Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL - 3

  

Simulizi : The Football 

Sehemu Ya Tatu (3)


Rais wa jamhuri ya muungano 

wa Tanzanai Dr Vivian Matope 

alilazimika kuahirisha kuhudhuria 

msiba wa aliyekuwa mkurugenzi 

wa idara ya usalama wa taifa 

George Mzabwa kutokana na 

maombi ya balozi wa Marekani 

nchini Tanzania na balozi wa 

umoja wa Ulaya walioomba 

kuonana naye kwa 

mazungumzo.Kwa sababu ya uzito 

wa hayo mazungumzo rais 

akamtuma makamu wa rais 

amuwakilishe katika msiba huo 

Saa nne na nusu balozi wa 

Marekani nchini Tanzania  

Abraham Clerck aliwasili ikulu na 

kupokewa na rais 

“Karibu sana mheshimiwa 

balozi” akasema Dr Vivian 

“Nashukuru mheshimiwa rais” 

akajibu Abraham.Baada ya 

maongezi mafupi ya utangulizi 

hatimaye balozi Abraham 

akajielekeza katika kile 

kilichomleta 

“Mheshimiwa rais kwanza 

kabisa utanisamehe kwa 

kukuvurugia ratiba zako leo hii 

.Sikuwa nimepanga kuja kukuona 

lakini imenilazimu kuja na 

ninashukuru kwa kukubali 

kuonana nami” akasema balozi 

Abraham “Mheshimiwa rais 

imenilazimu kuja kukuona baada 

ya kuelekezwa hivyo na serikali 

yangu nije nizungumze nawe 

mambo mawili makubwa.Jambo la 

kwanza ni mahusiano unayotaka 

kuyaanzisha na Korea 

Kaskazini.Mheshimiwa rais 

mahusiano haya hayatakuwa na 

manufaa yoyote kwa nchi ya 

Tanzania zaidi ya kuiingiza nchi 

katika matatizo.Korea Kaskazini 

imewekewa vikwazo vya kiuchumi 

na taifa lolote ambalo 

litashirikiana na Korea Kaskazini 

litahesabika kama msaliti kwa 

mataifa mengine wapenda amani 

duniani.Taifa hili la Korea 

Kaskazini wamekuwa wakitengeneza silaha kali za 

maangamizi na bila kujali 

marufuku na vikwazo iliyowekewa 

na umoja wa mataifa wameendelea 

kufanya majaribio ya makombora 

katika bahari ya Pacific na 

kuwatishio kwa nchi jirani zake na 

kwa usalama wa dunia.Wakati 

dunia yote ikipaaza sauti kukemea 

vitendo hivi vya Korea Kaskazini 

serikali ya Tanzania inataka 

kuanzisha mahusiano nayo na hata 

kutamka wazi wazi kwamba 

itawauzia Korea kaskazini madini 

ya Uranium ambayo Korea 

kaskazini wanataka kutayatumia 

katika kutengeneza silaha za 

nyuklia.Wakati mkutano wa 

baraza kuu la umoja wa mataifa ukiendelea Korea kaskazini 

imefanya majaribio mawili ya 

makombora na kusababisha hofu 

kubwa hasa kwa Japan.Kwa hivi 

sasa umoja wa mataifa 

unatafakari kuwaongezea vikwazo 

zaidi Korea kaskazini kufuatia 

kiburi chake na kuendelea kufanya 

majaribio ya makombora” akatulia 

kidogo na kuendelea 

“Mheshimiwa rais nimetumwa 

kuja kukwambia ufikiri upya 

kuhusu mpango wako wa kutaka 

kuanzisha mahusiano ya aina 

yoyote na taifa hili la Korea 

kaskazini.Tunafahamu Tanzania ni 

nchi huru na haiwezi kuchaguliwa 

marafiki lakini si Korea 

kaskazini.Hili ni taifa adui wa kila mtu hapa duniani.Kuamua 

kushirikiana na taifa hili ni 

kuwasaliti wapenda amani kote 

duniani na kujiweka katika 

matatizo makubwa kwani lazima 

nchi yako itawakewa vikwazo vya 

kiuchumi.Tanzania ni nchi 

masikini bado haijapiga hatua 

kubwa kiuchumi ,bado inategemea 

misaada na mikopo toka mataifa 

makubwa na hasa 

Marekani.Tanzania haina viwanda 

vya kutosha inategemea bado 

kuagiza baadhi ya bidhaa zake nje 

ya nchi.Kwa ujumla Tanzania bado 

inazihitaji sana nchi tajiri.Kuamua 

kushirikiana na Krea Kaskazini 

Tanzani itawekewa vikwazo vya 

kiuchumi na kurudisha nyuma juhudi zake za kujiondoa katika 

umasikini.Tanzania na Marekani 

ni marafiki wa muda mrefu na 

kama kuna tatzo lolote basi 

tunaweza kukaa 

tukazungumza.Marekani ni 

mchangiaji mkubwa wa miradi ya 

maendeleo na hata bajeti kuu ya 

serikali kwa hiyo Tanzania kuingia 

katika mgogoro na Marekani 

kutaiathiri sana kwani serikali ya 

Marekani italazimika kukata 

misaada yake kwa Tanzania.Miradi 

yote ya maendeleo 

itasitishwa.Mheshimiwa rais 

nimeombwa nikutaarifu kuhusu 

jambo hilo na ufikirie upya wazo 

lako la kuungana na Korea 

Kaskazini. Jambola pili ni kuhusiana na 

makampuni ya Kimarekani 

yaliyowekeza hapa 

Tanzania.Endapo utaendelea na 

maamuzi ya kutaka kushirikiana 

na Korea Kaskazini basi 

makampuni ya Kimarekani 

yaliyowekeza hapa nchini 

yataondoa uwekezaji wao mkubwa 

na kupeleka katika nchi 

nyingine.Hilo likitokea serikali 

itakosa kodi,wananchi watakosa 

ajira na nchi itayumba sana. Korea 

Kaskazini hawezi kufanya 

uwekezaji mkubwa kama 

uliofanywa na Wamarekani.Kwa 

ujumla hakuna faida yoyote 

inayoweza kupatikana kutokana 

na mashirikiano na Korea Kaskazini zaidi ya hasara 

.Mheshimiwa rais bado iko nafasi 

ya kuliweka sawa jambo 

hili.Serikali ya marekani 

inakaribisha kama utahitaji 

mazungumzo juu ya jambo 

hili.Tanzania inaihitaji sana 

Marekani zaidi ya Marekani 

inavyoihitaji Tanzania.Pamoja na 

hayo serikali ya Marekani imeahidi 

iko tayari kuongeza fedha katika 

miradi mingi ya 

maendeleo.Imeahidi kuongeza 

mara nne zaidi ya kiwango 

inachokitoa sasa hivi endapo 

Tanzania itaachana na mipango ya 

mashirikiano na Korea 

Kaskazini.Mheshimiwa rais hii si 

fursa ya kuiachia .Serikali ya Marekani haijawahi kuahidi kutoa 

fedha nyingi kiasi hiki kwa taifa 

lolote duniani na inafanya hivi kwa 

mara ya kwanza kwa Tanzania 

endapo tu mtakuwa tayari 

kuachana na Korea 

Kaskazini.Marekani haijawahi 

kuibembeleza nchi yoyote duniani 

lakini inafanya hivyo kwa 

Tanzania kwa kuwa wamarekani 

wanawapenda sana watanzania na 

ndiyo maana hata katika orodha ya 

watalii wanaokuja kila mwaka 

wamarekani wanaongoza.Hatutaki 

kuona Tanzania ikiingia katika 

matatizo.Mheshimiwa rais 

usikubali kuiacha ofa hii kubwa 

.Hii nifursa kubwa ya Tanzania 

kupiga hatua.Usikubali kutengwa na jumui ya kimataifa hivyo kama 

utakuwa tayari basi mazungumzo 

yaanze mara moja ili kuona ni 

maeneo gani hasa mngependa 

yapewe kipaumbele katika msaada 

huo mkubwa utakaotolewa na 

serikali ya Marekani.Mheshimiwa 

rais hayo ndiyo mambo 

niliyotumwa hapa kwako 

nashukuru kwa kunisikiliza” 

akasema balozi Abraham.Dr Vivian 

akatabasamu na kusema 

“Nakushukuru sana 

mheshimiwa balozi kwa kuja na 

kunifikishia ujumbe.Napenda 

kukufahamisha kwamba ujumbe 

wako nimeupokea kwa mikono 

miwili lakini kwa bahati mbaya 

umekuja kwa kuchelewa sana.Tayari watanzania 

tumekwisha fanya maamuzi 

.Tayari tumeamua kufanya 

mashirikiano na Korea Kaskazini 

.Tayari nimefanya mazungumzo na 

rais Kim wa Korea Kaskazini na 

tumekubaliana kuanzisha 

mashirikiano ya kibiashara na 

uchumi baina ya nchi zetu na vile 

vile mashirikiano ya 

kijeshi.Tanzania ni taifa masikini 

kama mnavyoliita lakini umasikini 

huu umetokana na unyonyaji na 

wizi mkubwa 

mnaotufanyia.Mnabeba rasilimali 

zetu na kutuacha masikini halafu 

mnarudi na kutudanganya kwa 

misaada ambayo imetokana na 

faida mliyoipata kutokana na mali mliyochuma huku 

kwetu.Watanzania tumeamka toka 

usingizini na hatutaki hayo mambo 

yajirudie tena,tumechoka kuibiwa 

rasilimali zetu.Tumesema basi na 

kuanzia sasa tunataka rasilimali 

tulizonazo zitunufaishe 

watanzania sasa na vizazi vijavyo 

hivyo basi tumeamua kuanza upya 

na kwa kuanzia tutaanzisha 

mashirikiano na Korea Kaskazini 

.Jambo hili halitawapendeza 

mataifa makubwa walioshika 

uchumi wa dunia na hivyo 

tunatishiwa sana kwamba 

tutawekewa vikwazo vya kiuchumi 

na nchi itayumba.Nalifahamu hilo 

na ninafahamu tutapitia wakati 

mgumu kama nchi lakini tutasimama imara na tututavuka 

salama.Tunaanza safari ya 

kuelekea kujitegemea kama nchi 

bila kutegemea misaada au 

mikopo ya wafadhili” akanyamza 

kidogo akamtazama Abraham 

aliyekuwa anavua miwani mara 

kwa mara na kufuta macho 

“Kwa hiyo balozi Abraham 

,katika suala la kwanza 

hakutakuwa na mazungumzo 

yoyote baina ya Tanzania na 

Marekani au nchi nyingine 

yoyote.Tumeamua kusonga mbele 

na hatutarudi nyuma 

kamwe.Waeleze wakuu wako 

kwamba Dr Vivian ameamua 

kuwaongoza watanzania katika 

vita ya uchumi ili Tanzania iweze kujitegemea na kuhusu 

mashirikiano na Korea Kaskazini 

yako pale pale na hatutarudi 

nyuma.Suala la pili ni kuhusiana 

na wawekezaji wa Marekani wa 

hapa nchini.Kweli kuna 

makampuni makuwa ya 

kimarekani yamewekeza hapa 

Tanzania katika sekta mbali 

mbali.Yapo yanayochimba 

madini,yapo yaliyowekeza kwenye 

mafuta na gesi na sehemu nyingine 

mbalimbali.Tayari nimekwisha 

waagiza wanasheria wangu kuanza 

mchakato wa namna 

tukakavyoweza kusitisha 

mikataba na makampuni haya 

.Nafahamu hili ni jambo 

litakalowaudhi sana wamarekani lakini hatuna namna nyingine ya 

kufanya .Tunahitaji marafiki na 

wawekezaji lakini si wale 

wanaokuja kutunyonya na kutaka 

kututawala kwa hiyo tutavunja 

mikataba yote na tutafuta 

wawekezaji wengine au 

tutahifadhi mali zetu hadi pale 

tutakapojenga uwezo wa ndani wa 

kuweza kuchimba” akasema 

rais.Balozi Abraham akavua 

miwani akafuta machoni na 

kusema 

“Mheshimiwa rais utakuwa 

umefanya kosa kubwa sana kama 

ukifanya hivyo.Utaiharibu 

Tanzania.Nimeishi hapa kwa muda 

wa miaka mitatu na nimetokea 

kuwapenda sana watanzania,ninafahamu matatizo 

yao na endapo ukifanya hivi 

unavyotaka kufanya utawaingiza 

katika matatizo 

makubwa.Marekani inafadhili 

miradi mingi mikubwa hapa 

nchini,ipo miradi ya 

afya,elimu,maji,nishati ,miundo 

mbinu na hii yote inasaidia 

mamilioni ya watanzania.Endapo 

Marekani itajitoa kufadhili hii 

miradi yote watu wengi 

wataathirika sana.Serikali ya 

Korea Kaskazini haina uwezo wa 

kuyafanya haya yote 

yanayofanywa na Marekani hapa 

nchini Tanzania.Mheshimiwa rais 

tafadhali naomba ulifikirie tena suala hili.” Akasema balozi 

Abraham 

“Mheshimiwa balozi ,naomba 

tafadhali tusiendelee kuliogelea 

hili suala.Tayari nimekwisha weka 

wazi msimamo wangu na wa 

tanzania na sipendi kuendelea 

kurudi rudia maongezi .Naomba 

unifikishie salamu zangu kwa rais 

Mike straw na umueleze haya 

niliyokueleza bila kupunguza hata 

neno moja” akasema Dr Vivian na 

kusimama akampa mkono balozi 

Abraham 

“Ahsante sana balozi kwa 

kunitembelea.Nomba umsalimu 

sana Mike straw” akasema Dr 

Vivian na kumsindikiza balozi nje 

akaondoka zake. “Wameanza kutapa tapa hawa 

jamaa.Eti wataongeza misaada 

mara nne ya ile wanayoitoa 

sasa.Hii inaonyesha wazi ni namna 

gani wanavyofaidika na rasilimali 

zetu.Kama si hivyo 

wasingehangaika namna hii kutoa 

matamko ya vitisho na sasa 

wanaona sitishiki na matamko yao 

na wanataka kujaribu kuja na 

maneno matamu.Sintogeuka 

nyuma ili niwe jiwe,nimeamua 

kusonga mbele na nitahakikisha 

ninaivusha nchi katika vita 

hii.Mwisho umefika wa 

kunyanyaswa na mataifa 

makubwa” akawaza Dr Vivian na 

kutaarifiwa kwamba balozi wa 

umoja wa ulaya amefika “Huyu naye nina imani 

atakuwa amekuja kuzungumza 

mambo haya haya” akawaza Dr 

Vivian na kuelekeza balozi huyo 

akaribishwe ndani 

*************** 

Mathew na Theresa waliwasili 

katika kijiji cha Mchangawima na 

kuelekezwa lilipo shamba la rais 

Anorld Mubara.Kulikuwa na 

barabara nzuri ya lami kuelekea 

katika shamba hilo.Miti mizuri 

iliyotoa maua mazuri ilipandwa 

kandoni mwa barabara 

ile.Mandhari ilikuwa ya kuvutia 

sana Walifika katika geti la kwanza 

kulikokuwa na askari wawili 

wakasimamishwa na kuulizwa 

wanakoelekea.Mathew na Theresa 

wakajitambulisha kwamba 

wanatoka ikulu na walikuwa na 

maagizo ya rais kwenda kwa bi 

April,wakaruhusiwa kupita 

“Ulinzi mkali sana mahala 

hapa.” Akasema Mathew.Theresa 

alikuwa kimya kabisa na 

hakuongea kitu.Mwili ulikuwa 

unamtetemeka kwa ndani 

alipokumbuka siku 

waliyoshambuliwa na wazazi wake 

kuuawa miaka kumi 

iliyopita.Walilikuta geti la pili 

wakakaguliwa na kuamriwa 

kuacha silaha zao.Bastora mbili za Mathew zikaachwa pale hadi 

wakatakapotoka.Hakuna 

aliyeruhusiwa kuingia na silaha 

katika nyumba ya Bi April 

Walifika katika geti la tatu na 

walinzi wawili walivalia suruali 

nyeusi na mashati meupe 

wakafungua geti wakawaonyesha 

sehemu ya kuegesha gari na 

mtumishi aliyevalia nadhifu 

akawasili wakakaribishwa 

sebuleni.Lililkuwa ni jumba jumba 

kubwa la ghorofa nne.Ukimya 

ulikuwa mkubwa eneo hili 

Walikirimiwa vinywaji na 

baada ya dakika chache akatokea 

mama mmoja mzungu 

“Karibuni jamani” akasema 

mama yule kwa kiswahilisafi.Mathew na Theresa 

wakasimama wakamsalimu kwa 

adabu 

“Nimefurahi sana kupata 

wageni leo.Mara chache huwa 

natembelewa na watu huku 

shambani.Labda wakati wa 

sherehe za kitaifa huwa nafuatwa 

na kualikwa”akasema bi April 

huku akitabasamu. 

“Huku kunaitwa shambani 

lakini ni sehemu tulivu mno.Hewa 

safi na ukimya mkubwa tofauti na 

huko mjini tulikosongama 

kulikojaa moshi wa magari na gesi 

za viwanda.Hatuwezi kupata hewa 

safi kama inayopatikana huku” 

Akasema Mathew “Usemayo ni ya kweli .Watu 

wanakimbilia mjini lakini kumejaa 

ghasia.Msongamano 

,kelele.uchafuzi wa hewa n.k.Kwa 

ujumla maisha ya huku ni mazuri 

mno.Haya niambieni nyie ni akina 

nani na mmetokea wapi? 

“Mimi naitwa Theresa na huyu 

mwenzangu anaitwa Mathew.Mimi 

ninafanaya kazi ikulu na huyu 

mwenzangu anafanya kazi katika 

idara ya usalama wa taifa” 

Bi April akastuka kidogo kwa 

utambulisho ule. 

“Karibuni sana.Mimi naamini 

mnanifahamu .Naitwa April 

hudson Mubara,mjane wa rais 

Anorld Mubara.Mneniletea nini 

Theresa na Mathew? “Ahsante sana mama kwa 

kutupokea na kwa makaribisho 

mazuri.Tumekuja kwako 

kuzungumza nawe mambo 

machache yanayohusiana na 

hayati rais Anorld Mubara” 

akasema Mathew.April 

akaonekana kusita kidogo halafu 

akasema 

“Nilidhani jambo hili 

limemalizika kumbe 

bado.Nimekwisha hojiwa na 

wengine wengi lakini 

walipoondoka hawakuwahi kurudi 

tena hapa kunipa mrejesho .Haya 

Mathew unahitaji kufahamu nini 

kuhusiana na marehemu mume 

wangu? “Mama ni miaka zaidi ya kumi 

sasa toka ilipotokea ajali 

iliyochukua uhai wa mumeo 

Anorld Mubara.Kwa muda huo 

wote uchunguzi wa ajali ile 

haujawahi kukamilika.Mtu pekee 

ambaye angeweza kutusaidia 

kufahamu kilichotokea ni kanali 

Sebastian Matope ambaye naamini 

unamfahamu na ambaye ndiye 

pekee aliyenusurika katika ajali 

ile” 

“Kanali Sebastian 

ninamfahamu vyema sana” 

akasema bi April 

“Kanali Sebastian alifariki 

miezi michache baada ya mumeo 

kufariki katika ajali,na matukio 

yote haya mawili la kifo cha mumeo na kifo cha Kanali 

Sebastian hayajaweza kupatiwa 

majibu hadi leo hii.Vifo hivi 

vimekuwa ni kama fumbo gumu 

lisiloweza kufumbuka.Rais Dr 

Vivian alipoingia madarakani 

amelifufua jambo hili na kutaka 

uchunguzi ufanyike kufahamu nani 

walimuua baba yake na tayari 

uchunguzi umeanza kufanyika 

.Mimi ni mmoja wa watu 

tunaochunguza suala hili na 

tunaanzia katika ajali ile ya ndege 

iliyomuua rais Anorld Mubara” 

Akanyamaza kidogo halafu 

akaendelea 

“Japo jambo hili limekuwa ni 

fumbo gumu lakini kuna 

mwangaza mdogo sana tumeanza kuuona ambao unaweza 

kutupeleka mahala tunakoweza 

kupata ukweli wa ile ajali ya 

ndege.Tumegundua kwamba 

kulikuwa na watu kumi na tisa 

ndege ilipoondoka hapa Dar es 

salaam kuelekea Misri na wakati 

wa kurudi watu waliongezeka 

kwani kulikuwa na waandishi wa 

habari nane walioomba lifti katika 

ndege ya rais baada ya kuchelewa 

ndege yao.Ilipotokea ajali 

alinusurika mtu mmoja tu na 

wengine wote walikufa lakini 

kinachoshangaza taarifa ya watu 

waliofariki katika ajali hiyo 

haionyeshi kama kulikuwa na 

waandishi hao wa 

habari.Tumegundua kwamba waandishi hao wa habari 

walisaidiwa na mtu na mtu mmoja 

anaitwa Fakrim Alnasor aliyekuwa 

mfanyakazi katika shirika la ndege 

la American airways na siku 

chache baada ya ajali kutokea 

alihamishiwa New york.Uchunguzi 

unaonyesha kwamba huyu Fakrim 

ni jasusi wa shirika la ujasusi la 

Marekani CIA.Tumeanza kuona 

chembe chembe za Marekani 

kuhusika katika ajali ile kupitia 

shirika lake la ujasusi la 

CIA.Uchunguzi unaendele a hivi 

sasa ili tuweze kumpata huyu 

Fakrim lakini tumejiuliza sababu 

ya Marekani kuhusika katika suala 

hili na kumuua rais Anorld 

Mubara.Lazima kuna sababu iliyowapeleka kufanya hivyo na 

ndiyo tunaitafuta hivyo tumekuja 

hapa kwako kwa kuwa wewe ni 

mke wa rais Anorld yawezekana 

kuna jambo ambalo unaweza kuwa 

unalifahamu halikuwa na kawaida 

ambalo linaweza kusababisha 

Marekani kufanya kitendo kile 

kibaya.Yawezekana kuna siri 

fulani aliwahi kukupa tunaomba 

utueleze ili itusaide katika 

kutafuta chanzo cha kifo chake” 

akasema Mathew 

“Mmenistua sana vijana.Kwa 

miaka hii yote nimekuwa nikilia 

nikiomba siku moja ukweli kuhusu 

kifo cha mume wangu ujulikane 

lakini hakuwahi kutokea mtu 

yeyote aliyenipa taarifa yoyote kuhusiana na ajali ile na hata 

nilipouliza kama uchunguzi tayari 

nikaambiwa kwamba uchunguzi 

bado unaendelea.Nimehoji hadi 

nikaamua kukaa kimya 

nikamwachia Mungu .Hiki 

mlichonieleza leo ni kitu 

kilichonistua sana na hata mimi 

nimeanza kuuona mwanga katika 

kupata majibu ya nani walimuua 

mume wangu.Hata hivyo 

umeniomba nikwaeleze kama 

kuna siri yoyote au kuna kitu 

chochote ambacho si cha kawaida 

inaweza kupelekea Marekani 

washiriki katika kumuua mume 

wangu ,ukweli ni kwamba Anorld 

hakuwa ananishirikisha katika 

masuala yake nyeti.Kitu kimoja ambacho namlaumu sana ni usiri 

wake katika hata mambo yale ya 

hatari.Hata kama kuna jambo 

linamsumbua lakini akirudi 

nyumbani haionyeshi kama ana 

tatizo lolote.Msiri wake mkubwa 

alikuwa ni Kanali Sebastian 

Matope.Huyu ndiye mwenye 

kufahamu siri nyingi za Anorld na 

laiti kama angekuwa hai angekuwa 

na msaada mkubwa sana kwenu na 

tungeufahamu ukweli.Siku 

alipouawa alikuwa anakuja 

kwangu kuniambia jambo fulani la 

siri lakini hakuweza kufika kwani 

aliuawa njiani na watu 

wasiojulikana”akasema bi April 

Mazungumzo kati yao 

yalidumu kwa zaidi ya dakika arobaini na Mathew alipoona 

hakuna chochote wanachoweza 

kukipata toka kwa yule mama 

wakaagana na kuondoka. 

“Sishangai kwa nini uchunguzi 

huu umechukua zaidi ya miaka 

kumi na hakuna kilichowahi 

kupatikana.Bado ni fumbo zito” 

akasema Mathew baada ya 

kuondoka kwa Bi April 

“Nilikushauri toka mwanzo 

Mathew kwamba tusipoteze muda 

kwa jambo hil………..”Akasema 

Theresa na simu ya Mathew 

ikaita,alikuwa ni Meshack Jumbo 

“Hallow mzee” akasema 

Meshack 

“Uko wapi Mathew? “Niko njiani narejea Dar es 

salaam.Nimetoka kuonana na bi 

April mjane wa rais Anorld.Kuna 

taarifa yoyote? 

“Ndiyo nimepigiwa simu sasa 

hivi na Jimmy ameniambia 

kwamba Fakrim amepigwa risasi 

na kufariki hapo hapo muda mfupi 

uliopita” 

Mathew akashusha pumzi 

“Amepigwa risasi?Mathew 

akashangaa 

“Ndiyo” 

“Kapigwa risasi na nani? 

“Kwa maelezo aliyonipa 

Jimmy,anasema kwamba 

aliwatuma vijana wake 

wamfuatilie na kumteka Fakrim ili 

wamuhoji lakini usiku huu wakati anakaribia kufika nyumbani 

kwake watu waliokuwa na 

bunduki walijitokeza katika gari 

lililokuwa linamfuatilia na 

kummiminia risasi kisha mmoja 

wao akashuka na kuliendea gari la 

Fakrim ili kuthibitisha kama kweli 

amekufa na ndipo vijana wake 

wakaanzisha mashambulizi 

kuwashambulia wale jamaa ambao 

walifanikiwa kukimbia na 

kutokomea kusikojulikana huku 

yule mmoja aliyeshuka akipoteza 

maisha.Vijana wa Jimmy 

walifanikiwa kuipata simu ya 

Fakrim pamoja na kompyuta yake 

ndogo.Hivi sasa wanakwenda 

kuifanyia uchunguzi hiyo simu na 

kompyuta kuona kama kuna kitu chochote wanaweza kukipata cha 

kutusaidia.Tafadhali njoo mara 

moja hapa nyumbani” Akasema 

Meshack Jumbo.Mathew akavuta 

pumzi ndefu. 

“Kuna nini Mathew? Theresa 

akauliza baada ya kuona 

mabadiliko katika uso wa Mathew 

“Fakrim ameuawa” 

“Ameuawa? Lini? 

“Muda mfupi uliopita” 

“Nani kamuua? 

“Bado haijulikani .Ameuawa 

akirejea nyumbani 

kwake.Tutapata taarifa kamili 

baadae” akasema Mathew 

“Mathew hili suala si 

jepesi.Linakoelekea ni suala 

linazidi kupanuka .Ninazidi kuwana hofu kuhusu hatima ya maisha 

yetu” akasema Theresa 

“Hili lililotokea linazidi 

kutupa uhakika kwamba Fakrim 

alikuwa anahusika na jambo hili 

na tayari waliomtuma 

wameshtushwa na mahala 

tulikofika katika uchunguzi wetu 

na ndiyo maana wameamua 

kumuua.Naamini wengi 

waliochunguza hili suala 

hawakufika katika sehemu 

tulikofika sisi na kugundua uwepo 

wa waandishi wa habari waliopata 

lifti katika ndege ya rais kwani 

balozi Zubery anasema hakuna 

aliyewahi kwenda kumuhoji yeye 

chochote kuhusiana na ajali ile 

kwani kwa zaidi ya miaka mitano 




SEHEMU YA 16

ENDELEA

Hili lililotokea linazidi 

kutupa uhakika kwamba Fakrim 

alikuwa anahusika na jambo hili 

na tayari waliomtuma 

wameshtushwa na mahala 

tulikofika katika uchunguzi wetu 

na ndiyo maana wameamua 

kumuua.Naamini wengi 

waliochunguza hili suala 

hawakufika katika sehemu 

tulikofika sisi na kugundua uwepo 

wa waandishi wa habari waliopata 

lifti katika ndege ya rais kwani 

balozi Zubery anasema hakuna 

aliyewahi kwenda kumuhoji yeye 

chochote kuhusiana na ajali ile 

kwani kwa zaidi ya miaka mitano alikuwa hospitali 

anatibiwa.Tumegundua kwamba 

Fakrim ndiye aliyewasaidia hao 

waandishi wa habari kupata lifti 

katika ndege ya rais na huyu 

Fakrim ni jasusi wa CIA kwa hiyo 

kuna mkono wa CIA katika ajali ile 

na ndiyo maana mara tu ilipotokea 

ajali Fakrim aliondolewa Misri 

akapelekwa New York baada ya 

kuikamilisha kazi 

aliyotumwa.Hatimaye baada ya 

miaka kumi tumegundua uhusika 

wake katika suala hii na 

wamemuua haraka ili tusiweze 

kupata taarifa zozote toka kwake 

na kuzidi kulifanya suala hili kuwa 

gumu.Usiogope Theresa mambo 

ndiyo kwanza yameanza.Huko tuendako kutakuwa kugumu zaidi 

lakini nitakulinda kama 

nilivyokwisha kuahidi.Twende 

tukaonane na Meshack Jumbo” 

akasema Mathew 

**************** 

Mathew na Theresa waliwasili 

nyumbani kwa Meshack Jumbo 

akawakaribisha kibarazani na bila 

kupoteza muda mazungumzo 

yakaanza 

“Karibuni sana.Naona uko na 

binti mrembo hapa,ni nani huyu? 

Nitambulishe tafadhali” akasema 

Meshack Jumbo huku akitabasamu 

“Anaitwa Theresa Matope ni 

ndugu wa rais na ndiye mwandishi wake wa hotuba.Zile hotuba zake 

nyingi ambazo huwa unazisikia 

zimejaa msisimko mwandishi 

wake ni huyu.Rais amenipa 

Theresa awe ni msaidizi wangu 

katika kazi hii ninayoifanya na 

ahakikishe hakuna mkwamo 

wowote ninaoupata” akasema 

Mathew na kumtazama Theresa 

“Theresa huyu ni mzee wangu 

anaitwa Meshack Jumbo.Aliwahi 

kuwa bosi wangu katika idara ya 

ujasusi na sasa amestaafu lakini 

rais amemuomba amsaidie 

kuiongoza tena idara ya usalama 

wa taifa kwa mwaka 

mmoja.”akasema Mathew na 

Theresa akainuka na kwenda 

kumpa mkono Meshack “Nimefurahi sana kukufahamu 

Theresa.Kwa kuwa uko karibu na 

Mathew basi tutakuwa tunaonana 

mara kwa mara” akasema Meshack 

Jumbo 

“Hata mimi nimefurahi 

kufahamiana nawe mzee 

Meshack.Mathew amekuwa 

anakutaja mara kwa mara” 

akasema Theresa 

“Kuna lolote mmelipata huko 

mlikoenda? Meshack Jumbo 

akamuuliza Mathew 

“Tulikwenda kuonana na bi 

April Hudson Mubara mjane wa 

rais Anorld.Tulitaka kufahamu 

endapo kuna kitu chochote 

anaweza akatueleza cha kutusaidia 

katika uchunguzi wetu lakini hatukuweza kupata chochote 

kwani April anadai Anorld hakuwa 

anamshirikisha katika mambo 

yake .Mshirika mkuu wa rais 

Anorld ambaye alikuwa 

anayafahamu mambo yake meng 

hata yale ya siri ni kanali Sebastian 

Matope.Hatukuweza kupata 

chochote kutoka kwake na tukiwa 

njiani tukirudi unanipa taarifa ile 

ya kustusha kuhusu 

Fakrim”akasema Mathew 

“Hata mimi nilistuka 

nilipopewa taarifa ile na 

Jimmy.Nimejiuliza kwa nini 

Fakrim auawe leo? Waliomuua ni 

nani? Ni majambazi?Baada ya 

kutafakari nimegundua 

waliomuua Fakrim wamenifanya hivyo kwa sababu maalum na 

kubwa kuna jambo wanalificha na 

hivyo inatupa sisi picha kwamba 

Fakrim alikuwa anahusika na kwa 

namna fulani katika ajali ile ya 

ndege ya rais Anorld.Yawezekana 

CIA au watu wanaomtumia 

wamefahamu kwamba tayari 

amefahamika na njia pekee ya 

kuendelea kulifanya jambo hili 

kuwa fumbo ni kumuua ili tusipate 

chochote toka kwake.Mathew ule 

mwanga mdogo uliousema jana 

kwamba umeanza 

kuonekana,unazidi kuongezeka na 

tukiufuata kwa umakini tunaweza 

kufika nuruni.Unaweza kufanikiwa 

kulifumbua fumbo hili” Akasema 

Meshack Jumbo “Jimmy hajakupigia tena 

kukupa habari zaidi kuhusiana na 

Fakrim? 

“Hapana bado lakini 

namuamini ni mtu wangu wa 

karibu.Atatusaidia sana” akasema 

Meshack Jumbo na kusimama 

“Mathew kama hutojali kuna 

kitu naomba ukanisaidie katika 

maktaba yangu.Kuna jambo 

limenishinda” akasema Meshack 

Jumbo 

“Theresa naomba nimuibe 

Mathew mara moja kuna kitu 

nataka akanisaidie katika 

kompyuta yangu maktaba.Unajua 

sisi tumekwisha kuwa wazee,ila 

anarudi sasa hivi,jisikie nyumbani tafadhali” akasema Meshack 

Jumbo 

“Usijali mzee hakuna tatizo” 

akasema Theresa na Mathew 

akaongozana na Meshack Jumbo 

wakaelekea ndani hadi katika 

maktaba ya Meshack. 

“Mathew nimekuleta huku ili 

tuzungumze.Sikutaka tuzungumze 

mbele ya Theresa.Kuna mambo 

mawili ambayo nataka nikueleze 

kwanza ni kuhusiana na wazo la 

kumshirikisha huyu mwanadada 

Theresa katika operesheni hatari 

kama hii.Hili si wazo zuri hata 

kidogo.Sikatai kwamba unahitaji 

mtu wa kukusaidia lakini si 

Theresa.Hafai kuongozana nawe 

hata kidogo kwani jambo hili linaonyesha kwamba lina mtandao 

mrefu na linawahusisha hadi CIA 

kwa hiyo ni jambo la hatari 

sana.Unahitaji msaidizi ambaye 

ana uwezo mkubwa wa kujilinda 

na kukulinda hata wewe kitu 

ambacho huyu Theresa 

hana.Nakushauri ukitoka hapa 

mrejeshe ikulu akaendelee na 

shughuli zake za kumuandikia rais 

hotuba na kama kuna kitu 

chochote utakihitai toka kwake 

utawasiliana naye na si 

kuongozana naye.Nadhani 

umenielewa Mathew” akasema 

mzee Jumbo 

“Nimekuelewa mzee Jumbo na 

hata mimi nimekwisha liona hilo 

na nilikuwa nina mawazo kama hayo.Jambo hili ni pana sana 

nakumuweka Theresa karibu 

yangu ni kumuweka katika hatari 

zaidi.Nitaachana na 

Theresa.”akasema Mathew 

“Good.Jambo la pili ni 

kuhusiana na mauaji ya 

Fakrim.Muda mfupi kabla hajafika 

hapa Jimmy Snow amenipigia simu 

na kunieleza kwamba mmoja kati 

ya watu waliokuwa wanamsaidia 

kumchunguza Fakrim ni binti yake 

Camilla ambaye anafanya kazi 

FBI.Anasema kwamba baada ya 

mauaji yale kutokea Camilla na 

wenzake walifanikiwa kuchukua 

simu na kompyuta kama 

nilivyokueleza .Wamevifanyia 

uchunguzi wa haraka haraka na kugundua kwamba mtu wa 

mwisho kuzungumza na Fakrim 

katika simu alikuwa ni Nathan 

Carter ambaye walipomchunguza 

vizuri wamegundua kwamba ni 

mchumba wa rais wa Tanzania 

.Wakati wakiendelea na uchunguzi 

kuhusiana na Nathan Carter kuna 

jambo likatokea,Camilla tayari 

ameingia matatizoni kufuatia 

kuonekana katika eneo la tukio 

akichukua kompyuta na simu ya 

Fakrim kwani yeye ndiye 

aliyekuwa kiongozi wa vijana 

waliotumwa kwenda 

kumchunguza Fakrim.Tayari 

ameanza kusakwa ili ahojiwe kwa 

hiyo Camilla amekimbilia Mexico 

na toka hapo atakwenda hadi Cuba na lengo ni kutafuta njia ya kuweza 

kukimbilia nchini Urusi aliko baba 

yake.Nimemshauri Jimmy kwamba 

kwa nini Camilla asije nchini 

Tanzania ili asaidiane nawe? 

Camilla anaweza kuwa msaada 

mkubwa sana kwako katika 

operesheni hii.Jimmy amekubali 

na atawasiliana na Camilla 

atakapokuwa amefika 

Havana.Endapo akikubali litakuwa 

ni jambo jema sana kwetu.Una 

wazo gani kuhusu hilo? 

“Sina cha kuongeza hapo 

mzee.Umefanya kitu kizuri 

kumshauri Jimmy kuhusu Camilla 

kuja Tanzania.Naamini atakuwa na 

msaada mkubwa 

kwetu.Kilichonistua zaidi ni kusikia kwamba Nathan Carter ni 

jasusi wa siri wa CIA.Huyu ni 

mchumba wa rais Dr Vivian na 

inaonekana amepandikizwa 

makusudi kabisa karibu na rais 

kwa lengo maalum” akasema 

Mathew 

“Kama Nathan ni CIA basi ni 

wazi alikuwa na kazi maalum.CIA 

wana mbinu nyingi sana za kuweza 

kupata taarifa mbali mbali 

wanazozitaka kwa hiyo si kitu cha 

kushangaza kuona kwamba hata 

Nathan aliwekwa hapa kimkakati” 

akasema Meshack 

“Kwa mujibu wa maelezo 

aliyonipa Theresa,Nathan na Dr 

Vivian kwa sasa wana mgogoro 

katika mahusiano yao na mipangya ndoa yao 

imevurugika.Nimeshuhudia leo 

Nathan akimpigia simu Theresa na 

akagoma kupokea kwa agizo la 

rais.Sijajua nini sababu ya 

mgogoro huo.Nadhani kuna 

ulazima wa kuuchimbua uhusiano 

huo wa Dr Vivian na Nathan kujua 

namna ulivyoanza na pengine 

tunaweza kufahamu lengo la 

Nathan.Yawezekana kutokana na 

kuzama mapenzini Dr Vivian 

hamjui mpenzi wake ni mtu wa 

aina gani kwani mapenzi ni 

upofu.Wakati tukiendelea 

kumchunguza Nathan Dr Vivian 

hapaswi kufahamishwa 

chochote.Uchunguzi utafanyika 

kimya kimya.Kingine tutakachokifanya ni kuhakikisha 

Nathan anakuja 

Tanzania.Nitazungumza na 

Theresa yeye atafanya mipango ya 

siri ili Nathan aweze kuja Tanzania 

kwa siri bila ya Dr Vivian kujua.Dr 

Vivian akifahamu kwamba mdogo 

wake amefanya jambo hili kwa siri 

linaweza kuleta mgogoro baina 

yao lakini litatusaidia sisi kuweza 

kumchunguza na kumfahamu 

vyema Nathan ni nani.Niachie 

suala hili nitalifanyia kazi” 

akasema Mathew halafu wakarejea 

mahala walikomuacha Theresa 

Mathew na Theresa wkaaga na 

wakaondoka. 




Kwa mujibu wa maelezo 

aliyonipa Theresa,Nathan na Dr 

Vivian kwa sasa wana mgogoro 

katika mahusiano yao na mipango 

ya ndoa yao 

imevurugika.Nimeshuhudia leo 

Nathan akimpigia simu Theresa na 

akagoma kupokea kwa agizo la 

rais.Sijajua nini sababu ya 

mgogoro huo.Nadhani kuna 

ulazima wa kuuchimbua uhusiano 

huo wa Dr Vivian na Nathan kujua 

namna ulivyoanza na pengine 

tunaweza kufahamu lengo la 

Nathan.Yawezekana kutokana na 

kuzama mapenzini Dr Vivian 

hamjui mpenzi wake ni mtu wa 

aina gani kwani mapenzi ni 

upofu.Wakati tukiendelea 

kumchunguza Nathan Dr Vivian 

hapaswi kufahamishwa 

chochote.Uchunguzi utafanyika 

kimya kimya.Kingine 

tutakachokifanya ni kuhakikisha 

Nathan anakuja 

Tanzania.Nitazungumza na 

Theresa yeye atafanya mipango ya 

siri ili Nathan aweze kuja Tanzania 

kwa siri bila ya Dr Vivian kujua.Dr 

Vivian akifahamu kwamba mdogo wake amefanya jambo hili kwa siri 

linaweza kuleta mgogoro baina 

yao lakini litatusaidia sisi kuweza 

kumchunguza na kumfahamu 

vyema Nathan ni nani.Niachie 

suala hili nitalifanyia kazi” 

akasema Mathew halafu wakarejea 

mahala walikomuacha Theresa 

Mathew na Theresa wkaaga na 

wakaondoka. 

ENDELEA

Ni siku iliyotawaliwa na 

vikao mfululizo vya 

kazi.Kwanza Dr Vivian 

alikutana na kufanya mazungumzo 

na balozi wa marekani nchini 

Tanzania halafu akakutana pia 

nakufanya mazungumzo na balozi 

wa umoja wa Ulaya.Wote hawa 

walikuja kuzungumza naye 

kuhusiana na mpango wake wa 

kutaka kuanzisha mahusiano na 

Korea Kaskazini.Waliwasilisha 

salamu za viongozi wao lakini 

walirejea kama walivyokuja kwani 

msimamo wa Dr Vivian 

haukubadilika.Aliwasisitizia 

kwamba azma yake ya 

kushirikiana na Korea Kaskazini 

iko pale pale.Baada ya kuonana na mabalozi wale alikutana na 

watendaji kadhaa wa serikali 

halafu akakutana na mjumbe 

maalum toka kwa rais wa Iran 

aliyemtumia salamu 

maalum.Katika salamu zake,rais 

wa Iran alimuhakikishia Dr Vivian 

kwamba yeye na serikali yake 

watamuunga mkono katika 

mpango wake wa kutaka 

kuanzisha mashirkiano na Korea 

Kaskazini.Alipomaliza maongezi 

na mjumbe huyo maalum kutoka 

kwa rais wa Iran,alitaarifiwa 

kwamba rais wa China alikuwa 

katika laini ya simu kwa ajili ya 

mazungumzo.Dr Vivian 

akaahirisha kwenda kula chakula cha mchana ili kuzungumza na rais 

wa China 

“Mr Wang Jing Xu habari yako” 

akaanzisha maongezi Dr Vivian 

“Habari nzuri kabisa Dr 

Vivian.Habari za Dar es salaam? 

“Huku kwema.Habari za 

Beijing? 

“Hapana siko Beijing.Niko 

hapa New york kuhudhuria 

mkutano wa baraza kuu la umoja 

wa mataifa lakini nategemea 

kuondoka mara tu 

nitakapohutubia hapo kesho” 

Akasema rais Wang 

“Mimi tayari nimekwisha 

ondoka baada ya kutoa hotuba 

yangu na sikupata wasaa wa 

kuweza kusalimiana nawe” “Usijali Dr Vivian,nimekupigia 

kwanza kukupa pongezi nyingi 

kwa hotuba yako nzuri uliyoitoa 

katika baraza kuu la umoja wa 

mataifa.Ni hotuba nzuri na uliitoa 

kwa wakati na sehemu 

sahihi.Afrika ilisubiri sana kupata 

kiongozi mwenye msimamo na 

mtazamo kama wewe.Pamoja na 

vitisho kuhusiana na vikwazo vya 

kiuchumi ambavyo Tanzania 

inatishiwa kuwekewa,nakuomba 

usilegeze msimamo wako.Usirudi 

nyuma hata hatua moja.Shikilia 

msimamo wako hapo hapo 

uliposhika.Utakapolegeza 

msimamo litakuwa ni anguko 

lako.Kwa vile umeamua kuingia 

katika vita hii,silaha yako kubwa ya kwanza ni msimamo.Usijaribu 

kuweka chini silaha yako hiyo na 

endelea kupambana hadi ushindi 

upatikane. 

China tuko nyuma yako na 

tutakuunga mkono katika kila 

hatua na hata katika hotuba yangu 

nitakayoitoa mbele ya baraza kuu 

la umoja wa mataifa nitaweka wazi 

msimamo wa China kuhusiana na 

kuiunga mkono Tanzania kufaya 

biashara na taifa lolote duniani 

bila kuwekewa mipaka.Siku zote 

China itasimama upande wa 

Tanzania.Marekani wametishia 

kuwasilisha vikwazo kwa umoja 

wa mataifa kwa ajili ya kuweka 

vikwazo vikali vya kiuchumi kwa 

Korea Kaskazini na nchi washirika wake ikiwamo Tanzania lakini sisi 

China tutatumia kura yetu ya 

turufu kuhakikisha hilo jambo 

halifanikiwi.Hatuko tayari kuona 

Tanzania inawekewa vikwazo eti 

kwa sababu ya kulinda na kutumia 

rasilimali zake.Nchi yoyote 

itakayothubutu kuichokoza 

Tanzania kwa namna yoyote ile 

iwe ndogo au kubwa itakutana na 

mkono wa China na tutamuadhibu 

vikali.Tutaungana na mataifa 

ambayo yako tayari na 

yametangaza kuiunga mkono 

Tanzania dhidi ya vitisho vya 

Marekani na washirika wake na 

tutahakikisha tunaisaidia 

Tanzania kwa kila  namna  tutakavyoweza ili iweze kukua 

kiuchumi 

Rais wa Korea kaskazini 

amenipigia simu na kunieleza 

kwamba mlizungumza kwa kirefu 

simuni kuhusiana na kuanzishwa 

kwa mashirikiano baina ya nchi 

zenu. Nimefurahishwa na hatua 

ambazo umeanza kzichukua 

kuhusiana na suala hili .Popote 

patakapokuwa na mkwamo na 

kuhitaji msaada usisite kuniomba 

msaada na nchi yangu iko tayari 

muda wowote kukusaidia.Naomba 

pia utumie mashirikiano hayo 

utakayoyajenga na Korea 

Kaskazini kuishawishi serikaliya 

Korea Kaskazini kuhusiana na 

majaribio yake ya makombora katika bahari ya Pacific” akasema 

rais Wang 

“Nakushukuru sana 

mheshimiwa rais kwa kuniunga 

mkono.Binafsi nimeamua kuingia 

katika vita hii kubwa ya uchumi 

dhidi ya mataifa makubwa na 

nitasimama imara sintageuka 

nyuma.Nashukuru mataifa rafiki 

ambayo yanasimama na sisi katika 

vita hii yakiongozwa na 

China.Endeleeni kutuunga mkono “ 

akasema Dr Vivian 

“Rais Kim alinieleza 

kuhusiana na ombi lako la kutaka 

kujengewa kinu cha nyuklia kwa 

ajili ya kuzalisha nishati ya 

umeme.Hilo ni wazo zuri sana na 

endapo likifanikiwa litaweza kuleta mageuzi makubwa sana ya 

kiuchumi nchini 

Tanzania.Ninaliunga mkono na 

niko tayari kushirikiana na Korea 

Kaskazini katika kujenga kinu 

hicho muhimu sana kwa uchumi 

wa Tanzania.Mipango yako hii 

itaipaisha Tanzania kiuchumi 

licha ya tishio la vikwazo” 

“Ni kweli mheshimiwa Wang 

,nimezungumza na rais Kim 

kuhusiana na kujengewa kinu cha 

nyuklia hapa nchini Tanzania ili 

tuweze kujitosheleza kwa nishati 

ya kutosha ya umeme kwani 

Tanzania kwa sasa tunafanya 

mageuzi makubwa ya kiuchumi na 

tunajenga viwanda vingi hivyo 

nishati ya uhakika ya umeme inahitajika .Tunayo hazina kubwa 

ya madini ya Urani kwa hiyo 

tunataka kuwa wazalishaji 

wakubwa wa umeme katika 

ukanda wa Afrika mashariki kwa 

kutumia madini ya Urani.Rais Kim 

amelipokea wazo langu na 

ameahidi kulifanyia kazi” akasema 

Dr Vivian na kuendelea na 

maongezi mengine na 

walipomaliza maongezi yao Dr 

Vivian akaelekea kupata chakula 

cha mchana 

Walipotoka nyumbani kwa 

Meshack Jumbo,Mathew na 

Theresa walielekea moja kwa moja 

katika hoteli moja maarufu 

ambayo Mathew hupenda sana 

kwenda kupata chakula.Ni hoteli 

iliyoko kandoni mwa bahari kwa 

hiyo mchana huu kulikuwa na 

upepo mzuri .Mathew alipenda 

sana kula samaki na ndiyo maana 

hupenda kuja katika hoteli hii 

inayosifika kwa kupika vizuri aina 

mbali mbali ya samaki.Chakula 

walichoagiza kikaletwa wakaanza 

kula taratibu huku wakipulizwa na 

upepo wa bahari “Theresa kuna mambo mawili 

nahitaji kuzungumza nawe” 

akaanzisha mazungumzo Mathew 

“Kwanza kabisa ninapenda 

nikushukuru sana kwa msaada 

mkubwa ambao umenisaidia toka 

jana tulipoanza kulishughulikia 

hili suala.Umenisaidia nimeweza 

kupata nyaraka mbali mbali 

ambazo nisingeweza kuzipata 

kama ningekuwa mwenyewe.Hata 

hivyo suala hili linazidi kuchukua 

sura mpya kila uchao na mpaka 

hivi sasa linaonekana kuwa ni 

suala linalovuka mipaka ya 

nchi.Marekani inaonekana 

kuhusika katika jambo hili ingawa 

bado hatuna uhakika mkubwa 

hadi hapo utakapofanyika uchunguzi .Kwa hapa tulipofika 

suala hili limeanza kuonyesha si 

suala rahisi na huko tuendako 

kunaonekana kuwa na giza nene 

na hatari kubwa kwa hiyo 

nimefikiria sana na nimeona 

itakuwa vyema endapo nitakuacha 

ukaendelee na shughuli zako za 

kawaida na mimi niendelee peke 

yangu na uchunguzi 

huu.Nimefanya hivyo kwa sababu 

sitaki kukuweka katika 

hatari.Umeona mwenyewe kadiri 

tunavyoendelea kulichunguza hili 

suala ndivyo mambo mengi 

yanavyozidi kuibuka na hivyo 

kuzidisha hatari kwa upande 

wetu.Kuwa karinu na mimi si suala 

zuri kwa sasa kwani hawa watu wanaohusika na matukio yote 

mawili ya kuanguka kwa ndege ya 

rais na kuuawa kwa baba yako ni 

mtandao mrefu na wanaweza 

wakafahamu kwamba tayari 

tumeanza kuwafuatilia kwa hiyo 

watajihami.Sitaki uingie katia 

matatizo hivyo kuanzia mchana 

huu utarudi ikulu.Nitampigia simu 

Dr Vivian na kumtaarifu kuhusu 

suala hili.Endapo nitahitaji msaada 

wowote kutoka kwako 

nitakujulisha lakini si kwa 

kuongozana huku nje kama hivi 

.Muda wowote hatari inaweza 

ikatokea na tukashambuliwa hivyo 

unahitajika uwe ni mtu mwenye 

uwezo wa kujilinda na kumlinda 

mwenzako” akasema Mathew Ukapita ukimya mfupi kidogo 

,Theresa akasema 

“Nilikuwa naisubiri kwa hamu 

kubwa kauli hii kwani jambo hili 

limeniogopesha mno toka mwanzo 

ila sikuwez kumkatalia dada 

aliponiomba niungane nawe 

nikusaidie.Siwezi kusema hapana 

kwani ni kitu nilichokisubiri hivyo 

nakushukuru kwa maamuzi hayo 

na endapo utahitaji kitu chochote 

kile nitakuwa tayari kukusaidia” 

akasema Theresa na Mathew 

akatabasamu 

“Nafurahi kusikia 

hivyo.Usikasirike pale 

nitakapokusumbua hata usiku wa 

manane” “Usihofu Mathew.Nitakuwa 

nalala jicho moja huku nikiamini 

kwamba kuna mtu yuko nje halali 

anafanya kazi ya kutafuta ukweli 

kuhusiana na wazazi wetu na 

nitakuombea sana” 

“Ahsante.Jambo la pili ambalo 

nataka liwe ni baina yangu mimi 

na wewe na asifahamu mtu 

mwingine yeyote na hasa dada 

yako Dr Vivian.” 

“Ni jambo gani hilo? 

“Uliniambia kwamba Dr 

Vivian na mpenzi wake 

wamekorofishana? 

“Ndiyo wamekorofishana 

.Kuna nini kwani? 

“Ninahitaji huyo mpenzi wa Dr 

Vivian aje Tanzania.Unaweza kunisaidia kumfanya aje Tanzania 

haraka? 

Theresa aliyekuwa anaipeleka 

glasi ya kinywaji mdomoni 

akaishusha na kuiweka 

chini.Alionekana kushtuka 

“Unamtaka Nathan? Kwa nini ? 

“Ninamuhitaji awepo hapa 

Tanzania karibu na Dr Vivian” 

akasema Mathew 

“Mathew itakuwa vyema 

endapo utanieleza kusudi la 

kumtaka Nathan aje Tanzania ili 

nikiridhika nione nitafanya nini 

kulitekeleza hilo” 

“Theresa kwa kuwa nahitaji 

sana msaada wako nitakueleza 

ukweli ila nakuomba sana sana hii 

iwe ni siri yako na usimueleze mtu yeyote hata Dr Vivian”akasema 

Mathew 

“Sina kawaida ya kumficha 

jambo dada yangu lakini kama 

kutakuwa na ulazima wa kuficha 

basi itanibidi kufanya hivyo. Ni 

jambo gani hilo nieleze Mathew 

nina hamu ya kulifahamu” 

akasema Theresa.Mathew 

akanywa funda moja la mvinyo na 

kusema 

“Kuna tetesi japo hazina 

uhakika bado kwamba Nathan 

ambaye ni mchumba wa dada yako 

,ni jasusi toka shirika la ujasusi la 

CIA” 

“What ?! Theresa akashangaa 

na kuweka kijiko chini 

“Tafadhali usistuke Theresa.” “Lazima nistuke 

Mathew.Nathan ni mpelelezi? 

“Kuna tetesi hizo kwamba ni 

jasusi wa CIA na kuna uwezekano 

yuko katika shughuli maalum hapa 

Tanzania kwa hiyo tunahitaji 

kumchunguza ili kuupata ukweli 

kama kweli yeye ni CIA na 

ametumwa kufanya kazi gani hapa 

Tanzania? akasema Mathew. 

“Mathew nimeogopa sana kwa 

hili uliloniambia.Ni vigumu sana 

kuamini lakini kwa namna 

nilivyokuwa namuona yule jamaa 

sikuwa namuelewa elewa na 

ninaweza kukubaliana nawe 

kwamba ni mpelelezi na yuko hapa 

kwa shughuli maalum” “Kama nilivyokwambia 

Theresa kwamba ukiingia katika 

kazi hizi kuna mambo mengi ya 

kuogofya na kushangaza 

utakutana yao kama hili la 

Nathan.Naamini hata Dr Vivian 

hawezi kukubali kama Nathan 

mchumba wake ni jasusi wa 

CIA.Hata hivyo tunatakiwa kupata 

uhakika kwanza kama kweli ni CIA 

na ametumwa kufanya kazi gani 

ndipo tutamueleza rais” 

Theresa akamtazama Mathew 

kwa uoga. 

“Unataka nifanye nini 

Mathew? Akauliza kwa sauti ya 

woga 

“Jana tukiwa garini alikupigia 

simu lakini hukupokea.Nataka umpigie simu na kuzungumza naye 

umwambie kwamba unataka 

umsaidie ili aweze kurudiana na 

dada yako na ili kufanya hivyo 

itamlazimu aje Tanzania.Jiweke 

upande wake na asigundue 

chochote kama hiki ni kitu cha 

kupanga.Mweleze kwamba 

asimpigie simu Dr Vivian 

kumjulisha kama anakuja 

Tanzania bali iwe ni siri yenu” 

akasema Mathew 

“Nini kitatokea atakapokuja? 

“Atakapokuja wewe utakuwa 

umemaliza kazi yako na litabaki 

jukumu langu kumchunguza na 

endapo nitahitaji msaada wako 

wowote nitakujulisha” akasema 

Mathew “Nitajitahidi kufanya hivyo 

lakini nimeogopa sana 

Mathew.Sikutegemea kabisa 

kusikia habari kama hii” akasema 

Theresa 

“Usiogope tafadhali 

.Unapaswa kuwa jasiri sana ili 

tuweze kulifanikisha suala hili” 

Theresa akafikiri kidogo na 

kuuliza 

“Mathew unadhani dada 

Vivian yuko katika hatari? 

“Inawezekana.Kama Nathan ni 

CIA basi lazima yuko karibu na 

dada yako kwa shughuli maalum 

na hii inatoa picha kwamba Dr 

Vivian hayuko salama lakini usiwe 

na hofu kwani muda si mrefu 

tutalifahamu jambo hili na kumuondoa Dr Vivian katika 

hatari” akasema Mathew na 

Theresa hakuweza kuendelea tena 

kula kutokana na woga 

alioupata.Ukimya ukatanda 

mezani,Mathew akaendelea kula 

kimya kimya.Baada ya muda 

Theresa akasema 

“Nina wazo Nathan.” 

“Karibu”akasema Mathew 

“Umenitaka nirejee ikulu 

nikaendelee na shughuli zangu za 

kawaida lakini sitaki kurejea ikulu 

kwa sasa nataka niutumie muda 

huu kupumzika.Dada akikuuliza 

mweleze kwamba bado uko na 

mimi.Unaweza kunisaidia kwa hilo 

tafadhali? “Usijali Theresa nitakusaidia 

ila jitahidi kwa kila uwezavyo 

Nathan aweze kuja Tanzania.” 

“Kuhusu Nathan hilo lisikupe 

shida kwani atakuja Tanzania 

.Nitafanya kila niwezalo na 

atakuja” 

“Basi usitie shaka nami 

nitafanya kama ulivyoniomba 

sintamueleza chochote Dr Vivian” 

akasema Mathew na kuendelea 

kula .Baada ya kumaliza kula 

wakaondoka moja kwa moja hadi 

nyumbani kwa Theresa .Mathew 

akamuacha hapo na kuondoka 

zake. 

“Nimestuka na kuogopa sana 

kusikia kwamba Nathan ni 

CIA.Anatafuta nini kwa dada? Kuna kitu gani ametumwa akichunguze? 

Akawaza Theresa baada ya 

Mathew kuondoka 

“ Kwa mujibu wa maelezo ya 

dada n kwamba alianza mapenzi 

na Nathan wakati angali anasoma 

chuo.Inawezekanaje Nathan awe 

anamchunguza kwa muda huo 

wote? Na kama anamchunguza ni 

kuhusu nini?Hili jambo 

linachanganya sana lakini ngoja 

nimuachie Mathew alichunguze 

halafu tutaufahamu ukweli.” 

Akawaza na kuchukua simu yake 

akazitafuta namba za Nathan na 

kutaka kumpigia akasita 

“Ninasita kabisa kumpigia 

huyu jamaa.Halafu ni vipi endapo 

dada Vivi akifahamu kwamba nimemzunguka na kufanya 

mawasiliano na Nathan bila ya 

yeye kujua wakati wamekwisha 

achana?Hii inaweza kuleta 

msuguano kati yetu .Lakini 

nisipofanya hivyo Mathew 

atashindwa kufanya uchunguzi 

wake na hatutajua nia ya Nathan 

kwa dada Vivi.Ngoja nimpigie simu 

na kitakachotokea tutaeleweshana 

huko mbele ya safari” akawaza 

Theresa na kumpigia Nathan.Simu 

ikaita bila kupokelewa na 

kukatika. 

“Ni saa tisa mchana huku 

kwetu ambapo ni asubuhi kwa 

Marekani ,yawezekana Nathan 

akawa amelala bado.Ngoja 

nimjaribu tena.Kabla hajapiga simu yake ikaita alikuwani 

Nathan,Theresa akaipokea 

“Hallow Nathan” akasema 

Theresa 

“Habari yako 

Theresa,samahani sikuweza 

kupokea simu yako nilikuwa 

bafuni .Habari za Dar es salaam? 

“Huku kwema kabisa.Habari 

za New york? 

“Huku kwema pia.Nimekuwa 

najaribu kukupigia lakini 

haupokei simu yangu.Kwa nini 

Theresa? 

“Utanisamehe sana 

Nathan.Sikuweza kupokea simu 

zako lakini si kwa makusudi bali ni 

kutokana na kubanwa na jukumu 

lingine wakati uliponipigia.Siwezi kushindwa kupokea simu yako na 

hata wewe unafahamu hilo.Vipi 

unaendeleaje na dada Vivi? Kuna 

hatua yoyote mmeifikia hadi hivi 

sasa? 

“Hakuna chochote 

tulichoongea hadi sasa kwani 

Vivian hataki kupokea simu 

yangu.Nimejaribu sana kumpigia 

ila hapokei kabisa na katika laini 

zake nyingine amenifungia.” 

“Dah ! lakini Nathan hebu 

nieleze nini hasa chanzo cha wewe 

na dada kuingia katika mgogoro 

kwa wakati huu ambao 

mmebakisha miezi miwili tu 

mfunge ndoa? 

“Theresa kilichotokea na 

kutufarakanisha ni kitu kidogo sana huwezi kuamini.Ni kuhusiana 

na mtoto.Nilitaka kufahamu 

msimamo wake kuhusiana na 

kuzaa mtoto tutakapofunga ndoa 

na hapo ndipo ugomvi ulipoanzia 

na mwisho akasema kwamba kila 

mmoja aendelee na maisha 

yake.Mpaka sasa bado siamini 

kama kweli eti mimi na Vivian 

tumetengana” akasema 

Nathan.Theresa akavuta pumzi 

ndefu na kuuliza 

“Nathan naomba uniambie 

kitu kimoja.Je unampenda kweli 

Vivian? 

“Ninampenda zaidi ya 

ninavyoweza kukueleza.Siwezi 

kuuelezea upendo wangu kwake.Ni 

zaidi ya upendo” “Kama kweli unampenda kiasi 

hicho basi usimuache aende.Tafuta 

namna ya kulipigania penzi lenu 

ambalo mmetumia muda mrefu 

kulijenga.” 

“Najitahidi sana Theresa 

kutaka kulipigania penzi letu 

lakini inaonekana mwenzangu 

tayari amekwisha fanya maamuzi 

na unajua dada yako alivyo akisha 

amua jambo huwa harudi 

nyuma.Msimamo wake umebaki 

ule ule kwamba kila mmoja 

aendelee na maisha yake” 

Ukapita ukimya kidogo na 

Theresa akasema 

“Nathan mimi sijafurahishwa 

kabisa na hiki kilichotokea kati 

yenu na niko tayari kusaidia ili jambo hili likae vizuri.Nitafanya 

kila lililo ndani ya uwezo wangu 

kwani Theresa hawezi 

kunishinda.Nitazungumza naye na 

atanielewa” 

“Kweli Theresa? Akauliza 

Nathan 

“Kweli kabisa.Nimeumizwa 

sana kuona mmefikia hatua 

hii.Penzi lenu lilikuwa ni mfano wa 

kuigwa na kila mtu alitamani kuwa 

kama ninyi.Sitaki mapenzi yale 

yaishie hewani.Nathan wewe ndiye 

pekee mwanaume unayemfaa dada 

yangu,hivyo nitaingilia kati na 

kuliweka sawa hili jambo na 

mambo yataendelea kama 

yalivyopangwa” “Nashukuru sana Theresa kwa 

hilo unalokwenda kulifanya.Hapa 

nilipo nimechanganyikiwa na sijui 

nifanye nini kwani marafiki zangu 

wote wamekwishajiandaa na 

wengine tayari wamekata hadi 

tiketi wakijiandaa kwa safari ya 

kuja Tanzania katika harusi yangu 

kwa hiyo nashindwa namna ya 

kuwaeleza kwamba hakutakuwa 

na harusi tena.Tafadhali naomba 

unisaidie Theresa na ndiyo maana 

nimekuwa nakupigia simu 

nikitaka kukuomba msaada wako 

kwani nafahamu uwezo wa 

kuliweka sawa jambo hili unao” 

“Mimi nitakusaidia Mathew 

kama nilivyokuahidi lakini kuna 

kitu kimoja unapaswa kukifanya” “Ni kitu gani Theresa? 

“Unapaswa kuja Tanzania 

haraka iwezekanavyo lakini njoo 

kimya kimya bila ya kumtaarifu 

Vivian na wala usimpigie 

simu.Mimi nitamaliza kila kitu na 

halafu utamshangaza kwa kutokea 

ghafla.Nitakupa maelekezo yote 

utakapofika huku lakini jitahidi 

sana kuja Tanzania haraka 

iwezekanavyo.Suala hili haliwezi 

kutatuliwa na wewe ukiwa mbali 

.Unapaswa kuwa karibu ili 

muweze kuonana na kuongea ana 

kwa ana” 

“Hilo si tatizo Theresa.Ninao 

uwezo wa kuja haraka 

iwezekanavyo.Kwa kuwa suala hili 

ni la muhimu sana kuliko mambo yangu mengine,kaka yangu ana 

ndege yake binafsi nitaongea naye 

asubuhi hii kama naweza kutumia 

ndege yake kuja Tanzania.Endapo 

akikubali basi hadi kesho saa nne 

au tano asubuhi nitakuwa 

nimefika Dar es salaam.Theresa 

suala hili ninalipa umuhimu 

mkubwa mno.Vivian ni kila kitu 

katika maisha yangu.Niko tayari 

kukosa kila kitu maishani lakini 

nimpate yeye tu.Kwa umuhimu 

wake huo nitakuja Tanzania 

haraka sana.Nataka 

nikudhihirishie namna gani Vivian 

alivyo muhimu kwangu.” Akasema 

Nathan 

“Sawa Nathan basi endelea 

kufanya taratibu za safari kama utapata ndege binafsi au utapanda 

ndege za abiria utanijulisha ila 

jitahidi kwa kila uwezavyo uweze 

kufika hapa Tanzania haraka 

uwezavyo” akasema Theresa na 

kukata simu na kuitupa kitandani 

“Kwa namna anavyoongea 

utadhani kweli ana mapenzi 

makubwa sana kwa Vivian kumbe 

ana kitu anakitafuta na ndiyo 

maana amefurahi sana kusikia 

kwamba ninataka kuwaunganisha 

tena na Vivian.Amefurahi kwa 

kujua kwamba endapo 

wakirudiana basi mipango yake 

itaendelea kama kawaida.Mambo 

kama haya ndiyo yanayonifanya 

nisiweze kumweleza mtu yeyote 

hata dada kile ninachofahamu kuhusiana na kuanguka kwa ndege 

ya rais Anord au hata kifo cha baba 

na zaidi sana Football.Tena 

nimekumbuka itanibidi 

kumuomba dada ulinzi kwani nina 

wasiwasi kwa siku hizi mbili 

ambazo nimekuwa na Mathew na 

nimekuwa nauliza uliza maswali 

na kutaka nyaraka totauti tofauti 

kuhusiana na ajali ya ndege ya rais 

ninaweza kuwa nimeanza 

kumulikwa kwani huwezi kujua 

nani anakufuatilia nyuma kama 

ambavyo ni vigumu kuamini kama 

Nathan ni jasusi wa CIA.” Akawaza 

Theresa. 

Kwa upande wa Mathew 

baada ya kuachana na Theresa 

akaenda mahali kunakojengwa kiwanda chake kufuatilia 

maendeleo ya ujenzi halafu 

akarejea nyumbani.Kitu cha 

kwanza alichokifanya alipofika 

nyumbani ni kumpigia simu rais 

Dr Vivian 

“Habari yako Mathew” 

Akasema Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais samahani 

sana kama nimekuvurugia 

shughuli zako kwa simu hii” 

“Hapana usijali kabisa 

Mathew haujaharibu chochote 

isitoshe ukinipigia ninafurahi zaidi 

kwani mimi kutokana na kutingwa 

sana na kazi ninashindwa hata 

kukupigia.Vipi maendeleo yako? 

Akauliza “Ninaendelea vyema 

mheshimiwa rais.Nimekupigia 

kuomba kuonana nawe usiku wa 

leo kama hautakuwa na jukumu 

lingine la kikazi” 

“Mimi nipo kazini kila wakati 

Mathew na sina muda wa 

kupumzika.Hata usiku huwa 

ninafanya mikutano kwa njia ya 

simu na watendaji wangu.Hata 

hivyo niko tayari kusimamisha 

shughuli zangu nyingine zote kwa 

ajili yako.Unahitaji kuonana nami 

kuanzia saa ngapi? 

“Kuanzia saa mbili za usiku 

mheshimiwa rais” 

“Kama ni saa mbili za usiku 

kwa nini basi usiwe mgeni wangu 

na tukaungana kwa chakula cha usiku huku tukiendelea na 

maongezi? 

“Hakuna tatizo kwa hilo 

mheshimiwa rais “ 

‘Sawa Mathew nakutegemea 

muda huo wa saa mbili za usiku” 

“Ahsante mheshimiwa rais” 

akasema Mathew na kukata simu 

halafu akampigia Meshack Jumbo 



Ahsante mheshimiwa rais” 

akasema Mathew na kukata simu 

halafu akampigia Meshack Jumbo 

“Mzee kuna lolote umepata 

kutoka kwa Jimmy kuhusuCamilla? 

Akauliza 

“Ndiyo Mathew.Jimmy 

amekuwa ananipigia kila pale 

anapowasiliana na 

Camila.Amenitaarifukwamba 

Camilla yuko ndegeni hivi sasa 

anaelekea Havana Cuba.Kutoka 

pale ndipo atakapoanza kutafuta namna atakavyoweza kufika 

Tanzania” 

“Sawa mzee.Basi akifika 

Havana asubiri pale mimi 

ninafanya mpango wa usafiri wa 

ndege ya kwenda kumchukua hapo 

Havana na kumleta Dar es 

salaam.Peniela ana shirika lake la 

ndege linaitwa Penny 

air.Nitamuomba msaada wa ndege 

ikamchukue Camilla pale Havana 

na kumleta Tanzania.Kitu kigumu 

ilikua ni kutoka Marekani 

anakotafutwa na kwa kuwa tayari 

amekwisha ondoka Marekani basi 

hakuna shaka atafika salama 

Tanzania.” “Una hakika Peniela anaweza 

akakubali kukusaidia?Meshack 

Jumbo akauliza 

“Ndiyo mzee.Hawezi kukataa 

kwani mimi ndiye chanzo cha haya 

mafanikio yake yote 

aliyonayo.Usihofu kuhusu hilo 

mzee.Mtaarifu Jimmy amueleze 

Camilla kwamba akifika Havana 

atulie hapo kwani ndege 

inakwenda kumchukua kumleta 

moja kwa moja Tanzania” 

“Sawa Mathew.Vipi kuna 

maendeleo yoyote ? 

“Nimezungumza na Theresa 

na amesema kwamba atafanya ila 

awezalo kuhakikisha Nathan 

anakuja Tanzania.Vile vile usiku 

wa leo ninakwena kuonana na rais.Tayari nimekwisha zungumza 

naye na amekubali tuonane usiku 

wa leo.Kikubwa ninataka kujua 

kuhusu mahusiano yake na 

Nathan.Nataka kuchunguza kama 

kuna kitu maalum Nathan 

anachokitafuta toka kwa rais” 

“Vizuri Mathew lakini kuwa 

makini sana unapozungumza na 

rais.Usimpe nafasi ya kugundua 

kama unamchunguza 

Nathan.Tumia ufundi mkubwa 

katika kuuliza maswali 

yako.Kingine cha muhimu wewe na 

raisi wote mko karibu umri 

sawa.Jizuie isitokee tamaa yoyote 

kati yenu .”akasema Meshack 

Jumbo na Mathew akacheka 

kidogo “Usihofu mzee.Mimi 

unanifahamu na hata utendaji kazi 

wangu unaufahamu.” 

“Ni angalizo nilikuwa natoa 

Mathew.Sawa tutawasiliana tena 

baadae utanijulisha kuhusiana na 

hiyo ndege itakayokwenda 

kumchukua Camilla.” Akasema 

Meshack na kukata simu 

“Mzee Jumbo ana wasiwasi 

labda naweza kujikuta nimevutiwa 

na rais” akawaza Mathew na 

kucheka huku akizitafuta namba 

za simu za Peniela akampigia. 

“Hallo Mathew habari yako” 

“Nzuri Peniela.Kabla 

sijaendelea uko na mpenzio? 

“Hapana kwa nini? “Sitaki ugomvi naye ndiyo 

maana nikauliza mapema kama 

uko naye karibu ili nikate simu” 

“Hapana siko naye hapa 

karibu.Unasemaje Mathew? 

‘Kwanza kabisa ni kuhusiana 

na siku ya kuzaliwa Anna Maria.” 

“Ndiyo ni jumatatu 

ijayo.Zimebaki siku mbili tu keshi 

jumamosi na jumapili .” 

“Umekwisha mnunulia zawadi 

niliyokuomba? 

“Tayari nimemchukulia ila 

nimeificha hadi siku ya sherehe” 

“Good” 

“Bado hauna mpango wa kuja 

Paris? 

“Hapana siwezi kuja 

Peniela.Nimetingwa sana huku” “Bado unafanya kazi ya rais 

Vivian? 

“Peniela naomba tusiende 

huko.” 

“Samahani nilitaka 

tukujua.Anyway kwanini umepiga 

simu? 

“Juzi uliniuliza kama kuna 

kitu unaweza ukanisaidia” 

“Ndiyo nilikuuliza kama kuna 

kitu naweza kukusaidia katika 

kazi yako ukasema hapana” 

“Sikuwa na kitu cha kuomba 

kwa wakati huo lakini kwa sasa 

ninahitaji msaada wako.” 

“Unahitaji nini Mathew? 

“Kuna mwadada mmoja 

anaelekea Havana Cuba hivi sasa 

na anahitajika kuja Tanzania.Ninaomba msaada wa 

ndege ya kwenda kumchukua 

Havana na kumleta Tanzania” 

Ukimya wa sekunde kadhaa 

ukapita Peniela akauliza 

“Anaitwa nani? Ni mpenzi 

wako? 

“Anaitwa Camilla.Si mpenzi 

wangu bali ni mtu muhimu sana na 

maisha yake yako 

hatarini.Tafadhali nakuomba 

unisaidie Peniela huyu mtu aweze 

kufika salama Tanzania” akasema 

Mathew. 

“Sawa Mathew naomba unipe 

taarifa kamili za huyo mtu halafu 

nitajua nini cha kufanya” “Ahsante Peniela nitakupa 

taarifa zake baadae kidogo” 

akasema Mathew na kukata simu 

“Asingeweza kukataa.Pamoja 

na kutengena lakini Peniela bado 

ananipenda sana .Anyway sitakiwi 

kuyawaza hayo kwa sasa.Ngoja 

nijipumzishe kabla ya kwenda 

kuonana na rais usiku wa leo” 

akawaza Mathew na kujipumzisha 

kitandani 

*************** 

 Saa moja na dakika ishirini za 

jioni Mathew akiwa mbele ya kioo 

chake kikubwa akijitazama kwa 

mara ya mwisho kama 

amependeza vya kutosha.Ni kweli alikuwa amependeza vya 

kutosha.Usiku huu alikuwa 

amevaa suti nyeusi iliyomkaa 

vyema tayari kabisa kukutana na 

rais Dr Vivian.Alionekana kweli 

alikuwa bilionea kutokana na 

mavazi yale ya gharama kubwa 

aliyovaa. 

“Sasa niko tayari kuonana na 

mkuu wa nchi.Ikulu si mahala pa 

kwenda umevaa hovyo hovyo.Ile ni 

sehemu kubwa sana na ukienda 

pale kuonana na mkuu wa nchi 

unatakiwa uwe umejiandaa 

vilivyo” akawaza Mathew huku 

akimalizia kujipulizia uturi mzuri 

wa gharama kubwa halafu 

akaondoka kuelekea ikulu.Akiwa 

njiani aliwasiliana na Theresa kuhusiana na jukumu alilokuwa 

amemkabidhi la kuhakikisha 

Nathan anakuja Tanzania bila ya 

Dr Vivian kufahamu 

chochote.Theresa alimjulisha 

Mathew kwamba tayari 

amekwisha wasiliana na Nathan na 

kwa muda ule tayari alikwisha 

anza safari ya kuja Tanzania. 

“Theresa anafanya kazi nzuri 

sana lakini itakuaje endapo dada 

yake atafahamu kwamba yeye 

ndiye aliyemuita Nathan 

Tanzania?Utaibuka mgogoro kati 

yao lakini nitaumaliza.Lazima 

tumfahamu Nathan ana kitu gani 

anakichunguza kwa rais.Nina 

uhakika mkubwa kama Nathan ni 

CIA basi ukaribu wake na Dr Vivian ni kwa ajili ya jambo fulani.Usiku 

wa leo nitakapozungumza na rais 

kuna kitu ninaweza nikakipata 

kuhusiana na Nathan” akawaza 

Mathew 

Aliwasili ikulu saa mbili 

kasoro dakika tatu kwa kuwa 

alikuwa tayari na kibali cha 

kumuwezesha kupita kuonana na 

rais muda wowote hakupata shida 

akaruhusiwa kuingia ndani ya 

ikulu na kupokelewa kisha 

akapelekwa moja kwa moja 

sebuleni kwa Dr Vivian ambaye 

kwa muda huo alikuwa chumbani 

kwake naye akijiandaa.Baada ya 

dakika zipatazo kumi akatoka 

akiwa amependeza kwa gauni refu 

jeupe lenye nakshi za kung’aa. “Mathew karibu sana.Umefika 

kwa wakati” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais.Ninaheshimu sana muda na 

ndiyo maana nimefika kwa wakati 

ule tuilokubaliana” akasema 

Mathew 

“Umependeza sana usiku wa 

leo” akasema Dr Vivian huku 

akitabasamu 

“Hata wewe pia umependeza” 

akasema Mathew na bila kupoteza 

muda Dr Vivian akamkaribisha 

katika chumba cha chakula 

kulikokuwa kumeandaliwa 

chakuls kizuri kwa ajili yao 

“Vipi shughuli zako 

zinakwendaje? Namaanisha 

biashara zako” akaanzisha mazungumzo Dr Vivian wakati 

wakipata chakula 

“Shughuli zangu zinakwenda 

vizuri.Wapo watu wanaosimamia 

biashara zangu kwa hiyo hata 

kama ninakuwa na majukumu 

mengine sina wasiwasi” 

“Unashughulika na biashara 

gani? 

“Kwa sasa ninajenga kiwanda 

cha kuchonga vipuri vya magari na 

mashine mbali mbali.Kitakuwa ni 

kiwanda kikubwa hapa nchini” 

“Oh ! Nimesikia kuhusiana na 

kiwanda hicho.Kumbe ni cha 

kwako!Hongera sana Mathew kwa 

uwekezaji huu mkubwa 

ulioufanya.Uko peke yako au una 

ubia na mtu? “Hiki ni kiwanda changu na 

ninakimiliki kwa asilimia mia 

moja .Sina ubia na mtu yeyote” 

akasema Mathew. 

“Hongera sana .Umefanya 

jambo la muhimu kuamua kuleta 

uwekezaji huu mkubwa hapa 

nyumbani kwani naamini 

ungeweza kuupeleka sehemu 

yoyote lakini ukaamua kurejea 

nyumbani.Serikali yagu 

inawahitaji sana wawekezaji 

wazalendo kama ninyi na itafanya 

kila iwezalo kuhakikisha 

inawetengenezea mazingira 

mazuri ya uwekezaji na unafuu wa 

kufanya biashara”akasema Dr 

Vivian “Nilipoachana na Peniela 

nilitafakari sana kitu cha 

kufanya.Nilitamani sana kufanya 

uwekezaji hapa 

nyumbani.Niliwatafuta washauri 

wa kibiashara na wakanishauri 

kuwekeza katika kiwanda cha 

kuchonga vipuri vya magari na 

mashine.Kwa hivi sasa hatuna 

kiwanda cha kuchonga vipuri 

mbalimbali vya magari na mashine 

hivyo nikaamua kuwekeza 

huko.Hata hivyo bado ninafanya 

utafiti wa kuwekeza pia katika 

kiwanda cha sukari ili kuongeza 

upatikanaji wa sukari hapa 

nchini.Nimewapa jukumu hilo 

wataalamu wangu na wanalifanyia 

kazi wakikamlisha utafiti wao basi nitaweza kuanza kujenga kiwanda 

cha sukari pia” 

“Unanifurahisha sana Mathew 

kwa namna ulivyo na mtazamo wa 

mbali.Nchi yetu kwa sasa bado ina 

uhitaji mkubwa wa sukari.Bado 

hatujaweza kujitosheleza kwa 

sukari yetu inayozalishwa ndani 

kwa hiyo tunalazimika kuagiza 

kiasi cha sukari kutoka nje ya nchi 

ili kuweza kukidhi 

mahitaji.Endapo tutakuwa na kiasi 

cha kutosha cha sukari basi pesa 

tunazotumia kuagizia sukari nje ya 

nchi tutazitumia kwa shughuli 

nyingine.Nakuhakikishia 

ushirikiano mkubwa sana katika 

uwekezaji huo wako.Nitakupa 

upendeleo mkubwa ili viwanda vyako viweze kukua na kuzalisha 

ajira nyingi” akasema Dr Vivian 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais” akasema Mathew 

“Mimi ndiye ninayepaswa 

kukushukuru wewe kwani licha ya 

kuwa na shughuli nyingi za 

uwekezaji lakini umeamua kuacha 

shughuli zote na kuja kunifanyia 

kazi yangu.Ninapaswa 

kukushukuru mno.” 

“Usijali mheshimiwa rais.Hii 

kazi imekwisha ingia katika 

damu,ni kama daktari hata kama 

amestaafu lakini bado haachi 

kutibu watu.Japokuwa siko tena 

katika shughuli hizo lakini 

nilishindwa kusema hapana baada ya kuliona tatizo ulilonalo na 

linanihitaji mno mimi” 

“Ahsante.Ungeweza kusema 

hapana lakini ulikubali kwa moyo 

mmoja.By the way kuna 

maendeleo yoyote hadi hivi sasa? 

Akauliza Dr Vivian 

“Maendeleo yapo japokuwa 

nisingepeda kusema chochote kwa 

sasa kwani ni mapema mno ila 

mwanga upo na baada ya siku si 

nyingi nitakuja na kukueleza kila 

kitu.Kwa sasa naomba unipe muda 

niendelee kulichunguza hili 

jambo” 

“Hakuna tatizo katika hilo 

Mathew utanieleza pale 

utakapoona inafaa mimi kujua lakini kwa mtazamo wako unaona 

kuna dalili za kufanikiwa? 

“Dalili zipo kwani hatua 

tuliyopiga mpaka sasa ni nzuri na 

kuna mwanga mdogo umejitokeza 

ambao tukiufuata unaweza 

ukatufikisha mahala pazuri japo 

suala hili ni gumu mno na ndiyo 

maana mpaka sasa majibu yake 

hayajapatikana na limebaki kuitwa 

fumbo gumu.Pamoja na ugumu 

wake lakini nakuhakikishia 

mheshimiwa rais kwamba 

nitafanya kila niwezalo 

kuhakikisha kwamba ninaupata 

mzizi wake na kuwapata 

waliomuua Kanali Sebastian” 

Dr Vivian akamtazama 

Mathew kwa muda na kusema “Ninajivunia kuongoza taifa 

lenye watu kama wewe 

Mathew.Kwa sasa nchi yetu 

inapitia changamoto nyingi na 

watanzania hasa vijana 

wanapaswa kuwa na uzalendo 

mkubwa kwa nchi yao.Tanzania 

inahitaji mshikamano mkubwa 

kuliko wakati mwingine 

wowote.Nadhani umekwisha sikia 

mambo yanayoendelea kati yetu 

na mataifa makubwa tajiri 

yakiongozwa na Marekani” 

“Nimesikia mheshimiwa rais” 

“Kwa hiyo mambo 

hayatakuwa rahisi na tunapaswa 

watanzania kuwa kitu 

kimoja.Tunapaswa kuimarisha 

uwekezaji wa ndani,kuimarisha biashara ya ndani na baina ya nchi 

zetu za Afrika ,tunapaswa 

kuyatumia vyema mahusiano yetu 

ya kikanda kwa kufanya 

biashara.Kwa ujumla tunayo safari 

ndefu kuelekea kujitegemea kama 

nchi.Tunapaswa kuachana na 

misaada ya wafadhili ambayo 

inatufanya tuwe watumwa na 

kufuata kila sharti 

wanalotupa.Nimedhamiria 

kuiondoa Tanzania katika 

utegemezi na hilo litafanikiwa 

endapo watanzania wote 

tutaungana na kuwa kitu 

kimoja.Ndiyo maana nakupongeza 

sana Mathew kwa kuamua kuja 

kuwekeza nyumbani.Tunahitaji 

wafanya biashara wazawa kama wewe.Tunahitaji kujitosheleza 

kwa bidhaa ndani ya nchi na kuuza 

nje.” 

“Mheshimiwa rais hii ni vita 

kubwa tuko nayo kwa sasa lakini 

nakuhakikishia kwamba vita hii 

tutashinda.Watanzania pia 

wamechoka kuwa tegemezi wa 

mataifa makubwa na wanataka 

kujitegemea.Haitakuwa rahisi 

lakini tutashinda.Tuko pamoja” 

“Ahsante Mathew kwa 

maneno hayo mazuri ya kutia 

moyo.Wengi wameungana 

nami,hata maraisi wa nchi nyingi 

wamenipigia simu na kunitaka 

nisilegeze msimamo wangu 

niendelee kupambana na kuitoa 

Tanzania katika utegemezi.Mungu ametupa rasilimali nyingi hivyo 

tunapaswa kufaidika kwa uwepo 

wa rasilimali hizo katika nchi 

yetu.Kesho kwa kupitia wazee wa 

Dar es salaam nitalihutubia taifa 

na kuweka wazi kwa watanzania 

hali tutakayopitia na kuwataka 

kuungana katika mapambano haya 

makubwa ya kiuchumi.Bila 

kuchukua maamuzi magumu nchi 

hii itabaki katika umasikini na 

kutegemea ufadhili.” Akasema Dr 

Vivian.Walimaliza kula chakula 

wakaenda kukaa sehemu maalum 

kwa ajili ya maongezi. 

“Mathew ahsante sana kwa 

kuungana nami kwa chakula usiku 

huu.Sasa ni wakati wa maongezi 

kuhusiana na kile ambacho ulisema unataka 

tuzungumze.Karibu” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais kwa chakula kizuri na kutenga 

pia muda kwa ajili ya 

mazungumzo.Kikubwa 

kilichonileta hapa kwako ni kutaka 

kukufahamu wewe” 

“Me?! Dr Vivian akaonyesha 

kustuka kidogo 

“Ndiyo mheshimiwa 

rais.Nahitaji kukufahamu vyema” 

Dr Vivian akacheka kidogo na 

kusema 

“Kwa nini unataka 

kunifahamu Mathew? 

“Ninafanya kazi yako kubwa 

na ya hatari kwa hiyo nahitaji 

kukufahamu vizuri” “Ukinifahamu mimi 

kutakusaidia nini katika kazi 

yako? Una wasi wasi na mimi? 

“Mheshimwa rais sina wasi 

wasi wowote nawe lakini 

ninahitaji tu kukufahamu vizuri na 

hata wewe pia endapo ukihitaji 

kufahamu chochote kuhusu mimi 

niko tayari kukueleza chochote” 

akasema Mathew.Dr Vivian 

akamtazama Mathew kwa muda na 

kusema 

“Mathew nashindwa niseme 

nini,hata hivyo ni kitu gani hasa 

unachohitaji kukifahamu toka 

kwangu? 

“Nataka kufahamu maisha 

yako kwa ujumla na zaidi sana 

tujikite katika maisha yako ya kimahusiano” akasema Mathew na 

Dr Vivian akacheka 

“Unataka kufahamu maisha 

yangu ya kimapenzi? Akauliza na 

kucheka tena 

“Ndiyo mheshimiwa rais” 

“Mathew wewe ni mtu wa 

kwanza kutaka kufahamu kuhusu 

maisha yangu ya kimapenzi.Hata 

hivyo kwa kuwa nilikuahidi 

kwamba nitakuwa tayari kukupa 

msaada wa kila aina basi sina budi 

kukueleza lakini kabla sijakueleza 

chochote nataka kufahamu,hii ina 

mahusiano yoyote na hili 

unalolichunguza? 

“Hapana mheshimiwa rais 

halina mahusiano yoyote.Hii ni 

kwa ajili yangu binafsi” akasema Mathew na Dr Vivian akatoa tena 

kicheko.Alionekana kufurahishwa 

na jambo lile 

“Sijui nikueleze nini Mathew 

kuhusu maisha yangu ya 

kimahusiano unayotaka 

kuyajua.Kwa ujumla naweza 

kusema kwamba sina bahati 

katika upande huo kwa hiyo sina 

maelezo marefu” akasema Dr 

Vivian na kunyamaza kidogo 

halafu akaendelea 

“Labda nikuanzie mbali 

kidogo.Toka nikiwa mdogo 

nilitamani sana kuwa 

mtawa.Sikutaka kuwa na 

mahusano ya 

kimapenzi.Niliyapenda maisha 

yale ya upweke na kumtumikia Mungu.Nilipomaliza shule ya 

msingi nilijiunga na shule ya 

sekondari ya masista kwa lengo la 

kutaka kuitimiza ndoto yangu ya 

kujifunza maisha ya kitawa.Kila 

mtu alitegemea kwamba siku moja 

ningekuwa mtawa lakini mara tu 

baada ya kumaliza kidato cha sita 

nikapata mtazamo mpya.Nikataka 

kuwa daktari wa 

binadamu.Nilitaka sana kutibu 

watoto hivyo nikajikuta ndoto 

yangu ikibadilika na sikuendelea 

tena na maisha yale ya utawa 

badala yake nikaendelea na 

masomo ya udaktari.Mpaka 

wakati huo sikuwa nimewahi 

kukutana na mwanaume yeyote au 

kuwa katika mahusiano yoyote ya kimapenzi.Nilipokuwa chuo kikuu 

nchini Marekani ndipo 

nilipokutana na Nathan.” 

“Nathan ni nani? Mathew 

akauliza kama vile 

hafahamuchochote kuhusu Nathan 

“Huyu ni mpenzi 

wangu.Alikuwa mpenzi wangu” 

“Alikuwa mpenzi wako?Hauko 

naye tena? 

“Tumekwisha achana.Hatuko 

tena katika mahusiano.” 

“Unaweza kunieleza namna 

ulivyokutana na Nathan? Mathew 

akauliza na bila kupepesa macho 

Dr Vivian akajibu 

“Nilipewa nafasi ya kutoa 

hotuba kwa niaba ya wanafunzi 

wenzagu katika sherehe za kuwakaribisha chuoni wanafunzi 

wapya.Ilikuwa ni hotuba nzuri na 

niliitoa kwa kujiamini sana na 

baada ya kutoa hotuba ile 

nilipongezwa na watu mbali 

.Mmoja wa watu waliokuja 

kunipongeza alikuwa ni 

Nathan.Alijitambulisha kwangu 

kwamba ni mwanafunzi wa mwaka 

wa pili pale chuoni lakini yeye 

alikuwa anasomea mambo ya 

mawasiliano.Alikuwa ni kijana 

mzuri sana.Alikuwa na nywele 

nzuri zenye kung’aa,ngozi laini 

,macho mazuri,sauti nzuri na 

alionekana kuwa ni kijana 

mwerevu na mnyenyekevu 

sana.Sifahamu nini kilinitokea 

lakini nikajikuta nikimpenda Nathan toka nilipomuona.Kwa 

mujibu wa maelezo yake aliyonipa 

baadae baada ya kuwa wapenzi ni 

kwamba hata yeye pia alikuwa 

amenipenda toka siku ya kwanza 

nilipoingia chuoni.Urafiki ukaanza 

kati yetu na alinisaidia sana 

kuyazoea maisha ya pale chuoni na 

akanisaidia pia kuifahamu nchi ya 

marekani.Nathan alikuwa anatoka 

katika familia yenye kujiweza 

kifedha,kaka zake wawili 

walikuwa ni mchezaji wakubwa na 

maarufu wa mpira wa kikapu na 

walikuwa na utajiri mkubwa hivyo 

waliiwezesha familia yao kiuchumi 

kwa kuwafungulia miradi mbali 

mbali.Kwa mara ya kwanza katika 

maisha yangu nilijikuta nikizama na kuyafurahia mapenzi.Nathan 

alinisaidia sana na nilitokea 

kumpenda mno.Hata alipomaliza 

chuo na mimi kuendelea na 

masomo katika vyuo vikuu mbali 

mbali vya nchi nyingine bado 

ukaribu wangu na Nathan ulikuwa 

mkubwa sana.Alikuwa na uwezo 

wa kuja walau mara moja au mbili 

kila mwezi kuja kuniona 

chuoni.Nilijiona mwanamke 

mwenye bahati sana na hata 

wanafunzi wenzangu walinionea 

wivu kwa kuwa na mwanaume 

anayenijali kama Nathan.” 

Akanyamaza kidogo na baada ya 

sekunde kadhaa akaendelea 

“Hayo yalikuwa ni mahusiano 

yangu ya kwanza kabisaTanzania

alikuwa ni mwanaume wangu wa 

kwanza kuingia naye mapenzini na 

alinifanya nijione ni mwanamke 

bora kabisa duniani.Nilipomaliza 

masomo yangu ya udaktari 

alinisaidia nikapata kazi katika 

hospitali moja kubwa nchini jijini 

Washington DC ambako nilifanya 

kazi hadi pale walipofariki wazazi 

wangu ndipo nilipoamua kurejea 

nyumbani na aliyenishauri kurejea 

nyumbani ni Nathan.Nilianza kazi 

katika hospitali ya taifa ya 

Muhimbili na baadae nikaanza 

kujiingiza katika siasa na kisha 

nikagongea urais na nikashinda na 

kuwa rais wa kwanza mwanamke 

kuiongoza jamhuri ya muungano 

wa Tanzania



Nilianza kazi 

katika hospitali ya taifa ya 

Muhimbili na baadae nikaanza 

kujiingiza katika siasa na kisha 

nikagongea urais na nikashinda na 

kuwa rais wa kwanza mwanamke 

kuiongoza jamhuri ya muungano 

wa Tanzania.Tulikwisha anza maandalizi ya harusi yetu lakini 

kuna mambo yametuingilia hapa 

kati na kutulazimu kuweka nukta 

katika mapenzi yetu.Ninaomba 

usiniulize kuhusu kitu 

kilichosababisha mimi na Nathan 

tukakorofishana na kuhitimisha 

safari yetu ndefu” akasema Dr 

Vivian na kucheka kidogo 

“Nashukuru sana mheshimiwa 

rais kwa maelezo hayo lakini bado 

utaendelea kunivumilia kwa 

maswali yangu.Nataka kufahamu 

mchango wa Nathan katika 

masuala yako ya kisiasa.Alikuwa 

na mchango wowote? 

“Nathan alikuwa na mchango 

mkubwa sana katika harakati 

zangu za kisiasa.Kuna nyakati nilitaka kukata tamaa baada ya 

kukumbana na vikwazo kadhaa 

kwanza kwa uchanga wangu katika 

siasa na pili kwa kuwa ni 

mwanamke lakini Nathan alinipa 

moyo sana na kunifanya nisikate 

tamaa nikaendelea na harakati 

zangu hadi nikawa rais.Ni mtu 

mwenye mchango mkubwa sana 

katika harakati zangu za 

kisiasa.Aliniunga mkono katika 

kampeni zangu na kuzunguka 

nami nchi nzima na mara nyingine 

alidiriki kusimama jukwaani 

akaninadi na kuwafurahisha sana 

watu kwa kiswahili chake cha 

kuunga unga.Nadhani nimejibu 

swali lako.Nathan ana mchango mkubwa sana katika maisha yangu 

ya kisiasa” 

“Kwa sasa Nathan anafanya 

kazi gani? 

“Ni mhandisi katika kampuni 

moja inaitwa A.D electronics iko 

Marekani lakini inafanya kazi 

katika nchi mbali mbali.Nathan si 

mtu wa kutulia sehemu moja 

amekuwa anasafiri safiri kwenda 

nchi mbali mbali kufanya kazi za 

kampuni yake” akasema Dr Vivian 

“Mtu kama huyu mwenye 

mchango mkubwa katika maisha 

yako lazima kuna sababu kubwa 

sana iliyosababisha mkatengana 

hasa katika wakati huu ambao 

mlikaribia sana kuitimiza ndoto 

yenu ya kufunga ndoa.Nimesikia kwamba ilibaki miezi mwili pekee 

mfunge ndoa.What real happened? 

“Mathew hili jambo linaumiza 

sana si kwangu tu bali kwa kila 

mtu aliye karibu yangu.Kila mtu 

alikuwa na mategemeo makubwa 

sana kwamba ndoto yangu ya 

muda mrefu ya kuolewa na Nathan 

itatimia ndani ya muda wa miezi 

miwili toka sasa lakini ndoto hiyo 

imetoweka.Hakuna tena ndoa kati 

yetu.Hii inaniumiza sana hata 

mimi lakini sina namna nyingine 

ya kufanya na ndiyo maana 

nikasema awali kwamba sina 

bahati katika mapenzi kwani ndoa 

yangu imeota mbawa katika hatua 

za mwisho.Maandalizi yote ya 

harusi yangu yamekwisha kamilika lakini inasikitisha 

kwamba hakutakuwa na ndoa 

tena.Kuna nyakati ninafikiria 

yawezekana labda nilifanya kosa 

kuamua kuachana na maisha ya 

utawa na ndiyo maana maisha 

yangu ya kimapenzi hayana 

mafanikio” 

“Hapana Dr Vivian usiwaze 

hivyo.Kuhitilafiana katika 

mahusiano ni kitu cha kawaida na 

mapenzi kuvunjika si mkosi.Ni 

mambo ambayo lazima 

tukubaliane nayo kwamba yapo na 

yanaweza kutoka katika uhusiano 

wowote ule.Nitazame 

mimi.Nilikuwa na mwanamke 

ninayempenda sana ambaye 

niliyatoa maisha yagu kwa ajili yake lakini tumekuja 

kukorofishana na kila mmoja sasa 

ana maisha yake.Iliniumiza kwa 

sababu nilikuwa nampenda mno 

Peniela lakini sasa tayari nimezoea 

na maisha 

yanaendelea.Nilichojifunza katika 

mahusiano ni kwamba kama 

unaona hauna furaha katika 

uhusiano wako,huna haja ya 

kuendelea kulazimisha na kuutesa 

moyo muache aende.Nenda 

katafute furaha yako ya maisha 

sehemu nyingine.Kwa hiyo Dr 

Vivian usijilaumu sana kwa 

maamuzi uliyoyafanya.Baada ya 

muda utazoea na maisha 

yataendelea.Some day you’ll be 

happy again” “Me ! happy? Akauliza Dr 

Vivian huku akicheka kidogo 

“Ndiyo Dr Vivian.Usikate 

tamaa siku moja naamini 

utampata mtu atakayeikamilisha 

furaha yako” 

“Sina hakika kama hilo 

litatokea.Hakuna mwanaume 

ambaye anaweza kutaka kuwa na 

mwanamke kama mimi.Kwa sasa 

sitaki kuelekeza macho yangu 

huko bali nataka niielekeze akili 

yangu katika kuwatumikia 

watanzania.Furaha yangu ni 

kuwatumikia waoa.Ninapopita na 

kuona nyuso zao zikiwa na furaha 

hiyo ndiyo furaha yangu.Mapenzi 

yangu yako kwao kwa hiyo sina 

muda wa kupoteza kwa ajili ya kumuhudumia mwanaume 

mmoja.Nina watu zaidi ya milioni 

hamsini ninaowaongoza na siwezi 

kupata muda wa kumuhudumia 

mpenzi” akasema Dr Vivian 

“Hiyo ndiyo sababu uliamua 

kuachana na Nathan? 

“Sipendi kuzungumzia hilo 

Mathew lakini hiyo ni moja wapo 

ya sababu.Nataka nitumie muda 

wangu mwingi kuwahudumia 

watanzania.By the way how’s 

Peniela? Akauliza Dr Vivian 

“Peniela anaendelea 

vizuri.Tunawasiliana bado na tuna 

mtoto anaitwa Anna 

Maria.Tuliamua kwa hiari yetu 

kuachana na kila mmoja 

akaendelee na maisha yake kwa hiyo hatuna ugomvi,bado 

tunaendelea kushirikiana katika 

mambo mbali mbali na bado ni 

marafiki wazuri pia.Tayari ana 

mume mpya na ninaliheshimu 

hilo” 

“Vipi kuhusu wewe una 

mipango gani? Umeoa au 

unatazamia kuoa mwanamke 

mwingine?Dr Vivian akauliza 

“ Kwa sasa sina mategemeo 

hayo ya kuoa au kutafuta 

mwanamke mwingine.Nimekuwa 

muoga kidogo baada ya mahusiano 

yangu na Peniela kuishia njiani” 

akasema Mathew na kucheka 

kidogo 

“Unaweza ukaniambia nini 

kilisababisha mkatengana? Au na wewe hauki tayari kuliongelea hilo 

kama mimi? Akauliza Dr Vivian na 

wote wakacheka 

“Mimi huwa sifichi 

kitu.Tulitengana kwa sababu ya 

Peniela.Alianzisha mahusiano na 

bilionea mmoja ambaye anamiliki 

kiwanda cha magari.Sikutaka 

kumkwaza kwani walionekana 

kuzama mapenzini sana na hivyo 

nikaamua tuachane ili aendee na 

huyo mpenzi wake lakini 

tuliachana kwa wema tu,hatuna 

tatizo lolote tunaendelea 

vizuri”Akasema Mathew na 

kikapita kimya kifupi.Dr Vivian 

akasema 

“Nadhani kwa upande huo wa 

maisha ya kimahusiano tumemaliza.Kitu gani kingine 

ambacho ungependa kukifahamu 

kuhusu mimi? 

“Bado kuna kitu kimoja 

ambacho ningetaka kukifahamu.Je 

akija Nathan leo na kukuomba 

msamaha hata kama si yeye 

aliyekosa utakuwa tayari 

kumsamehe na kurejesha mapenzi 

yenu? 

“Mathew nadhani bado 

hujanifahamu vizuri.Mimi ni 

mmoja wa wale watu ambao 

hawana ndimi mbili.Nikisema 

hapana ni hapana.Huwa sibadilishi 

kauli.Nimeamua kuachana na 

Nathan kwa hiyo hakuna tena 

tegemeo la mimi na yeye 

kurudiana.Nimekwisha weka nukta” akasema Dr Vivian na 

ukimya mfupi ukapita 

“Mheshimiwa rais nadhani 

tumeongea vya 

kutosha.Ninashukuru sana kwa 

kunipa nafasi hii ya kuzungumza 

na kukubali kuzungumzia masuala 

yako binafsi tena kwa uhuru 

mkubwa bila kuficha.This means a 

lot to me” akasema Mathew 

“Usijali Mathew.Ahadi ni deni 

na nilikuahidi kwamba chochote 

utakachokitaka utakipata lakini 

nataka kujua,haya tuliyoyaongea 

leo yanakusaidia nini? Yana 

muingiliano wowote na kazi 

unayoifanya? Akauliza Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais nilihitaji tu 

kukufahamu wewe ni mtu wa aina gani na ukitaka kumfahamu mtu 

vizuri basi yafahamu maisha yake 

ya kimahusiano.Baada ya 

mazungumzo haya nimekufahamu 

wewe ni mtu wa aina gani.Hii 

inanisaidia sana katika kazi zangu 

kwa kujua ninafanya kazi na mtu 

wa aina gani” 

Dr Vivian akatabasamu na 

kusema 

“Umenifahamu mimi ni mtu 

wa aina gani? Can you be honnest 

with me? 

“Kwanza nimefahamu wewe ni 

rais wa watu.Hauna ubinafsi na 

maamuzi yote unayoyafanya ni 

kwa ajili ya watu.Unaipenda 

Tanzania kiasi ambacho 

hakielezeki na ndiyo maana umekuwa unafanya maamuzi 

magumu hata katika maisha yako 

binafsi kwa ajili ya kuwatumikia 

watanzania.Mwisho kabisa 

nimefahamu wewe ni rais ambaye 

hauyumbi na haukubali 

kuyumbishwa.Nitafanya kazi 

yangu uliyonipoa kwa kuzingatia 

hayo niliyoyafahamu” akasema 

Mathew 

“Ahsante kwa kuyafahamu 

hayo.Ninashukuru sana kwa kuja 

kunitembelea na unakaribishwa 

muda wowote hapa ikulu na 

nitakuwa tayari kutenga muda 

kwa ajili ya kukusikiliza na kujua 

maendelo yako.Nitapenda sana 

kukaa nawe na kubadilishana 

mawazo si katika kazi hiiniliyokupa bali hata katika 

masuala mengine ya nchi,biashara 

n.k.” akasema Dr Vivian na 

kusimama 

“Nashukuru sana mheshimiwa 

rais kwa heshima hii 

kubwa.Nitakapohitaji tena 

kukuona sitasita kufanya 

hivyo.Naomba sasa nikuache 

upumzike na mimi nikaendelee na 

mambo mengine.Kabla sijaondoka 

kuna jambo nilikuwa 

nimesahau.Kuna mtu mmoja 

anatoka Cuba lakini ni raia wa 

marekani anaitwa Camilla Snow 

anakuja hapa Tanzania.Huyu 

nitakuwa nashirikiana naye katika 

uchunguzi wangu.Huyu ni rafiki 

yangu sana na amewahi kufanya kazi FBI lakini kwa sasa 

amekwisha acha na anafanya 

shughuli zake 

binafsi.Nimemuomba aje anisaidie 

katika uchunguzi wa jambo hili na 

amekubali hivyo ninakuomba 

unisaidie ili aweze kuingia hapa 

nchini bila matatizo na aweze 

kupata kibali cha kuishi hapa 

nchini” akasema Mathew 

“Hakuna tatizo kuhusu hilo 

Mathew.Nitatoa maelekezo kwa 

watu wangu walifanyie kazi hilo na 

ataruhusiwa kuingia na kuishi 

hapa nchini kwa muda 

atakaohitaji.Nilikuahidi chochote 

utakachokihitaji utakipata kwa 

hiyo usiwe na hofu yoyote 

kuhusiana na hilo jambo.Camilla snow ataingia nchini bila 

matatizo.Utanitaarifu ni lini 

atakuja nchini” 

“Nashukuru sana mheshimiwa 

rais kwa msaada huo 

mkubwa.Nitawasiliana nawe na 

kukupa taarifa zote kwa kina” 

akasema Mathew na rais 

akamsindikiza hadi katika gari 

lake akaondoka kuelekea nyumani 

kwake. 

Mara tu Mathew alipoondoka 

Dr Vivian akachukua simu na 

kumpigia Theresa. 

“Hallo Theresa,umekwisha 

lala? 

“Hapana bado ila ninajiandaa 

kulala” “Nimekupigia kukujulisha 

kwamba Mathew ametoka hapa 

muda si mefu.Nimekuwa naye kwa 

chakula cha usiku na baada ya 

hapo tukawa na maongezi kidogo” 

“Amekuja kukueleza mahala 

alikofikia katika uchunguzi wake? 

“Hapana Theresa alikuja kwa 

dhumuni lingine kabisa.Alitaka 

kufahamu kuhusu mahusiano 

yangu na Nathan.Amenidadisi 

mambo mengi kuhusu mimi na 

Nathan” 

“Umemueleza kila kitu? 

“Imenilazimu kumueleza kila 

kitu isipokuwa sababu ya mimi na 

Nathan kutengana.Nimeshindwa 

kuelewa sababu ya Mathew kutaka 

kufahamu masuala yangu binafsi ya kimahusiano.Hebu nieleze kuna 

chochote katika uchungzi wake 

ambacho kimemfanya atake 

kunifahamu mimi na maisha yangu 

ya ndani? 

“Hakuna dada.Niko naye 

muda wote na kila kitu tunafanya 

pamoja na hakuna chochote 

kinachohusiana nawe na wala 

hajaniambia kama anataka kuja 

kuonana nawe.Yawezekana labda 

anatafuta nafasi” akasema Theresa 

na kucheka kidogo 

“Theresa huu si wakati wa 

utani.Mathew hakuonekana kama 

ni mtu anayetafuta nafasi.Ni wazi 

alikuwa na sababu maalum ya 

kutaka kufahamu kuhusu 

mahusiano yangu na Nathan.Nakuomba jaribu 

kumchunguza ufahamu nia na 

dhumuni la kutaka kunifahamu 

kiundani na kuyafahamu 

mahusiano yangu.Fanya kila 

uwezalo kulifahamu hilo kwani 

amenipa wasiwasi kidogo” 

akasema Dr Vivian. 

“Usijali dada niachie hilo 

jukumu na nitalifanikisha ila 

nikutoe wasiwasi Mathew si mtu 

mbaya na hata kama alitaka 

kukufahamu basi ni kwa lengo 

zuri.Kama kungekuwa na tatizo 

lolote basi angekwisha 

nifahamisha kwani kila kitu 

anachokifanya huwa 

ananishirikisha” “Sawa Theresa lifanyie kazi 

hilo nataka kufahamu.Halafu kitu 

kingine kesho nazungumza na 

wazee wa Dar es salaam kama 

utapata nafasi ningependa 

uniandalie hotuba lakini kama 

hautaweza basi usijali nitaanda 

mwenyewe” akasema Dr Vivian na 

kuagana na Theresa. 

Mara tu alipokata simu 

Theresa akampigia Mathew 

“Hallow Theresa habari za 

usiku huu? 

“Habari nzuri Mathew.Uko 

wapi? 

“Niko njiani naelekea 

nyumbani nimetoka ikulu kuonana 

na rais” “Amenipigia simu muda mfupi 

uliopita kuhusiana na 

mazungumzo yenu ana wasi wasi 

sana kama yale mliyozungumza 

yana mahusiano yoyote na 

uchunguzi unaoendelea kuufanya 

lakini nimemtoa wasi wasi 

kwamba asihofu hakuna kitu kama 

hicho” 

“Good.Nimezungumza naye 

nilitaka kufahamu kuhusu yeye na 

Nathan.Nashukuru amekuwa 

muwazi kwangu na hajanificha 

kitu japokuwa sababu ya 

kutengana kwao hajanieleza” 

akasema Mathew 

“Kuna chochote ambacho 

umefanikiwa kukipata kuhusu 

Nathan katika mazungumzo hayo? “Kuna vitu kadhaa nimevipata 

ninakwenda kuvifanyia kazi halafu 

nitakuja kukujulisha kesho.Vipi 

kuhusu Nathan unawasiliana naye? 

“Ndiyo kama nilivyokueleza 

awali kwamba tayari amekwisha 

anza safari.Anakuja na ndege 

binafsi ya kaka yake na kesho mida 

ya saa nne au saa tano hivi 

atawasili.Nitakujulisha kila kitu” 

“Ahsante sana Theresa kwa 

msaada huo ila kumbuka kwamba 

jambo hili ni siri yangu na wewe.Dr 

Vivian hapaswi kufahamu 

chochote kuhusiana na jambo hili” 

akasema Mathew 

“Nalizingatia hilo Mathew na 

hata Nathan nimemueleza hivyo 

kwamba Dr Vivian hapaswi kufahamu chochote kuhusiana na 

safari yake ya kuja Tanzania” 

“Good.Uwe na usiku mwema 

Theresa tutaonana kesho” 

“Ahsante.Usiku mwema nawe 

Mathew” akajibu Theresa na 

kukata simu. 

“Mambo yanakwenda 

vizuri.Nina uhakika tukimfuatilia 

Nathan kuna mwanga utapatikana” 

akawaza Mathew na hakuelekea 

nyumbani kwake bali akaenda 

moja kwa moja nyumbani kwa 

Meshack Jumbo 

“Karibu Mathew” Meshack 

Jumbo akamkaribisha Mathew 

nyumbani kwake 

“Ahsante mzee.Natumai 

utanichoka kwa ujio wangu wa usiku” akasema Mathew na wote 

wakacheka 

“Usijali kijana.Haya niambie 

kwa mvao huo lazima umetoka 

ikulu” akasema Meshack Jumbo na 

wote wakacheka 

“Hujakosea mzee.Nimetoka 

kuonana na mkuu wa 

nchi.Tumepata chakula cha usiku 

pamoja halafu tukawa na 

maongezi kidogo.Nilitaka 

kufahamu kuhusiana na 

mahusiano yake na Nathan.” 

Meshack Jumbo akakaa vizuri 

na kusema 

“Kabla hatujaendelea 

nimepokea simu toka kwa Jimmy 

akinipa taarifa za Camilla.Tayari 

amekwisha wasili Havana Cuba na anasubiri maelekezo yetu.Sikutaka 

kukutaarifu kwani nilijua utakuwa 

ikulu kama ulivyokuwa 

umenitaarifu” akasema mzee 

Meshack na kumpatia Mathew 

maelezo yote aliyopewa na Jimmy 

kuhusu Camilla.Mathew akampigia 

simu Peniela na kumpa maelekezo 

hayo kuhusiana na Camilla halafu 

akaendelea na maongezi na 

Meshack 

“Tayari nimekwisha muachia 

jukumu lote Peniela na 

atalishughulikia.Tuendelee na 

maongezi yetu.Nimekuwa na 

mazungumzo na rais kuhusiana na 

maisha yake binafsi ya mahusiano 

na ninashukuru kwamba rais 

amenipa ushirikiano mkubwa amenieleza mambo mengi binafsi 

bila kunificha.Katika mazungumzo 

yetu kuna mambo 

nimeyagundua.Nathan amekuwa 

na mahusiano na Dr Vivian toka 

wakiwa chuoni .Wamesoma chuo 

kimoja na urafiki wao ulianzia 

huko.Ninajiuliza swali je wakati 

wanasoma Nathan tayari alikuwa 

amejiunga na CIA? Na kama ndiyo 

kuna kitu alikuwa anakichunguza 

kwa Dr Vivian au alitokea tu 

kumpenda? Inawezekana labda 

Nathan akawa ni CIA lakini akawa 

hana jambo lolote baya na Dr 

Vivian bali ana mapenzi ya kweli 

kwake lakini lazima tujiridhishe 

kwa hilo kwa kufanya 

uchunguzi”akasema Mathew “Hilo linawezekana Mathew 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog