Search This Blog

Friday 7 April 2023

I WAS WRONG | NILIKOSEA - 5

  


Simulizi : I Was Wrong | Nilikosea 

Sehemu Ya Tano (5)


nimekuchelewesha” akasema Paulie  “ Hapana Pauline.” Akajibu Grace 

wakaelekea moja kwa moja hadi katika 

mlango wa chumba cha Pauline 

 “ Nnahisi haja ndogo inataka 

kunitoka kwa namna ninavyoogopa kwa 

kile kinachokwenda kutokea humu ndani 

kama Fred hatakuwa amewahi 

kutoka.Help me Lord” Akawaza Pauline na 

kukinyonga kitasa cha mlango 

ukafunguka. 

 “ Karibu ndani Grace.” Pauline 

akamkaribsha Grace ndani.Akapata nguvu 

baada ya kutomuona Alfred mle 

chumbani.Akashusha pumzi 

 “ Thank you Lord..!! akashukuru 

kimya kimya 

 “ Wow ! Chumba chako kizuri sana 

Pauline.Hii hoteli nimeipenda sana.” 

Akasema Grace na kuketi sofani.Pauline 

akammiminia mvinyo katika glasi na 

kumpatia.Kabla ya kuanza kuywa Grace 

akaomba aelekezwe mlango wa 

choo,akaingia chooni na baada ya muda 

akatoka wakaendelea na maongezi. 

 “ Pauline nakupongeza sana kwa 

uamuzi wako wa kubaki hapa Moshi na 

kufungua mradi ule mkubwa.Umefanya 

maamuzi yenye kufaa .Licha ya kwamba 

utatengeneza faida lakini utasaidia watu wengi kwa upande wa vipimo” akasema 

Grace 

 “ Ahsante sana Grace.Anayepaswa 

kushukuriwa sana ni Alfred ambaye 

alinipa wazo hili la kuanzisha mradi 

huu.i”akasema Pauline huku akitoa 

tabasamu kubwa. 

 Waliendelea na maongezi na baada 

ya kama dakika kumi na tano hivi,Grace 

akaaga Pauline akamsindikiza hadi 

mahala alikoegesha gari akaondoka 

 “ Ahsante Mungu kwa kunisaidia 

katika suala hili gumu.Leo nilikuwa 

ninaumbuka .Nashukuru kwa kupata wazo 

lile la kumpigia simu Fred na kumtaka 

aondoke.Dah ! siamini kabisa kama suala 

hili limekwisha salama .Sina hamu na kitu 

kingine chochote nataka nikajifungie 

nilale mwili wote bado unanitetemeka” 

akawaza Pauline na kurejea chumbani 

kwake akajitupa kitandani 

 “ Nina uhakika mkubwa kwamba 

Grace tayari amekwisha hisi kitu kuhusu 

mimi na mume wake na ujio wake wa 

ghafla haukuwa wa bure.Alikuja kutafuta 

ushahidi.Ninahisi alimfuata mumewe 

nyuma nyuma ili kufahamu anaelekea 

wapi.Aliposema kwamba anataka 

akakifahamu chumba changu alikuwa na uhakika kabisa kwamba Fred yuko 

chumbani.Dah ! mwili wote bado 

unanitetemeka.I have to put an end to this 

relationship with Alfred .Yule ni mume wa 

mtu na tayari mke wake amekwisha anza 

kuwa na wasi wasi.Yawezekana Fred 

ameonyesha mabadiliko makubwa na 

ndiyo maana mke wake amestuka na 

kutakakujua kinachoendelea.Sitaki tena 

kuendelea na ujinga huu tunaofanya.Mke 

wa Fred tayari ameanza kuteseka kwa 

sababu yangu.Ndoa yake inaanza 

kutetereka kwa sababu yangu.Hapana 

siwezi kukubali jambo hili liendelee.Leo ni 

mwisho wangu na Fred..” akawaza Pauline 

na kumimina mvinyo katika glasi. 

 “ Ouh Fred ! Fred ! tayari umeniingia 

katika mishipa ya damu yangu .Nilikuja 

Moshi nikiyakimbia mapenzi lakini huku 

nako nimejikuta nikianguka tena 

mapenzini.What am I going to do ? 

akajiuliza Pauline na kunywa mvinyo wote 

uliokuwemo katika glasi na mara mlango 

ukagongwa ,akainuka na kwenda 

kuufungua . 

 “ Alfred !!!..” akasema Pauline kwa 

mshangao 

 “ I’m back my love” akasema Alfred 

huku akitabasamu  “ Fred please go home to your wife” 

akasema Pauline 

 “ Pauline I’m sorry kwa kukuweka 

katika wasi wasi.Nimerudi kwa sababu 

moja tu kuja kuangalia kama hakukuwa na 

matatizo yoyote huku nyuma” akasema 

Alfred 

 “ Everything was fine Alfred” 

 “Ouh thank you Lord” akasema 

Alfred 

 “ Fred what we’re doing is not 

right.We have to stop this immediately 

.Mke wako tayari amekwisha anza kuhisi 

kwamba kuna kitu kinaendelea baina 

yetu.Tafadhali Fred naomba tuachane na 

huu mchezo.Leo hii alikuja hapa akiwa na 

uhakika kabisa kwamba uko hapa kwangu 

na akanitaka nimlete chumbani kwangu 

apajue nikashindwa kukataa kwani kama 

ningekataa angejua lazima kuna kitu 

kinaendelea.Nilihisi kutokwa na haja 

ndogo.Sijawahi kutetemeka na kuogopa 

kama nilivyoogopa leo.Alfred I beg you let 

us stop this” akasema Pauline.Alfred 

akamsogelea Pauline akamshika mkono 

na kusema 

 “ Pauline my love please don’t say 

that.You know how much I love you my 

angel.Kwako nimechanghanyikiwa na sielewi wala sintasikia la mtu 

yeyote.Pauline hatuwezi kuuvunja urafiki 

wetu.We love each other so 

much.Kilichotokea leo ni taa ya kutuonya 

kwamba tuwe makini lakini si kuuvunja 

uhusiano wetu.Pauline I’m not ready to 

end this relationship .Ninakupenda kiasi 

ambacho siwezi kukueleza kwa hiyo sahau 

kabisa mimi kuachana nawe.Nimenja asali 

sasa ninataka nichonge mzinga 

kabisa.Lakini nakuahidi nitakuwa 

muangalifu sana ili nisije nikakuweka 

katika matatizo.Yawezekana kuna mahala 

niliteleza na kusababisha mke wangu 

akawa na wasi wasi.I promise you it won’t 

happen again.Nitajitahidi sana kujizuia 

nisionyeshe mabadiliko yoyote yale ili 

kumfanya Grace asistuke na sisi tuendelea 

na mambo yetu kama kawaida.” Akasema 

Alfred 

 “ Why are you doing this to your 

wife? Akauliza Pauline 

 “ pauline ni kwa sababu 

ninakupenda sana.kwa mke wangu 

ninapata kila kitu lakini moyo wangu 

umekupenda na nimeshindwa 

kujizuia.Usinielwe vibaya si kwamba nina 

tamaa ama vipi lakini imenitokea tu .”  “ Ouh Fred ! sijui umenipa nini.Yaani 

nikiuona tu akili yangu inahama kabisa na 

kila nilichokuwa nakiwaza kinapotea.” 

Akasema Pauline 

 “ Come here my love” akasema 

Alfred na kumvuta Pauline karibu yake 

akamkumbatia na kumbusu. 

 “ I love you Pauline so much.” 

Akasema Fred na kumbusu Pauline 

 “ I love you too Alfred,I love you so 

much” 

 “ Jumamosi hii nitakupeleka 

Arusha.” 

 “ No ! Fred No ! You don’t have to do 

that” 

 “ Usiogope Pauline nitakupeleka 

Arusha. I want to spend time with you 

there” 

 “ Fred hapana.Mke wako atakustukia 

na itakuwa mbaya kwetu.tayari 

nimekwisha mwambia kwamba 

ninakwenda Arusha jumamosi hii akisikia 

na wewe pia unakwenda huko basi 

atafahamu kabisa kwamba tunaongozana ” 

 “ Pauline naomba tusiweke mjadala 

katika jambo hili.Nitakupeleka 

Arusha.Please dont say no !” akasema 

Alfred.Pauline akajikuta hana uwezo wa 

kumkatalia Alfred.  “ Sijui Alferd amenipa nini kiasi cha 

kushindwa kumkatalia jambo lolote 

atakaloniambia.Muda mfupi uliopita 

nilikuwa nawaza kuachana naye lakini 

sasa hivi sitaki hata aondoke .Nini hiki 

kinanitokea jamani? Akajiulzia Pauline 

akiwa amekilaza kichwa chake kifuani 

kwa Alfred .




 “ I’m not crazy ! with my own eyes I 

saw Alfred going in that hotel.Hata gari 

lake nililikuta maegesho.Ni wazi kabisa 

Alfred alikuwa amekwenda kwa Pauline 

.lakini kwa nini sikumkuta chumbani kwa 

Pauline? Akajiuliza Grace akiwa njiani 

kuelekea nyumbani kwake baada ya 

kutoka hotelini kwa Pauline 

 “ Lazima kuna kitu kinaendelea kati 

ya Pauline na mume wangu.Alfred 

amebadilika sana tofauti na 

ninavyomfahamu.hakuwa na tabia ya 

kuondoka bila kuaga nanimemfuatili 

nikamuona kabisa anaingia ndani yahoteli 

ile anamoishi Pauline .Nina hakika kabsa 

alikwenda kuonana na Pauline..Ouh my gosh I’m confused !..” akaendelea kuwaza 

Grace. 

 “ Kuna kitu 

nimekumbuka.Nilipoingia mle chumbani 

kwa Pauline nilikuta kuna chupa ya 

mvinyo na glasi mbili na zote zilikuwa na 

mvinyo ndani yake.Inaonekana muda 

mfupi uliopita kabla ya mimi kuingia 

alikuwa na mgeni wanakunywa.nahis 

mgeni huyo anaweza kuwa ni mume 

wangu.Lakini kama alikuwa na 

mumewangu mbona sikumkuta mle 

chumbani? Alijificha wapi? Niliingia hadi 

chooni lakini hakuwemo.Na je kama 

hakuwa kwa Pauline alikuwa wapi? .Garce 

akaendelea kujuliza maswali mengi 

akakosa majibu.Akafika nyumbani kwake 

na kukaa sebuleni akitazama filamu lakini 

akili yote ilikuwa kwa Pauline. 

 “ Kuna kitu nimekumbuka.Wakati 

tunapanda kwenda chumbani kwa Pauline 

ghafla akasimama na kuniambia kwamba 

nimsubiri akachukue kinywaji cha 

kusindikiza maongezi yetu.lakini 

nilipofika chumbanibkwake nikashangaa 

kwa kuzikuta chupa tatu za mvinyo 

mezani.Kama kulikuwa na mvinyo 

chumbani kwa nini basi akachukue chupa 

nyingine? Akajiuliza Grace.  “ Ninahis kwamba Pauline alirejea 

kaunta kwa lengo la kumtaarifu Alfred 

kwamba niko pale hotelini na yeye 

aondoke mara moja.Nakubaliana kabisa 

na jambo kwamba inawezekana Fred 

alitahadharishwa aondoke mara moja mle 

chumbani.Ouh sasa nimeanza kupata 

picha .” Akatabasamu 

 “ huu ndio mchezo 

walionichezea.Nilijiuliza sana kwamba 

Fred alijificha wapi? Kumbe aliwahi 

kutoka kabla sijafika mle 

chumbani.Ninakubaliana na hili kwa 

sababu wakati ninaondoka gari lake 

halikuwepo tena pale maegesho,he was 

already gone.Ouh Alfred kitu gani 

kimekupelekea ukanifanyia hivi? 

Akawaza Grace na kuumia sana moyoni 

 “ lakini ngoja niendelee kuwafuatilia 

kwa siri .Nitafahamu tu kamakuna kitu 

kinaendelea .Nisiendelee kujiumiza kwa 

sasa bila ya kuwa na ushahidi wa 

kutosha.kama ni kweli mume wangu 

ananisaliti basi iko siku ukweli 

utajulikana tu.wanasema siku za mwizi ni 

arobaini iko siku arobaini yao 

itafika.Nitaumia sana kama nikigundua 

kweli mume wangu amenisaliti .I’ll never 

forgive him for that” akawaza Grace na kuendelea kutazama filamu.Kichwa chake 

kilijaa mawazo mengi sana. 

 Saa tano na dakika tatu kengele ya 

getini ikalia kuashiria kulikuwa na 

mtu,akainuka na kwenda kuchungulia ni 

nani aliyekuwa anagonga akaliona gari la 

mume wake. 

 “ He’s back”akamfungulia geti Fred 

akaliingiza gari ndani 

 “ bado hujalala? Akauliza Fred.Sauti 

yake ilionyesha wasi wasi kwa mbali 

 “ Nitalalaje bila ya kuhakikisha 

umerudi salama mume wangu? 

Ulipoondoka hukuniambia unaelekea 

wapi kwa hiyo siwezi kulala kabla 

hujarejea nyumbani ili nihakikishe kama 

uko salama” 

 “ Ahsante sana Grace.Sorry 

niliondoka ghafla bila kuaga.Sikutegemea 

kama ningechukua muda mrefu ” akasema 

Alfred na kumbusu mke wake. 

 “ Ulikwenda hospitali? Akauliza 

Grace 

 “ Kuna mgonjwa ambaye nilikwenda 

kumtembelea lakini kabla ya kwenda 

huko kwa mgonjwa nilipita kwanza 

hotelini kwa Pauline .Nilitaka kujua 

maendeleo ya mradi kwani nina siku tatu 

sijakwenda kuutembelea mradi wake.Baada ya hapo nikaenda kumtazama 

mgonjwa.” 

 “ Anaendeleaje Pauline?akauliza 

Grace 

 “ Anaendela vizuri sana na mradi 

wake unaendelea vizuri pia ukarabati 

unakaribia kumalizika na kinachobaki ni 

kuagiza vifaa tu” akasema Fred. 

 “ Amekubali kweli alikwenda 

kuonana na Pauline.Yawezekana labda ni 

kwa sababu ya kumpenda sana.Alfred 

ndiyo maana ninaona wivu kwa ukaribu 

alio nao na Pauline.Yawezekana hakuna 

chochote kinachoendelea kati yao zaidi 

yya urafiki wa kawaida .Lakini hata hivyo 

ninapaswa kujiridhisha kwamba hakuna 

kitu kinachoendelea baina 

yao.Nitaendelea kuwafuatilia.” akawaza 

Grace. 

*********************** 

Wingi wa kazi alizokuwa nazo uliifanya 

siku yake kuwa fupi sana. Saa kumi na 

moja na dakika arobaini ukaingia ujumbe 

mfupi katika simu yake uliotoka kwa Safia. 

 “ Tukutane saa moja za jioni baa 

mpya inaitwa Kemi bar ipo Kimandolu.” David akausoma ujumbe ule kisha 

akaiweka sehemu mezani akaendelea na 

shughuli zake.Ilipotimu saa kumi na mbili 

na nusu za jioni akafunga ofisi na kutoka 

kuelekea sehemu walikopanga waonane 

na Safia. 

 “ Huyu Safia anataka kunieleza 

jambo gani ? Akajiuliza akiwa garini 

kuelekea Kimandolu. 

 “ Sijawahi kumuona hata mara moja 

na nina hakika ni Vicky aliyempa taarifa 

zangu.Au yawezekana anataka kunieleza 

kitu kuhusiana na kinachoendelea kati 

yangu na Vicky” akaendelea kujiuliza 

David. 

 “ katika maisha yangu kitu kikubwa 

ambacho nitakijutia siku zote ni kitendo 

cha kukubali kutembea na mke wa mzee 

Zakaria.Hiki ni kitendo kibaya sana na 

kinaninyima amani kunifanya nishindwe 

hata kumtazama mzee Yule 

machoni.Ananilea na kuniamini kama 

mwanae na badala yake nimeingiwa na 

tamaa na nikakubali kuingia katika mtego 

wa Vicky.Ninakijutia mno kitendo 

hiki”akapunguza kidogo mwendo wa gari 

 “ kwa kuwa nimelifahamu kosa langu 

ninachotakiwia kukifanya si kuendelea 

kufanya mchezo huu wa kijinga.Ninatakiwa kuachana kabisa na 

Vicky madhahabu.Potelea mbali 

litakalotokea na litokee tu lakini sina 

namna zaidi ya kuachana naye haraka 

sana.kwa namna alivyoniganda Yule 

mwanamke najua haitakuwa kazi rahisi 

lakini lazima niwe na msmamo na 

nisimamie maamuzi yangu.” Akawaza 

David 

 Saa moja na dakika kumi na nne 

akawasili Kimandolu katika baa mpya 

aliyoelekezwa na Safia.Akatafuta kiti na 

kuketi akaagiza kinywaji akaendelea 

kunywa wakati akimsubiri Safia. 

 ‘” Sijawahi kuonana na Safia na sijui 

kama hata yeye ananifahamu.Lakini 

atakapofika lazima atanipigia simu” 

Akawaza David na baada ya kama dakika 

mbili hivi mwanake mnene wastani 

akatokea na kumfuata David pale mezani 

 “ hello David”akasema yule 

mwanamke bila wasi wasi na ilionekana 

kabisa alikuwa akimfahamu vyema David 

 “ hallow “ akajibu David kwani 

hakuwa akimfahamu yule mwanamke 

 “ Natumai hatujawahi kuonana hata 

mara mpja.Naitwa Safia”akasema yule 

mwanamke  “ Ouh Safia.Karibu sana.Ni kweli 

hatujawahi kuonana lakini nimeshangaa 

umenifahamu vipi? Akauliza David 

 “ Mimi ninakufahamu vizuri David “ 

akasema Safia 

 “Nimefurahi sana kukutana nawe 

jioni hii.Maisha yanakwendaje? Akauliza 

David 

 “maisha yanakwena vizuri.Kila kitu 

kinakwena vizuri sana.” Akasema 

Safia.Muhudumu akafika na kuwahudumia 

na kisha wakaendelea na maongezi 

 “Nilistushwa kidogo na mwito wako 

wa dharura nikaahirisha shughuli zangu 

zote za jioni ya leo nikaitika 

mwito”akasema David 

 “ Ninashukuru sana David kwa 

kukubali ombi langu na samahani pia kwa 

kuvuruga ratiba yako lakini suala 

nililokuitia hapa ni suala zito na kama 

lisingekuwa na uzito katu 

nisingekusumbua”akasema safia. 

 “ Ndiyo na kusikiliza Safia” akasema 

David.Safia akanywa juice halafu 

akatazama huku na huko kama kuna 

yeyote anayewasikia kisha akasema 

 “ Mimi na Vicky ni marafiki wakubwa 

na urafiki wetu umeanza toka tukiwa 

shule.Baadae mwenzangu alifanikiwa kuolewa na mzee Zakaria na maisha yake 

yakadilika.Pamoja na maisha yake kuwa 

mazuri lakini bado hajanitupa.Amekuwa 

akinipatia misaada mingi na 

ameniwezesha sana kufika hapa nilipofika 

.Hata mradi nilionao sasa hivi ni yeye 

alinikopesha pesa .Siwezi kusema mambo 

yote aliyonisaidia,kwani ni mengi sana.” 

Akanyamaza kidogo akameza mate na 

kuendelea 

 “ Kwa muda mrefu nimekuwa ni 

mshauri wake mkubwa katika mambo 

yake mengi na nimekuwa ni msiri wake 

pia.Jambo lolote ambalo hawezi 

kumweleza mtu mwingine yeyote 

hunieleza mimi kwa hiyo ninayafahamu 

mambo yake mengi sana..” akanyamaza 

kidogo na kuendelea 

 “ pamoja na kuwa mshauri wake wa 

kila jambo analotaka kulifanya lakini kuna 

mambo mengine ambayo sikubaliani naye 

na ndiyo maana nimekuita hapa ili 

kukueleza kuhusu suala moja kubwa 

ambalo sijakubaliana naye” 

 “ Ndiyo nakusikilza safia” akasema 

David akiwa na hamu ya kutaka kusikia 

kile ambacho safia anataka 

kumwambia.Moyoni alihisi lazima litakuwa ni suala la mahusiano yake na 

Vicky 

 “ najua baada ya kukueleza suala hili 

mimi na Vicky urafiki wetu utafikia 

mwisho na tutageuka maadui wakubwa 

lakini ni bora kuwa maadui kuliko 

kushiriki katika jambo kama hili.” 

 “ Ni jambo gani hilo Safia? Akauliza 

David 

 “ kwanza kabisa naomba niikuweke 

wazi kwamba Vicky aliolewa na mzee 

Zakaria kwa kufuata pesa na mali na si 

kwamba ana mapenzi ya dhati na Yule 

mzee.Baada ya mzee Zakaria kuanza 

kusumbuliwia na maradhi ,tabia ya Vicky 

ikabadilika sana.Alianza kubadilisha 

wanaume kwa kisingizio kwamba mzee 

Zakaria hana tena nguvu na uwezo wa 

kumridhisha .Baada ya kuruka ruka na 

wanaume mbali mbali hatimaye ukatokea 

na mkaanzisha mahusiano.Hakuna mtu 

mwingine anayefahamu kuhusu 

mahusiano yenu zaidi yangu.Kutokea 

kwako kumembadilisha kabisa 

Vicky.David umemchanganya kabisa rafiki 

yangu Vicky.Sijawahi kuona Vicky akiwa 

amechanganyikwia namna hii na 

mwanaume kama ilivyotokea 

kwako.Ninamfahamu vizuri kuliko mtu yeyote Yule na ninapokwambia kwamba 

amechanganyikiwa kwa jili yako 

ninamaanisha kweli kachanganyikiwa na 

hasikii la mtu juu yako.”akasema safia 

akanyamaza kidogo . David akasema 

“ Safia ni kweli nilijikuta nikiingia 

katika mapenzi na Vicky lakini najilaumu 

sana kwa kitendo kile cha kumzunguka 

mzee Zakaria ambaye ananipenda na 

kuniamini sana.Hata hivyo ninataka 

nisitishe kabisa hiki tunachokifanya 

kwani si kitu kizuri hata kidogo” akasena 

David. 

“ David si kwamba nakulaumu kwa 

ulichokifanya kwa sababu najua haikuwa 

ridhaa yako wewe kuingia katika 

mahusiano na Vicky.Ninamfahamu Vicky 

alivyo hata kama ungekataa angefanya 

kila namna kuhakikisha anakupata.Ni 

wanaume wengi tu wamekwisha nasa 

katika mitego yake.Hata hivyo sijawahi 

kuona akidata kwa mwanaume kama 

ilivyotokea kwako.” Akanyamaza tena 

kisha akasema 

“ Siku moja Vicky alinifuata 

akanichukua akanipeleka mahala kwa 

ajili ya maongezi.Aliniambia jambo 

ambalo sikuwa nimelitegemea kama 

nitakuja kulisikia likitoka katika mdomo wake.Mpaka leo siamini ni shetani gani 

amemkumba Vicky na kumfanya awe 

namna hii” akasema safia 

 “ alikueleza jambo gani? akauliza 

david 

 “ Alinieleza kwamba …” Safia akasita 

kusema 

 “ Alikueleza nini safia? Akauliza 

David 

 “ Alinieleza kwamba ..kutokana na 

ugonjwa unaomsumbua mzee Zakaria 

ameishiwa kabisa nguvu za kiume na 

hawezi tena kumridhisha.Akanieleza 

namna ulivyomchanganya kwa penzi la 

kiwango cha juu unalompatia.Akaniambia 

kwamba anatamani awe nawe kila 

wakati,anatamani muishi pamoja kama 

mume namke ..” 

 “ What ?!! david akashangaa 

 “Subiri kwanza niendelee david” 

akasema safia 

 “ Vicky akasema kwamba anatamani 

sana kama angeachana na mzee Zakaria 

na akaishi na wewe lakini hilo 

haliwezekani kwa sababu yuko katika 

ndoa na mzee zakaria na akisema aondoke 

kimya kimya basi ataukosa utajri mkubwa 

wa mzee zakaria kwa hiyo akaja na 

uamuzi .”  “Aliamua kitu gani? Akauliza David 

 “Alisema kwamba anataka mpango 

ambao utamuwezesha yeye kuupata 

utajiri wa mzee Zakaria na papo hapo 

wewe na yeey muishi kama mume na mke 

kwa hiyo akaona njia pekee ni kumuua 

mzee Zakaria” akasema Safia. Badala ya 

kushangaa David akacheka kidogo 

 “ Safia thata not true.NInamfahamu 

Vicky japokwa ni kwa muda mfupi lakini 

sina hakika kama anaweza akafikia hatua 

hiyo ya kumuua mzee Zakaria” akasema 

David 

 “ David ninachokueleza ni kitu cha 

kweli kabisa .Ninamfahamu Vicky zaidi ya 

unavyomfahamu wewe kwa hiyo 

ninachokueleza ni kitu cha kweli na wala 

si jambo la kufanyia masihara hata 

kidogo.Vicky amedhamiria kumuua mzee 

Zakaria na mipango tayari imekwisha 

fanyika kinachosubiriwa ni utekelezaji 

tu.Hakuna mtu mwingine anayelifahamu 

suala hili zaidi yangu na nimekueleza kwa 

kuwa nafsi yangu inanisuta na 

sikubalianai hata kidogo na kitu 

anachotaka kukifanya huyu rafiki yangu.” 

 “ Oh mungu wangu ! akasema David 

 “ kwa hiyo amepanga kumuua vipi 

mzee Zakaria? Kwa sumu? Akauliza david  “ Tayari amekwisha ongea na mtu 

mmoja anaitwa Chino ambaye ni jambazi 

mkubwa .Wamepanga kwamba tukio hilo 

lifanyike siku ya jumapili kuanzia saa nne 

za usiku.Chino na kundi lake watavamia 

nyumba ya mzee Zakaria na kumpiga 

risasi.Itaonekana kama ni tukio la 

ujambazi.Baada ya hapo Vicky atarithi kila 

kitu na atakuwa huru kuishi maisha yake 

akiwa na wewe” akasema Safia. 

 David akainama akazama katika 

mawazo mengi . 

 “ David ! akaita Safia na kumstua 

kutoka mawazoni 

 “ Nimekuita hapa nikueleze kuhusu 

jambo hili ili kwa pamoja tuweze kuzuia 

lisitokee.Tumzuie Vicky asiweze kufanya 

jambo hili baya.” 

 “ Safia ahsante sana kwa kunieleza 

jambo hili kubwa na zito.Najua haikuwa 

rahsi kwako kumsaliti rafiki yako na 

kuvujisha siri hii.Vicky ameingiwa na 

shetani gani hadi akafikia hatu hii ya 

kutaka kumuua Yule mzee? Sikufichi Safia 

sijawahi kuona mwanamke ambaye 

anatunzwa na kupatiwa kila 

anachokihitaji kama Vicky.Lakini pamoja 

na hayo bado hatosheki anamuibia mzee 

Zakaria pesa nyingi sana na mwishowe amefikia hatua ya kutaka kumuua..Dah ! 

Nimestuka sana.”’ 

 “ Ndiyo hivyo ilivyo David.” 

 “ Safia hapa nilipo kichwa changu 

kinanizunguka na sijui nifanye 

nini.Ninaomba uniache kwanza 

nikapumzishe akili yangu na halafu 

nitakupigia simu kesho kukueleza nini 

ufanye .” akasema David 

 “ David kumbuka hii ni siri kubwa 

sana na asifahamu mtu mwingine yeyote 

Yule na wala Vicky asifahamu chochote 

kama tayari unafahamu kuhusu mpango 

wake”akasema Safia 

 “ Usijali safia nitajtahidi sana 

kulifanya siri jambo hili na hatafahamu 

mtu yeyote” akasema David 

 Baada ya maongezi kidogo david 

akaondoka kwa makubaliano ya kuonana 

tena kesho yake 

 “ Nimestushwa sana na jambo 

alilonieleza Safia.Vicky ni shetani na hana 

kabisa roho ya ubinadamu.Kumuua 

mumeo wa ndoa ili arithi mali ! Dah ! 

inashangaza sana.Nimekuwa nikisikia 

mambo haya katika simulzi na sikuwahi 

kuhisi kama siku moja ninaweza 

kulishuhudia suala hili .” akawaza David 

akiwa ndani ya gari  “ Sasa nimepata picha.lazima 

atakuwa ni Vicky aliyemshawishi mzee 

Zakaria kwamba amuandikishe kisheria 

kama msimamizi wa mali zake 

zote.Kumbe alikuwa na nia yake lakini 

sasa ataumbuka.Mipango yake yote 

haitafanikiwa.Utajiri anaoutafuta hata 

kwa kumwaga damu hataupata kamwe. 

Nitahakikisha mpango huu haufanikiwi 

kwa namna yoyote ile.Ni bora nife mimi 

kuliko afe Yule mzee.I will save him. I need 

to find Pauline immediately .” Akawaza 

david na kuchukua simu yake akazitafuta 

namba za simu za Pauline akapiga lakini 

simu haikuwa ikipatikana. 

 “ Amezima kabisa simu.hata kama 

hatakuwepo nitahakikisha mpango huu 

wa Vicky haufanikiwi.mwisho wake 

umefika.Ni wakati sasa wa kulipiza kisasi 

kwa kila ovu alilomfanyia Zakaria na 

familia yake. Nilikuwa ninatafuta sana 

namna ya kuweza kuachana naye na sasa 

kila kitu kimejileta chenyewe.This is the 

end of Vicky Madhahabu….”akawaza 

David. 

“ Sijawahi kuwa na usiku mrefu kama huu 

katika maisha yangu.” Akawaza David na 

kuinuka kitandani akatazama saa 

yake.Ilikuwa ni saa nane za usiku lakini bado hakuwa amepata usingizi.Kichwa 

chake kilijaa mawazo mengi sana. 

 “ Natafakari lakini ninashindwa 

kupata jibu kwa nini utoe uhai wa 

binadamu mwenzako kwa sababu ya mali? 

Ama kweli binadamu wamegeuka wakatili 

kuliko hata wanyama 

mwitu.Ukimuangalia Vicky na mambo 

anayoyafanya katu huwezi kuamini.Lakini 

arobaini yake imekaribia sana.” 

 David akaichukua simu yake 

akazitafuta namba za Pauline akapiga 

lakini bado ya simu ya Pauline haikuwa 

ikipatikana. 

 “ yawezekana hataki tena 

mawasiliano na mtu yeyote ndiyo maana 

ameamua kuizima kabisa simu yake.Au 

atakuwa amebadili hata namba yake ya 

simu ili aweze kusahau kabisa 

kilichotokea.Pauline ni mtu muhimu sana 

ambaye ninatakiwa kumpata.Anatakiwa 

kufahamu kile kinachoendelea hapa 

nyumbani kwao.” 

 Baada ya kutafakari sana David 

akaamua kumuandikia ujumbe ili kama 

ikitokea akawasha simuyake aupate.. 

 “ Hata kama bado ana hasira na mimi 

natunai akiupata ujumbe huu lazima 

atanipigia simu.Huu si wakati wa kulumbana ni wakatiw a kuweka tofauti 

zetu pembeni ” akawaza David na kujilaza 

kitandani na mara kumbu kumbu Fulani 

ile ambayo humtesa sana pindi 

akiikumbuka ikamjia kichwani 

 “ Ninapoondoka hapa leo hii mimi si 

baba yako na wala sikutambui kama 

mwanangu.Ukimaliza kifungo chako usitie 

mguu nyumbani kwangu .Nikikuona 

nyumbani kwangu nitakuchapa risasi.” 

 Maneno haya yakajirudia kichwani 

kwa David 

 “ Ouh No! nitafanya nini ili niweze 

kulisahau kabisa tukio lile? Limekuwa 

likinitesa kila mara.Sitaki kukumbuka 

kabisa siku ile ambayo baba yangu 

alinitamkia maneno yale nikiwa gerezani.” 

Akainuka na kukaa.Machozi 

yakamdondoka 

 “ kwa nini baba yangu anichukie 

namna ile na kunitamkia maneno yale 

makali ? Alipandikizwa chuki mbaya sana 

kiasi cha kunichukia kiasi kile.Anyway 

someday I’ll be back home and I will save 

my father.I will show him that he was 

wrong about me..” Akawaza David **************** 

 Saa mbili za asubuhi Tino alikwisha 

amka .Haikuwa kawaida yake kuamka 

asubuhi namna hii. 

 “ Kaamka asubuhi asubuhi lazima 

kuna mahala anakwenda.Leo lazima 

niufahamu ukweli” akawaza Vivian 

akimtazama mumewe akivaa halafu 

wakaenda kunywa chai pamoja 

 “ Nitachelewa kurudi Leo na 

yawezekana nisirudi kabisa.” akasema 

Tino. Viviana akamtazama na kuuliza 

 “ Tino whats going on? Mbona siku 

hizi umebadilika kasi hiki? Akauliza 

 “ Nimebadilika nini Vivian? 

 “ Hukuwa namna hii.Ulikuwa 

unaniamabia kila kitu ,kama una 

tatizo,kama una safari lakini kwa hivi sasa 

mambo yamekuwa tofauti 

kabisa.Hunielezi chochote na hata kama 

una tatizo linabaki kuwa ni siri yako.Mimi 

ni mkeo na ndiye mtu wako wa karibu 

kabisa kwa hiyo ni haki yangu kujua kama 

una tatizo ama vipi.Unaniambia tu 

kwamba utachelewa kurudi au waweza 

usirudi kabisa na huniambii unakwenda 

wapi na kwa nini usirudi.Tafadhali Tino 

kama kuna tatizo naomba unieleze kuliko kuendelea kuniweka katika wakati 

mgumu kiasi hiki” akasema Vivian.Tino 

akamalizia chai katika kikombe chake 

akanyakua funguo zake akaelekea katika 

gari lake akaingia na kuondoka.Vivian 

naye akainuka na kukimbi a chumbani 

kwake akachukua funguo ya gari lake na 

kutoka akaanza kumfuata mume wake. 

 “ Leo lazima nitafahamu kila 

kitu.Nitamfuatilia kila mahala anakoenda 

“ akawaza Vivian akiendelea kumfuatilia 

mume wake kwa makini 

 Kituo cha kwanza cha Tino baada ya 

kutoka nyumbani ilikuwa ni dukani 

kwake.Akashuka garini na kuingia 

dukani.Vivian alisimamisha gari umbali 

wa kama mita mia mbili hivi halafu 

akashuka na kutembea hadi katika baa 

moja iliyoko karibu na duka la Tino 

ijulikanayo kama Lasana Bar.Pale 

panaegeshwa taksi bubu nyingi,akachagua 

taksi moja ambayo ingemfaa kwa shughuli 

yake akaingia na kisha taksi ile ikaenda 

kuegesha si mbali sana na dukani kwa 

Tino. 

 “ Dada kuna mtu tunamsubiri? 

Akauliza dereva taksi 

 “ Kuna mtu tunahitaji kumfuatilia.” 

Akajibu Vivian.  Baada ya dakika thelathini toka Tino 

aingie dukani akatoka na kuingia katika 

gari lake akaondoka. 

 “ Tulifuate lile gari”akasema Vivian 

 “ Yule ni papaa Tino magari 

“akasema Yule dereva taksi 

 “ Ni mume wangu.usiogope 

Mfuate.Lakini kuwa makini sana 

asigundue kama anafuatiliwa” akasema 

Vivian 

 “ Wewe kumbe ndiye mke wake?!! 

Yule dereva akashangaa sana 

 “ kwani vipi? Sifai kuwa make wake? 

 “ Unafaa sana shangazi nilihitaji tu 

kufahamu” akasema Yule dereva taksi na 

kuendelea kumfuata Tino. 

 Tino aliikamata barabara kuu ya 

Arusha Moshi huku Vivian na Yule dereva 

taksi wakiendelea kumfuata kwa nyuma 

bila ya yeye kuwa na habari kama 

anafuatiliwa. 

 Safari iliendelea hadi wakafika Usa 

river na Tino hakuonyesha dalili zozoteza 

kusimama . 

 “ Huku anakwenda wapi? Ni lazima 

mwanamke wake atakuwa huku..au 

amepanga akutane na mwanamke huku 

mbali ili wasionekane” akawaza Vivian  Hatimaye wakafika Bomang’ombe na 

Tino akapunguza mwendo na kukata 

kushoto.. 

 “ Anaelekea nyumbani kwao.Hii ni 

njia inayoyoeleka nyumbani kwa wazazi 

wake.Mbona hakuniambia kama 

anakwenda nyumbani kwao? Ama kweli 

Tino amebadilika sana.Lakini nijambo 

zuri kama anakwenda kwao ili 

tukakutane kwa wazazi wake niwaeleze 

tabia ya mtoto wao.Yawezekana tukapata 

suluhu .” akawaza Vivy na kumuelekeza 

dereva aendelee kumfuatilia Tino. 

 Kama alivyokuwa amehisi ndivyo 

ilivyokuwa.Tino alikuwa anaelekea 

nyumbani kwa wazazi wake wanaoishi 

Bomang’ombe. 

 Vivian akamlipa dereva dereva pesa 

yake halafu akashuka garini na kwenda 

kugonga geti.Aliyefungua ni mdogo wake 

Tino ambaye alifurahi sana kuonana na 

Vivian 

 “ Ouh wifi !!akasema Yule mdogo 

wake Tino wakakumbatiana 

 “ karibu sana wifi yangu..Kwema 

huko Arusha?akauliza 

 “ Arusha kwema kabisa haika” 

 “ Karibu sana Wifi 

yangu.Umeongozana na kaka naye amewasili muda si mrefu .” akasema Haika 

na kumshika mkono wifi yake wakaelekea 

sebuleni. 

 “ Vivian ?!!..Tino akashangaa baada 

ya kumuona mke wake pale kwao 

 “ Kumbe ulikuwa na safari ya kuja 

huku ? Si ungeniambia kama unakuja kwa 

sababu hata mimi nilikuwa nimepanga leo 

nije kumsalimu mama.” Akasema 

Vivian.Tino akamtazama kwa macho 

makali na kusema 

 “ Hukuwa na ratiba ya kuja huku 

ulikuwa unanifuatilia.Ulidhani kuna 

mahala ninakwenda? Akauliza Tino kwa 

ukali 

 “ Ndiyo nilikufuata kutaka kujua 

unakwenda wapi.kama ulikuwa unakuja 

huku kwa nini usingeniambia? Akauliza 

Vivian naye kwa ukali kidogo 

 “ kwanini unataka kila kitu 

nikwambie? 

 “ kwa sababu mimi ni mkeo na 

ninapaswa kufahamu kila kitu 

unachokifanya ! akasema Vivian kwa sauti 

ya juu 

 “ Unataka kufahamu kila 

ninachokifanya !!.Wewe unanieleza kila 

unachokifanya? Akauliza Tino  “ Sijawahi kukuficha kitu.Chochote 

ninachokifanya.Kila kitu 

ninakueleza..”akasema Vivian 

 “ Una hakika na unachokisema? 

 ‘Ndiyo nina hakika nacho.Hakuna 

siku nimewahi kukuficha kitu chochote.” 

 “ Jamani kuna nini humu? Akauliza 

mama yakeTino aliyetokea ghafla 

palesebuleni.Wakati Tino na mke wake 

wanawasili yeye hakuwepo alikuwa 

shambani 

 “ Mama shikamoo” Vivian 

akamsalimu mama mkwe wake 

 “marahaba mama hujambo? 

Kisha salimiana wote wakaketi 

 “ Niliuwa shambani nikapigiwa simu 

na Haika kwamba nyote 

mmekuja,nikastuka kidogo kwa nyote 

kuja kwa pamoja.Nilipokuja nimesikia 

mabishano kuna nini kimetokea? Akauliza 

mama yake Tino 

 “ hakuna tatizo mama bali sikujua 

kama mwenzangu naye anakuja 

huku.Nilishangaa ndiyo nikawa namuuliza 

kama alikuwa na safari ya kuja huku kwa 

nini hakuniambia? Akasema Tino 

 “ Hapana mama si kweli 

anavyokwambia Tino.Kuna tatizo “ 

Akasema Vivian  “ mama anakudanganya huyu 

hakuna tatizo lolote.Kama ana tatizo basi 

ni lake binafsi lakini mimi na yeye hatuna 

tatizo” akasema Tino 

 “ Mama kuna tatizo kati yetu na 

limekuwa jambo jema sote tuko hapa 

,tulizungumze suala hili” akasema Vivian. 

 “Mama usipteze muda wako hakuna 

tatizo lolote”akasisitiza Tino 

 ‘ jamani hebu tuelewane.Nyote mko 

hapa na kama kuna tatizo basi tuongee na 

tuliweke sawa.Tino ulinipigia simu jana na 

ukaniambia kwamba una tatizo na utakuja 

leo kuongea name.Ni tatizo gani hilo? 

Ndilo hilo analolisema mwenzako? 

Akauliza mama yake Tino 

 “ Mama ,mimi matatizo yangu ni 

mengine kabisa.kama yeye ana tatizo basi 

aliweke wazi tulisikie”akasema Tino 

 “ Vivy hebu tueleze kuna tatizo gani 

mama yangu? Akauliza mama Tino 

 “ Mama ,Tino anaogopa kuweka 

wazi lakini ni kweli kabisa ndani kwetu 

kuna matatizo na yeye ndiye tatizo” 

 “Mimi ?!! Tino akahamaki 

 “ Ndiyo wewe ni tatizo” akasema 

Vivian.Tino akasimama tayari alianza 

kupandwa na hasrira  “’Unasema mimi ni tatizo? Akauliza 

kwa ukali.Mama yake akamtuliza akakaa 

chini 

 “ Jamani kama mmekuja hapa mna 

matatizo hebu tukaeni kama watu wazima 

tuongee na tutaweke sawa matatizo 

yenu.Vivi hebu sema kuna tatizo 

gani?akauliza mama Tino 

 “ Mama ,mimi na Tino tumekaa 

kipindi kirefu sasa na hakujawahi kutokea 

na tatizo lolote.Hivi majuzi sote kwa 

pamoja tuliazimia kwamba sasa umefika 

wakati wa sisi kufunga ndoa na kuishi 

kihalali kabisa.Wakati ninaanza kuishi na 

Tino nilikuwa ndani ya ndoa kwa hiyo 

mpaka sasa mimi ninatambulika kama ni 

mke halali wa Yule mume wangu wa 

zamani.Ili mimi na Tino tuweze kufunga 

ndoa,inalazimu kwamba mimi na mume 

wangu ndoa yetu itenguliwe na 

kanisa.kwa bahati nzuri hata mume 

wangu wa zamani naye alikuwa na 

mawazo kama ya kwangu na tayari naye 

amepata mchumba na tukakubaliana 

kwamba tuanze taratibu za kutengua ndoa 

yetu.Wakati taratibu zikiendelea ghafla 

mwenzangu akabadilika tabia.Akaanza 

kuwa mlevi wa kupindukia.Anakunywa 

pombe hadi anajisahau.Kuna nyakati haonekani nyumbani hata siku mbili na 

hatoi maelezo yoyote.Nyumba yetu haina 

amani tena na hakuna chochote 

tunachokiongea wala kukipanga.Muda 

wote huwa amekasirika na hataki 

kuulizwa kitu chochote.Akiamka ni yeye 

na pombe.Leo hii unamuona katika hali hii 

ni kwa sababu alijua anakuja kwako ndiyo 

maana hajanywa pombe lakini siku zote 

mida kama hii huwa amelewa chakali.” 

Vivian akanyamaza kidogo halafu 

akaendelea 

 “ Kutokana na tabia yake kubadilika 

ghafla nimelazimika leo hii kumfuata ili 

kujua anakwenda wapi kwani katika simu 

yake kumekuwa na jumbe kadhaa toka 

kwa wanawake mbali mbali.Mama nina 

hakika mwanao tayari ana 

mwanamkemwingine na ndiyo maana 

hataki niliseme hili mbele yako” akasema 

Vivian 

 “ Umemaliza? Akauliza Tino 

akionyesha wazi kukerwa sana na maneno 

yale ya Vivian 

 “ Jamani mbona siwaeleweni nyie 

watoto? Mna matatizo gani? Tino haya 

anayoyasema mkeo ni ya kweli ? 

 “ Ameeleza vizuri sana kuhusu 

kilichotokea na kinachoendelea.Ni kweli nimekuwa nikilewa sana kwa siku hizi 

mbili tatu lakini nimefikia hatua hii kwa 

sababu yake yeye mwenyewe.Sikuwa na 

tabia ya kulewa hovyo hata wewe mama 

unanifahamu lakini nimeshindwa 

kuvumilia na ili niondoe mawazo 

niliyonayo inanilazimu ninywe pombe” 

akasema Tino 

 “ Usinisingizie mimi wakati wewe 

ndiye mwenye matatizo.Kuna kitu gani 

unachokikosa kwangu hadi ukaenda 

kutafuta wanawake huko nje? Akasema 

Vivian kwa ukali 

 “ Tino mkeo amekwisha eleza tatizo 

lake na wewe tueleze tatizo gani 

linakufanya wewe ufikie hatua ya kunywa 

pombe kiasi hicho? Kuna kitu 

amekukwaza? Akauliza mama yake Tino 

 “ Mama kwa kuwa sote tuko hapa 

hakuna haja ya kuficha kitu na kwa kuwa 

yeye mwenyewe amekiri kwamba kuna 

tatizo na akanilaumu mimi kwamba ndiye 

chanzo cha tatizo sasa ni bora tuweke wazi 

kila kitu ili tujue kitakachoendelea.” 

Akasema Tino.Akanyamaza akavuta pumzi 

ndefu na kusema 

 “ Mama ni kweli alivyokwambia Vivy 

kwamba bila kushawishiwa na mtu 

tuliamua sisi wenyewe kwa hiari yetu kwamba umefika wakati wa sisi kufunga 

ndoa na kuishi pamoja.Hatukuwataarifu 

kuhusu suala hili kwa sababu tulisubiri 

kwanza taratibu za kutengua ndoa ya 

Vivian na mume wake wa zamani 

zikamilike.Wakati tukilisubiri hilo 

nikapata taarifa za kustusha kidogo “ 

akanyamaza kidogo ,akaendelea 

 “ Niliumwa sikio na watu 

wanonipenda kwamba mke wangu hana 

uwezo wa kuzaa” 

Sura ya Vivian ikabadilika baada ya 

kusikia kauli ile.Tino akaendelea 

 “ Kipindi chote tulichokaa pamoja 

nimekuwa nikimsisitiza sana kuhusu 

suala la kupata mtoto lakini akasema 

kwamba atanizalia mtoto pindi tukifunga 

ndoa.Nilivumilia kwa sababu ninampenda 

sana mke wangu na ndiyo maana 

nilipopewa taarifa hizi sikutaka 

kuzikubali mara moja ikanilazimu nifanye 

utafiti ili nifahamu kama nilichoambiwa ni 

cha kweli ,na nikathibitishiwa bila chenga 

kwamba Vivian alikuwa na tabia ya kutoa 

mimba kwa sababu hakuwa tayari kuzaa. 

Mara ya mwisho alipotoa mimba aliumwa 

sana na ikagundulika kwamba alitoa 

mimba vibaya na kulikuwa na sifa katika 

kizazi chake kwa hiyo akafanyiwa upasuaji wa kuondoa kizazi .Wakati huo 

mimi nilikuwa nje ya nchi katika safari 

zangu za kibiashara na Vivy akanificha 

akaniambia kwamba amefanyiwa upasuaji 

wa kuondoa uvimbe ndani ya tumbo.Kwa 

muda wote huu Vivy amekuwa 

akinidanganya kwamba atanizalia mtoto 

pindi tukifunga ndoa wakati akijua kabisa 

kwamba hana uwezo wa kuzaa….” 

 Ghafla Vivian akaanguka chini 

akapoteza fahamu…………………. 

Vivian akapatiwa huduma ya kwanza 

akazinduka.Bado hakuonekana kuwa 

katika hali nzuri hivyo kuwalazimu Tino 

na mama yake wampeleke hospitali ili 

aweze kuchunguzwa afya yake.Alipelekwa 

katka hospitali ya St Joseph mjini moshi 

ambako alipumzishwa kwa muda.Wakati 

madaktari wakiendelea kumuangalia 

,Tino na mama yake walikuwa wamekaa 

nje wakisubiri madaktari wamalize kazi 

yao 

 “ Tino yale mambo uliyoyasema pale 

ndani ni mambo ya kweli? Akauliza mama 

yake 

 “ Mama yale ni mambo ya kweli 

kabisa.Vivian ni mke wangu na siwezi 

kumsemea uongo.Hata mimi 

nilipoambiwa suala hili kwa mara ya kwanza nilistuka sana na ilikuwa vigumu 

kuamini kama linaweza kuwa 

kweli.Nilikorofishana hadi na marafiki 

zangu walionipa taarifa hizi lakini badae 

nikaona ni bora niutafute 

ukweli.Nilionana na daktari ambaye 

alimfanyia Vivian upasuaji huo wa 

kuondoa kizazi na akanihakikishia 

kwamba ni kweli mke wangu hana uwezo 

tena wa kuzaa.Jambo hili mama 

liliniumiza mno .Unajua kwa kwa miaka 

mingi kiu yangu kuibwa ni kupata 

mtoto.Ninazo mali nyingi nani basi 

atakuwa mrithi wangu ? Niliumizwa mno 

na ndiyo maana nikaanza kunywa pombe 

kupoteza mawazo.Leo nilikuja ili 

kukutaarifu kuhusu suala hili na 

kukueleza kuhusu maamuzi yangu 

nitakayochukua lakini kumbe Vivian naye 

alikuwa ananifuata kwa nyuma akidhani 

labda ninakwenda kwa mwanamke 

mwingine.Sina mwanamke mwingine na 

kama ningehitaji kuwa na wanawake 

wengine ningekwisha kuwa nao wengi au 

hata kuwa na watoto wengi tu wa nje 

lakini sijafanya hivyo kwa sababu 

ninampenda sana mke wangu,lakini kwa 

hili alilolifanya itanilazimu kufikiri mara mbili tena kama mimi na yeye tunaweza 

kuendelea tena ama la” Akasema Tino 

 “ Pole sana Tino.Najua jambo hili 

limekuumiza sana lakini ninakushauri 

usichukue maamuzi yoyote kwa sasa.Ni 

mapema sana bado kufanya maamuzi 

yoyote.Suala hili linatakiwa lijadiliwe na 

muafaka ufikiwe.Kukosa mtoto si sababu 

ya ninyi kutengana au kuwa ni chanzo cha 

ugomvi ndaniya nyumba.Kama kweli 

mnapendana kwa dhati mnaweza mkaishi 

maisha yenu yenye amani na furaha hata 

kama hamna watoto.Kuna watoto wengi tu 

wasio na wazazi mnaweza mkamchukua 

mmoja mkamtunza na akawa mtoto 

wenu.” Akasema mama yake Tino 

 “ Sijui mama kama tunaweza 

tukaishi tena kwa amani kama 

mwanzo.Kinachoniumiza zaidi ni kwamba 

Vivian alinificha kuhusu suala hili na 

akawa ananihakikishia kila siku kwamba 

atanizalia watoto pindi tukiingia katika 

ndoa.Alifahamu kabisa kwamba tukiingia 

katika ndoa sintakuwa na ujanja tena 

kwani sintaweza kumuacha ,Hili 

limeniumiza sana.Ingekuwa vizuri kama 

angenieleza ukweli toka mapema ili nijue 

lakini amenificha na kunidanganya.Mama 

mwanamke huyu hafai kabisa.Kama ameweza kunificha kuhusu jambo hili ,ni 

mambo mangapi basi atakuwa 

amenidanganya? Ninahitaji mwanamke 

ambaye nitamuamini kwa kila jambo 

ambaye hatanificha kitu chochote kile 

hata kiwe kigumu namna gani lakini huyu 

amekuwa ni mlaghai..She’s there for my 

money only.” 

 “ Tino baba,hebu naomba upunguze 

hasira na baada ya kutoka hapa 

tutakwenda kuliongelea suala hli na 

kufikia maamuzi.Ni kweli mkeo amekosea 

kukuficha kuhusu suala hili na 

ninamlaumu kwa hilo lakini bado mnayo 

nafasi ya kuyaweka mambo yote pembeni 

na kuanza upya maisha yenu huku 

mkifahamu kabisa kwamba hamtakuwa 

na mtoto wa damu yenu.Ninafahamu 

mnapendana sana na mmekaa muda 

mrefu bila mataizo ya aina yoyote 

ile.Tafadhali Tino usifikirie kabisa 

kumuacha mkeo Anakupenda sana” 

 “ Upendo ?!! Tino akaonekana 

kuanza kupandisha sauti kidogo 

 “ Hakuna upendo hata kuidogo 

mama.Mwanamke huyu hanipendi kabisa 

.Kama kweli angekuwa ananipenda 

asingethubutu kutoa mimba na kuua 

watoto wangu wasio na hatia.Hata kama ukimtetea vipi ,Vivian hafai na hawezi 

kuwa mama.Huko alikotoka kwa mume 

wake wa zamani alimuacha mtoto mdogo 

kabisa na akakikimbia umasikini wa 

mume wake na kufuata utajiri wangu.Ni 

mwanamke ambaye anathamini pesa 

kuliko kitu chochote kile.Mama 

ninamfahamu Vivian kuliko mtu mwingine 

yeyote kwa hiyo hakuna haja ya 

kumtetea.Mimi nimekwisha fanya 

maamuzi yangu na sintarudi nyuma 

tena.Nimeishi naye muda mrefu kama mke 

wangu na niko tayari kugawana naye kila 

kilicho changu lakini si kuendelea kuishi 

naye kama mke wangu tena.” Akasema 

Tino 

 “Tino tusiongee mambo haya 

makubwa hapa hospitali.Tutaongea 

tukifika nyumbani.Nimempigia simu 

mjomba wako anakuja toka Machame na 

kwa pamoja tutalijadili suala hili na 

kupata muafaka.” Akasema mama Tino 

 “ Hahaha ! mama hakuna muafaka 

utakaopatikana.Tayari nimekwisha fanya 

maamuzi yangu na siwezi 

kuyabadilisha.Imetosha sasa kuishi 

maisha ya ulaghai.Ninataka nijipange upya 

kuanza maisha yangu na mtu mwngine 

ambaye ninaweza nikamuamini na si huyu.Kwa hiyo hakuna haja ya 

kuwasumbua akina mjomba ,hakuna 

watakachokibadilisha katika maamuzi 

yangu” akasema Tino na mama yake 

hakusema kitu tena 



Uso wa Pauline haukukaukiwa 

tabasamu wakati anakagua maendeleo ya 

ukarabati wa nyumba atakayoitumia 

kufungulia hospitali maalum ya vipimo . 

 “ Namshukuru Mungu kila kitu 

kinakwenda vizuri kwa sasa ni kuanza 

kuandaa pesa kwa ajili ya kununulia 

mashine na vifaa vingine.Ni pesa nyingi 

inahitajika .Nina kiasi cha pesa benki 

kinatohsa sana kuanzia na vile vile 

nitaongea na na baba naye lazima 

ataniongezea kiasi fulani cha pesa na kiasi 

kingine nitakopa benki,.Nataka jumamosi 

nikienda Arusha nianze taratibu za kupata 

mkopo.Najua siwezi kuchukua muda 

mrefu kwa sababu baba anafahamika sana 

katika mabenki yote kwa hiyo ndani ya 

wiki moja tu nina hakika nitakuwa nimepata pesa ninayoihitaji” akawaza 

Pauline 

 “ Nimemkumbuka sana baba 

yangu.Natamani kujua maendeleo yake 

.Najua hata yeye ana hamu sana ya 

kunisikia na kujua ninaendelea vipi.Kimya 

changu lazima kitampa wasi wasi mkubwa 

sana.Nikifika hotelini leo lazima nimpigie 

simu nimjulie hali.” Akawaza na mara 

akakumbuka kitu 

 “ Nikirudi Arusha lazima nitakutana 

na David.Sitaki kabisa hata kumtia 

machoni Yule kijana.Alinifanyia kitu 

kibaya na kuniumiza vibaya sana.Ninataka 

nimsahau kabisa katika maisha 

yangu.Lakini kwa upande mwinginge ni 

yeye aliyenifanya nikaondoka Arusha na 

kuja huku Moshi ambako nimepata wazo 

lingine zuri la biashara na akili yangu 

imepanuka sana.Kwa sasa mimi si Pauline 

Yule ambaye alimfahamu wiki kadhaa 

zilizopita.” Akasimama na kuegemea 

nguzo 

 “ Lakini kwa nini ninaogopa kuonana 

naye? Kwa sasa anaendelea na maisha 

yake na mpenzi wake Tamia na 

ninawatakia kila la heri katika mapenzi 

yao na kwa hiyo sipaswi kabisa kuogopa 

kuonana naye.Kuanzia sasa sitakiwi kumkimbia hata kidogo .I’ll face 

him.Natakiwa kumuona ni mtu wa 

kawaida kabisa” akawaza Pauline 

 Baada ya kutoka katika ukaguzi 

akapita madukani ambako alinunua 

baadhi ya vitu alivyovihitaji kisha 

akarejea hotelini .Kitu cha kwanza 

alichokifanya ni kufungua begi lake 

akachukua simu akaitazama na kisha 

akaiwasha.Jumbe nyingi zikaingia katika 

simu yake hakushughulika nazo moja kwa 

moja akazitafuta namba za simu za baa 

yake akapiga 

 “ Hallow Pauline? Akasema mzee 

Zakaria baada ya kupokea simu 

 “ Baba shkamoo” 

 “ Marahaba mwanangu habari za 

huko uliko? Mbona kimya sana? 

Nimekuwa ninajiuliza sana sababu ya 

wewe kuizima kabisa simu yako na 

kutokutaka kabisa kuwasiliana na sisi” 

akasema mzee Zakaria 

 “ Baba utanisamehe kwa hilo lakini 

nilikuwa sehemu ambayo mtandao 

haupatikani kirahisi ndiyo maana 

nikashindwa kuwasiliana 

nawe.Unaendeleaje baba? Akauliza 

 “ Ninaendelea vizuri sana.Hali yangu 

inazidi kuboreka.Kwa sasa ninapumzika tu na kufanya sughuli ndogo ndogo 

,siumizi kichwa tena kwani David 

ananisaidia sana katika masuala ya 

kibiashara.Pauline ulikuwa sahihi sana 

kunitaka kumuajiri David.Ni mtu sahihi 

kabisa.Anafanya kazi zake vizuri sana na 

kwa uaminifu mkubwa na mpaka sasa 

amekwisha okoa pesa nyingi sana 

zilizokuwa zinapotea kwa kukosa 

usimamizi. Akasema mzee Zakaria na 

Pauline Akakaa kimya 

 “ Pauline ! akaita mzee Zakaria 

baada ya kuona mwanae amekuwa kimya 

sana 

 “ Nipo baba” akajibu 

 “ Vipi maendeleo yako kwa ujumla? 

 “ Ninaendelea vizuri sana na wala 

usihofu kitu baba” 

 “ Nafurahi kusikia hivyo” akasema 

mzee Zakaria 

 “ Baba nimekupigia kukujulia hali na 

kukutaarifu kwamba kesho jumamosi 

nitakuja Arusha kuna jambo ninataka kuja 

kuongea nawe .Vile vile ninaweza 

kuambatana na rafiki zangu mmoja ama 

wawili.” akasema Pauline 

 “ Ouh ! hizo ni taarifa nzuri sana.Kwa 

kweli nitafurahi sana kukuona 

Pauline.Ninahitaji sana kukuona.Karibu tena nyumbani.Nitamwambia dada yako 

wa kazi aanze kukuandalia chumba chako 

haraka pamoja na cha wageni wako” 

akasema mzee Zakaria 

 “ Haya ahsante baba nadhani 

nitakupigia tena hiyo jumamosi” akasema 

Pauline na kukata simu.Akapata wazo la 

kuanza kuzisoma jumbe zile nyingi lakini 

wakati akisoma akakutana na ujumbe 

uliotoka kwa David ambao ulimstua 

kidogo.Akausoma na kuurudia tena kwa 

mara ya pilI na ya tatu. 

 “ Huyu David ana maanisha nini 

kunitumia ujumbe kama huu? Mbona 

simuelewi? Akajiuliza kisha akaamua 

kumpigia. 

 “ Hallo Pauline.Mzima? Siamini kama 

nimeisikia tena sauti yako” akasema David 

baada ya kupokea simu ya Pauline 

 “ David sitaki maneno mengi 

,nimeamua kukupigia simu baada ya 

kuupata ujumbe wako ambao 

umenishangaza kidogo na wala sijakupigia 

simu kwa ajili ya jambo lingine kwa hiyo 

naomba tafadhali unieleze maana ya 

kunitumia ujumbe wa namna hii” akasema 

Paline 

 “ Pauline kwanza nashukuru kwa 

kuamua kunipigia.Nimeona nikutumie ujumbe ule ili kukutaka kama uko 

karibuna Arusha basi urejee nyumbani 

mara moja,there is something going on 

here.You must be there before Sunday” 

akasema David 

 “ David kuna nini kiasi cha kunitaka 

nirejee haraka nyumbani? Mbona baba 

nimeongea naye muda si mrefu na 

anaendelea vizuri tu? Kuna tatizo gani 

lingine? 

 “ Kuna jambo kubwa linendelea 

huku .Pauline najua mmi na wewe kwa 

sasa tuna tofauti zetu lakini naomba 

tuziweke pembeni kwa wakati huu na uje 

Arusha mara moja.This is for you,your 

father and your family” akasema David 

 “ David kuna jambo gani? Kwa nini 

usinieleze kwenye simu? 

 “ Siwezi kukueleza simuni 

Pauline.Tafadhali naomba uje Arusha 

mara moja.Na tafadhali usimwambie 

chochote mzee Zakaria wala madam Vicky 

kama nimekwambia chochote.This is 

between us” akasema David 

 “ David mbona unaniogopesha? 

Akasema Pauline 

 “ Usiogope Pauline ila jitahidi sana 

kwa namna yoyote ile uje Arusha kabla ya 

jumapili” akasisitiza David.Pauline akabaki kimya kidogo akafikiri kisha 

akasema 

 “ David are you sure its something 

serious ?? 

 “ Very very serious” akasema David 

 “ Ok sawa.Kwa mara nyingine tena 

ninalazimika kukuamini lakini make sure 

its real something very serious.” Akasema 

Pauline 

 “ Nakuhakikishia Pauline its 

something very serious” 

 “ Sawa nitakuja jioni ya leo badala ya 

kesho kama nilivyokuwa nimepanga “ 

akasema Pauline 

 “ Ahsante sana nashukuru Pauline 

kwa kunielewa. Ninakusubiri jioni ya 

leo.By the way how are yo………………” 

David hakumaliza sentensi yake Pauline 

akakata simu 

 “ Amekata simu !!! lakini nashukuru 

kwamba amenielewa.” Akawaza David 

 Baada ya kukata simu Pauline 

akabaki katika mawazo mengi 

 “ Ni jambo gani ambalo David 

atakuwa ananiitia Arusha kiasi akaweka 

msisitizo mkubwa namna hii? Lazima 

kutakuwa na suala kubwa ambalo 

limetokea na ambalo hataki mtu mwingine 

alifahamu zaidi yangu.Itanilazimu  niende  Arusha jioni ya leo badala ya kesho kama 

nilivyokuwa nimepanga.kwa msisitizo ule 

lazima kuna kitu si bure.Itanibidi 

nimtaarifu Sanya kuhusu safari hii ya 

dharura .Vile vile nimtaarifu Alfred kwani 

alitaka kuongozana nami kwenda Arusha 

kesho lakini haitawezekana tena kwani 

mimi ninaondoka leo jioni” Akawaza 

Pauline kisha akazitafuta namba za simu 

za Alfred akampigia. 

 “ Hallo my queen” akasema Alfred 

baada ya kupokea simu.Pauline 

akatabasamu na kusema 

 “ You have your queen at home 

Alfred so please don’t call me queen.” 

Akasema huku akitoa kicheko kidogo 

 “ Vyovyote vile itakavyokuwa you 

are,and you’ll forever be my queen.” 

Akasema Fred 

 “ Any way tuachane na hayo Fred 

siwezi kushindana nawe.Nimekupigia 

kukutaarifu kwamba nimepata dharura 

natakiwa Arusha jioni ya leo kwa hiyo ile 

safari yetu tuliyoipanga kesho 

haitakuwepo tena.I’m so sorry for that 

Alfred najua ulitamani sana kuongozana 

nami Arusha.” Akasema Pauline  “ Pauline you don’t have to be 

sorry.Nitaongozana nawe jioni ya leo 

kwenda Arusha” akasema Alfred. 

 “ Stop that Alfred.What we are doing 

is not right ..” akasema Pauline 

 “ Pauline tafadhali tusibishane 

kuhusu hili.Nitangozana nawe jioni ya leo 

kwenda Arusha” akasema Alfred 

 “ Sawa Alfred kama umesisitiza 

hivyo” akasema Pauline kisha akaagana na 

Fred kwa miadi ya kukutana saa kumi na 

mbili za jioni kwa ajili ya kuanza safari ya 

kuelekea Arusha 

 “ Kuna nyakati ninaogopa sana kwa 

namna Alfred alivyokufa akaoza 

kwangu.Hasikii la mtu tena juu 

yangu.Yuko tayari kwa lolote lile.Nina 

wasi wasi ndo ayake itaingia katika 

mgogoro mzito muda si mrefu.Mke wake 

ataumia sana kwa kitakachotokea lakini 

nitafanya nini sasa? I’m in love too with 

Alfred and I cant let him go…Kwa muda 

huu mfupi ameniingia katika kila mshipa 

wa mwili wangu .I know I’m doing the 

wrong thing but I don’t have the power to 

say No to Alfred..” akawaza Pauline kisha 

akatoka chumbani kwake akaelekea 

chumbani kwa Sanya kumtaarifu kuhusiana na safari ile ya dharura.Sanya 

akakubali kuongozana naye jioni ile 

********************* 

 Alfred alirejea nyumbani kwake saa 

kumi na moja za jioni akaoga haraka 

haraka kisha akachukua sanduku lake 

dogo na kuanza kupakia baadhi ya vifaa 

vyake muhimu. 

 “ Una safari? Akauliza Grace 

aliyeingia ghafla mle chumbani.Wakati 

Fred aliporejea nyumbani mke wake 

hakuwepo. Fred akastuka 

 “ Ouh my love ,umenistua sana 

ulivyoingia ghafla kama malaika” 

Akasema na kumkumbatia akambusu 

 “ Mbona unapakia una safari? 

Akauliza Grace 

 “ Ndiyo nina safari.Nimeitwa kwa 

dharura hospitali ya Serian Arusha.Kuna 

mgonjwa anahitaji upasuaji wa haraka 

usiku wa leo” akasema Alferd huku 

akiendelea kupakia nguo na vifaa vyake 

vidogo vidogo 

 “ Pole sana.” Akasema Grace 

 “ Ahsante sana. Mke wangu” 

 “ Lini utarejea ? akauliza Grace  “ Sina hakika ndiyo maana 

nimechukua nguo za kutosha siku mbili 

tatu “ akajibu Alfred kisha akaagana na 

mke wake akaingia garini na kuondoka. 

 Mara tu alipoondoka mke wake naye 

akaingia katika gari lake na kuanza 

kumfuatilia.Bila kujua kama anafuatiliwa 

moja kwa moja Alfred akaelekea katika 

hoteli anakoishi Pauline.Akaegesha gari 

na kushuka akapanda ghorofani 

 “ Nilijua tu lazima atakuja 

hapa.Pauline aliniambia kwamba atakuwa 

na safari ya kuelekea Arusha kesho ghafla 

Fred naye anakuja na kuniambia amepata 

safari ya dharura kwenda Arusha.hawa 

watu kuna mchezo wananicheza.Ngoja 

nione kitakachoendelea” akawaza Grace 

akiwa ameegesha gari upande wa pili wa 

maegesho ya pale hotelini . 

 Baada ya dakika kama kumi hivi 

akamshuhudia Alfred akiwa ameongozana 

na Pauline na msichana mwingine ambaye 

hakumfahamu wakaingiza mabegi katika 

gari la Alfred kisha wakaondoka 

 “ Nilijua tu lazima kuna kitu 

kinaendela kati ya Fred na 

Pauline.Wanaelekea Arusha.” Akawaza 

Grace huku akiangusha machozi… ************************* 

Mpaka saa kumi na moja za jioni hali ya 

Vivian ilikuwa nzuri na madaktari 

walithibitisha kwamba anaweza akarejea 

nyumbani kwani hakuwa akisumbuliwa 

na kitu chochote . 

 “ Pole sana Vivian” akasema Tino 

lakini Vivian hakujibu k itu 

 “ Madaktari wamekwisha toa ruhusa 

.Tunaweza kuondoka .Tutaelekea kwanza 

nyumbani kwa mama kuna maongezi ya 

kifamilia na halafu tutaelekea Arusha” 

akasema Tino 

 “ Martin sitaki kabisa kwenda 

sehemu yoyote .Ninataka kurudi 

nyumbani Arusha.Nirudishe 

nyumbani”akasema Vivian 

 “ Vivian kuna mambo mengi 

ambayo tunatakiwa kuyajadili kama 

familia.Tutapitia kwanza nyumbani kwa 

mama halafu tuelekee nyumbani Arusha.” 

 “ Martin nimekwambia kwamba 

siendi sehemu yoyote ile.Nataka kurudi 

nyumbani Arusha.Kama kuna mambo ya 

kuongea tutakwenda kuongea huko huko 

nyumbani” akasisitiza Vivian 

 “ Sawa Vivian kama hivyo ndivyo 

unavyotaka basi tutakwenda Arusha.Jiandae tuweze kuondoka” 

akasema Tino kisha akatoka nje na 

kuongea na mama yake kidogo halafu 

wakaingia ndani wakamsaidia Vivian 

kutembea hadi garini kisha wakaondoka 

pale hospitali. 

 “ Nani kamueleza Martini kuhusu 

suala hili ?.Ama kweli dunianihakuna 

hakuna siri ya watu wawili.Hakuna mtu 

aliyekuwa akifahamu kitu chochote 

kuhusiana na jambo hili.Kumbukumbu 

zangu hazinionyeshi kama nimewahi 

kumueleza mtu mwingine yeyote 

kuhusiana na suala hili.Nilifanya jambo 

lile kimya kimya na aliyefahamu ni daktari 

na wale wauguzi wawili .Sijui sirihii 

imevujajena kumfikia Tino.” Akawaza 

Vivan akiwa ndaniya gari 

 “ Nilikuwa najiuliza sana sababu ya 

Tino kubadilika ghafla namna hii kumbe 

ni baada ya kuzipata taarifa hizi.Ni nani 

lakini aliyemwambia? Ama kweli kuna 

watu ambao hawataki kutuona mimi na 

Martin tukiishi maisha ya furaha.Kwa sasa 

baada ya Martin kuligundua jambo 

hili,sina ujanja tena its over.Hakuna kitu 

ambacho ninaweza kumweleza 

akanielewa.Hakuna neno ninaloweza 

kulitumia kumuomba msamaha na akakubali kunisamehe.” Akaendelea 

kuwaza Vivian 

 “ Nilimuangalia usoni Martin wakati 

akimueleza mama yake.Nina hakika 

kabisa kwamba hakuna tena muafaka wa 

aina yoyote iIe unaoweza kupatikana kati 

yetu.Martin amedhamira 

kuniacha.Nimehangaika naye kwa muda 

mrefu sana na tumechuma mali za 

kutosha siko tayari kukubali kuachwa na 

Martin halafu akaja mwanamke mwingine 

na kuanza kutumia mali nilizotolea jasho 

mimi.Ni bora tukose wote” akawaza Vivian 

 Walifika hadi Bomang’ombe 

nyumbani kwa wazazi wa Tino 

wakamshusha mama yao halafu bila 

kupoteza wakati wakaendelea na safari ya 

kuelekea Arusha.Safari ilikuwa ya kimya 

kimya ni sauti ya muziki tu iliyokuwa 

ikisikika . 

 “ Nitauficha wapi uso wangu kwa 

aibu hii kubwa nitakakayoipata baada ya 

kuachana na Martin? Nitachekwa kila 

kona na hasa ikigundulika kwamba sina 

tena uwezo wa kuzaa.Japokuwa nitakuwa 

na mali lakini sintakuwa na furaha tena 

katika maisha yangu.Hapana sitaki hilo 

litokee.Mjimzimawananijua kama mke wa Tinomagari itakuaje ikisikika kwamba 

nimeachwa kwa kutokuzaa? Akawaza 

Vivian huku gari likienda kwa kasi 

 Walifika eneo la kikatiti ambako 

kulikuwa na mteremko halafu kilima 

kidogo.Hakukuwa na magari mengi jioni 

hii kwa hiyo mwendo waliokuwa 

wakishuka nao ulikuwa mkali.Kutokea 

Arusha kulikuwa na gari moja kubwa la 

mizigo liilobeba kontena likishuka kwa 

kasi. 

 “ This is it ..! akawaza Vivian na 

ghafla akafanya kitendo ambacho Tino 

hakuwa amekitarajia.Kwa kasi ya ajabu 

Martin alipigwa ngumi moja usoni na 

kisha kwa kasi ya aina yake akaurukia 

usukani na kuunyonga kuelekea upande 

ule wa lile gari la mizigo lilikokuwa 

linateremka kwa kasi na mara kukapotea 

kishindo kikubwa.Ilikuwa ni ajali mbaya. 

******************** 

 Kiza kilikwisha tanda angani na 

safari ilikuwa inaendelea.Alfred 

aliyekuwa katika usukani aliendesha gari 

kwa mwendo wa kawaida hakutaka 

kuendesha kwa mwendo mkali.Safari 

ilitawaliwa na maongezi na vicheko.  “ Pauline ,tayari umepanga nitafikia 

wapi Arusha ? Akauliza Alfred 

 “ Utafikia nyumbani kwetu” akasema 

Pauline 

 “ Hahahaa..!! unataka mzee wako 

anikate shingo? Akatania Fred 

 “ Hapana Fred.Nyumba yetu ni 

kubwa na ina vyumba vya kutosha 

tu.Hakuna haja ya kulala hotelini wakati 

sehemu ya kulala ipo” akasema Pauline 

 “ Lakini Pauline unafahamu dhumuni 

langu kubwa la kuongozana nawe kuja 

Arusha.ninataka niutumie muda wote wa 

weekend hii nikiwa nawe.Huoni kama 

nyumbani kwenu hilo halitawezekana? 

Akauliza Fred 

 “ Fred wewe na Sanya ni wageni 

wangu ,mimi ndiye mwenyeji wenu kwa 

hiyo ni jukumu langu kuhakikisha 

kwamba mnapatiwa kila kitu 

mnachokihitaji.Usihofu kitu Fred.Kila kitu 

kitawezekana.Tutapata muda mwingi na 

mzuri wa kuwa pamoja.”akasema Pauline 

na mara Fred akafunga breki ya ghafla 

wote wakastuka baada ya kusikia 

kishindo kikubwa sana.Mbele yao 

kulitokea ajali mbaya. 

 “ What happened? Akauliza Sanya 

huku mwili wote ukimtetemeka  “ Kuna ajali mbaya imetokea kule 

mbele .Gari mbili zimegongana”akasema 

Alfred kisha akaegesha gari pembeni ya 

barabara.Pauline na Sanya waliogopa sana 

walikuwa wanatetemeka na hasa 

Pauline.Kishindo alichokisikia 

kilimuogopesha sana. 

 “ Twendeni tukatoe msaada 

yawezekana kukawa na majeruhi tuwahi 

kuwakimbiza hospitali”akasema Sanya 

kisha wakashuka garini na kuanza 

kukimbia kuelekea eneo la ajali.Kishindo 

kile kikubwa kilivuta watu wengi eneo lile 

ndani ya muda mfupi tayari 

walikwishafika eneo la ajali tayari kwa 

kutoa msaada ama ungehitajika.Ndani ya 

gari ndogo kulikuwa na watu wawili 

ambao walisadikiwa kuwa ni mke na 

mume na hali zao zilikuwa mbaya 

sana.Watu walijitahidi kwa kadiri 

walivyoweza na wakafanikiwa 

kuwachomoa majeruhi. 

 Akiwa ni mmoja wa watu waliosaidia 

kuwaokoa majeruhi wale wa ajali,Alfred 

akapendekeza wapakiwe katika gari lake 

ili waweze kuwahishwa haospitali.Kwa 

haraka wakasaidiana na kuwapakia 

majeruhi wale katika gari la Fred Pauline 

akashika usukani wakaondoka kwa kasi .  Katika wale majeruhi wawili ni 

mwanamke ambaye alikuwa anagugumia 

kwa maumivu makali huku akitaja jina la 

Penina.Yule mwanaume alikuwa 

anakoroma kwa mbali na hali yake 

ilionekana mbaya zaidi.haikuwa rahsi 

kuwatambua majeruhi walekutokana na 

kuchafuka damu.Wakiwa ndani ya gari 

Sanya na Alfred waliendelea na jitihada za 

kuizuia damu isiendelee kuwavuja 

majeruhi wale wakati Pauline alikuwa 

katika usukani wa gari akijaribu 

kuendesha kwa kasi na tahadhari kubwa 

kuwahi hospitali. 

Hatimaye waliwasili katika hospitali 

ya mkoa ya Mount Meru ambako 

majeruhiwakapokelewa na kukimbizwa 

katika chumba cha wagonjwa 

mahututi.Alfred na Sanya 

wakajitambulisha kama ni madaktari na 

wakaomba waruhusiwe kujumuika na 

madaktari wenzao ili kuwasaidia majeruhi 

wale.Kila aina ya msaada ilihitajika usiku 

ule kwa ajili ya kuokoa maisha ya 

majeruhi wale hivyo Alfred na Sanya 

wakaruhusiwa kujiunga na madaktari 

wenzao wa hospitali ya Mount Meru katika 

kuwasaidia majeruhi .  Pauline alibaki nje akiwasubiri akina 

Alfred wamalize kazi yao.Akiwa pale nje 

akaona ni vyema amjulishe baba yake 

kwamba tayari amekwisha wasili Arusha 

akachukua simu yake na kumpigia mzee 

Zakaria 

 “ Hallo Pauline“akasema mzee 

Zakaria baada ya kupokea simu 

 “ baba nimekupigia kukutaarifu 

kwamba niko Arusha tayari” 

 “Uko Arusha?akashangaa mzee 

Zakaria 

 “ Ndiyo baba.Niko Arusha” 

 “ Mbona uliniambia kwamba 

unakuja kesho? 

“ Ndiyo nilikuambia hivyo lakini 

nikabadili mawazo nikaona nije jioni ya 

leo .Lakini kwa sasa niko hapa Mount 

Meru hospitali.” 

 “ Kuna nini hapo 

hospitali.Unaumwa? Mzee Zakaria 

akauliza kwa wasi wasi 

 “ Hapana siumwi baba.Kuna watu 

tumewaleta hapa wamepata ajali.Rafiki 

zangu nilioambatana nao ni madaktari 

kwa hiyo wanasaidia katika kuokoa 

maisha ya majeruhi hao” akasema Pauline 

 “ Poleni sana.Nimestuka nikadhani 

labda wewe ndio mwenye matatizo.”  “ hapana baba si mimi .Naomba 

umwambie dada aniandalie chumba 

changu pamoja na chumba kimoja cha 

wageni nina wageni wawili wote 

watafikianyumbani.” Akasema Pauline 

kisha akaagana na baba yakena kukata 

simu.Mara akapata wazo 

 “ Sijui nimpigie na David 

nimfahamishe kwamba nimekwisha 

wasili? Akajiuliza 

 “ Ngoja nimpige tu nimjulishe 

kwamba nimefika.Niko mwenyewe hapa 

nje nimeboreka sana.lakini moyo unasita 

sana kumpigia tena Yule jamaa kwa 

mambo aliyonifanyia.Anyway tu ngoja 

nimpigie” akawaza Pauline na kuchukua 

simu yake akampigia David 

“ Hallo Pauline.Umekwisha 

fika?akauliza David mara tu alilipopokea 

simu 

 “ Siku hizi hata kujuliana hali hakuna 

moja kwa moja unauliza kama 

nimekwishafika” akasema Pauline 

 “ I’m sorry Pauline.Unajua nikipata 

simu yako huwa ninachanganyikiwa 

kidogo.”akasema David 

 “ Kinachokuchanganya nini au 

unaona aibu kwa mambo uliyoyafanya? 

Akauliza Pauline.David akabaki kimya  “ anyway David.Niko hapa Mount 

meru hospitali” 

 “Mount Meru? Kuna nini?unaumwa? 

akauliza David 

 “ Hapana siumwi ila kuna watu 

wamepata ajali tumewaleta hapa 

hospitali” akasema Pauline 

 “ Ok Pauline ninakuja hapo sasa 

hivi”akasema David 

 “ David anahisi aibu kubwa kwa 

jambo alilonifanyia na ndiyo maana kila 

akisikia sauti yangu anahisi 

kuchanganyikiwa.Anyway yeye awe na 

amani kabisa na Tamia wake kwani mimi 

tayari nimekwisha endelea na maisha 

yangu.Alfred amenisahaulisha machungu 

yote niliyoyapata baada ya kuumizwa na 

David.Amenifuta machozi yote na 

kunfanya nitabasamu tena.Japokuwa ni 

mume wa mtu lakini ameonyesha kunijali 

na kunithamini and I’m happy with 

him.Ninafahamu kwamba kutatokea 

mgogoro mkubwa katika ndoa yake hasa 

pale Grace mke wake atakapogundua 

kuhusu mahusiano yangu na mume wake 

lakini sina namna nyingine ya kufanya 

nimekwisha nasa kwa Fred na moyo 

wangu tayari umempenda.”akawaza 

Pauline.na kukumbuka siku ile ambayo Grace almanusura amfume mume wake 

ndani ya chumba cha Pauline 

 “ Dah ! Ama kweli siku ile niliogopa 

sana.Sikuwahi kutetemeka kama siku 

ile.Kufumwa na mume wa mtu si kitu 

kidogo.Ni aibu kubwa na hasa kwa mtu 

ambaye mnaheshimiana na kuaminiana 

kama Grace.Pamoja na kwamba alimkosa 

Fred siku ile lakini nina uhakika tayari 

atakuwa amekwisha hisi kwamba kuna 

kitu kinaendelea kati ya mume wake na 

mimi.Lakini kitu kinachonishangaza na 

kunifanya nijiulize maswali mengi kwa 

nini Fred aamue kumsaliti mke wake 

ambaye ana karibu sifa zote.Ni mzuri 

pengine kuliko hata mimi,ana roho zuri,ni 

mkarimu kupindukia ,kwa nini basi 

aamue kumuaacha na kuning’ang’ania 

mimi? Je kuna vitu anavikosa kwa mke 

wake lakini anavipata kwangu? Anyway 

siku moja nitamuuliza sababu iliyomfanya 

aamue kumsaliti mke wake..Ila wanaume 

mhh!!!..mimi wa kwangu pamoja na 

kumpenda kwa moyo wangu wote lakini 

akanisaliti tena na rafiki yangu na leo hii 

mume wa rafiki yangu anamsaliti na kuja 

kwangu..hahaah this is funny.Ninashindwa 

kuwaelewa wanaume.Ni kitu gani hasa 

wanakitafuta kwa mwanamke? Kwa sababu utakuta mtu ana mke wake mzuri 

sana lakini bado hatulii na anaruka ruka 

hovyo .”akaendelea kuwaza Pauline na 

mara David akampiga simu na kumuuliza 

mahala alipo,akamuelekeza na baada ya 

muda David akatokea .Wakatazamana 

kwa sekunde kadhaa kisha David akasema 

 “ Pole sana Pauline.Nini kimetokea? 

Ulipata ajali? akauliza David 

 “ Hapana David Si mimi niliyepata 

ajali.Wakati tukija Arusha gari ya mbele 

yetu ilipata ajali eneo la kikatiti hivyo 

kutulazimu kuwabeba majeruhi wa ajali 

na kuwakimbiza hapa hospitali .Kwa 

bahati nzuri watu nilioongozana nao wote 

ni madaktari kwa hiyo wameungana na 

madaktari wenzao wa hapa Maount Meru 

wanawasaidia majeruhi”akasema Pauline 

 “Vipi hali zao? 

 “ wameumia sana,na hasa Yule 

mwanaume ameumia zaidi na sina hakika 

kama anaweza akapona lakini tumuombee 

ili apone.Ilikuwa ni ajali mbaya sana 

kuwahi kuishuhudia.”akasema Pauline 

kisha kukawa kimya.Ni Pauline ndiye 

aliyeanzisha maongezi 

 “ Vipi maendeleo yako? Kazi 

zinakwendaje?  “Ninaendelea vizuri sana na hata 

kazi zinakwenda vizuri.Vipi wewe 

unaendeleje? 

 “ Ninamshukuru Mungu.Anazidi 

kunipa nguvu na uhai kila siku.I’m still 

breathing,I’m still smilling,life goes 

on”akasema Pauline huku 

akitabasamu.David akabaki kimya 

hakutaka kuongea tena. 

 “ By the way how is Tamia ? Akauliza 

Pauline na kumfanya David ainame kidogo 

akafikiria halafu akainua kichwa na 

kusema 

 “ I don’t know how she’s doing “ 

akajibu 

 “ You don’t know? What kind of 

boyfriend are you? Akauliza kwa 

mshangao Pauline 

 “ We’re not together anymore.. 

 “ What?!! Akauliza Pauline kwa 

mshangao 

 ‘ You are not together anymore? 

Akauliza tena 

 “ yes ! 

 “ hahahhaa..unanidanganya tena 

David.Haiwezi kuwa kweli.”akasema 

pauline 

 “ Sikudanganyi Pauline ni kitu cha 

kweli kabisa mimi na Tamia tumekwisha tengana.” Akasema David.Pauline 

akamtazama machoni akaamini kile 

alichokuwa anakisema David 

 “ What happened?akauliza huku uso 

wake umejaa tabasamu 

 David Akakaa kimya kidogo akafiri 

na kusema 

 “ Ulikuwa sahihi kwa yale 

uliyoniambia kuhusu Tamia.Nilimfuma na 

mwanaume ndani” 

 “ Oh Thank you Lord..Kile 

nilichokisema na hatimaye kimekuwa 

kweli.” Akawaza Pauline huku akihisi 

furaha ya ajabu sana kwa kile 

alichokisikia. 

 “ David nina hakika sasa utakuwa 

umejifunza .Siku nyingine ukiambiwa 

kwamba hapa kuna moto basi 

usikimbilie.Yatakukuta kama 

yaliyokukuta kwa Tamia.Yule ni rafiki 

yangu toka muda mrefu tukiwa shule 

ninamfahamu vizuri kuliko mtu mwingine 

yeyote na ndiyo maana nikawa mkali sana 

na kumtaka hata asikuzoee lakini 

ukanipuuza na matokeo yake ndiyo 

hayo.Anyway tuachane na hayo mambo 

kwani hata tukiongea sana hayatusaidia 

kitu tena.Ninachoshukuru ni kwamba 

umenipa funzo kubwa na ninathubutu kukiri kwamba umenifumbua akili yangu 

kwa kiwango kikubwa sana.Kama 

usingenifanyia vile nisingeweza kuwa na 

wazo la kuondoka hapa Arusha na akili 

yangu isingefunguka.Lakini ulinifanya 

nikaondoka na nimekwenda mahala 

nimejifunza maisha mapya na nimepata 

mawazo mapya ya maisha .Kwa kifupi 

ninaweza kusema kwamba I’m not a cry 

baby anymore.I know how to fight now 

and above all I’m happy.”akasema Pauline 

 “ Ninafurahi kusikia hivyo kwa 

sababu hilo ndilo lilikuwa ombi langu 

kubwa kwamba uwe na masha mazuri na 

yenye furha.” Akasema David 

 “ David badala ya kukulaumu mimi 

ninasema ahsante sana kwani machozi 

niliyoyadondosha kwa ajili yako 

yamegeuka asali na ninailamba kwa 

furaha kubwa.thank you david..”akasema 

Pauline na mara simu ya Alfred aliyokuwa 

nayo Paulineikaanza kuita.Aliyepiga 

alikuwa ni mke wake.Pauline akaitazama 

simu ile ikiita aliogopa sana. 

 “ Grace anapiga .Hapana siwezi 

kuipokea simu hii.Sitaki Grace ajue kama 

mimi na mumewe tuko pamoja “ akawaza 

Pauline na simu ikaita na kukata bila kupokelewa.Ikapiga kwa mara ya pili bila 

kupokelewa. 

 “Mbona hupokei hiyo simu” akauliza 

David 

 “ Hii ni simu ya rafiki yangu aliyeko 

ndani ya chumba cha upasuaji 

akiwahudumia wale majeruhi.”akasema 

Pauline kisha akaiweka simu ile ya Fred 

katika yake . 

 “ Mchana uliniambai kuna suala 

zito.what is it? Can you tell me now? 

akauliza Pauline 

 “ Ni kweli pauline kuna jambo kubwa 

lakini hapa si mahala pake pa 

kuliongelea.kesho tutapata muda mzuri 

wa kukaa na kupanga kuhusu jambo hilo.” 

 “ kwa nini hatuwezi kuongea sasa 

hivi? akauliza Pauline 

 “ Pauline usijali tutaongea kesho.Ni 

suala linalohitaji utulivu mkubwa” 

akasema David kisha wakaendelea 

kusubiri 

 Saa sita na dakika nane Alfred na 

Sanya wakiwa wameongozana na baadhi 

ya madaktari wa hospitali ya mount meru 

wakatoka ndani ya chumba cha 

upasuaji.Madaktari wale wa Mount Meru 

wakawashukuru akina Alfred kwa msaada mkubwa waliojitolea.Pauline akawafuata 

akawapokea 

 “ hallow Fred.What happened” 

akauliza Pauline 

 “ Ilikuwa ni ajali mbaya 

sana.Mwanamama ameumia sana 

tumelazimika kumkata miguu yote kwani 

mifupa ilisagika sana na isingewezekana 

kabisa kuungwa tena .Mkono mmoja pia 

umekatwa .mwanaume pia amepoteza 

miguu yote miwili“ 

 “ I’m so sorry”akasikitika sana 

pauline 

 “By the way this is David my 

brother.” Pauline akamtambulisha David 

kwa akina Fred 

 “ David hawa ni marafiki zangu.Huyu 

anaitwa Dr Fred na huyu hapa anaitwa Dr 

Sanya.Fred ni daktari wa moyo katika 

hospitali ya KCMC na Dr Sanya ni daktari 

wa mifupa anatokea nchini marekani.” 

 David akasalimiana na Fred kisha 

akamgeukia Sanya wakasalimiana 

 “ ouh mygosh ! what a beautifull 

woman…I’ver seen such ana angel !! 

akawaza david akimkodolea macho sanya. 

 Pauline akawaongoza Alfred na Sanya 

katika gari ,David naye akaelekea katika 

gari lake wakaondoka  “ Sanya !!..what a beautifull 

woman.Sifahamu ni kwa nini nimestuka 

sana baada ya kumuona .Yawezekana ni 

kwa sababu ya uzuri wake. Nimekutana 

na wanawake wengi wazuri lakini huyu 

amepitiliza.Ameustua moyo wangu 

ghafla”akawaza David akiwa ndaniya gari 

wakielekea nyumbani. 

Walifika nyumbani kwa akina 

Pauline,David aliyekuWa ametanguliA 

mbele na gari lake akshUka na kufungua 

geti ,Pauline na wageni wake wakaingia 

kisha akawafuata na kuwakaribisha ndani 

.Chakula kikaandaliwa wakala na kwa 

kuwa walikuwa wamechoka sana wote 

wkahitaji kwenda kupumzika. Alfred 

akapelekwa katika chumba 

kilichoandaliwa maalum kwa ajili 

yake,Sanya akaenda kulala na Pauline. 

 ”Pauline chumba chako kizuri sana” 

akasema Sanya 

 “ Ahsante sana Sanya.Jisikie 

nyumbani.” Akasema Pauline.Sanya 

akamuomba Pauline wapige magoti wasali 

sala fupi kabla ya kulala.Pauline akakubali 

wakasali sala fupi ikiwa ni pamoja na 

kuwaombea majeruhi wale wa ajali 

uponaji wa haraka.  “ Tukiwa pale katika chumba cha 

upasuaji kuna watu wengine wawili 

waliingizwa kwa ajili ya upasuaji wa 

dharua nao pia wamepata 

ajali,inaonekana Tanzania kiwango cha 

ajali ni kikubwa sana” akasema Sanya 

 “ Ni kweli Sanya.Ajali hapa nchini 

kwetu zinapoteza maisha ya watu wengi 

sana.Vipi Marekani kiwango cha ajali ni 

kikubwa? 

 “ kwa marekani magari ni mengi 

sana ukilinganisha na huku na ajali pia 

zipo lakini si kwa kiwango hiki.Hapa 

nilipo nina zaidi ya mwaka mmoja 

sijahudumia mgonjwa wa ajali aliyeumia 

kama hawa wa leo.Ajali zipi ndogo ndogo 

naza kawaida.Hawa majeruhi wa leo 

wameumia kiasi cha kutisha 

sana.Ninawahurumia hasa Yule 

mwanamke kwa kupoteza miguu yake 

yote miwili na mkono wake mmoja.Sijui 

maisha yake yatakuwaje baada ya ajali 

ile.” Akasema Sanya 

 “ Inasikitisha sana” akasema Pauline 

 “ Tuachane na hayo.Kwa nini 

hujalala chumba kimoja na Alfred wakati 

ninyini wachumba? Akauliza 

Sanya.pauline akatasamu na kusema  “ Ndiyo ni wachumba lakini kwa mila 

za kwetu hairuhusiwi kulala pamoja hadi 

hapo mtakapofunga ndoa na ndiyo maana 

Alfred ameandaliwa chumba chake peke 

yake.Vipi kuhusu wewe una mchumba? 

Akauliza Pauline 

 “ Hapana sina mchumba 

bado.Sehemu kubwa ya maisha yangu 

nimeitumia katika masomo na sikuwa 

nikihitaji kujiingiza katika mapenzi 

.Historia yangu ilinifanya nielekeze nguvu 

zote katika masomo na kuyajenga kwanza 

maisha yangu na kuachana kabisa na 

michezo hiyo ya mapenzi.Nilitaka 

nisimame mwenyewe kwa miguu yangu 

na siku moja niweze kuja kuwatafuta 

wazazi wangu na kama ni masikini basi 

niweze kuwaondoa katika lindi la 

umasikini.” Akanyamaza kidogo akafikiri 

halafu akamtazama Pauline na kuuliza 

 “ Pauline una hakika ninaweza 

kufanikiwa kweli kuwapata wazazi 

wangu? . 

Pauline akainuka akamshika bega na 

kusema 

 “ Usijali utawapata wazazi wako 

Sanya.Kama bado wako hai nina hakika 

kabisa kwamba utawapata.Jambo la msingi ni kumtanguliza Mungu mbele na 

kila kitu kitafaniwa” akasema Pauline 

 “ Ahsante sana kwa kunipa moyo 

Pauline japokuwa kuna nyakati ninakata 

tamaa kama ninaweza kuwapata wazazi 

wangu ndani ya watu milini arobaini na 

tano wa Tanzania.” Akasema Sanya 

 “ Sanya usikate tamaa hata 

kidogo.Niamini nikwambiavyo kwamba 

utawapata wazazi wako” akasema Pauline 

 “ Pauline unanifurahisha sana kwa 

namna unavyojiamini.” Akasema Sanya 

 “ Sanya katika maisha haya lazima 

ujiamini katika kila jambo .Nimejifunza 

kuhusu faida za kujiamini kwa hiyo 

usihofu kesho asubuhi tutakwenda 

kwanza hospitali kujua maendeleo ya 

wagonjwa wetu wale na halafu tutaelekea 

usa river kuanza harakati za mwanzo za 

kuwatafuta wazazi wako” akasema 

Pauline 

 “ Ahsante sana Pauline.Yule kaka 

yako anaitwa nani ? Nimemsahau jina” 

 “ Anaitwa David..” 

 “ Ouh ! jina zuri sana David.Naye 

tutaambatana naye kesho? 

 “ Sina hakika kama ataambatana 

nasi.David ni mtu mwenye kazi nyingi 

sana.Yeye ndiye msimamizi wa biashara zetu zote kwa hiyo ni mtu mwenye 

shughuli nyingi kila wakati.” Akasema 

pauline 

 “ Nimempenda kwa namnaalivyo 

mcheshi na mwenye adabu 

nyingi.Ametupokea na kutuhudumia 

vizuri sana.Mke wake atakuwa na bahati 

sana ” akasema Sanya.Pauline 

akatabasamu 

 “ David bado hajaoa “ akasema 

Pauline.Sanya akaonyesha mshangao 

 “ Wewe hutaki kuolewa na yeye 

hataki kuoa,mnasubiri nini wakati mna 

kila kitu ? Wewe tayari una mchumba 

nayeye pia nina hakika tayari ana 

mchumba.Wakati ni huu Pauline” akasema 

Saya.Pauline hakujibu kitu zaidi ya 

kucheka 

 “ Sanya anaonekana kuanza 

kuvutiwa na David.Nilimuangalia toka 

tukiwa sebuleni namna alivyokuwa 

anamuangalia.Inaonekana wazi kabisa 

kwamba amevutiwa naye.Ni afadhali 

David akawa na sanya kuliko kuwa na mtu 

kama Tamia.Nimefurahi san akusikia 

kwamba wamekorofishana na 

Tamia.Natamani sana kama angempata 

Sanya lakini David ninamfahamu ni mtu 

asiye na msimamo hata kidogo .Anaweza akamuumiza sana mtoto wa watu ambaye 

bado hajaingia katika ulimwengu wa 

mapenzi n kuyafahamu mateso yake” 

Akawaza Pauline 

 Mara tu Alfred alipoingia chumbani 

simu yake ikaita.Alikuwa ni mke wake 

aliyepiga.Fred akasita kuipokea lakini 

mwishowe akaamua kuipokea 

 “ Hallow Grace my love” akasema 

Fred 

 “ Hallow Fred..unaendeleaje? 

Nilikupigia simu lakini 

hukupokea.Nilitakanihakikishe kama uko 

salama kwani nilipata taarifa za kutokea 

kwa ajali mbaya usiku huu” 

 “ Nilikuwa katika chumba cha 

upasuaji uliponipigia.Ajali hiyo 

unayoisema ilitokea kwa gari lililokuwa 

mbele yetu ambalo liligongana na gari 

kubwa la mizigo ikatulazimu kuwachukua 

majeruhi na kuwawahisha katika hospitali 

ya Mount Meru kwa matibabu kwani hali 

zao hazikuwa nzuri.Baada ya kufika 

hospitali ikanilazimu kuungana na 

madaktari wa Mount Meru kuwafanyia 

majeruhi upasuaji kwa hiyo ulipopiga 

nilikuwa katika chumba cha upasuaji 

,simu alikuwa nayo Pauline.”  “ Simu alikuwa nayo 

Pauline?!!!!...akauliza Grace na kumstua 

sana Fred 

 “ Mungu wangu ! nimejisahau 

nimeharibu kila kitu” akawaza Alfred 

 “ Fred !! akaita Grace kwa ukali 

 “ Unasema simu alikuwa nayo 

Pauline yupi? Akauliza Grace 

 “ Picha imekwisha ungua hakuna 

namna nyingine ya kufanya zaidi ya 

kumueleza ukweli kwamba niliongozana 

na Pauline.Nimekwisha haribu kila 

kitu”akawaza Fred. 

 “ Grace utanisamehe mke wangu 

sikukjtaarifu kama katika safari hii 

niliongozana na Pauline .Aliposikia nina 

safari ya Arusha akaomab tongozane wote 

kwanihata naye alikuwa na safari ya kuja 

hku ” akasema Alfred.Kikapita kimya 

kidogo Grace akasema 

 “ Ok kwa sasa uko wapi?Hotelini au 

bado uko hospitali? 

 “ Kwa sasa niko nyumbani kwa 

akina Pauline.Wana nyumba kubwa kwa 

hiyo ameniomba nifikie kwao.” akasema 

Alfred.Kikapita tena kimya cha sekunde 

kadhaa Grace akasema 

 “ Fred unakumbuka wakati unaniaga 

uliniambia kwamba una dharura ya kwenda Serian hospital kuna upasuaji wa 

dharura unafanyika usiku huu.Sasa mbona 

upo kwa akina Pauline badala ya seriani 

katika upasuaji? 

 “ Upasuaji ule umeahirishwa hadi 

kesho” akajibu Alfred na kumfanya Grace 

aangue kicheko 

 “ Haya Ahsante sana Fred.Nakutakia 

usiku mwema na kazi njema.Ninakupenda 

sana” akasema Grace na kukata 

simu.Alfred bado aliendelea kuishikilia 

simu 

 “ Dah ! ama kweli siku ya kufa nyani 

miti yote huteleza.Imekuaje nikajisahau 

na kumtaja Pauline? Nimeharibu kila kitu 

na Grace tayari amekwisha pata 

kithibitisho tosha kwamba mimi nina 

mahusiano na Pauline.Nimefanya kosa 

kubwa na sijui nitamweleza nini Grace 

aweze kunielewa.” Akawaza Alfred akiwa 

ameinamisha kichwa 

 “ Nimekwisha haribu ninatakiwa 

kutafuta namna ya kuliweka sawa suala 

hili.Mipango yangu yote tayari 

imevurugika .Hata hivyo natakiwa 

kutafuta namna ya kulimaliza jambo 

hili.Nilimdanganya na ili kuendelea 

kuulinda uongo wangu wa kwanza 

ninalazimika kumdanganya tena.Sifurahii kumdanganya danganya Grace lakini kwa 

aajili ya Pauline niko tayari 

kudanganya.Hata mimi nimechoka na 

maisha ninayoishi na ninahitaji 

uhuru.Ninahitaji mtu ambaye na mimi 

nitampenda kwa moyo wangu wote na 

mtu huyo tayari amekwisha tokea naye ni 

Pauline.Ni wakati wangu na mimi 

kuyafurahia mapenzi.Grace atanisamehe 

lakini itafika wakati itanilazimu 

nimueleze ukweli kuhusu mimi na 

Pauline.” Akawaza Alfred. 

 “ Hizi nyumba zinaficha mambo 

mengi sana ndani yake na ndiyo maana 

watu wanaweza kuona wanandoa 

wakicheka na kufurahi lakini hawajui 

kinachoendelea ndani ya nyumba yao ni 

kitu gani.Mimi na Grace tumekuwa ni 

mfano wa kuigwa kwa namna 

tunavyoonekana katika jamii lakini 

hakuna aneyjua nini kinachoendelea 

ndani mwetu.” akawaza 

 “ Ngoja niachane na mawazo haya 

kwani yataniharibia kabisa mapumziko 

yangu ya mwisho wa wiki ambayo 

nimepanga yawe mazuri sana nikiwa na 

Pauline.Kilichotokea kimekwisha tokea na 

siwezi kurudi nyuma tena” Akawaza na 

kulala 




Taarifa za ajali iliyotokea eneo la 

kikatiti iliyolihusisha gari dogo na lingine 

kubwa la mizigo zilianza kusambaa kwa 

kasi kubwa jijini Arusha hasa kutokana na 

mtu aliyepata ajali ile kuwa ni mtu 

maarufu sana.Tino Magari alifahamika 

mno jijini Arusha.Akiwa katika baa na 

wafanya biashara wenzake wa madini 

Armando rafiki mkubwa wa Tino alizipata 

taarifa hizi za ajali hii na kustuka 

sana.Hakutaka kuziamini taarifa zile moja 

kwa moja hivyo kumlazimu kukimbia hadi 

katika hospitali ya mount Meru ili 

kuthibitisha taarifa zile kama ni za 

kweli.Alithibitisha ni kweli rafiki yake 

alipata ajali mbaya na amepoteza miguu 

yake yote miwili.Alilia sana . 

 Taarifa zikaendelea kusambaa 

karibu kila kona ya jiji.Saa saba na dakika 

kama kumi na nane hivi Robin akapigiwa 

simu na mmoja wa marafiki zake ambaye 

akamfahamisha kwamba mke wake wa 

zamani Vivian amepata ajali mbaya sana 

yeye pamoja na mume wake Tino na hali 

zao ni mbaya sana.Robin hakutaka kuziamini taarifa zile ikamlazimu 

kumpigia simu kamanda wa polisi mkoa 

wa Arusha ambaye ni rafki yake na 

kumuuliza kuhusu habari zile naye 

akamthibitihia kwamba ni kweli Tino 

magari na mke wake Vivian walipata ajali 

mbaya na wamekimbizwa katika hospitali 

ya mkoa ya Mount Meru. 

 “ Sifurahii kilichotokea lakini 

ninaamini hiki ni kibao Mungu 

amewachapa kwa mambo waliyoyafanya.” 

Akawaza Robin kisha akampigia simu 

mwalimu Lucy na kumfahamisha 

kuhusiana na taarifa zile .kwa kuwa 

ilikuwa ni usiku sana wakapanga kwamba 

siku ya kesho waende wakawatazame 

Tino na Vivian hospitali. 

********************* 

 Siku ya jumamosi ilianza vizuri 

sana.Asubuhi hii kiubaridi kilikuwa kikali 

kama kawaida ya jiji la Arusha..David 

aliamka asubuhi na mapema na kuwahi 

kazini kama ilivyo kawaida yake na 

kuwaacha watu wote wamelala.Dakika 

chache tu baada ya kuondoka Vicky 

madhahabu akaamka na kwenda kugonga chumbani kwa David lakini hakuwepo 

akamfuata msichana wa kazi akamuuliza 

kama amemuona David akataarifiwa 

kwamba alikwisha ondoka kitambo sana 

 Taarifa za kurejea kwa Pauline 

hazikuwa taarifa nzuri kwake.Zilimtesa 

usiku kucha na kumnyima usingizi. 

 “ Nina bahati mbaya sana na huyu 

mtoto.Kitu gani kimemrudisha? Akajiuliza 

Vicky 

 “ Lakini hata kama akirejea hakuna 

kitakachoharibika.Kila kitu kitaendelea 

kama kilivyopangwa na kama 

ikiwezekana hata yeye anaweza 

akaondolewa kabisa ili kuondoa kabisa 

kila aina ya kikwazo katika mipango 

yangu” akaendelea kuwaza kisha akarejea 

chumbani kwake na kumfuata mzee 

Zakaria kitandani 

 “ Darling,nimefurahi sana kwa 

Pauline kurejea.Alikueleza alikwenda 

wapi kupumzika? Akauliza 

 “ Hakuniambia alikuwa wapi lakini 

alichoniambia kwamba anakuja mara 

moja kuna suala la kibiashara anataka 

kuja kuzungumza na mimi halafu 

ataondoka tena.Amekuja na marafiki zake 

wawili “ akasema mzee Zakaria  Saa mbili za asubuhi Pauline na 

Sanya walikwisha amka.Wakati Sanya 

akijiandaa Pauline akatoka na kwenda 

chumbani kwa Alfred akagonga,Alfred 

akafungua mlango wakakumbatiana kwa 

furaha kubwa na kubusiana. 

 “ How was your night Fred? Akauliza 

Pauline 

 “ Ulikuwa ni usiku mzuri sana japo 

picha za wale majeruhi wa ile ajali 

zilinitesa sana lakini kwa ujumla nimelala 

vizuri sana.Vipi wewe? 

“mimi pia nililala vizuri sana na 

ningefurahi zaidi endapo ningelala nawe 

lakini kwa mazingira ya hapa ndani 

isingewezekana ila usijali tutapata muda 

wa kutosha wa kula bata kabla ya kurejea 

Moshi .Jiandae siku ya leo tuna ratiba 

ndefu .Tutaanzia hospitali,Sanya anataka 

kwenda kuwatazama wale majeruhi wa 

ajali,halafu tutaelekea usa river na kisha 

tukitoka hapo ni mwendo wa kula bata 

mpaka jioni”akasema Pauline kisha 

akatoka na kurejea chumbani kwake 

akajiandaa kisha wote kwa pamoja 

wakajumuika mezani kwa ajili ya kupata 

mlo wa asubuhi 

 “ David yuko wapi? Akauliza sanya 

wakiwa mezaniwakipata kifungua kinywa  “ David si rahis kumpata mida 

hii.Tayari amekwiha elekea kazini.Baade 

kama tunaweza kumualika kwa chakula 

cha mchana.” akasema Pauline na mara 

akatokea mzee Zakaria akiwa 

ameongozana na Vicky. 

 “ hallo vijana hamjambo? Akasalimu 

mzee Zakaria.Wote wakasimama na 

kumsalimu kwa heshima 

 “ Nimefurahi sana kuwaoneni vijana 

wangu na karibuni sana.Mimi naitwa mzee 

Zakaria ni baba mzazi wa Pauline na huyu 

hapa ni mama yake mdogo Pauline 

anaitwa Vicky.kwa pamoja 

tunawakaribisha a sana hapa nyumbani 

kwetu.Jisikieni nyumbani.Marafiki wa 

Pauline ni watoto wetu pia na 

tunawapenda sana”akasema Zakaria 

 “ Tunashukuru sana mzee”akasema 

Fred 

 “ Baba hawa ni marafiki zangu.Huyu 

anaitwa Alfred ni daktari wa moyo kutoka 

hospitali ya KCMC na huyu hapa ni Dr 

Sanya yeye anatokea Marekani ni daktari 

wa mifupa.” Pauline akafanya 

utambulisho.Mzee Zakaria akafurahi sana 

kukutana na vijana wale .kwa kuwa bado 

ilikuwa ni asubuhi hawakuongea mambo 

mengi wakakubaliana kukutana usiku kwa ajili ya chakula ili wapate nafasi ya 

kuongea mambo mengi zaidi. 

 Kisha pata kifungua kinywa Pauline 

na wageni wake wakaingia garini na 

kuondoka kuelekea hospitali ya Mount 

Meru. 

 “ Familia yako ni wakarimu sana.” 

Akasema Fred wakiwa garini.Pauline 

hakujibu kitu akatabasamu.Hakukuwa na 

maongezi mengi garini hadi walipofika 

hospitali ya Mount Meru .hali za majeruhi 

wale bado hazikuwa nzuri . 

 Kutoka pale hospitali safari ya 

kuelekea Usa river katika kituo cha 

kulelea watoto wadogo kuutafuta ukweli 

kuhusu wazazi wa Sanya ikaanza. 

“ Tunakwenda kufanya nini Usa river? 

Akauliza Alfred 

 “ Tunamsindikiza Sanya kuna kitu 

anahitaji pale Usa river” akasema Pauline 

 “ Pauline nilisahau kukwambia 

.Grace alipiga simu jana usiku” 

 “ Alipiga? Kuna tatizo lolote? 

Akauliza Pauline kwa wasi wasi 

 “ Hakuna tatizo alihitaji tu kujua 

kama niko salama” akasema Fred 

 “ Anafahamu kama mimi na wewe 

tumeongozana kuja Arusha? Akauliza 

Pauline  “ Ilinibidi nimweleze ukweli kwamba 

tumeongozana wote kuja Arusha” 

akasema Fred 

 “ Ouh Fred ! Fred ! Kwa nini 

ulimwambia? Ulifanya kosa kubwa 

sana.Hukupaswa kumueleza jambo 

hilo.Mkeo amekwisha hisi kuna kitu 

kinaendelea kati yetu ,huoni kwamba 

atazidi kuwa na uhakika kwamba hisia 

zake ni kweli mimi na wewe kuna jambo 

linaendelea kati yetu? Akasema Pauline 

 “ Usihofu kuhusu hilo Pauline.Hata 

kama akigundua hataweza kunirudisha 

nyuma.Nimekwisha aamua kuwa na wewe 

na hakuna wa kuubadili msimamo 

wangu.” Akasema Alfred.Pauline 

akamtazama akatabasamu na kusema 

 “ Fred inaonekana hujawahi 

kuumizwa na mapenzi na hujawahi 

kutendwa ndiyo maana unadiriki kusema 

hivyo.Grace akigundua kwamba mimi na 

wewe tuna mahusiano ataumia 

sana.Nakwambia Fred maumivu ya 

kutendwa na mpenzi ni makali kuliko 

maumivu ya kukatwa na kisu na hasa pale 

unapoumizwa na mtu ambaye unampenda 

,unamjali na kumthamini na ambaye 

umemuamini na kumkabidhi moyo 

wako.Ninayasema haya kwa sababu nimeyapitia.Yamenikuta na ninayafahamu 

vyema na ndiyo maana ninakwambia 

kwamba ni mateso makubwa sana .Sitaki 

mateso kama yale yamkute mwanamke 

mwenzangu na kumfanya akate tamaa 

kabisa ya maisha .” akasema Pauline. 

 “ Kumbe kuna mtu amewahi 

kukuumiza Paulne.Kwa nini hjawahi 

kuniambia? Nataka kufahamu ni nani 

huyo ambaye anathubutu kukufanyia 

hivyo malaika kama wewe? Ni mwanaume 

wa aina gani huyo ambaye anaweza 

kuichezea dhahabu hii ya thamani kubwa 

karibu na moto? akauliza Alfred.Pauline 

akatabasamu na kusema 

 “ Tuachane na hayo Fred.Ni mambo 

yaliyopita na imebaki historia.Ila 

ninaogopa sana kumuumiza Grace.Ni 

mwanamke ambaye hastahili kabisa 

kuumizwa kwa namna yoyote ile” 

akasema Pauline 

 “ laiti Pauline angejua ni mateso 

kiasi gani niliyonayo mimi angenionea 

huruma sana wala asingethubutu kusema 

kwamba Grace ataumia akigundua 

kwamba mimi na yeye tuna 

mahusiano.Kuna ule msemo unaosema 

kwamba ukisema unaumwa halafu 

ukakutana na wanaoumwa kweli kweli basi utapona bila hata dawa.Pauline 

anadai ameumizwa lakini angejua namna 

nilivyoumizwa mimi angenionea huruma 

sana..” Akawaza Alfred 

 “ Itabidi mnifundishe Kiswahili ili na 

mimi nisikie kile 

mnachokiongea.Kiswahili inaonekana ni 

lugha tamu sana.Naangalia namna nyuso 

zenu zilivyo na tabasamu mkiongea na 

ninatamani sana kufahamu 

mnachokiongea “ akasema Sanya ambaye 

muda mwingi alikuwa kimya akiwasikiliza 

akina Pauline wakiongea bila kujua 

wanaongea nini 

 “ Usijai Sanya tutakufundisha 

Kiswahili .Ni lugha nyepesi sana kujifunza 

na kuielewa “ akasema Pauline.Safari 

ikaendelea kimya kimya 

 Walikaribia sana kufika Usa river. 

 “ Sanya tumekaribia sana kufika Usa 

river.je kuna mabadiliko yoyote? Akauliza 

Pauline 

 “ Mabadiliko gani Pauline? Akauliza 

Sanya 

 “ Yawezekana labda ukawa 

umebadili mawazo kuhusiana na hiki 

unachotaka kukifanya” 

 “ Hapana Pauline siwezi kubadili 

mawazo .Nimesafiri kutoka marekani hadi huku kwa ajili ya jambo hili kwa hiyo 

lazima niufahamu ukweli.” Akasema 

Sanya.Pauline akawasha taa ya kushoto 

kuashiria kwamba anatoka njia kuu na 

kuingia katika barabara inayoelekea 

katika kituo cha kulelea watoto wadogo. 

 “ Pauline kwani kuna nini 

kinaendelea? Mbona siwaelewi? Sanya 

anataka kufanya nini? Akauliza Alfred 

 “ Hata nikikueleza sasa hivi 

hutanielewa Fred.Nitakueleza tukipata 

nafasi nzuri” akasema Pauline na 

kupunguza mwendo walipowasili katika 

geti kubwa la kituo hiki.Mlinzi 

akawafungulia geti wakaingia ndani. 

 “ Alfred naomba uendelee kutusubiri 

humu ndani ya gari hatutachukua muda 

mrefu sana” akasema Pauline kisha yeye 

na Sanya wakashuka na kuingia katika 

jengo la utawala. 

******************** 

 Saa nne na dakika kumi na saba 

Robin akawasili ofisini kwa Mwalimu 

Lucy.Hakukuwa na mtu mwingine ofisini 

mle hivyo Robin akapita moja kwa moja  “ Hello my love .Unaendeleaje? 

akauliza Robin huku akimbusu Lucy 

 “ Ninaendelea vizuri sana Robin” 

akasema Lucy.Robin akamshika tumbo na 

kutabasamu 

 “ How is my little prince doing? 

Akauliza na kumfanya Lucy atabasamu 

 “ Umejuaje kama ni mwanaume? 

 “ Hisia zangu zinanituma kwamba ni 

mwanaume.” Akasema Robin 

 “ Can we bet? Akauliza Lucy huku 

akitoa kicheko kidogo 

 “ Yes we can.” Akajibu Rbin 

 “ What if you loose.? 

 Robin akakuna kichwa na kusema 

 “ I’m not going to loose. Ila ikitokea 

hivyo utachagua mwenyewe nini cha 

kunifanya” 

 “ You will be my slave for two weeks 

.Deal? akauliza Lucy 

 “ Deal “ akajibu Robin na wote 

wakacheka. 

 “ Ok tuachane na hayo .Unaendeleaje 

mpenzi? 

 “ Ninaendelea vizuri sana Robin.Ila 

sikuweza kupata usingizi tena baada ya 

kupata taarifa zile za kuhusiana na ajali ya 

Martin na Vivian”  “ Oh my love hutakiwi kukosa 

usingizi kwa ajili ya mtu kama Yule.Nina 

hakika Mungu amempiga kibao kidogo 

yeye na mke wake” akasema Robin 

 “ Robin ninamuonea huruma sana 

Martin na Vivian.Watu wanaielezea ajali 

hiyo kwamba iilikuwa mbaya sana.” 

Akasema Lucy 

 “ Mimi wala sijaumizwa kabisa na 

kilichowapata.Vivian alinifanyia kitu 

kibaya sana mimi na mwanangu na mpaka 

leo hii sijasahau kashfa ,matusi na dharau 

alizozitoa kwangu achilia mbali 

kumtelekeza mwanae ” Akasema Robin 

 “ Hata mimi Martin aliniumiza sana 

ikiwa ni pamoja na kunipiga na kunitolea 

kashfa kibao lakini pamoja na hayo yote 

nmejikuta ninamuonea huruma sana . 

Pamoja na yote aliyokukosea Vivian, lakini 

bado ni mama wa mwanao na mpaka sasa 

anatambulika kama mkeo wa ndoa kwa 

hiyo unapaswa kumuonea huruma na 

kumfariji kwa lililompata.Naomba tuende 

hospitali tukawatazamae”akasema Lucy 

 “ Lucy mida hii si ya kuwatazama 

wagonjwa .Hatutaweza kuruhusiwa 

kuwatazama.Tusubiri mpaka jioni ndipo 

tukajaribu kama tunaweza kupata nafasi 

ya kuwatazama. “ akasema Robin  “ Sawa Robin kama umeamua hivyo. 

Penina anafahamu chochote kuhusiana na 

ajali iliyompata mama yake? 

 “ Hapana bado sijamueleza 

chochote” akasema Robin 

 “ Anatakiwa kufahamishwa ili ajue 

kinachoendelea.” 

 “ Nitamfahamisha jioni ya leo ila kwa 

sasa nimekuja kukuchukua kuna sehemu 

nataka twende” Akasema Robin 

 “ Unanipeleka wapi Robin? 

 “ It’s a surprise .” akajibu Robin 

 “ Ouh Robin unapenda sana 

suprises” akasema mwalimu Lucy huku 

akiinuka akavaa koti lake kisha wakatoka 

mle ofisini wakaingia katika gari la Robin 

na kuondoka. 

********************** 

 Kabla ya kwenda ofisini kwake Vicky 

madhahabu alielekea moja kwa moja hadi 

ofisini kwa Chino kumpelekea kiasi cha 

pesa walichokuwa wamekubaliana kabla 

ya kazi haijafanyika. 

 “ Karibu sana Vicky.Imekuwa vizuri 

umewahi kwani ungechelewa kidogo 

ungenikosa.” Akasema Chino  “ siwezi kuchelewa kabisa katika 

jambo la muhimu kama hili” akasema 

Vicky. 

 “ Umekuja kamili? Akauliza Chino 

 “ Ndiyo Chino.Nimekuja kamili kama 

tulivyokubaliana” akasema Vicky na 

kuliweka mezani sanduku dogo na 

kulifungua.Chino akatoa sigara akaiwasha 

na na kuivuta kisha akapuliza moshi 

mwingi hewani.Akatoa bunda moja na 

kulishika akaziangali noti zile nyekundu 

nyekundu halafu akalichukua sanduku lile 

akalifungia katika kasiki kubwa 

lililokuwamo mle ofisini kwake kisha 

akarejea mezani 

 “ Hutaki kuhakikisha kama ziko 

sahihi? Akauliza Vicky 

 “ Ninakuamini huwezi 

kunidanganya” akasema Chino akavuta 

tena sigara na kusema 

 “ Ahsante Vicky kwa kutimiza 

ahadi.Umeonyesha ni namna gani 

ulivyodhamiria kuhusu jambo 

hili.Ninakuahidi kwamba kila kitu 

kitakwenda kama vile tulivyopanga.Kabla 

ya saa sita za usiku kesho kila kitu 

kitakuwa kimekamilika na utabakiwa na 

utajiri wote” akasema Chino huku 

akipuliza moshi mwingi wa sigara.  “ Nitashukuru sana Chino lakini hata 

hivyo kuna tatizo kidogo limejitokeza.” 

Akasema Vicky 

 “ Tatizo gani Vicky? Akauliza Chino 

 “ Kuna Yule mtoto wa Zakaria 

aliyekuwa amesafiri ,amerejea jana usiku 

akiwa na rafiki zake.” Akasema Vicky 

 “ Unadhani kunaweza kuwa na tatizo 

lolote kwa kurejea kwake? Akauliza Chino. 

 “ Sina hakika kama kunaweza 

kutokea tatizo lolote.Nimeona ni vizuri 

nikakufahamisha ili ufahamu mle ndani 

kutakuwa na watu wangapi” 

 “ Ahsante kwa taarifa hizo lakini 

hicho si kikwazo kabisa kwetu.Kama 

nilivyokueleza awali kwamba sisi 

tunakuja kwa lengo moja tu la kumuua 

mzee Zakaria na kama kutatokea kizingizi 

chochote sisi tutakiondoa.Awe mtoto wake 

au awe nani sisi tutamuondoa”.akasema 

Chino na kumuogopesha Vicky 

 “ Chino kuna Yule kijana mmoja 

anaitwa David tafadhali naomba hata 

iweje msimdhuru.Ni mtu muhimu sana 

kwangu” akasema Vicky 

 “ Kama ni mtu wa muhimu kwako 

basi fanya mpango asiwepo nyumbani 

mida hiyo vinginevyo kama akiwepo na 

akatuletea kigingi sisi tutamvunja hata miguu.Hatuna mchezo tuwapo 

kazini.Tumeelewana? ” akasema Chino na 

kupuliza moshi mwingi 

 “ sawa chino nitajitahidi kufanya kila 

linalowezekana ili David asiwepo 

nyumbani mida hiyo” akasema 

Vicky.Chino akamtazama kwa makini na 

kusema 

 “ So this is it.Kumbuka mzigo wetu 

uliobaki tunauhitaji kesho kutwa baada ya 

kumaliza kazi.” Akasema Chino 

 “ Ninakumbuka Chino siwezi 

kusahau “ 

 “ Good.basi sisi ni wage ni wako 

kesho usiku.Kama kutatokea mabadiliko 

yoyote nitaarifu kabla ya saa sita mchana 

kesho .Baada ya saa sita mchana siku ya 

kesho sintapatikana katika simu tena” 

akasema Chino akaagana na Vicky 

akaondoka zake. 

 “ Mambo yameiva.Hata kama Pauline 

amerejea lakini hakuna 

kitakachoharibika.Kila kitu kitakwenda 

kama kilivyopangwa.Lazima kesho 

Zakaria auawe tu.” Akawaza Vicky akiwa 

garini baada ya kutoka kwa Chino 

 Kama ilivyo kawaida yake moja kwa 

moja baada ya kutoka kwa Chino 

akaelekea kwa shoga yake Safia.  “ Kuna habari mpya Vicky ? akauliza 

Safia 

 “ Kama kawaida angu Safia huwa 

sikosi habari mpya.Nimetoka kuonana na 

Chino na tayari nimempa kiasi cha pesa 

alichokitaka kabla ya kuanza kazi kwa 

hiyo kesho kila kitu kitakamilika.Shoga 

yangu vuta subira kidogo na baada ya siku 

chache sana mambo yetu yatabadilika .” 

 “ Mimi nakuombea heri Vicky 

ufanikiwe kwani ukifanikiwa wewe hata 

mmi pia nimefanikiwa” akasema Safia. 

 “ Ila kuna tatizo limejitokeza 

 “ tatizo gani tena Vicky? 

 “ si tatizo kama tatizo ila linaweza 

kuwa tatizo kama nisipolichukulia kwa 

uzito.Pauline amerejea jana usiku” 

akasema Vicky 

 “ Amerejea? Safia akaonyesha 

kushangaa 

 “ Ndiyo Safia .Amerejea jana usiku” 

 “ Kwa hiyo utafanya nini? 

 “ Hakuna cha kufanya.Kila kitu 

kitakwenda kama kilivyopangwa.Chino 

anasema kwamba ikitokea kama Pauline 

au mtu mwngine yeyote Yule ataonekana 

kuweka kizingiti basi naye pia 

watamuondoa haraka sana kwa hiyo 

Pauline naye kama akitaka kuleta kujua kwake naye pia ataondolewa vile vile“ 

akasema Vicky huku akitabasamu na 

kuendelea 

 “ Ila nimemuonya kuhusu David 

kwamba kwa namna yoyote ile hatakiwi 

kuguswa kwani mpango huu wote ni kwa 

ajili yake.”akasema 

 “ Basi tuombe kila kitu kiende kama 

kilivyopangwa na maisha yetu yabadilike” 

akasema Safia 

 “ Usihofu shoga yangu.Maisha yetu 

yatabadilika muda si mrefu sana.Basi 

mimi naomba niondoke nielekee dukani 

kwani sikuwa nimepita hata dukani” 

akasema Vicky na kuagana na Safia 

akaondoka 

 “ Shetani mkubwa we,hutafanikiwa 

kabisa katika mipango yako.” Akasema 

Safia baada ya Vicky kuondoka kisha 

akachukua simu yake na kumpigia David 

akamfahamisha kila kitu alichoelezwa na 

Vicky. 

****************** 

 Watu walifurika katika hospitali ya 

mkoa ya Mount Meru ili kuwajulai hali 

papaa Tino magari na mkewe Vivian.Taarifa za ajali waliyoipata 

ziliwastua wengi hivyo kuwafanya wafike 

hapa kutaka kujua maendeleo yao. 

 Pamoja na watu kufika kwa wingi 

bado hakuna aliyeruhusiwa kuingia katika 

vyumba walimolazwa majeruhi kwani 

bado hali zao hazikuwa nzuri. 

**************** 

Pauline na Sanya waliufungua mlango 

mkubwa wa kuingilia katika jengo kubwa 

la utawala la kituo kile kikubwa cha 

kulelea watoto wadogo walioachwa na 

mama zao wakati wa kujifungua ama 

waliookotwa baada ya kutupwa na wazazi 

wao.Walikaribishwa na mwanadada 

aliyekuwapo mapokezi na wakaeleza 

shida yao ya kuonana na mkuu wa kituo 

kile.Waliombwa wasubiri kwa muda 

kwani mkurugenzi wa kituo kile alikuwa 

amekwenda katika nyumba ya malezi 

kuwaona watoto. 

 Baada ya dakika kumi akaingia 

mama mmoja mnene akatambulishwa 

kwamba ndiye mkurugenzi wa kituo kile 

na akawakaribisha akina Pauline ofisini 

kwake.  “ karibuni sana katika kituo 

chetu.Niwasaidie nini? Akauliza Yule 

mama 

 “ Mama mimi ninaitwa Pauline na 

huyu mwenzangu anaitwa sanya.Mimi ni 

mwenyeji wa Arusha na mwenzangu yeye 

anatokea nchini Marekani.Kuna jambo 

kubwa ambalo limetuleta hapa” akasema 

Pauline 

 “ Ndiyo Pauline.Ni jambo gani hilo? 

 “ Jambo lenyewe linamuhusu huyu 

mwenzangu nadhani itakuwa vyema kama 

akikuelezea yeye mwenyewe japokuwa 

hajui Kiswahili.” Akasema Pauline na 

kumwambia Sanya aeleze tatizo lake. 

 “ Kama Pauiline alivyosema ninaitwa 

Sanya na ninatokea nchini Marekani.Ni 

raia wa Marekani lakini asili yangu ni 

Tanzania.Mlezi wangu ambaye amenilea 

toka nikiwa mdogo aliwahi kuishi hapa 

Tanzania kwa miaka kumi na aliwahi 

kumiliki kituo hiki cha kuelelea watoto 

wadogo hadi alipomaliza muda wake wa 

kuishi hapa nchini na kurejea Marekani.” 

Akanyamaza kidogo na kuendelea. 

 “ Sikuwa nimefahamu kuhusu 

historia yangu hadi pale nilipokuwa 

mkubwa kabisa ndipo mama mlezi 

aliponieleza ukweli kuhusiana na asili yangu.Aliniambia kwamba niliokotwa 

katika geti la kituo hiki baada ya 

kutelekezwa na mzazi wangu nikiwa bado 

mdogo sana na inakadiriwa nilikuwa na 

umri wa kati ya wiki moja au mbili na 

nikaanza kutunzwa hapa.Kwa bahati nzuri 

mama mlezi na familia yake walitokea 

kunipenda na walipoondoka kuerejea 

Marekani wakanichukua nikaondoka nao 

na hadi leo ninaishi Marekani na ni raia 

wa kule.” Akanyamaza kidogo kama ilivyo 

kawaida yake kuongea kwa vituo halafu 

akaendelea. 

 “ Kwa miaka kadhaa sasa baada ya 

kuufahamu ukweli kuhusu asili yangu 

nilikuwa ninatafakari jambo hili kwa 

undani na mwaka huu nimeamua kuja 

Tanzania ili kujaribu kutafuta bahati kama 

ninaweza kuonana na wazazi wangu kwa 

hiyo nimeona sehemu ya kwanza ambayo 

nimeona inaweza kunifaa kuanzia ni hapa 

mahala ambako ndiko niliokotwa na 

kulelewa.Nina hakika mtu aliyenitupa 

ambaye sifahamu kama ni mama yangu au 

ni nani baada ya kujitafakari anaweza 

akagundua kwamba alifanya kosa na 

akaamua kutaka kufahamu kama mtoto 

aliyemtupa yu hai ama vipi kwa hiyo 

sehemu ya kupata taarifa hizo ni hapa pekee.Ninatumai umenielewa na unaweza 

ukanisaidia kufuatilia katikakumbu 

kumbu zenu kama kama kuna kuna mtu 

yeyote amewahi kuja hapa kuulizia mtoto 

aliyetelekezwa” akasema 

Sanya.Mkurugenzi akavua miwani yake na 

kuchukua kitambaa akayafuta macho yake 

ambayo yalionekana kuloa machozi. 

 ” Sanya historia yako imenifanya 

nitoe machozi kwa sababu mtu aliyefanya 

kitendo hiki cha kukutupa alifanya 

kitendo kibaya sana na hakujua kama siku 

moja unaweza ukawa namna hii.Jangalie 

sasa ni msichana mkubwa na mrembo 

sana.Nina hakika hata yeye mwenyewe 

akikuona sasa hivi anaweza asiamini 

kama ni wewe Yule ambaye alikutupa 

getini.” Akasema mkurugenzi kisha 

akavaa miwani yake 

 “ Sanya karibu sana Tanzania,karibu 

sana nyumbani.Ninakupongeza sana kwa 

uamuzi wako wa kuamua kuja Tanzania ili 

kuitafuta asili yako na kuwatafuta wazazi 

wako.Huu si uamuzi rahisi kuufanya hasa 

ukikumbuka kwamba mzazi wako 

alikutupa wakati huo lakini pamoja na 

kitendo hicho alichokifanya bado 

umeamua kumtafuta na kuungana 

naye.Nakupongeza sana na ninakuahidi kukuunga mkono na kukupa kila aina ya 

ushirikiano hadi nihakishe kwamba 

umefanikiwa kumpata mzazi wako.” 

Akasema mkurugenzi 

 “ Nitashukuru sana mama” akajibu 

Sanya 

 “ Lakini pamoja na hayo ni miaka 

mingi sasa imekwisha pita toka mlezi 

wako alipoondoka na baada yake kituo 

hiki kumekuwa na wamiliki kadhaa kwa 

hiyo kupata kumbu kumbu za nyuma 

inakuwa ngumu sana.Kinacholeta ugumu 

zaidi ni kwamba jengo hili la utawala 

liliwahi kuungua moto na kuteteketeza 

kila kilichokuwemo .Ni sisi ambao 

tulilikarabati na kuanza tena kulitumia 

kwa hiyo hatuna kabisa kumbu kumbu 

yoyote ya nyuma tuliyonayo.” Akasema 

mkurugenzi. 

 Kauli ile ikaonekana 

kumnyong’onyeza kabisa Sanya na ni wazi 

alikata tamaa. 

 “ hakuna tena tumaini “ Sanya 

akamwambia Pauline 

 “ lakini kuna jambo lingine ambalo 

sina hakika sana kama linaweza kuwa na 

msaada” akasema mkurugenzi. 

 “ Tueleze mama linaweza kuwa na 

msaada “ akasema Pauline  “ Zimepita wiki kadhaa sasa walikuja 

hapa watu wawili ambao walikuwa 

wanatafuta taarifa za mtoto ambaye 

historia yake inafanana na ya kwako 

Sanya.Walidai kwamba kuna ndugu yao 

aliwahi kumtelekeza mtoto katika geti la 

hapa kituoni na akakimbia kwa hiyo 

wamekuja kutafuta taarifa za mtoto 

huyo.Nao pia niliwaeleza kama 

nilivyowaleza ninyi kwamba kuna ugumu 

wa kupata kumbu kumbu za nyuma ” 

akasema mkurugenzi 

 “ Ouh Ahsante Mungu..Ni akina nani 

hao? Unafahamu mahala walipo? Akauliza 

Sanya 

 “ Sanya ninapatwa na ugumu kidogo 

wa suala hili kwa sababu ipo tabia ya 

wazazi ambao hawataki kulea watoto wao 

ama kutokana na uwezo au sababu 

nyngine huja na kuwatelekeza katika geti 

la kituo chetu.Tunao watoto zaidi ya 

watano sasa ambao tumewaokota 

wametelekezwa katika geti letu.Kwa hiyo 

sina hakika kama mtoto waliyekuwa 

wakimtafuta ni wewe au kuna wengine 

ambao nao walitekekezwa getini wakati 

huo.”  “ Unawafahamu watu hao mahala 

walipo? Waliacha kumbu kumbu zao? 

Akauliza Sanya 

 “ Sifahamu mahala waliko wala sina 

mawasiliano yao lakini niliwaelekeza kwa 

mama mmoja ambaye amewahi kufanya 

kazi katika kituo hiki kwa miaka mingi 

sana ambaye kwa sasa ni mtu mzima sana 

na anasumbuliwa na maradhi.Sifahamu 

kama walifanikiwa kuonana naye na 

aliwaambia nini kwani hawajawahi 

kurejea tena hapa” akasema mkurugenzi 

 “ Huyo mama anaishi wapi ? 

Unaweza kutuelekeza tukamuone? 

yawezekana akawa na taarifa zinazoweza 

kutusaidia kuwapata wazazi wangu.Kama 

amefanya kazi hapa kwa muda mrefu 

yawezekana kuna mambo anaweza 

kuyafahamu yanayoweza kunisaidia 

kuwapata wazazi wangu.” akasema Sanya 

 “ninaweza kuwapelekea hadi mahala 

anakoishi kwani kwa kuwaelekeza 

mnaweza mkapotea” 

 “ Tutashukuru sana mama kwa 

msaada wako” akasema Pauline kisha 

mkurugenzi akaongozana nao wakaingia 

garini na kundoka kuelekea nyumbani 

kwa Bi Elizabeth ambaye aliwahi kufanya 

kazi katika kitu hiki kwa miaka mingi.  “ Kwa nini huku Tanzania vitendo 

vya utupaji watoto vimeshamiri sana? 

Akauliza Sanya wakiwa garini 

 “ Kuna sababu nyingi zinazopelekea 

watu kuamua kuwatupa watoto wao 

lakini kubwa ni mimba zisizotarajiwa.Hiki 

ni chanzo kikubwa cha wazazi kuamua 

kuwatupa watoto wao kwani 

wanapojifungua wanajikuta hawana 

uwezo wa kuwahudumia watoto wao kwa 

hiyo huamua kuwatupa.Wengine huenda 

mbali zaidi na kuamua kuwaua kabisa 

watoto na kuwatupa jalalani” akasema 

Mkurugenzi 

 “ Hakuna elimu ya uzazi inayotolewa 

mashuleni au hata kwa wale ambao 

wamekosa elimu ya darasani ? akauliza 

tena Sanya 

 “ Elimu ya uzazi inatolewa mashuleni 

lakini nadhani inahitaji kutiliwa mkazo 

zaidi ili iwafikie watu wengi hususan 

wale ambao hawakupata bahati ya 

kwenda shule” akasema Mkurugenzi. 

 “ Nimeguswa sana na suala hili na 

pengine nikirudi marekani ninaweza 

nikafanya kitu Fulani kwa ajili ya kusaidia 

kutoa elimu ya afya ya uzazi mashuleni 

n.k.Inawezekana kabisa kwamba wengi 

wa wanaofanya hivi wanakosa elimu sahihi ya masuala ya uzazi na mahusiano” 

akasema Sanya 

 “ Pamoja na ukosefu wa elimu ya 

uzazi “ akasema Alfred ambaye muda 

mwingi alikuwa kimya 

 “ Umasikini wa kipato nao una 

mchango mkubwa sana kwa watu 

kuwatupa ,kuwaua ama kuwatelekeza 

watoto wao.Hata kama mama amepata 

elimu ya uzazi ikatokea labda amepata 

mimba bila kukusudia mfano kwa 

kubakwa ama sababu nyingine na 

akajifungau mtoto huku akiwa hana 

uwezo wa kumtunza Yule mtoto wengi 

suluhisho lao huwa ni kuwatupa ama 

kuwaua watoto wao.” Akasema Alfred 

 “ Dr Alfred ameongea kitu cha msingi 

sana kwamba yawezekana umasikini wa 

kipato unachangia kwa kiwango kikubwa 

sana kwa tabia hizi za utupaji watoto 

kuota mizizi.Inawezekana hata mama 

yangu alinitupa kutokana na sababu kama 

hiyo ya umasikini” akasema sanya 

 “ Sanya unasema kwamba mama 

yako alikutupa? Akauliza Fred kwani 

hakuwa akifahamu chochte 

 “ Ndiyo Dr Alfred .Mama yangu 

alinitelekeza katika geti la kituo kile 

tulichotoka na ndiyo maana nimekuja Tanzania kutaka kuitafuta asili yangu na 

kuwafahamu wazazi wangu.Pauline 

hajakwambia? 

 “ hapana Pauline hajanieleza 

chochote.Pole sana.” Akasema Alfred 

 “ hakuna haja ya kunipa 

pole.Tunatakiwa kumshukuru Mungu kwa 

kuniweka hai mpaka hii leo kwani katika 

makuzi bila ya mama mengi yangeweza 

kutokea lakini kwa uweza wake mimi 

hapa leo hii nina afya njema kabisa ,nina 

jitegemea mwenyewe,nina elimuya 

kutosha na zaidi ni mrembo si ndiyo? 

Akasema Sanya na wote ndani ya gari 

wakacheka. 

 “ Mungu ana njia nyingi za kukuinua 

ndiyo maana baada ya kutafakari kwa 

miaka mingi nimemsamheme mama 

yangu kwani yawezekana Mungu ana 

mipango na mimi na alitaka nipite njia hii 

ili aweze kunitumia kwa mipango yake na 

sasa ninaanza kuona kitu ambacho Mungu 

anataka nikifanye kwa watu wake. “ 

akasema Sanya.Wote ndani ya gari 

wakawa kimya wakimsikiliza 

 “ Hata kama nisipowafanikiwa 

kuwapata wazazi wangu ,Lazima nirudi 

Afrika,lazima nirejee Tanzania kuna mambo mengi ambayo natakiwa 

kuyafanya huku” 

 Maongezi yalikuwa mengi ndani ya 

gari na hatimaye wakajikuta wamefika 

nyumbani kwa Bi Elizabeth kaaya mama 

ambaye amefanya kazi katika kituo kile 

kwa miaka mingi toka usichana wake hadi 

alipokuwa mzee. 

 Walishuka garini na kwenda kubisha 

hodi wakakaribishwa ndani na mama 

mmoja wa makamo. 

 “ Sisi tunatoka katika kituo cha 

malezi ya watoto ambako Bibi Elizabeth 

amefanya kazi kwa miaka 

mingi.Tunashida naye kubwa” akasema 

mkurugenzi 

 “ Elizabeth ni shangazi yangu na kwa 

bahati mbaya hamtaweza kuonana naye 

kwa sasa kwani ana siku ya tano leo 

amelazwa hspitali anaumwa sana na hali 

yake si nzuri hata kidogo.Anasumbuliwa 

na figo” akasema Yule mama .Sanya 

akashika kichwa ,taarifa ile ilimkatisha 

tamaa kabisa.Hakukuwa tena na namna 

nyingine ya kufanya zaidi ya kuondoka 

pale na kuelekea katika hospitali ambako 

Elizabeth alikuwa amelazwa. Kabla 

hawajatoka mle ndani Sanya akavutiwa na 

picha zilizokuwa juu ya kabati akaainuka na kuanza kuzitazama.Akaiona picha moja 

iliyomvutia akaichukua akaitazama na 

kutabasamu 

 “ Huyu ndiye Elizabeth? Akauliza 

 “ Ndiye mwenyewe” akajibu 

mkurugenzi 

 “ Basi huyu aliyepiga naye picha hii 

ndiye mama yangu mlezi” wote 

wakaitazama picha ile ambayo Elizabeth 

alipiga na mama mmoja wa kizungu kisha 

wakaondoka kuelekea hospitali 

 “ Sanya usikate tamaa tafadhali 

.Tumtangulize Mungu mbele katika suala 

hili na kama ni mapenzi yake basi 

atafanikisha jambo hili” akasema Fred. 

 Elizabeth alikuwa amelazwa katika 

hospitali ya mkoa ya Mount Meru .Kwa 

muda waliofika hali ya Elizabeth ilizidi 

kuwa mbaya zaidi iliyowaogopesha hadi 

ndugu zake na walikata tamaa 

kabisa.Baada ya kuiona hali ile Sanya 

alikata tamaa ya kuweza kupata taarifa 

zozote kuhusiana na wazazi wake kwani 

mtu aliyemtegemea labda angeweza 

kumpa mwanga hakuweza kufumbua hata 

macho.Walirejea mahala walikoegsha gari. 

 “ Tayari nimekata tamaa ya 

kuwapata wazazi wangu.kwa hali ya Elizabeth ilivyo sina hakika kama anaweza 

akapona.” Akasema Sanya 

 “ usiseme hivyo Sanya na wala 

usikate tamaa.Mungu ni muweza na 

Elizabeth anaweza akapona” 

 “ Mimi ni daktari na ninafahamu mtu 

ambaye hawezi kupona.Mpaka hapa 

nadhani nimeshindwa .Kilichobaki ni 

mimi kujipanga upya kwa mambo 

mengine “ akasema Sanya 

 “ Kwa nini tusitumienjia ya 

matangazo? Akauliza Fred 

 “ Ukitangaza leo hii wanaweza 

wakatokea wanawake zaidi ya elfu moja 

na likaanza tena zoezi la kupima vinasaba 

na unaweza ukafanya zoezi hilo ambalo 

litagharimu muda na mwisho wa siku 

ukashindwa kumpata mama 

yako.Nadhani tukubali kwamba mpaka 

hapa hakuna tena namna nyingine ya 

kufanya.Kuungana tena na wazazi wangu 

ni vigumu sana” akasema Sanya.Ghafla 

Mkurugenzi akakumbuka kitu 

 “ Kuna kitu nimekumbuka !.akasema 

 “ Umekumbuka nini Mkurgenzi” 

akauliza Pauline 

 “ Nimekumbuka kitu.Katika watu 

wale wawli waliokuja pale ofisini 

wakiulizia taarifa za Yule mtoto niliyewaelezeni kuna mmoja 

alijitambulisha kama mmiliki wa shule 

moja kubwa hapa mjini inaitwa St 

Lucia.Nadhani si vibaya kama tukimuona 

na huyu anaweza akawa na msaada 

mkubwa kwetu” akasema mkurugenzi 

 “ Kama uliwaelekeza kwa Elizabeth 

na hawakurejea tena kwako ni wazi 

kwamba hawakufanikiwa kupata 

walichokuwa wanakitafuta.Nadhani 

hakuna haja ya kuendelea kuumiza 

kichwa kwa jambo hili.Si suala rahisi hata 

kidogo .Tuachane nalo na tuendelee na 

mambo mengine.” Akasema Sanya.Pauline 

akamtazama na kusema 

 “ Sanya unakata tamaa mapema 

sana.” 

 “ Pauline suala hili liko wazi kabisa 

kwamba ni gumu na linahitaji muda mrefu 

sana.Kama ningekuwa na viza ya muda 

mrefu ya kuniwezesha kuishi hapa 

Tanzania basi ningejipa moyo kwamba 

ningeweza kuwapata wazazi wangu lakini 

sina muda mrefu sana na isitoshe nina 

kazi zinanisubiri Marekani kwa hiyo zoezi 

hili inabidi lisimame.Lakini siku moja 

nitarejea Tanzania kama nilivyoahidi na 

nitafanya mambo makubwa “ akasema 

Sanya.Pauline na wenzake hawakuwa tenana neno la kuweza kumshawishi Sanya 

.Pauline akawasha gari wakaondoka 

 “ Kwa sasa tunaelekea wapi? 

Akauliza Sanya 

 “ kwa sasa tunamrejesha 

mkurugenzi ofisini kwake Usa river halafu 

tuendelee na ratiba nyingine” akasema 

Pauline 

 “ Pauline sitaki tena kwenda usa 

river.Wasiliana na David kama anaweza 

kuwa na muda mchana huu ili nipate naye 

chakula ninyi mtaenda Usa river na 

tutaonana mkirejea jioni kwani najua 

mna mambo mengi ya kufanya jumamosi 

hii kama wapenzi.Mimi nitakuwa na David 

nataka vile vile anitembeze ndani ya jiji 

hili nilifahamu vizuri.” akasema Sanya na 

kumtazama Alfred ambaye alikuwa 

anatabasamu. 

 Pauline akachukua simu na 

kumpigia David akamuomba aende 

Silvano hoteli ambako atamkuta Sanya 

anamsubiri ili waweze kupata wote 

chakula cha mchana.Hii ilikuwa ni fursa 

ambayo David hakuwa ameitarajia 

kabisa.Alitamani sana kuipata nafasi ya 

kukaa na Sanya na kuongea lakini hakujua 

angeanza vipi kwani bado alikuwa 

anamuogopa Pauline.Alikatisha mkutano wake mchana huo na baadhi ya wafanya 

biashara na kuchoma mafuta kumuwahi 

sanya Silvano hotel 

 Sanya aliachwa Silvano akiendelea 

kumsubiri David ,Pauline na Alfred 

wakawarudisha mkurugenzi pamoja na 

Yule ndugu yake na bi Elizabeth. 

 Wakati akimsubiri David,Sanya 

aliendelea kupata kinywaji huku kichwa 

chake kikionekana kuvurugika kabisa 

 “Sitaki tena kuendelea na zoezi hili 

kwani mpaka hapa limekwisha 

shindikana.Kikubwa ni kwamba 

nimejitahidi kufanya jitihada za kumtafuta 

mama yangu lakini imeshindikana.Sina 

hakika kama huko aliko bado yuko hai au 

hata ananikumbuka na ana hamu ya 

kuonana nami. Nina hakika hana tena 

habari na mimi na hanikumbuki 

tena.yawezekana labda anajua siko hai 

.Hakunihitaji katika maisha yake na ndiyo 

maana akanitupa .Ninamshukuru Mungu 

kwamba nina watu wengi ambao 

wananipenda na wanayafanya maisha 

yangu yawe na furaha bila hata wazazi 

wangu.Ngoja niachane na mambo haya na 

nielekeze mawazo yangu katika mambo 

mengine ya maisha yangu na hususan 

David “ akawaza Sanya  “ Kuna kitu nimekiona kwa David 

ambacho sijakiona kwa wanaume wengi 

katika sehemu nyingi nilizopita.Ana kitu 

Fulani ambacho wengi hawana 

.Ninakumbuka jana alivyotupokea 

akatukaribisha ,anaonekana ni mtu 

mwenye moyo wa aina yake…” 

 “ Hallow Sanya” Sauti ikasikika 

nyuma yake na kumtoa Sanya katika 

mawazo mengi akageuka na kutazama 

nyuma yake.Akastuka sana.Alikuwa 

anatazamana na sura yenye tabasamu ya 

David. 

“ David umenistua sana.Nilikuwa mbali 

kimawazo .Sikujua kama utatokea kwa 

nyuma”akasema Sanya 

 “ Pole Sanya kwa kukustua.Hoteli 

hii ina sehemu mbili za maegesho.habari 

za toka jana? Toka tulipoachana jana 

usiku hatujaonana tena.Niliwahi sana 

kuondoka asubuhi na kuwaacha bado 

mmelala.” Akasema David 

 “ Pauline alinieleza na amekusifia 

sana kwa utendaji wako wa kazi .Hongera 

sana” akasema Sanya 

 “ahsante sana Sanya” akasema David 

na kuvuta kiti akaketi Muhudumu akafika wakaagiza chakula 

.Wakati wakisubiri chakula wakaendelea 

na maongezi 

 “ Karibu sana Arusha sanya.karibu 

sana Tanzania” akasema David.Sanya 

akatabasamu na kusema 

 “ Nadhani ungeniambia karibu 

nyumbani kwa sababu mimi Tanzania ni 

nyumbani “ 

 “ Wewe ni raia wa Tanzania? David 

akashangaa 

 “ Kwa sasa mimi ni raia wa 

Marekanani lakini asili yangu ni 

Tanzania.Nimelizaliwa Tanzania.Wazazi 

wangu ni watanzania.Nilihamia Marekani 

nikiwa mdogo sana na maisha yangu yote 

nimeishi kule” akasema Sanya na 

kumfanya David atabasamu 

 “ Ouh ! nimefurahi kusikia 

hivyo.Kwa hiyo hapa Tanzania unatokea 

mkoa gani? Akauliza David. 

 “ Sina hakika sana na asili ya wazazi 

wangu lakini yawezekana ni 

Arusha.”akajibu Sanya.David akashangaa 

kidogo na kuuliza. 

 “ kwani wazazi wako hawajakueleza 

wao wanatokea mkoa gani ?  “ kwa bahati mbaya sijawah 

kuwaona wazazi wangu”akasema Sanya na 

kuzidi kumshangaza David 

 “ Wametangulia mbele za haki? 

Akauliza 

 “ Sina hakika kama wametangulia 

mbele za haki lakini historia yangu 

inaonyesha kwamba mimi niliokotwa 

baada ya kutelekezwa na mama yangu 

katika geti la kituo cha kulelea watoto 

wadogo Usa river nikiwa na kama wiki 

moja au mbili hivi baada ya 

kuzaliwa.Nimelelewa katika kituo kile 

pale usa river na kwa bahati nzuri mlezi 

wangu alinipenda sana na alipomaliza 

muda wake wa kuishi hapa nchini 

akanichukua na nikaenda kuishi naye 

Marekani.Nimeishi kule mpaka sasa 

nilipoamua kuja Tanzania kujaribu bahati 

yangu kama ninaweza kuwapata wazazi 

wangu”akasema Pauline.David 

akamtazama na kumuonea huruma sana 

na akasema 

 “ Pole sana Pauline kwa historia 

hiyo.Mungu atakusaidia na utafanikiwa 

kuungana tena na wazazi 

wako.Ninakuhakikishia utawapata tena 

wazazi wako” akasema David na 

kumfanya Pauline atabasamu  “ Wewe na dada yako Pauline 

mnafanana sana.Nyote ni watu ambao 

hampendi kukata tamaa kabisa.Hata 

Pauline alikuwa ananiambia hivyo hivyo 

unavyoniambia”akasema sanya na wote 

wakacheka 

 “ Pauline umekutana naye wapi 

mkajuana? Akauliza David 

 “ Nimekutana naye Moshi katika 

hoteli niliyofikia .Nilikuja na wenzangu 

kutembelea mbuga za wanyama na 

kupanda mlima Kilimanjaro.baada ya 

kumaliza ziara yetu wenzangu waliondoka 

lakini mimi kwa kuwa nilikuwa na kazi ya 

kufanya nikabaki na katika hoteli 

niliyofikia mjini Moshi nikakutana na 

Pauline.Nilipomuona nilivutiwa sana 

kujenga naye urafiki,kwa bahati mbaya 

siku za mwanzo alikuwa ni mtu mwenye 

shghuli nyingi lakini baadae nikazoeana 

naye na tukawa marafiki.Nilifurahi 

aliponiambia kwamba yeye ni mwenyeji 

wa Arusha nikamuomba kwamba siku 

atakapokuja Arusha aongozane nami ili 

niweze kuja kuanza zoezi la kutafuta 

taarifa za wazazi wangu.Kwa bahati nzuri 

jana alinifuata na kuniambia kwamba 

amepata safari ya dharura ya kuja arusha 

hivyo nikaongozana naye pamoja na mchumba wake Dr Alfred.” David 

akastuka sana aliposikia kwamba Alfred 

na Pauline ni wachumba lakini hakutaka 

kuonyesha mstuko ule mbele ya Sanya 

akatabasamu na kusema 

 “ Vipi mchakato wa kuwatafuta 

wazazi wako umekwisha anza?akauliza 

David.Sanya akanywa juice halafu 

akasema 

 “ Leo asubuhi tumekwenda usa river 

katika kile kituo nilikolelewa.Nimeonana 

na Mkurgenzi wa kituo kile na kwa bahati 

mbaya sana hakuna taarifa zozote ambazo 

zingeweza kunisaidia kukutana na wazazi 

wangu.Mkurugenzi Yule ana roho nzuri 

sana kwani alitupeleka kwa mama 

mmmoja aitwaye Elizabeth ambaye 

amewahi kufanya kazi katika kituo kile 

kwa miaka mingi toka akiwa msichana 

ambaye tulitegemea kwamba anaweza 

akawa na kitu chochote anachokifahamu 

kuhusu mimi lakini kwa bahati mbaya 

sana mama huyo ni mgonjwa mahututi 

amelazwa hospitali anasumbuliwa na figo 

na muda wowote anaweza akafariki.Zoezi 

limekuwa gumu sana na linakatisha 

tamaa” akasema sanya akionekanakabisa 

kukata tamaa  “ Sanya usikate tamaa.kwa vile 

umekuja huku Tanzania kuwatafuta 

wazazi wako nakushauri usiondoke bila 

kuwaona wazazi wako.Sisi tupo 

tutakusaidia kwa kila namna hadi jambo 

hili lifanikiwe”akasema David na 

kumfanya Sanya atabasamu 

 “ Nimefurahi sana kwa namna 

mnavyonipa moyo .Nimeamini yale 

maneno kwamba watanzania ni watu 

wakarimu sana “akasema Sanya 

 “ Suala hili ni kubwa kwa hiyo 

hutakiwi kabisa kukata tamaa na sisi 

kama rafiki zako tunatakiw a tukushike 

mkono na kuhakkisha kwamba 

unafanikiwa kuungana tena na wazazi 

wako .Nakuhakikishia kwamba 

tutawasaka kokote waliko na kama wako 

hai basi tutawapata tu.Hata kama si leo 

lakini siku yoyote ile lazima 

wapatikane.”akasema David 

 “Ninakosa neno la kusema David 

kwa ukarimu wenu.Tayari nilikwisha kata 

tamaa kabisa na kuamua kuachana na 

suala hili lakini umekuja wewe na 

nimepata tumaini jipya la kusonga mbele 

kuwatafuta wazazi wangu.”akasema 

sanya.Muhudumu akafika na chakula walichoagiza akawandaalia meza 

wakaendelea kula taratibu 

 “ Sikuhisi kabisa kama historia ya 

Sanya inaweza ikawa namna 

hii.Ukimtazama hudhani kama asili yake 

ni Tanzania.Mtoto anang’aa kama 

Beyonce .kwa kweli hapa lazima nichange 

karata vizuri na mtoto huyu 

simuachi.Nitafanya kila niwezalo hadi 

nihakikishe nimempata .Ninachotakiwa 

kukifanya kwa sasa ni kuwa mstari wa 

mbele kumsaidia katika zoezi la kuwasaka 

wazaziwake ingawa sijui nitamsaidiaje 

lakini nitajarbu kila njia niwezayo.Sanya 

yuko tofauti sana na Yule kahaba 

Tamia.Huyu ni msichana mwenye heshima 

zake,ana elimu nzuri na anajtambua 

.Hata maongezi yake yanaonyesha wazi 

kwamba ni mtu mwenye akili ya kiwango 

cha juu sana tofauti na msichana kama 

Tamia.”akawaza David huku akimtazama 

sanya kwa kuibia 

 “ David mbona unanitazama hivyo ? 

Kuna kitu unataka kuniuliza? 

 “ uhmmm.hapana sanya nilikuwa 

natafakari tu.” 

 “ Unatafakari nini? Akaulzia 

sanya.David akasema  “ Natafakari kuhusu mama yako 

lazima atakuwa mrembo sana”akasema 

David na kumfanya sanya acheke kicheko 

kikubwa. 

 “kwa nini umeseam hivyo david” 

 “kama wewe ni mzuri hivi 

unategemea maaa yako atakuaje?lazima 

atakuwa ni mzuri mara mbili 

yako”akasema David na kuzidi kumvunja 

mbavu Sanya 

 “ David ninatamani sana kumfahamu 

mama yangu .Inawezekana hayo 

unayoyasema yakawa kweli na mama 

yangu akawa ni mrembo 

kupindukia”akasema Sanya na kuzama 

ghafla katika mawazo na baada ya muda 

akasema 

 “ Unaifahamu shule inatwa st Lucia? 

 “ Ndiyo ninaifahamu”akasem David 

 “ Basi nitapenda unipeleke siku ya 

jumatatu.” 

 “ usijali nitakupeleka.Kuna mtu 

unakwenda kumuona pale? 

 “ Ninataka nikaonane na mkuu wa 

shulehiyo” 

 “Unafahamiana naye? 

 “hapana sifahamiani naye.Kuna 

mradi ninafikiria kuuanzisha mara tu 

nitakaporejea marekani.Nimegundua kwamba matukio ya utupaji watoto hapa 

Tanzania ni mengi na hii inachangiwa na 

ukosefu wa uelewa wa kutosha wa elimu 

kuhusu afya ya uzazi na mahusiano.Vile 

vile nimegundua kwamba kiti kingine 

kinachochangia kwa tabia hii ya utupaji 

wa watoto kuongezeka ni umasikini wa 

wazazi.Nimepanga kuanzisha shirika 

ambalo kazi yake itakuwa ni kusambaza 

elimu ya uzazi na mahusiano mashuleni na 

vile vile litakuwa na jukumu la kuwasaidia 

wanawake masikini kujikwamua 

kiuchumi.Hili si jukumu dogo lakini 

nitakaporejea marekani nitachangisha 

fedha na kutafuta watu ambao wataniunga 

mkono ili nipate fedha za kutosha za 

kuendesha shirika hilo.Hilo si jukumu 

dogi lakini nitahakikisha 

ninalikamilisha.Mimi nilitupwa lakini 

nikabahatika kulelewa na familia tajiri 

ambayo imenifikisha hapa nilipo.Kama si 

bahatio hii hvi sasa sijui ningekuwa wapi 

.Lakini kabla ya kuanzisha shirika hili 

nitapenmda sana kwanza kutembelea 

katikamakazi ya watu masikini .Kuna 

mambo nnatak akujifunza.” Akasema 

Sanya 

 “ Sanya nimefurahishwa sana na 

wazolako nma ninakuahidi ushirkianao wangui mkubwa katiak sualahili 

.Nitakusaidia kwa kila kitu 

unachokihitaji.Jumatatu nitakupeleka 

katika shule unayotaka kwenda na kisha 

nitakutemeba sehemu mbalimbali za jinji 

hili la Arusha ,nitakupeleka katika sehemu 

zenye makazi duni ambako utajifunza 

mambo mengi. “akasema David



 Robin alimchukua mwalimu Lucy 

hadi katika hoteli moja kubwa iliyokuwa 

nje ya jiji la Arusha. 

 “ Robin huku tunakuja kufanya nini? 

Akauliza Lucy wakati wakiingia katika 

hoteli ile kubwa.Robin akageuka na 

kumtazama Lucy akasema 

 “ We’ll spend the weekend here” 

Lucy akapatwa na mshangao kisha 

akamkumbatia Robin kwa nguvu na 

kumpiga busu 

 “ Ouh Robin nimekosa neno la 

kusema .Thank yopu.Thank yopu so much 

my love” akasema Lucy huku akifuta 

machozi yaliyomtoka 

 “ Robin leo umeniweza kweli 

.Sikujua kama tunakuja hapa .Kweli hii ni syuprise kubwa kwangu” akasema 

Lucy.Bado machozi yaliendelea kumtoka. 

 “ Usilie Lucy.Bado kuna suprises 

kwako” akasema Robin 

 “ Another surprise? Lucy 

akashangaa.Robin akaegseha gari na 

kushuka haraka akaenda kumfungulia 

Lucy mlango akamshikamkono wakaeleka 

ndan I ya hoteli.Tayari alikwisha weka oda 

ya chumba ,hivyo moja kwa moja 

muhudumu akawaogoza hadi katka 

chumba chao kilichokuwa katika ghorofa 

ya tatu. 

 Ndani ya chumba kulikuwa na kila 

kitu ambacho Lucy anakitumia kuanzia 

mafuta,uturi hadi vipodozi.Akamtazama 

Robin na kumkumbatia. 

 “ Kweli Robin leo hii umeamua 

kunifanyia surprise.Sikutegemea kabisa 

kam aungeweza kunifanyia hivi” akasema 

Lucy na kuchukua kitambaa 

akafutamachozi 

 Robin akaagiza waletewe vinywaji 

kisha wakakaa kitandani. 

 “ Robin kabla hujanieleza chochote 

naomba niseme kwamba leo nimefurahi 

sana.Kutoka nje ya mji sehemu kimya 

kama hii ni kitu ninachokipenda 

sana.Nilikuwa nina panga kufany akitu kama hiki lakini umeniwahi .Ninasema 

ahsante sana.Nimefurahi sana “ akasema 

Lucy 

 “ Lucy sikujua kama unapenda jambo 

hili ila kwa sasa baada ya kujua basi 

tutalifaya mara nyinhi tu.Ila kwa leo kuna 

jambo maalum nililokuletea hapa” 

akasema Robin 

 “ Robin unanifanya hadi ninaogopa 

kwa suprises zako.” Akasema Lucy. 

Robin akaenda katika kabati la nguo 

akalifungua na kutoa sanduku dogo na 

kuliweka kitandani 

 “ Kuna nini humu Robin? Akauliza 

Lucy. 

 “ My love hii ni surprise ya kwanza 

kwako kwa siku ya leo .Ninakuoba 

ulifungue sanduku hili wewe mwenyewe 

kwa mkono wako na utazame kilichomo 

ndani” akasema Robn 

 “ Robin hebu nieleze kwanza 

,uilijuaje kama kuna sanduku mle 

kabatini? Robin akatabasamu na kusema 

 “ Nilifika hapa hapo kabla na 

nikaanda kila kitu .Fungua hilo sandulu 

Lucy” akasema Robin.Huku mikono 

ikimtetemeka akalifungua sanduku lile na 

ndani yake akakutana na bahasha kubwa.  “ Ichukue hiyo bahasha na usome 

kilichomo ndani yake” akaelekeza 

Robin.Lucy akaifungua ile bahasha akatoa 

karatasi iliyoonekana kama cheti na 

kuanza kuisoma na mara akaruka kwa 

furaha na kumkumbatia Robin.Machozi 

mengi yakamtoka.Alikuw ana furaha 

iliyopitliza.Alitaka kila neno zuri 

alioliofahamu kwa kweli ilikuwa ni siku 

yakeya futraha kubwa mno .Baada ya 

dakika zaidi ya kumi za kupandwa na 

wazimu wa furaha akaanza kutulia 

 “ Robin my love siku nyingine 

usinifanyie suprises kama hii.Utaufanya 

motyo wangu upasuke kwa furaha.” 

Akasema Lucy huku akiendelea 

kudondosha machozi.Robin akachukua 

kitambaa na kumfuta machozi halafu 

akasema 

 “ Leo asububi nlipigiwa simu 

kwamba ninahitajika katika ofisiya 

askofu.Sikupoteza muda nikafika kabla 

hata ya muda nilotakiw 

akufika.Nilifanikiw akuonana na askofu 

ambaye alinieleza kwamba lile ombi langu 

la kutenga ndoa yangu na Vivia tayari 

majibu yakeyalikuwa yamerudi.Kwa hivi 

sasa kanisa limerekebisha sheria na 

taratibu zake na ukichanganya na ukuaji wa teknolojia mambo hayachukuio mud 

amrefu kutolewa maamuzi na isitoshe 

viopngozi wakubwa wa kidini 

wamekasimiwa majukumu ya utoa 

maamuzi katika kesi kama hizi kwa niaba 

ya kiongozi mkuu wa kanisa .Baada ya 

suala langu kufika katikameza ya vongozi 

wa juu wa kanisa na kulijadii kwa kina 

hatmaye walifikia maamuzi na uamuzi 

walioufikia ni wa kukubaliana na ombi 

langu la kutaka kuitengua ndoa yanguna 

Vivian ka hiyo rasmi sasa mimi na Vivian 

si wanandoa tena na kila mmoja 

anaruhusiwa kuoa au kuolewa.”Robini na 

Lucy wakakumbatiana tena kwa furaha 

kubwa na kupongezana kwa ushindi ule 

mkubwa 

 “ Lucy nilipatwa na furaha ya ajabu 

sana na ndiyo maana nikafanya haya yote 

niliyoyafnya .Hii ni siku yetu kubwa 

sana.Nisiku ya furahakubwa katika 

maisha yetu.Huu ni mwanzo mpya kati 

yetu “ akasema Robin.Huku bado machozi 

yakiendelea kumtoka Lucy akasema 

 “ Robin nimeksoa neno la kusema 

.Badio siamini kama jambo hili ni 

kweli.Nilidhai labda ingecbhukua miaka 

hata zaidi ya m itatu kukamilika lakini 

imenishagaza kw anama jambo hili lilivyokwenda haraka haraka.Mungu 

ashukuriwe sana” 

 “ Lucy kama nilivyokueleza awali 

kwamba mambo ndaniya kanisa 

yamebadilika sana na kingine kilichowapa 

urahisi viongozi wa juu kulitolea maamuzi 

suala hili ni namna jambo lenyewe 

lilivyo.Namna Lucy alivyovunja kiapo 

chake cha ndoa na kunitelekeza mimi na 

mtoto.Niwazi kwamba 

hakustahilikuendelea kuwa mke wangu.” 

Akasema Robin kisha akainuka na kwenda 

tenakatika kabati akalifngua na kutoa 

kijikasha kidogo akakifugua na kutoa pete 

nzuri akaishka mkononi na kupiga goti 

moja mbele ya Lucy. 

 “ Nimewahi kuteswa na mwanamke 

na nikakata tama kabis aya kupenda tena 

lakini nilipokutana na wewe nikakivuna 

kiapo change na kuufugua myo wangu 

kwako.Toka nilipokutana nawe umekuwa 

ni furaha ya maisha yangu,taa imulikayo 

maisha yangu,dirana mwelekeo wa 

maisha yangu,umekluwa ni kila kitu 

kwagu na kwa mwanangu Penina.Kwetu 

umekuwa ni kama ua zuri ambalo 

huchanua kila siku na kusambaza harufu 

nzuri ya manukato .Lucy mmi na 

mwanangu Penina tunakuhitaji sana katika maisha yetu na nimepiga gotri 

mbele yako kukuomba jambo moja tu.Will 

you merry me ? 

 Midomo ya lucy ikamtetemeka 

akashindwa kuongea ,macho yake yalijaa 

machozi. 

 “ Will you merry me Lucy ? akauliza 

 “ Yees..!!!...Yes ‘ akajibu Lucy.Robin 

akainuka wakakumbatiana kwa nguvu 

“ basi imetosha Lucy,usilie tena.” Robin 

akambembeleza Lucy ambaye macho yake 

yalijaa machozi 

 “ Robin niache nilie.Ninakumbuka 

shida na mateso niliyoyapitia na siamini 

kama leo hii nimefikia hapa.Machozi 

yananitoka kwa furaha niliyonayo kwani 

niliamini kwamba maisha yangu yamejaa 

mikosi na labda sintampata mwanaume 

ninaye muhitaji katika maisha yangu 

atakayenipenda kwa moyo wake wote 

.Mungu bado ananipenda na amekuleta 

wewe Robin.Umenipandisha hadi 

uwinguni na kunifanya nijione ni 

mwanamke wa pekee na mwenye bahati 

kubwa.Sina hakika kama kuna mwanamke 

mwingine ambaye amewahi kuvishwa 

pete mbili za uchumba na 

mwanaumemmoja”akasema Luvy na wote wakaangua kicheko wakakumbatiana 

tena. 

 “ Robin wewe umelifanya hilo.Pete 

hii uliyonivisha leo ni pete ya pili.” 

Akasema Lucy.Robin akamtazama 

akambusu na kusema 

 “ Nilifanya hivyo makusudi 

Lucy.Pete ya kwanza nilikuvalisha wakati 

ule ambao bado nilikuwa ni mume wa 

Vivian tukisubiri ndoa yetu itenguliwe na 

kanisa.Sikujua zoezi lile la utenguzi 

lingechkua muda gani na ndiyo maana 

nikakuweka alama ili kila atakayekuona 

ajue kwamba tayari una mwenyewe.Kwa 

sasa niko huru .Si mume wa mtu tena na 

ndiyo maana nimeamua kukuvisha pete 

nyingine rasmi nikiwa mtu huru ambayo 

hii mbadala wake utakuwa ni pete ya 

ndoa.” akasema Robin na kuitoa pete ile ya 

zamani akamvisha mpya. 

 “ Robin kuna jambo moja ninataka 

kukuomba mpenzi wangu.”akasema Lucy 

 “ Omba chochote Lucy nitakupatia” 

 “ Ili furaha yangu ya leo ikamilike 

ninaomba tukawatembelee Vivian na 

Martin hospitali tuwape pole .Kwa nyakati 

tofauti waliwahi kuwa wapenzi wetu.Mimi 

nilikuwa na martin na wewe ulikuwa na 

Vivian.Najua wametutenda na kutuumiza sana lakini huu ni wakati wa kuyaweka 

pembeni yale yote waliyotufanyia na 

kwenda kuwajulia hali.Tayari tumekwisha 

kipata tulichokuwa tunakihitaji kwa hiyo 

hakuna haja ya kuendela kuweka visasi .” 

akasema Lucy . 

 “ Lucy wewe ni mwanamke mwenye 

moyo wa kipekee kabisa.pamoja na yote 

ambayo Martin amekufanyia lakini bado 

unamuonea huruma?”akasema Robin 

 “ Robin sisi ni binadamu na sote 

tunakosea.Hata wao pia walikosea na 

tunaagizwa kwamba tunapokosewa 

tunatakiwa kuwasamehe 

waliotukosea.Hata kama tukilipa kisasi 

haitatusaidia chochote.Tusahau yaliyopita 

na tuwasamehe.” Akasema Lucy 

 “ Robin nitakwenda hosptali 

kuwaona lakini ni kwa sababu yako 

tu.Sikuwa tayari kabisa kwenda 

kumtazama tena Vivian nikikumbuka 

mambo aliyonifanyia.”akasema Robin 

 “Ahsante kwa kunikubalia ombi 

langu mpenzi wangu.Mungu akubariki 

sana” akasema Lucy. 

**********************  Ni saa mbili za usiku ,nyumbani kwa 

mzee Zakaria familia imekutana mezani 

kwa chakula cha usiku ambacho 

kiliandaliwa maalum kabisa kwa ajili ya 

Pauline na wageni wake .Mzee Zakaria 

alitaka apate wasaa wa kufurahi tena na 

mwanae na vile vile kuwafahamu marafiki 

aliokuja nao.Mezani walikuwepo Mzee 

Zakaria , mkeweVicky madhahabu ,David 

,Sanya na mtumishi wa ndani.Pauline na 

Alfred hawakuwepo mezani.Toka 

walipoachana na Sanya mchana 

hawakurejea tena na hawakumfahamisha 

mtu yeyote walikuwa wapi 

 Baada ya kupata chakula kile kizuri 

wote wakajumuika katika chumba cha 

mapumziko kwa maongezi 

 “ Sanya karibu sana hapa 

kwetu,karibu sana Tanzania.”akasema 

mzee Zakaria 

 “ Ahsante sana baba nashukuru” 

akajibu Sanya 

 “ Mimi kama nilivyojitambulisha 

asubuhi,ninaita Zakariaa ,ni baba mzazi 

wa Pauline na huyu hapa ni mke wangu 

anaitwa Vicky.Yule pale kijana wangu 

David ambaye tayari umekwisha 

mfahamu.karibu sana katika famliaya 

pauline’”akasema mzee zakaria na maongezi yakaendelea.Waliongea mambo 

mengi sana hadi ilipotimu saa tano za 

usiku mzee Zakaria akaonekana kuchoka 

akaenda zake kulala.David na sanya pia 

wakaagana na kila mmoja akaingia 

chumbani kwake kulala. 

 “ Pauline yuko wapi leo? Akajiuliza 

David.Akachukua simu na kujaribu 

kumpigia lakini namba ya simu ya Pauline 

haikuwa ikipatikana. 

 “ Ananishangaza sana 

Pauline.Amezima simu bila kutujulisha 

yuko wapi.Pauline amebadilika 

sana.Lakini nisimlaumu kwani ni mimi 

ndiye niliyechangia sana katika 

mabadiliko haya kwa mambo 

niliyomfanyia.”akawaza David akiwa 

amekaa kitandani 

 “ Kumbe yeye na Fred ni wapenzi ? 

Nimefurahishwa na jambo hili.Fred 

anaonekana ni kijana mzuri ,msomi,na 

anampenda Pauline.Nina hakika 

hatamuumiza kama nilivyofanya 

mimi.Pauline na mimi tutabaki kuwa na 

mahusiano ya kaka na dada.” 

Akatabasamu na kuvua fulana yake 

akajilaza kitandani. 

 “ Pauline inaonekana 

amechaganyikiwa kabisa na penzi la Alfred na ndiyo maana amesahau hata lile 

suala ambalo nilimuitia .Tulikubaliana leo 

tutafute wasaa ili nimueleze kwa ufasaha 

kila kitu kinavyokwenda lakini 

ameonekana kulisahau kabisa jambo 

hili.Ninahisi yuko mahala yeye na mpenzi 

wake Alfred wakijivinjari.”akainuka na 

kukaa 

 “ Kesho ndiyo Jumapili siku ambayo 

Vicky amedhamiria kuutekeleza mpango 

wake wa kumuua mzee Zakaria.Hata kama 

Pauline hatakuwepo sintakubali jambo 

hilo litokee.Nitamlinda mzee 

Zakaria.Nitafanya kila linalowezekana 

kuhakikisha kwamba jambo hili 

halifanikiwi na huu utakuwa ni mwisho 

wa Vicky.Mwisho wake utakuwa wa aibu 

sana.Mambo yake yote yatawekwa 

hadharani.” akaendelea kuwaza David 

 “ Kesho itakuwa ni siku mbaya , sijui 

nini kitatokea lakini namuomba Mungu 

jambo hili analotaka kulifanya Vicky 

lisifanikiwe.Nilitaka Pauline alifahamu 

jam…” David akastuka toka mawazoni 

baada ya kusikia mlango wake 

unafunguliwa.Ni kweli kuna mtu aliingia 

mle ndani.Alikuwani Vicky madhahabu. 

 “ Vicky ?!!! akasema David  “Shhhh.!! Usipaaze sauti 

nimemtoroka Yule mzee nikamwambia 

kwamba ninakuja kuongea na Sanya.” 

Akasema Vicky kwa sauti ndogo 

 “ Vicky tafadhali naomba usinitafutie 

matatizo nenda chumbani kwako!! 

Akafoka David 

 “ David usiwe mkali mpenzi 

wangu.Nimeshindwa kuvumilia 

David.Mwili wote unawaka moto na siwezi 

kulala bila ya kuguswa nawe.Tafadhali 

David nakuomba hata kwa dakika chache 

tu.Lile zee kule ndani halitajua chochote .” 

Akasema Vicky. 

 “ Vicky tafadhalinaomba uondoke na 

ureje chumbani kwako.Siwezi kufanya 

kitendo hicho na wewe leo tena ndani ya 

nyumba ya mzee Zakaria.Kama unanihitaji 

tafuta siku nyingine na si leo hii” akasema 

David lakini ghafla Vicky madhahabu 

akamrukia pale kitandani na kuanza 

kumvua bukta kwa nguvu 

 “ David kwa nini unapenda nitumie 

nguvu katika jambo kama hili wakati 

unafahamu kabisa hali yangu ilivyo na 

wajibu wako kwangu ambao tulikwisha 

kubaliana? Akauliza Vicky . 

 “ Vicky nimesema kwamba siwezi 

kufanya kitu hicho unachotaka tufanye.Nimesema kwamba siko tayari 

kwa leo tena ndani ya nyumba hii.Kwa 

nini humuogopi mumeo? Hata kama 

unachepukalakini lazima umuheshimu 

.Tafadhali toka rudi chumbani kwako” 

akasema David huku akijinasua kutoka 

katika mikono ya Vicky. 

 “David mbona unataka kuniudhi 

mpenzi wangu? Kwa nini unakuwa hivyo? 

Akasema Vicky akiendelea kumbembeleza 

David 

 “Vicky wewe ndiye ambaye hutaki 

kunielewa ninapokwambia kwamba hicho 

unachokitaka leo hii hakiwezekani 

kabisa.” 

 “ David mwenzako nina hali mbaya 

sana na wewe unaendelea kuniumiza 

zaidi.Leo sitoki humu ndani bila ya 

kuguswa nawe.” Akasema Vicky huku 

akiivua nguo ya ndani na kuitupa 

pembeni. 

 “ Huyu mwanamke leo amedhamiria 

.Hapana siko tayari kufanya kitendo 

hiki.Imetosha sasa” akasema David na 

kuchomoka akitaka kutoka mle ndani 

lakini Vicky akamuwahi na kumdaka 

mkono akamvuta.Purukushani ikaanza 

mle chumbani kati ya David na Vicky  Hatimaye Vicky akafanikiwa 

kumuangusha chini David na kumkalia 

juu.. 

 “ David mpenzi wangu kwa nini 

lakini unataka tutumie nguvu? Tafadhali 

naomba tumalizane na mimi niondoke 

zangu.Dakika chache tu David”. 

 “ Vicky hivi tunavyofanya 

tutawafanya watu watusikie na kila kitu 

kitaharibika wakitugundua na taarifa 

zitamfikia mzee Zakaria.” 

 “Yote haya yamesababishwa na 

wewe David.Unafahau kabisa ni namna 

gani ninakuhitaji David lakini umekuwa 

unanikwepa kila siku.Tafadhali naomba 

penzi lako kwa dakika chache tu” akasema 

Vicky 

 “ haya Vicky umeshinda tusiendelee 

kulumbana hadi tukasikika huko 

nje.Nitafanya hivyo unavyotaka lakini 

naomba nikuweke wazi kwamba kitendo 

hiki sijakifurahia kabisa.” Akasema David 

huku akiivua bukta yake na kuzidi 

kuyapandisha mashetani ya Vicky ambaye 

alishindwa kuvumilia akamvuta 

wakaenda sofani . 

 Kukuru kakara zile chumbani kwa 

David zikamstua Sanya aliyekuwa katika chumba cha Pauline ambacho hakikuwa 

mbali na chumba cha David. 

 “ Kuna nini kinaendelea ? Mbona 

ninasikia vishindo vya kugongwa ukuta na 

vitu kuanguka?Kuna watu wanagombana? 

Akajiuliza halafu akafungua mlango 

akachungulia nje hakukuwa na mtu lakini 

akasikia kama sauti za 

watuwakibishana.Akatoka na kwenda 

kutega sikio katika mlango wa chumba 

cha David akasikia kama kuna watu 

wanagombana. 

 “ David anagombana na nani? 

Akajiuliza na kusimama pale mlangoni 

kwa dakika mbili 

 “ Huu ninaofanya hapa ni ujinga 

mkubwa.Ni vipi iwapo kuna mtu anataka 

kumdhuru David? Ngoja nihakikishe” 

akawaza Sanya na kukishika kitasa cha 

mlango ambao haukuwa umefungwa kwa 

funguo akaufungua mlango kidogo na 

kuchungulia ndani na kukutana na kitu 

kilichomstua sana 

 “ David !!,.. Aunt?!!! Akajiuliza huku 

amepigwa na butwaa .David na Vicky 

walikuwa sofani watupu wakifanya 

mapenzi. Taratibu akaufunga mlango na 

kutoka akarejea chumbani 

kwake.Akayafikicha macho  “ Hapana siko 

usingizini.Nilichokiona si ndoto bali ni 

kitu cha kweli kabisa.David na mama yake 

mdogo Pauline walikuwa wanafanya 

mapenzi.Ninayaamini sana macho yangu 

na nilichokiona ni kitu cha kweli kabisa na 

si cha kuhadithiwa.” Akawaza Sanya huku 

akihisi mwili ukimtetemeka kwa uoga kwa 

kitu alichokiona. 

 “ Nimeogopa sana kwa kitu 

nilichokiona.David anatembea na mama 

yake mdogo ? Mke wa baba yake ambaye 

ni sawa na mama take !! Halafu 

wamejiachia bila wasi wasi hata bila hata 

kufunga mlango,wanajiamini nini? 

Wangefanya nini kama wangekutwa na 

Pauline au baba yake? Tena inaonekana 

huu ni mchezo wameuzoea na ndiyo 

maana hawana wasi wasi hata 

chembe.Nashukuru nimegundua mapema 

kwamba David ni kijana mshenzi kabisa 

na hanifai hata kidogo.Tayari nilikwisha 

tokea kumpenda na nilichokuwa 

ninahitaji ni kumfahamu vizuri lakini kwa 

hiki nilichokiona leo hii,David hanifai 

kabisa.Lazima nimwambie Pauline kuhusu 

suala hili.Lazima afahamu uchafu 

unaofanyika ndani ya numba 

yao.Nimekuzwa katika msingi ya ukweli na kukataa uovu kwa hiyo Pauline lazima 

afahamu kila kinachoendelea humu 

ndani.”akaendelea kuwaza Sanya 

 Dakika kumi walizitumia David na 

Vicky kumaliza mzunguko mmoja kisha 

Vicky akavaa haraka haraka. 

 “ Thank you so much david.” 

Akasemahuku akimbusu 

 “ Vicky sitaki jambo hili lijirudie 

tena.Naomba leo iwe ni 

mwisho.Nimekubali kufanya hivi kwa 

kuogopa mgeni chumban ikwa Pauline 

asije akatusikia tunalumbana vinginevyo 

ningekufurusha vibaya” akasema David 

 “ Kwa nini unanifanyia hivi 

David.Unamuogopa Pauline? Au 

unamuogopa huyu mmarekani? 

Nimekuona ulivyokuwa 

unamuangalia.Ninakuonya David kama 

una mawazo naye yafute kabisa.Kwa sasa 

wewe ni wangu peke yangu” Akasema 

Vicky.David hakumjibu kitu akamuangalia 

kwa hasira.Vicky akambusu na kutoka mle 

chumbani akaondoka 

 “ Huu ni ukosefu mkubwa sana wa 

adabu lakini hii ya leo ni ya mwisho kwani 

kuanzia kesho hatadiriki tena kufanya 

kitu kama hiki.I hate you Vicky….I hate 

you so much!!..akawaza David na kuufunga mlango wake kwa funguo 

………………. 

****************** 

Chumba namba 76 Katika hoteli kubwa ya 

Kobe village ilyoko nje kidogo ya jijila 

Arusha, kilikuwa na mwanga mdogo wa 

bluu na muziki laini ulisikika kwa 

mbali.katika kitanda kikubwa 

kilichokuwamo mle chumbani watu 

wawili walionekana kuwa katika mahaba 

mazito. 

 “ Pauline sijui nikueleze nini kwa 

furaha kubwa niliyonayo leo hii kwa 

kupata nafasi hii ya kuwa nawe 

hapa.Nilikuwa ninatafuta sana kupata 

nafassi kama hii furaha kwa muda mrefu 

na hatimaye sasa nimefanikiwa kuipata 

toka kwako.Pauline wewe ni wa kipekee 

kabisa.Ahsante sana” 

 “ Alfred ,hata mimi ninapaswa 

kukushukuru kwani umenifuta machozi 

na kukiponyesha kidonda nilichokuwa 

nacho moyoni.Sikuwa na uhakika kama 

kidonda nilichoumizwa kingeweza kupona 

ndani ya muda mfupi lakini baada ya 

kukutana nawe sihisi tena maumivu Ahsante sana Alfred” akasema Pauline 

,Alfred akambusu na kusema 

 “Si mara ya kwanza unanitamkia 

suala hilo la kuumizwa.Ni nani 

aliyekuumiza moyo wako mtoto mzuri 

kama wewe? Ni nani huyo ambaye 

anathubutu kukutoa chozi?akauliza Alfred 

 “ Fred hayo yamekwisha pita.kwa 

sasa yamebaki historia.Ninanchokiangalia 

sasa ni maisha yangu ya mbeleni nikiwa 

na mwanaume wa kipekee kabisa kuwahi 

kukutana naye.Thats you Alfred.Pamoja 

na hayo bado kuna kitu kinanisumbua 

sana na kuninyima raha kila 

nikikifikiria”akasema pauline 

 “ Nini kinakunyima raha Pauline? 

Tafadhali niambie mpenzi wangu.Niko 

tayarikwenda hadi mwisho wa dunia 

kuitafuta furaha yako.Niambie tafadhali 

nini kinakutatiza? Akauliza Alfred huku 

akizichezea nywele za Pauline 

 “ Alfred ni kuhusu mkeo 

Grace.Ninaogopa sana endapo siku moja 

atagundua kwamba mimi na wewe tuna 

mahusiano ya siri.Grace ni mwanamke 

mpole na anayekupenda sana.Mnaye 

mtoto mzuri na mnaishi kwa amani.Sitaki 

niwe kikwazo cha kuivuruga familia 

yako.Ninafahamu maumivu ya kusalitiwa na mtu unayempenda kwa hiyo sitaki 

jambo kama hilo limkute Grace.Ndiyo 

maana ninakosa raha kabisa kila 

nikiliwaza hilo kwanininakupenda sana 

david na sitaki nikukose katika maisha 

yangu ” Akaema Pauline 

 “ Paline hilo si suala la kuhofu hata 

kidogo.Mimi ndiye mwenye uamuzi wa 

nini nifanye kuhusiana na maisha yangu 

.Nimekupenda na nitakuwa nawe na 

hakuna wa kunizuia kukupenda.Grace 

hawezi kunizuia kuitafuta furaha ya 

maisha yangu kwa hiyo usimuhofie 

kabisa.Agundue asigundue potelea mbali 

nimekwisha amua liwalo na 

liwe”akasema Alfred.Pauline 

akamuangalia ,akatabasamu halafu 

akaupeleka mkono wakae kifuani kwa 

Alfred akasema 

 “Why are you doing this to your wife? 

Why are you hurting her? 

 “ Pauline tafadhali naomba tuachane 

na mambo hayo ya Grace.Tuzame zaidi 

katika mapenzi yangu mimi na wewe” 

akasema Alfred 

 “ Fred ,mimi tayari nimezama 

mapenzini na mume wa mtu ambaye 

haonyeshi kujali kama kwa kufanya hivyo 

anamuumiza mkewe .Ninataka kufahamu unajisikiaje ukiona mkeo anadondosha 

machozi kwa sababu ya kitendo hiki 

tunachokifanya? Ni vipi kama na wewe 

ukigundua kwamba mkeo amekuwa na 

mahusiano na mwanaume mwingine? 

Akauliza Pauline.Alfred akanyamaza 

akatafakari kidogo kisha akasema 

 “ Pauline I real don’t care if she’ll get 

hurt or not. Kikubwa kwangu ni kwamba 

nimekupata wewe mwanamke ambaye 

unanipa furaha ya moyo niliyokuwa 

naitafuta kwa muda mrefu sana.”akasema 

Fred.Pauline akamtazama tena kwa 

makini akaguna kidogo kisha akauliza 

 “ Do you real love her? 

 “ Paline si watu wote unaowaona 

wako katika ndoa ukadhani wanapenda.” 

 “ Nijibu swali langu Fred.Do you love 

your wife? 

 “ I don’t” akajibu Fred na kumstua 

sana Pauline 

 “ Fred !!akasema pauline na kuinuka 

akakaa. 

 “ Pauline ndiyo maana nikakwambia 

kwamba tuachane na masuala ya mimi na 

Grace na tuongelee masuala yetu.” 

Akasema Alfred ” Fred umenistua sana.Yaani kwa 

macho makavu kabisa unadiriki kusema 

kwamba humpendi mkeo !!! 

 “ Ndiyo Pauline.Ulitaka kuufahamu 

ukweli basi ukweli ndio huo.I don’t love 

her at all” 

 “ This is weird “ akasema Pauline 

kwa sauti ndogo.Kikapita kimya kifupi 

Pauline akauliza 

 “ why are you doing this to her? Are 

you punishing her? Kuna kitu amewahi 

kukukosea Alfred? 

 “ Ouh pauine kwa nini unataka sana 

kufahamu kuhusu Grace? Nimekwambia 

tuachane naye atatuharibia usiku wetu 

mzuri.” 

 “ Fred ninahitaji kujua kila kitu kwa 

sababu tayari nimekwisha zama katika 

penzi lako nasitegemei kutoka lakini 

ninaogopa kama umethubutu kutamka 

kwamba humpendi mkeowa ndoa basi 

hata mimi unaweza ukaniacha muda 

wowote pindi ukipata mwanamke mzuri 

zaidi yangu”akasema Pauline 

 “Pauline tafadhali usiwaze mawazo 

kama hayo.Mimi ninakupenda kwa moyo 

wanguwote na ndiyo maana unaniona 

ninafanya mambo haya yote kwa ajili ya 

jambo moja tu kubwa.Kuwa na wewe maishani.Nimekueleza ukweli wa moyo 

wangu ili ujue kwamba simpendi mke 

wangu na ninakupenda wewe tu na 

kamwe katika maisha yangu siwezi 

kukuacha hata siku moja” 

 “ hebu nieleze Fred,mkeo 

amekufanya nini hadi umchukie kiasi 

hiki? Nina hakika kabisa kwamba ulifunga 

naye ndoa kwa sababu ulimpenda na 

uliona kwamba anakufaa kwa sababu 

huwezi kula kiapo na mtu usiyempenda.” 

Akasema Pauline.Alfred akanyamaza na 

kumtazama OPauline kwa makini 

halafuakasema 

 “ Do you real want to know the 

truth?akauliza Fred 

 “ Yes I do” akajibu Pauline.Fred 

akavuta pumzi ndefu kisha akasema 

 “ Kuna watu wasiozidi watano tu 

ambao wanaufahamu ukweli huu ambao 

ninataka kukueleza.Ni ukweli ambao 

hatakiwi kufahamu mtu mwingine yeyote 

zaidi ya sisi watano lakini kwa kuwa 

ninakupenda imenilazimu nikueleze tu.” 

Fred akanyamaza kidogo kisha akasema 

 “ Me and Grace we’re not married..” 

akasema Fred na kumstua Pauline 

 “ You are not married?How come? 

Mbona mnavaa pete za ndoa?  “ Pauline ndiyo maana nilikwambia 

kwamba tuachane na haya mambo.Ni 

mambo magumu kuyaelewa.” Akasema 

Fred 

 “ Fred umenishangaza sana.” 

Akasema Pauline 

 “ Pauline tafadhali naomba tuachane 

na hayo mambo kwa sasa.Nilichokueleza 

kinatosha na ninaomba iwe ni siri 

yako.Kama siku nyingine tukipata wasaa 

nitakueleza kwa undani zaidi kila kitu 

kuhusu mimi na Grace lakini kwa sasa 

naomba tuachane na hayo mambo ili usiku 

wetu usiharibike” akasema Alfred na 

Pauline hakutaka kuuliza tena 

“ Inawezekanaje Fred na Pauline 

wasiwe wanandoa wakati wanavaa pete za 

ndoa? Hapana bado siamini.Lakini kwa 

namna nilivyomtazama macho yake 

wakati ananieleza inawezekana ikawa 

kweli kwani dunia hii imejaa mambo 

mengi sana ya ajabu kama yake 

yanayotokea katika familia yetu ila 

mwaka” akawaza Pauline na 

kumkumbuka baba yake. 

 “ halafu nimekumbuka baba alisema 

kwamba ataandaa chakula usiku wa leo 

kwa ajili yetu.Najua watakuwa 

wametutafuta sana kwani sijawapa taarifa zozote kwamba sintakuwepo.Halafu 

nilipanga pia kuonana na David mchana 

wa leo ili anieleze kuhusiana na hicho kitu 

kikubwa alichosema anataka 

kunieleza.Nitaonana naye hata 

kesho.natumai leo hii atakuwa amepata 

wasaa mzuri wa kuwa na sanya.Nitafurahi 

sana kama watakuwa wapenzi kwani 

Sanya anaonekana wazi kuanza kuvutiwa 

na David.” akawaza Pauline. 

********************



 Kumepambazuka siku ya 

jumapili.Saa kumi na mbili za asubuhi 

ilimkuta Sanya akiwa tayari macho.Alipata 

usingizi wa mang’amu ng’amu .Tukio 

alilolishuhudia usiku chumbani kwa 

David lilimkosesha usingizi kabisa. 

 “ kwa nilichokiona jana 

usiku,ninaogopa hata kukaa karibu na 

David.Anawezaje kumtazama baba yake 

usoni kwa mambo ya aibu 

anayoyafanya?..Siwezi kulifumbia macho 

jambo hili lazima nimtaarifu Pauline ajue 

kinachoendelea ili watu hawa wakanywe 

waachane na mchezo wao.Huu ni ukosefu 

mkubwa sana wa adabu” akawaza Sanya Ilitimu saa nne za asubuhi lakini 

bado David hakuwa ametoka chumbani 

kwake.Alihisi uchovu na vile vile kichwa 

chake kilikuwa na mawazo mengi sana na 

kubwa lilikuwa ni kuhusiana na mpango 

wa Vicky wa kumuua mzee Zakaria 

mpango ambao ulipangwa kutekekezwa 

usiku wa siku ile ya jumapili 

 “ This is the day..Kila kitu 

kitakamilika leo kwa mujibu wa mipango 

ya Vicky.Nasikitika mpaka mida hii 

sijafanikiwa kumueleza Pauline kile 

kinachokwenda kutokea” akawaza na 

kuchukua simu yake akazitafuta namba za 

simu za Pauline akapiga lakini bado simu 

haikuwa ikipatikana. 

 “ Pauline atakuwa wapi? Kwa nini 

ameizima kabisa simu yake 

wakatinilimweleza kwamba kuna jambo 

kubwa ambalo anatakiwa kulifahamu? 

Anyway hakuna kitakachoharibika hata 

kama hayupo.Ila niltamani sana alifahamu 

jambo hili mapema kabla halijatokea.” 

 David akampigia safia akamuuliza 

kama kuna mabadiliko yoyote katika 

mpango wa Vivcky lakini mpaka muda huo 

Vicky hakuw amemtaarifu kama kuna 

mabadiliko yoyote katika mpango wake.  “ David leo lazima kila kitu ifanyike 

kwani tayari amekwisha lipa kiasi 

kikubwa cha pesa.lakini ngoja nimpigie 

nimuulize kama kuna mabadiliko yoyote’ 

akasema safia na baada ya dakika tatu 

akampgia David akamfahamisha kwamba 

tayari ameongoe na Vicky na hakuna 

mabadiliko yoyote 

 “ Good .Kilichobaki hapa ni 

kujiandaa kwa ajili ya usiku wa leo.Leo 

lazima uovu wote wa Vicky ufike mwisho 

na mimi nibaki huru kwani baada ya 

kuachana na Tamia tayari amekwisha 

sema kwamba hataki kuniona nikiwa na 

mwanamke mwingine.Tayari tayari 

nimekwisha mpenda Sanya na hata yeye 

ameonyesha muelekeo mzuri na safari hii 

sifanyi makosa.Ni lazima nimpate Sanya.Ni 

mwanamke ambaye nina hakika ndiye 

atakayenifaa katika maisha yangu kuliko 

hawa walaghai wengine ambao kwao pesa 

na mali ni vitu walivyoweka mbele zaidi” 

akawaza David kisha akainuka akafungua 

mlango akatoka nje akasalimiana na dada 

wa kazi akamuuliza kama amemuona 

Sanya akaambiwa kwamba Sanya bado 

hajaamka.David akashangaa kidogo 

akaenda hadi katika mlango wa chumba 

cha Pauline akagonga na Sanya akaufungua.Alistuka sana alipokutanisha 

macho na David. 

 “ Habari za asubuhi Sanya.Mbona 

umestuka namna hiyo uliponiona? 

Akauliza david huku akitabasamu.Sanya 

akajitahidi kutabasamu kisha akasema 

 “Nilidhani ni Pauline amerejea na 

ndiyo maana nilistuka baada ya kukutana 

na wewe badala ya Pauline.Una taarifa 

zake zozote? Akauliza Sanya 

 “hapana sina taarifa zake 

zozote.Nimejaribu kumtafuta katika simu 

lakini hapatikani” 

 “ Atakuwa na mpenzi w ake 

wanafurahia mapumziko ya wiki” akajibu 

Sanya. 

 “ Sanya tunaweza kutoka baadae 

kwenda sehemu kwa chakula cha 

mchana? Akauliza David 

 “ Ahsante david lakini kwa leo 

sintatoka kabisa nataka nipumzike tu 

ndani.” Akasema Sanya na hakuonekana 

kutaka maongezi marefu akamuomba 

David amuache akaendelee kupumzika 

 “ Sanya ana nini leo? Mbona 

anaonekana hana furaha hata kidogo? 

Halafu Mbona alistuka sana aliponiona? 

Siku ya jana alikuwa ni mwanamke 

mchangamfu sana na mwongeaji lakini leo ameonekana mkimya na asiyetaka 

maonegzi mengi.Anyway ngoja nimuache 

apumzike “akawaza David akaelekea 

chumhani kwake ambako akakuta ujumbe 

katika simu yake,uliotoka kwa Vicky 

madhahabu. 

 “ David nakushukuru sana mfalme 

wangu kwa jana usiku.Ulinifanya nikalala 

usingizi mzuri sana.Samahani sana kwa 

maneno niliyokutamkia jana kuhusu 

sanya.Usiku wa leo nimekuandalia 

chakula cha usiku sehemu Fulani maalum 

kwa ajili yako na Sanya Pekee.Naomba 

unipe jibu tafadhali kama utakuwa tayari 

kuongozana na Sanya kwenda kwa 

chakula cha usiku katika sehemu 

niliyowaandalia” 

 “ Tayari anaanza maandalizi ya 

mipango yake.Anataka jioni ya leo mimi 

na Sanya tusiwepo hapa ili aweze 

kutekeleza mpango wake.”akawaza David 

halafu akaandika ujumbe wa kumjibu 

 “ Asante Vicky lakini hatuna mpango 

wa kutoka leo.Niko nyumbani 

ninapumzika” 

Ujumbe ule ukamstua Vicky ambaye 

alikuwa anatafuta namna ya kuhakikisha 

kwamba wakati wa shambulio litakalofanyika usiku,David hatakuwepo 

nyumbani 

 “ Huyu kijana Mbona anaaza 

kuniweka roho juu ? Endapo akiwepo basi 

anaweza akadhurika kwani anapenda 

sana ushujaa.Ninavyomfahamu atajitahidi 

kupambana na akina Chino na kama 

walivyoniweka wazi ni kwamba yeyote 

atakayeonekana kuwa kikwazo kwao 

lazima watamuondoa tu.Nitafanyaje basi 

ili asiweze kuwepo hapa wakati wa 

uvamizi? Akajiuliza 

 “ Nimepata wazo.Nitalazimika 

kumpeleka Zakaria mapema sana 

chumbani kulala na hivyo watu wote 

wataelekea vyumbani kwao kulala.Sitaki 

jambo lolote limfike David mwanaume 

ninayempenda kuliko wote na haya yote 

ninayafanya kwa ajii yake” akawaza Vicky. 

 Muda ulisonga kwa kasi kubwa na 

hatimaye jua likazama na kiza kikachukua 

nafasi yake.Ilimlazimu Vicky kunywa 

mvinyo mkali ili kuondoa sura ya wasi 

wasi aliyokuwa nayo.Pamoja na kunywa 

mvinyo ule mkali lakini bado aliendelea 

kuwa na wasi mwingi.Hakuna aliyejua 

wasiwasi wake ulitokana na nini zaidi ya 

David pekee.  Saa nane nusu za usiku Pauline na 

Alfred wakarejea nyumbani na 

wakajumuika mezani na wenzao kupata 

chakula cha usiku.Ujio ule wa Pauline na 

Alfred ulimchanganya sana Vicky na 

kumfanya azidi kuwa na wasi wasi. 

 “ Huyu shetani naye ametokea wapi? 

Kwa nini amekuja muda huu ambao 

mambo yanakaribia? Akajiuliza Vicky. 

 “ Vyovyote itakavyokuwa lazima 

mpango ukamilike leo hii.lazima Zakaria 

auawe tu.Nina hakika muda huu Chino na 

kundi lake watakuwa njiani 

wanakuja.Ngoja nifanye haraka haraka 

nimpeleke Zakaria chumbani.”akawaza 

Vicky 

 “I missed you all so much”akasema 

Pauline.Mzee Zakaria akatabasamu na 

kusema 

 “We missed you too Pauline.Mlikuwa 

wapi? Tulipatwa na wasi wasi kidogo” 

 “ Kuna mahala nilikwenda na Alfred 

.Sanya unaendeleaje? 

 “Ninaendelea vizuri sana 

Pauline.”akajibu Sanya maongezi 

yakaendelea wakamaliza chakula na mzee 

Zakaria akaomba waelekee katika 

ukumbi wa mapumziko kwa maongezi ya 

hapa na pale  “ Pauline naomba sisi tuelekee 

chumbani kuna jambo ninataka kuongea 

nawe.” Akasema sanya kisha Pauline 

akaomba samahani akaondoka na Sanya 

wakaelekea chumbani. 

 “ Guys imekuwa ni siku ndefu sana 

nadhani hakuna haja ya kuwa na 

maongezi marefu na kumchosha 

mzee.Nadhani na ninyi pia mngeenda 

kupumzika ili kumpa mzee nafasi ya 

kupumzika”akasema Vicky 

 “ Hakuna tatizo kama tukiendelea na 

maongezi kidogo na mzee.Isitoshe 

anahitaji sana kufahamiana na mkwewe 

Dr Alfred”akasema David na kumfanya 

mzee Zakaria kushangaa 

 “Mkwe wangu? 

 “Ndiyo mzee.Utanisamehe kwa 

kuwahi kukujulisha suala hili kabla ya 

Pauline lakini hakuna 

kilichoharibika.Pauline amekuja na mkwe 

wako na ninadhani amekuja 

kumtambulisha rasmi kwako”akasema 

david. 

 “ Ouh hii ni habari njema 

sana.Pauline alinipigia simu na kuniambia 

kwamba ana jambo kubwa anataka 

kuongea na mimi kumbe alikuwa anakuja 

kumtambulisha mkwe wangu.karibu sana Dr Alfred .Nimefurahi sana 

kukufahamu”akasema mzee Zakaria 

akainuka na kwenda kumpa mkono Dr 

Fred wakapogezana. 

 “Mungu wangu hapa hakuna dalili za 

maongezi kumalizika sasa hivi.Nitawezaje 

kumuondoa David hapa ? nadhani muda 

huu Chino yuko karibu sana kufika 

inakaribia saa nne na nusu sasa”akawaza 

Vicky halafu akamgeukia David. 

 “ david kwa kuwa umekwisha 

mtambulisha shemejiyo kabla ya 

muhusika mwenyewe kumtambulisha 

kwanini basi usiwape nafasi mtu na 

mkwe wake waendelee na maongezi na 

kufahamiana zaidi? 

 “ Hapana Darling.David naye 

anatakiwa amfahamu vyema shemeji yake 

,kwa hiyo anatakiwa kuwepo 

hapa.”akasema mzee Zakaria 

 “ Ouh Mungu wangu nitafanya nini 

sasa ? kila mpango wa kumuondoa David 

mbona unashindikana? Akawaza Vicky 

akainuka na kuelekea chumbani 

 “ Nadhani muda wa tukio 

umekaribia sana ndiyo maana Vicky 

anahaha namna hii .Ee Mungu tusaidie” 

akawaza David “ Sanya samahani sana jana sikuweza 

kurudi.Kuna mahala tulikwenda mimi na 

Alfred na tukashindwa kabisa 

kurudi.Unaendeleaje? Nadhani 

haukuboreka kabisa kwa kukuacha peke 

yako.” akasema Pauline baada ya kuingia 

chumbani 

 “ Usijali Pauline hata mimi nilielewa 

kwamba kuna mahala mlikwenda 

kufurahia mapumziko.Mimi niko salama 

sina tatizo lolote na wala 

sijaboreka.Nimekuta filamu nyngi humu 

chumbani nakutwa nzima ya leo 

nimeshinda ninatazama.Vipi mambo 

yalikwendaje huko ? akauliza 

Sanya.Pauline akatabasamu na kusema 

 “ Mambo yalikwenda vizuri sana. 

Tulikuwa na wakati mzuri na 

kufahamiana zaidi kwani mimina Alfred 

hatuna muda mrefu katikamahusiano 

yetu..” Akasema Pauline 

 “ Nafurahi sana kusikia hivyo 

japokuwa bado naendelea kukusisitizia 

kuhusu suala la kuolewa kama kweli 

mnapenda kwa dhati nasi kuchezeana.” 

Akasema Sanya na kumfanya Pauline 

acheke kidogo. 

 “ Tuachane na hayo Pauline kuna 

jambo ambalo nimekuitia hapa.” Sanya akanyamaza akamtazama pauline halafu 

akaendelea 

 “ Pauline nitakuwa muwazi kwako 

na ninaomba unisamehe kama nitakuudhi. 

Lakini sualahili siwezi kulifumbia macho 

hata kidogo.Kuna kitu kimenisikitisha 

sana hapa ndani kwenu” akasema Sanya 

 “ Sanya anataka kusema nini? Kuna 

kitu amegundua kuhusu mimi na Alfred? 

Pauline akajiuliza.Sanya akaendelea 

 “ Jana usiku kuna jambo 

nimelishuhudia humu ndani limenifanya 

nikose kabisa usingizi.Sijalala usiku wa 

leo nimekesha nikitafakari na siwezi 

kulifumbia macho jambo hili hata kidogo 

na lazima nikueleze ukweli” 

 “ Sanya ni jambo gani hilo ,nieleze 

tafadhali” akasema Pauline kwa wasiw asi. 

 “ Kama unakumbuka jana baba 

alituandalia chakula maalum cha 

kutukaribisha ,baada ya chakula tulikuwa 

na maongezi kidogo na halafu kila mmoja 

akaelekea chumbani kwake kulala.Nikiwa 

chumbani nilianza kusikia vishindo kama 

watu wakigombana ikanilazimu kutoka 

chumbani ili kuona kama ni kweli kuna 

watu walikuwa 

wanagombana.Nililazimika kufuatilia 

vishindo vile na kugundua vilitoka katika chumba cha David.Niliogopa sana kwani 

nilihisi labda David kavamiwa chumbani 

ikanilazimu kuufungua mlango wa 

chumba chake ili nijue kinachoendelea na 

nikakutana na kitu ambacho niaibuhata 

kukisimuliza.” akasema Sanya na 

kunyamaza. 

 “ Uliona nini Sanya? Akaulizia Paline 

 “ Ni jambo la aibu lakini lazima 

tuuseme ukweli ili kulikomesha jambo hili 

lisijirudie tena” 

 “ Niambie Sanya uliona nini? 

 “ Nilimkuta David na mama yako 

mdogo wakifanya mapenzi” 

 “ Ouh my God !! akasema Pauline 

.Alistuka sana 

 “ samahani sana pauline kwa 

kukuambia jambo hili ambalo nina hakika 

limekustua sana lakini hakuna namna 

nyingine ya kufanya zaidi ya kulisema 

.Hata mimi limenistua na kunikosesha 

usingizi usiku .kwa nini david afanye 

hivi? Kutembea na mama yake mdogo? 

Hili ni jambo la aibu sana kwake na kwa 

familia yenu yote.Anawezaje kufanya 

jambo kama hili? Akauliza sanya.Pauline 

akainama akatafakari 

 “ Pauline nimekueleza hili ili uweze 

kulifanyia kazi na kuwakanya wasiendelee kufanya uchafu wao tena ndani ya 

nyumba ya baba yako na kibaya 

zaidiwanafanya kwa kujiamini kabisa bila 

hata kufunga mlango.Nivipi kama 

wangekutwa na baba? David anajitafutia 

laana kubwa .Kitedo anachokifanya katu 

hakivumiliki hata kidogo .Wewe kama 

ndugu yake unatakiwa umkanye aachane 

kabisa na suala hili baya analolifanya 

kabla hajagundulika na kuichafua familia 

yenu..Nilitokea kumpenda sana David na 

nilimuona ni kijana mwenye adabu zake 

lakini kwa hili nililomshuhudia analifanya 

nimemshusha thamani kabisa na hafai 

hata kidogo” akasema sanya ambaye hata 

uso wake ulionyesha kwamba alikuwa 

amekerwa sana na kitendo kile cha David 

 “ Mungu wangu aibu gani hii jamani? 

Akawaza Pauline 

 “ Nilikwisha hisi kitu kama hiki toka 

zamani lakini sikuwahi kupata nafasi ya 

kuwanasa kwaniwalikuwa wanafanya 

mambo yao kwa siri sana ila walisahau 

kwamba siku zote za mwizi ni arobaini 

hatimaye wamebainika 

wanachokifanya.Kwa kitendo hiki hata 

mimi nimemchukia sana David.Kumbe ni 

kijana mshenzi kiasihiki na hafai kabsa 

hata kuendelea kukaa humu ndani.Kwa nini lakini amfanyie baba mambo kama 

haya wakati baba anampenda na anamlea 

kama mtoto wake? Hapana suala hili 

halivumiliki hata kidogo” akawaza Pauline 

na macho yake yakaonekana kujaa 

machozi 

 “ Pauline samahani sana kwa 

kukueleza jambo hili ambalo najua 

limekuumiza sana lakini sina namna 

nyngine ya kufanya zaidi ya kukueleza 

ukweli .” akasema Sanya 

 “ Sanya ahsante kwa kunieleza 

ukweli.Wewe ni rafiki wa kweli.Angekuwa 

ni mwingine asingekubali kunieleza 

waziw azi kwa kuogopa kuniudhi lakini 

wewe umejitoa muhanga na kunieleza ili 

kuikomesha tabia hii chafu.Ninaomba 

samahani sana kwa ulichokiona ambacho 

najua kimetia doa katika ile taswira nzuri 

uliyokwisha ipata kwa familia yangu.Huu 

ni uchafu ulipotiliza na usiovumilika hata 

kidogo.najuta ni kwa nini nilimkaribisha 

Daid humu ndani.Mimi ndiye 

niliyesababisha haya yote kutokea.” 

 “ Pauline unasema nini? Sanya 

akashangaa 

 “ Sanya naomba nikuweke wazi 

kwamba David si ndugu yetu kabisa na 

wala hatufahamu ametoka wapi,hatuifahamu historia yakewala 

familiayake .Hivi sasa ndiyo tumeamza 

kuzifahamu tabia zake.” 

 “ Pauline unanishangaza sana ” 

 “ najua utashangaa sanya lani huo 

ndio ukweli.David si mtoto wa familia 

hiinawalahatuna nasaba naye lakini kwa 

namna tunavyoishi naye si rahisi kabisa 

kujua kwamba si mtoto wa familia yetu. 

Ilivyotokea hadi akafika hapa ni kwamba 

aliwahi kumsaidia baba alipopatwa na 

matatizo wakati akiendesha gari.Baba 

yangu anasumbuliwa na matatizo ya 

sukari na shinikizo la damunasiku 

hiyoalipatw ana matatizo njiani hivyo 

David alimsaida na alionyesha uaminifu 

mkubwa sana kwani siku ile baba alikuwa 

na milioni nyingi ambazo angeweza 

kuondoka nazo lakini hakutumia fedha 

zile na akaziwasilisha salama.Kitendo kile 

kilitufanya tumuamini sana na hasa mimi 

.Hakuwa na makazi wala ndugu hapa 

Arusha kwani siku hiyo hiyo alikuwa 

amema;liza kifungo chake 

gerezani.Nilimuonea huruma na 

kumchukua akaja kuishi nasi hapa.Baadae 

tukagundua kwamba ana taaluma ya 

biashara na kwa kuwa tulihitaji mtu wa 

kutusaidia katika masuala ya biashara tukampa kazi na akaifanya kazi yake 

vizuri sana na kwa uaminifu 

mkubwa.Baba akamuamini na kumfanya 

kuwa msimamizi wa biashara zake 

zote.David alikuwa ni kijana mzuri na 

mchapakazi sana hadi pale alipoanza 

kuwa na ushirika na mama mdogo” 

 “ ushirika na mama yako mdogo? !! 

akauliza sanya 

 “ Ndiyo sanya.mama yangu mdogo ni 

mwanamke ambaye kwake yeye vitu 

vyenye thamani ni pesa na mali tu na 

ndiyo maana mimi na yeye katu 

hatuelewani.Toka ameolewa na baba 

amekuwa akifuja sana mali za baba 

alizozihangaikia kwa muda mrefu .Huyu 

mwanamke ndiye aliyembadilisha David 

na kumfanya awe hivi alivyo. 

 “ Unataka kuniambia kwamba huyu 

mwanamke ndiye aliyemshawishi David 

hadi akakubali kufanya kitendo kile cha 

aibu? Ni mwanamke wa aina gani huyu? 

 “ Nina uhakika huo kwa sababu 

ninamfahamu vizuri mama mdogo,si 

mwanamkemwenye sifa nzuri na kila mtu 

alishangaa sana pale baba alipoamua 

kumuoa huyu mwanamke baada ya mama 

kufariki.Nina uhakika mkubwa ndiye 

aliyembadilisha David kwani mwanzoni alikuwa ni kijana mzuri na mwenye tabia 

njema “ akasema Pauline. 

 “ kama ni hivyo basi mwanamke 

huyu hafai hata kidogo lakini pamoja na 

hayo kwa nini David akubali kuingia 

katika ujinga wa namna hii? Kwa nini 

akubali kirahisi kufanya uchafu huui? 

Akauliza sanya 

 “ Ninamfahamu vizuri David ni 

mmwanamume dhaifu sana kwa 

wanawake na ni rahisi sana 

kushawishika.Sikuwa nimepanga 

kukueleza jambo hili lakini ni vyema kama 

ukijua.Mimi na david truliwahi kuwa 

wapenzi japo kwa siku chache.” 

 ” kweli ?!! sanya akashangaa sana. 

 “ kweli sanya .Nilitokea kumpenda 

sana David toka mara ya kwanza 

nilipomuona licha ya uchakavu 

wake.Nilimuweka moyoni na nilimpemda 

kwa dhati kabisa.kwa bahati mbaya david 

akanisaliti kwa kutembea na rafiki yangu 

mkubwa Tamia.Niliumia sana na ndiyo 

maana nikaamua kuondoka kabisa Arusha 

na kwenda kupumzika Moshi ambako 

nilikutana na Alfred ambaye amenifuta 

machungu yote niliyoumizwa na David 

kwa hiyo miminisababu nyingine ya Alfred 

kuwepo hapa nyumbani”  “ Pole sana Pauline.kwa nini 

hukunieleza jambo hili hapo kabla? Hata 

mimi nilipomuona david nikatokea 

kuvutiwa naye sana lakini bada ya 

kushuhudia akifanya uchafu ule jana na 

haya maneno uliyonieleza leo sina hamu 

naye hata kidogo na hanifai 

kabisa.Hujachunguza ni kwa nini 

alifungwa gerezani? Ametokea wapi? 

Familia yake iko wapi? Akauliza Sanya 

“ Hapana hatujawahi kuchunguza 

mambo hayo yote na hata yeye mwenyewe 

hataki kabisa kuongelea hayo mambo 

.Kwa kuwa tunamuamini tuliamua 

kuachana naye na tusimuulize chochote 

hadi hapo yeye mwenyewe atakapokuwa 

tayari kutueleza” akasema 

 “ Mlifanya kosa kubwa Pauline 

kumkaribisha ndani mtu ambaye 

hamuijuia historia yake.Mnaweza 

mkamkaribisha na mhalifu akawafanyieni 

kitu kibaya sana”akasema Sanya. 

 “ Usemayo ni ya kweli Sanya.lakini 

haya yote yalisababshwa na upendo 

wangu mkubwa kwake.Kama nisingetokea 

kumpenda David kwa kipindi kile 

asingekuwa hapa nyumbani na kutuletea 

aibu hii. Lakini mwisho wake umekaribia 

sana na sintauvumilia kabisa ujinga huu anaoufanya.Lazima aondoke hapa 

nyumbani haraka iwezekanavyo. 

Laz…………..” kabla hajamaliza sentensi 

yake ikasikika milio mitatu ya 

risasi.Pauline na Sanya wakastuka na 

kuogopa sana.Baada ya dakikamoja 

ikasikika tena milio mingine ya risasi 

safari hii ikiendelea mfululizo. 

 “ Sanya tumevamiwa !! akasema 

Pauline huku akitetemeka 

 “ Mungu tusaidie”akasema Sanya 

,wakafungua mlango wa choo na kujificha 

humo.Milio ya risasi iliendela kurindima 

kwa zaidi ya dakika ishirini halafu kukawa 

kimya na baada ya kama dakika tano hivi 

toka risasi zile zikome wakasiika watu 

wakiongea na mlango w a chumba cha 

Pauline ukafunguliwa. 

 “Hakuna mtu humu” ikasikika sauti 

ya mtu mmoja 

 “ Angalia sehemu zote hadi 

chooni.Wengine wanaweza kukimbilia 

wakajificha huko.i’ akasema mwingine. 

 Pauline na Sanya wakakumbatiana 

kwani walijua muda wao umefika. 

 “ Ee Mungu tuokoe”akasema sanya 

huku akilia na mara mlango ukapigwa 

teke na kufunguka wakaingia watu wawili.  “ Simameni “ Mtu Yule akatoa 

amri.Pauline akafumbua macho na 

kukutana na askari wawili wenye silaha. 

 “ Tafadhali tokeni humu ndani.Mko 

salama sasa.Kuna yeyote aliyeumia? 

Akauliza mmoja wa wale askari.Hakuna 

aliyeweza kujibu wote walikuwa 

wanatetemeka.Askari wakawachukua na 

kuwapeleka sebuleni. Ghafla Pauline 

akajikuta akiangua kilio kikubwa baada ya 

kuona askari wamembeba David 

wakimtoa nje akiwa amechafuka 

damu.Alikuwa amepigwa riasasi.. 

Kelele aliyopiga Pauline ilikuwa kubwa 

ikawalazimu maaskari wawili kumchukua 

na kumtoa pale sebuleni wakampeleka 

chumbani kumtuliza.Alikuwa 

anaweweseka huku akiongea maneno 

yasiyoeleweka..Sanya aliishiwa nguvu 

akakaa chini.Mwili wote ulikuwa 

unamtetemeka.Pale sebuleni kulikuwa na 

watu wawili ambao walikuwa 

wameanguka chini na hawakuonekana 

kuwa na uhai tena .Mzee Zakaria alilazwa 

sofani akipatiw a huduma na Alfred hali 

yake ilikuwa mbaya kutokanana mstuko 

alioupata.. 

 Mara askari wakawaingiza watu sita 

wakiwa wamefungwa pingu na wawili kati yao wakivuja damu kutokana na majeraha 

ya risasi. 

 “ Mna hakika hakuna tena jambazi 

mwingine aliyesalia ? akauliza kiongozi 

wa kikosi kile cha askari 

 “ hakuna afande”akajibu mmoja 

wapo 

 “ Mmezunguka nyumba yote na 

kuhakikisha kwamba hakuna mtu 

aliyejificha? 

 “ Ndiyo afande.Tumepekua kila 

mahala na hakuna jambazi yeyote 

aliyefanikiwa kutoroka wala kujificha.” 

Akasema Yule askari. 

 “ kazi nzuri sana.Silaha zao zote 

zimechukuliwa? 

 “ ndiyo afande.” Akajibu Yule askari 

kiukakamavu. 

 “ wachueni hao majeruhi 

muwakimbize hospitali,wale ambao 

hawajajeruhiwa wapelekwe moja kwa 

moja kituoni bila kumsahau muhusika 

mkuu.” Akaamuru askari kiongozi. 

 Vicky madhahabu akatolewa 

chumbani na kuletwa sebulnei akiwa 

amefungwa pingu.Macho yake yalijaa 

machozi na alikuwa analia akiomba 

aachiwe huru kwani hana kosa lolote.  “ Mpakieni garini na mumpele moja 

kwa moja kituoni muuaji mkubwa huyu” 

akaamuru kiongozi na bila kuchelewa 

Vicky madhahabu na wale watuhumiwa 

wengine wanne ambao hawakujeruhiwa 

wakapakiwa garini na kupelekwa moja 

kwa moja kituoni.Wale majeruhi wawili na 

wale watu wengine wawili waliokuwa 

wamelala pale sebuleni ambao 

hawakuonekana kuwa na uhai 

wakapakiwa katika gari lingine la polisi na 

kupelekwa hospitali 

“ Mzee anaendeleae? Askari mkuu 

akamuuliza Alfred.. 

 “ bado hali yake si nzuri 

sana,anatakiwa akimbizwe hospitali” 

akasema Alfred 

“ gari la wagonjwa liko njiani 

linakuja.Jitahidi kadiri ya unavyoweza 

kunusuru uhai wake hadi hapo gari la 

wagonjwa litakapofika” 

.Alfred akainuka na kumfuata sanya 

aliyekuwa amekaa chini hana nguvu 

 “ Sanya polesana kwa tukio hili la 

kustukiza ambalo najua limekustua 

sana.Sote tumestushwa sana na tukio hili 

lakini tunashukuru askari wamewadhibiti 

wale wahalifu na hakuna hatari tena. kwa 

sasa tuna hatari moja iliyobaki mbele yetu.Mzee Zakaria amepatw a namstuko 

mkubwa sana na mapigo yake ya moyo 

yako chini mno.Tunatakiwa kuhakikisha 

anakuwa salama hadi hapo gari la 

wagonjwa litakapowasili” akasema Alfred 

.Sanya bado alionekana kuwa katika ile 

hali ya taharuki kwa tukio lile. 

 “ Sanya tafadhali nakuomba 

sana.Jitahidi unisaidie .Tunafanya hivi 

kwa ajili ya Pauline” akasema Alfred na 

kumshika Sanya mkono akamsaidia 

kuinuka wakaenda kusaidiana kumpatia 

huduma mzee Zakaria . 

 Gari la wagonjwa likawasili ndani ya 

muda mfupi wakampakia mzee Zakaria 

na kumkimbiza hospitali.Sanya na Alfred 

nao pia waliambatana na gari la wagonjwa 

kuelekea hospitali. 

 Upekuzi mkubwa ukafanyika kwa 

mara ya pili ndani ya nyumba ya mzee 

Zakaria ilikuhakikisahkwamba hakuna 

hatari yoyote na kisha wakabaki askari 

kadhaa kwa ajili ya kuimarisha ulinzi 

mahala na wengine wakandoka kuelekea 

hospitali kufuatilia hali ya mzee Zakaria 

na wale majeruhi wengine pamoja na 

Pauline ambaye alionekana kupatw ana 

mstuko ***************** 

 Imekwisha timu saa nane za usiku na 

madaktari wa hospitali ya St Gasper 

wakisaidiana na Alfred na sanya 

walifanikiwa kuyarejesha mapigo ya moyo 

ya mzee Zakaria katika hali yake ya 

kawaida japokuwa bado hakuwa na uwezo 

wa kuongea.Mashine zilionyesha kwamba 

mifumo yote ya mwili ilikuwa inafanya 

kazi vizuri.Madaktari wakapongezana kwa 

kufanikiwa kumuondoa mzee Zakaria 

katika hatari.Alfred akataarifiwa kwamba 

Pauline naye alikuwa amepumzishwa kwa 

muda katika hospitali ile baada ya kupata 

mstuko alipomuona kutokana na tukio lile 

la kustusha. 

 Alfred na sanya wakaenda katika 

chumba alichopumzishwa Pauline ambaye 

mara tu alipowaona alitaka kujua hali ya 

baba yake na David 

 “ Mzee hali yake inaendelea vizuri na 

mapigo yake ya moyo yamerudia hali yake 

ya kawaida.Hayuko tena katika hatari kwa 

hiyo usihofu.Kuhusu David sina habari 

zake kwa sasa kwani amepelekwa katika 

hospitali kuu ya mkoa kwa hiyo ninataka kuelekea huko kujua maendeleo yake” 

akasema Alfred 

 “ Ee Mungu msaidie David aweze 

kupona” akaomba Pauline huku machozi 

yakimtoka 

 “ Usilie Pauline.Kilichopo hapa ni 

kumuombea sana David aweze 

kupona.he’s a hero.He saved your father” 

akasema Alfred huku naye akishindwa 

kuyazuia machozi kumtoka. 

 “ Fred mlikuwa wote pale sebuleni 

nini hasa kilitokea?Wavamizi wale ni 

akina nani na waliingiaje mle 

ndani?akauliza Sanya 

 “ hata mimi bado mwili 

unanitetemeka nikikumbuka tukio 

lile.Mlipoondoka tuliendelea na maongezi 

yetu na hatukujua kumbe kuna watu 

wanatuvamia.Tukiwa hatuna hili wala lile 

mara ghafla tukasikia milio mitatu ya 

risasi karibu sana na 

palenyumbani.Wakati tunajiuliza kama 

risasi zile zimelia wapi pale nyumbani au 

nyumba ya jirani wakatokea watu wawili 

wakiwa na bunduki.Walituamuru wote 

tulale chini lakini David akawahi 

kumrukia mzee Zakaria na mara nikasikia 

milio ya risasi mfululizo.Nilikuja 

kufumbua macho baada ya kusikia sauti za askari na ndipo nilipomuona David akiwa 

ametapakaa damu mwili mzima.wale 

jamaa wawili walioingia pale sebuleni 

wakiwa na silaha waliuawa na 

polisi.David is a hero,he saved your father” 

akasema Alfred.Pauline akaangua 

kilio.Sanya akambembeleza anyamaze. 

 “ Ouh David.He saved my father 

again” akasema Pauline huku akilia kwa 

uchungu 

 “ Pauline nyamaza kulia 

,tunachotakiwa ni kumuombea kwa 

Mungu ili aweze kupona .Kitendo 

alichokifanya ni cha kishujaa sana .kama 

asingekuwa yeye hivi sasa tungekuwa 

tunaongea mambo mengine.Endelea 

kupumzika Pauline sisi tunakwena 

kufuatilia maendeleo ya David “ akasema 

Fred 

 “ Fred tunakwenda wote.lazima na 

mimi nikajue maendeleo ya David” 

akasema Pauline huku akiinuka kitandani 

 “ Una hakika hali yako inaruhusu? 

Akauliza David 

 “ Ndiyo David.hapa nilipumzishwa 

kwa muda tu kutokana na mstuko 

nilioupata lakini hali yangu sasa ni 

nzuri.lakini kabla ya kuondoka nataka 

kwanza nikamuone baba yangu niridhike kwamba anaendelea vizuri” akasema 

Pauline kisha wote wakatoka na kueleka 

katika chumba alimolazwa mzee 

Zakaria.Hawakuruhusiwa kuingia mle 

chumbani bali alimtazama kupitia kioo 

cha mlangoni.Daktari aliyekuwa 

akimuhudumia Zakaria akamuhakikishia 

Pauline kwamba baba yake anaendelea 

vizuri sana na asihofu kitu 

 Hawakuwa na gari hivyo 

ikawalazimu kuomba msaada wa gari pale 

hospitali ili liwapeleke hospitali ya mkoa 

alikopelekwa David. 

 “ Alfred polisi wanasema watu wale 

waliotuvamia ni akina nani? Wamekwisha 

tambuliwa? Akauliza Pauline 

 “ Mpaka sasa bado hawajasema 

chochote kwani uchunguzi bado 

unaendelea lakini niliwasikia katika 

maongezi yao wakipongezana kwamba 

hatimaye baada ya kumtafuta kwa muda 

mrefu sasa wamempata.Inaonekana watu 

wale walikuwa ni majambazi na walikuwa 

wanawindwa sana na askari .Uchunguzi 

utakapokamilika tutajua kila kitu ila kuna 

kitu kingine unatakiwa ukifahamu,mama 

yako mdogo naye amechukuliwa na 

polisi.”  “ Amechukuliwa na polisi?!! Kwa 

nini? Pauline akashangaa sana. 

 “ Hatufahamu ni kwa nini na polisi 

hawajatoa maelezo yoyote .Yawezekana 

labda wamemchukua kwa ajili ya 

mahojiano na baadae wanaweza 

wakamuachia” akasema Alfred 

 “ Alfred bado mwili unanitetemeka 

nikikumbuka picha ile ya David akitolewa 

mle ndani akiwa ametapakaa 

damu.Ninamuomba Mungu amvushe 

katika hili kwani natakiwa nimshukuru 

kwa kumuokoa baba yangu.Hata David 

kama binadamu wengine ana mapungufu 

yake lakini binafsi nimemsamehe yale 

yote aliyonikosea na kuikosea familia 

yetu.Alfred I don’t want him to die” 

akasema Pauline na kuangua tena kilio. 

 “ Pauline tafadhali usiendelee 

kulia.Huu ni wakati wa kusimama imara 

kwa ajili ya kaka yako David.Kulia 

hakutasaidia kitu chochote.Tunatakiwa 

tusimame imara katika maombi na Mungu 

amponye David.Hiki ni kipindi kigumu 

sana kwa familia yako lakini tuko hapa 

pembeni yako tutasimama pamoja nawe 

hata katika nyakati zile ngumu 

sana.”akasema Alfred  “ Alfred ninashukuru sana ila 

ninasikia uchungu sana kwani 

nimemtamkia David maneno mengi 

mabaya sana ,nimemtolea laana za kila 

aina .Ninajilaumu sana kwa maneno 

niliyoyatamka juu yake hata kama 

alinikosea.Natamani nipate nafasi ya 

kumuomba msamaha.I don’t want him to 

die ”akasema Pauline na kuendelea kulia 

 Walifika katika hospitali kuu ya 

mkoa wakataarifiwa kwamba David 

alikuwa katika chumba cha upasuaji na 

madaktari waliendelea na jitihada za 

kuokoa maisha yake kwa kumfanyia 

upasuaji wa kuondoa risasi.Alfred 

akawaongoza akina Pauline wakaenda 

kukaa nje ya chumba cha upasuaji 

wakisubiri taarifa toka kwa 

madaktari.Usiku huu hali ya Arusha 

ilikuwa ni ya ubaridi,Alfred akavua koti 

lake na kumpatia Pauline halafu akavua 

shati na kumpatia Sanya ,yeye akabakiwa 

na fulana ya ndani .. 

 “ Thankyou Alfred”akasema Pauline. 

 “ Ouh David why always him? He 

saved my father once and this time he 

saved him again.Nina deni kubwa sana 

kwake na ndiyo maana ninamuomba 

Mungu amsaidie aweze kupona.Ninaapa sintamnyanyasa tena na wala sintamsema 

vibaya .Nitamuheshimu kama kaka yangu 

.Huyu ni mtu muhimu sana kwa familia 

yetu.Pamoja na yote aliyoyafanya kwangu 

na kwa baba lakini bado tuna deni kubwa 

kwake na tunatakiwa kumuhesabu kama 

mmoja wa wana familia yetu na si mtu 

baki.” Akawaza paulinena kufuta machozi 

,akamkumbuka mama yake mdogo 

 “ kwa nini polisi wanamshikilia 

mama mdogo? Yawezekana anahusika 

katika tukio hili? Ninamfahamu mama 

mdogo ni mtu anayependa sana maisha ya 

anasa lakini sidhani kama anaweza 

akafikia hatua ya kushirikiana na 

majambazi kuja kuiba kwani anapata kila 

kitu anachokitaka.Najua wamemchukua ili 

wamfanyie mahojiano kwani .Kitu kingine 

ninachojiuliza askari wale walitokea wapi 

na kufika pale nyumbani haraka namna 

ile na kufanikiw akuwadhibiti wale 

majambazi? Nimejiuliza sana swali hili 

nimekosa majibu.Au yawezekana 

walikuwa katika doria na wakawastukia 

watu wale na kuwafuatilia na 

kuwavamia,.au inawezekana kuna raia 

mwema alitoa taarifa kwa polisi 

kuhusiana nakuwepo kwa mpango wa 

kuvamia nyumba yetu hivyo wakaweka mtego.Kama yupo mtu huyo tunastahili 

kumjua na kumpa zawadi kubwa.Askari 

wale pia wanastahili sifa na pongezi kwa 

namna walivyopamba na watu wale na 

kuwadhibiti.”akaendelea kuwaza Pauline 

wakiwa wamekaa nje ya chumba cha 

upasuaji 

 “ Kuanzia sasa inatubidi tuweke 

ulinzi mkali palenyumbani .Tulijiamini 

sana kwamba tuko salama na ndiyo maana 

hatukusumbuka kutafuta walinzi.Lakini 

kwa tukio la leo tayari nimepata somo 

.lazima tutafute walinzi.Kuna makampuni 

mengi ya ulinzi tutatafuta kampuni moja 

watulindie nyumba yetu.Nitamshauri baba 

tufunge kamer…………”Pauline akastuliwa 

toka mawazoni baada ya mlango wa 

chumba cha upasuaji kufunguliwa na 

kitanda kikatolewa kikiwa na mgonjwa 

juu yake.Wote wakasimama na 

kuwakimbilia wauguzi waliokuwa 

wakikisukuma kitanda kile na kutaka 

kufahamu kama mgonjwa yule alikuwa ni 

david lakini wakataarifiwa kwamba 

badoDavid alikuwa katika 

upasuaji.Wakaendelea kukaa pale nje 

wakisubiri. 

******************  Vicky madhahabu alipiga ukele 

mkubwa palemlango wa mahabusu 

ulipofunguliwa ili aingizwe ndani ya 

chumba cha mahabusu wa kike.Askari 

alioongozana nao hawakumjali 

wakamsukumia ndani na kuufunga 

mlango ule imara.Vicky alikaa chini na 

kuendelea kulia kilio kikubwa na mara 

akatokewa mwanamke mmoja 

aliyekuwamo mle mahabusu akamshika 

nywele na kumuinua.Vicky akainua uso 

wake kwa hasira iliamtazame mtu 

aliyemuinua na mara akajikuta 

anatazamana na mwanamke mmoja 

mnene mwenye nywele timutimu ambaye 

katika mikono yake alijichora michoro. 

 “ Wewe mwanamke nakuomba 

unyamaze na usitupigie kelele humu 

ndani.Tumekaa tunatafakari namna ya 

kujikomboa na matatizo yetu na wewe 

unatupigia kelele.Nasema nyamaza haraka 

sana”akasema Yule mwanamama 

aliyeonekana mshari 

 Vicky alimtazama kwa dharau juu 

mpaka chini kisha akaendelea kupiga 

kelele akitaka atolewe mle mahabusu 

kulimokuwa na harufu mbaya .Yule mama 

akamfuata tena na safari hii bila kumsemesha akamnasa vibao vitatu vikali 

na Vicky akaanguka chini. 

 “ Nimekwambia hatutaki kelele zako 

humu ndani.”akasema Yule mama.Vicky 

akaogopa ma hakulia tena.Yule mama 

akamfuata pale chini. 

 “ Ni mara yako ya kwanza kuingia 

mahabusu?akamuuliza 

 “ Ndiyo ni mara ya kwanza” 

 “ Umefanya nini hadi ukaletwa 

humu? Unaonekana unatoka familia tajiri 

wewe” Akauliza Yule mama lakini Vicky 

hakujibu kitu.Machozi yaliendelea 

kumbubujika.Yule mwanamke akaamua 

kuachana naye. 

 “ Nimekwisha mimi Vicky.I’m totally 

finished.Mambo yote 

yameharibika.Nimechanganyikiwa kabisa 

na sijui nifanye nini.Mipango yangu yote 

imeshindikana.Nini kimetokea ?Askari 

wale wamejuaje kuhusu tukio lile? “ Vicky 

madhahabu akainama na kufuta machozi 

 “ Ama kweli nimecheza pata 

potea.Sikutegemea kabisa kama jambo hili 

lingefika hapa lilipofika.Ouh masikini 

mimi jamani ntafanya nini? Akina Chino 

wamekosea wapi ? Lazima kuna mtu 

aliyevujisha siri hii kwa askari.Ni nani basi 

aliye fanya hivyo? Hakuna mtu mwingine aliyekuwa akilifahamu jambo hili zaidi ya 

Safia.Yawezekana jambo hili limevuja kwa 

akina Chino. Nimechanganyikiwa na sijui 

nifanye nini.Maisha yangu 

yameharibika.Polisi tayari wanafahamu 

kila kitu.Ee Mungu nisaidie mimi 

jamani.Ninakwenda kuangamia.”akawaza 

Vicky na kuanza tena kulia kwa sauti 

kubwa. 



TWENDE KAZI 

Saa kumi na moja za alfajiri upasuaji 

ulikamilika na David akatolewa na na 

kupelekwa katika wodi ya uangalizi.Akina 

Pauline walifuatana na wauguzi wale 

waliokisikuma kitanda hadi katika wadi 

ya wagonjwa waliotoka katika 

upasuaji.Hawakuruhisiwa kuingia ndani 

wakabaki nje ya wodi.Pauline alikuwa 

anatetemeka kwa woga. 

 “ Pauline David will ok.He will fight 

this.Be strong “ Alfred akampa moyo 

Pauline.Baada ya daktari kuhakikisha 

kwamba mashine zote anazotakiwa 

kufungwa David ili kumsiaidia kwa 

wakati huo zilifanya kazi vizuri akawaita 

akina Pauline ofisini kwake.  “ Poleni sana lwa matatizo 

yaliyowakuta.” Akaanzisha maongezi 

daktari. 

 “ Ahsante sana Daktari” wakajibu 

kwa pamoja 

 “ Nimewaiteni hapa kuwapeni taarifa 

za mgonjwa wenu.David alipigwa risasi 

tano katika sehemu mbalimbali za mwili 

wake.Risasi moja ilimpata katika bega 

lake la kushoto ,risasi nyingine ikampata 

maeneo ya karibu na nyonga .Nyingine 

ikampiga katika paja na mbili alipgiwa 

tumboni.Upasuaji wa kuziondoa risasi zile 

umechukua muda mrefu lakini nafurahi 

kuwataarifu kwamba tumefanikiwa na 

risasi zote zimeondolewa mwilini mwa 

David .” akasema daktari. 

 “ Ouh thank God” akasema Pauline 

akiwa ameifumbata mikono yake kifuani. 

 “ Kwa hiyo vipi maendeleo yake kwa 

sasa? Akauliza Pauline 

 “ kwa sasa ni mapema sana kusema 

chochote kwani bado mgonjwa yuko 

katika usingizi.Tunasubiri 

atakapozinduka tumpime na tuanze 

kufuatilia maendeleo yake ndipo 

tunapoweza kusema chochote lakini kwa 

upande wetu sisi kama madaktari 

tumefanya kila lililowezekanakuhakikisha kwamba upasuaji unafanikiwa na endapo 

litatokea la kutokea basi yatakuwa ni 

mapenzi ya Mungu.” Akasema Daktari 

 “ daktari samahani lakini kwa 

kuuliza swali hili .Is he going to make it? 

Akauliza Pauline 

 “ kama nilivyowaeleza awali 

kwamba upasuaji umefanyika vizuri lakini 

hii haina maana ya moja kwa moja 

kwamba mgonjwa wenu anaweza akapona 

ama akafariki .Ninaomba niwe 

muwazikwenu kwamba kwamba nafasi ya 

kupona au vinginevyo ni hamsini kwa 

hamsini.Kwa wakati huu ambao 

tunaendelea kumuangalia mgonjwa wenu 

kwa ukaribu zaidi ni wakati wa kuzidisha 

maombi.Simameni katika maombi 

tumombee ndugu yetu kwani jitihada za 

madaktari pekee hazitoshi.Tumtangulize 

Mungu mbele na nina hakika ndugu yenu 

David atapona.” Akasema daktari na 

kuwataka akina Pauline warejee 

nyumbani wakapumzike 

 “ David I don’t want to go home. ! 

akasema Pauline 

 “ Pauline we have to go home.!! 

Madaktariwanaendelea kumuangalia 

David.usiku mzima tumekesha hapa 

unahitaji mapumziko na tutakuja tena baadae.David will be ok”akasema 

David.Pauline akakubali wakakodisha 

taksi ili iwapeleke nyumbani kwani tayari 

kulikwisha pambazuka 

 “ Kuna kanisa lolote maeneo ya hapa 

karibu? Akauliza Sanya.Pauline 

akamuelekeza dereva taksi awapaleke 

kanisani kwanza kabla ya kuelekea 

nyumbani. 

 Milango ya kanisa ilikuwa wazi na 

watu walikwisha anza kuingia kanisani 

kwa ajili ya ibada ya kila siku 

alfajiri.Sanya akashuka garini na kuingia 

kanisani. 

 “ Huingii kanisani kumshukuru 

Mungu kwa kutuokoa na tukio la jana? 

Alfred akamuuliza Pauline 

 “ Mbona nawe huendi kushukuru? 

Pauline naye akauliza. 

 “ Nina dhambi nyingi sana.Sistahili 

hata kuingia ndani ya nyumba ile ya 

Mungu” akasema Alfred. 

 “ Vijana nyumba ya Mungu nikwa 

ajili ya watu wote na hasa wenye 

dhambi.Mungu anawakaribisha nyote 

.”akasema dereva taksi ambaye umri wake 

ulikuwa mkubwa tofauti na akina 

Fred.Pauline na Alfred wakatazamana hawakuonge a kitu tena wakabaki kimya 

wakimsubiri Sanya atoke kanisani. 

 Baada ya kuingia kanisani Sanya 

akapiga magoti na macho yake 

yakaonekana kuwa na machozi 

 “ Ee Mungu baba nimekuja mbele 

zako kukushukuru kwa kutukinga na 

mkono wako dhidi ya wale watu waovu 

waliokuwa na nia ovu.Unatupenda sana na 

ndiyo maana hujaruhusu watu wale 

watudhuru.Ninakuomba ee baba umponye 

David.Usimchukue katika kipindi 

hiki.Ninampenda na ninamuhitaji sana 

katika maisha yangu.Mjalie mzee Zakaria 

uponaji wa haraka na uwape faraja familia 

yake hasa Pauline katika kipindi hiki 

kigumu wanachokipitia.Wewe ni muweza 

na neno lako moja tu linaweza kuigeuza 

dunia hivyo nakuomba tamka neno lako 

moja tu na David aweze kupona.Ahsante 

Mungu,ahsante ksa nafasi hii..Amen.” 

Sanya akamaliza maombi yake na kutoka 

kanisani akarejea garini wakaondoka 

kuelekea nyumbani. 

 “ Baada ya kushuhudia kitendo kile 

David alichokuwa anakifanya na Vicky 

nilimchukia sana na sikutaka hata 

kumuona tena katika macho yangu lakini 

nilikuwa najidanganya.David ndiye hasa mwanaume ambaye nilikuwa 

ninamuhitaji katika maisha yangu 

mwanaume ambaye yuko tayar kuutoa 

uhai wake kwa ajili ya 

wengine.Ninajilaumu kwa kumuhukumu 

kabla sijamfahamu vizuri.Sintachoka 

kumuomba na kumlilia Mungu amuondoe 

katika hatari na amponye kwani 

ninamuhitaji sana.David ameniingia 

moyoni mwangu kwa kasi na siwezi 

kushindana na nguvu hii kubwa 

inayoniaminisha kwamba David ndiye 

hasa mwanaumeni nayepaswa kuwa 

naye.Nina hakika safari yangu ya kuja 

Tanzania ni kwa ajiliya kunikutanisha 

naye.Kuna uwezekano mkubwa 

nikawakosa wazazi wangu lakini 

nikafanikiwa kumpata mwanaume wa 

maisha yangu ambaye ni David.”akawaza 

Sanya. 

 “Kitendo alichokifanya David ni cha 

kishujaa sana kwani aliona ni bora kama 

angekufa yeye lakini mzee Zakaria 

apone.Nadra sana katika dunia ya leo 

kuwapata watu wa namna hii ambao wako 

tayari kuyatoa maisha yao kwa ajili ya 

wengine.”akaendelea kuwaza 

Sanya.Walifika nyumbani na kila mmoja 

akaingai chumbani kupumzika  Saa nne za asubuhi kamanda wa 

polisi wa wilaya akawasili nyumbani kwa 

mzee Zakaria akiwa ameongozana na 

askari wengine kadhaa.Walizunguka 

nyumba nzima wakachunguza na kisha 

wakaingia ndani.Kamanda akataka 

kuonana na familia ya Zakaria .Pauline 

akajitambulisha halafu akawatambulisha 

na akina Alfred.Kamanda wa polisi wilaya 

naye akawatambulisha baadhi ya maafisa 

alioambatana nao halafu akaelekeza 

dhumuni la kufika pale. 

 “ Nimekuja hapa kwanza kuwapeni 

pole kwa tukio lile la jana.Binafsi mzee 

Zakaria ni rafiki yangu na nimeguswa sana 

na tukio hili kama mlivyoguswa ninyi kwa 

hiyo naomba mfahamu kwamba hamko 

peke yenu katika jambo hili wengi 

tumesikitishwa sana na 

kilichotokea.Kama kamanda wa polisi wa 

wilaya nimekuja kuangalia mazingira ya 

tukio na vile vile kuongea nanyi jambo 

moja la muhimu ambalo sina hakika kama 

mnalifahamu tayari.Tulifahamu toka 

mapema kuwapo kwa shambulio hili na 

hivyo tukajipanga vizuri kuweza 

kuwadhibiti wahalifu hao.Taarifa ya 

kuwepo kwa shambulio hili tulipewa na 

David.”  “ David !!.Pauline akauliza kwa 

mshangao 

 “ Ndiyo.Taarifa za kuwapo kwa 

shambulio tulizipata toka kwa 

David.Alikuja mwenyewe kituoni na 

kutufahamisha kuhusiana na mipango ya 

kuwapo kwa shambulio hili lililotokea.” 

Kamanda akanyamaza kidogo halafu 

akaendelea 

 “ Tukio lililotokea jana lilipangwa na 

mke wa mzee Zakaria aitwaye Vicky ” 

Pauline akastuka sana kwa taarifa ile 

 “ mama mdogo ?!! Pauline akasema 

kwa mshangao.. 

 “ kwa mujibu wa David ni kwamba 

Vicky mke wa mzee Zakaria amekuwa 

akimuhujumu sana mume wake kwa 

kumuibia pesa nyingi sana ambazo 

amekuwa akizificha katika akaunti zake 

mbalimbali.Katika maelezo aliyotupatia 

David ,alikiri kwamba yeye si mtoto wa 

familia hii bali alipewa hifadhi na mzee 

Zakaria .Alisema kwamba mara tu 

alipoanza kuishi hapa mzee Zakaria 

alitokea kumuamini na akamkabidhi 

biashara zake azisimamie.Mara tu 

alipoanza kuzisimamia biashara za mzee 

Zakaria Vicky akamfuata na kumtaka 

washirikiane katika baadhi ya mambo ambayo lengo lake ni kumuhujumu mzee 

Zakaria.Alimuahidi mambo mengi sana 

ikiwa ni pamoja na maisha mazuri kama 

atakubali kushirikiana naye.David 

alikubali kushirikiana naye lakini moyoni 

alikuwa na lengo la kutaka kumfahamu 

Vicky kwa undani zaidina kufahamu kila 

anachokifanya nyuma ya mgongo wa mzee 

Zakaria.Baade Vicky alianza kumtaka 

David kimapenzi.Kwa kuwa alikuwa na 

lengo lake David akakubali na hivyo 

wakawa na mahusiano ya siri .Vicky 

akamuamini David na alimfahamisha kila 

kitu anachokifanya.Kwa kumtumia David 

,Vicky alifanikiwa kuchukua mkopo 

mkubwa wa mamilioni benki bila ya mzee 

Zakaria kujua na kuzihifadhi katika 

akaunti yake ambayo David anaifahamu 

.Vile vile anasema kuna mambo 

mengiambayo aliyagundua kwa Vicky.kwa 

siku za hivi karibuni aligundua mpangowa 

Vicky wa kutaka kumuua mzee Zakaria ili 

aweze kurithi mali zote.Taarifa za kuwepo 

kwa mpango huo alizipata kupitia kwa 

rafiki mkubwa wa Vicky aitwaye 

Safia.Mara tu alipozipata taarifa zile David 

akaja kwetu na kutueleza kila kitu na sisi 

tukaanza kujiandaa.Mtu ambaye Vicky 

alimtumia katika mpango huo ni jambazi sugu aitwaye Chino ambaye sisi jeshi la 

polisi kwa muda mrefu tumekuwa 

tunamsaka lakini tulikosa ushahidi wa 

kuweza kumtia hatiani lakini hatimaye 

jana tulifanikiwa kumnasa 

..Tunamshukuru sana David kwani licha 

ya kuokoa uhai wa mzee Zakaria lakini pia 

ametusaidia sana kumkamata mshukiwa 

sugu wa ujambazi hapa Arusha.” Kamanda 

akanyamaza kidogo na kuendelea 

 “ kwa sasa upelelezi unaendelea na 

ukikamilika Vicky atapandishwa 

mahakamani kujibu mashitaka 

atakayokuwa anakabiliwa 

nayo.Tunachokiomba kutoka kwenu ni 

ushirikiano wenu wa hali na mali ili 

kuhakikisha kwamba wale wote 

waliohusika katika jambo hili 

wanachukuliwa hatua stahiki.Endapo 

kuna jambo lolote ambalo mnadhani 

tunatakiw a kulifahamu kuhusu Vicky 

msisiste kutueleza nasi tutalifanyia 

kazi.Rafiki wa Vicky aitwaye Safia yeye 

tayari anatusaidia katika upelelezi wetu 

na tunamuombea David aweze kupona 

kwani ni mtu muhimu sana katika kesi 

hii.Tuzidi kumuombea sana ili Mungu 

ampe nafuu ya haraka na aweze kupona ”akasema Kamanda na kuagana na akina 

pauline wakaondoka zao. 

 “ David alinipigia simu na kunitaka 

nije haraka Arusha kun jambo kubwa 

anataka kunitaarifu.Nadhani jambo 

lenyewe alilotaka kunitaarifu ni hili.” 

Akasema pauline 

 “Alikutaarifu kuhusu jambo hili? 

Sanya akashangaa 

 “ Hakupata nafasi ya kunieleza kama 

jambo lenyewe lakini alikuwa na nia ya 

dhati ya kunieleza.Ni mimi ndiye 

niliyepuuzia.”akajilaumu Pauline 

 “ Mwiliwote unanitetemeka ,bado 

siamini.Mama mdogo ?!! akasema pauline 

 “ Yaani pamojana maisha ya hali ya 

juu aliyokuwa anaishi lakini bado 

hakuridhika na akataka kumuua baba ili 

arithi mali? Akasema kwa uchungu 

Pauline na kuangua kilio.Sanya na Alferd 

wakambembeleza 

 “Ninalia kwa uchungu mkubwa 

nikikumbuka namna baba alivyokuwa 

anampenda na kumjali Vicky.Alimpatia 

kila alichohitaji lakini haya ndiyo malipo 

yake? Akazidi kulia 

 “ Basi Pauline.Imetosha usilie 

tena.Tunachotakiwa kukifanya kwa sasa 

ni kumuombea sana David apone kwani kama alivyosema kamanda David ni mtu 

muhimu sana katika kesi hii inayomkabili 

Vicky.David anafahamu vitu vingi sana 

kuhusiana na Pauline kwa hiyo akipona 

atakuwa na msaada mkubwa sana.” 

Akasema Alfred 

 “ I was wrong about David.Nilikosea 

sana kumuhukumu kabla ya kujua nini 

dhumuni la alichokuwa 

anakifanya.”akasema Pauline na 

kuendelea tena kulia ikawalazimu akina 

Alfred kufanya kazi ya ziada 

kumbembeleza. 

******************** 

 Saa kumi na mbili za asubuhi siku ya 

jumatatu Robin na Lucy wakaondoka 

katika hoteli ile waliyokaa kwa siku 

mbili,Robin akampeleka kwanza Lucy 

halafu naye akaelekea kwake kujiandaa 

kwa ajili ya siku ile ya kazi.Alipofika 

nyumbani alimkuta Penina akijiandaa kwa 

ajili ya kwenda shule wakasalimiana 

 “ Baba siku nyingine na mimi 

mnichukue niende na ninyi huko 

mlikokwenda.kwa nini mliniacha ? 

Akauliza Penina  “ Kuna mambo ambayo mimi na 

mama yako mdogo Lucy tulikuwa 

tunayazungumza ambayo yalihitaji kuwa 

sehemu tulivu sana”akasema Robin 

 “ Mlikuwa mnaongelea mambo gani? 

Unaweza ukaniambia? Akauliza 

hukuakicheka na kumfanya Robin naye 

acheke.walikwisha zoea kutaniana 

 “Ni mambo ya watu wazima 

yanayotuhusu mimi na mama yako 

mdogo” akajibu Robin 

 “ Baba ni lini mwalimu Lucy 

atahamia hapa na kuishi nasi? Nina hamu 

sana ya kuishi naye ” akasema 

Penina.Robina akacheka kidogo na 

kusema 

 “ Usijali Penina.Tunaendelea na 

mipango hiyo na itakapokuwa tayari 

nitakutaarifu.lakini mambo yanakwenda 

vizuri sana ” akasema Robin.penina 

akatabasamu 

 “ Pamoja na hayo kuna mambo 

mawili ninataka kukutaarifu” 

 “ Ni mambo gani baba? Akauliza 

Penina.Robin akamshika mkono Penina 

wakaenda kukaa sebuleni. 

 “ Penina nafahamu kwamba wewe na 

mama yako hamna mahusiano 

mazuri.Aliniacha angali ukiwa mdogo sana na katika muda huu wote hadi hivi sasa 

hajawahi hata kukutembelea kujua 

unaendeleaje.Ninafahamu hasira 

ulizonazo juu yake kwani kitendo 

alichokifanya ni kibaya .Alikuacha wakati 

ambao ulimuhitaji sana.Pamoja na hayo 

yote bado ukweli utabaki pale pale 

kwamba ndiye mama yako mzazi.Ndiye 

aliyekuleta hapa duniani.Hakuna mama 

mzazi mwingine ”akasema Robin 

 “ Baba unataka kusema nini? 

Akauliza Penina kwa wasi wasi 

 “ Penina mimi na mama yako mdogo 

Lucy tuna nia ya dhati ya kufunga ndoa na 

kuishi pamoja lakini kikwazo kilikuwa ni 

kwamba mimi na mama yako bado 

tulikuwa katika ndoa.Ili tuweze kufunga 

ndoa ili tulazimu kuitengua kwanza ndoa 

yetu.Tuliwasilisha suala hili katika idara 

zinazohusika na ninafuraha kukujulisha 

kwamba tayari wamekwisha lifanyia 

maamuzi suala letu na ndoa yangu mimi 

na mama yako imetenguliwa rasmi kwa 

hiyo niko huru sasa kumuoa mama yako 

mdogo Lucy.”akasema Robin.Penina 

akatoa tabasamu kubwa sana 

 “ Nimefurahi sana kusikia hivyo 

baba.Ninampenda sana Aunt Lucy na 

nitafurahi sana kuishi naye kwani naye ananipenda sana.Naomba baba mfanye 

haraka mfunge ndoa ili tuanze kuishi na 

Aunt Lucy”akasema Penina 

 “ Penina ninashukuru kama 

umelipokea suala hili kwa furaha.Hivi 

karibuni tutaanza maandalizi ya ndoa yetu 

na tutakapoanza tutakutaarifu mara moja” 

akasema Robin.Ukapita ukimya mfupi na 

kisha akasema 

 “ Ukiacha na hilo ,kuna jambo lingine 

pia ninataka kukutaarifu ingawa sizuri .” 

 “Jambo gani tena hilo baba mbona 

unataka kunipotezea furaha yote 

niliyoipata? Akauliza penina 

 “ Ni kuhusu mama yako mzazi” 

akasema 

 “ Mama ?! mama yupi tena? 

 “ penina kama nilivyotangulia 

kukueleza awali kwamba pamoja na yote 

aliyotukosea mama yako lakini bado 

ataendelea kuwa mama yako mzazi kwani 

ndiye aliyekuleta duniani.Hata kama ndoa 

yangu na yeye imetenguliwa lakini bado 

ataendelea kuwa mama yako tu.” 

 “ Baba naomba nikuweke wazi 

kwamba sitaki kusikia chochote kuhusu 

mama .Aliniacha nikiwa mdogo na hata 

siku moja hakutaka kufuatilia maendeleo 

yangu .Nimekosa upendo wake kwa hiyo hata mimi sihitaji kujua chochote kuhusu 

yeye.Ni kweli atabaki kuwa mama yangu 

aliyenileta hapa duniani lakini hatapata 

upendo wowote toka kwangu.Siwezi baba 

!! akasema penina 

 “ Penina nafahamu uchungu ulionao 

na hata mimi pia aliniumiza sana lakini 

nimekwisha msamehe.”akasema Robin na 

kumfanya penina atoe kicheko kidogo 

 “ baba unathubutuje kumsamehe 

mtu kama mama? Alikuumiza sana 

,alikudharau na kukukimbia wakati huna 

kitu leo hii unadiriki vipi kumsamehe? 

Hapana baba mimi siwezi kumsamehe 

hata kidogo.Atabaki kuwa mama yangu 

mzazi lakini hatapata kabisa upendo 

wangu” akasema Penina 

 “ Penina naomba unisikilize.lengo la 

kukueleza hivi ni kutaka kukufahamisha 

kwamba mama yako amepata ajali mbaya 

sana ya gari na amelazwa hospitali na hali 

yake ni mbaya sana.Pamoja na kwamba 

ametukosea sana lakini kwa wakati huu 

wa matatizo tusahau yote yaliyotokea na 

tushikamane naye,tuonyeshe upendo 

kwake kwani anahitaji sana faraja 

.”akasema Robin 

 “ Amepata ajali ?!!  “ Ndiyo amepata ajali mbaya na kwa 

mujibu wa taarifa ni kwamba hali yake si 

nzuri hata kidogo.” 

 “ Umekwenda kumuona? Akauliza 

Penina 

 “ hapana bado sijaenda 

kumtazama.Ninataka twende wote 

.Atafarijika sana akituona sote 

tumekwenda kumjulia hali.”akasema 

Robin.Penina akainama akafikiri kwa 

muda na kusema 

 “ sawa baba tutakwenda kumuona 

.lakini ninakwena kwa sababu yako tu ” 

akasema Penina 

 “ Ahsante sana penina.Ahsante 

sana.Tutakwenda kumtazama jioni baada 

ya kutoka masomoni.”akasema Robin 

*********************** 

Japokuwa usiku mzima walikesha 

hospitali,lakini bado Pauline 

hakuonekana kuwa na usingizi hata 

kidogo ingawa macho yake yalikuwa 

mazito.Wakati Alfred na Sanya wakiwa 

vyumbani wakipumzika ,Paulinealikuwa 

amekaa sebuleni akitafakari.Alifikiria 

mambo mengi sana namna familia yao 

inavyokumbwa na majanga ya mara kwa mara lakini kubwa zaidi ni hili tukio la 

uvamizi lililopangwa na mama yake 

mdogo.Akainuka sofani akaenda ukutani 

na kuitungua picha kubwa ambayo baba 

yake mzee Zakaria alikuwa amepiga na 

Vicky 

 “ Shetani mkubwa huyu ,sura yake 

haistahili kabisa kuonekana ndani ya 

nyumba hii.Toka mwanzo alipoingia humu 

ndani roho yangu ilimkataa kabisa huyu 

mwanamke na ndiyo maana mimi na yeye 

hatukuelewana.Nilijua kabisa kwamba 

hakuwa mtu mwema na hakuwa na nia 

njema na baba.Hakumpenda baba bali 

alifuata pesa zake tu.Nilijaribu mara 

kadhaa kumueleza baba kuhusiana na 

namna huyu mwanamke anavyotapanya 

mali lakini baba sijui alipewa nini kwani 

hakuwa akisikia la mtu yeyote kuhusu 

Vicky. Ametuingizia hasara kubwa sana 

kutokana na matumizi yake mabaya ya 

pesa.Hakuridhika na yote aliyokuwa 

anayapata akaona ni vyema kama 

akimuua kabisa baba ili arithi kila 

kitu.Ninamshukuru sana David kwani 

kama si yeye basi hivi sasa baba yangu 

tayari angekwisha uawa na mali zote 

zingepotelea mikononi mwa Yule shetani 

asiye .David ni kama malaika aliyetumwa na Mungu kuja kumlinda baba kwa sababu 

ni mara ya pili sasa anamuokoa na 

majanga.Mara yakwanza alimuokoa 

katika ajali na sasa hivi amemuokoa toka 

mdomo wa kifo.kama si yeye hivi sasa 

nyumba hii ingetawaliwa na vilio vingi 

kwani tayari baba angekwisha 

fariki.Risasi alizostahili baba amezibeba 

David.Huyu ni kijana wa ajabu sana. 

“akawaza Pauline 

 “ Lakini David ametokea wapi? 

familia yake iko wapi? Alifungwa gerezani 

kwa kosa gani? Kwa nini hataki kuweka 

wazi kuhusu historia yake? Akaendelea 

kuwaza Pauline 

 “ Baada ya tuko la jana nadhani kuna 

ulazima wa kumfahamu David kiundani na 

kuifahamu pia familia yake mahala 

walipo.Katika hali kama hii wanatakiwa 

wafahamu hali ya mtoto wao ikoje.Halafu 

kinachonipa wasiwasi ni endapo ikatokea 

labda David akafariki dunia kitu ambacho 

siombi kitokee tutawafahamuje familia 

yake? Mungu amjalie David apone na 

safari hii lazima atuonyese ilipo familia 

yake ili nao wafahamu mahala mtoto wao 

alipo.”akaendelea kuwaza Pauline na 

mara simu yake ikaita,zilikuwa ni namba 

ngeni  “ hallow” akasema Pauline 

 “ hallow ninaitwa Sakina ninapiga 

simu kutoka St Gasper 

hospitali.Ninaongea na nani tafadhali? 

 “ Unaongea na Pauline.Kuna habari 

gani hapo hospitali ? baba yangu mzee 

Zakaria anaendeleaje? Akauliza Pauline 

kwa wasiwasi 

 “ Usihofu Pauline baba yako 

anaendelea vizuri sana na ndiye 

aliyetuomba tukupigie simu hii” akasema 

Yule muuguzi 

 “ Amesema mnipigie simu? akauliza 

Pauline huku uso wake ukiwa na 

tabasamu 

 “ Baba yako alipoamka asubuhi hii 

ametaka kufahamu kama uko salama 

,tukamuhakikishia kwamba uko salama 

lakini bado haamini na anahitaji 

kukuona.Kwahiyo Pauline naomba uje 

hapa hospitali baba yako anahitaji 

kukuona”akasema Yule muuguzi 

 Pauline akaenda kuwastua akina 

Alfred na kuwaomba wajiandae kwa ajili 

ya kwenda hospitali kuonana na mzee 

Zakaria 

 Ndani ya dakika ishirini tayari 

walikwisha jiandaa na kuondoka kuelekea 

hospitali kuonana na mzee Zakaria.  “ Hakuna taarifa zozote za kuhusiana 

na maendeleo ya David ?akauliza Sanya 

 “ Hapana ,mpaka sasa hivi hakuna 

taarifa zozote kutoka hospitali.Tukitoka 

kumtazama baba tutaenda kujua 

maendeleo yake” akasema Pauline 

 “ Ee Mungu tunaomba umponye 

David,tunamuhitaji sana” akasema Sanya 

kwa sauti ndogo huku macho yake 

yakilengwa na machozi.Pauline akageuka 

akamtazama 

 “ I can see her eyes.She’s in 

love.Anampenda David na ameumia sana 

kwa kilichotokea.She’s the right woman 

for David.Nitahakikisha ninafanya kila 

linalowezekana hadi Sanya na David 

wawe pamoja.Hii ni zawadi kubwa 

ambayo nitampatia David.”akawaza 

Pauline 

 Walifika hospitali wakashuka garini 

na kuelekea moja kwa moja katika 

chumba alimolazwa mzee Zakaria 

aliyekuwa amekaa akizungumza na 

wauguzi ambao walitoka baada ya akina 

Pauline kuwasili.Pauline akamfuata na 

kumkumbatia kwa nguvu. 

 “ Ouh my daddy ! akasema Pauline  “ Pauline my queen” akasema mzee 

Zakaria na wote wawili machozi 

yakawatoa 

 “ Pole sana baba.Pole sana “akasema 

Pauline 

 “ Wewe ndiye unayepaswa kupewa 

pole.Unaendeleaje? 

 “ Ninaendelea vizuri sana baba.Vipi 

wewe maendeleo yako? Akauliza Pauline 

 “ Ninamshukuru Mungu ninaendelea 

vizuri .Nilipoamka niliwauliza madaktari 

kama familia yangu wote wazima 

wakaniambia kwamba mko salama 

sikuamini nikataka hadi niwashuhudie 

kwa macho.Nashukuru nimewaona nyote 

lakini kuna mtu mmoja sijamuona 

hapa.David yuko wapi? Akauliza mzee 

Zakaria akina Pauline wakatazamana. 

 “ Mbona mnatazamana? David yuko 

wapi? Tafadhali niambieni kama kuna 

tatizo “ akasema kwa wasi asiwasi 

 “ Daddy just relax everything is fine” 

akasema Pauline akijaribu kumtuliza baba 

yake. 

 “ Pauline kuna kitu unanificha.David 

yuko wapi? Halafu mama yako mdogo 

yuko wapi? Nilitegemea angekuwa hapa 

karibu yangu mida hii lakini 

sijamuona,whats going on?akauliza mzee Zakaria.Pauline akaogopa kusema 

kilichotokea akabaki kimya 

 “ Dr Alfred tell me what’s going on? 

Nini kilitokea jana? Ninachokumbuka ni 

kwamba tulisikia milio ya risasi na wakati 

tunajiuliza risasi zile zililia wapi mara 

tukavamiwa na watu wawili waliokuwa na 

silaha na wakatuamuru tulale 

chini.Ninakumbuka nilirukiwa na David 

na kilichofuata nikasikia milio ya risasi na 

sikujua tena nini kiliendelea.Tafadhali 

nieleze nini kilitokea? Majambazi wale 

waliotuvamia walichukua nini? Akauliza 

mzee Zakaria 

 David akamtazama Pauline halafu 

akageuka akamtazama Sanya kisha 

akamueleza mzee Zakaria kila 

kilichotokea usiku ule.Mzee Zakaria 

akashindwa kujizuia kutokwa na machozi 

 “ So it was him again.He saved me 

again!! Ouh David !!..”akasema mzee 

Zakaria .Pauline akampiga piga mgongoni 

 “ be strong daddy” akasema Pauline 

 “ Where is he now? Anaendeleaje 

David? Akauliza mzee Zakaria 

 “ Kwa sasa yuko hospitali kuu ya 

mkoa anapatiwa matibabu.Jana usiku 

amefanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi 

mwilini mwake na upasuaji ulifanikiwa .kwa hvi sasa yuko chini ya uangalizi wa 

madaktari.” Akasema Dr Alfred.Mzee 

Zakaria akamtazama na kusema 

 “ Dr Fred wewe ni daktari,please tell 

me the truth,is he going to live ?? akauliza 

mzee Zakaria 

 “ david will be ok.he’s going to 

live”akasema Alfred kwa kujiamini ili 

kumpa moyo mzee Zakaria. 

 “ tafadhali nipelekeni nikamuone 

kijana wangu “akasema mzeeZakaria na 

kutaka kuinuka kitandani 

 “ Mzee bado unahitaji kuwa katika 

mapumziko na pindi madaktari 

wakiridhika kwamba unaendelea vizuri 

basi watakuruhusu na tutakupeleka 

kumtazama David.usihofu mzee david 

yuko chini ya uangalzi makini sana na 

atapona na hata sisi tunaendelea 

kumfuatilia kwa karibu sana” akasema 

Alfred na mara simu yake ikaita alikuwa ni 

mke wake akatoka mle chumbani akaenda 

nje 

 “ Fuatilieni hali ya David na kama 

anapata matibau anayostahili kama kuna 

uwezekano tumpeleke nje ya nchi.Sitaki 

kumpoteza kijana wangu.” Mzee Zakaria 

akamwambia Pauline  “ mama yako mdogo naye yuko 

wapi? Anamuuguza David?Mzee Zakaria 

akauliza 

 “ daddy kuna jambo ambalo nadhani 

unapaswa kulifahamu kuhusu mama 

mdogo” 

 “ Ni jambo gani Pauline?Nieleze 

tafadhali.Yuko salama? 

 “ Yuko salama usihofu” akasema 

Pauline na kuvuta pumzi ndefu 

 “ kamanda wa polisi wa wilaya 

alikuja nyumbani leo akaongea 

nasi.Ametuambia kwamba majambazi 

wote waliofanya tukio lile la kutuvamia 

walidhibitiwa.wawili waliuawa na 

wengine wanashikiliwa na polisi.Alisema 

kwamba kiongozi wa majambazi wale 

anaitwa Chino ambaye anamiliki vituo 

kadhaa vya mafuta hapa jijini Arusha” 

 “ Chino ?!! Mzee zakaria akashangaa

 “Ndiyo baba” 

 “ Basi haya ni maajabu.Mbona Chino 

ni kijana ambaye tunafahamiana sana? 

Kwa nini amfanyie vile? Zakaria 

akashangaa 

 “ kwa mujibu wa kamanda wa polisi 

ni kwamba Chino alitumwa kuifanya hiyo 

kazi kwa malipo manono.  “ Alitumwa?..alitmwa na nani aje 

anivamie mimi na familia yangu? 

 “ alitumwa na mama mdogo Vicky” 

akasema Pauline na kwa sekunde kadhaa 

mzee Zakaria akabaki anamtazama 

mwanae kana kwamba ameona kitu cha 

kutisha 

 “ Vicky ?!! akauliza Zakaria kwa 

mshangao 

 “ Ndiyo .Ni mama mdogo Vicky ndiye 

aliyemtuma Chino na lengo lake lilikuwa 

ni kukuua ili arithi mali.Kwa hivi sasa 

anashikiliw ana polisi na pindi 

upeleleziukikamilika atapandishwa 

mahakamani”akasema Pauline na mara 

mzee Zakaria akaanguka 

kitandani.Pauline akapiga kelele kubwa 

kuomba msaada.Alfred na madaktari 

wengine wakangia mle ndani mbio kujua 

kilichotokea.Haraka haraka akina Pauline 

wakatolewa mle chumbani na kisha mzee 

Zakaria akapakiwa katika kitanda na 

kukimbizwa katika chumba cha dharura. 

 “ Pauline nini kimetokea? Akauliza 

Alfred lakini Pauline hakuweza kujibu kitu 

alikuwa anatetemeka 

 “ Sanya nini kimetokea mle 

ndani?Alfred akamuuliza sanya  “ Mimi sifahamu Pauline na baba 

yake walikuw wanaongea nini kwa sababu 

sifahamu lugha ya Kiswahili.Kuna mambo 

walikuwa wanaongea na mara mzee 

Zakaria akaanguka ghafla” akasema Sanya 

 “ Pauline ulimwambia nini mzee 

Zakaria?akauliza Alfred .pauline 

hakuweza kuongea alikuwa anatetemeka 

.David akamchukua na kumpeleka sehemu 

ya kupumzikia . 

 Baada ya nusu saa daktari akaomba 

kuona na akina Alfred 

 “ Hali ya mzee inaendelea 

vizuri,alipatwa na mstuko 

.Ninachowaomba katika wakati huu,mzee 

asielezwe jambo lolote la kustusha.Hata 

kama kuna mwanafamilia alipoteza 

maisha katika shambulio basi mzee 

asielezwe kwanza kwani endapo akipata 

tena mstuko mwingine kuna hatari kubwa 

ya kumpoteza.Nimewaiteni ili kuwapeni 

hilo angalizo.Jaribuni kuangalia maneno 

ya kumwambia mzee.Kwa sasa ataendelea 

kuwa chini ya uangalizi wetu hadi hapo 

hali yake itakapokuwa nzuri” akasema 

daktari. 

 “ Ahsante Mungu !akasema Pauline 

kimya kimya  Baada ya maelezo yale ya daktari 

wakaondoka na kulekea katika hospitali 

ya mkoa kufuatilia hali ya David.Bado 

hawakuruhusiwa kuingia lakini daktari 

aliwahakikishia kwamba David 

anaendelea vizuri na aliwataka warejee 

tena jioni pengine wangeweza kupewa 

nafasi ya kuiingia na kumuona kama hali 

yake bado itakuwa inaendelea kuwa nzuri. 




Saa kumi na moja za jioni 

Robin,mwalimu Lucy wakiwa 

wameambatana na Penina wakawasili 

hospitali kuu ya mkoa kwa dhumuni la 

kuwajulia hali Vivian pamoja na Tino 

magari,Kisha egesha gari wakashuka na 

moja kwa moja wakaelekea eneo la 

mapokezi ambako waliuliza na 

kuelekezwa mahala walikolazwa Vivian na 

mumewe Martin.Tayari walikwisha tolewa 

katika chumba cha wagonjwa mahututi na 

kila mmoja aliwekwa katika chumba 

chake . 

 Walianza kwanza katika chumba 

alimolazwa Martin.Marafiki zake kadhaa 

walikuwamo mle chumbani wakimjulia hali na wengine walikuwa nje ya chumba 

wakisubiri kupata nafasi ya kuingia . 

 “ watu ni wengi waliokuja kumtazam 

Fred,unadhani tutapata nafasi ya 

kuruhusiwa kuingia ndani na muda 

unazidi kwenda? Robin akamuuliza Lucy

 Kabla Lucy hajajibu kitu,akashikwa 

bega. 

 “ Lucy !! akasema Yule mtu 

aliyemshika bega 

 “ Armando !! akasema Lucy na 

wakasalimiana 

 “ Habari za siku nyingi ? 

 “ habari nzuri sana Lucy.Vipi 

maendeleo yako ? 

 “Ninaendelea vizuri sana .Poleni 

sana na matatizo” akasema Lucy 

 “ Tumekwisha poa Lucy.kwa kweli 

walipata ajali mbaya sana.Ni ajabu kabisa 

hata leo hii kuwa bado wako hai ingawa 

wameumia sana.Martin amekatwa miguu 

yote miwili,mke wake yeye amepotea 

miguu yote miwili pamoja na 

mkono”akasema Armando rafiki mkubwa 

wa Martin 

 “ dah ! ama kweli ilikuwa ni ajali 

mbaya sana”akasema Robin  “ By The way Armando nilisahau 

kukutambulisha,huyu anaitwa Robin ni 

mchumba wangu .Robin huyu anaitwa 

Armando ni rafiki mkubwa wa Martin.” 

Lucy akafanya utambulisho.Armando na 

Robin wakashikana mikono 

wakasalimiana na kisha Armando 

akawaongoza Robin na Lucy kuingia mle 

chumbani akawatoa watu wote 

waliokuwampo mle mchumbani 

wakabaki akina Lucy pekee.Tino magari 

alikuwa amelala kitandani,uso ukiwa 

umemvimba kutokana na majeraha 

makubwa aliyoyapata.Haikuwa rahisi 

kumtambua kwa haraka.Aliumia sana. 

 “ Tino,Lucy amekuja kukutazama” 

akasema Armando. 

 “ Karibu Lucy !! akasema Tino kwa 

sauti ya chini sana.Lucy akamsogelea 

palekitandani na kumuinamia 

 “ Martin pole sana”akasema Lucy 

huku machozi yakimdondoka 

 “ ahsante sana Lucy kwa kuja 

kuniona.Nashukuru Mungu nimesalimika 

katika ile ajali,Yule shetani alitaka 

kuniua..Alidhamiria kuniua.”akasemaTino 

lakini Lucy hakuweza 

kumuelewa.Akamtazama Armando  “bado hali yake si nzuri sana na toka 

asubuhi amekuwa akiongea maneno hayo 

hayo yasiyoeleweka.” Armando 

akamfahamisha Lucy. 

 “ basi sisi ngoja tuondoke tutakuja 

tena siku nyingine kumjulia hali 

Martin.”akasema Lucy kisha wakatoka mle 

chumbani .Bado machozi yaliendelea 

kumtoka 

 “ Its ok Lucy.Martin atapona 

tu”akasema Robin 

 “ Robin namuonea huruma Martin 

ameumia sana.Amewahi kuniumiza sana 

wakati Fulani lakini kwa hali niliyomuona 

nayo leo hii nimeshindwa kujizuia 

kudondosha machozi.Ameumia mno” 

akasema Lucy wakaongozana hadi katika 

chumba alimolazwa Vivian.Marafiki 

kadhaa wa Vivian walikuwepo nje ya 

chumba kile na wengi walionekana kuwa 

na nyuso zenye huzuni.Walikuwa 

wamesimama kivikundi wakiongea .Mara 

tu Lucy na Robin walipotokeza baadhi ya 

watu waliowafahamu wakaanza 

kusemezana 

 Ndani ya chumba kile kulikuwa na 

watu wawili tu,Lucy na Robin 

wakaingia.Vivian alikuwa amelala 

kitandani na kichwani hakuonekana kuwa na majeraha makubwa kama 

ilivyokuwa kwa mumewe Martin.Aliweza 

kuongea japo bado alionekana kuwa na 

maumivu makali sana. 

 “ hallo Lucy ! Pole sana”akasema 

Robin. 

 “ Robin umekuja kunitembelea..! 

Mimi maisha yangu 

yameharib…………”Vivian akashindwa 

kuendelea kuongea akabubujikwa na 

machozi 

 “ Vivian nyamaza usilie “akasema 

mwanamke mmoja aliyekuwa 

akimuhudumia huku akimfuta machozi. 

Pamoja na kubembelezwa anyamaze 

lakini bado Vivian aliendelea kububuji 

kwa na machozi.Robin akamsogelea na 

kukaa katika kitanda akachukua 

kitambaa na kumfuta machozi.Mwalimu 

Lucy akamshika mkono Penina . 

 “ Nyamaza usilie Vivy.” Akasema 

Robin. 

 “ Robin nashukuru umekuja 

kunitembelea. Mungu ameniadhibu kwa 

mambo niliyokufanyia .” akasema Vivy na 

kuendelea kulia 

 “ Vivy kwa hali yako hii hutakiwi 

kulia tafadhali.Jikaze usilie hii ni ajali 

kama ajali nyingine na ingeweza kumpata mtu yeyote Yule kwa hiyo usijilaumu sana 

kwa kilichotokea” akasema Robin.Vivian 

akamfanyia ishara Yule mama 

anayemuuguza asogee akamumba awatoe 

Lucy na Penina nje ili abaki na Robin 

pekee. 

 “ Robin nimetaka tubaki peke yetu 

kuna jambo ninataka kukwambia” 

akasema Vivian japo alionekana bado ana 

maumivu makali na aliongea taratibu kwa 

sauti ndogo . 

 “ Vivian huu si wakati muafaka wa 

kuzungumzia jambo lolote.Tusubiri hadi 

hapo utakapopona ndipo utanieleza 

unachotaka kunieleza kwani hata mimi 

kuna mambo ninaaka kuzungumza nawe 

.Tukiachana na hayo pole sana kwa ajali 

hii mbaya.Ilitokeaje ajali hii? Akauliza 

Robin 

 “ Robin naomba unisikilize kwani 

sina hakika kama nitaipata tena nafasi ya 

kuongea nawe.” Akasema Vivian 

 “ Kwa nini unaema hivyo Vivy? 

 “ Robin maisha yangu yameharibika 

kabisa na yote hii ninajua ni adhabu 

kutoka kwa Mungu kwa mambo 

niliyokufanyia.Nilikufanyia mambo 

mabaya sana na kibaya zaidi ni kitendo 

cha kumtelekeza mwanangu. Nilikiuka kiapo changu cha ndoa kwa sababu ya 

kuukimbia umasikini wako nikafuata 

maisha mazuri lakini pamoja na kupata 

maisha mazuri niliyokuwa nayakimbilia 

sijawahi kuwa na furaha.Robin ni mimi 

ndiye niliyesabisha ajali ile itokee kwa 

sababu nilitaka tufe.Mimi na Martin tuna 

mgogoro mkubwa na ndoa yetu inaweza 

ikavunjika muda wowote . Sikuwa tayari 

kuachana na Alfred na ndiyo maana 

nikasababisha ile ajali makusudi ili tufe 

wote lakini Mungu akaniadhibu kwa kosa 

lile .Ninachukua nafasi hii kukuomba sana 

msamaha wewe kwa yale yote 

niliyokukosea na ninakuomba uniombee 

pia msamaha kwa mwanangu Penina.Sina 

hakika kama atanisamehe kwa sababu 

sikuwahi kuwa mama kwake licha ya 

kumleta duniani.Nilimkimbia wakati 

akiwa mdogo kabisa na sik………..” 

 “ Basi imetosha Vivian.” Robin 

akazuia Vivian asiendelee tena kuongea 

 “ Tafadhali usiendelee kuongea Vivy 

unajiumiza sana.Mambo hayo yamekwisha 

pita na tutayaongea ukishapona.Kwa sasa 

si muda muafaka wa kuliongelea jambo 

hili.” Akasema Robin 

 “ Robin naoma unisamehe sana 

mume wangu,najua nilikukosea sana na kukuumiza sana lakini naomba 

unisamehe.Hebu nifunue shuka 

unitazame” akasema Vivian na Robin 

akamfunua shuka akastuka sana.Vivian 

hakuwa na miguu tena.Miguu yake yote 

miwili ilikatwa.Robin akadondosha 

machozi 

 “ Pole sana Vivian !! akasema 

 “ Robin hali yangu ndiyo hii kwa 

sasa.Maisha yangu yote yamebaki 

hivi.Nimekuwa mlemavu wa maisha.Sina 

miguu tena na sasa ninauona umuhimu 

wako.Robin ninawahitaji sana kwa wakati 

huu wewe na mwanangu.Tafadhali 

naomba unisamehe Robin na tuendelee na 

kuishi kiapo chetu cha ndoa.Ninakuahidi 

kwamba pamoja na hali yangu hii ya 

ulemavu nitawapenda ninyi nyote na….” 

 “ Vivian naomba tafadhali usiumize 

kichwa chako kwa mambo haya.Kitu 

kikubwa kwa sasa ni kuhakikisha kwanza 

unapona na baada ya hapo ndipo 

tutayazungumza mambo mengine kama 

hayo.Jitahidi kwa sasa kuepuka mawazo 

kama hayo.Naomba nikwambie vile vile 

kwamba nimeambatana na 

Penina.haikuwa kazi rahisi kumshawishi 

aje akuangalie kutokana na mambo 

uliyomfanyia.  “ Yuko wapi mwanangu? 

 “ Yuko hapo nje pamoja na mama 

yake mdogo.” Akasema Robin .Pamoja na 

maumivu yake yote lakini Vivian 

akaonyesha mstuko aliposikia Robin 

akimtaja mama mdogo wa Penina 

 “ Mama mdogo yupi? 

 “ Mwanamke ambaye ninatarajia 

kufuga naye ndoa hivi karibuni” akasema 

Robin 

 “ Robin tafadhali usiniache.Mimi 

ndiye mkeo wa ndoa.Tafadhali Robini 

najua nimekukosea sana lakini 

ninakuahidi kwamba nitakuwa muaminifu 

kwako na nitaw………………” 

 “ Stop that Vivian..!!! akasema Robin 

kwa sauti ya juu kidogo 

 “ Ninaomba matatizo haya yasiwe 

kigezo cha kutaka kunivurugia maisha 

yangu.Pamoja na kwamba unaumwa lakini 

naomba nikuweke wazi kwamba sina 

mpango wa kurudiana na wewe .Vivian 

wewe ni mwanamke katili na hufai kuwa 

mke.Vivian sikutaka kukueleza kuhusu 

jambo hili hadi hapo utakapokuwa 

umepona lakini umenilazimisha 

niliseme.Mimi na wewe si wanandoa 

tena.Tayari ndoa yetu imetenguliwa na 

kanisa kwa hiyo kila mtu hivi sasa ni huru Olewa na mwanaume wa maisha yako 

mwenye mali uliyemkimbilia na mimi 

ninamuoa mwanamke ambaye Mungu 

amenipangia niwe naye katika maisha 

yangu.Mwanamke anayenijali na 

kunithamini.Mwanamke mwenye mapenzi 

ya kweli na mvumilivu katika hali zote za 

maisha ambaye nina hakika hawezi 

kunikimbi hata kama nikiwa kipofu 

leo.Ninachokishukuru kutoka kwako ni 

kunizalia binti mzuri mwenye akili 

ambaye ulishindwa kumpa malezi na 

upendo kama mama na ukakimbilia 

utajiri.Samahani kwa maneno haya 

makali Vivy ambayo sikupaswa kabisa 

kukueleza hasa kwa wakati huu ambao 

unaumwa lakini sina namna nyingine zaidi 

ya kukueleza ili ufahamu kwamba mimi 

na wewe its over.Nimekuja kukutazama si 

kwamba bado ninakupenda ila ni kwa ajili 

ya kukuaga na kukutakia maisha mema.” 

Akasema Robin na kuinuka kitandani 

 “ Robin !!!...akalia Vivian lakini Robin 

hakumjali akafungua mlango akamuita 

Penina na Lucy wakaingia mle ndani na 

kumkuta Vivian akilia 

 “ What happened? Akauliza Lucy 

.Robin akamshika mkono Peninakumsogeza karibu na kitanda  “ Vivian ,Penina huyu hapa amekuja 

kukupa pole” akasema Robin.Vivian 

akafuta machozi na kumtazama 

 “ Ouh Penina !!..” 

Penina alibaki anamuangalia hakujua 

aseme nini 

 “ Penina mwanangu naomba 

unisamehe sana kwa mambo yote 

niliyokukosea na …..” akasema Vivian na 

kushindwa kuendelea akaanza kulia 

.Robin akatazamana na Lucy kisha 

wakapeana ishara watoke nje na 

kumuachia nafasi Penina ya kuongea na 

mama yake.Penina naye akatoka 

kuwafuata. 

 “ Penina tumekuachia nafasi uweze 

kuongea na mama yako .Rudi ndani 

ukaongee na mama yako” akasema Robin 

 “ Baba siwezi.Nitaongea naye nini ? 

Sina cha kuongea naye” akasema Penina. 

 “ Penina hii ni nafasi pekee umeipata 

kwa miaka mingi ya kukaa japo kwa muda 

mfupi na mama yako na uongee naye.Kwa 

wakati huu anahitaji sana faraja na 

unaweza kuongea naye jambo lolote 

lile.Atafurahi sana kusikia sauti yako.Neno 

lolote utakalomwambia atafurahi.Ongea 

naye kitu chochote” akasema Mwalimu 

Lucy  “ Nenda kaongee naye sisi 

tunakusubiri hapa nje” akasema 

Robin.Penina akaufungua mlango na na 

kuingia ndani 

****************** 

 Saa kumi za jioni akina Pauline 

wakaanza tena safari ya kuelekea 

hospitali.Safari hii walianzia hospitali kuu 

ya mkoa kumtazama David kabla ya 

kuelekea kwa mzee Zakaria. 

 “ Alfred mchana tulipokuwa na baba 

kule hospitali nani alikupigia simu? 

Akauliza Pauline wakiwa garini 

wakielekea hospitali 

 “ Alikuwa Grace” 

 “ Anataka nini? 

 “ Alitaka kujua maendeleo yangu na 

lini ninarejea Moshi” akajibu Alfred. 

 “ Ok good” akasema Pauline na safari 

ikaendelea. 

 “ Kwa siku hizi chache nilizokaa na 

Alfred ninajiona ni kama vile tayari Fred 

ni mume wangu.Ni mwanaume anayenifaa 

sana huyu .Nina hakika hata leo hii 

nikimtambulisha kwa baba lazima atamkubali tu.Lakini tatizo ni mume wa 

mtu.Ni hapo tu panaponiumiza 

kichwa.Siyo siri tena kwa namna 

nilivyotokea kumpenda Alfred ni lazima 

nitaingia katika vita ya kumgombania 

mume wa mtu.Sina ujanja tena 

nimekwisha nasa mtegoni na siwezi 

kujinasua .Najua Grace ataumia sana 

lakini sina namna nyingine mimi na yeye 

lazima tuingie katika mapambano ya 

kumgombania Alfred.” Akawaza Pauline. 

 Waliwasili hospitali na kufululiza 

moja kwa moja kwa daktari ambaye 

aliwapa taarifa nzuri kwamba kwa 

mchana wa siku ile David alizinduka na 

kuongea kidogo lakini kwa wakati ule 

alikuwa amechomwa sindano ya usingizi 

ili dawa kali anazotumia ziweze kufanya 

kazi .Kwa ujumla daktari alithibitisha 

kwamba maendeleo ya David yalikuwa 

mazuri.Hizi zilikuwa ni taarifa nzuri sana 

kwa akina Pauline. 

 Daktari akawaruhusu kuingia 

kumtazama David lakini kwa sharti la 

kuingia mmoja mmoja mle chumbani tena 

wakiwa na mavazi maalum.Wa kwanza 

kuingia mle ndani ya chumba alikuwa ni 

Sanya.David alikuwa amelala usingizi 

mzito ,Sanya akamsogelea na kumshika mkono.Akamtazama kwa makini na 

kusema 

 “ David najua hata ukiwa usingizini 

utayasikia maneno haya 

ninayokutamkia.Ni maneno yatokayo 

ndani kabisa mwa moyo wangu.David sijui 

nianzie wapi lakini ninachoweza 

kukisema ni kwamba nilikuja Tanzania 

kwa dhumuni la kuwatafuta wazazi wangu 

na sikujua kama nitakutana na 

mwanaume wa kwanza 

kumpenda.Nimekutana nawe na ghafla 

sana bila kujua sababu nimetokea 

kukupenda sana.Nina hakika safari yangu 

ya Tanzania ilikuwa ni maalum kwa 

kunikutanisha nawe kwani kwa muda 

mrefu nilijizuia kuingia mapenzini 

nikimuomba Mungu anijalie niweze 

kumpata kijana mwenye sifa 

ninazozihitaji na sifa nyingi kati ya hizo 

unazo wewe David.Ninakupenda 

David..Ninakupenda sana na sintoacha 

kumlilia Mungu usiku na mchana akupe 

uponaji wa haraka ili niweze kupata nafasi 

ya kukueleza haya nikwambiayo sasa 

huku ukinitazama machoni.” 

 Sanya akatoka mle chumbani huku 

akifuta machozi.Pauline akamkumbatia na 

kumpa moyo mkono.Akamtazama kwa makini na 

kusema 

 “ David najua hata ukiwa usingizini 

utayasikia maneno haya 

ninayokutamkia.Ni maneno yatokayo 

ndani kabisa mwa moyo wangu.David sijui 

nianzie wapi lakini ninachoweza 

kukisema ni kwamba nilikuja Tanzania 

kwa dhumuni la kuwatafuta wazazi wangu 

na sikujua kama nitakutana na 

mwanaume wa kwanza 

kumpenda.Nimekutana nawe na ghafla 

sana bila kujua sababu nimetokea 

kukupenda sana.Nina hakika safari yangu 

ya Tanzania ilikuwa ni maalum kwa 

kunikutanisha nawe kwani kwa muda 

mrefu nilijizuia kuingia mapenzini 

nikimuomba Mungu anijalie niweze 

kumpata kijana mwenye sifa 

ninazozihitaji na sifa nyingi kati ya hizo 

unazo wewe David.Ninakupenda 

David..Ninakupenda sana na sintoacha 

kumlilia Mungu usiku na mchana akupe 

uponaji wa haraka ili niweze kupata nafasi 

ya kukueleza haya nikwambiayo sasa 

huku ukinitazama machoni.” 

 Sanya akatoka mle chumbani huku 

akifuta machozi.Pauline akamkumbatia na 

kumpa moyo  “ Usijali Sanya David atapona tu” 

akasema Pauline na kisha ikafuata zamu 

yake kuingia mle chumbani 

 Wote watatu walifanikiwa kuingia 

chumbani mle kumtazama David na kwa 

kuwa hawakuwa na kitu kingine cha 

kufanya pale hospitali walijiandaa 

waondoke na kuelekea hospitali ya St 

Gasper alikolazwa mzee Zakaria.Kabla 

hawajaondoka Sanya akawakumbusha 

akina Pauline kitu 

 “ Mnawakumbuka wale wagonjwa 

wetu wa ajali? Kwa nini kabla 

hatujaondoka tusiende kuwatazama na 

kujua hali zao zinaendeleaje? 

 “ Ni kweli kabisa.Kwa sasa wakati 

tuna hakika kwamba David hayuko tena 

katika hatari nadhani ni jambo jema kama 

tukienda kuwatazama wale wagonjwa 

wetu kama tayari wamekwisha anza 

kupata nafuu” akasema Alfred na baada ya 

kwenda katika gari wakaelekea katika 

wadi walikolazwa akina Vivian.Walifika 

katika chumba cha Tino lakini kulikuwa 

na watu wengine ambao walikuwa 

wakisubiri kupata nafasi ya kumjulia hali 

na tayari muda ulikuwa umekwenda sana 

na tayari watu walianza kutakiwa 

kuondoka  “ Kwa hapa hatutaweza kupata 

nafasi ya kuingia.Twendeni tukajaribu 

kwa Yule mwanamama” akashauri Pauline 

wakaondoka kuelekea katika chumba 

alimolazwa Vivian. 

 Nje ya chumba cha Vivian hakukuwa 

na watu wengi,kwani tayari wengi wa 

waliokuja kumtazama tayari walikwisha 

ondoka.Katika mlango walisimama watu 

wawili mwanaume na mwanamke.Pauline 

akawasalimu na kuwauliza kama kuna 

mtu mle ndani .Yule mwanaume 

akawaaambia kwamba mgonjwa anaongea 

na mtoto wake 

 “ Ninyi ni ndugu zake? Akauliza Yule 

mwanaume mtanashati 

 “ Hapana sisi si ndugu zake ila sisi 

ndio tuliowachukua kutoka mahala 

walikopata ajali na kuwakimbi za hapa 

kwa hiyo tumekuja kujua maendeleo yao” 

akasema Pauline 

 “ Ouh ahsanteni sana.Wagonjwa 

wote wawili wanaendelea vizuri japokuwa 

wamepoteza baadhi ya viungo vya mwili 

lakini wanaendelea vizuri.” Akasema Yule 

mwanaume 

 “ Yah ilikuwa ni ajali mbaya sana” 

akasema Pauline  “ By the way ninaitwa Robin na huyu 

hapa anaitwa Lucy mke wangu ” Yule 

mwanaume akajitambulisha 

 “ Nafurahi kuwafahamu.Ninaitwa 

Pauline na wale pale ni wenzangu ambao 

nimeambatana nao” akasema Pauline 

 “ Wewe ni mwenyeji wa Arusha? 

Akauliza Lucy na mara simu yake ikaita 

akasogea pembeni 

 “ Mimi ni mwenyeji wa hapa Arusha 

lakini usiku ule wa ajali ile mimi na 

wenzangu tulikuwa tumetokea Moshi.” 

Akasema Pauline na kuendelea kusimama 

pal e nje wakimsubiri mtu aliyekuwamo 

mle chumbani atoke ili waingie.Sanya na 

Alfred walikuwa wamesimama kwa mbali 

kidogo wakiongea. 

 “ Aliyesema duniani wawili wawili 

hakukosea kabisa .Yule msichana 

amefanana mno na Lucy kwa kila kitu 

isipokuwa yeye amekuwa ni mweupe 

zaidi..Dah ! wamefanana mno..” akawaza 

Robin akiwa ameyaelekeza macho kwa 

Sanya.Pauline akatazama saa yake ya 

mkononi na kusema 

 “ Nadhani tutakuja tena siku 

nyingine kwani muda unakwenda sana na 

tunaye mgonjwa mwingine tunayekwenda kumtazama” akasema Pauline na kisha 

yeye na akina Fred wakaondoka. 

 “ Mhhh !!.huku si kufanana kwa 

kawaida.Yule msichana na Lucy 

wamefanana sana.Wamefanana macho 

midomo na hata kutembea.Sijui kama 

Lucy amemchunguza Yule msichana vizuri 

na kuona namna walivyofanana.Mhh !! 

akawaza Robin wakati akina Pauline 

wakiondoka kuelekea katika gari 

lao.Mlango ukafunguliwa Penina akatoka 

 “ Baba twendeni tuondoke.Aunt Lucy 

yuko wapi? ” akasema Penina 

 “ Lucy anaongea na simu.Umeongea 

na mama yako? Mmeongea nini? 

 “ Hakuna kitu cha maana 

tulichokiongea .Alinitaka nikae karibu 

naye na akawa anaongea mambo ambayo 

siyaelewi .Ananiambai eti nikuombe ili 

usije ukamuacha bali umrudishe tuishi 

pamoja.” Akasema Penina. 

 “ Wewe ukamjibu nini? Akauliza 

Robin 

 “ Sikumjibu kitu nikabaki 

ninamuagalia tu.” Akasema Penina 

 “ Wewe unasemaje? Tumrudishe 

mama yako nyumbani tuishi naye? 

Akauliza Robin na kumfanya Penina atoe 

kicheko kidogo  “ Baba mbona unanitega wakati jibu 

unalifahamu? Mwanamke ambaye 

anakufaa na ambaye mimi ninamuhitaji ni 

Aunt Lucy pekee na hakuna 

mwingine.Kwani mama alipokukimbia si 

alikwenda kuolewa? Basi akae na hao hao 

matajiri aliowakimbilia ” akasema Penina. 

 “ Mhh ! itachukua muda mrefu kwa 

Penian kumsamehe mama yake.Vivian 

hayupo kabisa kichwani kwa Penina.Haya 

ndiyo malipo ya mambo 

aliyoyafanya.Alimkimbia mtoto kwa 

wakati ambao alimuhitaji sana ,alihitaji 

mno malezi ya mama lakini naye 

amekataliwa kwa wakati ambao anahitaji 

sana mapenzi ya mtoto.Ukimfanyia mtu 

ubaya nawe utalipwa kadiri ya ubaya 

uliomfanyia.Ni wakati wake wa kujuta 

sasa kwa kila alichokifanya.Kama 

asingekimbia kwa wakati ule na 

akavumilia tukashikamana na hivi sasa 

angekuwa anaishi maisha mazuri 

anayoyataka lakini alikimbia umasikini 

kumbe akasahau kwamba Mungu 

aliyenipa mimi umasikini ndiye aliyempa 

utajiri huyo mwanaume aliyemkimbilia. .” 

akawaza Robin .Lucy akarejea 

wakaondoka zao. **************** 

 Wakiwa garini wakielekea St.Gasper 

hospitali kumtazma mzee Zakaria,simu ya 

Alfred ikaita.Alipotazama jina la mpigaji 

akastuka sana akamuomba Pauline 

aegeshe gari pembeni ili aweze kuongea 

na ile simu.Pauline akaegesha gari 

pembeni na Fred akashuka. 

 “ Hallow mzee shikamoo ! akasema 

Fred huku uso wake ukonekana kuwa na 

matone ya jasho 

 “ Fred ni mambo gani hayo uliyoanza 

kuyafanya? Akauliza mtu Yule upande wa 

pili wa simu 

 “ Mambo gani mzee? Akauliza Fred 

 “ Fred ninakuomba urejee haraka 

sana Moshi kwa mkeo.!! Akasema kwa 

ukali Yule mzee 

 “ Amekupigia simu akakueleza 

kwamba nimeondoka? 

 “ Ndiyo.Kwa nini unamfanyi a hivi 

mkeo? 

 “ Mzee nimekuja huku Arusha kwa 

dharura,nilihitajika katika hospitali ya 

Serian mara moja”  “ Tafadhali usinidananye Fred.Mimi 

ninafahamu kila kitu zaidi yako.Tayari 

nimewasiliana na hospitali ya Serian na 

wamenihakikishia kwamba hawajakuita 

na wala hakuna mgonjwa wa dharura wa 

moyo.Tafadhali naomba urejee Moshi 

haraka sana!!! 

 Alfred akakaa kimya 

 “ Alfred unanisikia? Akauliza Yule 

mzee kwa ukali 

 “ Ndiyo mzee nimekusikia.” 

 “ Vizuri.Saa mbili usiku leo nitapiga 

simu nyumbani kwako nataka nikusikie 

ukiwa Moshi.!!! Akasema kwa ukali Yule 

mzee na kukata simu.Alfred akatoa 

kitambaa na kujifuta jasho kisha akarejea 

katika gari.Sura yake ilikuwa imebadilika 

 “ Fred nini kimetokea? Mbona 

umebadilika hivyo? Akauliza Pauline 

 “ Pauline I’m sorry lakini jioni ya leo 

natakiwa kurejea Moshi” akasema Fred 

 “ Unarejea Moshi? Kuna tatizo gani? 

 “ NInahitajika hospitali kuna 

dharura” 

 “ Kwani huwezi ukawadanganya 

kwamba uko mbali na huwezi kufika kwa 

haraka? Akasema Pauline 

 “ Hapana Pauline.Lazima nirejee 

Moshi leo” akasema Alfred  “ C’mon Alfred please don’t leave us.I 

need you here.” Akasema Pauline lakini 

Alfred hakuweza kubadili msimamo wake 

 “ Nadhani sasa uvumilivu wangu 

umefika mwisho.Ni wakati wa kumaliza 

kila kitu .Siko tayari kuendelea kuvumilia 

tena upuuzi wa namna hii.Siko tayari 

kuendelea kuteseka namna hii” Akawaza 

Alfred 

Saa tatu za usiku Alfred akawasili 

nyumbani kwake Moshi.Mkewe Grace 

ndiye aliyemfungulia geti akamkaribisha 

ndani .Tayari mtoto wao alikwisha lala 

kitambo 

 “ Pole na safari darling” akasema 

Grace 

 “ Nashukuru sana G.Habari za hapa? 

Akauliza Fred 

 “ Habari za hapa nzuri sana.habari za 

Arusha ?” akajibu Grace huku akimsaidia 

mume wake kuvua viatu halafu akamvua 

shati na kumuongoza hadi chumbani kwao 

wakaingia bafuni wakaoaga halafu 

wakapata chakula kisha wakapanda 

kitandani 

 “ So you called him? Akauliza Alfred 

wakiwa kitandani  “ I’m sorry.sikuwa na namna 

nyingine ya kufanya kwani leo ni siku 

yako “akasema Grace 

 Alfred hakuonekana kutaka tena 

maongezi akageuka upande wa pili kwa 

dhumuni la kulala lakini Grace akamgeuza 

na kumbusu. 

 “ Grace I’m sorry kwa leo hatuwezi 

kufanya nimechoka sana’” akasema Fred 

 “ Pole sana Fred laknileo hii ni siku 

yako na hatuwezi kuacha.kwa mwenzi 

mzima nimekuwa ninaisubiria siku hii. 

Tafadhali Fred ,japo kidogo tu” akasema 

Grace 

 “ Grace siwezi kwa leo nimechoka 

sana.May be next time” akasema Fred. 

 “ Fred please ! Ukiacha leo 

nitakusubiri tenakwa mwezi mzimahadi 

mwenzi ujao.Pleae darling !! akasisitiza 

Grace lakini Fred hakuwa tayari.Grace 

akakasirika sana na kumtazama Fred kwa 

hasira 

 “ Whats wrong with you Fred ?!! 

Akauliza Grace baada ya jitihada zake zote 

zote za kumshawishi Alfred wafanye 

mapenzi usiku ule kushindikana 

 “ Grace nimekwambia nimechoka 

sana na kwa leo.Naomba unielewe” 

akasema Afred .Grace akamtazama kwa hasira na huku akilengwa na machozi 

akasema 

 “ Alfred nadhani ni wakati sasa wa 

kuelezana ukweli.Ni kweli umechoka or 

its because of her? Akauliza Grace. 

 “ tayari bomu limelipuka.She knows 

everything ”akawaza Alfred . 

 “ Alfred answer me !!unadhani 

sifahamu mambo unayoyafanya na 

Pauline? Ninajua kila kitu.Ninajua kabisa 

kwamba hukuwa umeitwa Serian bali 

ulikwenda kula raha na 

Pauline.Ninafahamu kila kitu 

mnachokifanya nanimeumia sana .” 

Akasema Grace kwa hasira.Fred hakujibu 

kitu 

 “ kwa nini A lfred unanifayia hivi? 

Kwa nini lakini unaniumiza kiasi hiki? 

Akauliza Grace huku akilia. 

 “ Nilikuamini sana Fred na siku 

tegemea kabisa kama siku moja ungeweza 

kunifanyia kitu kama hiki.You are a 

monster Fred.!! A monster !! akasema 

Grace huku akimpiga Fred na mito ya 

kulalia.Fred akamdaka mikono yake 

 “ Stop calling me a monster !! 

akasema Fred kwa ukali 

 “ between me and you who is a 

monster??? Akauliza David huku akitweta kwa hasira.Grace hakujibu kitu 

akaendelea kulia.David akakaa kitandani 

na kuinama akajishika kichwa akatafakari 

na kusema 

 “ Grace kama ulivyosema awali 

kwamba ni wakati wa kuelezana ukweli na 

nitakueleza ukweli bila 

kukuficha”akasema Alfred huku kifua 

chake kikiwa kimeloa jasho 

 “ Ni kweli sikuwa nimekwenda 

Serian kama nilivyokueleza.Nilikuwa n a 

Pauline” akasema Alfred.Grace akainuka 

na kuanza kumpiga Alfred makofi 

 “ How could you do this to me 

Fred??!! Akauliza Grace huku akilia na 

kuendelea kumpiga Fred makofi 

 “ Stop that Grace!! Akasema david na 

kumsukuma Grace akaangukia kitandani 

 “ Ni kweli mimi na Pauline tuna 

mahusiano and to be honest our 

relationship is going deeper” akasema 

Alfred 

 “ Please Alfred don’t hurt me please 

”akasema Grace huku ameuweka mkono 

wake kifuani sehemu uliko moyo na 

machozi yakimtiririka 

 “ You wanted the truth and I’m 

telling you the truth” akasema Fred na kumtazama Grace aliyekuwa amekaa 

kitandani akilia 

 “ Grace mimi na wewe tumeishi 

pamoja kwa miaka mingi sasa na katika 

muda huo wote tumevumiliana na 

hakukuwa na mgogoro wa aina yoyote ile 

lakini leo hii naomba nikuweke wazi 

kwamba siwezi tena kuendelea na aina hii 

ya maisha tunayoishi.I can t do this 

anymore Grace.” Akasema Fred na 

kumstua Grace 

 “Unataka kusema nini i Fred? 

Akauliza Grace 

 “ I’m sorry Grace but I have to leave 

you” 

Grace akastuka na kumtazama Fred 

kamavile anatazama kitu cha kutisha 

 “ You are leaving me?? Grce akauliza 

kwa ukali 

 “ yes .I’m leaving you”akajibu Fred 

 “ No you can’t do that.Huwezi 

kuniacha kwa sababu ya Yule kahaba.No 

Fred you can’t do that to me!!! Akalia 

Grace. 

 “ Yes I’m leaving you for her .I’m 

tired of this.I want to start a new life with 

Pauline.Haya si maisha ninayoyahitaji na 

ninevumilia sana hadi hapa nilipofika 

lakini siwezi kuendelea zaidi ya hapa.Tafadhali naomba unielewe 

Grace.Please let me go and find my 

happiness.Furaha yangu ninaipata kwa 

Pauline”akasema Fred 

 Ghafla Grace akainuka na kuanza 

kutupatupa vitu mle chumbani kwa hasira 

.Ikamlazimu Fred kufanya lazi ya ziada ya 

kumdhibiti. 

 “ Unafanya nini Grace?!! Tafadhali 

hebu tulia!! Akasema Fred na kumuweka 

Grace kitandani.Grace alikuwa 

anatetemeka kwa hasira 

zisizomithilika.Aakavua ngo zote na 

kubaki mtupu akaanza kugala gala pale 

kitandani akilia.Alionekana kama 

kuchanganyikiwa.. 

 “Grace !! Grace !!..akaita Fred lakini 

ghafla Graceakainukana kuzama Fred 

kibao .Fred akamuinua na kumnasa vibao 

viwili vikali 

 “ Unanipiga? Akauliza Grace akiwa 

amefura kwa hasira 

“ nakuuliza Fred unanipiga?!! Kw a 

nini umenipiga? Akauliza Grace 

 “ Grace nimekupiga ili uachane na 

mambo yako ya kitoto.Nataka tuzungume 

kama watu wazima.Sijawahi kukupiga 

hata siku moja lakini ukinilazimisha leo 

hii nitakufunza adabu” akasema Fred.  “ You want to kill me?!! Go ahead kill 

me.!!..Akasema Grace ka hasira na kuanza 

kulia ..Fred akamsogelea na kumshika 

mabegani kisha kwa sauti ya upole 

akasema 

 “Grace tafadhali naomba unisikilize.” 

 “ Fred you are killing me my 

love…..Please don’t kill me !! akasema 

Grace 

 “ Grace naomba unikilize..Me and 

you we can talk about this,right? Akasema 

Fred kwa sauti ya kubembeleza. 

 “ No Fred huna tena cha kuniambia 

kwani kila kitu kiko wazi .She’s everything 

to you now but I swear you can’t be with 

her..”akasema Grace 

 “ Grace kwa nini unataka kuyafanya 

mambo haya yawe magumu? akasema 

Fred 

 “ Fred kitu gani umekikosa kwangu ? 

baada ya miaka hii yote kw anini ubadilike 

leo hii? Tumevumiliana kwa muda mrefu 

sana iweje uniache leo hii? Iwont let that 

happen!! Akasema Grace 

 “ Grace unafahamu kabisa ni kwa 

miaka mingapi nimekuvumilia na hata 

siku moja sijawahi kukutamkia 

lolote.Nimefanya kila kitu ambacho 

nimetakiwa kukifanya na sijawahi kulalamika hata siku moja.Unadhani ni 

nani ambaye angekubali kufanya kama 

nilivyofanya mimi? Nakuapia hakuna 

anayeweza kufanya kitu kama hicho . 

Maisha yenu ni mazuri tu na kila 

mlichokuwa mnakitafuta mmekipata.Ni 

wakati wangu na mimiwa kuitafuta furaha 

ya maisha yangu.Tafadhali Grace 

naombeni mnipe nafasi hii na mimi 

niweze kufurahia maisha yangu na 

mwanamke ninayempenda “akasema 

Alfred 

 “ Fred nimesema hapana.!! Huwezi 

kuniacha “akasema Grace kw a hasira.Fred 

akainuka na kumtazama grace halafu 

akasema 

 “ Grace I’m tired of lying to the world 

that we’re married while we’re not! Hata 

kama ukikataa mimi nitaondoka 

tu.Nimekwisha fanya maamuzi na lolote 

litakalotokea na litokee tu.kama utajiua ni 

juu yako lakini mimi sihusiki na kitu 

chochote !! akasema Fred.Grace akafuta 

machozina kumtazama Fred 

 “ Fred unanilazimisha nikwambie 

mambo mengine ambayo sikutaka 

kukueleza lakini kwa hapa tulipofika 

lazima nikueleze.”akasema Grace  “Unataka kunieleza nini Grace? 

Hakuna utakachonieleza kitakachobadili 

msimamo wangu.”Akasema Fred huku uso 

wake ukionyesha wasi wasi kidogo. 

 “ The moment you leave me..you will 

die!! Akasema Grace 

 “ Are you going to kill me?!! Akauliza 

Fred 

“ Not me ! I won’t kill you because I 

love you.” Akasema Grace 

“ Who is going to kill me then? Your 

daddy? Akauliza Alfred 

“ No ! my daddy won’t kill you.Siku 

ile ulipokubali kuvaa pete ya ndoa katika 

kidole chako na kutamka yale maneno 

kilikuwa ni kiapo chako na ambacho 

ukikiuka lazima ufe.Alfred sikudanganyi 

lakini ukilipuuza jambo hili sintakuwa na 

namna nyingine ya kukusadia.You must 

die and because I love you so much I will 

die too.Siwezi kuisjhi bila wewe.Tafadhali 

naomba usifanye hivyo Fred ili uniokoe 

na mimi.Mtotowangu bado 

mdogo”akasema Grace 

“ Tafadhali usinitishe 

Grace.Anyeamua siku ya kufa kwa mtu ni 

Mungu peke yake na si mwanadamu au 

mtu mwingine yeyote.Hilo ulilolisema 

haliwezi kunirudisha nyuma hata kidogo”akasema Fred.Grace akamtazama 

na kusema 

 “ Show me your hands” Fred 

akamuonyesha mikono yake 

 “ Where is the ring? 

 “ Nimeivua.I don’t want to pretend 

anymore ” Akasema Fred na Grace 

akamtazama kwa macho makali kisha 

akasema 

 “ Katika safari yako yakwendana 

kurudi umenusurika ajali ama ulipatwa na 

tatizo lolote baya ukiw a Arusha? Akauliza 

Grace.Alfred akatafakari kidogo kisha 

akajibu 

 “ Ndiyo.Tulivamiwa nyumani kwa 

akina Pauline na majambazi i .How do you 

know? Akashangaa Alfred 

 “ Fred you were supposed to die 

.Pone pone yako ni kwamba hukuwa 

umeirudisha pete ile kwangu ama sivyo 

ungeuawa.Endapo ukithubutu kufanya 

hivyo unavyotaka kufanya I swear 

hautamaliza siku moja you must die” 

akasema Grace. 

 “ Ouh my God !!..yawezekana ni kweli 

hili analolisema Grace? Akawaza Fred 

.Grace akamsogelea na kumshika bega. 

 “ Fred najua nimekustua 

sana.Sikutaka kukueleza kuhusu jambo hili lakini umenilazimisha nikueleze..Fred 

I love you so much na hata mimi sifurahii 

maisha haya tunayoshi lakini nitafanya 

nini? najua unahitaji sana uhuru najua 

unahitaji sana kuishi maisha yenye uhuru 

na mwanamke unayempenda na ndiyo 

maana nimekuwa nijitahidi sana kufanya 

kila niwezalo ili uweze kuwa na furaha 

katika maisha yako .Tafadhali Fred 

usifanye hivi.Utajiletea matatizo na sisi 

sote tutakuwa matatizoni.tafadhaIi 

nakuomba utulie na tuendelee kuishi 

kama zamani.”akasema Grace. 

 “I need to talk to your father!! 

Akasema Fred na kuchukua simu 

akazitafuta namba za simu za baba yake 

Grace akampigia 

 “ hallo Fred.Umekwisha wasili 

Moshi? 

 “ Mzee kuna tatizo kubwa na 

ninahitaji sana kukuona.kesho mimi na 

Grace tutapanda ndege na kuja kukuona 

mara moja” akasema Fred 

 “ hamha haja ya kupanda ndege 

kunifuata kwani hata mimi ninaelewa 

kuna tatizo na nimekwisha jiandaa kesho 

nitakuja huko Moshi kuwaoneni.” 

Akasema baba yake Grace  “ sawa mzee” akajibu Fred na kukata 

simu .Jasho liliendelea kumtiririka 

mwilini. 

 “ dah sikujua kama mambo 

yangekuwa namna hii.kwa nini lakini 

niliamua kujiingiza katika maisha haya na 

kujitia kitanzi mimi mwenyewe? 

Nitajiokoaje na janga hili linalonikabili ? 

Najuta ! najuta kumfahamu 

Grace.”akawaza Fred 

 “ Ni kweli niliweka nadhiri ya kuishi 

na Grace kwa maisha yangu yote hadi kifo 

kitutenganishe.laiti kama ningefahamu 

kama nadhiri ile ni kisu kitakacho nichinja 

mimi mwenyewe,katu nisingekubali 

kabisa kuyatamka maneno yale.” 

Akaendelea kuwaza Fred. 

 “ Maneno aliyoniambia Grace yana 

ukweli ndaniyake na kama nikiyapuuza ni 

kweli ninaweza kupatwa na janga au hata 

kupoteza maisha.Nikweli wakati 

ninaelekea Arusha kulitokea ajali katika 

gari la mbele yetu na hata tukiwa kule 

Arusha nyumbani kwa akina Pauline 

tulivamiwa na majambazi ambao kama si 

kwa msaada wa polisi wangeweza kutuua 

sote.Nikithubutu kumrudishia pete hii 

Grace ninaweza kupatwa na janga kubwa 

.lakini siwezi kukubali kumkosa Pauline hata iwe vipi..Kwa ajili yake niko tayari 

kwa lolote.Ngoja kesho nitakapoonana na 

huyu mzee nitajua kila kitu kuhusu hatma 

ya maisha yangu..Nimechoshwa na maisha 

haya na litakalotokea na litokee tu” 

akawaza Fred. 

Nyumba ya mzee Zakaria ilikuwa kimya 

kama vile hakukuwa na watu.Sanya na 

Pauline walikuwa sebuleni wakitazama 

filamu wakati mtumishi wa ndani 

akiendelea na shughuli za usafi wa 

vyombo. 

 “ The house is too big for us.Watu 

wote waliokuwa wakiichangamsha 

nyumba hii hawapo.Baba ,David na hata 

Yule shetani Vicky.”akawaza Pauline na 

sura ya Alfred ikamjia 

 “ Ouh Alfred I miss you already.Kwa 

nini lakini ukaondoka na kuniacha peke 

yangu? Sasa ninaanza kuona adha ya 

kuzama katika mapenzi na mume wa 

mtu.Nimekaa na Fred kwa siku hizi chache 

tayari nilikwisha mzoea na kuhisi kama 

vile tayari ni mume wangu.Nitafanya nini 

basi ili niweze kummiliki Fred awe wangu 

peke yangu? Nitawezaje kumuondoa Fred 

kwa mke wake? Akajiuliza auline na 

kuinuka akaenda jikoni na kuchukua 

chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi.Sanya akamtazama bila kusema 

chochote alikuwa ameelekeza macho yake 

luningani akitazama filamu 

 “ Mambo haya ya kuzama mapenzini 

na mume wa mtu nilikuwa nayatazama 

katika filamu na sikutegemea kama siku 

moja na mimi yatanikuta.Sasa yamenikuta 

na nitalazimika kuingia katika vita ya 

kumgombania mwanaume kwani sina 

ujanja tena lazima nipambane kumpata 

Alfred.Hili si jambo zuri hata kidogo lakini 

nitafanya nini na mimi Alfred nimekufa 

nikaoza kwake na ndiye mwanaume 

ambaye ninamuhitaji katika maisha 

yangu? I must fight to get him.Hata kama 

nitamuumiza mwanamke mwenzangu 

lakini ninachokihitaji mimi ni kumpata 

Fred tu.”akawaza Pauline huku akiendelea 

kupata mvinyo taratibu. 

 “ Pauline ! akaita Sanya 

 “ Kuna jambo nataka kukuuliza na 

ninaomba unieleze ukweli.”akasema 

sanya 

 “ Uliza chochote sanya nitakujibu” 

akasema Pauline 

 “ Ulinieleza kwamba uliwahi kuwa 

katika mapenzi na David na akakutenda 

mkaachana.Badouna hisia zozote juu yake? Bado una mpenda?akauliza 

Sanya.Pauline akatabasamu na kusema 

 “ kwa nini umeuliza hivyo Sanya? 

 “ Nnahitaji tu kufahamu” 

 “ Ni kweli niliwahi kuzama katika 

penzi zito na David na akaniumiza sana 

alipotembea na rafiki yangu mkubwa 

Tamia na ilikuwa ndiyo sababu ya mimi 

kuondoka na kwenda Moshi ambako 

nilikutana na Alfred ambaye kwa muda 

mfupi alifanikiwa kuyatibu majeraha 

yangu yote niliyoumizwa na 

David.Kukujibu swali lako ni kwamba 

David ni mtu muhimu katika maisha 

yangu lakini kwa sasa sina hisia naye 

zozote za kimapenzi.Kwa sasa David ni 

kama kaka yangu .Yaliyopita yamekwisha 

pita”akasema Pauline 

 “ Nashukuru Pauline kwa kuwa 

muwazi kwangu.Huyo rafiki yako ambaye 

David alikusaliti naye yukoje ? Ni 

mrembo?akauliza tena Sanya 

 “ Anaitwa Tamia.Ni msichana 

mrembo sana lakini hawezi kukufikia 

wewe hata robo.” Akasema Pauline na 

kumfanya Sanya atabasamu. 

 “ Tatizo la Tamia “ Pauline 

akaendelea  “ ni msichana ambaye anatamani kila 

mwanaume mzuri anayepita mbele yake 

na hatulii na mwanaume 

mmoja.Nilimuonya David kuhusu kuwa 

mbali na Tamia hakunisikia lakini baadae 

akakubalina na kilie 

nilichomwambia.Alimfumania Tamia 

akiwa na mwanaume ndani wakifanya 

mapenzi.” 

 “ kweli ?!!..Sanya akashangaa 

 “ Kweli kabisa.Alimfumania na 

mwanaume chumbani” 

 “ Dah ! Ikawaje baada ya hapo? 

Akauliza sanya 

 “ Kilichofuata wakaachana na kila 

mmoja akaendelea na maisha yake” 

 Sanya akavuta pumzi ndefu na 

kuuliza tena 

 “ kwa hiyo unataka kuniambia David 

kwa sasa hayuko katika mahusiano na 

mwanamke mwingine? 

 “ Sina hakika kama ana mwanamke 

mwingine.Nina hakika David yuko huru” 

akasema Pauline na kumfanya Sanya 

atabasamu 

 “ Pauline uhhmm…”Sanya akataka 

kusema kitu lakini akasita 

 “ Unataka kusema nini Sanya? 

Usiogope”  “ Uhhmm..!! utajisiaje kama mimi na 

David tukawa na mahusiano? 

Uso wa Pauline ukatengeneza tabasamu 

kubwa 

 “ Hilo ni jambo ambalo nimekuwa 

nikiliota usiku na mchana 

litokee.Nitafurahi sana kama likitokea” 

Akasema Pauline 

 “ Pauline nimefurahi kusikia hivyo 

na ninaomba nikuweke wazi kwamba 

ninampenda sana David.Ninampenda kwa 

moyo wangu wote.Nilipomshuhudia 

akifanya kitendo kile na mama yako 

mdogo nilikasirika sana na nikatoa 

maneno makali juu yake lakini ilikuwa ni 

hasira tu.Toka ndani ya moyo wangu 

ninampenda sana David na ninaamini 

ndiye hasa mwanaumeambaye Mungu 

amenipangia niwe naye.Ninaamini 

kwamba safari yangu ya kuja Tanzania 

ilikuwa maalum kwa ajili ya 

kunikutanisha na mwanaume wa maisha 

yangu ambaye ninaamini ni 

David.”akasema Sanya.pauline akainuka 

alipokuwa amekaa na kwenda 

kumkumbatia Sanya kwa furaha 

 “ Ouh Sanya !! pamoja na matatizo 

yote niliyonayo umeufanya uso wangu 

ujae tabasamu tena.Nimefurahi sana.Toka siku ya kwanza nilipokuona nilijua tu 

wewe ndiye mwanamke ambaye ungemfaa 

sana David.Baada ya kusikia kwamba 

amekorofishana na Tamia niliamini huu ni 

mpango wa Mungu ili mkutane.Sikujua 

kumbe hata wewe ulikuwa umetokea 

kumpenda David “akasema Pauline kwa 

furaha kubwa. 

 “ Sanya mimi nitafanya kila 

linalowezekana hadi nihakikishe wewe na 

David mnakuwa pamoja .hata kama 

ukishindwa kuonana na wazazi wako basi 

utafanikiwa kumpata mwanaume 

unayempenda” akasema Pauline. 

******************* 

 Saa kumi na mbili za asubuhi 

iliwakuta Pauline na Sanya katika geti la 

kuingilia hospitali kuu ya mkoa wa 

Arusha.Kisha shuka garini wakaelekea 

moja kwa moja katika wodi ya uangalizi 

maalum ambako walipewa taarifa 

kwamba tayari David alikwisha ondolewa 

huko na kupelekwa katika wadi ya 

kawaida baada ya hali yake kuwa nzuri. 

 Hii ilikuwa ni taarifa nzuri sana kwa 

Pauline na Sanya ambao waliongozana na muuguzi hadi katika chumba 

kilichoandikwa Private 12 alimolazwa 

David. 

 David alikuwa amelala, muuguzi 

Yule akamuamsha. 

 “ David ndugu zako wamekuja 

kukusalimia”akasema muuguzi.David 

akafumbua macho na kukutana na sura 

zenye tabasamu za Pauline na Sanya.Kwa 

furaha Pauline akamfuata pale kitandani 

akamkumbatia. 

 “ Ouh David !!..akasema Pauline 

 “ Pole sana David.Unaendeleje? 

akauliza Pauline. 

 “ Ninaendelea vizuri sana 

.Namshukuru Mungu amenirejeshea uhai 

tena.Nilikwisha chungulia kifo.” Akasema 

David .Sanya akamsogelea karibu 

 “ Pole sana David.” “ akasema Sanya 

huku machozi yakimtoka 

 “ Usilie Sanya.Mimi sijambo 

.Ninawashukuru kwa maombi yenu na 

Mungu amenirejeshea tean uhai wangu.” 

akasema David kwa sauti ndogo. . 

 “ David ninashindwa kujizuia kulia 

kutokana na namna tulivyoogopa baada ya 

tukio lile.Ulipigwa risasi tano na kuwa hai 

na kuweza kuongea nasi mida hii ni kwa uweza wa Mungu tu.Tulimlilia sana na 

amesikia kilio chetu” akasema sanya 

 “ Msiogope tena.Madaktari 

wamenihakiksihia kwamba siko tena 

katka hatari na ninaendelea vizuri 

sana.Niambieni mzee Zakaria yuko wapi? 

 “ mzee yupo na anaendelea vizuri ” 

akajibu Pauline 

 “ Nashukuru kusikia hivyo.Nilikuwa 

nawaza sana kama mzee ni mzima.Wale 

jamaa walikuwa na lengo la 

kumuua.Ahsante Mungu kama lengo lao 

halikufanikiwa.Dr Alfred naye yuko wapi? 

 “ Alfred ameondoka jana kuelekea 

Moshi .Aliitwa kwa dharura “ akajibu 

Pauline. 

 “ Hakuna mtu mwingine yeyote 

aliyedhurika katika shambulio lile? 

Akauliza David 

 “ Hakuna aliyedhurika .David you 

saved us.Bila wewe sote 

tungeamia”akasema Pauline na 

kushindwa kujizuia kuangusha machozi. 

 “ Basi usilie Pauline.Tumshukuru 

Mungu kwa kutukinga na jambo lile baya.” 

Akasema David kisha akina Pauline 

wakamtayarishia uji .  “ Madam Vicky naye yuko wapi? 

Akauliza david .Pauline na Sanya 

wakaangaliana. 

 “ tafadhalini niambieni Vicky yuko 

wapi?akauliza tena David 

 “ Vicky anashikiliwa na polisi kwa 

hivi sasa akihusishwa na tukio lile” 

akasema Pauline 

 “ Ouh Ahsante Mungu.Nilikuwa na 

wasi wasi labda ametoroka”akasema 

David 

 “ Mwanamke yule ni katili sana” 

akasema David 

 “ David tayari tunafahamu kila siku 

kilichotokea.Kamanda wa polisi 

amekwisha tueleza kila kitu.”akasema 

Pauline 

 “ Amewaeleza kila kitu? 

 “ Ndiyo David.Kila kitu tunakifahamu 

.David kuna mambo mengi sana ya 

kuongea ukishapona lakini kwa sasa 

naomba niseme samahani sana kwa 

kupuuzia wito pale uliponiambia kwamba 

kuna kitu cha muhimu unataka 

kuniambia. Sikujua kama ulitaka 

kunieleza jambo kama hili“ akasema 

Pauline. 

 “ Usijali Pauline.Nilitaka 

kukufahamisha kuhusu jambo hili kabla halijatokea lakini hayo yamekwisha pita 

sasa hivi.Tutaongea zaidi nikitoka humu ” 

akasema David. 

***************** 

 Saa tano za asubuhi Helkopta ikatua 

katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa 

Kilimanjaro.Mzee Damian Mwamba 

mmoja wa mabilionea wakubwa afrika 

mashariki akashuka .Alikuwa amevaa koti 

refu jeusi lililoendana na kofia nyeusi ya 

mduara aliyoivaa kichwani.Mkononi 

alikuwa na fimbo ndefu yenye nakshi za 

dhahabu. 

 Alitembea taratibu akiwa 

ameambatana na walinzi wawili 

waliovalia suti nzuri nyeusi .Nje ya uwanja 

wa kimataifa wa Kilimanjaro gari aina ya 

range rover E vogue yenye rangi nyeusi 

ilikwisha andaliwa.Mzee Damian mwamba 

akafunguliwa mlango na kuingia kisha 

gari lile la kifahari likaondoka na safari ya 

kuelekea mjini Moshi ikaanza. 

 Dakika kama ishirini baadae 

akawasili mjini Moshi na kuelekea moja 

kwa moja nyumbani kwa Alfred.  “ What happened my queen? mzee 

Damian akamuuliza mwanae Grace mara 

tu baada ya kufika kwao na kumuona 

akiwa amevimba macho hali iliyoonyesha 

wazi kwamba alikuwa amelia sana usiku . 

 “ Usijali baba ni mambo ya 

kawaida.Karibu sana”akasema Grace 

 “ Grace wewe ni roho yangu na 

hatakiwi kabisa mtu yeyote Yule kukutoa 

chozi” akasema mzee Damian 

 “ Tell me did Alfred hurt you? 

Akauliza Damian.Grace hakujibu kitu 

akabaki anatoa machozi na mara akatokea 

Alfred akitokea chumbani.Mzee Damian 

akamtazama kwa hasira na kumnyoshea 

fimbo 

 “ I warned you,my daughter is my 

souls and she shouldn’t get hurt in 

anyway..Why did you hurt her?? Akauliza 

kwa ukali huku uso wake ukionyesha 

hasira za wazi .David hakujibu kitu 

akabaki anamtazama. 

 “Nimekuuliza Alfred kwa nini 

umemliza mwanangu? Akauliza mzee 

damian 

 “ mzee nadhani ungekaa kwanza ili 

tuweze kuongea kuhusu mambo haya ” 

Akasema Alfred.Mzee Damiana akaendelea kumtazama kwa hasira na 

kusema 

 “ Kabla ya kukaa nnarudia tena 

kukuonya kwamba hii iwe ni mara ya 

mwisho kwa mwanangu kudondosha 

chozi.!! Akasema kwa ukali mzee damian 

na kukaa 

 “ Grace please bring me my whisky 

please !! akasema mzee mwamba na Grace 

akamletea chupa kubwa ya pombe 

akammiminia katika glasi akanywa halafu 

akasema 

 “ habari za hapa? 

 “ Shikamoo mzee” akasema Alfred 

 “Marahaba.Nimewaulizeni habari za 

hapa? Akasema mzee Mwamba.Fred na 

Grace wakatazamana 

 “ Mbona hamnijibu? Nielezeni mna 

tatizo gani? Nimevunja ratiba zangu zote 

kwa ajili ya kuja kuwasiliza kwa hiyo 

naombeni mnisaidie kuokoa muda kwani 

kila dakika moja inayopotea ninapoteza 

millions of money…lakini kabla 

hamjanieleza chochote nataka niseme 

wazi kwamba Alfred sijapendezwa kabisa 

na kile ulichokifanya na ninakuonya 

kwamba iwe ni mara ya mwisho .Tabia hii 

imeanza lini ya kumdanganya mkeo 

kwamba unakwenda Arusha kikazi wakati unakwenda kutumbua raha na mwanamke 

mwingine? Honestly nimechukizwa sana 

sana na jambo hili na ninaomba iwe ni 

maraya mwisho kutokea.Sitaki tena 

kusikia kuhusu jambo hilo.Sitaki tena 

Grace adondoshe chozi.Unajua chozi la 

mwanangu lina gharama gani? Do you 

know? Akauliza mzee mwamba.Alfred 

hakujibu kitu 

 “ You don’t even know.Sasa kwa nini 

unamliza mwanangu wakati thamani ya 

chozi lake huijui? Nasema iwe ni mara ya 

kwanza na ya mwisho.Tumeelewana 

Alfred? akauliza mzee Mwamba lakini 

Fred hakujibu kitu.Alikasirishwa na 

maneno yale ya mzee Damian 

 “ Tumeelewana Fred? Akauliza tena 

 “ ndiyo mzee” akajibu Fred 

 “Good.sasa nielezeni matatizo yenu 

kabla ya mimi sijaongea chochote” 

akasema mzee mwamba 

Alfred na Grace wkatazamana. 

 “ Mwambie sasa wewe si ndiye 

uliyemuita? Akasema Grace 

 “ Mwambie wewe ,” Alfred na Grace 

wakaaza kutupiana mpira.mzee mwamba 

akacheka halafua akajimiminia mvinyo 

katika glasi akasema  “ Kama mmeshindwa kunieleza basi 

ngoja niseme ya kwangu.”akasema mzee 

Mwamba 

 “ Baba hatujashindwa kukueleza.Ni 

kweli mimi na Alfred tuna tatizo kubwa na 

ndiyo maana amekuita hapa” 

 “Nielezeni basi nitatizo gani hilo? 

Akasema damian na kumuita mmoja wa 

walinzi wake aliyekuwa amesimama 

mlangoni akamwambia ampate pakiti la 

sigara akatoa sigara kubwa akaiwasha na 

kuanza kuvuta 


TAMATI


0 comments:

Post a Comment

Blog