Search This Blog

Friday 7 April 2023

I WAS WRONG | NILIKOSEA - 3

  


Simulizi : I Was Wrong | Nilikosea 

Sehemu Ya Tatu (3)


nani mwanaume wa maisha yake.Pauline 

aliona ni vyema ampigie simu na 

amtamkie wazi wazi kilichomo moyoni 

mwake kwamba ni yeye ndiye mwanaume 

ambaye anamkosesha usingizi.Alipopiga 

alitaarifiwa kwamba mteja anayempigia 

anaongea na simu nyingine.  “ anaongea na na nani? Lazima 

atakuwa ni mama mdogo.yeye ndiye 

anayependa kumsumbua David mida 

kama hii.Kesho nitafuatilia nijue alikuwa 

anaongea na nani.Moyo unaniuma 

sana,nahisi lazima alikuwa anaongea na 

mwanamke.Nitafuatilia nifahamu ukweli..” 

Akawaza Pauline 

Saa kumi na mbili za asubuhiPauline 

akaamka kama ilivyo kawaida 

yake.Akafanya mazoezi kwa muda wa 

nusu saa halafu akaingia bafuni 

kuoga.Bado kichwa chake kilitawaliwa na 

jambo moja kubwa.Ni nanialiyekuwa 

anaongeasimunina Davidusiku? Hilindilo 

swalilililokuwa linamsumbua sana akili 

yake. 

 “ Lazima nimfahamu mtu aliyekuwa 

anaongea na David jana simuni alikuwa 

nani.Ninahisi lazima atakuwa ni mama 

mdogo.yeye ndiye ambaye amekuwa 

akitafuta sana ukaribu na David ” akawaza 

wakati akiendelea kuoga.Alipomaliza 

akarejea chumbani kwake na kukutana na 

ujumbe mfupi katika simu yake.Ulitoka 

kwa David “ Halow Pauline umeamkaje? Pauline 

akatabasamu na kuujibu 

 “ Nimeamka salama David.Wewe je 

umeamkaje? 

 Baada ya dakika moja David akajibu 

 “ Nimeamka salama Pauline” 

Pauline hakuandika tena ujumbe wowote 

wa kujibu ,akaendelea a kujiandaa 

alipomaliza akajumuika na David kupata 

kifungua kinywa 

 “ Jana mbona uliizima simu yako ? 

Nilisubiri unifahamishe shemeji yangu ni 

nani lakini simu yako haikuwa ikipatikana 

tena.” akasema David.Pauline 

akatabasamu na kusema 

 “ Nilikupigia ili nikwambie lakini 

nikakuta unaongea na mtu kwa kuwa 

simuyangu haikuwa na chajiya kutosha 

ikanilazimu kuizima na kuiweka katika 

chaji” akasema Pauline 

 Waliendelea kupata kifungua kinywa 

kimya kimya nawalipomaliza wakaingia 

garini wakaelekea kazini.Hakukuwa na 

maongezi mengi garini na baada tu ya 

kumfikisha David ofisini kwake Pauline 

akaendelea na safariyake kuelekea katika kampuni ya simu anakofanya kazi rafiki 

yake Maurine. 

 “ karibu sana Pauline” maurine 

akamkaribisha Pauline baada ya kufika 

 “ Ahsante sana 

Maurine.Unaendeleaje? 

 “ Ninaendelea vizuri sana Pauline.” 

 “ Nafurahi kusikia hivyo” akasema 

Maurine. 

 “ Maurine nimekuja hapa asubuhi hii 

nina shida ndugu yangu”akasema Pauline 

 “ Shida gani nikusaidie ? akauliza 

Maurine 

 “ Ni kuhusu ile namba niliyokutumia 

nikakuomba unisaidie kunipa taarifa zake 

“ 

 “ Ndiyo naikumbuka ile namba.” 

 “ Basi ninaomba nikusumbue tena 

shoga yangu uniangalizie tena namba ile 

ilikuwa inaongea namba gani jana usiku? 

Akasema Pauline na kuziandika namba za 

David katika kijikaratasi akampatia 

Maurine 

 “ Namba hii ni ya nani Pauline 

mbona unaifuatilia sana?akauliza Maurine 

huku akitabasamu.  “ Maurine wewe ni rafiki yangu 

mkubwa na siwezi kukuficha kitu.Namba 

hii ni ya kijana mmoja anaitwa David.Ni 

kijana ambaye ninampenda sana na nina 

mpango naye mikubwa .Tatizo ni kwamba 

siko peke yangu ninayempenda.Kuna watu 

wengine ambao wanamnyemelea kwa siri 

na ndiyo mana unaniona ninahangaika 

namna hii kutaka kuwafahamu.Naomba 

unisaidie Maurine.” 

 “ Unafanya jambo la maana sana 

Pauline.Kama una mtu wako 

unayempenda tafadhali jitahidi kumlinda 

dhidi ya wezi wa mabwana za 

watu.Ukizubaa tu wanakuchukulia bwana 

wako.Siwezi kusahau walivyonipora 

Christopher”akasema Maurine 

 “Kweli Pauline.Usipokaa imara 

kumlinda mtu wako wanakunyag’anya 

huku ukiona” 

 “Nisubiri hapa Pauline 

nikakushughulikie.Nitarejea baada ya 

muda mfupi” akasema Maurine na kutoka . 

 “ Nitapambana na yeyote 

anayejipitisha pitisha kwa 

David.Sintokubali mtu yeyote anichukulie 

mwanaume ninayempenda.David ni wangu peke yangu.Mimi ndiye 

niliyemfikisha hapa alipo sasa hadi wote 

wakamuona.Hakuwa anatazamika 

alipotoka gerezani lakini mimi sikuijali 

hali yake bali nilimpenda hivyo hivyo 

alivyo.Sifahamu ndani ya moyo wake 

anawaza nini lakini ninafahamu hata yeye 

ananipenda pia lakini anaogopa 

kuniambia”akawaza Pauline wakati 

akimsubiri Maurine arejee.Baada ya kama 

dakika kumi Maurine akarejea 

 “ Pauline taarifa yote ya mawasiliano 

ya jana ya namba ile iko humu katika 

karatasi.” Akasema Maurine huku 

akiiweka karatasi ile katika bahasha 

nakumpatia Pauline 

 “Maurine ahsante sana kwa msaada 

wako” akasemaPauline kisha akaagana na 

Maurine akatoka.Alpoingia katika gari 

lake aka ichukua karatasi ile na 

kuisoma.Alikuwa anaitafuta namba ya 

simu iliyokuwa ikiongea na simuya David 

usiku .Alistuka sana baada ya kukuta 

namba ya mwisho kuongea na David ni 

namba anayoifahamu vizuri. 

 “ Tamia ..!!!..akasemakwa sauti 

ndogo  “ Kumbe Tamia ndiye aliyekuwa 

akiongea na David jana usiku.Nimekwisha 

mfahamu mbaya wangu” akawaza Pauline 

halafu akawasha gari na kuondoka 

 “ Nilimuona Tamia toka siku ya 

kwanza niliyomtambulisha kwa David 

alianza kujipendekeza 

kwake.Ninamfahamu vizuri Tamia 

,ninazifahamu tabia zake si nzurihata 

kidogo.Kila mwanaume mzuri yeye 

humtaka.Hapa mjini amwekwisha tembea 

na wanaume wengi tu.Hapana siwezi 

kukubali afanye upuuzi wake kwa David.I 

have to stop her.”akawaza Pauline na 

kuendesha gari lake hadi nje ya duka lake 

hakushuka akachukua simu yake na 

kuzitafuta nkuzitafuta namba za simu za Tamia 

akampigia. 



Hapana siwezi 

kukubali afanye upuuzi wake kwa David.I 

have to stop her.”akawaza Pauline na 

kuendesha gari lake hadi nje ya duka lake 

hakushuka akachukua simu yake na 

kuzitafuta namba za simu za Tamia 

akampigia. 

 “ hallow Pauline”akasema Tamia 

 “ Hallow Tamia habariyako?” 

akasema Pauline.Sauti yake ikamstua 

kidogo Tamia.Haikuwa ni ile sauti 

aliyoizoea 

 “ Pauline mbona sauti yako naona 

kama haiko sawa? Is there any problem 

sweet baby?  “ I’mFineTamia.I’m ok” akajibu 

Pauline 

 “ Pauline you are not 

ok.Ninakufahamu vizuri na hata kama una 

matatizo ninafahamu.Tell me Baby girl 

what happened? 

 “ Tamia mbona hutaki kunielewa? 

Nimekwambia sina tatizo !! Akasema 

Pauline kwa ukali 

 “ Sawa Pauline .Kama uko shwari poa 

lakini mimi nina uhakika hauko shwari.” 

 ‘ Tuachane na hayo Tamia,did you 

call David last night?akauliza Pauine 

.Kikapita kimya cha sekunde 

kadhaa.Tamia akajibu 

 “ Last night? 

 “Yes ! Last night.Did you call david? 

 “Yes I did”akajibu Tamia. 

 “kwani kuna tatizo lolote Pauline? 

 “ Sikiliza Tamia,tena naomba 

unisikilize vizuri sana.Naomba kuanzia leo 

usimpigie tena simu David” 

 “ Pauline?!!..Tamia akashangaa 

 “Whats going on with you ? Akauliza 

 “ Nimekwambia hivyo 

Tamia.Naomba unielewe.Usimpigie tena 

simu David.Tamia ninakufahamu vizuri na ninazifahamu tabia zako.Wewe kila 

mwanaume unataka awe wako 

tu.Tafadhali achana na David” 

 “ Pauline mbona sikuelewi? Kuna 

kosa gani kumpigia simu David? 

 “Hakuna kosa ila sitaki tu umpigie 

simu David.Sitaki ukaribu wowote 

kwake.Stay far away from him” akasema 

Pauline.Tamia akaonekana kuchukizwa na 

maneno yale ya Pauline 

 “ Pauline naomba nawe unisikilize 

vizuri.Huna uwezowa kunizuia kumpigia 

simu David.kama angeniambia David 

mwenyewe ningemuelewa lakini wewe 

huna uwezo wa kunizuia kumpigia 

David.Nina haki ya kumpigia simu muda 

wowote nikitaka..” Akasema Tamia kwa 

sauti yenye kebehi 

 “ Tamia ninafahamu unachokitafuta 

kwa David na kamwe nakwambia 

hutaweza kukipata.Stay away from him” 

 “ Why should I stay away from him? 

He’s not even your husband so why are 

you jealousy? 

 “ Tamia kwa nini unakuwa mgumu 

kunielewa? Au unataka mpaka nikutamkie 

kwamba David ni mwanaume wangu”  “ He’s yours?!!!..Tamia akashangaa 

 “ David is yours? Mbona aliniambia 

kwamba hamna mahusiano yoyote ya 

mapenzi? I dont believe you Pauline” 

 “ Uamini,usiamini utajua mwenyewe 

lakini nimekwisha kuonya kwamba kaa 

mbali na David.Ni mwanaume 

wangu.Akasema Pauline na kukata simu 

 “ Bora nimemeweleza ukweli.Tamia 

ni msichana asiyetulia na kama akimtaka 

mwanaume lazima atampata.Halafu 

inaonekana tayari wameongea mambo 

mengi hadi David hadi kufikia hatua ya 

kumweleza kwamba mimi na yeye hatuna 

mahusiano yoyote .Natakiwa nifanye 

haraka sana kumdhibiti 

David,nikichelewa watamchukua hawa 

wanaomuwinda” akawaza Pauline 

akashuka garini na kuingia dukani kwake. 

Maneno aliyoambiwa na Pauline 

yalimchafua sana Tamia.Kwa dakika 

takribani kumi alikuwa ameinama 

akitafakari.Akachukua simu na kuzitafuta 

namba za David akampigia 

 “ Hallow Tamia .Habari za asubuhi? 

Akasema David baada ya kupokea simu 

 “ Habari za asubuhi si nzuri David”  “ Whats wrong Tamia? Unaumwa? 

Akauliza David 

 “ Siumwi David lakini kuna jambo 

limetokea asubuhi hii na kuniharibia 

kabisa siku yangu” 

 “ Nini Kimetokea Tamia? Tafadhali 

niambie” 

 “ Jana usiku nilipokupigia simu 

ulikuwa na nani? Akauliza Tamia 

 “ Nilikuwa peke yangu kwani vipi? 

 “ Una hakika ulikuwa peke yako? 

Haukuwa na Pauline? 

 “ Pauline?!! David akashangaa 

 “ Ndiyo.Hukuwa na Pauline wakati 

ninakupigia simu? 

 “ Hapana Tamia sikuwa na Pauline 

wakati ule.Yeye alikuwa chumbani kwake 

na mimi nilikuwa kwangu,Kwani kuna 

nini Tamia? 

 “ Kama hukuwa naye amejuaje basi 

kama nilikupigia simu jana usiku? 

Akauliza Tamia 

 “ Hapana hafahamu chochote kama 

ulinipigia simu” akasema David 

 “ She knows” akajibu Tamia 

 “ Anajua ? Alijuaje?   “ Swali hilo nikuulize wewe pengine 

unaqweza ukawa na majibu.” 

 “Kama amefahamu kwamba mimi na 

wewe tuliongea kwa simu jana usiku basi 

haya ni maajabu kwa sababu sikuwa naye 

na wala sikumwabia chochote .Umeonana 

naye leo asubuhi? 

 “ Amenipigia simu muda si mrefu 

amenikanya nisiwasiliane nawe 

tena.Amesema kwamba wewe ni mpenzi 

wake.Is that true David? maneno yale 

yakamstua sana David. 

 “ Amesema kwamba mimi ni mpenzi 

wake? 

 “Ndiyo amesema kwamba mna 

mahusiano ya kimapenzi” 

 “ No that’s not true.Mimi na yeye 

hatuna mahusiano yoyote ya kimapenzi na 

isitoshe tayari yeye ana mtu wake na 

ameahidi kunitambulisha kwake muda si 

mrefu” 

 “ Kama ana mtu wake kwa nini basi 

anipige marufuku kuwasiliana nawe ? na 

kwa nini atamke kwamba wewe na yeye 

mko katika mahusiano? 

 “Hata mimi nashangaa Tamia na 

sielewini kwa nini amesema hivyo lakini ukweli ni kwamba mimi na Pauline hatuna 

mahusiano yoyote kimapenzi na 

ninamuheshimu Pauline kama dada 

yangu.Naomba unipe dakika mbili niongee 

naye halafu nitakupigia tena” akasema 

David na kukata simu 

 “ Pauline amejuaje kama Tamia 

alinipigia simu jana usiku? Kwa nini 

ananifuatilia na kutaka kufahamu kila 

ninayeongea naye? Halafu kwa nini 

amwambie Tamia kwamba mimi 

nimpenzi wake?Ngoja nimpigie siu sasa 

hivi”akawaza david huku akizitafuta 

namba za simu za Pauline akampigia 

 “ Halow david”akasema Pauline 

 “ Pauline uko wapo mida hii? 

 “Niko dukani kwangu.We uko wapi? 

 “ Niko ofisini “akasema David halafu 

kukawa na kimya kifupi 

 “Unasemaje David “akasema 

Pauline. 

 “ Pauline kuna kitu umeongea na 

Tamia? 

 “ Tamia? Pauline akashangaa 

 “ Ndiyo.Tamia umeongea naye kitu 

chochote?  “ David nitaongea nawe baadae kwa 

hivi sasa kuna kazi ninaifanya .Nitakupitia 

mchana tuelekee mahala tukapate 

chakula halafu tutaongea” 

 “ Ok Pauline.Tutaonana baadae” 

akasema David na kukata simu .Akakaa 

mezani na kuzama mawazoni 

 “ kwa nini Pauline atamke maneno 

yale kwa Tamia? Kwa nini amzuie 

asinipigie simu? nashindwa kumuelewa 

kabisa Pauline.Kuna tatizo gani kwa mimi 

kuwasiliana na Tamia? Nini kinaendelea 

kati yao? Anyway nitafahamu yote mchana 

nitakapokutana na Pauline. Ninahisi kuna 

kitu kinaendelea baina yao. akawaza 

David 

******************* 

Saa sita na robo mchana Pauline 

alifika ofisini kwa david kisha 

wakaondoka kwenda kupata chakula cha 

machana.Hakukuwa na maongezi mengi 

garini.Walifika katika hoteli ambayo 

hupendelea sana kupata chakula cha 

mchana wakaagiza chakula.Walikula 

kimyakimya na ilionekana kana kwamba wanaogopana.Kila mmoja alionekana 

kumtegea mwenzake kuanzisha 

maongezi.Baada ya kumaliza kula ni David 

ndiye alieanzisha maongezi 

 “ Pauline nadhani ni muda muafaka 

sasa wa kuongea.Kuna mambo mawili 

matatu ambayo tunatakiwa tuyajadili 

lakini kwanza tuongelee kuhisiana na 

suala lililoibuka kati yako na Tamia 

“akasema David.Pauline aliyekuwa 

akinywa juice akakaa kimya kidogo kisha 

akasema 

 “ Kuna kitua gani kinaendelea 

katiyako na Tamia? 

 “ Mimi na Tamia ni marafiki 

tu.Hakuna chochote kibaya 

kinachoendelea kati yetu” akasema David 

 “ Alikupigia simu akakwambia nini? 

 “ Alisema kwamba ulimpigia simu 

ukamkanya asiwasiliane tena na mimi 

halafu ukamwambia kwamba mimi na 

wewe tuna mahusiano yakimapenzi” 

akasema David.Pauline akatabasamu na 

kusema 

 “ Ndiyo nilimkanya asiwasiliane 

nawe tena.”  “ kwa nini Pauline? Kuna ubaya gani 

kwa mimi kuwasiliana na Tamia? 

 “ Hakuna ubaya lakini nilimkanya 

asikuzoee kabisa” 

 “ Pauline nashindwa kuelewa ni kitu 

ganivkinachoendelea kati yako na 

Tamia.Kwa nini umzuie asizoeane nami ? 

 “ David haumfahamu Tamia.Mimi ni 

rafiki yangu na ninamfahamu vyema. 

Ninazifahamu tabia zake si nzuri hata 

kidogo na ndiyo maana sitaki kabisa uwe 

karibu naye.” 

 “ Tamia ana tabia zipi mbaya? 

 “ Tamia ana wanaume karibu kila 

kona ya jiji la Arusha.Kila mwanaume 

mzuri atakayemuona humtamani na 

akimtamani mwanaume ni lazima 

atampata tu.Ni msichana ambaye hajatulia 

hata kidogo.Tafadhali kaa naye mbali na 

wala usikubali kumzoea” akasema 

Pauline.David hakusema kitu akabaki 

anamuangalia. 

 “ Toka siku ya kwanza Tamia 

alipokuona alianza kujipitisha pitisha 

kwako na anafanya juhudi za kukuzoea 

kwa haraka.Nakuapia David ukishamzoea 

tu umekwisha.Atakuweka katikahimaya yake na baada ya kukutumia atampata 

mwnaume mwingine atakuacha.Wanaume 

wengi wamekwishal izwa na Tamia.” 

 “ dah ! ..akasema David 

 “ Sikufahamu kuhusu 

hilo.Nashukuru kwa kunifahamisha lakini 

mimi na yeye ni marafiki wa kawaida tu.” 

 “ Huanza namna hiyo.Huanza na 

urafiki wa kawaida lakini baada ya muda 

atakushawishi na mtaingia katika 

mahusiano ya kimapenzi.Tamia ni 

msichana anayefahamu kushawishi 

mpaka ukamkubalia 

anachokitaka.Anaitumia silaha ya uzuri 

wake kuwateka wanaume.Ana ulimi mzuri 

ambao huutumia kuwadanganya 

wanaume.” 

 “ Ok tuachane na hayo,ilikuaje 

ukamwambia kwamba mimi na wew tuna 

mahusiano ya kimapenzi? Akauliza 

David.Pauline akaona aibu kidogo halafu 

akasema 

 “ Nililazimika kumweleza hivyo ili 

aachane kabisa na wewe na 

asikuzoee.Akifahamu kama wewe ni 

mpenzi wagu hatakuzoea kabisa”  “ lakini Pauline si uliniambia 

kwamba una mtu ambaye unampenda 

sana na unaogopa kumwambia ukweli.? 

 “ Ndiyo nilikwambia” 

“Mtu huyo ni nani? Unaweza 

ukaniambia? 

 “ Elvis bado tu unakumbuka? 

 “ Ndiyo ninakumbuka Pauline 

.Uliniahidi wewe mwenyewe kuniambia ” 

 “ Nilitaka kukueleza jana lakini 

muda mrefu ukautumia na Tamia 

nikashindwa kukwambia” 

 “ Ok naomba uniambie leo.Ni nani 

huyo shemeji yangu? Akauliza 

David.Pauline akababaika sana kulijibu 

swali lile.Kila alipotaka kutamka kitu 

akahisi sauti inakwama. 

 “ Niambie Pauline nimfahamu mtu 

huyo anayekukosesha usingizi? David 

akaendelea kusisitiza. 

 “ Ngoja tu nimweleze ukweli.Siwezi 

kuendelea kuteseka kila siku kwa ajili 

yake.Nikizubaa zubaa watu 

watamchukua.Wengi wanamtamani” 

akawaza Pauline akanywa juice kidogo 

halafu akasema  “ David toka aliyekuwa mchumba 

wangu kufariki,sikuwa na hisia za 

kupenda tena.Sikuamini kama nitampata 

mtu kama yeye.Nilimpenda kupitiliza.I 

was wrong.” 

 Akanyamaza kidogona kuendelea 

 “ Katika dunia hii bado kuna 

wanaume wengi tu wazuri na wenye sifa 

zote ninazozihitaji kwa mwanaume wa 

maisha yangu.” 

 “ Nina hamu sana ya kumfahamu 

mwanaume huyo mwenye bahati kubwa 

ya kupendwa nawe.” Akasema 

David.Pauline akamkazia Macho David na 

kusema 

 “ David naomba usihamaki ,naomba 

usistuke wala usikasirike.Mwanaume 

anayenikosesha usingizi ni wewe.” 

 “ Me?!!..David akashangaa 

 “ Ndiyo David ni wewe” akasema 

Pauline.Ilikuwa ni vigumu sana kwa David 

kuamini 

 “ You are mistaken Pauline.Yu are 

wrong” 

 “ No I’m not wrong David.Its you 

whom I love with all my heart.Sikuwa 

nikiamini kama nitaweza kumpata mtu ambaye ataubadili msimamo wangu na 

kunifanya nipende tena.Ulipotokea wewe 

nimejikuta nikiufungua moyo wangu 

tena.Tafadhali David naomba uuufungue 

moyo wako kwangu kama mimi 

nilivyoufungua moyo wangu 

kwako.”akasema Pauline 

 “ Pauline No ! This cant happen” 

 “ why David? Kuna ubaya gani mimi 

na wewe tukawa wapenzi? 

 “ Pauline wewe ni kama dada yangu 

na ninakuheshimu mno.Naomba 

tusiongelee tena mambo kama hayo” 

akasema David.Pauline ambaye 

alinyong’onyea sana kwa namna David 

alivyobadilika akasema 

 “ David naomba usihamaki 

kuhusiana na suala hili.Nimekueleza 

ukweli kwamba ninakupenda kwa sababu 

ni jambo ambalo limekuwa linaniumiz a 

kila uchao kwa hiyo kukweleza ukweli 

tayari nimeutua mzigo mzito uliokuwa 

unanielemea.Nafahamu jambo hili 

limekustua sana kwani hukuwa 

umelitegemea lakini hata hivyo nakuomba 

jipe muda na ulifikirie vizuri jambo hili .” 

akasema Pauline kisha akainuka wakaongozana hadi katika gari na 

kuondoka.Ilikuwa ni safari ya kimya 

kimya .Hakuna aliyekuwa akimsemesha 

mwenzake.Pauline akampeleka David 

ofisini kwake halafu akaendelea na 

shughuli zake 

 Mara tu David alipoingia ofisini 

kwake akakutana na bahasha nzuri yenye 

nakshi za kuvutia iliyopenyezwa chini ya 

mlango.Akaifungua bahasha ile ndani yake 

akakuta kadi nzuri ya mwaliko.Tamia 

alikuwa anamualika katika birthday yake 

itakayofanyika siku ya jumamosi 

Dakika tatu zilipita David akiwa amekaa 

juu ya jmeza mkononi ameshika kadi ya 

Tamia.Alikuwa akiwaza mambo mengi 

kuhusiana na jambo aliloambiwa na 

Pauline na kitu gani amjibu.. 

 “ Nachanganikiwa na sijui nifanye 

nini.Pauline amekwishanitamkia kwamba 

ananipenda na nimemuona machoni 

alikiwa akimaanisha kile alichokisema.Ni 

Pauline aliyeniokota nikiwa hohehahe 

sitamaniki , sina hili wala lile.Hakujali hali 

yangu niliyokuw a nayo wakati ule 

,akanikaribisha kwao na kunikarimu kwa namna ya kipekee kabisa.y eye ni sababu 

ya mimi kuwepo hapa nilipo hivi sasa na 

kamwe siwezi kupingana na jambo hilo 

lakini kinachoniumiza kichwa ni kwamba 

sina hata chembe moja ya mapenzi 

kwake.Ninamuheshimu kama dada yangu 

.Nitawezaje kuingia katika mahusiano na 

mtu ambaye moyo wangu haudundi 

kwake? Endapo nikisema nimkubali 

Pauline itakuwana ni sawa na kulipa 

fadhila kwa mambo aliyonifanyia lakini 

sintakuwa namapenzi naye na nitakuwa 

nikimdanganya kitu ambacho 

sikitaki.Hapana siko tayari kumuumiza 

Pauline.Ni binti mzuri ambaye sitaki 

kuuchezea moyo wake.” Akawaza David 

halafu akakumbuka kitu 

 “ kwa upande mwingine nikisema 

nisiingie katika mahusiano na Pauline 

mipango yote ya madam Vicky itashidwa 

kwenda kwani Pauline ataendelea 

kutufanyia uchunguzi na endapo 

akigundua kitu kinachoendelea baina yetu 

basi nitapoteza kila kitu.Nitafanya nini? 

Nifanye kama alivyonitaka madam Vicky? 

akaendelea kuumiza kichwa chake kwa 

mawazo mengi .Akaenda kuketi kitini na kuchukua simu yake akazitafuta namba za 

Tamiana kumpigia 

 “ Hallow David habari yako? 

Akasema Tamia kwa sauti yake Tamu na 

laini.Usowa david ambao kwa dakika 

kadhaa zilizopita ulikuwa na simanzi kwa 

mawzo mengi ukapambwa na tabasamu 

 “ Hallow Tamia “ akasema David 

 “ David umesharudi ofisini kwako? 

Akauliza Tamia 

 “ Ndiyo Tamia nimekwisha rejea” 

 “ Umeupata mzigo wangu? 

 “ Ndiyo nimeupata .ahante kwa 

mwaliko” 

 “ Nilikuja ofisini kwako ili nikupatie 

wewe mwenyewe kwa mkono lakini 

hukuwepo nikaamua kuipitisha chiniya 

mlango ili ukija uikute.” 

 “ Usijali tamia nimeshaipata.” 

Akasema David halafu ukimya mfupi 

ukapita Tamia akasema 

 “ David tafadhali usikose kufika siku 

ya jumamosi.Wewe utakuwa ni wa 

muhimu sana katika sherehe hii.” 

Akasema Tamia.David akatabasamu na 

kusema  “ Nitajitahidi nisikose.natamani 

nikuone namna utakavyokuwa 

umependeza siku hiyo”akasema David na 

kumfanya Tamia acheke 

 “ Unataka nivaaje siku hiyo? 

Akauliza Tamia 

 “ Anything that can make you look 

amazing” akasema David 



“ Unataka nivaaje siku hiyo? 

Akauliza Tamia 

 “ Anything that can make you look 

amazing” akasema David 

 “ Ok tuachane na hayo,umeongea na 

Pauline? Umemuuliza kuhusu lile suala 

nililokwambia? 

 “ Ndiyo nimeongea naye na 

nimemuuliza kuhusina na suala lile” 

 “ amesemaje? Akauliza Tamia.David 

akashindwa aseme nini 

 “David answer me please” akasema 

Tamia 

 “ uhm.. Tamia unaonaje kama 

tukiacha kuongelea masuala haya kwa 

sasa? 

 “ No david we have to talk about 

this.Pauline hawezi kunikataza mimi 

kuwasiliana na wewe”akasema 

Tamia.David akawa kimya.Alishindwa 

amwambie nini Tamia 

 “ David,” akaita tamia  “ Ni kweli kwamba wewe na Pauline 

mna mahusiao ya kimapenzi? Akauliza 

 “ Dah ! huu ni mtihani mgumu 

sana.Nimwambieje? akajiuliza David 

 “ David !! akaita tena Tamia 

 “ Tamia mimi na Pauline hatuna 

mahusiano yoyote ya 

kimapenzi.Mahusiano yetu yamejengwa 

katika heshima ya kaka na dada.Hicho 

pekee ndicho ninachoweza kukwambia 

kwa sasa.” 

 “ Nafurahi kusikia hivyo toka kwako 

lakini iweje atamke kwamba wewe ni 

mpenzi wake? 

 “ Tamia hata mimi sifahamu ni kwa 

nini ametamka hivyo Labda alitaka 

kukurusha roho tu ” 

 “ David ,Pauline hakutamka katika 

hali ya kunirusha roho.Alikuwa 

akimaanisha alichokisema na kwa namna 

nilivyomsikia leo ni anaonekana yuko 

tayari hata urafikiwetu uvunjike kuliko 

mimi kuendelea kuwasiliana nawe.” 

Akasema Tamia 

 “ Tamia mambo haya 

yananichanganya sana.Naomba tuachane 

nayo na kitu cha msingi ambacho nataka ukifahamu ni kwamba mimi sina 

mahusiano na Pauline na ninakuomba 

usiache kuwasiliana nami” akasema David 

 “ Ok David nashukuru sana.Kabla 

sijakuacha uendelee na kazi kuna jambo 

nataka kukuomba.” 

 “Jambo gani Tamia? 

 “ Nitaomba muda wako siku ya kesho 

mchana kuna mahala nitaomba 

unisindikize” 

David akafikiri kwa sekunde kadhaa 

kisha akasema 

 “ Ok sawa tamia “ 

 “ Ahsante sana david.Mchana 

mwema”: akasema Tamia na kukata simu 

 “ dah ! mtihani mwingne huu kwa 

Tamia.Nimetokea kumpenda Tamia lakini 

mambo aliyonieleza Pauline leo 

yamenistua kidogo.Itanilazimu nifanye 

uchunguzi kwanza ili kubaini kama 

mambo niliyoelezwa ni ya kweli au 

yalikuwa ni maneno tu ya Pauline akitaka 

nisiwe karibu na Tamia.”akawaza David 

na kuendelea na kazi zake. 

*****************  Ni saa mbili za usiku Robin akiwa 

katika chumba cha kusome akimsaidia 

mwanae Penina maswali ambayo 

yalikuwa yakimsumbua.Ni utaratbu 

aliojiwekea wa kumsaidia mwanae 

maswala ambayo yalionekana kuwa 

magumu kwake.Hii ilimsaidia sana 

Penina kufahamu mambo mengi. 

 “ Dady !..akaita Penina 

 “ Unasemaje? Akauliza Robin 

 “ Unakumbuka Birthday ya mwalimu 

Lucy ni lini? 

 “ Nakumbukani jumamosi ijayo” 

 “ Umemuandalia zawadi gani? 

Akauliza penina.Robin akatabasamu na 

kusema 

 “ Unataka tumuandalie zawadi gani? 

 “ Dady hatuwezi kuwa na zawadi 

moja.Mimi nina ya kwangu na wewe 

unatakiwa utafute ya kwako” akasema 

Penina 

 “ Mwalimu Lucy anapendelea vitu 

gani? 

 “ Mhh mwalimu Lucy anapenda vitu 

vingi “ 

Robin akafikiri kidogo na kusema  “ Unanishauri nimtafutie zawadi gani 

ambayo anaweza akipenda? Akauliza 

Robin 

 “ dady mimi sifahamu zawadi 

mnazopeana watu wakubwa.Nyie 

mnazifahamu zawadi zenu” 

 “ Ok nitatafuta zawadi nzuri ya 

kumpa.” Akasema Robin na kuinuka 

 “ Ninakwenda chumbani ukimaliza 

hayo maswali uwahi kwenda kulala” 

Robin akamuaga binti yake na kuelekea 

chumbani kwake akajilaza kitandani 

 “ Nitampatia Lucy zawadi 

gani?akajiuliza 

 “ Najaribu kufikiri ni zawadi gani 

ambayo nitampatia Lucy ambayo 

itamfanya anikumbuke kila wakati 

akiiona? Akawaza Robin 

 “ Lucy ana kila kitu katika 

maisha.Ninataka nimpatie kitu cha tofauti 

ambacho hakukitegemea na wala hakuna 

aliyewahi kumzawadia”akawaza sana na 

baadae akapata jibu 

 “Nimepata jibu.Nitamtafutia zawadi 

Fulani ndogo lakini yenye umuhimu 

kwake.” Akawaza Robin  “ Mwalimu Lucy ametokea kuniteka 

akili yangu toka nilipomuona.Ana kila sifa 

ya mwanamke ninayemtaka.Nadhani ni 

wakati sasa wa kuliziba kovu nililoumizwa 

na mwanamke niliyempenda 

nikamthamini na kumuona kama 

malaika.Siwezi kuisahau siku ile Vivian 

aliponikimbia huku akinitolea maneno 

mazito ya kashfa.Niliumia sana na 

ilinichukua miaka mingi kuweza kulitibu 

jereha lile na kuizoea hali ya 

maisha.Ninamshukuru mwanangu penina 

ambaye amekuwa ndiye nguvu yangu.Kila 

nilipokata tamaa nilipata nguvu ya 

kusonga mbele tena baada ya 

kumtazama.Kwa sasa Mungu amenijalia 

maisha yangu yamekuwa mazuri,ninaishsi 

kwa furaha na mwanangu lakini baada ya 

miaka mingi kupita ninajisikia kupenda 

tena na mtu pekee ambaye moyo wangu 

umemtunuku ni Lucy .I hope this timeI’m 

not wrong ”akawaza Robin 

 ******************** 

 Ilikuwa ni moja ya siku ndefu sana 

kwa David.Kilichokuwa kinamuumiza sana kichwa chake ni kuhusiana na 

mambo aliyoelezwa na Pauline.Alilkuwa 

akitafakari ni kitu gani angemjibu.Alikuwa 

amekaa kitandani akitafakari namna 

atakavyolimaliza suala lile .Mkononi 

alikuwa ameshika pete ya dahabu ambayo 

siku zote amekuwa akiificha katika kabati 

lake. 

 “Siku moja nitakupata na 

kukurejeshea pete yako na kukushukuru 

kwa msaada wako kwa mama ingawa 

haukumuwezesha mama yangu 

kupona.”akawaza David huku akiitazama 

pete ile na mara mlango wake 

ukagongwa.Akastuka na kuificha pete ile 

chini ya mto. 

 “ Lazima atakuwa ni madam 

Vicky”akawaza David 

 “ Anafuata nini mida hii? Huu 

mchezo wake wa kuja chumbani kwangu 

usiku unazua maswali mengi na 

anawafanya watu wahisi vibaya.Nitampiga 

marufuku kuja kunigongea mida 

hii”akawaza David huku akivaa fulana 

yake na kuelekea mlangoni akaufungua 

.Alistuka baada ya kukutana na kitu ambacho hakukitegemea.Aliyegonga 

mlangohakuwa madamVick bali Pauline. 

 “ Pauline” akasema David kwa 

mshangao akimtumbulia macho Pauine 

aliyekuwa amevaa vazi la usiku ililokuwa 

likionyesha kila kitu alichpvaa ndani. 

 “ Shhh..!! Usiongee kwa sauti “ 

akasema Pauline hukuakipenya na 

kuingia ndani.David akafunga mlango na 

kuendelea kusimama akimkodolea macho 

Pauline aliyekuwa amekaa kitandani huku 

akitabsamu 

 “ Mbona unanishangaa David.Please 

come and sit near me” akasema Pauline 

 “ Pauline unatafuta nini hukumida 

hii? Ukikutwa huku utajibu nini? Akasema 

David huku akionekna ni mwenye wasi 

wasi mwingi 

 ‘Nikutwe na nani? Mma mdogo 

akauliza Pauline.David akabakikimya 

 “ Davidi mtu pekee ambaye najua 

unahofia anweza akanikuta huku ni mama 

mdogo,usiwe na hofu naye hata 

kidogo.amelala na mze wake chumbani 

mida hii” 

 “ Lakini Pauline wewe ni mto wa 

kike ukionekana chumbani kwangu mida hii inaweza kunieletea matatizo kwa 

upande wangu.Nitaonekana ni mtu nisiye 

na nidhamu hata kidogo” 

 “ Nidhamu ioi unayoiongelea 

David?Mbona mamamdogo huwa 

humwambii suala nanidhamu? Tafadhali 

hebu usiwe muoga.” 

 “ Ok Pauline niambie nikusaidie 

nini? 

 ‘ David nimeshingwa kulala 

chumbanikwangu ,nikaona nije kulala 

huu.Hupoendi kama nikilala huku? 

Akasema Pauline na kuzid kumchanganya 

david 

 “ Pauline nuyumba yenuina vyumba 

vingi na kama umeshidwa kulla chumbani 

kwako basi ungechagua chumba 

kimojawapo ukaenda kulala au hata kwa 

mtumishi wa ndani kuliko kuja huku.” 

 “ David hiki ndicho chumba 

ninachohitaji kulala leo usiku.Upende 

usipende nitalla humu usiku wa leo.davd 

ni kituani hasa nikifanye ili 

uaminikwamba ninakupenda? Si rahis 

kwa mtoto w kike kumtamkia mwanaume 

kwamba anampenda lakini 

miminimekutamkia kwamba ninakupenda kwa nini unakuw amgumu namna hiyo 

kunielewa? Kitu gani nikufanyie ili uweze 

kunuufungua moyo wakona kuniruhusu 

niingie ndani? Najua unanipenda lakini 

unashindwa kuniambai ukweli.Lini basi 

utanitamkia kwa mdomo wakkwamba 

unanipenda? Akasema Pauline kwa hisia 

kali sana. 

 “ David laity ungejua nai jinsigani 

unvyouumiza moyo wangu usingethubutu 

kusimama hapokama mlingoti wa bendera 

wakati unaniona kabisa niko hpanimekuja 

kwa ajili yako.Please david I need you in 

my life.Moyo wangu umekukubali na 

unakupenda.ijali historia yako,umeoka 

wapi,na ulifanyanini huko nyuma lakini 

uko na mimi sasa na ninakupenda kwa 

moyowangu wote.tafadhali nionee 

huruma nipunguziematesohaya”ksema 

Pauline.David aliyekuwa amesima 

aaameegemea mlang akapiga hatu ana 

kwenda kupiga magoti mbeleya Pauline 

akamshika mikonona kusema 

 “ Pauline 

tafadhalinaombausihuzinike.Suala hil 

linaongelek na tunaweza 

tukalimaliza.Umenipa wakati mgumu sana nikuleeze kile kilichomomoyoni 

mwangu.Pauline wewe ndiye uliyeniokota 

mtaani na kunisafisha 

nikang’aa.Nakuheshimu sana na 

ndiyomaana nimekuwa mzitokuufungua 

mdomo wanguna kukutamkia 

kwambaninakupenda japokuwa moyo 

wangu umekuwa unakulilia 

usikunamchana.” Kabla hajaendela mbele 

tyari Pauline akamrukia na kuanza 

kumporomoshea mabusu.hakutaka 

kumpa nafasi Davidya kuendelea kwani 

alichokuwa anakihitajitayari amekwisha 

kisikia.alikuwa anataka kusikia tu 

kwamba David anampenda.Pauline alikuw 

a ni kama aliyepandwa na na wazimu. 

Alikuwa amemkumbatia Davidi kwa 

nguvu huku wakinyonyana ndimi.david 

naye alipandwa na midadi akaivuanguo ile 

ya Pauline na kuitupa pembeni,Pauline 

akabaiki nanguo za ndani.Ilikuw ani mara 

ya kwanza david anakutana na 

mwanamke toka afungwe gerezani Puline 

naye ilikuw ani mara yake ya kwanza toka 

mpenziwake alipofarikimiaka kadhaa 

iliyopita.pauline alishindwa kuendela 

kuvumilia akamtaka David aanzekazi .david akamuinua na kumuweka kitandani 

lakinikabla hajafanya chochote 

mlangoukafunguliwa.Hakuwa 

amekumbukakuufunga mlango.Alikuwa ni 

Vicky Madhahabu 

David na Pauline wakastuka 

mno.Hawakutegemea kitu kama kile 

kutokea.Walibaki wameduwaa 

wakimtazama Vicky madhahabu 

aliyekuwa akiwatazama kwa jicho kali na 

ilionekana dhahiri kwamba alikuwa 

amekasirika .Pauline na David walijisikia 

aibu sana kwa kukutwa katika hali ile ya 

utupu. 

 “ Next time mnapotaka kufanya 

mambo yenu muwe makini sana na 

msifanyie hapa ndani.Tafuteni sehemu 

nyingine mkakutane mfanye mambo 

yenu.Ni utovu wa nidhamu kufanya hivyo 

ndani ya nyumba hii.And you Pauline I 

need to talk to you” akasema Vick 

 “ sasa hivi? Akauliza Pauline 

 “ Ndiyo sasa hivi!akasema Vick na 

kuufunga mlango akatoka nje 

 “ Damn ! ..” akasema Pauline kwa 

hasira.  “ Kwa nini hukuufunga mlango 

David? Mwanamke huyu ni kama mchawi 

amekuja kuvuruga starehe za 

watu.Ninamchukia sana .Ngoja 

nikamsikilize anataka nini ,yawezekana 

baba akawa ametusikia.Nitarudi baada ya 

muda mfupi” 

 “ Pauline No!.Dont come back.Kwa 

leo haitawezekana tena.Ni kweli tulifanya 

jambo la kijinga sana kutaka kufanya 

mapenzi humu ndani na tena tukasahau 

kabisa hata kufunga mlango..MadamVicky 

yuko sahihi kama tunataka kufanya 

mambo haya tutafute sehemu nyingine 

mbali na hapa na si humu 

ndani.Tutapanga siku nyingine tena ” 

Akasema David na kuzidi 

kumnyong’onyeza Pauline 

 “ Please David don’t do this to 

me.Usimsikilize yule mchawi.Ninakuhitaji 

sana usiku wa leo.Nina hamu sana nawe ” 

akasema Pauline 

 “ Pauline hata mimi ninahamu 

kubwa na wewe lakini kwa leo 

haitawezekana tena kuendelea.Tutapanga 

siku nyingine na mahala kwingine lakini si 

hapa ndani.Unafikiri ingekuwaje iwapo ni mzee Zakaria ndiye angetukuta? Niwazi 

asingenielewa kabisa na ninatumai 

asingeniamini tena.Please Pauline let us 

do this some other time” akasema David 

ambaye kijasho kilikuwa 

kinamtiririka.Pauline akasimama kwa 

unyonge akavaa nguo zake na kisha 

akamkumbatia David na kumbusu 

 “ I love you David.I love you so much” 

akasema Pauline.David alishindwa amjibu 

nini.Pauline akamuacha David kisha 

akatoka.Nje ya mlango wa David 

akamkuta Vicky madhahabu 

akimsubiri.Uso wake ulionyesha wazi 

kwamba alikuwa amechukia. 

 “ Unasemaje mama mdogo? Akauliza 

Pauline ambaye alikuwa akiona aibu 

 “ Twende chumbani kwako” 

akasema Vick wakaongozana hadi 

chumbani kwa Pauline 

 “ Pauline unafanaya mambogani? 

Akauliza Vicky 

 “ Kwani vipi ma mdogo? Akauliza 

Pauline 

 “ Pauline ninajua kwamba wewe na 

Davidi mnapendana sana lakini naomba 

uwe makini sana hasa mnapotaka kufanya mambo yenu.Msifanye mpaka kila mtu 

akajua kinachoendelea kati yenu na 

ukumbuke kwamba baba yako hataki uwe 

na mahusiano na David.Kitendo 

ulichokifanya leo ni kitendo cha kijinga 

sana.Unadiriki vipi kufanya mapenzi na 

David ndani ya nyumba ya baba yako? 

Unafikiri baba yako ndiye ambaye 

angewakuta katikahali ile angekuwa 

katika hali gani muda huu? Ni wazi 

angeanguka kwa mstuko.Kwa hiyo basi 

kuwa makini sana unapotaka kufanya 

mambo yako.Sikukatazi kufanya lakini 

kuwa makini.Halafu kitu kingine 

usikurupuke tu kufanya mapenzi.Jipe 

muda wa kumsoma na kumfahamu vizuri 

David.Ifahamu historia yake,ametoka 

wapi na kikubwa zaidi uwe na uhakika 

kama kweli anakupenda kabla ya kumpa 

mwili wako “ akasema Vicky 

 “ Ma mdogo ninakubali leo nilifanya 

kosa lakini ni kwa sababu nilishindwa 

kujizuia.Nilikuwa na hamu kubwa sana na 

David leo na ndiyo maana nikaamua 

tufanye mapenzi.Ninampenda David na 

nina hakika hata naye ananipenda sana” 

akasema Pauline  “ Amekutamkia kwa mdomo wake 

kwamba anakupenda? 

 “ Ndiyo amenitamkia” 

 “ Basi vizuri kama amekutamkia, 

lakini bado ushauri wangu kwako ni 

kwamba uwe makini hasa mnapofanya 

vitendo vyenu ili baba yako asifahamu 

kinachoendelea kati yako na David .Kitu 

kingine mnapokutana kimwili usisahau 

kutumia kinga.Ulikuwa tayari kufanya 

mapenzi bila kutumia kinga.Una uhakika 

na afya ya David? Una uhakika yuko 

salama? Akauliza Vicky.Pauline akainama 

chini hakujua ajibu n ini 

 “ Huna hakika.Thats too 

bad.Unatakiwa uangalie vitu kama hivyo 

kabla ya kukimbilia kufanya 

ngono.Umenielewa Pauline? Akasema 

Vicky 

 “Nimekuelewa ma mdogo” 

 “ Ok vizuri sasa usirejee tena kule 

chumbani kwa David usiku huu.Yafanyie 

kazi hayo niliyokushauri “akasema Vicky 

madhahabu na kutoka. 

 “ Moyo unaniuma sana kumkuta 

David na pauline wakiwa katika hali ile 

nilitamani hata nimvae Pauline nimtafune pua yake.Najua ni yeye ndiye aliyejipeleka 

kwa David na kutaka wafanye 

mapenzi.She’s too fast.Natamani 

niwavuruge wasiwe na mahusiano lakini 

naogopa mipango yangu haitwakwenda 

kama ninavyotaka. Ngoja niwaache 

waendelee lakini hata hivyo siwezi kukaa 

nikimuona Pauline akijivinjari na 

David.Hata mimi nina hamu sana na yule 

kijana.Hata miminina kiu naye . I have to 

do something as fast as I can ” akawaza 

madam Vicky na kuelekea chumbani 

kwake huku akiwa 

amechanganyikiwa.Picha ya Pauline na 

David wakiwa watupu ilimtesa sana 



“ Moyo unaniuma sana kumkuta David na 

pauline wakiwa katika hali ile nilitamani 

hata nimvae Pauline nimtafune pua 

yake.Najua ni yeye ndiye aliyejipeleka kwa 

David na kutaka wafanye mapenzi.She’s 

too fast.Natamani niwavuruge wasiwe na 

mahusiano lakini naogopa mipango yangu 

haitwakwenda kama ninavyotaka. Ngoja 

niwaache waendelee lakini hata hivyo 

siwezi kukaa nikimuona Pauline 

akijivinjari na David.Hata mimi nina hamu 

sana na yule kijana.Hata miminina kiu 

naye . I have to do something as fast as I 

can ” akawaza madam Vicky na kuelekea 

chumbani kwake huku akiwa 

amechanganyikiwa.Picha ya Pauline na 

David wakiwa watupu ilimtesa sana 

ENDELEA 

 Ni sauti za wadudu na mbwa 

waliokuwa wakibweka ndizo zilizosikika nje ya jumba hili kubwa la kifahari.Katika 

chumba kikubwa kilichokuwa na 

mwangaza hafifu wa bluu ,watu wawili 

wamejilaza kitandani wakiwa 

wamekumbatiana kimahaba.Mwanamke 

aliyekuwa amejifunika shuka hadi kiunoni 

na sehemu ya juu ikiwa wazi alikuwa 

amekilaza kichwa chake katika kifua cha 

mwamaume .Walionekana kuwa katika 

mahaba mazito sana.Mwanamke yule 

mwembamba mrefu mwenye nywele fupi 

na umbo la kuvutia alikuwa akikisugua 

kifua cha mwanaume yule kwa mkono 

wake laini. 

 “ Vivian !!a kaita yule mwanaume 

 “ Yes Raymond.Unasemaje darling? 

Akasema Vivian ambaye alifahamika sana 

kwa jina la Flaviana alilopewa kutokana 

na kufanana sana na yule mwanamitindo 

maarufu wa kitanzania anayefanya 

shughuli zake za mtindo nchini Marekan 

Flaviana matata 

 “ Vivian Its been years now,toka 

tulipoanza kukaa pamoja.Maisha yetu 

yamekuwa mazuri na kila kitu chetu 

kinakwenda vizuri .Pamoja na hayo yote 

kuna jambo ambalo limekuwa likiniumiza 

sana akili yangu.Ni kuhusu sisi kuhalalisha 

maisha yetu kwa kufunga ndoa”akasema Raymond mfanyabiashara maarufu 

ambaye anajulikana sana kwa jina la 

Papaa Ray. 

 “ Ni wewe tu niliyekuwa nakusubiria 

Ray kwani mimi niko tayari hata dakika 

hii kufunga ndoa na wewe.” Akasema 

Vivian 

 “ Nalifahamu hilo Viviana na hata 

mimi sina kigugumizi chochote kile cha 

kufunga ndoa nawe.Wewe ndiye 

mwanamke ninayekupenda sana kupita 

wote .Lakini kuna ugumu katika jambo 

hili.” Akasema Raymond 

 “Kuna ugumu gani katika suala hili? 

kama wote tuna nia ya dhati ya kuishi 

pamoja basi hakuna ugumu wowote wa 

kulitekeleza jambo hili.” 

 “ Tatizo lipo my love ,tena kubwa 

tu.” 

“ Niambie kuna tatizo gani ? Mbona 

mimi sioni kama kuna tatizo lolote? 

“ Tatizo nikwamba mpaka hivi sasa 

wewe bado ni mke wa mtu” 

 “ Mke wa mtu?!!...Vivian akashangaa 

 “ Ndiyo wewe bado ni mke wa 

mtu.Kisheria bado unafahamika kwamba 

ni mke halali wa mumeo yule uliyefunga 

naye ndoa” akasema Ray.Vivian akakaa kimya kwa muda akatafakari kisha 

akasema 

 “ Lakini hata hivyo mimi na Robin 

tulikwisha tengana miaka mingi imepita 

.Nina hakika ndoa yetu imekwisha jifuta 

yenyewe.” 

 “ Hapana Vivi,ndoa huwa haifutiki 

namna hiyo.Ndoa hizi za 

kikristu,ikifungwa imefungwa na kuisha 

kwake ni mpaka mmoja wenu afariki 

dunia na ndiyo maana ikaitwa pingu za 

maisha” akasema Raymond 

 “ kwa maana hiyo basi hatutaweza 

kufunga ndoa mimi na wewe? 

 “ Hilo ndilo jambo linaloisumbua 

sana akili yangu.Ingekuwa ni kwa ndoa za 

dini ya kiislamu ungeweza kudai talaka 

yako ukabaki huru na tukafunga ndoa 

lakini kwa dini yetu ya kikristu suala la 

ndoa kwetu ni gumu sana.Ukisha ingia 

umeingia nakutoka si rahisi ” 

 “ sasa tutafanya nini Ray? Kama 

suala la kufunga ndoa kanisani linakuwa 

gumu kwa nini tusifunge ndoa ya 

serikalini? 

 “ Hata huko nako bado ugumu 

utakuwa ule ule tu.Wewe bado ni mke 

halali wa Robin na anaweza akatuchukulia 

hatua za kisheria.Sitaki jambo kama hili linitokee na kuharibu jina 

langu.Unafahamu nina jina kubwa na 

ninaheshimika.Ikitokea nikapata kashfa 

kama hiyo labda ya kupelekwa 

mahakamani kwasababau ya mke wa mtu 

basi itaniathiri sana kibiashara” akasema 

Ray 

 “ kwa hiyo unashauri nini? Akauliza 

Vivian 

 “ Kwa sasa tuendelee kuishi hivi hivi 

wakati tukitafuta ufumbuzi wa suala hili” 

akajibu Raymond 

 “ Raymond ufumbuzi pekee wa 

kutuweka huru ili tuweze kufunga ndoa na 

kuendelea na maisha yetu ni mimi 

kuachana na Robin kisheria.Ndoa yetu 

inabidi ibatilishwe.” 

 “ Ndoa yenu ilifungwa kanisani na 

lazima kanisa ndilo libatilishe ndoa hiyo 

vinginevyo utaendelea kuwa mke halaliwa 

Robin labda hadi hapo robin 

atakapokuwa amekufa.Ni lini atafariki 

Robin ili uwe huru? Hilo ni swali ambalo 

hatuna majibu yake.Vivian hebu 

tusiendelee kuumiza vichwa vyetu kwa 

suala hili .Kuna mambo mengi ya msingi 

tunayopaswa kuyajadili”  “hili n ila msingi sana my 

love.Tunajadili mustakabali mzima wa 

maisha yetu ya usoni.” Akasema Vivian 

 “ Hata kama tukijadili hadi asubuhi 

hatutaweza kupata muafaka wa jambo 

hili.Liko nje ya uwezo wetu” 

 “ kwa hiyo tutaendelea kuishi namna 

hii hadi lini Raymond? 

 “ Hadi hapo utakapokuwa huru” 

akasema Raymond na kugeuka upande 

wa pili akalala 

Vivian mwili ulimchemka.Ile furaha yote 

aliyokuwa nayo dakika chache zilipita 

ilitoweka.Alihisi joto 

 “ Ninajuta sana kukubali kuolewa na 

Robin.Nilijitia mkosi bila mwenyewe 

kufahamu.Sifahamu kitu gani 

kilinichanganya hadinikakubali yuke 

sakala anivishe pete ya 

ndoa.Ninamchukia sana yule mwanaume 

mbaya kama msukule.Ni kwa sababu yake 

ndiyo maana leo hii ninashindwa kufunga 

ndoa na Raymond mwanaume 

ninayempenda kwa moyo wangu 

wote.Ray yuko tayari kunioa lakini ndoa 

niliyofunga na yule ibilisi ndiyo inafanya 

jambo hili liwe gumu.Siwezi kukubali 

Robin awe ni kikwazo kwangu cha 

kufunga ndoa na Ray.lazima nifanye juu chini hadi nifunge ndoa na Ray.Nikizubaa 

Raymond atatafuta mwanamke mwingine 

na kufunga naye ndoa halafu 

nikaachwa.Siko tayari kuuacha utajiri huu 

wote na kurejea tena katika maisha yale 

ya kimasikini kama niliyokuwa nikiishi 

kwa Robin.” Akawaza Vivian.Akainuka 

akavaa gauni lake la kulalia na kutoka 

mle chumbani akaenda kukaa kibarazani 

.Akiwa pale ghorofani alilishuhudia jiji la 

Arusha namna linavyoonekana usiku 

 “Maneno aliyoyatamka Raymond 

yamenifanya niwe na wasiwasi sana 

.Inaonekana wazi kabisa kwamba kama 

nisipofanya juhudi binafsi za kuhakikisha 

kwamba mimi na yeye tunafunga ndoa 

ninaweza nikaachwa.Kukaa naye kwa 

miaka mingi si kigezo ninaweza 

nikaachwa.Hawa watu wenye pesa zao 

wanawindwa sana na wanawake kila siku 

kwa hiyo kwake kuchukua mwanamke 

mwingine na kufunga naye ndoa ni kitu 

kidogo tu.” Akawaza 

 “ Kuna mambo kadhaa ambayo 

natakiwa kuyafanya.Kwanza ni kutafuta 

ushauri wa kisheria kuhusiana na namna 

nitakavyoweza kuachana na Robin 

kisheria.Kesho nitakwenda kwa 

mwanasheria ili nifafanuliwe kama ninaweza kutenganishwa na Robin.Pili ni 

wakati sasa wa kuzaa mtoto na Ray.Ili 

kujiweka katika nafasi nzuri zaidi kwake 

lazima nizae naye mtoto.Nina hakika Ray 

atafurahi kupita kiasi endapo nitamzalia 

mtoto kwani kwa muda mrefu amekuwa 

akinipigia sana kelele kuhusu mtoto.Now 

it’s the time” Alipowaza tu kuhusu 

masuala ya mtoto,moyo wake ukastuka na 

mapigo ya moyo kubadilika na kuanza 

kwenda kasi.Picha ya mtoto mdogo 

mwenye tabasamu la kuvutia ikamjia 

 “ Sijui mwanangu Penina anaishi 

maisha gani.Kwa hivi sasa atakuwa 

amekwisha kuwa msichana mkubwa. 

Nilimuacha akiwa mtoto mdogo 

sana.Siwezi kuelezea maumivu 

ninayoyapata kila nimuwazapo 

mwanangu na jinsi nilivyoshindwa 

kutimiza majukumu yangu kwake kama 

mama.Kuna nyakati huwa najiuliza kama 

nilikuwa sahihi kuondoka na kumuacha 

mtoto mdogokama yule .Kitu kingine 

kinachoniumiza moyo wangu ni kwamba 

toka nimeondoka hadi leo hii sijawahi 

hata kwenda kumuona tena.Penina 

hajawahi kuniytia machoni.Inaniumiza 

sana lakini kwa upande mwingine siwezi 

kujilaumu sana kwani nisingefanya maamuziya kuondoka basi nisingeyapata 

maisha haya mazuri.Ninatamani kama 

amwanangu Penina angeishi maisha 

mazuri kama ninayoishi na akasoma shule 

nzuri .Sina hakika kama yule sakala 

anamtunza mwanangu namna 

inavyotakiwa.Sina hakika kama 

anampatia huduma zote muhimu.” 

Akawaza Vivy 

 “Ninatamani sana kama ningepata 

nafasi ya kumuona tena mwanangu.Toka 

nilipomuacha ana miaka mitatu sijawahi 

kufuatilia tena maendeleo yake.Sijawahi 

kumtia tena machoni.Its time now to get to 

know her.Kesho nitaanza uchunguzi 

kufahamu wanaishi vipi,mwanangu 

anasoma wapi,anahudumiwaje n.k” 

************************* 

Siku mpya imeanza,saa mbili kasoro za 

asubuhi,David na Pauline wako mezani 

wakipata kifungua akinywa.Hawakuwa na 

maongezi mengi na David alionekana 

kujitahidi kukwepa aina yoyote ya 

maongezi na Pauline.Baada ya kupata 

kifungua kinywa,wakaingia katika gari la 

David tayari kuelekea makazini  “ David mbona leo umekuwa mkimya 

sana? Bado unawaza kilichotokea jana? 

Akauliza Pauline wakiwa garini 

 “ Pauline jana tulifanya jambo la 

kizembe sana.Bado natafakari ingekuwaje 

iwapo ni mzee Zakaria ndiye angetukuta? 

Sijui leo nigekuwa mgeni wa nani” 

akasema David 

 “ Usiogope David.Tunajifunza kwa 

makosa.Ni kweli jana wote 

tulichanganyikiwa na hatukukumbuka 

hata kufunga mlango.Lakini 

hakijaharibika kitu.Ninashukuru sana 

kwa maneno uliyonitamkia jana 

.Umeiwasha taa ya matumaini katika 

maisha yangu.Hujui ni jinsi gani 

nilivyokuwa nakufikiria David’akasema 

Pauline.David hakujibu kitu akabaki 

akitabasamu 

 “David vipi kuhusu mchana wa leo 

una ratiba gani? Kama hauna kazi nyingi 

nitakuja kukuchukua tukapate chakula 

cha mchana” akasema Pauline na mara 

David akakumbuka kwamba Tamia 

alimuomba waonane mchana wa siku ile 

kunavmahala anataka amsindikize 

 “ kwa leo mchana nitakuwa na 

shughuli nyingi kidogo .Nitaagiza chakula katika mgahawa wa pale karibu” David 

akadanganya 

 “ Au unaniogopa David? Nimekuona 

toka asubuhi umekuwa kama 

unanikwepa” 

 “Hapana si hivyo Pauline.Siwezi 

kukuogopa hata kidogo .Kitu ambacho 

tunatakiwa kukifanya tukiwa pale 

nyumbani ni kujilinda tusije tukavuka 

mipaka na kuonyesha waziwazi hisia 

zetu.Ninaogopa mzee Zakaria akigundua 

kitu gani kinaendelea katiyetu ataumia 

sana.Ananichukulia kama mwanae kwa 

hiyo sitaki kumuudhi.” 

 “ Usiogope david.Hata kama akijua 

hatakuwa na la kusema kwa sababu mimi 

ndiye niliyekuchagua wewe.Mwanaume 

wa maisha yangu nitamtafuta mimi 

mwenyewe” akasema Pauline 

 “ Vipi kuhusu madam Vicky? 

Hataweza kumweleza baba?akauliza 

David 

 “ Hapana hawezi kufanya 

hivyo.Anaogopa kufanya hivyo kwani 

atakuwa ametangaza vita na mimi na hata 

fedha ulizopendekeza kwamba aongezewe 

katika mtaji wake hatapata.Ananiogopa 

sana na hawezi kusema chochote kuhusu sisi”akasema Pauline na kwa mbali David 

akatabasamu 

 “ Kumbe ,madam Vicky alikuwa 

sahihi kabisa.Kilichokuwa kinamsumbua 

Pauline ni wivu tu na si kitu kingine.Kwa 

sasa baada ya kumtamkia kwamba 

ninampenda amesahau kabisa kuhusiana 

na Vicky na akili yake yote iko 

kwangu.Kwa sasa kila kitu cha madam 

Vicky kitakwendavizuri.” Akawaza David 

 Walifika hadi ofisini kwa David na 

kabla hajashuka Pauline akamvuta kwake 

na kumpa busu zito sana. 

 “ I love you David”akasema.David 

akamtazama huku akitabasamu na kisha 

akasema 

 “ I love you Pauline “ akashuka na 

kuelekea ofisini kwake.Pauline aliendelea 

kumkodolea macho hadi alipohakikisha 

amepotelea kabisa ndani ya jengo lile 

kubwa ndipo alipowasha gari na 

kuondoka 

 “ Dah! Sijui ni kitu gani kimenitokea 

na kunifanya nimpende David kiasi 

hiki.Ninahisi kuchanganyikiwa zaidi hasa 

baada ya kunitamkia kwamba hata naye 

ananipenda .Nitamlinda David dhidi ya 

yeyote yule anayetaka kumuiba.Huyu ni 

mwanaume wangu na atakuwa wangu daima.” Akawaza Pauline akiwa garini 

akielekea dukani kwake. 

 “Nimepata wazo.Tuna ile nyumba iko 

kule Kisongo imekamilika na hakuna mtu 

anayekaa.Ni wakati sasa wa kuwa huru na 

kuondoka pale numbani.Nahitaji kuwa 

huru na David.Pale nyumbani mazingira 

yananibana sana.Ngoja baadae 

nitakwenda kuitembelea nyumba ile ili 

nione kama inaweza kunifaa.Nina hakika 

nikimuomba baba lazima atanikubalia 

nikaishi pale.Kitendo cha kukatishwa 

starehe yangu jana kimeniumiza 

mno.Nimeteseka sana usiku.Sitaki jambo 

kama lile litokee tenandiyo maana 

ninataka niwe huru” akawaza Pauline 

 Kwa upande wake David aliingia 

ofisini kwake lakini alishindwa kufanya 

kazi,kichwa chake kilikuwa na mawazo 

mengi sana na kubwa ni kuhusiana na 

kilichotokea jana usiku.Alikumbuka kila 

kilichotokea na kutabasamu 

 “ Nilizidiwa sana jana na nikasahau 

hata kufunga mlango.Ni muda mrefu sana 

sikuwa nimekutana na mwanamke ndiyo 

maana Pauline aliponigusa tu maeneo 

nyeti nilishindwa kujizuia.Hata Pauline 

naye anaonekana alikuwa akihitaji sana 

kitendo kile na ndiyo maana alijileta mwenyewe chumbani kwangu.Madam 

Vicky alikuwa sahihi kabisa Pauline 

ananipenda sana na ndiyo maana usiku 

ule alishindwa kuvumilia ikamlazimu 

kunifuata chumbani.Inaniuma sana 

kumdanganya kwamba ninampenda 

wakati sina hisia zozote kwake.Hisia 

zangu ziko kwaTamia na si 

Pauline.Nitaendelea kumdanganya hadi 

lini? Sipati picha siku akigundua kwamba 

ninamdanganya na sina hisia za kweli 

kwake.Ataumia sana.Sikuwa nimelitaka 

jambo kama hili litokee lakini yote hii ni 

kwa sabab u ya madam Vicky.Yule ni 

mwanamke hatari sana .Laiti angejua 

kilichomo moyoni mwangu wala 

asingekuwa na ukaribu na mimi.” 

Akawaza David halafu akaendelea na kazi 

zake 

 Saa nne na dakika nane asubuhi 

mlango wa ofisi yake ukafunguliwa bila 

kubishwa hodi akaingia Vicky 

madhahabu.Alikuwa amependeza vilivyo 

kama kawaida yake akiwa anang’aa kwa 

vito vya dahabu 

 “ madam Vicky !! akasema David 

kwa mstuko kidogo.Hakuwa 

amemtegemea Vicky mida ile  “ Mbona umestuka David 

?Hujafurahia ujio wangu? 

 “ hapana si hivyo madam 

Vicky,umenistua tu kwa namna 

ulivyoingia” 

 “ Usiogope David hii ni ofisi yetu na 

tunaweza kuingia muda wowote bila hata 

kubisha hodi.Tuachane na 

hayo.Unaendeleaje? 

 “ Ninaendelea vizuri madam ” 

 “ Samahani kwa kukukatishia 

starehe zako jana.Najua ulichukia sana 

lakini sikuwa na namna nyingine ya 

kufanya zaidi ya kumuondoa Pauline ili 

msifanye kile kitendo.David kwa kweli 

nilichukizwa na ujinga mlioufanya 

jana.Siwazuii kufanya mambo yenu lakini 

si mle ndani wakati mzee Zakaria yupo.Ni 

ukosefu wa heshima na mbaya zaidi mzee 

akigundua kwamba ninyi mna mahusiano 

inaweza ikamletea matatizo makubwa 

kiafya.Kwa hali yake hatakiwi kupata 

mstuko au hasira.Pauline alikuwa akitoa 

ukelele mkubwa kasi kwamba kama 

Zakaria asingekuwa amelala angeweza 

kusikia mlichokuwa mnakifanya.Mimi 

nilikuwa ghorofani nikasikia na ndiyo 

maana nikashuka kuja kuona kilichokuwa 

kinaendelea.Siku nyingine mkitaka kufanya mambo yale tafuteni mahala 

kwingine nje na nyumbani”akasema 

Vicky.Davd hakujibu kitu 

 “ Kwa sasa naona mambo 

yanakwenda vizuri.Kila kitu chetu 

kitakwenda kama 

tulivyokipanga.Nina hakika Pauline 

hataweza kutufuatilia tena.Hata 

hivyo nitapunguza ukaribu na wewe 

ili asiweze kutia shaka yoyote kama 

kuna kitu kinaendelea kati yetu” 

akasema Vicky.Bado David 

aliendelea kuwa kimya 

 “ David una nafasi japo kidogo? 

Kuna mahala nataka twende kuna kitu 

nataka nikakuonyeshe” akasema Vicky 

 “ Kwa leo sina hakika kama 

nitakuwa na nafasiya kutoka.Nina kazi 

nyingi sana” 

 “ David please ni muhimu 

sana.Hatutachukua muda mrefu tutarudi.” 

Akasema Vicky huku akiifunika kompyuta 

ndogo ya David ambaye alijikuta hana 

namna nyingine zaidi ya kukubaliana na 

Vicky 

 “ kwa namna hii kazi zitafanyika 

kweli? Kila wakati ni mimi tu 

kutoka.Mchanawa leo nina miadi tena ya 

kutoka na Tamia Dah.! Sijui nifanye nini kuwakwepa watu hawa”akawaza David 

wakati akingiia katika Mercedece benz ya 

madam Vicky 

 “ How do you feel about her? 

Akauliza Vicky madhahabu wakiwa garini 

 “ Madam Vicky Pauline ni kweli 

ananipenda lakini kinachoniumiza ni 

kwamba mimi sina hisia zozote 

kwake.Ninamdanganya bure mtoto wa 

watu na siku akigundua ataumia sana’ 

 “ Usiwe muoga David.Nani 

alikwambia kwamba kuna mapenzi ya 

kweli siku hizi? Kila mtu anayeingia katika 

mahusiano siku h izi anaingia kwa ajili ya 

kutafuta maslahi Fulani.Kwa Pauline 

wewe hautafuti penzi bali unatafuta 

maisha y ako kwa hiyo hii ni vita ya 

kutafuta hivyo usiwe na uchungu wowote 

ule.” Akasema Vicky madhahabu 

 “ Vipi kuhusu wewe? Uliolewa na 

mzee Zakaria kwa kuwa ulikuwa 

unampenda au ni kama hivyo 

unavyosema kutafuta maslahi? 

 “ David ,wakati mwingine si kila kitu 

lazima uambiwe.Hivi wewe huwezi tu 

kuona kwamba mimi na yule mzee 

hatuendeni kabisa? Mimi katu siwezi 

kuanguka penzini na mzee kama 

yule.Damu yangu bado moto nahitaji rijali mwenye nguvu za samba wa kuniendesha 

.Ninachokitafuta mimi kwa yule m zee ni 

maisha mazuri tu.Muda wowote anaweza 

akafariki na nitarithi utajiri mkubwa 

sana.Mzee Zakaria ana utajiri mkubwa 

tofauti na unavyofikiri.Kuna mambo 

mengi ambayo haujayafahamu 

bado”akasema Vicky 

 “ Dunia imejaa ulaghai mkubwa sana 

siku hizi.Si wanaume si wanawake wote 

wamekuwa walaghai.Nadra sana kumpata 

mtu anayekupenda kwa dhati siku 

hizi.Pauline ananipenda na mimi 

simpendi lakini ninamdanganya kwamba 

ninampenda,mzee Zakaria anampenda 

Madam Vicky lakini mwenzake hana 

mpango naye na anatamani sana mzee 

yule afe hata leo.Nani basi ni mkweli kati 

hii dunia? Akawaza David wakiwa garini 

wakiendelea na safari. Vicky 

hakumfahamisha walikuwa wanaelekea 

wapi. 

*****************Vivian aliamka akiwa hana furaha 

hata chembe.Uso wake ulionyesha wazi 

kuna jambo lililokuwa linamsumbua akili 

yake.Usiku ulikuwamrefu sana kwake.Alijaribu k uwaza ni namna gani 

atakavyoweza kufanikisha masuala ya 

ndoa yake na Papaa Ray lakini hakupata 

jibu.Ray alikuwa tayari kufunga naye ndoa 

lakini kigezo kikubwa kilikuwa kwamba 

bado alikuwa akiheshabika ni mke wa 

mtu.Kisheria bado alikuwa ni mke wa 

Robin 

 Alifanya shughuli zake za asubuhi 

haraka haraka na alipomaliza akaingia 

katika gari lake akaelekea katika ofisi ya 

rafiki yake mmoja ambaye ni 

mwanasheria.Alikwisha mtaarifu toka 

asubuhi kwamba atakwenda kumuona 

kwa ajili ya tatizo analohitaji amsaidie 

hivyo alipofika alimkuta tayari Victor 

anamsubiri 

 “ karibu sana Vivian.mambo yako 

yanakwendaje ? 

 “akasema Victor akimkaribisha 

Vivian” 

 “ mambo yangu mazuri Victor.Si 

unaona mwenyewe tu,si lazima uambiwe” 

 “ Nimeona Vivian.karibu sana.” 

 “ Ahsante sana Victor.Samahani 

kama nimekuchelewesha kufanya 

shughuli zako nyingine” 

 “Bila samahani Vivi.Wewe ni mtu 

wangu wa karibu kwa hiyo usihofu kitu.” Akasema Victor.Vivian akakaa kimya 

kidogo halafu akasema 

 “ Victor nimekuja nahitaji msaada au 

ushauri wako wa kisheria” 

 ‘NdiyoVivian nakusikiliza” 

 “ Ninataka kufunga ndoa na Ray” 

 “ Wow ! hizo ni habari njema sana 

Vivian..Umeniletea kadi ya mchango? 

Nitachanga mchango mkubwa sana kwako 

Vivian”akasemaVictor 

 “ Victor bado hatujafikia hatua hiyo 

ya kuanza kuwatangazia watu lakini 

nimekwambia wewe kwa sababu ni mtu 

wangu wa karibu.Pamoja na nia yetu hiyo , 

kuna tatizo dogo ambalo linaweza 

likakwamisha nia hii njema.” 

 “tatizo gani Vivian? aKauliza 

Victor.Vivivan akavuta pumzi ndefu na 

kusema 

 “ Mimi bado ni mke wa mtu” 

akasema Vivian.Vivtor akamuangalia bila 

kumsemesha chochote.Vivi akaendelea 

 “ Kabla ya kuanza kuishi na 

Ray,nilikuwa nimeolewa na mtu mmoja 

anaitwa Robin ambaye nilizaa naye mtoto 

mmoja.Tatizo kubwa linakuja kwamba 

siwezi kufunga ndoa nyingine kabla ya ile 

niliyofunga awali 

kubatilishwa.Nimemshawishi Raytukafunge hata ndoa ya serikalini lakini 

amekataa kata kata anachotaka yeye ni 

kufunga ndoa halali inayofahamika 

kiimani pia.Nimeshindwa nifanye nini 

ndiyo maana nimeona nije kwako ili 

unisaidie msaada wa kisheria ni namna 

gani ninaweza kufanya ili niibatilishe 

ndoa yangu.Ninyi mnazifahamu sheria 

kwa hiyo naomb unisadie ndugu 

yangu.Nitakulipa kiasi chochote cha fedha 

utakachohitaji .”akasema Vivian.Victor 

akaegemea kiti chake huku akiuma 

kalamu na kufikiri kwa muda halafu 

akasema 

 “ Vivian hebu kwanza nieleze bila 

kunificha nini kilisababisha wewe na 

mumeo wa ndoa mkatengana? Naomba 

unieleze ukweli usinifiche ili nijue ni 

namna gani nitakusaidia” 

 “ Victor kwa kuwa ninatafuta 

msaada nitakueleza 

ukweli.Kilichotutenganisha mimi na Robin 

ni kwamba niliamua kuondoka kwa hiari 

yangu kutokana na maisha ya dhiki 

tuliyokuwa tukiishi.Maisha yetu yalikuwa 

magumu sana na wakatihuo huo 

nikafanikiwa kupendwa na Ray kwa hiyo 

nikaondoka mwenyewe.”  “ Kwa hiyo mumeo hakukufukuza 

wala hamkugombana?” 

 “ Kusema ukweli Robin 

hakunifukuza wala hatukugombana ila ni 

mimi tu mwenyewe ndiye niliyetaka 

kuondoka “ 

 “ Wakati unaondoka mwanenu 

alikuwa na umri gani? 

 “ alikuwa na miaka mitatu” 

Victor akafikiri kwa muda kisha akasema 

 “ Vivian ninatamani sana kukusaidia 

lakini suala lako si rahisi kama 

unavyolichukulia.Kwa mujibu wa imani 

ya dini yenu ni kwamba ndoa 

ikishafungwa duniani hakuna wa 

kuitenganisha.Ninavyofahamu mimi upo 

mchakato katika dini yenu wa kuweza 

kuibatilisha ndoa lakini unachukua muda 

mrefu sana na lazima kuwe na sababu 

nzito na ya msingi ya kuweza kuibatilisha 

ndoa hiyo.Sababu ya wewe kutaka 

kuibatilisha ndoa hiyo ni nyepesi mno na 

haina mashiko.Ulimkimbia mwanamume 

uliyefunga naye ndoa kwa kigezo tu cha 

umasikini wake.Hii si sababu ya kuweza 

kumshawishi mtu yeyote yule hata kama 

sheria zingekuwa rahisi kiasi gani 

,aibatilishe ndoa yako.Kwa maneno rahisi 

hata ukifungua kesi mahakamani ya kutaka kupewa talaka mahakama 

haitakusaida kwa sababu utaonekana 

kama mwanamke asiyefaa katika jamii 

kwani uliyakimbia majukumu yako kama 

mama.Ulimuacha mtoto wa miaka mitatu 

ambaye alihitaji sana malezi ya mama kwa 

sababu tu mwanaume uliyezaa naye hana 

uwezo kifedha .Ulitegemea nani ambaye 

angekulelea mwanao? Akasema Victor 

aliyeonekana kuchukizwa sana na kitendo 

alichokifanya Vivian 

 “ Kwa hiyo Victor utanisiadia ama 

vipi? Kwa sababu naona umeanza tena 

kunikatisha tamaa mapema.” 

 “ Vivian wewe ni rafikiyangu lakini 

nasikitika kwamba sintaweza kukusidia 

kwa kitendo ulichokifanya.Mimi ni 

mwanaume na imeniuma sana kumkimbia 

mwanaume mwenzangu kwa kigezo tu cha 

kutokuwa na fedha.Sintaweza kukusaidia 

Vivi na ninakuweka wazi kwamba hakuna 

mahala unakoweza ukapata msaada wa 

kisheria wala hakuna mahakama 

itakayoweza kusikiliza shauri la aina hii.” 

 “ kwa hiyo hutaki kunisaidia Victor? 

Akauliza Vivian 

 “ Si mimi tu bali hakuna 

mwanasheria ambaye utampelekea suala 

hili akakubali kukusaidia hata kama utamlipa shilingi ngapi.Ningejua kama 

jambo lenyewe ni hili wala 

nisingesumbuka kupoteza muda wangu 

mwingi ambao ningeutumia kufanya 

shughuli nyingine za msingi”akasema 

Victor huku akiinuka na kuvaa koti lake 

akachukua mkoba wake 

 “ Vivian nadhani tumemaliza 

unaweza ukaondoka,ninataka kuwahi 

mahakamani” akasema Victor .Vivian 

akainuka akiwa amefura kwa hasira na 

bila hata kuagana na Victor akapanda gari 

lake na kuondoka . 

 “ Nilitegemea Victor angenipa 

msaada mzuri kisheria kumbe naye ni 

mshenzi tu.hana lolote punguani 

yule.Asidhani nitakosa 

msaada.wanasheria wako wengi sana na 

ni hela tu inaongea”akawazaVivian na 

moja kwamoja akaelekea kwa rafikiyake 

mkubwa Caren akamueleza kila kitu . 

“dah Pole sana Vivi.”akasema Caren 

 “ Ahsante sana Caren’ 

 “ Kwa hiyo umefikiria kuchukua 

hatua gani tena? 

 “ Kwa sasa nimechanganyikiwa 

lakini nahitaji kitu kimoja toka kwako” 

 “ Kitu gani Vivi?’  “ Wewe unakaa karibu na nyumbani 

kwa Robin.Nataka unisaidie kufanya 

uchunguzi mwanangu anaishi maisha 

gani? Je Robin anamlea vizuri? Je 

Anasoma? nataka uchunguze maisha yake 

yote kwa ujumla.”akasema Vivian.Caren 

akatabasamu 

 “Vivi sina hata haja yakufanya 

uchunguzi shoga yangu.Ni kwamba 

sikutaka tu kukupa habari kuhusiana na 

maisha ya Robin na mwanao penina 

.”akasema caren 

 “ Kuna habarigani Caren? Akauliza 

Vivian 

 “Ina maanaVivi hujawahi hata 

kugongana na Robin kwa siku za karibuni? 

 “ Hapana sijaonana naye .Mimi na 

yeye tunaishi maisha tofauti sana .Kwa 

maisha yangu ya sasa ni vigumu sana 

kuonana nawatu wa aina ile ya 

Elvis.Ninachohitaji mimi ni kujua kuhusu 

mwanangu tu ili kama ikiwezekana basi 

nifanye jitihada za kumchukua niishi 

naye” akasema Vivian 

 “Basi umejidanganya shoga 

yangu.Robin siku hizi mambo yake mazuri 

sana.Amebadilika.Ile nyumba yenu ya 

zamani imebomolewa na kujengwa bonge 

la jumba .Penina amekuwa binti mkubwa na mrembo sana.Anasoma shule moja 

nzuri sana ya kimataifa.Maisha yao ni 

mazuri sana siku hizi.Kitu kizuri ni 

kwamba Robin hakuwahi kuoa tena 

mwanamke mwingine.Amemlea mwanae 

Penina peke yake na kila mtu anamsifu 

kwa namna alivyomlea mwanae” 

 Maneno yale ya Caren yakamuumiza 

sana Vivian. 

 “ Unafahamu shule anakosoma 

Penina?akauliza Vivi 

 “ Ndiyo ninaifahamu” 

 “ Unaweza ukanipeleka?Nataka 

walau nimuone” 

Caren alikubali kumpeleka Vivian katika 

shule ambayo Penina anasoma. Walifika 

shuleni anakosoma Penina,waka 

jitambulisha kama wageni waliokuja 

kumtembelea.Kwa kuwa ulikuwa muda 

wa mapumziko Penina alitafutwa na 

kuelezwa kwamba kuna wageni wake 

.Alielekea moja kwa moja mahala 

walikokuwa wageni wake.Akakutana na 

akina mama wawili.Akawasalimu kwa 

heshima.Vivian mwili ulimsisimka sana 

baada ya kumuona binti yake namna 

alivyokuwa mkubwa na 

mrembo.Alitamani amkumbatie lakini 

alishindwa kwani Penina hakuonekana kumtambua kabisa.Caren ndiye aliyekuwa 

muongeaji kwani Vivian alishindwa kabisa 

kusema chochote.Moyo uliumia sana. 

 “ Penina nadhani sisi hapa 

hautufahamu na haujawahi kuonana nasi 

.Mimi ninaitwa caren na huyu hapa 

anaitwa Vivian ni mama yako mzazi 

.Tumekuja hapa kukuangalia 

unaendeleaje “ akasema Caren 

 Penina akatabasamuna kusema 

 “ Nadhani mmekosea mtu 

mnamtafuta.Mimi sina mama.Mama yangu 

alinikimbia angali niko mdogo sana na 

sijui yuko wapi.Mtafuteni mtu 

mnayemtafuta na si mimi.” Akasema 

Penina na kuondoka.Vivian akahisi 

kuishiwa nguvu akashindwa kuinuka. 

Ilimlazimu Caeena amshike mkono Vivian 

na kumuongoza hadi katika gari.Vivian 

ahkuwa na hata nguvu za kuendesha gari 

 “ Vivian jikaze shoga yangu.Penina 

hajakuona mud amrefu na ndiyo sababu 

akatamka m,aneno yale .Kitu cha kufanya 

ni kumpa muda penina .Mtoto hajakuona 

kwa miaka mingi kwa hiyo si rahishata 

kidogo leo hii hii kukuchangamkia 

kamamama yake.Mpe muda ila usikate 

tama.Jitahidi kwa kila uwezavyo uwe 

karibu naye.Anza taratibu kujenga mazoea ya kumtembela kilamara na kumjulia 

hali,zikumbke siku zakemuhimu kama 

siku yake ya kuzaliwa n.k.Kwa staili hii 

utajikuta ukifanikiwa kumuweka karibu 

lakini nakuomya jambo hilisi la kuendea 

haraka.” Akasema Caren.Flavianaalikuwa 

ameinamia usukani akiwa na mawazo 

mengi sana.Akainua kichwa na kusema 

 “ Caren,moyo wangu uunaumia sana 

kwa kitendo nilichokifanya.Ninajutia sana 

kitendo kile cha kuondoka na kumtelekza 

mwanangu penina.Ningejua kama 

sikumojaningeumia namna hii 

ningeondoka naye.Maneno alioyoyatamka 

ni mazito na yamenichomasana” akasema 

Vivi nakushindwa kujizuia kuangusha 

machozi 

 “ Vivi nyamaza usilie shoga 

yangu.Hili nisuala ambalo unapaswa 

kulipamuda kama nilivyokwambia 

awali.Mpe muda mwanaopenina.Nina 

imani siku moja atalegezamsiomamo 

wake .” akasemacarenhuku akimuangalia 

shog yake aliyekuwa akifuta machozi 

 “ mmmh mwanamke hana haya huyu 

hata kidogo.yaani alidiriki kukimbia na 

kumuacha mtoto wakebado mdogo halafu 

leo hiibaada ya mwanae kuwa mkubwa 

anadiriki kutoa machozi.Mjinga sana huyu Vivian.Hata ningekuwa ni 

mimiPeninaningemtamkia kama 

alivyomtamkia.” Akawaza caren.Walikaa 

ndani ya gari kwa dakika kama kumi na 

tano hiiv haalfu Vivianakajikaza na 

kuendesha gariwakaondoka.Baadaya 

kumshuisha carenkatika shghuli zake 

hakutaka tena kwenda sehemu yoyote ile 

akarejea nyumbani kwake.Kichwa chake 

kilijawa na picha mpoja tu ya mwanae 

penina. 

 “penina amekuwa msichana 

mkubwa na mrembo sana.Sijui nitafanya 

kitu gani ili niweze kujiweka karibu 

naye.Najua kwa sasa Robinatakuwa 

amemlisha maneno mengi sana kuhusiana 

na mimi na ndiyo maana ananichukia 

nahataki hata kuniona.” Akawaza Vivian 

akiwa amejilaza kitandani chumbani 

kwake 

 “ Katia maisha yangusijawahi 

kuumia kama nilivyoumia leo.maneno 

yale ya Penina yamenichoma sana na 

kuniharibia siku.Katikamacho yake 

anaonekana hatakikabisa hata 

kumfahamu mamayake mzazi na 

alionyesha hasira zake kwa mama yake 

wazi wazi.Ninajuta kwa kitendo 

nilichokifanya cha kuondoka na kumuacha Penina peke yake.Kwa mara ya 

kwanza nakijutiakitendo kile cha 

kumuacha mwanangu.Nilikimbia ndoa 

yangu iliyokuwa umegubikwa na 

umasikini mkubw ana kufuata umaisha 

mazuri na utajir lakinikwa sasa naweza 

kukirikwamba I wa wrong.Lakini sipaswi 

kujiulaumu sana kwani sikuwa na 

namnanyingine ya kufanya kwa wakati 

ule.Ninachotakiw akufanya kwa sasani 

kuangalia kuhus maisha yangu ya usoni..” 

akaendelea kuwaza Vivian 

 “ Mungu amembariki Robin na kwa 

sasa maisha yake ni mazuritofauti na 

nilivyotegemea.Pamojana maisha yake 

kuwa mazuri lakin sina mpango wa kurudi 

kwake tena kwa sababu najua mpkaasasa 

hivi atakuwa tayari yuko katika 

mahusianina wanawake wenginne na 

hana mpango na mimi tena na wala mimi 

sina mpangonaye.Ninachkitafuta toka 

kwake ni kitukimoja tu kikubwa 

.Kubatilisha ndoa yetu ili niweze 

kuolewana Ray.Nitamzalia ray mtoto 

mwingine na tutamlea na nitakuwa na 

furaha.kwa sasa ngoja niwaache akina 

Robin nisiwasumbue.Wanaishai kwa 

furaha na maisha yao.hawanihitaji tena katika katika maisha yao.” Akawaza 

Vivian. 




Vicky madhahabu na David 

walikuwa ndani ya gari la Vicky 

wakielekea nje ya jiji.Safgariyao ilikuwa 

ya kimya kimya.Nimuziki tu ndioulikuwa 

uansikka. 

 “ Leomi lazima David anikate kiu 

yangu.,Siwezi kukubali kumuona Pauline 

akijivinjari naye ,lazima sote tumtumie 

ingawa kilammoja wka wakati na 

mazinira yake.David hana kauli kwangu 

na kitchochote nitkachimuamuru kukifaya 

atakifanya.Leonii leo” akawaza Vicky 

madhahabu hukumwili wote ukimsisimka 

kwa hisia kali akiwaza namna 

atakvyojivinjarina David. 

 Waklifgika hadi Usa river mahala 

ambako Vicky madhahabualkikuw 

aamejenga jumba lake kubwa la 

kifahari.David alishangaa sanakuliona 

jumba lile kubwa.Vicky akamtemeeba 

shemeu zote za jumbalile halafu chumba 

chamwisho kilikuwa ni chumba cha 

kulalacjha Vicky.LKilikuw ani chumba 

kikubwa chenye uzuri wa kipekee kabisa.  “ David hiki ni chumba change cha 

kulala.” 

 “wow ni chumba kizuri sana. 

Unastahili 

pongezimadamVicky.Umejitahidi sana” 

akasema David hukuakitabsamu 

 “ Ahsante sana David kwa pongezi 

zako.Hata wewe utawez kujenga jumba 

kubwa kama hili pengina hata kuzidi hili 

kama ukitumia vizuri nafasi 

yako.Ninarudia tena kukushauri Dafid 

wakati nii huu.Changamka sasa na 

uyajenge maisha yako.Mimi hata ikitokea 

mzee zakaria amefariki leo nitabaki na 

maisha yangu mazuri.Nina jumba langu na 

na biashara nyingine nyingi.”akasema 

Vicky.David akatabanu an kusema 

 “ Ahsante sana kwa 

ushaurimadamVicky nitaufanyia kazi 

ushauri wako” 

 “ halafu David kwa nini kila wakati 

unaniita tu madam Vicky? Just call me 

Vicky inatosha sana .Kuna watu 

wanaopaswa kuniita hivyo lakinisi wewe” 

 “ kwani kuna tatizo gani nikuita 

hivyo madam? Nimeskwisha zoea sana 

kukuita hivyo,nikikuita jina lako tu ulimi 

unakuwa mzito saa kutamka.Niruhusu 

nikuite madamVicky,.Unastahiliheshima hiyo” akasema David.Vicky akatabsamu na 

kumsogelea 

 “ David hupaswi kuniita 

hivyo.Kuanzia leo utanita madamVicky 

endapo tuko nyumbani au sehemu zenye 

watu wengi lakini ka sehemu kamahi 

ambako tuko peke yertu hutakiwi kuniita 

madam.” Akasema Vicky na kumshika 

mkono David wakaketi sofani. 

 “ David ! akasema Vicky 

 “ nam madam..ouh sorry Vicky” 

akasma David 

 “ Usijali utazoea tu.Kuna kitu nataka 

kukuuliza” 

 “ Uliza tu Vicky” 

 “ Mara yako ya mwisho kufanya 

mapenzi ilikuwa lini? 

David akastushwa kidogo kwa swali lile 

.Hakutegemea kama angeulizwa swali 

kama lile na Vicky. 

 “ Mbvona unanishangaa Dafid? 

Nimekustua kwa swali kamahilo? Akauliza 

Vicky 

 “ Nimestuka kidugo sikuwa 

nimetegemea swali kamahilo toka kwako” 

 “ Ni swali la kawaida tu usiogope 

David.” 

Kimyakifupi kikapita David 

akitafakarinamna ya kujibu  “ Mbona hunijibu David.? Akauliza 

Vicky 

 “ Ni swali gumu kidogo lakini kwa 

kukujibu ni kwamba ni mua mrefu 

sijakutana na mwanamke kimwili.Toka 

nilipopata matatizo na kufungwa gerezani 

sijakutanana mwanamke yeyote yule” 

akasema Dafid.Vicky madhahabu 

akamtazama David usoni kwa machoya 

kurembua halafu akasema 

 “ samahani sana kwa kukukatisha 

jana ulikuwa na Pauline.Sikujua kumbe 

ulikuwa na hamu namna hiyo” akasema 

Madma Vicky na kumfanya David 

atabasamu 

 “ Usijali Vicky ni mambiya kawada 

tu.hata hivyo hatukupaswa kufanya vile 

ndaniya nyumba yam zee Zakaria.” 

 Vicky madhahabu akamshika mkono 

David na kuugusisha katika paja lake 

laini.Davdi mapigoya moyo yakamuenda 

kasi kwani alikifahamu kilichokuwa 

kinataka kuendelea. 

 “ David,wewe ni kijana wangu,ni 

mshirika wangu mkubwa.mamboyangu 

mengi ambayo hakuna yeyote anayeyajua 

wewe nimekwambia.Siri yangu ni yako 

pia.” akasemaVicky halafu akanyamaza 

kidogo na kuendelea kuuminya mkono wa David na kumfanya damu izidi 

kumchemka 

 “ David najua una ogopasana kwa sisi 

kuw mahala hapa peke yetu lakini 

nakuomba usiogope kitu.Hakuna yeyeote 

anayejua kama tuko hapa .Nimekuleta 

hapa kwa dhumuni kubwa moja 

tu.Kukueleza kuhusiana na jambokubwa.” 

 “ Jambo gani hilo Vicky? Akauliza 

Daid kwa sautiya kukwama kwama . 

Vicky ambaye alikuwa ameushika mkono 

wa David na kuugusisha katika paja lake 

akasema kwa sauti ndogo huku akirembua 

machoyake akasema 

 “ David usistuke kwa 

nitakachokuambia kwani wewe ni mtu 

zima sasa na hakuna usichokijua.David 

japokuwa nimeolewa na mzee Zakaria 

lakini naomba nikir kwamba 

tokanilipokuona moyo wangu umekuwa 

ukihaha kila siku kwa 

ajiliyako.Umeichanganya akiliyangu kwa 

ghafla sana .nakupenda Daid nandiyo 

maana kuna nyakatininashindwa hata 

kvumilia ninajikuta nimekufuata hadi 

chumbani kwako.Kila 

wakatininatamaniniwe karibu yako.David 

naomba ufahamu kwamba hata jana 

nilipokukutana Pauline nliingiwa na wivu mkubwa sana nilipowakuta mkitaka 

kufanya mapenzi.Niliumia sana na 

sikuweza hata kupata usingizi.Nikwelini 

miminidiye nilyekushaiuri kwamba 

umtongoze poauline kwa ajilya 

maslahiyetulakini haliimebadilika tena na 

ninajisikia wivu sna.Sipendi kukuona 

ukiwa napauline lakjini sina namna ya 

kufanya.”akasema Vicky 

 “ Vicky ..!” David akauvuta mkono 

wake ambao Vicky alikuwa ameushikana 

kuuweka katika paja lake laini lilikuwa 

limeachwa wazi kufuatia nguoa fupi 

aliyokuw aameivaa kupanda juu . 

 “ Usitamke chochote David 

subirinimalize ninachotaka kukisema” 

akasema Vicky 

 “ david ninachotka ku kukweleza 

nikwamba nimeshindwa kuvumilia 

naninmeamua mahusiano yetu yaende 

mbali zaidi ya tulivyo sasa.Natakatuwe 

wapenzi wa siri.Utaendelea kuwa katika 

mahusianona Pauine lakini wakati huo 

huo mimina wewe tutakuwa tunakutana 

kwa siri.David ni wewe pekee ambaye 

ninaamini unaweza kuikata kiu yangu.Hii 

ndoiyosbabu nimekuleta huku leo ili 

niweze kujivinjari nawe.Mwili wanguwote 

unawakamoto hivi sasa kwa hamu niliyonayo.Nna imanihata wewe pia 

utakuwa na hamu sana na mimi.tafadhali 

Dacvid naomba unisadie kwa hilo” 

akasemaVicky madhahabu. 

 David alichanganyikiwa na hakujua 

ajibu nini.Hakuamini kama maneno yale 

yalitoka katika kinywa cha mwanamke 

yule anayemuheshimu sana. 

 “ madamVicky mambo gani tena 

hayo unaniambia? Wewew bimke wa mzee 

Zakaria ambayeninamchukulia kama baba 

yangu,ukimabia kwamba unataka 

kutembea nitakuwa ninatembeana mke 

wa baba yangukitu ambachgo 

hakiwezekani kabisa.Naomba tafadhali 

tusiofanyehivyo” akasema David 

 “ David usiogope mpenzi 

wangu,hakuna chochote 

kitakachoharibika.Mimina wewe 

tutakuwa tunakutaa kwa sirikubwa na 

hakuna yeyote atakayejua” 

 “ hata hvyo madma Vicky 

hilonijambo la kukosema heshma sana 

mze zakaria.Ananilea kama mwanae na 

siwezikumkosea heshima kiasi hiki” 

 “ Kama ni heshima kwa ninibasi 

unatembea na binti yake? 

Unadhaniakigundua kwamba unatembea 

na mwanae atakuamini tena? Ni wazi atakutimua .David naomba unisaidie 

mwenzio ninahalimbaya sana” akasema 

Vicky madhabau na kuvua fulana 

aliyokuwa ameivaa.David Nywele 

zikamsimama 

 “David usiogope hakuna yeyote 

atakayejua kamatuko hapa na 

tunajivinjari.” Akasema Vicky 

 “ Dah ! Hivi maisha yangu 

mimiyakoje? Mbona kila 

wakatininatawaliwa na majaribu 

makubwa? Hili nalo ni jaribu lingine 

kubwa .Huyu mwanamkeni shetani 

mkubwa kwa nini amfanyie hivi mume 

wake? Hapana siwezi kumfanyia hivi mzee 

Zakaria.Yule ni sawa na baba 

yangu.Ananipendana anaitunza kama 

mwanae” akawaza David na mara Vikcy 

akamfuata akamshika kwa nguvu akaanza 

kumfungua vifungo vya shati 

 “Mbona unachelewa snaa 

David.Nimekwambia mwenzakonina hali 

mbaya sana” akasema Vicky .David 

akamshika mikono iliasiendelee na 

kitendo kile. 

 “Nini David ? Unaogopa? Akauliza 

Vicky .kabla David hajajibu kitu simu yake 

ikaita.  “ Naomba kwanza nipokee hii simu” 

akasema Dafid 

 “ Achana na hiyo simu David.Huu ni 

wakati wetu wa kujivinjari”akasemaVicky 

 “ Hapana Vicky inawezaikawa ni ya 

muhimu sana” akasema david na Vicky 

akamuachia akaenda mezani kutazmani 

nani aliyempigia.Alikuwa ni mzee 

Zakaria.Davdi akahisi baridi .Mwiliwote 

ukamtetemeka 

 “ Hallow mzee” akasema David huku 

sauti yake ikitetemeka 

 “ Hallow Daid uko wapi? Nimekuja 

hapa ofisinikwako nimekukosa.Nina shida 

Fulani nahitaji tuonane”akasema mzee 

Zakaria 

 “ Ok mzee nakuja sasa hivi niko 

maeneo ya Kimandolu .” 

 “ haya sDavid.Ninakusubiri” 

akasema mzeezakariana kukata 

simu.Alipogeuza shingo akamkuta Vicky 

madhahabu akiwa amebakiwa na nguo ya 

ndani pekee za ndani.Nusura adondoshe 

simu 

 “ Mzee Zakaria ndiye aliyekupigia? 

Akauliza Vicky madhahabu 

 “ Anahitaji kuniona sasa hivi 

ananisubiri ofisini” akasemaDavid  “ Aaaaggghhhh..!!!! aksema Vicky 

kwa hasira 

 “ Ninamchukia sana yule 

mzee.Ninahisi atakuwa mwanga.kwa nini 

anaingilia starehe za watu? Kwa nini apige 

muda huu wakati tunataka kuanza mambo 

yetu? akasemaVicky 

 “ Naomba unirejeshe ofisini 

Vicky.Mzee ananisubiri sasa hivi”akasema 

David 

 “ Kwa nini usimwambie kwamba 

uko mbalina hautaweza kuwahi mapema? 

David mwili wote unaniwaka hivi 

sasa.Nahitaji hta kidogo tu” 

 “MadamVicky naomba unipeleke 

ofisini.Kama hautaki nitaenda kukodisha 

gari la kuniwahisha hospitali” 

 “ Ok David nitakupeleka 

lakininaomba uniahidikwamba 

ntutapanga tena siku nyingine 

tukutane.Please David” 

 “ Sawa MadamVick.Tutapanga siku 

nyingine” akasema David . 

 “Ok kabla hatujaondoka naomba 

walau unikumbatie “ 

 “ Madam Vicky tafadhali twende 

tuondoke”akasema David.Vicky akamfuta 

akamkumbatia na kumbusu halafu akavaa nguo zake wakaondoka kurejea ofisini 

kwa David 

Safari ya kurejea ofisinikwa Davidi 

ilikuwa ya kimya kimya .Hakukuwa na 

maongezi garini.Japokuwa Vicky 

aliendesha kwa mwendo wa kazi 

lakinikwa Davidi alitamanhata kama gari 

lilre lingepaa ili awze kuwahi ofisini 

kwake kuonanana mzee Zakariaaliyekuwa 

akimsubiri 

“ Mzee Zakaria ataniona kama 

mzembenanisiyekuwa makinina 

kazi.Lakini nitajitetea 

kwambanimetokakatika mizungukoya 

kibiashara” akawaza David halafu 

akamgeuki aVicky akamtazma kwa jicho la 

wizi. 

 “ Mwanamke 

shetanihuyu.Kumbesiku zote ambazo 

amekuwa na ukaribunamimiamekuwa 

akinitaka.Dah ! ama kweli dunia 

imekwiwsha.Anadiriki kunitamkia 

waziwazikwamba aliolewa namzeee 

Zakariakwa ajilituya pesa zake na 

hanamapenzi naye.Kwa nni amdanganye 

mzee wa watu? Ni vigumu sana kuyapata 

mapenzi ya kweli sikuhizi.Ulaghai 

umekuwa mwingi sana.Inaoneknani tabia 

yake kutembea nje ya ndoayake.Anatamani hata mzee Zakaria afe leo 

ili aweze kuwa huru.Nimetokea k 

umchukia sana huyu 

mwanamke.Mamboanayoyafanya 

hayafaikabisa katika jamii.” Akawaza 

David.Sketi fupi aliyokuw aamevaa Vicky 

ilikuwa imepanda ju nakuyaacha wazi 

mapaja yake mazuri meupe. 

 “ Dah ! ama kweli mwnanmekhuyu 

ana vishawishi.Ameniwekakatikajaribu 

kubwa sana leo.Nashukurunimeweza 

kulishinda lakini bado ataendelea 

kuniandama sana kwani atahakikisha 

lazimaanatembea na mimi.Siwezi kufanya 

hicgho anachotaka tukifanye..Hapa 

inanibidi nitumie akilinyingi kuweza 

kuwauweza kumuepuka,hata hivyo yataka 

moy sana kuweza kulishinda jaribu hili.” 

Akawaza David 

 “ David sintakufikisha ofisini ilimzee 

aasije akahisi chochote.Nitakuacha 

palekatika kitu cha taksi utachukua taksi 

na kuwahi ofisini’ akasema Vicky 

 “ Itakuwa vizui 

sana.hartamiminilikuw na wazo kama 

hilo” akajibu david 

 “ david tafadhali fanyia kazi lile suala 

letu .Naomba hadijipniya leouwe 

umenijbu.Kama ikiwezekana nitakuja chumbani kwako leo usiku.Sina 

hakikakamanitawezkulalaaleo bila ya 

kugiswa.Hali yangu si nzuir kabisa” 

 “ madamVicky tafadhalinaomba usije 

chumbani kwangu ,utasababisha Pauline 

aanze kuhisi mambomenginekabisa.” 

Akasema David 

 “ kwa hiyo tutafanya nini david.Nina 

hamu sananawewe.” 

 “ Madam vicky kwa siku ya leo 

haitawezekanakabisa.Nimekwisha 

kuahidi kwambanitalifikiria suala 

hilinanitakujibukwa hiyo naomba usiwe 

nawasi wasi wowote.” akasemaDavid 

huku akotabasamu 

 “ sawa david lakini naomba ufahamu 

kwamba ninateseka wsana kwa akliji 

yako.” Akasema Vicky na 

kuendeshagarikwa kutumia 

mkonowakewa kulia halafu mkonowake 

wa kushotoakaunyoshana kutaka 

kuzishikanyetiza David ,akawahikumzuia 

 “ hapana usifanye hivi madam Vicky” 

akasema David 

 “ David nimechanagnyikiwa na 

ninashindwa hata nifanye nini” akasema 

Vicky.David hakumjibu kitu safari 

ikaendelea hadi walipofika katika kituo cha taksi ,akashuka na uchukua taksi 

akaelekea ofisinikwake. 

 “ Itanibidi kutumia akili sana 

kumkwepa madamVicky.Amedhamiria 

kabisa lazimaafanye mapenzi na mimi 

.”akawaza Dafid akiwa katika taksi 

akielekea ofisnini kwake.Alipofika 

alioshuka garini harak harakana kuwahi 

ofisinikwake.Mzeezakaria alkuwa ameka 

katika sofa za lupumzikia zilizokuwa 

ofisdnikwa David 

 “ Mzee samahani sna kwa 

kuchelewa.”akasemaDavid nakuifungua 

ofisi yake wakaongandani 

 “ Leo nimejisikia kutoka na 

kutembea kidogo.Vipi shughuli 

zinakwenda vipi? 

 “ shughulizinakwenda vizuri sana 

mzee.Hakuna tatizo lolote” 

 “nafutrahi kusikia hivyo David.Kuna 

kitu kingine kilichioileta hapa kwako.” 

Akasema mzeeZakaria 

 “ David wewe ni kijana ambaye 

nakuchukulia kama mwanangu nasi 

kamamfanyakazi wangu.Kila nilichonaco 

mimini chako pia nadda 

yakoPauline.Nimeona umekuwa 

ukisumbuka sana masualaya usafri kwa 

hiyonimeonanikupatie gari ambalo utakuwa ukilituiakwa shughuli zako za 

kila siku.” Akasema mzee zakariana kutoa 

funguoa za gari akamkabidhi David. 

 “ gari lako likohapo nje.Ni 

gariambalo nililiagiza kwa ajilya 

kutembelea lakini kutokanana 

haliyanguilivyo hivi sasa sitaweza k 

ulituia.Ninakupawewe gari hilo.Twende 

nje ukalione gari lako jipya” akasema 

mzee zakaria na ksha wakaongozana 

wakashuka chini na kuelekea katika eneo 

la maegesho 

 “ Gari lako hili hapa “ akasema mzee 

Zakaria 

David akapigw ana mshangao mkubwa 

.Hakuamini alichokuwa anakiona.Gari 

lililokuwa mbele yake n i gari ambalo 

hakuwahi kuota kama sikumoja atakuja 

kulimiliki.N gari ainaya range rover E 

vogue.Lilikuw ani gari la kifahari sana. 

 David akashindwa kujizuia furaha 

yake na kujikuta akimrukia 

nakumkumbatia kwa nguvu.akliruka ruka 

kwa furaha kama mtoto. 

 “ Mzee sina cha kusema.Ninashukuru 

sana .Nimeishiwa maneno ya 

kusema.Ahsante sana” akasema David 

“ David you deserve this.Kazi 

unayoifanya ni kazi kubwa na unastahili kupata gari zurila kutembelea kama 

hili.Jisikie amani kijana wangu.Hii ni 

zawadi ndogo sana ukilinganisha na 

wemawako mkubwa kwangu” akasema 

mzee Zakaria .David akaingia ndani na 

kulijaribu.Alikuwa nafuraha ya aian 

yake.Mzee Zakaria akaondoka zake na 

kumuacha David akiwa a furaha 

isiyoelezeka.Machozi yalimtoka kila 

alipokumbuka wema ambao mzee Zakaria 

amemfanyia. 

 “ Mzee huyu sijui nimemfanyia 

jambo gani hadi akanipenda namna hii? 

Nitamlipa kitu gani kwa wema huu? 

Akawaza David .Alikaa ndaniya ile gari 

kwa zaidi ya dakika ishirini na 

kilichomstua ni simu ya Tamia 

 “ Hallow Tamia”akasema Daid 

baadaya kuipokea 

 “ David habari yako?Mzima? 

Hatujawasiliana toka asubuhi.Ninakuja 

hapo ofisini kwako kamatulivyokuwa 

tumeelewana jana” akasema tamiana 

kukata simu 

 “ Sijui mzee Zakaria atakuwa katika 

hali gani akigundua kwamba nina 

mahusianona mwanae Pauline? Atanfanya 

niniakigundua lkwamba nimekuwa na 

mtandaowa kumuibia fedha zake na madam,Vicky? Akawaza huku akipandisha 

ofisini kwake 

 “ Lazima niachane na mambo ya 

kijinga ninayoyafanya.Lazima niyavunje 

mahusiano yangu na 

Pauline.Lazimaniivunjilie mbali mipango 

yote ya madam Vicky na niache kabisa 

ukaribu wowote naye.Kama kweli 

ninamuheshimu mzee Zakaria basi lazima 

niachane na Pauline pamoja na madam 

Vicky.” Akawaza 

 “ Dah lakini nitawezaje kuuvunja 

uhusiano na Pauyline? 

Nitawezajekumtamkia kwamba sitaki tena 

mahusiano naye? Yule msichana 

anaipenda sana lakini mimi sina hisia 

zozote za kimapenzi kwake.Mzee Zakaria 

anatuchukulia mimina Pauline kama mtu 

na dada yake na sijui itakuaje endapo 

akigundua kwamba tuna mahusiano 

.lazima haraka sana kabla mahusianyetu 

hayajaenda mbali niyasimamishe.Potelea 

mbali kama atakasirika ama vipi lakini 

lazima niachane naye.Lazima niachane na 

madam Vicky pia haraa iwezekanavyo 

nakuivunjilia mbali mipnagoo yote 

anayoipanga dhidi ya mze zakaria” Akiwa 

katika m,awazo mengi mlangowa 

ofisiniukaongonwa akainga Tamia.davdi akainuka kwa furaha na kumkumbati 

Tamia na kumshangaza. 

 “ Tamia nashukur umekuja.Nina 

furaha sana leo kukuona”akasemaDavid 

 “ Ahsante sanaDaid hata 

mimininafurahi sana kukuona.Kitugani 

kimekufurahisha namnahiyo 

David?Nishirikishe namimi furaha 

yako.davdi akamshuka mkonona 

wakashuka chini na moja kwaoja 

wakaelekeasehemuya maegesho ya 

magari 

 “ This is my new baby”akasema 

David kwa furaha akimunyesha Tamia 

gari lake jjipya.Tamia naye alkaruka kwa 

furaha kubwa wakakumbatiana halafu 

wakaingiandnai ya gari 

 “ Ulisema kuna mahala 

unatakanikusidnikize leo,twende na gari 

jipya.” akasemaDavdi 

kishawakaondoka.Walikwenda hadi 

katikaduyka mojakubwa lamavazi 

ambako Tamia alikuwa kaitaka kununua 

vazi la kuvaa katika sherehe yake ya 

kuzaliwa.Kwa msaaa wa David alifanikwa 

kupata gaunizuri sanaambalo lilimafnay 

aaonekanekama binti mfalme.Toka 

hapowakeel;ekea hadi numbani kwa 

tamia.  “ david karibu 

sananyumbanikwangu.si nyumbakubwa 

sana lakini inanitosha” akasema tamia na 

kumkaribisha David sebuleni 

 “ Ni nyumba nzuri sana,imetulia hata 

mimi nimeipenda sana.Ninayapemda 

maishaya uhuru.” 

 “ Kama Pauline asingekuwa kikwazo 

ungehamia hapatuishiwote 

kwaninaboreka sanakukaa 

mwenyewe”akasema Tamia na kisha wote 

wakaangua kicheko 

 “ Pauline si anayeyaongoza maisha 

yangu.Mimi na yeye tunaheshimiana sana 

na kamwe hawezi kunichagulianni cha 

kufanya” 

 “ Lakini David kuna kitu ambacho 

bado kinaniumiza sana.Kwa nini Pauline 

ajitambe kwambawew ni mpenzi wake? Ni 

kweli hakuna kinachoendelea baina 

yenu?hamna mahusiano? 

 “ Tamia amini kile ninachokwabia 

kwamba hatuna mahusiano yoyote 

mimina Pauline.Uhusiano wetu ni wa mtu 

na dada yake.Kwa ninisuala hili 

linakuumiza sanakichwa? Umekuwa 

ukiniuliza mara kwa ,ara kuhusu jambo 

hili”  “ Ni kweli nimekuwa nikikuuliza 

mara kwa mara kuhusiananajambo hili 

kwa sbabu linanitesa sana.Unajua 

mimonaiopenda sanakampanai yako 

lakini Pauline hapendi kabisa 

kunionamimina wewe na ndiyomaana 

akadiriki hata kunipiga simu na kunionya 

kwamba nisiwasilaine nawe tena” 

 “ Kwani kunaninikinaendela kati 

yenu? 

 “ Hakuna chochote hata mimi 

nimeshangaa sana.” 

 “ Ok hebu tuachane na mambo ya 

Pauline.Do you have anything to drink?.” 

Akauliza David 

 “ Ouh unataka kinywaji.basi hapa ni 

mahala pake.” akasemaTamiana 

kumleytea David chupa ya wine halafu 

yeey akaelekea chumbani kwke.bda ya 

dakika nneakarejkea akiwa amevaa lile 

gauni walilolinunua 

 “ wow !Tania umeoendeza sana 

akayti hilo gauni.Sijiitakuwaje siku hiyo ya 

sherehe” 

 “ david naomba usije ukakosa siku 

hiyo” 

 “ Siwezikukosa.Is theeranything 

specia l for me on that day?  “ Kuna vitu viongi vitakuwepo siku 

hiyo lakini kunakimoja ambachokitakuwa 

ni maalum kwa ajiliyako pekee.” 

 “ Nikitu ganihicho? 

 “Unataka kukiona? 

 “ Nidyo ninahitajikukiona” 

 “ Ok inuka twendenikakuoyeshe” 

akasema tamia na kumshika mkono David 

akaelekea hadi chumbanikwake 

 “ Ok David cclose you 

ayes.Usifumbue hadi nitakapokwambia” 

akasema Tamia.Baada ya dakika tatu 

Tamia akasema 

 “ Ok fumbua macho yako” 

Davdi akafumbua macho.Akakutana na 

kitu ambacho hakuwa amekitarajia.Tamia 

alikuwa amesimama akiwa 

mtupu.Mailiukamsisimka 

damuikamchemka. 

“ suprisee !!..akasema Tamia huku 

akitabasamu 

 “ Tamia !! akasmea David kwa 

mshangao 

 “ Usishangae David.Hiki ndicho kitu 

ambacho nimekuandalia.David 

sinakingine cha kuua zaidi ya hiki.Iknow 

you need meright? Akasema Tamia na 

kupiga hatua kumsogelea David ambaye 

alkikuw amesimama akimkodoelea macho bintiyule.tamia akamsogelea akamshika 

shavuni 

 “ Haka kama husemi 

lakinimachoyako yananionyesha 

wazikwamba unanitaka.Ineed you to 

David” akasemaTamia kwa sauti laini 

ambayo ilipenya masikioni mwa davida 

kuifanya mwili wake uchemke kwa hisia 

kali.Tamia akamkubatia David 

 “ Dah ! sielewini kwa 

nininnaandamwanamahii 

nahawawanawake.Huku Pauline,huku 

madma Vicky nassa Tamia.Lakini kidogo 

Tamia moyo wangu umekuwa 

ukimuwaza.Ninampenda snahyu bint 

lakini taoz nihizotabia sake ambazo 

niliambiwa nasPauline.Niliambiwa 

kwamba hajatuliahuyu mtoto na ana 

wanaume wwngu tu ndaniya jiji la 

Arusha.” Wakati akiwaza kuhusanana 

Tamia mara mkono laini wa Tamia 

akagusa maeneo nyeti na akaisi kama 

amepitriw ana umeme. 

 “ Tokanimeinga gerezani 

sijakutanana mwanamkena hawa 

wanawake wamekuwa wakiniamsha 

hisiaa zangu tokajana.Leo siwezi kukubali 

lazimanimunyeshe kazihuyu Tamia.” 

Akawza david na bilakupoteza wakati akamuinua Tamia kwa nguvu na 

kumpeleka kitandani.Alikuwa na midadi 

isiyokifani nahakutaka kupteza muda 

akanza kushughulika.Chuma kilitawaliwa 

kwa vilioo vya utamutoka kwa 

Tamia.Kilichosaidia kelele ziole zisisikike 

njeni sauti kubwa ya muziki iliyokuwa 

imefunguliwa. 

Samahani kwa baadhi ya maneno kuingiliana, natumaini umeelewa.



Baada ya kutoka ofisini kwa 

David,mzeeZakaria kaelekea hadi 

dukanikwa Pauline ili 

kuangalioamaendelo yake.Pauline 

alifurtahi sana kumuonababa yakepale 

dukani kwake 

 “ Dadynimefurahi sanaleo umefika 

dukaini kwangu.N mudamrefu 

huajfikahapa” akasemaPayline 

 “Nikweli Pauline.Leo imejisikia 

afadhali nanikaonangojaniwatembelee 

vijanawangu.Vipi biashara inakwendaje? 

 “ Boasharta akwendavizuri sana 

baba.” 

 “ Good”akasma mzeezakaria 

 “ Babaafadhaliumekuja.KLuna 

jamboamba;o nilikuwa nataka kukuomba” 

aksema Paulie  “ Jambo gani Pauline?mbachochote 

mwanangu. Lakini kablahaujasema 

unachotaka kukisema kuna kitu nataka 

kukwambia.” 

 “Kitugani hicho baba? Akauliza 

Pauline 

 “ Unakumbuka lile gari nililoagiza 

lililokuwa njiani? 

 “ Ndiyo baba nakumbuka” 

 “Basi gari lile limekwisha fika na 

nimeamua kumkabidhi David 

alitumie.Nimeonaakisumbuka katika 

suala la usafiri hivyoieonabora awena gari 

lakeiliasitegemeefari lako.najua kwa hivi 

sasa atakuw ana mizunguko mingi ya 

kibiashara kwa hiyo atahitaji sana usafiri.” 

 Pauline akafurahi na kwenda 

kumkumbatia baba yake. 

 “ You are so kindmy father that’s why 

I loveyou.hatamminilikuwa ninataka 

kukushauri kitu hicho hicho.Ahsante sana 

kwa kuliona hilona kumpatia david 

usafiri.Anafanya kazi nzuri sana” 

 “ Dafidninamchukulia 

kamamwanangu .Ni kijana mwenye tabia 

nzuri sana na ninampenda sana” akasema 

mzee Zakaria 

 “ Laiti ungejua kwamba david ni 

mpenzi wangu sijui usingetamakhayo maneno unayoyasema hivi sasa” akawaza 

Pauline 

 “ Ulitaka kuniambia niniPauline? 

 “ Baba mimitayari nimekwisha kuwa 

mkubwa hivi sasa na sioni sababu ya 

kuendelea kuwabana pale nyumbani 

wewe namama.Nikiwa palenyumbani 

kunamambo ambay ninashindwa 

kuyafanay.Ninashindwa hata kuwaleta 

marafiki zangu ,ninashindwa hata 

uhudhuriamialiko ya usiku 

namambomengine 

mengi.Babannaombanikaihsikatika 

ilenyumba yetu ya kule Kisongo.” Akasema 

pauine.Mzee Zakaria hakumjibukitu 

akabaki anamuangalia.Baada yamuda 

akasma 

 “ Pauline hakuna kitu ambacho 

nimewahi ukunyima uliponiomba lakini 

kwa mara ya kwanza naomba niseme 

hapana kwa ombi lako hilila kutaka 

kuhamapale nyumbani.Badohaujafikia 

hatua ya 

kuishimwenyewe.Kituganiunachokimbilia

kuishi peke yako?Kuna 

mamboganiambayohutaki 

niyafahamuambayounataka ukayafanye 

ukiwa kule pekeyako? 

Hapanasintakuruhusu uhame nyumbani.Wewenibintiyangu na ni 

jukumu langu kuhakikisha kwamba 

unakuwa katika uangalizi makini hadi 

haponawewe utakapompata mwenzako na 

mkaanza maisha.Siku utakaoondoka pale 

nyumbani nisikiuambayo nitakukabidhi 

kw mumeo ili mkaanze maisha yenu kwa 

hiyosahauu kabisa sualala 

kuhama.Kitukingine ambacho siwezi 

kukubali uhamenyubani ni kwamba mimi 

hali yangu nikamaunavyoiona.Ni mgonjwa 

naninahitajiungalizi .Mama yakomdogo 

nikama unavyomjua ni mtu wa 

mizunguomingi na simtegemei sana 

.Wewe ndiye ambaye unatakiwa uwe 

karibu sana na mimi .Wewe nadavid ndiyo 

watuniaowategeema sana .Kwa hiyo 

Paulinenaomba unielewekwamba siko 

tayari kukuruhusu uondoke na ukaanze 

maisha yako mwenyewe.” Akasema mzee 

zakaria.Pauline akanyong’onyea sana 

 “ lakinibaba hata kamanikiendda 

kukaa kule badonitakuwa karibuyako 

tu.Usihofuu kitu” 

 “ hapana Pauline.Siotyariuhame na 

ukaanzemaisha yako.Hakna sababu ya 

msingi ambayo itakufaya uliache 

jumbalilekubwa na ukaishi peke yako.Jumba letuni kubwa na lina nafasi ya 

kutosha” akasema mzee Zakaria. 

 Waliendelea na mambo mengine na 

baadae mzee zakaria akaondoaka zake 

krejeanyumbani. 

 “ Baba kanikatalia nisihamie kule 

Kisongo . Lakini haina shida nitatafuta 

namna nyingine ya kufanya ili kuweza 

kukutana na David.Hakuna 

kinachoshindikana chini ya jua nahakluna 

cha kjnitenganisha na David.Ttakuwa 

tunakutana hata katika nyumba za 

wageni.Daid ninamopenda sana nakwa 

sababu yakenko tayari kufanya kila 

linalowezekanakwa ajiliya kuwa 

naye.Najua itakapofikawakati 

babaatagundua na anaweza akakasirika 

sanalakini hakuna namna David ndiye 

mwnaumeninayemoenda kuliko wote” 

akawaza Pauline na uchukua ismu yake 

akazitafuta namba za simu za David 

akampigia.Smu ikaita bila 

kupolewa,akapiga tene a mamboyakawa 

niyaale yale simu haikupokelewa 

 “ Davidyuko wapi? Kwa nijihapokei 

simu? Kajiuliza Pauline 

 “ Ninapompigia simuna ikaita tu bila 

kupokelewa huwa ninakuwa na 

mawazomengi sana kuhusiananamahala alipo david.Inawezekanaakawa na mama 

mdogo? Akajiuliza na kuzitafuta namba za 

simu za Vicky akampigia. 

 “ Hallow Pauline” akasemaVicky 

 “ Habari mama mdogo” 

 “ habari nzuri.Unasemaje Pauline? 

 “ Ninamuulizia dacid uko naye? 

 “ Hapana siko naye.Kwani hapatikani 

simuni? 

 “ Anapatikanalakinisimuyake 

haipokelewi nikadhani labda uko aye” 

 “Hapanapaulne siko naye”akajibu 

Vicky ,Pauline akakta simj 

 “ David yuko wapi? Au yawezekana 

akawa analijaribu gari lake jipya?akawaza 

Pauline 

 “ Hapanalazimanikamtafute nijue 

yukowapi.Moyo wangu huwa hautulii kila 

nikimigia simu na kumkosa” akawaza 

Pauline na kuingiakatika garilake 

akaondoka kueleke a ofisini kwa David 

******************* 

 Penina alirejea darasani baada ya 

kutoakakuonanana Vivinamama yake 

mzazi ,lakinialikuwa na mawazo mengi  “ Yule mama anadai eti yeye ndiye 

mama yangu mzazi ! akawza paneina na 

kuivuta sua ya yule mama 

 “ yawezekana kweliakawa ni mama 

yangu kwa sababu ninafana naye lakini 

miaka hii yote alikuwa wapi ? 

Nimemtambua kutokanapicjha 

niazozinapale nyumbani lakini 

katikakumukubuzangu 

hayupokabisa.Alitukimbia mimina baba 

angalinikiwa mdogo na toka alipoondoka 

sijawahi kumuona tenampaka 

alipojitokeza leo hii.Ninatumai sikufanya 

kosa kwa majibu yale niliyompa kwani 

sioni kama anastahili kuitwa 

mama.”akawaza Penina na kuanza 

kukumbuka maisha yake aliyoyaishai toka 

akiwa mdogo.Alikumbuka namna baba 

yake alivyohangaika katika kumpatia 

malezi. 

 “ Siku zote baba yangundiyte 

anayesstahili heshima .Amehangaika mno 

katika kunipatia malezi makubwa 

.Amehangaika sana baba.Ninakumbuka 

hadi wakati ninapata akili haliyetu 

kiuchumi haikuwa nzuri,lakini baba 

alijitahidi kwa kila namna kuhakikisha 

kwamba tunakuwa na maisha mazuri.baba 

anastahili heshima ya kipekee kabisa.” Akawaza Penina na kuinuka akatoka na 

kuelekea katika ofisi ya mwalimu 

Lucy.Katika ofisi ya mwalimu Lucy 

kulikuwa na wageni wawili ikamlazimu 

asubiri katika sofa za kusubiria.Baada ya 

kama dakika ishirinihivi wageni walke 

wakatokaPenina akaingia 

 “ Penina ,una matatizo ? 

 “ Ndiyto mwalimu Lucy nina 

matatizo” 

 “ Una tataizo gani Penina? 

 “ Mwalimu Lucy kuna kitu 

kimenitokea leo wakati wa mpumziko” 

 “Kitu gani Penina? Unaumwa? 

 “ Hpana siumwi malimu Lucy” 

 “Kama huumwi kuna tatizo gani? 

Akauliza Mwalimu Lucy.Penina 

akakaakimya kidogo ikamlazimu 

mwalimu Lucy ainuke na kumshika 

mkono wakaenda kuketi sofani 

 “ Niambie Penina una tatizo gani? 

Kitu gani kimekutokea? 

 “ Mama yangu amekuja leo 

kunitazaama” 

 “ Mama yako ? !...mwalimu Lucy 

akashangaa 

 “ mama yako yupi? 

 “ Mama yangu mzazi” akasema 

Penina.  “ Mama yako mzazi? 

 “ Ndiyo mama yangu mzazi” 

 “ Unamfahamu mama yako mzazi? 

 “ Ninamfahamu kupitia picha zilizo 

nyumbani lakini leo nimemuona kwa 

macho.Walikuja akina mama wawili 

wakati wa mapumziko na mmoja wao 

akajitambulisha kama mama yangu 

mzazi.Nilipomtazama ni kweli ni mama 

yangu mzazi” 

 “ Alikueleza nini? 

 “ Hakunieleza chochote wao walidai 

kwamba wamekuja kunitembelea.” 

 “ Ulimjibu nini? 

 “ Utanisamehe mwalimu Lucy lakini 

sikumpa jibu zuri” 

 “ Ulijibu nini? 

 “ Nilimjibu kwamba sina mama , 

mama yangu amekwisha fariki.Nilimjibu 

vibaya? 

“ Hapana usisikitike sana Penina 

hukufanya kosa.Ulimjibu vizuri 

sana.Mimi pia ni mwanamke na ni 

mama pia lakini nisingeweza 

kufanya kitendo kama alichokifanya 

mama yako.Kumuacha mtoto mdogo 

wa miaka mitatu ni jambo ambalo 

halivumiliki kabisa .Ni ukatilina 

ujinga uliopita kipimo.Lakini pamojana hayo yote bado atabaki 

kuwa mama yako.Huna mama mzazi 

mwingine .Unachotakiwa kufanya ni 

kujarbu kutafuta namna ya 

kumsamehe “ akasema mwalimu 

Lucy 

 “Mwalimu Lucy una roho nzuri 

sana.Ni mwepesiwa 

kusamehe.Ningefurahi sana kama 

ningepata mama kama wewe.”akasema 

Penina.Maneo yale yakamgusa sana 

mwalmu Lucy akatabsamu 

 “ Penina mama si lazima aweni yule 

aliyekuzaa.Mwanamkeyeyot yule ni mama 

yako.hata mimipia ni mama yako na 

ninashukuru sana kuwa na mtoto kama 

wew katika shule yangu.Siku zozte 

ninakulea kama mwanangu na si kama 

mwanafunzi wangu.” Akasema mwalimu 

Lucy 

 “ Kwani mwalimu Lucy watoto 

wakowako wapi? Mika yote hii 

tokanimeanzashulesijawahi 

kumuonawamao hta 

mmoja.Hunawatoto?akauliza Lucy.Swali 

lilenusura limtoe machozi Lucy.Akainama 

akafikir I na kusema 

 “ Penina naomba tusiongelee 

masuala hayo kwa leo.Kwa sasa nenda darasani ukaendlee na masomo 

nitawasiliana na baba yakona 

kumfahamisha kwamba mama yako 

alifika hapa kukutazama. 

 “sawa mwalimu Lucy” akasema 

Penina na kutoka akarejea darasani 

 “Wanawake wengine hata haya 

hawana.yaani umkimbie mtoto kwa miaka 

hiyoyote halafu leo unarudi baada ya 

mtoto kuwa mkubwa?Hu ni ujinga sana” 

akawazana halafu akakubuka kitu 

 “ Lakini kitendo alichokifanya mama 

yake Penina cha kumtelekeza mwanae na 

kukimbia ni sawa na kitendo 

nilichokifanya cha kumtupa mwamangu 

na kukimbia.Mpakaleo sina hakika kama 

mwanangu alifanikiw akuokotwa anma 

alifariki.Kama alifanikiwa kuwa hai yuko 

wapi?Natmani kujua anaishi maisha gani? 

Natamani kumuoa tenamwanangu 

.Nadhanini wakati muaafaksasawa kuanza 

kumtafuta mwanangu.Nilirejea tena 

tanzani kwa lengo la kumtafurta 

mwanangu lakini kilanikitaka kuanza 

zoezi hilohujikuta nikogopa.Ninaogopa 

itakuwaje iwapo mwanagu atakuwa hai 

,nitamwambia nini? Ninahisi hatia kubwa 

moyoni mwangu.Endapo mwanangu 

alifariki nitakuwa na dhambi ya kuua. “ Mwalimu Lucy akahisi kitu kama kisu 

kikali kinaukata moyo wake.Slhisi 

maumivu makali ya moyo 

 “ Ninadhani ni wakati sasa wa 

kuanza kumtafuta mwanangu .Safari hii 

sitwakiwi kuogopa ,.Nitamtafuta 

mwananguna kujuakama yu mzima au 

alifariki.Nadhanimuda wa kuuufahamu 

ukweliumewadia..kama mama yake 

Peninabaadaya miwkaamini leo hii 

amediriki tena kuja kumtazama mwanane 

ninadhani hata mimi ninapaswa kufanya 

hivyo.Ninapaswa kumtafuta 

Angela.Naaajua haliakuwa jambo rahisi 

lakini nitajitahidii kuutafuta ukweli.” 

Akawaza Lucy 

*********************** 

David alikuwa akitiririkwa na jasho kama 

mtu aliyemaliza kukimbia mbio za 

marathon.Shughuli iliyofanyika mle 

chumbani kwa Tamia haikuwa shughuli 

ndogo.Tamia alikuwa amejilaza pembeni 

akiwa hoi.Gwaride alilochezeshwa na 

David halikuwa dogo. 

 “ Mhh !!.nimetembea na wanaume 

kadhaa lakini sijawahi kukutana na mziki 

kama huu wa leo.Huwa ninapewa sifa lukuki kwamba mimi ni mjuzi wa mambo 

na mapenzi ninayaweza lakini leo 

nimekutana na kiboko yangu.” Akawaza 

Tamia huku akihisi mapigo ya moyo 

kumwenda mbio. 

 “ Katika wote niliowahi kutembea 

nao hakuna kama David.Kilichokuwa 

kinanifanya nibadili wanaume si kwamba 

nina pepo la ngono kama walivyokuwa 

wakinisema lakini hawajui kwamba kuna 

kitu nilikuwa nakitafuta ambacho 

sikuwahi kukipata kwa wanaume wote 

niliotembea nao na ndiyo maana 

nimekuwa nikibadilisha kila mara ili 

kujaribu kuona kama nitampata yule 

ambaye atanipatia kitu 

ninachokihitaji.Nilichokuwa nakihitaji 

mtu wa kunikuna na kunifikisha 

ninapopataka.Kwa mara ya kwanza leo 

nimekunwa na nimefika mahala 

ninapopataka.David ndiye shujaa wangu 

na ndiye amenifikisha mahala nilipokuwa 

napataka.He’s the man I’ve been searching 

for years ” akawaza Tamia na kujaribu 

kuinuka lakini akahisi kama miguu 

imekosa nguvu 

 “ Dah ! hata miguu inakosa nguvu ya 

kuinuka.Ninasikia huku chini ni kama 

moto unawaka.Ama kweli leo nimekutana na kidume.Leo nimekutana na mtu 

anayejua kuicheza ngoma kisawa 

sawa.Kuanzia sasa hakuna yeyote 

anayeweza akaniambia kitu kuhusiana na 

David.Nitafanya kila linalowezekana hadi 

David awe wangu.Kuanzia sasa 

ninaufungua ukurasa mpya wa 

mapenzi.Yote niliyoyafanya huko nyuma 

ilikuwa ni ngono tu na si 

mapenzi.Ninajiona kama mtu mpya.” 

Akatabasamu na mara akastukia 

amepigwa busu zito na kuzidi 

kuchanganyikiwa. 

 “ Ouh David ..David, you are driving 

me craaazy..!! akasema Tamia na 

kumkumbatia David kwa nguvu wakaanza 

kupeana mabusu 

 “ Tamia you are so wonderfull.You 

are amazing.Uzuri wako si wa sura tu.Kila 

mahala wewe ni mzuri.Sijawahi kukutana 

na mjuzi wa mambo kama wewe.” 

Akasema David.Tamia akambusu na 

kusema 

 “ David nimekosa neno la 

kusema.Ahsante sana .Kwa muda mrefu 

nilikuwa natafuta mtu wa kuweza 

kunikuna kama ulivyonikuna leo .David 

you are the best of all.Ni mara yangu ya kwanza leo kuyafurahia mapenzi toka 

nilipoyafahamu” akasema Tamia 

 “ Ina maana wanaume wote uliowahi 

kuwa nao hawajwahi kukururahisha ? 

akauliza David 

 “ Wanaume wengi? Tamia akauliza 

 “nani kakwambia kwamba nina 

wanaume wengi ? 

 “ Tayari nina taarifa zako zote 

Tamia” akasema David 

 “ Kutoka kwa Pauline? Najua ni yeye 

ndiye aliyekupa taarifa zangu kwamba 

mimi nina wanaume wengi.Hakuna 

mwingine ambaye anaweza akakueleza 

mambo yangu zaidi yake” akasema Tamia 

 “ Hata kama ni Pauline ndiye 

aliyeniambia ,je yana ukweli ndani yake ? 

akauliza David.Tamia akainuka na kukaa 

kitandani akainama akafikiri kidogo na 

kusema 

 “ Kwa vile tayari amekwisha kueleza 

siwezi kukataa .Ni kweli alivyokwambia.Ni 

kweli nilikuwa na tabia ya kubadilisha 

wanaume na nilikuwa nao wengi tu .” 

akasema Tamia.David hakustuka na 

badala yake akauzungusha mkono 

shingoni mwa Tamia na kusema 

 “ Tamia you are so beautiful.Una kila 

sifa ya mwanamke mzuri .Umekosa kitu gani hadi ukawa na wanaume lukuki? 

Unajua unapowabadili wanaume mara 

kwa mara thamani yako nayo inashuka 

kwa kiwango kikubwa.” Akasema 

David.Tamia akafuta machozi 

 “ David ni kweli nilikuwa na tabia 

hiyo lakini si kwamba nilikuwa 

naifurahia.Kuna kitu nilikuwa nakitafuta.” 

 “ Ulikuwa unatafuta nini? akauliza 

David 

 “ Nilikuwa natafuta mwanaume wa 

kweli.Mwanaume ambaye atanifikisha 

ninapopataka ,mwanaume ambaye 

nikimuona tu moyo wangu utastuka ,na 

kwa bahati baada ya kuzunguka na 

kubadili wanaume hatimaye nimetua 

kwako.David wewe ndiye yule mwanaume 

ambaye amenisababisha niyafanye hayo 

yote nilioyoyafanya kwa ajili ya kumtafuta 

.Ulikuwa wapi siku zote? Kwa nini 

hukutokea mapema ? David sina aibu 

kukutamkia kwamba ninakupenda na 

wewe ndiye yule mwnaume ambaye 

nimekuwa nikikutafuta kwa miaka 

mingi.Siku ile Pauline alipotutambulisha 

kwako nilijua tu wewe ndiye yule ambaye 

nilikuwa nakutafuta kwa muda 

mrefu.David tafadhali naomba usiyaamini 

maneno ya watu watakayokwambia kuhusu mimi na hasa Pauline.Nimekwisha 

mfahamu Pauline hataki kabisa kuniona 

nikiwa na wewe.Endapo kuna kitu 

chochite utahitaji kufahamu kuhusiana na 

mimi njoo uniulize moja kwa moja na 

nitakujibu kuliko kusikia toka kwa watu 

wengine.David ninakupenda na niko 

tayari kufanya kitu chochote kwa sababu 

ya kuwa nawe.Najua yawezekana siko 

moyoni mwako lakini naomba David 

ujaribu walau kuniingiza moyoni 

mwako.Wewe ndiye ambaye ninakuhitaji 

katika maisha yangu,wewe ndiye kila kitu 

kwangu.Sijali kama una mwanamke 

mwingine au una mahusiano lakini 

naomba ufahamu kwako sijiwezi na 

niamuru chochote nitakutii David.” Tamia 

aliongea kwa hisia kali.David akamfuta 

machozi na kusema 

 “ Usilie tamia.usiangushe machozi” 

 “ David nashindwa kujizuia kulia 

kwa sababu kwa miaka mingi nimekuwa 

nikitafuta mwanaume kama wewe na leo 

hii nimefanikiwa kukutapa .Nina furaha 

ambayo haielezeki” akasema Tamia 

 “ Tamia si wewe tu mwenye furaha 

kubwa bali hata mimi moyo wangu kwa 

mara ya kwanza umejihi kuwa na 

furaha.Maisha yangu yametawaliwa na huzuni nyingi kwa hiyo sijawahi kuhisi 

furaha na amani mpaka siku ya leo .Tamia 

hata mimi naomba nikiri kwako kwamba 

nimekuwa nikikuwaza sana.Umekuwa 

unanijia katika ndoto zangu kila siku toka 

nilipokuona.Nimetokea kukupenda sana 

lakini nilisita kukueleza mapema 

kilichomo moyoni mwangu kwa sababu ya 

maneno niliyoambiwa na Pauline.” David 

hakumaliza sentensi yake Tamia 

akamkumbatia kwa nguvu na 

kumporomoseha mabusu mengi 

 “ David tafadhali usimsikilize 

Pauline. Kama nilivyokueleza Pauline ana 

wivu sana na hataki kabisa kuniona 

nikiwa karibu yako,narudia tena kukiri 

kwamba nikweli nilikuwa na tabia 

aliyoisema lakini niliiacha baada ya kuona 

kwamba sijampata mtu niliyekuwa 

nikimtafuta kwa muda mrefu.Naomba 

uniamini kwamba tabia hiyo nilikuwa 

nayo zamani na si sasa hivi.Sina 

mwanaume yeyote ambaye niko naye 

katika mahusiano kwa sasa.” Akasema 

Tamia 

 “ Tamia sijui ni kwa nini nimetokea 

kukumaini kwa kila 

utakachoniambia.Nadhani ni kwa sababu 

ninakupenda .Ninaomba mimi na wewe kuanzia dakika hii tuufungue ukurasa 

mpya ,tuingie rasmi katika mahusiano .Ni 

wewe tu ambaye utanifanya niwe na 

furaha .Lakini ninaomba mahusiano yetu 

yawe ya siri kubwa na asifahamu mtu 

mwingine yeyote hasa hasa Pauline na 

Madam Vicky” akasema David .Tamia 

akamrukia na kumkumbatia kwa nguvu 

wakaanza kugaragazana kitandani .Wote 

walijawa na furaha isiyo kifani kwa hatua 

ile ya kuanzisha mahusiano.Wakati 

wakiwa kitandani wakijiandaa kuingia 

katika mzunguko mwingine wa huba simu 

ya David ikaita. 

 “ Tamia wait.Ngoja niangalie nani 

anapiga.Anaweza akawa ni mzee Zakaria” 

akasema David na kuinuka akaenda 

kuichukua simu yake .Ni Pauline ndiye 

aliyekuwa akipiga ile simu.David 

akaiangalia na kujishauri iwapo aipokee 

ama vipi,lakini mwishowe akaamua 

aipokee. 

 “ Hallow Pauline “akasema David 

 “ David uko wapi ? akauliza 

Pauline.David akasita kidogo kujibu 

 “ Pauline nimetoka kidogo.Kuna 

nini?  “ Uko maeneo gani? Nimeambiwa na 

baba kwamba una gari jipya.Uko maeneo 

gani sasahivi ? Akauliza Pauline 

 “ Wewe uko wapi Pauline? 

 “Mimi niko hapa ofisini kwako “ 

 “ aahm nimetoka kidogo niko 

mizunguko kulijaribu gari langu jipya 

,nimekuja huku maeneo ya ngara 

mtoni.”akasema David 

 “ David are you ok? Akauliza Pauline 

 “ I’m ok Pauline why? 

 “ Unaonekana kama hauko sawa, una 

wasiwasi sana” 

David akacheka kidogo na kusema 

 “ Hapana sina wasi wasi Pauline 

lakini yawezekana ni kwa sababu niko 

ndani ya chombo kipya cha thamani na 

ndiyo maana ninakuwa na wasi wasi” 

 “ Ok David kuwa makini barabarani 

na mimi ninakuja njia hiyo ya Ngara mtoni 

ili na mimi nilijaribu gari lako .Tutakutana 

njiani”akasema Pauline na kabla David 

hajasema chochote akakata simu. 

 “ Tamia I have to go”akasema David 

 “ David unakimbilia wapi ? Ni 

Pauline ndiye aliyekupigia simu? 

 “ Ndiyo” akasema David huku 

akichukua nguo yake ya ndani na 

kuvaa.Tamia akainuka akamfuata  “David hii ni siku yako kubwa.You 

have a new car and you have a new 

girlfriend too.sikubali kitu chochote 

kikuharibie siku yako.Tafadhali 

usimuogope Pauline.” Akasema Tamia 

 “ Ninakuelewa Tamia lakini kwa leo 

niache tu niondoke .Nina sababu zangu za 

kutaka kufanya hivyo” akasema David 

huku akiendelea kuvaa 

 “ Ok David basi kabla hujaondoka 

ingia kwanza bafuni uoge ndipo uondoke 

ili Pauline asihisi kwamba kuna mahala 

ulikuwa umepitia”akasema Tamia huku 

akimvua David shati halafu wakaingia 

bafuni wakaoga .Kisha oga David akavaa 

vizuri wakakumbatiana na kupeana busu 

zito,David akatoka akaingia garini 

akaondoka 

 “ Dah ! sasa ninaanza kuamini 

kwamba kuhamishiwa gereza la Kisongo 

Arusha hakukuwa ni kwa bahati 

mbaya.Ilipangwa nije huku na nikutane na 

Tamia msichana mwenye uzuri wa 

shani.Msichana ambaye ndiye niliyekuwa 

nikimuota kumpata katika maisha 

yangu.Tamia ana kila sifa nzuri na 

inawezekana ndiyo sababu kubwa 

inayowafanya wanaume wamfuate kila 

uchao.Toka nilipomuona kwa mara ya kwanza siku ile Pauline aliponitambulisha 

kwake niliamini kwamba huyu ndiye 

mwanamke wa ndoto zangu.Ninampenda 

sana Tamia na mambo aliyonionyesha leo 

ni makubwa.Ninaapa nitafanya kila njia ili 

niweze kuwa naye.Hakuna cha kuweza 

kunitenganisha naye.” Akawaza David na 

kutabasamu halafu akamkumbuka 

Pauline 

 “ Huyu Pauline naye kwa nini 

amevuruga starehe yangu? Nilikuwa na 

wakati mzuri sana na kipenzi cha roho 

yangu Tamia .Lakini wivu wa yule 

mwanamke kila dakika anataka kujua 

niko wapi ,niko na nani na ninafanya 

nini.Aaahgghh..!! ameanza kunikera 

sana.”akawaza David 

 “ Lazima nitafute njia yoyote ile ya 

kuweza kuuvuja uhusiaho wangu na 

Pauline.Kwa gharama yoyote ile lazima 

niachane na Pauline.Nisipofanya hivyo 

nitashindwa kuwa huru na Tamia na 

ninawasi wasi siku moja lazima mzee 

Zakaria atagundua na atapoteza kabisa 

imani kwangu.Sitaki jambo hilo 

litokee.Nataka niwe na mahsuaino mazuri 

na mzee Zakaria na vile vile niwe huru na 

Tamia.lakini nitawezaje kuyavunja 

mahusiano yangu na Pauline ? Tayari msichana yule hasikii haambiwi juu 

yangu.Lakini pamoja na hayo I must find a 

way to end this relation ship.Iwe isiwe 

lazima niachane na Pauline na lazima 

niachane pia na mipango yote ya madam 

Vicky.” Akawaza David 

 “ Mzee Zakaria ni mtu mwema sana 

kwangu na ananilea kama mwanane kwa 

hiyo siwezi kumfanyia jambo lolote la 

ukosefu wa adabu.Lazima nichukue hatua 

kabla mambo haya hayajafika mbali” 

akawaza 

 “Siku yangu imeanza vizuri 

sana.Nina gari jipya na nina mpenzi 

mpya.Mambo haya yamenitokea kwa 

haraka sana na kunifanya nijione kama 

mwenye bahati sana katika hii dunia.” 

Akawaza Davi huku akiwa ni mwenye 

furaha sana akiwa ndani ya gari lake 

jipya.Moja kwa moja akanyoosha hadi 

dukani kwa Pauline na kumkosa akapigia 

simu kumtaarifu kwamba tayari yuko pale 

dukani kwake. 

********************. 

 Robin alifika shuleni mara moja 

baada ya kupigiwa simu na mwalimu Lucy 

na kumtaka afike pale shuleni kuna jambo la muhimu la kujadili.Baada ya mwito ule 

Robin hakutaka kuendelea na kazi yoyote 

akaondoka haraka hadi ishleni 

 “ karibu sana Robin” akasema 

mwalimu Lucy huku akitabasamu 

 “ Ahsante sana Lucy.Kuna tatizo 

gani? Kuna nini kimetokea? Is Penina ok? 

Robina kauliza maswali mfululizo 

 “ relax Robin.Penina is ok “akasema 

mwalimu Lucy huku akitabasamu 

 “ dah akili yangu ilikuwa imehama 

kabisa nilidhani labda mwanangu 

amepatwa na matatizo.” 

 “ Hapana Robin.kama angekuwa na 

matatzo ningeyashughulikia hata mimi 

kwani Penina ni sawa na mwanangu” 

 “ Ahsante san Lucy .Ahsante kwa 

kumjali mwanangu” akajibu robin huku 

akijifuta kijasho usoni 

 “ Robin nimekuita kwa mambo 

mawili.kwanza kabla ya yote naomba 

unisamehe sana kwa kukupotezea muda 

wako na kuahirisha shughuli zako 

nyingine” 

 “ Usijali Lucy .” 

 “ Ahsante sana.Kitu cha kwanza 

nilichokuitia hapa ni kwamba leo hii 

wakati wa mapumziko ya asubuhi ,mkeo alifika hapa shuleni akitaka kumuona 

mtoto wake.” 

 “What ?! …Vivian alikuja hapa? Robin 

akahamaki 

 ‘ Relax Robin.” Akasema mwalimu 

Lucy 

 “ Lucy nimestuka sana kusikia eti 

yule mwanamke amekuja leo kuja 

kumuangalia mwanae.Mwanae yupi 

aliyekuja kumuangalia? Angejua Penina ni 

mwanae kwa nini alimkimbia? Akauliza 

Robin kwa ukali 

 “ Robin tafadhali naomba upunguze 

hasira ili tuongee” 

 “ Samahani Lucy nimepandwa na 

hasira za ghafla.Mwanamke yule 

amenistua sana” akasema Robin.Baada ya 

kuona Robin ametulia,Mwalimu Lucy 

akaendelea 

 “ Mimi sikubahatika kumuona lakini 

Penina ndiye aliyekuja kuniambia 

kwamba mama yake amekuja 

kumuona.Penina hakuwa tayari 

kumpokea na alimweleza kwamba yeye 

hana mama” 

 “Good..Alifanya vizuri sana.Alimjibu 

vizuri” akasema Robin 

 “ Yule mwanakehastahili kabisa 

kuitwa mama.She’s a devil”akasema David  “ David nakubaliana kabisa na wewe 

kwamba mama yake Penina alifanya kosa 

kubwa kuondoka na kumuacha mtoto 

lakini kwa sasa jambo alilolifanya 

linamtesa sana na ndiyo maana pamoja na 

kufahamu kabisa kwamba kutakuwa na 

ugumu katika jambo hili lakini bado 

amediriki kuja kumtazama 

mwanae.Nafahamu tukiliangalia suala hili 

kwa upande mmoja mwanamke huyo 

anastahili kulaaniwa lakini kwa upandewa 

pili ukweli utabaki kwamba ndiye mama 

mzazi wa Penina.Pamoja na yote 

aliyoyafanya lakini yeye ndiye aliyemleta 

Penina duniani na hadi mwisho wa dunia 

yeye ataendelea kuwa mama yake 

mzazi.Huo ni ukweli ambao lazima 

tuukubali na ana kila haki ya kumuona 

mwanae .Ninachoweza kukushauri kwa 

sasa ni kwamba ongea na mzazi mwenzio 

na umfahamishe kwamba jambo hili si la 

kuchukulia haraka.Anatakiwa ampe 

Penina nafasi ya kutosha kwanza ya 

kumzoea kwani amekua bila mama.Pili 

unatakiwa umfahamishe kwamba hata 

kama akitaka kumuona mwanae hapa 

shuleni si sehemu muafaka.Anapomfuata 

mtoto sehemu kama hii anamfanya 

ashindwe kufuatilia masomo.Mfano dhahiri ni leo Penina ameshindwa kabisa 

kufuatilia masomo vizuri baada ya 

kumuona.” akasema mwalimu Lucy 

 “ Lucy ninashindwa nimfanye nini 

huyu mwanamke.Kwa nini anaanza tena 

kutuingilia maisha yetu wakati 

tumekwisha msahau na tunaishi kwa 

furaha na mwanangu? akasemaRobin. 

 “ Robin suala hili si rahisi kama 

nilivyokwambia.Ili kutolifanya suala hili 

kuwa gumu unatakiwa unane na mzazi 

mwenzio mkae na muongee.Jambo la pili 

nililokuitia hapa ni kwamba siku ya 

jumamosi wiki hii ni siku yangu ya 

kuzaliwa.Ninawahitaji wewe na familia 

yako yote muwepo na kusheherekea 

pamoja nami.Hii ni siku yangu kubwa na 

ninapenda kusheherekea na watu wangu 

wachache wa karibu” akasema mwalimu 

Lucy 

 “Bila hata kunialika tayari Penina 

alikwisha nialika na tungekuja bila hata 

kubisha hodi “ akasema Robin na wote 

wakacheka 

 “ Ahsante sana mwalimu Lucy kwa 

kunialika mimi na familia yangu.”akasema 

Robin 

 “ Usijali Robin.Wewe na penina 

mmekuwa kama sehemu ya maisha yangu pia na ndiyo maana ninataka 

kusherehekea pamoja nanyi.Hakutakuwa 

na watu wengi.Ni mimi na ninyi basi” 

 “Ahsante sana kwa kutupa heshima 

hii Lucy.Tutakuja na tutajitahidi kuifanya 

siku yako iwe nzuri na ya furaha 

sana.Ninaweza kuonana na Penina? 

 “ Hapana kwa sasa yuko darasani na 

akishakuona tu basi hatasoma tena.Mtoto 

yule anakupenda sana baba 

yake.”akasema Mwalimu Lucy kisha 

wakaagana Robin akaondoka 

 “Yule mwanamke nadhani si mzima 

hata kidogo.kwa kitendo alichokifanya 

sina hakika kama angekuwa mzima 

angethubutu hata kumtazama mwanae 

machoni.Inawezekana huko aliko mambo 

yameanza kumchachi a na hivyo anatafuta 

njia ya kuanza kujirudisha kwangu 

taratibu baada ya kusikia kwamba kwa 

sasa maisha yetu mazuri.Hana nafasi tena 

katika maisha yangu na katika moyo 

wangu.Pete ya ndoa nilikwisha ivua na 

kwa sasa kilichobaki ni sahihi zetu tu 

katika hati za ndoa .Akili yangu yote kwa 

sasa imehamia kwa mwalimu 

Lucy.Nimekwisha uruhusu moyo wangu 

kupenda tena na mwanamke pekee 

ambaye moyo wangu umemchangua safari hii ni mwalimu Lucy.Ana sifa za kuwa 

mama na hata Penina anampenda 

sana.Nitaitumia siku ya jumamosi katika 

siku yake ya kuzaliwa kumweleza 

kilichomo moyoni mwangu.Yule ibilisi 

hana chake tena hapa.Alikimbia umasikini 

akafuata utajiri lakini hata mimi Mungu 

amenibariki na sasa maisha yangu 

mazuri”akawaza Robin akiwa garini 

Saa kumi na mbili za jioni Robin akarejea 

nyumbani kutoka katika shughuli 

zake.Kitu cha kwanza kutaka kujua aliko 

Penina. Mtumishi wao wa ndani 

akamtaarifu kwamba Penina alikuwa 

chumbani kwake 

amejipumzishalala.Robin akagonga 

mlango na Penina akafungua 

 “ Baba shikamoo” akasema 

 “ Marahaba Penina mbona umelala 

mapema namna hii? Unaumwa? 

 “ Hapana baba siumwi,sijisikii vizuri 

leo” akasema Penina 

 “ Pole sana.Nimekuja leo shuleni 

kwenu,Mwalimu Lucy aliniita” akasema 

Robin 

 “ Ulikuja shuleni leo? Akashangaa 

Penina 

 “ Ndiyo nilikuja” 

 “ Mbona hukunitafuta?  “ Mwalimu Lucy aliniambia kwamba 

uko katika masomo” akasema Robin 

halafu kikapita kimya kifupi Robin 

akauliza 

 “ Nimeambiwa mama yako alikuja 

kukuona leo.Amekwambia nini? Akauliza 

Robin 

 “ Hakuniambia kitu.Alikuwa 

ameongozana na mwanamke mwingine 

simfahamu ni nani na ndiye aliyekuwa 

msemaji lakini mama hakuwa akiongea 

chochote.Alikuwa amejiinamia” Akasema 

Penina 

 “ Hawezi kuzungumza kitu kutokana 

na kitendo alichokifanya” akasema Robin 

halafu kikapita kimya kifupi Penina 

akasema 

 “ Baba utanisamehe sikumjibu mama 

vizuri.Najua hujanifundisha kuwajibu 

watu namna ile lakini nilikasirika sana 

nilipoambiwa huyu ndiye mama yako na 

nikamjibu kwamba sina mama “ 

 “ Usisikitike mwanangu.Hukufanya 

kosa lolote kwa kumjibu hivyo mama yako 

kwa sababu kitendo alichokifanya ni cha 

kikatili sana,alikukimbia angali bado 

ukiwa mdogo na toka wakati huo hajawahi 

hata kukujulia hali hadi leo hii ndipo 

anapokumbuka kwamba ana mtoto.Hata mimi nilikasirika sana nilipoambiwa na 

mwalimu Lucy kwamba amekuja shuleni 

kukuona na laiti kama angekuwa karibu 

ningemchapa makofi.Baada ya miaka hii 

yote leo hii ndiyo anakuja na kudai wewe 

ni mwanae? Akasema Robin kwa ukali. 

 “ Baba sitaki kumsikia kabisa mama 

yangu.Hana hata chembe moja ya upendo 

kwangu.Angekuwa ananipenda 

asingenikimbia wakati niko mdogo na 

hajawahi hata kutaka kuju 

aninaendeleaje.Kama angekuwa na 

upendo kwetu kwanza asingetukimbia na 

wala asingekubali kuniacha katika wakati 

ambao nilimuhitaji sana.Kwa sasa 

nimekwisha kuwa mkubwa na simuhitaji 

tena.” Akasema Penina.Robin akaketi 

pembeni yake na kusema 

 “ Penina mwanangu kuna kitu 

nataka nikuombe.Najua mama yako 

ametukosea sana .Ametukimbia wakati 

ule tukiwa katika hali duni na wewe ukiwa 

bado mdogo na ulihitaji sana huduma yake 

kama mama lakini pamoja na hayo kuna 

ukweli ambao hatuwezi kuuepuka” 

akasema Robin 

 “ Ukweli gani baba? Akauliza 

Penina.Robin akavuta pumzi ndefu na 

kusema  “ Hata kama tukimchukia vipi Yule 

bado ni mama yako mzazi.Ndiyo 

aliyekuleta hapa duniani” akasema Robin. 

 “ Alinileta hapa duniani ili kuja 

kuteseka? Alipokimbia alitegemea 

ningelelewa na nani? Baba sitaki kusikia 

kitu chochote kuhusiana na mama.Kwa 

sasa maisha yangu ni mazuri na nina watu 

ambao ninawapenda na 

wananipenda,watu ambao ninaweza 

kuwaita mama “ akasema Penina 

 “ Penina nalifahamu hilo na hata 

mimi inaniwia ugumu sana kulikubali 

suala hili lakini huu ni ukweli ambao 

hatuwezi kuukataa.Pamoja na makosa 

yote lakini atabaki kuwa ni mama 

yako.Ninachokuomba tafuta ndani ya 

moyo wako siku moja uweze kumsamehe 

na ukubali kuonana naye.Ninajua tayari 

atakuwa amelijutia kosa lake na ndiyo 

maana akaamua leo hii kuja 

kukuona.Najua haitakuwa rahisi lakini 

jitahidi kutafuta namna ya kuweza 

kumsamehe kwa kosa alilolifanya.” 

Akasema Robin 

 “ Vipi kuhusu wew baba 

umekwishamsamehe? Alikukimbia wakati 

hauna kitu na kwenda kuolewa sehemu 

nyingine umekwisha msamehe kwa hilo? Akauliza Penina.Robin akakaa kimya 

kidogo halafu akajibu 

 “ Hapana bado sijamsamehe na 

itanichukua muda kumsamehe kwa 

sababu kidonda alichonisababishia ni 

kikubwa sana lakini sitaki kuendelea 

kumuwaza kwa sababu kwa sasa maisha 

yetu ni mazuri na tunapata kila 

tunachokitaka.” Akasema Robin 

 “ Umeona baba,ni vigumu sana 

kumsamehe mtu kama mama kwa kosa 

alilolifanya.Unajua ni vitu vingapi 

nimevikosa toka kwake? Kuna mambo 

ambayo mimi siwezi nikakwambia wewe 

na alitakiwa yeye awepo nimweleze 

anisaidie lakini tazama yuko wapi? 

Hayupo.Hana nafasi katika maisha yangu 

na ulimi wangu unakuwa mzito sana hata 

kulitamka jina lake” akasema Penina .Kila 

mmoja akabaki kimya akitafakari 

 “ Anachokiongea Penina ni ukweli 

mtupu.” Akawaza Robin halafu Penina 

akaulizia 

 “ Baba ,bado unampenda mama ? 

.Robin akainama akatafakari kidogo kisha 

akasema 

 “ Swali gumu sana umeniuliza 

Penina.” Akajibu Robin  “ Hakuina ugumu baba nijibu tu 

kama ni ndiyo au hapana” 

 “ Kwa kweli sina hakika kama bado 

ninampenda mama yako kutokana na 

namna alivyonitenda.Alishindwa kuishi 

kiapo chetu cha ndoa kwa hiyo sina hakika 

kama bado yupo moyoni mwangu” 

akasema Robin 

 “ Baba sishangai kwa 

hilo.Mwanamke kama mama hafai kuwa 

na mtu kama wewe.Baba wewe ni mu wa 

kipekee sana na ninajisikia fahari sana 

kuwa na baba kama wewe.Japokuwa sina 

mama lakini ninajivuna kuwa na baba 

bora kama wewe.Lakini baba kuna kitu 

nataka nikuulize” 

 “ Uliza Penina” 

 “ Kama mama yeye anaishi na 

mwanaume mwingine kwa nini na wewe 

usitafute mwanamke uishi naye? Hutaki 

kuoa tena katika maisha yako? Akauliza 

Penina.Robin akacheka kicheko kikubwa 

 “ Penina mambo huwa si rahisi kama 

unavyodhani.” 

 “ Kwani ugumu uko wapi baba? 

 “ Ugumu upo mkubwa.Ikitokea 

mmefunga ndoa basi ndoa hiyo huwa 

inadumu milele na unaweza kuoa au 

kuolewa endapo mwenzako atakuwa amefariki dunia.Kwa maana hiyo siwezi 

kuoa kwa sababu bado ninatambulika 

kama niko ndani ya ndoa..” Akasema 

Robin 

 “ Kwa hiyo utakaa hivyo mpaka lini 

baba? Mbona mama yeye ameolewa? Au 

unategemea siku moja umrudishe mama 

hapa nyumbani ? Akauliza Penina na 

kumfanya Robin azidi kucheka 

 “ Penina mimi na mama yako 

hatuwezi tena kurudiana na sifikirii kuoa 

tena na hata kama nikifikia uamuzi huo 

basi lazima awe ni mwanamke ambaye 

atakupenda wewe kama 

mwanae.Mwanamke yeyote ambaye 

akitaka nimpende kwanza lazima akupede 

sana wewe kuliko hata mimi kwa sababu 

wewe ndiye jicho langu” akasema Robin 

na wote wakacheka 

 “ Vipi kuhusu mwalimu Lucy? 

Ninampenda sana na yeye ananipenda 

sana.Kila siku ninaota kama ningempata 

mama kama Yule.Ananipenda na ananijali 

sana na kila kitu ambacho siwezi 

kukueleza wewe huwa ninamueleza yeye 

na ananisaidia.Amekuwa ni zaidi ya mama 

yangu” akasema Penina na kumfanya 

Robin acheke  “ Kuna kitu nataka nikuulize Penina 

kuhusiana na mwalimu Lucy.Watoto wake 

wako wapi?Umekwisha waona? Akauliza 

Robin 

 “ Sijawahi kumuona hata mtoto wake 

mmoja na wala sjawahi kumuuliza kama 

ana watoto au hana” akasema Penina 

 “Ina maana Lucy hana watoto? 

Inawezekanaje mwanamke mzuri kama 

Yule akose mume na watoto? Hapana 

haiwezekani.Kuna haja ya kumdadisi na 

kuufahamu ukweli.Nimetokea kumpenda 

sana Lucy lakini kabla ya yote ninatakiwa 

kumfahamu vizuri ametokea wapi na 

historia yake kwa ujumla.Nimekwisha 

umwa na nyoka kwa hiyo kwa sasa niko 

makini sana” Robin akastuliwa na 

mwanae Penina 

 “ Baba unawaza nini? 

 “ Hapana ninatafakari tu baadhi ya 

mambo” akasema Robin. 

 “ Umekwisha andaa zawadi ya 

mwalimu Lucy? Siku yake ya kuzaliwa 

inakaribia” akasema Penina 

 “ Tayari ninayo zawadi ya Lucy 

usijali Penina.Wewe je umekwisha andaa 

zawadi? 

 “ Ndiyo baba tayari nimekwisha 

muandalia zawadi” akajibu Penina ambaye alipata faraja sana baada ya 

maongezi yale na baba yake .Robin 

akatoka na kuelekea chumbani kwake 

 “ Uso wa Penina unamanisha kile 

alichokisema.Itakuwa ngumu sana 

kumkubali tena mma yake kwa kitendo 

chake cha kumkimbia kwa miaka 

mingi.Hata mimi Yule mwanamke 

ninamchukia sana.Bado ninaikumbuka 

siku ile alipokuwa anaondoka na maneno 

mazito aliyonitamkia .Hata hivyo kwa sasa 

amebaki ni historia tu.Tayari moyo wangu 

umekwisha anza kufunguka taratibu kwa 

mwanamke mwingine” akawaza Robin. 

 “ Lakini hata hivyo kesho 

nitalazimika kufumba macho na kwenda 

kumuona nimweleze kwamba aache 

kabisa kutufuata, atuache na maisha 

yetu.Asimfuate fuate kabisa Penina 

atamchanganya “ akawaza 



 Ni saa tatu za usiku amejilaza 

kitandani ,alikuw na furaha 

iliyopitiliza.Kwa furaha aliyokuwa nayo 

siku hii alishindwa hata kula chakula cha 

usiku.Furaha yake ya kwanza ni kupewa 

gari jipya na mzee Zakaria lakini kilichompa furaha zaidi ni kuingia tena 

katika ulimwengu wa mapenzi.Alikuwa 

ameufungua ukurasa mpya wa mahusiano 

ya mapenzi na Tamia msichana ambaye 

alimpenda siku ya kwanza tu alipomuona 

 “ Hatimaye nimeingia tena kwenye 

mapenzi.Safari hii ninaamini nimempata 

mtu sahihi ambaye ninampenda na yeye 

ananipenda.Siwezi kupingana na moyo 

wangu kwamba ninampenda sana Tamia 

na nitafanya kila kitu hadi uhusiano wetu 

uwe wa wazi na kama ikiwezekana basi 

nifunge naye ndoa.” Akawaza David 

.Pamoja na furaha ile lakini bado suala la 

kuuvunja uhusiano wake na Pauline 

lilimuumiza sana kichwa.Wakati 

akitafakari namna atakavyoweza 

kuuvunja mahusiano yale mara mlango 

wake ukafunguliwa akaingia 

Pauline.David akastuka sana 

 “ Pauline what are you doing here? 

Akauliza David 

 “ Aren’t you happy to see me here 

David? Akauliza Pauline huku 

akitabasamu na kumfuata David pale 

kitandani akambusu na kumkumbatia 

 “ I missed you so much 

today.Niliongea na baba ili aniruhusu 

nikaishi katika ile nyumba yetu iliyoko kule Kisongo ili niweze kuwa huru na 

wewe lakini amekataa.Amenikatili 

sana.Hajui ni namna gani ninatamani niwe 

huru kufanya mambo mengi na wewe 

kama wapenzi lakini kwa hapa ndani 

tunabanwa sana na sijui hata nifanye nini” 

akasema Pauline 

 “ Pauline usiwe na haraka.Mambo 

haya yatakwenda taratibu tu na kila kitu 

kitakwenda vizuri,hutakiwi kuyapeleka 

mambo haya kwa pupa.Ukiyachukulia 

haraka tutaharibu kila kitu na mzee 

Zakaria atagundua “ akasema David 

 “ Mbona unamuogopa sana baba? 

Kwa sababu ya hili gari alilokupa? 

Usiogope David.Mimi na wewe hatuna 

mahusiano yoyote ya kindugu kwa hiyo 

hakuna kinachoweza kutuzuia kuwa na 

mahusiano na hata kufunga ndoa 

ikibidi.Kwa maana hiyo usiogope hata 

kama baba akijua hatafanya 

chochote.Mimi ndiye mwamuzi wa maisha 

yangu na ndiye ninayezmua niwe na nani” 

akasema Pauline huku akikichezea kifua 

cha David 

 “David leo ulikuwa wapi? Akauliza 

Pauline na kumstua kidogo David 

 “ Kwa nini umeuliza hivyo Pauline?  “ Kwa sababu uliniambia uko 

Ngaramtoni na mimi nikaja na njia hiyo ya 

Ngaramtoni lakini hatukukutana na 

badala yake ukanipigia simu uko dukani 

kwangu” akasema Pauline 

 “ Wakati ule unanipigia simu 

nilikuwa njiani nikirejea” akasema David 

 “ Kwa nini basi hukunitaarifu kama 

unarejea na badala yake ukakubali 

kwamba tukutane njiani? 

 “ Ah Pauline si unajua tena 

mchecheto wa kupata gari jipya tena zuri 

..” akasema David huku akitabasamu 

 “ David I warn you ,don’t you ever try 

cheat on me..” akasema Pauline na 

kumbusu 

 “ I love you” akasema na kuinuka 

akatoka.David akabaki anamuangalia 

 “ Inawezekana akawa amepata 

taarifa kwamba nilikuwa kwa Tamia? 

Akajiuliza David 

 “ Potelea mbali hata kama akijua 

tena itakuwa vizuri sana mimi kuachana 

naye .Sitaki kuendelea na mahusiano naye 

hata kidogo” akawaza na kustuliwa na 

ujumbe wa simu.Akaufungua haraka 

haraka akidhani umetoka kwa Tamia 

lakini ulikuwa umetoka kwa Vicky  “ Hongera kwa gari jipya.Hizo zote ni 

juhudi zangu.Nakupenda sana natamani 

hata sasa hivi ningekuja chumbani kwako 

unikate kiu yangu lakini hili zee bado 

limekodoa macho kama bundi.Nalichukia “ 

ndivyo ulivyosomeka ujumbe ule. 

 “ Dah huyu mwanamke ameanza 

tena” akasema David na kuufuta ujumbe 

ule na hakumjibu 

******************* 

 Siku zilikwenda haraka na hatimaye 

ni siku ya jumamosi.Saa moja za jioni 

David akiwa amependeza vilivyo 

alimshika Pauline mkono wakaingia garini 

kuelekea katika sherehe ya kumbu kumbu 

ya kuzaliwa Tamia.Pauline ndiye 

aliyeomba aendeshe gari usiku huu 

 “ David ninakwenda katika sherehe 

hii kwa sababu umenitaka niongozane 

nawe lakini sikuwa nikitaka kabisa 

kwenda .” akasema Pauline wakiwa garini 

 “ Kwa nini Pauline? Tamia ni rafiki 

yako kipenzi kwa nini usihudhurie 

sherehe yake? Mmegombana?  “ Hatujagombana lakini kwa siku za 

karibuni mahusiano yetu yametetereka 

sana” 

 “ Kwa nini? Kuna tatizo gani? 

 “ Ah ! ni mambo ya wanawake tu 

achana nayo.” 

 “ Lakini nina haki ya kuyafahamu 

kwani ninyi nyote ni marafiki zangu” 

akasema David 

 “ Ni mambo ya kawaida tu 

David.Unajua Tamia ni msichana mwenye 

tamaa sana na endapo nisingemdhibiti 

mapema basi ungeweza kuangukia katika 

mikono yake.Msichana Yule ni mshenzi 

sana na ana mabwana kila kona na huwa 

akimkamata mwanaume hawezi 

kuchomoka.Inasemekna anatumia dawa 

kuwakamata wanaume kwa sababu 

akimtaka mwanaume Fulani hawezi 

kumkatalia.Halafu akimtaka mwanaume 

huwa hasubiri amtongoze ni yeye ndiye 

mwenye kumtongoza huyo mwanaume na 

hawezi kumkatalia.Nilimuonya mapema 

kuhusu wewe na ndiyo maana 

hatuelewani.” akasema Pauline. 

 “ Tamia hatumii dawa wala nini,ni 

mjuzi wa kitandani.Mapenzi anayafahamu 

na hiyo pekee ndiyo dawa yake “ akawaza 

David huku akitabasamu na mara ujumbe ukaingia katika simu,akaufungua na 

kuusoma 

 “ Mpenzi mbona sikuoni hapa? 

Tafadhali njoo nikuone ili roho yangu 

itulie..” 

 David akatabasamu na kumjibu 

 “ Tuko njiani tunakuja” 

 “ Mko njiani? Wewe na nani? 

Akauliza Tamia 

 “ Niko na shoga yako Pauline” 

 “ David sikuwa namtaka Pauline 

katika sherehe yangu lakini kwa vile 

umeamua kuja naye hakuna 

kitakachoharibika lakini muweke wazi 

kwamba asishangae kwa atakachokiona 

usiku wa leo” akasema Tamia.David 

akahisi kuchanganyikiwa 

 “ Nisingeweza kwenda kwenye 

sherehe ya Tamia bila kuongozanana na 

Pauline.Sijui nini kitatokea lakini hakuna 

kitakachoharibika” akawaza David 

Walifika nyumbani kwa Tamia ambako 

geti lilikuwa wazi wakaingia ndani.David 

akashuka haraka garini na kwenda 

kumfungulia Pauline mlango halafu 

akamshika mkono wakaelekea sehemu 

kulikokuwa na majani mazuri ambako 

sherehe ingefanyika.Watu walikuwa si 

wengi sana kwani Tamia hakuwa amealika watu wengi.Walipokewa na msichana 

mmoja aliyekuwa na kazi ya kuwapokea 

wageni akawaelekeza sehemu ya kukaa. 

 “ David umenileta katika herehe hii 

lakini sikuwa ninaka kabisa kuja 

hapa.Sina amani kabisa” akasema Pauline 

 “ Kwa nini Pauline? Tafadhali 

usifanye hivyo.Tamia ni rafiki yako 

mkubwa na wasiku nyingi.Mpe 

ushirikiano katika siku hii muhimu kwake 

” akasema David na mara akatokea Stella 

mmoja wa marafiki wakubwa wa Tamia na 

ambaye anafahamiana pia na Pauline 

.Wakasalimiana na Stella akashangaa sana 

kumuona Pauline kule katika viti vya 

wageni wakati yeye ni mtu muhimu sana 

ambaye alitakiwa kuwa mstari wa mbele 

katika sherehe ile ya rafiki yao.Stella 

akamnyayua Pauline na kumtaka 

waelekee jikoni kusaidiana katika 

maandalizi.Mara tu Pauline alipoondoka 

David akachukua simu yake na 

kumuandikia ujumbe Tamia 

 “ Tayari nimekwisha 

wasili.Nilishindwa kukutaarifu mapema 

nilikuwa nimekaa na Pauline na sasa 

ameelekea jikoni” akautuma ujumbe ule 

na baada ya muda ukarejea ujumbe toka 

kwa Tamia  “ Thank you soo much my love.Kuja 

kwako ni zawadi kubwa sana 

kwangu.Usimjali Pauline .Tutaonana 

baadae wakati sherehe ikiendelea” 

 David akatabasamu baada ya 

kuusoma ujumbe ule kisha akaiweka simu 

yake mfukoni 

 “ Dah ! kwa kweli niko katika wakati 

mgumu sana kwani ninampenda sasa 

Tamia lakini nashindwa kuwa naye huru 

kutokana na uhusiano wangu na Pauline 

ambaye sina hata chembe moja ya hisia 

kwake.Yote hii imesababishwa na madam 

Vicky.Mwanamke ibilisi Yule ndiye 

aliyenishawishi hadi nikakubali kuwa na 

mahusiano na Pauline.Ninajilaumu sana 

kwa kuwa mwepesi kukubaliana na 

Pauline.Lazima nichukue uamuzi mgumu 

wa kuachana na Pauline pamoja na 

madam Vicy.” Akawaza David huku 

akiendelea kupata kinywaji taratibu 

 “ Lakini nitawezaje kuachana na 

mipango ya madam Vicky wakati tayari 

tumekwisha piga hatua kubwa? Tayari 

tumeshirikiana katika mipango mbali 

mbali mibaya ya kumuhujumu mzee 

Zakaria.Nikisema kwamba ninataka 

kuachana na mipango ya madam Vicky 

inamaanisha kwamba lazima nimweleze ukweli mzee Zakaria kuhusiana na kila 

anachokifanya madam Vicky.Lakini je 

atanielewa? Ataniamini tena? Akaendelea 

kujiuliza David 

 “ Potelea mbali ,litakalotokea na 

litokee tu lakini lazima niachane na 

mipango yote ya madam Vicky.Mzee 

zakaria ni sawa na baba yangu na siwezi 

kuona akihujumiwa na mwanamke Yule 

mshenzi na kibaya zaidi mimi kuwa 

sehemu ya hujuma hizo.Mzee Yule 

ananipenda na kunijali kama mwanae kwa 

hiyo katu siwezi kumfanyia kitendo kama 

hiki cha ukosefu wa fadhila.Nawachukia 

sana wanawake wadanganyifu kama 

madam Vicky “ akawaza David.Mawazo 

yake yalikatishwa na muongoza shughuli 

aliyewatangazia wageni wote kwamba 

wajiweke tayari kwani sherehe 

zinakwenda kuanza 

 Wakati sherehe ikianza nyumbani 

kwa Tamia ,nyumbani kwa mwalimu Lucy 

nako sherehe ya kumbu kumbu ya 

kuzaliwa mwalimu Lucy ilikuwa 

inaendelea.Tofauti na sherehe za miaka 

mingine ,farai hii mwalimu Lucy alialika 

watu wachache sana.Walikuwepo waalimu 

wachache pamoja na baadhi ya wanafunzi 

na bila kuwahau wageni muhimu wa shughuli ile ambao ni familia ya 

Robin.Mwalimu Lucy akiwa amependeza 

sana ndani ya gauni refu jeupe lenye 

nakshi za kupendeza sana aliimbiwa 

wimbo maalum wa siku ya kuzaliwa na 

baada ya hapo likafuata zoezi la keki.Mtu 

wa kwanza ambaye alimtaka amlishe keki 

ni Penina.Alimpenda sana Penina.Baada 

ya Penina wakafuata watu wengine na wa 

mwisho kabisa alikuwa ni Robin.Kisha 

kukamilika kwa zoezi lile wageni wote 

wakakaribishwa mezani kwa ajili ya 

chakula na viywaji.Kuliandaliwa chakula 

kizuri sana na watu wote 

walikifurahia.Baada ya chakula baadhi wa 

wageni waliohudhuria wakaaga na 

kuondoka wakabaki watu wachache tu 

wakiburudika kwa vinywaji na muziki. 

 “ Its time for kids to enjoy.Tuwape 

nafasi” Mwalimu Lucy akamwambia Robin 

kisha wakatoka mle sebuleni na kuelekea 

bustanini ambako kulikuwa na meza 

iliyoandalia vizuri na kusheheni vinywaji 

 “ Sherehe ya watu wazima inafanyika 

huku kule tuwaache watoto.Karibu sana 

Robin.Niliandaa meza hii kwa ajili yetu.Ni 

wakati wetu na sisi kufurahi” akasema 

mwalimu Lucy huku akitabasamu  “ Nimeipenda sana sherehe 

yako.Umeipanga vizuri na imependeza 

mno” akasema Robin huku akimimina 

kinywaji 

 “ Ahante sana Robin kwa kufika 

kwenu.Nimefurahi sana 

mmefika,Mmenipa furaha sana” akasema 

mwalimu Lucy 

 “ Nisingeweza kuacha kufika katika 

siku yako kubwa kama hii.Binafsi 

nimekuja kukushukuru sana kwa namna 

unavyomlea mwanangu hapa 

shuleni.Umemsaidia sana katika mambo 

mengi na anakuona wewe kama mama 

yake.Kuna mambo ambayo mimi kama 

baba yake hawezi akanieleza lakini 

amekuchagua wewe kama mtu ambaye 

anaweza akakueleza shida zake zote 

.Nashukuru sana mwalimu Lucy,Ahsante 

sana.Kutokana na umuhimu wako kwa 

mwanangu Penina umekuwa pia muhimu 

sana kwa famila yetu.Kwa hiyo basi kuna 

zawadi nimekuandalia ni ndogo tu .” 

akasema Robin na kuingiza mkono wake 

katika koti na kutoa kitu Fulani kidogo 

lakini kilichofungwa vizuri sana kwa 

karatasi za zawadi akampatia mwalimu 

Lucy  “ Ouh Robin ahsante sana “ akasema 

mwalimu Lucy huku akifungua zawadi ile 

.Vilikuwa ni vitamba vizuri sana vya 

kufutia jasho vilivyokuwa na nakshi za 

kupendeza na jina Lucy.Mwalimu Lucy 

akashindwa kujizuia akatoa machozi 

 “ Robin ahsante sana kwa zawadi hii 

ndogo lakini kubwa na nzuri .Nimeipenda 

sana.Nimekwishapewa zawadi nyingi sana 

lakini hakuna aliyewahi kunipatia zawadi 

kubwa kama hii.Ahsante sana Robin.” 

Akasema mwalimu Lucy.Robin akainuka 

akachukua kitambaa kimoja na kumpatia 

Lucy afute machozi 

 “ Robin naweza nikakuuliza kitu? 

 “ Uliza Lucy” 

 “ Katika zawadi zote ambazo 

ungeweza kunipatia kwa nini ukanipa hii? 

Katu sikuwa nimeitegemea” Akauliza 

mwalimu Lucy 

 Robin akanywa funda moja la 

kinywaji kisha akasema 

 “ Nimekupa zawadi hii kwa ajili ya 

kufuta machozi “ akasema Robn 

 “ Am I a cry baby? Akauliza mwalimu 

Lucy. Na wote wakacheka 

 “ Lucy nimekusoma na nimegundua 

kitu kimoja kwako.Nimegundua kwamba 

hauna furaha .You are sad.Na ndiyo maana nikakuletea vitambaa hivi ili kila pale 

utakapokuwa na huzuni na machozi 

kukutoka basi uwe unachukua kimoja na 

kujifutia machozi na hapo hapo 

utakumbuka kwamba kuna watu ambao 

wanakujali sana “ akasema 

Robin.Mwalimu Lucy akashindwa aseme 

nini.Machozi yakamtoka akachukua tena 

kitambaa kile alichopewa na Robin 

akajifuta machozi na wote wakacheka. 

 “ You made me cray again” akasema 

Mwalimu Lucy 

 “ Robin unajua sana kuchunguza 

.Umejuaje kama sina furaha na maisha 

yangu? 

 “ Nimekuwa nikikuona kila siku na 

nimegundua kwamba tayari una maisha 

mazuri unapata kila unachokihitaji lakini 

kuna kitu kimekosekana .Hauna 

furaha.Sitaki kuingia sana katika maisha 

yako lakini baada ya kuligundua hilo ndio 

maana nikaona nikuletee vitambaa hivi ili 

uwe ukijifutia machozi” akasema Robin 

 “ Robin narudia tena kusema 

ahsante sana kwa zawadi hii.Ni kweli 

ulichokisema ni kwamba nina kila kitu 

katika maisha lakini nimejikuta nikiwa 

sina furaha.Thats how life is” akasema 

mwalimu Lucy  “ By the way where is your family? 

Akauliza Robin na swali lile likaonekana 

kumchoma sana mwalimu Lucy akainama 

na kufuta machozi 

 “ Lucy leo si siku yako ya kumwaga 

machozi.Leo ni siku yako ya kufurahi na 

ndiyo maana sisi sote tuko hapa kufurahi 

pamoja nawe kwa hiyo tafadhali usilie.” 

Akasema Robin .Mwalimu Lucy akainua 

kichwa na kusema 

 “ Samahani sana Robin kwa 

kumwaga machozi mbele yako.Sikutakiwa 

kufaya hivi hasa katika siku kama ya leo” 

 “ Usijali Lucy.Maisha yetu 

yametawaliwa na mambo mengi sana na 

mengine huwa hayavumiliki.” Akasema 

Robin 

 “ Kwa nini unataka kufahamu 

kuhusiana na familia yangu? Akauliza 

Lucy 

 “ Nilitaka tu kufahamu ilipo familia 

yako kwa sababu katika siku yako kubwa 

kama hii ya leo walitakiwa kuwepo hapa” 

akasema Robin 

 “ Sina familia Robin” 

 “ Huna familia? Robin akashangaa 

 “ Mwanamke mzuri kama wewe 

utakosaje familia? Usiniambie kwamba 

huna hata mume” akasema Robin Mwalimu Lucy akacheka kidogo na 

kusema 

 “ Ni kweli sina mume bado” akasema 

mwalimu Lucy 

 “ Kuna ule usemi unasema kwamba 

wanawake wazuri wenye kujaaliwa elimu 

nzuri na pesa huwa hawapendi sana 

kuolewa.Inaonekana hata wewe Lucy 

msemo huu unakuhusu” akasema Robin 

 “ Si hivyo Robin lakini ukweli ni 

kwamba ninaogopa sana kuingia katika 

mapenzi.Ninaogopa kuumizwa” akasema 

Lucy 

 “ Katika mapenzi kuumizwa ni kitu 

cha kawaida kwa hiyo usiogope kuingia 

katika mapenzi kwa kuhofia 

kuumizwa.Una kila sifa nzuri ya kuwa mke 

na kuwa mama bora” 

 “ Mama bora? Una hakika ninaweza 

kuwa mama bora? Akauliza Lucy 

 “ Una kila sifa ya kuwa mama bora” 

akasema Robn 

 “ Sidhani Robin kama ninastahili 

kupewa sifa kama hii ya kuwa mama bora” 

 “ Usiseme hivyo Lucy una sifa ya 

kuwa mama bora.Mwanangu Penina 

anaota kila siku kama angepata mama 

kama wewe kwa namna unavyompenda na kumtunza” akasema Robin.Mwalimu Lucy 

akainama akafikiri kidogo na kusema 

 “ Robin naomba nikuulize kitu “ 

 “ Uliza Lucy usiogope” 

 “ Aliyekuwa mkeo alikimbia na 

kukuacha wewe na mtoto mdogo ,nina 

tumai uliumia sana ,right? 

 “ Niliumia sana.Na kilichoniumiza 

zaidi ni kumuacha mtoto wetu akiwa 

mdogo na akihitaji sana huduma yake 

kama mama” akasema Robin 

 “ Ni miaka mingi imepita sasa je 

umeweza kumsamehe? Anastahili kuitwa 

mama? Akauliza mwalimu Lucy 

 “ Kwa kweli anastahili kuitwa mzazi 

kwa kuwa alizaa mtoto lakini hana sifa ya 

kuitwa mama kwa sababu angekuwa na 

ule upendo wa kweli wa mama kwa 

mwanae asingediriki kumkimbia mwanae 

tena bado mdogo.Kwa ufupi hana sifa ya 

kuitwa mama kwa sababu mama 

haimaanishi kuzaa tu mtoto na 

kumtelekeza bali unatakiwa umpe malezi 

pia mtoto uliyemzaa.” Akasema 

Robin.Maneno yale yakamchoma sana 

mwalimu Lucy akainama na kufuta 

machozi 

 “ Mwalimu Lucy ana nini leo ? Mbona 

analia sana? Mbona jambo hili la familia limeonekana kumchoma sana? Familia 

yake iko wapi? Ana historia gani katika 

safari yake ya mapenzi? Akajiuliza Robin 

 “ Robin mimi na mkeo wote tuko 

katika kundi moja”akasema mwalimu 

Lucy 

 “ Kundi moja? Una maana gani? 

akauliza Robin 

 “ Wote hatustahili kuitwa mama” 

 “ Lucy tafadhali usijifananishe kabisa 

na Yule ibilisi.Huwezi kufanana naye hata 

kwa chembe moja.Wewe ni mwanamke 

mwenye heshima zako na huwezi kufanya 

jambo la kijinga kama alilolifanya 

Vivian.Tafadhali Lucy usijifananishe 

kabisa na Yule mwanamke “ akasema 

Robin 

 “ Robin unasema hivyo kwa sababu 

hunifahamu na huifahamu historia yangu” 

akasema mwalimu Lucy 

 “ Kwani Lucy historia yako ina nini? 

Akauliza Robin 

 “ Ni historia ndefu sana na huwa 

sipendi kukumbuka” akasema mwalimu 

Lucy 

 “ Lucy unaweza ukanieleza historia 

yako? Kitu gani kimekusibu tafadhali 

nieleze Lucy.Nitakusikiliza “ akasema 

Robin. 




Sherehe ya Tamia iliendelea vizuri 

sana na hakukuwa na tatizo lolote.Ulifika 

wakati wa kucheza muziki na kuburudika 

kwa vinywaji .Wakati watu wakijimwaya 

na muziki msichana mmoja akamfuata 

David na kumshika bega. 

 “ Unaitwa na Tamia” akasema Yule 

msichana na David akaongozana naye 

kuelekea katika maegesho ya magari 

akamkuta Tamia ambaye alimshika 

mkono na kumuomba waingie katika gari 

lake wakaondoka 

 “ Tunaelekea wapi? Akauliza David 

lakini Tamia hakujibu kitu.Wakati 

wakiingia ndani ya gari Pauline ambaye 

wakati wote wa sherehe jicho lake 

lilikuwa kwa David ,aliwaona na kustuka 

sana.Gari la Tamia lilipoondoka Pauline 

naye akachanganyikiwa na kutaka 

kuwafuata lakini hakuwa na ufunguo wa 

gari.Ufunguo alikuwa nao David 

Pauline alichanganyikiwa.Alisimama 

katika gari la David asijue la 

kufanya.Kitendo kile cha kuwaona mpenzi wake David na Tamia wakiingia katika 

gari na kuondoka kilimchanganya sana 

 “ David na yule kahaba wanakwenda 

wapi? Kwa nini hajaniaga na kuniambia 

kwamba anaondoka? Akajiuliza Pauline 

 “ Ninamfahamu Tamia si mtu mzuri 

hata kidogo na ndiyo maana nikampiga 

marufuku kumsogelea David.Tabia ya 

Tamia huwa hataki kupitwa na 

mwanaume mzuri na nimekwisha muona 

toka siku ya kwanza alikuwa akimtaka 

David.safari hii nitapambana naye 

.Sintojali kama ni rafiki yangu .Urafiki 

gani huu wa kuibiana mabwana? Huu katu 

si urafiki.Ninasema lazima nitapambana 

naye.Kama ni urafiki ni bora ukavunjika 

na nikabaki bila rafiki kulikokuwa na 

rafiki mnafiki kama Tamia” akawaza 

Pauline huku uso wake ukiwa 

umekasirika sana.Akaichukua simu yake 

na kumpigia David . 

 Tamia na David Wakiwa garini simu 

ya David ikaita 

 “ Pauline anapiga.Inawezekana 

ametuona na anataka kufahamu 

tunaelekea wapi.” akasema David 

 “ Usiipokee simu yake na wala 

usimjali” akasema  Tamia  “ David huu si wakati wa 

kumuogopa Pauline tena.Sisi tunapendana 

na tumeridhiana kwa nini tukose amani 

kwa sababu ya Pauline.kwa nini 

tushindwe kujinafasi kwa sababu ya 

Pauline?.Au kuna kitu ambacho 

sikifahamu kinaendelea kati yako na 

Pauline ?akauliza Tamia 

 “ Hapana hakuna kinachoendelea 

kati yetu.Uhusiano wetu mimi na yeye ni 

kama wa kaka na dada na hakuna 

chochote kingine” akajibu David 

 “ kama ni hivyo kwa nini basi 

anakufuatilia namna hiyo? Kwa nini hataki 

kukupa nafasi ya kuusikiliza moyo wako ? 

Please David naomba usimsikilize 

Pauline. Yule msichana hapendi kabisa 

kuniona mimi na wewe na amenipiga hadi 

marufuku nisikupigie hata simu. Mimi 

siwezi kumjali mtu kama yule aliyejawa na 

wivu katika kila kona ya mwili wake.Mimi 

ninakupenda na nimechagua kuwa na 

wewe tu.Ninakuhakikishia David kwamba 

sintokubali mtu yeyote yule 

anitenganishe na wewe.Nitapambana na 

yeyote kwa ajili yako.Hawajui ni kwa 

miaka mingapi nimehangaika kumtafuta 

mtu kama wewe “ akasema Tamia na simu 

ya David ikaendelea kuita.Pauline aliendelea kupiga lakini simu yake 

haikupokelewa akahisi kuchanganyikwa. 

 “ David… David!! David..Ouh 

masikini david kwa nini unanifanyia hivi? 

“ akasema Pauline kwa uchungu mwingi 

baada ya kupiga mara tatu simu ya david 

bila kupokelewa. 

 “ Nahisi tayari nimempoteza 

David.Tayari amekwisha nyakuliwa na 

Tamia.Ninamfahamu vizuri Tamia huwa 

akimpenda mwanaume atahakikisha 

anatumia kila njia hadi anampata.Moyo 

unaniuma sana Ouh jamani nitafanya nini 

mimi ? Kwa nini Tamia ananifanyia hivi 

?Nitawezaje kuishi bila David? Mimi ndiye 

niliyemtoa David mavumbi aliyokuwa 

nayo na kumuweka katika hali ya 

kutazamika halafu leo hii baada ya kuwa 

mzuri anaonekana kijana mtanashati basi 

wameanza kummezea mate.Ninasema 

nitapambana na yeyote ambaye anataka 

kuniibia moyo wangu.David ndiye maisha 

yangu na ndiye kila kitu kwangu” 

akawaza Pauline na kuchukua tena simu 

yake akampigia Tamia.Simu ya Tamia 

ikaita halafu ikakatwa. 

 “ Amenikatia simu.!!..” akasema 

Pauline na kuegemea gari.  “ Tamia tunakwenda wapi? Akauliza 

David. 

 “ Subiri utaona David” akasema 

Tamia. 

 “ Sipati picha Pauline atakuwa katika 

hali gani huko aliko hasa kwa namna 

anavyomuogopa Tamia.Hata katika 

sherehe hii hakutaka kuja.Lakini 

nitaendelea kumdanganya hadi lini? Kwa 

nini nisimweleze ukweli ajue kwamba 

sina mapenzi naye? Lazima nifanye juu 

chini ili niweze kuachana na 

ye.Natakaniwe huru na tamia.Sitaki 

kuendelea kujificha wakati mimi na 

Tamia tunapendana.Najua ni jambo gumu 

kulifanya lakini hakuna namna nyingine 

ya kufanya .Ili niwe huru lazima niweke 

wazi hili suala.Lazima niuvunje uhusiano 

wangu na Pauline” akawaza David na 

safari ikaendelea hadi walipofika katika 

hoteli moja nzuri mpya.Haikuwa kubwa 

sana lakini ilikuwa ni nzuri na ya 

kuvutia.Tamia akasimamisha gari 

wakashuka akamuomba David 

amfuate.Wakapita mapokezi Tamia 

akasalimiana na dada mmoja wa 

mapokezi halafu akapewa ufunguo na 

kisha wakafuata ujia ulioelekea 

vyumbani.Tamia akafungua chumba namba 24 wakaingia.Kilikuwa ni chumba 

kizuri sana chenye kitanda kizuri ,choo na 

bafu. 

 “ Tumekuja kufanya nini hapa” 

akauliza David 

 “ Nimekuleta hapa ili unipe zawadi 

yangu in private”akasema Tamia na 

kumsukuma David akaangukia kitandani 

halafu akavua gauni lake na kulitupa chini 

akabakiwa na nguo ya ndani akamrukia 

David kitandani 

 “ David nilijua pale nyumbani 

kwangu kutakuwa na watu wengi leo kwa 

hiyo hatutaweza kuwa na faragha na mimi 

ninakutamani hivyo nikalazimika 

kuchukua chumba hiki ili nije nifurahi 

nawe.David nina hamu sana nawe na 

siwezi kuendelea kusubiri.Please take me 

to the moon”akasema Tamia huku 

akimvua David koti.David naye alionekana 

kuzidiwa sana akavua shati lake haraka 

haraka na bila kupoteza muda shughuli 

ikaanza. 

**************** 

 Mwalimu Lucy alimsimulia Robin 

historia ya maisha yake yote toka 

alikotoka hadi alipo sasa.Ilikuwa ni histora yenye kuhuzunisha sana.Mara 

kadhaa ilibidi kukatisha simulizi yake 

kutokana na kushindwa kujizuia kulia. 

 “ Pole sana Lucy.”akasema Robin 

baada ya mwalimu Lucy kumaliza 

kumsimulia historia ya maisha 

yake.Historia iIe ilimchoma sana Robin. 

 “ Kwa hiyo ndiyo hivyo Robin.Maisha 

yangu yako namna hiyo.Unaponiona sina 

furaha ni kwa sababu ya maisha 

niliyoyapitia.” 

 “ Pole sana Lucy.Kwa kweli umepitia 

mitihani mingi sana lakini Mungu 

hajakuacha na kwa sasa amekuinua na 

wale wote waliokudharau wakati 

ule,wakakunyanyasa wakati huo hivi sasa 

wanakuheshimu kwa sababu Lucy wa sasa 

si yule Lucy waliyemdhallisha miaka 

ile”akasema Robin 

 “ Ni kweli Robn.Baada ya maisha 

yangu kuwa mazuri niliamua kurejea 

Tanzania kwa madhumuni mawili 

tu,kumtafuta mwanangu Angela na 

kulipiza kisasi kwa watu walionitenda 

vibaya.Mpaka sasa hivi hakuna hata lengo 

moja kati ya hayo mawili 

nililolitimiza.Sijalipiza kisasi bado na wala 

mwanangu sijampata” akasema Lucy  “ Ulifanya jitihada zozote za kuulizia 

kuhusu Angela katika kile kituo ulikoenda 

kumuweka usiku ule?akauliza Robin 

 “Hapana mpaka sasa hivi bado 

sijapata nguvu ya kuweza kufika pale na 

kuuliza.Ninaogopa sana kuufahamu 

ukweli.Ninaogopa sana ni vipi iwapo 

mwanagu alifariki usiku ule kwa kuliwa 

na wanyama kama mbwa au paka? 

Ninaogopa sana Robin na ndiyo maana 

mpaka leo hii unaniona sina amani hata 

kidogo” akasema Lucy.Robin akamimina 

mvinyo katika glasi akanywa kidogo 

halafu akasema 

 “ Lucy nitakusaidia kumtafuta 

mwanao.” 

 “ unasemaje Robin?akauliza Lucy 

akitaka Robin arudie tena kutamka kile 

alichokitamka 

 “ Nimesema nitakusaidia kumtafuta 

mtoto wako Angela.Nitakushika mkono 

katika hili na nitakusaidia kuufahamu 

ukweli kama mwanao ni mzima ama 

alifariki na kama ni mzima yuko wapi? 

Akasema Robin 

 “ Ouh Robin ,nashukuru sana .Sijui 

hata niseme nini “ 

 “usiseme chochote Lucy.Wewe ni 

rafiki yangu na siku zote marafiki husaidiana katika matatizo.Tatizo lako ni 

la kwangu kama vile ambavyo tatizo langu 

linaweza kuwa la kwako.Mwanangu 

Penina unamlea kama mwanao kwa nini 

basi na mimi nisijiunge nawe katika 

kumtafuta mwanao? Usijali Lucy 

tutamtafuta Angela na 

utampata.Nakuhakikishia kwamba kama 

yuko hai basi tutampata tu” akasema 

Robin.Mwalimu Lucy akashindwa 

kuyazuia machozi kumtoka.Robin 

akainuka akachukua kitambaa na kumfuta 

machozi 

 “ Imetosha Lucy.usilie tena .Umelia 

sana usiku wa leo wakati ni siku ambayo 

ulitakiwa uwe na furaha kubwa.Tafadhali 

nyamaza kulia” akasema Robin 

 “ Robin kwa kweli ninashindwa 

kujizuia kulia kwa sababu kuna mambo 

ambayo Mungu ananifanyia ambayo 

sikuyatarajia kabisa.Sikuwa nimefikiria 

kumweleza ukweli wa maisha yangu mtu 

yeyeote yule lakini leo hii nimekueleza 

wewe na umejitolea kwa moyo mmoja 

kunisaida kumtafuta mwanangu 

Angela.Ahsante sana Robin kwa msaada 

huu lakini kuna jambo ambalo ninataka 

kukuuliza”  “ Uliza Lucy usiogope”akasema 

Robin.Lucy akafuta machozi akanywa 

wine kidogo kisha akauliza 

 “ Nimekueleza ukweli wangu na 

sijakuficha hata kitu kimoja.Ni historia 

chafu sana ambayo ninaona aibu 

kumweleza mtu yeyote.Baada ya 

kuifahamu historia yangu na mambo yote 

machafu niliyoyafanya na niliyofanyiwa,do 

you hate me? Akauliza mwalimu 

Lucy.Robin akanywa funda kubwa la 

mvinyo akamtazama mwalimu Lucy kisha 

akasema 

 “ No ! I don’t hate you” akasema 

mwalimu Lucy. 

 “ Are you sure? akauliza Lucy 

 “ Yes I’m sure.There is no any reason 

to hate you”akasema Robin halafu 

akanywa tena funda moja la mvinyo 

 “Mimi na mke wako wote tuko katika 

chungu kimoja wote tulikimbia 

watoto.Wote hatuna sifa za kuitwa 

mama.Kwa nini usinichuke na mimi pia 

Robin? Akauliza Lucy 

 “ Lucy ,mazingira yako na Vivian ni 

tofauti sana.Vivian alimkimbia mtoto 

wake bila kuwa na sababu ya kufanya 

hivyo.Alifanya hivyo kwa sababu ya tamaa 

zake.Wewe hukuwa na kitu chochote wakati huo hukuwa na kazi ,hukuwa na 

sehemu ya kuishi,hukuwa na chakula cha 

kumlisha mtoto na ndiyo maana ukafanya 

vile.Simaanishi kwamba ulifanya vizuri 

lakini hukuwa na namna nyingine ya 

kufanya kwa wakati ule.Kwa hiyo siwezi 

kukulinganisha na Vivian na wala siwezi 

kukuchukia.” Akasema Robin 

 “ Robin nimekosa neno la 

kusema.Sijawahi kukutana na mtu 

mwenye roho nzuri kama 

wewe.Ninashukuru sana kukufahamu” 

akasema mwalimu Lucy 

 “Lucy katika haya maisha tunapitia 

mitihani mingi sana .Binafsi nimepita 

mitihani mingi na nimejifunza mambo 

mengi kwa hiyo ninaelewa pale mwenzako 

anapokwambia kwamba ana shida ana 

maanisha nini na ndiyo maana kwa moyo 

mweupe kabisa nitakusaidia kumtafua 

Angela na tutampata.Ninataka uwe na 

furaha na tabasamu katika maisha yako 

na Mungu akipenda siku moja utaufungua 

tena moyo wako na utapenda tena” 

akasema Robin na kumfanya mwalimu 

Lucy atabasamu 

 “ Robin suala la kupenda tena siwezi 

kusema kwamba sintapenda lakini 

ninahisi itanichukua muda kidogo ili kumpata yule ambaye nina hakika 

hatayakwangua makovu ya vidonda 

vyangu vya nyuma,yule ambaye atanifanya 

niwe na tabasamu hadi siku ninaingia 

kaburini,yule ambaye atayatoa maisha 

yake kwa ajili yangu.Yule ambaye kila 

mshipa wa mwili wake utakuwa umejaa 

jina langu.Sina hakika kama bado wapo 

wanaume wa namna hiyo katika dunia ya 

leo.”akasema mwalumu Lucy na kumfanya 

Robin acheke kicheko kikubwa 

 “ Dunia hii bad ina watu wengi wema 

na wazuri wenye sifa zaidi ya hizo 

ulizozitaja.Ninaamini siku moja 

utaufungua moyo wako tena na nitafurahi 

sana kukuona ukiwa nafuraha “.akasema 

Robin 

 “ Kwa muda mrefu tumekuwa 

tukiongelea kuhusiana na masuala yangu 

na historia yangu mbaya na wewe 

unaweza ukanieleza historia yako ? 

akauliza Mwalimu Lucy.Robin akachukua 

glasi yake na kugugumia pombe yote 

liliyokuwamo katika glasi halafu 

akamimina tena pombe nyingne katika 

glasi akapiga tena funda moja 

*********************  David alkuwa alikuwa anatiririkwa 

na jasho jingi baada ya kumaliza 

mzunguko mmoja.Wote wawili walikuwa 

hoi kutokana na kila mmoja kuwa na 

hamu sana na mwenzake 

 “ Hiki ndicho nilichokuwa 

nikikitafuta.Kukutana na mwanaume 

ambaye nikifanya naye mapenzi 

natosheka na sihitaji tena.Sijui nifanye 

nini ili kumfanya David asije akamuona 

mwanamke mwingine zaidi yangu.Nataka 

anione mimi tu.Nataka Akili yake yote iwe 

kwangu tu. Akawaza Tamia 

“ Lakini kitu kikubwa ninachoweza 

kukifanya ili kumdhibiti David ni kwa 

kumpa mapenzi ya hali ya juu na ndiyo 

yatakayomfanya asione tena mwanamke 

mwingine zaidi yangu.Huo ndio uchawi 

pekee ninaoweza kuutumia kumroga 

David asione wala kusikia mwanamke 

mwingine” Akawaza Tamia halafu 

akainuka akajifunga taulo na kuichukua 

simu yake akamfuata David pale kitandani 

akamsogelea halafu akajipiga picha huku 

akimbusu. 

“ Tamia natamani sana kama 

ningepata nafasi ya kulala nawe kwa usiku 

mzima .Mambo unayonionyesha yananifanya nitake tena na tena” akasema 

david 

“kwani kuna ubaya gani David 

tukilala hapa hadi asubuhi? Hata mimi 

ninatamani sana kama tungelaa hapahadi 

asubuhi.Nyumbani kwangu kuna watu na 

sihofii chochote” 

“ Haitawezekana Tamia.Nimeondoka 

na funguo za gari na Endapo Pauline 

akitaka kuondoka hawezi kufanya hivyo 

mpaka anisubiri ” akasema David 

 “Nimekwisha kwambia kwamba 

usimuwaze Pauline.Kwa nini hutaki 

kumueleza ukweli kuhusiana na sisi 

kwamba ni wapenzi? Ninaona kama 

ameanza kuwa kero kubwa kwetu” 

akasemaTamia 

 “ Usijali nitalifanyia kazi hilo 

suala.kwa sasa twende tukaoge halafu 

tuondoke nikamuwahi Pauline”akasema 

David wakainuka na kwenda kuoga 

ingawa Tamia alipenda sana waendelee 

kukaa pale.Baada ya kuoga wakaondoka 

kurejea katika sherehe.Walipokuwa njiani 

David akamuomba Tamia wanunue 

vinywaji iliwatakapoulizwa walikokuwa 

waseme kwamba walikuwa wamekwenda 

kununua vinywaji  Walifika nyumbani kwa Tamia,bado 

kuna watu waliendelea kuburudika na 

vinywaji. Tamia akapitiliza moja kwa moja 

ndani na David akaenda sehemu ya 

sherehe.Alikuwa na wasi wasi 

mwingi.Baada ya kama dakika sita Pauline 

akamfuata. 

 “ twende tuondoke “ akasema 

Pauline ambaye alikuwa na uso 

uliokunjamana kwa hasira 

 “ Pauline mbona umekasirika hivyo? 

Kulikoni? Akauliza David 

 “ David usitake kunichafua zaidi 

naomba tuondoke” akasema 

Pauline.David akaamua kuinuka 

 “ Subiri kidogo nikamuage 

Tamia.Hatuwezi kuondoka bila kumuaga “ 

akasema David 

 “Nimekwambia hapana 

David.Twende tuondoke haraka 

sana.Hakuna kuonana na huyo 

kahaba”akafoka Pauline.Wakaingia garini 

David akaendesha gari wakaondoka 

 “ Ulikwenda wapi na yule 

kahaba?akauliza Pauline Pauline wakiwa 

garini 

 “ Pauline naomba usimuite Tamia 

kahaba.Hastahili kuitwa hivyo.Makahaba ni wale wanaofanya biashara ya kuuza 

miili yao na si Tamia”akasema David 

 “ Ni kabaha yule.Mimi ndiye 

ninayemfahamu kuwa ni kahaba yule 

mwizi wa mabwana za watu.kwa nini 

unamtetea? Alikupeleka wapi? Akauliza 

Pauline kwa ukali 

 “ Pauline tulikwenda kununua 

vinywaji” akajibu David 

 “ David mimi si mtoto mdogo. 

Niliwaona kila kitu 

mlichokifanya.Nilikuonya kwamba usije 

ukanidanyanga mimi” akasema Pauline 

 “ kwa nini nikudanganye Pauline? Ni 

kweli tulikwenda kufuatilia vinywaij 

naomba uniamni” 

 “ Ahsante sana David.Unadiriki 

kunidanganya hata mimi?!!... 

 “ Sikudanganyi Pauline” akasema 

David halafu safari ikaendelea kimya 

kimya. 

Walifika nyumani na bila kusemeshana 

kila mmoja akaelekea chumbani kwake 

 Kitu cha kwanza alichokifanya 

Paulne alipoingia chumbani kwake ni 

kuchukua simu yake na kuandika jumbe 

mfupi 

 “ Wewe kahaba nitumie lugha gani 

kukukataza usimsogelee David? Hujui David ni mpenzi wangu? Niongelee wapi ili 

unielewe? Ninakupa onyo la mwisho wewe 

mdandia mabwana za watu achana kabisa 

na David ama sivyo nitakufanya kitu 

kibaya….” 

 Pauline akautuma ujumbe ule kwa 

Tamia na baada ya dakika mbili Tamia 

akamtumia picha akiwa na David 

kitandani wamekubatiana wakibusiana 

bila ujumbe wowote.Pauline alishidnwa 

kuvumilia akatoka mbio akiwa amefura 

kwa hasira hadi katika mlango wa David 

na kuufungua kwa nguvu akaingia ndani 

David aliyekuwa amejilaza kitandani 

alistuka sana baada ya kumoana Pauline 

akiingia mle chumbani kwa kasi ya ajabu. 

 “ Pauline ?! akasema David na 

kuinuka kitandani 

 “ Pauline kulikoni hadi ukaingia 

chumbani kwangu namna hiyo? Huwezi 

kubisha hodi? Akauliza David ambaye 

alionekana kuchukizwa na kitendo kile 

cha Pauline kuingia mle chumbani kwake 

bila hodi.Uso wa Pauline ulikuwa 

umejikunja kwa hasira akamtazama David 

kwa macho makali sana. 

 “ Pauline kulikoni? Mbona hivyo? 

Kuna tatizo gani? Akauliza David naye akimshangaa Pauline kwa namna 

alivyokuwa amekasirika 

 Pauline akaendelea kumuangalia 

David huku machozi yakimtoka .David 

akamsogelea 

 “ Pauline hebu niambie kuna tatizo 

gani? Kitu gani kimekuchukiza namna 

hiyo? Kama ni suala la kuondoka na Tamia 

kule kwenye sherehe nimekwisha 

kwambia kwamba tulikwenda kufuatilia 

vinywaji.Naomba unielewe” akasema 

David na kutaka kumshika Pauline mkono 

 “ Don’t touch me !! akasema Pauline 

kwa ukali. 

 “ Pauline kuna nni? Akauliza David 

 “ naomba usinishike tafadhali.” 

Akasema Pauline huku akilia.David 

akamtazama na kushindwa kuelewa nini 

kilichomtokea Pauline. 

 “ Hiki nini? Akauliza Pauline na 

kumpatia David simu akamuonyesha 

picha aliyotumiwa na Tamia.David 

akaduwaa na kushindwa ajibu 

nini.Midomo ilikuwa inamcheza 

 “ Nakuuliza David hiki nini ? Mbona 

hunijibu? akauliza tena Pauline kwa 

ukali.David akabaki ameishika ile simu 

akakosa la kusema.Hakuwa na maelezo ya 

kutoa kwani picha ile ilijieleza wazi.Yeye na Tamia walionekana wakiwa kitandani 

wakibusiana na ilionyesha wazi kwamba 

walikuwa katika mahaba mazito sana. 

 “ David umekosa cha kunijibu? 

Akauliza Pauline 

 “ Pauline uhhmm.!! I can explain this 

“ akasema David na mara Pauline 

akamvamia na kuanza kumpiga makofi 

 “ You cant explain anything you 

pig!!..akasema kwa ukali huku akiendelea 

kumpiga David makofi 

 “ You lied to me !..why you did that 

David?akasema Pauline kwa hasira na 

mara David akamshika mikono 

 “Stop this Pauline..!!Stop..! akasema 

David kwa ukali na kumshika Pauline kwa 

nguvu 

 “ Shetani mkubwa wewe kwanini 

ukanidanganya? Mimi ndiye niliyekutoa 

vumbi na kukupendezesha lakini leo hii 

umekuja kunisaliti? Kwa nini huna 

shukrami wewe nyani? Umekosa nini 

kwangu hadi ukaangukia katika mikono 

ya yule kahaba? Nambie umekosa nini 

kwangu? Kuna kitu umeniomba 

nikakunyima? Akauliza Pauline kwa ukali 

na maneno yale yakamkera sana David 

 “ Niambie wewe shetani usiyekuwa 

na makao ni kwa nini ukanisaliti na yule kahaba wakati nilkwisha kutahadharisha 

mapema kuhusu tabia zake? Kwa kuwa 

umenisaliti na kuniona mimi sifai basi 

nakwambia utahama humu na kwenda 

kuishi kwa huyo nyani mwenzako 

anayewapanga wanaume kila siku.” 

Akasema Pauline na kuzidi kumchafua 

David 

 “ Enough Pauline!!.Enough 

!!..akasema David kwa hasira 

 “Nimekuvumilia sana Pauline na 

sintavumilia hata tusi moja tena.” 

Akasema David kwa ukali 

 “kwani utanifanya nini? Utanipiga? 

 “ Ukitaka kujua nitakufanya nini 

jaribu kunitukana tena nikuoyeshe 

kazi.Usinitukane na kunidharau kwa 

sababu tu ya hizi mali zenu.Hunifahami 

mimi ni nani na nimetokea wapi kwa hiyo 

naomba usinitukane kwa sababu ya 

utajiri wa baba yako.” 

 “ lazima nikutukane 

David.Umenisikitisha sana.Mambo yoye 

haya niliyokufanyai lakini bado 

hukutosheka na ukanisaliti.Bora 

ungenisaliti na mwanamke mwingine 

lakini si Tamia.Kwa nini ukanifanyia hivi 

David? Kitu gani ulikikosa kwangu wewe mkosa shukrani? Bado Pauline aliendelea 

kufoka 

 “ I love her!...akasema David kwa 

ukali 

 “ Unasemaje?! Akauliza Pauline 

 “ Si unataka nikwambieukweli ? 

Ninampenda Tamia sana na ndiye 

mwanamke pekee ambaye moyo wangu 

unamuhitaji.Awe kahaba asiwe kahaba 

ninampenda na nitakuwa naye na hakuna 

yeyote ambaye atanitenganisha naye” 

akasema David kwa ukali. 

 “ So you lied to me!! Everything you 

told me were all lies ?!akauliza Pauline 

 “ Yes I lied to you.I don’t love you and 

I will never love you so leave me and 

Tamia alone” akasema David na Pauline 

akashindwa kuvumilia akatoka chumbani 

akilia 

 Mara tu Pauline alipotoka mle 

chumbani kwa David mlango 

ukafunguliwa akaingia Vicky 

 “ David what happened? Kumetokea 

nini ? Nikiwa ghorofani nimesikia 

mnakwaruzana na Pauline.Nini 

kimetokea? akauliza Vicky 

 “ Wewe ndiye chanzo cha haya yote 

.Wewe ndiye uliyenishawishi mimi 

nianzishe mahusiano na Pauline na ndiyo maana haya yote yametokea” akasema 

David kwa ukali. 

 “Shhhhhhhhhhhh ! david unaongea 

mambo gani hayo? Tafadhali usiongee 

hivyo kuna watu wanaweza wakasikia 

.Tafadhali ongea taratibu” 

 “ I don’t care !!..akasema david 

“wasikie wasisikie mimi sijali mtu.” 

 “David please naomba uniambie ni 

kitu gani hasa kimetokea kati yako na 

Pauline? akauliza Vicky 

 “ Sina muda wa kutoa 

maelezo.Mfuate huyo huyo Pauline 

atakaueleza kila kitu.Mimi sina kitu cha 

kukueleza”akasema David huku 

akilifungua kabati lake na kuanza 

kupangua nguo .Alikuwa amekasirika sana 

 “ David unafanya nini? Akauliza 

Vicky 

 “ Wenye nyumba yao hawataki 

niendelee kukaa hapa.Nimedhalilishwa 

sana na Pauline na siwezi tena kuvumilia 

matusi haya makubwa 

aliyonitukana.Nitaondoka” Akasema 

David 

 “ David tafadhali usifanye hivyo 

unavyotaka kufanya.Usifanye maamuzi ya 

haraka namna hiyo NI vipi sasa kuhusu 

mipango yetu? Ukiondoka ina maana kila kitu chetu kitakuwa kimevurugika.Please 

David usifanye hivyo tafadhali.Mzee 

Zakaria anakutegemea sana wewe.Achana 

na Pauline lakini muonee huruma yule 

mzee hana mtu wa kusimamia biashara 

zake.” 

 “ Mzee Zakaria atanisamehe sana 

lakini huu ni uamuzi wangu na hakuna 

anayeweza kuubadili.Lazima niondoke 

katika nyumba hii” akasema David.Vicky 

akamtazama David halafu akatoka na 

kumfuata Pauline aliyekuwa akilia 

chumbani kwake 

 “Pauline nini kimetokea? Akauliza 

Vicky lakini Pauline hakuweza kumjibu 

alikuwa analia 

 “ Niambie Pauline nini kimetokea? 

Kitu gani kimewafanya mkakwaruzana na 

David? Tafadhali naomba uniambie” 

akasema Vick.Pauline akachukua simu 

yake na kumuonyesha Vicky picha 

aliyopiga David na Tamia 

 “Huyu ni Tamia ! Vicky akastuka 

sana 

 “ David anatembea na Tamia.David 

amenisaliti na yule kahaba”akasema 

Pauline huku akiendelea kulia 

 “ Dah ! David amefanya mambo gani 

tena? Nilimuonya kuhusiana na Tamia lakini hakutaka kunisikia Ona sasa kila 

kitu kimeharibika.Nisipokuwa makini 

hapa kila kitu kitaharibika.Lazima nifanye 

kitu” Akawaza Vicky na kumuinamia 

Pauline 

 “ Pauline naomba unisikilize.” 

 “ma mdogo sitaki kusikia mtu yeote 

yule.David amenifanyia kitendo cha 

kikatili sana na sitaki kabisa kumuona 

machoni pangu” akafoka Pauline 

 “ Pauline hebu 

nisikilize.Ninamfahamu vizuri David ni 

lazima atakuwa alishawishiwa na yule 

mwanamke na hakufanya kitendo hiki 

kwa ridhaa yake.Hata picha yenyewe 

inaonyesha wazi kwamba hakuwa 

amekifurahia kitendo hiki.Tamia alipiga 

makusudi picha hii ili kukurusha roho na 

alichokuwa anakitaka amekipata.lengo 

lake lilikuwa kuumiza na kukutenganisha 

na David .Usimpe Tamia nafasi hiyo 

.Wanaume kama David ni wachache sana 

kupatikana katika hii dunia.” 

 “ ma mdogo ni heri kukaa bila kuwa 

na mwanaume kuliko kuwa na nyoka 

kama david .nimemchukia sana david na 

sitaki hata kumuona tena.” 

 “ usiseme hivyo Pauline.David 

anakupenda sana na nina imani hata wewe toka ndani ya moyo wako 

unampenda sana David.Hivi tunavyoongea 

david anapakia mizigo yake kwa ajili ya 

kuondoka.Tafadhali usikubali David 

aondoke.Hutapata mwanaume kama 

yeye.” 

 “Nimekwisha sema simtaki David 

,Sitaki kumuona hapa nyumbani.Kama 

anaondoka basi aondoke tu mimi sijali 

kitu”akasema Pauline kwa ukali 

 “ Pauline najua kwa sasa una hasira 

lakini naomba usiache David aondoke 

hapa.Mzee Zakaria bado anamuhitaji sana 

.Tafadhali naoma usimpe wakati mgumu 

baba yako kwani anamtegemea sana 

David” akasemaVicky na kutoka mle 

chumbani akarejea chumbani kwa 

David.Bado David alikuwa akiendelea 

kupakia nguo zake katika sanduku 

 “ David tafadhali nakuomba tena 

usifanye hivyo unavyotaka kufanya.Hata 

kama Pauline amekuudhi ,amekutukana 

lakini muonee huruma mzee 

Zakaria.Anakuhutaji sana Yule mzee na 

hana mtu mwingine ambaye anaweza 

akamuamini kama alivyokuamini wewe 

.Tafadhali David hebu punguza hasira na 

usifanye maamuzi kwa pupa.Mimi ushauri 

wangu nui huo kwmaba kaa na fikiria uipya unachotaka kukifanya” Akasema 

Vicky na kutoka mle chumbani.David 

akaacha zoezi lile la kupakia nguo katika 

sanduku akakaa kitandani 

akitafakari.Maneno aliyoambiwa na Vicky 

yalimuingia na kumchoma sana. 

 “ Madam Vicky anaweza kuwa 

sahihi.Mzee Zakaria ananipenda sana na 

ananitegemea sana katika biashara 

zake.Kama nikiondoka mzee huyu atapata 

taabu sana.” Akawaza David 

 “ Nadhani natakiwa nipunguze 

hasira na kutofanya maamuzi kwa 

kukurupuka.Sipaswi kumlaumu mtu 

katika hili.Ni mimi mwenyewe ndiye wa 

kulaumiwa katika suala hili kwani 

nilikuwa mjinga na kumkubalia madam 

Vicky kuhusiana na mipango yake na haya 

ndiyo matokeo yake.Lazima nikubali 

kwamba nimekosea na nilazima 

nirekebishe makosa yangu na 

kurekebisha si kwa kuchukua maamuzi ya 

haraka ya kuondoka.Mzee Zakaria bado 

ananihitaji sana.” Akawaza David 

akalitazama begi alilokuwa akipakia nguo 

zake 

 “ Hapana sintaondoka.Nitabaki hapa 

hapa na hata kama ni kuondoka lazima 

nipate kwanza ruhusa ya mzee Zakaria kwani hii ni nyumba yake na yeye ndiye 

mwenye maamuzi ya mwisho.Lakini kama 

sintaondoka nitawezaje kuishi nyumba 

moja na Pauline baada ya tukio hili? 

Tutawezaje kutazamana usoni? Tutaishi 

ndani ya nyumba moja kama maadui? 

Hapana hapa ni nyumbani kwao na 

sitakiwi kuwa kikwazo .Hatuwezi kukaa 

nyumba moja na Pauline .Hapa hakuna 

ujanja lazima mimi niondoke lakini kabla 

ya kuondoka lazima kwanza niongee na 

mzee Zakaria na nimueleze ukweli wa 

kuhusiana na jambo hili ii hata kama ni 

kuondoka basi niwe nimeondoka kwa 

amani.Haitapendeza kama akisikia jambo 

hili toka kwa mtu mwingine” akawaza 

David na kuchukua tena nguo zake 

akazirudisha kabatini na kupanda 

kitandani akachukua simu na kumpigia 

Tamia 

 “ David I’m sorry” akasema Tamia 

 “ Hapana wala hujafanya vibaya 

Tamia” 

 “ Sikupaswa kufanya vile.Sikupaswa 

kumtumia Pauline ile picha.” 

 “ Umefanya vizuri sana Pauline 

kwani kwa sasa tuko huru.Hakuna kitu 

cha kuogopa tena.” 

 “ Nini kimetokea huko David?  “ Kumetokea mvurugano kati yangu 

na Pauline na hakuna maelewano 

tena.Nilifikiria kuondoka usiku huu hapa 

nyumbani kwao lakini nimeamua kusubiri 

hadi asubuhi niongee kwanza na mzee 

Zakaria na nimuage siwezi kuondoka bila 

kumtaarifu mzee huyu.” 

 “ David chochote 

kitakachotokea,njoo hapa nyumbani 

kwangu.Nyumba yangu ni ndogo lakini 

inatutosha sana.Tutaishi hapa kwa amani 

na raha mustarehe” 

 “ Nashukuru sana Tamia lakini hata 

kama nikiondoka hapa kwa mzee Zakaria 

siko tayari kuja kuishi hapo 

kwako.Maneno aliyonitamkia Pauline leo 

yamenifundisha jambo kubwa 

sana.Nahitaji kitu cha kwangu ” 

 “ David I’m not Pauline .Lakini hata 

hivyo ni wewe ndiye mwenye uamuzi na 

maisha yako “ 

 “ Ahsante sana kwa kunielewa 

Tamia.Nitawasikiana nawe 

kesho”akasema David na kukata 

simu.Maneno aliyoambiwa na Pauline 

yakaendelea kumjia kichwani akainuka na 

kufungua kabati lake 

 “ Nashukuru kwamba sikuweza 

kuzitupa nguo zile nilizotoka nazo gerezani.Hizi ndizo nitaondoka nazo 

kwani ndizo za kwangu.Hivi vingine vyote 

nimevipata hapa na lazima niviache hapa 

hapa.Siwezi kutukanwa hapa wakati 

nyumbani kwetu tuna utajiri mkubwa 

sana” akawaza David. 



Robin alimalizia pombe iliyokuwamo 

katika glasi yake halafu akainama 

chini.Mwalimu Lucy alijiuliza maswali 

mengi kuhusiana na kubadilika ghafla kwa 

Robin mara tu alipomtaka amsimulie 

historia ya maisha yake. 

 “ Robin kuna tatizo lolote? Mbona 

umebadilika ghafla? Is there anything 

wrong? Akauliza mwalimu Lucy,Robin 

akainua kichwa na kumtazama mwalimu 

Lucy kisha akasema 

 “ Lucy ,baada ya miaka mingi kupita 

umekuwa ni mtu wa kwanza kutaka 

kufahamu historia yangu” akasema Robin 

 “ Robin tafadhali kama hujisikii 

kunieleza usijali utanieleza hata siku 

nyingine ukiwa tayari”akasema Mwalimu 

Lucy  “ usijali Lucy nitakueleza japokuwa 

ni historia ambayo binafsi 

inanikumbusha mambo mengi ya huko 

nyuma ambayo nimekwisha kuyasahau” 

akasema Robin halafu akakaa kimya 

kidogo na kuendelea “ Nitakusimulia 

kwanza namna nilivyokutana na Vivian . 

Ilikuwa ni siku ya jumapili nilikwenda 

kumtembelea rafiki yangu Benard katika 

duka lake la madawa .Benard alikuwa ni 

rafiki yangu mkubwa ingawa kiumri na 

kielimu alikuwa amenizidi lakini tulitokea 

kuelewana sana na hakujali kama 

anatokea katika familia bora na mimi 

katikafamilia duni.Familia yake ilikuwa ni 

moja ya familia yenye kujiweza 

kimaisha.Baada ya kumaliza kozi yake ya 

ufamasia alikabidhiwa duka kubwa la 

dawa . 

Siku hiyo nilikwenda kuchukua 

fedha kwa Ben kwa ajili ya kulipia kodi ya 

pango kwani wakati huo nilikuwa 

nimepanga chumba baada ya shangazi 

yangu ambaye nilikuwa nikiishi kwake 

kuachana na mumewe.Sikuwa na kitu 

ndani zaidi ya godoro dogo na vitu 

vichache kama jiko n.k.Kipindi hicho 

ndiyo kwanza nimemaliza kidato cha sita 

na sikuwa na kazi wala ajira yoyote rasmi ya kuniingizia kipato cha kuniwezesha 

kuishi.Kilichokuwa kikinisiaidia kuweza 

kusukuma siku wakati nikisubiri matokeo 

yangu ni kwa kuwafundisha wanafunzi 

masomo ya ziada mtaani kwetu kwani 

nilikuwa nikizifahamu sana hesabu. 

 Benard alinikaribisha dukani kwake 

akanipatia kiti tukaanza maongezi 

yetu.Kitu kngien kilichonifanya nikawa 

karibu zaidi na Ben ni kwamba mimi ndiye 

niliyekuwa kuwadi wake.Alikuwa na pesa 

lakini hakuwa na uwezo wa kumtongoza 

mwanamke.Alikuwa muoga sana.Kila 

alipomtaka mwanamke Fulani basi mimi 

ndiye niliyekuwa nikiifanya kazi yote kwa 

kuwa sikuwa muoga na nilikuwa 

muongeaji sana. 

 Tukiwa pale dukani ,alikuja 

msichana mmoja akitafuta dawa Fulani 

alizokuwa ameandikiwa katika 

karatasi.Zilihtajka kwa haraka kwa ajili ya 

upasuaji wa babu yake.Dawa zile 

hazikuwepo pale dukani hivyo Ben 

akamuomba yule msichana kama hatajali 

azifuate nyumbani.Yule msichana 

akakubali kwa kuwa alikuwa amezunguka 

katika maduka kadhaa na 

kuzikosa.Kutoka pale dukani kwa Ben 

hadi nyumbani kwake si mbali sana.Alipanda gari lake mara moja na 

kwenda kuchukua hizo dawa.Mimi 

nilibaki pale dukani na yule msichana 

ambaye alikuwa ameiinamia simu yake na 

ilionyesha hakuwa akitaka maongezi na 

mimi.Nilikuwa mtundu sana nikaamua 

kumchokoza. 

 “ Babu anaumwa nini? Nikauliza na 

yule msichana akajifanya kama vile 

hakusikia swali nililomuuliza sikukata 

tamaa nikamuuliza tena 

 “ dada, babu anaumwa nini? 

Nikauliza na yule msichana akainua 

kichwa akanitazama na kunisaili kisha 

akasema 

 “ anatakiwa kufanyiwa upasuaji “ 

akajibu na kuinama akaendelea kuchati 

na simu yake.Sikumjali sana kwa 

kunidharau kwake kwani nilikwisha zoea 

dharau za namna ile.Nikamchokoza tena. 

 “ tatizo lake nini hasa hadi 

akafanyiwa upasuaji? Nikamuuliza 

 “ Ni uzee tu “ akajibu .Nikatabasamu 

nakutaka kumtwanga tena swali lingine 

simu yangu ikaita.Ilikuwa imechakaa na 

hata ilikuwa vigumu kusoma namba 

zake.Ben ndiye aliyenipigia simu 

 “ hallow’ nikasema baada ya 

kupokea simu  “ Robin, yule dada bado yuko hapo 

dukani? Akauliza 

 “ ndiyo” nikajibu kwa ufupi ili yule 

dada asije akagundua kwamba tulikuwa 

tunamzungumzia yeye 

 “ Umemuonaje ? 

akauliza.Ikanilazimu nitoke nje ili niongee 

naye vizuri 

 “ dah kile ni kifaa Ben.” nikasema 

 “ Unaweza ukanifanyia mchakato 

kwa hicho kifaa manake nilipomuona tu 

nimesisimka hadi kucha” Akasema 

.Nikaguna kidogo 

 “ Mmhh ! hii ngoma nzito Ben.Sina 

hakika kama ninaweza kufaulu lakini 

nitajaribu” nikasema 

 “ nakuamini sana Robin.Hakuna 

mwanamke anayeweza 

kukushinda.Tafadhali hebu nifanyie 

mchakato ili nimpate huyo 

mtoto.Amenisisimua mno.” 

 “ sawa nitajaribu.usikawie sana 

anaweza akaghairi na kuondoka.” 

Nikamwambia Ben halafu nikageuka 

kumtaza Yule msichana mle 

dukani.Alikuwa ni msichana mzuri 

mweupe mrefu aliyekuwa na nywele fupi 

alizoziweka katika mkao mzuri.Alikuwa ni 

msichana aliyebarikiwa uzuri wa kipekee.  “ Hapa kuna kazi” nikawaza na 

kuingia tena dukani. 

 “ Huyu jamaa amekwenda kuchukua 

hizo dawa wapi? Ninachelewa 

hospitali,wananisubiri mimi ” akasema 

yule dada. 

 “ Usijlai dada,nyumbani kwake si 

mbali sana .Ni hapo mtaa wa pili” 

nikasema na kuanza kutafuta namna 

nitakavyomuingia yule dada.Kwa kweli 

mimi na yeye tulikuwa ni watu madaraja 

tofauti sana lakini kwa ajili ya 

kumfurahisha Ben ilinilazimu kubuni njia 

ya kuweza kumuingia. 

 Ben akarejea na kumpatia Yule dada 

zile dawa.Wakati akijiandaa kutoka 

nikamuwahi 

 “ dada unaelekea wapi? nikamuuliza 

 “ Ninaelekea St Monica hospital” 

akajibu 

 “ Na mimi naelekea njia hiyo hiyo 

,unaweza ukanisaidia usafiri ukaniacha 

pale Kashuo Electornics ? nikamuomba 

 “ hakuna shida twende” akajibu 

nikamuaga Ben na kuingia ndani ya 

gari.Lilikuwa ni gari zuri la kfahari 

lililonukia harufu nzuri ajabu.Msichana 

yule akaliondoa gari na hakuwa akitaka 

kuongea chochte na mimi.Tulifika katika bara bara ya Maraba tukanasa katika 

foleni.Msichana yule akaonekana 

kuchaganyikiwa.Hakujua afanye nini na 

foleni haikuwa ikisogea.Hakuwa na ujanja 

tena,hatukuweza kwenda mbele wala 

kurudi tulikotoka.Niliamua kuitumia 

vyema nafasi ile.Nilifungua mlango wa gari 

na kutoka nje nikaangalia msururu ule 

mrefu wa magari kumbe kwa mbele 

kulikuwa na ajali kubwa imetokea na 

askari wa usalama barabarani walikuwa 

wanaendelea na vipimo.Nikarejea garini 

 “ Dada kuna ajali imetokea kule 

mbele kwa hiyo gari haziendi hadi askari 

wamalize kupima.’ 

 “ Ouh Mungu wangu nitaondoka saa 

ngapi hapa na mimi natakiwa niwahishe 

dawa hospitali babu anatakiwa 

akafanyiwe upasuaji? Akasema yule 

msichana 

 “ kwani ni hospitali gani amelazwa 

babu yako? 

 “ Amelazwa St Monica 

hospital.”akasema. 

 “ Nipatie hizo dawa nikusaidie 

kuziwahisha.” Nikasema na kumfanya yule 

dada aniangalie kwa mshangao 

 “ Mbona unaniangalia hivyo 

huniamini? Nataka nikusaide.kuwahisha hizo dawa hospitali.Hapa hutaondoka sasa 

hivi.kama huniamini nakuachia hiki hapa 

kitambulisho changu na endapo dawa 

zako zikipotea basi itakuwa rahisi kwako 

kunitafuta.” Nikamwambia .Akafikiri 

kidogo kisha akasema 

 “ Utapita njia gani? 

 ‘ Nikatisha pale uwanja wa mpira 

kisha nitashuka pale sheli na kuchukua 

piki piki hadi hosptali.Nitafika ndani ya 

dakika ishirini” nikamwambia na kisha 

akanipatia dawa na kunielekeza wadi 

aliyolazwa babu yake nikamrushia 

kitambulisha changu na kutoka mbio 

nikimuacha dada Yule akishangaa. 

 Ndani ya dakika kumi na tano tayari 

nilikwisha fika katika hospitali hiyo 

alikolazwa babu yake na nikazikabidhi 

dawa.Niliwakuta watu kadhaa pale na 

nikasaidiana nao katika kumuandaa yule 

babu kwa upasaji kwani walihitajika 

wanaume wenye nguvu kwa kumshika 

mzee yule aliyekuwa machachari sana na 

hakutaka kuingizwa katika chumba cha 

upasuaji.Tulifanikiwa kumdhibiti na 

akaingizwa katika chumba cha upasuaji 

.Sikuondoka niliendelea kukaa na watu 

wale nikimsubiri yule msichana afike na 

anipatie kitambulisho changu.Saa moja za jioni ndipo msichana yule alipofika 

hospitali.Alikuwa amechoka 

sana.Aliwaeleza wazazi wake kilichotokea 

na wote wakanishukuru sana.Niliendelea 

kukaa nao pale hadi ilipotimu saa tatu za 

usku na ndipo nilipowaaga kwamba 

ninaondoka.Msichana yule akasema 

kwamba atanipeleka hadi 

nyumbani..Niliendelea kukaa nao pale 

hospitali hadi saa nne za usiku na kisha 

yule dada akanipeleka nyumbani.Tayari 

tulikuwa marafiki na hakuwa tena na zile 

dharau .Kitendo nilichomfanyia kilimgusa 

sana na kumbadili kabisa.Njiani aliniuliza 

maswali mengi kuhusiana na maisha 

yangu na kama nina kazi au 

sina.Nilimweleza kila kitu bila kumficha 

kwamba sina kazi na ndiyo kwanza 

nmemaliza kidato cha sita.Alinifikisha 

nyumbani na kabla hatujaagana 

nilimchokoza 

 “ Lini tutaonana tena? 

Nikamuuliza.Akafikiri kidogo na kusema 

 “ Tunaweza kuonana hata jumapili 

kama nitakuwa na nafasi.” Akachukua 

namba zangu za simu na kuahidi 

kunitafuta” 

 Wiki ya kwanza ilipita,ya pili ikapita 

na nilianza kukata tamaa kwamba pengine hatanipigia tena.Jumamosi ya wiki ya tatu 

toka tulipoonana akanipgia 

simu.Aliniambia kwamba kama nina 

nafasi ninaweza kuonana naye siku 

itakayofuata.Nilimweleza kwamba kuna 

mwenzangu ambaye nitaambatana naye 

akakubali na kusema kwamba hata yeye 

atamtafuta mwenzake mmoja ili tuwe 

watu wanne.Nilimtaarifu Ben suala lile 

akafurahi sana.Sikuwa na nguo ya maana 

ya kuvaa katika mwaliko ule mkubwa 

.Nguo zangu zilikuwa ni za kawaida na kuu 

kuu.Ben alinipeleka katika duka moja 

kubwa nikachagua suti nzuri na 

viatu.Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza 

kuwa na suti kali namna ile. 

 Jumapili iliwadia na saa kumi na 

mbili za jioni Ben akaja kunipitia 

nyumbani tukaelekea mahala ambako 

yule msichana alisema tukutane.Sisi ndio 

tuliotangulia na baada ya muda 

wakawasili yule msichana na mwenzake 

mmoja.Yule msichana alinishangaa sana 

kwa namna nilivyobadilika.Hakuamini 

kama ni mimi yule ambaye tulikutana siku 

ile. 

 Usiku ule tulikula na kunywa na 

ilipotimu saa nne za usiku Ben akatoa 

wazo twende kwenye muziki.Wote tukakubaliana na wazo lile na safari ya 

kuelekea katika muziki ikaanza . Yule 

msichana niliyekutana naye mara ya 

kwanza alikuwa akiitwa Martha na yule 

mwenzake aliyekuja naye alikuwa anaitwa 

Vivian au Flaviana kwa namna alivyokuwa 

amefanana na yule mwana mitindo wa 

kitanzania anayefanya kazi zake nchini 

Marekani Flaviana matata.Mimi na ben 

tulikuwa tukiwafuata nyuma 

wakituongoza kuelekea katika ukumbi wa 

burudani walioutaka wao. 

 Tulifika katika ukumbi wa burudani 

waliouchagua wale wasichana tukaingia 

,ben ndiye aliyekuwa akilipa gharama 

zote.Wakati tukiendelea na 

vinywaji,nilimuita Martha pembeni na 

kuongea naye kuhusiana na Ben.Alikuwa 

ni msichana mgumu sana lakini nilitumia 

kila aina ya ufundi na akakubali.Ulikuwa 

ni ushindi kwangu.Nilimfuata ben 

nikamfahamisha kwamba kila kitu tayari 

kwa hiyo anatakiwa akakae naMartha 

waongee na mimi aniache na Vivian.Hapo 

ndipo mahusino yangu na Vivian 

yalipoanza.” Robin akamimina tena 

mvinyo katika glasi akanywa kidogona 

kuendelea  “Kama ilivyokuwa kwa rafiki yake 

Martha,Vivian naye pia alitokea katika 

familia yenye uwezo lakini si mkubwa 

sana kama ile ya Martha.Alikuwa akiuza 

duka la mavazi lililomilikiwa na familia 

yao.Alikuwa ni msichana aliyependa 

matumizi makubwa na kila mwisho wa 

wiki alikuwa akitaka kwenda kupata 

chakula cha usiku sehemu 

aliyoichagua.Sikuwa na kipato wakati huo 

na Ben ndiye aliyekuwa akiniwezesha 

pesa ya kumuhudumia.Mahusiano yetu 

yaliendelea kustawi siku hadi siku. 

 Matokea ya kidato cha sita yalitoka 

na sikuwa nimepata daraja zuri la 

kuniwezesha kuendelea na chuo kikuu 

hivyo Ben akanishauri kwamba nijiingize 

katika biashara.Sikuwa na namna 

nyingine ya kufanya zaidi ya kukubaliana 

na mawazo yake.Alinikopesha mtaji wa 

biashara na nikaanza biashara ya 

mbao.Nilikuwa nafuata mbao mikoani na 

kuja kuziuza hapa Arusha.Biashara ile 

iliendelea kustawi sana na baada ya miaka 

miwili tayari nilikuwa nimekwisha lipa 

deni lote la Ben na nilikuwa na mtaji 

wangu mkubwa.Niliongeza juhudi sana 

katika biashara na mafanikio 

yakaongezeka.Nilifanikiwa kujenga nyumba mbili za kuishi,nikanunua magari 

mawili pamoja na kuongeza biashara.Kwa 

kuwa tayari nilikwisha jiweza kiuchumi 

nikaamua kufunga ndoa na Vivian na 

baada ya mwaka mmoja tukapata mtoto 

wetu ambaye ni Penina. 

 Shughuli zangu mimi zilikuwa ni za 

kusafiri sana mikoani kwenda kutafuta 

mbao na kuzileta Arusha .Mwaka wa pili 

baada tu ya kumpata Penina siku moja 

nilifuatwa nyumbani na watu wa benki na 

kupewa wiki mbili niwe nimelipa deni la 

mamilioni ya fedha.Nilikana kukopa fedha 

zile benki lakini walikuja na uthibitisho 

wa hati ya nyumba zangu zilizowekwa 

kama dhamana ya mkopo uliokopwa na 

mke wangu.Kumbe wakati niki wa katika 

safari za kibiashara mikoani mke wangu 

Vivi aliutumia mwanya huo kukopa 

mkopo mkubwa katika benki bila ya 

kunishirikisha.Alishindwa kuulipa mkopo 

ule na kwa kuwa aliweka dhamana ya 

nyumba, benki walilazimika kuzipiga 

mnada nyumba zangu mbili pamoja na 

magari mawili ili kufidia deni lao.Siwezi 

kuelezea namna nilivyoumia wakati 

ule.Nilikuwa nimerudi tena chini.Sikuwa 

na mbele wala nyuma.Nilireje akatika 

lindi la umasikini.Akiba ndogo niliyobaki nayo niliitumia kununulia kisehemu 

kidogo nikajenga nyumba ndogo ya kuishi. 

 “ Nakumbuka ilikuwa ni tarehe 11 

september siku Vivian alipoamua 

kuondoka na kuniacha mimi na 

Penny.Siku hiyo tulikwaruzana kidogo na 

akanitolea maneno ya kejeli na 

kuondoka.Bado ninayakubuka maneno 

yale alisema 

“ Don’t fool yourself that I love you 

Robin.I’ve never loved you .I married you 

not for love.I just wanted to enjoy life but 

five years with you its been a hell to 

me.Robin sijawahi kuwa na furaha nikiwa 

nawe hata siku moja.Hujawahi kunipa 

furaha zaidi ya karaha” 

 Vivian hakuishia hapo bali 

aliendelea kusema 

“Robin you are a worthless man I’ve ever 

seen in this world.Its better if you die 

because you have no any value in this 

world.Kosa kubwa nililolifanya ni 

kukuonyesha utupu wangu.Hukustahili 

kabisa kuuona utupu wangu mtu kama 

wewe.Nitakijutia kitendo hiki kwa miaka 

yangu yote hadi ninaingia

 kaburini.Ninakuacha na kwenda zangu na 

mara tu nitakapokiacha hiki kibanda chako 

naomba usijaribu kunifuatilia .To me you 

are dead already so I’ll never think of you”

 Hayani baadhi tu ya maneno ya 

kejeli na matusi aliyoyatoa siku 

anaondoka .Alisema maneno mengi na 

mengine siwezi kukwambia.Nilianza 

maisha mapya nikiwa na mwanangu 

Penina ,ikanilazimu kuanza kusoma kozi 

fupi ya utalii na nikaanza kuwapandisha 

watalii mlima Kilimanjaro .Nilitumia fedha 

niliyoipata kujiendeleza kielimu na katika 

safari hizo nilikuwa nikijenga mahusiano 

mazuri na wageni na nilifanikiwa kumpata 

mfadhili mmoja toka nchini Sweden 

ambaye alinisaidia na nikaweza kufungua 

kampuni yangu ya utalii na maisha yangu 

yakarejea upya katika mstari hadi hivi 

sasa.Ninamshukuru sana Mungu 

amenirejeshea vitu vile vyote vilivyopotea 

na zaidi.Toka siku ile alipoondoka Vivian 

sijawahi kumtia machoni nasikia aliolewa 

na bwana mmoja tajiri anaitwa Tino 

nasikia anafanya biashara ya kuuuza 

magari.   “ Unamzungumzia papaa Tino 

magari? Lucy akastuka

 “ Ndiyo wanamuita 

hivyo.Unamfahamu? ikamchukua zaidi ya 

dakika moja Lucy kujibu 

 “ Ndiyo ninamfahamu.Nilipotoka 

Marekani niliingia katika mahusiano ya 

kimapenzi na baadae alikuja kuniumiza 

vibaya sana.He’s an animal !..akasema 

Lucy kwa uchungu. 

“ Hii imekuwa ni bahati sana kwetu 

kukutana.Kumbe sote tumewahi 

kuumizwa na mtu mmoja? Mke wangu 

aliondoka nyumbani kwa sababu ya pesa 

za Tino kumbe na wewe aliwahi 

kukuumiza? Akauliza Robin 

 “ Ndiyo Robin.Tino aliwahi 

kuniumiza vibaya sana na kunifanya nizidi 

kuwachukia wanaume na mapenzi kwa 

ujumla” akasema mwalimu Lucy 

 “ Ilikuaje Lucy hadi ukajikuta katika 

mahusiano na Tino? akauliza Robin 

 “ Robin ,hata sikumbuki ilikuwaje 

hata nikajikuta nimeingia katika mapenzi 

na Tino.Msemo ule unaosema kwamba 

mapenzi ni upofu ni wa kweli 

kabisa.”akasema mwalimu Lucy na 

kuendelea  “ Robin nimekuelezea historia yangu 

kwa urefu na ninadhani sasa una uelewa 

mkubwa kuhusu mimi ni mtu wa namna 

gani na mambo gani nimepitia.Nilipoamua 

kuondoka Marekani na kurudi Tanzania 

dhumuni kubwa lilikuwa ni kuja 

kumtafuta mwanangu Angela.Nilipofika 

hapa nilikuwa nikihesabika miongoni 

mwa watu matajiri.Nilikuwa na fedha 

nyingi tu.Kitu cha kwanza nilichokuwa 

nikihitaji kukifanya ni kutafuta sehemu ya 

kuwekeza.Nilitaka nifungue vitega uchumi 

kadhaa hapa nchini.Siku moja nilikwenda 

katika ofisi ya uwekezaji na ndipo 

nilipokutana na Tino ambaye kwa wakati 

huo alikuwa akifanya kazi katika kituo cha 

uwekezaji.Alinipokea vizuri sana na 

kunielekeza fursa kadhaa za kuwekeza 

hapa Tanzania.Nilimweleza lengo langu la 

kutaka kuwekeza jijini Arusha.lengo langu 

la kutaka kuwekeza Arusha ni kwa sababu 

nina historia napo ,ndipo historia yangu 

ilipoanzia,pia nilitaka kulipiza kisasi kwa 

wale wote ambao walinitenda matendo 

mbaya kwa wakati ule ,wakaninyanyasa 

na kunidharau.” Akanyamaza akanywa 

mvinyo kidogo na kuendelea 

 “ Kwa wakati ule hakuwa ni huyu 

Tino mnayemfahamu leo hii.Alikuwa mtu wa kawaida sana ambaye hakuwa na kitu 

chochote.Kwa kuwa nilihitaji kuja 

kuwekeza Arusha nilimuomba aongozane 

name hadi Arusha ili aweze kunipa 

ushauri mzuri sana kuhusiana na maeneo 

ya kuwekeza.Nilimlipia nauli ya ndege 

tukaja Arusha .Nilimuhudumia katika kila 

kitu na hapo ndipo urafiki wetu 

ulipoanzia. Alikuwa ni mtu mcheshi na 

mwongeaji mzuri.Alinifanya niwe na 

furaha muda wote na taratibu hisia za 

kimapenzi zikaanza kujengeka kati yetu 

na nilishindwa kukataa pale 

aliponitongoza kwani tayari nilikwisha 

tokea kumpenda.Sikujishauri kuufungua 

moyo wangu kwake kwani kwa wakati huo 

niliamini sikuwa yule Lucy wa kipindi kile 

ambaye nilidharauliwa na kuonewa 

kutokana na umasikini wangu lakini kwa 

sasa nilikuwa Lucy mwenye nguvu ya 

pesa.Nilikuwa na kila kitu lakini nilikosa 

kitu kimoja tu mtu wa kuniliwaza na ndiyo 

maana sikusita kabisa kuufungua 

moyowangu kwa Tino.Sikuhofia 

kuumizwa tena kwani Tino alinionyesha 

kunijali,alinionyesha upendo wa hali ya 

juu,alinifundisha mapenzi.Nilimshukuru 

Mungu kwa kunipa mtu kama Tino 

ambaye niliamini ndiye atakayenifuta kabisa makovu ya nyuma.Tulinunua 

jumba kubwa la kifahari hapa Arusha na 

kuanza kuishi kama mume na mke 

.Nilimfungulia Tino miradi kadhaa 

mikubwa yenye thamani ya mamiloni ya 

pesa.Hapo ndipo jina la Tino lilipoanza 

kusikika.Baadae alinishauri tufunge 

kabisa ndoa lakini sikuwa tayari kuapa 

kiapo kikubwa kama kile na hasa 

nikifikiria namna nilivyoumizwa huko 

nyuma.Tuliendelea kuishi huku 

tukiyafurahia maisha.Nilikuwa ni mtu 

mwenye furaha sana na nilisahau yote 

niliyopitia.” Akanyamza kidogo na baada 

ya sekunde kadha akaendelea 

 “ Tino aliniomba tuzae mtoto lakini 

sikuwa tayari kwa hilo kwani nilichokuwa 

nakihitaji ni kumpata mwanangu Angela 

.Tino hakufurahishwa na uamuzi wangu 

wa kukataa kuzaa naye mtoto kwa hiyo 

akaanza vituko.Maisha yetu yakaingia 

katika mikwaruzano ya mara kwa mara na 

hatimaye siku moja akanitamkia wazi 

kwamba hayuko tayari kukaa na 

mwanamke ambaye hana faida yoyote 

katika dunia hii.Alinitaka tuachane ili 

amtafute mwanamke atakayemzalia 

mtoto.Robin sikufichi niliumia sana kwa 

kitu alichonifanya Tino.Nilikesha nikilia kwa nini maisha yangu yamejaa machozi ? 

Nilimpenda sana Tino na siwezi 

kukuficha.Nilitegemea labda baada ya 

muda Fulani maisha yetu yatarejea kama 

kawaida lakini nilikuwa 

najidanganya.Vituko vilizidi na kibaya 

zaidi siku moja nikamfuma na mwanamke 

chumbani kwangu.On my own bed !!..” 

Lucy akashindwa kuendelea akanyamaza 

kwanza akanywa kinywaji kidogo halafu 

akasema 

 “ Kila ninapokumbuka kitendo hiki 

huwa ninapata uchungu sana.Ile ilikuwa ni 

dharau kubwa mno .Tino ambaye 

nilimpenda na kumthamini sikutegema 

kama siku moja angeweza kunifanyia 

kitendo cha dharau kama kile.Niliumia 

sana kuliko hata nilivyowahi kuumizwa 

huko kipindi cha nyuma.Niliamini 

yawezekana labda nina mkosi au 

sikuumbwa kwa ajili ya kupenda ama 

kupendwa.Kila ninapoingia katika 

mahusiano basi mwisho wake huwa ni 

kumwaga machozi.Nilimchukia sana Tino 

na sikutaka kumuona tena machoni pangu 

nikaamua kuondoka na kumuachia kila 

kitu.Nilirejea tena marekani nikaishi kule 

kwa miaka miwli lakini bado picha ya 

mwanangu Angela iliendelea kuniandama ila uchao hivyo nikaamua kurejea tena 

Tanzania kwa lengo la kumtafuta na kujua 

habari zake.Nilipofika safari hii sikutaka 

tena mahusiano na mtu mwingine yeyote 

na nikaamua kufungua shule hii ili niweze 

kuchangia katika kutoa elimu .Hivyo 

ndivyoilivyokuwa.Hivyo ndivyo 

nilivyokutana na Tino na ndivyo 

tulivyoachana .kwa hiyoTino huyu 

mnayemfahamu leo hii mimi ndiye 

chimbuko lake,.Ni mimi ndiye 

niliyemfikisha hapa alipofika leo hii kiasi 

cha kuitwa papaa Tino magari.Ni mtu 

ambaye ninamchukia kuliko watu wote 

katika hii duniani mtu ambaye aliniumiza 

kuliko wote waliowahi kuniumiza.Kumbe 

hakuwahi kuniumiza mimi tu hata wewe 

kumbe alikuumiza pia kwa 

kukutenganisha na mke wako.Pole sana 

Robin.Hiyo ndiyo dunia ilivyo” akasema 

mwalimu Lucy 

 “ Maelezo hayo yamenifanya nizidi 

kumchukia sanaTino .Lazima siku moja 

alipe kwa mambo aliyoyafanya.Kumbe 

kila kitu anachoringia leo hii na kuvunja 

nyumba za watu ni mali yako!!’akasema 

kwa ukali Robin 

 “ Robin hakuna sababau ya 

kumchukia Tino na kumuombea mabaya.Kumbuka kila jambo hutokea kwa 

sababu maalum ambayo sisi kwa macho 

yetu ya kibinadamu hatuwezi kuijua lakini 

yeye anayesababisha mambo yakatokea 

ndiye mwenye kufahamu.Wakati 

mwingine mambo kama haya hutokea ili 

kutujenga na kutufanya tuwe watu bora 

zadi.Tuwe makini zaidi katika kufanya 

maamuzi na hasa maamuz ya kuingia 

mapenzini.Mambo kama haya hutufanya 

tuwe majasiri na kutupa nguvu ya 

kupambana na kila changamopto 

inayokuja mbele yetu.Nimejifunza mengi 

katika safari yangu ya mapenzi lakini 

ninaamini siku moja Mungu ataniletea 

mtu ambaye amemuumba kwa ajili 

yangu.Bado sijakata tamaa katika hili na 

ninaendelea kumuomba Mungu siku zote 

nimpate mtu sahihi ili nisilie tena kwa 

hiyo Robin tafadhali usimchukie Tino bali 

fahamu kwamba kitendo alichokifanya 

kimekujenga sana na kukufanya uwe baba 

bora na wa mfano.Nilikuwa nataka 

kulipiza kisasi kwa wale wote 

walionitenda lakini baadae nimekuja 

kujifunza kwamba kulipa kisasi si njia 

bora ya kujisahaulisha mambo yaliyopita 

badala yake utazidi kujikumbusha mambo 

ya nyuma na kuumia zaidi.Tunachotakiwa kufanya sisi watu ambao tumekwisha 

umizwa ni kujitahidi kusonga mbele na 

kuitafuta furaha ya maisha yetu bila 

kukata tamaa. Muda ambao tunaweza 

kuutumia kwa kulipa kisasi ni muda 

ambao tungeweza kuutumia kwa kufanya 

shughuli nyingine za kimaendeleo za 

kujitafutia furaha ya maisha “akasema 

mwalimu Lucy.Sura ya Robin ikajenga 

tabasamu kwa maneno yale ya busara ya 

Lucy 

 “ Naomba nikiri kwamba sijawahi 

kukutana na mtu ambaye amenishauri 

jambo kubwa kama wewe Lucy.Uko sahihi 

kabisa hakuna haja ya kulipiza kisasi 

kwani ni Mungu pekee mwenye 

kuadhibu.Tunatakiwa kuutumia muda 

vizuri wa kuyajenga upya maisha yetu” 

Akasema Robin 

 “ Nashukuru kwa kunielewa 

Robin.Yaliyopita yabaki historia na 

tusonge mbele.” Akasema Lucy.Kikapita 

kimya kidogo Robin akauliza 

 “ Lucy kuna jambo nataka kukuuliza” 

 “ Uliza usihofu Robin.” 

 “ Nafahamu umeumizwa sana na 

mapenzi lakini kama akitokea mtu 

ambaye anakupenda kwa dhati ya moyo wake ,are you ready to open your heart 

again? 

 Mwalimu Lucy akatabasamu halafu 

akamtazama Robin na kusema 

 “ Ni kweli nimeumizwa sana lakini 

Bado sijakata tamaa na ninaamini 

kwamba si kila mwanaume ni mbaya 

.Bado wapo watu wazuri tu na ninaamini 

yupo yule ambaye Mungu ameniandikia 

kwamba atakuwa wangu milele.Akitokea 

na nikiridhika kwamba ni mwenyewe basi 

nitaufungua moyo wangu kwake” akasema 

mwalimu Lucy na kumsisimua sana Robin. 

 “ Robin tumekaa sana hapa ngoja 

nikawaangalie watoto kule ndani 

wanaendeleaje” akasema mwalimu Lucy 

na kuinuka akaelekea ndani 

 “ leo lazima nimweleze ukweli 

.Nafasi kama hii ni nafasi ambayo 

nikiipoteza itanichukua muda tena kuja 

kuipata kwa hiyo kila kitu nakimaliza 

usiku wa leo”akawaza Robin 

 “ Kumbe chimbuko la Tino ni 

mwalimu Lucy.Bila Lucy leo hii 

tusingemfahamu mtu aitwaye 

Tino.Alikosea sana kumtenda mtu kama 

Lucy.Huyu ni mwanamke ambaye 

anatakiwa atunzwe kama yai.Hatakiwi 

kulizwa wala kuumizwa kwa namna yoyote ile.Hata hivyo kama alivyosema 

Lucy kwamba mambo haya yanapotokea 

yanatujenga na kutufanya kwa watu bora 

zaidi nina hakika hata mimi nimejengeka 

vya kutosha .Kwa kitendo chake cha 

kumchukua wangu amenifanya nimekuwa 

bora zaidi kwani ninayafahamu maumivu 

ya kumuumiza mwenzako kihisia...” Robin 

akasitisha mawazo yake baada ya Lucy 

kurejea. 

 “Watoto wanaendelea kufurahi na 

muziki “ akasema Mwalimu Lucy 

 “ Ok Good.Tuwaache waendelee 

kuburudika.Tuendelee na maongezi 

yetu.Tuliishia wapi? Akauliza Robin 

 “ Oh Robin bado unataka tuendelee 

na maongezi yale? Binafsi huwa sitaki 

kuongelea kuhusu mambo yale kwani 

yamekwishapita na huwa 

yananikumbusha mbali 

sana.Nimekwambia wewe tu kwa sababu 

ni mtu ambaye ninakuamini na 

ninakuthamini.Nakumbuka kuna swali 

uliniuliza nikakujibu, “ 

 “ Ndiyo ulinijibu swali langu .” 

 “ Vipi kuhusu wewe? Baada ya mkeo 

kukufanyia kitendo kile uko tayari 

kuufungua moyo wako na kupenda tena? 

Akauliza Lucy “Ndiyo,niko tayari kuufungua moyo 

wangu wote kwa ajili ya mwanamke 

ninayempenda.Niko tayari kuingia tena 

katika mapenzi.”akajibu Robin 

 “ Safi sana.Ana bahati sana 

mwanamke ambaye atakupata 

mwanaume kama wewe Robin” akasema 

Lucy na wote wakacheka kicheko kikubwa 

 “ Mbona umecheka sana Robin kwani 

tayari umekwisha mpata yule ambaye 

utamfungulia moyo wako wote na 

kumruhusu aingie ndani? Akauliza 

Lucy.Ilimlazimu Robin apige funda kubwa 

la mvinyo na kusema 

 “ Nimekwishampata ingawa hajui 

kama ninakosa usingizi kwa ajili 

yake.”akajibu na kumfanya mwalimu Lucy 

anyong’onyee ghafla. 

 “ Ni nani huyo mwanamke mwenye 

bahati ? Can you show me ? akauliza Lucy 

huku ile furaha yote aliyokuwa nayo 

ikionekana kutoweka 

 “ Its time to start my new life” 

akawaza Robin halafu akainuka akavuta 

kiti nyuma halafu akamshika Lucy mikono 

na kumtazama kwa makini 

 “ Lucy its you” akasema taratibu 

 “ What ?!!  “ Lucy its you whom I love with all 

my heart.Mwanamke yule ambaye 

nimekwambia ninampenda lakini hajui 

kama ninampenda ni wewe.Lucy najua 

mimi kama binadamu si mkamilifu hata 

kidogo lakini toka katika sakafu ya moyo 

wangu ninathubutu kukutamkia kwamba 

wewe ndiye mwanamke ambaye 

ninaamini kabisa kwamba umeumwa kwa 

ajili yangu kwa sababu toka siku 

nilipokuona tu nilijua moja kwa moja 

kwamba ni wewe ninayekuhitaji.Lucy sina 

maelezo mengi ya kukueleza 

,ninachokuomba toka kwako nifungulie 

moyo wako,niingie ndani yake ,niyafute 

makovu yote ya vidonda ulivyowahi 

kuumizwa huko nyuma,nifungulie moyo 

wako niingie nikuonyeshe upendo wa 

kweli.Nitakufungulia pia moyo wangu 

uingie na uutawale.Naomba unikubalie 

niwe mpenzi wako .Nakuahidi nitakuenzi 

daima na kamwe sintakutoa chozi” 

akasema Robin.Macho ya mwalimu Lucy 

yalifunikwa na machozi.Alikuwa analia 

kwa kwikwi 

 “ Lucy ,kitu gani kinakuliza? Akauliza 

Robin 

 “ Robin ninalia kwa furaha 

niliyoipata.You don’t know how manynights I’ve been waiting for this day to 

come.The day that you can hold my hands 

and tell me that you love me.Robin 

huwezi kuamini mambo uliyokuwa 

ukiyawaza ndiyo na mimi nilikuwa 

nikiyawaza.Nilikupenda sana toka kipindi 

kirefu na ilikuwa ni siri yangu .Robin 

ninaufungua tena moyo wangu kwako bila 

kipigamizi kwako na nina imani safari hii 

niko sahihi” akasema mwalimu Lucy 

.Robin akamuinua wakakumbatiana kwa 

furaha kubwa.Mwalimu Lucy akafumba 

macho na kumshukuru Mungu kwani 

ndoto yake ya muda mrefu ya kuwa na 

Robin hatimaye imetimia. 

 “ Nakushukuru Mungu wangu 

hatimaye baada ya kuteseka na 

kuhangaika sana umeniletea mtu ambaye 

nina hakika ni sahihi kwangu.Moyo wangu 

unaniambia kwamba kwa Robin sintalia 

tena.Naomba udumishe upendo kati yetu 

na tupendane kwa dhati ya mioyo yetu na 

asitokee mmoja wetu wa kumuumiza 

mwenzake” akaomba Lucy kimya kimya. 

 Ukurasa mpya ukafunguliwa kati ya 

mwalimu Lucy na Robin.Waliingia tena 

katika mapenzi kwa mara nyingine baada 

ya kuumizwa na wapenzi wao wa awali. Robin na Lucy wakagoganisha glasi ishara 

ya kutakiana maisha marefu na upendo 

katika mahusiano yao mapya.Ulikuwa ni 

wakati wa furaha kubwa kwao. 

 “ penina atafurahi sana akisikia 

kuhusiana na jambo hili”akasema Robin 

 “are you goig to tell her that soon? 

akauliza mwalimu Lucy 

 “ Hapana sintamweleza mapema 

namna hii ingawa lazima tutamweleza 

afahamu kwani si unajua watoto wa siku 

hizi huwa hawakawii kugundua kitu 

kinachoendelea.Kwa siku nyingi Penina 

amekuwa akitamani sana kama 

ungempata mama kama wewe kwa hiyo 

ndoto yake itakuwa imetimia na atampata 

mama mzuri anayempenda ,anayemjali na 

kumthamini” akasema Robin.Mwalimu 

Lucy akatoa tabasamu pan asana na 

kusema 

 “ Robin nakiri kwako kwamba 

ninampenda mno Penina na nitampenda 

siku zote lakini hatuwezi kuukwepa 

ukweli kwamba mama yake mzazi yupo na 

lazima tufanye jitihada za kumkutanisha 

naye ili waweze kuwa na mahusiano 

mazuri pia.Tusimfanye Penina kamchukia 

mama yake kwa kosa alilolifanya bali 

amsamehe na tuendelee na maisha yetu ya furaha.Tumfundishe Penina umuhimu wa 

kusamehe waliotukosea hata kama 

walitukosea jambo kubwa kiasi gani .Dr 

Shanon alinifundisha jambo hilo na ndiyo 

maana mpaka leo hii wale wote ambao 

walinitenda ubaya sijawahi kuwafanyia 

jambo lolote baya japokuwa uwezo huo 

ninao.” Akasema mwalimu Lucy 

 “ Lucy nina bahati sana ya kumpata 

mwnamke kama wewe.Walifanya kosa 

kubwa wale waliokutoa machozi lakini 

nakuahidi kwangu hautalia 

tena.Ninajifunza mambo mengi kupitia 

kwako.Nitafuata ushauri wako nitajitahidi 

kujenga mahusiano mazuri kati ya Penina 

na mama yake.Kuna swali ambalo nataka 

kukuuliza pia.Baba wa mwanao Angela 

umewahi kuonana naye toka umerejea 

nchini? Lucy akafikri kidogo na kusema 

 “ Hapana sijawahi kuonana naye na 

wala sina haja ya kuonana 

naye.Nimekwisha msamehe na kumtoa 

kabisa moyoni wmangu.Amebaki sehemu 

ya historia yangu kwamba ndiye 

aliyenianzishia mikosi”akasema Lucy 

 ‘” Anafahamu chochote kuhusu 

Angela? Akauliza tena Robin 

 “ Hapanahafahamu 

chochote.Sikuwahi kumwambia kama ni mjamzito.Nilikuwa namchukia mno na 

sikuwa tayari afahamu kama nina mtoto” 

akasema Lucy 

 “ Endapo ukifanikiwa kumpata 

Angela uko tayari kumfuata baba yakena 

kumweleza kwamba yule ni 

mwanae?akauliza Robin 

 “ Robin swali lako ni gumu sana 

lakini jibu lake ni ndiyo.Niko tayati 

kumtafuta na kumfahamisha kwamba 

Angela ni mwanae na kama akikubali sawa 

akikataa sawa tu.” Akasema Lucy 

 “ nashukuru sana kusikia hivyo 

Lucy.U mwanamke mwenye upeo mkubwa 

sana.Ninajisikia fahari kubwa kukupata 

mwanamke kama wewe.Nitakutunza 

kama mboni ya jicho langu” akasema 

Robin 

 “ hata mimi ninafurahi sana 

kukupata mwanaume kama wewe ambaye 

wanawake wengi wanaota 

kukupata.Ninajiona ni mwenye bahati 

sana”akasema Lucy.Waliendelea na 

maongezi pale bustanini na kutahamaki 

ilikuwa ni saa nane za usiku.Hakuna 

aliyetamani hata kulala kutokana na 

furaha waliyokuwa nayo.Walitamani 

waendelee kuongea pale hadi asubuhi.  “ Lucy muda umekwenda sana na 

hivi sasa ni usiku mwingi Natakiwa 

niwapeleke watoto wakalale.”akasema 

Robin 

 “ Robin uwapeleke wapi watoto 

usiku huu? This is your house too.This is 

their house kwa hiyo wote mtalala hapa 

usiku wa leo.Hapani nyumbani kwako 

usihofu kitu.Sisi ni kitu kimoja .Changu 

chako na chako changu.Naomba kwa mara 

ya kwanza leo hii mlale hapa “akasema 

mwalimu Lucy.Robin hakuwa na 

kingamizi akakubalia na wazo lile la 

kulala pale kwa Lucy.Wakainuka na 

kuelekea sebuleni ambako wageni wote 

walikwisha ondoka na waliobaki ni Penina 

na mtumishi wao wa kazi za ndani ambao 

tayari walikuwa wamepitiwa na 

usingizi.Mwalimu Lucy akawaamsha na 

kuwapeleka chumbani kulala. 

 “ watoto wamelala ,ni zamu yetu sasa 

kwenda kulala” akasema mwalimu Lucy 

akamshika mkono wakaelekea chumbani 

.Chumba chamwalimuLucy kilikuwa 

kikubwa na kizuri.Ulikuwa ni usiku wao 

wa kwanza pamoja 




 Saa kumi na mbili za asubhi siku ya 

jumapili ,ilimkuta David yuko 

macho.Alikosa usingizi kabisa kutokana 

na mambo yaliyotokea usiku.Alitamani 

atoke na kujiandaa kwenda kanisani 

lakini aliogopa asikutane na 

Pauline.Kichwa chake kilijaa mawazo 

mengi na hasa kuhusiana na kilichotokea 

usiku wa jana.Wakati akiendelea 

kutafakari simu yake ikaita alikuwa ni 

Tamia.Akatabasamu na kusema 

 “ Tamia,umeamkaje ? 

 “ Nimeamka vizuri sana mpenzi 

wangu.Vipi wewe umeamkaje? 

 “ Mimi nilikosa kabisa usingizi 

jana.Naweza kusema kwamba nimekesha 

macho” 

 “ Pole sana David.Najua ni mimi 

ndiye niliyesababisha mambo yote yale ya 

jana.Kama nisingemtumia Pauline ile 

picha wala usingekuwa katika matatizo 

muda huu”akasema Tamia 

 “ Tamia naomba usijilaimu malaika 

wangu,ulifanya jambo sahihi kabisa.Bila 

kufanya vile tusingeweza kuwa huru 

.Pauline angeendelea kutuandama na 

asingekubali kutuona tukiwa 

pamoja“akasema David  “ Nasikitika sana nimempoteza rafiki 

yangu wa siku nyingi lakini nimempata 

mtu ambaye nitakuwa naye kwa maisha 

yangu yote” akasema Tamia na kumfanya 

David atabasamu 

 “ Hata mimi ninashukuru sana 

Tamia kukupata mtu kama wewe.” 

 “ Vipi umeonana na Pauline asubuhi 

hii?akauliza Tamia 

 “ Hapana sijaonana naye na wala 

sijatoka chumbani bado.” 

 “ Ok david,endelea kupumzika 

nitakupigia baadae kidogo” akasema 

Tamia akambusu David simuni na kukata 

simu 

 “ Tamia alinirahisishia kazi sana ya 

kuachana na Pauline.Nilikuwa naumiza 

kichwa ni namna gani ningeweza 

kuachana naye .” Akawaza david 

 “ Pauline ananipenda na ninajua 

ameumia sana kwa kitu nilichomfanyia 

lakini sikupanga kumuumiza kiasi hiki.Hii 

yote imetokana na madam Vicky.Yeye 

ndiye aliyenishawishi niingie katika 

mahusiano na Pauline na kumsababishia 

maumivu makali ya moyo.Naye zamu yake 

inakuja.Ataona kitu 

nitakachomfanyia.Mambo aliyomfanyia 

mzee Zakaria yanatosha sana” akawaza David na kustuliwa toka mawazoni na 

mtu aliyekuwa akibisha hodi.Akainuka na 

kwenda kuufungua mlango akakutana na 

Pauline.Akastuka sana.kwa karibu dakika 

moja wakabaki wakitazamana.Ni david 

aliyeuvunja ukimya 

 “ Pauline karibu ndani” akasema 

David na Pauline akaingia ndani akaketi 

kitandani 

 “ Pauline I’m…”David akataka 

kusema kitu lakini Pauline akamzuia 

 “ No David.You don’t have to say 

anything.Mimi ndiye ninayetakiwa 

kuongea”akasema Pauline ambaye macho 

yake yalikuwa yamevimba.Ilionyesha wazi 

alikuwa amelia sana. 

 “ David sikuwa nimepanga kuongea 

nawe jambo lolote lile lakini nimefumba 

macho na kuamua kuja kukueleza jambo 

muhimu.Nimefikiria sana kuhusiana 

nakilichotokea jana na nikajiona ni kwa 

namna gani nilivyo mjinga kwa 

kung’ang’ania mtu ambaye hana mapenzi 

na mimi.Nakuacha uendelee na Tamia 

.Haukuwa riziki yangu lakini bado 

sijakata tama na ninaamini siku moja 

maumivu haya yatapoa na Mungu 

atanijaalia na mimi nitampata yule 

ambaye atanipenda kwa dhati ya moyo wake na si kuichezea akili 

yangu.Ninaamini wewe na Tamia 

mnapendana na ninawatakia kila la heri” 

akasema Pauline 

 “ Paulin………….” David kataka 

kusema kitu lakini bado Pauline 

hakumtaka aseme chochote 

 “ David nimekwambia usiseme 

chochote.Mimi ndiye ninayesema leo.Mimi 

ndiye niliyekufuata kwa hiyo niache 

niseme kile kilichonileta” akasema 

Pauline akakaa kimya kidogo na 

kuendelea 

 “ samahani sana kwa maneno 

ambayo nilikutamkia jana 

usiku.Hayakuwa maneno mazuri yenye 

heshima wala ustaarabu.Nilitamka 

maneno yale kutokana na hasira 

niliyokuwa nayo kwa 

kudanganywa.Nadhani hata wewe 

ungekuwa katika nafasi kama yangu 

usingeshindwa kujizuia kutamka maneno 

mabovu lakini naomba 

unisamehe.Nikiyakumbuka maneno yale 

ninaumia sana “akasema Pauline na 

kufuta machozi akionyesha wazi 

kuchomwa na maneno ambayo 

alimtamkia David.  “ Paul…”akasema david lakini 

Pauline akamzuia asiseme chochote. 

 “ please david let me finish’ 

Akafuta machozi na kuendelea 

 “ David kilichotokea jana kitabaki 

katika kumbu kumbu zangu kwa miaka 

mingi na kwa sasa nina kazi kubwa ya 

kupambana kusahau kilichotokea ili 

maisha yangu yaendelee.Si kazi rahisi 

kutibu jeraha kama hili lakini nitajitahidi 

ili niweze kulisahau jambo hili .Ili kuweza 

kujisahaulisha jambo hili mimi na wewe 

hatuwezi kuishi katika nyumba moja.Sote 

hatuwezi kuwa na amani hasa pale 

tukionana.Kila nitakapokuwa nikikuona 

nitakuwa nikiumia sana na sana pale 

nitakapokuona ukiwa na Tamia.kwa 

maana hiyo kuna mambo mawili ambayo 

yanatakiwa yafanyike.Kati yetu sisi wawili 

mmoja wetu anatakiwa aondoke hapa 

nyumbani na kumuachia mwenzake nafasi 

ya kuponyesha maumivu.” Akasema 

Pauline. 

 “ P..Paul…………” David akafumbua 

tena mdomo kutaka kusema jambo lakini 

Pauline akamzuia 

 “ Subiri kwanza david.Subiri 

nimalize.kama ungekuwa na jambo la 

kusema basi ungenifuata lakini kwa kuwa nimekufuata mimi let me finish” akasema 

Pauline.Akanyamza kidogo akatazama 

chini halafu akainua kichwa na kuendelea 

 “ Hivi vyote uvionavyo hapa ni mali 

ya baba.Mimi sina hata kitu kimpja humu 

na kwa hiyo sina uwezo wa kukuondoa 

katika nyumba hii ambayo si mali 

yangu.Zaid ya yote baba bado anakuhitaji 

sana kwani hana mtu wa kumsaidia 

biashara zake kwa hiyo wewe utabaki 

hapa na mimi ndiye 

nitakayeondoka.Nitakuachia nafasi ya 

kuendelea na Tamia .Dhumuni langu la 

kuja kwako asubuhi hii ni kuja kukuaga 

kwamba ninaondoka na ninakutakia 

maisha mema wewe na huyo umpendaye” 

akasema Pauline na kushindwa kujizua 

kutoa machozi akafungua mlango na 

kutoka 

 “ Nimemuumiza sana Pauline.Ama 

kweli maumivu ya mapenzi hayana mfano 

wake.Sijui nifanye nini ili kuyaondoa 

mateso haya niliyomsababishia 

Pauline.Lakini yote haya yamesababishwa 

na madamVicky,.yeye ndiye 

aliyenishawishi niingie katika mahusiano 

na pauline na kumuumiza kiasi hiki.Hata 

mimi ninaumia sana kumuona akiwa 

katika hali hii lakini sina namna nyingine ya kufanya.Kinachofuata sasa ni 

kumgeukia madam Vicky.lazima 

nimuonyeshe kazi “ akawaza David na 

kuchukua simuyake akamuandikia Vicky 

ujumbe 

 “ Kuna mzigo nimetaarifiwa kwamba 

umefika.Una muda baadae tukauangalie? 

Akautuma ujumbe ule na haikupita hata 

dakika moja madam Vicky akajibu 

 “ sawa tutakwenda” 

David akaitupa simu pembeni na kuinama 

akaishika kichwa. 

 “ Huyu mwanamke anapata kila kitu 

anachokihitaji katika maisha yake lakini 

bado hatosheki bado anaendelea 

kumuibia huyu mzee kila 

uchao.Ameniudhi sana na lazima 

nimuonyeshe kwamba anachokifanya si 

kitu kizuri hata kidogo.Bila yeye 

nisingemuumiza Pauline kiasi 

hiki.Machoziya Pauline yamenichoma 

moyo sana”akawaza david 

******************* 

 Saa nane za mchana baada ya kupata 

chakula, David na madam Vicky wakaingia 

katika gari la david wakaondoka wakiaga kwamba wanakwenda kuukagua mzigo wa 

madini. 

 “ Vicky nilitumia ujanja ule wa 

kusema tunakwenda kukagua madini ili 

mzee Zakaria asiwe na wasiwasi na sisi 

lakini dhumuni langu kubwa ni kuwa na 

wewe” akasema david 

 “ Kweli david?! Akauliza Vicky kwa 

furaha kubwa 

 “kwa nini nikudanganye Vicky? 

Nikweli kabisa.Unajua nina hamu sana na 

wewe na nimefurahi umeachana na 

Pauline na kwa sasa tutakuwa huru.David 

huwezi kujua ni namna gani ninahamu 

nawe.Usiku huwa nakuota ukija na 

kufanya nami mapenzi.Niliumia sana 

ulipoanzisha mahusiano na Pauline 

japokuwa nilitaka sana jambo hilo litokee 

ili kumzuia Pauline asitufuatilie katika 

mambo yetu .Nimefurahi sana 

mlivyoachana.kwa sasa ni wakati wetu wa 

kujivinjari.Ni wakati wangu na mimi wa 

kufurahia raha za dunia.”akasema Vicky 

 “ Usijali Vicky ,nitakupatia kila kitu 

unachokihitaji.”akasema David na 

kumfanya Vick acheke kwa furaha kubwa 

****************  David na Vicky madhahabu 

walipoondoka Pauline akaitumia nafasi 

ile kwenda kuonana na baba yake mzee 

Zakaria 

 “ Pauline una matatizo gani leo? 

Hauko katika hali yako ya kawaida halafu 

macho yamekuvimba.Whats wrong? 

akauliza mzee zakaria aliyekuwa amekaa 

ghrofani akipunga upepo 

 “ hakuna tatizo baba ninasumbuliwa 

tu na macho lakini tayari nimekwisha 

weka dawa.Vipi maendeleo yako? 

 “ Ninaendela vizuri sana Pauline.” 

 “ nashukuru kusikia 

hivyo”akasemaPauline akakaa kimya 

kidogo na kusema 

 “ baba kuna jambo nimekuja 

kukuambia.” 

 “ jambo gani Pauline? Usiniambie 

kwamba umempata mchumba” akasema 

mze Zakaria na kumfanya Pauline acheke 

kicheko kikubwa na kusema 

 “ Si suala hilo baba.Mchumba 

itanichukua mud asana kumpata kwani 

wanaume wa siku hizi ni walaghai kama 

nyoka.Anyway tuachane na hayo baba 

nimekuja kukwambia kwamba kwa kuwa 

sasa hali yako imeboreka ,nitaondoka 

kidogo ninakwenda katika mapumziko.”  “ Unakwenda mapumzikoni?! Mzee 

Zakaria akashangaa 

 “Ndiyo baba ninakwenda 

mapumzikoni.” 

 “ Pauline una tatizo gani? Tafadhali 

naomba unieleze bila kunificha.Siku zote 

nimekuwa nikikusikiliza matatizo yako 

yote na ninafahamu mara nyingi huwa 

unakwenda katika mapumziko baada ya 

kusumbuliwa na jambo Fulani.What is it 

his time? ” 

 “ baba sina tatizo lolote.Kama 

ningekuwa na tatizo basi ningekwisha 

kueleza muda mrefu.Huwa sikufichi 

jambo lolote na wewe unajua hilo” 

 “ kama huna tatizo ni kitu gani hasa 

kinachokupeleka mapumzikoni? Akasema 

mzee Zakaria 

 “ Baba ninahitaji kutuliza akili yangu 

kidogo na kutafakari kuhusu maisha 

yangu na hatima yake.Kuna mmbo mengi 

ambayo nahitaji kuyatafakari kwa kina 

kama suala hili la septembe 11 

linaendelea kuntesa sana na sijui hatima 

yake ni nini.Kila mwaka ikifika tarehe hii 

lazima litokee jambo.Kwa mwaka huu 

naweza kusema ni afadhali kidogo kwani 

aliwahi kutokea mtu wa kukusaidia pale 

uliposhindwa kuendesha gari barabarani.Majanga yamekuwa 

yakituandama kila mwaka katika tarehe 

hii na kuninyima amani kabisa.Mama 

alifariki tarehe hiyo,mdogo wangu pia 

alifariki tarehe hiyo,na hata mpenzi 

wangu naye alifariki tarehe hiyo hiyo 

,mwaka huu umenusurika wewe ,sijui 

mwaka kesho nini kitatokea.Mambo haya 

yamekuwa yakininyima amani kabisa na 

kunifanya niwe na mawazo mengi . Kwa 

hiyo baba ninahitaji kwenda katika 

mapumziko ili kichwa changu kikae sawa” 

 Maneno yaleya Pauline yakamfanya 

mzee zakaria abaki kimya.Alizama katika 

mawazo mengi ghafla. 

 “ baba ! akaita Pauline baada ya 

kuona baba yake amekuwa kimya sana 

 “ Unawaza nini? Unaafikiana na 

mawazo yangu? 

 “ Siwezi kukukatalia 

Pauline.Umepanga unakwenda wapi 

kupumzika? 

 “ Nitakwenda sehemu tofauti tofauti 

lakini ni hapa hapa nchini.Nitakuwa 

nikikutaarifu kila mara kuhusiana na 

mahala nitakapokuwa” akasema Pauline 

 “ sawa Pauline mimi sina 

kipingamizi chochote cha wewe kwenda 

katika mapumziko hayo ila tu unihakikshie kwamba utakuwa 

ukiwasiliana nasi mara kwa mara na 

kutuelekeza mahala ulipo ili tujue kama 

uko salama.Mimi usinihofie kwa sasa hali 

yangu inaendelea vizuri na isitoshe niko 

na mama yako pamoja na David 

wananiangalia.Kama ikitokea hali yangu 

ikabadilika basi watakutaarifu mara 

moja”akasema mzee Zakaria .Pauline 

hakutaka kukaa sana na baba yake 

akaondoka zake na kumuacha mzee 

Zakaria akiwa katika mawazo mengi 

 “ Anachokisema Pauline ni cha kweli 

kabisa.Kila mwaka ifikapo tarehe 11 

septemba tumekuwa tukipatwa na 

majanga.Alifariki mke wangu tarehe kama 

hiyo,akafariki mwanagu,akafariki tena 

mchumba wa pauline na mwaka huu 

nimenusurika mimi.Bila David ilikuwa 

nife.Lakini hii yote ilitokana na kukiuka 

maagano na nikaipoteza ile pete.Hakuna 

ninachoweza kukifanya tena kwani 

majanga yataendelea kuniandama kila 

uchao hadi nipate tena pete ile 

niliyoipoteza.Nimekuwa nikilifikiria sana 

jambo hili na ndiyo sababu kubwa ya 

ugonjwa wangu.Nasikitika sana kuipoteza 

familia yangu.Japokuwa nina mali nyingi 

lakini sina amani,sina furaha hata kidogo.Nimeandamwa na majanga kila 

uchao.Sijui nifanye nini”akawaza mzee 

Zakaria na kumbukumhu zikamrejesha 

mbali miaka ya nyuma. 

Kiza kimetanda angani na pilika pilika za 

kial sikuza kujitafutaimaisha katikajiji hili 

la tanga zimeanza kupungua.Katika hoteli 

mojja tulivu sana iliyoko pembezoni mwa 

bahar ya hidni,mfanyabiashara wa 

vipurivya magari alikuwa narafiki zake 

wawili aliokutana nao badaya kupotezana 

siku nyinhi wakibadilidhanamawazo. 

 “ Zakaria biashara inakwendahe 

hapa Tanga? Akauliza Stanslaus mmoja wa 

wafanya biashara wakubwa wa magari 

jijini Dr es salaam 

 “ Biashara hapa Tanga inakwenda 

vizuri lakini si vizuri sana.Ninafikira 

kuhama na kuhamimi jijini Arusha 

pengine kule inaweza ikawa nzuri 

kidogo”akasema Zakaria 

 “ hata ukienda sehemu yoyote ile 

kama hujaipanga vizuri basibiashara 

itakuwa ngumu tu.Miminakushauri kitu 

kimoja Zakaria,jipange” akasema Ezekiah 

 “ Nimekwisha jipanga vizuri 

Ezekiah.Mtaji ninao wa 

kutoshalakininaonani biashara tu ndiyo 

hainiendei vizuri nandiyomaana nataka kuhama kwenda Arusha nikabadili 

biashara” akasema Zakaria. 

 “ Ninaposema ujipange 

ninamaanisha kwamba lazima utengeneze 

mazingira mazuri ya biashara.Zakaria 

wewe ni frafikiyetu wa sku nyng na hata 

sisi tunapenda sna kukuona ukwa na 

maisha mazuri kama sisi na kama 

utakuwa tayari tutakusadia ili uweze 

kutengeneza mazingira mazuri ya 

boashara “akasema Ezekiah 

 “ Ezekiah nitashukuru sana kama 

mmejitolea kunisiadia rafiki 

zangu.Nikweli nina tamani sana na 

mimisiku moja niwe kama ninyi.Niwe 

tajiri:” akasema Zakariah 

 “ Ndiyomaana tukasema kwamba 

tunataka kukusaidia ili siku moja na 

wewe uwe kama sisi.Lakini itatgemea sana 

kama na eweutakuwa tayari kusaidiwa ” 

Akasema Stanslaus 

 “ Niko tayarindugu zangu.Ni 

naniambaye hataki kusaidiwa ili awe na 

maisha mazuri? 

 “ Basivizuri kama uo tayari sisi 

tutakupeleka kwa mtaalamu wetu ambaye 

atakutengenza na utakuwa na utafanikiwa 

kama sisi” akasema Ezekiah na kumstua 

kidogo Zakaria  “ Mtaalamu yupi huyo 

unayemzungumzia? 

 “ Sisi tuna mtaalamu wetu ambaye 

ndiye aliyetusaidia hadi tukafika hapa 

tulipo.Nina hakika hata weweatakusaidia 

na utakuwa kama sisi.Anaitwa mzee 

Sangala.Huyu ni mganga hatari sana kwa 

dawa za utajiri.wanamfuata hadi watu wa 

kutoka nje ya nchi.Yey eni chimbuko la 

matajriwengi unaowaona hapa mjini.” 

Akasema Ezekieah 

 “ Mganga wa kienyeji?Zakaria 

akashangaa 

 “ Ndiyo Zakaria mbonaumestuka? 

 “ Nimestuka kwa sababu sijawahi 

kushiriki katika hayo mambo na sina 

imani kabia kuhus mamboya kishirina” 

akasema Zakaria 

 “ Zakaria ulimwengu umebadilika 

sana siku hizi.Ukisema ufanye biashara 

kwa nguvu zakomwenyewe basi utakufa 

masikini .Biashara za sasa zimejaa 

ushindani na unaoshindananao 

wanatumia nguvu za ziad na ndito maana 

wew ambaye hutumii chochote kwako 

unaionabiashara kuwa ngumu 

sana.Asilimia kubwa ya matajiri 

unaowaona hapa mjini wengi wanatumia 

nguvu za ziada katika biashara zao kwa hiyo ni wakati sasa wa kufanya maamuzi 

kama unahitaji kuwa tajiri basi jiunge nasi 

na ninakuhakikishia kwamba hautajutia 

uamuzi wako.” Akasema Ezekiah 

 “ Ezekiah ninajua mna lengo la dhatri 

la kunisiaidia lakini mimisi muuminiwa 

mambo hayo ya kishirkikan kwa hiyo 

nnapata wakati mgumu sana wa kufanya 

maamuzi.” Akasema Zakaria 

 “ Zakaria sisi hatukulazimishi 

kufanya hivyo tulivyokushauri lakini 

tunachokuomba nenda nyumbani 

kaafikiria na ufanye maauzi.kama unataka 

kuingia katika maish amapya basi 

uutatujulisha ili tukufanyia mpango lakini 

kama hutaki basi utaendelea kuogelea 

katika umasikini hadi kufa kwako.Chaguo 

ni lako” akasema Ezekiah na kumpa 

wakati mgumuu sana Zakaria. 

 Usiku wa siku ile ulikuw amrefu sana 

kwa Zakaria alifikiria mambo mengi sana 

kuhusiana nakile alichoambiwa na wale 

rafiki zake kuhusiana na kuingia katika 

imani za kishirikina ili aweze kupata 

utajiri mkubwa.Alifikiria sana na 

mwishowe akaamua kukubaliana na 

ushauri aliopewa na rafiki zake wa 

kuingia katika masuala ya 

kishirkikna.Siku iliyoguata akwapigia simu rafii zake na kuwatarifu kwamba 

amekubalianana nao na wakapanga 

wakutane joni ya siku hiyo ili waweze 

kumpa maelekezoya nini cha kufanya 

 Jioni ya siku ile kama walivyokuwa 

wamekubaliana wakakutana na Zakaria 

akakiri kwamba kwa moyo mmoja 

ameamua kujiunga nao. Bial kupoteza 

muda usiku ule ule wakamchukua Zakaria 

na kwenda naye hadi kwa mzee Sangala 

mganga wa kienyejialiyekuwa akiishi nje 

kidogoya jiji la tanga.Mzee Sangala ndiye 

aliyewafanyia dawa Ezekiahna Stanslau 

had wakawa matajiri wakubwa.Sangala 

aliwapokea wageniw ake na wakamueleza 

shida iliyowapeleka na kuomba Zakaria 

alale pale kwa siku mbili ili aweze 

kufanyiwa dawa na akitoka pale basi 

atakuwa tajirimkubw.Zakaria akakaubali 

na kukaa pale kwa mganga Sangala kwa 

siku mbli akifanyiwa dawa.Katika siku 

hizo mbili Zakaria alikutana na 

mambomengi a kutisha yaliyomuogopesha 

mno.hakuwahikuhsi hata siku moja 

kwamba katika maisha yake atakutana na 

mambo kama yale.Jioni ya siku ile pili 

mzee Sangala akamaliza kumfanyia dawa 

na kumpa masharti ya namna ya kufanya.  “ mwanangu mimi uganga wangu 

hauna masharti makubwa kama wengine 

wanavyofanya.Sikutumi ukaue mtu wala 

sikutumi ukafanya jambo lolote baya kwa 

mtu yeyote yule ili uwe tajiri.Kitu 

ninachokupatia ni hii pete.” Akasema 

mzee sangala na kufungua mkoba wake 

mdogo na kumpatia Zakaria pete ya 

dhabau iliyokuwa iking’ara sana 

 “ pete hii imetolewa na mizimu 

iliyoko Amboni kwa hiyo ni pete ambayo 

itakulinda na kila jambo na hii ndiyo 

chanzo cha utajiri.Hii si pete kama pete 

hizi za kawaida tunazozivaa bali hili ni jini 

Saiba ambalo kazi yake ni kukupa wewe 

utajiri kwa hiyo pete hii unatakiwa 

kuitunza kama mboni ya jicho lako.Jini 

huyu si mpenda makuu na siku zote yeye 

hufurahi pale watu wanapokuwa 

matajiri.Sharti lake yeye moja tu kwamba 

kila tarehe 11 september lazima umtolee 

sadaka ya mnyama.Mnyama anayetakiwa 

kumtolea sadaka mi mbuzi dume mweusi 

asiye na doa hata moja na mwenye pembe 

ndefu zilizopinda kwa 

nyuma.Nitakuelekeza namna ya kufanya 

sadaka hiyo.Hili ndilo sharti pekee ambalo 

jini Saiba anataka.Unapofanya sadaka hiyo 

lazima uwe na pete hii kidoleni mwako ndiyomaana nikakuambia kwamba pete hi 

unatakiwa uitunze kama mboni ya jicho 

lako na unatakiwa utembee nayo kwa kile 

sehemu unayokwenda.Hata siku moja 

haitakiwi kutoka mfukoni mwako. Hii 

ndiyo kinga yako,hii ndiyo kila kitu 

kwako.Siku ukiipoteza pete hii basi 

hakuna namna ya kukusadia tena kwani 

lazima jini Saiba atakuadhibu vikali kwani 

kila atakapokosa damu katika tarehe yake 

ya sadaka basi tegemea adhabu kali sana 

toka kwake.Saiba akikasirika huwa ni jini 

mbaya sana” akasema mzee Sangala na 

kumuelekeza Zakaria namna ya kuifanya 

ile sadaka aliyomuelekeza. 

 Kumbukumbu hii ikamtoa jasho 

mzee zakaria. 

 “ Niliipoteza ile pete na ndiyo sababu 

ya majanga haya yote kuniandama namna 

hii.Hii ni sababu kila tarehe 11 septemba 

basi ninapatwa na janga.Kila jambo 

linalonitokea katika tarehe hii ni adhabu 

toka kwa jini Sabaya kuipoteza pete 

ile.Sijui nitaipata wapi pete ile ili mambo 

haya yasiendelee kunitokea.kwanza 

ilianza kwa kila mwaka kupoteza mali 

kama vile magari kuanguka maduka 

kuungua ,pesa kupotea lakin kwa miaka 

ya hivi karibuni mambo yamehamia kwa familia yangu.Mkewangu 

alifariki,mwanangu,mchumba wa 

mwanangu,mwaka huu nimenusurika 

mimi kufariki sifahamau mwaka kesho 

nini kitatokea.Pauline mwanangu wa 

pekee niliyebaki naye anaumzwa sana na 

jambo hili lakini sijui namna 

nintakavyoweza kumueleza na 

akanielewa.Nina hakika akilifahamu 

jambo hiliatanichukia sana kwa 

kitendonilichokifanya.lakini nitaificha siri 

hi ihadilini? Akajiuliza mzee Zakaria lakini 

akashindwa kupata jibu akaondoakna 

kuelekea chumbani kwake 

******************* 

 Baada ya kuachana na baba yake 

Pauline akaenda kujifungua chumbani 

kwake.Alikaa kitandani na kuanza tena 

kulia. 

 “ Sijui kwa nini maisha yangu 

yamekuwa namna hii.hyana furaha hata 

chembe.Kila mara ni mimi tu ambaye 

nimekuwa nikilia.Kwa nini lakini maisha 

yangu yanakuwa namna hii ? Akajiuliza 

huku akilia  “ kwa zaidi ya miaka mitano sasa kila 

mwaka nimekuwa nikimwaga 

machozi.hakuna mwaka ambao umepita 

bila ya mimi kulia.Alifarikimama 

yangu,mdogo wangu,mpenzi wangu 

nikalia sana lakini mwaka huu nimeumia 

zaidi kwa kitendo alichonifanyia 

David.Ameniumiza sana .Sijawhai kuumiza 

namna hii kama alivyoniumiza 

.Niliaminikwamba David ndiye 

mwanaume oeke ambaye atayafuta 

makovu yangu ya nyuma lakini imekuwa 

ni tofauti.Yeye ndiye aliyeniumiza kuliko 

wote.” Akawaza Pauline 

 “ Lakini suluhisho pekee ni 

kuondoka hapa nyumbani .Lazima 

nijitahidi kwa kila niwezavyo niweze 

kujisahaulisha jambo hili 

lililotokea.Lazima nimsahahau David na 

tamia.Na hii ni tiketi nzuri ya kuondoka 

hapa nyumbani kwenda kuanza maisha 

mengine.Nimekwisha choshwa na maisha 

haya ya kulia kila mwaka.Maisha yetu 

yamekosa furaha ata chembe.Lazma 

nifaney jihudi za makusudi kabisa za 

kujikomboa na hali hii.Siwezi kuendelea 

kuishi maisha ya namna hii.” Akawaza 

Pauline na kuanza kupakia baadhi ya vitu 

vyake muhimu katika sanduku lake. ************** 

 “ David mbona hutaki kunieleza 

tunaelekea wapi? Akauliza Vicky 

madhahabu 

 “ Tunakwenda Usa river katika 

nyumba yako”: akasema David na Vicky 

madhahbu akafurahi kupita maelezo 

 “ Hunitanii David/ Ni kweli 

tunakwenda Usa river? Akauliza Vicky 

 “ Sikutanii Vicky.Ninataka tuwe huru 

na sehemu pekee ambayo mimina wewe 

tunaweza kuwa huru bila kubughudhiwa 

na mtu yeyote ni katka nyumba yako pale 

Usa river.” Akasema David 

 “ Oh David..hujui ni furaha ya namna 

gani umenipatia.Ninafuraha ya ajabu sana 

leo”akasema Vicky madhahabu huku 

mwili ukiaanza kumsisimka kila 

alipowaza kwamba anakwenda kufanya 

mapwnzi na David. 

 “ David nina hamu sana na 

wewe.Hujui tu ni shsida kiasi gani 

ninapata kwa yule mzee ambaye hawezi 

kufanya chochote.Tukiwa kitandani 

analala kama chatu aliyemeza 

kodnoaa.hawezihata kunipapasa.Ninapata 

shida sana basi tu ninavumilia kwa sababu 

ninayatengeneza maisha yangu.Huwa 

ninakesha ninaomba huyu mzee afariki 

dunia hata leo ili niwe huru kuishimaisha 

yangu.” Akasema Vicky madhahabu 

 “ Huyu mwanamke hana hata haya 

kutamka maneno hayo mbele 

yangu.Angejua ninavyomchukia wala 

asingethubutu kuongea maneno ya 

kipuuzi kama haya mbele yangu.” 

Akawaza David .safari ikaendela 

kimyakimya hukuu Vicky madhahbu 

akibadilimikaona kukaa mikao yakiahsra 

hasara ili kumuhamsisha David 

 “ Dah ! kwa kwleimwanamke huyu 

ana mitego sana.Hata hivyo hapa 

amegonga mwaba.Hatafanikiwa kunipata 

kirahisikamaanavyofikiria.” Akawaza 

david 

 “ David,mbona uko kimya 

sana.Unawaza nini? Unamuwaza Pauline? 

Akaulzia Vicky 

 “ Hapana madm simuwazi 

Vicky.Nimekosa neno la kusema.mwili 

wote unanisisimka.Ninatamani hata 

niegeshe gari hpa pembeni tuanze 

mambo” akasema David na kuzidi 

kumpagawisha Vicky 

 “ oh David,usiseme hivyo bhana 

unazidi kunipagawisha.” Akasema Vicky madhahabu na kuipandisha juu sketi yake 

fupi aliyokuwa ameivaa ma ngo yake 

nyeupe ya ndani kuonekana,akaushika 

mkono mmoja wa kushoto wa David na 

kutakakuup[eleka maeneo yake nyeti 

lakini david akawahi kuuchomoa. 

 “ Madma usifanye hivyo nihatari 

ninaweza kusababisha ajali 

barabarani.Vumulia karibu tunafika 

Usariver’ akasema David huku mapigo ya 

moyo yakimuenda kwa kasi kubwa. 

 “ Dah ! leo kazi 

ninayo.Lakininitafgnay kila 

linalowezekanahadi nihakikishe 

lengolangulinatimia”akawaza David.Vicky 

madhahabualiendela kujichezeamaeneo 

nyeti huku akitoa miguno na kuzidi 

kumuweka David katika wakati mgumu 

ambaye naye tayari maeneo nyeti 

yalikuwa ymechachamaa. 

 Walifika hadi katik anyuma ya Vicky 

madhahabu na david akapewa funguoa 


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog