Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL - 2

  

Simulizi : The Football 

Sehemu Ya Pili (2)


kidogo aliposikia kwamba 

Meshack Jumbo ametoka kuonana 

na rais 

“Amekuitia kitu gani? 

Akauliza Mathew 

“Kuna mambo yanayoendelea 

hapa nchini kwa sasa hivyo aliniita 

kupata ushauri wangu” 

“Ni kuhusiana na lile suala la 

Korea kaskazini?Naona linazidi 

kuchukua sura mpya kila uchao” 

“Hatukuzungumza sana suala 

hilo ila kuna mambo mengine 

mawili aliyoniitia” “Mzee Jumbo nina imani 

umekuja kunieleza kuhusiana na 

maongezi yako na rais but I’m not 

interested.Mimi siko tena katika 

haya mambo.Kama kweli hilo ndilo 

lililokuleta hapa naomba usipoteze 

wakati wako mzee 

wangu.Nitakuwa na muda kama 

tutazungumza mambo ya 

kibiashara” akasema Mathew. 

“Mathew nafahamu hutaki 

tena kusikia haya mambo ya 

wanasiasa na ndiyo maana 

nimekuja mwenyewe hivyo 

naomba unipe dakika kama tano 

tu unisikilize.Japokuwa sote kwa 

sasa tumeachana na hizi kazi but 

I’m still your boss so you have to 

listen tome !! Huu utajiri wako usikufanye ukawa kiburi” akasema 

mzee Jumbo kwa sauti ya juu 

kidogo Mathew hakujibu 

kitu.Meshack akaendelea 

“Kuna mambo mawili 

aliyoniitia rais leo.Moja ni 

kuhusiana na kifo cha mkurugenzi 

wa idara ya usalama wa taifa 

George Mzabwa aliyejipiga risasi 

ofisini kwake.Mheshimiwa rais 

ameniomba nirudi kazini kwa 

muda wa mwaka mmoja 

nikaiongoze idara ya usalama wa 

taifa kwani mpaka sasa bado 

hajapata mtu wa kuweza 

kuiongoza idara hiyo 

atakayemuamini hasa kwa wakati 

huu ambao nchi inahitaji ulinzi mkali sana”Meshack akanyamaza 

na Mathew akauliza 

“Kuna sababu yoyote ya huyo 

mkurugenzi kujiua? 

“Mpaka sasa hakuna sababu 

yoyote iliyogunduliwa kwa nini 

alijiua japokuwa uchunguzi bado 

unaendelea.” 

“Umekubali kurejea kazini? 

Mathew akauliza 

“Mathew kustaafu si mwisho 

wa utumishi.Sisi ni sawa na askari 

wa akiba pale tunapotakiwa 

kurejea katika mapambano kwa 

ajili ya nchi basi hatuwezi 

kukataa,hivyo nimekubali kurejea 

tena kuifanya kazi aliyoniomba 

mheshimiwa rais” akajibu 

Meshack “Lakini kuna watu wengi 

ambao wangeweza kuziba nafasi 

hiyo na rais angeweza kuwachagua 

na akakuacha mzee 

ukapumzike.Umelitumikia taifa 

kwa miaka mingi ni wakati wako 

wa kupumzika sasa” akasema 

Mathew 

“Ni kweli Mathew wapo watu 

wengi tu wanaoweza kufanya hiyo 

kazi lakini hawana uzoefu mkubwa 

kama mimi na ndiyo maana rais 

ameomba nimsaidie kuziba nafasi 

hiyo kwa mwaka mmoja .Nadhani 

kuna mambo ameona hayaendi 

sawa.Nimeridhia ombi lake na 

nitaifanya hiyo kazi kwa muda huo 

alionitaka” “Sawa mzee.Kama umeamua 

kurejea kazini kwa ombi maalum 

la mheshimiwa rais mimi 

nakutakia kila la heri katika 

majukumu yako ila 

nakukumbusha kwamba zama 

zimebadilika sana tofauti na 

wakati ule ambao ulikuwa 

kiongozi.Teknolojia imepanuka 

sana zama hizi” akasema Mathew 

“Nalifahamu hilo Mathew na 

ninao uzoefu wa kutosha isitoshe 

hata afya bado inaruhusu.Jambola 

pili aliloniitia rais linafanana na 

hili la kwanza.Rais anahitaji 

kukuona.Anahitaji msaada wako” 

“Me ?!! akauliza Mathew kwa 

mshangao halafu akacheka kidogo “Mimi nimekwisha achana na 

haya mambo kwa hiyo mweleze 

kwamba siwezi kuwa na msaada 

wowote kwake” akasema Mathew 

“Ninalifahamu hilo mathew na 

nimekuja hapa mimi mwenyewe 

kukuomba ukaonane na 

rais.Nafahamu umeachana na haya 

mambo na nisingeweza kuja hapa 

kama jambo analokuitia rais 

lisingekuwa la muhimu.Please my 

son nakuomba nenda ukamsikilize 

rais anachokuitia.Kuna jambo zito 

ambalo anahitaji msaada na ni 

wewe pekee unayeweza 

kumsaidia.Nakuomba sana 

Mathew” akasema mzee Meshack 

“Lakini mzee wewe 

unafahamu fika kwamba mimi kwa sasa sishughuliki na hayo mambo 

tena bali nimejikita katika 

biashara kwa hiyo mwambie rais 

kwamba siwezi kuwa na msaada 

wowote kwake.Kuna watu wengi 

sana katika idara ya usalama wa 

taifa,polisi n.k kwa nini 

asiwatumie hao wote hadi anitake 

mimi ? Tayari nimeingia katika 

maisha mapya kwa hiyo siwezi 

kurudi tena katika hizo kazi mzee 

wangu,utanisamehe sana” 

“Mathew nakuomba kijana 

wangu muonyeshe heshima mkuu 

wa nchi na uitike tu wito wake wa 

kutaka kukuona.Nenda kaonane 

naye usikie anachokuitia halafu 

umweleze kwamba kwa sasa 

haujishughulishi na hayomambo.Moja ya msingi wa kazi 

yetu ni nidhamu kwa uongozi wa 

juu kwa hiyo usidharau wito wa 

kiongozi wako,nenda kamsikilize 

usikie anakuitia nini.Mimi 

nilipoitwa sikujiuliza mara mbili 

nikaenda haraka na kusikia 

alichoniitia” Akasema Meshack 

Ilimchukua Mathew zaidi ya 

dakika mbili kutafakari halafu 

akasema 

“Mzee umeniweka katika 

wakati mgumu sana lakini kwa vile 

nina kuheshimu na umekuja 

mwenyewe kuniomba itanibidi 

niende kuonana na rais na 

kumsikiliza anachokitaka.Lini 

anataka nionane naye? “Anakuhitaji sasa 

hivi.Nitakupeleka” 

“Ananihitaji sasa hivi? Kwa 

nini isiwe wakati mwingine au 

hata kesho? Kwa sasa nina ratiba 

nyingine si unaona shughuli 

zilivyopamba moto hapa ? 

“Ahirisha shughuli zako kwa 

sasa twende ukamsikilize rais 

halafu utakuja kuendelea na 

shughuli zako” akasema Meshack 

Jumbo.Mathew akatoa maelekezo 

kadhaa kwa mkandarasi kisha 

wakaondoka 

“Ahsante sana Mathew kwa 

kukubali kwenda kuonana na 

rais.Hii ni heshima kubwa 

umetupa mimi na rais”akasema 

Meshack Jumbo “Nimekubali kwa heshima 

yako mzee wangu lakini angekuja 

mwingine nisingekubali.Ni jambo 

gani hasa ambalo rais ananiitia 

unaweza kunidokeza? 

“Itakuwa vyema kama yeye 

mwenyewe atakueleza.By the way 

mnawasiliaan na Peniela? Meshack 

Jumbo akauliza 

“Tunawasiliana .Hatuna 

ugomvi na isitoshe tuna mtoto 

mmoja,binti mzuri anaitwa Anna 

Maria hivyo hata kama hatuko 

pamoja lakini tunaunganishwa na 

mtoto hivyo mawasiliano yapo 

lakini ni kuhusiana na maendeleo 

ya mtoto tu” “Pole sana kwa kilichotokea 

kwenye ndoa yako” akasema mzee 

Jumbo 

“Ni mambo ya kawaida 

kutokea katika ndoa” akajibu 

Mathew kisha safari ikaendelea 

kimya kimya 

Walifika ikulu na rais 

akataarifiwa kuwasili kwao na 

alipomaliza kikao na wageni wake 

akawakaribisha Meshack na 

Mathew katika chumba cha 

maongezi ya faragha 

“Karibuni sana.Natumai 

Meshack umemleta Mathew 

Mulumbi” akasema Dr Vivian huku 

akitabasamu “Hujakosea mheshimiwa 

rais,huyu ndiye Mathew Wilibroad 

Mulumbi” akasema Meshack 

“Mathew karibu 

sana.Nimefurahi kukutana nawe” 

akasema Dr Vivian 

“Hata mimi pia nimefurahi 

sana kuonana nawe mheshimwia 

rais” akasema Mathew 

“Ni mara ya kwanza 

tunaonana Mathew.Ahsnate kwa 

kukubali wito wangu ingawa 

nafahamu Mzee Meshack alipata 

wakati mgumu kukushawishi 

ukubali kuja kuonana nami” 

akasema Dr Vivian na wote 

wakacheka 

“Uko sahihi mheshimiwa 

rais,haikuwa rahisi kukubali lakini kwa heshima kubwa kwako na 

kwa mzee imenilazimu kuitika 

wito wa mkuu wangu wa nchi 

hivyo nimeacha shughuli zangu 

zote na kuja kuonana nawe” 

akasema Mathew 

“Nashukuru sana.Mapema leo 

nilikuwa na mazungumzo marefu 

na Meshack na nina imani 

amekudokeza yale 

tuliyoyazungumza” akasema Dr 

Vivian 

“Amenidokeza baadhi ya 

mambo lakini kwa upana zaidi 

nategemea kusikia toka kwako” 

“Itakuwa vyema kama 

nikikuanzia mbali kidogo ili upate 

picha kamili ya kile nilichokuitia 

hapa.Ni siku mbili tu zimepita toka mkuu wa idara ya usalama wa taifa 

George Mzabwa ajiue kwa kujipiga 

risasi ofisini kwake.Mpaka sasa 

bado uchunguzi unaendelea 

kubaini sababu ya George 

kujiua.Kufuatia kifo hicho bado 

sijapata mtu sahihi wa kuweza 

kuiziba nafasi yake kwani pamoja 

na kujiua lakini utendaji wa 

George haukunivutia na nilikuwa 

katika mpango wa kumondoa na 

kumuweka mtu 

mwingine.Nimelazimika 

kumuomba mzee Jumbo anisaidie 

kuiziba nafasi hiyo kwa mwaka 

mmoja wakati nikiendelea 

kutafuta mtu anayeweza kufaa 

kuongoza idara hii kwa weledi 

mkubwa.Namshukuru mzee amekubali kwa moyo mmoja na 

kuacha shughuli zake zote kuja 

kuifanya kazi hii.Narudia tena 

kukushukuru mzee 

Meshack.Mungu azidi kukupa umri 

mrefu na nguvu” akasema Dr 

Vivian na Mzee Meshack 

akainamisha kichwa kushukuru 

“Mathew naamini kwamba 

tayari umekwisha sikia msuguano 

uliopo baina ya nchi yetu na 

mataifa makubwa.Wakati huu 

ninahitaji nchi iwe katika ulinzi 

imara na ndiyo maana ujuzi na 

uzoefu wa watu kama ninyi 

unahitajika sana.Lakini wewe 

Mathew nimekuita kwa suala 

lingine tofauti na hilo” akanyamaza tena kidogo huku 

akiendelea 

“Nadhani jina la Kanali 

Sebastian Matope si geni kwako” 

“Sina kumbu kumbu nzuri ya 

jina hilo labda unikumbushe” 

akasema Mathew 

“Kanali Sebastian Matope 

alikuwa mpambe wa rais ambaye 

kazi yake kubwa ilikuwa ni 

kulibeba begi lenye siri za rais 

lililopewa jina la Football 

wakililinganisha na lile begi la rais 

wa Marekani atembealo nalo kila 

aendako ambalo nalo linaitwa 

football.Rais Anorld Mubara 

alifariki katika jaali ya ndege 

akitokea nchini Misri na kanali 

Sebastian inaaminika ndiye pekee aliyenusurika katika ajali hiyo 

iliyotoa uhai wa wote walikuwemo 

ndegeni.Baada ya kunusurika 

katika ajali ile baba hakumaliza 

miezi sita akauawa yeye,mama na 

mdogo wangu Kelvin.Inasemekana 

waliuawa wakiwa njiani kwenda 

kumtembelea bi April Mubara 

mjane wa rais Anorld Mubara.Toka 

yamefanyika mauaji hayo 

imekwisha pita miaka zaidi ya 

kumi na mpaka leo hakuna taarifa 

yoyote kuhusiana na nani 

aliyefanya mauaji yale ya 

kinyama.Baada ya kuingia 

madarakani niliagiza idara ya 

usalama wa taifa kufanya 

uchunguzi wa suala hili na muuaji 

apatikane lakini imepita miaka miwili toka nilipotoa kazi hiyo na 

hakuna majibu yoyote.Juzi 

nilipokuwa nakwenda Marekani 

nilimweleza mkuu wa idara ya 

usalama wa taifa kwamba 

nitakaporejea kutoka marekani 

nikute tayari wana taarifa 

kuhusiana na mauaji ya familia 

yangu lakini nilichokikuta ni hii 

barua aliyoiandika George muda 

mfupi kabla ya kujipiga risasi” 

Dr Vivian akamkabidhi 

Mathew ile barua akaisoma halafu 

Dr Vivian akaendelea 

“Umeona mwenyewe 

alichokiandika George.Amekiri 

kwamba suala hili ni gumu na 

amenisisitiza kuachana nalo kwani 

sintaweza kupata majibu.Yawezekana kweli suala 

hili nigumu kwani zaidi ya miaka 

kumi hakuna ufumbuzi wowote 

uliopatikana.Binafsi bado siamini 

kama suala hili limeshindikana 

kupatiwa ufumbuzi.Bado nina 

imani kwamba jambo hili haliwezi 

kuachwa liende kimya kimya.Baba 

aliuawa na lazima wauaji wapo na 

sababu ya kumuua ipo hivyo 

lazima tuwafahamu hao 

waliomuua na sababu ya 

kumuua.Nimeamua kulivalia njuga 

suala hili mimi mwenyewe hadi 

ufumbuzi upatikane na ndiyo 

maana nikamuomba mzee Jumbo 

anisaidie kutafuta mtu maalum 

mwenye sifa za kipekee ambaye 

anaweza kulifumbua hili fumbo ambalo wenzake wameshindwa 

kulifumbua.Mzee Meshack amekiri 

kwamba mtu huyo maalum ni 

wewe ambaye umeonekana unafaa 

na unaweza kuutafuna mfupa 

uliowashinda wengine” akasema 

rais na Mathew akataka kusema 

kitu rais akamzuia 

“Mathew nafahamu 

unachotaka kukisema lakini 

nakuomba usikitamke bali 

naomba ukubali kunisaidia 

kulifumbua fumbo hili 

gumu.Nisaidie kama ndugu 

yako,kama rafiki 

yako.Sikulazimishi unisaidie ila 

nakuomba unisaidie niweze 

kupata ukweli kuhusu mauaji ya 

wazazi wangu waliouawa bila huruma.Baba alipigwa risasi zaidi 

ya sabini mwilini mwake.Huu ni 

ukatili ulipotiliza.Ingia katika 

viatu vyangu na uone machungu 

ninayoyapatra kila ninapofikiria 

kuhusu suala hili.Kinachoniumiza 

zaidi kwa nini vyombo vya 

uchunguzi vimeshindwa kuwapata 

wauaji? Akasema Dr Vivian na 

macho yake yakalengwa machozi 

“Inaumiza sana mheshimiwa 

rais.Huu ni ukatili mkubwa mno” 

akajibu Mathew 

“Ni zaidi ya ukatili na ndiyo 

maana nakuomba Mathew 

unisaide katika hili suala.Nina 

imani kubwa kwako kwamba 

unaweza ukalifumbua hili 

fumbo.Ninakuomba Mathew tafadhali usiseme hapana.Wewe 

ndiye tumaini langu la mwisho 

katika kuupata ukweli wa suala 

hili.Ukikataa wewe sintaweza 

kujua nani waliwaua wazazi wangu 

kikatili namna ile.Nitakuwezesha 

kwa kila kitu unachokitaka ili kazi 

yako isiwe ngumu” akasema Dr 

Vivian 




ndiye tumaini langu la mwisho 

katika kuupata ukweli wa suala 

hili.Ukikataa wewe sintaweza 

kujua nani waliwaua wazazi wangu 

kikatili namna ile.Nitakuwezesha 

kwa kila kitu unachokitaka ili kazi 

yako isiwe ngumu” akasema Dr 

Vivian 

“Mathew” akaita mzee 

Meshack Jumbo 

“Mheshimiwa rais ameomba 

sana.Tafadhali angalia uzito wa 

jambo hili.Fikiria mateso 

anayoyapata moyoni mwake kila 

siku akifikiria mauaji yale ya 

kikatili ya wazazi wake.Ingiwa na 

moyo wa huruma na ukubali 

kumsaidia dada yako.Wote ni vijana umri wenu unalingana na 

anakuomba umsaidie kama rafiki 

,kama ndugu yako.Mheshimiwa 

rais anahitaji msaada mkubwa hivi 

sasa kutoka kwetu na ndiyo maana 

hata mimi nimeamua kuachana na 

kila kitu na kuja 

kumsaidia.Nakufahamu Mathew 

hujawahi kuacha wahalifu 

wakatamba.Hauko hivyo.Tafadhali 

nakuomba kwa mara nyingine tena 

kubali kumsaidia rais.Mimi na 

yeye tutakuwa nyuma yako na 

kukusaidia katika kila 

utakachokihitaji” akasema 

Meshack Jumbo.Mathew 

akainamisha kichwa akaisoma 

tena barua ile iliyoandikwa na 

George Mzabwa halafu akainua kichwa akamtazama rais na 

kusema 

“Siwezi kulikataa ombi lako 

mheshimiwa rais na huyu mzee 

wangu ambaye mimi kwangu ni 

kama baba yangu” 

Dr Vivian akainuka na kumpa 

mkono Mathew 

“Mathew ahsante sana.Sijui 

nikuelezaje furaha niliyonayo kwa 

kukubali kwako kulishughulikia 

suala hili lililowashinda wengi” 

Akasema Dr Vivian na 

kumshukuru pia mzee Meshack 

“Mzee Meshack 

ninakushukuru sana kwa kumleta 

Mathew.Nina uhakika mkubwa 

kwamba sasa suala hili linakwenda kupatiwa majibu” akasema Dr 

Vivian kwa furaha 

“Mheshimiwa rais na mzee 

wangu Jumbo naomba niwaweke 

wazi kwamba japokuwa 

nimekubali kuifanya kazi hii lakini 

haiwezi kuwa rahisi na ni mapema 

sana kuwa na matumaini yoyote 

makubwa ila nawaahidi nitafanya 

kila nitakaloweza kuhakikisha 

ninapata majibu ya nani walifanya 

mauaji hayo na kwa nini.Ni 

kawaida yangu kila ninapoingia 

katika operesheni fulani basi huwa 

nahakikisha nimechimbua hadi 

mzizi wake.Ninaamini hata katika 

jambo hili sintafumba ukope hadi 

ninakikishe nimelichimba na 

kuupata mzizi wake.Palenitakaposhindwa au nitakapohitaji 

msaada nitwaeleza” akasema 

Mathew 

“Nafahamu hili si suala jepesi 

na ni hatari kubwa sana ndiyo 

maana nikasema kwamba 

chochote utakachokihitaji 

nitakupatia.Kuwa huru kusema 

chochote utakachokihitaji” 

akasema Dr Vivian 

“Nashukuru mheshimiwa 

rais.Kabla ya kuanza rasmi 

kulishughulikia suala hili naomba 

unipe muda niweke kwanza 

mambo yangu sawa ili 

nitakapoanza kulishughulikia hili 

jambo nisiingiliwe na mambo 

mengine binafsi.Nitakapokuwa 

tayari nitakuja kukuona na kukueleza kwamba sasa ninaanza 

rasmi kazi” 

“Ahsante Mathew.Jipe muda 

wa kutosha kuyapanga mambo 

yako na utakapokuwa tayari 

utanijulisha.Nitakupa namba 

yangu ya simu maalum ambayo 

hutumiwa na viongozi wakuu na 

wale wa kimataifa pekee kutokana 

na umuhimu wako na una ruhusa 

ya kupiga muda wowote unaotaka” 

akasema Dr Vivian 

“Kesho asubuhi nitakuja 

kukuona kwani tayari nitakuwa 

nimeweka sawa mambo yangu na 

kesho hiyo hiyo kazi itaanza” 

akasema Mathew 

“Utapewa kibali maalum cha 

kukuwezesha kuingia hapa ikulu muda wowote bila kuzuiliwa na 

mtu.Nataka kazi hii isiwe mzigo 

kwako hivyo chochote unachoona 

kinaweza kukusaidia nieleze na 

nitakusaidia” akasema Dr Vivian 

na kuagana na Meshack Jumbo na 

Mathew wakaondoka.Baada ya 

akina Mathew kuondoka Dr Vivian 

akamuita Theresa ofisini kwake 

ambaye alifika mara moja. 

“Karibu Theresa.Nimekuwa na 

mfululizo wa vikao toka asubuhi 

na sijapata nafasi ya kuonana 

nawe.Mambo yako yanakwendaje? 

Akauliza Dr Vivian 

“Ninaendelea vizuri 

dada.Nashughulikia hotuba yako 

katika mkutano madaktari hapo 

kesho kutwa” “Good.Nimekuita hapa 

kukufahamisha kwamba tayari 

nimempata mtu atakayeziba nafasi 

ya George anaitwa Meshack 

Jumbo.Ni mstaafu huyu ila aliwahi 

kuongoza idara ya ujasusi wa taifa 

kwa ufanisi mkubwa sana.Ni mtu 

mwenye uzoefu wa kutosha na 

nimemuomba anisaidie kuongoza 

idara ya usalama wa taifa kwa 

mwaka mmoja amekubali.Kingine 

ni kwamba nimempata mtu 

ambaye atafanya uchunguzi 

kuhusiana na mauaji ya baba 

anaitwa Mathew Mulumbi.Huyu 

ndiye aliyeshiriki katika lile sakata 

la Peniela kama utakumbuka” 

“Wow ! Nalikumbuka lile 

sakata.Umemtoa wapi? Yule jamaa nakumbuka alioana na 

Peniela,amekubali vipi kuja 

kuifanya hii kazi?Lazima 

umemuahidi kumlipa fedha nyingi 

sana kwani yule jamaa ni bilionea” 

akasema Theresa 

“Haikuwa rahisi kumpata hata 

hivyo yeye na Peniela wamekwisha 

achana .Kila mmoja kwa sasa ana 

maisha yake.Yule jamaa ni mtu 

mwelewa sana na sijui kwa nini 

Peniela alikubali kumuacha 

mwanaume kama yule aende 

zake.Hata hivyo napaswa 

kumshukuru sana Meshack Jumbo 

kwani kwa kiasi kikubwa ndiye 

aliyefanikisha mimi kuonana na 

Mathew.Kuhusiana na fedha bado 

hatujakubaliana ni kiasi gani atahitaji kwani bado hajaanza kazi 

rasmi hadi atakapoweka sawa 

mambo yake.Theresa nina imani 

kubwa kwamba suala hili 

linakwenda kupata majibu” 

“Kama ni yule jamaa basi hata 

mimi nina uhakika mkubwa 

kwamba fumbo hili linakwenda 

kufumbuliwa.Kama ungekuwa na 

wazo hili toka zamani hivi sasa 

tungekwisha jua nani 

walioteketeza familia 

yetu.Hongera sana dada kwa hatua 

hii kubwa.Tumtakie kila la heri 

aifanye vizuri kazi hii kwani ndani 

yake inaonekana kujaa hatari.By 

the way Nathan alinipigia simu 

akadai kwamba amejitahidi 

kukupigia simu toka asubuhi bila mafanikio.Anaomba umpigie” 

akasema Theresa 

‘Theresa tayari nimeweka 

nukta katika mahusiano 

yetu.Nimetafakari sana na kuona 

nitajiweka katika matatizo 

makubwa na ninaweza kushindwa 

kufanya shughuli zangu hivyo 

sintaweza kujigawa huku 

nihudumie watanzania na huku 

nimhudumie mume.Kuna 

wanawake hawajaumbwa kuolewa 

na mimi ni mmoja wao nadhani 

ndiyo maana nilipenda sana kuwa 

mtawa wakati nikiwa mdogo” 

akasema Dr Vivian 

“Dada..” Theresa akataka 

kusema kitu Dr Vivian akamzuia “Don’t say anything 

Theresa.I’ve never given up in 

anything in my life and this is my 

first time.Zaidi ya watu milioni 

hamsini wako chini ya uangalizi 

wangu.watoto wao wanapaswa 

waende shule ,wapate elimu 

bora,wananchi wangu bado 

wanaishi maisha duni ambayo 

nahitaji kufanya kila juhudi 

kuyaboresha,kutengeza ajira 

zaidi,unafuu wa maisha 

upatikane,akina mama wajifungue 

salama,sitaki hata mwanamke 

mmoja apoteze maisha wakati wa 

kujifungua.Uzazi unapaswa kuwa 

salama.Nchi inapaswa kuwa na 

chakula cha kutosha,wakulima 

wanahitaji tija katika kilimo chao.Vijana wanamaliza vyuo 

vikuu wanahitaji ajira haya ni 

machache kati ya mengi ambayo 

napaswa kuyashughulikia kwa 

hiyo siwezi kuwa na muda wa 

kuhudumia mume” akasema Dr 

Vivian 

“Haya yote uliyoyasema dada 

ni ya kweli lakini hata wewe 

unahitaji kuwa na maisha yako nje 

ya urais.Unahitaji furaha,unahitaji 

mtu wa kukuliwaza na kutuliza 

kichwa chako,unahitaji 

mume,kama Nathan hakufai basi 

tafuta mwanaume mwingine” 

akasema Theresa 

“Theresa ungekuwa umekalia 

hiki kiti ungenielewa nina 

maanisha nini.Nathan ni mwanaume mzuri lakini nadhani 

mimi si chaguo sahihi 

kwake.Mitazamo yetu haiendi 

sawa.Itakuwa vyema kama 

nitakuwa mwenyewe si lazima 

niwe na mume ili kichwa changu 

kikae sawa.Usiku wa leo 

nitakutana na Evans mwenyekiti 

wa maandalizi ya harusi yangu na 

nitampa rasmi taarifa ya kusitisha 

shughuli zote za kuhusiana na 

maandalizi ya ndoa yangu na 

Nathan na kila aliyetoa mchango 

wake arudishiwe” akasema Dr 

Vivian 

“Dada ni suala la mtoto pekee 

ndilo limepelekea ukafanya 

maamuzi haya magumu au kuna 

sababu nyingine hutaki kuiweka wazi?Yamekuwa ni maamuzi ya 

ghafla sana” akasema Theresa 

“Theresa labda nilikuwa na 

upofu wa penzi na sikuweza kuona 

mbele kuna nini lakini maneno 

yako uliyonieleza tukiwa ndegeni 

yalinitoa upofu na kunifanya 

nifikirie sana na kufanya maamuzi 

haya.Usihofu kitu mdogo wangu 

things will be fine.Nenda 

kaendelee na shughuli 

zako.Nilitaka nikueleze hayo 

mambo mawili” akasema Dr Vivian 

na Theresa akatoka 

************* 

“Ninatoa onyo kwa taifa lolote 

lile kubwa au dogo ambalo linaungana na Korea kaskazini 

kwamba waache mara moja 

kufanya hivyo ama sivyo 

yatawakuta matatizo 

makubwa.Marekani itawahesabu 

kama maadui zake na hatutasita 

kuziwekea vikwazo vigumu sana 

na ikibidi hata kutumia nguvu za 

kijeshi.Ninaonya kwa mara ya 

mwisho waache kabisa 

mashirikiano yoyote na Korea 

Kaskazini kabla hayajawafika 

makubwa” 

Hii ilikuwa ni kauli ya rais 

Mike straw wa Marekani aliyoitoa 

kufuatia mgogoro unaoendelea 

kufukuta kati ya nchi yake na 

Korea kaskazini “Sijui nini utakuwa mwisho 

wa suala hili.Endapo hatua za 

haraka za kulitafutia ufumbuzi 

jambo hili hazitachukuliwa dunia 

itajikuta sehemu mbaya 

sana.Tanzania tutajikuta kati kati 

ya mataifa makubwa.Marekani na 

washirika wake hawataki Tanzaia 

iwe na mashirikiano na Korea 

kaskazini na kuiuzia madini ya 

Urani lakini ziko nchi ambazo 

zinasimama na Tanzania kama vile 

China,Urusi,Iran n.k.Hawa wote ni 

wapinzani wakubwa wa 

Marekani.Hapa kuna shughuli 

pevu.Hizi nchi zinazosimama 

upande wa Tanzania nazo zina 

uwezo mkubwa kijeshi.Endapo 

Marekani na washirika wake watajaribu kwa namna yoyote 

kuishambulia Tanzania kuna 

uwezekano mkubwa wa kuibuka 

vita ya tatu ya dunia.Mungu 

aepushe mbali jambo hilo 

lisitokee.Maelfu ya watu wasio na 

hatia watapoteza maisha” akawaza 

mathew akiwa sebuleni kwake 

akitazama taarifa ya habari toka 

shirika la habari la uingereza BBC. 

Aliwahi sana kurejea 

nyumbani siku hii.Tayari 

alikwisha weka sawa mambo yake 

na alikuwa tayari kuanza kuifanya 

kazi ya rais.Katika meza ndogo 

iliyokuwa mbele yake kulikuwa na 

chupa ya mvinyo na glasi.Pembeni 

yake alikuwa na kompyuta yake 

mpakato na kitu alichokuwa anakifanya katika kompyuta ile 

toka aliporejea nyumbani ni 

kutafuta taarifa za Kanali 

Sebastian Matope.Taarifa nyingi 

alizozipata ni kuhusiana na yeye 

kunusurika katika ajali ya ndege 

ya rais Anorld Mubara.Nyingine 

zinahusiana na kifo 

chake.Hakukuwa na habari za 

kutosha kuhusiana na maisha yake 

“Kanali Sebastian hana taarifa 

nyingi mtandaoni zinazoeleza 

maisha yake binafsi.Hii inaonyesha 

kwamba hakuwa mtu maarufu na 

ameanza sana kuandikwa katika 

mitandao baada ya ajali ile ya 

ndege .Nahitaji kumfahamu yeye 

binafsi alikuwa ni mtu wa namna 

gani na ili kupata taarifa zake natakiwa kuonana na familia 

yake.Nitaonana na Dr Vivian kesho 

ili niweze kupata taarifa kamili 

kuhusiana na baba yake. Kwa 

kuanzia uchunguzi wangu kuna 

maswali ambayo natakiwa 

kujiuliza na kuyapatia 

majibu.Kwanza Kanali Matope 

alinusurika vipi katika ile ndege ya 

rais iliyoanguka?Taarifa zinasema 

kwamba ni yeye pekee aliyeweza 

kutoka salama ndani ya hiyo ndege 

lakini haijaelezwa kwa kirefu ni 

vipi alitoka salama.Ninavyofahamu 

mimi,endapo kutakuwa na tatizo 

lolote katika ndege ya rais kiasi 

cha kuhatarisha usalama wa rais 

basi yeye huwa ni mtu wa kwanza 

kuondolewa ndegeni kwa namna yoyote ile na kisha watu wengine 

hufuata.Hata kama rais yuko na 

familia yake huondolewa kwanza 

na halafu familia yake 

hufuata.Ndege ya rais 

imetenegzwa maalum ili hata 

kama kukitokea tatizo lolote iwe 

rahisi kumuokoa rais,najiuliza 

ilikuaje Kanali Matope akatoka 

ndegeni kabla ya rais?Uchunguzi 

lazima uanzie hapo” akawaza 

Mathew na kunywa funda la 

mvinyo na kuendelea kutafakari. 

“Swali lingine ambalo 

linahitaji majibu ni kwamba kanali 

Matope alikuwa ndiye mbebaji 

mkuu wa begi la rais lenye siri za 

nchi lililopewa jina la 

Football.Sifahamu kulikuwa na siri gani ndani ya hilo begi ila naamini 

lazima kulikuwa na siri kubwa na 

ndiyo maana rais alienda nalo kila 

mahala aendako na mbebaji mkuu 

alikuwa ni Kanali Sebastian 

Matope.Je begi lile liko 

wapi?Alifanikiwa kutoka nalo 

ndegeni? Na kama 

ndiyo,amelikabidhi ikulu? Kama 

hapana kwa nini? Nifahamuvyo 

mimi mtu anayebeba football 

anakuwa amekula kiapo cha 

kuhakikisha inakuwa salama hata 

uhai wake ukiwa shakani na huwa 

analindwa hivyo sitaki kuamini 

kwamba Kanali Sebastian Matope 

alinusurika katika ajali ile na 

kuipoteza football kitu alichoapa 

kukilinda hata ikimlazimu kuutoa uhai wake.Nitahitaji kulifahamu 

hili pia” akanywa tena mvinyo na 

kuendelea na tafakari. 

“Jambo la tatu ambalo 

natakiwa kulifahamu ni chanzo 

cha ajali ya ndege ya 

rais.Uchunguzi wa kisanduku 

cheusi cha kuhifadhi kumbu 

kumbu za mwenendo wa ndege 

unaonyesha nini kilikuwa chanzo 

cha kuanguka kwa ndege ya rais? 

Nikipata majibu ya mambo haya 

matatu ninaweza kupata sehemu 

ya kuanzia” Akawaza na kuichukua 

tena barua ambayo George 

Mzabwa alimuandikia rais 

akaisoma 

“Katika barua hii George 

anamuonya rais kwamba aachane na suala hili kwani ni gumu na 

hataweza kupata majibu ya kile 

anachokitafuta.Je kuna kitu 

chochote kisicho cha kawaida 

alichokigundua ? Sidhani mtu 

kama George anaweza akachukua 

maamuzi ya kujiua bila 

sabab…..”Mathew akatolewa 

mawazoni baada ya simu yake 

mtandao wa Skype kuita katika 

kompyuta.Haraka haraka 

akaipokea baada ya kuona mpigaji 

ni binti yake Anna Maria. 

“Hallo my princess how’re 

you? 

“I’m fine dady.How’re you? 

“I’m fine.How’s your mom 

doing? “She’s also fine.We miss you so 

much.When will you visit us? 

“Oh my princess I can’t say 

when but I promise I’ll come very 

soon to visit you” 

“Next week is my birthday,will 

you come? 

“I’m sorry my princess I wont 

come but I’ll send you a very good 

gift.Is your mother there with you? 

“Yes she’s here” 

“Tell her to call me on my 

mobile right now” 

“Ok dady .I love you” 

“I love you too my princess.Be 

a good daughter to your mother” 

akasema Mathew na simu 

ikakatwa na muda huo huo simu yake ya mkononi ikaita.Alikuwa ni 

Peniela 

“hallow Penny” akasema 

Mathew 

“Hallow Mathew.Mambo vipi? 

“Mambo poa 

kabisa.Mnaendeleaje? 

“Tunaendelea vizuri.Wewe 

unaendeleaje? 

“Ninaendela vizuri.Anna 

Maria ameniuliza kama nitakuja 

katika siku yake ya kuzaliwa” 

“Ni wiki ijayo.Are you coming? 

“I’m sorry I’m not coming.I 

have something very important to 

take care over here” 

“That something is important 

than your daughter’s birthday 

party? “Si hivyo Penny lakini ni 

jambo la muhimu sana” 

Peniela akavuta pumzi ndefu 

na kuuliza 

“Umerejea tena katika kazi 

zako za zamani? 

“Ndiyo.Sikutaka lakini 

imenibidi nimsaidie rais” 

“President Vivian? Are you 

working for her? 

“Peniela haya ni masuala 

yangu binafsi na hupaswi 

kuyaingilia.Ninacho kiomba kwako 

unisaidie kumnunulia Anna Maria 

zawadi yoyote nzuri sana kwa 

niaba yangu.Can you help me do 

that? 

Peniela akafikiri kidogo na 

kusema “Sawa nitafanya hivyo” 

“Thank you” 

“Kwa hiyo unashugulika na 

suala gani huko kwa rais? 

“Peniela haya ni mambo 

yangu hupaswi kujua” 

“Can I help? Akauliza Peniela 

“No you can’t.Peniela wakati 

tunaachana tulikubaliana kwamba 

hakuna wa kuingilia maisha ya 

mwenzake.Wewe unayo maisha 

yako na bilionea wako na mimi 

nina maisha yangu hivyo jitahidi 

sana kuangalia maisha yako.Kiss 

my daughter for me” 

akasemaMathew na kukata simu 

“Nasikitika sana kukosa 

sherehe ya kuzaliwa mwanangu 

Anna Maria.Ni mara ya kwanza ninaikosa.Lakini sijaikosa kwa 

makusudi bali ni kutokana na 

jukumu zito alilonipa rais” 

akawaza Mathew 




iku mpya imeanza na 

tayari rais wa jamhuri 

ya muungano wa 

Tanzania Dr Vivian Matope 

amekwisha jiandaa tayari kwa 

kuikabili siku.Akiwa katika 

chumba cha chakula akipata 

kifungua kinywa na walinzi na 

wasaidizi wake alikuwa anapitia 

habari mbali mbali katika 

magazeti ya hapa nchini na habari 

kubwa iliyotawala karibu magazeti 

yote bado ilikuwa ni msuguano 

unaoendelea kati ya Korea 

kaskazini na Marekani huku Tanzania ikijikuta kati kati ya 

mzozo huo.Wakati akiendelea 

kupitia magazeti,simu yake 

maalum ikaita ,akaitazama na 

mpigaji alikuwa ni Mathew 

akaipokea haraka 

“Hallow Mathew,habariz a 

asubuhi? 

“Habari nzuri mheshimiwa 

rais.Nimekupigia kukujulisha 

kwamba tayari mambo yangu 

nimekwisha yaweka sawa na leo 

ninaanza kazi.Asubuhi hii ninakuja 

kukuona.Kuna mambo kadhaa 

nitayahitaji toka kwako” 

“Ahsante sana 

Mathew.Nitakupa kila 

utakachohitaji.Niko hapaninakusubiri” akasema Dr Vivian 

na Mathew akakata simu 

“Sifahamu utendaji kazi wake 

lakini ,Mathew ananipa matumaini 

makubwa katika jambo hili na nina 

uhakika kuna hatua kubwa 

ataipiga.Nitampa ushirikiano 

mkubwa ili aweze kufanikisha 

jambo hili” akawaza Dr Vivian 

huku akiendealea kupata kifungua 

kinywa taratibu na kusoma 

magazeti mbali mbali.Alipomaliza 

akaelekea ofisini kwake tayari 

kuanza kazi.Mtu wa kwanza 

kuonana naye ofisini kwake 

asubuhi hii alikuwa ni waziri wa 

mambo ya nje ambaye alipewa 

kazi maalum ya kuhakikisha 

mchakato wa mazungumzo kati ya Tanzania na Korea kaskazini 

unaanza mara moja. 

“Dr Robert,natumai utakuwa 

na taarifa za kunipa asubuhi ya 

leo” akasema Dr Vivian 

“Ndiyo mheshimiwa rais,ni 

kuhusiana na kazi uliyonipa jana 

mheshimiwa rais” akasema Dr 

Robert 

“Kwa kushirikiana na balozi 

wa Korea Kaskazini hapa Tanzania 

nimefanikiwa kufanya 

mazungumzo na waziri wa mambo 

ya nje wa Korea 

Kaskazini.Tumezungumza mambo 

mengi kuhusiana na mchakato wa 

kuanzishwa kwa mazungumzo ya 

mashirikiano ya kibiashara baina 

ya nchi zetu mbili kama ulivyonielekeza.Korea kaskazini 

kupitia kwa waziri wao wa mambo 

ya nje wamelipokea jambo hili kwa 

mikono miwili na muda mfupi 

uliopita nimetoka kuzungumza 

tena na waziri wa mambo ya nje 

wa Korea Kaskazini na amanipa 

habari njema kwamba tayari 

amemfikishia salamu zako rais 

Kim Yun Hu wa Korea Kaskazini na 

ambaye ameomba kuzungumza 

nawe jioni ya leo kuhusiana na 

masuala kadhaa muhimu kabla ya 

kuanza kwa mashirikiano rasmi 

baina ya nchi hizi mbili” akasema 

Dr Robert 

“Hizi ni taarifa njema sana 

kwa kuanzia siku ya leo.Ahsante 

Dr Robert kwa kazi nzuri.Kwa sasa endelea kushughulikia maongezi 

hayo na rais Kim Hu jioni ya leo” 

akasema Dr Vivian 

“Sawa mheshimiwa rais.Hawa 

jamaa wanaonekana wana nia ya 

dhati ya kutaka kufanya 

mashirikiano ya kibiashara na sisi 

na ndiyo maana mambo 

hayachelewi.Hawana muda wa 

kupoteza.Hata hivyo mheshimiwa 

rais tunapaswa kujiridhisha zaidi 

kama kweli tunahitaji 

mashirikiano haya na Korea 

kaskazini .Jambo hili linaendelea 

kuleta mvutano mkubwa na dunia 

inajigawa katika pande mbili wale 

wanaounga mkono Marekani na 

wale wanaounga mkono Tanzania 

kuwa na mashirikiano na Korea Kaskazini.Nchi yetu imewekwa 

kati kati na imekuwa maarufu 

ghafla kwani inazungumziwa 

duniani kote” akasema Dr Robert 

“Dr Robert hatuna haja ya 

kujitathmini mara ya 

pili.Tunahitaji kufanya biashara na 

Korea kaskazini.Pamoja na kelele 

zote zinazopigwa lakini msimamo 

wangu bado uko pale pale kwamba 

Tanzania na Korea Kaskazini 

lazima zishirikiane 

kibiashara.Mashirikiano haya 

naamini yatakuwa na tija kwa 

taifa.Kaendelee kufanya 

maandalizi kwa ajili ya mkutano 

wangu na Kim leo jioni” akasema 

Dr Vivian baada ya simu kuita na 

kutaarifiwa kwamba Mathew Mulumbi amefika.Rais akaelekeza 

apelekwe katika chumba cha 

maongezi ya faragha.Hakupoteza 

muda akatoka na kwenda kuonana 

na Mathew 

“Hallow Mathew karibu 

sana.Habari za toka jana? Dr Vivan 

akaanzisha maongezi 

“Habari nzuri kabisa 

mheshimiwa rais.Nimefanikiwa 

jana kuweka sawa mambo yangu 

na sasa nimekuja rasmi kuanza 

kazi” 

Uso wa Dr Vivian ukachanua 

kwa tabasamu halafu akasema 

“Ahsante sana Mathew kwa 

kuamua kuahirisha shughuli zako 

na kuifanya kazi yangu.Hii ni 

heshima kubwa umetupa mimi na familia yangu.Vitu gani utavihitaji 

katika kazi hii nikuandalie mara 

moja? 

“Kwa sasa nitahitaji vitu 

vichache.Baada ya kutafakari sana 

sehemu ya kuanzia uchunguzi wa 

suala hili nimeona nianzie katika 

ajali ya ndege ya rais Anorld 

Mubara.Kwanza nitahitaji kuipata 

ripoti ya uchunguzi wa chanzo cha 

ajali ya ndege ile ambamo Kanali 

Sebastian alikuwemo na 

akanusurika peke yake.Ninaamini 

uchunguzi ulifanywa na ripoti yake 

kutolewa hivyo ningependa 

niipitie nijue chanzo cha ajali 

ile.Jambo la pili ninahitaji kupata 

nakala ya maelezo aliyoyatoa 

Kanali Sebastian katika mahojiano yake na jeshi la polisi.Nataka 

kufahamu aliwezaje kutoka salama 

peke yake ndani ya ndege 

ile?Jambo la tatu nataka kufahamu 

kuhusiana na begi ambalo alikuwa 

analibeba Kanali Sebastian 

lililopewa jina la 

football.Inaaminika kwamba 

kulikuwa na siri kuwa ndani ya ule 

mkoba nataka kujua mahala ulipo 

ili tujue ni siri gani hasa 

iliyokuwamo ndani yake? Jambo la 

mwisho ninahitaji kumfahamu 

vyema Kanali Sebastian Matope 

alikuwa ni mtu wa namna 

gani.Maisha yake yalikuaje na 

alipendelea mambo gani zaidi na 

kama kuna sehemu ninaweza 

kupata kumbukumbu zake itakuwa vyema zaidi ili nione kama 

kuna kitu ninaweza kukipata cha 

kutusaidia kufahamu sababu ya 

kifo chake” akasame Mathew.Dr 

Vivian aliyekuwa anamtazama kwa 

makini akameza mate na kusema 

“Nimekuelewa Mathew na 

nitahakikisha hivyovyote 

ulivyoomba vinapatikana kwa 

haraka sana kabla ya saa nane 

mchana wa leo.Taarifa ya 

uchunguzi wa chanzo cha ajali ya 

ndege iliyomuua rais Anorld 

sijawahi kuipata lakini nitaiomba 

kutoka vyombo husika na 

nitapewa.Nina imani ipo.Jambo la 

pili ni maelezo aliyoyatoa Kanali 

Sebastian kwa polisi baada ya 

kunusurika katika ajali.Haya pia ni rahisi kuyapata na nitaagiza 

yaletwe hapa mara moja.Jambo la 

tatu ni kuhusu football.Hapa 

kutakuwa na ugumu kwani hili 

begi halipo.Nilipoingia 

madarakani sijawahi kuliona hilo 

begi na hata mtangulizi wangu 

hakuwahi kunieleza chochote 

kuhusiana na Football na wala 

hata naye hakuwa nalo.Hakuna 

anayejua iko wapi hivyo inabidi 

kuifanyia uchunguzi iko 

wapi?Jambo la nne na la mwisho 

umetaka kumfahamu Kanali 

Sebastian alikuwa mtu wa aina 

gani na kama kuna mahala 

unakoweza kupata kumbukumbu 

zake .Ningeweza kumuelezea baba 

alikuwa ni mtu wa aina gani lakini muda wangu mwingi nimeutumia 

katika masomo hivyo sikuwa 

napata muda mzuri sana wa kukaa 

nyumbani kwa hiyo sintaweza 

kumuelezea baba kwa undani 

sana.Hata hivyo ninaye mdogo 

wangu anaitwa Theresa huyu 

amekuwa na baba muda mwingi 

na anaweza akamuelezea vizuri 

zaidi.Kuhusiana na kupata 

kumbukumbu za baba ni kwamba 

muda mfupi tu baada ya kifo chake 

nyumba yake iliungua moto ambao 

chanzo chake hakikujulikana na 

kuteketeza kila kitu kilichokumo 

ndani yake kwa hiyo hakuna 

mahala kokote tunakoweza kupata 

kumbu kumbu zake.Hii inaonyesha 

ni kwa namna gani hili jambo lilivyokuwa gumu na ndiyo maana 

limekuwa ni kama fumbo 

lisiloweza kufumbuka.Pamoja na 

ugumu huo lakini nakuomba 

Mathew jitahidi kuweza kulipatia 

majibu.Kuna mambo mengi 

yamejificha katika jambo hili” 

akasema Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais jambo hili 

si rahisi kama ulivyosema na kwa 

namna lilivyokaa linaonekana ni 

suala pana sana na lenye 

mkanganyiko wa mambo.Lakini 

nakuhakikishia kwamba nitafanya 

kila lililo ndani ya uwezo wangu 

kuweza kupata majibu ya fumbo 

hili.Ninaweza kuonana na 

Theresa? “Theresa unaweza kuonana 

naye.Yupo hapa ikulu ndiye 

mwandishi wa hotuba zangu” 

Akasema Dr Vivian na kuinua simu 

akampigia Theresa akamtaka afike 

ofisini kwake mara moja 

“Kuna vitu vingine ambavyo 

ungevihitaji Mathew?Mfano silaha 

au mtu wa kukusaidia katika 

uchunguzi wako?akauliza rais 

“Hivyo nilivyokuomba ndivyo 

ninavihitaji kwa sasa na endapo 

kutakuwa na vitu vingine ambavyo 

nitavihitaji nitakujulisha .Silaha 

ninazo na sihitaji mtu wa 

kunisaidia kwa sasa ila 

nitakapohitaji nitakueleza” 

“Are you sure? “Yes madam president I’m 

sure” akajibu Mathew 

“Kiasi gani cha fedha 

utakihitaji kwa shughuli hii nzima? 

“Fedha?! Mathew akashangaa 

na kutabasamu 

“Namaanisha malipo 

yako.Utahitaji nikulipe kiasi gani 

kwa kazi hii?akauliza rais na 

Mathew akacheka kidogo na 

kusema 

“Sihitaji chochote 

mheshimiwa rais.Ninazo fedha za 

kunitosha.Hili lilikuwa ni ombi 

maalum toka kwako na kwa mzee 

Meshack.Kama alivyosema 

Meshack Jumbo jana kwamba 

nimsaidie dada yangu na ndivyo 

ninavyofanya.Kwa hiyo usiwaze kabisa kuhusiana na malipo” 

akasema Mathew na Dr Vivian 

akamtazama kwa mshangao na 

kuuliza 

“Mathew una uhakika 

hauhitaji fedha za kukusaidia? 

Kabla Mathew hajajibu kitu 

mlango ukafunguliwa akaingia 

Theresa 

“Theresa karibu 

sana.Nimekuita ukutane na 

Mathew Mulumbi.Huyu ndiye 

atakayetusaidia kulitafutia 

ufumbuzi lile fumbo 

lililoshindikana kufumbuka.Ndiye 

atakaye fanya uchunguzi wa 

walioteketeza familia yetu.Mathew 

huyu ni mdogo wangu anaitwa 

Theresa ndiye mwandishi wa hotuba za rais” Dr Vivian akafanya 

utambulisho.Mathew akasimama 

na kumsabahi Theresa 

“Mathew karibu sana 

.Nimefurahi kuonana nawe” 

akasema Theresa 

“Ahsante sana Theresa.Ni 

furaha yangu kukutana nawe pia” 

akajibu Mathew 

“Mathew kama ujuavyo mimi 

nina kazi nyingi sana,vikao 

haviishi,natembelewa na wageni 

wengi kila siku kwa hiyo kuna 

nyakati unaweza ukanihitaji au 

ukahitaji msaada wangu na 

kunikosa.Kutokana na umuhimu 

wa suala hili ninakukabidhi 

Theresa utakuwa naye 

akikusaidia.Kuna mambo mengi utayahitaji mfano taarifa mbali 

mbali hivyo huyu ndiye 

atakayekusaidia kuzipata.Theresa 

utahakikisha kila anachokihitaji 

Mathew anakipata na endapo kuna 

kitu kitakushinda basi utanijulisha 

mara moja.Mimi nitakuwa 

nikiwasiliana nanyi mara kwa 

mara kujua maendeleo yenu” 

akasema Dr Vivian na kunyamaza 

kidogo halafu akaendelea 

“Mathew nakuomba mlinde 

sana Theresa kwa kadiri 

uwezavyo.Awali ulisema kwamba 

huhitaji mtu yeyote wa kukusaidia 

katika kazi hii lakini nimeona 

jukumu hili ni zito sana na huwezi 

kulifanya peke yako bila 

msaada.Sitaki ufike mahala ukakwama na ndiyo maana 

ninakukabidhi mdogo wangu wa 

pekee kusaidia na kukuwezesha 

shughuli zako ziende vizuri kwa 

hiyo mlinde sana .Hili jambo ni la 

hatari sana .Usikubali akaingia 

katika hatari yoyote.Kama kuna 

taarifa au nyaraka zozote 

unazihitaji yeye atakusaidia 

kuzipata.Yeye anafahamika na 

anaweza akaingia sehemu yoyote 

ile kwa jina langu.Narudia tena 

kukuomba Mathew mlinde 

Theresa” akasema Dr Vivian na 

kumgeukia Theresa 

“Theresa hautasafiri kwenda 

sehemu yoyote kwa sasa kwa ajili 

ya kumsaidia Mathew.Weka 

pembeni majukumu yako yote kwa muda.Hotuba zangu nitaandika 

mwenyewe.Mathew amejitolea 

kuifanya kazi hii bila hata kulipwa 

senti moja kwa hiyo na sisi kama 

familia tunapaswa kumpa 

ushirikiano mkubwa.Kuna tatizo 

lolote katika hilo? Akauliza rais 

“Hakuna tatizo dada.Mimi 

niko tayari kumsaidia 

Mathew.Isitoshe hili ni jambo la 

familia hivyo na sisi tunapaswa 

kushiriki” 

“Ahsante sana .Mathew 

nawatakia kila la heri ila kumbuka 

kwamba jambo hili kutokana na 

unyeti wake lazima lifanyike kwa 

usiri kwani hatujui ni akina nani 

wanahusika” akasema Dr Vivian “Ahsante sana mheshimiwa 

rais.Narudia tena kukuahidi 

kwamba nitajitahidi kwa kila 

namna ninavyoweza” akasema 

Mathew huku akisimama na 

kupeana mkono na rais akatoka 

mle ndani ya chumba akamuacha 

rais na Theresa wakiongea halafu 

Theresa akatoka na kumtaka 

Mathew waelekee ofisini kwake 

“Nimefurahi kuonana nawe 

Mathew.Karibu sana ofisini 

kwangu” akasema Theresa baada 

ya kuingia ofisini kwake 

“Ahsante sana Theresa” 

akajibu Mathew.Theresa akapakia 

kompyuta yake katika mkoba 

pamoja na baadhi ya vitu vyake na 

kumtaka Mathew waondoke. “Tunaelekea wapi? 

“Katika ofisi nyingine” akajibu 

Theresa kwa ufupi. Theresa 

alimtaka Mathew amfuate kwa 

nyuma na gari lake kisha 

wakaondoka maeneo ya ikulu 

“Nina mashaka na Mathew 

kama kweli ataweza kulifumbua 

fumbo hili ambalo limeshindwa 

kufumbuliwa na vyombo vya 

uchunguzi kwa miaka kumi 

sasa.Naona kama vile ana 

hatarisha maisha yake kwa 

kujiingiza katika hili suala.Kijana 

mzuri sana yule sipendi kumuona 

akipata matatizo.Sijapendezwa na 

mpango wa dada wa kutaka 

kulifufua suala hili ambalo kwa 

sasa limetulia.Mambo mengi yataibuka na kutuweka katika 

hatari kubwa sana.Sintamweleza 

mtu yeyote hiki 

ninachokifahamu.Itaendelea 

kubaki siri yangu” akawaza 

Theresa na kuushika msalaba 

ulikokuwa shingoni. 

“Naamini msalaba huu una siri 

kubwa ndani yake ndiyo maana 

baba akaamua kunipatia na 

kunisisitiza niulinde sana.” 

Akawaza Theresa 

Gari la Theresa lilisimama nje 

ya geti jekundu na haukupita muda 

geti hilo likafunguliwa na gari la 

Theresa likaingia ndani na Mathew 

naye akafuata .Ndani ya nyumba 

hii kulikuwa na uzuri wa 

kipekee.Nyasi za kupendeza zenye ukijani wa kung’aa zilipandwa kila 

kona na kukatwa kwa ustadi 

mkubwa.Miti ya aina mbali mbali 

yenye maua ya kupendeza 

ilipandwa kulizunguka jumba hili 

na kulifanya liwe na mandhari ya 

kupendeza sana.Alikuwepo kijana 

mmoja aliyeonekana akifanya kazi 

ya kumwagilia na kuhudumia 

bustani.Theresa akasimamisha 

gari mbele ya nyumba iliyokuwa 

na rengi nyeupe na kuezekwa kwa 

vigae vya rangi nyekundu. 

Akashuka na Mathew naye 

akashuka na kumfuata 

“Mathew hapa ni nyumbani 

kwanu.Karibu sana.Hapa ndipo 

nyumbani kwa Kanali Sebastian 

Matope.Rais Dr Vivian naye ameishi katika nyumba hii hadi 

alipopata urais.Nyumba ya zamani 

ilikuwa upande ule kule chini 

lakini iliungua moto hivyo hii 

nyumba ni mpya” Akasema 

Theresa huku akimuonyesha 

Mathew mazingira ya nyumba ile 

nzuri 

“Nimeyapenda 

mazingira.Mmejitahidi sana 

kuyaboresha” akasema Mathew 

“Baba mzee Matope alikuwa 

anapenda sana mazingira na sisi 

tumefuata nyayo zake.Ile miti yote 

unayoiona katika bara bara ya 

kuja huku nyumbani ameipanda 

yeye.Karibu ndani mathew.Hapa 

ndipo tutakapoweka ofisi yetu ya 

muda.Pale ikulu hapana usiri lakini tukiwa hapa tutafanya 

shughuli zetu kwa usiri” akasema 

Theresa na kuingia 

ndani.Waliingia katika chumba 

kimoja kizuri kilichokuwa na 

samani za kupendeza za ofisi. 

“Hii ni ofisi yangu ya 

nyumbani.Vivian kabla ya kuwa 

rais hii ndiyo ilikuwa ofisi 

yake.Kuna kila kitu 

utakachokihitaji humu kasoro 

silaha” akasema Theresa na wote 

wakacheka 

“Nadhani bila kupoteza wakati 

tuanze kazi” akasema Mathew 

“Dada aliniambia kwamba 

nikusaidie kwa chochote kile 

utakachokihitaji kwa hiyo nina kusikiliza wewe,niambie nini 

unahitaji? 

“Ahsante.Nilimuomba rais vitu 

vinne.Kwanza taarifa ya chanzo 

cha ajali ya ndege ya rais 

Anorld,pili nakala ya maelezo ya 

kanali Sebastian baada ya 

kunusurika katika ile ajali ya 

ndege,tatu ni begi alilokuwa 

analibeba kanali Sebastian 

maarufu kama Football,niliomba 

vile vile kama kuna sehemu 

naweza kupata kumbu kumbu za 

kanali Sebastian na mwisho 

nilitaka nimfahamu kanali 

Sebastian ni mtu wa namna gani 

.Rais ameniahidi kunitafutia 

taarifa ya uchunguzi wa chanzo cha 

ajali ya ndege ya rais Anorld pamoja na nakala ya maelezo ya 

kanali sebastian aliyoyatoa baada 

ya kunusurika ajalini.Kuhusu 

Football amesema kwamba begi 

lile halijawahi kuonekana toka 

ajali ilipotokea.Kuhusu kumbu 

kumbu za kanali Sebastian 

nimeambiwa hakuna 

kumbukumbu zozote kwani 

nyumba yake iliungua moto baada 

ya yeye kuuawa.Mwisho kabisa 

nilitaka nimfahamu baba yenu 

alikuwa ni mtu wa aina gani na 

akasema kwamba jukumu hilo 

atakuachia wewe kwa kuwa 

umekuwa na kanali Matope kwa 

muda mrefu na hivyo unaweza 

ukamuelezea kwa upana 

zaidi”akasema Mathew na kumtazama Theresa kwa muda na 

kusema 

“Kanali Sebastian Matope 

hakuuawa kwa bahati 

mbaya.Mauaji yake yalikuwa 

yamepangwa na lazima kuna 

jambo lipo nyuma yake hivyo 

nataka nianzie uchunguzi wangu 

mbali kidogo katika ajali ya ndege 

ya rais.Nataka kufahamu aliwezaje 

kutoka salama katika ndege 

ile?Ninavyofahamu mimi endapo 

kutatokea tatizo lolote la 

kuhatarisha usalama wa rais 

ndegeni,aidha hitilafu au uvamizi 

wowote basi rais huwa ni mtu wa 

kwanza kuondolewa ndegeni.Hata 

kama yuko na familia yake lakini 

yeye hupewa umuhimu mkubwa kwanza.Katika ajali ile kanali 

Sebastian Matope alinusurika peke 

yake.Nikipata jibu la namna 

alivyotoka ndani ya ndege nitapata 

mwanga kwa nini aliuawa.Wakati 

nikisubiri taarifa hiyo nataka 

nimfahamu huyu kanali Sebastian 

alikuwa ni mtu wa aina gani? 

Wakati ajali ile ya ndege ilipotokea 

Vivian alikuwa masomoni nje ya 

nchi kwa hiyo wewe ulikuwepo 

hapa,je kuna jambo lolote aliwahi 

kukueleza ambalo unahisi 

linaweza kutusaidia katika 

uchunguzi wetu? Akauliza Mathew 

“Kwa kuanzia mimi si mtoto 

wao wa kunizaa.Walinichukua 

katika kituo cha kulelea watoto 

yatima nikiwa mdogo sana.Naambiwa niliwa na umri wa 

miaka miwili.Taarifa zinasema 

kwamba Kanali Sebastian Matope 

hakuwahi kuwafahamu wazazi 

wake na alikulia katika kituo cha 

kulelea watoto yatima hivyo 

alipenda sana kutembelea vituo 

vya kulelea mayatima kila pale 

alipokuwa na nafasi.Inaelezwa 

kwamba kuna siku alikwenda na 

mke wake katika kituo 

nilichokuwa nalelewa na 

walipotaka kuondoka niliwalilia 

sana ikabidi waombe kuondoka 

nami na toka hapo wakawa ndio 

wazazi wangu.Wamenilea kwa 

mapenzi makubwa kama mtoto 

wao wa kumzaa.Nimekuwa nao 

karibu hivyo ninawafahamu vyema.Baba alikuwa ni mtu mpole 

na mwenye upendo.Japokuwa 

alikuwa ni mwanajeshi tena 

aliyewahi kupitia na kufuzu 

mafunzo ya komando lakini 

arudipo nyumbani hutambua 

kuwa yeye ni baba .Hakuwa na 

marafiki wengi kutokana na muda 

mwingi kuutumia katika kazi 

zake.Baba alikuwa mjenzi vile vile 

na inasemekana ile nyumba yake 

iliyoungua ni yeye 

aliyeijenga.Alikuwa mpenda 

mazingira pia.Hayo ndiyo 

machache ninayoweza kuyaeleza 

kuhusiana na baba” “Ahsante sana.Hakuna 

chochote alichowahi kukueleza 

baada ya kunusurika ndegeni? Hakuwahi kuwaelezeni namna 

alivyonusurika? 

“Hakuwahi kutufafanulia bali 

alieleza kwa ujumla tu kwamba 

alinusurika ndegeni kwa kutumia 

mbinu za kijeshi.Yawezekana 

labda alimfahamisha mama ila 

mimi hakuwahi kunieleza” 

“Siku ile alipouawa ilikuwa 

jumapili,wewe ulikuwa 

wapi?Ulimuona akiwa katika hali 

gani? 

“Siku ile mimi nilikwenda 

kuhudhuria ibada na nilichelewa 

kurudi kwa sababu kulikuwa na 

harambee na laiti ningewahi 

kurudi ningeambatana nao na 

mimi ningekufa kwani walinisubiri 

sana na walipoona wanazidi kuchelewa wakaondoka na 

kuniacha.Alikuwa kawaida na 

hakuonekana kuwa na tatizo 

lolote” akasema Theresa. 

“Siku ile ndege ya rais 

ilipopata ajali walikuwa wanatoka 

nchini Misri katika mkutano.Siku 

moja kabla ya safari ile 

alikuaje?Kuna kitu chochote 

unakikumbuka ambacho 

hakikuwa cha kawaida kwake? 

“Jioni ya siku ile nilikuwa naye 

sebuleni tukipata chakula pamoja 

na hakuonyesha utofauti wowote 

.Alikuwa kawaida kama siku zote” 

akajibu Theresa 



Jioni ya siku ile nilikuwa naye 

sebuleni tukipata chakula pamoja 

na hakuonyesha utofauti wowote 

.Alikuwa kawaida kama siku zote” 

akajibu Theresa 

“I see” akasema Mathew na 

kukaa kimya kidogo na kabla hajasema chochote simu yake 

ikaita.Alikuwa ni rais Dr Vivian 

“Rais anapiga” akasema na 

kuipokea 

“Hallow mheshimiwa rais” 

akasema Mathew 

“Mathew just call me Dr 

Vivian.Kila wakati mheshimiwa 

inachosha masikio.Nimekupigia 

kukupa taarifa kuhusiana na ile 

taarifa uliyoiomba ya uchunguzi 

wa chanzo cha ajali ya ndege ya 

rais Anorld.Taarifa nilizozipata 

zimenistua .Nimeambiwa kwamba 

taarifa hiyo haipo kwa sababu 

uchunguzi wa kubaini sababu ya 

kuanguka kwa ndege ya rais 

haukuwahi kukamilika kwa kuwa 

kisanduku cheusi maalum kwa ajili ya kuifadhi taarifa za mwenendo 

wa ndege hakikuwahi kuonekana” 

“Hakijawahi kuonekana? 

Mathew akashangaa 

“Mathew nilipokuambia 

kamba suala hili ni fumbo gumu 

nilikuwa namaanisha na sasa 

umeanza kuona ugumu 

wake”akasema Dr Vivian 

“Kweli Dr Vivian hili suala ni 

fumbo.Hainiingii akilini eti 

kisanduku hicho muhimu kipotee 

kisionekane na halafu isiwekwe 

wazi na jambo hili likabaki kuwa 

ni siri.Halafu cha kushangaza ni 

kwamba ndege ile iliangukia 

sehemu tambarare kabisa iweje 

kisanduku hicho 

kisionekane?Ingekuwa imeanguka katika maji au katika milima 

mikubwa hapo kidogo tungeweza 

kukubaliana na hilo jambo lakini 

hata hivyo ipo namna ya 

kukitafuta kisanduku hicho 

.Naamini kuna kitu hapa katika hii 

ajali ya ndege ya rais na ndiyo 

maana nikaamua kuanza 

uchunguzi wangu kutafuta kwa 

nini ndege hii ilianguka.Nina hisi 

lazima kisanduku hicho 

kiliondolewa makusudi na 

kufichwa ili kuzuia chanzo cha 

ajali ile kujulikana.Kama tukiweza 

kufahamu chanzo cha ajali hiyo 

basi tutaweza kupata urahisi wa 

kujua kwani nini kanali Sebastian 

aliuawa na waliomuua ni akina 

nani.Naamini mauaji ya Kanali Sebastian chanzo chake kimeanzia 

mbali” Akasema Mathew 

“Mathew nadhani mwanzo tu 

umeona utata ulipo hivyo nakusihi 

kuwa makini sana wakati 

unalichunguza hili jambo.Si jambo 

rahisi” 

“Nalifahamu hilo mheshimiwa 

rais,naomba unisaidie basi nipate 

maelezo ya kanali Sebastian 

wakati nikitafakari kuhusiana na 

hilo suala la kupotea kwa 

kisanduku cha kuhifadhi kumbu 

kumbu za ndege” akasema Mathew 

“Sawa Mathew nimekwisha 

agiza niletewe hiyo taarifa na mara 

tu itakapofika nitakujulisha mara 

moja” akasema rais na kukata 

simu “Kuna nini Mathew?akauliza 

Theresa 

“Nilimuomba rais anisaidie 

nipate taarifa ya uchunguzi wa 

chanzo cha ajali ya ndege ya rais 

Anorld na majibu aliyonipa 

yanashangaza sana.Inadaiwa 

uchunguzi huo wa kubaini sababu 

ya ndege hiyo kuanguka 

haukufanikiwa kwa sababu 

kisanduku cheusi ambacho 

huhifadhi taarifa za mwenendo wa 

ndege hakikuwahi kuonekana 

eneola ajali’ 

“Kimekwenda wapi? Nani 

kakichukua? Theresa akauliza 

“Hakuna mwenye jibu hilo 

lakini ni wazi kiliondolewa 

makusudi ili chanzo cha ajali hiyo kisijulikane.Theresa suala hli 

linaonekana ni kubwa.Chanzo cha 

kifo cha baba yenu kimeanzia 

mbali.Ninatakiwa kulichimbua 

hadi mzizi wake ili kuupata 

ukweli” 

Theresa akafikir kidogo na 

kusema 

“Mathew hili suala limeanza 

kuniogopesha .Kwa nini 

tusiachane nalo kama lilivyo?Sitaki 

familia yetu iingie katika hatari 

tena”akasema Theresa 

“Theresa hili si suala 

dogo.Watu waliofanya kitendo 

hicho cha kuondoka na kisanduku 

hicho ni watu wanaoelewa kitu 

wanachokifanya na wana sababu 

ya kufanya hivyo.Mimi huwa nikigundua mambo tata kama hili 

katu siwezi kukubali kuliacha 

likapita hivi hivi.Lazima 

nilichimbue jambo hili hadi mzizi 

wake na hadi niupate 

ukweli.Usihofu kuhusu hatari 

mimi nimekwisha zoea na kwa vile 

utakuwa karibu yangu nakuomba 

uwe jasiri “ akasema Mathew 

“Ninaogopa sana Mathew .Kwa 

hiyo nini kinafuata baada ya hapa? 

“Taa nyekundu imeniwakia 

katika ajali ya ndege ya 

rais,naamini kuna jambo 

limejificha hapo hivyo uchunguzi 

unatakiwa kijikita zaidi hapo 

katika ajali” akasema Mathew 

“Kama hicho kiboksi ambacho 

huhifadhi taarifa zote za mwenendo wa ndege hakipo 

utachunguza vipi?Theresa akauliza 

.Mathew akafikiri na kusema 

“Nahitaji kufahamu aliyekuwa 

balozi wa Tanzania nchini Misri 

wakati huo” 

“Unahitaji kuzungumza naye? 

“Ndiyo kuna mambo nahitaji 

kuzungumza naye” akasema 

Mathew na Theresa akazungumza 

na mtu simuni na baada ya muda 

akakata simu na kumtazama 

Mathew 

“Nimeambiwa nisubiri kwa 

dakika chache nitajulishwa” 

akasema Theresa 

“Nini unahitaji kufahamu 

kutoka kwa huyo balozi? Na vipi 

iwapo….” Hakumaliza alichotaka kukisema simu yake ikaita 

akazungumza kwa muda wa 

dakika tatu kisha akaagana na 

aliyekuwa anaongea naye akakata 

simu na kumgeukia Mathew 

“Nimetaarifiwa kwamba 

aliyekuwa balozi wa Tanzania 

nchini Misri wakati wa rais Anorld 

alipofariki ni Alhaj Zubery 

Msokwa.Nimeelekezwa anaishi mji 

wa kale Kigamboni 

“Good.Twende tukaonane 

naye” akasema Mathew wakatoka 

na kuingia katika gari la Theresa 

wakaondoka 

“Natamani Mathew 

asifanikiwe katika suala hili na 

akate tamaa aachane nalo.Ni suala 

la hatari kubwa na ninaamini maisha yetu yatakuwa hatarini 

pindi ikibainika kwamba 

tumeanza kulifuatilia hili 

jambo.Ninaogopa ila sijui nifanye 

nini kumkwamisha huyu jamaa 

asiendelee na kulichimba hili 

jambo.Yeye amedhamiria kuupata 

ukweli na nikimtazama machoni 

anamaanisha kile 

anachokisema.I’m so scared” 

akawaza Theresa wakiwa njiani 

kuelekea kwa Alhaj Zubery 

Msokwa aliyewahi kuwa balozi wa 

Tanzania nchini Misri wakati rais 

Anorld anapata ajali. 

“Kisanduku cheusi 

hakikuwahi kuonekana eneo la 

ajali.Hii inawezekana vipi?Mathew 

akajiuliza “Suala la kupotea kwa 

kisanduku cheusi linashangaza 

sana hasa kutokana na mahala 

ndege ilipoangukia kuwa ni 

sehemu tambarare.Ingekuwa 

katika maji labda ingeniingia 

akilini lakini siwezi kukubali eti 

kisanduku kisionekane sehemu 

kama ile.Kuna jambo gani 

linafichwa kuhusiana na ajali ile? 

Naamini kisanduku hicho 

kimeondolewa makusudi kabisa ili 

sababu ya kuanguka kwa ndege ile 

isijulikane.Kingine 

kinachonishangaza ni kwa nini 

jambo hili limefanywa siri?Kuna 

watu ndani ya serikali wanahusika 

na ajali ile na ndiyo maana hili 

jambo likafichwa lisijulikane? Hapa kuna siri kubwa .Napaswa 

kuongeza umakini sana katika hili 

jambo.Nikifanikiwa kugundua 

kilichotokea hadi ndege ya rais 

ikaanguka nitakuwa nimepiga 

hatua kubwa sana katika 

kufahamu kwa nini kanali 

Sebastian aliuawa.Hili jambo 

haliwezi kufanywa na mtu mmoja 

bali na mtandao mkubwa 

waliojipanga vyema” akawaza 

Mathew 

Safari iliendelea hadi 

walipofika katika nyumba 

aliyoelekezwa Theresa kwamba 

ndipo anaishi Alhaj Zubery 

Msokwa.Mathew akashuka garini 

na kwenda kugonga geti na baada 

ya muda mlango mdogo ukafunguliwa na binti mmoja 

akajitokeza akawasabahi 

“Niwasaidie nini? Akauliza 

“Hapa ndipo nyumbani kwa 

Alhaj Zubery Msokwa? Akauliza 

Mathew 

“Ndiyo hapa.karibuni sana” 

akasema yule msichana na 

kufungua geti .Theresa akaingiza 

gari ndani halafu wakakaribishwa 

sebuleni.Baada ya muda akatokea 

mama mmoja wa makamo 

“Karibuni jamani” akasema 

yule mwanamama mweupe sana 

na aliyeonekana kama 

amechanganya damu. 

“Ahsante sana,habari za hapa? 

Wakajibu Mathew na Theresa kwa 

pamoja “Za hapa nzuri sijui nyie huko 

mtokako” akauliza 

“Huko ni kwema 

kabisa.Samahani kwa kuwavamia 

bila taarifa” akasema Theresa 

“Bila samahani.Karibuni sana” 

“Ahsante.Mimi naitwa Theresa 

Matope na huyu mwenzangu 

anaitwa Mathew.Sote ni 

wafanyakazi wa ikulu” akasema 

Theresa. 

“Oh ! karibuni sana.Mimi 

naitwa Zaina Moskwa.” Akajibu 

yule mama na mara yule dada 

aliyewapokea akina Mathew 

akatokea akiwa na sinia lenye glasi 

mbili za juisi na sambusa nne 

akawakaribisha “Tunafurahi kukufahamu 

Zaina.Tumekuja hapa kutaka 

kuzungumza na Alhaj Zubery 

Msokwa ambaye naamini ni baba 

yako” 

“Ndiyo ni baba yangu.Mimi ni 

mtoto wake wa mwisho.Watoto 

wake wengine wote wako Arabuni 

na mimi ndiye niko hapa 

kumuhudumia kwani mama yetu 

alikwisha tangulia mbele za 

haki.Kwa sasa baba anasumbuliwa 

na maradhi mbalimbali.Alipooza 

upande wa kulia ingawqa kwa sasa 

hilo si tatizo sana kwani anaendela 

vyema,anasumbuliwa vile vile na 

sukari na shinikizola damu.Utu 

uzima nao unachangia ” “Dah ! pole sana.Vipi hali yake 

kwa sasa? Akauliza Mathew 

“Kwa sasa anaendelea vizuri 

ila tatizo ni mkono ndio 

unaomsumbua” 

“Pole Zaina hii ni mitihani ya 

maisha.Mungu akupe wepesi wa 

kuweza kumuuguza mzee” 

akasema Theresa 

“Nashukuru Theresa” 

akasema Zaina na ukimya wa 

sekunde kadhaa ukapita 

“ Maradhi haya yalimuanza 

wakati gani? Mathew akauliza 

“Alianza kuumwa angali akiwa 

balozi wa Tanzania nchini 

Misri.Alipata ajali ya gari na 

kulazwa kwa muda mrefu 

hospitali.Amekaa kwa muda wa miaka zaidi ya saba nchini Israel 

na Mungu akamjalia akapata nafuu 

ndipo tuliporejea nyumbani 

Tanzania.Toka wakati huo 

amekuwa ni mtu wa nyumbani 

.Mlitaka kuzungumza naye jambo 

gani? Akauliza Zaina 

“Kuna jambo fulani liliwahi 

kutokea kama miaka kumi 

iliyopita wakati yeye akiwa ni 

balozi wa Tanzania nchini Misri 

hivyo tunataka kujua kama 

anaweza kuwa anakumbuka 

chochote kuhusiana na hilo jambo” 

akasema Mathew 

“Mh ! baba amekuwa na tatizo 

la kupoteza kumbu kumbu.Kuna 

wakati anakuwa mzima kabisa na 

kumbu kumbu zake zinakuwa sana lakini kuna nyakati anapoteza 

kumbu kumbu na hata mimi 

mwenyewe huwa ananipotea na 

kuniuliza mimi ni nani.Hata hivyo 

nisiwakatishe tamaa mnaweza 

mkajaribu bahati yenu na mkapata 

kile mhachokitaka kwani kuna 

wakati kumbukumbu zake huwa 

zinakaa vizuri na hukumbuka 

mambo mengi hata ya zamani” 

akasema Zaina na kuwataka akina 

Mathew wamfuate wakaelekea 

bustanini ambako walimkuta mzee 

mmoja aliyevaa kofia nyekundu 

akiwa amekaa sofani mahala 

palipotengenezwa maalum kwa 

ajili ya kupumzika.Ilikuwa ni 

bustani nzuri .Mkononi mwake 

alikuwa na kitabu cha dini akisoma.Alipomuona Zaina na 

wageni akafunika kitabu kile na 

kukiweka pembeni 

“Baba nimekueletea wageni” 

akasema Zaina huku akitabasamu 

“Karibuni” akasema mzee 

Zubery 

“Shikamoo mzee” Mathew na 

Theresa wakamsalimu 

“Marahaba vijana.karbuni” 

“Ahsante mzee.”wakasema na 

kuketi katika viti vilivyokuwapo 

eneo lile maalum kwa kupumzika. 

“Baba hawa wageni wametoka 

ikulu ,watajitambulisha wenyewe 

na wataeleza kitu gani 

kilichowaleta hapa kwako” 

akasema Zaina “Karibuni vijana.Wanasemaje 

ikulu? 

“Mzee mimi naitwa Mathew na 

huyu mwenzangu anaitwa 

Theresa.Sote ni wafanyakazi wa 

ikulu.Tumekuja hapa kwako kuna 

mambo tunataka utusaidie 

kukumbuka” 

“Mambo gani? Akauliza mzee 

Zubery 

“Uliwahi kuwa balozi wa 

Tanzania nchini Misri wakati wa 

uongozi wa rais Anorld Mubara” 

“Ndiyo nimekuwa balozi wa 

Tanzania Misri miaka kumi na 

tatu.Nilikuwa balozi kabla hata 

rais Anorld hajaingia 

madarakani.Hata mke wangu wa 

pili nilimpata huko huko.Nilistaafu baada ya kupata ajali na 

nikashindwa kuendelea tena na 

kazi” 

“Pole sana mzee na hongera 

kwa kukaa kipindi kirefu katika 

ubalozi nchini Misri.Kazi yao 

ilikuwa nzuri na ndiyo maana 

ukaachwa sehemu moja kwa 

miaka mingi.Mzee Zubery kama 

utakumbuka rais Anorld alifariki 

katika ajali ya ndege akitokea 

nchini Misri katika kikao cha 

marais wa nchi zinazopitiwa na 

mto Nile.Katika ajali hiyo watu 

wote walifariki dunia.Chanzo cha 

ajali hiyo mpaka leo hajifahamika 

.Ukiwa kama balozi ulimpokea rais 

Anorld na ujumbe wake hadi 

walipoondoka.Kuna chochote unachoweza kukumbuka ambacho 

unahisi hakikuwa cha kawaida 

katika safari ile ya rais? Mathew 

akauliza.Kwa kutumia mkono 

wake wa kushoto mzee Zubery 

akafuta mdomo wake kwa 

kitambaa na kusema 

“Niliwapokea rais Anorld na 

ujumbe wake, wakahudhuria 

kikao ambacho na mimi 

nilihudhuria na baadae jioni 

akaondoka salama.Aliondoka 

salama na kuelekea Jamaica lakini 

ndege yake ikaanguka 

baharini.Nasikitika sana.Watu wa 

Jamaika wamempoteza rais mzuri 

sana.Alikuwa na mahusiano 

mazuri na Tanzania” akasema mzee Zubery .Mathew na Theresa 

wakatazamana. 

“Hiyo ndiyo hali yake.Huwa 

anapoteza kumbukumbu na 

kuongea mambo ya ajabu ajabu 

lakini kuna wakati kumbukumbu 

zake hukaa sawa na huongea 

mambo mengi ya 

maana.Anafahamu mambo mengi 

sana.Anawafahamu viongozi wengi 

wa Afrika waliowahi kupita” 

akasema Zaina 

“Kwani ninyi mmetoka nchi 

gani? Zambia?Mzee Zubery 

akauliza 

“Ndgu zangu tayari mambo 

yameharibika hapa na hamtaweza 

kupata kile 

mnachokihitaji.Nawashauri niachieni mawasiliano yenu na 

baadae akikaa sawa nitamuuliza 

kile mlichomuuliza na akiniambia 

chochote nitakujulisheni.” 

Akasema Zaina. 

“Nadhani hilo ndilo la 

msingi”akasema Mathew na 

kubadilishana namba zake za simu 

na Zaina kisha wakaondoka 

“Nashukuru hatujapata 

chochote toka kwa huyu mzee na 

ninaomba aendelee kupoteza 

kumbukumbu hivyo hivyo. Sitaki 

kabisa jambo hili lifanikiwe kwani 

litatuweka mimi na dada katika 

hatari kubwa” akawaza Theresa 

“Nini kinafuata baada ya 

hapa? Tumeshindwa kupata chochote toka kwa yule mzee” 

akasema Theresa 

“Bado nafikiria kitu cha 

kufanya .Nilimtegemea sana Alhaji 

Zubery lakini naye ndiyo hivyo 

tena kumbukumbu zinakuja na 

kupotea” akasema Mathew na 

simu ya Theresa ikaita.Akakunja 

sura baada ya kutazama 

mpigaji.Simu ikaita na kukatika 

bila kuipokea. 

“Mbona hupokei? Akauliza 

Mathew 

“I don’t want to talk to him” 

akasema Theresa .Mathew 

akatabasamu na kuuliza 

“Ni mpenzi wako? 

“Hapana ni mpenzi wa dada” “Kwa nini basi hupokei simu 

yake kama ni shemeji yako 

anakupigia? Pokea umsikilize” 

“Sitaki kuingilia mambo 

yao.Wamekwisha achana na dada 

Vivian hataki tena kuendelea na 

mahusiano naye kwa hiyo 

ananisumbua mimi kutaka 

nimsaidie warudiane” 

“Nini sababu ya kutengena 

kwao? 

“Wanajua wenyewe.Dada 

hajawahi kunieleza”akasema 

Theresa 

“Mambo ya mahusiano ni 

magumu na yanahitaji uvumilivu 

wa hali ya juu.Kama bado 

hujaingia katika ndoa nakushauri 

umuombe sana Mungu akujalie umpate mwanaume sahihi 

kwako.Endapo hautakuwa na 

uhakika na huyo mpenzi uliyenaye 

usiingie katika ndoa” akasema 

Mathew 

“Nalielewa hilo Mathew na 

niko makini sana .Niliamua 

kuvunja mahusiano na mpenzi 

wangu niliyekuwa naye 

nilipogundua kwamba mimi na 

yeye htuwezi kwenda sawa” 

“Good.Ulifanya vizuri 

sana.Usilazimishe mapenzi.Ni heri 

uwe mwenyewe na amani ya moyo 

kuliko kuwa katika mapenzi ya 

maigizo.Nimekuwa katika ndoa 

ninayafahamu vyema mambo haya 

na laiti nikipata nafasi nitafungua 

darasa huko mbeleni la kuwafunisha watu maisha ya ndoa 

yalivyo” 

“Oh kumbe umeshaoa? 

Akauliza Theresa huku 

akitabasamu 

“Nilioa lakini kwa sasa 

tumekwisha tengana .Maisha ya 

ndoa naweza kusema ni mazuri 

lakini si rahisi.Si maisha ya 

kukimbilia.Muombe sana Mungu 

wako akujalie umpate mchumba 

mwema.Ukipata pasua kichwa 

atakupasua hadi moyo”akasema 

Mathew 

“Unaonekana umepitia 

mambo mengi katika ndoa 

yako.Tukipata nafasi utanieleza 

mikasa uliyokutana nayo katika 

ndoa .Unao………………”Theresa akanyamza baada ya simu ya 

Mathew kuita.Akaitoa mfukoni 

akatazama mpigaji alikuwa ni 

Zaina 

‘Zaina anapiga” akasema 

Mathew na kuipokea 

“Hallow Zaina” akasema 

“Mathew kama nilivyokueleza 

kwamba kumbu kumbu za baba 

huwa zinakuja na 

kupotea.Mlipotoka tu kumbu 

kumbu zake zimekaa sawa na 

akasema niwaite ili ajue 

mlichokuwa mnakitaka 

nikamwambia mmekwisha ondoka 

hivyo nikamuuliza lile swali 

ulilokuwa umemuuliza” 

“Enhee ! amesemaje? “Amesema kwamba baada ya 

rais kumaliza kikao chake 

alielekea uwanja wa ndege na 

kuna kitu anasema kilitokea hapo 

uwanja wa ndege ambacho 

hakikuwa cha kawaida.Anasema 

kuna waandishi nane wa habari 

waliokuwa nchini Misri ila 

hakumbuki walitokea nchi gani 

lakini walikuwa wanaelekea 

Tanzania waliomba nafasi katika 

ndege ya rais na wakaruhusiwa 

kupanda.Anasema kwamba hiki 

alikiona ni kitu cha ajabu sana 

kwake.Anasema kwamba yeye 

ndiye aliyewaombea lifti kwa rais 

naye akakubali.Kingine 

anachokikumbuka ambacho 

anasema kimemsikitisha sana ni kwamba katika msafara ule wa 

rais kulikuwa na binti mzuri 

aliyekwenda Misri 

kutembea.Amemsahau jina lake ila 

anakumbuka binti huyo alikuwa 

mcheshi sana .Alipewa maelekezo 

kwamba amtafutie mtu wa 

kumtembeza jijini Cairo ili ajifunze 

mambo mbalimbali ya kihistoria 

yaliyomo katika jiji 

hilo.Anasikitika kamba binti yule 

naye alifariki katika ajali ile.Hayo 

ndiyo aliyoweza kuyakumbuka 

kwa sasa.Kama kuna kingine 

atakachoweza kukumbuka tena 

nitakujulisha” akasema Zaina 

“Ahsante sana Zaina kwa 

taarifa hiyo.Kama kuna chochote 

kingine atakueleza naomba unijuze tafadhali” akasema 

Mathew na kuagana na Zaina 




Ahsante sana Zaina kwa 

taarifa hiyo.Kama kuna chochote 

kingine atakueleza naomba unijuze tafadhali” akasema 

Mathew na kuagana na Zaina 

“Anasemaje Zaina? Theresa 

akauliza 

“Mzee Zubery kuna mambo 

amekumbuka.Anadai kwamba 

baada ya rais Anorld kumaliza 

kikao jijini Cairo na akiwa 

anajiandaa kurejea Tanzania 

kulitokea waandishi wa habari 

walioomba lifti katika ndege ya 

rais na yeye ndiye aliyewaombea 

kwa rais wakakubaliwa .Anasema 

kwamba hiki hakikuwa kitu cha 

kawaida kwake japokuwa yeye 

ndiye aliyewaombea lifti hiyo.Vile 

vile anakumbuka kwamba katika 

msafara wa rais kulikuwa na binti 

mwanafunzi aliyekwenda nchini Misri kujifunza mambo 

mbalimbali,naye alifariki katika 

ajali hiyo” 

Uso wa Theresa ulionyesha 

wasi wasi na mstuko mkubwa 

akajitahidi ili Mathew asigundue 

“Mathew una uhakika na yule 

mzee?Kwa namna alivyo sina 

hakika kama tunapaswa 

kumuamini.Akili yake haipo sawa” 

akasema Theresa 

“Lakini Zaina ndiye 

anayemfahamu vyema baba yake 

na ana uhakika kwamba hizi 

kumbu kumbu ni 

sahihi.Asingeweza kunipa taarifa 

ambazo anajua kabisa kwamba si 

za kweli” akasema Mathew “Yule mzee kweli kuna 

nyakati kumbukumbu zake 

zinakaa sawa.Ni kweli 

alichokisema.Kulikuwa na 

waandishi nane wa habari wakati 

tunarejea Dar es salaam.Binti 

mdogo aliyemsema nilikuwa 

mimi.Nimweleze Mathew ukweli? 

Akawaza 

“Theresa kuna jambo nataka 

ulifanye” akasema Mathew na 

kumtoa Theresa mawazoni 

“Sema Mathew unahitaji nini? 

“Nataka kufahamnu wakati 

rais Anorld anaondoka kuelekea 

Cairo Misri alikuwa ameongozana 

na akina nani? Kulikuwa na watu 

wangapi katika msafara wake? Naamini kumbu kumbu hizi zipo 

nisaidie kuzipata” 

“Sawa Mathew ngoja 

nilishughulikie hilo” akasema 

Theresa na kwa kuwa gari 

zilikuwa zinakwenda taratibu 

kutokana na foleni ndefu 

akachukua simu na kuzungumza 

na mtu fulani akaomba 

aangaliziwe idadi ya watu 

walioorodheshwa wakati rais 

Anorld alipokwenda Cairo Misri. 

Baada ya dakika tano simu ya 

Theresa ikaita,akazungumza kwa 

dakika mbili halafu akamgeukia 

Mathew 

“Wakati anaelekea Cairo Misri 

rais Anorld alikuwa ameongozana 

na mawaziri wawili,wasaidizi ,marubani,wahudumu na 

walinzi.Jumla ya watu ndegeni 

walikuwa kumi na nane” 

“Good.Kwa hiyo kama 

kulikuwa na jumla ya watu kumi 

na nane walioondoka na ndege ya 

rais na ukijumlisha na wale 

waandishi nane wa habari jumla ya 

watu waliokuwemo ndegeni 

wakati wa kurejea nyumbani ni 

ishirini na sita.Kanali Sebastian 

Matope alinusurika hivyo jumla ya 

maiti ambazo zinapaswa kuwa 

zilipatikana ni ishirini na tano.Ili 

kupata uhakika zaidi kama taarifa 

hii ya mzee Zubery ni sahihi 

nataka kujua ni maiti ngapi 

zilipatikana baada ya ndege 

kuanguka? Fuatilia taarifa hiyo nahitaji kujua”akasema Mathew na 

Theresa akachukua tena simu 

akazungumza na mtu na kusubiri 

na baada ya dakika tatu akapigiwa 

simu akaongea kwa muda halafu 

akamgeukia Mathew 

“Nimepewa taarifa kwamba 

maiti zilizopatikana katika ajali ya 

ndege ya rais Anorld ni kumi na 

saba” 

“Kumi na saba? 

“Ndiyo.Kumi na saba pekee” 

“Inawezekanaje kuwe na maiti 

kumi na saba wakati ndani ya 

ndege walikuwepo watu ishirini na 

sita na aliyesalimika ni kanali 

Sebastian pekee? Kulipaswa kuwa 

na jumla ya maiti ishirini na tano” “Hiyo ndiyo taarifa iliyopo 

Mathew kwamba maiti zilipatikana 

kumi na saba tu” 

“Inashangaza sana.Kwa hiyo 

watu tisa hawajulikani walipo” 

akasema mathew 

“Mathew nilikueleza toka 

awali kwamba usimuamini sana 

yule mzee kwani ana matatizo 

katika kumbu kumbu zake.Kichwa 

chake hakiko sawa.Hakukuwa na 

watu zaidi ya wale walio 

orodheshwa.Kama kungekuwa na 

watu zaidi basi maiti zao 

zingepatikana lakini ukipiga 

hesabu inaonyesha wazi kwamba 

hakukuwa na watu wa ziada.Ndege 

iliondoka na watu kumi na nane na 

baada ya ajali kutokea zikapatikana mati kumi na saba 

,na baba pekee ndiye 

aliyesalimikana hivyo hesabu 

kuwa watu kumi nane.Usiumize 

kichwa kwa taarifa za yule 

mzee.Hao watu nane anaodai 

walikuwemo ndegeni wako wapi? 

Akauliza Theresa.Mathew akabaki 

kimya 

“Nimestuka sana na hadi 

mikono inanitetemeka kusikia 

kwamba maiti zilizo patikana ni 

kumi na saba.Mimi sikuwahi 

kuingizwa katika hesabu za watu 

waliokuwemo ndani ya ndege na 

wala sikuorodheshwa sehemu 

yoyote kwa hiyo baba ndiye pekee 

anayejulikana kuwa ndiye 

aliyenusurika .Watu nane wako wapi? Ni akina nani?Walitoka vipi 

ndani ya ndege? Ninavyokumbuka 

mimi na baba ndio tulikuwa wa 

kwanza kutoka ndegeni.Kuna 

wengine walifuata baada ya sisi? 

Akajiuliza Theresa 

“Theresa” akaita Mathew 

“Unasemaje Mathew? Akauliza 

Theresa 

“Kama unavyoona suala hili 

linavyozidi kupanuka ,kuna kitu 

kimejificha na lazima 

tukijue.Japokuwa mzee Zubery 

kumbu kumhu zake kuna wakati 

haziko sawa lakini hatuwezi 

kumpuuza.Kuna kitu kinanituma 

nimuamini.Hata hivyo kuna jambo 

lingine nataka unisaidie 

kulifahamu” “Sema Mathew unahitaji nini? 

“Nataka nipate majina ya watu 

waliofariki katika ndege 

hiyo.Unaweza kuyapata? 

“Ndiyo Mathew.Pale ikulu 

tuna kumbu kumbu zote” akasema 

Theresa na kuchukua simu 

akapiga na kuomba apatiwe 

majina ya watu wote waliofariki 

katika ajali ile ya ndege ya rais. 

Waliwasili nyumbani kwa 

Theresa ambako ndiko waliweka 

ofisi yao.Theresa akapigiwa simu 

akataarifiwa kwamba majina yote 

ya watu waliofariki katika ajali ya 

ndege ya rais yametumwa katika 

akaunti yake ya barua pepe.Mara 

moja akaifungua na kumpatia 

Mathew majina yale,akayapitia na kutoa kitambaa akafuta uso wake 

ulioonekana kuloa jasho. 

“Theresa mimi nakwenda 

kupumzisha kwanza kichwa 

nilitafakari hili suala kwa undani 

zaidi kwani ni suala gumu na 

linalohitaji utulivu mkubwa.Ni 

muda mrefu kidogo umepita 

sijakabiliana na suala gumu kama 

hili.Nitakujulisha endapo kuna 

chochote nitahitaji” akasema 

Mathew 

“Vipi kuhusu ile taarifa ya 

polisi ya maelezo ya baba?Si 

uliomba kuipata nayo? 

“Ndiyo ikipatikana utanitumia 

katika barua pepe yangu. Rais 

kama atakupigia akikuuliza 

tulikofikia usimueleze chochote kwani bado ni mapesa sana kumpa 

taarifa yoyote” akasema Mathew 

huku akiinuka ,Theresa 

akamsindikiza hadi katika gari 

lake akaondoka 

“Nashukuru sana Mathew 

ameanza kukata tamaa mapema 

kulifuatilia suala hili.Naomba 

kuendelee kuwa na mkwamo hivi 

hivi ili asifanikiwe kugundua 

chochote.Naamini watu wale bado 

hawajalala,wako macho hivyo 

muda wowote wakigundua 

kwamba wanachunguzwa basi 

wataibuka tena na maisha yetu 

yatakuwa mashakani.Nilinusurika 

kifo ndani ya ndege baba 

akaniokoa,nikanusurika tena kifo 

kwa mara ya pili na mama akaniokoa.Safari ya tatu sijui nani 

ataniokoa.Sitaki kabisa kuingia 

katika mikonona wale jamaa 

tena.Watu wale si watu wa 

kawaida.Ni makatili sana na nina 

aamini mtandao huu 

unawahusisha hata watu waliomo 

serikalini kwani baba aliuawa na 

watu waliovaa mavazi ya askari 

polisi na hata magari yao yalikuwa 

ya polisi .Na hata baada ya kuuawa 

nasikia wao polisi ndio walichukua 

miili na kuipeleka hospitali kwa 

madai kwamba wameuawa na 

watu wasiojulikana.Nina wasi wasi 

hawa jamaa bado wanaendelea 

kumchunguza dada kwa siri 

wakijaribu kufahamu kama kuna 

chochote anakifahamu kuhusu Football na amekuwa salama hadi 

sasa kwa kuwa hajui chochote na 

nitakapo thubutu kufumbua tu 

mdomo wangu kumueleza 

wanaweza wakamuua” akawaza 

Theresa baada ya Mathew 

kuondoka 

“Najiuliza bado,hii football ina 

siri gani hadi damu nyingi namna 

ile imwagike bila huruma? Halafu 

orodha inaonyesha kwamba wale 

waliokufa wote ni watanzania 

hakukuwa na mgeni hata 

mmoja.Hii inaonyesha kwamba 

wale jamaa waliojiita waandishi 

wa habari na baadae wakageuka 

magaidi na kuiteka ndege ya rais 

walipona na hakuna hata mmoja 

aliyepoteza maisha.Inaonekana wale jamaa walichokuwa 

wanakitafuta ni football pekee na 

ndiyo maana nahisi baada ya baba 

kuruka na kuondoka waliona 

hakuna umuhimu wa kuendelea 

kubaki ndegeni kwa kuwa 

walichokuwa wanakitafuta 

hakikuwepo kwa hiyo wakatoka 

ndegeni na kuiacha 

ikaanguka.Najiuliza je 

waliochukua kisanduku cheusi cha 

kuhifadhi kumbu kumbu za 

mwenendo wa ndege ni wale 

jamaa au ni akina nani?Dah ! 

mambo haya ni magumu sana na 

ndiyo maana sitaki 

yaamshwe.Kuna mambo mengi 

hapa yamejificha” akaendelea 

kuwaza Theresa Kwa upande wa Mathew bado 

kichwa chake kilikuwa na mawazo 

mengi sana baada ya kuondoka 

kwa Theresa 

“Mwanzo umeanza kwa 

mgumu na bado naona giza 

nene.Japokuwa bado nipo gizani 

lakini kuna hatua niliyopiga 

ambayo inanifanya niamini 

kwamba ajali ile ilikuwa na 

walakini.Haikuwa ajali ya 

kawaida.Naamini hivyo baada ya 

kutoweka kwa kisanduku cha 

kuhifadhi mwenendo wa ndege na 

waliofanya hivyo hawakutaka 

sababu ya ndege ile kuanguka 

kujulikana.They’re very smart.Huu 

lazima ni mtandao mrefu wa watu” 

akawaza mambo mengi hadi alipofika nyumbani kwake na 

kwenda moja kwa moja chumbani 

akaketi kitandani 

“Alhaj Zubery amemweleza 

Zaina kwamba kuna watu wanane 

waliomba lift katika ndege ya 

rais.Hizi ni taarifa za kweli? Hali ya 

mzee yule inatia shaka 

kumuamini.Halafu akasema 

kwamba kulikuwa pia na binti 

mdogo ndegeni.Mbona sikuona 

jina lake katika orodha ya watu 

waliokuwemo ndegeni? Orodha ile 

inaonyesha wafanyakazi wote 

waliokuwemo ndegeni ni wa ikulu 

pamoja na wahudumu wa ndege na 

hakukuwa na jina la binti 

mdogo.Naingiwa na wasi wasi 

kidogo kuhusiana na kumuamini yule mzee yawezekana hakuna 

ukweli wowote katika hizi taarifa” 

akawaza Mathew na kuwasha 

kompyuta yake 

“Lakini Zaina ndiye 

anayemfahamu baba yake vizuri 

na anamfahamu ni wakati upi 

kumbu kumbu zake huwa sawa na 

wakati gani zinapotea .Mpaka 

aamue kunipa taarifa hizi ina 

maana ana uhakika baba yake 

alikuwa sawa sawa.Niamini lipi? 

Akaendelea kuwaza Mathew 

“Itanilazimu kurejea tena kwa 

alhaj Zubery.Natakiwa 

kuthibitisha taarifa hizi.Japokuwa 

ana matatizo katika kumbu kumbu 

zake lakini kuna kitu kinaniambia 

kwamba yule mzee anaweza kuwa na msaada kwangu.Lazima nirejee 

tena kwake” akawaza na kuchukua 

simu akalitafuta jina la mama 

Anna na kumpigia 

“Hallow” ikasema sauti ya 

upande wa pili 

“Hallow mnaendeleaje? 

Anaendeleaje Anna? Mathew 

akauliza 

“Anna anaendelea vyema” 

“Umekwisha mchukulia 

zawadi niliyokuomba?akauliza 

Mathew 

“Nitamchukulia usij……………..” 

Ghafla katika spika za simu 

ikasikika sauti ya mwanaume 

akiongea kwa ukali akimuuliza 

Peniela 

“Unazungumza na ani? “Ni baba yake Anna Maria” 

akajibuPeniela 

“Nipe simu,nataka 

kuzungumza naye” akasema jamaa 

yule kwa ukali 

“Hapana achana naye hana 

tatizo anataka kujua maendeleo ya 

mwanae” akajibu Peniela na 

wakasikika wakinyang’anyana 

simu halafu sauti ya kume 

ikasikika 

“Hallow ndugu.Tafadhali 

nakuomba uwe na heshima.Huyu 

si mkeo tena .Umekwisha achana 

naye kwa hiyo jitahidi kuheshimu 

maisha yetu.Nakuomba usimpigie 

tena simu .Ukitaka kujua 

maendeleo ya mwanao mpigie 

mtumishi wa ndani anayemuangalia.Unaingilia 

faragha za watu mimi na mke 

wangu kwa sasa tunafanya 

mapenzi.Natumai utalizingatia 

hilo” akasema yule jamaa na 

kukata simu.Mathew hakutaka 

kukasirika kwa jambo lile 

akatabasamu na kutikisa kichwa 

akajilaza kitandani 

“Sitaki malumbano na huyu 

jamaa ambaye anaonekana 

hajiamini.Anasumbuka bure mimi 

na Peniela tumekwisha achana na 

hakuna mategemeo ya kurudiana 

tena.Kilichobaki kati yetu ni mtoto 

tuliyezaa pamoja.Siwezi 

kumlaumu sana kwani ni wivu 

mkali alionao kwa mke wake 

lakini hata ampe nini Peniela kwake nitabaki ni mwanaume wa 

pekee kabisa .Sitakiwi kuwaza 

sana hili jambo ngoja nielekeze 

akili yangu katika kazi ngumu 

iliyoko mbele yangu” Akawaza 

Mathew Imekwisha timu saa moja na 

nusu za jioni wakati rais wa 

jamhuri ya muungano wa 

Tanzania Dr Vivian Matope 

alipofahamishwa kwamba rais wa 

Korea kaskazini Kim Yun Hu 

alikuwa tayari katika laini ya simu 

kwa ajili ya mazungumzo. Rais 

akaelekea katika chumba cha mikutano ya moja kwa moja 

kilichokuwa na runinga tatu 

kubwa akabonyeza runinga namba 

moja na rais Kim Yun Hu 

akaonekana runingani. 

“Mheshimiwa rais Kim,habari 

yako? Akaanzisha mazungumzo Dr 

Vivian 

“Habari nzuri kabisa Dr 

Vivian.Ni heshima kubwa kwangu 

kuzungumza nawe mida hii 

kuhusiana na masuala kadhaa 

muhimu kwa mustakabali wa nchi 

zetu mbili.Kwanza kabla ya yote 

napenda kukushukuru sana kwa 

kumpokea mjumbe wangu 

niliyemtuma kwako na 

ukamsikiliza.Vile vile napenda 

nichukue nafasi hii kukupongeza sana kwa msimamo wako 

usioyumba na kwa maamuzi 

makubwa ya kutaka kuanzishwa 

kwa mashirikiano ya kibiashara 

baina ya nchi yako na Korea 

kaskazini.Nilifurahi sana 

niliposikia kwamba umeagiza 

kuanzishwa kwa mchakato wa 

kuanzishwa kwa mashirikiano 

baina ya nchi zetu.Hii ni hatua 

kubwa kwa Tanzania katika 

maendeleo yake ya 

kiuchumi.Nafahamu maamuzi haya 

uliyoyafanya yatailetea Tanzania 

matatizo makubwa na hadi hivi 

sasa kelele na vitisho vingi 

vimetolewa na vinaendelea 

kutolewa na mataifa 

makubwa.Silaha yako kubwa ni msimamo wako .Simama imara na 

usiyumbe.Watakutisha sana 

kuhusiana na vikwavo vya 

kiuchumi lakini nakuomba 

usiwasikilize wewe endelea 

mbele.Ukitaka nchi yako ipige 

hatua usigeuke nyuma angalia 

mbele.Nchi hizi tajiri hazipenzi 

nchi kama Tanzania ipige hatua 

kimaendeleo kwani kuna mambo 

mengi wanafaidika na hali ya hivi 

sasa ya Tanzania.Hivyo endelea na 

msimamo wako huo huo kwani 

mpaka hivi sasa wewe tayari ni 

mshindi.Umewatoa jasho na ndiyo 

maana toka ulipotoa hotuba yako 

kule New york wanashindwa hata 

kulala.Kingine cha muhimu 

unapaswa kuzidisha ulinzi mara dufu.Hawa jamaa wanaweza 

wakapanga mipango ya kukuua 

hata kwa kuwatumia watu wako 

wa karibu.Usimuamini mtu yeyote 

kuanzia sasa.Umeingia katika vita 

ya uchumi ambayo ni ngumu sana 

kwani unapigana na mataifa 

makubwa yenye nguvu kubwa 

kiuchumi na hata kijeshi.Binafsi 

ninakuahidi ulinzi dhidi ya taifa 

lolote lile litakalotishia amani ya 

Tanzania. 

Kama 

yatafanikiwa,mashirikiano yetu 

yatakuwa ni yenye faida kwa 

pande zote mbili.Kwa sasa Korea 

Kaskazini tuko katika mageuzi 

makubwa ya kiuchumi.Tunataka 

kuwa taifa kubwa lenye nguvu kijeshi na kiuchumi pia na 

mahasimu wetu hawapendezwi na 

hilo.Tunawekeza sana katika 

viwanda na uchumi wetu kwa sasa 

unakua kwa kasi kubwa na kuzidi 

kuwapa hofu mataifa mahasimu 

wetu na ndiyo maana vikwazo 

vinaongezeka kila wakati lakini 

sisi hatujali tunasonga 

mbele.Tumeimarisha sana 

biashara na nchi za bara la Asia na 

sasa tunataka kupanua wigo wa 

biashara na kuanza kushirikiana 

na nchi za Afrika.Tuna viwanda 

vingi na tunatengeneza nguvo,vifaa 

vya elektroniki,magari,ujenzi na 

vinginevyo.Tunahitaji masoko 

mapya ya bidhaa zetu na vile vile 

tukaribisha bidhaa nyingine toka kwa nchi washirika wetu wa 

kibiashara pia tunauhitaji wa 

malighafi kama vile pamba kwa 

ajili ya viwanda vyetu vya 

nguo,tunahitaji chuma na mafuta 

safi.Tunahitaji pia kwa kiasi 

kikubwa madini ya Urani kwa ajili 

ya kuboresha vinu vyetu vya 

nyuklia na kutengeneza umeme wa 

uhakika kwa viwanda vyetu.Kwa 

hiyo basi mashirikiano kati ya 

Tanzania na Korea Kaskazini 

yatakuwa na faida kubwa sana kwa 

nchi zote mbili.Wawekezaji wa 

kutoka Korea Kaskazini 

wanapenda kuja Tanzania 

kuwekeza katika viwanda vya 

nguo,kusindika mazao ya kilimo 

na kuongeza thamani ya mazao ya wakulima na hivyo kumpatia 

mkulima wa Tanzania tija katika 

kilimo chake na sekta ya kilimo 

kwa ujumla ambayo ndiyo 

inayoajiri watu wengi 

itapanuka.Tunataka kuwekeza vile 

vile katika viwanda vya 

kutengeneza vifaa vya 

kielektroniki kama vile simu 

n.k.Tunataka vile vile kuwekeza 

katika mafuta.Tunahitaji sana 

kupata mafuta safi na kama 

haitoshi tunataka kuwekeza katika 

sekta ya madini kwa kujenga 

kiwanda cha kukata na kuongeza 

thamani ya madini ya vito na hata 

kuchenjua mchanga wa madini 

hapo hapo nchini Tanzania kuliko 

uwekezaji unaofanywa sasa hivi na makampuni ya kimarekani na 

ulaya ambayo huchota madini na 

kuyapeleka kwao kuyaongeza 

thamani na kupata faida kubwa na 

kuzidi kuiacha Tanzania kuwa 

masikini.Mwisho tunataka kujenga 

mgodi mkubwa wa madini ya 

Urani ambayo tutayanunua kwa 

bei nzuri na kuifaidisha sana 

Tanzania.Madini haya 

hatutayatumia kwa ajili ya ajili ya 

kutengeneza silaha za nyuklia 

kama mataifa makubwa 

wanavyodai bali tunayatumia kwa 

ajili ya kuzalisha nishati ya 

umeme. 

Mheshimiwa rais,mpaka hapo 

unaweza kuona kwamba 

uwekezaji toka Korea kaskazini utakuwa na faida kubwa kwa 

Tanzania kwani sisi lengo letu ni 

kusaidia uchumi wa Tanzania ukue 

tofauti na mataifa mengine 

yanayowekeza na kuchuma mali za 

watanzania na kwenda 

kuyafaidisha mataifa 

yao.Makampuni makubwa ya 

Marekani na Ulaya wanachimba 

madini,mnafaidikaje?Hamjui hata 

kiwango cha madini 

kinachochimbwa na hampati pato 

stahili.Sisi watanzania ni kama 

ndugu zetu kwani wamesimama 

pamoja nasi hata baada ya kupewa 

vitisho vya kuwekewa vikwazo 

hivyo tunahitajika kufaya 

uwekezaji wenye faida kubwa na 

kuipaisha Tanzania kiuchumi.Tunataka kubadili aina 

ya uwekezaji na tupate faida wote 

sawa sawa na ikiwezekana 

Tanzania ipate faida.Uwekezaji 

wetu utaongeza na kukuza pato la 

mwananchi mmoja mmoja 

,utaongeza mapato ya serikali na 

hivyo uchumi utakua.Kama hiyo 

haitoshi tutashiriki pia katika 

miradi mingi ya maendeleo kama 

kujenga 

mabarabara,mashule,mahospitali 

n.k. Kwa kuwa tutakuwa na 

uwekezaji mkubwa nchini kwako 

tuhakikisha kuna kuwa na 

mashirikiano makubwa ya 

kijeshi.Tutaipatia Tanzania 

msaada wa silaha za kisasa kwa 

ajili ya kujilinda na maadui,tutatoa mafunzo kwa jeshi la Tanzania na 

litakuwa jeshi la kuogopwa Afrika 

kutokana na uwezo na zana kali za 

kisasa.Tutajenga pia kiwanda cha 

silaha na Tanzania itajitosheleza 

kwa silaha za kila aina.Yeyote 

atakayeigusa Tanzania atakuwa 

ameigusa pia Korea Kaskazni na 

hatabaki salama kwani 

tutamuadhibu vikali” akasema rais 

Kim.Dr Vivian aliyekuwa kimya 

akisikiliza akasema 

“Ahsante kwa maelezo yako 

marefu.Nimevutiwa sana na 

mkakati huo wa nchi yako kwa 

Tanzania. Sisi kama nchi bado ni 

masikini na tunajitahidi sana 

tuweze kujiondoa katika umasikini 

na kufika nchi ya kipato cha kati.Tunazo rasilimali nyingi sana 

hapa nchini tuna madini ya kila 

aina,vivutio vya kitalii,ardhi 

nzuri,bahari,maziwa na mito lakini 

pamoja na kuwa na rasimali hizo 

zote bado hatujafaidika na uchumi 

wetu bado uko 

chini.Tumekaribisha wawekezaji 

lakini bado hatufaidiki na mali 

zetu kwani kinachofanyika ni wizi 

mtupu.Wanachota rasilimali zetu 

na kutuachia mashimo.Tumeamua 

kubadilika na kubadili sera zetu za 

uwekezaji.Tunataka rasilimali zetu 

zianze kutunufaisha na kila 

mtanzania aone faida ya rasilimali 

hizi kuwepo nchini kwao.Msimamo 

wangu kuhusiana na rasilimali 

zetu hautabadilika kwani wakubwa hawa wametunyonya 

vya kutosha na sasa 

imetosha.Tunataka wawekezaji 

watakaotunufaisha na nina imani 

Korea Kaskazini watatufaa 

sana.Nitawaelekeza wasaidizi 

wangu ili mambo haya yaanze 

kufanyiwa kazi haraka hakuna 

muda wa kupoteza.Nakuhakikishia 

mheshimiwa rais kwamba 

uwekezaji wa kutoka Korea 

Kaskazini unakaribishwa sana na 

hakuna kizingiti chochote.Hata 

hivyo kuna jambo nataka 

kukuomba” 

“Omba mheshimiwa rais” 

“Pamoja na mambo yote 

mazuri ambayo umeyaongea 

mazuri yatakayofanywa na Korea Kaskazini,Tanzania pia tunayo 

sera ya viwanda na muitikio ni 

mzuri kwani tumepata wawezekaji 

wengi wa ndani na nje ya 

nchi.Tatizo letu mpaka sasa bado 

hatuna umeme wa uhakika sana 

kuendesha viwanda vingi na hivyo 

kuwafanya wawekezaji wengine 

wasite kuja kuwekeza.Kwa kuwa 

tunayo madini ya Urani hapa 

nchini kwetu tunaomba tusaidiwe 

kujenga kinu cha nyuklia hapa 

nchini kwa ajili ya kuzalisha 

umeme wa uhakika na hivyo 

kuchochea uchumi” 

“Dr Vivian suala hili 

linawezekana kabisa na ni jambo 

la msingi mno umeliongea.Mkiwa 

na kinu cha nyuklia mtakuwa na uhakika wa umeme wa 

kutosha.Naomba nilichukue jambo 

hili na nilipeleke kwa wenzangu 

tukalijadili na naomba nikuahidi 

kwamba tutajenga kinu cha 

nyuklia hapo Tanzania japokuwa 

jambo hili litazidisha msuguano na 

mataifa makubwa kwani ni jambo 

ambalo hawalipendi” 

“Nalifahamu hilo Kim na niko 

tayari kusimama nao.Ili 

kufanikiwa dhidi ya mataifa haya 

makubwa lazima ujifunze kuwa 

kiburi” 

“Uko sahihi Dr Vivian.Na mimi 

kuna jambo nataka 

nikuombe”akasema Kim 




Nalifahamu hilo Kim na niko 

tayari kusimama nao.Ili 

kufanikiwa dhidi ya mataifa haya 

makubwa lazima ujifunze kuwa 

kiburi” 

“Uko sahihi Dr Vivian.Na mimi 

kuna jambo nataka 

nikuombe”akasema Kim 

“Karibu” “Kuna makampuni mengi ya 

kimarekani yamewekeza Tanzania 

.Kama ujuavyo sisi na Marekani ni 

mahasimu hivyo hatutaweza 

kufanya kazi 

pamoja.Ninachokuomba 

tukishakubaliana kuhusiana na 

biashara na uwekezaji,sitisha 

shughuli zote zinazofanywa na 

makampuni ya kimarekani na 

washirika wake kama 

Ufaransa,Ujerumani na uingereza 

.Nataka uvunje nayo mikataba na 

uyafurushe nchini mwako.Sisi 

tutalipa malipo yote ya fidia kama 

yatakuwepo kwani naamini lazima 

watakwenda kuwashitaki katika 

mahakama zao za kimataifa kwa 

kuvunja nao mikataba.Usiwe na hofu Dr Vivian hii ni vita ya 

kiuchumi kwa hiyo misuko suko 

lazima iwepo lakini kamwe 

usigeuke nyuma.Sisi tuko nyuma 

yako na tutakulinda” akasema rais 

Kim 

Mazungumzo kati ya Dr Vivian 

na Kim yalichukua takribani saa 

mbili.Walizungumza mambo 

mengi kuhusiana na mipango yao 

ya mashirikiano kisha wakaagana 

.Rais Kim aliahidi kutuma ujumbe 

wa watu nane wakiongozwa na 

mawaziri watatu kuja Tanzania ili 

kuanza mazungumzo na serikali ya 

Tanzania haraka iwezekanavyo 

Hii ilikuwa ni jioni ya faraja 

sana kwa Dr Vivian.Mazungumzo 

kati yake na rais Kim yalifanya uso wake upambwe na tabasamu 

kubwa. 

“Hii vita itakuwa kubwa sana 

.Nitapata misukosuko toka mataifa 

makubwa na tajiri ambayo 

yamekuwa yakiendeleza unyonyaji 

wa rasilimali zetu lakini sintorudi 

nyuma.Nimekwisha amua kuingiza 

nchi vitani lazima tupambane na 

lazima tushinde.Mali ni zetu na 

haiwezekani tuwe ombaomba” 

akawaza Dr Vivian 

***************** 

Saa mbili kasoro dakika kumi 

na nne za usiku,Mathew alibisha 

hodi nyumbani kwa Alhaj 

Zubery.Alikaribishwa na mtumishi wa ndani na sebuleni 

akamkuta Zaina akiwa 

amejipumzisha akitazama runinga 

“Mathew karibu tena.Mbona 

usiku huu? Zaina akauliza 

“Samahani kwa kuwavamieni 

usiku huu bila taarifa” akasema 

Mathew. 

“Usihofu karibu sana 

unakaribishwa muda wowote” 

Akasema Zaina 

“Nashukuru 

Zaina.Nimelazimika kurejea tena 

kufuatia ile taarifa uliyonipa 

mchana.Kuna mambo ambayo 

nataka kuyafahamu zaidi toka kwa 

mzee kama atakuwa katika hali 

nzuri” akasema Mathew “Mathew sijui kama 

nitakukwaza lakini ningependa 

kufahamu zaidi ni kitu gani hasa 

mnachokihitaji toka kwa mzee ili 

nione namna ya kusaidia hata 

kumuuliza?Nieleze ukweli usihofu” 

akasema Zaina 

“Kikubwa tunachokichunguza 

hapa ni chanzo cha ajali ya ndege 

ya rais Anorld.Mpaka leo hakuna 

taarifa yoyote iliyopatikana 

kuhusina na chanzo cha ajali ile 

hivyo tumeanza tena 

uchunguzi.Kuna taarifa 

zinakanganya.Ndege ilipoondoka 

hapa Dar es salaam ilikuwa na 

watu kumi na nane na taarifa 

uliyonipa mchana toka kwa mze 

Zubery inasema kwamba wakati wa kurudi Tanzania kuna 

waandishi nane wa habari 

waliongezeka wakielekea Dar es 

salaam hivyo jumla yao ikawa 

watu ishirini na sita.Ilipoanguka 

watu wote walikufa isipokuwa mtu 

mmoja tu kwa hiyo maiti zilipaswa 

kuwa ishirini na tano lakini taarifa 

inaonyesha kwamba kulikuwa na 

maiti kumi na saba pekee.Maiti 

nane hazionekani.Majina ya watu 

waliofariki yanaonyesha kwamba 

wote ni watanzania na hakuna 

mgeni hata mmoja.Taarifa hizi 

mbili zinakinzana na ndiyo maana 

nimekuja tena kutaka kuonana na 

mzee ili kupata uhakika kwamba 

taarifa zile alizokupa ni sahihi” 

akasema Mathew “Mathew ninamfahamu baba 

yangu vizuri .Nafahamu muda gani 

yuko vizuri na na muda gani 

hayuko sawa.Taarifa ile niliyokupa 

alinipa wakati kumbukumbu zake 

ziko sawa sawa na nisingeweza 

kukupa kitu ambacho najua 

hakiko sahihi.Hata hivyo itabidi 

kumuhoji tena pengine anaweza 

akakumbuka kitu chochote.Ngoja 

nikamlete” akasema Zaina na 

kuinuka akaelekea chumbani kwa 

mzee Zubery baada ya dakika tatu 

akarejea akiwa amemshika mkono 

baba yake na kumketisha sofani 

“Kijana umerudi tena” 

akasema mzee Zubery 

“Nimerudi tena mzee.Habari 

za usiku huu? “Nzuri.Karibu sana.Zaina 

amesema kuna mambo bado 

unahitaji kuyafahamu toka 

kwangu” akasema mzee Zubery 

“Ndiyo mzee.Nimelazimika 

kuja tena kuomba msaada 

wako.Ulisema kwamba kulikuwa 

na waandishi nane wa habari 

waliomba lifti katika ndege ya rais 

wakati anarejea Dar es 

salaam.Taarifa zinaonyesha 

ilipoondoka Dar es salaam ndege 

ilikuwa na watu kumi na nane na 

wakati wa kurudi ukijumlisha na 

watu hao nane waliomba lifti jumla 

kukawa na watu ishirini na sita 

ndegeni.Ni mtu mmoja tu aliyetoka 

salama ndani ya ndege hiyo 

ambaye ni kanali Sebastian matope kwa hiyo ndani ya ndege 

kulipaswa kuwa na watu ishirini 

na tano.Kinachoshangaza ni 

kwamba maiti zilizokutwa ndani 

ya ndege ni maiti kumi na saba 

pekee na zote ni za watanzania 

,hakuna maiti hata moja ya 

mgeni.Hili jambo limenichanganya 

na ndiyo maana nimeona nije tena 

kwako kupata ufafanuzi zaidi 

kuhusiana na hao watu nane 

uliodai waliongezeka wakati wa 

kurejea Dar es salaam ” akasema 

Mathew 

“Kwanza kabisa naomba 

nikusahihishe kwamba wakati rais 

Anorld anakuja Misri alikuwa na 

watu kumi na tisa ndani ya ndege 

kwani mimi ndiye niliyewapokea kule Cairo na si watu kumi na nane 

kama unavyosema.Wakati wa 

kuondoka waliongezeka watu nane 

ambao ni waandishi wa habari na 

waliletwa kwangu na mtu mmoja 

anaitwa Fakrim Alnasor.Huyu 

alikuwa anafanya kazi katika 

uwanja wa ndege na nilifahamiana 

naye wiki moja tu kabla ya rais 

hajafika Misri.Aliniomba 

niwaombee lifti watu hao katika 

ndege ya rais na nikaongea na rais 

akakubali na wakaondoka na 

ndege ya rais.Inawezekanaje 

kama watu wote walikufa maiti 

zao zisionekane?Mzee Zubery naye 

akashangaa.Usiku huu alikuwa 

anazugumza kana kwamba hana matatizo yoyote ya kupoteza 

kumbukumbu 

“Huyu Fakrim Alnasor 

alikuwa nani? 

“Alikuwa anafanya kazi katika 

shirika moja la ndege” 

“unaweza kuwakumbuka hao 

waandishi wa habari walitoka nchi 

gani?Mathew akauliza 

“Walitoka Marekani na hata 

lafudhi yao ilionyesha ni 

wamarekani” 

“Ulisema kwamba kulikuwa 

na binti moja mdogo lakini mbona 

jina lake halikuorodheshwa 

miongoni mwa watu 

waliokuwemo ndani ya ndege? 

“Sifahamu kwa nini 

hakuorodheshwa ila ninachokumbuka ni kwamba huyo 

binti alikabidhiwa kwa mama 

mmoja wa pale ubalozini ambaye 

nilimpa kazi ya kumtembeza huyo 

binti katika sehemu mbali mbali za 

Cairo.Mama Swai ambaye hivi sasa 

ni marehemu nilimpa hiyo 

kazi.Alimtembeza kuanzia Iraq 

akaja mpaka maeneo Syria kule ..” 

Zaina akamkonyeza Mathew 

ishara kwamba tayari 

kumbukumbu zimepotea 

“Mzee nakushukuru sana 

.Nitakuja kukutembelea tena siku 

nyingine” akasema Mathew huku 

akiinuka na kumpa mkono mzee 

Zubery halafu Zaina akamsindikiza 

“Zaina ahsante sana kwa 

kunisaidia .Naomba usinichoke kila pale nitakapohitaji msaada wa 

mzee” akasema Mathew 

“Usijali Mathew 

unakaribishwa sana muda wowote 

ukiwa na jambo lolote.Naamini 

sasa umepata uhakiki wa kile 

ulichokuwa unakitafuta” 

“Ndiyo sasa nimepata 

nilichokuwa nakitafuta” akasema 

Mathew na kuagana na Zaina 

akaondoka 

“Nilifanya vyema kurudi tena 

kuonana na mzee Zubery sasa 

nimeamini kile 

alichokisema.Amesisitiza kwamba 

kulikuwa na waandishi nane wa 

habari raia wa Marekani ambao 

walikuwemo ndani ya ndege 

yarais.Swali linaibuka wako wapi? Mbona maiti zao hazikuonekana ? 

Walitoka salama ndani ya ndege ? 

akajiuliza Mathew 

“Hapa kuna jambo limejificha 

na ili kufahamu natakiwa kwanza 

kuwafahamu hawa waandishi wa 

habari ni akina nani?Mzee Zubery 

amemtaja mtu mmoja anaitwa 

Fakrim Alnasor kwamba ndiye 

aliyewapeleka kwake wale 

waandishi ili awaombee nafasi 

katika ndege ya rais” akawaza 

“Laiti kumbu kumbu za mzee 

Zubery zingekuwa sawa muda 

wote angekuwa ni msaada 

mkubwa kweli hata hivyo kwa 

haya machache aliyoyakumbuka ni 

msaada mkubwa kangu.Ngoja 

niyafanyie kazi nione matokeo yake lakini naamini kabisa kuna 

jambo nitalipata.Halafu 

amesisitiza kwamba kulikuwa na 

binti mdogo aliyekwenda kufanya 

utalii Misri na kufanya jumla ya 

watu waliokuwemi ndegeni kuwa 

kumi na tisa badala ya kumi na 

nane waliorodheshwa.Najiuliza 

huyu binti kama ni kweli 

alikuwemo aliingiaje ndegeni bila 

kuwepo kwa taarifa zake? Ni binti 

wa nani ? Na baada ya ajali mwili 

wake haukuwahi kupatikana je 

alitoka salama ? Na kama alitoka 

salama yuko wapi? Akajiuliza 

maswali yaliyoendelea 

kumchanganya . 

“Hili kweli ni fumbo na ndiyo 

maana limewashinda waliojaribu kulichunguza.Lakini lazima 

niutafune huu mfupa na lazima hili 

fumbo nilifumbue” 

Mathew alielekea nyumbani 

kwa Theresa na kabla hajafika 

akachukua simu na kumjulisha 

kwamba anakwenda kwake 

“Unakuja kwangu? Mbona 

umekwisha kuwa usiku?Theresa 

akashangaa 

“Mimi hufanya kazi usiku na 

mchana kwa hiyo kama ulipewa 

jukumu la kuwa msaidizi 

wangu,inakubidi na wewe ufanye 

kazi kama mimi.Amka tafadhali 

nimekaribia kufika kwako” 

akasema Mathew na kukata 

simu.Alifika getini kwa Theresa na 

mlinzi tayari alikwisha pewa taarifa akamfungulia geti akaingia 

ndani akapokewa na Theresa 

“Karibu ndani” Theresa 

akamkaribisha Mathew ndani 

“Ahsante Theresa.Tayari 

ulikuwa umelala? 

“Ndiyo nilikwisha lala.Huwa 

nalala mapema sana” 

“Basi kuanzia sasa ratiba yako 

ya kulala itabadilika.Itakulazimu 

ujifunze kukesha.Habari za toka 

tulipoachana? 

“Hakuna habari yoyote zaidi 

ya dada kupiga simu na kuuliza 

maendeleo yetu na siumueleza 

chochote kama ulivyosema” 

“Good.” Akasema Mathew 

wakati wakiingia katika ofisi ya 

Theresa “Kuna habari gani usiku huu? 

Theresa akauliza 

“Nimetoka tena kuonana na 

yule mzee” 

“Kweli wewe king’ang’anizi. 

Mathew usipoteze muda na yule 

mzee hana msaada wowote 

kwetu.Hakuna chochote 

anachokumbuka zaidi ya 

kutuyumbisha kwa kumbu kumbu 

zake ” 

“Mzee yule yuko sahihi.Ni 

kweli ana tatizo la kupoteza 

kumbu kumbu lakini kuna wakati 

kumbu kumbu zake huwa zinarudi 

na anakuwa mzima kabisa kama 

alivyosema mwanae Zaina.Usiku 

huu nimezungumza naye na kwa 

bahati nzuri nimemkuta ametulia na ameendelea kusisitiza kwamba 

kulikuwa na waandishi nane wa 

habari ndani ya ndege ya rais 

wakati anarejea Dar es 

salaam.Anasema kwamba yeye 

ndiye aliyewaombea nafasi 

waandishi hao kwa rais na 

wakakubaliwa.Hata yeye 

mwenyewe anashangaa kusikia eti 

waandishi wale hawakuwemo 

katika orodha ya maiti 

zilizopatikana baada ya ajali 

kutokea.Swali la kujiuliza je wako 

wapi? Walikuwemo ndegeni 

wakati ajali inatokea au walishuka 

njiani? Maswali haya yangeweza 

kupata majibu yake katika kile 

kisanduku cha kuhifadhia kumbu 

kumbu za mwenendo wandege.Ninaamini kisanduku hicho 

kiliondolewa makusudi kabisa 

kuficha taarifa za ndege hiyo 

zisijulikane.Vile vile kuna huyu 

binti ambaye Zubery amesisitiza 

kwamba alikwemo ndegeni ni 

nani na yuko wapi? Je kama 

alifariki maiti yake iko wapi? 

Halafu kwa nini hakuwahi 

kuorodheshwa katika orodha ya 

watu waliokuwemo ndegeni? 

Akauliza Mathew 

“Mathew hapo ndipo huwa 

simuamini yule mzee.Kama watu 

hao anaosisitiza, walikuwemo 

ndegeni wako wapi? Maiti zao ziko 

wapi?Huyo binti anayemsema 

yuko wapi? Akauliza Theresa “That’s what we need to find 

out” akasema Mathew 

“Kwanza nataka kumfahamu 

huyu Fakrim Alnasor ni nani? 

Tukimfahamu huyu anaweza 

akatusaidia kufahamu mambo 

mengine kuhusiana na hao 

waandishi wa habari.Washa 

kompyuta yako tumtafute huyu 

mtu” akasema Mathew.Theresa 

akawasha kompyuta yake na 

kuanza kubofya .Baada ya dakika 

kama tano hivi akamuonyesha 

Mathew 

“Kuna Fakrim Alnasor zaidiya 

kumi lakini kuna huyu mmoja 

ambaye taarifa inaonyesha 

kwamba ni raia wa marekani 

.Anafanya kazi katika ofisi za shirika la ndege la American 

airways na anaishi jijini New York 

Marekani” 

“Nadhani anaweza kuwa 

mwenyewe kwani mzee Zubery 

alisema kwamba Fakrim alikuwa 

anafanya kazi katika shirika la 

ndege .Kuna umuhimu wa 

kumchimba zaidi huyu Fakrim 

.Kuna kitu tunaweza kukipata toka 

kwake”akasema Mathew 

“Kama ni mfanyakazi wa 

shirika la ndege la American 

airways basi sioni shaka yoyote 

kwake.Yawezekana kama 

mfanyakazi wa shirika la ndege 

alilazimika kuwatafutia usafiri 

hao waandishi wa habari.Huyu hatakuwa na msaada wowote 

kwetu” akasema Theresa 

“Kama aliwasaidia 

kuwatafutia usafiri hao waandishi 

wa habari wako wapi? Walitoka 

vyombo gani vya habari? Lazima 

tufahamu mambo hayo ili tuwe na 

uhakika kama waandishi wale 

walikufa na bado wako hai.Kama 

walikufa maiti zao ziko wapi?Kama 

walipona wako wapi?” akasema 

Mathew na kumuaga Theresa 

“Mimi ngoja niende tutaonana 

kesho ila muda wowote hata usiku 

wa manane nikihitaji jambo lolote 

nitakupigia simu” 

“Usihofu Mathew” 

akajibuTheresa na Mathew 

akaondoka “Yawezekana labda Fakrim 

hana mahusiano yoyote na ajali ile 

kwani yeye anafanya kazi katika 

shirika la ndege na inawezekana 

akawa aliwasaidia tu hao 

waandishi kupata usafiri lakini 

hata hivyo lazima uchunguzi 

ufanyike.Ninachotaka ni kufahamu 

hao waandishi walitoka katika 

vyombo gani vya habari? Je wako 

hai bado au walikufa? Akawaza 

Mathew baada ya kuondoka 

nyumbani kwa Theresa 

Ilipata saa tano za usiku na 

hakwenda nyumbani kwake moja 

kwa moja bali akaelekea nyumbani 

kwa Meshack Jumbo “Karibu sana 

Mathew”akasema mzee Jumbo 

akimkaribisha Mathew 

“Ahsante mzee.Samahani kwa 

kuja bila taarifa” 

“C’mon Mathew.Hapa ni 

nyumbani na unaweza kuja muda 

wowote karibu sana.Mimi bado 

nilikuwa najisomea vitabu mbali 

mbali.Unajua mambo 

yamebadilika sana zama hizi 

tofauti na wakati wetu hivyo ili 

niweze kuimudu vyema nafasi 

niliyopewa na rais lazima nijifunze 

mbinu mbali mbali za kisasa.Haya 

niambie ujio huu wa usiku si kwa 

ajili ya kunisabahi” akasema mzee 

Meshack “Ni kweli huu si muda wa 

salamu .Kuna jambo limenileta 

hapa kwako mzee na ninahitaji 

msaada”akasema Mathew na 

baada ya muda akasema 

“Nimeanza rasmi leo ile kazi 

ya rais” 

‘That’s good” akajibu Meshack 

“Kama alivyosema rais 

kwamba hili jambo ni fumbo zito 

ila kwa siku ya leo walau kuna 

mwanga mdogo sana nimeanza 

kuuona kwa mbali” akameza mate 

kulainisha koo na kusema 

“Uchunguzi wangu umeanzia 

katika ajali ya ndege ya rais 

Anorld.Niliomba nipatiwe taarifa 

za chanzo cha ajali ile lakini jibu 

nililolipata toka kwa rais ni kwamba hakuna ripoti yoyote ya 

uchunguzi kwa kuwa kisanduku 

cha kurekodi taarifa za mwenendo 

wa ndege maarufu kama 

kisanduku cheusi hakikuwahi 

kuonekana eneo la ajali kwa hiyo 

kilichosababisha ajali ile 

hakijulikani” 

“Kweli? Meshack Jumbo 

akashangaa 

“Kweli kabisa mzee.Hata Hiyo 

ndiyo taarifa aliyopewa rais baada 

ya kutaka apewe ripoti ya 

uchunguzi wa ile ajali” 

“Haya ni 

maajabu.Inawezekanaje 

kisanduku hicho kipotee?Halafu 

mbona jambo hili limefanywa siri? 

Haijawahi kutangazwa kwamba kisanduku hicho kimepotea” 

akasema Meshack 

“Hata mimi nimejiuliza 

nimekosa jibu lakini hii ni picha ya 

wazi kwamba kuna kitu kilifanyika 

hapa .Baada ya kulifahamu hili 

sikuishia hapo nilimtafuta 

aliyewahi kuwa balozi wa 

Tanzania nchini Misri wakati 

ilipotokea ajali ile anaitwa Alhaj 

Zubery Msokwa.Huyu ni mtu 

mzima sana kwa sasa na ana 

matatizo ya kiafya na wakati 

mwingine anapoteza kumbu 

kumbu japo kuna nyakati 

kumbukumbu hurejea na 

anakumbuka vitu mbali mbali 

vilivyopita.Hata hivyo kuna 

mambo amenieleza ambayo yamenifanya nije kwako usiku 

huu.Mzee Zubery amenieleza 

kwamba baada ya rais Anorld na 

rais wa Misri kumaliza kikao chao 

alielekea uwanja wa ndege kwa 

ajili ya kurejea Tanzania lakini 

kulijitokeza kundi la waandishi 

nane wa habari waliokuwa 

wanaelekea Tanzania lakini kwa 

bahati mbaya walichelewa ndege 

yao hivyo kuwalazimu kuomba lifti 

katika ndege ya rais.Jumla ya watu 

waliokuwemo ndegeni wakati 

ndege ya rais inaondoka Cairo 

walikuwa watu ishirini na saba 

.Baada ya ajali aliyetoka salama ni 

kanali Sebastian pekee kwa hiyo 

basi kulitakiwa kuwe na maiti 

ishirini na tano ndani ya ndege lakini cha kushangaza maiti 

zilizopatikana ni kumi na saba 

tu.Maiti nane hazipo na miongoni 

mwa maiti zilizopatikana hakuna 

hata maiti moja ambayo ni ya raia 

wa kigeni.Najiuliza hao watu nane 

wako wapi?Hao waandishi wa 

habari wako wapi?Hakuna 

anayeweza kutupa majibu haya 

hivyo yatupasa kutafuta majibu 

sisi wenyewe.” 

Akanyamaza.Meshack 

Jumboakatafakari kidogo na 

kuuliza 

“Umesema huyo mzee 

aliyewahi kuwa balozi ana tatizo la 

kumbu kumbu? 

“Ndiyo” “Unawezaje kumuamini mtu 

ambaye kumbu kumbu zake 

haziko sawa? Kama kweli 

kuliongezeka watu nane wako 

wapi? Mbona katika orodha ya 

maiti hawapo? Nina wasi wasi na 

taarifa yake kama ina ukweli 

wowote.Kwenye mambo mazito 

kama haya hatupaswi kuamini 

taarifa nyepesi kama hizo.Nadhani 

kitu cha maana hapo ni kufahamu 

kilipo kisanduku cheusi.Nani 

kakichukua na kwa nini?Hainiingii 

akilini eti kilipotea” akasema 

Meshack Jumbo 

“Mwanzoni hata mimi 

nilikuwa na mashaka sana 

kuhusiana na taarifa hii ya balozi 

Zubery na imenilazimu kurejea tena kwake usiku huu ili 

kujiridhisha na taarifa hii na kwa 

bahati nzuri nimemkuta akiwa 

mzima na kumbu kumbu zake ziko 

sawa na akanihakikishia kwamba 

alichokisema ni kitu cha kweli 

kabisa.Amemtaja pia mtu mmoja 

anaitwa Fakrim Alnasor kwamba 

ndiye aliyemfuata na kumtaka 

awaombee lifti waandishi wa 

habari katika ndege ya 

rais.Nimejaribu kutafuta taarifa za 

huyo Fakrim na zinaonyesha 

kwamba ni mfanyakazi wa shirika 

la ndege la American airways 

anaishi jijini New York.Ni raia wa 

marekani lakini amezaliwa 

Misri.Hii inanifanya nimuamini 

mzee Zubery kwamba anasema kitu anacho kifahamu.Nimekuja 

hapa kwako nataka unisaidie 

kumfahamu huyu Fakrim ni nani 

na kama amewahi kufanya kazi 

nchini Misri ili niwe na uhakika 

zaidi kama ndiye aliyetajwa na 

Alhaj Zubery.Kama ndiye basi 

atatusaidia kuwafahamu wale 

waandishi wa habari waliopata lift 

katika ndege ya rais ni akina nani 

na wako wapi.Tukifanikiwa 

kumpata huyu nina hakika 

atatusaidia sana” akasema Mathew 



Lakini Mathew kwa nini 

uingie katika kuchunguza chanzo 

cha kuanguka kwa ndege ya rais 

badala ya kuchunguza nani 

walimuua kanali Sebastian 

ambayo ndiyo kazi uliyopewa na rais? Mimi naona uachane na hilo 

suala la ndege ya rais kwani 

linaonekana kuwa na mzunguko 

mrefu sana na ujikite katika 

mauaji ya Sebastian” akasema 

Meshack Jumbo 

“Mzee Jumbo mauaji ya 

Sebastian hayakuibuka tu yana 

chanzo chake na waliomuua wana 

sababu zao hivyo nataka nifahamu 

nini kilitokea katika ndege ya rais? 

Kilichonifanya nitake kuanzia 

uchunguzi wangu katika ajali ya 

ndege ya rais ni namna kanali 

Sebastian alivyotoka salama katika 

ndege hiyo.Ninavyofahamu endapo 

kunakuwa na kitisho chochote 

katika ndege ya rais basi raisi 

huwa anakuwa wa kwanza kuondolewa ndegeni lakini hapa 

ilikuwa tofauti.Kanali Sebastian 

alikuwa wa kwanza kutoka 

ndegeni na rais akafika 

ndegeni.Huoni hiki ni kitu cha 

ajabu mzee? Jambo lingine Kanali 

Sebastian alikuwa mbebaji mkuu 

wa Football.Mtu anayebeba begi 

hili hula kiapo hata kama 

kutatokea jambo gani atahakikisha 

anailinda Fooftball ambamo ndani 

yake huwa kuna siri za nchi.Je 

kanali Sebastian alifanikiwa 

kutoka salama na football?Kama 

alitoka nayo iko wapi?Maswali 

haya yamenifanya nianzie 

uchunguzi wangu katika ajali ya 

ndege ya rais” akasema Mathew Mzee Meshack Jumbo akafikiri 

kwa muda kidogo na kusema 

“Kuna kitu hata mimi 

ninakiona hapo.Kweli kuna 

umuhimu wa kutafuta chanzo cha 

kuanguka kwa ndege ya rais lakini 

nakuhakikishia Mathew hili 

halitakuwa jambo jepesi.Huku 

tunakoenda tutafukunyua mambo 

na mengine ni hatari kubwa 

sana.Maelezo uliyonipa 

yanaonyesha kuna jambo si la 

kawaida katika suala hili.Ninaanza 

kuwa na hisia yawezekana hata ile 

ajali ya ndege ya rais ikawa ni ya 

kupangwa lakini lazima uchunguzi 

ufanyike ili kuupata ukweli” 

“Ndiyo maana nimekuja 

kwako mzee unisaidie.Nafahamu una ukaribu na mawasiliano na 

watu kadhaa wa Marekani ambao 

wanaweza wakatusaidia kupata 

taarifa za Fakrim” akasema 

Mathew.Mzee Jumbo akafikiri 

kidogo na kusema 

“Kuna rafiki yangu mmoja 

anaitwa Jimmy Snow.Huyu aliwahi 

kuwa afisa wa juu wa FBI lakini 

baadae alikimbilia urusi anakoishi 

hadi leo baada ya kugundua 

mpango wa siri wa kumuua 

uliopangwa na CIA baada ya 

kumsaidia jasusi mmoja wa Urusi 

kupaa taarifa nyeti za sri za 

Marekani.Jimmy anaweza 

akanisaidia kupata taarifa za huyo 

Fakrim.Aliwahi kunipa namba 

yake ya simu anayotumia kwa sasa nchini Urusi ngoja niwasiliane 

naye kama anaweza kunisaidia” 

akasema mzee Meshack na 

kufungua kitabu chake 

alimoandika namba nyingi za simu 

na kutafuta namba ya Jimmy Snow 

akaipata akaiandika katika simu 

yake na kupiga.Baada yamuda 

simu ikapokewa 

“Hallow Jimmy” akasema 

Meshack baada ya simu 

kupokelewa 

“Meshack Jumbo habari za 

siku? 

“Nzuri kabisa Jimmy habari 

yako? Unaendeleaje? 

“Ninaendelea vyema 

.Umekuwa kimya sana” ‘Ni kweli Jimmy nimekuwa 

kimya.Kama unavyojua maisha ya 

kustaafu” 

“Pamoja na kustaafu Meshack, 

lakini usitusahau sisi marafiki 

zako.Mimi mwenyewe naendelea 

vyema hivi sasa nina mpango wa 

kutembelea Afrika na ikiwezekana 

nitafika Tanzania.Nitafurahi 

kuonana nawe Meshack kwani 

tumekuwa tunashirikiana kwa 

muda mrefu na umenisaidia katika 

mambo mengi sana na hasa wakati 

ule nilipopatwa na matatizo 

uliwahi kudiriki hata kunitumia 

fedha za kujikimu” 

“Karibu sana Tanzania 

Jimmy.Itakuwa ni furaha yangu 

kukupokea hapa .Hata hivyo Jimmy kuna jambo nataka 

nikujulishe.Nimeombwa na rais 

nirudi tena kazini niongoze idara 

ya usalama wa taifa kwa muda wa 

mwaka mmoja baada ya kifo cha 

mkurugenzi wa idara hiyo” 

“Oh ! Hongera sana Meshack 

kwa kuaminiwa na kupewa tena 

jukumu kubwa kama hilo.Naamini 

kuna kitu rais amekiona kwako 

ndiyo maana akakupa nafasi hiyo 

nyeti sana” akasema Jimmy 

“Ahsante Jimmy kwa pongezi 

hata hivyo nimekupigia kukuomba 

msaada wako” 

“Msaada gani unauhitaji 

Meshack? 

“Kuna mtu mmoja anaitwa 

Fakrim alnasor ninahitaji kupota taarifa zake.Anafanya kazi katika 

shirika la ndege la American 

airways yupo New york.Nafahamu 

japokuwa uko nchini Urusi lakini 

huwezi kukosa mtu ndani ya FBI 

akakusaidia kupata taarifa za mtu 

huyu.Ni muhimu sana kwangu.” 

Akasema Meshack.Jimmy akafikiri 

kidogo halafu akasema 

“Taarifa zipi unahitaji kuhusu 

huyu mtu? 

“Nahitaji taarifa zake zote 

zinazomuhusu na zaidi kama 

amewahi kufanya kazi na kuishi 

nchini Misri” 

“Sawa Meshack nina vijana 

wangu pale FBI watanisaidia 

kupata taarifa za kuhusiana na huyo mtu.Vijana wakinitumia 

taarifa nitakutumia mara moja.” 

“Nakushukuru sana Jimmy” 

akasema Meshack na kukata simu 

“Suala lako linafanyiwa kazi 

na mara atakapopata taarifa 

zozote atatujulisha.Nakusihi sasa 

nenda kapumzike ili ujiandae na 

siku ya kesho” akasema Meshack 

jumbo na Mathew akainuka tayari 

kwa kuondoka mara mzee Jumbo 

akakumbuka kitu 

“Mathew kuna kitu 

nimekumbuka.Umekwisha fahamu 

ni akina nani walifanya uchunguzi 

wa ajali ya ndege ya rais? 

“Hapana sikuwa nimeliwaza 

hilo” “Basi lifanyie 

kazi.Wakijulikana watu hawa ni 

akina nani wanaweza wakahojiwa 

na wakaeleza kilichotokea 

kuhusiana na uchunguzi ule” 

“Ahsante kwa kunikumbusha 

kuhusu jambo hilo mzee.Halikuwa 

katika akili yangu kabisa.Nadhani 

ni kutokana na kukaa muda mrefu 

bila kufanya kazi hizi ndiyo maana 

ninasahau hata mambo muhimu 

kama haya.Nitalifanyia kazi hilo 

jambo kesho asubuhi” akasema 

Mathew na kuondoka 

Alipoyaacha makazi ya mzee 

Meshack Jumbo akampigia simu 

Theresa na kumtaka ajitahidi ili 

hadi kesho asubuhi awe na majina 

ya timu ya wachunguzi iliyochunguza chanzo cha 

kuanguka kwa ndege ya rais 

“Imekuwa ni siku ndefu lakini 

kidogo naona kuna mwanga fulani 

japo mdogo sana lakini kama 

nikiufuata nitafika mahala fulani” 

akawaza Mathew alipoingia 

chumbani kwake 

“Natamani kupigia simu na 

kuzungumza na mwanangu Anna 

Maria lakini muda huu ni usiku 

mwingi na tayari atakuwa amelala 

.Nitampigia simu yaya wake kesho 

kama nilivyopewa 

maelekezo.Sitaki tena kumpigia 

Peniela.Sitaki kuvuruga 

mahusiano yake na mpenzi wake 

ambaye hapendi nimpigie simu 

Peniela” akawaza Mathew na kutazama picha ya mwanae 

aliyoitundika ukutani 

“Nakupenda sana Anna 

Maria.Iko siku nitakuchukua na 

utakuja kuishi Tanzania kwani 

huku ndiko kwenu na si huko uliko 

sasa.Mungu azidi kunipa uhai 

mrefu” akawaza na kujilaza 

kitandani 

****************** 

Saa kumi na moja na nusu 

Mathew aliamka na kitu cha 

kwanza alichokifanya ni kupiga 

magoti akamshukuru Mungu kwa 

kumuamsha salama halafu 

akaingia katika chumba chake cha 

mazoezi ambako alifanya mazoezi ya nguvu ili kuweka mwili sawa 

halafu akaoga na kujiandaa kwa 

ajili ya kuikabili siku.Mpishi wake 

alitayarisha kifungua kinywa na 

kumjulisha na wakati akipata 

kifungua kinywa simu yake 

kwanza ikaita alikuwa ni Dr Vivian 

akaipokea haraka haraka 

“Hallo mheshimiwa rais” 

akasema Mathew 

“Mathew habari za asubuhi? 

“Habari nzuri kabisa 

mheshimiwa rais.Sijui 

umeamkaje” 

“Nimeamka salama 

kabisa.Sikupata nafasi ya 

kuzungumza nawe jana kujua 

maendeleo yakoje” “Ninaendelea vyema kabisa 

mheshimiwa rais .Jambo hili ni 

gumu na ni fumbo gumu kama 

unavyosema wewe mwenyewe 

lakini ninaendelea nalo.Kama 

nilivyokuahidi mheshimiwa rais 

kwamba nitajitahidi kwa kila 

niwezavyo kuhakikisha kwamba 

ninalichimba suala hili hadi mzizi 

wake.Kuna hatua kadhaa 

nimekwisha zifikia na kuna 

mambo kadhaa yamejitokeza na 

muelekeo si mbaya ila kwa sasa 

sintasema chochote nipe muda na 

nikipiga hatua kubwa 

nitakujulisha” 

“Nafurahi kusikia 

hivyoMathew.Ninarudia tena 

kukusisitiza kwamba uwe makini sana.Hili jambo lina siri kubwa 

ndani yake imejificha.Ukihitaji kitu 

chochote usisite kunijulisha mara 

moja” akasema rais na kuagana na 

Mathew 

Mara tu rais alipokata simu 

Mathew akampigia simu mzee 

Meshack Jumbo 

“Shikamoo mzee” akasema 

“Marahaba 

Mathew.Umeamkaje? 

“Nimeamka salama mzee.Vipi 

kuna lolote umelipata toka kwa 

Jimmy Snow? 

“Ndiyo.Amenipigia simu saa 

kumi na moja alfajiri.Amenitumia 

taarifa za kumuhusu Fakrim 

Alnasor.Ninakutumia sasa hivi katika simu yako” akasema 

Meshack Jumbo. 

“Ahante sana mzee.Naomba 

unitumie ili niipitie sasa hivi” 

akasema Mathew na kukata simu 

akampigia Theresa. 

“Habari za asubuhi Theresa? 

“Salama kabisa.Umekwisha 

amka? 

“Tayari nimekwisha 

amka.Mimi huamka saa kumi na 

moja za alfajri.Vipi kuna habari 

yoyote mpya? 

“Umefanikiwa kupata yale 

majina niliyokutaka uyatafute? 

“Bado sijatumiwa ila asubuhi 

hii nitayapata” 

“Good.Nitakuja hapo 

nyumbani kwako asubuhi hii” akasema Mathew na kukata simu 

akauona ujumbe wa kutoka kwa 

Meshack Jumbo.Akaufungua 

akausoma.Yalikuwa ni maelezo 

kuhusiana na Fakrim 

Alnasor.Maelezo yale yalionyesha 

kwamba Fakrim Alnasor alikuwa 

na umri wa miaka 49 na raia wa 

Marekani aliyezaliwa nchini 

Misri.Amesoma nchini Misri na 

Marekani na baada ya kuhitimu 

shahada yake ya kwanza ya 

biashara aliajiriwa na shirika la 

ndege la American 

airways.Amewahi kufanya kazi 

katika ofisi za shirika hili zilizoko 

Misri na baadae akahamishiwa 

nchini Marekani .Taarifa 

inaonyesha kwamba Fakrim ana mke na watoto watatu.Mathew 

akatabasamu 

“Mzee Zubery alikuwa 

sahihi.Huyu ndiye Fakrim 

aliyekuwa anamzungumzia.Huyu 

ndiye aliyewapeleka kwake wale 

waandishi wa habari na kumtaka 

awaombee nafasi katika ndege ya 

rais.Picha linaanzia hapa” akawaza 

Mathew na kuchukua simu 

akampigia Meshack Jumbo 

anamjulisha kwamba anakwenda 

kwake kuonana naye 

“Kuna kiti nimekigundua 

hapa.Taarifa hii inaonyesha 

kwamba Fakrim alihamishwa toka 

Cairo kwenda New york Marekani 

wiki moja tu baada ya ajali ile ya 

ndege ya rais kutokea.Je kuna mahusiano yoyote kati ya kuhama 

kwake na ile ajali? Mathew 

akajiuliza 

Alifika nyumbani kwa 

Meshack Jumbo na kumkuta 

anapata kifungua kinywa 

“Karibu Mathew” 

“Ahsante sana mzee” akajibu 

Mathew na kumsubiri mzee Jumbo 

amalize kupata kifungua kinywa 

halafu wakaelekea barazani 

“Mzee kwanza nakushukuru 

sana kwa taarifa uliyonitumia.Hata 

hivyo imenilazimu kuja tena 

kwako baada ya kuridhika 

kwamba Fakrim huyu ndiye yule 

aliyetajwa na Mzee Zubery 

.Nadhani sasa hata wewe umeamini kwamba yule mzee 

alikuwa anasema kweli” 

“Ndiyo.Nimeipitia ile taarifa 

na nimeona kuna muunganiko na 

yale aliyoyasema huyo balozi.” 

“Ahsante.Hata hivyo kuna 

mambo bado nahitaji msaada 

wako.Huyu Fakrim anapaswa 

kuhojiwa ili kufahamu kuhusu 

wale waandishi wa habari.Lengo ni 

kupata taarifa zao kwa undani ni 

akina nani na wako wapi? Kama 

wako hai bado walitokaje ndani ya 

ndege ya rais? 

“Ngoja niwasiliane tena na 

Jimmy Snow nione kama anaweza 

kutusaidia kwa hilo” akasema 

Meshack Jumbo na kumpigia simu 

Jimmy “Habari yako Jimmy” akasema 

Meshack baada ya Jimmy kupokea 

simu 

“habari yako Meshack Jumbo” 

“Samahani Jimmy kwa 

usumbufu.Ninahitaji msaada wako 

tena” 

“Usijali Meshack,sema 

nikusaidie nini? 

“Ninahitaji msaada bado kwa 

Fakrim” 

“Unachunguza nini kuhusu 

Fakrim? 

“Tunachunguza kuhusu ajali 

ya ndege ya rais Anorld iliyotokea 

miaka kumi iliyopita.Kunatajwa 

kuwepo kwa waandishi nane wa 

habari ambao waliomba lifti katika 

ndege ya rais wakati akirejea Tanzania akitokea Misri.Baada ya 

ajali hiyo kutokea ni mtu mmoja tu 

aliyenusurika lakini wengine wote 

walikufa.Kinachoshangaza ni 

kwamba waandishi hao nane wa 

habari maiti zao 

hazikuonekana.Ninataka 

kufahamu kupitia kwa Fakrim 

kwamba waandishi hao ni akina 

nani,walitoka vyombo gani vya 

habari na kama wako hai 

bado.Nahitaji sana msaada wako 

kwa hilo” akasema Meshack Jumbo 

.Jimmy Snow akavuta pumzi ndefu 

na kusema 

“Meshack Jumbo wewe ni 

rafiki yangu mkubwa na umewahi 

kunisaidia sana katika mambo 

mbali mbali na siwezi kukataa kukusaidia katika jambo kama hilo 

ambalo naamini lina umuhimu 

mkubwa kwa nchi yako.Kuna 

jambo moja ambalo naomba 

nikuweke wazi ambalo ni muhimu 

sana kuhusiana na Fakrim 

Alnasor” akanyamaza kwa 

sekunde kadhaa na kusema 

“Fakrim Alnasor ni jasusi wa 

shirika la ujasusi la Marekani 

CIA.Ni mmoja wa majasusi wa siri 

sana waliosambazwa sehemu 

mbali mbali duniani.Kama Fakrim 

anahusika katika ajali hiyo basi ni 

wazi kwamba alikuwa akifanya 

kazi za CIA.Tukimgusa Fakrim 

tutakuwa tayari tumeingia katika 

mgogoro na CIA lakini hata hivyo 

nitakusaidia.Ninao bado vijana wangu ndani ya FBI na mmoja wao 

ni binti yangu anaitwa 

Camilla.Nitawatumia kuweza 

kupata taarifa toka kwa Fakrim za 

kuhusiana na ajali hiyo ya ndege 

ya rais wa Tanzania na hao 

waandishi wa habari aliowasaidia 

wakasafiri na ndege ya 

rais.Nikipewa taarifa yoyote 

nitakujulisha”akasema Jimmy 

Snow. 

“Nashukuru sana Jimmy” 

akasema Meshack Jumbo na 

kukata simu akamgeukia Mathew 

“Mathew kijana wangu,suala 

hili si rahisi hata kidogo.Kadiri 

linavyozidi kuchimbuliwa ndivyo 

mambo yanavyozidi kuibuka na 

sijui huko mbele tutakutana na jambo gani.Jimmy Snow anadai 

kwamba Fakrim Alnasor ni jasusi 

wa CIA” 

Mathew na Meshack Jumbo 

wakatazamana kwa muda 

“Fakrim ni CIA? Mathew 

akauliza 

“Ndiyo ni CIA” 

“Mhh ! Hapa kuna shughuli 

.Kama Fakrim ni CIA basi picha ya 

kwanza ninayoipata ni kwamba 

yawezekana ni CIA ndio 

waliomuua rais Anorld” akasema 

Mathew 

“Ni mapema sana kujenga hoja 

hiyo japokuwa siwezi kukataa 

kwani inawezekana lakini 

tusiharakishe tuchunguze 

kwanza”akasema Meshack Jumbo “Mzee Jumbo kama Fakrim ni 

CIA basi nina uhakika mkubwa 

kwamba wao ndio wanaohusika 

katika ajali ile.Hebu jiulize kwa 

nini akahamishwa muda mfupi tu 

baada ya ajali kutokea?Ni wazi 

alikuwepo pale Misri kwa kazi 

maalum na kazi yake ilipokamilika 

akaondolewa.That’s how CIA 

works.Nina uhakika mkubwa huyu 

mtu tukimfuatilia kwa ukaribu 

tutagundua mengi” 

“Jimmy Snow amesema 

atawatumia vijana wake walio 

ndani ya FBI na mmoja wao 

ambaye ni binti yake anaitwa 

Camilla na watahakikisha 

wanamuhoji Fakrim kuhusiana na 

hao waandishi wa habari na ajali ya ndege ya rais na 

watakachokipata atatujulisha” 

akasema Meshack Jumbo na baada 

ya majadiliano Mathew akamuaga 

Meshack na kuondoka. 

“Kuna dalili za uhusika wa 

Marekani katika ajali ile ya ndege 

ya rais kupitia shirika lake la 

ujasusi la CIA.Fakrim ambaye ni 

jasusi wa CIA aliwaombea lifti 

waandishi wa habari wanaotoka 

Marekani na baadae ndege 

ikaanguka na miili ya waandishi 

hao haionekani.Baada ya muda wa 

wiki moja toka ilipotokea ajali ile 

Fakrim akahamishwa na 

kupelekwa New York.Kuna kitu 

hapa lazima tukifahamu.Huyu 

Fakrim ni mtu muhimu sana katika uchunguzi wetu.Lakini suala la 

kujiuliza kama Marekani ndio 

wanahusika na kusababisha ajali 

ya ndege ile na rais Anorld 

akafariki dunia kwa nini basi 

walifanya hivyo?Walihitaji 

nini?Lazima kuna siri imejificha 

hapa .Hili ni suala la kwenda nalo 

taratibu na kwa umakini mkubwa 

sana .Ukweli utabainika kwani 

tayari mwanga umeanza 

kujitokeza”akawaza Mathew 

wakati akielekea nyumbani kwa 

Theresa 

Alifika nyumbani kwa Theresa 

na kumkuta tayari yuko ofisini 

“Umechelewa sana kuanza 

kazi” akasema Theresa “Kuna sehemu muhimu 

nilipita.Kuna taarifa zozote 

umepata? 

“Ndiyo tayari nimetumiwa 

majina ya timu ya watu saba 

waliofanya uchunguzi wa chanzo 

cha kuanguka kwa ndege ya 

rais.Watano kati ya hao waliofanya 

uchunguzi huo wanatoka nje ya 

nchi na mmoja alitoka kikosi cha 

anga cha jeshi la wananchi wa 

Tanzania na mwingine ni mhandisi 

toka wizara ya mawasiliano.Kwa 

bahati mbaya hawa watazania 

wawili walioshiriki katika timu hii 

wamefariki dunia” akasema 

Theresa na kumpatia Mathew yale 

majina akayapitia “Hawa watanzania wawili 

walioshiriki katika uchunguzi huu 

nini sababu ya vifo vyao? Mathew 

akauliza 

“Hapana sijaelezwa sababu ya 

vifo vyao” akajibu Theresa 

“Kuna kitu cha ajabu 

nimeanza kukiona.Kuna vifo vya 

ajabu ajabu vinatokea kwa wale 

ambao wanahusika kwa namna 

fulani katika hili tukio la ajali ya 

dege ya rais.Ukianzia na mzee 

Zubery alipata ajali siku chache tu 

baada ya ajali ya ndege ya rais 

kutokea na toka muda huo 

hajawahi kurejea katika hali yake 

ya kawaida.Mwanae Zaina 

anasema baba yake ametumia 

zaidi ya miaka mitano katika matibabu.Hawa jamaa wawili 

waliotajwa kushiriki katika 

uchunguzi wa ajali ya ndege ile ya 

rais nao wamefariki dunia .Hii 

inazidi kutupa uhakika kwamba 

ajali ile haikuwa ya 

kawaida.Tuachane na hao wawili 

hebu tuwatazame hawa 

wachunguzi waliotoka nje ya nchi 

ambao wanatajwa kutokea katika 

kampuni iliyotengeza ndege 

hiyo.Itafute hiyo kampuni na 

uwaulize kuhusiana na hawa 

wachunguzi.Tunataka kufanya 

mahojiano na walau mmoja wao ili 

watuelekeze ni kitu gani 

walichokiona katika uchunguzi 

wao na tufahamu mazingira ya 

kupotea kwa kisanduku cheusi” akasema Mathew na kutoka nje 

akazitafuta namba za simu za 

mwanadada anayefanya shughuli 

za ndani katika jumba la Peniela 

akampigia 

“hallo kaka” akasema 

mwanadada aliyekuwa 

anazungumza kwa lugha ya 

kifaransa. 

“Hujambo Marie? 

“Sijambo kaka.Habari za 

Tanzania? 

“Huku kwema .Mnaendeleaje 

nyie hapo Paris? 

“Tunaendelea vyema kaka” 

“Nashukuru kusikia hivyo 

.Anna Maria anendeleaje? Tayari 

amekwisha kwenda shule? “Anaendelea vyema,na tayari 

amekwenda shule” 

“Vipi maandalizi ya siku yake 

ya kuzaliwa? Akauliza Mathew 

“Bado sijaona maandalizi 

yoyote kuanza” 

“Sawa Marie,naomba Anna 

Maria atakaporejea kutoka shule 

unipigie ninahitaji kuzungumza 

naye” 

“Nitakujulisha kaka 

atakaporejea.Lini unakuja 

kututembelea? 

“Kwa sasa nimebanwa kidogo 

na shughuli nyingi na nitakapopata 

nafasi nitakuja kuwatembelea” 

akasema Mathew na kukata simu 

halafu akawa na mazungumzo na 

mkandarasi anayesimamia ujenzi wa kiwanda chake.Baada ya hapo 

akawa na maongezi na watu 

wengine kadhaa wa muhimu 

halafu akarejea ndani na kumkuta 

Theresa bado anazungumza na 

simu.Alizungumza kwa takribani 

dakika kumi na tano halafu 

akakata simu na kumgeukia 

Mathew 

“Mathew hili suala mbona 

linazidi kuwa gumu? 

“Kwa nini Theresa? 

“Nimezungumza na kampuni 

ya ndege waliyotengeneza ile 

ndege ya rais iliyopata ajali 

wanasema kwamba hawakuwahi 

kutuma mtu yeyote kuja 

kuchunguza kuhusiana na ajali ile 

ya ndege.Nimezungumza na mkurugenzi wa kampuni hiyo 

anasema kwamba yeye ni mgeni 

katika nafasi yake akaniunganisha 

na mtu mwingine ambaye 

alikuwepo wakati ndege ile 

inapata ajali lakini naye akakana 

kabisa kutuma timu ya wataalamu 

kuja kuchunguza chanzo cha 

kuanguka kwa ndege ya rais 

iliyotengenezwa na kampuni 

yao.Anasema kwamba walisikia 

kuhusu kuanguka kwa ndege ile 

lakini hawakuwahi kupewa taarifa 

rasmi na serikali au hata kuitwa 

kufanya uchunguzi.Nilimuuliza 

kuhusiana na kutoonekana kwa 

kisanduku cheusi cha kurekodi 

taarifa za ndege na akashangaa 

sana.Nilimtajia majina ya wale ambao wanatajwa kwamba 

walikuja kufanya uchunguzi na 

akakana kuwa na watu kama hao 

katika kampuni yao.Tumekwama 

tena”akasema Theresa.Mathew 

akavuta pumzi ndefu 

“Dah ! Kweli hili suala ni 

fumbo zito.Kwa hiyo taarifa hii 

iliyokaa katika kumbukumbu za 

serikali si ya kweli.Nani 

aliyeidhinisha timu hii ifanye 

uchunguzi? Kila kitu kuhusiana na 

ajali ile ya ndege ni uongo 

mtupu.Kuna mambo mengi 

yanafichwa na ndiyo maana jambo 

hili limebaki kuwa ni fumbo 

lisiloweza kufumbuliwa.Kila 

aliyejaribu kufanya uchunguzi 

alifika mahala akashindwa kuendelea lakini mimi 

sintoshindwa nitahakikisha 

ninafika mwisho” akasema 

Mathew na kuinama akafikiri 

kidogo na kusema 



Kila 

aliyejaribu kufanya uchunguzi 

alifika mahala akashindwa kuendelea lakini mimi 

sintoshindwa nitahakikisha 

ninafika mwisho” akasema 

Mathew na kuinama akafikiri 

kidogo na kusema 

“Tuachane kwanza na hayo 

mambo.Hili suala linapaswa 

kushughulikiwa kwa umakini 

mkubwa.Tuende nalo hatua kwa 

hatua.Kabla ya kuja hapa nimetoka 

kufuatilia taarifa za kuhusiana na 

Fakrim.Kwa taarifa nilizopata toka 

marekani ni kwamba Fakrim ni 

raia wa Marekani mwenye asili ya 

Misri. Anafanya kazi katika shirika 

la ndege la british airways na 

amewahi kufanya kazi katika ofisi 

za shirika hili zilizopo Cairo Misri 

na baadae akahamishiwa nchini Marekani.Taarifa inaonyesha 

alipata uhamisho wiki mja tu 

baada ya ndege ya rais 

kuanguka.Kikubwa nilichokipata 

kuhus Fakrim ni kwamba ni jasusi 

kutoka CIA.Kwa kutumia watu 

wetu walioko New york Marekani 

tumeomba atafutwe huyu Fakrim 

na ahojiwe kuhusiana na wale 

waandishi wa habari na kuhusiana 

na kuanguka kwa ndege ya 

rais.Wakifanikiwa kumpata na 

kumuhoji basi tutapata mambo 

yatakayotusaidia sana .Mpaka 

hapa kunaanza kujitokeza chembe 

chembe za Marekani kuhusika 

katika kuanguka kwa ndege ile ya 

rais.Wakati tukisubiri taarifa 

kutoka New York kwa watu wetu wanaotusaidia kuna kitu 

ninahitaji” 

“Unahitaji nini Mathew? 

“Nahitaji kuonana na mjane 

wa rais Anorld” 

“Sifahamu chochote kuhusu 

yule mama ngoja nipige simu 

niulize” akasema Theresa na 

kupiga simu akapewa maelekezo 

halafu akamtazama Mathew 

“Nimeelekezwa kwamba 

mama huyu anaitwa April Mubara 

na kwa sasa anaishi katika shamba 

lake lililoko katika kijiji cha 

Mchangawima Chalinze Pwani” 

“Good.Twende huko sasa 

hivi.Tumuhoji pengine kuna kitu 

tunaweza kugundua” “Kitu gani unakihitaji toka 

kwa huyo mama? Unadhani kuna 

lolote analoweza katusaidia? 

“Ni mtu muhimu na anaweza 

akawa na jambo la kutusaidia.Yule 

ni mjane wa rais na yawezekana 

akawa anafahamu mambo mengi 

ya siri aliyoelezwa na mume wake 

.Najaribu kutafuta kiini cha 

Marekani kuhusika katika ajali 

ile.Je kama kweli ni wao walikuwa 

wanatafuta nini?Kwa nini wamuue 

rais Anorld?Yawezekana yule 

mama akawa anafahamu kitu” 

akasema Mathew wakatoka na 

kuingia katika gari la mathew 

wakaondoka kuelekea Chalinze 

kuonana na April Mubara mjane 

wa rais Anorld huku sura ya Theresa ikioyesha wasiwasi 

mkubwa sana 

“Mathew hili jambo limeanza 

kuniogopesha sana.Kwa haya 

mambo niliyoyaona toka jana 

nimeanza kuwa na 

hofu.Inawezekana jambo hili 

likawa kubwa zaidi ya uwezo 

wetu.Kama Marekani imeanza 

kujitokeza katika suala hili 

inawezekana likawa ni suala 

lililovuka hadi mipaka ya 

nchi.Najiuliza vile vile hao 

waliokuwepo serikalini kabla ya 

dada Vivian kuingia madarakani 

kwa nini hawakulishughulikia hili 

suala na kuliacha liendelee kuwa 

fumbo?Uchuguzi wa kuanguka kwa 

ndege ya rais umeishia hewani,uchunguzi wa mauaji ya 

baba umeishia hewani na viongozi 

wako kimya,kuna nini hapa? 

“Theresa hili suala kama 

ulivyosema linaonekana kuvuka 

mipaka ya nchi lakini haliwezi 

kunishinda.Hata kama Marekani 

wamehusika ninachohitaji 

kukifahamu ni sababu ya wao 

kufanya hivi 

walivyofanya.Hawawezi kufanya 

peke yao lazima kuna watu wa 

humu nchini walioshirikiana nao 

.Nakusihi usihofu nitakulinda” 

akasema Mathew na uso wa 

Theresa uliendelea kuonyesha 

wasiwasi 

“Tunaenda tena mahala 

walikouliwa wazazi wangu.Sielewi nifanye nini.Natamani nimueleze 

Mathew ukweli lakini 

naogopa.Ngoja tu niendelee kukaa 

na siri yangu.Waliofanya mambo 

haya ni mtandao mrefu na wenye 

nguvu na endapo wakigundua 

kwamba na mimi nilikuwepo 

katika matukio yote mawili lazima 

wataniua haraka sana kwani pekee 

ndiye niliyebaki hai ninayefahamu 

nini kilichotokea.Naamini bado 

wanaendelea kuitafuta 

football.Hapaswi mtu yeyote 

kufahamu siri hii.” Akawaza 

Theresa. 

**************** 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog