Search This Blog

Friday 7 April 2023

I WAS WRONG | NILIKOSEA - 2

  


Simulizi : I Was Wrong | Nilikosea 

Sehemu Ya Pili (2)


niliyekuwa nafanya kazi kwake” 

 Pendo akashika kichwa baada ya jibu lile.  “Lucy !! Pendo akauliza kwa mshangao 

mkubwa. 

 “Lucy una akili zote wewe? Unaweza kweli 

ukakubali kupewa mimba na yule 

mwanafunzi? Atakupa nini yule mtoto 

ambaye hata kiatu cha mguuni 

anategemea wazazi wake? Kumbe ulikuja 

hapa kwangu ukiwa na mimba na 

usiniambie? Siamini Lucy kama unaweza 

ukafanya jambo la kijinga namna 

hiyo.Wapo watu wa maana wanakutaka 

kila siku na unawakataa kumbe tayari una 

mimba.” Pendo akasema kwa ukali 

 “dada Pendo hata mimi mwenyewe 

sikujua kama nina mimba.Jackson 

nilifanya naye mapenzi siku moja tu na 

mama yake akatukuta ndiyo akanifukuza.” 

Lucy akajitetea 

 “Hata kama ingekuwa ni kila siku huwezi 

kukubali mtoto kama yule akakuchezea na 

kukupa ujauzito.Sasa nisikilize Kesho 

mimi na wewe mguu na njia hadi kwa 

huyo kidume aliyekupa mimba.Nataka 

afahamu kwamba mzigo huu ni wake kwa 

hiyo awe tayari kubeba majukumu “ 

 “dada Pendo samahani.naomba 

usinipeleke kabisa kule kwa akina Jack.”  “kama hutaki kwenda basi suluhisho ni 

kwenda kuitoa hiyo mimba kesho” Pendo 

akasema.Alikuwa amefura kwa hasira 

 “Mimi sintaweza kukulea wewe na 

mwanao wakati baba wa mtoto yupo na 

wazazi wake wana uwezo” 

 “Dada Pendo nafahamu kwamba 

kutokana na hali yangu sintaweza tena 

kuendelea kuishi hapa kwako.Sitaki kuwa 

kero kwako wala kukupa mzigo wa aina 

yoyote.Ninakuomba unipatie zile fedha 

zangu ili nikatafute chumba na kuyaanza 

maisha yangu.” Lucy akasema 

 Pendo aliposikia kuhusu suala lile la 

fedha akaanza kupoa na kupunguza ukali 

 “Lucy wewe ni mdogo 

wangu..Ninachojaribu kukueleza hapa ni 

kitu cha msingi.Sina lengo baya kwako 

lakini kama hauko tayari kufanya yale 

ninayokueleza basi mimi sina tatizo nawe 

hata kidogo.Tutaendelea kuishi hapa wote 

hadi hapo utakapojifungua.Siwezi 

kukubali uondoke hapa nyumbani ukiwa 

katika hali hii.Sitaki uende ukaishi maisha 

magumu na ya taabu huko 

uendako.Samahani kama maneno yangu 

yalikuudhi.Tusahau yaliyopita na tuangalie maisha ya mbele.” 

Pendoakasema huku akitabasamu 

 “Futa machozi mdogo wangu.Haya ndiyo 

maisha yetu sisi wanadamu.Jambo 

limeshatokea na kinachofuata sasa hivi ni 

kulikabili.Kesho asubuhi nitakupeleka 

kliniki.” Pendo akasema na kuufanya uso 

wa Lucy uchanue kwa tabasamu pana. 

 Maisha yaliendelea vizuri na Lucy 

akaendelea kuilea mimba yake bila 

matatizo.Pendo alionekana kumjali Lucy 

kwa kila hali.Kwa siku ambazo Lucy 

hakuweza kwenda kufungua biashara 

Pendo alimsaidia .Hali hii ya kujali 

aliyoionyesha Pendo ilimpa faraja kubwa 

Lucy na kumfanya awe ni mwenye furaha 

muda wote.Katika kipindi hiki chote 

alichokuwa akifanya kazi kwa Pendo 

hakuwahi kulipwa mshahara.Pendo alidai 

kwamba anamuwekea katika akaunti 

maalum aliyomfungulia ili pesa hizo 

zimsaidie katika maisha yake ya mbele 

pindi atakapoanza kujitegemea.Lucy 

hakujali kuuliza kuhusu malipo yake 

kwani alimuamini Pendo na hakutegemea 

kama angeweza kumfanyia aina yoyote ile 

ya dhuluma.  Ilikuwa ni siku ya jumamosi wakiwa 

katika sehemu yao ya biashara iliyokuwa 

imefurika wateja kama kawaida yake 

,zilikuja gari mbili za kifahari na 

wakashuka watu wanne.Hawa walikuwa 

ni wateja wa mara kwa mara wa 

Pendo.Watu hawa walikuwa wafanya 

biashara wakubwa wa madini .Wawili kati 

yao walikuwa wakimilki vitalu vya 

uchimbaji wa madini ya Tanzanite huko 

Mererani.Kiongozi wa watu hawa alikuwa 

kijana mmoja mfupi mwembamba 

aliyefahamika kwa jina moja tu la Sango 

alikuwa akivuta sigara na kuupuliza moshi 

mwingi hewani.Shingoni alikuwa amevaa 

cheni ya dhahabu ya gharama 

kubwa.Vidole vyake vyote vilienea pete za 

dhahabu..Sango anamiliki kitalu cha 

uchimbaji madini Mererani .Miaka minne 

iliyopita alifanikiwa kupata madini yenye 

thamani ya mamilioni ya shilingi.Baada ya 

kuipata fedha ile.Sango akiongozana na 

kundi kubwa la wapambe waliokuwa 

wakimfuata kila aendako walifanya 

matumizi makubwa kila siku.Alifunga 

safari za kwenda kutalii Ulaya na nchi 

mbali mbali .Taratibu fedha zilianza kuisha na kumfanya Sango kurejea 

Mererani na kuendelea na shughuli za 

uchimbaji.Kwa miaka mitatu mfululizo 

amekuwa akiendelea na uchimbaji bila 

mafanikio yoyote na kumfanya ayumbe 

kiuchumi hali iliyompelekea auze baadhi 

ya mali zake kama vile nyumba mbili 

alizokuwa amenunua maeneo ya Njiro na 

gari mbili .Alibakiwa na nyumba moja na 

gari moja. 

 Pendo alipowaona Sango na wenzake 

wamefika haraka haraka akawatafutia 

meza na kuwatengea sehemu yao peke 

yao kwani hawa ni wateja wake maalum 

na huwa hawapendi kuchangamana na 

wateja wengine.Kwa furaha Pendo 

akaanza kuwahudumia.Kila mara akina 

Sango wajapo hapa Pendo hupenda 

kuwahudumia yeye mwenyewe kwani 

waondokapo huwa wanamuachia fedha za 

kutosha..Pendo anafahamu vinywaji 

wanavyotumia na kwa haraka akawaletea 

vinywaji wakaanza kunywa . 

 Kiza kilikwisha tanda na tayari akina 

Sango walikwisha onyesha dalili za kulewa 

ingawa kwa Sango huwa inamchukua 

muda mrefu sana kulewa.Sango akamuomba Pendo watoke faragha kwa 

ajili ya maongezi muhimu.Kwa haraka 

haraka Pendo akafikiri kwamba Sango 

alikuwa akimuhitaji awe naye kwa usiku 

ule. 

 Pendo akachukua viti viwili na kuvipeleka 

sehemu yenye utulivu wakakaa. 

 “Niambie Sango unanihitaji leo? Pendo 

akasema huku akicheka lakini moyoni 

alikuwa akitamani kama Sango angetamka 

kwamba anamuhitaji kwa usiku ule kwa 

sababu angemuachia fedha za 

kutosha.Sango si mbahili katika kutoa 

fedha.Kiasi chochote atakachoambiwa 

yeye hutoa bila mabishano. 

 “Hapana Pendo.Nimekuita si kwa mambo 

hayo.Kuna jambo la msingi sana ambalo 

nataka kukueleza na ambalo linahitaji 

usiri mkubwa” Sango akasema 

 “Jambo gani hilo Sango? Pendo akauliza 

 “Ni jambo kubwa na nyeti 

sana.Nimeamua kukueleza kwa sababu 

ninakuamini na ninaamini utanisaidia” 

 “Usijali Sango wewe ni mtu wangu wa siku 

nyingi na nitakusaidia kwa lolote 

lile.Niambie tafadhali” 

 Sango akamtazama Pendo ,halafu akachukua chupa yake na kupiga funda 

moja kisha akasema 




 “Kama unavyofahamu kwamba kwa muda 

wa miaka mitatu sasa mambo yamekuwa 

hayaniendei vyema.Mashimo yangu yote 

yamegoma kutoa madini na hivyo 

kunilazimu kuuza baadhi ya mali ili 

niweze kuyaendesha maisha 

yangu.Nimeuza nyumba zangu mbili 

maeneo ya Njiro,nikauza vile vile gari 

zangu mbili lakini bado hali yangu kifedha 

si nzri hata kidogo.Sielewi sababu ya 

mashimo yangu kufunga namna hii wakati 

huko nyuma yalikuwa yakiongoza kwa 

kutoa madini mengi.” Sango akanyamaza 

kidogo na kumtazama Pendo. 

 “hayo unayoyasema ni ya kweli 

Sango.Unajua hata mimi nimekuwa 

nikijiuliza sana kuhusu mabadiliko yako 

siku hizi.Sango wa sasa si yule Sango 

tuliyezoea kumuita mfalme.” Pendo 

akasema 

 “Ni kweli Pendo hali yangu imebadilika 

sana kama nilivyokueleza.Sanog wa sasa si 

yule Sango wa miaka ile aliyekuwa 

akifunga baa na kuwanywesha watu bure 

kisah wakamuita mfalme.Nimechoka sana 

kifedha na hata marafiki zangu wengi 

wamenikimbia siku hizi.” 

 “Binadamu ndivyo walivyo Sango.Ukiwa 

na fedha utakuwa na marafiki wengi sana 

lakini baada ya kuishiwa marafiki wote 

hukimbia.”Pendo akasema 

 “Ni kweli Pendo .Nimejifunza mambo 

mengi sana katika kipindi hiki.Baada ya 

hali kuzidi kuniendea vibaya ikanilazmu 

kwenda kwa babu kuangalia kuna kitu 

gani ambacho kinanifanya niyumbe 

namna hii.” Sango akasema na kunyamaza 

 “Enhee ! Pendo akaitika huku akiuweka 

mkonowake mmoja shavuni na 

kumsikiliza Sango kwa makini 

 “Babu alinishughulikia na kusema 

kwamba mizimu imekasirika sana kwa 

sababu wakati nilipata zile fedha nyingi 

nilisahau kutoa sadaka na kufanya 

matambiko.Kwa hiyo ninahitaji kufanya 

tambiko na kuwaomba msamaha 

mizimu.Ili tambiko hilo likamilike 

ninahitaji vitu viwili.Babu alisema 

kwamba ili mizimu ifurahi na kuyafanya 

mashimo yangu yatoe madini tena kwanza 

natakiwa nitafute mbuzi dume mweusi 

mwenye mapembe marefu kwa ajili ya tambiko.Kitu cha pili ni kigumu kidogo na 

ndicho nimeamua kukushirikisha ili uone 

namna utakavyoweza kunisaidia.” 

 “Niambie Sango niko tayari 

kukusaidia”Pendo akasema 

 Sango akanyamaza ,akachukua chupa 

yake akanywa kidogo na kusema 

 “Ninatakiwa kufanya tambiko usiku wa 

manane katika moja ya mashimo 

yangu.Lakini kabla ya kufanya tambiko 

hilo ninatakiwa kwanza niwe nimelala na 

mwanamke mjamzito mwenye mimba ya 

miezi kati ya mitano au sita na mwanamke 

mwenyewe awe ni binti mwenye umri 

usiozidi miaka ishirini na moja.Kwa kweli 

huo ni mtihani mgumu sana kwangu kwa 

sababu ninajiuliza nitampata wapi binti 

huyo? Nimeamua kukushirikisha ili uone 

ni kwa namna gani unavyoweza kunisaidia 

kumpata binti huyo .Usihofu kuhusu 

gharama.Mimi niko tayari kwa gharama 

yoyote ile.Ninakufahamu wewe ni mtoto 

wa mjini unaweza ukaifanya kazi hii ya 

kunitafutia huyo binti.” Sango akasema na 

kumtazama Pendo ambaye alikuwa 

akitabasamu. 

 “Sango una uhakika baada ya mambo hayo kukamilika mashimo yako yataaanza 

kutoa mawe kama awali? Pendo akauliza 

 “Nina uhakika mkubwa kwa sababu mzee 

amenihakikishia hivyo kwa hiyo sina wasi 

wasi na hilo.” Sango akajibu 

 “Na endapo utampata binti huyo uko 

tayari kutoa kiasi gani cha fedha? 

 “Mimi niko tayari kutoa hata milioni tano” 

Sango akasema 

 “milioni tano !! 

 “Ndiyo tano” sango akasema tena 

 “Hapana Sango .tano hazitoshi hata 

kidogo.Hii si kazi rahisi kama 

unavyofikiri.Ili kumpata huyo binti 

unayemtaka inakubidi ufanye kila namna 

ya ushawishi ili mtu huyo akubali kwa 

hiyo inahitajika fedha ya kutosha.Kama 

kweli una nia ya dhati ya kurudia hali 

yako ya zamani basi naomba ongeza 

fedha.” Pendo akasisitiza. 

 “Unataka kiasi gani Pendo? 

 “kwa kuwa ni wewe ,naomba ongeza 

milioni tatu ziwe nane” 

 “Pendo wewe ni rafiki yangu wa siku 

nyingi,na nimekueleza ukweli kwamba 

kwa sasa hali yangu kifedha si 

nzuri.Naomba unisaidie katika jambo hili.mashimo yangu yatakapoanza kutoa 

mawe tena hata wewe utafurahi na roho 

yako.Lazima nikupe utajiri.wa 

kutosha.Nitaongeza milioni mbili ili ziwe 

saba” 

 “basi hakuna shida nitakusaidia kumpata 

huyo mtu unayehitaji” 

 “Nitashukuru sana Pendo.Nakuahidi 

kwamba mamboyakiwa safi nitakuachia 

hata hili gari langu ninalotumia sasa liwe 

lako ” 

 Kauli ile inamfanya Pendo atabasamu na 

kucheka kichini chini kisha akauliza 

 “Unamuhitaji lini mtu huyo? 

 “Tambiko linatakiwa lifanyike siku ya 

jumapili usiku kwa maana hiyo namuhitaji 

binti huyo kabla ya tambiko” 

 Huku akitabasamu Pendo akampa Sango 

mkono 

 “Suala lako limekwisha.Usihofu kuhusu 

hilo.Nitakuletea mtu unayemtaka siku ya 

jumapili.” 

 “nakuamini Pendo na ndiyo maana 

nikaamua kukushirkisha katika suala 

hili.” Sango akasema na kuingiza mkono 

katika koti lake akatoa kitabu cha hundi 

akaandika hundi ya shilingi millioni saba akampatia Pendo ambaye alitabasamu na 

kucheka kwa furaha.Alikuwa akihitaji 

fedha kwa ajili ya kufungua saluni ya 

wanawake na kwa sasa amezipata fedha 

hizo.Baada ya kumaliza biashara na Sango 

Pendo akarejea na kumkuta Lucy 

akiendelea kuwahudumia wateja. 

 “Mdogo wangu kaa upumzike nitakusaidia 

kuhudumia” Pendo akamwambia Lucy na 

kuonyesha upendo mkubwa.Lucy akaenda 

kupumzika huu akitabasamu kwa 

upendop ule mkubwa alioonyeshwa na 

Pendo. 

 “Mdogo wangu siku ya Jumapili 

hatutafungua biashara,tuna safari kidogo” 

akasema Pendo wakiwa katika gari 

wakirejea nyumbani baada ya kufunga 

biashara 

 “Safari ya kwenda wapi dada? Lucy 

akauliza 

 “Tutakwenda Mererani.Kuna watu 

wametuomba tukawatembelee kwa hiyo 

tutakwenda huko jumapili.Umewahi 

kufika Mererani? 

 “hapana dada,sijawahi kufika huko”. 

 “basi jumapili utakwenda kuushuhudia 

mji huu wa madini” Pendo akamweleza Lucy ambaye hakuwa na jibu zaidi ya 

kutabasamu 

 Baada ya kufika nyumbani Pendo 

akamuaga Lucy na kuelekea chumbani 

kwake kujipumzisha.Huu ulikuwa ni usiku 

mrefu sana kwake.Hakuweza kupata hata 

tone la usingizi .Alikuwa na mawazo mengi 

 “Huu ndio wakati wangu wa kutengeneza 

fedha.Milioni saba zimeingia kama utani. 

Sango alifanya jambo la maana sana kuja 

kwangu kwa sababu vigezo vya mtu 

anayemtafuta vinawiana kabisa na 

Lucy.Ana miaka kumi na tisa na mimba 

yake ina miezi sita sasa.Siwezi kuzikataa 

fedha hizi nyingi.Ninahitaji fedha kwa ajili 

ya mradi wangu wa saluni na zimekuja 

zenyewe mikononi kwa hiyo siwezi 

kuzikataa.Nimemtunza Lucy muda mrefi 

na hakuna faida yoyote anayonipatia zaidi 

ya hasara.Ninatumia gharama kubwa 

kumtunza yeye na hiyo mimba yake ,naye 

lazima aniingizie fedha.Tena ana bahati 

aliwahi kushika mimba na akagoma 

kuitoa vinginevyo ningetengeneza fedha 

nyingi sana kupitia kwake” akawaza 

Pendo ambaye alishindwa kupata usingizi 

na hivyo kumlazimu kutumia mvinyo mkali 

 ************************ 

Saa nne za asubuhi,siku ya jumapili Pendo 

na Lucy walikuwa ndani ya gari 

wakielekea Mererani.Safari ilikuwa nzuri 

yenye vicheko na maongezi mengi ya 

furaha Pendo alimuahidi Lucy vitu vingi 

vizuri na maisha mazuri.Alimuahida 

kumfungulia biashara nzuriasiku za usoni 

itakayomfanya aweze kujitegemea na 

kuyaendesha maisha yake. 

 Saa sita za mchana wakawasili 

Mererani,wakapokelewa na Sango na moja 

kwa moja akawapeleka katika jumba lake 

kubwa la kifahari.Lucy aliustaajabia uzuri 

wa jumba hili kubwa na la 

kupendeza.Chakula kitamu kilaletwa 

wakala na kisha wakaendelea na 

maongezi na vinywaji.Sango akiwa na 

marafiki zake watatu kwa pamoja na 

Pendo walikuwa wakinywa pombe kali na 

kufurahi.Mezanio palijaa chupa kubwa za mvinyo na kuku zilizokaangwa.Ni Lucy 

pekee ambaye hakuwa akitumia 

pombe.Yeye alikuwa akitumia 

Juice.Sherehe ile ndogo iliendelea hadi 

ilipotimu saa moja za jioni..Kiza kilikwisha 

ingia na mara Pendo akamwambia Lucy 

 “Lucy utatusubiri hapa hapa ndani 

.Ninataka kutoka kidogo na akina Sango 

tutarejea baada ya nusu saa.” 

 “Lucy naona umechoka sana.Wakati 

tunarejea ingekuwa vyema kama 

ungepumzika katika chumba cha 

wageni.Jisikie huru hapa ni nyumbani 

kwako.” Sango akasema na kumtazama 

Pendo 

 “kweli Lucy nenda ukapumzike katika 

chumba cha wageni .Tutarejea muda si 

mrefu” Pendo akamwambia Lucy na kisha 

Sango akamshika mkono na kumuongoza 

kuelekea katika chumba cha 

wageni.Kilikuwa ni chumba kikubwa 

kilichokuwa na kitanda kikubwa cha futi 

tano,televisheni kubwa ,choo,bafu 

n.k.Lucy akapanda kitandani na 

kujilaza.hakuwa na wasi wowote juu ya 

usalama wake. 

 “Pendo mbona umemleta mdogo wako ambaye ndiye anayekuuzia baa? Sango 

akamuuliza Pendo wakiwa katika gari. 

 “ Yule ndiye mtu ambaye ana kila vigezo 

unavyovitaka.Ana miaka kumi na tisa na 

mimba yake ina umri wa miezi sita.Hivyo 

si ndivyo vigezo ulivyokuwa ukivihitaji? 

 “Ndiyo Pendo lakini yule si ndugu yako? 

 “hapana si ndugu yangu.Yule ni msichana 

niliyemtoa huko Singida na kuja 

kumtafutia kazi hapa Arusha.Sina 

uhusiano naye wowote ule wa kindugu.” 

 “Ok hakuna tatizo “ Sango akasema 

 “basi usipoteze muda nenda kafanye 

mambo yako na ukisha maliza sisi 

tuondoke zetu” Pendo akasema. 

 “Umekwisha mweleza chochote kuhusu 

suala hili? 

 “hapana sijamweleza chochote kwa 

sababu asingeweza kukubali.Itakubidi 

utumie nguvu” 

 Sango akafikiri kidogo na kusema 

 “Hakuna tatizo.Sisi tutakuacha hapa na 

tukisha maliza nitakupigia simu “Sango 

akasema 

 “Ina maana mnarudi wote? 

 “Ndiyo wote tunatakiwa tufanye tambiko 

usiku huu kwa hiyo wote tunatakiwa tulale na mwanamke huyo mmoja” 

 “What !! Pendo akastuka 

 “unashangaa nini Pendo? Haya si ndiyo 

yalikuwa makubaliano yetu? 

 “Hapana Sango Hukunieleza kama 

kutakuwa na zaidi ya mtu mmoja” 

 “basi ndiyo hivyo lakini tuko watu watatu 

na ambao wote tunatakiwa kufanya dawa 

hiyo usiku wa leo” Sango akasema na kwa 

haraka akaingia katika gari lililokuwa 

nyuma yao wakageuza na kurudi 

nyumbani kwake 

 “Masikini Lucy hajui chochote 

kinachokwenda kutokea.Naomba 

wasimuumize mtoto wa watu.Watu watatu 

si mchezo.Lakini potelea mbali kwa 

kitakachokwenda kutokea.kwani ana 

faida gani kwangu zaidi ya kunitia hasara 

kila siku kumuhudumia? Lucy akawaza 

akiendesha gari lake taratibu kuelekea 

katika baa ya karibu ambako aliagiza 

kiywaji na kuanza kunywa taratibu. 

 Lucy akiwa chumbani amejipumzisha 

huku akitazama kipindi cha vichekesho 

kupitia luninga kubwa iliyokuwamo mle 

chumbani , mara taa zikazima na ndani 

kukawa na giza nene.Moja kwa moja akajua ni umeme umekatika.hakujua 

afanye nini akabaki amejilaza pale 

kitandani akisubiri watu wale warejee ili 

waweze kufanya uaratibu wa kuwasha taa. 

 Tataribu akasikia kama mlango 

ukifunguliwa.Akanyanyua kichwa lakini 

hakuweza kuona kitu chochote kutokana 

na giza lililokuwamo mle ndani. 

 “kuna mtu hapo mlangoni? Lucy akauliza 

 Mlango ulisikika ukifunguliwa na kuzidi 

kumuogopesha.Ghafla akamulikwa na 

mwanga mkali usoni akashindwa 

kuona,na kujikuta amesukumwa na 

kuanguka kitandani.Alitaka kupiga kelele 

lakini akajikuta amezibwa mdomo na 

mikono ya mtu mwenye nguvu.Alijaribu 

kufurukuta lakini hakuweza kwani 

alikuwa amezuiwa na mikono ya mtu zaidi 

ya mmoja waliokuwa na nguvu nyingi.Kwa 

haraka akavuliwa nguo yake ya ndani na 

bila huruma mtu mmoja akaanza 

kumuingilia.Maumivui makali 

yaliyoambatana na hasira vilimfanya Lucy 

ahisi kama anataka kupoteza uhai.Mtu 

yule alifanya unyama ule kwa nguvu na 

kuzidi kumpa Lucy maumivu 

makali.Alipomaliza akaingia mtu wa pili na baadaye akafuata mtu wa tatu.Lucy 

akashindwa kuvumilia akapoteza fahamu. 

Sango na kundi lake waliendelea kufanya 

kitendo chao cha kikatili na udhalilishaji 

na walipomaliza ndipo walipogundua 

kwamba Lucy hakuwa na 

fahamu.Wakaingiwa na hofu 

kubwa.Taratibu wakatoka na kuelekea 

sebuleni wakawasha taa. 

 “Nina wasi wasi tusijekuwa tumeua mtoto 

wa watu” Sango akasema.akiwa na wasi 

wasi mwingi huku mikonoyake ameiweka 

kifuani. 

 “Kinachotakiwa kwa sasa tumpigie simu 

Pendo tumtaarifu ili aje haraka sana .” 

akasema Sango huku akiichukua simu 

yake na kumpigia Pendo 

 “Niambie Sango mmeshamaliza? “ 

akauliza Pendo baada ya kupokea simu 

 “ Pendo tumemaliza lakini kuna tatizo 

limetokea” 

 “tatizo gani Sango? 

 “Lucy amepoteza fahamu.” Akasema 

Sango kwa wasi wasi 

Pendo akapumua kwa nguvu baada ya 

kupokea taarifa ile akafikiri kidogo na kusema 

 “Sango wewe ndiye umesababisha 

masuala haya yote.Hatukuwa tumepatana 

mtu zaidi ya mmoja. “ 

 “Pendo tafadhali njoo haraka sana .Huu si 

muda muafaka wa kuanza 

kulaumiana.Njoo tuangalie ni jinsi gani 

tutakavyoweza kumsaidia huyu binti” 

Sango akasema na kukata simu. 

 Pendo kwa haraka akaingia garini na 

kundoka kwa kasi kurudi nyumbani kwa 

Sango.Alihisi kuchanganyikiwa. 

 “Itakuwaje kama Lucy atakuwa amekufa? 

Ouh Gosh ! Hilo si jambo la kuomba hata 

kidogo kwa sababu mimi ndiye 

nitakayekuwa matatani.Lakini haya yote 

ameyataka Sango kwa sababu hatukuwa 

tumepatana mtu zaidi ya mmoja.Sikuw 

animetazamai kwama wangekuwepo watu 

watatu.Nilichikuwa nikikifahamu ni 

kwamba angekuwepo Sango mwenyewe 

lakini amenidanganya na amefanya 

hivi.Aombe Mungu Lucy asiwe amepatwa 

na tatizo lolote lile.Kama Lucy atakuwa 

amepatwa aa tatizo lolote kubwa 

atawajibika kwa kila kitu” akawaza Pendo 

huku akikanyaga mafuta kuelekea nyumbani kwa Sango. 

 “Sango niambie Lucy ni mzima? Pendo 

akauliza kwa wasi wasi mwingi baada ya 

kuwasili nyumbani kwa Sango. 

 “Usiwe na hofu Pendo Lucy amepoteza 

fahamu .Naomba tusiendelee kulumbana 

.Tuangalie namna ya kuweza kumsaidia” 

akaomba Sango huku akimuongoza Pendo 

kuelekea katika chumba alichokuwamo 

Lucy 

 Lucy alikuwa amelala kitandani akiwa 

hana fahamu.Pendo akamuinamia 

akamuangalia na kisha akaamuru 

madirisha yote yafunguliwe ili iwezee 

kupatikana hewa ya kutosha na kisha 

akaanza zoezi la kumpepea.Mapigo ya 

moyo yalikuwa yakienda kwa kasi ya 

ajabu sana.Alikuwa akiogopa mno.Alisikia 

uchungu mwingi alipoziona damu 

zimetapakaa pale kitandani. 

 “Watakuwa wamemuumiza mno “ 

akawaza Pendo. 

 “masikini ninasikia uchungu sana kwa 

kitendo nilichokifanya.Sijui nitamuangalia 

vipi usoni baada ya kitendo hiki.Japokuwa 

nimetengeneza fedha nyingi lakini moyoni 

ninasikia uchungu mwingi.” Akawaza Pendo 

 Dakika ishirini baadae Lucy 

akazinduka.Alikuwa akilia kwa maumivu 

makali aliyokuwa akiyasikia 

 “Lucy tafadhali nyamaza kulia Nieleze 

nini kimetokea? Pendo akauliza huku 

naye machozi yakimtoka 

 “dada …Da..da……………..” Lucy akashndwa 

kuongea kitu akaangua kilio huku 

akigugumia kwa maumivu makali 

 “Lucy tafadhali naomba unieleze ni kitu 

gani kimekutokea ? akasisitiza Pendo 

lakini Lucy hakuweza kuongea kitu 

alikuwa akilia kwa sauti kubwa.Alisikia 

uchungu mwingi kwa kitendo 

alichofanyiwa. 

 Pendo akaendelea na zoezi la kumfuta 

machozi na kisha akafanikiwa 

kumnyamazisha Lucy 

 “Lucy mdogo wangu naomba tafadhali 

niambie nini kimetokea? 

Lucy akamtazama Pendo kwa macho 

makali na kusema 

 “dada,muda mfupi baada ya ninyi 

kuondoka,taa za nyumba zikazima,halafu 

nikasikia mlango wa chumba 

ukifunguliwa na halafu nikavamiwa na watu nisiowafahamu ambao walinivua 

nguo na kuanza kunibak………………..” Lucy 

akashndwa kuvumilia akaangua tena kilio 

 “Nyamaza mdogo wangu.Pole sana kwa 

kitendo hiki cha kikatili 

ulichofanyiwa.Uliweza kumtambua hata 

mmoja wao? Pendo akauliza 

 “Sikuweza kumtambua hata mmoja wao 

kwa sababu kulikuwa na giza nene .Hata 

idadi yao siwezi kuikumbuka lakini 

ninachoweza kukumbuka ni kwamba 

kulikuwa na mtu zaidi ya mmoja kwa 

sababu niliingiliwa na mtu wa kwanza na 

alipomaliza akaja mtu wa pili na ndipo 

niliposhindwa kuvumiilia na kupoteza 

fahamu.Dada Pendo nimebakwa 

mimi..nimeb………………….” Lucy 

akaendelea kulia. 

 “Lucy pole sana kwa kitendo hiki .Hapa 

Mererani kumekuwa na watu wenye tabia 

chafu sana siku hizi.Ninahisi watakuwa ni 

vijana wa kihuni wa hapa hapa Mererani 

ambao wamezoea kuja hapa kwangu mara 

nyingi.Ninaahidi kuwatafuta vijana hao na 

kuwafundisha adabu.Nitawatafuta mpaka 

niwapate wahuni hao waliotenda kitendo 

hiki.” Sango akasema akiwa amesimama nyuma ya Pendo. 

 Lucy aliendelea kudondosha machozi na 

kisha akasema 

 “Dada Pendo naomba unipekeke kituo cha 

polisi nikatoe taarifa ili niweze kupatiwa 

karatasi ya kwenda kutibiwa 

hospitali.Nimeumizwa mno na kamwe 

sintaweza kuwasamehe hawa 

walionifanyia hivi” 

 Pendo akaingiwa na wasi wasi 

mwingi.Akamuangalia Lucy na 

kumwambia 

 “Lucy mdogo wangu tafadhali nakuomba 

usiende polisi.Suala hili likifika polisi sote 

tutakuwa katika matatizo makubwa na 

hasa Sango. Kwa vile Sango ameahidi 

kwamba atahakikisha kwamba hao vijana 

wa kihuni waliofanya jambo hili 

atawatafuta yeye mwenyewe na kisha 

kuwashikisha adabu,naomba tumuache 

aendelee na kuwatafuta kwa sababu yeye 

ni mtu mkubwa hapa Mererani.Kama 

ukiwataarifu polisi basi hata mimi dada 

yako nitakuwa matatani .Naomba 

tafadhali usiende polisi.Kuhusu kutibiwa 

nitakutafutia daktari atakayekutibu bila 

mtu yeyote kujua”  Lucy akainua uso wake na kumtazama 

Pendo kwa makini. 

 “dada Pendo kwa nini unanizuia kwenda 

polisi? Ninataka haki itendeke.Ninataka 

watu wote walionifanyia unyama huu 

wakamatwe na wachukuliwe 

hatua.Nisipokwenda kutoa taarifa polisi 

nitaipataje haki yangu? Lucy akauliza kwa 

ukali 

 “Lucy msikilize dada yako 

anavyokwambia.Iwapo utalipeleka suala 

hili polisi litatuweka matatani sisi 

sote.Jambo hili limetendeka ndani ya 

nyumba yangu kwa maana hiyo mimi 

ndiye nitakayekuwa mtu wa kwanza 

kushikiliwa na polisi na hata dada yako 

Pendo naye atakamatwa kwa kosa 

hili.Naomba tafadhali usiende polisi na 

mimi kama nilivyokuahidi kwamba 

nitawatafuta wale wote waliohusika na 

kitendo hiki na nikisha wapata nitakuita 

uwaone watu waliokufanyia kitendo hiki 

na wewe mwenyewe utaamua tuwafanye 

nini.Ninakuahidi kwamba nitawapata 

ndani ya muda mfupi sana kwa sababu 

vijana wote wa hapa Mererani 

ninawafahamu.Vile vile nitagharamia gharama zote za daktari za kukuangalia” 

akaomba Sango 

 Lucy hakujibu kitu akaendelea 

kulia.Pendo akamuinua na kumpeleka 

bafuni ambako alimfanyia usafi na kisha 

akampakia katika gari tayari kwa safari ya 

kurejea Arusha.Kabla hawajaondoka 

Sango akamfuata Lucy. 

 “Lucy kuna fedha shilingi millioni moja 

na nusu nimempa dada yako kwa ajili ya 

kulipia gharama za daktari na 

zitakazobaki ni kwa ajili yako.Naomba 

uniamini kwamba nitawatafuta wale wote 

waliofanya unyama huu ndani ya kipindi 

kifupi” 

 Lucy akatikisa kichwa halafu akaangalia 

chini.bado aliendelea kusikia maumivu 

makali sana katika sehemu zake za siri 

.Pendo akawasha gari na safari ya kurejea 

Arusha ikaanza. 

 “Nashindwa kuelewa mimi nina mkosi 

gani kwa sababu toka nimefanya mapenzi 

na Jack nimekuwa nikiandamwa na 

matukio mabaya mabaya tu.Nahisi 

mwanaume wangu wa kwanza alinipa 

mkosi na ndiyo sababu ninaandamwa na 

matukio ya ajabu ajabu namna hii.Kitendo nilichofanyiwa leo kimeniuma 

sana.Nimebakwa na watu zaidi ya 

mmoja.Ni kwa nini nimefanyiwa ukatili 

huu mkubwa? Roho inaniuma sana kwa 

kufanyiwa kitendo kama hiki na hasa 

nikiyakumbuka maumivu makali 

niliyoyapata.Kibaya zaidi sielewi kama 

nimeambukizwa magonjwa ya hatari 

kama vile ukimwi .Nilitamani sana 

kuwaona watu waliofanya kitendo hiki 

wakichukuliwa hatua stahili kwa unyama 

wao lakini dada Pendo amenizuia kwenda 

polisi.Hii si sawa hata kidogo.Nilipaswa 

kwenda kutoa taarifa kituoni.Kuna kila 

dalili kwamba kitendo kile kilikuwa cha 

kupangwa.Ninaweza kusema kweli 

kitendo kile kilipangwa kwa sababu 

kimetokea muda mfupi baada ya Pendo na 

akina Sango kusema kwamba kuna 

mahala wanaelekea.Inaonekana hata dada 

Pendo naye atakuwa akifahamu juu ya 

mpango ule na ndiyo maana akawa mstari 

wa mbele kunizuia nisiende kutoa taarifa 

kituo cha polisi.Kwa nini lakini wanifanyie 

mambo haya? Kwa nini wanitende hivi 

hali wakijua kwamba mimi ni mjamzito ? 

Ziko wapi haki zetu sisi masikini? Lucyakainama na kufuta machozi. 

 “Ee Mungu wewe ndiye unayeona kila 

jambo.Uwezo wako unashinda uwezo wetu 

sisi binadamu.Umeona kitendo cha kikatili 

nilichofanyiwa.Mimi ni msichana masikini 

nisiye na nguvu wala uwezo wa kuweza 

kupambana na watu wenye pesa na nguvu 

kubwa. Ninakukabidhi wewe Mungu 

utanisaidia kuwahukumu watu wale wote 

waliohusika na kitendo hiki kibaya.” Lucy 

akaomba kimoyo moyo. 

 Pendo alikuwa na wasi wasi mwingi 

baada ya kumuona Lucy akiwa kimya 

sana.Akamgeukia akamtazama na 

kumwambia 

 “Lucy mdogo wangu nasikia uchungu 

sana kwa kitendo hiki walichokifanya 

hawa wakatili.Tafadhali naomba usiumie 

sana kwa sababu ninai imani kwamba 

muda si mrefu Sango atawatambua wale 

wote walifanya kitendo hiki.” 

 “Dada Pendo hakuna mtu anayeweza 

kuyaona machungu niliyonayo sasa hivi. 

Tafadhali naomba uache kuniambia 

kwamba nisi huzunike .Nisihuzunike kwa 

kitendo cha kubakwa na watu zaidi ya 

mmoja? Kama binadamu yeyote yule anayefahamu thamani ya utu wake lazima 

nihuzunike kwa kudhalilishwa namna 

hii.Dada Pendo nina uchungu mkubwa 

sana.Nimeumia mno moyoni lakini sina 

kitu cha kufanya kwa sababu mimi ni 

mnyonge na haki yangu 

inadhulumiwa.Ninamuachia Mungu yeye 

ndiye atakayenilipia” akasema Lucy na 

kuinama chini. 

 Baada ya kufika nyumbani Lucy 

hakutaka maongezi akaelekea moja kwa 

moja chumbani kwake akajilaza kitandani 

kwake. 

 “Nina kila sababu ya kuamini kwamba 

Pendo anahusika na kitendo hiki 

nilichofanyiwa leo.Kama angekuwa 

hahusiki kwa namna yoyote ile basi 

asingenizuia kwenda kutoa taarifa kituo 

cha polisi.Nimefikia uamuzi wa kuondoka 

hapa nyumbani kwake na kwenda 

kuendelea na maisha yangu 

mwenyewe.Sijui nitakwenda wapi lakini 

kokote nitakakokwenda ili mradi iwe ni 

nje na hapa.Sitaki tena kuendelea kukaa 

hapa nyumbani kwake.Kesho asubuhi na 

mapema nitamueleza aweze kunipatia 

zile fedha zangu nilizompa aniwekee ili nikayaanze maisha yangu.” Lucy akawaza 

akiwa amejilaza kitandani kwake. 

 Saa kumi na mbili za asubuhi tayari 

Lucy alikuwa ameamka amekaa 

kitandani.Alihisi maumivu makali ya 

kichwa.Hakuweza kupata usingizi kwa 

usiku ule kutokana na mawazo mengi 

aliyokuwa nayo.Alikuwa amekaa 

kitandani amekishika kichwa kwa mikono 

yake miwili akiwa na mawazo 

 Taratibu mlango wa chumba chake 

ukafunguliwa na Pendo akaingia akaenda 

kukaa karibu na Lucy. 

 “Mdogo wangu umeamkaje? Akasema 

Pendo 

 “Nimeamka vizuri dada ila nasikia 

maumivu makali sana ya kichwa” 

 “Pole sana utapona tu mdogo wangu.Leo 

ninakwenda kumchukua daktari ili aanze 

kukuhudumia” akasema Pendo 

 “hakuna haja dada Pendo.Nimeamua 

kuondoka na kwenda kuanza maisha 

yangu mwenyewe” 

 “Unasemaje ? Pendo akauliza kwa 

mshangao 

 “Nimeamua kwenda kuyaanza maisha 

yangu mwenyewe.Naomba uniandalie zile fedha zangu ili niweze kuondoka hapa 

kwako” Lucy akasema 

 “ Kwa nini umeamua hivyo mdogo wangu? 

Nilikwisha kuambia kwamba mimi nitakaa 

nawe hapa kwangu hadi utakapojifungua” 

 “Ninataka kuanza maisha ya kujitegema 

.Sitaki kuwa tegemezi kwa mtu yeyote 

yule” Lucy akasema 

 “Mdogo wangu mimi nimejitolea kukaa 

nawe hapa kwa muda wote hadi 

utakapojifungua.” 

 “dada Pendo nakushukuru sana kwa 

wema wako lakini kutokana na kitendo 

kilichonitokea jana nimeamua itakuwa 

vyema kama nikiondoka hapa nyumbani 

kwako na nikaanze maisha yangu 

mwenyewe” 

 “Una maana gani kusema hivyo Lucy.” 

Pendo akauliza 

 “Sina maana mbaya ila nimeumia mno 

kwa kitendo cha kudhalilishwa namna ile 

na kibaya zaidi ulivyonizuia kutokwenda 

kutoa taarifa kituo cha polisi.Nimejiuliza 

ni kwa nini haki yanu inadhulumiwa 

namna hii na nimegundua kwamba hii 

yote inasabishwa na umasikini 

nilionao.Nimeamua kwenda kuyaanza maisha yangu mwenyewe ili niweze 

kujikomboa kutoka katika umasikini” 

 Pendo akakaa kimya akamtazama Lucy 

kwa muda na kisha akasema 

 “Lucy si kwamaba nilikuzuia kwenda 

kutoa taarifa kituo cha polisi bali nilifanya 

vile kwa sababu suala hili lingetutia 

matatani wengi” 

 “Dada Pendo huna upendo na mimi hata 

kidogo.” Lucy akasema.Siku hii alikuwa na 

ujasiri wa kipekee na hakuogopa kitu 

chochote 

 “Kwa nini unasema hivyo Lucy wakati 

unafahamu kabisa kwamba ninakupenda 

na ninakuhudumia kama mdogo wangu 

wa tumbo moja? 

 “Dada Pendo huna hata chembe ya 

upendo kwangu.Kama ungekuwa na 

upendo kwangu ungeongozana nami 

kwenda polisi kupeleka mashitaka 

.Ulinizuia kwenda polisi kwa sababu 

unazozijua wewe.Sitaki malumbano 

yoyote nawe dada yangu ninachoomba 

niandalie zile fedha zangu ili niweze 

kuondoka hapa” Lucy akasema na 

kumfanya Pendo kusimama na kushika 

kiuno chake akamtazama Lucy kwa macho makali yaliyojaa ghadhabu 

 “Ama kweli shukrani ya punda 

mateke.Kwa mema yote niliyokutendea 

leo hii Lucy unadiriki kunijibu mimi 

namna hiyo? Hukumbuki ni mambo 

mangapi nimekufanyia? Pendo akauliza 

kwa sauti ambayo ilikwisha badilika na 

kuanza kuwa ya ukali 

 “Dada Pendo ninakushukuru sana kwa 

msaada wako na kuniruhusu nikae hapa 

nyumbani kwako kwa muda huu 

wote.Lakini naomba usisahau kwamba 

siku zote nilizokaa hapa nyumbani kwako 

umekuwa ukinitumia kwa faida yako 

.Nimekuwa nikikufanyia biashara yako na 

hujanilipa hata senti tano toka nimeanza 

kazi hadi leo hii na sijawahi kukutamkia 

kuhusu suala hilo.Ninachokiomba ni ile 

fedha yangu uliyosema nikukabidhi 

uniwekee shilingi millioni moja na laki 

nne.Hizo fedha nyingine za mishahara na 

mambo mengne sizihitaji.Naomba 

unipatie fedha zile za kwangu niondoke 

hapa kwako” Lucy naye alikuwa akiongea 

kwa sauti yenye ukali .Alikwisha ghafirika. 

 “Unazitaka pesa zako? Subiri 

nikuletee”Pendo akatamka kwa hasira na 

kutoka mle chumbani kwa Lucy akaelekea 

chumbani kwake na baada ya muda mfupi 

akarejea akiwa ameshika kitita cha noti 

mkononi mwake akamrushia Lucy 

 “Pesa zako hizo hapo kama kuna 

nyinginge utabaki unanidai utazifuata siku 

nyingine lakini naomba leo hii hii uondoke 

hapa nyumbani kwangu binadamu 

uliyekosa shukrani.Muangalie kwanza 

sura yake ilivyokuwa mbaya.! 

Ninakwambia kwamba leo hii sitaki 

kukuona hapa nyumbani kwangu.Anza 

kufunga mizigo yako sasa hivi” Pendo 

akasema kwa hasira na kutoka mle 

chumbani mwa Lucy. 

 Lucy akainuka na kuanza kuzikusanya 

zile fedha alizorushiwa na 

Pendo.Akazihesabu na kukuta ni shilingi 

laki sita na thelathini.Akadondosha 

machozi. 

 “Fedha yangu ilikuwa millioni moja na 

laki nne.Hizi shilingi laki sita zitanifikisha 

wapi? Mbona nimekuwa nikidhulumiwa 

haki yangu namna hii? Lakini ngoja 

niondoke ili kujiepusha na maneno 

zaidi.Mungu atanisaidia.Nitamuomba 

Sharifa yule rafiki yangu anayeishi Kijenge niishi kwake kwa muda wakati nikijipanga 

na maisha yangu”. 

 Lucy akafunga mizigo yake na kuondoka 

akaenda nyumbani kwa rafiki yake Sharifa 

ambaye naye alikuwa ni muhudumu wa 

baa na alikuwa akiishi katika chumba 

kimoja . 



 Sharifa binti mfupi mweupe ambaye 

alikuwa ni mtumishi wa baa iliyokuwa 

karibu na mahala anakoishi alimpokea 

Lucy na kuamua kumsaidia ili aishi kwake 

wakati akijiandaa kuyaanza maisha yake 

ya kujitegemea.Alikuwa amekutana na 

Lucy wakati akifanya kazi ya kuuza 

vinywaji katika grosari la Pendo na 

wakawa marafiki hivyo hakuona sababu 

ya kutomsaidia rafiki yake katika kipindi 

hiki ambacho alikuwa na matatizo 

makubwa.Kwa moyo mkunjufu 

alimkaribisha Lucy waishi wote katika 

chumba kimoja alichokuwa anaishi 

maeneo ya Kijenge.Yalikuwa ni maisha 

magumu hasa kwa Lucy kwa sababu 

chumba hicho kimoja kilikuwa kimejaa 

vitu vingi kiasi kwamba hata nafasi ya kupita ilikosekana.Siku zote Sharifa 

alikuwa akimpa moyo rafiki yake na 

kumuomba avumilie maisha yale magumu. 

 Siku zilizidi kusonga ,maisha 

yakaendelea,mimba ya Lucy ikazidi kukua 

na hatimaye siku za kujifungua 

zikakaribia.Siku moja Sharifa aliwahi san 

kurejea nyumbani na uso wake ulikuwa na 

simanzi kubwa.Baada ya mapumziko 

,akamuomba Lucy wazungumze jambo 

moja muhimu. 

 “Lucy ndugu yangu kuna jambo 

limenitokea leo.Mwajiri wangu amenifuta 

kazi baada ya kukwaruzana na mmoja wa 

wateja aliyekosa adabu kwa kunishika 

shika maungoni mbele za 

watu.Sikupendezwa na kitendo kile na 

hivyo ikanibidi nimfundishe adabu 

mwanaume yule asiye na heshima hata 

chembe.Bosi wangu hakupendezwa na 

kitendo nilichokifanya akaamua kunifuta 

kazi.Kwa hiyo kuanzia sasa sina kazi na 

niko katika kuumiza kichwa ni wapi 

ninakoweza kupata ajira ya tofauti na hii 

ya kuuza baa kwani imejaa udhalilishaji 

mkubwa.Wahudumu wote wa baa 

tunadharaulika sana.Nataka nitafute kazi 

nyingine kabisa na kuachana na kazi hi ya 

uhudumu wa baa.” Sharifa akamtaarifu 

Lucy ambaye alionyesha kustuka 

 “Pole sana Sharifa.nimefanya kazi ya 

kuuza vinywaji ninafahamu ugumu 

wake.Nakupongeza kwa kuwa jasiri na 

kutokubali kudharauliwa.” Akaseam Lucy 

 “Lucy kuna jambo moja la muhimu 

ambalo ningependa tulijadili na kulipatia 

ufumbuzi” akasema Sharifa akiwa ameketi 

sofani na Lucy akiwa amelala kitandani 

 “nakusikilia Sharifa” akasema Lucy kwa 

sauti ya upole 

 “Lucy nadhani unafahamu kwamba siku 

zako za kujifungua zimekaribia sana 

.Muda wowote kama Mungu akijaalia 

unaweza ukajifungua.Nimejiuliza sana 

baada ya mkasa huu kunitokea kwamba 

maisha yako yatakuwaje baada ya 

kujifungua.Huna kazi,huna biashara 

yoyote ya kukuwezesha kuyamudu maisha 

ya hapa mjini nan mimi sina kazi kw 

sasa.Laiti ningekuwa na kazi au kipato 

kikubwa cha kutosha basi kusingekuwa na 

tatizo lolote lakini kazi ambayo japokuwa 

ina kipato kidogo lakini kilichotuwezesha 

kuyamudu maisha yeti nimeipoteza na sina kipato chochote.Kwa hali hii nikisema 

kwamba nitaweza kukulea wewe na 

mwanao kutokana na haliyangu ya sasa 

nitakuwa nikikudanganya.Bora niwe 

muwazi kuhusu jambo hili.Kuna jambo 

nimelifikiria” akasema Sharifa na 

kumfanya Lucy ainuke pale kitandani 

alaipokuwa amejilazana kukaa kitako. 

 “jambo gani hilo Sharifa? Lucy akauliza 

 ‘Nimejiuliza ni kwa nini basi tusimfuate 

baba wa mtoto ili afahamu juu ya 

kinachoendelea na asaidie katika suala 

zima la malezi ya mtoto? Uliniambia 

kwamba kijana aliyekupa mimba hiyo 

anatoka katika familia inayojiweza 

kimaisha ila tatizo ni kwamba bado ni 

mwanafunzi.Sioni kama kuna shida yoyote 

hata kama ni mwanafunzi.kwa vile wazazi 

wake wana uwezo basi itawabidi wasaidie 

malezi ya mjukuu wao.Unaonaje kama 

tukiwafuata na kuwaeleza kuhusiana na 

suala hili? 

 Wazo lile la Sharifa likamfanya Lucy 

ainame na kukishika kichwa chake.Kwa 

sekunde kadhaa alizama katika dimbwi la 

mawazo mengi.Alikumbuka jinsi mama 

yake Jackson alivyomfukuza baada yakumkuta akifanya mapenzi na 

mwanae.Alipoyakumbuka maneno makali 

na sura ya mama Jackson ilivyokuwa siku 

ile akainua kichwa na kusema 

 “Sharifa kwanza kabisa napenda 

kukushukuru kwa namna ulivyonisaidia 

katika kipindi hiki ambacho kilikuwa 

kigumu sana kwangu.Sikuwa na msaada 

wowote lakini umeniokota na kunipa 

makaazi.Umenilea kama ndugu 

yako.Nashukuru sana kwa hilo.Hilo suala 

unalolisema hata mimi limekuwa 

likiniumiza kichwa sana.Nafahamu hata 

kama ungekuwa na kazi lakini kipato 

chako ni kidogo sana na ambacho 

hakiwezi kukidhi kunihudumia mimi 

pamoja na mwanangu.” Akasema Lucy. 

 “ Kweli Lucy.hali ni ngumu sana .Laiti 

kama ningekuwa na kipato au ajira yenye 

uhakika kusingekuwa na tatizo lolote 

lile.Ndio maana nimekushauri kwamba 

tumfuate baba wa mtoto ili afahamu 

kinachoendelea na wajiandae kwa malezi 

ya mtoto.Kwa nini uhangaike wakati mtu 

aliyekupa hiyo Mimba ana uwezo wa 

kukutunza? Sharifa akasema 

 “Sharifa wazo lako ni zuri lakini sina hakika kama wahusika wanaweza 

wakalipokea .” 

 “kwa nini unasema hivyo Lucy? Akauliza 

Sharifa 

 “Nakumbuka mama yake Jack 

alivyonifukuza nyumbani 

kwake.Nilidhalilika sana siku ile.Sidhani 

kama leo hii nikienda tena kumuambia 

kwamba nina mimba ya mtoto wake 

atanielewa.Ninafahamu kutatokea 

matatizo makubwa iwapo nitawataarifu 

kuhusiana na suala hii kitu ambacho sitaki 

kitokee.Sitaki kuendelea tena kuumia kwa 

sababu ya suala hili.Nimekwisha umia vya 

kutosha na ndiyo maana nimeamua 

kwamba sintawaeleza lolote kuhusiana na 

suala hili “ akasema Lucy. 

 “Lucy kuna nyakati unanipa wasi wasi 

kama hiyo mimba kweli ni ya huyo Jack 

unayemsema.Mimi sioni ugumu uliopo wa 

kumfahamisha muhusika mkuu kuhusiana 

na mimba hii.Lucy naomba tafadhali 

unieleze ukweli mimba hii ni ya nani ili 

tumfuate “ Sharifa akasema huku 

akimkazia macho Lucy 

 “Sharifa siwezi kukudanganya mimba hii 

ni ya Jack.Yeye ndiye mwanaume wa kwanza mimi kufanya naye mapenzi na 

baada ya hapo sijawahi tena kufanya na 

mtu mwingine yeyote .Nina uhakika 

mkubwa mimba hii ni ya Jack na si 

kwamba sitaki kumueleza kuhusiana na 

suala hili” 

 “sasa kama hutaki kumueleza unaogopa 

nini ? “ Sharifa akaingilia kati 

 “Kinachonifanya niogope kumueleza 

ukweli kwamba nina mimba yake ni 

namna atakavyolipokea suala hilo.Sharifa 

sitaki kudhalilishwa tena na familia 

ile.Ninajua yataibuka mambo mengi iwapo 

nitawafuata na kuwaeleza kwamba nina 

mimba ya Jack.Hiyo ndiyo sababu 

inayonifanya nikae kimya na 

kutokuwaambia lolote.” Akasema 

Lucy.Sharifa ambaye alikuwa amekaa 

kimya akisikiliza,akainama akafikiri kwa 

muda halafu akainua kichwa akamtazama 

Lucy na kusema. 

 “Lucy ,ninapenda sana kukusaidia lakini 

hali yangu hainiruhusu kuendelea kufanya 

hivyo.Laiti kama ningekuwa na kazi ya 

kufanya basi kusingekuwa na ugumu 

wowote kwa sababu tungeweza kukitumia 

hicho hicho kidogo ambacho ningekipata,lakini kwa sasa sina kazi na 

wewe hutaki kumfuata mhusika wa 

mimba hii na kumueleza ili aweze 

kugharamia matumizi.Kwa sababu hiyo 

basi ninaonelea kwamba baada ya 

kujifungua mimi nitakutafutia nauli urejee 

kijijini ,ukakae huko hadi hapo mtoto 

wako atakapokuwa mkubwa na kisha 

unaweza ukamuacha kwa wazazi au ndugu 

halafu ukarudi tena mjini kuendelea 

kutafuta pesa.Nadhani hilo litakuwa ni 

jambo la msingi sana kwa sababu hakuna 

tena namna nyingine tunayoweza kufanya 

ili tuishi.Unaonaje kuhusu wazo 

hili?akauliza Sharifa.Lucy akainama na 

kuwaza.Suala lile lilkuwa limemstua 

sana.hakutegemea kama Sharifa 

angekuwa na wazo la kumrudisha kijijini 

kwao ambako ingembidi kwenda 

kuogelea tena katika dimbwi la umasikini 

mkubwa ulioko katika familia yao. 

 “Suala la kurudi kijijini ni suala ambalo 

halitawezekana hata kidogo.Nyumbani 

kwetu ni masikini sana na wote 

wanategemea msaada kutoka 

kwangu.Niliukimbia umasikini wa kijijini 

kwetu na kuja mjini kutafuta unafuu wa maisha ili niweze kuwasaidia ndugu zangu 

nyumbani.Iwapo nitarejea leo na mtoto 

nitakuwa nimeongeza matatizo katika 

familia yangu .Hapana siwezi kurudi 

kijijini.Hata itokee nini siwezi kurudi 

kijijini.Nitabaki hapa hapa mjini 

nikihangaika hadi hapo nitakapofanikiwa 

kupata maisha mazuri.Sharifa ana roho 

nzuri sana na amenilea kwa kipindi 

kirefu.Siwezi kumlaumu kwa sababu hata 

naye amechoka.Hana kazi kwa sasa na 

simlaumu kwa uamuzi wake wa kunitaka 

nirejee kijijini.Laiti kama angekuwa nna 

uwezo ina imani angeendele kunivumilia 

na kunilea.Sitaki kumuudhi itanibidi 

nikubaliane naye kwamba nitarejea kjijini 

baada ya kujifungua.” Akawaza Lucy 

 “Lucy unasemaje kuhusiana na mawazo 

yangu ya kwamba urejee kijijini mara 

utakapojifungua halafu mtoto akishakuwa 

mkubwa basi utarudi tena mjini ? sharifa 

akamuuliza tena Lucy 

 “Sharifa unalolisema ni ukweli 

mtupu.kwa hali ilivyo kwa sasa 

itanilazimu kurejea kijijini ili nikalee 

mtoto na baada ya mtoto kuwa mkubwa 

basi nitarejea tena mjini.nakubaliana nawe katika suala hili na wala sina 

kipingamizi.” Lucy akasema na kumfanya 

Sharifa atabasamu. 

 “Lucy si kwamba ninakufukuza hapa 

nyumbani kwangu lakini hii imetokana na 

hali halisi ilivyo.Siku zote hapa ni 

nyumbani kwako na unakaribishwa muda 

wowote.Mtoto akishafikisha umri wa 

kuweza kubaki na bibi zake nyumbani 

nitakutumia nauli ili uweze kurejea mjini 

na kuendelea kuhangaika kutafuta 

maisha.” Sharifa akasema. 

 “Sharifa usijali kuhusu hilo.Nafahamu 

hali yako ya kifedha kwa sasa si nzuri.Nina 

imani kwamba kama ungekuwa na hali 

nzuri ungeendelea kunihudumia .Siku zote 

nitaendelea kukushukuru sana kwa 

namna ulivyonilea hadi hivi sasa.Naomba 

uwe na amani moyoni kuhusu jambo hilo.” 

 Pamoja na mateso na mahangaiko 

yote ambayo Lucy aliyapata katika kipindi 

chote alichopata ujauzito hatimaye Mungu 

alimjaalia akajifungua salama salimini 

mtoto mzuri wa kike mwenye afya 

njema.Ilikuwa ni furaha kubwa sana kwa 

kumpata mtoto huyu ambaye bila 

kupoteza muda akampa jina la Anjela.Kila alipomuona mtoto wake huyu mzuri 

alikuwa akitabsamu na kujawa na furaha 

kubwa na kumshukuru Mungu kwa 

kuweza kumlinda na hatimaye 

akafanikiwa kujifungua salama bila 

matatizo yoyote.Siku ya pili yake 

akaruhusiwa kurejea nyumbani kwani 

yeye na mtoto wake walikuwa 

wakiendelea vizuri sana.Sharifa aliyekuwa 

karibu naye kwa wakati huu wote 

akambeba mtoto wakarejea nyumbani.. 

 Wiki mbili baada ya Lucy kujifungua 

mtoto wake Anjela ,Sharifa akarejea jioni 

moja akiwa na fedha taslimu shilingi elfu 

sitini akamkabidhi Lucy 

 “Lucy tayari nimefanikiwa kupata zile 

fedha za mauli ya kukufikisha kijijini 

kwenu.Kuna rafiki yangu mmoja 

amenikopesha.Kesho itakuwa ni siku ya 

kufanya maandalizi ya safari ikiwa ni 

pamoja na kukata tiketi ya basi” Sharifa 

akamweleza Lucy ambaye alikuwa 

amestuka kwa ndani lakini hakutaka 

kuonyesha .Akajilazimisha kutabasamu 

 “Nashukuru sana Sharifa kwa msaada 

wako huu mkubwa.Wewe ni zaidi ya 

ndugu.Kamwe sintaweza kukusahau hata kidogo.Kama utakwenda kunikatia tiketi 

naomba unikatie kwa lile basi 

linaloondoka alfajiri na mapema .Nataka 

niwahi gari linalokwenda kijijini kwetu 

.kutokea Singida mjini ambalo huwa 

linaondoka saa kumi za jioni kwa maana 

hiyo itanilazimu kulala katika stendi ya 

mabasi ili nisiweze kuchelewa basi la 

asubuhi sana“ Lucy akasema 

 “sawa Lucy nitafanya hivyo” akasema 

Sharifa. 

 Usiku wa siku hiyo ulikuwa ni usiku 

mrefu sana kwa Lucy.Hakuweza kupata 

usingizi kutokana na mawazo mengi 

aliyokuwa nayo.Alikuwa akiyafikiria 

maisha yake.Alikumbuka toka angali 

akiwa mdogo.Aliyakumbuka maisha ya 

umasikni ya kijijini kwao.Akakumbuka 

siku ya kwanza aliyokuja mjini akiwa na 

Pendo.Akakumbuka pia jinsi alivyokuwa 

akiishi vizuri na familia ya akina Jack na 

mara ikamjia picha akiwa amelala sofani 

akifanya mapenzi na jack.Akauma meno 

kwa hasira. 

 “Yule kijana ndiye chanzo cha haya 

yote.Kama isingekuwa ni tamaa yangu ya 

kutaka kufanya mapenzi yasingenikuta mahangaiko yote haya.Siku zote 

ninakijutia kitendo changu cha kukubali 

kufanya mapenzi na jack kwani matatizo 

yote yalianzia pale.Ninahisi labda 

mwanaume wangu wa kwanza alikuwa na 

mkosi kwa sababu toka siku ile nimekuwa 

nikiandamwa na mabalaa kila 

kukicha.Pamoja na hayo mabalaa 

yanayoniandama ,nashukuru kwa sababu 

nimejifunza mambo mengi sana.Nimeweza 

kuufahamu ulimwengu na watu wake 

wakoje.Hii yote ni mitihani katika maisha 

hivyo sipaswi kukata tamaa hata 

kidogo.Siku zote nitaendelea kuwa jasiri 

na siku moja Mungu anaweza akanisaidia 

na maisha yangu yakawa mazuri..” Lucy 

akawaza halafu ikamjia kichwani picha ya 

siku ile alipoingiliwa kwa nguvu na 

mibaba mitabu kule Mererani.Akafumba 

macho na kutikisha kichwa. 

 “Hiki kitu ambacho najitahidi 

kukisahamu na kukiondoa kabisa katika 

maisha yangu lakini 

nashindwa.Nilifanyiwa kitendo cha 

kikatili sana .Namuomba Mungu anisaidie 

ili niweze kukisahau kitendo hiki.” 

 Lucy akainama akamtazama mwanae aliyekuwa amelala,akambusu 

 “Siko tayari kurudi kijijini.Nitabaki hapa 

hapa mjini na nitapambana mpaka 

nihakikishe kwamba ninakuwa na maisha 

mazuri.Sitaki kunyanyasika tena 

.mwanangu Anjela utanisamehe sana kwa 

jambo nitakalolifanya lakini hii ni kwa 

sababu sina namna nyingine ya 

kufanya.Siku moja nitakutafuta na 

kukueleza ukweli na nina imani 

utanisamehe” Lucy akawaza huku machozi 

yakimtoka. 

 “Nakupenda sana Anjela wewe ni kila 

kitu kwangu lakini siko tayari 

kukurudisha kijijini ili ukaishi maisha 

kama niliyoyaishi mimi.Maisha yaliyojaa 

umasikini mkubwa sana.Nataka uishi hapa 

hapa mjini ili kama Mungu akikujaalia 

basi uweze kupata elimu bora na uwe na 

maisha mazuri na si kama mimi mama 

yako.” Lucy akazidi kudondosha machozi. 

 *************************** 

Asubuhi siku iliyofuata akadamka 

mapema na kuanza kufanya shughuli za usafi.Alifua nguo zake zote na za mtoto 

wake ikiwa ni maandalizi ya safari ya 

kuelekea kijijini kwao .Siku hii yote Lucy 

alikuwa na mawazo mengi sana.Kila 

alipomtazama mwanae machozi yalikuwa 

yakimtoka. 

 Saa kumi na moja za jioni Sharifa 

akarejea nyumbani akiwa tayari na tiketi 

ya basi akamkabidhi Lucy ambaye 

aliipokea na kushukuru.Juhudi za Sharifa 

kumshawishi Lucy kulala pale nyumbani 

hadi asubuhi zilishindikana kwani Lucy 

alibaki na msimamo wake wa kwenda 

kulala stendi ya mabasi kwa sababu ya 

kuogopa kuchelewa basi linaloondoka 

alfarjiri na mapema.Saa kumi na mbili za 

jioni Sharifa akamsindikiza Lucy kuelekea 

katika stendi kuu ya mabasi jijini 

Arusha.Waliongea mambo mengi sana na 

ilipotimu saa mbili za usiku Sharifa 

akamuaga Lucy na kisha akaondoka 

kurudi nyumbani kwake.Nusu saa baada 

ya Sharifa kuondoka Lucy naye akachukua 

kikapu chake kidogo chenye nguo za 

mtoto wake akaondoka pale stendi ya 

mabasi na kuanza kupiga hatua kwa kasi 

kuelekea katika stendi ya mabasi madogo ya abiria pale alikuwa akilitafuta gari 

linalokwenda usa river.Usiku huu magari 

ya kuelekea mji mdogo wa usa river 

yalipatikana kwa taabu sana.Akasimama 

katika kundi la watu waliokuwa 

wakisubiri gari kuelekea katika mji huo 

mdogo.Baada ya kusubiri kwa dakika 

kama ishirini hivi yakatokea mabasi 

mawili makubwa yaliyokuwa yakieleka 

mjini Moshi na hivyo wote waliokuwa 

wamesimama pale wakapata nafasi 

.Hakuna aliyekuwa akimtazama Lucy 

kutokana na mwanga mdogo uliokuwamo 

ndani ya ile gari lakini Lucy alikuwa 

akitiririkwa na machozi. 

 Gari lilikwenda kwa kasi kubwa na Lucy 

akaomba ashushwe katika sehemu moja 

iliyofahamika kama Denish.Baada ya 

kushuka Lucy akaangaza angaza pande 

zote ili kuona kama kuna mtu yeyote 

anayemfuatilia lakini hakukuwa na mtu 

yeyote maeneo yale.Taratibu Lucy 

akaanza kutembea akiifuata bara bara 

ielekeayo chuoni.Mita kama mia mbili hivi 

akakutana na geti kubwa jeusi. . 

 “Ni hapa.Siwezi kupasahau .Stella alikuwa 

akifanya kazi hapa .Ninapakumbuka vizuri sana.” Lucy akawaza akiwa amesimama 

karibu kabisana geti la kituo cha kulelea 

watoto wadogo ambao wamekuwa 

wakiokotwa sehemu mbali mbali za 

Arusha au wale ambao wazazi wao 

wamekuwa wakifariki na kuwaacha 

wakiwa bado wachanga.Mahala hapa 

aliwahi kuletwa na rafiki yake mmoja 

aliyeitwa Stella ambaye alikuwa akifanya 

kazi katika kituo hiki” Lucy akamtazama 

mwanae akambusu na kumuweka kifuani 

kwake na kisha kwa hatua za kunyata 

akaelekea katika geti lile .Akatandika 

nguo chini na kumlaza mwanae.Akainama 

na kumbusu tena na kisha akaanza 

kuondoka huku akikimbia. 

 “Ee Mungu naomba umlinde mwanangu 

.najua nimefanya kosa kubwa sana 

kumtelekeza mwanangu lakini sina namna 

nyingine ya kufanya.Natumaini utamlinda 

na mabaya yote na hatimaye ataokotwa na 

kutunzwa “ Lucy akaomba Mungu huku 

akikimbia machozi yakimdondoka. 

 “naomba walinzi wa kituo kile wawahi 

kumuokota mwanangu kabla hajadhuriwa 

na wanyama wabaya.” Akawaza Lucy 

akikimbie kuelekea Usa river. ************************ 

 Kwa mbali alisikia muungurumo wa 

gari.Hakuwa na nguvu za kuinuka.Miguu 

yote ilikuwa imekufa ganzi.Alikuwa 

ameanguka amelala pembeni ya bara bara 

na mwili wake ulikuwa umeganda kwa 

baridi kali ya usiku.Hakuweza 

kuyafumbua macho yake .Hakuwa na 

nguvu za kufumbua macho .Baada tu ya 

kumuacha mwanae Anjela katika geti la 

kituo cha kulelea watoto wachanga Lucy 

akaanza kukimbia bila kujua alikokuwa 

akielekea.Alihisi kama 

kuchanganyikiwa.Alikuwa akikimbia 

kuifuata bara bara ya vumbi iliyokuwa 

ikielekea mjini Arusha kutokea Usa river 

.Alikimbia kwa umbali mrefu na 

mwishowe akajikuta akiishiwa nguvu na 

kuanguka kandoni mwa bara 

bara.Hakuweza kuinuka tena 

 Akiwa hana uwezo wa kufanya lolote 

akasikia kama sauti za watu wakijadiliana 

jambo na kisha mwanga mkali 

ukammulika usoni.Taratibu akahisi akinyanyuliwa na kisha kuwekwa katika 

sehemu laini na kufunikwa kitu kizito 

mithili ya blanketi .Akaanza kuhisi joto na 

kisha akapoteza fahamu kabisa. 

************************ 

Sauti kama kitoto kichanga kikilia 

ilimfanya mlinzi aliyekuwa zamu ya usiku 

katika kituo cha kulelea watoto wadogo 

Usa river kuinuka na kuanza kuifuatilia ni 

wapi sauti ile ilitokea na hatimaye 

akagundua kwamba sauti ile ilikuwa 

ikitoka nje ya geti.Akalifungua geti ka 

haraka na kupigwa na mshangao mkubwa 

kwani chini ya geti kulikuwa na kitoto 

kidogo kimelazwa . 

 “Mungu wangu,ni kitoto kichanga” 

akasema kwa mstuko mlinzi yule huku 

akikiendea na kukiinua. 

 “Masiini jamani kitoto bado kidogo 

mno.Ukatili gani huu? Ni wazi kuna mtu 

amekuja na kukitelekeza kichanga hiki 

hapa getini..Masikini mtoto mdogo halafu 

mzuri sana.Wakati wengine wakihangaika 

usiku na mchana kutafuta watoto ,wengine 

waliojaaliwa kupata watoto wanawatupa.Ama kweli dunia imefikia 

ukingoni.” Akasema mlinzi yule akiwa 

amemshika Angela mtoto aliyetelekezwa 

na Lucy.Mlinzi akafunga geti na kuelekea 

ndani ambako alimkabidhi mtoto yule 

kwa wafanyakazi waliokuwa zamu ya 

usiku ambao kwa haraka walianza 

kumuhudumia. 

 “Afadhali huyu aliyekuja kumtupa mtoto 

getini akiamini kwamba anaweza 

akaokotwa na kulelewa kulikoni angeenda 

kumtupa jalalani” akasema mwanamama 

mmoja aliyekuwa amemshika Angela. 

 “Alaaniwe mwanamke aliyefanya kitendo 

kama hiki.Hii ni dhambi kubwa sana 

Kumtupa mtoto mzuri na mwenye afya 

namna hii si haki hata kidogo.” Akasema 

kwa ukali mwanamke mwingine 

aliyekuwa amesimama pembeni 

 “Mwamvita huwezi kujua ni kwa nini 

mama wa mtoto huyu ameamua kufanya 

kitendo kama hiki.Kama alivumilia na 

kulea mimba kwa miezi tisa ,hainiingii 

akilini kama anaweza akamtupa mwanae 

kirahisi rahisi namna hii.Lazima kuna 

sababu ya msingi ya kumfanya aamue 

kumtupa mwanae ” akasema mwanamke mmoja mrefu ambaye alikuwa 

amesimama pembeni 

 “Sikubaliani nawe hata kidogo.Kitendo 

chochote cha kumtupa mtoto kwa sababu 

zozote zile hakikubaliki na ni dhambi 

kubwa mbele za Mungu.Mtoto huyu ni 

mdogo sana na anahitaji malezi ya mama 

yake.Hiki ni kitendo cha uuaji.Ni kwa 

maongozi ya Mungu pekee mtoto huyu 

ameweza kuwa hai mpaka sasa kwa 

sababu angeweza hata kudhuriwa na 

wanyama kama mbwa na hata 

paka.Tafadhali naombeni tusiendelee 

kuliongela suala hili.Kila mmoja 

akaendelee na kazi zake “ akasema kwa 

uchungu Mwamvita ambaye alionekana 

kuchomwa sana na kitendo kilichofanywa 

na mama wa mtoto aliyeokotwa. 

 “Mtoto ana afya nzuri sana.Inakuwaje 

mzazi anakuwa na ukatili mkubwa wa 

namna hii wa kuamua kumtelekeza 

mtoto? Laiti ningemfahamu mama wa 

mtoto huyu angenitambua kwa kweli.Hiki 

ni kitendo cha kikatili sana.Kama hana 

uwezo wa kulea mtoto angekuja hata hapa 

kuomba msaada tungeona namna ya 

kuweza kumsaidia kulikoni kumtelekeza mtoto barabarani.Mtoto huyu amenitia 

uchungu sana .Nitahahakisha kwa muda 

wangu nitakaokuwa nikifanya kazi katika 

kituo hiki ninampa malezi yote kama 

mama “ akawaza Mwamvita ambaye ndiye 

alikuwa mkuu wa zamu hii ya usiku na 

kwa mbali machozi yalikuwa 

yakimdondoka. 

 Angela aliendelea kupatiwa huduma 

mbali mbali na hatimaye akapata usingizi 

akalala.Hakuwa na usumbufu wowote 

ule.Kulipambazuka salama na Angela 

akiwa mzima wa afya tele.Baadae mkuu 

wa kituo akafika na kuonyeshwa mtoto 

aliyeokotwa.Akapatwa na mshangao. 

 “mwanamke gani ambaye anaweza 

akamtupa mtoto mzuri namna hii? 

Akashangaa mkuu wa kituo.Akamshika 

Angela na kumkumbatia. 

 “Ouh my dear baby …from now on your 

name will be Sanya.” Akasema mama huyu 

raia wa Marekani ambaye akishirikiana na 

familia yake wamekuwa wakikiendesha 

kituo hiki kwa miaka kadhaa sasa. 

 “Sanya McNill will be your new name.You 

are now belong to our family” akasema 

bibi Melanie McNill.Kama ilivyokuwa kwa wafanyakazi wengine bibi Melanie naye 

alitokea kuvutiwa sana na Sanya na 

kuamua kumuhesabu kama mmoja wa 

wanafamilia yake.Akampigia simu mume 

wake kumfahamisha kwamba kuna mtoto 

mzuri ameokotwa na ameamua 

kumchukua na kumlea kama mmoja wa 

wanafamilia .Familia yake ilifurahi sana 

kwa uamuzi huo wa mama yao na kuahidi 

kuja Tanzani kumtembelea ndugu yao 

huyo mpya kipindi cha majira ya kiangazi. 




 “Msichana mzuri kama huyu anafanya 

nini usiku wote huu peke yake 

barabarani? Adolf aliyekuwa akiendesha 

gari akamuuliza mwenzake aliyekuwa 

amekaa kiti cha pembeni. 

 “Hata mimi nashindwa kuelewa ni kitu 

gani kimemtokea hadi akawaka sehemu 

hatari kama ile usiku huu mkubwa.” 

Akasema Leonard 

 “Nimemchunguza kwa haraka haraka,ni 

msichna mzuri sana.Ameumbika kiafrika 

haswaa” Adolf akasema  “hata mimi nimeliona hilo.kwa hiyo 

tunafanya nini kuhusiana na msichana 

huyu? Hatumjui,hatujui atokako na wala 

amepatwa na matatizo gani.Unaonaje 

kama tukimpeleka polisi? Leonard 

akashauri 

 “hapana Leonard .Hakuna haja ya 

kumpeleka sehemu yoyote ile.Huyu 

tunaenda naye nyumbani.Tutamchunguza 

anaumwa nini na tutamtibu.” Adolf 

akasema 

 “Tunaenda naye nyumbani? Kama ni 

kumtibu kwa nini basi tusimpeleke 

hospitali tukamkabidhi huko ili atibiwe? 

Leonard akauliza kwa mshangao 

 “Leonard,msichana huyu tunakwenda 

naye nyumbani.Tunamshuhulikia na 

akishapona atakuwa msichana wetu pale 

nyumbani.Tuko wanaume wawili peke 

yetu huoni kwamba tunatakiwa kuwa na 

msichana walau mmoja wa kutuhudumia? 

Nimechoka kila nikihitaji msichana wa 

kulala naye kwenda kutafuta katika 

mabaa.Tukiwa na huyu pale nyumbani 

hatutasumbuka kwenda katika kumbi za 

burudani na klabu za usiku kutafuta 

wanawake wanaojiuza kwa ajili ya kumaliza haja zetu.Huyu atatuhudumia 

kila kitu.Tutakuwa tukimpa matunzo 

mazuri na pesa na yeye atakuwa 

akituhudumia kila pale tutakapokuwa 

tukihitaji huduma ya 

ngono.Nimemuangalia kwa haraka haraka 

na nimemuona ni msichana anayefaa sana 

kuzidi hata wale makahaba ambao 

tumekuwa tukiwafuata katika klabu za 

usiku .Huoni kama hiyo ni plani nzuri 

Leonard? Akasema Adolf kijana 

aliyejengeka vyema kimisuli na mwenye 

nywele ndefu alizozifunga kwa nyuma. 

 “ Adolf hapo umekosea 

kabisa.Sikubaliani nawe katika jambo hilo 

hata kidogo.Huo ni ukatili 

mkubwa.Hatuwezi kumuweka ndani 

msichana halafu tukawa tukimtumia 

kingono.Hilo ni kosa kubwa sana na 

tukibainika tunaweza kufutiwa kibali cha 

kufanya utafiti na kufukuzwa nchini 

Tanzania.Sikushauri tufanye hivyo.Kama 

una lengo la kumsaidia msichana huyu 

tumsaidie lakini si kwa kumuweka 

nyumbani kwetu na kumtumia 

kingono.Kwa hilo mimi siko tayari hata 

kidogo” akasema Leonard.  “Leonard ,msichana huyu tumemuokota 

akiwa hajitambui.Hatujavamia mahala na 

kumteka nyara.Ninakushauri tuende naye 

nyumbani kwetu tumpatie huduma na 

halafu yeye mwenyewe ataamua kama 

atapenda kukaa nasi basi tutaishi 

naye.Kama wewe hutakuwa tayari kupewa 

huduma na msichana huyu mimi 

sikushurutishi lakini mimi nimechoka 

kwenda baa kila siku na kutafuta 

wasichana wanaojiuza.” Adolf akasema na 

kukaa kimya.Alionyesha wazi alikuwa 

amekasirishwa na mawazo ya Leonard. 

 Baada ya kufika nyumbani kwao 

wakamshusha Lucy na kumpeleka hadi 

katika chumba kimoja ambacho hakikuwa 

na vitu zaidi ya kitanda kimoja 

kidogo.Wakamlaza Lucy juu ya kitanda 

kile na kuanza kumfanyia uchunguzi ili 

waone anasumbuliwa na kitu gani.Baada 

ya dakika kama ishirini za kumfanyia 

uchunguzi wakagundua kwamba kiwango 

cha sukari katika mwili wa Lucy kilikuwa 

chini mno na hivyo wakamtundikia chupa 

ya maji yenye dawa maalum ndani yake ili 

kupandisha kiwango cha sukari ya mwili. ************************ 

 Lucy alifumbua macho na kitu cha 

kwanza alichokihisi ni maumivu katika 

mkono wake wa kulia.Akainua kichwa na 

kutazama kilichosababisha maumivu yale 

akakuta mkono wake ukiwa umefungwa 

na mpira uliotoka katika chupa ya maji 

iliyokuwa imefungwa juu ya kitanda 

chake.Akashangaa amefikaje fikaje pale na 

mara kumbukumbu zikaanza kumjia 

kichwani.Akakumbuka kwamba 

alimtelekeza mwanae Angela katika kituo 

cha kulelea watoto wadogo Usa river na 

baada ya hapo akakumbuka kwamba 

alianza kukimbia kwa kasi akiifuata njia 

ya vumbi ambayo hakujua ilielekea 

wapi.Anachokikumbuka ni kwamba 

alikimbia sana na ilipofika mahala 

alishindwa kuendelea kukimbia,hakuwa 

na nguvu tena na kitu cha mwisho 

kukumbuka ni kwamba aliishiwa nguvu 

na kuanguka chini na baada ya muda 

akasikia muungurumo wa gari na sauti za 

watu wakiongea na baada ya hapo hakujua 

tena kilichoendelea hadi muda huu 

alipoamka na kujikuta akiwa katika chumba hiki ametundikiwa chupa ya maji. 

 “Masikini mwanangu sijui atakuwa 

katika hali gani sasa hivi..Mungu nisamehe 

kwa kitendo hiki nilichokifanya.Halikuwa 

kusudio langu kufanya vile lakini 

imenilazimu kufanya hivi kutokana na hali 

ngumu ya maisha 

inayonikabili…Mwanangu….Ang..angel..aa

aaaa” Lucy akauma meno kwa uchungu 

huku machozi yakimtoka.Alikijutia 

kitendo alichokifanya cha kumtelekeza 

mwanae 

 “Mtoto wangu wa kwanza 

nimemtupa….sidhani kama nitakuwa na 

amani katika maisha yangu 

yaliyobakia.Sintamuona tena mwanangu” 

akawaza Lucy akiwa na uchungu mwingi 

 Akiwa bado katika mawazo huku 

machozi yakimtoka,mara mlango wa 

chumba alichokuwamo ukafunguliwa na 

akaingia mzungu mmoja mwenye kifua 

kipana na nywele nyingi. 

 “Ouh ! You are awake….” Akasema 

mzungu yule kwa mshangao huku 

akitabasamu halafu akatoka nje na 

kumuita mwenzake 

 “Leonard she’s awake.Lets go see her”  “real !! How’s she? She can say anything? 

Leonard akauliza maswali mfululizo 

wakati wakitembea kwa kasi kuelekea 

katika chumba alimolazwa Lucy 

 Wakaingia mle chumbani kwa kasi . 

 “Helo Pretty African girl.How are you? 

Akauliza Adolf huku amemuinamia Lucy 

 Lucy akabaki akishangaa .hakufahamu 

lugha ya kiingereza hivyo hakujua ajibu 

nini.Akabaki akiwakodolea macho 

wazungu wale waliokuwa wamesimama 

wakimshangaa. 

 “how do you feel now ? Leonard akauliza 

lakini Lucy hakuwajibu kitu 

 “Can you speak English ? Leonard 

akauliza tena lakini Lucy hakujibu kitu 

 “Try to ask her in Swahili” Leonard 

akamwambia Adolf ambaye alikuwa na 

uwezo wa kuzungumza kiswahili kidogo 

 “U..una…unaweza..zungumuza king..reza 

? Adolf akajaribu kumuuliza Lucy kwa 

kiswahili japo hakikuwa sanifu lakini Lucy 

akamuelewa na kutikisa kichwa ishara ya 

kwamba hawezi kuzungumza kiingereza 

 Adolf na Leonard wakatazamana kisha 

wote wakatabasamu. 

 “Dalili njema.Anaweza kusikia kiswahili Inaonyesha maendeleo yake ni mazuri “ 

Adolf akamwambia Leorand kisha 

akamgeukia Lucy. 

 “Jina…...jina yako nani? ..Adolf 

akamuuliza Lucy 

 “Lucy” Lucy akajibu kwa ufupi 

 “Ouh Lucy.Jina nzuri sana..It’s a good 

name.” 

 “Mimi jina yangu ni Adolf and my friend 

here jina yake ni Leonard” Adolf 

akamwambia Lucy 

“Lucy una…sikiaje mwili..I mean 

unajisikiaje sasa? Mzuri ? Adolf akauliza 

“Najisikia vizuri kwa sasa.” Lucy akajibu. 

 “Ok Lucy edelea kulala…mwili yako bado 

looks so weak” Adolf akasema huu 

akiiangalia ile chupa ya maji 

aliyotundikiwa Lucy .Wakatoka mle 

chumbani na kufunga mlango 

 “Leonard,umeuona uzuri wa Lucy? Adolf 

akauliza 

 “ Hawezi kulingana na mchumba wangu 

Lucia” Leonard akajibu 

 “Lucy ni msichana mzuri.Ana umbo zuri 

mno..” Adolf akasema huku akitabasamu 

 “Lucy ,Lucy wake up” Lucy alisikia 

sauti ya mtu akiongea pembeni yake huku akimpiga piga bagani.Alihisi ni kama vile 

alikuwa akiota lakini alipofumbua macho 

akagundua kwamba haikuwa ndoto.Adolf 

alikuwa pembeni yake akimuamsha 

 “Lucy ..wake up..amuka..its time to 

go..uhmm what do say in Swahili..ku..oga” 

Adolf akajitahidi kuongea kiswahili huku 

akionyesha kwa vitendo ili Lucy aweze 

kumuelewa. 

 Lucy akajitahidi kuinuka pale kitandani 

na Adolf akamshika mkono na kumsaidia 

kutembea na kumuongoza hadi katika 

bafu akamuelekeza jinsi ya kulitumia bafu 

lile la kisasa na kumuacha Lucy mle 

bafuni. 

 Baada ya dakika kama kumi hivi Lucy 

akafungua mlango na kumkuta Adolf 

akiwa amekaa katika kiti akimsubiri.Lucy 

sasa alikuwa akijisikia vizuri baada ya 

kujimwagia maji.Adolf akamuongoza hadi 

katika chumba kingine akamfungulia 

mlango. 

 “Hii ni chumba yako..utalala 

humu…unaonaje mzuri? Adolf akauliza na 

kumfanya Lucy atabasamu na kucheka 

kidogo kutokana na namna Adolf 

alivyokuwa akijaribu kuongea kiswahili  “Ni chumba kizuri sana.Ahsante” Lucy 

akasema na kisha Adolf akaondoka 

 Juu ya kitanda kulikuwa na nguo 

zimewekwa kwa ajili ya 

kubadilisha.Kulikuwa na suruali tatu za 

jeans na fulana nne halafu kukawa na 

nguo za ndani. 

 “Mungu awabariki wazungu hawa kwa 

kuniokoa.Ni watu wakarimu sana.Bila wao 

kuniokota sijui ningekuwa wapi mida hii” 

akawaza Lucy huku akizikagua nguo zile 

kama zinamtosha.Katika chumba kile 

kulikuwa pia na meza ya vipodozi ambayo 

ilikuwa na chupa kadhaa za mafuta ya 

kujipaka pamoja na uturi.Pembeni ya 

chumba hiki kulikuwa na mlango ambao 

baada ya kuufungua akagundua kwamba 

kilikuwa ni choo pamoja na bafu.Lucy 

akatabasamu. 

 “Wazungu hawa wana roho nzuri sana 

tofauti na sisi watu weusi.Waafrika 

wenzangu wamekuwa wakininyanyasa 

kama vile mimi si binadamu mwenzao ” 

Akawaza Lucy huku akijitazama katika 

kioo na kuangalia namna alivyokuwa 

amependeza. 

 “Hapa sielewi hata niko sehemu gani.Ninachoshukuru ni kwamba 

nimeokotwa na wasamaria wema ambao 

wanaweza wakanisaidia hata kunitafutia 

kazi ya kufanya itakayoniwezesha 

kuyaanza upya maisha yangu.” Akiwa 

amekaa kitandani akijaribu kutafakari juu 

ya maisha yake yatakavyoku amlango 

ukagongwa akainuka na kwenda 

kuufungua. 

 “wow ! Amazing !!! Alikuwa ni adolf 

aliyesimama mlangoni pale akiwa na 

mshangao mkubwa baada ya kumuona 

Lucy akiwa amependeza na mavazi yake 

mapya 

 “Lucy you are so beautiful..and sexy” Adolf 

akamwambia Lucy ambaye alibaki 

akitabasamu. 

 “Lucy you can join us for lunch 

now…karibu chakula” Adolf akasema na 

Lucy akaanza kumfuata kuelekea sehemu 

ya chakula. 

 “Leonard…look what I’vee just found 

..she’s amazing..I wonder how sweet she is 

on bed.. cant wait for the night to come” 

Adolf akasema kwa furaha kubwa huku 

akivuta kiti na Lucy akaketi.Wakapata 

chakula na kisha wakaenda kukaa katika meza iliyokuwa mbele ya kibaraza cha 

nyumba .Walikuwa wameizunguka meza 

iliyokuwa na vinywaji vya aina mbali 

mbali.Lucy alichagua juice iliyochorwa 

embe na akina Adolf walikuwa wakinywa 

mvinyo ulikuwa katika chupa kubwa. 

 “Lucy could you tell us your history? I 

mean history yako..umetoka wapi 

..parents wako wako wapi..Do you 

understand what I mean.Sorry I speak a 

very little Swahili..” Adolf akasema na 

kumfanya Lucy atabasamu.Alielewa 

alichokuwa ameulizwa. 

 “Mimi ninatokea mkoa wa 

Singida..Nimekuja hapa mjini kutafuta 

kazi.nyumbani kwetu ni masikini sana.Je 

mnaweza mkanisaidia kupata kazi? Kazi 

yoyote ile mimi ninaweza kuifanya” Lucy 

akasema kwa ufupi 

 “She says she’s from Singida region and 

she’s here to find a job .She says she comes 

from a very poor family and she is asking if 

we could help her find any kind of job” 

Adolf akamwambia Leonard ambaye 

hakufahamu kiswahili. 

 “Lucy .dont worry about work….utakaa 

na sisi hapa and we will be paying you lots of money..I mean kaa na sisi hapa and 

uhhmm tutakupa money that you will send 

to your family back home” Adolf ambaye 

tayari alikwisha anza kuonyesha dalili za 

kulewa akasema na kumfanya Lucy 

atabasamu. 

 “Namshukuru Mungu kwa bahati hii 

kubwa.Sikutegemea kama ningeweza 

kupata kazi mapema namna hii.Ninafurahi 

kufanya kazi kwa watu wema kama hawa” 

akawaza Lucy 

 Waliendelea kupata vinywaji pamoja na 

maongezi .Muda mwingi walionekana 

kama wamemsahau Lucy kwa sababu 

walikuwa wakiongea wao peke yao 

kiingereza ambacho Lucy hakuwa 

akifahamu hata neno moja.Lucy mawazo 

yake yote yalikuwa ni kwa mtoto wake 

aliyemtelekeza ambaye mpaka wakati huo 

hakujua alikuwa katika hali gani. 

 Jua lilizama na kulipisha giza lichukue 

nafasi yake.Adolf akatazama saa yake 

ilikuwa ni saa mbili za usiku.Akawaomba 

Lucy na Leonard waingie ndani na kupata 

chakula cha usiku.Kilikuwa ni chakula 

ambacho kilikuwa katika maboksi na 

hakikuhitaji kupikwa tena.Lucy hakuwahi kula chakula cha namna hii Baada ya kula 

Lucy akasimama na kuondoa vyombo 

akavipeleka katika sehemu ya 

kuoshea.Tayari alianza kuizoea nyumba 

ile.Akiwa ameishika sahani ya kwanza 

kwa lengo la kuisuuza akastukia mikono 

minene yenye nywele nyingi ikimshika 

kiuno chake.Akageuza kicha chake 

akakutana na sura ya Adolf ambaye 

hakuwa na wasi wasi hata chembe .Lucy 

akasimama hakujua afanye nini na bila 

kujali Adolf akakiachia kiuno cha Lucy na 

kuipandisha mikono yake hadi kifuani na 

kuanza kuyachezea matiti yaliyojaa ya 

Lucy.Ghafla Lucy akaiachia sahani 

aliyoishika ikaanguka chini.Adolf hakujali 

akaendelea na zoezi lake la kuuchezea 

mwili wa Lucy ambaye kwa hasira 

akajaribu kumsukuma Adolf lakini 

mikono yenye nguvu ya Adolf ikamdhibiti 

bara bara.Akajitahidi kufurukuta lakini 

hakuweza.Kwa nguvu Adolf akamuinua 

Lucy na kumtupa katika sofa. 

 “Its ok African girl..don’t cry ..don’t 

cry..you are gonna enjoy this…I’m sure you 

will “.Akasema Adolf huku akiivua suruali 

yake na kubakiwa na nguo ya ndani kisha akamfuata Lucy aliyekuwa amekaa akilia 

pale sofani.Akaivuta kwa juu na kuivua 

fulana aliyokuwa ameivaa Lucy na kisha 

akataka kumvua suruali lakini Lucy 

akajikunja na kumzuia Adolf asiweze 

kufanya alivyotaka.Kitendo kile 

kikamuudhi Adolf ambaye akamnasa 

kibao kikali Lucy na kumfanya aanguke 

chali pale sofani na kisha kwa nguvu 

akamvua suruali na Lucy akabakiwa na 

nguo ya ndani ya rangi nyekundu 

 “Uhuuuu !! what a sexy girl” akasema 

Adolf kisha akaivuta nguo ile ya ndani ya 

Lucy ambaye baada ya kupigwa kibao kile 

hakutaka tena kuendelea kubishana na 

mzungu yule kwa kuogopa kupgwa 

zaidi..Adolf alikuwa akitetemeka mwili 

kwa ashki alizokuwa nazo baada ya 

kumshuhudia Lucy akiwa mtupu na bila 

kupoteza wakati akaanza kumuingilia 

Lucy kwa kasi.Lucy akapiga kelele lakini 

kelele zake hazikusaidia kitu chochote 

kwani Adolf aliendelea na kitendo chake 

kwa nguvu.Huku akipiga kelele Adolf 

akafika mshindo na kuanguka kifuani kwa 

Lucy huku akihema kwa nguvu.Baada ya 

sekunde kadhaa za kulala kifuani kwa Lucy Adolf akainuliwa na kusukumwa 

pembeni na Leonard ambaye uume wake 

ulikuwa umesimama wima akashika 

usukani na kuendelea na kitendo kile.Lucy 

hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia na 

kutoa kila aina ya laana kwa wazungu 

wale . 

 Adolf na Leonard wakaendelea kufurahia 

kitendo walichokuwa 

wakikifanya.Walipohakikisha 

wameridhisha nafsi na miili yao 

wakamshika mikono Lucy ambaye kwa 

wakati huo hakuwa na nguvu kabisa 

wakamburuza hadi katika chumba chake 

walichomuandalia wakamlaza kitandani 

na kisha wakafunga mlango kwa funguo 

 “wow ! it was fantastic….I real enjoyed 

it..uupphhh…I need more whisky “ 

akasema Leonardo ambaye awali alikuwa 

mpinzani mkubwa wa Adolf kuhusiana na 

kumuweka Lucy pale ndani kwao na 

kumtumia kingono. 

 “You see ..you see.. I told you man …this 

lady is going to bring more fun in the house…” akasema Adolf kisha 

wakaendelea kunywa mvinyo hadi usiku 

wa manane 

 Taratibu Lucy akaanza kurejewa na 

nguvu akainuka pale kitandani na 

kukaa.Picha ya kitendo alichofanyiwa na 

wazungu wale ikamjia kichwani akaanza 

kulia kwa nguvu. 

 “Ee Mungu nafahamu nimekukosea sana 

na ndiyo maana ninapata mateso 

makubwa namna hii.Pamoja na yote 

niliyokukosea ee Mungu naomba 

unisamehe na uniondolee adhabu hii iliyo 

juu yangu kwani nimekuwa ni mtu wa 

kudhalilishwa kila mara.Maisha yangu 

yamekuwa ni ya kutanga tanga na hayana 

furaha hata chembe.Najua wewe ndiye 

mwenye kupanga kila jambo litokee na 

ninakuomba ee Mungu pamoja na makosa 

yangu yote niliyokukosea unitoe katika 

mateso haya makubwa niliyonayo kwa 

sasa kwani nimenasa katika nyumba hii na 

sijui namna ya kutoka.Naomba 

unionyeshe njia ya kutoka ee Mungu 

wangu” Lucy alikuwa akiomba huku akilia 

machozi kwa uchungu mkubwa.Kila 

alipojiangalia alilia sana.Hakuiona thamani ya utu wake. 

 “Ninakubaliana na mawazo yangu 

kwamba mwanaume wangu wa kwanza 

kufanya naye mapenzi katika hii dunia 

alinipa mkosi na ndiyo maana maisha 

yangu yamebadilika na kuwa ya mateso 

namna hii.Nikikumbuka huko nyuma 

maisha yangu yalikuwa mazuri na yenye 

furaha japokuwa nilikuwa nikifanya kazi 

majumbani kwa watu.Mara tu baada ya 

kufanya mapenzi na Jack mikosi ilianzia 

pale,nikafukuzwa kazi,nikapoteza fedha 

zangu kwa Pendo ambaye bila huruma 

aliniuza kwa watu ambao walinidhalilisha 

bila kujali haliyangu ya ujauzito .Sitaki 

hata hata kukumbuka kitendo kile.Mara 

yangu ya kwanza kufanya mapenzi na 

mwanaume wangu wa kwanza nilijikuta 

nikipata mimba na nikajifungua mtoto 

wangu wa kwanza katika mazingira 

magumu.Mkosi umeendelea kuniandama 

kwani mtoto wangu wa kwanza nilimtupa 

na sijui kama bado yuko hai .Nimeokotwa 

na hawa wazungu nikaamini niko katika 

mikono salama lakini kumbe nimejipeleka 

mwenyewe mdomoni mwa mamba.Bila 

huruma wazungu hawa wamenidhalilisha,wamejifurahisha na 

kuja kunifungia humu chumbani.Ni mkosi 

gani huu nilionao mimi ..!! “ akawaza Lucy 

huku akiuma meno kwa hasira kali na 

kuendelea kuangusha machozi. 

 “Sioni hata faida ya kuendelea kuishi 

maisha kama haya.Nina faida gani katika 

hii dunia?Sioni maana ya mimi kuendelea 

kuishi katika dunia hii iliyojaa mateso 

makubwa .Kila kukicha matatizo 

yananiandama mimi.Ni bora tu kama 

nikijitoa uhai kwa sababu sina faida 

yoyote hapa duniani zaidi ya kuteseka” 

akawaza Lucy huku akiinuka pale 

kitandani akasimama akaangalia juu ya 

dari akiwa na dhumuni la kutaka kujitoa 

uhai lakini mara sura ya mwanae mchanga 

ikamjia usoni akakaa tena kitandani 

 “masikini mwanangu Angela sijui kama 

bado ni mzima hadi hivi sasa.Hapana 

siwezi kujiua.Natakiwa nitafute namna ya 

kutoka katika nyumba hii na kwenda 

kutafuta maisha mazuri.Nikifanikiwa 

kupata maisha mazuri itanilazimu 

kumtafuta mwanangu kama bado ni 

mzima.” Akawaza Lucy na kisha akakaa 

kitandani  “Sikutegemea kama watu hawa 

wangenifanyia hivi.Niliwaona kama watu 

wema na nikawa na matumaini labda 

wangeweza kunisaidia katika maisha 

yangu haya magumu lakini kumbe wao 

wameyafanya yawe magumu 

zaidi.Nitafanya nini sasa?’Kila alipowaza 

na kufikia hapa alishindwa kupata jibu 

nini afanye ili aweze kutoka katika 

nyumba hii ya wazungu.Pembeni kabisa ya 

chumba hiki kulikuwa na mlango wa kioo 

kizito,Lucy akainuka na kwenda 

kuufungua mlango ule na akakutana na 

chumba kidogo kilichokuwa na choo na 

bafu.Akasimama pale mlangoni na kisha 

akavua nguo akajimwagia maji ya moto 

yaliyokuwa yakitoka katika bomba la 

kuogea.Baada ya kuoga akazishika nguo 

zake mkononi na kwenda kukaa 

kitandani.Akaziangalia nguo zile kwa 

hasira akazitupa chini .Baada ya dakika 

kadhaa akainuka na kwenda katika kabati 

la ukutani akafungua na kuchukua suruali 

moja na fulana akavaa akapanda 

kitandani na kujifunika blanketi. 

 “Nikifanikiwa kutoka salama katika 

nyumba hii nitaelekea wapi? Sina fedha sina mahala pa kwenda na sina mtu 

mwingine yeyote ambaye anaweza 

akanipa msaada wa kifedha.Nitaishi vipi? 

Nitaishi wapi? “ Maswali haya yaliendelea 

kukitesa kichwa cha Lucy na mwishowe 

usingizi ukamchukua akalala. 

Alikuwa ni Leonard ambaye alimuamsha 

Lucy kutoka katika usingizi .Kwa jinsi 

alivyokuwa amepitiwa na usingizi hakuwa 

na habari kama kumepambazuka.Leonard 

alikuwa na sinia lililokuwa na kikombe 

cha chai,glasi ya juice ,mkate pamoja na 

matunda ya aina mbali mbali. 

 “wake up pretty….” Akasema Leonard 

huku akimtikisa Lucy aamke.Lucy 

akastuka na kukurupuka kama mtu 

aliyekuwa ndotoni na kulitupa shuka chini 

mara akajikuta akitazamana na Leonard 

aliyekuwa amesimama pembeni ya 

kitanda akiwa na sinia lililosheheni mlo 

wa asubuhi.Lucy akamuangalia Leonard 

kwa macho makali sana baada ya 

kukumbuka kitendo walichomfanyia jana. 

 “How you feeling….? Akauliza Leonard 

kwa upole lakini Lucy hakumjibu kitu 

badala yake akasonya kwa nguvu na kumfanya Leonard ambaye hakuwa 

akifahamu kiswahili aliweke sinia lile la 

stafstahi chini na kutoka akamfuata Adolf 

aliyekuwa akitengeneza gari . 

 “Adolf you better go and talk to the 

girl.She looks so angry like a wounded 

buffalo” Leonard akamwambia Adolf. 

 “ Ok let me go see her” Adolf akasema 

huku akichukua kitambaa na kufuta 

mikono yake iliyokuwa imetapakaa 

mafuta ya gari.Taratibu akaufungua 

mlango wa chumba cha Lucy na kumkuta 

akiwa amejikunyata kitandani akilia. 

 “Lucy…una.lia..nini ? why you cry? 

Akasema Adolf huku akimsogelea Lucy na 

kumshika bega lakini kwa hasira Lucy 

akaushika mkono wake na kuurusha 

pembeni 

 “Mashetani wakubwa nyie..Nilitegemea 

nyie ni watu wazuri kumbe mna roho 

mbaya kama za wanyama” Lucy akasema 

kwa ukali 

 “Calm down Lucy..You don’t have to 

panic…I know why you are angry with 

us..You don’t have to be angry with us 

because we’re friends.You will live with us 

and we will payyou….Usika..kasirika.Lucy..sisi ..I mean I 

and my friend Leonard ni rafiki yako na 

tutapatia wewe pesa mingi kila 

siku…sawa? Akasema Adolf huku akiingiza 

mkono mfukoni na kutoa pochi yake 

akahesabu noti kumi za elfu kumi kumi na 

kumpatia Lucy. 

 “Tutapatia wewe..pesa mingi kila siku 

…wewe takaa hapa..fanya kazi with us and 

we’ll pay..you…You benefit from us and u 

entertain us just a bit..Sisi tunakwenda 

fanya tafiti mbali and tukirudi hapa 

..tu.mechoka.wewe patia sisi huduma and 

we give you money..hapana ogopa .Sisi 

patia wewe pesa mingi..sawa? Adolf 

akamwambia Lucy ambaye alikuwa 

amekaa pale kitandani akimsikiliza Adolf. 

 “Ok Lucy pata breakfast “ akasema Adolf 

huku akiliinua sinia lile na kuliweka 

mezani kisha akatoka 

 “Sina fedha na wazungu hawa 

wamenipatia shilingi laki moja kwa 

unyama walionifanyia jana fedha ambazo 

siwezi kuzikataa na kama nilimuelewa 

vizuri huyu jamaa amesema kwamba 

kama nikiendelea kukaa hapa watakuwa 

wakinilipa fedha kila siku.Kama wakinipa shilingi laki moja kila siku baada ya mwezi 

mmoja nitakuwa na fedha za kutosha 

kuniwezesha kuanzisha maisha 

yangu.Lakini inawezekana kweli 

wakanilipa kiasi hiki cha pesa kila siku 

kwa kuwafanyia kazi za ndani pekee?? 

Hapana lazima watakuwa wananitumia 

kimapenzi na ili kunipoza moyo ndiyo 

maana wananilipa kiasi hiki kikubwa cha 

pesa.Iweje nikubali kuudhalilisha utu 

wangu kwa sababu ya pesa japokuwa ni 

masikini? Kwa nini watu hawa hawana 

huruma hata kidogo dhidi ya binadamu 

wenzao? Lakini hata hivyo Itanibidi 

kuvumilia kukaa katika nyumba hii ili 

niweze kukusanya pesa za kuanzia maisha 

japokuwa nafahamu kwamba nitakuwa 

nikitoa machozi kila siku kutokana na 

vitendo nitakavyofanyiwa .Sina namna 

nyingine ya kufanya zaidi ya kukubali 

kuishi nao kama watakuwa wakinilipa 

fedha kwa sababu hata kama nikienda 

mtaani sintakuwa na kitu chochote cha 

kufanya.Sina fedha na sina mahala pa 

kuishi.Ngoja nivumilie kukaa na hawa 

wazungu ili niweze kutengeneza mtaji 

ambao utaniwezesha kufungua biashara mara baada ya kutoka hapa” akawaza Lucy 

na kisha akazichukua fedha zile 

akazihesabu na kuziweka katika lile 

kabati la ukutani halafu akarejea na 

kuingia bafuni akajimwagia maji na kisha 

akapata kifungua kinywa. 

 “Adolf have you talked to her? What she 

said ? Leonard akauliza baada ya kumuona 

Adolf akiwa na uso wenye furaha. 

 “Everything is ok brother. Though she 

didn’t say but she agreed to stay with us” 

Adolf akasema 

 “How did you convince her? 

 “Its just money..I gave her money and she 

didn’t say a word again.” 

 “wow ! so that means we have fun 

everyday in here “ akasema Leonard kwa 

furaha huku wakigonganisha mikono. 

 “How do you see a black girl” Adolf 

akauliza 

 “She’s so good…she makes me love 

Africa.Black girls are amazing” akasema 

Leonard na kisha wakaendelea na 

kutengeneza gari lao.Gari lilipokuwa 

tayari Adolf akarejea tena chumbani kwa 

Lucy. 

 “Lucy make youself at home…this is you home..feel free.Hapana ogopa sisi..sikia 

wewe huru na fanya kazi muzuri sisi lipa 

wewe pesa mingi sawa?” adolf akasema na 

kumfanya Lucy atabasamu 

 “Sawa..” akajibu Lucy na kumfanya Adolf 

atabasamu pia 

 “Good . Lucy..now come and join 

us…make your safe at home” Adolf 

akasema kwa furaha na kumshika mkono 

Lucy na kuanza kumuonyesha sehemu 

mbali mbali za nyumba ile kama sehemu 

za kufulia ,kupika nakadhalika. 

 “Lucy wewe fanyia sisi kazi muzuri..sisi 

nafurahi na kukupa pesa mingi na kama 

tutaweza sisi beba wewe Ulaya..sawa? 

Akasema Adolf na kumfanya Lucy 

atabasamu bila kusema chochote.Siku 

hiyo yote Adolf na Leonard walishinda 

nyumbani na Adolf alifanya kazi ya 

kumfundisha Lucy namna mbali mbali za 

kupika aina mbali mbali za vyakula .Jioni 

ilipofika wote wakajumuika katika meza 

na kwa mara ya kwanza wakamshawishi 

Lucy anywe mvinyo ambao ulimfanya 

akalewa sana na kama ilivyokuwa jana 

yake Adolf na Leonard wakamuingilia kwa 

zamu hadi pale waliporidhika na kisha wakamrudisha Lucy chumbani kwake 

akiwa hajitambui.Toka siku hiyo Lucy 

akawa mtumwa wa ngono wa wazungu 

hawa..Alifungiwa ndani na hakuweza 

kupata nafasi ya kutoroka kutokana na 

uimara wa jumba hili.Kila walipotoka na 

kwenda katika tafiti zao walihakikisha 

kwamba Lucy amefungiwa katika chumba 

maalum ambacho kilikuwa imara na 

ambacho isingekuwa rahisi kutoroka na 

waliporudi kutoka safari zao 

walijifurahisha juu ya mwili wa Lucy.Hayo 

ndiyo yakawa maisha ya Lucy na hakujua 

ni lini angeweza kuwa huru na 

kuondokana na utumwa na udhalilishaji 

huu mkubwa.Japokuwa alikuwa akilipwa 

fedha ambazo alizihitaji sana kwa ajili ya 

kuanzisha maisha yake pindi atakapotoka 

katika jumba hili lakini kila siku usiku 

Lucy alikuwa akitoa machozi na 

kumuomba Mungu amsaidie ili aweze 

kupata upenyo wa kuchomoka katika 

jumba lile.Kadiri siku zilivyozidi kwenda 

Lucy alijikuta akishindwa kuendelea 

kuvumilia na vitendo alivyokuwa 

akifanyiwa.Kilichomuuma zaidi ni siku 

ambayo Adolf na Leonard walikuja na rafiki zao wawili na wote wanne baada ya 

kulewa mvinyo wakamfanyia Lucy 

udhalilishaji mbaya sana.Siku hiyo alilia 

mno lakini hakuwa na namna ya kuweza 

kutoka katika jumba lile. 




Maisha yaliendelea kuwa magumu sana 

kwa upande wa Lucy.Kila siku alikuwa 

akilia machozi mengi na kumuomba 

Mungu ampe njia ya kuweza kutoka ndani 

ya nyumba ile ya wale wazungu.Alikwisha 

choka na udhalilishaji aliokuwa 

akifanyiwa kila siku kwa kufanywa 

mtumwa wa ngono wa wale 

wazungu.Machozi mengi yalikuwa 

yakimtoka kila siku usiku baada ya 

kuwastarehesha wale wazungu na kisha 

wakamlipa fedha. 

 "Nitaendelea kufanyiwa unyama wa 

namna hii mpaka lini? Nimechoka sasa na 

mambo ninayofanyiwa humu.Japokuwa 

wananilipa lakini fedha wanazonilipa si 

sawa na thamani ya utu wangu 

wanaoudhalilisha kwa sababau tu mimi ni 

masikini na sina namna nyingine ya kufanya.Lazima nitafute namna ya kuweza 

kutoka katika nyumba hii na kwenda 

kuanza maisha yangu.Kiasi cha pesa 

nilichonacho kwa sasa kinanitosha kabisa 

kuweza kuanza maisha yangu kwa 

kuendesha biashara japo ndogo.Lazima 

nitafute njia niweze kuondoka humu..." 

akawaza Lucy huku machozi 

yakimdondoka.Alikuwa amekaa kitandani 

kwake akiwasubiri akina Adolf warudi 

kutoka katika safari zao ili aweze 

kuwastarehesha kama ulivyokuwa 

utaratibu.Hakutakiwa kulala hadi 

wazungu wale warejee na kisha 

awastareheshe kwa kufanya nao mapenzi 

na baada ya hapo humlipa pesa kiasi 

chochote wanachotaka kwa siku hiyo na 

mara nyingie hawakumpa kitu.Kila 

watokapo asubuhi hubaki wamemfungia 

Lucy kiasi ambacho si rahisi kwa yeye 

kuweza kutoroka.Toka siku ya kwanza 

aliyoingia katika nyumba hii hakuwahi 

tena kutoka nje japo kuchungulia 

mandhari yake ikoje na wala hakufahamu 

pale walipo ni maeneo gani.Kuna nyakati 

Lucy alifikiria pengine kuwawekea sumu 

katika chakula wazungu wale waweze kufa ili aweze kupata nafasi ya kutoroka 

lakini moyo wake ukawa mzito sana 

kufaya hivyo akihofia endapo atakamatwa 

anaweza akaozea gerezani.Mipango yake 

ilikuwa ni kwenda kuanziasha biashara 

mara tu atakapopata nafasi ya kutoka 

katika nyumba hii na baadae aanze kazi ya 

kumtafuta mwanae ambaye hakujua kama 

alikuwa hai au ameshakufa. Kila 

alipomuwaza mwanae Angela alilia sana 

na kujilaumu kwa ukatili alioufanya wa 

kumtelekeza mtoto wake.Alijifananisha na 

muuaji kwa kitendo alichomfanyia 

mwanae. 

 Siku zilizidi kukatika na Lucy bado 

akiendelea kuwa mtumwa wa ngono wa 

wazungu hawa wawili.Siku moja Adolf na 

Leonard walikuwa wamekaa sebuleni 

wakiongea huku wakitazama televisheni 

na katika meza ndogo kulikuwa na chupa 

kadhaa za mvinyo kama ilivyo kawaida 

yao.Siku hii ya leo walionekana kutokuwa 

na habari kabisa na Lucy .Ilionekana 

walikuwa na jambo zito la kulijadili.Hali 

hii ilimshangaza hadi Lucy kwa sababu 

kwa siku hii ya leo walirudi mapema sana 

nyumbani kupita kawaida yao na toka waliporudi walikuwa wamekaa sebuleni 

wakiongea kiingereza na kunywa mvinyo 

kwa fujo.Mkononi Adolf alikuwa ameshika 

karatasi fulani ambayo alikuwa akiisoma 

na kuirudia tena na tena . 

 " Leonard " akaita Adolf 

 " Unasemaje Adolf? Leonard akaitika kwa 

unyonge 

 " Najaribu kuisoma barua pepe hii lakini 

bado sijaelewa sababu ya sisi kuhamishwa 

na kupelekwa nchini Brazil wakati bado 

utafiti wetu haujamalizika.Unadhani kuna 

jambo tutakuwa hatujalifanya 

inavyotakiwa? akauliza Adolf akiwa 

ameishika ile karatasi mkononi.Leonard 

akainua glasi yake ya mvinyo akanywa 

funda kubwa na kusema 

 " Sina hakika kama kuna jambo ambalo 

hatujafanya sawa.Kila kitu tumekifanya 

kwa mujibu wa taratibu.Nafikiri lengo la 

kutuhamisha ni kujaribu kutujengea 

uzoefu zaidi ." akasema Leonard ambaye 

kwa muonekano wake ni kijana mtaratibu 

sana . 

 " Taarifa hii inatutaka tujiandae na baada 

ya siku mbili tuwe tumeondoka kwani 

taratibu zote za safari zinashughulikiwa na ofisi yetu ya Dar es salaam.Tutafanya 

nini na huyu Lucy? akauliza tena Adolf 

 " Hata mimi suala hili la Lucy limekuwa 

likinumiza kichwa sana kwa sababu iwapo 

tutamuachia huru kabla hatujaondoka 

anaweza akaenda kutushitaki na 

tukakakamatwa kabla hatujaiacha ardhi 

ya Tanzania .Unajua Adolf kitendo 

tulichomfanyia Lucy si kitendo cha 

kibinadamu hata kidogo.Tumemchukua 

msichana huyu na kumuweka ndani na 

kumtumia kingono kwa muda mrefu.Hii si 

sawa hata kidogo.Dhamiri yangu inanisuta 

sana kwa mambo yote tuliyomfanyia Lucy. 

Nasikia uchungu sana 

moyoni..Inatu................." Leonard akasema 

lakini Adolf akaonekana kukerwa na 

maneno yake na kabla Leonard hajamaliza 

alichotaka kukisema Adolf akaingilia kati. 

 " Leonard huu si wakati wa kulamuiana 

au kuhisi una hatia.Hakuna jambo baya 

tulilolifanya kwa sababu kila 

alipotuhudumia tulimlipa pesa. Hata yeye 

mwenyewe alikuwa akipata raha na ndiyo 

maama alikuwa akitoa 

ushirikiano.Kumbuka msichana huyu ambaye unamuonea huruma tulimuokota 

usiku mnene akiwa peke yake na sisi ndio 

tuliyaokoa maisha yake .Tumemuhifadhi 

hapa kwetu na kumhudumia kwa kila 

kitu.Tulichokifanya ni halali kabisa na 

wala usiwe na wasi wasi .Kuna mambo 

mawili hapa ambayo tunatakiwa 

tuyafanye kuhusiana na Lucy.Taarifa 

inasema kwamba kesho atakuja Dr 

Shanon ambaye ndiye atakayeishi humu 

baada ya sisi kuondoka.Taarifa 

inatuelekeza kwamba tumuonyeshe Dr 

Shanon mazingira ya nyumba ili aone 

kama anaweza akaishi hapa au atafutiwe 

nyumba nyingine.Tunachotakwia 

kukifanya hapa ni kumficha Lucy ili 

Shanon asiweze kumuona.Kuna kile 

chumba ambacho huwa tunahifadi spea za 

gari pamoja na matairi,kule ndiko 

tutakakomficha Lucy.Tutamnywesha Lucy 

dawa ya usingizi na akisha lala 

tutamchukua na kumficha kule na Dr 

Shanon atakapoondoka tutamrudisha 

Lucy katika chumba chake.Dr Shanon 

baada ya kuiona nyumba atakuwa na 

safari ya kuelekea hifadhi ya Ngoro ngoro 

ambako atakaa kwa siku mbili na kisha atarejea na kutukuta sisi tayari 

tumekwisha ondoka.Atazikuta funguo 

katika ofisi zetu ndogo za hapa Arusha. 

Atakapokwenda kuitazama nyumba 

atakutana na Lucy na wakati huo sisi 

hatutakuwepo tena Tanzania na hata 

kama tukiulizwa itakuwa rahisi kwetu 

kukataa kwamba hatumjui mtu 

huyu.Unaonaje mpango huu Leonard? 

akauliza Adolf na mara uso wa Leonard 

ukajenga tabasamu pana sana. 

 " Adolf wewe ni mtu mwenye akili 

nyingi.Nafurahi sana kufanya kufanya kazi 

nawe .Umewaza kitu cha muhimu sana 

ambacho kitatusaidia sisi kuondoka hapa 

Tanzania bila kuingia matatizoni kwa 

sababu ya huyu msichana.Tutafanya kama 

ulivyoshauri" akasema Leonard kwa 

furaha kisha wakagonganisha glasi. 

 " Nasikitika sana kumuacha mrembo 

huyu wa kiafrika anayevutia.Afrika 

imejaaliwa kuwa na wanawake wazuri 

mno " akasema Adolf huku akicheka 

 Waliendelea kunywa mpaka saa saba za 

usiku.Lucy bado alikuwa macho akisubiri 

pengine angekuja kuchukuliwa ili aende 

akawastareheshe wale wazungu lakini mpaka inafika saa nane kasoro za usiku 

hakuwa ameitwa.Akiwa ameanza kusinzia 

mlango wa chumba chake ukagongwa kitu 

ambacho hakikuwa kawaida. Siku zote 

kama wakimuhitaji hawakugonga mlango 

bali huingia moja kwa moja lakini kitendo 

cha leo cha kugonga mlango 

kikamshangaza kidogo Lucy.Akainuka na 

kwenda kufungua mlango akakutana na 

Adolf. 

 " Lucy mimi nakuja kuaga 

wewe.Nakweda lala.Leo wewe napumzika. 

sawa? sisi hapana fanyia tena wewe ile 

mambo ya sex ..sawa? Gud night .." 

akasema Adolf katika hali ya ulevi.Lucy 

akabaki akishangaa. 

 Hakukuwa na siku hata moja ambao 

wazungu hawa waliongea naye katika hali 

ya urafiki namna ile. 

 " Kuna nini leo? siku zote wakilewa 

wamekuwa wakija na kunichukua na 

kunifanyisha mapenzi tena kwa nguvu 

sana nashangaa leo anakuja na kusema 

kwamba hawatanifanyia tena mambo haya 

ambayo wamekuwa 

wakinifanyia.Yawezekana Mungu 

amesikia kilio changu na kuwafanya washenzi hawa kugundua kwamba 

kitendo walichokuwa wanakifanya si 

kitendo kizuri.Nimedhalilika sana kwa 

sababu ya umasikni wangu.Nikitoka 

katika nyumba hii nitafanya kazi kwa bidii 

sana ili siku moja niweze kuondokana na 

umasikini huu nilionao ambao umeufanya 

utu wangu ukose thamani.Kwa kuwa 

tayari nina kiasi cha pesa cha kutosha 

kuanzisha biashara nitafanya kazi kwa 

juhudi sana ili niwze kuondoka katika 

umasikini na baada ya hapo nitaanza 

juhudi za kumtafuta mwanangu Angela 

kujua kama bado atakuwa hai.Masikini 

mwanangu..sijui kama atakuwa aliokotwa 

au alifariki kabla hajaonwa na mtu yeyote 

yule.Kitendo hiki nilichokifanya ni kitendo 

cha kinyama sana .Lakini nilifanya vile 

kutokana na umasikini mkubwa niliokuwa 

nao kwa sababu kwa wakati ule sikuwa na 

mbele wala nyuma. Sikuwa na mwelekeo 

na sikujua ningeishi vipi na mtoto yule." 

Lucy akawaza akiwa bado amesimama 

pale mlangoni.Taratibu akafunga mlango 

na kurudi kitandani kwake.Akakaa 

akawaza sana halafu akalala.  

 *************************************

** 

 Asubuhi na mapema siku iliyofuata 

Adolf na Leonard waliamka na kufanya 

usafi kila sehemu ya nyumba.Lucy 

alipoamka aliwakuta wakiendelea na 

zoezi la usafi.Adolf akamwambia Lucy 

kwamba siku hiyo yeye hakutakiwa afanye 

kazi yoyote ile zaidi ya kupumzika.Lucy 

akatabasamu kwa mabadiliko yale ya 

ghafla ya wazungu wale.Walianza 

kuonekana ni wema na wenye 

huruma.Akarudi chumbani kwake 

kupumzika na kuwaacha akina Adolf 

wakiendelea na kazi.Walipomaliza kazi ya 

usafi wakaelekea jikoni ambako Adolf 

alianza maandalizi ya mlo wa 

asubuhi.Mida hiyo ilipata saa tatu za 

asubuhi. 

 " Adolf fanya haraka haraka muda 

unakimbia sana. Dr Shanon atafika hapa 

saa nne asubuhi hii." akasema Leonard. 

 Adolf akatengeneza stafstahi na kisha 

akaandaa meza.Katika glasi ya juice 

ambayo ilikuwa maalum kwa ajili ya Lucyiliwekwa dawa ya usingizi itakayomlaza 

Lucy.Kila kitu kilipokuwa tayari Adolf 

akaenda chumbani kwa Lucy na kumuita 

ajumuike nao katika kupata kifungua 

kinywa.Lucy alibaki akitabasamu kwa 

wema huu mkubwa waliounyesha 

wazungu hawa. 

 Hakukuwa na maongezi mengi sana 

mezani na baada ya kumaliza kupata 

kifungua kinywa Lucy akaambiwa 

akaendelee kupumzika. 

 " Ndani ya dakika tano tayari dawa 

itaanza kufanya kazi." adolf akasema 

akimweleza leonard 

 " Anatakwa alale haraka sana kabla ya Dr 

Shanon hajawasili hapa" akasema Leonard 

 " usiwe na hofu Leonard.Atalala muda si 

mrefu" akajibu Adolf huku akiiangalia saa 

yake. 

 Lucy baada ya kufika chumbani kwake 

alianza kusikia macho mazito akaamua 

kujitupa kitandani . 

 " Mbona nimeanza kuhisi macho mazito 

sana na kuhisi usingizi ghafla? 

Inawezekana labda ni kwa sababu 

nimekuwa nikilala usiku mwingi kila siku 

." akawaza Lucy huku taratibu akianza kusinzia . 

 Baada ya dakika kumi toka Lucy aende 

chumbani wkake Adolf na Lenard 

wakaenda katika chumba cha Lucy 

wakagonga mlango lakini hakukuwa na 

majibu yoyote. 

"Tayari amekwisha lala.nilikwambia dawa 

ile si mchezo" akasema Adolf huku 

akitabasamu na kukiminya kitasa cha 

mlango ukafunguka wakaingia ndani.Lucy 

alikuwa amelala fofofo hajitambui.Adolf 

akamsogelea na kumtikisa huku akimuita 

jina lake lakini Lucy hakuweza 

kuamka.Akatabasamu kisha wakamuinua 

wakamtoa katika chumba kile na kwenda 

kumficha katika chumba kidogo ambacho 

huwa wanakitumia kuhifadhia matairi na 

vifaa vingine vya gari.Chumba kile kidogo 

kikafungwa kisha wakarejea katika 

chumba cha Lucy na kuondoa kila kitu 

ambacho kingeweza kuonyesha dalili za 

kulala mtu katika chumba 

kile.Wakagonganisha mikono baada ya 

kuhakikisha kwamba kila kitu 

kimekwenda vizuri.Wakajiweka tayari 

kwa ajili ya kumsubiri Dr Shanon. 

 Saa nne na nusu za asubuhi Dr Shanon akawasili.Alikuwa ni msichana wa miaka 

ishirini na saba.Walimkaribisha kwa 

furaha sana daktari huyu mtafiri wa 

wanyama.Baada ya maongezi mafupi kwa 

kuwa alikuwa na safari ya kwenda 

kutembelea bonde la Ngoro ngoro 

wakaanza kumtembeza kumuonyesha 

nyumba nzima na mazingira yake.Dr 

Shanon akaonyesha furaha yake na 

kuridhika kuishi katika nyumba ile 

nzuri.Wakapeana maelekezo kisha 

akaondoka na kuendelea na safari yake ya 

kuelekea Ngorongoro.Hakuweza 

kugundua chochote kuhusu kuwepo kwa 

msichana wa kitanzania katika nyumba 

ile.Baada ya Dr Shanon kondoka 

wakamchukua Lucy na kumrudisha katika 

chumba chake na wao wakaendelea na 

kunywa pombe kwa fujo huku 

wakijiandaa na safari ya kuondoka 

Tanzania kesho yake. 

 Usiku wa siku hiyo ulikuwa ni usiku wao 

wa mwisho kuwepo hapa nchini 

Tanzania.Walikunywa pombe hadi saa 

saba za usiku na kisha wakafanya 

mapenzi na Lucy kwa mara ya mwisho 

halafu wakamnywesha juice iliyowekwa dawa za usingizi ambayo ilimfanya Lucy 

alale fofofo.Wakautumia mwanya huo wa 

Lucy kulala kufunga kila kilicho chao na 

kujiandaa kwa safari.Kabla hawajaondoka 

walihakikisha wamemuwekea Lucy 

chakula cha kutosha na kila kitu ambacho 

angekihitaji halafu wakaondoka. 

 " Kwa heri Lucy.Sijawahi kukutana na 

msichana mzuri kama wewe katika 

maisha yangu.I'll miss you alot" akasema 

Adolf akimuaga Lucy ambaye kwa wakati 

huo alikuwa amezama katika usingizi 

mzito. 

 "I hope you'll find yoursefl a way out of 

here and please forgive us for everything." 

akasema Leonard huku akimshika Lucy 

kichwani halafu akaliweka bunda kubwa 

la noti yekundu nyekundu pembeni ya 

Lucy wakaondoka. 

 *************************************

******** 

 Saa tano za subuhi Lucy akaamka 

usingizini.Alikuwa amechoka na kichwa 

kilimuuma sana.Akawaza mambo yaliyotoke usiku uliopita akakumbuka 

namna walivyomtenda wale wazungu 

akauma meno kwa hasira. 

 " Mateso haya yatakwisha lini? Hapana 

siwezi kuendelea kuteseka namna hii kila 

siku.Nimevumilia sasa 

imetosha.Nitakalolifanya kwa sasa Mungu 

atanisamehe.Hiyo ndiyo itakuwa ni njia 

pekee ya kuweza kunitoa humu 

ndani.Lazima niwaue hawa wazungu.Bila 

hivyo sintaweza kamwe kutoka humu na 

wataendelea kunifanyia udhalilishaji huu 

kila siku" akawaza Lucy huku akipandwa 

na hasira na machozi kumtoka lakini 

ghafla akahisi kama amegusa kitu fulani 

kama karatasi ,akageuza shingo yake 

kuangalia akakutana na bunda kubwa la 

noti za shilingi elfu kumi kumi.Akapatwa 

na mshangao kwa bunda lile kubwa la 

fedha.Akalifungua kwa haraka na kuanza 

kuzihesau.Zilikuwa ni shilingi millioni 

tano na laki saba fedha za kitanzania.Uso 

wake ukajengwa na tabasamu pana sana 

kwa kiasi kikubwa kile cha fedha. 

 " Hivi ni kweli ninachokiona au niko 

ndotoni? Ni kweli pesa hizi zote ni zangu? 

Katika maisha yangu yote sijawahi kushika kiasi hiki kikubwa cha pesa.kwa 

nini wameamua kunipa fedha hizi zote? 

Pesa hizi zinanitosha kabisa kuanzisha 

biashara ya kati na kuyaendesha maisha 

yangu.Ukichanganya na zile fedha ambao 

wamekuwa wakinipa kila wakinifanyisha 

mapenzi ninapata jumla ya shilini milioni 

tisa .Ni fedha nyingi ambazo sikutegemea 

kuzishika katika maisha yangu." akawaza 

Lucy akiwa tayari amerejewa na nguvu 

zake na tabasamu pana sana 

usoni.Alizishika fedha zile na 

kuzikumbatia kwa furaha.Kwa sasa 

aliweza kuyaona maisha yake ya mbele 

namna yatakavyokuwa. 

 " Umasikini kwa heri.Nimeuaga 

umasikini tayari.Kwa fedha hizi zote 

sijihesabu kamani masikini tena. 

Nitafanya kazi kwa bidii sana ili niweze 

kuiondoa familia yangu katika umasikini 

mkubwa iliyonao.Nitawasomesha shule 

wadogo zangu wote.Nataka wapate elimu 

na hata mimi mwenyewe itanilazimu 

kuendelea na masomo ya 

sekondari.Nasikia kuna yale masomo ya 

sekondari kwa ,miaka miwili.Nitajunga 

huko ili niweze kupata elimu na baada ya hapo nijiunge katika masomo ya 

biashara.Nataka nipate shahada ya 

biashara na siku moja niweze kuwa 

mmoja wa wafanya biashara 

wakubwa.Lakini ndoto hizi zote 

zingekuwa nzuri kama ningekuwa na 

mwanangu Angela.Masikini mwananu sijui 

atakuwa katika hali gani sasa hivi.Sjui 

kama ni mzima au amefariki.." Kila Lucy 

anapomuwaza mwanae hujikuta 

akiangusha machozi ya uchungu. 

 " Lazima nihakikishe ninampata 

mwanangu baada ya mambo yangu yote 

kukaa sawa.Nitatafuta taarifa zake ili 

kujua kama alifanikiwa kuokotwa au 

alifariki.Lazima nimtafute 

mwanangu.maisha yangu hayatakuwa na 

furaha tena kama sintampata mwanangu 

Angela" akawaza Lucy machozi yakiendela 

kumtiririka. 

 hatimaye jioni ikaingia bila ya dalili 

zozote za akina Adolf.Usiku mzima ukapita 

bila ya wazungu wale kuonekana.Hali hii 

ikaanza kumpa wasi wasi mkubwa 

Lucy.Haikuwa kawaida yao kutorejea 

nyumbani.Siku mpya ikanza na bila ya 

wazungu wale konekana.Siku ikaisha  na  usiku ukaingia lakini hakuna mtu 

aliyerejea.Usiku ukapita na hatimaye 

ikawa asubuhi.Adolf na Leonard 

hawakurejea nyumbani. 

 " Nahisi wazungu hawa watakuwa 

wamesafiri na ndio maana wakaniachia 

fedha nyingi namna ile.Huu ni wakati 

wangu wa kutafuta namna ya kuweza 

kuondoka humu ndani.Lakini nitatokaje 

wakati milango yote imefungwa?.Lazima 

nitafute njia ya kuweza kunitoa humu 

ndani.lazima nitoke humu" akasema Lucy 

huku akiinuka kitandani na kwenda 

kujaribu kuufungua mlango uliokuwa 

umefungwa kwa funguo.Akautazama 

mlango ule kwa makini akapata 

wazo.Akachukua kisu na kuanza zoezi la 

kujaribu kung'oa misumari ya kitasa 

.Lilikuwa ni zoezi gumu sana lakini 

hakukata tamaa.Baada ya zoezi lake 

kushindikana akapandwa na hasira na 

kuanza kuupiga mlango kwa 

nguvu.Akakaa chini ya mlango na kuanza 

kulia kwa kwikwi.Ghafla kwa mbali 

akasikia kama sauti za watu 

wakinong'ona.Akasimama akakishika 

kisu.  " Kama ni hawa wazungu leo 

nawaua.Nimechoka kabisa kufanywa 

mtumwa ndani ya hii nyumba." akawaza 

Lucy akiwa na hasira kali.Mara mlango 

ukafunguliwa na ukelele mkubwa 

ukapigwa 

 " 

Aaaaaaaaaaaaaaaaagggggggggghhhhhhhh

hhhhhhhhhhhh ..............!!!!!!!!!!!!..." Lucy 

akapatwa na mshangao mkubwa 

akaanguka na kupoteza fahamu. 

 Mlangoni alikuwa amesimama Dr Shanon 

akiwa na rafiki yake mmoja raia wa 

Kenya.Wote walistuka na kupiga ukelele 

mkubwa sana baada ya kumkuta Lucy mle 

ndani.Hawakujua amengiaje mle ndani.Dr 

Shanon alikuwa akitetemeka.Aliona ni 

kama mazingaombwe.Hakuamini kama 

Lucy alikuwa ni binadamu kweli au ni 

mzimu.Akamtazama Rachel rafiki yake . 

 " Tunafanya nini Rachel.?Twende 

tukimbie huu ni mzimu .Twende tuondoke 

humu" .Akasema Dr Shanon akimshika 

mkono Rachel na kumtaka waondoke 

haraka sana katika nyumba ile ambayo 

aliamini ilikuwa na mauza uza. 

 " Hapana Dr Shanon.Ngoja kwanza" akasema Rachel huku akiinama na kuanza 

kumchunguza Lucy. 

 " Dr Shanon huyu si mzimu.Huyu ni 

binadamu halisi" akasema Rachel 

 " Ameingiaje humu wakati milango yote 

imefungwa? akauliza Dr Shanon. 

 " Siwezi kufahamu hata mimi msichana 

huyu amewezaje kuingia humu ndani 

wakati milango yote imefungwa" 

 " Rachel twende tuondoke haraka.Huyu si 

msichana wa kawaida.Twende tukaishi 

hotelini.Sitaki tena kuishi mahala hapa" 

akasema Dr Shanon 

 " Dr Shanon huyu si mzimu.Huyu ni mtu 

halisi.Tumpatie kwanza huduma na akisha 

zinduka tutapata majibu.Atatueleza yeye 

ni nani na amefikaje humu.Ninafahamu 

kiswahili nitamuhoji." akasema Rachel na 

kwa uoga Dr Shanon akamsogelea Lucy 

Wakamuinua na kumpeleka sebuleni na 

kuanza kumpatia huduma ya 

kwanza.Baada ya muda Lucy akafumbua 

Macho na kujikuta akiwa mikononi mwa 

wanawake wawili mmoja mwafrika na 

mwingine mzungu.Dr Shanon akaogopa na 

kusogea mbali kidogo na Lucy. 

 " Tafadhali usiogope..hatuna nia mbaya ya na wewe..." akasema Rachel akimsihi 

Lucy atulize hasira 

 " Nyie ni akina nani? akauliza Lucy kwa 

ukali 

 " Ninaitwa Rachel na yule mwenzangu 

anaitwa Dr Shanon.Sisi ndio tunaokuja 

kuishi katika nyumba hii " akasema 

Rachel 

 "mnakuja kuishi katika nyumba hii? 

Leonard na Adolf wako wapi? akauliza 

Lucy. 

 Dr Shanon aliposikia Lucy akitamka 

majina ya Adolf na Lenard akasogea 

karibu zaidi na kumuuliza rachel 

 " Anasemaje? Nimesikia akitamka majina 

ya Adolf na Leonard" 

 " Nimemfahamisha kwamba sisi ndio 

tunaoanza kuishi katika nyumba hii na 

akashanga akauliza kuhusu Adolf na 

Leonard." Rachel akajibu 

 " Inawezekana anawafahamu 

vizuri.Muhoji amewafahamu vipi Adolf na 

Leonard? akasema Dr Shanon.Rachel 

akamgeukia tena Lucy 

 " Unaweza ukaniambia umewafahamu 

vipi Leonard na Adolf? akauliza Rachel. 

 Lucy akafumba macho na mara michirizi ya machozi ikaanza kumtoka.Rachel 

akamgeukia Dr Shanon. 

 " Dr Shanon inaonekana kuna jambo zito 

linalomfanya aangushe 

machozi.Tunatakiwa tumuache apumzike 

na kisha tumuhoji taratibu tujue kitu gani 

kimemsibu" akashauri Rachel na Dr 

Shanon akakubaliana naye. 

Rachel akachukua maji ya kunywa 

akampa Lucy 

 " Kunywa maji haya ujasikia vizuri" 

akasema Rachel..Lucy akachukua glasi ile 


ya maji akanywa 

 " Kaa upumzike..usiogope tafadhali.Jina 

lako nani?" 

" Naitwa Lucy" 

 " Ouh Lucy ! nafurahi kukufahamu 

,pumzika tafadhali.." Rachel akamwambia 

Lucy ambaye alitikisa kichwa na kisha 

akajilaza sofani. 

 " Dr Shanon nimemuuliza jina huyu 

msichana anaitwa Lucy.Anaonekana ana 

matatizo makubwa sana.Tumsubiri 

akitulia atatueleza kila kitu." akasema 

Rachel akimwambia Dr Shanon aliyekuwa 

amesimama mlangoni. 

 ""Rachel unafikiri Lucy aliingia vipi humundani? 

 " Siwezi kufahamu Dr Shanon kwa sababu 

wote tumemkuta humu ndani.Tutapata 

jibu la uhakika kama tukimuuliza yeye 

mwenyewe namna alivyofanikiwa kuingia 

humu ndani." akasema Rachel 

 " Mimi nahisi anaweza akawa ni 

msichana kahaba kwa sababu 

haiw......................." kabla Dr Shanon 

hajamaliza sentensi yake Rachel akasema 

 " Hapana Dr Shanon.Msichana yule Lucy 

haonekani kama kahaba.Msichana yule 

anaonekana ana matatizo 

makubwa.Tusubiri apumzike halafu 

tutamuhoji na kujua kitu gani hasa 

kilichomsibu.Twende tukaendelee 

kuikagua nyumba hii" akasema Rachel 

 " Hapana Rachel.hatuwezi kutoka hapa na 

kumuacha Lucy peke yake.Itakuwaje kama 

atakimbia? Tukae hapa hapa tukimlinda 

na akisha tulia tutamuhoji vizuri" 

akasema Dr Shanon. 

 " Ina maana wale akina Adolf 

wameondoka na hawatarudi tena kuishi 

katika hii nyumba? Mwanamke yule 

aliniambia kwamba wao ndio wanaokuja 

kuishi hapa...Ninaanza kupata picha inawezekana ni kweli Adolf na Leonard 

watakuwa wameondoka zao." akawaza 

Lucy na kisha kwa mbali tabasamu 

likaanza kujengeka usoni mwake. 

 " Nitamshukuru Mungu sana kama ni 

kweli wanyama wale wamendoka..Nahisi 

waliniwekea dawa za usingizi nikalala 

sana hadi nikashindwa kujua muda gani 

waliondoka.Nimeteseka sana ndani ya 

nyumba hii.Kama ni kweli maharamia 

wale wameondoka Mungu atakuwa 

amesikia kilo changu na itakuwa ni fursa 

kwangu ya kuanza maisha mapya.Ngoja 

nimuulize yule mwanamke aliyekuwa 

akiongea nami kama ni kweli hawa 

wanyama wameondoka " akawaza Lucy 

kisha akainuka pale sofani na kwenda 

kuchungulia nje.Rachel na Dr Shanon 

walikuwa wameketi kibarazani 

wakiongea. 

 " Dada samahani naomba kukuuliza" 

Lucy akamwambia Rachel ambaye 

aligeuka akamuangalia kwa tabasamu 

kisha akamgeukia Dr Shanon. 

 " nafikiri tayari ameshatulia.Ni wakati 

muafaka wa kupata majibu." akasema 

Rachel na kuinuka kuelekea ndani  " Halo Lucy..unajisikiaje sasa? akauliza 

Rachel 

 " Najisikia vizuri " akajibu Lucy. 

 "Lucy mimi naitwa Rachel na yule 

mwenzangu anaitwa Dr Shanon.Kwa 

pamoja sisi tuko katika utafiti na 

tutakuwepo hapa kwa muda mrefu kidogo 

hadi hapo tutakapomaliza utafiti wetu" 

akasema Rachel huku 

akitabasamu.Akamtazama Lucy usoni 

kisha akaendelea 

 " Sisi ni wanawake wenzio na usituogope 

hata kidogo.Tuone ni kama marafiki 

zako.Naomba utueleze Lucy nini 

kimekutokea hadi ukafungiwa humu 

ndani? Akina Adolf na Leonard 

umewafahamu vipi? akauliza Rachel kwa 

sauti ya upole akiwa amekaa pembeni ya 

Lucy ambaye aliinama akafikiri kidogo na 

kusema 

 " Adolf na Leonard waliniokota njiani 

baada ya kunikuta nimeanguka kutokana 

na kutembea kwa muda mrefu .Usiku huo 

ulikuwa na baridi kali sana.Baada ya 

kuniokota wakanileta hapa nyumbani 

kwao wakanihudumia na kunitibu 

nikapona.Baada ya kupona Adolf ambaye alikuwa akifahamu kiswahili kidogo 

akaniambia kwamba wao wanaishi peke 

yao humu ndani na kwa hiyo wangefurahi 

kama ningeishi nao hapa ili niweze 

kuwasaida kazi za ndani na watakuwa 

wakinilipa pesa.Kwa kuwa kwa wakati 

huo sikuwa na kazi wala sehemu ya kuishi 

nilikubali na kushukuru sana nikiamini 

kwamba nilikuwa sehemu salama" 

akasema Lucy kisha akamtazama Rachel 

usoni 

 " Lucy unasema kwamba hukuwa na 

sehemu ya kuishi ? rachel akauliza 

 " Ndiyo kwa wakati huo sikuwa na 

sehemu yoyote ya kuishi baada ya 

kufukuzwa sehemu niliyokuwa nikiishi na 

kufanya kazi za ndani.Nilkuwa nikitembea 

bila kujua ni wapi nilikokuwa nikielekea 

na ndiyo sababu nilianguka njiani na 

akina Adolf wakaniokota"Akasema Lucy 

 " Enhe ! endelea..."akasema Rachel 

 " Nilianza kufanya kazi za ndani hapa na 

ilipofika usiku nikiwa naosha vyombo 

tulivyotumia kwa chakula cha usiku 

,alikuja Adolf na kuanza kunifanyia 

vitendo vya kuhamasisha kufanya 

mapenzi" akasema Lucy na kunyamaza akatazama chini.Rachel akaonekana 

kushangazwa na kauli ile akamuangalia 

Lucy na kusema. 

 " Nini kikatokea Lucy.Niambie tafadhali." 

akasisitiza rachel.Lucy akafuta machozi 

ambayo tayari yalianza kumtoka akasema 

 " wakanilazimisha kufanya nao 

mapenzi..Niliumia sana" akasema Lucy na 

kuanza kulia.Rachel akamuonea huruma 

akampiga piga mgongoni. 

 " Nyamaza usilie Lucy...." Rachel 

akambembelea Lucy. 

 " Rachel kitu gani kinamliza Lucy" Dr 

Shanon ambaye alikuwa amesimama 

akisikiliza maongezi kati ya Lucy na 

Rachel akauliza. 

 " Dr Shanon Lucy ana matatizo makubwa 

yaliyomsibu.tumsubiri amalize kusimulia 

mkasa wake halafu nitakueleza kila kitu" 

akasema Rachel. 

 " Lucy nyamaza kulia .tafadhali nieleze 

nini kiliendelea kati yako na wazungu 

wale? akasema rachel akimuangalia Lucy 

kwa huruma.Lucy akakohoa kidogo na 

kusema 

 " Toka siku hiyo nikawa nafungiwa humu 

ndani.Sijawahi kutoka nje hata mara moja na kila siku nilifungiwa chumbani 

nikawekewa chakula hadi usiku 

wanaporudi.Wakisharudi usiku nilikuwa 

nachukuliwa na kulazimishwa kufanya 

mapenzi na wote wawili ndipo niruhusiwe 

kwenda kulala.Kila waliponifanyisha 

mapenzi walinipa pesa.Dada rachel ni 

kweli wazungu wale wameondoka? 

akauliza Lucy 

 " Pole sana Lucy kwa masahibu yote 

yaliyokupata. Ni kweli Adolf na Leonard 

wameondoka .Ina maana hawakukuambia 

kwamba wanaondoka? akauliza rachel 

 " Hapana hawakuniambia.Nahisi walinipa 

dawa za usingizi na wakaondoka wakati 

nimelala sijifahamu" akasema Lucy. 

 " Pole sana Lucy. Unaweza ukanieleza 

wazazi wako wako wapi? 

 " wazazi wangu wako Singida na huku 

Arusha nilikuja kufanya kazi za ndani" 

 " Una ndugu yeyote hapa Arusha? 

 " Hapana sina ndugu hapa Arusha na 

ndiyo maana baada ya kufukuzwa mahala 

nilikokuwa nikiishi sikuwa na mwelekeo 

nikatembea bila kujua ninakwenda wapi 

nikaanguka njiani na ndipo Adolf na 

Leonard wakaniokota wakanileta hapa."  " Umesoma hadi darasa la ngapi Lucy? 

 " Nimesoma hadi darasa la tano,nikaacha 

shule .Nyumbani kwetu ni masikini sana." 

 " Una mpango gani na maisha yako ya 

mbele? akauliza Rachel 

 " Nilikuwa nikifikiria kwamba kama siku 

mja wazungu wale wangeniachia huru 

ningeanzisha biashara japo ndogo ya 

kuweza kunisaidia kuendesha maisha 

yangu kwa kutumia kiasi cha pesa 

walichokuwa wakinilipa wale wazungu 

kila waliponifanyisha mapenzi." akasema 

Lucy. 

 " walikuwa wakikulipa shilingi ngapi? 

 " hakukuwa na kiwano maalum ila 

walinipa kiasi chochote kile walichojisikia 

kunipa na siku nyingine hawakunipa kitu" 

Rachel akainama akafikiri kidogo na 

kusema 

 " Lucy ungependa tukusaidie kitu gani ? 

sema chochote ambacho ungependa 

tukusaidie ili uweze kuyaendesha maisha 

yako" 

Lucy bila kufikiri akasema kwa haraka 

 "Ninataka kutoka hapa na kwenda 

kuanza maisha yangu.Ninahitaji kuwa 

huru baada ya kuwa mtumwa kwa muda mrefu ." akasema Lucy huku machozi ya 

furaha yakimtoka. 

 Rachel akamsogelea akamkumbatia na 

kumwambia 

 " Lucy uko huru sasa.Pole sana kwa 

matatizo yote yaliyokupata.Mungu 

amesikia kilio chako na sasa amekufanya 

kuwa huru tena" Lucy akaruka kwa furaha 

huku akiyafuta machozi kwa kauli ile ya 

Rachel. 

 " Rachel umemwambia kitu gani Lucy 

mbona amekuwa na furaha ya ghafla 

namna hii? akauliza Dr Shanon. 

 Rachel akamsogelea Dr Shanon na kuanza 

kumweleza mkasa mzima wa Lucy 

ulivyokuwa.Dr Shaon akabaki mdomo 

wazi akashindwa kuamini kama ni kweli 

wale wenzake walimfanyia Lucy kitendo 

cha kinyama namna ile. 

 " Damn you Adolf " akasema Dr Shanon 

kwa hasira akainuka akazunguka zunguka 

mle sebuleni. 

 "Kitendo walichokifanya hawa wenzangu 

ni cha kikatili sana na hakikubaliki hata 

kidogo si hapa duniani pekee bali hata 

mbinguni.Kumfanya binadamu mwenzako 

mtumwa na kumfanyisha ngono kila siku ! Hili si jambo dogo hata kidogo.Hili si 

jambo la kufumbia macho" Dr Shanon 

akasema kwa ukali . 

 " Rachel nimeumizwa sana na kitendo 

walichokifanya hawa wenzangu.Ni kitendo 

ambacho kimetudhalilisha sana sisi raia 

wa kigeni..kitendo ambacho 

kimetudhalilisha sisi kama wanawake..ni 

kitendo ambacho kimemdhalilisha mtu 

mweusi..Nimeumizwa sana na kitendo 

hiki.Msichana yule masikini alipaswa 

kusaidiwa na si kufungiwa ndani na 

kutumikishwa kufanya ngono." akasema 

Dr Shanon.Kimya kifupi kikapita Dr 

Shanon akasema 

 " Rachel tunatakiwa kufanya kitu 

fulani...." 

 " Kitu gani Dr Shanon? 

 " Tunatakiwa kumsaidia Lucy..Moyo 

wangu umeumia sana kwa vitendo vya 

ukatili alivyofanyiwa na wale 

wenzangu.Ninajua ndani ya moyo wake 

atakuwa ameumia sana na tayari 

amekwisha kata tamaa ya 

maisha.Tunatakiwa kumsaidia kuyajenga 

maisha yake.Yule ni mwanamke 

mwenzetu na kumwambia tu kwamba sasa uko huru haitoshi..tunapaswa kumsaidia 

kwa kila namna tunayoweza ili majeraha 

aliyoyapata moyoni mwake yaweze 

kufutika na aweze kuishi akiwa na amani 

ya moyo." akasema Dr Shanon. 

 " wazo lako ni zuri sana Dr Shanon.Lakini 

tutamsaidia vipi wakati yeye anataka 

kwenda kuanza maisha yake? akauliza 

rachel. 

 " Hapana .tusimruhusu akaondoka na 

kwenda kuyaanza maisha yake 

mwenyewe.Huko atakakoenda atakuwa na 

roho ya kisasi na hatakuwa raia mwema 

hata kidogo.Siku zote atakuwa 

akikumbuka mambo aliyofanyiwa na 

kuumia sana.Hatutakiwi kumuacha 

akaishi namna hiyo.Tunatakiwa 

kumshawishi aendelee kuishi nasi hapa 

.Tukiwa naye hapa tutajitahidi 

kumsahaulisha maisha magumu 

aliyopitia,tutamsaidia kuanza maisha 

mapya.Tutamsaidia aweze kuishi kwa 

amani na upendo tutamfanya afahamu 

kwamba katika dunia hii si kila mtu ni 

mbaya.Tutamfundisha upendo na 

kumsaidia kupata elimu na kuyafurahia 

maisha.Unaonaje kuhusu mpango huu? 



Tutamfundisha upendo na 

kumsaidia kupata elimu na kuyafurahia 

maisha.Unaonaje kuhusu mpango huu? akasema Dr Shanon 

 " Mpango huu ni mzuri .Tunatakiwa 

kufanya hivyo kumsaidia Lucy" 

 " Ok nenda haraka kajaribu kumshawishi 

ili aweze kukubali kubaki nasi hapa." Dr 

Shanon akamwambia rachel ambaye 

aliinuka na kumfuata Lucy chumbani 

kwake na kumkuta akikunja nguo zake 

tayari kwa kuondoka.Bado machozi 

yaliendelea kumtoka.Hakuamini kama 

alikuwa huru ..Rachel akamtazama Lucy 

kwa huruma sana. 

Taratibu Rachel akamsogelea Lucy na 

kukaa karibu yake.Akazungusha mikono 

yake katika shingo ya Lucy.Akamwambia 

taratibu 

 " nyamaza kulia Lucy.Mambo 

yamekwisha na uko huru sasa hivi" 

 Lucy akafuta machozi halafu akamtazama 

rachel usoni akasema 

 " Nashukuru sana dada Rachel kwa 

kunisaidia nimekuwa huru tena.Mungu 

amesikia kilio changu cha muda mrefu na 

sasa ameamua kuniweka huru.Siamini 

kama ninakwenda kuyaanza tena maisha 

yangu " akasema Lucy akatabasamu 

kidogo na kumfanya Rachel naye atabasamu 

 " Lucy mdogo wangu ni kweli uko 

huru.Mungu amekuweka huru toka katika 

kifungo cha mwili.lakini je uko huru 

katika kifungo cha roho? Fahamu kuna 

vifungo vya mwili na vifungo vya roho 

pia.Kwa sasa uko huru kimwili je kiroho 

uko huru? akauliza Rachel na kumfanya 

Lucy ashangae kidogo 

 " Sijakuelewa unamaanisha nini dada 

Rachel" 

 " Ninaposema kifungo cha roho 

ninamaanisha kwamba unafungwa na yale 

mambo ambayo yanakufanya uwe mbali 

na Mungu.mambo ya kidunia kama vile 

ulevi,uzinzi,wizi kwa ufupi ni yale mambo 

yote ambayo hayapendezi machoni pa 

Mungu.Ili kuwa huru na kifungo hiki cha 

roho unatakiwa umpokee yesu na kumkiri 

kwamba yeye ni bwana na mwokozi wa 

maishayako.Unatakiwa umkubali yeye tu 

kwamba ayaongoze maisha yako na 

ayatawale .Kwa sasa uko huru kimwili 

lakini nani umemkabidhi maisha yako 

ayaongoze? Wengi tunafikwa na matatizo 

mengi katka maisha kwa sababu maisha 

yetu hatuyakabidhi kwa Mungu.Ili usiweze kujikuta tena katika mambo kama haya 

yaliyokukuta unatakiwa kumkabidihi 

bwana maisha yako ayaongoze na 

ayatawale.Unatakiwa umpokee Yesu na 

akae ndani mwako. Watu walioko katika 

kristu wanakuwa na maisha mazuri yenye 

amani na upendo.Unatakiwa umpokee 

yesu ili uweze kuyasahu yote yaliyokupata 

na uweze kuanza maisha 

mapya.Unatakiwa kuwasamehe wale wote 

waliokutenda vibaya na kuwaombea .Uko 

tayari sasa kuondokana na kifungo cha 

roho? Uko tayari kuanza maisha mapya 

yaliyojaa upendo na amani? Uko tayari 

kuwasamehe wale wote waliokutenda 

vibaya ? 

 Lucy akainama akafikiri na baada ya 

muda mfupi akainua kichwa akasema 

 " Dada Rachel ninashukuru Mungu 

kwamba ameniweka huru .Toka ndani ya 

moyo wangu ninahisi kwamba ninahitaji 

kuyabadili maisha yangu na kuanza kuishi 

maisha mapya kabisa.Kusema ukweli 

maisha niliyoishi huko nyuma si maisha 

mazuri na hayafai kukumbukwa 

.Ninapenda sana kuanza maisha mapya 

lakini siwezi kufanya hivyo" akasema Lucy  " Kwa nini Lucy? Ugumu uko wapi katika 

kuyaanza maisha mapya? Baada ya 

mambo yote haya kukutokea unatakiwa 

kuanza kuishi maisha mapya yaliyojaa 

furaha amani na upendo Nafuraha hiyo ya 

moyo utaipata tu kama uko ndani ya 

Yesu.tafadhali usiache nafasi hii ikakupita 

Lucy.Mungu bado ana nia na wewe mdogo 

wangu." 

 Lucy akainama tena akafikiri na kuuliza 

 " Dada Rachel wewe una watoto wangapi? 

 Rachel akatabasamu na kujibu 

 " Sina hata mtoto mmoja" 

 " Umeokoka? akauliza tena Lucy 

 " Ndiyo nimeokoka na nimemkabidhi 

bwana maisha yangu ayatawale na 

kuyaongoza yeye mwenyewe. na hii ndiyo 

sababu maisha yangu yamezungukwa na 

upendo na amani kila dakika Ninasikia 

furaha kubwa moyoni mwangu" akasema 

Rachel na kumfanya Lucy atabasamu 

 " Ninatamani sana kuwa kama wewe 

dada Rachel .Ninatamani kuishi kwa 

furaha na amani lakini siwezi kufanya 

hivyo kwa sasa" 

 " Kwa nini unashindwa kufanya hivyo 

Lucy? Kuna kitu gani kinazuia kufanya hivyo? Rachel akauliza 

 " Dada rachel kuna mambo mengi 

yanayonifanya nishidwe kufanya hivyo 

kwa sasa" akasema Lucy huku uso wake 

ukiwa na mabadiliko 

 " Unaweza ukanieleza ni jambo gani 

linalokufanya usiyabadili maisha yako 

Lucy? Tafadhali nieleze mimi ni rafiki 

yako na lengo langu ni kukusaidia kama 

ndugu yangu ili uweze kuyaanza maisha 

yako upya yakiwa yamejaa furaha amani 

na upendo " 

 Lucy akainama akafikiri kwa muda halafu 

akainua kichwa na kusema 

 " Dada rachel mambo mengi yamenitokea 

katika maisha yangu hadi sasa hivi.Maisha 

yangu niliyoishi huko nyuma ndiyo 

yanayonifanya nisiweze kuwa tayari 

kuokoka kwa sasa.Bado moyo wangu 

umejaa hasira na kisasi.Bado moyo wangu 

unaumia kwa mambo niliyoyafanya na 

niliyofanyiwa.Halafu kingine ni kwamba 

siko tayari kwa sasa kuwasamehe Adolf na 

Leonard kwa mambo 

waliyonifanyia.Pamoja na kwamba 

hawako tena mbele ya macho yangu kwa 

sasa lakini moyo wangu una kisasi kikubwa kwao.Nafahamu siku moja 

tunaweza tukaonana na hivyo nikalipa 

kisasi .Dada rachel nashukuru sana kwa 

kutaka kunisaidia lakini kwa sasa sidhani 

kama ni muda muafaka wa kufanya 

hivyo.Natakiwa nikaanze kuyatengeneza 

tena maisha yangu yaliyoharibika na 

baadae kama hasira zangu zitatulia basi 

ninaweza nikaamua kuokoka." akasema 

Lucy huku akiendelea kukunja nguo zake. 

 " Lucy Bwana Mungu anatuambia kwamba 

inatubidi tujifunze kusamehe hata yale 

mambo ambayo ni magumu 

kuyasamehe.Bwana yesu aliteswa na 

kuuawa kifo cha aibu msalabani lakini 

kabla hajafa aliwasamehe wale wote 

waliomtesa na kuwaombea kwa Mungu ili 

awasemehe pia.Hata sisi tunatakiwa 

kuufuata mfano wa Yesu na kuwasamehe 

wale wote waliotukosea na 

kuwaombea.Tafadhali Lucy usijaribu 

kuufanya moyo wako uwe 

mgumu.Mkaribishe bwana katika maisha 

yako ili aweze kuuponda ponda moyo huo 

mguu na kukupa moyo wenye amani ,na 

upendo" akasema Rachel.Lucy akaacha 

kukunja nguo akainama kwa muda na kisha akainua uso wake ukiwa na machozi. 

 " Dada Rachel hebu fikiria wewe ulivyo 

hivi sasa halafu wanatokea watu wawili 

wanakuvamia,wanakuvua nguo na kuanza 

kukubaka kwa zamu na baada ya kumaliza 

wanacheka ,wanapongezana na 

kufurahi.Kesho yake wanakuja tena 

wanakubaka na kuendelea na mchezo huo 

kila siku.Hivi unaweza ukawasamehe watu 

kama hao? 

 Lucy akauliza.Rachel akamtazama usoni 

hakujibu kitu 

 " Niambie dada Rachel ungeweza 

kuwasamehe watu hao kama ungekuwa ni 

wewe? Lucy akauliza tena. 

 Rachel akafikiri kisha akasema 

 " Kuna nyakati katika maisha haya 

tunatokewa na mambo ambayo ni vigumu 

kwa sisi kama binadamu 

kuyasamehe.Shetani anaitumia nafasi hiyo 

kuzidi kutupa hasira na kujenga visasi 

mioyoni mwetu.Lakini bwana Mungu 

anatufundisha kwamba hata kama 

tukitendwa vibaya na walimwengu ni yeye 

tu ambaye anaweza akatoa hukumu iliyo 

ya haki.Kwa maana hiyo bado maandiko 

yanatukumbusha kuwapenda na kuwaombea hata wale watesi wetu kama 

alivyoifanya Yesu msalabani.Kwa kulijibu 

sali lako ndiyo ningewasamehe" akasema 

rachel. 

 " Hayo maandiko yaliandikwa na nani? 

akauliza Lucy 

 " Mungu aliwatumia manabii na 

waandishi mbali mbali ili kuweza 

kulifikisha neno lake kwa watu wake" 

akajibu rachel 

 " Ouh kumbe ni watu ndio walioandika 

hayo maandiko basi hawakuwahi kupitia 

mambo niliyoyapitia mimi.Hawakuwahi 

kubakwa kama mimi..Hawakuwahi 

ku......................." Lucy akashindwa 

kuendelea akaanza kulia.Rachel 

akamkumbatia na kumfuta machozi. 

 " Nyamaza kulia Lucy...Inatosha sasa" 

akasema rachel 

 " Niache nilie dada Rachel ....mambo 

niliyoyapitia ni mengi na yananifanya 

niwe na moyo mgumu kukubaliana na 

ombi lako la kunitaka niokoke." akasema 

Lucy. 

 " Basi usilie Lucy..nyamaza kulia." 

 Baada ya muda Lucy akanyamaza na kisha 

akaendelea na kukunja nguo zake tayari kwa kuondoka.Rachel akamuangalia kisha 

akauliza 

 " Lucy una mahala unakotegemea kwenda 

kuishi baada ya kutoka hapa? 

 Lucy akafikiri kwa muda akajibu 

 " Sina mahala kokote kule ambako 

ninategemea kwenda kuishi kwa sasa bali 

nitakwenda kupanga chumba changu na 

kuanza kuishi maisha yangu 

mwenyewe.Nina kiasi cha pesa cha 

kuanzia maisha.Japokuwa nimemkosea 

sana lakini naamini Mungu atanisaidia na 

maisha yangu yatakuwa mazuri" akasema 

Lucy 

 " Lucy nina jambo ninataka kukueleza" 

 " jambo gani hilo dada Rachel" 

 " Nimejadiliana na Dr Shanon kabla ya 

kuja hapa kwako na tukafikiria namna ya 

kukusaidia katika maisha yako.Wewe ni 

mwanamke mwenzetu na kamwe 

hatuwezi kukuacha peke yako.Kwa nini 

usiendelee kuishi nasi hapa ? Tutaishi 

kama ndugu na tutakusaidia kuyasahau 

yale yote yaliyotokea huko 

nyuma.Unaonaje kuhusu mpango huo? 

akauliza rachel 

 Lucy akamtazama Rachel kwa makini usoni kisha akatabasamu 

 " Kuendelea kuishi ndani ya nyumba 

hii????????? 

 " Ndiyo Lucy ..tunataka kuishi nawe ndani 

ya nyumba hii" 

 Lucy akacheka kidogo na kusema 

 " Dada rachel hapana.Nashukuru sana 

kwa wema wenu lakini kwa sasa ninahitaji 

kuwa huru kuyaendesha maisha yangu 

mimi mwenyewe.Nyumba hii tayari ina 

historia mbaya sana kwangu.Mambo 

mengi mabaya yamenitokea ndani ya 

nyumba hii kwa hiyo sitaki kuiona 

tena.Kama nitaendelea kuishi katika 

nyumba hii nitaendelea kukumbuka kila 

kitu kilichinitokea na kuzidi 

kuniumiza.Sitaki tena kuishi ndani ya 

nyumba hii..Ninataka nikaishi mbali na 

hapa ili niweze kuyaendesha maisha 

yangu kwa uhuru" akasema Lucy. 

 " Lucy hii ni nafasi nyingine unaipata ya 

kuweza kuyatengeneza maisha 

yako.tafadhali kubali tukusaidide na 

tunakuahidi kwamba hakuna jambo lolote 

ambalo lilikutokea huko nyuma 

litakutokea tena ukiwa na 

sisi.Tutakutunza kama mdogo wetu na kukujali.Tafadhali Lucy kubali kuja kukaa 

nasi hapa na tutaishi kama familia moja" 

akaendelea kushawishi Rachel. 

 "Dada rachel hakuna jambo lolote ambalo 

unaweza ukanishawishi litakalonifanya 

niweze kubadili maamuzi yangu Sitaki 

kuishi katika nyumba hii na zaidi ya yote 

napenda ufahamu kwamba ninawachukia 

wazungu sana kwa mambo niliyofanyiwa 

na akina Adolf.Nilikuwa nikifikiria 

kwamba wazungu wana roho nzuri tofauti 

na sisi watu weusi lakini kumbe wana 

roho za kinyama sana.Tafadhali naomba 

usiendelee kunishawishi nibaki humu." 

 " Lucy ukiwa nasi hapa si kwamba 

tutakufungia ndani kama walivyofanya 

akina Adolf.Ukiwa nasi utakuwa huru 

kwenda kokote na kufanya jambo 

lolote.Hata kama unataka kufanya 

biashara sisi tuko tayari kukusadia 

kuanzisha biashara kubwa na yenye faida 

nzuri ambayo itakufanya uweze 

kuyaendesha maisha yako .Tutakuaidia 

kupata elimu ambayo itakusaidia sana 

katika masuala ya kibiashara.Sisi si raia 

wa nchi hii na hatuwezi kuishi hapa muda 

mrefu kwa maana hiyo tunataka kukusaidia ili hadi pale tutakapoondoka 

uwe tayari na maisha yako 

mazuri.Tutakupa kila aiana ya msaada 

unaouhitaji.Tuambie nini unataka 

tukusaidie? 

 Lucy akafikri kwa muda halafu akasema 

 " Dada rachel ninyi mnataka mnisaidie 

kitu gani? 

 " Sisi tunataka kukujengea msingi mzuri 

wa maisha yako.Tunataka upate elimu 

bora ya biashara na kisha kukusaidia 

kuweza kuwa na biashara kubwa na yenye 

faida nzuri.Hebu wafikirie ndugu zako 

kijijini ambao wote wanahitaji msaada 

wako kwa sasa.Ili kuwasaidi unatakiwa 

kwanza kuyajenga maisha yako na ndipo 

utakapoweza kuwasaidia nduguzo.Kubali 

kubaki nasi hapa na tutakusaidia 

kuyabadili maisha yako" akasema rachel 

 Lucy akainama akawaza kwa muda 

halafu akauliza 

 " Dada rachel unasema kwamba nikibaki 

hapa sintakuwa nikifungiwa ndani tena? 

 " Hapana Lucy.Wewe ni mdogo wetu na 

kamwe hatutakufungia ndani.Tunataka 

kuishi nawe kama ndugu yetu na 

kukusaidia kuyafikia malengo yako yote maishani.Hakuna jambo lolote baya 

litakalokutokea ukiwa na sisi." 

 " Na shule unasema mtanipeleka? 

akauliza tena Lucy 

 " ndiyo tutakupeleka shule ukapate elimu 

na kisha tutakusaidia kuanzisha biashara 

kubwa na yenye faida."akasema rachel 

huku akitabasamu 

 " Dada Rachel umefanikiwa 

kunishawishi..Nitabaki hapa nitaishi na 

ninyi lakini naomba tafadhali msinifanyie 

kama walivyonifanyia akina Adolf" 

akasema Lucy na kisha rachel 

akamkumbatia kwa furaha 

 " Lucy umefanya maamuzi yenye busara 

sana.Kuanzia sasa tunaishi kama familia 

moja" akasema Rachel huku akimshika 

mkono Lucy na kumuongoza hadi sebuleni 

alikokuwa amekaa Dr Shanon akisoma 

kitabu. 

 " Dr Shanon ..I have good news..She's 

going to stay with us" akasema Rachel na 

kisha Dr Shanon akakiweka mezani kitabu 

alichokuwa akikisoma na kwenda 

kuwakumbatia Lucy na Rachel. 

 " Thank you Lucy...thank you sooo 

much..we love you very much..you'll be very happy here with us" akasema Dr 

Shanon. 

Lucy akaufungua ukurasa mpya wa maisha 

yake.Akaanza maisha mapya akiishi na Dr 

Shanon na Rachel.Maisha yake yalikuwa 

na mabadiliko makubwa sana.Dr Shanon 

na Rachel walimpenda na kujitahidi 

kumuonyesha kila aina ya 

upendo.Walimtunza na kumjali kama 

mdogo wao.Alianza kwa kufanya kazi za 

kawaida za nyumbani..Lengo likiwa ni 

kumfanya azoee maisha mapya 

.Ilimlazimu Dr Shanon kujifunza kiswahili 

kwa bidii ili aweze kuwasiliana vizuri na 

Lucy ambaye alitokea kumpenda na 

kumfanya kuwa rafiki yake mkubwa.Kila 

mwisho wa wiki waliongozana wote 

kwenda sehemu mbali mbali za 

mapumziko ambazo Lucy hakuwahi 

kufika.Hali hii ilimfanya Lucy taratibu 

kuanza kusahau yale yote yaliyomtokea 

siku za nyuma.Alitokea kumpenda sana Dr 

Shanon kwani alikuwa akimsikiliza kwa 

kila alichokitaka.Maisha ndani ya nyumba 

ile yalikuwa ya furaha na amani.Dr Shanon 

na Rachel walimfundisha Lucy kwa 

vitendo nini maana ya upendo.  Taratibu Lucy akaanza kubadilika na 

kupendeza sana kutokana na maisha 

mazuri aliyokuwa akiishi na matunzo 

mazuri.Lucy alibadilika kiasi kwamba 

ilikuwa vigumu kumfananisha na yule 

Lucy wa miezi kadhaa iliyopita.Mwili wake 

ulinawiri na kupendeza.Ngozi yake nzuri 

yenye weupe wa kung'aa ilizidi kung'aa 

zaidi kutokana na matunzo mazuri 

aliyokuwa akiipatia kwa maelekezo ya Dr 

Shanon na Rachel.Nywele zake zilizokuwa 

zikitunzwa vizuri zilikuwa ndefu na zenye 

afya.Uso wake haukukaukiwa tabasamu 

muda wote.Hakuna kitu ambacho Dr 

Shanon alikifurahia kama kumuona Lucy 

akiwa na furaha daima.Kwake kurudisha 

tabasamu la furaha na matumaini katika 

uso uliopoteza tabasamu na kukata tamaa 

kilikuwa ni kitu kikubwa sana. 

 Pamoja na kumpa kila kitu alichokihitaji 

ikiwa ni pamoja na kumrejeshea tumaini 

la maisha yake tena,Dr Shanon aligundua 

kwamba kuna kitu bado kiliendelea 

kumtesa Lucy ingawa hakuwa tayari 

kukiweka wazi.Zaidi ya mara tatu 

amewahi kumkuta akiwa mwenyewe 

akilia.Dr Shanon aliumiza kichwa kutaka kufahamu ni jambo gani hilo lililoendelea 

kumtesa Lucy bila mafanikio .Alitamani 

kumuuliza ni jambo gani lililokuwa 

likimsumbua lakini akaona asubiri 

kwanza hadi hapo Lucy atakapokuwa 

tayari yeye mwenyewe kuliweka 

wazi.Alichokifanya Dr Shanon ni kuongeza 

ukaribu zaidi na Lucy ili asiogope 

kumweleza kila kinachomsumbua. 

 " Rachel unamuonaje Lucy? Unaonaje 

maendeleo yake? Dr Shanon akamuuliza 

Rachel siku moja wakiwa njiani kurejea 

nyumbani. 

 "Lucy anaendelea vizuri sana.maisha yake 

yamebadilika tofauti na yalivyokuwa huko 

awali.kwa sasa anaishi maisha ya uhuru 

na furaha siku zote.Above all she's so 

pretty.." akasema Rachel na kumfanya Dr 

Shanon atabasamu 

 " Ni kweli maisha ya Lucy yamebadilika 

sana tofauti na awali.Hilo ni jambo la 

kushukuru kwa sababu tumefanikiwa 

kumrejeshea Lucy ile furaha ya maisha 

yake aliyokuwa ameipoteza.Lakini pamoja 

na hayo yote kuna jambo ambalo 

nimeligundua kuhusu Lucy" 

 " Jambo gani Dr Shanon? akauliza Rachel " Kuna kitu bado kinamsumbua Lucy" 

 Rachel akafikiri kidogo na kusema 

 " Kwa nini umesema hivyo Dr Shanon? 

 " Nimekuwa nikimfuatilia Lucy kwa 

karibu ili kufahamu maendeleo yake na 

kama ni kweli ana furaha ndani ya moyo 

wake lakini nimegundua kuna jambo 

ambalo bado linamsumbua sana kichwa 

chake.Kuna jambo ambalo limekuwa 

likimtesa sana kila 

akilikumbuka.Nimewahi kumkuta zaidi ya 

mara tatu akiwa peke yake analia." 

akasema Dr Shanon na kumfanya Rachel 

apatwe na mshangao. 

 " Lakini mbona ana maisha mazuri na 

yenye furaha .Sina hakika kama kuna 

jambo ambalo tumemfanyia la kumfanya 

awe na hali ya namna hiyo.Tumempa kila 

aina ya uhuru.Au ile picha ya kitendo cha 

akina adolf bado haijafutika kichwani 

mwake na ndiyo maana kila akiikumbuka 

analia" akasema Rachel 

 " Hapana si hivyo Rachel..Nina uhakika 

kwamba kile kitendo cha akina Adolf sicho 

kinachomsumbua Lucy.lazima kuna kitu 

kingine tofauti na kile" akasema Dr 

Shanon  " kama hivyo ndivyo,jambo gani basi 

linaloisumbua akili ya Lucy? akauliza 

rachel 

 " Lazima kitakuwa ni kitu 

kinachohusiana na maisha yake ya nyuma 

.Unajua Lucy amepitia maisha magumu 

sana na amekumbana na mambo mengi 

licha ya umri wake mdogo.Hawezi 

kutueleza kila jambo alilopitia lakini 

niamini nikwambiavyo kuwa kuna kitu 

ambacho kila akikikumbuka analia." 

akasema Dr Shanon. 

 " Kama ni hivyo basi bado tuna kazi 

kubwa ya kufanya ili kuweza kuzifuta 

kumbu kumbu zote mbaya za maisha ya 

nyuma aliyoishi Lucy." akasema rachel 

 " Nimefikiria ni wakati muafaka sasa 

kumpeleka Lucy shule.Nimesikia hapa 

Tanzania kuna ile elimu ya kidato cha nne 

kwa miaka miwili .Hii itamfaa sana Lucy 

.Tutajitahidi kuwalipa walimu wa 

kumfundisha hata katika muda wa ziada 

ili aweze kufaulu vizuri katika masomo 

yake.Baada ya kumaliza masomo yake 

tutaangalia nini cha kufanya ili kumsaidia 

zaidi.Rachel nafsi yangu haitakuwa na 

furaha kamwe katika maisha yangu kama Lucy hatakuwa na furaha .Nitafanya kila 

niwezalo mpaka nihakikishe kwamba 

Lucy anaishi maisha mazuri yenye 

furaha.." akasema Dr Shanon na kumfanya 

Rachel atabasamu 

 " Hilo ni wazo zuri sana..lakini hii 

itasaidia kuweza kumuondolea Lucy 

kumbukumbu zake za nyuma? kwa nini 

tusijaribu kumuhoji na atueleze 

kinachomsumbua? 

 " Hapana rachel..Lucy ni msichana 

ambaye amekuwa muwazi sana 

kwetu.Kama kuna jambo hataki kutueleza 

basi lazima kuna sababu maalum kwa hiyo 

hatuwezi kumlazimisha 

atueleze.Tutasubiri mpaka atakapokuwa 

tayari kutueleza.Kitu cha msingi ni 

kwanza apate elimu ili aweze kutimiza 

ndoto zake maishani." 



Maisha ya Lucy yakaingia katika hatua 

nyingine,akaanza kusoma.Huu ukawa ni 

ukurasa mwingine mpya katika maisha 

yake mapya.Katika awamu hii mpya Lucy aliamua kubadilisha kabisa jina lake 

akaomba aitwe Linda Adamson .Hakutaka 

kabisa kulitumia jina lake la zamani 

katika maisha yake mapya aliamini jina 

lile lilikuwa na mkosi.Ilikuwa ni furaha 

kubwa kwake kuhudhuria darasani na 

kuanza masomo.Alianza masomo yake 

kwa kasi na kwa bidii kubwa.Kila nafasi 

aliyoipata aliitumia kwa kusoma.Juhudi 

zake katika masomo zilimfurahisha sana 

Dr Shanon. 

 " Kazana katika masomo Lucy ouh ! sorry 

Linda.unajua nimelizoea jina la Lucy .Siku 

moja utakuwa ni mtu mkubwa na 

utatimiza ndoto zako zote ulizokuwa nazo 

katika maisha yako. Maendeleo yako ni 

mazuri na yanatia moyo sana" Dr Shanon 

akampa moyo Lucy baada ya ripoti ya 

awali kuonyesha namna maendeleo ya 

Lucy yalivyo mazuri. 

 " Nashukuru sana Dr Shanon kwa namna 

ulivyonisaidia.Ninakuahidi nitasoma kwa 

bidii sana na hatimaye niweze kufanikisha 

kila ndoto yangu." akasema Lucy na 

kumfanya Dr Shanon kuzidi kufurahi. 

 Pamoja na kuhudhuria masomo 

darasani,kufundishwa na walimu wa ziada Dr Shanon na Rachel hawakuwa nyuma 

pia.Nao kila siku jioni walikuwa na ratiba 

ya kumsaidia Lucy katika masomo kama 

hesabu ,kiingereza na masomo ya 

sayansi.Walimfundisha kwa bidii na Lucy 

kwa uhodari aliokuwa nao alielewa 

haraka sana. 

 Ilikuwa ni siku ya jumatatu siku ambayo 

jiji la Arusha lilikuwa limetawaliwa na 

mawingu ya mvua kwani ulikuwa ni 

msimu wa mvua za masika.Ni mwaka wa 

pili wa masomo yake mwaka ambao 

alitegemea kufanya mtihani wake wa 

kidato cha nne.Akiwa pale darasani 

akiendelea na shughuli zake akaingia 

mkuu wa kituo kile alichokuwa akisoma 

Lucy.Alikuwa ameongozana na kijana 

mmoja mtanashati sana.Moyo wa Lucy 

ukastuka baada ya kuiona sura ya kijana 

yule aliyekuwa ameongozana na mkuu wa 

kituo kile.Kijasho kikaanza 

kumtoka.Alihisi ni kama vile ameona 

mzimu.Akaivua miwani yake akayafikicha 

macho yake na kuivaa tena. 

 " No ! This isnt true..hawezi kuwa 

mwenyewe..lazima nitakuwa ndotoni" 

akawaza Lucy huku akijifuta jasho.  " Wanafunzi nadhani mnafahamu 

kwamba kwa siku za hivi karibuni 

tumekuwa na tatizo la mwalimu wa 

hesabu.Mwalimu tuliyekuwa naye 

ameondoka kwenda kuendelea na 

masomo yake.kwa bahati nzuri 

tumefanikiwa kumpata mwalimu 

mwingine ambaye atakuwa akifundisha 

somo la hesabu.Anaitwa Jackson 

Ndukalyo.Natumai mtashirikiana naye 

vizuri kama mnavyofanya kwa walimu 

wengine."Akasema mkuu wa kituo kile. 

 Lucy nusura aanguke na kupoteza 

fahamu mara tu alipolisikia jina lile la 

Jackson Ndukalyo likitajwa. 

 " Mungu wangu ..huyu shetani amenifuata 

tena huku? akawaza Lucy jasho jingi 

likimtiririka.Mbele ya darasa ilikuwa ni 

zamu ya Mwalimu Jackson kujitambulisha 

 " Kama mkuu alivyowaeleza ninaitwa 

Jackson Ndukalyo ni mwanafunzi wa 

mwaka wa tatu chuo kikuu cha 

Makumira.Mkuu hapa ameniomba 

nimsadie kuwafundisha somo la hesabu 

wakati anatafuta mwalimu wa kudumu 

kwahiyo kwa kipindi hiki tutakuwa 

pampja.Ninachohitaji toka kwenu ni ushirikiano wenu.Kwa kuanzia itakuwa si 

vibaya kama nikiwafahamu kwa majina" 

akasema Jackson na ghafla akakutanisha 

macho na sura ambayo haikuwa ngeni 

machoni pake akastuka sana. 

 " Lucy !! .akasema kwa sauti kubwa na 

toka nyuma ya darasa akasimama 

msichana moja na kumfanya Jack 

ashangae. 

 " Hapana si wewe nimemuita huyu dada 

hapo kiti cha tatu ,wewe mwenye miwani" 

akasema Jack bado akiwa katika mstuko. 

 " Huyo si Lucy.Lucy ni mimi 

hapa.Ninaitwa Lucy swai" akasema yule 

msichana aliyesimama 

 " Aren't you Lucy? akauliza Jackson huku 

akimkaribia Lucy. 

 " No ! I'm not Lucy..My name is 

Linda..Linda Adamson" akasema Lucy na 

kumfanya Jack asimame na kumkazia 

macho. 

 " It Cant be...ni yeye mwenyewe 

kabisa.Hawezi kunipotea.Hata sauti yake 

ni ile ile japokuwa anaongea kiingereza 

vizuri kama mzungu..lakini amefanana 

sana na Lucy.." akawaza Jack kisha akatoa 

kitambaa na kujifuta jasho.  " Kama si yeye basi duniani wawili 

wawli.Msichana huyu anafanana sana na 

Lucy..Lakini huyu Linda japokuwa 

anafanana kwa kila kitu na Lucy yeye 

anaonekana ni kama anatokea katika 

familia yenye uwezo tofauti na 

Lucy..yawezekana nikawa 

nimewafananisha tu..ngoja nitafanya 

uchunguzi." akawaza jack huku wanafunzi 

wakiendelea kujitambulisha mmoja 

mmoja lakini Jack hakuwa akisikia 

mawazo yake yalikuwa mbali sana. 

 " Nilistuka sana nilipoiona sura ile ya 

Linda..Kwa kweli amefanana sana na 

Lucy...Amenikumbusha mbali sana kipindi 

Lucy anafanya kazi nyumbani 

kwetu..niliwahi kufanya naye mapenzi 

mara moja tu na mama akatufuma 

akamtimua Lucy nyumbani.Toka siku ile 

sijawahi tena kumtia machoni na sijui 

yuko wapi....Du ! lazima nifanye uchunguzi 

pengine labda huyu Linda ana undugu na 

Lucy haiwezekani wakafanana namna hii 

kwa kila kitu.." Jack akaendelea kuwaza 

.Ni sauti za wanafunzi wakicheka ndizo 

zilizomstua kutoka katika mawazo mengi. 

 " Mwalimu tayari tumeshamaliza.!!!!! wakasema wanafunzi huku 

wakicheka.Zoezi la kujitambulisha 

lilikwisha kitambo lakini Jack 

hakufahamu kama wanafunzi tayari 

wamemaliza kujitambulisha.Akili yake 

yote iliuw kwa Lucy Akaona aibu sana.. 

 "Nafurahi kuwafahamu nadhani kesho 

nitaanza rasmi kuwafundisha..kwa leo 

tuendelee kujisomea na kufanya mazoezi 

tuliyopewa." akasema Jack kisha akageuka 

na kupiga hatua akiondoka. 

 " Linda.Linda.....Linda.........." akawaza 

jack..Sura ya Linda tayari ilikwisha mpa 

wazimu.Alitamani arudi tena darasani 

lakini alikwisha waaga wanafunzi.Akiwa 

amesimama akiwaza ikatokea gari moja 

ikaegeshwa pembeni ya darasa la akina 

Lucy akashuka mzungu mmoja na 

kusimama nje ya gari akawa anaongea na 

simu.Jack akalikodolea macho gari lile na 

mara toka ndani ya darasa akatoka Lucy 

akaliendea lile gari.Yule mzungu 

akampokea Lucy begi lake halafu 

akamfungulia mlango wa gari akaingia na 

gari likaondoka kwa kasi 

 " Linda !..." Jack akasema kwa sauti ndogo 

huku akihisi fulana aliyoivaa ndani ikilowana kwa jasho . 

 ******************************* 

 " Nilistuka sana uliponitumia ujumbe 

kwamba nije nikuchukue haraka,..Nilihisi 

pengine unaumwa au kuna jambo 

limetokea" akasema Dr Shanom wakiwa 

njiani kueleka nyumbani. 

 " Samahani sana Dr Shanon kwa 

kukusumbua.Nilikutumia ule ujumbe kwa 

sababu nilianza kujisikia vibaya ghafla 

nikahsi kichwa kinaniuma na 

kizunguzungu ndiyo maana nikakuomba 

uje unichukue.Samahani sana." akasema 

Lucy 

 " Usijali Lucy..unajisikiaje sasa? 

Tunaweza kupita hospitali? 

 " Kwa sasa ninajisikia vizuri Dr 

Shanon.Hakuna haja ya kwenda hospitali" 

akasema Lucy 

 " Lucy umekuwa ukisoma sana hadi usiku 

mwingi.Muda mwingine unatakiwa 

kupumzika na kuiacha akili itulie" 

akasema Dr Shanon. 

 " Sawa Dr Shanon kuanzia sasa 

nitajitahidi nisisome hadi usiku mwingi" akasema Lucy kisha akazama katika 

mawazo.. 

 " Yule shetani amenifanya nikapoteza 

kabisa hamu ya kukaa darasani...Mungu 

kwa nini umenikutanisha tena na yule 

ibilisi? Historia yangu yote ya nyuma 

ambayo ninajitahid kuisahau imerudi 

upya baada ya kumuona jack..Uchungu 

umeanza upya..Nimemkumbuka 

mwanangu Angela.." akawaza Lucy. 

 " Nilifanya jambo zuri kubadilsha 

jina.Nina hakika Jack alinitambua lakini 

jina ndilo lililonisaidia kuniweka tofauti 

na Lucy anayemfahamu yeye.Jack ndiye 

chanzo cha matatizo yote 

niliyoyapata.Yeye ndiye aliyenipa mkosi 

katika maisha yangu.Ninamchukia sana 

jack...Laiti angeingia moyoni mwangu na 

kuona jinsi ninavyomchukia angehama 

huu mji.Lakini iko siku nitajitambulisha 

kwake ana kwa ana na siku hiyo ataomba 

ardhi ipasuke aingie ndani.Kwa sasa ngoja 

niendelee na masomo yangu kwa bidii" 

akawaza Lucy na kuuma meno kwa hasira. 

Jioni ya siku hiyo Lucy aliwahi kuingia 

chumbani kwake kulala,hali hii 

ikawashangaza sana Dr Shanon na Rachel kwa sababu siku zote Lucy huwa ni mtu wa 

mwisho kulala. 

 "Kuna kitu kinamsumbua Lucy." akasema 

Dr Shanon 

 " Hata mimi nimegundua utofauti 

mkubwa katika hali yake leo.Anaonekana 

kama anaumwa" akasema rachel 

 " Sidhani kama anaumwa.Kuna jambo 

linamsumbua sana akili yake.Alinipigia 

simu nimfuate shuleni,akaniambia 

kwamba alianza kujisikia vibaya na ndiyo 

maana akaniomba niwahi kwenda 

kumchukua.Nilipomwambia kwamba 

tupitie kwa daktari alikataa kata kata." 

Akasema Dr Shanon . 

 " Inatubidi tufahamu kile 

kinachomsumbua Lucy ili tuweze 

kumsaidia" akasema Rachel. 

 "Ninatamani sana kumuuliza nini 

kinamsumbua lakini nina imani 

hatanieleza ..bado hayuko tayari kuweka 

wazi kitu gani kinamsumbua.Nina hakika 

liko jambo linaisumbua akili yake na siku 

moja ataamua kuliweka wazi.Tusubiri 

hadi siku hiyo itakapofika." akasema Dr 

Shanon. 

 Lucy alikuwa amekaa kitandani amekiegemeza kichwa chake katika 

kiganja cha mkono.Alikuwa katika 

mawazo mengi 

 " Bado siamini kama ni kweli nimekutana 

na Jack tena.Sikupanga kabisa kukutana 

naye katika maisha yangu.Simpendi sana 

yule kijana kwa sababu yeye ndiye chanzo 

cha maisha ya mateso niliyopitia.Yeye 

ndiye aliyenishawishi kufanya mapenzi 

siku ile pale sebuleni tukakutwa na mama 

yake.Maisha yangu yalianza mkosi siku 

ile.Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza 

kufanya mapenzi na ni siku hiyo hiyo 

nikashika mimba nikajifungua mtoto 

wangu wa kwanza Angela 

nikamtelekeza.Sijui kama mwanangu yuko 

hai au amekufa." Alipowaza kuhusu 

mwanae Angela akashindwa kujizuia 

kudondosha machozi . 

 " Masikini mwanangu sijui yuko wapi saa 

hizi.Nilifanya kosa kubwa sana 

kumtelekeza mwanangu lakini sikuwa na 

jinsi zaidi ya kufanya vile.Sikuwa na 

mahala pa kuishi,.sikuwa na fedha wala 

chakula.Ningeishi vipi na mwanangu? " 

akawaza Lucy huku akifuta machozi. 

 " Nina imani Mungu atakuwa alimlinda mwanangu asidhirike.Nina imani siku 

moja maisha yangu yatakuwa mazuri na 

nitafanya utafiti kuhusu mwanangu kama 

yuko hai au alikufa." 

 Sura ya Jack ikamjia tena kichwani 

akauma meno kwa hasira 

 " simpendi sana Jack na sijui ni kwa nini 

nimekutana naye tena.Nayachukia 

mapenzi na ninawachukia sana wanaume 

kwa mambo waliyonifanyia.Moyo wangu 

hauna hata chembe ya mapenzi kwa 

viumbe hawa.Ninawachukia mno 

nikianzia na Jack.nashukuru 

hajanitambua kama mimi ni Lucy 

japokuwa bado ana mashaka na 

mimi.Sintampa nafasi ya kunifahamu 

shetani yule.Siku ile wakati mama yake 

akinifukuza nyumbani kwao kama mbwa 

alikuwa amesimama akiniangalia bila hata 

kujaribu kunitetea kwamba yeye ndiye 

aliyenishawishi tukafanya mapenzi.Siku 

moja nitalipa kisasi.Nitalipa kisasi kwa 

wale wote walionitenda vibaya kwa 

sababu ya umasikini wangu." akaendelea 

kuwaza Lucy. 

 " laiti kama ingekuwa ni kwa maamuzi 

yangu basi ningehama kabisa katika kituo kile ili nisiweze kuonana na Jack.Lakini 

kwa hatua niliyofikia sasa ngoja tu 

nivumilie na nimalizie muda huu 

uliobakia.Kitu cha msingi ninachotakiwa 

kukifanya ni kujiweka mbali kabisa na 

Jack na kutompa nafasi ya kunifahamu au 

kunizoea. " 

 wakati Lucy akiwa katika mawazo mengi 

kuhusiana na kukutana tena na Jack 

kijana wa kwanza kufanya naye mapenzi 

na anayeamini kwamba ndiye chanzo cha 

maisha yake yote ya shida,kwa upande wa 

Jack naye alikuwa na mawazo mengi sana 

kuhusiana na msichana aliyemkuta katika 

darasa analotarajia kuanza kulifundisha 

,msichana ambaye anafanana mno na Lucy 

msichana aliyewahi kufanya kazi 

nyumbani kwao na akafukuzwa na mama 

yake baada ya kuwafuma wakifanya 

mapenzi sebuleni. 

 " Linda....!! Amefanana mno na 

Lucy.Yaani ukimuangalia Lucy na Linda ni 

kama mapacha vile.Hata sauti ni ile 

ile.Ama kweli duniani wawili 

wawili.Tofauti iliyopo ni kwamba Linda 

anaonekana mrembo zaidi.Ana ngozi 

nyororo ya kung'aa,ana nywele ndefu ana umbo zuri Lucy yeye pamoja na kwamba 

alikuwa na uzuri wa asili lakini uzuri wake 

ulikuwa umejificha Linda anaishi na 

wazungu na hata tabia zake ni kama za 

kizungu.Linda amenivutia sana 

Nitalazimika kuanza kujenga ukaribu naye 

ili niweze kuzoeana naye.Ni binti mzuri 

mno...." 

 "Kila nikimtazama Linda ananikumbusha 

kuhusu Lucy.Mimi ndiye mwanaume wake 

wa kwanza kufanya naye mapenzi.Mimi 

ndiye niliyemtoa usichana wake.Msichana 

mzuri kama yule hakuwa ameguswa na 

mwanaume yeyote yule..Ni nadra sana kaa 

miaka hii ya sasa kumkuta binti kama yule 

akiwa bado hajaanza mchezo huu wa 

mapenzi" 

 jack akachukua glasi ya maji akanywa na 

kisha akajilaza kitandani 

 " Sijui ni kwa nini mawazo ya kuhusu 

Lucy yamenijia ghafla toka nilipomuona 

Linda.Bado ninaikumbuka sura yenye 

tabasamu ya Lucy msichana aliyekuwa na 

heshima nyingi.Ninaanza kuhisi msichana 

kama Lucy iwapo angepata elimu ya 

kutosha na matunzo mazuri anafaa sana 

kuwa mke.Hawa wasichana wetu wa mijini siku hizi wanachoangalia ni maslahi yao 

tu.Sikutegemea kabisa kama Salha 

angekuja kunifanya kama 

alivyonifanyia.Nilimpenda na kumpa kila 

alichokihitaji lakini mwisho wa siku 

aliamua kuachana na mimi kwa kuwa 

bado mwanafunzi na kuanza mahusiano 

na muuza madini.Nilikwisha msahau Lucy 

kabisa lakini kama ningemuona 

ningeweza kumsaidia kwa kumpeleka 

shule akasome na kisha ningemfanyia 

mpango wa kazi au biashara.Msichana 

kama yule sina hakika kama anaweza 

akakusaliti .Nina hamu ya kumuona Lucy 

lakini sifahamu ninaweza kumuona 

wapi..anyway nitajitahidi kujenga 

mahusiano mazuri na Linda msichana 

ambaye kila nikimuona ninahisi 

nimemuona Lucy.Pengine yawezekana 

Lucy na Linda wakawa na uhusiano 

fulani.Haiwezekani wakafanana namna ile 

kwa kila kitu'" akawaza Jack. 

 ************************************* Hatimaye Jack akaanza kufundisha 

somo la hesabu katika darasa la akina 

Lucy.Kwa siku chache za mwanzo Jack 

alijitahidi kufundisha vizuri kiasi cha 

kuwafanya wanafunzi wamfurahie.Wiki ya 

kwanza ilikatika na kuanza ya pili bado 

hakukuwa na tatizo lolote baina yake na 

Linda.Jumatatu ya wiki ya tatu toka Jack 

aanze kufundisha Dr Shanon alichelewa 

kidogo kwenda kumchukua Lucy kama 

ilivyo kawaida na kumuomba amsubiri 

hapo hapo shuleni hadi atakapofika.Dr 

Shanon hakutaka kabisa Lucy atembee 

kwa miguu umbali mrefu wa kutoka hapo 

shuleni hadi nyumbani.Wanafunzi wote 

waliondoka na kubaki Lucy peke yake.Jack 

alifunga ofisi na kwa mbali alimuona 

msichana amekaa peke yake akichezea 

simu yake.Mara moja akamtambua 

msichana yule alikuwa ni Linda. 

 " Linda anafanya nini mpaka mida hii? 

akajiuliza Jack huku akipiga hatua 

kumwendea. 

 " Linda leo huendi nyumbani? akauliza 

Jack.Lucy akaacha kuichezea simu yake 

akamtazama Jack na kuse ma 

 "Namsubiri Dada Shanon anakuja kunichukua sasa hivi" 

 "Hautajali kama nikikaa nawe hadi 

atakapokuja dada yako kukuchukua? 

NInaogopa kukuacha hapa peke yako" 

akasema Jack na kwa mara ya kwanza 

toka amemfahamu Linda akatabasamu na 

kusema 

 " Hakuna tatizo wewe unaweza ukaenda 

zako.Mimi siogopi kitu isitoshe hapa kuna 

mlinzi" akajibu Lucy 

 " Usiogope Linda..mimi si mtu 

mbaya..niruhusu tafadhali niweze kukaa 

nawe kwa muda huu mfupi..Linda 

nimekuwa nikiitafuta nafasi ya kukaa 

nawe walau tufahamiane lakini 

nimekosa.Naomba tafadhali hata dakika 

mbili tuongee tufahamiane zaidi." 

akaomba Jack 

 " Mwalimu tufahamiane kivipi tena 

wakati tayari tunafahamiana? wewe 

unaitwa mwalimu Jack na mimi ninaitwa 

Linda..sasa tufahamiane nini tena? 

akauliza Linda akionyesha kuanza 

kukerwa kukaa na Jack karibu. 

 " Linda si hivyo tu,sisi kama vijana kuna 

mambo mengi ambayo tunaweza tukakaa 

na kujadili ikiwemo hata masomo.Nimeangalia taarifa za matokeo 

ya mitihani mliyokuwa mkifanya huko 

nyuma nimefurahishwa sana na matokeo 

yako.Unaonekana ni msichana mwenye 

maendeleo mazuri sana 

darasani.Nimeangalia katika somo la 

hesabu na unaonekana kufanya 

vizuri.Pamoja na hayo bado ninaweza 

kukuongezea maarifa zaidi ya somo hili la 

hesabu pamoja na masomo mengine ya 

sayansi na kukusadia ukafaulu vizuri." 

akasema Jack na kisha Lucy akamtazama 

na kusema 

 " Mwalimu wewe unafundisha pia 

masomo ya sayansi? 

 " Ndiyo ,mimi ni mtaalamu sana wa 

hesabu,kemia fizikia na hata baiolojia 

masomo ambayo kama ukiyazingatia na 

kufaulu vizuri halafu ukaendelea na hadi 

elimu ya juu basi ajira zake ziko wazi sana 

na zina maslahi mazuri .Unaweza ukawa 

daktari au mhandisi n.k. " akasema Jack na 

kumfanya Lucy atabasamu 

 " Kama hutakuwa na shughuli nyingi siku 

za jumamosi unaweza kuwa unakuja hapa 

shuleni nikakufundisha bila malipo 

yoyote.Ni msaada wangu kwako ili kukuwezesha ufaulu vizuri" akasema jack 

 "Nitaangalia jumamosi hii kama nikipata 

nafasi nitakuja" akasema Lucy. 

 " Jitahidi sana Linda unajua kuna mambo 

mengi ya kusoma na muda wenyewe 

umebaki kidogo.Mimi niko tayari 

kukusaidia kwa hali na mali" akasema 

Jack .Lucy akataka kusema jambo lakini 

gari la Dr Shanon likawa limefika. 

 " Mwalimu tutaonana..usiku mwema." 

Lucy akamuaga jack na kuingia garini. 

 " Samahani Lucy..ouh sorry Linda 

.nimechelewa kuna mahala nilikuwa 

nimepitia.Habari za masomo? akuliza Dr 

Shanon. 

 " habari za masomo ni nzuri Dr Shanon" 

akajibu Lucy. 

 " Yule kijana ulikuwa umekaa naye 

mkiongea naye ni mwanafunzi? 

 " hapana yule ni mwalimu wetu mpya wa 

hesabu anaitwa Jack." 

 " ouh ok..Lucy unaonekana unapenda 

sana hesabu" 

 " Ndiyo Dr Shanon ,ninapenda sana 

hesabu na masomo ya sayansi" 

 " vizuri sana ..mimi nilifikiri unapenda 

sana masomo ya biashara."  " Awali nilikuwa napenda sana kusoma 

biashara lakini kwa sasa nimeamua 

kuongeza bidii katika masomo ya 

sayansi.Nataka kuwa daktari kama wewe" 

akasema Lucy na kumfanya Dr Shanon 

atabasamu. 

 Jioni wakiwa mezani wakipata chakula 

cha usiku Dr Shanon akasema 

 " Rachel na Lucy kuna jambo ambalo 

ninataka kuwafahamisha" Rachel na Lucy 

wakastuka kidogo 

 "Jambo gani hilo Dr Shanon? " akauliza 

Rachel 

 " Leo nimepata taarifa kutoka ofisi yetu 

kuu..nimetaarifiwa kwamba mwishoni 

mwa mwaka huu nitakapomaliza utafiti 

wangu ninatakiwa kurejea nchini 

Marekani.Ni taarifa ambayo imenistua 

sana kwa sababu sikutegemea kama 

ningeweza kuondoka Tanzania hivi 

karibuni.Nimeipenda sana Tanzania,ni 

nchi nzuri." akasema Dr Shanon 

 Rachel na Lucy wakashikwa na 

mshangao wakabaki wakimuangalia Dr 

Shanon 

 " Nafahamu mmestuka sana .Hata mimi 

nimestuka sana ...." akasema Dr Shanon.  Lucy akashindwa kuendelea kula 

akaweka kijiko chini. 

 " Baada ya kupata taarifa hii kuna jambo 

ambalo nimeliwaza..Lucy umekuwa ni 

rafiki yetu mkubwa.tumeishi nawe kwa 

muda mrefu sasa na ningependa sana 

kuendelea kuishi nawe na kukusaidia 

kutimiza malengo yako.Nimefikiria kama 

utakuwa tayari kwa ridhaa yako 

mwenyewe ukubali tuongozane kwenda 

wote Marekani ukaishi huko.Kama 

ukiamua kuongozana na mimi itakuwa ni 

fursa yako nzuri ya kuweza kutimiza 

ndoto zako." Lucy akamtazama Dr Shanon 

na kisha akasema 

 " Dr Shanon sipati neno la kukushukuru 

kwa namna unavyonisaidia.Umekuwa 

nami kwa muda mrefu na umenitunza 

kama ndugu yako wa damu.Nashukuru pia 

kwa nafasi hii uliyonipatia ya kuongozana 

nawe kwenda Marekani.Ninaomba Dr 

Shanon unipe muda wa kuweza kulifikiria 

jambo hili halafu nitakupa jibu" akasema 

Lucy na kumfanya Dr Shanon atabasamu 

 " Usijali Lucy..bado una muda mrefu wa 

kuweza kutafakari na kupata jibu.Pindi 

ukiwa tayari nieleze msimamo wako ili kama ukiamua kuongozana nami nianze 

mara moja kushughulikia taratibu za 

kuondoka na wewe kwenda Marekani." 

Usiku huo ulikuwa ni usiku mrefu sana 

kwa Lucy .Alikuwa akiwaza juu ya jambo 

aliloambiwa la kuongozana na Dr Sjanon 

kwenda Marekani.Suala hili lilimuumiza 

kichwa sana. 

 " Ni kweli hii ni fursa yangu ya kipekee 

kabisa ambayo sikuwahi kuiota kama 

nitakuja kuipata katika maisha 

yangu,fursa ya kwenda kuishi Marekani.Ni 

nafasi pekee ya kuniwezesha kutimiza 

ndoto zangu nyingi.Nikiwa kule nitaweza 

kupata elimu bora na maisha mazuri .Nina 

kila sababu ya kukubali kuongozana na Dr 

Shanon kwenda Marekani lakini papo 

hapo moyo wangu unakuwa mgumu 

kukubali kuondoka hapa nchini kwenda 

kuishi Marekani kwa sababu moja 

kubwa.Ninataka kuutafuta ukweli juu ya 

mwanangu Angela.Nataka nifahamu kama 

Angela alifanikiwa kuishi au alipoteza 

maisha.Angela ni mwanangu wa kwanza 

na dhamiri yangu inanisuta kila 

nikikumbuka kitendo nilichokifanya cha 

kumtelekeza.Kila nikifikiria suala hili ninaumia sana moyoni na hii ndiyo sababu 

ambayo inanifanya nisite kuongozana na 

Dr Shanon kwenda Marekani.Iwapo 

nikienda Marekani ndoto zangu za 

kumtafuta mwanangu zinaweza 

zikapotea.Ninaweza nisiipate tena nafasi 

ya kurudi na kuja kuutafuta ukweli 

kuhusu mwanangu..." Lucy akainuka 

kitandani na kukaa. 

 " Hapana sintakwenda 

Marekani.Itanilazimu kuikataa nafasi hii 

adimu sana kutokea kwa ajili ya sababu 

moja tu nayo ni kuendelea kubaki hapa 

hapa nchini kwa lengo la kumtafuta 

mwanangu ambaye kila usiku ninaisikia 

sauti yake masikioni mwangu.Sura yake 

ya kitoto inanijia akilini mwangu kila siku 

na kunifanya nikijutie kitendo changu cha 

kumtelekeza.Kwa sasa nimegundua kosa 

nililolifanya ,sikupaswa kumtelekeza 

mwanangu hata kidogo kwa kigezo cha 

ugumu wa maisha.Kitendo kile ni sawa na 

kitendo cha uuaji.Suala hili sintaweza 

kulivumilia hata kidogo.Iwapo 

nisipolitafutia ufumbuzi wa haraka suala 

hili litanitesa katika maisha yangu yote 

yaliyobakia.Angela ndiye furaha yangu,ndiye kila kitu kwangu..lazima 

nifanye kila njia ili niweze kumtafuta.Kitu 

kikubwa ninachotaka kukifanya kwa sasa 

ni kwanza nimalize masomo yangu halafu 

nitengeneze maisha yangu na ndipo 

nianze mchakato wa kuutafuta ukweli 

kuhusu mwanangu.Hata kama itanichukua 

muda mrefu kiasi gani lakini lazima 

niutafute ukweli kuhusu 

mwanangu.Lazima nifahamu kama 

mwanangu alikufa au yuko hai.Kama 

alikufa sijui nitafanya nini ili niweze 

kukisahau kitendo nilichokifanya.Lakini 

kama atakuwa yuko hai nitafanya kila 

niwezalo ili kuhakikisha kwamba 

ninampata " akawaza Lucy na katika 

macho yake yalionekana machozi 

yakimtoka. 

 " Najua maamuzi haya yanaweza 

yakamsikitisha sana Dr Shanon kwa 

sababu ana lengo zuri la kuhakikisha 

ninakuwa na maisha bora.Dr Shanon ni 

mtu ambaye sintaweza kumsahau hata 

kidogo kwani ndiye mtu aliyeyabadilisha 

maisha yangu.Amenitoa mavumbini 

amenitakatisha na kunifanya ning'ae tena 

na kuonekana ni mmoja kati ya watu.Sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya 

kuikataa ofa yake ya kwenda 

Marekani.Najua atataka kufahamu ni kwa 

nini nimekataa kuongozana naye lakini hii 

itabaki ni siri yangu na sintamueleza mtu 

yeyote yule." Lucy akainuka pale kitandani 

akaenda kufungua dirisha akachungulia 

nje.Juu angani mbalamwezi ilikuwa 

ikiangaza na kuling'arisha anga.Kwa muda 

wa dakika kadhaa Lucy akabaki akiangalia 

angani. 

 " Mawazo juu ya mwanangu Lucy 

yamenipeleka mbali na kunifanya 

nimkumbuke Jack baba yake.Mpaka sasa 

hivi bado hajagundua kwamba mimi ni 

Lucy na sitaki alijue hilo.Tayari 

amekwisha kubaliana na ukweli kwamba 

mimi ni Linda na si Lucy.Jack amenifanya 

niwachukie wanaume wote kwa sababu 

yeye ndiye chanzo cha mateso yangu 

yote.Kama si yeye basi nisingepitia maisha 

haya ya shida niliyoyapata baada ya 

kufukuzwa pale nyumbani kwao." 

 Lucy akachukua maji katika kikombe 

akamwagia ua lililokuwa pembeni ya 

dirisha halafu akaendelea kukaa pale 

dirishani.  " Siku hizi Jack amebadilika .Amependeza 

sana.Hata muonekano wake umebadilika 

kabisa tofauti na kipindi kile.Hata hivyo 

ninamshukuru kwa sababu ameonekana 

kuwa na moyo wa kunisaidia katika 

masomo ya hesabu na sayansi.Sielewi 

kama ana nia ya kweli kutoka moyoni ya 

kunisaidia ama ana lake jambo.Lakini 

mpaka sasa hivi bado sijaona kama ana 

nia mbaya na mimi.Anaonekana ni kijana 

mwenye ukomavu mkubwa wa akili 

tofauti na kipndi kile nilipokuwa nakaa 

kwao.Vyovyote itakavyokuwa 

sintathubutu kumweleza kwamba yeye 

ndiye baba wa mwanangu.Ninasikitika 

kwa hilo lakini kama mwanangu Angela 

atakuwa bado hai,hatafanikiwa 

kumfahamu baba yake ambaye ndiye 

chanzo cha maisha yangu magumu na 

yenye mateso mengi.Kila nikikumbuka 

mateso na magumu niliyopitia ninashikwa 

na hasira nyingi na ninajikuta 

nikimchukia Jack zaidi." akawaza Lucy

halafu akafunga dirisha na kurudi zake 

kulala. 




 Jack aliendelea kumsaidia Lucy 

kulifahamu vyema somo la hesabu pamoja 

na masomo mengine ya sayansi .Lucy 

alijifunza kwa bidii kubwa sana na 

maendeleo yake yalitia moyo.Katika muda 

huu wote Jack bado alikuwa na mawazo 

mengi kuhusu kufanana kwa kiwango 

kikubwa kati ya Lucy na Linda.Kila mara 

awapo karibu na Linda alikuwa 

akimkumbuka Lucy. 

 " Ninajitajidi kuamini kwamba duniani 

watu wameumbwa wawili wawili lakini 

inakuwa vigumu kuamini kuhusu Lucy na 

huyu Linda.Haiwezekani wakafanana kiasi 

hiki.Ninamfahamu vizuri Lucy.Alikuja 

nyumbani kwetu akiwa bado mdogo 

kabisa.Amepevuka akiwa nyumbani 

kwetu kwa maana hiyo ninamfahamu 

vizuri sana na ndiyo maana ninastuka kila 

nimuonapo Linda.Inawezekana wakawa ni 

ndugu? ..iko siku nitajaribu kuupata 

ukweli" akawaza Jack. 

 Siku ya jumamosi Lucy akahudhuria 

masomo kama ilivyokuwa kawaida.Siku 

hii Jack alikuwa amejitolea kumfundisha bure masomo ya sayansi pamoja na 

hesabu.Saa tatu za asubuhi masomo 

yakaanza hadi ilipotimu saa saba za 

mchana.Mpaka mida hiyo bado gari 

inayokuja kumchukua Lucy ilikuwa 

haijafika.Wakati Jack akiendelea 

kufundisha mara ujumbe wa maandishi 

ukaingia katika simu ya Linda.Akaufungua 

akausoma na kisha akaanza kukusanya 

vitabu vyake .Jack akashangaa. 

 " Linda vipi mbona unakusanya vitabu? 

akauliza Jack 

 " Dr Shanon amenitumia ujumbe kwamba 

amepata dharura kwa hiyo hataweza kuja 

kunichukua leo.Ameniomba nichukue 

taksi hadi nyumbani.Mwalimu naomba 

tuishie hapa kwa leo." akasema Lucy huku 

akilivaa begi lake na kuinuka tayari kwa 

kuondoka 

 " Linda kama gari ya kukuchukua haiji 

leo, unaonaje kama tukiongozana hadi 

kwa rafiki yangu mmoja nikakupatie ile 

mitihani ya zamani ukaifanyie mazoezi 

kwa siku ya leo? akasema Jack na kisha 

Lucy akatabasamu 

 " Hilo ni wazo zuri mwalimu.Si mbali sana 

kutoka hapa? kwa sababu sitaki kuchelewa nyumbani" 

 " Hapana si mbali hata kidogo.Ni mwendo 

wa dakika kumi kwa miguu lakini 

tukichukua taksi ni dakika nne tu" akajibu 

Jack huku akiifuta mikono yake kwa 

kitambaa . 

 Bila kusita Lucy akamkubalia Jack 

waongozane wote kwenda kuchukua 

mitihani ya zamani kwa ajili ya 

mazoezi.Jack akafunga kila kitu 

wakaondoka pale shuleni hadi katika 

kituo cha taksi wakachukua taksi hadi 

katika nyumba ambayo alikuwa akiishi 

huyo rafiki wa Jack. 

 " Tumefika..." akasema Jack na kisha Lucy 

akateremka.Jack akamlipa dereva pesa 

yake na kumwambia aondoke zake. 

 " Mwalimu Jack usimruhusu aondoke 

.Mwambie anisubiri nichukue hiyo 

mitihani halafu anipeleke nyumbani" 

akasema Lucy. 

 " Usijali Linda.Kuna kituo cha taksi hapo 

mtaa wa pili.Ninavyowafahamu madereva 

taksi ukimwambia akusubiri inakubidi 

ulipe muda atakaokaa kukusubiri " 

akasema Jack kisha akafungua geti la ile 

nyumba kubwa ambayo ilionekana kama ujenzi wake ulikuwa ukiendelea. 

 " Karibu ndani Linda..Hapa ndipo 

anapoishi rafiki yangu..anaitwa Frank" 

akasema Jack huku akitabasamu. 

Akagonga mlango wa sebuleni na mara 

sauti toka ndani ikamruhusu aingie .Jack 

akaufugua mlango na kuingia ndani 

akamkaribisha Lucy naye aingie 

ndani.Katika ile sebule kubwa alikuwepo 

kijana mmoja aliyekuwa amevaa fulana 

nyeupe amejilaza sofani akitazama 

luninga kubwa huku pembeni yake akiwa 

na chupa ya bia. 

 " hallow Frank" akasema Jack 

 " Ouh Jack karibu sana ..karibu ndani" 

akasema Frank huku akiinuka sofani 

baada ya kumuona Lucy. 

 " Ouh Jack umetuletea mgeni ..karibu sana 

 " Ahsante sana" akasema Lucy. 

 " Anaitwa Linda.Ni yule mwanafunzi 

niliyekwambia kwamba ninamfundisha 

hesabu na masomo ya sayansi.Nimekuja 

naye ili n iweze kumpatia ile mitihani ya 

zamani akafanyie mazoezi." akasema Jack 

 "Jack huyu ni rafiki yangu anaitwa 

Frank.Wote ni wanafunzi tunasoma chuo kimoja .Hapa ni nyumbani kwake anaishi 

yeye mwenyewe wazazi wake wako ulaya 

." akasema Jack. 

 " Nafurahi sana kukufahamu Linda.Jack 

amekuwa akikusifia sana juu ya uwezo 

wako darasani na kunifanya niwe na hamu 

ya kukuona.Nimefurahi leo kukutana 

nawe.Karibu sana Linda..Make yourself at 

home" akasema Frank huku akiinuka na 

kuliendea friji kubwa akalifungua na 

kutoa vinywaji akaweka mezani. 

 " Linda unatumia kinywaji gani? akauliza 

Frank. 

 " ninaomba maji ya kunywa " akajibu 

Lucy 

 " C'mon Linda ,kuwa huru..usiogope 

kitu..chagua kinywaji chochote 

unachokipenda" akasema Frank 

 " Nashukuru Frank lakini kwa leo nina 

haraka kidogo..siku nyingine nitakunywa 

kinywaji usijali." akasema Lucy 

 " Linda wewe ni mgeni wetu na 

umetutembelea nyumbani 

kwetu.Nakuomba tafadhali ukae japo kwa 

siku ya leo upate chakula cha mchana 

pamoja nasi halafu tutakurudisha 

nyumbani.Mgeni kama wewe umekuja halafu uondoke bila hata kutia baraka 

katika nyumba yetu si jambo la busara" 

akasema Frank na Jack naye akaingilia 

kati 

 " Kweli Linda..nakuomba ukubali kukaa 

nasi siku ya leo na upate chakula cha 

mchana pamoja nasi.Nitakurudisha mimi 

mwenyewe nyumbani kwenu.usihofu kitu" 

akasema Jack 

 Lucy akafikiri kidogo na kusema.. 

 " Ok mwalimu Jack nitabaki kwa heshima 

yako lakini naomba nisichelewe 

sana.Ngoja niongee na dada Rachel 

nimweleze kwamba nitachelewa kidogo" 

akasema Lucy huku akichukua simu yake 

na kutoka nje. 

 " Wow ! Jack nitafutie nafasi ya 

kufundisha katika hiyo shule yako kumbe 

kuna watoto wazuri namna hii? akatania 

Frank 

 " Shhhhhhhhh..!! Frank utaacha Linda 

akusikie" akasema Jack kwa sauti ndogo 

 " Nikwambie kitu Jack..nimemuona huyu 

mtoto katika macho yake..the way she 

look at you ,she loves you brother.This is 

the chance dont waste it. " 

 " C'mon Frank unataka kusema nini ? akauliza Jack 

 " Ina maana huelewi Frank? This is tha 

chance you've got..use it.kama huwezi nipe 

mimi halafu uone 

nitakavyofanya..atatamani ahamie 

kwangu..." 

 " Ouh frank frank dont let me do that 

please.." 

 " Usiwe mshamba Jack..Huyu mtoto 

anakutaka na ndiyo maana akakubali 

kuongozana nawe kuja huku.Nenda naye 

chumbani mimi nitakuletea kinywaji huko 

huko chumbani na kisha fanya kila 

unaloweza ili uweze kufanya naye 

mapenzi." 

 " Fran.................." Jack akataka kusema 

neno lakini Frank akamkatisha 

 " No...Jack do as I tell you to do..Go 

men..go.." akasema Frank na mara Lucy 

akarejea tena sebuleni. 

 " Jack mimi ninakwenda jikoni kuandaa 

chakula wewe unaweza ukaendelea 

kumuonyesha Linda ile mitihani yote ya 

nyuma.Tazama katika kabati la pembeni" 

akasema Frank kisha akaondoka pale 

sebuleni akaelekea jikoni. 

 " Hapana leo sikubali msichana huyu aondoke hivi hivi.Linda atatudharau sana 

kama ataondoka katika nyumba hii bila 

hata kuguswa.Kama Jack akishinda mimi 

sintakubali ..mtoto ni mzuri mno..mtoto 

ameumbwa akaumbika..Leo lazima aimbe 

wimbo wa kwao" akawaza Frank wakati 

akianza kuandaa chakula . 

 " Linda , kama alivyosema Frank wakati 

yeye akiandaa chakula tusipoteze wakati 

twende nikakuonyeshe ile mitihani yote 

ya nyuma uchague ni ipi itakayokufaa" 

akasema Jack huku akisimama na kuanza 

kuongoza njia Lucy akamfuata.Moja kwa 

moja wakaingia katika chumba cha kulala 

cha Frank.Kilikuwa ni chumba kikubwa 

chenye samani za kuvutia. 

 " Linda hakuna kiti humu ndani,karibu 

uketi hapo kitandani usiogope kitu" 

akasema Jack halafu akalifungua kabati 

aliloelekezwa na Frank na kutoa mitihani 

mingi akaenda kuimwaga pale kitandani. 

 " Kila mtihani unaouhitaji uko hapa 

Linda..Utaangalia wewe mwenyewe kama 

utachukua yote au utachagua baadhi" 

akasema Jack huku akitabasamu 

 "Nashukuru sana mwalimu Jack..Nina 

imani mitihani hii itanisaidia sana.Unaweza ukaniruhusu niondoke 

nayo yote? akauliza Lucy lakini kabla Jack 

hajajibu mlango ukafunguliwa akaingia 

Frank akiwa na glasi mbili zenye juice . 

 " Wakati chakula kikiandaliwa,endeleeni 

kupata vinywaji" akasema Frank na 

kumpatia kila mmoja glasi moja. 

 Frank akatoka mle chumbani na 

kuwaacha Lucy na Jack wakiendelea 

kuchambua mitihani ile.Jack alikuwa 

akimtazama Lucy usoni. 

 " mwalimu mbona unaniangalai hivyo? 

akauliza Lucy. 

 " Linda kila nikikuona ninamkumbuka 

msichana mmoja ambaye sijui nitamuona 

wapi.Yaani umefanana naye mno." 

akasema Lucy 

 " Msichana huyo alikuwa ni mpenzi wako? 

akauliza Lucy 

 " Hapana Linda msichana huyo hakuwa 

mpenzi wangu lakini nina historia na 

msichana huyo .Ni mtu ambaye nimeishi 

naye kwa muda mrefu na ninaheshimiana 

naye sana." akajibu Jack 

 " Ouh mimi nilidhani labda ni mpenzi 

wako.kwani wewe mwalimu Jack una 

mke? akaliza Lucy " Hapana Linda sina mke " akajibu Jack . 

 "Unasubiri nini? akauliza Lucy 

 "Linda mbona una maswali magumu 

namna hiyo? akauliza Jack huku akicheka 

 " Ninataka kufahamu tu mwalimu..Kuna 

ubaya wowote nikijua? 

 " hakuna ubaya..vipi kuhusu wewe una 

mpenzi? akauliza Jack na mara Lucy 

akastuka 

 " Mbona umestuka Linda ? akauliza Jack 

 " Nimestushwa na swali lako..Mimi sina 

mpenzi na sitaki kuwa na mpenzi kwa 

sasa" akasema Lucy na kisha akajilaza 

kitandani.Alianza kuhisi mabadiliko ya 

ghafla..Alihisi macho yake nayakuwa 

mazito. 

 Lucy alipojilaza kitandani kinguo 

alichokuwa amekivaa kikapanda juu na 

kulifanya tumbo lake jeupe lionekane 

wazi wazi..Jack akastuka na mapigo ya 

moyo yakaanza kwenda mbio. 

“ Mbona naanza kuhisi usingizi wa ghafla? 

Macho yangu yanakuwa mazito sa…..” 

akawaza Lucy na kujikuta akishindwa hata 

kufumbua jicho lake.Usingizi mzito 

ukamchukua. 

 Jack alibaki mdomo wazi akimtazama Lucy aliyekuwa amejilaza pale 

kitandani.Kinguo chake kifupi kilipanda 

juu na kuliacha wazi tumbo lake 

jeupe.Msisimko wa ajabu 

ukampata.Akaiweka glasi yake chini na 

kuendelea kumtazama Lucy . 

 “ Dah ! Linda ni msichana mzuri sijawahi 

kuona.. mbona ananitia majaribuni kwa 

huu ukaaji wake? Akawaza Jack kisha 

akamuita Lucy lakini hakuitika. Akamuita 

tena kwa mara ya pili bado Lucy hakuitika. 

 “ Ina maana Linda amelala usingizi kiasi 

cha kutosikia ninavyomuita? Akawaza 

Jack huku akimsogelea taratibu 

.Akamtingisha lakini Lucy hakustuka.Jack 

akaanza kupatwa na wasi wasi . 

 “ Huu usingizi gani wa ghafla namna hii? 

…akawaza Jack na kuendelea kumtingisha 

Lucy kwa mara nyingine tena lakini bado 

Lucy hakuamka.Jack kijasho kikaanza 

kumtoka 

 “ What happened ? akajiuliza huku 

akimuangalia Lucy aliyekuwa amelala 

usingizi mzito pale kitandani. 

 “ Huu si usingizi wa kawaida..muda mfupi 

uliopita nilikuwa nikiongea naye na 

kucheka lakini amelala ghafla tu….” Akawaza Jack tayari kijasho kilianza 

kumtoka kwa uoga. 

 Akamuangalia tena Lucy aliyekuwa 

amelala usingizi mzito pale kitandani 

halafu akatoka kwa kasi akamfuata Frank 

jikoni. 

 “ Frank umeweka nini katika ile juice ya 

Linda? Akauliza Jack kwa ukali 

 “ Kwani vipi Jack ? 

 “ naomba uniambie umeweka nini katika 

juisi ya Linda? 

 “ Calm down Jack…hebu punguza jazba …” 

akasema Frank huku akitabasamu halafu 

akamimina maji ya kunywa katika glasi 

akampatia Jack 

 “ Kunywa maji Jack ..” akasema Frank 

Jack akalishika glasi lile na kuliweka 

pembeni. 

 “ Niambie Jack ,kitu gani kimetokea.? 

Akauliza Frank 

 “ Linda amepata usingizi wa ghafla 

sana….amelala fofofo hajitambui..” 

akasema Jack kwa wasi wasi na kumfanya 

Frank atabasamu 

 “ C’mon Jack..mbona unakuwa mwoga 

namna hiyo? Kama amelala ni vizuri 

sana."Akasema Frank .Jack akamuangalia kwa macho makali 

 “ Frank acha masihara yako..Linda ni 

mwanafunzi wangu mimi na lolote 

litakalompata ni mimi ndiye 

nitakayejibu.Tafadhali niambie umeweka 

nini katika juisi ya Linda? Akauliza Jack 

huku akilizima jiko na kumfanya Frank 

ageuke na kumtazama 

 “ unataka kuufahamu ukweli? Akasema 

Frank kwa sauti iliyokuwa na ghadhabu 

kutokana na kitendo cha Jack kulizima 

jiko ..Jack hakumjibu kitu. 

 “ Nilimuwekea dawa ya usingizi katika 

kinywaji….” Akasema Frank Jack akakunja 

sura kwa hasira 

 “ Kwa nini ulifanya hivyo Frank 

?..akafoka Jack 

 “ Jack mbona unakuwa mgumu kuelewa? 

Msichana mrembo kama yule hawezi kuja 

na kuondoka hivi hivi bila 

kuguswa.Itakuwa ni dharau kubwa kwetu 

kama tukimuacha akiondoka hivi hivi..Ili 

kuweka heshima lazima tustarehe naye na 

njia pekee ya kumpata ni kwa kumuwekea 

dawa za usingizi ili alale fofofo.” Akasema 

Frank 

 “ Stupid.! Yule ni mwanafunzi wangu.Frank Mbona unataka kunitia 

matatizoni? 

“ Acha uoga Jack..Hakuna kitu chochote 

kibaya kitakachokupata..Sikiliza 

nikwambie huyu mtoto hatakwenda 

kuripoti mahala kokote kule.Mbona 

Melanie yule wa chuo kikuu cha Dodoma 

tulimfanyia hivyo na hakwenda kuripoti 

sehemu yoyote? …” akasema Frank.Jack 

alikuwa kimya akimsikiliza 

 “ Kama wewe hutaki basi niachie mimi 

mzigo huu .Kwa utamu atakaousikia kesho 

lazima atarejea na kutaka tena” akasema 

Frank uso wake ukiwa umejenga 

tabasamu 

 “ Frank please don’t do that..msichana 

huyu anajiheshimu sana” akasema Jack 

 “ C’mon Jack..mpaka lini nitakuwa 

nikikupa somo la kugundua kama 

mwanamke anakutaka? Huyu msichana 

anakutaka lakini hawezi kukwambia na 

kitu pekee unachotakiwa kufanya kwa 

sasa ni kulala naye.Look Jack, I know 

women,I know how they think ” Akasema 

Frank .Akamshika Jack bega na kusema 

 “ Kila siku umekuwa ukija na kuniambia 

kwamba kuna msichana ambaye anakuumiza kichwa chako sana..Leo uko 

naye ana kwa ana so be a man .” akasema 

Frank.Jack bado aliinama akiwaza. 

 “ C’mon dude..muda unasonga kwa kasi 

sana..amua haraka kabla hajaamka.” 

Akasema Frank 

 “ Frank,nashindwa kuamua..Nafsi yangu 

inakataa kabisa kufanya hivyo unavyotaka 

nifanye….” Akasema Jack 

 “ Hey Jack are you a gay ? akasema Frank 

na kumfanya Jack ahamaki 

 “ Unasemaje ? 

 “ are you a gay ? akauliza tena Frank 

 Kwa hasira Jack akamfuata Frank na 

kumnyooshea kidole usoni. 

 “ Frank naomba heshima kati yetu 

iendelee kudumishwa..naona umevuka 

mpaka..Unafikia hatua ya kunifananisha 

mimi na mashoga !!” akasema Jack kwa 

ukali 

 “Jack. Hata kama ukichukia lakini huo 

ndio ukweli..if you are a real man go and 

hit that girl..if you fail then you are a 

gay….” Akasema Frank..Jack akahamaki 

zaidi 

 “ Frank..!! akasema Jack huku akihema 

kwa nguvu.Alipandwa na hasira za ghafla kwa kauli ile ya Frank kumfananisha yeye 

na shoga.Akamtazama Frank kwa hasira . 

 “ Sikutegemea kama ungefikia hatua ya 

kuniita mimi shoga..This is too much” 

akasema Jack kwa hasira halafu 

akamshika mkono Frank 

 “ Nataka nikakuonyeshe kwamba mimi si 

shoga kama ulivyoniita…..” akasema Jack 

huku akitembea kwa kasi kuelekea katika 

chumba alichokuwa amelala Lucy. 

 “ Jack anawachukia sana mashoga na 

ndiyo maana nilimuita vile ili 

kumpandisha hasira..” akawaza Frank 

huku akimfuata Jack. 

 Jack akingia chumbani kwa kasi.Bado 

Lucy alikuwa amelala fofofo kitandani.Jack 

akamtazama halafu akageuka na 

kumtazama Frank.. 

 “Usiniangalie jack..do it” akasema 

Frank..Jack akavua suruali yake na 

kuitupa pembeni halafu akapanda 

kitandani na kuanza kumpiga mabusu 

Lucy ambaye alikuwa hajitambui. 

 “ Kweli kauli ile imemuuma sana 

Jack..muangalie anavyofanya mambo kwa 

pupa.Hivi ndivyo nilikuwa nataka ” 

akawaza Frank akiwa amesimama huku mkono wake wa kulia akiwa ameuweka 

sehemu zake za siri.Jack aliendelea na 

zoezi lake la kumpiga mabusu Lucy na 

kumlamba kila mahala kwa ulimi wake 

.Kila alivyoendelea na zoezi lile ndivyo 

alivyojikuta akizidi kuhisi raha ya aina 

yake.Akapiga magoti akalitoa shati lake na 

kulitupa pembeni akavua nguo yake ya 

ndani akaitupa pembeni akabaki 

mtupu.Taratibu akafungua zipu ya suruali 

aliyokuwa ameivaa Lucy na kuanza 

kuivua. 

 “Ouh Gosh !..mtoto mzuri kama 

malaika..Kweli lingekuwa kosa kubwa 

kumuacha mtoto kama huyu aende zake..” 

akawaza Jack huku mate yakimtoka baada 

ya kumshuhudia Lucy akiwa amebakiwa 

na nguo ya ndani… 

 Frank yeye alikuwa bado amesimama 

akimuangalia Jack alivyokuwa 

akifanya.Tayari alikwisha pandwa na 

ashki baada ya Jack kumvua Lucy nguo. 

 “ C’mon Jack do it faster “ akawaza Frank 

huku akiifungua zipu ya suruali yake na 

kuupeleka mkono wake sirini kulikokuwa 

kumechachamaa.. 

 Jack akamvua Lucy nguo yake ya ndani halafu akamtazama na kutabasamu. 

 “ Ningefanya kosa kubwa kukuacha 

ukaondoka hivi hivi..” akasema Jack kwa 

sauti ndogo na kisha akaipanua miguu ya 

Lucy na kuanza kumuingilia . 

 * * 

“ Frank tumefanya kitendo kibaya 

sana..Nafsi yangu inajuta kwa jambo 

tulilolifanya” akasema Jack akiwa 

ameinama chini akiwaza. 

 “ Linda ni msichana ambaye 

ananiheshimu sana kama mwalimu wake 

Ouh My !.why I had to do that??. 

akaendelea kulalama Jack.. 

 “ Frank umenishawishi tukamfanyia 

Linda kitendo hiki kibaya..Nasikitika 

sana..Najuta sana kwa kitendo hiki..Huu ni 

ubakaji..Tumembaka Linda…Ouh 

Gosh..why ?? ..akasema Jack kwa hasira 

kisha akaupiga ngumi ukuta. 

 “ Don’t be stupid Jack…imeshatokea 

tayari na hakuna mtu wa kumlaumu.Wote 

tulishawishika na hatimaye tukambaka 

Linda..Tunachotakiwa kufanya hapa ni kutafuta namna ya kufanya na si 

kuendelea kulaumiana kitu ambacho 

hakitatusaida chochote.” Akasema Frank 

ambaye alionekana kutokujali kitu. 

 “ Tutafanya nini Frank? Lucy akiamka na 

kugundua kwamba ameingiliwa kimwili 

lazima atakwenda kushitaki polisi na 

unafahanu adhabu ya kitendo kama 

hiki..Frank kwa nini ukanishawishi 

tukafanya kitendo kama hiki ambacho 

kinaweza kikatuharibia kabisa maisha 

yetu..? I hate you devil…” akasema kwa 

hasira Jack. 

 “ Jack hebu tulia na acha kumsingizia 

shetani wakati kitendo umekifanya 

wewe.Tunachotakiwa kukifanya kwa sasa 

ni kupotea kabisa eneo hili.Andika ujumbe 

katika karatasi tukauweke juu ya droo ya 

kitanda ukimuelekeza Linda kwamba 

umepatwa na dharura na unaweza 

kukawia kurudi.Ujumbe huu ndio 

utakaotusaidia sisi tuonekane kwamba 

tuliwahi kuondoka hapa tukimuacha 

Linda bado amelala.Lengo hapa ni 

kumchanganya Linda ili ajiulize kama ni 

sisi au ni watu wengine ndio waliomfanyia 

kitendo kile..” akasema Frank ,Jack bado aliendelea kumsikiliza .Sura yake ilikuwa 

na wasi wasi mwingi.Midomo yake 

ilimtetemeka kwa woga 

 “ Jack unanisikia ninavyokwambia? 

Akasema Frank 

 “ Nimekusikia Frank..”akajibu Jack kwa 

uoga. 

 “ Good..Sasa andika haraka ujumbe huo 

kama nilivyokuelekeza” akasema Frank 

.Jack akaandika ujumbe ule halafu Frank 

akaenda kuuweka pembeni ya kitanda ili 

Lucy atakapoamka auone.Akamuangalia 

Lucy aliyekuwa bado amelala kitandani 

hajitambui. 

 “ She’s so hot..“ Frank akatabasamu na 

kuanza kupiga hatua taratibu kuondoka 

mle chumbani. 

 “ Twende tuondoke Jack “ akasema Frank 

wakaingia katika gari la Frank na 

kuondoka.. 

 “ She was so sweet..wasn't she? Akasema 

Frank huku akitabasamu .Jack 

akamtazama kwa hasira 

 “ Jack just relax…hili si suala la 

kukuumiza kichwa hata kidogo...” 

akasema Frank 

 “ Tafadhali usiseme hivyo Frank…Si suala rahisi kwako kwa sababu unajiamini kwa 

fedha zako.Kwangu mimi ni suala zito na 

gumu mno.Huwezi kujua nafsi yangu 

inaumia kiasi gani kwa kitendo hiki 

tulichokifanya..Linda hakustahili 

kufanyiwa vile tulivyomfanyia.Linda ni 

msichana anayejiheshimu sana .Najuta 

sana…Hili ni kosa ambalo sintolisahau 

hadi siku naingia kaburini ” akasema Jack 

kisha akainama na kukishika kichwa 

.Alikuwa na mawazo mengi 

 “ C’mon Jack ,usiwe mwoga namna hiyo 

.Forget about what happened.Twende 

katika sherehe ya kuzaliwa Mourine 

ukapoteze mawazo” akasema Frank 

 “ No ! take me home” akafoka Jack akiwa 

bado ameinama akisikitika 

 “ Hapana jack..huwezi kwenda nyumbani 

kwa sasa..Tunakwenda katika sherehe ya 

Mourine” akasema Frank. 

 Jack hakujibu kitu,aliendelea kuinama 

akisikitika kila alipokumbuka kitendo 

walichomfanyia Lucy. 



 Ni saa moja za jioni.Jua lilikwisha 

futika kabisa machoni pa dunia na giza 

lilianza kuchukua nafasi yake.Taratibu 

Lucy akafumbua macho.Bado alihisi 

usingizi mzito sana.Macho yalikuwa 

mazito kufumbuka.Alijilazimisha 

kufumbua macho zaidi na kukuta chumba 

kikiwa kimya na chenye 

giza.Akashangazwa kwa ukimya na giza 

lile.hakuwa na mazoea ya kuzima taa 

chumbani kwake .Akajaribu kuinua 

kichwa lakini akakirudisha chini kutokana 

na maumivu makali aliyokuwa 

akiyasikia.Akainua mkono wake wa kulia 

na kuupeleka kichwani akayafikicha 

macho yake na kuurudisha mkono kifuani 

.Mara mkono wake wa kushoto ukagusa 

kitu kidogo chenye asii ya 

chuma.Akakishika kitu kile na kugundua 

ulikuwa ni mkufu.Fahamu zikaanza 

kumrejea akaupekeleka mkono shingoni 

akapapasa lakini mkufu wake mdogo wa 

dhahabu alipopewa kama zawadi na Dr 

Shanon haukuwepo shingoni.Akastuka na 

kujikaza akainuka na kukaa 

kitandani.Chumba kilikuwa na giza na 

kupitia dirisha kubwa aliweza kuona mwangaza wa taa nje ya chumba 

kile.Akaanza kuingiwa na wasi wasi baada 

ya kuyaona mazingira yale si mazingira 

aliyoyazoea. Akataka kuinuka akahisi 

kizunguzungu na mwili wote ulikuwa na 

maumivu.Akajitahidi tena kuinuka , miguu 

ilikuwa ikimtetemeka.Hakuwa na nguvu 

kabisa.Akakaa tena kitandani.Mara 

akagundua kwamba suruali yake haikuwa 

imefungwa zipu..Akastuka na kuupeleka 

mkono wake kutaka kuifunga suruali ile 

lakini akastuka zaidi baada ya kugundua 

utofauti.Alihisi kama nguo yake ya ndani 

ilikuwa imegeuzwa tofauti na alivyokuwa 

ameiva asubuhi..Akaupeleka mkono ili 

ahakikishe ,akazidi kustuka zaidi baada ya 

kuikuta ikiwa imelowa maji 

maji.Akaupeleka mkono sirini na kustuka 

kwa hali aliyoikuta. 

 “ Ouh Mungu wangu nimeshafanyiwa 

mchezo mbaya” akasema Lucy kwa wasi 

wasi.Ndipo hapo akili 

zilipomrudia.Akakumbuka kwamba 

mahala pale alikuwa amekuja na Jack 

mwalimu wake kwa dhumuni la kuchukua 

mitihani ya taifa ya miaka iliyopita 

.Akakumbuka namna alivyoanza kusikia usingizi wa ghafla baada ya kunywa juisi 

iliyoandaliwa na frank rafiki yake Jack. 

 “ Ouh jamani ! masikini mimi…tayari 

wameshanifanyia kitu kibaya” Lucy 

akaanza kulia kwa uchungu. 

 alikuwa na hasira nyingi ,alilia kwa 

uchungu sana.Alihisi kama moyo wake 

unakatwa vipande vipande .Akashuka 

kitandani na kukaa chini akaegemea 

kitanda na kuendelea kulia 

 " Nimemkosea nini Mungu kiasi cha 

kuadhibiwa namna hii? Kwa nini kila mara 

ninafanyiwa hivi? akazidi kulia Lucy. 

 " Jack mwanaume ambaye 

amenisababishia maisha ya taabu na 

mateso leo hii kwa mara nyingine tena 

ananifanyia hivi? Jack kwa nini 

umenifanyia hivi?????...Lucy akalia kwa 

uchungu mwingi .Mara akasikia simu yake 

ikiita.Chumba kilikuwa na giza akainuka 

pale chini alipokuwa amekaa akaanza 

kuufuata mlio wa simu ile na hatimaye 

akaupata mahala ulipokuwa mkoba 

wake.Akaitoa simu na kuangalia mpigaji 

alikuwa ni Dr Shanon.Lucy akafuta 

machozi halafu akabonyeza kitufe cha 

kupokelea .  " Hallo Dr Shanon " akasema Lucy 

 " Lucy uko wapi mpaka mida hii ? 

akauliza Dr Shanon.Lucy akakaa kimya 

machozi yakazidi kumtiririka. 

 " Lucy uko wapi ? Halafu nasikia kama 

unalia? Kuna tatizo lolote? akauliza Dr 

Shanon 

 "Hakuna tatizo Dr Shanon,ninakuja sasa 

hivi nyumbani." akasema Lucy na kukata 

simu.Aliegemea kitanda kwa dakika tatu 

akatafakari halafu akawasha tochi ya simu 

yake akamulika chini ya kitanda na kuiona 

viatu vyake akavaa kisha akachukua 

mkoba wake na kutoka mle chumbani. 

 " Sijui wamekimbilia wapi hawa 

mashetani..nitapambana nao tu 

.Nitawatafuta hadi niwapate.Sintavumilia 

tena aina yoyote ile ya unyanyasaji na 

kudhalilishwa.Nimekwisha nyanyasika 

vya kutosha na safari hii siwezi kukaa 

kimya.Lazima nitapamba 

nao.Nitapambana na yeyote yule 

atakayejaribu kuudhalilisha utu wangu" 

akawaza Lucy huku akiutafuta mlango 

mkubwa wa kutokea nje kwa msaada wa 

tochi ya simu yake.Nyumba yote ilikuwa 

kimya na yenye giza.Baada ya kutoka mle ndani akasimama getini akajiuliza aelekee 

wapi na mara simu yake ikaita 

tena.Alikuwa ni Dr Shanon. 

 " Hallo Dr Shanon" akasema Lucy 

 " Lucy uko wapi? Mbona unanipa wasi 

wasi? Una tatizo gani? 

 " Sina tatizo Dr Shanon" akajibu Lucy. 

 ' Nielekeze uko wapi nije nikuchukue" 

akasema Dr Shanon.Lucy akashindwa 

amjibu nini. 

 " Lucy nielekeze uko wapi nije 

nikuchukue.." akasema tena Dr Shanon 

 " Dr shanon naomba usisumbuke,nitafika 

hapo nyumbani muda si mrefu ninakuja 

na taksi " akajibu Lucy na kukata 

simu.Akatembea kwa kasi hadi katika baa 

moja iliyokuwa hapo jirani akamuuliza 

mzee mmoja mahala ambapo angeweza 

kupata taksi ,akaelekezwa na kwa kasi 

akaelekea mtaa wa pili ambako kulikuwa 

na kituo cha taksi.Bado machozi yalikuwa 

yakimtoka kila alipokumbuka kitendo 

alichofanyiwa. 

 " Hapana ! siwezi kuvumilia tena kitendo 

hiki.Nimevumilia mengi sana lakini kwa 

kitendo hiki cha leo sintaweza kuvumilia 

hata kidogo." akawaza Lucy.  " Kwa sasa nitapambana..nimechoka 

kudhalilishwa namna hii? akawaza Lucy 

wakati akivuka uchochoro kuelekea 

mahali alikoelekezwa angeweza kupata 

taksi. 

 Madereva taksi walipomuona akiangaza 

angaza kila mmoja akaanza kumuita lakini 

akaingia katika taksi moja ya rangi nyeusi. 

 " Dereva nipeleke kituo cha polisi" 

akasema Lucy. 

 " Kituo kipi cha polisi kwa maana kuna 

vituo vingi vya polisi" 

 " Kituo kikuu cha polisi" akasema Lucy 

huku akiyafuta machozi yaliyokuwa 

yakimtoka. 

 " Sifahamu kosa langu ni nini katika 

dunia hii kiasi cha kuadhibiwa kiasi 

hikii.Ama kweli binadamu wamekuwa 

wanyama kushinda hata wanyama wa 

mwitu.Jack anathubutu kunifanyia 

kitendo kama hiki kweli !!.....nashindwa 

kuamini kama ni kweli nimefanyiwa 

hivi.Tena nahisi wameniingilia wote 

wawili kwa zamu...Jack kwa nini lakini 

umenifanyia hivi? ..akawaza Lucy na 

kuinama akaanza kulia kwa sauti 

ndogo.Dereva wa lile gari akapunguza  " Kwa sasa nitapambana..nimechoka 

kudhalilishwa namna hii? akawaza Lucy 

wakati akivuka uchochoro kuelekea 

mahali alikoelekezwa angeweza kupata 

taksi. 

 Madereva taksi walipomuona akiangaza 

angaza kila mmoja akaanza kumuita lakini 

akaingia katika taksi moja ya rangi nyeusi. 

 " Dereva nipeleke kituo cha polisi" 

akasema Lucy. 

 " Kituo kipi cha polisi kwa maana kuna 

vituo vingi vya polisi" 

 " Kituo kikuu cha polisi" akasema Lucy 

huku akiyafuta machozi yaliyokuwa 

yakimtoka. 

 " Sifahamu kosa langu ni nini katika 

dunia hii kiasi cha kuadhibiwa kiasi 

hikii.Ama kweli binadamu wamekuwa 

wanyama kushinda hata wanyama wa 

mwitu.Jack anathubutu kunifanyia 

kitendo kama hiki kweli !!.....nashindwa 

kuamini kama ni kweli nimefanyiwa 

hivi.Tena nahisi wameniingilia wote 

wawili kwa zamu...Jack kwa nini lakini 

umenifanyia hivi? ..akawaza Lucy na 

kuinama akaanza kulia kwa sauti 

ndogo.Dereva wa lile gari akapunguza mwendo wa gari ,akamtazama Lucy 

aliyekuwa ameinama akilia. 

 " Dada una matatizo gani..? akauliza yule 

dereva.Lucy hakumjibu kitu akaendela 

kulia 

 " Dada kama una matatizo niambie 

nitakusaidia? Kuna mtu amekupiga? 

akauliza yule dereva taksi.Lucy akainua 

uso wake uliolowa machozi akasema 

 " Nipeleke polisi tafadhali" Dereva taksi 

akaelekeza macho yake mbele kuelekea 

kituo kikuu cha polisi. 

 "Siku zote nimekuwa nikifanyiwa 

unyama lakini nakaa kimya..Hii ya safari 

hii sintaivumilia hata 

kidogo.Nitahakikisha haki 

inatendeka.Lazima nisimame imara 

kuitafuta haki yangu.Nimechoka 

kunyanyasika kila mara kutokana na 

umasikini wangu.Safari hii lazima 

nipambane hadi mwisho" akawaza Lucy 

na mara sura ya Jack ikamjia kichwani. 

 " Sikutegemea kabisa kama Jack anaweza 

akageuka na kuwa mnyama kiasi 

hiki.Atajisikiaje akigundua kwamba 

alinifanyia kitendo kama hiki hali nikiwa 

mama wa mtoto wake? .  Lucy akainua uso wake akafuta machozi 

,kuna kitu alikuwa akikiwaza. 

 " Jack ndiye mwanaume wangu wa 

kwanza ,ni baba wa mwanangu na ndiye 

mtu aliyenisababishia matatizo yote 

haya.Japokuwa hana tarifa kwamba 

nilikuwa na mimba yake lakini siku moja 

ukweli utajulikana tu kama mwanangu 

bado yuko hai.Atajilaumu sana kwa kosa 

alilolifanya." Lucy akatazama nje halafu 

akainama chini 

 " Kosa la kubaka adhabu yake ni kifungo 

kirefu gerezani.Nina hakika lazima Jack na 

mwenzake watafungwa gerezani..Baba wa 

manangu atafungwa gerezani..Mbona kuna 

kitu kinaanza kunizuia nisifanye 

ninavyotaka kufanya? Lucy akainua tena 

kichwa akatazama nje . 

 " Jack amefanya kosa kubwa lakini hata 

mimi kuna kosa nimelifanya.Kumficha 

Jack ukweli ndilo kosa nililolifanya.Nina 

hakika kama jack angeufahamu ukweli 

mimi ni Lucy yule niliyekuwa mfanyakazi 

wao na nina mtoto wake asingeweza 

kunifanyia kitendo hiki.Nashindwa 

nifanye kitu gani .Niendelee na mipango 

yangu ya kumshitaki Jack au niache? Lucyakafikiri akashindwa kupata jibu. 

 " Dada tumefika " Dereva taksi 

akamwambia Lucy ambaye alikuwa 

ameinama akiwaza.Lucy akastuka 

akatazama nje akafikri kidogo kisha 

akasema 

 " Dereva samahani kwa 

usumbufu..twende tuondoke" 

Dereva akabaki akimshangaa Lucy halafu 

akawasha gari na kuondoka maeneo yale 

ya kituo cha polisi. 

 " Nimebadili maamuzi,Hata kama 

nikimshitaki Jack sintaweza kupata haki 

ninayostahili kutokana na umasikini 

wangu.Familia yao ina pesa na wanaweza 

kununua haki kwa fedha zao.Siwezi 

kushindana nao mahakamani.Nina imani 

watanishinda.." Lucy akauma meno kwa 

hasira. 

 " Sitaki haki ya mahakamani.Nitaitafuta 

haki kwa namna ninayojua mimi 

mwenyewe .Nitalipa kisasi kwa wale wote 

walionitenda vibaya nikianzia na 

Jack.Sintajali kama ni baba wa 

mwanangu.I will make his life a living 

hell.Ninahisi kama roho yangu inabadilika 

na kuwa ya kikatili sana.Sipendi kuwa hivi lakini ninalazimika kutokana na vitendo 

walivyonifanyia wanadamu.Kila mtu 

ambaye alinifanya nikadondosha chozi 

lazima atalipa machozi yangu kwa 

gharama kubwa sana .They will all pay 

dearly." akawaza Lucy 

 " Nimefanya kosa kubwa kuamua 

kutowashitaki akina Jack.Ni vipi kama 

nitakuwa nimepata maambukizi ya virusi 

vya ukimwi? Nitamlilia nani ? Mungu 

anisaidie nisiwe navyo kwa sababu kama 

watakuwa wameniambukiza nitawafanyia 

kitu kibaya zaidi ya ninavyofikiri.Mungu 

anipishie mbali kwa nitakalowafanyia." 

akaipeleka mikono ulipo moyo wake 

 Walifika nyumbani Lucy akashuka na 

kabla hajaingia ndani akajifuta 

machozi,hakutaka kuonekana alikuwa 

akilia.Taratibu akaingia ndani na 

kuwakuta Dr Shanon na Rachel 

wakijadiliana jambo.Walipomuona wote 

wakastuka.Dr Shanon akamkimbilia na 

kumkumbatria 

 " Ouh Lucy..tumekuwa na wasi wasi 

mwingi sana .Hapa tulikuwa tunajadiliana 

namna gani tungeweza 

kukupata.Umepatwa na tatizo gani Lucy? akauliza Dr Shanon. 

 " hakuna tatizo lolote Dr Shanon" 

akadanganya Lucy halafu akaelekea 

chumbani kwake akajifungia.Akakaa 

kitandani akafikiri kwa muda kisha 

akaingia bafuni kuoga . Kisha oga 

akaelekea sebuleni . Dr Shanon na Rachel 

walikuwa mezani wakimsubiri kwa ajili ya 

chakula cha usiku.Wakati wakila Lucy 

akamtazama Dr Shanon na kusema 

 " Dr Shanon , nitaongozana nawe kwenda 

marekani.Nataka nikaishi huko." 

 Dr Shanon akafurahi sana kusikia Lucy 

amekubali kuongozana naye kwenda 

Marekani. 

 " hii ni hatua yangu ya 

kwanza..Nitaondoka na nitakaporudi 

nitakuwa na kazi mbili tu,kumtafuta 

mwanangu na kulipa kisasi kwa wale wote 

walioninyanyasa na kunipa maisha 

magumu.Hii itakuwa ni fundisho kwa 

wengine wote wenye tabia kama hizi 

ambazo si za kibinadamu. " akawaza Lucy 

halafu akaweka kijiko chini akainuka 

mezani na kuelekea chumbani kwake. 

Dr Shanon akamtazama Rachel na kusema 

 " Umemchunguza vizuri Lucy?  " Naona kama hayuko sawa."akajibu 

Rachel. 

" Kuna kitu kinamsumbua Lucy.Lazima 

kuna jambo zito ambalo 

analificha.Nimemchunguza toka aliporudi 

usiku huu amebadilika sana.Macho yake 

yanaonekana mekundu nadhani alikuwa 

analia.Atakuwa na tatizo gani? akasema Dr 

Shanon. 

 " Ninadhani tuna ulazima wa kutafuta 

kinachomsumbua.Tunatakiwa tumuulize 

ili kama kuna kitu kinamsumbua 

atueleze" akasema Rachel. 

 " Hapana Rachel,hatuwezi kufanya 

hivyo.Lucy ni mtu mzima sasa na kama 

kuna jambo linamsumbua na hataki sisi 

tulifahamu basi ana maana yake kufanya 

hivyo.Lucy tumeishi naye vizuri na kwa 

upendo mkubwa na siku zote kama ana 

tatizo amekuwa akituambia.Tumuache 

kwanza na kama akipenda tulifahamu hilo 

linalomsumbua basi atatueleza." 

 " Dr Shanon mimi nina wasi wasi sana 

.Lucy anaweza kuwa na tatizo kubwa 

.Tunapaswa tumuite na tumuulize kitu 

kinachomsumbua.Kuna kitu ambacho 

kimekuwa kikimsumbua kwa muda mrefu sana na hataki kutueleza.Kumbuka 

ulipomueleza kuhusu kuondoka naye 

akaishi Marekani alionyesha aina fulani ya 

kusita lakini leo amekuja na kusema 

kwamba ataongozana nawe.Iweje abadili 

mawazo ghafla namna hii? Lazima kuna 

kitu kilichomfanya abadili mawazo 

yake.Tunatakiwa tulifahamu tatizo lake ili 

tuone njia bora ya kuweza kumsaidia." 

akashauri Rachel. 

 " Nakubaliaana nawe Rachel kwamba 

lazima Lucy ana tatizo linalomsumbua na 

sisi kama watu tunaomlea tunapaswa 

kulifahamu.Lakini hatuwezi kumlazimisha 

Lucy atueleze tatizo lake.Inawezekana ni 

suala la ndani zaidi na hataki mtu 

mwingine alifahamu.Kama ni hivyo 

hatuwezi kumlazimisha atueleze ,itatubidi 

tusubiri hadi atakapokuwa tayari 

kutuambia" akasema Dr Shanon. 

 " Muda unakwena Dr Shanon na hatuwezi 

kusubiri wakati Lucy anaendelea kuteseka 

na kitu alichonacho rohoni.Lazima 

tumsaidie" akasema Rachel. 

 " Rachel suala hili hatuwezi kulipeleka 

namna hii.Lazima yeye mwenyewe awe 

tayari kutueleza tatizo lake.Hatuwezi kumlazimisha atuambie kwa sababu kuna 

masuala mengine ni ya ndani zaidi." 

akasema Dr Shanon. 

 " Kitu kikubwa na cha msingi kwa sasa .." 

akaendelea Dr Shanon 

 " ni kuhakikisha kwamba tunamjengea 

msingi mzuri wa maisha yake ya sasa na 

baadae.Lucy ni msichana mwenye akili 

nyingi na ndoto nyingi maishani.Nina 

uhakika kinachomtesa kwa sasa ni 

maisha yake ya nyuma aliyoyapitia 

ambayo yalikuwa magumu na katika 

maisha hayo lazima amekutana na mambo 

mengi ambayo kila akikumbuka lazima 

atakuwa katika hali hii. Tunatakiwa 

tumsaidie aweze kujenga maisha yake na 

familia yake ambayo Mungu atamjalia 

kuipata.Mimi nimekwisha jitolea 

kumchukua nikaishi naye Marekani Kule 

kuna fursa nyingi ambazo tutazitumia ili 

kuyajenga maisha yake .Nitajitahidi kwa 

kila nitakavyoweza ili kumsaidia 

Lucy.Nina hakika nitakapomsaidia Lucy 

akawa na maisha mazuri nitakuwa 

nimeisaidia na jamii yake kwa 

ujumla.Watoto wake watasoma na kuishi 

maisha mazuri,ndugu zake nao watafaidika pia." akasema Dr Shanon. 

 " Nakubaliana nawe Dr Shano ni kweli 

tuna kila sababu ya kumsaidia Lucy 

kuyajenga maisha yake ya 

baadae.Ninaungana nawe kwa maamuzi 

yako ya kuondoka naye kwenda 

Marekani.Japokuwa sintakuwa nawe 

Marekani lakini nitajitahidi kwa kila 

nitakavyoweza ili niweze kusaidiana nawe 

katika kuyajenga maisha ya 

Lucy.Nitafanya kila niwezalo ili kwa 

pamoja tuujenge msingi mzuri wa maisha 

yake." akasema Rachel. 

 " Ninafurahi sana kusikia hivyo 

Rachel.Lucy ni mdogo wetu na tuna kila 

sababu ya kujitolea kumsaidia yeye ili 

naye aweze kuisaidia familia yake na jamii 

yake kwa ujumla." akasema Dr Shanon 

huku akitoa vyombo walivyovitumia kwa 

chakula na kuvipeleka jikoni. 

 Baada ya kuondoka pale mezani na 

kuwaacha Dr Shanon na Rachel wakibaki 

na mshangao Lucy alikwenda chumbani 

kwake akajifungia na kuanza kulia.Kila 

alipokumbuka kitendo alichofanyiwa 

alisikia uchungu mwingi. 

 "Sifahamu nina mkosi gani kiasi kwamba kila mara ninafanyiwa mambo ya 

udhalilishaji namna hii.Kitu ambacho 

nimekigundua ni kwamba yote haya 

yanatokana na umasikini 

nilionao.Nimetokea katika familia duni 

isiyokuwa na hata chembe ya 

utajiri.Niliondoka kijijini kwa malengo ya 

kuja kutafuta maisha bora mjini ili niweze 

kuwasaidia ndugu zangu lakini badala 

yake nimekuja kutafuta maumivu ya 

moyo.Kuna nyakati ninajuta ni kwa nini 

nilikuja mjini.Ni bora ningebaki kijijini 

.Japokuwa ni masikini lakini tunaishi kwa 

amani na upendo tukiridhika na 

kumshukuru Mungu kwa kidogo 

tulichonacho." Lucy akachukua kitambaa 

akafuta machozi na kukiweka pembeni. 

 " Sikuwahi kufanya mapenzi .Nilijitahidi 

kutokujiingiza katika masuala ya mapenzi 

lakini ukuaji wa teknolojia ndio 

ulinishawishi nikaingia huko.Nakumbuka 

niliitazama filamu ya ngono chumbani 

kwa Jack.Toka siku ile nikajikuta nikiwa 

na hamu ya kutaka kujaribu mchezo 

ule.Nilitaka kuisikia raha ile kama 

niliyoiona wanaipata wanawake wengine 

katika filamu na simulizi wanazonisimulia.I was so stupid kwani 

nilikuwa tayari kufanya mapenzi na mtu 

yeyote yule ili niione raha hiyo. Tamaa 

zangu zikanifanya nikubali kufanya 

mapenzi na Jack na hatimaye mama yake 

akatukuta na akanitimua nyumbani 

kwake.Toka siku ile mikosi na mabalaa 

yakaanza kuniandama kila kukicha." 

akawaza Lucy .Picha ya yeye akiondoka 

nyumbani kwa akina Jack ikamjia 

kichwani.Alikuwa na begi lake na hakujua 

angekwenda wapi. 

 " Alinifukuza kinyama sana yule 

mama.Jack ambaye ndiye alinisababishia 

matatizo yote haya hakuthubutu hata 

kutokea na kunitetea kwa mama yake." 

akawaza Lucy huku ameuma meno kwa 

hasira.Akakumbuka pia namna 

alivyopokelewa na Pendo ambaye ndiye 

mwanamke aliyemchukua kijijini na 

kumleta mjini.Akakumbuka alivyompatia 

Pendo kiasi chote cha pesa alichokuwa 

nacho ambacho hakuwahi 

kurudishiwa.Akakumbuka namna Pendo 

alivyomfanyisha kazi ya kuuza vinywaji 

bila malipo yoyote. 

 " Nilimfanyia kazi yake ya kuuza vinywaji lakini hakuwahi hata mara moja kunilipa 

badala yake alikuwa akitaka kuniuza kwa 

wanaume ili ajipatie fedha." akawaza Lucy 

 " Sintamsahau Pendo alivyoniuza kwa 

wale wachimba madini wa Mererani 

ambao walinifanyia udhalilishaji mkubwa 

bila kujali ujauzito niliokuwa 

nao.Walinibaka kwa zamu.Yote hii ilikuwa 

ni mipango ya Pendo ya kujipatia fedha 

kupitia kwangu.Hadi naingia kaburini 

sintamsamehe Pendo kwa kitendo hiki na 

siku moja lazima nitalipa kisasi kwake 

yeye na kwa wale maharamia 

walionifanyia unyama ule." Lucy akainuka 

kitandani na kusimama dirishani. 

 "Baada ya kitendo kile Pendo alinifukuza 

kinyama nyumbani kwake bila kunipa 

pesa zangu.Namshukuru Sharifa ambaye 

alinihifadhi kwake na kunilea hadi 

nilipojifungua.Japokuwa hakuwa na kazi 

ya maana lakini alijitahidi kunitunza hadi 

nikajifungua salama.Sina ubaya na Sharifa 

hata kidogo kwani hata yeye asingeweza 

kunilea mimi na mwanangu kwa kazi yake 

ya kuuza baa." 

 akaendelea kukumbuka maisha ya nyuma 

aliyoyapitia.  " Nikimtaja Sharifa ninamkumbuka 

mwanangu Angela kwani nilijifungua 

nikiwa naishi kwake.Sharifa aliniomba 

nirejee kijijini hadi mtoto atakapokua 

mkubwa ndipo nirudi mjini kwani kwa 

wakati ule sikuwa na kazi wala njia yoyote 

ya kuniingizia kipato.Naumia sana kila 

nikikukumbuka namna nilivyomtelekeza 

mwanangu katika geti la kituo kile cha 

kulelea watoto halafu nikakimbia.Kitendo 

hiki sintakisahau katika maisha yangu 

yote.Ninajihisi kama nilimuua 

mwanangu.Nilifanya kosa kubwa sana 

ingawa kwa wakati ule niliona kama 

nilikuwa sahihi kwa sababu sikuwa na 

namna nyingine ya kufanya. Sijui mpaka 

leo kama mwanangu ni mzima au 

amekwisha fariki.Hakuna ajuaye moyo 

wangu unaumia kiasi gani kila 

nikimkumbuka mwanangu Angela." Lucy 

akashindwa kujizuia akatoa machozi . 

 " Ee Mungu sijui nikuombaje msamaha ili 

uweze kunisamehe katika dhambi hii 

kubwa niliyoifanya.Maumivu ya moyo 

ninayoyapata ni makubwa sana ni wewe 

pekee unayefahamu." akaomba Lucy. 

 Picha ya wazungu wawili Adolf na Leorad waliomuokota njiani ikamjia tena akilini. 

 " Wazungu wale walinifanyia ukatili 

mkubwa sana.Walinifanya mtumwa wa 

ngono na kunidhalilisha namna 

walivyotaka wao.Mungu atawasemehe 

kwa mambo waliyonifanyia." akasema 

Lucy . 

 " Namshukuru Mungu kwa kunikutanisha 

na Dr Shanon na Rachel ambao ninawaona 

ni kama malaika waliotumwa na Mungu 

kuja kuniletea faraja katika wakati 

mgumu niliokuwa nao.Wamenifanya niwe 

mtu mpya tena.wamenifundisha maisha 

mapya,maisha ya furaha,amani na 

upendo.Sijui niwashukuru vipi watu hawa 

ambao wananitunza kama mdogo 

wao.Niliamini matatizo yangu 

yamekwisha ,ghafla amejitokeza tena Jack 

na kukitonesha kidonda kilichokwisha 

pona.Jack ambaye ndiye chanzo cha 

mikosi na mabalaa yote niliyonayo 

amediriki kunidhalilisha tena.Amenifanya 

niwe na mtazamo mpya wa maisha yangu. 

Nilikwisha sahau yaliyopita lakini kwa 

kitendo hiki alichokifanya ameyarudisha 

maumivu yote niliyoyapata toka 

mwanzo.Nimechoka na mambo ninayofanyiwa na watu hawa kila 

siku.Kwa sasa nimeamua kulipa 

kisasi.Sintamvumilia mtu yeyote yule 

ambaye amewahi kunifanyia au 

atakayenifanyia udhalilishaji wa namna 

yoyote ile.Ninataka liwe fundisho kwa 

wale wote wenye tabia za namna hii za 

kuwanyanyasa watoto wa kike kutokana 

na umasikini walionao.Najua wapo 

wasichana wengi wanaofanya kazi 

majumbani mwa watu ambao 

wanafanyiwa ukatili mkubwa na 

udhalilishaji usioelezeka na waajiri 

wao.Wasichana hawa ambao wengi wao 

bado ni wadogo hawasemi vitendo 

wanavyofanyiwa kutokana na umasikini 

walionao. Ninayafahamu haya yote kwa 

sababu nimeyapitia na ninayaelewa 

fika.Nimefanyiwa unyanyasaji wa kila 

namna,udhalilishaji wa kila namna na 

watu ambao naweza kusema kwamba 

hawa hata chembe ya ubinadamu.Kwa 

sasa nimefika mwisho.Sintakubali tena 

vitendo vya namna hii viendelee." 

akawaza Lucy huku ameikutanisha 

mikono yake.alikuwa na hasira kali. 

 " Sikuwa na lengo la kwenda Marekani kama alivyokuwa ameniomba Dr 

Shanon.Nilitaka nibaki hapa hapa 

Tanzania ili niendelee kumtafuta 

mwanangu lakini kwa kitendo 

alichonifanyia Jack nimebadili maamuzi 

yangu.Nitakwenda Marekani na Dr Shanon 

ambaye nina imani ana nia ya dhati ya 

kunisaidia. Kule nitasoma na kufanyakazi 

kwa bidii kubwa ili niweze kutimiza 

malengo yangu.Baadae nitarudi nyumbani 

na hapo ndipo nitakapoanza kulipa kisasi 

changu kwa wale wote ambao 

wamenitenda kwa wakati huu ambao ni 

masikini na sina elimu.Kila mtu ambaye 

alnitoa machozi atalipa.Mungu 

atanisamehe kwa jambo nitakalokuja 

kulifanya kama nitabahatika kurudi 

Tanzania." Lucy aliwaza haya akiwa 

amefura kwa hasira. 

Lucy hakuhudhuria tena masomo katika 

kituo kile alichokuwa akisoma.Hakutaka 

kuonana na jack.Alimchukia jack kupita kiasi.Hakutoa sababu za kutotaka kurejea 

tena kusoma katika kile kituo.Hakutaka 

watu wafahamu kitendo alichofanyiwa na 

Jack.Dr Shanon hakukata tamaa akaamua 

kutafuta walimu ambao walikuja 

kumfundisha Lucy nyumbani. Maisha ya 

Lucy yalibadilika sana baada ya kitendo 

kile alichofanyiwa na Jack.Hakupenda 

kutoka nje.Muda mwingi aliutumia akiwa 

ndani akisoma.Vile vile alibadilika na 

kuwa mkimya sana tofauti na 

alivyokuwa.Mabadiliko haya yalimtesa 

sana Dr Shanon ambaye alihitaji 

kufahamu kilichomfanya Lucy abadilikie 

ghafla namna hii lakini alishindwa 

kumlazimisha Lucy aweze kumwambia 

kinachomsumbua.Aliamua kusubiri hadi 

pale Lucy atakapokuwa tayari kumweleza. 

 Baada ya kitendo kile alichomfanyia 

Lucy,Jack hakuonekana tena katika kile 

kituo alichokuwa akifundisha.Aliamua 

kukimbilia Dar es salaam kwa muda ili 

kujificha .Aliamini kwamba lazima Lucy 

angeripoti suala lile polisi na endapo 

angekamatwa asingekiepuka kifungo 

kirefu gerezani. 

 Siku zilisonga kwa kasi na hatimaye 

Lucy akafanya mtihani wake wa kidato cha 

nne kama mwanafunzi wa 

kujitegemea.Aliamini lazima angefanya 

vizuri kutokana na kufanya maandalizi ya 

kutosha.Alifurahi sana kuumaliza mtihani 

ule salama kwani aliamini ulikuwa ni 

mwanzo wa kuzitimiza ndoto zake. 

 taratibu zote za safari zilikamilika na 

hatimaye mwezi wa kumi na mbili Dr 

Shanon na Lucy wakaondoka nchini 

kuelekea Marekani.Ilikuwa ni safari yenye 

huzuni na furaha kubwa kwa 

Lucy.Alihuzunika kwa kuiacha Tanzania 

nchi aliyozaliwa.Alihuzunika kuwaacha 

wazazi na ndugu zake ambao siku tatu 

kabla ya kuondoka alikwenda kijijini 

kuwaaga.Machozi yalikuwa 

yanamchuruzika kila akiwakumbuka 

wazazi wake masikini namna 

walivyokuwa wakimuombea ili akaishi 

kwa amani katika nchi ya 

ugenini.Aliwaahidi kufanya kazi kwa bidii 

huko aendako ili kuwasaidia kuondokana 

na umasikini mkubwa walionao.Kingine 

kilichomuhuzunisha zaidi ni kuiacha ardhi 

ya Tanzania bila kuwa na taarifa zozote 

kuhusu mwanae Angela kama bado alikuwa hai au alifariki dunia. 

 " Siku moja nitarudi Tanzania na 

kuutafuta ukweli kuhusu mwanangu 

Angela.Ninaumia sana roho kila 

nikimfikiria.Naahidi lazima nitarejea 

nyumbani na kumtafuta mwanangu .Kama 

atakuwa bado hai nitamuomba msamaha 

na kuungana naye tena na kama atakuwa 

alifariki dunia siku ile nilipomtelekeza 

nitamuomba Mungu anisamehe kwa kosa 

hili." akawaza Lucy huku machozi 

yakimtiririka wakiwa garini kuelekea 

uwanja wa ndege wa Kimataifa wa 

Kilimanjaro.Dr Shanon akamfuta machozi 

na kumsihi asilie. 

 " Kweli Mungu ni wa ajabu 

sana.Sikutegemea katika maisha yangu 

kama siku moja nitapanda ndege na 

kwenda Marekani.Nimejifunza kitu 

kikubwa sana kwamba katika haya maisha 

hatutakiwi kumdharau mtu yeyote 

kutokana na umasikini wake kwani 

Mungu anaweza akampandisha daraja 

katika sekunde yoyote ile.Jana nilikuwa 

msichana mbumbumbu ,masikini nisiye na 

mbele wala nyuma ,nisiye hata na sehemu 

ya kuuweka ubavu wangu lakini leo ninakwenda kupanda ndege na kwenda 

kuishi nchini marekani.Nitaendelea 

kumshukuru Mungu kwa muujiza huu 

mkubwa alionitendea.Ninaamini pamoja 

na dhambi zangu na udhaifu wangu wote 

atanisamehe na kunisaidia kutimiza ndoto 

zangu" Aliendelea kuwaza Lucy huku gari 

walilopanda likichanja mbuga kuelekea 

uwanja wa ndege wa kimataifa wa 

Kilimanjaro. 

 Pamoja na huzuni zote alizokuwa nazo 

Lucy kwa kuondoka Tanzania,lakini 

moyoni alifurahi kupita kiasi kwani 

alitegemea kuitumia nafasi hii aliyoipata, 

kuzitimiza ndoto zake na kubwa ni 

kufanya kazi kwa bidii ili kuiondoa familia 

yake toka katika lindi la umasikini.Vile 

vile alidhamiria kufanya kazi bila kuchoka 

ili kujitengenezea maisha mazuri na 

hatimaye aweze kurejea Tanzaina kwa 

malengo mawili makubwa,moja likiwa ni 

kuutafuta ukweli kuhusu mwanae Angela 

na pili ni kulipa kisasi kwa wale wote 

waliomtenda.. 

 Hatimaye ule muda aliokuwa akiuota 

ukawadia.Alikuwa tayari ndegeni na 

wakaombwa wafunge mikanda kwani ndege ilikuwa tayari kwa kuondoka katika 

uwanja wa ndege wa kimataifa wa 

Kilimanjaro.Alijisikia uoga 

uliochanganyika na furaha.Huu ulikuwa ni 

kama muujiza kwake.Hakutegemea katika 

maisha yake kama siku moja angepanda 

ndege.Alimshukuru Mungu na kumuomba 

awafikishe salama safari yao.Taratibu 

ndege ikaanza kushika kasi na kupaa. 

Majengo yalionekana kwa mbali sana na 

hapo akajua kwamba tayari walikuwa 

angani. 

 " Kwa heri tanzania.Kwa heri nchi 

yangu.Naahidi nitarudi siku moja katika 

ardhi niliyozaliwa na wakati huo nitakuwa 

ni Lucy mwingine na si Lucy yule ambaye 

alizoea kulia kila mara kutokana na 

udhalilishaji na unyanyasaji aliofanyiwa." 

Lucy akawaza Kimoyo moyo akiiaga 

Tanzania. 




 Ni saa mbili za usiku baada ya mlo 

wa jioni,familia yote imekutana 

sebuleni.Ni siku ambayo David aliitakiwa 

kuwasilisha ripoti yake aliyoifanyia 

kazikwa muda wa wiki 

nzima.Mkononialikuwa na faili ambalo 

ndimo aliandika kila kitu.Vicky 

madhahabu alikuwa amekaa pembeni ya 

mumewe mzee Zakaria na kama iliyo 

kawaida yake alikuwa na chupa ya whysky 

pembeni yake.Pauline ambaye naye 

alikuwa ameshika kitabu mkononi 

alionekana ni mwenye furaha muda wote. 

 “Leo ujanja wote wa mama mdogo 

unaisha.Nina hakika baba hawezi 

kuyakataa mapendekezo ya David.Huyu 

mama mdogo ndiye amekuwa chanzo cha 

sisi kuyumba kiuchumi.Mwisho wake 

umefika leo.Najua atakasirika sana lakini 

lazima tumuondoe katika miradi yetu ya 

familia.Simpendi sana huyu 

mwanamke”akawaza Pauline .Kwa upande 

wake Vicky madhahabu kila alipomuona 

Davidi alikuwa akisisimka. 

 “ Nina hakika hawezi kuniangusha 

.Endapo atafanya kama nilivyomuelekeza 

lazima nimfanyie mambo makubwa sana.Nitamnunulia kiwanja ili aanze 

ujenzi wa nyumba yake ya 

kuishi.Nitamfundisha namna ya 

kutengeneza pesa.Nitamfundisha namna 

ya kumkamua huyu mzee kabla 

hajafa.Mambo yangu yote lazima yaende 

vizuri kwa kumtumia yeye.Ukiacha sababu 

hizo za kumtumia kiuchumi ,Davidi ni 

kijana ambaye atakuwa akinisaidia kukata 

kiu yangu ya mapenzi.Huyu mzee hanipi 

raha yoyote na siwezi kuendelea kufanya 

mapenzi na mfu mtarajiwa.Sitaki siku 

moja anifie kifuani.” Akawaza Vicky huku 

akiendelea kupiga mafunda ya mvinyo 

 Mzee Zakaria akamkaribisha David 

ili aweze kuwasilisha ripoti yake .David 

akaanza kwanza kwa kuelezea hali ya 

kifedha ilivyo mpaka wakati huo.Ilikuwa 

ni ripoti ndefu iliyoainisha mapungufu 

mengi aliyoyagundua katika uendeshaji na 

usimamizi wa miradi yote na hatimaye 

akafika katika mapendekezo .Pauline 

alimuangalia David huku 

akitabasamu.Vicky madhahabu naye 

alikuwa anahema juu juu.David 

akawatazama wote na kusema  “ Japokuwa kumeonekana kuwapo 

kwa udhaifu wa uendeshaji na usimamizi 

katika miradi mingi lakini hali yake si 

mbaya sana na endapo maboresho 

niliyoyapendekeza yakifanyiwa kazi basi 

ndani ya muda mfupi ujao mambo 

yatakuwa mazuri” akanyamaza 

akalitazama faili lake. 

 “ Hiki ni kipindi kigumu sana na 

siwezi kuyatekeleza matakwa ya kila 

mmoja.Lazima nifanye maamuzi”akawaza 

 “Katika ukaguzi wangu ,matatizo 

makuwa nimeyakuta katika duka la vito 

na katika biashara ya kununua 

madini.Biashara hizi toka zimeanzishwa 

hazijaonyesha kuleta faida na imeonekana 

zimetumia fedha nyingi kama 

mtaji.Ukitazama kwa miaka miwili 

mfululizo zimeingiza hasara ya mamilioni 

ya fedha na hivyo kusababisha pesa 

kutoka katika vyanzo vingine vya fedha 

zitumike katika kuziendesha biashara 

hizi mbili. “ akasema David halafu 

akanyamaza na kuwaangalia wote mle 

sebuleni .Vicky madhahabu moyo ulikuwa 

unamdunda .Kwa upande wa Pauline yeye 

alikuwa akifurahi kwani yale aliyowahi kumueleza baba yake ndiyo hayo 

anayoyasema Davidi muda huu.David 

akaendelea 

 “Nilifanya uchunguzi ni kwa nini 

kumekuwa hakuna faida katika biashara 

hizi mbili ikagundua kwamba ili 

kutengeneza faida katika baishara kama 

ya madini inahitaji mtaji 

mkubwa.Niligundua kwamba kulikuwa na 

hasara kubwa katika ununuzi wa madini 

katika mwaka uliopita uliotokana na 

kununua madini yasiyofaa.Madini 

yaliyonunuliwa hayakuwa na ubora katika 

soko hivyo kupelekea kupata hasara 

kubwa.Baada ya kugundua haya yote 

kuna mapendekezo ambayo 

nimeyatoa.kwanza hatupaswi kuzifunga 

biashara hizi mbili” akasema David na 

moyo wa Pauline ukastuka kana kwamba 

unataka kuchomoka.Alimuangalia David 

kwa mshangao kana kwamba anaangalia 

filamu ya kutisha.Kwa upande wake Vick 

alishusha pumzi ndefu na kushukuru 

kimoyo moyo kwani dakika chache 

zilizopita alikuwa akihema kijuu juu 

 “Biashara hizi hazitakiwi 

kufungwa”akaendelea David  “ Ni biashara ambazo zinatakiwa 

zifanyiwe maboresho makubwa.Endapo 

zikiboreshwa ni biashara ambazo 

zinaweza kutengeza faida kubwa.Huu ni 

uwekezaji na unapowekeza unaweza 

usitengeneze faida kwa haraka .Kwa hiyo 

basi nimependekeza miradi hii iongezewe 

pesa.Iwapo zitaongezwa shlingi milioni 

mia nne basi nina hakika tutaweza 

kuhimili ushindani mkubwa uliopo katika 

biashara hii ya madini.” 

 “ No ! This cant be !!...akasema 

Pauline kwa sauti kali.Alikuwa amechukia 

sana 

 “ Pauline kuna tatizo gani? Akauliza 

mzee Zakaria 

 “ Baba hili analolisema David katu 

haliwezekani kabisa.Hatuwezi kuongeza 

fedha katika biashara ambazo hazituletei 

faida yoyote zaidi ya kutuingizia hasara 

kubwa kila kukicha.Biashara hizi za 

madini hazina faida yoyote kwetu na 

itakuwa vyema endapo zitafungwa na 

kuzuia upotevu zaidi wa fedha” akasema 

Pauline. 

 “ Mume wangu,anavyoongea David ni 

mambo ya kweli kabisa.Yeye mwenyewe ameshuhudia namna tunavyoendesha 

biashara ile na ushindani uliopo.Yule mtu 

ambaye nilimuajiri kama mtaalamu wa 

madini ni ndiye aliyekuwa akinunua 

madini yasiyokuwa na ubora na 

kutuingiza katika hasara hii kubwa.Kwa 

hivi sasa nataka kutafuta mtaalamu 

mwingine anayefahamu vizuri mambo 

haya ya madini na kila kitu sasa kitakuwa 

chiniya usimamizi wa David.Tumekwisha 

tupa fedha nyingi hadi hivi sasa na 

kuzifunga biashara hizi itakuwa ni hasara 

kubwa.Ni bora tujaribu kwa mara 

nyingine tena” akashauri 

Vicky.MzeeZakaria akainama akafikiri na 

kusema 

 “Ok David nakushukuru sana kwa 

kazi kubwa uliyoifanya .Ninashukuru kwa 

ushauri na mapendekezo 

uliyoyatoa.Ninakuahidi nitayafanyia kazi 

lakini kwa sasa itabidi nikae kwanza na 

mama yako na tujadili nini tuanze nacho 

kwani mapendekezo yote ni mazuri na 

mengine yanahitaji fedha nyingi kama hili 

la kuboresha ofisi yaa ununuzi wa 

madini.Good job David” akasema mzee 

Zakaria.Pauline akainuka kwa hasira  “ Baba endapo utakubaliana na 

mapendekezo aliyoyatoa David,kuhusu 

kuongeza pesa kwenye madini ,basi mimi 

usinihusishe tena katika masuala yako 

yoyote yanayohusiana na biashara zako” 

akasema kwa hasira Pauline na kutoka 

mle sebuleni akaelekea chumbani 

kwake.David aliumia sana moyoni kwani 

alikwenda kinyume na makubaliano 

aliyokubaliana na pauline 

“ David tafadhali usikwazike na 

maneno ya Pauline.Bado ni mchanaga 

sana katika biashara na haelewi namna 

biashara zinavyoendeshwa.Nakubaliana 

nawe kwamba si kila biashara inaweza 

kutengeza faida ndani ya kipindi 

kifupi.Nitayafanyia kazi mapendekezo 

yako yote kama nilivyokuahidi.” Akasema 

mzee Zakaria 

 “Nashukuru sana mzee kwa 

kunielewa” akasema David halafu 

akainuka na kuelekea chumbani kwake. 

 Pauline alikuwa amejifungia 

chumbani kwake akibubujikwa na 

machozi 

 “Siamini kama David amenigeuka 

wakati tulikwisha kubaliana.Kwa nini afanye vile.Kwa nini akiuke makubaliano 

yetu? Nini kimetokea wakati anafahamu 

fika kwamba hakuna faida yoyote 

inayopatikana katika biashara zile za 

mama mdogo? Juhudi zangu zote za 

kumuondoa mama mdogo katika biashara 

zetu zimekwamishwa na David na sasa 

ninaanza kuamini kwamba David na 

mama mdogo wako kitu kimoja.Nguvu 

yangu na mategemeo yangu yote ilikuw a 

ni David lakini amenigeuka na kwa 

mapendekezo yale aliyoyatoa mama 

mdogo hivi sasa atakuwa na nguvu na 

atafuja mali anavyotaka.”akaendelea 

kuwaza Pauline huku machozi 

yakimdondoka 

 “ Lazima David na mama mdogo 

wana lao jambo,si bure.Sina imani tena na 

David.Ninachotakiwa kufanya kwa sasa ni 

kuanza kufanya uchunguzi wa kubaini ni 

kitu gani kinaendelea kati yao na endapo 

nikigundua chochote basi nitakuwa na 

nguvu mbele ya baba na hatawaamini 

tena” akawaza Pauline. 

 “ Mawazo yangu yanaweza kuwa 

sawa kabisa kwa sababu kwa siku za hivi 

karibuni,ukaribu wao umeongezeka sana.Ninamfahamu Davidi ,yale hayakuwa 

mawazo yake.Yalikuwa ni mawazo ya 

mama mdogo.”akawaza 

 David alikuwa amekaa kitandani 

kwake akiwa kifua wazi jasho likimtoka 

japo hali ya hewa ilikuwa ni ya kiubaridi 

lakini jasho liliokuw a linamtoka. 

 “ Nimemkasirisha sana Pauline na 

sina hakika kama ukaribu wetu 

utaendelea.Nilimtazama machoni wakati 

akiongea alikuwa amekasirika 

mno.Hakutegemea kabisa kama 

ningeweza kufanya tofauti na 

makubaliano yetu.Ni kweli biashara zile 

hazina faida yoyote na zinamnufaisha tu 

madam Vicky na Pauline alikuwa sahihi 

kabisa kwamba zifungwe .Nitafanya nini 

sasa? Nimejiingiza katika mgogoro 

mkubwa ” mara akastuliwa toka 

mawazoni na mlio wa ujumbe mfupi wa 

simu,akaufungua na kuusoma.Ulitoka 

kwa Vicky 

“ Thank you David.You are a 

man.You did the right thing.Thank you 

again and again.Subri utekelezaji wa ahadi 

zangu” ndivyo ulivysomeka ujumbe ule.David akasonya na kuitupa simu ile 

pembeni. 

 “Huyu mwanamke amekosa nini 

toka kwa mzee Zakaria? Kila kitu 

anachokihitaji katika maisha yake 

anakipata.Anaishi maisha ya kifahari 

lakini bado haridhiki na anadiriki 

kumzunguka na kumuibia mume 

wake.Anafuja pesa kwa kigezo cha 

kujitengenezea maisha ya mbele akiamini 

kwamba hali ya mzee kiafya si nzuri na 

kwamba eti anaweza kufariki muda 

wowote hivyo anachukua chake angali 

mchana.dah ! wanawake !....akawaza 

David na kuikumbuka kauli ya Vicky 

 “ David ndani ya biashara zile mbili 

kuna manufaa yangu ambayo Zakaria na 

Pauline hawafahamu na ndiyo maana 

sitaki miradi hii iguswe na mtu yeyote 

.Once they find out what I’m doing I’m 

finished and all my efforts to build my 

future will be for nothing” 

 “ bastard !!...akasema kwa hasira 

 “ Nimekutana na mambo yale yale 

ambayo nimejitahidi kuyakimbia.Any way 

safari hii sintakimbia tena.Nitasimama 

katika maamuzi yangu” akawaza David *************** 

 Macho ya mwalimu Lucy yalifunikwa 

na machozi alipokumbuka maisha yake 

ya nyuma. 

 “ Sijui nifanye nini niweze kuifuta 

historia hii mbaya kichwani 

kwangu.Nahitaji kuufungua tena moyo 

wangu,nahitaji kupenda tena.” Akawaza 

Lucy 

 “ Hapana sintoweza kuwa na maisha 

mapya kabla ya sijalipa kisasi kwa wale 

wote walionitenda vibaya wakati 

ule.Lazima wote walipe na ninaapa lazima 

nilipe kisasi.Waliniumiza mno watu wale” 

akauma meno kwa hasira 

 “ Pamoja na unyama wote 

walionitendea lakini Mungu bado amekuja 

kuniinua na kunifkisha hapa 

nilipofika.Namshukuru sana pia Dr 

Shanon kwani ni yeye ndiye aliyenisaidia 

kwa hali na mali hadi nikafika hapa 

nilipofika.Siku zote sintaacha 

kumuombea Mungu amrehemu huko 

aliko.Alipambana sana kuhakiksha 

kwamba ninakuwa na maisha mazuri.” Akawaza Lucy na kuanza kukumbuka 

historia ya maisha yake akiwa nchini 

Marekani. 

*********************** 

Tayari Lucy ameanza kuyazoea maisha ya 

Jiji la Chicago walikokuwa wakiishi na Dr 

Shanon.Aliyafurahia maisha yale ya kuwa 

mbali na sehemu ambayo alitendwa 

mambo mengi.Alijitahidi sana 

kujisahaulisha maisha yaliyopita na 

kuelekeza nguvu katika maisha mapya 

aliyoanza kuyaishi.Dr Shanon kwa upande 

wake naye pia alijitahidi kwa kila 

alivyoweza ili kumsahaulisha Lucy 

historia yake ya nyuma.Japokuwa Lucy 

hakuwahi kumueleza nini kilimtokea 

huko nyuma katika maisha yake lakini Dr 

Shanon aliamini lazima kuna jambo 

kubwa lililowahi kumtokea Lucy na 

alijitaidi kufanya kila aliloweza ili 

kumsahaulisha kuhusu historia hiyo ya 

nyuma. 

 Dr Shanon alimiliki utajiri mkubwa 

alioachiwa na wazazi wake baada ya 

kufariki.Mama yake ndiye aliyeanza kuiaga dunia kwa ugonjwa wa kansa 

wakati Dr Shanon akiwa na umri wa miaka 

kumi na tatu.Aliendelea kuishi na baba 

yake aliyekuwa profesa katika chuo kikuu 

hadi pale alipofariki dunia na kumuachia 

mali lukuki.Dr Shanon hakuwa na ndugu 

mwingine kwani alikuwa ni mtoto wa 

pekee kwa wazazi wake. 

 Licha ya kuachiwa utajiri mkubwa 

ambao ungemuwezesha kuendelea kuishi 

bila kutegemea kazi aliyokuwa akiifanya 

,Dr Shanon hakutaka kubweteka kwani 

toka akiwa mdogo alipenda sana kufanya 

utafiti kwa wanyama.Kuizunguka nyumba 

yake kulikuwa na bustani ambayo alikuwa 

akifuga wanyama mbali mbali ambao 

walimsaidia pia katika tafiti mbali mbali 

alizokuwa akizifanya. 

 Maisha yalikuwa ni mazuri sana jijini 

Chicago.Lucy alipata kila kitu 

alichokihitaji.Kwa msaada wa DrShanon 

alifanikiwa kuendelea na masomo yake na 

baadae akajiunga na chuo akisomea 

ualimu wa watoto wadogo.Dr Shanon 

alimlea na kumtunza kama mdogo wake. 

 Siku moja Dr Shanon alimtaarifu 

Lucy kwamba wanatarajia kupokea mgeni.Hakumtaja ni nani huyo mgeni 

lakini kwa namna kulivyokuwa na 

maandalizi makubwa Lucy alitambua 

lazima atakuwa ni mgeni muhimu 

sana.Maandalizi yalifanyika na siku ya 

kuwasili kwa mgeni huyo ikawadia.Dr 

Shanon akamuomba Lucy waongozane 

naye uwanja wa ndege kwa ajili ya 

kumpokea mgeni huyo. 

 Waliwasili uwanja wa ndege na 

baada ya ndege kutua alishuka kijana 

mmoja mwenye mwili uliojengeka 

kimazoezi.Alikumbatiana na kubusiana na 

Dr Shanon kwa furaha kubwa. 

 “ Robert,kutana na Lucy.Ni mdogo 

wangu Yule ambaye nimekuwa nikikupa 

taarifa zake .Nimekutana naye Tanzania” 

akasema Dr Shanon halafu akamgeukia 

Lucy 

 “ Lucy kutana na Robert, ni mpenzi 

wangu.Toka tumefika hapa hujawahi 

kumuona kwa sababu alikuwa akiishi 

kikazi nchini Norway na kwa sasa 

amerejea nyumbani.” Dr Shanon akafanya 

utambulisho.Lucy na Robert 

wakasalimiana na kisha wote wakapanda 

gari wakarejea nyumbani kulikoandaliwa sherehe ndogo ya kumkaribisha nyumbani 

Robert.Robert alikuwa ni kijana 

aliyeonekana mkimya na asiyependa 

maongezi mengi. 

 Maisha yaliendelea kama kawaida 

ndani ya jumba lile la Dr Shanon na kwa 

sasa yalikuwa mazuri zaidi baadaya 

kuongezeka Robert.Lucy naye aliendelea 

na masomo yake kama kawaida na 

maendelo yake yalikuwa mazuri 

sana.Alikuwa amebadilika mno na kama 

ulimuona miaka kadhaa iliyopita 

usingeamini kama ungeonana naye kwa 

sasa kwa namna alivyobadilika na 

kupendeza.Alikuwa mrembo mno.Kila 

uchao hakuacha kumshukuru Mungu kwa 

muujiza ule mkubwa aliomtendea kwani 

hakuamini katika maisha yake kama siku 

moja angekuwa na maisha kama yale 

,hakuamini kama siku moja angeishi 

nchini marekani.Maisha yake ya nyuma na 

umasikini mkubwa alioupitia vilimfanya 

afanye bidii mno katika masomo yake 

.Toka amefika nchini Marekani hakuwahi 

kuwaza kuhusiana na mapenzi hata mara 

moja.Aliyachukia na hakutaka kuwa na 

mpenzi .  Siku moja hakuwa na kazi nyingi 

chuoni hivyo akaamua kurejea 

nyumbani.Mara tu alipoingia ndani 

alikutana na kitu ambacho kilimstua sana. 

Robert akiwa na wenzake wawili 

walikuwa wamekaa sebuleni wakivuta 

bangi na kujidunga dawa za 

kulevya.Jambo hili likamstua sana Lucy 

kwani hakuwahi kuhisi hata mara moja 

kama Robert alikuwa mtumiaji wa 

madawa ya kulevya.Aliogopa na akataka 

kukimbia lakini wale jamaa tayari 

walikwisha muona.Mmoja wa wale vijana 

akamkimbilia na kumkamata akampeleka 

ndani.Lucy alipiga kelele kubwa lakini ili 

kuzizima kelele zile wale jamaa 

wakaongeza sauti ya muziki 

.Wakamkamata Lucy kwa 

nguvu,wakamvua nguo na kuanza 

kumuingilia kwa nguvu 

******************* 

 Jumatatu saa mbili za asubuhi tayari 

David yuko ofisini akiendelea na shughuli 

zake .Siku hii Pauline hakutaka kuongea 

chochote na David.Alimpakia katika gari  Siku moja hakuwa na kazi nyingi 

chuoni hivyo akaamua kurejea 

nyumbani.Mara tu alipoingia ndani 

alikutana na kitu ambacho kilimstua sana. 

Robert akiwa na wenzake wawili 

walikuwa wamekaa sebuleni wakivuta 

bangi na kujidunga dawa za 

kulevya.Jambo hili likamstua sana Lucy 

kwani hakuwahi kuhisi hata mara moja 

kama Robert alikuwa mtumiaji wa 

madawa ya kulevya.Aliogopa na akataka 

kukimbia lakini wale jamaa tayari 

walikwisha muona.Mmoja wa wale vijana 

akamkimbilia na kumkamata akampeleka 

ndani.Lucy alipiga kelele kubwa lakini ili 

kuzizima kelele zile wale jamaa 

wakaongeza sauti ya muziki 

.Wakamkamata Lucy kwa 

nguvu,wakamvua nguo na kuanza 

kumuingilia kwa nguvu 

******************* 

 Jumatatu saa mbili za asubuhi tayari 

David yuko ofisini akiendelea na shughuli 

zake .Siku hii Pauline hakutaka kuongea 

chochote na David.Alimpakia katika gari lake na alipomfikisha kazini kwake David 

akashuka na Pauline akaendelea na safari 

zake.Wakati akiendelea na kazi zake Vicky 

akaingia 

 “ Hello David,” akasema huku 

akitabasamu 

 “ Madam ! karibu” 

 “ Ahsante David.Nimekuja mara moja 

kukushukuru kwa kitendo cha kijasiri 

ulichokifanya jana.You did a great 

thing.Nataka kukuonyesha kwamba mimi 

ni mtekelezaji wa ahadi zangu .Nataka 

nikuchukue nikakuonyeshe kitu Fulani” 

akasema Vicky 

 “ Sasa hivi? Akauliza David 

 “ Ndiyo David .Sasa 

hivi.Hatutachukua muda mrefu sana 

tutarejea” akasema Vicky.David akainuka 

japokuwa kwa shingo upande lakini 

alishindwa kukataa wakaingia katika gari 

la Vicky wakaondoka . 

 “ Tayari nimekwisha kupata 

David.Huna ujanja tena.Kuanzia sasa 

utafanya kila nitakachokuamuru” 

akawaza Vicky 

 Walielekea nje kidogo ya mji wa Usa 

river.Vicky akasimamisha gari katika eneo moja kubwa ililozungushiwa uzio wa 

seng’enge. 

 “ David hili ni eneo lako.Ni eneo 

ambalo nimeamua kukupatia kama 

zawadi yangu ya kwanza kwako.Eneo hili 

lina ukubwa wa ekari tano na nusu.Ni 

eneo zuri ambalo unaweza ukajenga 

nyumba ya kuishi na kuendesha shughuli 

nyingine kama vile ufugaji n.k” akasema 

Vicky.David alikuwa anatabasamu 

 “ Wow ! Madam Vicky ahsante sana 

.Nimebaini kwamba wewe ni mtekelezaji 

mzuri wa ahadi zako” akasema David kwa 

furaha. 

 “ Siku zote mimi huwa siongei 

maneno matupu bali huongea kwa 

vitendo.Huu ni mwanzo tu bado kuna 

mengi mazuri yanakuja.Ndani ya muda 

mfupi utayapata yale yote niliyokuahidi.” 

Akasema Vicky kisha wakapanda gari na 

kurejea ofisini kwa David 

 “ David kabla sijaondoka kuna jambo 

ambalo nataka nikushirikishe.” Akasema 

Vicky na kuufungua mkoba wake na kutoa 

faili dogo akamsogezea David 

 “ Hili faili ni la nini? Akauliza David  “ David we’re a team and I cant hide 

anything from you.Hizo ni nyaraka za 

benki.Kuna mkopo nimeuomba wa shilingi 

milioni mia sita” akasema Vicky na 

kumstua David 

 “ Milioni mia sita? David akashangaa 

 “ Ndiyo David.Mkopo huu ni wa siri 

.Si mzee Zakaria wala Pauline 

wanaofahamu chochote.Kwa kukuweka 

wazi tu ni kwamba huwa ninachukua 

mikopo ya siri benki na kuifanyia biashara 

na kisha huirejesha kila mwezi kwa 

mapato yatokanayo na ile biashara ya 

madini na vito.Kwa kuwa mimi na wewe ni 

washirika , nimeona nichukue mkopo 

mkubwa kama huu na nitakupatia wewe 

kiasi cha shilingi milioni mia mbili na 

mimi nitabakia na milioni mia 

nne.Tutaurejesha mkopo huu kwa kumega 

faida inayopatikana kila mwezi toka 

katika biashara zetu mbali mbali.David 

ninaanza kukufundisha kutengeneza pesa 

. Nakuhakikishia ndani ya kipindi kifupi 

kijacho,maisha yako yatabadilika sana “ 

akasema Vicky.David alikuwa anazipitia 

karatasi zile huku mikono yake ikimtetemeka na alipomaliza akalifunga 

faili lile na kumrejeshea Vicky 

 “ I cant do this Madam Vicky” 

 “ Yes you can David” akajibu Vicky 

 “ Usiwe muoga .Tunapambana 

kupata maisha mazuri .Tunatakiwa 

kuitumia vizuri kila fursa tunayoipata.” 

Akasema Vicky 

 “ Madam Vicky mkopo huu ni 

mkubwa na endapo nitatia saini basi 

utakuwa ni mkopo wa kampuni.Itakuwaje 

endapo mzee Zakaria atagundua? 

 “ Usiogope David.Zakaria ni mfu 

anayetembea.Anaweza akafariki muda 

wowote .Amekukabidhi kila kitu.Miradi 

yote iko chini yako .You are a manager 

now.Ni wakati wako wa 

kujijenga.Usiogope kutia sahihi hizi 

karatasi “ akasema Vicky huku 

akimuonyesha David sehemu anazotakiwa 

kusaini.David akashika kichwa chake 

akatafakari na kusema 

 “ Hivi viambatanisho vinavyohitajika 

utavipata vipi? 

 “ David wewe jukumu lako ni kutia 

saini tu masuala mengine yote niachie 

mimi nitamaliza kila kitu.” Akasema Vicky David akatafakari kwa muda wa 

kama dakika tano hivi halafu akachukua 

kalamu na kutia sahihi katika zile 

karatasi. 

 “ Good.Napenda sana watu majasiri 

kama wewe David.Kwa sasa subiri 

utekelezaji.Soon utakuwa 

bilionea.”akasema Vicky akalichukua faili 

lile akaliweka katika mkoba wake 

akamuaga David na kuondoka 



Pauline baada ya kufika dukani 

kwake alitoa maelekezo ya kupangwa kwa 

mzigo mpya uliowasili halafu akaondoka. 

 “ Nataka nianze kuutafuta ukweli 

kuhusiana na David na mama mdogo na 

kitu gani kinachoendelea kati 

yao.Nitaonana kwanza na Safia.Yeye ni 

rafiki yake mkubwa na mama mdogo na 

nina hakika kuna mambo mengi 

anayoyafahamu kuhusiana na mama 

mdogo” akawaza Pauline 

 “ Nilimuamini sana David lakini kwa 

kitendo alichokifanya jana imani yangu 

kwake imeanza kupungua .Sikutegemea kama angefanya kitendo kama 

kile.Lazima kuna kitu kimetokea na 

lazima nikifahamu” akawaza Pauline 

,akaendelea na safari yake hadi alipofika 

katika saluni inayomilikiwa na Safia rafiki 

mkubwa wa Vicky madhahabu.Akashuka 

na kuingia ndani.Hakukuwa na watu 

wengi asubuhi hii na Safia alikuwa amekaa 

akipaka rangi za kucha 

 “ Hallow Pauline” akasema kwa 

furaha Safia baada ya kumuona Pauline. 

 “ hallow Safia habari yako? 

 “ Habari nzuri sana Pauline.Karibu 

sana Pauline.Ni muda mrefu haujafika 

hapa.Unahitaji huduma gani? 

 “ Safia leo sihitaji huduma yoyote 

kuna jambo ninataka tuongee” 

 “ Sawa Pauline.Unataka tuongelee 

hapa au tusogee pembeni? 

 “ Tusogee pembeni.” Akasema 

Pauline wakatoka nje 

 “ Kuna tatizo gani Pauline? 

 “ Safia nina shida kubwa na ni wewe 

pekee unayeweza kunisaidia” 

 “ Niambie Pauline ni shida gani hiyo? 

Nitakusaidia”  “ Kwanza kabisa naomba 

unihakikishie kwamba yote 

tutakayoongea hapa yatabaki kuwa siri 

yetu.” 

 “ Usijali Pauline.Naomba uniamini” 

 “ Ahsante sana.Safia wewe ni rafiki 

mkubwa wa mama mdogo na mambo yake 

mengi unayafahamu” 

 “ Ndiyo Pauline.Kuna baadhi ya 

mambo yake ninayafahamu ambayo huwa 

ananishirikisha na mimi pia.Kuna tatizo 

gani Pauline? 

 “ Kuna kijana mmoja anaitwa David 

ambaye anaishi pale nyumbani 

kwetu.Amewahi kukueleza chochote 

kuhusiana na kijana huyu? 

 Safia akastuka na midomo 

ikamcheza akashindwa namna ya kujibu 

“ David ?!!..akasema Safia kwa mshangao 

 “ Ndiyo .Mama mdogo hajawahi 

kukueleza chochote kuhusiana na kijana 

huyu? 

 “ Hapana Pauline.Mimi ndiyo kwanza 

ninamsikia toka kwako.Simfahamu na 

wala Vicky hajawahi kunieleza chochote 

.Ni nani kijana huyu?” akauliza Safia  “Huyu kijana ni meneja wetu mpya 

na kwa ghafla yeye na mama mdogo 

wamekuwa na ukaribu mkubwa.Nimewahi 

kumkuta mama mdogo usiku akigonga 

chumbani kwa David.Ninataka kufahamu 

kuna nni kinaendelea kati yao? Safia kwa 

kuwa mama mdogo ni rafiki yako 

ninaomba unisaidie kufanya uchunguzi 

wa jambo hili.Ninataka kufahamu 

kinachoendelea kati ya mama mdogo na 

David.Nitakulipa kiasi chochote cha pesa 

utakachokitaka.Jambo hili ni muhimu 

sana kwangu”akasema Pauline 

 “ Unataka nichunguze nini Pauline” 

 “ Nataka uchunguze nini sababu ya 

ukaribu wao wa ghafla.Nataka uchunguze 

kama wana mahusiano ya siri ya mapenzi 

Nataka vile vile uchunguze kama kuna 

mipango yoyote wanaifanya kwa 

siri,nataka uchunguze kila kitu 

kuhusianana urafiki wao” akasema 

Pauline halafu akafungua mkoba wake na 

kutoa kitita che pesa akampatia safia 

 “ kamata hizi.Ni shilingi laki tatu kwa 

ajili ya kuanzia kunifanyia kazi 

yangu.Utakaponipa taarifa nzuri nitakuongeza nyingine nyingi zaidi ya hizi” 

akasema Pauline 

 “ Ahsante sana 

Pauline.Nitalichunguza suala hili mpaka 

nifahamu nini kinaendelea kati ya Vicky 

na huyo kijana David.Naomba unipe siku 

mbili tu nitakuwa tayari na jibu” 

 “ Ahsante sana safia kwa msaada 

wako.Jambo hili ni muhimu sana 

kwangu.Naomba vile vile ufanye 

uchunguzi wako kwa siri kubwa sifahamu 

mtu yeyote.” Akasema Pauline na kuagana 

na Safia akapanda gari lake na kuondoka. 

 “Mbele ya pesa mtu anaweza hata 

kutoa siri za baba yake mzazi.Nina hakika 

Safia atanifanyia kazi yangu vizuri.Yeye na 

mama mdogo ni marafiki wakubwa na 

lazima atakuwa akifahamu kila 

anachokifanya.Lazima niufahamu ukweli” 

akawaza Pauline akiwa garini 

 Safia bado aliendelea kulishikilia 

bunda lile la noti mkononi akatabsamu 

 “ Mambo yameharibika.Pauline 

tayari amekwisha stuka kwamba kuna 

kitu knaendelea kati ya Vicky na 

david.Nilimuonya Vicky awe makini sana 

na suala hili lakinihajanisikia na sasaanataka kuharibu kila kitu.Ameyafanya 

mambo yake kwa pupa” akawaza na kisha 

akachukua simu na kumpigia Vicky na 

kumtaka afike mara moja pale kwenye 

saluni yake. 

 “ Safia kuna nini? Mbona 

unanitisha?Kuna tatizo lolote? Akauliza 

Vicky 

 “ hakuna tatizo Vicky lakini kuna 

jambo nataka tuongee”akasema Safia na 

kukata simu. 

Ilimchukua Vicky zaidi ya dakika ishirini 

kufika katika saluni ya Safia. 

 “ Enhee hebu nieleze safia kuna nini? 

Umenifanya niendeshe gari kama kichaa 

kuwahi nikjua lazima kuna tatizo kubwa.” 

Akasema Vicky huku akijiweka sawa kitini 

 “ Pauline amefika hapa asubuhi” 

 “ Pauline ?!..Vicky akastuka 

 “ Ndiyo.Pauline alikuja hapa na 

ameondoka si muda mrefu sana” 

 “ Alikuwa anatafuta nini?akauliza 

Vicky 

 “ Vicky unatakiwa uwe muangalifu 

sana na kila kitu unachokifanya .Tayari 

Pauline ameanza kuhisi kuna kitu 

kinaendelea kati yako na David”  “ Amekwambia nini? Amegundua 

nini? 

 “ Hajagundua kitu lakini kuna kitu 

amekihisi.Lengo la kuja kwangu ni 

kunitaka nifanye uchunguzi ni kitu gani 

kinachoendelea kati yako na David na 

endepo kuna kitu chochote cha siri 

kinachoendelea kati yenu nimfahamishe ” 

 “ Seriously?!! Akauliza Vicky 

 “ Ndiyo.Na tena ameniachia kitita 

hiki hapa cha fedha na ameniahidi 

kuniongeza nyingine zaidi ya hizi endapo 

nitampa taarifa anazozihitaji kuhusu 

wewe na david” akasema Safia 

 “ Damn !..”akasema Vicky 

.Alistushwa sana na taarifa ile 

 “ Nini kimetokea Vicky kiasi cha 

kumfanya Pauline ahisi kwamba kuna kitu 

kinaendelea baina yenu? Akauliza safia 

 “ Juzi usiku alinikuta katika mlango 

wa chumba cha David nikiongea 

naye.Nafikiri hilo lilimfanya aanze kuhisi 

pengine kuna kitu kinaendelea baina yetu” 

akasema Vicky 

 “ Ulifanya kosa Vicky.Nilikuonya 

mapema kwamba jambo hili halitaki 

haraka.Hukutakiwa kwenda chumbani kwa David na kugonga mlango usiku 

wakati wengine wote wamelala.Mtu 

yeyote ambaye angekukuta mlangoni kwa 

David lazima angejua kwamba una 

mahusiano naye.Unatakiwa uwe makini 

sana Vicky” 

 “ Safia sikuwa na namna nyingine ya 

kufanya.David ametokea kunichanganya 

sana yule kijana.Kila nikimuwaza basi 

mwili wote hunisisimka.Siku ile 

nilishindwa kujizuia kulala bila kuonana 

na David na ndiyo maana nikaenda 

kumgongea ili walau tunimuone .Kitu 

kingine ambacho kilinifanya niwe karibu 

zaidi naye katika kipindi kifupi ni 

kutokana na ukaguzi aliokuwa anaufanya 

katika biashara zetu zote kwa hiyo 

ikanilazimu kujiweka karibu naye ili 

asiweze kufichua mambo 

ninayoyafanya.Ukaribu wangu huo 

umezaa matunda na leo hii tayari mkopo 

wa milinoni mia sita umesainiwa.Biashara 

zangu zote zimepata uhai tena.Yote haya 

yamewezekana kwa kumuweka karibu 

David.Pauline asitake kupambana na 

mimi hivi sasa.Sintakubali kuwe na

 kizingiti chochote katika mipango 

yangu”akasema Vicky kwa ghadhabu 

 “ Vicky tafadhali suala hili 

usilichukulie kwa ghadhabu.Ni suala 

ambalo unatakiwa kulimaliza kiakili 

sana.” Akasema Safia.Vicky akainama 

akafikri na kusema 

 “ hebu nishauri Safia nifanye nini? 

 “ Kuna jambo nimeliona 

hapa.Pauline anasumbuliwa na wivu wa 

mapenzi .Inaonekana Pauline ana hisia za 

kimapenzi kwa David na hicho ndicho 

kilichomsukuma hadi akaamua kuanza 

kufanya uchunguzi .Ni wivu ndio unamtesa 

Pauline” 

 “ Nakubaliana nawe safia.Hata mimi 

nimekwisha liona hilo na hata baba yake 

aligundua kuwepo kwa hisia hizo za 

kimapenzi na amewahi kumtahadharisha 

hata Pauline kuhusu jambo hilo” 

 “ Kama ni hivyo basi kazi ni ndogo 

sana” akasema Safia huku akitabasamu 

 “ Mshawishi David amtongoze 

Pauline na waanzishe mahusiano ya 

kimapenzi” 

 “ What !!!Vicky akashangaa  “ Sitanii Vicky.Mshawishi David 

aanzishe mahusiano na Pauline na hiyo 

itakuwa pone pone yako” 

 “ Hapana Safia.Siwezi kuruhusu 

jambo hilo litokee.Nina mipango mikubwa 

sana kwa David na kamwe siwezi 

kuruhusu aanzishe mahusiano ya 

kimapenzi na pauline na hasa kwa wakati 

huu ambao tayari nimekwisha tengeneza 

mazingira mazuri ya kumtumia 

David.Ukumbuke ni wewe mwenyewe 

uliyenishawishi nitengeneze mazingira ya 

ukaribu na David ili niweze 

kumtumia.Nimefanikiwa kufanya hivyo na 

kwa sasa nimekwisha anza kumtumia 

kiuchumi na bado kidogo nitaanza 

kumtumia kwa mambo mengine ikiwamo 

kunikata kiu yangu pale ninapokuwa na 

hamu” akasema Vicky 

 “ Vicky sipingani na hayo 

unayoyasema wala sikatai kumtumia 

David kiuchumi au kingono.Vyovyote 

utakavyotaka kumtumia its fine with me 

lakini ushauri wangu mimi kwa ajili ya 

kukusaidia ni kwamba, tayari Pauline 

amekwisha anza kuwa na wasi wasi sana 

kuhusu mwenendo wako na David na anahisi kuna kitu kinachoendelea na 

ndiyo maana anataka kufanya uchunguzi 

lakini ili kumpoteza malengo yake ni 

lazima David aanzishe mahusiano ya 

kimapenzi naye.Ninakuhakikishia endapo 

David akifanikiwa kuanzisha mahusianoya 

kimapenzi na Pauline hatakufuatilia wala 

kukuchunguza tena.Niamini 

ninavyokwambia Vicky ninayafahamu 

haya mambo” akasema Safia 

 Vicky akafikiri kwa muda na kusema 

 “ Nimekuelewa Safia.Nitafanya hivyo 

japokuwa moyo wangu unauma sana 

lakinisina namna nyingine ya kufanya 

zaidi ya kukubaliana na ushauri wako.” 

Wakaendelea na maongezi kidogo kisha 

Vicky akaondoka 

 ******************** 

 Baada ya kutoka kwa Safia Pauline 

akarejea nyumbani.Mzee Zakaria 

akashangaa kumuona pale mida ile kwani 

haikuwa kawaida yake 

 “ Pauline kulikoni? Mbona umerudi 

mapema sana leo,kuna tatizo ? Akauliza  “ Hakuna tatizo baba,kuna kitu 

nimekisahau nimekuja kukichukua mara 

moja”akasema Pauline halafu akaelekea 

chumbani kwake akachukua funguo za 

akiba akafungua mlango wa chumba cha 

David na kuingia ndani.Alianza kufungua 

droo moja baada ya nyingine lakini 

hakupata alichokuwa anakitafuta 

 “ Lazima kuna fedha David kapewa 

na mama mdogo.Kazificha wapi? .. 

akajiuliza Pauline halafu akafungua kabati 

kubwa la nguo na kuanza kutoa nguo 

moja moja na chini kabisa akakuta pochi 

ndogo kuu kuu.Akaichukua pochi ile 

akaifungua na ndani yake akakuta kuna 

shilingi elfu moja na mia tano na pete ya 

dhahabu.Akaiweka mkononi pete ile na 

kuitazama 

 “ Pete nzuri sana na inaonekana ni 

ya thamani kubwa.Kwa nini Davidi hataki 

kuivaa na kuificha humu kabatini? 

Akajiuliza na kujaribisha kuivaa kidoleni 

lakini haikumtosha akaivua na kuirejesha 

katika ile pochi halafu akarejesha kila kitu 

namna kilivyokuwa 

 “ lazima kuna kitu katiyao si 

bure.Lazima mama mdogo alimrubuni David kwa fedha na ndiyo maana akatoa 

mapendekezo yale kwa baba.Na kama 

alipewa pesa ,itakuwa ni shilingi ngapi 

kiasi cha kusema uongo ule mkubwa? Pesa 

hizo kazificha wapi? Akaendelea kuwaza 

Pauline akiwa amekaa kitandani 

 “ Nimepata wazo moja.Ngoja 

niwasiliane na Maurine yeye anafanya 

kazi kwenye ofisi za mtandao wa simu 

anaoutumia David.Nitamuomba 

aniangalizie kama kuna muamala wowote 

wa fedha David ameufanya kwa siku za 

hivi karibuni.” akawaza Pauline halafu 

akatoka mle chumbani kwa David 

akaelekea chumbani kwake akachukua 

simu na kumpigia rafiki yake Maurine 

 ‘ Hallo Pauline”akasema Maurine 

baada ya kupokea simu 

 “ Hallo Maurine.Umenitupa sana siku 

hizi.Unaendeleaje? 

 “ Sijakutupa mpenzi.Nimetingwa na 

shughuli nyingi sana siku hizi na ndiyo 

maana umeona sijawasiliana 

nawe.Uliipata kadi niliyokutumia ya 

mchango wa harusi ya kaka yangu?  “ Ndiyo Maurine niliipata.Nashukuru 

umenikumbusha nitakutumia mchango 

wangu sasa hivi” 

 “ Ahsante sana Pauline.Nitakutafuta 

mwishoni mwa wiki hii nikipata nafasi” 

akasemaMaurine na kimya kifupi kikapita 

 “ Maurine nina shida Fulani naomba 

unisaidie” 

 “ Sema tu Pauline ni shida gani? 

 “ Kuna namba Fulani za simu 

nitakutumia sasa hivi naomba unisaidie 

kutazama kama kuna muamala wowote 

umefanyika kupitia namba hiyo .Nataka 

vile vile kufahamu namba za simu 

zlizowasiliana na namba hiyo kwa siku 

tatu zilizopita.Unaweza ukanisaidia kwa 

hilo Maurine? Please its very important 

to me” akasema Pauline 

 “ Ok !.Usijali Pauline 

nitakusaidia.Nitumie hizo namba 

nizifanyie kazi” akasema Maurine na kwa 

haraka Pauline akamtumia namba zile za 

David.Maurine akamtaka asubri baada ya 

kama dakika kumi na tano atamjibu. 

 Baada ya kama dakika kumi na tano 

hivi,Maurine akampigia simu na 

kumtaarifu kwamba tayari amekwisha mtumia taarifa ile kupitia anuani yake ya 

barua pepe. 

 Pauline akaifungua akaunti yake ya 

barua pepe na kuipata ile taarifa 

aliyotumiwa na Maurine akaanza kuipitia . 

Taarifa ile ilionyesha kwamba David na 

Vicky waliwasiliana mara moja tu kwa 

ujumbe mfupi wa maandishi.Ukiacha 

ujumbe huo mfupi hakukuwa na 

mawasiliano yoyote ya simu baina yao 

wala muamala wowote wa fedha. 

 “ Hakuna muamala wa pesa,hakuna 

mawasiliano yoyote baina 

yao,hawapigiani simu ,so how do they 

meet? Inaonekana wanafanyamambo yao 

kwa siri kubwa”akawaza Pauline na 

kuendelea kuipitia taarifa ile .Ghafla 

macho yake yakakutana na namba 

ambayo aliifahamu 

 “Tamia !..”akasema taratibu 

 “ Hii ni namba ya Tamia.Ina maana 

Tamia na David wana mwasiliano? 

aKajiuliza 

 “ Tamia kazipataje namba za David? 

Waliongea nini? Ouh Gosh kama Tamia 

amezipata namba za simu za David basi 

lazima atamuingiza katika himaya yake.Ninamfahamu Tamia ni msichana 

mwenye tabia ya kubadilisha wanaume 

.Anatamani kila mwanaume 

mzuri.Aakimtaka mwanaume atafanya ila 

awezalo mpaka ahakikishe 

amempata.Tayari ameanza harakati zake 

kwa David na lazima atampata tu.No I 

cant let that happen.I cant let her win 

David.”akasema Pauline kwa hasira na 

kutoka akaingia katika gari lake 

akaondoka 

 “ Mimindiye niliyemuokota David na 

kumfanya awe hivi alivyo leo.Hakuwa 

akitamanika wakati ule alipotoka 

gerezani,kila ambaye angemuona kwa 

wakati ule asingekubali hata kidogo kuwa 

na ukaribu naye lakini leo hii baada ya 

kupendeza amekuwa kekina kila mmoja 

anamng’ang’ania.Hapana sintokubali 

kabisa kuhusu jambo hili.David ni wa 

kwangu na nitapambana na yeyote 

ambaye atataka kumpora .” akawaza 

Pauline akiwa garini akielekea katika 

shughuli zake. 

 *********************  Mwalimu Lucy alihisi maumizu 

makali ya moyo baada ya picha ya maisha 

yake kuendelea kujirudia.Akachukua 

kitambaa na kujifuta machozi. 

 “ Sina hakika kama nitaweza 

kuzifuta picha hizi mbaya kichwani 

kwangu.Kila ninapojaribu kusahau 

mambo yaliyopita lakini 

ninashindwa.Picha za matukio 

yaliyonitokea numa zinakuja tena na 

tena..Miaka mingi sasa imepita lakini 

bado picha ya tukio lile la Marekani 

inanijia kama vile limetokea jana tu.What 

am I going to do? Lini machozi yataacha 

kunitoka na uso wangu utawaliwe na 

tabasamu kama wenzangu? Akawaza Lucy 

na kufumba macho akauma meno yake 

kwa hasira kumbu kumbu ile ya namna 

alivyodalilishwa kule marekani iliendelea 

kumjia kichwani. 

 Wale vijana wahuni wakiongozwa na 

Robert mchumba wa Dr Shanon 

waliendelea kumfanyia Lucy udhalilishaji 

mkubwa kwa kumuingilia kwa zamu huku 

wakicheka na kufurahi .Robert alikuwa 

ameketi sofani akivuta bangi yake huku 

mkononi akiwa na glasi ya mvinyo akifurahia namna wale wenzake 

walivyokuwa wakimdhalilisha Lucy.Kitu 

kibaya zaidi baada ya kumfanyia 

udhalilishaji ule mkubwa walimvutisha 

Lucy dawa za kulevya . 

 Kelele za Lucy za kuomba msaada 

zilimezwa na msitu uliokuwa 

umeizunguka nyumba ya Dr Shanon,lakini 

zilimfikia mfanyakazi aliyekuwa 

akishughulika na kutunza wanyama 

,akakimbia haraka kwenda kuangalia 

kuna nini kilichotokea na kusababisha 

kelee zile.Alipochungulia dirishani akaona 

kilichokuwa kinafanyika mle 

ndani,akaogopa na kwa haraka sana 

akmpigia simu Dr Shanon na kumtaka 

afike haraka pale nyumbani kwa ajili ya 

kumukoa Lucy kabla wale wahuni 

hawajamdhuru. 

 Ilimchukua dakika arobaini kwa Dr 

Shanon kuwasili pale nyumbani kwake na 

kushuhudia ukatili mkubwa uliofanywa 

na akina Robert.Hakuamini macho 

yake.Hakuwa akifahamu kama Robert 

alikuwa akitumia dawa za kulevya.Lucy 

alikuwa amelala sakafuni akiwa mtupu 

hajitambui.Mezani kulichafuliwa na bangi na dawa za kulevya.Dr Shanon alipatwa na 

mstuko wa ghafla akaanguka na kupoteza 

fahamu. 

 Wale vijana waliogopa sana 

wakakimbia.Mfanyakazi wa mifugo 

akaomba msaada wa gari la wagonjwa 

ambalo lilkifika mara moja na 

kuwachukua Lucy na Dr Shanon na 

kuwakimbiza hospitali kwani hali zao 

zilikuwa mbaya. 

 Zilipita siku tatu ndipo Lucy 

alipoanza kupata unafuu.Hakutamani tena 

kuendelea kuishi.Alitamani kufa ili 

aondokane na mikosi ile ya kudhalilishwa 

kila wakati.Alijiona ni mwenye mkosi 

mkubwa sana kwani kila mara amekuwa 

akifanyiwa udhalilishaji huu 

mkubwa.Madaktari walijtahidi kufanya 

kila lililowezekana ili kumsaidia . 

 Lucy alipata pigo lingine baada ya 

kupewa taarifa kwamba Dr Shanon 

alifariki dunia kutokana na mstuko ule 

mkubwa alioupata .Kwa Lucy hili lilikuwa 

ni jambo lililomuumiza mno kupita 

yote.Alimpenda mno Dr Shanon na 

alimchukulia kama ndugu yake.Dr Shanon 

alijitahidi kwa kila namnavalivyoweza kuhakikisha kwamba Lucy anakuwa na 

maisha mazuri.Alimpoteza mtu muhimu 

mno katika maisha yake. 

 Wiki mbili baada ya kifo cha Dr 

Shanon,alikuja Dickson wiliams 

mwanasheria wa Dr Shanon ambaye 

alimtaarifu Lucy kwamba alifanikiwa 

kuongea na Dr Shanon kabla ya kifo chake 

na alitoa maelekezo kwamba kila kitu 

kilicho chake akabidhiwe Lucy.Hizi 

zilikuwa ni taarifa zilizompa Lucy mstuko 

mkubwa .Hakuwa amelitegemea jambo 

kama lile kutokea.Dr Shanon alikuwa na 

utajiri mkubwa ambao sasa ungekuwa ni 

wa Lucy.Alimshukuru Mungu kwa 

kuendelea kusimama upande wake licha 

ya mitihani mingi mikubwa anayoipitia 

katika maisha yake 

 Lucy akaufungua ukurasa wa maisha 

mapya akiwa na utajiri wa 

kurithi.Heshima yake iliongezeka 

kutokana na utajiri alioumiliki.Hakuna 

aliyefahamu kwamba miaka kadhaa huko 

nyuma msichna huyu ambaye leohii 

alikuwa akitembelea magari ya kifahari na 

kupata heshima kubwa alikuwa ni 

mfanyakazi wa ndani,mbumbumbu asiyejua lolote.Ili kujiwekavizuri zaidi 

alijiendeleza na masomo katika vyuo 

mbalimbali nchini Marekani .A.litaka awe 

na elimu ya kutosha ili aweze kuuendeleza 

utajiri alioachiwa na Dr Shanon.Pamoja na 

kuwa na maisha mazuri ya kitajiri bado 

kuna picha iliyokuwa ikimjia kila siku na 

kumkosesha usingizi.Mtoto wake 

Angela.Alitamani sana kufahamu 

kuhusiana na mtoto wake Angela.Hili 

ndilo jambo lillomfanya Lucy kurejea 

nchini Tanzania 

 “ Nilirejea nyumbani nikiwa 

nimeinuliwa na kubarikiwa kwa utajiri 

mkubwa na nilidhani ulikuwa ni mwisho 

wa mateso yangu lakini nilikuwa 

najidanganya.Niliumizwa tena.” 

Alipoondoka ofisini kwa Safia Vicky 

madhahabu akaanyosha moja kwa moja 

hadi ofisni kwa David. 

 “ Hallow madam Vicky.Vipi mbona 

umekuja wangu wangu namna hiyo? 

Kwema huko utokako? Akauliza David 

 “ David nimekuja wangu wangu 

namna hii nina tatizo” 

 “ Kuna tatizo gani? Akauliza David  “ Kuna jambo ambalo ninataka 

tuliongee. Lakini nje ya hapa.Tunaweza 

tukatoka mara moja? Akasema Vicky 

 “ Madam Vicky,jambo hilo ni jambo 

gani ambalo hatuwezi kuliongelea hapa 

ofisini? Zaidi ya yote nina miadi ya 

kukutana na watu Fulani baadae kwa 

masuala muhimu ya kibiashara.” 

 “ David hapa si sehemu nzuri ya 

kuliongelea suala hilo.Twende tukatafute 

mahala tulivu tukae tuongee 

.hatutachukua muda mrefu utarejea 

kuendelea na shughuli zako .” akasema 

Vicky.David akainuka akavaa koti lake na 

kufunga ofisi yake akaongozana na Vicky 

hadi katika gari wakaingia na 

kuondoka.Hawakuongea kitu chochote 

ndani ya gari hadi walipofika katika baa 

moja tulivu maeneo ya Sakina 

 “ madam Vicky mbona sura yako 

inaonyesha kama una tatizo Fulani? Nini 

kimetokea?akauliza David 

 “ Kuna tatizo David lakini si kubwa 

sana na linaweza kutatulika” akasema 

Vicky huku akicheka kidogo na jino lake la 

dhahabu kuonekana  “ Kuna tatizo gani? Please tell me” 

akasema David 

 “ Pauline ameanza kuhisi kuna kitu 

kinaendelea yetu” akasema Vicky 

 ‘ Pauline ?!... David akashangaa 

 “ Amegunduaje? 

 ‘”Kwanza ni siku ile aliyonikuta 

katika mlango wako usiku tukiongea 

.Halafu mapendekezo uliyoyatoa 

kuhusiana na kuongezewa pesa biashara 

zangu za madini hakuyategemea kabisa 

.lengo lake kwa muda mrefu ni kuzifunga 

biashara zangu.Siyo siri mimi na 

Paulionekwa muda mrefu hatuendi sawa 

hanipendi sana yule binti na hataki 

nijishughulishe na kitu chochote.Kwa 

muda mrefu amekuwa akimshawishi baba 

yake azifunge biashara zangu kwa kigezo 

kwamba zinaingiza hasara.Pendekezo 

lako la kwamba biashara zangu zisifungwe 

bali ziongezewe fedha limemchanganya 

sana na anahisi kwamba lazima mimi na 

wewe tuko kitu kimoja .Leo asubuhi 

amekwenda kuonana na rafikiyangu 

mkubwa Safia na kumpeleleza kama 

anafahamu chochote kinachoendelea baina yetu” Akasema Vicky na kumstua 

sana David 

 “ Safia anafahamu chochote 

kinachoendelea ? akauliza 

 “ Relax David.Hata kama anafahamu 

kitu chochote katu hawezi kumueleza mtu 

kitu chochote kuhusiana na mimi kwani 

mimi ndiye ninayemuweka hapa 

mjini.Kamwe hawezi kunisaliti” akasema 

Vicky.David akaonekana kuzama katika 

mawazo mengi 

 “ Kwa hiyo tutafanya nini madam? 

Akauliza 

 “ Usiogope David.Lipo suluhisho la 

jambo hili.” 

 “ Suluhisho gani hilo? 

 “ Unatakiwa umtongoze Pauline na 

muanzishe mahusiano” 

 “ What !!!!..David akastuka 

 “ Ndiyo David.Unatakiwa umtongoze 

Pauline na uanzishe mahusiano naye.Hilo 

pekee ndilo suluhisho la jambo hili.” 

 “ No !Madam No !!....Hilo ni jambo 

lisilowezekana kabisa.Pauline 

ninamheshimu kama dada yangu na katu 

siwezi kumtamkia neno lolote la 

kimapenzi .Ni yeye aliyeniokota mtaani na ndiye aliyenifikisha hapa nilipo.Ni mtu 

ninayemuheshimu mno ” akasema David 

 “ David naomba unisikilize vizuri . 

Nataka nikuweke wazi kwamba 

kinachomsumbua Pauline ni wivu tu 

.Pauline anakupenda na anashindwa 

kukuweka wazi na ndiyo maana anaumia 

akikuona una ukaribu na mwanamke 

mwingine. Katika mawazo yake anahisi 

pengine mimi na wewe tuna mahusiano ya 

kimapenzi na ndiyo maana ameanza 

kufanya uchunguzi.Ili kumpoteza lengo na 

kuifanya mipango yetu iende kama 

tunavyotaka unatakiwa umtongoze na 

uanzishe mahusioano naye.Hiyo ndiyo njia 

pekee ya kumfanya asiendelee 

kuchunguza nini tunafanya.Endapo 

usipofanya hivyo anaweza akaharibu kila 

kitu.Hebu lifikirie suala hili vizuri David” 

akasema Vicky 

 David akainama akafikri kwa muda 

na kusema 

 “ Madam Vicky,naomba usinielewe 

vibaya lakini jambo hilo 

haliwezekani.Katu siwezi kumtongoza 

Pauline mtu ninayemuheshimu kama dada 

yangu.Tutafute namna nyingine ya kufanya ili kumpoteza malengo Pauline 

na si hivyo unavyosema” 

 “ David hakuna njia nyingine kwa 

sasa ya kuweza kumzuia Pauline 

asituchunguze.Kumtongoza Pauline na 

kuanzisha mahusiano naye ndiyo njia 

pekee kwa sasa.That girl loves you 

David.Hata matendo yake yanaonyesha 

wazi kwamba anakutaka.Tukitaka tuwe 

salama basi fanya hivyo 

ninavyokwambia.Ninafuatilia mkopo wa 

fedha nyingi na endapo nikiupata tu basi 

maisha yetu yatabadilika sana .Endapo 

Pauline akiendelea kutuchunguza 

anaweza akaligundua jambo hili na 

akimweleza baba yake tutapoteza kila kitu 

na tunaweza hata kuishia 

gerezani.Tusisubiri hadi hayo yatokee.We 

have to stop her ,and the only way is to 

make her fall for you” akasema Vicky 

 “ Madam Vicky umenipa mtihani 

mgumu sana na sina hakika kama 

nitauweza.Zadi ya yote sina hisia zozote za 

kimapenzi kwa Pauline.Nitawezaje 

kuanzisha mahusiano na mtu 

nisiyempenda hata kama yeye 

ananipenda?  “ David hii ni kwa ajili ya kufanikisha 

mipango yetu tu na si kwa ajili ya 

mapenzi.Once you have money and 

everything utamtafuta mwanamke wa 

ndoto zako lakini kwa sasa you have to 

pretend that you are madly in love with 

her”akasema Vicky 

 “MadamVicky ,sitaki kumdanganya 

Pauline kwamba ninampenda na kucheza 

na hisia zake.Siku akigundua kwamba 

nilimdanganya ataumia sana.I dont want 

to hurt her feelings” akasema David na 

Vicky akacheka kidogo na kusema 

 “David tayari tumekwisha danganya 

sana.Maisha yetu yametwaliwa na uongo 

mwingi kwa hiyo hatuna budi kuendelea 

kudanganya tu.” 

 “ MadamVicky naomba nipe muda 

wa kulifikiria vizuri jambo hili ,japokuwa 

moyo wangu unakuwa mzito sana 

kukubali mpango huu” 

 “ Hakuna muda wa kufikiria 

David.You have to do it.Mimi nimemaliza 

nasubiri utekelezaji” akasema Vicky na 

kuinuka ,David naye akainuka wakaingia 

garini na kuondoka. 



 Baada ya kumrejesha David ofisini 

kwake,Vicky akampigia simu Pauline 

akamuuliza mahala aliko ,akamjibu 

kwamba yuko dukani kwake.Bila 

kupoteza muda akakanyaga mafuta hadi 

dukani kwa Pauline 

 “ hallow Pauline” akasema Vicky 

baada ya kuingia dukani kwa Pauline 

 “ karibu mama mdogo.”akasema 

Pauline huku akijilazimisha kutabasamu 

 “ Ahsante sana Pauline.Sijafika 

dukanikwako kitambo,kumependeza 

sana”akasema Vicky 

 “ Karibu sana .Kuna mzigo mpya 

umeingia .”akasema Pauline.Vicky 

akaangalia baadhi ya vitu halafu 

akamgeukia Pauline. 

 “ Pauline nimekuja kwako nina 

shida kidogo” 

 “ Kuna tatizo gani mama mdogo? si 

kawaida yako kuonekana maeneo haya “ 

 “ Ni kweliPauline.Nimekuja hapa 

kuna jambo ambalo ninataka 

tuzungumze.”  “ .Ni jambo la kiofisi au la kibinafsi? 

Akauliza Pauline 

 “ Si la kiofisi.Ni mazungumzo ya 

kawaida tu” 

 “ Ok twende tukakae hapo jirani “ 

 Walitoka na kwenda kukaa katika 

baa jirani na duka la Pauline 

 “ Pauline kuna suala ambalo nataka 

tuliongee mimi na wewe” akaanzisha 

mazungumzo Vicky 

 “ Kuhusu nini? Akauliza Pauline 

 “ Ni kuhsu wewe na David” akasema 

Vicky 

 “Mimi na David tumefanya nini? 

Hutaki aendele kukaa pale nyumbani? 

Akauliza Pauline 

 “ Hapana si hivyo Pauline” 

 “ Kama si hivyo kuna jambo gani 

kuhusianamimina David? 

 “ Pauline si muda mrefu toka David 

aanze kuishi nasi pale 

nyumbani.Nimekuwa nikimchunguza sana 

,nimejaribu kuwa karibu naye ili 

kumfahamu vyema,na nimeundua 

kwamba David ni kijana mwenye sifa za 

kipekee kabisa.Utanisamehe kwa 

manenoniliyoyatoa mwanzoni kuhusu yeye ,sikuwa nikimfahamu 

vyema.Nimekuwa pia nikiwa chunguza 

namna mnavyoishi na nimegudnua 

kwamba kuna kitu kipo kati yenu” 

 “ Kitu? Pauline akashangaa 

 “ Ndiyo.Nimegundua kwamba kuna 

kitu Fulani kinawaunganisha bila ya ninyi 

kufahamu.Pauline mimi ni mtu mzima ni 

mwanamke kama wewe,na nina uwezo wa 

kugundua jambo na nimegundua kwamba 

wewe na David mnapendana.Hili nijambo 

ambalo liko wazi na ndiyo maana hata 

baba yako aliliona na akakutahadharisha 

mapema” akasema Vicky na Pauline 

akacheka kidogo akanywa funda la Juice 

na kusema 

 “ Usicheke Pauline,hiki ni kitu cha 

kweli kabisa.I’m a woman and I know 

when a woman is in love” 

Pauline hakusema kitu akabaki kimya 

akimtazama Vicky 

 “ Niambie kitu kimoja Pauline bila 

kunificha.Do you love him? Akauliza 

Vicky.Pauline akatabasamu 

 “ Niambie ukweli Pauline kwa 

sababu ninataka nikusaidie.Niambie 

kwama unampenda David.” Pauline akaifumbata mikono yake kifuani 

na kusema 

 “ Mama mdogo unayosema ni ya 

kweli na siwezi kukuficha ni kweli 

nimejikuta ninampenda David.Hata hivyo 

sina hakika kama hisia zangu ni za kweli 

na sina hakika kama hata yeye ana hisia 

zozote juu yangu.Ni kweli kuna nyakati 

najikuta nikishindwa kujizuia na 

kuonyesha wazi wazi kwamba 

ninampenda David” 

 “ Pauline tafadhali naomba uwe na 

mawazo chanya siku zote.Si jambo baya 

kuzama mapenzini na jambo la 

kufurahisha zaidi ni kwamba hata David 

naye anakupenda sana lakini anashindwa 

namna ya kukueleza hasa kutokana na 

namna ulivyomsaidia na hadi kumfikisha 

hapa alipofika.Kama kweli unampenda 

David basi unatakiwa uanze kuchukua 

hatua sasa.Usisubiri hadi David akutamkie 

kwamba anakupenda kwa sababu hilo 

halitakuja kutokea kwa namna 

anavyokuogopa.Anza kumuweka karibu 

na kumfanya akuone wa kawaida na 

asikuogope.Ukiwa karibu naye 

usizungumze naye sana masuala ya kazi bali maongezi yenu yatawaliwe zaidi na 

mambo ya mapenzi.Pauline,David ni 

kijana mzuri mwenye kila sifa 

nzuri,usikubali akakuponyoka.Usiache 

wenzako wakakupokonya dhahabu hii 

uliyoishika mkononi.Wewe ni msichana 

mzuri,mrembo na unastahili kuwa na 

mwanaume mzuri kama David”akasema 

Vicky 

 Pauline ambaye uso wake 

ulionyesha tabasamu pana baada ya 

kusikia maneno yake mazuri toka kwa 

Vicky akasema 

 “mama mdogo nakushukuru sana 

kwa ushauri wako.Toka tumekuwa 

pamoja leo umenipa ushauri mzuri mno 

na nitaufanyia kazi.Pamoja na hayo bado 

nina tatizo moja.Namuogopa baba.Endapo 

akigundua kwamba nina mahusiano na 

David hatanielewa” 

 “ Hilo lisikupe shaka Pauline.Niachie 

mimi nitashughulika nalo.Endapo 

akigundua nitaongea naye na kumuweka 

sawa.Umekwisha kuwa mtu mzima na 

unaweza ukafanya maamuziyako yenye 

kufaa.Kwa hiyo hakuna wa kukuingilia 

katika masuala yako ya kimahusiano.Unahitaji kuwa na maisha 

yenye furaha na mwanaume pekee 

ambaye ninaamini anaweza akakupatia 

furaha hiyo ni David,so make you first 

move” akasema Vikcy kisha wakaendelea 

na maongezi.Baada ya muda mrefu wa 

kuwa katika misuguano ya mara kwa 

mara hatimaye leo hii walikuwa wamekaa 

meza moja wakiongea na kucheka .Baada 

ya maongezi wakaagana Vikcy akaondoka 

zake. 

 “ Pauline lazima atafanya kila 

linalowezekana na kuanzisha mahusiano 

na David.Sikutaka jambo hili litokee kwani 

nilimuandaa David kwa ajiliyangu lakini 

kutokana na hali ya mambo ilivyo 

inanilazimu kuliacha jambo hili litokee 

tu.” Akawaza Vicky . 

******************************* 

Mwalimu Lucy alikuwa amesimama 

dirishani akitazama nje.Alionekana kuwa 

na mawazo mengi sana.Mkononi alikuwa 

ameshika kikombe cha kahawa akanywa 

kidogo na kuendelea kutazama nje. kimahusiano.Unahitaji kuwa na maisha 

yenye furaha na mwanaume pekee 

ambaye ninaamini anaweza akakupatia 

furaha hiyo ni David,so make you first 

move” akasema Vikcy kisha wakaendelea 

na maongezi.Baada ya muda mrefu wa 

kuwa katika misuguano ya mara kwa 

mara hatimaye leo hii walikuwa wamekaa 

meza moja wakiongea na kucheka .Baada 

ya maongezi wakaagana Vikcy akaondoka 

zake. 

 “ Pauline lazima atafanya kila 

linalowezekana na kuanzisha mahusiano 

na David.Sikutaka jambo hili litokee kwani 

nilimuandaa David kwa ajiliyangu lakini 

kutokana na hali ya mambo ilivyo 

inanilazimu kuliacha jambo hili litokee 

tu.” Akawaza Vicky . 

******************************* 

Mwalimu Lucy alikuwa amesimama 

dirishani akitazama nje.Alionekana kuwa 

na mawazo mengi sana.Mkononi alikuwa 

ameshika kikombe cha kahawa akanywa 

kidogo na kuendelea kutazama nje.  “ Historia ya maisha yangu ya huko 

nyuma imenikumbusha mambo mengi 

ambayo tayari mengine nilikiwisha anza 

kuyasahau.” Akawaza halafu akanywa 

kahawa kidogo 

 “ Japokuwa moyo wangu bado 

unamakovu yaliyotokana na maisha 

niliyoyapitia na hasa kwa mambo 

niliyotendwa na wanadamu waliokosa utu 

lakini natakiwa kusonga mbele na maisha 

yangu.Siwezi kuendelea kuishi maisha ya 

namna hii.Natakiwa niyafurahie maisha 

.Nadhani ni wakati sasa wa kuufungua 

moyo wangu na kuuruhusu kupenda 

tena.Baada ya yote yaliyonitokea na 

kunifanya nikate tamaa ya kujiingiza tena 

katika maoenzi hatimaye najisikia 

kupenda tena.Nimetokea kumpenda 

Robin.Ni mwanaume ambaye nina uhakika 

atanifaa katika maisha yangu.Ni mzuri, 

anajali ,ananifanya niwe na furaha kila 

ninapokuwa karibu naye.” Akawaza na 

kutabasamu baada ya kuikumbuka sura ya 

Robin.Ghafla sura yake ikabadilika baada 

ya kukumbuka jambo Fulani 

 “ Sura ya Tino nayo bado inanijia kila 

mara.I need to get him out ofmy life. I’m trying to collect pieces and rebuild my life 

again.Ineed to forget him and move on 

with my life” akasema kwa hasira na 

kurejea mezani pake 

 “ Baada ya kurejea toka marekani 

nilitoke a kumpenda sana 

Tino,nikamuamini na kumuona tofauti na 

wanaume wengine ,nilimuona kama 

malaika aliyetumwa kuyafuta machozi 

yangu na kuniponya majeraha.Niliamini 

hatanitenda kama walivyonitenda 

wengine.I was wrong.Aliniumiza tena 

vibaya sana .Mpaka leo hii siamini kama 

kweli Tino mwanaume niliyempa moyo 

wangu alinitenda namna ile.lakini pamoja 

na yote aliyonifanyia bado moyo wangu 

unamuwaza.Yawezekana kwa sababu ni 

mwanaumewangu wa kwanza 

kumpenda.Yawezekana nilimpenda kupita 

kiasi .Nadhani ni wakati muafaka sasa wa 

kumsahau na kuendelea na maisha 

yangu.Tayari Robin ameanza kuniingia 

moyoni mwangu na nina hakika ndiye 

mwanaume niliyepangiwa niwe naye 

katika haya amaisha.This time I’m not 

wrong.Robin tayari amekwisha onyesha 

kila dalili za kunipenda na nina hakika ataweza kunishaulisha kuhusu Tino” 

akawaza mwalimu Lucy 

 “ Jumamosi ya wiki hii ni siku yangu 

ya kuzaliwa.Bado sijapata jawabu nifanye 

nini siku hiyo lakini kitu pekee 

ninachokifahamu ni kwamba ninahitaji 

kuifanya siku hiyo iwe maalum kabisa 

kwangu.Kila mwaka nimekuwa 

nikisherehekea peke yangu na mara 

nyingine na watoto yatima au wanafunzi 

wachache lakini safari hii nataka 

kusherehekea na watu wangu wa karibu 

hususan Robin na Pamela.” Akawaza. 

 “ Kwa kuwa natafuta ukaribu na 

Robin hii inaweza ikawa ni siku muhimu 

sana kwetu ya kutuweka karibu zaidi na 

kama ikiwezekana tunaweza tukaufungua 

ukurasa mpya ndani ya siku hii.I need to 

make it very special.Nitafanya kila 

linalowezekana hadi Robin na Pamela 

walale nyumbani kwangu.Endapo hilo 

litafanikiwa basi ndoto yangu ya kumpata 

Robin mwanaume ambaye ametokea 

kunikosesha usingizi itatimia.Nitautumia 

usiku huo kumfahamu zaidi Robin 

,ametoka wapi,maisha yake yalikuwaje 

n.k.Ngoja nianze maandalizi mapema kwanajili ya siku hii muhimu.” Akawaza 

mwalimu Lucy na kuegemea kiti chake 

akawaza namna ambavyo ataifanya siku 

hiyo iwe ni ya aina ake.. 

******************** 

Ni saa tatu za usiku baada ya 

shughuli za kutwa nzima ,David alikuwa 

amejipumzisha chumbani kwake 

akitafakari namna siku yake 

ilivyokwenda. 

 “ Siku yangu ilianza vizuri lakini yale 

maneno aliyonieleza madam Vicky eti 

nimtongoze Pauline yamenifanya nikose 

raha kutwa nzima ya leo.Hili ni jambo 

ambalo haliniingii akilini kabisa 

.Ninamuheshimu sana Pauline kama dada 

yangu.Ameniokota mtaani na 

kunipandisha hadi hapa nilipofika.Familia 

yake imeniamini na kunipa majukumu ya 

kusimamia biashara zao.Kitendo cha 

kuanzisha mahusiano ya kimapenzi na 

Pauline kitapunguza heshima kubwa 

niliyo nayo kwa Pauline.Ukiachilia mbali 

namna tunavyoheshimiana ,sina hisia 

zozote za kimapenzi kwake.Hata  nikimuona moyo wangu haustuki 

kabisa.Hapana .Siko tayari kufanya 

hivyo.Hata kama yeye ananipenda lakini 

siko tayarikuuvunja moyo wake kqwa 

kumdanganya kwamba ninampenda.” 

Akawaza David halafu akatabasamu baada 

ya sura Fulani kumjia kichwani 

 “ Kidogo Tamia nimeanza kuvutiwa 

naye.Ana vitu Fulani Fulani 

vinavyonifanya nivutiwe naye.Ni 

mcheshi,mchangamfu, na kuna kitu Fulani 

nisichokifahamu kinanifanya nijisikie 

furaha sana kila nimuonapo.Sikupanga 

kujiingiza katika masuala ya kimapenzi 

kwa sasa lakini ninahisi ninahitaji 

kupenda tena.Ninahitaji mtu wa kunipa 

faraja .Ninahitaji mtu wa kucheka na 

kufurahi naye,mtu wa kuzungumza 

naye.Pauline amepunguza ukaribu na 

mimi hasa baada ya kutoa ushauri ule wa 

kumuongezea madam Vicky pesa katika 

biashara zake.” akawaza David na 

kustushwa na mlio wa ujumbe mfupi wa 

simu.Akanyoosha mkono akaichukua simu 

yake .Ujumbe ule ulitoka kwa Pauline 

“ umelala? Ndivyo ulivyosomeka 

ujumbe ule .  “ Hapana bado.” David akajibu.Baada 

ya sekunde kadhaa ukaingia ujumbe 

mwingine toka kwa Pauline 

 “ Unafanya nini? 

 “Nimejilaza hapa kitandani 

natafakari maisha yangu .Wewe unafanya 

nini? David akajibu 

 “ Nimeshindwa kupata usingizi 

.Kichwa changu kina mawazo mengi 

sana.I need someone to talk to ” Pauline 

akajibu.David akainuka na kukaa 

kitandani 

 “ I’m here Pauline .You can talk to 

me” 

 “ Thank you David” akajibu Pauline 

 “ Pauline kitu gani kinakufanya uwe 

na mawazo mengi? Una kila kitu 

unachokihitaji katika maisha 

yako,mawazo ya nini? Akautuma ujumbe 

ule na baada ya sekunde kadhaa Pauline 

akajibu. 

 “ Ni kweli nina kila kitu lakini kuna 

kitu nimekikosa na ambacho ndicho 

kinaninyima usingizi” 

 “ Ni kitu gani hicho Pauline? Can you 

tell me?May be I can help” akasema David  “ Do you real want to know? Akajibu 

Pauline 

 “ Yes .You can tell me if its ok with 

you” akasema David 

 Baada ya sekunde chache Pauline 

akatuma tena ujumbe 

 “ Nimekosa mwanaume wa kweli wa 

maisha yangu” 

 David akatabasamu baada ya 

kuusoma ujumbe ule na kujibu 

 “ Usijali Pauline.Kuna maelfu ya 

wanaume wazuri na wenye mapenzi 

ambao wanaota kukupata msichana 

mzuri kama wewe” 

 “ Nakubaliana nawe David lakini ni 

vigumu sana kumpata mwanaume w a 

kweli siku hizi.The world is full of liars” 

 Davidiakaonekana kuvutiwa na 

majibizano yale naye akajibu 

 “ Zipi sifa za mwanaume wa ndoto 

yako? Baada ya sekunde kadhaa Pauline 

akajibu 

 “ Mwanaume 

mpole,mwaminifu,mchapakazi,anayemuo

gopa Mungu na mwenye kujua kupenda na 

ambaye atanifanya nijione malkia katika 

hii dunia” “ wow ! Nina hakika wapo wanaume 

wa aina hii.Unachotajiwa ni kutokata 

tamaa.Endelea kuvumilia na kumuomba 

Mungu akusaidie uweze kumpata” akajibu 

David 

 “ Mungu amekwisha sikia kilio 

changu na tayari ameniletea mwanaume 

wa maisha yangu ,mwanaume ambaye 

ninampenda kuliko ninavyoweza 

kueleza,mwanaume ambaye amenifanya 

nikose usingizi usiku huu kwa kumuwaza 

yeye,mwanaume ambaye hunisismua kila 

nimuwazapo” 

 David akausoma ujumbe ule na 

kujibu 

 “ Kumbe tayari,umempata 

mwanaume unayemtaka.Hongera sana 

.Kama hivyo ndivyo kwa nini basi ukose 

furaha? 

 “Ninakosa furaha kwa sababu 

mwanume huyo bado hajui kama yeye 

ndiye mwanaume wa maisha yangu.Hajui 

kama ni yeye anayeninyima usingizi” 

 “Pauline ushauri wangu kwako,kama 

unampenda mtu huyo na una hakika 

kwamba ndiye mwanaume anayekufaa 

,usisubiri .Muweke wazi hisia zako Mwambie ukweli” David akautuma 

ujumbe ule na kutabasamu 

 “ Nashukuru sana kama tayari 

Pauline amempata mwanaume kwani 

mpango wa madam Vicky wa kunitaka 

nimtongoze hautafanikiwa.” Akawaza 

David na ujumbe mwingine ukaingia 

 “ Nashukuru kwa ushauri lakini sina 

hakika kama naye ananipenda au 

atakubaliana na ombi langu endapo 

nikimueleza.Nitaumia sana kama akisema 

hanipendi.Hicho ndicho 

kinachoniogopesha hata kumweleza 

ukweli” 

 “Usiogope Pauline.Kama unashindwa 

kumueleza ukweli ,nionyeshe mtu huyo 

nimfuate mimi nikamueleze ukweli.” 

Akajibu David 

 Baada ya sekunde chache Pauline 

akajibu 

 “ Do real want to know him David? 

 “ Yes I do “akajibu David.Wakati 

akisubiri majibu toka kwa Pauline simu 

yake ikaita.Alikuwa ni Tamia.David 

akatabasamu halafu akabonyeza kitufe 

cha kupokelea 

 “ hallow Tamia” akasema David  “ Hallow David,mambo” akasema 

Tamia kwa sauti laini sana. 

 “ Mambo poa Tamia .Umeshindaje 

leo? 

 “Nimeshinda salama David.Wewe je 

umeshindaje? 

 ‘ Hata mimi nimeshinda salama “ 

akajibu David 

 “Nafurahi kusikia hivyo David. I miss 

you so much Davie,nilitamani sana 

kukuona leo lakini nikakosa 

muda.Umeshalala? 

 “Hapana bado sijalala 

Tamia.Nimekaa tu hapa kitandani 

nikitafakari kuhusu siku ilivyokwenda.” 

 “ Ouh Jamani,Davidi unawaza nini? 

 “ Ninawaza mambo mengi tu 

kuhusiana na maisha” 

 “ Usiwaze sana David.Yachukulie 

maisha namna yanavyokuja” 

 “ sawa Tamia.wewe unafanya nini 

sasa hivi? 

 “ NImejilaza atu hapa kitandani 

ninatafakari siku ilivyokwenda”akajibu 

Tamia na wote wakacheka  “ David nafurahi sana kuongea na 

wewe.Kila ninapozungumza nawe nasikia 

furaha sana moyoni” 

 “ Hata mimi Tamia.Ninafurahi sana 

kila ninapozungumza nawe hasa mida 

kama hii.Una sauti tamu ambayo 

haichoshi masikioni,Natamani niendelee 

kuongea nawe hadi nitakapopitiw a na 

usingizi” 

 “ Ouh David,nafurahi sana kusikia 

hivyo.Natamani nipate nafasi siku moja 

nikae nawe tufahamiane zaidi.” 

 “Usihofu Tamia .Siku moja tutapata 

wasaa mimi na wewe tutakaa na kuongea 

mambo mengi tu.Hata mimi nina hamu 

sana ya kukufahamu zaidi.” 

 “ Una ratiba gani mwishoni mwa wiki 

hii? 

 “Bado sijajua nini nitafanya 

.Nitakufahamisha kamanitakuwa na 

nafasi” 

 “ Nitashukuru sana kama utakuwa 

na nafasi tutaweza tukakutana” 

 “ Usijali Tamia nitakujulisha” 

 “ David nimemfurahi sana kuongea 

nawe.Lala salama “ akasema Tamia kwa sauti laini ya kubembeleza na kukata 

simu. 

 “ Gosh !Tamia amebarikiwa sauti 

tamu ya kubembeleza.Kila ninapoongea 

naye najikuta nikivutiwa naye 

zaidi.Siwezikupingana na nafsi yangu ni 

kweli nimetokea kumpenda sana 

Tamia.Ngoja niwe karibu yake nimzoee na 

nimfahamu alivyo.Kama tabia zake 

zitakuwa ni za kuridhisha Tamia ndiye 

atakayekuwa mpenzi wangu” akawaza 

David na mara akakumbuka kwamba 

alikuwa akichat na Pauline kabla ya 

kupokea simu ya Tamia.Akazitafuta 

namba za Pauline ili ampigie na kumtakia 

usiku mwema lakini simu ya Pauline 

haikuw a ikipatikana 

 “Mbona amezima simu ? akajiuliza 

 Kabla Tamia hajapiga simu David 

alikuwa amemuomba Pauline amueleze ni 

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog