Search This Blog

Friday 7 April 2023

SCANDLE (KASHFA) (3) - 1

  

IMEANDIKWA NA : PATRICK CK

***************************************************************

Simulizi : Scandle (Kashfa) (3)

Sehemu Ya Kwanza (1)


 “Bado naendelea kujiuliza 

kwa nini wale jamaa 

hawajasambaza zile picha? 

Wameogopa? Nahisi hivyo 

watakuwa wametafakari na 

wameogopa kufanya hivyo kwa 

hofu kwamba wangesakwa kwa nguvu kubwa hadi 

wapatikane” akawaza na 

kukumbuka kitu 

 “Ngoja niwasiliane na 

akina Mathew niwajulishe 

kuwa picha bado 

hazijasambazwa na niwatake 

wafanye haraka zaidi 

kuwasaka hawa jamaa” 

 Rais Festus akachukua 

simu yake akazitafuta namba 

za Zari akampigia 

 “Mheshimiwa Rais” 

akasema Zari na Rais Festus 

akastuka  “Zari are you okay? 

 “Yes I’m okay Mr 

President” 

 “No you are not.Niambie 

tafadhali kuna tatizo lolote? 

 “It’s Mathew” 

 “Mathew kafanya nini? 

 “Amepigwa risasi” 

 “Nini? 

 “Amepigwa risasi 

mheshimiwa Rais” 

 “Saa ngapi? 

 “Usiku huu”  “Vipi hali yake?akauliza 

Rais 

 “Hali yake si nzuri.Yuko 

katika chumba cha upasaji 

hapa SNSA madaktari 

wanaendelea na jitihada za 

kuokoa maisha yake” akasema 

Zari 

 “Zari ninakuja hapo mara 

moja” akasema Rais Festus 

 “Sawa mheshimiwa Rais” 

akajibu Zari na Rais akakata 

simu 

 “Mathew Mulumbi 

amepigwa risasi ! It’s getting ugly ! akawaza Rais 

Festus. 

 “Nadhani hii ndiyo sababu 

wale jamaa hawajasambaza 

zile picha kwa sababu wanajua 

wamekwisha mpata Yule 

waliyekuwa 

wanamtafuta.Wanajua 

wamekwisha muua” akawaza 

na kutoa maelekezo kwa 

walinzi wake kujiandaa.Akavaa 

haraka haraka na kuelekea 

katika gari msafara wa magari 

manne ukaondoka usiku ule 

kuelekea ofisi za SNSA ambazo 

hazikuwa mbali sana na ikulu.  “Bora angepigwa risasi 

mtu mwingine lakini si 

Mathew 

Mulumbi.Tunamtegemea sana 

Mathew katika vita hii.Endapo 

ikitokea ameuawa basi 

litakuwa ni pigo kubwa sana 

kwetu.Mathew anatakiwa 

apone ili aendeleze 

mapambano haya” akawaza 

Festus akiwa garini 





Ruby akiwa na makomando wa wawili waliwasili ofisi kuu za SNSA akapokewa na Lutengano aliyetumwa na Zari


“Karibu mama


Ruby.Naitwa Lutengano ni mkurugenzi msaidizi wa SNSA” akasema Lutengano na kumpa mkono Ruby


“Ahsante sana.Yuko wapi


Zari”


“This way madam” akasema Lutengano na kumuongoza Ruby kuelekea ndani.Baadhi ya watu waliowahi kufanya kazi na Ruby wakati wa uongozi wake wakastuka kumuona tena pale usiku ule na kujiuliza kitu gani kinachoendelea.Moja kwa moja Lutengano akampeleka Ruby upande wa Afya iliko hospitali inayohudumia wafanyakazi wa SNSA. Ni hospitali iliyosheheni kila kitu.


Zari alipomuona Ruby akamfuata akamkumbatia kwa nguvu na wote wawili machozi yakawatoka


“Tell me he’s still alive ! akasema Ruby


“Bado yuko katika chumba cha upasuaji.Madaktari wanaendelea na upasuaji” akasema Zari na kumshika mkono Ruby wakaenda kuketi sofani.


“Zari nini kimetokea? Ilikuaje hadi Mathew akapigwa risasi? Akauliza Ruby


“Nashindwaa hata nianzie wapi Ruby.Bado mwili wangu unanitetemeka kwa kile kilichotokea”


“Nieleze tafadhali ! akasema Ruby na Zari akafuta machozi na kusema


“Mimi ndiye niliyepaswa aidha kuwa ndani ya chumba cha upasuaji muda huu au niwe tayari nimepoteza maisha.Risasi zile alizopigwa Mathew zilielekezwa kwangu.He saved my life ! akasema Zari na Lutengano akamfuata


“Nimejulishwa Rais amefika” akasema Lutengano na Zari akafuta machozi “Ruby ninakwenda kumpokea Rais” akasema Zari na kushuka chini kwenda kumpokea Rais na kukutana naye akielekea ndani.


“Mheshimiwa Rais karibu sana” akasema Zari


“Ahsante Zari.Where is he? Akauliza Rais


“This way please” akasema Zari na kumuongoza Rais kuelekea ndani.Watu wote


waliokuwa kazini ndani ya


ukumbi mkubwa wakasimama baada ya Rais kutokea


“Habari za usiku huu ndugu zangu.Poleni sana na majukumu ya kila siku” Rais Festus akawasalimu


“Nimekuja mara moja kuonana na mkurugenzi wenu siku nyingine nitakuja tena tukae tuzungumze nisikie matatizo yenu kama yapo.Kwa sasa endeleeni na kazi na hongereni sana kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuhakikisha nchi yetu inakuwa salama” akasema Festus kisha akaongozana na Zari wakaelekea upande wa afya “How’s he? Akauliza Rais


Fstus


“Bado upasuaji unaendelea” akajibu Zari


“Are you sure he’s going to make it?


“I don’t know mr


President” akajibu Zari


“Ruby ! akasema Rais


Festus baada ya kufika katika chumba cha mapumziko na kumkuta


Ruby.Wakakumbatiana


“It’ s okay Ruby.Dont cry.He’ll be fine” akasema Rais Festus na kumgeukia Zari


“Tangu upasuaji umeanza kuna taarifa zozote kutoka kwa madaktari? Akauliza Rais Festus


“Hapana hawajatoa taarifa yoyote” akajibu Zari


“Nani kiongozi wa madaktari?


“Dr Fred !


“I need to talk to him !


“Mr President ! akasema


Zari


“Zari I need to talk to him now ! I want to tell him how important this man is so that they do all they can to save his life” akasema Rais Festus kwa sauti ya juu.Zari akainuka akaenda katikachumba cha upasuaji akabonyeza kengele na baada ya sekunde chache mlango ukafunguliwa na muuguzi aliyekuwa amevaa mavazi maalum


“Mwambie Dr Fred ,Rais yuko hapa anataka kuzungumza naye sasa hivi” akasema Zari.Baada ya dakika chache Dr Fred akatoka katika chumba cha upasuaji akaelekea katika chumba cha mapumziko alikokuwa Rais


“Mheshimiwa Rais” akasema Dr Fred


“DrFred samahani


nimekutoa katika upasuaji


“Usijali mheshimiwa


Rais”akasema Dr Festus


“Mnaendeleaje na


upasuaji? Akauliza Rais


“Tunaendelea.Tayari


tumekwisha toa risasi mbili zilizokuwa tumboni lakini limejitokeza tena tatizo lingine.Kuna damu nyingi inaendelea kuvuja tunaendelea kutafuta kujua mahala inakovuja damu hiyo tuweze kuizuia” akasema DrFred


“Dr Fred kwanza ninakushukuru wewe na wenzako wote kwa jitihada mnazoendelea nazo kuokoa maisha ya Mathew lakini nataka nikwambie jambo moja kwamba huyu mtu ambaye mnahangaika kuokoa maisha yake ni mtu muhimu mno kwangu na kwa nchi pia na ndiyo maana umeniona hapa usiku huu.Nataka nikuombe wewe na timu yako kufanya kila linalowezekana kuokoa maisha ya huyu mtu.Mimi nitakuwepo hapa hadi upasuaji utakapokamilika na chochote kile ambacho kitahitajika uniambie kitapatikana na hata kama ni kuongeza madaktari na vifaa nieleze tafadhali” akasema Rais Festus


“Ahsante sana mheshimiwa Rais.Ninakuahidi tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha tunaokoa maisha ya Mathew” akasema DrFred na kurejea katika chumba cha upasuaji


“Ladies najua jambo hili limetustua sote lakini nawaomba tuwe na imani tumuombe Mungu amlinde Mathew.Tuwe na imani na madaktari watafanya kila linalowezekana kuokoa maisha ya Mathew Mulumbi” akasema Rais Festus kisha wakaelekea katika ofisi ya Zari


“Zari nini hasa kilitokea hadi Mathew akapigwa risasi? Akauliza Rais Festus.Zari akafuta machozi na kuanza kuwaelezea kilichotokea nyumbani kwa mchungaji Lucas.


“Walifahamuje kama mko pale? Akauliza Ruby na mara Zari akakumbuka kitu


“Find..if..t.t.ther..e is hidden cameras !


Maneno yale aliyoambiwa na Mathew yakajirudia kichwani kwake


“Kuna kitu Mathew


Mulumbi aliniambia wakati tukiwa njiani kuja huku hospitali lakini kwa wakati ule nilikuwa nimechanganyikiwa na sikutilia maanani lakini sasa ninaanza kuelewa kile alichokimaanisha”


“Alisemaje


Mathew?Akauliza Rais Festus


“Aliniambia nitafute kamera za siri nadhani alimaanisha ndani ya ile nyumba kuna kamera za siri zimefungwa na watu waliofunga kamera hizo za siri walikuwa wanafuatilia kila kinachoendelea na ndiyo maana wakaweza kujua kama tuko pale wakaja mara moja na kufanya mauji yale.Mtu wa kwanza kabisa kuuawa alikuwa ni mchungaji Lucas na waliwahi kumuua ili


asiendelee kuzungumza nasi” akasema zari


“Zari tuma timu ya wataalamu wa ufundi waende haraka sana ndani ya hiyo nyumba wafanye uchunguzi kama kuna kamera za siri


humo ndani”akasema Rais festus


“Mheshimiwa Rais kuna uwezekano mpaka sasa polisi watakuwa wamepata taarifa za mauaji hayo na watakuwa eneo


la tukio.Watu wetu hawataweza kuingia mle ndani” akasema Zari “Hata kama wakikuta kuna askari polisi wamekwisha fika watoe taarifa na mimi nitatoa kibali waingie ndani wafanye kazi yao.Lazima tujue kama kuna kamera za siri zimefungwa ndani ya hiyo nyumba”akasema Rais Festus na Zari akaenda kutoa maelekezo kwa timu ya wataalamu wa kamera wakaondoka kuelekea nyumbani kwa mchungaji


Lucas na Zari akarejea ofisini


“Jamani kuna jambo bado lina ukakasi” akasema Ruby “Tuna imani kabisa kwamba waliofanya mauaji hayo ni watu kutoka kundi la Black mafia ambao ndiyo tunapambana nao.Ninajiuliza kuna nini hadi Black Mafia wafunge kamera za siri nyumbani kwa mchungaji Lucas.Kwa nini wamfuatilie kupitia kamera? Akauliza Ruby


“Kweli hapo


panachanganya sana lakini ngoja kwanza tujiridhishe kama kweli kuna kamera za siri humo ndani ya nyumba ya mchungaji halafu tutajua nini cha kufanya” akasema Rais Festus


“Kabla hajauawa mchugaji Lucas kuna kitu gani alikuwa amewaeleza? Ruby akauliza


“Mazungumzo yetu ndiyo kwanza yalikuwa yameanza.Tulimuuliza kuhusu sababu ya mchungaji Adam kusafiri na kuna mambo alitueleza.Alisema kwamba siku ile yeye na baadhi na wachungaji waliitwa kushiriki katika maombi maalum ya kumuombea mtoto wa mchungaji Adam aliyekuwa ametoweka shuleni katika mazingira ya kutatanisha.Wakati wakiendelea na maombi nabii mkuu Kasiano akasimamisha maombi na kuwaeleza kwamba Mungu amempa maono wakati tukiomba na kumuonyesha kuwa mtoto yuko salama.Baada ya hapo mchungaji Adam na mke wake wakaelekea ofisini kwa nabii Kasiano na yeye Lucas hakujua kilichoendelea tena hadi pale alipopata taarifa kwamba Adam na mke wake wamefariki kwa ajali ya gari wakati wakielekea Morogoro” akasema Zari


“Awali ulipojifanya mwandishi na kumuuliza nabii Kasiano kuhusu safari ya Adam alidai kuwa yeye ndiye aliyemtuma Morogoro kwa shughuli za kikanisa.Tulikuwa tunajiuliza inawezekanaje mchungaji Adam kuacha kumtafuta mwanae aliyepotea na badala yake akafunga safari ya kwenda Morogoro?Sasa nimepata picha kwamba Nabii Kasiano baada ya kuonyeshwa maono ya kinabii kwamba mtoto wa mchungaji Adam yuko salama ndipo akamtuma kwenda Morogoro na inawezekana alikuwa katika mwendo mkali sana ili aweze kufika Morogoro na kurejea ili aweze kumtafuta mwanae na ndiyo maana wakapata ajali mbaya wakafariki dunia.Lakini


swali ninalojiuliza kwa nini hakumuacha mke wake aendelee kumfuatilia mtoto wao na yeye akaenda Morogoro peke yake badala ya wote kuongozana katika safari hiyo? Akauliza Ruby


“Tulimuuliza mchungaji


Lucas kama kulikuwa na shughuli yoyote ya kikanisa iliyomlazimu Adam kwenda Morogo……………” akanyamaza


Zari baada ya simu yake kuita


“Hallow”


“Madam unahitajika Afya” akasema muuguzi na Zari akiwa ameongoza na Rais Festus na Ruby wakatoka mbio kuelekea upande wa Afya moja kwa moja ofisini kwa Dr Fred


“Kuna nini Dr Fred? Akauliza Rais Festus


“We need


blood.Tumeishiwa damu na mgonjwa bado anapoteza damu nyingi”


“Bado hamjafanikiwa kujua sehemu inakovuja ndani kwa ndani? Akauliza Rais Festus


“Tunaendelea mheshimiwa Rais.Tunaendelea


kulishughulikia hilo ndiyo maana tunaomba msaada wa damu tumeishiwa”


“Ni damu ya kundi gani mnaihitaji?


“Mathew ni kundi B- hivyo anapokea damu kutoka kundi B- au kundi O- tu”


“Mimi ni kundi O- hivyo hakuna muda wa kupoteza.Nitoeni damu awezekewe Mathew mara moja” akasema Rais Festus na taratibu za kutoa damu zikaanza mara moja.





************ 

 Kwa zaidi ya saa moja 

mama Bella mke wa Rais 

Festus alikuwa katika simu akizungumza na mtu na 

maongezi yao yalionekana 

kujaa mahaba mazito.Sauti 

ilikuwa ya chini na 

laini.Wakati Bella akiendelea 

na mazungumzo simuni mara 

akasikia mlio katika simu yake 

kuashiria kuna simu ilikuwa 

inapigwa. 

 “Patrick samahani naomba 

nikate simu,kuna simu 

nyingine nataka 

kuipokea.Nitakupigia tena 

baada ya muda mfupi” 

akasema mama Bella na 

kukata simu halafu akaipokea 

simu ile nyingine  “Kelvin” akasema mama 

Bella 

 “Mama ulinipa maelekezo 

kwamba nikujulishe kila 

mahala anakoenda Rais” 

 “Ndiyo Kelvin” 

 “Mama tumekuja hapa 

kwenye ofisi Fulani panaitwa 

SNSA.Kuna hospitali kubwa 

humu ndani na Rais hivi sasa 

anatolewa damu” 

 “Anatolewa damu?! 

Akauliza Bella kwa mshangao 

 “Ndiyo mama.Anatolewa 

damu.Nimesikia kuna mgonjwa amejeruhiwa kwa 

risasi anaitwa Mathew ambaye 

kwa sasa yuko katika chumba 

cha upasuaji na hali yake 

inasemwa si nzuri,nadhani 

anatoa damu kwa ajili hiyo” 

 “Kelvin una hakika 

umesikia vizuri jina hilo la 

mgonjwa anayefanyiwa 

upasuaji? 

 “Ndiyo mama.Nimesikia 

wakimtaja kwa jina hilo la 

Mathew” akasema Kelvin 

 “Ahsante sana Kelvin 

endelea kufanya uchunguzi 

zaidi upate taarifa za kutoshaza mgonjwa huyo halafu 

utanijulisha.One more 

thing,umenifurahisha sana 

Kelvin kwa kazi yako nzuri 

,nitakupa mara tatu zaidi ya 

kiasi kile nilichokuahidi 

kukupa” akasema Bella 

 “Ahsante sana mama 

nashukuru” akasema Kelvin na 

Bella akakata simu 

 “Ni kweli hiki 

nilichokisikia au niko ndotoni? 

Ngoja kwanza nipate uhakika 

zaidi” akawaza Bella na 

kuchukua simu akampigia 

nabii Kasiano  “Mama Bella”akasema 

Kasiano 

 “Kasiano nataka kufahamu 

kuna tukio lolote limetokea 

usiku huu linahusisha vijana 

wako? Akauliza Bella 

 “Ndiyo mama.Nilipata 

taarifa kwamba kuna watu 

wamekwenda kwa mmoja wa 

wachungaji wa kanisa langu na 

wanamuhoji mchungaji huyo 

kuhusiana na kifo cha 

mchungaji Adam.Katika 

nyumba zangu zote wanakoishi 

wafanyakazi kuanzia 

wachungaji na wanafanyakazi wengine kumefungwa kamera 

za siri ambazo zinafuatiliwa 

kwa saa ishirini na nne na 

watu wa Black Mafia.Lengo ni 

kuhakikisha kwamba hakuna 

yeyote anayegeuka na kuwa 

hatari kwangu.Baada ya 

kupata taarifa hiyo nilitoa 

maelekezo kwa vijana kwenda 

kulimaliza hilo jambo.Kuna 

nini mama Bella hadi 

ukaniuliza? Akauliza Kasiano 

 “Mathew Mulumbi 

alikuwemo katika hiyo 

nyumba’ akasema Bella“Mathew Mulumbi?! 

Kasiano akashangaa 

 “Ndiyo.Kwa bahati mbaya 

amejeruhiwa kwa risasi na kwa 

sasa anapatiwa matibabu 

katika ofisi za SNSA” 

 “SNSA? 

 “Ndiyo.Nimepata taarifa 

hivi sasa kuwa Mathew yuko 

huko na anapatiwa 

matibabu.Festus amejulishwa 

kuhusu hilo tukio naye 

ametoka hapa na kuelekea 

huko SNSA na hivi 

tuzungumzavyo anatoa damu 

kwa ajili ya kuwekewa Mathew ambaye amepoteza damu 

nyingi.Kasiano tumempata 

Mathew.Muda si mrefu vita 

itamalizika na amani itarejea” 

akasema Bella 

 “Mama Bella nakushukuru 

mno kwa taarifa hii njema kwa 

sasa ni kuanza mipango ya 

kuhakikisha tunafanikiwa 

kuingia hapo SNSA na 

kummaliza kabisa Mathew 

Mulumbi .Huyu pekee ndiye 

wanayemtegemea na kama 

tukifanikiwa kumuondoa huyu 

mtu basi ushindi utakuwa 

wetu.Usiku huu huu 

maandalizi ya kuingia ndani ya jengo hilo yanaanza na mpaka 

kufika kesho asubuhi tayari 

tutakuwa na mpango wa 

kutuwezesha kuingia na 

kummaliza Mathew Mulumbi” 

akasema Kasiano 

 “Kasiano vita hii nataka 

ifike mwisho,sitaki kusikia 

tena kuna kosa lolote 

limetokea na tukashindwa 

kummaliza huyo Mathew 

Mulumbi.Sitaki kusikia hadi 

kufika kesho jioni kuna 

kiumbe hapa duniani kinaitwa 

Mathew Mulumbi.Nadhani 

umenielewa Kasiano”  “Nimekuelewa mama” 

akasema Kasiano na Bella 

akakata simu 

 “Siamini kama 

tumefanikiwa kumpata mtu 

ambaye amekuwa akituumiza 

vichwa vyetu sana.Nitawapa 

zawadi hao jamaa 

waliofanikiwa kumpiga risasi 

huyo Mathew Mulumbi.Wao 

ndiyo wamesababisha 

tukaweza kufahamu alipo huyu 

mtu” akawaza Bella 

 “Baada ya kumuondoa 

Mathew sasa tutamgeukia 

Festus.Lazima atafanya kila tutakachomuelekeza akifanye ! 

akaendelea kuwaza 

************ 

 Wakati Rais Festus 

akiendelea kutolewa damu 

kwa ajili ya kumuwekea 

Mathew Mulumbi,Zari na 

Ruby walikuwa katika chumba 

cha mapumziko na kila moja 

akiwa mawazoni. 

 “Mam do you need 

anything” sauti ya kiume 

ikasikika, Zari na Ruby wote 

wakainua vichwa na kumuona 

moja wa walinzi wa Rais 

akiwatazama  “No thank you” akajibu 

Zari 

 “Samahani kwa 

kuuliza.Huyu mtu ambaye 

yuko kwenye upasuaji ni nani? 

Akauliza Yule mlinzi wa 

Rais.Kabla Zari hajajibu simu 

yake ikaita .Alikuwa ni 

kiongozi wa ile timu ya wa 

wataalamu waliotumwa 

kwenda katika nyumba ya 

mchungaji Lucas kuchunguza 

kama kuna kamera za siri 

zimefungwa humo ndani 

 “Hallo Jacob” akasema 

Zari  “Mkurugenzi tumefika 

hapa mahala ulipotuelekeza 

lakini kuna tukio limetokea 

hapa” 

 “Kuna tukio gani hapo? 

 “Nyumba uliyotutuma 

inateketea kwa moto hivi sasa”

 “Inawaka moto? 

 “Ndiyo mkurugenzi.Kuna 

moto mkubwa unawaka hapa 

na tayari vikosi vya zimamoto 

na uokoaji vimekwisha fika 

vinaendelea na kazi ya kuuzima moto huu mkubwa” 

akasema Jacob 

 “Thank you Jacob.Rudini 

ofisini” akasema Zari 

 “Kuna nini? Akauliza Ruby 

 “Nimetaarifiwa na ile timu 

niliyoituma kwenda 

kuchunguza ile nyumba kama 

kuna kamera za siri ndani yake 

kuwa nyumba hiyo kwa sasa 

inawaka moto 

 “Inawaka moto? Ruby 

akauliza 

 “Ndiyo.Inawezekana 

jamaa walihisi penginetungeweza kurejea na kufanya 

uchunguzi kubaini kama kuna 

kamera za siri na wakaamua 

kuichoma moto”akasema Zari 

 “Inawezekanaje hawa 

jamaa wakawa wanafahamu 

kila tunachotaka kukifanya? 

Wamegundua kama akina 

Mathew wamekwenda 

kumuhoji mchungaji Lucas na 

wakaenda 

kumuua,wamegundua kuna 

watu wanakwenda kuchunguza 

ile nyumba kama kuna kamera 

za siri wakawahi kuichoma 

moto.Niliwahi kumueleza 

Mathew wasiwasi wangu

 kuhusianana huyu Zari .I 

don’t trust her.Haiwezekani 

kila tunapopanga mpango 

Fulani tarifa zake zinavuja na 

na jamaa wanawahi kufahamu 

kabla hatujafika.Kama Mathew 

Mulumbi akifariki I swear I’ll 

kill her ! akawaza Ruby akiwa 

amekasirika kupita kifani. 

 “Lakini kama Zari ana 

mahusiano na hawa jamaa kwa 

nini wakataka 

kumuua?Ametueleza kuwa ni 

Mathew ndiye aliyeyaokoa 

maisha yake leo kwa kumkinga 

na risasi.Hapana sina hakika 

kama Zari ana mawasiliano na hawa jamaa.Sasa wanajuaje 

mipango yetu? Akajiuliza Ruby 

na mara akaingia Rais Festus 

 “Pole mheshimiwa Rais” 

Zari na Ruby wakampa Rais 

pole 

 “Ahsanteni 

sana.Nawaomba tusichoke 

tuendelee kumuombea 

Mathew na Mungu atasikia 

maombi yetu” akasema Rais 

Festus na kuwataka walinzi 

wake waende nje wawaache 

peke yao mle ndani 

 “Mheshimiwa Rais 

tumepokea taarifa kutoka kwa wale wataalamu niliowatuma 

kwenda kufanya uchunguzi 

katika ile nyumba ya 

mchungaji Lucas kama kuna 

kamera za siri kwamba 

nyumba hiyo hivi sasa 

inateketea kwa moto” akasema 

Zari 

 “Inateketea moto? Rais 

akashangaa 

 “Ndiyo mheshimiwa 

Rais.Nyumba hiyo kwa sasa 

inateketea kwa moto” 

 “Wamejuaje kuna watu 

wanakwenda kuchunguza ile 

nyumba?” akauliza Rais Festus “Mheshimiwa Rais hata 

sisi sote tunashangaa namna 

walivyoweza kugundua kuna 

watu wetu wanakwenda hapo 

na wakaichoma nyumba moto” 

akasema Zari 

 “Hawa watu wanatumia 

nguvu za giza” akasema Rais 

Festus 

 “Kama hawatumii nguvu 

za giza katika mambo yao basi 

lazima kuna watu wao hata 

hapa SNSA ambao wanawapa 

taarifa kwa sababu 

haiwezekani tumeliamua 

jambo hili hapa halafu linawafikia hawa 

jamaa.Imenishangaza 

sana.Kuweni makini sana 

katika hili suala msiwape 

taarifa zozote watu wale 

ambao hamuwaamini.Sina 

imani kabisa hivi sasa kwani 

hawa jamaa wameweza 

kupenyeza mizizi yao sehemu 

mbali mbali” akasema Rais 

Festus na kuwataka akina 

warejee ofisini. 

 “Ladies kama 

mnavyoshuhudia wenyewe 

mambo yanavyokwenda 

wenzetu hawalali katika 

kuhakikisha wanashinda vita hii hivyo sisi pia hakuna 

kulala.Tutafanya kazi usiku na 

mchana.Ninajua mmeumizwa 

mno na tukio hili la kuumizwa 

Mathew lakini vyovyote vile 

itakavyokuwa lazima kazi 

iendelee.Hawa jamaa 

watafanya kila wawezalo 

kuturudisha nyuma lakini katu 

tusikubali kurudishwa nyuma 

na washeni hawa.Tunapaswa 

kuendelea kupambana bila 

kuchoka.Wakati madaktari 

wakiendelea na jitihada za 

kuokoa maisha ya Mathew sisi 

tuendelee na kazi”akasema 

Rais Festus  “Mheshimiwa rais tukio 

hili lililotokea ni kubwa.Kama 

si kwa Mathew Mulumbi 

kujitoa mhanga na kupigwa 

yeye risasi badala yangu hivi 

sasa ningekwisha poteza 

maisha.Utanisamehe 

mheshimiwa rais kwa sasa 

akili yangu haijakaa sawa bado 

na siwezi tena kuendelea na 

chochote hadi nitakapofahamu 

hatima ya Mathew Mulumbi” 

akasema Zari 

 “Zari please ! 

 “Utanisamehe 

mheshimiwa Rais.Kwa sasa kipaumbele kinatakwia kuwa 

ni kwa Mathew 

Mulumbi.Siwezi kupepesa 

macho kusema kwamba yeye 

ndiye kinara wetu katika 

misheni hii na siwezi kuficha 

kwamba bila yeye misheni au 

vita hii itakuwa imefika 

mwisho.Si mimi wala Ruby 

anayeweza akafanya yale 

anayoyafanya Mathew 

Mulumbi” Akasema Zari 

 “Zari is right Mr 

President.Tusimamishe kila 

kitu kwa sasa na tujielekeze 

katika kuhakikisha Mathew 

Mulumbi anapona.Lolotelinaloweza kufanyika basi 

lifanyike ili Mathew apone” 

akasema Ruby 

 “Sawa 

nimewaelewa”akasema Rais 

Festus kisha wakaenda katika 

chumba cha mapumziko 

kusubiri madaktari waweze 

kumaliza upasuaji 

 “Wanangu wanaendeleaje 

mheshimiwa Rais? Akauliza 

Ruby na Rais Festus 

akachukua muda kidogo 

kujibu halafu akasema  “Ruby kuna jambo ambalo 

sikuwa nimekueleza” akasema 

Rais na Ruby akastuka sana 

 “Kuna nini mheshimiwa 

Rais? Akauliza Ruby 

 “Kuna jambo ambalo 

sikuwa nimekueleza.Watoto 

wako hawako hapa Tanzania” 

“Hawako Tanzania? 

Akauliza Ruby kwa mshangao 

mkubwa 

“Niliwapeleka kwa Rais wa 

Rwanda ambaye ni rafiki 

yangu mkubwa” akasema Rais 

Festus  “Kwa nini mheshimiwa 

Rais ukafanya hivyo bila 

kunijulisha? 

 “Usihofu Ruby wanao 

wako salama kabisa.Sikutaka 

ijulikane kuwa wanao wako 

ikulu wangekuwa katika hatari 

zaidi ndiyo maana 

nikawahamisha kimya kimya 

kuwapeleka kwa Rais wa 

Rwanda.Ninawasiliana naye 

kila siku na wanaendelea 

vyema usiwe na hofu yoyote” 

akasema Rais Festus 

 “Mheshimiwa Rais 

hukutakiwa kufanya hivyo bila kunishirikisha kwanza 

mimi.Umenichanganya zaidi! 

Akasema Ruby 

 “Ruby ulinikabidhi watoto 

wako niwahifadhi na 

kuhakikisha wanakuwa salama 

na ndivyo 

nilivyofanya.Nimewapeleka 

mahala ambako watakuwa 

salama.Naomba uniamini 

katika hilo na watoto wako 

salama kabisa” akasema Rais 

Festus 

 “If anything happens to 

them I’ll never forgive you ! 

akasema Ruby  “Hakuna chochote 

kitakachotokea kwa wanao 

Ruby niamini” akasema rais 

Festus na ukimya ukatawala 

wote wakiendelea kutafakari 

huku wakisubiri kupata taarifa 

kutoka kwa madaktari. 

 “Mheshimiwa Rais 

unadhani kwa nini hadi sasa 

wale jamaa hawajaweza 

kuzisambaza picha zako kama 

walivyokuwa wamekusudia? 

Akauliza Zari 

 “Hata mimi nimekuwa 

najiuliza sijapata jibu ni kwa 

nini hawajasambaza zile picha zangu kama walivyokuwa 

wametishia kufanya” 

 “Unadhani wameogopa 

kufanya hivyo? 

 “Sijui kama wameogopa au 

nini kimetokea lakini 

ninachojua ni kwamba 

mapambano 

hayajakwisha.Kama 

hawajasambaza leo hata kesho 

au siku nyingine yoyote 

wanaweza wakasambaza lakini 

hata siku moja hawawezi 

kuogopa lazima tuendelee 

kupambana” akasema Rais 

Festus  “Lazima ipo sababu 

iliyowafanya hao jamaa 

wakaacha kusambaza picha 

hizo kama walivyokuwa 

wamekusudia” akasema Zari 

 “Kwa vyovyote vile 

watakavyofanya lakini 

haturudi nyuma nimekwisha 

kubali kubeba aibu ile lakini 

sintainua mikono na kukubali 

kushindwa vita” akasema Rais 

Festus 

 “Mheshimiwa Rais 

samahani kwa hiki 

nitakachouliza yawezekana ni 

jambo binafsi sana lakini kama itakupendeza unaweza 

ukanipa jibu”akasema Ruby 

 “Uliza Ruby usihofu” 

 “Wewe na Zandile 

Wepener.Ilikuaje mkaingia 

katika mahusiano? Akauliza 

Ruby “Msiniambie 

mmeanza kuchunguza 

mahusiano yangu na Zandile” 

akasema Festus 

 “Hapana mheshimiwa 

Rais hatuwezi kufanya 

hivyo.Ninahitaji tu 

kufahamu.Mimi ni mmoja wa 

watu wanaomfuatilia sana 

Zandile hasa katika mavazi na niliposikia kwamba uko naye 

katika mahusiano nilihisi hadi 

nywele zangu 

zinasisimka.Zandile ni 

mwanamke mrembo mno.How 

did you guys meet? Akauliza 

Ruby na kwa mara ya kwanza 

tangu amefika pale usiku ule 

Rais Festus akatabasamu 

 “Kuingia katika mahusiano 

na Zandile halikuwa jambo 

jepesi.Kwanza ni mwanamke 

mwenye jina kubwa 

duniani,ukiachana na utajiri 

wake sifa kubwa iliyowahi 

kumtambulisha duniani ni 

kuolewa na kuachana na mfalme wa Eswatini ndoa yao 

ikiwa na miaka miwili tu.Kama 

mnafuatilia habari 

mtakumbuka ni namna gani 

habari hiyo ilivyotawala katika 

vyombo mbali mbali vya 

habari duniani na umaarufu 

wa Zandile ukapaa 

mawinguni” akasema Rais 

Festus 

 “Ninyi ni watu wangu na 

leo nitawapa siri ila naomba 

nitakayowaeleza yabaki humu 

humu yasitoke nje” 

 “You can trust us mr 

President” akasema Ruby “Kwanza kabisa mimi na 

mke wangu kwa muda mrefu 

sasa hatuna maelewano 

mazuri.Kuna mgogoro 

mkubwa kati yetu na sitaki 

kulizungumzia 

hilo.Ninawashauri kabla ya 

kufunga ndoa kwa wale ambao 

bado,mjitafakari mara mbili 

mbili kama kweli huyo 

uliyenaye anakufaa.Ukikosea 

utateseka hadi 

kaburini.Tunaulizwa swali na 

wanaotufungisha ndoa 

kwamba Fulani bin Fulani uko 

tayari kumpoke Fulani kuwa 

mumeo au mkeo na tunajibu ndiyo.Lile neno ndiyo ni 

kubwa mno japo ni rahisi sana 

kulitamka.Kama huna uhakika 

na mtu anayekutaka mfunge 

naye ndoa tafadhali usitamke 

ndiyo.Hayo ndiyo 

tunayokutana nayo katika 

ndoa.Ni mambo 

mazito.Tukirudi katika swali 

uliloniuliza ni kwamba Zandile 

nilikutana naye nchini Afrika 

kusini katika mkutano wa 

SADC ulifanyika nchini 

humo.Wakati nikizungukia 

mabanda ya wafanya biashara 

waliofika katika mkutano huo 

kuonyesha na kutangazabiashara zao nilimkuta Zandile 

katika banda la shirika la 

hifadhi la taifa akipata taarifa 

mbalimbali kuhusiana na 

vivutio mbali mbali 

vinavyopatikana nchini 

Tanzania.Wakati huo bado 

alikuwa ni mke wa mfalme na 

akajitambulisha kwangu 

tukasalimiana akaniambia 

kwamba amefurahi sana kwa 

taarifa alizozipata katika 

banda la hifadhi za taifa na 

mimi nikatumia nafasi hiyo 

kumkaribisha sana nchini 

Tanzania na akaahidi atakuja 

kutembea.Siku moja nikapigiwa simu na 

kufahamishwa kwamba mke 

wa mfalme wa Eswatini 

anataka kuja kutembelea 

Tanzania nikaelekeza taratibu 

zifuatwe na akafika 

akapokelewa kama mke wa 

kiongozi wa nchi akatembezwa 

katika hifadhi mbali mbali na 

alifurahi sana.Aliporejea kwao 

Eswatini akanipigia simu 

akanijulisha kwamba 

ameipenda sana Tanzania na 

angependa awe na makazi yake 

hapa.Mimi nilimkubalia na 

kuahidi kumsaidia hivyo 

nikanunua jumba moja kubwa kandoni mwa bahari kwa jina 

langu na nikamtumia picha 

akalitazama akafurahi sana na 

baada ya wiki mbili akaja tena 

Tanzania lakini safari hii 

alitaka iwe ni ziara ya kimya 

kimya na asitangazwe kwani 

hakutaka watu wajue kama 

yuko Tanzania.Alifikia katika 

jumba lile nililokuwa 

nimemnunulia akalipenda 

sana.Jioni ya siku hiyo 

akanialika tukapate chakula 

cha usiku.Wakati huo tayari 

mgogoro kati yangu na mke 

wangu umepamba moto 

nikajikuta nikivutiwa sana na Zandile.Licha ya uzuri wake 

lakini ni mwanamke mwenye 

adabu nyingi,anajua kujali na 

hata kubembeleza pia mambo 

ambayo niliyakosa sana katika 

ndoa yangu.Nakumbuka 

nilimuomba tukakae nje 

tupunge upepo na mambo yote 

yalianzia siku ile” 

 “So did you uhm….did 

you…….” Ruby akataka kuuliza 

kitu 

 “Yes we did it kama una 

maanisha mapenzi.Tulifanya 

usiku ule na huo ukawa ni 

mwanzo wa mke wangu 

kuhama chumba baada 

yakugundua kwamba 

nimekutana kimwili na 

mwanamke mwingine.Mimi na 

Zandile tulitokea kupendana 

mno na akawa akija Tanzania 

mara kwa mara nadhani hiyo 

ni sababu kubwa iliyovunja 

ndoa yake na mfalme wa 

Eswatini.Hakuwahi kutamka 

hadharani sababu ya ndoa 

yake kuvunjika bali 

kilichosemwa tu ni Zandile 

kukosa uaminifu ila sababu 

kubwa ni hiyo.Baada ya 

kuachana na mume wake 

mapenzi yetu yamezidi kupamba moto na Zandi 

amekuwa akija Tanzania 

karibu kila mwisho wa 

wiki.Wanaolifahamu jambo 

hili ni watu wangu wa karibu 

sana na imekuwa ni siri kubwa 

lakini nashangaa kwa namna 

picha zile zilivyopigwa” 

akasema Rais Festus 

 “Dah ! Simulizi hii 

inasisimua sana mheshimiwa 

Rais.Mama Bella anafahamu 

kama uko na Zandile? 

 “Anafahamu kuwa niko 

katika mahusiano na 

mwanamke fulani lakini hajui kama ni Zandile.Hata kama 

akifahamu haitaharibu 

chochote katika mahusiano 

yangu na Zandi kwani 

tumekwisha kubaliana kuwa 

tuendelee kubaki kama mume 

na mke hadi pale 

nitakapokuwa nimemaliza 

muhula wangu wa urais kisha 

kila mmoja ataendelea na 

maisha yake” akasema Rais 

Festus 

 “Mheshimiwa rais kama 

mfalme wa Eswatin alifahamu 

kuhusu mahusiano yako na 

mke wake na wakaachana kwa 

sababu hiyo hudhani labda katika suala hili la picha 

anaweza kuwa anahusika? 

Akauliza Zari 

 “Sina hakika na mfalme 

Yule hana sababu ya kufanya 

hivyo.Hili jambo limefanywa 

na hawa wahuni majambazi 

wakubwa na ninaapa 

kuwasaka hadi mtu wao wa 

mwisho” 

 “Unadhani Zandile 

atalichukuliaje suala hili la 

kusambaa kwa picha zenu za 

faragha? Ruby akauliza 

 “Bado sijamfahamisha 

chochote kuhusiana na suala hili lakini itanilazimu 

kumfahamisha ili ajue 

kinachoendelea na hata kama 

picha hizi zitavuja basi awe 

akifahamu” akasema Rais 

Festus  





Nabii Kasiano alifika katika hospitaliya Mtodora ambako miili ya marehemu mchungaji Lucas na familia yake ilipelekwa.Ilikuwa imeungua vibaya sana kwa moto kiasi cha kutoweza kutambulika.Akiwa na mke wake Rita walionyeshwa miili ile ya marehemu na Kasiano akatoa machozi.Akainua mikono juu na kuomba halafu


wakarejea katika gari lao na kuondoka akamuelekeza dereva wake awapeleke katika nyumba iliyoungua ya mchungaji Lucas.Nyumba yote ilikuwa imeteketea na hakuna hata kitu kimoja kilichookolewa.Hawakukaa


sana eneo lile wakarejea nyumbani


“Lucas alikuwa bado kijana sana na ni mmoja wa wachungaji aliyekuwa anapendwa mno na watu na hata mimi nilimpenda sana.Nasikitika mwisho wake umekuwa namna hii.Sikuwahi kutegemea kabisa kama siku moja ningeyaondoa maisha ya kijana Yule.Yote haya yamesababishwa na Mathew Mulumbi.Usingizi aliolala sasa pone pone yake asiamke kwani akiamka mateso atakayoyapata ni makubwa mno.Hakutakuwa na kumkabidhi kwa jeshi la polisi nitahakikisha ninamuua mimi mwenyewe kwa mkono wangu.Hajawahi kutokea mtu aliyewahi kunisumbua mimi na mtandao wangu kama huyu jamaa.Baada ya kumuondoa nitaendelea na vita na Rais nataka apige magoti na kuinua mikono juu na hapo ndipo tutakapofanya shughuli zetu kwa amani bila kusumbuliwa na kitu chochote ! akawaza Kasiano


“Rita nimeumia sana


baada ya kuiona miili ya Lucas na familia yake.Sikutegemea kama mwishowa Lucas ungekuwa namna hii” akasema Kasiano wakiwa chumbani baada ya kuwasili nyumbani kwao


“Kasiano tumefanya mengi na tumeondoa uhai wa watu wengi pia ila kwa hili la Lucas hata mimi imeniumiza sana.Tafadhali nakuomba uhakikishe Mathew Mulumbi anapatikana kwani yeye ndiye chanzo cha haya yote yaliyotokea leo na kutulazimisha kumpoteza Yule mchungaji kijana” akasema


Rita


“Mathew Mulumbi saa zake zinahesabika.Hana muda mrefu kuanzia sasa kama bado ataendelea kuwa hai huko aliko.Nataka suala hili lifike mwisho ! akasema kwa hasira Kasiano na kunyamaza baada ya simu yake kuita walikuwa ni walinzi wake wakamjlisha kwamba kuna mgeni wake amefika,akatoka kwenda kumpokea,alikuwa ni DCI David Chamwino akamkaribisha katika sebule yake.


“Pole sana Kasiano kwa haya yaliyotokea leo” akasema David’


“Ahsante sana


David.Mambo yanazidi kubadilika kila siku lakini tunaelekea mwishoni.Vipi kwa upande wako mambo yanakwendaje?


“Kwa upande wangu mambo yanakwenda vizuri kama mlivyosikia tayari Dr Fabian amekwisha fikishwa mahakamani na kesi imeanza kusomwa.Kitu cha msingi ni kuhakikisha Mathew Mulumbi anapatikana kwani yeye ndiye


muhusika mkuu katika kesi


hii”


“Akipatikana


hatutamkabidhi kwa jeshi la polisi.We’ll kill him ! akasema Kasiano


“Tukimuondoa Mathew


kesi ya Dr Fabian haitakuwa na nguvu na anaweza akaachiwa huru”


“I don’t care lakini ninachokihitaji ni Mathew Mulumbi aondoke kabisa katika picha hii.Hawa wengine akina Fabian hawana madhara makubwa na tunaweza tukawaondoa taratibu au tukawafunga kabisa midomo yao wakabaki kimya.Kama tumeweza kumpa joto Rais wa nchi na akakiri makosa yake hadharani hatuwezi kushindwa kuwanyamazisha watu kama akina Fabian wasio na nguvu yoyote.We’re powerfull people David.Ni mtu mmoja tu ambaye anatuumiza vichwa vyetu huyu Mathew Mulumbi lakini naye hana muda mrefu”Simu ya Kasiano ikaita akajulishwa kwamba mgeni wake mwingine amewasili huyu alikuwa ni naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi Keofas Mabula.


“Ndugu zangu karibuni sana na mtanisamehe kwa kuwasumbua usiku huu ambao ni muda wa mapumziko” akasema Kasiano


“Kasiano hakuna muda wa mapumziko.Sisi muda wote tuko kazini hivyo usione kama vile umetusumbua.Sisi ni watu wako hivyo kuwa huru kutuita muda wowote na kutuhabarisha au kutupa kazi” akasema David Chamwino “Ahsanteni.Nadhani


tuendelee na kikao na wale watakaochelewa watakuta sisi tunaendelea.Nimewaiteni usiku huu kuna taarifa ninataka kuwapeni ambayo ni nzuri.Ni kwamba tumefanikiwa kujua mahala aliko Mathew Mulumbi”


“Mmefanikiwa kujua mahala aliko Mathew Mulumbi? Akauliza Keofas


“Ndiyo Keo” akajibu Kasiano na kujulishwa kwamba kuna mgeni mwigine alikuwa amewasili huyu alikuwa ni Paul Lewis.


“Karibu Paul bado hujachelewa kwani tumeanza kikao muda mfupi uliopita” akasema Kasiano


“Usiku huu nilijulishwa kuwa kwa mmoja wa wachungaji wangu kuna watu wawili wanamfanyia mahojiano kuhusiana na kifo cha mchungaji Adam.Nilijua moja kwa moja watu hao wametumwa au wana mahusiano na Mathew Mulumbi nikawaagiza vijana wangu wafike haraka sana mahala hapo na kuwaondoa wote.Vijana wamefanya kazi nzuri sana leo na walifika kwa haraka wakamuondoa Lucas familia yake na wale jamaa waliofika kumuhoji Lucas.Baadae nikapewa ushauri na Paul kuwa tuichome moto nyumba ile ili watu wasijue kama Lucas na familia yake wameuawa kwa


risasi na ndilo tukio lililotokea usiku huu.Hakuna anayefahamu kama kabla ya kuchomwa moto Lucas na familia yake tayari walikwisha uawa kwa risasi”akanyamaza kidogo


“Baadaye nikapata taarifa kutoka kwa vyanzo vyangu vya taarifa kwamba mtu aliyepigwa risasi katika nyumba ile ni Mathew Mulumbi na amepelekwa katika ofisi za SNSA ambako anapatiwa matibabu na hali yake si nzuri.Kama mtakumbuka mara ya mwisho tulipokutana niliwaeleza kuhusu mashirikiano ya Rais na idara hii ya siri.Huko ndiko aliko Mathew Mulumbi kwa sasa.Nimewaiteni hapa usiku huu kuwapeni taarifa hizo kwamba tunakaribia kufika mwisho wa vita hii hivyo tunapaswa kujipanga vizuri kuhakikisha tunaimaliza vyema vita hii na kupata ushindi.Kikubwa hapa ni kutengeneza mpango wa namna ya kuvamia SNSA na kumchukua au kumuua kabisa Mathew Mulumbi.Kama ataendelea kuwa hai baada ya upasuaji huo basi lazima ataendelea kuwepo hapo SNSA akitibiwa na hiyo ni nafasi yetu ya kuvamia mahala hapo na kumchukua” akasema Kasiano.


“Sijui niseme nini kwa mafanikio haya makubwa.Nitachinja ng’ombe na kununua mvinyo ghali kabisa pale tutakapokuwa tumefanikiwa kumuondoa huyu Mwewe” akasema Keofas


“Hawa SNSA ofisi zao ziko wapi? Akauliza David Chamwino


“Kwa maelekezo


niliyopewa ni kwamba jengo la ofisi zao liko karibu na ikulu” “Kama wako karibu na


ikulu basi eneo hilo ni eneo hatari sana.Ulinzi wa maeneo yote ya kuzunguka ikulu ni mkubwa hivyo kama kuna mpango wa kuvamia ofisi hizo kumchukua Mathew lazima tujiandae kweli kweli” akasema Paul Lewis


“Ndiyo maana wakawepo


Black Mafia.Hawa si watalii wamekuja hapa kufanya kazi na nyakati kama hizi ndipo kazi yao inapaswa kuonekana.Ndani ya kundi hilo kuna watu wengi wenye ujuzi na uwezo mkubwa kuna watu ambao ni majasusi,kuna wanajeshi kuna wataalamu wa


kila aina na hata wale waliowahi kuwa makomando nao wapo.Wanalipwa fedha nyingi sana hivyo lazima wafanye kazi tena yenye ufanisi bila kujali wanaifanyia wapi.Hata kama ingekuwa ni kwenda kumchomoa Mathew kutoka ikulu sina shaka na uwezo wa Black Mafia ! akasema Kasiano




 “Sikuwahi kuisikia idara 

hii hapo kabla na mara ya 

kwanza kuisikia ilikuwa kwako 

.Nimejaribu kufanyauchunguzi wangu na 

nimefanikiwa kumpata mtu 

ambaye amewahi kufanya kazi 

mahala hapo lakini kwa sasa 

amekwisha achana na kazi 

hiyo ana kampuni yake ya 

ulinzi.Huyu anaweza 

akatusaidia sana kufahamu 

namna jengo hilo lilivyo na 

namna ya kuweza kuingia 

humo ndani” akasema Keofas 

 “Safi sana Keo.Tunapaswa 

kumtumia mtu huyo.Fanya 

mpango wa kuonana naye kiasi 

chochote atakachokihitaji 

tutampatia”  “Vipi kuhusu zile picha za 

Rais? Mbona hazijasambazwa? 

Akauliza David na Kasiano 

akawaeleza namna ilivyokuwa 

na wote wakakubaliana na 

mawazo yale ya 

Kasiano.Wakaendelea na 

majadiliano mengine na kisha 

wakatawanyika na kuondoka. 

************ 

 Hatimaye baada ya kupita 

saa sita tangu Mathew 

aingizwe katika chumba cha pasuaji mlango wa chumba 

cha upasuaji ukafunguliwa na 

Dr Fred pamoja na madakari 

wengine waliokuwa 

wanamfanyia Mathew upasuaji 

wakatoka na wote wakaelekea 

alikokuwa Rais na akina Zari 

 “Poleni sana madaktari” 

akasema Rais Festus 

 “Ahsante mheshimiwa 

Rais” wakaitika madaktari 

wale na Rais akawaelekeza 

waketi “Mheshimiwa Rais 

upasuaji umekamilika na 

tumefanikiwa kuziondoa risasi 

zote tatu.Mbili zilipigwatumboni na moja katika 

kalio.Kwa bahati nzuri risasi 

zile hazikuweza kuleta 

madhara makubwa 

tumboni.Wote tulihofia 

kuharibiwa kwa viungo kama 

ini,uti wa mgongo nk lakini 

kote huko kulikuwa salama ila 

kilichofanya upasuaji uchukue 

muda mrefu ni kutokana na 

kuvuja kwa damu ndani ya 

mwili na tumechukua muda 

mrefu kuitafuta sehemu 

iliyokuwa ikivuja na 

tulifanikiwa kuipata na 

kuiziba.Kwa ujumla upasuaji ulikuwa na mafanikio” 

akasema Dr Fred 

 “Ninawashukuru sana Dr 

Fred na wengine wote kwa 

namna mlivyoweza kujituma 

na kufanikisha upasuaji huu 

mkubwa.Mmeokoa maisha ya 

mtu muhimu sana kwa nchi 

yetu.Ni kutokana na umuhimu 

wake ndiyo maana hata mimi 

niko hapa muda 

huu.Ninachowaomba 

madaktari muwe karibu sana 

na mgonjwa kuhakikisha 

anapata nafuu ya 

haraka.Nitaomba orodha yenu 

nyote na kesho nitamtuma msaidizi wangu awaletee kila 

mmoja tsh milioni 5 lakini 

nawaomba kitu kimoja ndugu 

zangu hiki kilichofanyika hapa 

leo kiwe siri na asitokee mtu 

yeyote akavujisha siri hii kwa 

mtu yeyote huko nje.Huyu mtu 

maisha yake yako hatarini 

sana na wanaomtafuta 

wakifahamu yuko hapa 

hawatashindwa kuja kuvamia 

mahala hapa na 

kumuua.Tumeelewana ndugu 

zangu? Akauliza Rais na 

madaktari wakamuitikia 

 “Nashukuru sana kwa 

kunielewa.Je ninaweza kuruhusiwa kwenda 

kumtazama mgonjwa kwa 

sasa? Najua hawezi 

kuzungumza lakini nataka 

nimuone sura yake tu 

inatosha.Ni mtu wangu wa 

muhimu sana” akasema Rais 

Festus akavalishwa mavazi 

maalum na kupelekwa katika 

chumba alimo Mathew 

Mulumbi.Alikuwa 

amezungukwa na mashine 

nyingi zilizokuwa 

zimeunganishwa katika mwili 

wake kwa ajili ya kumsaidia. 

 “Pona haraka Mathew.Kila 

kitu kimesimama.Vita imesimama tunakusubiri 

wewe.Pona haraka shujaa 

wangu uje umalizie kazi 

uliyokwisha ianza” akasema 

Rais Festus kisha akatoka mle 

ndani 

 “Zari vipi kuhusu ulinzi wa 

mahali hapa? 

 “Ulinzi ni wa uhakika sana 

mheshimiwa Rais’ 

 “Good.Kama mkihitaji 

ulinzi zaidi nijulishe nami 

nitaleta walinzi zaidi” 

 “Hakuna haja mheshimiwa 

Rais ulinzi ni wa uhakika sana hapa” akasema Zari 

wakamsindikiza Rais hadi 

katika gari lake akaondoka 

kurejea ikulu. 

 Baada ya Rais kuondoka 

Zari akaomba kuingia katika 

chumba alimo Mathew 

Mulumbi,alipoziona mashine 

zile zilizonganishwa mwilini 

mwa Mathew machozi 

yakaanza kumtoka 

 “Why you Mathew 

MulumBi? Why now? Akauliza 

Zari huku akilia 

 “Niliwahi kukuuliza kwa 

nini huogopi kufa ukanipa jibu ambalo mpaka leo siwezi 

kulisahau.Nimekufahamu siku 

chache zilizopita lakini nakiri 

sijawahi kukutana na mtu wa 

pekee kama wewe.Mathew 

nashindwa nikuelezeaje .Nina 

deni kubwa kwako Mathew 

tafadhali nakuomba amka 

haraka ili nikulipe deni hili 

ambalo hakuna kiasi cha fedha 

kinachoweza kutosha 

kulilipa.Get well quick Mathew 

Mulumbi” akasema Zari na 

kushindwa kuendelea kukaa 

mle chumbani akatoka akilia. 

 “Kwa leo sintakwenda 

kumtazama Mathew ninaweza nikapoteza fahamu” akasema 

Ruby kisha wakaenda ofisini 

kwa Zari. 

 “Zari kuna kitu nimekuwa 

nakiwaza” 

 “Kitu gani Ruby? 

 “Upasuaji aliofanyiwa 

Mathew ni mkubwa na 

anaweza akachukua siku 

kadhaa ktandani.Kwa 

ninavyomfahamu Mathew 

akipata nafuu tu anaweza 

akataka kuendelea na kazi kitu 

ambacho ni hatari sana kwa 

afya yake”  “Kwa hilo nakubaliana 

nawe Ruby.Mathew hata 

akifanikiwa kuamka sasa hivi 

anaweza akataka kwenda 

kazini.Nini ushauri wako 

katika hilo? Akauliza Zari 

 “Ushauri wangu ni 

kwamba hatuwezi kuendelea 

kumsubiri Mathew hadi 

atakapopona kwani hawa 

tunaowatafuta hawana muda 

wa kusubiri wao kila sekunde 

kila dakika kila saa kila siku 

wako vitani kuhakikisha 

wanaondoa vikwazo vyote 

katika biashara zao hivyo 

lazima mapambano yaendelee.Kuna mtu anaitwa 

Nawal” 

 “Nawal ? akauliza Zari 

 “Ndiyo.Huyu ni rafiki yake 

Mathew amewahi kufanya kazi 

CIA na kwa sasa anafanya 

biashara.Ni mtu ambaye 

tunaweza kumtumia katika 

operesheni hii wakati Mathew 

akiwa kitandani.Nawal ni mtu 

jasiri sana na nimewahi 

kushiriki naye katika misheni 

Fulani” akasema Ruby 

 “Yuko wapi huyo Nawal? 

Akauliza Zari  “Kwa sasa anaishi nchini 

Saudi Arabia.Amekwisha 

achana na masuala ya ujasusi 

na anafanya biashara lakini 

nikimueleza kuhusu Mathew 

atakuja hata usiku huu huu 

kama ataweza” 

 “Una mawasiliano yake? 

 “Ndiyo nina mawasiliano 

yake” 

 “Tafadhali wasiliana naye 

kama anaweza akaja haraka 

itakuwa vyema sana 

tukasaidiana katika 

mapambano haya” “Nawal ni mwanamke 

mwenye ujasiri mkubwa kama 

Mathew naamini anaweza 

akawa na msaada mkubwa 

kwetu” Ruby akastuka baada 

ya mlio wa ujumbe mfupi 

kusikika.Akaitoa katika mkoba 

wake na kuonyesha mshangao. 

 “Ni mara ya pili leo 

kitendo hiki kinafanyika cha 

kuwasha simu yangu wakati 

nimeizima” akasema Ruby 

 “Yawezekana ina hitilafu” 

 “Hapana haina hitilafu 

y0yote.Hii hufanywa na 

wabobezi katika teknolojia.Unaweza ukaiwasha 

simu ya mtu hata ukiwa mbali 

au ukawasha kamera na 

kumpiga picha akiwa 

hafahamu ukiifahamu 

teknolojia unaweza ukacheza 

nayo utakavyo” akasema Ruby 

na kuufungua ujumbe 

ulioingia 

 “Zero again ! akasema 

Ruby 

 “Anasemaje Zero? 

Akauliza Zari na sura ya Ruby 

ikabadilika baada ya kuusoma 

ujumbe aliotumiwa “Kuna nini Ruby? Akauliza 

Zari na Ruby akampa ujumbe 

ule ausome 

“They’re coming for 

him.Take him out of there ! 

 “Tayari wamefahamu 

Mathew yuko hapa ! akasema 

Ruby 

 “How ? akauliza Zari 

 “I don’t know how” 

akasema Ruby 

 “What are we going to do? 

Akauliza Zari 

 “Alituma ujumbe akinitaka 

niondoke pale nyumbanikwako na kweli watu wakaja 

kuvamia.Hata katika hili 

nalazimika kumuamini.Hivi 

sasa watakuwa wanajiandaa 

kuja hapa kummaliza Mathew”

 “Ruby kwanza tujiulize 

imewezekanaje watu hawa 

wakapata taarifa zetu na 

kufahamu mahala alipo 

Mathew? Bila kutafuta na 

kufahamu ni namna gani 

wanapata taarifa zetu bado 

Mathew atakuwa katika hatari” 

akasema Zari  “KItu cha kwanza ni 

kumuondoa Mathew mahala 

hapa” akasema Ruby na simu 

ikaita Zari akaipokea. 

 “Ruby tunatakiwa haraka 

sana.Hali ya Mathew 

imebadilika ghafla! Akasema 

Zari kisha wakatoka mbio 

kuelekea hospitali 



Katika chumba cha mikutano ndani ya jengo zilimo ofisi za Black Mafia,Paul Lewis alikutana na viongozi wenzake wa kundi hilo hatari kabisa baada ya kutoka katika kikao cha dharura nyumbani kwa nabii Kasiano


“Nimetoka katika kikao cha dharura usiku huu kwa mkuu.Kuna habari njema” akasema Paul


“Mathew amepatikana” akasema Paul na nyuso zote ndani ya kile chumba cha mikutano zikatabasamu.


“Hizo ni habari njema sana.Amepatikana wapi? Akauliza John Mkizi


“Katika tukio la usiku huu nyumbani kwa mchungaji Lucas alikuwemo pia Mathew Mulumbi na ni mmoja wa watu waliojeruhiwa.Kwa sasa anapatiwa matibabu katika ofisi za SNSA nasikia wana hospitali yao hapo hapo katika


jengo lao na hali yake si nzuri.Kuna uwezekano anaweza akapotea hata maisha”akasema Paul na kunyamaza kidogo


“Baada ya kufahamu mahala alipo Mathew sasa tunaanza kuandaa mpango wa namna ya kuweza kuingia ndani ya jengo hilo na kumchukua.Ninasubiri kupata taarifa na ramni za jengo hilo la idara ya siri ya usalama wa ndani wa nchi lakini wakati tunaendelea kusubiri tuanze kujiandaa kwani itakuwa ni misheni kubwa kwasababu tunaamini jengo hilo lina ulinzi wa kutosha mbaya zaidi haliko mbali sana na ikulu na


kama mnavyofahamu eneo lile lote la karibu na ikulu lina ulinzi mkali hivo tunatakiwa kuandaa mpango kabambe kabisa wa kutuwezesha


kuingia ndani ya jengo hilo na kuondoka na Mathew Mulumbi au kummaliza akiwa humo humo ndani” akasema Paul na mawazo mbali mbali yakaanza kutolewa kuhusu namna ya kuweza kuingia katika jengo la SNSA kumchukua Mathew




************


Gari la naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi mheshimiwa Keofas Mabula lilisimama nje ya geti la nyumba iliyozungushiwa ukuta mfupi na juu yake kukawa na uzio wa vyuma.Alifika mahala hapo baada ya kutoka nyumbani kwa nabii Kasiano walikokuwa na kikao cha dharura.Mlinzi wa nyumba ile aliyekuwa ameshika mbwa mkubwa akalisogelea gari na kabla hajalifikia simu yake ikaita akaipokea na kupewa maelekezo ya kufungua geti akalifungua haraka haraka gari la naibu waziri likaingia ndani.Katika kibaraza alikuwepo jamaa mmoja mnene wastani akiwa amevalia fulana na kaptura .Keofas akashuka garini na kumfuata Yule jamaa wakasalimiana halafu wakaeleka ndani


“Mheshimiwa naibu waziri umenistua ulivyosema unakuja kwangu usiku huu” akasema Yule jamaa


“Martin nimelazimka kuja hapa kwako usiku na samahani kwa usumbufu”


“Bila samahani karibu sana” akasema Martin


“Nina shida ndugu yangu nimekuja nataka unisaidie” “Shida gani mheshimiwa?


“Wewe uliwahi kufanya kazi SNSA naamini utakuwa unalifahamu vyema jengo lote namna lilivyokaa na njia zote hata zile za siri za kuingilia ndani ya jengo hilo”akasema Keofas


“Mheshimiwa, mimi


nilikuwa mlinzi wa nje na mara chache niliingia ndani kwenda kuonana na mkurugenzi hivyo kwa kiasi kikubwa mambo ya ndani ya jengo lile siyafahamu sana.Kuna nini mheshimiwa naibu waziri unakitafuta ndani ya jengo hilo?akauliza Martin


“Kuna mtu muhimu


anashikiliwa hapo SNSA bila kosa lolote ndiyo maana nataka nitume vijana wangu wakamchomoe kabla hawajaanza kumtesa” akasema Keofas


“Ouh kama ni hivyo basi kuna mtu ambaye kama ukifanikiwa kumpata angeweza kukusaidia sana.Anaitwa Frank Kangole.Huyu amewahi kufanya kazi SNSA kwa muda mrefu na ni mtu ambaye nina uhakika mkubwa sana anaweza akakusaidia katika hilo jambo”


“Nitampataje huyo Frank? Akauliza Keofas


“Kwa sasa Frank hayuko tena SNSA amefungwa katika gereza la siri.Alifanya kosa kubwa aliwasaidia majambazi kuingia na kupora mamilioni benki kwa kutumia mfumo wa SNSA”


“Gereza la siri?! Keofas akashangaa


“Ndiyo.Hufahamu kama kuna gereza la siri?


“Hapana.Ni mara ya kwanza ninasikia kutoka kwako kwamba Tanzania kuna gereza la siri.Liko wapi hilo gereza? Nani wanafungwa huko?Akauliza Keofas.


“Mheshimiwa naibu waziri unanishangaza kwa


kutokufahamu uwepo wa


gereza hilo la siri wakati wewe uko katika wizara ya mambo ya ndani ambayo mnahusika na magereza yote yaliyoko hapa nchini” akasema Martin


“Martin ni kweli sifahamu uwepo wa gereza hilo la siri.Katika wizara yetu hatuna magereza ya siri ndiyo maana hilo unalolisema limenishangaza kidogo.Liko wapi hilo gereza?


“Hata mimi sifahamu


lilipo hilo gereza la siri lakini ukitafuta mahala lilipo huwezi kushindwa kulipata.Nakuhakikishia mheshimiwa naibu waziri kama ukimpata huyo jamaa anaweza akakupa taarifa nyingi za kuhusu SNSA na anaweza hata akakusaidia kumtoa huyo mtu wako.Tumia nafasi yako kulitafuta hilo gereza na ukilipata onana na huyo jamaa atakusaidia”akasema Martin




“Ninashukuru Martin kwa ushauri wako utanisaidia sana” akasema Keofas na kuagana na Martin akaondoka.


“Ni mara ya kwanza ninasikia kuhusu uwepo wa gereza la siri.Nani anasimamia gereza hilo ni SNSA? Nani wanafungwa huko? Akajiuliza Keofas akiwa garini


Baada ya kutoka nyumbani kwa Martin alielekea moja kwa moja nyumbani kwake na kitu cha kwanza alichokifanya baada ya kufika nyumbani kwake ni kumpigia simu nabii Kasiano


“Keofas kuna habari gani? Akauliza Kasiano


“Nimetoka kuonana na Martin Yule jamaa nilikwambia amewahi kufanya kazi ya ulinzi SNSA”


“Ndiyo kuna chochote umekipata toka kwake? Akauliza Kasiano


“Martin amenieleza kwamba kwa kiasi kikubwa kazi zake zilikuwa ni ulinzi wa nje lakini amenielekeza kwa mtu anaitwa Frank Kangole ambaye amewahi kufanya kazi SNSA ila kwa sasa amefungwa katika gereza la siri.Umewahi kusikia kuhusu uwepo wa gereza hilo la siri hapa nchini?Keofas akauliza


“Hapana sijawahi kusikia uwepo wa gereza hilo”


“Basi huko ndiko alikofungwa huyo Frank ambaye kama tukimpata atatusaidia sana katika mpango wetu wa kuingia SNSA na kumchomoa Mathew Mulumbi” akasema Keofas


“Kama kweli lipo hilo gereza basi hakuna tatizo tutalitafuta na kulifahamu mahala lilipo.Nakuhakikishia Keofas tutalipata hilo gereza” akasema Kasiano na kuagana na Keofas


“Gereza la siri.Liko wapi hapa nchini? Nisiumize kichwa sana ngoja niwasiliane na Bella yeye anaweza akatusaidia kutafuta kujua kuhusu uwepo wa gereza hilo,anafahamu mambo mengi sana ya nchi


hii” akawaza Kasiano na kumpigia simu Bella


“Kasiano unasemaje?


Akauliza Bella ambaye tayari alikuwa usingizini na kuamka baada ya simu yake kuita


“Mama Bella samahani kwa usumbufu nimekupigia kuomba msaada kuna mahala tumegonga kisiki na tunahitaji msaada wako”


“Nini mnahitaji


Kasiano?akauliza Bella


“Bado tunaendelea kutengeneza mpango namna ya kuingia SNSA,kuna mtu amewahi kufanya kazi katika idara hiyo anaitwa Frank Kangole ambaye amefungwa katika gereza la siri.Hapo ndipo tumekwama mama ni mara yangu ya kwanza kusikia uwepo wa gereza hilo la siri.Tunahitaji msaada wako ili tuweze kumpata huyo mtu” akasema Kasiano “Umesema gereza la siri?


“Ndiyo mama”


“Mhh ! hata mimi sijawahi kusikia kitu kama hicho.Ngoja nipige simu mbili tatu nitafute taarifa nitakupigia tena baadae kama nitakuwa nimepata chochote” akasema Bella na kukata simu akainuka na kukaa kitandani


“Huyu Mathew Mulumbi


ambaye anatufanya tushindwe kulala usingizi ninaapa lazima apatikane” akawaza Bella na kuzitafuta namba za Yeremia Mwaipopo mkuu wa jeshi la polisi akampigia


“Mama Bella”akasema


Yeremia


“Yeremia samahani kwa usumbufu usiku huu.Kuna kitu nataka unisaidie”


“Ndiyo mama Bella


nikusaidie nini?Kuna taarifa zozote umezipata kuhusu Mathew? Akauliza Yeremia huku akiinuka kitandani na kutoka chumbani


“Tayari tumefahamu Mathew yuko SNSA na anapatiwa matibabu hapo baada ya kujeruhiwa kwa risasi usiku huu.Hata Festus alikwenda huko usiku huu kumjulia hali”


“Safi sana.Nini mipango ya kumpata baada ya kufahamu mahala alipo?


“Tunaendelea na mipango ya kutuma waingie humo SNSA wamchukue Mathew Mulumbi tumkabidhi kwa hao jamaa na mambo yamalizike”akasema Bella


“Bella nina vijana mahiri kabisa ndani ya jeshi la polisi ambao ninaweza kuwatumia kwenda kumchukua Mathew Mulumbi kama yupo SNSA”


“Hilo ni jambo la hatari sana Yeremia.Hatutaki kulihusisha jeshi la polisi katika mpango huu.Tutatafuta vijana wengine ambao wataweza kuingia humo ndani ya SNSA na kumchukua Mathew


Mulumbi.Nimekupigia kukuuliza kama unafahamu uwepo wa gereza la siri hapa nchini” akasema Bella


“Gereza la siri? Akauliza Yeremia huku akiinuka na kutoka chumbani “Ndiyo.Una taarifa zake?


“Nimewahi kulisikia hilo


gereza lakini liko chini ya idara ya kupambana na kudhibiti ugaidi.Gereza hilo ni maalum kwa ajili ya kuwafunga magaidi na watu wengine hatari kwa nchi”akasema Yeremia


“Kuna mtu anashikiliwa katika gereza hilo ambaye anaweza akasaidia katika mpango huo.Unadhani nani ninaweza kuzungumza naye akanisaidia? Akauliza Bella


“Zungumza na mkurugenzi wa idara ya kupambana na


ugaidi anaitwa Asajile Mlabwa.Yeye anaweza akakusaidia sana katika hilo” akasema Yeremia


“Nakushukuru sana Yeremia”


“Bella nashauri wakati unazungumza na Asajile tuwe wote ili suala hilo liwe na uzito mkubwa” akasema Yeremia


“Sawa Yeremia ninaomba mawasiliano yake huyo Asajie


ili niwasiliane naye na


kumuomba kuonana naye asubuhi” akasema Bella na kukata simu.Baada ya muda Yeremia akamtumia Bella namba za simu za Asajile Mlabwa mkurugenzi wa idara ya kupambana na ugaidi Bella hakuchelewa akampigia simu


“Hallow” ikasema sauti ya upande wa pili baada ya simu kupokelewa


“Mkurugenzi Asajile habari za usiku huu”


“Nzuri


kabisa.Nazungumza na nani?


“Mimi ni Bella mke wa Rais”


“Mama Bella?! Asajile akashangaa


“Ndiyo Asajile.Samahani kwa kukuamsha usiku huu.Nina mazungumzo nawe nataka tuonane kesho”


“Hakuna tatizo mama


Bella.Unataka nikufuate ikulu?


“Hapana.Nitakuelekeza mahala tutakapokutana” “Sawa mama Bella”


“Ahsante sana Asajile usiku mwema”akasema Bella na kukata simu


“Sikutaka jambo hili lihusishe watu wengi lakini kadiri muda unavyozidi kwenda tunajikuta tukilazimika kuogeza watu katika mtandao huu.Huyu Asajile imekuaje mpaka leo hii hajaingia katika mtandao wangu? Anatakiwa awepo katika mtandao wangu huyu mtu anaonekana ni mtu muhimu mwenye msaada” akawaza Bella na kujlaza kitandani




Zari na Ruby walifika kwa haraka katika chumba


alimokuwa amelazwa Mathew “Nini kimetokea? Zari akamuuliza mmoja wa wauguzi aliyekuwa anakimbia kuingia katika chumba alimo Mathew


“Mkurugenzi tunawaomba msubiri kwanza hapo nje” akasema Yule muuguzi na kuufunga mlango akina Zari wakabaki nje


“Mungu wangu nini kimetokea humo ndani? Akauliza Ruby midomo ikimtetemeka


“I can’t stay here.I’m going in ! akasema Zari na kuufungua mlango akaingia ndani na kuwakuta madaktari wakiwa katika heka heka za khakikisha hali ya Mathew inakaa sawa.Zari na Bella wakakaa pembeni na kuwaacha madaktari wafanye kazi yao.


Baada ya dakika kumi na tano hali ya Mathew ikawa vizuri


“Mkurugenzi usihofu mgonjwa anaendelea vizuri.Kulitokea tatizo kidogo lakini tumelitatua na sasa anaendelea vyema.Msiwe na hofu yoyote tunafanya kila tuwezalo kuhakikisha mgonjwa anapona” Dr Fred akawaeleza akina Zari


“Ahsante sana Dr Fred,tulipata wasiwasi mkubwa” wakajibu Zari na Ruby kisha wakatoka mle ndani.


“Nahisi mwili unaishiwa nguvu kabisa” akasema Zari


“JItahidi Zari huu si wakati wa kuishiwa nguvu.Mathew anatutegemea sana kwa wakati huu”akasema


Ruby


“Tunafanya nini kuhusiana na ule ujumbe wa Ziro? Akauliza Zari


“Ujumbe ule si wa kupuuza.Lazima wamekwisha fahamu mahala alipo Mathew Mulumbi na wanajiandaa kuja mahala hapa kummaliza”


“Wamejuaje kama Mathew


yuko hapa?Zari akauliza


“Hakuna anayejua lakini kitu kikubwa kwa sasa ni kuanza mipango ya kumuondoa Mathew mahala hapa”akasema Ruby


“Itabidi tupate ushauri wa daktari kama itafaa


kumuhamisha Mathew katika


hali hii”


“Zari hatuna namna lazima tumuondoe Mathew hapa” akasema Ruby


“Ruby hali ya Mathew ni kama unavyoiona amefanyiwa upasuaji mkubwa na anahitaji uangalizi mkubwa wa madaktari.Tazama muda mfupi tu uliopita kumetokea tatizo katika mfumo wake wa upumuaji hivyo hatuwezi kumuondoa hapa kwa haraka kama unavyotaka.Bado anahitaji kuwepo hapa hadi tutakapohakikisha amepata unafuu mkubwa”akasema Zari


“Zari wewe mwenyewe umesoma ujumbe uliotumwa na Ziro hawa watu tayari wamejua Mathew yuko hapa lazima watakuja hapa.Unataka Mathew auawe? Akauliza Ruby


“Sina maana hiyo Ruby lakini hatuwezi kuwaogopa watu hao na kuhatarisha maisha ya Mathew Mulumbi.Tunao ulinzi wa kutosha mahala hapa.Wewe umewahi kuwa mkurugenzi wa hapa na unafahamu ulinzi wa jengo hili ulivyo.Ulinzi hapa ni mkubwa sana,ukiacha walinzi tulionao waliosambaa katika kila kona kuna silaha kali zimewekwa sehemu mbali mbali za hili jengo ambazo zinaendeshwa kielektroniki.Silaha hizo zimefichwa na watu hao watakaovamia jengo letu hawajui zilipo hivyo basi kama wakijidanganya wavamie hapa tutawamaliza kama wadudu.Hili ni jengo hatari kabisa kuthubutu kuvamia.Nakuomba Ruby usiwe na wasi wasi Mathew atakuwa salama.Tusubiri kwanza apate nafuu halafu tutamuondoa hapa kumpeleka sehemu salama zaidi” akasema Zari


“Sawa Zari” akajibu Ruby


“Nina maswali mengi kuhusu huyu Ziro ni nani hasa? Umekwisha jaribu kumtafuta na kujua ni nani? Akauliza Zari


“Simfahamu huyu Ziro ni nani lakini ninachofahamu yuko katika mtandao wa hawa jamaa tunaowatafuta Black mafia”akajibu Ruby


“Kama yuko katika mtandao wao iweje basi anatusaidia kwa kutupa taarifa zao?Ni wazi ni mtu ambaye anakufahamu hasa wewe na kila pale kunapokuwa na


mpango wowote wameupanga dhidi yako anakupa taarifa mapema ili uchukue tahadhari”akasema Zari


“Hata mimi ninashindwa kuelewa kwa nini anatusaidia? Ninachohisi huyu mtu atakuwa ana mahusiano na sisi na huko aliko he or she’s undercover” akasema Ruby


“Huyu mtu lazima atakuwa anakulinda sana wewe kwa sababu hakuna mwingine ambaye amewahi kumtumia ujumbe wa tadhari zaidi yako.Think


Ruby.Tunaweza tukafanikiwa kumfahamu ni nani huyu mtu” akasema Zari


“Hawa ni watu


wanaotumia teknolojia ya hali ya juu kuhakikisha hawajulikani ni akina nani lakini iko siku atajitokeza tu au ataacha mwanya tutamfahamu ni nani.Kwa sasa tujielekeze kwa Mathew,huyu Ziro kama yuko upande wetu basi ataendelea kutupa taarifa kila pale tunapokuwa katika hatari.” akasema Ruby


“Ulinieleza kuna mtu unaweza ukawasiliana naye akafika kuja kutusaidia.Kama una mawasiliano naye huyo mtu wasiliana naye tafadhali ili aje mara moja.Tunahitaji msaada” akasema Zari


“Ahsante kwa kunikumbusha” akasema Ruby na kufungua sehemu anakohifadhi namba za watu akatafuta namba ya simu ya Nawal akapiga


“Ruby ! akasema Nawal baada ya kupokea simu


“Nawal habari za usiku huu?


“Nzuri kabisa.Vipi maendeleo yako?


“Sisi huku mambo si mazuri ndiyo maana nimekupigia usiku huu”


“Kuna nini Ruby ? Nawal akauliza


“Mathew yuko katika hatari kubwa”


“Mathew?Yuko Tanzania? Akauliza Nawal


“Ndiyo amerejea Tanzania lakini amekutana na matatizo makubwa na muda mfupi uliopita ametoka kufanyiwa upasuaji baada ya kupigwa risasi”


“Mathew amepigwa risasi?


“Ndiyo Nawal”


“Nani kafanya tukio hilo?


“Sikiliza Nawal ninakuomba uje Dar es salaam tunahitaji sana msaada wako.Kuna mambo mazito yanayoendelea hapa.Utakapofika nitakueleza kwa kirefu sana kile kinachoendelea hapa”


“Kuja hapo nitakuja Ruby.Gosu Gosu naye anaendeleaje?Uko naye hapo karibu?


“Gosu Gosu naye alipatwa na matatizo.Amefungwa kifungo cha maisha gerezani”


“Kifungo cha maisha? Nawal akashangaa


“Ndiyo Nawal.Amefungwa kifungo cha maisha.Nawal utakapokuja huku nitakueleza kila kitu kilichotokea”


“Ruby umenistua


sana.Kwa kuwa Rais aliyepita alinipatia uraia wa Tanzania basi sintapata tatizo lolote kuingia hapo nchini.Kesho nitakuja Dar es salaam”


“Nashukuru


Nawal.Utakapoanza safari utanijulisha” akasema Ruby wakaagana.


“Amekubali na atafika hapa nchini kesho”Ruby akamjulisha Zari


“Itakuwa vizuri sana akifika ili aendelee pale ambapo ameishia Mathew.Unadhani kuna ulazima wa kumjulisha Rais kuhusu jambo hilo? Akauliza Zari


“Kuna kitu nataka nishauri.Kuanzia sasa tusimshirikishe Rais katika mipango yetu hasa ya kuhusiana na Mathew Mulumbi” akasema Ruby na


Zari akashangaa


“Kwa nini


Ruby?Humuamini Rais?


“Sina tatizo na Rais ila tatizo langu liko kwa watu wanaomzunguka.Tukirejea


katika lile sakata la picha zake za faragha hata yeye mwenye Rais amekiri hafahamu ni namna gani picha hizo zimepigwa kwa sababu kwanza mahusiano yake na Zandile ni ya siri kubwa na wanaofahamu jambo hili ni watu wachache sana tena watu wake wa karibu.Nahisi miongoni mwa watu wake hao wa karibu yupo mtu anayetumiwa na hawa jamaa na ndiyo maana wanapata siri zote za


Rais.Tukimfahamisha kuhusu Mathew na kama kuna mtu wake wa karibu anaweza akafuatilia na kufahamu mahala tutakakompeleka na hawa jamaa watapata taarifa.Tutakuwa watu wa kuhama hama mpaka lini? Ninashauri tuanze kufanya mambo yetu kwa siri sana bila kushirikisha watu wengi akiwemo Rais”


“Ni vipi kama akigundua tumefanya mambo bila kumshirikisha? Atakasirika sana” akasema Zari


“Atakasirika ndiyo lakini tutamueleza ukweli kwa nini tumefanya hivyo tulivyofanya” akasema Ruby


“Kwa nini tusimueleze wakati huu?akauliza Zari


“Zari that’s not a good idea.Tukimueleza Rais kwamba tunamuhamisha Mathew Mulumbi lazima atataka kufahamu mahala tunakompeleka na anaweza akataka kwenda kumtembelea kujua maendeleo yake na huko hatakwenda peke yake kwani kila aendako Rais huongozana na walinzi na wasaidizi wake na kama miongoni mwao yupo mmoja ambaye atakuwa ana mahusiano na hao jamaa tunaowatafuta basi atapeleka taarifa kwao na maisha ya Mathew yatakuwa mashakani.Ninashauri tuwe majasiri katika jambo hili na kama akituuliza Mathew amepelekwa wapi tutamjibu yuko sehemu salama na tutamueleza sababu kwa nini hatukumshirikisha” akasema Ruby


“Ruby nashauri


tumshirikishe Rais katika suala hili.Nitakwenda mimi ikulu na kuzungumza naye atatuelewa.Isitoshe ni yeye ambaye tutamuomba atusaidie kupata makazi salama kwa ajili ya Mathew” akasema Zari wakaendelea kujadiliana na kukubaliana na wazo lile la Zari


Kitu cha kwanza


alichokifanya Rais Festus baada ya kufumbua macho saa kumi na mbili kasoro dakika saba asubuhi ni kuchukua simu na kumpigia Zari


“Zari nataka nijue maendeleo ya Mathew Mulumbi” akasema Rais Festus


“Mathew Mulumbi


anaendelea vizuri mheshimiwa Rais.Alizinduka na madaktari wamekuwa wakifuatilia kwa karibu sana maendeleo yake.Mpaka sasa hali yake


inaendelea vizuri”akajibu Zari




“Ahsante kwa taarifa hii nzuri.Tafadhali msiondoke hapo SNSA hakikisha Mathew anapata matibabu ya hali ya juu nataka apone haraka akaendelee na shughuli yake ya kuwasaka hawa mashetani ! Nikipata wasaa ninaweza kuja kumjulia hali hapo baadae”


“Hakuna haja mheshimiwa


Rais,sisi tuko hapa na kama kuna tatizo lote litatokea tutakujulisha haraka sana.Halafu mheshimiwa Rais ninataka kuja kuonana nawe baadae kuna masuala nataka kuzungumza nawe”akasema


Zari


“Nashukuru


Zari.Tutaonana hiyo baadaye” akasema Rais Festus na kukata simu


“Maendeleo mazuri ya Mathew Mulumbi ndicho kitu pekee nilichohitaji kukisikia asubuhi hii” akawaza huku akiinuka kitandani na kujinyoosha halafu akakumbuka kitu akachukua simu na kumpigia mkurugenzi wake wa habari


“Shikamoo mheshimiwa


rais”


“Marahaba.Gidion


umepitia magazeti ya leo tayari? Hakuna taarifa yoyote mbaya? Akauliza Festus


“Mheshimiwa Rais tayari ninayo magazeti yote ya leo na kubwa lililoandikwa ni lile suala lako la mtoto wa nje.Ukiacha hilo hakuna habari yako nyingine” “Ahsante Gidion” akajibu Rais Festus ambaye kwa kawaida yeye si mpenzi sana wa kusoma magazeti.


“Kwa nini wale jamaa hadi asubuhi hii hawajasambaza picha zangu? Wameogopa au kuna kitu gani kinaendelea? Akawaza na kuchukua tena simu akazitafuta namba za katibu mkuu profesa Simon akampigia simu ikaanza kuita


“Afadhali leo simu yake inaita nilikwisha anza kupata wasiwasi”


“Mheshimiwa Rais” akasema profesa Simon “Mzee Simba shikamoo”


“Marahaba.Unaendeleaje?




“Nimekutafuta sana jana hukuwa unapatikana simuni kuna tatizo gani lilikupata?


“Simu yangu ilipata matatizo kidogo mheshimiwa Rais”


“Tayari nilikwisha anza kuingiwa na hofu”


“Usihofu mheshimiwa


Rais ni matatizo madogo tu” “Sawa mzee


Simba.Ninataka kufahamu kama wale jamaa waliwasiliana nawe tena siku ya jana.Nimeshangaa kwa nini mpaka sasa hawaja sambaza zile picha kama walivyokuwa wamekusudia endapo nisingetimiza madai yao”


“Mheshimiwa Rais hata mimi ninashangaa kwa nini hawajasambaza.Nilidhani labda umekubali madai yao”


“Hapana siwezi kukubaliana nao kabisa.Msimamo wangu haubadiliki mzee Simba”


“Nini basi nini kimetokea hadi wakashindwa kusambaza picha?akauliza profesa Simon


“Hujawasiliana nao



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog