Search This Blog

Monday 27 March 2023

GARI LA KUKODI - 4

  



Simulizi : Gari La Kukodi

Sehemu Ya Nne (4)



“Wote hawajambo, mama…” Joyce alijibu huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani, kisha kikatokea kitambo kifupi cha ukimya kila mmoja akimwangalia mwenziwe kwa namna iliyokosa tafsiri, ilikuwa kama mzazi na bintiye waliopotezana muda mrefu na sasa walikuwa wanaonana kwa mara ya kwanza.


Muda wote yule msichana aliyeambatana na Madame Norah alikuwa amesimama kimya akiwatazama kwa zamu. Uso wake ulikuwa umepambwa na tabasamu pana.


“Nimefurahi sana kukuona tena, naomba mnifuate,” Madame Norah alivunja ukimya huku akiwaashiria Joyce na yule msichana wamfuate.


Wote watatu walielekea upande wa kulia wa lile jumba kulikokuwa na bustani nzuri ya kupumzika na bwawa kubwa la kuogelea lililokuwa limezungukwa na viti vizuri vya kujipumzisha chini ya miamvuli mikubwa ya kivuli.


“Joyce, kwanza kabisa ninakushukuru sana kwa kuacha shughuli zako na kuitika wito wangu, umekuwa unanipa heshima kubwa sana…” Madame Norah alisema baada ya wote kuketi kwenye viti, alikuwa anaonekana mtu mwenye furaha kubwa tofauti na siku nyingine.


“Nisingeweza kukosa kuja kuonana nawe, mama yangu, wewe umekuwa mtu muhimu sana kwangu katika kutimiza ndoto zangu,” Joyce alisema huku akishusha pumzi.




“Sasa nimekuita ili nikukutanishe na mtu atakayekusaidia kwenye majukumu yako kama nilivyokuahidi…” Madame Norah alisita kidogo na kugeuza shingo yake kumtazama yule msichana mrembo aliyeambatana naye.


“Ni huyu hapa… anaitwa Nyaso Gilbert, ni binti mwanamkakati mzuri hasa, msomi wa Shahada ya Kwanza ya Sanaa katika Uchumi na Takwimu, naamini ataweza kusimamia vizuri program zako,” Madame Norah alimwambia Joyce.


“Ooh, thank you, mam,” Joyce alisema huku akimkumbatia Madame Norah kwa upendo, kisha alimgeukia yule msichana. “Habari yako? Naona hata hatujasalimiana!” Joyce alisema kwa furaha huku akinyoosha mkono wake kumpa Nyaso.


“Nzuri tu dada’angu, nimefurahi sana kukutana na wewe maana Madame alikuwa anakusifia sana,” Nyaso alisema huku akinyoosha mkono wake na kukutanisha kiganja chake na kile cha Joyce. Wakasalimiana kwa bashasha zote huku wakifurahi.


Muda ule ule simu ya Madame Norah ilianza kuita, Madame Norah aliiangalia kwa makini na kuminya midomo yake huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani, kisha akaipokea.


“Hello, Mr. Mafuru,” Madame Norah alitamka mara baada ya kuiweka simu sikioni.


“Nipo hapa getini kwako,” sauti ya Mafuru ikasikika kutoka upande wa pili wa simu.


“Ooh umeshafika, waambie wakuruhusu, nipo huku bustanini,” Madame Norah alisema huku akijiinua kutoka kwenye kiti.


“Sasa Joyce, ngoja niwaache mpange mambo yenu, nimepata mgeni. Ila ukitaka kuondoka niambie ili nikupe dereva akuwahishe,” Madame Norah alisema huku akijiandaa kuondoka eneo lile.


“Sawa, mama,” Joyce alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


Muda ule ule Mafuru alitokea na kusimama akiwaangalia kwa makini. Alikuwa amevaa suti ya kijivu na miwani myeusi na mkononi alibeba mkoba mdogo mweusi wa kiofisi.


“Habari zenu warembo?” Mafuru aliwasalimia huku akiachia tabasamu.


“Salama,” Joyce na Nyaso waliitikia kwa pamoja. Mafuru aliwatazama kwa makini, macho yake yakavutwa zaidi kumtazama Joyce. Alimtazama kwa kitambo hadi aliposhtuliwa na Madame Norah.


“Twende basi, unatazama watu hadi wanaona aibu!” Madame Norah alimwambia Mafuru kwa utani.


“Huyo ni binti yako, naona mnafanana sana!” Mafuru alimuuliza Madame Norah huku akielekeza kidole chake kwa Joyce.


“Kwani umekuja hapa kuzungumza na mimi au kupeleleza maisha ya watu wanaonihusu?” Madame Norah alimuuliza Mafuru akionekana kukerwa kidogo.


“Samahani! Sikukusudia kukuudhi,” Mafuru alisema kisha akaanza kumfuata Madame Norah aliyemuongoza kuelekea ofisini kwake ndani ya lile jengo huku wakiwaacha Joyce na Nyaso wameketi kwenye bustani wakipanga program zao.


“Hongera sana Madame, wewe ni mwanamke jasiri sana ambaye juhudi zako zinastahili kuungwa mkono, umeonesha ujasiri mkubwa kwa hiki ulichoamua kukifanya. Kwa hilo lazima nikupongeze,” Mafuru alimwambia Madame Norah wakati wakiingia kwenye ofisi binafsi ya Madame Norah.


“Ni wajibu wetu kurudisha sehemu fulani kwa jamii,” Madame Norah alisema huku akifungua mlango wa ofisini kwake na kumkaribisha Mafuru. Wakaingia na kuketi kwenye viti kwa mazungumzo.


“Uliponipigia simu kuomba kuniona nilishtuka sana, hadi sasa bado nina mshtuko na sijui unahitaji kuongea na mimi kuhusu nini!” Madame Norah alimwambia Mafuru maara baada ya kuketi.


“Kwanza kabisa naomba nikufikishie ujumbe wa Mr. Oduya kwako…” Mafuru alianza kuongea lakini akakatizwa.


“Mr. Oduya! Anataka nini kwangu huyo mzee?” Madame Norah alionekana kushtuka sana.


“Mbona umestuka sana, Madame, kwani Mr. Oduya hapaswi kukusalimia?” Mafuru aliuliza kwa sauti tulivu ya kusihi.


“That old man is a monster… hata wewe sikuamini sana, nimekubali kuonana na wewe kwa vile tu pacha wako, Balozi Mafuru kamuoa mdogo wangu, vinginevyo sina ushirika na ninyi kabisa…” Madame Norah alisema na kushusha pumzi.


“Halafu umenishangaza sana kuniambia una ujumbe wangu kutoka kwa huyo mzee wako wakati mimi na yeye hatuna mazoea, nadhani lazima kuna jambo analitafuta kwangu, siyo bure,” Madame Norah alisema huku akikunja uso wake na kutengeneza matuta madogo.


“Watu hubadilika, Madame, hivyo usimhukumu mtu kwa aliyoyafanya jana wakati leo kabadilika… Mr. Oduya si mtu mbaya kama unavyomfikiria. Amenituma nikwambie kuwa anakupongeza sana kwa juhudi ulizozianzisha na anahitaji kuonana na wewe leo saa kumi na mbili jioni pale Paradise Club mjadili kuhusiana na hii project yako mpya. Ameguswa sana na anahitaji kuchangia…” Mafuru alisema na kumfanya Madame Norah amkate kauli.


“Kwa hiyo anataka kunitumia kama mtaji wake wa kisiasa baada ya kuona mambo yamekwama, siyo? Mimi na yeye wapi na wapi! Toka lini tukachangiana fedha kwenye masuala ya kijamii!” Madame Norah alizidi kushangaa.


“Mr. Oduya ni mtu wa kusaidia sana taasisi mbalimbali zinazofanya mambo makubwa kwa jamii, amekwisha saidia taasisi nyingi tu hadi sasa! Alipata taarifa zako kupitia runinga kuhusu lengo lako la kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga kituo na shule ya watoto wenye mahitaji maalumu, pamoja na makazi bora ya wazee… hujui tu hiki ni kitu alikuwa nacho siku nyingi na ameguswa kuona wewe pia una wazo kama lake, hivyo anataka kutoa mchango wake. Hakutaka kuja mwenyewe lakini amenituma nikwambie kwamba anahitaji kuonana nawe jioni ya leo,” Mafuru alisema huku akimkazia macho Madame Norah.


Kilipita kitambo kirefu cha ukimya, Madame Norah alionekana kuwaza sana, alikuwa njia panda ya ama akubali mwaliko au akatae.


“Sijajua hasa kwa nini atake kufanya hivyo sasa na si wakati mwingine wowote, kwani siku zote alikuwa hajui kuwa huwa ninasaidia makundi yenye mahitaji maalumu?” Madame Norah aliuliza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Mafuru.


“Hupaswi kuhofia, Madame, hakuna jambo lolote baya ingawa ni kweli kama ulivyosema kwamba wewe na yeye hamna mazoea ya karibu lakini naamini kuanzia sasa mtakuwa karibu zaidi, I’m here because I know something you don’t know,” (Nipo hapa kwa kuwa najua jambo usilolijua) Mafuru alimalizia kwa Kiingereza kuonesha msisitizo wake na kumfanya Madame Norah amtazame kwa mshangao Zaidi.


Madame Norah alitulia kwa sekunde chache akijaribu kuyatafakari maneno ya Mafuru pasipo kupata majibu.




“Mpe nafasi naamini kukutana kwenu kutakuwa na faida kwenu wote na hili suala linahitaji utayari wako tu, hayo mengine yote yatakushangaza na kukusisimua zaidi! Kama uko tayari niambie nimpigie simu hapa hapa mbele yako, la kama unadhani hauko tayari pia niambie nimweleze sasa hivi,” Mafuru aliongeza huku macho yake yakiwa yameweka kituo kwenye uso wa Madame Norah.


Madame Norah alishusha pumzi za ndani kwa ndani, alikaa kimya kwa takriban dakika mbili akifikiria sana bila kupata majibu.


“Unaweza kunidokeza, ni mambo gani hayo ambayo unayajua lakini mimi siyajui?” hatimaye Madame Norah alivunja tena ukimya, alikuwa bado ana wasiwasi.


“Ni mambo mazito ambayo hayahitaji kuzungumzwa hapa na wala nisingeweza kukueleza kwenye simu. Ni wewe, yeye na mimi tu tunaopaswa kuendelea kuyajua kwa sasa, labda hadi hapo baadaye kama itahitajika,” Mafuru alisisitiza.


“Okay, nipo tayari kuonana naye Paradise Club saa kumi na mbili jioni,” Madame Norah alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.


* * * * *


Saa kumi jioni, Winifrida Kolimba alikuwa anatembea kwa maringo yaliyoonekana wazi. Hayakuwa maringo ya kutafuta kiki bali alijua wazi alivyokuwa mrembo na wengi walimchukulia kama malaika aliyekuwa ameshushwa duniani kimakosa, hivyo kuonesha maringo ilikuwa ni kichagizo tu cha jinsi alivyo.


Alikuwa na umbile dogo lililovutia mno na kuonekana wazi hata kama angevaa sare za shule, umbile lake lilimshawishi kila mwanamume aliyekamilika kumwangalia kwa uchu wa mahaba mazito. Ilikuwa vigumu sana kwa Winifrida kupita mbele ya mwanamume bila kukata shingo kumwangalia. Kiukweli alikuwa amezawadiwa urembo wa kutosha!


Kwa umbile lake na ile miondoko ya maringo alizidi kutoa tafsiri ya kuwa na ule uzuri usiomithilika, hasa kwa sababu ya weupe wake wa asili usiochanganywa na vipodozi vya aina yoyote na hivyo kuwafanya wanaume wakware wachanganyikiwe, pasipo kujali kama alikuwa mwanafunzi.


Jioni hiyo Winifrida alikuwa anatoka twisheni akiwa amevaa sketi ya rangi ya samawati, blauzi ya rangi ya pundamilia ya mikono mirefu na begi kubwa la madaftari alilokuwa amelibeba mgongoni, na alikuwa anatembea taratibu kando kando ya barabara iliyoelekea mtaani kwao eneo la Tabata Chang’ombe, jijini Dar es Salaam.


Wanafunzi wengine waliokuwa wameongozana naye walikuwa wakimkodolea macho wakati akitembea taratibu huku akionekana kutokuwa na haraka. Ni kweli hakuwa na haraka maana safari yake ilikuwa inaishia mtaa ule ule.


Mbele yake kulikuwa na wanafunzi wengine watatu wa kike walioonekana wakitembea kwa kujikongoja kutokana na uchovu. Wote walikuwa wamebeba mabegi makubwa yaliyowaelemea kwa uzito.


Winifrida alikuwa akiwacheka na kuwafanyia mzaha. Mara kwa mara walikuwa wakigeuka kumtazama kwa hasira lakini yeye aliendelea kuwafanyia mzaha.


Walionekana kumsubiri ili wampe ‘displini’ lakini yeye aling’amua na kusimama kupisha kwanza gari lipite kisha alivuka barabara kuwakwepa na kuelekea upande wa pili wa ile barabara, kwani alikuwa amefika usawa wa nyumbani kwao.


Wale wanafunzi walikonyezana kisha wakavuka barabara kuelekea upande wa pili wakiwa na lengo la kutaka kumkamata lakini Winifrida aligundua hila yao na kukimbilia ndani huku akiendelea kuwafanyia mzaha.


Alipoingia sebuleni, alijitupa kwenye sofa na kulibwaga begi lake juu ya sofa, kisha akajiegemeza kwa mgongo na kupeleka macho yake kuangalia juu ya dari huku akionekana kuwaza.


Mara simu yake iliyokuwa kwenye begi la madaftari ilianza kutoa mtetemo uliomshtua sana, aliangalia huku na kule kuhakikisha hakukuwa na mtu yeyote aliyeshtukia kisha aliinuka haraka, akachukua begi lake na kukimbilia chumbani kwake.


“Jacky, nilishakwambia usinipigie simu hadi nikubip… sasa hivi nipo nyumbani, tutaongea usiku,” Winifrida alisema kwa sauti ya kunong’ona mara tu alipoingia chumbani kwake, kisha aliikata ile simu na kuizima kabisa.


Alizungusha macho yake kukitazama kile chumba chake kwa makini, kilikuwa kikubwa kikiwa na kitanda kikubwa cha samadari cha futi sita kwa sita, cha mbao ngumu za mninga kikiwa na droo mbili kila upande na juu ya droo hizo kulikuwa na taa mbili zilizotoa mwanga hafifu.


Kilikuwa na kabati la nguo la ukutani na pembeni ya lile kabati kulikuwa na meza ya vipodozi yenye kioo kirefu cha kujitazama. Chumba pia kilikuwa na madirisha mawili mapana yaliyofunikwa kwa mapazia marefu yenye nakshi za michoro ya maua yaliyodariziwa vizuri na kuyafanya yapendeze.


Winifrida alijibwaga juu ya kitanda kilichokuwa kimetandikwa vizuri kwa shuka la rangi ya waridi lililofumwa maua katikati akionekana kuchoka, kisha akajilaza chali, miguu kaining’iniza sakafuni na kushusha pumzi. Sasa alionekana kujiwa na mawazo, aligaragara juu ya kitanda kile, kisha aliuchukua mmoja wa mito miwili iliyovikwa foronya rangi moja na ya lile shuka na kuukumbatia halafu akajilaza kifudifudi.


Hapo tena fikra zilianza kutembea kichwani mwake na kuaza kujiuliza vipi angeweza kuendelea kuvikabili vishawishi kutoka kwa wanaume wakware waliokuwa wakimwita kila alikopita? Na vipi angeweza kuyakabili mapenzi ya kijana Jackson yaliyoanza kumwingia moyoni na kuitawala akili yake ilhali yu bado mwanafunzi?


Alifikiria kwa kitambo kidogo huku fikra zikizidi kuranda na kupigana vikumbo ndani ya kichwa chake, mara aligutuka na kunyanyuka kutoka pale kitandani. Sasa mawazo yote aliyokuwa nayo yalipeperuka kwa muda na kuanza kuvua zile nguo alizovaa.


Alipogeuka alikikabili kile kioo kirefu cha kujitazama kilichopachikwa kwenye meza ya vipodozi, na kama kioo kile kilikuwa kikimtua, aliinuka na kukisogelea. Alianza kujianglia kwenye kioo namna alivyoumbika. Alijitazama na kujitazama tena, halafu akageuka na kujitazama huku na huku na alipohisi hajajifaidi bado, alikwenda kufunga mlango.


Alisimama mbele ya kioo akaendelea kuvua nguo zake na kubakiwa na chupi tu. Alijishika kiunoni kwa mikono yake na kujitazama tena huku na huku. Alijigeuza nyuma na kujiangalia matiti yake na kuyatomasatomasa huku akiyachezea.


Endelea kufuatilia stori hii hadi mwisho ili uyajue yote yaliyojificha ndani ya taxi...




Winifrida alijibwaga juu ya kitanda kilichokuwa kimetandikwa vizuri kwa shuka la rangi ya waridi lililofumwa maua katikati akionekana kuchoka, kisha akajilaza chali, miguu kaining’iniza sakafuni na kushusha pumzi. Sasa alionekana kujiwa na mawazo, aligaragara juu ya kitanda kile, kisha aliuchukua mmoja wa mito miwili iliyovikwa foronya rangi moja na ya lile shuka na kuukumbatia halafu akajilaza kifudifudi.


Hapo tena fikra zilianza kutembea kichwani mwake na kuanza kujiuliza vipi angeweza kuendelea kuvikabili vishawishi kutoka kwa wanaume wakware waliokuwa wakimwita kila alikopita? Na vipi angeweza kuyakabili mapenzi ya kijana Jackson yaliyoanza kumwingia moyoni na kuitawala akili yake ilhali yu bado mwanafunzi?


Alifikiria kwa kitambo kidogo huku fikra zikizidi kuranda na kupigana vikumbo ndani ya kichwa chake, mara aligutuka na kunyanyuka kutoka pale kitandani. Sasa mawazo yote aliyokuwa nayo yalipeperuka kwa muda na kuanza kuvua zile nguo alizovaa.


Alipogeuka alikikabili kile kioo kirefu cha kujitazama kilichopachikwa kwenye meza ya vipodozi, na kama kioo kile kilikuwa kikimtua, aliinuka na kukisogelea. Alianza kujianglia kwenye kioo namna alivyoumbika. Alijitazama na kujitazama tena, halafu akageuka na kujitazama huku na huku na alipohisi hajajifaidi bado, alikwenda kufunga mlango.


Alisimama mbele ya kioo akaendelea kuvua nguo zake na kubakiwa na chupi tu. Alijishika kiunoni kwa mikono yake na kujitazama tena huku na huku. Alijigeuza nyuma na kujiangalia matiti yake na kuyatomasatomasa huku akiyachezea.


sasa endelea...


Alijigeuza tena mbele na nyuma na mara kwa ghafla, kama mtu aliyeshtuliwa, aliondoka mbele ya kioo na kufungua kabati la nguo, alitoa sketi fupi ya pundamilia na blauzi nyepesi nyeusi, akavaa haraka na kutoka.


* * * * *


Kwenye ukumbi wa kisasa wa chakula katika mgahawa wa Elli’s, Sammy na Elli walikuwa wameketi kwenye kona moja ukumbini wakinywa sharubati na kuongea. Sammy alikuwa na wasiwasi kuhusu namna ambavyo angemkabili mkewe kumweleza suala la kununua gari, kwa kuwa hakuwa amemshirikisha tangu mwanzo.


“Ukweli hata mimi najiuliza, utamwelezaje mkeo, kwamba hili gari umelipataje?” Elli alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.


“Hata sijui, maana ataniuliza kwa nini hatukushauriana kwanza kabla sijalinunua!” Sammy alisema huku akishusha pumzi.


“Kwa hiyo bado utaendelea kumficha kuhusu matatizo ya kazini kwako?” Elli alimuuliza Sammy huku akimkazia macho.


Sammy aliachia tabasamu, akashusha pumzi za ndani kwa ndani na kuzungusha macho yake mle ukumbini, aliwaangalia kwa muda wateja wachache waliokuwemo mle ndani muda huo, kisha akatoa leso mfukoni na kufuta paji la uso wake.


“Sidhani kama bado nahitaji kumficha ukweli, nimefikia uamuzi wa kumweleza kila kitu leo, natumai atanielewa,” Sammy alisema na kumeza mate kutowesha koo lake.


“Ni bora ufanya hivyo, maana hizi ni changamoto tu katika maisha na kila mtu humtokea, isitoshe mkeo ni mwelewa sana,” Elli alisema huku akibetua kichwa chake akionesha kukubaliana na Sammy.


“Kumficha mkeo ni kuruhusu matatizo zaidi yaibuke ndani ya ndoa yenu, hasa pale atakapokuja kujua kuwa ulimficha. Si hivyo tu, anaweza kunichukia hata mimi kwa kudhani nilikupotosha. Kwa hiyo jaribu kuweka mambo wazi ili mjadili na msonge mbele,” Elli alisisitiza na kumfanya Sammy ashushe pumzi.


“Sasa vipi kuhusu suala la vibali? Nataka gari lianze biashara mara moja.”


“Suala la vibali niachie mimi, hilo limo ndani ya uwezo wangu. Ninaye mtu kwenye mamlaka husika, ni ndani ya siku tatu tu kila kitu kitakuwa kimekamilika,” Elli alisema akimhakikishia Sammy. Na hapo tabasamu pana likachanua kwenye uso wa Sammy.


* * * * *


Saa kumi na mbili kamili Madame Norah aliwasili katika viunga vya Paradise Club akiwa ndani ya gari lake aina ya Mercedes Benz E-Class la rangi nyeusi. Aliingia baada ya kuvuka vizuizi vitatu vyenye ulinzi wa uhakika.


Alikuwa amevaa suti nadhifu ya kike ya rangi ya kijivu iliyokuwa imemkaa vyema na kumpendeza, begani alitundika mkoba mzuri wa nguo ya pundamilia uliomgharimu fedha nyingi na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio.


Mkono wa kushoto alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe na mkono wake wa kulia alivaa saa ghali ya kike aina ya Cartier La Dona iliyotengenezwa kwa dhahabu nyeupe ya karati 18, ikiwa na gerentii ya miaka hamsini.


Aliambatana na wanaume wawili wenye miraba minne, walinzi wake waliokuwa wamevaa suti maridadi nyeusi, miwani mikubwa myeusi iliyofunika macho yao na miguuni walikuwa wamevaa buti ngumu nyeusi za ngozi imara ya mamba.


Madame Norah na walinzi wake waliwasili na kupokewa na Mafuru aliyekuwa akiwasubiri muda wote katika viunga vya maegesho ya Paradise Club, kisha aliwaongoza kuelekea ghorofani kwa Mr. Oduya.


Kama kawaida, wale walinzi hawakuwaruhusu wapite hivi hivi bila kukaguliwa, japo walikuwa na taarifa zao, waliwakagua na kuhakikisha hawakuwa na silaha au kitu chochote hatarishi walichobeba, kisha waliwaruhusu wapite.


Mafuru aliwaongoza kuingia katika sebule kubwa walikomkuta Mr. Oduya akiongea na simu lakini mara tu alipowaona alisitisha mara moja maongezi na mtu aliyekuwa akiongea naye kwenye simu na kusimama kwa heshima kumlaki Madame Norah, huku uso wake ukipambwa na tabasamu la bashasha.


“Madame, karibu sana Paradise Club,” Mr. Oduya alisema huku akimpa mkono Madame Norah.


“Ahsante sana mheshimiwa Rais mtarajiwa,” Madame Norah alisema kwa utani na kuwafanya wote waangue kicheko.


“Mdomo wako uwe wa heri, na iwe kama usemavyo,” Mr. Oduya alisema huku akiendelea kucheka kwa furaha kisha aliwaelekeza wageni wake sehemu ya kuketi.


“Madame ni furaha yangu kukutana nawe siku ya leo na kabla ya yote

ninapenda kwanza kusema ahsante sana kwa kukubali mwaliko wangu wa kutaka kuonana nawe jioni hii,” Mr. Oduya aliongeza baada ya wote kuketi kitako.


“Kiukweli mwaliko wako umenishtua sana,” Madame Norah alisema huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.


“Najua, hata hivyo mimi ni nduguyo kabisa, tena ndugu wa damu…”


“Undugu huo veepe, mbona sikuelewi! Wewe Jaluo na mimi Mbondei wapi na wapi!” Madame Norah alisema huku akiendelea kumtazama Mr. Oduya kwa makini zaidi.


“Ni ndugu kwa kuwa wote ni Watanzania, hata hivyo kabla ya yote sijui mtatumia vinywaji gani?” Mr. Oduya aliuliza huku akiwatazama kwa zamu.


“Nadhani ungeeleza kwanza ulichoniitia, suala la vinywaji siyo lililonileta hapa,” Madame Norah alisema huku akionekana kuwa makini zaidi, hakuwa na muda wa kupoteza.


“Okay, sitaki nichukue muda mrefu sana wa kuongea nawe… kwa kifupi nimefuatilia baadhi ya shughuli unazozifanya na nimejikuta nikiguswa sana. Hongera sana kwa kujitoa kusaidia jamii, ni wengi tunajaribu kufanya kama unavyofanya lakini wengi hatufanyi kwa kujitolea kama unavyofanya. Nimeguswa zaidi na hiki ulichoamua kukianzisha sasa…” Mr. Oduya alisema na kunyamaza kidogo. Madame Norah alibaki kimya akimsikiliza lakini akiwa makini kuliko simba jike.




“Najua huamini hiki ninachosema, lakini sote lengo letu ni moja tu, kuisaidia jamii yetu ingawa ni kwa njia tofauti kidogo. Kwa hiyo ninataka tushirikiane katika suala hili ili wewe upate fedha za kusaidia wahitaji na mimi inisaidie katika kampeni yangu ya kuwania urais,” Mr. Oduya alisema kwa sauti tulivu.


“Hilo haliwezekani Mr. Oduya. Siwezi kuwa na ushirika na wewe,” Madame Norah alisema huku akitingisha kichwa chake taratibu.


“Kama unadhani hilo haliwezekani then you’re very wrong, my dear,” Mr. Oduya alisema huku akitabasamu.


“I’m not wrong, Siku zote niko sahihi kwenye masuala yanayohusu mustakabari wangu,” Madame Norah alisema kwa kujiamini huku akiwa amekunja sura yake.


“Lakini hilo ni jambo la kwanza kuna jambo la pili litakalokusisimua zaidi, ninakwenda kukuonesha kitu ambacho you’ve been dying to see,” Mr. Oduya alisema na kuinuka huku akimtaka Madame Norah naye ainuke. Muda huo huo walinzi wa Madame Norah nao wakainuka wakiwa tayari kwa lolote. Mr. Oduya aliwageukia huku akiachia tabasamu.


“Mnaweza tu kusubiri hapa, she’ll be fine,” Mr. Oduya alisema lakini wale walinzi walionesha kutokukubaliana naye.


“Msijali, hawezi kunifanya kitu chochote kibaya,” Madame Norah aliwaambia walinzi wake, wakaonekana kumtii kisha alimfuata Mr. Oduya kuelekea chumbani huku wakiwaacha walinzi wake na Mafuru pale sebuleni. Mlango wa chumbani ulifunguliwa, wakaingia.


Madame Norah alisimama ghafla akiwa anashangaa, alikuwa anatazamana na mwanadada mrembo aliyekuwa ameketi kitandani huku machozi yakimbubujika machoni kwake utadhani mirija ya machozi ilikuwa imepasuka.


Madame Norah alimtazama kwa makini Zainab, alihisi kumfahamu ingawa hakujua walikutana wapi, aligeuka kumtazama Mr. Oduya huku akiendelea kujiuliza ni wapi alikutana na mrembo yule kwani sura yake haikuwa ngeni kabisa machoni kwake.


“What is the meaning of this, Mr. Oduya?” (Hii maana yake nini, Oduya?) Madame Norah alimuuliza Mr. Oduya kwa mshangao akiwa haelewi kilichokuwa kikiendelea.


“Mi’ nilidhani ungefurahi baada ya kukutana na huyu mtu, kwani ulikuwa unaomba usiku na mchana ukutane naye, au siyo!” Mr. Oduya alimwambia Madame Norah huku akitabasamu.


“Ni nani, mbona kama…!” Madame Norah alitaka kusema huku akimwangalia Zainab kwa makini lakini hakumalizia sentensi yake kwani Zainab alishindwa kujizuia, alimrukia Madame Norah na kumkumbatia kwa nguvu huku akizidi kububujikwa na machozi.


“Dada Nuru!” Zainab alisema huku akilia kwa furaha na kuzidi kumng’ang’ania Madame Norah aliyekuwa bado amepigwa na butwaa.


“Kwa-ni wewe n-ni nani?” Madame Norah aliuliza huku akijaribu kujinasua kutoka kwenye mikono ya Zainab aliyeendelea kulia kwa uchungu huku akiwa hataki kumwachia.


“Mimi Zainab Semaya, mdogo wako!” Zainab alisema huku akilia.


“Zainab who! Oh my God!” Madame Norah alimaka kwa mshangao mkubwa sana. Hakuwa ametegemea kabisa kuonana na Zainab baada ya miaka mingi kupita.


Madame Norah hakuweza kujizuia, donge la fadhaa lilimkaba kooni, alijikuta akisononeka sana rohoni, mara kikohozi kidogo kilimtoka na nyuma yake wimbi la machozi lilikuja mbio, alijikuta akilia sana huku akimkumbatia Zainab.


Kwa muda wa dakika kadhaa hali ndani ya chumba kile iligeuka kuwa sehemu ya vilio, wote walijikuta wakilia pasipo kupenda. Baada ya kitambo fulani Madame Norah alimwachia Zainab na kufuta machozi yake, kisha alimwangalia kwa makini.


“Kweli wewe ni Zainab, sura yako haijabadilika kabisa!” Madame Norah alisema huku akishusha pumzi ndefu. Zainab alibaki kimya, alikuwa anafuta machozi.


“Nadhani sasa niwaache, kwa vyovyote mtakuwa na mengi ya kuzungumza,” Mr. Oduya alisema huku akiachia tabasamu, kisha akaanza kupiga hatua kutoka, alipoufikia mlango aligeuka kumtazama Madame Norah.


“Nadhani sasa huna sababu ya kukataa kushirikiana na mimi,” alisema na kufungua mlango, akatoka na kuurudisha nyuma yake.


* * * * *


Winifrida alikuwa amesimama kwenye karo la kuoshea vyombo, alikuwa akisuuza vyombo viwili vitatu alivyolia chakula na kuweka mabaki ya vyakula kwenye chombo maalumu cha kuhifadhia uchafu. Alionekana kuwaza mbali sana.


Pendo alikuwa ananyata nyuma yake kwa tahadhari kubwa akitaka kumshtua lakini Winifrida alihisi uwepo wa mtu nyuma yake, aligeuka haraka lakini Pendo aliwahi kujificha huku akitabasamu.


Winifrida alipuuza na kuendelea kusuuza vyombo. Pendo alijitokeza tena na kuanza kunyata taratibu kumsogelea, Winifrida aligeuka haraka huku akikodoa macho yake kwa hofu na kumuona Pendo akiwa takriban hatua tatu nyuma yake.


“Mtu mwenyewe hujui hata kunyatia,” Winifrida alisema huku akiachia kicheko hafifu.


“Eeh umeogopa! Umeogopa!” Pendo alisema kwa sauti ya juu huku akicheka kisha aliondoka na kuelekea ndani akimwacha Winifrida anamalizia kusuuza vyombo huku akionekana kuwaza mbali.


Joyce alitokea na kusimama mlangoni, akamtazama Winifrida kwa makini. Macho yake yalikuwa yakikitazama zaidi kifua cha Winifrida aliyekuwa amevaa blauzi nyepesi nyeusi na sketi fupi ya pundamilia.


Blauzi ya Winifrida ilikuwa imeloa maji kidogo eneo la kifuani na kuzifanya chuchu zake zilizochomoza juu ya matiti yake magumu ya mviringo ndani ya blauzi nyepesi aliyovaa kiasi cha kuvuta hisia za watu zionekane waziwazi.


“Wee Winnie,” Joyce alimwita Winifrida na kumshtua sana.


Winifrida aliiachia bilauri aliyokuwa akiizuuza kwa mshtuko, ikaanguka sakafuni na kupasuka. Aligeuza shingo yake kutazama kule mlangoni ambako sauti ya Joyce ilitokea na macho yake yaligongana na macho ya Joyce aliyekuwa amesimama akimtazama kwa makini.


“Umenishtua sana, wifi. Nilisikia moyo umefanya, pah!” Winifrida alilalamika huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani. Aliyaondosha macho yake kwa aibu huku akiachia tabasamu la aibu.


“Kwa nini umeshtuka sana! Kwani ulikuwa unawaza nini?” Joyce alimuuliza Winifrida huku akimkazia macho.


“Aka! Nilikuwa siwazi chochote!” Winifrida alijitetea huku akionekana kutaharuki kidogo. Alimtazama wifi yake kwa jicho la wizi na kugundua kuwa alikuwa bado akimtazama kwa makini.






“Kwani kuna nini, wifi?” Winifrida aliuliza huku uso wake ukionesha wasiwasi.


“Usihofu, wifi yangu, kama umemaliza kuosha vyombo njoo sebuleni, nataka tuongee mambo ya kawaida tu yanayokuhusu. Hatujawahi kukaa tukazungumza vizuri,” Joyce alisema kwa sauti tulivu ya upole huku akiachia tabasamu.


“Sawa, wifi,” Winifrida alisema huku akiendelea kuwa na wasiwasi, hakujua wifi yake alitaka kumwambia nini. Alikusanya vyombo vyake na kuelekea ndani.


Baada ya dakika chache, Winifrida na Joyce walikuwa wameketi sebuleni, peke yao tayari kwa mazungumzo. Joyce alikuwa amemuondoa Pendo na kumtaka akacheze nje.


“Sasa, Winnie, unafahamu kwamba hivi sasa wewe ni binti uliyepevuka,” Joyce alisema huku akimtazama kwa makini.


Uchangamfu aliokuwa nao Winifrida ulitoweka ghafla na akawa makini akionesha woga kiasi. Alikaa kimya, Joyce alimkazia macho kwa makini.


“Nadhani unaelewa?” Joyce alimuuliza huku akizidi kumkazia macho.


Winifrida alibaki kimya akiangalia viganja vyake alivyoviweka juu ya mapaja yake. Joyce aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyoingiwa na hofu, alitabasamu na kutafuta namna ya kuyaelekeza mazungumzo.


“Nimekwambia usihofu, wifi yangu, nataka nikwambie hivi, mwili wako sasa una mabadiliko makubwa sana. Umekua,” Joyce alisema na kunyamaza kidogo akiendelea kumtazama Winifrida kwa makini.


Winifrida alivuta pumzi ndefu na kifua chake kikapanda na kushuka. Alitabasamu kidogo kwa ahueni huku akimtupia jicho la wizi wifi yake.


“Najua umeshawahi kuona tofauti mwilini mwako, au siyo?” Joyce alimuuliza Winifrida kwa namna ya kubembeleza alipoona yupo kimya.


“Naziona, wifi,” Winifrida alijibu kwa sauti ya chini.


“Kama zipi?” Joyce aliuliza huku macho yake yakiweka kituo kwenye uso wa Winifrida.


“Wifi bwana!” Winifrida alisema kwa aibu huku akitazama sakafuni.


“Usiniogope, hapa tupo wawili tu, mimi na wewe, na wote ni wanawake. Huna sababu ya kunionea aibu, wifi yangu,” Joyce alisema kwa sauti tulivu ya upole.


“Sawa, wifi,” Winifrida alijibu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Sawa, tufanye kwamba umeziona hizo tofauti, je, unachukua hatua gani kuzikabili?” Joyce aliuliza tena kwa upole.


“Hatua?” Winifrida aliuliza kwa mshangao huku akimtazama Joyce kutaka ufafanuzi wa neno hilo.


“Labda niulize hivi, ni mambo gani unakumbana nayo kila siku unapokuwa shuleni au ukiwa njiani?” Joyce alijaribu kufafanua.


Winifrida alishusha tena pumzi ndefu za ndani kwa ndani, na taratibu kujiamini kukaanza kumrudia.


“Kama kufuatwa na wavulana, wananiita na kuniambia wananitaka.”


“Sasa hao wavulana unawachukuliaje, maana inaonekana ni wengi wanaokuita na kukutaka!” Joyce aliuliza huku akiachia tabasamu.


“Mimi wananikera tu, huwa siwajibu kitu,” Winifrida alisema huku akiukunja uso wake.


“Unayosema ni ya kweli, wifi?” Joyce alimuuliza akiwa kamkazia macho usoni.


“Kweli, wifi,” Winifrida alisema huku akipitisha kidole chake cha shahada shingoni na kukikung’uta hewani.


“Mbona hujawahi kuniambia?” Joyce alimuuliza tena huku akimkazia macho.


“Nilikuwa naogopa.”


“Uliogopa kunieleza? Kwa nini uniogope?” Joyce aliuliza na kumfanya Winifrida abaki kimya asijue la kusema. Alikuwa akinyonganyonga vidole vyake.


“Hakuna mvulana yeyote uliyewahi kumkubalia au hata aliyewahi kukushika shika kifuani na kukwambia una matiti mazuri?”


Winifrida alitingisha kichwa chake kukataa. Joyce alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.


“Hebu angalia kifua chako, jinsi matiti yako yanavyochomoza juu ya blauzi na nguo nyingine unazovaa! Usipende kuvaa nguo nyepesi kama hivyo, mtoto wa kike unatakiwa kuusitiri mwili wako ili kuwapunguzia wavulana shauku,” Joyce alisema kwa sauti ya upole.


“Kama ulikuwa umeanza mchezo mbaya au ulifikiria kuuanza naomba uache kabisa, kazania masomo, wanaume ni walaghai tu, watakudanganya wanakupenda kumbe wanataka kukuchezea tu, na pengine wakuambukize magonjwa ya zinaa au ukimwi, nadhani unafahamu hilo. Pia kuna mimba, nadhani umenielewa vizuri wifi yangu,” Joyce alitoa nasaha zake.


Winifrida alibetua kichwa chake kukubali.


“Sawa, kuanzia leo anza kuusitiri mwili wako vizuri, usivae nguo kama hizi mbele ya kaka yako, si heshima. Inabidi sasa uwe unavaa sidiria nilizokununulia ili kusitiri matiti yako, na hivi vinguo vyako vya ajabu ajabu usivivae tena. Ni hayo tu wifi yangu,” Joyce alisema na kuinuka, akaelekea jikoni.


Winifrida alishusha pumzi ndefu za ahueni.


* * * * *


Saa kumi na mbili na nusu jioni, Sammy alikuwa akiendesha gari lake aina ya Cadillac DeVille akipita barabara iliyotoka Tabata Barakuda kuelekea nyumbani kwake Tabata Chang’ombe.


Aliiacha ile barabara kubwa ya lami na kuchepuka kuingia kushoto akiifuata barabara iliyoelekea nyumbani kwake, alizipita nyumba kadhaa za jirani na kufika mbele ya nyumba yake. Alikunja na kuingiza gari lake kwenye uwanja mpana wa mbele ya nyumba, akasimamisha gari mbele ya geti kubwa jeusi lililokuwa mbele ya ile nyumba yake na kupiga honi.


Baada ya kitambo kifupi geti dogo lililokuwa kwenye lile geti kubwa likafunguliwa nusu na muda huo huo Winifrida akiwa ameongozana na Pendo walichungulia nje na kuliona lile gari lakini hawakujua ni la nani.


Walibaki wakilitazama kwa makini kwa kitambo huku wakionekana kujiuliza maswali yaliyokosa majibu. Sammy aliendelea kutulia ndani ya gari lake akiwatazama kwa tabasamu pasipo kuwashtua. Pendo alilisogelea karibu lile gari na mara akamuona Sammy na kuruka kwa furaha.


“Baba! Baba!” Pendo aliita kwa nguvu na kumfanya Winifrida asogee karibu zaidi, akamtambua Sammy na kuachia yowe dogo la mshangao huku akibaki mdomo wazi.


“Ha! Kaka Sammy!” Winifrida alisema huku akifungua geti kubwa haraka kuruhusu lile gari liingie ndani ya uzio wa ile nyumba.





“Kwani kuna nini, wifi?” Winifrida aliuliza huku uso wake ukionesha wasiwasi.


“Usihofu, wifi yangu, kama umemaliza kuosha vyombo njoo sebuleni, nataka tuongee mambo ya kawaida tu yanayokuhusu. Hatujawahi kukaa tukazungumza vizuri,” Joyce alisema kwa sauti tulivu ya upole huku akiachia tabasamu.


“Sawa, wifi,” Winifrida alisema huku akiendelea kuwa na wasiwasi, hakujua wifi yake alitaka kumwambia nini. Alikusanya vyombo vyake na kuelekea ndani.


Baada ya dakika chache, Winifrida na Joyce walikuwa wameketi sebuleni, peke yao tayari kwa mazungumzo. Joyce alikuwa amemuondoa Pendo na kumtaka akacheze nje.


“Sasa, Winnie, unafahamu kwamba hivi sasa wewe ni binti uliyepevuka,” Joyce alisema huku akimtazama kwa makini.


Uchangamfu aliokuwa nao Winifrida ulitoweka ghafla na akawa makini akionesha woga kiasi. Alikaa kimya, Joyce alimkazia macho kwa makini.


“Nadhani unaelewa?” Joyce alimuuliza huku akizidi kumkazia macho.


Winifrida alibaki kimya akiangalia viganja vyake alivyoviweka juu ya mapaja yake. Joyce aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyoingiwa na hofu, alitabasamu na kutafuta namna ya kuyaelekeza mazungumzo.


“Nimekwambia usihofu, wifi yangu, nataka nikwambie hivi, mwili wako sasa una mabadiliko makubwa sana. Umekua,” Joyce alisema na kunyamaza kidogo akiendelea kumtazama Winifrida kwa makini.


Winifrida alivuta pumzi ndefu na kifua chake kikapanda na kushuka. Alitabasamu kidogo kwa ahueni huku akimtupia jicho la wizi wifi yake.


“Najua umeshawahi kuona tofauti mwilini mwako, au siyo?” Joyce alimuuliza Winifrida kwa namna ya kubembeleza alipoona yupo kimya.


“Naziona, wifi,” Winifrida alijibu kwa sauti ya chini.


“Kama zipi?” Joyce aliuliza huku macho yake yakiweka kituo kwenye uso wa Winifrida.


“Wifi bwana!” Winifrida alisema kwa aibu huku akitazama sakafuni.


“Usiniogope, hapa tupo wawili tu, mimi na wewe, na wote ni wanawake. Huna sababu ya kunionea aibu, wifi yangu,” Joyce alisema kwa sauti tulivu ya upole.


“Sawa, wifi,” Winifrida alijibu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Sawa, tufanye kwamba umeziona hizo tofauti, je, unachukua hatua gani kuzikabili?” Joyce aliuliza tena kwa upole.


“Hatua?” Winifrida aliuliza kwa mshangao huku akimtazama Joyce kutaka ufafanuzi wa neno hilo.


“Labda niulize hivi, ni mambo gani unakumbana nayo kila siku unapokuwa shuleni au ukiwa njiani?” Joyce alijaribu kufafanua.


Winifrida alishusha tena pumzi ndefu za ndani kwa ndani, na taratibu kujiamini kukaanza kumrudia.


“Kama kufuatwa na wavulana, wananiita na kuniambia wananitaka.”


“Sasa hao wavulana unawachukuliaje, maana inaonekana ni wengi wanaokuita na kukutaka!” Joyce aliuliza huku akiachia tabasamu.


“Mimi wananikera tu, huwa siwajibu kitu,” Winifrida alisema huku akiukunja uso wake.


“Unayosema ni ya kweli, wifi?” Joyce alimuuliza akiwa kamkazia macho usoni.


“Kweli, wifi,” Winifrida alisema huku akipitisha kidole chake cha shahada shingoni na kukikung’uta hewani.


“Mbona hujawahi kuniambia?” Joyce alimuuliza tena huku akimkazia macho.


“Nilikuwa naogopa.”


“Uliogopa kunieleza? Kwa nini uniogope?” Joyce aliuliza na kumfanya Winifrida abaki kimya asijue la kusema. Alikuwa akinyonganyonga vidole vyake.


“Hakuna mvulana yeyote uliyewahi kumkubalia au hata aliyewahi kukushika shika kifuani na kukwambia una matiti mazuri?”


Winifrida alitingisha kichwa chake kukataa. Joyce alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.


“Hebu angalia kifua chako, jinsi matiti yako yanavyochomoza juu ya blauzi na nguo nyingine unazovaa! Usipende kuvaa nguo nyepesi kama hivyo, mtoto wa kike unatakiwa kuusitiri mwili wako ili kuwapunguzia wavulana shauku,” Joyce alisema kwa sauti ya upole.


“Kama ulikuwa umeanza mchezo mbaya au ulifikiria kuuanza naomba uache kabisa, kazania masomo, wanaume ni walaghai tu, watakudanganya wanakupenda kumbe wanataka kukuchezea tu, na pengine wakuambukize magonjwa ya zinaa au ukimwi, nadhani unafahamu hilo. Pia kuna mimba, nadhani umenielewa vizuri wifi yangu,” Joyce alitoa nasaha zake.


Winifrida alibetua kichwa chake kukubali.


“Sawa, kuanzia leo anza kuusitiri mwili wako vizuri, usivae nguo kama hizi mbele ya kaka yako, si heshima. Inabidi sasa uwe unavaa sidiria nilizokununulia ili kusitiri matiti yako, na hivi vinguo vyako vya ajabu ajabu usivivae tena. Ni hayo tu wifi yangu,” Joyce alisema na kuinuka, akaelekea jikoni.


Winifrida alishusha pumzi ndefu za ahueni.


* * * * *


Saa kumi na mbili na nusu jioni, Sammy alikuwa akiendesha gari lake aina ya Cadillac DeVille akipita barabara iliyotoka Tabata Barakuda kuelekea nyumbani kwake Tabata Chang’ombe.


Aliiacha ile barabara kubwa ya lami na kuchepuka kuingia kushoto akiifuata barabara iliyoelekea nyumbani kwake, alizipita nyumba kadhaa za jirani na kufika mbele ya nyumba yake. Alikunja na kuingiza gari lake kwenye uwanja mpana wa mbele ya nyumba, akasimamisha gari mbele ya geti kubwa jeusi lililokuwa mbele ya ile nyumba yake na kupiga honi.


Baada ya kitambo kifupi geti dogo lililokuwa kwenye lile geti kubwa likafunguliwa nusu na muda huo huo Winifrida akiwa ameongozana na Pendo walichungulia nje na kuliona lile gari lakini hawakujua ni la nani.


Walibaki wakilitazama kwa makini kwa kitambo huku wakionekana kujiuliza maswali yaliyokosa majibu. Sammy aliendelea kutulia ndani ya gari lake akiwatazama kwa tabasamu pasipo kuwashtua. Pendo alilisogelea karibu lile gari na mara akamuona Sammy na kuruka kwa furaha.


“Baba! Baba!” Pendo aliita kwa nguvu na kumfanya Winifrida asogee karibu zaidi, akamtambua Sammy na kuachia yowe dogo la mshangao huku akibaki mdomo wazi.


“Ha! Kaka Sammy!” Winifrida alisema huku akifungua geti kubwa haraka kuruhusu lile gari liingie ndani ya uzio wa ile nyumba.



“Kwa kweli mdogo wangu umepitia mambo makubwa sana,” Madame Norah aliongeza akisema kwa sauti tulivu huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wa Zainab.


“Sikufikii wewe, dada!” Zainab alisema huku akibetua mabega yake juu, na kuongeza, “Hivi una taarifa zozote za dada Zuena?”


“Zuena yupo Ghana, mambo yake si mabaya. Ameolewa na Dk. Aden Mafuru, Balozi wa Tanzania nchini Ghana,” Madame Norah alisema na kumfanya Zainab ashtuke.


“Huyo balozi ana uhusiano gani na huyu Mafuru, mwanasheria wa Mr. Oduya?” Zainab aliuliza kwa mshangao.


“Ni mapacha. Yule balozi ni mkubwa huyu mwanasheria ni mdogo,” Madame Norah alisema huku akijiweka sawa pale kitandani kisha akainua mkono wake kutazama saa yake ya mkononi.


“Kwa hiyo dada Zuena anaishi Ghana?” Zainab aliuliza tena kwa mshangao uliochanganyika na furaha.


Sasa endelea...


“Ndiyo maana yake, ila yeye hakupata changamoto nyingi kama sisi. Baadaye nitampigia simu nimtaarifu jambo hili…” Madame Norah alikatishwa na simu yake ya mkononi iliyoanza kuita, aliitazama vizuri na kuguna, kisha alipokea na kuongea kwa kitambo kifupi.


“Nilisahau, nina kikao muhimu sana na wadau wangu wa mitindo, nitakutafuta kesho tuongee vizuri, mdogo wangu,” Madame alisema huku akiinuka, waliagana na Madame Norah akatoka.


* * * * *


Saa tatu na nusu usiku iliwakuta Sammy na Joyce wakiwa chumbani kwao, Sammy alikuwa amevaa bukta na singlet na kuketi kwenye pembe ya kitanda na Joyce alikuwa amevaa nguo ya kulalia na alijilaza chali huku akiegemeza kichwa chake kwenye mto laini.


Usiku ule Sammy alikuwa amedhamiria kumweleza ukweli Joyce, kama alivyokuwa ameshauriwa na Elli. Alikohoa kusafisha koo lake akijiandaa kusema jambo lakini alionekana kusita sana.


Joyce alimtupia jicho Sammy kwa makini na kuminya midomo yake. alijua kuwa lipo jambo lililomtatiza Sammy, hata hivyo, aliendelea kubaki kimya akisubiri kuona mwisho wake.


Sammy alikuwa anaangalia chini akionekana kuwaza kwa kitambo kirefu kisha aliinua uso wake kumtazama Joyce na kushusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.


“Mbona sasa hutaki kusema ulichotaka kuniambia!” Joyce alimuuliza Sammy baada ya kumwona muda mrefu akiwa kimya.


Sammy alishusha tena pumzi za ndani kwa ndani na kujisogeza karibu ya Joyce, alijiegemeza kwenye mto huku akimwangalia Joyce kwa makini zaidi. Alikohoa tena kusafisha koo lake.


“Amm…” Sammy alitaka kusema neno lakini alisita kidogo, alijikuta akipata wakati mgumu, mawazo yalianza kumjia, akajiuliza vipi kama Joyce angepokea taarifa tofauti na matarajio yake?


Alianza kupata wakati mgumu sana. Picha ya mtafaruku kati yake na Joyce ilianza kujengeka kichwani kwake, alihisi huenda mambo yangekuwa kama hivi:


“Unajua… nilikuwa nimekuficha ila ukweli ni kwamba nimefukuzwa kazi,” Sammy alimwambia Joyce kwa sauti tulivu.


Joyce alishtuka sana na kumkodolea macho Sammy.


“Sijakuelewa, hebu fafanua,” Joyce alisema huku akijiinua kutoka pale alipokuwa amelala na kuegemea ukuta huku akimtumbulia macho Sammy.


“Nimefukuzwa kazi takriban mwezi sasa, siku ile niliporudi nimelewa chakari ndiyo siku niliyokuwa nimepewa barua ya kuachishwa kazi, tangu wakati huo nipo tu kijiweni… na hili gari nimelinunua kwa fedha ya…” Sammy alijaribu kujieleza.


“Stop!” Joyce alimkata kauli huku akiyatuliza macho yake usoni kwa Sammy, “Umefukuzwa kazi takriban mwezi sasa halafu unakuja kuniambia leo! Hivi wewe ni mume wa aina gani!” alisema kwa hasira na kunyanyuka, akasimama mbele ya Sammy huku akiwa kashika kiuno chake. Alimtazama Sammy kwa kitambo huku akiwa kachukia sana.


Sammy naye alisimama, akataka kusema neno lakini Joyce alimfanyia ishara ya kuwa hakutaka kabisa kumsikiliza.


“Uliamua kunificha, sasa kilichokutuma leo kunieleza ni nini?” Joyce alimuuliza Sammy huku akiendelea kumkazia macho kwa hasira.


“Lakini…” Sammy alitaka kujitetea lakini Joyce alimkata tena kauli.


“Sihitaji kusikia chochote kwa sasa, kama umeweza kuniaminisha siku zote kuwa unakwenda kazini na kumbe kazini ulikuwa huendi, unadhani nitaweza tena kukuamini!” Joyce alibwata kwa hasira. Sasa alikuwa anatokwa na machozi. Sammy alibaki kimya akimkodolea macho.


“Au unaye mtu unayemweleza matatizo yako? Ndiyo maana unaniona mimi mpumbavu, siyo?” Joyce aliuliza huku akilia kwa uchungu.


“Sioni kwa nini unapaniki kiasi hiki, hili ni suala la kukaa na kuongea, mke wangu. Sioni kama…” Sammy aliongea lakini Joyce alimkatisha.


“How could you do this to me, Sammy, uh? Umekuwa ukiniaminisha kuwa unakwenda kazini kumbe huendi, nitakuamini vipi huko ulikokuwa unashinda?” Joyce aliuliza kwa hasira, alikuwa anapumua kwa nguvu.


“Kwa vyovyote ningekwambia, wewe ni mke wangu na ndiye mtu muhimu kwangu…”


“Liar! Mimi nina umuhimu gani kwako?” Joyce aliuliza huku akimkazia macho Sammy.


“Swali gani hilo unauliza Joyce? You are my wife and you are important to me,” Sammy alijaribu kujitetea.


“Save your breath, Sammy. I mean nothing to you.”


“Una hakika na hayo unayoyasema?” Sammy alimuuliza Joyce huku akimkazia macho.


“Ningekuwa na thamani kwako basi ungenithamini na kunieleza ukweli siku ile ile na usingefanya uamuzi wa kipumbavu kama ulivyofanya. Sikutegema kama…” Joyce alisema kwa hasira lakini sammy alimkatisha.


“Mama Pendo, naomba iwe mwanzo na mwisho kunitusi, sawa!” Sammy aliongea kwa hasira huku akinyoosha kidole chake kumwelekea Joyce.


“Huwezi kunizuia kuongea, Sammy, nitaongea chochote na hutanifanya kitu,” Joyce alifoka huku akimtazama Sammy kwa hasira. Hakuwa akimwita tena Baba Pendo bali Sammy.


Maneno yale ya Joyce yalionekana kumuumiza sana Sammy, alimsogelea Joyce na kumshika kwa nguvu, akamtingisha kwa hasira.


“Mama Pendo, nakupa onyo la mwisho, naomba tafadhali usithubutu kunijibu namna hiyo…”


“Usinitishe, kama umenichoka ni bora uniache kwa amani…” Joyce aliongea kwa sauti ya juu na kwa kujiamini.


Sammy alimshika shingoni kwa hasira, akamminya. “Nilikuoa kwa sababu nakupenda, kwa hiyo usijaribu kutaka kunitingisha, ukiendelea kutoniheshimu nitakuvunja shingo yako,” Sammy alisema kwa hasira na kutoka mle chumbani. Akaubamiza mlango.


Joyce alionekana kuogopa, ujasiri wote aliokuwa nao ulianza kutoweka, alijikuta akiogopa ghafla kwani hakuwahi kumwona Sammy akiwa amekasirika namna ile.


“What a stupid husband,” Joyce alisema kwa sauti ndogo huku akijibwaga juu ya kitanda.





Sammy alikwenda kuketi kwenye sofa sebuleni, mara akawaona Pendo na Winifrida wakimfuata pale kwenye sofa huku wakionesha wasiwasi mkubwa. Sammy alimkumbatia Pendo na wakati huo Winifrida aliketi kimya kwenye sofa huku akimtazama Sammy kwa makini.


“Joyce hajawahi kunidharau kama alivyofanya leo. Nlijua tu mambo kama haya lazima yatatokea ndiyo maana nilikuwa nasita kumweleza ukweli. Cha msingi hapa ni kukabiliana na chochote kitakachojitokeza,” Sammy aliwaza huku akiwa amefura kwa hasira.


Aliendelea kuketi pale akiwa amemkumbatia Pendo aliyekuwa akimtazama kwa makini pasipo kusema chochote. Sammy alikuwa bado ameduwaa, hakujua afanye nini.


Mara walimuona Joyce akitoka chumbani akiwa amevaa gauni na mkononi alikuwa anaburuza begi kubwa la magurudumu. Wote walimtazama kwa mshangao.


“Nashukuru kwa kunionesha kuwa mimi ni mtu nisiye na maana, narudi kwa wazazi wangu Tanga,” Joyce alisema na kuanza kupiga hatua zake taratibu kuelekea kwenye mlango mkubwa ili aondoke.


Sammy alionekana kuchanganyikiwa, aliinuka haraka na kujaribu kumshika Joyce katika hali ya kutaka kumzuia lakini Joyce alimsukuma kisha akamzaba kibao kikali cha shavuni. Alikuwa amekasirika sana na macho yake yalikuwa yanawaka kwa hasira.


“Niache niondoke. Siwezi kukuamini tena!” Joyce alisema kwa hasira.


“Ungenisikiliza kwanza basi…” Sammy alisema huku akimkodolea macho yaliyokuwa yakibembeleza.


“Muda huo sina, wapo watu wa muhimu kwako watakaokusikiliza siyo mimi!”


Pendo alianza kulia kwa uchungu huku akimshika mama yake miguuni kumzuia asiondoke. Winifrida alikuwa amesimama akiwaangalia wote kwa zamu, hakujua afanye nini. Alimshika Pendo aliyekuwa analia kwa uchungu na kumtoa eneo lile akitaka kumpeleka chumbani, japo Pendo alikuwa akirusharusha miguu akitaka aachwe.


“Mwache!” Joyce alisema kwa hasira na kumshika Pendo mkono huku akiwatazama Sammy na Winifrida kwa uchungu.


“Naondoka na mwanangu, siwezi kumwacha kwa mwanaume mwongo na laghai kama wewe,” Joyce alisema na kuanza kupiga hatua huku kamshika Pendo aliyekuwa bado analia. Walitoka nje wakimwacha Sammy amepigwa butwaa.


Sammy alitaka kusema neno lakini sauti haikutoka. Winifrida alisimama akimtazama Sammy kwa huzuni na kushusha pumzi, kisha alitingisha kichwa chake kwa huzuni na kuelekea chumbani kwake…


“Baba Pendo, mbona umenikodolea macho tu na husemi ulichotaka kunimbia, kwani kuna nini!” sauti ya Joyce ilimgutusha Sammy kutoka kwenye mawazo yake.


Sammy alimtazama Joyce na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, alishukuru Mungu kuwa yalikuwa ni mawazo tu yaliyompeleka mbali sana kiasi cha kumwogopesha hata kumweleza Joyce alichokusudia kusema. Uso wake ulikuwa umefifia na alionekana kusita sana.


Joyce alimtazama kwa udadisi zaidi, akajiinua kutoka pale kitandani na kujiegemeza kwenye ukuta huku akiendelea kuyatuliza macho yake kwenye uso wa Sammy.


“Una nini, Baba Pendo, mbona unanitisha!” Joyce alisema huku akimeza mate kutowesha koo lake lililoanza kukauka.


Sammy alimtazama Joyce kwa makini na kushusha pumzi huku akilazimisha tabasamu, alionekana kusita sana. Picha aliyoiona mawazoni kwake iliendelea kumtisha, alihisi kuwa endapo angemweleza ukweli Joyce basi hali ingekuwa kama ambavyo picha ile ilionekana mawazoni mwake.


“Amm… amm… hakuna kitu!” Sammy alimudu kusema na kumfanya Joyce ashangae zaidi. Alimkodolea macho Sammy kama vile alikuwa ameona kiumbe cha ajabu kutoka sayari ya mbali.


“Hakuna kitu! Mbona sikuelewi? Ni nini kinachoendelea ambacho hutaki nikijue?” Joyce aliuliza huku akimtazama Sammy kwa udadisi.


Sammy alionekana kupata kigugumizi, aliangalia chini kwa kitambo kifupi akiwa hana cha kusema, aliogopa kumpoteza Joyce. Wakati huo Joyce aliendelea kumkazia macho Sammy kwa udadisi.


“Mimi ni mkeo, kama unanificha jambo unadhani ni nani wa muhimu kwako wa kumweleza? Halafu hadi sasa hujanieleza kuhusu hili gari ulilokuja nalo!” Joyce aliuliza na kumfanya Sammy ahisi kijasho chembamba kikimtoka, hata hivyo aliamua kuuvaa ujasiri. Aliachia tabasamu, akakohoa kusafisha koo lake.


“Nimeamini kweli unanijali mumeo, nilitaka kukupima nione… ukweli ni kwamba niliamua kukufanyia sapraizi…” Sammy alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Sapraizi ya nini?” Joyce aliuliza huku akiendelea kuyatuliza macho yake kwenye uso wa Sammy akijaribu kuyapima yale maneno.


“Nimepandishwa cheo kuwa Naibu Meneja Mkuu, na hilo gari nimepewa, ni la kwangu. Ni la kwetu, Mama Pendo!” Sammy alisema huku akiachia tabasamu pana na kumfanya Joyce amtazame kwa kitambo bila kusema neno akiwa haamini alichokisikia.


Sammy alimtazama Joyce kwa wasiwasi hadi pale alipoliona tabasamu pana likichanua usoni kwake.


“Ooh… hongera sana mume wangu!” Joyce alisema kwa furaha huku akimkumbatia Sammy kwa nguvu


“Ni wewe unayestahili pongezi, mafanikio yangu yote yamechangiwa na wewe,” Sammy alisema huku akishusha pumzi za ahueni, hata hivyo, dhamiri yake ilikuwa inamsuta.


* * * * *


Saa tatu na nusu za usiku Mr. Oduya alitoka kwenye jengo lake la ghorofa kumi na mbili katika barabara ya Bagamoyo, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, baada ya kuwa na kikao kifupi na Balozi Aldolf Mageuzi.


Balozi Mageuzi alikuwa amefika ofisini kwa Mr. Oduya kwa mazungumzo mafupi ili kumpa mrejesho wa kile walichokubaliana walipokutana mara ya kwanza. Hakutaka kumweleza kwenye simu kwa kuogopa mawasiliano yao yangeweza kudukuliwa.


“Enhe, nipe mrejesho mheshimiwa Balozi,” Mr. Oduya alisema kwa shauku baada ya Balozi Mageuzi kuketi.


“Mambo siyo mabaya, mzee Fabian Magulu ameonesha kukuunga mkono katika harakati zako kutokana na jinsi unavyojitoa kukisaidia chama na jamii, hii ni habari njema na kama ujuavyo, huyu mzee ni mtu mwenye ushawishi mkubwa ndani ya chama na serikalini…” Balozi Mageuzi alisema na kumfanya Mr. Oduya aachie tabasamu pana.


“Pia amesikitiswa sana na kitendo cha mheshimiwa Tumbo kuanza kampeni mapema huku akitumia siasa za majitaka kuchafua wengine. Kwa kutumia umaarufu na nguvu alizo nazo ndani ya chama amekwishaanza kukigawa chama, tumenasa mawasiliano ya simu akipanga mambo machafu dhidi ya wanasiasa anaodhani ni tishio kwake, jambo hili limemkasirisha sana mzee Magulu na anatarajia kupeleka maoni yake kwa Rais ili Tumbo aitwe Kamati Kuu na kujadiliwa. Hili peke yake linaweza kumpotezea sifa…”


“Wow! Hahahaaaa… that’s good news! Hahahaaaaa,” Mr. Oduya alisema na kucheka kicheko kikubwa sana kwa furaha baada ya kusikia taarifa ile.


“Ila kuna jambo sijakueleza bado,” Balozi Mageuzi alisema baada ya kicheko kile kwisha, huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.


“Jambo gani tena Balozi?” Mr. Oduya aliuliza kwa pupa huku akionekana kushtuka kidogo, lile tabasamu pana usoni kwake liliyeyuka ghafla na badala yake alimkazia macho Balozi Mageuzi.


“Katika uchunguzi wangu nimegundua kwamba mzee Magulu ana imani kubwa na Dk. Hussein Abbas, na anampa nafasi ya kwanza wakati wewe amekuweka ya pili…” Balozi Mageuzi alisema kwa sauti tulivu.


Maneno yale yalikuwa kama msumali wa moto uliochoma moyo wa Mr. Oduya, alijikuta akiwa hana la kusema na kubaki kimya akimkodolea macho Balozi Mageuzi.


“Najua wewe ni mpambanaji… hili ni jambo dogo sana, kama mheshimiwa Tumbo mwenye mtandao mkubwa na tishio ndani ya chama anamalizwa kirahisi, kwa vyovyote vile Dk. Hussein Abbas ni kazi ndogo zaidi,” Balozi Mageuzi alisema huku akiachia tabasamu.


“Una uhakika, Balozi?” Mr. Oduya aliuliza huku sura yake ikionesha shaka kidogo.


“Naomba uniamini, ninao watu wa kusaidia kwenye hili, ni suala la muda tu na kila kitu kitakaa sawa.”


“Oh, thank you, Mr. Ambassador, sijajua hadi sasa nikutunuku zawadi gani…” Mr. Oduya alisema huku matumaini yakirejea.


“Usijali, suala la kuvuka daraja tutalijadili tukishaufikia mto,” Balozi Mageuzi alisema huku akiinuka kutaka kuondoka, kisha kama aliyekumbuka jambo alimkabili tena Mr. Oduya.


“Jambo lingine, tafuta mtu ambaye ni mwanamkakati mzuri wa kiufundi na matukio, mkutanishe na mimi ili nimpe mbinu za kukuandalia mikakati na utekelezaji wa jinsi gani utafanikisha mambo yako,” Balozi Mageuzi alisema huku akimpa mikono wake Mr. Oduya, wakaagana wakiahidiana kupeana taarifa kila kunapotokea jambo jipya.


Kwa kweli ilikuwa ni habari njema kwa Mr. Oduya iliyomuongezea matumaini fulani. Mr. Oduya aliingia kwenye gari lake la kifahari aina ya Range Rover Velar la rangi nyeupe, Madjid Chege akaliondoa gari na safari ya kuelekea nyumbani kwake ikaanza.


Kauli ya kwamba atafute mwanamkakati mzuri wa kiufundi na matukio ilimfanya amfikirie Sammy, hakuona mtu mwingine mzuri zaidi ya Sammy.


Sasa alipanga kwenda ofisini kwa Dk. Masanja kesho yake asubuhi ili kumtaka amshawishi Sammy akubali kujiunga na timu yake, na kama angeendelea kukataa basi angetafuta njia nyingine ya kumlazimisha.


Kutoka pale ofisini kwake Kijitonyama waliifuata barabara ya Bagamoyo iliyokuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo safari yao ilikuwa ya taratibu na muda huo ilikuwa inakaribia kabisa saa nne ya usiku.


Moyoni Mr. Oduya alikuwa ana amani ya kutosha sana kwani Balozi Mageuzi alikuwa ameusuuza sana moyo wake kwa habari mpya alizompa kuhusu uamuzi wa Fabian Magulu kumuunga mkono.


Hata hivyo, alijua kuwa akifika nyumbani tu ni lazima kungekuwa na kitimtim kwani alikuwa na takriban wiki nzima hajalala nyumbani kwake. Alimfahamu sana mke wake Dk. Oduya. Alikuwa mwanamke mwenye hasira za karibu sana na alikuwa radhi kufanya uamuzi wowote ule. Ilikuwa yataka moyo sana kuishi na mwanamke yule.


Madjid alipofika katika eneo la Tume ya Sayansi na Teknolojia aliingia kulia akaifuata barabara ya Rose Garden iliyokwenda kutokea eneo la Mikocheni kwa Mwalimu Nyerere. Barabara ile ilifunikwa na vivuli vya matawi makubwa ya miti kando yake.


Muda wote Mr. Oduya alikuwa amezama kwenye kutazama nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha akiangalia mandhari ya ile barabara. Kupitia pale dirishani aliweza kuona mawingu mepesi yaliyokuwa yakijikusanya angani kana kwamba mvua ya rasharasha ilitaka kunyesha.


Walipofika mwisho wa barabara ile ya Rose Garden katika eneo la Mwalimu Nyerere, Madjid alikunja kona kuingia kushoto akaifuata barabara ya Mwai Kibaki akiwa katika mwendo wa wastani.


Waliyavuka majengo mazuri ya makazi ya viongozi wastaafu, maduka, supermarket, vituo vya kujazia mafuta, ofisi za binafsi na migahawa ya kisasa iliyopakana na barabara.


Baada ya safari fupi hatimaye wakaja kukutana na barabara ya CocaCola kwa upande wa kushoto. Barabara ya CocaCola ilikuwa ni barabara maarufu eneo lile na yenye msongamano mkubwa wa magari yaliyotoka na kwenda eneo la Mwenge yakipitia eneo la kiwanda cha soda za CocaCola.


Baada ya umbali mfupi walifika kwenye daraja, wakalivuka na mbele kidogo wakayavuka majengo ya Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT Mlalakua) upande wao wa kushoto, hapo dereva akaongeza mwendo na kulipita lori la mafuta lililokuwa mbele yao.


Baada ya mwendo wa dakika kadhaa mbele yao wakalivuka jengo la kampuni ya teknolojia ya Infortech upande wao wa kulia halafu wakaufikia mzunguko wa barabara ulioziunganisha barabara za Mwai Kibaki na Old Bagamoyo.


Dereva akauvuka ule mzunguko na kuifuata barabara ya Mwai Kibaki iliyoelekea eneo la Mbezi Beach huku wakipishana na magari mengi ya kifahari katika barabara ile.


Baada ya safari ndefu katika barabara ile ya Mwai Kibaki wakayafikia makutano ya barabara ile za Mwai Kibaki na Ally Sykes, wakavuka na baadaye wakaikuta barabara ya Bahari kwa upande wao wa kulia. Dereva akaingia upande ule akiufuata ile barabara iliyopita katikati ya majumba ya kifahari yaliyozungukwa na kuta zenye ulinzi hadi alipokutana na barabara nyingine ya Ufukweni iliyoelekea kushoto, akakunja kuelekea kushoto akiifuata ile barabara.



Baada ya mwendo wa dakika mbili wakaikuta barabara nyingine ya Hassan Oduya, iliyopewa jina kwa heshima ya bilionea Hassan Oduya iliyoingia upande wa kulia ikielekea ufukweni mwa Bahari ya Hindi kwenye majumba ya kifahari.


Ilikuwa barabara ya kisasa yenye lami na isiyokuwa na msongamano ikikatisha katikati ya yale majumba makubwa ya kisasa yenye ulinzi madhubuti. Kulikuwa na utulivu wa hali ya juu katika barabara ya Hassan Oduya na hata msongamano wa watu na magari haukuwepo.


Baada ya kitambo kifupi cha safari dereva alipunguza mwendo na hatimaye akasimama nje ya geti kubwa jeusi kwenye kasri la kifahari la Mr. Oduya, kisha akapiga honi mara mbili. Haukupita muda mrefu geti dogo lililokuwa kando ya lile geti kubwa likafunguliwa na askari mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi akachungulia.


Alipoliona gari la Mr. Oduya hakuuliza chochote, alifungua lile geti kubwa la mbele na Madjid akaingiza gari ndani ya uzio wa lile jumba na geti likafungwa nyuma yao, na hapo akajitokeza askari mwingine aliyeshika bunduki yake mikononi na kusimama kando akilitazama lile gari kwa makini.


Gari lilianza kupita katika barabara ya vitofali iliyopakana na bustani nzuri ya maua, miti ya kivuli na nyasi laini na kwenda kusimama mbele ya baraza pana ya jumba lile. Na hapo wale askari wa ulinzi wakarejea kwenye kibanda chao cha ulinzi mle ndani kando ya lile geti.


Madjid aliposimamisha gari, alifungua mlango na kushuka kutoka garini pasipo kuzima injini na kuzunguka upande alikokuwa amekaa Mr. Oduya. Alimfungulia mlango, na muda huo huo kijana wa kazi alitoka haraka ndani ya nyumba baada ya kusikia gari limesimama mbele ya nyumba na kumpokea Mr. Oduya kwa adabu zote.


Wakati huo ilikuwa kama majira ya saa tano kasoro dakika tano hivi. Hali ya jumba lile ilikuwa ya ukimya sana na ilitisha kweli kweli. Mr. Oduya aliingia na kupanda ngazi haraka haraka hadi ghorofa ya kwanza.


Alipoingia tu chumbani alimkuta mkewe Dk. Oduya akiwa amefura kwelikweli, alikuwa amesimama mlangoni huku akimsubiri kwa hamu.


“Haya niambie mwanaume wewe, wiki nzima ulikuwa unalala wapi na nani hadi leo ndiyo unarudi usiku wote huu?” Dk. Oduya aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa alikuwa amechukia kwelikweli.


“Sasa ndiyo maswali gani hayo, mke wangu? Inamaana hujui kuwa niko bize na mchakato wa kukutana na watu muhimu wa kunisapoti kuwania nafasi ya urais wa nchi hii?” Mr. Oduya alimjibu kwa swali.


“Mimi ni mke wako hivyo ninapaswa kujua ulikuwa unashinda na kulala wapi na ulikuwa na nani!”


“Hivi humu ndani nani ni mwanamume hasa? Mbona unazidi kunipanda kichwani wewe mwanamke?” Mr. Oduya alimjibu mkewe kwa fedhuli.


“Okay! Kwa kuwa wewe ni mwanamume na mimi mwanamke ndiyo unaniletea dharau siyo?” Dk. Oduya aliongea kwa hasira, na kuongeza, “Kumbuka mimi si mtoto mdogo na wala si mpumbavu kama unavyofikiria, naelewa kila kitu kinachoendelea kwako.”


“Humu ndani mimi ndiye kichwa cha familia na ndiye ninayevaa suruali, kwa hiyo naomba unipe heshima yang...”


Mr. Oduya alikatishwa na kibao kikali cha ghafla ambacho hakukitegemea kabisa kilichotua kwenye shavu lake na kumpeleka sakafuni. Alishangaa sana, akajishika shavu lake akiwa haamini macho yake huku akimkodolea macho Dk. Oduya.


Hakupewa hata nafasi ya kutafakari, Dk. Oduya akaanza kumshushia makofi mfululizo yaliyopigwa pasipo mpangilio mwilini mwa Mr. Oduya huku akilia kwa uchungu. Aliporidhika alifungua mlango na kutoka nje ya kile chumba huku akimwacha Mr. Oduya akiugulia maumivu makali.


Hakurudi, alikwenda kulala kwenye chumba cha wageni katika ghorofa ya tatu na kujifungia humo hadi asubuhi.


* * * * *


Wiki mbili baadaye, majira ya saa tano asubuhi, katika eneo la Ilala Sharif Shamba, bibi mmoja mwenye umri wa miaka sitini na ushee alikuwa anatembea kwa kujikongoja akielekea katika uelekeo wa mgahawa wa kisasa wa Elli’s.


Yule bibi alikuwa nadhifu na mfupi mwenye ngozi ya rangi ya maji ya kunde na alikuwa amevaa vazi la kitenge lililoshonwa na kudariziwa vizuri na kilemba kikubwa kichwani. Mkononi alikuwa amebeba begi lake dogo na mfuko mdogo wa plastiki uliopigwa marufuku na serikali.


Alikuwa akiyakaza macho yake kutazama eneo la nje la maegesho ya magari mbele ya mgahawa wa Elli’s, eneo ambalo gari la Sammy aina ya Cadillac DeVille la rangi nyeupe lenye muundo wa kizamani lililokuwa na kibao chenye maandishi ya “Taxi” juu yake lilikuwa limeegeshwa.


Sammy alikuwa amesajili kampuni ya magari ya kukodisha (car rental), lakini kwa kuwa alikuwa na gari moja aliamua kulitumia kama teksi. Alikuwa amejiegemeza kwenye gari lake na alionekana mtanashati kwelikweli. Alivaa suti nzuri ya rangi ya kijivu, shati la rangi ya samawati na tai ya rangi ya bluu.


Yule bibi alizidi kusogea karibu huku akimkazia macho Sammy aliyekuwa kashika simu yake ya mkononi akionekana kuperuzi. “Hiyo ni teksi?” yule bibi aliuliza kwa shauku alipokuwa takriban mita ishirini kutoka lilipokuwa lile gari la Sammy.


“Ndiyo bibi, ni teksi,” Sammy alisema baada ya kugeuka na kumwona yule bibi akimtazama kwa makini.


“Niwekee kwenye gari,” yule bibi alisema huku akimwashiria Sammy amsaidie mzigo wake kuuweka kwenye gari.


Sammy alimfuata yule bibi akionekana kuchangamka, akapokea lile begi dogo na ule mfuko wa plastiki, akafungua mlango wa nyuma wa gari lake na kuviweka kwenye siti. Kisha alimshika mkono yule bibi kwa upole na kumsaidia kuingia ndani ya lile gari, akaketi kwenye siti ya nyuma. Yule bibi alimtazama Sammy kwa jicho la shukrani.


“Asante sana mjukuu wangu,” yule bibi alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Usijali bibi… natakiwa kuwatendea wateja wangu kwa namna ambayo ningependa mama yangu atendewe,” Sammy alisema huku akifungua mlango wa dereva, akaingia na kuketi.


Mambo yanazidi kunoga... Usikose kufuatilia stori hii ya kusisimua kuijua safari ya Sammy aliyekuwa Meneja Matukio wa hoteli kubwa ya kitalii ya Udzungwa Beach Resort na sasa amekuwa Taxi Driver! Pia utajua kwa nini stori inaizungumzia taxi na si Sammy wala mtu mwingine, nini kimejificha nyuma ya taxi?





Sammy alimfuata yule bibi akionekana kuchangamka, akapokea lile begi dogo na ule mfuko wa plastiki, akafungua mlango wa nyuma wa gari lake na kuviweka kwenye siti. Kisha alimshika mkono yule bibi kwa upole na kumsaidia kuingia ndani ya lile gari, akaketi kwenye siti ya nyuma. Yule bibi alimtazama Sammy kwa jicho la shukrani.


“Asante sana mjukuu wangu,” yule bibi alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Usijali bibi… natakiwa kuwatendea wateja wangu kwa namna ambayo ningependa mama yangu atendewe,” Sammy alisema huku akifungua mlango wa dereva, akaingia na kuketi.


SASA ENDELEA NAYO...


“Wewe ni kijana mwema… sasa unaweza kunipeleka Karakata,” yule bibi alisema huku akiachia tabasamu.


“Hakuna tatizo bibi, shilingi elfu tano tu,” Sammy alimwambia yule bibi huku akigeuza shingo yake kumtazama.


“Sawa, lakini tupitie barabara inayoelekea Mnazi Mmoja,” yule bibi alisema huku akijiegemeza kwenye siti.


“Huko tutakuwa tunazunguka sana, bibi… ipo barabara rahisi ya kupitia Mnyamani halafu Vingunguti kisha tunakwenda kutokea Karakata…”


“Sijali kama tutakuwa tunazunguka, sina haraka,” yule bibi alisema huku akiachia tabasamu.


“Lakini gharama inaweza kuwa kubwa zaidi.”


“Usijali kuhusu gharama, wewe fuata maelekezo yangu.”


Sammy alimtazama yule bibi kwa makini kupitia kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. Yule bibi alitulia tuli huku akiwa amejiegemeza kwenye siti, alionekana kuchoka sana.


“Daktari wangu ameniambia kuwa ninahitaji kufurahi zaidi ili niweze kuishi muda mrefu kidogo, vinginevyo sina muda mrefu wa kuishi,” yule bibi alimwambia Sammy huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


Sammy hakusema neno, alibaki kimya huku akimtupia jicho yule bibi kupitia kile kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma, alibana taya zake na kuwasha injini ya gari, akaliondoa gari lake taratibu akiingia katika barabara ya lami iliyokuwa ikienda kutokea hospitali ya Amana.


Walipita kwenye ile barabara iliyokatisha katikati ya majumba mazuri na makazi ya kisasa ya watu wenye ukwasi yaliyozungukwa na kuta zenye usalama wa uhakika. Na baada ya mwendo mfupi wa safari yao waliyafikia makutano ya barabara ile na barabara iliyoelekea Hospitali ya Amana.


Sammy alikata kona na kuingia upande wa kulia akaenda kuungana na barabara ya Uhuru katika eneo la Amana Vijana, kisha akakunja tena kuingia upande wa kushoto akiifuata barabara ya Uhuru.


Katika barabara ile ya Uhuru kulikuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo safari yao ilikuwa ya taratibu. Yule bibi alikuwa hasemi kitu badala yake alikuwa amezama kwenye kutazama mandhari ya ile barabara ya Uhuru.


Ule mwendo wa wastani ulimruhusu yule bibi kuona vizuri mandhari ya nje. Alikuwa anaona vitu vikiwa vinapita mbele ya macho yake na kurudi nyuma taratibu wakati lile gari likiwa linakwenda, mara wakayapita mabanda yaliyotumika kama vyumba vya wasusi wa Kimasai.


Akiwa bado anayatazama yale mabanda ya wasusi wa Kimasai kwa makini wakaikuta barabara ya Mafao iliyokuwa ikiingia kushoto, wakaivuka na kulipita jengo refu zaidi maarufu kama Mafao House. Yule bibi alilitazama lile jengo kwa makini na kuminya midomo yake.


Baada ya safari fupi hatimaye wakalifikia jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, eneo la Ilala Boma. Yule bibi aliliangalia kwa makini lile jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kukohoa ili kusafisha koo lake, kisha akamuonesha Sammy jengo hilo.


“Enzi za ujana wangu nilifanya kazi hapo kama Katibu Muhtasi,” yule bibi alisema. Sammy alilitupia jicho lile jengo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kubaki kimya.


Muda huo walikuwa wamefika katika makutano ya barabara ya Kawawa na Uhuru kwenye taa za kuongozea magari barabarani. Bahati nzuri walimkuta askari wa usalama barabarani aliyekuwa akiruhusu magari na kuwaruhusu wapite.


Gari la Sammy likapita huku watu wakilisindikiza kwa macho yaliyoonesha kulishangaa na baadaye wakazipita daladala zilizokuwa zimesimama katika kituo cha daladala cha Karume. Kisha wakaikuta barabara ya Shaurimoyo upande wao wa kulia na kuipita, na hapo Sammy aliongeza mwendo na kuyapita majengo ya kiwanda cha bia (TBL).


Lile gari lilizidi kwenda mbele na kuvuka taa za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Msimbazi na Uhuru, eneo la Kariakoo. Sammy aliendelea kuendesha gari kimya kimya akiifuata barabara ile ya Uhuru hadi walipozifikia taa za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Uhuru na Lumumba.


“Endelea mbele hadi utakapofika Mtaa wa Indira Gandhi, kisha uingie kushoto kuufata mtaa huo,” yule bibi alimwambia Sammy huku akitupa macho yake nje na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.


Sammy alitii na kuendesha akizivuka taa za kuongozea magari barabarani za makutano ya barabara za Uhuru na Lumumba, akakivuka kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja, kisha akazivuka taa nyingine za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Uhuru na Bibi Titi Mohammed.


Baada ya mwendo mfupi hatimaye wakaufikia Mtaa wa Indira Gandhi, Sammy akakata kuingia kushoto akiufuata ule mtaa hadi mbele kidogo walipoukuta Mtaa wa Aggrey uliokatiza mbele yao.


“Umeiona hiyo hoteli hapo mbele, ni hoteli ambayo mimi na marehemu mume wangu tulikuja kwa ajili ya fungate mara tu tulipotoka kufunga ndoa,” yule bibi alimwambia Sammy huku akimwonesha kwa kidole. Sammy aliiangalia ile hoteli akiwa hajui aseme nini.


“Unaweza kusimama hapo kando?” yule bibi alimuuliza Sammy, na bila kuchelewa alisimamisha gari lake kando ya barabara ya mtaa ule. Yule bibi alibaki kimya kabisa akilitazama lile jengo la hoteli kwa kitambo kirefu.


Sammy alionekana kukerwa kidogo lakini hakuwa na namna ya kufanya. Aliwaza: kama kazi ya kuendesha teksi ilikuwa na usumbufu kiasi kile ni heri angetafuta kazi nyingine ya kufanya. Alikuwa amepatikana! Kutoka Meneja Matukio katika hoteli kubwa yenye hadhi ya nyota tano hadi kazi ya kuendesha teksi! Haiaminiki kabisa!


Alitaka amweleze ukweli yule bibi kuwa hakupendezwa na kile kilichokuwa kikiendelea na ikibidi amtake atafute gari nyingine lakini alipokumbuka maneno ya yule bibi kuwa, “daktari wake alimtaka kufurahi zaidi ili aweze kuishi muda mrefu kidogo…” alishindwa kusema chochote.




Alimtupia jicho yule bibi kupitia kile kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma huku akijilaumu kukubali kumchukua, aliamua kuwa mvumilivu na hakutaka kumkera bibi wa watu. Yule bibi aliendelea kuliangalia lile jengo la hoteli kwa kitambo kirefu kisha alionekana kuridhika, akashusha pumzi ndefu.


“Ahsante sana mjukuu wangu, kwa kunikumbusha enzi za ujana wangu, nimeridhika. Sasa tunaweza kwenda Karakata,” yule bibi alisema huku akijiegemeza kwenye siti yake, akafumba macho.


Sammy alimtupia jicho yule bibi na kushusha pumzi kisha akaondoa gari lake taratibu akiendesha kimya kimya kuelekea Karakata. Aliufuata Mtaa wa Aggrey hadi alipoikuta barabara ya Bibi Titi Mohammed, akakata kuingia kushoto akiifuata ile barabara.


Safari yao iliendelea kimya kimya, muda ule yule bibi alikuwa amepitiwa na usingizi. Sammy alikwenda hadi alipoikuta barabara ya Nkrumah, akaifuata barabara ile hadi kwenye makutano ya barabara za Nkrumah, Msimbazi, Nyerere na Gerezani.


Sammy aliitazama saa yake ya mkononi na kugundua kuwa ilikuwa imekwishatimu saa sita mchana, akashusha pumzi akiifuata barabara ya Nyerere iliyokuwa na magari machache muda ule, akaongeza mwendo.


Baada ya safari ya takriban dakika arobaini walifika eneo la Jet Club, Sammy akaamua kumwamsha yule bibi na kumuuliza uelekeo wake. Yule bibi alimweleza aingie kulia na kuifuata barabara nyembamba ya vumbi iliyopita katikati ya viwanda na kwenda kutokea reli ya kati kisha akakunja kushoto akiifuata ile barabara nyembamba.


Walipovuka reli waliikuta barabara nyingine ya vumbi iliyopita mbele ya shule za Majani ya Chai na Ilala, yule bibi akamwelekeza kuwa aelekee upande wa kushoto akiifuata ile barabara na baadaye aingie upande wa kulia kabla hajayavuka majengo ya Veta Kipawa.


Aliingia akiifuata barabara nyingine nyembamba ya vumbi akayavuka majengo ya Veta kipawa yaliyokuwa upande wake wa kushoto, na baada ya safari ya takriban dakika tano yule bibi alimwonesha Sammy nyumba moja iliyokuwa mbele yao.


Ilikuwa nyumba ndogo lakini ya kisasa ikiwa imezungushiwa ukuta mfupi na ilikuwa na geti kubwa la rangi ya damu ya mzee mbele yake. Sammy alisimama mbele ya ile nyumba, kisha alifungua mlango na kushuka, akazunguka kumfungulia mlango yule bibi.


Wakati yule bibi akishuka, Sammy alishusha begi lake dogo na ule mfuko wa plastiki. Muda ule ule alijitokeza binti mmoja aliyekuwa na umri wa miaka isiyozidi ishirini, akapokea lile begi huku akimsalimia Sammy kwa adabu.


“Ubarikiwe sana kijana wangu, leo umempa bibi yako furaha isiyo na kifani, furaha itakayoniongezea siku za kuishi. Ahsante sana,” yule bibi alisema huku akifungua pochi yake, akatoa noti tatu za shilingi elfu kumi kumi na kumpa Sammy. Kisha akaanza kupiga hatua kuelekea ndani kabla Sammy hajasema chochote.


* * * * *


Saa sita mchana kwenye ukumbi mkubwa wa kisasa wa burudani wenye jukwaa la kisasa lililotazamana na viti vingi kwenye ghorofa ya saba ya jengo la kituo cha runinga, Nuru TV, kulikuwa na warembo kadhaa waonesha mitindo ya mavazi waliokuwa wakifanya mazoezi jukwaani.


Jengo lile la ghorofa saba la kituo cha Nuru TV lilimilikiwa na Madame Norah, lilikuwa katika Barabara ya Bagamoyo eneo la Makumbusho.


Ndani ya ule ukumbi Joyce alikuwa amesimama akiwatazama wale warembo jinsi walivyokuwa wakipita jukwaani kwa miondoko ya aina yake wakionesha ubunifu wake. Walikuwa katika hatua za mwisho za kufanya, mazoezi yaliyochukua takriban wiki mbili, kabla ya tukio rasmi lililopangwa kufanywa na Joyce.


Joyce alikuwa amevaa gauni refu la kitenge cha wax la mikono mirefu lililoshonwa kwa ubunifu wa hali ya juu, mtindo wa pencil dress, likiwa limedariziwa kwa nyuzi za dhahabu na kuushika mwili wake huku likilichora vyema umbo lake maridhawa.


Mkononi Joyce alikuwa ameshika picha za warembo wakiwa katika mitindo tofauti na michoro mingine mbalimbali ya mitindo ya mavazi. Joyce alikuwa makini zaidi akifuatilia mazoezi ya wale warembo pale jukwaani


Kando yake alisimama msaidizi wake, Nyaso Gilbert Nyaso aliyevalia blauzi nyepesi ya pinki na suruali ya jeans ya rangi ya bluu mpauko yenye matobo maeneo ya mapajani na iliyombana na kulichora vyema umbo lake refu maridhawa lenye tumbo dogo.


Mkononi alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe, miwani myeusi ya jua usoni, viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio miguuni na wigi la nywele ndefu kichwani lililomfanya aonekane mrembo hasa. Pia kulikuwa na mpiga picha mmoja aliyekuwa akipiga picha za video za mazoezi hayo kwa maelekezo ya Nyaso.


Madame Norah akiwa ameongozana na msaidizi wake, Jessica waliingia mle ukumbini na kusimama wakiwaangalia kwa makini wale warembo walivyokuwa wakifanya mazoezi. Joyce alimuona Madame Norah na kuachia tabasamu pana kisha akamfuata pale alipokuwa amesimama, walisalimiana kwa bashasha zote.


Madame Norah alifika hapo kutaka kujua maendeleo ya Joyce na ule mradi wake mkubwa na wa kwanza kufanywa na Joyce tangu aingie kwenye tasnia ya mitindo.


Madame Norah hakuwa akijua kilichokuwa kinaendelea kwenye ule mradi, hasa tangu alipomkabidhi Nyaso kuwa msaidizi wa Joyce na yeye akasafiri kwenda nchini Ghana kumuona mdogo wake Zuena, mke wa Balozi wa Tanzania nchini Ghana, Balozi Mafuru.


Ilikuwa ni safari ya ghafla iliyoibuka baada ya kukutana na Zainab, waliyepotezana miaka mingi na wasijue alikokuwa amekimbilia baada ya kutuhumiwa kwenye mauaji ya mumewe Hemed Kimaro, miaka kumi na mbili iliyokuwa imepita.


Ni baada ya safari ile ya Ghana walikokutana ndugu watatu, wakaongea na kupeana ahadi ya kuendelea kuwasiliana na kushirikiana kwa kila kitu, ndipo Madame Norah alipoanza kuhisi ile furaha iliyokuwa imetoweka miaka mingi maishani kwake ikianza kurejea.


Alikuwa mtu mwenye furaha kiasi na Joyce aliweza kubaini mara moja ingawa hakumuuliza. Madame Norah na Joyce waliongea kwa kitambo kirefu wakipeana mikakati ya namna ya kufanikisha mradi ule mkubwa wa Joyce.


Jambo ambalo Madame Norah hakulijua na aliendelea kujiuliza bila majibu ni kwamba: kwa nini aliamua kumsaidia Joyce aliyemhesabu kama mmoja wa washindani wake kwenye tasnia ya mitindo? Tena hakumsaidia tu kwa kumtafutia msaidizi, ukumbi au kulipia gharama za maandalizi, bali alifikia hadi kumpa mikakati na mbinu mbalimbali za kufanikisha mradi ambao ungekuja kuwa tishio kwake!





Huyu Joyce alikuwa na nini hasa kilichomfanya Madame Norah afanye yale asiyokusudia kuyafanya? Hata hivyo, kitu kimoja alichokuwa na uhakika nacho ni kwamba alijisikia furaha sana moyoni kila alipoamua kumsaidia Joyce, basi!


Baada ya kitambo kirefu cha majadiliano kati yao, Madame Norah aliaga na kuondoka akiwaacha Joyce na Nyaso wanakamilisha maandalizi ya mradi ule.


* * * * *


Baada ya kutoka eneo la Karakata, Sammy alimchukua mtu mmoja aliyemkuta Jet Club na kumpeleka katika ofisi za Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) zilizopo barabara ya Mandela, katika eneo la Tazara.


Alimwacha yule abiria pale TSN kisha akageuza gari lake na kutaka kuingia katika barabara ya Mandela akitaka kwenda Ilala Sharif Shamba, mara akamuona mwanamume mmoja raia wa kigeni aliyekuwa anatokea ndani ya majengo ya kituo cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) aliyemjia mbio huku akimpungia mkono.


Alikuwa mwanamume wa makamo, mrefu na kipande cha mtu aliyejazia vyema. Mwili wake ulichorwa michoro mbalimbali na alikuwa amevaa fulana nyeusi ya mikono mifupi, kaptura ya rangi ya khaki yenye mifuko mikubwa pembeni na miguuni alivaa raba. Mgongoni alikuwa amebeba begi kubwa la safari.


Sammy aliamua kumsubiri. Hata hivyo, alikuwa amesimama katikati ya barabara ya mchepuko iliyotokea katika jengo la TSN na hivyo kuzuia magari mengine. Gari moja aina ya Toyota RAV4 jeusi lililokuwa nyuma yake likitaka kuingia katika barabara ya Mandela lilianza kupiga honi, dereva wa gari lile alionekana kutokuwa na uvumilivu.


Sammy aliendelea kusubiri pasipo kumjali yule dereva wa RAV4 aliyeendelea kupiga honi kwa fujo. Hakutaka kumkosa yule abiria Mzungu aliyekuwa akivuka barabara ya Mandela akionekana kuwa na safari muhimu.


Baada ya dakika takriban mbili yule mwanamume alifanikiwa kuvuka ile barabara na kufungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy kisha aliliweka begi lake na kuingia, akakaa katika siti ya nyuma.


“Airport please… and thanks for waiting,” (Kiwanja cha Ndege tafadhali… na ahsante kwa kusubiri) alisema yule mwanamume wa kizungu huku akijiegemeza kwenye siti.


Sammy aliliondoa gari lake na kungia katika barabara ya Mandela bila kumjibu chochote yule mwanamume wa kizungu kisha akakata kushoto akiifuata barabara ya Nyerere iliyoelekea Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.


Muda ule wa mchana barabara ya Nyerere haikuwa na msongamano mkubwa wa magari, hivyo Sammy alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi. Walikuwa kimya kabisa.


Kufumba na kufumbua gari lilikuwa likiivuka yadi ya kuhifadhi makontena ya African Inland Container Depot (AFICD) katika eneo maarufu la Mchicha na sasa walikuwa wakilisogelea eneo la Karakana ya Tazara, hapo yule mzungu akakohoa kidogo kusafisha koo lake kisha akaanzisha mazungumzo.


“Do you know English?” (Unajua Kiingereza?) yule mzungu alimuuliza Sammy huku akiachia tabasamu pana la kirafiki.


“Yes,” Sammy alijibu kwa ufupi bila kumtazama yule mwanamume.


“How did you get this car? I real like it, it’s a unique type of taxi that everyone should want to use it,” (Umeipataje hii gari? Nimeipenda sana, ni aina ya teksi yenye upekee ambayo kila mtu angependa kupanda) yule mzungu alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.


Sammy aliachia tabasamu huku akimtupia jicho yule abiria wake kupitia kioo cha katikati cha gari kinachotumika kuangalia nyuma.


“You know…” (Unajua…) Sammy alianza kujieleza lakini akasita baada ya kumuona Winifrida akiwa hajavaa sare za shule na badala yake alivaa suruali ya kubana ya jeans rangi ya samawati yenye matobo mapajani na kitopu cheupe na mgongoni alikuwa amebeba begi lake la madaftari.


Winifrida alikuwa ameongozana na kijana mmoja wa kiume aliyekadiriwa kuwa na miaka ishirini na ishirini na mbili, akiwa amevaa suruali nyeupe ya jeans na fulana nyeusi, kichwani alivaa kofia nyeusi ya kapelo. Alikuwa mrefu maji ya kunde na mtanashati sana.


Walikuwa wanatembea taratibu huku wameshikana mikono wakiifuata barabara ya vumbi iliyokatisha katikati ya majengo ya kampuni za Spedag Interfreight na Bureau Veritas Tanzania kuelekea eneo la Kiwalani.


“Shit!” Sammy aling’aka kwa hasira huku akipiga ngumi juu ya usukani na kukanyaga breki ya ghafla, gari lake likaserereka huku likiyumba barabarani na kusimama kando ya barabara ya Nyerere, usawa wa jengo la kampuni ya Bureau Veritas Tanzania.


Alishuka haraka akimwacha abiria wake na kukimbilia kule walikokuwa Winifrida na yule kijana huku akiwa amekasirika sana. Yule kijana alishtuka na kutazama nyuma, alipomuona akija mbio alikimbia akimwacha Winifrida ambaye hakuwa na ujanja. Sammy alimfikia Winifrida na kumkamata mkono kwa nguvu huku akifoka.


Winifrida aliishiwa nguvu, Sammy alimkokota kumpeleka kwenye gari lake lililokuwa limesimama kando ya ile barabara ya Nyerere. Muda wote yule abiria mzungu aliyekuwa ndani ya lile gari la Sammy alikuwa amepigwa na butwaa.


Kama mtu aliyeshtuka aliiangalia saa yake ya mkononi na kusonya huku akionekana kukata tamaa. Kwa vidole vyake viwili vya shahada na dole gumba vya mkono wa kulia aliminya pua yake kama anayevuta kamasi huku akiwatazama kwa makini Sammy na Winifrida wakivutana. Akaangalia tena saa yake ya mkononi.


“What’s wrong with you?” (Una shida gani?) yule mzungu alimuuliza Sammy kwa mshangao huku akishuka kutoka ndani ya lile gari la Sammy, mara akaiona teksi ikija upande ule, akaipungia mkono, “Taxi! Taxi!”


Ile teksi ilipunguza mwendo na kusimama mbele ya gari la Sammy, yule mzungu alifungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy na kuchukua begi lake, akamtazama Sammy kwa mara ya mwisho huku akitoa kadi yake.


“You’ve been a prank but I want to give you a second chance, not for you but for the car. I may need it for one of my representative’s meetings,” (Umenifanyia mzaha lakini nataka nikupe nafasi nyingine, siyo yako bali kwa sababu ya gari lako. Huenda nikalihitaji kwenye moja ya mikutano yangu) yule mzungu alisema huku akimpa Sammy ile kadi yake.




Sammy aliipokea ile kadi huku akiitazama kwa makini na kubetua kichwa chake. Yule mzungu aliingia kwenye ile teksi aliyoisimamisha, kisha ikaondoka kwa mwendo wa kasi na kuyafanya magurudumu yake yachimbe ardhi.


Winifrida aliingalia kwa makini ile teksi iliyombeba yule mzungu wakati ikiondoka kisha akageuza shingo yake kulitazama gari la Sammy kwa udadisi, akakiona kibao kidogo chenye maandishi ya ‘Taxi’ juu ya gari. Akashangaa sana.


“Kumbe wewe ni dereva wa teksi! Mi’ nilidhani meneja!” Winifrida alisema kwa mshangao huku akimkazia macho Sammy.


“Achana na habari za teksi, niambie kwa nini hujaenda shule na badala yake unazurura na wanaume?” Sammy alimuuliza Winifrida huku akionekana kukasirika sana.


“Nakubali nimekosa, na wewe kwa nini unaendesha teksi badala ya kuwa ofisini?” Winifrida naye alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.


Sammy alitaka kusema neno lakini akasita, aligeuza shingo yake kulitazama gari lake, akakiona kile kibao chenye maandishi ya ‘Taxi’ na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akijiegemeza kwenye gari. Sasa siri yake ilikuwa imefichuka! Winifrida alilitambua hilo na kuachia kicheko hafifu.


“Naamini hutapenda wifi ajue kuhusu jambo hili!” Winifrida alisema huku akiendelea kumwangalia Sammy kwa makini.


“Tafadhali usitake kuingiza mambo yasiyohusiana, suala hapa ni kwa nini huendi shule na badala yake unakuja huku ukiwa umevaa nguo za ajabu ajabu?” Sammy alimuuliza Winifrida huku akijaribu kumtisha.


“Sawa nimekosa, lakini na wewe kwa nini umdanganye wifi kuwa umepandishwa cheo kumbe siku hizi unaendesha teksi? Unataka nimwambie ukweli?” Winifrida aliongea kwa msisitizo bila kuteteleka.


“Naomba usithubutu kumweleza chochote wifi yako, haya mambo hayakuhusu! Ninachotaka uniahidi kuwa utaacha huu ujinga na kwenda shule,” Sammy alisema kwa sauti ya kusihi.


“Ukinisamehe sitasema chochote kwa wifi,” Winifrida alisema huku akifungua mlango wa nyuma wa gari la Sammy na kuingia.


Sammy alimtazama kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kisha akaingia ndani ya gari, akaliondoa na kuelekea eneo la Vingunguti, alipofika usawa wa jengo la kampuni ya East African Cables (Tz) Ltd aliliingiza gari kwenye barabara mchepuko na kugeuza kurudi alikotoka.


Gari liliongeza mwendo likiyapita majengo ya East African Cables (Tz) Ltd, Hoteli ya Blue Supphire, Azania, Spedag Interfreight, Bureau Veritas Tanzania, Karakana ya Tazara na African Inland Container Depot, katika eneo maarufu la Mchicha, wakachepuka na kuingia barabara ya Nyerere, kisha safari ikaendelea.


* * * * *


Saa nane mchana, gari dogo la kifahari aina ya Range Rover Sport L494 la rangi ya bluu lilikuwa linaegeshwa kwenye viunga vya maegesho vya jengo la ghorofa saba la Nuru TV, eneo la Makumbusho jijini Dar es Salaam.


Ndani ya lile gari kulikuwa na watu watatu. Dereva wa gari na mwanamume mmoja mrefu mwenye umbo kubwa kakamavu kutokana na mazoezi makali. Kwenye siti ya nyuma aliketi kijana mtanashati aliyeonekana kujiamini sana. Hakuwa mwingine bali mwanamuziki maarufu wa Bongo Fleva, Dynamo Plus, aliyekadiriwa kuwa na umri wa miaka thetathini.


Alikuwa mrefu kiasi mwenye mwili mdogo lakini uliojengeka kwa mazoezi, akiwa amevaa suruali nyeupe ya jeans iliyokuwa imechanwa chanwa sehemu ya mapajani hadi uswa wa magoti na fulani nyeusi yenye picha yake kifuani.


Kichwani alikuwa amezisuka nywele zake katika mtindo wa rasta na alivaa kofia nyeupe ya kapelo na miwani mikubwa ya jua usoni.


Kwa kiasi fulani Dynamo Plus alikuwa amejitosheleza, kwani mbali na muziki alikuwa anamiliki miradi kadhaa ikiwemo studio ya kurekodi muziki, na alikuwa mbioni kuanzisha vituo vya redio na televisheni, kwa msaada wa Madame Norah.


Kwa kifupi Madame Norah alimshawishi Dynamo Plus na wakakubaliana kuingia ubia ili waanzishe vituo hivyo vya runinga na redio kwa kuwa Dynamo Plus alijionesha kuwa kijana mbunifu na mwenye kujituma sana, kiasi cha kuwa mfano kwa wasanii wengi.


Dynamo Plus alishuka kutoka kwenye gari lake na kuongozana na mlinzi wake huku wakimwacha dereva ndani ya gari. Aalipiga hatua akitembea kwa mwendo wa kunesa kuelekea ndani ya jengo akifuatisha midundo ya muziki aliousikiliza kupitia spika (headphone) alizovaa masikioni.


Alielekea kwenye lango la kuingia la jengo lile la Nuru TV huku ile suruali yake ikiwa imevaliwa chini kidogo ya kiuno chake. Alipokuwa akikaribia lile lango la kuingilia alimwona mwanadada mmoja mrembo aliyevaa gauni refu la kitenge cha wax lenye mikono mirefu la mtindo wa pencil dress, akitokea ndani ya lile jengo akionekana kuwa na haraka kidogo.


Dynamo Plus alimtupia jicho mara moja tu na kuendelea na safari yake kuelekea ndani lakini alisita baada ya kusikia sauti laini ikimsemesha.


“Kaka Nasri, hata salamu?” yule mwanadada alimwambia Dynamo Plus na kumfanya ageuza shingo yake kumtazama kwa makini na hapo akakutana na macho legevu ya Joyce yaliyong’ara.


Dynamo Plus alimwangalia Joyce kwa wasiwasi kidogo huku akijiuliza ni wapi alikutana na mwanadada yule, kwani hata jina alilomwita ni jina lake halisi lililojulikana na watu wachache wa karibu. Jina lake halisi aliitwa Nasri Abood.


Dynamo Plus alikunja mkono wake wa kulia na kuupeleka kifuani kwake huku akiinama kidogo mbele katika hali ya kuomba radhi kwa kutosalimia.


“Wakati mwingine unaweza kupoteza video vixen hivi hivi... huyu mdada anafaa sana kupamba video yangu mpya,” Dynamo Plus aliwaza na kuachia tabasamu.


Walitazamana, Joyce naye aliachia tabasamu kabambe huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Habari yako dada yangu?” Dynamo Plus alisalimia huku akinyoosha mkono wake kumpa Joyce.


“Salama, sasa mambo si hayo? Kwani ulivyonisalimia umekufa?” Joyce alisema na kumfanya Dynamo Plus acheke kidogo.


“Nimefurahi sana leo nimekutana na wewe, mimi ni shabiki wako. You are my favorite musician,” Joyce alisema huku tabasamu pana likishindwa kwenda likizo usoni kwake.


Dynamo Plus alijisikia fahari sana kusifiwa na Joyce, aliendelea kuung’ang’ania mkono wa Joyce huku akimtazama kwa makini usoni.


“Nafurahi kusikia kwamba hata watu kama ninyi mnazikubali kazi zangu,” Dynamo Plus alisema huku akishusha pumzi.


Mambo yanazidi kunoga. Winifrida ameshaigundua siri ya Sammy, je atamweleza Joyce au atauchuna? Kukutana kwa Joyce na mwanamuziki Dynamo Plus kinaashiria nini? Usikose kufuatilia stori hii ya kusisimua hapa



Walitazamana, Joyce naye aliachia tabasamu kabambe huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.


“Habari yako dada yangu?” Dynamo Plus alisalimia huku akinyoosha mkono wake kumpa Joyce.


“Salama, sasa mambo si hayo? Kwani ulivyonisalimia umekufa?” Joyce alisema na kumfanya Dynamo Plus acheke kidogo.


“Nimefurahi sana leo nimekutana na wewe, mimi ni shabiki wako. You are my favorite musician,” Joyce alisema huku tabasamu pana likishindwa kwenda likizo usoni kwake.


Dynamo Plus alijisikia fahari sana kusifiwa na Joyce, aliendelea kuung’ang’ania mkono wa Joyce huku akimtazama kwa makini usoni.


“Nafurahi kusikia kwamba hata watu kama ninyi mnazikubali kazi zangu,” Dynamo Plus alisema huku akishusha pumzi.


SASA ENDELEA...

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog