Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL (2) - 3

   

Simulizi : The Football (2)

Sehemu Ya Tatu (3)


“Majibu ya maswali haya yote 

anayo Dr Robert” akasema Camilla 

“Tusipoteze muda wakati mtu 

wa kutujibu yupo.Twende 

tukaanze mahojiano lazima 

tuufahamu ukweli” akasema 

Mathew na wote wakaingia katika 

chumba alimo DrRobert ambaye tayari alikuwa amerejewa na 

fahamu .Alipowaona Mathew na 

Camilla wakiingia mle ndani 

akakunja sura na kuwatazama kwa 

hasira 

“Mashetani wakubwa 

ninyi.Nini maana ya kunifanya 

hivi?Ninaombeni mnifungue 

mkono wsangu haraka sana” 

akasema Dr Robert kwa ukali 

.Mathew akavuta kiti na 

kuketi,Camilla akasimama karibu 

na mlango. 

“Vijana naombeni mnifungue 

haraka sana mkono wangu.Mimi ni 

mtu mkubwa na sipaswi kufanyiwa 

hivi.Mnataka nini toka kwangu? 

Nani kawatuma mnifanyie 

hivi?Kama mnataka pesa

 niambieni nitawapa kiasi chochote 

kile mnachokihitaji lakini 

msinifanyie udhalilishaji wa 

namna hii.Napaswa kuheshimiwa 

utu wangu.Kwa wadhifa nilionao 

sipaswi kufanyiwa kitu kama hiki 

na vijana wadogo kama ninyi !! 

akasema kwa ukali Dr Robert.Bado 

Mathew aliendelea kumtazama 

bila kumsemesha chochote 

“Vijana nawahakikishieni 

mnajiweka katika hatari kubwa 

sana kwa hiki mnachokifanya 

kwani mpaka hivi sasa tayari 

vyombo vya ulinzi vinafahamu 

kwamba niko hapa na muda 

wowote mtavamiwa hapa na 

adhabu mtakayoipata ni kubwa 

sana.Hata hivyo ninaweza kuwasaidia kama mtajutia kosa 

lenu na kunifungua haraka sana” 

akasema Dr Robert na kumtazama 

Mathew aliyekuwa amekaa karibu 

yake akimtazama bila kusema 

chochote.Dr Robert akapandwa na 

hasira 

“Say something bastard !!! 

akasema kwa ukali 

“Nani kawatuma mnifanyie 

hivi? Anawalipa kiasi gani kwa 

ujinga huu mnaoufanya? Akauliza 

tena kwa ukali 

“Dr Robert naomba uwe 

mtulivu mzee wangu.Hatuna shida 

kubwa nawe ila tumekuleta hapa 

kwa kutumia njia hii tunahitaji 

kuzungumza nawe kuhusu 

masuala fulani muhimu.Hakuna yeyote anayefahamu kama uko 

hapa na wala hakuna yeyote 

atakayekuja kukuokoa hivyo ni 

kitu kimoja tu kitakachokuokoa na 

kukufanya utoke humu salama ni 

ushirikiao wako kwetu.Tupe 

majibu ya kweli kwa kila 

tutakachokuuliza.Ukifanya kama 

tunavyotaka utatoka hapa salama 

salimini lakini ukileta ukaidi na 

kiburi nakuhakikishia kwamba 

hautatoka salama hapa 

ndani.Hautaliona tena jua la kesho 

na mipango yako yote 

hautaikamilisha” akasema Mathew 

na sura ya Dr Robert ikaonyesha 

woga mkubwa hasa kwa namna 

Mathew alivyokuwa anazungumza 

kwa kituo bila wasi wasi wowote “Nadhani ni jambo la busara 

endapo tutajitambulisha kwako 

sisi ni akina nani ili twende 

sawa.Mimi naitwa Mathew 

Mulumbi.Nimewahi kufanya kazi 

katika idara ya ujasusi ya Taifa 

lakini kwa sasa ninafanya kazi 

zangu binafsi.Yule pale anaitwa 

Camilla Snow anatokea marekani 

na anafanya kazi FBI.Kwa pamoja 

tunafanya kazi ya uchunguzi 

tuliyopewa na rais Dr Vivian hivyo 

kila tunachokifanya rais ana 

taarifa nacho” 

Dr Robert akaonyesha mstuko 

mkubwa 



Dr Robert akaonyesha mstuko 

mkubwa 

“Rais ndiye aliyewatuma 

mnikamate na kunileta hapa? 

Akauliza kwa ukali 

“Hajatutuma tukukamate ila 

tunatekeleza kazi aliyotupa na kwa 

hiyo ana taarifa za sisi kukuchukua 

na kukuleta hapa” 

“No that’s not true!! akasema 

DrRobert 

“Kama hauamini sasa 

utaamini hapo baadae.baada ya 

kutufahamu sisi ni akina nani 

tuelekee katika mazungumzo yetu 

narudia tena kukuomba 

mheshimiwa waziri kwamba 

tunafahamu kila kitu kuhusu wewe 

kwa hiyo usithubutu 

kutudanganya.Usijaribu kutuudhi 

kwani utaomba ukutane na mtoa 

roho kuliko kutukorofisha 

sisi.Hatuna huruma tunapokuwa 

katika utekelezaji wa majukumu yetu.Hiyo ni tahadhari tumekupa” 

akasema Mathew 

“Go to hell!! Akasema Dr 

Robert na Camilla aliyekuwa 

amesimama akiwa na kompyuta 

yake akainua kichwa na 

kumtazama Dr Robert.Mathew 

akatabasamu na kukaa sawa kitini 

kisha akasema 

“Tutaona nani atakayekuwa 

wa kwanza kwenda huko 

unakonitaka niende” akasema na 

kumtazama kwa macho 

makali.Tayari alikwisha anza 

kukasirika kufuatia Dr Robert 

kuanza kuonyesha kiburi 

“Dr Robert kwanza kabisa 

nataka kukujulisha kwamba Olivia 

au Tausi kama anavyojiita hayup tena duniani amekwisha fariki na 

kama hautakuwa na ushirikiano 

kwetu basi wewe ndiye 

utakayefuata” 

Sura ya Dr Robert ikaonyesha 

mstuko mkubwa sana na uso wake 

uliloa jasho.Mathew akaendelea 

“Olivia au Tausi tumegundua 

alikuwa ni jasusi toka shirika la 

ujasusi la CIA na amepandikizwa 

ikulu kwa kazi maalum ya 

kumchunguza rais.Marekani 

wamekuwa wanamchunguza rais 

wetu kwa muda mrefu sasa toka 

angali anasoma chuo kikuu nchini 

humo.Walimpandikiza jasusi 

mwingine anaitwa Nathan na 

akaanzisha mahusiano ya 

kimapenzi na Dr Vivian na huyo Nathan kwa sasa ni 

marehemu.Baada ya Nathan 

kupotea ameletwa tena huyu Tausi 

au Olivia ambalo ndilo jina lake 

halisi. Tumegundua kwamba jana 

jioni Tausi aliwasiliana nawe 

pamoja na balozi Abraham Clerk 

na mkakutana nyumbani 

kwake.Leo hii asubuhi 

umewasiliana naye tena na hata 

mchana huu ulikuwa unawasiliana 

naye bila kujua kama ulikuwa 

unawasiliana nami kwani tayari 

Tausi alikwisha kufa.Tumekuta 

ramani ya jiji la Dar es salaam 

chumbani kwa Tausi na katika 

kompyuta yake tumekuta kuna 

ramani ya uwanja wa ndege wa 

Julius Nyerere.Nimewasiliana na balozi Clerk kwa kutumia simu 

yako na akasema kwamba vijana 

wako tayari wanakusubiri kwa 

maelekezo kwani mtu wenu 

anakaribia sana kufika.Nataka 

utueleze nani mnayemtegea 

kuwasili na nini mipango yenu? 

Akauliza Mathew.Dr Robert 

alikuwa ameinamisha kichwa 

“Dr Robert nadhani 

umenisikia naomba unipe 

jibu.Nani mnayemtegemea 

kuwasili na na mpango wenu ni upi 

ambao mmekuwa mnauandaa 

wewe na balozi Clerk? Akauliza 

tena Mathew lakini Dr Robert 

hakujbu kitu. 

“Mathew ! akaita Camilla na 

kumpa ishara Mathew waende nje “Huyu hataweza kutueleza 

chochote na kwa kuwa ni mtu wetu 

wa muhimu sana hatupaswi 

kutumia njia zetu za kumuhoji kwa 

kumtesa kwani tunaweza 

kumuumiza wakati bado 

tunamuhitaji kuna mamboa mengi 

tunapaswa kuyafahamu toka 

kwake” akasema Camilla 

“Anaonekana kuwa kiburi 

sana lakini kiburi chake leo 

kitakwisha ” akasema Mathew 

“Mathew nina wazo” akasema 

Camilla 

“Kama nilivyosema kwamba 

huyu Dr Robert hataweza 

kutueleza chochote kwa sasa na 

hatupaswi kutumia njia zetu za 

kumfanya mtu aweze kufungua mdomo wake kwani ana taarifa 

muhimu sana za kutusaidia hivyo 

ushauri wangu ni kumlazimisha 

aongee kwa kutumia familia 

yake.Wakati ukimuhoji mimi 

nilikuwa nadukua taarifa 

zake.Nimegundua kwamba ana 

watoto wawili mapacha wanaitwa 

Juliana na Julieth wanasoma 

St.Patrick international 

School.Tuwatumie watoto hao 

wawili kumlazimisha 

azungumze.Tumtishie kuwadhuru 

wanae na hatakubali kabisa 

watoto wake wadhurike na 

atasema kila kitu” akasema 

Camilla 

“Ni wazo zuri japo sipendi 

sana kuwahusisha watoto katika mambo kama haya lakini kwa hapa 

tulipofika hatuna namna lazima 

tufanye hivyo.Ngoja niende huko 

mimi mwenyewe,wewe endelea 

kuwachunguza hawa jamaa tujue 

ni akina nani na wametoka wapi 

na kwa nini wako hapa nchini.” 

akasema Mathew na kuelekea 

chumbani kwake akajiandaa 

haraka haraka .Alivaa suti nzuri 

nyeusi akachukua gari lingine la 

kifahari miongoni mwa magari 

yake sita na kabla hajaondoka 

akaitafuta namba ya simu ya shule 

wanakosoma watoto wa Dr Robert 

na kwa kutumia simu yake ya 

mkononi akapiga akaomba 

kupewa namba za mkuu wa shule 

akapewa na akaipekua simu ya Dr Robet akaiona ile namba ya mkuu 

wa shule ipo akamuandikia 

ujumbe mfupi akimjulisha 

kwamba anamtuma mtu kwenda 

kuwachukua watoto wake Juliana 

na Julieth kuna dharura ya 

kifamilia.Alipoutuma ujumbe ule 

akaondoka 

“Mpango gani ambao Dr 

Robert na marekani wanaupanga 

kuutekeleza? Ni nani 

wanayemtegemea awasili leo? 

Haya ni maswali yaliyoumiza sana 

kichwa cha Mathew 

“Dr Vivian amezungukwa na 

nyoka watupu .Dr Robert ni mmoja 

wa watu anaowaamini mno na hata 

alidiriki kukasirika nilipotaka 

kumfanyia uchunguzi.Rais alikosea sana kunizuia nisimfanyie 

uchunguzi Dr Robert,hakufahamu 

mtu anayempigania ni mtu wa aina 

gani.Huyu ni mtu mwenye sura 

mbili na inawezekana Dr Vivian 

hajalitambua hilo bado.Yeye 

anaifahamu sura moja tu ya mtu 

mwadilifu na mzalendo anayefaa 

hata kuwa rais wa nchi.Sura ya pili 

imejificha na inahitaji kazi ya ziada 

kuing’amua lakini kwa sasa tayari 

nimekwisha ing’amua na sina 

shaka kwamba Dr Robert 

anashirikiana na CIA .Kupitia 

kwake tutaweza kupata mwanga 

kuhusiana na huu mtandao ambao 

CIA wameujenga hapa nchini na 

nini kusudi lao.” Akawaza na 

kukumbuka kitu “Mpaka sasa sijapata 

mrejesho wowote toka kwa 

Peniela.Ana tatizo gani? 

Aliniambia atanipigia simu lakini 

mpaka sasa bado sijapata simu 

yake.Ngoja niendelee kuvuta 

subira yawezekana bado 

hajakamilisha lile zoezi na 

anahitaji muda” Mathew 

akaondolewa mawazoni baada ya 

simu yake kuita.Zilikuwa namba 

ngeni kabisa katika simu yake 

akaitazama vizuri akagundua ni 

namba za Dr Robert. Akajua lazima 

atakuwa ni Camilla akaipokea 

“Hallow” akasema 

“Mathew ni mimi Camilla 

nimelazimika kutumia simu hii ya 

Dr Robert” “Usijali Camilla.Kuna tatizo 

lolote? 

“Nimechunguza majina ya 

wale watu tuliyoyakuta katika 

mkoba wa Dr Robert nimegundua 

kwamba yale si majina yao halisi ni 

majina bandia.Wale wote watatu ni 

raia wa Korea Kusini 

.Nimewasiliana na yule rafiki 

yangu kule Marekani anisaidie 

kutafuta taarifa zao kama 

wanashirikiana na CIA ama 

vipi.Ninapata wasiwasi 

yawezekana wakawa 

wanashirikiana na CIA” 

“Kazi nzuri sana 

Camilla.Endelea kuwafuatilia tujue 

kama nao ni CIA.Mimi ninakaribia 

kufika katika shule wanakosoma watoto wa Dr Robert.Ukipata 

taarifa yoyote kabla sijarejea 

utanijulisha” 

“Sawa Mathew nitafanya 

hivyo” akasema Camilla na kukata 

simu 

“Hawa jamaa wanazidi 

kuniumiza kichwa.Kuna kitu gani 

wanakipanga hapa 

Tanzania?Wametoka wapi na kwa 

nini watumie majina bandia?Hata 

hivyo lazima tutajua kila kitu 

wanachokipanga.Haitaanza siku ya 

kesho kabla kila kitu hakijawekwa 

wazi”akawaza Mathew 

akapunguza mwendo wa gari na 

kukata kona akifuata barabara 

inayoelekea katika shule ya 

kimataifa ya St Patrick .Toka kwa mbali shule hii iliweza kuonekana 

uzuri wake 

“Hi ni shule ya kimataifa hasa 

ndiyo maana wanasoma watoto wa 

watu wazito” akawaza Mathew 

akiyafurahia mazingira ya shule ile 

Alifika katika geti la shule 

likafunguliwa na mlinzi aliyevaa 

sare za kampuni binafsi ya 

ulinzi.Mathew akashusha kioo na 

kusalimiana na yule mlinzi 

aliyetaka kufahamu shida 

yake.Mathew akajieleza kwamba 

anatoka kwa waziri wa mambo ya 

nje na mkuu wa shule tayari ana 

taarifa zake.Yule mlinzi akaingia 

katika kibanda chake akachukua 

simu na kupiga katika ofisi ya 

mkuu wa shule akauliza kama mkuu wa shule ana taarifa za mtu 

kutoka kwa waziri wa mambo ya 

nje,akaombwa amruhusu 

apite.Mathew akaruhusiwa kupita 

akaelekezwa liliko jengo la 

utawala iliko ofisi ya mkuu wa 

shule 

Aliegesha gari katika 

maegesho iliyokuwa karibu na 

jengo la utawala akashuka na 

kufuata kibao kilichomfikisha 

katika ofisi ya mkuu wa 

shule.Aligonga mlango wa ofisi ile 

na sauti ya mwanadada ikamruhsu 

aingie akakutana na mwanadada 

mmoja mweupe mwenye nywele 

nyeusi zenye 

kung’aa.Wakasalimiana na 

Mathew akaomba kuonana na mkuu wa shule ambaye tayari ana 

taarifa zake.Bila hiyana yule 

mwanadada akamruhusu Mathew 

afungue mlango wa mkuu washule 

akaingia ndani na kukutana na 

mama wa makamo akamsalimu 

kwa adabu na kujitambulisha 

kwamba ndiye aliyetumwa na 

waziri wa mambo ya nje ya 

nchi.Mwalimu yule hakupoteza 

muda akainua simu na kupiga 

simu kwa mwalimu wa darasa na 

kumtaka awapeleke wale watoto 

wawili ofisini kwake tayari kwa 

kuondoka.Haukupita muda mrefu 

Julieth na Juliana wakawasili na 

Mathew akakabidhiwa akaagana 

na mwalimu mkuu pamoja na yule 

katibu muhtasi wa mkuu wa shule akaongozana na wale watoto hadi 

katika gari lake la kifahari 

akawafungulia mlango wakaingia 

ndani na kuondoka pale shuleni. 

“Sipendi sana kuwaingiza 

watoto katika mambo kama haya 

kwani wao hawana kosa lolote ila 

kuna nyakati ambazo inatulazimu 

kufanya hivi ili kuweza kupata 

taarifa za muhimu.Dr Robert anazo 

taarifa za muhimu sana lakini 

hataweza kuzitoa bila kutishia 

maisha ya watoto wake” akawaza 

Mathew huku akiwatazama wale 

watoto wawili pacha wazuri 

wakiwa wamekaa kiti cha nyuma 

wakiwa hawana wasi wasi wowote 

“Watoto wachangamfu sana 

hawa wananikumbusha mwanangu Anna Maria.Baada ya 

seke seke hizi kumalizika lazima 

niende Paris kumtembelea na 

kujua maendeleo yake” akawaza 

Mathew 

*************** 

Aliwasili nyumbani 

kwake,akawakaribisha ndani wale 

watoto wakapewa vinywaji na 

kuwadanganya kwamba baba yao 

atawafuata pale muda si mrefu. 

“Camilla kuna kingine 

chochote umekigundua kuhusu 

wale jamaa? Mathew akauliza 

“Hapana, bado sijapata 

mrejesho wowote toka kwa yule rafiki yangu wa kule Marekani” 

akasema Camilla 

“Sawa .Muda unakwenda mbio 

na hatujui huyo mtu 

wanayemtarajia atafika saa 

ngapi.Ni wakati wa kuanza 

kutafuta majibu.walete watoto 

chumbani kwa baba yao” akasema 

Mathew 

“Mathew naomba kwa 

vyovyote itakavyokuwa 

tusiwaumize hawa watoto” 

akasema Camilla 

“Nalifahamu hilo Camiila 

lakini ikinilazimu kuwafanya 

chochote ili kumfanya Dr Robert 

atupe kile tunachohitaji kukisikia 

basi nitafanya ila nitajitahidi 

kujizuia kutokufika huko.Tusipoteze wakati Camilla 

walete watoto chumbani” akasema 

Mathew halafu akatangulia 

chumbani aliko Dr Robert 

akaufungua mlango na kuingia 

ndani.Dr Robert alikuwa amejilaza 

kitandani bado akiwa amefungwa 

pingu mkononi.Alipomuona 

Mathew akainuka na kukaa 

“Hallow Dr Robert.Nimerejea 

tena lakini safari hii siko peke 

yangu nimekuletea wageni” 

akasema Mathew na mlango 

ukafunguliwa Camilla akaiangia 

ndani akiwa ameongozana na 

Juliana na Julieth 

Dr robert alihisi roho inataka 

kumtoka baada ya kuwaona 

watoto wake pale.Watoto wake nao wakastuka wakataka 

kumkimbilia baba yao lakini 

Camilla akawazuia. 

“Dady what are you doing 

here? Akauliza Julieth 

Dr Robert alitaka kusema kitu 

akashindwa.Midomo ikabaki 

inamtetemeka.Uso ukaloa 

jasho.Akamtazama Mathew kwa 

hasira na kutaka kuinuka Mathew 

akatoa bastora na kumtaka 

atulie.Watoto wale walipoona baba 

yao anaelekezewa bastora 

wakaanza kulia Camilla 

akawanyamazisha.Dr Robert huku 

akitetemeka kwa hasira akasema 

“Fenyeni mnachotaka 

kukifanya kwangu lakini msiwaguse watoto wangu 

tafadhali!! 

“Dr Robert hatukuwa na 

sababu ya kuwaleta watoto wako 

hapa lakini kiburi chako 

kimetufanya tuwalete na 

tukuonyeshe kwamba tunao 

uwezo wa kufanya chochote .Hata 

hivyo hatukusudii wala hatuna 

sababu ya kuwadhuru watoto 

wako unaowapenda lakini 

ukitulazimisha kufanya hivyo 

hatutasita kuwadhuru mbele yako 

ukishuhudia” akasema Mathew na 

kumsogelea Dr Robert 

“Nitazame vizuri machoni Dr 

Robert.Sitanii kwa kile 

ninachokisema.Endapo hautatupa 

ushirikiano nitabadilika na kuwa mnyama.Usitake kuniona wakati 

nimekasirika kwani nitawakata 

wanao pumzi kikatili sana nawe 

ukishuhudia!! Akasema Mathew na 

kumtaka Camilla awatoe mle 

chumbani wale watoto 

“Dr Robert mimi pia ni mzazi 

nina watoto na siwezi kukubali 

hata siku moja kuwaweka watoto 

wangu katika hatari.Nitafanya kila 

niwezalo kuwaokoa 

wanangu.Waonyeshe wanao 

kwamba wewe ni baba bora kabisa 

na ambaye uko tayari kufanya 

jambo lolote kwa ajili 

yao.Watazame wanao ni wacheshi 

wana furaha na wana malengo 

makubwa ya maisha yao.Usitake 

kunilazimisha nikayakatisha malengoyao.Nieleze kile 

ninachokitaka na wanao 

watakuwa salama” 

“Shetani mkubwa wewe !! 

Watoto wangu wamekufanya nini? 

Waache watoto wangu haraka sana 

waondoke.Kama unashida na mimi 

usiwahusishe wanangu!! 

“Sikiliza DrRobert kwa sasa 

hauko katika nafasi yoyote ya 

kutoa amri.Unachotakiwa kufanya 

kwa sasa ni kufuata kile 

nitakachokuamuru.Utakapofanya 

ninavyokuelekeza basi wanao 

wataendelea kuwa salama.Nataka 

kufahamu wewe na wenzako akina 

Tausi na balozi Clerk mna mpango 

gani mnaopanga kuufanya leo? Nani mnayemtarajia kuwasili jioni 

ya leo? 

Dr Robert hakujibu kitu 

akabaki kimya 

“Dr robert naomba 

usinipotezee wakati.Nijibu haraka 

maswali yangu” 

“mwanaharamu mkubwa 

wewe.Niue tu lakini usitegemee 

kupata kitu chochote toka 

kwangu.Niue mjinga 

wewe!!Unadhani kwa kuwaleta 

watoto wangu hapa utanifanya 

nikwambie unachokitaka? 

Unapoteza muda wako bure 

kijana.Mimi si mtu rahisi kama 

unavyodhani” akasema kwa ukali 

Dr Robert Mathew akamtazama halafu 

akatazama saa yake ilikaribia sa 

kumi na moja za jioni.Akafungua 

mlango na kumtaka Camilla 

awalete watoto wa Dr Robert mle 

chumbani.Mathew akamshika 

Julieth 

“Nataka nikuonyeshe kwamba 

nina maanisha ninachokisema 

.Nitaanza na huyu halafu 

nitamalizia na yule mwingine 

,atakuja mama yao na kama bado 

hautataka kutupa tunachokitaka 

tutaendelea kuwamaliza ndugu 

zako mmoja baada ya 

mwingine”akasema Mathew na 

kumtaka Julieth amtazame baba 

yake “Kiburi chako Dr Robert 

kinayaondoa maisha ya mwanao 

Julieth” akasema Mathew na 

kuiweka bastora kichwani kwa 

Julieth ambaye alikuwa analia.Dr 

Robert alikuwa anatetemeka mwili 

na kuuma meno kwa hasira kali 

alizokuwa nazo. 

“Tano !! Mathew akaanza 

kuhesabu 

“Nne !! akaendelea kuhesabu 

huku Julieth akitoa kilio. 

“Kijana tafadhali nakuomba 

waache wanangu.kama unashida 

na mimi niue mimi na si 

wanangu.hawana kosa lolote.Niue 

mimi tafadhali na uwaache huru!! 

Akasema Dr Robert huku macho yake yakionekana kuwa na 

machozi. 

“Tatu !! Mathew akahesabu 

“ Baba wape kitu 

wanachokitaka wasituue !! 

akasema Julieth huku akilia.Dr 

Robert alikuwa anahema kwa kasi 

na michirizi ya machozi 

ikaonekana machoni pake 

“Mbili !! 

Julieth akaongeza 

kulia.Mathew akamtazama Dr 

Robert kwa hasira 

“Moj..” 

“Basi !! Basi !! Usimuue 

mwanangu !! akapiga ukelele Dr 

Robert 

Mathew akamsukuma 

pembeni Julieth akaanguka chini Camilla akamuinua na 

kumbembeleza anyamaze,Mathew 

akamfuata Dr Robert 

“Haraka sana nieleze ama 

sivyo nitawatoa uhai wanao sasa 

hivi!! Akafoka 

“sawa sawa nitakueleza kila 

kitu lakini naomba unihakikishie 

kwamba wanangu watakuwa 

salama”akasema Dr Robert huku 

machozi yakimtoka.Mathew 

akamfanyia ishara Camilla awatoe 

mle ndani wale watoto 

“Haya anza kunieleza!! 

Akafoka Mathew baada ya watoto 

wa Dr Robert kutoka mle ndani.Dr 

Robert akavuta pumzi ndefu na 

kwa sauti yenye kitetemeshi 

akasema “Nataka uniahidi kitu kimoja 

kabla sijakueleza chochote” 

akasema Dr Robert 

“Unahitaji nini? 

“Nikikueleza kile unachotaka 

kukifahamu tayari nitakuwa 

ninajihesabu mimi ni 

mfu.Ninaomba unihakikishie ulinzi 

mimi na familia yangu na 

nitakueleza kila kitu” akasema Dr 

Robert.Mathew akamtazama na 

kusema 

“Nieleze kwanza kila kitu na 

nikiona uzito wa hicho 

utakachokuwa umenieleza basi 

nitaamua kama nikusaidie au vipi 

lakini kwa sasa siwezi kukuahidi 

chochote” akasema Mathew .Dr Robert akavuta pumzi ndefu na 

kusema 

“Helmet Brian waziri wa 

mambo ya nje wa Marekani 

anawasili jioni ya leo” akanyamaza 

“Endelea ! akafoka Mathew na 

maco yake yalitisha kwa namna 

alivyokasirika.Dr Robert 

akaonekana kusita kuendelea. 

“Dr Rober…..” Mathew akataka 

kusema ktu lakini Dr Robert 

akamuwahi 

“Nitakueleza” akasema na 

kumeza mate 

“Inapangwa mipango ya 

kumuua mara atakapofika hapa 

Dar es salaam” akasema na 

kunyamaza akatazama chini “Mnataka kumuua waziri wa 

mambo ya nje wa marekani? 

Akauliza Mathew.Alishangazwa 

sana na taarifa zile.Dr Robert bado 

aliendelea kutazama 

chini.Akamsogelea Dr Robert na 

kumshika kichwa akamuinua 

“Dr Robert tafadhali naomba 

unieleze nielewe.Nani wanataka 

kumuua waziri wa mambo ya nje 

wa Marekani na kwa nini? 

Akauliza Mathew lakini bado Dr 

Robert hakutaka kujibu 

“Nakuhakikishia DrRobert 

safari hii sintahesabu mpaka 

tano.Nitawaondoa wanao mmoja 

baada ya mwingine!! 

“Tafadhali naomba usiwaguse 

tena wanangu.Mpaka sasa umekwisha wapa mstuko mkubwa 

sana na sijui nitafanya nini 

kuwasahaulisha tukio hili la 

kinyama ulilolifanya !! akasema Dr 

Robert 

“Narudia kwa mara ya mwisho 

kama unataka wanao waendelee 

kuwa hai nieleze nani wanataka 

kumuua waziri wa mambo ya nje 

wa Marekani na kwa nini? 

“Helmet Brian anataka 

kuuawa na marekani”akasema 

DrRobert 

“Anataka kuuawa na 

Marekani?!! Mathew akashangaa 

“ndiyo ” 

“Kwa nini Marekani watake 

kumuua waziri wao wa mambo ya 

nje? Dr Robert akawa kimya 

“Nataka jibu Dr Robert kwa 

nini marekani watake kumuua 

waziri wao wa mambo ya nje? 

“Kwa sababu wanataka 

kupata sababu ya kushambulia 

Korea Kaskazini” 

“Mmepangaje kumuua Helmet 

Brian? 

“Kuna watu tayari wako hapa 

nchini wameletwa kwa ajili ya hiyo 

kazi ya kumuua Helmet.Watu hao 

baada ya kufanikisha mauaji hayo 

watakamatwa na wakihojiwa 

watadai kwamba wametumwa na 

Korea Kaskazini wamuue waziri 

Helmet na hicho kitakuwa ni 

kigezo cha marekani kuanzisha 

vita na Korea kaskazini” “Tumekuta karatasi yenye 

picha tatu katika mkoba 

wako.Tumeyachunguza majina ya 

watu hao na kukuta ni majina 

bandia,je watu hao ndio 

waliotumwa kuja kumuua waziri 

Helmet? Akauliza Mathew 

“Ndiyo ni hao” 

“wanatokea nchi gani? 

“Mimi sifahamu bali jukumu 

langu lilikuwa ni kuhakikisha watu 

hao wanaingia,niwatafutie hoteli 

za kukaa na kuwapanga kila 

mmoja na eneo lake” akasema Dr 

Robert.Mathew akamtazama kwa 

hasira na kusema 

“Dr Robert wewe ni mtu 

mkubwa mwenye heshima kubwa 

sana ndani na nje ya nchi.Kwa nini umeshiriki katika mpango kama 

huu wa mauaji ya mtu mkubwa 

kama huyu wakati unafahamu fika 

kuwa jambo hili litaleta mvutano 

mkubwa sana kati ya nchi yetu na 

Marekani? Kama umeweza 

kushiriki katika kupanga mauaji 

ya kiongozi huyu wa Marekani 

utashindwaje kushiriki katika 

mauaji ya rais wetu kama 

ukishawishiwa na pesa? Akauliza 

Mathew lakini Dr Robert hakujibu 

kitu akainamisha kichwa 

“Mimi nawe bado tuna 

mzungumzo marefu hapo 

baadae.Kwa sasa nataka unieleze 

mlivyopanga kutekeleza mauaji ya 

Helmet” akasema Mathew “Siwezi kukueleza zaidi ya 

hapa,sitaki mpango huu uvurugike 

kwani unanitegemea sana mimi na 

endapo usipofanikiwa na 

wakafanya uchunguzi wakafahamu 

kwamba ni mimi ndiye chanzo cha 

mpango kushindwa kufanikiwa I’m 

dead” akasema Dr Robert. 

“Dr Robert mpaka hapa tayari 

mpango huu umeshindikana.Siko 

tayari waziri wa mambo ya nje wa 

marekani auawe katika ardhi ya 

Tanzania.Lazima nifanye kila 

niwezalo kuhakikisha mpango huu 

haufanikiwi hivyo naomba 

tusipoteze wakati nieleze mpango 

mzima wa mauaji namna 

mlivyoupanga” Dr Robert akafikiri kidogo na 

kusema 

“Hapana siwezi kukueleza 

chochote” 

“Dr Robert usitake niwaite 

tena watoto wako humu chumbani 

na ushuhudie namna uhai 

unavyowatoka” akasema Mathew 

na kauli ile ikamuogopesha Dr 

Robert akalazimika kumweleza 

Mathew ukweli wote.Baada ya 

kuelezwa namna mpango wote 

ulivyopangwa Mathew akamfuata 

Camilla 

“Wanaendeleaje watoto? 

“Wamelala.Wamepatwa na 

mstuko mkubwa” 

“Hatukuwa na namna 

nyingine ya kumfanya Dr Robert aongee zaidi ya kuwatumia watoto 

wake.Hata hivyo amefunguka kila 

kitu.Jioni ya leo anawasili waziri 

wa mambo ya nje wa Marekani 

Helmet Brian.Kuna mpango wa 

kumuua unaandaliwa na seriali ya 

marekani” 

Camilla akastuka na 

kumtazama Mathew kwa 

mshangao 

“Marekani wanataka kumuua 

waziri wao wa mambo ya nje? Kwa 

nini wafanye hivyo? 

“Kwa mujibu wa maelezo ya 

Dr Robert ni kwamba Marekani 

wanatafuta sababu ya kuanzisha 

vita na Korea kaskazini.Wale watu 

tuliokuta picha zao katika karatasi 

kwenye mkoba wa Dr Robert ni wadunguaji walioletwa hapa 

nchini kwa ajili ya kazi hiyo ya 

kumuua Helmet.kwa maelezo ya 

Dr Robert ni kwamba baada ya 

kutekeleza mpango wa mauaji ya 

Helmet watu hao watakamatwa na 

watakiri kwamba wametumwa na 

serikali ya Korea Kaskazini na 

hapo Marekani watakuwa 

wamepata sababu ya kuishambulia 

Korea Kaskazini kwa kigezo cha 

kulipiza kisasi kwa mauaji ya 

waziri wake wa mambo ya nje” 

akasema Mathew 

“Mathew tafadhali tusiruhusu 

jambo hili likatokea katika ardhi 

ya Tanzania.Kwa namna yoyote ile 

lazima tumuokoe Helmet Brian” 

akasema Camilla “Ndiyo Camilla.Katu jambo hili 

haliwezi kutokea na lazima 

tulizime jaribio hili kwa gharama 

zozote” akasema Mathew na 

kumpigia simu Hamis Chuma 

akamtaka aje na kijana mmoja 

“Kwa hiyo tunafanyaje 

kumuokoa Helmet asiuawe? 

Akauliza Camilla 

“Bado tunaye Dr Robert .Huyu 

atatusaidia katika kuuvuruga 

mpango huu wa mauaji.Kwa 

kumtumia yeye atatusaidia kuingia 

ndani ya uwanja wa 

ndege.Tutakuwa na magari mawili 

na ndani ya gari moja tutatega 

bomu.Kwa kuwa tutakuwa 

tumeongozana naye 

hatutakaguliwa.Muda mfupi baada ya Helmet Brian kuwasili bomu 

hilo tutakalolotega garini 

litalipuka na kuzua kizaa zaa 

kikubwa pale uwanjani na huo ni 

wakati wetu sisi wa kumchukua 

Helmet Brian na kuondoka 

naye.Katika mpango huo kuna 

maisha ya watu yanaweza kupotea 

lakini hatuna namna lazima kwa 

gharama zozote tumuokoe Helmet 

na tuiokoe dunia kuingia katika 

vita nyingine kubwa isiyoweza 

kuelezeka kwani mataifa 

washirika wa Korea kaskazini 

hawatakaa kimya wakiomba 

mshirika wao anashambuliwa 

hivyo wataingia vitani.Washirika 

wa marekani nao wataingia pia 

vitani na vita hiyo itazidi kutanuka.Lazima tuzuie dunia 

kutumbukia katika janga lingine 

kubwa” akasema Mathew na 

Camilla akaukubali mpango 

ule.Mathew akaelekea katika 

chumba alimo Dr Robert. 

“Dr Robert nisikilize kwa 

makini.Mimi na wenzangu 

tumeazimia kuuvuruga mpango wa 

kumuua waziri Helmet 

Brian.Hatuwezi kukubali mauaji 

haya yakafanyika katika ardhi ya 

Tanzania.Kama ni kumuua 

wakamuulie katika ardhi yao na si 

hapa kwetu.Ninakushangaa sana 

Dr Robert kwa kukubali kuingia 

katika mpango huu bila ya kupima 

athari zake kwa nchi na kwa 

dunia.Pamoja na hayo utafuata maelekezo yetu.Kwanza utampigia 

simu balozi wa marekani na wale 

wote ambao mnashirikiana nao 

katika mpango huu na wajulishe 

kwamba kila kitu kinakwenda 

kama kilivyopangwa.Waambie 

kwamba ulipatwa na dharura na 

ndiyo maana hukuweza 

kuwasiliana nao.Baada ya hapo 

mpigie simu mkeo mjulishe kuwa 

watoto uko nao hivyo 

asihofu.Ukimaliza upande huo wa 

mawasiliano tutaelekea uwanja wa 

ndege kumpokea Helmet na 

utatumia uwezo wako wote katika 

kuhakikisha kwamba mimi na 

vijana wangu tunaingia uwanja wa 

ndege bila matatizo wala 

kukaguliwa.Ukithubutu kufanya chochote kinyume na maelekezo 

yetu basi hutawaona watoto 

wako.Tumeelewana?? akauliza 

Mathew na Dr Robert akaitika kwa 

kichwa.Mathew akamfungua pingu 

na kumpa simu yake 

akamuelekezea bastora na 

kumtaka apige simu wakati 

amesimama pale ili aweze kusikia 

anachokizungumza.Dr Robert 

akafanya kama alivyoelekezwa 

akapiga simu na alipomaliza 

Mathew akaichukua simu na 

kumtaka ainuke na kumpeleka 

chumbani kwake katika kioo na 

kumtaka ajiweke vizuri kwani 

alikuwa amesawajika sana 

Wakati Dr Robert akijiandaa 

Hamis Chuma na kijana wake mmoja wakawasili kwa kutumia 

piki piki.Mathew akamuita Camilla 

na kumtaka amsimamie Dr Robert 

wakati anajiweka sawa akaenda 

kuonana na akina Hamis 

“Ahsanteni sana kwa kufika 

kwa wakati” Mathew akawaambia 

akina Hamis. 

“Tumeamua kutumia piki piki 

ili kufika kwa wakati kama 

ulivyotutaka.” Akasema Hamis 

Chuma,Mathew akawaongoza 

sebuleni na bila kupoteza wakati 

akawaeleza alichowaitia 

“Kuna kiongozi mmoja 

ambaye anatakiwa kuuawa lakini 

kazi yetu sisi ni kwenda 

kumuokoa.Ni kiongozi mkubwa.Ni 

waziri wa mambo ya nje wa Marekani.Tukio hilo tutalifanya 

katika uwanja wandege wa Julius 

Nyerere ambayo ni sehemu yenye 

ulinzi mkali.Wanaopanga 

kutekeleza mpango huo wana 

utaalamu mkubwa hivyo 

operesheni hii ni operesheni yenye 

kuhitaji matumizi makubwa ya 

akili,ujuzi na uzoefu.Naomba 

niwaweke wazi ndugu zangu 

kwamba hii ni operesheni yenye 

hatari kubwa kwa hiyo yeyote 

ambaye anahisi hatakuwa tayari 

aweke wazi angali mapema” 

“Mathew sisi ni wazee wa kazi 

na hizi ndizo kazi zetu.Sote hapa 

tumepitia jeshi,tunafahamu mbinu 

zote za mapambano na katu 

hatuogopi kupambana.Kwetu kucheza na silaha ni kama vile 

kuchezea simu kwa hiyo kwa niaba 

ya wenzangu nakuhakikishia 

kwamba tuko tayari ,tupe kazi 

tuifanye” akasema Hamis 

“Good” akasema Mathew na 

kuwaelekeza akina Hamis namna 

mpango ule wa kumuokoa Helmet 

utakavyokuwa.Akaingia chumbani 

kwake na kumkuta tayari Dr 

Robert amekwisha 

jiandaa,akachagua suti tatu na 

kuwapelekea akina Hamis.Akatoa 

katika gereji gari mbili aina ya 

Mercedece benz.Akalitazama 

mojawapo ya gari kwa uchungu 

“Gari langu jipya kabisa 

linakwenda kuteketea lakini kwa 

ajili ya kuokoa mtu muhimu asiuawe.” Akawaza na 

kumuelekeza Kijana wa Hamis 

azifanyie usafi zile gari halafu 

akamchukua Hamis wakaeleka 

katika chumba cha siri cha 

kuhifadhia silaha wakachagua 

silaha ambazo 

zingewasaidia.Wakachukua 

mabomu mawili na kwenda 

kuyatega katika gari moja kati ya 

zile mbili watakazotumia usiku 

ule. 

“Sikujua kama una hazina ya 

silaha kali nzito kama hizi” 

akasema Hamis Chuma wakati 

wakilitega bomu ndani ya gari 

“Mimi hupenda kuhifadhi 

silaha kama hivi kwa sababu hujitokeza operesheni za dharura 

kama hizi” akasema Mathew 

Walipomaliza maandalizi 

Mathew akaenda chumbani alimo 

DrRobert na kumtaka waondoke. 

Muda umefika Dr 

Robert,twende tuondoke tuelekee 

uwanja wa ndege” akasema 

Mathew na kumtaka Camilla abaki 

pale nyumbani akiwalinda watoto 

wa Dr Robert.Kabla hawajaondoka 

Dr Robert akataka kuwaona 

watoto wake. 

“Zingatia yale yote 

niliyokuagiza na utawaona tena 

wanao ila ukifanya kinyume na 

maelekezo hautawaona tena 

wanao wazuri” akasema Mathew 

wakaelekea katika magari.Mathew na Dr Robert wakaingia katika gari 

moja,Hamis Chuma na kijana wake 

aliyejulikana kama Gidion 

wakaingia katika gari lingine 

lililokua na bomu na safari ikaanza 

kuelekea uwanja wa ndege wa 

kimataifa wa Julius Nyerere. 




Hali katika uwanja wa ndege 

wa kimataifa wa Julius Nyerere 

Dar es salaam ilikuwa ni ya utulivu 

mkubwa na ndege ziliendelea 

kutua na kupaa kama 

kawaida.Magari mawili ya akina 

Mathew yaliwasili uwanjani hapo 

na kwa kumtumia Dr Robert 

walifanikiwa kuingia ndani ya uwanja ambako kulikuwa na gari 

tano zimejipanga kwa ajili ya 

msafara utakaomchukua waziri 

Helmet Brian kutoka pale uwanja 

wa ndege.Gari walilokuwa 

wamepanda Mathew na Dr Robert 

likasimama mbele kabisa ya 

magari ya msafara na lile 

walilopanda Hamis chuma na 

kijana wale lililokuwa na bomu 

likaenda kuegeshwa pembeni ya 

magari mengine.Kijana aliyekuwa 

na Hamis chuma akashuka katika 

lile gari na kwenda kuingia katika 

gari walilokuwamo Mathew na Dr 

Robert na kukaa katika kiti cha 

dereva,Mathew na Hamis Chuma 

wakaongozana na Dr Robert 

kuelekea mahala ambako wangempokelea Helmet 

Brian.Tayari maafisa kadhaa wa 

ubalozi wa Marekani na kutoka 

wizara ya mambo ya nje walikuwa 

wamewasili pale uwanjani 

akiwemo pia balozi wa Marekani 

nchini Tanzania Abraham 

Clerk.Alimvuta pembeni Dr Robert 

wakazungumza kwa takribani 

dakika kumi na kisha wakaja 

kujiunga na wenzao. 

Tayari kiza kimekwishatanda 

angani wakati ndege iliyombeba 

waziri wa mambo ya nje wa 

Marekani Helmet Brian ilipogusa 

ardhi ya Tanzania.Mlango 

ukafunguliwa wakashuka maofisa 

wanne wakapokewa na balozi wa 

Marekani nchini Tanzania nadakika tatu baadae Helmet Brian 

akashuka ndegeni akiwa 

amezungukwa na walinzi wake 

watatu.Alipokewa na balozi wa 

marekani nchini,wakasalimiana na 

kisha akamtambulisha kwa 

DrRobert ambaye ndiye mwenyeji 

wake naye akamtambulisha 

Helmet watu kadhaa waliokuwepo 

pale uwanjani kumpokea halafu 

wakaanza kutembea kuelekea 

ulipo msafara wa magari tayari 

kwa kuondoka pale uwanjani. 

Mita kama hamsini hivi kabla 

ya kuufikia msafara wa magari 

kikasikika kishindo cha mlipuko 

wa bomu na moto mkubwa 

ukatokea katika gari lililokuwa 

limeegeshwa pembeni ya magari ya msafara.Taharuki kubwa 

ikazuka na watu wakaanza 

kukimbia hovyo ili kuokoa maisha 

yao.Mara tu mlipuko ule 

ulipotokea Hamis Chuma 

akamuwahi Dr Robert na 

kumdhibiti.Walinzi wa Helmet 

Brian wakamchukua kiongozi wao 

na kuanza kumkimbiza 

kumrejesha ndegeni lakini Mathew 

tayari alikwishakiona kitendo kile 

akachomoa bastora mbili zote 

zenye kiwambo cha kuzuia sauti na 

kuanza kuwamiminia risasi wale 

walinzi wakaanguka chini na 

Helmet akajikuta akiwa peke 

yake.Alistuka na kuogopa 

akageuka nyuma akamuona 

Mathew akimfuata akiwa na bastora mbili,mwili 

ukamtetemeka.Mathew akamvaa 

na kumpa pigo moja kali 

akaanguka na kupoteza 

fahamu.Akamuinua akamuweka 

begani na kuanza kukimbia naye 

hadi katika gari lake.Hamis Chuma 

ambaye tayari alikuwa amekwisha 

fika garini akiwa na Dr Robert 

akamfungulia buti ya gari 

wakamuingiza Helmet na 

kuondoka.Kiza kikubwa 

kilikuwepo pale uwanjani watu 

wakikimbia kwenda mbali na 

uwanja.Akina Mathew hawakupata 

wakati mgumu kutoka kwani 

sehemu zote za mageti hazikuwa 

na walinzi kwani karibu kila mtu 

alikuwa amekimbia kuokoa maisha yake.Walifanikiwa kutoka 

salama nje ya uwanja ule na safari 

ya kuelekea nyumbani kwa 

Mathew ikaanza. 

“Hakuna 

aliyejeruhiwa?Mathew akauliza 

“Hapana wote tuko salama” 

akasema Hamis 

“Good” akasema Mathew na 

kumtazama Dr Robert ambaye 

alikuwa ameloa jasho mwili mzima 

“Nimepoteza gari langu zuri 

lakini tumefanikisha kumuokoa 

waziri Helmet.Operesheni 

imekuwa rahisi zaidi ya 

nilivyotegemea japokuwa 

imegharimu baadhi ya maisha ya 

watu.Pamoja na hayo 

tumefanikiwa kuepusha dunia na vita ya tatu ya dunia ambayo 

ingeibuka kama Helmet angeuawa 

na Marekani kuanza kuishambulia 

Korea kaskazini” akawaza Mathew. 

Hakukuwa na maongezi 

yoyote garini hadi walipofika 

nyumbani kwa Mathew,Camilla 

akafungua geti wakamshusha 

Helmet na kumuweka 

sebuleni,bado hakuwa 

amezinduka 

“Hamis nashukuruni sana kwa 

kazi yenu kubwa usiku huu wa leo 

hadi tumefanikisha kuokoa maisha 

ya huyu mtu ambaye alikuwa 

hatarini kuuawa lakini bado kuna 

kazi moja bado nahitaji kutoka 

kwenu.Nahitaji ulinzi kwa usiku 

wa leo hapa nyumbani kwangu.” “Usihofu kuhusu hilo 

Mathew.Hata ukitaka mwaka 

mzima sisi tuko tayari kukufanyia 

kazi.Nitawaongeza vijana wangu 

wawili katika kuongeza nguvu 

zaidi” akasema Hamis 

Mathew akaingia ndani na 

kumkuta Dr Robert akiwa amevua 

shati huku jasho likiendelea 

kumtiririka .Mathew akachukau 

chupa ya mvinyo na kummiminia 

katika glasi akanywa wote na 

kuhitaji tena mwingine akanywa 

wote.Mathew akamtaka ainuke 

akampeleka katika kile chumba 

alichokuwa amemfungia 

“Nimefanya kama 

mlivyonitaka 

nifanye,nimewasaidia mmefanikisha mpango 

wenu.Msingeweza kuingia mle 

uwanjani bila mimi.Kwa kuwa 

mmepata mlichokihitaji ni zamu 

yenu sasa kunisaidia na mimi 

kwani tayari maisha yangu yako 

hatarini,muda wowote ninaweza 

kuuawa.Mpango huu ulikuwa ni 

wa siri kubwa lakini mimi ndiye 

niliyeuharibu.Bila msaada wenu 

mimi na familia yangu 

tutaangamia”akasema Dr Robert 

“Mimi na wewe bado 

hatujamaliza mazungumzo yetu” 

akasema Mathew na kumfunga 

pingu 

“Tafadhali naomba msaada 

wenu.” Akasema Dr Robert lakini Mathew hakujibu kitu akageuka 

kuondoka 

“Naomba usiondoke 

tafadhali,nisikilize!! Akasema 

DrRobert na Mathew akageuka 

“Nakuomba tafadhali 

usimueleze Helmet jambo lolote 

kuhusu Marekani kutaka 

kumuua.Kwa kuwa tayari 

umefanikiwa kumuokoa fanya 

utaratibu aondoke nchini arejee 

kwao na asifahamu chchote.Kuna 

mambo makubwa nitakueleza 

endapo utafanya kama 

ninavyokuomba” akasema Dr 

Robert .Sura yake ilionyesha woga 

mkubwa.Mathew akaubamiza 

mlango na kutoka akaenda sebuleni alikokuwapo Camilla 

akimpa msaada Helmet kuzinduka. 

“Wanaendeleaje watoto? 

Akauliza 

“Wanaendelea vyema.Pole 

sana” 

“Ahsante .Tumefanikiwa 

kumuokoa Helmet lakini maisha 

ya watu kadhaa 

wamepotea.Sifahamu ni wangapi 

ila kuna watu wamekufa” akasema 

Mathew 

“Ahsante sana kwa kuokoa 

uhai wa mtu ambaye alitakiwa 

kuuawa bila kosa lolote.Usijali 

kuhusu hao waliopoteza maisha 

yao.Katika kila vita lazima kuna 

watu wasio na hatia watapoteza 

maisha” akasema Camilla na mara Helmet akazinduka.Akina Mathew 

wakamsaidia na akarejea katika 

hali yake ya kawaida. 

“Ninyi ni akina nani? Hapo 

nipo wapi? Akauliza 

“Usihofu mheshimiwa 

waziri,uko sehemu salama” 

akasema Mathew na Helmet 

akaanza kuvuta kumbu kumbu 

akakumbuka kilichotokea usiku 

ule katika uwanja wa ndege wa 

Julius Nyerere 

“Ulitokea mlipuko pale 

uwanja wa ndege,nani waolitega 

mlipuko ule na kwa kusudi gani? 

Walikuwa wananilenga mimi? 

Akauliza Helmet halafu 

akamtazama Mathew kwa macho 

makali “Wewe !! Nimekukumbuka!! 

Nilikuona na bastora.Uliwaua 

walinzi wangu ..!!Ninyi ni akina 

nani? Akauliza Helmet kwa wasi 

wasi 

Mathew akammiminia mvinyo 

katika glasi akanywa 

“Naitwa Mathew 

Mulumbi.Nimewahi kufanya kazi 

na idara ya ujasusi ya Tanzania 

lakini kwa sasa ninafanya shughuli 

zangu binafsi.Huyu mwenzangu 

anaitwa Camilla Snow.Ni raia wa 

Marekani na anafanya kazi FBI? 

“FBI ?!! akauliza Helmet kwa 

mshangao 

“Ndiyo” akajibu Camilla“Wewe !! Nimekukumbuka!! 

Nilikuona na bastora.Uliwaua 

walinzi wangu ..!!Ninyi ni akina 

nani? Akauliza Helmet kwa wasi 

wasi 

Mathew akammiminia mvinyo 

katika glasi akanywa 

“Naitwa Mathew 

Mulumbi.Nimewahi kufanya kazi 

na idara ya ujasusi ya Tanzania 

lakini kwa sasa ninafanya shughuli 

zangu binafsi.Huyu mwenzangu 

anaitwa Camilla Snow.Ni raia wa 

Marekani na anafanya kazi FBI? 

“FBI ?!! akauliza Helmet kwa 

mshangao 

“Ndiyo” akajibu Camilla “Kuna nini kinaendelea hapa? 

Umekuja kufuata nini huku 

Tanzania? Akauliza Helmet. 

Mathew hakupoteza muda 

akamueleza kuhusiana na mpango 

wa kumuua ulioandaliwa na 

serikali ya marekani.Helmet 

akainuka na kupandwa na hasira 

“Hapana si kweli hata 

kidogo.Serikali ya marekani 

haiwezi kufanya kitu kama 

hicho.Huu ni uongo wa mchana!! 

Akasema na kuibinua meza kwa 

hasira 

“Huo ni uongo mkubwa!! Rais 

Mike ni mtu wangu wa karibu na 

hawezi kupanga kuniua mimi!! 

Akazidi kufoka “Mheshimiwa waziri amini 

tunachokueleza ni kitu cha kweli 

kabisa na ndiyo maana tumefanya 

kila juhudi kukuokoa” akasema 

Camilla.Waziri Helmet 

akawatazama kwa sekunde 

kadhaa na kuuliza 

“Mmefahamuje kuhusiana na 

mpango wa kuniua? Akauliza na 

sasa alionekana kuanza kutulia 

“DrRobert ndiye aliyegundua 

mpango huo na akatujulisha.Kwa 

pamoja tumeshirikiana naye 

katika mpango huu na kukuokoa” 

akasema Mathew.Helmet 

akainamisha kichwa akazama 

katika mawazo mengi .Mathew 

akainuka na kwenda katika 

chumba alimokuwemo Dr Robert “Sikiliza Dr 

Robert.Nimemueleza Helmet 

kuhusu mpango wote uliokuwa 

umepangwa wa kumuua lakini 

sijakutaja kama nawe unahusika 

badala yake nimekutaja kama 

ndiye uliyegundua kuwepo kwa 

mpango ule na ukatujulisha na 

tumeshirikiana katika 

kumuokoa.Nimefanya hivi ili 

kukulindia heshima yako na hivyo 

ujiandae kunieleza mambo mengi 

zaidi pale nitakapokuja 

kuzungumza nawe baadae” 

akasema Mathew na kutoka mle 

chumbani akaelekea sebuleni na 

kumkuta waziri Helemt akiwa 

amejiinamia akionekana kuwa na 

mawazo mengi “Bado siamini.Nchi yangu 

ninayoitumikia kwa moyo wangu 

wote ndiyo wanataka kunitoa 

kafara kwa ajili ya kupata sababu 

ya kuishambulia Korea 

kaskazini.Na wewe Camilla uko 

hapa Tanzania kwa dhumuni 

gani?Kuna kazi yoyote umetumwa 

huku?akauliza Helmet 

“Niko hapa Tanzania kwa 

mambo binafsi nimekuja kwa huyu 

mpenzi wangu na kwa bahati nzuri 

jambo hili likanikuta na 

tukashirikiana pamoja” akasema 

Camilla na kumtazama Mathew na 

wote wakatabasamu 

“Naomba simu niwasiliane na 

familia yangu niwajulishe kwamba 

niko salama” akasema Helmet “Hapana mheshmiwa 

waziri,utapata nafasi ya kupiga 

simu pale utakapokuwa katika 

sehemu salama zaidi” 

“Sehemu salama? Helmet 

akashangaa 

“Ndiyo mheshimiwa 

waziri.Nitakukabidhi katika 

mikono salama zaidi” akasema 

Mathew na kuchukua simu 

akampigia rais 

“Mathew siwezi kuzungumza 

nawe kwa sasa nataka kuingia 

katika kikao kizito cha 

dharura.Kuna mambo makubwa 

yametokea usiku huu.Naomba 

unitafute baadae!! Akasema Dr 

Vivian “Mheshmiwa rais tafadhali 

naomba usikate simu” 

“Unahitaji nini Mathew?Kama 

una shida nimekwambia nitafute 

baadae kwa sasa ninasubiriwa 

katika kikao muhimu sana” 

“Mheshimiwa rais ninahitaji 

kukuona sasa hivi.Nina jambo 

kubwa nataka nikueleze na siwezi 

kusubiri hadi hapo baadae.Ni 

muhimu sana” 

Dr Vivian akafikiri kidogo na 

kusema 

“Unataka kuja ikulu? 

“Vipi hali ya Theresa? 

“Mathew naomba ujibu swali 

nililokuuliza 

 “Mheshimiwa rais nimeuliza 

hivyo ili kama ikiwezekana tukutane pale hospitali alikolazwa 

Theresa.Ahirisha kikao hicho kwa 

muda kwa kisingizio cha hali ya 

Theresa kubadilika ili uweze 

kupata nafasi ya kuja tuonane pale 

hospitali.Mheshimiwa rais 

nisingeweza kuharibu ratiba zako 

kama jambo ninalokuitia si la 

muhimu” akasema Mathew 

Kwa sekunde kadhaa Dr 

Vivian akawa kimya akitafakari 

kisha akasema 

“Sawa tukutane pale hospitali 

sasa hivi !! 

“Ahsante mheshmiwa rais” 

akasema Mathew na kukata simu 

akamuita Camilla pembeni 

“Camilla tunampeleka waziri 

Helmet kumkabidhi kwa rais.Atakuwa katika mikono 

salama zaidi akiwa ikulu” 

“Vipi kuhusu hapa nyumbani 

tutawaacha Dr Robert na wanae 

peke yao? 

“Hapana hawatakuwa peke 

yao.Kuna ulinzi mkubwa upo 

hapa.Hamis Chuma na wenzake 

wanalinda hapa usiku wa leo.Hata 

hivyo hatutachukua muda mrefu 

tutarejea bado tuna mazungumzo 

na Dr Robert,ameahidi kunieleza 

mambo mengi makubwa endapo 

nitamsaidia kuondoka nchini yeye 

na familia yake” 

“Umemuahidi kumsaidia 

kuondoka nchini? 

“Sijamuahidi chochote lakini 

itategemea na uzito wa kile atakachonieleza” akasema Mathew 

na kumfuata Helmet 

“Mheshimiwa waziri 

tunakuondoa hapa kama 

nilivyokueleza na tunakupeleka 

sehemu salama” akasema Mathew 

“Mnanipeleka wapi? Sitaki 

mnipeleke katika ubalozi au 

taasisi yoyote yenye mahusiano na 

Marekani!! Akasema Helmet kwa 

hasira 

“Hapana hatutakupeleka 

huko,tunakupeleka katika mikono 

salama ambako Marekani 

hawataweza kukupata kirahisi.Sisi 

uwezo wetu wa kuendelea 

kukuweka salama ni mdogo na 

hivyo unahitaji kuwepo katika 

mikono yenye uwezo mkubwa zaidi wa kuhakikisha unakuwa 

salama.Naamini Marekani 

wakisikia uko hai bado na 

umefahamu mpango wao wa 

kutaka kukuua wataendelea 

kukusaka usiku na mchana hadi 

wahakikishe wametimiza azma 

yao” akasema Mathew na 

kumchukua waziri Helmet 

wakaondoka na kuacha nyumba 

ikiwa chini ya ulinzi wa Hamis 

Chuma na vijana wake 

“Dr Robert yuko wapi? 

“Hatufahamu mahala aliko 

kwa sababu ya ule mvurugano 

uliotokea pale uwanja wa ndege 

baada ya bomu kulipuka” 

“kwa hiyo lile bomu ninyi ndio 

mliolitega? “Ndiyo.Ilitulazimu kutega 

bomu lile kwa lengo la kuzua 

taharuki pale uwanjani ili tuweze 

kukupata kabla haujatoka nje ya 

uwanja ambako kuna watu 

walikuwa wameandaliwa 

kukuua.Tunawafahamu watu hao 

na hoteli walikofikia na usiku huu 

tutahakikisha wote 

wanakamatwa” 

“kwa nini lakini Dr Robert 

hakunieleza kuhusiana na mpango 

huu wa kuniua? Yule ni rafiki 

yangu na kama angenieleza 

mapema nisingekuja Tanzania” 

“Inawezekana aliupata 

mpango ule katika dakika za 

mwisho kabisa ndiyo maana hakukueleza mapema” akasema 

Mathew na safari ikaendelea. 

******************** 

Taarifa za kulipuka kwa bomu 

katika uwanja wa ndege wa 

kimataifa wa Julius Nyerere muda 

mfupi tu baada ya waziri wa 

mambo ya nje wa Marekani Helmet 

Brian kuwasili nchini Tanzania 

zilisambaa kwa kasi kubwa na 

vyombo vingi vya habari duniani 

vilitangaza kutokea kwa tukio lile 

.Taarifa zile ziliwasua sana 

wamarekani kwani waliamini 

tukio lile lilikuwa limemlenga 

waziri wao Helmet Brian na wengi 

walianza kuinyooshea vidole Korea Kaskazini na serikali ya 

Tanzania kwamba wanahusika 

katika tukio lile.Dakika thelathini 

baada ya shambulio lile kutokea 

Mike straw rais wa Marekani 

akatoa hotuba fupi kwa taifa yenye 

lengo la kuwatuliza na kuwaondoa 

hofu wamarekani kufuatia tukio 

lile liliotokea nchini Tanzania 

“Wamarekani wenzangu” 

ndivyoMike straw alivyoanza 

hotuba yake 

“Muda mfupi uliopita 

nimepokea taarifa kwamba 

umetokea mlipuko wa bomu 

katika uwanja wa ndege wa 

kimataifa wa Julius Nyerere nchini 

Tanzania dakika chache baada ya 

waziri wetu wa mambo ya nje 

Helmet Brian kuwasili uwanjani 

hapo.Nilimtuma Helmet 

aendeTanzania katika jitihada za 

kumshawishi rais wa Tanzania 

asitishe mpango wake wa 

kuanzisha mashirikiano na nchi ya 

Korea kaskazini. 

Tunasubiri kupata taarifa 

rasmi toka serikali ya Tanzania 

kuhusiana na watu wetu kama 

wako salama na hakuna yeyote 

aliyepoteza maisha katika mlipuko 

huo,hata hivyo wakati tukisubiri 

taarifa kutoka serikali ya Tanzania 

nitatuma kikosi cha watu kumi na 

tano kwenda Tanzania 

kuchunguza suala hili na kupata 

majibu ya uhakika ni nani hasa 

waliohusika katika shambulio lile.Suala hili linatuhusu sisi hivyo 

linapaswa kuchunguzwa na 

vyombo vyetu wenyewe hivyo 

naamini serikali ya Tanzania 

watatoa ushirikiano kwa watu 

wetu ili waweze kufanikisha 

uchunguzi wa jambo hili na 

mwisho kumleta waziri wetu 

Helmet na wote aliombatana nao 

nyumbani 

Napenda kutoa angalizo kwa 

wale wote waliofanya tukio hili 

waanze kutafuta sehemu ya 

kwenda kujificha kwani 

hakutakuwa na huruma kwa 

yeyote aliyeshiriki katika jambo 

hili la kuhatarisha usalama wa 

watu wetu.Taifa lolote lenye 

mkono wake katika jambo hili liwe kubwa au dogo litalipa uovu wao 

na tutawaonyesha hasira 

zetu.Hatutafumba macho hadi mtu 

wa mwisho aliyehusika katika 

shambulio hili atakapoadhibiwa 

vikali.Narudia tena taifa lolote lile 

ambalo lina mkono wake katika 

jambo hili tutaliharibu vibaya. 

Nawaomba wamarekani 

muwe watulivu suala hili 

linashughulikiwa kikamilifu na 

mtafahamishwa kila 

kinachoendelea. 

Mungu ibariki Marekani 

Ilikuwa ni hotuba fupi lakini 

iliyobeba ujumbe mzito.Mataifa 

mengine yaliungana na Marekani 

kutoa matamko ya kulaani 

shambulio lile na kutaka hatua kali zichukuliwe kwa yeyote 

aliyehusika katika shambulio lile 




Mathew na Camilla wakiwa na 

waziri Helmet Brian waliwasili 

katika hospitali ya Mt Clara 

ambako Theresa alipelekwa baada 

ya kushambuliwa kwa 

risasi.Mathew akashuka na 

kuwataka Camilla na Helmet 

wabaki garini,akaenda mapokezi 

akauliza kuhusu hali ya 

Theresa.Dada aliyekuwepo 

mapokezi akabonyeza kompyuta 

yake na kusoma orodha ya 

wagonjwa kisha akasema “Mgonjwa Theresa Matope 

hatuwezi kukupa taarifa zake 

labda uonane na daktari mkuu wa 

zamu” akasema yule mwanadada 

na kumuelekeza Mathew ilipo ofisi 

ya daktari mkuu wa zamu usiku 

ule akaenda haraka na kugonga 

mlango akaruhusiwa kuingia 

ndani.Alimkuta daktari mmoja 

kijana wakasalimiana 

akajitambulisha kisha akaeleza 

shida yake 

“Utanisamehe ndugu yangu 

kwani sintaweza kukuruhusu 

kwenda kumtazama mgonjwa 

huyo hadi hapo utakapopata kibali 

cha rais kwani ndiye aliyetoa 

maelekezo hayo kwamba mtu 

yeyote asiruhusiwe kuingia katika chumba cha Theresa kama si 

mwanafamilia .Ni 

madaktari,wauguzi na wanafamilia 

pekee ambao wanaruhusiwa 

kuingia katika chumba alimolazwa 

Theresa” 

“Daktari mimi ndiye 

niliyemleta hapa Theresa baada ya 

kushambuliwa na hata rais 

mwenyewe ananifahamu 

vyema.Naomba tafadhali 

uniruhusu ndugu yangu 

nikamtazame Theresa” akasema 

Mathew lakini msimamo wa 

daktari uliendelea kuwa pale pale 

kwamba akitaka kumuna Theresa 

lazima apate kwanza kibali cha 

rais “Ahsante daktari” akasema 

Mathew na kuondoka akaelekea 

katika gari lake 

“Theresa anaendeleaje? 

Akauliza Camilla 

“Sijaruhusiwa kumuona.Ili 

kuingia katika chumba alimolazwa 

lazima upate kibali toka kwa 

rais.Ameelekeza mtu yeyote 

ambaye si mwanafamlia 

asiruhusiwe kuingia” akasema 

Mathew 

“Tunamsubiri nani hapa 

hospitali? Waziri Helmet akauliza 

“Kuna mtu tunamsubiri hapa” 

akajibu Mathew na ukimya 

ukaendelea kutawala 

garini.Zilipita dakika ishirini toka 

wawasili pale hospitali mara kikasikika king’ora cha polisi na 

rais akawasili.Mathew akashuka 

na kumfuata rais. 

“Vipi hali ya Theresa? 

Anaendeleaje?Mimi nimezuiliwa 

kwenda kumtazama kwa kuwa si 

mwanafamilia.Mheshimiwa rais 

naomba kibali cha kuweza kufika 

na kumuona Theresa bila vikwazo” 

akasema Mathew baada ya 

kuonana na rais 

“Nimetaarifiwa hali yake bado 

si nzuri.Ametolewa katika chumba 

cha upasuaji ila bado 

hajitambui.Nimetoa maelekezo 

kwa uongozi wa hospitali 

asiruhusiwe mtu yeyote kuingia 

katika chumba cha Theresa kama 

si mwanafamilia ili kuhakikisha ndugu yangu anakuwa salama ” 

akasema rais na akatokea daktari 

mkuu wa zamu usiku ule ambaye 

alistuka sana alipomuona Mathew 

akiwa amesimama na rais 

wakizungumza.Daktari yule 

akajitambulisha na rais akamtaka 

waelekee katika chumba alimo 

Theresa 

“Daktari” akaita rais wakati 

wakielekea katika chumba 

alimolazwa Theresa 

“Huyu niliyeongozana naye 

anaitwa Mathew ni mtu wa karibu 

sana na familia yetu kwa hiyo 

naomba aruhusiwe muda wowote 

akija hapa hospitali kumuona 

Theresa” akasema Rais na yule 

daktari akaitika kwa adabu Waliingia katika chumba 

alimo Theresa bado alikuwa 

amezungukwa na mashine kadhaa 

zikimsaidia kuendesha mifumo 

kadhaa ya mwili ambayo bado 

ilikuwa dhaifu. 

“Mungu atakuponya Theresa 

na utakuwa mzima tena.Siwezi 

kujisamehe kwa sababu yote haya 

yaliyotokea mimi ndiye 

chanzo.Sikumlinda ipasavyo” 

akawaza Mathew wakati daktari 

akimpa rais maelezo kuhusiana na 

maendeleo ya Theresa.Walitoka 

mle chumbani na rais akamuomba 

Mathew waelekee katika gari lake 

kwa ajili ya 

mazungumzo.Wakaingia katika gari la rais na Dr Vivian akafuta 

machozi. 

“Kila nikimuona Theresa 

akiwa katika hali ile ninaumia 

sana.Nadhani sasa ni wakati 

wakufahamu nini hasa 

kilichomtokea mdogo wangu? Nani 

aliyetaka kuondoa uhai wake? 

Tafadhali nieleze Mathew nahitaji 

kujua kilichotokea” akasema rais 

“Pole sana mheshimiwa rais 

lakini nakuhakikishia kwamba 

Theresa atapona tu.Sote 

tunamuombea na Mungu atasikia 

dua zetu na atamponya” akasema 

Mathew na rais akafuta tena 

machozi. 

“Mathew naamini umesikia 

kilichotokea usiku huu katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa 

Julius Nyerere.Kufuatia tukio hilo 

nilitakiwa kuwa katika kikao 

muhimu sana muda huu kujadili 

kilichotokea na hali ya amani hapa 

nchini lakini nimelazimika 

kuahirisha kila kitu na kuja 

kukusikiliza.Naomba tusipoteze 

muda nieleze mara moja kile 

ulichoniitia hapa” akasema rais 

“Kwanza nakupa pole nyingi 

kwa matukio yaliyotokea 

leo.Ninakushukuru pia kwa 

kukubali mwito wangu na kuja 

kunisikiliza.Kama nilivyokueleza 

ni kwamba nisingeweza kukuomba 

uahirishe shughuli zako kama 

jambo lenyewe halingekuwa na 

umuhimu mkubwa.” “Ni jambo gani Mathew nenda 

moja kwa moja katika pointi sitaki 

mizunguko kwa muda huu.Kichwa 

changu kina mambo mengi sana” 

akasema Dr Vivian 

“Ni kuhusiana na kilichotokea 

uwanja wa ndege wa Julius 

Nyerere.” Akasema Mathew na 

DrVivian akamtumbulia macho 

“Mimi ndiye ninayehusika na 

kilichotokea pale uwanja wa 

ndege.Mimi ndiye niliye lipua lile 

bomu” 

Dr Vivian akamtazama 

Mathew kwa mshangao mkubwa 

kama vile ni mara yake ya kwanza 

anamuona. 

“You ?!! akauliza 

akimnyooshea kidole “Ndiyo mheshimiwa rais,mimi 

ndiye niliyehusika” akasema 

Mathew na Dr Vivian akashusha 

pumzi. 

“Kwa mara ya kwanza 

nimekosa neno la kusema!! 

Akasema Dr Vivian 

“Hutakiwi kusema kitu 

mheshimiwa rais mimi ndiye 

mwenye kitu cha 

kusema.Nimefanya tukio lile kwa 

ajili ya kumuokoa waziri wa 

mambo ya nje wa Marekani Helmet 

Brian asiuawe.Niligundua kuwepo 

kwa mpango wa kumuua Helmet 

uliopangwa na serikali ya 

marekani kwa kushirikiana na 

washirika wao wa hapa Tanzania” “Serikali ya Marekani 

wanataka kumuua waziri wao wa 

mambo ya nje? Akauliza Dr Vivian 

kwa mshangao 

“Ndiyo madam president” 

“That’s not true.Kwanza kwa 

nini wafanye hivyo? Hiyo siyo 

namna Marekani wanavyofanya 

mambo yao” 

“Huo ndio ukweli 

mheshimiwa rais kwamba 

Marekani walipanga mauaji ya 

waziri wao wa masuala ya nje kwa 

lengo la kupata sababu ya 

kuishambulia Korea 

kaskazini.Kuna watu ambao 

wameandaliwa maalum kwa kazi 

hiyo ya kumuua Helmet na baada 

ya kumuua Marekani wangetuma wachunguzi wao kuja Tanzania na 

wangewakamata watu hao na 

baada ya kuwahoji watu hao 

wangekiri kutumwa na serikali ya 

Korea Kaskazini kumuua Helmet 

na hapo marekani wangeanza 

kuishambulia Korea kaskazini kwa 

kigezo cha kulipiza kisasi” 

“Mathew natamani sana 

nikuamini lakini naogopa 

kukuamini kwa sababu jambo hili 

ni kubwa na sidhani kama 

Marekani wanaweza kuwa tayari 

kumuua waziri wao wenyewe” 

“Mheshimiwa rais jambo hili 

nina uhakika nalo na nimelipata 

kutoka kwa mtu ambaye marekani 

wamekuwa wakimtumia kuratibu 

hili suala kwa hapa Tanzania ambaye huwezi kuamini 

nikikutajia” 

“Ni nani? Akauliza rais huku 

sura yake ikionyesha wasi wasi 

“Ni mtu wako wa karibu 

ambaye uko tayari kufanya kila 

uwezalo kumlinda.Ni Dr Robert 

Mwainamela” akasema Mathew na 

mstuko alioupata Dr Vivian 

ulikuwa mkubwa sana.kwa dakika 

nzima alikuwa anamtazama 

Mathew 

“I cant believe you Mathew!! 

akasema 

“Mheshimiwa rais 

sikulazimishi uniamini lakini huo 

ndio ukweli wenyewe.Dr Robert 

ndiye aliyekuwa akiratibu mpango 

huo wa kumuua Helmet na amekuwa akitumiwa na serikali ya 

marekani katika mipango yake 

mbalimbali hapa nchini” 

“Mathew are you sure of this? 

Akauliza rais 

“Madam president kuna kitu 

kimoja ambacho hukifahamu 

kuhusu mimi,I’m always 

right.Nikikuambia mtu fulani 

anapaswa kuchunguzwa amini 

kuna kitu tayari 

nimekiona.Nilikuomba 

nimchunguze Dr Robert lakini 

ukamtetea kwa nguvu kubwa ila 

ungefahamu mambo anayoyafanya 

DrRobert nyuma yako ungeanguka 

na kuzimia” akasema Mathew. 

“Yuko wapi hivi sasa Dr 

Robert? “Ninaye bado namfanyia 

mahojiano.Kuna mambo mengi 

nahitaji kuyafahamu kutoka 

kwake na baada ya kukamilisha 

uchunguzi wangu nitakuja 

kukueleza kama utakuwa tayari 

lakini kuna jambo lingine la 

muhimu ambalo ningependa 

ulifahamu.Mwanamke aliyeletwa 

ofisini kwako akitambulishwa 

kama Tausi mtoto wa marehemu 

mzee Anorld Mubara ni pandikizi 

la Marekani na hana mahusiano 

yoyote na mzee 

Mubara.Ulidanganywa.Tausi 

Mubara si jina lake halisi ni jina 

bandia.Jina lake halisi anaitwa 

Olivia na hata vyeti vyote 

alivyokuja kuwaonyesha ni bandia hajawahi kusoma katika shule na 

vyuo alivyoorodhesha.Kwa kifupi 

ni kwamba Tausi ni pandikizi la 

CIA.Baada ya Nathan CIA 

wakamleta Tausi.Huyu Tausi na Dr 

Robert wamekuwa na mawasiliano 

ya karibu na wamekuwa pamoja 

katika mpango huu wa kumuua 

Helmet Brian.Nafahamu haitakuwa 

rahisi kuniamini lakini huo ndio 

ukweli na ninaomba ufahamu pia 

kwamba Tausi tayari 

amefariki,amejipiga risasi na ndiye 

aliyempiga risasi Theresa” 

“No !! That’s not true !! 

akasema Rais 

“Ni vigumu kuamini lakini huo 

ndio ukweli wenyewe.Sasa twende 

katika gari langu kuna kitu nataka nikuonyeshe” akasema Mathew na 

kufungua mlango akashuka.Rais 

akamtaka amsubiri kwa muda 

.Baada ya dakika nne rais 

akashuka wakaelekea katika gari 

la Mathew,akafungua mlango na 

kuwasha taa 

“Madam president 

ninakukabidhi waziri wa mambo 

ya nje wa Marekani Helmet Brian 

akiwa mzima na hana hata 

mchubuko.Ana hitaji ulinzi 

mkubwa kwani bila kufanya hivyo 

marekani lazima watamuua” 

“Oh Jesus Christ !!akasema Dr 

Vivian 

“Mheshimiwa waziri 

nakuomba ushuke garini.Kuanzia 

sasa utakua chini ya uangalizi wa rais yeye atakupa ulinzi wa 

uhakika zaidi” akasema Mathew na 

waziri Helmet akashuka garini 

akasalimiana na Dr Vivian.Mathew 

akatoa karatasi mfukoni na 

kumpatia rais 

“Madam president hawa ni 

raia wa kigeni waliotumwa kuja 

kumuua waziri Helmet.Majina ya 

hoteli walizofikia yameandikwa na 

tuna imani bado hawajatoka 

nchini.Watu hawa watafutwe 

haraka sana wakamatwe na 

wataeleza ukweli wote kuhusiana 

na mpango huu wa kumuua waziri 

Helmet.Ahsante mheshimiwa rais 

kwa kunisikiliza” akasema Mathew 

na kuagana na waziri Helmet 

ambaye aliwashukuru kwa kumuokoa akaingia garini 

wakaondoka akimuacha rais akiwa 

amesimama akilitazama gari la 

Mathew likiondoka. 

“Kwa sasa waziri Helmet yuko 

katika mikono salama.Kazi yetu 

sisi tumeimaliza na kilichobaki ni 

jambo la kiserikali 

zaidi.Tunakwenda kuendelea na 

uchunguzi wetu.Kuna mambo 

mengi tunakwenda kuyafahamu 

kwa Dr Robert” akasema Mathew 

na simu yake ikapigwa alikuwa ni 

Hamis Chuma.Mathew akaipokea 

haraka 

“Mathew ..Mathew..!!.” 

akasema Hamis 

“Hamis kuna nini? Akauliza 

Mathew “Mathew tumevamiwa na 

kundi la watu wenye silaha nzito 

vijana wangu wawili wote 

wameuawa na mimi nimefanikiwa 

kukimbia lakini nimejeruhiwa 

mguuni kwa risasi.” 

“Vipi kuhusu Dr Robert?!!! 

Akauliza Mathew 

“Sijui kilichoendelea huko 

ndani kwani baada ya 

kutushambulia mimi nilikimbia na 

sijui kilichoendelea” akasema 

Hamis 

“Hamis uko wapi hivi sasa? 

“Tayari nimewaita vijana 

wangu wamenichukua 

wananipeleka hospitali.Jeraha 

linamwaga damu nyingi” “Pole sana Hamis.Mimi 

ninaelekea huko nyumbani sasa 

hivi”akasema Mathew na kukata 

simu akaongeza mwendo wa gari. 

“Kuna jambo limetokea 

nyumbani.Watu wenye silaha 

wamevamia,wameua walinzi 

tuliowaacha na kwa bahati nzuri 

Hamis Chuma amefanikiwa 

kutoroka lakini amejeruhiwa na 

risasi mguuni” 

“Oh Mungu wangu !! Ni akina 

nani hao? Vipi kuhsu DrRobert na 

wanae? Akauliza Camilla ambaye 

alistushwa sana na taarifa 

ile.Mathew hakujibu kitu 

akaongeza mwendo wa gari 

kuwahi nyumbani kwake “Naamini waliovamia 

nyumbani kwangu ni ule 

mtandanowa CIA hapa 

nchini.Yawezekana tayari 

wamefahamu kwamba waziri 

Helmet yuko nyumbani kwangu na 

wamevamia ili 

kumchukua.Lilikuwa wazo zuri 

kuamua kumpeleka waziri Helmet 

na kumkabidhi kwa rais.Wasiwasi 

wangu ni kwa Dr Robert.Endapo 

wakimkuta mle ndani 

watamchukua na kumtorosha na 

sintopata yale mambo yote 

muhimu toka kwake” akawaza 

Mathew 

Waliwasili nyumbani kwa 

Mathew na kukuta nyumba yake imezingirwa na askari wenye 

silaha 

“Askari polisi tayari 

wamekwisha pata taarifa za 

kilichotokea hapa 

nyumbani.Inawezekana majirani 

waliwapigia simu na wakafika kwa 

haraka kuwadhibiti wale wavamizi 

waliovamia” akasema Mathew 

huku akifungua mlango na 

kushuka.Askari mmoja 

akamsimamisha na kumtaka 

ajitambulishe yeye ni nani.Mathew 

akajitambulisha kwamba yeye 

ndiye mmiliki wa ile nyumba na 

hakuwepo nyumbani wakati 

ilipovamiwa.Mara moja akasikia 

vyuma vikilia askari walikuwa wanaweka sawa silaha zao.Mmoja 

wa askari wale akamsoglea karibu. 

“Mathew Mulumbi uko chini 

ya ulinzi kwa mauaji ya waziri wa 

mambo ya ndani ya nchi na 

kuwateka watoto wake na 

kuwafungia chumbani” akasema 

yule askari na kumsogelea Mathew 

akamtaka ainue mikono 

juu.Mathew alihisi miguu 

inaishiwa nguvu.Askari yule 

akamsogelea akamshika mkono 

akamfunga pingu na kumtaka 

apige magoti.Mathew hakuwa na 

ujanja tayari alikuwa katika 

mikono ya polisi.Haraka haraka 

akasachiwa na silaha zake zote 

zikachukuliwa.Askari 

wakalisogelea gari la Mathew na kumtaka Camilla ashuke 

garini.Akatii na kufungua mlango 

akashuka.Akasachiwa na 

hakukutwa na silaha 

yoyote.Akapigishwa magoti 

pembeni ya Mathew na muda huo 

huo askari wakatoka ndani 

wakiwa wamebeba mwili katika 

machela ukiwa umefunikwa 

shuka.Nyuma ya mwili ule 

wakatokea watoto wawili wa Dr 

Robert Juliana na Julieth wakiwa 

wameshikwa mikono na askari 

huku wakilia kwa nguvu.Camilla 

machozi yakamtoka alipowaona 

watoto wake wakilia. 




Mathew Mulumbi uko chini 

ya ulinzi kwa mauaji ya waziri wa 

mambo ya ndani ya nchi na 

kuwateka watoto wake na 

kuwafungia chumbani” akasema 

yule askari na kumsogelea Mathew 

akamtaka ainue mikono 

juu.Mathew alihisi miguun inaishiwa nguvu.Askari yule 

akamsogelea akamshika mkono 

akamfunga pingu na kumtaka 

apige magoti.Mathew hakuwa na 

ujanja tayari alikuwa katika 

mikono ya polisi.Haraka haraka 

akasachiwa na silaha zake zote 

zikachukuliwa.Askari 

wakalisogelea gari la Mathew na 

kumtaka Camilla ashuke 

garini.Akatii na kufungua mlango 

akashuka.Akasachiwa na 

hakukutwa na silaha 

yoyote.Akapigishwa magoti 

pembeni ya Mathew na muda huo 

huo askari wakatoka ndani 

wakiwa wamebeba mwili katika 

machela ukiwa umefunikwa 

shuka.Nyuma ya mwili ule wakatokea watoto wawili wa Dr 

Robert Juliana na Julieth wakiwa 

wameshikwa mikono na askari 

huku wakilia kwa nguvu.Camilla 

machozi yakamtoka alipowaona 

watoto wake wakilia. “Yuko wapi hivi sasa Dr 

Robert? 

“Ninaye,bado namfanyia 

mahojiano.Kuna mambo mengi 

nahitaji kuyafahamu kutoka 

kwake na baada ya kukamilisha 

uchunguzi wangu nitakuja 

kukueleza kama utakuwa 

tayari,lakini kuna jambo lingine la 

muhimu ambalo ningependa 

ulifahamu.Mwanamke aliyeletwa 

ofisini kwako akitambulishwa 

kama Tausi mtoto wa marehemu 

mzee Anorld Mubara ni pandikizi 

la Marekani na hana mahusiano 

yoyote na mzee Mubara.Ulidanganywa.Tausi 

Mubara si jina lake halisi ni jina 

bandia.Jina lake halisi anaitwa 

Olivia na hata vyeti vyote 

alivyokuja kuwaonyesha ni bandia 

hajawahi kusoma katika shule na 

vyuo alivyoorodhesha.Kwa kifupi 

ni kwamba Tausi ni pandikizi la 

CIA.Baada ya Nathan,CIA 

wakamleta Tausi.Huyu Tausi na Dr 

Robert wamekuwa na mawasiliano 

ya karibu na wamekuwa pamoja 

katika mpango huu wa kumuua 

Helmet Brian.Nafahamu haitakuwa 

rahisi kuniamini lakini huo ndio 

ukweli na ninaomba ufahamu pia 

kwamba Tausi tayari 

amefariki,amejipiga risasi na ndiye 

aliyempiga risasi Theresa” “No !! That’s not true !! 

akasema Rais 

“Ni vigumu kuamini lakini huo 

ndio ukweli wenyewe.Sasa twende 

katika gari langu kuna kitu nataka 

nikuonyeshe” akasema Mathew na 

kufungua mlango akashuka.Rais 

akamtaka amsubiri kwa 

muda.Mathew akashuka na 

kumuacha Dr Vivian peke yake 

garini.Dr Vivian akavuta pumzi 

ndefu na kuufunika uso wake kwa 

viganja vya mikono 

“Oh my God!! Its getting ugly” 

akanong’ona 

“Nilimzuia Mathew asiendelee 

na upelelezi wake baada ya kuona 

mwenendo wake si 

mzuri.Niling’amua anakoelekea si kuzuri hata kidogo na anaweza 

akavuka mstari na akafahamu 

mambo ambayo hapaswi 

kuyafahamu lakini yule jamaa ni 

mkaidi sana na hakubali 

kushindwa ameendelea na 

upelelezi wake licha ya kumkataza 

na tayari amekwisha kanyaga 

mstari.Kitendo cha kumshikilia Dr 

Robert ni ishara tosha kwamba 

amekanyaga mstari na muda si 

mrefu anaweza akauvuka jambo 

ambalo sitaki litokee.Nilipomtaka 

achunguze kuhusu mauaji ya baba 

yangu sikutegemea kama angefika 

hapa alipofiuka.Naikubali sana 

kazi yake,ni mtu shupavu na 

amefanya makubwa na anastahili 

pongezi hasa kwa hili alilolifanya leo la kumuokoa waziri wa Helmet 

Brian asiuawe kwani endapo 

mpango huo ungefanikiwa basi 

Marekani wangepata sababu ya 

kuishambulia Korea kaskazini na 

ingeibuka vita kubwa na ule 

mpango wetu wa mashirikiano ya 

kibiashara na Korea Kaskazini 

ungeishia hewani.Namshukuru 

sana Mathew kwa hilo lakini sina 

budi kutumia uwezo wangu 

kumsimamisha asiendelee na 

uchunguzi wake kwani mahala 

alipofika hatakiwi kuendelea 

mbele zaidi.Uchunguzi wa kifo cha 

baba ameuweka pembeni na 

ameingia katika mambo mengine 

kabisa yasiyohusiana na jambo 

nililomtaka achunguze.Mdogo wangu Theresa uhai wake 

unashikiliwa na mashine hivi sasa 

na yote hii ni kwa sababu yake.I 

must stop him !! akawaza Dr Vivian 

na kuchukua simu akampigia 

mkurugenzi wa idara ya usalama 

wa taifa Meshack Jumbo. 

“Madam president” akasema 

Meshack Jumbo baada ya kupokea 

simu 

“Meshack naomba usogee 

pembeni mahala kusiko na watu 

nina mazungmzo nawe ya muhimu 

sana” akasema rais na baada ya 

skeunde chache Meshack akasema 

“Endelea madam president” 

“Naomba unisikilize kwa 

makini na ninaomba yalenitakayoelekeza yafanyike kwa 

haraka sana” 

“Sawa mheshimiwa rais 

nitafanya kama utakavyoelekeza.” 

Akasema Meshack Jumbo 

“Hivi tuongeavyo waziri wa 

mambo ya nje wa Tanzania Dr 

Robert Mwainamela anashikiliwa 

nyumbani kwa Mathew.Muda 

mfupi ujao Mathew atamfanyia 

mahojiano na ninaamini kuna 

mambo ambayo Dr Robert 

atamuleza ambayo Mathew 

hapaswi kuyafahamu” akanyamaza 

kwa sekunde tano na kuendelea 

“Mr Jumbo sitaki jambo hili 

litokee.Sitaki Mathew amfanyie 

mahojiano Dr Robert.Haraka sana 

nataka utume watu nyumbani kwa Mathew wakamuue Dr Robert.Kwa 

sasa Mathew niko naye hapa St 

Clara hospital na akitoka hapa 

atarejea nyumbani kwake 

kumuhoji Dr Robert.Siaki amkute 

akiwa bado hai.Naomba sana 

jambo hili litekelezwe haraka” 

akasema Dr Vivian 

“Madam president …” akataka 

kusema kitu Meshack Jumbo lakini 

rais akamzuia. 

“Mzee Jumbo nafahamu 

unachotaka kukisema lakini 

sihitaji maelezo au ushauri 

wowote katika hili.Naomba 

litekelezwe haraka sana kama 

ninavyoagiza,hili si ombi bali ni 

amri.Umenielewa Jumbo? “Mheshimiwa rais,wewe ni 

kiongiozi wangu ambaye 

ninapaswa kutii kila 

unachoniagiza lakini katika hili 

ninapatwa na kigugumizi 

kidogo.Kwanza ni kuhusiana na Dr 

Robert.Huyu ni waziri wetu wa 

mambo ya nje kwa nini 

tumuue?Pili Mathew ni kijana 

wangu ninamfahamu vyema 

hakurupuki katika kufanya kazi 

zake .Anafahamu 

anachokifanya,tena kuna 

uwezekano mkubwa Dr Robert 

akawa anahusika katika suala 

analolifanyia uchunguzi hivi 

sasa,huoni kama tukimuondoa Dr 

Robert atashindwa kupata mambo 

muhimu katika uchunguzi wake? “Meshack sitaki kurudia suala 

hili mara mbili,naomba ulifanyie 

kazi suala hilo na unijulishe 

litakapokuwa tayari.Kabla ya 

Mathew kurejea nyumbani kwake 

nataka Dr Robert awe tayari 

amekwisha malizwa na unijulishe 

pindi zoezi hilo 

likikamilika.Naomba usiondoke 

hapo ikulu kwani nitakuwa na 

mazungumzo nawe nitakaporejea” 

akasema Dr Vivian 

“madam president..” 

“Meshack fanya hivyo 

nilivyokuelekeza tafadhali !! 

akasema Dr Vivian na kukata 

simu.Akavuta pumzi ndefu 

“Yote haya ameyataka Mathew 

mwenyewe kwa ukaidi wake.Nilimzuia asiendelee na 

uchunguzi akanipuuza na 

akaendelea kwa siri na sasa 

anataka kuingia mahala 

asikotakiwa kufika na sina namna 

nyingine ya kufanya zaidi ya 

kutumia uwezo wangu kumzuia 

asiende mbele zaidi na kufika 

huko asikotakiwa”akawaza Dr 

Vivian na kushuka garini 

akaongozana na Mathew hadi 

katika gari lake akafungua mlango 

na kuwasha taa 

““Madam president 

ninakukabidhi waziri wa mambo 

ya nje wa Marekani Helmet Brian 

akiwa mzima na hana hata 

mchubuko.Anahitaji ulinzi mkubwa kwani bila kufanya hivyo 

Marekani watamuua” 

“Oh Jesus Christ !!akasema Dr 

Vivian 

“Mheshimiwa waziri 

nakuomba ushuke garini.Kuanzia 

sasa utakua chini ya uangalizi wa 

rais yeye atakupa ulinzi wa 

uhakika zaidi” akasema Mathew na 

waziri Helmet akashuka garini 

akasalimiana na Dr Vivian.Mathew 

akatoa karatasi mfukoni na 

kumpatia rais 

“Madam president hawa ni 

raia wa kigeni waliotumwa kuja 

kumuua waziri Helmet.Majina ya 

hoteli walizofikia yameandikwa na 

tuna imani bado hawajatoka 

nchini.Watu hawa watafutwe haraka sana wakamatwe na 

wataeleza ukweli wote kuhusiana 

na mpango huu wa kumuua waziri 

Helmet.Ahsante mheshimiwa rais 

kwa kunipa nafasiya kunisikiliza” 

akasema Mathew na kumpa mkono 

waziri Helmet 

“Tafadhali naomba 

unikumbushe jina lako” akasema 

Helmet 

“Naitwa Mathew Mulumbi” 

“Mathew ahsante sana kwa 

kuyaokoa maisha yangu leo.Sina 

neno zuri la kukushukuru kwa hili 

ulilolifanya.Taifa la Tanzania 

linapaswa kujivunia sana kuwa na 

mtu mahiri kama wewe.Nifikishie 

salamu zangu na shukrani za 

pekee kabisa kwa wenzako wote mlioshirikiana katika zoezi hili na 

ninawaahidi baada ya sakata hili 

kumalizika salama nitahitaji 

kuonana nanyi wote niwashukuru 

kwa pamoja.” Akasema Helmet 

“Ahsante sana mheshimiwa 

waziri.Muda wowote ukihitaji 

kuonana nami utamueleza rais 

naye anajua mahala kwa kunipata” 

akasema Mathew na kuagana na 

Helmet akaingia garini 

wakaondoka akimuacha rais akiwa 

amesimama akilitazama gari la 

Mathew likiondoka 

“Mheshimiwa rais” akaita 

waziri Helmet baada ya kumuona 

rais Dr Vivian amezama mawazoni 

akilitazama gari la Mathew 

likipotea “Oh ! Mheshimiwa waziri” Dr 

Vivian akastuka 

“Pole sana kwa masahibu yote 

yaliyokupata.Ni jambo la 

kushangaza sana lililofanywa na 

serikali ya Marekani.Karibu 

Tanzania na hapa utakuwa 

salama” akasema Dr Vivian na 

kumuongoza Helmet hadi katika 

gari lake wakaondoka pale 

hospitali kuelekea ikulu 

“Mheshmiwa rais bado naona 

suala hili kama ndoto.Bado siamini 

kama kweli serikali yangu ambayo 

ninaitumikia kwa uadilifu mkubwa 

wanaweza kupanga mpango wa 

kuniua.Inashangaza 

sana.Nimejiuliza maswali elfu moja 

kwa nini wafanye hivi sijapata jibu hata moja.Nakuomba mheshimiwa 

rais uchunguzi wa kina ufanywe 

kuhusiana na jambo hili ili ukweli 

ubainike” akasema Helmet 

“Mheshimiwa waziri,sina 

mashaka hata kidogo na Mathew ni 

mmoja wa watu ninaowamini mno 

na kama amegundua kuwepo kwa 

mpango huu wa kukuua 

ulioandaliwa na Marekani basi 

amini ni kitu cha kweli lakini hata 

hivyo uchunguzi wa kina lazima 

ufanyike ili tufahamu ni kwa nini 

wamefanya hivi.Nitalikabidhi suala 

hili kwa vyombo vyangu vya 

uchunguzi ili haraka sana 

uchunguzi uanze na ukweli 

ubainike” akasema Dr Vivian “Ahsante sana mheshimiwa 

rais ila naomba kwa muda huu 

ambao uchunguzi utakuwa 

unaendelea jambo hili liwe siri na 

serikali ya Marekani 

isifahamishwe chochote.Sitaki 

wafahamu kama niko hai kwani 

kama walipanga kuniua na 

mpango wao ukashindikana 

wakijua niko hai watafanya kila 

namna hadi wafanikishe mpango 

wao.Uchunguzi utakapokamilika 

na ukweli kujulikana basi 

nitajitokeza” 

“Usijali kuhusu hilo 

mheshimiwa waziri,nitalizingatia” 

“Nashukur sana” akajibu 

Helmet na simu ya Dr Vivian ikaita 

alikuwa ni Meshack Jumbo “Nipe taarifa 

Meshack.Maagizo yangu 

yametekelezwa? Akauliza Dr 

Vivian 

“Ndiyo mheshimiwa 

rais,tayari maagizo yako 

yametekelezwa na Dr Robert 

amekwisha ondolewa” 

“Good.Niko njiani ninakuja 

ikulu nitakuwa na mazungmzo 

nawe hivyo usitoke hapo” akasema 

Dr Vivian na kukata simu 

akazitafuta namba za mkuu wa 

jeshi la polisi nchini Inspekta 

jenerali John Aminiel Mkoka 

akampigia 

“Mheshimiwa rais” akasema 

Inspekta jenerali John Mkoka “IGP nimepokea sasa hivi 

taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa 

idara ya usalama wa taifa Meshack 

Jumbo kwamba waziri wa mambo 

ya nje ya nchi wa Tanzania Dr 

Robert mwainamela ameuawa 

nyumbani kwa mtu mmoja ambaye 

amewahi kufanya kazi katika idara 

ya ujasusi.Naomba tafadhali 

elekeza jambo hili lifanyiwe kazi 

haraka sana na huyo mtu 

aliyefanya ukatili huo asakwe 

kokote aliko na akamatwe kabla ya 

kesho asubuhi.Onana na Mr 

Meshack Jumbo mkuu mpya wa 

idara ya usalama wa taifa yuko 

hapo ikulu atakuelekeza mahala 

yalipofanyika mauaji hayo” “Ahsante sana kwa taarifa hizi 

za kustusha mheshimiwa rais.Mr 

Jumbo niko naye hapa ikulu 

tukikusubiri,ngoja nizungumze 

naye mara moja” akasema mkuu 

wa jeshi la polisi. 

“Good” akajibu Dr Vivian na 

kukata simu 

Waliwasili ikulu rais 

akaongozana na Helmet hadi 

katika sebule yake 

“Helmet karibu katika makazi 

yangu ikulu.Hapa ni sehemu 

salama na tafadhali jisikie 

nyumbani.Endelea kupumzika 

hapa mimi bado nina majukumu 

mengine yananisubiri kwa wakati 

huu hivyo naomba nikuache kwa 

muda tutaonana baadae kidogo “Ahsante sana mheshmiwa 

rais.Kabla hujaondoka kuna kitu 

kimoja ninaomba 

nisaidiwe.Nahitaji kuwasiliana na 

familia yangu na kuwajulisha kuwa 

niko salama na wasihofu” 

“Sawa Helmet,wapo 

wahudumu hapa watakusaidia 

kwa chochote utakachohitaji” 

akasema Dr Vivian na 

kutoka.Kabla hajaingia katika 

kikao na wakuu wa vyombo vya 

usalama akamuita kwanza 

Meshack Jumbo wakaingia katika 

chumba cha mazungumzo ya 

faragha 

“Madam president ..” Meshack 

Jumbo akataka kusema kitu lakini 

rais akamzuia “Thank you 

Meshack.Nashukuru kwa 

kutekeleza agizo langu” 

“madam …” 

“Meshack kuna mambo mengi 

yananikabili usiku wa leo hivyo 

nina muda mchache wa maongezi 

nawe na ninaomba unisikie vizuri” 

akasema Dr Vivian ambaye sura 

yake haikuonyesha mzaha hata 

kidogo 

“Nimetoka kuonana na 

Mathew.Alinipigia simu na 

kunitaka nikaonane naye kuna 

jambo kubwa anataka kunieleza” 

Dr Vivian akanyamaza kwa muda 

halafu akaendelea 

“Tukio lililotokea usiku huu 

pale uwanja wa ndege JNIA anahusika nalo.Yeye ndiye 

aliyelifanya” 

“Mathew anahusika ?!! 

Meshack Jumbo akashangaa. 

“Ndiyo.Anadai kwamba 

aligundua mpango wa Marekani 

wa kutaka kumuua waziri Helmet 

Brian hapa Tanzania na lengo lao 

ni ili wapate sababu ya 

kuishambulia Korea kaskazini” 

akasema Dr Vivan na kutoa 

karatasi akampa Meshack 

“Hao watu watatu unaowaona 

picha zao katika hiyo karatasi ni 

wadunguaji walioletwa na 

Marekani hapa nchini kwa ajili ya 

kumuua Helmet.Baada ya 

kutekeleza jukumu lao hilo 

serikali ya Marekani ingewakamata halafu wangedai 

kwamba walitumwa kufanya 

hivyo na serikali ya Korea 

Kaskazini na hicho ndicho 

wanachokitafuta Marekani yaani 

kupata sababu ya kuishambulia 

kijeshi Korea Kaskazini.Watu hao 

bado wako hapa nchini na kabla ya 

mapambazuko nataka wawe tayari 

wametiwa nguvuni” 

“Dah ! Huyu kijana Mathew ni 

mtu wa ajabu sana.Amewezaje 

kugundua kuwepo kwa mpango 

mkubwa kama huu? Akauliza 

Meshack 

“Marekani wameshirikiana na 

watu wetu hapa ndani ili 

kufanikisha mpango huo na 

miongoni mwao ni viongozi serikalini.Huwezi kuamini Dr 

Robert ni mmoja wa watu 

waliokuwa wanatumiwa na 

Marekani katika kuufanikisha 

mpango huo” 

“Dr Robert?! Meshack Jumbo 

akashangaa 

“Ndiyo.Hata mimi nilistuka 

sana Mathew aliponiambia.Kumbe 

nimezungukwa na nyoka bila 

kujua. Dr Robert ni mmoja wa 

watu ninaowaamini mno.Uadilifu 

wake si wa kutiliwa 

shaka.Nilikuwa nafikiria hata 

kumpendekeza awe rais pale 

nitakapomaliza kipindi changu 

kumbe sikujua alikuwa ni chui 

aliyevaa ngozi ya kondoo.Mathew 

alikuja kwangu na kuniambia amchunguze Dr Robert lakini 

nikamkatalia kumbe kuna kitu 

tayari alikwishakiona kwa Dr 

Robert” akasema Dr 

Vivian.Meshack Jumbo 

akamtazama Dr Vivian kwa macho 

makali na kusema 

“Madam president kama 

Mathew amefanya mambo haya 

makubwa kwa nini basi 

ukamfanyia hivi 

ulivyomfanyia?Kwa nini ukaamua 

kumuua Dr Robert ambaye kumbe 

ni msaliti mkubwa na endapo 

Mathew angeendelea kumfanyia 

mahojiano angeweza kugundua 

mambo mengi makubwa?Marekani 

wametengeneza mtandao wao 

hapa nchini na kama Dr Robert ni mmoja wao basi angeweza 

kufunguka na kutuonyesha 

mtandao wake.Mathew ana mbinu 

nyingi za kumfanya mtu aweze 

kufunguka na kutoa taarifa 

muhimu lakini hukutaka kumpa 

nafasi,kwanza kuendelea na 

uchunguzi aliokuwa anaufanya 

kuhusu kifo cha baba yako ambao 

tayari alikwisha piga hatua 

kubwa.Pili hukutaka amuhoji Dr 

Robert ambaye ni mtu muhimu 

mno na ambaye angewezesha 

mambo mengi kujulikana lakini 

umeamua auawe.Kwa nini madam 

president? Wewe mwenyewe 

ulimpa kazi Mathew kwa nini 

hutaki afanikiwe kuikamilisha kazi 

uliyompa? Nahitaji kufahamu madam president kwa sababu 

Mathew ni kama mwanangu na 

katika kazi uliyompa aifanye toka 

mwanzo nimekuwa nikimsaidia 

sana na kwa sababu ya jambo hili 

nimepoteza nyumba yangu na 

nusura nipoteze maisha yangu na 

familia yangu hivyo ninahitaji sana 

kuona jambo hili linafika mwisho 

na watu hawa kujulikana ni akina 

nani na mtu pekee ambaye anao 

uwezo wa kulifikisha mwisho 

jambo hili ni Mathew ambaye hivi 

tunavyoongea atakuwa katika 

mikono ya polisi kwa maelekezo 

yako mheshimiwa rais.Umetoea 

maelekezo kwa IGP kwamba 

ahakikishe Mathew anakamatwa 

kwa kosa la kumuua waziri wa mambo ya nje Dr Robert 

Mwainamela.Madam president 

kwa nini unamuangamiza Mathew 

wakati unafahamu fika kwamba 

siye aliyemuua Dr Robert?Kwa 

kesi hii kubwa uliyomtwisha 

Mathew ni wazi hawezi kuponyoka 

na ninaweza kusema kwamba 

ndoto zake zote za maisha 

zimeishia hapa kwani ataozea 

gerezani,why madam president? 

Why are you destroying this 

innocent man? Amekufanyia nini 

kiasi cha kukasirika na kuamua 

kumtenda hivi? Mtu huyu 

aliyejitolea kuifanya kazi yako bila 

hata kulipwa senti moja kwa nini 

umfanyie hivi?Nahitaji majibu 

mheshimiwa rais katika suala hili kwa sababu Mathew ni kama 

mwanangu hivyo siwezi kukubali 

maisha yake yaharibike huku 

nikishuhudia na mimi nikiwa 

sehemu ya kuyaharibu maisha 

yake” akasema Meshack Jumbo 

ambaye alionekana kukasirika 

sana.Dr Vivian akavuta pumzi 

ndefu akatazama chini kwa 

sekunde kadhaa alionekana 

kufikiria jambo halafu akainua 

kichwa akamtazama Meshack 

Jumbo usoni na kusema 

“Sikiliza mzee Jumbo.Wengi 

wanalilia kukalia kiti cha urais 

lakini ni kiti cha moto ukikikalia.Ni 

mzigo mzito na kuna nyakati 

inakulazimu kufanya mambo 

ambayo hukuwahi kufikiria kuyafanya ili mambo yakae 

sawa.Toka nilipomfahamu Mathew 

hivi karibuni sikuwahi kufikiri 

kama siku moja ningefanya 

maamuzi kama haya niliyoyafanya 

leo kwake.Naikubali na kuheshimu 

sana kazi yake na mimi pia 

ninatamani kuona kazi niliyompa 

inafika mwisho lakini 

nimelazimika kufanya haya 

niliyoyafanya” 

“kwanini madam president? 

Hicho ndicho pekee ninachotaka 

kukifahamu” akasema Meshack 

Jumbo 

“Mzee Jumbo naomba 

tusiendelee zaidi na suala 

hili.Tuendelee na mambo 

mengine.Tuna mambo makubwa ya kujadili ambayo yanatakiwa 

yatekelezwe usiku huu” akasema 

Dr Vivian 

“Madam president lazima 

kwanza suala hili 

limalizike.Mathew is like a son to 

me so I need to know why you are 

destroying him? After all he has 

done to you and to this country is 

this what he deserves? I need 

answers madam president !! 

akasema Meshack Jumbo huku 

sauti yake ikiwa kali kidogo 

“Mr Meshack mimi naweza 

kuwa binti yako lakini naomba 

usithubutu tena kuongea na mimi 

kwa kunikaripia.Chunga sana sauti 

yako unapozungumza na 

mimi.Hapa unazungumza na rais wa jamhuri ya muungano wa 

Tanzania.Umenielewa mr Jumbo? 

Akasema Dr Vivian kwa ukali 

“I’m sorry madam president” 

akasema Meshack Jumbo.Zikapita 

sekunde kadhaa Dr Vivian 

akasema 



 I’m sorry madam president” 

akasema Meshack Jumbo.Zikapita 

sekunde kadhaa Dr Vivian 

akasema 

“Mathew amekaribia kufika 

mahala ambako hatakiwi kufika na 

ndiyo maana nimefanya hivi ili 

kumzuia asiendelee mbele zaidi na 

kufika mahala ambako ni hatari 

kwa maisha yake.Amekaribia 

kuvuka mstari.Mathew ni aina ya 

watu ambao hawakubali 

kushindwa katika jambo lolote lile 

walifanyalo kwa hiyo ili kumzuia 

lazima kwanza aende gerezani na 

akitoka huko basi hataweza kuendelea tena” akasema Dr 

Vivian 

“Madam president 

sijakuelewa una maanisha nini 

unaposema kwamba Mathew 

amekaribia kuvuka mstari?Kwani 

ulipompa kazi yako akufanyie 

ulitegemea akwame? Au kuna 

mipaka ulimuwekea asifike? 

Akauliza Meshack.Dr Vivian 

akainama akafikiri kidogo na 

kusema 

“Mr Jumbo kwa kuwa 

unahitaji sana kufahamu basi 

nitakueleza lakini yote 

utakayoyasikia yatabaki hapa 

ndani.Endapo kuna lolote 

litakalovuja you are dead.You and 

your family will all die.You understand me ?!! akauliza Dr 

Vivian.Meshack Jumbo 

akamtazama kwa muda na kusema 

“You are not a killer madam 

president and you cant kill me !! 

“Kama unadhani hivyo basi 

jaribu kunizunguka na utafahamu 

vyema mimi ni nani” akasema Dr 

Vivian kwa ukali na ukimya 

ukatanda mle chumbani.Baada ya 

muda akasema 

“Kuna mambo ambayo Dr 

Robert anayafahamu kuhusu mimi 

ambayo endapo angehojiwa na 

Mathew ni lazima angemueleza na 

sitaki mtu mwingine yeyote 

ayafahamu.Dr Robert alikuwa 

mshirika na msiri wangu mkubwa 

na anayafahamu mambo yangu mengi.Njia pekee ya kuzuia 

mambo yangu yasitoke nje ni kwa 

kumfumba mdomo.Pamoja na 

kumuua Dr Robert Mathew kwa 

umahiri wake engeweza 

kuchuguza na kugundua nani 

aliyemuua ndiyo maana nikaona ni 

vyema kama naye akiwekwa 

kizuizini kwa muda.Nadhani 

mpaka hapo umenielewa kwa nini 

nimefanya haya niliyoyafanya” 

akasema Dr Vivian.Meshack Jumbo 

akakuna kichwa na ukimya 

ukatawala mle ndani 

“Say something Mr Jumbo!! 

Mbona umekuwa kimya ghafla? 

Akauliza Dr Vivian “Madam president ..” Meshack 

Jumbo akataka kusema kitu 

akanyamaza 

“Say it Meshack !! akasema Dr 

Vivian 

“Madam 

president,nimehudumu katika 

idara hii ya usalama wa taifa kwa 

zaidi ya miaka ishirini.Nimefanya 

kazi kwa ukaribu na marais wawili 

nikiwa kama mkuu wa idara 

hii.Kila rais niliyefanya naye kazi 

alikuwa na siri zake.Nyingine 

binafsi nyingine za 

kikazi.Unapokalia kiti hicho 

huwezi kutenda mambo yote sawa 

lazima kuna mahali unaweza 

kuteleza.Rais ni mwanadamu 

kama wengine na si malaika hivyo kukosea ni kawaida.Ulipokuwa na 

suala kama hili ungeniita 

ukanieleza nikakushauri namna 

bora zaidi ya 

kufanya.Nimeaminiwa na marais 

wote niliofanya kazi nao na 

sikuwahi 

kuwaangusha.Niliwafanyia kazi 

zao za siri na mpaka leo hii siri zao 

ziko salama hapa kifuani 

kwangu.Nawe pia unapaswa 

kuniamini mheshimiwa rais.Kama 

una suala lolote la binafsi au la 

kikazi ambalo ungependa 

limalizwe kimya kimya usiogope 

kunishirikisha nami nitakushauri 

namna bora ya kulimaliza kama 

tulivyolimaliza suala la Dr 

Robert.Tukiachana na hayo turejee katika suala la Mathew.Naomba 

nikuweke wazi mheshimwia rais 

kwamba katika hili umekosea sana 

kwa haya maamuzi 

uliyoyachukua.Laiti 

ungenishirikisha ingekuwa rahisi 

mimi kuzungumza na Mathew na 

yale mambo unayohofia kwamba 

angeyafahamu asingeyagusa bali 

yeye angeendelea na uchunguzi 

wake wa jambo ulilomtuma” 

“Meshack tumekwisha 

limaliza hilo na sitaki tuendelee 

kulijadili kwani sintabadili 

msimamo wangu.Mimi ni tofauti 

na marais wengine walionitangulia 

ambao walikuita na kukueleza siri 

zao.Siri zangu ni za kwangu na siko 

tayari zivuje na kufika katika mikono ya adui zangu hivyo yeyote 

ambaye akionekana kuwa hatari 

kwangu basi nitamundoa mara 

moja bila kusita.Hata wewe 

nikikuona umekuwa hatari 

kwangu sintasita kukuondoa 

haraka sana kwa hiyo jichunge 

sana mzee Meshack nimekuamini 

na ninaomba hata siku moja 

usivunje uaminifu wangu kwako” 

akasema Dr Vivian. 

“With respect madam 

president what you did to Mathew 

is unfair and it is the biggest 

mistake you’ve ever done in your 

life.Umefanya mambo mengi 

makubwa na mazuri lakini kwa hili 

umekosea sana.Hukupaswa 

kufanya hivi” “Mr Jumbo narudia tena 

kukuonya kwamba usinifundishe 

namna ya kuifanya kazi 

yangu.Nimekwisha fanya maamuzi 

na hakuna wa kuyapinga.Naruidia 

kwa mara nyingine tena mjadala 

kuhusu Mathew nimekwisha 

ufunga!! 

“Hapana madam 

president.Suala hili si dogo na 

haliwezi kuchukuliwa kimzaha 

mzaha.Mjadala kuhusu Mathew 

bado mrefu na hatujafikia 

muafaka.Wewe ni rais na unao 

uwezo wa kufanya jambo lolote 

ulitakalo ndani ya nchi lakini kwa 

mara nyingine nakuhakikishia 

kwamba kwa hili la Mathew 

umekosea sana.Hukupaswa kabisa kuingia katika vita na 

Mathew.Akifahamu kuwa ni wewe 

ndiye uliyemfanyia haya Iswear 

you are finished.Ninamfahamu 

Mathew vyema ni kiumbe mbaya 

sana akikasirika” 

“Are you threatening me Mr 

Jumbo? Akauliza Dr Vivian kwa 

ukali.Tayari alikwisha kasirika 

“I’m not threatening you 

madam president,I’m telling you 

the truth.What you did is totaly 

wrong and once Mathew find out 

that it is you behind everything 

that’s heppening to him,you are 

finished.You’ll go down madam 

president!! Akasema Meshack 

Jumbo.Dr Vivian huku akivuta 

pumzi haraka haraka akasema “Don’t say another word 

Jumbo or I’m going to destroy you 

as well !! 

“No you cant madam 

president !! akasema Meshack 

Jumbo 

“There is a button under that 

table.Once I push it my men will be 

here in a second and will take you 

away and that’ll be the end of 

you.Dont force me to destroy you 

old man.I don’t want to hear the 

name Mathew again,you 

understand me mr Jumbo?!! 

Akauliza Dr Vivian akiwa amejaa 

hasira 

“Madam president naomba 

nikuweke wazi kwamba Mathew ni 

kijana wangu na alikubali kufanya kazi yako kwa sababu ya heshima 

yangu.Siwezi kukubali kuona 

akiangamia bila kosa lolot…..” 

kabla Meshack hajamaliza sentensi 

yake Dr Vivian akabonyeza kitufe 

chini ya meza na ghafla walinzi 

wanne wa rais wakaingia mle 

ndani kwa kasi kubwa 

‘That’s a mistake madam 

president.If you lock me up then 

you are finished.You need me so 

badly right now.I’m the only one 

who can get you out of this mess 

you are in right now!! Akasema 

Meshack Jumbo.Dr Vivian 

akamtazama kwa makini na 

kuwataka wale walinzi wake 

watoke nje “Thank you madam president 

!! akasema Meshack baada ya wale 

walinzi wa rais kutoka 

“Mshukuru malaika wako ana 

nguvu sana kwani ni mara chache 

nimefanya maamuzi na 

kuyabatilisha.Wakati mwingine 

nikikwambia lazima 

unisikilize.Wewe ni mkubwa 

kiumri lakini kimamlaka mimi ni 

mkubwa wako hivyo unapaswa 

kunitii hata kama nina umri sawa 

na mwanao !! akasema Dr Vivian 

“I’m sorry madam president .It 

wont happen again” akasema 

Meshack 

“Na iwe hivyo” akasema Dr 

Vivian “Kuhusu huyu kijana wako 

Mathew.Hata mimi sifurahii 

kumfanyia hivi na ni moja wapo ya 

maamuzi magumu sana ambayo 

nimewahi kuyafanya kama 

rais.Nafahamu Mathew hana kosa 

lolote lakini siwezi kumuacha huru 

kwani lazima ataendelea 

kuchimba na kufahamu mambo 

ambayo hapaswi kuyafahamu na 

mimi sitaki siri zangu 

zijulikane.Kwa hiyo basi Mathew 

lazima asimamishwe kwa muda 

lakini hapo baadae ataachiwa 

huru.Mjadala kuhusu yeye 

unaishia hapa na suala hili ni mimi 

na wewe pekee tunaolifahamu.Siri 

hii ikivuja nitajua ni wewe na huo 

utakuwa ni mwisho wako Meshack Jumbo.Je bado una dukuduku 

lolote kuhusu suala hili? 

“Hapana mheshimiwa 

rais.Ninakubaliana na maamuzi 

yako kwani kuna nyakati kama 

kiongozi unalazimika kufanya 

jambo ambalo hukuwa umepanga 

kulifanya.Nimekutazama machoni 

mheshimiwa rais hata wewe 

umeumizwa na jambo hili lakini 

hakuna namna.Tukubaliane na 

kilichotokea tusonge mbele” 

“Good ! Tuachane na hayo ya 

Mathew.Hatukuwa tumemaliza 

suala la Helmet Brian.Nataka kabla 

ya mapambazuko ya kesho wale 

watu watatu ambao nilikupa 

karatasi yenye picha zao wawe 

tayari wamekwisha tiwa nguvuni.Nataka wahojiwe na 

tufahamu nani 

aliyewatuma.Ukiacha hilo 

namkabidhi kwako Helmet 

Brian.Nataka afichwe mahala pa 

siri sana.Mnazo sehemu zenu 

ambazo huwa mnahifadhi watu 

muhimu.Marekani lazima 

watataka kufahamu mahala alipo 

na hawatachoka hadi wahakikishe 

wamempata hivyo basi jitahidi 

kwa kila namna uwezavyo 

kuhakikisha 

hawafanikiwi.Tukifanikiwa kupata 

ushahidi wa kutosha kwamba 

kweli Marekani walikuwa na 

mpango wa kumuua Helmet 

tutakuwa tumepata fimbo ya 

kuwachapia na tutawanyamazisha kelele zao.Hivyo basi naomba 

fanya kila uwezavyo hakikisha 

tunafanikiwa kuwapata hao jamaa 

waliotumwa kumuua 

Helmet.Ninakukabidhi jukumu hili 

kwa kuwa ninakuamini na nina 

imani kwamba Helmet yuko katika 

mikono salama” akasema Dr 

Vivian 

“Mheshimiwa rais,waziri 

Helmet tutamuhifadhi mahala 

salama na pa siri.Watu wachache 

tu wanaoweza kufika mahala 

hapo.Hao wadunguaji walioingia 

nchini kwa kazi moja ya kumuua 

Helmet nakuhakikishia kabla ya 

kufika asubuhi watakuwa 

wamepatikana.Pamoja na hayo 

mheshimiwa rais kuna jambo nataka kukushauri ila naomba 

usikasirike” 

“Jambo gani Meshack? 

“Jambo hili ambaye angeweza 

kulikamilisha kwa ufanisi mkubwa 

ni aliyeligundua ambaye ni 

Mathew.Tayari anafahamu mambo 

mengi kuhusiana na mpango huu 

hivyo endapo angeshiriki 

ingependeza zaidi” akasema 

Meshack 

“Meshack umeniomba 

nisikasirike na mimi sintakasirika 

ila nataka nikuweke wazi kwamba 

kwa sasa hakuna namna yoyote ya 

kumsaidia Mathew.Habari yake 

imekwisha.Katika idara yako ya 

usalama wa taifa wapo vijana 

wengi ambao wanaweza kuifanya kazi hii kwa ufanisi mkubwa kama 

Mathew hivyo nakuomba usiwe na 

hofu.Tunao watu wengi mahiri 

sana kwa hiyo tumuweke Mathew 

pembeni kwa sasa na tuwatumie 

watu wengine.Tumeelewana 

Meshack? Akauliza Dr Vivian 

“Sawa madam president” 

akajibu Meshack 

“Good.Nataka suala la 

kuwatafuta wale jamaa lianze 

mara moja vile vile shughulikia 

sehemu ya kumuhifadhi 

Helmet.Ninaingia katika kikao na 

nitakapomaliza kikao naomba 

nipate mrejesho mahala ulikofikia” 

“Sawa mhesimiwa rais” 

akasema Meshack Jumbo 

wakatoka na rais akaelekea katika kikao cha dharura alichokiitisha 

kwa lengo la kujadili kile 

kilichokuwa kimetokea jioni 

katika uwanja wa ndege wa 

kimataifa wa Julius Nyerere. Kabla 

ya kikao kuanza rais akamuita 

mmoja wa walinzi wake 

akamnong’oneza jambo 

“Nataka weka vijana wawili 

wamfuatilie Meshack 

Jumbo.Nataka kujua kila 

anachokifanya kuanzia usiku wa 

leo.Nataka nipewe taarifa kila 

baada ya nusu saa.Achunguzwe 

anakwenda wapi na anakutana na 

kina nani” akasema Dr Vivian na 

kuendelea na kikao 

Meshack Jumbo baada ya 

kuachana na Dr Vivian,akaenda katika sebule ya rais alikokuwepo 

Helmet Brian na kumkuta 

akizungumza na simu akamfanyia 

ishara akate mazungumzo yale na 

bila kupoteza muda Helmet 

akakata simu 

“Helmet Brian,naitwa 

Meshack Jumbo mkurugenzi wa 

idara ya usalama wa taifa.Idara 

yangu imekabidhiwa na rais 

jukumu lote la usalama wako hivyo 

usihofu uko katika nchi na mikono 

salama.kwa sasa endelea 

kupumzika wakati makazi yako 

yanaandaliwa.Nitakuja baadae 

kukuchukua na kukupeleka 

mahala salama utakapoishi” 

“Mnaniondoa hapa ikulu? 

Helmet akashangaa “Ndiyo mheshimiwa 

waziri.Usihofu utapelekwa sehemu 

salama zaidi ya hapa ambako ni 

watu wachache tu wanaopafahamu 

tofauti na hapa ikulu ambapo ni 

sehemu wanapoingia watu wengi 

na hivyo hakuna usiri.Serikali ya 

Marekani hawapaswi kufahamu 

mahala ulipo” 

“sawa Meshack” akajibu 

Helmet 

“jambo lingine” Meshack 

akaendelea 

“Hutakiwi kupiga simu kwa 

mtu yeyote nchini kwako” 

“Niliwasiliana na mke wangu 

na kumjulisha kwamba niko 

salama na kumuondoa hofu ila 

nimemtaka asimueleze mtu mwingine yeyote kama niko 

salama” akasema Helmet 

“Ulifanya kosa.Hupaswi 

kuwasiliana na mtu yeyote hata 

familia yako kwani kuna 

uwezekano mkubwa wakawa 

wanachunguzwa na makachero wa 

Marekani.Utawaweka katika hatari 

kubwa.Utafika wakati utawasiliana 

nao lakini si sasa” akasema 

Meshack Jumbo na kutoka mle 

sebuleni 

“Siwezi kuwa sehemu ya 

kuyaharibu maisha ya 

Mathew.Siko tayari kuona kijana 

yule akiangamia lazima nitafute 

namna ya kumuokoa.Siamini kama 

Dr Vivian anaweza kuwa na roho 

ngumu ya kikatili namna hii kiasi cha kuamua kuyaharibu maisha ya 

Mathew wakati akijua kabisa 

kwamba hajatenda kosa 

analotuhumiwa nalo.Kuna kitu 

gani anakiogopa Mathew 

asigundue kuhusu yeye? Dr Robert 

lazima kuna siri kubwa 

anaifahamu je ni siri gani hiyo?Dr 

Robert alikuwamo katika mtandao 

wa Marekani hapa nchini je Dr 

Vivian hakulifahamu hilo?Kuna 

mambo mengi ya kuyafahamu 

hapa lakini ngoja kwanza 

nishughulikie suala a kumtoa 

Mathew katika mikono ya polisi 

ambalo lazima lifanyike usiku huu 

huu.Hata kama ni kuvamia kituo 

cha polisi na kumtoa Mathew 

lazima ifanyike hivyo ili mradi Mathew aokolewe.Kuna mambo 

mazito kuhusu rais Dr Vivian 

ambayo lazima tuyafahamu.Kuna 

siri kubwa anaificha lakini 

tutaitafuta hadi tuifahamu” 

akawaza Meshack Jumbo na 

kuingia chooni akachukua pochi 

yake akatoa laini ya simu 

akaiweka katika simu yake 

akazitafuta namba fulani akapiga. 

****************** 

Savanna 5 star hotel,moja kati 

ya hoteli kubwa jijini Dar es 

salaam,usiku huu ilijaa 

wateja.Watu huwa wengi sana 

katika hoteli hii hasa nyakati za 

usiku kutokana na huduma zake nzuri.Vyakula vya mataifa mbali 

mbali hupikwa na hivyo 

kuwafanya wageni kutoka mataifa 

mbali mbali kufika hapa kupata 

vyakula vya asili yao.Ukiacha 

huduma nzuri za chakula na 

malazi,wengi hupenda kufika hapa 

kupata mvinyo safi uitwao 

Amarachi.Ni mvinyo 

unaotengenezwa kwa matunda na 

ambao umejizolea sifa kemkem 

hasa kutokana na ladha yake nzuri. 

Austin January anayemiliki 

hoteli hii kwa pamoja na mke wake 

Amarachi,akiwa amekaa na kundi 

la wageni wakitokea nchini 

Sweden wakiufurahia mvinyo 

Amarachi,simu yake ikaita.Akaitoa 

mfukoni na kutazama mpigaji.Hakuna jina lililojitokeza 

katika kioo cha simu bali kulikuwa 

na namba.Austin alipoziona namba 

zile akastuka sana,akainuka 

mahala alipokuwa amekaa 

akasogea pembeni mahala kusiko 

na watu.Simu ile ilianza kuita kwa 

mara ya pili akaipokea 

“Hallow mzee” akasema 

Austin sauti yake ikionyesha 

wasiwasi kidogo 

“Hujambo Austin? 

“Sijambo mzee shikamoo” 

“marahaba.Vipi maendeleo 

yako? 

“Maendeleo yangu 

mazuri.Nimestuka sana kuona 

namba zako mida hii” “C’mon Austin kwa nini 

ustuke? 

“Mara nyingi nionapo namba 

zako huwa ninastuka sana sijui 

kwa nini” 

“Usihofu Austin.Ninyi ni vijana 

wangu na ndiyo maana huwa sitaki 

kuwapigia simu mara kwa mara 

kwani nafahamu mzionapo namba 

zangu katika simu zenu huwa 

mnastuka sana” 

“Ndiyo mzee.Namba zako 

hufanya mioyo yetu iende 

mbio.Tuachane na hayo mzee 

wangu habari za siku nyingi? 

“Austin utanisamehe sina 

muda mrefu wa maongezi nawe 

nimekupigia ninahitaji msaada 

wako wa haraka sana” akasema Meshack na kupitia spika za simu 

akasikia Austin akishusha pumzi 

“Msaada upi unauhitaji mzee? 

Akauliza Austin 

“Kuna mtu nahitaji 

kumuondoa katika hatari kubwa 

aliyomo.Endapo nisipofanya 

juhudi za kumuondoa katika hatari 

hiyo nitampoteza.Nahitaji sana 

msaada wako kwa hilo” akasema 

Meshack Jumbo 

“Mzee kwa sasa nimekwisha 

achana na hizo shughuli na 

nimejiajiri katika shughuli zangu 

binafsi.Labda nikusaidie kutafuta 

kijana mwingine akusaidie katika 

jambo hilo” 

“Austin ninafahamu kwamba 

kwa sasa unajishughulisha na shughuli zako binafsi lakini bado 

ujuzi na uzoefu wako uko pale pale 

hivyo ninakuomba unisaidie 

katika kazi hiyo.Ukichelewa 

nitampoteza kijana wangu.Ninao 

vijana wengi ambao ningeweza 

kuwaomba msaada lakini 

nimekuchagua wewe kwani 

ninaufahamu uwezo wako” 

akasema Meshack.Ukatawala 

ukimya na baada ya muda Austin 

akauliza 

“Ni nani huyo unayehitaji 

kumuokoa,kafanya nini na yuko 

wapi? 

“Ni Mathew Mulumbi” 

akasema Meshack na Austin 

akastuka 

“Mathew?! Austin akashangaa “Ndiyo.Ni Mathew” 

“Kafanya nini? 

“Alikuwa katika operesheni 

fulani na akagundua jambo kubwa 

lakini akawekewa mtego na sasa 

yuko katika mikono ya polisi hivyo 

nahitaji mtu wa kwenda 

kumuokoa toka mikononi mwa 

polisi” akasema Meshack jUmbo 

“Mzee,huyu Mathew alikwisha 

achana na hizi shughuli kama mimi 

na anajishughulisha na shughuli 

zake pia.Mara ya mwisho 

nilikutana naye Paris akiwa na 

mke wake Peniela amekuja lini 

hapa nchini? 

‘Tutazungumza baadae Austin 

kwani kwa sasa muda unazidi 

kwenda na endapo tutachelewa tunaweza kumpoteza” akasema 

Meshack 

“Kama ni Mathew basi niko 

tayari kufanya kila niwezalo 

kumuokoa.Yule ni mtu aliyewahi 

kunisaidia sana wakati 

fulani.Tayari amekwisha pelekwa 

kituo cha polisi? Akauliza Austin 

“Hapana bado ameshikiliwa 

nyumbani kwake upekuzi 

unafanyika” akasema 

Meshack.Baada ya sekunde kadhaa 

Austin akasema 

“Mzee nina ushauri mmoja 

ambao unaweza kutusaidia 

tukampata Mathew bila kutumia 

nguvu.” 

“Ushauri gani huo? “Wewe uliwahi kuwa mkuu 

wa idara ya usalama wa taifa na 

una heshima kubwa sana katika 

idara ile.Una mawasiliano na mkuu 

wa sasa wa idara ya usalama wa 

taifa? 

“Kuna jambo ambalo sikuwa 

nimekutaarifu Austin.Mkuu wa 

idara ya usalama wa taifa 

amefariki alijipiga risasi na rais 

ameniteua mimi niongoze idara hii 

kwamuda.Kwa sasa mimi ndiye 

mkuu wa idara ya usalama wa 

taifa” 

‘That’s not true” akasema 

Austin 

“Its true.Rais aliniomba 

nimsaidie kuiongoza idara hii kwa 

muda wa mwaka mmoja hadi hapo atakapokuwa amempata mtu 

ambaye atafaa kuiongoza idara hii” 

“Kama ni hivyo basi kazi 

itakuwa rahisi sana.Wasiliana na 

kamanda wa polisi kanda maalum 

ya Dar es salaam na mwelekeze 

kwamba Mathew aliwahi fanya 

kazi idara ya usalama wa taifa kwa 

hiyo unamuhitaji kwa ajili ya 

mahojiano halafu atakabidhiwa 

kwa jeshi la polisi baada ya 

kumfanyia mahojiano.Waambie 

kuna suala zito la usalama wa nchi 

ambalo tunahitaji kumuhoji 

Mathew.Kwa kufanya hivyo 

tunaweza kumchukua Mathew bila 

kutumia nguvu” akasema Austin 




Waambie 

kuna suala zito la usalama wa nchi 

ambalo tunahitaji kumuhoji 

Mathew.Kwa kufanya hivyo 

tunaweza kumchukua Mathew bila 

kutumia nguvu” akasema Austin 

‘Wazo lako ni zuri sana Austin 

lakini ni gumu kulitekeleza.Rais tayari analifahamu jambo hili kwa 

hiyo kutakuwa na ugumu 

kuruhusu tumchukue Mathew” 

“Mzee kama wewe ni mkuu wa 

idara ya usalama wa taifa basi una 

nguvu kubwa sana ya kuweza 

kumuokoa Mathew.Uko wapi hivi 

sasa? 

“Niko ikulu lakini muda si 

mrefu nitatoka” akasema Meshack 

“Mzee tumia nguvu yako 

kumuokoa kijana wako” 

“Austin kama ningekuwa na 

uwezo wa kumsaidia Mathew 

nisingekupigia simu kukuomba 

msaada.Do what you have to do to 

rescue Mathew.Hata kama ni 

kuvamia kituo cha polisi basi fanya hivyo ili mradi Mathew awe huru” 

akasema Meshack 

“Mzee hatupaswi kufika 

huko.Hiyo ni hatua kubwa sana 

ambayo itakuwa ya mwisho baada 

ya jitihada nyingine zote 

kushindikana.Hivyo basi 

utachagua aidha kumsaidia 

Mathew au kumtii rais” 

“Austin..!! akasema Meshack 

akionyesha kukerwa na kauli ile ya 

Austin 

“Mzee muda unakwenda na 

unatakiwa ufanye uchaguzi aidha 

umsaidie Mathew na kumtoa 

katika mikono ya polisi au umtii 

rais na kijana wako apotee” Ukapita ukimya wa sekunde 

kadhaa halafu Meshack Jumbo 

akauliza 

“Uko wapi Austin? 

“Niko hapa katika hoteli 

yangu” 

“Ninakuja hapo sasa hivi” 

akasema Meshack na kukata simu 

akatoka na kumuelekeza dereva 

wake waelekee Savana 5 star hotel. 

“Mawazo ya Austin ni 

mazuri.Ninaweza kutumia nguvu 

yangu kama mkuu wa idara ya 

usalama wa taifa na kumuokoa 

Mathew.Hawa vijana bado akili zao 

zinachemka na wanafikiri haraka 

haraka sana kuzidi mimi ambaye 

tayari umri wangu 

umekwenda.Nadhani napaswa kulizingatia wazo hili na kulifanyia 

kazi .Lakini nikiamua kufuata 

wazo la Austin nitajiingiza katika 

matatizo makubwa na rais na 

ndiyo maana Austin akaniambia 

kwamba ninapaswa kuchagua 

nimsaidie Mathew au nimtii rais na 

kumuacha Mathew akiangamia.” 

Akawaza Meshack akiwa garini 

“Mathew hana kosa lolote na 

kwa kosa hili alilotuhumiwa nalo 

anaweza kufungwa hata kifungo 

cha maisha gerezani.Siko tayari 

kuona kijana yule ambaye 

alijitolea kuifanya kazi ya rais kwa 

moyo mmoja anaozea 

gerezani.Kwa hiyo basi ninachagua 

kumsaidia Mathew.Potelea mbali 

kama nitakuwa nimetangaza vita na rais kwa maamuzi yangu haya 

lakini lazima nimsaidie Mathew” 

akawaza Meshack na kuchukua 

simu akampigia katibu muhtasi 

wake na kumtaka amtafutie namba 

za kamanda wa polisi kanda 

maalum ya Dar es salaam.Baada ya 

dakika tano akatumiwa namba zile 

na bila kupoteza muda akapiga 

“Hallo” ikasema sauti ya 

upande wa pili 

“Kamanda unazungumza na 

Meshack Jumbo mkurugenzi wa 

idara ya usalama wa taifa” 

“Nikusaidie nini mkurugenzi? 

“Nilimpa taarifa mheshmiwa 

rais usiku huu kuhusiana na 

kuuawa kwa waziri wa mambo ya 

nje Dr Robert Mwainamela mauaji yanayosadikiwa kufanywa na 

Mathew Mulumbi na kwa taarifa 

niliyoipata hivi punde ni kwamba 

tayari amekwisha tiwa nguvuni” 

“Ndiyo mkurugenzi.Huyu 

kijana Mathew tayari amekwisha 

tiwa nguvuni na sasa utaratibu 

unafanyika kumpeleka katika 

kituo cha kati cha polisi” akasema 

kamanda wa polisi kanda maalum 

ya Dar es salaam 

“Kamanda,huyu jamaa aliwahi 

kufanya kazi katika idara ya 

usalama wa taifa na kuna mambo 

muhimu tunahitaji kuyafahamu 

toka kwake kwa hiyo tunahitaji 

kumfanyia mahojiano.Baada ya 

kumfanyia mahojiano basi 

tutawakabidhi muendelee na taratibu nyingine za upelelezi na 

mashtaka hivyo naomba 

asipelekwe kwanza kituoni ili 

tumfanyie mahojiano hapo 

nyumbani kwake” 

“Sawa mkurugenzi.Sisi sote 

tunafanya kazi moja kulinda nchi 

yetu kwa hiyo mtaruhusiwa 

kumfanyia mahojiano huyo jamaa 

na mtakapomaliza mtatukabidhi 

mhalifu huyo kwa ajili ya 

kuendelea na taratibu 

nyingine.Ninampigia simu sasa 

hivi kiongozi wa kikosi 

kilichotumwa nyumbani kwa 

Mathew ili awaruhusu watu wako 

wamuhoji hapo hapo nyumbani 

kwake” akasema kamanda wa 

polisi “Ahsante sana kwa 

ushirikiano wako kamanda” 

akasema Meshack Jumbo na 

kukata simu. 

“Wazo la Austin ni zuri sana” 

akawaza Meshack huku safari 

ikiendelea 

 Meshack Jumbo aliwasili 

Savana 5 star hotel akampigia 

simu Austin akamfahamisha 

kwamba tayari amekwisha 

fika.Austin akamtaka amfuate 

ofisini kwake.Meshack akashuka 

na kuelekea katika jengo la hoteli 

akahakiki kwanza usalama wake 

halafu akapanda lifti hadi ghorofa 

ya tatu ziliko ofisi akaitafuta ofisi 

ya mkurugenzi akagonga na 

mlango ukafunguliwa na mwanamke mmoja mwenye sura 

iliyojaa tabasamu 

“Shikamoo mzee” 

“Marahaba nahitaji kuonana 

na ndugu Austin January” 

“Karibu ndani” 

Meshack akaingia ndani ya 

ofisi na kukutana na Austin 

“Karibu sana mzee 

wangu.Nafurahi tumeonana tena 

baada ya kitambo kirefu” 

‘Hata mimi nimefurahi 

kukutana tena nawe 

Austin.Nilipata wazo la kukutafuta 

ila sikuwa na uhakika kama bado 

unatumia ile namba yako hivyo 

nilipiga kwa kubahatisha.Vipi 

maendeleo yako? “Nendelea vyema.By the way 

huyu ni mke wangu anaitwa 

Amarachi” Austin akafanya 

utambulisho 

“Amarachi huyu anaitwa 

Meshack Jumbo ni mkurugenzi wa 

idara ya usalama wa taifa.Ni mzee 

ambaye amenilea mimi na wengi 

tuliopita katika idara hii na 

tunamuita baba” 

“Nafurahi kukufahamu mzee 

Meshack” akasema Amarachi 

“Mimi pia nafurahi sana 

kukufahamu Amarachi” akasema 

Meshack na kumgeukia Austin 

“Austin tutatapa wasaa wa 

kutosha kuzungumza mambo yetu 

ya maisha hapo baadae lakini kwa sasa tujadili namna ya kumsaidia 

Mathew” 

“Kama nilivyokueleza mzee 

kwamba tunapaswa kutafuta 

namna nzuri ya kumsaidia Mathew 

.Wazo lako la kuvamia na kufanya 

si muafaka kwa sasa.Tayari 

amezungukwa na polisi wenye 

silaha na sisi tuko wachache hivyo 

hatutaweza kupambana nao ndiyo 

maana nakushauri kutumia nafasi 

yako kama mkuu wa idara ya 

usalama wa taifa kuweza kumtoa 

Mathew katika mikono ya askari 

bila mapambano au kumwaga 

damu” akasema Austin 

“Ahsante kwa wazo lile zuri na 

kama nilivyokufahamisha tayari 

nimewasiliana na kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es 

salaam na kumwambia kwamba 

tunamuhitaji Mathew kwa 

mahojiano kabla hawajampeleka 

kituoni.Hivi sasa watakuwa 

wanatusubiri sisi kwa hiyo 

tunatakiwa kufanya haraka.Nipe 

maoni yako tufanyaje kuweza 

kumtoa Mathew pale? 

“Good.Tukifika pale 

utajitambulisha halafu utaomba 

upewe nafasi ya kumuhoji Mathew 

na baada ya muda utaomba 

uondoke naye kwa ajili ya kwenda 

kumuhoji zaidi na Mathew 

hatarejea tena mikononi 

mwao.Mpango huu ni mzuri lakini 

una athari pia na athari kubwa 

itakuwa upande wako kwani itakulazimu kubeba mzigo wote 

wa kupotea kwa Mathew.Utaingia 

katika msuko suko mkubwa sana 

kiasi cha kuhatarisha hata 

kupoteza kazi yako kwa hiyo mzee 

kabla hatujaenda huko unapaswa 

kutafakari na kufanya maamuzi 

kama uko tayari kubeba dhaman 

hii kubwa” 

Meshack Jumbo akainamisha 

kichwa na kutafakari kwa muda 

akasema 

“Mathew ni kijana wangu na 

siko tayari kumuacha akiangamia.I 

must do everything to save him.I’m 

ready.let us go ! akasema 

Meshack.Austin akampa ishara 

Amarachi akalibeba begi 

lililokuwa juu ya meza.Meshack akataka kusema kitu lakini Austin 

akamuwahi 

“It’s ok .She’s coming with 

us.She’s good at this” akasema 

Austin wakatoka nje ya ofisi na 

Meshack akapata wazo 

“Austin kuna jambo linanipa 

wasi wasi kidogo” 

“ Jambo gani mzee? 

“Rais tayari anazo taarifa za 

kushikiliwa kwa Mathew na kabla 

ya kuja hapa kulitokea hali ya 

kutokuelewana kati yangu naye 

kuhusiana suala hili la Mathew 

kukamatwa.Ilinilazimu 

kukubaliana naye ili niweze 

kupata nafasi ya kutoka na 

kumsaidia Mathew,hata hivyo 

baada ya sintofahamu ile kutokea rais hana imani nami kwani tayari 

anaelewa msimamo wangu kuhusu 

suala hili na anajua Mathew ni 

kijana wangu hivyo siwezi katu 

kukubali atiwe nguvuni na hawezi 

kuniacha hivi hivi lazima atakuwa 

ameweka watu kunifuatilia kujua 

ninafanya nini.Ili kuepuka mpango 

wetu kuvurugika tusitumie gari 

langu.Tutumie gari lako Austin” 

akasema Meshack 

“Ahsante kwa kuling’amua 

hilo mzee Meshack.Tutatumia gari 

langu usihofu” akasema 

Austin.Wakatokea upande wa 

nyuma na kuelekea hadi katika 

maegesho maalum ya viongozi wa 

hoteli ile wakaingia katika gari la 

Austin na kuondoka.Baada ya kuondoka Meshack akachukua 

simu na kumpigia dereva wake 

akamtaka aendelee kumsubiri 

kwani bado ana mazungumzo 

muhimu na mtu aliyemfuata pale 

hotelini 

“Mzee nini hasa 

kinachoendelea?Mathew amefanya 

nini hadi ashikiliwe na 

polisi?Austin akauliza 

“Austin kuna mambo 

makubwa yanayoendela hapa 

nchini kwa sasa na Mathew 

alikuwa katika kuchunguza na 

ndipo masahibu haya 

yalipomkuta.Anashikiliwa na jeshi 

la polisi kwa tuhuma za mauaji ya 

waziri wa mambo ya nje wa 

Tanzania Dr Robert Mwainamela” “Mathew amemuua waziri wa 

mambo ya nje wa nchi?Austin 

akashangaa 

“He didn’t do it.He didn’t kill 

him” akasema Meshack 

“kama hakumuua kwa nini 

ashikiliwe na polisi? 

“kama nilivyokueleza Austin 

kwamba kuna mambo makubwa 

yanayoendelea hapa nchini hivi 

sasa na Mathew yupo katika 

uchunguzi.Hiki kilichomtokea ni 

harakati za watu wenye nguvu 

kutaka kumpoteza kwani tayari 

amekwisha gusa maslahi ya watu 

wakubwa.Kwa hiyo basi ni jukumu 

letu sisi kufanya kila tuwezalo 

kuhakikisha tunamuokoa kwani 

bila kufanya hivyo huu utakuwa ni mwisho wake” akasema Meshack 

Jumbo.Austin aliyekuwa katika 

usukani akavuta pumzi ndefu na 

kuuliza 

“Jambo gani Mathew 

analichunguza? Amewahi 

kukueleza? 

“Kuna jambo kubwa alilokuwa 

analichunguza na ndani ya 

uchunguzi huo yameibuka mambo 

mengine makubwa ambayo 

yamemuweka katika matatizo 

haya makubwa aliyonayo.Tutapata 

wasaa wa kuzungumza hapo 

baadae lakini kwa sasa 

tuhakikishe kwanza tunamuokoa 

Mathew” akasema Meshack 

“Nafahamu Mathew ni mfanya 

biashara mkubwa hivi sasa na hadi kuamua kuacha shughuli zake za 

biashara na kurudia kuifanya kazi 

hii si kwa ajili ya fedha,lazima 

kuna jambo zito lililompelekea 

akafanya hiyo kazi” akasema 

Austin 

“Hakufanya kazi hii kwa ajili 

ya kipato.Ipo sababu 

iliyompelekea aifanye hii 

kazi.Pamoja na kwamba kwa sasa 

tayari anajishughulisha na 

shughuli zake za biashara lakini 

kazi hii bado iko damuni mwake 

na ndiyo maana alilazimika 

kuingia tena uwanjani pale 

alipoona kuna ulazima wa kufanya 

hivyo.Nataka niwaweke wazi 

vijana wangu kwamba mwisho wa 

kazi hii ni pale utakapokuwa umefariki dunia lakini kama bado 

unavuta pumzi basi utaendelea 

kuifanya kazi hii kila pale 

itakapojitokeza.Tazama mimi 

tayari nimekwisha staafu lakini 

nimelazimika kurejea tena 

ofisini.Tuachane na hayo vipi 

maendeleo yako? 

“Ninaendeleea vizuri .Mimi na 

mke wangu tumewekeza sana 

katika biashara ya mvinyo uitwao 

Amarachi jina la mke wangu 

ambaye ndiye aliyeugundua na 

tayari tumejenga kiwanda kingine 

hapa Dar es salaam cha 

kutengeneza mvinyo huo kwa hiyo 

tuna viwanda viwili hivi 

sasa.Tumejenga pia hoteli mbili 

kubwa hapa jijini dar es salaam kwa ujumla tunaendelea 

vyema.Nina kila sababu ya 

kumshukuru Mungu kwa 

mafanikio haya makubwa” 

akasema Austin 

Safari iliendelea huku 

wakizungumza mambo kadha wa 

kadha hadi walipokaribia kufika 

nyumbani kwa Mathew.Austin 

akapunguza mwendo baada ya 

kunekana umati wa watu uliofika 

eneo la karibu na nyumba ya 

Mathew kushuhudia kile 

kilichokuwa kimetokea 

pale.Austin akapiga honi na watu 

waliokuwa wametanda barabarani 

wakasogea pembeni na kulipisha 

gari lipite.Magari kadhaa ya polisi 

yalikuwa yameegeshwa huku polisi wenye silaha wakiwa 

wametanda kila kona kuizunguka 

nyumba ya Mathew 

“Austin ulisema kweli kwa 

ulinzi huu wa askari tusingeweza 

kupambana nao.Ulinzi ni mkali 

sana” akasema Meshack Jumbo na 

Austin akasimamisha gari kwani 

kulizungushwa utepe uliozuia 

watu kuvuka.Wakashuka garini na 

Meshack akajitambulisha kwa 

kamanda wa polisi mkoa wa 

kipolisi Mzizima Anangisye 

Mwalukosi ambaye alikuwepo 

mahala pale 

“Mzee,taarifa zako tayari 

ninazo na tunakusubiri wewe 

uhojiane na mtuhumiwa ili tuweze kuondoka naye” akasema 

kamanda Anangisye. 

“Ahsante sana 

kamanda.Kutokana na umuhimu 

wake huyu jamaa imenilazimu 

kuja mwenyewe na vijana wangu 

ili tuweze kumuhoji kuhusiana na 

masuala kadhaa muhimu.Naomba 

dakika ishirini tu kisha 

nitamkabidhi kwenu” akasema 

Meshack na kuongozana na 

kamanda Anangisye hadi sebuleni 

walikokuwapo Mathew na Camilla 

wakiwa wamefungwa pingu huku 

wakilindwa na askari wenye 

silaha.Mathew alikuwa amefungwa 

pingu mikononi na miguuni 

“Mtuhumiwa huyu hapa ila 

utatusamhe mzee kwani hatutaweza kumfungua pingu 

kwani tumeambiwa ni mtu 

hatari.Utamfanyia mahojiano 

akiwa amefungwa hivyo hivyo” 

akasema Anangisye 

“Usijali kamanda.Ahsante 

sana.Naomba sasa askari mtupe 

nafasi na sisi tufanye kazi yetu 

halafu tutawaachia muendelee na 

taratibu zenu” akasema Meshack 

na askari wakatoka mle sebuleni. 

“Pole sana brother” akasema 

Austin 

“Good to see you Austin” 

akasema Mathew 

“Jamani huu si muda wa 

salamu.Tuna muda mchache sana 

hivyo tujielekeze katika suala la kumtoa Mathew hapa” akasema 

Meshack 

“Mzee, I didn’t kill Dr 

Robert.This is a set up!! Akasema 

Mathew 

“I know 

Mathew.Tutazungumza baadae 

lakini kwa sasa tutafute namna ya 

kumtoa Mathew katika dhahama 

hii iliyomkuta.Tuna dakika kumi 

na saba tu kutoka sasa” akasema 

Meshack 

“Mzee mimi nadhani 

tuendelee na ule mpango wetu 

tuliokuwa tumepanga.Ongea na 

kamanda wa polisi mwambie 

kwamba mtuhumiwa amekataa 

kutoa ushirikiano hivyo unaomba 

umchukue umpeleke katika ofisi zenu mkatumie njia zenu za 

kumuhoji halafu utamkabidhi tena 

kwao baada ya kumaliza 

kumuhoji.Hiyo ndiyo njia rahisi ya 

kuweza kumtoa Mathew hapa 

kwani hatutaweza kupambana na 

polisi hawa waliotanda kila kona 

ya nyumba hii” akasema Austin 

“Hapana.Hatupaswi kufanya 

hivyo.Tutamuweka mzee Jumbo 

katika matatizo makubwa na 

anaweza kufungulia mashtaka kwa 

kumtorosha mtuhumiwa wa 

mauaji ya waziri .Tusimpe mzee 

matatizo ambayo hakuwa 

ameyatarajia.Hili ni tatizo langu na 

sitaki mtu mwingine apate 

matatizo kwa ajili 

yangu.Ninachowaomba kwa sasa ni kujaribu kufanya kila 

linalowezekana kumsaidia 

Camilla.Hapaswi kwa namna 

yoyote ile kuingia katika mikono 

ya polisi” akasema Mathew 

“Mathew sikiliza .Kwa hapa 

tulipofika hili si suala lako peke 

yako.Ni suala letu sote kwa hiyo 

hatuwezi kukuacha peke 

yako.Lazima tukutoe hapa utake 

usitake.Mimi nitaubeba mzigo 

wote huu.Kumbuka kwamba ni 

mimi ndiye niliyekuingiza katika 

kazi hii kwa hiyo siwezi kukubali 

hata kidogo jambo kama hili 

likutokee.Niko tayari na nitabeba 

dhamana hii.Lazima tukuondoe 

hapa” akasema Meshack Jumbo Mathew akataka kusema kitu 

lakini Austin akamzuia 

“Usiseme chochote 

kaka.Tuache tufanye kazi yetu.This 

is our mission now” akasema 

Austin 

Zilipita dakika kumi mlango 

ukafunguliwa Meshack Jumbo 

akatoka na kumfuata kamanda 

Anangisye. 

“Afande,huyu jamaa amekuwa 

mgumu sana kufunguka na kuna 

kila dalili hataweza kusema 

chochote.Kuna jambo ambalo 

tunahitaji kulifahamu toka kwake 

linalohusu usalama wa nchi lakini 

hayuko tayari kufunguka.Kama 

ujuavyo huyu jamaa amewahi 

kufanya kazi katika idara ya ujasusi hivyo si rahisi kumfungua 

kwa muda huu mchache.Kwa 

sababu hiyo basi nina ombi moja 

kwako” 

“Ndiyo mzee” akasema 

Anangisye 

“Ninataka kuondoka na huyu 

mtuhumiwa ,tunakwenda naye 

katika sehemu yetu maalum kwa 

ajili ya kufanyia mahojiano.Kwa 

hapa hata kama tukitumia usiku 

mzima hatutaweza kupata 

chochote toka kwake.Katika 

chumba chetu cha mahojiano kuna 

vifaa maalum vya kutuwezesha 

kumfumbua mdomo mtu yeyote 

yule na hasa wale wagumu kama 

huyu.Baada ya kupata kule 

tunachokihitaji basi tutamkabidhi kwenu tena.Ninaomba hivyo kwa 

sababu taratibu zenu za kipolisi 

zikianza itakuwa kazi ngumu 

kwetu kumpata na kumuhoji hivyo 

basi tunataka tumalize kila kitu 

kabla hamjaaanza taratibu za 

kumshitaki” Kamanda Anangisye 

akainamisha kichwa kwa muda 

akatafakari na kusema 

“Mzee suala lako ni la msingi 

mkubwa lakini siwezi kulitolea 

maamuzi ya moja kwa moja hadi 

hapo itakapotolewa ruhusa kutoka 

kwa wakuu wangu.Huyu tayari ni 

mtuhumiwa wa mauaji ya waziri ni 

vipi endapo atapotea katika 

mikono yako? Nani ambaye 

atakuwa katika matatizo?Jibu ni 

rahisi ni mimi.Mzigo wote utaniangukia mimi.Naomba 

usubiri mzee nimfikishe kwanza 

sehemu husika na halafu ufuate 

taratibu za kuweza kumpata kwa 

mahojiano” akasema Kamanda 

Anangisye 

“Kamanda Anangisye mimi na 

wewe tuko idara tofauti lakini 

jukumu letu ni lile lile yaani 

kulinda nchi na raia wake kwa 

hiyo ninaomba 

uniamini.Mtuhumiwa hawezi 

kupotea katika mikono yetu.Sisi ni 

watu makini na tunafahamu 

tunachokifanya” 

“Mzee Jumbo ninakuamini 

lakini kila kitu kina taratibu 

zake.Hili suala si gumu lakini 

tufuate taratibu zilizowekwa na si kufanya kienyeji enyeji kisha 

tukawekana katika matatizo!! 

Akasema Kamanda Anangisye 

“Naomba nikufahamishe 

jambo moja kamanda 

Anangisye.Leo jioni kumetokea 

shambulio la bomu katika uwanja 

wa ndege wa Julius Nyerere 

likimlenga waziri wa mambo ya 

nje wa Marekani.Watu kadhaa 

wanadaiwa kupoteza maisha na 

hadi hivi sasa waziri huyo wa 

mambo ya nje wa Marekani 

hajulikani mahala alipo.Mathew 

anazo taarifa muhimu sana za 

kuhusiana na shambulio hilo na 

ambazo zinaweza kutusaida 

kuwafahamu waliofanya hilo 

shambulio na mahala alipo waziri huyo aliyetoweka.Ninyi 

mnamshikilia Mathew kwa tuhuma 

za mauaji na akishafikishwa 

kituoni taratibu za kufuata ili 

kumuhoji zina mlolongo mrefu na 

sisi tunahitaji kupata taarifa kwa 

haraka.Naomba uniamini ili 

tukamilishe kazi yetu na kisha 

tutamkabidhi kwenu akiwa mzima 

wa afya.Hatupaswi kuwekeana 

vizingiti wakato sote tunafanya 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog