Search This Blog

Friday, 28 October 2022

JINI MWEUPE - 5

 









    Simulizi : Jini Mweupe

    Sehemu Ya Tano (5)





    …………………………………



    Milio ya risasi ikamkulupua usingizini kamanda Kendrick,akavaa suruali, akachukua bastola yake, akafungua mlango taratibu, huku akijiuliza maswali mengi, hakujua amefikaje katika chumba hiki cha wageni, chumba ambacho alipaswa kulala kamanda Catherine.



    “,Jitokeze kabla sijawaua wazazi wako, moja, mbili tatu ……”,gaidi lile lilianza kuhesabu, Kendrick hakuwa tayali kuwapoteza ndugu zake,  akajibanza ukutani, uso kwa uso na kamanda Catherine akiwa amelala chini.



    “,Chuchumaa chini, watakuona, vipi tunafanyaje hapa?,nimefikilia mbinu ya kutumia nimeshindwa”,Catherine alimuuliza Kendrick.



    “,Bunduki yako umeweka sailensa(silent mode )?”,Kendrick aliuliza.



    “,Ndiyo, nimeweka …”,Catherine alijibu.



    “,Piga kule mlangoni, wakiwa bize kuangaza mlangoni risasi hizo, tutaruka na kuwashambulia ,kwanza wako bize wanamuhudumia mwenzao, amefanya nini?……”,Kendrick aliuliza.



    “,Nimempiga risasi kwenye dudu lake, alitaka kumubaka mdogo wako, “Catherine aliongea.



    “,Sita, saba, nikifika kumi nauwa familia yako yote, nane, “gaidi aliendelea kuhesabu, akatoa onyo, akaendelea tena kuhesabu, Catherine na Kendrick wakasitisha mazungumzo yao, Catherine akapiga bastola kwenye mlango wa kutokea ndani ya nyumba, wote wakageuka, wakautazama.



    “,Vuuuup, kwaaacha……”,Kendrick aliluka mateke mawili yaliyosindikizwa na ngumi, akamtandika ngumi gaidi D47 namba sitini ,mateke mawili yakawapata magaidi wawili waliokuwa wanampatia huduma mwenzao, wote wakagagaa. Catherine akawanyoshea bastola, akawateka, Kendrick na yeye akawanyoshea bastola yake.



    “,Paaaa! “,alipiga risasi chini, magaidi yakarudisha mikono yao, yalitaka kuzichuka bastola zao zilizodondoka mita kadhaa na mahali yalipodondokea.



    “,Mmejileta wenyewe, tulikuwa tumepanga leo tuwasake kona zote za mji huu wa makonda, karibuni sana nyumbani kwangu, “Kendrick aliongea, mkono wake wa kulia ulishika bastola, mkono wake mwingine alikuwa akiwafungua kamba wazazi wake, ghafla mlango ukafunguliwa, kamanda Philipo alikuwa amefika.



    “,Ewalaaa! asante sana Mungu, leo sitalala kama maiti ,jana nimechoka sana sababu yenu, kazi ya leo imeisha asubuhi tu, sasa mtakipata cha mtema kuni! “,Kamanda Philipo aliongea, akayafunga kamba magaidi haya manne, huku Jackline akiyapiga teke kwa hasira na kuyatemea mate.



    “,Asante wifi, umeyaokoa maisha yangu! “,Catherine alilia kwa furaha akamkumbatia Catherine.



    “,Usjali wifi yangu, ni kazi yangu …”,Catherine alijibu.



    “,Huyu ndiyo mkwe sasa, Kendrick unajua kuchagua ……”,mzee Steward na mke wake waliongea, wote wakamkumbatia Catherine, walishuhudia ushujaa wake, Kendrick yeye alikuwa amepigwa na butwaa, hakujua chochote kile, Catherine akakonyezana macho na kamanda Philipo, kamanda Philipo alifahamu kila kitu, wote wakatabasamu.



    “,Saluti afandee! “,askari watano wenye virungu waliingia ndani, wakapiga saluti.



    “,Salutiii, chukueni washenzi hawa, pakieni kwenye karandinga, mpaka chumba cha mateso, tutafika huko kufanya nao mahojiano, “Kendrick aliongea.



    “Sawa mkuu, tumefika na kukagua gari lao, tumekuta maiti ya askari wetu anayelinda geti lako, “,askari wale waliendelea kuripoti.



    “,Kwahyo wameuaa?”,aliuliza kwa hasira.



    “,Ndiyo bosi,maiti iko kwenye gari lao”askari wale waliitikia.



    “,Andika kwenye faili, jana wameua watu ishirini na moja, wakateketeza na kituo chetu, huyu ni mtu wa ishirini na mbili, toa taarifa kwa waziri pamoja na vyombo vya habari wapate taarifa hii ……”,Kendrick aliongea.



    “,Sawa mkuu, salutii …”,vijana wale waliitikia, wakapiga saluti, wakawabeba msobemsobe magaidi wanne wa D47,wakaondoka nao.



    …………………………………



    “,Kabla ya yote,usiku mmelala pamoja, sisi kama wazazi tumeshuhudia, kulingana na mila yetu ya , tunapaswa kuwafungisha ndoa na kuwapatia baraka zote, tukiwa tunasubili ndoa rasmi, tucheze ngoma na kuburudika, “mama yake Kendrick aliongea, Catherine akatabasamu, Philipo akatabasamu, Kendrick akatabasamu japo kwa shingo upande.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Mama mimi sikulala naye chumba kimoja, sasa sijui nitamlisha nini! “,Kendrick aliongea, hofu ya majukumu ilimuandama moyoni.Isitoshe hakutambua chochote kile, Philipo na Catherine wakiwa wanachekelea kwa furaha, sio Philipo tu, Jackline alikuwa anafurahi kwa kile ambacho kilikuwa kinafanyika.



    “,umelala naye hujalala naye sisi haituhusu, mpatie mkono mwenzako! “,mama Kendrick aliongea, alichoka kusubili mkwe kila siku,akiishia kuambulia ahadi zisizotimia kutoka kwa mtoto wake, leo alimkamatisha.



    Catherine akamshika mkono Kendrick, akafunga na kanga mikono yao, akaongea maneno ya kimila, akatoa baraka zake zote yeye na mume wake, wote wakapiga kelele za shangwe. Mama Kendrick akapiga meza kama ngoma, mdundiko ukapigwa, Catherine akacheza, Phipo akacheza, wote uvumilivu ukawashinda, wakaanza kucheza ngoma kwa furaha.



    Mtoni Kijichi :08:40am



              Nyumba ya Kendrick ilijawa na furaha tele, kila mmoja alicheza kadiri alivyoweza, walisahau kabisa kuwa ilikuwa ni muda wa kazi, burudani iliwafanya wasahau kila kitu, walisahau majukumu mazito yaliyokuwa mbele yao.



    “,Kendrick! saa tatu kasoro! “,Catherine aliitazama saa yake, akashtuka sana, muda ulikuwa unazidi kwenda mbele, walikuwa hawajafika ofisini.



    “,What!twendeni,bila shaka wanatusubili…”,Philipo aliongea,kila mtu akachukua kilicho chake,Kendrick akaenda kuvaa suti yake nyeusi,wote wakaondoka kuelekea kazini



    “,Oooh sitaki kuoa, ooh sijajipanga, utajipanga mpaka lini, utaoa kwa lazima ,mimi ndiyo mama Kendrick ……”,yalikuwa maneno ya mama Kendrick, akiwa amebaki nyumbani, yeye, mume wake pamoja na mwanae wa kike.



    “,Kweli kabisa, lakini mimi bado nawafikilia wale majambazi, mimi naona kaka abadilishe kazi, kazi yake ni ya hatari  watakuja kufa siku moja! “,Jacline aliongea.



    “,Sasa askari wote wakiacha kazi, nani atakulinda?, acha watimize majukumu yao, kila mmoja atakufa, hakuna mtu yoyote atakayeishi milele …”,baba yake Kendrick, mzee Steward aliongea, binti yake akakaa kimya.



    “,Haya sasa, mwanangu na mkwe wangu wote askari, nikiguswa tu na majirani,cha moto watakiona! “,mama yake Kendrick aliongea,licha ya kula chumvi nyingi, tabia za uswahilini alikua bado anazo. Waswahili husema ng’ombe hazeeki maini.



    “,Sawa mke wangu, ngoja mi nijiandaee,nikazulule mtaani, maana muda mrefu sijaona magari, “mzee Steward aliongea.



    “,weweee naye, tabia zako hujaziacha tu,bila shaka umekumbuka wanawake zako,haya kila laheri, uwasalimie wake wenza ……!”,mama Kendrick alizungumza.



    “,Mama Kendrick, maneno gani unazungumza mbele ya binti yako, unamfundisha nini huyu mtoto! ……”,baba Kendrick aliongea, hasira zilimjaa usoni, sura yake ikakunjamana.



    ”  ,Wewe naye hutaniwii! nilikua nimekukumbuka mume wangu, nisamehe bure …”,mama Kendrick aliongea, mzee Steward akaelekea chumbani, Jacline akacheka, utani wa wazazi wake ulimfurahisha sana.



    ………………………………



    Chumba cha mateso :



              Kendrick, Catherine pamoja na Philipo, walifika chumba cha mateso, chumba ambacho kilipatikana katika gereza kuu la Segerea.Ulinzi uliimarishwa, kila aliyeingia na kutoka, alikaguliwa kwa mashine maalumu ya umeme,hakuna aliyeruhusiwa kuingia na silaha isipokuwa kwa kibali maalumu.



    “,You are not allowed to get in, unless you put down your guns ……”,(Hamruhusiwi kuingia ndani, mpaka tu mtakapo weka bunduki zenu chini …).



    Mashine ya ukaguzi pembeni ya mlango iliongea kwa sauti, Kendrick, Catherine pamoja na Philipo, wote walikuwa na bastola katika miili yao, Kendrick alikuwa ameipachika kwenye kiatu chake, Philipo alikuwa ameipachika katika koti la suti yake, Catherine alikuwa ameipachika katikati ya mkanda wake.



    “,Haina jinsi, milango hii ni ya umeme, msipo weka silaha zenu, milango haitafunguka ……”,askari magereza aliyekuwa anawaongoza aliongea, wote wakachomoa bastola zao, wakampatia mmoja kati ya askari magereza, akazihifadhi kisha wakarudi tena, mashine ikawakagua, walikuwa hawana silaha, mlango ukafunguka, wakaingia ndani, askari mkuu wa magereza alikuwa mbele akiongoza msafara, Kendrick alifuatia, kisha Catherine pamoja na Philipo walifata kwa nyuma.



    “,Hawa ndiyo walifanya shambulio la kigaidi, wakateketeza kituo chenu? “,askari magereza aliuliza.



    “,Ndio mkuu, tunapaswa kuwahoji tujue Donald Mbeto yuko wapi kwa sasa, ikiwezekana wafanye mawasiliano nao, tukawakamate! “,Catherine aliongea.



    “,Magaidi wana roho ngumu, huwa hawasemi kirahisi namna hiyo, mmejipangaje? “,askari magereza aliongea.



    “,Watasema tu, twende ukaone! “,kamanda Philipo aliongea, askari magereza aliwaamini sana vijana hawa, siku zote kazi yao ilikua ya uhakika.



    Wakatembea korido ndefu, wakapita gereza la kwanza lililojaa wafungwa takribani elfu moja, wakiwa wamelaliana kama ndizi,baada ya dakika tano wakalivuka gereza hili, wakakata kona mkono wa kulia, wakakata kushoto, uso kwa uso na chumba kikubwa kilichozungushiwa nyavu kila kona. Mlangoni kilifungwa na kufuli kubwa la kilo tano, ndani ya chumba hiki kulikuwa na viti vitano, viti ambavyo vilikuwa maalumu kwa ajili ya kutoa mateso pamoja na kunyonga.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Karibuni sana, naona mmefurahi sana, lakini tambueni kuwa, wenzetu wakitambua jambo hili, watakuja kutukomboa ……”,chuma cha pua aliongea, alikuwa na roho ngumu sana, nyeti zake zilikuwa zimefungwa bandeji,haja ndogo alitumia mpira maalumu, lakini hakukoma, aliendelea kuwa katili kama kawaida.Mara tu baada ya kundi la the super three soldiers kuingia ndani ya chumba walichokuwa wamefungwa, aliwakaribisha kwa kejeli.



    “,Hahaaaaa, mmekuja na malaya humu ndani! “,magaidi wote watatu walicheka, wakamkejeli Catherine. Catherine akataka kuwasogelea awatandike makonde, Kendrick akamzuia.



    “,Nilitaka wote mtumie mipira kukojoa kama mwenzenu, muda mfupi ujao mtalia machozi, chekeni mara ya mwisho! “,Catherine alifoka, ngumi yake alikuwa ameikunja, akachomoa sindano za kibanio chake cha nywele, akajiandaa kutoa mateso wakati utakapofika.



    Kendrick alijua nini cha kufanya,akasogelea meza yenye batani nyekundu,akafika, akakaa juu yake. Catherine pamoja na Philipo wakasimama katikati ya magaidi wanne.



    “,Mnaweza kutwambia uwezo wa meli yenu ya D47paraquaat ……?”,Kendrick aliuliza swali la kwanza.



    “,Hahaaaaa!,kirahisi rahisi hivyo, hata ufanye nini, kuingia ndani ya meli yetu hutaweza dunia yote imeshindwa, sembuse wewe sisimizi mdogo tu ……”,Chuma cha pua alicheka sana, akaongea kwa kejeli, akawaponza wenzake.



    “,Yalaaa…aaaa, yalaa…aaa …”,Kendrick alibonyeza batani nyekundu iliyokuwa mezani, kelele za magaidi zikasikika, walipigwa na shoti ya umeme kutoka kwenye viti vya chuma walivyokalia, jasho likawatoka kama maji kwa sekunde moja tu. Baada ya dakika mbili Kendrick akabonyeza tena, shoti ikakata, zingezidi dakika mbili basi angewaua kabisa magaidi hawa.



    “,Hehee…ee, bola utuue tu …”,chuma cha pua alicheka tena, Kendrick akakasilika, akabonyeza tena mtambo wa shoti ya umeme.



    “,Yaaala…aa, uwiiii…ii! “,,yalipiga kelele, yakalia kwa uchungu.Catherine akayachoma na sindano zake mgongoni, kila mmoja, yakaugulia maumivu.



    “,Hatusemi, tuueni tuu! “,yaligoma kutaja, Catherine akapataa wazo, akawaita pembeni wenzake,akawaeleza wazo lake.



    “,Sikilizeni, tuyapatie nafasi yawasiliane na wenzao,sisi tujifanye wajinga,yatumie simu yetu kuwasiliana ,kisha tutaunganisha simu yetu pamoja na kompyuta tutajua imepigwa kutoka wapi,hawa wana roho ya paka hawawezi kusema.’ ,Catherine aliongea wenzake wakamuelewa.



    “,Kwahiyo mnasema wenzenu wakipata taarifa watakuja kuwakomboa……?”,Catherine aliuliza.



    “,Ndiyo,sasa hivi mnajifanya wajanja kwa vile hawana taarifa,Donald Mbeto atawaua nyoteee…”,magaidi haya manne yalijitamba na kuchimba mkwala.



    “,Sasa sisi tunataka tuwapige mbele yenu hao mnaowategemea,simu inaletwa,muwapigie,waambieni mmekamatwa,waje wawaokoe……” Kendrick aliongea, yakatikisa kichwa, yakakonyezana.Dakika mbili tu, askari magereza alileta simu, akawakabidhi,chuma cha pua akafunguliwa mkono mmoja, akapatiwa simu,simu ilikuwa imewekwa raudi spika.Akabonyeza namba alizozifahamu yeye, akapiga.



    “,Vipi imekuaje, mbona kimya? “,upande wa pili wa simu ulipokea.



    “,Njoeni mtuokoe, tumekamatwa,tumebahatisha simu tuwapatie taarifa, “Chuma cha pua aliongea.



    “,Hao mbwa wanajiamini nini, ndani ya nusu saa ijayo vijana watakuja kuwakomboa, “upande wa pili wa simu uliongea, simu ikakatwa, Philipo akachukua kompyuta yake, akaunganisha na simu ambayo imetumika,akabonyeza bonyeza, kisha akatoa jibu.



    “,simu imepigwa kutoka katika ndege yao, iko futi sitini angani, tayali nimedukua (hack)  mifumo yao ya mawasiliano,tuwafuateni huko huko,nyie maboya mmefeli ,hawatatambua mahali mlipo tena……”,Philipo aliongea,akatoka nje,yeye na wenzake,wakaondoka zao.



    “,Shiit,roho yangu ilisita,sijui ilikuaje mpaka tukaingia mtegoni…”,magaidi walibaki wanalalamika,hakuna akiyewasikia,chumba chao kilifungwa kwa kufuli kubwa,huku wao wakiwa wamefungwa katika viti maalumu,miguu na mikono.



    Mkuu wa kitengo cha mawasiliano, katika kundi la D47,alipokea taarifa iliyomshitua sana,baada ya sekunde tu simu ikakatwa, ghafla mifumo yote ya mawasiliano ikazima.



    “,Banard kuna nini?, “mmoja wa magaidi alimuuliza Bernard, mkuu na mtaalamu wa mitambo ya mawasiliano katika meli ya magaidi wa D47.



    “,Wenzetu wanne ,kitengo cha Dar es salaam, Tanzania wamekamatwa! inatakiwa wakombolewe kabla hawajauawa, lakini ghafla simu imekatwa,nilipojaribu kutafuta mahali ilipotokea, mifumo yote imezima ……”,Benard aliongea.



    “,Ina maana mifumo yetu ya ulinzi imedukuliwa? “,mmoja kati ya magaidi, chumba cha mawasiliano aliuliza.



    “,Itakua hivyo, kampatie taarifa bosi haraka sana! “,Benard aliongea, akajaribu kurekebisha mitambo ikagoma, kompyuta zote zilikuwa zimezima. Ndani ya dakika tano tu, bilionea Paresh Kumar alifika katika ofisi hii, akiwa ameongozana na Donald Mbeto.



    “,Bosi nimepokea taarifa, wenzetu wa Dar es salaam wamekamatwa! nilipojaribu kutaka kujua eneo walilopo, kompyuta zote zikazima, mifumo yetu imedukuliwa, ndiyo narekebisha, mpaka turudi hewani, saa moja litakua limepita tayali! “,Benard alitoa maelezo kwa bosi wake.



    “,Sawa, weka mambo sawa, kisha fanya utundu wako tujue eneo walilopo,tutume vijana waende kuwakomboa! “,Paresh Kumar aliongea, Benard akatikisa kichwa, aliyaelewa maelekezo aliyopewa, akaanza kutekeleza kama alivyoelekezwa. Paresh Kumar akaondoka zake, akiwa pamoja na rafiki yake kipenzi, kijana wake wa kazi, jini mweupe au Donald Mbeto.



    …………………………………



    Kamanda Kendrick, Catherine, pamoja na Philipo walikuwa katika mavazi yaleyale ya kazi,usoni walivalia miwani yao ya mionzi,bastola zao zilikuwa kiunoni. Helikopta ya kivita iliiacha ardhi ya jiji la Dar es salaam saa tano kamili asubuhi, siku ya jumamosi.



    “,ndege yao iko futi sitini juu,upande wa kaskazini,tunapaswa kuingia ndani ya ndege yao kabla mifumo yao ya mawasiliano  haijawa activated ndani ya saa moja!”,kamanda Philipo alitoa maelekezo,akaeleweka,rubani akaendelea kutimiza majukumu yake.Makamanda watatu walijiandaa,walikuwa tayali kwa lolote lile,Catherine alikuwa bize akichukua silaha za kumfaa,silaha moja baada nyingine,katika sanduku kubwa ambalo walilipakia katika ndege,silaha za kila aina,silaha kubwa na ndogo.



    “,Mabomu haya yatanifaa,visu hivi vitanifaa kufyeka shingo zao,bunduki kubwaa sitaki,bastola yangu inanitosha……”,Catherine aliongea,alikuwa amekamilika.



    “,Mimi sichukui chochote kile,kisu changu,bastola yangu,pamoja na miwani yetu ya mionzi inatosha,……”,Kendrick aliongea,akatazama saa yake,ilikua saa tano na dakika kumi na tano,walikuwa wamekalibia,mahali ndege ya magaidi ilipoweka kambi angani.



    “,Haloo,haloo ovaa,usawa wa ndege,usawa wa ndege mnatupata ovaa!”,simu ya mkonga ilisikika,upande wa pili wa simu uliongea.



    “,tunawapata,tunawapata ovaa!”,rubani alizungumza.



    “,Mmekalibia,angalieni mbele yenu,kazi ianze mara moja…”,kitengo cha mawasiliano cha jeshi walifatilia kila hatua za ndege yao,hawakutaka ishambuliwe kwa mara nyingine tena.Wakampatia maelekezo rubani wa ndege yao,kisha simu ikakatwa.



    “,Tumefika,nazani ndiyo ndege hiyo kubwa mnayoiona mbelee yenuu……”,rubani aliongea,huku akishangaa,hakuwahi kuona ndege kubwa na ya ajabu kiasi kile.



    “,Whaaat!ndege nzuri sana na kubwaa,Kendrick,tusitumie milipuko yoyote,tunapaswa kuilinda iwe salama,tukishinda vita hii,ndege itaifishwe iwe mali ya serikali ……”,Catherine aliongea, alishangazwa na ndege iliyonekana mbele yao.



    “,Kweli kabisa, wazo zuri sana, ina maana hii ndiyo ilitushambulia? “,Philipo aliongea, akauliza swali, macho yake yalitazama mita mia mbili mbele yake, helikopta yao ikasogea karibu kabisa na ndege hii, ili wapate nafasi ya kuikamata kwa mikono sehemu yoyote ile, waweze kuingia ndani.



    “,Ndiyo hii, kazi ianze mara moja! “,Kendrick aliongea kwa kifupi, akakamata bawa la ndege ya maadui wakapanda juu yake, alilikamatilia bawa kwa nguvu, akishindana na upepo mkali. Wenzake wakafanya kama yeye, wote wakakamatilia bawa la ndege ya magaidi wakaanza kuisogelea taratibu, upepo mkali ukivuma, lakini walikua imara, hawakutikisika, miwani ya mionzi ilifanya kazi yake ipasavyo, ikawakinga na upepo mkali machoni.



    “,tumia emergency exit! kioo hicho hapo mbele, kisogeze chini juu, tuingie wote haraka sana kabla upepo haujaingia ndani ya ndege na kutuzidi nguvu …”,kamanda Philipo alitoa maelekezo,Kamanda Kendrick akafanya kama alivyoelekezwa, dirisha likafunguka, akaingia ndani, Catherine akafuatia, Philipo akawa wa mwisho, akarudisha kioo cha dirisha mahala pake, wote wakatokea ndani ya chumba cha choo.Huku ndege ikitikisika kwa sekunde kadhaa kisha ikarudi mahala pake.



    …………………………………



    “,Mbona ndege imetikisika kiasi hiki, ina maana kuna sehemu ya ndege yetu iko wazii, au tumevamiwa? “,rubani wa ndege hii ya magaidi alizungumza, machale yakamcheza,akamtuma msaidizi wake,kepteni ambaye alifanya kazi ya kuongoza ndege hii inaposafiri kama meli baharini, alikuwa na wasiwasi uliopitiliza.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Mwambie bosi,walinzi wakague kila sehemu, ulinzi uimalishwe, kila mtu achukue pozisheni yake,dirisha la dharula bila shaka lilikuwa wazi”rubani wa magaidi aliongea.



    “,Sawa, hata mimi nimewaza jambo hilo! “,kepteni wa magaidi aliongea, akatoka chumba cha kuongoza ndege hii ya D47paraquaat, akaondoka zake.



    …………………………………



    “,bosi, bosi! “,kepteni alifika katika ofisi ya Paresh Kumar, bosi akashtuka, alikuwa ananyonyana ndimi na wanawake zake wa kizungu, wakakurupuka, walishtukizwa.



    “,Mbona unaingia ofisi ya bosi wako bila taarifa, kuna tatizo gani? “,Paresh Kumar alifoka kwa hasira.



    “,Bosi, dirisha la dharula lilifunguliwa muda mfupi uliopita, kisha likafungwa tena, hatujui kama aliyefanya hivyo ni mtu wetu au adui yetu, nimetumwa kuleta ripoti, ulinzi unapaswa kuimalishwa “,kepteni aliongea,maneno yakapenya vizuri katika kichwa chake, akawasukumia mbali wanawake zake, akafunga vifungo vya shati lake, akaondoka zake, akawaacha wanawake zake wa kizungu wakiwa na hasira, mmoja alikuwa na sindilia, mwingne alikuwa amebaki na bikini yake, ofisi ya Paresh Kumar ilikua zaidi ya kasino,uovu mwingi ulifanyika masaa yote. Akatoka nje ya ofisi yake, uso kwa uso na Donald Mbeto.



    “,Kila mtu achukue pozisheni yake, hakikisheni aliyeingia ndani ya ngome yetu hatoki salama, maraisi wao waliowatuma, watajuta!!nitafanya mauaji mpaka nikabidhiwe migodi ninayohitaji, haiwezekani waingie madarakani kwa msaada wangu harafu waninyime ninachohitaji, walizani pesa zangu za kampeni ninawapa bure, kijani wangu utaendelea kufanya mauaji mpaka niseme basi, haya ondoka mara moja,kafanye kama nilivyokuagiza! “,Donald Mbeto alipokea maelezo kutoka kwa bosi wake, akaanza kazi, bosi wake alikuwa amekasirika, kengele ya hatari ikapigwa.



    “,danger! danger! everyone should take his position (hatari! hatari!, kila mtu achukue nafasi yake…) ,Donald Mbeto maarufu kama jini mweupe alipiga kelele, magaidi wakakimbia huku na kule, kila mmoja akikamata silaha inayomfaa kwa mapambano.



    Catherine, Kendrick pamoja na Philipo, walichungulia kupitia matundu madogo, katikati ya mlango, hawakuona mtu yoyote yule,Wote wakiwa na miwani yao ya mionzi mikali yenye lenzi, wakakitazama kitasa cha mlango kwa sekunde mbili, kitasa kikayeyushwa na mionzi mikali kutoka kwenye miwani, kitasa kikayeyuka,mlango ukafunguka. Wakatoka nje, uso kwa uso na bunduki nane, kulia na kushoto, mbele yao, kote kulikuwa na bunduki, waliwekwa chini ya ulinzi na magaidi waliovalia suti za bluu, zenye nembo ya D47.



    “,Tumewakamata! hahaaa, tuwapeleke kwa bosi! “,magaidi yale yalicheka, the super three soldiers hawakuongea kitu chochote kile, walizitazama bunduki walizowekewa kichwani, sekunde mbili tu, bunduki za magaidi wale zilipigwa na mionzi kutoka kwenye miwani, bunduki zikayeyuka,zikawa kama uji.



    “,What! nini hiki, maajabu haya! “,magaidi wale walishangaa,kitendo cha bunduki zao kuyeyuka kiliwashangaza sana, wakasahau kama walikuwa wamewaweka watu chini ya ulinzi.



    “,Vuuuup, vuuuup, vuuup …”,Kendrick alipiga ngumi tatu, zikawapata magaidi watatu kichwani,wakadondoka chini, Catherine akaluka mateke mawili, magaidi wawili wakandoka chini, wakabaki wawili, wakiwa wamesimama, walikuwa hawajielewi, kitendo cha bunduki zao kuyeyuka mbele yao walikiona cha ajabu sana, wakawa kama vichaa, wakataka kukimbia, Kamanda Philipo alichomoa visu viwili, akavirusha, vikawapata mguuni, wakadondoka chini.



    “,Yala…aaa, mmetuumiza washenzii nyie ……”,magaidi yale yalitukana,lakini haikubadirisha kitu chochote kile, Kendrick, Catherine pamoja na Philipo walichomoa bastola zao wakayanyoshea magaidi yale.



    “„Nyote ingieni humo chooni haraka sana, nasema ingieeni! “,Kendrick aliyakalipia, magaidi sita yakiwa yameweka mikono kichwani yakaingia, kamanda Philipo akayaburuta magaidi ambayo yalichomwa na visu mguuni, yalikuw hayawezi kutembea, wote wakawekwa chooni.



    “,Catherine akachomoa bomu lake dogo, akachomoa pini, akalitupilia ndani ya chumba cha choo.



    “,Puuuuuu, puuuuuu! “,mlipuko ukasikika, ndege ikatikisika tena, kisha ikarudi katika hali yake ya kawaida, Kendrick na wenzake walilukia upande wa pili, wakalala chini, hawakujeluhiwa popote pale.



    “,Umefanya nini, tulikubaliana vipi? situlisema hakuna kutumia milipuko …”,Kendrick alilamika.



    “,Haina jinsi, hiyo ndiyo mbinu ya kuwaua kwa urahisi, muda mfupi ujao, wote watafika eneo hili, utaona watakavyo kufa,”Catherine aliongea, akachomoa mabomu yake mawili madogo, akayaseti yalipuke ndani ya dakika tano, wote wakatembea harakaharaka, mpaka mahali kulipokuwa na magari pamoja na ndege za kivita nyingi sana.



    “,Waooooh! “,Philipo hakusita kuonesha furaha  yake,alitazama ndege,magari pamoja na vifalu vya kivita,ghafla kundi kubwa la magaidi lilisikika,wakija mahali kuliposikika mlipuko,Catherine na kundi lake wakaingia chini ya magari,wakajificha,hawakuonekana,magaidi yakapita bila kukagua kona zote,lilikuwa kundi la magaidi takribani mia moja.



    “,Hawa wehu,wametuchokoza,wameua wenzetu,mimi ndiye Donald Mbeto mwenyewe,nasema hivi,hawatoki salama mahali hapa……”,Donald Mbeto aliongea,alikuwa hana silaha yoyote ile mkononi,tofauti na wenzake ambao kila mmoja alikuwa ameshika bunduki yake.Alizigeuza geuza maiti za wenzao,moshi ukiwa unaishia na kubaki kweupe,mlipuko huu haukuhalibu ndege hii,bali iliwasambaratisha vipande vipande magaidi nane.



    “,Kuna mabomu!kuna mtego”,Donald Mbeto aliongea,akaluka serekasi,akatua upande wa pili,akalala chini.



    “,Puuuuu,puuuuu,puuuu,”mlipuko ulisikika tena,mabomu ambayo Catherine aliyatega,akayaweka chini ya maiti,yalililipuka,magaidi mia moja ambao waliongozwa na Donald Mbeto walijeruhiwa vibaya sana,wengine wakafa palepale.Isipokuwa Donald Mbeto ambaye hakujeruhiwa mahali popote pale.Akanyenyuka ,vijana wake walikuwa wameumia vibaya,wengine walivunjika shingo,miguu na wengine walikatika viuno.



    “,Huo ni uzembe katika kazi,hunifaaii……”,Donald Mbeto aliongea,akammalizia gaidi mwenzake ambaye alivunjika miguu yote miwili,lakini alikuwa bado mzima,akilia na kuhitaji msaada.



    “,Twendeni,twendeni tukaone,watakua wamekufa!,huo mlipuko sio wa kawaida…”,Philipo alitoa wazo lake.



    “,Hapana,tusiende,wenzao najua watasogea tena,tusubili kidogo…”,Kendrick akakataa,akatoa sababu,wote wakakubaliana naye.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Jitokezeni,mbona mnajificha,kama nyie ni mashujaa kweli jitokezeni!”,sauti ilisikika,Donald Mbeto alipiga kelele,akafoka kwa hasira.



    “,Hajafa,unamsikia anavyotukana,muda ukifika tutajitokeza,asiwe na shaka……”,Catherine alizungumza,mkono wake wa kulia alikuwa ameshika bastola mkono wa kushoto ulishika mabomu mawili.Aliona ndio silaha pekee ya kuua watu wengi kwa muda mfupi tu.



    Ghafla sauti za watu kukimbia zilisikika,wote wakageuza shingo zao,wakatazama mahali sauti za vishindo zilikuwa zinatokea,jeshi kubwa lilikiongozwa na mwanaume wa kihindi lilisogea mahali mlipuko ulikuwa umetokea,mikononi walishika bunduki zao,walijiamini sana.



    “,Kendrick tunafanya nini!”,Catherine aliomba ushauri kwa Kendrick,huku akifikilia mbinu ya kufanya.



    “,Wote hawajui mahali tulipo,pembeni yetu kuna ndege nyingi kubwa,ndege zenye makombola,tukipanda ndege moja,shambulio moja tu tunawatekeza woteee!”,kamanda Philipo alitoa mawazo yake.



    “,Wazo zuri sana,lakini vipi kuhusu mtuhumiwa wetu,tunapaswa kuondoka na Donald Mbeto kutoka mahali hapa,lazima akaonje joto la jiwe,asife kirahisi tu,anapaswa kufa kama alivyotesa raia wasio na hatia…”,Kendrick aliongea.



    “,Nimewapata hilo niachieni mimi,pandeni ndani ya ndege,lakini msifanye chochote mpaka niwajulishe……”,Catherine alizungumza,kamanda Kendrick aliangalia kushoto na kulia,hakuna aliyewaona,akaingia ndani ya ndege ya kivita,kamanda Philipo akafuatia,wakasubili amri kutoka kwa Catherine,Catherine alipita chini ya magari,hakuonekana,jeshi la magaidi liliendelea kusogea mahali mlipuko ulikuwa umesikika,akarusha mabomu mawili,katikati ya miguu ya magaidi,kisha akarudi ,akipenyeza chini ya uvungu wa mataili ya gari pamoja na ndege.



    “,Ukisikia mlipuko,washeni ndege,watakua bize na kujihami,nyie mtatumia upenyo huo kuwasogelea na kuwashambulia,hakikisheni mtu yoyote hapati upenyo kusogelea eneo hili,akaingia ndani ya vifaru,mtakua mmekwisha…”,Catherine aliongea.



    “,Puuuu,puuu,puuuu,”mlipuko ukasikika,magaidi wengi wakafyekelewa mbali,bilionea Paresh Kumar alikufa palepale,magaidi wengine walizitupa silaha zao,wakalala chini kuepuka mlipuko huu,Kendrick akatumia mwanya huu,akawasha helikopta kubwa ya kivita,kamanda Philipo akachomoa makombola,yakatokeza pembe zote,mbele makombola mawili,nyuma makombola mawili,wakaanza kupaa hewani,ndani ya ndege hii kubwa yenye vioo kwa juu,kiasi kwamba anga lote lilionekana,ndege ya magaidi ikitaka kujigeuza umbo la meli,vioo ambavyo vimeifunika ndege vinajifunua,mabawa yanarudi kwa ndani.



    Kendrick alipaa,hakutaka kupaa juu zaidi,angegonga vioo ,upepo ukaingia ndani ya ndege kubwa ya magaidi,akahatarisha maisha yao,alipofika usawa wa kufanya mashambulizi,futi kumi kwenda juu,akaisogeza helikopta eneo la magaidi,akafyatua makombola mawili,yakatekeza kundi lotee.



    “,Bosiiiiiii ,bosiiii!”,Donald Mbeto alishuhudia kitendo cha bosi wake kushambuliwa,akakimbia mpaka eneo la tukio,kila kiungo cha bosi wake kilikuwa mahali pake,akakasirika.



    Catherine alitabasamu,ushindi ulikuwa umekalibia,akaanza kusogea taratibu,kwa mara ya kwanza alikutana uso kwa uso na Donald Mbeto.Catherine alitazama juu,Kendrick alikuwa ameelekeza makombola kwa Donald Mbeto,alitaka kummalizia palepale.



    “,Hapana,usimuue,nataka nimvunje miguu,mimi mwenyewe!”,Catherine aliongea kwa sauti,akawakataza wasimuue,kisha akakunja ngumi,Donald Mbeto akazifunga rasta zake nyeupe,akajikuna kidevu chake,akakunja ngumi.



    11:40am



          Donald Mbeto alimtazama Catherine juu mpaka chini,akamtazama usoni, kisha akaitazama miguu yake,alikuwa anafikilia mbinu ya kumshambulia, aivunje miguu yake. Donald Mbeto aliluka mateke mawili hewani, Catherine akazuia mateke yote kwa mikono yake,hajakaa sawa alipigwa ngwala akadondoka chini, Donald Mbeto akaluka hewani, akarudi chini kwa kasi akiwa amekunja kifuti cha mkono wake, akafika juu ya mguu wa Catherine, akaupiga na kifuti.



    “,Kachwaaaaa!!, “mguu wa Catherine uliitikia.



    “,Yalaa…aa! “,Catherine alipiga kelele, akajigeuza upande wa pili, akampiga Donald Mbeto na teke usoni, akadondokea upande wa pili, damu zikimvuja mapuani.



    “,Shiiit! amemuumiza, atamuua, tushuke chini



    ……”,Kendrick akiwa juu ya helikopta, aliona kila kitu kilichokuwa kinaendelea,hisia za mapenzi zikamsumbua, alikuwa na hofu ya kumpoteza Catherine.



    “,Usiwe na hofu, naona sasa mapenzi yameshakuingia, umeshapenda tayali ,usjali Catherine ni komandoo……”,kamanda Philipo alimuondoa shaka Kendrick.



    “,Hapana, mwanamke ni mwanamke siku zote, isitoshe mtu anayepambana naye ni hatari sana,ameshamtemgua mguu ……”,kamanda Kendrick aliongea.



    Catherine alijaribu kusimama,alishindwa,mguu wake wa kushoto ulikuwa na maumivu makali, aliteguliwa, alimanusura avunjwe mguu, akajaribu kusimama tena, akadondoka chini, mguu wake ulimuuma sana, alikuwa hananguvu kabisa.



    “,Lazima ufe,huwezi kutoka salama, huwezi kumuuwa bosi wangu halafu uwe salama,mimi ndiyo jini mweupe,shujaa wa dunia”Donald Mbeto aliongea, akazishika rasta zake nyeup, akazifunga vizuri, akajikuna kidevu chake, akaanza kumsogelea Catherine aweze kummalizia.



    Catherine alimuona Donald Mbeto akimsogelea, alimuangalia usoni, akayatazama macho yake kwa makini, akazitambua hisia zake, alikuwa anakuja kumshambulia, Catherine akajiandaa, japo alishindwa kusimama, lakini alijiamini, Donald Mbeto alipofika mahali Catherine alipokuwa, aliluka tena juu, akashuka chini kwa kasi na pigo lile lile, alitaka kuvunja mguu mwingine wa Catherine, Catherine alinyanyuka juu kama mzuka, akaluka hewani,mkononi alishika kisu chake, wote wakakutana hewani, alilipangua teke la Donald Mbeto akamsindikiza na visu viwili, alichoma visu viwili Donald Mbeto miguu yote ,kulia na kushoto,haikutosha, akampiga na teke, akadondokea mita kadhaa kama mzigo. Donald Mbeto akalia kwa uchungu,hakuwa na uwezo wa kusimama tena.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “,Haya sasa, wote viwete! “,Catherine aliongea,akatazama helikopta juu yake, akawanyoshea mkono Kendrick na Philipo, wakaishusha helikopta,Kendrick akachomoa pingu, akamfunga Donald Mbeto, wakamnyenyua na kumuweka kwenye helikopta,Kendrick akaipaisha juu, ikapasua vioo vya ndege kubwa ya magaidi hawa,ikatokomea hewani.



    “,Bado kuna magaidi, wamejificha, lipua ndege yoteee! “,Kendrick aliongea,kamanda Philipo akafanya kama alivyoelekezwa, akaruhusu makombola mawili, yakaipiga ndege, ikapepesuka, ikapoteza mwelekeo, akaipiga tena na makombola mengine mawili, ikalipuka na kuungua moto, Kendrick akageuza helikopta, akaanza kurudi kusini,kisha akakunja tena kona, akaelekea mashariki, akaanza kuishusha chini helikopta, futi arobaini mpaka therathini,akaanza kurudi Dar es salaam,Tanzania



    …………………………………



    Chumba cha mateso :2:20



            Magaidi wanne walisubili waweze kukombolewa,muda ukazidi kwenda, hakuna chochote kile kiliweza kutokea.



    “,Tujikomboe sisi wenyewe, bila hivyo tutakufa, kifo chetu ni kunyongwa, hakuna hukumu nyingine tofauti na hiyo ambayo tunaweza kupewa …”,chuma cha pua aliongea.



    “,Kweli kabisa, lakini gereza hili lina ulinzi mkali, hatuwezi kutoka kirahisi kama unavyofikilia ……”,gaidi D47 namba sitini aliongea.



    “,Ngoja niwaoneshe,askari atakaye tuletea chakula, akitufungua tu mahali hapa,mimi naan.……”,chuma cha pua kabla hajamaliza kuongea,Catherine, Kendrick pamoja na Philipo walitokeza, Kendrick alikuwa anamburuta mtu hatari sana ambaye hawakutegemea kama angeweza kukamatwa.



    “,Donald, wamekukamata! “,magaidi walishangaa, wakanyongonyea,nguvu zikawaishia.



    “,Mliyekuwa mnategemea atakuja kuwakomboa huyu hapa, huu ndiyo mwisho wenu, chombo chenu tumekilipua,hakuna aliyetoka mzima zaidi ya huyu mtuhumiwa wetu, tunataka afe mbele ya raia ……”,Catherine aliongea, akiwa anatembea kwa kuchechemea, akamnyenyua Donald Mbeto, akamkalisha kwenye kiti cha mateso kilichokuwa wazi, wakamfunga mikono na miguu.



    “,Hapa hamuwezi kutoroka kamwe! hata mfanye nini hamtaweza, subilini hukumu yenu ya kunyongwa hapohapo kwenye viti vyenu ……”,Kendrick aliongea,akamshika mkono Catherine, akambusu, akamsaidia kutoka ndani ya chumba cha mateso, walikuwa wamekamilisha kazi, kama ilivyotakiwa.

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Taarifa za kukamatwa kwa Donald Mbeto zikasambaa duniani kote,waandishi wa habari kutoka mataifa mbalimbali duniani walifika nchini Tanzania, walitaka kufanya mahojiano na Donald Mbeto, wampige picha na kuitambua sura yake,hawakutaka kupitwa na taarifa za mtu huyu,lakini ulinzi ulikuwa mkali,wengi walizuiliwa,vyombo vya habari kutoka Tanzania vikaifanya kazi hiyo.Huku hukumu ya magaidi hawa watano ikisubiliwa kwa hamu na watu wote duniani.



    …MWISHO…………………



    The super three soldiers walizawadiwa tuzo za heshima, kutoka mataifa yote ambayo Donald Mbeto maarufu kama jini mweupe alitekeleza mauaji ya sumu, Kendrick na Catherine wakafunga ndoa, huku kamanda philipo akiwa Mc wa ndoa yao.…







    JINI MWEUPE - 4

     









      Simulizi : Jini Mweupe

      Sehemu Ya Nne (4)





      Kisiwa cha Comoro :



           Kendrick aliyafumbua macho yake,akapapasa mikono yake huku na kule, akashika magome ya miti, akashtuka, akanyenyuka na kuketi, uso kwa uso na mzee mwenye umri sawa na marehemu baba yake, alipoyageuza macho yake upande wa pili, pembeni na mzee yule, alikutanisha macho yake na msichana mweupe,akiwa amevalia magome ya miti yaliyozuia sehemu zake za siri pamoja na matiti yake, macho yake yakashindwa kuvumilia,kope zake zikayaachia uhuru macho yake, yakatazama uzuri wa msichana huyu juu mpaka chini, akatabasamu, akamshukuru Mungu kwa uumbaji wake wa ajabu.



      “,Hapa ni wapi?,nyie ni akina nani? “,Kendrick aliuliza, akasimama, akaangaza huku na kule, aliona nyumba moja ya makuti iliyozungukwa na minazi mingi.



      “,Huu ni ufukwe wa kisiwa cha Komoro! “,mzee yule alimjibu Kendrick, akazidi kumpatia maswali mengi kichwani mwake yasiyokuwa na majibu.



      “,Nimefikaje hapa? “,Kendrick aliuliza tena.



      “,Nilikuokota baharini ukiogelea katikati ya bahari,nilikua navua samaki, nikasogeza mtumbwi wangu karibu nawe, ulikuwa umeishiwa nguvu, ukapoteza fahamu, kabla hujazama nilikuokoa na kukuweka katika mtumbwi wangu, nikakuleta mpaka hapa, naitwa mzee Fedinand, huyu ni binti yangu, anaitwa Upendo ………”,mzee yule alimaliza kumwelezea Kendrick, akajitambulisha, akamtambulisha na binti yake wa kike, wote wakatabasamu, walifurahi sana kukutana na mswahili mwenzao kwa takribani miaka kumi sasa, wakiishi peke yao ufukweni, wakivua samaki, kula matunda na kuwinda wanyama.



      “,Kabla sijajitambulisha,kwanini mko hapa, makazi haya yanaonekana yako mbali na binadamu, hamuogopi kuishi peke yenu?, hamuogopi maharamia, vipi kuhusu wanyama wakali, hamuwaogopi? “,Kendrick aliongea kwa mshangao, macho yake yakiangaza umbali wa mita kadhaa mbele yake, akaona bahari, kushoto aliona msitu mkubwa wa minazi, akageuza shingo yake mkono wa kulia, aliona minazi mingi sana, nyuma yake vivyo hivyo, kulikuwa na msitu mkubwa wa minazi, akapigwa na butwaa!



      “,Huyu ni binti yangu, ana miaka ishirini na mbili kwa sasa, akiwa na miaka kumi na mbili, tulisafiri naye kwenda Zanzibar kwa mapumziko  mafupi, tukapata ajari na Mv Spice,tulifanikiwa kuwahi maboya mimi na mwanangu, nikaogelea naye, nikiwa nimemshika ipasavyo mpaka tukafika hapa, tumeishi naye mpaka leo hii, sijawahi kuona binadamu yoyote, leo ndio nimekuona wewe eneo hili ……”,mzee yule alitoa maelezo marefu, kamanda Kendrick akamuangalia machoni, macho ya mzee yule yalisema ukweli, hayakudanganya chochote kile, Kendrick akamuamini mzee yule.



      “,Naitwa kamanda Kendrick, askari mkuu wa kikundi cha upelelezi cha the super three soldiers kutoka Tanzania, tukiwa katika majukumu yetu, ndege yetu ililipuliwa na maharamia, mpaka sasa sijui wenzangu wako hai au wamekufa! “,kamanda Kendrick alijitambulisha,mzee Fedinand na binti yake wakatazamana, kisha wakamtazama tena Kendrick.



      “,Mzee, haukuona mtu yoyote eneo hilo la bahari tofauti na mimi? “,Kendrick aliuliza tena.



      “,Hapana, sikuona chochote kile! “,mzee yule aliongea, binti yake akanyenyuka, akaenda ndani ya kibanda cha makuti, akarejea tena, mkononi alishika samaki waliochomwa,wakiwa wamefungwa vizuri kwenye majani ya miti, akasogea karibu na Kendrick, akapiga magoti kwa heshima, akamnawisha, akampatia samaki, akaanza kula.



      “,Sasa itakuaje?, natamani sana mwanangu kurudi Tanzania, nazani nyumbani mke wangu na watoto wanne wanazani tumeshapoteza maisha, isitoshe kwa sasa wamekua, natamani sana kuwaona! “,mzee yule aliongea kwa hisia kali, akadondosha chozi, binti yake na yeye uvumilivu ulimshinda,akamfuta machozi baba yake, huku na yeye chozi likimtiririka.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Msijali ondoeni shaka, mko mikono salama, mshukuruni Mungu kuwalinda kwa miaka kumi,kama mko salama mpaka leo hii, basi hamtapatwa na kitu chochote kile katika mikono yangu ……”,Kendrick aliongea, akitafuna samaki wazima wazima, njaa aliyokuwa nayo haikuwa ya kawaida, akamaliza kutafuna samaki watano, akatosheka, akanawa, akaifutafuta saa yake, akaiwasha, ilikua imezima baada ya kuingiliwa na maji, ikawaka kwa mara nyingine tena, akatabasamu, ghafla tabasamu lake likatoweka, saa yake iliwaka taa mbili tu za kijani badala ya tatu,akajiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu, mmoja kati yao hakuwa salama.



      …………………………………



      Kisiwa cha Mafia :



              Kamanda Philipo alikasirika, kicheko cha kejeli kutoka kwa watu waliomsaidia ndicho kilichomkasilisha,akajitoa mikononi mwao kwa nguvu, akasimama.



      “,Asanteni kwa msaada wenu, niacheni niondokee! “,kamanda Philipo aliongea, akaondoka zake, nahodha na mabaharia waliokuwa wanamuhudumia wakabaki midomo wazi,wakaachana naye,wakaendelea na shughuli zao, huku wakijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu.



      “,Mimi niliwambia, ameshakua kichaa, kupona kifo baharini lazima uwe na kiwewe, ona sasa, yuko kama mwendawazimu! “,mmoja kati ya mabaharia wa mv Mafia aliongea, wote wakiwa makini kumsikiliza.



      “,Kweli kabisa, lakini asikuumize kichwa, achana naye, cha muhimu tumeshampatia msaada! “,baharia mwingine alizungumza, akatoa mawazo yake, wote wakaelekea kwenye majukumu yao.



      “,Mungu wangu wee! wote saa zao hazifanyi kazi,taa hata moja ya kwao  haiwaki, yes! imewaka, yes nyingine labda itawaka bado moja! “,Philipo aliongea kama kichaa, akiwa bize kuitazama saa yake mara tu baada ya kuiwasha, akaandika ujumbe kwa kupitia saa, akaituma, ili ajue wenzake wako mahali gani.



      “,Anyone online! Comrade Philipo, available in Mafia ……”,(Yoyote yule aliyeko hewani!, kamanda Philipo napatikana Mafia …”,)



      Alituma ujumbe kupitia saa yake, saa iliyounganishwa na saa za wenzake, akasimama kusubili majibu,wapita njia wakimshangaa kwa mavazi yake, mavazi ambayo yalikuwa maalumu kwa ajili ya kutekeleza misheni ambayo haikufanikiwa, misheni ya kuivamia meli ya D47.



      …………………………………



      “,Help me! Help me! nisaidieniii, nisaidieenii! “,kamanda Catherine alipiga kelele kuomba msaada, mikono yake ilichoka kuogelea, muda wowote angeweza kuzama,boti kubwa ikaanza kumsogelea, “Bakhresa “, ilisomeka, akaitambua, ilikua boti ya abiria kutoka Dar es salaam kwenda Zanzibar, mabaharia wawili wakajitupa ndani ya maji, wakampatia msaada, akaponea chupuchupu kufa maji.



      “,kulikoni kamanda, imekuaje? “,mabaharia wale walimuuliza swali Catherine, walimtambua, alikua maarufu sana jijini Dar es salaam yeye pamoja na kundi lake.



      “,Ndege yetu ilipata hitilafu, ikaanguka baharini, asanteni kwa msaada wenu! “,Catherine aliongea, akashukuru, akaiwasha saa yake, ajue kama wenzake wako hai au wamekufa, akatoa tabasamu zuri sana, saa iliwaka taa tatu za kijani,makamanda wote walikuwa wazima.



      “,Wenzako wako wapi, tuambie mlipoangukia tukawatafute, nyie ndio mnailinda nchi yetu, bila nyie sisi sio kitu! “,mabaharia wawili waliongea, huku abiria wakitikisa vichwa, walikubaliana na wazo hili, wakasubili majibu kutoka kwa Catherine.



      “,Msiwe na hofu, wote tayali ni wazima, asanteni kwa upendo wenu …”,Catherine aliongea,wakakubaliana naye, boti ikaendelea na safari ya kuelekea Dar es salaam Tanzania.



      “,Anyone online! Philipo available in Mafia …”,(Yoyote yule aliyeko hewani!, Philipo anapatikana Mafia …),meseji iliingia kwenye saa maalumu ya Catherine, akaisoma, akaandika ujumbe kujibu ujumbe ulioingia katika saa yake.



      “,Anyone online! Catherine is on the way to Dar es salaam, via mv Bakhresa …”,(Yoyote yule aliyeko hewani, Catherine yuko njiani anaelekea Dar es salaam Tanzania, kwa kutumia mv Bakhresa) “,alimaliza kuandika ujumbe mfupi, akatuma.



      ………………………………



      Kisiwa cha Comoro :



            Mzee Fedinand aliongoza njia, binti yake Upendo akafuatia, wakaongoza njia, kumtembeza Kendrick katika maeneo mbalimbali ya kisiwa hiki. Kendrick aliwaza mbali sana, alikua na hasira ya misheni kuharibika, isitoshe mwenzao mmoja saa yake ya mawasiliano haikuwa hewani.



      Ghafla ujumbe ukaingia, alikuwa ni Philipo, akausoma, Philipo alikuwa katika kisiwa cha Mafia, hofu ikazidi kumtanda, mtu aliyempenda, Catherine hakuwa hewani,ghafla taa nyingine ya saa yake ikawaka, taa zikawa tatu, wote walikua hai, ujumbe mwingine ukaingia katika saa yake, akaufungua, akausoma, Catherine alikua njiani anaelekea Tanzania, akafikiria, akajua nini cha kufanya, akaandika ujumbe.



      “,Kendrick is online, aim available in Comoro islands, Catherine just go to take helikopter, then come back to pick us ……”,(Kendrick yuko hewani, napatikana katika visiwa vya Komoro, Catherine nenda kachukue helikopta, kisha uje kutuchukua …”,)Kendrick alimaliza kuandika ujumbe, akautuma, moyo wake ukawa na amani.



      “,Hapa ndipo tunachukua minazi kwa ajili ya kutumia nyumbani. “,mzee Fedinand aliongea.



      “,Unasema? “,Kendrick hakuelewa, mawazo yake yalikua mbali, akauliza tena.



      “,Inaonekana hauko sawa, kuna tatizo lolote? “,mzee Fedinand aliuliza swali kwa Kendrick.



      “,Nilikua nashughulikia usafiri, muda wowote helikopta itakuja kutuchukua, kwa sasa niko ok kabisaa “,Kendrick aliongea, tabasamu zikaipamba sura ya mzee Fedinand pamoja na binti yake, wakamkumbatia Kendrick kwa furaha, hawakuamini kama muda mfupi ujao wangerejea tena Dar es salaam, baada ya kuishi miaka kumi katika kisiwa cha Komoro, Upendo akiwa binti mdogo, mpaka akawa mtu mzima.



      Makao makuu ya polisi :



             Catherine alichanganyikiwa, kituo cha polisi kitengo cha upelelezi kilikuwa kimevurugika, maiti nyingi zilitapakaa kila kona,watu wa huduma ya kwanza wakitimiza wajibu wao kubeba maiti na kuzipelekea mochwali, Catherine nguvu zilimuishia, akadondoka chini, akapiga magoti, alikuwa anatazama moja ya maiti iliypopigwa risasi nyingi sana tumboni, machozi yakamchuruzika kama maji bombani.



      “,D47 inatoshaa! nasema inatoshaa! mwisho wenu umekalibia,mmetuzidi ujanja lakini hamtatuzidi ujanja milele ……!Catherine alizungumza kwa uchungu, akaguswa begani, akageuka.



      “,Imekuaje! mlikuwa wapi mpaka tunaaibika kiasi hiki, shambulio hili limetuaibisha, lakini nimeshajua wakina nani wamefanya hivi…!”,kamanda Catherine alifoka kwa hasira, jasho jembamba likimtoka, mikono yake ilitetemeka, waziri wa ulinzi akaogopa,alizitambua hasira za Catherine.



      “,Askari wote leo wako bize na ulinzi,raisi ameingia bara, ana ziara huko kila mkoa,ndio maana ilikua rahisi kutekeleza shambulio hili,magaidi wameondoka na gari letu pamoja na sare za vijana wetu! “,waziri wa ulinzi aliongea,akajikuna kichwani, akaweka miwani yake vizuri, kisha akajiandaa kuzungumza kitu.



      “,wenzako wako wapi?, imekuaje ?,ndege yenu ilipotea kwenye rada zetu, tumeitafuta bila mafanikio, nikataka kutuma vijana waje kuwatafuta, ghafla nikapewa taarifa umerejea, nilikua njiani nakuja hapa, ghafla ndio tumekutana, hebu nieleze!! “,waziri wa ulinzi aliongea.



      “,Tulishambuliwa na magaidi, wengine nimewaponyoka,kundi limesambaratika, kila mtu yuko eneo lake, Philipo yuko Mafia, Kendrick yuko Komoro ,naomba muheshimiwa fanya jambo kwa ajili yao, tuma helikopta ikawachukue, ulinzi haujakaa vizuri kwa sasa ……” Catherine alitoa maelezo mafupi, akijifuta machozi kwa kutumia kitambaa chake.



      “,ok nafanya hivyo,helikopta itaenda kuwachukua nusu. saa kuanzia sasa, kabla jua halijazama, unachotakiwa kufanya, chunguza undani wa tukio hili, kisha nitumie taarifa ofisini kwangu …”,waziri wa ulinzi alizungumza, Catherine akatikisa kichwa, akapiga saluti,waziri akapanda kwenye gari lake, akaondoka zake,waandishi wa habari wakijitahidi kufanya mahojiano naye bila mafanikio, alikataa kuzungumzia chochote kile kuhusu tukio hili la kuvamiwa kwa kituo cha polisi kitengo cha upelelezi.



      …………………………………



      Helikopta ndogo yenye uwezo wa kubeba abiria sita, iliacha ardhi ya jeshi la anga,Dar es salaam,Tanzania, rubani wa helikopta alitimiza majukumu aliyoelekezwa,alipaswa kuwachukua makamanda wawili wa kitengo cha upelelezi, mmoja akiwa katika kisiwa cha Mafia, mwingine akiwa kisiwa cha Komoro.



      “,Usawa wa kisiwa, usawa wa kisiwa,unanipataa ovaaa! “,rubani wa helikopta alizungumza kupitia simu yake kubwa ya mkonga.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Halooo, halooo! ,oooh shiit! watakua hawana mawasiliano ya simu, hawapatikani hewani,”,aliendelea kuzungumza, akabonyeza tena simu yake ya mkonga, akaiunganisha na saa za kijeshi, saa za upelelezi.



      “,Haloo, halooo, niko Mafia, mko wapi ovaaa? “,aliuliza, akasubili jibu. Akiwa katika anga, usawa wa kisiwa cha Mafia.



      “,Niko Mafia, sogea bandarini, utaniona …”,sauti ilisikika upande wa pili.



      “,Nashuka sasa hivi,hakuna kupoteza hata sekunde, nimepewa nusu saa tu ya kuwachukua! “,rubani wa helikopta aliongea, akakata mawasiliano, akaiweka simu yake kwenye mifuko ya suti yake ya kijeshi. Baada ya dakika tano tu, alianza kuishusha ndege bandarini, ikatua juu ya meli moja, kamanda Philipo akaiona, akasogea karibu na meli hiyo, akaingia, moja kwa moja mpaka usawa wa helikopta, akapanda na kutokomea, wavuvi, mabaharia na abiria waliokuwa eneo hili la bandari wakabaki midomo wazi, wakijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu.



      “,tunaelekea Komoro, kumchukua Kendrick, kisha tutarudi tena Dar es salaam Tanzania …”,rubani yule aliongea, helikopta ikipaa juu futi sitini, ikakunja kona na kuelekea upande wa kusini,bahari ya hindi.



      …………………………………



      6;02pm



            Kamanda Kendrick alisubili helikopta kwa hamu sana, alikuwa na shauku kubwa ya kutaka kufika Dar es salaam,taarifa za kituo chao cha polisi kushambuliwa, askari wakauawa kinyama zilimshtua na kumsikitisha sana.



      “,Mbona hauna raha, nini tatizo Kendrick?, japo ni masaa kumi tu tumeweza kukutana, lakini nimetokea kukuzoea, unaonekana kijana mwenye huruma na hekima, sipendi uwe na majonzi ……”,mtoto wa mzee Fedinand aliongea, akamsogelea Kendrick, akakaa pembeni yake.



      “,Kuna taarifa mbaya kutoka serikalini, lakini usjali ni majukumu tu ya kikazi ……”,Kendrick aliongea, hakutaka kueleza kile ambacho kilikua kinamsumbua, akaficha,hakupaswa kumwamini mtu yoyote katika shughuli za kiserikali na kuziweka wazi.



      “,Papapapapapapapa! …”,muungurumo wa helikopta ulisikika, helikopta ndogo yenye rangi za kijeshi ilipita mita kadhaa usawa wa eneo lao, Kendrick akatazama juu, akaitambua ndege hii, ilikuwa helikopta ya Tanzania, akamshika mkono msichana wa mzee Fedinand.



      “,Twendeni wamekuja kutuchukua,baba, babaa, njoo twendee! “,Kendrick aliita, mzee Fedinand akatoka nje ya kibanda, mwilini akiwa amevaa magome ya miti, kwa miaka kumi sasa walitumia magome ya miti kama mavazi, nguo walizopotea nazo miaka kumi iliyopita walizivaa mpaka zikaisha. Hawakupata zingine, wakaamua watumie magome ya miti kusitiri miili yao.



      “,Philipo,!”,Kendrick aliita.



      “,Yes afande!”,philipo aliitikia,akamsogelea rafiki yake,wakakumbatiana.



      “,Hao ni wa kina nani,wanajua kiswahili?”,Philipo aliuliza.



      “,Yes wanajua,salimiana nao,mambo mengine tutazungumza baadae!”,Kendrick aliongea,akamsogelea mzee ambaye alikuwa amesimama sambamba na binti yake.



      “,Shikamoo mzee!”,Philipo alisalimia,akampatia mkono wa kulia,wakashikana kama salamu ya heshima.



      “,Marhaba!”,mzee yule aliitikia.



      “,Habari yako dada!”,alisalimia tena.



      “,Salama,asanteni sana kuja kutu……”,kabla Upendo hajamalizia kuongea, sauti ilisikika,sauti iliyomshitua na kumfanya ageuke haraka.



      “,Kamanda,tuondokeni!nilipewa nusu saa tu,nikichelewa nitaadhibiwa!”,rubani wa helikopta aliongea,Kendrick na Philipo wakamuelewa,walizitambua vizuri sana sheria za.kijeshi,wakajipakia ndani ya helikopta,helikopta ikapaa na kutokomea angani.



      …………………………………



      Bahari ya Hindi :6:30



               Mkuu wa kikundi cha magaidi wa D47,bilionea Paresh Kumar, alipata taarifa kutoka Tanzania,zilizidi kumfurahisha, akawa na furaha zilizopitiliza, tofauti na siku zote.



      “,Wale walikuwa askari wa Tanzania hatari wanaotutafuta kila siku, hasa Donald Mbeto ndiye muhusika mkuu,ndugu zetu kutoka Dar es salaam ndio wamenipatia taarifa hizi,wamemuua D47 namba mia moja, maana aligundulika kushirikiana na sisi, akapewa adhabu kama askari na kusema siri zetu zote, wameshambulia kituo cha polisi, wameua askari wote, ni shangwe na nderemo kwetu sisi, tunachopaswa kufanya ni kuwa makini, lazima watarudi kututafuta!! “,bilionea Paresh Kumar aliongea,mguu wake mmoja alikunja nne, kushoto aliketi mrembo wa kihindi, kulia aliketi mrembo wa kichina, wote walimpapasa na kumshika shika mwilini, alipenda sana wanawake, aliwateka kutoka pembe zote za dunia, akafuta kumbukumbu zao kichwani, wakamtumikia katika kundi lake katika shughuli mbalimbali.



      “,Kwa kuwa wameshajua eneo tulilopo,meli yetu ipae angani kama ndege, usawa wa mawingu, watahangaika kututafuta mpaka wanazeeka! “,Paresh Kumar alitoa amri, vijana wake wakaluka juu kwa shangwe, burudani zikaendelea, mziki ukapigwa, kila mtu akaendelea na starehe yake aliyoipenda, kufurahia ushindi, meli yao ikajigeuza, bawa likachomoza upande wa kulia, bawa lingine likachomoza upande wa kushoto, ikaanza kupaa hewani, ikaiacha bahari, haikuwa meli ya paraquat tena, bali ndege kubwa yenye uwezo wa ajabu.Makombola ya nyukilia yakachomoza kila upande wa ndege hii, kwa ajili ya ulinzi.



      Ofisi ya ukombozi: 7:00



             Catherine alianza upelelezi,aweze kuwapata washirika wa D47 waliofanya shambulio,akiwa anatafakari, akapata jibu, akaondoka haraka sana, kutoka katika kituo cha polisi kilichoshambuliwa, mpaka katika ofisi yao ya ukombozi, ndani ya jengo la China plaza, Kariakoo.



      “,This bastard kahusika! picha zake zisambazwe kila kona, tukimpata huyu, tutafahamu mengi ……”,Catherine aliongea, alimkumbuka raia wa kisomali waliyegongana vikumbo siku moja iliyopita,kijana aliyejaribu kufungua ofisi yao bila mafanikio na kuambulia kupigwa picha alipokosea neno siri la kufungulia mlango, Catherine akamkimbiza bila mafanikio, alitaka kumuhoji ajue nini alichotaka katika ofisi yao.



      “,Work done, kazi imekwisha,ngoja nikapige picha na eneo la tukio,ni attach kwenye picha yake,kisha nitume kwa waziri,vyombo vya habari viripoti taarifa hii…”,Catherine aliongea,akiitazama sura ya gaidi aliyetaka kuingia ndani ya ofisi yao siku moja iliyopita,akiwa ndani ya suti nyeusi,akiwa ameyavua mavazi yake ya kazi,akatoka nje ya ofisi ya ukombozi,akatokomea.



      …………………………………



      7:10pm



             Kendrick na Philipo walitaka kushushiwa katika eneo la tukio,mahali ambao kitengo chao cha cha upelelezi kilipatikana,kabla ya kushambuliwa,rubani wa helikopta akafanya hivyo,akashusha helikopta,ikatua ardhini na kuikanyaga ardhi ya Dar es salaam kwa mara nyingine tena,Kendrick akashuka,mkono wake wa kulia ulimshika Upendo,mtoto wa mzee Fedinand,Philipo akashuka,akiwa ameongozana na mzee Fedinand,uso kwa uso wakakutana na maiki nyingi za waandishi wa habari,wakitaka kuzungumza nao.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



      “,Naripoti kutoka ITV the super brand Afrika mashariki,naitwa Abdalah Said Abdulah,wewe kama mkuu wa kitengo hiki,unaweza kutueleza chochote kuhusu shambulio hili……”,mwandishi wa habari aliuliza,mwilini alivaa suti nyeusi iliyofiti mwili wake ipasavyo.



      “,Sijui chochote,ndiyo narejea baada ya helikopta yetu kupotea baharini,tukiwa katika majukumu yetu,lakini naahidi, tutawakamata watu hawa ndani masaa ishirini na nne yajayo!”,Kendrick aliongea,mwandishi wa habari akimtazama Upendo kuanzia chini hadi juu,alishangazwa sana na mavazi yake.



      “,Huyu naye umemtoa wapi?, amevaa mavazi tofauti na asili ya mtanzania,”mwandishi aliendelea kuhoji.



      “,Huyu anaitwa Upendo,baba yake anaitwa mzee Fedinad,walipotea na meli ya mv spice miaka kumi iliyopita,walifanikiwa kupona kifo cha maji,baada ya kuogelea mpaka pwani ya kisiwa cha Komoro, eneo lisilo na watu,wakaishi huko wakila matunda na samaki,wameniokoa mimi leo hii,pengine bila wao nisingekuwa hai,popote walipo ndugu zao,wafike nyumbani kwangu,mtoni kijichi,wakiulizia kamanda Kendrick,watafikishwa mpaka mlangoni…”,kamanda Kendrick alitoa maelezo,akamshika mkono Upendo,wakasogea kabisa eneo la tukio.



      “,Sasa,unaweza,ukaa……”,mwandishi yule alitaka kuendelea kuhoji,Kendrick alichoka mahojiano,akaondoka zake,akafika eneo la tukio,akatazama kila kona,damu zilikuwa zimeganda na kutapakaa eneo lote.



      “,Kendrick uko salama,na huyu ni nani?”,Catherine alifika,akauliza swali.



      “,Nitakueleza kila kitu,endelea kuchukua taarifa za upelelezi wa mwanzo,sisi tunaelekea nyumbani na kamanda Philipo,baada ya upelelezi,mpatie waziri majibu taarifa za upelelezi kama sheria zinavyosema, kisha fika haraka nyumbani kwangu,tuzungumze suala hili.”Kendrick aliongea,akatoa maelezo mafupi,wakaongozana na Philipo,pamoja na mzee Fedinand,wakapanda gari ya polisi, wakatokomea.



      …………………………………



      Kendrick aliishi nyumba moja na mama yake mzazi,kaka zake wawili walipoteza maishi kwa mshituko, waliposikia taarifa za meli ya mv spice kuzama, meli ikiwa imembeba baba yao ambaye alikuwa ni tegemeo kubwa katika familia yao,mama yao alichanganyikiwa,akaugua ugonjwa wa akili kutokana na kupata pigo kubwa kwa wakati mmoja, mme wake na mtoto wake wa mwisho, walipoteza maisha kwa ajari ya meli, watoto wake wakafa kwa mshituko wa moyo,mara baada ya kupokea taarifa za kifo cha baba yao, pamoja na mdogo wao.



      Kendrick akiwa kidato cha nne, aliamua kumpeleka mama yake hospitali kuu ya vichaa mkoani Dodoma, hospitali ya Mirembe. Akatibiwa, huku Kendrick akijiunga na jeshi la kujenga taifa, akamaliza mafunzo ya miezi sita, akajiunga na jeshi la polisi, kutokana na utendaji wake, akapandishwa cheo kila kukicha, huku mama yake akipona ugonjwa wake wa akili, akamrudisha nyumbani, wakaishi tena pamoja.Kendrick alifikili baba yake, pamoja na mdogo wake walikuwa wamepoteza maisha katika ajali ya mv spice,kumbe sivyo, Mungu aliwakutanisha tena pamoja.



      “,Baba Josephat! “,mama yake Kendrick alipigwa na butwaa,hakuwahi kuisahau sura ya mume wake hata siku moja, aliitambua vizuri sana,alipigwa na butwaa baada ya Kendrick kurudi nyumbani na wageni,mmoja kati ya wageni akiwa ni mume wake wa ndoa.



      “,Mamaaa Josephat, ni wewe?,nyumba yetu imebadilika! “,mzee Fedinand aliita kwa mshango, akamkimbilia mke wake, wakakumbatiana.



      “,Mbona sielewiii, ina maana, wewe ndiye baba yangu ……?”,Kendrick aliuliza swali kwa mshangao, chozi la furaha likaanza kumtoka.



      “,Ndiyo kendrick, huyu ndiye baba yako,sijui umemtoa wapi? “,mama yake Kendrick aliongea, machozi yakimtiririka.



      “,Mama Josephat, huyu ndiye mtoto wetu wa mwisho Jacline, huyu ndiye nilisafiri naye kwenda Zanzibar,”mzee Fedinand aliongea.



      “,Mamaaa! “,Upendo aliita.



      “,Mwanangu! “,mama Kendrick aliitika.



      “,Mamaaaa! “,Upendo akaita tena.



      “,Jamani mwananguuu …”,mama Kendrick akaita  tena, akamkimbilia mwanae, wakakumbatiana, kila mmoja akiona kama ndoto.



      “,Kendrick mwanangu, najua unajiuliza maswali mengi, mimi sio Fedinand, naitwa Steward, siwezi kukwambia ukweli katika hali kama ambayo umetukata nayo kule, tulikuwa hatujui wewe ni mtu mwema au mbaya kwetu, ndiyo maana nilikuficha majina yetu halisi, na huyo siyo Upendo, bali ni mdogo wako Jacline, wahenga walisema usimtendee mema binadamu unayemfahamu peke yake, leo hii nimekuokoa baharini, kumbe namuokoa mtoto wangu, Mungu katumia njia ya ajabu kutukutanisha. “,mzee Fedinand alitoa maelezo marefu, kumbe jina lake sio Fedinand, alidanganya,jina lake halisi aliitwa Steward, Kendrick akamsogelea baba yake na kumkumbatia, furaha ikazaliwa upya katika familia ya kamanda Kendrick.



      Kamanda Philipo alijifuta chozi ambalo lilikuwa linamdondoka, alishuhudia kila kitu,Catherine alikuwa amesimama mlangoni, alikuwa tayali ameshafika muda mrefu, akajikuta anasimama mlangoni kama sanamu, alishindwa kuendelea mbele, nguvu zilimuishia, historia ya kustaajabisha aliyoisikia ilimchanganya sana, hakuamini kama Kendrick alipitia mkasa wa kutisha kiasi hicho, hakuwahi kumweleza hata siku moja, alikua msiri sana.



      “,Catherine! umefika, kumbe uko hapa, karibu ndani, nilitaka nikueleze kuhusu kukutana na watu hawa,tujue namna ya kuwasaidia kuwapata ndugu zao, lakini kumbe tayali wameshafika nyumbani! “,Kendrick aliongea kwa furaha, Catherine akatabasamu, akasogea sebureni, akakaa kwenye sofa.



      “„Josephat na Yohana wako wapi?  ,au wameshaoa, wako na familia zao? “,mzee Steward, baba yake Kendrick aliuliza, mama yake Kendrick akanyongonyea, tabasamu ikatoweka usoni mwake, vivyo hivyo kwa Kendrick, akapoteza furaha kabisa, akapiga moyo konde, akajikaza kiume na kuongea ukweli.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Kwa sasa ni marehemu, tuliwazika siku moja tu baada ya kupokea taarifa za meli kuzama na abiria wote kupoteza maisha, walipatwa na mshituko, wakafa palepale, mama naye akachanganyikiwa, lakini namshukuru Mungu, mama alipatiwa matibabu, kwa sasa ni mzima ……”,Kendrick aliongea,baba yake akadondosha chozi, haikusaidia chochote kile,watoto wake walikuwa tayali wameshapoteza maisha, wasingerudi tena.



      “,Wapumzikee kwa amani wanangu! “,mzee Steward alizungumza, mke wake akamkumbatia, akambembeleza, akajikaza kiume, akajaribu kuificha huzuni yake lakini hakuweza, machozi yake yaliendelea kutoka, alihuzunika sana kuwapoteza watoto wake.



      Mbezi :8:02



               Magaidi wa D47,kanda ya Dar es salaam, walikuwa wameketi katika nyumba yao ya kifahari,chupa za bia zilikua mezani, walikunywa mpaka wakatapika,walikamilisha kazi kama walivyopanga, bosi wao akafurahishwa zaidi na kitendo hicho, akamuingizia kila mtu dola elfu moja kwenye akaunti yake. Akawapatia kazi nyingine kubwa, kuhakikisha wanawaua maaskari watatu wanaolifuatilia kundi lao.



      “,Kesho asubuhi na mapema tunaanza kazi, hawa watu lazima tuwauee, tusipo waua sisi, watatuua! “,D47 namba sitini alizungumza, wenzake watatu wakiwa. pembeni yake,kila mmoja alikuwa ameshika chupa ya bia mkononi.



      “,Kweli kabisa,mimi nina plani,nina mipango ambayo itaifanya kazi hii kuwa rahisi kabisa……”,gaidi mwembamba,mrefu,mweupe,alizungumza,akawatazama wenzake usoni.Wote wakaweka bia zao,wakatulia kusikiliza mbinu hiyo,walikuwa na shauku ya kupata pesa nyingi kama wakifanikiwa kuwaua wapelelezi watatu hatari wa kundi la the super three soldiers.



      “,Mbinu gani hiyo chuma cha puaa?”,gaidi mwingine aliuliza,mweusi,mfupi,kichwani alikua na kipara.



      “,Tuteke familia zao,hasa ya kiongozi wao wa kundi,lazima watajileta wenyewe,wote watatu,kutaka kuwakomboa,sisi tutaacha eneo hili likiwa limetegwa mabomu,wakifika eneo hili kukomboa ndugu zao,tunalilipua,wanakufa woteeee!”,gaidi yule aliyejulikana kwa jina la chuma cha pua aliongea,licha ya wembamba pamoja na urefu wake,alikuwa amekomaa kama chuma,ngumi yake ilikuwa na uwezo wa kupasua matofauli kumi ya bloko,aliwahi kumuua gaidi mwenzake,allimpiga na kichwa chake,akampasua fuvu la kichwa,wote wakiwa mazoezini,wakamubatiza jina hilo,mwili wake ulikomaa kwelikweli.



      ” ,Yeeeeeeh!,”waligonga chupa zao kwa furaha,walikubaliana na plani ya mwenzao,kilichobakia ni utekelezaji,wakanywa bia kwa fujo, wakalewa chakali,usingizi ukawachukua,wakalaliana kama mizigo,wakiwa hawajitambui.



      …………………………………



      Ofisi ya Ukombozi:9:00pm



      Makamanda watatu walikutana tena,mara baada ya kutoka nyumbani kwa kamanda Kendrick.Kila mmoja aliketi katika kiti chake,ndani ya ofisi ya ukombozi.



      “,Catherine nipe ripoti!”,Kendrick aliongea,akijizungusha zungusha kwenye kiti chake.



      “,Kila kitu kiko sawa,picha za mmoja kati ya magaidi anayetuhumiwa kuhusika na shambulio,zimefika katika vyombo vya habari,kesho asubuhi taarifa zitaenea na kutangazwa kila kona.”,Catherine alimaliza kutoa ripoti yake.



      “,Ok sawa,sasa nazani mnafahamu magaidi walipo,mahali tuliposhambuliwa,walitugundua mapema,meli yao ikajibadirisha kama nyambizi,ikawa rahisi kutushambulia,hivyo basi,kabla ya mapambano tuelewe,meli yao ni ulinzi tosha kwao,ina uwezo kujigeuza katika maumbo mbalimbali,ikawa kama meli,nyambizi au hata ndege ,ikapaa angani kama ndege zingine!”,Kendrick alitoa maelezo mafupi.



      “,Sasa Kendrick ,tunafanya nini hapa? ,tutumie mbinu gani?”,Catherine aliuliza.



      “,Nafahamu nini cha kufanya,nikipata uhakika wa eneo walilopo,iwe baharini au angani,nitaweza kudukua(kuhack) mifumo yote ya mawasiliano kwenye chombo chao,itakua rahisi kuwavamia,hawatatuona wakati wa kukivamia chombo chao.



      “,Sawa,naona tukiwakamata hawa magaidi walioko Dar es salaam,watatusaidia kujua wenzao wako wapi,itakua rahisi kufanya udukuzi!”,Catherine aliongea.



      “,Wazo zuri,tukutane hapa saa kumi na mbili asubuhi,tuanze kazi,kila mmoja awe makini kujilinda,kila tunapopiga hatua,maadui zetu wako nyuma,zingatieni suala hili……”,Kendrick alizungumza.



      “,Sawa afandee!”,wote waliitikia,wakapigiana saluti za heshima,kila mmoja akatoka nje, kuelekea nyumbani kwake kupumzika..



      …………………………………



      Hisia za kimapenzi ziliusumbua moyo wake, kadri siku zilivyozidi kwenda, Kendrick hakuonesha hisia zozote za mapenzi juu yake,uvumilivu ukamshinda kabisa, moyo wake ulichoka kuteseka na mapenzi,akafikiria, akapata wazo, wazo aliliona sahihi.…



      “,Kendrick,nimepoteza funguo za nyumba yangu, sijui hata nafanya nini, hotelini siyo salama, siwezi kulala kabisa ……”,Catherine alidanganya, akiwa pembeni ya gari lake, sura yake ilikuwa siliasi, haikuonesha hata chembe ya uongo, alijiamini kwa yale aliyoyazungumza.



      “,Kwa nini usije kulala nyumbani kwangu, kuna vyumba vya kutosha, kesho tutatafuta funguo zako au kuchongesha zinginee! “,Kendrick aliongea.



      “,Hapo utakua umenisaidia saanaa, lakini ujue sasa hivi familia yako imeongezeka, mzee wako, mama yako pamoja na mdogo wako, hawawezi kukufikilia vibaya,wakafikili umeleta mwanamke ndani? “,Catherine alifurahi plani yake kufanikiwa kama alivyo panga,akajifanya kama hakupanga jambo hilo, akaendelea kuuliza maswali ya uchokozi.



      “,Hapana,wewe ni rafiki yangu,tunafanya kazi pamoja, hawezi kuwaza chochote kile, japo mama yangu kila siku ananiuliza kuhusu suala la kuoa, mimi bado sijawa tayali, nitamlisha nini mie? “,Kendrick alimjibu Catherine, uso wake ukaachia tabasamu kwa mbali. .



      “,Hahaaa, “wote wakacheka, wakajipakia kwenye magari yao, nje ya jengo la ofisi ya ukombozi, wakatokomea, kamanda Philipo alikuwa tayali ameshaondoka zake dakika takribani kumi zilizopita.



      …………………………………



      Mtoni Kijichi :



             Catherine na Kendrick walifika nyumbani, mama yake Kendrick, baba yake, pamoja na mdogo wake Jacline walikuwa tayali wamelala.



      “,Tutaonana kesho,kalale chumba cha wageni, pita korido hii, chumba cha kwanza mkono wa kushoto! “,Kendrick aliongea, baada ya kumaliza kula, yeye pamoja na Catherine.Kendrick alinyanyuka, akataka kwenda kuchukua maji ya kunywa kwenye friji.



      “,Sawa nimekuelewa, mbona unasimama, unaenda wapi? “,Catherine aliuliza.



      “,Naenda kunywa maji “,Kendrick alijibu.



      “,Subili nikuletee! “,Catherine aliongea, akanyanyuka kwenye sofa, akaisogelea friji, akachukua chupa ya maji ndani ya friji, akamimina kwenye grasi. Akageuka nyuma, Kendrick alikuwa anasinzia sinzia, usingizi ulikuwa unamzidi nguvu, hakutambua chochote kile kilichokuwa kinaendelea, catherine akaingiza mkono ndani ya koti lake la suti, akachukua kidonge cha usingizi, vidonge ambavyo walivitumia katika oparesheni mbalimbali za kijeshi. Baada ya kuweka kidonge kile ndani ya maji, akatikisa vizuri kiweze kuyeyuka, kisha akampelekea Kendrick.



      “,Kendrick, Kendrick! “,Catherine aliita.



      “,Yeeees, nanambiee! “,Aliitika kwa kigugumizi, usingizi ulimzidi nguvu, isitoshe alichoka sana, tangu asubuhi alizunguka huku na kule bila kupumzika.



      “,Kunywa maji, haya hapa! “,Catherine aliongea, Kendrick akachukua glasi ya maji, akanywa maji yote,akaweka glasi mezani, ndani ya sekunde mbili tu, akalala fofo.



      “,Hahaaa, leo unalala na mimi, kila siku nikigusia suala la mapenzi unaona kama natania, sasa leo tunalala wote, kesho wakitukuta, lazima tufunge ndoa ya mkeka, unasema huoi askari kama wewe, sasa utaoa kwa lazima…”,Catherine alisahau vita kubwa mbele yao kwa muda mfupi tu, hisia za mapenzi zilikuwa zimemtawala, akamnyenyua Kendrick, akampeleka katika chumba cha wageni, chumba ambacho alielekezwa akalale, wote wakalala huko.



      Mtoni kijichi :7:30am



            Magaidi wanne wa kundi la D47,walipaki gari nyeusi aina Toyota Hallier, pembeni, nje ya jumba la kamanda Kendrick, jumba ambalo lilizungushiwa geti kubwa.



      “,Hapa ndipo nyumbani kwake,waliotuelekeza hawajadanganya, kama unavyo ona, kuna askari getini, anatimiza majukumu yake ya ulinzi



      ……”,gaidi D47 alioongea.



      “,’Nazani mwenyewe ameshaelekea ofisini,chuma cha pua, toka kaongee na mlinzi, fanya lolote tuweze kuingia ndani! “,gaidi D47 aliendelea kuongea.



      “,Sawa bosi”,chuma cha pua aliitikia, akatoka nje, akalisogelea geti,mpaka mahali alipokuwa amesimama mlinzi.



      “,Karibu muheshimiwa, sijui nikusaidie nini? “,askari mwenye kirungu mkononi aliuliza,akamkaribisha kwa heshima zote gaidi, kutokana na suti nyeusi ya heshima aliyokuwa amevaa.



      “,Nina mazungumzo na bosi wako, tulisoma naye, ni muda mrefu hatujaonana, naomba kuzungumza naye…”,gaidi aliyejulikana kwa jina la chuma cha pua aliongea,askari yule akaonekana kuyaamini maneno ya mgeni huyu.



      “,Japo bosi hayupo, ameshaenda kazini, unaitwa nani? “,askari yule aliuliza swali tena,huku akidanganya kuwa Kendrick hayupo, alielekezwa kusema hivyo kwa mtu yoyote asiyemfahamu.



      “,Acha maswali yako kijana, au nimpigie simu uongee naye, utamwaga unga sasa hivi …”,chuma cha pua aliongea, akaingiza mikono yake mfukoni, akatoa simu, akajifanya kama anataka kupiga, askari yule akaanza kutetemeka kwa hofu.



      “,basi baba! basii, yaishee, ingia ndani ,lakini bosi hayupo……,”askari yule aliongea,akadanganya, hakuna aliyemsikiliza, akafungua mlango, chuma cha pua aliangalia kulia, akaangalia tena kushoto, hakuona mtu yoyote yule, alimpiga kabali askari yule, akaivunja shingo yake, ulimi wa askari yule ukatokeza kwa nje, akafa palepale. Chuma cha pua akambeba, akamuweka kwenye buti la gari,walitaka mauaji yafanyike kimya kimya, asigundue mtu yoyote yule, baada ya kumfyekelea mbali, magaidi wote watatu wakatoka ndani ya gari, wakaingia ndani ya jengo la kamanda Kendrick, wakafunga geti kwa ndani, asije akaingia mtu yoyote yuke, akaharibu mipango yao.



      “,Kaka yuko wapi?”,Jacline aliuliza,akiwa anaandaa chai mezani.



      “,Yuko na wifi yako,nimeona viatu vya kike mlangoni tofauti na vyangu wala vyako,leo amechelewa kwenda kazini,muache apumzikee…”,mama yake Kendrick aliongea,huku akitabasamu.



      “,Jana walikula naye,nilichungulia sebureni,ni yule msichana wanayefanya naye kazi,ni mrembo kwakweli,nilipomtambua nikarudi kulala…”,baba yake Kendrick,mzee Steward aliongea.



      “,Hahaaaa……”,wote wakacheka,wakaendelea kunywa chai.



      “,Hapo hapo mlipo,asijitikise mtu yoyote,mkijitikisa tunawaua!……”,sauti ya kutisha ilisikika,walipogeuza shingo zao,wakatazama mlangoni,uso kwa uso na wanaume wanne wenye bastola mkononi,usoni walivaa miwani rangi nyeusi,rangi ambayo ilifanana na suti zao pamoja na mabuti yao meusi.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



      “,Nyie ni wakina nani?mnataka nini?”,mama yake Kendrick aliuliza swali.



      “,paaaaaaa!”,alichapwa kibao,akadondokea upande wa pili wa sofa.



      “,Mamaaaaaaa!”,Jacline alipiga kelele,hasira za mama yake kupigwa mbele yake zikampanda,akakosa cha kufanya.



      “,Kelele malaya wewe!”,Jackline alifokewa.Akazidi kukasirika.



      “,Malaya mwenyewe!”,Jackline hakuogopa chochote kile,akawatukana magaidi.wale,akamtemea makohozi usoni,gaidi ambaye alikuwa amemchapa kibao mama yake,huku akimwita Jackline malaya.



      “,Tunakubaka sote wanne sasa hivi,mbele ya baba yako,pamoja na mama yako,halafu tuone sisi na wewe nani malaya……”,chuma cha pua alizungumza,wakamfunga kamba mama yake Kendrick mkononi na miguuni,wakamfunga na baba yake.Wakajiandaa kumubaka Jackline,chuma.cha pua alianza kuifungua zipu yake.



      …………………………………



      Kamanda Catherine alikuwa amechoka sana,alilala na mtu aliyempenda kwa mara ya kwanza, lakini hakufanya naye chochote kile, alitaka kutimiza malengo yake, Kendrick aweze kufungishwa ndoa ya mkeka pamoja naye, watakapokutwa wamelala pamoja asubuhi. Usingizi hauna ndugu, alilala fofofo tofauti na siku zote, Kendrick ndiyo kabisaa, dawa ya usingizi aliyopatiwa usiku uliopita, iliendelea kutimiza majukumu yake, akauchapa usingizi bila hata kushtuka.



      Ghafla Catherine alikurupuka usingizi, mapigo ya moyo wake yalienda kasi sana,akageuka upande wa pili, akamgusa gusa Kendrick begani, hakushtuka! alikuwa bado amelala. Catherine akaitazama saa yake ya kijeshi, “8:00am”,saa yake ilisomeka.



      “,Saa mbili kamilii! “,aliongea peke yake kwa mshangao, akachukua viatu vyake, akavaa suti yake, akaziweka vizuri nywele zake, kwa mbali akasikia vitisho sebureni, akasikiliza kwa makini, mapigo ya moyo wake yakapiga kwa kasi sana,walikuwa wamevamiwa, akasogea kitandani, akampiga piga Kendrick aweze kushtuka,Kendrick hakushtuka, aliendelea kukoroma kama kawaida.



      “,Kendrick, Kendrick, tumevamiwa, najuta mimi! amka tukapambane! “,Catherine aliita, bila mafanikio,hakua na budi kuubeba mzigo yeye mwenyewe, bila hivyo chochote kile kingeweza kutokea, wazazi wa Kendrick wasije wakauawa, akalaumiwa,akakosa mume pamoja na kuharibu kazi yake.



      “,Kakaa, nabakwaa, kaka nabakwaaa, njooo unisaidiee ……”,Jackline alipiga kelele,kelele zikapenya katika matundu mawili ya masikio ya Catherine, akakasirika.



      “,Hahaaahaaa, hakuna atakayekuja kukusaidia, hahaa……”,magaidi yale yalizungumza, yakacheka kwa kejeli, Catherine akazidi kukasirika,alisikia kila kitu.



      “,nimelala kwa Kendrick, najua uko ofisini, njoo, tumevamiwa …”,Catherine alituma ujumbe kwa kamanda Philipo kupitia saa yake iliyotumika kama simu,akapiga mahesabu namna ya kuwavamia magaidi, awashambulie kabla hawajafanya ubakaji. Akafungua mlango taratibu, akachungulia,akamuona jambazi aliyegongana naye uso kwa uso, alimtambua vizuri sana.



      “,Wamejileta wenyewe, watakufa, “Catherine aliongea, akaifunga bastola yake mfumo wa sauti, akalala chini, hakuweza kuonekana, sofa zilimzuia. Chuma cha pua akachomoa uume wake uliosimama kwa njaa kali, bila aibu akamsogelea Jacline.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Yalaaaaaa ……”,uume wa chuma cha pua ulisambaratika, damu zikaruka, akapiga kelele za uchungu, hawakutambua risasi imetokea wapi. Wakaanza kupiga hovyo risasi, kwenye sofa, ukutani, dirishani, milangoni, walikuwa kama wamechanganyikiwa.



      “,Mtafuteni tumuue! jitokeze kabla hatujaua familia yako ……”,kiongozi wa kundi hili aliongea, alikuwa D47 namba sitini, bastola yake aliinyosha kuelekea juu, akafyatua risasi, zikapiga juu ya dali.



      “,Nasema jitokeze tutawauaa wazazi wako! “,gaidi alitoa amri kwa mara nyingine tena.







      ITAENDELEA

    JINI MWEUPE - 3

     









      Simulizi : Jini Mweupe

      Sehemu Ya Tatu (3)





      Ofisi ya Ukombozi; 9;00am



             Kamanda Catherine, kiongozi mkuu wa idara ya mawasiliano na teknolojia, katika kundi lake la wapelelezi watatu, maarufu kama the super three soldiers, alikuwa amechanganyikiwa, taarifa aliyoipokea kwa mfumo wa barua pepe ya ofisi yao, pamoja na radio na televisheni zilizidi kumchanganya kupita maelezo. Alijizungusha kwenye kiti chake, ndani ya ofisi yao maarufu kama ofisi ya Ukombozi, kabla ya kuelekea kituoni itakapofika saa sita mchana, kwenda kujua nini kinaendelea …



      “,We have to go, tunapaswa kwenda,gaidi aliyeuawa alisema ukweli mtupu, tungemuhoji kabla hajafa tungejua mambo mengi zaidi, lakini ndo hivyo, they have killed him, wamemuua, hakijaharibika kitu, tukienda Gano, tutapata mahali pa kuanzia, tujue alipotoka Gano alielekea wapi tena, na kwanini anaua? Mauaji ya kufanana, sio bure, kuna kitu! “,kamanda Catherine, akiwa peke yake ofisini, ilikuwa kawaida yake kuwahi kazini siku zote, aliongea, akatafakari, akanyenyua simu yake, akampigia kamanda Kendrick, mkuu wake wa kazi …



      “,Yes kamanda, mzima? “,kamanda Kendrick aliongea, baada ya kupokea simu.



      “,Mimi mzima, vipi umefuatilia habari zilizopamba mtaani, Donald Mbeto ameshafanya yake nchini Gano, taifa letu linatutaka kwende haraka sana kisiwa cha Gano tukamtafute muuaji wetu, serikali ya Gano na wenyewe wametutumia ujumbe twende tukawasaidie uchunguzi wa mauaji yaliyofanyika! “,kamanda Catherine alieleza kwa kirefu zaidi.



      “,Nimeshapata taarifa hizo, ndiyo taarifa ambazo zimenichelewesha kufika ofisini mpaka sasa hivi, lakini tayali nimeshapata majibu, namna ya kumpata Donald Mbeto, nakuja sasa hivi ofisini, mpatie taarifa kamanda Philipo tukutane hapo ofisini, ndani ya nusu saa ijayo, “kamanda Kendrick aliongea.



      “,Sawa bosi, “kamanda Catherine aliongea, akakata simu, kisha akabonyeza tena simu yake, akaitafuta namba ya simu ya kamanda Philipo, akaipata, akapiga, kisha akaisogeza simu yake sikioni.



      “,Haloo Cathe,umesikia kuhusu Donald Mbeto huko Gano, yani huko ni kilio na kusaga meno kama jehanamu vile, niko njiani nakuja ofisini, tujue nini cha kufanya! kamanda Kendrick ameshafika ofisini? “,



      “,Yani simu hii ni kwa ajili ya huyu mshenzi,tumekubaliana tukutane hapa ndani ya nusu saa ijayo, kamanda Kendrick hajafika ofisini, lakini yuko njiani anakuja, usichelewe, usinywe bia yoyote, najua vizuri matatizo yako, usipo nisikiliza, utakwamisha kila kitu ……”,



      “,Hahahaa, sawa, nakuja, siwezi kulewa,nitalewa mpaka Donald Mbeto, huyu jini mweupe awe katika mikono yetu, “



      Yalikuwa ni maongezi ya simu kati ya kamanda Philipo, pamoja na Kamanda Catherine, kisha simu zilikatwa.



      Ofisi ya ukombozi; 10:02



      Kikao kifupi kiliendelea, kamanda Kendrick aliongoza majadiriano, kila mmoja alichangia maoni yake, akatoa mbinu mbalimbali za kumkamata Donald Mbeto.



      “,Kabla hatujafika mbali, kamanda Kendrick, hebu tueleze! nilipokupigia ulinambia kuna mbinu ambayo umeipata, hebu tuelezee na sisi tuitambue kama mbinu hiyo inafaa au haifai! “,kamanda Catherine aliongea,wenzake wakimsikiliza kwa makini.



      “,Usjali kuhusu hilo, vipi kuhusu ujumbe kutoka Gano,unasemaje, hebu tuusome halafu nitawaeleza mbinu hiyo ya kumkamata huyu Mwanaharamu. “,kamanda Kendrick aliongea, akijizungusha kwenye kiti chake huku na kule,wenzake wakimsikiliza kwa umakini wa hali ya juu.



      “,Mauaji yametokea tena kwa mara ya pili sasa, mauaji yanayofanana, kila tukio muuaji katumia sumu, sumu ambayo imetumika kwenye mauji huko nchini kwenu Tanzania, Ufilipino na nchi kadhaa za Afrika, Asia na Ulaya, tunahitaji msaada wenu, mje mara moja kushirikiana na vijana wetu kumsaka adui huyu! “,kamanda Catherine alimaliza kuusoma ujumbe wa barua pepe kutoka nchini Gano, akainua kichwa chake,wote watatu wakatazamana.



      “,Haya sasa, nazani umesikia, tueleze hiyo mbinu kisha tuanze kazi haraka sana…”,kamanda Philipo alichangia mawazo yake.



      “,Ok! kabla ya kuelekea nchini Gano, tunapaswa kulifumbua fumbo la kifo cha gaidi mshirika wa Donald Mbeto, gaidi aliyeuawa mahabusu, tukifanikiwa! lazima tujue mahali alipojificha Donald Mbeto, hata tukienda Gano, yatatokea kama yaliyotokea Ufilipino. “,kamanda Kendrick aliongea kwa hisia kali,wote wakatikisa vichwa vyao,bila shaka walikubaliana na mawazo yake.



      “,Kweli kabisa, kama vile ulikua kichwani mwangu,hata mimi niliwaza hivyo hivyo! mimi ninaona tukamuhoji vizuri askari aliyekuwa zamu, maana mpaka sasa hatujamuhoji kwa kipigo, lazima atasema ukweli,kuna kitu anajua tu yule, maana usiku wakati tunamuhoji hakujiamini hata kidogo “,kamanda Catherine aliongea,akanyenyuka kwenye kiti chake.



      “,Twendeni, twendeni kituoni haraka sana, tusipoteze muda, nazani tayali tumefikia muafaka! ,askari yule ahojiwe kwa kipigo, kama siyo yeye muuaji basi nitalipa kila kitu kwa ajili yake”,kamanda Kendrick aliongea, na yeye akanyenyuka kwenye kiti, akaweka tai yake vizuri,akajiandaa kwa ajili ya kutoka nje ya ofisi ya ukombozi.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      Kamanda Philipo alichukua kompyuta ya ofisi, akaiweka kwenye begi lake, akanyenyuka kwenye kiti,kamanda Kendrick akatoka nje, kamanda Catherine akafuatia, kisha kamanda Philipo akafuata, akasimama nje ya mlango wa ofisi yao, akabonyeza bonyeza mashine pembeni ya mlango,akaingiza nywila (neno siri), mlango ukajiloki. Wakatoweka, wakaelekea kituoni.



      …………………………………



      Makao makuu ya polisi; 11:02



               Kamanda Catherine alikuwa amesimama, mkononi alikuwa ameshika plaizi,kamanda Philipo alikuwa amesimama pembeni ya Catherine, mkononi mwake alishika bakola, fimbo kubwa ya chuma isiyo katika, kamanda Kendrick yeye alikuwa amechuchumaa,mkononi alishika mjeledi, akamtazama askari wa zamu aliyelala chini kama mzigo, akiwa amefungwa mikono na miguu.



      “,Ukweli wako ndiyo utakuweka huru, jana tulikuhoji kwa upole, ukazani tunatania, hatujawahi kutania kazini hata siku moja, ndiyo maana tunategemewa na taifa letu, tuko hapa kwa ajili yako! “,kamanda Kendrick aliongea, kamanda Catherine akachuchumaa, akasogeza plaizi yake kwenye masikio ya askari yule, akayabana kwa nguvu bila huruma.



      “,yalaaaa! nakufa…a …”,kelele za uchungu zilisikika,askari yule alilia kama mtoto,damu ilichuruzika katika sikio lake,alitamani ajikune lakini hakuweza, mikono yake ilifungwa kwa pingu za chuma.



      “,Kufaaa! si hautaki kusema ukweli? “,kamanda Catherine alifoka.



      “,Sisemi, nasema sihusiki na chochote! “,askari yule aliongea kwa jeuli.



      “,Pyaaa! pyaaa! “,



      “,Yalaaaa! mama…aa”,



      Sauti za bakola zilisikika, kamanda Philipo alimchapa bakola mbili askari yule kwenye unyayo wa miguu yake,unyayo ukaacha mistali miwili iliyovuja damu,askari yule akaikunja na kuinyosha miguu yake, alitamani kujikuna lakini hakuweza.



      “,Nitasema, nitasema! msiniuee ……!”,askari yule alipiga kelele,maumivu yalimzidi nguvu, mwili wake ukashindwa kustahimili mateso ya kipigo ambacho nd’o kwanza kilikua kinaanza.



      “,Sema! semaa kabla sijakuchalaza na mjeledi wangu! “,kamanda Kendrick alifoka, akiwa amenyenyua mkono wake wa kulia juu, akijiandaa kumtandika nao askari yule.



      “,Nitasema mkuu, msinipigee! “,askari yule mamluki alililia, akaomba msamaha,alikuwa tayali kusema ukweli, wote wakaweka silaha zao za mateso pembeni, wakakaa tayali kwa ajili ya kumsikiliza.



      “,Haya tueleze, nani aliua? “,kamanda Philipo aliuliza swali.



      “,Mimi ndiye niliye muua gaidi yule, nilipewa sumu na kundi la D47 niweze kummaliza, kwa muda mrefu nashirikiana nao, nawapatia habari za upelelezi kisha wananipatia pesa, ndiyo maana imekua vigumu hata kumkamata Donald Mbeto”,askari yule aliongea, akaeleza kila kitu, hasira zikampanda kamanda Catherine, akamsogelea askari yule, akamkaba shingoni..



      “,Muachee, utamuua! Catherine utamuuaaa! “,kamanda Kendrick aliongea kwa taharuki, akiwa anafanya kazi ya ziada kutoa mkono wa Catherine katika shingo ya askari yule, huku kamanda Philipo akishirikiana naye kufanya shughuli hiyo.



      “,Haiwezekani kila siku tuhangaike kumsaka mtuhumiwa kumbe mchawi tunaye ndani,stupid comrade! hautufai katika jeshi letu, lazima sheria ichukue mkondo wake …”,kamanda Catherine alifoka,huku akiiweka vizuri suti yake, baada ya mkono wake kufanikiwa kutolewa na makamanda wenzake katika shingo ya askari yule msaliti.



      “,Sawa! tumesikia,makazi ya D47 yako wapi?  ,Donald Mbeto na yeye tunampata wapi?”,kamanda Kendrick aliuliza swali jingine,akimtazama askari yule msaliti,akijaribu kuinyosha shingo yake bila mafanikio,alimanusura kamanda Catherine amtoe koromeo.



      “,D47 wanapatikana katikati ya Bahari ya hindi,wana meli yao kubwa aneo hilo,hata Donald Mbeto hurudi eneo hilo kila anapomaliza kutekeleza tukio,huenda kupumzika kabla ya kupewa kazi nyingine…,ni hayo tu nayofahamu bosi!”,askari yule aliongea,kamanda Catherine akachana shati la askari yule,akamgeuza,uso ukalamba vumbi,mgongo wake ukabaki wazi,”D47 namba mia moja,”kamanda Philipo aliongea,alisoma chata kubwa iliyozungushiwa duara katika mgongo wa askari yule.Askari yule hakuwa mamluki tu,bali alikuwa mwanachama halisi wa D47.



      “,Ndio maana Tanzania hatuendelei,China watu kama hawa wanapigwa risasi mbele ya umma…”,kamanda Kendrick aliongea,akaanza kutoka mahabusu,wenzake wakamfuata.



      “,Mahabusu yake iongezewe ulinzi, asiingie wala kutoka mtu yoyote, kamanda Petro andaa helikopta ya kivita! tunapaswa kuelekea nchini Gano, kisha tutaelekea moja kwa moja katikati ya bahari ……” ,kamanda Kendrick alitoa maagizo,kisha wote watatu wakaelekea stoo ya silaha (Amala),wakachukua silaha zote zilizowafaa kwenye mapambano,visu, bastola, kamba, saa zao za kipelelezi pamoja na miwani ya mionzi mikali.



      ………………………………



      01:20



            Helikopta ya jeshi iliacha ardhi ya Dar es salaam Tanzania, siku ya ijumaa, saa saba mchana, ilipaa futi sitini kwenda juu, ikaelekea mashariki mwa mji wa Dar es salaam, katikati ya bahari.Askari wa the super three soldiers wote walivalia mavazi maalumu meusi, rangi ya shaba, yasiyo pitisha risasi(bullet proof), machoni walivaa miwani ya mionzi, mkono wa kushoto walivaa saa zao za kipelelezi kwa ajili ya mawasiliano.



      “,Kaa tayali kwa misheni, kushindwa ni dhambi, tuna dakika kumi za kufika eneo la tukio nchini Gano, tuna saa moja la kutekeleza misheni na kumpata Donald Mbeto, tunaelewana? “,kamanda Kendrick aliongea, akauliza swali askari wake.



      “,Ndiyo afande, tumeelewana! “,wote waliitikia,walikubaliana na maelekezo kutoka kwa mkuu wa kikundi, kamanda Kendrick, safari ikaendelea, helikopta ikaendelea kukata mawimbi.



      Gano:02:02pm



             Pilikapilika ziliendelea katika hospitali ya jiji la Gano,watu waliingia kuchukua miili ya ndugu zao,waliopoteza maisha kwa sumu hospitalini hapo,waandishi wa habari hawakuchoka, waliendelea kutimiza majukumu ya kuchukua taarifa mbalimbali kama kawaida yao. Polisi waliendelea kufanya uchunguzi wao, wakiongozwa na kamanda wao mkuu wa upelelezi kisiwani Gano.



      “,Jiandaeni kupokea wapelelezi kutoka Tanzania, watafanya uchunguzi kwa dakika kumi tu, kisha tutaongozana nao kwenye misheni katikati ya bahari …”,kamanda mkuu wa upelelezi kisiwa cha Gano aliongea,vijana wake ishirini wakapanga mstali, uwanja wa hospitali ya Gano,macho yao yalitazama anga, kaskazini, mashariki na magharibi.Kila mmoja akisimama wima kwa ushupavu, kupokea askari watatu wenye sifa kubwa dunia nzima, kwa upelelezi wao wa kishujaa.



      “,Simama wima, heshima toa! “,kamanda yule alitoa amri, helikopta ilipita katika anga la hospitali kwa spidi ya ajabu,ikapigiwa saluti za heshima, ikakunja kona ,kaskazini, kisha ikarudi tena magharibi, ikapunguza kasi, ikaanza kushuka chini iweze kutua.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



      “,Makamanda wakishuka, piga saluti za heshima, kisha tutawaongoza mpaka eneo la tukio …”,kamanda yule aliongea kwa sauti kubwa, kisha akavuta pumzi ndefu. Macho yake yakiitazama helikopta kubwa ya kijeshi yenye chapa ya Tanzania, ikitua na kutimua vumbi zito eneo lote la uwanja wa hospitali ya Gano.



      “,Ndiyo afande, tumesikia, tuko tayali kutekeleza amri mkuu! “,sauti ilisikika, vijana waliopanga mistali miwili iliyonyooka waliitikia amri ya kiongozi wao, wakajiweka sawa, wakasimama wima bila kutikisika.



      …………………………………



      Helikopta ya jeshi la Tanzania ilitembea kilomita takribani ishirini,ikafika anga la kisiwa cha Gano,ikaanza kushuka taratibu, futi hamsini, arobaini, therathini, mpaka ishirini, ikaanza kufuata ramani mpaka mahali pa tukio, hospitali ya jiji la Gano, kisiwa kinachopatikana bahari ya hindi, jirani kabisa na nchi ya Tanzania.



      “,Tumefika, hakuna muda wa kupoteza, kila mtu atimize majukumu yake …”,kamanda Kendrick aliongea,akawakumbusha tena askari wenzake.



      “,Ndiyo afande! “,waliitikia, helikopta ikazunguka eneo la hospitali,ikakata kona, kisha ikatua katika uwanja wa hospitali, wakashuka wakitembea harakaharaka,huku wakipigiwa saluti za heshima, kisha askari wenyeji wakawaongoza mpaka eneo la tukio.



      “,Eneo lenyewe ndiyo hili, kama unavyoliona, aliingia kupitia choo hiki, akatoa mfuniko wa dali,akapita ndani kwa ndani mpaka chumba cha madawa, akaweka sumu kwenye madawa yote ya kimiminika, hivyo basi yoyote yule aliyetumia dawa hizo asubuhi ya leo aliweza kufa, mpaka sasa wamefariki dunia wananchi elfu tatu! “,kamanda mkuu wa upelelezi nchini Gano alitoa maelezo ya upelelezi wa awali,kamanda Kendrick akatikisa kichwa, akakagua choo chini na juu, kisha akatoka nje, akaangaza huku na kule.



      “,Hiyo karatasi vipi?”,kamanda Kendrick aliuliza swali, akasogea ukutani, mahali kulipokuwa na karatasi yenye wino mwekundu.



      “,Hiyo ndo karatasi iliyotuongezea taharuki, imeandikwa Jini mweupe, maandishi ya damu …!”,kamanda yule aliendelea kutoa maelezo yake.



      “,Sawa nilishapata jibu, huyu ni Donald Mbeto, hakuna mwingine, tuachieni kazi hii, tunaenda kuifanyia kazi, tukihitaji msaada tutawajulisha! “,kamanda Kendrick aliongea,aliona kazi hiyo aifanye yeye mwenyewe pamoja na vijana wake alio wazoea,ombi lake likakubaliwa, askari wa nchini Gano wakapiga saluti, wakaanza kutoka nje,waandishi wa habari wakitimiza majukumu yao kupiga picha na kurekodi kila tukio.



      “,Kwa niaba ya waziri wa ulinzi, tunawatakia safari njema na misheni njema, tulitamani sana kuongozana na nyinyi maana tuna hasira na huyu muuaji, kwa msaada wowote msisite kutufahamisha …”,kamanda mkuu wa upelelezi kisiwani Gano aliongea,wakapigiana saluti, the super three soldiers wakaingia ndani ya helikopta,baada ya dakika tano, helikopta ilikua futi sitini juu angani, ikaanza kuelekea kaskazini, kukiacha kisiwa cha Gano, kuelekea katikati ya bahari, kutekeleza misheni ngumu kuliko zote katika maisha yao ya kipelelezi, achilia mbali oparesheni ya kumsaka muuaji hatari Yuan Liang nchini Gano mwaka mmoja uliopita, hii ya Donald Mbeto iliwaumiza kichwa kila siku.



      …………………………………



      Mbezi, Dar es salaam :2:00



                  Magaidi wa D47 kanda ya Dar es salaam, walikuwa wameketi kikao cha dharula, wakibadilishana mawazo,askari wa serikali,aliyewapatia taarifa kutoka serikalini na kufanikisha shughuli zao mbalimbali alikua hapatikani kwa simu tofauti na siku zote,tangu usiku wa saa nane walimtafuta wajue nini kinaendelea serikalini, lakini hakupatikana, simu yake haikuwa hewani kabisa, kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo hofu ilizidi kutanda.



      “,Hapa kuna kitu,sio kawaida yake kabisa,mimi nashauri twendeni kituoni,mmoja aingie mpaka kituoni,kama kuna lolote baya limemkuta,tumsaidie,bila hivyo kila kitu kitaharibika…”,gaidi D47 namba sitini aliongea,wenzake watatu wakiwa makini kumsikiliza.



      “,kweli kabisa,yule ana siri nyingi kama mwenzetu,akiwa pabaya hata sisi tuko pabaya,tuchukue silaha,mmoja ajifanye ameenda kushtaki,apeleleze kisha atuletee taarifa nje tujue mwenzetu yuko salama,au kagundulika,”gaidi D47 namba ishirini aliongea,wote wakanyenyuka,wakasogelea stoo yao ya silaha,wakachukua bunduki zao,mikanda ya risasi,wakatoka kwenye nyumba yao ya kifahari,wakaingia kwenye BMW nyeusi,wakatoweka katika makazi yao haraka sana kwa kasi ya ajabu.



      …………………………………



      Bahari ya Hindi:



              Burudani ziliendelea katikati ya bahari,kila mmoja aliyekuwa katika meli ya D47paraquaat aliburudika kwa starehe aliyohitaji,wengine walikunywa pombe,wengine walijidunga madawa ya kokeini,huku wengine wakizini,kila mmoja alifanya starehe aliyohitaji kufurahia ushindi wa Donald Mbeto,alifanikiwa kukamilisha kazi aliyotumwa na bosi kwa mataifa yote matano aliyotumwa kuua kwa sumu,akaitikisa dunia,jina lake likaenea duniani kote.



      “,Danger!danger!our kingdom is in danger!dange!danger!”,(Hatari!hatari!ufalme wetu uko hatarini!hatari!hatari!)



      Sauti ya hatari ilisikika,ikapenya katika masikio ya kila gaidi,kifaa maalumu kilitoa taarifa ya hatari, katika kila chumba,pamoja na kumbi za starehe ndani ya meli, magaidi wakaanza kukimbia huku na kule, kila mmoja alitambua jambo la kufanya anaposikia kengele hii, anaacha shughuli zake, anaenda kupanga mstali katika uwanja wa mazoezi.



      “,Kuna ndege imeonekana katika rada zetu, kuna ndege kubwa inasogea eneo letu, kutokea mashariki, bila shaka nchini Gano, mahali Donald Mbeto alipotekeleza mauaji muda mfupi uliopita, meli yetu itazama baharini, futi kumi kwenda chini kama nyambizi, lakini lolote linaweza kutokea, jiandaeni! “,bilionea wa kihindi, Paresh Kumar, aliongea kwa kiswahili,alikuwa na miaka  mingi pwani hii ya waswahili,alikifahamu kiswahili vizuri sana, baada ya kutoa amri kila gaidi alikimbilia eneo lake, kutimiza majukumu yake,waliamini helikopta hiyo ilikuja ukanda wao kwa vita na wala sio kitu kingine, walikua sahihi kabisa.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      Bahari ya hindi; 2;40pm



       Donald Mbeto alikuwa amezungukwa na wanawake sita wa kizungu,hakuna aliyekuwa na akili zake,kila mmoja alikuwa amelewa chakali, akiwa uchi wa mnyama,chupa za pombe ya ya kizungu, “queen elizabeth”,zilizagaa kila kona ya chumba hiki chenye mwonekano wa kifahari zaidi, godoro la plastiki lillilojaa hewa ndani lilikuwa kitandani, Donald Mbeto alicheza mchezo mchafu na mwanamke mmoja baada ya mwingine, wanawake ambao walitekwa kutoka nchi mbalimbali za dunia, kumbukumbu zao zikafutwa kwa kutumia kompyuta, wakatumikishwa bila kujitambua, huku wakiingiziwa madawa ya kulevya mwilini ili kudumaza akili zao, wakatumika katika kila kazi, uzinzi, kusafirisha madawa(drugs)  pamoja na kuua.



      “,Ngo! ngo! ngo hodiii! “,licha ya kengele ya hatari kupigwa kwenye chumba cha Donald Mbeto hakuweza kusikia, ikabidi atumwe mtu kumgongea, maana alitegemewa sana kwenye kazi mbalimbali, mawazo yake siku zote yalileta matokeo chanya kwenye kazi za D47.



      “,Donald! Donald! kuna hatariii …!”,gaidi mwenye cheo cha chini sana aliita, akaongea kwa sauti kubwaa! .



      “,Kwichi, kwichii, kwichiii ………”,sauti ilisikika, sauti ambayo haikua ya Donald Mbeto, bali kelele za kitanda kilichokuwa kimezidiwa nguvu, gaidi yule hakuendelea kuita tena,alirudi kwa unyonge, kumpatia jibu mtu aliyemtuma, maana hakua na njia nyingine ya kufanya.



      “,Bosi! amelewa sana, nasikia sauti za walevi ndani ya chumba, nimeita sana hakuna aliyenijali …”,gaidi D47 namba arobaini na mbili aliongea, Paresh Kumar akakasirika, ujumbe alioupokea ulikuwa kinyume na matarajio yake.



      “,Ina maana mpaka sasa bado yuko chumbani na wanawake zake? “,bilionea wa kihindi, mmiliki wa kundi la kigaidi la D47 ,Paresh Kumar ,aliuliza swali kwa mshangao.



      “,Ndio bosi! “,gaidi yule aliitikia kinyonge, kwa heshima iliyojaa uoga mwingi ndani yake.



      Paresh Kumar alinyenyuka ofisini kwake,akatembea kwa haraka,kuelekea katika chumba cha kijana wake machachali, aliyemtegemea kwa kila jambo, mzee wa miaka sitini bwana Donald Mbeto.



      “,Paaaaa! “,alipiga kitasa na bastola kikaachia, akaingia ndani, uso kwa uso na wanawake sita wakivunja amri ya sita na kizee wa miaka sitini, mwenye damu mbichi kama kijana wa miaka ishirini tu, bilionea Paresh Kumar hakushtuka,hakuona cha ajabu chochote kile.



      “,boosi, ninini tatizo, mbonaaaa umekujaa mbioo?,”Donald Mbeto akiwa uchi wa mnyama, alijitoa mikononi mwa wanawake wale wa kizungu, akasogelea mavazi yake, akaanza kuvaa nguo moja baada ya nyingine, huku akimuuliza maswali bosi wake.



      “,Kengele ya hatari imepigwa, haujasikia! nimetuma watu kukuita haujasikia!, kuna tatizo kubwa, tena kubwa kabisaa! “,Paresh Kumar aliongea, mikono yake ikizungusha bastola yake kwenye kidole chake cha kati, mkono wa kulia.



      “,Tatizo gani hilo bosi?, na nyie malaya, ondokeni hapa, mnasubili nini? “,pombe zilimuishia Donald Mbeto,akauliza swali kwa mshangao, sura yake akaikunja kwa hasira, akawafukuza wanawake aliokuwa anakula nao raha, kwani walikuwa bado wanasubili kuendelea na starehe zao.



      “,Kuna ndege ya kivita inakuja kwenye ukanda wetu baharini,bila shaka imekuja kwa ubaya. “,Paresh Kumar aliongea.



      “,Unasemaje bosi? “,Donald  Mbeto aliongea kwa mshangao.



      “,Ndiyo, twende ukaone …!”,Paresh Kumar aliongea, akaweka bastola yake kwenye koti lake,akaongozana na bosi wake, mpaka chumba cha mawasiliano na teknolojia katika kundi la D47.



      “,Banard! “,



      “,Yes bosi! “,



      “,Vipi,bado ndege hiyo inakuja eneo tulilopo…”,



      ” „Ndio bosi,kama unavyo ona,”



      “,Hawa ni watu wabaya kwetu,Donald nazani umeona ndege hiyo ?”,



      “,Ndio bosi,waambie makepteni wazamishe meli kwenda chini kama nyambizi,tusionekane kwenye uso wa bahari,wakifika kwenye anga zetu tuwashambulie kwa makombola…”,



      “,Kweli kabisa Donald,hiyo ndiyo mipango yangu,tayali meli yetu imezama kama nyambizi,nenda kashirikiane na askari wa makombola,wapatia maelekezo,ndege ikifika usawa wa bahari yetu tulipue ndege yao,”



      “,Sawa bosi!”,



      Donald Mbeto aliitikia amri ya bosi wake,akatoka chumba cha mawasiliano,akamuacha Benard akiendelea na majukumu yake,kufuatilia mitambo ya ulinzi katika meli yao yenye uwezo wa kujigeuza kama ndege au nyambizi.



      “,Unazani watatumia dakika ngapi hawa washenzi mpaka kufika hapa?”,Paresh Kumar alimuuliza Benard,mkuu wa kitengo cha mawasiliano katika kundi la D47.



      “,Dakika kumi zijazo,watakua katika anga letu…”,Benard aliongea.



      “,Ok sawa,ngoja nikawapange vijana wangu,hii ndege tuishambulie,isivuke anga letu.……”,Paresh Kumar aliongea,akaondoka zake.



      …………………………………



      2;00pm



              Kamanda Philipo alichukua kompyuta yake, akabonyeza kitufe,akafanya utundu wake, alibonyeza huku na kule, akapata alichokihitaji.



      “,Tumefika, meli yao inatakiwa iwe mahali hapa, lakini mbona hatuioni ,iko wapi? “,kamanda Philipo aliongea kwa mshangao, wote wakashangaa.



      “,Ina maana tumefika! “,kamanda Catherine aliuliza kwa mshangao.



      “,Ndio Cathe, tumefika, meli inaonekana iko hapa lakini hatuioni, nikisachi mtandao uneonesha hiyo meli ya Paraquat iko hapa ……!”,kamanda Philipo alitoa maelezo.



      “,Nimekumbuka kitu, kepteni! Kepteni! ondoa ndege yetu mahali hapa, meli yao inauwezo wa kujigeuza kama nyambizi, kama wametuona bila shakaa wametutega watushambulie ……”,kamanda Kendrick aliongea.



      “,Unasemaje?? “,wote waliuliza kwa mshangao, wote wakamgeukia kamanda Kendrick, walitaka afafanue vizuri kile alichozungumza.



      “,Puuuuuuu, puuuuu …”,



      “,Tumeshambuliwa, luka baharini …!”,



      “,Puuuuuuh puuuuuh!



      “,Nakufaaa…a……”,..



      Ghafla mripuko ulisikika,kabla hata kamanda Kendrick hajamaliza kuongea,helikopta ya the super three soldiers ilipasuka vipande vipande,kelele za kilio zilisikika ,kila mmoja aliipigania roho yake.



      …………………………………



      Makao makuu ya polisi; 4;02pm



               BMW ilipaki pembeni ya barabara, gaidi D47 namba sitini alishuka, akavuka barabara,akazisogelea ofisi za kituo cha polisi.



      “,Tukusaidie nini kijana! “,askari wa zamu mapokezi aliuliza.



      “,Nataka kuonana na polisi aliyekuwa zamu jana, kuna kesi niliandikisha kwake jana? “,gaidi D47 namba sitini aliongea..



      “,Yule mshenzi, msaliti wa serikali yetu, yuko mahabusu, hawezi kushirikiana na wauaji, niambie kesi hiyo inaitwaje, niangalie faili lake kabatini …”,askari wa zamu aliongea. Hakujibiwa,tayali alipata alichohitaji, gaidi alitoka nje haraka sana, aliona ulinzi ulikuwa dhaifu, akawajulisha wenzake.



      “,Twendeni,shambulia washenzi wote, asipone hata mbwa mmoja, mwenzetu yuko mahabusu, anapaswa kuuawa, kasema siri zetu …”,D47 namba sitini aliongea kwa hasira, akachukua bunduki, akavaa mkanda wa risasi begani, wenzake wakafanya vivyo hivyo, kila mmoja alichukua bunduki yake pamoja na mkanda begani, wakavuka barabara bila kuogopa kitu chochote kile, wakatembea kikomando kusogelea kituo cha polisi.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      Makao makuu ya polisi:



            Shambulio la kushtukiza lilipelekea askari wengi kupoteza maisha,magaidi wanne wa D47 walikuwa moto wa kuotea mbali, walifyatua risasi kama mashine, wakaua askari wote waliowasogelea kizembe,hawakuogopa chochote kile, walijiamini na kuendelea kushambulia huku wakiingia ndani kabisa ya kituo cha polisi.



      “,Mmoja aingie mahabusu, akamilishe kazi kisha tutoweke eneo hili,sisi tuko hapa nje tunadumisha ulinzi”,sauti ilisikika, gaidi D47 namba sitini alitoa amri,magaidi wawili wakaelekea mahabusu, huku wakisafisha njia kwa kuwafyekelea mbali askari ambao walikutana nao.



      “,Paaaaa, paaaaa! “,risasi mbili zilisikika, walimfyatulia risasi askari aliyekuwa gaidi mwenzao na kutoa siri zao, wakamuua, kisha wakarudi haraka sana.



      “,Tuondoke! tuondokee! “,



      “,Tubadirishe nguo, tuvae nguo zao, tutatoroka kwa urahisi, “



      “,Vipi kuhusu gari letu? “,



      “,Haina haja, tutaliacha palepale, tuchukue moja kati ya magari yao, itakua rahisi hata kupita barabarani ……”,



      “,Sawa mkuu …”,



      Magaidi wa D47 walijadiriana, wakakubaliana, wakawavua askari watano waliowaua, wakavaa sare zao za polisi, wakatoka nje haraka sana, wakajipakia katika difenda ya polisi yenye king’ora juu, wakatoweka eneo hilo, wakiwa wameua askari takribani ishirini, askari wengine haijulikani walikuwa wapi.



      …………………………………



      Nusu saa iliyopita;



              Donald Mbeto aliwaongoza magaidi wenzake, kitengo cha makombola,wote walikuwa makini kuitazama helikopta ya jeshi, helikopta ambayo ilitokea kisiwani Gano, ikafika katika ukanda wao,ikaonekana vizuri kupitia kompyuta na sattelite zao.



      “,Ni watanzania, washambulieni haraka sana, hawa ni watu hatari sana kwetu …!”,Donald Mbeto alitoa amri,magaidi wenzake wakabonyeza vitufe vya makombola, makombola mawili yakafyatuka baharini, moja likaipiga helikopta kwenye mkia, ikapepesuka na kupoteza mwelekeo, kombola la pili likaipiga kwenye kichwa na kuisambaratisha vipande vipande.



      “,Yeeeeeee!,wamekwishaa “,



      Magaidi wote walipiga kelele za shangwe, wakiongozwa na Donald Mbeto,aliyejiita jini mweupe kutokana na mnvi nyingi zilizomtapakaa kidevuni na kichwani,siku zote alitekeleza matukio hatari sana ya mauji, na kijifananisha kama jini asiye onekana, alijiamini na kujikubali kuliko kiumbe yoyote yule.



      “,Hapa kazi imekwisha, ngoja nikale zangu kuku bwanaaa wewe, wametukatishia starehe zetu hawa maboya, wakamsalimie shetani kuzimu ……”,Donald Mbeto alitukana,akaondoka zake, uso wake ulijaa tabasamu licha ya sura yake yenye mikunjo kwa mbali,kutokana na kula chumvi nyingi sana.



      …………………………………



      Kamanda Kendrick alitoa amri,vijana wake wajitupe kwenye maji, helikopta yao ililipuliwa kwenye mkia, ikaanza kuzunguka zunguka, rubani akashindwa kuiongoza, ikalipuliwa tena, kichwa kikasambaratika, wote watatu wakaruka, isipokuwa rubani aliyepasuka na kuchanika vipande vipande, akalia kwa uchungu na kufa palepale.



      Kila mmoja alijitupa kwenye maji na kuangukia upande wake, walikua wamepoteana,hawakuangukia sehemu moja.



      “,Kendrick! Kendrick! Philipo mko wapi? “,Catherine aliita,mikono yake akiitupa nyuma na mbele kuogelea, uso wake ulijaa huzuni, macho yake yakadondosha chozi, kelele alizozisikia kipindi ndege inalipuliwa zilimchanganya, hakujua nani amekufa, hakujua kama wenzake walifanikiwa kuluka, kila mmoja alijitupa kwenye maji bila kutambua kama mwenzake aliluka na kujiokoa.



      “,Kendrick don’t die please, usife kabla sijakuambia ukweli wa moyo wangu! “,Catherine aliendelea kuogelea kama samaki, huku akiongea maneno ya huzuni moyoni mwake, alizani kamanda Kendrick pamoja na kamanda Philipo walikuwa wamepoteza maisha, kumbe sivyo.



      …………………………………



      Kisiwa cha Comoro; 4;20pm



               Mtumbwi ulisogea mpaka ufukweni, mvuvi mwenye umri wa miaka hamsini alishangazwa na binadamu aliyemuokota baharini, akiwa amepoteza fahamu, akamkandamiza tumboni,akatapika takribani lita tatu za maji, akaendelea kumkandamiza tumboni, akatapika maji, macho yake yalifumba, pumzi yake ilikua kwa mbali sana, akamnyenyua mpaka kwenye kibanda chake cha makuti, kilomita moja kutoka baharini, samaki aliziacha palepale.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Babaa! huyu ni nani?, halafu mbona ana sura ya kitanzania, au ni mwenzetu? “,binti mrembo, mweupe, mwenye macho meupe ya duara, aliongea, akimshanga mwanaume aliyevutia, akiwa amevaa mavazi ya ajabu sana, usoni akiwa na miwani, mkononi alivaa saa ya dhahabu.



      “,Nimemuokota akiwa anahangaika kuogelea, nilipofika tu mahali alipokuwa, aliishiwa nguvu na kupoteza fahamu, nikamchukua na mtumbwi wangu mpaka mahali hapa! kabla ya yote, kachukue samaki ,nimeziacha kwenye mtumbwi, halafu njoo nazo, tuchemshe mgeni ale atakapopata fahamu …”,mzee yule aliongea, akamlaza kamanda Kendrick kwenye magome ya miti, apigwe na upepo, chini ya mti. Akimsubili aweze kuamka, awasimulie yaliyomkuta.



      …………………………………



      Kisiwa cha Mafia;



            Boti ya Mv Mafia ikiwa na abiria hamsini, ilitia nanga katika bandari ya mjini Mafia, abiria walijaa taharuki, mabaharia nao walijaa taharuki,mavazi aliyoyavaa mtu waliyemuokota katikati ya bahari akinywa maji na kuhangaika kujiokoa yalizidi kuwachanganya,abiria walishuka kwenye meli, walikuwa wamefika mwisho wa safari, akabaki nahodha na mabaharia wakimpatia huduma ya kwanza kamanda Philipo,alitema maji mengi takribani lita tano.



      “,Watokea wapi yahee,watoka Unguja au Pemba,wewe raia wa wapi?”,kamanda Philipo aliyafumbua macho yake,uso kwa uso na watu wanne wenye sare nyeupe zilizofanana,begani zilifanana na sare za polisi.



      “,Nyie polisi wa wapi?”,kamanda Philipo aliuliza.



      “,Hahaaaa,kachanganyikiwa huyu,lakini atakua mtanzania wa bara,anaongea kiswahili…!”,walicheka sana,kamanda Philipo alishindwa kujibu alichoulizwa,wakamuona kama amepagawa,wakaendelea kumpatia huduma ya kwanza ili akili yake irudi katika hali yake ya kawaida.



      …………………………………



      “,Hapo hapo ulipo we malaya,ukijitikisa tunakumaliza……!”,kamanda Catherine aliangukia mikononi mwa magaidi takribani ishirini wa kisomali, walimzunguka na spidi boti, huku wakimtaka ajisalimishe.



      “,Nyie ni wakina nani? “,kamanda Catherine aliuliza, mikono yake ikiwa imekamatwa na magaidi kwa nguvu, wakamtupia ndani,katika boti zao.



      “,Alshabaab! huuu ni ukanda wetu wa Afrika mashariki, yoyote anayekatiza eneo hili ni mali yetu …!”,gaidi moja lenye rasta ndefu zilizosokotana liliongea, Catherine akashtuka, akaanza kuwaangaza kwa umakini, akitafuta mbinu ya kujiokoa.

      http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

      “,Mkamateni, mfungeni pingu, tuondokee naye! “,gaidi yule alitoa amri, magaidi wawili wakamsogelea kamanda Catherine, hapo ndipo walikipata cha mtema kuni, wakajuta kumsogelea, aliluka mateke mawili hewani, yakawapiga usoni magaidi wale, wakadondokea ndani ya maji, akachomoa bomu dogo,akachomoa pini akalitupa ndani ya boti,akajitupa ndani ya maji kama samaki.



      “,Puuuuuu! puuuuu! “,mlipuko ulisikika, boti moja ya magaidi ikalipuka,kiongozi wao aliunguzwa na mlipuko, akafa palepale pamoja na vijana wake wawili, magaidi wengine wakashindwa kuendelea kumtafuta Catherine, wakasogeza boti zao karibu, wakiwa hawaamini kilichotokea, bosi wao alikuwa amekufa palepale, machozi yakawatoka kwa uchungu,shambulio la sekunde moja tu kutoka kwa Catherine liliwachanganya sana na kuharibu kila kitu katika kundi lao.







      ITAENDELEA

    Blog