Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL - 1

 

IMEANDIKWA NA : PATRICK CK

******************************************

Simulizi : The Football 

Sehemu Ya Kwanza (1)


Msafara wa rais wa 

jamhuri ya muungano wa 

Tanzania,uliwasili katika 

uwanja wa ndege wa kimataifa wa 

Julius Nyerere jijini Dar es 

salaam.Dr Vivian Sebastian Matope 

rais wa jamhuri ya muungano wa 

Tanzania akashuka garini akiwa 

amevalia suti ya rangi nyeupe 

iliyompendeza vilivyo.Kichwani 

hakuwa amebadili mtindo wake 

wa nywele.Dr Vivian hakupenda 

kuweka madoido katika nywele 

zake.Alipenda kuzipunguza na 

kuzifanya fupi.Alikuwa na mwili 

mwembamba wastani na 

kumfanya awe ni mmoja kati ya 

marais wanawake wazuri zaidi 

duniani. 

Akiwa katika ulinzi mkali Dr 

Vivian alianza kuelekea ndegeni 

huku akisalimiana na kuagana na 

baadhi ya viongozi waliofika pale 

uwanjani kumuaga.Alipomaliza 

kuagana na viongozi mbali mbali 

akamuita pembeni mkurugenzi wa 

idara ya idara ya usalama wa taifa 

ndugu George Mzabwa 

“George umefikia wapi 

kuhusu lile suala ?Kuna chchote 

kimepatikana mpaka leo? Akauliza 

Dr Vivian 

“Madam president lile suala 

bado gumu lakini tunaendelea 

kulifanyia kazi.Mpaka sasa bado 

hatujafikia hatua ya kuridhisha na 

ndiyo maana umeona nimekuwa 

kimya sijafika kwako kukupa mrejesho wowote” Akasema 

George.Dr Vivian akamtazama 

akatabasamu na kusema 

“Nitakaporejea nataka nikute 

tayari kuna hatua imekwisha 

pigwa ama sivyo nitakuondoa 

katika nafasi hiyo na kuwapa 

wengine wenye uwezo wa kufanya 

kazi kwa kasi kama 

ninavyotaka.Sioni sababu ya 

kukukwamisha katika 

kulishugulikia suala hili wakati 

kila kitu unacho.Naomba ulifanyie 

kazi hilo nililokwambia na 

nitakaporejea nikute aidha ripoti 

ya hili suala,au barua ya kuachia 

ngazi au nikuondoe mwenyewe 

katika nafasi hiyo.Tumeelewana 

George? Akauliza Dr Vivian “Nimekuelewa madam 

president” akajibu George 

“ Good” akasema Dr Vivian na 

kupanda ngazi kuingia 

ndegeni.Alipofika katika mlango 

wa ndege akageuka na 

kuwapungia mkono watu 

waliokuja kumuaga halafu 

akaingia ndegeni 

Dr Vivian ni rais wa kwanza 

mwanamke kuongoza jamhuri ya 

muungano wa Tanzania .Alizaliwa 

22 Octoba 1970 akiwa mtoto wa 

kwanza wa Kanali Sebastian 

Matope na mke wake Getruda 

Mazimbo.Alipata elimu yake ya 

msingi katika shule ya msingi 

Azimio mjini Dodoma ambako 

baba yake alikuwa akifanya kazi wakati huo.Alijiunga na shule ya 

sekondari ya St Bernadetha 

inayomilikiwa na masista wa 

shirika la mtakatifu Bernadetha 

iliyoko mkoani Kilimanjaro.Lengo 

kuu la kujiunga na shule hiyo iliyo 

chini ya watawa ilikuwa ni 

kujiunga na maishaya utawa.Toka 

akiwa mtoto dogo Dr Vivian 

aliyapernda maisha yale ya 

kitawa.Alisoma katika shule hiyo 

hadi kidato cha sita na matokeo 

yalipotoka Vivian alifaulu kwa 

kiwango cha juu kwa kupata 

daraja la kwanza.Matokeo hayo 

yalimfanya Vivian abadili lengo 

lake la kuwa mtawa na akachagua 

kuendelea na masomo ya udaktari 

.Aliendelea na elimu ya juu katika fani ya udaktari katika vyuo vikuu 

kwenye nchi mbali mbali kama vile 

Israel,Cuba,Urusi,Marekani na 

China.Mwaka 2007 aliamua 

kurejea nchini Tanzania baada ya 

familia yake yaani wazazi wake 

wote na mdogo wake kuuawa na 

watu wasiojulikana. 

Baada ya kurejea nchini Dr 

Vivian alifanya kazi kama daktari 

wa watoto katika hospitali ya taifa 

ya Muhimbili.Alianza kujiingiza 

taratibu katika siasa na kutokana 

na kipawa chake kikubwa cha 

uongozi alichokuwa nacho,Dr 

Vivian alijikuta akishika nafasi 

kadhaa ndani ya chama na hapo 

ndipo alipoanza 

kujulikana.Daktari huyu mwenye haiba ya kipekee,mwenye urefu wa 

5.8.ngozi nyororo na uso 

usiokauka tabasamu alifahamika 

sana kwa misimamo yake thabiti 

isiyoyumba katika yale mambo 

anayoyaamini na hasa katika 

kusimamia haki za watu wa hali za 

chini wanaokandamizwa. 

Tabia yake hii ya msimamo 

usiotetereka ilianza kuonekana 

pale alipokuwa rais wa serikali ya 

wanafunzi katika chuo kikuu 

kimoja alichosoma nchini 

Marekani.Katika chuo hicho kikuu 

wanafunzi wenye asili ya Afrika 

walikuwa wanabaguliwa na 

kutopewa kipaumbele katika 

mambo mengi.Haikuwa rahisi 

kwake kuweza kushinda nafasi ya rais wa serikali ya wanafunzi na 

aliposhinda kitu cha kwanza 

alichoanza kukishughulikia ni 

suala la ubaguzi uliokithiri hapo 

chuoni.Jambo hili lilimletea 

misukosuko mikubwa na hata 

kuondolewa katika nafasi yake ya 

rais wa wanafunzi baada ya 

kuonekana anakiuka sheria za 

chuo lakini hii haikumkatisha 

tamaa kuendelea kuwapigania 

wale waliokuwa 

wanabaguliwa.Baada ya mvutano 

mkali na chuo hicho hatimaye 

ushindi ukapatikana na taratibu za 

chuo zikabadilishwa,wanafunzo 

wote wakawa na haki sawa.Kwa 

wale wanaofuatilia mambo ya 

nyota,hii ilikuwa ni ishara tosha kwamba nyota ya Dr Vivian ilianza 

kung’aa na siku moja ingeweza 

kung’aa na kutoa mwangaza 

mkubwa 

Wakati akiendelea na 

masomo yake aliwahi kuchaguliwa 

kuwa msemaji wa wanafunzi 

wenye asili ya Afrika katika katika 

vyuo vikuu vya Marekani na katika 

mojawapo ya hotuba aliyowahi 

kuitoa katika kongamano 

lililofanyika siku ya kuikumbuka 

hotuba aliyoitoa mwanaharakati 

aliyepigania haki za watu weusi 

nchini Marekani Martin Luther 

aliyoitoa 28 August 1963,Vivian 

aliweka wazi ndoto yake ya 

kuliona siku moja bara la Afrika 

linatoka gizani na kuwa bara lenye nuru na nguvu.Alieleza 

kusikitishwa kwake na 

ukandamizwaji na unyonyaji 

unaofanywa na mataifa makubwa 

yenye nguvu dhidi ya mataifa 

masikini ya bara la Afrika.Hotuba 

hii iliyojaa msisimko iliwavutia 

watu wengi na kumfanya Vivian 

ajulikane na kualikuwa katika 

makongamano mbali mbali.Katika 

mojawapo ya hotuba alizowahi 

kutoa aliweka wazi nia yake ya 

siku moja kuwa kiongozi na 

kuziunganisha nchi zote za Afrika 

na kuwa nchi nmoja yenye nguvu 

kijeshi na kiuchumi. Alitamani 

siku moja awe rais wa kwanza wa 

Afrika na kuongoza bara hili lenye 

kila aina ya utajiri. Alipofanikiwa kushinda nafasi 

ya urais wa Tanzania,Dr Vivian 

amefanya mambo makubwa kwa 

muda wa miaka miwili ambayo 

amekuwa madarakani.Ni rais 

mdogo kwa umri ukilinganisha na 

marais wengi wa mataifa mengine 

lakini mambo makubwa 

aliyoyafanya yamewashangaza 

wengi.Ni rais asiyesita kuchukua 

maamuzi magumu na 

asiyetetereka katika maamuzi 

yake.Huyu ndiye Dr Vivian rais wa 

jamhuri ya muungano wa Tanzania 

ambaye amepewa jina la utani la 

Dr White kutokana na staili yake 

ya kipekee ya kupenda rangi 

nyeupe kuanzia mavazi yake hadi 

magari yanayotumika katika msafara wake.Mara chache sana 

huonekana katika mavazi ya rangi 

nyingine lakini siku zote huwa 

katika mavazi meupe. 

Baada ya kuingia ndegeni Dr 

Vivian akasalimiana na marubani 

na wahudumu wa ndege yake na 

kujiandaa kwa ajili ya kuelekea 

jijini New York Marekani 

kuhudhuria mkutano mkuu wa 

umoja wa mataifa unaofanyika kila 

mwaka na ambao huudhuriwa na 

wakuu wote wa nchi wanachama 

wa umoja wa mataifa.Huu ni 

mkutano wake wa kwanza 

kuhudhuria tangu achaguliwe 

kuwa rais wa jamhuri ya 

Muungano wa Tanzania.Mkutano 

uliopita aliwakilishwa na makamu wa rais na mwaka huu 

anahudhuria yeye 

mwenyewe.Katika safari hii 

aliongozana na mawaziri 

wanne,maafisa wengine kadhaa 

pamoja na walinzi wake na jumla 

msafara wake ulikuwa na watu 

ishirini. 

Ndege ilikaa katika njia yake 

ya kurukia ikaanza kuondoka 

taratibu na kuongeza kasi kisha 

ikapaa huku viongozi waliofika 

pale uwanjani kumuaga rais 

wakipunga mikono kumtakia rais 

na ujumbe wake safari 

njema.Ndege ilipokaa sawa 

angani,Dr Viviana akaitisha kikao 

na watendaji alioambatana nao 

katika safari ile.Walikutana katika chumba cha mikutano kilichomo 

ndani ya ndege ile kubwa chenye 

uwezo wa kuchukua watu zaidi ya 

ishirini.Walijadiliana mambo 

kadhaa kuhusiana na safari yao ile 

na baada ya takribani saa moja na 

nusu kikao kikamalizika wajumbe 

wakatoka na rais akaenda katika 

chumba chake kupumzika kwani 

safari ile ilikuwa ndefu.Akiwa 

chumbani akamuita mdogo wake 

Theresa. 

Theresa Sebastian Matope ni 

msichana mwenye weusi wa 

kung’aa na umbo la 

kupendeza.Wazazi wa Dr Vivian 

walimchukua Theresa toka katika 

kituo cha kulelea watoto yatima 

akiwa mtoto mdogo sana na kumlea kama mtoto wao wa 

kumzaa.Kwa hivi sasa ndiye 

mwandishi wa hotuba za rais 

“Theresa naomba nione 

hotuba uliyoiandaa ninayokwenda 

kuitoa New York” Akasema Dr 

Vivian baada ya Theresa kuingia 

mle chumbani kwake.Theresa 

akatoka na kwenda kuchukua 

kompyuta yake akarejea na 

kumuonyesha Dr Vivian hotuba ile 

aliyokuwa anaiandaa 

“Imebaki sehemu ndogo ya 

kumalizia kuhusiana na 

mabadiliko ya tabia nchi Afrika” 

Akasema Theresa na Dr Vivian 

akaipitia hotuba ile taratibu halafu 

akasema “Hii ni hotuba nzuri sana 

lakini bado haijafikia kiwango 

ninachokihitaji.Hii ni hotuba 

yangu ya kwanza katika mkutano 

huu mkubwa na ninataka iwe kali 

na yenye msisimko.Nimezoeleka 

hotuba zangu huwa zinakuwa kali 

na zenye msisimko.Nataka 

viongozi wa dunia waelewe 

msimamo wangu na wa Tanzania 

katika mambo mbali mbali hivyo 

iongeze ukali hotuba hii” akasema 

Dr Vivian 

“Dada labda uniweke wazi 

unataka nilenge maeneo yapi 

hasa.Ulinipa mambo ya kuzingatia 

wakati wa kuiandaa hotuba hii na 

nimeyafuata ,nimelenga mambo ya 

uchumi,misaada ya masharti na unyonyaji wa rasilimali 

zetu,mabadiliko ya tabia nchi na 

mengineyo” akasema Theresa.Dr 

Vivian akaitazama tena hotuba ile 

na kusema 

“Hotuba hii si mbaya,imekaa 

vizuri lakini kuna sehemu ambazo 

zinahitaji lugha kali zaidi 

kuonyesha msisitizo.Hotuba hii 

imepoa sana.Lakini usijali endelea 

nayo na utakapomaliza niletee 

nitaisahihisha 

mwenyewe,samahani kama 

nimekukwaza” akasema Dr Vivian 

“Usijali dada” akasema 

Theresa na kuchukua kompyuta 

yake ili atoke Vivian akamuomba 

asubiri. “Kaa nami kidogo 

Theresa,bado tunayo safari 

ndefu.Nyakati kama hizi ndipo 

tunaweza kukaa na kuongea 

mambo yanayotuhusu sisi.Tukifika 

marekani kutakuwa na mikutano 

mingi hivyo hatutaweza kupata 

nafasi nzuri ya kuzungumza 

mambo yetu” akasema Dr Vivian 

“Ni kweli dada.Japokuwa tuko 

pamoja muda mwingi lakini 

hatupati nafasi ya kuzungumza 

mambo yetu ya kifamilia” akasema 

Theresa na kujimiminia juice 

katika glasi 

“Kabla sijaingia ndegeni 

nilikuwa na mazungumzo na 

George Mzabwa.Nilimuuliza 

amefikia wapi kuhusiana na kazi niliyompa ya kuchunguza mauaji 

ya familia yetu.Amekuwa 

ananikimbia kimbia kila 

ninapotaka kulizungumzia jambo 

hili.Jibu alilonipa 

halijaniridhisha.Amesema 

kwamba mpaka sasa bado 

hajafanikiwa kugundua lolote.Ni 

miaka miwili imepita sasa toka 

nimempa kazi hiyo na ameniudhi 

sana.Nimemwambia nitakaporejea 

aidha nikute taarifa kwamba watu 

waliofanya kitendo kile kiovu 

wamepatikana au nikute barua 

yake ya kuachia ngazi mezani 

kwangu ama sivyo nitamuondoa 

na kumpeleka sehemu nyingine 

kwani ameshindwa kazi.Sielewi 

kuna nini katika jambo hili hadi lishindwe kupatiwa 

majibu.Ninafikiria kutafuta mtu 

mwingine wa kuongoza idara ya 

usalama wa taifa kwa kasi 

ninayoihitaji.George hawezi 

kuendana na kasi yangu” akasema 

Dr Vivian 

“Hata mimi nashangaa na 

kujiuliza kulikoni katika suala hili? 

Inawezekajane mpaka leo hii 

hakuna taarifa yoyote kuhusiana 

na wauaji wa familia yetu?Jeshi la 

polisi wamefanya 

uchunguzi,usalama wa taifa pia 

lakini mpaka leo hii hakuna 

chombo chochote kilichotoa 

majibu ni nani waliua familia yetu 

na kwa nini.Vyombo hivi vyote 

viwili wanazo rasilimali za kutosha kuwawezesha kufanikisha 

uchunguzi wa jambo hili lakini 

mpaka leo wameshindwa kubaini 

watu waliofanya unyama ule.Hapa 

kuna kitu kinatia shaka dada” 

akasema Theresa 

“Tuachane na hayo 

nitayashughulikia nitakaporejea 

kwani suala hili kwa sasa 

linaonekana kama fumbo gumu 

lisiloweza kufumbuka.Nitalivalia 

njuga mimi mwenyewe na safari 

hii lazima nitapata majibu,lazima 

fumbo hili lifumbuke” akasema Dr 

Vivian na kumuomba Theresa 

amletee juice ya mchanganyiko wa 

matunda kinywaji anachokipenda 

sana. “Nathan kanipigia simu leo 

asubuhi na kunitaarifu kwamba ile 

kazi yake aliyokwenda kuifanya 

Uswisi imemalizika na hivyo 

atanifuata New York na baada ya 

mkutano kumalizika tutarejea 

wote Da es salaam kuendelea na 

maandalizi ya ndoa yetu.Theresa 

siwezi kueleza furaha niliyonayo 

kwani imebaki miezi mwili tu na 

mimi niingie katika ndoa na 

mwanaume ninayempenda kwa 

dhati.Hata hivyo kuna kitu nataka 

kukisikia toka kwako.Watu 

wanaongeaje huko mitaani 

kuhusiana na ndoa yangu na 

Nathan? Nilitaka jambo hili liwe la 

kimya kimya lakini watu 

wamefukunyua hadi wakagundua ninataka kufunga ndoa”Akauliza 

Dr Vivian huku 

akitabasamu.Theresa akanywa 

funda la juice halafu akasema 

“Japokuwa Nathan ulikuwa 

naye katika kipindi chote cha 

kampeni na kuzunguka naye nchi 

nzima lakini bado watu 

hawamfahamu vizuri ni 

nani.Nimekuwa napitia baadhi ya 

maoni ya watu mtandaoni na 

nimeona watu wanahoji kwa nini 

rais wao aolewe na mtu wa kutoka 

nje ya nchi?Tanzania imejaa vijana 

wa kila aina wasomi na wabobezi 

wa mambo mbali 

mbali,haujawaona hao wote hadi 

moyo wako ufunguke kwa mtu wa 

taifa lingine?Lakini haya yasikuogopeshe ni mawazo tu ya 

watu yanayotokea katika mijadala 

mbali mbali inayoendelea huko 

mitandaoni” akasema Theresa .Dr 

Vivian akatabasamu nba kuuliza 

“Wewe je una maoni gani? 

“Kuhusu nini dada Vivi? 

“Kuhusu mimi na 

Nathan.Nakufahamu wewe huna 

tabia ya kuficha kitu bali husema 

kweli toka moyoni.Sijawahi kupata 

maoni yako kuhusiana na hili suala 

langu na 

Nathani.Unaliongeleaje?Nathani ni 

mwanaume ambaye naweza 

kusema kwamba ninampenda kwa 

dhati ya moyo wangu lakini je 

unadhani watu wangu 

watampenda na kumkubali?Tafadhali kuwa 

muwazi kwangu.You are my 

sister” akasema Dr Vivian 

“Dada ,mapenzi kama yalivyo 

hayachagui rangi,umri hata 

taifa.Moyo unaweza kufunguka 

kwa mtu yeyote awe 

mweusi,mweupe n.k.Wewe 

umeufungua moyo wako kwa 

Nathan na hakuna ubaya wowote 

lakini….” Theresa akasita kidogo 

akanywa maji ya matunda na 

kuendelea 

“Umeomba nikueleze ukweli 

wangu na nitakueleza ukweli 

wangu japo hautakuwa mzuri sana 

lakini lazima niuseme kwa kuwa 

umeomba.Hakuna mtu 

atakayeweza kukuzuia usiolewe na Nathan mwanaume unayempenda 

kwa dhati ya moyo wako lakini 

ndoa hii ingekuwa na tija zaidi 

kama Nathan angekuwa ni 

mtanzania.Anaweza akabadili 

uraia wake na kuwa mtanzania 

lakini damu yake bado ni 

Marekani.Kama akiwa mumeo 

yeye ndiye atakayekuwa mshauri 

wako mkuu kwa mambo mbali 

mbali hivyo anapaswa awe ni mtu 

anayeipenda Tanzania na 

kuifahamu vyema,ayafahamu 

matatizo ya waTanzania na 

yamguse ili aweze kukushauri 

vizuri namna ya kuzitatua 

changamoto mbali mbali 

unazokumbana nazo katika kazi 

yako.Nathani yeye ni mmarekani na Tanzania ameifahamu kwa 

sababu yako tu na sina hakika 

kama anaweza kuwa mshauri 

mzuri katika masuala yanayohusu 

Tanzania.Ikitokea akashindwa 

kukushauri au akakushauri vibaya 

mzigo wote wa lawama utakuwa 

juu yako.Lakini haya ni mawazo 

yangu tu na usiyachukulie kama 

ndiyo mtazamo wa 

watanzania.Nathan ni kijana mzuri 

na sioni kama ana tatizo lolote” 

akasema Theresa 

“Theresa ahsante sana.Ndiyo 

maana huwa ninapenda kukuomba 

ushauri.Una mtazamo wa 

mbali.Unafaa sana kuwa mshauri 

wa rais na nitalitazama hilo siku za 

usoni.Umezungumza mambo ya msingi na ambayo sikuwa 

nimeyafikiria kabla sijakubali 

kuolewa na Nathan.Vipi kuhusu 

wewe na yule mtu wako Damian? 

Bado mnaendelea na ugomvi 

wenu? Kwa nini masuala yenu 

msiyatafutie ufumbuzi na 

kuyamaliza ili msonge mbele kwa 

amani? 

“Dada Vivi kuna mambo 

mengine hayafai 

kuyalazimisha.Nimetafakari sana 

na kugundua mimi ndiye 

niliyekuwa nalazimisha penzi 

wakati mwenzangu hana muda 

nami.Kila wakati mimi ndiye 

niliyekuwa nikipiga magoti 

kuomba msamaha hata kama si 

mimi niliyekosa.Lengo lilikuwa ni kunusuru penzi letu kwa kuwa 

Damian nilimpenda zaidi ya 

ninavyoweza kueleza.Lakini ulifika 

wakati nikasema imetosha na 

nikaamua kila mmoja aendelee na 

maisha yake.Niliumia mwanzoni 

but now I’m happy.Nina amani ya 

moyo na ninasubiri yule ambaye 

ameumbwa kwa ajili yangu 

ajitokeze.Naamini yupo mahala 

fulani na muda ukifika nitampata” 

akasema Theresa 

“Hongera kwa maamuzi 

hayo.Mimi nilitamani sana 

kukushauri hivyo toka awali lakini 

sikutaka kuingilia masuala 

yako.Unapoona uko katika 

mahusiano halafu wewe ndiye 

mwenye kuumia kila siku na mwenzako hajali basi chukua 

hatua haraka,huo uhusiano 

hautakufikisha mahala 

kokote.Natumai tayari umepata 

somo la kutosha na utakuwa 

makini safari hii kutafuta 

mwanaume yule ambaye atakufaa 

katika maisha yako.Ukikosea 

kuchagua utaumia sana.Mapenzi 

yanaumiza mno.Kuna nyakati hata 

mimi ninawaza kuhusu Nathan 

kama hatutakuwa na migogoro 

pindi tutakapofunga ndoa.Nataka 

nielekeze akili yangu katika 

kuwasadia watanzania 

walionichagua na kuwatatulia kero 

zao na nitakuwa na muda mdogo 

sana wa kushughulikia masuala ya 

mapenzi.Hiki hawezi kuwa kikwazo kwa Nathan na kikaleta 

mgogoro kati yetu?Laiti Mungu 

angeweza kunionyesha maisha 

nitakayoishi nikiwa na Nathan 

ningeweza kufanya maamuzi lakini 

Mungu ametuficha na hatuelewi 

chochote kuhusu dakika ijayo” 

akasema Dr Vivian 

“Usiwe na wasi wasi 

dada.Nathan ni kijana mzuri,mpole 

na hana matatizo.Lakini …” 

Theresa akasita 



ENDELEA

Usiwe na wasi wasi 

dada.Nathan ni kijana mzuri,mpole 

na hana matatizo.Lakini …” 

Theresa akasita 

“Lakini nini Theresa? Mbona 

umesita? Sema unachotaka 

kukisema” akasema Dr 

Vivian.Theresa akafikiri kidogo na 

kusema 

“Nothing.Ngoja nikuache 

upumzike,mimi naenda kuimalizia hotuba hii halafu na mimi 

nipumzike” akasema Theresa na 

kuchukua kompyuta yake akatoka 

mle chumbani. 

“Theresa alitaka kuniambia 

nini halafu akasita? Akajiuliza Dr 

Vivian baada ya Theresa kutoka 

mle chumbani 

“Theresa si mtu wa kuficha 

jambo,au aliona halina maana 

ndiyo maana akaamua kuachana 

nalo.Hata hivyo kuna jambo 

amelizungumza la maana sana 

kwangu na sikuwa nimelitilia 

maanani hapo kabla.Nikiolewa na 

Nathan yeye ndiye atakayekuwa 

mshauri wangu katika mambo 

mengi lakini atanishauri kitu gani 

kama haifahamu vyema Tanzania wala matatizo ya watanzania? 

Akajiuliza 

“Nimetoka mbali na Nathan na 

ninamfahamu vyema.Hata kama 

haifahamu vizuri Tanzania wala 

matatizo yake lakini nina imani 

atanishauri vizuri kwani ni kijana 

mpole na mwenye busara ya hali 

ya juu.Sina shaka hata kidogo na 

upendo wake kwangu na hata 

mimi ninampenda mno na ndiyo 

maana hata aliponitamkia kwamba 

anataka kunioa niliruka ruka kwa 

furaha.Mengi yatasemwa lakini 

sitakiwi kuyasikilza.Natakiwa 

kuziba masikio na kuyapuuza 

kwani huyu ndiye chaguo 

langu.Nathan ameingia katika kila 

mshipa wa mwili wangu” akawaza na kuinuka kitandani akachukua 

kompyuta yake akafungua mahala 

anakohifadhi picha na kuzitazama 

picha za gauni lake zuri atakalovaa 

siku ya harusi yake,akatabasamu 

“Sipati picha namna 

nitakavyopendeza ndani ya gauni 

hili lililobuniwa na mbunifu 

chipukizi wa mavazi wa 

kitanzania.Naamini 

nitakapoonekana nimelivaa gauni 

hili jina lake litapaa ulimwenguni 

kwani wengi watataka kufahamu 

nani alibuni vazi zuri kama hili.” 

Akatabasamu na kuanza kutazama 

picha nyingine za wabunifu mbali 

mbali wa mavazi ya harusi 

Alipotoka chumbani kwa 

rais,Theresa akaenda katika moja wapo ya ofisi zilizomo ndani ya 

ndege hii kubwa akachomeka 

spika za masikioni katika 

kompyuta yake akaanza kusikiliza 

muziki.Uso wake ulionyesha 

mabadiliko 

“Mambo tuliyozungumza na 

dada Vivi yameniharibia kabisa 

siku yangu.Kwanza ni kuhusu yule 

mchumba wake Nathan.Moyo 

wangu haumkubali kabisa na hata 

mwenyewe analifahamu hilo na 

sijui kwa nini simpendi.Kila 

nimuonapo karibu na dada amani 

hutoweka kabisa.Najua 

wanapendana lakini moyoni 

mwangu hana kibali.Si kwamba 

ninamchukia ila ninaona hafai 

kuwa na Vivian.Nilitaka nimueleze hivyo dada lakini nikasita kwani 

asingefurahia maneno hayo.Hata 

hivyo siwezi kuingilia mapenzi 

yao.Kama wanapendana acha 

waoane lakini ningefurahi sana 

kama dada yangu angeolewa na 

kijana mtanzania” akawaza 

Theresa na kufumbua macho 

baada ya mlango kufunguliwa na 

mtu kuingia mle ofisini.Alikuwa ni 

waziri wa mambo ya nje 

“Theresa nimekufuata 

wewe,kuna kitu nataka 

unisaidie.Naomba uipitie hii 

hotuba yangu na uirekebishe kama 

kuna mapungufu” akasema waziri 

huyo na kutoka .Theresa 

akaendelea kusikiliza mziki huku 

akiipitia hotuba ile ya yule waziri na mara kumbu kumbu fulani 

ikamjia akaacha kazi aliyokuwa 

anaifanya akajiegemeza kitini 

“Ni miaka zaidi ya kumi sasa 

imepita lakini bado picha ya 

yaliyomkuta baba haijafutika 

kichwani na inanitesa kila 

uchao.Nilikuwepo na nilishuhudia 

kila kilichotokea.Najiuliza kwa 

nini mimi?Kwa nini Mungu 

akanichagua mimi niyashuhudie 

yale yote? Naamini Mungu ana 

sababu zake na ndiyo maana 

katika watu wote ambao 

walimzunguka baba alinichagua 

mimi na kunibebesha mzigo huu 

mzito.Kila siku ninapolikumbuka 

jambo hili mwili wote hupata 

baridi.Bado ile milio ya risasi zilizochukua uhai wa baba,mama 

na kaka Kelvin ninaisikia 

masikioni kila nilalapo.Nimebaki 

natembea na siri hii nzito ambayo 

hakuna anayeifahamu hata dada 

Vivian hafahamu chochote , Ni mimi 

pekee ninayefahamu sababu ya 

baba ,mama na kaka Kelvin 

kuuawa.Ni kwa sababu ya 

Football” Machozi yakamtoka 

“Nimekuwa najilazimisha 

kutaka kulisahau jambo hili lakini 

nimeshindwa.Ninaogopa kuliweka 

wazi suala hili kwa ajili ya usalama 

wangu na dada.Ninaogopa hata 

kumueleza dada Vivian kwani 

yanaweza kumkuta kama 

yaliyomkuta baba .Waliomuua 

baba walikuwa wanaitafuta hiyo football ni vipi endapo mpaka sasa 

wakawa bado wanaitafuta? 

Nitayaweka hatarini sana maisha 

ya dada nikimueleza kuhusiana na 

hili suala.Ngoja niendelee kulibeba 

na itakuwa ni siri yangu pekee na 

Mungu wangu.Nimeibeba na 

kutembea na siri hii kwa zaidi ya 

miaka kumi na nitaendelea 

kutembea nayo.Yawezekana wale 

jamaa bado wanaendelea 

kutuchunguza.Sina hakika kama 

watakuwa wamekata 

tamaa.Lazima watakuwa 

wanachunguza kwa siri ili kujua 

football iko wapi.Lakini hii football 

ni kitu gani?Ina siri gani ndani 

yake?Baba hakuwahi kunieleza 

chochote kuhusiana nayo.Ninavyofahamu mimi mkoba 

ule uliopewa jina la football asili 

yake ni nchini Marekani ambako 

kila asafiripo rais wa Marekani 

huwa anasafiri nao na ndani yake 

kuna mambo ya siri ya kiusalama 

kuhusiana na mambo ya 

nyuklia.Hapa Tanzania rais Anorld 

alianzisha mtindo wa kutembea na 

begi kila anakoenda na akalipa 

jina la football na baba ndiye 

aliyekuwa mbebaji wake mkuu,je 

kulikuwa na siri gani humo ndani 

yake? Akajiuliza Theresa na 

kukumbuka zikamrejesha mbali 

JUNE 2007 – DAR ES SALAAM 

Saa tatu za usiku familia ya 

Kanali Sebastian Matope wamekaa 

sebuleni wakitazama filamu baada 

ya kumaliza kupata mlo wa 

usiku.Theresa akainuka akaenda 

chumbani kwake na kurejea na 

bahasha ya khaki akampatia baba 

yake 

“Nini hii,mchango? Akauliza 

kanali Sebastian.Theresa hakujibu 

kitu akatabasamu.Baba yake 

akaifungua na kukuta ni ripoti ya 

matokeo ya mtihani.Akaipitia na 

kutabasamu 

“Theresa hujawahi 

kuniangusha hata mara 

moja.Safari hii tena umeshika namba mbili.Hongera 

sana.Unastahili zawadi kubwa kwa 

bidii kubwa unayoionyesha 

shuleni” akasema Kanali Sebastian 

na kumpa mkewe ripoti ile naye 

aipitie 

“Zawadi gani utanipatia safari 

hii baba? Theresa akauliza.Kanali 

Matope akafikiri kidogo na 

kusema 

“Kwa kuwa umenifurahisha 

sana kwa matokeo haya mazuri 

nitasafiri nawe kwenda nje ya 

nchi” 

“Kweli baba? Akauliza 

Theresa kwa furaha 

“Ndiyo.Kesho rais ana safari 

ya kwenda Misri.Kuna kikao kifupi 

cha marais wa nchi zinazopitiwa na mto Nile na kwa kuwa mto Nile 

chanzo chake ni Tanzania basi rais 

wetu naye atahudhuria kikao 

hicho.Wakati kikao kinaendelea 

wewe utapata nafasi ya kuzunguka 

katika jiji la Cairo na kama muda 

utaruhusu basi waweza pata nafasi 

kufika katika mapiramidi na 

utajifunza mambo mengi kwa 

kuona kwa macho kuliko kusoma 

tu vitabuni” 

“Ahsante sana baba.Siwezi 

kuelezea furaha yangu.Siamini 

kama na mimi nitasafiri na rais 

hapo kesho” 

“Nitakutambulisha kwa rais 

na kumueleza juhudi zako katika 

masomo.Naamini hata yeye 

mwenyewe atafurahi kwani anapenda sana vijana wanaojituma 

katika kazi na masomo” Akasema 

Kanali Matope na Theresa akaruka 

ruka kwa furaha kubwa. 

“Nitafutahi sana baba kama 

nitapata nafasi ya kwenda 

kujionea mapiramidi kwani 

tumekuwa tunayasoma katika 

historia.Itakuwa ni somo zuri sana 

kwangu kuyashuhudia ana kwa 

ana na nitakuja vile vile 

kuwasimulia wenzangu maajabu 

hayo makubwa ya 

dunia.Tutakwenda sote huko 

katika mapiramidi? Akauliza 

Theresa 

“Hautaongozana na mimi 

Theresa ila nitakutafutia mtu 

kutoka ubalozi wetu ambaye atakutembeza katika sehemu 

mbali mbali za jiji la Cairo na kama 

nafasi itapatikana basi 

atakufikisha hadi katika 

mapiramidi” 

“Jamani baba kwa nini 

usitafute nafasi tukaongozana 

wote?Nitafurahi sana nikiwa nawe 

mtu niliyemzoea ili iwe rahisi hata 

kuuliza maswali” 

“Hata mimi ningefurahi sana 

kama ningepata nafasi ya 

kukutembeza katika jiji la Cairo 

lakini kazi yangu 

hainiruhusu.Natakiwa kuwa 

karibu na rais muda 

wote.Usiogope mtu 

nitakayekutafutia atakuwa 

anaongea kiswahili na utamuuliza kitu chochote utakacho” akasema 

Kanali Matope 

“Kwani baba lile begi ambalo 

huwa unalibeba kila unaposafiri 

na rais lina nini ndani 

yake?Hakuna mtu mwingine 

anayeweza kukusaidia 

kulibeba?Sijawahi kuona mtu 

mwingine analibeba zaidi yako” 

akasema Theresa na kumfanya 

baba yake atabasamu 

“Lile si begi kama mabegi 

mengine.Lile ni begi maalum 

linaitwa football” 

“Football?? Theresa 

akashangaa na kuangua kicheko 

“Ndiyo linaitwa Football.Najua 

umeshangaa kusikia jina hili 

linalomaanisha mpira wa miguu lakini haimaanishi kama begi hili 

linabeba mpira wa miguu.Mle kuna 

mambo ya siri na hubebwa na mtu 

ambaye amekula kiapo cha 

kuhakikisha kwa vyovyote vile 

hata kutokee nini football 

linakuwa salama.Kulibeba begi lile 

lazima upitie mafunzo maalum ya 

komando na kufuzu kwa kiwango 

cha juu.Lengo ni kuhakikisha 

anayelibeba begi lile anakuwa ni 

mtu mwenye mbinu na uwezo 

mkubwa wa kujilinda na kuilinda 

football.Asili ya jina hili ni 

Marekani ambako rais wa 

Marekani ana begi lake ambao 

husafiri nalo kila aendako na 

mataifa mengine yakaiga mtindo 

huo japokuwa kila taifa lina jambo lake linalowekwa ndani yake 

lakini mara nyingi huwa ni siri za 

nchi zinazohusiana masuala ya 

usalama.Hata hivyo muda wangu 

wa kustaafu umekaribia na kuna 

mtu mwingine anayeandaliwa 

kushika nafasi yangu.Nadhani 

nimejibu swali lao” akasema 

kanali Matope 

“Ndiyo nimekuelewa 

baba.Kumbe jukumu ulilolibeba ni 

kubwa na la hatari sana” 

“Ni jukumu kubwa na la hatari 

lakini ulinzi wake ni wa kutosha na 

wa uhakika.Pamoja na uwezo 

wangu mkubwa wa kujilinda na 

kuilinda football lakini kuna 

walinzi wanne ambao kazi yao ni kunilinda mimi na hilo begi” 

akasema Kanali Matope 

“Nini kitatokea endapo begi 

hilo litapotea?akauliza Theresa na 

kanali Sebastian akacheka 

“Football haiwezi 

kupotea.Tumekula kiapo cha 

kuhakikisha tunailinda hadi tone 

la mwisho la damu yetu kwa hiyo 

unapolibeba begi kama lile basi 

uhai wako unauweka rehani ili 

kulilinda.Siku zote football ni 

salama pengine kuliko hata rais” 

akasema kanali Sebastian 

“Baba ahsante ngoja niende 

nikajiandae kwa hiyo safari ya 

kesho” akasema Theresa 

“Theresa kesho vaa mavazi ya 

kawaida na usibebe mzigo mkubwa kwani ni safari ya siku 

moja tu.Chukua vitu vichache 

utakavyovihitaji kwa masaa 

machache” akasema kanali 

Sebastian. 

************** 

Mkutano wa wakuu wa nchi 

zinazopitiwa na mto Nile 

ulimalizika jijini Cairo Misri na saa 

kumi na mbili za jioni rais wa 

Tanzania akaagana na mwenyeji 

wake ambaye ni rais wa Misri 

akaondoka kurejea 

Tanzania.Ilikuwa ni safari nzuri 

sana kwa Theresa ambaye alipata 

nafasi ya kutembelea sehemu mbali mbali za kihistoria 

zinazopatikana jijini Cairo 

Katika safari ya kurejea 

Tanzania walikuwepo pia 

waandishi nane wa habari 

wanaotoka nchini Marekani 

wakielekea nchini Tanzania lakini 

kwa bahati mbaya walichelewa 

ndege yao hivyo ikawalazimu 

kuomba lifti katika ndege ya rais 

ili wawahi ratiba yao ya kuandika 

habari kuhusiana na mbuga za 

wanyama zinazopatikana nchini 

Tanzania.Rais alifurahishwa sana 

na namna waandishi wale 

walivyojitolea kutaka 

kuifahamisha dunia juu ya vivutio 

mbali mbali vya utalii 

vinavyopatikana nchini Tanzania.Ndani ya ndege rais 

alifanya mazungumzo na 

waandishi wale na walijadiliana 

mambo mbali mbali kuhusu 

ukuzaji wa utalii nchini na namna 

ya kutangaza vivutio vilivyopo 

nchini Tanzania.Baada ya 

maongezi ya takribani saa moja na 

nusu waandishi wale wakamuacha 

rais apumzike nao wakaenda 

kuchukua nafasi zao.Ni safari ya 

takribani masaa matano hivyo 

hakukuwa na maongezi mengi mle 

ndegeni na kila mmoja alikuwa 

amejipumzisha baada ya uchovu 

wa kutwa nzima.Hakuna 

aliyetegemea kama kulikuwa na 

hatari yoyote mbele yao Safari iliendelea hadi jijini 

Nairobi ambako ndege ya rais 

ililazimika kutua kwa dharura 

baada ya marubani kubaini 

kwamba ndege imepungukiwa 

mafuta na walikuwa na wasi wasi 

mafuta yaliyopo yasingetosha 

kuwafikisha Dar es 

salaam.Yaliibuka mabishano 

makali kati ya walinzi wa rais na 

marubani wakihoji kwa nini ndege 

ya rais ipungukiwe mafuta? 

Ilimlazimu rais kuingilia kati 

mabishano yale na mafuta 

yakawekwa kisha safari 

ikaendelea 

Muda mfupi baada ya kuingia 

katika anga la Tanzania,ghafla 

kukatokea jambo lililowastua walinzi wa rais.Sehemu ya jikoni 

kulianza kufuka moshi.Iliwalazimu 

walinzi wawili wa rais kwenda 

haraka sana eneo la jikoni kwenda 

kuangalia chanzo cha moto ule na 

mara ikasikika milio ya risasi na 

kuibuka kizaazaa kikubwa mle 

ndegeni.Wale jamaa walioingia 

ndegeni kama waandishi wa 

habari wakainuka na kukimbilia 

eneo la jikoni na baada ya muda 

kila mmoja wao akawa na silaha 

kali.Wote walionekana ni watu 

wenye mafunzo makubwa sana ya 

kupambana kwa kutumia 

silaha.Walianza kushambuliana na 

walinzi wa rais na kuua watu 

hovyo mle ndegeni.Mara tu risasi 

za kwanza ziliposikika na kuzua taharuki,Kanali Sebastian 

alichukuliwa haraka sana pamoja 

na football na kukimbizwa katika 

chumba cha rais ambacho 

kinaaminika ni salama 

sana.Hakumuacha nyuma Theresa 

“Nini kimetokea huko nje? 

Rais akauliza kwa wasi wasi huku 

jasho likimtiririka 

“Tumevamiwa” akasema 

mmoja wa walinzi wa rais huku 

akimvisha rais fulana ya kuzuia 

risasi 

“Tumevamiwa na ani? 

Akauliza rais kwa woga 

“Mzee tunatakiwa tukuondoe 

haraka sana humu ndegeni kwani 

hawa jamaa…...” Hakumaliza 

sentensi yake kwani ikaanza kusikika milio ya risasi karibu na 

chumba cha rais.Watu wote mle 

ndani ya chumba cha rais walivaa 

fulana za kuwakinga na risasi 

pamoja na miavuli mgongoni 

tayari kabisa kwa kuondoka mle 

ndegeni. 

“Mheshimiwa rais 

tuondoke,tayari hawa jamaa 

wamekaribia.Tunakushusha chini 

kwa mwavuli” 

“Hapana.Kitu cha kwanza 

tuhakikishe football iko 

salama.Kabla ya kunitoa mimi 

lazima kwanza tuhakikishe 

Sebastian na football ametoka 

humu ndegeni” akasema rais 

“Mheshimiwa rais jukumu letu 

kubwa ni kuhakikisha unakuwa salama.Wewe kwanza halafu 

wengine watafuata” akasema 

mmoja wa walinzi wake akiwa 

amemshika mkono rais 

“Hapana kwanza footb…….” 

Kabla hajamaliza sentensi yake 

ukatokea mlipuko wa baruti na 

kuusambaratisha mlango wa 

kuingilia mle chumbani mwa rais 

na risasi zikaanza 

kumiminwa.Walinzi wa rais nao 

wakajibu mapigo kwa kumimina 

risasi wakimkinga rais 

asishambuliwe. 

‘Seba run..!!! akapiga kelele 

rais na kwa kasi ya aina yake 

Sebastian akamshika mkono 

Theresa akamvuta wakaingia 

jikoni huku mlinzi wake mmoja akiwa nyuma yao.Sebastian 

alifahamu vyema ndege hii ya rais 

na mfumo wake wote wa 

usalama.Pale jikoni kulikuwa na 

mlango unaoingia chumba cha 

stoo.Wakaingia na kulifunua zuria 

katikati ya stoo kulikuwa na 

mlango mdogo unaofunguliwa kwa 

namba.Akabonyeza namba kadhaa 

haraka haraka na mlango 

ukafunguka.Kulikuwa na ngazi ya 

kushuka chini.Akaingia na 

kumshika mkono Theresa 

wakaingia ndani na kushuka ngazi 

kuelekea chini.Ghafla milio ya 

risasi ikasikika mle stoo. 

“The football !!!!..akapiga 

kelele mmoja wa wale jamaa 

aliyeingia stoo na kukuta mlango umefunguliwa na kuna ngazi za 

kushuka chini.Wenzake watatu 

wakaja na kuungana naye kisha 

kwa haraka wakaanza kushuka 

chini kuifuata ile ngazi 

waliyotumia akina Sebastian 

kushukia chini 

Sebastian na mwanae Theresa 

na mlinzi mmoja walifika katika 

sehemu ya kufungulia mlango wa 

dharura wa ndege ambao ni 

maalum kwa ajili ya kumuokoa 

rais.Wakiwa wanajadiliana ghafla 

wakatokea wale jamaa na kuanza 

kuwarushia risasi.Umahiri wa 

Kanali Sebastian na mlinzi wake 

katika silaha ulisaidia kiasi cha 

kuwafanya wale jamaa wajifiche 

na Sebastian akautumia mwanya huo kubonyeza sehemu ya 

kufungulia mlango wa dharura 

ukafunguka.Mara ghafla wale 

jamaa wakaibuka wote watatu kwa 

pamoja toka mahala walipokuwa 

wamejificha na kuanza kumimina 

risasi.Kanali Sebastian akamshika 

mkono mwanae Theresa na 

kuruka nje.Sebastian hakumuachia 

Theresa katika upepo ule mkali na 

giza nene,walishuka kwa kasi 

kubwa na mara mwavuli aliokuwa 

ameuvaa kanali Sebastian 

mgongoni ukafunguka na 

wakaanza kushuka chini taratibu. 

Kumbukumbu ile ikamfanya 

Theresa ahisi baridi ghafla na 

woga mkubwa.Akatoka mle katika 

ofisi akaenda kuzunguka zunguka ndegeni kuhakiki kwamba hakuna 

mtu yeyote wa kumtilia shaka mle 

ndani ya ndege.Kumbu kumbu ya 

tukio lile lililotokea kwa miaka 

kumi iliyopita ilimstua 

mno.Alibadilishana mawazo na 

walinzi wa rais halafu akaenda 

kuketi kitini.Alihisi hali yake 

kuanza kubadilika 

“Miaka zaidi ya kumi imepita 

sasa lakini bado naona kama tukio 

lile limetokea jana.Bado ninakuwa 

na woga mkubwa kila ninaposafiri 

na rais.Mimi na baba ndiyo pekee 

tulitoka salama katika ile ndege 

kwani ilianguka karibu na wanja 

wa ndege wa kimataifa wa 

Kilimanjaro na wote waliokuwemo 

ndani walifariki dunia.Kwa sasa ni mimi pekee niliyebaki hai ambaye 

ninafahamu nini kilitokea usiku 

ule.Ni tukio la kutisha sana ambalo 

halitaweza kamwe kunitoka 

kichwani mwangu.Siwezi 

kulisahau giza lile nene kama vile 

tuko jehanamu. Namshukuru sana 

baba kwani alipambana kwa kila 

alivyoweza hadi akafanikiwa 

kuniokoa vinginevyo na mimi 

ningekufa kwani hakuna yeyote 

aliyekuwa ananijali zaidi yake” 

akaendelea kuwaza 

“Watu wale waliofanya lile 

shambulio walikuwa na lengo la 

kuipata football lakini baba kwa 

umahiri alifanya kila awezalo na 

kuhakikisha hawafanikiwi lengo 

lao na football ikawa salama.Hii inaonyesha ni namna gani begi lile 

lilivyokuwa na thamani kubwa 

sana.Limebeba mambo mazito 

.Hata rais mwenyewe alipotakiwa 

awe wa kwanza kutoka mle 

ndegeni alisema hawezi kutoka 

yeye kabla football haijatoka 

ndegeni.Wote waliipa football 

uzito mkubwa sana.Kuna siri gani 

ndani ya hiyo football?Liko wapi 

lile begi?Nakumbuka tulipofika 

chini tulitua katika msitu mmoja 

uliokuwa karibu na makazi ya 

watu.Sikumbuki ilikuwa saa ngapi 

ila tulitembea hadi tulipoikuta 

barabara kuu.Baba akaniambia 

kwamba pale tulipo palikuwa ni 

usa river.Tulilala pale na asubuhi 

siku iliyofuata tulipanda basi hadi Dar es salaam.Baba alikuwa na lile 

begi na baada ya hapo sikuwahi 

kuliona tena.Sifahamu amelificha 

wapi ila aliniachia mkufu huu 

wenye msalaba wa dhahabu na 

kunitaka niutunze na niuvae kwa 

siku zote za maisha 

yangu.Alinielekeza nimpatie 

mkufu huu rais atakayekuwepo 

madarakani baada ya miaka kumi 

kupita toka ajali ile kutokea.Rais 

aliyepo madarakani baada ya hiyo 

miaka kumi kupita ni mwanae 

Vivian.Alihisi kwamba mwanae 

anaweza kuwa rais kwa kipindi 

hiki? Hata hivyo nimeogopa 

kumpatia dada Vivian huu mkufu 

kwa kuhofia maisha yake.Naamini 

mkufu huu una jambo kubwa na ndiyo maana akaniomba niutunze 

na nije kumpa rais wa 

sasa.Nimekuwa najiuliza maswali 

mengi sana kuhusiana na mkufu 

huu,je una muunganiko wowote na 

football?Begi lile la football baba 

alilificha wapi? Au alilirejesha 

ikulu?Kila mara maswali haya 

yamekuwa yanakifanya kichwa 

changu kigonge kwani sijawahi 

pata majibu yake.Baba ameniachia 

mzigo mzito sana na sijui nitautua 

vipi au nani nimtwishe? Akawaza 

Theresa na kumbu kumbu 

nyingine ikamjia.



NOVEMBER 2007 – DAR ES 

SALAAM 

Imekwisha pita miezi minne 

toka ilipotokea ajali ya ndege ya 

rais na kuua watu wote 

waliokuwemo ndani yake 

isipokuwa kanali Sebastian na 

Theresa pekee.Kanali Sebastian 

alipata wakati mgumu sana kwani 

vyombo vya uchunguzi ambavyo 

vilimuhoji sana kuhusiana na 

kilichotoka katika ajali ile na 

namna alivyoweza 

kusalimika.Pamoja na kuhojiwa 

sana lakini Kanali Sebastian 

hakuwahi kuweka wazi kwamba 

alinusurika yeye na Theresa.Mara 

zote alisimama katika msimamo 

wake mmoja kwamba aliyenusurika katika ajali ile 

alikuwa ni yeye peke yake na 

hakutaka kumuhusisha kabisa na 

Theresa.Kama mtu pekee 

aliyekuwa amelibeba begi la siri 

maarfu kama football alihojiwa 

mahala liliko begi hilo na 

hakuwahi kueleza 

ukweli.Alichokieleza na ambacho 

hakikuwa kweli ni kwamba walinzi 

wawili wa rais waliasi na kutaka 

kumuua rais na kikatokea kizaa 

zaa ndegeni na alipotaka kutoroka 

na mkoba ule wa football ulipigwa 

risasi na ili kuokoa maisha yake 

akaamua kuachia na kuruka nje . 

“Mpaka leo sielewi ni kwa nini 

baba hakutaka kuweka wazi 

kuhusiana na kile kilichotokea ndegeni na kuhusu ile 

football.Hajawahi mweleza mtu 

yeyote mahala alikoificha.Kwa nini 

aliamua kuificha badala ya 

kuirejesha serikalini wakati akijua 

kabisa kwamba kuna siri za 

serikali mle ndani? Kwa nini afiche 

siri za nchi? akajiuliza Theresa 

“Ninajiuliza maswali haya 

lakini siwezi kuyapatia majibu.Mtu 

pekee ambaye angeweza kuwa na 

majibu sahihi ni baba lakini 

hayupo.Hapo ndipo huwa 

ninachoka na kuamua kuliacha 

suala hili kama lilivyo na 

kuendelea kuibeba siri hii hadi 

siku nitakapoingia kaburini japo 

naamini baba alikuwa namakusudi yake kufanya vile 

alivyofanya” akawaza 

“Lakini ni kweli niko tayari 

kuendelea kuibeba siri hii hadi 

kaburini? Nimekuwa najiuliza 

swali hili mara kadhaa lakini kila 

ninapomuangalia dada najikuta 

sina namna ya kufanya zaidi ya 

kuendelea kuibeba japo baba 

alinitaka nimpatie rais wa sasa 

mkufu huu.Sina hakika kama alijua 

mwanae ndiye atakayekuwa rais 

wa Tanzania baada ya kipindi cha 

miaka kumi.Hapana sintamueleza 

Vivian kwani kufanya hivyo ni 

kumuweka hatarini.Baba alitolewa 

uhai wake kwa sababu ya jambo 

hili na hata mimi nilinusurika 

kuuawa kwa sababu kwanza nilikuwa mwanafunzi na pili baba 

hakuwahi kuweka wazi kwamba 

nilikuwemo katika ndege ile ya 

rais.Kama ningejulikana lazima 

ningeuawa pia” akaendelea 

kuwaza Theresa na machozi 

yakamtoka akawahi kuyafuta ili 

mtu yeyote asigundue kwamba 

alikuwa katika mawazo mazito 

“Masikini familia yangu 

waliuawa kikatili mno na 

nilishuhudia kila kitu.Mpaka leo 

bado picha za mauaji yale zinanijia 

usingizini.Bado namuona baba 

akianguka na kufa huku 

akimiminiwa risasi kama 

mnyama” 

Theresa akashindwa kuyazuia 

machozi yasimtoke.Kumbu kumbu ya namna walivyouawa wazazi 

wake ilipomjia. 

April Hudson Mubara mjane 

wa rais Anorld Mubara alirejea 

nchini akitokea Marekani 

alikoenda mapumzikoni baada ya 

kifo cha mume wake.Moja kwa 

moja alienda kuishi katika shamba 

lao lililokuwepo katika kijiji cha 

mchangawima Chalinze.Alitaka 

apumzike sehemu yenye utulivu 

mkubwa.Baada ya kufahamu 

kwamba amerejea nchini Kanali 

Sebastian alimpigia simu na 

kumtaarifu kwamba atakwenda 

kuonana naye kumpa pole kwani 

toka yalipofanyika mazishi ya rais 

Anorld hawakuwahi kuonana 

tena.Bi April alikubali kuonana na Kanali Sebastian kwani alikuwa 

mtu wa karibu sana na mumewe 

na wakapanga siku ya 

kuonana.Siku ilipofika Kanali 

Sebastian akaichukua familia yake 

yote ili kwenda kumpa pole Bi 

April kwa kifo cha mume wake. 

Wakiwa wameikamata 

barabara inayoelekea katika 

shamba la rais Anorld,mara kwa 

mbele wakakuta kizuizi cha askari 

na magari mawili ya askari 

yameegeshwa pembeni.Ni eneo 

lililokuwa kimya sana na 

hakukuwa na watu eneo hili na 

mahala polisi walipoweka kizuizi 

chao kulikuwa na vichaka vichaka. 

“Hawa askari wanafanya nini 

huku? Mbona wameweka kizuizi kwani kuna magari yanakuja huku 

zaidi ya machache yanayokwenda 

katika shamba la rais Anorld? 

Akauliza mke wa kanali 

Sebastian.Alionyesha wasiwasi 

“Barabara hii inakwenda 

katika shamba la rais.Inawezekena 

wanaimarisha ulinzi ili kuzuia 

watu wasiotambulika kwenda 

katika nyumba ya rais wakati huu 

ambao bi April yupo huku kwa 

mapumziko” akasema kanali 

Sebastian 

“Hata kama ni ulinzi kwa nini 

wasilinde askari wachache?Mbona 

hawa wako zaidi ya kumi? 

Akauliza mke wa Sebastian na 

askari mmoja akasimama kati kati 

ya barabara akanyoosha mkono akamtaka kanali Sebastian 

asimamishe gari.Taratibu 

akapunguza mwendo na 

kusimamisha gari pembeni ya 

barabara kama 

alivyotakiwa.Akafungua mlango na 

kushuka ili ajitambulishe kwa 

askari wale na wamruhusu apite 

lakini alipopiga hatua kama tatu 

kuwaendea,ghafla ikasikika milio 

ya risasi.Kanali Sebastian 

akaanguka chini.Ndani ya gari mke 

wake, ,mwanae Kelvin na Theresa 

walipatwa na mshangao mkubwa 

sana kwa kitendo kile.Haraka 

haraka Kelvin akashuka garini ili 

kumkimbilia baba yake 

aliyeanguka pale chini lakini 

alipotaka kumuinamia baba yake naye akachezea mvua ya risasi na 

kuanguka karibu na baba yake 

“Theresa hawa si 

polisi.Tafadhali fanya 

nitakavyokuelekeza.Jifiche chini ya 

kiti na usiinue kichwa hadi 

nitakapokuelekeza.Ninataka 

kulirudisha nyuma gari hili ili 

tujaribu kujiokoa vinginevyo 

watatuua” Akasema mke wa kanali 

Matope na kukaa sehemu ya 

dereva akaukamata usukani na 

kuweka gia ya kurudi nyuma kisha 

akakanyaga pedeli ya mafuta na 

kwa kasi ya aina yake gari likaanza 

kurudi nyuma.Askari kama 

watano wakaanza kulikimbiza lile 

gari huku wakirusha risasi lakini 

kwa ujasiri mkubwa Getruda Matope mke wa kanali Sebastian 

matope akafanikiwa kulirudisha 

gari nyuma na kupata sehemu ya 

kugeuza na kisha akaliondoa kwa 

kazi kubwa.Theresa aliyekuwa 

amejificha chini ya kiti cha nyuma 

akainua kichwa baada ya kusikia 

mama yake anakoroma. 

“Mama” akaita Theresa na 

kugundua kwamba mama yake 

alikuwa anatokwa na damu 

mdomoni.Alikuwa amepigwa risasi 

tumboni.Ghafla akakanyaga breki 

kwa nguvu na gari likaserereka 

hadi katika shamba la 

mpunga.Getruda alikuwa anavuta 

pumzi kwa taabu sana na damu 

ikimtoka mdomoni “mama !! akaita Theresa huku 

akilia 

“Theresa…r..un..ruuuuun..!! 

“Hapana mama.Siwezi 

kukuacha hapa peke yako !! 

akasema Theresa 

“Run..Thr..ru…rr…runnnnn!! 

akasema Getruda kwa taabu na 

kuvuta pumzi ndefu akaangukia 

usukani.Theresa akaliona vumbi 

kubwa nyuma yao linakuja kwa 

kasi akajua ni zile gari mbili za 

askari akafungua mlango na 

kushuka akaanza kukimbia 

akikatisha katika shamba la 

mpunga.Alihisi miguu yake haina 

nguvu lakini akajitahidi kwa kadiri 

alivyoweza hadi alipolipita shamba la mpunga na kuingia katika 

shamba la michungwa. 

Akaweka mikono masikioni 

mwake na kuhisi kutetemeka 

mwili 

“Bado nasikia milio ie ya risasi 

masikioni mwangu hadi leo 

hii.Kwa mara ya pili nilinusurika 

kuuawa.Bila ujasiri wa mama na 

mimi hivi sasa ningekuwa mfu” 

akawaza na kufuta machozi 

“Nahisi baba alitabiri kifo 

chake kwani wiki moja tu kabla ya 

kifo chake ndipo aliponipa huu 

mkufu wenye msalaba.Aliamini 

hataweza kufika wakati huu na 

ndiyo maana akanibebesha mimi 

siri kubwa iliyo katika msalaba 

huu na laiti kama ningejulikana basi ningekwisha 

uawa.Nitaendelea kuubeba huu 

msalaba hadi siku naingia 

kaburini.Nitakapofungua tu 

mdomo wangu na kuropoka 

chochote ndio utakua mwisho 

wangu,sintabaki salama” 

akaendelea kuwaza Theresa na 

kuinuka akaelekea bafuni akalia 

machozi mengi sana halafu 

akanawa uso na kujipaka poda 

upya usoni ili asitambulike kama 

alikuwa analia.Akavaa miwani 

myeusi kuficha macho yake na 

kurejea kukaa akaendelea na kazi 

zake huku dege likiendelea 

kuchana anga kuelekea New york 

Marekani. 

OFISI ZA USALAMA WA TAIFA 

– DAR ES SALAAM 

Shughuli ziliendelea kama 

kawaida katika jengo hili la ofisi za 

usalama wa taifa.Baada ya kurejea 

toka uwanja wa ndege wa 

kimataifa wa Julius Nyerere 

kumuaga rais,mkurugenzi wa 

idara ya usalama wa taifa George 

Mzabwa akahudhuria vikao viwili 

vya kazi halafu akaenda kujifungia 

ofisini kwake.Alijiegemeza kitini 

na kuzama mawazoni.Aliwaza sana 

na halafu akachukua karatasi 

akaanza kuandika.Alipomaliza 

akasoma kile alichokiandika 

akaridhika na kuiweka karatasi ile katika bahasha na juu ya bahasha 

ile akaandika 

TO MADAM PRESIDENT.Akaiweka 

mezani barua ile halafu akafunga 

mlango kwa funguo na kusimama 

kati kati ya ofisi.Akaitazama ofisi 

yake ,akatoa bastora na kuitazama 

kwa uchungu 

Wafanyakazi wa ofisi hii ya 

usalama wa taifa wakiwa 

wanaendelea na shughuli zao za 

kawaida walistushwa na mlio wa 

risasi.Shughuli zikasimama ghafla 

na wote wakijiuliza nini 

kimetokea.Tahadhari zikaanza 

kuchukuliwa haraka kubaini risasi 

ile imelia toka wapi ndani ya jengo 

lile.Wakati wakijiuliza huku kila 

mmoja akiwa katika tahadhari kubwa na ulinzi ukiwa 

umeimarishwa katika sehemu zote 

za kuingilia na kutokea,Stella 

katibu muhtasi wa George Mzabwa 

alishuka ngazi huku akikimbia na 

kupiga kelele.Akatoa taarifa 

kwamba amesikia mlio wa risasi 

katika ofisi ya George.Haraka 

haraka watu wakakimbilia ofisini 

kwa George na kujaribu kugonga 

mlango lakini hakukuwa na mtu 

yeyote aliyeitikia toka 

ndani,wakapiga simu ya George 

ikaita bila kupokelewa hivyo 

ikawalazimu kuuvunja mlango na 

kuingia ndani wakamkuta George 

Mzabwa amelala sakafuni damu 

ikimvuja na pembeni yake 

kulikuwa na bastora.Hakuwa na uhai na ubongo wake 

ulisambaa.Alikuwa amejipiga 

risasi kichwani.Uchunguzi 

ukafanyika ili kuona kama 

shambulio lile lilifanywa na mtu 

kutokea nje lakini hakukuwa na 

dalili zozote za kuonyesha kama 

George alishambuliwa kutokea 

nje.Hili lilikuwa ni tukio 

lililomshangaza kila 

mmoja.Hakuna aliyefahamu 

sababu ya George kujiua kwani 

muda mfupi uliopita alikuwa na 

uso wenye furaha kabisa na 

hakuonyesha kama ana tatizo 

lolote.Juu ya meza yake kulikutwa 

barua aliyomuandikia rais muda 

mfupi kabla ya kifo chake. Polisi walitaarifiwa wakafika 

kwa haraka na baada ya 

kujiridhisha kwamba George 

alijiua mwenyewe wakaondoka na 

mwili wake kuupeleka hospitali 

kwa ajili ya kuuhifadhi na taratibu 

nyingine kabla ya kuukabidhi kwa 

familia yake 

************ 

Dr Vivian akiwa 

amejipumzika katika chumba 

chake huku dege likiendelea 

kupasua anga kuelekea 

Marekani,simu iliyomo mle 

chumbani inayotumia mtandao wa 

intanet ikaita.Akainua mkono wa 

simu na kuipokea “Hallow” akasema Dr Vivian 

“Madam president pole na 

safari ni mimi Dr Makame” 

akasema makamu wa rais wa 

jamhuri ya muungano wa Tanzania 

“Ahsante Dr Makame.Sisi tuko 

angani tunaendelea na 

safari.Mnaendeleaje huko? 

“Habari za huku si njema 

sana.Kuna tukio limetokea ambalo 

nimeona ni vyema nikikujulisha 

mapema” 

“Nini kimetokea Dr makame? 

“George Mzabwa mkurugenzi 

wa idara ya usalama wa taifa 

amefariki dunia” 

“George amefariki dunia?!! Dr 

Vivian akastuka “Ndiyo mheshimiwa 

rais.Nimeletewa taarifa hizo na 

nimezithibtisha kupitia inspekta 

generali wa polisi” akasema Dr 

makame na rais akavuta pumzi 

ndefu 

“Amefariki vipi?Amepata 

ajali? 

“Amejipiga risasi kichwani 

mheshimiwa rais” 

Uso wa Dr Vivian ulionyesha 

mstuko mkubwa.Hakuwa 

ametarajia kusikia habari kama ile 

“Madam president” akaita 

makamu wa rais baada ya kuona 

kumekuwa kimya. 

“Nimestushwa sana na taarifa 

hizi.Imekuaje hadi George 

akachukua maamuzi hayo magumu ya kujiua?akauliza Dr 

Vivian 

“Hilo ni jambo 

linalomshangaza kila 

mmoja.Hakuna aliyetegemea kama 

angeweza kuchukua maamuzi 

kama haya ya kujiua.Tulikuwa 

wote uwanja wa ndege asubuhi 

tukasalimiana na alikuwa vizuri 

tu,hakuonyesha tatizo 

lolote.Hatujui nini kilimsibu hadi 

akachukua mamauzi haya,hata 

hivyo kuna barua imekutwa 

mezani kwake ambayo 

amekuandikia wewe.Tunadhani 

aliiandika muda mfupi kabla 

hajajiua” “Ameniandikia barua? Kuna 

yeyote ameifungua na kuisoma? 

Akauliza Dr Vivian 

“Hapana madam president 

hakuna aliyeifungua.Imefungwa 

ndani ya bahasha” 

“Good.Ihifadhi hadi 

nitakaporejea” 

“Sawa madam president” 

“Jambo lingine,nataka 

ufanyike uchunguzi kwa mara 

nyingine wa kina kujiridhisha 

kama kweli George Mzabwa 

amejiua au kuna watu 

waliomuua.Inashangaza sana kwa 

mtu kama George kuchukua 

maamuzi haya magumu” 

“Sawa madam president 

nitaelekeza hivyo.Nawatakieni 

safari njema” 

“Ahsante sana Dr Makame 

kwa taarifa.Hakikisha uchunguzi 

huo unafanyika haraka.Kuanzia 

nyumbani kwake,ofisini kote 

kupekuliwe ili sababu ya George 

kujiua ijulikane” akasema Dr 

Vivian na kukata simu 

“George amejiua …” akasema 

na kuzidi kushangaa 

“Lakini kwa nini afanye hivi? 

Kwa nini ajiue?Kwa nini iwe sasa? 

Kuna kitu gani kimemkwaza 

?akaendelea kujiuliza maswali 

“Jambo hili linahitaji 

uchunguzi wa kina kubaini sababu 

ya kujiua.Nitaisoma hiyo barua aliyoniandikia kujua alichokisema 

lakini nimestuka 

sana,sikutegemea kama anaweza 

akafanya jambo kama hili” 

akawaza Dr Vivian 

“Au yale maneno 

niliyomwambia asubuhi pale 

uwanja wa ndege yamemkwaza? 

Nilimtaka nitakaporejea nikute 

ripoti ya uchunguzi au nikute 

barua yake ya kuachia nafasi 

yake.Yawezekana amefikiria sana 

na akaamua kujiua.Apumzike kwa 

amani huko aliko kwani hata hivyo 

alikuwa katika orodha ya viongozi 

ambao utendaji wao wa kazi 

haujaniridhisha.Nitatafuta mtu 

mahiri na mchapakazi 

atakayechukua nafasi yake na atakayekuwa tayari kufanya kazi 

kwa kasi ninayoitaka.Kipimo cha 

mtendaji ninayemtaka ni kutegua 

kitendawili cha vifo vya wazazi 

wangu.Haiwezekani mpaka leo hii 

yapata miaka kumi suala hili 

limeshindwa kupata 

majibu.Limekuwa ni fumbo 

lililoshindwa kufumbuliwa.Tuna 

vyombo mahiri kabisa kwa 

uchunguzi lakini kwa nini 

wameshindwa kubaini nani 

aliteketeza familia yangu?Halafu 

kuna hili begi ambalo baba 

alikuwa analibeba enzi za utawala 

wa rais Anorld liko wapi? Lilipotea 

rais Anorld alipofariki katika 

ajali?Nahisi hivyo kwani hata rais 

aliyefuata baada ya Anorld hakuwahi kuwa na lile begi ambalo 

rais Anorld alikuwa anatembea 

nalo kila aendako.Mfumo ule 

uliigwa toka marekani ambao wao 

ndani ya begi hilo wanaloliita 

football kuna nuclea codes lakini 

sisa hatuna nyuklia je kwa nini rais 

Anold alikuwa anatembea na begi 

lile kila aendako?Siri gani alikuwa 

anatembea nayo?Swali lingine 

ambalo bado mpaka leo sijapata 

majibu yake ni je baba aliokoka 

vipi toka katika ndege ile ya 

rais?Maelezo aliyotoa baba 

hayajawahi kuniingia akilini.Bado 

naamini kuna vitu vinakosekana 

katika maelezo yake aliyoyatoa 

kwa vyombo vya uchunguzi baada 

ya ajali.Kwa bahati mbaya nyumba yake iliungua moto muda mfupi 

baada ya kufariki kwahiyo hakuna 

mahala kokote tunakoweza kupata 

taarifa zake zozote.Laiti 

kungekuwa na nyaraka zake 

zozote tungeweza kuzichambua na 

kugundua kama kuna jambo 

alikuwa analificha.Hili jambo kweli 

ni fumbo gumu na ili kulifumbua 

ninahitaji mtu jasiri na mahiri 

ambaye anaweza kulishughulikia 

jambo hili na kulipatia majibu.Kwa 

miaka takribani miwili sasa tangu 

nilipompa George alishughulikie 

jambo hili hakuna majibu yoyote 

na badala yake leo amejipiga risasi 

na kufa.Ukiacha hii miaka miwili 

niliyompa George,vyombo vya 

uchunguzi vimelichunguza jambo hili kwa miaka zaidi ya kumi sasa 

na mpaka leo hakuna majibu 

yoyote.Kuna nini hapa?Hii 

inanifanya nizidi kuamini kwamba 

kuna kitu kimejificha katika jambo 

hili na sintachoka hadi nihakikishe 

nimeufahamu ukweli na wahusika 

wanakamatwa na kufikishwa 

mbele ya sheria” akawaza Dr 

Vivian na kutoka mle chumbani 

akamuita Edwin Swai mmoja kati 

ya washauri watatu wa mambo ya 

usalama wakaenda katika chumba 

cha mazungumzo ya faragha 

“Edwin kuna taarifa 

nimeipokea muda mfupi uliopita 

toka Dar es salaam ambayo si 

nzuri.George Mzabwa amefariki 

dunia” akasema Dr Vivian “George amefariki dunia?Nini 

kimemuua?Amepata ajali?Akauliza 

Edwin naye akishangazwa na 

taarifa zile 

“Hajapata ajali amejiua kwa 

kujipiga risasi” 

“Amejipiga risasi? 

“Ndiyo amejipiga risasi ofisini 

kwake” 

“Oh my God !! akasema Edwin 

kwa masikitiko 

“Inasikitisha lakini pia 

inashangaza sana kwa maamuzi 

haya aliyoamua kuyachukua 

George.Mungu ampumzishe kwa 

amani” akasema rais 

“Amen” akajibu Edwin . 

“Kufuatia tukio hilo nahitaji 

kuiziba nafasi ya George hivyo nahitaji kumpata mtu mahiri sana 

ambaye anaweza kuiongoza idara 

ya usalama wa taifa kwa umahiri 

mkubwa.Utendaji wa George 

haukuwa umeniridhisha hata 

kidogo na hata hivyo nilikuwa 

katika mipango ya 

kumuondoa.Wewe umekuwa 

katika mambo haya ya usalama 

kwa muda mrefu hivyo naamini 

unawafahamu watu wengi wazuri 

na wanafaa kuongoza idara ya 

usalama wa taifa,ninakuomba 

upendekeze watu watatu 

unaowaamini na mimi nitachagua 

mmoja” akasema Dr Vivian 

Edwin akafikiri kwa muda 

kisha akasema “Sawa madam president 

nitajitahidi kulifanyia kazi hilo 

jambo kuanzia sasa na hadi 

tutakaporejea Dar es salaam 

nitakukabidhi mafaili ya watu 

watatu nitakaowapendekeza kwa 

ajili ya kuziba nafasi ya George 

Mzabwa” akasema Edwin 

“Nitashukuru sana.Zingatia 

sihitaji tu mtu wa kuziba nafasi 

bali nahitaji mtu ambaye 

anafahamu nini anakifanya na 

anayeweza kufanya kazi zake kwa 

umahiri mkubwa sana.Idara ya 

usalama wa taifa ni idara nyeti 

kwa nchi hivyo hatuwezi kuiweka 

kwa mtu kwa kuwa ni rafiki yetu 

bali anatakiwa mtu mwenye uwezo wa kuiongoza kwa weledi 

mkubwa” akasema Dr Vivian 

“Nitalizingatia hilo 

mheshimiwa rais katika 

mapendekezo yangu 

nitakayokupa” akasema Edwin 

“Good.Jambo la pili nahitaji 

kupata mpelelezi mahiri sana kuna 

kazi nyeti nataka anisaidie 

kuifanya.Naamini unaweza 

ukamfahamu mpelelezi yoyote 

mahiri sana hivyo nisaidie niweze 

kumpata” akasema Dr Vivian 

“Madam president tunao 

wapelelezi wengi mahiri hapa 

nchini.Wapo waliobobea katika 

chunguzi za ndani,wapo wabobezi 

katika chunguzi za kimataifa,tunao 

wa kila aina.Sijui unahitaji mpelelezi mwenye sifa zipi? 

Akauliza Edwin 

“Edwin itakuwa vyema kama 

nikikuweka wazi kuhusu jambo 

ninalotaka kulichunguza.Nataka 

kuchunguza na kuupata ukweli 

kuhusiana na mauaji ya familia 

yangu.Nadhani unafahamu kama 

familia yangu iliuawa kwa siku 

moja na na mpaka leo hii imepita 

miaka zaidi ya kumi hakujawahi 

kutolewa ripoti yoyote ya 

uchunguzi na wala hakuna 

aliyewahi kukamatwa kuhusiana 

na mauaji yale.Jambo hili limebaki 

kuwa kama fumbo gumu 

kulifumbua.Jeshi la polisi,usalama 

wa taifa wote wamelichunguza 

jambo hili na mpaka leo hakuna ripoti yoyote.Nahitaji mtu wa 

kuweza kulifumbua fumbo hili.Mtu 

ambaye anaweza kutafuna mfupa 

huu uliowashinda wengi.Hata 

kama ni mtu wa kutoka nje niko 

tayari kumlipa kiasi chochote cha 

fedha ili mradi uwe na uhakika 

kwamba ana uwezo wa kulifumbua 

fumbo hili.Sitaki kuamini eti suala 

hili limeshindwa kupatiwa 

ufumbuzi hadi leo kama Marekani 

walivyoshidwa hadi leo hii kupata 

ufumbuzi kuhusiana na mauaji ya 

wanamuziki Tupac na Christopher 

Wallace.Bado nina matumaini 

makubwa kwamba endapo 

utafanyika uchunguzi wa kina 

walioufanya mauaji haya lazima 

watapatikana.Hayakuwa mauaji ya bahati mbaya waliotekeleza 

mauaji yale walikuwa na sababu 

zao na ninataka kufahamu hiyo 

sababu ndiyo maana nahitaji mtu 

mahiri sana ambaye nitampa kila 

nyenzo atakayohitaji ili aweze 

kufanikisha uchunguzi huu” 

Akasema Dr Vivian.Edwin Swai 

akakuna kichwa kidogo na kusema 

“Mheshimiwa rais 

nakubaliana nawe kwamba hili 

suala la kifo cha kanali Sebastian 

ni gumu na kama ulivyosema 

uchunguzi wake umechukua zaidi 

ya miaka kumi.Nadhani huu ni 

uchunguzi uliokuwa mrefu zaidi 

kuwahi kufanyika hapa nchini na 

kama kwa muda huo wote 

hawajapata wahusika basi ni wazi hawataweza kufanikiwa 

kuwapata.Wazo la kumtafuta 

mpelelezi ambaye ataweza 

kulifumbua fumbo hili ni wazo zuri 

na hata mimi nakubaliana nalo 

lakini..” akasita kidogo 

“Mbona umesita Edwin? 

Akauliza akauliza Dr Vivian 

“Kwa uchunguzi mkubwa 

kama huu anahitaji mtu mwenye 

umahiri wa pekee.Kwa wale 

ninaowafahamu mimi sina uhakika 

kama kuna mmoja wao anaweza 

kuwa na sifa ya kulichunguza suala 

hili.Kuna mtu mmoja ambaye yeye 

anaweza kukusaidia katika jambo 

hili.Anaitwa Meshack Jumbo.Huyu 

mzee aliwahi kuiongoza idara ya 

ujasusi wa kimataifa kwa miaka mingi na kwa ufanisi 

mkubwa.Huyu nina imani anaweza 

kukutafutia mtu sahihi 

atakayekufaa” akasema Edwin 

“Anapatikana wapi huyo 

Meshack Jumbo? 

“Anaishi Dr es 

salaam.Amekwisha staafu kazi na 

kwa sasa anapumzika 

anajishughulisha na shughuli zake 

ndogo ndogo.Ninaweza 

kumuandaa ili mkutane muongee 

tutakaporejea Dar es salaam” 

Dr Vivian akafikiri kidogo na 

kusema 

“Sawa nahitaji kuonana 

naye.Usimweleze chochote 

kuhusiana na haya niliyokwambia.Nitamwambia mimi 

mwenyewe” 

“Sawa madam president” 

akasema Edwin na kutoka mle 

katika kile chumba.Rais 

akazunguka zunguka ndegeni 

kuzungumza na watu alioongozana 

nao na mara akamuona Theresa 

na kustuka kidogo 



Sawa madam president” 

akasema Edwin na kutoka mle 

katika kile chumba.Rais 

akazunguka zunguka ndegeni 

kuzungumza na watu alioongozana 

nao na mara akamuona Theresa 

na kustuka kidogo 

“Kuna tatizo Theresa,mbona 

umejitenga huku peke 

yako?akauliza 

“Hapana dada Vivian.Sina 

tatizo lolote ni uchovu tu” akajibu 

Dr Vivian akaketi katika kiti cha 

pembeni yake 

“Nakufahamu vizuri 

Theresa,kama kuna jambo 

linakusumbua au limekukwaza huwa unapenda kujitenga na 

kukaa peke yako.Niambie tafadhali 

kama kuna tatizo lolote.Au 

umekwazika na yale maneno 

nilikwambia kuhusiana na ile 

hotuba? Akauliza Dr Vivian 

“Dada Vivi sina tatizo 

lolote.Nimeamua nikae hapa 

nitafakari mambo yangu .Kama 

ningekuwa na tatizo ningekwisha 

kueleza” akasema Theresa 

“Bado tuna safari ya saa 

kadhaa jitahidi basi upate nafasi ya 

kutosha ya kupumzika.Tukifika 

New York nitakuwa na mambo 

mengi ya kufanya kwa hiyo nafasi 

ya kupumzika ni finyu sana” 

akasema Dr Vivian huku akiinuka na mara akakumbuka kitu na 

kukaa 

“Nimepewa taarifa na 

makamu wa rais muda mfupi 

uliopita George Mzabwa amefariki 

dunia” 

“George amefariki?! Theresa 

akastuka 

“Ndiyo kafariki.Amejipiga 

risasi ofisini kwake” 

Theresa akamtazama dada 

yake kwa mshangao 

“Kwa nini amefanya hivyo? 

Kwa nini kachukua maamuzi hayo 

ya kujitoa uhai? Akauliza 

“Hakuna anayejua kwa nini 

amechukua maamuzi 

haya.Nimeagiza uchunguzi wa kina 

ufanyike kubaini sababu ya yeye kujiua.Kwa upande mwingine 

nahisi labda yale maneno 

niliyomwambia pale uwanja wa 

ndege wakati naondoka 

yalimkwaza na akaamua kujiua 

kwani nimeambiwa kuna barua 

ameniandikia.Nahisi ndani ya 

barua hiyo atakuwa ameeleza 

sababu ya kuchukua maamuzi ya 

kujiua” akasema Dr Vivian 

akanyamaza kidogo na kusema 

“Mkurugenzi wa idara ya 

usalama wa taifa ni mtu mkubwa 

na mpaka achukue maamuzi ya 

kujiua lazima ipo sababu kubwa na 

nzito.Hata hivyo tusubiri 

uchunguzi ufanyike na tutafahamu 

kwa nini alichukua maamuzi 

yale.Jambo lingine nimeamua kumtafuta mpelelezi mwenye 

uwezo mkubwa wa kulichunguza 

suala la vifo vya familia 

yetu.Lazima tuwapate wale 

walioiteketeza familia yetu.Bado 

sijakata tamaa na siwezi kuamini 

eti jambo hili 

limeshindikana.Nimeamua 

kulivalia njuga mimi mwenyewe 

hili jambo na nitahakikisha jambo 

hili linafika mwisho.Nitakaporejea 

Dar es salaam nitaonana na mtu 

ambaye atanisaidia kumpata mtu 

mpelelezi mahiri wa kuifanya kazi 

hii” akasema Dr Vivian na kurejea 

chumbani kwake 

“Hili suala linazidi kuchukua 

sura mpya na kuzidi 

kuniogopesha.George Mzabwa kujitoa uhai si kwa bahati 

mbaya.Kuna sababu kubwa.Hisia 

za dada zinaweza kuwa kweli 

kwamba yale maneno 

aliyomueleza asubuhi wakati 

anaondoka yamechangia kwa yeye 

kujitoa uhai lakini kama suala la 

kifo cha baba limesababisha ajitoe 

uhai basi suala hili lina siri kubwa 

ndani yake.Yawezekana labda 

kuna kitu alikigundua na ambacho 

hawezi kukiweka wazi na ndiyo 

maana akachukua maamuzi ya 

kujiua.Unapozungumzia kifo cha 

baba unazungumzia pia football 

lile begi alilokuwa analibeba na 

ambalo mpaka leo hii hakuna 

anayefahamu liko 

wapi.Nilichonacho hapa ni huu msalaba pekee ambao alinitaka 

nisiutoe shingoni mwangu hadi 

nitakapomkabidhi rais wa wakati 

huu na hakunipa maelezo yoyote 

ya kina.Mwili 

unanitetemeka,natamani 

nimueleze dada Vivian ukweli 

lakini naogopa” akawaza Theresa 

“Ni mpelelezi gani huyo 

anayeweza kulifumbua fumbo hili 

lililowashidna hata idara ya 

usalama wa taifa? Natamani 

nimuone na nina imani hata yeye 

mwenyewe hatafika popote 

ataishia njiani.Mimi sintafumbua 

mdomo wangu na nitaendela 

kukaa na siri hii .Sitaki 

kuhatarisha uhai wangu na wa 

dada yangu Vivian.” Akaendelea kuwaza Theresa huku dege 

likiendelea kupasua anga 

NEW YORK - MAREKANI 

Saa moja za jioni kwa saa za 

Marekani ambayo ni saa tisa za 

usiku kwa saa za Afrika 

mashariki,dege la rais wa jamhuri 

ya muungano wa Tanzania liligusa 

ardhi ya jiji la New york 

Marekani.Dr Vivian na ujumbe 

wake walipokewa kwa mujibu wa 

itifaki na kupelekwa katika hoteli 

waliyopangiwa kufikia ambako 

rais na ujumbe wake wote 

walifikia.Rais hakutaka hata 

mmoja aliyeongozana naye 

akafikie sehemu nyingine.Baada ya kuoga na kupumzika rais na 

ujumbe wake wakapata chakula 

cha usiku na kisha akawa na 

mazungumzo na balozi wa 

Tanzania nchini Marekani.Balozi 

alimtaarifu rais kwamba wale 

watu aliomtaarifu kwamba 

walihitaji kuonana na kuzungumza 

naye kuhusiana na mambo kadhaa 

ya uwekezaji nchini Tanzania 

watakuja usiku ule kuonana 

naye.Rais hakuwa na kipingamizi 

hivyo akakubali kuonana na hao 

wawekezaji. 

Wakati rais na balozi wa 

Tanzania nchini marekani 

wakiendelea na mazungumzo 

wakafahamishwa kwamba kuna 

watu wanne walikuwa wamefika kwa ajili ya kuuonana na 

rais.Balozi akamtaarifu rais 

kwamba watu aliokuwa 

amemweleza wamefika na rais 

akawakaribisha.Ulikuwa ni 

ujumbe wa watu wanne.Kiongozi 

wa ujumbe ule alijitambulisha 

kama Jing wang halafu 

akawatambulisha na wenzake 

alioambatana nao ambao ni Ling 

Huang,Peng Li na wote hawa 

walitoka nchini China.Mwisho 

akamtambulisha Kim Yung Su 

mjumbe maalum wa rais wa Korea 

Kaskazini . 

Dr Vivian akatabasamu baada 

ya Jing wang kufanya utambulisho 

ule ingawa kwa ndani alistuka sana kusikia katika ujumbe ule 

kuna mtu anatoka Korea kaskazini 

“Karibu sana Jing wang na 

ujumbe wako.Nafurahi kuonana 

nanyi” akasema Dr Vivian 

“Hata sisi tunafurahi kuonana 

kuonana nawe mheshimiwa 

rais.Kwa kuwa umechoka kwa 

safari ndefu tutajitahidi 

mazungumzo yetu yawe mafupi” 

akasema Jing na kunyamaza baada 

ya mlinzi kuingia mle ndani na 

kumnong’oneza rais kitu 

“Mr Nathan amewasili yuko 

mapokezi” akasema yule mlinzi 

kwa kunong’ona 

“Apelekwe chumbani nina 

mazungumzo na wageni wangu 

sasa hivi” akasema rais na yule mlinzi akatoka na rais akamtaka 

Jing aendelee 

“mheshimiwa rais 

,utatusamehe kwa kuingilia ratiba 

yako kwa ujio huu usio rasmi 

lakini kutokana na umuhimu wake 

imetulazimu kumuomba balozi 

wako atusaidie tuweze kuonana 

nawe kwani tunafahamu utakuwa 

na majukumu mengi hapa New 

York na tusingeweza kupata nafasi 

ya kuonana na 

kuzungumza.Tunashukuru sana 

kwa kukubali kuonana 

nasi.Mheshimiwa rais sisi ni 

wawakilishi wa wafanya biashara 

wakubwa wenye makampuni 

makubwa toka China.Nadhani 

dunia nzima inafahamu juu ya urafiki wa China na Tanzania 

lakini kwa usiku huu hatukuja 

kuzungumzia juu ya China na 

Tanzania bali tumemsindikiza 

mwenzetu huyu ambaye ni mmoja 

wa wajumbe wa kutoka Korea 

Kaskazini wanaohudhuria 

mkutano wa umoja wa mataifa 

lakini yeye amekuja na salamu 

maalum kutoka kwa rais wa Korea 

Kaskazini.Tumeongozana naye 

kwa sababu isingekuwa rahisi yeye 

kuja kuonana nawe moja kwa moja 

hata hivyo naomba niseme 

machache .Nchi ya Korea Kaskazini 

iko katika mageuzi makubwa ya 

kiuchumi kwa sasa kwa hiyo 

wanatafuta mashirikiano ya 

kibiashara na mataifa mbali mbali na wanaelekeza nguvu kutafuta 

masoko ya bidhaa zao,kununua 

malighafi na kuwekeza barani 

Afrika.Kutokana na Korea 

kaskazini kufahamika sana katika 

harakati zake za kijeshi nchi nyingi 

zinasita au kutotaka kuwa na 

mashirikiano yoyote na Korea 

kaskazini hivyo kutulazimu China 

kuwasaidia wenzetu 

kuwaunganisha na marafiki zetu 

mbali mbali duniani.Tanzania kwa 

sasa inafanya mageuzi makubwa 

ya kiuchumi na kwa kuwa ina sera 

nzuri za kuvutia wawekezaji 

,wafanya biashara kutoka Korea 

kaskazini wamependa sana kuwa 

na mashirikiano ya kibiashara na 

Tanzania lakini nchi hizi hazina mashirikiano ya kibiashara kwa 

sasa hivyo panahitajika sehemu ya 

kuanzia na kikao hiki ni sehemu ya 

kuanzia.Kwa hiyo mheshimiwa 

rais naomba nisiwe msemaji mkuu 

wa kikao hiki na nimuachie Kim 

Yung Su ana mengi atakueleza 

alichotumwa na kiongozi wake” 

akasema Jing Wang 

“Karibu sana Kim” akasema 

Dr Vivian. 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais.Kama alivyosema Jing Wang 

ninatokea Korea Kaskazini na 

nimetumwa salamu maalum toka 

kwa rais wetu.Kwanza anakupa 

pongezi nyingi kwa mafanikio 

makubwa ambayo Tanzania 

imeyapata kwa muda mfupi uliokaa madarakani.Umeonyesha 

dira na mfano kwa viongozi wengi 

duniani. 

Korea Kaskazini inajulikana 

sana duniani kote kwa harakati 

zake za kijeshi hasa msuguano kati 

yake na Marekani unaotokana na 

majaribio ya silaha kali.Msuguano 

huu umesababisha lakini nchi 

nyingi zisitake kuwa na 

mashirikiano ya kibiashara kwa 

kuogopa vikwazo toka nchi kubwa 

zenye nguvu na tajiri 

duniani.China imekuwa ni 

mshirika mkubwa wa kibiashara 

wa Korea Kaskazini.Zipo pia nchi 

nyingine zinazofanya biashara na 

sisi kama vile Russia.Kwa upande 

wa Afrika kuna Burkina faso n.k.Kwa sasa nchi yetu iko katika 

mageuzi makubwa ya 

kiuchumi.Tunataka kuukuza 

uchumi wetu uwe imara na ili 

kufanikisha hilo imetulazimu 

kubadili sera zetu za 

uchumi.Tumeanza kukaribisha 

wawekezaji toka nje jambo ambalo 

halikuwepo hapo kabla.Kama 

haitoshi wafanya biashara wetu 

sasa wanaruhusiwa kutoka na 

kwenda kufanya uwekezaji katika 

nchi nyingine pia.Tumeona fursa 

kubwa ya kuimarisha 

mashirikiano zaidi na Tanzania 

kwani tumegundua kuna fursa 

nyingi za kuwekeza na nchi zote 

mbili zikafaidika.Wafanya 

biashara wa Korea Kaskazini wako tayari kuwekeza nchini Tanzania 

katika viwanda vya nguo 

vitakavyotumia pamba ya 

wakulima wa Tanzania na hivyo 

kuachana na kuagiza guo 

zilizotumika toka Marekani na 

mataifa ya ulaya.Hivi karibuni 

Tanzania mmetangaza ugunduzi 

mkubwa wa mafuta na gesi na 

Korea kaskazini tunahitaji sana 

mafuta safi ambayo kwa sasa 

tunayapata kutoka China” 

akanyamaza kidogo halafu 

akasema 

“Haya yote niliyoyaeleza ni 

madogo lakini kubwa zaidi ni 

kwamba Korea Kaskazini inataka 

kufanya uwekezaji mkubwa katika 

uchimbaji wa madini ya Uranium.Tanzania ina kiwango 

kikubwa sana cha madini ya Urani 

na mpaka sasa hakuna uwekezaji 

wowote uliokwisha fanywa 

kutokana vikwazo na masharti 

yaliyowekwa na umoja wa mataifa 

kuhusiana na uchumbaji wa 

madini ya Urani.Tunahitaji sana 

Urani kwa ajili ya kuzalisha nishati 

ya umeme wa uhakika kwa 

viwanda vyetu hivyo basi 

tunahitaji madini haya kwa 

kiwango kikubwa.Uwekezaji huu 

mkubwa katika madini haya ya 

Urani utaupaisha sana uchumi wa 

Tanzania.Mheshimiwa rais kwa 

kuwa muda wetu ni mfupi hizo 

ndizo salamu nilizotumwa na 

kiongozi wetu niziwasilishe kwako nina imani umezipokea na 

kiongozi wetu angefurahi sana 

kusikia jibu zuri toka kwako 

kuhusiana na hizi salamu zake” 

akasema Kim Yung Su.Dr Vivian 

akawatazama wale watu mle ndani 

kwa zamu halafu akasema 

“Ahsanteni sana kwa kuja 

kuniona.Ujumbe wenu umefika na 

nimezipokea salamu.Tanzania na 

china tuna urafiki mkubwa wa 

tangu enzi za waasisi wa mataifa 

yetu mawili.Biashara kati ya China 

na Tanzani ni kubwa sana hivi sasa 

na kiwango cha uwekezaji 

kimeongezeka kwa nchi zote 

mbili.Korea Kaskazini hatujawahi 

kuwa ma mahusiano ya kibiashara 

japokuwa tuna mahusiano ya kibalozi na balozi wa Korea 

kaskazini yuko nchini Tanzania 

japokuwa Tanzania hatuna balozi 

wetu Korea kaskazini na hata 

mahusiano ya Tanzania na Korea 

kaskazini ni madogo sana siku 

hizi.Ni mara ya kwanza kusikia 

kwamba Korea kaskazini 

wanataka kufanya biashara na 

Tanzania.Hili si jambo rahisi 

kulifanyia maamuzi kutokana na 

sera na mwonekano wa nchi hii 

machoni pa dunia.Japokuwa Korea 

kaskazini wameamua kubadili 

sera zao za kiuchumi lakini bado 

inaendelea kuwekewa vikwazo 

mbali mbali na umoja wa mataifa 

kutokana na sera zake za 

silaha.Sitaki kuingia katika mambo ya kisiasa ya nchi yako Kim bali 

nataka nijielekeze katika hili suala 

mlilolileta kwangu kutafuta 

mashirikiano ya kibiashara na 

uchumi.Hili ni wazo jema na mimi 

binafsi nimelipokea.Tanzania vile 

vile tuko katika mageuzi makubwa 

ya kiuchumi kwa hiyo 

tunakaribisha uwekezaji toka 

sehemu mbali mbali ili mradi uwe 

ni uwekezaji wenye kuleta faida 

kwa nchi yangu na watu 

wake.Tunalima pamba nyingi na 

litakuwa jambo lenye manufaa 

makubwa endapo tutapata 

viwanda vingi vya nguo kutakuwa 

na soko la uhakika kwa pamba ya 

wakulima wetu na hivyo kuinua 

kilimo cha pamba kwa hiyo wazo la kuwekeza katika viwanda vya 

nguo ninalikaribisha kwani lina 

tija kwa wakulima wangu na 

ninataka Tanzania iwe kinara 

katika uzalishaji wa nguo barani 

Afrika.Kuhusu Tanzania kuiuzia 

mafuta na gesi Korea Kaskazini 

hilo halina tatizo kwani tuna 

hazina kubwa sana ya mafuta na 

gesi na bado tunaendelea 

kugundua gesi zaidi katika maeneo 

mbali mbali.Korea kaskazini 

mmeonyesha nia ya kutaka 

kuwekeza katika madini ya Urani.” 

Akanyamaza kidogo na kuvuta 

pumzi ndefu na kusema 

“Ni kweli Tanzania tuna 

karibu ratili milioni 70 za madini 

ya Urani na bado utafiti unaendelea katika sehemu 

nyingine mbali mbali na mwelekeo 

unaonyesha kwamba kuna 

uwezekano wa kupata kiasi 

kingine kikubwa zaidi cha madini 

ya Uranium.Pamoja na kuwa na 

kiwango kikubwa cha madini ya 

Urani lakini mpaka leo bado 

hatujafanya uwekezaji wowote na 

hatujanufaika chochote kwa 

uwepo wa madini haya nchini 

kwetu.Kumekuwa na shinikizo 

kadhaa toka kwa umoja wa mataifa 

na toka nchi tajiri kutishia 

kutuwekea vikwazo vya kiuchumi 

endapo tutaanza uchimbaji na 

biashara ya Urani.Shinikizo 

zinatoka sehemu mbali mbali ili 

tusichimbe madini ya Urani.Nilipoingia madarakani 

nimewaelekeza wataalamu wangu 

wapitie upya sera yetu kuhusu 

madini haya ya urani na kutoa 

mapendekezo nini tufanye ili 

tuanze uchimbaji na kunufaika na 

rasilimali tuliopewa na 

Mungu.Mmeonyesha nia ya 

kujenga mgodi mkubwa wa madini 

haya ya Urani ni wazo zuri.Nitakaa 

na wataalamu wangu tutalijadili 

hilo halafu tutawaelezeni nini 

tumeamua” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais kwa kutupokea na kuzipokea 

salamu za mkuu wetu.Kama 

nilivyosema awali kwamba ujio 

huu umebisha hodi na rais 

angependa sana kujua kama tulipobisha hodi tulifunguliwa 

mlango na kukaribishwa ndani? 

Akauliza Kim huku 

akitabasamu.Dr Vivian naye 

akatabasamu na kusema 

“Tanzania ni rafiki wa kila 

mmoja.Hatuna maadui.Maadui 

zetu ni wale wanaopinga 

maendeleo yetu na kukwamisha 

kusonga mbele.Wale wote 

wanaokuja kwetu kwa nia njema 

ya kuwekeza tunawakaribisha kwa 

mikono miwili.Tanzania 

hatufungamani na upande wowote 

na hiyo ndiyo sera yetu toka 

wakati wa muasisi wa taifa 

letu.Hatuchaguliwi marafiki wala 

mtu wa kufanya naye biashara na 

tunaweza kufanya biashara hata na Korea kaskazini japokuwa 

hatukubaliani nao kuhusiana na 

sera zake za silaha na majaribio ya 

makombora inayoyafanya lakini 

milango iko wazi kwa mtu yeyote 

kuja kuwekeza Tanzania ili mradi 

uwe ni uwekezaji wenye manufaa 

kwetu na si wale wanaokuja 

kuchukua rasilimali zetu na 

kutuacha masikini” akasema Dr 

Vivian.Waliendelea na maongezi 

na baadae wakaagana na moja kwa 

moja akaelekea chumbani 

kwake.Alielekeza kutosumbuliwa 

tena kwani alihitaji 

kupumzika.Aliingia chumbani 

kwake na kumkuta Nathan 

amejilaza kitandani.Nyuso zao 

wote zikachanua kwa tabasamu.Dr Vivian akamfuata Nathan pale 

kitandani wakakumbatiana na 

kuanza kubusiana.Kila mmoja 

alionekana kuwa na hamu sana na 

mwenzake 

“Nath…” Dr Vivian akataka 

kusema kitu Nathan akamzuia 

“Tutaongea baadae lakini 

kwanza tumalize shughuli 

muhimu” akasema Nathan huku 

mikono yake yenye nguvu 

ikiendelea kukivinjari kifua cha 

Vivian ambaye taratibu alianza 

kuzidiwa kutokana na utundu wa 

Nathan.Alishindwa kujizuia 

ikamlazimu amuachie Nathan 

afanye kile alichokikusudia Ulikuwa ni mtanange wa 

dakika arobaini na Nathan 

alimpeleka Dr Vivian vilivyo. 

“Ninajivunia sana kuwa na 

mwanaume kama wewe una nguvu 

za ajabu .Unanifikisha pale 

ninapotaka.Ahsante sana Nathan” 

akasema Dr Vivian na kumbusu 

Nathan 

Waliongea mambo mengi 

yanayowahusu kuhusiana na ndoa 

yao na maisha yao ya usoni na 

mara Nathan akauliza 

“Nilipokuja niliambiwa 

kwamba kuna wageni 

unazungumza nao faragha.Ni 

wageni gani hao? 

“Nilikutana na ujumbe wa 

wafanyabiashara wa China wakiwa wameambatana na mjumbe 

maalum wa rais wa Korea 

Kaskazini” akasema Dr Vivian na 

kumstua Nathan 

“Walikuwa wanataka nini? 

Akauliza 

“Korea kaskazini wanataka 

kuanzisha mahusiano ya 

kibiashara na Tanzania 

.Tumezungumzia kuhusu 

uanzishwaji wa viwanda vya nguo 

na lingine kubwa wanataka 

kuwekeza katika uchimbaji wa 

Uranium” 

“Umewapa jibu gani? 

“Tanzania inakaribisha 

wawekezaji toka sehemu mbali 

mbali duniani na sioni tatizo kwa 

wawekezaji toka Korea kaskazini kuwekeza Tanzania.Nitajadiliana 

na wenzangu tuangalie suala hili 

kwa mapana zaidi.Wewe una 

maoni gani kuhusu jambo hili? 

Unatarajia kuwa mume wa rais na 

utakuwa ndiye mshauri wangu 

mkubwa.Nipe maoni yako katika 

jambo hili” 

“kwa upande wangu sina 

kipingamizi chochote katika 

kukaribisha uwekezaji nchini 

Tanzania ila lazima muwe makini 

na watu wanaotaka kuja 

kuwekeza.Uwekezaji wowote 

kutoka Korea Kaskazini na hasa 

katika madini ya Urani utaiweka 

nchi ya Tanzania pabaya sana 

kimataifa.Kwanza kuwa mshirika 

tu na Korea kaskazini ambayo ina maadui wengi inaweza kuiletea 

mtatizo Tanzania lakini kwenda 

mbali zaidi na kuwaruhusu 

wachimbe madini ya Urani 

kutaongeza mgogoro.Korea 

kaskazini wapo katika msuguano 

mkubwa na mataifa makubwa 

kutokana na sera zake za 

utengenezaji wa makombora na 

inadaiwa wana makombora 

kadhaa ya nyuklia na wakipata 

madini hayo ya urani wataongeza 

nguvu katika kutengeneza silaha 

za nyuklia na watazidi kuwa tishio 

kwa dunia.Hilo ni jambo 

mnalopaswa kulitazama kwa 

macho sita.Si suala la kufanyia 

mzaha” akasema Nathan 

“Nini basi ushauri wako? “Tanzania bado ni nchi 

masikini,bado inahitaji misaada 

toka mataifa makubwa 

yaliyoendelea.Sitaki kuona 

ukiingiza nchi yako katika 

matatizo au migongano na mataifa 

wafadhili.Nashauri uachane kabisa 

na hao wakorea.Watawawekeni 

katika matatizo makubwa. 

Tanzania itawekewa vikwazo vya 

kiuchumi,mtafungiwa kuuza nje 

bidhaa zenu na kunyimwa 

misaada.Hili likitokea uchumi wa 

Tanzania utayumba sana” akasema 

Nathan 

“Tanzania ni nchi huru na 

haiwezi kupangiwa taifa la kufanya 

nalo biashara .Tutafanya biashara 

na yeyote yule ambaye tutaonana ana maslahi kwetu.Tumechoshwa 

na huu ukandamizwaji 

unaofanywa na haya mataifa 

makubwa.Ni wakati wa Afrika 

kusimama na kuungana kupinga 

huu unyanyasaji mkubwa 

unaofanywa na haya mataifa 

yakiongozwa na nchi yako 

marekani.Mungu katupa rasilimali 

zitufaidishe kwa nini tunakatazwa 

kuzitumia?Kwa nini tuendelee 

kuwa masikini wakati utajiri 

tunao?Utajiri wetu unaporwa na 

sisi tunaachiwa mashimo na 

hazina za hawa wakubwa 

zinaendelea kunona kwa madini 

wanayoyachuma toka 

kwetu.Siwezi kuivumilia hali kama 

hii iendelee.Afrika lazima tufaidike na rasilimali Mungu alizotupa 

kuliko kuacha zichukuliwe na 

hawa wakubwa na sisi kubaki 

masikini” akasema Dr Vivian. 

“Tuachane na hayo Vivian huo 

ulikuwa ni ushauri wangu.Tujikite 

katika mambo yanayotuhusu sisi 

wawili.Tuna maisha yanatusubiri 

baada ya kufunga ndoa kwa hiyo ni 

muda muafaka wa kupanga 

kuhusu maisha yatu ya 

baadae.Halafu mpenzi wangu 

kuna jambo ninataka kukuuliza” 

“Uliza Nathan na samahani 

kwa sauti ya juu niliyoitoa 

kutokana na lile suala.Unajua 

linapokua suala la maslahi ya 

Tanzania huwa ninaweka uzito 

mkubwa sana” “Usijali mpenzi.Wewe hivi 

sasa ni rais wa nchi na 

ikimpendeza Mungu baada ya 

miezi miwili toka sasa tunaweza 

kufunga ndoa.Ninajiuliza kuhusu 

suala la familia,namaanisha 

watoto.Umekwisha wahi kulifikiria 

hilo kuhusu namna tutakavyoweza 

kupata watoto wetu? 

Swali lile likaonekana 

kumstua Dr Vivian.Akafikiri 

kidogo na kusema 

“Nathan naomba tuliache hilo 

suala tutalizungumza siku 

nyingine huu si wakati wake” 

akasema Dr Vivian 

“Vivian huu ni wakati wetu 

mzuri wa kulizungumza hili 

jambo.Muda uliobaki ni mdogo na kutokana a kutingwa na mambo 

mengi kuna uwezekano tusipate 

nafasi ya kuliongelea.Kabla ya 

kuingia katika ndoa tunapaswa 

kulizungumza na kupata muafaka 

ili lisituletee mgogoro huko 

mbeleni”akasema Nathan 

“Nimekuelewa Nathan lakini 

sijui nikujibu nini” akasema Dr 

Vivian na kuiamisha kichwa 

akafikiri kidogo halafu akasema 

“Kwani lazima kuwa na 

watoto? 



Nimekuelewa Nathan lakini 

sijui nikujibu nini” akasema Dr 

Vivian na kuiamisha kichwa 

akafikiri kidogo halafu akasema 

“Kwani lazima kuwa na 

watoto? 

“Ulazima upo mpenzi tena 

mkubwa.Watu wawili 

mnapoungana na kuwa mwili 

mmoja kwa kufunga ndoa,kikubwa 

kinachotarajiwa ni kupata watoto 

na kutengeneza familia yenye furaha.Kama hakuna tatizo lolote 

la kimaumbile kwa mmoja kati ya 

wanandoa basi watoto ni 

lazima.Hilo ni agizo tumepewa na 

Mungu kwamba nendeni 

mkazaane muijaze 

dunia.Mnapofunga pingu za 

maisha Mungu anawatumia 

kuendelea kazi yake ya uumbaji 

kwa kuwajalia watoto” akasema 

Nathan 

“Bila watoto ndoa haiwezi 

kuwa na furaha? Dr Vivian 

akauliza 

“Ndoa inaweza kuwa na 

furaha bila watoto lakini endapo 

hakuna tatizo lolote linaloweza 

kutuzuia kupata watoto kwa nini tusizae?Mbona umeuliza maswali 

hayo huna mpango wa kuzaa? 

“Nathan naomba niwe mkweli 

kwako kwamba sina wazo la kuwa 

na mtoto hasa kwa wakati 

huu.Kwa hivi sasa akili yangu 

nimeielekeza katika kuwahudumia 

waTanzania.Sitaki niingie katika 

jambo lingine lolote 

litakalonifanya nishindwe 

kuwatumikia watu wangu 

walionichagua kwa mapenzi 

makubwa.Suala la mtoto itabidi 

lisubiri labda hadi hapo 

nitakapomaliza kipindi changu cha 

uongozi” akasema Dr Vivian 

“Hapana mpenzi hatuwezi 

kusubiri hadi muda huo.Kwa sasa 

una miaka 47,ukimaliza kipindi chako cha kwanza cha uongozi 

utakuwa na miaka 

50.Ukichaguliwa katika kipindi cha 

pili utakuwa na miaka 55 unataka 

upate mtoto wa kwanza ukiwa na 

umri huo wa uzee? 

“Nathan naomba unielewe 

kwa sasa nina majukumu mazito 

kwa nchi yangu na sintakuwa na 

muda kulea mtoto.Utanisamehe 

sana kwa hilo.Kama ni mtoto wapo 

wengi tunaweza kuchukua wawili 

au watatu katika vituo vya kulelea 

watoto yatima tukawalea kama 

watoto wetu kwa maopenzi 

makubwa” 

“Hapana Vivian.Sitaki mtoto 

asiye wangu.Nataka kulea mtoto 

wa damu yangu na si mtoto wa kuokota.Kama unaona kutakuwa 

na ugumu kulea nizalie mtoto na 

mimi nitalea mwenyewe wakati 

ukiendelea na majukumu yako ya 

urais” akasema Nathan.Dr Vivian 

akamtazama na kusema 

“Hilo haliwezeka ni 

Nathan.Bado siko tayari kuwa 

mama na pengine sitakuwa mama 

katika maisha yangu yote” 

Jibu lile la Dr Vivian 

likaonekana kumkasirisha sana 

Nathan. 

“Vivian kwa nini 

unanifanyia?Kwa nini hutaki kuzaa 

mtoto na mimi? Kuna faida gani ya 

kuingia katika ndoa ambayo 

haitakuwa na uzao?Nakupenda 

mno Vivian lakini kwa msimamo wako juu ya suala la mtoto 

umenifanya nijifikirie mara mbili 

kama kweli tuko tayari kuingia 

katika ndoa.Umenishangaza sana 

Vivian” akasema Nathan.Vivian 

akasimama na kumtazama Nathan 

kwa muda akasema 

“Nathan nakupenda sana zaidi 

ya unavyoweza kufikiri lakini siko 

tayari kwa sasa kuwa na mtoto 

hivyo basi una fursa mbili za 

kuchagua.Aidha wewe na mimi 

tuishi bila mtoto au tuachane 

ukatafute mwanamke 

atakayekuzalia mtoto.Chagua moja 

mimi niko tayari kwa lolote” 

akasema Dr Vivian.Nathan 

akasimama na kutaka kumshika 

mkono lakini Dr Vivian akamzuia “Usinishike tafadhali.Naomba 

ufahamu kwamba mimi ni 

mwanamke nisiyependa 

kuyumbishwa na mtu 

yeyote.Katika maisha yangu 

ninamuogopa Mungu pekee na si 

mwanadamu yeyote.Nataka mtu 

ambaye nitaolewa naye awe ni mtu 

atakayeendana na mimi na 

misimamo yangu.Ninaomba 

uchague kati ya hayo mawili 

niliyokwambia.Au nikuchagulie? 

Akauliza Dr Vivian kwa ukali 

“Vivian mpenzi nakuomba 

haya mambo yasifike huko 

tafadhali.Mimi na wewe hatupaswi 

kufika hatua kama hiyo ya 

kulumbana kiasi hiki.Haya mambo 

yanazungumzika na tukae chini tuzungumze.Tumetoka mbali na 

tusianze kukorofishana kwa 

wakati huu ambao tuko karibu 

sana kuifikia ile ndoto yetu ya 

kufunga ndoa na kuwa kitu 

kimoja.Siko tayari kutengana nawe 

kwa sababu nakupenda lakini 

suala la mtoto naomba ulifikirie 

mpenzi wangu,ni la muhimu 

sana.Hatuwezi kamwe kuwa na 

furaha katika ndoa yetu bila kuwa 

na watoto.” akasema Nathan 

“Nathan unaonekana bado 

hujanifahamu vyema.Nimekupa 

fursa ya kuchagua lakini 

umeshindwa kufanya hivyo na 

badala yake bado unaendelea 

kunichefua.Sasa nisikilize kwa 

makini.Mimi ni rais na ninaongoza waTanzania zaidi ya milioni 

hamsini kwa hiyo akili yangu yote 

nimeielekeza huko.Walinichagua 

kwa mapenzi makubwa na wana 

imani kubwa na mimi kwamba 

nitawasaidia kuboresha maisha 

yao.Watoto wa watanzania ni 

watoto wangu pia hivyo natakiwa 

kuhakikisha kwamba wako salama 

kila siku na wana afya 

njema.Natakiwa kuhakikisha 

wanapata elimu iliyo 

bora,natakiwa kuhakikisha wazazi 

wao wana maisha mazuri na yaliyo 

bora kwa hiyo kila dakika ambayo 

Mungu ananijalia kuishi 

ninaielekeza katika kutatua kero 

za watanzania na ndiyo maana 

mara nyingi hata usiku silali ninakesha nikifanya kazi kwa 

ajiliya watanzania masikini hivyo 

sintakuwa na muda wa kulea 

mtoto.Pamoja na kukuelewesha 

huko lakini bado umeonyesha 

kwamba hauko tayari kuishi bila 

mtoto na mimi siko tayari kuwa na 

mtoto hivyo katu hatutaweza kuwa 

na amani katika hiyo ndoa 

yetu.Kwa sababu hiyo ninaona kitu 

cha msingi ni mapenzi yetu kuishia 

hapa.Ile safari yetu na zile ndoto 

zetu zote ziishie hapa.Inaniuma 

lakini sina namna nyingine ya 

kufanya kwani Tanzania ni 

muhimu zaidi kwangu kuliko 

mapenzi.Siku zote huwa ninasema 

nchi yangu kwanza na mambo 

mengine baadae” “Vivian !! akasema Nathan 

kwa mstuko mkubwa 

“Nathan tafadhali usiseme 

chochote.Inuka chukua kila kilicho 

chako uondoke” 

“hapana Vivian,usifanye 

hivyo.Punguza hasira tulimalize 

hili suala.Usichukue maamuzi 

kama hayo.Mimi nawe hatupaswi 

kufika huko” 

“Nathan nimekwisha tamka na 

mimi nikitamka neno huwa 

sitengui kauli yangu hivyo 

nakuomba uinuke uondoke.Kila 

kitu chetu kimeishia hapa.Kama ni 

kuzungumza tutazungumza siku 

nyingine lakini si leo.Naomba 

uniache nina mambo mengi ya 

kufanya kwa nchi yanguTanzania.Nina watu zaidi ya 

milioni hamsini ninawaongoza 

kwa hiyo sitaki kumizwa kichwa 

na mtu mmoja.Naomba uinuke 

uondoke kabla sijawaita walinzi 

wangu wakutoe humu kwa nguvu” 

akasema Dr Vivian.Nathan hakuwa 

na ujanja kwani anamfahamu 

vyema Dr Vivian akiamua jambo 

hivyo akainuka taratibu akavaa 

nguo zake 

“Vivian natumai hizo ni hasira 

tu lakini utakapokuwa umetulia 

yatafakari niliyokwambia ni 

mambo ya muhimu 

sana.Ninaondoka ila tutaonana 

tena kesho,nitakuja 

tuzungume.Mimi na wewe 

anayeweza kututenganisha ni Mungu pekee hivyo suala la mimi 

na wewe kutengana naomba 

uliondoe kichwani kwako.Katu 

haliwezekani” akasema Nathan na 

kutoka mle chumbani.Dr Vivian 

akaketi kitandani na kuinamisha 

kichwa machozi yakamtoka 

“I’ve lost him! Nimempoteza 

mwanaume niliyempenda kuliko 

wote” akawaza Dr Vivian 

“Lakini sipaswi kuumia kwani 

nimelazimika kufanya hivi kwa 

ajili ya nchi yangu.Nampenda mno 

Nathan lakini sijui nimepata wapi 

nguvu za kuweza kumtamkia 

maneno mazito kama yale.Siku 

zote nimekuwa dhaifu sana kwake 

na kila analoniambia nimekuwa 

nalitekeleza ila leo nimepata nguvu na ghafla tu nimezima ndoto 

yetu ya kuwa pamoja milele katika 

ndoa.Bado miezi miwili tufunge 

ndoa lakini hilo halitanipa shida 

ila siwezi kuingia katika ndoa na 

mtu ambaye haendani na 

misimamo yangu.Ndoa yetu 

haitakuwa na amani kwani kila 

siku atakuwa ananidai mtoto na 

mimi siko tayari kuwa na mtoto 

kwa sasa.Sitaki kabisa mambo 

yatakayonifanya nikapoteza 

mwelekeo katika kazi 

yangu.Ninawaongoza watu wengi 

hivyo kichwa changu kinahitaji 

utulivu mkubwa.Sitaki mambo ya 

mapenzi yanifanye nishindwe 

kutekeleza majukumu yangu kama 

rais.” Akawaza Dr Vivian “Nadhani mambo ya mapenzi 

si fungu langu.Sina bahati katika 

upande huo.Kila ninapojaribu 

huishia kuumia na 

kulia.Enough.Sitaki kuendelea 

kupoteza muda kwa mambo ya 

mapenzi.Nina ndoto nyingi za 

kutimiza kwa nchi yangu na si 

kusumbukia mambo ya 

mapenzi.Nadhani ni vyema kama 

nitaishi mwenyewe.Nimekuwa mtu 

nisiye penda kuyumbishwa na mtu 

yeyote toka utoto wangu 

namuomba Mungu anisaidie 

niendele kuwa na msimamo thabiti 

na nisiyume katika maamuzi 

yangu ninayoyafanya.Nathan 

alikuwa ni furaha yangu,alinipa 

tabasamu usoni kila palenilipomuona lakini kuna kitu 

kimoja nimekigundua kwake 

ananipenda mimi na si 

Tanzania.Theresa aliniambia kitu 

kimoja cha msingi 

sana.Alinikumbusha kama Nathan 

anaweza kuwa mshauri mzuri 

kwangu.Kwa hili nililoliona muda 

mfupi uliopita hawezi kuwa 

mshauri mzuri hata kidogo kwa 

kuwa hana mapenzi na 

Tanzania,haijui Tanzania na wala 

hayafahamu matatizo ya 

waTanzania” akawaza 

NEW YORK - MKUTANO WA 

BARAZA KUU LA UMOJA WA 

MATAIFA 

Mkutano ambao huchukiliwa 

kama ndio mkusanyiko mkubwa 

kabisa wa viongozi wa 

dunia,unaofanyika kila mwaka 

katika makao makuu ya umoja wa 

mataifa yaliyopo New York 

Marekani,ulifunguliwa rasmi na 

katibu mkuu wa umoja wa mataifa 

ndugu Alfredo Perez.Viongozi 

kutoka mataifa karibu yote 

wanachama wa umoja huu 

walihudhuria wakiwemo wale wa 

kutoka mataifa makubwa kama 

Marekani,China,Urusi,Ujerumani,U

faransa,Uingereza.Miongoni mwa marais waliohudhuria mkutano 

huu walikuwepo pia ambao ni 

mara ya kwanza kuhudhuria kama 

rais wa Tanzania Dr Vivian 

Matope. 

Katibu mkuu wa umoja wa 

mataifa Alfredo Perez aliwasilisha 

taarifa ya mwaka ya utendaji wa 

chombo hicho .Baada ya hotuba ya 

uwasilishwaji wa iliyosheheni 

mambo lukuki ,marais wa kutoka 

mataifa mbali mbali walianza 

kutoa hotuba zao 

Hotuba kubwa iliyokuwa 

inasubiriwa kwa hamu ni ya rais 

wa Marekani,Mike Straw.Wengi 

walitaka kusikia 

atakachokizungumza rais huyu 

mwenye kujulikana sana kwa kusema hovyo,kutoa matamshi 

yasiyo na staha na kupenda 

ubaguzi hasa kwa nchi za bara la 

Afrika. Ujumbe wa Tanzania 

ulirejea katika hoteli walikofikia 

kwa mapumziko na chakula cha 

mchana kabla ya kurejea tena 

katika ukumbi wa mikutano 

kuendelea na kikao.Siku hii Dr 

Vivian alionekana kuwa tofauti na 

alivyozoeleka.Usoni pake hakuwa 

na lile tabasamu watu walilozoea 

kuliona hali iliyowafanya watu 

walio karibu naye kujiuliza 

kulikoni 

Baada ya kurejea hotelini kwa 

mapumziko,Dr Vivian alielekea 

chumbani kwake kupumzika na 

akamtaka Theresa amfuate “Dada Vivi una tatizo lolote 

leo? Akauliza Theresa 

“Kwa nini Theresa? 

“Hauko katika hali yako ya 

kawaida tuliyokuzoea.Kuna tatizo 

lolote? 

Dr Vivian akafikiri kidogo na 

kusema 

“Nimeachana na Nathan” 

“Nini? Akauliza Theresa kwa 

mshangao 

“Nimeamua kuachana na 

Nathan.Mimi na yeye kila mtu 

atafuata maisha yake” 

Theresa na Dr Vivian 

wakatazamana kwa muda halafu 

Theresa akauliza 

“Kwa nini umechukua 

maamuzi haya dada Vivi? “Ah ! nimelazimika kufanya 

hivyo.Sikuwa na namna nyingine” 

“Nieleze tafadhali nini 

kilitokea ? akauliza Theresa 

“Jana usiku tukiwa katika 

mazungumo kuhusiana na ndoa 

yetu na mambo mengine ya maisha 

aliniuliza swali lililoleta mtafaruku 

na nikachukua maamuzi haya” 

“Aliuliza swali gani? 

“Aliniuliza kuhusu suala la 

kupata mtoto” 

“Mtoto? Mtoto yupi? Theresa 

akauliza 

“Alitaka kufahamu ninafikiria 

nini kuhsu kupata mtoto.Anataka 

mara tukisha funga ndoa tuzae 

mtoto.Mimi sina tabia ya kuficha 

nikamueleza ukweli kwamba kwa sasa sina wazo la kuwa na mtoto 

labda hadi hapo nitakapomaliza 

kipindi changu cha uongozi.Nina 

mambo mengi ya kushughulikia 

kwa sasa na siwezi kupata muda 

wa kulea.Kulitokea kupishana kwa 

maneno na nikaona isiwe taabu 

kila mmoja achukue hamsini zake 

tumalizane nikaweka nukta katika 

kitabu chetu na 

kukifunga.Nafahamu tulikaribia 

sana kuifikia ndoto yetu ya muda 

mrefu lakini yawezekana labda 

hatukuwa tumepangiwa kuwa 

pamoja” 

“Dah ! lakini dada naona kama 

maamuzi haya umeyafanya kwa 

haraka sana.kwa nini msikae 

mkazungumza? “Hakuna tena muda wa kukaa 

kuzungumza Theresa.Nimekwisha 

amua hivyo na huo ndio msimamo 

wangu hautabadilika.Sitaki 

kuumiza kichwa na mapenzi 

nikashindwa kuwatumikia 

waTanzania.Nahitaji kufikiria 

maisha ya watu ninaowaongoza na 

si kumuwaza mjinga mmoja!! 

Akasema Dr Vivian kwa hasira 

“Tuachane na hayo,ile hotuba 

umeifanyia marekebisho 

niliyokuelekeza?Ratiba 

inaonyesha usiku wa leo natarajia 

kutoa hotuba yangu” 

“Iko tayari dada” 

“Good.Naomba niipitie” 

akasema Dr Vivian na Theresa akampatia hotuba ile Dr Vivian 

akaipitia 

“Iko vizuri.Imekaa vizuri sana 

ahsante.Mambo yote muhimu 

yapo” akasema Dr Vivian 

“Dada bado nataka 

tuzungumze kuhusu hili suala lako 

na Nathan.Unadhani ni maamuzi 

ya busara kuachana kwa sasa 

wakati mmebakiza miezi miwili 

mfunge ndoa? 

“Theresa tafadhali sitaki 

kuzungumza kuhusu Nathan kwa 

sasa.Nimekwisha fanya maamuzi 

na huwa sina ndimi mbili.Nikisema 

hapana ni hapana.Kuhusu 

gharama za maandalizi 

yaliyofanyika zisikuumize kichwa 

,hakutakuwa na ndoa tena kwa hiyo yoyote aliyetoa mchango 

wake atarejeshewa.Nenda 

kapumzike Theresa usiku wa leo 

nitatoa hotuba yangu kesho 

nitakuwa na mikutano mbali mbali 

ba kesho kutwa nitakutana na 

waTanzania wanaoishi hapa 

Marekani ,nitazungumza nao na 

siku itakayofuata tutarejea 

nyumbani” akasema Dr Vivian. 

************** 

Baada ya mapumziko ya 

mchana viongozi walirejea tena 

katika ukumbi wa mikutano na 

jioni hii viongozi kadhaa 

walitarajia kuzungumza.Miongoni 

mwa viongozi waliopangiwa kuzungumza jioni hii ni rais wa 

Marekani vile vile rais wa 

Tanzania ambaye angehutubia 

kwa mara ya kwanza 

Viongozi walianza kutoa 

hotuba zao wakizungumzia 

mambo mbali mbali ya nchi zao na 

dunia kwa ujumla.Saa moja na 

dakika kumi ikafuata zamu ya rais 

wa Marekani kutoa hotuba yake.Ni 

hotuba iliyokuwa inasubiriwa sana 

na watu wengi.Katika hotuba yake 

alizungumzia mambo mengi na 

halafu akaligeukia bara la Afrika 

“Katika hotuba yake asubuhi 

ya leo” akasema Mike Straw 

“Katibu mkuu wa umoja wa 

mataifa alieleza kwa urefu 

kuhusiana na mambo kadhaa yanayolikumba bara la afrika kwa 

sasa na kwa kirefu amezungumzia 

athari za mabadiliko ya tabia nchi 

zilizolikumba bara la Afrika na 

kuyataka mataifa makubwa 

yanayoongoza kwa viwanda kutoa 

fedha nyingi kama fidia kwa nchi 

za afrika ambazo zimeathirika kwa 

kiasi kikubwa kutokana na gesi za 

viwandani zinazozalishwa na 

mataifa makubwa yanayoongoza 

kwa viwanda duniani.Naomba 

mnisikie vizuri viongozi wenzangu 

wa dunia” akasema na kunyamaza 

kidogo akawatazama viongozi 

wale ukumbini halafu akaendelea 

“Si kweli hata kidogo kwamba 

sisi mataifa makubwa ndio chanzo 

cha mabadiliko ya tabia nchi yanayolikumba bara la Afrika kwa 

sasa.Ni kweli tunazalisha hewa 

ukaa kwa wingi toka katika 

viwanda vyetu na tumeanza 

kuchukua hatua katika hilo lakini 

matatizo haya yanayosemwa 

kutokea Afrika yangepaswa 

kuanzia kwetu sisi ambao ndio 

wazalishaji wakubwa wa hewa 

ukaa inayotajwa kwenda kuliathri 

bara la Afrika.Tungepoteza misitu 

yetu ,tungekuwa na ukame 

mkubwa,mito ingekauka na 

uzalishaji wa mazao ya chakula 

ungepungua,lakini hali haiko 

hivyo.Misitu yetu ipo tena 

mikubwa na inastawi,vyanzo vya 

maji bado vinaendelea 

kububujisha maji mwaka hadi mwaka,mito yetu inaendelea kujaa 

na kutiririsha maji na hakuna 

tishio la kukauka kwa hiyo si kweli 

kwamba sisi ndio tunaosababisha 

ukame ,misitu kupotea,mvua 

kutokunyesha barani 

Afrika.Matatizo haya yote 

yamesababishwa na waafrika 

wenyewe.Kwa sababu ya ufinyu 

wao wa kufikiri,wanaharibu misitu 

ya asili ambayo ni chanzo kikubwa 

cha mvua ,wanalima katika vyanzo 

vya maji na kusababisha vyanzo 

hivyo kukauka ,mito 

inakauka,mvua hainyeshi tena,na 

hata ikinyesha mara nyingi 

inakuwa chini au juu zaidi ya 

kiwango hivyo kupelekea 

uzalishaji wa mazao kushuka na njaa kuenea katika kila pembe ya 

bara la Afrika.Yote haya 

yanasababishwa na uvivu wa 

kufikiri na kutokuona 

mbali.Ukiharibu leo mti uliodumu 

kwa zaidi ya miaka mia moja 

unategemea nini? Nawaambia 

Afrika njaa ,ujinga ,umasikini 

vitaendelea kuwatafuna kama 

hamtachukua hatua za dhati 

kufanya mabadiliko ya haraka 

kuhakikisha mnalinda uoto wenu 

wa asili kwa ajili ya watoto wa 

watoto wenu.Bara lile la kijani 

lililokuwa na vijito vyenye 

kutiririsha maji kila kona,sasa 

limegeuka jangwa na hata nyasi za 

kulisha mifugo yenu 

mnakosa.Badilikeni Afrika na muache kutafuta visingizio ili 

mlipwe fedha na mataifa ya nje 

wakati mazingira mmeyaharibu 

wenyewe”Akanyamaza kidogo na 

kuendelea na hotuba yake 

“Baada ya kuliharibu bara lao 

kwa kulifanya jangwa sasa 

wanakimbia kwa mamia kwenda 

nchi za Ulaya kutafuta 

maisha.Huko mnakoenda mnataka 

mkayaharibu mazingira kama 

mlivyofanya katika nchi zenu? 

Suala la wahamiaji toka nchi za 

Afrika limekuwa ni ajenda katika 

kila mkutano,mimi naona ni 

upuuzi mkubwa na hatuwezi 

kupoteza muda wetu kuwajadili 

watu ambao hawawezi kujiongoza 

wao wenyewe,hawawezikuyatawala mazingira yao 

wenyewe na hawawezi kuwa na 

mtazamo wa mbali wa kujua 

kwamba wakiyaharibu mazingira 

wanayaharibu pia maisha 

yao.Wanapigana wenyewe kwa 

wenyewe kugombea madaraka na 

kusababisha matumizi makubwa 

ya fedha kuwahudumia 

wakimbizi.Ninawambia viongozi 

wenzangu hasa wale wa mataifa 

ambayo yamekuwa yakiwapokea 

na kuwapa hifadhi hawa watu 

wanaokimbia nchi zao,muache 

haraka kufanya hivyo.Wakamateni 

wote na muwarejeshe katika nchi 

walikotoka.Ni wakati wa waafrika 

kupambana na maisha yao 

wenyewe.Wakianzisha vita watafute wenyewe namna ya 

kupata suluhu.Tukiendelea 

kuwapokea wakimbizi wao na 

kuwapa hifadhi bara zima la Afrika 

litahamia huku na mnajua nini 

kitakachotokea? Watazaana huku 

na kuwa kizazi kikubwa kiasi 

kwamba baadae watoto wa watoto 

wetu watapata shida ,watakosa 

sehemu za makazi kwahi hawa 

waafrika ni watu wenye kuzaana 

bila mpangilio “ akanyamaza 

halafu akaendelea 

“Imenilazimu kuzungumza 

maneno haya makali si kwamba 

ninawachukia waafrika la 

hasha,bali nataka waufahamu 

ukweli na wajitambue.Tusiendelee 

kuwapa maneno matamu kila mara lazima tuwaambie kwa ukali 

ili wazinduke toka katika usingizi 

waliolala.Viongozi wa Afrika 

imarisheni demokrasia katika nchi 

zenu ,heshimuni katiba zenu na 

msing’ang’anie madaraka kwani 

mmekuwa ndiyo vyanzo vya 

migogoro mingi.Nchi yangu 

imeanza kubadili sera zake za nje 

hususan kwa bara la 

Afrika.Tunataka tupunguze 

misaada yetu na tutaielekeza kwa 

nchi zile tu ambazo zitastawisha 

demokrasia na utawala 

bora.Viongozi wale ambao 

watavunja katiba za nchi zao kwa 

lengo la kujiongezea muda wa 

kutawala au kutawala nchi zao 

kwa mabavu hawataonja hata senti moja toka kwa 

Marekani.Anzeni pia kujifunza 

kujiendesha bila kutegemea 

misaada ya kutoka nje.Waambieni 

watu wenu wasikimbilie Ulaya bali 

wabaki katika nchi zao na wafanye 

kazi.Huku wanakokimbilia hakuna 

maisha ya bure.Si lengo la 

marekani kuingilia masuala ya 

ndani ya nchi zenu lakini natoa 

onyo kwa kiongozi yoyote ambaye 

atang’ang’ania madarakani au 

kutawala kwa mabavu bila kufuata 

katiba sisi hatutasita kumtoa 

madarakani kwa nguvu ili 

wananchi wake waishi kwa 

amani.Nawafahamu maraisi 

kadhaa wa Afrika ambao 

wamezigeuza ikulu za nchi zao kuwa kama nyumba zao za 

kudumu,siku zao 

zinahesabika.Nawaonya 

waheshimu katiba na waondoke 

madarakani.Ninawaonya vile vile 

baadhi ya maraisi ambao 

wanafadhili kushirikiana na 

vikundi vyenye kuleta machafuko 

na hasa ugaidi hamtabaki 

salama.Tunawafahamu na 

tunaendelea kuwafuatilia na muda 

ukifika nawahakikishia 

tutawaondoa bila 

kigugumizi.Kama mmeshindwa 

kujiongoza wenyewe basi 

itatulazimu kuja kuwatawala tena” 

rais Mike akanyamza baada ya 

viongozi wa kutoka bara la Afrika 

kusimama na kutaka kutoka nje ya ukumbi kufuatia matamshi yale 

makali ya kuudhi.Juhudi 

zikafanyika na kuwasihi wabaki 

ukumbini na wakatii na hotuba 

ikaendelea. 

“Kitendo kilichotaka 

kufanywa na viongozi wa kutoka 

Afrika kinadhihirisha yale 

niliyokuwa nayasema muda mfupi 

uliopita kwamba viongozi hawa 

hawapendi kuelezwa ukweli.Kwao 

ukweli ni kutukanwa,mtawezaje 

kukuza demokrasia katika nchi 

zenu kama hamtaki 

kukosolewa?Lazima muwe tayari 

kuambiwa ukweli hata kama 

unauma na muupookee,hiyo ndiyo 

demokrasia.Afrika bado kuna 

ombwe kubwa la uongozi na kama kusipofanyika mabadiliko 

makubwa ya kiuongozi basi 

matatizo ya bara hili 

hayatakwisha.Afrika inahitaji 

viongozi wenye mtazamo 

mpya,wanaokubali kukosolewa na 

wakajirekebisha” akanyamaza 

baada ya minong’ono kuzidi.Baada 

ya ukumbi kutulia akaendelea 

“Dunia inaendelea 

kupambana na matizo ya ugaidi 

toka katika vikundi vya kigaidi 

vinavyoendelea kuibuka kila 

uchao na kutishia amani ya 

dunia.Mashambulio kadhaa 

tunaona yametokea katika bara la 

Ulaya na watu wasio na hatia 

wamepoteza maisha yao.Jijini 

London kwa mfano ,watu kadhaa wamepoteza maisha yao kwa 

vitendo vya ugaidi,nchini ufaransa 

vile vile na nchi kadhaa za 

Ulaya.Vitendo hivi vinavyoendelea 

kushamiri siku hadi siku 

vinaonyesha kwamba bado kuna 

kazi kubwa ya kufanya ili 

kuutokomeza kabisa ugaidi 

duniani.Wakati juhudi za 

kupambana na makundi haya ya 

ugaidi zikiendelea,kumeibuka 

kitisho kingine kwa amani ya 

dunia ambacho ni Korea 

Kaskazini.Kwa muda mrefu sasa 

taifa la Korea kaskazini limekuwa 

likijiimarisha kijeshi kwa 

kutengeneza silaha kali za 

maangamizi na makombora ya 

masafa marefu.Kama haitoshi taifa hilo limekuwa likifanya majaribio 

ya makombora na kuleta wasiwasi 

mkubwa kwa nchi majirani zake 

na kwa usalama wa dunia.Taarifa 

za kiintelijensia zinaonyesha 

kwamba Korea Kaskazini wanayo 

hazina kubwa ya makombora ya 

masafa marefu yanayoweza 

kuvuka bara hadi bara.Umoja wa 

mataifa umekuwa unachukua 

hatua mbali mbali za kuiwekea 

vikwazo Korea Kaskazini katika 

harakazi zake za kujimarisha 

kijeshi lakini pamoja na vikwazo 

hivyo bado taifa hili limekuwa 

kiburi na linaendelea na 

utengenezaji na kujaribu 

makombora yake.Ni siku mbili tu 

kabla ya mkutano huu kuanza,Korea Kaskazini 

wamefanya jaribio kubwa la 

Kombora lililopita juu ya kisiwa 

kilicho chini ya Japan.Huu ni 

uchokozi mkubwa na 

usiovumilika.” Akanyamaza kidogo 

halafu akaendelea 

“Wakati Marekani na jumuiya 

za kimataifa wanaendelea na 

jitihada za kuidhibiti Korea 

Kaskazini juu ya mpango wake wa 

silaha kali,yapo mataifa ambayo 

kwa makusudi kabisa wameamua 

kuiunga mkono Korea Kaskazini.” 

Akanyamaza tena kwa muda 

“Jana usiku muwakilishi wa 

rais wa Korea kaskazini 

amekutana na mmoja wa marais 

wa kutoka nchi moja ya Afrika na wakaongelea kuhusiana na 

kuanzishwa kwa mashirikiano ya 

kibiashara baina ya nchi zao na 

kama haitoshi walizungumza pia 

kuhusiana na kuiuzia Korea 

Kaskazini madiniya 

Uranium.Niliposema awali 

kwamba baadhi ya viongozi wa 

Afrika wana matatizo sikuwa 

nawatukana bali nilikuwa 

namaanisha na hiki kilichotokea 

jana usiku ni mfano tosha.Kama 

kiongozi wa nchi hii ana akili 

timamu anawezaje kuahidi kuiuzia 

Korea Kaskazini madini hatari ya 

Uranium wakati akijua kabisa 

kwamba Korea kaskazini 

wanataka kuyatumia madini hayo 

kutengeneza silaha za nyuklia ambazo ni tishio kwa 

dunia?Ninatoa onyo kwa kiongozi 

huyo ambaye sitaki kumtaja lakini 

yumo ndani ya ukumbi huu na 

ananisikia, asithubutu kufanya 

biashara yoyote na Korea 

kaskazini.Tunaendelea 

kumfuatilia kwa karibu 

sana.Akikaidi onyo hili atakuwa 

amejiingiza katika matatizo 

makubwa sana.Hatutavumilia 

kitendo chochote cha kufifisha 

juhudi za kimataifa za kuizuia 

Korea Kaskazini isiendelee 

kutengeneza makombora na silaha 

za maangamizi.Narudia tena 

tutachukua hatua kali mno kwa 

taifa hili masikini la Afrika lenye 

kutaka kuanzisha mahusiano na Korea Kaskazini” Aliongea kwa 

ukali rais Mike straw. 

Aliendelea kuongelea pia 

masuala mengine na kisha 

akamalizia hotuba yake iliyoja 

ubabe na maneno ya kuudhi. 

Baada ya hotuba ile ya rais wa 

Marekani kumalizka zikafuata 

hotuba nyingine mbili toka kwa 

rais wa Equado na Mauritius halafu 

ikafuata zamu ya rais wa Tanzania 

kutoa hotuba yake.Alipanda 

jukwaani na kuanza kuhutubia 



Baada ya hotuba ile ya rais wa 

Marekani kumalizka zikafuata 

hotuba nyingine mbili toka kwa 

rais wa Equado na Mauritius halafu 

ikafuata zamu ya rais wa Tanzania 

kutoa hotuba yake.Alipanda 

jukwaani na kuanza kuhutubia 

“Katibu mkuu wa umoja wa 

mataifa na viongozi wengine wa 

mataifa mlioko hapa,ni mara 

yangu ya kwanza kuhutubia katika 

mkutano huu mkubwa na 

adhimu,na ni heshima kubwa kwangu kusimama mbele yenu 

baba na mama zangu” akasema 

huku akitabasamu na kupigiwa 

makofi 

“Nilikuwa nimejiandaa kutoa 

hotuba hii hapa” akaiinua hotuba 

aliyokuwa ameindaa na 

kuionyesha halafu akaiweka chini 

“Lakini sitaitoa hotuba hii na 

badala yake nitasema maneno 

machache” akanyamaza kidogo 

halafu akaendelea 

“Viongozi wa dunia mlioko 

hapa,naomba mfahamu kwamba 

kuzaliwa Afrika si bahati mbaya,si 

dhambi na wala si mkosi .Mungu 

aliyetukuka ndiye aliyeamua 

kuwepo na Afrika 

,Asia,Ulaya,Amerika na mabara mengine.Ndiye aliyeamua 

waafrika,wazungu,wachina 

waarabu na akaona 

inampendeza.Kuwabagua,kuwadh

arau kwa namna yoyote ile 

waafrika au watu wa bara lingine 

waliumbwa na Mungu yule yule 

aliyekuumba wewe ni kudharau 

uumbaji wake Mungu na 

kumkosoa kwamba alikosea katika 

uumbaji.Mimi ni 

mwafrika,ninajivunia kuwa 

mwafrika na ninamshukuru 

Mungu kuniumba mwafrika na 

katika maisha yangu 

sintomdharau mtu kwa sababu ya 

mahala atokako au kuwa na rangi 

tofauti na mimi.Huu ni ubaguzi wa kiwango cha juu mno” akanyamaza 

baada ya makofi mengi kupigwa. 

“Mmemsikia rais Mike straw 

aliyetoka kutoa hotuba yake hapa 

muda si mrefu sana.Ni hotuba 

iliyojaa dharau na ubaguzi 

mkubwa kwa waafrika.Nathubutu 

kusema kwamba hii ni hotuba ya 

kiwango cha chini mno niliyowahi 

kusikia inatolewa na rais wa taifa 

kubwa kama hili na ninasema bila 

kuogopa kwamba hii ni aibu 

kubwa kwa taifa kama Marekani 

ambalo linajinasibu kuwa kinara 

wa demokrasia duniani” Makofi 

yakapigwa akaendelea 

“Nimesoma Marekani katika 

moja ya vyuo vikuu,nilibahatika 

kuwa rais wa serikali ya wanafunzi.Niligundua wanafunzi 

wenye asili ya Afrika walikuwa 

hawapewi kipaumbele katika chuo 

nilichosoma hivyo nikapambana 

na kuhakikisha kunakuwa na haki 

na usawa kwa wanafunzi wote.Hili 

lilifanikiwa lakini kwa kupitia 

mambo magumu mno ambayo 

sitaki kuyaeleza hapa.Katika 

mojawapo ya hotuba niliyowahi 

kuitoa katika kongamano la 

kumkumbuka mwanaharakati 

mtetea haki za weusi Martin 

Luther niliwahi kueleza ndoto 

yangu ya kuiona siku moja Afrika 

iliyoungana na kuwa moja.Hii 

ndiyo Afrika waliyoiota viongozi 

wetu mashupavu walioikomboa 

Afrika,Mungu awarehemu.Viongozi hawa akina 

hayati mwalimu Nyerere,Nkrumah 

na wengine wengi walitaka kuwa 

na Afrika moja ambayo ndiyo 

itakuwa suluhu ya matatizo 

yetu.Tukiwa wamoja tutakuwa na 

nguvu na kupiga hatua za haraka 

kimaendeleo.Leo hii ninarejea 

tena kuitamka ndoto yangu ya 

kutaka kuiona Afrika ikisimama na 

kuwa moja” makofi mengi 

yakapigwa 

“Amkeni viongozi wa 

Afrika.Simameni tuungane na 

kuwa na sauti moja yenye nguvu 

kuweza kupinga ukandamizwaji 

unaofanywa na mataifa makubwa 

yakiongozwa na 

Marekani.Tumesikia matamshi ya kubeza waafrika na viongozi wao 

kutoka kwa rais wa 

Marekani.Dharau hizi 

zinasababishwa na ubinafsi wetu 

sisi viongozi wa mataifa ya 

Afrika.Laiti kama tungekuwa na 

nguvu moja tungekuwa na nguvu 

ya kupambana na mtu yeyote yule 

awe mkubwa au mdogo.Narudia 

kuwaasa tena baba na mama zangu 

mlioko hapa leo ni wakati wa 

Afrika kuungana na hiyo ndiyo njia 

pekee ya kuondoa kauli kama hizi 

za kejeli kwetu na ubaguzi 

mkubwa tunaofanyiwa.Mwana wa 

Afrika Mu’ammar Gaddafi alikuwa 

na ndoto kama yangu ya kuiona 

siku moja Afrika inaungana na 

kuwa moja lakini hakupendwa na wakuu wa mataifa makubwa na 

wakafanya kila wawezalo 

wakamuua.Niwaulizeni enyi 

viongozi mnaotoka mataifa 

makubwa yenye kukomaa 

kidemokrasia,baada ya 

kumuondoa Gaddafi nchi ya Libya 

iko salama?Mmewapa wana Libya 

demokrasia mliyowaahidi 

wataipata baada ya kumng’oa mtu 

mliyemuita dikteta? Hao watu 

wanaokuja kwa mamia katika nchi 

zenu kutafuta maisha mazuri ni 

matokeo ya harakati zenu 

mnazofanya katika Afrika”Makofi 

mengi yakapigwa.Dr Vivian 

akaendelea 

“Bara la Afrika linaitwa bara 

masikini lakini Afrika si masikini.Ni bara tajiri pengine 

kuliko yote.Umasikini wetu 

unasababishwa na wizi 

unaofanywa na mataifa makubwa 

kwa kubeba rasilimali zetu na 

kwenda kuzitajirisha nchi zao na 

kutuacha katika umasikini 

mkubwa.Mungu ametupatia mali 

nyingi,kila pembe ya Afrika kuna 

mali lakini mnakuja kwa kujifanya 

mnawekeza na kuchuma mali zetu 

kisha mnatuachia mashimo na 

huku hazina zenu zinanona kwa 

madini yetu.Pamoja na wizi huu 

mkubwa bado mnatudharau na 

kutuita kila aina ya majina ya 

dharau.Ninasimama hapa mbele 

yenu baba na mama zangu na 

ninasema bila woga kwamba wizi huu wa madini yetu na mali 

nyingine umefika mwisho katika 

nchi yangu.Ninawaomba na 

viongozi wengine wa Afrika 

mniunge mkono ili tuweze 

kufaidika na mali ambazo Mungu 

ametupa katika maeneo 

yetu.Tanzania ni nchi 

huru,tunajiendesha wenyewe na 

hatutaki kuchaguliwa marafiki au 

watu wa kufanya nao 

biashara.Hatutaki kupangiwa na 

taifa lolote kuhusu namna ya 

kutumia rasilimali zetu.Mali ni za 

kwetu tutaamua wenyewe namna 

ya kuzitumia au tumuuzie 

nani.Nataka kumpa salamu rais wa 

Marekani na washirika wake 

kwamba mimi naweza kuwa rais mdogo kuliko wote na wanaweza 

kuniona dhaifu lakini nina 

msimamo usioyumba.Nikisema 

hapana ni hapana.Sina ndimi mbili 

na huwa sigeuki nyuma nikifanya 

maamuzi.Siogopi vitisho vyovyote 

toka taifa lolote lile kubwa au 

dogo.Kama alivyosema Mike straw 

nimefanya mazungumzo na 

mjumbe wa rais wa Korea 

kaskazini jana usiku.” Minong’ono 

ikaanza kusikika mle ukumbini 

“Nawaeleza bila kuwaficha 

kwamba rais ambaye Mike straw 

hakumtaja jina na alimtolea 

maonyo makali ni mimi na 

nilikutana na mjumbe kutoka 

Korea Kaskazini jana usiku 

tukafanya mazungumzo kuhusiana na kuanzisha kwa mashirikiano ya 

kibiashara baina ya nchi 

zetu.Narudia tena kuweka wazi 

kwamba nitaendelea na 

mazungumzo na Korea Kaskazini 

na kama tutafikia makubaliano 

basi tutawauzia madini ya 

Uranium ambayo tunayo mengi 

sana nchini kwetu.Si Korea 

Kaskazini pekee bali taifa lolote 

lile ambalo litataka kufanya 

biashara na sisi 

tunalikaribisha.Tunachokitaka ni 

madini yetu yatunufaishe.Sihofii 

vikwavyo vyenu vya kiuchumi au 

hata kunyimwa misaada yenu 

ambayo ndiyo imekuwa kigezo 

kikuu cha kutunyonya.Mimi na 

wananchi wangu tutafunga mikanda na kuanza safari ya 

kujitegemea.Itatuchukua muda 

kufikia nchi ya kujitegemea lakini 

watoto wa watoto wetu watakuja 

kunufaika na maamuzi yetu ya leo 

na kutusoma katika historia 

namna tulivyokataa unyonyaji na 

kuamua kufanya maamuzi 

magumu kwa manufaa 

yao.Nitasimama mbele ya watu 

wangu na nitawaongoza katika 

safari hii na nitahakikisha 

ninawafikisha salama katika nchi 

ya maziwa na asali isiyohitaji 

kujiendesha kwa misaada ya 

mabeberu.Kwenu viongozi wa 

Afrika na waafrika kwa ujumla 

wakati wa kufanya mapinduzi na 

kuondokana na unyonyaji wa mataifa makubwa umefika.Amkeni 

toka usingizini tuungane na tuanze 

kwa pamoja safari ya kujitegemea 

kiuchumi.Tukuze biashara baina 

ya nchi na nchi na hatimaye bara 

zima .Tukuze pia biashara na wale 

ambao watakuwa tayari kutuunga 

mkono katika safari hii kama vile 

China na wengine 

watakaojitokeza.Kwa viongozi wa 

umoja wa mataifa ninawaomba 

muwe na nguvu.Msikubali taifa 

moja liwe na nguvu na sauti kubwa 

ndani ya chombo hiki kikubwa na 

kushinikiza kufanyika mambo 

watakavyo wao.Japo 

tunatofautiana kiuchumi lakini 

mbele ya chombo hiki tunapaswa 

kuwa sawa.Kama mtaendelea kuipa upendeleo wa kipekee 

Marekani kwa sababu ya mchango 

wake mkubwa,chombo hiki 

kitapoteza dira na hakitakuwa na 

maana yoyote,kitakuwa ni chombo 

cha Marekani kukandamiza 

mataifa madogo na ninawaomba 

viongozi wa mataifa mengine 

kususia mikutano kama hii 

ambayo inakuwa haina tija yoyote 

kwa nchi zetu” akanyamaza na 

kushangiliwa 

“Ndugu katibu mkuu wa 

umoja wa mataifa na viongozi wote 

wa mataifa mlioko hapa,machache 

niliyotaka kuyazungumza ni 

hayo.Narudia tena kuwakumbusha 

viongozi wenzangu wa Afrika na 

wale wa nchi zisizokubaliana na ukandamizwaji unaofanywa na 

mataifa makubwa tuunganishe 

nguvu na hata ikiwezekana tuwe 

na sisi na umoja wetu na hata jeshi 

letu ili asitokee mtu yeyote 

mkubwa au mdogo akatutisha 

kutokana na uwezo wake.Siku zote 

nitasimama katika ukweli na 

sintochoka kumkosoa yeyote awe 

mkubwa au mdogo.Ahsanteni sana 

kwa kuniskiliza,Mungu awabariki” 

Dr Vivian akamaliza kutoa maneno 

yake machache na ukumbi 

ukasimama kumshangilia.Ni 

viongozi wachache tu waliobaki 

vitini wameketi.Hotuba ile fupi 

iliwakuna wengi hasa viongozi wa 

kutoka Afrika. Baada ya kutoa hotuba ile Dr 

Vivian hakutaka kuendelea kukaa 

pale ukumbini akawaamuru watu 

wake waondoke zao wakarejea 

hotelini.Akawaita wote katika 

ukumbi wa chakula na 

kuwashukuru kwa kasi kubwa 

walizofanya na kisha akawaeleza 

kitu kilichowashangaza. 

“Tunarejea Tanzania usiku 

huu” 

Wote wakastuka lakini 

hakuna aliyehoji kwani wote 

wanafahamu msimamo wa kongozi 

wao.Wakaanza kujiandaa kwa ajili 

ya kuondoka.Ni Theresa pekee 

aliyemfuata Dr Vivian chumbani 

kwake “Dada mbona ratiba 

inaonyesha kwamba bado kuna 

mikutano kadhaa ambayo 

unapaswa kuihudhuria.Kuna 

mkutano umeandaliwa na Kenya 

kuhusiana na Malaria,na vile vile 

kuna mkutano umeandaliwa na 

India kuhusiana na kupunguza vifo 

vya wajawazito wakati wa 

kujifungua” 

“Yote hiyo haina umuhimu 

kwetu.Tunarejea nyumbani usiku 

huu” akasema Dr Vivian. 

“Sawa dada.Hata hivyo 

hongera sana kwa hotuba kali 

uliyoitoa.Dada umeishangaza 

dunia kwa ujasiri wako.Wakati 

tunarejea nilikuwa napitia maoni 

mitandaoni kuhusiana na hotuba yako.Inaongelewa zaidi kuliko 

hata hotuba ya rais wa 

Marekani.Wengi hata wamarekani 

wenyewe hawajafurahishwa na 

hotuba iliyojaa matamshi ya 

kibaguzi ya rais wao na ndiyo 

maana ulipoamua kumjibu wengi 

wamefurahi na kukupongeza kwa 

ujasiri wa kuweza kusimama na 

kumpa za uso Mike straw” 

akasema Theresa na Dr Vivian 

akatabasamu. 

“Sikuwa nimepanga 

kuyazungumza yale lakini 

kutokana na hotuba ile ya kishenzi 

ya Mike straw iliyojaa ubaguzi 

mkubwa na kejeli kwa waafrika 

nililazimika kutoa hotuba ile 

kumjibu.Theresa wakati wa kuwaogopa hawa viongozi 

wakubwa umekwisha hivi sasa ni 

jino kwa jino.Ni wakati wa Afrika 

kusonga mbele” 

“Dada umeamsha upya ari ya 

waafrika na ninatumai kila 

mwafrika aliyeisikia hotuba yako 

atabadili mtazamo na kujenga 

uzalendo kwa nchi zao.Mjadala 

mwingine unaoendelea hivi sasa ni 

kuhusiana na Tanzania na Korea 

Kaskazini.Ni kweli dada 

umedhamiria kuanzisha 

mahusiano na Korea Kaskazini na 

kuwauzia madini ya Urani? 

Theresa akauliza. 

“Samahani sikuwa 

nimekushirikisha katika hili 

suala.Jana usiku nilipokea ujumbe wa watu wanne na miongoni mwao 

alikuwepo mmoja kutoka Korea 

Kaskazini.Huyu alikuwa ni 

mjumbe maalum aliyetumwa na 

rais wa Korea kaskazini 

.Tulizungumza masuala kadhaa na 

kubwa lililobeba mazungumzo 

yetu ni mashrikiano ya kibiashara 

baina ya nchi zetu .Wafanya 

biashara wa Korea Kaskazini 

wanataka kuwekeza nchini 

Tanzania kwa kuanzisha viwanda 

vya nguo lakini serikali ya Korea 

kaskazini wanataka kuanzisha 

mgodi mkubwa wa kuchimba 

madini ya Urani.Nilizipokea 

salamu hizo na sikuwa nimetoa 

jibu lolote kwao lakini kwa namna 

alivyoniudhi Mike straw nimeamua kuendelea na mchakato 

wa kuanzisha mashirikiano na 

Korea Kaskazini.Nafahamu nchi 

itaingia katika matatizo makubwa 

ya kiuchumi lakini tutakipita hiki 

kipindi kigumu.Sisi ni taifa 

masikini lakini tukisimama imara 

na kulinda kilicho chetu,kujenga 

biashara ya ndani pamoja na za 

kikanda,kutumia vizuri mapato ya 

serikali,kujiwekea akiba kubwa ya 

chakula nina uhakika tutavuka 

salama.Kinachonishangaza Mike 

straw amefahamu vipi kuhusu 

mazungumzo yangu na wale 

wageni? Nimejiuliza sana swali hili 

nimekosa jibu.Je Marekani 

wamekuwa wananifuatilia? Kama ndiyo kwa nini? Hili suala lazima 

lichunguzwe” akasema Dr Vivian 

“Dada Vivi,suala hili linanipa 

hofu sana.Tukiwekewa vikwazo 

vya kiuchumi nchi itayumba sana 

na lawama zote zitakuja kwako” 

akasema Theresa 

“Usiogope 

Theresa.Nimekwisha amua kuingia 

vitani na nitawaongoza watanzania 

katika vita hii.Tutavuka 

salama.Nitawafikisha kule 

mnakohitaji kufika.Vikwazo 

lazima viwepo lakini haviwezi 

kuturudisha nyuma.Palipo na nia 

pana njia.Usiwe na hofu Theresa 

dada yako niko imara na huwa 

sitetereki.Nenda kaanze kujiandaa 

turejee nyumbani” akasema Dr Vivian na Theresa akatoka kisha 

rais akamuita Edwin Swai. 

“Hongera sana madam 

president kwa hotuba nzuri 

ambayo naweza kuiita ni hotuba ya 

kimapinduzi.Ulipokuwa jukwaani 

unatoa hotuba ile mikono yangu 

ilikuwa kifuani mwili ukinisisimka 

na hali hiyo iliwapata wengi.Kila 

mtu ameshangazwa na ujasiri 

wako.Hotuba kama hizi tulizoea 

kuzisikia kwa viongozi wale 

majasiri wasiowaogopa hawa 

wakubwa kama akina mzee 

Mugabe,Gaddafi n.k” akasema 

Edwin na Dr Vivian akatabasamu 

“Ahsante sana 

Edwin.Nimekuita hapa kwa 

masuala mawili.Kwanza ni kukujulisha kwamba hatuna 

sababu ya kuendelea kuk hapa 

hasa baada ya matamshi yale ya 

kibaguzi toka kwa rais wa 

Marekani.Najua ratiba yetu 

inatuelekeza bado kuna mikutano 

kadhaa nahitaji kuhudhuria lakini 

siwezi kuhudhuria mkutano 

wowote tena.Sitaki kuendelea 

kukaa ndani ya nchi hii inayonuka 

ubaguzi huku yenyewe ikiwa 

kinara wa kunyooshea wenzake 

kidole” 

“Madam president mimi 

nadhani ungempuuza tu yule 

jamaa.Dunia nzima wanamfahamu 

ni mropokaji .Tukiondoka 

mapema na kuiacha mikutano haitaleta picha nzuri kwa wale 

walioandaa” 

“Edwin hatulali Marekani,leo 

tunarejea nyumbani.Tayari 

nimeanzisha vita na siwezi 

kuendelea kukaa katika ardhi ya 

adui ni mbaya hata kiusalama” 

akasema Dr Vivian. 

“Jambo lingine ni kwamba 

jana nilifanya mazungumzo na 

mjumbe wa rais wa Korea 

Kaskazini lakini sikuwa 

nimefanya maamuzi yoyote 

kuhusiana na ombi lao la kutaka 

kuwepo kwa mashirikiano ya 

kibiashara baina ya nchi zetu mbili 

na vile vile kuhusu ombi lao la 

kutaka kuwekeza katika uchimbaji 

wa madini ya Urani.Nililipokea ombi lao na nilitaka kwanza 

nikakae na baraza langu la 

mawaziri pamoja na washauri 

wangu tulijadili hili suala lakini 

kwa maneno aliyoyatamka Mike 

straw usiku huu nimeamua 

kufanya mashirikiano na Korea 

Kaskazini” 

“Madam Pres…..” 

“Edwin sitaki ushauri wowote 

katika hilo suala.Jambo lingine 

nataka uchunguzi wa kina 

ufanyike kujua ni kwa namna gani 

rais wa Marekani amepata taarifa 

za mimi kukutana na mjumbe wa 

rais wa Korea Kaskazini jana usiku 

na hata mambo 

tuliyoyazungumza.Nimeshangaa 

sana” akasema Dr Vivian. “Madam president 

inawezekana kuna moja wao 

alikuwa anarekodi mazungumzo 

yenu.Yawezekana kati ya watu 

wale kuna mmoja alikuwa 

mpelelezi.watu wako wa usalama 

wanapaswa kufanya kazi ya ziada 

kuanzia sasa kuwachunguza watu 

wote unaokutana nao.Yawezekana 

kabisa wengine wakawa ni 

wapelekezi wanakuja 

kukuchunguza.Unahitajika 

umakini mkubwa sana.Hta hivyo 

tukisema tulichunguze jambo hili 

itatuchukua muda mrefu kitu 

ambacho hatuna.Kwa muda huu 

mfupi sidhani kama tutaweza 

kugundua chochote” akasema 

Edwin.Dr Vivian akainamisha kichwa akafikiri kwa muda halafu 

akasema 

“Achana na hilo 

suala.Mjiandae tuondoke” 




DAR ES SALAAM – TANZANIA 

Safari ya saa kumi na tano 

ilihitimishwa pale ndege ya rais 

ilipotua katika uwanja wa ndege 

wa kimataifa wa Julius 

Nyerere.Tayari ni saa saba za usiku kwa saa za Afrika 

mashariki.Toka uwanja wa ndege 

wa kimataifa wa Julius Nyerere 

rais akaelekea moja kwa moja 

ikulu ambako aliagana na watu 

alioongozana nao katika safari ile 

akaenda chumbani kwake 

kupumzika.Baada ya kuoga 

akamshukuru Mungu kwa 

kumfikisha nyumbani salama 

halafu akakaa kitandani 

“Hii ilikuwa ni safari yangu 

mbaya kabisa lakini nashukuru 

nimeweka msimamo wangu kwa 

dunia.Kuna msemo unapendwa 

sana siku hizi wanasema 

nimeliamsha dude.Na kweli dude 

limeamka haswa.Nimeingia katika 

mgogoro mkubwa na Marekani ambao ni wadu wetu wakubwa wa 

maendeleo,wanachangia fedha 

nyingi kila mwaka katika bajeti 

yetu.Hii hainisumbui sana 

japokuwa kama nchi tutayumba 

lakini lazima tuingie vitani ili 

tuweze kujifunza kujitegemea.Hii 

misaada ndiyo inayotulemaza na 

kutufanya tuwe wanyonge na 

kushindwa hata kupiga kelele pale 

tunapoibiwa huku tukiona au hata 

pale 

tunapokandamizwa.Nitawaelewes

ha watanzania nitawaomba 

tuungane pamoja katika safari hii 

ya kuelekea kujitegemea na kama 

tukiunganisha nguvu na kuwa kitu 

kimoja tutavuka salama.Mimi 

sintabadili msimamo wangu na sintageuka nyuma nimeamua 

kwenda mbele na lazima tuende 

mbele.Dunia tayari imenielewa na 

imeelewa msimamo wangu 

kwamba Tanzania sasa imeamka 

na hatutaki tena mzaha katika 

rasilimali zetu na hatutaki 

kupangiwa nani wa kufanya naye 

biashara.Ndani ya kipindi kifupi 

nitasimamisha shughuli zote za 

uchimbaji wa madini zinazofanywa 

na makampuni ya kigeni na 

tutapitia upya sera na sheria zetu 

za madini na kuweka sheria na 

masharti mapya ili Tanzania ianze 

kunufaika na rasilimali 

zake.Mikataba yote ya madini 

lazima ifumuliwe na kuandikwa 

upya.Endapo kuna kampuni yoyote itakayopingana na jambo hili 

itafungashiwa virago ndani ya 

kipindi kifupi.Hii ni vita kwa hiyo 

kuanzia sasa natakiwa kuongeza 

ulinzi wangu mara dufu pamoja na 

wale wanaonizunguka.Kitendo cha 

rais wa Marekani kupata taarifa za 

kukutana na kufanya mazungumo 

na mjumbe wa rais wa Korea 

Kaskazini kimenifanya nigundue 

kwamba siko salama.Watu wa 

usalama lazima walifanyie 

uchunguzi hili jambo haraka sana.” 

Akawaza na kujilaza kitandani 

“Nataka kesho bila kuchelewa 

mchakato wa mazungumzo na 

Korea kaskazini uanze mara 

moja.Asubuhi nitakuwa na kikao 

cha dharura cha baraza la mawaziri na nitatoa maelekezo ili 

jambo hili lisichelewe.Kuna jambo 

lingine nimekuwa nalifikiria 

nikiwa njiani.Kwa nini 

nisizungumze na hawa Korea 

Kaskazini watujengee kinu cha 

nyuklia hapa nchini kwa ajili ya 

kuzalisha nishati ya umeme? Kama 

madini ya Urani tunayo kwa nini 

basi tushindwe kuyatumia 

kuzalisha umeme na kuwa na 

nishati ya uhakika kwa viwanda 

vyetu na ikiwezekana hata tuuze 

nje ya nchi?Tukiwa na umeme wa 

uhakika utachochea viwanda vingi 

kujengwa na hivyo nchi kupiga 

hatua kiuchumi.Hili ni jambo la 

msingi na ninaona ushirikiano na 

Korea kaskazini unaweza ukawa na manufaa makubwa kwa 

Tanzania.” Akawaza Dr Vivian. 

************** 

Bado rais wa Tanzania Dr 

Vivian Matope aliendelea kuviteka 

vyombo vya habari Tanzania na 

sehemu mbalimbali 

duniani.Asubuhi hii kila gazeti 

liliandika habari zake.Mitandaoni 

bado watu waliendelea na 

mijadala mbali mbali kumuhusu 

huyu rais na mambo aliyoyaongea 

katika kikao cha baraza kuu la 

umoja wa mataifa na kubwa likiwa ni mashirikiano ya Tanzania na 

Korea kaskazini. 

Ni kawaida ya Dr Vivian 

kuamka asubuhi na kusali kabla ya 

kuelekea katika mazoezi halafu 

akaoga na kujiweka tayari kwa 

ajili ya kuikabili siku.Saa mbili na 

nusu rais akaingia ofisini kwake 

tayari kwa kuanza kazi.Saa nne za 

asubuhi akaingia katika kikao cha 

dharura cha baraza la mawaziri 

Wakati Dr Vivian akiongoza 

kikao cha baraza la mawaziri 

,Edwin Swai mshauri wake wa 

masuala ya usalama alikuwa garini 

kuelekea Mbezi kuonana na 

Meshack Jumbo mkurugenzi 

mstaafu wa idara ya 

ujasusi.Aliwasili nyumbani kwa Meshack Jumbo na kujitambulisha 

kwa walinzi wakamruhusu apite 

akaelekea ndani ambako 

alipokewa na mke wa Meshack 

Jumbo akamkaribisha 

sebuleni.Mama yule mchangamfu 

akamkirimu Edwin kahawa halafu 

akaagiza mtumishi wake akamuite 

Meshack Jumbo aliyekuwa katika 

shughuli ya kukagua mifugo 

yake.Aliposikia Edwin amekuja 

akaacha shughuli zake akarejea 

sebuleni 

“Karibu sana Mr Swai” 

akasema Meshack Jumbo baada ya 

kusalimia.Mkewe akamletea maji 

ya nanasi kinywaji anachokipenda 

sana kisha akatoka na kuwaacha 

wanaendelea na maongezi “Vipi maisha yanakwendaje 

Meshack? Akaanzisha 

mazungumzo Edwin.Meshack 

Jumbo akatabasamu na kusema 

“Maisha yanakwenda vizuri 

sana.Kustaafu ukiwa umejiandaa 

ni kutamu sana.Nina mashamba 

yangu yanazalisha mavuno ya 

kutosha,nina mifungo mingi ya 

kutosha na hivi sasa niko katika 

mipango ya kuanzisha kiwanda 

kidogo cha kusindika mvinyo wa 

matunda.Kwa ujumla maisha ni 

mazuri.Vipi nyie huko serikalini 

mnaendeleaje na Dr Vivian? 

“Tunaendelea vyema ingawa 

mambo si mepesi kama ujuavyo Dr 

Vivian ni rais mwenye msimamo 

mkali sana.Husimama katika yale mambo anayoyaamini hata kama 

hayana tija kwake lakini akiamini 

kitu fulani huwa habadiliki” 

akasema Edwin 

“Ni mara ya kwanza Tanzania 

tunaongozwa na rais mwanamke 

tena kijana bado,unaonaje 

utendaji kazi wake? Hiyo 

misimamo yake mikali unadhani 

inaleta tija au anafanya hivyo 

kuwadhihirishia watu kwamba 

anaweza ili wamuogope kwa kuwa 

ni mwanamama?akauliza Meshack 

Jumbo 

“Kuna watu huwa dhaifu 

lakini hujitutumua na kujifanya 

majasiri ili kuficha udhaifu wao wa 

ndani.Isije kuwa na rais wetu naye 

yuko hivyo kwani sijabahatika kufanya naye kazi na simfahamu 

vyema” akaongeza Meshack 

“Dr Vivian ni kiongozi na 

ninaweza kusema ni mwanamama 

shupavu na jasiri sana.Kwa sisi 

tulio karibu naye tunamfahamu 

vyema na wakati mwingine 

tunashangazwa na ujasiri 

wake.Akiamua jambo huwa 

hageuki nyuma.Akitaka jambo liwe 

basi litakuwa.Hii ni tabia yake toka 

akiwa mdogo kwa mujibu wa 

maelezo yake yeye mwenyewe na 

wale wanaomjua toka angali 

mdogo.Kwa ujumla naweza 

kusema kwamba ni rais 

anayetufaa zama hivi.We need 

some one strong and powerfull and 

that someone is Dr Vivian.Mpaka sasa bado sijaona udhaifu wake 

wowote katika kufanya maamuzi” 

“I see” akasema Meshack 

Jumbo na kunywa maji ya nanasi 

kisha akauliza 

“Niliitazama hotuba yake 

aliyoitoa juzi usiku katika kikao 

cha umoja wa mataifa hata mimi 

nilistushwa sana na hotuba 

ile.Nimekuwa nairudia rudia ile 

hotuba mara kwa mara ili niweze 

kumfahamu vyema huyu rais 

ambaye ni mdogo pengine kuliko 

maraisi wote duniani.Haijazoeleka 

kwa rais wa kutoka nchi za afrika 

kusimama hadharani na 

kumshambulia rais wa Marekani 

kama alivyofanya Dr Vivian.Ujasiri 

kama huu walikuwa nao waasisi wetu wa afrika akina mwalimu 

Nyerere na wenzake ambao 

hawakuthubutu kumuonea aibu 

yeyote yule ambaye anaendekeza 

vitendo vya kibaguzi.Viongozi 

wetu wengi wa kizazi cha sasa 

hawana ujasiri huo wa kusimama 

na kuwakemea viongozi wa 

mataifa makubwa kama 

alivyofanya Dr Vivian na huu ni 

udhaifu mkubwa sana wa 

kiuongozi ila nashukuru rais wetu 

ameonyesha njia.Nimeipenda sana 

hotuba ile na ninaweza kusema ni 

hotuba bora kabisa niliyowahi 

kuisikia toka kwa kiongozi wa 

Afrika kwa miaka ya hivi 

karibuni.Tumezikosa sana hotuba 

kama hizi ambazo tungeweza kuzikia kwa mzee Mugabe au mzee 

Gadaffi Mungu amrehemu.Hawa ni 

viongozi wachache wa Afrika 

ambao walikuwa na uwezo wa 

kusimama na kukemea mataifa 

makubwa.Mungu amuongoze rais 

wetu asije kuyumba katika 

misimamo yake.By the way kuna 

hili suala la mahusiano na Korea 

kaskazini.Rais Mike straw 

alilizungumza kwa ukali sana na 

baadae Dr Vivian akakiri kwamba 

ataanzisha mahusiano na Korea 

kaskazini.Ninyi mlio karibu na rais 

mmelichukuliaje suala hili au 

mmemshauri nini? Akauliza 

Meshack Jumbo. 

“Hili suala hata sisi kwa mara 

ya kwanza tumelisikia akilitamka rais wa Marekani na baadae Dr 

Vivian akakiri kwamba ni kweli 

amefanya mazungumzo na 

mjumbe wa kutoka Korea 

Kaskazini.Tulipofika New York rais 

alikuwa na maongezi na wageni 

wanne na mmoja wa wageni hao 

alitokea Korea Kaskazini.Dr Vivian 

hakumueleza mtu yeyote 

walichoongea hadi pale 

alipotamka katika hotuba 

yake.Tunachojiuliza ni namna rais 

wa Marekani alivyopata taarifa za 

mazungumzo yale kati ya Dr Vivian 

na mjumbe wa rais wa Korea 

kaskazini” Akasema Edwin 

“Lazima kuna udhaifu 

mkubwa katika ulinzi wa rais.Kuna 

mahala uliachwa mwanya na wakaweza kudukua mazungumzo 

ya rais na hao wageni wake” 

akasema Meshack Jumbo 

“Usemalo ni la kweli kabisa 

Meshack na hata mimi nimehisi 

hivyo na rais pia amekiri hivyo na 

ameagiza vyombo vyake vya 

usalama vilishughulikie hili suala 

haraka sana” 

“Edwin,marekani si taifa la 

mchezo.Wamepiga hatua kubwa 

sana katika teknolojia na 

wanawekeza fedha nyingi katika 

ulinzi wa taifa lao.Ninahisi 

wanamchunguza rais wetu kwa 

muda sasa kutokana na mienendo 

yake.Lazima walikuwa na wasi 

wasi naye na ndiyo maana 

wakaanza kumchunguza.Idara zinazohusika na ulinzi wa rais 

zinapaswa kuwa macho sana hasa 

kwa sasa ambapo ameingia katika 

msuguano na Marekani.Kama 

ameamua kuanzisha mahusiano na 

Korea kaskazini tutakuwa 

tumejiweka kati kati ya Korea 

kaskazini na Marekani na 

kuongeza msuguano.Sisi ni taifa 

masikini na hatuna uwezo wowote 

wa kupambana na Marekani 

kijeshi tutajikuta sehemu mbaya 

kama nchi.Sikosoi maamuzi au 

mtazamo wa rais kuhusu ushirika 

na Korea Kaskazini ila nina wasi 

wasi na usalama wetu.Ninyi 

washauri wake hamjaliona hilo? 

Akauliza Meshack “Mzee Jumbo suala hili ndiyo 

kwanza limeibuka na hata 

mazungumzo rasmi hayajafanyika 

kati ya Korea kaskazini na 

Tanzania.Hivi sasa kuna kikao cha 

baraza la mawaziri kinaendelea 

ikulu na nina imani suala hili 

litajadiliwa pia na kufanyiwa 

maamuzi ila rais yuko tayari 

kabisa kwa jambo hili.Utakapofika 

wakati wetu wa kumshauri 

tutatimiza wajibu wetu kwa 

kumshauri kwa upana sana 

kuhusu jambo hili na athari zake” 

“Tafadhali liangalieni sana hili 

jambo na mumshawishi vizuri rais 

lakini sikieni pia maoni na 

mtazamo wake yawekana kuna 

kitu kizuri amekiona japokuwa kama atafanya maamuzi hapaswi 

maamuzi ya pupa tutajikuta 

sehemu mbaya” akasema Meshack 

Jumbo 

“Tutalizingatia hilo mzee 

Meshack” akasema Edwin 

“Tuachane na hayo.Naamini 

mguu huu wa mapema namna hii 

haukuwa kuja kunijulia hali” 

akasema Meshack na wote 

wakacheka 

“Tunatamani sana 

kuwatembelea wazee wetu 

wastaafu na kuchota maarifa lakini 

majukumu yanatubana,kama 

ujuavyo kuwa karibu na rais.Hata 

hivyo nimefurahi sana kupata 

wasaa wa kuja kwako asubuhi hii 

ya leo japokuwa kuna jambo limenileta hapa” akasema Edwin 

na wote wakacheka 

“haya niambie umeniletea 

nini? Akauliza Meshack Jumbo 

“Nimetumwa na rais” akasema 

Edwin na kunyamaza kidogo 

akamtazama Mzee Jumbo ambaye 

alitoa kicheko kidogo 

“Rais amekutuma? Akauliza 

“Ndiyo nimetumwa na rais 

anahitaji kukuona” akasema 

Edwin 

“Anahitaji kuniona? Kuna 

nini? 

“Hajanieleza kuna nini ila 

amenituma nikutaarifu kwamba 

anahitaji sana kuonana nawe “ 

Mzee Jumbo akafikiri kidogo 

na kusema “Nimeshangazwa kidogo na 

wito huo wa rais,kwani nilistaafu 

kazi kabla hajaingia madarakani 

na sina hakika kama ananifahamu” 

“Mzee Meshack,yule ni rais wa 

nchi na anao uwezo wa kupata 

taarifa za mtu yeyote 

amtakaye.Yawezekana hajawahi 

kukuona lakini anazo taarifa zako 

na ndiyo maana anahitaji 

kukuona” akasema Edwin 

“Anahitaji kuniona lini? 

“leo hii.Nimekuja kukuchukua 

ili twende ikulu ukaonane naye” 

“Leo hii? Meshack Jumbo 

akashangaa 

“Mbona ghafla sana.Kuna 

tatizo lolote? “Sifahamu kuna nini mzee 

wangu lakini inaonekana kuna 

jambo la muhimu sana hadi rais 

wa nchi aamue kukuita 

ikulu.Yawezekana kuna ushauri 

anauhitaji” akasema Edwin.Mzee 

Jumbo akatafakari kidogo na 

kusema 

“Sawa Edwin.Ngoja nijiandae” 

 akasema Meshack Jumbo na 

kwenda kujiandaa.Edwin 

akautumia muda huo kupitia 

jumbe mbali mbali alizotumiwa 

katika simu yake.Moja kati ya 

jumbe alizotumiwa ni video fupi 

inayoonyesha viongozi toka nchi 

za Japan,Uingereza na Ujerumani 

wakilaani hotuba ya rais wa 

Tanzania na kuahidi kuungana na Marekani kuichukulia hatua kali 

sana Tanzania endapo itaendelea 

na azma yake ya kutaka kuanzisha 

mashirikiano na Korea Kaskazini. 

“Things are starting to get 

ugly.Sijui suala hili litatupeleka 

wapi” akawaza Edwin 

Mzee Meshack Jumbo 

alipokuwa tayari akatoka akiwa 

amevaa suti ya rangi nyeusi na 

kuingia katika gari la Edwin 

wakaondoka kuelekea ikulu 

kuonana na rais 

“Nani mkuu wa idara ya 

usalama wa taifa kwa sasa ? 

akauliza mzee Jumbo 

“Alikuwa ni George Mzabwa” 

akajibu Edwin 

“Alikuwa? “Ndiyo.Alikuwa ni George 

Mzabwa lakini baada ya kifo chake 

bado hajateuliwa mwingine kuziba 

nafasi yake” 

“Amekufa? 

“Inamaana hujasikia bado 

kilichotokea? 

“hapana sijasikia 

chochote.Mimi ni mfuatiliaji sana 

wa habari za nje kuliko za hapa 

nyumbani” 

“George Mzabwa alijiua kwa 

kujipiga risasi ofisini kwake juzi” 

“Alijiua? Kwa nini alifanya 

hivyo? Akauliza mzee Jumbo 

“Hakuna anayefahamu sababu 

ya kujiua kwake.Uchunguzi 

unaendelea” “Hii ni ajabu sana kwa mtu 

mkubwa kama huyu kujiua.Lazima 

kuna sababu kubwa.Yawezekana 

labda rais ananiitia suala hilo? 

“Sifahamu anachokuitia rais” 

akasema Edwin na safari 

ikaendelea. 

************* 

Kikao cha dharura cha baraza 

la mawaziri kilichoanza saa nne za 

asubuhi kilimalizika saa nane za 

mchana.Kikubwa kilichojadiliwa 

katika kikao hiki ni kile 

kilichotokea katika mkutano mkuu 

wa baraza la umoja wa mataifa na 

vile vile suala la kuanzishwa kwa 

mashirikiano na Korea kaskazini lilichukua nafasi kubwa.Wengi wa 

mawaziri walionyesha wasi wasi 

wao mkubwa juu ya kuanzishwa 

kwa uhusiano na Korea kaskazini 

wakihofu kuitumbukiza nchi 

katika matatizo 

makubwa.Mawaziri waliomba 

kutokuharakishwa kwa jambo lile 

hata kama lina manufaa kwa 

nchi.Pamoja na mawaziri wengi 

kuonyesha wasi wasi kuhusu suala 

hili na hoja mbali mbali nzito 

kutolewa kuhusiana na athari za 

kuwa na mashirikiano na Korea 

kaskazini lakini bado rais Dr 

Vivian aliendelea kusimama katika 

msimamo wake wa kuanzisha 

mahusiano na Korea kaskazini na 

akamuuagiza waziri wa mambo ya nje kuanza mara moja 

mawasiliano na mwenzake wa 

Korea kaskazini ili mzungumzo 

baina ya mataifa haya mawili 

yaanze mara moja.Baada ya kikao 

kumalizika rais akawa na 

mazungumzo mafupi na makamu 

wa rais ofisini kwake. 

“Dr Makame ,kuna taarifa 

yoyote iliyopatikana hadi sasa kwa 

nini George mzabwa alijiua ? 

akauliza rais 

“Mheshimiwa rais mpaka sasa 

hakuna taarifa yoyote 

iliyopatikana kwa nini George 

alijua.Uchunguzi unaendelea lakini 

nategemea makubwa yapo katika 

barua hii aliyokuandikia.Tunahisi 

yawezekana amekueleza lolote” akasema Dr Makame na kuitoa 

bahasha toka katika mfuko wa koti 

na kumkabidhi rais 

“Una hakika hakuna 

aliyefungua barua hii? Akauliza Dr 

Vivian 

“Hakuna mheshimiwa 

rais.Nimeitunza mimi mwenyewe 

na hakuna ajuaye 

kilichoandikwamo” 

“Good.Ahsante Dr 

Makame.Kaendelee na shughuli 

zako tutaonana baadae” akasema 

rais na Dr Makame akatoka. Dr 

Vivian akaifungua na kuisoma 

barua ile 

Kwako mheshimiwa rais Rejea mazungumzo yetu leo 

asubuhi.Umenitaka hadi 

utakaporejea,tayari niwe na majibu 

ya ile kazi uliyonipa. 

Mheshimiwa rais kazi 

uliyonipa si nyepesi na mpaka hapa 

nilipo nimekosa jibu la kukupa 

lakini kwa ufupi ni kwamba 

nimeshindwa kupata majibu ya hili 

suala na hiyo ni aibu kubwa kwa 

kiongozi mkubwa kama 

mimi.Sijafanikiwa kujua nani 

waliua familia yako na kwa nini. 

Mheshimiwa rais,nakushauri 

usipoteze muda wako kwa ajili ya 

suala hili kwani hutoweza kupata 

majibu yake.Hili suala ni fumbo 

kubwa na gumu kulifumbua.Nakushauri achana 

nalo. 

I failed you madam president 

and I’m sorry for that.Siko tayari 

kushushwa cheo kwa kushindwa 

kupata majibu ya suala hili ambalo 

nimetumia kila aina ya uwezo nilio 

nao lakini nimeshindwa kulipatia 

majibu 

Nakushukuru kwa imani 

kubwa uliyokuwa nayo kwangu 

mheshimiwa rais.Pamoja na 

kukuangusha lakini naomba 

familia yangu iendelee kuangaliwa 

na kupewa matunzo 

George Mzabwa 

Dr Vivian akahisi kulengwa na 

machozi baada ya kuisoma barua ile akainama na kuweka mikono 

kichwani. 

“Ningejua nisingemwambia 

yale maneno.Nimesababisha 

akajitoa uhai” akawaza 

“Hata hivyo kitu alichokifanya 

ni cha kijinga.Hakupaswa kujitoa 

uhai.Kama suala hili ni gumu na 

ameshindwa kupata majibu 

alipaswa kunieleza na kwa pamoja 

tungeamua nini tufanye lakini yeye 

akachagua kutoa uhai.Naionea 

huruma familia yake,nitahakikisha 

inahudumiwa kwa kila kitu na 

nitakwenda kesho kutoa pole kwa 

familia” 

Dr Vivian akatolewa 

mawazoni baada ya mlango 

kufunguliwa akaingia Edwin Swai “Samahani mheshimiwa rais” 

akasema Edwin baada ya kuuona 

mstuko wa rais 

“Karibu Edwin.Take a sit” 

akasema Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais kama 

utakumbuka tulipokuwa 

tunaelekea New York kuna jambo 

uliniomba nikakwambia kwamba 

nitakuletea mtu” 

“Ndiyo nakumbuka 

Edwin.Umekwisha mpata? 

“Ndiyo madam 

president.Meshack Jumbo yupo 

hapa toka asubuhi” 

“Ahsante sana Edwin.Naomba 

nikaongee naye katika faragha” 

“Sawa mheshimiwa rais” 

akasema Edwin na kutoka akampeleka Meshack Jumbo 

katika chumba cha maongezi ya 

faragha.Baada ya dakika tano rais 

akaingia.Meshack Jumbo 

akasimama wakasalimiana 

“Shikamoo mzee Meshack 

Jumbo”Dr Vivian akamsalimu 

mzee Jumbo kwa adabu 

“Marahaba Dr Vivian.Pole na 

majukumu” 

“Ahsante sana mzee 

Jumbo.karibu sana na samahani 

kwa kukusumbua” 

“Usihofu mheshimiwa rais,sisi 

wastaafu tunaheshimu sana wito 

wa rais kwa hiyo usione kama vile 

umenisumbua bali ni heshima 

kubwa umenipa” akasema 

Meshack “Ahsante sana baba.Nafurahi 

kusikia hivyo.Vipi maisha ya 

kustaafu yanakwendaje? 

“Maisha mazuri.Baada ya 

kustaafu utumishi wa umma 

nimejikita katika kilimo na 

ufugaji.Nina mashamba yangu 

yanazalisha mazao ya kutosha ,vile 

vile nina mifugo 

ng’ombe,kuku,mbuzi bata na 

nguruwe.Kwa ujumla maisha ni 

mazuri” akasema Meshack 

“Hongera sana.Nitakuja 

kukutembea siku moja kujifunza 

mambo mengi toka kwako” 

“Karibu sana mheshimiwa 

rais” akasema Meshack “Mzee Meshack mimi na wewe 

nadhani ni mara yetu ya kwanza 

tunakutana” 

“Kweli mheshimiwa rais.Mimi 

nimestaafu kazi kabla hujaingia 

madarakani kwa hiyo 

hatufahamiani” 

“Sikuwa nikikufahamu hadi 

pale Edwin Swai alipokutaja kuwa 

unaweza kuwa na msaada 

kwangu” 

“Edwin ni kijana wangu 

nimewahi kufanya naye kazi 

ananifahamu vyema.Ni msaada 

gani unauhitaji? 

“Labda nikupe historia kidogo 

ndipo nikueleze ninachohitaji.Nina 

uhakika utakuwa unamfahamu 

Kanali Sebastian Matope” “Ndiyo ninafahamiana naye 

japokuwa sikuwa na ukaribu sana 

naye ila tunafahamiana kwani sote 

tulikuwa watu wa karibu na 

rais.Kifo chake kiliniumiza sana.” 

“Wakati baba na familia yangu 

walipouawa mimi nilikuwa 

masomoni nje ya nchi.Nilirejea 

nyumbani kuwazika familia 

yangu.Japokuwa ni miaka mingi 

imepita sasa lakini bado 

nakumbuka namna baba na familia 

yangu walivyouliwa kwa kupigwa 

risasi nyingi hasa baba.Ripoti ya 

madaktari wanasema risasi zaidi 

ya sabini zilimuingia 

mwilini.Yalikuwa ni mauaji ya 

kinyama mno” 

“Pole sana mheshimiwa rais” 



Ahsante mzee Meshack.” 

Akasema Dr Vivian na kutulia 

kidogo halafu akaendelea 

“Hadi ninaingia madarakani 

hakukuwa na na mtu yeyote 

ambaye amewahi kukamatwa 

kutokana na mauji ya familia 

yangu.Mara tu nilipoingia 

madarakani nilitaka nipewe ripoti 

ya uchunguzi lakini hakukuwa na 

ripoti yoyote zaidi ya kutupiana 

mpira mara hili mara lile ndipo 

nilipolazimika kuitumia idara ya 

usalama wa taifa kulichunguza hili 

suala.Miaka miwili imepita toka 

nilipokabidhi jukumu hilo kwa 

idara ya usalama wa taifa na 

kumtaka mkurugenzi George 

Mzabwa alishughulikie kwa karibu sana na ahakikishe suala hili 

linapatiwa majibu.Juzi wakati 

ninaelekea New York kuhudhuria 

mkutano mkuu wa umoja wa 

mataifa nilionana na George 

uwanja wa ndege nikamwambia 

kwamba nitakaporejea nikute 

ripoti mezani kwangu ama sivyo 

nitamuondoa katika nafasi yake na 

kumpa mtu mwingine.Kwa bahati 

mbaya George akajitoa uhai kwa 

kujipiga risasi.Nimejiuliza sana 

kwa nini vifo vya familia yangu 

viwe ni kama fumbo lisiloweza 

kufumbuka? Niliamua kulivalia 

njuga hili jambo na ndipo 

nilipomuomba Edwin anisaidie 

niweze kumpata mpelelezi yeyote 

mahiri wa nje au ndani ya nchi aweze kulichunguza hili jambo na 

kujipatia majibu.Edwin alilipima 

hili jambo na akasema kwamba 

kuna mtu mmoja ambaye anaweza 

akawa na msaada mkubwa sana 

kwangu ambaye ni wewe hivyo 

nikamtaka mara tutakaporejea 

Dar es salaam akutafute nionane 

nawe.Nashukuru umekuja mzee 

wangu ninahitaji sana msaada 

wako.Nahitaji unisaidie kumpata 

mpelelezi mahiri ambaye ataweza 

kulifumbua hili fumbo ambalo 

polisi na idara ya usalama wa taifa 

wameshindwa kulifumbua kwa 

zaidi ya miaka kumi sasa.Hili ni 

jambo la kwanza kubwa.Jambo la 

pili ninataka mtu wa kuongoza 

idara ya usalama wa taifa kwa muda wakati natafuta mtu wa 

kuziba nafasi ya George 

Mzabwa.Nimefikiria sana ni nani 

ninaweza kumpa nafasi hiyo lakini 

mpaka sasa sijaona nani anaweza 

kunifaa hivyo nimeona nikuombe 

unisaidie kuongoza idara ya 

usalama wa taifa kwa muda wakati 

ninaendelea kutafuta taratibu mtu 

anayeweza kuziba nafasi 

hiyo.Mzee Meshack umewahi 

kuongoza idara ya ujasusi ya taifa 

ambayo uliiongoza kwa mafanikio 

makubwa,una uzoefu wa kutosha 

katika masuala ya usalama.Nina 

uhakika unaweza kunifaa sana 

hasa kwa wakati huu ambao 

nimeingia katika msuguano 

mkubwa na mataifa makubwa.Nina imani tayari umekwisha sikia kile 

kilichotokea New York katika 

mkutano mkuu wa umoja wa 

mataifa hivyo basi nchi inahitaji 

ulinzi thabiti na intelijensia 

kubwa.Idara ya usalama wa taifa ni 

muhimu sana kwa wakati 

huu.Mzee Meshack tafadhali 

naomba usiseme 

hapana.Ninakuomba kama binti 

yako kama rais wako unisaidie 

kwa mwaka mmoja tu na ndani ya 

muda huo tayari nitakuwa 

nimepata mtu maalum wa 

kuiongoza hiyo idara na wewe 

utakwenda kupumzika.Nakuomba 

sana mzee wangu” akasema Dr 

Vivian “Mheshimiwa rais sijui nianzie 

wapi lakini naomba nianze na hilo 

suala la pili.Kwanza nataka 

nikushukuru sana mheshimiwa 

rais kwa heshima ya kuniita hapa 

ikulu.Pili ninashukuru sana kwa 

kuniona ninaweza kuwa na 

msaada bado japokuwa umri 

umesogea.Pamoja na hayo 

utanisamehe sana rais wangu 

kwamba kwa sasa siko tayari 

kurejea katika kazi.Nilianza kazi 

hii nikiwa kijana mdogo na nusu ya 

umri wangu nimeitumia katika hii 

kazi kwa hiyo ni wakati wangu wa 

kupumzika.Hata mke wangu sina 

hakika kama anaweza kukubali 

jambo hili kwani muda wote 

ambao nilikuwa kazini alikuwa ananikosa sana na hivi sasa ana 

furaha kwa kuwa niko karibu naye 

kila wakati.Mheshimiwa rais wapo 

vijana wengi mahiri wanaoweza 

kuziba nafasi hiyo ila niko tayari 

kwa ushauri muda wowote 

nikiombwa” 

“Mzee Meshack nafahamu 

vijana wengi wazuri lakini hawana 

uzoefu kama wako.Ni mwaka 

mmoja tu kisha utaendela na 

mapumziko yako.Kama ni mama 

ndiye kikwazo nitakwenda 

kuzungumza naye mimi na 

nitamuomba akuruhusu kwani hili 

ni suala la kitaifa.Niko hapa kwa 

niaba ya watanzania.Wameniweka 

hapa niwaongoze kwa hiyo 

ninapokuomba uiongoze idara ya usalama wa taifa kwa mwaka 

mmoja ni watanzania 

wanakuomba hivyo.Tafadhali 

mzee wangu nakuomba sana 

unisaidie kwa hilo” 

Meshack Jumbo akafikiri tena 

kidogo na kusema 

“Mheshimiwa rais sioni neno 

ninaloweza kusema kukataa tena 

ombi lako hilo.Sisi ni sawa na 

wanajeshi wa akiba hivyo itokeapo 

vita tunavaa gwanda tunabeba 

silaha na kuingia katika 

mapambano kupigania 

nchi.Nitakusaidia kwa huo mwaka 

mmoja ulioniomba japokuwa kuna 

mambo ambayo lazima tuyajadili” 

“Ahsante sana mzee Meshack 

Jumbo.Sijui nikushukuruje kwa kukubali kwako.Kitu chochote 

utakachokihitaji utakipata mzee 

wangu na nitajitahidi kukuwekea 

mazingira mazuri ya kufanya kazi 

yako.Nahitaji idara ya usalama wa 

taifa ile iliyokuwepo wakati ule” 

akasema Dr Vivian 

“Usijali mheshmiwa rais 

nitafanya kazi kwa kutumia uwezo 

wangu wote.Kuhusu suala la 

kwanza uliloniomba nikusaidie 

kupata mpelelezi wa kuweza 

kukusaidia kutafuta majibu ya 

watu walioua wazazi wako.Suala 

hili linahitaji mtu maalum.Kuna 

kijana mmoja anaitwa Mathew 

Mulumbi.Huyu aliwahi kufanya 

kazi katika idara ya ujasusi 

alikuwa ni tegemeo kubwa kutokana na umahiri wake lakini 

baadae akapata matatizo na 

kuamua kuacha kazi.Nina imani 

utakuwa umemsikia kwani ndiye 

muhusika mkuu katika lile sakata 

la Peniela” akasema Meshack na Dr 

Vivian akatabasamu 

“Niliwahi kulisikia sakata hilo 

wakati nikiwa ujerumani wakati 

huo nikiendelea na 

masomo.Alifanya kazi kubwa na 

alifahamika dunia 

nzima.Nakumbuka mwisho wa 

sakata lile walioana” 

“Ni kweli walioana lakini 

wameachana” akasema Meshack 

“Wameachana?Dr Vivian 

akashangaa “Ndiyo wameachana na 

Mathew amerejea hapa nchini 

.Kwa sasa ana shughulikia ujenzi 

wa kiwanda chake cha 

kutengeneza vipuri vya magari na 

mashine mbalimbali.Kitakuwa ni 

kiwanda kikubwa cha kuchonga 

vipuri hapa nchini” 

“Nini hasa sababu ya 

kuachana kwao? 

“kwa maelezo aliyonipa 

Mathew ni kwamba Peniela ndiye 

chanzo cha ndoa yao kuvunjika 

kwani alianzisha mahusiano na 

bilionea mmoja huko Paris 

walikokuwa wakiishi.Baada ya 

kuachana Mathew amerejea 

nyumbani ambako anawekeza 

katika kiwanda” “Dah ! so sorry for him.Kwa 

hiyo unaamini anaweza kufaa 

kuifanya kazi hii? 

“Ndiyo ninamuamini sana.Ni 

mahiri katika kazi zake na 

hajawahi kushindwa katika kazi 

yoyote aliyowahi kupewa” 

“Nafurahi kusikia 

hivyo.Anapatikanaje huyo 

Mathew? Unaweza kunipa namba 

zake za simu niwasiliane naye? 

“Hapana mheshimiwa rais hilo 

haliwezi kuwa wazo zuri.Kuna 

namna ya kumshawishi Mathew 

akubali kufanya kazi yako.Kwa 

sasa hayuko tena katika hizi kazi 

na anawekeza katika biashara 

zake kwa hiyo itahitaji mtu 

maalum wa kuweza kumshawishi aweze kukubali.Nitaifanya hiyo 

kazi na nitajitahidi hadi 

nihakikishe nimemleta hapa 

kwako” akasema Meshack Jumbo. 

Maongezi kati ya rais na 

Meshack Jumbo yalichukua zaidi 

ya saa moja kisha wakaagana. 

“Kidogo sasa ninaanza kuwa 

na matumaini baada ya Meshack 

Jumbo kunihakikishia kwamba 

Mathew anao uwezo mkubwa wa 

kulifumbua fumbo lililoshindwa 

kufumbuliwa la wazazi wangu 

kuuawa.Kingine kizuri ni kwamba 

amekubali kuiongoza idara ya 

usalama wa taifa kwa mwaka 

mmoja.Sijui kwa nini nimekuwa na 

imani kubwa na yule mzee 

japokuwa nimeonana naye leo hii.Nilipomuona tu nikahisi amani 

moyoni naamini idara hii ikiwa 

chini ya yule mzee kwa mwaka 

mmoja itakuwa na mabadiiko 

makubwa sana kitu ambacho 

ninakihitaji” akawaza Dr Vivian 

baada ya Meshack Jumbo 

kuondoka. 

************* 

Baada ya nchi za Uingereza 

,Ujerumani,Ufaransa na Japan 

kutoa matamko yao kulaani 

majaribio ya makombora 

yanayoendelea kufanywa na Korea 

Kaskazini na kuionya nchi ya 

Tanzania dhidi ya kuanzisha mashirikiano na Korea Kaskazini 

,nchi za China Korea Kaskazini na 

Urusi nazo kwa pamoja zikatoa 

tamko ambalo walizionya nchi 

kubwa kutothubutu kuigusa 

Tanzania kwa namna yoyote ile 

kwani ni nchi huru na iachwe 

itumie rasilimali zake kwa 

manufaa ya wananchi wake. 

Tamko hili lilizidi kukoleza 

moshi ulioanza kufuka na 

kulifanya suala hili lizidi kuteka 

vichwa vya habari duniani.Baada 

ya matamko hayo kutolewa na nchi 

hizo tatu,waziri wa mambo ya nje 

wa Marekani naye akajitokeza 

mbele ya waandishi wa habari na 

kulaani tamko hilo la nchi hizo tatu 

na kuzishutumu kwa kuikumbatia nchi ya Korea kaskazini.Aliliita 

tamko hilo kuwa ni la kipuuzi na 

akazionya nchi hizo kwamba 

Marekani haitasita kuzichukulia 

hatua kali ikiwamo kuvunja 

mahusiano yake ya kidiplomasia 

na nchi yoyote ambayo inaendelea 

kuiunga mkono Korea Kaskazini 

Muda mfupi baada ya tamko 

hilo la waziri wa mambo ya nje wa 

Marekani kutolewa,nchi za Irani 

,Venezuela ,Cuba na India nazo 

zikatoa matamko kuiunga mkono 

Tanzania juu ya kutumia rasilimali 

zake bila kuingiliwa na taifa lolote. 

Edwin alimrejesha Meshack 

Jumbo nyumbani.Alizungumza 

kwa kifupi na mke wake halafu 

akaondoka kuelekea mahala 

kunakojengwa kiwanda cha 

kuchonga vizuri vya magari na 

mashine mbali mbali 

kinachomilikiwa na bilionea 

Mathew Mulumbi. 

Aliwasili katika eneo 

kunakojengwa kiwanda hicho 

ambako shughuli zilikiwa 

zinaendelea.Akashuka garini na 

kuelekezwa mahala aliko Mathew 

akamfuata 

“Mzee Jumbo karibu 

sana.Mbona umekuja kimya 

kimya? Akauliza Mathew “Nimeogopa kukujulisha kama 

ninakuja kuogopa kupewa sababu 

lukuki kutokana na kazi nyingi 

ulizonazo” Akasema Meshack 

Jumbo huku akitoa kicheko na 

Mathew naye akacheka,akanawa 

mikono na kumpeleka Meshack 

Jumbo katika kibanda cha 

kupumzikia 

“karibu sana mzee Jumbo.Nina 

imani umekuja kujua kuhusiana na 

zile mashine za kiwanda chako cha 

mvinyo” akasema Mathew 

“Hapana Mathew,ulikwisha 

nieleza kwamba zinakuja kwa meli 

hivyo sina wasi wasi zitakapofika 

utanijulisha.Nimekuja kwa jambo 

lingine kabisa” akasema mzee Jumbo na kunyamaza kidogo 

halafu akasema 

“Rais ameniita ikulu nilikua 

na mazungumzo naye” 

Sura ya Mathew ikabadilika 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog