kuhakikisha 

kwamba Korea Kaskazini na 

Tanzania hazianzishi mashirikiano 

ya kibiashara.Hebu nieleze kitu 

gani kimetokea?akauliza Mike 

Straw rais wa Marekani.“Kuna tatizo limetokea 

Tanzania ambalo ni muhimu 

ukajulishwa mapema ili ufahamu 

kinachoendelea huko hasa 

kutokana na umuhimu wa 

Tanzania kwa sasa.Asubuhi ya leo 

kituo 1212 ambacho ni rais wa 

Tanzania na 1214 ambacho ni 

mdogo wake vilika mawasiliano 

ghafla na mpaka sasa bado 

hatujafahamu nini kimetokea na 

wala hatujafanikiwa kurejesha 

mawasiliano na kompyuta 

zetu.Hawa watu wawili ni muhimu 

sana hivyo kupotea kwao ghafla 

kumetustua lakini tayari 

nimekwisha toa maelekezo kwa 

110C alishughulikie jambo hili na 

ahakikishe anafanya kila awezalo ili mawasiliano kati ya vituo hivyo 

viwili muhimu na Washington 

yarejee” 

“Mawasiliano hayo 

yamekatikaje? Mike straw akauliza 

“Bado hatufahamu nini 

sababu ya mawasiliano 

kukatika.Inawezekana labda vifaa 

vile vimeharibika kwani 

mawasilino yetu yanapitia katika 

simu za kampuni ambazo zina 

programu maalum ambazo 

huiwezesha ofisi yetu ya 

Washington kuweza kunasa 

mawasiliano yote.Kuanzia asubuhi 

ya leo kompyuta zetuzinaonyesha 

kwamba rais wa Tanzania 

hajatumia simu yake wala 

kompyuta na hata mdogo wake naye ni hivyo hivyo.Kukatika kwa 

mawasiliano kwa pamoja 

kunatufanya tuamini kwamba lipo 

tatizo Tanzania na tumemuachia 

110C afuatiie kuna tatizo gani na 

alitatue haraka sana” akasema 

Willy Gadner 

“Gadner tafadhali sana 

naomba wekeza nguvu kubwa sana 

Tanzania.Usikubali hata kidogo 

kumpoteza Dr.Vivian.Ni mtu 

muhimu sana kwetu kwa 

sasa.Lazima tufahamu kila kitu 

anachokifanya .Lazima tunase 

mawasiliano yake yote ili 

tufahamu mipango yake na Korea 

Kaskazini.Tanzania hawawezi 

kutuzidi sisi maarifa .Lile ni taifa 

dogo masikini na sisi ni taifa kubwa na tajiri duniani.Uwezo 

wetu kiteknolojia ni mkubwa sana 

na tunaweza kupata taarifa yoyote 

toka kwa mtu yeyote duniani hivyo 

lazima tuhakikishe kwamba vitaifa 

vidogo kama Tanzania 

havituyumbishi.Wekeza nguvu 

kubwa na teknolojia ya kutosha ili 

tupate kila tunachokihitaji.CIA 

tunao watu wenye ujuzi mkubwa 

,watume waende Tanzania 

wakafanye kazi kwa ajili ya taifa 

lao la marekani.Tusiweke mzaha 

katika suala hili ambalo ni la 

muhimu mno kwa sasa” akasema 

Mike straw 

“Mheshimiwa rais,kuhusu 

rasilimali watu tunao wa kutosha 

na tayari kuna mtandao mrefu umekwisha tengenezwa ambao 

unatusaidia sana katika 

kufanikisha mambo yetu mengi 

nchini Tanzania.Tuna watu wetu 

kule na wamejipanga vizuri.Karibu 

katika kila idara nyeti ya serikali 

kuna watu wetu hata ikulu.Itoshe 

kusema tu kwamba hiki 

kilichotokea hatukuwa 

tumekitegemea na tunakifanyia 

kazi kujua kimetokeaje na tutafute 

namna ya kulimaliza.Kama 

nilivyosema kwamba mtandao 

wetu ni mpana na tunaweza 

kufanya jambo lolote kwa muda 

wowote na ninakuhakikishia 

mheshimiwa rais kwamba suala 

hilo la kukatika kwa mawasiliano 

tunalifanyia kazi na litapatiwa fumbuzi muda si mrefu” akasema 

Willy akanyamaza kidogo halafu 

akasema 

“Kuna tatizo lingine 

mheshimiwa rais.Kuna mtu wetu 

ambaye ni seli 12A.Huyu 

tumemuweka karibu na Dr.Vivian 

na wana mahusiano ya 

kimapenzi.Anaitwa Nathan.Kama 

hukuwa ukijua mheshimwa rais ni 

kwamba tumeanza kumfuatilia 

Vivian toka angali anasoma hapa 

marekani.Kuna sababu 

zilizopelekea tukaanza kumfuatilia 

ila nitakueleza siku nyingine 

.Tulimtumia huyu Nathan 

kuanzisha urafiki na baadae 

mahusiano ya kimapenzi .Taarifa 

hizi zote tunazozipata sasa kutoka kwa Dr.Vivian ni kwa sababu ya 

Nathan.Amefanya kazi kubwa sana 

lakini kwa siku za karibuni 

ameanza kujisahau na kuzama 

mapenzini baada ya kutanganza 

kutaka kumuoa 

Dr.Vivian.Tulimuonya kuhusiana 

na suala hili na kumkumbusha 

kwamba hatakiwi kuzama 

mapenzini.Pamoja na 

kumkumbusha majukumu yake 

Nathan aliendelea na mipango 

yake ya kumuoa Dr.Vivian na juzi 

ameondoka marekani baada ya 

kuitelekeza kazi aliyokuwa 

amepewa na akaenda 

Tanzania.Leo kompyuta yetu 

ilionyeha kuna tatizo kwa 

Nathan.Labda kwa kukufahamisha mheshimiwa rais,Nathan ni mmoja 

wa maajenti wetu ambaye alikuwa 

katika mfumo wa majaribio wa 

kuwatambua na kuwafuatilia 

maajenti wote duniani.Huu ni 

mfumo mpya na bado uko katika 

majaribio japokuwa umeonyesha 

matunda japokuwa kuna 

changamoto chache ambazo 

yatupasa kuzifanyia kazi.Kuna 

kifaa kidogo hufungwa katika 

mwili ambacho hurekodi 

mwenendo wa mapigo ya moyo na 

taarifa hizo huweza kusomwa kwa 

kutumia saa ambayo huivaa 

mkononi.Saa hiyo ambayo 

imetengenezwa maalum huweza 

kusomwa na kompyuta zetu na 

kupata taarifa zote za ajenti na kujua maendeleo yake.Hapo awali 

maajenti wetu walikuwa 

wanapotea sana lakini kwa sasa 

baada ya kuanza kwa mfumo huu 

tumekuwa tunawafuatilia maajenti 

wetu kote duniani na kujua kama 

wako salama.Umetuwezesha 

kufahamu kama ajenti ametekwa 

au amekufa” akanyamaza kidogo 

halafu akaendelea 

“Mapigo ya moyo yalianza 

kupunguza kasi yake na baadae 

kompyuta ikaonyesha mstari 

mnyoofu hii ni ishara kwamba 

hakuna mapigo ya moyo na ajenti 

amekufa au ameivua ile saa ambao 

hatakiwi kuivua hadi siku ya kufa 

kwake.Saa yake ya mkononi bado 

inaendelea kusomwa na kompyuta zetu na tumewaagiza watu wetu 

walioko Tanzania wafuatilie 

kufahamu kama Nathan ni mzima 

au amekufa.Tumewatuma wafanye 

kila juhudi kuweza kuipata saa 

hiyo ambayo ni muhimu sana 

kwetu kwani si saa kama saa za 

kawaida tunazovaa kutazama 

wakati.Ni saa iliyotengenezwa 

maalum kabisa kwa kazi 

maalum.Juhudi za watu wetu 

kuifuatilia na kuipata hiyo saa 

zinaendelea lakini mpaka sasa 

bado hakuna mafanikio na saa 

haijapatikana.Saa hiyo inaweza 

kutujulisha kama Nathan amekufa 

au bado.Ina kumbu kumbu 

zote.Hiyo saa pia ina programu 

maalum ya kuweza kuwasiliana na maajenti wengine walioko sehemu 

mbali mbali duniani na kama kuna 

tatizo basi hujulishwa kwa 

kuwashwa taa nyekundu na hapo 

ajenti huweza kujua kuna hatari na 

akawasiliana na ofisi kuu au ajenti 

aliyepo karibu.Endapo akiipata 

mtu ambaye ana ufahamu na 

mambo ya kielektroniki anaweza 

akaitumia saa hiyo kufahamu 

walipo maajenti wa Marekani 

sehemu mbali mbali za dunia na 

akawafanyia kitu kibaya.Taarifa 

iliyonifikia wakati tunakuja hapa 

ni kwamba kompyuta zetu 

zinaonyesha kwamba saa hiyo iko 

ikulu ya Tanzania na hiyo 

inatuthbitishia kwamba Dr.Vivian 

anayo.Tumeanza mikakati ya namna ya kuipata saa hiyo ili 

tuweze kuwa na uhakika kama 

Nathan amekufa au bado mzima” 

akasema Willy na kumtazama rais 

“Gadner hizo ni taarifa za 

kustusha sana.Ninachotaka kujua 

mna uhakika kwamba huyo 

Nathan amekufa? Isije kuwa 

ametekwa nyara” akasema Rais 

“Uhakika wa kwamba 

amekufa ni mkubwa kwani kama 

ametekwa kuna namna ya 

kutambua mapigo yake ya moyo 

yanavyokwenda.Lakini haya ya 

Nathan yalipanda ghafla kupita 

kawaida halafu yakaanza kushuka 

.Hii inatupa uhakika asilimia 99 

kwamba atakuwa amekufa lakini 

ni muhimu kuipata saa hiyo ili tuweze kuwa na uhakika kama 

kweli amekufa” 

“Kama amekufa hamjaweza 

kugundua nini kinaweza 

kusababisha kifo 

chake.Yawezekana akatekwa na 

kuteswa sana hadi 

akauliwa.Mnahisi kuna uwezekano 

akawa amefahamika nini 

anafanya?akauliza Mike straw 

“Kuna uwezekano mkubwa 

serikali ya Tanzania wakawa 

wamemfahamu ni nani na 

wakaamuua au akajiua kabla ya 

kutoa siri.Nikiliunganisha tukio 

hili la Nathan na lile la kupotea 

ghafla kwa mawasiliano ya Rais 

ninapata wasiwasi kwamba kama 

amekufa serikali ya Tanzania itakuwa inahusika katika kifo 

chake.Saa yake kuendelea 

kuonekana ikulu ni ishara tosha 

kwamba kuna mkono wa serikali 

katika masahibu yaliyomkuta 

Nathan.Kupotea kwa Nathan 

naweza kusema ni pigo kwetu 

kwani alikuwa ni muhimu sana 

hasa katika jitihada za muda mrefu 

za kuitafuta football” akasema 

Willy na Mike straw akastuka 

“Football? Akauliza kwa 

mshangao 

“Ndiyo mheshimiwa 

rais.Kumekuwa na juhudi za 

kuitafuta football.Rais Anorld 

Mubara wa Tanzania aliwahi 

kuanzisha utaratibu wa kutembea 

na begi alilolipa jina la footbal.Begi hilo linabeba siri kubwa ambayo 

raisi alikuwa anatembea nayo na 

ilitulazimu kufanya operesheni 

maalum ya kulipata begi hilo lakini 

hatukufanikiwa na badala yake 

ndege ya rais ikaanguka na rais 

Anold Mubara akafariki dunia na 

Sebastian Matope ambaye alikuwa 

mbebaji wa Football akitoka 

salama ndani ya ndege akiwa na 

begi hilo.Baadae Sebastian aliuawa 

lakini football haijawahi 

kuonekana.Dr.Vivian ni mtoto wa 

Sebastian na ameanzisha 

uchunguzi wa kutaka kujua nani 

waliomuua baba yake na vile vile 

kutafuta begi hilo la 

football.Wapelelezi anaowatumia 

katika uchunguzi huo tayari wamekwisha piga hatua kubwa na 

tuna uhakika watafanikiwa 

kugundua mahala lilipo football 

kwani Sebastian matope alitoka 

ndegeni akiwa na begi hilo na tuna 

uhakika kuna mahala 

alilificha.Ingekuwa rahisi sana 

kwetu kufahamu kila kitu kama 

Nathan angeendelea kuwa karibu 

na rais kwani wachunguzi hao 

wanaripoti kwa rais.” 

“Mna hakika hao wachunguzi 

hawataweza kugundua ushiriki wa 

Marekani katika ajali ya ndege ya 

rais wa Tanzania?akauliza Mike 

kwa wasi wasi 

“Hapana mheshimiwa rais 

hawataweza kugundua 

chochote.Hakuna chochote cha kutuunganisha na ajali ile kwani 

watu wote waliokuwemo ndani ya 

ile ndege walifariki dunia.Usiwe na 

wasi wasi kabisa na hilo” akasema 

Willy 

“Kwa hiyo mheshimiw arais” 

Will akaendelea. 

“Tumekuja kukufahamisha 

matatizo hayo tuliyonayo nchini 

Tanzania lakini tunajitahidi 

kuhakikisha kila kitu kinakwenda 

vizuri.” Akasema Will Gadner na 

ukimya ukatanda.Baada ya muda 

Mike straw akasema 

“Gadner kuna mzaha 

ninauona unafanyika kuhusu suala 

la Tanzania.Suala la Tanzania 

naona halipewi kipaumbele stahiki 

hadi mambo haya yakatokea.Sitaki kusikia tena mambo kama haya 

yakiendelea kutokea 

Tanzania.Kwa hivi sasa Tanzania 

ni nchi ambayo tunaitolea macho 

sana kutokana na ukaribu wake na 

Korea kaskazini.Tukiweka mzaha 

na mashirikiano kati ya tanzania 

na Korea Kaskazini yakafanikiwa 

na ikapata madini ya Urani na 

kuongeza idadi ya silaha zake za 

nyuklia,Usalama wa Marekani 

utakuwa shakani.Uchumi wa Korea 

Kaskazini unakua kwa kasi kubwa 

na hatupaswi kuiacha nchi ile 

ikajiimarisha zaidi kijeshi kwani 

litakuwa ni taifa hatari sana kwa 

usalama wa dunia.Katika suala hili 

tunawategemea sana CIA ili 

kuweza kupata taarifa mbali mbali za kila kinachoendelea katika 

mchakato wa mashirikiano baina 

ya mataifa haya mawili.Mnapaswa 

kuifanya kazi yenu kwa umahiri 

mkubwa sana.CIA ni shirika kubwa 

la ujasusi duniani na hatuwezi 

kusumbuliwa na kitaifa kidogo 

kama Tanzania.Narudia tena 

Gadner fanyeni kazi yenu 

inavyotakiwa .Sitaki kuletewa 

taarifa za operesheni 

kushindikana.Nataka safari 

nyingine ukija hapa uwe na taarifa 

zitakazonipa tabasamu na si 

taarifa za kunifanya nikune 

kichwa.Mna watu wenye viwango 

vya juu mno kuliko nchi nyingine 

yoyote chini ya jua,wapelekeni 

wakafanye kazi Tanzania .Kama rais wa Tanzania ndiye kikwazo 

nileteeni mapendekezo ya 

kumuondoa na mimi nitasaini 

haraka sana.Hawezi mtu mmoja 

akatuumiza vichwa 

vyetu.Tunaumiza akili zetu kwa 

nchi korofi kama Korea Kaskazini 

na si nchi ndogo kama 

Tanzania.Nileteeni pendekezo hilo 

mkiona linafaa nami mimi 

sintasita kuidhinisha aondolewe 

mara moja.Tunazo mbinu nyingi za 

kuweza kumuondoa ili asiweze 

kuwa kikwazo kwetu.Nataka 

mpaka kesho mchana muwe 

mmeniletea mpango mkakati 

namna mtakavyoweza kukabiliana 

na hali iliyokoTanzania.Nataka 

suala la Tanzania lipewe kipaumbele kikubwa sana katika 

mipango yenu yote.Mkishindwa 

katika jambo hili mtakuwa 

mmeliangusha taifa la 

Marekani.Msiwe sababu ya wa 

marekani kuishi kwa hofu 

kutokana na vitisho vya Korea 

Kaskazini.Tukishindwa kumdhibiti 

sasa na kumuacha akayapata 

madini ya Urani toka Tanzania 

watu wetu wataishi kwa hofu 

kubwa kwani ataongeza uwezo 

wake wa kuishambulia 

Marekani.Kama zoezi hili litakuwa 

gumu niambieni ili niweze 

kutafuta watu wengine wenye 

kuweza kuifanya kazi hiyo.Narudia 

tena kwamba kama Dr Vivian ni 

kikwazo kwenu nielezeni ili niwape ruhusa ya 

kumuondoa.Tunao uwezo wa 

kumuondoa rais yoyote wa nchi 

yoyote duniani.” Akasema Mike 

straw kwa ukali 

“Tumekuelewa mheshimiwa 

rais lakini suala kama hili 

linahitaji umakini mkubwa sana 

katika utekelezaji wake na hasa 

kwa wakati huu ambao kuna 

mvutano mkali.Tunao uwezo wa 

kumuondoa rais wa Tanzania 

lakini dunia nzima itafahamu 

kwamba ni sisi na haitaleta picha 

nzuri kwa washirika 

wetu.Kikubwa tunachoshughulikia 

kwa sasa ni kurejesha mawasiliano 

kati ya Dr.Vivian na ofisi yetu hapa 

Washington ambayo yatatuwezesha kufahamu kuhusu 

mipango yote anayoipanga kuhusu 

mashirikiano yake na Korea 

kaskazini” akasema Willy Gadner 




DAR ES SALAAM – TANZANIA 

Ndege ya shirika la ndege ya 

Penny air ilitua katika uwanja wa 

ndege wa kimataifa wa Julius 

Nyerere jijini Dar es salaam.Hii ni 

ndege iliyomchukua Camilla Snow 

kutoka Havana Cuba kumleta Dar 

es salaam.Walinzi waliotumwa na 

rais wakiwa wameambatana na 

Mathew na Theresa walikuwepo 

uwanjani pale kumlaki 

Camilla.Ndege ikasimama mlango 

ukafunguliwa na mwanamke mmoja mwenye umri kati ya miaka 

ishirini na tano au na sita 

akashuka ndegeni.Alikuwa amevaa 

gauni fupi jeusi,viatu virefu vyeusi 

na mkononi alikuwa ameshika 

mkoba mweusi.Nywele zake ndefu 

zenye weusi wa kung’aa zilipepea 

kwa sababu ya upepo mkali 

ikamlazimu kuutumia mkono 

wake mmoja kuziweka sawa 

Alishuka ngazi taratibu na 

nyuma yake wakafuata watu 

wanne wakiwa wamebeba 

masanduku makubwa 

matatu.Mathew na wale 

alioongozana nao walikuwa chini 

ya ngazi wakimsubiri Camilla.Mara 

tu alipogusa ardhi ya Tanzania Mathew akamsogelea na kumpa 

mkono 

“Karibu Tanzania Camilla 

Snow” akasema Mathew .Camila 

hakujibu kitu akatabasamu na 

kutikisa kichwa ishara ya 

kushukuru.Mathew 

akamtambulisha kwa Theresa na 

wale walinzi wa rais halafu 

wakaelekea katika gari.Mathew 

akawashukuru wale jamaa 

waliomsaidia Camilla kubeba 

mabegi yake.Mizigo ya Camilla 

ikapakiwa garini ,Mathew 

akawaelekeza wale walinzi 

wakaendelee na shughuli zao 

halafu yeye,Theresa na Camilla 

wakaingia katika gari wakaondoka.Tayari ilipata saa 

moja za asubuhi 

“Mathew mimi naomba 

unipitishe nyumbani kwangu 

nikapumzike kama utanihitaji 

utanijulisha” akasema Theresa 

“Sawa Theresa wewe pumzika 

ila muda wowote nitakapokuhitaji 

nitakujulisha .Pole sana kwa 

kukesha macho usiku wa jana” 

akasema Mathew.Camilla akatoa 

kifaa cha kuhifadhia miziki mithili 

ya simu akachomeka spika za 

masikioni na kuvaa akaanza 

kusikiliza muziki.Theresa 

aliyekuwa amekaa kiti cha mbele 

pembeni ya Mathew akasema 

“Huyu mgeni wako mbona ana 

nyodo namna hii? Kwa nini hataki kusalimia? Anadhani hatufahamu 

kiingereza?akasema Theresa 

“Theresa ni mapema sana 

kutamka chochote kuhusu huyu 

mgeni wetu.Inatakiwa kwanza 

tumsome tabia zake.Tumsome 

taratibu na tutamuelewa” akasema 

Mathew na Theresa akabetua 

midomo 

“Wanawake !! akawaza 

mathew na kutabasamu 

akachukua simu na kumpigia 

Hamis Chuma 

“Mathew habari za asubuhi? 

“Habari nzuri kabisa 

Chuma.Sijapata mrejesho wowote 

toka kwako kama kazi ilikwenda 

vizuri.” “Nilikuwa mbioni kukupigia 

simu kukupa taarifa .Tumerejea 

dakika kama kumi zilizopita .Usiku 

mzima tumefanya ile kazi na 

tumeikamilisha .Mahala 

tulikouficha ule mwili hakuna 

atakayeweza kugundua 

chochote.Tumeufukia mwili 

katikati ya makaburi ya kwa 

sadala” 

“Mna hakika hakuna yeyote 

anayeweza kutia shaka mahala 

hapo? 

“Hakuna Mathew.Tunafanya 

hii kazi kwa utaalamu mkubwa 

sana” 

“Ok Ahsante .Kuna jambo 

nataka unisaidie .Nisaidie gari 

langu kuvutwa hadi gereji kwa Somji Kipara libadilishwe matairi 

yote.Nitalipitiai hapo baadae” 

“Sawa Mathew nitakusaidia” 

akasema Hamis Chuma na kukata 

simu.Mathew akamgeukia Theresa 

“Wale jamaa tayari 

wamekamilisha kazi.Hakuna 

atakayeuona tena mwili wa 

Nathan” akasema Mathew 

“Sikufikiria kama siku moja 

ningeweza kuingia katika orodha 

ya wauaji.Nimetoa roho ya mtu 

lakini ni kwa ajili ya kujilinda 

mimi na dada yangu.Watu hawa 

waliua familia yetu na sasa bado 

wanaendelea kutuifuatilia mimi na 

dada.Angeendelea kuwa hai 

tugekuwa hatarini na sisi 

kuuawa”akasema Theresa “Usijilaumu sana Theresa 

kwani jambo ulilolifanya lina 

manufaa makubwa.Bila kufanya 

vile tusingefahamu kuhusu kile 

kikundi cha askari ambao 

wametuvamia jana.Kikundi kile 

kimeibuka baada ya Nathan 

kufariki.Pamoja na hayo jambo hili 

limesababisha doa kati yako na 

Vivian.Japokuwa walikuwa 

wamekorofishana lakini Vivian 

bado alikuwa anampenda Nathan 

kwa hiyo ana kidonda kikubwa 

moyoni mwake na kitachukua 

muda kupona.Ninakushauri mpe 

muda kidonda chake kipone.Kwa 

sasa mahusiano yenu hayatakuwa 

kama zamani ila nakuomba 

usivunjike moyo ,endeleakumpenda na kumuheshjimu.Iko 

siku naamini mambo yatakaa 

sawa” akasema Mathew 

“nalifahamu hilo Mathew na 

ndiyo maana nataka nijiweke 

mbali naye kwa muda huu ili 

asinione mara kwa mara karibu 

yake na kupata 

hasira.Nilichokifanya si kitu kizuri 

na hata kama ningekuwa mimi 

mahala pake 

ningekasirika.Naamini iko siku 

yatakwisha” akasema Theresa 

Mathew alimpitisha Theresa 

nyumbani halafu yeyena Camilla 

wakaendelea na safari .Hadi 

walipofika katika makazi ya 

Mathew, Camilla hakuwa 

ameongea hata neno moja “Safari hii nimekutana na mtu 

wa aina yake.Hataki kuongea.Ni 

mgeni hapa Dar es salaam lakini 

hageuzi hata shingo kutazama nje 

kama wafanyavyo wageni 

wengine.Inawezekana labda ni 

kwa sababu ya ugeni.Hata hivyo 

lazima nitafute namna ya 

kuendana naye.Ninamshukuru 

Mungu amenijalia uwezo wa 

kuweza kuishi na mtu yeyote.Hata 

shetani ninaweza kuishi naye” 

akawaza na kutabasamu wakati 

akimtazama Camilla kwa wizi 

kupitia kioo kidogo cha 

kumuwezesha dereva kutazama 

nyuma 

“Hata hivyo mhh ! Hiki kweli 

kipusa.Mtoto amekamilika kila idara.Hakuna sehemu unayoweza 

kutoa kasoro.Yawezekana 

anajifahamu namna alivyo mzuri 

ndiyo maana ana nyodo namna hii” 

akawaza Mathew 

Walifika katika makazi ya 

Mathew ,akamkaribisha Camilla 

ndani 

“Hapa ni wapi? Kwa mara ya 

kwanza Camilla akaongea na 

Mathew akatabasamu 

“Hapa ni nyumbani 

kwangu.Ndipo utakapoishi kwa 

sasa.Jisikie nyumbani ila endapo 

hautajisikia huru hapa 

nitakutafutia makazi mengine 

lakini hapa ni sehemu salama” 

“Unaishi na nani hapa? “Ninaishi mwenyewe hapa ila 

nina wafanyakazi wawili ambao 

huja asubuhi na kufanya kazi kisha 

huondoka saa kumi na nusu jioni” 

“Huna mke? 

“Sina” 

“Vizuri.Sipendi sehemu yenye 

watu wengi .Nionyeshe chumba 

changu nikapumzike” akasema 

Camilla.Mmoja wa watumishi wa 

Mathew ambaye hushughulika na 

usafi akakokota mizigo ya Camilla 

hadi katika chumba cha wageni 

“Hiki ndicho chumba 

utakacholala .Kuna wahudumu 

wako hapa na chochote 

utakachokihitaji utawaeleza 

watakusaidia.Pumzika tutaonana 

baadae” akasema Mathew “Ahsante sana Mathew” 

akasema Camilla na kukaa 

kitandani Mathew akafungua 

mlango ili atoke Camilla akamuita. 

“Mathew naweza kupata 

kahawa tafadhali? 

“Bila wasi wasi unaweza pata.” 

Akasema Mathew na kutoka 

akamuelekeza mpishi wake 

kwamba amuandalie Camilla 

kahawa. 

“Taratibu ninaanza kumsoma 

Camilla.Nitamzoea tu na nitafanya 

naye kazi vizuri” akawaza Mathew 

baada ya kuingia chumbani kwake 

akajimwagia maji baridi na 

kujilaza kitandani.Akachukua 

simu na kumpigia Peniela 

akamjulisha kwamba Camilla amefika salama na kumshukuru 

kwa msaada ule mkubwa.Kwa 

mbali kengele za kanisani 

zikasikika zikilia na 

kuwakumbusha watu kwamba 

siku ile ni jumapili siku ya 

bwana.Mathew akajilaza kwani 

alihisi macho mazito sana hakuwa 

amelala usiku mzima. 

**************** 

Ni jumapili,siku ya 

mapumziko lakini kwa rais wa 

Jamhuri ya muungano wa Tanzania 

alikuwa anaendelea na majukumu 

yake ya kuwatumikia 

wananchi.Saa mbili na nusu za 

asubuhi tayari alikuwa katika kikao na viongozi wa juu wa jeshi 

la polisi .Katika kikao hicho 

alihudhuria waziri wa mambo ya 

ndani ya nchi,mkuu wa jeshi la 

polisi Tanzania na maafisa 

wengine wa ngazi za juu waliofika 

kwa wakati kufuatia wito wa rais 

aliyewataka wafike asubuhi na 

mapema 

Rais alipoingia katika chumba 

cha mkutano wote wakasimama 

wakatoa heshima na rais akaketi 

na ndipo wote wakaketi.Bila 

kupoteza wakati Dr.Vivian 

akafungua kikao 

“Habari za asubuhi 

waheshimiwa.Nawashukuru sana 

kwa kufika kwenu kwa 

wakati.Najua leo ni jumapili siku ya mapumziko lakini sisi tulio 

katika kazi hizi za kuwatumikia 

watu hatuna mapumziko.Muda 

wote tuko kazini.Nawashukuru 

kwa kuwa mnalifahamu hilo na 

mmefika wote” akasema rais na 

kuwatazama maafisa wale 

akaendelea 

“Kikao hiki hakitakuwa kirefu 

na nimewaiteni hapa niwaeleze 

jambo moja muhimu sana kwa 

usalama wa nchi yetu.Naamini 

tayari nyote mmekwisha pata 

taarifa ya mambo yaliyotokea 

usiku wa kuamkia leo.Kuna 

matukio mawili yametokea usiku 

wa kuamkia leo.Kwanza ni tukio la 

kuvamiwa watumishi wawili wa 

ofisi yangu akiwemo mdogowangu Theresa.Wakiwa katika barabara 

ya uwazi walivamiwa na kikosi cha 

askari.Nasema walivamiwa kwa 

sababu taratibu za kawaida za 

jeshi la polisi kumsimamisha mtu 

wanayemtilia shaka 

hazikufuatwa.Walichokifanya 

askari hao walipiga risasi tairi 

moja na gari likapoteza uelekeo 

lakini wakajitahidi kulidhibiti 

likasimama.Askari hao baada ya 

kuona gari limesimama wakaanza 

kulimiminia risasi kwa bahati 

nzuri gari hilo halipenyi 

risasi.Kama isingekuwa hivyo 

nadhani lengo lao lilikuwa ni 

kuwadhuru.Kuona hivyo ikawabidi 

wanipigie mimi kuniomba msaada 

na mimi nikawasiliana na IGP nikamuomba atume askari haraka 

sana.Kitu cha kushangaza ni 

kwamba askari wale wavamizi 

walipewa taarifa ya kikosi cha 

askari kilichokuwa kinakwenda 

eneo lile wakaingia katika magari 

yao na kuondoka haraka.Hii inatoa 

picha ya wazi kwamba askari wale 

ambao nawaita wavamizi 

walikuwa na lengo baya na wale 

wafanyakazi wangu na 

inawezekana walikuwa na watu 

wao ndani ya jeshi la polisi ambao 

waliwapa taarifa za kuhusiana na 

kikosi cha askari kilichokuwa 

kinakwenda pale.” Akanyamaza 

kidogo halafu akaendelea 

“Haikuishia hapo.Askari hao 

hao walikwenda kuvamia tena nyumbani kwa mkuu wa idara ya 

ujasusi mstaafu Meshack Jumbo na 

kufanya uharibifu mkubwa na 

halafu wakaichoma nyumba 

yake.Kwa bahati nzuri yeye na 

familia yake hawakupata madhara 

yoyote.Kufuatia matukio hayo 

mawili vijana wangu walifanya 

operesheni ya usiku mzima 

kuwabaini watu hawa ni akina 

nani na wakafanikiwa kuwapata 

ila katika mapambano askari hao 

wavamizi wapatao tisa walifariki 

dunia” Akanyamaza tena 

akawatazama maafisa wale halafu 

akaendelea 

“Ninazo hapa picha za askari 

hao waliopoteza maisha kufuatia 

mtego uliowekwa na vijana wangu jana usiku.Mheshimiwa waziri 

nitakukabidhi picha hizo na 

ninataka zifanyiwe kazi haraka 

sana kuwabaini hawa watu ni 

akina nani na ninataka mpaka saa 

saba mchana wa leo wawe 

wametambuliwa ni akina nani.Je ni 

askari wetu ndani ya jeshi la 

polisi? Kama ndiyo walitumwa na 

nani kufanya matukio yale 

ambayo naweza kuyaita ni ya 

kihalifu?Nataka niufahamu 

mtandao wao wote.Lakini kama 

siyo nataka nifahamu wametoa 

wapi sare na vifaa vya jeshi letu? 

Nataka silaha hizi zichunguzwe je 

ni za jeshi letu la polisi? Tatu watu 

hawa wanaonekana kuwa na 

mashirikiano na watu toka ndani ya jeshi la polisi nataka 

muwatafute watu hao na 

wapatikane.Mheshimiwa waziri 

fuatilia suala hili nataka mpaka 

saa saba mchana wa leo niwe 

nimepata majina ya watu hawa ni 

akina nani.” Akasema rais na 

kumkabidhi waziri wa mambo ya 

ndani ya nchi bahasha yenye picha 

za wale jamaa waliouliwa na akina 

Mathew .Kikao kikafungwa 

akaagana na maafisa wale 

wakaondoka 

Alipomaliza kikao na maafisa 

wale wa polisi akakutana na waziri 

wa mambo ya nje ofisini kwake 

wakawa na mazungumzo 

mafupi.Katika mazungumzo hayo 

waziri wa mambo ya nje alimjulisha rais kuhusu ujio wa 

waziri wa mambo ya nje wa 

Marekani. 

“Mbona imekuwa ghafla sana? 

Akauliza Dr.Vivian 

“Hata mimi nimemuuliza 

hivyo akadai ni safari ya dharura” 

“Amekueleza sababu ya ziara 

yake hiyo? 

“Mheshimiwa rais hajanieleza 

lakini amesema ni kwa ajili ya 

kuzungumzia masuala muhimu 

sana.Mheshimiwa rais serikali ya 

Marekani kwa sasa wanajitahidi 

kufanya kila njia ili kukushawishi 

uweze kuachana na mpango wako 

wa kuanzisha mashirikiano na 

Korea Kaskazini.Nadhani hilo ndilo kubwa linalomleta Tanzania 

kwa dharura” 

Dr.Vivian akafikiri kidogo na 

kusema 

“Marekani wanajisumbua 

sana.Msimamo wangu 

hautabadilika kamwe.Nimekwisha 

amua kusonga mbele na hakuna 

kurudi nyuma.Watapoteza muda 

wao bure” akasema Dr Vivian na 

kutoa maelekezo kadhaa kwa 

waziri yule wakaagana akarejea 

kwake kupumzika 

“Mike Straw bado hajaamini 

kama kweli nimedhamiria 

kuanzisha mashirikiano na Korea 

Kaskazini.Muda si mrefu sana 

atalishuhudia jambo hili likiwa 

kweli na atazidi kuchanganyikiwa.Nimechoshwa 

kwa nchi zetu kupangiwa mambo 

ya kufanya kwa vile tu ni 

masikini.Tanzania inahitaji 

maendeleo ya haraka na 

maendeleo hayo yatapatikana kwa 

kufanya maamuzi 

magumu.Naamini hiki 

nilichokifanya ni sahihi kwa nchi” 

akawaza Dr.Vivian akiwa sebuleni 

kwake anapumzika 

WASHINGTON DC – MAREKANI 

Ni saa nane za usiku kwa saa 

za Marekani,Willy Gadner mkuu 

wa shirika la ujasuri la Marekani 

CIA alipowasili ikulu ya Marekani kufuatia wito wa dharura wa rais 

Mike straw. 

“Ahsante sana Gadner kwa 

kufika kwa wakati.Nimelazimika 

kukuita ili tuzungumzie suala la 

muhimu sana ila lenye usiri 

mkubwa ndiyo maana sikutaka 

kuzungumza wakati uko na wale 

wenzako” akasema Mike straw na 

kunyamaza kidogo 

“Gadner tulipopewa dhamana 

hii ya kuwaongoza wamarekani 

tuliapa na kuwaahidi utumishi 

uliotukuka na zaidi sana 

tuliwahakikishia usalama 

wao.Wamarekani wana imani 

kubwa na serikali yao kwamba 

itawalinda na sisi kama serikali 

tuna imani kubwa sana na vyombo vyetu vya ulinzi na hasa shirika 

letu la ujasusi CIA.Dhamana 

uliyonayo Gadner ni kubwa sana 

hivyo wewe na watu wako 

hampaswi mlale usingizi ili 

wamarekani waweze kupata 

usingizi na wawe 

salama.Wamarekani hawapaswi 

kuishi kwa hofu hata 

kidogo.Ukiondoa vitisho vya ugaidi 

ambavyo tumekuwa tunapambana 

kuwadhibiti, kuna taifa moja 

ambalo limekuwa linawapa sana 

hofu wamarekani nalo ni Korea 

Kaskazini” akanyamza kwa muda 

kisha akaendelea 

“Hili ni taifa ambalo uchumi 

wake kwa hivi sasa unakua kwa 

kasi kubwa na wachumi wanatabiri kwamba kama uchumi 

wa Korea Kaskazini utaendelea 

kukua kwa kasi hii baada ya miaka 

mitano unaweza kuwa umefikia 

robo tatu ya uchumi wa China.Huu 

utakuwa ni uchumi mkubwa na 

taifa hili litazidi kuwa imara sana 

kiuchumi na kijeshi pia.Hofu yetu 

ni kwamba kadiri taifa hili 

linavyozidi kujiimarisha kiuchumi 

ndivyo linavyozidi kujiimarisha 

pia kijeshi.Wanawekeza sana 

katika teknolojia mpya za 

kutengeneza silaha na hasa 

makombora ya masafa marefu na 

hivi karibuni wamefanya 

majaribio ya kombora ambalo 

linatajwa kuwa linaweza kufika 

katika moja ya majiji makubwa ya Marekani.Haya ni mafanikio 

makubwa kwa Korea Kaskazini na 

hivyo kuzidisha hofu kwa 

wamarekani.Kama haitoshi 

wanataka pia kununua madini ya 

Urani kutoka Tanzania na na lengo 

kubwa ni kuongeza idadi ya silaha 

zao za nyuklia.Hatuwezi kuiacha 

Korea kaskazini ikaendelea na 

harakati zake na kuwatishia kwa 

Marekani.Lazima tufanye kila 

tunaloweza kulifanya kuhakikisha 

kwamba hawafanikiwi malengo 

yao.Tumejitahidi kwa upande wa 

vikwazo lakini mpaka leo 

inaonekanaa vikwazo hivyo havina 

nguvu yoyote na sasa kinachofuata 

ni sisi kutafuta sababu ya 

kuiadhibu vikali sana nchi hii na kufifisha juhudi zote za 

kutengeneza makombora na silaha 

kali za maangamizi.Umoja wa 

mataifa hauwezi kuidhinisha 

matumizi ya nguvu kwa Korea 

Kaskazini kwa kuogopa kuzuka 

kwa vita kubwa kwa hiyo sisi 

lazima tutafute njia zetu wenyewe 

za kutufanya tuingie vitani na 

Korea kaskazini.Kuna mpango 

nimeubuni ambao unaweza 

ukalifanikisha hilo” akasema Mike 

straw. 

“Kwa ajili ya manufaa 

makubwa kwa nchi,kuna nyakati 

inatulazimu kufanya jambo gumu 

ili watu wetu waendelee kuwa 

salama.Kwa kuwa Korea Kaskazini 

anaonekana kuwa hatari kwa usalama wetu hivyo basi 

tunalazimika kumchapa.Dunia 

mzima hivi sasa inafahamu kuhusu 

mashirikiano yanayotaka 

kuanzishwa kati ya Korea 

kaskazini na Tanzania na 

wanafahamu kwamba Marekani 

tunalipinga hili suala kwa nguvu 

zote.Kwa hiyo basi ninamtuma 

waziri wa mambo ya nje wa 

Marekani aende Tanzania kwa 

lengo la kutaka kumshawishi rais 

wa Tanzania asitishe mpango wa 

kushirikiana na Korea Kaskazini 

kibiashara.Nataka CIA mumuue 

waziri wetu wa mambo ya nje 

Helmet Brian akiwa katika ardhi 

ya Tanzania” akanyamaza baada ya kuuona mstuko mkubwa usoni 

kwa Willy Gadner 

“Tumuue waziri wetu wa 

mambo ya nje? Akauliza Willy 

“Ndiyo Gadner.Tunatakiwa 

kumuua Helmet Brian .Jambo hii 

linapaswa kufanywa kwa ufundi 

mkubwa ili ionekane ni Korea 

Kaskazini ndio waliomuua waziri 

wetu na baada ya hapo 

tutalazimika kuchukua hatua 

kufuatia mauaji hayo na tutapata 

sababu ya kuiadhibu Korea 

kijeshi.CIA mnao uwezo mkubwa 

wa kuifanya dunia nzima iamini 

kwamba Korea Kaskazini ndio 

waliomuua waziri wetu na nchi 

zote watasimama upande wetu na 

tutahakikisha tunaiharibu vibaya sana Pyongyang na kuyateketeza 

kabisa makombora yake 

yote.Hatutaweza kupata sababu 

nyingine ya kumpiga Korea 

Kaskazini zaidi ya 

hii.Ninakukabidhi jukumu hilo 

Gadner hakikisha unakaa na 

maafisa wako mlipange vizuri sana 

namna ya kulitekeleza ila 

kumbukeni sitaki kusikia 

kumetokeauzembe au makosa 

yoyote.Suala hili ni nyeti na 

muhimu mno kwa nchi yetu” 

Willy Gadner akavuta pumzi 

ndefu na kusema 

“Mheshimiwa rais 

nimekusikia na kukuelewa 

vizuri,pia sababu ulizotoa 

nimezielewa lakini naingiwa na hofu kwa maamuzi hayo ya 

kumuua waziri wetu wa mambo ya 

nje.Hauwezi kutafuta namna 

nyingine ya kutimiza lengo letu hili 

bila kumuua Helmet” 

“Zipo njia nyingine lakini 

nimechagua hii kwani ni muafaka 

kwa wakati huu.Dunia nzima 

watajua kwamba Korea Kaskazini 

ndio waliomuua waziri wetu.Hivyo 

italeta mzozo mkubwa na itakuwa 

ni sababu nzuri kwetu kuichapa 

Korea Kaskazini.Hiyo ndiyo njia 

pekee ninayoitaka kwa sasa na 

ninaomba ujipange vizuri na 

maofisa wako mlitekeleze suala 

hili.Narudia tena suala hili ni la siri 

na la muhimu sana hivyo sitaki 

kusikia kuna makosa au uzembe wowote umefanyika.Tumieni 

mbinu na maarifa yote kufanikisha 

jambo hii” akasema Mike straw na 

kuendelea na mjadala kuhusiana 

na suala lile 



DAR ES SALAAM – TANZANIA 

Mlio wa simu ulimuondoa 

Mathew usingizini akatazama 

mpigaji na jina lilionekana ni 

Somji.Akapokea haraka 

“Hallow Somji” 

“Mathew gari lako lililetwa 

hapa gereji na Hamis Chuma tayari 

tumebadili matairi na kuweka tairi 

zile uzipendazo.Unaweza kuja 

muda wowote kulichukua.” 

“Ahsante sana Somji.Nitumie 

gharama nikutumie sasa hivi” 

akasema Mathew na Somji 

akamtumia gharama za jumla 

akamlipa kwa kumtumia simu. 

“Kama si simu hii toka kwa 

Somji ningeendelea kulala.Nahisi usingizi sana” akawaza Mathew na 

kuingia bafuni kujimwagia maji 

baridi halafu akaelekea jikoni na 

kujimiminia Whiski katika glasi 

akagugumia yote 

“Hapa sasa najisikia vizuri.Ni 

wakati wa kumuamsha Camilla ili 

kazi iendelee” akawaza na kwenda 

chumbani kwa Camilla akagonga 

mlango mara tatu bila 

majibu.Akagonga tena 

hakujibiwa.Akaingiwa na wasi 

wasi akakinyonga kitasa mlango 

haukuwa 

umefungwa,akachungulia ndani 

chumba kilikuwa kitupu.Camilla 

hakuwepo.Mathew akahisi mapigo 

ya moyo wake 

yanabadilika.Haraka akaenda kumuuliza mmoja wa watumishi 

wake alipo Camilla,akamueleza 

kwamba amekwenda kukaa katika 

bwawa la kuogelea.Mathew 

akashusha pumzi akatoka haraka 

akaelekea katika bwawa la 

kuogelea akamuona Camilla akiwa 

amekaa ametulia akisoma kitabu 

huku akiwa amevaa spika za 

masikioni akisikiliza 

muziki.Alikuwa amevaa fulana 

ndogo nyeupe iliyofunika kifua 

chake na kuliacha wazi tumbo 

lake.Alivaa pia kaptura fupi 

nyeupe na sehemu kubwa ya 

mapaja yake ilikuwa 

wazi.Alionekana kuifurahia sana 

mandhari ile ya kupendeza pale 

nyumbani .Mathew akaenda kukaa katika kiti cha pembeni.Camilla 

akavua spika za masikioni 

“Nimegonga chumbani kwako 

nikastuka baada ya kukuta 

chumba kitupu” akasema Mathew 

“Sikuwa na usingizi nikaamua 

kuja kupumzika hapa.Ninapenda 

sana maji na hupenda kupumzika 

kandoni mwa bahari hata nyumba 

yangu iko karibu na bahari.” 

Akasema Camilla na 

alipotabasamu vishimo vikatokea 

mashavuni pake.Mathew akaishika 

chupa ya mvinyo aliokuwa 

anakunywa Camilla 

“Mvinyo huu unatengenezwa 

na zabibu ya 

Tanzania,umeupenda? “Nilimtuma yule mtumishi 

wako Za..Zan..” 

“Zamda.Anaitwa Zamda” 

akasema Mathew 

“Ndiyo Zamda.Nilimtuma 

akaninunulie mvinyo wa Tanzania 

akaniletea huu.Nimeupenda ni 

mzuri sana.Sijawahi kutumia 

bidhaa za kutoka Tanzania 

nimeshangaa kwa mvinyo huu safi 

ambao unaweza hata kuuzwa 

katika masoko ya 

kimataifa”akasema Camilla 

“Tunazalisha bidhaa nyingi 

nzuri ila changamoto inakuwa ni 

ushindani mkubwa uliopo katika 

soko la kimataifa.Ni mara yako ya 

kwanza kufika Tanzania?“Ni mara yangu ya 

kwanza.Baba aliponiambia 

kwamba ninakuja Tanzania 

nilistuka sana kwani ni nchi 

ambayo haikuwemo katika akili 

yangu kuitembelea.Nimewahi 

kuisikia hapo kabla lakini hivi 

majuzi Tanzania imekuwa 

inatajwa sana duniani kote 

kutokana na mambo yaliyotokea 

ambayo naamini 

unayafahamu.Sijawahi kufika bara 

la Afrika ila kuna nchi ninasizikia 

kama vile Afrika 

kusini,Nigeria,Somalia na 

Ethiopia.Ilinilazimu kutenga muda 

kuisoma Tanzania ili niweze 

kuifahamu vyema.Hata hivyo 

nimesoma mambo mazuri sana kuhusu Tanzania.Ni nchi 

iliyojaliwa utajiri mkubwa wa 

madini ,ardhi nzuri,mbuga za 

wanyama ,mlima mrefu sana 

Kilimanjaro na zaidi sana watu 

wenye upendo mkubwa.Ni nchi 

nzuri kuishi ningependa 

kuzunguka nchi yote na 

kuushuhudia uzuri huu mkubwa 

iliyojaliwa nchi hii.Kwa ufupi 

nimeipenda sana” akasema 

Camilla na kutabasamu 

“Unaonekana unapenda sana 

utalii” akasema Mathew 

“Ni kweli ninapenda sana 

utalii.Kila nipatapo nafasi huwa 

ninakwenda sehemu mbali mbali 

kutalii na kupumzika.Napenda 

kujifunza mambo mapya,kujua mila na tamaduni za watu mbali 

mbali duniani.” Akasema Camilla 

na kunywa mvinyo 

“Nisaidie kuhusu bonde la 

Ngorongoro .Natamani nipate 

picha namna kulivyo kabla 

sijatembelea huko” akasema 

Camilla.Mathew akatabasamu 

“Sijawahi kufika bonde la 

Ngorongoro kwa hiyo siwezi 

kuelezea uzuri uliopo huko” 

Camilla akatoa miwani na 

kumtazama Mathew kwa 

mshangao mkubwa 

“Hujawahi kutembelea bonde 

la ngorongoro?kwa nini? 

“Sijawahi kwenda huko 

japokuwa natamani siku moja 

niende” “Umenishangaza sana.Kwa 

nini msipende vya kwenu kwanza 

kabla ya wageni kutoka nje ?Ninyi 

kama watanzania mlipaswa kuwa 

mstari wa mbele kutembelea 

vivutio vilivyomo nchini kwenu na 

kuipatia serikali 

mapato.Nimesoma takwimu,idadi 

ya watu ni zaidi ya milioni hamsini 

na endapo nusu yao wangekuwa 

wanatembelea hifadhi za taifa kila 

mwaka serikali yenu ingepata 

mapato mengi sana.Jifunzeni 

kupenda vya kwenu na ndiyo 

maana nilimtuma Zamda 

akanitafutie mvinyo 

uliotengenezwa 

Tanzania.Nitakuwa mtu wa ajabu 

nikija hapa na kutumia bidhaa za Marekani.Inaonyesha somo la 

uzalendo bado linahitajika sana 

hapa Tanzania.Mimi ni mmarekani 

na ninaitanguliza Marekani kwa 

kila ninachokifanya.Tunaipenda 

nchi yetu na tunaipigania.Ninyi 

vile vile mnapaswa kuwa 

hivyo.Mnapaswa kuweka nchi 

yenu mbele msisubiri watu wa nje 

waje kuwajengea nchi.Tanzania 

itajengwa na watanzania 

wenyewe” akasema Camilla 

“Dah ! Unafaa sana kuwa 

mwanasiasa.” Akasema Mathew na 

kwa mara ya kwanza akakisikia 

kicheko cha Camilla 

“Tunapokutana vijana kama 

hivi tunabadilishana mawazo na 

kupanuana akili.Tunajifunza mambo mapya.Kuhusu siasa 

sipendi sana kuwa 

mwanasiasa.Baba yangu alipenda 

sana siku moja niwe mwanasiasa 

kwani aliona chembe chembe za 

siaza ndani mwangu lakini badala 

yake nimeshia kuwa FBI kazi 

ninayoipenda sana.Nilipenda kazi 

hii toka nikiwa mdogo na hadi sasa 

ndiyo kazi pekee ninayoipenda 

.Napenda sana kufanya 

uchunguzi,kufichua uovu 

japokuwa watu wanasema 

kwamba sifanani na hii kazi” 

akasema Camilla na wote 

wakacheka 

“Nilipokuona wakati tunatoka 

uwanja wa ndege nilipata wasiwasi 

namna ya kuweza kuwa karibu nawe ulionekana ni mtu 

usiyependa maongezi lakini 

kumbe uko tofauti na vile 

nilivyofikiria” akasema Mathew na 

Camilla akatabasamu 

“Ninaitwa kinyonga kwa jina 

la utani kwa sababu ninabadilika 

marakwa mara.Naweza kuwa mtu 

nisiyependa maongezi,naweza 

kuwa mtu wa watu,na nikawa 

mkatili zaidi ya Hitler.Unatakiwa 

unizoee.halafu …” Camilla akasita 

“Niliambiwa kwamba 

nitapokewa na mtu anaitwa 

Meshack Jumbo lakini nikapokewa 

na mtu anaitwa Mathew .Je jina 

lako lingine ni Meshack Jumbo? 

“Hapana mimi si Meshack 

Jumbo.Huyo ni mstaafu aliwahi kuiongoza idara ya ujasusi ya taifa 

.Baba yako Jimmy Snow na 

Meshack Jumbo ni marafiki 

wakubwa sana.Mimi niliwahi 

kufanya kazi katika idara ya 

ujasusi lakini kwa sasa 

nimekwisha achana na shughuli 

hizo,ninafanya shughuli zangu za 

biashara.Niliombwa na rais 

nimfanyie kazi yake sikuweza 

kukataa na nilipokwama 

nikamshirikisha Mzee Jumbo naye 

akaomba msaada kwa Jimmy Snow 

na hapo ndipo ulipotokea na 

yakatokea haya yote 

yaliokupata.Kwa namna ya pekee 

naomba nikushukuru sana kwa 

msaada mkubwa uliotusaidia 

ambao hatuwezi kuulipa.Vile vile pole sana kwa matatizo yote 

yaliyokupata wakati ukiwa katika 

harakati za kutusaidia kuupata 

ukweli wa jambo tunalolichunguza 

.Pamoja na yote yaliyokupata 

nakuahidi kwamba utaishi 

Tanzania kwa raha na 

amani.Meshack Jumbo 

nitakupeleka kwake atafurahi 

sana kukuona vile vie kesho 

nitakutambulisha kwa rais pia” 

akasema Mathew 

“Niliposoma kwamba 

watanzania ni watu wakarimu 

sana nilidhani labda ni maneno ya 

kutuga lakini pale nilipoambiwa 

kwamba kuna ndege maalum 

inakuja kunichukua kunileta 

Tanzania niliyaamii maneno hayo.Sikutegemea kabisa kama 

ndege ile kubwa ingekuja Havana 

kwa ajili ya kunichukua mimi 

pekee.Ahsanteni sana nyote kwa 

msaada huu mkubwa” akasema 

Camilla 

“Camilla wewe ni mtu muhimu 

sana kwetu hivyo kila juhudi ilibidi 

ifanyike kuhakikisha unafika 

salama Tanzania” 

Camilla akanywa mvinyo na 

kusema 

“Baada ya mambo kuharibika 

kule Marekani nilitaka kwenda 

Urusi kujificha huko aliko baba 

lakini akaniomba kwamba nije 

Tanzania kusaidia katika 

uchunguzi.Nilikubali kwa kuwa 

aliniomba sana hivyo nimekuja.Nataka nifahamu ni 

uchunguzi gani ambao nimekuja 

kusaidia? Akauliza Camilla 

Mathew akamueleza Camilla 

kila kitu kuhusiana na suala lile la 

kuanguka kwa ndege ya 

rais,mauaji ya kanali Sebastian na 

kupotea kwa begi la siri lililopewa 

jina la football.Camila alisikiliza 

kwa makini sana halafu akanywa 

mvinyo wake na kusema 

“Ushiriki wa Fakrim Alnasor 

ambaye ni CIA katika suala hili 

unaweka picha ya wazi kwamba 

alitumwa kufanya kazi hiyo na 

shirika lake la CIA kwa hiyo 

serikali ya Marekani inahusika 

katika sakata hili.Hii ni aibu kwa 

Marekani kwa kitendo kibaya kama hiki.Nakuahidi Mathew 

kukusaidia katika jambo hili hadi 

tuufahamu ukweli” akatulia kidogo 

kisha akasema 

“Ninaamini kabisa kwamba 

Fakrim aliuawa na CIA na 

inaonyesha kwamba walifahamu 

kwamba tayari amekwisha 

gundulika kuwa anahusika katika 

sakata lile na anafuatiliwa.Ili 

kuendelea kuificha siri yao 

ikawalazimu wamuue.Hii ni mbinu 

inayotumiwa sana na CIA endapo 

watagundua kwamba kuna mmoja 

wa watu wao amekuwa hatari 

kwao.Kwa hiyo basi taarifa za 

Fakrim kujulikana na kufuatiliwa 

zilitoka hapa Tanzania.Tunapaswa 

kuchunguza na kufahamu ni nani aliyetuma taarifa hizo.CIA lazima 

wana watu wao hapa Tanzania .Pili 

baada ya kupekua simu ya Fakrim 

tuligundua kwamba mtu wa 

mwisho kuwasiliana naye alikuwa 

ni Nathan ambaye niliambiwa ni 

mpenzi wa rais wa Tanzania” 

“Ndiyo Nathan na Dr.Vivian ni 

wapenzi.Ahsante kwa taarifa yako 

hii imetusaidia sana.Tumefanikiwa 

kugundua kwamba Nathan 

alipandikizwa kumchunguza rais 

ila bado hatujafamu nini hasa 

wanachokitafuta .Tumegundua 

kwamba Nathan ana mahusiano na 

kikundi fulani cha watu hapa 

Tanzania,bado tunaendelea 

kuwafuatilia na pengine baadae leo tunaweza kupata jibu watu hao 

ni akina nani”akasema Mathew 

“Kama ni hivyo Nathan ni mtu 

muhimu sana.Kwa kuwa ni mtu wa 

karibu na rais,inapaswa kufanywa 

mipango ili aweze kuja Tanzania 

mara moja ili tuanze 

kumchunguza” akasema Camilla 

“Nathan amekwisha fariki” 

akasema Mathew na kumstua 

Camilla 

“Nathan naye kafariki lini? 

Umepata wapi taarifa hizo? 

Akauliza Camilla 

“Nathan kafariki jana 

usiku.Amefia hapa Tanzania 

“Amekufaje?Nini kimemuua? 

Mathew akamueleza kila kitu 

kilichotokea kuhusiana na Nathan.Camilla akabaki na 

mshangao. 

“Mpaka hapa ulipofika tayari 

umepiga hatua kubwa 

sana.Mwanga tayari umepatikana 

.Nathan ni njia nzuri ya kuelekea 

kuupata ukweli.Kilichotokea usiku 

wa jana kinaonyesha dhahiri kuna 

mtandao hapa Tanzania ambao 

unatumiwa na CIA.Ili kuufahamu 

vizuri tuchunguze vifaa vile vya 

mawasiliano ulivyotoa kwa Nathan 

tufahamu kama kuna mtu yeyote 

hapa Tanzania aliyekuwa 

anawasiliana naye” akasema 

Camilla wakaelekea ndani.Mathew 

akaleta zile simu alizotoa kwa 

Nathan na kumpa Camilla “Hii ni simu maalum ambayo 

hutumiwa na watuw a CIA kwa 

shughuli za kiofisi pekee.Nina 

rafiki zangu wako CIA na wana 

simu kama hizi.Tunaweza 

kufahamu mambo mengi kupitia 

simu hi.Hii simu nyingine ni simu 

yake ya matumizi ya kawaida .Hii 

nyingine ya tatu ni simu 

inayotumia mtandao wa intaneti 

na hutumiwa mahala kusiko na 

mtandao wa simu” akasema 

Camilla na kuifungua kompyuta ya 

Nathan 

“Hii kompyuta ina namba za 

siri ambazo ukifanikiwa kuzipata 

basi unaingia moja kwa moja 

katika mtandao wa CIA lakini 

endapo ajenti akigundulika kupotea basi namba za siri 

hubadilishwa haraka haraka sana 

kuhofia labda ametekwa 

nyara.Tuiweke kwanza pembeni 

na tuyachunguze kwanza 

mawasiliano yake ya simu.” 

Akasema Camila akaenda 

kuchukua moja wapo ya sanduku 

lake kubwa akaja nalo sebuleni 

akalifungua na kutoa kompyuta na 

vifaa vingine vingi akaanza 

kuviunganisha na alipomaliza 

akaichukua ile simu ya Nathan 

akaiunganisha na kompyuta yake 

akaiwasha. 

“Camilla,hawawezi 

wakagundua kwamba uko 

Tanzania baada ya kuiwasha simu 

ya Nathan? Akauliza Mathew “Hawawezi kugundua 

chochote kwani tayari nimekwisha 

iingiza katika programu maalum 

.Usihofu Mathew ninao utaalamu 

mkubwa sana katika haya mambo” 

akasema Camilla na sura yake 

ilionyesha muda huo alikuwa 

kazini.Alibonyeza bonyeza 

kompyuta yake kwa muda halafu 

akasubiri kidogo na mafaili mengi 

yakaanza kufunguka .Baada ya 

dakika tano likatokea faili 

lililokuwa na kumbu kumbu za 

mawasiliano ya Nathan 

“Haya ndiyo mawasiliano yote 

ya Nathan katika simu hii toka 

alipoanza kuitumia.Ni orodha 

ndefu sana lakini tuangalie 

mawasilino ya hivi karibuni hasa kwa mwezi huu” akasema Camilla 

na kuanza kubonyeza tena lakini 

mara akaguna 

“Mathew kuna tatizo.Mfumo 

wao wa mawasiliano ni kwa 

kutumia namba maalum.Kila ajenti 

wa CIA ana namba yake na hakuna 

jina la mtu wala namba yake ya 

simu inayoonekana bali 

kinachoonekana ni namba ya 

ajenti.Ni vigumu kutambua nani 

yuko wapi” 

“Hakuna namna yoyote ya 

kuweza kuzitambua namba hizo ili 

tuwafahamu watu wake walioko 

Tanzania? Au kama kuna ugumu 

tuichunguze hii simu yake 

anayotumia kwa mawasiliano ya 

kawaida “Hatuwezi pata chochote cha 

kutusaidia katika simu hiyo kwani 

mambo yote ya muhimu yako 

katika simu hii anayotumiwa kwa 

shughuli za kiofisi” akasema 

Camilla na kutafakari kwa muda 

halafu akasema 

“Itanilazimu kuomba msaada 

Marekani ili tuweze kupata 

tunachokihitaji.Kuna rafiki yangu 

anafanya kazi CIA nitamuomba 

anisaidie kuzitambua namba hizi” 

“Camilla hilo ni jambo la 

hatari sana.Unatafutwa na CIA 

halafu unataka kuwasiliana nao? 

Ni vipi kama wakifahamu kuwa 

upo Tanzania?Sikushauri ufanye 

hivyo Camilla.Tutafute namna 

nyingine ya kufanya” “Hakuna namna nyingine ya 

kufanya Mathew zaidi ya kuomba 

msaada.Mtu ninayetaka 

kumuomba msaada ninamuamini 

niliwahi kuwa katika mahusiano 

naye ya kimapenzi na amekuwa 

ananisaidia mara kwa 

mara.Usiogope hatari Mathew 

kwani maisha yetu yamezungukwa 

na hatari kila kona.Naomba simu 

yako” akasema Camilla na Mathew 

akampa simu yake.Akaandika 

namba na kupiga simu ikaita 

“Hallow” ikasema sauti ya 

upande wa pili 

“Jack,tafadhali naomba 

usistuke wala usitamke jina langu 

kama uko na watu karibu.Ni 

mim….” “Catherine nimekuelewa 

nitakujulisha baadae” akasema 

yule jamaa wa upande wa pili na 

kukata simu. 

“Amekata simu ! akasema 

Camilla 

“Lazima atakuwa karibu na 

watu ila atapiga tena”akasema 

Camilla 

“Camilla una hakika 

hakutakuwa na tatizo lolote kwa 

kuwasil……………………..” Mathew 

hakumaliza sentensi yake simu 

ikaita 

“Amepiga” akasema Camilla 

na kuipokea 

“Hallo Jack” 

“Camilla mambo gani hayo 

unafanya? Kwa nini unanipigia wakati unafahamu kabisa kwamba 

unatafutwa?Huogopi? Kuna msako 

mkali sana unaendelea hivi sasa 

kukutafuta” 

“Usihofu Jack.Nafahamu kama 

ninatafutwa lakini hawatoweza 

kunipata kama hutawaambia 

nilipo” akasema Camilla na ukimya 

ukapita 

“Nafahamu huwezi kufanya 

hivyo Jack na ndiyo maana 

nimekupigia.Nahitaji msaada 

wako” 

“Unahitaji nini Camilla? 

“Ninakutumia namba ya simu 

ya mmoja wa watu wenu,nataka 

uingie katika kumbu kumbu zenu 

uangalie kwa mwezi huu 

amewasiliana na mtu yeyote wa Tanzania ? Kama yupo naomba 

nipate namba zake za simu” 

“Camilla hilo 

haliwezekani.Nitajiingiza kwenye 

matatizo makubwa .Hicho 

unachotaka nikifanye ni kitu cha 

hatari sana halafu sina uwezo wa 

kuingia mahala zinakohifadhiwa 

kumbukumbu hizo.Watu wa daraja 

la juu zaidi yangu ndio wenye 

kuruhusiwa kuingia katika 

kompyuta za kuhifadhi 

kumbukumbu hizo.Samahani 

sintaweza kukusaidia 

Camilla.Naomba huko ulikochukua 

tahadhari sana kwani unatafutwa 

mno.Mimi sintamueleza mtu 

yeyote,itabaki siri yangu kwamba 

uko Tanzania ila nakuomba usinipigie simu tena utaniweka 

katika matatizo makubwa” 

“Jack tafadhali usikate simu” 

akasema Camilla 

“Nafahamu kitu 

ninachokuomba unisaidie ni 

kigumu sana na cha hatari lakini 

tafuta namna ya kufanya uweze 

kunisaidia .Ni muhimu mno 

kwangu.Ukishindwa wewe 

kunisaidia hakuna mwingine 

atakayenisaidia.Nakuomba sana 

Jack unisaidie.Siku zote umekuwa 

unaniomba turudiane ukidai 

kwamba unanipenda kuliko kitu 

chochote ,huu ni wakati wa 

kuthibitisha maneno yako.Kama 

kweli unanipenda,unanijali na 

kunithamini hutaogopa kuingia katika hatari kwa ajili yangu,kama 

ambavyo mimi sikuogopa kuingia 

katika hatari wakati ule kwa ajili 

yako” akasema Camila.Jack 

akafikiri kwa muda na kusema 

“Naomba unipe kama dakika 

kumi halafu nitakupigia” 

“Ahsante Jack” akasema 

Camilla na kukata simu 




Jack ameniomba nimpe muda 

alifanyie kazi hilo suala na 

atanipigia simu baada ya dakika 

kumi.Si suala rahisi na ni kitu cha 

hatari sana lakini sina mtu 

mwingine anayeweza 

kunisaidia.Tunahitaji taarifa na 

mtu pekee anayeweza kutusaidia 

kwa sasa ni Jack ambaye yuko 

katika ofisi za CIA. Hawezi kukataa kunisaidia kwa sababu kwanza 

ananipenda sana,pili hata mimi 

nimewahi kumsaidia sana wakati 

fulani na niliyaweka maisha yangu 

hatarini kwa ajili yake.Tatu 

ninayafahamu mambo yake mengi 

kwa hiyo hawezi kukataa 

kunisaidia wakati nina 

shida.Usihofu Mathew tutapata 

jibu ndani ya muda mfupi ujao” 

akasema Camilla.Aliendelea 

kubonyeza kompyuta yake na 

mafaili mbali mbali yakaendelea 

kufunguka 

“Camilla amenikumbusha 

niliwahi kuwa na rafiki yangu 

anaitwa Anitha alikuwa ni 

mtaalamu sana wa kompyuta na 

alinisaidia mno katika shughuli zangu nyingi.Katu siwezi 

kumsahau Anitha” akawaza 

Mathew 

Zilipita dakika ishirini,simu ya 

Mathew ikapigwa alikuwa ni 

Jack,Camilla akapokea 

“hallow Jack” 

“Nisikilize Camilla.Nimefanya 

jambo ambalo sikuwa 

nimetegemea kulifanya na tayari 

nimeingia katika matatizo 

makubwa.Hapa niongeapo tayari 

ninafuatwa kwa hiyo nitakueleza 

haraka haraka nilichokipata.Kuna 

Seli mbili ambazo Nathan alikuwa 

na mawasiliano nazo 

nchiniTanzania ambazo ni 214A na 

110C.Nimefanikiwa kupata namba 

za simu za 214A naomba uchukue kalamu na karatasi nikutajie.” 

Akasema Jack na haraka haraka 

Camilla akachukua kalamu na 

karatasi akaandika namba 

alizotajiwa na Jack. 

“Hiyo seli nyingine hujapata 

namba zake? Camilla akauliza 

“Hapana sikufanikiwa kupata 

namba zake.Wakati nakaribia 

kuzipata nilikutwa katika chumba 

hicho na kulazimika kuua mtu ili 

niweze kutoka salama na kukupa 

taarifa hizi hivyo sikufanikiwa 

kuzipata namba za seli 

110C.Camilla nimeifanya kazi yako 

na nimekuthibitishia kwamba nina 

kupenda na niko tayari kufanya 

chochote kwa ajili yako.Ninataka 

ufahamu jambo moja ,hapa nilipo ninafuatwa na muda wowote 

wanaweza wakanikamata,sitaki 

wanikamate wanitese ili niwaeleze 

kwa nini nimefanya vile 

nilivyofanya kwani lazima 

niwaeleze mahala 

ulipo.Nimalizapo kuzungumza 

nawe hapa ninaichoma moto hii 

laini ya siku halafu na mimi …” 

akasita kidogo kisha akasema 

“Nitajiua” 

“Jack !!..akaita Camilla kwa 

sauti kubwa ya mstuko 

“Nakupenda sana 

Camilla.Nakupenda sana na 

ninayafanya haya yote kwa sababu 

ya upendo wangu mkubwa 

kwako.Jitahidi sana kujiweka 

salama kwani unatafutwa mno.Kwa heri Camilla” akasema 

Jack na kukata simu.Camilla 

akajaribu kupiga lakini 

haikupatikana tena.Sura yake 

ilibadilika na kuonyesha woga 

mkubwa 

“Kuna nini Camilla? 

“Ile kazi niliyomuomba Jack 

anisaidie imemletea matatizo, 

amegundulika na anasakwa.Ili 

kuepuka kuteswa na kutoa siri 

kwamba ni mimi niliyemtuma 

aifanye kazi ile hivyo ameamua 

kujiua.” Akasema Camilla na 

macho yake yakalengwa machozi 

“Jikaze Camilla.Jack ni shujaa 

na ana upendo wa dhati kwani na 

ndiyo maana ameamua hata 

kuyatoa maisha yake kwa ajili ya kukulinda wewe” akasema Mathew 

na Camilla akafuta machozi 

“Tuendelee” akasema 

‘Jack ameniambia kwamba 

katika seli hizi zote,ni seli mbili tu 

ambazo Nathan amekuwa 

akiwasiliana nazo nchini 

Tanzania.Amezitaja seli hizo ni 

214A na 110C.Amefanikiwa kupata 

namba za simu za seli 214A 

ambazo ni hizi hapa” akasema 

Camilla na kumpa Mathew ile 

karatasi aliyoandika namba zile za 

simu. 

“Hakufanikiwa kupata namba 

za seli nyingine” Camilla 

akashindwa kuyazuia machozi 

kumtoka “Pole sana 

Camilla.Tumuombee Jack ili 

Mungu aweze kumsamehe makosa 

yake na kumuweka mahala pazuri 

ikiwezekana abadilishe nia yake ya 

kutaka kujiua” akasema Mathew 

“Alikuwa ni mtu mwema na 

alinipenda sana.Mathew naomba 

dakika chache nitarejea” akasema 

Camilla na kuondoka akaelekea 

chumbani kwake machozi mengi 

yakimtoka 

“Camilla ameumizwa sana 

lakini haya ndiyo mambo ya 

kuumiza tunayokutana nayo 

wakati tunafanya hizi 

kazi.Nakumbuka hata mimi 

niliwahi kuumia sana 

nilipowapoteza watu wangu wawili wa karibu sana Noah na 

Anitha.Siwezi kuwasahau wale 

marafiki zangu.Niliumia sana 

wakati ule kwa hiyo ninaufahamu 

uchugu alionao Camilla wa 

kumpoteza Jack” akawaza Mathew 

na kuishika ile karatasi yenye zile 

namba za simu ambazo Camilla 

alipewa na Jack akazitazama 

“Jack anasema hizi ni namba 

za simu za Tanzania lakini mbona 

haziko kama namba za simu 

tulizozizoea?Huu ni mtandao gani 

wa simu?akajiuliza baada ya 

namba zile kuonekana ziko tofauti 

na zile za mitandao mbalimbali ya 

simu iliyoipo Tanzania 

“Sipaswi kuumiza kichwa 

wakati msaada ninao” akawaza Mathew na kuchukua simu yake 

akazitafuta namba za rais 

akampigia 

“Mathew habari za muda huu? 

“Nzuri kabisa mheshimiwa 

rais.Samahani kwa usumbufu” 

“Hakuna usumbufu wowote 

Mathew.Nilikuomba mwenyewe 

kwamba unipigie muda wowote 

utakaohitaji kuzungumza nami 

jambo lolote.” 

“Ahsante mheshimiwa 

rais,nimekupigia kuna msaada 

mdogo ninahitaji lakini kabla ya 

kuomba msaada napenda kwanza 

nishukuru kwa msaada wako yule 

mtu wangu niliyekuomba 

amewasili nchini salama.Ahsante 

sana kwa hilo” akasema Mathew “Usijali Mathew ni furaha 

yangu kama amefika salama.Kama 

kuna kingine chochote unahitaji 

usisite kunijulisha.Nimekwisha 

kuahidi kitu chochote kilicho 

ndani ya uwezo wangu 

nitakusaidia” 

“Nashukuru mheshimiwa 

rais.Nina suala dogo nahitaji 

msaada wako.Kuna namba fulani 

za simu lakini zinaonekana ni 

namba maalum haziko kama 

namba za simu 

tulizozizoea.Nahitaji kufahamu 

namba hizi ni za nani” akasema 

Mathew 

“Namba hizo za simu 

zinahusiana chochote na 

uchunguzi wako? “Ndiyo mheshimiwa rais 

nikimfahamu huyo mtu mwenye 

hizi namba nitashukuru sana” 

akasema Mathew na kumtajia rais 

zile namba 

“Sawa Mathew nitakupa jibu 

muda si mrefu baada ya kupewa 

jibu namba hizi ni za nani” 

akasema Dr.Vivian na kuagana na 

Mathew akakata simu. 

“Camilla amenisaidia sana 

kwani nisingeweza kupata mtu 

ndani ya CIA wa kuweza kunisaidia 

kuzifahamu namba hizi.Suala hili 

sasa limeanza kuwa na 

mwangaza.Nikifanikiwa kumpata 

huyu mmoja basi nitafanikiwa 

kumpata yule mwingine ambaye 

Jack ameshindwa kumpata.Kama Nathan amekuwa na mawasiliano 

nao basi watakuwa na mahusiano 

na CIA na yawezekana wakawa 

ndio viongozi wa mtandao 

uliotengenezwa na CIA.Swali 

ninalojiuliza ni kwa nini Marekani 

wafanye jambo hili?Wamemuua 

rais Anorld Mubara,wakamuua 

kanali Sebastian lakini bado 

hawajakata tamaa wanaendelea na 

harakati zao na sasa 

wanamchunguza rais 

Dr.Vivian.Wanatafuta kitu gani? 

Wanataka kumuua naye? Hapana 

sina hakika kama wanataka 

kumuua bali kuna kitu 

wanakitafuta hapa Tanzania 

ambacho lazima 

nikifahamu.Wamewekeza sana katika jambo hilo wanalolitafuta 

na lazima ni jambo lenye maslahi 

makubwa kwao” akaendelea 

kuwaza Mathew halafu akatoka 

pale sebuleni akaenda chumbani 

kwa Camilla akagonga 

mlango.Camilla akamruhusu 

mgongaji aingie ndani 

“Mathew samahani kwa hili 

lililotokea nimeshindwa 

kujizuia.Jack ni mtu wangu wa 

karibu sana na ndiyo maana 

kitendo hiki kilichotokea 

kimeniumiza mno.Mimi na Jack 

tumewahi kuwa na nyakati za 

furaha sana.Tulikuwa 

tunapendana mno hata baada ya 

kutengana lakini bado tuliendelea 

kuonyeshana upendo.Sikutegemea kama mwisho wa Jack utakuwa 

namna hii” akasema Camilla 

“Pole sana Camilla.Nafahamu 

uchungu ulio nao.Hata mimi 

nimewahi kuwapoteza watu wangu 

wawili wa karibu sana ambao ni 

zaidi ya ndugu zangu.Walifariki 

katika mazingira ya kikazi kama 

haya yaliyomkuta Jack.Haya ndiyo 

madhira tunayokutana nayo katika 

kazi hizi.Jipe muda wa kutosha wa 

kupumzika.Tutaendelea na kazi 

zetu baadae” 

“Mathew hata kama nikilala 

hapa kitandani kwa mwezi mzima 

siwezi kubadili kilichotokea.Kama 

Jack amekufa sintaweza 

kumrudisha.Twende tukaendelee 

na kazi.Tayari nimekwisha poteza kazi yangu na nimeikimbia nchi 

yangu kwa sababu ya hii kazi na 

zaidi ya yote nimempoteza mtu 

muhimu sana katika maisha 

yangu.Tunachotakiwa kufanya ni 

kuhakikisha haya yote hayaendi 

bure bali yanakuwa na matunda” 

akasema Camilla 

“Nimemtumia rais zile namba 

za simu tulizozipata toka kwa Jack 

ili atusaidie tuweze kufahamu 

namba zile ni za nani.Yeye ana 

mkono mrefu kwa hiyo ni rahisi 

sana kufahamu kuliko tukianza 

kulichunguza suala hilo 

sisi.Analifanyia kazi jambo hilo na 

baada ya kupata nani mwenye hizo 

namba ataujulisha” akasema Mathew na ukapita ukimya huku 

Camilla akiwa amejiinamia 

“Camilla ndani tunaweza 

kuutumia muda huu kufahamiana 

zaidi kama hutajali”akasema 

Mathew na Camilla akainuka. 

“Naomba tukaketi katika 

bwawa la kuogelea.Nikikaa karibu 

na maji mara nyingi huwa 

inanisaidia sana kupunguza 

mawazo niliyo nayo” akasema 

Camilla wakatoka wakaenda 

katika bwawa la kuogelea. 

“Historia yangu si nzuri sana 

na mara nyingi huwa sipendi 

kuongelea kuhusu maisha yangu 

binafsi kwani huamsha donge 

kubwa lililonikaba kooni lakini 

nadhani huu ni muda muafaka wa kuliondoa donge hilo” akasema 

Camilla 

“Kuwa huru nieleze kama 

utaona inafaa” akasema 

Mathew.Camilla akafikiri kwa 

muda na kusema 

“Nitakueleza kwa kifupi” 

“Nimechanganya damu.Baba 

yangu ni mzungu na mama ni 

mwafrika.Historia ya mapenzi yao 

baba aliniambia kwamba 

walikutana katika tamasha la 

muziki wakawa marafiki.Mama 

alitokea katika familia masikini 

sana wakati familia ya baba ilikua 

na uwezo makubwa 

kifedha.Walipendana na wakawa 

wapenzi na baadae wakafunga 

ndoa na wakanizaa mimi lakini kitendo cha baba kufunga ndoa na 

mwanamke mweusi 

hakikuwapendeza ndugu na 

marafiki zake na kukawa na chuki 

kubwa.Siku moja mama yangu 

alitekwa akitokea kufanya 

manunuzi tukamtafuta na kesho 

yake akaokotwa akiwa amekufa 

kwa kupigwa risasi.Hadi leo hii 

hatufahamu ni nani waliomuua 

lakini naamini ni mipango ya 

ndugu za baba ambao walichukia 

sana baba alipoamua kumuoa 

mwanamke mweusi.Kitu hicho 

kimenikaa kooni na kila 

nikikumbuka huwa naumia 

sana.Mama yangu alifariki nikiwa 

mdogo na sikupata nafasi ya kukaa 

naye kwa muda mrefu.Inaniumiza sana Mathew” akanyamaza na 

kuinamisha kichwa 

“Pole sana” akasema Mathew 

“Ahsante” 

“Niliamua kujiunga na FBI ili 

niweze kufanya uchunguzi nani 

alimuua mama yangu.Japo 

sijafanikiwa bado kulifanya hilo 

lakini ninaamini siku moja 

nitafanya na nitawafahamu wale 

waliomuua mama yangu na 

watafikishwa mbele za 

sheria.Kitendo cha kumpoteza Jack 

leo kimekwangua tena kidonda 

cha mama yangu.Naomba 

nikwambie kitu kimoja Mathew 

ambacho sijawahi kumwambia 

mtu mwingine yeyote” 

“Niambie tafadhali” “Naichukia Marekani sana.Ni 

nchi yangu lakini naichukia mno.Ni 

ngumu sana kuwa mweusi nchini 

Marekani ingawa ni nchi yenye 

kujipambanua kwamba ina 

demokrasia ya kiwango cha juu 

lakini sisi watu wenye asili ya 

Afrika tunabaguliwa mno.Uwepo 

wangu hapa Tanzania ndani ya 

bara la Afrika najiona huru,nina 

furaha na amani.Sina mpango wa 

kurejea Marekani tena.Ila kuna 

jambo moja nataka nilifanye na 

nitahitaji msaada wako” 

“Sema unahitaji nini Camilla? 

Camilla akatafakari kidogo na 

kusema 

“Nataka tuhakikishe tunapata 

ushahidi wa kutosha wa Marekani kujihusisha katika jambo hili 

unalolichunguza na kisha 

nitaianika nchi hii kwa dunia 

nzima ifahamu namna taifa hili 

kubwa linavyotumia nguvu zake 

kukandamiza nchi ndogo.Mimi 

nitakusaidia kwa kila namna 

nitakavyoweza ili jambo hili liweze 

kukamilika na tuufahamu 

ukweli.Nataka nilipize kisasi kwa 

kumuua mama yangu” akasema 

Camilla. 

“Camilla ahsante sana kwa 

kuniamini na kunieleza historia 

yako.Inaumiza na ninakupa pole 

sana kwa kumpoteza mama yako. 

Pili nakuahidi kwamba endapo 

utapendezwa kuishi hapa 

Tanzania mimi binafsi nitajitahidi kufanya kila linalowezekana ili 

uweze kuyafurahia maisha ya hapa 

ya amani na tatu suala hili 

litafanikiwa kama tutashirikiana 

kwa pamoja.Nakuahidi 

litamalizika na ukweli utaujua 

kwani hadi hapa lilipofika tayari 

kuna mwanga umejitokeza.Kitu 

muhimu ni kushirikiana na kwa 

pamoja tutaweza kulifumbua 

fumbo hili gumu” 

“Mimi niko tayari kukupatia 

kila aina ya ushirikiano Mathew ili 

kufanikisha jambo hili na ndiyo 

maana nilikubali kuja huku baada 

ya kunusa harufu ya ushiriki wa 

Marekani katika suala hili.Nina 

ujuzi mwingi nina utaalamu 

mkubwa katika teknolojia,nina uwezo wa kucheza na silaha kama 

nimezaliwa nazo nina weza 

kupigana kwa ujumla ninaweza 

mambo mengi kwa hiyo ukiwa na 

mimi jisikie amani jihesabu kama 

uko na askari mia moja.” Akasema 

Camila na Mathew akatabasamu 

“Ahsante sana na karibu 

katika operesheni hii” akasema 

Mathew 

“Vipi kuhusu wewe? Unaweza 

ukanieleza japo kwa ufupi historia 

yako?Camilla akauliza 

“Historia yangu kama ilivyo 

yako si nzuri sana na 

nimekumbana na mambo mengi ya 

kusikitisha pia na mimi pia wapo 

wapendwa wangu nimewahi 

kuwapoteza lakini nitakueleza kwa ufupi pia” akasema Mathew na 

kumsimulia Camilla historia ya 

maisha yake na mambo magumu 

aliyopitia hadi alivyopoteza familia 

yake na hadi alivyokutana na 

Peniela wakaoana na mwisho 

wakaachana 

“Umepitia mambo mengi sana 

Mathew pole” akasema Camilla 

“Ahsante.Wengi tulio katika 

kazi hizi tumepitia mambo mengi 

ya kusikitisha lakini imekuwa ni 

sehemu ya maisha yetu na ndiyo 

maana ninajitahidi sana kuwekeza 

katika biashara ili niweze kusahau 

kabisa maisha haya.Nataka kuishi 

maisha ya kawaida.Nataka nikae 

mbali kabisa na hizi kazi lakini 

kadiri ninavyojitahidi kukaa mbali nazo inaonekana zinanitafuata 

zenyewe.Kwa mfano kazi hii 

sikuwa nimefikiria kama 

ningeweza kuifanya.Toka 

nilipokutana na Peniela sikuwahi 

kufanya kazi yoyote ile na 

niliamini nimekwisha achana na 

kazi hizi na nikaanza kuyafurahia 

maisha lakini baada ya kuachana 

na Peniela nikarudi nyumbani 

nimekutana tena na hii kazi 

nikashindwa kukataa ila naamini 

sintafanya tena kazi nyingine 

baada ya hii.Kwa wale wapenzi wa 

mchezo wa mpira kuna lugha huwa 

inatumika kwa wachezaji 

wanaostaafu kwamba 

wanatundika daruga.Na mimi nitatundika daruga endapo kazi hii 

itakamilika na kuniacha salama.” 

“Usihofu Mathew utakuwa 

salama.Mungu ana makusudi yake 

na siku zote atasimama upande 

wetu kwani tunajitolea nafsi zetu 

kwa ajili ya nchi zetu,kwa ajili ya 

usalama wa watu wake” akasema 

Camilla 

“Vipi kuhusu huyu mwanamke 

uliyeachana naye?Bado 

mnawasiliana?Camilla akauliza 

“Tunawasiliana .Tuna mtoto 

mmoja mrembo anaitwa Anna 

Maria hivyo mawasiliano yetu ni 

mazuri,hatuna sababu ya kuwa na 

ugomvi” 

“Nini sababu ya kuachana 

kwenu? “Ni migogoro tu inayotokea 

katika ndoa” 

“Nafahamu kuna migogoro 

mingi ndani ya ndoa japokuwa 

bado sijawahi kupitia huko ila 

nafahamu kuna migogoro.Kwako 

wewe na Peniela nini kilivunja 

ndoa yenu? 

“Ni usaliti.” 

“Nani alimsaliti mwenzake? 

“Peniela alianzisha mahusiano 

ya kimapenzi na bilionea mmoja 

wa kifaransa hivyo sikuona sababu 

ya mimi kuendelea kung’ang’ania 

mapenzi ambayo yamegeuka 

mchezo wa kuigiza.Ni mimi ndiye 

niliyeomba tuachane na kila 

mmoja akaendelee na maisha 

yake” “Bado anakupenda?Na wewe 

bado unampenda? 

“Masuala ya mapenzi hayo 

yamekwisha kwani 

kinachotuunganisha hivi sasa ni 

mtoto wetu Ana Maria pekee.” 

akasema Mathew na Camilla 

akatabasamu 

“Ukiona mtu anakwepa 

kulijibu Swali kama hilo ujue bado 

wanapendana” akasema Camilla 

na wote wakacheka 

“Kuachana si uadui na siwezi 

kuwa na uadui na mama wa mtoto 

wangu na isitoshe bado tuna 

miradi kadhaa tunashirikiana kwa 

hiyo lazima tuwasiliane” 

“Nimekuelewa 

Mathew.Mwenzako ameolewa vipi kuhusu wewe? Unasubiri nini 

kuoa? 

“Kwa sasa jambo hilo 

nimeliweka pembeni na 

ninawekeza katika biashara zangu 

labda hapo baadae ninaweza 

kulifikiria hilo suala.” 

“Wengi baada ya kuachana na 

wapenzi wao huwa wanasema 

hivyo kwamba hawafikirii mapenzi 

tena lakini kumbe ana wapenzi wa 

siri zaidi ya wawili wa 

kumfariji.Nakushauri Mathew 

kama utampata mwanamke 

ambaye unaona anakufaa na 

anaweza kuendana nawe basi 

usimuache.Maisha ni mafupi sana” 

“Ahsante kwa ushauri huo 

Camilla” “Unawekeza katika biashara 

gani ? 

Kabla Mathew hajajibu simu 

yake ikaita alikuwa ni 

rais,akaipokea 

“Hallo mheshimiwa rais” 

“Mathew lile suala 

limekwisha fanyiwa kazi na watu 

wangu na nimeletewa 

majibu.Namba Ile kweli ni ya 

Tanzania na namba kama zile 

huwa zinatolewa kwa watu 

maalum.Nimestuka kidogo baada 

ya kumfahamu mwenye ile namba 

kwamba ni George Mzabwa mkuu 

wa idara ya usalama wa taifa 

aliyejiua” 

“George Mzabwa?! Mathew 

akashangaa “Ndiyo Mathew” akasema rais 

na ukimya ukatanda 

“Mathew ! akaita rais baada ya 

kuona kumekuwa kimya 

“Mheshimiwa rais ahsante 

sana nitawasiliana nawe baadae” 

“Mathew kabla hujakata simu 

naomba kuuliza.Ulisema kwamba 

namba hizi zinahusiana na kile 

unachokichunguza je huyu George 

alikuwa anahusika pia katika 

jambo hili? Akauliza 

“Mheshimiwa rais 

nitawasiliana nawe baadae na 

tutazungumza zaidi.Vipi kuhusu 

zile picha kuna taarifa yoyote 

tayari umeipata? 

“Mpaka sasa bado ila 

nimewapa wakuu wa jeshi la polisi hadi saa saba mchana wa leo niwe 

nimepata majibu watu wale ni 

akina nani.Nitakapoletewa majibu 

nitakujulisha mara moja” 

“Ahsante mheshimiwa 

rais,uwe na siku njema” akasema 

Mathew na kukata simu 

“Vipi Mathew mbona 

umestuka ?akauliza Camilla 

“Kuna kitu kimenistua 

kidogo.Siku chache zilizopita 

mkuu wa idara ya suala wa Taifa 

alijiua kwa kujipiga risasi ofisini 

kwake na chanzo cha kujiua kwake 

hakikufahamika japo bado 

uchunguzi unaendelea.Namba hizi 

ambazo ametupa Jack zilizotoka 

katika simu ya Nathan ni za huyo 

George Mzabwa” akasema Mathew “Mambo yameanza kuiva.Ni 

wazi huyo mkuu wa idara ya 

usalama wa taifa alikuwa na 

mawasiliano na Nathan hivyo naye 

anahusika katika jambo 

hili”akasema Camilla 

“Kama ni hivyo basi mtandao 

huu ni hatari sana na 

unawahusisha watu wazito.Mkuu 

wa usalama wa taifa ni mtu mzito 

na ndiyo maana sishangazwi na 

mambo haya yaliyotokea kumbe 

kuna mikono ya watu wazito kama 

huyu.George alijipiga risasi ofisini 

kwake na kuacha ujumbe kwa rais 

na katika ujumbe huo alimweleza 

rais kwamba ameshindwa kupata 

majibu ya suala hili na akataka rais 

pia kuachana nalo kwani hataweza kupata majibu.George alikuwa 

mshirika wa Nathan na nina 

hakika alifahamu kila kitu kuhusu 

sakata hili ila swali ni kwa nini 

alijiua?Hapa lazima kuna sababu 

iliyopelekea akachukua maamuzi 

haya .Itabidi twende nyumbani 

kwake tukazungumze na mke 

wake na pengine tunaweza 

kubahatika kupata kitu chochote 

cha kuweza kutusaidia.George 

ndiye atakayeweza kutuunganisha 

na mtandao wote wa Nathan” 

akasema Mathew na kuchukua 

simu akampigia Theresa 

“Unaendelea na huyo 

mmarekani wako? Akauliza 

Theresa na kumfanya Mathew 

atabasamu “Hana tatizo huyu mtoto 

ametulia hapa karibu yangu” 

akasema Mathew 

“Mhhn !! Theresa akaguna 

“Mbona unaguna Theresa? 

Akauliza Mathew 

“Kwa nini hukunieleza kama 

una mpenzi mwingine baada ya 

kuachana na Peniela? 

“Huyu si mpenzi wangu bali ni 

rafiki yangu na amekuja kunisaidia 

katika kazi hii” akasema Mathew 

“Hongera” 

“Tuachane na hayo 

Theresa.Nimekupigia kukupa 

taarifa za jambo moja la 

muhimu.Nilichukua simu tatu kwa 

Nathan.Camilla amezitambua na 

katika simu hizo kuna moja ambayo huitumia kwa masuala 

yake ya kikazi na katika simu hiyo 

kwa msaada wa Camilla tumeweza 

kugundua kwamba alikuwa na 

mawasiliano na watu wawili hapa 

Tanzania.Mtu ambaye tumeweza 

kufahamu kwamba alikuwa 

anawasiliana na Nathan ni George 

Mzabwa” 

“George Mzabwa? Akauliza 

Theresa kwa mshangao mkubwa 

“Ndiyo Theresa.Nathan 

alikuwa anawasiliana na 

George.Kuna mtu mwingine pia 

alikuwa anawasiliana naye lakini 

hatukuweza kupata namba 

zake.George alikuwa na 

mawasiliano na Nathan na hii 

inatudhihirishia kwamba alikuwa anafahamu kinachoendelea na 

inawezekana akawa alishiriki kwa 

namna moja au nyingine katika 

matukio yale mawili” akasema 

Mathew 

“Nimestuka sana.Kumbe 

George naye alikuwa ana 

mahusiano na Nathan! Mathew 

nimezidi kuogopa kama watu 

wakubwa kama George wanakuwa 

wasaliti kwa taifa lao” 

“Nguvu kubwa kwa sasa 

inaelekezwa kwa George ili 

kufahamu watu wengine 

anaoshirikiana nao.Naomba 

unielekeze nyumbani kwake ili 

nikazungumze na mke wake” 

akasema Mathew na Theresa akamuelekeza nyumbani kwa 

George mzabwa 

“Nitakutaarifu baadae 

nikitoka nyumbani kwa 

George.Wewe endelea kupumzika” 

akasema Mathew na kukata simu 

“Tunaweza kuondoka sasa 

kwenda nyumbani kwa George” 

Mathew akamwambia Camilla 

wakajiandaa na kuondoka 

kuelekea nyumbani kwa 

George.Walipita gereji ambako 

gari la Mathew lilipelekwa 

akachukua gari lake na kuliacha 

lile la Meshack Jumbo wakaelekea 

nyumbani kwa George 

Waliwasili nyumbani kwa 

George Mzabwa kama 

alivyoelekezwa na Theresa na kukuta watu wengi wakiendelea 

na matanga.Mathew na Camilla 

wakatoa pole kwa wafiwa halafu 

wakataka kuonana na mke wa 

marehemu.Jibu walilopewa 

likamstua kidogo Mathew 

“Amekuja kuchukuliwa hapa 

muda si mrefu na mtu 

fulani.Walitoka nje wakazungumza 

na baada ya muda mama Mzabwa 

akaja akatuaga kwamba kuna 

mahala anakwenda atarejea muda 

si mrefu,wakaingia katika gari na 

kuondoka” akasema mama mmoja. 

“Hakuwaeleza anakwenda 

wapi? 

“Hapana hakueleza chochote 

na hakuna anayefahamu 

anakwenda wapi.” Akasema mama yule na mara uso wake 

ukaonekana kubadilika.Mathew 

akagundua kitu usoni pa yule 

mama akageuka nyuma na 

kukutana na wanawake watatu 

waliovaa mavazi marefu na 

kujifunika nyuso zao wakabaki 

wanaonekana macho pekee. 

“Mbona huyu mama 

ameogopa baada ya kuwaona hawa 

wanawake wakiingia hapa? 

Akajiuliza Mathew na ghafla 

kukatokea jambo ambalo hakuna 

aliyelitegemea.Wale wanawake 

watatu waliokuwa wamevaa 

magauni marefu kila mmoja 

akatoa bunduki ndogo aliyokuwa 

ameificha ndani ya gauni lile na 

kuanza kuachia risasi na kuwataka watu wote walale chini .Watu wale 

walitawanyika haraka sana na 

kumbe hawakuwa peke yao 

walikuwepo wengine nje na idadi 

yao ikaongezeka mle ndani.Ndani 

ya sekunde chache watu wote 

waliokuwepo eneo lile wakalala 

chini wakiwamo Mathew na 

Camilla 

NINI KITATOKEA HAPO 

MSIBANI? NANI KAMCHUKUA MKE 

WA GEORGE MZABWA? USIKOSE 

SEASON 2



MWISHO WA SEASON 1



0 comments:

Post a Comment

Blog