Search This Blog

Friday 7 April 2023

THE FOOTBALL - 4

  

Simulizi : The Football 

Sehemu Ya Nne (4)


lakini vipi kuhusu mawasiliano 

yake na Fakrim?Wote wawili ni 

CIA na Nathan ndiye mtu wa 

mwisho kuwasiliana na Fakrim 

kwa mujibu wa maelezo 

tuliyoyapata.Lazima kuna kitu 

hapa tunapaswa kukifahamu 

kuhusu yeye.Huyu kwa sasa ni mtu 

wetu wa muhimu 

sana.Tukimfanyia uchunguzi wa 

kina kuna jambo 

tutalifahamu.Hawa CIA huwa 

hawang’ang’anii sehemu bila 

faida.Kitu cha msingi tujaribu 

kufahamu lini alijiunga na 

CIA.Kama tukigundua kwamba 

alikuwa tayari CIA kabla ya 

kuanza mahusiano na Dr Vivian basi tutakuwa na uhakika kwamba 

kuna jambo analitafuta” akasema 

Meshack Jumbo 

“Jambo la pili ambalo 

nimeligundua kutokana na 

mazungumzo yetu ni kwamba 

Nathan anafanya kazi katika 

kampuni inaitwa A.D 

electronics.Nataka tuichunguze 

kampuni hii inahusika na mambo 

gani ili tuunganishe na kazi 

anayoifanya Nathan” akasema 

Mathew 

“Dr Vivian hajakueleza 

inahusiana na mambo gani hii 

kampuni? 

“Sikutaka kumuhoji kwa 

undani zaidi aliponitajia tu jina la kampuni kwangu ilitosha kabisa 

na sikutaka kumuhoji kwa undani” 

“Ok sawa twende katika 

maktaba yangu ndiko iliko 

kompyuta yangu” akasema 

Meshack Jumbo wakaelekea katika 

maktaba yake.Mathew akaitumia 

kompyuta ya Meshack Jumbo 

kuitafuta kampuni ya A.D 

electronics na majibu yaliyokuja 

yalionyesha kwamba A.D 

electronics ni kampuni kubwa 

inayojihusha na utengenezaji wa 

vifaa mbali mbali vya kielekroniki 

.Wanatengeneza vitu kama 

simu,vifaa na programu mbali 

mbali za kompyuta na wana 

matawi yao karibu sehemu kubwa 

ya dunia. “Nathan ni CIA na uwepo wake 

katika kampuni hii uanipa 

mashaka kidogo inawezekana 

akawa yuko hapa katika hii 

kampuni kwa kazi maalum kwa 

kuwa yeye ni mtaalamu wa 

mawasiliano kwa mujibu wa Dr 

Vivian.Naomba umpigie simu 

Jimmy Snow na umuombe 

akusaidie kuichunguza au kama 

kuna lolote analofahamu 

kuhusiana na hii kampuni ya A.D 

Electronics” akasema Mathew na 

Meshack Jumbo bila kusita 

akachukua simu na kumpigia 

Jimmy 



Hallow Meshack Jumbo” 

akasema Jimmy 

“Habari ya saa hizi Jimmy.” “Nzuri sana Meshack Jumbo” 

“Jimmy utanisamehe kwa 

usumbufu mwingi ninaokupatia 

lakini kabla ya kukueleza sababu 

ya kukupigia napenda nikujulishe 

kwamba tayari inaandaliwa ndege 

maalum ya kwenda kumchukua 

Camilla kule Havana na rais wetu 

tayari amekwisha taarifiwa na 

ametoa kibali kwa Camilla kuingia 

nchini hivyo usiwe na wasi wasi 

kabisa kuhusiana na usalama 

wake” 

“Hizo ni habari njema sana 

Meshack.Bado nazidi kukusisitiza 

kwamba naomba usalama kwa 

mwanangu Camila uimarishwe 

kwani nimekubali aje huko 

kutokana na urafiki wetu mkubwa kwa hiyo sitaki kusikia ameingia 

katika matatizo yoyote” 

“Usihofu kuhusu hilo 

Jimmy,Camilla atakuwa salama 

naomba uniamini” akasema 

Meshack Jumbo. 

“Jimmy nimekupigia kuomba 

msaada wako tena.Kuna kampuni 

inaitwa A.D 

electronics.Tumegundua kwamba 

Nathan anafanya kazi katika 

kampuni hii hivyo tunataka 

kuifahamu vyema hii kampuni 

.Naomba kama unaw….” 

“Meshack ninaifahamu hii 

kampuni A.D electronics” akasema 

Jimmy 

“Hii ni kampuni ambayo 

inamilikiwa na serikaliya 

Marekani kupitia shirika lake la 

ujasusi la CIA japo jambo hili ni siri 

kubwa.Kampuni hii imejizolea 

umaarufu mkubwa siku za 

karibuni ndani ya Marekani 

kwenyewe na katika nchi nyingi 

kutokana na kutengeneza bidhaa 

zenye ubora mkubwa lakini kwa 

bei nafuu.Wanatengeneza simu 

,kompyuta,programu za kompyuta 

na vituvingine mbali mbali vya 

kielektroniki.Ni maarufu sana kwa 

simu za EZZY ambazo ni simu 

ngumu na za kisasa sana 

zilizojizolea umaarufu mkubwa 

hapa Marekani na duniani kwa 

ujumla kutokana na ubora na 

uimara wake .Siri kubwa iliyopo 

katika bidhaa zinazotengenezwa na kampuni hii ni kwamba kuna 

program maalum za siri huwekwa 

ambazo ni vigumu kuonekana au 

kugundulika ambazo zinakusanya 

taarifa za mtumiaji na 

kuwawezesha CIA kuzipata.Kila 

unachokifanya katika simu yako 

CIA wanakifahamu na hiyo 

inawasaidia sana kuwa na taarifa 

mbali mbali za watu 

wengi.Wamejikita zaidi katika nchi 

za uarabuni na ni kampuni 

inayoongoza kwa kugawa misaada 

mikubwa katika ya kompyuta 

mashuleni,viwandani n.k upande 

huo wa mashariki ya kati kumbe 

wana lengo la kutafuta taarifa.Hii 

kampuni imewasaidia sana 

kuweza kunasa mambomengi ya wale watu wanaowatafuta .Kama 

Nathan anafanya kazi katika 

kampuni hii basi hilo si suala la 

kushanganza kwani ni kampuni 

iliyo chini ya CIA lakini 

wanaolifahamu hili ni watu 

wachache sana ” akasema Jimmy 

Snow 

“Ahsante sana Jimmy kwa 

taarifa hiyo nzuri.Nitawasiliana 

nawe tena baadae” akasema 

Meshack Jumbo na kukata 

simu.Akafuta jasho katika kipara 

chake 

“Mathew hili jambo linazidi 

kuwa kubwa na ule mwanga 

mdogo uliokuwepo unazidi 

kuongezeka.Jimmy snow anasema 

kwamba kampuni hii ya A.D eletrocnics ikochiniya serikaliya 

Marekani kupitia shirikal ake la 

ujasusi la CIA.Hili ni mojawapo ya 

siri za nchi ya Marekani.Kama 

tulivyoona katika yale maelezo 

tuliyoyatoa mtandanoi,biadhaa za 

kampuni hii zinasifiwa kwa ubora 

na bei nafuu.Wanafanya hivi kwa 

kuwa kuna ruzuku ya serikali ya 

marekani kwa hiyo kampuni hii si 

haiko kwa ajili ya kutengeneza 

faida.Wanatengeneza simu aina ya 

EZZY ambazo ni maarufu sana 

nchini Marekani. Jimmy anasema 

kwamba katika vifaa 

vinavyotengenezwa na kampuni 

hii kama vile kompyuta,simu na 

vinginevyo kuna programu za siri 

huwekwa ambazo si rahisi kugundulika ambazo 

huwawezesha CIA kupata taarifa 

zote za mtumiaji. Wanatumia 

taarifa hizi katika kufahamu 

mambo mbali mbali hasa ya watu 

wanaojishughulisha na mambo ya 

ugaidi na ndiyo maana kampuni hii 

imejielekeza zaidi katika nchi za 

kiarabu” akasema Meshack Jumbo 

“Dah ! kweli hili jambo 

linazidi kutanuka.Kama Nathan ni 

mfanyakazi wa kampuni hii na 

yuko karibu na rais wa Tanzania je 

yuko pale kwa ajili ya 

kumchunguza rais au ni kwa ajili 

ya mapenzi? Akauliza Mathew 

“Kama yupo kumchunguza 

rais wetu lazima tujiulize kwa nini 

afanye hivyo?Kuna sababu yoyote ya Marekani kutaka kumchunguza 

rais wetu ? Kama ni kumchunguza 

labda waanze sasa baada ya 

kuingia katika mgogoro nao lakini 

kwa huko nyuma Tanzania na 

Marekani hazikuwa na matatizo 

yoyote na Marekani wamekuwa 

wafadhili wakubwa sana wa 

miradi mbali mbali ya maendeleo 

katika nchi yetu hivyo sina hakika 

kama walikuwa na chochote cha 

kuhofia hadi wamchunguze rais 

wetu.Uchunguzi wa kina 

unahitajika hapa kwani Marekani 

wanaweza wakamtumia katika 

kupata taarifa muhimu hasa katika 

huu msuguano unaoendelea hivi 

sasa” akasema Meshack“Mzee ninaamini kwamba 

lazima Nathan atatupeleka sehemu 

ambako tunaweza kupata mwanga 

wa kutosha wa jambo hili ambalo 

limeanza kuchukua sura 

mpya.Naomba nikuache upumzike 

mimi ninaondoka ,nitawasiliana 

nawe tena kesho asubuhi kukujuza 

kama nimepata taarifa yoyote.Lini 

unaanza kazi rasmi? 

“Jumatatu nitaanza.Nina siku 

mbili za kesho na kesho kutwa 

kujiandaa na jumatatu 

nitakabidhiwa rasmi ofisi” 

“Sawa mzee usiku mwema” 

akasema Mathew 

“Kuwa makini sana Mathew 

hili jambo limeanza kuelekea 

sehemu mbaya sana” “Usijali mzee nitakuwa makini 

sana” akasema Mathew na kuingia 

katika gari lake akaondoka huku 

kichwa chake kikiwa na mawazo 

mengi sana akachukua simu na 

kumpigia Theresa 

“ Hallow Mathew” akasema 

Theresa kwa sauti ya uchovu 

baada ya kuipokea simu ya 

Mathew 

“Theresa umekwisha lala? 

“NdiyoMathew.Unasemaje? 

“Ninakuja hapo kwako sasa 

hivi” 

“Kuna nini Mathew? 

“Kuna jambo la muhimu 

.Tafadhali usinichoke” akasema 

Mathew na kukata simu “Bado akili yangu inaamini 

lazima kuna jambo ambalo Nathan 

analichunguza kwa rais.Ninaamini 

hana mapenzi ya kweli bali 

amepandikizwa kwa sababu 

maalum.je ni jambo gani hilo? 

Lazima nifahamu kuhusu hilo” 

akawaza Mathew akiwa katika 

mwendo mkali kuelekea kwa 

Theresa. 

Haikumchukua muda mrefu 

kuwasili nyumbani kwa Theresa 

kwani usiku huu magari hayakuwa 

mengi sana 

barabarani.Alifunguliwa geti na 

kukaribishwa ndani na Theresa. 

“Mathew karibu.Umependeza 

sana usiku huu” akasema Theresa “Nilitoka kuonana na rais 

kama nilivyokueleza na sijafika 

bado nyumbani kubadili 

mavazi.Samahani kwa usumbufu 

wangu ,nakuomba 

usinichoke.Kuna jambo la msingi 

sana limenileta kwako usiku 

huu”akanyamaza kidogo na 

kulegeza tai yake 

“You have anything to drink in 

here?Nahisi koo likimekauka 

“Unahitaji kinywaji gani? 

Maji?Theresa akauliza 

“Naomba kama kuna wine 

tafadhali” 

Theresa akaondoka na 

kurejea na chupa kubwa ya wine 

na glasi mbili akaziweka mezani na kumimina kinywaji kile katika 

glasi.Mathew akaigugumia yote. 

“Theresa una siku ngapi? 

Akauliz aMathew na Theresa 

akashangaa 

“Ninazo simu tatu.Kuna nini 

kwani? 

“Ninaziomba hapa siku zako 

zote pamoja na kompyuta yako 

mpakato na kama una kifaa 

kingine chochote ambacho 

unakitumia kwa ajili ya 

mawasiliano ninakiomba hapa” 

akasema Mathew na Theresa huku 

akiwa katika mshangao akaenda 

chumbani kwake na kurejea na 

simu tatu na kompyuta ndogo 

mbili.Mathew akazikagua simu zile 

na kukuta mbili zina jina la EZZY akahisi mapigo ya moyo wake 

kubadilika akazichuka na 

kompyuta zile akazitazama na 

kukta zote zina jina la EZZy 

akamtazama Theresa 

“Hizi kmpyuta na hii simu 

ulizinunua wapi? Akauliza 

“Hizi sikununua, nilipewa na 

Nathan” 

Mathew akahisi jasho linaanza 

kumchuruzika usoni akavua koti. 

“Kwani kuna nini Mathew? 

Theresa akauliza 

“Katika maongezi yangu na 

rais usiku huu ”akasema Mathew 

“Kuna mambo kadhaa 

niliyagundua lakini kubwa ni 

kwamba Nathan anafanya kazi 

katika kampuni inayoitwa A.D electronics.Imenilazimu kuifanyia 

uchunguzi kampuni hiyo kujua 

shughuli inayofanya.A.D 

electronics ni kampuni ya 

kimarekanio ambayo 

wanatengeneza vifaa vya 

kielektroniki kama vile 

simu,kompyuta na programu 

mbalimbali za kompyuta.Hizi simu 

na hizi kompyuta zote zenye 

majina ya EZZY zinategenezwa na 

kampuni hiyo na ndiyo maana 

Nathan akakupatia” akasema 

Mathew na baada ya sekunde 

kadhaa akasema 

“Kuna siri kubwa katika 

kampuni hii anayofanyia kazi 

Nathan.Hii kampuni inamilikiwa 

na serikali ya Marekani kwa kupitia shirika lake la ujasusi la 

CIA lakini hii ni siri kubwa na watu 

wachache sana wanalifahamu hilo 

ingawa kampuni hii inatajwa 

kumilikiwa na matajiri wawili 

wakubwa wa Marekani lakini huo 

ni uongo kwani mmilki mkuu wa 

hii kampuni ni serikali ya 

Marekani na ndiyo maana bidhaa 

za kampuni hii zina ubora mkubwa 

lakini bei yake ndogo.Hii ni kwa 

sababu kampuni hii haiko 

kibiashara bali kwa lengo maalum” 

Sura ya Theresa ikabadilika 

baada ya kupata taarifa ile toka 

kwa Mathew. 

“Katika simu na vifaa 

vinavyotengenezwa na kampuni 

hii kuna programu za siri zinawekwa ambazo kazi yake ni 

kuwawezesha CIA kukusanya 

taarifa zote za mtumiaji.Kupitia 

program hiyoya siri wana uwezo 

wa kufuatilia mawasiliano yako 

yote ya simu ,barua pepe n.k Hii ni 

njia wanayoitumia siku hizi kwa 

ajili ya kubaini watu wenye nia 

mbaya na nchi yao kama magaidi 

n.k.Unapoanza kutumia simu hizi 

wanafahamu kabisa kwamba simu 

yao au kompyuta namba fulani 

inatumiwa na nani na yuko wapi 

na kila siku wanauwezo wa kupata 

taarifa zako” 

“What ?!! Theresa akastuka 

“Ndiyo hivyo Theresa.Hizi 

simu zina programu maalum ya siri ambayo huwawezesha kuwa na 

kila taarifa ya mtumiaji” 

“Oh my God ! akasema 

Theresa kwa mstuko 

“Mbona umestuka hivyo 

Theresa? 

“Kama ni hivyo basi dada 

atakuwa katika hatari kubwa sana 

kwani hata dada naye anatumia 

simu hizi.Nathan aligawa simu na 

kompyuta hizi kuanzia kwa dada 

hadi kwa wasaidizi wake wote na 

ndizo wanazotumia kutokana na 

ubora na uwezo wake mkubwa” 

“Jesus Christ !! akasema 

Mathew. 

“Mpaka hapa tayari nimepata 

picha kwamba Mathew yuko hapa 

kwa kazi maalum.CIA wanazo taarifa zote za mawasiliano ya rais 

kwa kuwa anatumia simu ile 

aliyopewa na Nathan.Kama 

aligawa simu na kompyuta kwa 

wafanyakazi wote basi lengo lao ni 

kubwa .Wanataka wawe na taarifa 

nyingi nyeti za kuhusu rais na nchi 

kwa ujumla.Mpaka sasa tayari 

watakuwa na taarifa nyingi 

kuhusiana na kila kinachoendelea 

hapa nchini.Rais wetu hayuko 

salama kwani hawa jamaa 

wanafahamu kila kitu 

kinachoendelea ikulu”akawaza 

Mathew 

“Mathew tutafanya nini 

kumlinda rais? Kumbe yule jamaa 

ni shetani mkubwa namna hii? 

Sikutegemea kabisa kama Nathan ambaye analia kila siku kuwa na 

mapenzi makubwa kwa dada 

anaweza kuwa hivi.Mathew do 

something! Akasema Theresa 

“Kama rais na watu wote 

wanaomzunguka walipwa simu na 

kompyuta za kampuni hii basi ni 

wazi ilikuwa ni kwa sababu 

maalum ya kupata taarifa 

mbalimbali nyeti za rais na nchi 

kwa ujumla.Kitu kikubwa cha 

kujuliza hapa ni je kitu gani hasa 

wanakitafuta?Kwa nini 

wanamchunguza rais? Lazima ipo 

sababu kubwa” akasema Mathew 

na kumtazama Theresa 

aliyeonekana kujawa na woga 

mwingi “Theresa unaweza ukanieleza 

sababu ya Nathan na Dr Vivian 

kutofautiana na kuamua kila 

mmoja aendelee na maisha yake? 

Kama unafahamu naomba unieleze 

tafadhali”Mathew akasema 

“Sababu kubwa aliyonieleza 

dada ambayo ilisababisha 

washindwe kuelewana ni 

mtoto.Nathan alikuwa anahitaji 

mara tu watakapofunga ndoa basi 

dada amzalie mtoto lakini dada 

alikataa jambo hilo na kudai kwa 

sasa ana majukumu mengi na 

hawezi kupata muda wa kulea.Kwa 

mujibu wa dada,Nathan alimtolea 

maneno ambayo hakuyapenda na 

ndiyo maana akakasirika na kuamua kutengana” akasema 

Theresa 

“Sasa nimepata picha.Nathan 

hakukurupuka katika kudai Dr 

Vivian amzalie mtoto.Tunapaswa 

kujiuliza kwa nini iwe sasa? Kwa 

nini Nathan hakuwahi kudai mtoto 

muda wote ambao walikuwa 

katika mahusiano hadi aje adai 

mtoto wakati huu ambao Dr Vivian 

amekuwa rais?Huoni kwamba 

huyu jamaa alifahamu kabisa 

kwamba Dr Vivian hawezi 

kukubaliana na jambo hilo hivyo 

akataka kuanzisha mgogoro kati 

yao ili mapoenzi yao 

yasiendelee?Ni wazi kwa wakati 

huu Dr Vivia ana majukumu mengi 

na mazito kama mkuu wa nchi na hataweza kuwa na muda wa 

kutosha kulea.Nathan alilifahamu 

hilo fika lakini akaamua kuanzisha 

mgogoro ili ndoa isifungwe.Kwa 

ufupi naweza kusema kwamba 

huyu jamaa hana mapenzi yoyote 

kwa Dr Vivian bali alikuwa 

ametumwa kuifanya kazi maalum 

lakini swali linalokuja ni kazi gani 

aliyotumwa? Ni uchunguzi gani 

aliokuwa anaufanya toka angali 

wako chuo?Kuna jambo ambalo Dr 

Vivian amewahi kulifanya ambalo 

limewafanya CIA waanze 

kumchunguza toka wakati 

anasoma?akasema 

Mathew.Theresa hakujibu kitu 

alionekana kuchanganyikiwa “Theresa hivi ndivyo 

tutakavyofanya.Kuanzia sasa 

usizitumie kabisa hizi simu.Kesho 

tutakwenda kutafuta simu 

nyingine.Rais pia anapaswa 

kuacha mara moja kutumia simu 

na vifaa vyote vya mawasiliano 

alivyopewa na Nathan.Wale wote 

waliopewa vifaa vya mawasiliano 

na Nathan wote wanapaswa 

kuacha kuvitumia haraka sana 

lakini si kwa wakati mmoja ili 

kuzuia hawa jamaa wasiweze 

kustuka kwa nini imetokea ghafla 

hawapati taarifa tena.” Akasema 

Mathew 

“Mathew lazima tumuonye 

dada kuhusu suala hili lazima 

aache haraka sana kutumia vifaa hivi vya Nathan.Ikiwezekana hata 

usiku huu” akasema Theresa 

“Hapana Theresa hatuwezi 

kufanya kwa haraka namna 

hiyo.Kesho asubuhi mimi na wewe 

tutaongozana hadi ikulu tukiwa na 

simu mpya na nitajua namna ya 

kumueleza rais ili asigundue 

chochote kuhusiana na 

Nathan.Tafadhali nakuomba 

Theresa hili suala ni la siri kubwa 

kati yetu na hapaswi mtu 

mwingine yeyote kulifahamu kwa 

sasa.Tunaofahamu mpaka sasa 

kuhusiana na Nathan ni mimi 

,wewe na mzee Meshck 

Jumbo.Itunze siri hii na 

usimweleze mtu yeyote hadi pale 

tutakapokamilisha uchunguzi wetu” akasema Mathew na kutoa 

laini katika zile simu za Theresa na 

kumtaka asizitumie kabisa zile 

kompyuta au hata kuhamisha 

mafaili katika kompyuta 

nyingine.Mathew akaagana na 

Theresa akaondoka kuelekea 

nyumbani.Alifika nyumbani kwake 

saa nane za usiku na kujilaza 

kitandani 

“Ni kitu gani ambacho Nathan 

anakichunguza kwa Dr 

Vivian?Kuna jambo ambalo si la 

kawaida alilonalo Dr Vivian hata 

CIA wamchunguze? Kompyuta zile 

zimegawiwa kwa watu wa ikulu na 

lengo likiwa ni kupata taarifa za 

kumuhusu rais.Wanapata taarifa 

zake zote kila siku na wanafahamu kila kitu anachokifanya au 

anachopanga kukifanya.Hii ni 

hatari sana kwa rais wetu hasa 

katika wakati huu ambao ameingia 

katika mgogoro na 

Marekani.Wanaweza wakamfanya 

lolote kwa wakati wowote 

wanaotaka kwani wanazo taarifa 

zake zote hadi ratiba zake 

zote.Nathan ana mambo mengi ya 

kuchunguzwa.Ni mtu muhimu mno 

kwetu.Hata hivyo kuna umuhimu 

wa kumchunguza pia rais 

yawezekana kuna jambo fulani la 

siri analo na ndiyo maana serikali 

ya Marekani wanamchunguza kwa 

siri” akawaza 

“Kesho itakuwa jumamosi 

ndefu sana.Kwanza asubuhi nataka kwenda tena kuona na rais na 

kubadilisha simu zake zote pamoja 

na kompyuta na kila kitu.Baada ya 

hapo nitajiandaa kwa ajili ya 

kumkabili Nathan ambaye 

anategemea kuwasili saa nne au 

saa tano za asubuhi.Kesho lazima 

ukweli ujulikane kwa nini 

wanamchunguza rais? akawaza 

Mathew na kuanza kuutafuta 

usingizi 



Ni kama ilikuwa kufumba na 

kufumbua 

kukapambazuka.Mathew alilala 

masaa machache sana na kuamka 

akajiandaa kwa ajili ya kuianza siku.Alifanya mazoezi ya kutosha 

akaoga na kabla ya kupata 

kifungua kinywa akampigia simu 

rais na kumjulisha kwamba 

asubuhi ile angefika ikulu alikuwa 

na jambo muhimu la kuzungumza 

naye.Alipata kifungua kinywa 

halafu akaondoka kuelekea kwa 

Theresa.Alimkuta tayari 

amekwisha jiandaa kwa kazi za 

sikuile.Kama ratiba yao 

walivyoipanga wakaondoka 

kuelekea katika maduka ya vifaa 

vya elektroniki 

“Mathew sikuweza kupata 

usingizi usiku wa leo.Nilikuwa na 

mawazo mengi mno.Lile jambo 

nililolifahamu jana kuhusu Nathan 

limeninyima amani kabisa” 

akasema Theresa 

“Usihofu Theresa na ndiyo 

maana nikakwambia kwamba 

unapoaswa kurejea ikulu katika 

shughuli zako za kila siku kwani 

kazi hizi zina hatari nyingi mno 

ndani yake.Hata hivyo usijali 

nitakulinda kila pale utakapokuwa 

nami.Nitahakikisha wewe na dada 

yako mnakuwa 

salama.Ninachokuomba katika hali 

kama hii usimuamini mtu yeyote 

yule.Hata kama una mpenzi 

unayempenda sana usithubutu 

kumuamini kwa asilimia mia 

moja.Unaona kilichotokea kwa Dr 

Vivian? Alimpenda mno Nathan 

bila kujua ni mtu wa namna gani.Umakini mkubwa unatakiwa 

kuanzia sasa.Kitu chochote 

unachoona si cha kawaida 

nitaarifu mara moja”akasema 

Mathew.Theresa alikuwa 

anatazama nje akionekana mwingi 

wa mawazo. 

“Nilifanya jambo la maana 

sana kutokumueleza dada 

chochote kuhusiana na siri hii 

ninayoifahamu ya Football.Endapo 

angekuwa anafahamu hivi sasa 

naamini angekwisha uawa 

.Natamani kumueleza Mathew 

kuhusu siri hii lakini bado 

ninaogopa kwani kwa kufanya 

hivyo nitakuwa ninayaweka 

hatarini maisha yangu na dada kwani hawa jamaa wanadukua 

taarifa zetu” akawaza Theresa 

“Ngoja jambo hili liendelee 

kuwa siri yangu na hatafahamu 

mtu mwingine yeyote.Naamini 

hata Mathew akifanya uchunguzi 

wake hataweza kufahamu kama na 

mimi nilikuwemo ndani ya ndege 

ile ya rais kwani watu wote 

walioniona ndegeni wamekwisha 

fariki” akaendelea kuwaza 

Theresa. 

Walipita katika maduka ya 

simu na kununua simu kadhaa za 

bei ghali pamoja na 

kompyuta.Theresa akapewa simu 

mbili na pamoja na kompyuta 

mpya mbili .Simu nyingine tatu 

pamoja na kompyuta wakaenda navyo ikulu kwa ajili ya kumpatia 

rais. 

Rais Dr Vivian aliwakaribisha 

akina Mathew katika chumba cha 

maongezi ya faragha.Hakupenda 

kuzungumza na Mathew katika 

ofisi yake. 

“Karibuni sana.Habari za toka 

jana? 

“Nzuri kabisa mheshimiwa 

rais” akasema Mathew na ukimya 

mfupi wa sekunde kadhaa ukapita 

kisha Mathew akasema 

“Mheshimiwa rasi tumekuja 

kwako mara moja kwa dharura na 

tunashukuru umetupokea.Kuna 

jambo limetuleta hapa” 

“Usijali Mathew nilikwisha 

sema muda wowote mtakaonihitaji mimi nipo pamoja nanyi kwa hiyo 

msisite kuja kuniona kama kuna 

jambo lolote lenye ulazima wa kuja 

kuniona” akasema Dr Vivian 

“Ahsante sana.Mheshimiwa 

rais tumekueletea simu tatu na 

komputa mbili.Kuanzia sasa 

hautatumia zile simu zako za 

zamani hivyo nakuomba 

ubadilishe simu zako unazotumia 

na uanze kutumia hizi 

nilizokuletea.Hizi ni simu mpya 

kabisa ambazo nimezinunua 

asubuhi hii nikiwa na 

Theresa.Kompyuta yako 

unayotumia sasa hautaitumia tena 

bali utaitumia hii niliyokuletea 

.Nafahamu swali la kwanza 

utakalouliza ni kwa nini? Naomba usiniulize swali hilo kwa sasa 

mheshimiwa rais bali naomba 

ufanye hivyo nilivyokueleza .Hii ni 

kwa ajili ya kuhakikisha unakuwa 

salama mheshimiwa rais.Hapo 

baadae nitakuja na kukueleza kila 

kitu kuhusiana na suala hili” 

akasema Mathew 

Dr Vivian akachukua muda 

kidogo kuwatazama Mathew na 

Theresa halafu akaishika 

mojawapo ya simu aliyoletewa na 

Mathew akaitazama kama kwamba 

anaikagua halafu akasema 

“Mathew mimi na wewe 

hatukuwahi kufahamiana hapo 

kabla.Leo ni siku ya tatu kama si ya 

nne toka nimekufahamu 

.Nilipokuona tu nafsi yangu iliniambia kwamba nimempata 

mtu sahihi kwa ajili ya kuifanya 

kazi iliyoshindikana kwa zaidi ya 

miaka kumi.Nilikuamini kabla 

hata ya kukupa kazi hii 

uifanye.Ninakuamini sana Mathew 

zaidi ya ninavyowaamni hata wale 

ninaofanya nao kazi lakini kuna 

mambo yameanza kunipa 

wasiwasi.Jana umekuja kunihoji 

kuhusiana na maisha yangu binafsi 

na leo hii unakuja na kunitaka 

nibadilishe simu zangu.What’s 

going on Mathew? Kuna nini 

ambacho hutaki kunieleza? 

Sikakatai yawezekana labda kuna 

tatizo umeligundua lakini kwa nini 

hutaki kunieleza?Nijuze na mimi 

nifahamu.Inaniwia ugumu kuweza kukubaliana na mambomengine 

kirahisi rahisi bila kufahamu 

sababu.Naomba kufahamu 

tafadhali hizi zimu zangu zina 

tatizo gani? 

“Mheshimiwa rais kwanza 

ninashukuru kwa kuniamini na 

ninakuomba undelee kuniamini na 

mimi ninakuahidi kwamba 

sintakuangusha.Ninafahamu kiu 

yako ya kutaka kujua kila 

kinachoendelea katikauchunguzi 

wangu lakini kuna mambo 

mengine ambayo siwezi kukueleza 

kwa sasa hadi hapo nitakapokuwa 

nimeyachimbua kwa kina kwa hiyo 

nakuomba unipe muda kidogo na 

mimi nitakuja kukueleza kila kitu 

na mahala nilikofikia lakini kwa sasa itoshe tu kukuomba ukubali 

kufanya hiki 

nilichokueleza.Naomba ubadilishe 

simu zako kuanzia sasa na uanze 

kutumia hizi simu nilizokupa 

pamoja na hii kompyuta.Tafadhali 

sana mheshmiwa rais naomba 

ukubali” 

“Mathew sijakataa kufanya 

hivyo lakini ninachotaka 

kufahamu ni je simu hizi zina shida 

gani? Akauliza Dr Vivian 

“Kama nilivyosema 

mheshimiwa rais kwamba ni 

mapema sana kusema chochote 

kwa sasa.Nipe muda wa siku mbili 

nitakuja hapa na kukueleza kila 

kitu.Tafadhali sana mheshimiwa 

rais.Kama uliweza kuniamini hata kabla hujanipa kazi hii naomba 

uniamini pia katika hili” akasema 

Mathew.Dr Vivian akafikiri kidogo 

na kusema 

“ Sawa Mathew nitafanya 

hivyo.Ninakuamini na nitaendelea 

kukuamini na ninaomba 

nisikuharakishe kuja kunieleza 

kuhusu maendeleo ya uchunguzi 

wako.Endelea kuchunguza taratibu 

na pale utakapoona kuna 

umuhimu wa mimi kufahamu 

chochote unakaribishwa” akasema 

Dr Vivian na kumtuma Theresa 

aende ofisini kwake akazilete simu 

zake. 

“Mathew nakuomba kama 

kuna jambo lolote ambalo 

unaliona si la kawaida ila linaweza kuwa na hatari kwangu au kwetu 

basi usisubiri njoo unitaarifu mara 

moja na kama kuna hatua za 

kuchukua tufanye hivyo mara 

moja.Tuko katika wakati mbaya 

sana kama nchi” Akasema Dr 

Vivian baada ya Theresa kutoka 

“Sawa mheshimiwa rais 

nitafanya hivyo” akajibu Mathew 

“Vipi hakuna sehemu yoyote 

uliyokwama kitu chochote? 

“Hakuna mheshimiwa 

rais.Theresa yuko makini sana 

kuhakikisha kwamba hakuna 

mahala ninakwama ” 

“Halafu nimekumbuka 

kitu.Uliniomba nikupatie nakala ya 

maelezo ya kanali sebastian toka 

polisi aliyoyatoa wakati wa mahojiano baada ya kunusurika 

katika ndege .Sijafanikiwa kuipata 

taarifa hiyo.Kumekuwa na dana 

dana nyingi katika suala hili toka 

nilipoomba ripoti hiyo na mpaka 

sasa sijaipata.Maelezo niliyoyapata 

ni kwamba jalada hilo halionekani 

kwani imekwishakuwa ni muda 

mrefu na kuna uwezekano jalada 

likawa limekwisha fungwa” 

akasema Dr Vivian 

“Usijali mheshimiwa 

rais.Suala hili lina vizingiti vingi 

toka mwanzo lakini hatuwezi 

kukata tamaa,tutatafuta namna 

nyingine ya kuweza kufanya 

uchunguzi.Ninachokuomba 

nahitaji kupata ripoti ya daktari 

aliyefanya uchunguzi kwa miili ya wale waliofariki katika ajali hiyo 

kwani kwa maelezo niliyoyapata ni 

kwamba ndege hiyo iliwaka moto 

baada ya kuanguka.Nahitaji kujua 

nini alikigundua katika miili ya 

marehemu? 

“Sawa Mathew nitajitahidi 

kufanya hivyo na mpaka mchana 

wa leo nitajitahidi niwe tayari 

nimeipata ripoti hiyo” akasema Dr 

Vivian na Theresa akarudi akiwa 

na simu tatu za rais.Akabilisha 

laini za simu na kuziweka katika 

simu zile mpya walizoleta 

“Ninafanya nini na hizi simu 

za zamani? 

“Naomba unipatie.Ile 

kompyuta yako ya zamani 

usiitumie tena bali utaanza kuitumia hii na wala usihamishe 

faili lolote kutoka katika ile 

kompyuta yako ya zamani” 

akasema Mathew na kuzichukua 

zile simu za rais kisha wakaagana 

na rais,wakaondoka 

“Ahsante sana Mathew kwa 

kumundoa dada yangu katika 

hatari” akasema Theresa 

“Theresa bado Dr Vivian 

hajatoka katika hatari.Hawa 

majasusi wana njia nyingi za 

kuweza kufanikisha malengo 

yao.Mambo mengi tutayafahamu 

tukifanikiwa kumpata Nathan.Saa 

ngapi anawasili leo? Umekwisha 

wasiliana naye kufahamu atafika 

saa ngapi? “Jana aliniambia anatarajia 

kufika leo saa nne au saa tano” 

“Kama ni muda huo basi 

zimebaki dakika kama ishirini hivi 

ifike saa nne.Twende tuelekee 

huko.Utaratibu ni kwamba ukisha 

mpokea utaondoka na gari langu 

na utampeleka hotelini 

akapumzike na halafu jioni ya leo 

utamualika nyumbani kwako kwa 

chakula na mazungumzo na mimi 

nitautumia muda huo kwenda 

kuingia katika chumba chake na 

kufanya uchunguzi .Nikisha maliza 

nitakujulisha na utaachana naye 

kisha tutakutana nikujuze 

nilichokipata katika uchunguzi 

wangu” “Sawa Mathew.Nikitumia gari 

lako wewe utatumia nini? 

“Nitatumia taksi.Msisitize 

Nathan kwamba safari hii iwe ya 

siri kubwa na asimueleze mtu 

yeyote kama amekuja hadi hapo 

mipango ya kumuunganisha tena 

na Dr Vivian itakapokamilika” 

akasema Mathew 

“Usijali Mathew nitatekeleza 

hilo” akasema Theresa na 

wakaelekea moja kwa moja hadi 

uwanja wa ndege wa kimataifa wa 

Julius Nyerere kwa ajili ya 

kumsubiri Nathan.Akiwa pale 

uwanjani akawasiliana na Peniela 

na kujulishwa kwamba tayari 

amekwisha tuma ndege ya kwenda Havana Cuba kumchukua Camilla 

Snow . 

“Kwa mujibu wa Peniela 

ndege iliyomchukua Camilla tayari 

imeondoka Havana Cuba saa kumi 

na mbili alfajiri ya leo kuja Dar es 

salaam kwa hiyo tumtegemee 

Camilla kesho alfajiri” akawaza 

Mathew wakati wakiendelea 

kumsubiri Nathan.Wakiwa hapo 

uwanjani Meshack Jumbo akapiga 

simu ikamlazimu Mathew asogee 

mbali kidogo na Theresa ili aweze 

kuzungumza na mzee Jumbo 

“Mzee shikamoo” 

“Marahaba Mathew habari za 

toka jana? 

“Nzuri mzee 

wangu.Umeamkaje? “Nimeamka salama.Nimeona 

kimya nikaona ngoja nikujulie hali 

na kujua mambo yako 

yanakwendaje” 

“Mambo yanakwenda vyema 

mzee.Jana nilipotoka kwako 

nilipata wazo la kwenda kwa 

Theresa na nikakuta anatumia 

simu aina ya EZZY zile 

zinatotengenezwa na kampuni ya 

A.D electronics.Nilimkuta na simu 

mbili na kompyuta mbili.Theresa 

anadai kwamba vifaa hivyo 

alipewa na Nathan kama 

zawadi.Anadai kwamba hakupewa 

yeye peke yake bali hata rais na 

watumishi karibu wengi wa ikulu 

walipewa kama zawadi kila mmoja 

simu na kompyuta bila kujua kama zina madhara makubwa kwao. 

Nilimzuia asiendelee kuzitumia na 

nikamueleza hali halisi kwa nini 

asitumie tena hivyo vifaa.Hii ni 

picha nyingine tunayoipata kuhusu 

Nathan kwamba yuko karibu na 

rais kwa kazi maalum” 

“Kwa hiyo kwa muda huu 

wote walikuwa wanapata taarifa 

zote za rais..Dah ! akasema 

Meshack Jumbo 

“Ndiyo mzee.Kwa muda mrefu 

sasa wamekuwa wakipata taarifa 

zote za rais na watu 

wanaomzunguka kwa maana hiyo 

wanafahamu kila kitu kuhusiana 

na rais na hata yale mambo nyeti 

ya nchi .Rais wetu yuko katika 

hatari kubwa na hasa kwa sasa baada ya kuingia katika msuguano 

na Marekani.Asubuhi ya leo 

nimekwenda kununua simu 

nyingine mpya na kumpelekea rais 

pamoja na kompyuta na kumtaka 

aache kutumia zile simu na 

kompyuta alizopewa na 

Nathan.Haikuwa kazi rahisi 

kumshawishi lakini amekubali na 

ameachana na zile simu kwa hiyo 

kwa upande wa rais hakuna tatizo 

tena bado kwa wasaidizi wake na 

wale wanaomzunguka. 

Tunatakiwa taratibu kuanza 

kuziondoa kompyuta zile toka 

mikononi mwao pamoja na zile 

simu .Uchunguzi ukikamilika na 

tukiwa na uhakika wa nini 

wanakichunguza tutalifikisha hili suala kwa rais na hatua 

zichukuliwe ikiw ani pamojana 

kubadili kompyuta na mfumo 

mzima wa mawasiliano wa 

ikulu”akasema Mathew 

“Nimekosa neno la kusema 

Mathew.Hili jambo linaumiza 

kichwa changu sana toka 

nimelifahamu.Ni kitu gani hasa 

ambacho wanakichunguza kwa 

rais? 

“Hilo ni swali ambalo majibu 

yake tutayapata baada ya kumpata 

Nathan.Yeye ndiye anayejua ni kitu 

gani hasa anakitafuta kwa 

rais.Hivi sasa tuko hapa uwanja wa 

ndege tukimsubiri kwani 

alimuahidi Theresa kwamba leo 

saa nne hadi saa tano atakuwa amewasili kwani anakuja na ndege 

binafsi ya kaka yake.Kutoka hapa 

Theresa atamchukua na 

kumpeleka hotelini na usiku wa 

leo atamkaribisha nyumbani 

kwake na hiyo itakuwa ni nafasi 

yangu ya kwenda katika chumba 

alichofikia Nathan na kufanya 

uchunguzi.Endapo nitashindwa 

kupata kitu chochote kwa leo 

itanilazimu kuweka mtego na 

kama mtego huo utashindwa 

kufanikiwa basi itanilazimu 

kumteka Nathan na kumuhoji” 

“Sawa Mathew sina tatizo na 

huo mpango wako ila umakini 

unatakiwa kwani huyu jamaa naye 

ni mtaalamu sana wa haya mambo 

kwa hiyo muda wote yuko katika tahadhari kubwa.Vipi kuhusu 

Camilla? 

“Nimezungumza na Penie…” 

Mathew akastuka kidogo baada ya 

kutazama katika sehemu ya 

kutokea abiria wanaowasili na 

kumuona Theresa akiwa 

ameongozana na kijana mmoja 

mtanashati sana aliyevalia 

nadhifu. 

“Mathew ! akaita mzee Jumbo 

“Mzee mambo 

yameiva.Ninamuona Theresa 

akiwa ameongozana na kijana 

ambaye ninahisi ndiye Nathan na 

wanaelekea katika gari langu.Mzee 

nakuomba nikuache ili niweze 

kuwafuatilia na kuhakikisha 

mpango wetu unakwenda kama tulivyopanga” akasema Mathew 

huku akitembea kuelekea zilipo 

taksi 

“Sawa Mathew utanijulisha 

baadae kila hatua utakayokuwa 

umefikia” akasema Meshack 

Jumbo 

“Nitakujulisha mzee.Kuhusu 

Camilla nimezungumza na Peniela 

muda si mrefu na amenieleza 

kwamba tayari ndege aliyoituma 

kwenda Havana kumchukua 

imeondoka saa tano za usiku kule 

Havana ambayo ni sawa na kumi 

na mbili za alfajiiri kwa saa za 

afrika mashariki na safari ya 

kutoka Havana hadi Dar es salama 

inaweza kuchukua saa ishirini na 

mbili au zaidi kwa hiyo tumtegemee Camilla kesho 

asubuhi” akasema Mathew na 

kuagana na mzee Meshack Jumbo 

akamuelekeza dereva aifuate gari 

ile waliyopanda Theresa na 

Nathan. 

***************** 

“Karibu sana Dar es salaam 

Nathan” akasema Theresa wakiwa 

ndani ya gari wakielekea hotelini 

“Ahsante Theresa.Gari lako 

zuri mno.Ni la kifahari mno.Magari 

kama haya hata Marekani 

yanaendeshwa na matajiri 

wakubwa au viongozi wakubwa 

kwani sifa yake kubwa hayapenyi risasi” akasema Nathan.Theresa 

akatabasamu na kusema 

“Hili si gari langu.Ni gari la 

mpenzi wangu mpya anafanya 

biashara ya madini na kwa kuwa 

amesafiri kwenda nje ya nchi 

katika biashara zake ameniachia 

nilitumie.Sina uwezo wa kununua 

gari kama hii” akasema Theresa 

“Hongera sana .Kumbe tayari 

una mpenzi mpya tena tajiri” 

akasema Nathan na wote 

wakacheka. 

“Anaendeleaje Vivian? 

Akauliza Nathan 

“Dada anaendelea 

vizuri.Nimekuwa naye jana 

tumekaa hadi usiku tunazungumza 

kuhusiana na suala lenu na ameniahidi kunipa jibu baada ya 

kufikiria.Asubuhi ya leo kabla 

sijaenda uwanja wa ndege 

kukusubiri nimekutana naye 

lakini hatukuzugumza mengi 

nilikuwa namuandalia hotuba 

fulani” 

“Umeonaje muelekeo wake? 

Yuko tayari kuweza kurudisha 

moyo na kuendelea na mchakato 

wa harusi yetu? Theresa 

ninampenda mno Vivian na sijui 

nikuelezaje namna 

ninavyompenda.Sifahamu 

nitakupa zawadi gani 

utakaponisaidia kuurejesha tena 

uhusiano wangu na Vivian” 

“Usiogope Nathan niachie hilo 

jukumu na nitalimaliza.Vivian hawezi kunishinda .Kitu cha 

msingi ni kufuata maelekezo yangu 

tu na kila kitu kitakwenda sawa” 

“Hivi sasa tunaelekea wapi? 

“Tunaelekea hotelini.Utafikia 

hotelini utapumzika na baadae 

jioni nitakuja kukuchukua 

tutakwenda nyumbani kwangu 

kupata chakula na nitakupa 

mrejesho wa kila 

kinachoendelea.Kitu cha msingi 

zingatia usiri.Asifahamu mtu 

yeyote aliye karibu na dada kama 

unakuja Tanzania.Tunao fahamu 

kuhusu ujio wako ni mimi na wewe 

pekee.Nataka kumshangaza dada 

Vivian na hataamini macho yake” 

akasema Theresa na kumfanya 

Nathan atabasamu. Walielekea moja kwa moja 

hoteli Pentagone moja ya hoteli 

kubwa jijini Dar es slaam yenye 

umbo la pembe tano.Pale Nathan 

alichukua chumba . 

“Nathan,pumzika hapa mimi 

ninakwenda kuendelea na 

majukumu mengine na baadae 

jioni ujiandae nitakuja kukuchuku 

atuende nyumbani kwangu 

nitaandaa chakula na 

tutalizungumzia suala lenu na 

kama ikimpendeza Mungu basi 

Vivian anaweza akajiunga 

nasi.Ninakwenda kujaribu 

kulifanikisha hilo” akasema 

Theresa.Nathan akainuka na 

kumkumbatia kwa furaha 

 “Theresa tafadhali nakuomba 

fanya kila uwezalo kuhakikisha 

ninakutana na kuzungumza na 

Vivian” akasema Nathan 

wakaagana na Theresa 

akaondoka.Mara tu alipoondoka 

hoteli Pentagone akampigia simu 

Mathew na kumfahamisha kila kitu 

kilivyoenda .Mathew 

akamuelekeza mahali alipo na 

kumtaka amfuate 

“Nilipomuona Nathan moyo 

wangu ulipatwa na hasira kali.Yule 

shetani kumbe kwa muda huu 

wote amekuwa anatuchunguza na 

kudukua habari zetu.Hana maana 

yoyote shetani mkubwa 

yule.Anayaweka maisha yetu 

katika hatari kubwa.Nilijitahidi kutabasamu nilipokuwa karibu 

naye lakini angejua ninachokiwaza 

moyoni mwangu angekaa mbali 

kabisa na mimi” akawaza Theresa. 

Alimfuata Mathew mahala 

alikomuelekeza na kumkuta 

akipata supu wote wakakaa na 

kuendelea kupata supu. 



Alimfuata Mathew mahala 

alikomuelekeza na kumkuta 

akipata supu wote wakakaa na 

kuendelea kupata supu. 

“Mathew mambo 

yamekamilika.Nathan tayari 

nimempeleka hoteli Pentagone 

amepewa chumba namba 202 

ghorofa ya tatu” Akasema Theresa 

na kuvuta pumzi ndefu 

“Pole Theresa najua haikuwa 

rahisi kwako lakini nakuomba 

ujenge ujasiri ili Nathan asigundue 

chochote.Uso wako ujenge 

tabasamu kila wakati.Huyu ni mtu muhimu sana kwetu.Kuna mambo 

mengi ambayo tunahitaji 

kuyafahamu kutoka kwake.Kazi 

yako ni kuhakikisha unakuwa naye 

karibu wakati mimi nitakamilisha 

jukumu la kumchunguza na 

kuhakikisha ninamfahamu ni nani 

na nini lengo lake” akasema 

Mathew.Wakati wakiendelea 

kupata supu simu ya Mathew 

ikaita,alikuwa ni Dr Vivian 

“Hallo mheshimiwa rais” 

akasema Mathew 

“Mathew nimeipata ile taarifa 

ya uchunguzi wa madaktari kwa ile 

miili ya watu waliofariki katika 

ajali ya ndege ya rais.Ninakutumia 

sasa hivi katika simu yako” 

akasema rais “Ahsante sana mheshimiwa 

rais.Nitumie ili niipitie” akasema 

Mathew 

“Kama utahitaji maelezo zaidi 

utayapata kwa daktari aliyeongoza 

kuichunguza miili ya marehemu 

wa ajali ile ya ndege anaitwa Dr 

Proches Masawe.Kwa sasa ni 

mstaafu na anamiliki hospitali 

yake inaitwa tumaini hospital” 

akasema Dr Vivian 

“Nashukuru sana mheshimiwa 

rais ngoja niifanyie kazi hiyo 

taarifa” akasema Mathew na 

kumgeukia Theresa 

“Asubuhi ya leo nilimuomba 

rais anisaidie niweze kupata 

taarifa ya madaktari waliofanyia 

uchunguzi miili ya marehemu wa ajali ya ndege ya rais 

Anorld.Ameipata taarifa hiyo na 

atanitumia muda si mrefu.Vile vile 

amesema kwamba kwa maelezo 

zaidi nikaonane na daktari 

anaitwa Proches masawe ana 

hospitali yake inaitwa 

Tumaini.Nitakupeleka nyumbani 

ukaendelee na maandalizi ya 

kukutana na Nathan jioni ya leo 

mimi nitakwenda kwa Dr Masawe 

nikazungumze naye ana kwa 

ana.Nataka kupata picha ya 

majeraha ya marehemu hao 

japokuwa inasemekana wengi 

walikuwa wameunguzwa na moto 

na wengine vibaya sana hadi 

kulazimika kuwatambua kwa 

kutumia vinasaba.” akasema Mathew na muda huo huo mlio wa 

ujumbe mfupi ukalia katika simu 

yake akaufungua na kuusoma.Rais 

alikuwa amemtumia ripoti ile ya 

madaktari.Mathew akaipitia 

haraka haraka na kumuonyesha 

Theresa.Wakaingia garini 

wakaenda hadi nyumbani kwa 

Theresa halafu Mathew 

akaendelea na safari ya kuelekea 

Tumaini hospitali kuonana na Dr 

Masawe. 

Alifika hospitali ya Tumaini na 

kushuka garini akamuuliza 

muuguzi mmoja angewezaje 

kuonana na Dr Masawe.Muuguzi 

yule akamuelekeza mahala ilipo 

ofisi ya Dr Masawe.Mathew 

akaenda hadi katika ofisi ile na kukuta kuna watu kadhaa 

wamejipanga mstari wakisubiri 

kuonana na daktari na walikuwa 

wanaingia mmoja mmoja. 

“Watu ninaowaona hapa 

hawapungui thelathini na bado 

wanazidi kuongezeka.Itanibidi 

nitafute namna ya kufanya ili 

niweze kuonana na huyu Dr 

Masawe” akawaza Mathew na 

kuondoka eneo lile akamfuata 

daktari mmoja aliyekuwa 

anazungumza na simu .Akamsubiri 

amalize mazungumzo yake halafu 

akamsabahi 

“Habari yako daktari” 

akasema Mathew 

“Nzuri kaka habari yako” “Nzuri kabisa” akasema 

Mathew na kumuomba daktari 

yule kama angeweza kupata nafasi 

wakaongea pembeni kidogo.Bila 

hiyana daktari yule akamuomba 

waelekee nyuma ya mgahawa wa 

hospitali.Mathew akamueleza yule 

daktari kwamba alikuwa na shida 

ya kuonana na Dr Masawe lakini 

kuna watu wengi hivyo anaomba 

msaada.Bila kusita daktari yule 

akakubali kumsaidia Mathew 

kuonana na Dr Masawe.Mathew 

akamuomba namba zake za simu 

na haraka haraka akamrushia 

kiasi cha shilingi laki moja na yule 

daktari alitabasamu na kuondoka 

haraka na baada ya kama dakika 

kumi hivi akarejea na kumtaka Mathew amfuate.Waliekea katika 

ofisi fulani na walipoingia 

wakamkuta mzee mmoja mnene 

akiwa amekaa katika kiti cha 

kuzunguka mara moja Mathew 

akajua yule ndiye Dr 

Masawe.Akamsalimu kwa 

adabu.Daktari yule ambaye 

alimsaidia Mathew kuonana na Dr 

Masawe akamtambulisha mzee 

yule kuwa ndiye Dr Masawe halafu 

akatoka 

“Kijana karibu sana” akasema 

Dr Masawe 

“Ahsante Dr Masawe na 

samahani sana kwa usumbufu“ 

“Usijali kijana 

wangu.Nimeelezwa kwamba 

umetokea ikulu na nikaacha wagonjwa nikaona nije 

nikusikilize” 

“Ni kweli mzee.Mimi naitwa 

Mathew natokea 

ikulu.Nimeelekezwa nije hapa 

kwako na rais ili niweze kupata 

ufafanuzi wa kuhusiana na jambo 

fulani lililowahi kutokea yapata 

miaka kumi sasa” akasema 

Mathew. 

“Ni jambo gani hilo Mathew? 

Akauliza Dr Masawe huku sura 

yake ikionyesha wasi wasi 

“Ni kuhusiana na ajali ya 

ndege ya rais Anorld.Kuna hii 

ripoti hapa mliitoa kuhusiana na 

uchunguzi mlioufanya katika miili 

ya marehemu wa ajali ile” akasema 

Mathew na kuitoa simu yake akamuonyesha Dr Masawe ile 

taarifa akaipitia na kukunja sura 

“This is not true !! akasema 

kwa ukali 

“Kivipi Dr Masawe? 

“Huu ni upuuzi mtupu.Hii si 

ripoti yetu tuliyoitoa” akasema Dr 

Masawe.Mathew naye akashangaa 

“Una hakika hii si ripoti yenu 

Dr Masawe? 

“Ndiyo kijana wangu.Hii si 

ripoti yetu.Huu ni upuuzi 

mkubwa.Umeitoa wapi ripoti 

hii?Nani kafanya hivi? 

“Ripoti hii nimetumiwa na rais 

mwenyewe na ndiyo maana 

nikaamua kuja hapa kupata 

uthibitisho kama kweli ni 

yenyewe” “Rais amedanganywa .Hii si 

ripoti yenyewe.Kuna mchezo 

umefanywa hapa kuibadili taarifa 

yetu.Hatukutoa sisi ripoti ya aina 

hii” akasema Dr Masawe na 

kurudia tena kuipitia ile taarifa na 

kutikisa kichwa 

“Taarifa yenu ilikuwaje Dr 

Masawe? Mathew akauliza 

“Sikiliza Mathew ni kweli 

niliongoza madaktari wengine 

wawili katika kuifanyia uchuguzi 

miili ya marehemu na baada ya 

kukamilisha uchunguzi wetu 

tukaandika ripoti na kuikabidhi 

kwa wahusika ikiwa imefungwa 

kabisa kwani ni nyaraka ya 

siri.Kwa hiyo kuna watu huko 

serikalini kwa makusudi na kwa manufaa yao wameibadili taarifa 

yetu” 

“Dr Masawe unaweza 

ukanieleza mlichokiandika katika 

taarifa yenu ambayo ni halisi 

tofauti na hii taarifa bandia ? 

Mathew akauliza 

“Mathew ningependa sana 

kukueleza kuhusiana na taarifa 

hiyo lakini hiyo huwa ni taarifa ya 

siri na huwa inakabidhiwa kwa 

vyombo husika .Nadhani ingekuwa 

vyema mngewafuata watu 

waliokabidhiwa taarifa hiyo na 

kujua kwa nini walibadili taarifa 

yetu na kuandika taarifa ya 

uongo?akasema Dr Masawe 

“Dr Masawe nisingekuja hapa 

kwako kama kungekuwa na mahala ninakoweza kupata 

msaada.Nimekuja hapa kwako ili 

kupata ukweli halisi wa kile 

mlichokigundua baada ya kufanya 

uchunguzi wenu.Ninaomba sana 

unisaidie mzee wangu” akasema 

Mathew 

“Kijana nasikitika kwamba 

siwezi kuongea chochote kuhusu 

jambo hilo ambalo tulilikamilisha 

na tukatoa ripoti yetu ya 

uchunguzi.Walioibadilisha wana 

makusudi yao kwa hiyo ni jukumu 

lako wewe kama mchunguzi 

kufahamu ni nani walibadilisha 

hiyo taarifa na kuandika upuuzi 

huu mkubwa. Nakushauri Mathew 

wafuate wakubwa zako huko 

serikalini na uanze kulifuatilia suala hili utagundua mchezo huu 

mchafu uliofanywa” akasema Dr 

Masawe huku akiinuka. 

“Dr Masawe kama hutaki 

kuufumbua mdomo wako 

kunieleza kuhusiana na kile 

mlichokigundua ,ni vipi kama 

tutakwenda hatua ya mbele zaidi 

na nikayanunua maneno 

yako.Unasemaje kuhusu 

hilo?Mathew akauliza.Dr Masawe 

akang’aka 

“Money ? You want to buy me? 

Akauliza Dr Masawe 

“Sikiliza mzee 

wangu.Ninachokihitaji toka kwako 

ni maneno yako machahe tu na 

wala sihitaji taarifa nzima.Name 

your price and I’ll pay you right now” akasema Mathew.Dr Masawe 

akafikiri kidogo na kusema 

“How much are you going to 

pay me?akauliza huku 

akitabasamu 

“Sema unahitaji kiasi gani? 

“Unajua kijana sisi madaktari 

huwa haturuhusiwi kutoa 

sir………….” 

“Dr Masawe!! Mathew 

akamkatisha. 

“Nafahamu unachotaka 

kukisema kwa hiyo tufupishe 

mjadala .Just name your price.Kiasi 

gani unakihitaji?Two 

Million?Three or four? 

“Kwa uzito wa taarifa yenyewe 

nakuomba uamue mwenyewe utanipa kiasi gani”akasema Dr 

Masawe 

Mathew hakutaka kupoteza 

wakati akachukua simu yake na 

kumuomba Dr Masawe namba 

zake za simu akamtumia shilingi 

milioni mbili.Dr Masawe 

alipoziona akasema 

“Kijana wewe unafahamu 

namna ya kuishi mjini.Nina hisi 

lazima utakuwa unatokea Moshi 

wewe.” Akasema Dr Masawe na 

wote wakacheka 

“Ni hivi,mimi na madaktari 

wenzangu tulifanya uchunguzi wa 

miili ile na tuligundua kwamba 

kuna uwezekano mkubwa watu 

wale walikufa kabla ya ndege 

kuanguka.Uchunguzi ulionyesha walikosa hewa safi na inaonekana 

walivuta hewa yenye sumu au 

hewa isiyo safi na wengi aidha 

walikufa au kupoteza fahamu 

kabla ndege haijaanguka.Kingine 

tulichogundua ni matundu ya 

risasi kwa baadhi ya miili 

isipokuwa mwili wa rais wenyewe 

haukuwa na tundu la 

risasi.Tuliyaandika haya yote 

katika taarifa yetu na tukaikabidhi 

kwa vyombo vya uchunguzi na 

sijui kwa nini wakaamua 

kuibadilisha taarifa hii na 

kuandika huu upuuzi japo kuwa 

sahihi hii ni ya 

kwangu.Nimeshangaa sana kama 

kuna mambo ya ajabu kama haya 

yanaendelea serikalini.Unapaswa kuchunguza na kugundua 

waliofanya upuuzi huu walikuwa 

na lengo gani” akasema Dr 

Masawe. 

“Nashukuru sana Dr Masawe 

kwa msaada huu mkubwa” 

akasema Mathew na kuagana na 

Dr masawe na kuelekea mahala 

alikoegesha gari lake akaingia na 

kujifuta jasho. 

“Toka awali nilikuwa na 

wasiwasi sana kuhusiana na ajali 

ile ya ndege ya rais.Baada ya 

kuanza kuchunguza kuhusiana na 

ile ajali nimegundua mambo 

kadhaa ya kustaajabisha.Kwanza 

kisanduku cheusi cha kuhifadhi 

mwenendo wa ndege kilitoweka na 

kukawa na majina bandia ya watu waliotumwa kuja kufanya 

uchunguzi wa chanzo cha 

kuanguka kwa ndege ile.Leo tena 

linaibuka jambo lingine kwamba 

taarifa hii inayodaiwa ni ya 

madkatari walioifanyia uchunguzi 

miili ya marehemu wa ajali ile ya 

ndege si sahihi na 

ilibadilishwa.Taarifa hii haielezi 

chochote kuhusiana na baadhi ya 

miili ya marehemu kukutwa na 

matundu ya risasi na haionyeshi 

kama watu wale ndani ya ndege 

walikufa kabla ndege haijaanguka 

na wala kusaidikiwa kuvuta hewa 

chafu au hewa yenye sumu .Hii ni 

habari mpya kabisa na itanisaidia 

sana kufahamu kilichotokea ndani ya ndege ile na kusababisha 

ianguke” akawaza Mathew 

“Kumeonekana matundu ya 

risasi kwa baadhi ya miili,swali 

ninalojiuliza ni je kulikuwa na 

mashambulizi ndani ya ndege? 

Kama ndiyo,nani alikuwa 

anashambulia na kwa dhumuni 

gani?Hiyo hewa chafu au ya sumu 

anayosema Dr Masawe kwamba 

inahisiwa walivuta watu 

waliokuwamo ndani ya ndege 

ilitoka wapi?Nikifanikiwa kupata 

majibu ya haya maswali nitakuwa 

nimefanikiwa kujua kwa nini 

ndege ile ilianguka.Kanali 

Sebastian alikuwa ni mtu muhimu 

mno katika uchunguzi huu.Endapo 

angekuwa hai mpaka sasa angeweza kutusaida kujua nini 

kilichotokea ndani ya ndege.Hata 

hivyo tayari tumeanza kupata 

mwanga mdogo kuhusiana na ajali 

ile.Tayari ninafahamukwamba 

kulikuwa na kurushiana risasi 

ndani ya ndege kabla haijaanguka” 

akawaza Mathew 

Kutoka Tumaini hospital 

,Mathew aliekea moja kwa moja 

kwa Meshack Jumbo. 

“Mathew karibu sana.Habari 

za huko utokako?Meshack Jumbo 

akamkaribisha 

“Huko kwema kabisa mzee 

mambo yanakwenda vizuri” 

“Nafurahi kusikia hivyo.Vipi 

kuna habari yoyote mpya? “Ndiyo Mzee.Kuna jambo 

nimelipata ambalo linaweza 

kutusaidia sana katika uchunguzi 

.Kwanza kabla ya yote 

nikujulishe,tayari Nathan 

amekwisha wasili na hivi sasa 

yuko hotelini na jioni ya leo 

atakwenda nyumbani kwa Theresa 

na mimi nitautumia mwanya huo 

kwenda kufanya uchunguzi katika 

chumba chake.Naamini kuna kitu 

lazima nitakigundua katika 

chumba cha Nathan.Kuhusu 

Camilla kama nilivyokueleza ni 

kwamba yuko angani muda huu 

anakuja Tanzania tumtegemee 

hapa kesho alfajiri” Akasema 

mathew “Maendeleo mazuri.Ila 

nakushauri uwe makini sana 

kuhusu Nathan na umuonye hata 

Theresa pia kwamba asifanye 

mchezo na yule jamaa.Ni mtu 

hatari sana” 

“Nitafanya hivyo mzee.Vile 

vile tayari nimekwisha mbadilishia 

rais simu na sasa hatumii tena zile 

simu alizopewa na 

Nathan.Kinachofuata kwa sasa ni 

kuanza kuziondoa kompyuta zote 

na simu ambazo Nathan aligawa 

kwa wafanyakazi wa ikulu wale 

wanaomzunguka rais.Zoezi hili 

likikamilika tutakuwa na imani 

kwamba hawataweza tena kupata 

taarifa za ikulu japo hawatakata tamaa na wanaweza wakatafuta 

njia nyingine” akasema Mathew 

“Tuachane na hayo.Leo 

asubuhi nilipokwenda ikulu 

kuonana na rais nilimuomba 

anisaidie niipate taarifa ya daktari 

aliyefanya uchunguzi miili ya 

marehemu waliofariki katika ajali 

ile ya ndege.Rais akanitumia 

taarifa ambayo ni hii hapa” 

akasema Mathew na kumpa mzee 

Meshack ile taarifa katika simu 

yake akaisoma 

“Hiyo ni taarifa ambayo 

inadaiwa ndiyo ya madaktari 

walioifanyia uchunguzi miili ya 

marehemu walikuwamo ndani ya 

ndege.Baada ya kuipata 

nilimtafuta daktari aliyeongoza uchunguzi huo anaitwa Dr Proches 

Masawe ambaye kwa sasa ni 

mstaafu lakini anamiliki hospitali 

yake inaitwa Tumaini 

Hospital.Nilimuonyesha Dr 

Masawe ripoti hii na akastuka sana 

akadai kwamba huu ni upuuzi 

umefanywa kwani ripoti 

waliyoitoa wao si hii.Anadai 

kwamba kuna mchezo mchafu 

umefanyika na ripoti yao 

ikabadilishwa.Nilimuomba 

anieleze 

walichokigundua.Haikuwa rahisi 

lakini nikatumia ushawishi kidogo 

na akanieleza kwamba waligundua 

kwamba watu wale waliokuwamo 

ndegeni kuna uwezekano mkubwa 

walikufa au kupoteza fahamu kabla ya ajali kutokea kutokana na 

kuvuta hewa chafu au yenye 

sumu.Kingine waligundua 

matundu ya risasi katika badhi ya 

miili ya marehemu.” 

“Jesus christ ! akasema 

Meshack Jumbo . 

“Hili suala mbona linakuwa 

hivi?Mbona kila siku linaibuka 

jipya? Akasema kwa sauti ndogo 

“Kutokana na taarifa hii 

niliyoipata toka kwa Dr Masawe 

inaonyesha wazi kwamba kuna 

jambo lilitokea ndani ya ile 

ndege.Kwanza uwepo wa matundu 

ya risasi kwa baadhiya miili 

inatupa uhakika kwamba 

kulikuwa na kurushiana risasi japo 

hatujui nani na nani waliokuwa wanashambuliana.Jambo la pili ni 

kuhusiana na hiyo hewa chafu au 

yenye sumu wanayohisiwa kuivuta 

watu waliokuwamo 

ndegeni.Tukiweza kuyafumbua 

hayo mawili tutakuwa tumepata 

ukweli wa kilichosababisha ndege 

kuanguka bila hata ya kutegemea 

kisanduku cheusi.” Akasema 

Mathew.Meshack akafikiri kidogo 

na kusema 

“Usemayo ni ya kweli Mathew 

lakini ni wapi tutapata majibu 

hayo?Tungeweza kupata majibu 

kama tungeweza kumpata mtu 

ambaye alikuwamo ndani ya hiyo 

ndege ambaye angetueleza kama 

kulikuwa na kurushiana risasi na 

ni akina nani waliokuwa wanashambuliana?Kanali 

Sebastian alikuwa ni mtu muhimu 

sana kwetu.Kama angekuwa hai 

angeweza kutueleza nini hasa 

kilichotokea lakini naye amefariki” 

akasema Meshack Jumbo 

“Kuna hawa waandishi 

aliowasema Alhaj Zuberi kwamba 

walikuwamo ndani ya ndege 

ambao mpaka sasa hatujapata 

uhakika kama kweli walikuwamo 

ndani ya ndege au vipi kwani mtu 

pekee ambaye angeweza kutusaia 

kuwafahamu ni Fakrim ambaye 

naye tayari ameuawa.Dah ! suala 

hili linazidi kuwa fumbo 

gumu,lakini ngoja tumsubiri 

Camilla tuone atakuwa na taarifa 

gani za kumuhusu Fakrim.Yawezekana tunaweza 

kupata taarifa nzuri ya kutusaidia 

kutoka kwake” akasema Mathew 

“Mathew nakubaliana 

nawe.Jambo hili linazidi 

kuchangana mno.Ngoja tumsubiri 

Camilla hiyo kesho tujue naye 

atakuja na habari gani” akasema 

Meshack Jumbo. 

Waliendelea na maongezi na 

baadae Mathew akaaga 

“Mzee nimetaarifiwa kwamba 

kuna mizigo yangu imewasili 

bandarini kwa hiyo nataka nifike 

huko kuanza taratibu za kuitoa 

halafu tutaonana labda baadae 

usiku nitakapotoka kufanya 

uchunguzi kwa Nathan” akasema 

Mathew na kuondoka 




Ukumbi wa mikutano wa 

mwalimu Nyerere ulifurika wazee 

wa jiji la Dar es salaam walioitika 

wito wa rais wa kufika hapa.Rais 

wa jamhuri ya muungano wa 

Tanzania Dr Vivian matope alitaka 

kuzungumza na taifa kupitia kwa 

wazee wa jiji la Dar es 

salaam.Ulinzi ulikuwa mkali sana 

katika ukumbi huu.Burudani mbali 

mbali zilikuwa zinaendelea wakati 

wakimsubiri rais awasili. 

Saa tisa za alasiri juu ya 

alama rais akiwa ameongozana na 

makamu wa rais na waziri mkuu 

wakaingia ndani ya ukumbi tayari kwa kuwahutubia wazee wa Dar es 

salaam.Watu wote ukumbini 

wakasimama huku 

wakimshangilia rais hadi 

alipochukua nafasi yake wimbo wa 

taifa ukaimbwa halafu wote 

wakaketi.Muongoza shughuli 

akamkaribisha kiongozi wa wazee 

wa jiji la Dar es salaam aweze 

kuzungumza machache na kisha 

amkaribishe rais aweze 

kuzungumza na watanzania kwa 

kupitia wazee wa Dar es 

salaam.Mzee Said seif said akatoa 

salamu za wazee wa Dar es salaam 

na kisha akamkaribisha rais aweze 

kuzungumza nao.Makofi mengi 

yakapigwa rais aliposimama na 

kuelekea katika sehemu iliyoandaliwa rasmi kwa ajili ya 

kutolea hotuba. 

“Mheshimiwa makamu wa rais 

was jamhuri ya muungano wa 

Tanzania,Mheshimiwa waziri 

mkuu wa jamhuri ya muungano 

wa Tanzania,mheshimiwa mkuu 

wa mkoa wa Dar es 

salaam,waheshimiwa wakuu wa 

wilaya za Dar es 

salaam,waheshimiwa wabunge wa 

Dar es salaam mlioko 

hapa,viongozi wa vyama vya siasa 

mliopo hapa,wakuu wa vyombo 

vya ulinzi na usalama mlioko 

hapa,kiongozi wa wazee wa Dar es 

salaam mzee Said Seif said,wazee 

wote mliopo katika ukumbi huu 

shikamooni” Wazee wote wakaitika halafu 

akaendelea 

“Awali ya yote napenda 

kuanza kwa kumshukuru sana 

mwenyezi Mungu mwingi wa 

rehema kwa kutupa afya njema na 

kutuwezesha kukutana hapa leo 

hii.Wapendwa wazee wangu 

umekuwa ni utaratibu uliojengwa 

na viongozi wetu waliotangulia 

kwamba kila pale kunapokuwa na 

jambo kubwa la kitaifa ambalo 

linapaswa kuwafikia watanzania 

wote basi hulifikisha kwa 

watanzania kwa mtindo huu wa 

kuzungumza na wazee.Imezoeleka 

wazee wa Dar es salaam lakini 

inaweza kuwa wazee wa sehemu 

yoyote ile,Arusha Mwanza,Dodoma na kwingineko 

kutegemea na mahala alipo 

rais.Nimeurithi utaratibu huu 

kutoka kwa viongozi 

walionitangulia na mimi 

nitaendelea nao na kila pale 

litakapotokea suala kubwa la 

kitaifa nitakuwa nazungumza na 

watanzania kwa kupitia kwenu 

ninyi wazee” akasema Dr Vivian na 

kupigiwa makofi 

“Wapendwa wazee 

wangu,nimewaiteni hapa kuweza 

kuzungumza nanyi masuala 

kadhaa yanayohusiana taifa 

letu.Awali ya yote napenda kupitia 

kwenu kuwafahamisha watanzania 

kwamba nchi yetu ni salama,na 

hakuna kitisho chochote cha usalama.Mipaka ya nchi yetu bado 

iko salama na vyombo vyetu vya 

ulinzi viko imara muda wote 

kuhakikisha nchi yetu inakuwa 

salama kwa hiyo nawaomba msiwe 

na hofu yoyote ya usalama 

endeleeni kufanya shughuli zenu 

kama kawaida” 

Wazee wangu kuna mambo 

mawili au matatu ambayo nataka 

kuzungumza nanyi mchana wa 

leo.Kwanza ni kuhusiana na 

yaliyotokea katika mkutano wa 

baraza kuu la umoja wa 

mataifa.Huu ni mkutano wa kila 

mwaka ambao hukutanisha 

viongozi wa mataifa yote ya dunia 

ambayo ni wanachama wa umoja 

huu au wawakilishi wao.Mwaka jana niliwakilishwa na makamu wa 

rais na safari hii niliamua niende 

mwenyewe.Wengi mmesikia 

kilichotokea kule 

Marekani,vyombo vya habari 

vimelitangaza sana,magazeti ya 

ndani na nje ya nchi yameandika 

sana jambo hili.Naomba kidogo 

nieleze japo kwa ufupi nini hasa 

kilijiri huko na kuleta 

sintofahamu kubwa. 

Baada ya kufika Marekani 

nilikutana na ujumbe wa watu 

wanne watatu wakitoka China 

ambao ni wawakilishi wa wafanya 

biashara wakubwa wa China na 

mmoja alikuwa ni mjumbe 

maalum wa rais wa Korea 

Kaskazini.Walikuja kwangu tukazungumza mambo mbali 

mbali.Mjumbe maalum wa kutoka 

Korea Kaskazini alitumwa na rais 

wa Korea Kaskazini kuniletea 

salamu maalum na katika salamu 

hizo rais wa Korea Kaskazini 

aliniomba tuweze kuzungumza 

kuhusiana na kuanzishwa kwa 

mashirikiano ya kibiashara baina 

ya nchi zetu.Katika salamu hizo 

aliweka wazi kwamba Korea 

kaskazini wanahitaji mashirikiano 

ya kibiashara na 

Tanzania.Wafanya biashara wa 

Korea Kaskazini wako tayari 

kuwekeza nchini Tanzania katika 

sekta mbali mbali na hasa katika 

viwanda hasa vya nguo.Vile vile 

alionyesha nia ya kutaka kuwekeza katika uchimbaji wa 

madini ya Urani ambayo tunayo 

mengi hapa nchini.Nilizipokea 

salamu hizo ila sikutoa jibu lolote 

hadi kwanza nitakaposhauriana na 

wenzangu katika serikali ili tuone 

kama tunaweza kufanya 

mashirikiano hayo na kama 

yatakuwa na faida yoyote kwa 

Tanzania. 

Kesho yake wakati akitoa 

hotuba yake, rais wa Marekani 

Mike straw alitoa matamshi makali 

sana na kuishutumu Tanzania 

kuwa na mashirikiano na Korea 

Kaskazini na hata kujadiliana 

kuhusiana na biashara ya madini 

ya Uranium.Hakuishia hapo 

alikwenda mbali zaidi na kutoa vitisho vya kuwekewa vikwazo 

vikali kwa Tanzania na nchi 

nyingine ambazo zinashirikiana na 

Korea Kaskazini.Kwa ujumla 

hotubayake ilikuwa na matamshi 

makali iliyojaa ubaguzi mkubwa 

na dharau hasa kwa nchi na 

viongozi wa Afrika.Nadhani wengi 

wenu tayari mmeisikia hotuba 

hiyo ambayo naweza kuiita ni 

hotuba ya hovyo sana kuwahi 

kutolewa na rais wa taifa kubwa 

kama Marekani. 

Binafsi sikupendezwa na 

shutuma na dharau zile za rais wa 

Marekani kwa nchi yangu pendwa 

na kwa bara letu la Afrika na ndiyo 

maana sikuweza kutoa hotuba 

niliyokuwa nimeiandaa kuitoa na badala yake nikaamua kumjibu pia 

rais wa Marekani kwa maneno 

makali pia.Katika houba yangu 

niliweka wazi kwamba tutafanya 

mazungumzo na mashirikiano na 

Korea Kaskazini endapo 

yataoneana kuwa na faida kwa 

nchi yetu. Baada ya hotuba yangu 

ile ukaibuka msuguano mkubwa 

Wazee wangu na watanzania 

naomba mfahamu kwamba 

kumekuwa na ukandamizwaji 

mkubwa sana katika nchi zetu 

zinazoendelea kutoka kwa nchi 

tajiri zikitutaka tufanye kila 

wanachokitaka wao na tukikataa 

wanatishia kutunyima misaada ya 

kimaendeleo.Nchi zetu nyingi bado 

zinaendelea kutegemea misaada kutoka nchi tajiri.Bajeti zetu bado 

ni tegemezi kwa kiasi kikubwa na 

ni nchi chache sana barani Afrika 

ambazo zimejenga uwezo wake wa 

ndani lakini nyingi bado 

zinategemea nchi wahisani.Hisani 

hii inaendelea kutufanya waafrika 

tuwe watumwa na umasikini 

usiishe katika nchi 

zetu.Tunaogopa kufanya maamuzi 

magumu kwa ajili ya maendeleo ya 

nchi zetu kwa kuogopa kuwaudhi 

wahisani wetu ambao wanaweza 

wakatunyima misaada endapo 

hawataridhika na maamuzi hayo 

na hii imetufanya tuendele kuwa 

masikini kiazi hata 

kizazi.Tunasema kwamba tuko 

huru lakini kama huwezi bado kujitegemea kiuchumi na 

tunategemea kuendesha nchi zetu 

kwa misaada yenye masharti 

kutoka mataifa yale makubwa basi 

huu si uhuru kamili.Uhuru kamili 

ni pale tutakapoweza kujitegemea 

kiuchumi kuachana na omba omba 

ambayo inaturejesha katika 

utumwa wa kiuchumi.Tunazo 

rasilimali nyingi lakini 

hazitunufaishi kwa sababu hatuna 

uwezo wala teknolojia ya 

kutosha,hatuna uhuru wa kupanga 

bei wa bidhaa zetu za 

kilimo.Rasilimali ni zetu lakini 

tunapangiwa bei na hawa 

wakubwa.Ninawahakikishia baba 

na mama zangu na watanzania kwa 

ujumla kama hali ikiendelea hivi,dunia itafika mwisho na sisi 

tukiwa bado masikini wakubwa . 

Wazee wangu wa Dar es 

salama na watanzania,matamshi 

ya rais Mike straw aliyoyatoa na 

anayoendelea kuyatoa 

yanaonyesha picha halisi ya hiki 

ninachokizungumza.China ni 

mshirika mkubwa wa Korea 

Kaskazini na wanafanya biashara 

kubwa lakini Marekani 

haimuongelei China kwa kuwa ni 

taifa kubwa kiuchumi na kijeshi 

badala yake anatutolea vitisho sisi 

mataifa madogo na masikini 

kwamba tutakiona cha mtema 

kuni tukithubutu kushirikiana kwa 

namna yoyote ile na Korea Kaskazini.Huu ni unyanyasaji 

ulipovuka mipaka. 

Umasikini wetu kama 

Tanzania na kama waafrika 

unasababishwa na viongozi wetu 

waliopo sasa na wale waliopita 

kushindwa kufanya maamuzi 

magumu kwa ajili ya kufanya 

mapinduzi makubwa ya uchumi 

kwa nchi zetu na hivyo nchi yetu 

kuendelea kuitwa nchi masikini 

wakati tuna utajiri wa kila 

aina.Siwalaumu sana wazee wetu 

kwani walifanya kazi kubwa ya 

kupambana wakaikomboa nchi 

yetuna kutujengea misingi mizuri 

ya amani ,utulivu na mshikamano 

lakini sasa umefika wakati wetu 

sisi kufanya mapinduzi makubwa ya uchumi na kwa kuwa bado tuko 

katika ukoloni wa kiuchumi ambao 

kwa kiasi kikubwa uchumi wetu 

unamilikiwa na mataifa makubwa 

ya nje,lazima tufanye maamuzi 

magumu sana.Matokeo ya 

maamuzi tutakayoyafanya leo hii 

hatutanufaika nayo bali watoto na 

watoto wa watoto wetu.Nchi zote 

zilizopiga hatua kimaendeleo 

zilifanya maamuzi ya kuondokana 

na umasikini na wakasimama 

katika maamuzi yao na baada ya 

vizazi leo hii wamekuwa mataifa 

tajiri na nchi nyingine ambazo ni 

tajiri sasa hazina rasilimali kama 

tulizonazo sisi kwa hiyo hata sisi 

tukiamua kuanza leo hii kuchukua 

hatua madhubuti juu ya kuubadili uchumi wetu tunaweza” Makofi 

mengi yakapigwa 

“Nawaambieni ukweli wazee 

wangu na watanzania kwamba 

tunaweza tukiamua na lazima 

tuamue.Hatuwezi kukubali hali hii 

ikaendelea.Hatuwezi kuendelea 

kuwa omba omba kwa nchi tajiri 

wakati tunazo rasilimali nyingi 

zimejaa kila kona ya nchi 

yetu.Hatuwezi kuendelea 

kuruhusu madini yetu na 

rasilimali nyingine kuchukuliwa 

na wageni kwa kisingizio cha 

uwekezaji wakati wananchi wetu 

wakiendelea kuwa masikini na 

tunaachiwa mashimo.Tunaibiwa 

halafu tunaletewa pesa kama 

misaada kwa masharti wakati pesa hizo zinatokana na wizi mkubwa 

wanaoufanya kwetu.Kufuatia hali 

hiyo mimi kama rais wenu 

mliyenichagua kwa kura nyingi 

sana niwaongoze nimefanya 

maamuzi magumu” akanyamaza 

kidogo akanywa funda la maji na 

kuendelea 

“Wazee wangu wapendwa na 

watanzania kwa ujumla nimeamua 

kuiingiza nchi katika vita ya 

kiuchumi.Nimechagua njia ngumu 

ambayo wengi hawatapenda 

kuipita lakini sisi lazima 

tuipite.Nimeamua kuanzisha 

mashirikiano ya kibiashara na 

Korea kaskazini.Kelele nyingi sana 

na vitisho vinatolewa kwa nchi zile 

ambazo zinashirikiana na Korea Kaskazini lakini hayo yote 

nimeamua kuyaweka kando na 

kuamua kushirikiana na nchi hii” 

Akanyamaza kidogo baada ya 

kusikia kumekuwa na minong’ono 

mle ukumbini akawatazama wazee 

halafu akanywa maji kidogo na 

kuendelea 

“Wazee wangu nimefanya 

maamuzi haya magumu sana licha 

ya vitisho kwa nchi yetu kwa 

sababu kubwa moja.Nchi ya Korea 

kaskazini licha ya harakati zake za 

kijeshi na kufanya majaribio 

kadhaa ya makombora baharini 

kitu ambacho sisi kama nchi 

hatukiungi mkono lakini 

wanafanya mageuzi makubwa sana 

ya uchumi na uchumi wao unakua kwa kasi kubwa kiasi kwamba 

wakubwa hawa wakiongozwa na 

Marekani wanaanza kuwa nawasi 

wasi kwamba uchumi wa Korea 

Kaskazini ukiwa mkubwa sana 

taufa hili litakuwa tishio kubwa 

kwao na ndiyo maana wanafanya 

kila wawezalo kuweza 

kuizorotesha Korea Kaskazini 

kiuchumi kwa kuweka vikwazo 

vya kila mara vya kiuchumi lakini 

pamoja na hayo bado uchumi wa 

Korea kaskazini umeendelea 

kupaa.Wamebadili sera zao za 

uwekezaji na sasa wawekezaji 

kutoka nchi nyingine 

wanaruhusiwa kwenda kuwekeza 

na kuna wawekezaji wengi kutoka 

China na baadhi ya nchi za Asia.Wana viwanda vingi sana sasa 

hivi na wanatengeneza bidhaa 

nyingi sana ambazo masoko yake 

makubwa ni nchi za Asia ,baadhi ya 

nchi za Afrika na Ulaya.Wamekuza 

teknolojia yao na wanatengeneza 

bidhaa za kielekroniki kwa 

teknolojia yao.Haya ni mageuzi 

makubwa sana wameyafanya 

ambayo hata sisi tunaweza 

kuyafanya.Inakadiriwa kama 

ukuaji huo wa uchumi wa Korea 

Kaskazini utaendelea kama ulivyo 

hivi sasa ,kwa miaka kumi ijayo 

itakaribiana kulingana kiuchumi 

na China. 

Ukuaji huo wa kiuchumi wa 

Korea Kaskazini unawafanya 

wahitaji sana kupata malighafi nyingi kwa ajili ya viwanda 

vyao.Wanahitaji pamba nyingi kwa 

kuwa wana viwanda vingi vya nguo 

na kama haitoshi watajenga pia 

viwanda vya nguo hapahapa 

Tanzania na hawatanunua pamba 

ghafi bali watajenga viwanda vya 

kutengeneza nyuzi na kutengeneza 

vitambaa hapa hapa nchini kwa 

hiyo watanunua vitambaa kutoka 

Tanzania na hiyo itaongeza 

thamani ya Pamba ya Tanzania na 

kuongeza mapato ya 

nchi.Wanahitaji mafuta safi ya 

magari na mitambo,wanahitaji gesi 

wanahitaji madini na watajenga 

kiwanda kikubwa cha kukata na 

kuongeza thamani ya madini ya 

vito hapa nchini hivyo hakutakuwa na madini yatakayopelekwa nje ya 

nchi kukatwa kila kitu kitafanyika 

hapa hapa Tanzania.Wanahitaji pia 

mazao mengine ya kilimo kama 

kahawa n.k.Wanahitaji pia madini 

ya Urani kwa ajili ya kuzalisha 

umeme wa kutosha wa viwanda 

vyao tofautina maneno 

yanayosemwa na Marekani na 

washirika wake kwamba wanataka 

kutumia madini hayo kuongeza 

idadi ya silaha zao za nyuklia. 

Sisi Tanzania pia tuko katika 

mageuzi ya kiuchumi,viwanda 

vingi vinajengwa hapa kwa hiyo 

tutahitaji umeme wa 

uhakika.Nimezungumza na 

kiongozi wa Korea kaskazini na 

ameahidi kutujengea kinu cha nyuklia hapa nchini kwetu kwa 

ajili ya kuzalisha umeme kwani 

tunacho kiwango kikubwa cha 

madini ya Urani.Endapo 

tutalifanikisha hilo Tanzania 

tutakuwa wazalishaji wakubwa wa 

umeme afrika mashariki na 

tutauza umeme mwingine kwa 

jirani zetu kwani tutakuwa na 

kiwango kikubwa cha umeme.Haya 

na mengi ambayo sijayasema hapa 

ni picha ya wazi kwamba Tanzania 

itanufaika sana kama itaanzisha 

mashirikiano ya kibiashara na 

Korea kaskazini.Kwa sasa 

Marekani ndio wawekezaji 

wakubwa hapa Tanzania katika 

sekta muhimu kama gesi,na 

madini lakini pamoja uwekezaji huo mkubwa walioufanya lakini 

bado hatunufaiki chochote,ni wizi 

mtupu unaoendelea huko,madini 

yetu yanazidi kuisha bila ya sisi 

kunufaika.Nimesema imetosha na 

sasa tunataka kuanza kunufaika na 

madini yetu wenyewe kwa hiyo 

basi tutachukua hatua za kupitia 

upya sera na sheria zetu za madini 

na kwa wakati huo wote 

makampuni haya yatasimamisha 

shughuli zao hapa Tanzania hadi 

hapo tutakapobadilisha sheria 

zetu za madini ambazo tunataka 

Tanzania inufaike kwa kiwango 

kikubwa.Kama kuna kampuni 

itakayoshindwa kukubaliana na 

sheria zetu mpya milango iko wazi 

na wanaruhusiwa kuondoka.Hatubembelezi 

mwekezaji tena kwa hiyo yeyote 

ambaye hajisikii kuwekeza 

Tanzania anaweza kuondoka mara 

moja.Tunataka kujenga uwezo wa 

ndani ili tuweze kuchimba 

wenyewe na kupata faida. 

Wazee wangu na watanzania 

,tumeanza kuchukua hatua za 

kufanya mabadiliko katika uchumi 

wetu na baadhi ya hatua hizo kama 

vile mashirikiano na Korea 

kaskazini hazitakuwa rahisi kwani 

hazitawapendeza mataifa tajiri 

kwa hiyo tutawekewa vikwazo 

vikali vya kiuchumi.Tutazuiwa 

kuuza bidhaa zetu katika masoko 

ya kimataifa ,tutawekewa vile vile 

vikwazo vya kuagiza bidhaa mbali mbali kutoa nje ya nchi,pamoja na 

vikwazo vingine vingi lengo ni 

kuudhoofisha uchumi wetu ili 

tuwapigie magoti.Tutapitia kipindi 

kigumu sana katika historia ya 

nchi lakini 

tutashinda.Nawahakikishia 

tunashinda na mimi kiongozi wenu 

nitasimama imara na kutangulia 

mbele kuwaongoza hadi 

nihakikishe nimewafikisha katika 

Tanzania ya maziwa na 

asali.”Makofi mengi yakapigwa 

“Ndugu zangu narudia tena 

kuwahakikishia kwamba 

tutashinda hii vita japo 

ngumu.Lakini hatutashinda kwa 

maneo matupu bali kwa 

vitendo.Kwanza kabisa sote tunapaswa kutambua kwamba 

nchi iko vitani na si vita ya 

kushambuliana kwa silaha kali bali 

vita ya kiuchumi ambayo ni mbaya 

sana.Baada ya kulifahamu hilo kila 

mmoja anapaswa aiunge mkono 

vita hii na nchi yote inapaswa ije 

pamoja .Tukijiunga na kwenda 

pamoja kama nchi basi vita hii 

haitakuwa ngumu kwetu lakini 

endapo tutajigawa wenyewe kwa 

wenyewe tutawapa nafasi maadui 

zetu kwa hiyo nawaomba sote 

tushikamane katika vita hii.Najua 

si wote watakubaliana na haya 

tunayoyafanya lakini naomba hata 

wale wasiokubaliana nasi 

wasiwavunje moyo wale ambao 

wamekubali kuingia vitani.Tunataka kuiondoa nchi 

katika utegemezi kwa hiyo 

tutakuwa wakali sana kwa yeyote 

atakayejaribu kuturudisha nyuma. 

Tunaanza kwa kujenga 

biashara ya ndani,tujenge 

utamaduni wa kutumia bidhaa 

zetu zinazozalishwa na viwanda 

vya ndani,tuvae nguo zetu,viatu 

vyetu na hivyo kuvijengea uwezo 

viwanda vyetu vya ndani. 

Tutaimarisha biashara baina ya 

nchi majirani na kuzitumia vyema 

fursa za kikanda kufanya biashara 

na vile vile tutajenga mashirikiano 

makubwa na nchi ambazo 

zitatuunga mkono katika vita 

hii.Tayari nimekwisha pata 

uthibitsho kutoka kwa rais wa China ambaye ametangaza rasmi 

kutuunga mkono,Urusi wako na 

sisi,India,Iran,Venezuela,Mexico,Br

azil,Qatar na nchi nyingine mbali 

mbali za kiarabu.Hawa na wengine 

ambao wataendelea kutuunga 

mkono tutajenga nao mashirikiano 

mazuri ya kibiashara na hivyo 

uchumi wetu utaendelea 

kuiamarika licha ya 

vikwazo.Kikubwa zaidi tunapaswa 

kufaya kazi kwa bidii sana na 

kuhakikisha kila kaya 

inajitosheleza kwa chakula na nchi 

kwa ujumla na kuweka 

akiba.Tujifunze matumizi mazuri 

ya fedha tunazozipata.Kuhusu ajira 

nawaomba msihofu ndugu 

watanzania kwani viwanda vingi vitajengwa na tutazalisha ajira 

nyingi.Mambo yote haya 

yatafanikiwa endapo 

tutashikamana ndiyo maana 

narudia tena kuwasisitiza ndugu 

watanzania tushikamane sana na 

kufanya kazi kwa bidii.Mtuunge 

mkono katika kila hatua 

tunazochukua kwa manufaa ya 

nchi yetu.Endapo tukienda pamoja 

tutafanikiwa katika vita hii na 

Tanzania itakuwa ni taifa kubwa 

kiuchumi Afrika,tutaweza 

kujitegemea wenyewe na 

hatutayumbishwa na mtu au taifa 

lolote” 

Hotuba hii ya rais Dr Vivian 

ilisimamisha nchi kwa muda wote 

aliokuwa anaitoa.Ilikuwa inarushwa mubashara katika 

runinga na katika redio zote hivyo 

wananchi wote hata wale wa 

vijijini waliweza kuipata.Wengi 

walifurahishwa sana na hotuba ile 

hasa msimamo wa rais kuhusiana 

na mageuzi makubwa ya 

uchumi.Wengi waliokuwa na hofu 

waliondolewa hofu baada ya 

kumuona rais wao namna 

alivyokuwa amejiamini na 

akiongea bila woga wowote.Wengi 

waliipongeza sana hotuba ile nzuri 

na waliahidi kumuunga mkono 

rais katika vita ile ya kiuchumi 

aliyoitangaza. 




Tayari kiza kimekwisha ingia 

na Theresa amekwisha jiandaa 

tayari kuelekea hoteli Pentagone 

kumchukua Nathan kama 

alivyokuwa amemuahidi kwamba 

atakwenda kumchukua.Kwa zaidi 

ya dakika kumi na tano sasa 

Theresa amekuwa mbele ya kioo 

kikubwa cha kujitazamia 

akijiangalia na uso wake 

ukionyesha wasiwasi mkubwa 

aliokuwa nao. 

“Kuna sauti ninaisikia 

inaniambia kwamba nisifanye hivi 

ninavyotaka kufanya lakini kila 

nikimfikiria Nathan naikumbuka 

picha ya risasi zaidi ya sabini alizopigwa baba,namkumbuka 

mama alivyoyatoa maisha yake 

kuniokoa.Japokuwa bado haina 

uthibitisho lakini naamini Nathan 

ni mmoja wa watu walio katika 

mtandao wa wale walioteketeza 

familia yangu na bado anaendelea 

kutuchunguza na kusabisha tuishi 

kwa wasi wasi.Nikikumbuka 

mambo haya ninajikuta nikipata 

hasira na kuendelea na mipango 

yangu.I’ll never be the same after 

tonight but I have to do it to 

protect myself and my 

sister”Theresa akatolewa 

mawazoni na simu ya Mathew 

“Hallow Theresa” 

“hallow Mathew” “Theresa are you ok? Mathew 

akauliza baada ya kugundua kitu 

katika sauti ya Theresa 

“I’m ok Mathew.Uko wapi? 

‘Niko nyumbani kwangu 

nimekwisha jiandaa na ninasubiri 

simu yako.Nimeona kimya ndiyo 

maana nimeamua kukupigia” 

akasema Mathew 

“Niko hapa nyumbani 

ninajiandaa kuelekea hoteli 

Pentagone kumchukua Nathan” 

“Ok sawa ukishamchukua 

utanijulisha kwa ujumbe mfupi” 

akasema Mathew na kukata simu 

“Miguu yangu mizito hata 

kunyanyuka lakini lazima nijikaze 

na nikamilishe mpango wangu.Bila 

kufanya hivi dada na mimi tutakuwa hatarini” akawaza 

Theresa na kuchukua mkoba wake 

akaingia garini na kuondoka 

kuelekea hoteli Pentagone. 

“Ukimuona alivyo kama 

malaika kumbe ni shetani nyoka 

mkubwa yule.Kwa muda huu wote 

amekuwa 

anatuchunguza.Amekuwa anapata 

taarifa zetu zote na sielewi ni kitu 

gani anakichunguza kwetu? Kitu 

gani anakichunguza kwa 

dada?Kuna nyakati ninafikiri 

yawezekana labda bado 

wanatuchunguza kufahamu 

kuhusu football? Hisia zinanituma 

hivyo yawezekana hawa jamaa 

wamekaa kimya muda huu wote na 

wanatuchunguza.Kama ni hivyo basi Marekani ndio waliomuua rais 

Anorld na kuiteketeza pia familia 

yangu.Ninashukuru sijawahi 

kumueleza mtu yeyote kuhusu siri 

hii na kama ningefanya hivyo 

wangekwisha tuua mimi na 

dada.Nathan ametumwa makusudi 

kwa lengo la kutuchunguza lakini 

usiku wa leo ni mwisho wa 

sarakasi zake” akaendelea kuwaza 

Theresa huku sura yake ikijikunja 

kwa hasira 

Alifika hoteli Pentagone na 

kwenda kugonga chumbani kwa 

Nathan akafunguliwa na kumkuta 

Natha akiwa amekaa sofani 

amependeza kwa suti nyeusi huku 

uso wake ukiwa na tabasamu.Theresa akavuta pumzi 

ndefu na kutabasamu 

“tabasamu kwa mara ya 

mwisho paka wewe” akawaza 

Theresa na kwenda kumkumbatia 

Nathan 

“Umeshindaje leo? 

“Nimeshinda salama 

Theresa.Sijui wewe” 

“Hata mimi nimeshinda 

salama” 

“Nilikuwa na hofu pengine 

hautakuja tena” akasema Nathan 

na wote wakacheka 

“Kwa nini nishindwe kuja 

wakati ni mimi ndiye 

niliyekuomba uje? Akasema 

Theresa huku akicheka kidogo “Uko tayari?Tunaweza 

kuondoka? Akauliza Theresa 

“Niko tayari tunaweza 

kuondoka” akasema Nathan 

wakatoka mle chumbani 

wakaingia katika gari la Theresa 

wakaondoka 

“Vivian 

anaendeleaje?Umefanikiwa 

kuonana naye? Nathan akauliza 

“Usiwe na haraka hivyo 

Nathan,utafahamu kila 

kitu”akasema Theresa huku 

akitabasamu 

“Moyo wangu hautulii kila 

nikimuwaza Vivian.Toka 

tulipoingia katika mgogoro siko 

sawa kabisa” “Ushofu Nathan suala hili 

limekwisha malizika na kama 

ikimpendeza Mungu usiku wa leo 

utakuwa ni usiku wa furaha kubwa 

katika maisha yako” 

“Kweli Theresa? Akasema 

Nathan kwa furaha kubwa 

“Mimi huwa ninaongea kwa 

vitendo.Twende nyumbani tupate 

chakula na kisha mambo mengine 

yatafuata ila leo kuna mambo 

makubwa.” Akasema Theresa . 

Walifika nyumbani kwa 

Theresa na Nathan akakaribishwa 

sebuleni 

“Una nyumba nzuri sana 

Theresa” 

“Ahsante Nathan.Kabla ya yote 

ngoja kwanza niandae chakula tule halafu nikueleze mwanzo hadi 

mwisho kuhusu suala lenu” 

Akasema Theresa na kwenda 

jikoni akaitazama chupa yenye 

mvinyo akaishika na akahisi 

mikono inamtetemeka.Akaiweka 

chupa chini na kuchukua simu 

yake akamtumia ujumbe Mathew 

akamjulisha kwamba tayari 

Nathan alikuwa pale nyumbani 

kwake.Akachukua tena chupa ile 

akaitazama na kuchukua glasi 

akaelekea sebuleni akammiminia 

Nathan katika glasi 

 “Nathan karibu kinywaji mimi 

naandaa chakula.Jisikienyumbani” 

akasema Theresa na kuondoka 

pale sebuleni akaenda kuandaa 

chakula . “Mungu atanisamehe kwa hili 

nililolifanya lakini sina namna 

nyingine ya kufanya.Nina hasira 

sana yule kenge.Ni mtu hatari 

sana kwetu.Huyu ni nyoka mwenye 

sumu kali ambaye anapaswa 

kupondwa kichwa haraka sana 

kabla hajatujeruhi” akawaza 

Theresa.Alionekana kuwa na wasi 

wasi mwingi.Aliandaa chakula 

mezani na kuelekea sebuleni 

kuchungulia. 

Nathan alikuwa ameanguka 

amelala sakafuni akiwa 

amejikunja.Mdomoni alionekana 

kutokwa na mapovu mengi huku 

akikoroma kwa nguvu.Theresa 

akapata ujasiri akamfuata 

akajaribu kumtikisa lakini Nathan hakuwa na fahamu na aliendelea 

kukoroma kwa nguvu na mara 

akawa kimya .Theresa akashindwa 

kujizuia akaenda chumbani kwake 

akilia. 

“Please Lord forgive me.I’ve 

killed him !! akalia kwa woga.Mwili 

wote ulikuwa unamtetemeka. 

“Sikuwahi kuhisi kama siku 

moja na mimi nitaingia katika 

dhambi kubwa kama hii ya kuua 

mtu.Lakini huyu ni mtu hatari sana 

kwa usalama wa nchi yetu na kwa 

familia yangu.Angeendelea kubaki 

hai angetuteketeza wote na kuleta 

madhara makubwa kwa 

nchi.Sitakiwi kulia,napaswa kuwa 

jasiri.Hawa ndio walioiteketeza 

familia yangu kikatili sana.Nilikuwepo siku ile na 

nilishuhudiwa namna baba 

alivyouawa.Lazima nilipe kisasi 

kwa ajili ya baba na mama 

waliouawa kikatili” akawaza na 

kuinuka akaenda jikoni akachukua 

chupa ile yenye mvinyo akaenda 

kuumwaga wote chooni na kwena 

nje akaivunja vunja ile chupa na 

kutupa vipande vyake katika 

shimo la maji machafu akarejea 

sebuleni.Nathan alikuwa ameloa 

mapovu na alikuwa ametoa ulimi 

nje.Akamtikisa kwa mguu 

“He’s 

gone”akawaza.Akaichukua glasi ila 

ya kinywaji aliyokuwa anaitumia 

Nathan na kwenda kuitupa katika shimo la maji taka akarejea 

sebuleni 

***************** 

Mathew alipopata ujumbe wa 

Theresa kwamba tayari 

amekwisha mchukua 

Nathan,hakuwa mbali na hoteli 

Pentagone hivyo akawasha gari 

akaelekea moja kwa moja hoteli 

Pentagone.Usiku huu hoteli hii 

ilikuwa inang’aa kutokana na taa 

nyingi za kila rangi.akaegesha gari 

na kushuka akaelekea 

ndani.Kulikuwa na watu wengi 

katika sehemu ya chini 

kulikokuwa na hoteli na 

baa.Kulikuwa na bendi iliyokuwa inapiga muziki wa kiafrika na 

kuwaburudisha wageni waliofika 

hotelini hapa.Hakuna aliyekuwa 

na mashaka na Mathew akapanda 

lifti hadi ghorofa ya tatu.Ndani ya 

lifti alikuwa peke yake na alipofika 

ghorofa ya tatu akashuka akaanza 

kutafuta chumba namba 202 

ambacho ndicho chumba cha 

Nathan.Alikuwa amevalia nadhifu 

kabisa akiwa katika suti nzuri ya 

kijivu na mkoba mzuri wa 

gharama kubwa, alionekana ni mtu 

mwenye uwezo kifedha.Alipishana 

na watu kadhaa na halafu 

akakipata chumba namba 

202.Akatazama pande zote na 

hakuona mtu yeyote.Kulikuwa 

kimya.Akatoa mashine fulani ndogo toka katika mkoba wake 

akaigundisha pembeni ya sehemu 

ya kupitishia kadi ya kufunguilia 

mlango halafu akachukua kadi 

fulani akaiingiza katika kile kifaa 

alichokigundisha mlangoni na 

kubonyeza namba kadhaa na 

kusubiri kwa muda wa sekunde 

kadhaa na taa ya kijani ikawaka 

halafu akaipitisha kadi ile katika 

sehemu ya kuwekea kadi na 

namba fulani zikajitokeza katika 

kile kifaa alichokigundisha 

pembeni na mlango 

ukafunguka.Taa ilikuwa inawaka 

chumbani akaizima haraka halafu 

akawasha kifaa fulani kidogo na 

mara akaona mwangaza wa bluu 

pembeni ya dirisha akasogea na kukiondoa kile kifaa kilichokuwa 

karibu na dirisha akakikanyaga 

kwa mguu kikasambaratika.Bado 

kifaa kile alichokuwa amekiwasha 

kiliendelea kutoa mlio akatazama 

chini ya kitanda na kuona kuna 

mwanga wa bluu akafunua godoro 

na kutoa kifaa hicho akakiharibu 

vile vile.Baada ya hapo akatoa 

kopo fulani akapuliza mle 

chumbani na kuvaa miwani 

maalum na kuona kitu fulani 

kidogo kilichokuwa juu ya meza 

ambacho unaweza 

ukakidharau.Akakichukua 

akafungua dirisha na kukitupa nje. 

“Clear” akasema na kuwasha 

taa “Kweli huyu jamaa ni 

jasusi.Alikuwa amechukua kila 

hatua ya kujihami.” Akawaza 

Mathew na kuanza kuchunguza.Juu 

ya meza kulikuwa na kompyuta 

mpakato,akaichukua na kuiweka 

katika mkoba wake.Akalifungua 

sanduku lake na kumwaga kila 

kitu kitandani akaanza kukagua 

kitu kimoja kimoja akakutana na 

simu tatu,akazichukua zote 

akaziweka katika mkoba 

wake.Kitu cha mwisho 

alichokipata kilikuwa ni kimkebe 

fulani kidogo cha rangi nyekundu 

akavichukua vyote na wakati 

akirejesha nguo katika sanduku 

mara simu yake ikaita,alikuwa ni 

Theresa “hallow Theresa” 

“Mathew uko wapi? 

“Niko hapa chumbani kwa 

Nathan najiandaa niondoke.Tayari 

amekwisha ondoka? 

“Mathew nakuomba uje hapa 

nyumbani kwangu haraka 

sana.Chukua kila unachotaka 

kikichukua na uje hapa nyumbani 

haraka”akasema Theresa 

“Kuna nini Theresa? Nathan 

amekwisha ondoka hapo? 

“Mathew naomba uje hapa 

haraka sana .Kuna tatizo 

limetokea” 

“Kuna tatizo gani? 

“Siwezi kukueleza simuni 

Mathew nakuomba uje haraka” 

akasema Theresa na kukata simu.Mathew akapakia vitu haraka 

haraka katika sanduku na kutoka 

mle chumbani akachungulia kama 

kuna mtu yeyote pale karibu lakini 

hakukuwa na mtu akatoka haraka 

haraka na kupitia sehemu ya baa 

halafu akaelekea mahala 

alikoegesha gari akaondoka hoteli 

Pentagone 

“Theresa ana tatizo 

gani?Nathan amegundua kitu na 

anataka kumdhuru? Akajiuliza 

huku akiongeza mwendo wa gari 

na kuyapita magari kadhaa 

“Lazima kutakuwa na tatizo 

kubwa .Huyu jamaa ni mtu hatari 

alikuwa amejihami sana.Ndani ya 

chumba kile kulikuwa na kifaa kile 

alichokuwa amekiweka pembeni ya dirisha ambacho kazi yake 

ilikuwa ni kuhisi aina ya mtu 

aliyeingia chumbani na 

kumjulisha Nathan kama kuna mtu 

chumbani kwake.Hiki ni kifaa 

kinachomchunguza mtu 

kibaolojia.Kinahisi hadi harufu ya 

mtu.Huyu jamaa atatuongoza 

kuelekea kupata majibu ya 

maswali yetu” akawaza Mathew 

Alifika nyumbani na mara tu 

Mathew aliposhuka garini Theresa 

akamfuata akamkubatia 

“Thank you Mathew for 

coming” akasema na kumshangaza 

Mathew. 

 “Theresa kuna atizo gani? 

Umenistua sana uliponipigia 

nikahisi umepata tatizo kubwa.Yuko wapi Nathan? 

ameondoka? Akauliza 

Mathew.Theresa alionekana kuwa 

na woga mwingi 

“Mathew twende ndani 

tafadhali” akasema Theresa na 

wakaelekea sebuleni.Mathew 

akastuka sana baada ya kumuona 

Nathan akiwa amelala sakafuni 

amejaa mapovu mdomoni na 

alionekna hana uhai. 

“Nini kimetokea? Akauliza 

Mathew huku akimsogelea Nathan 

na kutaka kumshika Theresa 

akamzuia 

“Don’t touch him ! akasema 

Theresa na kuzidi kumshangaza 

Mathew “Theresa kuna nini ?Nathan 

amefanya nini?Mathew akauliza 

 “He’s dead” 

“Dead? How? Mathew akauliza 

“Nini kimetokea hapa 

Theresa? Akauliza Mathew huku 

akiwa amemkazia macho Theresa 

“Theresa niambie nini 

kimetokea hapa? Nini kimemuua 

Nathan?akauliza Mathew lakini 

Theresa alishinda kujibu alikuwa 

anatetemea midomo 

“You did this? Akauliza 

Mathew lakini Theresa hakujibu 

kitu 

“C’mon Theresa answer me 

you did this?akauliza kwa ukali na 

Theresa akatikisa kichwa 

kukubali. “Oh my God !! akasema 

Mathew na kumtazama Theresa 

kwa hasira 

“Kwa nini Theresa?Why 

????akauliza Mathew 

“Mathew I’m sorry.I had no 

choice” 

“No choice? Just that? Akauliza 

Mathew. 

“Mathew I’m sorry.” 

“Stop Theresa!! Akasema 

Mathew kwa ukali 

“How could you be so stupid?!! 

Akafoka Mathew 

“Kwa nini ukafanya jambo hili 

la kijinga bila kupima athari zake? 

Akaendelea kufoka 

Mathew.Maneno yale ya Mathew yakaonekana kumkera sana 

Theresa akapandwa na hasira 

“Mathew naomba usirudioe 

tena kuniita mimi 

mjinga.Nimelazimika kufanya hivi 

nilivyofanya kwa usalama 

wetu.Huyu mtu ni hatari na wewe 

unafahamu.Ameweka maisha 

yangu na dada hatarini.Huyu na 

mtandao wake ndio waliochukua 

uhai wa baba kikatili 

sana.Nitawezaje kumuacha hai mtu 

kama huyu ambaye anatuwinda 

usiku na mchana?Anatafuta taarifa 

zetu kila uchao,nimeshindwa 

kuvumilia Mathew nimeamua 

kuingia katika dhambi ya uuaji 

kwa ajili ya kuilinda familia 

yangu,kumlinda dada yangu.Unajua ni taarifa ngapi 

kuhusu dada zimewafikia 

wanaomtafuta usiku na mchana 

kupitia huyu mtu? Hukufanikiwa 

kuziona maiti za wazazi 

wangu,baba alipigwa risasi zaidi ya 

sabini,unadhani mwili wake 

ulikuaje?Yalikuwa ni mauaji ya 

kikatili sana ambayo yalifanywa na 

mtandao wa huyu mtu.Siwezi 

kumuacha akaenda hivi hivi 

nimeamua kumuua.Nimemuwekea 

sumu kali katika kinywaji yenye 

uwezo wa kuua kwa 

haraka.Vyovyote utakavyoamua 

kufanya mimi niko tayari kama ni 

kunipeleka polisi just do it I’m 

ready to pay for what I’ve done” 

akasema Theresa.Mathew akainama na kushika 

kiuno.Alizama mawazoni 

“Mathew do it quick.Call the 

police! Akasema Theresa kwa 

hasira 

“Theresa tafadhali usifanye 

utani katika suala kama 

hili.Nathan alikuwa ni mtu 

muhimu sana katika uchunguzi 

wetu na tulitegemea kupata 

mambo mengi kupitia kwake na 

ndiyo maana nikakuomba ufanye 

juu chini aweze kuja nchini .Kama 

ni kumuua ningeweza kumuulia 

huko huko Marekani lakini 

sikutaka afe kwani kuna mambo ya 

muhimu sana ninayahitaji kutoka 

kwake. Kwa hiki ulichokifanya 

tumerudi tena kwenye ziro hatuna tena mwanga.Kama ulikuwa na 

mawazo ya kumuua Nathan 

ungenieleza mapema ili tusubiri 

kwanza baada ya kufanya 

uchunguzi wangu ndipo nikuachie 

umuue uondoe hasira zako” 

“Mathew hawa watu 

wameteketeza familia yangu.Hujui 

ni uchungu kiasi gani nilionao 

baada ya kugundua kwamba huyu 

yuko katika mtandao wa watu 

waliowateketeza wazazi wetu na 

bado anaendelea kutufuatilia 

usiku na mchana.Hata wewe 

ungekuwa mahala pangu 

usingeweza kumuacha hai.Potelea 

mbali Mathew kama uchunguzi 

utashindikana lakini ili mradi mtu 

huyu hatari nimekwisha muondoa duniani na mimi na dada yangu 

tuko salama !! akasema Theresa 

“Usijidanganye Theresa.Dr 

Vivian hayuko salama.Umezidi 

kuyaweka maisha yake katika 

hatari kubwa kwa hiki 

ulichokifanya.Umeongeza mzigo 

wa matatizo” akasema Mathew na 

Theresa akainamisha kichwa 

akafuta machozi halafu kwa sauti 

ya upole akasema 

“Mathew please help 

me.Rightnow I’m don’t know what 

I’m going to do” akasema 

Theresa.Mathew akamtazama kwa 

muda halafu akasema 

“Kuna mtu mwingine yeyote 

anafahamu au umempigia simu kuhusiana na hiki kilichotokea? 

Akauliza Mathew 

“Hapana sijamjulisha mtu 

yeyote zaidi yako” 

“Good” akasema Mathew na 

kuinamisha kichwa akafikiri 

kidogo na kumtazama tena 

Theresa 

“Jambo hili tunapaswa 

kulifanya liwe siri kubwa ili rais 

asilifahamu.Tunapaswa kutafuta 

namna ya kuficha huu mwili 

usionekane kabisa na mtu yeyote 

na hata kama ikigundulika basi 

awe tayari hatambuliki” akasema 

Mathew 

“Una maanisha tukamzike? “Kama ikiwezekana iwe hivyo 

itakuwa vizuri lakini tutamzika 

wapi usiku huu? 

“Mathew sifahamu 

chochote.Ninahisi 

kuchanganyikiwa tafadhali fanya 

kile unachoweza kukifanya uweze 

kuuondoa mwili huu na 

kuuficha.Akili yangu haifanyi kazi 

tena” akasema Theresa huku 

akiendelea kumwaga machozi 

Mathew akainamisha kichwa 

na kuanza kufikiria,akatazama saa 

yake ilionyesha ni saa tano za 

usiku.Akachukua simu yake na 

kuzitafuta namba fulani akapiga na 

simu ikapokelewa 

“Hallow Casian naomba 

kuzungumza na Hamis Chuma mara moja” akasema Mathew na 

hakutoa simu sikioni na baada ya 

dakika mbili ikasikika sauti nzito 

“Bilionea Mathew,habari yako 

kaka? 

“Nzuri kabisa Hamis.Uko wapi 

mida hii? 

“Niko sehemu fulani 

tunajiandaa kwenda kazini” 

“C’mon Hamis hamuachi 

shughuli hizo? 

“Tukiacha tutaishije ndugu 

yangu mji wenyewe huu halafu na 

nyie watu wakubwa mmetukimbia 

siku hizi hata mawasiliano nasi 

hamtaki? 

“Si hivyo 

Hamis,ninawakumbuka sana watu 

wangu lakini naomba muachane na hizo shughuli mimi nitatafuta 

namna ya kuwawezesha” 

“Ndiyo maana nakukubali 

sana Mathew wewe uko tofauti na 

wengine.Unapenda kutatua shida 

za watu.Haya nieleze mkubwa 

wangu kuna nini usiku huu 

manaake najua haujanitafuta ili 

kunisabahi.Ukinipigia usiku kama 

huu lazima kuna kazi unataka 

kunipa” 

“Ni kweli Hamis kuna kazi 

nataka kukupa.Uko na vijana 

wangapi? 

“Niko na vijana watano” 

“Good.Kuna kazi nataka 

niwape na nitawalipa vizuri sana 

ila nataka muifanye kadiri ya maelekezo yangu” akasema 

Mathew 

“Usihofu mathew wewe 

unajua namna sisi tunavyofanya 

kazi zetu.Tukutane wapi? 

“Mbele ya Balale Bridge kuna 

ghorofa limetelekezwa kwa miaka 

mingi.Tukutane pale ndani ya 

dakika ishirini.” akasema Mathew 

na kukata simu 

Theresa nahitaji mfuko 

wowote mkubwa au karatasi 

kubwa la nailoni pamoja na 

kamba” Akasema Mathew.Theresa 

akaenda stoo na kurejea na 

karatasi kubwa la nailoni na 

kamba pamoja na glovu.Mathew 

akamlaza Nathan juu ya karatasi 

ile halafu akamsachi hakuwa na kitu chochote zaidi ya saa ya 

mkononi akaivua na kuiweka 

mfukoni.Akamviringisha vizuri 

ndani ya ile karatasi na kumfunga 

kamba.BadoTheresa alikuwa 

analia. 

“Mlinzi wako anajua 

kuendesha gari? 

“Ndiyo anafahamu” 

“Good.Mpe funguo mwambie 

aende akakuletee mvinyo.Mtume 

mbali kidogo sitaki aone wakati 

tunautoa mwili huu na kuupakia 

garini.Kuna mtu mwingine ambaye 

you humu ndani mida hii ? 

“Hakuna mtu 

mwingine.Mtumishi wangu 

amesafiri” akasema Theresa. “Haya fanya haraka 

kamuondoe mlinzi pale getini” 

akasema Mathew na Theresa 

akatoka baada ya dakika tano 

akarejea 

‘Tayari amekwisha ondoka na 

gari.” Akasema Theresa 

“Good”akasema Mathew na 

kumbeba Nathan hadi katika gari 

lake wakampakia katika buti 

“Kuna kitu chochote unahisi 

hakijakaa sawa hapo ndani? 

“Kila kitu kiko safi” 

“sasa mpigie simu mlinzi 

wako mwambie arudi umepata 

dharura kuna mahala 

unakwenda”akasema Mathew na 

kumpigia simu mlinzi wake akamtaka arudi nyumbani kwani 

yeye amepata dharura ametoka 

“Now let’s go” akasema 

Mathew na kuondoka. 

“Wale uliokuwa unazungumza 

nao kwenye simu ni akina nani? 

Theresa akauliza 

“Ni watu wangu” 

“Wanafanya shughuli gani? 

“Watoto wa mjini” 

“Watoto wa mjini? Hawana 

shughuli? 

“Wanashughulika na 

ujambazi” akasema Mathew na 

sura ya Theresa ikaonyesha 

mstuko mkubwa sana 

“Usistuke Theresa.Katika 

shughuli zetu huwa tunajikuta 

tunafahamiana na watu mbalimbali na kuna wakati huwa 

tunasaidiwa na watu kama 

hawa.Kuna kazi nyingine ambazo 

hatuwezi kuzifanya na huwa 

tunawatumia watu kama hawa 

wakazifanye.Wao ndio 

watakaoshughulikia huu mwili na 

hautaonekana tena” 

“Do you trust them? Theresa 

akauliza 

“Relax Theresa.Let me fix this.

akasema Mathew.



CENTRAL INTELLIGENCE 

AGENCY (CIA) – WASHINGTON DC 

Saa tisa alasiri jijini 

Washington DC kikao kilikuwa 

kinaendelea katika ofisi za shirika 

la ujasusi la Marekani CIA.Ndani ya 

chumba cha mikutano kulikuwa na 

watu kumi na tatu.Wakati kikao 

kikiendelea mlango ukafunguliwa 

akaingia mwanadada mmoja 

aliyekuwa amevaa sketi fupi na 

kufanya kikao kisimame akamuita 

mkubwa wake ambaye aliwaomba 

samahani wajumbe akatoka nje. 

“Kuna nini Monica? Akauliza 

“Mr Edger kuna tatizo 

limetokea naomba kama hutajali 

twende ofisini kwangu” akasema Monica na Edger akaingia tena 

katika kile chumba cha mkutano 

akawaomba wajumbe wamsubiri 

kuna dharura imejitokeza na 

atarejea muda si mrefu halafu 

akaelekea moja kwa moja ofisini 

kwa Monica 

“Kuna nini Monica? Akauliza 

Edger Brown 

“Kuna tatizo limetokea kwa 

Cell 12A.” akasema Monica na 

kumstua kidogo Edger 

“Kuna nini kimetokea? 

“Cell 12A aliondoka jana 

kuelekea Tanzania na nilikuwa 

nafuatilia maendeleo yake.Dakika 

chache zilizopita mawasiliano yake 

yalikatika” “Nini? Akauliza Edger kwa 

mshangao.Monica akabonyeza 

kompyuta yake na katika runinga 

kubwa iliyokuwamo mle ofisini 

kukatokea kitu mfano wa chati 

iliyokuwa na mstari mmoja 

ulionyooka katikati. 

“Mr Brown,Cell 12A alikuwa 

katika orodha ya wale maajenti wa 

CIA walioingizwa katika mfumo 

mpya wa utambuzi ambao 

wamefungiwa kifaa maalum ndani 

ya miili yao ambacho hurekodi 

mwenendo wa mapigo ya moyo na 

ambacho huwa kinaunganishwa 

kwa saa maalum anayoivaa 

mkononi ambayo hutuwezesha sisi 

kupata taarifa zake kila wakati na 

hapaswi kuivua saa hiyo katika siku zote za maisha yake.Iwe mvua 

au jua saa hiyo haitoki mkononi 

kwani imetengenezwa maalum na 

haipitishi maji wala 

haiharibiki.Muda mfupi uliopita 

kulitokea tatizo kwa Cell 

12A.Nilisikia kengele ya thadhari 

ikilia na nilipofuatilia nikagundua 

mapigo ya moyo ya Cell12A 

yalikuwa yameshuka chini isivyo 

kawaida na hii ni ishara kwamba 

alikuwa katika hali mbaya na 

baadae hali ikawa kama 

unavyoona katika chati .Ikiwa hivi 

inamaanisha kwamba ajenti huyo 

tayari amefariki dunia” 

“Mungu wangu!! Akasema 

Edger Brown. “Umejaribu njia zote za 

kuwasiliana naye zimeshindikana? 

“Njia zote za kuweza kupata 

mawasiliano yake na kufahamu 

yuko wapi zimekatika ghafla na 

hakuna inayofanya kazi.Ni saa 

yake tu ambayo bado ninaendelea 

kuisoma hapa” 

“Hizi ni taarifa za kustusha 

sana” 

“Kitu kingine” akasema 

Monica 

“Kuanzia leo asubuhi taarifa 

kutoka kwa namba 1212 ambaye 

ni rais wa jamhuri ya muungano 

wa Tanzania zimekatika na mpaka 

sasa hakuna rekodi zozote kutoka 

kwake wala kutoka kwa namba 

1214.Wote hawa wawili taarifa zao zimekatika asubuhi ya leo kitu 

ambacho kinatia shaka kidogo 

halafu hawa ni ndugu.Namba 1214 

ni mdogo wake na 1212.” 

“Kuna kitu hakiko sawa 

Tanzania.Hatua za haraka sana 

zinatakiwa kuchukuliwa.Usifanye 

chochote ngoja kwanza 

niwasiliane na wakuu wangu 

niwape taarifa” akasema Edger 

brown na kuchukua simu 

akawasiliana wakuu wake 

akawajulisha kile ambacho 

alikuwa ameelezwa na 

Monica.Taarifa zile ziliwastua hata 

wakubwa wake 

“Kitu cha kwanza 

unachopaswa kukifanya Mr Brown 

wasiliana na 110C huyu atafanya mipango ya kwenda kumnusuru 

12A kama yuko kwenye hatari 

.Baada ya hapo suala la 1212 na 

1214 lianze kushughulikiwa 

haraka sana kwani hatuwezi 

kuwapoteza hawa hasa kwa wakati 

huu.Ni watu muhimu sana.110C 

afanye kazi ya ziada kuhakikisha 

kila kitu kinakaa sawa mpaka 

kufikia kesho jioni.Kitu kingine Mr 

Brown endapo kunatokea jambo 

kubwa kama hili toa taarifa makao 

makuu haraka sana kwa ajili ya 

maamuzi ya haraka.Elekeza macho 

yako Tanzania ambako ni muhumu 

sana kwetu kwa sasa.Tumekaribia 

sana kwa hiyo hatuwezi 

kushindwa hapa.110C ahakikishe 

suala hili halitokei tena.Tunamuhitaji sana 1212 

kuliko kawaida” akasema Steven 

Camp 

Edger brown akarejea katika 

ofisi ya Monica haraka 

“Monica mpigie simu haraka 

110C nahitaji kuzungumza naye” 

akasema Edger.Monica akapiga 

simu maalum kwa namba 110C na 

ilipoanza kuita akampatia Edger 

“Hallow 110C 

ninazungumza.Naongea na namba 

ngapi? 

“Unazungumza na Eger Brown 

CIA washigton DC.Kuna tatizo 

limetokea muda si mrefu na 

nimepewa maelekezo kwamba 

ulishughulikie haraka sana.Cell 

12A aliondoka huku marekani kuelekea Tanzania jana na amefika 

leo.Muda mfupi uliuopita 

mawasiliano yetu yameonyesha 

kwamba mapigo yake ya moyo 

yalianza kushuka sana na baadae 

yakakatika kabisa.Hii 

inatuonyesha kwamba yuko katika 

hatari au tayari amekufa kwa hiyo 

tunataka ulishughulikie hilo 

haraka sana na uhakikishe 

anapatikana akiwa katika hali 

yoyote ile mzima au 

amekufa.Wasiliana nasi kila baada 

ya dakika kumi na tano kutupa 

taarifa.Monica anakutumia ramani 

inayoonyesha mahala alipo 12A 

ambako mpaka sasa bado 

tunaendelea kumsoma lakini hatuna taarifa za mapigo ya moyo 

wake” 

“Sawa ngoja nilishughulikie 

hilo haraka sana.” 

“Jambo la pili” akasema Edger 

“1212 na 1214 wamekatika 

kuanzia asubuhi ya leo.Fuatilia 

ujue kuna tatizo gani?Tunataka 

mawasiliano yarejeshwe haraka 

sana kabla ya kesho jioni” akasema 

Edger 

“Sawa Edger ngoja 

nishughulikie kwanza hili la 12A” 

akasema 110C na kukata simu 

DAR ES SALAAM – TANZANIA 

“Umepata nini kule chumbani 

kwa Nathan? Akauliza Theresa wakiwa wamesimama katika taa 

za kuongozea magari za barabara 

ya Serengeti.Hakukuwa na magari 

mengi katika barabara hii.Taa 

zikawaruhusu kupita wakaishika 

barabara ya Uwazi.Hii ni barabara 

inayopita kandoni mwa bahari na 

kwa usiku huu hakuna magari 

mengi.Mathew alitaka wawahi 

kufika mahala walikopanga 

wakutane na akina Hamisi Chuma 

“Mathew haukunijibu swali 

langu”Theresa akakumbusha 

“Nilikuuliza ulipata vitu gani 

kule chumbani kwa Nathan.Kuna 

chochote ulifanikiwa kukigundua? 

“Kuna vitu vichache 

nimevipata .Nimepata kompyuta 

ndogo,simu tat……………” akasema Mathew na mara akasikia 

muungurumo wa 

helkopta.Haikuwa juu sana akatoa 

kichwa kutazama nje.Helkopta ile 

ilikuwa chini chini sana na ilikuwa 

inakwenda sambamba nao 

Kwa mbali nyuma yao 

zikaonekana gari mbili zikija kwa 

kasi kubwa sana.Mathew 

hakushangaa kwani ni kawaida ya 

gari kukimbia katika barara hii 

ambayo kwa usiku huu huwa haina 

magari mengi. 

“Tutakapolimaliza hili suala 

nitavipitia vifaa vile na kuona 

kama kuna chochote tunaweza 

kugundua.” 

Piki piki mbili zilizokuwa 

zinakwenda kwa kasi kubwa zikawapita kwa kasi na helkopta 

ile ikaendelea kutembea juu yao. 

“Theresa kuna hali naiona si 

ya kawaida hapa.Kuna hizi gari 

mbili zinakuja nyuma yetu kwa 

kazi kubwa halafu kuna hizi piki 

piki mbili zimetupita kwa kasi na 

zilipofika mbele yetu zimepunguza 

mwendo na ile helkopta naona 

inaanza kupaa juu zaidi” akasema 

Mathew.Alianza kuhisi hatari. 

“Una wasi wasi labda 

tunafuatiliwa? Akauliza Theresa 

huku akitazama nyuma 

“Ninahisi hivyo”akasema 

Mathew 

“Nani atufuatilie?Hakuna 

yeyote anayefahamu kitu chochote kuhusiana na Nathan” akasema 

Theresa 

“Yawezekana hivyo lakini 

ninahisi kuna hali isiyo ya 

kawaida” akasema Mathew na 

kuachia usukani wa gari akatoa 

bastora zake akaziweka 

karibu.Theresa akaanza kuhisi 

baridi.Aliogopa sana.Ghafla piki 

piki zile zikageuza na kuanza 

kurudi kwa kasi kubwa na huku 

taa zao zikimmulika Mathew na 

kumfanya aone kwa taabu 

kutokana na mwanga mkali wa taa 

toka kwa zilie pikipiki 

“Theresa haraka ruka kiti cha 

nyuma” akasema Mathew na 

Theresa akaruka haraka katika 

kiti cha nyuma.Ghafla gari la akina Mathew likaanza kuyumba na 

kutaka kuhama njia .Tairi moja la 

mbele lilipasuka .Mathew hakuwa 

na papara aliushika usukani kwa 

nguvu na kulielekeza gari mbele 

huku akiondoa mguu katika pedeli 

ya mafuta. 

“Mathew what’s going on? 

Akauliza Theresa kwa wasi 

mkubwa baada ya kuona namna 

gari lilivyoyumba.Mathew 

hakujibu kitu bali aliendelea 

kulidhibiti gari na taratibu 

likaanza kupunguza mwendo na 

kusimama.Gari mbili zilizokuwa 

zikija nyuma kwa kasi nazo 

zikasimama.Mathew akataka 

kushuka garini lakini ghafla 

ikasikika milio ya risasi “Mathew tunashambuliwa !! 

akasema Theresa kwa wasi wasi 

mkubwa 

“Theresa lala chini!!! Akasema 

Mathew.Kwa haraka akabinua kiti 

cha pembeni na chini yake kukawa 

na sanduku ambalo alilifungua na 

ndani yake kulikuwemo na 

silaha.Akachukua kopo moja dogo 

mithili ya kopo la dawa ya kuulia 

wadudu akangoa kifuniko 

akafungua mlango kidogo na 

kulirusha kwa nyuma likaanza 

kutoa moshi mzito,akachukua 

lingine akalirusha na eneo la 

nyuma ya gari likawa na moshi 

mzito.Akiwa na bunduki ndogo 

mkononi akatazama nyuma na hakuona mtu na hakusikia tena 

risasi. 

“Theresa tuko katika hatari 

hivyo usishuke garini.Ngoja 

nipambane na hawa jamaa” 

akasema Mathew 

“Mathew please don’t!! 

akasema Theresa na mara ghafla 

kwa mbele yao zikatokea gari tatu 

za polisi zikiwasha vimuli muli 

halafu kwa juu ikatokea tena 

helkopta iliyowasha taa ikumulika 

gari la akina Mathew.Watu 

waliovalia mavazi ya polisi wakiwa 

wamejihami kwa silaha na fulana 

za kujikinga na risasi wakashuka 

ndani ya zile gari mbili na 

kujipanga,mmoja aliyekuwa na 

kipaza sauti akaanza kupaaza sauti kuwataka watu waliokuwamo 

katika lile gari la akina Mathew 

washuke garini kabla 

hawajashambuliwa 

“Mathew what are we going to 

do?Hawa polisi wanataka nini 

kwetu? akauliza Theresa huku 

akilia alikuwa amechanganyikiwa 

“Be strong Theresa !! 

Tumezungukwa na hawa askari 

kila kona.Wote wana silaha kali 

hatutaweza kupambana nao,wako 

wengi na jaribio lolote la 

kupambana nao linaweza 

kutuletea matatizo.Hata hivyo 

usihofu gari hili ni maalum kabisa 

halipenyi risasi hivyo tunaweza 

kutafuta msaada wa haraka” 

akasema Mathew “Then do something to get us 

out of here!! Akazidi kulia Theresa 

huku akisali kumuomba Mungu 

awaokoe.Mathew akachukua simu 

na kupiga zile namba maalum za 

rais. 

“Hallow Mathew” akasema Dr 

Vivian na Mathew akashusha 

pumzi baada ya simu yake 

kupokelewa 

“Mheshimiwa rais ninaomba 

msaada wako wa haraka sana.Niko 

mahala na Theresa tumezingirwa 

na askari polisi kila kona na 

wanataka kutushambulia kwa 

risasi.Ninaomba msaada wako wa 

haraka sana.Kuna gari zaidi ya nne 

na helkopta moja iko juu.Fanya 

haraka tafadhali” “Unasema mmezingirwa na 

polisi?!! Dr Vivian akashangaa 

“Ndiyo mheshimwia rais” 

“Dada tuokoe! Akasema 

Theresa kwa sauti huku akilia 

“Huyo ni Theresa?akauliza 

DrVivian 

“Ndiyo mheshimiwa rais ni 

Theresa” 

“Oh my God ! ni polisi gani hao 

na kwa nini watake 

kuwashambulia?kwa nini 

wawazingire? 

“Mheshimiwa rais fanya 

haraka msaada tafadhali.” 

Akasema Mathew 

“Ok ngoja nione 

nitakachofanya.Mko wapi?” “Tuko katika barabara ya 

Uwazi karibu na kanisa kubwa la 

Jerusalem temple” Akasema 

Mathew na kukata simu.Baada ya 

kuongea na rais akampigia simu 

Hamis 

“Mathew tayari tumekwisha 

fika hapa mahala tulipokubaliana 

tukutane.Uko wapi? 

“Hamis nimepata 

tatizo.Nimezingirwa na askari na 

wanataka 

kunishambulia.Tafadhali 

naombeni msaada.Niko hapa 

karibu na kanisa la Jerusalem 

temple.Tafadhali naombeni mje 

hapa haraka sana na muanzishe 

mashambulizi ili niweze kupata 

nafasi ya kutoka” “Sawa Mathew ninakuja hapo 

na kikosi sasa hivi” akasema 

Hamis 

“Mathew what are we going to 

do?Hao watu uliowasiliana nao 

watawahi kufika kabla ya hawa 

polisi hawajatukamata na kukuta 

maiti ya Nathan garini? Mathew do 

something !! 

“Usiogope Theresa.Gari hili 

halipenyi risasi na hawataweza 

kutupata.Hata hivyo I have to do 

something to buy time” akasema 

Mathew na kutoa bomu dogo la 

kurusha kwa mkono akafungua 

mlango kidogo na kulirusha 

upande wa mbele karibu na 

zilipokuwa na gari za polisi 

likalipuka na kuzua taharuki kubwa.Risasi zikaanza kumiminwa 

kuelekea katika gari la Mathew na 

mmoja wa wale askari akaonekana 

kuwazuia wenzake kulishambulia 

gari la akina Mathew. 

“Hawa polisi wamejuaje 

kuhusu sisi hadi wakaamua 

kutufuatilia? Kuna mtu pale 

nyumbani kwa Theresa aliona 

wakati tunapakia maiti ya Nathan 

ndani ya gari na akawajulisha 

polisi? Akajiuliza Mathew. 

Mara ghafla wale polisi 

wakaonekana wakiingia katika 

magari yao na kuondoka kwa kasi 

ya ajabu.Kitendo kile 

kiliwashangaza sana akina Mathew “Mbona 

wanaondoka?Wanakwenda 

wapi?Theresa akauliza 

“Hata mimi nashangaa 

sana.Wamepewa amri ya 

kuondoka ? Mbona ghafla sana 

halafu wanaondoka kwa kasi 

kubwa namna hii?akauliza Mathew 

“Inashangaza sana.” Akasema 

Theresa.Kutokea nyuma yao 

zikaonekana gari za polisi zikija 

kwa kasi 

“Wamerudi tena.”akasema 

Theresa 

“Hawa ni wengine” akasema 

Mathew na kuwapigia simu akina 

Hamis akawataka wasifike kwanza 

eneo lile hadi atakapowapa taarifa Magari matatu yaliyosheheni 

askari wenye silaha yakafunga 

breki mita kadhaa kutoka katika 

gari la akina Mathew.Askari 

wakashuka na kuanza kulisogelea 

gari la akina Mathew kwa 

tahadhari.Walipolifikia mmoja wa 

askari akaenda kugonga katika 

kioo cha gari na kuwafanyia ishara 

wafungue mlango na watoke nje. 

“Mathew please don’t get out” 

akasema Theresa 

“Stay in the car.Ngoja 

nishuke.Hawa askari nawaona 

wako tofauti sana na wale 

wengine.Nikitoka garini funga 

milango na chochote 

kitakachotokea usifungue mlango” akasema Mathew na kushuka chini 

akiwa na bastora mkononi 

“Weka silaha yako chini 

tafadhali kisha piga magoti na 

uinue mikono juu” Mathew 

akaamriwa.Bila ubishi akaiweka 

chini bastora yake na kuisukumiza 

mita kadhaa mbele halafu 

akaweka mikono kichwani 

“Jitambulishe” akaamuru 

askari kiongozi wa kikosi kile 

“Naitwa Mathew ninafanya 

kazi ikulu.Garini niko na mdogo 

wa rais anaitwa Theresa” akasema 

Mathew na kuamriwa 

kusimama.Askari yule kiongozi 

akamfuata 

“Naitwa Meja Allan.Nini 

kimetokea hapa? Tumepewa taarifa ya kufika hapa kwa haraka 

sana kwani ulikuwa umewekwa 

chini ya ulinzi wa askari na 

walikuwa wanawashambulia” 

“Mimi na Theresa tulikuwa 

katika safari zetu na ghafla 

zikatokea gari mbili zikitufuata 

kwa nyuma na mara zikatokea piki 

piki mbili zikatupita halafu 

zikarejea tena kwa kasi na mara 

tairi moja la gari langu likapata 

pancha nahisi lilipigwa 

risasi.Nikajitahidi kulimudu gari 

hadi likasimama na tukaanza 

kushambuliwa kutokea 

nyuma.Kwa habati nzuri gari langu 

hili halipenyi risasi.Tukiwa 

tunatafakari nini cha kufanya 

zikatokea gari mbili za polisi mbele yetu na wakashuka polisi 

wakiwa wamejihami kwa silaha na 

kutuamuru kushuka 

chini.Ikatokea helkopta ikasimama 

juu angani na kutumulika kwa 

juu.Nikawasiliana na rais na 

kumuomba msaada kwani askari 

wale walionekana kutokuwa na 

nia nzuri na sisi” 

“Una hakika watu hao ni 

askari?Wameelekea wapi? 

Akauliza Meja Allan 

“Ni askari na walikuwa na 

mavazi na magari ya askari 

polisi.Baada ya ninyi kusikika 

mkija na magari yenu mara ghafla 

wakaingia katika magari yao na 

kuondoka haraka sana.Ni kama vile walipata taarifa ya ujio wenu” 

akasema Mathew 

Askari wakalikagua gari la 

Mathew halikuwa limeharibiwa 

zaidi ya matairi yote kutobolewa 

kwa risasi 

“Huyo mdogo wake rais ana 

hali gani? Akauliza Meja Allan 

“Amepatwa na mstuko kidogo 

na nitaomba mnisaidie kumfikisha 

ikulu.Mimi nitabaki hapa 

nimeagiza niletewe matairi 

nibadilishe niendelee na safari 

yangu” akasema Mathew 

“Hatuwezi kukuacha hapa 

peke yako hasa baada ya tukio hili 

kutokea.Tutawapeleka ikulu au 

sehemu mnayotaka kwenda na 

askari polisi watalilinda gari lako hadi kesho asubuhi 

litakapotengenezwa na uchunguzi 

kufanyika.Tunatakiwa 

kuwafahamu hao askari 

waliofanya tukio hili” akasema 

Meja Allan 

“Meja Allan ninaomba 

tuzungumze pembeni kidogo” 

akasema Mathew na kusogea 

pembeni na Meja Allan 

“Afande Allan naomba 

nikuweke wazi kwamba niko 

katika operesheni fulani nzito 

niliyopewa na rais kwa hiyo 

kuendelea kukaa hapa ni kuharibu 

kila kitu.Nafahamu uko katika 

majukumu yako ya kazi lakini rais 

akisikia kwamba operesheni 

yangu imeshindwa kufanikiwa kwa sababu ya kuzuiliwa hapa 

hatafurahi.Ninakuomba afande 

kwa kuwa suala hili limekwisha 

malizika niacheni niendelee na 

operesheni yangu” akasema 

Mathew na Meja Allan akafikiri 

kwa muda na kusema 

“Kumbe sote tuko kundi 

moja.Ulitakiwa kujitambulisha 

mara moja.Una hakika hauhitaji 

msaada wowote ? 

“Hapana afande.Ninachoomba 

ni kumpeleka yule mwadada ikulu 

kwa rais na mimi nikisha maliza 

operesheni yangu nitaelekea 

huko” akasema 

Mathew.Akaongoza na na Afande 

Allan wakarejea garini Mathew akafungua mlango na kumtaka 

Theresa ashuke 

“Theresa utaongozana na 

hawa askari watakupeleka ikulu 

mimi naendelea kulimaliza lile 

zoezi halafu nitakuja ikulu” 

akasema Mathew 

“Mathew are you 

sure?akauliza Theresa 

“Usihofu Theresa.”akasema 

Mathew .Askari wale 

wakamchukua Theresa 

wakampakia katika gari lao moja 

na kuondoka kuelekea ikulu 

wengine wakabaki akiendelea na 

kupima.Mathew akawapigia simu 

akina Hamis na kuwataka wafike 

mara moja ili waendelee na lile zoezi.Hazikupita dakika kumi 

wakawasili 

“Mathew nini kimetokea 

hapa? 

“Kuna tukio 

lilitokea.Nilivamiwa na watu 

wenye mavazi na magari ya polisi 

na angani walikuwa na 

helkopta.Kwa bahati nzuri gari 

langu hili halipenyi risasi 

ikanilazimu kuomba msaada na 

askari walipotokea wale 

waliokuwa wanatushambulia 

wakakimbia.Tusipoteze muda 

twendeni tuondoke eneo hili.” 

akasema Mathew gari lake 

likafungwa kamba likaanza 

kuvutwa na gari la akina Hamis wakaondoka hadi walipofika 

sehemu walikopanga wakutane. 

“Haya Mathew ni kazi gani 

ulotaka kutupa? Hamis akauliza 

“Kuna mwili wa mtu mmoja 

nahitaji kuupoteza.Nataka 

mkaufiche mahala ambako 

hautaonekana.Ninyi ni wataalamu 

wa haya mambo tumieni uzoefu 

wenu na mwili huu usiweze 

kuonekana” akasema Mathew na 

kufungua buti ya gari akina Hamis 

wakahamisha mwili wa Nathan na 

kuuingiza katika buti ya gari lao 

kisha Mathew akatoa shilingi 

milioni tano katika droo ya gali 

lake akawapa wakalivuta gari la 

Mathew hadi alipofika katika kituo 

cha mafuta akaegesha hapo na kuomba msaada wa ulinzi wa gari 

lake hadi kesho asubuhi akaita 

taksi na kupanda akaondoka. 

“Wale askari polisi walitokea 

wapi? Walifahamu kuhusu uwepo 

wa mwili wa Nathan mle garini? 

Kama ndiyo walifahamu vipi?Kuna 

mtu aliona wakati tunaupakia 

mwili ule na kutoa taarifa polisi? 

Akajiuliza Mathew 

“Nimeshangazwa mno na wale 

askari polisi.Walianza 

kushambulia kwa risasi kitu 

ambacho si cha kawaida kwa 

askari polisi.Ukitakiwa kusimama 

na askari polisi unatakiwa kwanza 

ushuke garini ujisalimishe na 

ukikataa inawalazimu watumie 

nguvu.Askari polisi hawawezi kushambulia kabla hawajatoa 

amri ya 

kujisalimisha.Watakushambulia 

kama umekataa kutii amri na 

kuwashambulia.Inaonekana askari 

wale walikuja kwa kazi maalum 

halafu ni kama vile walipewa 

taarifa kwamba kuna askari 

wanakuja hivyo wakaondoka 

haraka haraka.Hii inanishangaza 

sana.Kama walikuwa kazini kwa 

nini wakakimbia walipojua kuna 

askari wenzao 

wanakuja?Ninaanza kuingiwa na 

wasi wasi kuhusiana na wale 

askari.” Akawaza Mathew na 

kumuelekeza dereva ampeleke 

kwa Meshack Jumbo. “Umekuwa ni usiku mbaya 

sana.Sikutegem…………….” Mathew 

akatolewa mawazoni baada ya 

simu yake kuita.Alikuwa ni rais Dr 

Vivian 

“Hallow mheshimiwa 

rais”akasema Mathew 

“Mathew uko wapi sasa hivi? 

“Niko njiani naelekea 

nyumbani kwa Meshack Jumbo” 

“Nakuomba ikulu haraka 

sana” akasema rais na ukata 

simu.Mathew akavuta pumzi ndefu 

“Mambo yameiva.Dr Vivian 

anaonekana kubadilika sana 

.Amezungumza kwa hasira 

sana.Inawezekana tayari Theresa 

amefika ikulu na inawezekana 

labda akawa anataka kufahamu kilichotokea.Ninaomba Theresa 

asiwe amemueleza chochote 

kuhusu Nathan kwani atakuwa 

ameharibu kila.Sijui atafanya nini 

akisikia kwamba Nathan 

amekufa.Dah ! Theresa ameharibu 

sana kwa kuamua kumuua 

Nathan.Sikutegemea kabisa kama 

anaweza akafanya jambo la hatari 

kama lile,anway I have to fix it” 

akawaza Mathew 





Mathew alifika nyumbani kwa 

Meshack Jumbo na kukaribishwa 

ndani.Meshack Jumbo akahisi kuna tatizo baada ya kuiona hali 

aliyokuwa nayo Mathew 

“Nini kimetokea 

Mathew?akauliza 

“Mzee kuna tatizo kubwa 

limetokea na sijui nianzie wapi 

kukueleza” akasema Mathew 

“Nieleze tafadhali.Nini 

kimetokea? 

Mathew akamueleza mzee 

Jumbo kila kitu kilichotokea 

kuhusiana na Nathan. 

“Mhh! Mzee Jumbo akaguna 

“Hili suala linakanganya sana” 

Akasema 

“Mzee ninahitaji kwenda 

kuonana na rais usiku huu 

amenipigia simu wakati ninakuja 

huku nakunitaka nifike ikulu haraka sana.Yawezekana mambo 

tayari yameharibika” 

“Atakuwa tayari amefahamu 

kilichotokea? 

“Sina hakika lakini 

uwezekano ni 

mkubwa.Yawezekana labda 

Theresa amekwisha mueleza kila 

kilichotokea na ndiyo maana 

akaniita kwa haraka namna 

ile.Ngoja nikamsikilize nifahamu 

alichoniitia.Kama kuna tatizo 

lolote nitalimaliza” akasema 

Mathew 

“Hili suala la kifo cha Nathan 

limebadili kabisa upepo wa hili 

suala na sasa limekuwa la 

kimataifa.Mzozo kati ya Tanzania 

na Marekani utaongezeka haraka sana.Yawezekana mambo 

tayari yameharibika” 

“Atakuwa tayari amefahamu 

kilichotokea? 

“Sina hakika lakini 

uwezekano ni 

mkubwa.Yawezekana labda 

Theresa amekwisha mueleza kila 

kilichotokea na ndiyo maana 

akaniita kwa haraka namna 

ile.Ngoja nikamsikilize nifahamu 

alichoniitia.Kama kuna tatizo 

lolote nitalimaliza” akasema 

Mathew 

“Hili suala la kifo cha Nathan 

limebadili kabisa upepo wa hili 

suala na sasa limekuwa la 

kimataifa.Mzozo kati ya Tanzania 

na Marekani utaongezeka maradufu na watahitaji maelekezo 

ya kina kuhusiana na kifo cha mtu 

wao.Halikuwa wazo zuri 

kumshirikisha yule msichana 

Theresa katika operesheni 

hii.Toka mwanzo sikuwa 

nimeliafiki jambo hili na ndiyo 

maana nikakuomba umrudishe 

ikulu akaendelee na shughuli zake 

za kuandika hotuba.Ona sasa 

amekuweka katika hatari kubwa 

na kila kitu inabidi kisimame kwa 

ajili ya kulishughulkia suala moja 

tu la Nathan” 

“Mzee ngoja nikamsikilize rais 

na nitakujuza chochote 

kitakachojiri huko.Naomba 

unihifadhie hili begi langu halafu 

nitaondoka na gari lako ” akasema Mathew na kuchukua gari la 

Meshack Jumbo akaondoka 

kuelekea ikulu 

“Asemayo mzee Jumbo ni ya 

kweli kabisa.Hakukuwa na 

ulazima wa kumshirikisha Theresa 

katika operesheni hii kwani 

ameharibu kila kitu na 

kunirudisha nyuma sana.Sijui nini 

kitatokea Dr.Vivian akifahamu 

kuhusiana na kifo cha mpenzi 

wake Nathan.Endapo Marekani 

wakifahamu kama Nathan 

amekufa basi watahitaji maelezo 

ya kina amekufaje.Hili suala 

litaleta mvutano mkubwa sana” 

akawaza Mathew akiwa garini 

kuelekea ikulu kuonana na rais Aliwasili ikulu na kupelekwa 

moja kwa moja sebuleni kwa 

rais.Dr.Vivian aliyekuwa chumbani 

kwake akafahamishwa kuhusu ujio 

wa Mathew na baada ya muda 

akafika sebuleni.Uso wake 

uliionyesha hasira kali.Akawataka 

walinzi wake watoke pale sebuleni 

na kuwaacha yeye na Nathan 

pekee.Dr.Vivian akamtazama 

Mathew kwa macho makali na 

kusema 

“Kuna kitu kimoja tu ambacho 

nataka kukifahamu kwa sasa,nini 

kimetokea Mathew? Akauliza bila 

hata salamu.Wote wawili 

walikuwa wamesimama.Mathew 

akabaki kimya “Mathew nieleze haraka nini 

kimetokea? 

“Theresa hajakueleza 

chochote? Akauliza Mathew baada 

ya Theresa kuingia pale sebuleni 

na kwenda kuketi sofani 

“Hajanieleza chochote.Toka 

amefika hapa analia na kusema 

“I’m sorry sister”Nini 

kimetokea?Kuna kitu gani 

kimetokea ambacho hataki 

kunieleza? Tafadhali niambie 

Mathew nini kimewakuta 

huko?Sijawahi kumuona Theresa 

akiwa katika hali hii hata mara 

moja na ndiyo maana 

nimestuka.Nieleze tafadhali” 

akasema Dr.Vivian Mathew akamtazama Theresa 

aliyekuwa amejiinamia sofani 

.Halafu akasema 

“Kuna sehemu mimi na 

Theresa tulikuwa tunakwenda 

usiku huu kuonana na watu 

fulani.Tukiwa njiani nikagundua 

tulikuwa tunafuatwa na gari mbili 

nyuma yetu halafu juu yetu 

kukawa na helkopta na ghafla 

zikatokea piki piki mbili zikatupita 

halafu zikaanza kurudi kwa kasi na 

tairi moja katika gari langu 

likapigwa risasi nikajitahidi 

kulimudu gari lisiache bara bara 

na mara tu gari liliposimama 

zikamiminwa risasi kutoka katika 

gari zilizokuwa zinatufuata nyuma 

yetu na kutoboa matairi yote.Kwa bahati nzuri gari langu halipenyi 

risasi hivyo ikawa nafuu 

kwetu.Mara kwa mbele yetu 

zikatokea gari tatu za polisi na 

wakashuka watu waliovalia 

mavazi ya polisi na wakiwa 

wamejihami kwa silaha 

.Walitutaka kushuka garini na 

ndipo nilipoamua kukuomba 

msaada.Nashukuru sana kwa 

kutuma msaada wa haraka kwani 

polisi walikifika kwa wakati na 

wale wavamizi wakaondoka kwa 

haraka sana.Inaonekana walipata 

taarifa kwamba askari polisi 

wanakuja hivyo wakaondoka 

haraka sana.Jambo hili 

limenishangaza sana.Najiuliza je 

wale walikuwa askari wa jeshi letu la polisi au ni watu waliotumia 

sare na vifaa vya jeshi letu? Kama 

walikuwa ni polisi kweli kwa nini 

wakakimbia baada ya wale askari 

wenzao kuwasili?Kuna maswali 

hapa bado nayatafutia majibu.Kwa 

hiyo mheshimiwa rais hiyio ndiyo 

hali halisi iliyotokea usiku huu na 

ninakuomba ondoa 

hofu.Tunaendelea vizuri japo 

mambo yanazidi kuwa magumu” 

akasema Mathew.Dr.Viviana 

akaenda kuketi sofani. 

“Mhh! Jambo hili hata mimi 

mwenyewe linanichanganya .Hao 

askari ni akina nani na 

walifahamuje kuhusu ninyi?Hizo 

sare na vifaa vya jeshila polisi walivitoa wapi?Hiyo helkopta 

waliyokuwa nayo ni ya polisi pia? 

“Sikupata nafasi ya 

kuichunguza helkopta lakini 

magari na sare ni za polisi” 

akasema Mathew 

“Sawa, nitaagiza uchunguzi wa 

kina ufanyikekuhusiana na askari 

hao na tuwabaini ni akina nani au 

kama kuna watu wanatumia sare 

na vifaa vya jeshi letu kwa kazi zao 

binafsi basi tuwabaini lakini hii 

inaonyesha kwamba tayari 

mmekwisha fahamu na na hii 

inaongeza hatari kubwa 

kwenu.Inabidi umakini uongezeke 

na ikibidi nitawapa ulinzi ili 

muweze kuwa salama katika 

shuhuli zenu.Hiki kilichotokea leo kimeniwashia taa nyekundu 

kwamba hamko salama na 

kwamba kwa hizo siku chache 

mlizoanza uchunguzi kuna watu 

tayari mmekwisha wagusa na ndio 

maana wanajitokeza kuwakab…...” 

“Sister !! Theresa akasema na 

kumkatisha dada yake 

“Unasemaje Theresa? 

Akauliza Dr.Vivian.Mapigo ya 

moyo wa Mathew yakabadilika 

“Dada naomba niwe mkweli 

.Kuna jambo hatujakueleza 

ukweli” akasema na kufuta 

machozi 

“Jambo gani 

Theresa?Dr.Vivian akashangaa “Theresa !! akasema Mathew 

huku akimtazama Theresa kwa 

macho makali 

“ Mathew we have to tell her 

the truth.She needs to know” 

akasema Theresa 

“Not now Theresa !! akasema 

mathew kwa sauti ya 

juu.Dr.Viviana akazidi kupata hofu 

“Kuna nini Theresa? Kuna kitu 

gani ambacho nahitaji 

kukifahamu? Akauliza Dr.Vivian 

“It’s about Nath…..”kabla 

hajamaliza sentensi yake Mathew 

akaingilia kati 

“Madam president ngoja mimi 

nikueleze ukweli” akasema 

Mathew “No Mathew mimi ndiye 

ninayepaswa kumweleza dada kwa 

kuwa mimi ndiye niliyetenda” 

akasema Theresa 

“Jamani mbona nashindwa 

kuwaelewa?Kuna nini kimetokea 

na mnasita kunieleza? 

“Ni kuhusu Nathan”

“Nathan?? Dr.Vivian akastuka 

sana. 

“Ndiyo dada” 

“Nathan…….” 

“Madam president let me 

explain !! akasema Mathew 

“No ! let her explain to me 

what happened” akasema 

Dr.Vivian na kumsogelea Theresa 

“Niambie Theresa kuna nini 

imetokea?Nathan kafanya nini? Theresa akafuta machozi na 

kumtazama dada yake kisha 

akasema 

“Nathan is dead” 

Dr.Vivian akabaki mdomo 

wazi akimtazama Theresa.Kwa 

sekunde kadhaa alibaki na 

mshangao mkubwa na hakuweza 

kuzungumza chochote.Baada ya 

muda akasema 

“That’s not true !! 

“It’s true .He’s dead.I killed 

him” akasema na kuzidi 

kumchanganya 

Dr.Vivian.Akamfuata Mathew 

“Mathew hebu niambie 

Theresa ana matatizo gani? Mbona 

anaongea vitu ambavyo havielewi? 

Akauliza Dr.Vivian.Mathew akamshika mkono na kumketisha 

sofani. 

“Tell me Mathew.What’s going 

on? Theresa amepatwa na nini? 

Akauliza Dr.Vivian akiwa katika 

wasi wasi mkubwa 

“Dr.Vivian naomba unipe 

dakika chache nikueleze japo kwa 

ufupi jambo moja muhimu sana” 

“Nieleze Mathew” akasema 

Dr.Vivian huku bado sura yake 

ikionyesha wasi wasi mkubwa 

“Kama nilivyokueleza 

kwamba ninataka kuanza 

uchunguzi wangu katika ajali ya 

ndege ya rais kwani naamini 

chanzo cha kuuawa kwa kanali 

Sebastian kina mahusiano na ajali 

ya ndege ya rais.Nimegundua kwamba wakati ikiondoka hapa 

Dar es salaam kwenda Cairo 

Misri,kulikuwa na watu kumi na 

tisa ndani ya ndege ya rais na 

mmoja ambaye inasadikiwa 

alikuwa ni binti mdogo hakuwa 

ameorodheshwa miongoni mwa 

abiria waliokuwamo ndegeni na 

mpaka sasa sijafahamu kwa nini 

ila bado naendelea kulichunguza 

hilo.Wakati wa kurejea Tanzania 

kulijitokeza kundi la waandishi 

nane wa habari ambao 

walichelewa ndege yao na kuomba 

lifti katika ndege ya rais na rais 

akaruhusu wapande.Hatujui bado 

chanzo cha ajali ile lakini taarifa 

iliyopo inaonyesha kwamba baada 

ya ajali ile miili iliyopatikana ni kumi na saba tu .Miili mingine 

haikupatikana.Swali la kujuliza je 

iko wapi?hawakufika Tanzania au 

walishukia njiani? Bado naendelea 

kulifanyia kazi hilo lakini 

nimefanikiwa kumfahamu mtu 

mmoja anaitwa Fakrim Alnasor 

huyu ni mzaliwa wa Misri lakini 

ana uraia wa Marekani kwamba 

ndiye aliyewaombea lifti hao 

waandishi nane wa habari katika 

ndege ya rais.Kwa kuwatumia 

watu ambao tuna mashirikiano 

nao wa Marekani wametusaidia 

kuchunguza na kugundua kwamba 

Fakrim alihamishwa nchini Misri 

muda mfupi baada ya ajali ile ya 

rais kutokea na kupelekwa 

Marekani.Watu wetu hao walikwenda mbali zaidi na 

kugundua kwamba Fakrim 

alikuwa ni jasusi wa shirika la 

ujasusi la marekani CIA.” 

Sura ya Dr.Vivian ikabadilika 

baada ya kusikia neno CIA 

likitajwa. 

“CIA? 

“Ndiyo alikuwa ni jasusi wa 

CIA na inaonyesha kwamba 

alikuwa nchini Misri kwa shughuli 

maalum na alipomaliza shughuli 

yake akaondolewa.Tuliwataka 

watusaidie kumchunguza zaidi 

Fakrim kuhusana na hao 

waandishi nane wa habari 

aliowasaidia wakaingia katika 

ndege ya rais lakini kitu cha ajabu 

Fakrim alipigwa risasi na kufariki dunia kabla hao watu wetu 

hawajampata kwa 

mahojiano.Walifanikiwa kuondoka 

na simu na kompyuta yake ndogo 

na baada ya kufanya uchunguzi 

wakagundua kwamba mtu wa 

mwisho kuwasiliana na Fakrim 

alikuwa ni Nathan” 

Dr.Vivian akazidi kuonyesha 

uso wa mshangao. 

“Nathan? 

“Ndiyo madam 

president.Nathan alikuwa na 

mawasiliano na 

Fakrim.Tulimchunguza pia Nathan 

na tukagundua kwamba hata naye 

ni jasusi wa CIA” 

“No ! That’s not true !! 

akasema kwa ukali Dr.Vivian “Najua ni jambo gumu 

kuliamini lakini tuna uhakika 

mkubwa kwamba Nathan ni jasusi 

wa siri wa CIA na tunahisi alikuwa 

karibu nawe kwa kazi 

maalum.Serikali ya Marekani 

wanakufuatilia Dr.Vivian kwa 

kupitia shirika lake la ujasusi 

ambao nao wanamtumia Nathan 

kukuchunguza” 

“Mathew unazidi 

kunichanganya.Mimi ndiye 

nnayemfahamu Nathan kuliko 

mnavyomfahamu ninyi.Katu 

Nathan hawezi kuwa hivyo 

unavyosema.Hawezi kuwa 

mpelelezi na kibaya zaidi eti 

anatumiwa kunipeleleza mimi.Hilo 

nalikataa haliwezekani kabisa.Nimetoka mbali naye na 

ninamfahamu zaidi ya mtu yeyote 

anavyoweza kumuelezea.Labda 

uwe unamzungumzia Nathan 

mwingine na si huyu ninamfahamu 

mimi,my Nathan” akasema 

Dr.Vivian 

“Ni vigumu kuamini Dr.Vivian 

lakini huo ni ukweli na tulikwenda 

mbali zaidi kwa kuichunguza hadi 

kampuni anayofanya kazi Nathan 

ya A.D electronics tukagundua 

kwamba ni kampuni ambayo iko 

chini ya serikali ya Marekani 

kupitia shirika lake la ujasusi la 

CIA ingawa hili halifahamiki kwa 

watu.Walianzisha kampuni hii kwa 

lengo maalum na ndiyo maana 

wanatengeneza bidhaa zenye ubora mkubwa lakini kwa bei ya 

chini kwa sababu hawako kwa ajili 

ya kutengeneza faida bali wana 

lengo lao maalum.Katika simu na 

kompyuta wanazotengeneza kuna 

programu maalum inawekwa 

ambayo huwawezesha wao wapate 

taarifa zako zote katika kifaa 

hicho.Kama unatumia simu basi 

mawasiliano yako yote 

wanayapata na kama unatumia 

compyuta basi wana uwezo pia wa 

kupata kila unachokifanya katika 

kompyuta yako.Hii inawasaidia 

sana kuweza kupata taarifa 

mbalimbali hasa za magaidi na 

watu ambao wanahatarisha 

usalama wa Marekani.Nimegundua 

kwamba Nathan alikupa simu na kompyuta zinazotengenezwa na 

kampuni yao na si wewe tu bali 

aligawa pia kwa watu wote 

wanaokuzunguka.Alifanya hivi 

kwa sababu maalum na kupata 

taarifa zako zote na ndiyo maana 

baada ya kuligundua hilo jana 

nikaja kubadilisha simu zako ili 

taarifa zako ziwe salama” 

“Oh my God !! akasema 

Dr.Vivian.Alistuka sana 

“Una uhakika na hilo jambo 

Mathew? 

“Ndiyo mheshimiwa rais nina 

uhakika nalo” 

“Kama ni hivyo kwa nini 

hukutaka kunieleza mapema? 

“Kwa sababu ingekuwa 

vigumu kuamini na hata hivyo bado nilikuwa naendelea na 

uchunguzi wangu kuhusiana na 

kwa nini Marekani 

wanakuchunguza” 

“Ulipokuja kunihoji kuhusu 

maisha yangu ya kimahusiano 

ulikuwa tayari na taarifa 

kuhusiana na Nathan kuwa jasusi 

na ananipeleleza? 

“Ndiyo mheshimiwa 

rais,tayari nilikuwa na taarifa hizo 

lakini kuna vitu ambavyo nilihitaji 

kuvifahamu kutoka kwako” 

“Mathew umenisikitisha sana 

.Kwa nini ukagundua jambo kubwa 

kama hili na ukakaa kimya huku 

nikiendelea kuwa katika hatari? 

Akauliza Dr.Vivian akionekana 

kukasirika . “Madam president si kila 

jambo linaloendelea katika 

uchunguzi unapaswa kuelezwa 

haraka haraka,kuna mambo 

mengine ukielezwa haraka 

yanaweza yakaharibu uchunguzi 

na hasa suala kama hili ambalo 

linamuhusisha mtu wako wa 

karibu na mtu 

unayempenda.Isingekuwa rahisi 

kuturuhusu kuendelea na 

uchunguzi kwa mtu wako wa 

karibu” 

“Hapana Mathew ulipaswa 

kunieleza na kama ningekubaliana 

nawe ningetoa kibali cha 

kuendelea kumchunguza na hata 

ningeweza kukupa ushirikiano 

mkubwa sana wa kusaidia katika uchunguzi wako.Umechukua hatu 

gani sasa? Umefikia wapi katika 

uchunguzi wako huo? 

“Sikutaka kufahamu kitu 

chochote kabla sijakamilisha 

uchunguzi wangu hivyo 

inanilazimu kuongea na Theresa 

nikamueleza kila kitu na tukaamua 

kumuita Nathan aje Tanzania 

kimya kimya bila wewe kufahamu” 

Dr.Vivian akakunja sura 

baada ya kusikia kauli ile toka kwa 

Mathew 

“Nathan amekuja Tanzania 

bila ya mimi kujulishwa?How 

could you do that Mathew?And you 

Theresa how can do that to me? 

Akasema Dr.Vivian kwa ukali “Mheshimiwa rais tuliamua 

hivyo kwa sababu nilitaka nipate 

nafasi ya kumchunguza Nathan 

bila yeye kufahamu kama 

anachunguzwa.Naamini kama 

tungekujulisha jambo hili 

usingekubali Nathan aje Tanzania 

kutokana na mafarakano yenu 

hivyo tusingeweza kupata taarifa 

zozote za kumuhusu yeye ndiyo 

maana nikamuomba Theresa 

afanye mpango ili Nathan aweze 

kuja kwa siri Tanzani bila 

kukujulisha ili nipate nafasi ya 

kumfanyia uchunguzi” 

“He came? Akauliza Dr.Vivian 

“Ndiyo alikuja” “Yuko wapi? Tayari umefanya 

uchunguzi wako? Akauliza 

Dr.Vivian 

“Amekuja asubuhi ya leo na 

kwa mujibu wa mipango 

tuliyoipanga ni kwamba jioni ya 

leo Theresa alimkaribisha Nathan 

nyumbani kwake halafu mimi 

nikaenda kufanya uchunguzi 

chumbani kwa Nathan.Nikiwa 

naendelea na uchunguzi wangu 

chumbani kwa Nathan nikapigiwa 

simu na Theresa akanitaka niende 

nyumbani kwake haraka 

sana.Nilifanya hivyo na nilipofika 

nyumbani kwake…” Mathew 

akasita 

“Sema Mathew ulipofika 

nyumbani kwa Theresa ikawaje? Mathew akageuka na 

kumtazama Theresa. 

“Tell me Mathew !! akasema 

Dr.Vivian kwa ukali akionekana 

kuwa na wasiwasi mkubwa 

“I found him dead” akasema 

Mathew na ukimya 

ukatanda.Dr.Vivian akawatazama 

Mathew na Theresa kwa zamu 

halafu akamfuata Theresa sofani 

“Theresa tell me is that true? 

Theresa hakujbu kitu bali 

akatikisa kichwa ishara ya 

kukubali.Dr.Vivian akaweka 

mikono 

kichwani.Alichanganyikiwa.Akaka

a chini.Alishindwa 

kulia,alishindwa kuzungumza 

akabaki anamtazama Theresa kwa macho makali yaliyojaa hasira 

huku midomo 

ikimtetemeka.Akamgeukia 

Mathew 

“Mathew nakuamini sana 

please tell me it’s a joke” 

“It’s true madam 

president.Nathan is dead”Ghafla 

Dr.Vivian akainuka na kwenda 

kumvaa Mathew akaanza 

kumtandika vibao,Nathan 

akamdaka mikono. 

“Nilikuamini sana Mathew 

kwa nini umenifanyia hivi? Why 

you killed him?!! Akauliza Dr 

Theresa huku akilia.Dr Theresa 

akakaa chini na kuanza kulia 

“Dada usimlaumu 

Mathew.Yeye alikuwa na lengo zuri tu la kutaka kumchunguza Nathan 

lakini mimi ndiye 

niliyemuua.Unapaswa kunilaumu 

mimi si Mathew.!! Akasema 

Theresa 

“Get out of my face Theresa !! I 

hate you so much.Sikutegemea 

kama siku moja unaweza 

ukanifanyia jambo baya kama hili? 

Why you killed him? Why you 

killed an innocent soul? akauliza 

Dr.Vivian huku akilia 

“Dada nililazimika kufanya 

vile kwa ajili ya usalama 

wako.Nathan was a 

monster.Hakuwa na mapenzi 

yoyote nawe bali alikuwa hapa 

kwa kazi maalum alizotumwa 

kama ulivyoambiwa na Mathew.Hakuna anayejua nini 

sababu ya kukuchunguza na 

hatujui mpaka sasa amekwisha 

pata mambo gani kuhusu wewe” 

“Hiyo haikuhalalishi wewe 

kumuua Nathan !! akafoka 

Dr.Vivian 

“Hakukuwa na namna 

nyingine ya kuweza kumzuia 

Nathan zaidi ya kumuua?Oh God 

please give me strength..” akasema 

Dr.Vivian na kusimama 

“Dada najua nimekuudhi kwa 

hiki nilichokifanya .Hata mimi 

nakubali sijafanya kitu kizuri 

lakini sikuwa na namna nyingine 

ya kufanya.Nathan ni mtu mbaya 

sana na japokuwa hatuna 

uthibitisho bado lakini naamini watu anaoshirikiana nao ndio 

waliomuua baba.Siwezi kumuacha 

hai mtu kama huyu ambaye 

pamoja na kuiteketeza familia yetu 

bado anaendelea kutufuatilia.Can’t 

you see that Vivian? Akauliza 

Theresa ambaye alionekana 

kupandwa na hasira 

“Sikuwahi kufikiri hata siku 

moja kama nitaingia katika 

dhambi ya uuaji lakini 

imenilazimu kufanya hivyo kwa 

sababu ya usalama wangu na 

wako.Najua hili ni kosa la jinai kwa 

hiyo niko tayari kuipokea adhabu 

inayostahili kwa sababu ya kitendo 

nilichokifanya.So madam 

president call the police now.Mimi 

ni muuaji na ninastahili adhabu kama wauaji wengine.Najua 

nitafungwa maisha au kifungo 

kirefu gerezani lakini nitatumikia 

kifungo kwa furaha nikijua uko 

salama na nimelipa kisasi vile vile 

kwa watu walioteketeza familia 

yetu.So make that call now !!! 

akasema Theresa.Dr.Vivian 

akamsogelea na kumnasa kibao 

kikali 

“Umefanya makusudi kumuua 

Nathan kwa vile unajua kwamba 

siwezi kukupeleka mbele ya 

sheria? Akauliza Dr.Vivian kwa 

ukali 

“Dada mimi niko tayari kwa 

lolote lile.Siogopi kukutana na 

mkono wa sheria na wala usijaribu 

kunionea huruma!! “Theresa wewe si damu yangu 

na sioni ugumu kukuharibu.I 

swear I’ll never forgive you for this 

and I’ll destroy you!! Akasema 

Dr.Vivian na kuiendea simu kabla 

hajainua mkono wa simu Mathew 

akamuawahi na kumdaka mkono 

akamzuia kupiga ile simu 

“Don’t make that call !! 

akasema Mathew 

“Dr.Vivian suala hili linahitaji 

busara kubwa sana na 

ninakuomba usichukulie hasira 

kwani utashindwa kulimaliza hili 

jambo.Usimuhukumu wala 

usijaribu kumfanya chochote 

Theresa kwani mimi ndiye 

niliyemuomba amuite Nathan 

huku Tanzania.Kilichotokea kimekwisha tokea na hatuna 

namna zaidi ya kukabiliana na 

kilichotokea.Najua wewe ni rais na 

una uwezo wa kupiga simu hata 

sasa na ukaamuru Theresa 

akamatwe na hata kama atafungwa 

gerezani bado haitamrejesha 

Nathan.Theresa amefanya hivi 

aliivyofanya kwa upendo mkubwa 

alio nao kwako.Ametanguliza 

usalama wako mbele ndiyo maana 

akaamua kufanya maamuzi haya 

magumu .Kutoa roho ya mtu si 

jambo rahisi.Badala ya kupoteza 

muda kulumbana tutafute suluhu 

ya suala hili” 




Stay away from us 

Mathew.Wewe ndiye sababu ya 

haya yote yaliyotokea.Kwanza sitaki tena uendelee na uchunguzi 

wako kwani imekuwa ni balaa 

tupu na hakuna chochote 

unachokipata.Uchunguzi wako 

wote unaishia hapa.Sitaki tena 

kuendelea na suala hili.Ahsante 

kwa msaada wako ambao 

umegeuka karaha.Nilitegemea 

makubwa sana kutoka kwako 

kumbe wewe nawe ni sawa na wale 

wale.Kaendelee na biashara zako 

sitaki tena uendelee na hii 

kazi.Kila mara suala hili limekuwa 

linanigharimu maisha ya watu 

sitaki kuendelea nalo 

tena.Imetosha” akasema Dr.Vivian 

kwa hasira 

“Dr.Vivian tafadhali 

usichukulie hasira.Hili ni suala zito sana na bado linahitaji uchunguzi 

wa kina.Tafadhali niache 

niendelee na uchunguzi wangu 

mpaka mwisho kwani tayari 

nimekwisha pata mwanga na 

nikiendelea kidogo ninaweza 

kupata ufumbuzi na kubaini ni 

nani waliwaua wazazi 

wako.Tafadhali sana mheshimiwa 

rais” akasema Mathew 

“Mathew nilikwisha 

kutahadharisha hapo awali 

kwamba nikisema jambo huwa 

sibadilishi kauli yangu.Nimesema 

kwamba sitaki kuendelea na hili 

zoezi.Imefika mwisho ahsante sana 

kwa kila kitu na kwa balaa 

ulilolisababisha” 

“Mhesh………………” “Stop !! akasema Dr.Vivian 

kwa ukali 

“Ninachohitaji kusikia ni kitu 

kimoja tu toka kwako.Nataka 

kufahamu mwili wa Nathan uko 

wapi? Nionyesheni uliko mwili wa 

mpenzi wangu na wewe 

ukaendelee na maisha yako ila 

huyu mwenzako aliyejipa 

dhamana ya kutoa roho za watu 

nitashughulika naye.Hawezi 

kukwepa mkono wa sheria!! 

“Madam president nakuomba 

sana niko chini ya miguu yako 

nakuomba usimfanye chochote 

Theresa.Kama ni kunipeleka 

kwenye sheria nipeleke mimi 

ambaye ndiye niliyemuomba 

Theresa katika dhambi hii.Kama nisingemuomba anisaidie 

kumfanya Nathan aje Tanzania 

asingeweza kupata wazo la 

kufanya hivi alivyofanya.Kwa hiyo 

naendelea kukuomba usimfanye 

chochote Theresa.” Akasema 

Mathew 

“Mathew tafadhali nakuomba 

usitake kunijaribu.Mimi ni tofauti 

sana na viongozi wengine.Usitake 

kunijaribu na ukajikuta 

nikikuharibu.Theresa must face 

the law.Siwezi kuliacha hili 

likaenda hivi hivi” akasema Dr 

Vivian.Mathew akamtazama na 

kusema 

“Una uhakika gani kwamba 

Theresa ndiye aliyemuua 

Nathan?Ukimfikisha mbele ya sheria unao ushahidi kama ni yeye 

ndiye aliyemuua? Ni vipi kama 

akisema kwamba ni wewe ndiye 

uliyemtuma amuue Nathan?Dunia 

nzima kwa sasa inafahamu una 

ugomvi na Marekani kwa hiyo 

wataamini umemuua Nathan kwa 

hasira zako kwa Marekani.Why 

don’t we skip that part and do 

things right? Akauliza Mathew na 

Dr.Vivian akapandwa na hasira 

kali 

“Unataka kupambana na 

mimi Mathew? Unataka 

kushindana na mimi? Akauliza Dr 

Vivian kwa hasira 

“Madam president 

utanisamehe sina lengo na wala 

siwezi kupambana nawe.Nilichokiongea ni ili 

kuliweka suala hili kwa ukubwa 

wake na badala ya kukaa 

tukilumbana tufikirie namna ya 

kuweza kukabiliana na hili suala.” 

“Mathew its over.Nimekwisha 

kwambia kwamba sitaki tena 

kuendelea na wewe na wala 

uchunguzi wa suala hili sitaki 

kabisa uendelee.Ninachokitaka 

mnionyeshe mwili wa Nathan 

ulipo.Nionyesheni ulipo mwili wa 

mpenzi wangu.Ili tuende sawa 

nakuomba unionyeshe ulipo mwili 

wa Nathan” akasema 

Dr.Vivian.Mathew na Theresa 

wakatazamana 

“Hamtaki kunionyesha ulipo 

mwili wa Nathan? “Madam president,kutokana 

na mambo unayoyapitia kwa sasa 

hasa msuguano wako na nchi ya 

marekani nadhani si vizuri jambo 

hili likajulikana.Mpaka sasa 

tunaofahamu kuhusu suala hili ni 

mimi,Theresa na Meshack Jumbo 

ambaye nimemweleza muda mfupi 

kabla sijafika hapa.Serikali ya 

Marekani itakubana katika kona 

kwa kutaka uchunguzi wa kina 

ufanyike kuhusu mwili wa 

Nathan.Dunia nzima watajua 

kwamba nawe unahusika katika 

mauaji hayo.Tanzania tutaingia 

katika msuguano mwingine 

mkubwa .Watatumia kigezo hicho 

kukuondoa katika mstari.Uko 

tayari kwa jambo hilo kutokea?Nakushauri mheshimiwa 

rais jambo hili liendelee kuwa siri 

na asifahamu mtu 

mwingine.Usiliweke jambo hili 

kwa vyombo vya uchunguzi litaleta 

shida kubwa” 

Dr.Vivian akashika kiono na 

kutazama chini.Kwa mara ya 

kwanza toka amekuwa rais 

alijikuta katika wakati mgumu 

sana na alishindwa kufanya 

maamuzi 

“Sikutegemea kama mnaweza 

kuniweka katika wakati mgumu 

kama huu.I don’t know what to do” 

akasema Dr.Vivian 

“Fanya maamuzi Dr.Vivian 

muda unakwenda sana” akasema 

Mathew “Mathew nimesema sijui 

nifanye nini.Mmekwisha haribu 

kila kitu.Mmenitwisha jiwe 

zito.Mmeniingiza katika vita mpya 

ambayo sikiwa nimeitegemea hasa 

kwa wakati huu ambao 

ninaiongoza nchi katika vita 

kubwa .Pamoja na hayo siwezi 

kulifumbia macho jambo 

hili.Lazima niliweke wazi.Kama 

Nathan amekufa lazima nchi yake 

ifahamu na lazima mwili wake 

upelekwe kwao ukazikwe kwa 

heshima .Hiyo ndiyo namna 

ninayoweza kulimaliza hili jambo 

na mwisho kabisa wale wote 

waliohusika katika jambo hili 

watachukuliwa hatua kali za 

kisheria.Tafadhali naomba mnionyeshe ulipo mwili wa Nathan 

nianze taratibu za kuukabidhi kwa 

serikali yake” akasema Dr.Vivian 

na machozi yakamtoka 

“Mathew tafadhali nauhitaj 

mwili wa Nathan.Nipeleni mahala 

ulipo mwili wake nikashuhudie na 

kuamini kama kweli amekufa” 

akaendelea kusisistiza Dr.Vivian 

“No madam president I wont 

do that.Suala hili linapaswa 

kuendelea kuwa siri kubwa.Jambo 

hili likiwekwa wazi litaleta 

msuguano mkubwa sana.Madam 

president nakuomba unikubalie 

suala hili liendelee kuwa siri yetu” 

“Mathew siwezi kulifanya siri 

jambo kubwa kama hili.Lazima 

niliweke wazi,muuaji afahamike na afikishwe mbele ya sheria” 

akasema Dr.Vivian 

“Dr.Vivian nakuomba tena 

usithubutu kufanya hivyo kwani 

utaharibu kila kitu.Mpaka sasa 

tuna uhakika kwamba serikali ya 

Marekani kupitia shirika lake la 

CIA wana mkono wao katika 

mambo haya yaliyotokea kuanzia 

ajali ile ya ndege ya rais Anorld na 

tunaamini hata mauaji ya kanali 

Sebastian Matope watakuwa 

wanahusika.Tumegundua 

wamekuwa wanakufuatilia na 

kupata habari zako,hatujui bado 

kwa nini wanafanya hivyo lakini 

lazima ipo sababu kubwa ya 

kudukua taarifa za mkuu wa 

nchi.Endapo ukiliweka wazi hili suala na ikajulikana kwamba 

Theresa ndiye aliyemuua Nathan 

itaharibu kila kitu na tutashindwa 

kupata majibu wanachunguza 

jambo gani toka kwako.Nakuomba 

usikie ushauri wangu ,jambo hili 

liendelee kuwa siri yetu.Nafahamu 

umeumia sana na kila mmoja wetu 

hapa ameumia kwani Nathan 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog