Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL (2) - 1

  

IMEANDIKWA NA : PATRICK CK

******************************************

Simulizi : The Football (2)

Sehemu Ya Kwanza (1)


“Hapana hakueleza chochote 

na hakuna anayefahamu 

anakwenda wapi.” Akasema mama yule na mara uso wake 

ukaonekana kubadilika.Mathew 

akagundua kitu usoni pa yule 

mama akageuka nyuma na 

kukutana na wanawake watatu 

waliovaa mavazi marefu na 

kujifunika nyuso zao wakabaki 

wanaonekana macho pekee. 

“Mbona huyu mama 

ameogopa baada ya kuwaona hawa 

wanawake wakiingia hapa? 

Akajiuliza Mathew na ghafla 

kukatokea jambo ambalo hakuna 

aliyelitegemea.Wale wanawake 

watatu waliokuwa wamevaa 

magauni marefu kila mmoja 

akatoa bunduki ndogo aliyokuwa 

ameificha ndani ya gauni lile na 

kuanza kuachia risasi na kuwataka watu wote walale chini .Watu wale 

walitawanyika haraka sana na 

kumbe hawakuwa peke yao 

walikuwepo wengine nje na idadi 

yao ikaongezeka mle ndani.Ndani 

ya sekunde chache watu wote 

waliokuwepo eneo lile wakalala 

chini wakiwamo Mathew na 

Camilla 



Mbona huyu mama ameogopa 

baada ya kuwaona hawa wanawake 

wakiingia hapa? Akajiuliza Mathew 

na ghafla kukatokea jambo ambalo 

hakuna aliyelitegemea.Wale 

wanawake watatu waliokuwa 

wamevaa magauni marefu kila 

mmoja akatoa bunduki ndogo 

aliyokuwa ameificha ndani ya gauni 

lile na kuanza kuachia risasi na 

kuwataka watu wote walale chini 

.Watu wale walitawanyika haraka 

sana na kumbe hawakuwa peke yao 

walikuwepo wengine nje na idadi yao 

ikaongezeka mle ndani.Ndani ya 

sekunde chache watu wote 

waliokuwepo eneo lile wakalala 

chini wakiwamo Mathew na Camilla 

ENDELEA

“Tulieni nyote.Hatuna lengo 

baya nanyi na wala hatutaki 

kumdhuru mtu yeyote” Akasema 

mmoja wa wale jamaa aliyekuwa 

amejitanda mavazi marefu na 

kufunika uso kama 

mwanamke.Watu wote walikuwa 

kimya wamelala chini kama 

walivyoamriwa na wale jamaa 

ambao idadi yao ilizidi ishirini na 

walikuwa wamezingira katika kila 

kona ya nyumba. 

“Tunamuhitaji mjane wa 

marehemu.Naomba ajitokeze 

tafadhali” akasema yule jamaa na kuingia ndani waliko kuwa 

wamekaa akina mama. 

“Tunamuhitaji haraka sana 

mjane wa marehemu !! akaendelea 

kusema yule jamaa akiwa katika 

chumba walichokuwamo akina 

mama wengi.Hakuna yeyote 

aliyesimama.Yule jamaa akawapa 

maelekezo watu wake wanne 

waliokuwa mle ndani ambao wote 

walikuwa wamefunika nyuso zao 

waingie katika kila chumba 

wapekue.Nyumba ya George 

Mzabwa ilikuwa na vyumba vinne 

vya 

kulala,sebule,maktaba,jiko,vyoo na 

mabafu.Wale jamaa wakaingia 

ndani ya vyumba haraka haraka 

kila mmoja na chumba chake wakaanza kupekua lakini 

hawakufanikiwa kukipata 

walichokuwa wanakitafuta.Yule 

jamaa aliyeonekana ndiye kiongozi 

wao akasema kwa ukali 

“Nataka haraka sana mjane 

wa marehemu ajitokeze ama sivyo 

tutawateketezeni nyote !! 

Pamoja na vitisho vile lakini 

hakuna aliyejitokeza.Kwa hasira 

akamfuata mama moja akamuinua 

“Naomba msiniue jamani !! 

akasema yule mama huku akilia 

“Nitakuacha hai endapo 

utanionyesha mjane wa marehemu 

alipo !! akasema yule jamaa kwa 

sauti kali 

“Hayupo ametoka na hatujui 

amekwenda wapi” “Unanidanganya? Nakupa 

sekunde kumi unionyeshe mahala 

alipo mjane wa marehemu” 

akasema yule jamaa 

“Naomba uniamini kweli 

ametok….” Hakumaliza neno la 

mwisho yule jamaa akammiminia 

risasi.Akina mama waliokuwepo 

mle ndani wakapiga yowe lakini 

yule jamaa akawatuliza kwa 

kupiga risasi juu akitishia 

kuwamaliza wote kama 

wangeendelea kupiga kelele.Akiwa 

amefura kwa hasira akamuinua 

mwanamke mwingine na kumtaka 

amuonyeshe alipo mjane wa 

marehemu 

“ Baba utatuua sote lakini 

huyo unayemtafuta hayupo.Ametoka na hatujui 

amekwenda wapi” akasema yule 

mama huku akitetemeka kwa 

hofu.Yule jamaa kwa hasira 

akammiminia risasi na kumuua 

“Camilla hawa jamaa 

wataendelea kuua watu huko 

ndani bila hatia.Hizo risasi 

zimesikika kuna mtu mwingine 

ameuawa.Lazima tufanye jambo 

kuwazuia wasiendelee kuua watu” 

Mathew akamwambia Camilla kwa 

kunong’ona 

“Unataka kufanya nini 

Mathew? Hawa jamaa wako wengi 

na wana silaha kali.Hatuwezi 

kupambana nao hata 

kidogo.Tuwaache wafanye wanachotaka waondoke” akasema 

Camilla 

“Kweli wako wengi lakini 

hawa ndio wale 

tunaowatafuta.lazima tufanye kila 

linalowezekana kuwadhibiti” 

akasema Mathew 

“ Mathew tafadhali usi…” 

“Usiogope Camilla.Mimi 

ninawafuata” akasema Mathew na 

kuinuka akainua mikono juu.Watu 

wawili waliokuwa eneo lile 

wakamsogelea wakimuelekezea 

silaha zao na kumtaka alale 

chini,akapiga magoti 

“Mimi ni mdogo wa marehemu 

na ninaweza kuwasaidia kupata 

hicho mnachokitafuta” akasema Mathew.Wale jamaa 

wakatazamana. 

“ Tafadhali msiendelee kuua 

watu,nitawasaidia kupata kile 

mnachokitafuta” akasema 

Mathew.Mmoja wa wale jamaa 

akamuongoza Mathew kuelekea 

ndani akiwa ameinua mikono juu 

.Akina mama wote walikuwa 

wameondolewa kutoka katika 

vyumba walimokuwa wamekaa na 

kuwekwa sebuleni.Yule jamaa 

kiongozi wa wale wavamizi 

akageuka na kumuona Mathew 

akiingizwa sebuleni akiwa



ameinua mikono juu 

“Huyu naye kafanya 

nini?akauliza “Huyu ni mdogo wake na 

marehemu” akasema yule jama 

aliyekuwa nyuma ya Mathew na 

silaha 

“Piga magoti haraka” akasema 

yule kiongozi kwa ukali na Mathew 

akapiga magoti. 

“Wewe ni mdogo wake na 

marehemu? 

“Ndiyo ni mdogo wake 

Marehemu.Naweza kusaidia 

kupata kile mnachokitafuta ila 

msiendelee kuua watu .Kitu gani 

mnakihitaji? Akasema 

Mathew.Yule jamaa akamtazama 

kwa hasira na kuuliza 

“Mjane wa marehemu yuko 

wapi? “Amekwenda kaburini 

kuonyeshwa kaburi la mumewe na 

kuwasha mshumaa.Jana hakuweza 

kushuhudia mazishi ya mume 

wake alikuwa amepoteza fahamu” 

Mathew akadanganya.Yule jamaa 

akamtazama kwa sekunde kadhaa 

akamtaka asimame wakaelekea 

chumbani kwa George 

“Nataka simu za 

marehemu.Haraka sana tuonyeshe 

mahala zilipo” akasema yule jamaa 

“Mnahitaji kwa dhumuni 

gani?Ninyi ni polisi?Mathew 

akauliza ni swali lile likaonekana 

kumkera yule jamaa 

“Nakupa sekunde kumi ,kama 

ukishindwa kuonyesha zilipo simu 

za marehemu nitakumaliza kama nilivyowamaliza hao wanawake 

uliowaona wamekufa sebuleni!! 

“George ana kasiki la siri 

ambalo yeye na mke wake huficha 

vitu vyao muhimu na nina hakika 

humo ndimo mke wake alimoweka 

vifaa muhimu vya mumewe 

alivyokabidhiwa baada ya 

mumewe kujiua.Kasiki hilo liko 

nyuma ya kabati la nguo” akasema 

Mathew na kuanza kulisogeza 

kabati la nguo ili aweze kupata 

nafasi ya kulifungua kasiki alilodai 

liko nyuma ya kabati la nguo. 

“Hii ndiyo nafasi yangu 

ambayo sitakiwi kuipoteza” 

akawaza Mathew na kuzunguka 

nyuma ya kabati,akatoa bastora 

yake haraka haraka halafu kwa nguvu kubwa akalisukuma kabati 

likaanguka kwa mbele.Yule 

kiongozi wa lile genge la wavamizi 

aliliona kabati likianguka akaruka 

pembeni kulikwepa na hiyo ndiyo 

nafasi Mathew alikuwa 

anaitafuta.Kwa kasi ya umeme 

akaachia risasi kadhaa toka katika 

bastora yake yenye kiwambo cha 

sauti na kumfumua yule jamaa 

kichwa na kwa wepesi wa aina 

yake akaruka na kunyakua 

bunduki ya yule jamaa.Kishindo 

cha kuanguka kwa kabati 

kiliwastua jamaa wengine 

waliokuwamo mle ndani na huku 

wakikimbia jamaa wanne 

wakaingia mle chumbani na 

kumkuta Mathew akiwa tayari amejiandaa akiwa na bunuki ya 

yule jamaa aliyemuua na 

hakufanya ajizi akavurumisha 

mvua ya risasi ambazo wale jamaa 

hawakuwa wamezitarajia na wote 

wanne wakaanguka chini 

.Hawakuwa na uhai tena.Akaitupa 

ile bunduki na kuchukua nyingine 

halafu akamvua mmoja wao kofia 

aliyokuwa ameivaa ya kufunika 

uso akavaa pamoja na fulana ya 

kujikinga risasi na kutoka mle 

ndani kwa tahadhari kubwa 

akanyata hadi sebuleni na 

kuwakuta akina mama peke yao 

bila kuwepo wale jamaa 

waliokuwa wamewashika 

mateka.Kutokea nje akasikia sauti 

za magari,akavua kofia ile ya kufunika uso,akatoka na kuwakuta 

watu bado wamelala chini 

akawapigia ukelel 

wainuke,akakimbia kwa tahadhari 

hadi nje lakini alikwisha chelewa 

wale jamaa walikwisha ingia 

katika magari yao na kukimbia 

“Wamekimbia !! ikasema sauti 

ya Camilla nyuma yake 

“Tumewakosa tena” akasema 

Mathew 

“Iliposikika milio ya risasi 

alitoka jamaa mmoja mbio na 

kuwaita wenzake kwa ishara na 

wote wakatoka na kukimbia .Nini 

kimetokea ndani?Nilikuwa na 

wasiwasi sana kuhusu usalama 

wako baada ya kusikia ile milio ya 

risasi” akasema Camilla.Mathew akamsimulia kila kitu kilichotokea 

mle ndani 

“Watu hawa lazima wana 

mahusiano na kile kikundi cha 

askari wanotumiwa kufanya 

uvamizi.Lazima kuna jambo 

wanataka kulificha lisijulikane 

ndiyo maana walikuwa wanahitaji 

simu za George” akasema Mathew 

“Lakini kwa nini iwe sasa? 

Kwa nini watafute simu hiyo leo 

tena baada ya sisi kufahamu 

kuhusu George kuwa na 

mawasiliano na Nathan?Tujiulize 

maswali haya na yanaweza 

yakatusaidia kufahamu mambo 

mengi” akasema Camilla 

“Ni kweli Camilla,kuna kitu 

hata mimi ninakiona hapa.Hawa jamaa walifahamu fika kwamba 

tunakuja huku kuonana na mjane 

wa marehemu hivyo wakajitahidi 

kuwahi kutudhibiti tusipate 

tunachokitafuta lakini waliku




ya rais na kifo cha baba 

,wangekwisha nimaliza muda 

mrefu sana.Hakuna mpaka leo 

anayefahamu kama nilikuwemo 

katika ile ndege.Wanachofahamu 

ni kwamba abiria wote walifariki 

.Siri hii haipaswi kujulikana na 

lazima nifanye kila niwezalo 

kumkwamisha Mathew asiufikie 

ukweli” akaendelea kuumiza 

kichwa kwa mawazo mengi hadi 

alipofika nyumbani kwa George 

Mzabwa.Akashuka na kuwasabahi akina mama waliokuwa 

wanaokota mchele na kuwaomba 

wamuelekeze alipo mke wa 

George.Mama mmoja 

akamuongoza hadi katika chumba 

kilichokuwa na akina mama 

sita.Mama mmoja aliyevaa mavazi 

meupe alikuwa amelala juu ya 

godoro na Theresa akawasalimu 

wale akina mama kwa adabu 

halafu akaenda kuketi pembeni ya 

mfiwa. 

“Pole sana mama” akasema 

kwa sauti ndogo 

“Ahsante sana mwanagu” 

akajibu mama yule ambaye bado 

macho yake yalikuwa yamevimba 

“Mama mimi naitwa Theresa 

natokea ikulu katika ofisi ya rais.Kuna mambo yamenileta hapa 

kuhusiana na mumeo” 

“Ni mambo gani? 

“Unaweza ukajikaza tukaenda 

kuzungumza hapa nje tafadhali ni 

mambo ya siri kidogo”akasema 

Theresa na yule mama akainuka 

wakaingia katika chumba cha 

kulala 

“karibu” akasema mke wa 

George 

“Ahsante sana.Mama mumeo 

George alijipiga risasi hivyo nataka 

kufahamu umeshakabidhiwa vitu 

vyake vyote?Alikuwa na vitu mbali 

mbali kama vile simu ,kompyuta 

nk.Wameshakuletea vitu hivyo 

tayari? “Hapana bado.Alinifuata mtu 

mmoja anaitwa Inspekta Msibi 

Makwala Msibi akanihoji kama 

naweza kufahamu sababu ya 

mume wangu kujiua,akaniambia 

pia kwamba yeye ndiye 

anayesimamia uchunguzi wa suala 

la kujiua mume wangu na kuna 

baadhi ya vifaa vya marehemu 

wanavyo kama hiyo simu na 

kompyuta ili viwasaidie katika 

uchunguzi wao wa kubaini 

kilichosabisha George ajiue na 

uchunguzi wao utakapokamilika 

watavirejesha” 

“Sawa mama naomba twende 

ofisini kuna vitu vingine vya 

marehemu vya kutambua na 

kuvichkua na hawezi kupewa mtu mwingine zaidi yako.Nafahamu 

umechoka bado na hauna nguvu 

lakini jikaze twende hatutachukua 

muda mrefu” akasema Theresa 

.Mke wa George akatafakari kidogo 

halafu akaomba ajiandae 

Wakati mke wa George 

akijiandaa Theresa akachukua 

simu na kumpigia Dr Vivian. 

“Unasemaje Theresa? 

Akauliza Dr Vivian baada ya 

kupokea simu 

“Dada naomba msaada 

wako.Nataka kufahamu inspekta 

Msibi Makwala msibi anapatikana 

kituo gani cha polisi? 

“Kuna tatizo lolote na huyo 

mtu” “Hapana dada namuhitaji nina 

shida naye binafsi “ akasema 

Theresa 

“Nipe dakika mbili niulize” 

akasema Dr Vivian na kukata simu 

Mke wa George alipomaliza 

kujiandaa wakaongozana hadi 

garini wakaondoka.Dakika chache 

baada ya kuondoka nyumbani kwa 

George ,simu ya Theresa ikaita 

alikuwa ni rais.Akapunguza 

mwendo wa gari na kuipokea 

“Hallow dada” akasema 

“Theresa huyo askari 

unayemuulizia nimeambiwa yuko 

katika ofisi za upelelezi kanda 

maalum” 

“Ahsante dada nashukuru” 

akasema Theresa na kukata simu.Hakutaka kumpa dada yake 

nafasi ya kuendeleza 

maongezi.Hakukuwa na maongezi 

garini hadi walipofika nyumbani 

kwa Theresa.Mke wa George 

alionekana kuwa na wasi wasi 

“mama karibu ndani” 

akasema Theresa wakaingia 

sebuleni 

“Mama utanisamehe kwa 

kutokueleza ukweli lakini hakuna 

vitu vya marehemu bali nilitaka tu 

nikutoe pale nyumbani ili tuweze 

kuzungumza mambo ya msingi 

kuhusiana na kifo cha mumeo” 

akasema Theresa na sura ya mke 

wa George ikajikunja kwa hasira 

“Mama usikasirike lakini 

suala ninalotaka kuzungumza nawe ni muhimu sana kwa 

usalama wako na familia yako” 

akasema Theresa na kauli ile 

ikamstua yule mama. 

“Unamaanisha nini 

unaposema 

hivyo?akauliza.Theresa akakohoa 

kidogo kurekebisha koo lake na 

kusema 

“Tutakayozungumza hapa 

naomba iwe ni siri kubwa kati 

yangu nawe” 

“Mbona unazidi kunipa wasi 

wasi? 

“Usiogope mama nitakueleza 

kila kitu.Kuna uchunguzi 

unafanyika hivi sasa kubaini 

sababu ya kuanguka kwa ndege ya 

rais Anorld Mubara na kusababisha kifo chake miaka 

kumi iliyopita.Katika uchunguzi 

huo imebainika kwamba



 mumeo 

George Mzabwa alikuwa na 

mawasiliano na watu 

wanaosadikiwa kusababisha ajali 

ile na kumuua rais Anorld” 

Mstuko alioupata mke wa 

George ulikuwa mkubwa 

“Mume wangu anahusika 

katika kuilipua ndege ya rais? 

Akauliza 

“Bado haijathibitika hivyo 

lakini kitendo cha kuwa na 

mawasiliano na watu 

waliosababisha ajali hiyo 

kinaashiria kwamba mumeo 

anaweza kuwa alihusika katika 

ajali ile.George aliamua kujipiga risasi ili kuilinda familia yake 

kwani watu aliokuwa 

anashirikiana nao ni watu hatari 

na wangeweza hata kuteketeza 

familia yote ili kuharibu ushahidi 

wasigundulike” 

“Oh Mungu wangu !! akasema 

yule mama 

“Simu ya George” Theresa 

akaendelea 

“Alikuwa anaitumia kwa 

mawasiliano ina ushahidi wa 

kutosha wa mawasiliano yote kati 

yake na hao wenzake na hiyo ni 

hatari kubwa sana kwenu kwani 

hao jamaa hawatalala hadi 

wahakikishe wameipata simu hiyo 

yenye mawasiliano kati ya George 

na hao watu .Hamtakuwa salama kwani watu hao watawawinda kila 

dakika hadi wahakikishe 

wameipata hiyo simu ili kuendelea 

kuificha siri yao” 

“Kwa hiyo 

nifanyaje?Nimechanganyikiwa 

sijui cha kufanya” 

“Sikiliza mama,mimi ni ndugu 

wa rais na ninao uwezo wa 

kukulinda lakini kikubwa 

unachoweza kukifanya ni 

kuhakikisha unaipata hiyo simu ya 

mumeo na kufahamu watu 

aliokuwa anashirikiana nao 

.Nakuahidi kwamba ukifanikiwa 

kunipa hiyo simu na tukafanikiwa 

kuwafahamu hao washirika wake 

nitakuombea ulinzi mkali toka kwa rais na familia yako itakuwa 

salama” 

“Unanichanganya sana na 

sielewi nitaipataje hiyo simu toka 

kwa polisi kabla hawajamaliza 

uchunguzi wao.Lakini….” akasita 

kidogo 



Unanichanganya sana na 

sielewi nitaipataje hiyo simu toka 

kwa polisi kabla hawajamaliza 

uchunguzi wao.Lakini….” akasita 

kidogo 

“Kuna kitu nimekumbuka 

labda kinaweza kuwa na msaada 

kwako.Tunayo nyumba yetu mpya 

ambayo George alipanga tuhamie 

baadae iko miembe pacha .Katika 

chumba cha kulala kuna kasiki 

ambalo alikuwa anahifadhi vitu 

vyake vya siri.Inawezekana labda 

katika kasiki hilo kuna vitu vya 

msingi vinavyoweza kukusaidia 

kuwafahamu hao watu aliokuwa 

anashirikiana nao.Nilihisi lazima kuna jambo alikuwa ananificha na 

sikujua kama linaweza kuwa 

jambo kubwa kama hili la 

kushirikiana na wauaji wa rais” 

“Tunaweza kwenda huko 

miembe pacha” 

“Hakuna tatizo tunaweza 

kwani nahisi yawezekana hata 

katika kasiki hilo kutakuwa na 

fedha alikuwa anaficha” akasema 

mke wa George wakaondoka 

kuelekea miembe pacha.Wakiwa 

njiani mke wa George akapigiwa 

simu na kupatwa na mstuko 

mkubwa kwa taarifa aliyopewa 

“Mungu wangu !! akasema 

“Kuna nini mbona umestuka? 

Theresa akauliza “Nimetaarifiwa kwamba kuna 

kundi la watu wamevamia 

nyumbani kwangu wakiwa na 

silaha wakinitafuta mimi na 

wameua watu wawili kwa 

risasi.Nimeambia alijitokeza mtu 

mmoja akadai kwamba yeye ni 

ndugu wa marehemu na 

akapambana nao akafanikiwa 

kuua wavamizi watano na wengine 

wakakimbia.Polisi tayari 

wamefika na ninatakiwa kurejea 

nyumbani mara moja.Ee Mungu 

mitihani gani hii inatupata? Mbona 

ni mgumu kuzidi uwezo wangu? 

Akasema mke wa George akilia 

kwa uchungu 

“Watu hao ndio wale 

niliokuwa nakueleza kwamba mumeo alikuwa anashirkiana 

nao.Nadhani sasa umeyaamini 

maneno yangu” 

“Jamani nitawapeleka wapi 

watoto wangu?Mbona George 

ametuachia matatizo makubwa 

namna hii? Akaendelea kulia mke 

wa George 

“Usilie mama tutakulinda 

.Kitu cha msingi ni wewe kufuata 

maelekezo nitakayokupa.Hawa 

jamaa lazima watarudi tena na 

tena hadi watakapohakikisha 

wanapata kile 

wanachokihitaji.Nitakuombea 

ulinzi kwa rais lakini nawe 

unapaswa kunipa ushirikiano ili 

tuweze kuwafahamu hao watu ni 

akina nani”akasema Theresa na safari ikaendelea huku mke wa 

George akiendelea kutiririsha 

machozi 

“Hizi ndizo athari za kujiingiza 

katika makundi hatari kwa tamaa 

ya fedha na unapoondoka 

unawaachia familia yako matatizo 

makubwa kama George 

aliyomuachia mke 

wake.Namuonea huruma sana 

huyu mama hakuwa akifahamu 

chochote kuhusu mambo 

aliyokuwa anayafanya mume 

wake” akawaza Theresa 

Kwa maelekezo ya mke wa 

George waliwasili eneo la miembe 

pacha katika nyumba mpya ya 

George.Ilikuwa ni nyumba kubwa 

nzuri.Pembeni ya nyumba hiyo kulikuwa na nyumba nyingine 

ndogo ambayo aliishi muangalizi 

wa ile nyumba kubwa.Mke wa 

Georgia akamtaka yule jamaa 

amletee funguo za nyumba kubwa 

wakaingia ndani 

“Nyumba nzuri sana na kuna 

kila kitu humu kwanini hamtaki 

kuhamia huku? Theresa akauliza 

“George hakutaka tuishi 

huku.Nahisi alitaka kuifanya kama 

sehemu yake ya siri ya kufichia 

mambo yake” akasema yule mama 

na kuufungua mlango wa chumba 

kikubwa cha kulala. 

“Hiki ni chumba chetu cha 

kulala” akasema yule mama na 

kufunua zuria kisha akang’oa 

kigae na likaonekana kasiki “Kasiki hili ndilo George huwa 

analitumia kuhifadhia mambo 

yake ya siri” akasema yula mama 

na kuanza kubonyeza namba 

kadhaa akijaribu kulifungua 

.Alijaribu kubadilisha namba mbali 

mbali bila mafanikio. 

“Limegoma kufunguka 

.Sifahamu namba anayotumia 

kufungulia hili kasiki” akasema 

yule mama.Theresa 

akachanganyikiwa 

******************* 

Mathew na Camilla waliwasili 

ikulu na kukaribishwa sebuleni 

kwa rais “Unafahamika sana hapa ikulu 

kwani hatujapata usumbufu 

wowote wa kuja kuonana na rais” 

akasema Camilla wakiwa sebuleni 

wakimsubiri rais 

“Rais alinipa kibali cha 

kuingia hapa ikulu muda wowote 

niutakao bila kuzuiliwa na mtu 

yeyote ili kurahisisha kazi yangu 

kwa hiyo kuingia hapa ikulu ni 

kama kuingia chumbani kwangu” 

akasema Mathew 

“Ni bahati kubwa kuwa na 

ukaribu na rais.Mambo yako 

mengi yatakwenda vizuri” 

akasema Camilla na muda huo huo 

akaingia rais Dr Vivian.Mathew na 

Camilla wakasimama kwa adabu “karibuni sana.Habari za 

jumapili? 

“Habari nzuri mheshimiwa 

rais,sijui kwa upande wako” 

“Hivyo hivyo.Naona 

umeniletea mrembo leo” akasema 

Dr Vivian na kuachia tabasamu 

“Huyu ndiye yule mgeni 

wangu niliyekuomba kibali cha 

kuingia nchini anaitwa Camilla 

snow.Anatokea Marekani na 

amekuja kunisaidia katika kufanya 

uchunguzi wa lile suala” akasema 

Mathew na kumgeukia Camilla 

“Camilla huyu ni rais wa 

jamhuri wa muungano wa 

Tanzania anaitwa Dr Vivian 

matope” Camilla akainuka na kwenda 

kumpa mkono rais 

“Nimefurahi sana kukutana 

nawe mheshimiwa rais.U 

mwanamke jasiri na usiyeyumba 

.Hivi sasa dunia nzima 

wanafahamu barani Afrika kuna 

kiongozi mmoja mwanamama 

mwenye ujasiri wa aina yake.Hii ni 

heshima kubwa umetupa 

wanawake.Hongera sana 

mheshimiwa rais” akasema 

Camilla.Dr Vivian akaachia 

tabasamu pana sana 

“Ahsante Camilla.Ni furaha 

kubwa kwangu kukutana 

nawe.Kwa kuwa uko karibu na 

Mathew basi tutakuwa tunaonana 

mara kwa mara kwani hapa ikulu Mathew huja kama nyumbani 

kwake” akasema Dr Vivian 

“Mathew nipe taarifa za 

kilichotokea nyumbani kwa 

George” akasema Dr Vivian na 

Mathew akamsimulia kila kitu 

kilichotokea Dr Vivian akashika 

kichwa 

“Watu hawa ni akina 

nani?Mbona wanatuumiza vichwa 

vyetu namna hii?akauliza Dr 

Vivian akiwa amekasirika 

“Hakuna taarifa zozote toka 

polisi kuhusu kuwatambua wale 

jamaa tuliowaua jana kule 

makaburini? Mathew akauliza 

“Mpaka sasa bado sijapata 

jibu lolote kutokea 

kwao.Nimewapa muda hadi saa saba mchana wa leo niwe 

nimepata jibu .Tukiwafahamu ni 

akina nani itatusaidia kufahamu 

viongozi wao.Sikuwahi kufikiri 

kama Nathan anaweza akanifanyia 

hivi.Mapenzi yetu yalikuwa 

makubwa,yalivuka kiwango cha 

kawaida na ndiyo maana nikawa 

kipofu,sikuona wala kusikia 

kuhusu Nathan.Alinidekeza na 

nikajiona ni mwanamke wa pekee 

ninayependwa kuliko wote 

duniani kumbe alinipofusha kwa 

malengo yake.I hope he’s in hell 

right now!! Akasema Dr Vivian 

kwa hasira 

“Ninapata hasira kila 

nikimuwaza Nathan.Tuachane na 

hayo .Uliniuliza kama nilikuwa na mtu wakati nikipewa majibu ya 

zile namba za simu .Kama 

nilivyokueleza simuni nilikuwa na 

Dr Robert Mwainamela waziri wa 

mambo ya nje.Huyu ni mtu 

ninayemuamini sana na hawezi 

kuwa na tatizo lolote ndiyo maana 

nikamueleza kuhusiana na George 

kuwa na mashirikiano na CIA.Ni 

mmoja wa watu wanaonisaidia 

mno nafikiria hata kumpendekeza 

urais pale nitakapomaliza muda 

wangu,anafaa sana kuwa kiongozi 

mkubwa” akasema Dr Vivian 

“Mheshimiwa rais,kumekuwa 

na uvujaji wa taarifa zetu mbali 

mbali na hata tukio lililotokea leo 

linadhihirisha hilo.Wale jamaa 

walipata taarifa kwamba tayari tumefahamu kuhusiana na George 

kuwa na mawasiliano na Nathan 

na walifika pale kwa lengo moja 

kuhakikisha kwamba wanaipata 

simu ya George .Wanafahamu 

kwamba tukiipata tutafahamu 

mambo mengi.Ukiacha mimi,wewe 

na Theresa ambao tunafahamu 

kuhusu George kuwa na 

mawasiliano na Nathan mtu 

mwingine anayefahamu alikuwa ni 

Dr Robert.Mheshimiwa rais 

nafahamu hautapendezwa na hili 

ninalotaka kulisema lakini nahitaji 

ufahamu kwamba nataka 

kumchunguza Dr 

Robert.Ningeweza kufanya hivyo 

kimya kimya bila kukueleza 

chochote lakini sitaki yaliyotokea kwa Nathan yajirudie tena na 

ndiyo maana nimeona kabla 

sijafanya chochote niombe kwanza 

ruhusa yako.Nafahamu huyu ni 

mtu wako wa karibu na 

unayemuamini sana lakini 

anatakiwa achunguzwe hivyo 

naomba ruhusa yako ya kufanya 

hivyo” akasema Mathew na sura ya 

Dr Vivian ikabadilika akamtazama 

Mathew kwa macho makali 

“Kwa nini ufanye hivyo 

Mathew? Unadhani Dr Robert 

anaweza kuwa anashirikiana na 

hao watu ? akauliza 

“Siwezi kusema moja kwa 

moja kwamba anashirikiana nao 

lakini tunapaswa kulithibitishahilo kwa kufanya uchunguzi” 

akasema Mathew 

“Mathew siwezi kamwe 

kuliruhusu jambo kama hilo 

likafanyika .Dr Robert ni mtu wa 

heshima sana katika taifa hili 

.Anaheshimika mno ndani na nje 

ya nchi na ni mmoja kati ya hazina 

ya viongozi tulio nao.Zaidi ya yote 

ninamuamini mno na kumfanyia 

uchunguzi mtu kama huyu ni kama 

kumdhalilisha” 

“Mheshimiwa rais,tafadh…..” 

“Mathew my word is 

final.Nikisema hapana ni 

hapana,tena nakuomba 

usizunguke na kwenda kufanya 

uchunguzi wako kwa 

siri.Nikifahamu mimi na wewe tutaingia katika 

mgogoro.Namuheshimu sana Dr 

Robert na nina muamini pia hivyo 

siwezi kwa namna yoyote ile 

kuruh…..” Rais akakatisha 

alichotaka kukisema baada ya 

mmoja wa wasaidizi wake kuingia 

na kumtaarifu kwamba kuna 

mgeni alikuwa amefika anahitaji 

kumuona 

“Mathew natumai tumemaliza 

na umenielewa.Sitaki uchunguzi 

wowote kwa Dr Robert.Nikipata 

taarifa zozote toka polisi kuhusu 

wale watu nitakujulisha.Ahsante 

sana kwa kuja kuniona na sasa 

mnaweza kwenda kwani nina 

wageni muhimu wamekuja 

kunitembelea.Kama kuna lingine lolote nipigie simu” akasema Dr 

Vivian na kuinuka akaagana na 

akina Mathew wakaondoka 

“Siwezi hata kidogo kuruhusu 

Dr Robert akachunguzwa.Yule ni 

mtu mwenye heshima kubwa sana 

na siwezi kumdhalilisha kiasi 

hicho.Mathew atafute wahusika 

halisi wa hili jambo na si kurukia 

rukia hata watu wengine 

wasiohusika .Nina mfahamu vizuri 

Dr Robert hawezi katu kujihusisha 

na mambo ya kijinga kama hayo.Ni 

mwanasiasa mzoefu,msomi mzuri 

na mwenye kujiweza kimaisha” 

akawaza Dr Vivian baada ya akina 

Mathew kuondoka. 

Mlango wa sebuleni 

ukafunguliwa akaingia bi April Hudson Mubara mjane wa rais 

Anorld Mubara akiwa 

ameongozana na msichana mmoja 

mwembamba mrefu wastani 

mwenye nywele ndefu.Dr Vivian 

akasimama na kuwalaki wageni 

wake 

“Shikamoo mama” Dr Vivian 

akamsalimu bi April kwa adabu 

“Marahaba Dr Vivian habari za 

siku? 

“Nzuri kabisa 

mama.Unaendeleaje mama yangu? 

“Ninaendelea vyema.Habari za 

hapa?Mnaendeleaje nyie? 

“Ninaendelea vyema mama” 

“Nafurahi kusikia 

hivyo.Utatusamehe kwa kuja bila 

taarifa” “Usijali mama.Hapa ni 

nyumbani unakaribishwa muda 

wowote bila hata kutoa taarifa” 

akasema Dr Vivian,wahudumu 

wakafika na kuwahudumia wageni 

vinywaji na vitafunwa 

“Huyu ni mwanangu anaitwa 

Tausi” 

“Wow ! Tausi.Unaendana 

kabisa na hilo jina lako.You are so 

pretty” akasema Dr Vivian 

“Thank you” akasema Tausi 

“Mzee Mubara alimzaa Tausi 

na mwanamke mmoja toka Brazil 

lakini mimi ndiye niliyemlea akiwa 

mdogo na baadae akaenda kuishi 

nchini Marekani na ndiyo maana 

unaona hafahamu vyema kiswahili 

”akasema bi April “Karibu sana 

Tausi.Nimefurahi kukufahamu” 

“Nashukuru sana mheshimiwa 

rais.Hata mimi pia nimefurahi sana 

kukufahamu” akasema Tausi 

“Siku hizi umekuwa kimya 

sana Dr Vivian.Mbona umenitupa 

mama yako namna hiyo?Hata simu 

hunipigii siku hizi.Au unasubiri 

hadi katika sherehe za kitaifa 

ndipo tuonane ? 

“Hapana mama,sijakutupa na 

siwezi kufanya hivyo.Mambo ni 

mengi sana.Wewe umekaa ikulu na 

unafahamu namna mzee 

alivyokuwa anatingwa na mambo 

mengi.Hata hivyo nilifikiri 

umekwenda Marekani kutokana 

na ukimya mwingi” “Tanzania ndiyo nyumbani 

kwangu kwa sasa na si 

Marekani.Muda mwingi niko 

shambani kwangu napumzika.Pole 

na misuko suko iliyotokea 

.Nimeona ngoja nije nimpe pole 

mwanangu kwani urais ni kazi 

ngumu.Usikatishwe tamaa na haya 

yanayoendelea kutokea.Wewe 

songa mbele wasaidie 

waTanzania.Hata hivyo 

nakupongeza sana kwa namna 

unavyokabiliana na changamoto 

mbali mbali unazokutana nazo” 

akasema bi April 

“Ahsante sana 

mama,nashukuru.Kwa ujumla 

tunaendelea vizuri.Changamoto ni 

nyingi lakini tunazikabili.Nashukuru napata 

uungwaji mkono mkubwa toka 

kwa wananchi” 

“Nafurahi kusikia hivyo .Vipi 

kuhusu hili linaloendelea hivi sasa 

la mvutano na Marekani,tayari 

limekwisha patiwa muafaka? 

“mama suala hili halina 

muafaka .Tayari nimekiwisha 

fanya maamuzi kwamba 

nitaendelea na mchakato wa 

mashirikiano na Korea Kaskazini” 

“Sawa Dr Vivian kama unaona 

suala hilo lina maslahi kwa taifa 

basi endelea nalo” 

“Ndiyo mama kuna maslahi 

makubwa kwa nchi yetu kama 

tutaanzisha mashirikiano ya 

kiuchumi na Korea Kaskazini.Tutafaidika na kukuza 

uchumi wetu.Tanzania tunapaswa 

tuanze kujitegemea na ili tufikie 

huko lazima maamuzi magumu 

yafanwe.Tayari nimekwisha fanya 

maamuzi hayo magumu na 

nitahakikisha ninawaongoza 

waTanzania katika safari hii hadi 

tufikie kuwa nchi 

inayojitegemea.Ni wakati wa 

waTanzania kuamua aidha 

kuungana nami katika safari hii na 

kujikwamua kiuchumi au kubaki 

nyuma na nchi kuendelea kuwa 

omba omba lakini mimi rais wao 

sintageuka nyuma.Sitaki kugeuka 

jiwe,nitaangalia mbele daima.Kwa 

hiyo mama safari ndiyo imeanza 

na tutapitia misuko suko mingi sana.Mataifa tajiri yanaendelea 

kutupa vitisho kuhusiana na 

kuwekewa vikwazo vya kiuchumi 

lakini mimi nasonga mbele.Kuwe 

au kusiwe na vikwazo lazima 

Tanzania ijitegemee kiuchumi” 

akasema Dr Vivian 

“Naamini huko aliko baba wa 

taifa hili amejaa tabasamu usoni 

pake kwa nchi kupata kiongozi 

shupavu kama wewe.Endelea na 

ari hiyo hiyo kuwasaidia 

waTanzania” 

“Ndiyo mama,waTanzania 

wana shida nyingi sana na 

ninayanya haya yote kwa ajili ya 

kuwasaidia wao na vizazi vyao” 

“Sawa Vivian.Tuachane na 

hayo,vipi kuhusu masuala yako ya ndoa?Mmefikia wapi?Mara ya 

mwisho tulipokutana uliniambia 

kwamba bado maandalizi 

yanaendelea” 

“Kumetokea matatizo kidogo 

kwa hiyo ile ndoa haitakuwepo 

tena.Utaratibu unafanywa ili wale 

wote waliotoa michango yao 

waweze kurejeshewa” 

“Pole sana .Nini kimetokea 

Vivian na kusababisha haya yote? 

“Ni mambo ya kibinafsi zaidi 

sipendi kuliongelea kwa undani ila 

ndoa ile haipo tena” 

“Usijali mwanangu ,Mungu 

ana makusudi yake.Kama 

imeshindikana sasa,baadae 

itawezekana.Vuta subira na 

usikate tamaa” “Ahsante mama” akasema Dr 

Vivian na ukimya ukatawala.Bi 

April akasema 

“Dr Vivian,pamoja na kuja 

kukujulia hali,lakini nina shida 

nyingine imenileta” 

“Niambie mama ni shida gani? 

“Ni huyu mdogo 

wako.Ameamua kuja kuishi nami 

hapa Tanzania lakini hana 

kazi.Naomba umsaidie apate japo 

kijikazi chochote hapa ikulu.Ni 

msomi mzuri ana shahada ya 

teknolojia ya mawasiliano na vile 

vile anayo sahahada ya mahusiano 

ya kimataifa.Aliponieleza wazo 

lake hilo nikaona nikufuate 

mwanangu umsaidie mdogo 

wako.Nina sehemu nyingi ambazo ningeweza kumtafutia kazi lakini 

nimeamua nije hapa kwako 

kutokana na heshima ya mahala 

hapa.Mtu anayefanya kazi ofisi ya 

rais anakuwa na heshima kubwa” 

akasema bi April 

“Sawa mama nimekusikia na 

ombi lako siwezi kulikataa.Kwa 

sababu ya heshima yako na mzee 

Mubara,Tausi atapata kazi hapa 

ikulu.Nitakuomba Tausi uje kesho 

asubuhi saa moja na nusu tayari 

kuanza kazi.Njoo na vyeti vyako 

vyote ili uhakikiwe na kuingizwa 

katika mfumo wa ajira wa serikali” 

“Ahsante sana mheshimiwa 

rais kwa msaada huo mkubwa” 

akasema Tausi “Usijali Tausi.Niite dada 

inatosha” akasema Dr Vivian 

wakaendelea na maongezi 

mengine ya maisha yaliyochukua 

zaidi ya saa moja kisha bi April 

akasema 

“Dr Vivian ,sisi inatubidi 

tuondoke tukuache uendelee na 

majukumu mengine kwani 

tumekuvamia bila taarifa na 

kuvuruga ratiba zako .Halafu kabla 

sijasahau nina namba mpya ya 

simu ninayoutumia hivi 

sasa.Ihifadhi tafadhali” akasema bi 

April na Dr Vivian akaingia 

chumbani kwake akachukua simu 

na kuhifadhi namba ya bi April 

halafu akawasindikiza hadi nje 

wakaagana na kuondoka“Nimefurahi sana 

kutembelewa na wageni kama 

hawa.Bi April amebaki mpweke 

lakini nitahakikisha wale wote 

waliomuua mumewe 

wanapatikana na kufikishwa 

katika sheria” akawaza Dr Vivian 




Kwa zaidi ya dakika ishirini 

,Theresa na mke wake wa George 

Mzabwa walikuwa wanajaribu 

kulifungua kasiki bila 

mafaniio.Mke wa George Mzabwa 

aliyekuwa amechoka alikaa 

pembeni na kumuacha Theresa 

naye ajaribu kufungua lakini jitihada zake zote hazikuzaa 

matunda 

“Tuondoke hatutaweza 

kulifungua kasiki hili 

leo.Nitakwenda kupekua katika 

makablasha yake pengine naweza 

kupata namba za kufungulia hili 

kasiki” 

‘hapana lazima tufungue hili 

kasiki” akasema Theresa 

“Hakuna namna 

tutakavyoweza kulifungua hili 

kasiki bila kuwa na namba 

maalum za kufungulia.Twende 

tuondoke nitakujulisha 

nikifanikiwa kuzipata hizo 

namba,ninasubiriwa nyumbani” 

“Hatuwezi kuondoka hapa bila 

kasiki hili kufunguliwa” akasema Theresa na kusimama akajishika 

kiuno na kutafakari kwa muda 

“Hapa sina namna lazima 

niombe msaada kwa 

Mathew.Nilitaka jambo hili liwe 

siri lakini kwa hapa tulipofika maji 

yamenifika shingoni.Sina utaalamu 

wowote wa kufungua kasiki hili” 

akawaza Theresa na kuchukua 

simu akampigia Mathew 

“Hallow Theresa” akasema 

“Mathew kuna jambo 

limetokea naomba msaada wako” 

“Nini kimetokea Theresa? 

Akauliza Mathew kwa wasi wasi 

“Siwezi kukueleza simuni ila 

nitakuelekeza mahala uje mara 

moja kuna jambo la msingi sana 

ambalo linaweza kutusaidia” akasema Theresa na Mathew 

akasita kidogo 

“Mathew” akaita Theresa 

“Nielekeze mahala ulipo 

Theresa” akasema Mathew na 

Theresa akamuelekeza mahala 

alipo.Mathew akabadili uelekeo na 

kuanza kuelekea mahala aliko 

Theresa 

“Rais anafanya kazi yetu kuwa 

ngumu kwa kuzuia kumchunguza 

Dr Robert.Niko kwenye kazi hii 

kwa muda mrefu na ninafahamu 

mambo mengi na ndiyo maana 

sikukurupuka kutaka kumfanyia 

uchunguzi Dr Robert .Rais 

amekosea sana kuzuia hili 

lisifanyike kwani kwa sasa 

hapaswi kumuamini mtu yeyote.Mtandao huu ni mpana 

sana na yawezekana kuna watu 

wakubwa wanahusika pia.Pamoja 

na rais kumtetea sana Dr Robert 

lakini bado nafsi yangu inataka 

kumchunguza kiundani.Mara 

nyingi nikiwa na hisia na kitu au 

mtu fulani huwa ni kweli.Mara 

chache sana hisia zangu hazijawa 

kweli.Lazima nitafute namna ya 

kumchunguza Dr Robert kwa siri” 

akawaza Mathew 

Iliwachukua dakika arobaini 

na sita kuwasili mahala alipo 

Theresa.walishuka garini kwa 

tahadhari kubwa wakaenda 

kugonga geti likafunguliwa na 

jamaa mmoja akawakaribisha 

ndani .Gari la Theresa lilikuwepo ndani.Yule jamaa akawapeleka 

sebuleni ambako walikuwepo 

Theresa na mwanamke mmoja 

wameketi 

“Mathew karibu” akasema 

Theresa 

“Theresa kuna tatizo gani? 

Akauliza 

“Mathew huyu ni mke wa 

GeorgeMzabwa” akasema Theresa 

“Mke wa George?!! Mathew 

akashangaa 

“Ndiyo Mathew.Najua 

umestuka sana lakini nitakupa 

maelekezo hapa baadae kwa sasa 

tuelekee katika jambo muhimu 

nililokuitia hapa” akasema 

Theresa na kumtaka Mathew na 

Camilla wamfuate wakaingia katika chumba cha 

kulala,akawaonyesha kasiki 

lililokuwa katika sakafu ya 

chumba 

“Hapa ndipo George Mzabwa 

huficha nyaraka zake za siri.Nina 

uhakika mkubwa kwamba 

tukifanikiwa kulifungua tutapata 

mambo mengi kuhusiana na 

George” akasema Theresa 

“Theresa umefikaje 

huku?Umewezaje kuyajua haya 

yote? Mathew akauliza 

“Mathew tafadhali tusipoteze 

muda.Tulifungue hili kasiki na 

haya mambo mengine 

tutazungumza baadae “ akasema 

Theresa“Mke wa George hafahamu 

namba za siri za kufunguliwa 

kasiki hili? Mathew akauliza 

“Kama angekuwa 

anazifahamu ningekuomba uje 

Mathew?Amejaribu namba zote 

anazozifahamu lakini 

imeshindikana” 

“Nini kimetokea hapa? Camilla 

akauliza 

“Tunahitaji kulifungua hili 

kasiki.George alikuwa anaficha 

baadhi ya vitu vyake hapa” 

akasema Mathew 

“Niacheni nilifungue .Ninao 

utaalamu wa haya mambo japo 

itachukua muda kidogo” akasema 

Camilla “Wakati Camilla akijaribu 

kulifungua hili kasiki naomba 

tuongee Theresa” akasema 

Mathew walipofika sebuleni 

walimkuta mke wa george 

“Mama hawa ni wenzangu 

,wote ni wafanyakazi ikulu na 

tunashirikiana pamoja”Theresa 

akamwambia 

“Pole sana mama kwa yote 

yaliyotokea.Kuna mambo 

makubwa yametokea nyumbani 

kwako leo na a……….” 

“Tayari nimekwisha pewa 

taarifa.Hapa nilipo 

nimechanganyikiwa na sielewi 

nitafanya nini kulinda familia 

yangu” “Usihofu mama.Tutakulinda 

kitu cha msingi ukubali 

kushirikiana nasi” 

“Mwenzenu Theresa 

amenielza kila kitu na ndiyo 

maana nikamleta hapa.Kitendo 

alichokifanya George kushirikiana 

na hawa watu waovu 

kimenisikitisha sana na niko tayari 

kutoa ushirikiano mkubwa kwenu 

ili mradi mnihakikishie ulinzi 

kwangu na familia yangu” 

“Usihofu kuhusu ulinzi 

utapata.Juhudi za kuwatambua 

wale jamaa waliovamia nyumbani 

kwako zinaendelea na kwa bahati 

nzuri nilifanikiwa kupambana nao 

na kuwaua watano” akasema 

Mathew na mke wa George akainuka na kukaa akimtazama 

Mathew kwa mshangao. 

 “Ni wewe ndiye uliyepambana 

nao? 

“Ndiye mimi” 

“Niliambiwa kuna mtu mmoja 

alijitokeza na kupambana na hao 

wavamizi akafanikiwa 

kuwashinda.Nilitamani sana 

kumfahamu mtu huyo nimshukuru 

kwa jambo la kishujaa 

alilolifanya.Nimefurahi kukuona” 

“Usihofu mama,uko salama” 

akasema Mathew akatoka nje na 

Theresa 

“Haya nieleze nini 

kimetokea?Umemtoa wapi mke wa 

George? Mathew akauliza “Mathew naomba usinielewe 

vibaya kwa kile nitakachokueleza 

lakini ilinilazimu nifanye 

hivyo.Mara tu uliponipigia simu na 

kunifahamisha kuhusu George 

kuwa na mawasiliano na Nathan 

na ukataka kupafahamu nyumbani 

kwake nilihisi lazima utakuwa na 

mpango wa kwenda nyumbani kwa 

George kuzungumza na mke 

wake.Nilijua lazima ungekwenda 

na Camilla na msingefanikiwa 

kupata kitu chochote kwani yule 

mama aisngekubali kutoa 

ushirikiano wowote kwenu hivyo 

nikalazimika kwenda haraka 

haraka kuzungumza naye, 

nikamdanganya na kuondoka 

naye.Ili anipe ushirikiano nilimueleza ukweli kuhusu mume 

wake kuwa na mashirikiano na 

watu wabaya.Lengo kuu lilikua ni 

kuitafuta simu ya 

mumewe.Alinieleza kwambaa 

hakuwa amekabidhiwa vifaa vya 

marehemu kwani bado uchunguzi 

wa kifo chake ulikuwa 

unaendelea.Baadae akakumbuka 

kwamba mumewe alikuwa 

anaficha baadhi ya vitu vyake 

katika hii nyumba yao mpya hivyo 

tukaja hapa.Tukiwa njiani kuja 

huku akapigiwa simu na 

kufahamishwa kuhusiana na 

kilichotokea nyumbani 

kwake.Tumefika hapa 

tumehagaika sana kulifungua lile 

kasiki bila mafanikio ndipo nilipoamua kukupigia 

simu.Utanisamehe sana Mathew 

kwa kufanya jambo hili kimya 

kimya bila kukushirikisha lakini 

lengo langu ni zuri tu.Chochote 

ambacho ningekipata hapa lazima 

ningekujulisha tu” akasema 

Theresa.Mathew akatumia 

sekunde kadhaa kumtazama usoni 

halafu akasema 

“Nilipaswa nikasirike kwa hiki 

ulichokifanya kwani ni kitu cha 

hatari sana lakini kwa mara 

nyingine tena maamuzi yako 

uliyoyafanya yamekuwa na faida 

kwetu.Mara ya kwanza ulifanya 

maamuzi na kumuua Nathan 

nilichukia sana lakini yakaibuka 

mambo makubwa likiwamo hili kundi la watu wenye kutumia sare 

na zana za jeshi la polisi.Leo tena 

umefanya maamuzi ya kwenda 

kumchukua mke wa George na 

kuna mambo 

yamejitokeza.Ulifanya jambo la 

maana sana kwani endapo mke wa 

George angekuwepo pale 

nyumbani kwake sijui nini 

kingetokea.Yawezekana 

tusingeweza hata kufahamu kama 

kuna sehemu ya siri george 

alikuwa anahifadhi vitu 

vyake.Ninaamini endapo 

tutafanikiwa kulifungua hili kasiki 

tutafahamu mambo mengi.Ila siku 

nyingine usijaribu tafadhali 

kufanya mambo kimya kimya bila 

kunishirikisha.Mambo haya ni hatari kubwa sana kwako.Laiti 

wale jamaa wangefahamu kama 

umeondoka na mtu waliyekuwa 

wanamtafuta hivi sasa ungekuwa 

katika hatari kubwa” 

“Samahani Mathew sintarudia 

tena” 

“Na iwe hivyo” akasema 

Mathew 

“Nini kilitokea nyumbani kwa 

George?akauliza Theresa.Mathew 

akamsimulia mkasa wote 

“Dah ! poleni sana .Kuna 

ulazima wa kufanya kila juhudi 

kuwabaini watu hao ni akina nani 

kwani wanaonekana ni watu 

waliojipanga vizuri na wana uwezo 

mkubwa wa kupata taarifa zozote 

muda wowote ndiyo maana kila tunachokifanya wao tayari 

wanakuwa na taarifa.Kuna watu 

wakubwa katika mtandao huu na 

tusipowatambua juhudi zetu zote 

zitakwamishwa na hili genge 

hatari” 

“Theresa wakati unapiga simu 

nilikuwa nimetoka kuonana na 

rais.Kuna jambo lilinipeleka 

ikulu.Nilimuuliza rais wakati 

anapewa majibu kuhusiana na ile 

namba ya George alikuwa na nani? 

Rais akajibu kwamba alikuwa na 

waziri wa mambo ya nje Dr Robert 

Mwainamela.Ninataka 

kumchunguza huyo Dr Robert” 

“Unahisi ana mahusiano na 

hao watu? Theresa akauliza ‘Sina uhakika na hilo lakini 

nina wasi wasi naye ndiyo maana 

nataka kumchunguza” 

“Lakini Dr Robert ni mtu 

mwenye heshima zake na hawezi 

kujihusisha na mitandao kama hii 

ya maharamia” akasema Theresa 

“Hata rais naye amenijibu 

hivyo” 

“Tayari umemwambia 

kwamba unataka kumchunguza Dr 

Robert? 

“Ndiyo imenilazimu 

kumweleza .Sikutaka yatokee tena 

kama yale yaliyotokea kwa Nathan 

hivyo nikamfuata kuomba kibali 

chake nimchunguze Dr Robert” 

“Amesemaje? 

“Amekataa” “Hawezi kukubali .Hata mimi 

siafikiani na wazo hilo la 

kumchunguza Dr Robert .Kuwa 

karibu na rais wakati anapewa 

majibu yale ya kuhusiana na 

namba za simu za George si sababu 

ya yeye kuwa 

anahusika.Tuwatafute watu sahihi 

lakini Dr Robert ninaweza 

kusimama na kumtetea” akasema 

Theresa 

“Nimewasikia nyote lakini 

kwa uzoefu nilionao katika mambo 

haya naamini kabisa kuna ulazima 

wa kumchunguza Dr 

Robert.Mtanisamehe sana kama 

nitakuwa ninamvunjia heshima 

kwa kutaka kumchunguza Dr 

Robert lakini ni kawaida yangu kutokuamini watu”akasema 

Mathew 

“So how’s she? Theresa 

akabadili maongezi 

“Nani ? 

“Your girl friend” 

“Theresa nimekwisha kueleza 

kwamba Camilla ni rafiki na 

mshirika wangu” 

“Mhh !! Theresa akaguna 

“Haya tutaona” akasema 

“Twende tukamsaidie 

Camilla,yawezekana anahitaji 

msaada” akasema Mathew 

wakaingia ndani.Simu ya Theresa 

ikaita akatoka tena nje kwani 

mpigaji alikuwa Dr Vivian 

“Theresa uko wapi? “Niko sehemu fulani na 

Mathew” 

“Oh ok.Nakuomba kesho 

asubuhi ufike hapa ikulu kuna mtu 

nataka umpe maelekezo 

machache,atakuwa anatumia ofisi 

yako kwa wakati huu ambao 

utakuwa unasaidiana na Mathew” 

“Umepata mtu mwingine wa 

kushika nafasi yangu?Theresa 

akauliza 

“Sina maana kwamba 

ninakuondoa katika nafasi yako.Ni 

hivi,amekuja bi April Mubara 

mchana huu akiwa na binti yake 

akaomba nimpatie kazi hapa ikulu 

na mimi kwa heshima ya baba 

yake nimeshindwa kumkatalia 

hivyo nimemuagiza aje kesho kuanza kazi na kwa wakati huu 

ambao hautakuwepo hapa ofisini 

basi atatumia ofisi yako wakati 

nikitafuta sehemu ya kumuweka. 

Halafu nitaomba uwe karibu naye 

kwani bado hajui sana kiswahili” 

“Ametokea wapi hadi asijue 

kiswahili? 

“Ametokea Marekani ndiko 

alikokuwa anaishi kwa muda 

mrefu” 

“Sawa dada nitakuja hiyo 

asubuhi” akasema Theresa na 

kukata simu 

“Hii ni mipango ya dada ya 

kutaka kuniondoa taratibu katika 

ofisi yake.Kitendo nilichokifanya 

cha kumuua Nathan bado 

kinaniumiza sana.Vyovyote atakavyoamua mimi niko tayari” 

akawaza Theresa wakati akirejea 

ndani.Bado Camilla hakuwa 

amefanikiwa kulifungua lile kasiki 

“Ninao utaalamu wa 

kuyafungua makasiki lakini hili 

limenitoa jasho” akasema Camilla 

“Tutapoteza muda mwingi 

sana hapa na hatutaweza 

kulifungua.Kitu pekee 

tunachoweza kufanya hapa ni 

kulichimba hili kasiki na 

kuondoka nalo” akasema Mathew 

“Lakini hatutaweza kufanya 

hivyo hadi tuwasiliane kwanza na 

mwenye nyumba ili akubali” 

akasema Theresa na kumuita mke 

wa George wakamuomba 

waliondoe lile kasiki ili wakalikate.Haikuwa rahisi kwa 

mke wa George kukubali lakini 

alikubali na vifaa vikaletwa 

likaanza kuchimbuliwa.Ilichukua 

zaidi ya saa moja kuweza 

kuliondoa 

“Theresa wewe utamrejesha 

mke wa George nyumbani kwake 

na sisi tunakwenda 

kulishughulikia hili kasiki na 

chochote tutakachokikuta 

tutakujulisha” akasema Mathew 

“Mathew mke wa George 

anahisi mumewe alikuwa 

anahifadhi fedha nyingi humu kwa 

hiyo kama mtakuta kuna fedha 

huyu mama apewe” 

“Usihofu Theresa,chochote 

kitakachopatikana humu hakuna atakayekigusa” akasema 

Mathew,wakalipakia kasiki lile 

katika gari wakaondoka.Wakiwa 

njiani kurejea nyumbani Mathew 

akapigiwa simu na rais 

“Hallow Mheshimiwa rais” 

“Mathew habari za mchana? 

“Nzuri kabisa mheshimiwa 

rais” 

“Mathew nimepigiwa simu na 

waziri wa mambo ya ndani muda 

mfupi uliopita anasema kwamba 

jeshi la polisi limefanya uchunguzi 

wa zile picha na wamesema wale si 

askari wao.Ni watu waliotumia 

sare za jeshi la polisi lakini si 

askari polisi” “Kama si askari polisi basi 

lazima wana watu wao ndani ya 

jesho la polisi”akasema Mathew 

“Mathew nakuomba jitahidi 

sana tuweze kuwabaini hawa watu 

ni akina nani.Wanazidi kuwa tishio 

na wanaonekana ni watu hatari” 

“Nitajitahidi mheshimiwa 

rais” akasema Mathew na kukata 

simu 

“Rais amepewa taarifa 

kwamba wale sio askari polisi bali 

ni watu wanaotumia sare na vifaa 

vya polisi”Mathew akamwambia 

Camilla 

“Marekani kuna jambo kubwa 

wanalitafuta Tanzania na ndiyo 

maana wametengeneza mtandao 

mkubwa na nina imani mtandao huu umetawanyika katika kila 

idara nyeti ya serikali .Rais 

anapaswa kuwa makini sana 

kwani yawezekana hata katika 

watu wanaomzunguka kuna walio 

katika huu mtandao” akasema 

Camilla 

“hilo nalikubali kabisa lakini 

sisi ndio tunaopaswa kumlinda 

kwa kuwa ndio tunaoitambua 

hatari iliyopo.Yeye ana uhakika na 

ulinzi alio nao lakini hapaswi 

kumuamini mtu yeyote kwa 

sasa.Hao anaowaamini leo 

wanaweza kugeuka nyoka wenye 

sumu kali kesho” akasema Mathew

 ******************* 

Dr Vivian akiwa 

amejipumzisha akitafakari namna 

mambo yanavyokwenda akapewa 

taarifa kwamba balozi wa 

Marekani amefika 

kumuona.Hakuweza kukataa 

akaagiza akaribishwe ndani 

“Amekuja kutafuta nini tena 

huyu balozi? Wanataka 

nizungumze lugha gani ili 

wanielewe? Wanajaribu kutumia 

kila mbinu kunishawishi lakini 

hawatafanikiwa” akawaza Dr 

Vivian na kujiweka tayari hkwenda 

kuonana na balozi 

“Balozi Abraham Clerck 

karibu sana.habari za jumapili? 

“Habari nzuri mheshimiwa 

rais,samahani sana kwa kuvamia 

bila taarifa” 

“Usijali mheshimiwa 

balozi,karibu sana” 

“Ahsante” akasema balozi 

Clerk na rais akamtaka waende 

kuzungumza katika chumba cha 

mazungumzo ya faragha 

“Mheshimiwa balozi,naamini 

kuna jambo lililokuleta hapa 

mchana huu.Ujumbe gani 

umeniletea? 

“Mheshimiwa rais nimetumwa 

kwako kama muwakilishi wa taifa 

la Marekani hapa Tanzania na raia 

wote wanaoingia na walioko hapa 

nchini wote wako chini 

yangu.Nimepigiwa simu na ndugu wa mtu aitwaye Nathan ambaye 

nimeambiwa ni mchumba wako na 

mko katika maandalizi ya kufunga 

ndoa.Ndugu hao wanadai kwamba 

Nathan aliondoka na kuja 

Tanzania siku mbili zilizopita na 

alifika hapa wa kutumia ndege ya 

kaka yake ambaye ni mchezaji 

maarufu na tajiri wa mpira wa 

kikapu.Alipofika aliwajulisha 

ndugu zake kwamba amefika 

salama Tanzania na toka wakati 

huo hawajawasiliana tena.Hii 

imewapa wasiwasi mkubwa ndugu 

zake na wamejaribu kumtafuta 

sana kwa njia ya simu au mtandao 

bila mafanikio ndipo walipoamua 

kunijulisha mimi kama 

muwakilishi wa wamarekani walioko hapa Tanzania ili niweze 

kusaidiana na serikali ya Tanzania 

kumtafuta.Hii si kawaida yake 

kutokuwasiliana na ndugu zake. 

Kwa bahati mbaya Nathan 

hakufika ubalozini kutoa taarifa za 

kufika kwake hivyo sina taarifa 

zake na mimi kama kiongozi wa 

wamarekani hapa nchini ni 

jukumu langu kujua na 

kuhakikisha wamarekani wote 

wanaoishi au kutembelea hapa 

Tanzania wako salama hivyo 

Nathan kama raia wa Marekani ni 

jukumu langu kufahamu mahala 

alipo na kama yuko salama” 

akanyamaza kidogo halafu 

akasema“Mheshimiwa rais 

nimelazimika kuja kwanza hapa 

kwako kutokana na mahusiano 

yako na Nathan ambaye ni 

mchumba wako na mnatarajia 

kufunga ndoa hivi karibuni hivyo 

kama amekuja Tanzania ni wazi 

alikuwa amekuja kwako kwani 

hana shughuli nyingine inayoweza 

kumleta Tanzania zaidiya 

kukufuata wewe mchumba wake 

hivyo kamaanakuja Tanzania 

lazima akujulishe. Nataka 

kufahamu mheshimiwa rais 

,Nathan yuko wapi? Yuko 

salama?akauliza balozi Abraham 

.Dr Vivian akatazamana balozi kwa 

muda akatabasamu na kusema “Kwanza naomba 

nikufahamishe mheshimiwa balozi 

kwamba mimi na Nathan kwa sasa 

hatuna mahusiano tena.Tayari 

tumekwisha tengana na hata ile 

ndoa tuliyotegemea kuifunga 

haipo tena.Sielewi kwa nini 

amewaficha ndugu zake jambo 

hili” 

“Mmetengana? Toka lini? 

Akauliza balozi Abraham 

“Sitaki kuingia ndani zaid 

kuhusiana na jambo hilo ila itoshe 

tu kufahamu kwamba mimi na 

Nathan hatuna tena mahusiano 

.Hakuna tena ndoa.Kuhusu kuja 

Tanzania sina taarifa hizo na 

sijawasiliana naye na hakuwa na 

sababu ya kunijulisha kama anakuja Tanzania wakati sina 

mahusiano naye tena.Kama alikuja 

Tanzania basi ni kwa shughuli 

zake binafsi na si kwamba 

amenifuata mimi” 

“Mheshimiwa rais,halitakuwa 

jambo rahisi kuwaeleza hivyo 

ndugu zake.Nathan hana shughuli 

yoyote ya kumleta Tanzania zaidi 

ya kukufuata wewe mpenzi wake” 

“Mheshimiwa balozi,nadhani 

unanifahamu nilivyo,sina tabia ya 

kurudia rudia jambo moja mara 

mbili.Nimekwisha sema kwamba 

sina mawasiliano wala mahusiano 

na Nathan kwa sasa na taarifa za 

yeye kuwepo Tanzania ninazisikia 

kwa mara ya kwanza sasa hivi toka 

kwako.Amekuja kutafuta nini Tanzania wakati mimi na yeye 

hatuna mawasiliano? Lazima na 

mimi nifahamu alichokuja 

kukifanya Tanzania na kama 

sintopata sababu ya msingi ya yeye 

kuja nitampiga marufuku 

asikanyage ardhi ya 

Tanzania.Sitaki atumie ukaribu 

wangu naye kwa mambo yake 

binafsi!! Akasema Dr Vivian kwa 

ukali 

“Mheshimiwa rais ,kama 

unakiri huna taarifa zozote za 

kumhusu Nathan basi naomba kwa 

kutumia vyombo vyako mtu huyu 

atafutwe kokote aliko ili serikali 

ya Marekani iwe na uhakika 

kwamba mtu wao yuko 

salama.Wewe kama rais unao wigo mpana zaidi wa kuweza kupata 

kwa haraka taarifa za kumuhusu 

mtu yeyote yule.Ni hicho tu 

tunachokuomba mheshimiwa rais” 

“Kama mna uhakika Nathan 

alikuja Tanzania basi nitaagiza 

vyombo husika vifanye uchunguzi 

na kufahamu yuko wapi” 

“Saa ngapi nitegemee majibu 

mheshimiwa rais? 

“Siwezi kukupa muda 

balozi.Pale vyombo vyangu 

vitakaponipa mrejesho 

nitakujulisha” 

“Mheshimiwa rais ningependa 

suala hili lisichukue muda mrefu 

,naomba ndani ya saa kumi na 

mbili toka sasa niwe nimepata 

majibu” “Na kama usipopata majibu 

katika muda huo utafanya nini? 

Akauliza Dr Vivian kwa ukali 

“Nina uhakika mkubwa 

kwamba ndani ya muda huo lazima 

majibu yatakuwa yamepatikana 

kuhusu aliko Nathan.Tanzania ina 

vyombo mahiri vya uchunguzi 

lakini endapo utapita muda huo 

bila kupata jibu lolote tutalazimika 

kuleta watu wetu kuja kufanya 

uchunguzi ili tufahamu mtu wetu 

aliko.Raia wa Marekani akipotea 

katika nchi ya kigeni kila juhudi 

itafanyika kuhakikisha 

anapatikana akiwa hai au amekufa 

na ndivyo tutakavyofanya kwa 

Nathan.Kama sintapata mrejesho 

toka kwako basi lazima watakuja hapa watu wetu kuchunguza na 

kufahamu aliko Nathan” 

Maneno yale ya balozi 

Abraham Clerk yakaonekana 

kumkera sana Dr Vivian akainuka 

akamsogelea balozi Abraham. 

“Nisikilize vizuri balozi,mimi 

huwa sitishwi na binadamu 

anayevuta pumzi kama 

mimi.Namuogopa Mungu pekee 

anayenipa pumzi.Hakuna mtu 

yeyote wa Marekani atakayeingia 

hapa nchini kufanya uchunguzi wa 

kumtafuta huyo Nathan.Mimi 

ndiye mkuu wa nchi hii na neno 

langu ni la mwisho!! 

“Nimekueelwa mheshimiwa 

rais.Mimi naondoka ila nitasubiri 

simu yako na muda ninaanza kuuhesabu sasa” akasema balozi 

Abraham na kusimama akaondoka 

“ Mathew na Theresa 

wameiiniza tena katika matatizo 

mengine makubwa ambayo sikuwa 

nimeyategemea.Walifanya kosa 

kubwa kumuua Nathan na hawa 

jamaa tayari wamekwisha fahamu 

kwamba Nathan ameuawa lakini 

wanahitaji wathibitishe kama 

kweli amekufa ama 

la.Wakifanikiwa kulithibitisha hilo 

utakuwa ni mgogoro mwingine 

mpya.Sasa nimeona umuhimu wa 

kile alichokuwa anakisema 

Mathew kwamba jambo hili libaki 

siri na lisifahamike.Nadhani hiyo 

ndiyo njia pekee ya kuepusha mgogoro na Marekani.Kifo cha 

Nathan kitaendelea kuwa siri” 




Ilimlazimu Mathew kumuita 

Hamis Chuma nyumbani kwake ili 

amsaidie kulikata kasiki 

walilolitoa nyumbani kwa George 

Mzabwa.Hamis na vijana wake 

wawili walifika kwa wakati na 

wakaanza zoezi la kulikata lile 

kasiki.Iliwachukua zaidi ya saa 

moja kulikata na hatimaye 

wakafanikiwa.Mathew akawalipa 

ujira wao wakaondoka 

“Ni muda wa kufahamu 

ukweli” akasema 

Mathew.Hakukuwa na fedha ndani 

ya lile kasiki kama alivyosema mke 

wa George bali kulikuwa na mafaili 

mawili yenye nyaraka mbali mbali halafu kukawa na simu ambayo 

alipoichunguza akagundua 

kwamba haikuwa na laini ndani 

“Mjanja sana huyu .Simu hii 

ameitoa laini na hii inaonyesha 

kwamba ilikuwa na umuhimu 

kwake na ndiyo maana akaja 

kuificha huku” Akasema Mathew 

na kulifungua faili la kwanza 

akaanza kulipitia nyaraka 

zilizomo.Kulikuwa na risiti kadhaa 

za benki zikionyesha tarehe tofauti 

ambazo George alitoa fedha .Kila 

risiti ilionyesha kiasi kikubwa cha 

fedha .Hakuna risiti iliyoonyesha 

chini ya milioni mia moja.Pesa hizo 

zote alizitoa katika akaunti ya 

benki moja iliyoko kwenye benki 

ya Escom tawi la Tanzania. “Pesa nyingi sana hizi.Kwa 

hesabu za haraka haraka 

inaonyesha fedha hizi si chini ya 

milioni mia tano.George alikuwa 

na biashara gani ya kumuingizia 

kiasi kikubwa namna hii cha 

fedha? Akajiuliza Mathew na 

kuendelea kupekua nyaraka 

nyingine mbali mbali.Katika faili la 

pili akakuta risiti tatu zikionyesha 

George aliweka fedha katika 

kampuni tatu tofauti zote zikiwa 

katika benki ya Escom. 

“Risiti zinaonyesha kwamba 

George alitoa kiasi kikubwa cha 

fedha katika akaunti moja na kisha 

akaweka tena fedha katika akaunti 

tatu tofauti zilizo katika benki hii 

ya Escom.George ni mtumishi wa umma,anafanya biashara gani ya 

kumuwezesha kuwa na fedha 

nyingi kiasi hiki?Kuna risiti zaidi 

ya tano hapa na hakuna hata risiti 

moja inayoonyesha alitoa chini ya 

shilingi milioni mia moja.Nadhani 

tuchunguze hii akaunti ni ya 

nani.Siamini kama akaunti hii ni ya 

George.Kama ni yake basi 

tufahamu anafanya biashara gani 

hadi awe na fedha nyingi kiasi 

hiki.Vile vile tuchunguze na zile 

akaunti nyingine ambazo risiti 

zinaonyesha kwamba aliweka 

fedha” akasema Mathew halafu 

akachukua simu akampigia 

Theresa akamjulisha 

walichokikuta katika kasiki “Ahsante kwa taarifa Mathew” 

akasema Theresa na Mathew 

akagundua kitu katika sauti yake 

“Theresa una tatizo lolote? 

“Mathew kuna jambo sikuwa 

nimekueleza.Dada ameonyesha 

wazi kwamba amekasirishwa na 

kile nilichoikifanya kuhusu Nathan 

na hanihitaji tena.Ameanza 

kuniondoa taratibu ikulu karibu 

yake” 

“Amekuondoa ikulu? Kivipi? 

Mathew akauliza 

“Ametafuta mtu mwingine wa 

kushika nafasi yangu na kesho 

asubuhi amenitaka niwahi 

nikamkabidhi ofisi” 

“Amepata mtu mwingine wa 

kumuandikia hotuba? “Hajasema hivyo lakini huyo 

mtu aliyemtafuta ataitumia ofisi 

yangu” 

“Theresa bado sijakuelewa 

vizuri.Kama rais hajatamka 

kwamba anakuondoa katika nafasi 

yako kwa nini uwe na wasi wasi? 

“Amenipigia simu akaniambia 

kwamba ananihitaji kesho asubuhi 

nifike ikulu nimkabidhi ofisi mtu 

mpya na kumuelekeza mambo 

kadhaa ya pale ofisini.Ameniambia 

mtu huyo anaitwa Tausi Mubara 

mtoto wa marehemu Anorld 

Mubara.Kuna ofisi nyingi pale 

ikulu ambazo angeweza kumpa 

huyu mtu wake azitumie lakini 

ameacha zote na kuchagua ya kwangu.Hii ni dalili tosha kwamba 

hanitaki tena” 

“Umeseema amempa kazi 

mtoto wa rais Anorld Mubara? 

Mathew akauliza 

“Ndiyo.Anaitwa Tausi” 

“Usiogope 

Theresa,hakutakuwa na tatizo 

lolote.Dr Vivian hawezi kutafuta 

mbadala wako kwani wewe ni 

mwandishi mahiri sana wa hotuba 

.Fanya kama alivyokuelekeza 

.Halafu kesho nitaomba msaada 

wako nataka kufuatilia hizi 

akaunti katika benki ya Escom 

kufahamu ni za nani” 

“Sawa Mathew,nikitoka ikulu 

tutakwenda kufanya hiyo kazi” 

akasema Theresa wakaagana “Nini kinafuata baada ya 

hapa? Camilla akauliza 

“Kilichopo mezani kwa sasa ni 

kuhusu George.Tunapaswa 

kumchunguza kufahamu hizi 

akaunti za benki ni zake ama za 

nani.Kama ni zake tufahamu 

ametoa wapi pesa nyingi namna 

hii” 

“Hilo ni wazo zuri lakini bado 

haitoshi.Ni vipi endapo atakuwa na 

biashara zake anafanya zenye 

kumuingizia kiasi hicho kikubwa 

cha fedha?Katika kulipitia faili hili 

nimegundua kwamba kuna risiti 

zinaonyesha kwamba wiki 

iliyopita amelipia makontena 

mawili bandarini ambayo 

yalikuwa na mzigo wa baiskeli.Najiuliza mtu kama huyu 

ambaye risiti zinaonyesha kwamba 

ametoa mamilioni ya fedha benki 

ameagiza kontena mbili za baiskeli 

kwa dhumuni gani? Ana duka la 

kuuza baiskeli?Hata kama akiuza 

kontena hizo mbili zilizojaa 

basikeli haziwezi kumpatia kiasi 

kikubwa namna ile cha fedha 

tulichokiona katika risiti.Kitu 

kingine cha kujiuliza kwa nini 

afiche risiti hizi huku ? Kama ana 

biashara ya basikeli kwa nini risiti 

hizi asigeziweka nyumbani 

kwake?Hapa kuna jambo 

limejificha? 

“Ahsante Camilla kwa kuliona 

hilo mimi nimepitia kwa haraka 

haraka na sikutilia maanani suala hilo.Kama unavyosema hapa kuna 

jambo.Nadhani tufuatilie kontena 

hizi zilikwenda wapi ili 

tujiridhishe kama kweli kontena 

hizi zilikuwa na 

baiskeli.Yawezekana labda kuna 

mambo mengine tukayagundua 

anayoyafanya George.Kwa kuwa 

leo ofisi nyingi zimefungwa 

itatubidi kazi hiyo tuifanye 

kesho.Kwa muda huu wa siku 

uliobaki tupate chakula tupumzike 

tujiandae kwa siku ya kesho 

ambayo naamini itakuwa ndefu 

sana.Wewe utaendelea kupumzika 

na mimi nitaelekea kuangalia 

maendeleo ya ujenzi wa kiwanda” 

“Hujaweka mkandarasi? “Mkandarasi yupo lakini 

lazima na mimi nifuatilie kwa 

karibu maendeleo ya mradi kuona 

kama mambo yanakwenda sawa.” 

Akasema Mathew 

********************** 

Mlango wa chumba cha 

Mathew uligongwa taratibu na 

Mathew ambaye tayari alikwisha 

pitiwa na usingizi akastuka toka 

usingizini na kitu cha kwanza 

alichokifanya ni kupeleka mkono 

wake ilipo bastora yake ambayo 

huiweka pembeni.Akatazama saa 

ilikuwa ni saa tano na dakika kumi 

na saba za usiku.Mlango ukagonwa 

tena ,akainuka akachukua bastora na kuelekea 

mlangoni.Akachungulia katika 

kitobo kidogo cha kumuwezesha 

kuona mtu aliyeko nje akamuona 

Camilla 

“Camilla anatafuta nini hapa 

muda huu? Akajiuliza na kufungua 

mlango 

“Camilla!! Akasema Mathew 

“Mathew samahani kwa 

kukuamsha mida hii” akasema 

Camilla akiwa na kompyuta yake 

mkononi 

“Usijali Camilla.Karibu” 

akasema Mathew na kumkaribisha 

Camilla chumbani kwake 

“Hujalala mpaka mida hii? 

Mathew akauliza “Mimi hulala saa mbili au tatu 

pekee na muda wote huwa nafanya 

kazi.Tulipoachana wewe ukaja 

kupumzika ,mimi nimeendelea na 

kazi.Nilikuwa nachunguza hii 

benki ya Escom” 

“Umegundua nini kuhusu 

benki hii? 

“Nimegundua kwamba awali 

benki hii ilikuwa inamilikiwa na 

tajiri mmoja wa kifaransa na 

ilikuwa inajulikana kama Pazera 

commercial bank .Baada ya tajiri 

huyo kufariki watoto wake 

wakaiuza benki hiyo kwa tajiri 

mwingine aliyewekeza sana nchini 

Ufaransa anaitwa Andrew Pillar” 

“Andrew Pillar?!! Mathew 

akashangaa “Ndiyo. Andrew Pillar.Huyu 

ndiye aliyeinunua hii benki na 

kuibadili jina ikaitwa Escom bank” 

“Namfahamu Andrew ni baba 

mzazi wa Anderson Pillar 

aliyevunja ndoa yangu na 

Peniela.Sikujua kama Andrew 

ndiye mmiliki wa hii benki.Ama 

kweli dunia ni kijiji” akasema 

Mathew. 

“Sikuishia hapo” akasema 

Camilla 

“Nimeendelea kuichunguza 

zaidi nikagundua kwamba katika 

benki hii kuna wanahisa wengine 

ambao niAnderson Pillar na 

Peniela Mwaulaya” 

“Peniela?! Akauliza Mathew 

kwa mshangao mkubwa “Ndiyo.Naye ni mmoja wa 

wamiliki wa hii benki.Anamiliki 

asilimia thelathini na tano ya mtaji 

wa hii benki” 

“Umewezaje kuyafahamu haya 

yote? Mathew akauliza 

“Mimi ni mdukuaji mkubwa 

sana na hata FBI wamekuwa 

wananitumia sana kudukua taarifa 

mbalimbali.Ninaweza kuingia 

katika mtandao wowote ule na 

kuchukua taarifa 

ninayoitaka.Nimeweza kuingia 

katika mtandao wa benki hii na 

kupata taarifa hizi 

zote.Nimekwenda mbali zaidi na 

kugundua kwamba akaunti ile ya 

benki inayoonyesha George alitoa 

fedha ilifunguliwa nchini marekani na Geroge mwenyewe na kwa mara 

ya mwisho kiasi cha shilingi za 

kitandania milioni mia saba na 

sabini ziliwekwa katika akaunti 

hiyo kutoka kwa kampuni ya 

kutengeneza saa za mkononi ya 

Flamingo.Nilichunguza tena 

kampuni hii ya Flamingo 

nikagundua nikampuni pacha na 

A.D Electronics kwani mmiliki 

wake ni mmoja lakini kama 

unavyofahamu kwamba A.D 

Electronics ni kampuni iliyo chini 

ya serikali ya Marekani kupitia 

shirika lake la ujasusi la CIA kwa 

hiyo hata hii kampuni ya saa ya 

Flamingo nayo vile vile iko chini ya 

serikali ya Marekani kwa siri” 

akasema Camilla “Nimechimba zaidi” 

akaendelea 

“Nimegundua kwamba George 

alitoa fedha nyingi katika akaunti 

yake na kuziweka katika akaunti 

tatu tofauti.Nimezifuatilia akaunti 

zile nimegundua kwamba zote tatu 

ni za kampuni ya kuchonga madini 

ya vito ambayo mkewe Herieth 

Mzabwa ni mkurugenzi” 

Usowa Mathew ulionyesha 

mshangao 

“Camilla una uhakika na hayo 

unayonieleza? Akauliza 

“Asilimia mia moja nina 

uhakika nayo.Nina utaalamu wa 

hali ya juu wa kufanya udukuzi 

kama nilivyokueleza” “Herieth 

ametudanganya.Anafahamu kila 

kitu kuhusu mumewe.Ahsante 

sana Camilla kwa kazi hii kubwa 

uliyoifanya ambayo imetupa 

mwanga katika uchunguzi 

wetu.Nimestushwa sana kusikia 

kwamba Peniela ni mwanahisa 

katika benki ambayo imetumika 

kupitishia fedha ambazo naweza 

kuziita ni chafu ambazo 

zinatumika kufanikisha 

operesheni mbali mbali za 

Marekani hapa Tanzania.Kwa 

kifupi naweza kusema kwamba 

Escom bank inatumiwa au 

inashirikiana na CIA.Nina wasi 

wasi yawezekana hata Anderson 

na baba yake Andrew Pillar wote wakawa ni CIA na wanatumia 

benki yao kwa ajili ya shughuli 

mbali mbali za siri za CIA.Wafanyie 

uchunguzi hawa watu wawili 

Anderson na baba yake li tujue 

kama nao pia ni CIA” akasema 

Mathew 

“Kwa sasa sina mtu ndani ya 

CIA anayeweza kunipa msaada 

wowote.Kuna njia moja tu ya 

kuufahamu ukweli ambayo sina 

hakika kama utaipenda lakini 

ndiyo pekee inayoweza kutusadia 

kuwafahamu hawa watu wawili ni 

akina nani.” Akasema Camilla 

“Niambie Camilla ni njia ipi? 

“Ni kumtumia Peniela” 

“Peniela amezama katika 

mapenzi mazito na Anderson na sina hakika kama anaweza 

kukubali kunisaidia kumchunguza 

mpenzi wake” 

“Yawezekana hafahamu 

ukweli wa jambo hili.Mpigie simu 

uzungumze naye anaweza 

akatusaidia na hata mwenyewe pia 

itamsaidia kama akimfahamu 

mpenzi wake vyema” akasema 

Camilla.Mathew akachukua simu 

na kuzitafuta namba za Peniela 

akataka kupiga akasita 

“Piga Mathew” Camilla 

akasisitiza.Mathew akabonyeza 

sehemu ya kupigia na simu 

ikaanza kuita.Simu iliita bila 

kupokelewa 

“Hawezi kupokea muda 

huu”akasema Mathew na mara simu yake ikaanza kuita,alikuwa ni 

Peniela aliyempigia,akaipokea 

haraka haraka 

“Mathew mbona umepiga 

usiku mwingi namna hii? 

“Samahani Peniela kwa 

usumbufu.Uko na mumeo? 

“Ndiyo niko naye ila 

nimelazimika kutoka chumbani na 

kuja kuzungumza nawe huku 

mbali kwani akifahamu kama 

umenipigia muda huu utaibuka 

ugomvi,ana wivu sana Anderson.” 

“Samahani sana Peniela kwa 

kukusumua usiku huu,si lengo 

langu kukuletea matatizo katika 

maisha yako na mpenzi lakini 

nimekupigia mida hii kwa sababu 

nahitaji msaada wako” “Msaada wangu? 

“Ndiyo.Unakumbuka ulikuwa 

unaniuliza kama kuna chochote 

unaweza kunisaidia? Basi nahitaji 

sasa msaada wako” akasema 

Mathew na Peniela akasikika 

akishusha pumzi 

“Mathew muda huu si mzuri 

kuzungumza mambo 

hayo.Nitakupigia simu mimi 

mwenyewe kesho asubuhi na 

tutazungumza utanieleza unahitaji 

msaada gani na kama ni jambo 

lililo ndani ya uwezo wangu 

nitakusaidia” akasema Peniela na 

kukata simu 

“Mathew usiogope kumuomba 

msaada.Nina hakika hafahamu 

chochote kuhusu huyo mpenzi wake na baba yake” akasema 

Camilla 

“Wakati tunamsubiri Peniela 

kesho asubuhi,usiku huu lazima 

operesheni iendelee.Mke wa 

George kuna mambo anayafahamu 

lazima tumfuate na atupe majibu 

kuhusiana na mumewe” akasema 

Mathew na kumtaka Camilla 

akajiandae waelekee kwa Herieth 

Mzabwa mke wa George.Wakati 

Camilla akijiandaa Mathew 

akampigia simu Theresa 

akamjulisha kila kitu 

walichokigundua na kumtaka 

naye ajiandae kwani wanakwenda 

wote nyumbani kwa Herieth 

“Kwa nini Herieth akaamua 

kutudanganya ? Ni wazi hakutaka tuufahamu ukweli ndiyo maana 

akaamua kutuambia uongo.Usiku 

wa leo utabaki wa kihistoria 

kwake kwa yale atakayokutana 

nayo” akawaza Mathew huku 

akiendelea kujiandaa.Walipokuwa 

tayari wakaingia garini na 

kuondoka wakaelekea kwanza 

kwa Theresa kabla ya kwenda kwa 

Herieth

******************* 

Watu wachache tu waliokuwa 

macho wakati akina Mathew 

walipowasili nyumbani kwa 

Herieth Mzabwa.Kulikuwa na 

ulinzi wa askari polisi kufuatia 

tukio lililotokea mchana .Akina 

Mathew wakajitambulisha kwa 

askari polisi wale na 

wakaruhusiwa kuingia 

ndani.Mathew akamtaka Theresa 

ashuke amfuate Herieth ndani na 

amdanganye kwamba kuna 

mamilioni ya fedha wameyakuta 

katika kasiki hivyo anahitajika 

akayachukue.Theresa akaingia 

ndani na baada ya kama dakika 

kumi akarejea akiwa 

ameongozana na Herieth 

akamfungulia mlango akaingia 

garini wakaondoka. “Habari za usiku huu Herieth? 

Akauliza Mathew aliyekuwa katika 

usukani.Herieth akastuka 

“Unanifahamu jina langu? 

“Ndiyo” akajibu Mathew na 

safari ikaendelea kimya kimya 

“Tunakwenda wapi? Herieth 

akauliza 

“Theresa hajakueleza 

chochote? 

“Ameniomba tuongozane 

tukaone kilichokuwamo ndani ya 

kasiki” akasema Herieth 

“Ndiyo tunakwenda 

huko.Samahani kwa kukusumbua” 

“Bila samahani”akajibu 

Herieth halafu kukawa kimya 

safari ikaendelea hadi walipofika nyumbani kwa Mathew,wote 

wakashuka na kuingia ndani 

“Herieth karibu sana.Ahsante 

kwa kukubali kuongozana nasi 

kuja huku usiku huu.Nitakuwa na 

maneno machache sana ya kusema 

kwani tayari ni usiku na unahitaji 

kwenda kupumzika” akasema 

Mathew na kuingia chumbani 

akarejea akiwa na mafaili mawili 

akayaweka mezani 

“Tumefanikiwa kulifungua lile 

kasiki lakini hatujakuta fedha 

kama tulivyokueleza” Akasema 

Mathew akamstua Herieth 

“Hamjakuta fedha? Akauliza 

“Ndiyo.Hakukuwa na fedha 

zozote bali tumekuta vitu vichache 

tu.Cha kwanza ni hii simu lakini kwa bahati mbaya haina laini na 

hatujafanikiwa kupata chochote 

ndani yake.Kingine tumekuta 

mafaili hayo mawili yenye nyaraka 

mbali mbali.Baada ya kuchambua 

nyaraka zilizomo tumekutana na 

risiti hizi za benki” akazichukua 

risiti zile na kumuonyesha Herieth 

“Risiti hizo zinaonyesha 

kwamba kwa nyakati tofauti 

George alitoa kiasi kikubwa cha 

fedha katika akaunti iliyoko benki 

ya Escom.Risiti nyingine 

zinaonyesha pia kwamba kwa 

nyakati tofauti George aliweka 

fedha katika akaunti tatu tofauti 

zilizopo katika benki hiyo ya 

Escom.Tunataka utuambie je 

akaunti hii ya mumeo unaifahamu? Akauliza Mathew na Herieth 

akazitazama zile risiti na kusema 

“Hapana siifahamu akaunti 

hii.Nimestuka sana kwa jambo 

hili.George hakuwahi kunieleza 

chochote kuhusiana na kuwa na 

akaunti katika hii 

benki.Ninazifahamu akaunti tatu 

alizonazo katika benki mbali mbali 

na zile ambazo tumewafungulia 

watoto wetu na hazina kiwango 

kikubwa cha fedha kama hiki 

kinachoonyeshwa katika risiti 

hizi.Hatuna biashara au mradi 

wowote mkubwa kutuwezesha 

kuwa na kiasi kikubwa namna hii 

cha fedha.Sikujua kama George 

kuna mambo ananificha” akasema 

Herieth akionekana kushangazwa na risiti zile.Mathew akamtazama 

kwa makini sana na kuuliza 

“Hizo akaunti tatu ambazo 

George aliweka fedha kwa nyakati 

tofauti na zote ziko katika benki 

hii ya Escom.Unazifahamu? 

Herieth akazipitia zile risiti 

kwa makini na kutikisa kichwa 

“Hapana sizifahamu akaunti 

hizi” 

“Una hakika Herieth? Theresa 

akauliza 

“Kama nilivyowaeleza 

kwamba jambo hili ni geni kwangu 

na George hakuwahi kunieleza 

chochote.Alinificha mambo haya 

yote.Kama ningefahamu moja 

wapo ya hizi akaunti ningewaeleza” akasema Herieth. 

Mathew alionyesha kukasirika. 

“Sikiliza Herieth,naomba 

utueleze ukweli.Una hakika 

hauzifahamu hizi akaunti?Una 

hakika George hakuwahi 

kukushirikisha katika hizi fedha? 

Akauliza Mathew 

“Jamani nimekwisha waeleza 

kwamba sifahamu chochote 

kuhusiana na hizi fedha wala 

akaunti hizi.Mambo haya yote 

nimeyafahamu sasa hivi 

kwenu.George alikuwa ananificha 

mambo yake mengi ya siri” 

“Herieth unafanya kazi gani 

na wapi? Mathew akauliza 

“Mimi? Herieth akauliza “Ndiyo.Unafanya kazi gani na 

wapi?Mathew akarudia swali 

“Ninafanya kazi Tanbest 

Gemstone” akasema Herieth huku 

sauti yake ikionyesha kitetemeshi 

“Unafanya kazi gani katika 

kampuni hiyo? 

“Mimi ni mkurugenzi.Kwani 

vipi? Akauliza Herieth akionekana 

kustushwa sana na kuulizwa kazi 

yake 

“Herieth mimi na wenzangu 

hawa unaotuona hatulali 

tukipambana kwa ajili ya 

kuhakikisha nchi inakuwa salama 

kwa hiyo pale anapotokea mtu au 

kikundi cha watu wakawa kikwazo 

katika kufanikisha majukumu 

yetu,huwa tunakuwa wakatili sana” akasema Mathew huku 

akimtazama Herieth kwa macho 

makali na kumuogopesha 

“Tumegundua unatudanganya 

na umetuudhi 

sana.Umetulazimisha tuvae sura za 

kazi na endapo utaendelea 

kutudanganya yawezekana 

usilione jua la kesho” 

Kauli ile ikamuogopesha sana 

Herieth midomo ikamtetemeka 

“Narudia tena kukuuliza 

Herieth hizi akaunti unazifahamu? 

Herieth hakujibu kitu 

akatazama chini 

“Ninaomba jibu 

Herieth,unazifahamu hizi akaunti? 

Mathew akauliza kwa sauti ya juu “Sizifahamu” akajibu .Mathew 

akamtazama na kushusha pumzi 

“Sikiliza Herieth,tayari 

tunafahamu kila kitu ila tunakata 

tufahamu zaidi toka kwako ila 

umeamua kutudanganya 

.Tunafahamu akaunti ile ambayo 

mumeo alitoa fedha ni ya kwake 

.Mumeo alilipwa fedha nyingi toka 

kampuni ya Flamingo 

inayotengeneza saa za 

mkononi.Baada ya kulipwa fedha 

hizo akazitoa na kuziweka katika 

akaunti tatu tofauti za kampuni ya 

Tanbest ambayo wewe unafanya 

kazi kama mkurugenzi.Herieth 

naomba niwe wazi kwako kwamba 

hapa hauna ujanja na 

kitakachokuokoa ni kusema ukweli.Nataka kufahamu 

mahusiano ya George na hii 

kampuni ya Flamingo.Kwa nini 

fedha iwekwe katika akaunti yake 

halafu ihamishwe na kuwekwa 

katika akaunti za kampuni 

yenu?akauliza Mathew 

“Mimi sifahamu chochote 

kuhusiana na masuala ya fedha za 

kampuni yetu” 

“Herieth unazidi 

kuniudhi.Tafadhali nieleze ukweli 

ama sivyo nitakuharibu sura 

yako.Sitaki kukupa maumivu 

mengine hasa kwa wakati huu 

unaoendelea kumlilia mumeo” 

“Kweli sifahamu chochote 

kuhusiana na hizi fedha za kampuni wala mahusiano ya 

George na kampuni unayoisema” 

“Muda wa mchezo 

umekwisha” akasema Mathew na 

kuinuka akaenda chumbani kwake 

na kurejea na kisanduku kidogo 

akatoa kifaa fulani kidogo mithili 

ya mashine ya kunyolea nywele 

akakichomeka katika umeme 

kikatoa cheche 

“Huu ni umeme na endapo 

hautakuwa tayari kusema ukweli 

nitakuchoma na umeme utasikia 

maumivu makali mwili 

mzima,utatamani roho ikutoke 

lakini hautakufa bali utahisi 

maumivu kama uko 

jehanamu.Sitaki kufika huko 

naomba unieleze ukweli ili ujiepushe na mateso makali.Najua 

unaufahamu ukweli ila unatuficha” 

akasema Mathew 

“Jamani mtaniumiza bure 

mimi sifahamu chochote.Japokuwa 

ni mkurugenzi lakini jambo hili 

silifahamu kabisa.Naomba 

mniamini.Kama ningetaka 

kuwaficha jambo nisingekubali 

kuwapeleka mahala mume wangu 

anakoficha siri zake.Naomba 

mniamini jamani sifahamu 

chochote” 

Mathew akampa ishara 

Camilla ambaye kwa kasi ya aina 

yake akaikamata mikono ya 

Herieth akaifunga kamba na 

Mathew akakiwasha kifaa kile na 

kukigusisha katika ngozi ya Herieth ambaye alipiga ukelee 

mkubwa sana. 

“Nadhani sasa umeyaona 

maumivu yake na hapa ni mwanzo 

tu,nitakuwa naongeza chaji kila 

wakati hadi utakaposema ukweli” 

akasema Mathew 

Huku akitetemeka mwili na 

machozi kumtoka,Herieth 

akasema 

“Mtaniua bure jamani 

sifahamu choch……” Kabla 

hajamaliza sentensi yake Mathew 

akakiweka tena kila kifaa mguuni 

na Herieth akapiga kelele 

“Sema ukweli!! Akafoka 

Mathew 

“S..ss..sss..ifa..sffaaham….” 

“Mathew !! akaita Camilla

 “Huyu hatatueleza 

chochote.Naomba unipe dakika 

tatu tu nimfumbue 

mdomo.Hatuwezi kupoteza muda 

kwa mtu mmoja” akasema Camilla 

na kumfungua Herieth mikono 

halafu akafungua kiboksi kile cha 

Mathew alichokiweka mezani 

akatoa kifaa kidogo kwa ajili ya 

kushikia vitu vidogo kijulikanacho 

kama koleo akamfuata Herieth na 

kumnasa kibao 

“Nitazame usoni !! akasema 

kwa ukali na kumuinua Herieth 

kichwa 

“Nimepewa dakika tatu tu za 

kumaliza kiburi chako.Nataka 

kabla ya muda huo kuisha utueleze 

ukweli.Kabla sijaanza kukuharibu naomba utupe ukweli!!! Akasema 

Camilla lakini Herieth hakufumbua 

mdomo 

“Nitahesabu sekunde tano 

ufumbue mdomo wako na kusema 

ukweli !! akasema Camilla na 

kuanza kuhesabu sekunde na 

zilipotimu sekunde tano bila 

Herieth kufumbua mdomo,mara 

ghafla kwa kasi ya umeme Camilla 

akaukamata mkono wake wa 

kushoto na kukikamata kidole 

kidogo cha mwisho kwa kutumia 

ile koleo na mlio wa kitu kigumu 

kuvunjika ukasikika.Alikuwa 

amekikata kidole .Akawahi 

kumziba Herieth mdomo asipige 

kelele “Huu ni mwanzo tu na kama 

hautatueleza tunayoyataka ndani 

ya dakika tatu nitamaliza vidole 

vyako vyote !! akasema Camilla 

kwa ukali.Damu nyingi ilikua 

inatoka kwenye jereha .Theresa 

aliyekuwa pembeni akishuhudia 

kilichokuwa kinaendelea mle 

ndani akaogopa sana.Camilla 

akaukamata tena kwa nguvu 

mkono wa Herieth alioukata 

kidole na kukibana kidole cha pili 

“Basi !! basi !!! nitasema..” 

akasema Herieth kabla Camilla 

hajakuondoa kile kidole 

alichokuwa anajiandaa kukikata 

“Nitasema !!..Nitasema !! 

akasema Herieth huku 

akiweweseka.Mathew akachukua dawa na kumwagia lile jeraha na 

kulifunga damu isiendelee kutoka 

“Haya tueleze” akasema 

Camilla.Herieth akafuta machozi 

akasema 



“Kampuni yetu na kampuni ya 

Flamingo ni washirika wa biashara 

.Tunawauzia madini ya vito kwa 

ajili ya kutengenezea saa za 

thamani.Kuhusu masuala ya fedha 

mimi sifahamu chochote kwani 

mimi kazi yangu ni usimamizi tu 

na sishiriki kabisa na masuala 

yoyote ya kifedha.George na 

mkurugenzi mkuu ni marafiki na 

ndiyo maana ilikuwa rahisi mimi 

kupata kazi katika hii kampuni ila 

sifahamu kuhusiana na hayo 

masuala ya fedha” “Mkurugenzi wako mkuu 

anaitwa nani? Mathew akauliza 

“Anaitwa Ranbir Kumar .Huyu 

ndiye anayeweza kuwaeleza kila 

kitu kuhusiana na fedha na 

chochote mtakachohitaji 

kufahamu kuhusu hii kampuni” 

akasema Herieth 

“Unatupeleka sasa hivi mahala 

anakoishi huyo mkurugenzi wako” 

“Sifahamu anakoishi “ 

akasema Herieth .Kwa kasi ya aina 

yake Camilla akaushika mkono wa 

Herieth na kukibana kidole kimoja 

kwa koleo.Herieth akapiga kelele 

akitaka Camilla asimkate kidole 

“Msiniumize jamani.Kweli 

sifahamu nyumbani kwa Ranbir 

labda naweza kuwasaidia mkaonana naye.Nitampigia simu 

na kumjulisha kwamba nina tatizo 

na atakuja mara moja” akasema 

Herieth na Mathew akatoa simu 

yake ana kumtaka amtajie namba 

za simu za Ranbir 

Kumar,akampigia na simu ikaita 

akampa Herieth 

“hallow !! ikaita sauti ya 

upande wa pili 

“Mr Ranbir ni mimi Herieth” 

“Herieth !! 

‘Ndiyo .Samahani kwa 

kukupigia mida hii” 

“Herieth kuna tatizo lolote? 

“Ndiyo Ranbir nina tatizo ila 

siwezi kukueleza simuni naomba 

tuonane ni muhimu sana” Ranbir Kumar akasikika 

akivuta pumzi ndefu na kuuliza 

“Herieth ni tatizo gani ambalo 

huwezi kunieleza 

simuni?Hatuwezi kuonana kesho? 

“Hapana Ranbir.Nadhani 

umesikia kilichotokea leo 

nyumbani kwangu.Maisha yangu 

yako mashakani nahitaji msaada 

wako wa haraka.Nisingeweza 

kukupigia kama sina shida ya 

muhimu” 

“Sasa hivi uko wapi ? Ranbir 

akauliza 

“Niko katika nyumba yetu 

nyingine.Sitaki kulala pale 

nyumbani ulipo msiba ndiyo 

maana nimekuja hapa mahala ambako hapajulikani” akasema 

Herieth 

“Nieleze mahala ulipo” 

akasema Ranbir 

“Ninakutumia sasa hivi 

ujumbe wenye maelekezo ya 

mahala nilipo na namna 

unavyoweza kufika” akasema 

Herieth na kumpa simu Mathew 

ambaye alimuandikia ujumbe 

Ranbir na kumtumia.Baada ya 

muda Ranbir akapiga. 

“Herieth huko ulikonielekeza 

sintaweza kufika kwa sababu 

umekwishakuwa usiku mwingi na 

isitoshe sijawahi fika.Kama 

unaweza tukutane pale shimoni 

Casino nyuma ya Jamina

 Tower.Ukifika hapo nipigie simu 

unijulishe” 

“Tujiandae tuondoke.” 

Akasema Mathew.Herieth 

akabadilishwa mavazi kwani yale 

aliyokuwa nayo yalikuwa 

yamechafuka kwa damu ,akapewa 

pia dawa ya kutuliza maumivu 

kisha wakaondoka. 

“Mmeniumiza sana bila kosa 

lolote na kunipa ulemavu wa 

kudumu.Sintawasahau wala 

kuwasamhehe kwa hili 

mlilonifanyia.Sijawahi kukutana 

na watu wakatili kama ninyi” 

akasema Herieth kwa hasira 

akitazama mkono wake 

“Haya yote yametokea kwa 

sababu ya ubishi wako.Ungeshirikiana nasi 

yasingekukuta haya.Jilaumu 

mwenyewe na kiburi chako!! 

Akasema Mathew na safari 

ikaendelea kimya kimya 

“Sijawahi kushuhudia mtu 

akifanyiwa ukatili mkubwa wa 

kukatwa kidole 

chake.Nimewaogopa sana hawa 

watu wawili.Afadhali Mathew ana 

moyo wa huruma lakini huyu 

Camilla ni mbaya sana.Ana roho ya 

kikatili.Sura yake na mambo 

anayoyafanya haviendani kabisa” 

akawaza Theresa ambaye alikuwa 

kimya sana toka aliposhuhudia 

Herieth akikatwa kidole 

“Lakini hawa jamaa kweli 

wamebobea katika mambo ya uchunguzi.Wamewezaje kufahamu 

mambo haya yote kuhusu George 

na mkewe?tayari kuna dalili za 

Marekani kuhusika katika mauaji 

ya baba lakini sitaki Mathew 

aufahamu ukweli kwa nini 

walimuua.Ni mimi pekee 

ninayeufahamu kwa nini baba 

aliuawa na nimekwisha jilisha 

kiapo cha kutomueleza chochote 

mtu yeyote .Nina hakika hata naye 

kama ilivyokuwa kwa 

waliomtangulia atakutana na giza 

nene.Atayafumbua mengi 

yaliyojificha lakini hataweza 

kuifahamu siri hii niliyo nayo.” 

Akawaza Theresa huku gari 

likienda kwa kasi kubwa .Walifika shimoni Casino,moja 

ya Kasino kubwa lililojengwa chini 

ya Ardhi.Mathew akampa simu 

Herieth akamtaka ampigie Ranbir 

amjulishe kwamba tayari 

amekwisha fika.Herieth akampigia 

simu Ranbir akamjulisha 

amekwisha wasili pale kasino 

“Nenda katika maegesho ya 

upande wa kusini angalia gari 

litakalowasha taa mara tatu 

haraka haraka kisha usimame 

hatua kumi na tano” Ranbir akatoa 

maelekezo. 

Herieth akawaeleza akina 

Mathew alivyoelekezwa na 

Ranbir.Mathew akamtaka 

waongozane “Hapana hilo si wazo zuri 

Ranbir akiona nimeongozana nawe 

atapata wasiwasi.Kama 

hauniamini nitaongozana na 

Theresa na nikisha onana na 

Ranbir nitampa ishara aje 

awastue” akasema Herieth.Mathew 

akamtazama Theresa 

“Ngoja niende naye” akasema 

Theresa 

“Herieth nakuonya don’t try 

anything stupid !! akasema 

Mathew .Herieth na Theresa 

wakashuka garini wakaanza 

kutembea kuelekea mahala 

alikoelekeza Ranbir Kumar.Taa za 

gari zikawaza mara tatu haraka 

haraka na ile ilikuwa ni ishara 

kwamba tayari Ranbir amekwisha muona akasimama kama 

alivyokuwa ameelekezwa.Baada ya 

dakika nne mlango wa gari 

ukafunguliwa akashuka jamaa 

mmoja mfupi mnene akawafuata 

akina Herieth 

“Herieth ! akasema 

“Ranbir ,samahan sana kwa 

kukusumbua” 

“Bila samahani .Huyu ni nani? 

“Huyu ni rafiki yangu ndiye 

aliyenileta hapa anaitwa Theresa” 

akajbu Herieth halafu akamgeukia 

Theresa 

“Theresa naomba ukanisubiri 

garini nina mazungumzo ya 

faragha na Mr Ranbir” akasema 

Herieth na Theresa akageuka akaondoka kurejea garini waliko 

akina Mathew 

“Herieth kuna nini?Kwanza 

pole sana kwa mambo yaliyotokea 

leo nyumbani kwako.Uko salama 

lakini? Ranbir akauliza baada ya 

Theresa kuondoka 

“”Ranbir haraka sana ingia 

garini tuondoke eneo hili” 

akasema Herieth huku akimvuta 

mkono Ranbir akimuongoza 

kuelekea garini 

“Theresa ulisema una tatizo 

na nimekuja kukusikiliza.Nieleze 

tafadhali tatizo lako” 

“Ranbir tafadhali ondoa 

kwanza gari tutazungumza huko 

mbele baada ya kutoka hapa” akasema Herieth lakini bado 

Kumar aliendelea kumtazama 

“Ondoa gari Ranbir.Hili si 

eneo salama.Kuna hatari kubwa 

hapa” 

“Sikuelewi Herieth,kuna 

hatari gani?Eneo hili upo ulinzi wa 

kutosha na ni sehemu salama 

ndiyo maana nikaomba tukutane 

hapa.Una tatizo gani? Akauliza 

Ranbir 

“Ranbir kuna watu 

wanakutafuta.Wanataka 

wakukamate 

wakuhoji.Wamenitesa sana hadi 

wamenikata kidole” 

“Kuna watu wananitafuta?!! 

Ranbir akashangaa “Ndiyo.Ondoa gari haraka 

nitakueleza kila kitu” akasema 

Herieth 

“Herieth nashindwa 

kukuelewa una maanisha nini? 

Hebu jaribu kuwa muwazi nini 

hasa kimekutokea?Akina nani 

wamekukata kidole?Kwa nini 

wananitafuta mimi? Hebu 

funguka” 

“Yule mwanamke niliyekuwa 

naye hapa amekwenda kuwaita 

wenzake na muda wowote 

watafika hapa.Wanakutafuta 

wewe.Wamenitesa sana 

niwaelekeze mahala ulipo 

na..”Herieth hakumaliza sentensi 

yake Mathew na Camilla wakatoea “Hawa hapa wamefika.Ondoa 

gari !! akapiga ukelele Herieth na 

Ranbir akawasha gari akaliondoa 

kwa kasi.Camilla akatoa bastora 

yake lakini Mathew akamzuia 

“Kuna ulinzi mkali eneo hili 

hatupaswi kufanya vurugu 

zozote.Twende tuwafuate” 

akasema Mathew wakakimbia kwa 

kasi kurejea katika gari lao 

.Mathew akaliwasha gari na wakati 

huo gari la Ranbir lilikuwa 

linatoka getini.Mathew akaliondoa 

gari kwa kasi kubwa kuwafuata 

“I’m so stupid !! Kwa nini 

nilimuamini Herieth aende peke 

yake? Tayari ametuchezea 

mchezo.Lazima kwa namna yoyote 

ile tuwapate.Herieth anafahamaukila kitu na ndiyo 

maana licha ya kumtesa alikuwa 

mgumu sana kufunguka.Lazima 

tuwapate kwa namna yoyote 

ile.Hawa waatupa ufumbuzi wa 

mambo mengi” akawaza Mathew 

akiwa ameuma meno kwa hasira 

“Wale ni akina 

nani?Unawafahamu? akauliza 

Ranbir akiwa na wasi wasi 

mwingi.Herieth akamueleza kila 

kitu.Ranbir aliogopa sana 

akageuka nyuma na kuona kuna 

gari mbili yuma yao.Akaongeza 

mwendo na kukata kushoto 

kuingia katika barabara ambayo 

usiku huu haikuwa na 

magari.Mojawapo ya zile gari mbili zilizokuwa nyuma yao nayo 

ikakata kona 

“Wanatufuata !! akasema 

Ranbir kwa woga.Akamuelekeza 

Herieth afungue droo ya gari atoe 

simu aiwashe.Herieth akafanya 

hivyo na kumpa,akatafuta namba 

fulani akapiga 

Gari la akina Mathew likiwa 

katika mwendo mkali sana mara 

simu yake ikaita ,akatazama 

mpigaji alikuwa ni rais 

“Rais anataka nini usiku huu? 

Akajiuliza na kuipokea 

“Hallow Mheshimiwa rais” 

akasema 

“Mathew samahani kwa 

kukuamsha mida hii” “Usijali mheshimiwa rais 

sijalala bado niko barabarani 

naendelea na kazi yangu” 

“Usiku wote huu?! 

“Ndiyo mheshimiwa rais kazi 

zetu hizi hazina muda maalum” 

“Sawa Mathew naomba 

unisikilize vizuri .Sitisha kwanza 

operesheni zako zote ninakuhitaji 

hapa ikulu mara moja” 

Mathew akastuka 

“Mheshimiwa rais tuko katika 

operesheni muhimu sana ambayo 

inaweza ikatupa mwangaza 

mkubwa hivyo hatuwezi kuja huko 

sasa hivi hadi hapo 

tutakapokamilisha operesheni 

yetu” “Mathew hili si ombi bali ni 

amri na ninakuonya usijaribu 

kuipuuza amri ya rais wa jamhuri 

ya muungano wa Tanzania !! 

“Mheshimiwa rais umetupa 

kazi tuifanye na ndicho 

tunachokifanya hivi sasa.Kuna mtu 

muhimu sana ninamfukuzia 

mwenye taarifa za muhimu na 

ambaye nikimpata atatusaidia 

kufahamu mambo mengi” akasema 

Mathew na kukata simu 

akamuamuru Camilla aizime 

kabisa 

“Rais anataka nini? Theresa 

akauliza 

“Anataka tuachane na kazi hii 

haraka tuelekee ikulu” 

“Ana tatizo lolote? “Hajasema kama ana tatizo ila 

ametoa amri tuachane na 

operesheni hii tuwahi ikulu 

haraka” 

“Yawezekana labda amepatwa 

na tatizo au ana jambo la muhimu 

la kutuambia ndiyo maana 

amesema hivyo” 

“Hata kama ana jambo la 

msingi sana la kutuambia 

atatusubiri hadi hapo 

tutakapomaliza operesheni 

yetu.Hatuwezi kuwaacha akina 

Ranbiri wakapotea wakati tayari 

wamekwisha onyesha kwamba 

kuna mambo wanayaficha” 

“Lakini Math……………!! 

“No Theresa.Hatuendi kokote 

hadi kwanza tuhakikishe tumewapata akina Kumar.Rais 

atatusubiri”akasema Mathew na 

kuongeza mwendo wa gari 

kulifukuzia gari la akina Kumar 

lililokuwa linakwenda mwendo 

mkali sana.Kabla hawajafika 

katika makutano ya barabara ya 

Twiga na Mangaka ghafla kikasikia 

kishindo kikubwa .Gari la Ranbir 

liliacha njia likagonga nguzo ya taa 

ya barabarani na kwa kasi 

iliyokuwa nayo ikabiringika zaidi 

ya mara tatu halafu ikaangukia 

katika mtaro.Umbali uliokuwepo 

kati ya gari la Kumar na la kina 

Mathew haukuwa mrefu hivyo 

ilipotokea ajali ile ilimlazimu 

Mathew kufunga breki ya ghafla na 

gari likaserereka hadi mtaroni.Hakuna aliyeumia zaidi ya 

michubuko midogo 

midogo.Milango ilikuwa 

imejifunga hivyo jitihada za 

kujiokoa zikaanza.Camilla ambaye 

upande wake ulikuwa 

juu,akakipiga kioo kikavunjika na 

kutoka kupitia dirishani na mara 

tu alipotoka akaona kitu 

kilichomstua.Watu wawili wakiwa 

na makoti meusi na mmoja wao 

akiwa na bunduki ndogo 

iliyofungwa kiwambo cha sauti 

wakitokea katika gari la akina 

Ranbir lililopata ajali,kisha 

wakapanda piki piki na kuondoka 

kwa kasi kubwa.Camilla 

hakuwajali akaendelea na jitihada za kuwatoa akina Mathew mle 

garini 

Japokuwa tayari ni 

usiku,lakini kishindo 

kilichotokana na ajali ya gari lile la 

Ranbir kiliwastua watu na ndani 

ya muda mfupi ajali ya jali ya gari 

lile la Ranbir kiliwastua watu na 

ndani ya muda mfupi tayari watu 

walikuwa wamefika eneo la ajali 

na juhudi za uokozi 

zikaanza.Mathew na Theresa 

wakasaidiwa wakatoka garini na 

Mathew akaelekea katika gari la 

Kumar ambako watu walikuwa 

wanajitahidi kuwatoa ndani ya 

gari.Wa kwanza kutolewa garini 

alikuwa ni Ranbir.Tayari alikwisha 

fariki.Mathew akajitahidi kusogea karibu zaidi akamchunguza na 

kustuka baada ya kugundua 

matundu mawili ya risasi katika 

paji lauso 

“Risasi?!! Akashangaa 

“Macho yangu hayajawahi 

kunidanganya .Yale ni majeraha ya 

risasi.Nani kampiga ris……………….” 

Akatolewa mawazoni baada ya 

Herieth naye kutolewa garini 

akiwa tayari 

amekwishakufa.Alilazwa pembeni 

ya Ranbir na Mathew akapata 

nafasi ya kumchunguza na 

japokuwa alikuwa ameloa damu 

lakini alifanikiwa kuyaona 

matundu ya risasi .Akahisi baridi 

ghafla na taratibu akajiondoa 

katika lile kundi la watu akaelekea liliko gari lake.Theresa alikuwa 

amekaa chini akilia 

“Unajisikiaje Theresa ? 

“Sijielewi Mathew,nahisi 

kuchanganyikiwa” 

“Pole sana” akasema Mathew 

na kuwaomba vijana waliokuwepo 

pale wamsaidie kutoa gari mtaroni 

kwa ujira.Ndani ya dakika kumi 

walifanikiwa kulitoa gari lile 

mtaroni ,Mathew na akina Camilla 

wakaingia na kuondoka 

“Ranbir na Herieth wote 

wamekufa” akasema Mathew na 

Theresa akazidisha kilio 

“Usilie Theresa hizi kazi 

ndivyo zilivyo.Nilikutahadharisha 

toka awali kwamba ujasiri 

mkubwa unatakiwa hivyo nyamaza kulia shughuli bado pevu” 

akasema Mathew na kumgeukia 

Camilla 

 “Kuna jambo sikuwa 

nimekueleza Mathew.Nilipotoka 

ndani ya gari bado hakukuwa na 

watu waliokuwa wamefika eneo la 

ajali hivyo nilifanikiwa kuwaona 

watu wawili wakitokea katika gari 

lile tulilokuwa 

tunalifukuzia.Mmoja wa watu wale 

niliowaona alikuwa na bunduki 

ndogo iliyofungwa kiwambo cha 

sauti wakapanda pikipiki yao na 

kuondoka kwa kasi 

kubwa.Sikuweza kufanya chochote 

kwani kwa wakati ule hata mimi 

nilikuwa 

nimechanganyikiwa”akasema Camilla na Mathew akavuta pmzi 

ndefu 

“Inawezekana hao jamaa ndio 

waliosababisha ajali ile kwani 

naamini walikuwa wanawasubiri 

akina Kumar na walifahamu 

kabisa kwamba anapita njia hii 

hivyo toka kwa mbali wakaanza 

kuwashambulia kwa risasi na 

kusababisha gari kupotea 

mwelekeo na kupata 

ajali.Ninaamini kabisa watu hao ni 

kutoka katika ule mtandao wa CIA 

kwani waliofanya jambo hili 

wamelifanya kitaalamu sana.Huu 

mtandao unazidi kunipasua 

kichwa dhangu.Ranbir na Herieth 

wasingeweza kukimbia kama 

kusingekuwa na jambo wanalolificha tusilifahamu.Kwa 

sasa wote wamekufa na tumerudi 

katika sifuri.Tungeweza kuwapata 

tungefahamu mambo mengi toka 

kwao na ndiyo maana wameuliwa 

ili kutuzuia tusiweze kupata 

chochote.Ninachojiuliza 

wamefaamuje kama tulikuwa 

tunawafuatilia akina 

Ranbir?akauliza Mathew. 

“Ninahisi Ranbir baada ya 

kugundua kwamba tunamfuatilia 

aliomba msaada na ili kulimaliza 

hili suala wakalazimika kuwaua ili 

kuendelea kuificha siri 

yao”akasema Camilla 

“Mtandao huu ni mrefu na 

ndiyo maana wana uwezo wa kufahamu kila kile 

tunachokifanya” akasema Mathew 

‘Tumaini pekee lililobaki kwa 

sasa ni Peniela ambaye endapo 

atatusaidia kutupa taarifa 

tunaweza kugundua mambo mengi 

kuhusiana na hii benki ya Escom” 

akasema Camilla 

“Mathew tunakwenda 

kumuona dada? Theresa akauliza 

“Hapana .Hatuwezi kwenda 

usiku huu.Tutakwenda kuonana 

naye kesho.Lazima ajifunze 

kuheshimu kazi zetu.Alitupa kazi 

na atuache tuifanye bila 

kutuingilia.Kitendo alichokifanya 

usiku huu kututaka tuachane na 

operesheni yetu sijakipenda.Kesho 

tutakapokwenda kumuona nitamuuliza kwa nini alitaka 

tuachane na kile tulichokuwa 

tunakifanya? 

“Mathew yawezekana ana 

tatizo au ana jambo la maana 

analotaka kutueleza” Theresa 

akasisitiza 

“Basi atasubiri hadi kesho” 

akajibu Mathew na safari 

ikaendelea kimya kimya hadi 

nyumbani kwa Theresa 

wakamuacha hapo na wao 

wakaendelea na safari.Walifika 

nyumbani Camilla akamtibu 

majeraha yake madogo madogo 

aliyoyapata halafu wakaketi 

sebuleni 

“Mathew nilichokigundua 

hapa ni kwamba CIA wameweka mtandao mkubwa hapa nchini 

kuna jambo kubwa wanalitafuta 

hivyo inatubidi kuongeza 

umakini.Mtandao waliotengeneza 

una nguvu na umesambaa 

sana.Tukio lililotokea usiku huu 

linathibitisha hayo ninayoyasema 

.Waligundua kwamba 

tunawafuatilia akina Ranbir na 

kama tungefanikiwa kuwakamata 

kuna mambo tungeyafahamu toka 

kwao hivyo wakatuma wale watu 

wawili wawamalize haraka na 

hivyo kuturudisha nyuma.Kila 

hatua tutakayopiga toka sasa 

lazima tuwe makini mno” akasema 

Camilla 

“Usemayo ni ya kweli 

Camilla.Hii kampuni ya Tanbest Gemstone ltd inatakiwa 

kuchunguzwa tuwafahamu 

wamiliki wake ni akina ni kwani 

inaonyesha wazi kwamba 

inatumiwa na CIA kupitisha fedha 

kwa ajili ya kufadhili operesheni 

mbalimbali wanazozifanya hapa 

Tanzania.George aliwekewa kiasi 

kikubwa cha pesa na yeye 

akakigawa katika akaunti tatu za 

kampuni hii ya Tanbest.Itatubidi 

tuchunguze fedha hizi 

zilizoingizwa katika akaunti za 

Tanbest Gemstone ltd zimekwenda 

wapi.Kwa ujumla tupate matumizi 

ya hizi pesa ili tujiridhishe 

kwamba hazitumiki katika 

kufadhili operesheni za CIA hapa 

nchini hivyo itakuwa ni kazi ya kesho” akasema Mathew 

wakaagana na kila mmoja akaingia 

chumbani kwake kujipumzisha 

.Mathew akarudisha kumbukumbu 

ya matukio yote yaliyotokea kwa 

siku nzima 

“Matukio yote haya 

yaliyotokea yanafanywa na 

mtandao uliotengenezwa na 

Marekani.Ni kitu gani hasa 

wanachokitafuta hapa Tanzania? 

Toka walipomuua rais Anorld ni 

miaka zaidi ya kumi sasa lakini 

bado wanaendelea na harakati 

zao.Nini wanachokitafuta? Bado 

kuna kazi kubwa ya kufanya 

kufahamu ni kitu gani 

wanakitafuta na kufumua kabisa 

mtandaa wote” akawaza Mathew na kutazama saa ilikuwa ni sa 

kumi na dakika nane.Akafumba 

macho na kuutafuta usingizi 



Siku mpya imeanza na 

asubuhi hii taifa liliamshwa na 

taarifa za kustusha kufuatia vifo 

vya mkurugenzi mkuu wa kampuni 

ya kuchonga madini ya vito ya 

Tanbest ltd na mke wa aliyekuwa 

mkurugenzi wa idara ya usalama 

wa taifa Herieth Mzabwa 

waliofariki katika ajali.Sambamba 

na taarifa hiyo kulikuwa na taarifa 

nyingine iliyoeleza kwamba ofisi 

za kampuni ya kuchonga madini ya 

vito ya Tanbest Gemstone ltd zilikuwa zimeteketea kwa moto 

usiku huo huo.Taarifa nyingi 

zilizoandikwa magazetini zilidai 

kwamba Ranbir Kumar na Herieth 

walifariki katika ajali wakati 

wakielekea katika ofisi yao baada 

ya kupata taarifa za kuungua 

moto.Taarifa hizi za ofisi za 

Tanbest Genstone ltd kuungua 

moto zilimstua Theresa na hivyo 

kumlazimu kumpigia simu Mathew 

Simu ya Theresa ilimuondoa 

Mathew usingizini akapokea 

“Hallow Theresa” 

“Bado umelala Mathew? 

Theresa akauliza 

‘Ndiyo bado nimelala.Macho 

mazito sana” 

“C’mon Mathew amka” “Unasemaje Theresa? 

‘Umekwisha pata taarifa za 

kilichotokea jana usiku? 

“Hapana.Nini kimetokea? 

“Ofisi za kampuni ya Tanbest 

zimeteketea kwa moto usiku wa 

kuamkia leo” 

“What ?!! 

“Ndiyo habari iliyoandikwa 

karibu katika magazeti yote” 

‘This is weird!! Akasema 

Mathew 

“Mathew nimekupigia kukupa 

taarifa hizo.Mimi najiandaa niende 

ikulu kukabidhi ofisi” 

“Ahsante kwa taarifa 

Theresa.Tutaonana huko ikulu sisi 

pia tunakuja ikulu asubuhi hii 

kuonana na rais kufahamu alikuwa anatuitia jambo gani jana usiku” 

akasema Mathew na Theresa 

akakata simu 

“Dah ! mambo yanazidi kuwa 

mambo.Ofisi za Tanbest 

zimeteketea kwa moto.Hii inazidi 

kunipa picha kwamba kuna jambo 

linafichwa hapa ambalo lazima 

tufanye juhudi kulijua.Tayari 

wamejua kwamba tunafahamu 

kuhusu Tanbest kuwa na 

mashirikiano na kampuni ya 

Flamingo hivyo baada ya kuwaua 

Ranbir na Herieth wameamua 

kuteketeza kabisa kampuni hii ili 

kuhakikisha kwamba hakuna 

nyaraka yoyote tunayoweza 

kupatikana.Mapambano yanazidi 

kuwa makali.Tayari tumeanza kuwatikisa na ndiyo maana haya 

yote yanatokea.Upo usemi 

unaosema kwamba giza 

linapokuwa nene basi kunakaribia 

kupambazuka.Haya yanayoanza 

kutokea sasa ni ishara kwamba 

tunaukaribia ukweli.Kikubwa 

tunachopaswa kukifanya ni 

kuongeza umakini zaidi kwani 

naamini mida hii watakuwa 

wanatuwinda watuondoe” 

akawaza Mathew na kutoka 

akaenda kugonga chumbani kwa 

Camilla na hakukuwa na 

mtu.Akasikia sauti ya vyombo 

jikoni akaenda na kumkuta mpishi 

wake wakasalimiana akamuuliza 

alipo Camilla akamueleza kwamba 

ameenda kufanya mazoezi ya kukimbia.Mathew akarejea 

chumbani kwake kwa ajili ya 

kujiandaa kuianza siku.Akiwa 

bafuni akasikia mlango wa chumba 

chake unafunguliwa 

“Nani huyo? Akauliza 

“Ni mimi Camilla” 

Mathew akaoga haraka 

haraka na kutoka akamkuta 

Camilla amekaa sofani 

“Nimekutafuta nikaambiwa 

umekwenda mazoezi” akasema 

Mathew 

“Nilikwenda kukimbia.Huwa 

ninakimbia kilometa kadhaa kila 

asubuhi.Vipi wewe umeamkaje? 

“Nimeamka salama kabisa” 

“Kuna loote toka kwa Peniela? 

Akauliza Camilla “Hapana mpaka sasa 

hajanipigia simu.Kwa kuwa 

aliahidi kunipigia yeye mwenyewe 

ngoja nimpe muda na kama 

asipopiga hadi saa nne 

nitampigia.Hata hivyo kuna taarifa 

nyingine nimepewa na Theresa 

asubuhi hii kwamba kampuni ya 

Tanbest aliyokuwa anafanya kazi 

Herieth imeteketea kwa moto jana 

usiku.Hii ni picha ya wazi kwamba 

kuna jambo linafichwa” akasema 

Mathew na Camilla akashusha 

pumzi 

“Kama nilivyokueleza jana 

kwamba vita hii inapamba 

moto,hivyo umakini na tahadhari 

kubwa vinatakiwa.Watu hawa 

tayari wamestushwa na hatua tunazopiga na wanafanya kila 

juhudi kuhakikisha hatufanikiwi 

malengo yetu.Kama wameteketeza 

ofisi za Tanbest ni wazi 

wameturejesha kwenye 

sifuri.Hawa jamaa wako makini 

mno katika kila wanachokifanya” 

akasema Camilla 

“Ni kweli wameturudisha 

nyuma lakini wamezidi kutupa 

uhakika kwamba kuna jambo 

ambalo hawakutaka 

tulifahamu.Tutafuta namna 

nyingine ya kuendelea na 

uchunguzi wetu na 

ninakuhakikishia kwamba lazima 

tutafahamu hicho wanachokificha” 

“Tunaanzia wapi leo? Camilla 

akauliza “Asubuhi hii tunakwenda 

ikulu kuonana na rais halafu 

tutakwenda bandarini kuchunguza 

kuhusu zile kontena mbili 

alizoziingiza George ambazo 

nyaraka zake zinaonyesha ni 

basikeli” Mathew akanyamaza 

baada ya simu yake kuita alikuwa 

ni Meshack Jumbo 

“Mzee Shikamoo” 

“Marahaba Mathew habari 

yako? Unaendeleaje? 

“Naendelea vyema mzee” 

“Nimekupigia kukujulia hali 

na kukufahamisha kwamba leo 

ninaanza rasmi kazi kama mkuu 

wa idara ya usalama wa taifa.Hivi 

sasa naelekea ikulu na baada ya kutoka kwa rais nitaelekea ofisini 

kuanza kazi” 

“Ahsante kwa taarifa mzee 

Jumbo mimi pia naelekea ikulu 

tutakutana huko.Nahitaji kuonana 

na rais asubuhi hii” 

“Vipi umefikia wapi katika 

uchunguzi wako? 

“Bado mambo magumu ila 

tukionana nitakueleza kila 

kitu”akasema Mathew na kukata 

simu na kumtaka Camilla 

akajiandaa waanze 

kazi.Walipojiandaa wakakutana 

katika chumba cha chakula kwa 

ajili ya kupata chai.Wakati 

wakiendelea kupata chai simu ya 

Mathew ikaita.Alikuwa ni Peniela “Hallow Peniela” akasema 

Mathew baada ya kupokea 

“Habari yako Mathew” 

“Nzuri .Habari za huko? 

Hajambo Anna Maria? 

“Anna Maria hajambo 

anaendelea vyema.Kesho ni siku 

yake ya kuzaliwa” 

“Nasikitika sana kwamba 

sintoweza kuhudhuria.Nimebanwa 

sana” 

“Usijali.Jana ulinipigia simu 

ukasema kwamba una jambo la 

kuzungumza na una hitaji msaada” 

“Ndiyo Peniela nahitaji 

msaada wako .Kuna mahala 

nimekwama nahitaji unikwamue” 

“Sema unahitaji nini Mathew? “Nilikueleza kwamba kuna 

uchunguzi ninaufanya” 

“Ndiyo ulinieleza” Peniela 

akadakia 

“Uchunguzi wangu 

umenifikisha hadi Escom Bank” 

akanyamza na baada ya sekunde 

kadhaa Peniela akauliza 

“Umefika Escom bank? 

“Ndio .Nimegundua kwamba 

benki hii inamilikiwa na watu 

watatu, Andrew Pillar mwenye 

asilimia hamsini za hisa ,wewe una 

asilimia thelathni na tano na 

Anderson Pilla ana asilimia kuni 

na tano” akasema 

“Baada ya kugundua hivyo 

nini basi unachokitaka?Siruhusiwi 

kuwa na hisa benki? “Si hivyo Peniela naomba 

unisikilize hadi nitakapomaliza” 

“Endelea” 

“Nimegundua kwamba benki 

ya Escom inatumiwa kupitisha 

fedha kwa ajili ya shughuli haramu 

za serikali ya Marekani nchini 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog