Search This Blog

Friday, 28 October 2022

KISASI - 1

 







    IMEANDIKWA NA : FRANK MUSHI



    *********************************************************************************



    Simulizi : Kisasi

    Sehemu Ya Kwanza (1)





    “Nayajua mengi kwakuwa nimempa kila mtu nafasi ya kuwa mwalimu wangu,,kila mtu hunifunza kwa yale atakayo,,naheshimu kauli na mawazo ya wote kwa uzito sawa, LAKINI UELEWA NI JUU YANGU”…



    **MTANGAZAJI**



    “Leo katika kipindi chetu, tutaendelea kusikiliza mahojiano kati ya Patrick na mwandishi wa habari waliowahi kuyafanya kipindi cha nyuma kabla ya leo, tulia kwenye redio yako na kila kitu kitakujia hapohapo ulipo, hatutakuwa na matangazo mengi kutokana na uzito wa simulizi hii ya kusisimua” ilikuwa ni sauti ya mtangazaji wa kituo cha redio cha SPEAK LOUD FM kilichokuwa kikirusha kipindi cha STORY za Iam Frank, saa yangu ya mkononi ilinionyesha kuwa ilikuwa saa nne usiku na pombe zilikuwa zimeivuruga akili yangu, lakini nilikwenda mpaka kwenye jokofu na kuchukua Redbul kisha niliinywa haraka haraka na kurudi ili niweze kusikiliza bila kupata chembe ya usingizi…ile kanda yenye ile simulizi ilichezeshwa na sauti ya msimuliaji ilianza kusikika.



    **PATRICK ANASIMULIA**



    ".........ulifikiri nitanyamaza sio,sikutaka kufanya yote haya ila you forced my hand(uliulazimisha mkono wangu).."ndo sauti ya mwisho niliyoisikia katika masikio yangu ikifuatiwa na maumivu ya kitu chenye ncha kilichoingizwa kwenye mshipa wa damu kichwani mwangu,niligundua ni sindano baada ya kuhisi kama dawa ikisukumwa kuingia ndani ya mshipa ule, hali ya kulewa na usingizi vilianza kunisonga lakini kwa mbali niliweza kuona kama vile Mary alikuwa amezimia, nikajitahidi kutoa sauti lakini sikuweza kabisa, wale watu sikuwaona vizuri lakini walikuwa ni zaidi ya wawili kwakuwa nilizisikia sauti zao kwa mbali wakishauriana, sikuifahamu hata sauti moja, gari letu lilikuwa limeharibika vibaya na ile ajali, sikumbuki ilikuwaje mpaka tukagongana na ile gari ila nilishtuka tu na kukuta tayari ajali imetokea na wale waliokuwa kwenye ile gari ndio walioshuka na kuja kunichoma ile sindano. Maumivu makali yaliutesa moyo wangu haswa pale nilipotaka kukumbuka hata jina langu lakini nikashindwa,,,sikukumbuka kitu chochote, niliishi maisha ya tabu sana katika siku za ukubwa wangu, kila kitu kwenye maisha yangu kilikuwa kipya kabisa, sikumfahamu yeyote katika eneo lile. Sikukumbuka nilipokuwa wala nilifikaje,sikufahamu chochote kuhusu ulimwengu,kila kitu kilikuwa ni giza ndani ya maisha yangu,sikutamani kufa kwasababu sikujua nini maana ya kuishi na nini faida ya kufa kwa wakati huo,,kwa kweli yalikuwa maisha ambayo sikuwahi kufikiri kama ningeishi. Miaka sita mbeleni nilikuja kutoka nje na ndipo nilipoona bango kubwa nje ya jengo hilo nililokuwemo bango hilo lilisomeka Dr. ANDERSON MENTAL CLINIC,ilikuwa pia anuani chini yake iliyonijulisha kuwa nilikuwa SUVA huko FIJI, mandhari niliyokuwepo niliipenda sana ila sikukumbuka chochote juu ya eneo hilo,niliichukia sana hali niliyokuwa nayo wakati ule,hakuna aliyekuwa akionekana kunijali,kila mtu alikuwa ‘busy’ na kazi yake. Nilijihisi pengine nilikuwa kichaa, iweje kila mtu asinijali au kuniuliza chochote pale nilipokuwa. Hayo yalikuwa maisha yangu kipindi cha mwanzoni mwa uzima wangu wagu wa mara ya pili, niliona watu ambao nilihisi ni tofauti sana na mimi,,,,,nilisogea mpaka mbele kwenye bustani kubwa na kutazama mbele mita 200 nikagundua pale ni karibu kabisa na ufukwe wa bahari.



    ****



    "hallo,,!"niliskia sauti ikiniita wakati nipo pale kwenye bustani nikageuka,alikuwa ni msichana mwenye asili kama yangu lakini sikuwa namfahamu,,alinisogelea karibu nakuanza kunisemesha,nilielewa lugha aliyokuwa akiiongea, niliwahi kuwa nikiiongea sehemu fulani lakini sikukumbuka ni wapi.

    “Patrick namshukuru sana mungu uko hai, nashukuru umerudisha fahamu zako” aliongea huku akionekana kweli kuwa alikuwa akilifurahia hilo. Sikumjua huyu dada wala sikufahamu yeye amenijuaje.

    “utapona kabisa na utakumbuka kila kitu, tunafanya tuwezavyo kuhakikisha kuwa unarudisha fahamu zako” alizidi kusisitiza huku akifuta machozi.

    “wewe ni nani” nilimuuliza huku nikimtazama usoni, hakika sura yake sikuijua kabisa, hata kama sikuwa na fahamu lakini sura yake ni kweli sikuwahi kuiona hata kidogo.

    “Naitwa Pamela, ndiye daktari ninayemsaidia dokta Anderson katika matibabu yako, ni mimi ambaye ndiye nakuwa na wewe muda wote kuangalia afya yako, wewe ni sababu ya mimi kuendelea kuwa hapa” aliongea huku akionekana kuangalia pembeni kana kwamba alikuwa akifuta machozi.

    “kwanini unalia” nilimuuliza huku nikimgeuza ili aniangalie.

    “silii, ni furaha tu kwakuwa umeamka leo” kichwa changu kilikuwa kimejaa maswali mengi sana, lakini sikujua namna ya kuyauliza, kila kitu pale kilikuwa ni michoro kwangu isiyoashiria chochote, nilikuwa nimevurugwa akili na kila kitu kabisa, sikumfahamu yule Pamela na wala sikujua yeye ni nani, sikujua anaposema nimeamka je nililala toka lini, na kwanini kuamka kwangu kuwe ni furaha kwake, kwanini alie kwa mimi kuamka, kwanini alionyesha furaha na kusema nitapona, yeye alikuwa nani kwangu, mimi nilikuwa na thamani gani kwake, hiyo yote ilikuwa ni jakamoyo ndani ya moyo wangu, nilikuwa kama teja lililokuwa likihudhuria kliniki ya ukichaa.

    “Pamela, mimi sielewi chochote” nilimuuliza huku nikilia baada ya kujitahidi sana kukumbuka lakini ikashindikana. Hakunijibu chochote badala yake alinishika mkono na kuondoka na mimi mpaka ndani ya ile hospitali. Tulipofika pale aliingia ndani na kutoka na daktari mmoja mzungu aliyekuja pale na kuanza kuongea na mimi kisha Pamela alikuwa akinitafsiria.

    “Hellow Patrick am doctor Anderson”(habari Patrick, naitwa dokta Anderson). Alinisalimu na kunipa mkono, na mimi nilimpa mkono.

    “We want to discharge you, but you will be under the care of doctor Pamela, you will stay at her place until we are sure that you can stand on your own”(tunataka tukuruhusu lakini utakuwa chini ya uangalizi wa dokta Pamela, utakaa nyumbani kwake hadi tutakapokuwa na uhakika kuwa kuwa unaweza kujitegemea) sauti ya Pamela ilisikika ikitafsiri maneno ya dokta Anderson.

    “Pamela don’t bother to interpret, I do understand the language” (Pamela usihangaike kutafsiri, naielewa hiyo lugha), nilimuambia hayo Pamela na yeye alinyamaza kimya.

    ***

    Niliruhusiwa kutoka pale hospitali na sasa tuliingia kwenye gari ya dokta Pamela kuelekea kwake, hapakuwa mbali sana na pale hospitali, muda wa dakika kumi tulikuwa tumeshafika.

    “karibu sana Patrick, hapa ni nyumbani kwangu, ndiko ninapoishi, na ndipo ambapo na wewe utaishi” alinikaribisha huku akitabasamu na kuruhusu vishimo vidogo kwenye mashavu yake vionekane, nilikaribia na kuketi huku nikitazama kila kona ya ile nyumba. Ilikuwa ni nyumba ndogo lakini ilikuwa ni nzuri na ilikuwa na mazingira mazuri yaliyovutia.

    “Unaishi na nani hapa” nilimuuliza swali wakati alipokuwa akienda kuchukua kinywaji kwenye jokofu.

    “naishi mwenyewe, lakini kwasasa nitakuwa nikiishi na Patrick” aliongea hayo na kucheka. Sikumbuki kama niliwahi kucheka toka pale hospitali. Kwa muda mfupi niliokuwa na Pamela nilikuwa nimegundua kuwa alikuwa mtu mwenye kupenda sana kucheka, alikuwa ni mtu mcheshi na anayependa utani muda mwingi. Nilianza maisha haya ya kuishi kwa Pamela na muda mwingi dokta Anderson alikuwa akija pale nyumbani kuniangalia. Pamela na dokta Anderson walikuwa kama ndugu vile ingawaje Pamela alikuwa na asili tofauti kidogo.

    ****

    Asubuhi tulivu ya desemba 1999 ilinikuta nikiwa Suva huko Fiji, ilikuwa ni miezi mitatu sasa toka nitoke hospitali lakini mpaka wakati huo bado sikujua chochote, mbali na kumuuliza Pamela maswali mengi lakini hakuwa tayari kabisa kunieleza chochote, siku zote historia ya maisha yangu na sababu za kwanini sina kumbukumbu yeye hakuziona za maana.

    “Patrick leo tunatoka” nilimsikia Pamela akinipa taarifa hiyo asubuhi wakati alipokuja kugonga chumba changu.

    “tunaenda wapi” nilimuuliza huku nijiachanisha na shuka zito nililokuwa nimejifunika.

    “tunaenda Albert Park, amka ujiandae tunaondoka muda sio mrefu” niliamka na kuanza kujiandaa.

    ***

    Safari ya kuelekea Albert Park ilianza, tulikwenda mpaka Tanoa plaza tukipitia Amy Roas na hapo tulisimama, kisha Pamela aliniambia tushuke tuingie ndani ya lile jengo. Tuliingia mpaka ndani ya jengo lile na kwenda upande wakulia mpaka juu kabisa ambapo tuliweza kuona mandhari yote ya Fiji na kwambali alinionyesha nchi ya Australia. Nikiwa pale juu nilisikia kama sauti yamsichana ikiniita na nilipogeuka nyuma sikuona mtu.

    “ni nini Patrick” aliniuliza Pamela lakini sikuwa na la kumjibu, nilipokuwa nimegeuka sikumuona mtu yoyote lakini kwa uhakika kabisa niliona kama kivuli cha msichana niliyehisi kumfahamu, najua hata ningesema Pamela asingenielewa.

    “hamna kitu, sijui ni nini nimeona” nilimueleza hayo na yeye alinifata na kunishika kichwa akiniambia kuwa amenileta pale kwasababu japo hakunieleza ni sababu gani hiyo. Alitnitoa pale na kunipeleka ndani zaidi kwenye chumba fulani na hapo nilianza kuhisi mapigo ya moyo yakinienda mbio.

    “Pamela kuna nini hapa” nilimuuliza Pamela lakini hakuniambia kitu badala yake alinifunga kitambaa usoni na kuniambia niketi, niliketi huku nikiwa na wasiwasi juu ya kilichokuwa kikitokea pale. Giza lilikuwa limetanda kwenye macho yangu na hofu ilinifika. Nilianza kuona picha ya msichana kwa mbali na sikujua ni nani. Alikuwa msichana mrembo mweupe ambaye nilikuwa naye sehemu kama ufukweni mwa bahari, yule msichana alikuwa akifurahi na mimi nilikuwa nikimkumbatia kama vile tulikuwa wapenzi,,niliogopa sana kwakuwa haikuwa kawaida, alinifungua tena kile kitambaa na kuniuliza nimeona nini lakini sikuwa na la kumjibu.

    “mimi ni nani Pamela?” nilimuuliza huku nikiwa kama natetemeka, alinitazama machoni huku akionekana kuzuia machozi.

    “ukitaka kujua wewe ni nani lazima uwe makini na kile kikujiacho kwenye fikra zako” aliniambia nakuninyanyua kisha tulienda mpaka kwenye chumba kilichokuwa kulekule ndani kisha alivua nguo zake mbele yangu na kuvaa taulo na kuelekea bafuni, akiwa bafuni nilisikia akiniita lakini kwa uwoga nilivua nguo zangu na kuvaa taulo kisha nikamfata bafuni, nilipoingia alinikumbatia na kuanza kunipiga mabusu mwili mzima, mihemko ya mwili wangu ilikuwa karibu kabisa na hisia zangu hivyo nilianza kulipiza mashambulizi, kila nilipokuwa nikimshika kuna picha ya mwanamke ilikuwa ikinijia, tulitoana bafuni na kuja mpaka kitandania kisha kazi ilianza pale, Pamela alikuwa mtundu sana kitandani lakini kila alipojitahidi kunifanyia mambo flani taswira ya mwanamke mwingine ilikuwa ikinijia, tuliendelea kusumbuana na kuchokozana hisia zetu na mwishowe tulikutanisha maungo yetu ya uzazi, nilipokuwa katikati ya mchezo wakati Pamela akiwa juu kuongoza jahazi niliona sura ya yule msichana tena na kushtuka ana hapo Pamela alizidisha kasi, nilikuwa kama mtoto mdogo vile jinsi ambavyo nilikuwa nikilia na ile sura ya yule mwanamke ilikuwa ikinijia bado.
    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mary,,,Mary” nilijikuta nikitamka lile jina na hapo Pamela aliacha na kunishika kichwa,,kisha alikuwa akiniangalia kwa makini.

    “kafanyaje” aliniuliza kama vile hakuelewa ninachomaanisha, nilinyamaza kwakuwa sikujua namna ya kuendelea kuelezea, hapo Pamela alianza tena kuushika mwili wangu na kuendelea na shughulia yake mpaka nilipokumbuka baadhi ya vitu.

    “Mary ni nani Pamela” nilimuuliza kisha alinyanyuka vilevile akiwa uchi na kuondoka kuelekea bafuni, alipokuwa akiondoka nilimtizama na ile picha ilinijia tena. Nilijivuta pale kitandani na kwenda kumfata kule bafuni, alifungua lile bomba la mvua na kunivuta kisha alinikumbatia huku maji yakitumwagikia. Nilikuwa nimetumbua macho na yeye hakuwa anaongea zaidi ya kufungwa macho akiyaruhusu maji yazilowanishe nywele zake laini.

    *****



    USIKU WA SIKU HIYO.



    Tulikuwa tumelala nyumbani kwa Pamela na siku hiyo ilikuwa mara ya kwanza mimi na Pamela kufanya yote yaliyotokea mchana huo.

    “Mary ni nani” lilikuwa swali la kwanza kumuuliza Pamela usiku ule. Alikuwa amenilalia kifuani lakini nilipomuuliza alinyanyuka na kuketi.

    “Mary ni msichana uliyekuja naye Fiji miaka zaidi ya sita sasa, ni mke wako na alikaa hapa akikuuguza kwa zaidi ya miezi sita ila baadaye aliamua kuondoka baada ya kumwambia kuwa si rahisi wewe kurudisha fahamu tena, aliondoka na hatukujua ni wapi alikwenda, tumejaribu sana kutafuta kumbukumbu zako lakini hatukupata” alinieleza hiku akijikaza ili asilie.

    “kwanini sikuwa na fahamu” nilimuuliza.

    “ulichomwa sindano ya dicomenzol, inayotumiwa kuchoma wanyama wakali ili kuwafanya watulie, walikuchoma wakazidisha kipimo na hii ilikuwa ni baada ya wewe kupata ajali ambayo hata hivyo tunahisi ilikuwa ni ya kukusudiwa, yani kuna mtu aliitengeneza ili itokee ndo wakuchome sindano ile ambayo ilimaliza kila kitu kichwani mwako”

    “Mary Robert”nilikumbuka.



    “Unaweza kuwa si wa kwanza kwake, wala wa mwisho kwake, Aliwahi kupenda kabla na anaweza kupenda tena. Lakini kama anakupenda wewe, unajali nini tena? Yeye si mkamilifu, na wewe pia si mkamilifu, na wote wawili hamuwezi kuwa wakamilifu pamoja, lakini kama anaweza kukufanya ucheke, anakunfanya ufikiri mara mbili na anakiri kuwa yeye ni binadamu a anatenda makosa basi mshikilie yeye na mpe kwa kadiri uwezavyo. Anaweza kuwa hakufikirii kila sekunde katika siku, lakini atakupa sehemu ya utu na mwili wake anayojua utaivunja YANI MOYO WAKE. Usimbadilishe, usimchambue, usitegemee makubwa zaidi ya yale awezayo kukupa au yale anayomudu. Tabasamu pale akufurahishapo, muambie pale anapokukasirisha, ana ummis pale anapokuwa hayupo. HAPO UTAKUWA NA FURAHA YA MAPENZI NA WASIWASI WA MAPENZI UTAONDOKA” HII NI SEHEMU YA PILI.



    Ile CD yenye ile simulizi iliendelea kusikika redioni na usingizi ulikatika kabisa, nilikuwa najiuliza huyu Mary ndiyo nani na kafanya nini. Baada ya matangazo machache yule mtangazaji wa redio alirudi hewani na kusema kuwa sasa wataweka sehemu ya pili ambayo ni mahojiano kati ya Pamela na Mtangazaji. Nilijiweka tayari kusikiliza na kwenye ile CD ilisikika sauti ya mtangazaji ikimwambia Pamela aeleze kila kitu alichotaka kukisimulia pale.



    **PAMELA**

    Patrick alikuwa ameanza kurudisha fahamu kitu ambacho nilikuwa nikikiota siku nyingi, ingawaje kitaaluma nilikuwa daktari tena mtaalamu wa magonjwa ya akili na ubongo na taaluma yangu hainiruhusu kukata tamaa ya kumuhudumia mgonjwa ambaye bado anapumua vizuri ila kwa Patrick ilikuwa tofauti, kuna muda nilikuwa nakata tamaa kabisa, alipotelekezwa pale hospitali niliamua kujibebesha mzigo mzima wa jukumu la kusimamia matibabu yake japo nilipata msaada mkubwa sana toka kwa dokta Anderson na mkewe Sara.

    Historia ya maisha yangu kipindi cha nyuma ilinifanya kuwa mtu mkatili sana lakini sikuwa hivyo kwa Patrick. Yeye ndiye aliyeanza kunionyesha tumaini jipya lililopotea siku nyingi na kunifanya nianze kuwa mtu wa tofauti kabisa katika maisha yangu.

    Nilizaliwa na kuwa yatima miaka mingi sana iliyopita, nilikulia kwenye kituo cha kulelea watoto yatima cha masista na huko tulifundishwa tabia njema na namna ya kuishi na kila mtu, nilipofika kidato cha nne nilianza kujihusisha na mapenzi, sikuwa na akili vizuri, nikajiingiza kwenye mapenzi na kijana Alex ambaye na yeye alikuwa ni yatima pia ila mara nyingi tulikuwa tukionana pale walipokuwa wanakuja kusali kanisani. Nilimpenda sana Alex na niliamini kuwa alikuwa akinipenda pia, nikiwa kidato cha tano nilipata ujauzito na sikujua cha kufanya, nilifukuzwa pale kituoni na baada ya kukataa kusema nani alinipa ujauzito, http://deusdeditmahunda.blogspot.com/nisingeweza kabisa kumtaja Alex kwakuwa ningekuwa nimemuharibia mipango yake ya kimaisha. Nilikuwa tayari kuubeba ule mzigo wa mimba kwakuwa nilimtakia mema hasa nikitegemea kabisa kuwa angekuja kuwa baba wa yule mtoto, hivyo ile mimba ilibaki kuwa ya kwangu na wala Alex hakutaka kusikia, siku moja nilikwenda kama kawaida pale ambapo huwa tunakutana na nikamweleza kuhusu ujauzito ule na aliukana kabisa akasema hajawahi kuwa na mahusiano na mimi, nilimweleza kuwa nia yangu si kumwambia yoyote kuwa yeye ndiye aliyenibebesha ujauzito ila nia yangu ni kumtaka tu ajue kuwa kuna kiumbe chake tumboni mwangu, alikuwa mkali sana na kuniona kama nilikuwa Malaya, siku hiyo alinipiga sana na kunisababishia maumivu makali, niliondoka na kurudi kwenye magofu ya nyumba za watu nilikokuwa nikilala na mchana nilikuwa nikila mabaki ya vyakula vya wahindi. Kila mtu aliniona kama mimi ni Malaya lakini sikujilaumu kwakuwa nilitambua athari za nilichokuwa nafanya na Alex ila niliamua kufanya kwakuwa nampenda.

    Siku tatu mbele nilianza kupata maumivu makali sana ya tumbo na baadaye nilianza kutokwa na damu mabongemabonge, sikuwa na wakumlilia zaidi ya kumuomba mungu anisaidie, nilitokwa na damu siku mbili mfululizo huku maumivu ya tumbo yakizidi, sikuwa na dawa ya kumeza kwakuwa sikujua ni dawa gani nimeze na hata fedha ya kununulia dawa sikujua ningeipata wapi, nilikaa nikitafuna majani ya alovera na baada ya kutokwa damu kwa muda wa siku mbili tumbo lilitulia na sikujua madhara ya kile kilichonitokea yatakuwa wapi ila nilichofahamu ni kuwa mimba imetoka.

    Katika mihangaiko yangu jijini nilikutana na msichana wa umri kama wangu kwakipindi hicho na yeye aliniambia anakwake hivyo tukakae nae na atanifundisha biashara, nilimkubalia kwakuwa sikuwa na machaguo ya kutosha na hapo alinipeleka kwake, palikuwa na chumba kimoja tu lakini kilichojaa vitu mbalimbali vya thamani, nilikaa pale siku moja lakini nilikuwa nimeshagundua kuwa alikuwa akijiuza,kuna muda mwanaume alikuja pale na walianza kushikana mbele yangu, nilinyanyuka na kutaka kutoka lakini yule dada alinikataza na kuniambia kuwa ile ndiyo biashara na natakiwa nijifunze, nilijizuia sana na kutaka kuondoka lakini bado maisha yale niliyokuwa nikiishi yalikuwa ni hatari sana. Hivyo nilikubaliana na yule dada na tulianza biashara hiyo, nilifanya kwa shingo upande lakini kazi ilikuja kunishinda pale wateja waliokuwa wakija pale walipotaka kufanya mapenzi na mimi kinyume na maumbile, nilikataa katakata na hapo yule msichana alinifukuza kwake, niliondoka na kwenda kwenye kile kituo kuomba wanisaidie lakini walinikataa, hivyo ikabidi niingie mtaani tena, nilikutana na mzee mmoja akaniahidi atanipatia kazi nyumbani kwake na mimi nilikubaliana naye na hapo nilipata kazi ya ndani kwa huyo mzee, baada ya mwezi mmoja tu wa kazi vioja vilianza baada ya watoto wake wa kiume kuanza kunitaka, nilikataa mara nyingi lakini kuna siku wakati yule baba amesafiri tukabaki na wanae watatu wa kiume tu, siku hiyo nilitoka bafuni na kuingia chumbani kwangu, nilipovua kanga na kuanza kujifuta maji nilishtuka kuona wale vijana ndani ya chumba changu, nikajifunika na ile kanga lakini walininyang’anya na wawili walinishika kwa nguvu kisha waliniingilia kwa zamu, niliumia sana kwakuwa walitumia nguvu nyingi sana lakini nilipanga kuja kumuambia baba yao japo waliniambia wangenifanyia kitu kibaya kama ningesema kwa baba yao. Mzee wao aliporudi nilimueleza ukweli lakini hakunielewa zaidi ya kunifokea kuwa nimeleta umalaya wangu ndani ya nyumba yake, niliamua kunyamaza kimya na kuendelea na kazi zangu, ile nyumba hakukuwa na mwanamke kwakuwa mke wa huyo mzee alikuwa nje ya nchi kwa masomo na hata watoto wake walikuwa ni watu ambao hawakuwa wakukaa nyumbani sana.

    Wiki tatu baada ya kubakwa na wale watoto, niliamka asubuhi na kujikuta chumbani kwa yule mzee, nilikuwa nimechoka na nilishangaa nilifikaje lakini akili yangu ilikumbuka kuwa jana usiku yule mzee alileta juice na kunipa ili ninywe, nikagundua kuwa aliniwekea kilevi kwenye ile juice na kunibeba hadi chumbani kwake. Kilichoniliza sio yeye kuniingilia kimwili bila ridhaa yangu ila ni yeye kuniingilia kinyume na maumbile, nililia sana lakini hakuonekana kujali;

    “sio sawa ulivyonifanyia” nilimuambia huku nikilia lakini hakunisikiliza.

    “binti wewe kazi yako hapa nyumbani ndiyo hiyo, yani wewe mimi nikulipe elfu 15 kwa mwezi na nikulishe na ulale kwangu kwa kazi ya kupika, kudeki, kufua nguo za watu wote humu ndani na kufanya usafi mwingine tu?,,ni sawa hivyo kweli? Fedha yote hiyo kwa kazi ndogo tu ya kufanya usafi” aliniambia huku akicheka.

    “utajisikiaje kama binti yako ndo angefanyiwa hivyo” nilimuuliza huku nikimtazama.

    “mwanangu hawezi kuwa beki tatu, tena nyamaza kabisa usianze kunihubiria hapa, kafungashe mizigo yako uondoke maana utatuwekea sumu huku ndani, fungasha nikitoka hapa uwe nje ya hii nyumba, chukua fedha zako hizo” alinisukuma na kunipa shilingi elfu 30, nililia sana lakini sikuwa na mahali pa kwenda, nilikwenda polisi kuripoti lakini chakushangaza mwanamke mwenzangu aliyekuwa pale ambaye ni polisi alikuwa wakwanza kunifukuza na kuniita mimi Malaya, aliyeonyesha nia ya kunisaidia alikuwa kijana mwingine askari lakini tulishindwana baada ya yeye kunitaka kimapenzi kama rushwa. Niliamua kumuachia mungu kila kitu lakini nilimchukia kila mwanaume duniani na nilipanga kutokuja kuolewa wala kubeba ujauzito kwakuwa kama ingetokea ningezaa mtoto wa kiume nisingempenda kabisa.

    Nakumbuka ilikuwa ni siku ya ukimwi duniani ambapo shirika la misaada la marekani lilikuwa likifanya kampeni ya kupima kwa hiari, nilikwenda kupima ili nijue afya yangu na hapo ndipo nilikutana na dokta Anderson, nilimueleza kila kitu kuhusu maisha yangu wakati alipokuwa akinipima, na alisema kuwa angenisaidia kurudi shule na mpaka pale ambapo ningetaka kwenda kitaaluma. Nilirudia kidato cha nne kwa msaada wa fedha za mzee Anderson na mkewe Sara, walikuwa nje ya nchi lakini walikuwa wakinitumia fedha vizuri na kwa wakati, nilianza kuona matumaini ya maisha tena na baada ya kumaliza kidato cha nne nilifaulu vizuri na kuchaguliwa kwenda kidato cha tano kilakala sekondari kwa mchepuo wa PCB (fizikia, kemia na baiolojia), kidato cha sita nilifanikiwa kufaulu kwa daraja la kwanza na hapo ndipo dokta Anderson aliponichukua na kunipeleka kusoma nchini Australia kama daktari na baadaye shahada yangu ya pili nilisomea mambo ya magonjwa ya akili, nilifanya kazi na dokta Anderson miaka yangu yote mpaka nilipoomba uraia wa huko na kujivua uraia wa Tanzania, sikuwa na hisia na wanaume kabisa na mwaka mmoja kabla ya kumfahamu Patrick nilikuwa kwenye mahusiano na mwanamke mwenzangu, nilikuwa msagaji lakini yote haya ni kwakuwa hisia zangu zilihama na kwenda kwa wanawake wenzangu.

    Yaliyomtokea Patrick yalinikumbusha sana yaliyotokea Tanzania na hiyo ilikuwa sababu ya mimi kujitolea kumsaidia. Kwa ufupi Patrick alirudisha hisia zangu juu ya wanaume, mwanaume pekee niliyekuwa nikimuona kama mungu wangu ni mzee Anderson lakini wengine wote hata madaktari wenzangu niliofanya nao kazi walinijua kuwa sikuwa nawapenda hata kidogo, wengi walijua kuwa mimi ni msagaji na walichukia tabia yangu hiyo lakini kwangu ilikuwa ni faraja na nilijisikia vizuri sana kuwa kwenye mapenzi na mwanamke mwenzangu, nilimpenda sana na yeye alinipenda na alinipa kila nitakacho na wala sikuhitaji mwanaume. Lakini uwepo wa Patrick pale hospitali ulinibadilisha taratibu na hata Nancy ambaye ndiye alikuwa mpenzi wangu alianza kulalamika kuwa nimemsahau, nilimueleza ukweli kuwa kwasasa sitaweza tena kuwa naye kwakuwa nahisi nampenda mtu mwingine. Alilia lakini nilipomueleza kiundani alinielewa. Kwa miaka sita yote Patrick akiwa kitandania kama mfu nilikuwa naye pembeni, kuna muda nililala pembeni naye usiku kucha, kuna wakati nilikuwa siendi kwangu baada ya kazi na badala yake nilikuwa nikikaa pale chumbani kusubiri mda atakaofungua macho, nilitaka japo kuisikia sauti yake, sura yake nzuri na ya kitoto ilinifanya nimpende, nilimuonea huruma kwa alichotendewa lakini pia niliona nina nafasi ya kumsaidia, miaka sita na mwezi mmoja ulipotimia siku hiyo ilikuwa asubuhi nikaona manesi wakikimbizana huku na huko na dokta Anderson alikuwa akikimbia kuelekea chumba alichokuwa amelazwa Patrick, sikujua kilichoendelea ila nilijikuta nikianza kulia kwakuwa nilidhani Patrick amefariki kwasababu jana yake usiku hali yake haikuwa nzuri, sikuweza kwenda kule kwakuwa nilikuwa naingia kwenye chumba cha upasuaji hivyo nilijikaza na kuingia na jopo la madaktari wengine, tulifanya upasuaji kwa masaa manne mfululizo, baada ya kutoka nilikutana na dokta Anderson aliyekuwa anaonekana akitabasamu;

    “Ameamka na yuko salama kabisa” aliniambia huku akinifata na kunikumbatia, niliona kabisa machozi yakinitoka.

    “Natumaini furaha yako itazidi Pamela na kazi kubwa kwasasa ni kuhakikisha Patrick anakuwa salama na hali yake inarudi kama mwanzo, naamini hiyo ndiyo kazi kubwa uliyokuwa nayo kwasasa binti yangu” alinieleza hayo na mimi nilipata faraja sana, dokta Anderson aliielewa furaha yangu na siku zote alinichukulia kama Semphroza ambaye ni binti yake aishiye marekani na mumewe. Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu kabla ya Patrick kuamka.

    *******

    “Mary Robert” nilisikia Patrick akitaja jina la yule mwanamke aliyemtelekeza, nililia kwa furaha japo nilijua lengo langu la kuwa na Patrick lingekuwa gumu sana kama angekuwa bado anampenda Mary. Nilifanikiwa kukaa na Mary na kuongea naye miezi michache kabla ya yeye kuondoka, alikuwa anaonekana kama msichana wa kisasa zaidi, alikuwa ni mtu wa kuongea na simu kila saa, mtu ambaye ni msiri sana na mtu anayekwenda na mda, hakuwa muongeaji sana wala hakutaka kukaa na mtu mda mrefu, sikuweza kujua kama anampenda kweli Patrick au la japo baada ya yeye kuondoka ndiyo nilikuja kujua kuwa hakuwa mvumilivu.

    “Unamkumbukaje Mary Robert” nilimuuliza Patrick ambaye alionekana akiwa ameduwaa huku machozi yakimtiririka.

    “sikumbuki, simkumbuki Mary, sielewi kitu” alizidi kulia huku akitazama mbele kama alikuwa akiona kitu, nilimshika na kumkumbatia huku na mimi machozi yakinitoka, ilionekana kama anajitahidi sana kukumbuka lakini haikumsaidia hiyo.

    “Tafadhali kama unajua chochote kuhusu Mary nieleze, yeye ni nani, anafanya nini kwenye maisha yangu” aliniuliza huku akilia.

    Nilimuacha pale na kwenda kufungua kabati kisha nilitoa boksi lenye barua na pesa ambayo Mary aliiacha kwenye mfuko pale hospitali kabla hajaondoka bila kuaga, sikuwahi kuisoma ile barua kwa miaka yote hiyo, wala sikuwahi hata siku moja kutumia zile pesa. Nilifungua lile boksi na kutoa ile barua na yale mabunda ya pesa nikayaweka pale kitandani kisha nilimkabidhi ile barua na yeye akaifungua, niliona machozi yakimtoka kila alipokuwa akisoma mstari mmoja wa ile barua, sikuwa najua ni nini kimeandikwa kule ndani mpaka nilipoichukua ile barua na kuanza kuisoma. Nilitokwa na machozi na kumgeukia Patrick.

    “Pamela ni nini kinaendelea mbona sielewi kila kitu” aliniuliza huku machozi yakiwa yameufumba uso wake, nilimuonea huruma kwakuwa nilielewa maumivu ayapatayo kwa hilo limtokealo. Ile barua ilisomeka hivi;

    mpendwa mume wangu,

    Nakuandikia ujumbe huu kwa uchungu na masikitiko makubwa. Najua huwezi kupona tena katika maisha yako kwani daktari amenieleza kuwa uwezekano wa wewe kurudisha kumbukumbu zako ni mdogo sana,,nilipenda kuwa na wewe Patrick na unalijua hilo lakini sikuwahi kufikiri kuwa nitakuja kuishi na wewe katika hali hiyo uliyokuwa nayo,,honeymoon ndo chanzo cha yote, huwezi kunikumbuka hata mimi najua,,nilikupenda sana Patrick, lakini nina malengo mengi ya kuyatimiza kabla ya kuingia kaburin hivyo sina budi kukuacha na kwenda kuendeleza maisha huko nyumbani,,nisamehe, sina jinsi ya kufanya zaidi ya kwenda kuwaambia nyumbani kuwa tulipata ajali kwenye boti na ulipotelea baharini,,nimeacha kiasi cha fedha cha kutosha naamini kitakusogeza,, ikiwa hutafanikiwa kuisoma barua hii na ikitokea kuwa umepoteza maisha basi jua kuwa ninakazi kubwa ya KUMALIZIA MENGI NILIYOANZISHA NAKUPENDA,nakupenda sana ila siwezi kuendelea kuishi na wewe hapa maana itakuwa napoteza muda.

    MAISHA MEMA Patrick.



    Mimi Mary

    Ilisomeka sehemu ya barua hiyo.









    Ilikuwa inaelekea saa 5 ya usiku, ile simulizi ilikuwa imenishika sana na sikutamani wamalize, niliendelea kusikiliza mahojiano yale kwa makini sana na yule msichana Pamela alikuwa anaendelea kusimulia.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    **PAMELA**

    Niliendelea kumtazama Patrick huku nimeshikilia ile barua, alikuwa akifikiria mbali sana na sikujua nimuanzeje kwakuwa alikuwa kwenye wakati mgumu sana.

    “Patrick” nilimuita huku nikimshika bega. Alinigeukia na kunitazama huku machozi yakimtoka.

    “Usilie Patrick nipo hapa kwaajili yako” nilimsogelea na kumkumbatia, haikuwa rahisi kuvumilia kumuona mtu umpendaye akilia mbele yako kwa maumivu ambayo wewe usingeyavumilia kama ungehitajika kuyakabili.

    “Kwanini Mary amenifanyia hivi, sikustahili kufanyiwa hivi” aliongea hayo huku akiendelea kutoa machozi. Alikuwa tayari amesharudisha fahamu na sasa alielewa kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Hii ilinipa faraja sana kwakuwa siku zote nilitamani akumbuke kila kitu tena ili na mimi niwe na furaha, nilimtazama usoni na kuona jinsi gani alikuwa akimpenda Mary na alikuwa anaumia moyoni kwa kilichotokea.

    *SIKU TATU MBELE*

    “Patrick una mpango gani kwahiyo maana leo ni siku ya pili huongei chochote” nilimuuliza baada ya kuchoka kumuona kila mara akikaa peke yake na kutaka kuwa peke yake, ile hali iliniumiza sana sikuelewa wala kujua nimsaidie vipi, lakini utatuzi pekee niliokuwa nao kwa wakati huo ni kumpenda kwa dhati na kumfanya amsahau Mary japo nilijua fika kuwa kumsahau mtu uliyempenda kwa dhati ni sawa na kujaribu kumkumbuka mtu ambaye hujawahi kukutana naye.

    “sijui mpango nilionao Pamela, sijui ni nini nafikiria wala namna ya kufanya chochote” aliongea hayo huku akitazama mbele kabisa ya ufukwe wa bahari.

    “Ulijuana wapi na Mary?” ndilo swali nililomuuliza wakati akiendelea kutafakari, alinishika mkono na kuondoka na mimi kuelekea ufukweni na tulipofika alianza kunisimulia historia yake na Mary.

    “Nilimjua Mary miaka miwili kabla ya kufunga nae ndoa. Tulikuwa tukiishi naye mtaa mmoja na sikumjua kwa kipindi cha udogo wake bali kipindi cha ukubwa wake. Alizaliwa pale mtaani kwetu kule Tanzania, mimi sikuzaliwa pale, nilizaliwa sehemu nyingine lakini kwakuwa wazazi wangu walikuwa wameachana toka utoto mwangu nililazimika kuja kuishi na baba na mama mwingine ambaye alikuwa na mtoto mmoja aitwaye Mark, kwaiyo katika familia hii tulikuwa wawili tu, mimi na mdogo wangu Mark, katika muda wote tuliokaa pale, nyumba ya kina Mary ilikuwa ikikaliwa na mfanyakazi tu, nilielezwa kuwa mwenye nyumba ile anaishi marekani na anafanya kazi huko, ana mtoto mmoja wa kike na mkewe nalishafariki siku nyingi nyuma. Miaka mingi baadaye walirudi yule mzee na mwanae Mary, alikuwa ni msichana mrembo sana, mrefu wa wastani, mwenye kila aina ya sifa, alikuwa ni mtoto wa kisukuma aliyechanganyika na mnyakyusa, mchanganyiko huo ulizalisha kitu kinachoonekana. Nilipomuona sikushtuka sana kwakuwa sikuwa na mawazo naye. Mara nyingi nilimsikia Mark akimsifu na walikuwa wakiongea mara kwa mara kwenye simu, ni wakati huo ndipo nilikuwa nimeshahama nyumbani na kuanzisha kampuni yangu ya harusi na mapambo, iliyoitwa PATRICK WEDDING AND DECORATION COMPANY LTD, ilikuwa ni kampuni kubwa kuliko zote Tanzania kwenye mambo ya upangaji wa harusi na upambaji. Kampuni hii ilikuwa inachukua tenda kamili za harusi, yaani mtu kama anaharusi au sherehe yoyote anakuja na kutoa fedha yote kwaajili ya sherehe na sisi tulikuwa tunatafuta ukumbi, tunahusika na kuandaa mavazi yao, sare na kadi za waalikwa, muziki na mshereheshaji,tulikuwa tunachukua video kwenye hayo maharusi na kutoa usafiri, pia baada ya kumaliza mkataba wa kusimamia harusi hizo ilikuwa mteja akitaka kwenda mapumizikoni basi tunaingia naye mkataba wa kumfanyia utaratibu wa kwenda na kuhakikisha usalama wake mpaka atakaporudi. Hii ilikuwa ni kampuni kubwa sana iliyoajiri watu zaidi ya hamsini wenye fani mbalimbali, ni kampuni ya ndoto yangu. Nilipokuwa katika shughuli zangu za kikazi nilikuja kukutana na Mary siku alipokuja ofisini kwangu kwaajili ya kuomba kuonana na mimi ili afanye mahojiano juu ya mafanikio yangu na maisha ya mapenzi, hapo ndipo niligundua kuwa Mary alikuwa akimiliki kampuni iliyokuwa ikichapisha jarida la EXLENT MEN lilikokuwa likitoka kila mwezi na kuelezea juu ya wanaume wenye mafanikio walio chini ya umri wa miaka 35. Alikuwa ni msichana mcheshi sana, mjanja na ambaye alijitolea maisha yake kujiimarisha na kuwa mfano wa kuigwa, alikuwa mmoja kati ya wanawake wachache ambao hawakuwa maarufu lakini walikuwa machachari na wachapakazi tena akiwa na umri wa miaka 25 tu.

    ****

    “karibu sana Mary” ilikuwa ni siku aliyokuja rasmi kwaajili ya yale mahojiano, alikuja na timu ya wafanyakazi wake ambao ni wapiga picha na waandishi wengine, ni mara chache saba meneja akaja kuhoji mtu badala ya waandishi waajiriwa ila kwangu mimi alikuja kunihoji yeye mwenyewe, hivyo niliwakaribisha hadi sehemu maalumu iliyokuwa imeandaliwa kwajili ya mahojiano hayo.

    “Asante sana ndugu Patrick, najua mimi na wewe tunajuana ila leo nimekuja kikazi zaidi,,hahaa” aliongea huku akicheka na wakati huo wale wengine walikuwa wakifunga kamera zao na muda sio mrefu mahojiano yalianza;

    “kwanza nilitaka kujua juu ya mafanikio yako bwana Patrick” aliniuliza swali huku akitabasamu, hapo ndiyo nilianza kugundua hisia zangu kwa Mary, japo alionekana kabisa kuwa alikuwa si msichana mwepesi sana kukubali hisia za mwanaume kuingilia maamuzi ya fikra zake.

    “mh,,baada ya kumaliza chuo kikuu ambapo nilisoma mambo ya ujasiriamali, ndiyo niliandika mradi huu wa kuanzisha kampuni, sasa zilikuwa zikihitajika milioni 150 ilikuanzisha mradi lakini niliweza kufanikisha kupata milioni tano tu toka kwa mzee wangu, hivyo nililazimika kuingia benki kuomba mkopo wa milioni 30 kwa kutumia kiwanja nilichopewa na mzee, baada ya kupata mkopo nikaanza mradi wa kuku elf 3 ambao ndio ulionipa mtaji wa kuanzisha hii kampuni” wakati nikimueleza hayo yeye alikuwa makini sana kunitazama usoni, niliona upendo toka kwenye sura yake pale nilipomtazama.

    “uuum,,unakipato cha shilingi ngapi kwa project zako zote” aliniuliza huku akicheka.

    “napata wastani wa milioni 40 kwa mwezi baada ya kutoa matumizi yote” nilimjibu na kumtazama tena machoni na yeye aliona aibu na kutazama pembeni.

    “kwanini hujaoa” aliniuliza huku akitabasamu.

    “mmh, nadhani muda bado kidogo, lakini pia wakumuoa bado sijampata, wengi wanatamani mali nilizonazo lakini mimi nahitaji mtu wa kumpenda Patrick na si mali za Patrick” mahojiano kwa siku hiyo yaliendelea kwa muda kidogo na baada ya pale tulipata chakula cha mchana na wafanyakazi wake aliokuja nao pamoja na baadhi ya wafanyakazi wangu. Tulibadilishana namba za simu za mkononi na hapo tulianzisha urafiki wetu. Nilimuajiri Mark kama muhasibu kwenye kampuni yangu na nilikuwa nikimlipa mshahara mara tano zaidi ya wafanyakazi wengine waliokuwa na vyeo vinavyoendana na yeye, yote ni kumfanya yeye kama ndugu yangu awe na maisha bora, ingawaje mimi na Mark hatukuwa karibu sana au kuwa tunakaa na kuzungumza kuhusu mapenzi, bali mda mwingi tukikaa tulikuwa tukiongelea kazi na maisha tu.







    **MIEZI MIWILI BAADA YA MAHOJIANO**



    Ikawa ni miezi miwili toka Mary aje kunihoji, wakati huo nilikuwa nimeshuka uwanja wa ndege nikitokea Afrika ya Kusini kwenye biashara zangu, nikashtuka kumkuta Mary pale uwanja wa ndege akinisubiri, kilichonishangaza ni kwamba toka baada ya mahojiano nilikuwa nimeongea naye kwenye simu mara mbili tu na sikuwahi kumwambia naenda nje wala kumuambia narudi Dar hivi karibuni.

    “umekuja kufanya nini Mary” nilimuuliza pale alipokuja na kunikumbatia.

    “Nimekuja kukupokea” aliongea huku akicheka kama kawaida yake.

    “Nani kakuambia juu ya safari yangu” nilimuuliza wakati tukitembea kuelekea nje, hakunijibu haraka ila alipokea mizigo yangu na kuingiza kwenye gari yake kisha alinifungulia mlango na kuniambia niingie.

    “vijana wangu wale pale wamekuja kutuchukua” nilimuambia huku nikiwa nimesimama namtazama jinsi alivyokuwa akicheka.

    “mwambie sekretari wako aende akapande kule na huyo kijana wako mwingine, mimi leo nitakuwa dereva wako na napenda twende kwangu kwanza then nitakupeleka kwako” nilimtizama na kutabasamu, sikuwa na la kusema zaidi ya kumkubalia name niliingia kwenye gari yake tayari kwa kuondoka. Nilipofika kwake hakukuwa na mtu zaidi ya mlinzi wake, ilikuwa ni nyumba ndogo ila yenye bustani kubwa na iliyonakshiwa vizuri sana kwa rangi za kuvutia, alikuwa na magari mawili ya kifahari yaliyopendezesha muonekano wa ile nyumba. Tuliingia mpaka ndani na kisha aliniacha pale sebuleni huku nikishangaa jinsi alivyokuwa amepapamba pale ndani, alirudi na kuniambia kuwa bafu liko tayari kama nataka kwenda kuoga.

    “hahaa sio busara kuoga nyumba ya mtoto wa kike” nilimueleza huku nikicheka kama yeye alivyokuwa akicheka wakati akinieleza hayo.

    “mimi kwako ni zaidi ya mtoto wa kike, tafadhali nifate nikuonyeshe bafu lilipo na nguo zipo za wewe kubadilisha nilinunua kwaajili yako” aliongea hayo na hakunipa muda wa kuongea chochote, alinitazama huku akitabasamu na kuelekea kwenye korido na mimi nilimfata, aliingia chumbani na kunionyesha bafu la chumba chake na nguo zilikuwa zipo pale kisha alifunga mlango na kurudi sebuleni, nilijiuliza sana nini nia ya Mary kufanya vile.

    “Happy birthday Patrick” niliisikia ile sauti baada ya kutoka bafuni na kwenda kwenye meza ya chakula aliyokuwa ameandaa, kiukweli sikuwa na habari kuwa siku hiyo ilikuwa ni kumbukumbu ya siku yangu ya kuzaliwa, lakini swali lilikuwa ni je Mary alijulia wapi siku yangu ya kuzaliwa na alifanya vile kwa nia gani.

    “umejuaje siku hii Mary” nilimuuliza baada ya kumaliza kuzima ile mishumaa.

    “Nakupenda Patrick, ndiyo maana nafatilia kila linalokuhusu, natamani sana uwe mume wangu, naamini wewe utanijali na kunipenda kwakuwa nimeona upendo kwenye macho yako” aliongea hayo huku akimaanisha, niliyaamini maneno yake kwakuwa aliyaongea kwa sauti ya ujazo wenye kumaanisha.

    “Mary unauhakika na unalolisema hapa? Nakupenda pia na nina hisia na wewe toka siku ulipokuja kunihoji pale ofisini kwangu, lakini nayajua mapenzi vizuri, si kitu cha kukikurupukia sana kama tunavyoweza kukurupukia mambo mengine” nilimuuliza jambo ambalo nilikuwa na uhakika nalo kuwa jibu lake lilikuwa chanya.

    “nina jiweza Patrick kiuwezo na kimaisha ninachofata kwako ni penzi tu” aliongea huku akinishogelea na kunishika midomo yangu. Siku ile ilikuwa ndiyo siku ya kwanza ya mapenzi yangu na Mary, nilimvisha pete ya uchumba kama miezi mitatu baadaye na yeye ndiye alikuwa maisha yangu tena, alikuwa faraja yangu na kiongozi wa hisia zangu.

    Baaya miezi sita toka nimvishe pete Mary nilisikia kuwa Mary alikuwa na mahusiano na Mark, nilishtuka lakini kwakuwa nilikuwa nina kazi nyingi za kufanya sikutaka kufatilia kwanza lile jambo. Mary nayeye hakuwepo nchini hivyo sikuwa na namna ya kumuuliza kwa ukaribu, nilisubiri hadi siku aliporudi ndipo nilipomuuliza;

    “haikuwa hata ni mahusiano, ni utoto tu, mimi na Mark tulisoma shule moja ya msingi na tuliishi kipindi kirefu sana kwa ukaribu na hata sekondari tulisoma nae, yeye ndiye aliyenitoa bikra lakini ilikuwa ni katika hali ya utoto, nilipofika kidato cha tatu mama yangu alifariki na nililazimika kwenda kuishi na baba nchini marekani, niliporudi nilikuwa na mawasiliano na Mark lakini sikuwa nampenda tena” alinieleza hayo na mengine mengi lakini nikaona busara ni kumfata Mark na kumuuliza.

    ****

    Niliondoka jioni ya siku ya jumatano na kwenda nyumbani kwa Mark, haikuwa kawaida kwa mimi kumtembelea sana nyumbani kwake mara kwa mara.

    “karibu bro, leo naona umepotea njia” alinikaribisha huku akinitania, Mark alikuwa ni ndugu yangu wa damu, tulizaliwa mama tofauti lakini baba yetu alikuwa mmoja lakini yeye alikuwa na tabia ya tofauti na mimi, mimi nilikuwa muwazi sana, nikikasirishwa huwa nasema ila yeye hata umkasirishe sio rahisi sana kusema au kukuonyesha.

    “hapana leo nimekuja kukucheki isijekuwa ushaoa na watoto unao huku ndani lakini husemi,,hahaa” nilimtania na kuingia ndani kisha nilikwenda kwenye jokofu na kujichukulia kinywaji.

    “Vipi tena bro, ni kuhusu wazee au ni nini” aliniuliza huku akiwa amesimama.

    “Hapana ni kitu kingine, embu keti chini” nilimuambia na yeye aliketi.

    “Mark nakaribia kuoa, umri unaenda na nina kila kitu, nafikiri sasa ni muda wa mimi kuoa na kuanzisha familia mapema kabla sijaishiwa nguvu za kutafuta pesa” nilimuambia hayo na kuvuta pumzi, sikujua niliielezee vipi lile swala.

    “Ni wazo zuri bro, na naamini Mary atakuwa mke bora kwako” aliongea kwa sauti ya upole iliyojaa unyonge.

    “natumaini hivyo lakini kuna swala linanitatiza kidogo” nilimuambia hayo huku nikimtazama usoni.

    “ni nini tena bro?” aliniuliza huku akionekana kuhofia kitu fulani.

    “Ni kuhusu mahusiano yako na Mary” nilimueleza hayo na kumfanya abadilishe mkao, alionekana hakuwa tayari san kuanza kuliongelea hilo lakini sikuelewa sababu ni nini.

    “Bro, mimi na Mary tulikuwa wapenzi, na nadhani kwasasa hakuna linaloendela baina yetu mimi na yeye, kwahiyo wewe endelea tu” alinijibu kwa kifupi sana na alionekana alikuwa amebadilika kabisa, sikujua ilikuwaje mpaka akawa vile lakini niliyachukua maneno yake kama Baraka zake kwangu, hivyo baada ya kumsoma Mary kwa muda mrefu sasa tuliamua kuunganisha kampuni zetu na kuwa kampuni moja, tulikuwa tukishughulika na utoaji wa majarida na mambo ya harusi kwa pamoja, kampuni mpya iliitwa PATRIMARY GENERAL ENTERPRISES LTD, na Mary alikuwa Meneja Masoko na Muhariri mtendaji wa Jarida, Mark alikuwa ni Muhasibu na Mkurugenzi mtendaji, mimi nilibaki kuwa Meneja mkuu, wafanyakazi wote walibaki kama walivyokuwa na wengine tuliwapandisha cheo. Baadaye nilifunga ndo takatifu na Mary na baadaye tulikuja mapunziko huku FIJI, yote yaliyotokea yalitokea tukiwa huku Fiji”. Alielezea Patrick huku akibubujikwa na machozi.

    “bado unampenda Mary” nilimuuliza huku machozi yakinitoka, sikutaka aseme kuwa anampenda kwakuwa tayari mimi nilikuwa nampenda yeye.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nampenda sana, sikuwahi kuacha kumpenda” maneno hayo yaliuchoma sana moyo wangu, nilinyanyuka pale na kuondoka kurudi nyumbani, Patrick alibaki pale ufukweni, nilifika mbele kidogo nikasikia mlio mkubwa wa bunduki, nilishtuka na machozi yangu yalikauka, nilipotazama nyuma niliona kwa mbali Patrick akianguka.







    “Ulemavu wa fikra mgando tulizonazo juu ya maisha na juu yetu wenyewe huzaa mawazo mpauko yasiyoakisi umuhimu na umaana wa utu wetu na malengo yetu, kuna muda tunafikiri kuwa watu wa aina fulani ndio wawezao kufanya mambo ya maana na yenye maendeleo kwa wao wenyewe, na sisi kujiweka nyuma kwa miakisio ya ubovu wa uteuzi wa fikra sahihi dhidi ya fikra mtambuka. Tunawaza zaidi kuliko kufikiri juu ya hatima ya uzio wa upeo wetu na malengo yetu. Akili zetu hutuongoza katika mwambao wa kukata tamaa na kutojikubali. Tunahangaikiwa kuona kuliko kutazama na kuyafanya ya mwisho kuwa ya kwanza. Sisi ni zao la umakini hafifu wenye kichefuchefu cha kutambua tunapotaka kwenda na njia tupitayo. Ukungu wa fikra potofu huyasonga mawazo machachu tuliyonayo juu ya yale tuyaamaniyo kwenye maisha ya wengine. MABADILIKO NI WEWE,,WEWE NI SERIKALI YA AKILI YAKO.” HII NI SEHEMU YA NNE.”

    Ni saa sita na nusu usiku bado sauti ya yule dada ilikuwa ikisikika ikihadithia,,mawazo yalikijaa kichwa changu kwakuwa sikujua majibu ya maswali mengi niliyokuwa nayo, kibaya zaidi ni kuhusu huyu Patrick, mkojo ulikuwa umenibana na sikutaka kutoka nje kwakuwa nilihisi kukosa baadhi ya sehemu, hivyo niliibana miguu yangu vizuri ili kuuzuia, muda kidogo nilisikia mtangazaji akisema kuwa ni mda wa matangazo hapo ndiyo nilikurupuka na kwenda chooni, niliporeje Pamela alikuwa anaendelea kusimulia ule mkasa.

    ***PAMELA***

    Ule mlio wa bunduki uliuumiza sana moyo wangu hasa nilipoona Patrick akidondoka, nilisikia tena mlio mwingine na hapo nikatazama huku na kule kuangalia ni nini kimetokea, nilikimbia bila kujali kuwa na mimi ningeweza kupigwa na risasi, nilipofika pale Parick alikuwa chini, nikapiga haraka simu pale hospitali na ndani ya dakika tatu gari ilikuwa imefika tukampakia na kumpeleka hospitali. Hakuwa na jeraha lolote.

    *****

    “Ni mshtuko tu na inabidi tumchome sindano ya usingizi apate masaa mengi ya kupumzika, utamuhudumia wewe kwa ukaribu zaidi” alikuwa ni dokta Anderson akinieleza hayo baada ya kutoka kwenye kile chumba Patrick alichokuwa amewekwa. Sikujibu chochote bali nilitoka na kwenda kuchukua mabomba ya sindano nikamchoma kwa haraka sana na kuondoka kuelekea nyumbani kwangu, nilichukua bastola yangu na kwenda mpaka kule ufukweni, nilizunguka kote na pembeni ya vile vichaka lakini sikuona mtu yeyote, nilisogea mpaka pale mbele karibu na Patrick alipokuwa ameanguka na nilipotazama wenye mti niliona ile risasi ikiwa imepenya kwenye ule mti, nilichukua kichuma kidogo nikahangaika mpaka nikaichomoa ile risasi.

    “ngriiiii,,,ngriiii” ulikuwa mlio wasimu ukiita ndani ya simu yangu.

    “Habari yako Pamela” aliongea yule mtu baada ya kupokea simu.

    “Nzuri Felicity habari ya kwako mpenzi” tulisalimiana lakini sikuwa na maneno mengi sana ya kusema.

    “upo kwako? Nataka kuja hapo nina shida” nilimuliza huku nikionekana mwenye haraka.

    “ndio njoo,,kuna tatizo gani?” aliniuliza lakini kabla hata sijamjibu nilikuwa nimeshakata simu na kuanza kukimbia kuelekea nyumbani, niliwasha gari na kuelekea kwa Felicity ambapo ni mwendo wa dakika kumi na tano toka kwangu, nilikuwa na mawazo sana na nilikuwa nimeshachoka kwa kufikiri ni nani anataka kumuua Patrick na kwanini, nilihisi kama pengine Patrick alikuwa kwenye matatizo makubwa na sasa alitakiwa kuuwawa ila sikujua nani muhusika na kwanini afe.

    ***

    “karibu Pamela” Felly alinikaribisha na hapo niliingia mpaka ndani kwake, alienda kunichukulia juice kitu ambacho niliona kama ni kupoteza muda ila sikuweza kumwambia aache kakuwa hakuniambia kama anaenda kuleta juice.

    “karibu Pamela” alinikabidhi ile juice huku akinitazama usoni.

    “kunanini Pamela?” aliniuliza.

    “unakumbuka nilikuambia nina boyfriend sasa hivi ila nikakuelezea kuhusu ile ajali yake na kila kitu?” nilimuuliza kwanza.

    “Ndio nakumbuka” aliitika huku macho yakiwa yamemtoka, nilijua kuwa aliwaza moyoni pengine Patrick amefariki hivyo sikumuacha akae na mafikirio hayo kichwani mwake hata kwa sekunde moja kwakuwa sikutaka yeyote awaze hayo.

    “Leo kama lisaa limoja lililopita amekoswa na risasi kule ufukweni na amepoteza fahamu, sijui ni nani kafanya hivyo lakini naamini wewe unaweza kunisaidia kufanya hivyo” nilimtazama kwa makini huku kijasho chembamba kikinitoka.

    “umefanikiwa kuipata hiyo risasi” aliniuliza.

    “ndiyo ninayo hapa” niliitoa ile risasi na kumkabidhi.

    “sawa nipe muda nitakujibu kesho nitakachokuwa nimekigundua” nilinyanyuka nikamkumbatia na kuondoka.

    Felicity alikuwa ni rafiki yangu wa siku nyingi toka nikisoma shahada ya kwanza tulisoma chuo kimoja, na nilipokwenda kusoma shahada ya pili naye pia tulisoma nae lakini yeye alisoma mambo ya uchunguzi wa kisayansi wa makosa ya jinai(criminal and forensic investigation), baada ya kumaliza shahada ya pili aliajiriwa kwenye maabara ya mkemia mkuu na baadaye alikwenda kitengo cha polisi wa upelelezi, hivyo ni mtu ambaye ni mtaalamu sana wa kufanya uchunguzi wa mambo hayo, nilikuwa na shahuku sana ya kutaka kujua.

    KESHO YAKE.

    “pipii,,,pipiiii” zilikuwa honi za gari, nilikurupuka toka usingizini na kuchukua shati la Patrick lililokuwa limetundikwa ukutani kisha nikalivaa na kuchingulia dirishani. Niliona gari kule nje nikagundua alikuwa ni Felly, hata sikuhangaika kufungwa shati nikatoka vilevile nikiwa nimelivaa huku nikiwa na chupi tu, nilisogea pale getini na kufungua geti kisha aliingia.

    “hey unakuwa kichaa au ni nini” aliniuliza huku akicheka. Alikuwa amependeza, Felly alikuwa ni mzuri ila sikuzote alikuwa akijiweka katika namna ambayo wanaumea wengi waliogopa kumfata, alikuwa ni mrefu na mara zote alikuwa akivaa nguo zake za upelelezi na kuweka bastola yake kiunoni, alikuwa ni msichana lakini ningeweza kumfananisha na nikita au Angelina Jolie kwenye Salt, au Nina Myer kwenye 24 au Anny Walker kwenye Covert affairs, alikuwa ni mtu wa mazoezi na mwalimu wa karate katika chuo cha polisi pia, hayo yaliwafanya wanaume wengi sana wamuogope, japo mwanaume mmoja tu alifanikiwa kuuteka moyo wake lakini alifariki akiwa vitani nchini Iraq kwahiyo mar azote amekuwa akishindwa kutafuta mtu mwingine kwakuwa anashindwa kumsahau yule aliyekuwa nae.

    “Felly acha tu mpenzi, nakosa usingizi sasa yani nimepata usingizi asubuhi hii” nilimwambia huku nikitangulia ndani.

    “mimi sikai nataka unipeleke hapo ulipoitoa hii risasi” aliniambia huku ameshikilia kiuno na kuyatazama makalio yangu.

    “Hey stop that, have you become a Lesb?”(hey acha, umekuwa msagaji) nilimwambia huku nikivuta shati langu na kuingia ndani.

    “hahaa you are”(wewe ndiye msagaji) alicheka na mimi niliingia ndani nikavaa suruali na kutoka nje kisha tuliteremka kuelekea ufukweni. Nikamuonyesha ile sehemu.

    “sasa kama risasi imekuja hapa inamaana imepita mkono wa kulia wa Patrick kwa futi sita toka alipokuwepo, na itakuwa imetoka mita miamoja mbele yake kwenye kale kamsitu pale, sasa hii inamaana kama angekuwa anataka kumuua Patrick basi risasi isingepita mbali hivyo, na isingepigwa mara ya pili na isionekane kujia upande huu. Lakini pia kama alipanga kumuua Patrick basi huyo mtu atakuwa sio muuaji anayejua kuua na atakuwa ni mwanamke, kwakuwa risasi inapotoka inatoka na mtetemo hivyo kama mkono sio imara basi lazima iyumbe na isifike pale inapotakiwa kufika, hivyo muhalifu wetu hapa kama alikuwa hana shida ya kuua atakuwa ni mwanaume au mwanamke ila kama alidhamiria kumduru Patrick atakuwa ni mwanamke ambaye ni laini na muoga.” Alimaliza kuniambia Felicity na kunishika mkono kisha tuliondoka na kurudi nyumbani. Akili yangu ilijua wazi kabisa hapa itakuwa ni Mary, nilikuwa siwezi hata kuongea.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “unahisi anaweza kuwa ni nani” aliniuliza Felly

    “sihisi chochote, au pengine atakuwa ni Mary yule mpenzi wake aliyemtelekeza huku” nilimuambia hayo huku nikiwa ninahasira kweli.

    “inawezekanaje wakati alishaondoka” Felly aliniuliza na hata hivyo sikuwa nina uhakika na nilichokiongea lakini hiyo ilikuwa ni fikirio langu ka kwanza.

    “Sielewi Felly ila fanya uwezavyo umgundue huyo mtu aliyefanya hivyo, hata kama hakuwa na nia ya kumdhuru Patrick lakini nataka kumjua”. Tuliachana yeye akaelekea kazini na mimi nilijiandaa kuondoka kwenda kazini. Nilipofika nilimkuta Patrick amesharudi katika hali ya kawaida na sasa alikuwa nje ya hospitali.

    “vipi unajisikiaje Patrick” nilimuuliza kwa shauku nikitaka kusikia tu sauti yake.

    “niko salama, nimekumis” ooh aliongea maneno yaliyonipa sana faraja aisee, Patrick alikuwa si mtu hata wa kucheka kwa dakika moja toka arudishe fahamu alikuwa ni mtu wa kukaa kimya tu na kutabasamu kwa mbali.

    “oooh Patrick nimekumis pia mpenzi wangu” nilimshika kichwa kwa mikono yangu miwili na kupeleka ulimi wangu mdomoni mwake bila hata ya uwoga.

    “inabidi nimtafute mtu aliyenyuma ya haya yote Pamela hivyo nitahitaji kurudi Tanzania” kauli hii ilinivuruga akili na moyo kwakuwa sasa hii haikuwa tena nzuri kwangu. Nilimuachia pale na kunyanyuka nikizunguka huku na kule kama chizi huku machozi yakinitoka, ilikuwa ni ngumu kwangu kwakuwa sikuwa na namna ya kumuachia Patrick asiondoke.

    “Pamela, najua hii ni ngumu kwako, natambua hisia zako kwangu lakini nakosa Amani kuishi bila kujua sababu iliyopelekea mimi kukaa kitandani, nataka kujua kila kitu ili nafsi yangu utulie, nataka kufahamu hatma ya mali zangu zote nilizozisumbukia” Alinikumbatia kwa nyuma akapitisha mikono yake kiunoni mwangu na kuikutanisha kwa mbele.

    “ni mapema mno Patrick, mimi ni daktari wako, bado ugonjwa wako haujaisha kabisa” nilimuambia huku nilimtoa mikono yake na kumgeukia kisha nilimshika mashavu yake na kumwambia katika sauti ya upole ambayo hata hivyo haikumshawishi.

    “nitakuwa salama usijali” aliniambia hivyo na kuondoka pale kisha alisogea mbele kidogo na kugeuka akinitazama.

    “Pamela, kukaa hivi bila kazi wala chochote ni shida kwangu, mimi sina cha kufanya hapa, ni bora niende kujua nini kimetokea” aliniambia huku akionekana kujizuia asitoe machozi.

    “nimehangaika sana katika maisha yangu Pamela, nimehangaika kufika nilipokuwa nimefika, nilikesha usiku na mchana nikihangaika kila nchi kutafuta maisha, haiwezekani vikapotea tu kirahisi hivi” aliongea huku machozi yakimtoka.

    “Patrick naelewa hayo ila yupo mtu atatusaidia kujua hayo tukiwa hapa, na utajua kila kitu na wakati huo utakuwa ukifanya kazi hapa nchini nimeshaongea na dokta Anderson na amesema anaanza kukutafutia kwanza kibali cha kukaa hapa na cha kufanya kazi, kisha tutaanza kufatilia upate kazi hapa” nilimuambia huku nikijitahidi kuongea kwa sauti ambayo angeweza kuielewa vizuri na kumshawishi.

    “nitakaa huku hadi lini?” aliuliza

    “sijui hadi lini lakini ni hadi upone kabisa na sumu iwe imeondoka mwilini, Patrick nakuhitaji, siko tayari kukupoteza, huwezi kwenda Tanzania kama hujui kila kitu kuhusu safari yako, huwezi kwenda Tanzania ukiwa na milioni 15 tu na ukategemea utafanya kila kitu, hapana ni lazima uwe umejipanga na uwe unajua utaanzia wapi na utaishia wapi, bado hatujajua nani alikufanyia hivyo na kwaiyo unaweza ukaenda nso ukaisha kabisa, nina rafiki yangu anaweza akasaidia” nilimuambia na kumuona akiwa kimya nikajua dhahiri ameshanielewa.

    “nataka kuonana na huyo rafiki yako kwanza nimuambie vitu vya kunisaidia kufatilia” aliniambia huku akinitazama kwa jicho kali usoni.

    “usijali ila kwasasa anafatilia ni nani alikufyatulia risasi pale ufukweni” nilimueleza huku nikimshika mkono kuelekea kule hospitalini, alikuwa na mawazo sana, nilimpeleka mpaka hospitalini kwangu na kumchukulia dawa kisha alikunywa na hapo nilisaini na kuondoka naye mpaka nyumbani, aliingia kuoga na mimi nianza kumuandalia chakula, alipomaliza alikaa sebuleni huku akionekana kuwa na hasira sana, nilipomaliza kula mimi nilikwenda kuoga na nilipotoka nilikuja mpaka sebuleni nikiwa na kitaulo kifupi ila nilishtuka kumkuta mtu pale.

    “hee, umekuja saa ngapi wewe” nilishtuka na kujifunika na pazia.

    “hahaa,,nimefika mda sio mrefu na ninaondoka muda sio mrefu, hivyo njoo hapa tuelezane kwanza kisha utafanya kazi zako nyingine” nilitoka na kile kijitaulo mpaka pale sebuleni.

    “Patrick usiniangalie” nilimtania huku nikicheka, nilikwenda mpaka pale akanivuta na kunipakata.

    “Patrick huyu anaitwa Felicity, ni rafiki yangu, Felicity huyu ni mpenzi wangu anaitwa Patrick, najua hamjawahi kukutana ila kipindi yuko hospitali Felicity aliwahi kuja mara kadhaa kukuangalia” niliwatambulisha kila mmoja kwa mwenzio.

    “nashukuru sana kukufahamu Felicity” walishikana mkono na kama kawaida ya Felly huwa hapendagi kupoteza muda.

    “Nimefanya uchunguzi na nimeichunguza ile risasi, sasa nataka nikuonyesheni kitu hapa” aliwasha ‘projector’ aliyokuwa ameiweka pale mezani kisha akawasha na laptop yake na kuanza kuelezea.

    “Risasi ile uliyoiokota pale inaitwa 2.34 mm rimfire, inatengenezwa uswis na ina milimita 2.3, bastola yake ina 6.1 milimita ni rimedrife, imesajiliwa kwa namba 23kyt45, mwaka jana, ilipigwa kwenye kona ya nyuzi 75 toka upande wa kulia wa alipokuwa Patrick, hii inaonyesha kuwa kama mpigaji alikuwa ni mzoefu wa kutumia bastola basi angeweza kumlenga kama mkono usingecheza. Lakini kwakuwa ulicheza na kupiga futi sita kushoto kwa Patrick inamaana alikuwa amelegeza mkono hivyo mtu kama huyu atakuwa ameshtuka kiwiko cha mkono wake, pia niliende pale eneo la tukio jana baada ya kuachana na wewe pale,,nilikuta kuna miguu ya viatu visivyo na soli na inaonekana aliyepiga aliegemea mti na nywele zake zilibaki kwenye zilishika kwenye magome ya miti na hivyo kuacha nywele kidogo pale ambazo nilichukua na kwenda kuangalia DNA, hivyo baada ya uchunguzi wote nimegundua kuwa aliyefyatua risasi ni NANCY ROVELT”

    “WHAAAAT”



    “Hakuna haja ya kukata tamaa na kujiona kuwa huna thamani katika mapenzi yako kwakuwa tu kila mahusiano uanzishayo hayawi na mwisho mzuri au ulioutarajia, maisha ya mapenzi ni maisha dhalimu muda mwingine. Unaweza kukutana na mtu sahihi katika muda usio sahihi, na unaweza kukutana na aliyesahihi katika muda usio sahihi. Unachotakiwa kufanya si kukata tamaa bali kuwa makini na muda na unaokutana nao. Kila mtu anapacha wake hapa duniani, inapotokea umekutana na pacha wa mtu, ndipo shida na matatizo huanzia hapo. ATAKUJA MTU KATIKA MAISHA YAKO ATAKAYEKUFANYA UGUNDUE KWANINI HUKUDUMU NA ULIOACHANA NAO” HII NI SEHEMU YA TANO.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Msisimko wa simulizi ile uliufanya uso wangu upauke kama kipande cha muogo wa kiangazi, niligundua kuwa baridi lilikuwa likipenya kwenye lile dirisha dogo la chumba changu na kunifanya nikakamae, lakini hiyo haikunifanya nichoke kusikiliza, tayari yule msichana Felicity ambaye ni mpelelezi alikuwa ameshagundua kuwa Nancy ndiye aliyefyatua ile risasi, moyoni nikajiuliza kwanini Nancy afanye hivyo, lakini sikuwa na jibu. Nilifunga lile dirisha vizuri na kuchomeka makaratasi ili lisifunguke tena na kupitisha baridi kisha nikachukua ‘headphones’ zangu na kuchomeka kwenye redio kisha nikaweka masikioni ili nipate kusikia kwa ukaribu zaidi. Na sasa Pamela alikuwa na kibarua kizito cha kueleza Nancy ni nani. Ikawa hivi;







    ITAENDELEA

JINI MWEUPE - 5

 









    Simulizi : Jini Mweupe

    Sehemu Ya Tano (5)





    …………………………………



    Milio ya risasi ikamkulupua usingizini kamanda Kendrick,akavaa suruali, akachukua bastola yake, akafungua mlango taratibu, huku akijiuliza maswali mengi, hakujua amefikaje katika chumba hiki cha wageni, chumba ambacho alipaswa kulala kamanda Catherine.



    “,Jitokeze kabla sijawaua wazazi wako, moja, mbili tatu ……”,gaidi lile lilianza kuhesabu, Kendrick hakuwa tayali kuwapoteza ndugu zake,  akajibanza ukutani, uso kwa uso na kamanda Catherine akiwa amelala chini.



    “,Chuchumaa chini, watakuona, vipi tunafanyaje hapa?,nimefikilia mbinu ya kutumia nimeshindwa”,Catherine alimuuliza Kendrick.



    “,Bunduki yako umeweka sailensa(silent mode )?”,Kendrick aliuliza.



    “,Ndiyo, nimeweka …”,Catherine alijibu.



    “,Piga kule mlangoni, wakiwa bize kuangaza mlangoni risasi hizo, tutaruka na kuwashambulia ,kwanza wako bize wanamuhudumia mwenzao, amefanya nini?……”,Kendrick aliuliza.



    “,Nimempiga risasi kwenye dudu lake, alitaka kumubaka mdogo wako, “Catherine aliongea.



    “,Sita, saba, nikifika kumi nauwa familia yako yote, nane, “gaidi aliendelea kuhesabu, akatoa onyo, akaendelea tena kuhesabu, Catherine na Kendrick wakasitisha mazungumzo yao, Catherine akapiga bastola kwenye mlango wa kutokea ndani ya nyumba, wote wakageuka, wakautazama.



    “,Vuuuup, kwaaacha……”,Kendrick aliluka mateke mawili yaliyosindikizwa na ngumi, akamtandika ngumi gaidi D47 namba sitini ,mateke mawili yakawapata magaidi wawili waliokuwa wanampatia huduma mwenzao, wote wakagagaa. Catherine akawanyoshea bastola, akawateka, Kendrick na yeye akawanyoshea bastola yake.



    “,Paaaa! “,alipiga risasi chini, magaidi yakarudisha mikono yao, yalitaka kuzichuka bastola zao zilizodondoka mita kadhaa na mahali yalipodondokea.



    “,Mmejileta wenyewe, tulikuwa tumepanga leo tuwasake kona zote za mji huu wa makonda, karibuni sana nyumbani kwangu, “Kendrick aliongea, mkono wake wa kulia ulishika bastola, mkono wake mwingine alikuwa akiwafungua kamba wazazi wake, ghafla mlango ukafunguliwa, kamanda Philipo alikuwa amefika.



    “,Ewalaaa! asante sana Mungu, leo sitalala kama maiti ,jana nimechoka sana sababu yenu, kazi ya leo imeisha asubuhi tu, sasa mtakipata cha mtema kuni! “,Kamanda Philipo aliongea, akayafunga kamba magaidi haya manne, huku Jackline akiyapiga teke kwa hasira na kuyatemea mate.



    “,Asante wifi, umeyaokoa maisha yangu! “,Catherine alilia kwa furaha akamkumbatia Catherine.



    “,Usjali wifi yangu, ni kazi yangu …”,Catherine alijibu.



    “,Huyu ndiyo mkwe sasa, Kendrick unajua kuchagua ……”,mzee Steward na mke wake waliongea, wote wakamkumbatia Catherine, walishuhudia ushujaa wake, Kendrick yeye alikuwa amepigwa na butwaa, hakujua chochote kile, Catherine akakonyezana macho na kamanda Philipo, kamanda Philipo alifahamu kila kitu, wote wakatabasamu.



    “,Saluti afandee! “,askari watano wenye virungu waliingia ndani, wakapiga saluti.



    “,Salutiii, chukueni washenzi hawa, pakieni kwenye karandinga, mpaka chumba cha mateso, tutafika huko kufanya nao mahojiano, “Kendrick aliongea.



    “Sawa mkuu, tumefika na kukagua gari lao, tumekuta maiti ya askari wetu anayelinda geti lako, “,askari wale waliendelea kuripoti.



    “,Kwahyo wameuaa?”,aliuliza kwa hasira.



    “,Ndiyo bosi,maiti iko kwenye gari lao”askari wale waliitikia.



    “,Andika kwenye faili, jana wameua watu ishirini na moja, wakateketeza na kituo chetu, huyu ni mtu wa ishirini na mbili, toa taarifa kwa waziri pamoja na vyombo vya habari wapate taarifa hii ……”,Kendrick aliongea.



    “,Sawa mkuu, salutii …”,vijana wale waliitikia, wakapiga saluti, wakawabeba msobemsobe magaidi wanne wa D47,wakaondoka nao.



    …………………………………



    “,Kabla ya yote,usiku mmelala pamoja, sisi kama wazazi tumeshuhudia, kulingana na mila yetu ya , tunapaswa kuwafungisha ndoa na kuwapatia baraka zote, tukiwa tunasubili ndoa rasmi, tucheze ngoma na kuburudika, “mama yake Kendrick aliongea, Catherine akatabasamu, Philipo akatabasamu, Kendrick akatabasamu japo kwa shingo upande.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Mama mimi sikulala naye chumba kimoja, sasa sijui nitamlisha nini! “,Kendrick aliongea, hofu ya majukumu ilimuandama moyoni.Isitoshe hakutambua chochote kile, Philipo na Catherine wakiwa wanachekelea kwa furaha, sio Philipo tu, Jackline alikuwa anafurahi kwa kile ambacho kilikuwa kinafanyika.



    “,umelala naye hujalala naye sisi haituhusu, mpatie mkono mwenzako! “,mama Kendrick aliongea, alichoka kusubili mkwe kila siku,akiishia kuambulia ahadi zisizotimia kutoka kwa mtoto wake, leo alimkamatisha.



    Catherine akamshika mkono Kendrick, akafunga na kanga mikono yao, akaongea maneno ya kimila, akatoa baraka zake zote yeye na mume wake, wote wakapiga kelele za shangwe. Mama Kendrick akapiga meza kama ngoma, mdundiko ukapigwa, Catherine akacheza, Phipo akacheza, wote uvumilivu ukawashinda, wakaanza kucheza ngoma kwa furaha.



    Mtoni Kijichi :08:40am



              Nyumba ya Kendrick ilijawa na furaha tele, kila mmoja alicheza kadiri alivyoweza, walisahau kabisa kuwa ilikuwa ni muda wa kazi, burudani iliwafanya wasahau kila kitu, walisahau majukumu mazito yaliyokuwa mbele yao.



    “,Kendrick! saa tatu kasoro! “,Catherine aliitazama saa yake, akashtuka sana, muda ulikuwa unazidi kwenda mbele, walikuwa hawajafika ofisini.



    “,What!twendeni,bila shaka wanatusubili…”,Philipo aliongea,kila mtu akachukua kilicho chake,Kendrick akaenda kuvaa suti yake nyeusi,wote wakaondoka kuelekea kazini



    “,Oooh sitaki kuoa, ooh sijajipanga, utajipanga mpaka lini, utaoa kwa lazima ,mimi ndiyo mama Kendrick ……”,yalikuwa maneno ya mama Kendrick, akiwa amebaki nyumbani, yeye, mume wake pamoja na mwanae wa kike.



    “,Kweli kabisa, lakini mimi bado nawafikilia wale majambazi, mimi naona kaka abadilishe kazi, kazi yake ni ya hatari  watakuja kufa siku moja! “,Jacline aliongea.



    “,Sasa askari wote wakiacha kazi, nani atakulinda?, acha watimize majukumu yao, kila mmoja atakufa, hakuna mtu yoyote atakayeishi milele …”,baba yake Kendrick, mzee Steward aliongea, binti yake akakaa kimya.



    “,Haya sasa, mwanangu na mkwe wangu wote askari, nikiguswa tu na majirani,cha moto watakiona! “,mama yake Kendrick aliongea,licha ya kula chumvi nyingi, tabia za uswahilini alikua bado anazo. Waswahili husema ng’ombe hazeeki maini.



    “,Sawa mke wangu, ngoja mi nijiandaee,nikazulule mtaani, maana muda mrefu sijaona magari, “mzee Steward aliongea.



    “,weweee naye, tabia zako hujaziacha tu,bila shaka umekumbuka wanawake zako,haya kila laheri, uwasalimie wake wenza ……!”,mama Kendrick alizungumza.



    “,Mama Kendrick, maneno gani unazungumza mbele ya binti yako, unamfundisha nini huyu mtoto! ……”,baba Kendrick aliongea, hasira zilimjaa usoni, sura yake ikakunjamana.



    ”  ,Wewe naye hutaniwii! nilikua nimekukumbuka mume wangu, nisamehe bure …”,mama Kendrick aliongea, mzee Steward akaelekea chumbani, Jacline akacheka, utani wa wazazi wake ulimfurahisha sana.



    ………………………………



    Chumba cha mateso :



              Kendrick, Catherine pamoja na Philipo, walifika chumba cha mateso, chumba ambacho kilipatikana katika gereza kuu la Segerea.Ulinzi uliimarishwa, kila aliyeingia na kutoka, alikaguliwa kwa mashine maalumu ya umeme,hakuna aliyeruhusiwa kuingia na silaha isipokuwa kwa kibali maalumu.



    “,You are not allowed to get in, unless you put down your guns ……”,(Hamruhusiwi kuingia ndani, mpaka tu mtakapo weka bunduki zenu chini …).



    Mashine ya ukaguzi pembeni ya mlango iliongea kwa sauti, Kendrick, Catherine pamoja na Philipo, wote walikuwa na bastola katika miili yao, Kendrick alikuwa ameipachika kwenye kiatu chake, Philipo alikuwa ameipachika katika koti la suti yake, Catherine alikuwa ameipachika katikati ya mkanda wake.



    “,Haina jinsi, milango hii ni ya umeme, msipo weka silaha zenu, milango haitafunguka ……”,askari magereza aliyekuwa anawaongoza aliongea, wote wakachomoa bastola zao, wakampatia mmoja kati ya askari magereza, akazihifadhi kisha wakarudi tena, mashine ikawakagua, walikuwa hawana silaha, mlango ukafunguka, wakaingia ndani, askari mkuu wa magereza alikuwa mbele akiongoza msafara, Kendrick alifuatia, kisha Catherine pamoja na Philipo walifata kwa nyuma.



    “,Hawa ndiyo walifanya shambulio la kigaidi, wakateketeza kituo chenu? “,askari magereza aliuliza.



    “,Ndio mkuu, tunapaswa kuwahoji tujue Donald Mbeto yuko wapi kwa sasa, ikiwezekana wafanye mawasiliano nao, tukawakamate! “,Catherine aliongea.



    “,Magaidi wana roho ngumu, huwa hawasemi kirahisi namna hiyo, mmejipangaje? “,askari magereza aliongea.



    “,Watasema tu, twende ukaone! “,kamanda Philipo aliongea, askari magereza aliwaamini sana vijana hawa, siku zote kazi yao ilikua ya uhakika.



    Wakatembea korido ndefu, wakapita gereza la kwanza lililojaa wafungwa takribani elfu moja, wakiwa wamelaliana kama ndizi,baada ya dakika tano wakalivuka gereza hili, wakakata kona mkono wa kulia, wakakata kushoto, uso kwa uso na chumba kikubwa kilichozungushiwa nyavu kila kona. Mlangoni kilifungwa na kufuli kubwa la kilo tano, ndani ya chumba hiki kulikuwa na viti vitano, viti ambavyo vilikuwa maalumu kwa ajili ya kutoa mateso pamoja na kunyonga.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Karibuni sana, naona mmefurahi sana, lakini tambueni kuwa, wenzetu wakitambua jambo hili, watakuja kutukomboa ……”,chuma cha pua aliongea, alikuwa na roho ngumu sana, nyeti zake zilikuwa zimefungwa bandeji,haja ndogo alitumia mpira maalumu, lakini hakukoma, aliendelea kuwa katili kama kawaida.Mara tu baada ya kundi la the super three soldiers kuingia ndani ya chumba walichokuwa wamefungwa, aliwakaribisha kwa kejeli.



    “,Hahaaaaa, mmekuja na malaya humu ndani! “,magaidi wote watatu walicheka, wakamkejeli Catherine. Catherine akataka kuwasogelea awatandike makonde, Kendrick akamzuia.



    “,Nilitaka wote mtumie mipira kukojoa kama mwenzenu, muda mfupi ujao mtalia machozi, chekeni mara ya mwisho! “,Catherine alifoka, ngumi yake alikuwa ameikunja, akachomoa sindano za kibanio chake cha nywele, akajiandaa kutoa mateso wakati utakapofika.



    Kendrick alijua nini cha kufanya,akasogelea meza yenye batani nyekundu,akafika, akakaa juu yake. Catherine pamoja na Philipo wakasimama katikati ya magaidi wanne.



    “,Mnaweza kutwambia uwezo wa meli yenu ya D47paraquaat ……?”,Kendrick aliuliza swali la kwanza.



    “,Hahaaaaa!,kirahisi rahisi hivyo, hata ufanye nini, kuingia ndani ya meli yetu hutaweza dunia yote imeshindwa, sembuse wewe sisimizi mdogo tu ……”,Chuma cha pua alicheka sana, akaongea kwa kejeli, akawaponza wenzake.



    “,Yalaaa…aaaa, yalaa…aaa …”,Kendrick alibonyeza batani nyekundu iliyokuwa mezani, kelele za magaidi zikasikika, walipigwa na shoti ya umeme kutoka kwenye viti vya chuma walivyokalia, jasho likawatoka kama maji kwa sekunde moja tu. Baada ya dakika mbili Kendrick akabonyeza tena, shoti ikakata, zingezidi dakika mbili basi angewaua kabisa magaidi hawa.



    “,Hehee…ee, bola utuue tu …”,chuma cha pua alicheka tena, Kendrick akakasilika, akabonyeza tena mtambo wa shoti ya umeme.



    “,Yaaala…aa, uwiiii…ii! “,,yalipiga kelele, yakalia kwa uchungu.Catherine akayachoma na sindano zake mgongoni, kila mmoja, yakaugulia maumivu.



    “,Hatusemi, tuueni tuu! “,yaligoma kutaja, Catherine akapataa wazo, akawaita pembeni wenzake,akawaeleza wazo lake.



    “,Sikilizeni, tuyapatie nafasi yawasiliane na wenzao,sisi tujifanye wajinga,yatumie simu yetu kuwasiliana ,kisha tutaunganisha simu yetu pamoja na kompyuta tutajua imepigwa kutoka wapi,hawa wana roho ya paka hawawezi kusema.’ ,Catherine aliongea wenzake wakamuelewa.



    “,Kwahiyo mnasema wenzenu wakipata taarifa watakuja kuwakomboa……?”,Catherine aliuliza.



    “,Ndiyo,sasa hivi mnajifanya wajanja kwa vile hawana taarifa,Donald Mbeto atawaua nyoteee…”,magaidi haya manne yalijitamba na kuchimba mkwala.



    “,Sasa sisi tunataka tuwapige mbele yenu hao mnaowategemea,simu inaletwa,muwapigie,waambieni mmekamatwa,waje wawaokoe……” Kendrick aliongea, yakatikisa kichwa, yakakonyezana.Dakika mbili tu, askari magereza alileta simu, akawakabidhi,chuma cha pua akafunguliwa mkono mmoja, akapatiwa simu,simu ilikuwa imewekwa raudi spika.Akabonyeza namba alizozifahamu yeye, akapiga.



    “,Vipi imekuaje, mbona kimya? “,upande wa pili wa simu ulipokea.



    “,Njoeni mtuokoe, tumekamatwa,tumebahatisha simu tuwapatie taarifa, “Chuma cha pua aliongea.



    “,Hao mbwa wanajiamini nini, ndani ya nusu saa ijayo vijana watakuja kuwakomboa, “upande wa pili wa simu uliongea, simu ikakatwa, Philipo akachukua kompyuta yake, akaunganisha na simu ambayo imetumika,akabonyeza bonyeza, kisha akatoa jibu.



    “,simu imepigwa kutoka katika ndege yao, iko futi sitini angani, tayali nimedukua (hack)  mifumo yao ya mawasiliano,tuwafuateni huko huko,nyie maboya mmefeli ,hawatatambua mahali mlipo tena……”,Philipo aliongea,akatoka nje,yeye na wenzake,wakaondoka zao.



    “,Shiit,roho yangu ilisita,sijui ilikuaje mpaka tukaingia mtegoni…”,magaidi walibaki wanalalamika,hakuna akiyewasikia,chumba chao kilifungwa kwa kufuli kubwa,huku wao wakiwa wamefungwa katika viti maalumu,miguu na mikono.



    Mkuu wa kitengo cha mawasiliano, katika kundi la D47,alipokea taarifa iliyomshitua sana,baada ya sekunde tu simu ikakatwa, ghafla mifumo yote ya mawasiliano ikazima.



    “,Banard kuna nini?, “mmoja wa magaidi alimuuliza Bernard, mkuu na mtaalamu wa mitambo ya mawasiliano katika meli ya magaidi wa D47.



    “,Wenzetu wanne ,kitengo cha Dar es salaam, Tanzania wamekamatwa! inatakiwa wakombolewe kabla hawajauawa, lakini ghafla simu imekatwa,nilipojaribu kutafuta mahali ilipotokea, mifumo yote imezima ……”,Benard aliongea.



    “,Ina maana mifumo yetu ya ulinzi imedukuliwa? “,mmoja kati ya magaidi, chumba cha mawasiliano aliuliza.



    “,Itakua hivyo, kampatie taarifa bosi haraka sana! “,Benard aliongea, akajaribu kurekebisha mitambo ikagoma, kompyuta zote zilikuwa zimezima. Ndani ya dakika tano tu, bilionea Paresh Kumar alifika katika ofisi hii, akiwa ameongozana na Donald Mbeto.



    “,Bosi nimepokea taarifa, wenzetu wa Dar es salaam wamekamatwa! nilipojaribu kutaka kujua eneo walilopo, kompyuta zote zikazima, mifumo yetu imedukuliwa, ndiyo narekebisha, mpaka turudi hewani, saa moja litakua limepita tayali! “,Benard alitoa maelezo kwa bosi wake.



    “,Sawa, weka mambo sawa, kisha fanya utundu wako tujue eneo walilopo,tutume vijana waende kuwakomboa! “,Paresh Kumar aliongea, Benard akatikisa kichwa, aliyaelewa maelekezo aliyopewa, akaanza kutekeleza kama alivyoelekezwa. Paresh Kumar akaondoka zake, akiwa pamoja na rafiki yake kipenzi, kijana wake wa kazi, jini mweupe au Donald Mbeto.



    …………………………………



    Kamanda Kendrick, Catherine, pamoja na Philipo walikuwa katika mavazi yaleyale ya kazi,usoni walivalia miwani yao ya mionzi,bastola zao zilikuwa kiunoni. Helikopta ya kivita iliiacha ardhi ya jiji la Dar es salaam saa tano kamili asubuhi, siku ya jumamosi.



    “,ndege yao iko futi sitini juu,upande wa kaskazini,tunapaswa kuingia ndani ya ndege yao kabla mifumo yao ya mawasiliano  haijawa activated ndani ya saa moja!”,kamanda Philipo alitoa maelekezo,akaeleweka,rubani akaendelea kutimiza majukumu yake.Makamanda watatu walijiandaa,walikuwa tayali kwa lolote lile,Catherine alikuwa bize akichukua silaha za kumfaa,silaha moja baada nyingine,katika sanduku kubwa ambalo walilipakia katika ndege,silaha za kila aina,silaha kubwa na ndogo.



    “,Mabomu haya yatanifaa,visu hivi vitanifaa kufyeka shingo zao,bunduki kubwaa sitaki,bastola yangu inanitosha……”,Catherine aliongea,alikuwa amekamilika.



    “,Mimi sichukui chochote kile,kisu changu,bastola yangu,pamoja na miwani yetu ya mionzi inatosha,……”,Kendrick aliongea,akatazama saa yake,ilikua saa tano na dakika kumi na tano,walikuwa wamekalibia,mahali ndege ya magaidi ilipoweka kambi angani.



    “,Haloo,haloo ovaa,usawa wa ndege,usawa wa ndege mnatupata ovaa!”,simu ya mkonga ilisikika,upande wa pili wa simu uliongea.



    “,tunawapata,tunawapata ovaa!”,rubani alizungumza.



    “,Mmekalibia,angalieni mbele yenu,kazi ianze mara moja…”,kitengo cha mawasiliano cha jeshi walifatilia kila hatua za ndege yao,hawakutaka ishambuliwe kwa mara nyingine tena.Wakampatia maelekezo rubani wa ndege yao,kisha simu ikakatwa.



    “,Tumefika,nazani ndiyo ndege hiyo kubwa mnayoiona mbelee yenuu……”,rubani aliongea,huku akishangaa,hakuwahi kuona ndege kubwa na ya ajabu kiasi kile.



    “,Whaaat!ndege nzuri sana na kubwaa,Kendrick,tusitumie milipuko yoyote,tunapaswa kuilinda iwe salama,tukishinda vita hii,ndege itaifishwe iwe mali ya serikali ……”,Catherine aliongea, alishangazwa na ndege iliyonekana mbele yao.



    “,Kweli kabisa, wazo zuri sana, ina maana hii ndiyo ilitushambulia? “,Philipo aliongea, akauliza swali, macho yake yalitazama mita mia mbili mbele yake, helikopta yao ikasogea karibu kabisa na ndege hii, ili wapate nafasi ya kuikamata kwa mikono sehemu yoyote ile, waweze kuingia ndani.



    “,Ndiyo hii, kazi ianze mara moja! “,Kendrick aliongea kwa kifupi, akakamata bawa la ndege ya maadui wakapanda juu yake, alilikamatilia bawa kwa nguvu, akishindana na upepo mkali. Wenzake wakafanya kama yeye, wote wakakamatilia bawa la ndege ya magaidi wakaanza kuisogelea taratibu, upepo mkali ukivuma, lakini walikua imara, hawakutikisika, miwani ya mionzi ilifanya kazi yake ipasavyo, ikawakinga na upepo mkali machoni.



    “,tumia emergency exit! kioo hicho hapo mbele, kisogeze chini juu, tuingie wote haraka sana kabla upepo haujaingia ndani ya ndege na kutuzidi nguvu …”,kamanda Philipo alitoa maelekezo,Kamanda Kendrick akafanya kama alivyoelekezwa, dirisha likafunguka, akaingia ndani, Catherine akafuatia, Philipo akawa wa mwisho, akarudisha kioo cha dirisha mahala pake, wote wakatokea ndani ya chumba cha choo.Huku ndege ikitikisika kwa sekunde kadhaa kisha ikarudi mahala pake.



    …………………………………



    “,Mbona ndege imetikisika kiasi hiki, ina maana kuna sehemu ya ndege yetu iko wazii, au tumevamiwa? “,rubani wa ndege hii ya magaidi alizungumza, machale yakamcheza,akamtuma msaidizi wake,kepteni ambaye alifanya kazi ya kuongoza ndege hii inaposafiri kama meli baharini, alikuwa na wasiwasi uliopitiliza.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Mwambie bosi,walinzi wakague kila sehemu, ulinzi uimalishwe, kila mtu achukue pozisheni yake,dirisha la dharula bila shaka lilikuwa wazi”rubani wa magaidi aliongea.



    “,Sawa, hata mimi nimewaza jambo hilo! “,kepteni wa magaidi aliongea, akatoka chumba cha kuongoza ndege hii ya D47paraquaat, akaondoka zake.



    …………………………………



    “,bosi, bosi! “,kepteni alifika katika ofisi ya Paresh Kumar, bosi akashtuka, alikuwa ananyonyana ndimi na wanawake zake wa kizungu, wakakurupuka, walishtukizwa.



    “,Mbona unaingia ofisi ya bosi wako bila taarifa, kuna tatizo gani? “,Paresh Kumar alifoka kwa hasira.



    “,Bosi, dirisha la dharula lilifunguliwa muda mfupi uliopita, kisha likafungwa tena, hatujui kama aliyefanya hivyo ni mtu wetu au adui yetu, nimetumwa kuleta ripoti, ulinzi unapaswa kuimalishwa “,kepteni aliongea,maneno yakapenya vizuri katika kichwa chake, akawasukumia mbali wanawake zake, akafunga vifungo vya shati lake, akaondoka zake, akawaacha wanawake zake wa kizungu wakiwa na hasira, mmoja alikuwa na sindilia, mwingne alikuwa amebaki na bikini yake, ofisi ya Paresh Kumar ilikua zaidi ya kasino,uovu mwingi ulifanyika masaa yote. Akatoka nje ya ofisi yake, uso kwa uso na Donald Mbeto.



    “,Kila mtu achukue pozisheni yake, hakikisheni aliyeingia ndani ya ngome yetu hatoki salama, maraisi wao waliowatuma, watajuta!!nitafanya mauaji mpaka nikabidhiwe migodi ninayohitaji, haiwezekani waingie madarakani kwa msaada wangu harafu waninyime ninachohitaji, walizani pesa zangu za kampeni ninawapa bure, kijani wangu utaendelea kufanya mauaji mpaka niseme basi, haya ondoka mara moja,kafanye kama nilivyokuagiza! “,Donald Mbeto alipokea maelezo kutoka kwa bosi wake, akaanza kazi, bosi wake alikuwa amekasirika, kengele ya hatari ikapigwa.



    “,danger! danger! everyone should take his position (hatari! hatari!, kila mtu achukue nafasi yake…) ,Donald Mbeto maarufu kama jini mweupe alipiga kelele, magaidi wakakimbia huku na kule, kila mmoja akikamata silaha inayomfaa kwa mapambano.



    Catherine, Kendrick pamoja na Philipo, walichungulia kupitia matundu madogo, katikati ya mlango, hawakuona mtu yoyote yule,Wote wakiwa na miwani yao ya mionzi mikali yenye lenzi, wakakitazama kitasa cha mlango kwa sekunde mbili, kitasa kikayeyushwa na mionzi mikali kutoka kwenye miwani, kitasa kikayeyuka,mlango ukafunguka. Wakatoka nje, uso kwa uso na bunduki nane, kulia na kushoto, mbele yao, kote kulikuwa na bunduki, waliwekwa chini ya ulinzi na magaidi waliovalia suti za bluu, zenye nembo ya D47.



    “,Tumewakamata! hahaaa, tuwapeleke kwa bosi! “,magaidi yale yalicheka, the super three soldiers hawakuongea kitu chochote kile, walizitazama bunduki walizowekewa kichwani, sekunde mbili tu, bunduki za magaidi wale zilipigwa na mionzi kutoka kwenye miwani, bunduki zikayeyuka,zikawa kama uji.



    “,What! nini hiki, maajabu haya! “,magaidi wale walishangaa,kitendo cha bunduki zao kuyeyuka kiliwashangaza sana, wakasahau kama walikuwa wamewaweka watu chini ya ulinzi.



    “,Vuuuup, vuuuup, vuuup …”,Kendrick alipiga ngumi tatu, zikawapata magaidi watatu kichwani,wakadondoka chini, Catherine akaluka mateke mawili, magaidi wawili wakandoka chini, wakabaki wawili, wakiwa wamesimama, walikuwa hawajielewi, kitendo cha bunduki zao kuyeyuka mbele yao walikiona cha ajabu sana, wakawa kama vichaa, wakataka kukimbia, Kamanda Philipo alichomoa visu viwili, akavirusha, vikawapata mguuni, wakadondoka chini.



    “,Yala…aaa, mmetuumiza washenzii nyie ……”,magaidi yale yalitukana,lakini haikubadirisha kitu chochote kile, Kendrick, Catherine pamoja na Philipo walichomoa bastola zao wakayanyoshea magaidi yale.



    “„Nyote ingieni humo chooni haraka sana, nasema ingieeni! “,Kendrick aliyakalipia, magaidi sita yakiwa yameweka mikono kichwani yakaingia, kamanda Philipo akayaburuta magaidi ambayo yalichomwa na visu mguuni, yalikuw hayawezi kutembea, wote wakawekwa chooni.



    “,Catherine akachomoa bomu lake dogo, akachomoa pini, akalitupilia ndani ya chumba cha choo.



    “,Puuuuuu, puuuuuu! “,mlipuko ukasikika, ndege ikatikisika tena, kisha ikarudi katika hali yake ya kawaida, Kendrick na wenzake walilukia upande wa pili, wakalala chini, hawakujeluhiwa popote pale.



    “,Umefanya nini, tulikubaliana vipi? situlisema hakuna kutumia milipuko …”,Kendrick alilamika.



    “,Haina jinsi, hiyo ndiyo mbinu ya kuwaua kwa urahisi, muda mfupi ujao, wote watafika eneo hili, utaona watakavyo kufa,”Catherine aliongea, akachomoa mabomu yake mawili madogo, akayaseti yalipuke ndani ya dakika tano, wote wakatembea harakaharaka, mpaka mahali kulipokuwa na magari pamoja na ndege za kivita nyingi sana.



    “,Waooooh! “,Philipo hakusita kuonesha furaha  yake,alitazama ndege,magari pamoja na vifalu vya kivita,ghafla kundi kubwa la magaidi lilisikika,wakija mahali kuliposikika mlipuko,Catherine na kundi lake wakaingia chini ya magari,wakajificha,hawakuonekana,magaidi yakapita bila kukagua kona zote,lilikuwa kundi la magaidi takribani mia moja.



    “,Hawa wehu,wametuchokoza,wameua wenzetu,mimi ndiye Donald Mbeto mwenyewe,nasema hivi,hawatoki salama mahali hapa……”,Donald Mbeto aliongea,alikuwa hana silaha yoyote ile mkononi,tofauti na wenzake ambao kila mmoja alikuwa ameshika bunduki yake.Alizigeuza geuza maiti za wenzao,moshi ukiwa unaishia na kubaki kweupe,mlipuko huu haukuhalibu ndege hii,bali iliwasambaratisha vipande vipande magaidi nane.



    “,Kuna mabomu!kuna mtego”,Donald Mbeto aliongea,akaluka serekasi,akatua upande wa pili,akalala chini.



    “,Puuuuu,puuuuu,puuuu,”mlipuko ulisikika tena,mabomu ambayo Catherine aliyatega,akayaweka chini ya maiti,yalililipuka,magaidi mia moja ambao waliongozwa na Donald Mbeto walijeruhiwa vibaya sana,wengine wakafa palepale.Isipokuwa Donald Mbeto ambaye hakujeruhiwa mahali popote pale.Akanyenyuka ,vijana wake walikuwa wameumia vibaya,wengine walivunjika shingo,miguu na wengine walikatika viuno.



    “,Huo ni uzembe katika kazi,hunifaaii……”,Donald Mbeto aliongea,akammalizia gaidi mwenzake ambaye alivunjika miguu yote miwili,lakini alikuwa bado mzima,akilia na kuhitaji msaada.



    “,Twendeni,twendeni tukaone,watakua wamekufa!,huo mlipuko sio wa kawaida…”,Philipo alitoa wazo lake.



    “,Hapana,tusiende,wenzao najua watasogea tena,tusubili kidogo…”,Kendrick akakataa,akatoa sababu,wote wakakubaliana naye.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Jitokezeni,mbona mnajificha,kama nyie ni mashujaa kweli jitokezeni!”,sauti ilisikika,Donald Mbeto alipiga kelele,akafoka kwa hasira.



    “,Hajafa,unamsikia anavyotukana,muda ukifika tutajitokeza,asiwe na shaka……”,Catherine alizungumza,mkono wake wa kulia alikuwa ameshika bastola mkono wa kushoto ulishika mabomu mawili.Aliona ndio silaha pekee ya kuua watu wengi kwa muda mfupi tu.



    Ghafla sauti za watu kukimbia zilisikika,wote wakageuza shingo zao,wakatazama mahali sauti za vishindo zilikuwa zinatokea,jeshi kubwa lilikiongozwa na mwanaume wa kihindi lilisogea mahali mlipuko ulikuwa umetokea,mikononi walishika bunduki zao,walijiamini sana.



    “,Kendrick tunafanya nini!”,Catherine aliomba ushauri kwa Kendrick,huku akifikilia mbinu ya kufanya.



    “,Wote hawajui mahali tulipo,pembeni yetu kuna ndege nyingi kubwa,ndege zenye makombola,tukipanda ndege moja,shambulio moja tu tunawatekeza woteee!”,kamanda Philipo alitoa mawazo yake.



    “,Wazo zuri sana,lakini vipi kuhusu mtuhumiwa wetu,tunapaswa kuondoka na Donald Mbeto kutoka mahali hapa,lazima akaonje joto la jiwe,asife kirahisi tu,anapaswa kufa kama alivyotesa raia wasio na hatia…”,Kendrick aliongea.



    “,Nimewapata hilo niachieni mimi,pandeni ndani ya ndege,lakini msifanye chochote mpaka niwajulishe……”,Catherine alizungumza,kamanda Kendrick aliangalia kushoto na kulia,hakuna aliyewaona,akaingia ndani ya ndege ya kivita,kamanda Philipo akafuatia,wakasubili amri kutoka kwa Catherine,Catherine alipita chini ya magari,hakuonekana,jeshi la magaidi liliendelea kusogea mahali mlipuko ulikuwa umesikika,akarusha mabomu mawili,katikati ya miguu ya magaidi,kisha akarudi ,akipenyeza chini ya uvungu wa mataili ya gari pamoja na ndege.



    “,Ukisikia mlipuko,washeni ndege,watakua bize na kujihami,nyie mtatumia upenyo huo kuwasogelea na kuwashambulia,hakikisheni mtu yoyote hapati upenyo kusogelea eneo hili,akaingia ndani ya vifaru,mtakua mmekwisha…”,Catherine aliongea.



    “,Puuuu,puuu,puuuu,”mlipuko ukasikika,magaidi wengi wakafyekelewa mbali,bilionea Paresh Kumar alikufa palepale,magaidi wengine walizitupa silaha zao,wakalala chini kuepuka mlipuko huu,Kendrick akatumia mwanya huu,akawasha helikopta kubwa ya kivita,kamanda Philipo akachomoa makombola,yakatokeza pembe zote,mbele makombola mawili,nyuma makombola mawili,wakaanza kupaa hewani,ndani ya ndege hii kubwa yenye vioo kwa juu,kiasi kwamba anga lote lilionekana,ndege ya magaidi ikitaka kujigeuza umbo la meli,vioo ambavyo vimeifunika ndege vinajifunua,mabawa yanarudi kwa ndani.



    Kendrick alipaa,hakutaka kupaa juu zaidi,angegonga vioo ,upepo ukaingia ndani ya ndege kubwa ya magaidi,akahatarisha maisha yao,alipofika usawa wa kufanya mashambulizi,futi kumi kwenda juu,akaisogeza helikopta eneo la magaidi,akafyatua makombola mawili,yakatekeza kundi lotee.



    “,Bosiiiiiii ,bosiiii!”,Donald Mbeto alishuhudia kitendo cha bosi wake kushambuliwa,akakimbia mpaka eneo la tukio,kila kiungo cha bosi wake kilikuwa mahali pake,akakasirika.



    Catherine alitabasamu,ushindi ulikuwa umekalibia,akaanza kusogea taratibu,kwa mara ya kwanza alikutana uso kwa uso na Donald Mbeto.Catherine alitazama juu,Kendrick alikuwa ameelekeza makombola kwa Donald Mbeto,alitaka kummalizia palepale.



    “,Hapana,usimuue,nataka nimvunje miguu,mimi mwenyewe!”,Catherine aliongea kwa sauti,akawakataza wasimuue,kisha akakunja ngumi,Donald Mbeto akazifunga rasta zake nyeupe,akajikuna kidevu chake,akakunja ngumi.



    11:40am



          Donald Mbeto alimtazama Catherine juu mpaka chini,akamtazama usoni, kisha akaitazama miguu yake,alikuwa anafikilia mbinu ya kumshambulia, aivunje miguu yake. Donald Mbeto aliluka mateke mawili hewani, Catherine akazuia mateke yote kwa mikono yake,hajakaa sawa alipigwa ngwala akadondoka chini, Donald Mbeto akaluka hewani, akarudi chini kwa kasi akiwa amekunja kifuti cha mkono wake, akafika juu ya mguu wa Catherine, akaupiga na kifuti.



    “,Kachwaaaaa!!, “mguu wa Catherine uliitikia.



    “,Yalaa…aa! “,Catherine alipiga kelele, akajigeuza upande wa pili, akampiga Donald Mbeto na teke usoni, akadondokea upande wa pili, damu zikimvuja mapuani.



    “,Shiiit! amemuumiza, atamuua, tushuke chini



    ……”,Kendrick akiwa juu ya helikopta, aliona kila kitu kilichokuwa kinaendelea,hisia za mapenzi zikamsumbua, alikuwa na hofu ya kumpoteza Catherine.



    “,Usiwe na hofu, naona sasa mapenzi yameshakuingia, umeshapenda tayali ,usjali Catherine ni komandoo……”,kamanda Philipo alimuondoa shaka Kendrick.



    “,Hapana, mwanamke ni mwanamke siku zote, isitoshe mtu anayepambana naye ni hatari sana,ameshamtemgua mguu ……”,kamanda Kendrick aliongea.



    Catherine alijaribu kusimama,alishindwa,mguu wake wa kushoto ulikuwa na maumivu makali, aliteguliwa, alimanusura avunjwe mguu, akajaribu kusimama tena, akadondoka chini, mguu wake ulimuuma sana, alikuwa hananguvu kabisa.



    “,Lazima ufe,huwezi kutoka salama, huwezi kumuuwa bosi wangu halafu uwe salama,mimi ndiyo jini mweupe,shujaa wa dunia”Donald Mbeto aliongea, akazishika rasta zake nyeup, akazifunga vizuri, akajikuna kidevu chake, akaanza kumsogelea Catherine aweze kummalizia.



    Catherine alimuona Donald Mbeto akimsogelea, alimuangalia usoni, akayatazama macho yake kwa makini, akazitambua hisia zake, alikuwa anakuja kumshambulia, Catherine akajiandaa, japo alishindwa kusimama, lakini alijiamini, Donald Mbeto alipofika mahali Catherine alipokuwa, aliluka tena juu, akashuka chini kwa kasi na pigo lile lile, alitaka kuvunja mguu mwingine wa Catherine, Catherine alinyanyuka juu kama mzuka, akaluka hewani,mkononi alishika kisu chake, wote wakakutana hewani, alilipangua teke la Donald Mbeto akamsindikiza na visu viwili, alichoma visu viwili Donald Mbeto miguu yote ,kulia na kushoto,haikutosha, akampiga na teke, akadondokea mita kadhaa kama mzigo. Donald Mbeto akalia kwa uchungu,hakuwa na uwezo wa kusimama tena.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Haya sasa, wote viwete! “,Catherine aliongea,akatazama helikopta juu yake, akawanyoshea mkono Kendrick na Philipo, wakaishusha helikopta,Kendrick akachomoa pingu, akamfunga Donald Mbeto, wakamnyenyua na kumuweka kwenye helikopta,Kendrick akaipaisha juu, ikapasua vioo vya ndege kubwa ya magaidi hawa,ikatokomea hewani.



    “,Bado kuna magaidi, wamejificha, lipua ndege yoteee! “,Kendrick aliongea,kamanda Philipo akafanya kama alivyoelekezwa, akaruhusu makombola mawili, yakaipiga ndege, ikapepesuka, ikapoteza mwelekeo, akaipiga tena na makombola mengine mawili, ikalipuka na kuungua moto, Kendrick akageuza helikopta, akaanza kurudi kusini,kisha akakunja tena kona, akaelekea mashariki, akaanza kuishusha chini helikopta, futi arobaini mpaka therathini,akaanza kurudi Dar es salaam,Tanzania



    …………………………………



    Chumba cha mateso :2:20



            Magaidi wanne walisubili waweze kukombolewa,muda ukazidi kwenda, hakuna chochote kile kiliweza kutokea.



    “,Tujikomboe sisi wenyewe, bila hivyo tutakufa, kifo chetu ni kunyongwa, hakuna hukumu nyingine tofauti na hiyo ambayo tunaweza kupewa …”,chuma cha pua aliongea.



    “,Kweli kabisa, lakini gereza hili lina ulinzi mkali, hatuwezi kutoka kirahisi kama unavyofikilia ……”,gaidi D47 namba sitini aliongea.



    “,Ngoja niwaoneshe,askari atakaye tuletea chakula, akitufungua tu mahali hapa,mimi naan.……”,chuma cha pua kabla hajamaliza kuongea,Catherine, Kendrick pamoja na Philipo walitokeza, Kendrick alikuwa anamburuta mtu hatari sana ambaye hawakutegemea kama angeweza kukamatwa.



    “,Donald, wamekukamata! “,magaidi walishangaa, wakanyongonyea,nguvu zikawaishia.



    “,Mliyekuwa mnategemea atakuja kuwakomboa huyu hapa, huu ndiyo mwisho wenu, chombo chenu tumekilipua,hakuna aliyetoka mzima zaidi ya huyu mtuhumiwa wetu, tunataka afe mbele ya raia ……”,Catherine aliongea, akiwa anatembea kwa kuchechemea, akamnyenyua Donald Mbeto, akamkalisha kwenye kiti cha mateso kilichokuwa wazi, wakamfunga mikono na miguu.



    “,Hapa hamuwezi kutoroka kamwe! hata mfanye nini hamtaweza, subilini hukumu yenu ya kunyongwa hapohapo kwenye viti vyenu ……”,Kendrick aliongea,akamshika mkono Catherine, akambusu, akamsaidia kutoka ndani ya chumba cha mateso, walikuwa wamekamilisha kazi, kama ilivyotakiwa.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Taarifa za kukamatwa kwa Donald Mbeto zikasambaa duniani kote,waandishi wa habari kutoka mataifa mbalimbali duniani walifika nchini Tanzania, walitaka kufanya mahojiano na Donald Mbeto, wampige picha na kuitambua sura yake,hawakutaka kupitwa na taarifa za mtu huyu,lakini ulinzi ulikuwa mkali,wengi walizuiliwa,vyombo vya habari kutoka Tanzania vikaifanya kazi hiyo.Huku hukumu ya magaidi hawa watano ikisubiliwa kwa hamu na watu wote duniani.



    …MWISHO…………………



    The super three soldiers walizawadiwa tuzo za heshima, kutoka mataifa yote ambayo Donald Mbeto maarufu kama jini mweupe alitekeleza mauaji ya sumu, Kendrick na Catherine wakafunga ndoa, huku kamanda philipo akiwa Mc wa ndoa yao.…







    JINI MWEUPE - 4

     









      Simulizi : Jini Mweupe

      Sehemu Ya Nne (4)





      Kisiwa cha Comoro :



           Kendrick aliyafumbua macho yake,akapapasa mikono yake huku na kule, akashika magome ya miti, akashtuka, akanyenyuka na kuketi, uso kwa uso na mzee mwenye umri sawa na marehemu baba yake, alipoyageuza macho yake upande wa pili, pembeni na mzee yule, alikutanisha macho yake na msichana mweupe,akiwa amevalia magome ya miti yaliyozuia sehemu zake za siri pamoja na matiti yake, macho yake yakashindwa kuvumilia,kope zake zikayaachia uhuru macho yake, yakatazama uzuri wa msichana huyu juu mpaka chini, akatabasamu, akamshukuru Mungu kwa uumbaji wake wa ajabu.



      “,Hapa ni wapi?,nyie ni akina nani? “,Kendrick aliuliza, akasimama, akaangaza huku na kule, aliona nyumba moja ya makuti iliyozungukwa na minazi mingi.



      “,Huu ni ufukwe wa kisiwa cha Komoro! “,mzee yule alimjibu Kendrick, akazidi kumpatia maswali mengi kichwani mwake yasiyokuwa na majibu.



      “,Nimefikaje hapa? “,Kendrick aliuliza tena.



      “,Nilikuokota baharini ukiogelea katikati ya bahari,nilikua navua samaki, nikasogeza mtumbwi wangu karibu nawe, ulikuwa umeishiwa nguvu, ukapoteza fahamu, kabla hujazama nilikuokoa na kukuweka katika mtumbwi wangu, nikakuleta mpaka hapa, naitwa mzee Fedinand, huyu ni binti yangu, anaitwa Upendo ………”,mzee yule alimaliza kumwelezea Kendrick, akajitambulisha, akamtambulisha na binti yake wa kike, wote wakatabasamu, walifurahi sana kukutana na mswahili mwenzao kwa takribani miaka kumi sasa, wakiishi peke yao ufukweni, wakivua samaki, kula matunda na kuwinda wanyama.



      “,Kabla sijajitambulisha,kwanini mko hapa, makazi haya yanaonekana yako mbali na binadamu, hamuogopi kuishi peke yenu?, hamuogopi maharamia, vipi kuhusu wanyama wakali, hamuwaogopi? “,Kendrick aliongea kwa mshangao, macho yake yakiangaza umbali wa mita kadhaa mbele yake, akaona bahari, kushoto aliona msitu mkubwa wa minazi, akageuza shingo yake mkono wa kulia, aliona minazi mingi sana, nyuma yake vivyo hivyo, kulikuwa na msitu mkubwa wa minazi, akapigwa na butwaa!



      “,Huyu ni binti yangu, ana miaka ishirini na mbili kwa sasa, akiwa na miaka kumi na mbili, tulisafiri naye kwenda Zanzibar kwa mapumziko  mafupi, tukapata ajari na Mv Spice,tulifanikiwa kuwahi maboya mimi na mwanangu, nikaogelea naye, nikiwa nimemshika ipasavyo mpaka tukafika hapa, tumeishi naye mpaka leo hii, sijawahi kuona binadamu yoyote, leo ndio nimekuona wewe eneo hili ……”,mzee yule alitoa maelezo marefu, kamanda Kendrick akamuangalia machoni, macho ya mzee yule yalisema ukweli, hayakudanganya chochote kile, Kendrick akamuamini mzee yule.



      “,Naitwa kamanda Kendrick, askari mkuu wa kikundi cha upelelezi cha the super three soldiers kutoka Tanzania, tukiwa katika majukumu yetu, ndege yetu ililipuliwa na maharamia, mpaka sasa sijui wenzangu wako hai au wamekufa! “,kamanda Kendrick alijitambulisha,mzee Fedinand na binti yake wakatazamana, kisha wakamtazama tena Kendrick.



      “,Mzee, haukuona mtu yoyote eneo hilo la bahari tofauti na mimi? “,Kendrick aliuliza tena.



      “,Hapana, sikuona chochote kile! “,mzee yule aliongea, binti yake akanyenyuka, akaenda ndani ya kibanda cha makuti, akarejea tena, mkononi alishika samaki waliochomwa,wakiwa wamefungwa vizuri kwenye majani ya miti, akasogea karibu na Kendrick, akapiga magoti kwa heshima, akamnawisha, akampatia samaki, akaanza kula.



      “,Sasa itakuaje?, natamani sana mwanangu kurudi Tanzania, nazani nyumbani mke wangu na watoto wanne wanazani tumeshapoteza maisha, isitoshe kwa sasa wamekua, natamani sana kuwaona! “,mzee yule aliongea kwa hisia kali, akadondosha chozi, binti yake na yeye uvumilivu ulimshinda,akamfuta machozi baba yake, huku na yeye chozi likimtiririka.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Msijali ondoeni shaka, mko mikono salama, mshukuruni Mungu kuwalinda kwa miaka kumi,kama mko salama mpaka leo hii, basi hamtapatwa na kitu chochote kile katika mikono yangu ……”,Kendrick aliongea, akitafuna samaki wazima wazima, njaa aliyokuwa nayo haikuwa ya kawaida, akamaliza kutafuna samaki watano, akatosheka, akanawa, akaifutafuta saa yake, akaiwasha, ilikua imezima baada ya kuingiliwa na maji, ikawaka kwa mara nyingine tena, akatabasamu, ghafla tabasamu lake likatoweka, saa yake iliwaka taa mbili tu za kijani badala ya tatu,akajiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu, mmoja kati yao hakuwa salama.



      …………………………………



      Kisiwa cha Mafia :



              Kamanda Philipo alikasirika, kicheko cha kejeli kutoka kwa watu waliomsaidia ndicho kilichomkasilisha,akajitoa mikononi mwao kwa nguvu, akasimama.



      “,Asanteni kwa msaada wenu, niacheni niondokee! “,kamanda Philipo aliongea, akaondoka zake, nahodha na mabaharia waliokuwa wanamuhudumia wakabaki midomo wazi,wakaachana naye,wakaendelea na shughuli zao, huku wakijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu.



      “,Mimi niliwambia, ameshakua kichaa, kupona kifo baharini lazima uwe na kiwewe, ona sasa, yuko kama mwendawazimu! “,mmoja kati ya mabaharia wa mv Mafia aliongea, wote wakiwa makini kumsikiliza.



      “,Kweli kabisa, lakini asikuumize kichwa, achana naye, cha muhimu tumeshampatia msaada! “,baharia mwingine alizungumza, akatoa mawazo yake, wote wakaelekea kwenye majukumu yao.



      “,Mungu wangu wee! wote saa zao hazifanyi kazi,taa hata moja ya kwao  haiwaki, yes! imewaka, yes nyingine labda itawaka bado moja! “,Philipo aliongea kama kichaa, akiwa bize kuitazama saa yake mara tu baada ya kuiwasha, akaandika ujumbe kwa kupitia saa, akaituma, ili ajue wenzake wako mahali gani.



      “,Anyone online! Comrade Philipo, available in Mafia ……”,(Yoyote yule aliyeko hewani!, kamanda Philipo napatikana Mafia …”,)



      Alituma ujumbe kupitia saa yake, saa iliyounganishwa na saa za wenzake, akasimama kusubili majibu,wapita njia wakimshangaa kwa mavazi yake, mavazi ambayo yalikuwa maalumu kwa ajili ya kutekeleza misheni ambayo haikufanikiwa, misheni ya kuivamia meli ya D47.



      …………………………………



      “,Help me! Help me! nisaidieniii, nisaidieenii! “,kamanda Catherine alipiga kelele kuomba msaada, mikono yake ilichoka kuogelea, muda wowote angeweza kuzama,boti kubwa ikaanza kumsogelea, “Bakhresa “, ilisomeka, akaitambua, ilikua boti ya abiria kutoka Dar es salaam kwenda Zanzibar, mabaharia wawili wakajitupa ndani ya maji, wakampatia msaada, akaponea chupuchupu kufa maji.



      “,kulikoni kamanda, imekuaje? “,mabaharia wale walimuuliza swali Catherine, walimtambua, alikua maarufu sana jijini Dar es salaam yeye pamoja na kundi lake.



      “,Ndege yetu ilipata hitilafu, ikaanguka baharini, asanteni kwa msaada wenu! “,Catherine aliongea, akashukuru, akaiwasha saa yake, ajue kama wenzake wako hai au wamekufa, akatoa tabasamu zuri sana, saa iliwaka taa tatu za kijani,makamanda wote walikuwa wazima.



      “,Wenzako wako wapi, tuambie mlipoangukia tukawatafute, nyie ndio mnailinda nchi yetu, bila nyie sisi sio kitu! “,mabaharia wawili waliongea, huku abiria wakitikisa vichwa, walikubaliana na wazo hili, wakasubili majibu kutoka kwa Catherine.



      “,Msiwe na hofu, wote tayali ni wazima, asanteni kwa upendo wenu …”,Catherine aliongea,wakakubaliana naye, boti ikaendelea na safari ya kuelekea Dar es salaam Tanzania.



      “,Anyone online! Philipo available in Mafia …”,(Yoyote yule aliyeko hewani!, Philipo anapatikana Mafia …),meseji iliingia kwenye saa maalumu ya Catherine, akaisoma, akaandika ujumbe kujibu ujumbe ulioingia katika saa yake.



      “,Anyone online! Catherine is on the way to Dar es salaam, via mv Bakhresa …”,(Yoyote yule aliyeko hewani, Catherine yuko njiani anaelekea Dar es salaam Tanzania, kwa kutumia mv Bakhresa) “,alimaliza kuandika ujumbe mfupi, akatuma.



      ………………………………



      Kisiwa cha Comoro :



            Mzee Fedinand aliongoza njia, binti yake Upendo akafuatia, wakaongoza njia, kumtembeza Kendrick katika maeneo mbalimbali ya kisiwa hiki. Kendrick aliwaza mbali sana, alikua na hasira ya misheni kuharibika, isitoshe mwenzao mmoja saa yake ya mawasiliano haikuwa hewani.



      Ghafla ujumbe ukaingia, alikuwa ni Philipo, akausoma, Philipo alikuwa katika kisiwa cha Mafia, hofu ikazidi kumtanda, mtu aliyempenda, Catherine hakuwa hewani,ghafla taa nyingine ya saa yake ikawaka, taa zikawa tatu, wote walikua hai, ujumbe mwingine ukaingia katika saa yake, akaufungua, akausoma, Catherine alikua njiani anaelekea Tanzania, akafikiria, akajua nini cha kufanya, akaandika ujumbe.



      “,Kendrick is online, aim available in Comoro islands, Catherine just go to take helikopter, then come back to pick us ……”,(Kendrick yuko hewani, napatikana katika visiwa vya Komoro, Catherine nenda kachukue helikopta, kisha uje kutuchukua …”,)Kendrick alimaliza kuandika ujumbe, akautuma, moyo wake ukawa na amani.



      “,Hapa ndipo tunachukua minazi kwa ajili ya kutumia nyumbani. “,mzee Fedinand aliongea.



      “,Unasema? “,Kendrick hakuelewa, mawazo yake yalikua mbali, akauliza tena.



      “,Inaonekana hauko sawa, kuna tatizo lolote? “,mzee Fedinand aliuliza swali kwa Kendrick.



      “,Nilikua nashughulikia usafiri, muda wowote helikopta itakuja kutuchukua, kwa sasa niko ok kabisaa “,Kendrick aliongea, tabasamu zikaipamba sura ya mzee Fedinand pamoja na binti yake, wakamkumbatia Kendrick kwa furaha, hawakuamini kama muda mfupi ujao wangerejea tena Dar es salaam, baada ya kuishi miaka kumi katika kisiwa cha Komoro, Upendo akiwa binti mdogo, mpaka akawa mtu mzima.



      Makao makuu ya polisi :



             Catherine alichanganyikiwa, kituo cha polisi kitengo cha upelelezi kilikuwa kimevurugika, maiti nyingi zilitapakaa kila kona,watu wa huduma ya kwanza wakitimiza wajibu wao kubeba maiti na kuzipelekea mochwali, Catherine nguvu zilimuishia, akadondoka chini, akapiga magoti, alikuwa anatazama moja ya maiti iliypopigwa risasi nyingi sana tumboni, machozi yakamchuruzika kama maji bombani.



      “,D47 inatoshaa! nasema inatoshaa! mwisho wenu umekalibia,mmetuzidi ujanja lakini hamtatuzidi ujanja milele ……!Catherine alizungumza kwa uchungu, akaguswa begani, akageuka.



      “,Imekuaje! mlikuwa wapi mpaka tunaaibika kiasi hiki, shambulio hili limetuaibisha, lakini nimeshajua wakina nani wamefanya hivi…!”,kamanda Catherine alifoka kwa hasira, jasho jembamba likimtoka, mikono yake ilitetemeka, waziri wa ulinzi akaogopa,alizitambua hasira za Catherine.



      “,Askari wote leo wako bize na ulinzi,raisi ameingia bara, ana ziara huko kila mkoa,ndio maana ilikua rahisi kutekeleza shambulio hili,magaidi wameondoka na gari letu pamoja na sare za vijana wetu! “,waziri wa ulinzi aliongea,akajikuna kichwani, akaweka miwani yake vizuri, kisha akajiandaa kuzungumza kitu.



      “,wenzako wako wapi?, imekuaje ?,ndege yenu ilipotea kwenye rada zetu, tumeitafuta bila mafanikio, nikataka kutuma vijana waje kuwatafuta, ghafla nikapewa taarifa umerejea, nilikua njiani nakuja hapa, ghafla ndio tumekutana, hebu nieleze!! “,waziri wa ulinzi aliongea.



      “,Tulishambuliwa na magaidi, wengine nimewaponyoka,kundi limesambaratika, kila mtu yuko eneo lake, Philipo yuko Mafia, Kendrick yuko Komoro ,naomba muheshimiwa fanya jambo kwa ajili yao, tuma helikopta ikawachukue, ulinzi haujakaa vizuri kwa sasa ……” Catherine alitoa maelezo mafupi, akijifuta machozi kwa kutumia kitambaa chake.



      “,ok nafanya hivyo,helikopta itaenda kuwachukua nusu. saa kuanzia sasa, kabla jua halijazama, unachotakiwa kufanya, chunguza undani wa tukio hili, kisha nitumie taarifa ofisini kwangu …”,waziri wa ulinzi alizungumza, Catherine akatikisa kichwa, akapiga saluti,waziri akapanda kwenye gari lake, akaondoka zake,waandishi wa habari wakijitahidi kufanya mahojiano naye bila mafanikio, alikataa kuzungumzia chochote kile kuhusu tukio hili la kuvamiwa kwa kituo cha polisi kitengo cha upelelezi.



      …………………………………



      Helikopta ndogo yenye uwezo wa kubeba abiria sita, iliacha ardhi ya jeshi la anga,Dar es salaam,Tanzania, rubani wa helikopta alitimiza majukumu aliyoelekezwa,alipaswa kuwachukua makamanda wawili wa kitengo cha upelelezi, mmoja akiwa katika kisiwa cha Mafia, mwingine akiwa kisiwa cha Komoro.



      “,Usawa wa kisiwa, usawa wa kisiwa,unanipataa ovaaa! “,rubani wa helikopta alizungumza kupitia simu yake kubwa ya mkonga.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Halooo, halooo! ,oooh shiit! watakua hawana mawasiliano ya simu, hawapatikani hewani,”,aliendelea kuzungumza, akabonyeza tena simu yake ya mkonga, akaiunganisha na saa za kijeshi, saa za upelelezi.



      “,Haloo, halooo, niko Mafia, mko wapi ovaaa? “,aliuliza, akasubili jibu. Akiwa katika anga, usawa wa kisiwa cha Mafia.



      “,Niko Mafia, sogea bandarini, utaniona …”,sauti ilisikika upande wa pili.



      “,Nashuka sasa hivi,hakuna kupoteza hata sekunde, nimepewa nusu saa tu ya kuwachukua! “,rubani wa helikopta aliongea, akakata mawasiliano, akaiweka simu yake kwenye mifuko ya suti yake ya kijeshi. Baada ya dakika tano tu, alianza kuishusha ndege bandarini, ikatua juu ya meli moja, kamanda Philipo akaiona, akasogea karibu na meli hiyo, akaingia, moja kwa moja mpaka usawa wa helikopta, akapanda na kutokomea, wavuvi, mabaharia na abiria waliokuwa eneo hili la bandari wakabaki midomo wazi, wakijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu.



      “,tunaelekea Komoro, kumchukua Kendrick, kisha tutarudi tena Dar es salaam Tanzania …”,rubani yule aliongea, helikopta ikipaa juu futi sitini, ikakunja kona na kuelekea upande wa kusini,bahari ya hindi.



      …………………………………



      6;02pm



            Kamanda Kendrick alisubili helikopta kwa hamu sana, alikuwa na shauku kubwa ya kutaka kufika Dar es salaam,taarifa za kituo chao cha polisi kushambuliwa, askari wakauawa kinyama zilimshtua na kumsikitisha sana.



      “,Mbona hauna raha, nini tatizo Kendrick?, japo ni masaa kumi tu tumeweza kukutana, lakini nimetokea kukuzoea, unaonekana kijana mwenye huruma na hekima, sipendi uwe na majonzi ……”,mtoto wa mzee Fedinand aliongea, akamsogelea Kendrick, akakaa pembeni yake.



      “,Kuna taarifa mbaya kutoka serikalini, lakini usjali ni majukumu tu ya kikazi ……”,Kendrick aliongea, hakutaka kueleza kile ambacho kilikua kinamsumbua, akaficha,hakupaswa kumwamini mtu yoyote katika shughuli za kiserikali na kuziweka wazi.



      “,Papapapapapapapa! …”,muungurumo wa helikopta ulisikika, helikopta ndogo yenye rangi za kijeshi ilipita mita kadhaa usawa wa eneo lao, Kendrick akatazama juu, akaitambua ndege hii, ilikuwa helikopta ya Tanzania, akamshika mkono msichana wa mzee Fedinand.



      “,Twendeni wamekuja kutuchukua,baba, babaa, njoo twendee! “,Kendrick aliita, mzee Fedinand akatoka nje ya kibanda, mwilini akiwa amevaa magome ya miti, kwa miaka kumi sasa walitumia magome ya miti kama mavazi, nguo walizopotea nazo miaka kumi iliyopita walizivaa mpaka zikaisha. Hawakupata zingine, wakaamua watumie magome ya miti kusitiri miili yao.



      “,Philipo,!”,Kendrick aliita.



      “,Yes afande!”,philipo aliitikia,akamsogelea rafiki yake,wakakumbatiana.



      “,Hao ni wa kina nani,wanajua kiswahili?”,Philipo aliuliza.



      “,Yes wanajua,salimiana nao,mambo mengine tutazungumza baadae!”,Kendrick aliongea,akamsogelea mzee ambaye alikuwa amesimama sambamba na binti yake.



      “,Shikamoo mzee!”,Philipo alisalimia,akampatia mkono wa kulia,wakashikana kama salamu ya heshima.



      “,Marhaba!”,mzee yule aliitikia.



      “,Habari yako dada!”,alisalimia tena.



      “,Salama,asanteni sana kuja kutu……”,kabla Upendo hajamalizia kuongea, sauti ilisikika,sauti iliyomshitua na kumfanya ageuke haraka.



      “,Kamanda,tuondokeni!nilipewa nusu saa tu,nikichelewa nitaadhibiwa!”,rubani wa helikopta aliongea,Kendrick na Philipo wakamuelewa,walizitambua vizuri sana sheria za.kijeshi,wakajipakia ndani ya helikopta,helikopta ikapaa na kutokomea angani.



      …………………………………



      Bahari ya Hindi :6:30



               Mkuu wa kikundi cha magaidi wa D47,bilionea Paresh Kumar, alipata taarifa kutoka Tanzania,zilizidi kumfurahisha, akawa na furaha zilizopitiliza, tofauti na siku zote.



      “,Wale walikuwa askari wa Tanzania hatari wanaotutafuta kila siku, hasa Donald Mbeto ndiye muhusika mkuu,ndugu zetu kutoka Dar es salaam ndio wamenipatia taarifa hizi,wamemuua D47 namba mia moja, maana aligundulika kushirikiana na sisi, akapewa adhabu kama askari na kusema siri zetu zote, wameshambulia kituo cha polisi, wameua askari wote, ni shangwe na nderemo kwetu sisi, tunachopaswa kufanya ni kuwa makini, lazima watarudi kututafuta!! “,bilionea Paresh Kumar aliongea,mguu wake mmoja alikunja nne, kushoto aliketi mrembo wa kihindi, kulia aliketi mrembo wa kichina, wote walimpapasa na kumshika shika mwilini, alipenda sana wanawake, aliwateka kutoka pembe zote za dunia, akafuta kumbukumbu zao kichwani, wakamtumikia katika kundi lake katika shughuli mbalimbali.



      “,Kwa kuwa wameshajua eneo tulilopo,meli yetu ipae angani kama ndege, usawa wa mawingu, watahangaika kututafuta mpaka wanazeeka! “,Paresh Kumar alitoa amri, vijana wake wakaluka juu kwa shangwe, burudani zikaendelea, mziki ukapigwa, kila mtu akaendelea na starehe yake aliyoipenda, kufurahia ushindi, meli yao ikajigeuza, bawa likachomoza upande wa kulia, bawa lingine likachomoza upande wa kushoto, ikaanza kupaa hewani, ikaiacha bahari, haikuwa meli ya paraquat tena, bali ndege kubwa yenye uwezo wa ajabu.Makombola ya nyukilia yakachomoza kila upande wa ndege hii, kwa ajili ya ulinzi.



      Ofisi ya ukombozi: 7:00



             Catherine alianza upelelezi,aweze kuwapata washirika wa D47 waliofanya shambulio,akiwa anatafakari, akapata jibu, akaondoka haraka sana, kutoka katika kituo cha polisi kilichoshambuliwa, mpaka katika ofisi yao ya ukombozi, ndani ya jengo la China plaza, Kariakoo.



      “,This bastard kahusika! picha zake zisambazwe kila kona, tukimpata huyu, tutafahamu mengi ……”,Catherine aliongea, alimkumbuka raia wa kisomali waliyegongana vikumbo siku moja iliyopita,kijana aliyejaribu kufungua ofisi yao bila mafanikio na kuambulia kupigwa picha alipokosea neno siri la kufungulia mlango, Catherine akamkimbiza bila mafanikio, alitaka kumuhoji ajue nini alichotaka katika ofisi yao.



      “,Work done, kazi imekwisha,ngoja nikapige picha na eneo la tukio,ni attach kwenye picha yake,kisha nitume kwa waziri,vyombo vya habari viripoti taarifa hii…”,Catherine aliongea,akiitazama sura ya gaidi aliyetaka kuingia ndani ya ofisi yao siku moja iliyopita,akiwa ndani ya suti nyeusi,akiwa ameyavua mavazi yake ya kazi,akatoka nje ya ofisi ya ukombozi,akatokomea.



      …………………………………



      7:10pm



             Kendrick na Philipo walitaka kushushiwa katika eneo la tukio,mahali ambao kitengo chao cha cha upelelezi kilipatikana,kabla ya kushambuliwa,rubani wa helikopta akafanya hivyo,akashusha helikopta,ikatua ardhini na kuikanyaga ardhi ya Dar es salaam kwa mara nyingine tena,Kendrick akashuka,mkono wake wa kulia ulimshika Upendo,mtoto wa mzee Fedinand,Philipo akashuka,akiwa ameongozana na mzee Fedinand,uso kwa uso wakakutana na maiki nyingi za waandishi wa habari,wakitaka kuzungumza nao.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



      “,Naripoti kutoka ITV the super brand Afrika mashariki,naitwa Abdalah Said Abdulah,wewe kama mkuu wa kitengo hiki,unaweza kutueleza chochote kuhusu shambulio hili……”,mwandishi wa habari aliuliza,mwilini alivaa suti nyeusi iliyofiti mwili wake ipasavyo.



      “,Sijui chochote,ndiyo narejea baada ya helikopta yetu kupotea baharini,tukiwa katika majukumu yetu,lakini naahidi, tutawakamata watu hawa ndani masaa ishirini na nne yajayo!”,Kendrick aliongea,mwandishi wa habari akimtazama Upendo kuanzia chini hadi juu,alishangazwa sana na mavazi yake.



      “,Huyu naye umemtoa wapi?, amevaa mavazi tofauti na asili ya mtanzania,”mwandishi aliendelea kuhoji.



      “,Huyu anaitwa Upendo,baba yake anaitwa mzee Fedinad,walipotea na meli ya mv spice miaka kumi iliyopita,walifanikiwa kupona kifo cha maji,baada ya kuogelea mpaka pwani ya kisiwa cha Komoro, eneo lisilo na watu,wakaishi huko wakila matunda na samaki,wameniokoa mimi leo hii,pengine bila wao nisingekuwa hai,popote walipo ndugu zao,wafike nyumbani kwangu,mtoni kijichi,wakiulizia kamanda Kendrick,watafikishwa mpaka mlangoni…”,kamanda Kendrick alitoa maelezo,akamshika mkono Upendo,wakasogea kabisa eneo la tukio.



      “,Sasa,unaweza,ukaa……”,mwandishi yule alitaka kuendelea kuhoji,Kendrick alichoka mahojiano,akaondoka zake,akafika eneo la tukio,akatazama kila kona,damu zilikuwa zimeganda na kutapakaa eneo lote.



      “,Kendrick uko salama,na huyu ni nani?”,Catherine alifika,akauliza swali.



      “,Nitakueleza kila kitu,endelea kuchukua taarifa za upelelezi wa mwanzo,sisi tunaelekea nyumbani na kamanda Philipo,baada ya upelelezi,mpatie waziri majibu taarifa za upelelezi kama sheria zinavyosema, kisha fika haraka nyumbani kwangu,tuzungumze suala hili.”Kendrick aliongea,akatoa maelezo mafupi,wakaongozana na Philipo,pamoja na mzee Fedinand,wakapanda gari ya polisi, wakatokomea.



      …………………………………



      Kendrick aliishi nyumba moja na mama yake mzazi,kaka zake wawili walipoteza maishi kwa mshituko, waliposikia taarifa za meli ya mv spice kuzama, meli ikiwa imembeba baba yao ambaye alikuwa ni tegemeo kubwa katika familia yao,mama yao alichanganyikiwa,akaugua ugonjwa wa akili kutokana na kupata pigo kubwa kwa wakati mmoja, mme wake na mtoto wake wa mwisho, walipoteza maisha kwa ajari ya meli, watoto wake wakafa kwa mshituko wa moyo,mara baada ya kupokea taarifa za kifo cha baba yao, pamoja na mdogo wao.



      Kendrick akiwa kidato cha nne, aliamua kumpeleka mama yake hospitali kuu ya vichaa mkoani Dodoma, hospitali ya Mirembe. Akatibiwa, huku Kendrick akijiunga na jeshi la kujenga taifa, akamaliza mafunzo ya miezi sita, akajiunga na jeshi la polisi, kutokana na utendaji wake, akapandishwa cheo kila kukicha, huku mama yake akipona ugonjwa wake wa akili, akamrudisha nyumbani, wakaishi tena pamoja.Kendrick alifikili baba yake, pamoja na mdogo wake walikuwa wamepoteza maisha katika ajali ya mv spice,kumbe sivyo, Mungu aliwakutanisha tena pamoja.



      “,Baba Josephat! “,mama yake Kendrick alipigwa na butwaa,hakuwahi kuisahau sura ya mume wake hata siku moja, aliitambua vizuri sana,alipigwa na butwaa baada ya Kendrick kurudi nyumbani na wageni,mmoja kati ya wageni akiwa ni mume wake wa ndoa.



      “,Mamaaa Josephat, ni wewe?,nyumba yetu imebadilika! “,mzee Fedinand aliita kwa mshango, akamkimbilia mke wake, wakakumbatiana.



      “,Mbona sielewiii, ina maana, wewe ndiye baba yangu ……?”,Kendrick aliuliza swali kwa mshangao, chozi la furaha likaanza kumtoka.



      “,Ndiyo kendrick, huyu ndiye baba yako,sijui umemtoa wapi? “,mama yake Kendrick aliongea, machozi yakimtiririka.



      “,Mama Josephat, huyu ndiye mtoto wetu wa mwisho Jacline, huyu ndiye nilisafiri naye kwenda Zanzibar,”mzee Fedinand aliongea.



      “,Mamaaa! “,Upendo aliita.



      “,Mwanangu! “,mama Kendrick aliitika.



      “,Mamaaaa! “,Upendo akaita tena.



      “,Jamani mwananguuu …”,mama Kendrick akaita  tena, akamkimbilia mwanae, wakakumbatiana, kila mmoja akiona kama ndoto.



      “,Kendrick mwanangu, najua unajiuliza maswali mengi, mimi sio Fedinand, naitwa Steward, siwezi kukwambia ukweli katika hali kama ambayo umetukata nayo kule, tulikuwa hatujui wewe ni mtu mwema au mbaya kwetu, ndiyo maana nilikuficha majina yetu halisi, na huyo siyo Upendo, bali ni mdogo wako Jacline, wahenga walisema usimtendee mema binadamu unayemfahamu peke yake, leo hii nimekuokoa baharini, kumbe namuokoa mtoto wangu, Mungu katumia njia ya ajabu kutukutanisha. “,mzee Fedinand alitoa maelezo marefu, kumbe jina lake sio Fedinand, alidanganya,jina lake halisi aliitwa Steward, Kendrick akamsogelea baba yake na kumkumbatia, furaha ikazaliwa upya katika familia ya kamanda Kendrick.



      Kamanda Philipo alijifuta chozi ambalo lilikuwa linamdondoka, alishuhudia kila kitu,Catherine alikuwa amesimama mlangoni, alikuwa tayali ameshafika muda mrefu, akajikuta anasimama mlangoni kama sanamu, alishindwa kuendelea mbele, nguvu zilimuishia, historia ya kustaajabisha aliyoisikia ilimchanganya sana, hakuamini kama Kendrick alipitia mkasa wa kutisha kiasi hicho, hakuwahi kumweleza hata siku moja, alikua msiri sana.



      “,Catherine! umefika, kumbe uko hapa, karibu ndani, nilitaka nikueleze kuhusu kukutana na watu hawa,tujue namna ya kuwasaidia kuwapata ndugu zao, lakini kumbe tayali wameshafika nyumbani! “,Kendrick aliongea kwa furaha, Catherine akatabasamu, akasogea sebureni, akakaa kwenye sofa.



      “„Josephat na Yohana wako wapi?  ,au wameshaoa, wako na familia zao? “,mzee Steward, baba yake Kendrick aliuliza, mama yake Kendrick akanyongonyea, tabasamu ikatoweka usoni mwake, vivyo hivyo kwa Kendrick, akapoteza furaha kabisa, akapiga moyo konde, akajikaza kiume na kuongea ukweli.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Kwa sasa ni marehemu, tuliwazika siku moja tu baada ya kupokea taarifa za meli kuzama na abiria wote kupoteza maisha, walipatwa na mshituko, wakafa palepale, mama naye akachanganyikiwa, lakini namshukuru Mungu, mama alipatiwa matibabu, kwa sasa ni mzima ……”,Kendrick aliongea,baba yake akadondosha chozi, haikusaidia chochote kile,watoto wake walikuwa tayali wameshapoteza maisha, wasingerudi tena.



      “,Wapumzikee kwa amani wanangu! “,mzee Steward alizungumza, mke wake akamkumbatia, akambembeleza, akajikaza kiume, akajaribu kuificha huzuni yake lakini hakuweza, machozi yake yaliendelea kutoka, alihuzunika sana kuwapoteza watoto wake.



      Mbezi :8:02



               Magaidi wa D47,kanda ya Dar es salaam, walikuwa wameketi katika nyumba yao ya kifahari,chupa za bia zilikua mezani, walikunywa mpaka wakatapika,walikamilisha kazi kama walivyopanga, bosi wao akafurahishwa zaidi na kitendo hicho, akamuingizia kila mtu dola elfu moja kwenye akaunti yake. Akawapatia kazi nyingine kubwa, kuhakikisha wanawaua maaskari watatu wanaolifuatilia kundi lao.



      “,Kesho asubuhi na mapema tunaanza kazi, hawa watu lazima tuwauee, tusipo waua sisi, watatuua! “,D47 namba sitini alizungumza, wenzake watatu wakiwa. pembeni yake,kila mmoja alikuwa ameshika chupa ya bia mkononi.



      “,Kweli kabisa,mimi nina plani,nina mipango ambayo itaifanya kazi hii kuwa rahisi kabisa……”,gaidi mwembamba,mrefu,mweupe,alizungumza,akawatazama wenzake usoni.Wote wakaweka bia zao,wakatulia kusikiliza mbinu hiyo,walikuwa na shauku ya kupata pesa nyingi kama wakifanikiwa kuwaua wapelelezi watatu hatari wa kundi la the super three soldiers.



      “,Mbinu gani hiyo chuma cha puaa?”,gaidi mwingine aliuliza,mweusi,mfupi,kichwani alikua na kipara.



      “,Tuteke familia zao,hasa ya kiongozi wao wa kundi,lazima watajileta wenyewe,wote watatu,kutaka kuwakomboa,sisi tutaacha eneo hili likiwa limetegwa mabomu,wakifika eneo hili kukomboa ndugu zao,tunalilipua,wanakufa woteeee!”,gaidi yule aliyejulikana kwa jina la chuma cha pua aliongea,licha ya wembamba pamoja na urefu wake,alikuwa amekomaa kama chuma,ngumi yake ilikuwa na uwezo wa kupasua matofauli kumi ya bloko,aliwahi kumuua gaidi mwenzake,allimpiga na kichwa chake,akampasua fuvu la kichwa,wote wakiwa mazoezini,wakamubatiza jina hilo,mwili wake ulikomaa kwelikweli.



      ” ,Yeeeeeeh!,”waligonga chupa zao kwa furaha,walikubaliana na plani ya mwenzao,kilichobakia ni utekelezaji,wakanywa bia kwa fujo, wakalewa chakali,usingizi ukawachukua,wakalaliana kama mizigo,wakiwa hawajitambui.



      …………………………………



      Ofisi ya Ukombozi:9:00pm



      Makamanda watatu walikutana tena,mara baada ya kutoka nyumbani kwa kamanda Kendrick.Kila mmoja aliketi katika kiti chake,ndani ya ofisi ya ukombozi.



      “,Catherine nipe ripoti!”,Kendrick aliongea,akijizungusha zungusha kwenye kiti chake.



      “,Kila kitu kiko sawa,picha za mmoja kati ya magaidi anayetuhumiwa kuhusika na shambulio,zimefika katika vyombo vya habari,kesho asubuhi taarifa zitaenea na kutangazwa kila kona.”,Catherine alimaliza kutoa ripoti yake.



      “,Ok sawa,sasa nazani mnafahamu magaidi walipo,mahali tuliposhambuliwa,walitugundua mapema,meli yao ikajibadirisha kama nyambizi,ikawa rahisi kutushambulia,hivyo basi,kabla ya mapambano tuelewe,meli yao ni ulinzi tosha kwao,ina uwezo kujigeuza katika maumbo mbalimbali,ikawa kama meli,nyambizi au hata ndege ,ikapaa angani kama ndege zingine!”,Kendrick alitoa maelezo mafupi.



      “,Sasa Kendrick ,tunafanya nini hapa? ,tutumie mbinu gani?”,Catherine aliuliza.



      “,Nafahamu nini cha kufanya,nikipata uhakika wa eneo walilopo,iwe baharini au angani,nitaweza kudukua(kuhack) mifumo yote ya mawasiliano kwenye chombo chao,itakua rahisi kuwavamia,hawatatuona wakati wa kukivamia chombo chao.



      “,Sawa,naona tukiwakamata hawa magaidi walioko Dar es salaam,watatusaidia kujua wenzao wako wapi,itakua rahisi kufanya udukuzi!”,Catherine aliongea.



      “,Wazo zuri,tukutane hapa saa kumi na mbili asubuhi,tuanze kazi,kila mmoja awe makini kujilinda,kila tunapopiga hatua,maadui zetu wako nyuma,zingatieni suala hili……”,Kendrick alizungumza.



      “,Sawa afandee!”,wote waliitikia,wakapigiana saluti za heshima,kila mmoja akatoka nje, kuelekea nyumbani kwake kupumzika..



      …………………………………



      Hisia za kimapenzi ziliusumbua moyo wake, kadri siku zilivyozidi kwenda, Kendrick hakuonesha hisia zozote za mapenzi juu yake,uvumilivu ukamshinda kabisa, moyo wake ulichoka kuteseka na mapenzi,akafikiria, akapata wazo, wazo aliliona sahihi.…



      “,Kendrick,nimepoteza funguo za nyumba yangu, sijui hata nafanya nini, hotelini siyo salama, siwezi kulala kabisa ……”,Catherine alidanganya, akiwa pembeni ya gari lake, sura yake ilikuwa siliasi, haikuonesha hata chembe ya uongo, alijiamini kwa yale aliyoyazungumza.



      “,Kwa nini usije kulala nyumbani kwangu, kuna vyumba vya kutosha, kesho tutatafuta funguo zako au kuchongesha zinginee! “,Kendrick aliongea.



      “,Hapo utakua umenisaidia saanaa, lakini ujue sasa hivi familia yako imeongezeka, mzee wako, mama yako pamoja na mdogo wako, hawawezi kukufikilia vibaya,wakafikili umeleta mwanamke ndani? “,Catherine alifurahi plani yake kufanikiwa kama alivyo panga,akajifanya kama hakupanga jambo hilo, akaendelea kuuliza maswali ya uchokozi.



      “,Hapana,wewe ni rafiki yangu,tunafanya kazi pamoja, hawezi kuwaza chochote kile, japo mama yangu kila siku ananiuliza kuhusu suala la kuoa, mimi bado sijawa tayali, nitamlisha nini mie? “,Kendrick alimjibu Catherine, uso wake ukaachia tabasamu kwa mbali. .



      “,Hahaaa, “wote wakacheka, wakajipakia kwenye magari yao, nje ya jengo la ofisi ya ukombozi, wakatokomea, kamanda Philipo alikuwa tayali ameshaondoka zake dakika takribani kumi zilizopita.



      …………………………………



      Mtoni Kijichi :



             Catherine na Kendrick walifika nyumbani, mama yake Kendrick, baba yake, pamoja na mdogo wake Jacline walikuwa tayali wamelala.



      “,Tutaonana kesho,kalale chumba cha wageni, pita korido hii, chumba cha kwanza mkono wa kushoto! “,Kendrick aliongea, baada ya kumaliza kula, yeye pamoja na Catherine.Kendrick alinyanyuka, akataka kwenda kuchukua maji ya kunywa kwenye friji.



      “,Sawa nimekuelewa, mbona unasimama, unaenda wapi? “,Catherine aliuliza.



      “,Naenda kunywa maji “,Kendrick alijibu.



      “,Subili nikuletee! “,Catherine aliongea, akanyanyuka kwenye sofa, akaisogelea friji, akachukua chupa ya maji ndani ya friji, akamimina kwenye grasi. Akageuka nyuma, Kendrick alikuwa anasinzia sinzia, usingizi ulikuwa unamzidi nguvu, hakutambua chochote kile kilichokuwa kinaendelea, catherine akaingiza mkono ndani ya koti lake la suti, akachukua kidonge cha usingizi, vidonge ambavyo walivitumia katika oparesheni mbalimbali za kijeshi. Baada ya kuweka kidonge kile ndani ya maji, akatikisa vizuri kiweze kuyeyuka, kisha akampelekea Kendrick.



      “,Kendrick, Kendrick! “,Catherine aliita.



      “,Yeeees, nanambiee! “,Aliitika kwa kigugumizi, usingizi ulimzidi nguvu, isitoshe alichoka sana, tangu asubuhi alizunguka huku na kule bila kupumzika.



      “,Kunywa maji, haya hapa! “,Catherine aliongea, Kendrick akachukua glasi ya maji, akanywa maji yote,akaweka glasi mezani, ndani ya sekunde mbili tu, akalala fofo.



      “,Hahaaa, leo unalala na mimi, kila siku nikigusia suala la mapenzi unaona kama natania, sasa leo tunalala wote, kesho wakitukuta, lazima tufunge ndoa ya mkeka, unasema huoi askari kama wewe, sasa utaoa kwa lazima…”,Catherine alisahau vita kubwa mbele yao kwa muda mfupi tu, hisia za mapenzi zilikuwa zimemtawala, akamnyenyua Kendrick, akampeleka katika chumba cha wageni, chumba ambacho alielekezwa akalale, wote wakalala huko.



      Mtoni kijichi :7:30am



            Magaidi wanne wa kundi la D47,walipaki gari nyeusi aina Toyota Hallier, pembeni, nje ya jumba la kamanda Kendrick, jumba ambalo lilizungushiwa geti kubwa.



      “,Hapa ndipo nyumbani kwake,waliotuelekeza hawajadanganya, kama unavyo ona, kuna askari getini, anatimiza majukumu yake ya ulinzi



      ……”,gaidi D47 alioongea.



      “,’Nazani mwenyewe ameshaelekea ofisini,chuma cha pua, toka kaongee na mlinzi, fanya lolote tuweze kuingia ndani! “,gaidi D47 aliendelea kuongea.



      “,Sawa bosi”,chuma cha pua aliitikia, akatoka nje, akalisogelea geti,mpaka mahali alipokuwa amesimama mlinzi.



      “,Karibu muheshimiwa, sijui nikusaidie nini? “,askari mwenye kirungu mkononi aliuliza,akamkaribisha kwa heshima zote gaidi, kutokana na suti nyeusi ya heshima aliyokuwa amevaa.



      “,Nina mazungumzo na bosi wako, tulisoma naye, ni muda mrefu hatujaonana, naomba kuzungumza naye…”,gaidi aliyejulikana kwa jina la chuma cha pua aliongea,askari yule akaonekana kuyaamini maneno ya mgeni huyu.



      “,Japo bosi hayupo, ameshaenda kazini, unaitwa nani? “,askari yule aliuliza swali tena,huku akidanganya kuwa Kendrick hayupo, alielekezwa kusema hivyo kwa mtu yoyote asiyemfahamu.



      “,Acha maswali yako kijana, au nimpigie simu uongee naye, utamwaga unga sasa hivi …”,chuma cha pua aliongea, akaingiza mikono yake mfukoni, akatoa simu, akajifanya kama anataka kupiga, askari yule akaanza kutetemeka kwa hofu.



      “,basi baba! basii, yaishee, ingia ndani ,lakini bosi hayupo……,”askari yule aliongea,akadanganya, hakuna aliyemsikiliza, akafungua mlango, chuma cha pua aliangalia kulia, akaangalia tena kushoto, hakuona mtu yoyote yule, alimpiga kabali askari yule, akaivunja shingo yake, ulimi wa askari yule ukatokeza kwa nje, akafa palepale. Chuma cha pua akambeba, akamuweka kwenye buti la gari,walitaka mauaji yafanyike kimya kimya, asigundue mtu yoyote yule, baada ya kumfyekelea mbali, magaidi wote watatu wakatoka ndani ya gari, wakaingia ndani ya jengo la kamanda Kendrick, wakafunga geti kwa ndani, asije akaingia mtu yoyote yuke, akaharibu mipango yao.



      “,Kaka yuko wapi?”,Jacline aliuliza,akiwa anaandaa chai mezani.



      “,Yuko na wifi yako,nimeona viatu vya kike mlangoni tofauti na vyangu wala vyako,leo amechelewa kwenda kazini,muache apumzikee…”,mama yake Kendrick aliongea,huku akitabasamu.



      “,Jana walikula naye,nilichungulia sebureni,ni yule msichana wanayefanya naye kazi,ni mrembo kwakweli,nilipomtambua nikarudi kulala…”,baba yake Kendrick,mzee Steward aliongea.



      “,Hahaaaa……”,wote wakacheka,wakaendelea kunywa chai.



      “,Hapo hapo mlipo,asijitikise mtu yoyote,mkijitikisa tunawaua!……”,sauti ya kutisha ilisikika,walipogeuza shingo zao,wakatazama mlangoni,uso kwa uso na wanaume wanne wenye bastola mkononi,usoni walivaa miwani rangi nyeusi,rangi ambayo ilifanana na suti zao pamoja na mabuti yao meusi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



      “,Nyie ni wakina nani?mnataka nini?”,mama yake Kendrick aliuliza swali.



      “,paaaaaaa!”,alichapwa kibao,akadondokea upande wa pili wa sofa.



      “,Mamaaaaaaa!”,Jacline alipiga kelele,hasira za mama yake kupigwa mbele yake zikampanda,akakosa cha kufanya.



      “,Kelele malaya wewe!”,Jackline alifokewa.Akazidi kukasirika.



      “,Malaya mwenyewe!”,Jackline hakuogopa chochote kile,akawatukana magaidi.wale,akamtemea makohozi usoni,gaidi ambaye alikuwa amemchapa kibao mama yake,huku akimwita Jackline malaya.



      “,Tunakubaka sote wanne sasa hivi,mbele ya baba yako,pamoja na mama yako,halafu tuone sisi na wewe nani malaya……”,chuma cha pua alizungumza,wakamfunga kamba mama yake Kendrick mkononi na miguuni,wakamfunga na baba yake.Wakajiandaa kumubaka Jackline,chuma.cha pua alianza kuifungua zipu yake.



      …………………………………



      Kamanda Catherine alikuwa amechoka sana,alilala na mtu aliyempenda kwa mara ya kwanza, lakini hakufanya naye chochote kile, alitaka kutimiza malengo yake, Kendrick aweze kufungishwa ndoa ya mkeka pamoja naye, watakapokutwa wamelala pamoja asubuhi. Usingizi hauna ndugu, alilala fofofo tofauti na siku zote, Kendrick ndiyo kabisaa, dawa ya usingizi aliyopatiwa usiku uliopita, iliendelea kutimiza majukumu yake, akauchapa usingizi bila hata kushtuka.



      Ghafla Catherine alikurupuka usingizi, mapigo ya moyo wake yalienda kasi sana,akageuka upande wa pili, akamgusa gusa Kendrick begani, hakushtuka! alikuwa bado amelala. Catherine akaitazama saa yake ya kijeshi, “8:00am”,saa yake ilisomeka.



      “,Saa mbili kamilii! “,aliongea peke yake kwa mshangao, akachukua viatu vyake, akavaa suti yake, akaziweka vizuri nywele zake, kwa mbali akasikia vitisho sebureni, akasikiliza kwa makini, mapigo ya moyo wake yakapiga kwa kasi sana,walikuwa wamevamiwa, akasogea kitandani, akampiga piga Kendrick aweze kushtuka,Kendrick hakushtuka, aliendelea kukoroma kama kawaida.



      “,Kendrick, Kendrick, tumevamiwa, najuta mimi! amka tukapambane! “,Catherine aliita, bila mafanikio,hakua na budi kuubeba mzigo yeye mwenyewe, bila hivyo chochote kile kingeweza kutokea, wazazi wa Kendrick wasije wakauawa, akalaumiwa,akakosa mume pamoja na kuharibu kazi yake.



      “,Kakaa, nabakwaa, kaka nabakwaaa, njooo unisaidiee ……”,Jackline alipiga kelele,kelele zikapenya katika matundu mawili ya masikio ya Catherine, akakasirika.



      “,Hahaaahaaa, hakuna atakayekuja kukusaidia, hahaa……”,magaidi yale yalizungumza, yakacheka kwa kejeli, Catherine akazidi kukasirika,alisikia kila kitu.



      “,nimelala kwa Kendrick, najua uko ofisini, njoo, tumevamiwa …”,Catherine alituma ujumbe kwa kamanda Philipo kupitia saa yake iliyotumika kama simu,akapiga mahesabu namna ya kuwavamia magaidi, awashambulie kabla hawajafanya ubakaji. Akafungua mlango taratibu, akachungulia,akamuona jambazi aliyegongana naye uso kwa uso, alimtambua vizuri sana.



      “,Wamejileta wenyewe, watakufa, “Catherine aliongea, akaifunga bastola yake mfumo wa sauti, akalala chini, hakuweza kuonekana, sofa zilimzuia. Chuma cha pua akachomoa uume wake uliosimama kwa njaa kali, bila aibu akamsogelea Jacline.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Yalaaaaaa ……”,uume wa chuma cha pua ulisambaratika, damu zikaruka, akapiga kelele za uchungu, hawakutambua risasi imetokea wapi. Wakaanza kupiga hovyo risasi, kwenye sofa, ukutani, dirishani, milangoni, walikuwa kama wamechanganyikiwa.



      “,Mtafuteni tumuue! jitokeze kabla hatujaua familia yako ……”,kiongozi wa kundi hili aliongea, alikuwa D47 namba sitini, bastola yake aliinyosha kuelekea juu, akafyatua risasi, zikapiga juu ya dali.



      “,Nasema jitokeze tutawauaa wazazi wako! “,gaidi alitoa amri kwa mara nyingine tena.







      ITAENDELEA

    Blog