Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

UKURASA WA GAIDI - 1

 

IMEANDIKWA NA : BAHATI MWAMBA

***********************************************

Simulizi : Ukurasa Wa Gaidi 

Sehemu Ya : Kwanza (1)


Saa nane na dakika ishirini mchana yalionekana

magari matatu yanayofanana, yakiwa na umbo

kama yale magari ya kusafirishia fedha kwa jinsi

yalivyo na mtenganisho kati ya kichwa cha gari na

'bodi' lake. Magari haya yaliyokuwa mapya yakiwa

na kichwa cha ranngi nyeusi na michirizi ya rangi

ya silva na bodi yake rangi ya maziwa,yalikuwa

katika mfuatano huku yakiongozwa na magari

mawili aina ya Nissan Patrol 'model' mpya rangi

nyeusi mbele huku yakifuatiwa na magari mengine

mawili ya aina hiyo nyuma. Magari haya aina ya

'Nissan patrol' yaliyokuwa na vioo

visivyomuwezesha mtu aliye nje kumuona aliye

ndani (tinted), yalipiga king'ora huku yakiwa

yamesheheni askari makini kabisa kutoka kitengo

maalum cha jeshi la polisi. Mbele ya msafara wa

magari haya umbali wa mita mia hivi kulikuwa na

piki piki mbili za police zilizoenda sambamba huku

zikitawanya magari ili kupisha msafara huu.

Kilichotofautisha msafara huu na misafara mingine

ni ile kasi kubwa iliyokuwa ikiendwa na magari

haya kwa muonekano wa nje kwa wananchi na

muonekano wa ndani ambao watu hawakuuona ni

wale askari maalum ambao ulikuwapo ndani ya

magari haya.

"Eeh bwana eh. Msafara wa 'mapene' huo."

Mwananchi mmoja alisikika akiongea.Na kweli ,

kwa muonekano wa nje, magari haya yalionekana

kama yale magari ya kusafirisha fedha kutoka

benki kuu ya Tanzania iliyo na makao makuu huko

jijini Dar es salaamvna kuzipeleka katika mikoa

mbali mbali. Kitu pekee ambacho watu hawa

hawakujiuliza ni kwamba mbona leo magari haya

yametokea upande wa nyanda za juu kusini.Kwa

bara bara hii ambapo magari yalikuwa yanapita,

ilikuwa dhahiri kuwa magari haya yametokea mkoa

wa Mbeya. .Labda kama magari haya yalipeleka

fedha huko na sasa yanarudi, Lakini pengine cha

kushangaza zaidi ni ule ulinzi mkali uliokuwa

katika magari haya. Kulikuwa na kitu ambacho

hakuna aliyekifahamu zaidi ya waliokuwa ndani ya

magari haya.

*************************************

Saa kumi kasorobo. Msafara huu ulikuwa katikati

ya msitu wa miti mirefu maarufu kama milingoti

kama ilivyotoholewa kutoka neno la kiingereza

'Long tree'. Miti hii ilitengeneza kichaka

kilichopakana na msitu mkubwa zaidi wa miti

inayojulikana kama mipaina au ' pines tree' nayo

pia kama ilivyotoholewa kutoka lugha ya kiingereza

na wakazi wa mkoa wa Iringa.Misitu hii ipo katika

wilaya ya Mafinga huko Iringa.

Msafara huu ulikuwa katika kasi kali sana, wakati

ambapo askari waliokuwa katika gari la mbele

waliposhuhudia pikipiki za police zilizokuwa mbele

ya msafara zikianguka chini mara baada ya askari

waliokuwa wakiziendesha, kushambuliwa kwa

risasi kutoka katika kichaka kimoja ndani ya

msitu.Lilikuwa ni tukio la kushtukiza sana

lililosababisha magari yote kufunga breki kwa

ghafla .Kutokana na ustadi waliokuwa nao

walioendesha magari haya ,haikutokea hitilafu

yoyote wakati walipofunga breki kwa ghafla.

Askari wote waliokuwa katika 'Nissan patrol'

walishuka kwa tahadhari na kuweka silaha zao

tayari kwa lolote. Lakini kabla hata hawajafanya

lolote, walishangaa kuona askari mmoja kati yao

akianguka chini huku akivuja damu nyingi

shingoni. Risasi iliyotokea msituni upande wao wa

kushoto ilimuondoa uhai askari huyu. Hapo ndipo

askari wote walifyatua risasi huku wakizielekeza

bunduki zao kutoka upande wao wa kushoto

ambako ndiko risasi iliyoondoa uhai wa mwenzao

ilitokea.

Askari mwingine akaanguka chini huku akivuja

damu katika goti mguu wa kulia. Safari hii risasi

ilitokeaupande wa nyuma yao na kusambaratisha

mguu wa askari huyu.

''We being shot by snipers.All units take

cover".Ilikuwa ni sauti ya kapteni Joshua akitaka

vikosi vyote vijifiche kutokana na shambulio la

'udunguaji'.Kisha "sniper one and two take your

position(mdunguaji namba moja na namba mbili

kaeni tayari)".Kutokana na kuwepo kwa

mchanganyiko wa askari wa weledi wa Tanzania na

Marekani katika msafara huu, ililazimika kutumika

lugha ya kiingereza ambayo wote waliielewa

vyema.

Hapo moja kati ya yale magari ya kusafirisha pesa

yakalegezwa vifungio vya milango kutokea ndani,

wakashuka askari wawili waliovalia nguo

zilizotengenezwa kwa mfano wa majani makavu ya

mgomba kwa rangi yake na jinsi matambara

yalivyoachwa kuning'inia hovyo katika nguo

hizi.Kichwani walivalia vilemba vilivyopambwa

kiustadi na aidha nyasi kavu au mfano wa nyasi

kavu. Ni kama vile walijua nini kingeweza

kuwapata iwapo wangeshuka bila uangalifu, hivyo

walichukua tahadhari kubwa sana. Askari hawa

walishuka kutoka ndani ya gari kwa kupiga

vikumbo milango kwa ghafla na kujidondosha chini

kama vifurushi.Sekunde hiyohiyo risasi mbili

zililenga usawa wa milango ambayo askari wale

waliipiga kikumbo. Zilitokea upande wa porini na

pengine zililenga kuwadhuru askari wale.

Wadunguaji hawa wawili mmoja kutoka Idara ya

kupambana na ugaidi Tanzania C.T.I (Counter

Terrorism Inteligence) na Mwenzie kutoka Idara

kuu ya ujasusi ya Marekani C.I.A (Central

Inteligence Agency) walijificha nyuma ya miti na

kuanza kazi yao mara moja.Bunduki kubwa za

kisasa maalum kwa kudungua zilikuwa kazini.

Mara walipoanza kufanya kazi yao ,wakitumia lenzi

zilizofungwa katika bunduki hizi ili waone kama

watawaona adui hawa ndipo walipopata

changamoto kubwa sana. Kutokana na msitu huu

kuwa na miti iliyoshonana sana,haikuwa rahisi

kuweza kumuona mtu aliye ndani ya msitu huu.

Miti hii ilifanya kuwe na giza ndani ya misitu hii.


itaendelea.....



Wakati huu ambapo wadunguaji walikuwa

wakijaribu kila namna ili wafanikishe kuwaona na

kuwapiga adui zao,ghafla ilisikika sauti ya helkopta

mahali hapo. Risasi kutoka helkopta mbili ambazo

zilitokea kusikojulikana zilianza kushambulia

msafara wa magari hayo.Hapo magari ya

kusafirisha pesa yakafunguliwa milango kisha

askari kadhaa waliovalia gwanda nyeusi,kofia

ngumu pamoja na fulana nzito maalum kwa kuzuia

risasi , walitoka kutoka ndani ya magari haya.Hawa

walikuwa ni askari wa weledi kutoka katika kikosi

maalum cha United States Marine Corps Forces

Special Operations Command(MARSOC ).Askari

hawa walianza kuzishambulia helkopta zile kwa

kutumia bunduki zao za kisasa kabisa aina ya HK

MP7.Lakini hawakufua dafu japo walitumia bunduki

za kisasa sana ambazo hutumiwa na Kikosi

maalum kingine maarufu sana cha makomando

kutoka katika taifa lao kijulikanacho kama Navy

Seal DEVGRU. Pengine ni kwa sababu katika

mapambano ni rahisi sana kwa aliye juu

kumuangamiza aliye chini kuliko aliye chini

kumuangamiza aliye juu. Adui waliokuwa katika

helkopta waliendelea kumwaga risasi nzito nzito

kama njugu bila kuwapa upenyo askari hawa

maalum kulenga shabaha.Vikosi vyote yaani askari

wa kitanzania na wale wa Marekani waliendelea

kupambana lakini kazi ilikuwa bado ni nzito sana.

Wakati mapambano makali yakiendelea , helkopta

nyingine ya tatu ikatokea upande wa mashariki.Hii

ilikuwa ya tofauti na hizi helkopta nyingine kiumbo

na ilikuja kwa lengo tofauti kabisa.

Helkopta hii ilikuwaimetundikwa ndoano kubwa

sana ambayo ilichomekwa minyororo minene na

imara sana minne.Minyororo hii kwa pamoja

iliunganishiwa sumaku kubwa sana iliyokuwa na

umbo la mche mraba iliyokuwa kama mita mbili za

mraba kila upande.Helkopta hii ilienda hadi juu ya

gari mojawapo kati ya yale magari yanayotumika

kusafirisha pesa, kisha ikagusisha lile sumaku juu

ya paa la bodi la gari hilo kisha ikaanza kupaa

tena.Kadri helikopta ile ilivyopaa ndivyo gari lile

lilivyoanza kunyanyuliwa polepole.Mwisho gari

lilinyanyuliwa juu zaidi na zaidi kisha kutokomea

angani.

Wakati huu ndipo adui wengine walijitokeza

kutokea porini na kuanza kushambulia.Map

ambano yakawa makali zaidi na kufanya eneo lote

kuwa kama eneo la vita kwa kelele za risasi.Askari

wa weledi wa idara ya C.T.I na wenzao wa kikosi

cha MARSOC waliendelea kupambana na adui

hawa waliokuwa wengi sana na waliopigana kwa

ari ya juu sana.Hata adui waliouawa kwa wingi

bado waliendelea kupambana kwa ari ya juu sana

kitu kilichosababisha vita kuwa ngumu zaidi na

zaidi. Kiongozi wa kikosi cha askari hawa wa

weledi wa kitanzania Kapteni Joshua na yule wa

kikosi cha Marekani cha MARSOC kamanda Lucas

Bradock waliongoza vyema vikosi vyao na

kuonesha uwezo wa hali ya juu kimapambano

.Lakini kutokana na ari na uwingi wa adui, vikosi

hivi vilianza kuzidiwa nguvu.

"We are out numbered,sergent John request for

backup". Kamanda wa kikosi cha MARSOC alitoa

maelekezo kwa askari wake kwamba afanye

mawasiliano kuomba usaidizi. "Okey Cover

me".Alijibu sajenti John akitaka kulindwa wakati

akifanya mawasiliano. Kwa kutumia kifaa maalum

cha mawasiliano alichokivaa katika sikio lake la

kushoto na kuanza kuwasiliana na makao makuu

ya muda kuomba usaidizi. Makao makuu haya ya

muda yaliweka kambi ndani. Huku makao makuu

helkopta tatu za kisasa ziendazo kasi aina ya

'Chinook' zilikuwa ziko tayari na makomando tisa

kutoka vikosi vya Navy SeAL Marekani pamoja na

makomando kutoka JWTZ Tanzania. Kikosi hiki

cha Navy Seal kilikuwepo Tanzania tangu miezi

mitatu iliyopita kwa ajili ya kufanya mazoezi ya

pamoja na vikosi vya makomando vya JWTZ ili

kuwaongezea uzoefu makomando hawa wa

Tanzania.

Kikosi hiki kilichojumuisha watanzania na

wamarekani kilikuwa tayari kutoa usaidizi tangu

walipopata taarifa za kiintelijensia kuwa msafara

ule umevamiwa.Walikuwa wanasubiri amri ya

kwenda kutoa usaidizi tu.Mara tu walipopata

mawasiliano, makomando hawa (Navy Seal na

JWTZ) walipaa na helkopta zao muda huo huo.

Uwanja wa mapambano kulikuwa na kelele za

risasi kutoka katika bunduki za wanausalama na

adui.Majibizano ya risasi yaliendelea huku idadi za

majeruhi na maiti zikiendelea kuongezeka kila

upande.Upande wa kikosi cha ' MARSOC' tayari

askari wawili walipoteza maisha na wanne

kujeruhiwa huku Tanzania ikipoteza askari wa

weledi wanne na mmoja kujeruhiwa. Upande wa

adui, walipoteza askari wengi zaidi kwa idadi

isiyojulikana. "Cease fire and take cover". Amri

nyingine ilisikika kutoka kwa kiongozi wa kikosi

cha 'MARSOC' na ambaye ndiye alikuwa mkuu wa

msafara huu kamanda Bradock.Amri hiibiliwataka

askari wote kuacha kupambana bali

wajifiche.Wakati huu ndipo kundi kubwa la adui

likajitokeza kutokea msituni na kuanza

kuyasogelea magari ya wanauslama wale kutoka

pande zote.Sura zao zilionesha kuwa ni watu walio

na asili ya somalia. Wengi kati yao walionekana

kuwa wachafu sana na wengine wadhoofu wa miili.

Lakini ni hawahawa walionekana kuvipa shida

vikosi hivi kwa muda wa saa moja na dakika

thelathini sasa.

Adui walizidi kuyasogelea magari ambayo

yaliwaficha wanausalama wale ndani yake.

Walionekana kuwa na uchu kama fisi mwenye njaa

aliyeona mzoga mahali.Sasa walizidi kusogelea

magari yale huku wakipiga kelele na kunyoosha

bunduki zao mbele.Wakiwa karibu sana na magari

yale,walisikia kelele za helkopta zaidi ya

moja.Kadri sekunde zilivyosogea ,mvumo ule wa

helkopta uliongezeka kuonesha kuwa pengine

helkopta ilikuwa inaelekea upande ule waliokuwapo

wao. Mara wakaanza kuziona helkopta zile

zikiwaelekea na wakati huo huo risasi zikaanza

kurushwa kuwaelekea adui wale . Adui walianza

kuanguka mmoja baada ya mwingine kwa kasi

kubwa.Vikosi vya uokozi vilikuwa vimefika tayari.

Bunduki aina ya FN Minimi 7.62 zilizofungwa

katika helcopter zilifanya kazi yake ipasavyo.

Makomandoo walioshuka kwa miamvuli mita

chache kabla ya kufika uwanja wa mapambano,

nao wakaanzisha mashambulizi ya ardhini na

kufanya adui kuzidiwa nguvu. Vikosi vya usalama

vilivyojificha ndani ya magari navyo vikaendeleza

mashambulizi kama mwanzo.Maadui wakaanza

kuzidiwa nguvu na kuamua kukimbilia msituni

huku wakibeba maiti za wenzao.

Hadi kufika saa kumi na mbili jioni,hakukuwa na

mapambano tena wala sauti ya risasi. Eneo

palipotokea mapambano , lilizungushiwa utepe

maalum na jeshi la polisi ili mtu yeyote asipite na

kuharibu upelelezi. Kisha askari kadhaa wakaletwa

kulilinda eneo hilo.

*********************************************

****************************************************

Mtaalamu wa teknolojia ya kompyuta ambaye pia

alikuwa mtaalamu wa kuvunjavunja ' password'

bwana Abdallah Yusoof,alifanya kila jitihada

kuhakikisha anafungua loki iliyofunga mlango wa

nyuma wa gari lile. Ni lile gari lililobebwa na

helkopta kule katika uwanja wa mapambano.

Alikwisha wahi kufungua loki nyingi sana lakini hii

ya leo ilihitaji umakini wa hali ya juu zaidi. Loki hii

ilitengenezwa kwa mfumo maalum ambapo

mfunguaji alipewa nafasi mbili za kuifungua.

Kukosea mara ya kwanza kungempa mfunguaji

nafasi ya pili.Kukosea mara ya pili kungesababisha

mlipuko kama wa bomu ambao ungeteketeza gari

pamoja na watu ambao wapo karibu na gari.

Abdallah au kama alivyozoeleka kwa ubini wake

Yusoof,alichukua waya fulani wa 'USB'

akauchomeka katika simu yake iliyokuwa na

programu maalum kisha upande wa pili wa waya

huo akauchomeka mahala fulani pembeni ya

kidubwasha kilichobeba vitufe vilivyo na namba

sifuri hadi tisa.Kidubwasha hiki kilifanana na mita

za umeme wa LUKU za TANESCO. Mara

alipochomeka waya huo, namba fulani zilionekana

zikipita na kubadilika kwa kasi katika kioo cha

simu yake kisha zikajitokeza tarakimu sita. Yusoof

akazibonyeza tarakimu zile katika kidubwasha

kile.Ukasikika mlio 'krack'. Loki ilikuwa

imefunguka.

Yusoof akafungua milango ya gari lile ,ndani ya

gari lile akaonekana mtu mwenye ndevu nyingi na

ndefu sana huku akiwa na upara wa haja. Mtu huyu

alikuwa amesheheni pingu madhubuti sana

zilizofungwa mikononi na miguuni. Yusoof

alizitawanyisha pingu hizi kwa risasi kutoka katika

bastola yake.Yule bwana akashuka kutoka katika

gari.

Naam.Labda ni kimo cha gari like kilichomfanya

atoke akiwa kainama kilichangia kumfanya

aonekane kuwa mtu wa kimo cha kawaida

tu.Aliposhuka kutoka katika gari lile alionekana

sasa kuwa mtu mwenye tambo kubwa na mrefu

sana. Japo alikuwa katika vazi kubwa la asili kama

yale yanayovaliwa na 'Wanigeria', lakini haikusaidia

kuficha kuonekana kwa misuli mikubwa

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog