Search This Blog

Wednesday, 22 March 2023

UKURASA WA GAIDI - 3

  

Simulizi : Ukurasa Wa Gaidi 

Sehemu Ya : Tatu (3)


wa idara ya kupambana na ugaidi Tanzania yaani

C.T.I(Counter Terrorism Intelligence). Ni ajenti

namba moja kati ya maajenti wanaokwenda mstari

wa mbele kufanya kazi kwa vitendo (field agent) na

ni ajenti pekee aliyekuwa na uwezo wa kufanya

upelelezi na hata mapambano peke yake bila ya

kuwa na usaidizi.Mick ni ajenti namba moja kati ya

Maajenti sita wa idara ya C.T.I, maajenti watatu

wakiwa ni wa mstari mwa mbele kivitendo(field

agents) na watatu wakiwa ni maajenti wa usaidizi

(back up) waliofanya kazi zao nyingi ndani ya ofisi

na mara chache sana nje ya ofisi.

JIONI YA SIKU HIYO

Katika moja ya hoteli zilizopo katika kisiwa hiki cha

Ibiza, Mick anaonekana akipata chakula cha

jioni.Wakati huu ndipo alipowasha simu yake ya

mkononi aliyoifunga wiki nzima.Hakutaka

kusumbuliwa katika likizo yake.Hata televisheni na

kompyuta yake,alivitumia kwa nadra sana wakati

kama huu anapokuwa likizo.Alipenda kuishi kiasili

sana anapokuwa likizo. Muda mwingi

alijishughulisha kutembelea vivutio mbali mbali vya

Hispania ikiwapo majumba ya makumbusho ya

kihistoria na kujifunza mambo mbalimbali ya

kihistoria. Wakati mwingine alitembelea nchi

nyingine mbali mbali kama Italia,Ugiriki,

Korea,China na hata Japan.Yaani moja ya starehe

zake ilikuwa ni kujifunza historia mbali mbali na

hasa kwa nchi zilizokuwa na historia ndefu sana

tangu zama za kale(ancient time).Moja ya historia

aliyoipenda sana ni ile ya Korea ya kale na Mataifa

matatu yaliyowahi kuwapo katika nyakati hizo yaani

Koguryeo, Baekje na Silla.Lakini pia aliipenda

historia ya tawala za kirumi.

Wakati huu Mick alipoiwasha simu yake, message

mbalimbali ziliingia katika simu yake.Kulikuwa na

meseji mbali mbali kutoka mitandao ya kijamii na

zile za kawaida. Moja ya message iliyomvutia zaidi

ni ile ya kawaida iliyoingia katika laini yake namba

mbili ambayo hakupenda kuitumia sana na ni watu

wachache sana walioifahamu. Message ilisomeka

kwa Lugha ya kiingereza 'When the house is

burning call the resque team' (nyumba inapoungua

wapigie zimamoto).

"Kumekucha".Alijisemea Mick mara baada ya

kupata meseji hiyo.Dakika kadhaa baadaye Mick

alikwisha kufuatilia habari zaidi na kujua kinaga

ubaga nini kimetokea nchini.Baada ya kufuata

taratibu za kukodi ndege,saa chache baadaye

alikuwa yuko ndani ya 'pipa' ngani akielekea

nyumbani Tanzania, kuungana na idara nzima

kufanya kazi ngumu iliyokuwa mbele yao.

*********************************************

*****************************************************

Ndege aliyopanda Mick iliwasili uwanja wa ndege

wa JKIA(Julius Kambarage International Airport)

saa sita mchana.Mara baada ya kukamilisha

taratibu zote za ukaguzi wa uwanja wa ndege,

alielekea sehemu ya maegesho ya magari ambako

alikuta magari mbali mbali yakiwa yamepaki lakini

yeye akaliendea gari aina ya Range rover sport

nyeusi.Mick alikwenda moja kwa moja eneo la

matairi ya nyuma ya gari hilo, akapenyeza mkono

katika mlsehemu ya juu ya moja kati ya matairi

hayo kisha akapapasa katika.eneo hilo.Hapo

alifanikiwa kupata ufunguo wa gari hilo.

Moja kwa moja Mick alifungua mlango wa gari hilo

na kuingia ndani ambako alifungua droo katika

'dash board' ya gari hilo.Hapo akakuta bastola

mbili moja aina ya Beretta na nyingine ndogo aina

ya 'colt 45', pia kulikuwa na kiwambo cha kuzuia

sauti kwa jija lingine 'sailensa', magazine nne za

'beretta' zilizosheheni risasi, kiboksi cha risasi za

'colt 45'. Pia chini kabisa ya vitu hivyo alikuta

kikaratasi kimeandikwa 'Mahali salama Iringa.

Wengine watafuata'.Hapo Mick aliwasha gari na

kuondoka kwa kasi kuelekea Iringa.

Message iliingia katika simu ya Makassy "IRINGA".

Hapo hapo Makassy akamuita katibu muhtasi wa

C.T.I, Clara Makene. Sekunde chache baadaye

Clara alikuwa mbele ya mkuu wake wa kazi

akipewa maagizo. "Andaa kikao Maajenti wote

wahudhurie.Pia wasiliana na Kamanda wa E.C.S

( Elite Combat Squad). Mwambie nahitaji kuonana

naye masaa matatu kuanzia sasa.Ila kikao hiki

kiandae sasa hivi. Ndani ya nusu saa maajenti

wote muwe ndani ya chumba cha mikutano."

Alizungumza Makassy.

"Sawa boss". Alijibu Clara,katibu muhtasi wa C.T.I.

Wakati ambao idara ya C.T.I haikuwa na kazi

maalum zaidi ya upelelezi ule wa kung'amua kama

kuna tishio lolote la ugaidi linalotishia taifa, Clara

Makene alifanya kazi kama katibu muhtasi wa

C.T.I. Lakini kwa nyakati kama hizi ambazo

kulikuwa na kazi maalum iliyohitaji kupewa

kipaumbele , Clara alikuwa ni ajenti aliyepewa

namba nne katika idara ya C.T.I na namba moja

katika utaalamu wa teknolojia ya kompyuta.Clara

alikuwa na shahada ya pili ya teknolojia ya habari

na mawasiliano (information and communication

technology) aliyoipata katika chuo kikuu cha M.I.T

huko Marekani.Pia alikuwa ni mtaalamu wa 'data

analysis' kwa hiyo alikuwa ni data analyst

(mchambua data) wa C.T.I .Wataalamu wengine wa

kompyuta walikuwa ni ajenti Morris ambaye pia

alibobea katika masuala yote ya maabara na ajenti

Rachel ambaye pia alikuwa Daktari wa idara.

*************************************

Nusu saa baadaye, chumba cha vikao ndani ya

ofisi za C.T.I, maajenti wote kasoro ajenti Mick,

walikwisha kufika na kukaa katika viti vilivyomo

humo ndani. Zaidi ya ajenti Clara, Ajenti Morris na

Ajenti Rachel ; pia alikuwemo Paul Kumwembe,

ajenti namba mbili wa C.T.I ambaye alikuwa ni

ajenti wa mstari wa mbele(field agent) ambaye pia

alikuwa ni mtaalamu aliyebobea katika masuala ya

ulengaji wa shabaha, na mwisho alikuwepo ajenti

Jackline, ajenti namba tatu kati ya maajenti wa

mstari wa mbele( field agent) ambaye pia ni

mtaalamu wa kupangilia vikosi vya kimapigano.

Jukumu namba mbili Jackline lilikuwa ni kumsaidia

kiongozi wa kikosi maalum cha mapigano cha

C.T.I cha E.C.S kamanda Joshua Mwambinga

katika uwanja wa vita.Kwa lugha ya kitaalam

Jackline alikuwa ni 'Second in comand' wa E.C.S.

"Nadhani wote mumekwisha kuhisi sababu ya

kuwaita katika kikao hiki. Tukio lililotokea hapa

nchini ni tukio linalotuhusu sisi kuliko mtu

mwingine yeyote. Idara hii ilianzishwa ili ilifae taifa

kwa nyakati kama hizi.Kwa sababu hiyo ,tuna

sababu ya kuanza kazi mara moja.Tunaachana na

masuala mengine yote ya kiusalama na tunalipa

suala hili kipaumbele. Tuna chini ya miezi mitatu

kukamilisha kazi iliyo mbele yetu. Nimeongea juu

juu kwa kuwa Clara atatueleza mambo haya yote

kwa kina."Aliongea Mkurugenzi Eliackim Makassy.

Clara Makene, binti mzuri na mrembo kwelikweli,

alitembea kutoka alipokaa na kwenda katika meza

iliyokuwa mbele yake umbqli wa mita kama sita

hivi mbele yake. Juu ya meza hiyo kulikuwa na

kompyuta mpakato pamoja na 'projector'.Clara

akachomeka waya maalum wa 'AVG' upande

mmoja katika 'projector' na upande mwingine

katika kompyuta mpakato. Kisha akabonyeza hapa

na pale katika vifaa hivi vilivyokuwa mbele

yake,'projector' na kompyuta vikawaka.Taa katika

chumba hicho zikazimwa nakufanya 'projector'

kufanya kazi yake vizuri zaidi. Kilichokuwa

kikionekana katika kompyuta ile kilionekana katika

ukuta mweupe , mbele walikokuwa wanatazama

maajenti wote wa C.T.I.Taswira mbili zilionekana

ukutani kwa msaada wa 'projector'.Picha za Omar

AL-Mahmood na Abdallah Yusoof zilionekana

vizuri kabisa mbele yao wote.

"Omar Al Mahmood,mrefu wa futi nane,mtaalamu

wa kutengeneza milipuko ya aina mbalimbali

kutoka huko Urusi.Amewahi kufanya kazi katika

idara ya kipelelezi ya KGB enzi za serikali ya ki-

SOVIET. Alikuwa ni 'special agent' na pia 'head of

field operations' ndani ya KGB kabla ya

kubadilishiwa majukumu na kuwa mkufunzi wa

'martial arts' na matumizi ya silaha kwa maajenti

wanafunzi.Aliondoka katika nchi ya Urusi mara tu

baada ya USSR( United States ofSoviet Repablic)

kuvunjika mwanzoni mwa miaka ya 90 kwa kuwa

alikuwa mkereketwa wa sera za ki-soviet.Alirudi

katika asili yake na alikozaliwa nchini

Afghanistani.Alipotea machoni pa wengi kabla ya

baadaye kusemekana kuwa amejiunga na kikundi

cha kigaidi cha Alquaeda.kisha baadaye kuhamia

Somalia kama moja ya viongozi wa ngazi za juu

na waanzilishi wa kikundi cha kigaidi cha

Alshabaab." Aliongea Clara kisha akakohoa kidogo

kuiandaa sauti yake kuanza kutoa maelezo

mengine tena.

Ajent Clara akaanza kubonyeza keyboard ya

kompyuta ile tena.Mara baada ya kubonyeza hapa

na pale,picha ya Omar Al Mahomood

ikapotea,picha nyingine ikajitokeza kwa ukubwa

kama ile picha iliyopita.

"Mtuhumiwa namba mbili, Abdallah Yusoof

Fatawi.Mtaalamu wa teknolojia ya habari na

mawasiliano ama 'ICT' aliyebobea sana na

mtaalam wa mambo yote ya kompyuta

kiujumla.Amekwisha wahi kufanya kazi idala ya

inteligensia ya ISI(Inter Service Intelligegence) ya

huko Pakistani.Alitoroka na kukimbilia India baada

ya kugundulika kuwa anavujisha siri za ki-

intelijensia za Pakistani kwa idara ya kipelelezi ya

nchi ya india 'RAW'.Baada ya kukaa kwa muda

nchini India, Yusoof alihamia Afghanistani na

kulowea huko kwa muda mrefu kabla hajajiunga na

kikundi cha kigaidi cha Alquaeda. Mara utaalamu

na ujuzi wake ulipoonekana kuwa na tija ndani ya

kikundi hicho,alipandishwa na kuwa katika uongozi

wa juu wa Alquaeda. Alikuja kuhamishiwa Somalia

baada ya miaka kadhaa ili kukiongeza nguvu

kikundi cha Alishabaab. Yusoof ni mtaalamu pia

wa mapigano ya mwili kwa mitindo ya

karate,taekwondo na kick-box , mrefu wa futi 7.8

na kati ya waharifu hatari zaidi na asiyewahi

kukamatika duniani".Akamaliza kuongea

Clara,kisha akarudi mahali alipokaa mwanzoni.

Kikao kiliendelea kwa kuongelea na kupanga

mambo mbalimbali kuhusiana na kazi iliyokuwa

inaikabili idara hii nyeti.

"Jambo la muhimu ni kuwatambua hawa walengwa

wetu wakuu kwa sasa.Tufanye jitihada za hali ya

juu kuwatambua mahali walipo ili hatua nyingine

zifuate.twapaswa kutambua kuwa tunaenda

kupambana vita nzito sana na hawa wahalifu wa

kimataifa."aliongea mkurugenzi kisha akaendelea

"Kwa kuhitimisha naomba tujiandae kwa safari ya

kwenda 'safe house' ya Iringa ambako ndiyo

kitakuwa kituo chetu kikuu katika kesi hii.Tukutane

Iringa kesho asubuhi na pia bila kusahau,tumepew

a miezi mitatu tu kukamilisha suala hili.Miezi hii

ikiisha basi tutanyang'anywa hili suala na kisha

litakuwa mikononi mwa Taifa la Marekani.Hii

itakuwa aibu kwetu.Kwa hiyo kabla miezi mitatu

haijaisha angalau tuwe na uelekeo wa kung'amua

wahalifu hawa walipo."Alimaliza kuongea

mkurugenzi na kikao kikaahirishwa.

Baada ya muda mkurugenzi Makassy alikuwa na

kikao na kamanda wa kikosi cha ECS , Kamanda

Joshua. Waliongea wakipanga hili na lile kisha

wakaagana.Kamanda wa ECS(Elite Combat Squad),

akaenda kupangilia askari wake wa weledi kwa ajili

ya safari ya kuhamia Iringa pamoja na kuwaweka

tayari kimapigano wakati watakapohitajika kufanya

hivyo



IRINGA

SAFE HOUSE

Hadi kufikia siku iliyofuata asubuhi, idara yote ilikuwa imehamia Iringa katika moja ya nyumba ambazo inazimiliki Tanzania. Katika mikoa yote iliyo jirani na mikoa iliyo mpakani mwa nchi,C.T.I ilimiliki nyumba moja kama hii. Kwa kuwa mkoa wa Mbeya unapakana na nchi ya Malawi na Zambia, nyumba ilijengwa katika mkoa jirani wa Iringa.

Kiuhalisia si kwamba nyumba ilikuwa mpya. Nyumba ile ilikuwa imefanyiwa ukarabati kutoka kuwa ghala la chakula na kurekebishwa kuwa jumba la kisasa sana.Jumba hili lilikuwa na vyumba kadhaa vya kulala pamoja na ofisi kubwa na ofisi ndogo ndogo pamoja na vitu vingine vingi sana.Hata namna ya kuingia katika nyumba ile haikuwa kazi nyepesi. Kulikuw na vitasa vya kisasa katika nyumba hii ambavyo vilihitaji namba ya siri, alama za vidole pamoja na mtazamo wa mboni ya jicho ili kufungua.Walio weza kuingia ndani ya nyumba hii ni wale wahusika tu. Hawa ndio pekee ambao teknolojia inayohusika kwa sababu za usalama katika nyumba hii ilikuwa imelishwa taarifa zao.

Maajenti wa idara hii ya CTI,walikuwa wamekusanyika katika ofisi kubwa ya pamoja wakifanya hili na lile pamoja na kupanga hiki na kile ili mradi kuweka mambo sawa.Chumba hiki cha ofisi, kilikuwa kimetawaliwa na kompyuta kadhaa zilizounganishwa kwa utaalamu wa hali ya juu huku zikitumia 'soft wares' za kisasa kabisa zinazohusika na kazi hii ya upelelezi. Yaani kwa kifupi kazi ilikuwa inaanza kuoamba moto rasmi wakati huu.

********************************************************

"Clara, hebu jaribu ku-hack mfumo wa kamera za CCTV za jeshi kikosi cha jkt Mafinga uangalie kilichorekodiwa kwa muda wa wiki moja nyuma kabla ya tukio kutokea." Aliongea Mick na kusikika kwa ajenti Clara upande wa pili kupitia kifaa cha mawasiliano alichokivaa sikioni.

"Ok acha nifanye yangu ".Alijibu Clara kutoka upande wa pili na kisha sauti ya vitufe vya kompyuta ikaanza kusikika ikibonyezwa bonyezwa kwa kasi ya ajabu.

Wakati huu ambao wawili hao walikuwa wanawasiliana, Clara alikuwa yupo ofisini wakati Mick yupo msituni,mahali ambapo palitokea tukio siku mbili tatu nyuma.Tukio lililosababisha wanaidara wa C.T.I kujikuta wana jukumu zito la kufanya mara baada ya kuwa na majukumu ya kawaida tu kwa muda mrefu.

Tangu asubuhi,wakati idara yote ya C.T.I ilipokuwa imewasili katika eneo hili, Mick alikwenda mahali pale na kuanza kazi yake eneo la tukio mara moja.Akiwa amekwishapata taarifa za awali za nini kilichojiri,moja kwa moja Mick alijua ni wapi pa kuanzia. Alikumbuka moja ya kauli mbiu ya idara yake iliyosema "katika tukio lolote, ni vizuri na lazima upelelezi uanzie eneo la tukio kwa sababu ndiyo mahali pekee ambapo utapata ushahidi au fununu zitakazokupeleka kwenye ushahidi". Na ni ukweli mtupu unaoongelewa katika kauli mbiu hii.Idara yoyote ya usalama duniani inapofanya upelelezi wa tukio fulani,ni lazima itafika eneo la tukio kwa sababu ya mambo mawili.Ushahidiau fununu au kama mataifa ya magharibi yaliyotufundisha mambo haya wanavyosema kwa lugha yao 'either clue or evidence'.

Kwanza kabisa baada ya kufika eneo la tukio,ajenti Mick alimuhoji mmoja wa askari waliokuwa wanalinda eneo hilo.Wakati alipomuhoji,Mick aliweza kung'amua kuwa magaidi wale walikhwapo muda mrefu,pengine masaa mawili matatu kabla ya msafara kupita na kushambuliwa.Aling'amua kuwa magaidi wale walikuja kwa pamoja eneo hilo na kisha wakatawanyika kila upande nyuma ya misitu ya eneo lile la tukio na ndiyo maana ilikuwa vigumu kupambana nao.Pia alihisi,kwa jinsi eneo lilivyokuwa msituni basi magaidi hawa yawezekana waliletwa eneo lile kwa usafiri fulani mahali pale.Kwa maelezo ya askari aliyehojiwa Mick ,aliweza kung'amua upande ambao inawezekana ndiko magaidi wale walikoikia kabla ya kutawanyika kuzingira eneo lote.

Ndiyo.Ilikuwa ni rahisi kwa Mick kung'amua mambo haya kutokana na maelezo ya askari yule wa weledi wa E.C.S waliokuwa chini ya C.T.I ambaye alikuwa miongoni mwa askari waliokuwa wakilinda eneo lile la tukio ili ushahidi usipotee.Kilichopelekea askari yule kutoa maelezo kwa kina ni kwa kuwa pia alikuwa ni miongoni mwa askari waliosindikiza msafara uke uliovamiwa.Askari yule alimueleza ajenti Mick upande ambao risasi nzito zaidi kutoka kwa adui ziliwashambulia.Na ni upande huo huo ambako upinzani mkubwa ulitokea kuliko upande wowote.Mick aliposikia hayo aliweza kuhisi kuwa yawezekana upande huo ndiko upande ambao adui walikuwa wengi zaidi.Pia yawezekana risasi nzito kwa maelezo ya askari,zilitokea katika bunduki nzito nzito zilizofungwa katika magari ya adui.Basi kwa kusikiliza hayo na kuyachambua kichwani Mick aliuhisi upande huo na kuanza kufuatilia,akitokea barabara ya lami na kuingia msituni.

Mick alipasua msitu na kuukabili hadi kilometa moja na nusu msitu ukipoishia. Wakati huu wote,alikuwa anafuata njia za vumbi ambazo zilitawaliwa na tope katika msimu huu wa mvua Akitumia gari alilokabidhiwa,aina ya Range rover sport nyeusi iliyong'ara sana,Mick alifuatisha barabara ya vumbi iliyokuwa inapita nyuma,upande wa pili wa msitu huu kwa umbali wa kilomita moja tena. Kama ingepigwa picha kutoka juu sana,ama kama ilivyoonekana kwa picha za satelite, barabara hii ilikuwa upande wa pili wa msitu huu wa 'mipaina' ikionekana kwenda ki-msambamba na barabara ya lami.

Kilomita moja mbele ,Mick aliweza kung'amua alama za matairi ya magari zinazoingia msituni.Kilichompa dukuduku zaidi kuwa huenda hicho ndicho alichokuwa ankitafuta,ni kuwa alama zile zilizojichora katika tope zilionesha kuwa magari zaidi ya nane yalipita eneo hili na kuchepuka kuingia msituni.Alama hizi zilinoga zaidi eneo la miti michanga ambapo miti ilikanyagwa sana.Akiwa ameshuka kutoka garini,kwa miguu yake Mick alipasua pori na kuanza kufuatilia matairi hayo huku bastola yake aina ya bereta ikiwa kiunoni na ile ndogo ya 'colt 45' ikiwa imepachikwa katika soksi mguu wa kulia.Kufuatilia huku kulimpeleka hadi mita 300 ndani ya msitu ule,eneo ambalo alama za matairi ya magari yale ziliishia.Hapo Mick aliona kitu ambacho kilimuhakikishia kuwa adui walifikia katika eneo hili na kisha kutawanyika.Eneo lilikuwa limetawaliwa na maganda ya risasi kwa uwingi hasa. Maganda ya risasi kutoka katika bunduki nzito nzito yalikuwa yametawanyika katika eneo hili.Bunduki ambazo aidha zilikuwa zimefungwa kwenye magari au hata kama zilibebwa na magaidi wale basi wasingeweza kutembea nazo kwa umbali mrefu kutoka katika gari kutokana na uzito wake.Hili nalo lilizidi kumthibitishia kuwa hapa ndipo maadui walifikia nakutawanyika kufanya mashambulizi.

Baada ya kujihakikishia kwa hili,Mick alirudi katika gari lake na kuanza kufuatilia alama zile.za magari zilizokatisha msituni na kuishia mahali alikokuta maganda ya risasi mengi,upande zilikotokea kabla yakukatisha porini hapo.

Akiwa anaendesha gari lake huku akifuatilia alama za matairi za magari haya mahali zilikotokea, alama hizi zilimpeleka kilomita nane mbele,mahali ambako barabara hii ilipita nyuma ya kambi la jeshi la kujenga taifa.Kambi ya Mafinga.

Hapa Mick aliona alama za matairi zikiwa zimechepuka kidogo na kisha mbele kurudi usawa wa mwanzo.Alama hii ilikuwa ni ya matairi ya gari dogo.Mick alipaki gari pembeni, akashuka na kuchuchumaa kuangalia kwa umakini alama zile huku akionekana kutafakari jambo.

"Hapa yalipita magari madogo mawili na makubwa au labda malori sita.Kati ya haya magari makubwa kulikuwa na magari aina ya TATA mawili, IVECO mawili na ISUZU mawili.Hapa alama za matairi zinazoonekana kwenda pembeni kidogo nakisha kurudi usawa wa mwanzo na kutengeneza 'curve', kuna gari moja kati ya magari makubwa lilipaki kando na kisha kuendelea na safari,labda kuna jambo wahusika walifanya nje ya gari."Aliwaza ajenti Mick ndani ya kichwa chake.Kisha akageuka nyuma na kuona ukuta wa fensi upande wa nyuma wa kambi hilo ulivyo mrefu.Kisha baada ya ukuta huo kwa ndani kulikuwa na msitu wa miti mingi aina ya milingoti na miti ya matunda mingi. Majengo hayakuonekana labda utumie kiona mbali kutokana na msitu ulivyoshona mahali hapo,hivyo Mick akatambua kuwa si rahisi kwa walio ndani kujua nini kinaendelea nje.Lakini alipokaza macho vizuri, aliona kamera za CCTV zilizofungwa kwa juu katika jengo hilo ambapo kama si utaalamu na uzoefu wa kazi yake pengine asingeziona.

Na hapo ndipo alipowasiliana na ajenti Clara ili amsaidie kwa utundu wa kompyuta kuingilia mfumo wa kamera hizi na ikiwezekana kuibia mambo yaliyorekodiwa nyakati za tukio lile lilipotokea.

Mara baada ya kuwasiliana na ajenti Clara,Mick alirudi katika gari lake na kuendelea kufuatilia alama za matairi alizokuwa anazifuatilia tangu mwanzo.Alifuatilia zilikotokea kabla ya eneo hili alikotoka.Mbelealimaliza eneo la usawa wa jeshi.Mbele kidogo ya hapo alikutana na magari yanayobeba mbao yakitokea katika upande mmoja wa barabara hii ya tope na kwenda porini kwa kufuata barabara nyingine.Hii barabara iliyofuatwa na malori haya na ile inayotoka nyuma ya jeshi zimeunganishwa kwa barabara moja huko zilikotokea.Kwa sababu hiyo ikawa siyo rahisi kwa Mick kuweza kuendelea kung'amua alama zile za matairi alizokuwa anazifuatilia kwani zilichanganyika na alama za matairi za malori yale naa pengine zilifutwa kabisa na kubaki alama za malori yale.

Akiwa amekata tamaa ya kufuatilia kile alichokuwa anakifuatilia,akaona si vibaya akiuliza kitu kutoka kwa bwana mmoja aliyekuwa akibadilisha tairi katika roli lake lililokuwa tupu.Bwana huyu alionekana kama ndiye dereva wa gari lile na kwa upande ambao gari lake lilitazama,ilionekana kuwa ndiyo anaenda kufuata mzigo wa mbao.

"Samahani braza".Mick alianzisha mazungumzo na dreva yule ambaye ndiyo kwanza alikuwa amegundua kuwa kuna mtu nyuma yake.

"Bila samahani kaka sijui nikusaidie nini".Alijibu kwa staha dreva yule hasa kutokana na unadhifu wa huyu mgeni wa ghafla(Mick).Ama kwa hakika jinsi dreva huyu alivyoongea kwa adabu ungeweza kudhani kuwa madreva wa malori ni watu wa staarabu sana.Lakini kumbe...........

"Hivi ni kwa nini mnapita njia ndefu na malori yenu. Mbona kuna njia fupi hii inayopita nyuma ya jeshi au wajeda wanamaindi nini.?" Alihoji Mick.

Yule dreva aliyeulizwa swali hili akamuangalia Mick usoni kwa sekunde kadhaa kwa kukereka kisha akafungua mdomo wake.

ITAENDELEA

UKURASA WA GAIDI - 2

  

Simulizi : Ukurasa Wa Gaidi 

Sehemu Ya : Pili (2)


iliyojengeka katika mwili wake ule.Usoni

alionekana kama mtu aliye na umri wa miaka

mwishoni mwa arobaini au mwanzoni mwa miaka

hamsini.

Mara mtu huyu alipokanyaga ardhi,watu kadhaa

waliokuwepo mahali hapo wakiwa webeba bunduki

zao, walipiga goti moja chini na kukunja mkono wa

kulia mbele huku wakiinamisha ichwa chini usawa

wa mkono uliokunjwa kama ishara ya heshima

kubwa.Kwa kuwaangalia tu, ilionekana huyu

aliyekuwa mbele yao alikuwa mtu mkubwa na

mwenye kuheshimiwa sana na watu hawa.

Bwana yule akawataka watu wale

wasimame,akawakumbatia kila mmoja na

kuwabusu katika paji la uso huku akizungumza nao

kwa lugha ya kiarabu.Wakati huo huo helkopta

nyingine ikawasili eneo hilo.Hii ilikuwa na chapa

ya shirika la utangazaji la CNN. Bwana mkubwa

yule akaongozwa na watu wake hadi katika

helkopta ile na baada ya kupanda ikapaa na

kutokomea kutoka katika eneo hilo. Sekunde

chache baada ya helkopta ile kupaa, ile helkopta

iliyotumika kubeba gari, ililipuka na kuteketea

kabisa.

*********************************************

*****************************************************

"Breaking news".Ndivyo vioo vya luninga

vilivyosomeka siku hiyo.Vituo mbali mbali vya

televisheni vilikatisha matangazo ya kawaida na

kurusha habari hizi mpya zilizokuwa na msisimko

kuliko habari nyingine.Vituo vikubwa vya

televisheni na radio viliripoti moja kwa moja

kutoka eneo la tukio.Makamanda waliohusika

kuongoza msafara ule walihojiwa nao wakatoa

ushirikiano wa kutosha. Vyombo vya habari vya

kimataifa kama BBC,CNN,ALJAZEERA na Sky News

navyo viliripoti kupitia wawakilishi wake.Dunia

nzima ilipata habari hizi za kuogofya moja kwa

moja kwamba yule gaidi aliyeisumbua dunia kwa

uhusika wake katika matukio mbalimbali bwana

'Omar Al-Mahmood' ametoroka tena kutoka katika

ulinzi mkali sana.

Usiku ulipita,siku mpya ikaanza kwa mchaka

mchaka wa hali ya juu.Jua lilichomoza wakati

makachero wa polisi na wanausalama wa vitengo

na idara mbali mbali wakiwa wamemwagwa kila

kona ya nchi. Wanausalama walipewa maagizo ya

kuacha kazi nyingine zote zisizo na uhitaji wa

haraka na kipaumbele chao kiwe ni kesi hii

iliyokuwa mbele yao. Kesi ya kutoroshwa kwa

gaidi aliyesemwa kuwa ni hatari sana zaidi ya

magaidi waliowahi kutokea katika historia ya bara

la Africa.

Baadhi ya wananchi walisikika wakitoa sifa kwa

kituo cha habari cha CNN kwa kuwahi kuelekea

eneo la tukio kabla hata mapambano hayajapoa

vizuri. Watu wengine walienda mbali zaidi kwa

kusema kuwa vyombo vya habari vya Tanzania

vimelala sana.Wapelelezi waliomwagwa kila kona

ya nchi walisikia habari ya helkopta ya shirika la

habari la ' CNN' kuonekana ikielekea eneo la tukio

kabla hata watu hawajajua ni nini kinaendelea.Lak

ini haikuchukua muda kwa wapelelezi kujua kuwa

ilikuwa ni helkopta ya 'CNN feki'. Magazeti nayo

hayakuwa nyuma kiripoti habari hii.

Gazeti la 'MTANZANIA MZAWA' liliandika " Gaidi wa

kimataifa aliyekamatwa na vyombo vya usalama

vya marekani kwa kushirikiana na Tanzania

ametoroshwa kutoka chini ya ulinzi mkali

alipokuwa anasafirishwa mara baada ya kutokea

mapambano makali sana.Gaidi huyo alikamatwa

katika mpaka wa Tunduma mkoani Mbeya wakati

alipokuwa akitaka kutorokea nchini

Zambia.Mapambano haya yalitokea baada ya

msafara huo kuvamiwa na kundi kubwa la watu

wanaodaiwa kuwa ni magaidi kutoka nchini

Somalia. Aidha maswali ambalo watu wengi

wanajiuliza sasa ni kuwa inawezekana vipi kundi

kubwa la magaidi kuvuka mipaka yetu na kuingia

nchini kwetu bila vyombo vya usalama kung'amua?

Na ni vipi watu hawa wavushe silaha nyingi kiasi

kike bila vyombo vya usalama kuona?"



AGOST 7, 1998

Siku hii ni kati ya siku ambazo wanaafrika

mashariki hawataisahau. Ofisi za ubalozi wa

Marekani nchini Tanzania na ubalozi wa Marekani

nchini Kenya zililipuliwa na Magaidi.Wahusika

walikuwa ni magaidi wa kikundi cha Alquaeda.

Moja kati ya watu waliotekeleza kusuka mipango

ya kufanikisha tukio hilo ni Omar Al-Mahmood.

Waweza kujiuliza Omar Al-Mahmood ni nani

kiundani sana? Ni mmoja wa viongozi wa ngazi za

juu wa Al-shabaab.Anasifika sana kwa kuwa na

ushawishi,utashi na kuwa na misimamo mikali

sana. Wakati wa mkakati wa kutekeleza matukio ya

kigaidi katika balozi za marekani nchini Tanzania

na Kenya, kikundi cha alquaeda kilifanya

mazungumzo na kikundi rafiki cha al-

shabaab.Wakati huo kikundi cha Alshabaab

hakikuwa na umaarufu kama ilivyo sasa bali

kilikuw ndiyo kwanza kinachipua bado.Mawasiliano

haya yalikuwa yamefanyika kwa kuwa iliaminika

Somalia iko karibu na Kenya na Tanzania hivyo

wanafahamu vizuri nchi hizi kuliko alquaeda

ambao makao makuu yao yapo Afghanistan. Omar

Al Mahmood alifanikisha tukio hili kwa mipango

yake yenye utashi na utaalamu wa hali ya juu.

Siku hiyo (August 7, 1998) alfajiri,gari lililobeba

milipuko (mabomu) lilionekana nje ya ubalozi wa

Marekani barabara ya Laiboni mahali ambako

ubalozi huu ulikuwepo.Gari hilo lilikuwa likienda

kasi na kutaka kuingia ubalozini moja kwa moja.

Lakini lilizuiliwa na lori la maji lililokuwa

linamilikiwa na ubalozi huo.Baada ya muda kidogo,

gari hili lililipuka kwa kishindo na kujeruhi na kuua

watu kadhaa.

********:*************

C.T.I

Idara ya kupambana na ugaidi Tanzania iliundwa

mwaka 2002. Hii ilikuwa ni miaka minne imepita

tangu lilipotokea shambulio la ugaidi katika ubalozi

wa Marekani nchini.Mara tu baada ya tukio la

ugaidi kutokea, nchi ya Tanzania iliona ni vyema

kuanzishwa kwa idara hii huru. Hili lilishauriwa na

wakuu wa mambo ya usalama kwa kuzingatia

kuwa ,suala la kupambana na ugaida lilikuwa chini

ya idara ya usalama wa taifa (TISS) ambayo ndiyo

idara kubwa ya intelijensia nchini.Kwa kuwa

Tanzania ilikwishaonja joto la ugaidi wakati huo,

ilionekana ni vyema ikianzishwa idara maalum kwa

ajili ya kupambana na ugaidi pekee. Hapo ndipo

idara hii ilianzishwa ikiwa na mamlaka kamili ya

kupambana dhidi ya ugaidi au tishio lolote la

ugaidi kutoka ndani na nje ya nchi.

Idara ya C.T.I(Counter Terrorism Inteligence),il

iundwa na vitengo vikuu vinne. Wapelelezi

walioenda kufanya kazi kwa vitendo uwanja wa

mapambano ( field agent ), wataalamu wa

teknolojia ya kompyuta(information technology/

data analysis), wataalamu wa maabala na kikosi

cha askari maalum wenye weledi wa hali ya juu

kwa mapambano kinachoitwa E.C.S(Elite Combat

Squad).

OFISI ZA C.T.I DODOMA

Mkurugenzi wa idara hii nyeti bwana Eliakim

Makassy alikuwa ana harakati nyingi sana ofisini

mwake.Hii ilitokana na kazi ngumu ambayo ilikuwa

inaikabili idara hii iliyo chini yake.Tangia hapo jana

alipopata taarifa rasmi ya matukio yote

yaliyojitokeza likiwepo la kutoroka kwa gaidi hatari

zaidi Africa kwa kuratibu matukio mbalimbali ya

ugaidi, hakutulia kabisa. Mara ashike karatasi

hili,mara apige simu pale, mara acheze na

kompyuta iliyokuwapo mezani.Yaani ili mradi

alikuwa bize kuliko kawaida.

Kazi kubwa aliyokuwa anaifanya katika kompyuta

iliyokuwa mbele yake, ni kufuatilia kiumakini zaidi

majina mawili.Omar Al-Mahmood na Abdallah

Yusoof.Si kwamba ilikuwa ni mara ya kwanza

kuwafuatilia watu hawa.La hasha.Hata kuanzishwa

kwa idara hii ulitokana na tukio lililomuhusisha

Omar Al Mahmood.Baada ya kuanzishwa kwa idara

hii, kazi yao kubwa ya kwanza ilihusiana na

kukusanya data mbali mbali kumuhusu Omar.Na

hata wakati wakikusanya data mbalimbali

kumuhusu, ndipo jina La abdallah Yusoof

likajitokeza mara kadhaa ndani ya upelelezi

wao.Kujirudia kwa jina La Abdallah Yusoof katika

matukio yaliyofanywa kwa mipango ya Omar Al

Mahmood, kulisababisha waanze kufuatilia haba ri

zinazomuhusu Abdallah Yusoof. Upelelezi huu

ulipofika hatua kadhaa mbele, ulisababisha Yusoof

awekwe katika vipaumbele vyao kati ya watu

wanaotafutwa zaidi.

Eliakim Makassy alikuwa akichambua taarifa

mbalimbali muhimu kutoka katika taarifa nyingi

walizokuwa nazo ndani ya idara.Pengine inaweza

kushangaza.Kwamba mkurugenzi ni mtu mzito

sana.Kwa nini afanye kazi ya kuchambua taarifa

badala ya kumpa kazi hiyo mtaalamu wa

kuchambua data(data analyst)? Makassy alikuwa

mkurugenzi wa tofauti sana. Kwanza alipenda

kujishughulisha kwa kila jambo ambalo lilikuwa

ndani ya uwezo wake. Yaani wakati mwingine

kama mtu angeingia katika ofisi za idara hii,

pengine angeweza kukaa hata masaa mawili bila

kutambua kuwa mkurugenzi wa idara hii ni

nani.Alijichanganya na maajenti wengine na

kufanya nao kazi kila alipopata nafasi. Lakini mbali

na kupenda kujishughulisha tu,Makassy alikuwa ni

mtaalamu wa mambo ya kompyuta.Hivyo wakati

mwingine maajenti wanaohusiana na utaalamu wa

kompyuta wakiwa na majukumu mengi sana

aliwasaidia kazi hii kwa mikono yake.

"Ngrii ngrii". Simu ya mezani iliita.Makassy ni

kama alitegemea simu hii kuita kwa namna ali

yoipokea haraka kabla haijaita mara ya pili.

"Hallow. C.T.I hapa."

"Unahitajika Ikulu haraka kadri inavyowezekana."

Upande wa pili ukaongea

"Sawa . Niko njiani".Alijibu Makassy.Kisha alipanga

makabrasha mawili matatu na kompyuta mpakato

yake katika begi dogo la mkononi kisha

akatokaofisini kwake.Alielekea moja kwa moja

katika kiwanja kidogo kilichokuwa nje ya ofisi za

C.T.I.Hapo alipanda katika helkopta moja iliyokuwa

imepaki hapo, kisha akaipaisha kuelekea Dar es

salaam.

IKULU.Dar es salaam

Baada ya muda,Makassy alitua helkopta yake

sehemu maalum ndani ya viwanja vya ikulu.Mara

baada ya taratibu mbili tatu kukamilika, aliongozwa

na mtu mmoja anayehusika na usalama ikulu hadi

katika ofisi ya Rais George Katumba.Mara

alipoingia katika ofisi hii, alimkuta rais anaongea

katika simu ya mezani.Zaidi ya raisi pia alikuwepo

waziri mkuu wa Tanzania mheshimiwa Abdulahman

Mohamed, pamoja na waziri wa ulinzi

muheshimiwa Michael Josheph Magombe. Rais

akaonesha kwa ishara tu, kumtaka Makassy akae

kwenye moja ya sofa zilizokuwa katika ofisi

hiyo.Mara baada ya kumaliza kuongea na simu,rais

alisabahiana na Makassy kisha akatoka katika kiti

chake cha kiofisi, na kwenda kukaa katika sofa

nyingine iliyokuwa inamtazama kiupande upande

Makassy.

"Ndiyo bwana Makassy, nadhani utakuwa

umekwisha kuhisi jambo tunaloelekea

kuzungumza.Ama niseme nadhani ulikuwa

unasubiri kusikia kutoka kwangu ili uanze mara

moja kufanya jambo hili linaloihusu idara

yako."Alianza kuongea Rais kisha akaendelea"

Sasa ninaweka suala hili mikononi mwako kuanzia

sasa kazi ianze mara moja. Nimeongea na

Marekani ambao ndiyo walikuwa wanaendesha

oparesheni ya kumkamata Omar Al Mahmood

kabla hajakimbia na kukamatwa mpakani akitaka

kwenda Zambia kisha kutoroshwa tena. Wao

wamesema kuwa kwa kuwa haya ni mambo ya

ndani ya Afrika, yanausikiliza umoja wa nchi za

Afrika utakavyoamua. Nimezungumza na umoja wa

Afrika, tumefikia muafaka.Tumepewa miezi mitatu,

kama hakutakuwa hata na mafanikio kidogo, basi

itabidi tuwaachie Marekani wafanye kazi hii. Kwa

hiyo idara yako inatakiwa kuonesha mafanikio juu

ya kazi hii kabla miezi mitatu haijaisha. Serikali

itakuwa bega kwa bega nyuma yako na itakupa

kila msaada utakaohitaji katikakufanikisha

hili.Tambua Afrika yote, na nchi zote zilizo mstari

wa mbele kupambana na ugaidi ziko nyuma

yako."Alimaliza kuongea rais.

"Ahsante sana muheshimiwa kwa kuiamini idara hii

na kuikabidhi kazi kubwa hivi.Naahidi

hatutakuangusha. Ila ninaomba tu vyombo vingine

vyote vya usalama viendelee na majukumu yao ya

kawaida na waachane na kesi hii, hadi pale idara

hii itakapo hitaji msaada wao".Aliongea Makassy.

"Sawa hilo halina shaka".Aliongea rais.

"Sijui kama kuna la nyongeza"Alihoji rais huku

akiwaangalia waziri mkuu na waziri wa ulinzi.

"Nadhani uko sawa kabisa"Aliongea kwa kifupi

waziri mkuu.

"Hata mimi nadhani muheshimiwa umeongea vizuri

sana.Nadhani hii idara inastahili kabisa kufanya

kazi hii kwa kuwa inaongozwa na mtu makini

sana.Nadhani cha msingi tu kuendelea

kushikamana na kuwasiliana kila mahali ambapo

idara hii itafikia. Nadhani tutalifumbua fumbo hili

kwa ustadi wa hali ya juu." Aliongea pia waziri wa

ulinzi.Mmoja wa mawaziri waliosifika sana kwa

kuwa wazalendo.

Baada ya hapo waliongea kuhusu mipango mbali

mbali ambayo Makassy alikwishafikiria kuhusiana

na suala lililokuwa mbele yao.Baada ya hapo

waliagana, Makassy alirudi Dodoma kuanza

kutekeleza kazi ambayo idara ya C.T.I ilipewa.

HISPANIA

Visiwa ya Ibiza

Jua lisilo na miale mikali liliwaka huku upepo

mwanana wa bahari ukivuma taratibu bila

bugdha.Watu wengi walikuwepo katika eneo la

ufukwe wakipunga upepo ,wengine wakiwa na

wenzi wao na wengine na familia zao.Ilikuwa ni

kipindi cha mwisho wa wiki hivyo watu wengi

walifika pale kwa mapumziko ya wikiendi.

Japo wengine walifika kwa mapumzikobya wiki

endi tu, lakini kuna baadhi ya watu walikuwa katika

mapumziko ya likizo ya muda mrefu.Hasa wale

waliokuwa na pesa za kutosha na waliojua

kuzitumbua pesa hizo walikaa mahali hapa

hadibpake limizo zao zilipokwisha. Mmoja wa watu

hawa ni kijana Mmoja wa Kitanzania.Kwa

muonekano wake ,ni mrefu wa wastani mwenye

sura na haiba ya kuvutia, mwenye mwili wa

wastani uliojengeka kimazoezi. Kwa Jina anaitwa

Mick-Reuben Garino.

Wakati huu alikuwa amejilaza katika mchanga

akiwa na mrembo mmoja wa kihispania ambaye

amekuwa akimpa kampani kwa kipindi chote cha

likizo hii.Hadi sasa,Mick alikiwa ni kijana wa umri

wa miaka 28.

Ni mwezi wa pili sasa tangu Mick afike katika

visiwa hivi na amefanya anasa sana tu. Katika

wakati ambao anakuwa nje ya majukumu yake

halisi, Mick alikuwa ni mfanyabiashara wa madini.

Alikuwa na ofisi yake Dar es salaam Tanzania

ambako watu walienda kuuza na wengine walienda

kununua madini na vito aina mbalimbali, biashara

iliyomuingizia pesa nyingi na kumuweka katika

watu waliokuwa na pesa nyingi.

Lakini kitu ambacho wengi hawakukijua,katika

majukumu yake halisi Mick ni ajenti namba moja

ITAENDELEA

UKURASA WA GAIDI - 1

 

IMEANDIKWA NA : BAHATI MWAMBA

***********************************************

Simulizi : Ukurasa Wa Gaidi 

Sehemu Ya : Kwanza (1)


Saa nane na dakika ishirini mchana yalionekana

magari matatu yanayofanana, yakiwa na umbo

kama yale magari ya kusafirishia fedha kwa jinsi

yalivyo na mtenganisho kati ya kichwa cha gari na

'bodi' lake. Magari haya yaliyokuwa mapya yakiwa

na kichwa cha ranngi nyeusi na michirizi ya rangi

ya silva na bodi yake rangi ya maziwa,yalikuwa

katika mfuatano huku yakiongozwa na magari

mawili aina ya Nissan Patrol 'model' mpya rangi

nyeusi mbele huku yakifuatiwa na magari mengine

mawili ya aina hiyo nyuma. Magari haya aina ya

'Nissan patrol' yaliyokuwa na vioo

visivyomuwezesha mtu aliye nje kumuona aliye

ndani (tinted), yalipiga king'ora huku yakiwa

yamesheheni askari makini kabisa kutoka kitengo

maalum cha jeshi la polisi. Mbele ya msafara wa

magari haya umbali wa mita mia hivi kulikuwa na

piki piki mbili za police zilizoenda sambamba huku

zikitawanya magari ili kupisha msafara huu.

Kilichotofautisha msafara huu na misafara mingine

ni ile kasi kubwa iliyokuwa ikiendwa na magari

haya kwa muonekano wa nje kwa wananchi na

muonekano wa ndani ambao watu hawakuuona ni

wale askari maalum ambao ulikuwapo ndani ya

magari haya.

"Eeh bwana eh. Msafara wa 'mapene' huo."

Mwananchi mmoja alisikika akiongea.Na kweli ,

kwa muonekano wa nje, magari haya yalionekana

kama yale magari ya kusafirisha fedha kutoka

benki kuu ya Tanzania iliyo na makao makuu huko

jijini Dar es salaamvna kuzipeleka katika mikoa

mbali mbali. Kitu pekee ambacho watu hawa

hawakujiuliza ni kwamba mbona leo magari haya

yametokea upande wa nyanda za juu kusini.Kwa

bara bara hii ambapo magari yalikuwa yanapita,

ilikuwa dhahiri kuwa magari haya yametokea mkoa

wa Mbeya. .Labda kama magari haya yalipeleka

fedha huko na sasa yanarudi, Lakini pengine cha

kushangaza zaidi ni ule ulinzi mkali uliokuwa

katika magari haya. Kulikuwa na kitu ambacho

hakuna aliyekifahamu zaidi ya waliokuwa ndani ya

magari haya.

*************************************

Saa kumi kasorobo. Msafara huu ulikuwa katikati

ya msitu wa miti mirefu maarufu kama milingoti

kama ilivyotoholewa kutoka neno la kiingereza

'Long tree'. Miti hii ilitengeneza kichaka

kilichopakana na msitu mkubwa zaidi wa miti

inayojulikana kama mipaina au ' pines tree' nayo

pia kama ilivyotoholewa kutoka lugha ya kiingereza

na wakazi wa mkoa wa Iringa.Misitu hii ipo katika

wilaya ya Mafinga huko Iringa.

Msafara huu ulikuwa katika kasi kali sana, wakati

ambapo askari waliokuwa katika gari la mbele

waliposhuhudia pikipiki za police zilizokuwa mbele

ya msafara zikianguka chini mara baada ya askari

waliokuwa wakiziendesha, kushambuliwa kwa

risasi kutoka katika kichaka kimoja ndani ya

msitu.Lilikuwa ni tukio la kushtukiza sana

lililosababisha magari yote kufunga breki kwa

ghafla .Kutokana na ustadi waliokuwa nao

walioendesha magari haya ,haikutokea hitilafu

yoyote wakati walipofunga breki kwa ghafla.

Askari wote waliokuwa katika 'Nissan patrol'

walishuka kwa tahadhari na kuweka silaha zao

tayari kwa lolote. Lakini kabla hata hawajafanya

lolote, walishangaa kuona askari mmoja kati yao

akianguka chini huku akivuja damu nyingi

shingoni. Risasi iliyotokea msituni upande wao wa

kushoto ilimuondoa uhai askari huyu. Hapo ndipo

askari wote walifyatua risasi huku wakizielekeza

bunduki zao kutoka upande wao wa kushoto

ambako ndiko risasi iliyoondoa uhai wa mwenzao

ilitokea.

Askari mwingine akaanguka chini huku akivuja

damu katika goti mguu wa kulia. Safari hii risasi

ilitokeaupande wa nyuma yao na kusambaratisha

mguu wa askari huyu.

''We being shot by snipers.All units take

cover".Ilikuwa ni sauti ya kapteni Joshua akitaka

vikosi vyote vijifiche kutokana na shambulio la

'udunguaji'.Kisha "sniper one and two take your

position(mdunguaji namba moja na namba mbili

kaeni tayari)".Kutokana na kuwepo kwa

mchanganyiko wa askari wa weledi wa Tanzania na

Marekani katika msafara huu, ililazimika kutumika

lugha ya kiingereza ambayo wote waliielewa

vyema.

Hapo moja kati ya yale magari ya kusafirisha pesa

yakalegezwa vifungio vya milango kutokea ndani,

wakashuka askari wawili waliovalia nguo

zilizotengenezwa kwa mfano wa majani makavu ya

mgomba kwa rangi yake na jinsi matambara

yalivyoachwa kuning'inia hovyo katika nguo

hizi.Kichwani walivalia vilemba vilivyopambwa

kiustadi na aidha nyasi kavu au mfano wa nyasi

kavu. Ni kama vile walijua nini kingeweza

kuwapata iwapo wangeshuka bila uangalifu, hivyo

walichukua tahadhari kubwa sana. Askari hawa

walishuka kutoka ndani ya gari kwa kupiga

vikumbo milango kwa ghafla na kujidondosha chini

kama vifurushi.Sekunde hiyohiyo risasi mbili

zililenga usawa wa milango ambayo askari wale

waliipiga kikumbo. Zilitokea upande wa porini na

pengine zililenga kuwadhuru askari wale.

Wadunguaji hawa wawili mmoja kutoka Idara ya

kupambana na ugaidi Tanzania C.T.I (Counter

Terrorism Inteligence) na Mwenzie kutoka Idara

kuu ya ujasusi ya Marekani C.I.A (Central

Inteligence Agency) walijificha nyuma ya miti na

kuanza kazi yao mara moja.Bunduki kubwa za

kisasa maalum kwa kudungua zilikuwa kazini.

Mara walipoanza kufanya kazi yao ,wakitumia lenzi

zilizofungwa katika bunduki hizi ili waone kama

watawaona adui hawa ndipo walipopata

changamoto kubwa sana. Kutokana na msitu huu

kuwa na miti iliyoshonana sana,haikuwa rahisi

kuweza kumuona mtu aliye ndani ya msitu huu.

Miti hii ilifanya kuwe na giza ndani ya misitu hii.


itaendelea.....



Wakati huu ambapo wadunguaji walikuwa

wakijaribu kila namna ili wafanikishe kuwaona na

kuwapiga adui zao,ghafla ilisikika sauti ya helkopta

mahali hapo. Risasi kutoka helkopta mbili ambazo

zilitokea kusikojulikana zilianza kushambulia

msafara wa magari hayo.Hapo magari ya

kusafirisha pesa yakafunguliwa milango kisha

askari kadhaa waliovalia gwanda nyeusi,kofia

ngumu pamoja na fulana nzito maalum kwa kuzuia

risasi , walitoka kutoka ndani ya magari haya.Hawa

walikuwa ni askari wa weledi kutoka katika kikosi

maalum cha United States Marine Corps Forces

Special Operations Command(MARSOC ).Askari

hawa walianza kuzishambulia helkopta zile kwa

kutumia bunduki zao za kisasa kabisa aina ya HK

MP7.Lakini hawakufua dafu japo walitumia bunduki

za kisasa sana ambazo hutumiwa na Kikosi

maalum kingine maarufu sana cha makomando

kutoka katika taifa lao kijulikanacho kama Navy

Seal DEVGRU. Pengine ni kwa sababu katika

mapambano ni rahisi sana kwa aliye juu

kumuangamiza aliye chini kuliko aliye chini

kumuangamiza aliye juu. Adui waliokuwa katika

helkopta waliendelea kumwaga risasi nzito nzito

kama njugu bila kuwapa upenyo askari hawa

maalum kulenga shabaha.Vikosi vyote yaani askari

wa kitanzania na wale wa Marekani waliendelea

kupambana lakini kazi ilikuwa bado ni nzito sana.

Wakati mapambano makali yakiendelea , helkopta

nyingine ya tatu ikatokea upande wa mashariki.Hii

ilikuwa ya tofauti na hizi helkopta nyingine kiumbo

na ilikuja kwa lengo tofauti kabisa.

Helkopta hii ilikuwaimetundikwa ndoano kubwa

sana ambayo ilichomekwa minyororo minene na

imara sana minne.Minyororo hii kwa pamoja

iliunganishiwa sumaku kubwa sana iliyokuwa na

umbo la mche mraba iliyokuwa kama mita mbili za

mraba kila upande.Helkopta hii ilienda hadi juu ya

gari mojawapo kati ya yale magari yanayotumika

kusafirisha pesa, kisha ikagusisha lile sumaku juu

ya paa la bodi la gari hilo kisha ikaanza kupaa

tena.Kadri helikopta ile ilivyopaa ndivyo gari lile

lilivyoanza kunyanyuliwa polepole.Mwisho gari

lilinyanyuliwa juu zaidi na zaidi kisha kutokomea

angani.

Wakati huu ndipo adui wengine walijitokeza

kutokea porini na kuanza kushambulia.Map

ambano yakawa makali zaidi na kufanya eneo lote

kuwa kama eneo la vita kwa kelele za risasi.Askari

wa weledi wa idara ya C.T.I na wenzao wa kikosi

cha MARSOC waliendelea kupambana na adui

hawa waliokuwa wengi sana na waliopigana kwa

ari ya juu sana.Hata adui waliouawa kwa wingi

bado waliendelea kupambana kwa ari ya juu sana

kitu kilichosababisha vita kuwa ngumu zaidi na

zaidi. Kiongozi wa kikosi cha askari hawa wa

weledi wa kitanzania Kapteni Joshua na yule wa

kikosi cha Marekani cha MARSOC kamanda Lucas

Bradock waliongoza vyema vikosi vyao na

kuonesha uwezo wa hali ya juu kimapambano

.Lakini kutokana na ari na uwingi wa adui, vikosi

hivi vilianza kuzidiwa nguvu.

"We are out numbered,sergent John request for

backup". Kamanda wa kikosi cha MARSOC alitoa

maelekezo kwa askari wake kwamba afanye

mawasiliano kuomba usaidizi. "Okey Cover

me".Alijibu sajenti John akitaka kulindwa wakati

akifanya mawasiliano. Kwa kutumia kifaa maalum

cha mawasiliano alichokivaa katika sikio lake la

kushoto na kuanza kuwasiliana na makao makuu

ya muda kuomba usaidizi. Makao makuu haya ya

muda yaliweka kambi ndani. Huku makao makuu

helkopta tatu za kisasa ziendazo kasi aina ya

'Chinook' zilikuwa ziko tayari na makomando tisa

kutoka vikosi vya Navy SeAL Marekani pamoja na

makomando kutoka JWTZ Tanzania. Kikosi hiki

cha Navy Seal kilikuwepo Tanzania tangu miezi

mitatu iliyopita kwa ajili ya kufanya mazoezi ya

pamoja na vikosi vya makomando vya JWTZ ili

kuwaongezea uzoefu makomando hawa wa

Tanzania.

Kikosi hiki kilichojumuisha watanzania na

wamarekani kilikuwa tayari kutoa usaidizi tangu

walipopata taarifa za kiintelijensia kuwa msafara

ule umevamiwa.Walikuwa wanasubiri amri ya

kwenda kutoa usaidizi tu.Mara tu walipopata

mawasiliano, makomando hawa (Navy Seal na

JWTZ) walipaa na helkopta zao muda huo huo.

Uwanja wa mapambano kulikuwa na kelele za

risasi kutoka katika bunduki za wanausalama na

adui.Majibizano ya risasi yaliendelea huku idadi za

majeruhi na maiti zikiendelea kuongezeka kila

upande.Upande wa kikosi cha ' MARSOC' tayari

askari wawili walipoteza maisha na wanne

kujeruhiwa huku Tanzania ikipoteza askari wa

weledi wanne na mmoja kujeruhiwa. Upande wa

adui, walipoteza askari wengi zaidi kwa idadi

isiyojulikana. "Cease fire and take cover". Amri

nyingine ilisikika kutoka kwa kiongozi wa kikosi

cha 'MARSOC' na ambaye ndiye alikuwa mkuu wa

msafara huu kamanda Bradock.Amri hiibiliwataka

askari wote kuacha kupambana bali

wajifiche.Wakati huu ndipo kundi kubwa la adui

likajitokeza kutokea msituni na kuanza

kuyasogelea magari ya wanauslama wale kutoka

pande zote.Sura zao zilionesha kuwa ni watu walio

na asili ya somalia. Wengi kati yao walionekana

kuwa wachafu sana na wengine wadhoofu wa miili.

Lakini ni hawahawa walionekana kuvipa shida

vikosi hivi kwa muda wa saa moja na dakika

thelathini sasa.

Adui walizidi kuyasogelea magari ambayo

yaliwaficha wanausalama wale ndani yake.

Walionekana kuwa na uchu kama fisi mwenye njaa

aliyeona mzoga mahali.Sasa walizidi kusogelea

magari yale huku wakipiga kelele na kunyoosha

bunduki zao mbele.Wakiwa karibu sana na magari

yale,walisikia kelele za helkopta zaidi ya

moja.Kadri sekunde zilivyosogea ,mvumo ule wa

helkopta uliongezeka kuonesha kuwa pengine

helkopta ilikuwa inaelekea upande ule waliokuwapo

wao. Mara wakaanza kuziona helkopta zile

zikiwaelekea na wakati huo huo risasi zikaanza

kurushwa kuwaelekea adui wale . Adui walianza

kuanguka mmoja baada ya mwingine kwa kasi

kubwa.Vikosi vya uokozi vilikuwa vimefika tayari.

Bunduki aina ya FN Minimi 7.62 zilizofungwa

katika helcopter zilifanya kazi yake ipasavyo.

Makomandoo walioshuka kwa miamvuli mita

chache kabla ya kufika uwanja wa mapambano,

nao wakaanzisha mashambulizi ya ardhini na

kufanya adui kuzidiwa nguvu. Vikosi vya usalama

vilivyojificha ndani ya magari navyo vikaendeleza

mashambulizi kama mwanzo.Maadui wakaanza

kuzidiwa nguvu na kuamua kukimbilia msituni

huku wakibeba maiti za wenzao.

Hadi kufika saa kumi na mbili jioni,hakukuwa na

mapambano tena wala sauti ya risasi. Eneo

palipotokea mapambano , lilizungushiwa utepe

maalum na jeshi la polisi ili mtu yeyote asipite na

kuharibu upelelezi. Kisha askari kadhaa wakaletwa

kulilinda eneo hilo.

*********************************************

****************************************************

Mtaalamu wa teknolojia ya kompyuta ambaye pia

alikuwa mtaalamu wa kuvunjavunja ' password'

bwana Abdallah Yusoof,alifanya kila jitihada

kuhakikisha anafungua loki iliyofunga mlango wa

nyuma wa gari lile. Ni lile gari lililobebwa na

helkopta kule katika uwanja wa mapambano.

Alikwisha wahi kufungua loki nyingi sana lakini hii

ya leo ilihitaji umakini wa hali ya juu zaidi. Loki hii

ilitengenezwa kwa mfumo maalum ambapo

mfunguaji alipewa nafasi mbili za kuifungua.

Kukosea mara ya kwanza kungempa mfunguaji

nafasi ya pili.Kukosea mara ya pili kungesababisha

mlipuko kama wa bomu ambao ungeteketeza gari

pamoja na watu ambao wapo karibu na gari.

Abdallah au kama alivyozoeleka kwa ubini wake

Yusoof,alichukua waya fulani wa 'USB'

akauchomeka katika simu yake iliyokuwa na

programu maalum kisha upande wa pili wa waya

huo akauchomeka mahala fulani pembeni ya

kidubwasha kilichobeba vitufe vilivyo na namba

sifuri hadi tisa.Kidubwasha hiki kilifanana na mita

za umeme wa LUKU za TANESCO. Mara

alipochomeka waya huo, namba fulani zilionekana

zikipita na kubadilika kwa kasi katika kioo cha

simu yake kisha zikajitokeza tarakimu sita. Yusoof

akazibonyeza tarakimu zile katika kidubwasha

kile.Ukasikika mlio 'krack'. Loki ilikuwa

imefunguka.

Yusoof akafungua milango ya gari lile ,ndani ya

gari lile akaonekana mtu mwenye ndevu nyingi na

ndefu sana huku akiwa na upara wa haja. Mtu huyu

alikuwa amesheheni pingu madhubuti sana

zilizofungwa mikononi na miguuni. Yusoof

alizitawanyisha pingu hizi kwa risasi kutoka katika

bastola yake.Yule bwana akashuka kutoka katika

gari.

Naam.Labda ni kimo cha gari like kilichomfanya

atoke akiwa kainama kilichangia kumfanya

aonekane kuwa mtu wa kimo cha kawaida

tu.Aliposhuka kutoka katika gari lile alionekana

sasa kuwa mtu mwenye tambo kubwa na mrefu

sana. Japo alikuwa katika vazi kubwa la asili kama

yale yanayovaliwa na 'Wanigeria', lakini haikusaidia

kuficha kuonekana kwa misuli mikubwa

ITAENDELEA

Friday, 30 December 2022

HEKAHEKA MSITUNI - 5

    


Simulizi : Hekaheka Msituni 


Sehemu Ya Tano (5)


“Sasa tunafanyaje hapa?” Inspekta Tom Green aliuliza.

“Tunahitaji boti” Latoya aliongea.

SASA ENDELEA

“Tutaipata wapi maana muda unazidi kusonga mbele na nina imani wale jamaa kule kambini watakuwa wameligundua hili na watakuwa tayari wameanza kutusaka?” Inspekta Tom Green aliongea akiuliza.

“Ngoja nichunguze mazingira” Latoya aliongea.
Latoya alianza kuzunguzunguka ukingoni mwa mto akitafuta kama anaweza kupata chombo ambacho kingewawezesha kusafari kwa maji.

“Heeeeey!”

Latoya alipiga kelele akimwita Inspekta Tom Green upande ule ambako alikuwako. Inspekta Tom Green alimbeba Martin na kuanza kwenda kule alikokuwa Latoya.

“Tuna mtumbwi hapa. Nadhani utatufaa” Latoya aliongea akimwonyesha Inspekta Tom Green mtumbwi uliokuwa ukingoni mwa mto.

“Safi sana!” Inspekta Tom Green aliongea huku uso wake ukionyesha tabasamu la furaha. Alimpakia Martin Samweli haraka haraka.

Baadaye Latoya naye alipakiwa na kisha mtumbwi ulianza kuongozwa majini. Safari iliendelea kwa muda mrefu huku Inspekta Tom Green na Latoya wakiwa makini kujikinga na hatari yoyote ambayo ingetokea.

“Mwanipeleka wapi? Ninyi ni akina nani?” Martin Samweli aliuliza. Kwa sasa alikuwa amerejewa na fahamu baada ya kuzimia kwa muda mrefu sana.

“Nadhani habari zetu ulikwishazipata tangu hapo awali. Sina haja ya kurudia tena kuongea kitu ambacho nilikwishakiongea!” Latoya aliongea.

Hapo ndipo kumbukumbu za Martin Samweli zilipomrejea. Alikumbuka kila kitu toka alipovamiwa kule kambini na huyu mwanamke.

“Mmejipalia makaa. Hamtafika kokote kabla Kanali Edson hajawanasa” Martin Samweli aliongea.

“Sisi ni watu tusiokamatika. Safari hii huyo kamanda wako ndiye ambaye atakamatwa” Inspekta Tom Green aliongea.

“Unajidanganya. Tena naamini kwa sasa kamanda atakuwa njiani kuja kuwanasa!” Martin aliongea huku akicheka.

“Wewe ndiye ambaye unajidanganya. Sisi tupo katika kazi hii kwa muda mrefu. Kamanda wako hafahamu hata kidogo kama sisi tuko katika misitu hii. Anachokifahamu ni kwamba wewe umetoroka kambini kwa sababu umeasi jeshi na unakwenda kuungana na serikali. Huo ndiyo ujumbe ambao niliuacha pale kambini. Kwa sababu wazifahamu siri nyingi za jeshi hili basi kwa sasa unasakwa kama dhahabu” Inspekta Tom Green aliongea akicheka.

“Shiiiit! Mmeniangamiza ninyi mbwa. Makoko akinikamata atanichinja kabisa!” Martin aliongea akiporomosha machozi.

“Yes, sasa uamuzi ni wako. Kuendelea na safari ili ukatoe msaada kaw mheshimiwa Rais na ufutiwe makosa yako kisha uishi kwa amani kama shujaa wa Taifa au urudi kwa Makoko kukifuata kifo chako cha kikatili. Na kumbuka kwamba Makoko pamoja na BMM yake mwisho wake ni sasa!” Inspekta Tom Green aliongea.

Martin Samweli hakujibu lolote zaidi ya kubaki akiporomosha machozi. Wababe hawa walikuwa wamemuweza hasa. Alikuwa amebaki njia panda.

Safari ilikuwa ikiendelea katika mto ule. Mtumbwi ulikuwa ukiteleza juu ya maji mithili ya nyoka juu ya majani. Inspekta Tom Green alikuwa akipiga makasia kuuongezea kasi mtumbwi ule. Latoya na Martin Samweli walikuwa wamekaa juu ya mtumbwi ule huku Martin Samweli akiwa bado amefungwa mikono yake kwa nyuma.

Ni wakati huohuo ndipo sauti ya chopa ilianza kusikika ikija upande wao kuufuata mto. Jeshi la Kanali Edson Makoko lilikuwa limeshawakaribia.

“Yes, mambo ni moto sasa. Muda wa kuucheza muziki wetu umekwishakaribia!” Inspekta Tom Green aliongea huku akiiseti vema bunduki yake aina ya AK 47.

“Yes, ngoja tuwaonyeshe namna wababe vile tunafanya!” Latoya alijibu naye akiiseti bunduki yake aina ya AK 47.

“Jamani mnifungue mikono. Nitauawa mimi!” Martin alilalamika akiomba kufunguliwa mikono yake.

“Bado hatujakuamini. Unaweza ukatugeuka. Waonesha una kichwa kigumu cha kuelewa mambo na kuchukua maamuzi sahihi. Hii ndiyo njia salama kwako!” Inspekta Tom Green aliongea.

“We mbwa wewe! Nasema nifun ……..!” Martin Samweli hakuweza kuimalizia kauli yake.

Chopa ya wale waasi ilikuwa imekwishawakaribia. Kombora lilikuwa limeachiwa na lilitua pembeni yao na kufumuka.

“Diiiiiiive!” Inspekta Tom Green alipiga kelele.
Wote walijirusha ndani ya maji pindi kombora jingine lilipotua juu ya ule mtumbwi na kuusambaratisha.

“Ha ha ha haaaaaa! Kwisha habari yao. Halafu kumbe yuko na wengine?” askari mmoja kwenye chopa aliongea.

“Basi leo wameingia choo cha kike!” askari mwingine naye aliongea.

Inspekta Tom Green aliogolea chini kwa chini ndani ya maji huku akiwa amemshika mkono bwana Martin Samweli. Baadaye wote waliibukia ng’ambo yam to mahali ambapo palikuwa na kichaka.

“Yaani wewe kenge ni mnyama kabisa. Utaniua wewe!” Martin alilalamika. Inspekta Tom Green hakujibu chochote.

“Nifungue tafadhali, nitashindwa kujitetea na hawa jamaa wataniua!” Martin aliongea huku sasa machozi yakimtoka.

“Hii ni nafasi yako ya mwisho ya kujisafisha. Ukifanya ujinga tu, basi kumbuka sisi ni zaidi ya shetani!” Inspekta Tom Green aliongea huku akizikata kamba za mikono zilizomfunga Samweli.

Wakati huo huo Latoya alimrushia Martin bunduki aina ya AK 47.

“Ahsante sana. Sasa tuingie uwanjani. Mimi naufahamu vema msitu huu. Nitawaongoza!” Martin Samweli aliongea akiikoki bunduki yake.

Inspekta Tom Green na wenzake walianza kuchanja mbuga ndani yam situ ule. Walikuwa wakikimbia huku wakiongozwa na Martin. Msitu ule kwa sasa ulikuwa umetapaa wanajeshi kila mahali.
*******


Inspekta Tom Green na wenzake walianza kuchanja mbuga ndani yam situ ule. Walikuwa wakikimbia huku wakiongozwa na Martin. Msitu ule kwa sasa ulikuwa umetapaa wanajeshi kila mahali.

SASA ENDELEA

Baada ya mwendo kidogo kuna kikundi cha askari kama saba wa jeshi la BMM kiliwaona akina Inspekta Tom Green. Hapo ndipo mapambano ya risasi yalipoanza. Ilikuwa ni hatari kubwa sana kwani eneo lile la msitu lilipambwa kwa mivumo ya risasi ambazo zilikuwa zikikohoa kutoka katika bunduki za kila upande. Ndani ya dakika kumi mahaini wale walikuwa wamekwishakandamizwa na kupoteza uhai wao. Akina Inspekta Tom Green waliendelea kusonga mbele.

Dakika kumi mbele walikutana na muziki wa kundi la wanajeshi kama kumi na mbili ambao walikuwa na silaha nzito. Inspekta Tom Green na wenzake ndiyo walikuwa wa kwanza kuwaona wanajeshi wale.

“Sasa hapa tunapaswa tutumie akili!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Yap!” Martin Samweli alijibu.

“Tunatakiwa tutawanyike. Latoya utajipeleka na kujikamatisha kwa wanajeshi wale. Mimi nitashambulia kutoka kushoto na wewe Martin utashambulia kutoka kulia. Latoya unajua nini cha kufanya ikitokea hali hiyo!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Rodger that boss!” Latoya alijibu.

“Haya tutawanyike!” Inspekta Tom Green aliamuru na wote walitawanyika.

Latoya alijipeleka kwa askari wale na kunyoosha mikono juu ishara ya kusalimu amri. Wanajeshi wale walifurahi sana kwani waliona kama wamekwishapunguza sehemu ya kazi yao. Wanajeshi wale walimsogelea Latoya huku bunduki zao zikiwa tayari mikononi.

“Wenzako wako wapi?” mwanajeshi mmoja aliuliza huku akimpiga Latoya ngumi moja ya tumbo.

“Wameuawa!” Latoya alijibu huku akiigiza huzuni.

“Ha ha ha haaaaa! Pumbvu sana. Kazi kwisha!” mwanajeshi mmoja aliongea.

Ghafla mashambulizi ya risasi yalianza kutokea kila upande wa wanajeshi wale. Hapo ndipo Latoya naye alipowaonyesha uwezo wake. Mithili ya umeme alimfuata mwanajeshi mmoja na kumkandika ngumi ya uso na kisha alichomoa bastola iliyokuwa imewekwa katika mfuko wake kiunoni. Alianza kuwacharaza risasi wanajeshi wale huku akijiviringisha huku na huko kuepa risasi za maadui.

Baadaye maadui wote walikuwa chini wakiwa wameuawa. Wazee wale wa kazi walikutana tena na kupena mikono ya pongezi.

“Safi sana Martin!” Inspekta Tom Green alimpongeza Martin.

“Ahsante sana. Sasa tunakikaribia kijiji. Pale kuna bwana mmoja ambaye ana chopa. Tunapaswa kwenda kuiiba chopa ile ili itutoe kutoka hapa msituni maana safari ni ndefu sana kutoka hapa na hakuna namna yoyote ya usafiri tunayoweza kuipata!” Martin alijibu.

“Sawa. Tufanye hivyo pasi kupoteza muda!” Inspekta Tom Green aliongea.

Wote walianza kukimbia kutoka eneo lile walilokuwepo kuelekea kijijini huku wakichukua tahadhari kubwa sana.
******
Kijiji kilikuwa hakina wanajeshi kabisa. Wanajeshi wote walikuwa wameelekea ndani yam situ kwenye uwanja wa vita. Wananchi wote waliambiwa wajifungie ndani kwani kulikuwa na mapigano ambayo yalikuwa yakiendelea. Hali hii ilifanya kijiji kiwe kitulivu kabisa.

Kwa upande wao akina Inspekta Tom Green ilikuwa ni safi kabisa kwani iliwawezesha kufika katika nyumba ya mwanajeshi yule ambaye alikuwa akimiliki helkopta bila ya tatizo.

Kwa bahati nzuri mwanajeshi yule naye alikuwa amekwenda kwenye uwanja wa vita kwa kutumia gari. Akina Inspekta Tom Green hawakupenda kuipoteza fursa ile. Waliifungua milango ya chopa.

Kwa kutumia utundu mkubwa Inspekta Tom Green aliweza kuiwasha chopa ile. Chopa iliposhika moto, Inspekta Tom Green aliipaisha na kuanza safari ya kuuacha msitu ule. Huku msituni wanajeshi waliendelea kuwasaka akina Inspekta Tom Green wakiamini kwamba walikuwa bado wamenasa mle msituni.
*******
Saa nne za usiku Inspekta Tom Green, Latoya pamoja na Martin Samweli waliingia jijini Kano. Moja kwa moja chopa ile ilielekezwa mpaka katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano. Maafisa wote wa usalama hawakuamini kile ambacho walikuwa wakikiona. Chopa ilipotua, Inspekta Tom Green, Latoya pamoja na Martin Samweli walishuka. Inspekta Tom Green alianza kumwongoza Martin kuingia hospitali.

“Dokta Morgan, huyu hapa ni Martin Samweli. Naomba kazi ya kuokoa maisha ya Rais iendelee!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Ahsante sana Tom. You guys you are the bests!” dokta Morgan aliongea huku akimpokea Martin Samweli na kumwomba amfuate ndani ya hospitali.

Maafisa wote walipiga makofi na kushangilia. Hawakuamini kama Inspekta Tom Green na Latoya walikuwa wameweza kuifanikisha kazi ile.

“Chifu naomba uongee na waziri wa ulinzi na mkuu wa majeshi waweze kutuma jeshi kule Masolo. Wale jamaa wametawanyika ovyo kutokana na moto tuliowawashia. Mpaka sasa wanahaha kutusaka. Huu ndio muda muafaka wa kuwavamia na kuwatawanyisha. Mashambulizi ya anga ndiyo yanafaa zaidi kwa kambi ile!” Inspekta Tom Green aliongea.
“Sawa Tom” Chifu alijibu.

“Na pia wakumbuke kwamba kijiji cha kwanza wanaishi watu wa kawaida. Eneo linalofuata ndiyo kambi yenyewe ya BMM. Watumie ramani hii ambayo itawaongoza vizuri kabisa!” Inspekta Tom Green aliongezea.

“Umesomeka Tom” Chifu aliongea huku wakati huo akiwa ameanza kufanya mawasiliano na waziri wa ulinzi pamoja na mkuu wa jeshi.
******
Ghafla hali ya hewa pale hospitalini ilichafuka. Kanali Edson Makoko pamoja na baadhi ya wanajeshi wa jeshi lake walivamia hospitali ile. Kumbe Kanali Edson Makoko alikuja kutambua kwamba Martin Samweli alikuwa ameshirikiana na akina Inspekta Tom Green na walikuwa wametoroka kule msituni.

Na pia alikuja kutambua kwamba misheni ya kumwua Rais ambaye aliitekeleza hapo awali haikuwa na mafanikio. Rais alinusurika lakini alikuwa mahututi hospitalini. Pia alifahamu kwamba Rais alikuwa akihitaji damu na damu ambayo ilikuwa ikimfaa ilikuwa ni ya bwana Martin Samweli ambaye alikuwa ni askari wake. Na hii ndiyo sababu ya akina Inspekta Tom Green kumtorosha bwana Martin kule msituni Masolo.

Sasa Kanali Edson Makoko yeye mwenyewe aliamua kuja jijini Kano na kuendesha operesheni ya kumwua Rais pamoja na yule askari aliyemsaliti.
*******

Sasa Kanali Edson Makoko yeye mwenyewe aliamua kuja jijini Kano na kuendesha operesheni ya kumwua Rais pamoja na yule askari aliyemsaliti.

SASA ENDELEA

“Code 002 …. Code 003 …. Code 004 and Code 005. Are there?” Inspekta Tom Green aliongea kupitia kifaa chake cha mawasiliano.

“Tunakupata poa kabisa toka huku nje. Yaani huku nje hali ni tete kabisa!” Amina alijibu.

“Sasa mimi nitacheza huku ndani na ninyi mtacheza kutoka nje kuja ndani. Hakikisheni hakuna kiumbe chochote chenye asili ya hawa waasi kinachotoka salama hapa!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Rodger that boss!” Hashim alijibu.

“Haya wazee, mambo ni moto. Sasa naomba mwende kwenye chumba cha mheshimiwa Rais mkaimarishe ulinzi huku. Mimi nitacheza nao hawa kunguni na nitahakikisha hawafiki huko!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Sawa kijana!” Chifu aliongea na kuwaongoza wenzake huku bastola zao zikiwa mikononi.

Inspekta Tom Green aliwaamuru manesi na madaktari kufunga milango ya mawodi na ofisi. Pia aliwaambia wawatulize wagonjwa watulie pindi yeye anapopambana na wale wahaini. Manesi na madaktari walifanya kama vile ambavyo Inspekta Tom Green alikuwa amewaamuru kufanya.

Wakati huohuo Kanali Edson Makoko pamoja na jeshi lake walikuwa wamekwishaanza kuingia ndani ya hospitali. Huko ndani walipokelewa na Inspekta Tom Green wakati nyuma walisindikizwa na maafisa wale wengine wa BSA pamoja na maafisa wengine wa Idara mbalimbali za usalama.

Polisi na Jeshi la wananchi pia walikuwa wamewasili pale hospitali kuwasha moto. Hakika mambo yalikuwa ni bambam. Ulikuwa ni mpambano mzito sana ambapo askari waasi waliuawa sana. Hakuna hata mmoja ambaye aliachwa. Vile ambavyo walitegemea na kuaminishwa na kamanda wao ilikuwa tofauti kabisa.

Naye Inspekta Tom Green upande wa ndani alizidi kuwashusha na kuwaounguza wote ambao walijaribu kuingia ndani ya hospitali. Hakika moto wa Inspekta Tom Green ulikuwa ni balaa. Hata Kanali Edson Makoko mwenyewe ilifika kipindi alishangaa. Hakutaka kuamini kama Inspekta Tom Green alikuwa ni binadamu wa kawaida.

Mtu wa mwisho kusalia katika jeshi la Kanali Edson Makoko alikuwa ni Kanali Edson Makoko mwenyewe. Na sasa alikuwa amekutana ana kwa ana na Inspekta Tom Green. Na kwa bahati nzuri walikutana kila mmoja bunduki yake ikiwa imeisha silaha.

“Umeniharibia sana. Nitahakikisha nakuua kikatili sana!” Kanali Edson Makoko alifoka.

“Hapa umekutana na mwamba. Nadhani ingelikuwa vema kama ungelikuwa unasali kumwomba Mungu msamaha kwa dhambi ambazo umezitenda. Unayekwenda kufa ni wewe!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Haya na tuone sasa!” Kanali Edson Makoko aliongea huku akimjia wanguwangu Inspekta Tom Green.

Kanali Edson Makoko aliachia konde zito ambalo Inspekta Tom Green alilipangua kwa mkono wake wa kushoto. Kanali Edson Makoko aliliachia konde jingine ambapo Inspekta Tom Green alibonyea na kuliepa.

Baada ya hapo Inspekta Tom Green alimbandika Kanali Edson Makoko konde moja tu zito kwa mkono wake wa kulia ambapo Kanali Edson Makoko alishindwa kuyahimili maumivu ya konde lile. Alijishika taya lake kwa maumivu huku akipiga kelele.

Inspekta Tom Green hakutaka kumpa nafasi kabisa. Alirusha teke kali ambalo lilimpata Kanali Edson Makoko tumboni. Kanali Makoko alijikunja na kulishika tumbo lake akiugulia maumivu. Ni wakati huo ndipo ambapo Inspekta Tom Green alianza kumpa dozi ya ngumi na mateke ya mfululizo.

Kanali Edson Makoko alilainika na kuwa zaidi ya mlenda. Inspekta Tom Green alihitimisha mchezo kwa kuukamata mkono wa Kanali Edson Makoko na kuuvunja. Kanali Edson Makoko alilia sana kwani maumivu ambayo aliyapata yalikuwa ni makali sana. Wakati huohuo askari walifika na kumtia nguvuni.

“Wekeni ulinzi wa kutosha sana kwani mtu huyu ni hatari sana. Ana mengi sana ya kuijibu serikali” Inspekta Tom Green aliongea.

Kanali Edson Makoko aliondolewa pale na kupelekwa cjhumba cha matibabu huku akiwa chini ya ulinzi mkali sana wa polisi pamoja na wanajeshi. Baadaye hali ilikuwa tulivu kabisa pale hospitali. Mheshimiwa Rais aliendelea kupewa matibabu. Aliongezewa damu mara baada ya kuitoa katika mwili wa Martin Samweli.
******
MSITUNI MASOLO

Katika msitu wa Masolo nako mambo yalikuwa ni moto sana. Wanajeshi wa Jeshi la wananchi waliuvamia msitu na kuanza kupambana na waasi. Waasi wa kikundi cha BMM walishambuliwa vilivyo na kuteketezwa kabisa. Hawakuwa na pa kukimbilia.

Wale waliosalia walikamatwa na kushikiliwa mateka. Kambi yao iliteketezwa na kusambaratishwa kabisa. Hakuna alama yoyote ya BMM ambayo iliachwa. Na huo ulikuwa ndiyo mwisho wa BMM.
******
Kanali Edson Makoko alifikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka ya uhaini. Alionekana na makosa na alihukumiwa kifungo cha maisha gerezani pamoja na adhabu kali sana.
Matibabu ya mheshimiwa Rais Ditric Mazimba yalichukua kama miezi miwili ambapo alirejea kuwa ahueni kabisa.
Bwana Martin Samweli alisamehewa makosa yake na kupongezwa kama mzalendo wan chi ya Bantu kwa kukubali kuokoa maisha ya Rais wake.

Pia Inspekta Tom Green pamoja na maafisa wenzake wa BSA walipongezwa kwa namna ya pekee kwa kazi kubwa ambayo waliifanya. Rais aliwapa shukrani za pekee sana.
Chifu naye alipongezwa kwa kuwapika vijana imara kabisa kwa usalama wa Taifa.
**** MWISHO ***

HEKAHEKA MSITUNI - 4

    


Simulizi : Hekaheka Msituni 


Sehemu Ya Nne (4)

  
    

Simulizi : Hekaheka Msituni 

Sehemu Ya Nne (4)





“Kuingia katika kikosi cha waasi halafu na kumchukua mwanajeshi mmoja miongoni mwao. Duh! Jambo hili kweli mtihani mzito sana!” afisa mwingine naye aliongezea kumuunga mkono yule wa mwanzo.



“Kwa hiyo kwa kusema hivyo mnamaanisha nini? Mna maana kwamba tumwache mheshimiwa Rais apoteze maisha?” Chifu aliuliza.



“Hapana, tulikuwa tunajaribu kuweka wazi ugumu wa jambo lililopo mbele yetu” yule aliyetoa kauli mara ya kwanza aliongea.



“Kauli zenu ni za kukatisha tama. Kwa sasa tunatakiwa tufikirie namna ya kulitatua tatizo hili na si kukatishana tama!” Chifu aliongea huku akionyesha wazi kwamba alikuwa amekerwa na kauli za maafisa wale wa mwanzo.



“Tusamehe ndugu!” maafisa wale waliomba radhi.



“Mimi nitakwenda katika misitu ya Masolo. Nitaingia katika kikundi cha waasi cha BMM na nitamleta bwana Martin Samweli hapa!” Inspekta Tom Green aliongea.



Maafisa wote pale walishindwa kuamini kile ambacho walikuwa wakikisikia. Walihisi huenda Inspekta Tom Green alikuwa ameanza kuchanganyikiwa. Haikuwa rahisi kwa mwanadamu wa kawaida kufanya maamuzi yenye kuhatarisha maisha kwa kiasi kile.



Ukiachilia mbali kuhatarisha maisha lakini maamuzi yale yalikuwa hayawezekani. Haikuwa rahisi kwa mtu yeyote kuingia katika kambi ile na akatoka salama kabisa. Kwanza ataingiaje pasi kupoteza maisha kabla hata hajaingia katika kambi ile maana ulinzi ambao ulikuwa katika kambi ile haukuwa wa kawaida. Kauli ya Inspekta Tom Green iliwafanya maafisa wale wapigwe na butwaa la mwaka.



Ni Chifu pekee ndiye ambaye hakushangazwa na kauli ya Inspekta Tom Green. Yeye alimfahamu kijana wake huyu kwamba alikuwa na uwezo wa pekee sana. Alikuwa na uwezo mkubwa sana katika tasnia nzima ya ujasusi pamoja na mapigano.



Alikuwa na uwezo wa kupambana na jeshi kubwa kwa wakati mmoja na akatoka na ushindi. Kwa upoande wake maamuzi ya Inspekta Tom Green aliyabariki kwa moyo mkunjufu kabisa. Hakuwa na wasi hata kidogo katika moyo wake.



“Heeee! Itawezekanaje?” afisa mmoja alishindwa kujizuia na kuamua kuuliza.



“Hili ni jambo la uzalendo linalohitaji moyo wa pekee. Ukiwa na moyo dhaifu huwezi kufanya jambo kama hili. Rais wetu anahitaji msaada kwa sasa katika kuyaokoa maisha yake. Nina imani na kijana wangu. Ataikamilisha misheni hii!” Chifu aliongea.



Maafisa wengine walikuwa bado wameduwaa. Hawakuwa wameyaamini maneno ya Chifu. Waliona jambo lile kama haliwezekani kabisa.



“Nimesema nitaifanya shughuli hii. Wakuu hebu ondoeni shaka zeni na tufokasi zaidi katika afya ya Rais” Inspekta Tom Green aliongea.



“Dokta Morgan naomba schedule to the deadline!” Inspekta Tom Green aliongea akimtazama dokta Morgan ambaye alikuwa ameshikilia nyaraka fulani mkononi.



“Kwa sasa tumefanikiwa kuizuia damu isiendelee kuvuja katika jeraha. Kwa kiwango cha damu kilichopo katika mwili wa Rais, hatakuwa na maisha marefu kama hataongezwa. Kwa makadirio ni masaa tisini na sita. Yaani tuna siku nne kabla ya mheshimiwa Rais hajapoteza maisha kama hatoongezwa damu!” dokta Morgan aliongea.



“Siku nne nyingi sana kwangu. Kabla ya masaa tisini na sita nitakuwa hapa na Martin Samweli. Dokta Morgan trust me. I will bring you Martin Samweli before the deadline!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Nakuamini sana kamanda. Naamini kila kitu kitakwenda salama kabisa na Rais atarejea katika kiti chake salama” dokta Morgan aliongea.



“Wakuu, naomba nikaanze safari. Sina muda wa kuendelea kupoteza!” Inspekta Tom Green aliwaaga wale wakuu wa usalama.



“Nadhani ninahitaji kwenda na kijana wangu kwa maandalizi. Tutakutana baadaye kidogo wakuu!” Chifu naye aliongea akianza kuondoka akiambatana na Inspekta Tom Green.

******

KATIKA OFISI ZA BSA



“Wazee, kama ambavyo nilizungumza hapo awali, nina misheni kubwa sana katika misitu ya Masolo ambako ninatakiwa nimlete bwana Martin Samweli mwanajeshi kutoka kikosi cha waasi cha BMM kwa ajili ya blood donation kwa mheshimiwa Rais” Inspekta Tom Green aliongea.



“Kwa nini tusiende wote mkuu maana misheni hii ni ya hatari” Inspekta John Michael aliongea.



“Kama ulivyokwishasema kwamba misheni hii ni ya hatari sana. Hatutakiwi kukirisk kikosi chote. Acha niende mwenyewe. Ninawamudu wale jamaa katu hawawezi kunipa shida!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Uko sahihi kabisa mkuu. Pekee wawaweza wale jamaa but you need mya company!” Latoya aliongea.



Inspekta Tom Green alibaki kimya akimtazama Latoya. Hakufahamu ajibu nini.



“You don’t have to say no. tutakwenda pamoja!” Latoya alisisitiza.



“Yes boss. Unahitaji kampani ya Latoya!” Hashim naye alisisitiza.



“Ok, hebu kajiandae tuanze safari kwani hatuna muda wa kupoteza. Muda ni finyu sana kwetu!” Inspekta Tom Green aliongea akimtazama Latoya.



“Rodger that boss!” Latoya alijibu na kusimama kwa ajili ya kwenda kujiandaa.

******





“Ok, hebu kajiandae tuanze safari kwani hatuna muda wa kupoteza. Muda ni finyu sana kwetu!” Inspekta Tom Green aliongea akimtazama Latoya.



“Rodger that boss!” Latoya alijibu na kusimama kwa ajili ya kwenda kujiandaa.



SASA ENDELEA



NDANI YA CHOPA



“Kwa jinsi uhitaji wa damu hii ulivyokuwa wa muhimu, tunahitaji kutumia siku moja tu kuhakikisha kwamba tumempata bwana Martin Samweli na kumfikisha Kano” Inspekta Tom Green aliongea.



“Ni kweli usemayo kamanda. Lakini naona mazingira ya kambi ile siyo rafiki kuitimiza misheni hii kwa haraka kiasi hicho” Latoya aliongea.



“Umeongea sahihi kabisa Latoya. Ni kweli katika kambi ile kwa mujibu wa ramani imegawanyika katika sehemu mbili. Kwanza kabisa kuna makazi ya wananchi wa kawaida na upande wa pili kuna kambi ya jeshi. Sasa katika misheni hii tunatakiwa tuvifanye vile visivyowezakana viwezekane. Sisi ni askari wenye mafunzo ya hali ya juu. Naamini hili litawezekana. Kumbuka maisha ya Rais kwa sasa yapo mikononi mwetu!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Kuvamia kambi ni jambo dogo. Ugumu ninaouona hapa ni namna ya kumshawishi askari huyu kuondoka na sisi” Latoya aliongea.



“Hiyo itawezekana tu. Akikataa basi itatubidi kutumia njia ya pili yaani kuhakikisha kwamba anafika Kano ndani ya muda uliopangwa apende asipende!” Inspekta Tom Green aliongea.



Wakati huo chopa iliendelea kukata anga. Rubani alikuwa makini kabisa kuhakikisha kwamba anakiongoza chombo katika hali ya usalama. Kipindi hicho chote Inspekta Tom Green pamoja na Latoya waliendelea luzungumza hiki na kile katika kuiboresha mikakati yao ya uvamizi katika kambi ile ya waasi. Mioyo yao ilikuwa na ari kubwa sana ya kufanya misheni ile kwa mafanikio ili kuyaokoa maisha ya mheshimiwa Rais.



Mwendo wa masaa matano uliwafikisha katika eneo la misitu ya Masolo.



“Nadhani wewe utushushe hapa na ugeuke kurejea Kano. Eneo hili kwa sasa siyo salama kabisa. Haitakiwi waasi hawa wabaini uwepo wetu mapema kabla ya misheni kukamilika!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Sawa mkuu!” rubani alijibu huku akiishusha chopa ile mahali fulani ndani yam situ.



Baada ya hapo Inspekta Tom Green na Latoya walishuka. Chopa ilipaa na kurudi ilikotoka.



“Haya mama. Let’s start the game!” Inspekta Tom Green huku akibeba begi lake ambalo lilikuwa na silaha.



“Rodger that darling!” Latoya alijibu huku naye akilibeba begi lake mgongoni.



Baada ya hapo walianza safari ya kusonga mbele huku silaha zao zikiwa mikononi mwao. Walikuwa makini sana kila walipotembea kwani walifahamu kwamba msitu ule ulikuwa ukimilikiwa na waasi hivyo hatari yoyote yaweza kutokea.



Mwendo wa saa moja uliwafikisha katika kijiji ambacho kilikuwa kikimilikiwa na waasi lakini walikuwa wakiishi raia wa kawaida. Hii ina maana kwamba utawala uliokuwepo katika kijiji kile ulikuwa ni utawala wa waasi chini ya Kanali Edson Makoko.



Inspekta Tom Green na Latoya hawakutaka kupita katika kijiji hiki. Hii ilikuwa ni kwa sababu za kiusalama. Walichokifanya ni kuambaa ambaa pembezoni mwa kijiji kile na kuendelea kusonga mbele wakiifuata ramani ya msitu ule ambayo walikuwa nayo.



Baada ya muda fulani wa kutembea, hatimaye walianza kuyaona majengo ya kambi ya jeshi. Majengo hayo vilikuwa ni vibanda ambavyo vilikuwa vimejengwa kwa miti na kuezekwa nyasi wakati vingine viliezekwa kwa bati.



“Haya sweetheart, tumekwishafika tayari. Ngoja tuwaonyeshe shoo moja matata sana!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Yes darling, let’s pop in!” Latoya alijibu.



Walianza kutembea kwa tahadhari kubwa sana mpaka walipokifikia kibanda cha kwanza ambacho kilikuwa kimejengwa miti na turubai.



Walipochunguza vizuri kuna kitu walikigundua. Vibanda vile vilikuwa na majina. Majina yale yalikuwa ni ya askari ambao wanaishi ndani ya vibanda hivyo.



Mungu alikuwa upande wao kwani kibanda ambacho walikuwa wamekifikia kwa mara ya kwanza kilikuwa kimeandikwa Martin Samweli hii ikimaanisha kwamba mtu wao ambaye walikuwa wamemfuata ambaye ni Martin Samweli alikuwa akiishi ndani ya kibanda kile.



Inspekta Tom Green alimwonyesha ishara Latoya kwa kutumia kichwa chake na Latoya alijibu kwa kuonesha idara ya dole gumba. Hii ilimaanisha kwamba alikuwa amemwelewa Inspekta Tom Green. Kwa tahadhari kubwa sana Latoya alizama ndani ya kibanda kile huku Inspekta Tom Green akiwa anaangalia usalama upande wa nje.



Kwa wakati huo yalikuwa ni majira ya saa nane za mchana. Martin Samweli alikuwa amejipumzisha juu ya kitanda chake ndani ya kibanda kile usingizi ukiwa umempitia. Latoya alimgusa Martin Samweli kumuamsha ambapo Martin alishtuka ghafla na kuishika bastola yake mkononi.



“Wewe ni nani na umefuata nini hapa!” Martin Samweli alifoka huku akimtazama Latoya.



“Naitwa Latoya. Ninatoka Kano. Nimekuja hapa kwako kwa sababu nina shida kubwa sana. Na sina muda mrefu wa kuendelea kuwepo hapa!” Latoya aliongea.



Martin Samweli alimtazama Latoya usoni na kuvutiwa na sura nzuri nay a kirembo ya Latoya. Sura ile ilimfanya Martin Samweli apunguze munkari wake kwani aliamini mwanamke huyu hawezi kuwa hatari kwake. Na hili ndilo kosa kubwa sana alilolifanya. Alikosea sana kumwamini Latoya. Hakufahamu kwamba Latoya alikuwa ni mwanamke hatari zaidi ya hatari yenyewe.



“Una shida gani?” Martin Samweli aliuliza.



“Hali ya mheshimiwa Rais ni mbaya sana kwani amejeruhiwa kwa kuchomwa kisu. Kuna uhaba wa damu ya kumwongezea. Rekodi zimeonyesha kwamba damu yako ndiyo inafanana na ya mheshimiwa Rais” Latoya aliongea.



“Unasemaje wewe kenge. Yaani huyo mtu unayemsema ni adui yangu namba moja. Kwanza ilikuwa inafahamika kwamba amekufa, kumbe amenusurika. Halafu nashangaa umefikaje hapa pasi kuonekana!” Martin Samweli aliongea huku sasa akiwa amemwonyeshea Latoya bastola.



“Martin Samweli nadhani kuna mambo mengi sana ambayo mnapotoshwa na huyu kiongozi wenu Kanali Edson Makoko. Yeye anachokitaka ni kuwatumia ili aweze kutekeleza adhma yake ya kuwa Rais wa Bantu. Ninachokuomba kuwa mzalendo na itetee nchi yako!” Latoya aliongea.



“Hebu ondoa ngonjera zako hapa!” Martin Samweli alizidi kufoka.

****





“Martin Samweli nadhani kuna mambo mengi sana ambayo mnapotoshwa na huyu kiongozi wenu Kanali Edson Makoko. Yeye anachokitaka ni kuwatumia ili aweze kutekeleza adhma yake ya kuwa Rais wa Bantu. Ninachokuomba kuwa mzalendo na itetee nchi yako!” Latoya aliongea.



“Hebu ondoa ngonjera zako hapa!” Martin Samweli alizidi kufoka.



SASA ENDELEA



“Hebu fikiria athari zitakazopatikana na vita ambayo mnataka kuianzisha. Hebu fikiri ni maisha ya watu wangapi wasio na hatia ambayo yatapotea. Fikiria kama katika wahanga wa vifo hivyo wanakuwepo watu wa familia yako. Ni uchungu kiasi gani utaupata? Hebu kuwa mzalendo kwa kuokoa maisha ya Rais. Hakika utatangazwa shujaa wa Taifa na makosa yako yote yatafutwa!” Latoya aliongea.



“Nimekwambia nyamaza kunguni wewe. Kwanza inabidi nikuripoti ili uweze kukamatwa na kuuawa kidudumtu wewe!” Martin Samweli alifoka.



“Samahani sana brother. Hilo haliwezi kutokea!” Latoya aliongea.



Wakati huohuo aliipangua bastola ya Martin Samweli na kisha alimbandika ngumi ya uso. Martin Samweli alihisi nyotanyota. Kabla hajatahamaki mateke matatu mfululizo yalitua kichwani kwake na kumbwaga chini.



Baada ya hapo Latoya alimpa Martin Samweli pigo la nyuma ya kisogo ambalo lilimfanya apoteze fahamu. Latoya aliibonya batani Fulani katika saa yake ambapo muda huohuo saa ya Inspekta Tom Green kule nje ilipiga mlio. Inspekta Tom Green aliingia haraka sana ndani ya kibanda kile. Ndani ya kibanda aliweza kuushuhudia muziki ambao alikuwa ameucheza Latoya.



“Ha ha ha haaaaa! You are the beast!” Inspekta Tom Green aliongea huku akimbeba Martin Samweli begani mwake.



Baada ya hapo safari ya kutoka katika kambi ile ilianza. Mwendo ulikuwa ni wa haraka sana. Mbele kidogo waliweza kuliona gari ambalo lilikuwa limeegeshwa. Walimwingiza Martin Samweli ndani ya gari lile. Inspekta Tom Green aliliwasha na kasha waliondoka kutoka eneo lile.

*******

Mwendo wao ulikuwa ni wa kasi sana. Ndani ya muda mfupi walikuwa wamekwishakikaribia kile kijiji ambacho kinamilikiwa na waasi. Pale waliamua kutumia akili ya kikomando. Waliamini kwamba kama wangelipita na gari lile pale kijijini, basi waasi wangeliweza kushtuka na kuanza kuwaandama.



Inspekta Tom Green alichepusha gari kutoka barabarani na kuliingiza ndani ya msitu. Aliliingiza ndani kabisa na kasha alisimama. Kwa wakati huo bwana Martin Samweli alikuwa bado amezirai. Na alikuwa amefungwa mikono yake ili kama ataamka basi asiweze kuleta matata.



“Now we walk!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Yes ofcourse!” Latoya alijibu.



Walishuka kutoka kwenye gari. Inspekta Tom Green alimbeba bwana Martin Samweli begani na kisha safari ya kusonga mbele ilianza.

*******

KAMBINI BMM



“Mkuu kuna tatizo limejitokeza!” mwanajeshi mmoja aliongea mbele ya Kanali Edson Makoko.



Hii ilikuwa ni ndani ya ofisi ya Kanali Edson Makoko ambaye alikuwa bize toka asubuhi akiuandaa mpango wa mapinduzi.



“Tatizo gani?” Kanali Edson Makoko aliuliza.



“Martin Samweli ametoroka kambini” mwanajeshi yule aliongea.



“Una maana gani?” Kanali Edson Makoko aliuliza tena.



“Ameasi mkuu. Ameacha ujumbe kwamba ameamua kurudi serikalini na kuomba msamaha” mwanajeshi yule aliongea.



“Shiiiit! Asakwe mara moja na kurudishwa hapa. Anaifahamu siri na mipango yetu mingi sana!” Kanali Edson Makoko alifoka.



Wakati wanaondoka baada ya kumteka Martin Samweli, Inspekta Tom Green aliacha ujumbe kwamba akijifanya ni Martin Samweli ndiye ambaye aliuacha. Kitendo hiki kilikuwa na maana kubwa sana kumbuka kamba maafisa hawa wa BSA kila jambo walitendalo, hulitenda kwa kutumia akili kubwa sana.



“Ita paredi mara moja. Mbwa huyu ni lazima arejeshwe hapa mara moja!” Kanali Edson Makoko alifoka.



“Sawa mkuu!” mwanajeshi yule alijibu huku akipiga saluti na kuondoka mle ofisini.



Baada ya dakika mbili king’ora kilisikika pale kambini. King’ora hiki kiliashiria kwamba kulikuwa na hali ya hatari ambayo ilikuwa imetokea. Wanajeshi kutoka kila kona ya kambi ile walianza kukusanyika katika uwanja mkubwa sana pale kambini ambao hutumika kwa ajili ya paredi.



Baada ya kujipanga katika mistari mingi iliyonyooka, Kanali Edson Makoko aliwasili eneo lile. Kila mwanajeshi alikuwa kimya akiwa na shauku ya kusikia ni nini kilikuwa kimetokea.



“Soldiers, kuna tatizo moja limetokea. Kuna mmoja miongoni mwetu ameasi jeshi na sasa yuko mbioni kwenda kujikabidhi kwa serikali. Mwenzetu huyu ni askari Martin Samweli!” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo.



“Haaaaaa!” wanajeshi wote walishangaa.



“Sasa bwana huyu anazijua siri zetu nyingi pamoja na mipango yetu yote. Akifika mikononi mwa serikali tu, basi itakuwa ni rahisi sana kwa serikali kutuvamia na kutushinda. Hivyo basi ninaagiza kwamba ndani ya muda mfupi bwana huyu awe amerejeshwa hapa akiwa mzima kabisa. Nitamuua kwa mkono wangu!” Kanali Edson Makoko aliongea.



“Haya tawanyikaaaaa!” Kanali Edson Makoko alifoka.



Wanajeshi walianza kutawanyika na kwenda katika ghala la kuhifadhia silaha. Walichukua silaha na kisha waliingia msituni tayari kumsaka bwana Martin Samweli. Kulikuwa na askari wa miguu ambao walikuwa na mbwa maalum, kulikuwa na askari wa anga pamoja na askari wa miguu. Kwa kifupi jeshi la Kanali Edson Makoko lilikuwa limekamilika hasa.

*******

Safari ya Inspekta Tom Green, Latoya pamoja na mateka wao ilikuwa bado inaendelea ndani ya msitu wa Masolo. Mateka wao alikuwa bado yupo katika hali ya kupoteza fahamu. Hii kwa kiasi kikubwa iliwapa urahisi wa kusonga mbele pasi upinzani kutoka kwa mateka wao. Kwa sasa walikuwa eneo ambalo lilikuwa na mto mkubwa sana. Hiki kilikuwa ni kizingiti kikubwa sana katika kuendelea na safari yao.



“Sasa tunafanyaje hapa?” Inspekta Tom Green aliuliza.

“Tunahitaji boti” Latoya aliongea.

*****





“Sasa tunafanyaje hapa?” Inspekta Tom Green aliuliza.

ITAENDELEA

ITAENDELEA

HEKAHEKA MSITUNI - 3

    


Simulizi : Hekaheka Msituni 


Sehemu Ya Tatu (3)


Simulizi : Hekaheka Msituni 

Sehemu Ya Tatu (3)





Kumbe haikuwa imejulikana. Mheshimiwa Rais Ditric Mazimba alikuwa katika hatari kubwa sana. Walinzi hawa wawili ambao walikuwa wakilinda hapa mlangini walikuwa ni wanajeshi kutoka katika kikundi cha uasi cha Bantu Military Movement. Walikuwa hapa kwa shughuli maalum ambayo walitakiwa kuitekeleza kwa haraka sana na kwa ufanisi mkubwa. Kwa mara nyingine tena Kanali Edson Makoko alikuwa amefanya mambo yake.



Mlinzi mwanajeshi mmoja aliitoa kadi yake mfukoni na kuipachika katika mashine maalum ambayo ilikuwa pale mlangoni. Baada ya hapo alibonyabonya namba kadhaa na mlango ulifunguka. Hatimaye mlinzi yule aliufungua mlango ule taratibu na kisha aliingia ndani.



Kwa wakati huo mheshimiwa Rais Ditric Mazimba alikuwa amekwishalala. Askari Yule mmoja aliyekuwemo mle ndani naye alikuwa amepitiwa na kausingizi kidogo hivyo alikuwa amejiegesha kitini.



Bila ya kupoteza wakati mwanajeshi yule alikirusha kisu chake ambacho kilitua katika shingo ya mlinzi yule na kuzama katika koromeo. Mlinzi yule alianguka chini na kuanza kutapatapa huku akikoroma kuupigania uhai wake.



Upande wa nje ya chumba alicholala mheshimiwa Rais Ditric Mazimba yule askari inchaji aliendelea kufanya doria ya kuyazungukia maeneo yote ambayo yalikuwa yamewekewa ulinzi. Ghafla kichwa cha askari yule afisa inchaji wa ulinzi kilichemka haraka haraka, alihisi palikuwa na tatizo katika chumba cha mheshimiwa Rais.



Katika mlango wa chumba kile alionekana amesimama askari mmoja wakati pale walikuwa wamepangwa askari wawili.



“Huyu mwingine ameenda wapi?” inchaji yule alijiuliza swali lile kwa sauti ya chini. Baadaye aliamua kwenda kuangalia palikuwa na tatizo gani pale.



“Mwenzako yuko wapi?” askari yule inchaji aliuliza.

Askari yule ichaji hakupata jibu kutoka kwa mlinzi yule. Alichokipata ni ngumi kali ambayo ilifuatiwa na teke ambalo lilimkalisha chini. Kisu kilirushwa kumfuata pale chini lakini alikiona na kukikwepa. Hapo ndipo askari yule inchaji alipotambua kwamba walikuwa wameingiliwa na maisha ya mheshimiwa Rais yalikuwa hatarini.



Kutoka pale chini alijibinua na kusimama dede tayari kwa mashambulizi. Alijipanga kwa mapigo ya karate ambapo jambazi yule mlinzi naye alifanya vivyohivyo. Jambazi yule alirusha pigo la mkono ambapo askari inchaji alibonyea na kuliepa. Teke kali lilimfuata lakini nalo alilikinga kwa mikono yake yote miwili.



Ndipo naye askari inchaji alipomfyatua teke jambazi yule na kumfya ale mweleka. Alipotaka kusimama alitulizwa kwa ngumi mbili mfululizo ambazo zilifuatia na pigo la karate katika koo lake. Pigo lile lilizikata kabisa pumzi za jambazi yule na hatimaye alikata roho. Kwa kujiridhisha askari inchaji yule alichomoa bastola na kumimina risasi katika kichwa cha jambazi yule.



“Section A ….. Section B …. Section C …. We have the situation! Over!” askari inchaji aliongea katika kifaa chake cha mawasiliano akiwataarifu walinzi wote katika ikulu ile kwamba walikuwa wamevamiwa.







“Section A ….. Section B …. Section C …. We have the situation! Over!” askari inchaji aliongea katika kifaa chake cha mawasiliano akiwataarifu walinzi wote katika ikulu ile kwamba walikuwa wamevamiwa.



SASA ENDELEA



Askari inchaji yule alichomoa kadi yake maalum na kuitumbukiza katika mashine maalum iliyokuwa katika mlango wa chumba ambamo alikuwa amelala mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba. Bastola ikiwa mkononi aliusukuma mlango ule mara baada ya kufunguka na kisha aliingia ndani kwa tahadhari kubwa sana.



Askari inchaji yule hakuamini kile ambacho alikiona mkle ndani. Mlinzi wa Rais alikuwa chini amelala akiwa maiti. Katika kitanda alionekana mheshimiwa Rais akiwa amelala huku mtu mmoja akiwa amekishika kisu kilichokuwa kikimeremeta kwa makali tayari kwa kushusha pigo moja kwa mheshimiwa Rais.



Askari inchaji yule alipiga hesabu za haraka haraka. Kufumba na kufumbua alizimimina risasi mfululizo kuelekea kwa jambazi yule.



Lakini askari inchaji yule alikuwa amechelewa. Kisu kilikuwa kimeshuka na kuzama katika tumbo la mheshimiwa Ditrick Mazimba. Jambazi yule naye alikuwa amepigwa risasi nyingi sana ambazo zilimwangusha chini akiwa maiti.



Tukio lile lilitisha sana. Ikulu ndogo ya Soweni ilikuwa imechafuka. Upekuzi mkubwa sana ulianza kufanyika ili kubaini kama kulikuwa na majambazi wengine ambao walikuwa wamesalia miongoni mwa walinzi wa ikulu ile.



Wakati huo huo hali ya mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba ilikuwa mbaya sana. Madaktari bingwa wa wilaya walikuwa wamewasili pale ikulu na walikuwa wakijaribu kuokoa maisha ya mheshimiwa Rais.



Wakati huohuo kuna helkopta ambayo ilikuwa njiani ambayo ilikuwa inatakiwa imsafirishe mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba kutoka pale Soweni mpaka katika mkoa wa Dolayo ambako mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba angesafirishwa kwa ndege mpaka jijini Kano ambako angepatiwa matibabu.



Taarifa za kuvamiwa mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba pale ikulu ndogo ya Soweni zilikuwa zimefanywa siri kubwa sana. Hii yote ilikuwa ni kwa ajili ya sababu za kiusalama.

*******

“BMM oyeeeee!”

“Oyeeeee!”



“Bantu mpya safiiiiiii!”



“Saaaafiiiiiiiii!”



Hii ilikuwa ni salamu kati ya Kanali Edson Makoko na wanajeshi wake wa BMM pindi alipokuwa amekutana nao kwa dharura. Hii ilikuwa ni pindi alipopata mrejesho wa uvamizi wa kumwua mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba ambao ulikuwa umefanywa na vijana wake.



Kanali Edson Makoko alikuwa na furaha sana. Furaha ambayo alikuwa nayo siku ile hakuwahi kuwa nayo hapo kabla katika maisha yake. Habari ambazo alikuwa amezipata zilikuwa ni habari njema sana kuwahi kutokea katika maisha yake. Habari zile zilikuwa ni muhimu zaidi ya chakula ambacho alikuwa akila.



Wafuasi wa Kanali Edson Makoko walikuwa walimeibaini furaha ambayo bosi wao alikuwa nayo. Hii iliwafanya nao wawe na furaha kubwa sana. Hii ilikuwa ni kwa sababu bosi wao Kanali Edson Makoko anapokuwa na furaha basi hufanya sherehe kubwa sana pale kambini. Watu hunywa na kulewa sana. Pia wanawake Malaya huletwa pale kambini ambapo wanajeshi huburudika kwa kulala nao kimapenzi. Hii ndiyo sababu kuu iliyowafanya wanajeshi wale kufurahi.



“Nina habari njema sana ambazo ninataka niwaletee leo hii!” Kanali Edson Makoko alianza kuongea.



“Kama ambavyo niliwahi kuwataarifu kipindi furani hapo nyuma kwamba Rais Ditrick Mazimba ndiye ambaye alimwua mzee wetu Shukuru Kizibo. Siku zote jambo hili lilikuwa likinitesa sana kwani nilikuwa nikiumia sana kwa unyama huu ambao Rais alikuwa ametutendea. Unyama ule ambao alikuwa ametutendea lilikuwa ni pigo kubwa sana kwetu. Aliturudisha nyuma katika harakati zetu kwa hatua nyingi sana” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo na kuwatazama wanajeshi wao namna ambavyo wanaipokea taarifa yake.



Wanajeshi wote kwa wakati huo walikuwa kimya kabisa. Mioyo yao ilionyesha kuguswa sana na kuchomwa na habari zile ambazo Kanali Edson Makoko alikuwa akiwapa. Hii hasa ilitokana na namna ambavyo walikuwa wamemzoea marehemu mzee Shukuru Kizibo.



“Binafsi sikupenda kuona mwanaharamu yule akiendelea kuvuta pumzi ya dunia hii. Nilitaka na niliazimia kumfanya aulipe uovu wake. Sikutaka kusubiri mpaka siku ya mapinduzi itakapofika. Kwa sababu yeye alikuwa ameyakoroga mambo, basi nasi ilibidi tuyakoroge vilevile” Kanali Edson Makoko aliendelea kumwaga cheche.



Wanajeshi waliendelea kuwa kimya wakiwa na shauku ya kutaka kujua ni jambo gani ambalo limetokea ambalo kiongozi wao Kanali Edson Makoko alikuwa akitaka kuwaambia. Mioyo yao ilikuwa na shauku kubwa sana.



“Basi hapo nilianza kuandaa mpango wa kuhakikisha Rais Ditrick Mazimba anatoweka duniani. Mpango huu nilikaa na kuupanga kwa muda mrefu sana kwani ulikuwa ni mpango ambao ulikuwa unahitaji umakini wa hali ya juu sana hasa ukichukulia hadhi ya mtu ambaye alikuwa akitakiwa kuondolewa duniani” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo.



“Mpango wangu lipokamilika, basi niliuingiza katika utekelezaji. Niliwateua wanajeshi wawili miongoni mwenu kwa ajili ya kuutekeleza mpango huu. Kwanza kabisa ninaleta kwenu habari za huzuni kwani wale wenzetu wawili wameyapoteza maisha yao. Waliuawa wakiwa wanautekeleza mpango huu” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo akiwatazama wanajeshi wake ambao waliviinamisha vichwa vyao kwa huzuni.



“Lakini hatupaswi kuhuzunika sana kwa sababu wenzetu wale walikuwa ni wazalendo ambao walikuwa wamejitolea maisha yao kwa ajili ya kuyatetea maslahi mapana ya jeshi la BMM na wananchi wa Bantu kwa ujumla” Kanali Edson Makoko al;itulia kidogo.



“Habari njema ni kwamba mpango wetu huu umefanikiwa kwani wenzetu wale walifanikiwa kumwua Rais Ditrick Mazimba. Hivyo ninatangaza rasmi kwamba Rais Ditrick Mazimba ameuawa na kisasi cha kifo cha kiongozi wetu kimelipwa. Jambo pekee ambalo tutakuwa nalo kwa sasa ni maandalizi ya mpango wa mapinduzi. Tunatakiwa tuifyekelee mbali serikali nzima ya Bantu. Viongozi hawa hawastahili kabisa kuendelea kuwepo madarakani” Kanali Edson Makoko aliongea.



“Hureeeeeeeee!” wanajeshi wote walipiga kelele za shangwe huku wakizinyanyua juu bunduki zao.



Walionyesha kuwa na furaha kubwa sana kwa habari hizi ambazo walikuwa wameletewa na kiongozi wao. Habari hizi ziliwafanya warukeruke kwa furaha. Hawakuamini kama kilio cha kisasi kwa mtu ambaye alikuwa amemwuua kiongozi wao kilikuwa kimesikika.



Lakini wanajeshi hawa hawakufahamu siri kubwa sanaambayo ilikuwa nyuma ya mambo yale. Wao waliendelea kulishwa unga wa sumu ndani ya fikra zao.

*****





Lakini wanajeshi hawa hawakufahamu siri kubwa sanaambayo ilikuwa nyuma ya mambo yale. Wao waliendelea kulishwa unga wa sumu ndani ya fikra zao.



SASA ENDELEA



“Kwa sasa ninatangaza sherehe za ushindi. Kwa muda wa wiki nzima iktakuwa ni sherehe hapa kambini ambapo tutakunywa pombe na kuburudika. Yaani raha na starehe za aina zote zitakuwepo hapa kambini kwa muda wa wiki nzima!” Kanali Edson Makoko aliongea.



“Hureeeee! Long live our Cornel!” wanajeshi walipiga kelele za furaha huku wakimimina risasi ovyo angani.

******

OFISI ZA BSA JIJINI KANO



Habari zakuvamiwa mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba zilikuwa zimeifikia ofisi ya Idara ya usalama wa Taifa ya BSA. Habari hizi hazikuwa njema hata kidogo. Maafisa waandamizi wakiongozwa na mkuu wao yaani Chifu walikuwa wamekusanyana na kujaribu kutafakari ni vipi tukio baya kama lile liliweza kutokea. Hali ya ulinzi na usalama wa Rais ilikuwaje mpaka mahaini hao wakaweza kujipenyeza na kufanya maafa yale?



Waliamini kwamba ni lazima kulikuwa na uzembe katika kikosi cha usalama wa Taifa na kikosi cha ulinzi na usalama wa Rais.



Wakati huu Dokta Morgan aliwasili katika ofisi za BSA kwa ajili ya kufanya mazungumzo muhim sana na Chifu.



“Karibu sana dokta” Chifu alimkaribisha dokta Morgan



“Ahsante sana Chifu” dokta Morgan alijibu.



“Karibu uketi hapo” Chifu alimwelekeza dokta Morgan mahali pa kuketi katika sofa.



“Starehe!” dokta Morgan alijibu.



“Nadhani umekwishasikia kile ambacho kimetokea kwa Rais wa Jamhuri ya Bantu” Chifu alianza kuongea.



“Ndiyo Chifu. Nimesikia” dokta Morgan alijibu.



“Basi hali ni mbaya dokta. Maisha ya mtukufu Rais Ditrick Mazimba yako hatarini sana” Chifu alitulia kidogo na kumtazama dokta Morgan.



“Nimepokea ujumbe kutoka Idara ya usalama wa Rais ikulu. Wananiomba msaada wa kuokoa maisha ya Rais. Hii ina maana kwamba taaluma yako pamoja na umahiri wako katika tiba vinatakiwa sasa katika kuyaokoa maisha ya Rais. Nadhani umenielewa dokta!” Chifu aliongea.



“Nimekuelewa Chifu. Naamini Mungu atasaidia na maisha ya mheshimiwa Rais yatakuwa salama kabisa” dokta Morgan aliongea.



“Ok, basi nifuate kwa zoezi hilo linaanza sasa!” Chifu aliongea.



Chifu alisimama na kuanza kutoka mle ofisini huku akifuatwa na dokta Morgan. Moja kwa moja walienda mpaka mahali ambapo maafisa waandamizi wa BSA walikuwepo wakifanya mazungumzo.



“Attention! Kama vile ambavyo kila mmoja ana taarifa, ni kwamba mheshimiwa Rais amevamiwa na kuchomwa kisu katika ikulu ndogo ya Soweni. Kwa taarifa nilizonazo ni kwamba hali yake mpaka sasa ni mbaya. Kwa sasa yuko njiani analetwa hapa Kano. Atakuwepo katika hospitali ya Kano kwa ajili ya matibabu ya awali kwa ajili ya kuweka afya yake katika hali ya usalama!” Chifu alitulia kidogo na kuvuta funda la mate.



“Nadhani mpaka hapo mtakuwa mmefahamu kazi nzito ambayo iko mbele yetu kama Idara ya usalama wa Taifa. Kwanza kabisa itakuwa ni kuwatafuta watu waliofanya uhaini huo. Na pili ni kuhakikisha kwamba hakuna jambo linguine la hatari ambalo litampata mheshimiwa Rais” Chifu aliongea.



“Sawa mkuu!” maafisa walijibu kwa umoja.



“Kwa sasa Code 001 utakiongoza kikosi. Naomba umfikishe dokta Morgan mpaka katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano ambapo yeye atasimamia matibabu ya mheshimiwa Rais. Wengine wote pia myahakikisha kwamba mnafanya track katika eneo lote la hospitali ile ili kuhakikisha kwamba hakuna hatari nyingine ambayo itakuwa imepangwa. Hii ndiyo misheni ya awali. Misheni nyingine mtapata taarifa” Chifu aliongea kwa msisitizo.



“Sawa mkuu umeeleweka!” maafisa wote walijibu kwa pamoja huku wakionyesha munkari mkubwa.



“Haya nendeni sasa” Chifu aliongea na kasha aliondoka kutoka eneo lile.



Maafisa wale walijiandaa kwa haraka sana. Baada ya kujiandaa walimchukua dokta Morgan na kuanza msafara wa kuelekea katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano.

*******

HOSPITALI YA RUFAA YA TAIFA YA KANO



Mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba alikuwa amefikishwa katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano. Madaktari walikuwa wakihaha huku na huku katika kuhakikisha kwamba hali ya mheshimiwa Rais inakuwa ahueni.



Dokta Morgan daktari kutoka Idara ya usalama wa Taifa ya BSA ndiye alikuwa daktari ambaye alikuwa ameteuliwa kuhakikisha kwamba maisha ya mheshimiwa Rais yanakuwa salama. Sababu za kumpendekeza na kumteua daktari huyu ilikuwa ni kutokana na umahiri wake katika masuala ya tiba.



Hali ya ulinzi kuzunguka eneo lote la hospitali ile ilikuwa imeimarishwa sana. Askari mbalimbali kutoka katika idara mbalimbali za usalama wa Taifa walikuwa wametapakaa kila mahali katika kuhakikisha hakuna hatari yoyote ambayo inatokea kwa mheshimiwa Rais.



“Hali ni mbaya. Mheshimiwa Rais amepoteza damu nyingi sana. Hivyo anatakiwa kuongezewa damu haraka sana!” dokta Morgan aliongea mbele ya wakuu wa idara mbalimbali za usalama.



“Sasa si aongezewe haraka dokta?” mkuu wa idara ya usalama wa Rais ikulu aliongea.



“Uko sahihi mkuu. Nadhani kila mmoja anawaza kama ambavyo wewe wawaza. Lakini kuna tatizo kubwa sana” dokta Morgan aliongea.



“Tatizo gani dokta?” Chifu aliuliza.



“Damu ya mheshimiwa Rais ipo katika kundi maalum. Watu ambao wana damu ambayo ipo katika kundi hili ni wachache sana. Hivyo hii inaleta ugumu katika upatikanaji wa damu ya kumwongezea mheshimiwa Rais” dokta Morgan aliongea.



“Duh!” wakuu wale wa Idara za usalama wa Taifa walijibu kwa pamoja wakionyesha kuchoka kabisa kwa majibu yale kutoka kwa dokta Morgan.



“Sasa tunafanyaje dokta?” afisa mwingine aliuliza



“Kwa mujibu wa rekodi zilizopo ni kwamba hapa nchini kuna watu sita ambao wana damu ya kundi hili la mheshimiwa Rais. Hawa watano rekodi za upatikanaji wao hazijawekwa vizuri. Lakini yupo huyu mmoja ambaye rekodi zake zipo clear kabisa!” dokta Morgan aliongea.



“Basi huyo aletwe hapa mara moja pasi kupoteza muda” Chifu aliongea.



“Kwa mujibu wa rekodi zilizopo ni kwamba hapa nchini kuna watu sita ambao wana damu ya kundi hili la mheshimiwa Rais. Hawa watano rekodi za upatikanaji wao hazijawekwa vizuri. Lakini yupo huyu mmoja ambaye rekodi zake zipo clear kabisa!” dokta Morgan aliongea.



“Basi huyo aletwe hapa mara moja pasi kupoteza muda” Chifu aliongea.



SASA ENDELEA



“Huyu bwana anaitwa Martin Samweli. Ni askari jeshi katika jeshi la BMM. Hapo awali alikuwa ni mwanajeshi katika Jeshi la wananchi wa Bantu lakini baadaye aliasi na kujiunga na kikundi cha waasi cha BMM” dokta Morgan aliongea.



“Mungu wangu!” wakuu wale waliongea kwa pamoja vinywa vyao vikiwa wazi kabisa kuonyesha kukata tama kabisa.



“Hii ina maana kwamba inatakiwa kwenda katika kikundi hicho cha waasi na kumchukua huyu bwana ili aje awe msaada hapa kwa maisha ya mheshimiwa Rais” dokta Morgan aliongea.



“Aiseee! Hapa tuna changamoto kubwa sana. Litawezekanaje jambo hili?” afisa mmoja alihoji.

ITAENDELEA

   

ITAENDELEA

Blog