Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL (2) - 5

   

Simulizi : The Football (2)

Sehemu Ya Tano (5)


atumie busara katika suala la 

Korea kaskazini.Kwa sasa amebaki 

na watu wanaomsikiliza kwa kila 

jambo anaweza akaingia katika 

vita na Korea Kaskazini.Wakati 

mwingine ninahisi yawezekana 

labda ametaka niuawe kwa kuwa 

nilikuwa nampinga sana katika 

suala la kutaka kuanzisha vita na Korea kaskazini.Sasa anayo nafasi 

kubwa ya kufanya kila 

anachokitaka bila kupata upinzani 

mkubwa” akasema Helmet .Dr 

Vivian akamtazama na kusema 

“Helmet mimi na wewe 

tunaweza kufanya jambo kumzuia 

Mike straw asifikie malengo yake 

ya kutaka kuanzisha vita” 

“Kwa sasa sina nguvu ya 

kufanya jambo lolote na..” 

akasema Hemet lakini Dr Vivian 

akamkatisha 

“Bado unayo nguvu Helmet” 

akasema Dr Vivian na kumtazama 

Helmet 

“Tunao watu walioletwa 

kufanya kazi moja tu ya 

kukuua.Tutawahoji watu hao na tutapata ukweli wa jambo hili.Ni 

vipi endapo tutapata ushahidi usio 

na chembe ya shaka kwamba 

Marekani wamesuka mpango wa 

kukuua,halafu ukaanzisha 

mchakato wa kumuondoa Mike 

straw madarakani? Helmet 

wamarekani wanakupenda sana 

na endapo usingejitoa katika mbio 

za urais hivi sasa ungekalia kiti cha 

urais.Ninataka uanzishe vugu vugu 

la kumtoa madarakani rais Mike 

straw na serikali yake na kwa 

kuwa unao uungwaji mkono 

mkubwa utachaguliwa kuwa rais 

wa Marekani na kwa pamoja 

tutafanya mambo ambayo 

yataishangaza dunia.Ninakuahidi 

Helmet kuumaliza mgogoro huu unaofukuta hivi sasa.Sitaki unijibu 

kwa sasa.Nenda kalifikirie hili 

jambo na baadae tutazungumza” 

akasema Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais 

umezungumza suala zito sana ila 

nashukru kwa busara zako kwa 

kunipa nafasi ya kulitafakari suala 

hili kwa kina na kisha kukupa 

jibu.Ila ninapenda kukuhakikishia 

kwamba hili ni jambo 

linalowezekana kabisa.Ninao 

ushawishi mkubwa sana ndani ya 

serikali ya Marekani na ninaweza 

kuendesha kampeni hiyo ya 

kumuondoa madarakani rais Mike 

straw lakini suala la mimi 

kuchukua nafasi yake ya urais 

ninahitaji muda wa kutafakari.Nimefurahiswa sana na 

kauli yako kuhusiana na 

kuumaliza mgogoro mkubwa 

unaofukuta hivi sasa duniani 

ambao kwa kiasi kikubwa ni Mike 

straw ndiye aliyeuanzisha.Nina 

tamani kuona mambo haya 

yanamalizika na dunia inakuwa 

kitu kimoja na mahala salama pa 

kuishi.Ninatamani kuona nchi zote 

zinazomiliki silaha kali za 

maangamizi zinaingia 

makubaliano ya kuteketeza silaha 

zao na kuifanya dunia iwe sehemu 

salama ya kuishi” 

Mlinzi wa rais akaingia pale 

sebuleni. “Mheshimiwa rais,Mathew 

tayari amefika ” akasema na Dr 

Vivian akavuta pumzi ndefu. 

“Aruhusiwe aingie ndani” 

akasema Dr Vivian halafu 

akamtaka radhi Helmet akatoka na 

kukutana na Meshack Jumbo. 

“You were right Meshack,I 

need him.We need him” akasema 

Dr Vivian 

“Unamzungumzia nani 

mheshimiwa rais? 

“Mathew.Ulikuwa sahihi 

nilikosea sana kwa nilichotaka 

kumfanyia.Mathew ni muhimu 

kwetu.Bado tunamuhitaji sana” 

akasema Dr Vivian na tabasamu 

likaonekana usoni pa Meshack 

Jumbo. “Nilikwambia mheshimiwa 

rais ,bado tutamuhitaji sana 

Mathew” akasema Meshack Jumbo 

“Kuna mambo nimezungumza 

na Helmet Brian na nimejikuta 

nikimuhitaji tena Mathew katika 

kuyatekeleza” akasema Dr Vivian 

“Vipi kuhusu suala lake kule 

polisi? 

“Nitalimaliza” akajibu Dr 

Vivian na Mathew akajitokeza 

akiwa ameongozana na walinzi 

wawili 

“Madam president” akasema 

Mathew 

“Mathew karibu sana.Pole 

kwa matatizo yote yaliyotokea” 

akasema Dr Vivian “Ahsante sana mheshimiwa 

rais” akasema Mathew na 

kumtazama Meshack Jumbo 

“Mzee nimekuja kuifanya ile 

kazi uliyonieleza” 

“Mathew kabla hujaifanya kazi 

hiyo nina mazungumzo nawe 

mafupi” akasema Dr Vivian na 

kusogea pembeni 

“Nadhani Meshack Jumbo 

amekwisha kueleza kuhusiana na 

Helmet.Amegoma kuondoka hapa 

bila kukuona.Ametokea kukuamini 

sana hivyo nataka umpeleka 

mahala alipoandaliwa kisha urejee 

hapa ikulu nina mazungumzo 

nawe muhimu” akasema Dr Vivian “Sawa mheshimiwa rais” 

akajibu Mathew na wakabaki 

wanatazamana 

“Kuna taarifa zozote 

kuhusiana na maendeleo ya 

Theresa? 

“Taarifa ya mwisho niliyoipata 

alikuwa hajazinduka bado lakini 

madaktari wamenihakikishia 

kwamba anaendelea vizuri na 

atazinduka.Tuendelee 

kumuombea” akasema Dr Vivian 

kwa sauti ya upole. 

“Mathew ni hilo tu nililotaka 

kuzungumza nawe.Sasa ni wakati 

wa kumuondoa Helmet brian na 

kumpeleka kupumzika” akasema 

Dr Vivian akaongozana na Mathew 

hadi sebuleni kwake “Helmet ,rafiki yako Mathew 

tayari amefika” akasema Dr Vivian 

huku akitabasamu.Helmet Brian 

akatabasamu pia baada ya 

kumuona Mathew 

“Simfahamu Mathew lakini 

nimetokea kumuamini 

mno.Ahsante sana Mathew kwa 

kuja.Niliomba uwepo karibu yangu 

wakati ninapelekwa mahala 

nitakapokuwa ninaishi” akasema 

Helmet 

“Usijali mheshimiwa 

waziri.Uko salama” akasema 

Mathew na kutaka apewe 

utaratibu wa namna ya 

kumuondoa Helmet pale 

ikulu.Meshack Jumbo akamueleza 

kila kitu namna walivyojipanga na Mathew akatoa maelekezo yake 

halafu wakamchukua Helmet na 

kuondoka naye kumpeleka 

sehemu ya siri. 




WASHINGTON DC - MAREKANI 

Kikao alichokiitisha rais wa 

Marekani Mike Straw kwa ajili ya 

kuwasilisha pendekezo lake la 

kwenda Tanzania kilimalizika bila 

kupata muafaka.Wajumbe wa 

kikao kile hawakuridhia wazo la 

Mike la kwenda Tanzania kuonana 

ana kwa ana na rais Dr Vivian na 

kuumaliza mzozo uliopo.Badala 

yake wajumbe walitaka kwanza 

kikosi ambacho tayari kimetumwa 

kwenda Tanzania kuchunguza kuhusu shambulio lile lililotokea 

uwanja wa ndege wa Julius 

Nyerere kiachwe kifanye 

uchunguzi wake na kama 

kutaonekana ulazima wa Mike 

kwenda Tanzania basi wataamua 

lakini kwa muda huo hali ya 

usalama ya Tanzania ilitia shaka 

kwa rais wa Marekani kufanya 

ziara 

Pamoja na mvutano mkali 

uliojitokeza katika kikao hicho 

bado Mike straw alishikilia 

msimamo wake wa kwenda 

Tanzania kuzungumza ana kwa 

ana na rais Dr Vivian.Kikao 

kilimazika bila muafaka na Mike 

straw kwa kutumia nguvu yake 

kama rais akaagiza ndege yake iandaliwe kwa ajili ya safari ya 

kwenda Tanzania ambayo alipanga 

kuianza saa nne za usiku.Baada ya 

kikao kile kumalizika akampigia 

simu Willy Gadner 

“Willy nimefanya 

maamuzi.Ninakwenda Tanzania” 

“Mheshimiwa rais !! Gadner 

akashangaa 

“Usiseme chochote 

Willy,nimeamua kwenda Tanzania 

kulimaliza hili suala.Ninataka 

kuonana ana kwa ana na Dr Vivian 

na kulifikisha mwisho hili 

jambo.Ni mimi ndiye niliyeanzisha 

hili suala na kama nisipochukua 

juhudi za kulimaliza basi 

litaniletea matatizo makubwa 

hivyo basi nataka nipate taarifa zote za kuhusiana na yule mtoto 

wa Dr Vivian ambazo naamini 

zitanisaidia sana kuweza 

kumshawishi akubaliane na 

matakwa yangu” akasema Mike 

“Lakini mheshimiwa rais hali 

ya usalama kwa sasa nchini 

Tanzania si nzuri na sikushauri 

ufanye hivyo unavyotaka kufanya” 

“Willy hakuna anayeweza 

kunizuia kufanya jambo 

lolote.Ninao ulinzi wa kutosha wa 

hiyo siwezi kuogopa kwenda 

katika nchi ndogo kama 

Tanzania.Ninaomba faili lenye 

taarifa zote za kumuhusu mtoto wa 

Dr Vivian linifikie hapa kabla ya 

saa tatu za usiku kwani ninaondoka saa nne usiku wa leo” 

akasema Mike na kukata simu 

“Lazima nifanye juhudi za 

kulimaliza suala hili kwa njia 

yoyote na njia pekee ninayoiona 

kwa sasa ni kwenda Tanzania 

mimi mwenyewe na kuzungumza 

na Dr Vivian.Sitaki Helmet 

afahamu kuhusiana na mpango 

huu wa kumuua” akawaza Mike 

DAR ES SALAAM – TANZANIA 

Baada ya kumfikisha Helmet 

Brian mahala ambako iliaminiwa 

ni salama zaidi kwa yeye kuwepo, 

Mathew na Meshack Jumbo 

walirejea ikulu kama alivyokuwa ameelekeza rais Dr Vivian.Moja 

kwa moja wakaelekea katika 

sehemu ya kupumzikia 

“Mathew” rais akaanzisha 

maongezi 

“Awali ya yote naomba 

nikushukuru sana kwa yote 

uliyoyafanya leo hii na vile vile 

kukupa pole kwa matatizo 

yaliyokupata usiku wa leo” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais .Yote yaliyotokea ni sehemu ya 

kazi.Ninamshukuru sana mzee 

Meshack kwa kuniondoa mikononi 

mwa polisi lakini naomba 

nikuweke wazi mheshimiwa rais 

kwamba si mimi niliyemuua Dr 

Robert Mwainamela.Kuna watu 

waliomuua na mimi nikaangushiwa mzigo ule mzito wa 

mauaji.Naomba uniamini na 

unisaidie mheshimiwa rais katika 

hilo kwani jeshi la polisi ninaamini 

hivi sasa wananitafuta kila kona 

hadi wahakikishe wamenipata na 

kunifikisha mahakamani kwa kosa 

la mauaji” akasema Mathew 

“Usihofu Mathew.Suala lako 

limekwisha malizika.Tayari 

nimekwisha toa maelekezo 

watafutwe wauaji halisi na wewe 

uachwe huru kwani hauhusiki kwa 

namna yoyote ile licha ya mauaji 

hayo kufanyika nyumbani kwako” 

akasema Dr Vivian 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais.Ahsante sana kwa kuniokoa”akasema Mathew kwa 

furaha kubwa 

“Mathew nilikueleza kwamba 

kuna mambo muhimu ambayo 

nataka tuzungumze.Nimeamua 

kufunguka kwako na kukueleza 

baadhi ya mambo ambayo nadhani 

unapaswa 

kuyafahamu.Nimechagua 

kuwaamini wewe na mzee 

Meshack na kuamua kuwaeleza 

baadhi ya mambo yangu ya siri na 

ninaamini mnavyo vifua vya 

kuweza kuyahifadhi haya mambo 

kwani sitaki kusikia mambo haya 

yametoka vinywani mwenu na 

kuwafikia watu wengine ambao 

hawatakiwi kuyafahamu” Akasema Dr Vivian na kunyamaza kisha 

akaendelea 

“Mathew nilikuondoa katika 

shughuli zako za biashara na 

kukuomba unisaidie kuchunguza 

nani waliomuua baba 

yangu.Wakati ukiendelea na 

uchunguzi wako nimekuzuia mara 

mbili usiendelee na 

uchunguzi.Nilifanya vile kwa 

sababu kuna mambo ambayo 

sikutaka uyafahamu kwani endapo 

ungeendelea zaidi na uchunguzi 

basi ungeweza kuyafahamu.Hata 

hivyo nilikuwa najidanganya 

kwani kila nilivyokuwa najaribu 

kukuzuia ndivyo ulivyokuwa 

unakaribia kuyafakia mambo hayo 

ambayo sikutaka uyafikie.Baada ya kutafakari nimegundua kwamba 

kuna ulazima wa kukueleza ukweli 

na nimekuita hapa kukueleza 

ukweli mtupu na nina hakika 

baada ya kumaliza mazungumzo 

haya tutakwenda sawa” 

akanyamaza kidogo halafu 

akaendelea 

“Ulinifuata ukanieleza 

kwamba una mashaka na Dr 

Robert na ukaniomba ruhusa 

umchunguze nikakataa.Nilikataa 

kwa sababu Dr Robert ni mtu 

ambaye anayafahamu mambo 

yangu kadhaa ambayo wengine 

hawayafahamu na kwa ufupi 

naweza kusema kwamba ni mtu 

niliyemuamini sana.Nilijua 

kwamba kama utamchunguza Dr Robert lazima kuna mambo 

utayafahamu kuhusu mimi ambayo 

sikutaka wewe au mtu mwingine 

ayafahamu kwani yangeweza 

kuniletea matatizo kama rais 

endapo yangefika kwa mahasimu 

zangu wa kisiasa.Pamoja na 

kujitahidi kuzuia usimfanyie 

uchunguzi lakini bado ulijikuta 

ukilazimika kufanya hivyo 

kutokana na umuhimu wake 

katika uchunguzi wake.Sikujua 

kama Dr robert alitumia ukaribu 

wangu kufanya mambo mengine 

kama ulivyogundua kwamba 

alikwa anashirkiana na 

Marekani.Sikulifahamu hilo na 

kama ningelifahamu hilo mapema 

ningekwisha muondoa katika serikali yangu zamani.Niliamini Dr 

Robert ni mtu safi na uadilifu wake 

si wa kutiliwa shaka.Uliponieleza 

kwamba Dr Robert ni mmoja wa 

watu walioshiriki katika mpango 

wa kumuua waziri Helmet Brian na 

kwamba amekuwa akitumiwa na 

Marekani katika mambo yao mbali 

mbali hapa nchini nilistuka 

sana.Nilikuwa naishi na nyoka 

mwenye sumu kali.Uliponieleza 

kuwa yuko nyumbani kwako 

nikamtuma Meshack Jumbo atume 

watu wake wakamuue.Niliamini 

endapo ungemuhoji basi 

angekueleza mambo mengi kuhusu 

mimi kitu ambacho sikuwa tayari 

kitokee.” Sura ya Mathew ikabadilika 

baada ya maneno yale ya Dr Vivian 

“You?! Akauliza kwa 

hasira.Meshack na Dr Vivian 

wakatazamana 

“Mathew kaa chini endelea 

kumsikiliza rais kwani ana mambo 

mengi ya kukueleza” akasema 

Meshack Jumbo 

“Siamini kabisa.Kumbe na 

wewe mzee umeshiriki katika 

jambo hili?Ninakuamini sana mzee 

wangu na siamini kama leo 

umenitenda hivi!! Akasema 

Mathew 

“Mathew tafadhali kaa chini 

bado kuna mengi nataka 

nikueleze.Yale yote uliyotaka 

kuyafahamu kutoka kwa Dr Robert utayapata hapa.Nitakueleza kila 

kitu”akasema Dr Vivian na Mathew 

akakaa chini lakini alikuwa 

amekasirika mno 

“Mathew naomba uelewe 

kwamba si jambo jepesi kuamua 

kufunguka mambo haya 

kwako,mambo ambayo sikutaka 

uyafahamu kabisa lakini kutokana 

na umuhimu wako nimeamua 

kufunguka kwako kila kitu na 

ninakuomba hata kama utaumia 

kiasi gani basi uvumilie hadi hapo 

nitakapomaliza.” Akasema Dr 

Vivian 

“Sawa mheshimiwa rais” 

akasema Mathew huku akitikisa 

kichwa kuonyesha kushangazwa 

kwake na maelezo yale ya rais “Baada ya kumuua Dr Robert 

niliwasiliana na polisi na wakafika 

nyumbani kwako mara moja na 

ulipoofika tu ukatiwa 

nguvuni.Lengo lilikuwa ni 

kukuondoa katika uchunguzi 

uliokuwa unaufanya ili usifike 

mahala ambako sikutaka ufike” 

“You wanted me to go to jail?!! 

Akauliza Mathew kwa ukali 

“Nilitaka kukuondoa 

usiendelee na uchunguzi” akasema 

Dr Vivian na Mathew akamtazama 

kwa hasira 

 “Kwa haya yote 

niliyokufanyia kwa nini 

ukanifanyia haya mheshimiwa 

rais? Jambo gani baya nilikufanyia 

mheshimiwa rais hadi ukafikia hatua ya kufanya maamuzi 

haya?Niliifanya kazi yako kwa 

moyo na kwa kujituma lakini 

kumbe nyuma yangu unapanga 

kuniangamiza”akasema Mathew 

“Mathew kama nilivyokueleza 

kwamba jambo hili si rahisi 

kwangu.Unadhani ni jambo rahisi 

kukuita hapa na kukueleza haya 

yote? Lakini nimeamua kuweka 

kila kitu wazi kwako ili baada ya 

kutoka hapa tuwe wote katika 

ukurasa mmoja.Naomba uendelee 

kuwa mvumilivu na usubiri hadi 

nitakapomaliza kile nilichopanga 

kukueleza.Tunaelewana Mathew? 

“Ndiyo mheshimiwa rais” 

akajibu Mathew. “Mzee Meshack 

hakukubaliana na kile nilichotaka 

kukifanya na akatumia akili yake 

kuweza kukuondoa katika mikono 

ya polisi.Aliponieleza kwamba 

amekuchukua toka mikononi mwa 

polisi tulishindwa kuelewana na 

japo nilikuwa naongea kwa ukali 

lakini kwa ndani nilikuwa na hofu 

kubwa kwani tayari nimekwisha 

kuogopa kwamba utafahamu 

mambo yangu jambo ambalo 

linaweza kuniweka katika 

matatizo makubwa.Baadae 

nikatafakari na kugundua kwamba 

bado ninakuhitaji sana na ndiyo 

maana nimekuita hapa na kuamua 

kukueleza mambo haya yote” akanyamaza na kumtazama 

Mathew halafu akaendelea 

“Kubwa ambalo sikutaka 

ulifahamu na ambalo niliamini 

endapo ungemuhoji Dr Robert 

angekueleza ni kuhusiana na 

mahusiano yangu na kampuni ya 

Tanbest Gemstone ltd.Tayari 

unazo taarifa za mimi kuwa na 

mahusiano na kampuni hii ya 

Tanbest na nimejilaumu sana 

kwani kitu ambacho nilikuwa 

najitahidi kukizuia lakini hatimaye 

umekifahamu hata hivyo nimeona 

nikueleze kwa kina ili uweze 

kuelewa kwani naamini taarifa 

hiyo uliyoipata haijakamilika” 

akanyamaza tena kwa muda wa 

sekunde kadhaa halafu akaendelea “Ni kweli kampuni ya Tanbest 

ni kampuni yangu”akanyamaza na 

kumtazama Mathew,akaendelea 

“Hii kampuni awali ilikuwa ya 

rais Anorld Mubara ambayo 

aliianzisha kabla hata ya kuwa rais 

na baada ya kupata urais 

alishindwa kuiendesha kutokana 

na kutingwa na majukumu mengi 

hivyo ikaanza kusua sua na kwa 

kuwa alikuwa na mahusiano 

mazuri na baba akamtaka 

amuuzie.Baba hakuwa na fedha za 

kuinunua kampuni hii hivyo 

akawatafuta wenzake 

wakaunganana ambao ni 

marehemu George Mzabwa na 

mwingine ni marehemu pia 

anaitwa Isdory mteka.Walifanikiwa kuinunua 

kampuni hii na kuanza kuiendesha 

kwa pamoja lakini baadae 

kukatokea mvurugano na chanzo 

cha mvurugano huo ni George 

Mzabwa.Baba hakuwahi kunieleza 

chanzo cha mvurugano huo ila 

anieleza kwamba kutokana na 

ukorofi wake George Mzabwa 

alipewa mgao wake na kuachana 

na kampuni hiyo wakabaki baba 

na Isdory wakiendeleza kampuni 

hiyo.Kutokana na baba kutingwa 

na shughuli nyingi alimuachia 

Isdory aiongoze kampuni hiyo hadi 

pale alipofariki kwa ajali ya gari na 

baba akabaki mmiliki pekee.Kwa 

mujibu wa baba,Isdory hakuwahi 

kuwa na mtoto na mke wake alitangulia kufariki na kutokana 

na urafiki mkubwa uliokuwepo 

baina yao,kwa hiari yake aliamua 

kuniandika mimi kama mrithi 

wake.Baada ya kufariki 

nikarithishwa hisa zote za Isdory 

lakini kwa wakati huo bado 

nilikuwa ninasoma hivyo baba 

hakutaka kunishirikisha katika 

biashara ila alinieleza kila kitu na 

pale nilipomaliza masomo 

alinitaka nirejee nyumbani 

niendeshe kampuni yetu kwani 

yeye alikuwa ametingwa na 

majukumu mengi ya kikazi lakini 

kwa wakati huo nilikuwa tayari na 

kazi nyingine nje ya nchi hivyo 

nikachagua kubaki 

huko.Aliponusurika katika ajali ya ndege alinipigia simu na 

kunifahamisha kwamba anataka 

nirejee nyumbani kwani alikwisha 

anza kuona hali ya usalama wake 

si nzuri lakini nilipuuza hadi pale 

alipofariki.Nilirejea nyumbani na 

kuamua kubaki hapa ndipo 

nilipoingia rasmi katika 

kuiendesha kampuni hiyo” 

akanyamaza kidogo akawatazama 

Mathew na Meshack halafu 

akaendelea 

“Nilipoingia katika harakati za 

kuwania urais ikanilazimu 

kutafuta mtu ambaye 

nitamkabidhi kampuni ile aweze 

kuiendesha kwani kama mtumishi 

wa umma sikutakiwa kuchanganya 

biashara na kazi ndipo nilipoikabidhi kampuni kwa mtu 

anaitwa Ranbir Kumar aweze 

kuiendesha.Kuna kitu kimoja 

katika kampuni hii ambacho 

nilikikuta na ambacho hata mimi 

niliendelea nacho.Ni kwamba 

kampuni hii inachuma fedha 

nyingi lakini hailipi kodi 

serikalini” akatulia kidogo na 

kuwatazama Mathew na Meshack 

halafu akaendelea 

“Kampuni hii ilikuwa ni ya 

watu wakubwa kwa hiyo walifanya 

mambo yao bila kulipa kodi 

serikalini na mfumo huo hata mimi 

nimeukuta na nikaurithi kwani 

kiwango chakodi ambacho 

wanapaswa kukilipa ni kikubwa 

mno.Sikutaka jambo hili lifahamike kwani tuliokua 

tunalifahamu ni watu watatu 

tu.Mimi ,Dr Robert na Ranbir 

Kumar.Ulifanikiwa kufahamu 

kuhusu Ranbir Kumar na ukaanza 

kumfuatilia ili kumuhoji 

kuhusiana na kampuni ile na 

aliogopa sana akanipigia simu 

akanieleza kwamba unamfuatilia 

na kama utakumbuka nilikupigia 

simu na kukutaka uachane na kila 

unachokifanya uje ikulu lakini 

hukufanya hivyo na kwa kuwa 

sikutaka umpate Ranbir nikatuma 

vijana waliomuua Ranbir pamoja 

na mke wa George Mzabwa 

aliyekuwa anafanya kazi katika 

kampuni hii.Usiku huo huo 

nikaagiza ofisi za kampuni ya Tanbest zichomwe moto na 

zikateketezwa.Sikutaka ufahamu 

chochote.Nilikua na hofu kwamba 

endapo ungefahamu siri hizi basi 

ungeweza kuzianika kwa watu 

wakazifahamu .Baada ya hapo 

niliamini nimemaliza kazi na 

sikuwa na wasiwasi kama 

ungeweza kupata 

chochote”Akanyamaza 

akamtazama Mathew aliyekuwa 

ameuma meno kwa hasira huku 

sura yake ameikunja. 

“Just relax Mathew.Nimeamua 

kukueleza ukweli na siku zote 

ukweli si mtamu.Vumilia kidogo 

nimalizie” akasema Dr 

Vivian.Meshack Jumbo alikuwa 

kimya kabisa akisikiliza na mara kadhaa alionekana akifuta jasho 

katika kipara chake 

“Mahusiano ya kampuni hii na 

Dr Robert yalianza pale 

aliponifuata na kunieleza kwamba 

kuna kampuni inaitwa Flamingo 

na ambayo wanataka kufanya 

biashara na kampuni 

yangu.Nilimuachia Dr Robert na 

Ranbir walishughulikie jambo hilo 

kwa kuwa tayari mimi nilikuwa 

rais na shughuli zote za uendeshaji 

wa kampni ile nilimuachia Ranbir 

Kumar.Walishughulikia suala hilo 

na baadae wakanijulisha kwamba 

wamekwisha malizana na kampuni 

hiyo ya Flamingo na Dr Robert 

akanieleza kwamba 

nimefunguliwa akaunti maalum katika benki ya Escom ambayo 

Flamingo watakuwa wananiwekea 

fedha ambazo zitanisaidia katika 

mamboyangu mbali mbali.Benki 

hii ya Escom ina sifa ya kuficha 

fedha chafu zisizolipiwa kodi na ni 

kimbilio la matajiri na viongozi 

mbalimbali ambao hawataki 

utajiri wao ujulikane hivyo benki 

hii ni kimbilio lao.Nilihakikishiwa 

kwamba akaunti hiyo ni ya siri na 

hakuna anayeweza 

kuifahamu.Sijawahi kuchukua hata 

senti moja katika akaunti hiyo na 

sifahamu mpaka sasa kuna kiasi 

lakini naamini kuna fedha nyingi 

sana.” akanyamaza kidogo 

akamtazama Mathew “Mathew naomba ufahamu 

kwamba tunaokalia kiti hiki cha 

urais si malaika ni wanadamu na 

kila mwanadamu hakosi 

mapungufu.Pamoja na mengi 

mazuri ambayo nimeyafanya na 

ninaendelea kuyafanya lakini hata 

mimi si mkamilifu ninayo 

mapungufu yangu na moja kati ya 

mambo mabaya ambayo nakiri 

nimeyafanya katika uongozi 

wangu ni hili la kuwa na kampuni 

isiyolipa kodi na kuwa na akaunti 

ya siri yenye fedha nyingi 

zisizotozwa kodi.Madini haya ni ya 

watanzania na sikupaswa kufanya 

hivi nilivyofanya” akanyamaza na 

kumtazama Mathew “Mathew hayo ndiyo mambo 

niliyotaka nikueleze” 

Mathew akashusha pumzi na 

baada ya muda akauliza 

“Why are you telling me all 

these madam president? 

“Kwa sababu nataka twende 

sawa.Katika uchunguzi wako 

lazima ungekutana na haya 

mambo kwa hiyo ni vyema endapo 

nikakueleza mapema na kwa 

mdomo wangu ili uyafahamu na 

twende pamoja.Hii ni siri yangu 

kubwa na ambayo ili kuificha 

imegharimu uhai wa watu kadhaa 

lakini nimeamua kukueleza kwani 

naamini yote mliyoyasikia hapa 

yatabaki katika vifua vyenu” 

akasema Dr Vivian.Ukimya ukapita “Mathew say something !! 

akasema Dr Vivian 

“Sina cha kusema 

mheshimiwa rais.Mambo haya 

uliyonieleza ni makubwa lakini 

mimi hayanihusu.Haya mambo 

ulipaswa kuwaeleza watanzania na 

si mimi.Kodi iliyokwepwa ni ya 

watanzania kwa hiyo kama ni 

kuwaomba msamaha unapaswa 

kujitokeza mbele yao na 

kuwaeleza kisha kuwaomba 

msamaha.Lakini mheshimiwa rais 

kwa nini ufanye hivi ulivyofanya? 

Umekuwa kinara wa kupambana 

na ukwepaji kodi na ufisadi lakini 

kumbe na wewe pia ni mmoja wa 

wakwepaji kodi wakubwa.Hii ni 

kashfa kubwa sana kuwahi kutokea katika nchi yetu na 

endapo wananchi watalifahamu 

jambo hili sijui nini yatakuwa 

maamuzi yao lakini tuachane na 

hayo kwanza ninashukuru sana 

kwa kuamua kuwa muwazi kwetu 

na kutueleza mambo haya 

mazito.Hayo mengine ya kodi na 

nini mimi hayanihusu utajua 

mwenyewe namna 

utakavyoyamaliza.Hata hivyo kuna 

mambo kadhaa nataka 

kuyafahamu toka kwako na kwa 

kuwa umeamua kunieleza ukweli 

basi naamini utanieleza ukweli 

wote” akasema Mathew na 

kunyamaza akamtazama Dr Vivian 

“Umeniambia kwamba George 

Mzabwa aliwahi kuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni hii 

akishirikiana na baba yako na 

mzee Isdory na baadae 

akatimuliwa lakini uchunguzi wetu 

umegundua kwamba George 

Mzabwa bado ana mashirikiano na 

kampuni hii ya Tanbest.Kuna 

fedha amekuwa anapokea kutoka 

kampuni ya Flamingo na kiasi cha 

mwisho kilichoingizwa katika 

akaunti yake iliyopo katika benki 

ya Escom ni shilingi milioni mia 

saba na sabini.George alitoa fedha 

hizo na kuziingiza katika akaunti 

tatu tofauti katika benki hiyo hiyo 

ya Escom.Akaunti hizo zote ni za 

kampuni ya Tanbest gemstone 

ltd.Akunti ya kwanza aliweka kiasi 

cha shilingi milioni sabini na hizi zikatolewa na Ranbir 

Kumar.Akaunti ya pili akaweka 

kiasi cha shilingi milioni mia sita 

na hamsini.Hizi zilitolewa na Dr 

Robert na akaunti ya tatu aliweka 

kiasi cha shilingi milioni hamsini 

na hizi zikatolewa na Ranbir 

Kumar.Kampuni hii ya Flamingo 

na kampuni ya A.D Electronics 

ambayo alikuwa anafanya kazi 

Nathan zote ni kampuni zilizo chini 

ya serikali ya Marekani kupitia 

shirika lake la ujasusi CIA.George 

alikuwa na mawasiliano na Nathan 

na alikuwa katika mtandao wa CIA 

na hii ni sababu kubwa 

iliyomfanya ajiue,Dr Robert pia 

alikuwemo katika mtandao wa CIA 

kwani alishiriki katika mpango wa kumuua waziri Helmet 

Brian.Flamingo ambayo ni 

kampuni ya CIA wanapitishia fedha 

katika benki ya Escom kupitia 

kampuni yako ya Tanbest 

Gemstone kwa ajili ya kufadhili 

operesheni zao mbalimbali hapa 

nchini Tanzania.Haya yote 

hukuyafahamu? Akauliza Mathew 

na sura ya Dr Vivian ilionyesha 

mshangao mkubwa 




Haya yote 

hukuyafahamu? Akauliza Mathew 

na sura ya Dr Vivian ilionyesha 

mshangao mkubwa 

“Mathew hayo mambo 

unayonieleza ni mageni 

kabisa.Kama nilivyokueleza 

kwamba shughuli zote za 

uendeshaji wa kampuni ya Tanbest 

niliziacha kwa Ranbir Kumar 

ambaye ndiye aliyekuwa 

akiniletea taarifa za maendeleo ya kampuni na baadae Dr Robert 

naye akaingia baada ya kuwaleta 

Flamingo.Kuna kiasi fulani cha 

fedha Dr Robert alikuwa anakipata 

kila mauzo yanapofanyika lakini 

hakuwa anahusika na chochote 

katika mambo ya kifedha na 

uendeshaji mzima wa 

kampuni.George Mzabwa ni mtu 

ambaye alikwisha ondolewa 

zamani katika kampuni toka 

wakati wa baba na hakuwa 

anahusika na chochote, Nimestuka 

sana kusikia kwamba watu hawa 

wawili wanajihusisha na masuala 

ya fedha za kampuni 

yangu.Kwanza kampuni ina 

akaunti moja tu na si tatu kama 

unavyodai.Nitakupa namba za akaunti hiyo ya kampuni 

uichunguze ili uamini 

ninachokwambia.Kama kuna 

akaunti nyingine zimefunguliwa 

basi zimefunguliwa bila ya mimi 

kufahamu.Inawezekana 

walinizunguka wakaamua 

kufungua akaunti hizo kwa jina la 

kampuni ya Tanbest kwa ajili ya 

mambo yao wenyewe” akasema Dr 

Vivian 

“Maelezo yako mheshimiw 

arais yananifanya niamini kwamba 

kulikuwa na mashirikiano baina ya 

George Mzabwa ,Dr Robert na 

Flamingo na walitumia kampuni 

yako kwa ajili ya kupitishia fedha 

zao chafu.Kingine ambacho 

unapaswa ukifahamu ni kwamba benki hii ya Escom inamilikiwa na 

Anderw Pillar au Edwin 

Washington ambaye ndiye mmiliki 

wa kampuni za Flamingo na A.D 

Electronics.Huyu amewekwa kama 

mmiliki wa kampuni hizi lakini 

ukweli ni kwamba ziko chini ya 

CIA na walimtumia Dr Robert 

ambaye ni mtu wao 

wakakufunguliwa akaunti katika 

benki yao na kukuwekea fedha 

ambazo hazikatwi kodi na huu 

unaonekana ulikuwa ni mtego wa 

CIA na wewe ukaingia kichwa 

kichwa bila kujua na sasa wanazo 

taarifa zako na wanaweza 

wakazitumia katika mapambano 

haya yanayoendelea hivi sasa 

kukuchafua kwamba nawe ni mmoja wa marais wakwepa kodi 

duniani” akasema Mathew 

“Oh my God !! akasema Dr 

Vivian na kushika kichwa chake 

“How could I be so stupid ?!! 

Huu ulikuwa ni mtego na 

nikaingia bila kujua.Dr Robert set 

me up.Nilimuamini sana Dr Robert 

kwa nini akanitenda hivi?Kwa nini 

sikuliona hili hapo kabla? 

“Watu hawa” akasema 

Meshack Jumbo ambaye muda 

mwingi alikuwa kimya akisikiliza 

“ Walifahamu kwamba siku 

moja watamuhitaji Dr Vivian 

kuwafanyia jambo fulani,hivyo 

wakatafuta kitu ambacho 

wanaweza wakakitumia kumfanya 

Dr Vivian akubali kufanya kile watakachomtaka awafanyie kwa 

kutishia kuvujisha taarifa zake za 

kumiliki akaunti ya siri yenye 

fedha zisizokatwa.Lakini na wewe 

mheshmiwa rais kwa nini 

ukakubali kwanza kuendesha 

kampuni isiyolipa kodi na pili 

kufunguliwa akaunti ya siri na 

kuwekewa fedha nyingi ambazo 

hazilipiwi kodi?.Hukujua kama 

hawa jamaa siku moja wanaweza 

wakatumia jambo hili kama fimbo 

ya kukuchapia? Unadhani ni kitu 

gani kitatokea endapo watanzania 

wanaokuamini watagundua 

kwamba rais wao wanayempenda 

ni mmoja wa mafisadi na wakwepa 

kodi? Huu utakua ni mwisho wako 

Dr Vivian na hawa maadui zako hawatakuacha 

salama.Watakuchapa kwa kila 

fimbo waliyonayo hadi 

wahakikishe hauwi kikwazo 

kwao.Watakupeleka wanavyotaka 

wao.Hautakuwa na kauli tena 

kwao.Haya yote hukuyafahamu 

Madam President? Akauliza 

Meshack Jumbo 

“Niliambiwa kwamba marais 

wengi wanahifadhi fedha zao kwa 

siri katika benki ya Escom na 

ambazo zimekuwa zinawasaidia 

kuishi maisha mazuri pale 

wanapokuwa wamemaliza kipindi 

chao cha uongozi.Niliona ni wazo 

zuri nikakubali niwe na akaunti ya 

siri.Sikufanya uchunguzi kubaini 

kama siku moja suala hili

 lingeweza kunigeukia.Sikuwahi 

kusikia hata siku moja taarifa za 

rais kuficha fedha katika benki ya 

Escom zimevuja.Niliamini hata 

mimi siri hii haiwezi kuvuja na 

ndiyo maana nikatumia nguvu 

yangu kulinda siri hii 

isijulikane.Ninajiamini katika 

maamuzi yangu mbali mbali 

ninayoyafanya na mara nyingi 

nimekuwa sahihi lakini katika hili 

nakiri nilikosea.I was so 

stupid.Sikupaswa kufanya hivi 

nilivyofanya”akasema Dr Vivian na 

kuinamisha kichwa. 

“Hii ni kashfa kubwa kuwahi 

kumpata rais wetu.Toka enzi za 

baba wa taifa kumepita marais 

kadhaa lakini hawajawahi kukumbwa na kashfa kubwa kama 

hii”akasema Mathew.Ukimya 

mfupi ukapita na Meshack Jumbo 

akakuna kipara chake na kusema 

“Dr Vivina naomba utuambie 

ukweli,hujawahi kuchukua hata 

senti moja katika fedha hizo 

ambazo unawekewa katika akauni 

ya siri? 

“Hapana Meshack sijawahi 

kugusa fedha hizo na wala sijui 

ziko kiasi gani na wala sijawahi 

kuweka fedhayangu huko bali 

fedha zote ninawekewa na 

kampuni ya Flamingo wakidai ni 

ahsante yao kwangu kwa kufanya 

nao biashara kwani madini yote 

yanayochakatwa katika kampuni 

ya Tanbest wanauziwa wao” akajibu Dr Vivian na Meshack 

akamtazama kwa makini kwa 

muda na kusema 

“Sijafanya nawe kazi kwa 

muda mrefu,lakini kwa muda huu 

mfupi niliokuwa karibu nawe 

nimegundua wewe ni mtu mkweli 

japo katika hili jambo uliteleza 

lakini hatuwezi kukuacha hivi 

hivi.Mimi kama mkuu wako wa 

idara ya usalama wa taifa siwezi 

kukubali kuona kashfa hii 

inaibuliwa na kukushusha 

chini.Mathew rais wetu 

amekwama na ni wajibu wetu 

kumkwamua.Hii ni kashfa kubwa 

sana endapo Marekani wataamua 

kuitumia dhidi ya rais wetu.We 

need to do something to get her out of this.Hili si suala lake tena.Ni 

suala letu sote.Huyu ni kiongozi 

wetu katika mapambano haya 

yanayoendelea kwa hiyo haijalishi 

amekosea au hajakosea lakini 

lazima tupambane tuhakikishe 

kwamba tunamtoa katika hili 

suala” akasema Meshack Jumbo na 

Mathew akawa kimya 

“C’mon Mathew think fast.You 

need to come up with something !! 

akasema Meshack Jumbo 

“Ndugu zangu kama kuna 

namna yoyote ile mnayoweza 

kunisaidia kunitoa katika janga 

hili ninaomba mnisaidie kwani 

sijui nitafanya nini endapo 

Marekani wataamua kutumia 

jambo hili kama fimbo ya

 kunichapia.Sikujua kama benki ile 

nayo ina mahusiano na CIA.Please 

help me.Mathew najua 

nimekukosea sana lakini naomba 

kwa sasa tuyaweke hayo yote 

pembeni na unisaidie katika 

hili.Kama kuna namna yoyote 

unaweza kufanya tafadhali 

nisaidie.Ninaamini uwezo wako na 

ninaamini unaweza kabisa 

kunisadia kulimaliza hili 

jambo.Please help me” akasema Dr 

Vivian na Mathew akainama 

akafikiri kwa muda na kusema 

“Ok.Niachie suala hili nitaona 

namna ya kufanya.Nitajitahidi 

kadiri ya uwezo wangu lakini 

siwezi kukupa uhakika wa moja 

kwa moja kwamba ninaweza kulimaliza ila nitajitahidi” 

akasema Mathew 

“Mathew ahsante sana.Laiti 

ungeuona moyo wangu namna 

unavyoshukuru….” 

“Pamoja na hayo” akaendelea 

Mathew 

“ Bado kuna mambo ambayo 

nahitaji kuyafahamu kutoka 

kwako “ 

“Kabla ya hapo kuna jambo 

ambalo ninataka niwafahamishe.” 

Akasema Dr Vivian 

“Nilizungumza na Helmet 

Brian.Huyu ni mtu mwenye nguvu 

sana ndani ya chama chake na 

alipaswa kuwa rais wa Marekani 

lakini kwa urafiki mkubwa uliopo 

kati yake na Mike Straw aliamua kujitoa katika harakati za kuwania 

urais akamuachia Mike.Helmet 

amechukizwa mno na kitendo cha 

Mike straw kuandaa mpango wa 

kumuua na yuko tayari kuanzisha 

vuguvugu la kumuondoa 

madarakani Mike straw lakini ni 

pale tu ambapo ushahidi wa 

kutosha utapatikana 

ukimuhusisha Mike straw katika 

mpango wa kumuua Helmet.Kwa 

kuwa Helmet ana nguvu sana 

katika chama chake akifanikiwa 

kumuondoa Mike straw na 

makamu wake wa rais madarakani 

atapendekezwa yeye kushika 

nafasi hiyo ya urais kwa muda na 

kwa kushirikiana naye tutaweza 

kuuzima mgogoro mkubwa unaofukuta hivi sasa baina ya 

mataifa yenye kumiliki silaha 

nzito.Kwa hiyo basi ninataka 

Mathew uwahoji wale watu ambao 

walitumwa kuja kumuua 

Helmet.Jitahidi kwa kila uwezavyo 

kuweza kupata taarifa muhimu 

kutoka kwao.Meshack Jumbo 

atakuwezesha kwa kila kitu katika 

kufanikisha hili jambo”akasema Dr 

Vivian 

“Ahsante mheshimiwa rais 

kwa kunikabidhi jukumu hilo na 

ninakuahidi nitafanya kila 

linalowezekana hadi nipate 

ushahidi huo usiona hata chembe 

ya shaka” akasema Mathew 

“Ahsante sana.Meshack mpe 

Mathew msaada wowote 

atakouhitaji katika kulifanikisha 

hilo jambo muhimu”akasema rais 

“Sawa mheshimiwa 

rais.Atapata kila aina ya 

ushirikiano anaohitaji” 

“Good”akasema Dr Vivian 

“Mathew nilikukatisha kuna 

jambo ulitaka kuuliza” 

“Mheshimiwa rais bado kuna 

jambo moja ambalo nahitaji 

kulifahamu toka kwako kabla 

sijaondoka hapa usiku huu” 

akasema Mathew 

“Jambo gani Mathew? 

“CIA wamekuwa 

wanakufuatilia kwa muda 

mrefu.Toka angali unasoma chuo 

kikuu nchini Marekani 

walimpandikiza Nathan ambaye alikuwa na kazi ya kukuchunguza 

na ambaye baadae mkawa wapenzi 

na mlikaribia hata kufunga 

ndoa.Baada ya Nathan wakamtuma 

tena Tausi ambaye jina lake halisi 

ni Olivia Howard.Wote hawa 

walikuwa na kazi moja tu ya 

kukuchunguza na kuhakikisha 

wanapata taarifa zako 

mbalimbali.Nimejiuliza maswali 

mengi kuhusiana na CIA kutumia 

muda mrefu kukufuatilia.Kuna 

jambo lolote ambalo 

wanalichunguza toka kwako?Kuna 

siri yoyote ambayo unayo na 

wanataka kuifahamu? Kama kuna 

chochote unakifahamu kuhusiana 

na hili mheshimiwa rais ni bora 

ukaweka wazi kwetu ili kwa pamoja tuweze kujua namna ya 

kukusaidia kwani hatujui mpaka 

sasa CIA ni taarifa gani 

wamekwisha zipata kwani 

wamekuchunguza kwa muda 

mrefu sana” akasema Mathew 

“Anachokisema Mathew ni 

sahihi mheshimiwa rais kama 

kuna jambo ambalo unadhani 

tunapaswa kulifahamu tafadhali 

tueleze angali bado mapema.Sisi ni 

washirika wako na 

tutakulinda.Tutaichukua siri yako 

katika vifua vyetu kwa maisha yetu 

yote” akasema Meshack 

Jumbo.Baada ya tafakari fupi Dr 

Vivian akasema 

“Naomba jambo hili 

tulizungumze siku nyingine.Kwa usiku huu haya tuliyoyazungumza 

yanatosha.Tushughulikieni 

kwanza haya mambo 

tuliyoyaongea usiku wa leo” 

akasema Dr Vivian 

“Sawa mheshimiwa 

rais,tunakwenda kuanza kazi hiyo 

sasa hivi” akasema Meshack 

Jumbo.Wakainuka na kuagana na 

kuanza kuondoka.Baada ya kama 

hatua tano hivi Dr Vivian akamuita 

Mathew 

“Naam mheshimiwa rais” 

akaitika Mathew kwa adabu na 

kurejea mahala alipokuwa amekaa 

rais 

“Thank you so much for 

today.Umefanya kazi kubwa sana 

na unastahili pongezi.Sahau yale yote yaliyopita na tuanze ukurasa 

mpya.Wewe ni mtu muhimu sana 

kwangu.Nipigie simu muda 

wowote ule uutakao” akasema Dr 

Vivian.Mathew akatabasamu na 

kusema 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais kwa heshima hii kubwa” 

akasema Mathew na 

kuondoka.Wakaingia katika gari la 

Mathew na kuondoka.Safari 

haikuwa na maongezi.Meshack 

Jumbo akagundua kitu 

“Mathew I’m sorry.” Akasema 

“Umenisikitisha sana mzee 

Jumbo.How can you do this to me? 

Kwa nini hukunieleza kama 

ulituma watu wakamuue Dr Robert mpaka ukaniacha nikaingia katika 

matatizo? 

“Mathew I’m sorry.I was just 

following orders” akajibu mzee 

Meshack 

“Hata kama ulitumwa kufanya 

hivyo ulipaswa kuniambia mzee 

Jumbo.Wewe ni mtu ambae 

ninakuamini sana na sikutegemea 

kama unaweza kunificha jambo 

kubwa kama hili na kuniacha 

nikaingia katik amikono ya 

polisi.Tulianza pamoja operesheni 

hii lakini umeanza 

kunigeuka.Yawezekana hata kama 

kungekuwa na mpango wa kuniua 

ungenificha!! 

“Kwa nini unadiriki kusema 

hivyo Mathew wakati unafahamu kabisa kwamba siwezi kufanya 

hivyo?Mathew wewe ni kama 

mwanangu.Jambo hili lilikuwa nje 

ya uwezo wangu.Ilikuwa ni amri ya 

rais ambayo nisingeweza 

kuipinga.Unafahamu ni mambo 

gani niliyokumbana nayo katika 

suala hili hadi ukawa 

huru?Nimepata misuko suko 

mikubwa toka kwa rais kwa 

sababu sikumuunga mkono katika 

kitendo chake cha kutaka 

kukuangushia mzigo ule mkubwa 

wa kesi ya mauaji lakini 

nimesimama imara na 

kuhakikisha unakuwa 

huru.Mambo haya yanatokea sana 

katika hizi kazi na hata wewe 

unafahamu Mathew.Nakubali nilifanya kosa na ninaomba 

samahani” 

“Jambo gani lingine 

unalifahamu ulilotumwa na rais 

ulifanye ambalo 

hujanieleza?akauliza Mathew 

“Hakuna jambo lingine” 

“Are you sure? 

“Yes I’m sure” 

“Good.If we want to suceed in 

this mission we need to trust each 

other” 

“You have to trust me 

Mathew” akasema Meshack na 

safari ikaendelea 

“ Tunaanzia wapi? Akauliza 

Meshack Jumbo 

“Tunaanza kwanza 

kulishughulikia suala la ile akaunti ya Dr Vivian.” Akasema Mathew na 

kunyamaza kwa muda na kusema. 

“Kwa nini lakini akafanya 

vile? Hakujua kama siku moja 

jambo hili lingefahamika? 

“CIA walitumia mbinu kubwa 

ya kumtumia mtu wa karibu na Dr 

Vivian ili kulifanikisha 

hilo.Tunapaswa kulishughulikia 

suala hili kwa haraka zaidi ili 

wasije wakalitumia kutaka 

kumshinikiza aweze kufanya 

wanavyotaka wao”akasema 

Meshack 

“Suala hili litamalizika 

usihofu.Hata hivyo ninashukuru 

kwa Dr Vivian kuamua kuwa 

muwazi kuhusiana na mambo 

yake.Kama angefunguka kuanzia mapema tayari tungekwisha 

maliza haya mambo muda mrefu” 

akasema Mathew 

Walifika nyumbani kwa 

Austin na kukuta shughuli ya 

udukuzi inaendelea 

“Kuna chochote mmekipata 

hadi sasa? Akauliza 

“Kuna jambo 

tumeligundua.Pesa ambazo Dr 

Robert alizitoa katika akaunti ya 

kampuni ya Tanbest aliweka kiasi 

cha shilingi milioni mia moja na 

ishirini katika akaunti nyingine ya 

siri iliyopo kwenye benki ya 

Escom na baada ya kuichunguza 

akaunti hiyo tumegundua kwamba 

akaunti hiyo ni ya John Aminiel Mkoka mkuu wa jeshi la polisi 

nchini.” 

“IGP? Akauliza Mathew 

“Ndiyo Mathew.”akajibu 

Austin 

“Hii ni hatari.Hata mkuu wa 

jeshi la polisi naye yumo katika 

mtandao huu?akasema Mathew na 

kunyamaza kidogo halafu akasema 

“Sasa nimepata jibu 

kuhusiana na wale watu 

waliokuwa wanavamia wakiwa na 

sare na magari ya polisi.Huyu 

mkuu wa jeshi la polisi anayo 

majibu.Good job guys” akasema na 

kuchukua simu yake akampigia 

rais 

“Hallow Mathew” akasema Dr 

Vivian “Mheshimiwa rais kuna jambo 

tumeligundua katika uchunguzi 

wetu.Tumegundua kwamba mkuu 

wa jeshi la polisi nchini Inspekta 

jenerali John Aminiel Mkoka naye 

ni mmoja wa watu waliomo katika 

mtandao wa CIA.Ninaomba haraka 

sana atiwe nguvuni ili tumfanyie 

mahojiano” akasema Mathew na 

Dr Vivian akavuta pumzi ndefu 

“Mathew hili si suala 

jepesi.Una uhakika nalo ? 

“Yes I’m sure madam 

president” akasema Mathew 

“Ok sawa.Nitamuweka katika 

kizuizi cha nyumbani kwake hadi 

hapo mtakapomfanyia 

mahojiano.Huyu ni mtu mkubwa 

na hatuwezi kumuweka nguvuni bila kuwa na uhakika wa kutosha 

wa tuhuma zinazomkabili.” 

“Ahsante mheshimiwa rais” 

“Mathew” akaita Dr Vivian 

“Umeanza kulishughulikia lile 

suala? Akauliza 

“Ninalishughulikia 

mheshimiwa rais” 

“It is getting ugly please do it 

fast” 

“I’m on it madam 

president”akajibu Mathew 

“Thank you” akasema Dr 

Vivian na kukata simu 

“Jamani usiku wa leo hakuna 

kufumba ukope kwani kuna 

mambo makubwa ambayo 

tunapaswa kuyakamilisha kabla hakujapambazuka” akasema 

Mathew 

“Mimi na Mzee Jumbo 

tumetoka ikulu tulikuwa na 

mazungumzo mazito na 

mheshimiwa rais” 

Mathew akawaeleza 

kuhusiana na mazungumzo yao na 

rais,kila mmoja akabaki na 

mshangao 

“Mshangao huo mlioupata 

ndio huo hata mimi na mzee 

Meshack tuliupata alipotueleza 

mambo haya.Hata hivyo hatupaswi 

kuendelea kushangaa.Tunapaswa 

kumuondoa rais katika hili janga 

kwani aliwekewa mtego na 

akaingia kichwa kichwa bila 

kupima athari zake” “Do you trust her? Akauliza 

Peniela 

“Yes I do” akajibu Mathew 

“Mathew hili ni suala 

kubwa.Ukwepaji wa kodi ni jambo 

ambalo Dr Vivian amekuwa 

akipambana nalo toka ameingia 

madarakani lakini kumbe na yeye 

mwenyewe ni mkwepaji mkubwa 

wa kodi.Mathew hili suala 

linapaswa kwenda kwa wananchi 

walifahamu,wamfahamu rais wao 

ni mtu wa namna gani.Mimi siwezi 

kuwa sehemu ya kumsafisha mtu 

kama huyu.Huu ni uhalifu mkubwa 

na anapaswa awajibike kwa 

uhalifu wake huu mkubwa!! 

Akasema Austin kwa hasira “Austin naomba unielewe.Ni 

kweli rais alikosea na amekiri 

kwamba alikosea lakini ufahamu 

kwamba hii ni vita na hawa jamaa 

walifahamu kwamba itafika siku 

ambayo watamtaka Dr Vivian 

afanye watakavyo kwa kuwa 

wanazifahamu siri zake na Dr 

Vivian kwa kuogopa siri zake 

kuvuja na hata kushtakiwa 

angefanya kama ambavyo 

wangemtaka afanye.Hajawahi 

kugusa hata senti moja katika 

akaunti hiyo na wala hajui kuna 

shilingi ngapi mpaka sasa.Pamoja 

na hayo yote aliyoyafanya lakini 

tunapaswa tumsaidie.Hii si vita 

yake sasa ni vita yetu 

sote.Hatuwezi kuwaaacha Marekani wakashinda vita hii 

kwani rais wetu akiwa mtumwa 

wao na kufanya kila wakitakacho 

watakaoumia si Dr Vivian bali ni 

wananchi ambao rasilimali zao 

zinanyonywa.Hivyo basi kumsaidia 

Dr Vivian ni kuisaidia nchi 

pia.Hakuna kati yetu aliye 

mkamilifu kwa hiyo hata Dr Vivian 

naye si mkamilifu,ana mapungufu 

pia hivyo kama amekosea 

tumrekebishe na makosa 

aliyoyatenda yasijirudie tena 

lakini kwa sasa mategemeo yake 

yote yako kwetu.We have to help 

her” akasema Mathew 

“Mathew kama nilivyosema 

kwamba siwezi kuwa sehemu ya 

ujinga huu wa kumsafisha rais anayekwepa kodi.Unafahamu ni 

kiasi gani cha kodi ninalipa kila 

mwaka serikalini halafu mtu 

mkubwa kama rais anakwepa 

kodi?Hili halivumiliki lazima 

afikishwe katika vyombo husika na 

hatua stahiki zichukuliwe dhidi 

yake.Amarachi twende tuondoke 

zetu hatuwezi kuwa sehemu ya 

ujinga huu unaotaka 

kufanywa.Huu ni uhalifu 

mkubwa.Let’s go!! Akasema Austin 

kwa hasira huku akimshika mkono 

mke wake Amarachi na kumvuta 

waondoke 

“No Austin! Akasema 

Amarachi na kumfanya Austin 

amtazame kwa hasira. “Siendi kokote.Mathew 

ameeleza wazi kuhusu suala hili ni 

suala letu pia.Tunatakaiwa 

tupambane tuhakikishe 

tunamuondoa rais katika janga 

hili.I’m staying with them” 

akasema Amarachi na kwa hasira 

Austin akataka kumnasa kibao 

lakini ghafla Camilla akageuka na 

kumpa Austin pigo moja kali 

lililompeleka chini.Wakati 

akishangaa nini kilichotokea 

akapewa tena pigo lingine na 

Camilla akamfuata pale chini 

akiwa na waya mkononi 

akamfunga mikono. 

“Samahani” akasema na 

kwenda kukaa.Wote mle ndani wakabaki wameduwaa kwa wepesi 

ule wa Camilla 

“Peniela tupe chumba 

tafadhali.We need to lock him 

up.Hatuwezi kushindwa kufanya 

kazi zetu kwa sababu yake” 

akasema Mathew na kuchukua 

waya mwingine akamfunga miguu 

na kisha akamvuta na kwenda 

kumfungia katika chumba 

alichoelekeza Peniela 

“I’m sorry Austin.Haya yote 

umeyataka mwenyewe” akasema 

Mathew na kutoka akaufunga 

mlango akimuacha Austin akipiga 

kelele 

“Naomba niweke wazi ndugu 

zangu kwamba jambo hili si jepesi 

hata kidogo lakini lazima tulifanye ili kumlinda rais wetu kwani 

aliingia katika mtego bila ya yeye 

kufahamu.Marekani watalitumia 

jambo hili ili kumlizimisha Dr 

Vivian afanye watakavyo wao na 

tukiruhusu hilo litokee ni jambo 

baya sana kwa nchi 

yetu.Watachota rasilimali zetu 

watakavyo kwani Dr Vivian 

hataweza kuwazuia kwa kuogopa 

siri yake hii isijulikane.We have to 

take her out of this in anyway we 

can.It’s not right but we have to do 

it.Kama kuna yeyote ambaye 

hajisikii kuendelea na sisi aweke 

wazi msimamo wake” akasema 

Mathew na wote wakawa kimya. 

“Good.Wote tuko pamoja” 

akasema “Mathew tumekwishakuelewa 

hivyo tupe kazi yakufanya kwani 

muda unakwenda kwa kasi” 

akasema Peniela 

“Peniela wewe utatusaidia 

sana kuhusu suala hili.Wewe ni 

mmoja wa wamiliki wa benki hii ya 

Escom tafadhali tupe namna bora 

ya kufanya.Tutawezaje kuzitoa zile 

fedha zote zilizomo katika akaunti 

ya Dr Vivian? Tutawezaje kuifunga 

hiyo akaunti? Akauliza Mathew 

Peniela akafikiri kidogo na 

kusema 

“Akaunti hii ni ya siri kwa hiyo 

taratibu zake huwa ngumu vile 

vile.Hata hivyo bado tunaweza 

kufanya hivyo ulivyoshauri yaani 

kuhamisha fedha kutoka katika akaunti hiyo na kuifunga 

kabisa.Tunachoweza kukifanya ni 

kuzihamishia fedha hizo katika 

akaunti yangu na halafu tutaifuta 

kabisa hiyo akaunti ya Dr Vivian” 

“Thank you so much 

Peniela.Utasaidiana na Camilla 

yeye ni mtaalamu sana wa 

kompyuta na ni mbobezi katika 

masuala ya udukuzi kwa hiyo 

utakuwa naye mkisaidiana.Mimi 

na Meshack Jumbo tuna kazi 

kubwa ya kwenda kuwafanyia 

mahojiano wale watu waliotumwa 

kuja kumuua Helmet 

Brian.Mtakapomaliza 

tutawasiliana tuwajulishe na sisi 

kitu tutakachokuwa tumefanikiwa 

kukipata”akasema Mathew “Mathew I’m coming with you” 

akasema Amarachi 

“Amarachi utabaki hapa na 

akina Peniela” 

“Hapana Mathew ninakwenda 

nanyi.Huwezi kwenda huko peke 

yako” akasema Amarachi na 

Mathew hakutaka kumkatalia 

wakaongozana hadi garini 

wakaondoka 

“’I’m sorry about your 

husband” akasema Mathew 

wakiwa garini 

“You don’t have 

to.Alichokifaya ni kitu cha kijinga 

sana na anastahili adhabu ile.Hili 

ni suala la kitaifa na kama 

tusipounganisha nguvu 

tutashindwa hii vita” akasema Amarachi.Baada ya muda Mathew 

akauliza 

“Amarachi unajua kutumia 

silaha? Akauliza Mathew 

“Austin hajawahi kukueleza 

chochote kuhusu mimi? Akauliza 

Amarachi 

“Hapana hajawahi kunieleza 

chochote. Ni muda mrefu umepita 

hatujaonana hadi leo hii” 

“Ninajua kutumia silaha” 

akasema Amarachi na kuwaeleza 

Mathew na Meshack Jumbo kwa 

ufupi kuhusu maisha yake namna 

alivyotekwa na kuishi msituni na 

kikundi cha kigaidi cha Boko 

Haram.Mathew alishangaa sana 

kusikia historia ile ya maisha ya 

Amarachi “Pole sana Amarachi kwa 

maisha haya uliyopitia” akasema 

Mathew 

“Imebaki ni historia.Nina 

furaha na maisha yangu ya 

sasa”akasema Amarachi.Wakiwa 

njiani Mathew akapigiwa simu na 

Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais” akasema 

Mathew baada ya kupokea simu 

“How is it going?akauliza Dr 

Vivian 

“Tayari tumeanza 

kulishughulikia lile suala na hivi 

sasa tunaelekea katika mahojiano 

na wale wauaji” 

“Mathew nimekupigia 

kukujulisha kwamba tayari mkuu 

wa jeshi la polisi nchini Inspekta jenerali John Aminiel Mkoka 

amewekwa kizuizini nyumbani 

kwake hadi hapo mtakapomfanyia 

mahojiano.Jitahidi kila kitu 

kimalizike usiku wa leo” akasema 

Dr Vivian 

“Nitajitahidi mheshimiwa 

rais” akasema Mathew na kukata 

simu 

“Tayari Inspekta jenerali John 

Mkoka amewekwa katika kizuizi 

cha nyumbani” Mathew 

akamwambia Meshack Jumbo 

“ Good.Mtandao wote wa 

Marekani hapa nchini lazima 

ujulikane leo” akasema Meshack. 




Mathew,Meshack Jumbo na 

Amarachi waliwasili katika 

nyumba ambayo watu watatu 

walioletwa nchini kwa kazi moja tu 

ya kumuua Helmet Brian walikuwa 

wamehifadhiwa.Hii ilikua ni 

nyumba maalum ambayo idara ya 

usalam wa taifa walikuwa 

wakiitumia kuwafanyia watu 

mahojiano.Kulikuwa na sehemu 

zaidi ya nane za mahojiano 

kutegemea na aina ya mtu na 

taarifa ambayo wanaihitaji. 

Kutokana na umuhimu 

wao,Meshack Jumbo alielekeza 

watu wale wafanyiwe mahojiano katika chumba kilichopo chini ya 

ardhi. 

“Watahojiwa mmoja mmoja” 

akasema Mathew na bila kupoteza 

muda mtu wa kwanza akaingizwa 

ndaniya kile chumba.Alikuwa 

amefunikwa mfuko kichwani 

akaketishwa katika kiti maalum 

kilichombana miguu na mikono 

halafu mfuko ule ukatolewa 

kichwani.Mathew aliyekuwa 

amesimama nje ya kile chumba 

akamtazama kupitia kioo kikubwa 

kilichowawezesha waliokuwa nje 

kuona ndani halafu akachukua 

karatasi iliyokuwa na picha za 

wale jamaa akaitazama kwa muda 

na kusema. “It’s time” akasema na 

kuufungua mlango akaingia ndani. 

WASHINGTON DC- MAREKANI 

Willy Gadner mkurugenzi wa 

shirika la ujasusi la Marekani 

aliwasili katika ikulu ya 

Marekani.Tayari ni saa mbili za 

usiku kwa saa za Marekani.Rais 

Mike straw akataarifiwa kuwa 

Willy gadner amefika na wakaenda 

katika chumba cha mazungumzo. 

“Natumai umekuja na taarifa 

zote kuhusiana na mtoto wa Dr 

Vivian” akasema Mike straw 

“Ndiyo mheshimiwa 

rais.Taarifa zote ziko humu” 

akasema Willy na kumkabidhi rais Mike straw faili lenye taarifa zote 

za Florentina mtoto wa Dr 

Vivian.Mike akalifungua na kuanza 

kupitia nyaraka zilizokuwemo 

ndani yake. 

“Ni mrembo sana huyu binti” 

akasema Mike na kulifunga lile 

faili 

“Ahsante sana Willy.Saa nne 

kamili nitaanza safari ya kuelekea 

Tanzania.Ni safari 

itakayonichukua saa kumi na mbili 

hadi kumi na tatu na ninategemea 

kesho jioni niwe nchini 

Tanzania.Ninataka nikalimalize 

suala hili mimi mwenyewe” 

akasema Mike 

“Mheshimiwa rais una hakika 

unataka kufanya hivi? “Ndiyo Willy.Ninataka kwenda 

kuweka mambo sawa.Ninafahamu 

athari za Helmet kuendelea kukaa 

Tanzania na ndiyo maana ninataka 

kufanya kila niwezalo kuhakikisha 

ninamrejesha nyumbani” 

“Mheshimiwa rais kitendo cha 

kumfuata rais Dr Vivian nchini 

kwake ni wazi kitaonyesha 

kwamba tayari umeshindwa na 

ndiyo maana ukaamua kwenda 

mwenyewe kumshawishi.Huu ni 

udhaifu mkubwa sana 

mheshimiwa rais.Kwa mtazamo 

wangu ninaona kama vile tunampa 

ushindi Dr Vivian katika hii vita” 

“Wengi watafikiri hivyo 

kwamba niko dhaifu na hadi 

nikaamua kumfuata Dr Vivian Tanzania lakini ukweli ni kwamba 

baada ya mpango ule wa kumuua 

Helmet kushindwa kufanikiwa 

tumeharibu kila kitu na hakuna 

mwingine anayeweza kuliweka 

sawa hili jambo zaidi yangu.Ni 

ziara itakayowastua wengi na 

wengi watajiuliza kwa nini 

nimeamua kwenda mwenyewe 

Tanzania ila ukweli wote 

ninaufahamu mimi.Bila kufanya 

hivyo sote tutakwenda na 

maji.Ninamfahamu vyema Helmet 

ni mtu mwenye nguvu hapa 

Marekani kwa hiyo lazima niende 

Tanzania kusawazisha mambo” 

Akasema Mike 

“Sawa mheshimiwa 

rais.Tayari umekwisha mtaarifu rais wa Tanzania kwamba 

unakwenda? 

“Sina mpango wa 

kumjulisha.Nataka nimjulishe 

wakati niko juu ya anga la 

Tanzania” 

“Hapana mheshimiwa rais hilo 

si wazo zuri.Ni vyema endapo 

utamjulisha kuwa unakwenda 

kuonana naye ili taratibu zianze 

kuchukuliwa” 

“Wasiwasi wangu ni kwamba 

anaweza akagoma nisiende nchini 

kwake na ndiyo maana ninataka 

nimfahamishe wakati tayari niko 

juu ya anga la Tanzania.” 

Willy Gadner akatoa faili 

katika mkoba wake na kumpatia 

Mike straw “Hiki nini Mike? 

“Hiyo ni taarifa nyingine 

inayomuhusu Dr Vivian ambayo 

inaweza kutusaidia katikampango 

wako.Dr Vivian ana akaunti ya siri 

katika benki ya Escom yenye fedha 

nyingi ambazo hazilipiwi 

kodi.Hatakubali taarifa hii 

ikawafikia wananchi wake kuwa 

naye ni mkwepaji wa kodi hivyo 

naamini akiliona faili hili atakubali 

kufanya kila utakachomuelekeza 

bila hata kumtumia mtoto wake” 

akasema Willy Gadner.Mike 

akalipitia lile faili na kutabasamu 

“Ahsnate sana Willy.Hili ni 

jambo kubwa sana 

mmelifanya.Nina uhakika wa 

kurejea hapa Marekani na Helmet Brian na wale watu wetu 

waliopotea”akasema Mike straw 

DAR ES SALAAM – TANZANIA 

Ni saa kumi na moja za alfajiri 

Mathew akishirikiana na Meshack 

Jumbo na Amarachi 

walipokamilisha zoezi la kuwahoji 

watu waliotumwa kuja nchini 

kumuua waziri wa mambo ya nje 

wa Marekani Helmet 

Brian.Haikuwa kazi rahisi lakini 

walifanikiwa kupata taarifa 

muhimu walizokuwa 

wakizihitaji.Wakati wa kuitekeleza 

kazi ile ilimlazimu Mathew kuzima 

simu yake na baada ya kumaliza 

zoezi akaiwasha na kukutana na taarifa ya namba kadhaa 

zilizomtafuta.Miongoni mwa 

namna hizo ilikuwa namba ya simu 

ya rais pia namba ya simu ya 

Peniela.Simu ya kwanza kupiga 

ilikuwa ni simu ya Peniela 

“Hallow Peniela” akasema 

Mathew baada ya Peniela kupokea 

simu 

“Mathew ! Umetupa wasiwasi 

mkubwa sana kila mara tulipopiga 

simu yako haikuwa 

ikipatikana.Uko salama? 

“Samahani sana kwa 

kuwaweka roho juu lakini niko 

salama kabisa.Nililazimika 

kuizima simu kutokana na 

shughuli nzito iliyokuwepo hapa 

lakini nashukuru tumemaliza na tumefanikiwa kupata taarifa 

muhimu tulizokuwa 

tunazihitaji.Vipi kwa upande wenu 

mmefikia wapi kuhusu lile zoezi? 

“Sisi pia tumelimaliza.Haikua 

kazi nyepesi lakini namshukuru 

Camilla ana utalaamu wa ajabu 

sana wa kompyuta na ndiye 

aliyesaidia kwa kiasi kikubwa 

tukafanikisha lile zoezi.Ilinilazimu 

kumshirikisha pia mtu wangu kule 

Ufaransa anaitwa Lydie ambaye 

naye kuna watu aliwashirikisha 

katika hii kazi lakini 

tumefanikiwa.Akaunti ilikuwa na 

fedha jumla ya shilingi trilioni tatu 

na bilioni mia sita.Fedha hizi zote 

zimeingizwa katika akaunti zangu 

na akaunti ile ya Dr Vivian imefungwa kabisa.Rais yuko 

salama” akasema Peniela.Mathew 

akashusha pumzi na kusema 

“Ahsante sana Peniela kwa 

jambo hili kubwa ulilolifanya.Hivi 

sasa bado kuna shughuli 

ninakwenda kuifanya sehemu 

fulani na baadae asubuhi nitakuja 

hapo” akasema Mathew na kukata 

simu kisha akampigia rais 

“Habari yako 

Mathew.Nimekutafuteni sana 

wewe na Meshack Jumbo lakini 

nyote hamkuwa mkipatikana 

simuni nikapata wasiwasi kuhusu 

usalama wenu.Vipi maendelo 

yenu? 

“Tunaendelea vyema 

mheshimiwa rais.Ilitulazimu kuzima simu zetu kutokana na kazi 

kubwa iliyokuwa inandelea lakini 

nashukuru tumefanikiwa kumaliza 

salama.Kwanza tumefanikiwa 

kuwahoji wale watu na tayari 

tumekwisha pata taarifa muhimu 

tulizokuwa tunazihitaji” akasema 

Mathew 

“Really ? akauliza Dr Vivian 

“Ndiyo mheshimiwa rais.Kuna 

mambo ya msingi tumeyapata 

kutoka kwa wale jamaa na 

nitakueleza tutakapoonana 

asubuhi” akasema Mathew 

“Vipi kuhusu ile akaunti? 

Akauliza Dr Vivian 

“Kuhusu ile akaunti tayari 

suala hilo nalo limemalizika” “Mathew ni Alfajiri sasa 

naomba kusiwe na masihara 

katika hili” 

“Hakuna masihara 

mheshimiwa rais.Jambo hili 

limemalizika tayari .Nitakupa 

maelezo kamili hapo baadae 

tutakapoonana.Kwa sasa naelekea 

nyumbani kwa mkuu wa jeshi la 

polisi nchini Inspekta jenerali John 

Mkoka kumfanyia mahojiano kisha 

nitakuja ikulu” akasema Mathew 

“Poleni sana Mathew kwa kazi 

kubwa mliyoifanya katika usiku 

wa leo.Nilipewa taarifa mida ya saa 

tisa hivi kwamba kuna ndege 

imetoka Marekani imebeba watu 

waliotumwa kuja kuchunguza 

kuhusiana na tukio la jana lililotokea pale uwanja wa ndege 

na ufahamu alipo Helmet.Kama 

ulivyosema kwamba baada ya 

kufanya mauaji wangetuma kikosi 

chao kuja Tanzania na 

kuwakamata wale watu 

waliowatuma na kama mpango 

wao ulivyokuwa watu wale 

wangekiri kutumwa na serikali ya 

Korea Kaskazini na mpango wa 

kuishambulia Korea Kaskazini 

ungefanikiwa.Nimewazuia watu 

hao kuingia nchini wala kutua 

katika uwanja wa ndege wowote 

hapa nchini na kwa taarifa 

niliyopewa waligeuza na kwenda 

kutua Nairobi kenya.Mathew 

ahsante sana kwa kuung’amua ule 

mpango wao” akasema Dr Vivian “Umefanya jambo zuri 

mheshimiwa rais la kuwazuia 

kuingia nchini kwani lengo lao 

lilikuwa hilo kuja kuwakamata 

wale jamaa ambao tayari 

tumekwisha watia mikononi na 

wameeleza kila kitu” akasema 

Mathew 

“Ahsante Mathew.Endelea na 

kazi tutaonana baadae.Kama kuna 

jambo lolote mnalihitaji tafadhali 

naomba unijulishe” akasema Dr 

Vivian na kukata simu. 

“Marekani tayari wametuma 

watu wao kuja nchini kwa ajili ya 

kufanya uchunguzi wa tukio la 

kushambuliwa Helmet.Kama 

walivyokuwa wamepanga walitaka 

kuja kuwakamata hawa jamaa ambao wangekiri kutumwa na 

Korea kaskazini lakini 

tumewawahi na kwa bahati nzuri 

rais hajawaruhusu waingie 

nchini”Mathew akamwambia 

Meshack Jumbo 

“Amefanya vizuri sana 

kuwazuia kutokuingia nchini.Vipi 

kuhusu akina Peniela 

umewasiliana nao? 

“Tayari nimewasiliana nao na 

wamefanikiwa lile zoezi” 

“Thank you Lord ! akasema 

Meshack Jumbo 

“Tusipoteze muda twendeni 

nyumbani kwa mkuu wa jeshi la 

polisi” akasema Mathew wakaingia 

ndani ya gari na kuondoka 

kuelekea nyumbani kwa mkuu wa jeshi la polisi nchini Inspekta 

jenerali John Mkoka 

“Amarachi nakupongeza sana 

kwa kazi kubwa uliyoifanya usiku 

wa leo.Nimefurahi sana kufanya 

kazi nawe.Umeonyesha kiwango 

kikubwa sana ambacho sikuwa 

nimekitarajia.Umesaidia mno 

katika kuwafanya wale jamaa 

wafunguke.Ahsante sana” akasema 

Mathew 

“Kama nilivyowaeleza 

kwamba niliishi na Boko Haram 

kwa muda wamiaka kadhaa na 

walinifunza mbinu nyingi za 

kuweza kumfungua mtu mgumu ili 

kupata taarifa muhimu” akasema 

Amarachi “Vijana mmefanya kazi kubwa 

na nzuri sana usiku wa 

leo.Sikuamini kama tungeweza 

kuwafungua wale jamaa kwani ni 

majasusi wenye kuelewa mbinu 

zote za kuhoji mateka lakini 

mlifanikiwa kuwafungua” akasema 

Meshack Jumbo 

Walifika nyumbani kwa mkuu 

wa jeshi la polisi nchini Inspekta 

jenerali John Mkoka ambako 

kulikuwa na watu kama kumi 

kutoka idara ya usalama wa taifa 

wameizunguka nyumba 

yake.Tayari kulikwisha anza 

kupambazuka.Sebuleni kulikuwa 

na watu sita na wote walikuwa na 

silaha na mkuu wa jeshi la polisi 

nchini Inspekta jenerali John Aminiel Mkoka alikuwa amejilaza 

sofani akiwa chini ya ulinzi na 

hakuruhusiwa kuondoka pale 

kwani hata alipokwenda chooni 

alikuwa chini ya 

ulinzi.Hakuruhusiwa kushika 

chochote wala kuzungumza na 

yeyote kwani hata simu yake 

ilikuwa imechukuliwa.Meshack 

Jumbo akawataka wale jamaa 

watoke nje na wawape nafasi ya 

kuweza kumuhoji mkuu yule wa 

jeshi la polisi. 

“Meshack Jumbo nini maana 

ya hiki mlichonifanyia? Akauliza 

John Mkoma kwa hasira 

“John,haya ni mambo ya 

kazi.Kuna mambo muhimu 

tunataka kuyaweka sawa halafu tutaona nini kitafuata.Vijana 

wangu wana mazungumzo nawe 

naomba uwape ushirikiano” 

akasema Meshack Jumbo 

“Mathew he’s all yours.Make 

sure he talks” Meshack 

akamwambia Mathew halafu 

akatoka nje wakabaki sebuleni 

Mathew,Amarachi na John Mkoka 

“Kama alivyosema mzee 

Meshack huu ni muda wa kazi na 

tutakuwa na maneno machache 

sana ya kuzungumza nawe na 

tunakuomba utupe 

ushirikiano”akasema Mathew 

“Nini hasa mnachokihitaji 

kwangu? Akauliza 

“Taratibu utafahamu mzee 

wangu” akasema Mathew na kuchukua kiti akamsoglea 

karibu.Amarachi akiwa na bastora 

alikuwa makini sana kujihami 

endapo hatari yoyote ingetokea 

“George Mzabwa aliyekuwa 

mkuu wa idara ya usalama wa taifa 

unafahamiana naye? 

“George nafahamiana naye 

ndiyo,japo hatukuwa na ukaribu 

sana.Mara nyingi tulikuwa 

tunakutana katika vikao vya 

kiserikali” 

“Vipi kuhusu Dr Robert 

Mwainamela unafahamiana naye? 

“Dr Robert ninafahamiana 

naye sana na kifo chake 

kimenistua mno” 

“Unafahamu chochote 

kuhusiana na Escom bank? “Escom bank?! 

“Ndiyo.Unaifahamu ? 

“Huwa naisikia sikia tu lakini 

siifahamu kiundani” 

“Hujawahi kufungua akaunti 

Escom Bank? 

“Hapana sina akaunti Escom 

bank na wala sifahamu mahala 

ilipo”akasema John Mkoka na uso 

wake ulionyesha wasi wasi 

“Kama alivyosema 

mkurugenzi wa idara ya usalama 

wa taifa hatuna muda wa kutosha 

kwa hiyo nataka nikueleze 

kwamba nimechukizwa na kitendo 

chako cha kutokutupa 

ushirikiano.Umetudanganya.Taarif

a zako zote tunazo”akasema Mathew na kuzidi kumchanganya 

yule mzee 

“Sjawadangana vijana wangu 

siifahamu hiyo benki kabisa” 

“Ngoja nikueleze ukweli mzee 

wangu.George Mzabwa alikuwa 

akipokea fedha kutoka kampuni 

ya Flamingo ambayo iko nchini 

Marekani na mara ya mwisho 

alipokea kiasi cha shilingi milioni 

mia saba na sabini akaziweka 

fedha hizo katika akaunti tatu za 

kampuni ya kuchonga madini ya 

Tanbest Gemstone.Katika moja ya 

akaunti,fedha zilichukuliwa na Dr 

Robert na akaweka katika akaunti 

yako iliyopo benki ya Escom kiasi 

cha shilingi milioni mia moja na 

ishirini” “No ! No No ! that’s a 

mistake.Mmekosea hiyo akaunti si 

yangu!akasema John Mkoka huku 

akitaka kuinuka 

“Sit down !! akasema Mathew 

kwa ukali 

“George Mzabwa alikuwa 

katika mtandao wa CIA hapa nchini 

na alikuwa akisaidia kufanikisha 

baadhi ya operesheni zao na 

alikuwa akilipwa pesa nyingi 

zilizopitia benki ya Escom.George 

ndiye aliyekuwa akipokea fedha 

halafu huzitawanya kwa watu 

wengine walio katika mtandao 

huo.Mtu mwingine ambaye 

alikuwa katika mtandao huo ni Dr 

Robert Mwainamela na sasa 

tumegundua kwamba wewe nawe ni mmoja wa watu waliomo katika 

mtandao huo na umekuwa 

ukipokea fedha kutoka CIA.Nataka 

kujua ni nani wengine walioko 

katika mtandao huu? Nani 

kiongozi wenu hapa nchini? Nini 

mipango yenu hapa nchini? Ukijibu 

maswali hayo mzee wangu nitaona 

namna ya kukusaidia lakini kama 

utaonyesha ukaidi nakuhakikishia 

huu utakuwa ndio mwisho 

wako.Maisha yako yote yaliyobaki 

yatakuwa gerezani” akasema 

Mathew 

“Vijana wangu kama 

nilivyowaeleza kwamba sina 

ukaribu wowote na watu hao 

wawili uliowataja ila 

tunafahamiana kwa kuwa wote walikuwa watumishi wa umma na 

tulikuwa tunakutana mara kadhaa 

sehemu mbali mbali.Kuhusu kuwa 

na akaunti katika benki ya Escom 

hilo ni jambo ninalolisikia kwa 

mara ya kwanza toka kwenu kwani 

sijui hata ilipo hiyo benki.Hizo 

fedha unazodai zimetumwa 

kwangu ni kichekesho 

kikubwa.Fedha zote hizo kwa kazi 

gani ? Mmi ninaishi kwa mshahara 

wangu na sina biashara yoyote ya 

kuweza kuniingizia kiasi hicho 

kikubwa cha fedha.Naomba 

mniamini vijana wangu” akasema 

Mkuu yule wa jeshi la polisi 

“Mzee hivi utuonavyo 

hatujafunga hata ukope,kwa usiku 

mzima tumekuwa tunapambana kwa maslahi ya taifa letu kwa hiyo 

hatutapenda kupoteza muda na 

wewe wakati kila kitu kuhusu 

wewe tunakifahamu.Inuka twende 

chumbani kwako” akasema 

Mathew na wakaongozana 

kuelekea katika chumba cha kulala 

akaufungua mlango wakaingia 

ndani. 

“Adabu gani hiyo mnaingia 

chumbani kwangu bila hodi? 

Akauliza kwa ukali mke John 

Mkoka 

“Samahani mama” akasema 

Mathew 

“Kitu gani hasa 

mnachokitafuta toka kwetu?Mume 

wangu halali usiku akifanya kazi ya kuhakikisha nchi iko salama 

kwa nini leo mnamfanyia hivi? 

“Mama,tunakubali kazi kubwa 

anayoifanya mumeo katika 

kuhakikisha raia wa nchi hii na 

mali zao wanakuwa salama lakini 

mumeo si malaika.Anajihusisha na 

mtandao ambao umekuwa 

ukifanya mambo mbali mbali 

maovu hapa nchini mtandao 

ambao unaundwa na shirika la 

ujasusi la Marekani CIA.Mtandao 

huo ndio unahusika katika kifo cha 

rais Anorld Mubara na matukio 

mengine mengi.Tunachotaka 

kutoka kwa mumeo ni kuufahamu 

mtandao wake wote na mambo 

gani waliyopanga kuyafanya halafu tutamsaidia lakini hataki 

kuonyesha ushir…” 

“Mathew” akaita Amarachi na 

Mathew akageuka 

“Kuna kasiki hapa pembeni ya 

kabati” akasema na Mathew 

akamgeukia mke wa IGP 

“Fungua lile kasiki” 

“Siwezi kulifungua sina namba 

za siri za kufungulia lile 

kasiki.Huwa analifungua yeye 

mwenyewe.Huhifadhi mamboyake 

ya siri” akasema 

“Fungua hilo kasiki” Mathew 

akamwambia John Mkoka lakini 

hakuonyesha kutaka kulifungua 

“Baba Judy ni kweli haya 

wanayoyasema hawa vijana? Akauliza mke wake lakini hakujibu 

kitu akabaki kimya 

“Nakuuliza baba Judy haya ni 

ya kweli? Akauliza mke wake. 

“Mbona hujibu unaninangalia 

kama bubu?Nataka unijibu haya 

wanayosema vijana ni ya kweli?! 

Akauliza mke wake kwa ukali 

lakini bado John hakujibu kitu 

chochote. 

“Fungua lile kasik..” 

Mlango ukagongwa na 

akaingia Meshack Jumbo akiwa na 

simu mkononi. 



Mlango ukagongwa na 

akaingia Meshack Jumbo akiwa na 

simu mkononi. 

“Mathew nimepewa simu ya 

John kuna hii namba imekuwa 

inampigia kwa karibu usiku 

mzima.” Akasema Meshack na kumpa Mathew ile simu.Jina 

lililoandikwa lilikuwa ni 110C 

“Huyu 110C ni nani? Akauliza 

Mathew lakini John hakujibu kitu 

Mathew akaipokea simu ile na 

kuiweka katika sauti kubwa ili kila 

mtu aliyemo mle ndani aweze 

kusikia. 

“Hallow” akasema na mtu 

aliyepiga ile simu aliyeonekana 

kuwa na haraka alidhani 

aliyepokea simu ile ni John Mkoka 

“John nimekutafuta kwa usiku 

mzima haukupokea simu 

yangu.Kwa nini ? Kuna tatizo 

lilikupata? Anyway tutazungumza 

baadae lakini kuna jambo la 

dharura ambalo ninataka 

kukujulisha na 

 kufanyiwa kazi haraka sana” 

akasema yule mpigaji ambaye jina 

lake lilionyesha ni 110C 

“Hey John are you listening to 

me? Akauliza 110C na kwa haraka 

Mathew akatoa bastora na 

kumnyooshea 

“I’m listening” akajibu John 

“Good.Nimepokea taarifa jana 

kwamba kuna mwanamke mmoja 

anaitwa Peniela amekuja hapa 

nchini.Huyu anazo taarifa muhimu 

sana ambazo zinaweza kuharibu 

mipango yetu yote.Anatakiwa 

ashughulikie haraka sana.Tayari 

amekwisha fahamika mahala alipo 

na unachopaswa kufanya kwa 

haraka andaa kikosi kiweze 

kumshughulikia haraka sana kabla hajakutana na watu wake akawapa 

taarifa muhimu.Ukisha andaa 

kikosi nijulishe mara moja ili 

niweze kukujulisha mahala 

alipo.Fanya hima hili jambo 

lilitakiwa liwe limemalizika toka 

usiku wa jana” akasema 110C.John 

akavuta pumzi ndefu na kusema 

kwa haraka 

“Niko mikononi mwa 

polisi.Please run they’re coming 

for y..”kabla hajamaliza sentensi 

yake Mathew akampiga ngumi 

nzito iliyompeleka chini na 

kuinyakua simu tayari 

ilikwishakatwa. 

“Mzee kwa haraka sana 

hakikisha unafuatilia hizi namba 

tujue ni namba za nani? Huyu mtu ambaye amempigia simu 

anaonekana ndiye kiongozi wa 

mtandao huu hapa nchini na 

anaokana ndiye anayepokea 

maelekezo kutoka makao makuu 

CIA na kisha kuyagawa majukumu 

kwa watu wa hapa Tanzania.We 

need to find her as quick as 

possible! Mathew akamwambia 

Meshack Jumbo na Meshack 

akatoka.Mathew akachukua simu 

na kumpigia Peniela akamtaka 

ampe simu Austin azungumze naye 

“Nakusikiliza Mathew” 

“Austin naomba 

unisikilize.Peniela amekwisha 

julikana kuwa you hapa nchini na 

kuna watu wanaweza wakatumwa 

sasa hivi kufika hapo kuwadhuru.Naomba uwatoe hapo 

nyumbani watu wote wapeleke 

sehemu salama.Nakuomba sana 

ndugu yangu” 

“Sawa Mathew nitafanya 

hivyo” 

“Ahsante Austin” akasema 

Mathew na kukata simu 

“Do you trust him? Amarachi 

akauliza baada ya Mathew 

kumaliza kuongea na Austin 

simuni 

“I trust him” akajibu Mathew 

na kumgeukia John 

“Nani aliyekupigia simu? 

Mathew akamuuliza lakini 

aliendelea kubaki kimya hakujibu 

chochote “Hata usipojibu kitu,muda si 

mrefu tutamfahamu mtu 

aliyekupigia simu na kwa kitendo 

ulichokifanya kimedhihirisha wazi 

kwamba wewe ni mmoja watu mlio 

katika mtandao wa Marekani hapa 

nchini” akasema Mathew na 

kumgeukia mke wa John 

“Mama nadhani umeshuhudia 

mwenyewe.Mumeo amekuwa 

anajihusisha na mtandao 

ulioundwa na shirika la ujasusi la 

Marekani hapa nchini,mtandao 

ambao umekuwa ukijihusisha na 

mambo kadhaa maovu.Mtandao 

huu umekuwa ukihusika na kuua 

watu, viongozi na ndio waliomuua 

rais Anorld Mubara na kwa sasa 

wanamuwinda rais Vivian.Mumeo amekuwa akipokea kiasi kikubwa 

cha fedha kutoka kwa CIA na mara 

ya mwisho amepokea kiasi cha 

shilingi milioni mia moja na 

ishirini zilizowekwa katika 

akaunti yake ya siri katika benki 

ya Escom” akasema Mathew na 

sura ya mke wa John ikabadilika 

“Baba Judy kwa nini 

umejiingiza katika hayo mambo? 

Shetani gani amekuingia na 

kukufanya ujiingize katika mambo 

hayo maovu? Hukujua kama siku 

moja unaweza kugundulika kama 

ulivyogundulika leo na kutuletea 

matatizo makubwa?!! Mama yule 

aliongea kwa hisia kubwa huku 

machozi yakimtoka “Mama,mumeo amejihusisha 

katika jambo kubwa na la hatari 

kwa usalama wa nchi na endapo 

atafikishwa mbele ya vyombo vya 

sheria basi maisha yake yote 

yanaweza yakamalizikia gerezani 

lakini endapo akionyesha 

ushirikiano kwetu tunaweza 

kumsaidia.Zungumza nay…..” 

Akasema Mathew lakini 

akakatishwa na Meshack Jumbo 

aliyeingia mle ndani na kumuita 

Mathew pembeni 

“Namba ile tayari 

imechunguzwa na imegundulika ni 

namba ya April Mubara mke wa 

marehemu rais Anorld Mubara” 

akasema Meshack Jumbo.Kwa 

takribani sekunde thelathini Mathew alishindwa kuzungumza 

akabaki anamtazama Meshack 

Jumbo.Taarifa ile ilimstua sana 

“Nimestuka sana.Sikutegemea 

kabisa kitu kama hiki.April 

Mubara?!! Akasema Mathew kwa 

mshangao 

“Tuma watu haraka sana 

wamuwahi wakamdhibiti kwani 

tayari amekwisha pewa angalizo 

kwamba tunamtafuta” akasema 

Mathew. 

“Mimi pia ninakwenda huko 

kuhakikisha kwamba kila kitu 

kinakwenda vyema.Hatupaswi 

kufanya kosa” akasema Meshack 

Jumbo 

Mathew aliamuru mkuu wa 

jeshi la polisi nchini Inspekta jenerali John Aminiel Mkoka na 

mke wake wachukuliwe kwa ajili 

ya kufanyiwa mahojiano kwani 

kwa wakati ule hakuonekana 

kutaka kusema chochote.Mathew 

na Amarachi wakapekua chumbani 

na kupata nyaraka mbali mbali 

ambazo waliona zingeweza 

kuwasaidia katika uchunguzi 

wao.Iliwalazimu pia kuling’oa 

kasiki lile na kuondoka nalo ili 

kwenda kulifungua na kujua 

kilichomo ndani yake. 

Kutoka nyumbani kwa 

Inspekta jenerali John Mkoka 

Mathew na Amarachi wakaelekea 

ikulu kuonana na rais.Walifika 

ikulu wakakaribishwa na rais akajulishwa kuhusu ujio wao na 

akaenda kuonana nao haraka 

“Mathew poleni sana” 

akasema Dr Vivian 

“Ahsante mheshimiwa 

rais”akasemaMathew na rais 

akaketi 

“ Mheshimiwa rais huyu 

anaitwa Amarachi january ni mke 

wa mwenzangu anayeitwa Austin 

ambao wanashirikiana nasi pia 

katika kazi tunayoendelea nayo” 

Mathew akafanya utambulisho 

“Karibu sana 

Amarachi.Nimefurahi kukuona” 

akasema rais na kusalimiana na 

Amarachi 

“Nipe habari Mathew” 

akasema rais “Mheshimiwa rais kama 

nilivyokueleza kwamba usiku wa 

leo ulikuwa ni usiku wa 

kazi.Tumepata mafanikio 

makubwa.kwanza tumefanikiwa 

kulimaliza lile suala la ile akanti ya 

siri na fedha zote ziko salama na 

akaunti ile imefungwa” akasema 

Mathew na Dr Vivian akashindwa 

kuyazuia machozi ya furaha 

kumtoka 

“I’m sorry nimeshindwa 

kujizuia kutoa machozi kwa furaha 

niliyonayo kwa jambo hili 

kumalizika kwani nijambo 

lililonifanya nikapungua uzito 

ghafla.Ni kashfa kubwa sana 

ambayo ingeweza kuniharibia 

kabisa taswira yangu katika jamii.Hata hivyo ninawahakikishia 

ndugu zangu kwamba fedha hizo 

ambazo zilikuwemo katika hiyo 

akaunti zitakwenda katika miradi 

ya maendeleo.Zote zitakwenda 

katika miradi ya elimu” 

“Mheshimiwa rais sisi kazi 

yetu ilikuwa ni kuhakikisha 

tunakusaidia kulimaliza hilo suala 

na namna utakavyozitumia fedha 

hizo ni juu yako.Tuachane na 

hilo.Tumewafanyia mahojiano 

wale watu watatu waliotumwa 

kuja kumuua Helmet 

Brian.Haikuwa rahisi lakini 

tumefanikiwa kupata taarifa 

muhimu tulizokuwa tunazihitaji.” 

“Oh thank you Lord! Akasema 

DrVivian “Watu wale wamekiri 

kutumwa na CIA kuifanya kazi ile 

ya kumuua waziri Helmet Brian na 

wamenieleza kila kitu ila kwa 

masharti kwamba tutahakikisha 

hawashtakiwi na hawarejeshwi 

Marekani bali wanapelekwa katika 

nchi wanazozitaka wao.” 

“Hilo halina shaka 

tutawatekelezea.Tunachohitaji sisi 

ni taaarifa hizo 

muhimu.Nitamtaarifu 

mwanasheria mkuu wa serikali 

alishughulikie hilo haraka 

sana”akasema rais 

“Ahsante mheshimiwa 

rais.Tukiachana na hilo turejee 

katika lile suala la mkuu wa 

polisi.Tuligundua kwamba mkuu huyu wa polisi alipokea kiasi 

kikubwa cha fedha kutoka kwa Dr 

Robert na ahsante kwa 

kunikubalia kumuweka 

kizuizini.Tumemfanyia mahojiano 

lakini amekuwa mgumu 

kufunguka hivyo tumempeleka 

sehemu maalum kwa ajili ya 

kuendelea kumuhoji.Wakati 

tukiwa nyumbani kwake alipigiwa 

simu na mtu ambaye jina lake 

liliandikwa 110C na 

tulipozichunguza hizo namba 

tukagundua kwamba ni namba za 

April Mubara mjane wa rais Anorld 

Mubara” 

“April Mubara?!! Dr Vivian 

akashangaa “Ndiyo mheshimiwa rais.April 

Mubara alimtaarifu John Mkoka 

kwamba Peniela yuko hapa nchini 

na kwamba amekuja na taarifa 

muhimu hivyo wanapaswa 

wamshughulikie haraka lakini 

mkuu wa polisi akamjulisha April 

kwamba akimbie kwani 

tunamfuatilia” 

“I cant believe this.Madam 

April?! Dr Vivian akazidi 

kushangaa 

“Ni kweli inashangaza sana 

mheshimiwa rais” 

“Kama ni hivyo basi sina wa 

kumuamuni tena kwani 

nimezungukwa na nyoka 

watupu.Huyu bi April ni mtu 

niliyemuheshimu kama mama yangu.Sasa nimepata picha 

kwamba anahusika na mtandao 

huu kwanindiye aliyemleta yule 

msichana Tausi akaniomba nimpe 

kazi ikulu na mimi kwa kuwa 

ninamheshimu sana nikampa kazi 

bila wasiwasi kumbe nilikuwa 

najipeleka mwenyewe katika 

mdomo wa Mamba.Mathew 

ahsante sana kwa kunifumbua 

macho.Mmechukua hatua gani za 

kumkamata huyu April? 

“Meshack Jumbo na vijana wa 

usalama wa taifa wako njiani hivi 

sasa wanaelekaa huko nyumbani 

kwa April Mubara kwenda 

kumkamata” “Good job Mathew” akasema 

Dr Vivian na kuinamisha kichwa 

akazama mawazoni 

“Madam president sisi 

tumepita mara moja 

kukufahamisha mahali tulikofikia 

katika kazi uliyotupa.Kwa sasa 

tunakwenda kuendelea kumfanyia 

mahojiano John Mkoka na baadae 

April Mubara mara tu 

atakapofanikiwa 

kukamatwa.Tutakujulisha kila 

kitakachojiri ila naomba suala la 

wale jamaa lifanyiwe kazi haraka 

kwani tayari nimekwisha waahidi 

kuwa tutawatekelezea kile 

wanachokihitaji” akasema Mathew 

na kuagana na rais wakaondoka 

moja kwamoja wakaeleka nyumbani kwa Austin ambako 

walikuwepo akina Peniela.Mara tu 

baada ya kufika mtu wa kwanza 

aliyetaka kuonana naye ni mwanae 

AnnaMaria lakini bado alikuwa 

amelala na hivyo wakaendelea na 

majadiliano ya kazi 

“Austin ahsante sana kwa 

msaada huu mkubwa kwa familia 

yangu” Mathew akamwambia 

Austin 

“Mathew naomba samahani 

sana kwa ujinga nilioufanya jana 

usiku.Nimejifikiria na nimeumia 

mno moyoni kwa mambo 

niliyoyafanya. Naomba unisamehe 

sana ndugu yangu na unishirikishe 

tena katika operesheni hii.” 

Akasema Austin “It’s ok Austin forget what 

happened last night .What we did 

wasn’t right lakini ilitulazimu 

kufanya vile kwa ajili ya manufaa 

ya nchi kwani watu wale walikuwa 

wamemuingiza Dr Vivian katika 

mtego naye akaingia bila kujua na 

wangetumia kigezo kile 

kumlazimisha afanye kila 

wakitakacho na nchi yetu 

ingeyumba sana kwani rais wetu 

angefuata kila amacho 

angeelekezwa na 

marekani.Rasilimali zetu 

zingeendelea kuchotwa kila uchao 

kwa sababu rais wetu anaogopa 

siri yake kujulikana.Tumelimaliza 

suala hilo na kwa sasa rais yuko 

salama.Hawataweza kutumia tena kigezo cha ile akaunti 

kumlazimisha rais wetu afanye 

mambo wanayoyataka wao hata 

hivyo rais ameliona kosa lake 

analijutia na ameahidi kutumia 

kiasi chote cha fedha 

kilichokuwemo katika akaunti ile 

kwa ajili ya miradi ya 

elimu.Tuachane na hayo usiku wa 

leo tumepiga hatua kubwa sana” 

Mathew akamueleza kila kitu 

walichokifanya usiku na Austin 

akajilaumu sana kwa kutokuwa 

sehemu yao kwa usiku ule. 

Wakiwa pale kwa Austin 

walifanikiwa kulifungua lile kasiki 

na ndani yake walikuta mabunda 

ya fedha yakiwa yamepangwa na 

vile vile wakakuta kuna nyaraka mbali mbali za muhimu ambazo 

zilionyesha kwamba John Mkoka 

alikuwa anapeleka kiasi kikubwa 

cha fedha kwa miezi minne 

mfululizo kwa kampuni ya ulinzi 

ya Chemi Security company 

“Sasa nimepata picha kwamba 

wale watu waliokuwa wakitumia 

sare na magari ya askari polisi 

wakifanya kazi ya kuvamia 

sehemu mbalimbali wanatoka 

katika kampuni hii ya 

ulinzi.Nilikuwa najiuliza namna 

wale jamaa wanavyopata vifaa vya 

jeshi la polisi wanavyotumia 

katika shughuli zao za 

uvamizi.Walikuwa wanapata 

ufadhili kutoka kwa huyu mkuu wa 

jeshi la polisi nchini Inspekta jenerali John Aminiel 

Mkoka.Kampuni hii napaswa 

kuwekwa chini ya ulinzi na 

kuchunguzwa kwa kina.Lazima 

wamilki wake wapatikane haraka 

sana na tufahamu ni matukio 

mangapi wamekuwa wakishiriki 

na wanatumwa na nani” akasema 

Mathew halafu wakaondoka 

kuelekea mahala walikopelekwa 

mkuu wa polisi John Mkoka na 

mke wake kwa ajili ya kuwafanyia 

mahojiano.Wakiwa njiani 

akapigiwa simu na Meshack jumbo 

ambaye alimjulisha kwamba 

wamefanikiwa kumpata April 

Mubara akiwa njiani kuelekea 

Zanzibar na boti na kulitokea 

mapigano na mmoja wa vijana wa Meshack alipigwa risasi na walinzi 

wa April akafariki dunia. 

****************** 

Saa tano za asubuhi rais wa 

Tanzania Dr Vivian alijulishwa 

kuhusu kuwepo angani kwa ndege 

ya rais wa Marekani.Taarifa hiyo 

ilimstua Dr Vivian kwani 

hakukuwa na taarifa zozote rasmi 

za ujio huo wa rais wa 

Marekani.Dege hilo liliruhusiwa 

kutua na Dr Vivian akamtuma 

makamu wa rais aende uwanja wa 

ndege akampokee rais huyo wa 

taifa lenye nguvu kubwa duniani. Dr Vivian alijiuliza maswali 

mengi kuhusiana na ujio ule wa 

kimya kimya wa Mike straw. 

“Anakuja kutafuta nini na kwa 

nini anakuja kimya kimya ? Hii 

inashangaza sana” akawaza Dr 

Vivian na kumpigia simu Mathew 

“Madam president” akasema 

Mathew baada ya kupokea simu 

“Mathew vipi maendeleo 

yenu? 

“Tunaendelea vyema 

mheshimiwa rais.Tumekwisha 

maliza kumfanyia mahojiano John 

Mkoka na sasa tunamfanyia 

mahojiano April Mubara ambaye 

ameletwa hapa muda si mrefu” 

“Good.Kuna jambo limetokea 

ambalo nimeona ni vyema nikakujulisha.Rais wa Marekani 

Mike straw yuko hapa nchini” 

“Yuko nchini? How? 

“Amekuja ghafla na mimi 

nimepata taarifa muda mfupi 

uliopita kwamba yuko katika anga 

ya Tanzania” 

“Anakuja kutafuta nini ?Kwa 

nini aje kimya kimya? 

“Hata mimi nimejiuliza 

maswali hayo lakini sijapata 

jibu.Nahisi kilichomleta ni hili 

suala la Helmet Brian.Kwa sababu 

hiyo kuna mambo nataka tufanye” 

akasema Dr Vivian na kuwapa 

maelekezo Mathew na Meshack 

Jumbo ya kuwapeleka ikulu 

Helmet Brian na wale wadunguaji 

watatu waliotumwa na Marekani kuja kumuua Helmet Brian jambo 

ambalo iliwalazimu Mathew na 

Meshack wawaache Austin na 

Camilla wakiendelea kumuhoji 

April Mubara na wao 

wakalishughulikia kwa haraka 

agizo la rais 

Helmet Brian alifikishwa ikulu 

haraka sana kama alivyoelekeza 

rais 

“Helmet natumai unaendelea 

vyema.Nimekuleta hapa kwa 

haraka kutokana na dharura 

iliyojitokeza.Hivi tuongeavyo rais 

Mike straw yupo hapa nchini na 

muda si mrefu atafika hapa ikulu” 

“Mike yupo hapa nchini? 

Helmet Brian naye akashangaa “Ndiyo.Amekuja kimya kimya 

na mimi nimejulishwa wakati 

tayari amekwisha ingia katika 

anga ya Tanzania” 

“Nini kimemleta ? 

“Nina hakika lazima litakuwa 

ni lile suala linalokuhusu wewe na 

ndiyo maana nikakuita uje hapa ili 

mpango wetu uweze kukamilika 

leo” 

“Imekuwa vizuri sana 

ameamua kuja yeye 

mwenyewe.Mungu ana makusudi 

yake kumleta mtu huyu na kazi 

yetu inakwenda kuwa 

rahisi”akasema Helmet na 

kuendelea na maongezi yao juu ya 

jambo alilomuitia pale Katika uwanja wa ndege wa 

Julius Nyerere Mike straw 

akapokewa na makamu wa rais na 

kupelekwa moja kwa moja 

ikulu.Hakukuwa na maandalizi 

makubwa yaliyofanywa kutokana 

na ujio ule wa ghafla lakini ulinzi 

aliokuja nao Mike ulikuwa mkali 

sana 

Mike straw aliwasili ikulu na 

kupokewa na Dr Vivian 

“Karibu sana 

Mike,nimeshangazwa sana na ujio 

wako wa ghafla” 

“Utanisamehe kwa kuja 

namna hii bila taarifa lakini 

sikutaka kuwapa wakati mgumu 

wa kufanya maandalizi hata hivyo 

safari yenyewe ilikuwa ya ghafla sana sikuwa nimepanga kuja 

Tanzania.Pole sana kwa yale yote 

yaliyotokea jana” akasema Mike 

“Ahsante sana Mike” akasema 

Dr Vivian 

“Dr Vivian kwakuwa ziara hii 

haitambuliki rasmi kiserikali 

sitaki nichukue muda wako 

mwingi hivyo ninaomba nimalize 

kile kilichonileta kwako.Tunaweza 

kupata faragha kwa mazungumzo? 

Akauliza Mike na Dr Vivian 

akampeleka katika chumba cha 

mazungumzo ya faragha 

“Dr Vivian narudia tena 

kukuomba samahani kwa kuja bila 

taarifa na kukuvurugia ratiba zako 

hata hivyo nitaenda moja kwa 

moja katika kitu cha msingi kilichonileta” akasema Mike na Dr 

Vivian hakujibu kitu akawa kimya 

akimsikiliza 

“Kikubwa kilichonileta hapa 

ni mazungumzo nawe.Nataka 

tuyamalize mambo yaliyojitokeza 

baina ya nchi zetu na ambayo 

yanaendelea kujitokeza.Tanzania 

na Marekani ni marafiki kwa 

miaka mingi na Marekani 

tumekuwa tukifadhili miradi mingi 

ya maendeleo hapa Tanzania,vile 

vile tumekuwa ni wachangiaji 

wakubwa wa bajeti kuu ya serikali 

kwa miaka mingi.Tanzania na 

Marekani hazipaswi kuingia katika 

msuguano kama huu unaoendelea 

hivi sasa na ndiyo maana 

nimeamua kuja mimi mwenyewe kulimaliza hili suala” akanyamaza 

kidogo na kuendelea 

“Nilimtuma waziri wangu wa 

mambo ya nje aje kuzungumza 

nawe kuhusiana na ule mpango 

wako wa mashirikiano na Korea 

kaskazini lakini likatokea 

shambulio ambao tunaamini 

lilimlenga yeye na mpaka sasa 

hajulikani alipo na hatujapokea 

taarifa yoyote rasmi kutoka 

serikali ya Tanzania kuhusiana na 

nani aliyefanya shambulio lile na 

waziri wetu yuko wapi hadi hivi 

sasa” 

akanyamaza tena na kuendelea 

“Tukiweka pembeni 

hayo,mimi na wewe tunafahamu 

fika nini hasa kilichotokea na unafahamu ni wapi alipo Helmet 

Brian.Tunazo taarifa zote za 

kilichotokea na sitaki kupoteza 

muda hapa kuzungumzia hayo 

mambo kwani unayafahamu na 

ndiyo maana nimekuja mwenyewe 

ili tulimalize hili suala kimya 

kimya” Akanyamaza akamtazama 

Dr Vivian na kuendelea 

“Vijana wako tayari 

wamekupa taarifa zote kuhusiana 

na nini ulikuwa mpango wa 

Marekani.Kwa bahati mbaya 

mpango wetu haukwenda kama 

tulivyokuwa tumeupanga na 

ninafahamu kwamba kutokana na 

msuguano kati yetu unaweza 

ukautangazia ulimwengu nini 

tulitaka kukifanya kwa waziri Helmet Brian jambo ambalo 

linaweza kutushushia heshima 

yetu duniani.Nimekuja kufanya 

makubaliano nawe ili jambo hilo 

libaki siri kati yetu” akasema Mike 

straw na Dr Vivian akatoa kicheko 

kidogo 

“Makubaliano? Hicho ndicho 

kilichokutoa Marekani hadi 

Tanzania kufanya makubaliano 

nami? Akauliza Dr Vivian



Makubaliano? Hicho ndicho 

kilichokutoa Marekani hadi 

Tanzania kufanya makubaliano 

nami? Akauliza Dr Vivian 

“Ndiyo Dr Vivian.Mimi na 

wewe tayari tunafahamiana vyema 

na kila mmoja ana mambo yake ya 

siri ambayo hataki yajulikane 

hivyo basi tutafanya makubaliano 

ambayo yatafanya midomo yetu 

ifungwe na kila mmoja apate 

anachokihitaji na siri zetu ziendelee kuwa salama”akaema 

Mike na Dr Vivian akatoa tena 

kicheko 

“Mike umenifurahisha 

sana.Hukupaswa kupoteza mafuta 

yako ya ndege kutoka Marekani 

kuja hadi Tanzania wakati 

ukifahamu fika kwamba mimi 

nawe hatuwezi kufanya 

makubaliano yoyote.Hakuna 

chochote tunachoweza kukiongea 

kwa sasa au kuweka makubaliano 

yoyote.”akasema Dr Vivian na sauti 

yake ilianza kuonyesha kukasirika 

“Dr Vivian naomba 

usikasirike.Maongezi haya ni ya 

amani tupu.Twende taratibu 

tutafikia makubaliano” akasema 

Mike na kufungua mkoba wake akatoa faili na kumkabidhi Dr 

Vivian. 

“Tuanze kwanza na hili.Faili 

hilo lina maelezo yote ya 

kuhusiana na akaunti yako ya siri 

ambayo iko katika benki ya Escom 

ambako umekuwa ukificha fedha 

nyingi ambazo hazilipiwi kodi.Dr 

Vivian wewe ni mmoja kati ya 

marais waliotajwa kufanikiwa kwa 

kiasi kikubwa katika mapambano 

dhidi ya rushwa na ukwepaji kodi 

barani Afrika na kuwa rais wa 

mfano.Unadhani itakuaje 

wananchi wako,bara la afrika na 

dunia nzima watakapofahamu 

kwamba umekuwa ni mkwepaji 

kodi mkubwa na unaficha fedha 

zako katika akaunti ya siri? Hii ni kashfa kubwa sana ambayo 

haijawahi kutokea katika nchi ya 

Tanzania na hili litakuwa ni 

anguko lako kubwa kwani 

utashtakiwa kwa uhujumu 

uchumi.Kwa nini basi jambo hili 

lisiendelee kuwa siri na wewe 

ukaendelea kumiliki fedha zako 

zote na utakapomaliza muda wako 

wa uongozi uishi maisha mazuri 

kama malaika? Hili litaendelea 

kuwa siri endapo tu utakubaliana 

na masharti yangu” akanyamaza 

na kumpa nafasi DrVivian alipitie 

lile faili.Alipomaliza akamtazama 

Mike 

“Nini hasa unachokihtaji 

kwangu Mike? Akauliza.Mike akatabasamu na kwa haraka 

akasema 

“Kwanza nataka umrejeshe 

Helmet Brian kwani najua kuna 

mahala umemficha,nataka vile vile 

uwarejeshe watu wetu wawili 

waliopotelea hapa nchini kwako 

ambao naamini unafahamu mahala 

walipo,tatu nataka uufunge 

mdomo wako kuhusiana na 

mpango wa Marekani kutaka 

kumuua Helmet Brian na nne 

nataka mpango wa mashirikiano 

baina ya Tanzania na Korea 

kaskazini usitishwe haraka sana 

na uitangazie dunia kwamba 

Tanzania imewakamata watu 

watatu waliotumwa na Korea 

Kaskazini kumuua Helmet Brian.Ukifanya hayo hili suala 

litabaki kuwa siri” akasema Mike 

na Dr Vivian akamtazama kwa 

dharau na kutoa kicheko kidogo 

halafu akamrushia Mike lile faili 

“Mike kwa nini unaidhalilisha 

Marekani kiasi hiki? Kwa nini 

umechoma mafuta 

yanayonunuliwa kwa kodi za 

wananchi wako kwa ajili ya kuja 

kunieleza upuuzi huu? Una 

uhakika na hiki 

ulichokisema?Mimi siwezi kufanya 

ujinga wa namna hiyo Mike.Mimi 

ni rais ninayetembea katika 

maneno yangu na siku zote 

ninakuwa ni mfano wa 

kuigwa.Siwezi kamwe kupambana 

na wakwepaji kodi na wakati huohuo mimi nikawa mkwepaji 

kodi wa kiwango hiki.Ninaomba 

uwasiliane na watu wako 

waliokupa taarifa hii na 

wathibitishe kuhusu mimi kuwa na 

akaunti hii na kama ni kweli nina 

akaunti hii basi nitafanya kama 

unavyotaka.Nakupa dakika tano 

kunithibitishia hilo unalolisema na 

kisha tutaendelea na 

mazungumzo” akasema Dr Vivian 

kwa kujiamini.Mike akaomba 

mmoja wa walinzi wake aitwe 

akamuelekeza jambo fulani 

akatoka na baada ya dakika 

kadhaa akaingia mle ndani mtu 

mmoja akiwa na kompyuta ndogo 

Mike akamtaka amthibitishie 

kuhusu wepo wa akaunti ile ya Dr Vivian katika benki ya Escom.Yule 

jamaa kwa haraka akaanza 

kubonyesa bonyeza kompyuta 

yake hukuMIke 

akitabasamu.Mapigo ya moyo ya 

Dr Vivian yalikuwa yanakwenda 

kwa kasi kubwa 

“Please help me Lord” 

akaomba kimya kimya 

Yule jamaa aliendelea 

kubonyeza kompyuta yake na sura 

yake ikaanza kubadilika 

“Vipi bado? Mike akamuuliza 

“Mheshimiwa rais kuna 

tatizo.Ile akaunti haionekani 

tena”akasema yule jamaa na 

kumstua Mike 

“Haionekani? Akauliza Mike 

kwa ukali “Inawezekanaje? 

“Mheshimiwa rais nipe dakika 

chache niwasiliane na wataalamu 

wa benki hii wanieleze kwa nini 

akaunti hii haionekani tena” 

akasema yule jamaa na 

kutoka.Mike Straw akaonekana 

kuchanganyikiwa 

“Mike kwa nini umeamua 

kunikashifu kiasi hiki?akauliza Dr 

Vivian na Mike hakujibu kitu 

akabaki akizunguka zuguka mle 

chumbani baada ya dakika tatu 

yule jamaa akarejea na kumpa jibu 

ambalo lilimfanya akae 

chini.Akaunti ile haikuwepo 

ilikwisha fungwa na fedha zote 

kuondolewa “Mike nadhani hatuna tena 

kitu cha kuzungumza.Mipango 

yako imeshindikana” akasema Dr 

Vivian huku akitoa kicheko cha 

dharau 

“Bado kuna jambo moja la 

kuzungumza.Wewe unajifanya ni 

mtu mwenye akili nyingi siyo? 

Akauliza Mike na kufungua tena 

mkoba wake na kutoa faili lingine 

na kumpa Dr Vivian akalifungua na 

kustuka sana Mike akatabasamu 

“Anaitwa Florentina 

Paul.Mbona umestuka 

ulipomuona? Akasema Mike lakini 

Dr Vivian hakujibu kitu akabaki 

anatazama picha zilizokuwemo 

ndani ya lile faili “Naomba nikusaidie ili 

kuokoa muda.Huyo binti anaitwa 

Florentina Paul.Hilo ni jina lake la 

sasa lakini jina lake halisi ni Nasrat 

Said.Huyu ndiye mtoto ambaye 

uliwahi kumzaa na Said Bazharan 

kiongozi wa kikundi cha kigaidi 

kinachopambana na serikali ya 

Syria na kuua watu wengi wasio na 

hatia.Nasrat alitelekezwa na baba 

yake na akachukuliwa na watawa 

wakambatiza na kumpa jina la 

Florentina Paul na sasa yuko 

Marekani anasoma.Ni binti 

mrembo na mwenye akili nyingi 

lakini hafahamu chochote 

kuhusiana na wazazi 

wake.Anachokijua ni kwamba yeye 

kwa sasa ni yatima”akanyamza baada ya kumuona Dr Vivian 

akifuta machozi 

“Dr Vivian naamini hapo 

umeguswa.Hakuna anayefahamu 

kama uliwahi kuzaa mtoto na 

ukamtelekeza.Hii ni siri yako 

kubwa na itaendelea kubaki siri 

endapo utakubaliana na mambo 

niliyokueleza na ninakuahidi 

kukuunganisha tena na mwanao 

na dunia haitajua kama uliwahi 

kuwa na mahusiano na Said 

Bazharan.Naomba ufikirie na 

unipe jibu mheshimiwa rais” 

akasema Mike na Dr Vivian akafuta 

machozi na kulifunika lile faili 

akaenda mezani akainua mkono 

wa simu na kuzungumza na mtu na 

baada ya dakika mbili mlango ukafunguliwa wakingia mle ndani 

watu wanne na mmoja wa watu 

walioingia mle ndani.Sura ya Mike 

straw ikabadilika baada ya 

kumuona Helmet 

Brian.Wakatazamana kwa muda 

wa sekunde kadhaa na Dr Vivian 

akamuelekeza Helmet aketi 

“Hallow Helmet” akasema 

Mike kwa sauti ambayo ilionyesha 

woga ndani yake lakini Helmet 

hakujibu kitu.Dr Vivian 

akamtazama Mike straw na 

kusema 

“Mike mbele yako ni waziri 

wako wako wa mambo ya nje wa 

Marekani na rafiki yako 

mkubwa.Mimi sitaki kuwa msemaji.Helmet atazungumza 

badala yangu” akasema Dr Vivian 

“Imekuwa vyema umekuja 

mheshimiwa rais na nimefurahi 

kukuona.Nitakuwa na machache 

sana ya kuzungumza nawe.Hawa 

watu watatu uwaonao ni watu 

waliotumwa kuja Tanzania 

kufanya kazi moja tu ya kunitoa 

roho yangu mpango ambao 

uliubariki. Tayari 

wamekwishajieleza na kila kitu 

kiko wazi hivi sasa.Mpango wenu 

wote umejulikana.Ushahidi wote 

upo na wako tayari kusimama 

mbele ya runinga na kuieleza 

dunia unyama wako na serikali 

yako.Kwa nini ukafanya haya Mike? Akauliza Helmet na Mike 

bado alikuwa kimya 

 “Helmet …”Mike akataka 

kusema kitu akazuiwa 

“Mike hupaswi kusema 

chochote.Kila kitu kinajulikana na 

kwa sababu hiyo nitakuwa na 

maneno machache sana ya 

kusema”akasema Helmet Brian na 

Mike akakaa kimya 

 “Nitakwambia maneno 

machache tu.Ndani ya dakika kumi 

kutokea sasa utaondoka kuelekea 

uwanja wa ndege na utaondoka 

Tanzania kurejea Marekani na 

kesho asubuhi nataka kitu cha 

kwanza cha kufanya wewe na 

makamu wako wa rais 

muwasilishe barua zenu za kujiuzulu nafasi zenu.Nataka 

mfanye hivyo kimya kimya na 

mchague sababu yoyote ile 

ambayo itawafanya watu waamini 

na endapo mkifanya hivyo mambo 

haya yote mliyoyafanya wewe na 

serikali yako yatazikwa kimya 

kimya na mtaondoka na heshima 

zenu lakini endapo mtashindwa 

kufanya hivyo dunia nzima 

itafahamu mambo yote maovu 

unayoyafanya wewe na serikali 

yako na nitaanzisha kampeni 

kubwa ya kuwaondoa Marekani na 

mtaondolewa madarakani kwa 

aibu.Nadhani unaifahamu nguvu 

yangu ilivyo kwani kampeni yangu 

itachukua muda mfupi sana 

kuwaondoa katika nyadhifa zenu kwa aibu hivyo nakuomba 

uzingatie hayo 

niliyokueleza.Nitayaelekeza 

masikio yangu katika vyombo vya 

habari vya Marekani kusikia 

kesho asubuhi nini kitatokea 

Marekani na endapo sintasikia 

chochote basi utaiona nguvu 

yangu” akasema Helmet Brian na 

kumgeukia rais 

“Dr Vivian ni wakati sasa wa 

kumpeleka Mike straw uwanja wa 

ndege na arejee Marekani.Hii 

itakuwa ni mara yake ya mwisho 

kupanda airfoce one.Kwa heri 

mheshimiwa rais” akasema Helmet 

“Mheshimiwa Mike,nadhani 

umemsikia vyema Helmet na 

ninakutakia utekelezaji mwema wa maagizo yote aliyokupa” 

akasema Dr Vivian na kumpigia 

simu makamu wa rais afanye 

maandalizi kwa ajili ya Mike Straw 

kuondoka kuelekea uwanja wa 

ndege 

“Mungu ni mkubwa sana na 

siku zote ana mipango 

yake.Sikujua kama Mike straw 

angekuja mwenyewe 

Tanzania.Nini hasa kilichomleta? 

Akauliza Helmet 

“Suala lako ndilo lililomleta 

hapa.Alitaka tulimalize suala hili 

kimya kimya hakujua kama 

tumekwisha fahamu kila kitu 

kuhusu mpango wako”akasema Dr 

Vivian na kulificha lile faili la 

Florentina “Usijali Dr Vivian 

nakushukuru sana kwa kazi kubwa 

uliyoifanya na baada ya kufikiri 

sana nimeamua kufanya kampeni 

ili niweze kuchukua nafasi ya Mike 

baada ya kuachia ngazi” akasema 

Helmet na furaha ya Dr Vivian 

haikuweza kuzuilika akaenda 

kumpa mkono Helmet 

“Helmet uamuzi huu 

ulioufanya ni uamuzi wa busara 

sana.Naamini ukichukua nafasi 

hiyo mimi na wewe tutafanya 

mambo makubwa”akasema Dr 

Vivian 

Helmet Brian alirudishwa 

mahala salama anakoishi na akina 

Mathew wakaenda kuendelea na 

kazi ya kumfanyia mahojiano April Mubara ili kufahamu kwa undani 

kuhusiana na mtandao wa CIA 

hapa nchini 

****************** 

“Nilikutana na rais Anorld 

Mubara wakati anasoma nchini 

Marekani.Tulifanya ziara chuoni 

kwao na tulipokutana urafiki wetu 

ukaanzia hapo.Tuliwasiliana na 

kutembeleana mara kwa mara na 

baadae urafiki wetu ukakua na 

tukawa wapenzi.Hata baada ya 

kumaliza chuo mapenzi yetu 

yaliendea na baadae tukafunga 

ndoa na wakati huo alikuwa 

anafanya kazi katika wizara ya 

mambo ya nje.Anorld alifanya kazi zake kwa bidii kubwa na baadae 

akateuliwa kuwa naibu waziri na 

baadae akawa waziri kamili wa 

wizara ya mambo ya nje na hapo 

ndipo safari yake ya kuelekea 

ikulu ilipoanzia” April Mubara 

alianza kutoa maelezo yake mbele 

ya akina Mathew baada ya 

kufikishwa katika chumba cha 

kufanyia mahojiano 

“Anorld alipopata urais 

nilifuatwa na watu wawili 

wakitokea Marekani na kunieleza 

kwamba Anorld anashirikiana na 

mataifa mengine kadhaa hasimu 

wa Marekani kuihujumu 

Marekani.Kuna jambo wanapanga 

kulifanya kwa hiyo wakanitaka 

nianze kumchunguza Anorld.Mimi ni mmarekani,wazazi 

wangu,ndugu zangu wote wako 

Marekani kwa hiyo sikutaka nchi 

yangu ifanyiwe jambo lolote baya 

hivyo nikakubali kumchunguza 

mume wangu bila yeye kujua.Na 

hapo ndipo nikaanza uwakala wa 

CIA.Nilichunguza kila kitu 

alichokifanya Anorld na kuwapa 

taarifa na nililipwa fedha kila 

mwezi kupitia kwa marehemu 

George Mzabwa.” Akanyamaza na 

kutazama chini kwa muda halafu 

akaendelea 

“Nilielekezwa kuuchunguza 

mkoba wa Anorld aliokuwa 

anatembea nao kila mahala 

ulioitwa Football lakini 

sikufanikiwa kujua chochote kilichokuwamo ndani ya mkoba 

ule na ndipo CIA walipopanga 

mpango wa kuteka ndege yake na 

kuichukua hiyo football ambayo 

walidai ina siri kubwa ndani yake 

kuhusiana na mpango mbaya dhidi 

ya Marekani.Utekaji huo 

haukufanikiwa na Anorld na watu 

wengine wote wakafariki 

isipokuwa Seba” 

“Ulijisikiaje uliposikia mumeo 

amefariki dunia katika ajali ya 

ndege? Akauliza Amarachi 

“ Niliumia moyoni lakini 

sikuwa na namna nyingine ya 

kufanya kwani Anorld alikuwa 

katika mpango mbaya dhidi ya 

Marekani.” Akajibu April “Nini kilifuata baada ya 

Anorld kufariki? 

“Sebastian ambaye ndiye 

alikuwa mbebaji mkuu wa football 

alinusurika na hivyo kutuaminisha 

kwamba anafahamu mahala 

football ilipo hivyo bado 

tuliendelea kumchunguza kwa 

miezi kadhaa bila kupata chochote 

na tuligundua kwamba alifahamu 

kila kitu kilichotokea ndani ya 

ndege ile na alikuwa tayari kuanza 

kufunguka kilichotokea hivyo 

ikalazimu auawe.” 

“Nani walimuua Sebastian 

Matope? Akauliza Mathew 

“Kuna kampuni moja ya ulinzi 

inaitwa Chemi security hii ni 

kampuni ya John Mkoka ambaye ni mkuu wa jeshi la polisi nchini na 

shughuli zetu zote zinafanywa na 

watu kutoka kampuni hii ambao 

hupewa mafunzo ya hali ya juu na 

katika operesheni za siri hutumia 

sare na vifaa vya jeshi la 

polisi.Sebastian Matope aliuawa na 

watu kutoka kampuni hii lakini 

ikasemwa kwamba aliuawa na 

majambazi.Aliuawa wakati akija 

nyumbani kwangu.Hili ilikuwa ni 

agizo kutoka kwa CIA makao 

makuu” April akaeleza kila kitu 

kuhusiana na mtandao wao na 

kuwataja watu wengine waliomo 

katika mtandao ule ulioundwa na 

CIA hapa nchini.Yalikuwa ni 

maelezo ya kushangaza sana. Baada ya kumaliza mahojiano 

na April Mubara wakaondoka 

kuelekea ikulu kuonana na na rais 

ambaye walimueleza kila kitu 

walichokipata.Dr Vivian 

aliwashukuru sana kwa kazi ile 

kubwa na kwa msaada wote 

waliomsaidia. 

 “Mheshimiwa rais nadhani 

sasa ninaweza kusema kwamba 

lile fumbo gumu lililoshindwa 

kufumbuliwa limefumbuka na kila 

kitu kiko wazi.Kazi uliyonituma 

nimeikamilisha na watu 

waliomuua kanali Sebastian 

Matope wamejulikana.” akasema 

Mathew na kumkabidhi Dr Vivian 

karatasi yenye majina ya watu 

wote walio katika mtandao wa CIA.Dr Vivian akaisoma karatasi ile 

na kufuta machozi 

“Sina cha kusema Mathew kwa 

kazi hii kubwa 

uliyoifanya.Ahsan….” akashindwa 

kujizuia na kumwaga 

machozi.Mathew akamfuata na 

kumsihi asiendelee kulia kwani 

kazi bado inaendelea 

“Kazi ya kwanza imemalizika 

kwa mafanikio.Bado kuna swali 

linahitaji majibu.Begi la football 

liko wapi? Akauliza Mathew 

“Kabla ya kuanza 

kulishughulikia hilo Mathew kuna 

mambo ambayo nahitaji 

kuzungumza nanyi” akasema Dr 

Vivian “Jana usiku uliniuliza swali 

kwanini CIA wamekuwa 

wananifuatilia kwa muda 

mrefu?Kuna sababu ya CIA 

kunifuatilia kwa muda mrefu na 

bado wanaendelea kunifuatilia na 

mimi ninafahamu kwamba 

ninachunguzwa japo sikujua kama 

Nathan ni mtu ambaye alitumwa 

kuja kunichunguza.Niliumia sana 

niliposikia kwamba ndiye 

aliyetumwa kunichunguza” Dr 

Vivian akawaeleza kila kitu 

kuhusiana na maisha yake na kwa 

nini CIA wanamfuatilia.Aliwaeleza 

kila kitu kuhusiana na Said 

Bazharan na pia kuhusiana na yeye 

kuandaliwa kuja kuwa rais wa 

Tanzania.Yalikuwa ni maelezo yaliyowaacha midomo wazi akina 

Mathew 

“Kwa hiyo jamani hayo ndiyo 

mambo yanayonifanya 

nichunguzwe na CIA” akasema Dr 

Vivian 

“Ahsante Dr Vivian kutuweka 

wazi kuhusiana na maisha 

yako.Vipi kuhusiana na huyu 

mwanao Florentina una mpango 

gani naye? Mathw akauliza na 

kabla Dr Vivian hajajibu kitu 

akapigiwa simu akazungumza na 

alipomaliza akasema 

“ Kwa sasa siwezi kulijibu 

swali lako Mathew kwani 

nimetaarifiwa kwamba Theresa 

amekwisha zinduka na anahitaji 

kuniona.Ninakwenda hospitali.Mtapenda kuongozana 

nami? Akauliza Dr Vivian 

akaongozana na akina Mathew 

kuelekea hospitali kumuona 

Theresa ambaye alikwisha zinduka 

na alikuwa anaendelea 

vyema.Alitaka kufahamu kuhusu 

maendeleo ya uchuguzi na ndipo 

walipomfahamisha kila kitu 

kilichotokea. 

“Dada Vivian nimefurahi 

kusikia yote yaliyotokea.Baada ya 

kunusurika kifo kuna jambo 

muhimu nataka kuwaelezeni” 

akasema Theresa na kuwaeleza 

kila kitu kuhusiana na 

kilichotokea ndani ya ndege na 

hadi walivyofanikiwa kutoka 

salama yeye na baba yake na hadi baba yake alivyouawa.Ilikuwa ni 

simulizi iliyomfanya Dr Vivian atoe 

machozi mengi.Ilimuumiza 

sana.Mwisho aliweka wazi 

kuhusiana na ule mkufu wa 

dhahabu aliopewa na baba yake na 

ndipo Mathew alipokumbuka 

kwamba alipewa vifaa vya Theresa 

na kwenda moja kwa moja garini 

akafungua buti ya gari na kukuta 

ule mkufu upo pamoja na nguo za 

Theresa.Akauchukua ule mkufu na 

kwenda nao ndani.Theresa akatoa 

machozi alipuona ule mkufu na 

kumkabidhi Mathew aufanyie kazi 

ili wajue kuna nini.Mathew 

akauchunguza ule mkufu na 

akagundua kwamba ule msalaba 

ulikuwa ni kifaa cha kuhifadhi kumbu kumbu.Akampigia simu 

Austin na kumuomba ampeleke 

Camilla haraka sana pale hospitali 

na baada ya dakika ishirini Camilla 

akafika akapewa ule msalaba 

akauchomeka katika kompyuta 

yake na kukatokea kitu mfano wa 

ramani ambayo walipoichunguza 

iliwaelekeza kwamba kuna kitu 

kimefichwa ardhini sehemu fulani 

katika nyumba ya kanali Sebastian 

Matope. 

Walitoka pale hospitali na 

kuelekea moja kwa moja 

nyumbani kwa Theresa na Dr 

Vivian akawaelekeza ilipokuwa 

nyumba ya baba yake iliyoungua 

moto na kwa kufuata maelekezo 

yaliyokuwamo katika msalaba ule wakafanikiwa kuipata sehemu 

ambayo ilielekeza mahala 

kulikofichwa kitu alichoelekeza 

Sebastian.Walichimba mahala pale 

na kulikuta begi lililofichwa 

kiustadi mno. 

“Madam president we have 

the football !! akasema Mathew 

kwa furaha na kumkabidhi rais lile 

begi ambaye alimwaga machozi. 

“Hatimaye football begi 

lililochukua uhai wa baba yangu 

limepatikana” akasema kwa sauti 

ndogo 

Kwa pamoja walichunguza 

kilichokuwamo ndani ya lile begi 

na wakagundua kwamba zilikuwa 

ni nyaraka zinazohusiana na 

utengenezaji wa gezi ya sumu katika ambacho kilikuwa chini ya 

hospitali kuu ya Msindima 

 “Jambo hili limekuwa siri kwa 

miaka mingi na walioificha siri hii 

walitegemea sisi tuje kufanya 

maamuzi kuhusiana na kiwanda 

hiki.Binafsi siafikiani na 

utengenezwaji wa gesi ya sumu 

uliokuwa unafanyika katika 

kiwanda hiki hivyo kiwanda hii 

kitaharibiwa na badala yake 

tutatengeneza kiwanda cha 

kutengeneza dawa za 

binadamu.Gesi hii ya sumu ni 

silaha ya maangamizi na sisi tuko 

mstari wa mbele katika kupinga 

silaha za maangamizi hivyo 

tunatakiw akuanza kuonyesha 

mfano sisi wenyewe.Nyaraka zote zilizomo katika mkoba huu wa 

football zinazohusiana na 

kutengeneza gesi ya sumu 

zitachomwa moto ili kuuzika 

kabisa mradi huu.Huu utakuwa ni 

mwisho wa the football begi 

ambalo lilibeba siri kubwa na 

maisha ya watu wengi yamepotea 

kwa sababu ya begi hili.” Hayo 

yalikuwa ni maamuzi ya rais Dr 

Vivian kuhusiana na kiwanda kile 

cha kutengeneza gesi ya sumu 

“Mathew siwezi kuchoka 

kukushukuru wewe na wenzako 

kwa kazi kubwa 

mliyoifanya.Nisamehe sana pia 

kwa sintofahamu zilizojitokeza 

baina yetu wakati ukitekeleza 

jukumu hili.Wewe ni mtu ambaye sina namna ya kukushukuru kwani 

umeniokoa kutoka katika janga 

zito.Kama si wewe sijui hivi sasa 

ningekuwa katika hali gani.Pamoja 

na kunisaidia kuniondoa katika 

kashfa ile napenda 

kuwahakikishia kwamba zile fedha 

zote nitazipeleka katika miradi ya 

elimu.Kampuni ile ya Tanbest 

ambayo iliharibiwa kwa moto 

haitakuwepo tena na ninafunga 

kila kitu na sitaki tena kujihusisha 

na masuala ya biashara.Nataka 

niwe mtumishi mwaminifu wa 

waTanzania.” 

“Hayo ni maamuzi yenye 

busara sana mheshimiwa 

rais.Jambo hili litabaki katika vifua 

vyetu tutalibeba hadi siku

 tunaingia kaburini.Hatafahamu 

mtu mwingine yeyote” akasema 

Meshack Jumbo. 

“Jambo lingine ambalo 

naliomba kutoka kwenu ni 

ushirikiano wenu wa karibu 

sana.Tumeumaliza mtandao wa 

Marekani hapa nchini na wale 

wote walioshiriki katika mtandao 

huo lazima wafikishwe mbele ya 

sheria na kupata adhabu kali 

kulingana na makosa mbali mbali 

waliyoyafanya.Nawaomba muwe 

karibu sana nami.Kila pale 

ninapowahitaji ninawaomba 

msinikimbie.Mathew ikulu ni 

kama nyumbani kwako 

unakaribishwa kufika muda 

wowote.Time to time let’s us have drinks and exchange ideas.Ushauri 

wako nitauhitaji sana.Camilla 

utapewa uraia wa Tanzania na 

utaishi hapa kama 

ukipenda.Nimefurahishwa sana na 

kazi yako kubwa 

uliyoifanya.Pamoja na hayo 

nitaandaa chakula maalum na 

kuwaita wote ikulu ili niweze 

kuwashukuru kwa kazi kubwa 

mliyoifanya.Mwisho kabisa 

Mathew nitahitaji kufahamu 

mahala alikozikwa 

Nathan.Nitahitaji pia mwili wa 

Tausi upatikane ili tuweze 

kuikabidhi kwa familia zao na 

kuzikwa kwa heshima ” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais.Ni heshima kubwa umenipa na nitakuja kukutembelea mara kwa 

mara.Kuhusu miili ninakuahidi 

yote itapatikana na nitakukabidhi” 

akasema Mathew kisha wakaagana 

wakaondoa pale nyumbani na 

kuwaacha rais na Meshack Jumbo 





OHaikua kazi nyepesi ila 

tumeimaliza.Ni kazi iliyochukua 

miaka zaidi ya kumi bila 

kukamilika lakini sisi 

tumeikamilisa ndani ya kipindi 

kifupi tu.Ahsanteni sana ndugu 

zangu kwani bila ninyi kujitoa kwa 

hali na mali tusingeweza 

kuikamilisha ile kazi ngumu na 

iliyojaa hatari” akasema Mathew 

na safari ikaelekea nyumbani kwa 

Austin walikokuwapo akina 

Peniela. Mathew alimkumbatia kwa 

furaha mwanae Anna Maria 

ambaye alifurahi mno kumuona 

tena baba yake 

“Nimefurahi sana kukuona 

baba” akasema Anna 

“It’s over.Kila kitu 

kimekwisha.Peniela ahsante sana 

kwa msaada wako mkubwa bila 

wewe kuja Tanzania sijui 

tungemsaidiaje Dr Vivian” 

akasema Mathew 

“Mathew umejitoa sana 

kumsaidia Dr Vivian inaonyesha ni 

rafiki yako mkubwa.Is she single? 

Akauliza Peniela 

“yes she’s single” akajibu 

Mathew 

“Mathew” akaita Peniela “Sifahamu nianzie wapi 

kukueleza kuhusiana na jambo 

hili” 

“Jambo gani Peniela?akauliza 

Mathew na Peniela akafikiri 

kidogo kisha akasema 

“Mathew nilikukosea sana 

wakati ule.Nilifanya kosa kubwa 

sana kuachana nawe kwani 

nilirubuniwa na Anderson.Katika 

kipindi nilichokaa na Anderson 

nimegundua kwamba hakuna 

mwanaume ambaye anaweza 

akanifaa zaidi yako.Mathew wewe 

ni wa kipekee kabisa na kwa muda 

ambao nilikuwa mbali nawe 

nimeona umuhimu wako.Tafadhali 

Mathew nakuomba urudishe moyo 

na unisamehe kwa yale yote niliyokukosea.Bado nakuhitaji 

sana Mathew.Nataka mapenzi yetu 

yarejee” akasema Peniela huku 

machozi yakimtoka akapiga 

magoti kumuomba Mathew 

msamaha. 

“Inuka Peniela.” Akasema 

Mathew 

“Mimi na wewe tulikula kiapo 

mbele ya madhabahu ya Mungu 

kwamba hautatengana lakini 

ulipita upepo ukatutikisa na 

yakatoke ayale yaliyotokea.Pamoja 

na kutengana lakini sikuwahi 

kuwa na mpenzi yeyote kwani 

ninaamini mwanamke pekee 

ambaye Mungu alinipa niwe naye 

ni wewe pekee.Bado ninakupenda 

sana na nio tayari kukupokea tena na kuendelea na maisha yetu kama 

tulivyoapa mbele za madhabahu” 

akasema Mathew na Peniela 

akamkumbatia kwa nguvu huku 

akimwagia mabusu mengi.Huo 

ukawa ni mwanzo mpya wa 

wapenzi hawa ambao meli yao 

ilikumbwa na dhoruba kali kiasi 

cha kuwafanya watengane 

MIEZI MINNE BAADAE 

Viongozi zaidi ya ishirini wa 

mataifa mbalimbali duniani 

walikusanyika katika ukumbi wa 

kimataifa wa mikutano wa 

mwalimu Nyerere kushuhudia 

kutiwa saini kwa makubaliano ya 

kwanza ya kudhibiti silaha kali kati ya vongozi wa mataifa ya 

Marekani na Korea Kaskazini.Hii 

iliwezekana baada ya rais Mike 

straw na makamu wake kuachia 

madaraka na kuchaguliwa rais wa 

mpito Helmet Brian ambaye kwa 

kusaidiana na rais wa Tanzania Dr 

Vivian Matope walifanikiwa 

kuumaliza mgogoro wa miaka 

mingi wa Korea Kaskazini na 

Marekani baada ya viongozi wa 

mataifa haya mawili kukubali 

kukaa meza moja na kuzungumza 

na hatimaye wakakubali kuweka 

kando tofauti zao na hatimaye 

kusaini mkataba wa amani baina 

ya nchi hizi mbili na huu ukawa ni 

mwanzo mpya wa mashirikiano 

kati ya Marekani na Korea Kaskazini jambo ambalo hakuna 

aliyewahi kuota kama 

lingewezekana 

Kwa mara nyingine tena 

Tanzania ikangia katika historia ya 

dunia kwa kuumaliza mgogoro huu 

uliotishia amani ya dunia.Amani 

kwa dunia ikarejea kwani 

hakukuwa tena na kitisho cha 

kuibuka vita ya tatu ya dunia 

Ilikuwa ni siku ya furaha 

kubwa kwa Mathew kuonana tena 

na Camilla ambaye kwa sasa ni 

mmoja kati ya walinzi wa rais 

Helmet Brian.Camilla alifurahi 

sana kumuona Theresa akiwa 

tayari amepona na anaendelea 

vyema. “Nimepitia operesheni nyingi 

ngumu lakini sikuwahi kupitia 

operesheni ngumu kama hii ya 

kulifumbua fumbo la THE 

FOOTBALL” akasema Mathew na 

wote wakakumbatiana kwa furaha 

wakipongezana kwa kuifanikisha 

operesheni ile ngumu. 


TAMATI


0 comments:

Post a Comment

Blog