Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL (2) - 4

   

Simulizi : The Football (2)

Sehemu Ya Nne (4)


kazi moja” akasema Meshack 

Jumbo.Maneno yale yalionekana 

kumuingia kamanda Anangisye 

lakini bado akawa na mashaka 

“Naona unashindwa kufanya 

maamuzi.Ngoja nimpigie simu rais 

nimueleze hali halisi halafu yeye 

atatoa maelekezo.Hili jambo ni dogo sana na halipaswi kumfikia 

rais ila kwa kuwa huniamini ngoja 

nimjulishe ” akasema Meshack na 

kuchukua simu yake akaanza 

kuzitafuta namba za rais 

“Usipige simu hiyo tafadhali 

mzee.Nitaonekana mtu 

nisiyefahamu majukumu yangu” 

akasema Anangisye 

“Nini maamuzi yako basi? 

Nahitaji kujua kwani muda 

unakwendea mbio” 

“Mtatumia muda gani 

kumfanyia mahojiano? 

“Siwezi kukisia muda kwani 

inategemea na ugumu wa mtu ila 

tunajitahidi sana isichukue muda 

mrefu” “Sawa ninakukabidhi 

mtuhumiwa uondoke naye lakini 

naomba apewe uangalizi wa hali ya 

juu sana kwani tuhuma 

zinazomkabili ni kubwa.Hata hivyo 

mtaongozana na timu ya vijana 

wangu ili punde tu mtakapomaliza 

mahojiano wamchukue 

mtuhumiwa na kumrejesha 

kituoni mara moja” 

“Hapana kamanda Anangisye 

hatuwezi kuongozana na vijana 

wako.Mahala tunakompeleka 

Mathew kwa maojiano ni mahala 

pa siri na hapaswi mtu asiyehusika 

kupafahamu.Usihofu chochote 

baada tu ya kumaliza upande wetu 

tutamrejesha sisi wenyewe na 

kumkabidhi kwenu.Mimi ndiye ninayebeba dhamana yote hivyo 

nawaomba muendele kutusibiri 

hapa hapa ili tukimaliza mahojiano 

basi mtuhumiwa aletwe hapa moja 

kwa moja” 

Kamanda Anangisye 

akakubali Meshack Jumbo 

aondoke na Mathew.Akaamuru 

afunguliwe pingu za miguuni ila 

mikono ikabaki imefungwa na 

Meshack akapewa funguo ya 

kufungulia pingu 

“Ahsante sana 

kamanda.Tunaonana hapo baadae” 

akasema Meshack baada ya 

kukabidhiwa Mathew 

Meshack ,Mathew na Austin 

wakaingia katika gari la 

Mathew,Amarachi na Camilla wakaingia katika lile gari 

walilokuja nalo wakaondoka 

wakiwaacha askari wakishangaa 

wasielewe nini kimetokea 



Meshack ,Mathew na Austin 

wakaingia katika gari la 

Mathew,Amarachi na Camilla wakaingia katika lile gari 

walilokuja nalo wakaondoka 

wakiwaacha askari wakishangaa 

wasielewe nini kimetokea 

“Ahsante sana mzee” akasema 

Mathew 

“You don’t have to thank 

me.Ni wajibu wangu kufanya hivi 

kwani mimi ndiye niliyekufanya 

ukakubali kufanya kazi hii hivyo 

napaswa kuhakikisha unakuwa 

salama” 

“Pole sana Mathew” akasema 

Austin 

“Ahsante Austin.Umepataje 

taarifa zangu? Umekutana wapi na 

mzee Jumbo? Akauliza Mathew 

“Mimi ndiye niliyempigia simu 

na kumtaka anisaidie tuweze kukuondoa katika mikono ya 

polisi” akasema Meshack 

“Nina deni kubwa kwako mzee 

jambo.Nilikuwa nimekwama na 

sikujua ningewezaje kutoka katika 

mikono ya polisi.Tuhuma ile ni 

nzito na huu ungekuwa ni mwisho 

wangu.Mzee nakuahidi sintofumba 

jicho hadi nihakikishe wale wote 

waliofanya tukio lile la mauaji ya 

Dr Robert wanapatikana” 

“Tutayazungumza haya 

Mathew lakini kwa sasa nataka 

kujua wapi tunaelekea? Tunahitaji 

sehemu salama ambako Mathew 

atakaa kwa sasa” akasema 

Meshack Jumbo 

“Tunaendelea nyumbani 

kwangu.Usalama pale ni wa uhakika halafu hakuna anayeweza 

kuhisi kama Mathew yuko pale” 

akasema Austin.Meshack Jumbo 

akachukua simu akampigia dereva 

wake akamjulisha kwamba 

atachelewa kidogo na kumtaka 

aingie hotelini apate kinywaji na 

atakapomaliza mambo yake 

atamjulisha. 

Walifika nyumbani kwa 

Austin wakakaribishwa ndani. 

“Vijana ahsanteni sana kwa 

kulifanikisha zoezi la kumuokoa 

Mathew toka mikono ya polisi na 

tumefanikiwa kumpata bila 

kumwaga damu.Hata hivyo 

nitawaacha kwa muda kuna 

mambo ambayo bado nahitaji 

kuyaweka sawa.Nitarejea hapo baadae kidogo.Austin I need your 

car.Nahitaji kurejea tena kule 

hotelini liliko gari langu.Natakiwa 

kurejea tena ikulu usiku huu kuna 

suala muhimu la kukamilisha” 

akasema Meshack Jumbo na sura 

za Mathew na Austin zikaonyesha 

wasi wasi 

“Msihofu I’ll be fine.Kamanda 

Anangisye na askari wake bado 

wako nyumbani kwa Mathew 

wanatusubiri kwa hiyo nataka 

kuitumia fursa hii kukamilisha 

baadhi ya mambo muhimu kabla 

suala hili halijafika ngazi za 

juu.Nitakapomaliza nitarejea na 

tutaungana sote kuhakikisha 

jambo hili linafika mwisho” 

akasema Meshack Jumbo na Austin akamtaka Amarachi ampeleke 

Meshack Jumbo hotelini alikoacha 

gari lake. 

 “Sasa uko huru Mathew.Pole 

sana”akasema Austin baadaya 

Meshack kuondoka 

“Ahsante Austin.Sikutegemea 

kabisa kukutana nawe katika 

mazingira haya” 

“Kila kitu ni kwa maongozi ya 

Mungu.Hata mimi sikutegmea 

kabisa kama ningekutana nawe 

kaka hadi pale mzee Meshack 

aliponipigia simu na kunijulisha 

kwamba uko katika matatizo na 

hivyo tunahitaji kukusaidia 

kukutoa katika mikono ya 

polisi.Nilishangaa kwani niliamini 

uko Paris na mke wako sikujua kama uko hapa Dar es salaa” 

akasema Austin 

“Nimekwisha rejea Tanzania 

na ninaendelea na shughuli zangu 

za biashara.Kulitokea matatizo 

katika ndoa yangu na Peniela 

tukaachana.Vipi wewe maisha 

yako yanakwendaje? 

”Namshukuru Mungu mambo 

yangu yanakwenda vyema na kwa 

sasa tumefungua kiwanda kingine 

hapa Tanzania cha kutengeneza 

mvinyo.Kwa ujumla kila kitu 

kinakwenda vyema” 

“Nafurahi kusikia hivyo” 

akasema Mathew.Austin akatoka 

na kurejea na chupa kubwa ya 

mvinyo akawamiminia Mathew na Camilla katika glasi na 

kuwakaribisha 

“Hakuna majeraha yoyote 

mliyoyapata katika rabsha ile? 

Akauliza Austin 

“Hapana Austin.Hakukuwa na 

vurugu yoyote ile, kila kitu 

kilifanyika kwa amani.Tulitii kila 

walilotuambia kwani tusingeweza 

kupambana na askari wale wengi 

wenye silaha za moto.By the way 

huyu anaitwa Camilla snow ni 

rafiki yangu anatokea Marekani na 

yuko hapa nchini kwa ajili ya 

kusaidiana nami katika kazi 

ninayoifanya ya 

uchunguzi.Samahani kwa 

kutokutambulisha mapema” akasema Mathew na kumgeukia 

Camilla 

“Camilla huyu anaitwa Austin 

January ni mmoja wa marafiki 

zangu ambaye tumewahi wote 

kufanya kazi katika idara ya 

ujasusi na sasa kila mmoja 

anafanya shughuli zake binafsi.” 

Austin na Camilla 

wakasalimiana 

“Mathew nadhani ni wakati 

sasa wa kufahamu ni kitu gani 

kinachoendelea .Unachunguza 

jambo gani hadi ukajikuta katika 

dhahama hii kubwa? Akauliza 

Austin.Mathew akavuta pumzi 

ndefu na kutafakari kwa sekunde 

kadhaa akasema “Sikuwa nimetarajia kama 

ningeweza kurejea kufanya 

shughuli hizi za uchunguzi tena 

kwani tayari nimekwisha jiwekeza 

vya kutosha katika biashara.Lakini 

alinifuata mzee Meshack na 

kuniambia kwamba rais anahitaji 

kuniona.Mzee Meshack tuna 

mawasiliano mazuri kwani 

ninamsaidia kupata mashine kwa 

ajili ya kiwanda chake cha 

kutengeneza bidhaa za maziwa 

anachotaka 

kukifungua.Nilikwenda kuonana 

na rais kama alivyonitaka na 

akanieleza alichoniitia.Alinitaka 

nimsaidie kuchunguza chanzo cha 

baba yake kuuawa na nani 

waliomuua.Kifo cha baba yake kilitokea yapata miaka kumi 

iliyopita na mpaka sasa hakuna 

taarifa yoyote iliyowahi kutolewa 

kuhusiana na mauji yale wala 

wauaji kupatikana.Limekuwa ni 

kama fumbo gumu.Sikutaka 

kuifanya hiyo kazi lakini mzee 

Jumbo akanishawishi na kuniomba 

sana nikubali kuifanya hivyo 

nikakubali.Nilianza kwanza kwa 

kuchunguza ajali ya ndege 

iliyomuua rais Anorld Mubara 

kwani nilihisi kuna muunganiko 

kati ya kifo cha Kanali Matope na 

ile ajali.Hapo ndipo mambo 

yalipoanza” akanyamaza akanywa 

mvinyo kidogo na kuendelea 

“Niligundua kwamba mpaka 

leo hakuna taarifa ya chanzo cha kuanguka kwa ile ndege ya rais 

kwani kisanduku ambacho 

huhifadhi taarifa zote za 

mwenendo wa ndege hakikuwahi 

kupatikana.Hii ilinipa mshangao 

sana kuhusiana na kutoonekana 

kwa kisanduku hicho cheusi 

kwasababu mahala ndege 

ilipoangukia si sehemu ambayo 

kisanduku hakiwezi 

kupotea.Ndege ya Rais ilipata ajali 

wakati akirejea kutokea nchini 

Misri katika kikao cha wakuu wa 

nchi zinazopitiwa na mto 

Nile.Niligundua kwamba wakati 

wakirudi kutokea Misri ndani ya 

ndege hiyo kulikuwa na watu nane 

walioomba lifti baada ya 

kuchelewa ndege yao.Watu hao walikuwa waandishi wa habari 

wakitokea Marekani wakielekea 

Tanzania kufanya vipindi katika 

moja wapo ya mbuga zilizopo hapa 

nchini.Baada ya ajali kutokea na 

kutangazwa kwamba watu wote 

waliokuwemo ndegeni walikufa 

miili ya watu hao 

haikupatikana.Hii ilizidi 

kuniwashia taa nyekundu kwamba 

hapa kuna jambo kubwa” 

akanyamaza akanywa kinywaji 

tena na kuendelea 

“Niligundua pia kwamba mtu 

aliyewaombea lifti waandishi hao 

wa habari Fakrim Alnasor 

alihamishiwa nchini Marekani siku 

chache baada ya ajali ile ya ndege 

kutokea.Katika kumfuatilia mtu huyo nikagundua kwamba alikuwa 

na mawasiliano na mtu mmoja 

anaitwa Nathan ambaye ni 

mchumba wa rais Dr 

Vivian.Niliomba msaada kwa rafiki 

zangu waliokuwa nchini Marekani 

wa kumfuatilia huyo jamaa na mtu 

aliyeifanya hiyo kazi ni huyu 

Camilla.Fakrim aliuawa wakati 

akiingia nyumbani 

kwake.Iligundulika kwamba 

Fakrim alikuwa ni jasusi wa 

CIA.Baada ya kugundua kwamba 

Nathan alikuwa na mawasiliano na 

huyo mtu ilitulazimu kutumia 

ujanja na kumleta Nathan hapa 

nchini bila rais kufahamu.Kwa 

wakati huo rais na huyo mchumba 

wake walikuwa katika mgogoro mkubwa na hata ndoa yao 

waliyokuwa wanatarajia kuifunga 

ilikuwa imesitishwa.Nathan alikuja 

Tanzania lakini wakati 

nikimfanyia uchunguzi aliuawa na 

mdogo wake rais anaitwa 

Theresa.” Akanyamaza kwa 

sekunde kadhaa na kuendelea 

“Nilitaka kifo cha Nathan kiwe 

siri lakini wakati tukielekea 

kuuficha mwili huo tukavamiwa na 

watu ambao wanatumia sare na 

vifaa vya jeshi la polisi na 

kutushambulia nikaomba msaada 

toka kwa rais na wale wavamizi 

wakatoweka.Usiku huo huo 

nyumba ya mzee Jumbo ikavamiwa 

na kuchomwa moto na wale wale 

jamaa na ndipo nilipogundua kwamba walikuwa wanaifuatilia 

saa ya Nathan ambayo baadae 

nilimkabidhi rais na iko ikulu hadi 

sasa.Tuligundua kwamba Nathan 

alikuwa na mawasiliano na George 

Mzabwa aliyekuwa mkurugenzi wa 

idara ya usalama wa taifa aliyejiua 

kwa kujipiga risasi.Tulihitaji 

kumchunguza George na 

tukampata mke wake ambaye 

alitupeleka katika nyumba yao 

ambayo George huhifadhi nyaraka 

zake za siri katika 

kasiki.Tulipolifungua kasiki 

tukagunuda kuwepo kwa risiti za 

benki.Risiti hizo zilionyesha 

kwamba George alitoa kiasi 

kikubwa cha fedha katika benki ya 

Escom tawi la Tanzania na kuziweka katika akaunti tatu 

tofauti zilizopo katika hiyo benki 

ya Escom ambazo tuligundua ni za 

kampuni ya kuchonga madini ya 

vito ambayo mke wake Herieth ni 

mkurugenzi.Tulimpata Herieth 

tukamuhoji na akatuelekeza kwa 

mkuu wake Ranbir Kumar ambaye 

angeweza kutupa majibu ya 

maswali yetu.Tulipomfuata Ranbir 

yeye na Herieth wakakimbia kwa 

gari na wakati tukiwafukuzia 

wakauawa.Kesho yake tukaitwa 

ikulu na rais akazuia tusiendelee 

tena na uchunguzi tuliokuwa 

tunaufanya.Kwa kuwa ni yeye 

aliyekuwa ametupa kazi hii 

ililazimu kutii wito wake na 

nikaazimia kurejea tena katika shughuli zangu za biashara lakini 

baadae akanipigia simu Theresa 

akaniambia kwamba kuna 

mwanadada yuko pale ikulu ni 

mgeni na ana wasiwasi 

naye.Ikatulazimu kumfanyia 

uchunguzi huyo mwanadada na 

kugundua kwamba taarifa zote 

alizotoa hazikuwa za kweli.Katika 

maelezo yake alidai kwamba yeye 

ni mtoto wa nje wa rais Anord 

Mubara jambo ambalo si kweli 

kwani hawana mahusiano 

yoyote.Tuligundua hata elimu 

anayodai kuwa nayo si kweli 

kwani tulifuatilia katika vyuo 

anavyodai kusoma lakini 

hakuwahi kusoma 

huko.Tulipomfuatilia nyumbani kwake tukagundua kwamba 

alikuwa na mawasiliano na waziri 

wa mambo ya nje wa nchi Dr 

Robert Mwainamela na balozi wa 

Marekani hapa nchini.Tulifanya 

jitihada hadi tukafanikiwa 

kumpata Dr Robert na kumfanyia 

mahojiano na ndipo tulipogundua 

kuwepo kwa mpango wa kumuua 

waziri wa mambo ya nje wa 

Marekani Helmet Brian mara tu 

atakapotua katika uwanja wa 

ndege wa kimataifa wa Julius 

Nyerere.Mpango huu umesukwa 

na serikali ya Marekani 

wakishirikiana na watu wao wa 

hapa Tanzania.Marekani wana 

mtandao mkubwa hapa Tanzania” “Hebu subiri kidogo 

Mathew.Marekani wanataka 

kumuua waziri wao wa mambo ya 

nje ndani katika ardhi ya Tanzania 

kwa nini? Akauliza Austin 

“Kuna msuguano unaoendelea 

hivi sasa duniani kati ya Korea 

kaskazini na Marekani na 

kilichozidisha msuguano huo ni 

baada ya Tanzania kutangaza 

kuanzisha mashirikiano ya 

kibiasharana na Korea Kaskazini 

na kuiuzia madini ya Urani kitu 

ambacho Marekani hawakiafiki 

kwa hiyo wamekuja na mpango 

huo wa kumuua waziri wao wa 

mambo ya nje hapa Tanzania na 

kudai kwamba mauaji hayo 

yamefanywa na watu waliotumwa na Korea Kaskazini na kwa njia 

hiyo watapata sababu ya 

kuishambulia Korea kaskazini kwa 

kigezo cha kulipiza kisasi.Baada ya 

kugundua mpango huo mimi na 

wenzangu tukaandaa mpango wa 

kuzima shambulio hilo na 

kumuokoa waziri 

Helmet.Ulichosikia kimetokea 

usiku huu pale uwanja wa Julius 

Nyerere ni mimi na wenzangu 

tunahusika nalo na tukafanikiwa 

kumuokoa waziri 

Helmet.Tulimchukua Helmet hadi 

nyumbani kwangu kisha nikaenda 

kuonana na rais nikamueleza kila 

kitu kuhusiana na kilichotokea 

nikamkabidhi kwake Helmet 

aweze kumuwekea ulinzi kwani naamini Marekani watatumia kila 

njia kumuua.Nilipotoka hospitali 

kuonana na rais nikapigiwa simu 

na mmoja wa vijana wangu 

niliowaacha nyumbani wakimlinda 

Dr Robert kwamba wamevamiwa 

na watu wenye silaha na vijana 

wawili wameuawa na watu hao 

wameingia ndani.Nilifika mara 

moja nikakuta nyumba 

imezingirwa na askari polisi 

wakaniweka chini ya ulinzi kwa 

mauaji ya Dr Robert.Wale watu 

waliovamia nyumbani kwangu 

walimuua Dr Robert .Hiyo ndiyo 

hali halisi hadi mlipokuja kunitoa 

katia mikono ya polisi” akasema 

Mathew.Austin akachukua glasi yake ya kinywaji akagugumia 

mvinyo wote 

“Pole sana Austin.Ni masahibu 

makubwa yaliyokupata .Sikujua 

kama kuna mambo makubwa 

namna hii yanaendelea nchini 

kwetu.” 

“Ni mambo makubwa Austin 

ambayo ukisimuliwa huwezi 

kuamini.Marekani wametengeneza 

mtandao mkubwa hapa nchini 

wanaoutumia kwa shughuli 

zao.Kitu ambacho tayari nina 

uhakika nacho ni kwanza 

Marekani walishiriki katika 

kuiangusha ndege ya rais Anorld 

na kumuua kwani kwa mujibu wa 

taarifa ya daktari aliyefanya 

uchunguzi miili ya marehemu ni kulikuwa na matundu ya risasi 

katika baadhi ya miili ya 

marehemu na hii inaonyesha 

kwamba kulikuwa na shambulio 

kabla ya ndege 

kuanguka.Hatujafahamu bado 

sababu ya wao kufanya hivyo ila 

tutafahamu kwa kuwa bado 

tunaendelea kuchunguza.Pili 

shirika la ujasusi la Marekani 

wamekuwa wakimfuatilia rais Dr 

Vivian kwa muda mrefu toka 

angali anasoma chuo kikuu nchini 

humo.Walimpandikiza Nathan 

ambaye alianzisha mahusiano ya 

kimapenzi lakini lengo lake 

lilikuwa ni kumchunguza.Mpaka 

sasa bado hatujafahamu ni kitu 

gani hasa ambacho Marekani wanakichunguza kwa Dr 

Vivian.Inaonekana kuna jambo 

ambalo wanalichunguza kwa 

miaka hii yote bila 

kuchoka.Tunapaswa pia kufahamu 

kama kuna siri yoyote anayo Dr 

Vivian anayo ambayo inawafanya 

Marekani wamfuatilie kwa muda 

huu mrefu.Hayo ni mambo mawili 

ambayo lazima tuyatafutie majibu 

yake ila kwa sasa tuna jambo 

ambalo tunapaswa kulifanya kwa 

haraka nalo ni kuwapata 

waliomuua Dr Robert kwani ni 

wazi wamefanya hivyo kwa sababu 

maalum.Kuna jambo walikuwa 

wanalificha lisijulikane.Watu hawa 

wako makini sana na kibaya zaidi 

wanafahamu kila ninachokifanya.Walifahamu kuwa 

sipo nyumbani na Dr Robert yuko 

pale kwangu na wakavamia 

wakamuua na muda huo huo 

askari wakapewa taarifa na mimi 

kuangushiwa mzigo wote wa 

mauaji.Naamini hiki ni kitu 

kilichopangwa na ndiyo maana 

nikakueleza awali kwamba safari 

hii nimeingia katika anga za watu 

wenye nguvu.Mtandao wa hawa 

jamaa ni mrefu na wanaweza 

wakafanya jambo lolote kwa 

wakati wowote wautakao na ndiyo 

maana wamefahamu kuhusu Dr 

Robert na wakamuua” Mathew 

akanyamaza baada ya simu yake 

kuita.Akastuka sana “Dah ! Nimesahau hadi kuzima 

simu.Hii ni hatari kwani watu 

hawa wanaweza wakanitafuta kwa 

kutumia mawimbi ya simu na 

wakafahamu niko mahala gani” 

akasema na kuitoa simu yake 

mfukoni na kustuka alipoziona 

namba zilizompigia.Ni namba 

alizokuwa anazifahamu 

“Peniela!! Akasema Mathew 

kwa mshangao 

“Hizi ni namba zake za simu 

ambazo hutumia akiwa 

Tanzania.Inawezekanaje atumie 

namba hizi wakati yuko Paris 

Ufaransa? Au kuna mtu mwingine 

ambaye anazitumia badala yake? 

Akajiuliza Mathew na kuamua 

kuipokea ile simu. “Hallow ” akasema 

“Mathew habari yako”ikasema 

sauti ya upande wa pili ambayo 

Mathew aliitambua ni ya Peniela 

“Peniela?! Akauliza kwa 

mshangao 

“Ina maana huifahamu hii 

sauti ni ya nani? Akauliza Peniela 

“Ninaifahamu ila nimestuka 

kwa kuona unatumia hizi namba 

ambazo huzitumia ukiwa Tanzania 

wakati wewe uko Paris Ufaransa” 

“Niko Tanzania Mathew.” 

“Uko Tanzania? Umekuja 

muda gani wakati mara ya mwisho 

nilizungumza nawe ukiwa Paris 

Ufaransa? 

“Nimepata dharura na 

kuamua kuja mara moja Tanzania.Tutazungumza baadae 

kwa sasa ninaondoka hapa 

Bandarini Dar es salaam hivyo 

nakuomba tukutane nyumbani 

kwangu.Kokote uliko nakuomba 

usitishe shuguli zako na tukutane 

nyumbani” 

“Unasema uko bandarini Dar 

es salaam? Mathew akashangaa 

“Ndiyo,nimetokea 

Zanzibar.Ndege zimezuiwa kutua 

katika uwanja wa ndege wa Julius 

Nyerere kwa muda kufuatia tukio 

lililotokea uwanjani hapo mapema 

usiku huu hivyo ikatulazimu 

kwenda kutua Zanzibar na kutoka 

pale nikachukua boti hadi dar es 

salaam.Naomba tukutane Mathew nina mazungumzo muhimu sana 

nawe” 

“Umekuja na Anna Maria? 

Akauliza Mathew 

“Ndiyo niko naye siwezi 

kumuacha” akasema Peniela 

“Ahsante sana nakuja hapo 

sasa hivi.Ahsante sana kwa 

kunileta furaha yangu ya maisha” 

akasema Mathew na kukata simu 

akamtazama Austin kwa uso 

uliojaa furaha na tabasamu kubwa. 

“She’s here.!! Akasema kwa 

furaha 

“She’s here!!Peniela is here in 

Tanzania!! Akasema Mathew huku 

akiinuka 

“ Austin we have to go see her 

right now” “Mathew subiri 

kwanza.Uliniambia kwamba 

uliwasiliana na Peniela akiwa 

Paris Ufaransa imekuaje akaamua 

kuja Tanzania ghafla hivi ?Ujio 

wake huu unanipa mashaka isije 

kuwa anatumiwa” akasema Austin 

“Usihofu Austin.Lazima kuna 

jambo kubwa na la dharura 

lililomfanya Peniela akaja 

nchini.Ninamfahamu vyema 

Peniela hawezi katu kutumiwa na 

mtu yeyote kunizunguka 

mimi.Tumeachana lakini she’s 

very royal to me.Inawezekana 

labda Anna Maria amekataa 

kusherehekea siku yake 

yakuzaliwa bila mimi na ndiyo 

maana Peniela akaamua kuja tanzania.Yule bi bilionea sasa na 

anaweza akaenda kokote 

anakotaka muda wowote.Anayo 

ndege yake binafsi yenye kasi 

mara mbili ya kasi ya sauti” 

akasema Mathew 

“Pamoja na hayo Mathew 

lazima tuchukue tahadhari kwa 

jambo hili.Ujio huu wa haraka wa 

Peniela lazima una jambo” 

“Sikiliza Austin,kama 

nilivyokueleza kwamba tuligundua 

George Mzabwa alikuwa na 

akaunti katika benki ya Escom 

ambayo Peniela ni mmoja wa 

wamiliki.Escom bank inamilikiwa 

na watu watatu ambao ni Andrew 

Pillar,mwanae Anderson Pillar na 

Peniela.Tuligundua kwamba kampuni ya kuchonga madini ya 

vito ambayo mke wa George 

alikuwa mkurugenzi ina 

mashirikiano ya kibiashara na 

kampuni moja ya Marekani ya 

kutenegeza saa za 

mkononi.Kampuni hiyo ya saa 

ndiyo walioingiza kiasi kikubwa 

cha fedha katika akaunti ya 

George.Kampuni hiyo ya 

kutengeneza saa za mkononi ina 

mahusiano na kampuni ya A.D 

Electronics ambayo inamilikiwa 

kwa siri na serikali ya Marekani 

kupitia shirika lake la ujasusi la 

CIA.Baada ya kugundua hayo 

nilimwambia Peniela anisaidie 

kufanya uchunguzi kubaini kama 

mpenzi wake Anderson na baba yake Andrew Pillar ni mawakala 

wa CIA.Sijapata mrejesho wowote 

toka kwake hadi muda huu 

aliponipigia simu na kunijulisha 

kuwa yuko Dar es 

salaam.Ninaamini safari yake ya 

ghafla kuja Tanzania ina sababu 

kubwa.Twende tukaonane naye” 

akasema Mathew 

“Mpaka hapa nimekuelewa 

Mathew.Twende tukamuone 

yawezekana kweli akawa na 

taarifa muhimu za kutusaidia” 

akasema Austin wakatoka na 

kuingia katika gari la Austin 

wakaondoka 

“Huku njiani yatupasa tuwe 

makini sana Mathew kwani wewe 

bado ni mtuhumiwa” “Usihofu kuhusu hilo” 

akasema Mathew 

“Nini sababu ya CIA 

kutengeneza mtandao wake hapa 

Tanzania? Kuna jambo gani 

wanalitafuta? Austin akauliza 

“Hilo ndilo swali ambalo mimi 

na wenzangu tumekuwa 

tunalitafutia majibu” akajibu 

Mathew 

“Vipi kuhusiana na watu 

waliomuua kanali Sebastia 

Matope? Umefikia wapi katika 

kuwabaini? 

“Mauaji ya Kanali Sebastian 

Matope hayakuibuka tu hivi hivi 

bali yana sababu yake.Ili kupata 

sababu ya kwa nini aliuawa 

inapaswa kwanza kujua kwa nini rais Anorld aliuwa? Inasemekana 

Kanali Matope ndiye pekee 

aliyenusurika katika ile ajali ya 

ndege iliyomuua rais Anorld 

Mubara na miezi michache baadae 

akauawa.Katika uchunguzi wangu 

nimebaini kuna siri ambayo kanali 

matope na rais Anorld walikuwa 

wanaifahamu na hiyo ndiyo 

iliyopelekea vifo vyao.Kanali 

Matope alikuwa ndiye mbebaji 

mkuu wa begi la rais lililopewa 

jina la football.Begi hilo lilikuwa 

na siri ambazo rais alikwenda nazo 

kila mahala alikoenda na lilibebwa 

na mtu moja tu ambaye ni kanali 

Matope.Baada ya ajali ile Football 

halikuwahi kuonekana tena na 

hakuna ajuaye mahala lilipo.Mpaka sasa uchunguzi 

unaonyesha wazi kwamba CIA 

wanahusika katika kuratibu ajali 

ile ya ndege ya rais lakini bado 

sijafahamu kwa nini.Ili kupata jibu 

kwa nini walifanya vile tunapaswa 

kuingia katika vita na shirika 

kubwa la ujasusi duniani 

CIA.Tuufahamu mtandao wao 

tuufumue na tutapata majibu ya 

maswali yetu” akasema Mathew na 

Austin akawa kimya.Baada ya 

muda akasema 

“Mathew pole sana hata hivyo 

nakupongeza kwani kazi 

uliyoifanya katika kipindi hiki 

kifupi ni kubwa.Umegundua 

mambo mengi mazito.Kuanzia 

hapa tutashirikiana sote.Lazima tulifikishe hili suala mwisho” 

akasema Austin 

“Ahsante Austin kwa kuamua 

kujiunga nami.Jambo hili ni kama 

fumbo kubwa ambalo wengi 

wameshindwa kulifumbua lakini 

naamini safari hii litafumbuliwa” 

akasema Mathew 

“Kutokana na mtiririko wa 

mambo ulivyo,toka ulipoanza 

kulichunguza hili suala ni wazi 

watu hawa tayari wamekwisha 

kufahamu.Unapambana na watu 

ambao wanakufahamu lakini 

wewe hujawafahamu bado.Hii ni 

mbaya kwani muda wowote 

wanaweza wakafanya chochote 

bila wewe kutarajia.Ni muhimu kuchukua tahadhari ya kutosha” 

akasema Camilla 

“Anachokisema Camilla ni kitu 

cha kweli kabisa.hawa watu tayari 

wanakufahamu na ndiyo maana 

wamethubutu hata kufahamu 

kwamba hauko nyumbani na Dr 

Robert yuko pale hivyo wakavamia 

wakamuua.Mathew kuna 

umuhimu wa kuchukua tahadhari 

kubwa kama Camilla alivyoshauri” 

akasema Austin na Mathew 

akaitika kwa kichwa akionekana 

kujawa mawazo 




WASHINGTON DC 

Saa tisa za alasiri kwa sasa za 

Marekani,Will Gadner mkurugenzi 

wa shirika la ujasiri Marekani CIA 

aliwasili katika ikulu ya Marekani 

kufuatia wito wa haraka wa rais 

Mike straw.Moja kwa moja 

akaeleka katika ofisi ya rais 

“Will Gadner 

karibu.Sintakuwa na maneno 

mengi kwa sasa.Nataka kufahamu 

nini kimetokea Tanzania? Kwa nini 

operesheni haikufanikiwa? 

Akauliza Mike straw ambaye sura 

yake ilibadilika kwa hasira nyingi 

alizokuwa nazo.Alionekana wazi 

kulemewa na mzigo wa mambo.Will Gadner akarekebisha 

koo na kusema 

“Hakuna aliyetegemea kama 

kungetokea jambo kama lile kila 

kitu kilikwisha andaliwa vizuri na 

kilichokuwa kimebaki ni 

kutekeleza mpango wetu” 

“Will sihitaji siasa hapa 

.Nataka sababu kwa nini mpango 

wa kumuua Helmet Brian 

haukufanikiwa? Akauliza Mike 

kwa ukali 

“Mheshimiwa rais naomba 

unipe nafasi nikueleze kile 

kilichotokea.Nakushauri tuwe 

watulivu ili tuweze kutafuta 

suluhu ya hili jambo” akasema 

Gadner na Mike hakujibu kitu.Will 

akaendelea “Kilichotokea Dar es salaam 

kimetushangaza sote.Bado 

tunaendelea na uchunguzi kubaini 

kilichotokea lakini kuna taarifa 

tayari tumezipata kutoka 

Tanzania.Waziri wa mambo ya nje 

wa Tanzania ambaye ni mmoja wa 

watu wetu na ambaye tulimtumia 

sana katika kuandaa operesheni 

hii ameuawa muda mfupi tu baada 

ya shambulio kutokea na waziri 

Helmet kutoweka.Inaaminika 

kwamba alitekwa na kwenda 

kuuawa na maiti yake imekutwa 

kwa mtu aitwaye Mathew 

Mulumbi.Hii inatupa picha 

kwamba watu waliofanya 

shambulio lile walipata taarifa za 

kuwepo kwa mpango wa kumuua Helmet kutoka kwa Dr 

Robert.Tuliopata taarifa hizi 

tumetafuta kumjua huyu Mathew 

ambaye inadaiwa ndiye aliyemuua 

Dr Robert ni nani? Tumegundua 

kwamba anaitwa Mathew Mulumbi 

aliwahi kufanya kazi katika idara 

ya ujasusi ya tanzania lakini kwa 

sasa anajishughulisha na 

biashara.Wakati nakuja huku 

nikapata taarifa nyingine kwamba 

Mathew Mulumbi ndiye aliyefanya 

shambulio lile uwanja wa ndege 

wa Julius Nyerere na kuvuruga 

mpango wetu.Taarifa hiyo toka 

110C inasema kuwa Helmet Brian 

ni mzima wa afya na kwa sasa 

amekabidhiwa kwa rais Dr Vivian 

na yuko ikulu” Sura ya Mike straw 

ikabadilika kwa taarifa ile ya Willy 

Gadner.Akashika kichwa na 

kuvuruga nywele 

zake.Alichanganyikiwa 

“Hii ni taarifa mbaya ambayo 

sikuwa nimetegemea kuisikia.Kwa 

mara ya kwanza taifa kubwa 

duniani kama Marekani linazidiwa 

maarifa na nchi ndogo masikini 

kama Tanzania.Nchi hii ni 

mshirika wa Korea Kaskazini 

ambaye ni hasimu wetu mkubwa 

na kwa kuwa tayari wameifahamu 

mipango yetu basi tayari 

wamepata fimbo ya kutuchapia” 

Akainamisha tena kichwa na 

kuzama katika tafakari baada ya 

muda akasema “Gadner kwa nini lakini 

ukaruhusu ufanyike uzembe na 

kusababisha maadui zetu 

wazifahamu mbinu zetu za 

mapambano? 

“Mheshimiwa rais ,hakuna 

uzembe uliofanyika,kila kitu 

kilikwenda vizuri lakini hatuelewi 

kwa namna gani Mathew aliweza 

kugundua kuhusu mpango 

huu.Tutafahamu hayo uchunguzi 

utakapokamilika lakini kuna suala 

lingine ambalo si zuri sana pia” 

akasema Gadner.Sura ya Mike 

ikazidi kuonyesha woga 

“Msichana Olivia ambaye 

tulimpandikiza ikulu ili awe 

karibu na Dr Vivian ametoweka na hafahamiki mahala aliko.Jitihada 

za kumsaka zinaendelea” 

“Oh Mungu wangu !! akasema 

Mike straw kwa masikitiko 

“Yawezekana akawa 

ametekwa nyara au tayari naye 

ameuawa? Akauliza 

“Bado hatuna uhakika 

mheshiwa rais ila uchunguzi 

unaendelea” akasema Gadner na 

ukimya ukatanda halafu baada ya 

muda akasema 

“Huyu ni mtu wetu wa pili 

anapotea nchini Tanzania na wote 

ni wale mliowapandikiza karibu na 

rais.Hii inatupa picha ya wazi 

kwamba tayari mbinu zetu 

wamekwisha zifahamu.Gadner 

hatuwezi kuendelea namna hii.Amekwisha fahamu kwamba 

tunamchunguza na ndiyo maana 

watu wetu wote wanauawa na hii 

ina maana kwamba tumeshindwa 

kumzuia rais Vivian asianzishe 

mahusiano na Korea 

Kaskazini.Tumekosa sababu ya 

kuishambulia Korea Kaskazini na 

yote hii ni kwa sababu ya mipango 

yako mibovu.Nilikuamni sana 

lakini umeniangusha Gadner.Si 

mimi pekee uliyeniangusha bali 

umewaangusha wamarekani wote 

kwani Korea kaskazini ni adui wa 

wamarekani wote.” Akasema Mike 

na kuinamisha kichwa akafikiri 

kwa muda akamtazama Willy 

Gadner na kusema “Najaribu kutafakari ni vipi 

endapo Dr Vivian akaufahamu na 

kuamua kuuanika mpango wetu 

tulioupanga wa kumuua Helmet 

Brian?Hili liitakuwa jambo baya 

sana kisiasa.Hatutaaminiwa tena 

na wananchi na hili ni anguko 

langu kubwa kisiasa.Nimeshindwa 

kuwalinda wananchi wangu kama 

nilivyowaahidi na kuiruhusu 

Korea kaskazini kuendelea 

kujiimarisha kijeshi na kuzidi 

kutishia amani ya Marekani” 

akasema Mike na kunyamaza kwa 

muda kisha akaendelea 

“Helmet Brian ni mmoja wa 

watu wangu wa karibu 

sana.Tumesoma chuo kimoja na 

tulianza pamoja harakati zetu za siasa na ana mchango mkubwa 

sana kwa mimi kufika hapa 

nilipofika leo.Kiti hiki cha rais ni 

yeye ndiye aliyekuwa anatakiwa 

akikalie kwani ndiye aliyekuwa 

chaguo la wengi ndani ya chama 

lakini aliposikia kwamba na mimi 

nipo katika mbio za kuwania urais 

akajitoa na kuniunga mkono mimi 

na hivyo nikapata nafasi hii ya 

kuwa rais.Helmet si rafiki tu bali ni 

zaidi ya ndugu na maaumuzi ya 

kumuua hayakuwa rahisia 

kwangu.Itakuaje endapo 

atafahamu kuwa mimi ndiye 

niliyeidhinisha 

auawe?Nimechanganyikiwa Willy 

na sijui nifanye nini.Hebu nishauri 

nifanye nini kwani ninaweza kuchukua maamuzi magunu 

sana.Ninaweza kutuma kikosi 

kikavamie ikulu ya Tanzania na 

wamchukue Helmet .Uwezo huo 

ninao lakini siwezi kufanya hivyo 

ila pale nitakapokuwa sina njia 

nyingine nitalazimika kufanya 

hivyo” akasema Mike kwa hasira 

“Mheshimiwa rais,jambo hili 

linahitaji umakini mkubwa 

sana.Mpaka hapa tayari Dr Vivian 

amekwisha fahamu mipango yetu 

ya siri na anaweza akaanika kila 

kitu kwa dunia na kutufanya 

tudharaulike sana.Ipo namna ya 

kuweza kujaribu kumnyamazisha 

Dr Vivian na kumzuia asifanye 

chochote na akafuata kila 

tutakachomtaka afanye” “Enhe nakusikiliza” akasema 

Mike 

“Niliwahi kukueleza kwamba 

CIA tumekuwa tunamfuatilia Dr 

Vivian kwa muda mrefu sasa toka 

alipoanza kusoma hapa Marekani 

Kuna sababu maalum iliyotufanya 

tumfuatilie kwa karibu kwa muda 

huu mrefu na bado tunaendelea 

kumfuatilia” Willy Gadner 

akanyamaza kidogo halafu 

akaendelea 

“Dr Vivian alihamia Marekani 

kuendelea na masomo yake ya 

udaktari akitokea nchni Cuba 

alikokuwa anasoma.Akiwa Cuba 

ambako aliishi kwa miaka 

minne,Dr Vivian alikutana na mtu 

mmoja anaitwa Said Bazharan raia wa Syria ambaye naye alikuwa 

nchini humo kwa ajili ya 

masomo.Familia ya Said ambao ni 

watu matajiri sana wanaomiliki 

visima kadhaa vya mafuta 

walikuwa wanachunguzwa kwa 

tuhuma za kusaidia vikundi 

kadhaa vya kigaidi 

vilivyounganisha nguvu kwa ajili 

ya kupambana na serikali ya 

Syria.Urafiki wa Said na Vivian 

ulikuwa mkubwa na hatimaye 

wakawa wapenzi na katika 

mapenzi yao Vivian akapata 

ujauzito.Familia ya Said 

haikupendezwa na kitendo kile 

cha mtoto wao kumpa mimba 

mwanamke ambaye kwanza si wa 

dini yao na pili ni mwafrika.Ili wa Syria ambaye naye alikuwa 

nchini humo kwa ajili ya 

masomo.Familia ya Said ambao ni 

watu matajiri sana wanaomiliki 

visima kadhaa vya mafuta 

walikuwa wanachunguzwa kwa 

tuhuma za kusaidia vikundi 

kadhaa vya kigaidi 

vilivyounganisha nguvu kwa ajili 

ya kupambana na serikali ya 

Syria.Urafiki wa Said na Vivian 

ulikuwa mkubwa na hatimaye 

wakawa wapenzi na katika 

mapenzi yao Vivian akapata 

ujauzito.Familia ya Said 

haikupendezwa na kitendo kile 

cha mtoto wao kumpa mimba 

mwanamke ambaye kwanza si wa 

dini yao na pili ni mwafrika.Ili kujaribu kuliweka sawa suala hilo 

Said alimshawishi Vivian abadili 

dini ili aweze kukubalika na 

familia yake lakini Vivian hakuwa 

tayari kwa hilo.Baada ya 

kujifungua mtoto wa kike ambaye 

alipewa jina la Nasrat shinikizo 

toka kwa familia ya Said 

liliongezeka na Said akapata 

taarifa za siri kwamba kuna watu 

wametumwa nchini Cuba kwa ajili 

ya kuwaua yeye ,Vivian na mtoto 

wao Nasrat.Said akamueleza 

Vivian jambo lile na kwa pamoja 

wakapanga mpango ambao Said na 

Nasrat wakatoroka na kwenda 

nchini Palestina na kwa bahati 

mbaya akagunduliwa.Alipofahamu 

kuwa tayari amegundulika mahala alikoenda kujificha na kwamba 

kuna watu waliokuwa 

wanamfuatilia 

wamuue,akamtelekeza mwanae 

Nasrat katika kituo cha watawa na 

muda mfupi baadae nyumba 

aliyokuwa akiishi ikalipuliwa kwa 

bomu na Said Bazharan hakuwahi 

kuonekana tena na wengi 

waliamini kwamba alifariki katika 

ule mlipuko.Baadae uchunguzi wa 

CIA ulibaini kwamba Said hakufa 

katika ule mlipuko bali ni mzima 

na alipoondoka alikwenda 

kujificha nchini Syria na huko 

alianzisha kikundi cha kigaidi 

ambacho kinashirikiana na 

kikundi cha IS kupambana na 

serikali ya Syria na sasa anajiita Samir Alzahir”Willy Gadner 

akanyamaza kidogo na kisha 

akaendelea 

“Licha ya kutoka katika 

familia yenye kuhusishwa na 

kufadhili ugaidi,lakini CIA 

walianza kumfuatilia Said baada ya 

kugundulika kuwa na mawasiliano 

na mwanamfunzi mmoja kutoka 

Iraq aliye lipua bomu katika chuko 

kikuu kimoja hapa Marekani na 

kuua wanafunzi 

sitini.Tulichunguza nyenzo zake 

hadi pale alipokimbia Cuba. 

Alipoanza harakati zake za 

kupambana na serikali ya Syria 

watu wengi waliuawa wasio na 

hatia wakiwamo watoto.Hii 

ililazimu serikali ya Marekani na washirika wake kuamua kuingilia 

kati.Wanamgambo wanaomtii Said 

au Samir kwa sasa walifanya 

shambulio kubwa na kuua 

wanajeshi zaidi ya arobaini wa 

majeshi ya pamoja kwa hiyo 

serikali ya Marekani inamsaka 

kwa udi na uvumba hadi 

sasa.Baada ya kutoka Cuba,Dr 

Vivian alikuja kuendelea na 

masomo yake hapa Marekani na 

kwa kuwa tayari CIA walikwisha 

anza kumchunguza aliyekuwa 

mpenzi wake Said Bazharan 

aliyetoweka ililazimu kuanza 

kumchunguza Dr Vivian pia 

tukiamini kuwa lazima watakuwa 

wanawasiliana.Hivyo basi 

akapandikizwa mtu ambaye alianzisha urafiki naye na baaade 

wakawa wapenzi na huyu ni 

Nathan ambaye amepotea.Pamoja 

na kumchunguza Dr Vivian kwa 

muda mrefu hatujafanikiwa mpaka 

leo kunasa mawasiliano yake na 

Said.Hii ndiyo sababu CIA 

tunaendelea kumchunguza Dr 

Vivian tukiamini kwamba kupitia 

kwake tutaweza kufahamu mahala 

alipo Said.Baada ya maelezo hayo 

marefu turejee katika suala 

letu.CIA tumefuatilia na kugundua 

kwamba mtoto wa Dr Vivian yuko 

hapa Marekani 

anasoma.Alipokabidhiwa kwa 

watawa,Nasrat alibatizwa 

akabadilishwa jina na sasa anaitwa 

Florentina dawson” Uso wa rais Mike straw 

ukajenga tabasamu kubwa na 

kusema 

“Hizo ni habari nzuri sana.CIA 

mnafanya kazi kubwa na nzuri 

mno na ndiyo maana ni shirika 

kubwa la ujasusi 

duniani.Mnastahili pongezi 

kubwa.Dr Vivian anafahamu lolote 

kuhusiana na huyu 

mwanae?Anajua kama yuko hapa 

Marekani? 

“Nasrat aliokotwa na watawa 

baada ya kutelekezwa na baba 

yake ,akapelekwa nchini Israel 

akabatizwa akabadilishwa jina na 

baadae akaletwa Marekani 

kusoma.Said wala Dr Vivian 

hawafahamu alipo mtoto wao” “Una uhakika Gadner kwamba 

hata Dr Vivian hana taarifa zozote 

kuhusu mwanae? 

“Ndiyo mheshimwia rais.Hii ni 

siri kubwa aliyonayo Dr Vivian na 

hata nchini mwake hawafahamu 

kama aliwahi kuwa na mtoto.Hata 

ndugu zake hawafahamu 

chochote” 

“Safi sana.Kwa hapo Dr Vivian 

tumemuweka 

kwapani.Hatafurukuta tena.Nataka 

kupata taarifa zote za kuhusiana 

na huyo binti haraka sana kabla ya 

kufika saa mbili usiku wa 

leo.Nataka usiku wa leo 

nizungumze na Dr Vivian na 

kufanya naye makubaliano ili 

kwanza aturejeshee waziri wetu Helmet Brian ,pili asithubutu 

kufungua mdomo wake na 

kuiambia dunia kwamba ni sisi 

tuliopanga kumuua waziri wetu 

Helmet.Tatu ajiondoe katika 

mashirikiano na Korea 

Kaskazini.Mwisho awaachie huru 

watu wetu wawili walipotea nchini 

mwake ambao nina uhakika 

mkubwa kwamba anafahamu 

mahala walipo.Akikubali kufanya 

haya basi tutamuunganisha na 

mwanae Florentina na kama 

akipuuza basi nitatishia kuanika 

siri yake hii kubwa kwa dunia 

jambo ambalo hatakubali 

lifanyike.Hatakuwa tayari 

ajulikane kwamba amewahi kuzaa 

na gaidi na akatelekeza mtoto kwani jambo hili litampunguzia 

heshima yake aliyoijenga kwa 

watu wake na dunaini kwa 

ujumla.Kwa hapa Dr Vivian hana 

njia nyingine zaidi ya kuweza 

kufanya kile tutakachomtaka 

akifanye.Nataka nipate taarifa zote 

za kuhusiana na huyo mtoto kabla 

ya saa mbili usiku wa leo na 

ninaomba kuanzia sasa CIA 

muweke walinzi wa kumlinda 

Florentina.Mumfuatilie kila 

mahala aendako na kujua nyendo 

zake zote”akasema Mike ambaye 

uso wake ulianza kuonyesha 

tabasamu 

“Mheshimiwa rais tunaweza 

kufanya hivyo lakini njia hiyo si 

muafaka na haitakuwa na tija kwetu japo inaweza kumfanya Dr 

Vivian akakubaliana nasi katika 

baadhi ya mambo” akasema Will 

Gadner 

“Kwa nini unasema hivyo 

Willy?akauliza Mike straw 

akionekana kutokufurahishwa na 

kauli ile ya Willy Gadner 

“Kufahamu mahala aliko Said 

Bazharan au Samir Alzahir kama 

anavyojulikana sasa si sababu 

pekee kwa CIA kuwekeza nguvu 

kubwa katika kumchunguza Dr 

Vivian .Ipo sababu nyingine kubwa 

zaidi” 

“Kuna jambo lingine?akauliza 

Mike straw kwa mshangao 

“Ndiyo mheshimiwa rais” 

akajibu Will Gadner halafu ukafuata ukimya mfupo.Will 

gadner akaonekana kufikiri jambo 

“Ni jambo gani hilo Gadner? 

Tafadhali naomba unifahamishe” 

akasema Mike straw 

Gadner akavuta pumzi ndefu 

na kusema 

“Dr Vivian kuwa rais wa 

Tanzania si jambo lililokuja hivi 

hivi bali ni kitu kilichoandaliwa 

kwa muda mrefu” akanyamaza 

kwa sekunde kadhaa kisha 

akaendelea 

“Dr Vivian alipoanza masomo 

yake nchini Marekani akitokea 

Cuba alianzisha harakati za 

kutetea wanafunzi wenye asili ya 

afrika waliokuwa wakibaguliwa 

katika vyuo vikuu mbali mbali vya hapa Marekani na kwa ujasiri 

wake alianza kuwavutia watu 

wengi wakiwamo baadhi ya 

viongozi wa mataifa.Mmoja wa 

viongozi aliyeonyesha kuvutiwa 

sana na harakati za Dr Vivian 

alikuwa ni rais wa Cuba wa wakati 

huo Alfredo Marcus.Huyu aliwahi 

hadi kumualika Dr Vivian nchini 

mwake na kufanya mazungumzo 

naye ya siri.Hatujui walizungumza 

nini lakini mwezi mmoja baada ya 

rais Alfredo kumualika Dr Vivian 

nchini Cuba alifanya ziara nchini 

Tanzania ambako alikuwa na 

mazungumzo na rais wa Tanzania 

ambaye ina mashirikiano 

makubwa na nchi ya Cuba toka 

enzi za waasisi wa mataifa haya mawili.Baada ya kutoka nchini 

Tanzania rais Alfredo akaelekea 

nchini China ambako alifanya 

mazungumzo na kiongozi wa China 

kisha akarejea nchini mwake.Ziara 

hizi mbili alizozifanya katika nchi 

za Tanzania na China zilikuwa na 

lengo la kuwashawishi waweze 

kumuandaa Dr Vivian aweze kuwa 

rais wa Tanzania kwani kuna kitu 

kikubwa alikiona kwake.Mipango 

ya kumuandaa Dr Vivian kuwa rais 

wa Tanzania ilianzia hapo.Aliwahi 

kutoa hotuba yake katika moja ya 

makongamano aliyowahi kualikwa 

na katika hotuba yake hiyo aliwahi 

kueleza nia yake ya kutaka 

kuiunganisha Afrika na kuwa kitu 

kimoja.Alisema kwamba ana ndoto ya kuwa mtawala wa kwanza wa 

Afrika iliyoungana na kuwa 

moja.Alipotoa hutuba ile tayari 

alikwisha fahamishwa kwamba 

anaandaliwa kuja kuwa mtawala 

wa Tanzania siku za usoni.” 

Akanyamaza na Mike akachukua 

kitambaa akavua miwani na kufuta 

macho yake,Willy akaendelea 

“Miaka miwili baadae 

ukafanyika uchaguzi na rais 

aliyekuwepo madarakani wakati 

huo alimaliza muda wake akaingia 

madarakani rais Anorld Mubara 

ambaye naye alirithishwa mpango 

ule wa kumuandaa Dr Vivian kuwa 

rais wa Tanzania hapo 

baadae.Katika mwaka wa pili wa 

uongozi wake rais Anorldalitembelea nchini Cuba na kule 

akakutana na wanasayansi ambao 

walimuomba rais Anorld 

kuwekeza katika kiwanda cha 

kutengeneza gesi kwa ajili ya 

matumizi ya hospitali na rais 

akawakaribisha nchini 

Tanzania.Ujenzi wa kiwanda hiki 

ulikuwa wa siri na ni watu 

wachache tu waliokuwa 

wakifahamu mahala kilipojengwa 

kiwanda hicho.Kiwanda hicho 

kilikuwa kinazalisha gesi 

inayotumiwa mahospitalini lakini 

kwa kiasi kikubwa walikuwa 

wanatengeneza gesi ya sumu 

ambayo walikuwa wanaisafirisha 

nchini kwao kwa lengo la kujihami 

kwani Marekani walikuwa wametishia kuishambulia Cuba 

kijeshi.Siri hii ilijulikana baada ya 

gesi hiyo kuvuja wakati 

ikisafirishwa na kuua watu wote 

waliokuwemo ndani ya meli 

iliyokuwa ikisafirisha gesi hiyo 

kwenda Cuba.Uchunguzi 

ulipofanyika ikagundulika 

kwamba gesi hiyo haikuwa gesi ya 

mahospitalini bali ilikuwa ni gesi 

ya sumu yenye uwezo wa kuua 

kwa muda mfupi sana baada ya 

mtu kuivuta. Serikali ya Cuba 

ilificha ukweli wa jambo hili na 

badala yake ikatoa sababu 

nyingine ya uongo kuhusiana na 

watu wake kufariki ndani ya 

meli.Baada ya tukio hilo rais 

Anorld alikifunga kiwanda hicho na kuondoa wanasayansi wote 

waliokuwa wakifanya kazi nchini 

Tanzania.Funguo za kuingilia 

katika kiwanda hicho alikuwa nazo 

yeye mwenyewe pamoja na 

nyaraka zote muhimu za 

kutengenezea gesi hiyo ya sumu 

alizichukua na kwa bahati mbaya 

wale wanasayansi wote waliokuwa 

wakifanya kazi nchini Tanzania 

walifariki kwa ajali ya ndege 

wakati wakirejeshwa kwao kwa 

hiyo siri ya mahala kilipo kiwanda 

hicho cha kutengeneza gesi ya 

sumu ilibaki kwa rais Anorld na 

baada ya hapo ndipo alipoanza 

kutembea na mkoba alioupa jina 

fotball ambao ulikuwa na siri zote 

za kuhusiana na  kiwanda  hicho.Mkoba ule ulikuwa na ulinzi 

mkali na mbebaji mkuu alikuwa ni 

kanali Sebastian Matope ambaye ni 

baba yake na Dr Vivian.” 

Akanyamaza tena kwa muda kisha 

akaendelea 

“Baada ya CIA kufanya 

uchunguzi wake na kubaini jambo 

hilo tulianza mikakati ya kulipata 

lile begi au football kama 

walivyokuwa 

wakiliita.Tulifanikiwa 

kuwapandikiza watu wetu katika 

ndege ya rais Anorld wakati 

akirejea Tanzania akitokea nchini 

Misri alikoenda kuhudhuria kikao 

cha wakuu wa nchi zinazopitia na 

mto Nile lakini hatukufanikiwa 

kulipata hilo begi la football kwani kanali Sebastian Matope 

alifanikiwa kutoroka nalo 

ndegeni.baada ya ….” 

“Subiri kidogo 

Gadner.Unataka kuniambia 

kwamba serikali ya Marekani 

wanahusika katika kifo cha rais 

Anorld Mubara? Akauliza Mike 

straw 

“Ndiyo mheshimiwa 

rais.Marekani ndiyo iliyomuua rais 

Anorld Mubara” 

Mike straw akavuta pumzi 

ndefu na kusema 

“Kwa nini sikuwahi 

kufahamishwa kuhusiana na 

jambo hili hadi leo hii? 

“Mheshimiwa rais haya ni 

mambo ya siri kubwa na sisi tunaofahamu tumeapa kulinda siri 

hii katika kipindi chote cha uhai 

wetu lakini leo hii nimevunja 

kiapo changu kwa kukueleza 

jambo hili” akasema Willy 

“Tutazungumza baadae 

kuhusu suala hili,endelea na lile 

suala tulilonalo sasa” akasema 

Mike baada ya tafakari 

“Baada ya kufanikiwa kutoka 

salama ndegeni tuliendelea 

kumfuatilia Kanali Sebastian 

Matope ili kufahamu mahala 

alikolificha lile begi tunalolitafuta 

lakini hatukuweza kuambulia 

chochote na hadi sasa hatufahamu 

mahala alikolificha hivyo 

tulazimika kumuua kwani alikuwa 

tayari kueleza kile kilichotokea ndegeni.Baada ya kumuua kanali 

Sebastian kila kitu kimebaki 

siri.Hakuna anayejua nini kilitokea 

ndani ya ndege ile ya 

rais.Tunaamini kwamba Dr Vivian 

kuna kitu anafahamu kuhusiana na 

siri hii na mahala kilipo kiwanda 

kile cha kutengeneza gesi ya sumu 

lakini mpaka sasa hatujafanikiwa 

kupata kitu chochote.Mtu wetu 

ambaye ni Nathan alijitahidi kwa 

kila namna alivyoweza 

kumchunguza Dr Vivian kuhusiana 

na suala hili lakini hakuweza 

kupata kitu chochote.Bado 

tunaamini kwamba tukiendelea 

kumfuatilia Dr Vivian tutagundua 

mahala kilipo kiwanda hicho cha 

kutengeneza gesi ya sumu ambacho ni hatari sana kwa 

Marekani.Ziara ya kwanza ya Dr 

Vivian baada ya kuwa rais ilikuwa 

nchini Cuba.Alifanya mazungumzo 

na rais wa sasa wa Cuba na 

mojawapo ya mambo 

waliyoyazungumza ni kukifungua 

tena kiwanda hicho.Tunazo taarifa 

za uhakika kuhusiana na hilo 

lakini Dr Vivian hakuweza kutoa 

jibu la moja kwa moja kwamba 

amekubali kukifungua tena 

kiwanda hicho.Kwa sasa jambo hili 

linakuwa hatari zaidi endapo 

mashirikiano kati ya Tanzania na 

Korea Kaskazini yatafanikiwa 

kuanzishwa.Korea kaskazini 

inaweza ikatumia gesi hiyo kwa 

ajili ya kutengeneza silaha za maangamizi.Tuko katika hatari 

kubwa mheshimiwa rais na bado 

Dr Vivian ametushika 

pabaya



Tuko katika hatari 

kubwa mheshimiwa rais na bado 

Dr Vivian ametushika 

pabaya.Tunaendelea 

kumchunguza taratibu ili tuweze 

kufahamu mahala kilipo kiwanda 

hicho na tukiteketeze.Tunaweza 

kumtumia mtoto wake kwa ajili ya 

kumlazimisha afanye kile 

tunachokitaka lakini kama 

ujuavyo Dr Vivian ni mmoja wa 

binadamu wenye kujiamini kwa 

kiwango cha juu sana na ana kiburi 

kikubwa kwa hiyo anaweza 

akapata hasira na kuamua kufanya 

mambo ambayo hatukuwa 

tumeyakusudia.Anaweza akaamua 

kushirikiana na Cuba au Korea 

Kaskazini katika kutengeneza gesi ile ya sumu na 

kutushambulia.Jambo lingine ni 

kwamba tayari ameanzisha 

uchunguzi kuhusiana na nani 

waliomuua baba yake kanali 

Sebastian Matope.Kazi hiyo 

amempatia Mathew Mulumbi 

ambaye kama nilivyokueleza awali 

amewahi kufanya kazi katika idara 

ya ujasusi Tanzania na tayari 

amekwisha piga hatua kubwa 

katika uchunguzi wake na kuna 

mambo ambayo tayari amekwisha 

yagundua ambayo yatampelekea 

katika kugundua kwamba 

Marekani walihusika katika ajali 

ile na kumuua rais Anorld 

Mubara.Kwa kuwa alitumwa na 

rais kuifanya kazi hiyo lolote analoligundua katika uchunguzi 

wake anamueleza pia rais wake” 

“Unamaanisha tayari Dr 

Vivian ana taarifa za Marekani 

kuhusika katika ajali ile? Akauliza 

Mike 

“Hatuna uhakika bado lakini 

kwa kuwa Mathew alitumwa na Dr 

Vivian afanye uchunguzi basi ni 

lazima atakuwa anamueleza kila 

hatua anayoipiga.Huyo Mathew 

ndiye aliyemuokoa Helmet” 

“Mungu wangu !! akasema 

Mike straw 

“Mnasubiri nini 

kumshughulikia huyo mtu ambaye 

ni wazi anaonekana ni hatari 

kwetu? Kwa nini mmemuacha hai 

mpaka hivi sasa? Hamuoni kwamba akipata ushahidi wa 

Marekani kuhusika katika kifo cha 

rais Anorld itakuwa ni mbaya sana 

kwa upande wetu?Willy tafadhali 

usiruhusu jambo hili liendelee 

mmalize mtu huyo haraka sana” 

akasema Mike 

“Si rahisi namna hiyo 

mheshimiwa rais” akasema Will 

Gadner na Mike akamtazama kwa 

hasira. 

“Kwa nini si rahisi? CIA mna 

kila kitu.Unao watu mahiri 

wanaoweza kufanya kazi yoyote 

sehemu yoyote duniani na isitoshe 

tayari umekwisha tengeneza 

mtandao nchini Tanzania.Kwa nini 

mnashindwa kummaliza huyo mtu mmoja ambaye anaweza kuwa 

hatari kwetu? Akauliza Mike straw 

“Kama nilivyokueleza 

mheshimiwa rais kwamba huyu 

jamaa aliwahi kuwa jasusi na 

anafahamu mbinu zote za kujihami 

na isitoshe imegundulika ana 

shirikiana na watu waliomo ndani 

ya CIA na FBI na mipango yote 

itakayopangwa basi ataifahamu 

mara moja.Tunachoendelea 

kukifanya kwa sasa ni kuwabaini 

watu anaoshirikiana nao kutoka 

CIA ambao wanampa siri 

zetu.Tunataka tuubaini pia 

mtandao wake wote na kujua ni 

mambo gani ambayo tayari 

anayafahamu kuhusiana na 

Marekani.Baada ya hapo ndipo tutakapotafuta namna ya kuweza 

kumuondoa.Bado tunamuhitaji 

mtu huyu kwani kupitia yeye 

tunaamini tunaweza kufahamu 

mambo mengine ambayo 

tumekuwa tukiyatafuta hivyo wazo 

la kumuua kwa sasa si muafaka” 

Mike straw akamtazama Will 

Gadner kwa hasira na kusema 

“Willy ninakuamini sana 

ninaomba usitake nipoteze imani 

na wewe kwa kushindwa 

kutekeleza majukumu yako 

ipasavyo.Sioni sababu yoyote ya 

kumuacha hai huyu jamaa ambaye 

ni hatari sana kwa nchi yetu.Kama 

tayari amekwisha fahamu 

kuhusiana na mambo 

tuliyoyafanya wanaweza wakatuanika kwa dunia 

nikafahamu mambo yanayofanywa 

kwa siri na Marekani.” Akasema 

Mike na kunyamaza baada ya simu 

ya Will Gadner kuita na kuomba 

atoke nje kwenda kupokea kwani 

ilikuwa ni simu muhimu.Baada ya 

dakika tatu akarejea ndani 

“Mheshimiwa rais kuna 

taarifa ambazo si nzuri kutoka 

Tanzania” akasema Willy Gadner 

“Kuna taarifa gani Willy? 

Akauliza Mike 

“Nimetaarifiwa kwamba wale 

watu wetu ambao tulikuwa 

tumewaweka kwa ajili ya kumuua 

Helmet na baadae wakamatwe na 

kukiri kwamba wametumwa na 

Korea kaskazini wote wametiwa nguvuni jijini Dar es salaam” 

akasema Willy na Mike akavuta 

pumzi ndefu 

“Mambo gani haya yanatokea? 

Akasema kwa sauti ndogo 

“Gadner haya yote yanatokea 

kwa sababu ya uzembe wako.Licha 

ya kufahamu umuhimu wa suala 

lile lakini wewe na wenzako 

hamkujipanga vizuri.Sasa mambo 

yote yanaanza kutugeukia.Nataka 

ukakae na watu wako na kabla ya 

saa nne za usiku nakutaka uje tena 

hapa ukiwa na mpango ni namna 

gani mnashughulikia suala la 

Tanzania.Nataka suala hili 

limalizike mara moja.Sitaki 

Marekani iendeshwe na nchi 

ndogo masikini kama Tanzania.Sitaki wamarekani 

waishi kwa hofu.Kama ni kumuua 

rais wa Tanzania na hao wote 

wanaoshirikiana naye mimi niko 

tayari nileteeni mapendekezo na 

nitasaini.Tusiendelee kupoteza 

muda hapa nataka ukakae na watu 

wako mlijadili suala hili kwa 

upana wake na kama 

nilivyokuambia kabla ya saa nne 

za usiku uwe hapa tayari na ukiwa 

na mpango wa namna ya kulitatua 

suala la Tanzania.Huu ni mtihani 

wako wa mwisho ninakupa nafasi 

ya mwisho kurekebisha makosa 

yako kama ukishindwa na hili 

ntakuondoa na kumpa nafasi yako 

mtu nitakayeona anafaa kwa kazi 

hiyo.Unaweza kwenda” akasema Mike straw na Will Gadner 

akainuka akachukua mkoba wake 

akafungua mlango akatoka.Mike 

straw akachukua chupa ya mvinyo 

akamimina katika glasi 

akagugumia wote na kuvuruga 

nywele. 

“Nilimuamini sana Willy 

Gadner lakini mpaka hapa 

anaonekana ameshindwa kufanya 

kazi yake vyema.Ameniingiza 

katika matatizo makubwa na sijui 

nitatokaje.Ngoja nisubiri muda 

huo niliompa nione kama atakuja 

na mpango mzuri vinginevyo 

nitamuondoa na kumpa nafasi 

yake mtu mwingine na kisha 

nitafanya vile nitakavyoona 

inafaa” akawaza Mike straw baada ya Will gadner kutoka ofisini 

kwake. 

“Dr Vivian !! akasema kwa 

sauti ndogo huku amekuja sura 

yake 

“Binti mdogo kama Dr Vivian 

hawezi kukisumbua kichwa 

changu namna hii.Kama 

akiendelea kuwa kiburi 

nitamuondoa kwani uwezo huo 

ninao ! akawaza Mike akiwa 

amekunja sura kwa hasira 

“Lakini kuna mambo 

ameyazungumza Will Gadner 

yanaonekana kuwa na 

msingi.Inahitajika akili kubwa 

kukabiliana na Dr Vivian na si 

nguvu.Kwa hapa tulipofika ni wazi 

kwamba ametuweka kwenye kona na ili kujiondoa inahitaji busara na 

akili nyingi.Natakiwa kutuliza 

kichwa changu na kama 

nikiliendea jambo hili kwa haraka 

ninaweza kuharibu kila 

kitu.Nitafanya nini basi? Akawaza 

Mike straw na kuminina tena 

mvinyo katika glasi akanywa 

wote.Mlango ukafunguliwa 

akaingia mmoja wa mawaziri 

akitaka kumuona lakini Mike 

akamuomba waonane baadae 

kwani kwa wakati huo alikuwa 

katika kushughulikia jambo 

zito.Alizunguka zunguka mle 

ofisini akiwaza na baada ya muda 

akapata wazo 

“Suala hili haliwezi kumalizwa 

kwa simu wala kwa vitisho.Natakiwa kuonana ana kwa 

ana na Dr Vivian na kuzungumza 

naye na hii ina maana kwamba 

natakiwa kwenda Tanzania haraka 

iwezekanavyo.” Akaketi kitini 

“Hili ni wazo zuri.Natakiwa 

kwenda Tanzania mara moja.Sina 

namna kwa vyovyote vile lazima 

niende Tanzania.Lazima nionane 

na Dr Vivian ana kwa ana 

nizungumze naye na tuyamalize 

haya mambo” akawaza Mike na 

kuchukua simu na kuitisha kikao 

cha dharura ili kujadili suala lile la 

yeye kwenda Tanzania

DAR ES SALAAM – TANZANIA 

Kikao cha dharura kati ya rais 

na wakuu wa vyombo vya ulinzi na 

usalama kilichokuwa maalum kwa 

ajili ya kujadili tukio lililokuwa 

limetokea uwanja wa ndege wa 

Julius Nyerere usiku huo 

kilimalizika na wajumbe wakatoka 

kwa ajili ya kwenda kutimiza 

majukumu waliyopewa na 

rais.Wakati akielekea katika ofisi 

yake,Dr Vivian alisimama kwa ajili 

ya mazungumzo na mkuu wa 

majeshi na wakati wakiendelea 

kuzungumza akatokea mkuu wa 

jeshi la polisi nchini Inspekta 

jenerali John Aminiel Mkoka “Madam president ninaweza 

kuzungumza nawe kwa dakika 

kadhaa? Kuna suala la muhimu 

sana nataka nikujulishe” akasema 

John Mkoka na rais akamuomba 

radhi mkuu wa majeshi ili aweze 

kuzungumza na mkuu wa jeshi la 

polisi nchini 

“John kuna tatizo gani? 

Akauliza rais 

“Nimepokea simu kutoka kwa 

mmoja wa askari wangu akisema 

kwamba mtuhumiwa wa mauaji ya 

waziri wa mambo ya nje hayuko 

tena katika mikono ya polisi” 

Taarifa ile ikamstua sana Dr 

Vivian “Mathew hayupo katika 

mikono ya polisi? Ametoweka vipi? 

Akauliza rais kwa mshangao 

“Baada ya kupokea taarifa 

hiyo nimempigia simu kamanda 

wa polisi kanda ya Dar es salaam 

na kumtaka anipe taarifa kwa nini 

mtuhumiwa huyo hayuko tena 

katia mikono ya polisi na baada ya 

kufuatilia amenijbu kwamba 

Mathew amechukuliwa na mkuu 

wa idara ya usalama wa taifa 

Meshack Jumbo kwa ajili ya 

kumfanyia mahojiano na ameahidi 

kwamba akishakamilisha 

mahojiano naye atamrejesha 

katika mikono ya 

polisi.Mjheshimwia rais huyu 

mtuhumiwa amefanya mauaji makubwa ya kiongozi na anapaswa 

kuwa katika mikono ya polisi kwa 

nini Meshack Jumbo amchukue 

bila kupata ruhusa au kufuata 

taratibu? Kama kuna jambo 

alihitaji kulifahamu kutoka kwa 

Mathew angefuata taratibu 

lakini…..” Mkuu wa jeshi la polisi 

nchini Inspekta jenerali John 

Aminiel Mkoka akanyamaza baada 

ya Meshack Jumbo kutokea.Wote 

wakageuka kumtazama.Dr Vivian 

akamtazama kwa jicho kali sana na 

Meshack hakuonyesha kujali 

akamfuata. 

“Meshack ! akaita rais kwa 

ukali 

“Madam president “ Meshack 

Jumbo akaitika “Twende ofisini kwangu !! 

akasema Dr Vivian na kuongozana 

na Meshack Jumbo kuelekea ofisini 

kwake. 

Walipoingia ofisini wote 

wawili wakasimama 

wakitazamana 

“What have you done 

Meshack?!! Akauliza Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais kuna 

mambo mawili nataka 

nikujulishe.Kwanza ni kuwa wale 

watu watatu ambao ulinipa picha 

zao kwamba ndio walotumwa kuja 

kumuua waziri Helmet Brian 

tayari wamekamatwa na 

wanashikiliwa mahala salama hivi 

sasa kwa ajili ya kuanza mahojiano 

nao.Hii inaonyesha ushupavu wa vijana wetu wa usalama wa taifa 

namna wanavyoweza kufanya kazi 

kwa haraka na kwa ufanisi 

mkubwa.Napenda kukuhakikishia 

mheshimiwa rais kwamba idara hii 

tayari imerudi katika ubora wake” 

akajigamba Meshack Jumbo. 

“Jambo la pili ni kwamba 

tayari tumekwisha andaa makazi 

ya muda ya Helmet 

Brian.Nimekuja kumchukua na 

kumpeleka kwenda kupumzika” 

akasema Meshack 

“Ahsante kwa kazi nzuri 

Meshack lakini hukunijbu swali 

langu nililokuuliza kwamba 

umefanya nini usiku huu?Ulidhani 

sintafahamu? “Kuna nini mheshimiwa rais? 

Akauliza Meshack Jumbo 

“Umempeleka wapi Mathew? 

Akauliza rais 

“Mathew? 

“Ndiyo Mathew.Umemchukua 

kutoka mikononi mwa polisi na 

kumpeleka kusikojulikana.Toka 

awali nilikwisha kuona 

hukukubaliana na mpango wangu 

kuhusu Mathew.Kwa hili 

ulilolifanya umevuka mstari na 

umenidharau.Oh Meshack don’t 

force me to destroy you old 

man,just bring back Mathew and 

I’ll let you go” akasema Dr Vivian 

huku akiuma meno kwa hasira 

“Napenda kufanya kazi na 

watu wanaonitii na kufuata maagizo yangu .Sipendi 

wasaliti.Kwa hiki ulichokifanya 

umekuwa ni msaliti 

kwangu.Nimekushirikisha mambo 

yangu binafsi nikiamini kwamba 

wewe utakuwa upande wangu 

lakini umenisaliti na kuamua 

kumsaidia Mathew wakati 

ukifahamu fika kwamba yule ni 

mtu hatari sana 

kwangu.Sikutegemea kama 

ungekuwa namna hii Meshack 

Jumbo.Ninakuheshimu sana mzee 

wangu hivyo ninachokuomba ni 

kitu kimoja tu kwamba mrudishe 

Mathew katika mikono ya polisi 

halafu nitakuacha uende zako na 

nitatafuta mkuu mwingine wa 

idara ya suala wa taifa.Siwezi kabisa kuendelea kufanya kazi 

nawe.Tayari umekwishaonyesha 

picha mbaya kwamba si 

muaminifu na hutaki kufuata 

maagizo na maelekezo yangu” 

Akasema Dr Vivian.Meshack Jumbo 

akavuta pumzi ndefu na kusema 

“ Madam president,ni kweli 

nimemchukua Mathew toka 

mikononi mwa polisi.I’m so sorry 

for that but I had no choice.Mimi 

na wewe sote tunafahamu kwamba 

Mathew hana kosa lolote na 

anakwenda kupotea bure.Kesi ile 

innaweza kumuweka gerezani kwa 

muda wote wa maisha yake 

uliobaki.Kama nilivyokueleza 

awali kwamba Mathew ni kijana 

wangu na ninamchukulia kama mwanangu kwa hiyo siwezi 

kukubali kuona akiangamia bila 

sababu.Siwezi kuishi kwa amani 

katika maisha yangu yaliyobaki 

kama Mathew atafungwa gerezani 

kwa kosa ambalo hakulitenda.You 

can live with that but I cant! 

Akasema Meshack Jumbo 

“Oh my God !! akasema Dr 

Vivian kwa sauti ndogo 

“Meshack huu si utani hata 

kidogo.Nakuamuru umrejeshe 

Mathew haraka sana katika 

mikono ya polisi kwani bila 

kufanya hivyo utafanya mambo 

yazidi kuwa magumu.Nakuonya 

kwa mara ya mwisho Meshack 

mrejeshe Mathew katika mikono 

ya jeshi la polisi ili mimi na wewe twende sawa vinginevyo 

hautaamini kile 

nitakachokufanyia” akasema Dr 

Vivian 

“Madam president huu si 

utani.Mathew hatarejea tena 

katika mikono ya jeshi la 

polisi.Siwezi kukubali kijana 

wangu akaangamia hivi hivi wakati 

amefanya kila juhudi kuifanya kazi 

yako uliyompatia.Kwa nini hauna 

huruma Dr Vivian? Mathew 

alikubali kuacha shughuli zake 

zote na kwa heshima yangu 

akakubali kuifanya kazi yako tena 

bila hata malipo lakini leo hii 

amegeuka adui kwako na unataka 

kumuangamiza ? Siwezi kukubali 

hilo litokee.Niko tayari kuimwaga hata damu yangu kwa ajili ya 

kuhakikisha kwamba Mathew 

anakuwa salama.Fanya uwezacho 

madam president.Kama unaweza 

kuniua usisite kufanya hivyo au 

kama ni kunifunga gerezani ni 

sawa kwangu lakini nitakuwa na 

amani ya moyo kwamba Mathew 

yuko salama” akasema Meshack na 

Dr Vivian akaendelea kumtazama 

kwa hasira 

“Meshack why are you doing 

this? Akauliza 

“Because it’s the right thing to 

do” akasema Meshack 

“Madam president nafahamu 

wasiwasi wako kwamba Mathew 

anaweza akafahamu mambo 

ambayo hutaki ayafahamu lakini yule ni kijana mwelewa 

sana.Ukimuelewesha jambo 

anakuelewa na ninakuhakikishia 

madam president kwamba 

Mathew ni mtu ambaye 

unamuhitaji sana katika kazi 

zako.Ni mtu ambaye hutakiwi 

kumpoteza kabisa kwani kuna 

mengi utahitaji akufanyie.Mpaka 

sasa bado hajafahamu kama ni 

wewe uliyemfanyia haya na 

endapo akijua kwamba wewe 

unahusika katika hili lililotokea 

narudia kukuhakikishia madam 

president kwamba utakuwa katika 

hatari kubwa sana.Hata kama 

akiwa gerezani Mathew anao 

uwezo wa kuweza kukuangusha 

kwani ana mtandao mrefu.Mathew amefanikiwa kuufahamu mpango 

wa siri wa kumuua Helmet Brian 

jambao ambalo hata idara yetu ya 

ujasusi haikuweza kulifahamu na 

yeye kwa kusaidiana na wenzake 

wachache wamefanikiwa 

kumuokoa waziri huyo.Unadhani 

nini kingetokea endapo mpango 

huo wa Marekani ungefanikiwa? Ni 

wazi kwamba mpango wa 

mashirikiano na Korea Kaskazini 

ungeota mbawa kwani Korea 

ingeingia katika vita na Marekani 

lakini ni Mathew aliyefanikisha 

hilo kutokea.Madam president 

unamuhitaji sana Mathew hasa 

kwa wakati huu na si 

kumuangamiza.Kama unaona kuna 

jambo lolote la siri ambalo anahitaji kulifahamu kuhusu wewe 

basi unaweza ukamueleza 

mapema ili alifahamu na 

ninakuhakikshia kwamba Mathew 

ni muelewa na atakusikiliza” 

akasema Meshack 

Dr Vivian akainamisha kichwa 

akatafakari kwa muda na kabla 

hajasema lolote simu ya mezani 

ikaita akataarifiwa kwamba rais 

wa Korea Kaskazini Kim Hun Yu 

alikuwa katika laini ya simu ya 

moja kwa moja kwa ajili ya 

kuzungumza naye 

“Rais wa Korea kaskazini yuko 

katika laini ya simu hivi sasa 

anahitaji kuzungumza 

nami.Mpeleke kwanza Helmet 

Brian akapumzike na halafu urejee hapa bado nina mazungumzo 

nawe.Hakikisha usalama upo wa 

kutosha kwani CIA wameeneza 

mtandao wao hapa nchini” 

“Usihofu kuhusu usalama 

madam president” akasema 

Meshack na rais akatoka mle 

ofisini akaelekea katika chumba 

cha mazungumzo ya moja kwa 

moja. 

Meshack Jumbo akaeleka 

katika sebule ya rais alikokuwa 

waziri Helmet Brian 

“Mheshimiwa waziri vipi 

maendelo yako?Kuna tatizo lolote 

la kiafya unahisi? Yawezekana 

labda kuna mahala uliumia katika 

purukushani ile” “Ninajisikia vizuri sana 

sijaumia na sihisi maumivu 

sehemu yoyote”akajibu Helmet 

“Vizuri sana.Tayari 

maandalizi yamekamilika na 

nimekuja kukuchukua kukupeleka 

mahala pa siri utakapoishi kwa 

muda utakaokuwa hapa Tanzania 

ambapo ni mahala salama zaidi” 

akasema Meshack Jumbo 

“Asante sana.Nani 

wanaonipeleka huko mahala 

ninakotakiwa kwenda? Akauliza 

Helmet 

“Mimi na vijana wangu wa 

usalama wa taifa” 

“Mathew hayupo? “Hapana Mathew hayupo 

mheshimiwa waziri”akajibu 

Meshack 

“Utanisamehe lakini 

namuhitaji Mathew yule kijana 

aliyeniokoa kule uwanja wa ndege 

na akanikabdhi kwa rais awemo 

katika timu ya watu wako 

watakaonipeleka huko mahala 

mnakotaka kunipeleka” akasema 

Helmet Brian 

“Mheshimiwa waziri kwa sasa 

Mathew hawezi kupatikana kwani 

yuko katika shughuli 

nyingine.Ninaomba uniamini 

nimekuja na vijana wenye uwezo 

mkubwa wa kukulinda na ndio 

watakaokuwa wakikulinda huko 

mahala utakakokuwa kwa hiyo nakusihi usiwe na hofu yoyote” 

akasema Meshack 

“Si kwamba siamini uwezo wa 

vijana wako lakini ninamuamini 

sana Mathew na ndiyo maana 

ninataka awepo wakati 

ninapelekwa mahala mnakotaka 

kunipeleka” 

“Naomba uniamini Helmet 

kwamba utakuwa salama bila hata 

Mathew kwa hiyo usihofu 

chochote.”Meshack akasisitiza 

“Na mimi naomba niwe wazi 

kwamba sitoi mguu wangu hapa 

bila kumuona Mathew.Rais yuko 

wapi nahitaji kuzungumza naye” 

“Kwa sasa rais ana 

mazungumzo muhimu kwenye simu,hivyo itakulazimu kusubiri 

hadi atakapomaliza” 

“Hakuna shaka nitaendelea 

kusubiri” akasema Helmet na 

Meshack Jumbo akatoka na 

kuchukua simu yake na kumpigia 

Mathew. 




Hakuna shaka nitaendelea 

kusubiri” akasema Helmet na 

Meshack Jumbo akatoka na 

kuchukua simu yake na kumpigia 

Mathew. 

“Hallow mzee Meshack” 

“Mathew niko hapa ikulu na 

ninahitaji msaada wako.Kabla ya 

yote napenda kukujulisha kwamba 

rais alinipa karatasi yenye picha za 

watu watatu ambao waliletwa 

nchini kwa ajili ya kumuua Helmet 

Brian akanitaka tuwatafute hao 

jamaa na tayari wote watatu 

wamekamatwa na wako sehemu 

salama tunataka kuwafanyia 

mahojiano” “Hizo ni habari 

njema.Hongera sana mzee kwa 

uharaka huo mkubwa wa 

kuwakamata watu hao.Ila nina 

ombi moja kwako.” 

“Omba Mathew” 

“Endapo itawezekana naomba 

nipewe nafasi ya kuwafanyia 

mahojiano hao jamaa” 

Meshack Jumbo akanyamaza 

kimya alishindwa ajibu nini 

“Mzee Meshack” akaita 

Mathew 

“Mathew nimekaa kimya 

nikitafakari nikupe jibu gani lakini 

nitajitahidi kufanya kila niwezalo 

ili uweze kuipata nafasi hiyo ya 

kuwafanyia mahojiano hao 

jamaa.Tukiachana na hilo rais alinitaka niandae makazi ya siri 

kwa ajili ya Helmet Brian kwa 

muda wote atakaokuwa hapa 

Tanzania.Tayari makazi yake 

yameandaliwa na nimekuja hapa 

ikulu kumchukua kumpeleka huko 

lakini amegoma hatakwenda 

kokote kule hadi akuone.Anataka 

na wewe uwepo katika timu 

itakayomtoa hapa ikulu 

kumpeleka mahala alikoandaliwa 

kukaa.Nakuomba sana Mathew 

unisaidie kwa hilo ili Helmet 

aweze kukuona na akubali 

kuondoka hapa ikulu.Anakuamini 

wewe pekee” akasema Meshack 

Jumbo 

“Mzee Meshak kwa sasa 

nimeondoka pale nyumbani kwa Austin ninakwenda kuonana na 

Peniela.Amewasili usiku huu na 

amenitaka nikaonane naye.Kuna 

masuala ya muhimu sana 

nilimuomba anisaide kufanya 

uchunguzi na ninakwena kupata 

majibu.Labda nikitoka huko ndipo 

niweze kuja ikulu kumchukua 

Helmet” 

“Ouh sawa 

Mathew.Utakapomaliza huko kwa 

Peniela utanijulisha na mimi 

nitazungumza na rais kuhusu suala 

hili ili ukija uweze kuruhusiwa 

kuingia moja bila wasiwasi” 

“Ahsante mzee nitawasiliana 

nawe baadae.Vipi kuhusu polisi? 

Hakuna tatizo lolote hadi hivi sasa? 

Akauliza Mathew “Hakuna tatizo niachie lile 

suala nitalimaliza” akasema 

Meshack Jumbo na kuondoka 

kuelekea katika sebule ya rais 

aliko Helmet Brian 

akamfahamisha kwamba tayari 

amewasiliana na Mathew na 

atafika pale 

******************* 

Akina Mathew waliwasili 

nyumbani kwa bilionea Peniela.Ni 

jumba kubwa lililokuwa na ulinzi 

wa kutosha.Walinzi 

wakawaruhusu wapite na baada ya 

kushuka garini wakapokewa na 

mtumishi wa ndani 

akawakaribisha sebuleni.Baada ya dakika mbili akatokea 

Peniela.Akawasalimia wote kwa 

kuwakumbatia na kuketi sofani 

“Karibuni sana na samahani 

kwa kuwasumbueni usiku huu” 

akasema Peniela 

“Usijali Peniela.Naomba 

kwanza nikutambulishe kwa hawa 

wenzangu nilioambatana nao.Huyu 

hapa anaitwa Austin January ni 

rafiki yangu wa muda mrefu 

tumewahi kufanya kazi pamoja na 

sasa anajishughulisha na biashara 

zake.Yule pale ni Camilla Snow 

ambaye nilikuomba ndege 

ikamchukue Havana.Yeye 

anafanya kazi FBI lakini kwa sasa 

yuko hapa nchini nikisaidiana 

naye katika uchunguzi ninaoufanya” akasema Mathew na 

kuwageukia akina Austin 

“Jamani huyu ndiye 

Peniela.Mimi naye tuliwahi kuwa 

wapenzi lakini kwa sasa kila 

mmoja anaendelea na maisha yake 

ila tuko vizuri hatuna tatizo 

lolote.Tuna mtoto mmoja anaitwa 

Anna Maria” akasema Mathew na 

Peniela akatabasamu . 

“Karibuni sana .Nimefurahi 

kuwafahamuni” akasema Peniela 

“Yuko wapi Anna Maria? 

Akauliza Mathew 

“Yuko chumbani kwake 

amelala.Amechoka sana safari 

ilikuwa ndefu.Utaonana naye 

kesho” “Hapana siwezi kusubiri hadi 

kesho.Nipeleke mara moja 

nikaonane naye sasa hivi” akasema 

Mathew na Peniela akainuka 

akampeleka Mathew katika 

chumba cha Anna Maria aliyekuwa 

amelala usingizi mzito.Mathew 

akainama akambusu usoni 

“I love you my 

princess.Welcome to your beloved 

country.This is where you belong” 

akasema Mathew taratibu na 

kumfunika vizuri mwanae 

wakatoka mle chumbani na 

Peniela akamshikamkkono 

wakaingia katika sebule nyingine. 

“Poleni sana kwa safari 

ndefu.Imekuaje ukaamua kuja ghafla namna hii? Mathew 

akaanzisha mazungumzo 

“Sikuwa nimepanga kuja 

Tanzania lakini ilinilazimu kuja 

kwa dharura.Nilistuka tulipozuiwa 

kutua katika uwanja wa ndege wa 

Julius Nyerere.Tuliambiwa uwanja 

umefungwa kwa muda hivyo 

tukatue Zanzibar.Nini hasa 

kimetokea hapa Tanzania usiku 

huu?Peniela akauliza 

“Waziri wa mambo ya nje wa 

Marekani Helmet Brian alitaka 

kuuawa pale uwanja wa ndege 

usiku wa leo na ndiyo sababu 

uwanja umefungwa kwa muda ili 

kupisha uchunguzi na kuhakikisha 

ni salama kwa ndege kutua” “Nani waliotaka kumuua 

waziri huyo? Akauliza Peniela 

“Ni hadithi ndefu kidogo lakini 

ni Marekani wenyewe ndio 

waliotaka kumuua waziri wao ili 

wasingizie Korea Kaskazini na 

wapate sababu ya 

kuishambulia.Vipi kuhusu wewe 

unaendeleaje? Sikupata mrejesho 

wowote toka kwako kuhusu ile 

kazi niliyokuomba unisaidie” 

akasema Mathew 

“Mathew nashindwa nianzie 

wapi lakini kwanza napenda 

nikushukuru sana kwa 

kunifumbua macho.Nilikupinga 

mwanzoni lakini baada ya kufanya 

uchunguzi nilifahamu mambo 

ambayo sikuwa nimeyajua kuhusu Anderson na baba yake Andrew 

Pillar” Akasema Peniela na 

kumvutia zaidi Mathew 

“Uligundua nini?akauliza 

Mathew 

“Mathew kabla sijakueleza 

chochote vipi kuhusu wale rafiki 

zako hawataboreka kule sebuleni 

peke yao? Maelezo yangu ni 

marefu kidogo” akasema Peniela 

“Usijali endelea”akasema 

Mathew. 

“Ulinitaka nifanye uchunguzi 

katika akaunti ya George Mzabwa 

na vile vile kuwachunguza 

Anderson na baba yake Andrew 

Pillar.Ninaye mtu wangu 

anayeshughulikia maslahi yangu 

ndani ya Escom Bank kwa hiyo nilimtumia huyo kuweza kufanya 

uchunguzi.Majibu aliyonipa ni 

kwamba George Mzabwa amekuwa 

akipokea fedha kutoka kampuni ya 

kutengeneza saa ya Flamingo na 

kiasi cha mwisho kulipwa kilikuwa 

shilingi milioni mia saba na 

sabini.George Mzabwa aliziondoa 

fedha hizo kutoka katika akaunti 

yake na kuziweka katika akaunti 

tatu tofauti za kampuni ya 

kuchonga madini ya vito ya 

Tanbest Gemstone ltd ambayo 

wamekuwa wakifanya biashara na 

kampuni ya Flamingo.Katika 

akaunti zile tatu za kampuni ya 

Tanbest ambazo George aliweka 

fedha,zilitolewa kama 

ifuatavyo.Akaunti ya kwanza fedha zilitolewa na mtu anaitwa 

Ranbir Kumar.Zilikuwa shilingi 

milioni sabini.Akaunti ya pili fedha 

zilitolewa na kuingizwa katika 

akaunti ya Robert Mwainamela na 

baadae zikatolewa zote.Zilikuwa 

shilingi milioni mia sita na 

hamsini.Akaunti ya tatu fedha 

kiasi cha shilingi milioni hamsini 

zilitolewa na Ranbir Kumar.Huo 

ndio mtiririko wa fedha ulivyo 

katika akaunti ile uliyoniomba 

niichunguze” akasema Peniela na 

kunyamaza kidogo halafu akasema 

“Ulinitaka pia niwachunguze 

Anderson na baba yake 

Andrew.Nilifanya kama 

ulivyoniagiza.Kwanza nilianza 

kumchunguza Andrew Pillar.Nilimfuata nyumbani 

kwake.Kwa muda mrefu Andrew 

alikuwa ananitaka kimapenzi na 

nikaamua kuitumia fursa hiyo 

kuweza kupata taarifa 

unazozihitaji” akasema Peniela 

“I’m sorry.” Akasema Mathew 

“Sorry for what? Akauliza 

Peniela 

“Nimekufanya ukarejea tena 

katika yale maisha yako ya awali 

ya kutumia mwili wako kupata 

taarifa” 

“Usijali kuhusu hilo.Yale ndiyo 

maisha yangu na nimekwisha 

yakubali.Nitakapolazimika 

kufanya hivyo ili kupata taarifa za 

muhimu sintasita ” akasema Peniela na kunyamaza kidogo 

halafu akaendelea 

“Nilimuwekea dawa ya 

usingizi katika kinywaji na akalala 

kama mfu nikapata nafasi ya 

kufanya uchunguzi wangu.Kwanza 

nilichunguza kompyuta 

yake.Niligundua Andrew amekuwa 

akitoa maelekezo katika kampuni 

za Flamingo na ile ya A.D 

Electronics.Amekuwa akiwatuma 

kazi wakurugenzi wakuu wa 

kampuni hizi mbili jambo 

lililonifanya nijiulize maswali 

kuhusu nguvu yake katika 

kampuni hizi mbili.Nimechukua 

barua pepe zake nimezihifadhi 

katika hiki kihifadhi data na 

utazipitia pengine zinaweza kuwa na msaada wowote kwako.Kutoka 

kwenye kompyuta nikafungua 

droo ndogo iliyoko pembeni mwa 

kitanda na kukuta kuna hati mbili 

za kusafiria.Moja ina jina la Edwin 

Washington na nyingine ina jina la 

Andrew Pillar na zote mbili zikiwa 

na picha ya Andrew.Nikaendelea 

kujiuliza maswali kuhusu jina 

halisi la Andrew na kwa nini awe 

na pasi mbili za kusafiria zikiwa na 

majina tofauti?Nikarejea tena 

katika kompyuta na kukuta kuna 

barua pepe zimeingia na 

mojawapo ilitoka kwa mtu anaitwa 

Willy gadner ambayo ilimtaarifu 

kuwasiliana na ofisi kuu kuna 

tatizo limetokea Tanzania.Hizo 

barua pepe zote nimekuwekea katika kihifadhi data hicho 

nilichokupatia.Nilichunguza pia 

kuhusu uhusika wa Andrew Pillar 

katika kampuni za Flamingo na A.D 

Eletronics nikagundua kwamba 

kampuni hizi zote mbili 

zinamilikiwa na mtu mmoja 

anaitwa Edwin Washington 

ambaye ndiye huyo huyo Andrew 

Pillar.Nilikwenda pia nyubani kwa 

Anderson lakini wakati nikifanya 

uchunguzi kumbe Anderson 

ameweka mtambo maalum wa 

kufuatilia kila kinachoendelea 

chumbani kwake wakati hayupo 

na hivyo akagundua kwamba 

nilikuwa napekua chumba chake 

na kufunga kila kitu kwa kutumia 

simu yake.Baadae akaja mle chumbani lakini nilifanikiwa 

kumpiga na kitu kichwani 

akapoteza fahamu na ndipo 

nilipoamua kuondoka Paris 

haraka na kuja Tanzania.Hayo 

ndiyo niliyofanikiwa kuyafahamu 

na ninakushukuru sana Mathew 

kwa kunisaidia kuwafahamu wale 

watu kuwa ni waongo na kuna 

mambo mengi 

wanayaficha.Ninachotaka 

kufahamu,ni kitu gani hasa 

kinachoendelea kuwahusu 

wao?akauliza Peniela 

“Peniela kwanza kabisa 

nashukuru sana kwa kazi hii 

kubwa na ya hatari uliyoifanya 

ambayo itatusaidia sana katika 

uchunguzi wetu.Kwa ufupi tu kwa kuwa hatuna muda wa kutosha 

nitakueleza kwa kifupi.Kuna 

mtandao wa CIA hapa Tanzania 

ambao umetengenezwa kwa 

malengo maalum.Mtandao huu 

ndio uliohusika na kifo cha rais 

Anorld Mubara ambaye alifariki 

katika ajali ya ndege.Rais Dr Vivian 

aliniomba nimsaidie kufanya 

uchunguzi kuhusiana na nani 

waliomuua baba yake kanali 

Sebastian matope.Baada ya kuanza 

kuchunguza ndipo nilipogundua 

kwamba Marekani wanahusika 

katika kifo kile na nikabaini kuna 

mtandao wa CIA hapa nchini na 

unawahusisha hadi viongozi 

walioko serikalini na mmoja wa 

watu hao alikuwa ni mkurugenzi wa idara ya usalama wa taifa 

ambaye alijiua kwa kujipiga risasi 

vile vile waziri wa mambo ya nje 

Dr Robert Mwainamela ambaye 

ameuawa usiku huu na mauaji 

yake yamefanyikanyikia nyumbani 

kwangu na mimi kubebeshwa 

mzigo huo wa mauaji ya huyo 

waziri”akasema Mathew 

“Unatuhumiwa kwa mauaji?!! 

Peniela akauliza kwa mshangao 

“Ndiyo nina tuhuma za 

kumuua waziri wa mambo ya nje” 

“Hivi sasa unatafutwa? 

Akauliza tena Peniela 

“Nilikuwa katika mikono ya 

polisi lakini nimeondolewa kwa 

muda .Tuachane na hayo ambayo 

kwangu ni mambo ya kawaida.Baada ya kumchunguza 

George Mzabwa ndipo tukagundua 

kwamba ana akaunti katika benki 

ya Escom ambayo na wewe ni 

mmoja wa wamiliki ndipo 

nilipokuomba msaada wako 

unisaidie kuchunguza lengo likiwa 

ni kuufahamu mtandao wote wa 

CIA hapa nchini.Umefanya kazi 

nzuri sana na sasa twende 

tukaungane na akina Austin na 

kwa pamoja tujadiliane nini 

tufanye” akasema Mathew 

“Mathew kabla hatujaenda 

huko kuonana na wenzako 

nakuomba samahani sana kwa 

mambo yale mabaya 

niliyokutendea.I did many awfull 

things to you and I’m so sorry for that” akasema Peniela lakini 

Mathew akamzuia asiendelee 

“Penny tutazungumza mambo 

hayo kwa wakati wake na isitoshe 

hayo yote ni mambo yaliyokwisha 

pita.Kwa sasa tujielekeze katika 

mambo makubwa yanayotukabili” 

akasema Mathew 

“That woman Camilla is she 

your lover? Akauliza Peniela 

“Peniela naomba tuachane na 

hayo mambo kwa 

sasa.Tutazungumza baadae” 

akasema Mathew kisha wakatoka 

na kuelekea sebuleni 

walikokuwapo Austin na Camilla 

“Samahani kwa kuwaacha 

wenyewe kuna mambo ambayo Peniela alikuwa ananieleza” 

akasema Mathew 

“Kwanza ni kuhusiana na 

uchunguzi wa ile akaunti ya 

George Mzabwa.Peniela ni mmoja 

wa wamiliki wa Escom bank kwa 

hiyo imekuwa rahisi kwake 

kuweza kupata taarifa za 

kuhusiana na akaunti ile ya 

George.Taarifa alizozipata ni 

kwamba George aliingiziwa fedha 

nyingi kiasi cha shilini milioni mia 

saba na sabini kutoka katika 

kampuni ya kutengeneza saa ya 

Flamingo ya nchini 

Marekani.Baadae fedha hivi 

alizitoa na kuzitawanya katika 

akaunti tatu ambazo zote ni za 

kampuni ya Tanbest Gemstone.Katika akaunti ya 

kwanza pesa zilitolewa na Ranbir 

Kumar kiasi cha shilingi milioni 

sabini.Katika akaunti ya pili pesa 

zikatolewa na Robert 

Mwainamela.Hizi zilikuwa nyingi 

kiasi cha shilingi milioni mia sita 

na hamsini.Akaunti ya tatu fedha 

zikatolewa na Ranbir Kumar kiasi 

cha shilingi milioni hamsini.Huo 

ndio mgawanyo wa fedha ambayo 

George alipokea kutoka kampuni 

ya Flamingo.Baada ya kupata 

taarifa hizo kuna maswali ambayo 

lazima tujiulize na kuyatafutia 

majibu.Kwanza tuliambiwa 

kwamba kampuni ya Tanbest na 

Flamingo zinafanya biashara lakini 

fedha kutoka Flamingo zinapitia katika akaunti binafsi ya George 

Mzabwa badala ya akaunti ya 

kampuni.Akipokea fedha hizo 

George huzigawanya katika 

akaunti za kampuni hiyo.je Gerge 

ndiye mmiliki wa kampuni ya 

Tanbest hadi fedha zote zipitie 

kwake?Tunaona pia fedha 

zilizowekwa katika akaunti tatu za 

kampuni ya Tanbest 

zinavyochukuliwa.Ranbir Kumar 

anachukua kiasi cha shilingi 

milioni mia moja na ishirini na 

zilizobaki kiasi cha shilingi milioni 

mia sita hamsini zilichukuliwa na 

Dr Robert.Swali la kujiuliza je Dr 

Robert ana uhusiano gani na 

kampuni hii hadi awe na uwezo wa 

kuingia katika akaunti ya kampuni na kuchukua fedha nyingi kiasi 

hiki?Je naye ni mmoja wa wamiliki 

wa kampuni hii?Amezipeleka wapi 

fedha nyingi kiasi hicho? Akauliza 

Mathew na kunyamaza kidogo 

halafu akaendelea. 

“Tukiachana na hilo 

nilimuomba pia Peniela anisaidie 

kuwafanyia uchunguzi wa kina 

Anderson pillar na baba yake 

Andrew Pillar ili tujue kwa nini 

benki wanayomiliki inatumiwa na 

Flamingo kupitishia fedha kuja 

Tanzania.Peniela amefanya 

uchunguzi na amegundua kwamba 

Andrew Pillar ana hati mbili za 

kusafiria.Moja ina jina la Andrew 

Pillar na nyingine ina jina la Edwin 

Washington.Alikwenda mbali zaidi na akagundua kwamba Edwin 

washington ndiye mmiliki wa 

kampuni za Flamingo na A.D 

Elecronics.Sasa tumepata picha 

kwamba kampuni hizi zote mbili 

ziko chini ya serikali ya Marekani 

kupitia shirika lake la ujasusi la 

CIA na moja kwa moja Andrew au 

Edwin vyovyote anavyojiita ni 

jasusi wa CIA.Ili kulithibtisha hilo 

Peniela amekuja na na barua pepe 

ambazo alizitoa katika kompyuta 

ya Andrew” akasema Mathew na 

kuchukua kompyuta ya Peniela 

akachomeka kile kifaa cha 

kuhifadhi kumbu kumbu na barua 

pepe zile ambazo Peniela 

alizichukua kutoka katika 

kompyuta ya Andrew Pillar zikajitokeza na kompyuta akapewa 

Camilla akaanza kuzipitia. 

“Willy gadner? Akauliza baada 

ya kusoma barua pepe ya mwisho 

“Huyu ni mkurugenzi wa 

CIA.Hapa hakuna shaka kwamba 

Andrew ni jasusi wa CIA” akasema 

Camilla baada ya kuzipitia zile 

barua pepe 

“Oh my God ! kwa nini 

sikuliona hili toka mapema? Watu 

hawa walikuwa na lengo gani 

kwangu? Akauliza Peniela 

“Usihofu Peniela watu hawa 

walikuwa wanataka kukutumia tu 

kwa faida zao.Imekuwa vyema 

umewafahamu mapema” akasema 

Mathew “Baada ya kugundua kuhusu 

hilo nini kinaendelea? Austin 

akauliza 

“Tunachotakiwa kukifanya 

kwa sasa ni kuhakikisha tunaupata 

mtandao wote wa CIA hapa 

nchini.Ninaamini fedha zile 

ambazo Dr Robert alizichukua 

zilikuwa ni kwa madhumuni ya 

kufanikisha mipango mbali mbali 

ya CIA hapa nchini.Kampuni hii ya 

Tanbest ni kichaka tu cha 

kupitishia fedha za CIA.Inatakiwa 

kuchunguzwa sana” akasema 

Mathew 

“Kwa kuwa Peniela tunaye 

hapa ambaye ni mmoja wa 

wamiliki wa benki ya Escom 

ninashauri tuendelee kudukua ili tuweze kufahamu zaidi kuhusiana 

na hii kampuni ya Tanbest ambayo 

inaonekana ndiyo inayotumika 

kupitishia fedha za CIA kuja 

Tanzania kufadhili operesheni 

mbalimbali za CIA kwa kigezo cha 

kufanya biashara na kampuni ya 

Flamingo.Ninaweza kuingia katika 

mtandao wa benki hii na kudukua 

zaidi ili tufahamu zaidi kuhusiana 

na hii benki” akasema Camilla. 

“Hilo ni wazo zuri 

sana.Peniela utamsaidia Camilla 

kuingia katika mtandao wa benki 

yenu na kudukua taarifa muhimu 

za kutusaidia” akasema Mathew na 

bila kupoteza muda Camilla 

akaanza kazi yake ya 

udukuzi.Wakati Camilla akiendelea Peniela akamuomba 

Mathew wakaongee 

chumbani.Wakawaacha Camilla na 

Austin sebuleni wakaenda 

chumbani kwa Peniela. 

“Unasemaje Peniela? Akauliza 

Mathew 

“Mathew mimi na wewe 

tumetoka mbali.Ninathubutu 

kukiri kwamba wewe ni kama 

malaika ambaye Mungu alikutuma 

uje unikomboe.Nimefika hapa 

nilipo kwa sababu ya jitihada 

zako.Kama usingeyatoa maisha 

yako kupambana kufa na kupona 

kwa ajili yangu leo nisingekuwa 

Peniela huyu ambaye dunia nzima 

inaniheshimu.Mathew sipati neno 

zuri la kueleza ni jinsi gani nimeumizwa na mambo 

niliyokutendea.Baada ya 

kugundua kwamba Anderson na 

baba yake walinifanya nikaachana 

nawe kwa faida yao wenyewe 

nimeumia sana.Nimejiona ni kwa 

jinsi gani nilivyokuwa mjinga kwa 

kuacha mbachao kwa msala 

upitao.Nikiwa angani nilimuomba 

sana Mungu anifikishe salama 

Tanzania ili niweze kukwambia 

maneno haya ana kwa ana 

kwamba ninaomba sana msamaha 

wako kwa mambo yale 

niliyokukosea.Najua una moyo wa 

kipekee kabisa na utatafuta namna 

ya kunisamehe.Fahamu kwamba 

nafasi yako moyoni mwangu bado 

ipo japo sijui kama ..” “Peniela stop that.” Akasema 

Mathew. 

“Kwa sasa kuna mambo 

makubwa 

yanayonikabili.Ninakabiliwa na 

tuhuma za mauaji na kama si kwa 

jitihada za mzee Meshack Jumbo 

ningeozea gerezani.Kuna mambo 

makubwa yanaoendelea hapa 

nchini.Mpaka sasa bado 

sijafanikiwa kufahamu mahala 

ilipo football,maisha ya rais Dr 

Vivian yanaonekana yako hatarini 

na mimi ninapaswa kumuokoa” 

akasema Mathew 

“Mathew mimi niko pamoja 

nawe katika suala hili na 

tutapambana bega kwa bega hadi 

tuhakikishe tunamaliza masuala haya salama na ninaomba uniahidi 

kitu kimopja tu kwamba baada ya 

mambo haya kumalizika basi 

tutazungumza kuhusu masuala 

yetu mimi na wewe” 

“Sawa tutazungumza” 

akasema Mathew 

“Thank you so much 

Mathew.Sasa nisikilize kwa 

makini.Nimekuita huku pembeni 

kwa jambo mahsusi ambalo 

sikutaka kukueleza mbele ya wale 

wenzako kutokana na unyeti 

wake” akasema Peniela 

 “Kuna siri ambayo bado 

hujaifahamu kuhusu kampuni ya 

Tanbest gemstone ltd.Hii ni 

kampuni inayomilikiwa kwa siri 

na rais Dr Vivian matope”Sura ya Mathew ilionyesha 

mstuko mkubwa kwa taarifa ile 

toka kwa Peniela 

“No that’s not true !! akasema 

Mathew huku akitoa kicheko 

kidogo 

“Ninamfahamu Dr Vivian ni 

mmoja kati ya viongozi wachache 

waadilifu sana katika bara hili la 

Afrika na hawezi kamwe 

kujihusisha na kampuni kama hii 

ambayo inatumiwa na Marekani 

katika kufadhili operesheni zake 

chafu nchini Tanzania”akasema 

Mathew 

“Mathew ndiyo maana 

nikakwambia kwamba hili jambo 

ni siri kubwa na wengi 

hawalifahamu.Nimeamua kukwambia wewe ukweli na 

ninaomba uniamini” akasema 

Peniela na Mathew akamtazama 

kwa sekunde kadhaa 

“Peniela we’re at very serious 

situation right now so I don’t need 

any joke” akasema Mathew 

“Mathew this is not a 

joke.Please trust me.Kampuni hii 

ya Tanbest gemstone ltd mmiliki 

wake ni Vivian Matope” 

“Dr Vivian ?!! akauliza Mathew 

ambaye bado alikuwa katika 

mshangao mkubwa sana. 

“Mathew najua taarifa hizi 

zimekustua sana lakini huo ndio 

ukweli”akasema Peniela 

“Peniela sijawahi kutilia 

shaka taarifa yoyote ile uliyowahi kunipa lakini ninapatwa na wakati 

mgumu kukuamini katika 

hili.Tanbest ni kampuni ambayo 

inatumiwa na Marekani katika 

kupitisha fedha ambazo 

wanazitumia katika operesheni 

zao chafu hapa Tanzania.Iweje Dr 

Vivian asilifahamu hilo? Akauliza 

Mathew 

“Mathew kama hujawahi 

kuniamini huko nyuma katika 

jambo lolote naomba uniamini 

katika hili.Ni kweli Dr Vivian 

matope ndiye mmiliki wa kampuni 

ya Tanbest” akasema 

Peniela.Mathew bado aliendelea 

kumtazama kwa macho ya 

mshangao “Peniela are you sure about 

this? 

“Ndiyo Mathew.Nina uhakika 

na hili ninalokwambia.Kama bado 

huniamini nakuomba ufanye 

uchunguzi na utabaini kwamba 

sisemi uongo” akasema Peniela na 

Mathew akashika kiuno 

alionekana kuwa na mawazo 

mengi. 

“Kampuni hii tunaituhumu 

kwa kutumiwa na Marekani 

kupitia CIA kupitishia fedha chafu 

zinazofadhili operesheni 

mbalimbali za CIA hapa nchini na 

sikuwahi kuhisi kama inaweza 

ikamuhusisha Dr Vivian.Hata hivyo 

uchunguzi wa kutosha unatakiwa kufanyika ili kubaini ukweli wa 

jambo hili” akasema Mathew 

“Ukiachana na hilobado kuna 

jambo lingine ambalo naamini 

bado hulifahamu”akasema Peniela 

na kumtazama Mathew 

“Dr Vivian ana akauntiya siri 

katika benki ya Escom ambayo 

huhifadhi fedha nyingi isiyolipiwa 

kodi.Viongozi wengi kutoka 

mataifa mbali mbali huficha fedha 

katika benki hii na Dr Vivian ni 

mmoja wao” akasema Peniela 

Ilimchukua Mathew dakika 

moja kusema chochote. 

“Peniela haya mambo 

uliyonieleza yamenistua sana na 

sikutegemea kuyasikia masikioni 

mwangu.Sijui nifanye nini”akasema Mathew na kurejea 

sebuleni walikowaacha Austin na 

Camilla 

“Kuna chochote 

kimepatikana? Akauliza Mathew 

“Hapana bado” akajibu 

Austin.Mathew akavuta pumzi 

ndefu na kusema 

“Kuna jambo ambalo 

nimeelezwa na Peniela limenistua 

sana” 

Camilla akaacha kazi 

aliyokuwa anaifanya na 

kumgeukia Mathew 

“Ni jambo gani? Akauliza 

Austin “Peniela amenieleza kwamba 

kampuni ya Tanbest Gemstone inamilikiwa kwa siri na rais Dr 

Vivian matope” 

Wote wawili Austin na Camilla 

wakapatwa na mshangao mkubwa. 

“Mathew hizi ni taarifa nzito 

sana.Peniela ana uhakika nazo? 

“Ndiyo nina uhakika nazo 

lakini kama mnazitilia shaka 

ninawaomba mfanye uchunguzi na 

mtaubaini ukweli” akasema 

Peniela kwa kujiamini. 

“Mathew do you trust her? 

Akauliza Austin.Mathew 

akamtazama Peniela halafu 

akasema 

“I do” 

“Peniela ni mmoja wa 

wamiliki wa benki ya Escom 

ambayo Tanbest wana akaunti pale kwa hiyo ni rahisi kwake 

kufahamu kuhusiana na benki hii 

lakini pamoja na hayo lazima 

tujiridhishe kwamba ni kweli Dr 

Vivian ndiye mmiliki wa hii 

kampuni? Kama ndiyo anafahamu 

kinachoendelea kupitia kampuni 

yake? Swali lingine ambalo 

nimejiuliza baada ya kupata 

taarifa hii ni je George Mzabwa 

anaingiaje katika kampuni hii?Dr 

Robert naye anahusika vipi katika 

hii kampuni hadi afikie hatua ya 

kuingia katika akaunti ya kampuni 

na kuchota fedha?Haya ni maswali 

ambayo yanaweza kutusaidia 

katika kuufahamu ukweli wa 

jambo hili.Ukiacha hilo kuna 

jambo lingine” akasema Mathew na simu yake ikaita akasogea 

pembeni kuipokea.Alikuwa ni 

Meshack Jumbo 



Hallow mzee Jumbo” 

“Mathew umefika wapi? 

Tayari umekwisha anza safari ya 

kuja ikulu? Akauliza Meshack 

Jumbo 

“Hapana mzee Jumbo bado 

sijaanza safari ya kuja 

huko.Nimekuja kuonana na 

Peniela” 

“Mathew kama nilivyokueleza 

kwamba Helmet Brian amegoma 

kuondoka hapa ikulu bila ya 

kukuona wewe hivyo nakuomba 

uahirishe shughuli zako nyingine 

na uje mara moja hapa ikulu 

tuweze kumuondoa Helmet hapa na kumpeleka mapumzikoni” 

akasema Meshack Jumbo 

“Mzee kuna jambo ambalo 

nataka nikushirikishe” 

“Jambo gani Mathew? 

“Kuna kitu nimekipata 

ambacho kimenistua kidogo.Kuna 

hii kampuni ya kuchonga madini 

ya vito ya Tanbset Gemstone ltd 

ambayo tumegundua na 

mashirikiano ya kibiashara na 

kampuni ya kutengeneza saa ya 

Flamingo iliyoko 

Marekani.Kampuni hii ya Flamingo 

na kampuni ya A.D Electronics 

aliyokuwa anafanya kazi Nathan 

zote ni kampuni zilizo chini ya 

serikali ya Marekani kupitia 

shirika lake la CIA.Flamingo wamekuwa wakinunua madini ya 

vito kutoka kwa kampuni ya 

Tanbest lakini kitu cha kushangaza 

tumegundua kwamba kuna fedha 

kiasi cha shilingi milioni mia saba 

na sabini ziliweka katika akaunti 

ya George iliyo katika benki ya 

Escom kutoka kampuni ya 

Flamingo na baadae George 

alizitoa fedha hizo akaziweka 

katika akaunti tatu tofauti ambazo 

tulipozifuatilia tukagundua zote ni 

akaunti za kampuni ya 

Tanbest.Tumechimba zaidi na 

kugundua kwamba katika moja ya 

akaunti hizi tatu ambazo George 

aliweka kiasi cha shilingi milini 

mia sita na hamsini fedha hizo 

zilichukuliwa na waziri wa mambo ya nje wa nchi Dr Robert 

Mwainamela.Tumejiuliza maswali 

Dr Robert au George wanahusikaje 

na kampuni hii ya Tanbest?George 

Mzabwa na Dr Robert Mwainamela 

wote walikuwa katika mtandao wa 

CIA kwa hiyo ni wazi Marekani 

wanaitumia kampuni ya Tanbest 

kupitishia fedha zao chafu kwa ajili 

ya kufadhili operesheni zao mbali 

mbali hapa nchini.Kikubwa zaidi 

kilichonistua ni kwamba kampuni 

hii ya Tanbest mmiliki wake ni rais 

Dr Vivian matope” 

“What ?!! Meshack Jumbo naye 

akapatwa na mshangao mkubwa 

“Mathew una hakika na hilo 

unalolisema?akauliza “Ndiyo mzee Jumbo.Nina 

uhakika nalo.Nimelipata toka kwa 

mtu ambaye siwezi kumtilia 

shaka” akasema Mathew 

“Una ushahidi wowote wa 

kumuonyesha Dr Vivian kwamba 

ndiye mmiliki wa hiyo kampuni ya 

Tanbest? 

“Ninalifanyia kazi hilo suala 

na nitakapopata ushahidi 

wakutosha nitakujulisha” akasema 

Mathew.Ukimya wa sekunde 

chache ukapita kisha Meshack 

Jumbo akasema 

“Mathew jambo hili ni zito 

hivyo ninakuomba 

usiliharakishe.Nenda nalo taratibu 

na ulifanyie uchunguzi wa kina na 

upate ushahidi wa kutosha wa kumuhusisha rais Dr Vivian na 

hiyo kampuni.Yawezekana ikawa 

ni njama iliyotengenezwa 

kumchafua hivyo kuwa makini 

sana na taarifa kama hizi.Wakati 

ukiendelea na uchunguzi wako 

nakuomba uje hapa ikulu ili 

tuweze kumuondoa Helmet Brian 

hapa na kumpeleka sehemu 

salama halafu utaendelea na 

uchunguzi wako.Umenielewa 

Mathew? 

“Nimekuelewa mzee” 

“Ahsante sana.Kama kuna 

chochote ambacho unaona 

ninaweza kukusaidia basi usisite 

kunieleza na mimi nitakusaidia ili 

uweze kuukamilisha uchunguzi 

wako.Nakuomba mara moja hapa ikulu” akasema Meshack Jumbo na 

kukata simu.Mathew akawafuata 

wenzake 

“ Nimeitwa ikulu mara 

moja.Nahitajika kwenda 

kumchukua waziri Helmet Brian 

na kumpeleka sehemu 

salama.Amegoma kutoka ikulu 

hadi anione” akasema Mathew 

“Mathew una uhakika na 

hicho walichokueleza? Usije kuwa 

unawekwa mtegoni ili 

wakukamate tena” akasema Austin 

“Hapana huu si 

mtego.Meshack Jumbo hawezi 

kunidanganya.Lazima litakuwa ni 

jambo la kweli” akasema Mathew 

na kuwataka waendelee kuchunguza wakati akielekea 

ikulu 

“Mathew are you sure you 

want to go there? Peniela 

akamuuliza Mathew wakati 

akiingia garini 

“Ndiyo Peniela.Nadhani 

unanifahamu vyema kuliko mtu 

yeyote mimi huwa siogopi.Usihofu 

I’ll be fine” akasema Mathew na 

kuwasha gari lake akaondoka 

kuelekea ikulu 

***************** 

Dr Vivian alimaliza 

mazungumzo na rais Kim Hun Yu 

na mara tu alipotoka akakutana na 

Meshack Jumbo akimsubiri “Jumbo bado uko hapa? 

Hujampeleka Helmet 

kupumzika?akauliza Dr Vivian 

“Madam president we need to 

talk” 

“Not right now Jumbo.I have 

some many important things to 

do.Take Helmet to safe house then 

come back and we’ll talk” akasema 

DrVivian ambaye alionekana kuwa 

na haraka 

“Mheshimiwa rais tuna tatizo 

kidogo kuhusu Helmet” akasema 

Meshack na kumfanya Dr Vivian 

asimame akamtazama kwa muda 

halafu akamtaka waelekee katika 

chumba cha maongezi ya faragha. 

“Kuna nini Meshack? Helmet 

ana tatizo gani? Akauliza Dr Vivian “Helmet amegoma kuondoka 

hapa hadi atakapomuona Mathew” 

“Is he crazy?!! 

“Hayo ndiyo masharti yake 

aliyoyatoa kwamba hatanyanyua 

mguu wake hapa ikulu hadi 

atakapomuona 

Mathew.Hamuamini mtu yeyote 

zaidi ya Mathew ambaye ndiye 

aliyemuokoa kutoka katika ule 

mpango wa kumuua” 

“Oh my Gosh ! akasema Dr 

Vivian na kushika kiuno. 

“I told you madam president 

that we still need him.Mathew 

bado ana msaada mkubwa kwetu” 

“Ninakwenda kuzungumza na 

Helmet kwamba Mathew hataweza 

kupatikana na nitampa ulinzi mkali kuelekea huko mahala 

anakopelekwa hata wanajeshi 

ikibidi.Simuhitaji Mathew hapa 

tena.Ninataka kusikia Mathew 

yuko katika mikono ya polisi” 

akasema Dr Vivian huku akianza 

kupiga hatua 

“Madam president don’t do 

that” akasema Meshack na Dr 

Vivian akasimama 

“Tayari nimemuhakikishia 

Helmet kwamba Mathew yuko 

njiani anakuja na hivi tuongeavyo 

tayari nimekwisha wasiliana naye 

atafika hapa ikulu muda wowote” 

“What ?!! How can you do that 

Meshack?Kwa nini 

unanipuuza?Kwa nini hutaki 

kufuata kile ninachokuelekeza?Nimekuelekeza 

kwamba Mathew arejeshwe katika 

mikono ya polisi lakini umepuuza 

na badala yake unamruhusu aje 

hapa ikulu.Unataka kunijaribu? 

Akauliza Dr Vivian kwa hasira 

“Si hivyo madam 

president.Sina nia ya kukujaribu” 

“Kama huna nia ya kunijaribu 

kwa nini unafanya mambo 

kinyume na maelekezo yangu? 

“Nilidhani tulikwishalimaliza 

hili suala la Mathew na 

tukaelewana” akasema Meshack 

Jumbo 

“Meshack hatukuwa 

tumeelewana chochote.Msimamo 

wangu uko pale pale kwamba 

Mathew arejeshwe haraka sana mikononi mwa polisi na 

afunguliwe mashtaka ya mauaji.I 

want Mathew to disapear !! 

akasema Dr Vivian kwa 

hasira.Akamtazama Meshack 

Jumbo kwa macho makali 

“Madam presdient kuna 

jambo ambalo nataka 

nikufahamishe” 

“kama ni kuhusu Mathew 

sitaki kusikia tena nataka 

arudishwe katika mikono ya polisi 

ndani ya dakika thelathi kutoka 

sasa vinginevyo nitakuharibu 

Meshack.Mimi sijaribiwi.Ni mtu 

mbaya sana ukitaka kujaribu 

nguvu yangu hivyo kama unataka 

usalama na mimi mrudishe Mathew haraka sana kwa polisi!! 

Akafoka Dr Vivian 

“Madam president jambo 

ulilotaka Mathew asilifahamu 

tayari amekwisha lijua” akasema 

Meshack na kumstua Dr Vivian 

“Unasemaje? 

“Nnasema kwamba lile jambo 

ulilotaka Mathew asilifahamu 

tayari amekwisha lifahamu” 

“Sikuelewei unachokisema 

Meshack.Amejua jambo 

gani?akauliza Dr Vivian 

“Mathew tayari amefahamu 

kwamba wewe ndiye mwenye 

kampuni ya Tanbest Gemstone ltd” 

Sura ya Dr Vivian ilionyesha 

mstuko mkubwa sana na kwa 

sekunde kadhaa alibaki mdomo wazi akashindwa aseme 

nini.Walitazamana kwa muda 

halafu akatoa kicheko kidogo 

“Hicho mbona 

kichekesho?Kampuni ya Tanbest? 

Inajushughulisha na nini hiyo 

kampuni kwani siifahamu kabisa” 

akasema Dr Vivian 

“Madam president japokuwa 

midomo yako inakana kuifahamu 

kampuni hii lakini sura yako 

inaonyesha wazi mstuko ulio upata 

kwa hiyo tusiendelee kupoteza 

muda hali kila kitu kiko 

wazi.Kampuni hii ya Tanbest 

imekuwa inatumiwa na kampuni 

ya Flamingo ambayo inamilikiwa 

na CIA kupitishia fedha kwa ajili ya 

operesheni zake chafu nchni Tanzania.Hizi operesheni zote za 

Marekani zinazofanyika hapa 

Tanzania fedha zake zinapitia 

katika kampuni hii.Taarifa zote 

Mathew anazo na hivi sasa yuko 

njiani kuja hapa ikulu and he need 

answers,I also need answers!! 

Kwa mara ya kwanza Meshack 

Jumbo akamshuhudia Dr Vivian 

mwanamke anayetajwa kuwa na 

ujasiri wa ajabu, midomo 

ikimtetemeka akishindwa kujibu 

swali 

“Madam president please 

trust me and tell me the truth.Is 

this company yours?!! Akauliza 

Meshack Jumbo lakini Dr Vivian 

alibaki kimya hakujibu kitu “Mheshimiwa rais toka 

mwanzo nilikueleza kwamba 

unaweza kuniamini na kunieleza 

siri yoyote ile na mimi nitakuwa 

msiri wako.Mpaka sasa Mathew 

hajui kama amri ya kumuua Dr 

Robert Mwainamela imetoka 

kwako.Hii ni siri ambayo 

nitakwenda nayo 

kaburini.Ninakuonyesha ni kwa 

namna gani unavyoweza 

kuniamini heshimiwa rais.Mimi 

sipaswi kuwa adui yako bali 

unapaswa kunifanya mtu wako wa 

karibu kwani ninayafahamu 

mambo mengi ya kiusalama 

ninafahamu namna ya kuweza 

kuyamaliza mambo kimya kimya 

na hata marais wote niliofanya nao kazi awali wamenitumia sana 

katika mambo yao ya siri.Hata hili 

la Mathew ninaweza kulimaliza na 

mambo yakaenda vizuri ili mradi 

unieleze ukweli bila 

kunificha.Niweke wazi baadhi ya 

mambo ambayo unadhani 

ninapaswa kuyafahamu” akasema 

Meshack Jumbo 

Dr Vivian akainamisha kichwa 

akafikiri kwa muda na kusema 

“Nataka nionane na Mathew 

pindi akifika hapa” 

“Sawa madam president” 

akasema Meshack Jumbo kisha 

rais akatoka na kuelekea sebuleni 

alikokuwa amekaa waziri Helmet 

Brian “ Helmet Brian” akasema Dr 

Vivian 

“Mheshimiwa rais” akasema 

Helmet 

“Kama nilivyokueleza awali 

kwamba tutakupeleka sehemu 

salama ya kukaa kwani hivi sasa 

Marekani watakuwa wanakusaka 

kila kona.Ninaamini tayari 

wamekwisha fahamu kwamba 

mpango wao umeshindwa 

kufanikiwa hivyo watakutafuta 

kwa udi na uvumba na ndiyo 

maana nimeagiza upelekwe 

sehemu salama ambako utaishi 

huko hadi tutakapopata ushahidi 

usio na shaka kwamba ni kweli 

Marekani walipanga mpango wa 

kukuua.Nimeambiwa kwamba umegoma kuondoka hadi 

utakapomuona Mathew” akasema 

Dr Vivian 

“Ahsante sana mheshmiwa 

rais,ni kweli nimekataa kuondoka 

hapa hadi nitakapomuona yule 

kijana Mathew.Nimetokea 

kumuamini sana kwani ndiye 

aliyeyaokoa maisha 

yangu.Mheshimiwa rais yule kijana 

ni mahiri sana na Tanzania ina 

bahati mno kuwa na mtu mahiri 

kama yule” akasema Helmet na Dr 

Vivian akatabasamu 

“Watu watatu ambao 

walitumwa kuja Tanzania kwa kazi 

ya kukuua tayari wamekamatwa 

na muda si mrefu tutaanza 

kuwahoji ili tupate taarifa za kutosha kutoka kwao.Hao ndio 

watakaotupa ukweli kuhusu 

mpango huu” akasema Dr Vivian 

na tabasamu likajengeka usoni 

kwa Helmet Brian 

“Vyombo vyako vya ulinzi 

vinafanya kazi nzuri sana hadi 

vimeweza kuwakamata watu hao 

ndani ya kipindi kifupi.Tafadhali 

naomba watu hao wahojiwe hadi 

waseme ukweli.” Akasema Helmet 

na ukimya mfupi ukapita kisha 

Helmet akasema 

“Nimewaza sana kwa nini 

watake kunitoa kafara? Nimekuwa 

mtiifu sana kwa nchi yangu na 

nimefanya kila lililowezekana kwa 

ajili ya nchi yangu lakini malipo 

yangu ndiyo haya.Nimeumizwa sana na hili 

jambo.Kinachonisikitisha zaidi ni 

kwamba Mike straw ni rafiki yangu 

mkubwa sana na nina hakika 

jambo hili analifahamu lakini 

hakufanya chochote na akabariki 

niuawe.Mheshmiwa rais naomba 

unisaidie kupata ushahidi usio na 

shaka kuhusu hili jambo halafu 

nitajua nini cha 

kufanya.Wamarekani wanapaswa 

kufahamu serikali yao ilivyo na 

watafanya maamuzi” akasema 

Helmet 

“Siwezi kumtetea Mike straw 

lakini unapokalia kiti kama hiki 

kuna nyakati unajikuta 

unalazimika kufanya maamuzi 

ambayo hukuwa umefikiria kuyafanya.Ninaamini hata Mike 

hakupenda kufanya hivi lakini 

alilazimika kufanya hivyo kwa 

maslahi mapana na taifa 

lake.Sitaki kuhalalisha 

alichokifanya lakini kuna nyakati 

sisi kama marais tunalazimika 

kufanya maamuzi magumu kama 

hayo” akasema Dr Vivian 

“Nalifahamu hilo Dr 

Vivian.Nafahamu ugumu wa 

kukalia hicho kiti lakini kwa Mike 

hakupaswa kunifanyia kitu kama 

hiki hasa baada ya mambo yote 

niliyomfanyia.Mimi ndiye 

niliyepaswa kuwa rais wa 

Marekani lakini kutokana na 

urafiki wetu mkubwa niliamua 

kujitoa katika mbio za kuwania urais na kumpa yeye nafasi lakini 

amesahau hayo hote na anataka 

kuniua.Nimemshauri sana kutumia 

busara katika suala la Korea 

Kaskazini lakini Lengo lake ni 

kuanzisha vita na ndiyo maana 

anafikia hatua ya kufanya 

maamuzi kama haya.Marekani 

hatuwezi kukubali kuwa na rais 

kama huyu lazima nihakikishe 

nimemuondoa madarakani” 

akasema Helmet na Dr Vivian 

akatabasamu 

“Tatizo kubwa alilonalo rais 

wenu ni kukosa busara na kufanya 

maamuzi ya hasira bila kufikiri 

athari za maamuzi 

anayoyachukua.Matamshi yake 

hayamuonyeshi kama anafaa kuwa rais wa Marekani.Kwa miaka yote 

marais wa taifa hili kubwa duniani 

wamekuwa ni mfano kwa maraisi 

wa mataifa mengine kwa matendo 

na maamuzi yao lakini kwa huyu 

amekuwa ni tofauti sana.Amekuwa 

ni rais mwenye matamshi na kauli 

za hovyo sana kuwahi kutokea 

katika taifa la Marekani na 

kuifanya heshima ya taifa hili 

machoni pa mataifa ishuke.Sikuwa 

nimepanga kuingia katika 

mashirikiano na Korea Kaskazini 

na wala siungi mkono mpango 

wake wa kutengeneza makombora 

lakini kauli za dharau kutoka kwa 

Mike straw zilinifanya nikubali 

kufanya mashirikiano na Korea 

kaskazini.Kwa sababu ya kauli zake za dharau dunia hivi sasa 

imegawanyika sehemu mbili nchi 

zinazoiunga mkono Marekani na 

nchi zinazounga mkono Korea 

Kaskazini.Pamoja na mgawanyiko 

huo bado anataka kuanzisha vita 

na Korea kaskazini na hii inaweza 

kupelekea kuzuka kwa vita 

inayoweza kuitwa ya tatu ya dunia 

kwani mataifa yanayoiunga mkono 

Marekani yatapigana na yale 

yaliyotanganza kuiunga mkono 

Korea kaskazini na hii 

itasababisha maangamizi 

makubwa dunaini kwani mataifa 

mengi yana umiliki wa silaha kali 

na mengine ya silaha za 

nyuklia.Nimetoka kuzungumza na 

rais wa Korea kaskazini sasa hivi anasema kwamba ameyaweka 

majeshi yake katika tahadhari 

baada ya kupata taarifa kwamba 

kuna mipango ya siri ya Marekani 

kuishambulia nchi yake.Kim Yun 

Hu ameapa kutumia silaha zake 

kali kuiangamiza Marekani.Korea 

Kaskazini ina makombora yenye 

kubeba vichwa vya nyuklia na 

uwezo wa kuishambulia 

Marekani.Damu itamwagika kila 

kona ya dunia”akasema Dr 

Vivian.Helmet akainamisha kichwa 

akazama mawazoni.Baada ya 

dakika moja akasema 

“Unachokisema mheshimiwa 

rais ni kitu cha kweli kabisa na 

mimi kama waziri wake wa 

mambo ya nje nimekuwanikijitahidi sana kuepuka jambo 

hilo lisitokee kwani namfahamu 

vizuri Mike ni mtu ambaye hana 

uvumilivu hata kidogo na ilikuwa 

ndoto yake ya muda mrefu siku 

moja kuishambulia Korea 

kaskazini na sasa anatafuta kila 

njia ya kuitimiza ndoto yake.Ni 

mimi pekee ambaye nimekuwa na 

uwezo wa kusimama na kumtaka 

atumie busara katika suala la 

Korea kaskazini.Kwa sasa amebaki 

na watu wanaomsikiliza kwa kila 

jambo anaweza akaingia katika 

vita na Korea Kaskazini.Wakati 

mwingine ninahisi yawezekana 

labda ametaka niuawe kwa kuwa 

nilikuwa nampinga sana katika 

suala la kutaka kuanzisha vita na nikijitahidi sana kuepuka jambo 

hilo lisitokee kwani namfahamu 

vizuri Mike ni mtu ambaye hana 

uvumilivu hata kidogo na ilikuwa 

ndoto yake ya muda mrefu siku 

moja kuishambulia Korea 

kaskazini na sasa anatafuta kila 

njia ya kuitimiza ndoto yake.Ni 

mimi pekee ambaye nimekuwa na 

uwezo wa kusimama na kumtaka 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog