Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

JINO KWA JINO (2) - 1

  

IMEANDIKWA NA : KAICHI M MUSSA

***********************************************

Simulizi : Jino Kwa Jino (2)

Sehemu Ya : Kwanza (1)


   “Tulipanga mimi na kijana wangu siku zilizopita hata bila nyie kuingia hapa GTL kuwa tutaenda kumkabidhi sisi wenyewe huku tukimpa na maelekezo juu ya mauaji ya marehemu Mariapan ilikuwaje aliuliwa huku akimpatia Norman flashdisk… Hii inatokana kuwa siku ya pili tu ya kifo cha mkurugenzi Mariapan alinipigia kuniuliza kulikoni yeye kutokuwepo kwake nchini mtu wetu wa karibu anauliwa na watu wasiojulikana, pia alitaka maelezo nahisi kuna nini nyuma yake kinachojificha katika mauaji yale… Niliweza kumueleza kifupi nachowaza pia nikasema ameacha flash ambayo anataka tumkabaidhi yeye mheshimiwa Rais… Hivyo makubaliano yetu baina yetu na yeye ni kumpatia hiyo flash tukiwa wote wawili ikulu pale pale katika hafla ya kurejea kwake salama itakayofanyika kuanzia saa kumi na mbili na nusu” Akajibu mzee kamanda Muniain.

  “Ulinzi wa Rais unaundwa na taasisi yake ikishirikisha vyombo vyote vya usalama wa nchi kuanzia jeshi la wananchi mpaka askari polisi na vyombo vyao vyote vya kiintelejensia, nafikiri vyombo vilivyo chini ya wizara ya usalama ambayo tunamuhusisha moja kwa moja waziri wa wizara hii na genge la TRJ kwa maelezo aliyotupa Kamishina Salivita Muniero, vyombo vinaweza kutumika katika kuwazuia nyinyi kumsogelea Rais kwa namna yoyote tusiyoweza sisi kuifahamu kwa njiia zetu.. Hivyo basi nina wazo ambalo likipita litaweza fanya kukwepa mambo ambayo naweza kuhisi yanaweza kutumika kuwazuia nyie kuonana na mheshimiwa” Agent Kai alieleza kirefu katika yale aliyokuwa akihisi katika halmashauri ya ubongo wake iliyo vizuri sana katika mambo ya sanaa inayoitwa na wajuzi wa mambo ya kijasusi kuwa ni ‘sanaa ya gizani’ lakini si giza lile la sanaa ya kichawi (washirikina laanakum) hii ikimaanishwa ni sanaa ya mambo yaliyojificha chini ya wengine kisha wewe unatakiwa kuyajua kwa kuyachimba iwe kwa siri au kwa nguvu utaalamu ukihitajika zaidi.

ENDELEA NA NONDO…!

CHIMALTENANGO, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

   “Muda wa sisi kuendelea kufanya chunguzi zaidi bila kuingia kuzifanyia kazi chunguzi umeisha ni muda wa kuweka mitego na kunasa wateja wetu wa mbolea ila kwa hili la flashdisk hatutaweka mtego tutatakiwa kuifikisha flash mahala husika kwa mheshimiwa mwenyewe tena tukitumia mbinu tofauti na wao wanavyoweza kuzania kwa urahisi hao maadui zetu… Flashdisk itapelekwa airport na Rais atapewa maelezo papo hapo airport, hivyo kwakuwa wewe huko karibu na mheshimiwa Rais ningeomba utume ujumbe kwake ukimtaarifu kuwa utaenda airport ukiwa katika sura asiyoijua ukiwa na Norman akiwa katika sura tofauti pia huko airport timu yetu itakuwepo kwa kudhibiti lolote linaloweza kutokea ambalo litakuwa tofauti na mpango wetu… Hapa maskani atabaki mtu mmoja ambaye atakuwa akiongoza mipango yetu kama kiunganishi… Kazi ni kwako Kamanda Muniain..” Maelezo endelevu yalitolewa na nahodha wa kikosi timu hiki Agent Kai ‘The Sole Cat’ alipoacha kuongea alinyanyua glasi ya maji akanywa yote alipoitua chini ilikuwa na kimiminika kisichojaa hata kizibo cha soda.

   “Nimekuelewa kijana wangu.. Ni wazo zuri sana kwa kweli… Akili zako zinafanya kazi vizuri sana, acha nimpigie madam kumuomba namba ambazo mheshimiwa anatumia akiwa kwenye ndege maana mara nyingi akiwa kwenye ndege yake anarudi toka safari za nje uwa muda mwingi anautumia kuongea na mke wake wakiwa safarini hivyo kwa sasa watakuwa karibu karibu na mkewe si mtu wa kubadili namba kwa vyovyote vile” Kamanda Muniain aliongea kwa kuanza akisifia wazo la TSC’ kisha akaeleza anachotaka kufanya kwanza, wasikilizaji walimsikiliza aliponyamaza kuwatizama kwa zamu wakatingisha vichwa vyao kukubali.

Kamanda Muniain akapiga namba za mke wa Rais ambaye Kamanda Muniain mara nyingi anapotaka kuongea na mheshimiwa Rais basi umpigia Madam na kumuomba anataka kuongea na mheshimiwa hii ikawa ni kawaida kwao iliyojenga mazoea.

Simu ilitafuta kwa muda wa dakika mbili kisha ikakata bila kuita upande wa pili, akarudia tena kupiga napo ikafanya vile vile.

   “Vipi haiiti?” Akauliza S.A Silla.

   “Inatafuta tu kisha inakata… Acha nirudie tena, maana wako kwenye ndege hawa so si kazi rahisi kupatikana hewani.

Alirudia tena ikafanya kama ilivyofanya wakati wa mwanzo hapo akasubiri dakika moja akajaribu tena sasa ikawa kama bahati simu ikaanza kuita mzee wa watu akatabasamu kwa furaha.

    “Halloow!” Sauti ya mwanamke ilisikika kwa mbali.

    “Unaongea na shemeji yako Kamanda Muniain..!”

    “Lete habari shemeji.. Habari za nchini kwetu?”

    “Nzuri kabisa tunamshukuru Mungu tunaendela vizuri na majukumu ya kazi… Mko angani?”

    “Ndiyo shemeji tuko angani.. Unataka kuongea na kaka yako?”

    “Yaah! Kuna habari muhimu sana za kumwambia mheshimiwa Rais… Naomba niongee naye!”

Haikusikika tena sauti ya mwanamama mke wa Rais kujibu kingine tena bali ulipita ukimya simu ikiwa hewani na mara Kamanda Muniain akasikia mwangwi hapo akajua Rais sasa yupo hewani.

   “Kaka Muniain..! habari yako ndugu yangu?” Sauti nzito ilisikika tokea upande wa mpigiwa simu.

   “Nzuri mheshimiwa… Poleni na safari ndefu ya kuchosha!”

   “Ahsante sana ndugu yangu… Ndiyo tunakaribia anga letu muda si mrefu tutatua Guatemala.. Lete habari?”

   “Tulipewa taarifa ya awali kuwa mnafika saa kumi na moja kamili jioni, imekuwaje tena mnawai mheshimiwa kabla ya muda huo?”

   “Hatukutua baadhi ya viwanja vya ndege, vijana wangu wa usalama waliomba tuwai tofauti na muda tulioutolea taarifa kwa sababu walizozisema wao kuwa ni za kiusalama zaidi nimewahoji wamepata habari gani? Majibu yakawa ni kucheza kiintelejensia tu kutokana na muda wa miezi inayokaribia miwili kuwa nje ya nchi hatuwezi kuamini tu na katika upendo wa watu wetu pia wapo wasio na mema wanaweza fanya tofauti na tuaminivyo… Na wewe fundi unajua haya… Najua kuna jambo pia unataka niambie tafadhali niambie haraka ndugu yangu” 

   “Nimefurahi sana kusikia utofauti na muda wenu mlioutangaza awali, vijana wako sahihi kaka yangu.. Nina mengi ya kuongea na wewe lakini bado sijatimiza ushahidi kamili katika ninayotaka kuyasema kwako hivyo ni kuombeana heri na pumzi za mmiliki wa uhai wetu… Taarifa ambayo imenifanya nipige simu wakati huu ninataka kukwambia kuhusu flashdisk tuliyoachiwa na kupewa maagizo na marehemu Mariapan kukupatia wewe tunataka kukuletea uwanja wa ndege…. Ila kwa hali iliyopo sasa hapa nchini mwetu ni hali ambayo inaweza kukustua na kukushangaza sana mheshimiwa hivyo sitaweza kuja nikiwa katika sura unayoijua itanibidi nije katika sura ya bandia nikiwa na kijana wako muaminifu Norman naye akiwa katika sura ya bandia tutakupatia flash kisha tutaondoka wote mpaka ikulu ambapo tutakupatia taarifa kamili ya mambo yote tunayoyafuatilia sasa.”

   “Eeeeh! Wahuni gani hao wanafanya mambo kama nchi yetu haina vyombo vya dola?”

   “Relax! Muda si mrefu utayajua yale ambayo tunayafanyia kazi.. Acha sisi tuwai kuja Antigua kabla ndege haijatua tukuwai hapo mkishatua utafungua simu yako data nitakutumia picha ya sura ambazo zitakuwa zimeficha sura zetu halisi hili vijana wako wasituzuie kukusogelea”

   “Sawa nitafanya hivyo… Poleni sana na kuishi kama wakimbizi ndani ya nchi yenu”

   “Ahsante… Muwe na safari njema mheshimiwa.” Alimalizia hivi Kamanda Muniain akakata simu na kuinua macho kuwatizama wenzake waliokuwa wakimsikiliza kwakuwa aliweka loud speaker yaani maongezi haya hadi mwanadada Angelica aliyasikia vizuri sana kitu ambacho kiliweza kumvuta kuwa watu hawa kumbe wako karibu kikazi za usalama na mheshimiwa Rais wa nchi hii ya Guatemala, mwanamke huyu baba yake ni mmexico na mama yake ni muaguatemala amelelewa zaidi nchi hii kuliko upande wa baba yake huko Mexico ambako ndiko anakoishi kwakuwa binti huyu alizaliwa tu bila wazazi wake kuwa wameoana.

   “Safi… Watu wa usalama wa Rais ni kama walikuwa mawazoni mwetu wamefanya jambo zuri kwenda tofauti na muda halisi uliotangazwa awali kuwa mheshimiwa Rais atafika airport ya GTL na kama mheshimiwa waziri wa usalama atakuwa hajapewa mabadiliko juu ya ujio wa Rais itakuwa vizuri zaidi kwetu.. Sasa ni saa kumi kasoro dakika ishirini tufanye haraka tuelekee airport… Hapa atabakia Silla akitufuatilia usalama wetu tukiingia matatizoni atawajibika kufanya uokozi wetu…!” Alitoa maelekezo Agent Kai akizungusha shingo huku na huko kuwatizma wenzake na macho yalipofika kwa Angelica aliganda kumtizama macho yao yakaongea jambo baada ya kila mmoja kwenye hisia zake kuwaza kitu fulani.

   “Angelica… Sisi sote unaotuona hapa ni kikosi ambacho kinahusika na kupambana na biashara haramu ya ulanguzi wa madawa ya kulevya… Unayemuita bwana wako tupo katika kumfanyia uchunguzi juu ya kujihusisha kwake na mambo haya hivyo nakuomba kwa sasa utuvumilie kidogo kuna kazi tunaenda ifanya kisha tutarudi kufanya mazungumzo na wewe… Muda kwa sasa hautoshi tunaenda hakikisha jambo moja muhimu linamfikia mheshimiwa Rais..” Agent Kai akaongea kwa kilatini akiwa kasimama na wengine walikuwa washashika njia kuondoka pale sebuleni akiwa amebaki Special Agent Silla ambaye yeye ndiyo mtu aliyeelekezwa kuwa atabaki hapa.

   “Mbona sijawai kuhisi ubaya wowote kwa Mr. Alexis?” Akahoji kwa sauti yenye kiburi kidogo kuonyesha bado hajaridhika kuwa pale.

   “Muda mdogo mambo mengi bibie… Nafikiri tutahitaji muda wa kuelekezana kwanini huko hapa.. Kistaarabu tu elewa hilo na unavyoona hapa wengi wetu sisi ni wageni tunatokea Marekani na wenyeji wetu ni yule mzee mwenye kipara ni mkurugenzi wa shirika la muungano wa nchi za ukanda huu wa Latin America la kupambana na mihadarati ‘OCLA’ anaitwa Kamanda Muniain na mwenyeji wetu mwingine ni kijana mwenzako mzalendo wa nchi yenu niliyekuja naye kule tulipokutoa… Hivyo basi kazi hii si ya kuonea ni kazi ya kiuchunguzi unaohitaji ushahidi ya yale yaliyo katika giza ambayo hata wewe huwezi kuyajua iwe kwa makusudi au kwa kufichwa mpaka mwenyewe muhusika aamue kukujulisha sisi ndiyo kazi yetu kuyajua yaliyo gizani.. Nakuomba tu kwa upole tu mrembo kaa na mheshimiwa hapa mkitusubiri turudi shida yoyote uliyonayo utamueleza huyu, nyumba kubwa sana hii ila kiusalama hautakaa mahala ambapo Silla atakuwa hakuoni mtakuwa wote mahala pamoja muda wote na si kama humu ndani hakuna watu wengine wapo watu tunaowashikilia kwa nguvu wapo kwenye chumba maalumu ambacho ukileta jeuri yoyote ile Silla atasita kukupeleka katika chumba icho ukakae nao watu ambao tunawashikilia si kwa hiyari yao bali kwa hiyari na matakwa yetu” Haya yalikuwa maelezo ya mwisho toka ‘TSC’ kwenda kwa Angelica kwani aligeuka na kuondoka kasi walipokuwa wakiongea.

   *****  *****  *****

GUATEMALA CITY CENTRE-GUATEMALA

Palacio Nacional De Cultura a.k.a Palacio Verde iliyoko eneo la Parque Centre, eneo linalovutia watalii kufika na kupiga picha za kumbukumbu angalau kwa mbali na jengo hili la kuvutia ndipo ilipo ikulu na ofisi ya Rais wa nchi ya Guatemala pilika pilika za watu makini wa usalama na hata watu wengine walioalikwa kufika hapa muda huu kwa ajili ya kumlaki mheshimiwa Rais aliyekuwa nje ya nchi kwa kipindi ca miezi miwili akifanya ziara ndefu sana katika baadhi ya nchi za bara la Asia na kisha akimalizia katika baadhi ya nchi kubwa na muhimu za barani Ulaya ikiwa ni mara ya kwanza kwake kufanya ziara ndefu zaidi nje ya nchi yake toka achaguliwe kuwa Rais wa nchi hii miaka miwili iliyopita.

Mheshimiwa Rafael Valdes Ceni waziri wa usalama wa serikali tukufu ya kidemokrasia ya Guatemala alikuwa miongoni mwa mawaziri waliofika mapema kabisa kwenye viwanja vya ikulu kasoro yake yeye na waheshimiwa mawaziri wengine ilikuwa katika utuliaji wake, yeye kila muda alikuwa mtu wa kuinuka toka mahala anapotakiwa kukaa pamoja na waheshimiwa wenzake simu mojawapo kati ya simu zake zinapoita  anasogea mahala atakapoongea bila kusikika na kupokea simu husika ilikuwa haipiti dakika tano mpaka waheshimiwa wenzake wakaona sasa ni kawaida hivyo yeye walimuacha tu bila kumuhusisha moja kwa moja na hoja zao mbalimbali za nchi walizokuwa wakizijadili kwa kifupi juu ya maendeleo katika nchi na hata matatizo yenye kuleta changamoto mbalimbali katika kazi zao za uwaziri.

Saa kumi na dakika mbili aliinuka tena toka mahala alipokaa akasogea mbele karibu na jukwaa ambalo lina kapeti jekundu, kapeti la heshima ambalo litakanyagwa na mheshimiwa Rais punde atakapofika kwenye viwanja vya ikulu, hapa aliwapita maafisa wa kadhaa wa usalama ambao nao kama kawaida walisogea pembeni kumpisha mheshimiwa wao aongee na simu kwa uhuru zaidi.

   “Lete habari Loris!” Akaongea akiziba mdomo wake kwa kiganja kingine ukiacha cha mkono wa kulia kilichoshika simu yake alitaka sauti isiende mbali kwakuwa aliuliza kwa sauti ambayo haraka alihisi itasogea zaidi na kuwafikia asiotaka wasikie anachoongea.

   “Mheshimiwa hapa airport tangazo la kutua kwa ndege ya Rais limetangazwa.. Imetushangaza kidogo maana awali tuliambiwa anafika saa kumi na moja kamili jioni hii..” Akaongea kwa kasi wa upande wapili ambaye hata kama yeye mheshimiwa waziri Ceni alikuwa hamuoni ila sauti ilimjulisha muongeaji wa upande huo ana mashaka na wasiwasi tele.

   “Eeeh! Imekuwaje tena? Mbona haitokeagi hilo? Okay! Haina shida kuweni makini kuangalia watu waliofika hapo kumpokea hakikisheni hakuna watu ambao tutahisi wana ajenda ya siri na mheshimiwa Rais… Umenielewa?” Aliuliza maswali ambayo hayakuwa na majibu kisha akamalizia kwa swali la kuuliza kama ameeleweka.

   “Naam..Niko kwenye korido ya ofisi za uhamiaji hapa, nimewaita kina Nuno tuone tunafanyaje maana vijana tulioomba watusaidie katika hali ya hapa kutoka TRJ ambao tumewapa vitambulisho vya GIS tuliwaambia wakae mbali kidogo katika kuepusha kustukiwa kwao tukitaraji ratiba itakuwa vile vile sasa inashangaza imekuwa ghafla kwetu tena nashangaa hata wewe hukuwa unajua mabadiliko ya ratiba mheshimiwa..!!”

   “Rais analindwa na taasisi yake kwa umakini sana nahisi kutokana na kutokuwepo kwake kwa muda mrefu hapa nchini imesababisha wasitoe siri rasmi ya muda ambao anawasili… Basi changamkeni kudhibiti sura za watu niliowapa picha zao kutomsogelea Rais kwa namna yoyote ile hata kwa kuwasingizia kuwa ni watu hatari.. Maafisa wa polisi nimeshawaandaa kwa hilo hapo airport hata hapa Palacio Verde” Alimalizia mheshimiwa Ceni kisha akakata simu kwakuwa simu ingine iliingia meseji akawa anahitaji aisome.

Aliisoma kimya kimya ikiwa ni maelekezo kuwa makamu wa Rais wa nchi, waziri mkuu, mkuu wa majeshi na mkuu wa polisi (IGP) wamefika airport tayari, hawa ni watu ambao kwenye ratiba wao ndiyo walikuwa ni wateuliwa kuwa watafika airport ya GUA kumpokea mheshimiwa Rais.

Alipomaliza kuisoma meseji ile akasogea mbali na eneo la jukwaa la Rais kwakuwa wanausalama na wao walikuwa wameshaletewa taarifa kuwa ndege ya Rais inatua huko La Aurora International Airport, alisogea hili apige simu kwa mtu mwingine aliyenaye katika mambo yake.

   “Mariana..!” Aliita baada ya upande wa pili kupokea simu>

   “Mheshimiwa.. Letea habari?..”

   “Naomba uwape taarifa uliowaandaa kwa ajili ya lolote lile litakaloleta tatizo juu ya usalama wetu wasogee barabara ya Avenida Calle ila wasiingie barabara ya Zone 1 kama mjuavyo hapa kamera za cctv mpaka ikulu zimejaa kwenye majengo ya barabara hii”

   “Nilitaka kukupigia muda si mrefu kukupa taarifa kuwa washasogea toka saa tisa na nusu kuna jengo refu la Mr. Alexis mtaa huu ndimo wamo wanafuatilia kila kitu maana tumefunga mawasiliano yanayotuongoza humo kwa muda”

   “ Vizuri! So walio airport nao mko nao bega kwa bega naamini… Mimi sitaweza tena kuwa nafuatilia kila kitu maana ndege ya Rais naambiwa imetua tayari huko Aurora…. Sitakiwi kuwa naongea na simu mara kwa mara punde atakapokuwa kashafika ni kazi ya maafisa wangu wa usalama huku nikitakiwa kwenda kutulia meza kuu na waheshimiwa wenzangu”

   “Sawa… Kazi njema mheshimiwa, naamini tutafanikiwa katika mpango wetu..!” Alimalizia Mariana akakata simu upande wake huku upande wa Ceni akiizima hii simu aliyotoka kuitumia kuongea na Mariana kwa sababu za kiusalama akabakiwa na simu zingine ambazo hazitumii kwa mawasiliano na watu wa genge lao la TRJ, hii inatokana na mheshimiwa Rais anapowasili mahala kama hapa ana mitambo inayoambatana na msafara wake ambao inanasa maongezi ya watu wengine wanaotumia simu kwa muda wote anapokuwa eneo la kama hapa ikulu mpaka maeneo ya jirani na ikulu kilometa zaidi ya nne na si hapa tu ikulu hadi anapotoka kwenda mahala popote kunagari ya mtambo huu ambayo ipo kwa ajili ya kazi hii kwa ajili ya usalama wa Rais.

Mwisho wa sehemu ya sitini na sita (66)

Kazi imenoga!

Mitego ya panya binadamu imenoga sasa, wawindwa wanawindwa bila kujua wanawindwa, flashdisk inatakiwa isifike mikononi mwa mheshimiwa Rais.

Ujanja wa kimawazo wa Agent Kai unakutana na ujanja wa maafisa wa usalama wanaohusika na ulinzi wa Rais wakiamua ndege ya Rais iwai kufika Guatemala kabla ya muda uliopangwa awali.

Je Mbinu za timu ipi zitafanikiwa katika kuzuia na kufanikisha yale wanayoyapanga?

Je itakuwaje kwa mheshimiwa Ceni na wafuasi wake?



Alipomaliza kuisoma meseji ile akasogea mbali na eneo la jukwaa la Rais kwakuwa wanausalama na wao walikuwa wameshaletewa taarifa kuwa ndege ya Rais inatua huko La Aurora International Airport, alisogea hili apige simu kwa mtu mwingine aliyenaye katika mambo yake.

   “Mariana..!” Aliita baada ya upande wa pili kupokea simu.

   “Mheshimiwa.. Lete habari?..”

   “Naomba uwape taarifa uliowaandaa kwa ajili ya lolote lile litakaloleta tatizo juu ya usalama wetu wasogee barabara ya Avenida Calle ila wasiingie barabara ya Zone 1 kama mjuavyo hapa kamera za cctv mpaka ikulu zimejaa kwenye majengo ya barabara hii”

   “Nilitaka kukupigia muda si mrefu kukupa taarifa kuwa washasogea toka saa tisa na nusu kuna jengo refu la Mr. Alexis mtaa huu ndimo wamo wanafuatilia kila kitu maana tumefunga mawasiliano yanayotuongoza humo kwa muda”

   “ Vizuri! So walio airport nao mko nao bega kwa bega naamini… Mimi sitaweza tena kuwa nafuatilia kila kitu maana ndege ya Rais naambiwa imetua tayari huko Aurora…. Sitakiwi kuwa naongea na simu mara kwa mara punde atakapokuwa kashafika ni kazi ya maafisa wangu wa usalama huku nikitakiwa kwenda kutulia meza kuu na waheshimiwa wenzangu”

   “Sawa… Kazi njema mheshimiwa, naamini tutafanikiwa katika mpango wetu..!” Alimalizia Mariana akakata simu upande wake huku upande wa Ceni akiizima hii simu aliyotoka kuitumia kuongea na Mariana kwa sababu za kiusalama akabakiwa na simu zingine ambazo hazitumii kwa mawasiliano na watu wa genge lao la TRJ, hii inatokana na mheshimiwa Rais anapowasili mahala kama hapa ana mitambo inayoambatana na msafara wake ambao inanasa maongezi ya watu wengine wanaotumia simu kwa muda wote anapokuwa eneo la kama hapa ikulu mpaka maeneo ya jirani na ikulu kilometa zaidi ya nne na si hapa tu ikulu hadi anapotoka kwenda mahala popote kuna gari ya mtambo huu ambayo ipo kwa ajili ya kazi hii kwa ajili ya usalama wa Rais.

ENDELEA NA NONDO..!!

KAZI IMEANZA I

GUATEMALA CITY CENTRE-GUATEMALA

   “Nyinyi ndiyo wageni wa mheshimiwa Rais?” Lilikuwa swali stukiza toka kwa kijana mmoja wa ki Guatemala likienda kwa watu wawili waliosimama wakiwa na mabegi yao wakionekana ni wasafiri waliofika airport ya kimataifa ya La Aurora International Airport uwanja wa ndege wa kimataifa ulio mkuu kuliko viwanja vingine vya ndege vya nchi ya Guatemala.

Kabla anayeulizwa hajajibu simu ya muulizaji illita na haraka akaitoa mfukoni mwake kuangalia mpigaji wakati huo huo eneo lote la uwanja wa ndege kuanzia kule zinakotua ndege za abiria wa kawaida na hata eneo la viongozi wa kiserikali kulikuwa na pilika pilika za wana usalama wa vyombo mbalimbali vya kiusalama vya nchini Guatemala hii ilitokana na mkuu wa nchi, Rais anayetawala na kuongoza nchi hii ndege anayoitumia kusafiri nayo kwa safari za nje na hata ndani ya nchi ilikuwa imetua dakika kumi na tano zilizopita wakitangulia kushuka walinzi wake kisha baada ya waliofika kumpokea kupanga mstari pembeni ya kapeti jekundu akawa wanasubiriwa mheshimiwa na mkewe ‘the first lady’ kushuka.

   “Umewaona?” Ilisikika sauti ikiuliza katika lugha yao watu wa Guatemala wanaotumia kihispaniola (kilatini) baada tu ya muulizaji aliye karibu kabisa na watu aliofika na kuwauliza ‘wao ndiyo wageni wa mheshimiwa Rais’.

   “Ndiyo mheshimiwa! Nimewaona..!” Akajibu kijana huyu huku akiwatizama wazungu kama yeye aliosiamama mbele yao akijifanya kama hana habari nao kwenye macho ya watu wengine.

   “Fanya kama nilivyokuelekeza..!!” Sauti ikasikika tena, kijana akaondoa simu yake sikioni na kwakuwa kati ya watu hawa mmoja alikuwa ni Kamanda Muniain akiwa katika sura ya bandia aliweza kuing’amua sauti inayosikika toka kwenye spika zisizo na siri za mtu aliyewasogelea na kuwauliza swali akijifanya kama hataki kuongea nao katika msongamano wa watu waliokuwa wameamriwa kusubiri eneo hili kwa pamoja mpka msafara wa Rais utakapoondoka hapa uwanja wa ndege.

   “Nina maelekezo yenu toka kwa mheshimiwa… Anasema niwasaidie muingie kwenye moja ya gari zilizo kwenye msafara wake kuelekea ikulu hivyo naomba mnifuate.. Tunaenda kwenye moja ya gari za walinzi wake wanaojihusisha na kuzuia vilipuzi hivyo nifuateni kwa mwendo wa haraka na msisite wala kuangalia pembeni..!” Akaongea mtu yule kuwaambia watu hawa ambao walikuwa ni mkurugenzi wa OCLA Guatemala na kijana wake Detective Muniain wote wakiwa kwenye sura bandia wakionekana wote ni vijana maana hata Muniain alivaa sura ya muonekano wa kijana nyuma ya waliposimama hatua kama kumi hivi alisimama Agent Kai ‘TSC’ naye akiwa amevaa sura ya bandia ya kizungu na pembeni yake hatua kama tano alikuwepo mwanadada hatari Special Agent Rebecca Smith wote kwa pamoja walikuwa makini kufuatilia nyendo za maafisa wa OCLA, miwani meusi iliyo machoni mwao si miwani urembo ilikuwa ikifanya kazi ya kuyasaidia macho yao kuona mengi yaliyo mbali na hapa na hata yaliyo karibu na wao.

Waliweza kuona hadi gari waliloingia watu wao lakini kwa tahadhari waliogopa kufanya mawasiliano kwa kuwa tayari Muniain na Norman walishaelekeza kuwa katika uwepo wa Rais uwa kuna utaratibu wa kiulinzi unaonasa mawasiliano yote ya watu walio karibu na eneo aliyopo hivyo wao walipoona imekuwa salama kabisa hakuna mushkeri walipeana ishara kisha wakatoka eneo la kusubiria abiria wakipita kando kando hadi kwenye gari waliyokuja nayo hapa Airport wote wakaingia ndani ya gari.

   “Kazi imeenda vizuri… Sasa tukasubiri mahala tukisubiri maelekezo yao..!” Akaeleza Agent Kai wakitizamana na Rebecca ambaye yeye alikuwa amevaa wigi jeusi kichwani mwake kuzuia nywele zake zoeleka kimuonekano ambazo ni nywele za rangi ya blonde ila sura yake aliongeza vinywele kidogo katika nyusi nah ii ilimfanya abadilike kidogo ukimuona kwa ghafala huwezi mtambua mpaka usogee karibu yake na uwe unamjua sana si juujuu.

   “Yah! Nimependa u smart wa mheshimiwa Rais, yuko makini sana… Nashauri tusiondoke hapa mpaka msafara wote wa Rais uwe umemalizika hili tuhakiishe jamaa zetu wameondoka salama salimini… Kumbuka hali halisi ya hapa watu wa usalama wanavyoshirikiana bila hofu na magenge ya uhalifu” Akaongea Rebecca akiweka hoja yake wasiondoke kama alivyotaka Agent Kai.

   “Wazo zuri sana.. Nilitamani tuondoke hili tufanye mawasiliano na Miller aliyepo Parque Centre na pia kujua na Silla naye yuko vipi huko, eneo hili hatuwezi kuwasiliana kama tulivyoelekezwa na kina Norman.!”

   “Vumilia kidogo boss… Tutajua tu wanaendeleaje na kama unaona vipi tumia meseji hakuna mtambo wa kuweza kuiba mawasiliano ya whatssap papo kwa hapo… Hahahaha hahahah.. Jasusi mbobezi unajisahau na wewe kumbe wakati mwingine”

   “Sijasahu.. Nimetuma meseji sijajibiwa na yoyote kati yao..!”

   “Basi tuvute subira kwanza kazi iliyotuleta hapa haijaisha bado” Akamalizia Rebecca na wote wakacheka kicheko kidogo.

Dakika mbili mbele watu wanaonekana ni wana usalama wakaanza mbio mbio wakipishana huku na huko kuhakiki usalama, haikupita dakika nyingi ikaanza kusikika ngoma na matarumbeta yakipiga sambamba na watu wanaosikika wanaimba ilikuwa ni wimbo wa taifa alikuwa sasa Rais ameshuka anapewa ukaribisho wa heshima inayomstahili mkuu wa nchi yoyote anaporudi nchini mwake.

Zilikata dakika ishirini mpaka kufikia saa kumi na dakika arobaini msafara wa watu kutokea ndani ya viunga vya majengo ya kiwanja cha ndege kuja kwenye barabara zinazoanzia ndani ambazo uwa zinatumika kwa ajili ya waheshimiwa wa serikali ulitokea kwa nje na kuwafanya ‘TSC’ na mshirika Rebecca kuona sasa msafara tarajiwa unatoka ndani ya eneo la kiwanja cha ndege, magari yalitoka kwa mwendo wa kawaida kisha yakakamata kasi yakielekea barabara kuu itokayo uwanja wa ndege kuelekea ‘Guatemala Centre’.

   “Wameondoka salama salimini naamini zoezi letu kwa hapa airport limeenda bila kizuizi’’ Akaongea Special Agent Rebecca wakiwa wanaangaliana na Agent Kai ambaye muda mwingi alikuwa kimya akifuatilia msafara wa magari kana kwamba anahesabu magari.

   “Twen’zetu!” Akaongea neno hili kisha akawasha gari kuondoka pale maegeshoni huku hali ya kawaida iliyozoeleka ikirejea kwa pilika pilika za watu wakipishana kwenda eneo la majengo ya uwanja na wengine wakitoka kama ilivyo viwanja vyote vikubwa vya ndege hapa duniani.

       *****  *****  *****

PALACIO VERDE, GUATEMALA CENTRE-GUATEMALA

Wasiwasi kwa kawaida ni kitu ambacho uwa ni kawaida kwa binadamu anayefanya jambo ambalo anajua si zuri kwenye jamii inayomzunguka na hata ile isiyomzunguka (ya mbali) lakini wasiwasi mwingine uwa unaoweza wewe mwenye wasiwasi kuuzuia usionekane kwa mtu au watu walio karibu nao kwa wakati huo lakini pia inaweza ikawa wasiwasi wako ukaona au kuhisi umeuzuia usionekane kwa mtu au watu wengine lakini ikashindikana kuwa siri tena ikawa wazi hata kama ni kawaida kwako kuwa na ujasiri lakini ukavuruga na kujulikana una wasiwasi, ndivyo ilivyokuwa kwa mheshimiwa waziri wa usalama Rafael Valdes Ceni.

Mawaziri ambao kikawaida ikiwa wanakuja hapa ikulu kwa boss wao, uwa wanakuwa karibu naye kimaongezi wakishirikishana kimaongezi tena wakifurahi sana walimstukia rafiki yao wakaambiana leo mbona mwenzetu hayupo kikawaida sana lakini hawakuweza kumuuliza lolote wakaacha waje waone wenyewe nini kitatokea wakiongeza umakini wa siri katika kumfuatilia sababu kati yao wapo waliokuwa wakijua mambo yake ya siri ila walikosa ushahidi kamili pia urafiki wake na mheshimiwa Rais uliwafanya wawe wakimya wasije wakawa wanaingilia jambo ambalo kumbe lina maslahi pia na kwa boss wao mheshimiwa Rais wa nchi.

Ving’ora vya magari ya msafara wa Rais vilizidi kusogea karibu na eneo la ikulu hii ikimaanisha sasa muda wowote magari ya msafara yatafika ndani ya barabara nzuri na safi zinazoingia ndani ya viwanja vya Palacio Verde, mawaziri wote hasa wale ambao kiukweli wa dhahiri shairi mioyoni mwao walikuwa na hamu ya kuiona sura ya mheshimiwa Rais wao walikuwa wakitabasamu kwa bashasha tele ingawa walikuwepo pia ambao uwa hawakosekani ambao midomoni wanacheka lakini si cheko halisi bali cheko la kihusuda nao kwa sasa walikuwa wakikenua meno yao wakiwa katika mavazi ya suti za rangi tofauti lakini ni suti za gharama, safi za kupendeza wote kwa kweli waheshimwa walikuwa wamependeza sana.

Sauti ya ving’ora ilipokuwa imezidi kuhanikiza mbele ya meza hizi za mawaziri karibu na kiti alichokaa waziri wa usalama mheshimiwa Ceni alikuja mtu ambaye naye alikuwepo eneo hili la ikulu kutokana na umuhimu wake pamoja na cheo chake, mkurugenzi wa uhamiaji Brigedia Kristein Granell alimtizama bila kupepesa uso waziri na waziri mara moja alielewa mtu aliye mbele yake anahitaji kuongea naye jambo la siri hivyo hatakiwi kuendelea kukaa pale ainuke.

Mheshimiwa waziri aliinuka kwa kasi akarudisha kiti chake nyuma na kutoka kwa  nyuma ya viti vya waheshimiwa wenzake wakaongozana kutoka eneo lile wakisogea karibu na vyoo vinavyotumika na wageni wanaofika eneo la viwanja vya ikulu katika warsha mbalimbali.

   “… Kijana wangu mmoja anataka kuongea na wewe tukiwa pamoja nasi kwa haraka sana, yupo chooni anatusubiri anasema ana siri ameigundua muda si mrefu akiwa ameambiwa kwa meseji na rafiki yake mmoja ambaye ni mmoja wa walinzi wa juu kabisa katika timu ya walinzi wa Rais..” Aliongea kwa haraka mkurugenzi Brigedia Granell, sauti yake ilitosha kumuongezea wasiwasi usoni rafiki yake anayemwambia.

   “Aisee.. Mbona amechelewa sana?” Akahoji kwa sauti kama ya mwenzie yenye uharaka tena yeye haraka ikizidi zaidi na macho hayakuacha kuangalia huku na huko.

   “Amefika hapa muda si mrefu… Kama hujuavyo hapa ikulu mheshimiwa akifika tu hakuna simu ya siri hivyo hatuna muda wa kulemba tujifanye tunaingia chooni tumsikilize kwa haraka..”

   “Duh! Mheshimiwa pikipiki za kuongoza msafara hizo zimeingia… Aisee tuwai!” Akakubali na mbio kila mmoja akajifanya ameshika zipu na ana haraka, haraka iliyo na ukweli lakini mikono yao kushika zipu ilikuwa zuga maana macho ya walinzi wa ikulu yalikuwa yanawafuatilia kwa sana hata kama wanawajua lakini hawakuacha kuwaangaza.

Waliingia kwa kasi kwenye korido ya vyoo wakatokea mahala ambapo kuna masinki ya vyoo vya kukojolea vilivyopangwa ukutani kwa saizi ya mtu kuweza kusimama na kukojoa.

   “Huyu hapa..” Akaongea Brigedia Granell punde walipofika na kumkuta kijana aliyevaa suti za wanausalama wa kutoka uhamiaji rangi ya kijivu.

   “Kijana ongea haraka kuna nini? Mheshimiwa ameshafika nitaonekana wa ajabu kama sitaonekana katika meza kuu” Akaongea kwa haraka bila hata kutaka kushikana naye mkono kijana yule waliyemkuta kasimama licha ya kuwa alionyesha anataka kumsalimu kwa kumshika mkono mheshimiwa waziri.

   “Cornell eleza upesi ulichotaka kutueleza..” Akaongea Brigedia, kijana akajiweka sawa akawatizama kwa zamu kwa kasi.

   “Nimepewa taarifa mnawatafuta mkurugenzi wa OCLA na kijana wake Detective Norman… Hii meseji nimetumiwa na mmoja wa walinzi wa Rais anasema Norman na Kamanda Muniain ni miongoni mwa watu walio katika gari la mtambo wa kuzuia rimoti za vilipuzi na makombora kufanya kazi.. Alichosema  yeye ni mmoja wa watu wako anaomba nikufikishie ujumbe huu ndipo mimi nikaona nimwambie boss wangu hapa” Akaongea yule kijana kisha akaanza hatua za kuondoka huku waheshimiwa wake kila mmoja akisogea kwa haraka kwenye masinki ya kukojolea kwakuwa maafisa wengine wa usalama wanaohudumu ikulu walitokea wakiwa kama watatu wakiwa wameongozana na si kama walikuwa wakiwafuatilia hawa walikuwa ni kati ya waliofika na msafara wa Rais ni kweli walikuwa wamebanwa na haja ndogo.

Waheshimiwa walitoka wakiwa wameongozana na kila mmoja akashika njia ya kuelekea eneo linalomuhusu kukaa.

Kichwa chini jasho likiwa linaanza kumtiririka mheshimiwa Ceni alifika kwenye kiti chake hadi koo likiwa limekauka akafikia kunyanyua chupa ya maji ya kunywa akafungua kzibo na kupiga maji mtindo wa tarumbeta.

Mheshimiwa Rais alishuka kwenye gari lake akiwa mwenye furaha tele kurejea nchini mwake akapunga mikono ishara ya kuwashukuru watu mbalimbali waliofika viwanjwa vya ikulu jioni hii kisha akatembea kwenye zulia jekundu akisogea ilipo familia yake ikiwa ni watoto na hata wajukuu zake ambao ni watoto wadogo wadogo hawa wajukuu kwakuwa watoto wake mheshimiwa walikuwa si watoto wakubwa wa umri kuweza na wao kumilki watoto wao wakawa wakubwa wakubwa.

Alipomaliza kuwasalimu watu wa familia yake akiwa ameambatana na mkewe wakasogea eneo la mawaziri wake napo wakapita wakitoa salamu akamalizia kwa maafisa wake wengine nako kwa furaha akawasalimu na kisha akatoa neno kidogo la kuwashukuru.

Macho ya mheshimiwa Ceni yalikuwa ni kusaka wapi ataiona sura mojawapo kati ya sura alizoambiwa kitaarifa kuwa mawindo yao yamekuja ikulu yakiwa yameongozana na msafara wa mheshimiwa Rais, kila akiangalia anavyoangalia hakuona sura shuku, mwisho akaamua awashirikishe watu wake waliozagaa kwa wingi eneo hili la viwanja vya ikulu akiwatumia meseji ambao na wao walistuka sana wakazidisha umakini lakini na wao kwa kweli hali iliwashangaza kwakuwa hawakuambulia kitu kiasi ya kwamba wapo walioamini boss wao amewapa taarifa ya uongo.

Shamra shamra za ujio wa kurudi wa kurudi nyumbani mheshimiwa Rais ziliendelea kwa watu waalikwa wote kujumuika kwa pamoja wakipata vinywaji mbalimbali pamoja na bendi ambayo utumika katika kupiga nyimbo ya taifa kila anapokuwa Rais ikihitajika hilo na yenyewe ilikuwa ikiendelea kutoa burudani ama kweli ilikuwa ni siku ya furaha sana hasa familia ya mheshimiwa Rais ilikuwa na furaha iliyopitiliza kuwaona kiongozi wa familia yao pamoja na mama kiongozi wa familia yao.

Ilipofika saa moja giza likiwa linaanza kushika hatamu mheshimiwa Rais aliwaaga wageni waalikwa wote kuwa anahitaji sasa kubaki na familia yake waweze kuzungumza mengi ya kifamilia kisha wapumzike, vijana wa kazi wa mheshimiwa Ceni walijichanganya kila kona na watu wengine lakini wao dhumuni lao kuu lilikuwa ni kuona kile ambacho boss hakuacha kuwasisitiza kuwa wajitahidi kuhakikisha lile ambalo aliambiwa na hata wakati sherehe zinaendelea  kijana aliyetuma meseji kwa kijana wa Brigedia Granell alifanikiwa kuonana naye na yeye akamsisitizia ndivyo ilivyo na anajaribu kufuatilia zaidi wamewekwa wapi kisha atamjuza lakini mpaka muda huo unafika kulikuwa hakuna habari kamili, Muniain na Norman walikuwa tayari wako chumba cha mikutano cha siri cha mheshimiwa Rais wakimsubiri mheshimiwa amalize mambo ya sherehe za ukaribisho waje wajadili kwa pamoja mambo mengi waliyonayo.

Saa moja na nusu usiku waheshimiwa mawaziri wote walifanikiwa kumaliza kuagana na boss wao Rais wa nchi akiwemo Ceni mwenyewe kisha taratibu za magari ya waheshimiwa hawa kuondoka eneo la viwanja vya ikulu ilifuata.

Mwisho wa sehemu ya sitini na saba (67)

Wakicheza kama Messi aliyekuwa kazungukwa na majembe kama kina Iniesta na Xavi, Kamanda Muniain na kijana Detective wanafanikiwa kuingia ikulu bila waziri anayehusika na usalama kujua kama mawindo aliyokuwa akijaribu kuyazuia yasiingie ikulu yameingia bila yeye na vijana wake kuyaona kwa macho licha ya kupewa taarifa mawindo yameingia.

Mheshimiwa atafanyaje akijua ni kweli adui zake wako ndani ya ikulu ya ‘Palacio Verde’?



Macho ya mheshimiwa Ceni yalikuwa ni kusaka wapi ataiona sura mojawapo kati ya sura alizoambiwa kitaarifa kuwa mawindo yao yamekuja ikulu yakiwa yameongozana na msafara wa mheshimiwa Rais, kila akiangalia anavyoangalia hakuona sura shuku, mwisho akaamua awashirikishe watu wake waliozagaa kwa wingi eneo hili la viwanja vya ikulu akiwatumia meseji ambao na wao walistuka sana wakazidisha umakini lakini na wao kwa kweli hali iliwashangaza kwakuwa hawakuambulia kitu kiasi ya kwamba wapo walioamini boss wao amewapa taarifa ya uongo.

Shamra shamra za ujio wa kurudi wa kurudi nyumbani mheshimiwa Rais ziliendelea kwa watu waalikwa wote kujumuika kwa pamoja wakipata vinywaji mbalimbali pamoja na bendi ambayo utumika katika kupiga nyimbo ya taifa kila anapokuwa Rais ikihitajika hilo na yenyewe ilikuwa ikiendelea kutoa burudani ama kweli ilikuwa ni siku ya furaha sana hasa familia ya mheshimiwa Rais ilikuwa na furaha iliyopitiliza kuwaona kiongozi wa familia yao pamoja na mama kiongozi wa familia yao.

Ilipofika saa moja giza likiwa linaanza kushika hatamu mheshimiwa Rais aliwaaga wageni waalikwa wote kuwa anahitaji sasa kubaki na familia yake waweze kuzungumza mengi ya kifamilia kisha wapumzike, vijana wa kazi wa mheshimiwa Ceni walijichanganya kila kona na watu wengine lakini wao dhumuni lao kuu lilikuwa ni kuona kile ambacho boss hakuacha kuwasisitiza kuwa wajitahidi kuhakikisha lile ambalo aliambiwa na hata wakati sherehe zinaendelea  kijana aliyetuma meseji kwa kijana wa Brigedia Granell alifanikiwa kuonana naye na yeye akamsisitizia ndivyo ilivyo na anajaribu kufuatilia zaidi wamewekwa wapi kisha atamjuza lakini mpaka muda huo unafika kulikuwa hakuna habari kamili, Muniain na Norman walikuwa tayari wako chumba cha mikutano cha siri cha mheshimiwa Rais wakimsubiri mheshimiwa amalize mambo ya sherehe za ukaribisho waje wajadili kwa pamoja mambo mengi waliyonayo.

Saa moja na nusu usiku waheshimiwa mawaziri wote walifanikiwa kumaliza kuagana na boss wao Rais wa nchi akiwemo Ceni mwenyewe kisha taratibu za magari ya waheshimiwa hawa kuondoka eneo la viwanja vya ikulu ilifuata.

ENDELEA NA NONDO KALI..!!

SAA MBILI NA NUSU USIKU, IJUMAA

PALACIO VERDE, GUATEMALA CENTRE-GUATEMALA

   “Poleni sana kaka kwa kusubiri muda mrefu sana..” Alikuwa ni mheshimiwa Rais aliongea baada ya kufungua tu mlango wa chumba chake cha mikutano cha siri ambacho yeye ufanya vikao humu na watu wake anaowaamini sana na hii si mara ya kwanza yeye kukutana kimaongezi na Kamanda Muniain Salivita Muniero katika chumba hiki kidogo kinachotosha masofa makubwa mawili tu pamoja na meza ndogo ambayo ilikuwa katikati ya chumba huku ukuta wa upande wa kushoto kwao ukiwa na screan (kioo cha tv) chini yake kukiwa na deki na hata upande wa kulia kwao ukuta wake nao ulikuwa na screan ya ukubwa kama wa hii ya kushoto na yenyewe chini yake kukiwa na deki lakini pia kulikuwa na mashine ya desktop (kompyuta ya mezani).

   “Tumevumilia si leo tu, tumevumilia mwezi sasa hili tuonane na wewe mheshimiwa hivyo usihofu kabisa kuhusu uvumilivu wetu hatuwezi kuchoka kwenye kukutumikia mheshimiwa… Siku zote mimi usema kukwambia niko tayari kufa kwa ajili yako damu yangu wewe..” Akaongea Kamanda Muniain tabasamu pana likiwa limechanua usoni mwake kisha wote yeye na Detective Norman wakasimama kumsalimia mheshimiwa.

Walipeana salamu za heshima kisha kwa ishara ya mkono mheshimiwa Rais akawaonyesha warudi kuketi kwenye masofa kuanza kwa maongezi yaliyowafanya wakutane hapa mahala pa siri.

   “Nilivyoingia na kuwakuta katika sura zenu halisi ilinifanya nifurahi sana na kuona katika nchi yetu pia tuna wataalamu wa mambo walio makini na kazi ya ujasusi kwa kweli nazidi kujivunia kuwa na ndugu kama wewe Muniain pamoja na huyu kijana wako Norman… Nafikiria umuhimu wenu ulivyo mkubwa sana kwangu pamoja na mioyo yenu isiyo na tamaa na mambo machafu ambayo kiukweli najitahidi kuyafagia lakini kila navyofagia uchafu unamwagwa tena…  Kijana hongera sana na nafikiri hii ni mara ya pili tunakutana mimi na wewe hivyo naomba nizoee na usiogope kuendelea kunywa maana naona glasi iko nyeupe huweki kinywaji wakati mzinga ndiyo kwanza huko nusu..” Aliongea kirefu kidogo Rais akimalizia kumuomba Norman apige kinywaji bila hofu.

   “Ni kweli mheshimiwa Rais hii ni mara ya pili napata bahati ya kuheshimishwa kukutana na wewe mahala faragha hakika mheshimiwa usihofu juu yangu katika kukutumikia wala kukuzoea kama mzazi au rafiki mkubwa kama ilivyo kwa ndugu yangu na boss wangu ambaye kwangu ni kama mzazi wangu kwakuwa mimi sina wazazi wote nyinyi ndiyo watu pekee ninaojivunia kuwa nao kwakuwa napata upendo mzito toka kwenu… Mheshimiwa umekuwa mwepesi kuniulizia mara kwa mara kwa boss wangu na hata kuuliza nina tatizo gani katika matumizi yangu ya kibinadamu, shukrani kuu kutoka moyoni mwangu zikufikie nathubutu kusema niko tayari kufa kwa ajili ya nchi yangu na kwa ajili yako mheshimiwa Rais!” Akajibu kwa furaha Norman kisha akamimina kinywaji aina ya Licuados katika glasi kinywaji aina ya pombe kali sana kinachopendwa sana na vijana wa Guatemala hasa wale wenye uwezo wa kujimudu kipesa kwakuwa ni kinywaji ambacho chupa moja ya mzinga wake ni aghali.

   “Naam nimepokea kwa dhati shukrani yako nami sina budi kusema shukrani kwa ushirikiano wako wenye uaminifu kwa kaka yangu hapa na nchi kwa ujumla… Leteni habari ya shauku mliyonayo inayofanana na shauku niliyonayo juu ya mazungumzo haya nyeti?” Aliongea mhehimiwa Rais akiomba sasa ni ruhusa kwa kuingia katika dhumuni kuu la uwepo wao hapa.

   “Kwanza mheshimiwa naomba nitoe pole kwako na serikali yako kwa kumpoteza mtu shujaa, muaminifu na mzoefu katika masuala mbalimbali ya kiserikali rafiki yako mkubwa Mr. Funtes Jota Mariapan” Alianza kuongea hivyo Muniain lakini akakatiziwa na badiliko la haraka la sura ya ndugu yake binamu.

  “ Aiseeh… Inauma sana, asubuhi ya kesho jumamosi nitafanya kikao na mkurugenzi wa usalama wa taifa pamoja na waziri wa usalama nimewapa taarifa hiyo viwanjani nina maswali juu yao wamefikia wapi juu ya upelelezi wa kifo cha swahiba wangu… Mshenzi gani anaweza kumpiga risasi nyumbani kwake mteule wangu? Ahsante sana kwa pole ni pole yetu sote taifa kwa ujumla bwana Mariapn alikuwa mchapakazi na muaminifu sana kwa nchi hii” Akajibu pole ile uso akiwa kaukunja na kwa weupe wake wa kizungu uliokolea sana akabadilika rangi akawa mwekundu damu ilichangamka zaidi kupita kwenye njia zake hali ikawa hivi.

   “Ndiyo mheshimiwa… Kabla ya yote nataka kukwambia kabla marehemu Mariapan hajapigwa risasi alikuwa ametembelewa  na huyu kijana wetu Norman alikua amemuita kwakuwa wiki moja nyuma yake tulifika kuonana naye ofisini kwake tukawa tumempa orodha ya majina ya watu ambao tulitaka taasisi yake ya kupambana na rushwa itusaidie kuwafuatilia kwa ukaribu kwakuwa tulikuwa tunahisia nao wanajishusisha na rushwa katika masuala ya njia yanakopita madawa ya kulevya katika barabara mbalimbali za nchi yetu hasa za mipakani… Bahati nzuri akatuambia yeye pia watu hao hao walio katika orodha ile ameanza kuwashuku katika mambo ya uhujumu uchumi na hata kujishusisha kwao katika kurahisisha magenge ya madawa ya kulevya ya nchini Mexico kufanya shughuli zao hapa nchini mwetu akasema kuna jambo analiandaa yeye na kijana wake mmoja kinahusiana na video ambayo itakuwa ushahidi kwetu na hata kwako mheshimiwa Rais juu ya vigogo wa rushwa na vigogo wa mihadarati hapa nchini kwetu wanaotumika na magenge ya Mexico” Alieleza kirefu kidogo Muniain lakini ilibidi anyamaze kwakuwa mheshimiwa Rais alionyesha ana jambo anataka kuuliza akamuonyesha ishara aulize.

   “Mna maana Norman alivyotoka kuonana tu na Mr. Mariapan ndipo alipigwa risasi?” Akauliza mheshimiwa Rais.

  “Ndiyo mheshimiwa.. Wakati naongea naye nilikuwa naongea naye katika chumba chake cha siri ambacho ufanya mambo yake ya kama kiofisi akiwa nyumbani kwake.. Wakati tukiendelea  na maongezi akaja mtumishi wake wa ndani kugonga akisema kuwa kuna wageni wanataka kuonana naye mlinzi anauliza kama waruhusiwe kuingia ndani ikabidi marehemu Mariapan atoke mpaka sebuleni kwake ambako kuna screan ya cctv camera ambayo uwa anawaona wanaofika kwake wakiwa huko getini alipomuoina alirudi haraka sana kwenye chumba tulichokuwemo akaniambia niondoke haraka sana hataki mtu anayefika pale anione kwakuwa mtu huyo ananituhumu mambo mengi mimi kuwa nawaharibia biashara zao, nikamuuliza Mariapan haraka haraka je haoni kama anashirikiana na watu wabaya akanijibu yeye hana uwezo wa kukwepa mambo mengine sababu yapo katika mfumo, nikashangaa sana kwa jibu la mzee yule niliyekuwa namuamini sana nikataka kugoma kuondoka hili nimjue nani huyo mtu akanisihi nisifanye nachotaka tutaumia au kuuliwa wote nikamwambia mzee mimi ni afisa mkubwa wa usalama niko tayari kufa lakini marehemu alifungua droo haraka akatoa flash iliyoko katika kiboksi kilichofungwa vizuri kwa sildi akasema flash hii usiiangalie hakikisha unampatia Rais kwa hali yoyote kwakuwa sina hakika na hali yangu ya baadaye mambo yameharibika, alisema hivyo kisha akanishika mkono akanitoa mpaka uwani kwake akaniambia nitokee mlango mdogo wa nyuma akanifungulia nikaondoka…Lakini wakati naondoka niliona watu fulani niliowatilia mashaka ambao waliponiona walinikazia sana macho wakitamani kunifuatilia wakaongea kwa simu wakati huo mimi nikawa nishafika nilipoacha gari yangu nyumba ya tatu toka nyumbani kwa marehemu nikaingia na kuondoka kwa kasi.. Nikiwa njiani kuelekea kwangu nikapigiwa simu na mke wa marehemu kuwa mumewe amepigwa risasi na mwanamke aliyeingia kwa nguvu ndani mwao akiwa na wanaume wawili wakawa wanamlazimisha aseme amenipa nini mimi lakini mumewe aligoma mwanamke yule akampiga risasi mume wake wakatoka kasi wakiwa wanapigizana makelele kuwa Norman asakwe haraka sana yaani mimi… Mkewe anasema mumewe kabla hajakata roho alichora chini kwa damu yake akiandika jina langu na namba yangu ya simu akaeleza niambiwe nijifiche mbali na pia nihakikishe kwa kila hali nakupatia flashdisk aliyoiandaa ambayo ni hii hapa mheshimiwa” Maelezo marefu ya bila kuruhusu koo kupumzika toka kwa Norman yalifikia hapa akatoa flashdisk na kumkabidhi mheshimiwa Rais.

   “Eeeh! Kumbe ndivyo ilivyokuwa…Mariapan kwanini alikuwa anaruhusu kuzoeleka kwa watu wabaya mpaka wanafika kwake? Sawa acha tuiangalie kwa pamoja kisha tutaendelea na maongezi, hatari sana huyo mwanamke anayempiga risasi mtu mbele ya familia yake amejiamini sana” Akaongea mheshimiwa Rais akiwa kashainuka kusogea ilipo cpu ya kompyuta ya desktop ambayo kioo chake ndiyo screan iliyofungwa ukutani upande wa kulia kwao.

Aliwasha kompyuta iliporuhusu window kuwa tayari kutumika akafungua box na kuikuta flash akaichomeka kwenye tundu mojawapo la usb ndipo ikasoma na baada ya dakika moja ikaanza kuonyesha yaliyomo.

Ilikuwa ni video ndiyo iliyoanza ambayo haikuwa katika quality sana ikionyesha imechukuliwa na kamera ambayo si maalumu hasa kwa kuchukua video ambazo zinakuwa mahususi kwa burudani au vinginevyo hii kamera ilionyesha ni kamera ndogo za kama kamera za majasusi ambazo mara nyingi kwa ilivyo hii video itakuwa imechukuliwa na peni za kijasusi hivyo vinavyoonekana vilikuwa na giza giza.

Kwa jinsi watu walivyokaa ilionekana ni kikao cha watu fulani kinachoongozwa na mtu ambaye kamera ndiyo haswa ililenga kumchukua au ilikuwa imeelekezwa zaidi kwake kwakuwa alikuwa haonekani vizuri ilibidi mheshimiwa Rais asimamishe ilipofika sura yake kisha akazoom.

  “Hivi macho yenu yanaona kama mimi? Hiki ni kikao lakini video hii inaonekana haijachukuliwa vizuri kabisa jamani… Lakini mtu huyu sura yake ni kama mtu nayemfahamu” Akaongea mheshimiwa Rais kiasi ya kwamba licha yaku zoom aliinuka sofani akasimama na kusogea ukutani karibu luninga.

   “Hii video! Mheshimiwa ni video iliyochukuliwa ki wasiwasi sura hiyo unayoifananisha kuwa ya mtu ambaye ni kama unamjua ni sura ya ambayo inafanana na mheshimiwa waziri wa usalama bwana Rafael Valdes Ceni… “ Akaongea Kamanda Muniain pale pale alipokuwa amekaa hakuwa na haja ya kuinuka kama ndugu yake ambaye kiumri wanafanana tu.

   “Ceni?!” Akauliza kwa sauti kubwa mheshimiwa Rais kisha akageuka kuwatizama wanaomuangalia yeye baada ya kuwa wanaangalia luninga.

   “Usistuke mheshimiwa… Huyo ni mheshimiwa waziri wa usalama Ceni… Mtu huyu si mtu wa kuheshimiwa katika serikali yako hastahili kuwa hivyo.. Naomba usogeze mbele tuone kuna kipi kinaendelea..!” Aliongea Muniain tena.

Mheshimiwa Rais akavua koti lake la suti akalitupia sofani kisha akashika mouse ya kompyuta na kuanza kusogeza mbele ambako sasa wakakuta video ingine hii ikiwa na sauti kabisa lakini pia haikuwa na quality (ubora).

Hapa ilisikika sauti kwa mbali ya mtu anayeongea kimaelekezo akiwaelekeza watu wanaomsikilia kuwa wajitahidi kuweka mambo sawa mambo ambayo hayakuelezwa ni mambo gani lakini wenzake wakawa wanauliza jambo ambalo halikusikika vizuri video ikaishia hapo ilikuwa fupi kama ile ya mwanzo ambayo haikuwa na sauti, lakininilipoisha hii ikafunguka ingine ikiwa sasa ni nzuri zaidi ya za mwanzo hii ikiwa ya marehemu mkurugenzi wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa  ‘Corrupt Law Enforcement Istitution’ (CLES).

Mheshimiwa hapa aliongeza sauti mpaka mwisho waweze kusikia kinachoongelewa na marehemu Mariapn aliyejirekodi enzi za uhai wake.

   “Kwanza kabisa napenda nitoe shukrani zangu za dhati kwako mheshimiwa Rais kwa kunipa nafasi ya kukutumikia katika serikali yako ukiniamini kwa kuniweka katika kitengo ambacho ni muhimu sana kwa mustakabali wa uongozi wako kwa wananchi wako.. Nimeamua kujirekodi video hii baada ya kuchoka na kushirikishwa katika mambo ambayo si kwa hiyari yangu ni kwa hiyari ya mtu mwingine kwa manufaa yake, nimekuwa mtumwa wa kulazimishwa kufanya mambo ambayo kwa kweli ni aibu kwa mtu mzima na makini kama mimi kulazimishwa kuyafanya kwa kutishiwa kuuwawa mimi mwenyewe au familia yangu nisipoyafanya au kuyaruhusu yafanyike.. Mara kadhaa nimekuwa nikitishiwa kuuliwa kama nitaingilia mambo ambayo nilikuwa naambiwa hayanihusu na pia naweza kuyafanya yakanihusu tena yakanipa faida kubwa kama nitaruhusu kwa matakwa yangu kushirika katika mambo hayo… Mheshimiwa Rais! Toka siku ya kwanza unaniteua kushika ukurugenzi wa taasisi ngumu sana ya kupambana na rushwa uliniteua ukiniamini kwa asilimia zote kwakuwa mimi na wewe ni watu tunaojuana kwa hali na mali tokea tukiwa wadogo tulipokutana sekondari tumekuwa tukishirikiana katika mambo mengi sana mpaka ulipofanikiwa kushinda urais wa nchi hii, nataka nikwambie ukweli hakuna wakati ambao nimekuwa na wakati mgumu kama wakati huu ambao nilikamata taasisi hii kiuongozi na hata wewe unalijua hilo umekuwa ukinitia moyo tukikamata watu wakubwa wakubwa wanaojishusha na rushwa kubwa kubwa  lakini kati ya hao wote mtu mmoja katika watu ambao unawaamini sana kama unavyoniamini mimi na watu wengine uliotoka nao mbali amekuwa akiiharibu nchi hii kwa kutumia kigezo chake cha kuwa ameshika wizara nyeti sana katika mambo ya usalama wa nchi… Mtu huyu ni waziri wa usalama wa nchi mheshimiwa Rafael Valdes Ceni mtu ambaye mimi na wewe tulikutana naye chuo kikuu na tukawa marafiki wakubwa sana tukiaminiana sana na hata kupeana mioyo katika mambo mbalimbali ya kuipambania nchi yetu.. Mheshimiwa Rais video za kwanza nilizozitangulia ni video ambazo mimi nilijaribu kwa wizi kuzichukua katika vikao mabavyo yeye Ceni na watu wake waliniomba kuhudhuria ambavyo vikao hivyo uwa vinafanyika kila mtu akizuiliwa kuwa na simu yake ya mkononi wala kifaa chochote cha mawasiliano kwa ukaguzi mkali pengine bila hivyo ningeweza kuwa na ushahidi mwingine mzuri zaidi ambao ningeuaminisha kwako na kumtia hatiani Ceni ambaye ni mtu mjanja sana na kazi kubwa kumkuta na ushahidi wowote katika maasi yake…  Mheshimiwa Ceni ameunda mtandao ambao ameuunda ukianzia ngazi ya mapolisi wa kikamishina wa mikoa hadi hadi watu walio katika usalama, mheshimiwa huyu anafanya hivi kwakuwa ni mtu anayejihusisha na mambo ya madawa ya kulevya bila sisi kujua tokea tukiwa chuo na ndiyo maana mwenzetu alikuwa akitugharamia kwa kila kitu kwa kigezo cha urafiki wetu sisi tukawa tunaamini alichokuwa akituaminisha kuwa wazazi wake wana uwezo kipesa kwakuwa ni wafanyabiashara wakubwa hapa Guatemala… Kama utakumbuka wakati unachukua fomu ya kugombea urais Ceni alijitokeza kwetu akisema anatudhamini katika safari yetu nasi tukamkubali kwakuwa ni rafiki yetu mkubwa kumbe mwenzetu ana lililo nyuma yake tukakubali kila msaada wake mpaka unaingia ikulu ndipo naye akapata ubunge wake ukamchagua kuwa waziri wa usalama kumbe alichagua umpe wizara hii hili afanye yake.. Mheshimiwa Rais bwana huyu amekuwa akiwaweka watu walio kwenye malipo yake akipewa nguvu na genge kubwa la ulanguzi wa mihadarati la nchini Mexico linaloitwa ‘THE RED JAGUAR’ (TRJ) amekuwa akishirikiana nao kwa yeye kushika biashara yote ya kuwaumiza kwa madawa wananchi wetu pia kuifanya njia nchi yetu kwa kupitisha unga utokao Bolivia, Honduras na Peru… Nataka kukujulisha kuwa utakapomaliza kuipitia hii taarifa yangu kwako usafishe mara moja jeshi lote la polisi kuanzia IGP wake mpaka makamishina wote hawafai pia vyombo vyako vya usalama wa taifa hasa taasisi kuu ya Guatemala Intelligence Security (GIS) na wengine hadi ulio nao karibu wanatumika na mheshimiwa huyu kuharibu usalama wan chi mpaka yanakuwa yanatokea mauaji ya kiholela mara kwa mara ni kwa sababu watu wa usalama hawawajibiki ipasavyo kwakuwa wapo kwenye malipo ya kirushwa ukacha mishahara yao… Jambo hili ni jambo hatarishi sana linalofanywa na rafiki yetu akijilimbikizia utajiri mkubwa wa haramu unaowaumiza wananchi wa ukanda wetu wa latin America.. Nilipenda nikuandalie orodha ya watu ambao nina uhakika wa asilimia nyingi kuwa hawafai lakini nib ado niko katika uhakiki juu yao lakini mmojawapo anayefanya kazi kwa ukaribu na Ceni ni huyo IGP, mkurugenzi wa usalama wa taifa na mkurugenzi wa uhamiaji Brigedia Granell.. Naomba niishie hapa kwa sababu nimeandaa hii flashdisk nikiwa katika hali ya wasiwasi juu usalama wangu hivyo kwa pokea haya machache na endapo nitaendelea kuvuta hewa hii baada ya kutoa siri hii nitazidi kukujulisha mengi zaidi kwa manufaa ya uongozi wetu na si kama nina chuki na Ceni ni upendo wa taifa letu na kwako mheshimiwa Rais..” Sauti na video ya kujirekodi ya marehemu mkurugenzi wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini Guatemala iliishia hapa, flashdisk ikakata na kuonyesha hapa ndipo mwisho.

Mheshimiwa Rais alirudi kwenye sofa akajibwaga matako yake mpaka miguu yote miwili ikaruka juu na kurudi sakafuni kwa kasi (alichoka sana).

Mwisho wa sehemu ya sitini na nane (68)

Siri ya muda mrefu iliyokuwa ikifichwa kwa gharama kubwa imefichuka na kumfikia mkubwa wa nchi, mtu aliyemuamini kupita kiasi mtu mwenye nguvu kubwa katika nchi yake pengine kutoka yeye alifuata huyu mtu yaani ilikuwa hata makamu wake wa Rais na waziri mkuu wake hawamfikii nguvu za mtu huyu ambaye pia ni rafii yake mkubwa sana aliyemsaidia yeye katika kuhakikisha ndoto zake za kuwa Rais wa Guatemala zinatimia.

Atafanya nini baada ya taarifa hii? Je atawaondoa maafisa wote wa polisi na kulisafisha jeshi zima la polisi? Je yeye pia hamuogopi rafiki yake na nguvu kubwa aliyonayo licha ya kuwa yeye ni Rais wa nchi? 




Mheshimiwa Ceni ameunda mtandao ambao ameuunda ukianzia ngazi ya mapolisi wa kikamishina wa mikoa hadi hadi watu walio katika usalama, mheshimiwa huyu anafanya hivi kwakuwa ni mtu anayejihusisha na mambo ya madawa ya kulevya bila sisi kujua tokea tukiwa chuo na ndiyo maana mwenzetu alikuwa akitugharamia kwa kila kitu kwa kigezo cha urafiki wetu sisi tukawa tunaamini alichokuwa akituaminisha kuwa wazazi wake wana uwezo kipesa kwakuwa ni wafanyabiashara wakubwa hapa Guatemala… Kama utakumbuka wakati unachukua fomu ya kugombea urais Ceni alijitokeza kwetu akisema anatudhamini katika safari yetu nasi tukamkubali kwakuwa ni rafiki yetu mkubwa kumbe mwenzetu ana lililo nyuma yake tukakubali kila msaada wake mpaka unaingia ikulu ndipo naye akapata ubunge wake ukamchagua kuwa waziri wa usalama kumbe alichagua umpe wizara hii hili afanye yake.. Mheshimiwa Rais bwana huyu amekuwa akiwaweka watu walio kwenye malipo yake akipewa nguvu na genge kubwa la ulanguzi wa mihadarati la nchini Mexico linaloitwa ‘THE RED JAGUAR’ (TRJ) amekuwa akishirikiana nao kwa yeye kushika biashara yote ya kuwaumiza kwa madawa wananchi wetu pia kuifanya njia nchi yetu kwa kupitisha unga utokao Bolivia, Honduras na Peru… Nataka kukujulisha kuwa utakapomaliza kuipitia hii taarifa yangu kwako usafishe mara moja jeshi lote la polisi kuanzia IGP wake mpaka makamishina wote hawafai pia vyombo vyako vya usalama wa taifa hasa taasisi kuu ya Guatemala Intelligence Security (GIS) na wengine hadi ulio nao karibu wanatumika na mheshimiwa huyu kuharibu usalama wan chi mpaka yanakuwa yanatokea mauaji ya kiholela mara kwa mara ni kwa sababu watu wa usalama hawawajibiki ipasavyo kwakuwa wapo kwenye malipo ya kirushwa ukacha mishahara yao… Jambo hili ni jambo hatarishi sana linalofanywa na rafiki yetu akijilimbikizia utajiri mkubwa wa haramu unaowaumiza wananchi wa ukanda wetu wa latin America.. Nilipenda nikuandalie orodha ya watu ambao nina uhakika wa asilimia nyingi kuwa hawafai lakini nib ado niko katika uhakiki juu yao lakini mmojawapo anayefanya kazi kwa ukaribu na Ceni ni huyo IGP, mkurugenzi wa usalama wa taifa na mkurugenzi wa uhamiaji Brigedia Granell.. Naomba niishie hapa kwa sababu nimeandaa hii flashdisk nikiwa katika hali ya wasiwasi juu usalama wangu hivyo kwa pokea haya machache na endapo nitaendelea kuvuta hewa hii baada ya kutoa siri hii nitazidi kukujulisha mengi zaidi kwa manufaa ya uongozi wetu na si kama nina chuki na Ceni ni upendo wa taifa letu na kwako mheshimiwa Rais..” Sauti na video ya kujirekodi ya marehemu mkurugenzi wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini Guatemala iliishia hapa, flashdisk ikakata na kuonyesha hapa ndipo mwisho.

Mheshimiwa Rais alirudi kwenye sofa akajibwaga matako yake mpaka miguu yote miwili ikaruka juu na kurudi sakafuni kwa kasi (alichoka sana).

ENDELEA NA NONDO..!!

PALACIO VERDE, GUATEMALA CENTRE-GUATEMALA

Tai ilifunguliwa kwa kasi kutoka shingoni kisha mheshimiwa naye akajimiminia kinywaji aina ya Victoria beer ambacho ni kinywaji aina ya pombe ambacho anakipenda sana wakati akiwa na mawazo au jambo linalomtatiza anapenda kutumia kinywaji hiki, alimimina kwenye glasi mpaka juu kisha akanywa funda mbili za kufuatana aliposhusha glasi chini akaufuta mdomo wake kwa kitambaa (leso).

   “Mmmh! Hii sasa vita ndani ya nchi ndugu zangu…!!” Akaongea akiwaangalia kina Muniain kwa macho ambayo yalibadilika na kuwa mekundu akasonya msonyo mrefu.

   “Ukiona sisi tunaomba kuonana na wewe tukiwa katika sura za bandia ujue tulishindwa tutaonana na wewe kivipi mheshimiwa… Lakini upele huko kwako mkuu sasa inabidi uukune sisi tuko tayari kwa lolote lile na nataka nikujulishe maamuzi yako ndiyo mustakabali wa nchi..!”Akaongea Kamanda Muniain wakiangaliana na kaka yake binamu.

   “Muniain kaka yangu!” Akaongea mheshimiwa Rais akimtizama ndugu yake akaweka pozi na kuendelea “Umekuwa ukinijua mimi kama mimi ninavyokujua wewe, tumekua pamoja tukicheza pamoja katika makuzi yetu katika shida na raha tukipeana moyo wa ujasiri katika michezo yetu hadi elimu zetu, imekuwa bahati mbaya mimi na wewe tumepita shule tofauti kutokana na utundu wetu uliowafanya wazazi wetu kuhofu tukisoma shule moja kwa kuambatana basi hatutaweza kusoma vizuri… Matakwa yao yamekuwa vile walivyohitaji kwani mwenyezi Mungu aliweza kututenganisha kila tulivyokuwa tunafaulu bado hatukuwa tunapangwa kukutana shule moja tulipangwa shule tofauti kana kwamba wapangaji walikuwa wakikaa meza moja na wazazi wetu na kuamua mimi niende shule hii na wewe shule hii mpaka chuo sote tulianza mwaka unaofanana lakini hatukuweza kupangwa chuo kimoja hili ajabu tuliwai kulijadili siku moja nakumbuka tukiwa mwaka wa tatu katika elimu zetu za chuo ni jambo zuri sana upande mwingine kwani ilileta changamoto kwetu huku tukikosa kuwekeana wivu kwakuwa hakuna aliyekuwa anakaa juu ya mwenzie katika namba za nafasi darasani pengine wivu nafasi za darasani katika masomo na katika mitihani  ungeweza kutufanya leo hii kuwa tukasema kuwa kuna mwaka tulipishana maneno tukagombana lakini hakuna kitu kama icho tumeishi vizuri sana kwa kweli… Nimesema haya nataka Norman asikie.. Rafael Ceni anayewinda akuue wewe Muniain na wewe Norman kwa stahili anayoamini itasaidia kuziba midomo yenu ni mtu ambaye nilifikia kumuamini kwangu kuwe kama navyomuamini ndugu yangu Muniain, hakuna jambo ambalo linahusu usalama wa nchi ambalo siwezi kukaa na watu wa usalama bila kumuita yeye na kumwambia kwanza hii ni imani ya ajabu niliyokuwa naifanya bila kujua kuwa naamini pasipo na imani naamini kwenye chungu cha kichawi… Wakati mimi najenga nchi na serikali ambayo wananchi wake wana imani nayo napiga deki malumalu yeye anamwaga tope ninapogeuza kisogo tu… Kwa jinsi nilivyosikiliza taarifa hii ya Mariapan ni kwamba nchi hii ni kama ina serikali mbili bila kujua maana kiukweli serikali ni dola na dola inahusisha vyombo vyote vya usalama sasa kama mimi ninaita wakuu wangu wote wa usalama hapa ikulu nafanya nao maongezi halafu kuna mtu mwingine naye ana nguvu kama niliyonayo anawaita na kuwapangia kazi ikiwa ni kwa utashi wake kazi yake ni hatari sana” Aliongea kwa kirefu Mheshimiwa Rais aliposimama akanyanyua glasi na kupiga funda mbili kubwa za bia na kufanya glasi ibaki na povu tu.

  “Ni kweli yote uliyoyasema ndiyo hali halisi ya sasa hapa Guatemala.. Hali ya usalama kwetu sisi watu tunaojihusisha na usalama imekuwa ngumu sana jana tu usiku nimetoka kuokolewa kwa nguvu nikiwa tayari nimeingia katika midomo ya vijana wa GIS wanaofanya kazi kwa amri yake na mkurugenzi wao ambaye ni miongoni mwa vibaraka watiifu wa mheshimiwa Ceni .. Leo ijumaa sijafika ofisini kwangu nawindwa na watu wa genge la TRJ na pia na watu wa usalama wa taifa na maafisa wa polisi kwa amri ya mheshimiwa waziri Ceni” Akaongea Muniain akiwa kakaziana macho na nfugu yake aliyekuwa kafura kwa hasira kwa taarifa hii mpya anayopewa.

   “Hivi unazungumza kweli kaka?” Akahoji kwa sauti ya ukali.

   “Kwa bahati mbaya au nzuri ni kweli mheshimiwa Rais… Lakini tuna habari ya kutia matumaini ni hivi kwa sasa ni kama tumepata bahati ya sisi kuongezewa nguvu na watu ambao si kama tuliomba msaada kwao, watu hawa walikuwa na operesheni yao inayohusu kupotea katika mazingira ya kutatanisha maafisa wenzao ambao kwa mujibu wao wanasema watu wao walipotea katika hali ya kuonyesha wametekwa na watu wasiojulikana ndani ya nchi yao ya Marekani miaka saba iliyopita na..!” Norman aliweka msisitizo kisha akaeleza juu ya mashirikisho yao lakini ghafla alikatizia sababu mheshimiwa alionyesha ishara anataka kuuliza jambo.

   “Habari ya kutia matumaini? Wamarekani wanawapa msaada gani?” Akahoji  mheshimiwa Rais.

   “Kaka! Ni hivi siku mbili hizi kama utakuwa umewai sikia au kupewa taarifa toka kwa maafisa wako wa usalama kuwa yalitokea mauaji katika mgahawa mmoja wa kitalii huko Jocotenango pale yalipotokea mauaji ilikuwa tumevamiwa sisi yaani mimi hapa na Norman tulikuwa katika maongezi na maafisa wa kijasusi toka Marekani wanatokea shirika la kijasusi la Drug Enforcement Administration ‘DEA’, tukavamiwa na watu wa genge la mihadarati la ‘TRJ’ wakiwa na dhumuni kuu la kutuua au kututeka kwa ajili ya hii flashdisk lakini bahati nzuri wakati tunavamiwa jasusi mmoja wa DEA alikuwa ndiyo anakuja kwenye kikao chetu kujiunga nasi kwa maongezi yeye ndiyo akatuokoa… Maafisa hawa wa DEA imekuwa kama bahati kwetu walitutafuta kutuomba msaada sisi ikiwa pia ni bahati kwao kwa maana laiti kama wangeomba msaada kwa watu wengine wangeweza kujikuta wamejiingiza katika matatizo na leo kwa ilivyo wangekuwa mateka au wameuliwa.. “ Alieleza Muniain baada ya kuona mheshimiwa Rais anahitaji ufafanuzi zaidi juu ya watu anaoambiwa wametoka Marekani kuja kuongeza nguvu kwao, Muniain na Norman hawakuishia hapo wakamueleza kila kitu juu ya kina Agent Kai na uamuzi wao wa pamoja kuunganisha nguvu kuutokomeza utawala wa kishenzi wa mheshimiwa Ceni na watu wake wote kwa ujumla ikiwemo genge la TRJ katika Guatemala ikibidi mpaka ulipo mzizi wao huko Mexico.

   “Aiseeh.. Hapa sasa mmenipa matumaini na uwoga nimeuondoa juu ya uwezekano wa kufanya ninalotaraji kulifanya… Kuwemo kwa Amerika hapa ni nguvu kubwa sana kwetu na natumaini huyu mpumbavu Ceni hajaweza kuharibu maafisa wetu wa jeshi hivyo hana vibaraka wake huko hivyo kazi ya kusambaratisha nguvu yao itafanywa na jeshi lakini kwa sasa nipeni muda wa kutafakari tunajipanga vipi kisha jumapili asubuhi nitahitaji kikao nanyi mkiwa na majasusi wa Marekani, nachotaka muendelee na uchunguzi wenu mlipofikia hili tuweze kukusanya ushahidi kamili juu ya wahusika wote wa uchafu huu hili tusiache jiwe juu ya jiwe likaja kutudhuru au kufanya kisasi juu ya tutakayoyafanya, nataka operesheni yetu iwe ‘short and clear’ na lolote lile litakalokuwa lina waletea mazibe zibe msikose kunipa taarifa haraka  hili niwape msaada waambie majasusi wa Amerika ruhusa kufanya lolote kuanzia sasa wasiogope wafanye kazi mkono wa baraka kutoka kwangu huko nao” Aliongea hili kisha akatizama saa mheshimiwa Rais.

Maongezi yao yaliishia hapa wakaagana ukafanywa mpango wa kisiri kuwaondoa eneo la ikulu wakirudisha sura zao za bandia walizavaa awali wakati wanaelekea uwanja wa ndege, wakatoka eneo la ikulu wakitumia usafiri wa gari kubwa la mafuta (tanki)ambalo lilifika hapa ikulu kuleta mafuta usiku huu kwa ajili ya magari ya ikulu.

   *****  *****  *****

 PANAJACHEL, SAN MARCOS-GUATEMALA

Main Street eneo lililo katikati ya mji wa San Marcos mji wa mkoa wa jina hili hili la San Marcos mkoa ulioko pembezoni mwa nchi ya Guatemala mpakani mwa nchi hii na nchi ya Mexico katika boda ya Tacana inayogawanya nchi hizi huko karibu na milima ya Tajumulco eneo maarufu la kilimo cha kahawa zao maarufu na kubwa la kiuchumi nchini Guatemala, eneo kubwa lililohodhiwa na mfanyabiashara mkubwa mwenye uraia wa Mexico akifanya uwekezaji mkubwa eneo hili la Tajumulco.

Muda wa saa sita usiku, muda unaogawanya siku inayoisha kwenda siku mpya wakiipisha ijumaa iliyokuwa ndefu sana kwao kwenda jumamosi ndani ya mtaa wa Main Street nyumba moja ya kifahari ambayo wakazi wengi wa eneo hili walikuwa wakiijua kuwa inamilikiwa na gavana wa mkoa wao lakini akimpangisha mwanadada mrembo sana aliyechanganya umexico na uguatemala mwanadada anayesimamia kampuni inayojihusisha na mambo ya urembo Miss Angelica Linares, wengi pia walikuwa wakimjua kama mchumba wa tajiri na mwekezaji Alexis Carlos Codrado.

Baada ya uvamizi wa nyumbani kwake huko Galarias Del Sur mtaa wa Calzada Aguillar Batres bara bara ya Zone 11, Mr. Alexis aliona si vizuri akiendelea kuwepo jijini Guatemala kwa sababu alizoona operesheni ya uvamizi wa nyumbani sit u iliongozwa na mtu aliyekuja kumjua baadaye kuwa anaitwa Agent Ka Hamisi wa CIA ni operesheni ambayo wanajeshi wa ulinzi walioko ubalozi wa Marekani wamehusika pia, haraka alimuomba kaka yake yeye kwakuwa hajazoea mikiki mikiki aje ajifiche mkoa wake wa kujidai wa San Marcos kwakuwa pia ni mpakani likitokea lolote lililo tofauti basi atakimbilia mpakani Tacana kisha kuingia nchini kwao Mexico.

Feca aliona ni sahihi kwa mdogo wake wa pekee anachoomba akafanya mpango wa mdogo alindwe vizuri mpaka afike San Marcos na hata akiwa hapa napo ulinzi mzuri uimarishwe.

   “Halloo mheshimiwa waziri!” Alipokea simu iliyoita kwa mlio mmoja tu kwakuwa muda wote haikuwa mbali na mkono wake hivyo ilivyoanza kuita akasoma jina la mpigaji kwa kasi kisha akasugua kioo kupokea ikaamia sikioni akaongea kwa kasi.

   “Ndiyo nafika kwangu… Muda wote toka uliponiambia huko njini kuelekea San Marcos nilikuwa ikulu… Kichwa kinaniuma sana nashindwa kuelewa inakuwaje?” Akaongea mpigaji ambaye ni mheshimiwa waziri wa usalama Mr. Ceni.

   “Unajua mheshimiwa! Lazima kichwa kikuume, tambua ya kuwa mimi na wewe tuko katika TRJ lakini tuko kiusimamizi wa mipango hatuingii katika vitendo vingi zaidi ya kuelekeza sasa inapotokea mambo yanakuwa ovyo bila kutarajia tena tukistukizwa lazima tukumbwe na ombwe la uwoga mkubwa kama hivi.. Haya mambo ya kujificha na kukimbia kimbia si mambo yangu wala yako mheshimiwa” Akajibu alilosikia toka mwenzake akiweka ufafanuzi.

   “Ni kweli uyasemayo ndugu yangu.. Nimekaa mwenyewe eneo la tukio nikiwa makini zaidi ya mamba mtoni lakini taarifa niliyopewa sikuweza ithibitisha kutoka kwa watu zaidi ya thelathini niliowaweka eneo lote la viwanja vya ikulu pamoja na wengine kuwa macho na masikio yangu kwenye viunga vya ndani hakuna sura ya watu tulio na mashaka nao niliyoiona hii imenishangaza sana yaani mheshimiwa kunizidi akili katika hili siamini na ndiyo maana nasema hivi pengine kijana aliyetupa taarifa hakuwa na hakika katika alilotupatia kuhusu kamanda na kijana wake… Umakini ulikuwepo hadi katika kumfuatilia mheshimiwa asifanye maongezi na mtu yoyote tusiyemtambua kwa kuhofu pengine wasakwa wetu wanaweza wakatumia sura bandia kufika pale ikulu na kikukweli mpaka anatuaga anaenda kupumzika hakuna aliyeongea naye tukiwa sisi hatumjui, nasubiri taarifa toka kwa mmoja wa walinzi wake ambaye yeye ushika nafasi ya usiku tu kila siku nimemuagiza ahakikishe anaona anayeingia na kutoka ikulu muda wote huku watu wetu wengine wakikaba njia zote za kuelekea ikulu tuone kama kuna kitakachoingia na kutoka wanaweza kuwemo virusi wetu” Aliongea kirefu kidogo mheshimiwa waziri Ceni.

   “Marekani wamesihikilia hii operesheni lakini sijaambiwa kama walikuwa na jambo gani juu ya hili suala katika taarifa fupi niliyotumiwa na Sajenti Lara kiongozi wa TRJ kanda ya mpaka wa Marekani lakini yeye alivyofuatilia kidogo amevujishiwa taarifa hiyo” Alexis akaongea kumwambia Ceni kile ambacho ametoka kutumiwa kwa njia ya mtandao muda si mrefu ikiwa ni taarifa kati ya taarifa mbalimbali anazotumiwa juu ya kilichotokea kwake na yanayotokea kwa sasa Guatemala ikiwa ni siku tatu wanaona mambo tofauti tena yakiharibu usalama wao.

   “Nafikiri mheshimiwa Rais ameomba msaada huko lakini kwanini sikuhusishwa? Hili ni swali pasua kichwa kwa jinsi ilivyo kati yangu na Rais.. Swali lingine kihashiria gani kimesababisha yeye aombe msaada huko?” Akahoji Ceni ikiwa tayari anahisi ni maswali ambayo angetakiwa ajiulize yeye mwenyewe na kisha kuyafanyia kazi yeye mwenyewe kabla hakujakucha na kuifikia asubuhi ya siku ya jumamosi.

   “Maswali hayo nimeulizwa na kaka nimeshindwa kumjibu.. Nilimwambia majibu tutayapata kwako lakini na wewe ni maswali yako makuu.. Nafikiri watu tulioletewa kutusaidia tuwatumie vizuri lakini jambo la kuhisi Rais anahusika moja kwa moja sina imani nalo moja kwa moja nafikiri kukikucha tutapata majibu mengi zaidi… Sababu Mariana na wenzake wameniambia hawatalala leo mpaka wajue ni mpango wa nani juu ya wanausalama wa DEA wakiwemo na huyo wa CIA kuja hapa Guatemala?”

   “Ndiyo hata mimi nimewaomba watu wangu wasilale leo washirikiane na kina Mariana kujua ipi na ipi kabla hakujakucha hili kama ni mpango wa Rais tujue tunafanyaje kwa usalama wetu maana taasisi ya Rais ikisimamia jambo itakuwa hasara kwetu kama hatutapenyeza hujuma”

   “Basi sawa mheshimiwa… Mimi niko nafuatilia kwa umakini huku nikifanya mawasiliano na watu mbalimbali kama kaka naye alivyosema yuko makini kufuatilia imekuwaje kwa marafiki zake walioko ndani ya vyombo vya usalama vya Marekani… Hatuwezi tena kulala mpaka tuzime huu mfukuto”

   “Haya nikutakie kazi njema… Nachohitaji tushirikiane kwa umakini katika jambo hili nami pamoja na watu wote walio chini yangu tuko makini kujua kila ambalo tuna mashaka nalo kwanini linatusumbua na tunawaona maadui wakisogeza tu pua zao kunusa harufu zetu” Alimalizia mheshimiwa Ceni kisha akakata simu.

Hapo Alexis alirudi kwenye kiti alichokuwa kakiacha baada ya kupokea simu aliposimama na kusogea pembeni, alipofika kitini akapata wazo apige simu kwingine akanyanyua simu yake na kupiga sehemu ingine.

   “Umeingia ofisini?” Aliuliza swali baada ya kupokelewa na upande wa pili.

   “Ndiyo ndiyo! Niko ofisini nashukuru walinzi wa hapa hawakuwa makini niliwakuta wamelala nimewaua wote watatu na nikafanikiwa kuja hadi ofisini kwako bila tabu nishaanza kufuatilia kazi yako ndugu yangu”

   “Vizuri! Angalia katika droo zangu zote uondoe mafahili yote niliyokuelekeza hayatakiwi kukutwa humo acha ambayo wewe mwenyewe unajua hata ukiyaacha hayatafuatiliwa sana… Kisha ya hapo nenda katika kasiki langu ninalohifadhi nyaraka zangu za hati za nyumba nywila zangu za siri andika neno ‘Angelxis’ ondoa hizo nyaraka zote”

   “Usihofu.. Sijawai potea maelekezo..”

   “Kazi njema!!” Akamalizia mpigaji simu Mr. Alexis Carlos na kukata simu hii ilimaanisha kuna mtu wa kazi amemtuma aende zilipo ofisi zake kati ya ofisi zake ambayo moja ipo hapa San Marcos aliopo kwa sasa na ingine ikiwa huko jijini Guatemala na ndiyo ofisi ambayo katibu wa balozi aliomba iwekewe ulinzi na jeshi la polisi lakini jeshi la polisi ikaweka walinzi walio wazembe kazini na kufanya wavamiwe na mtu mmoja tu akawaua na kuingia ndani na kufanya alichoagizwa na Mr. Alexis.

Mwisho wa sehemu ya sitini na tisa (69)

Taarifa kamili juu ya ushenzi wa kiuasi kwake yeye na serikali yake ilikuwa imemfikia mheshimiwa Rais wa GTL akasikiliza kwa makini maelezo yote toka kwa watu anaowaamini sana na mwisho aliamua kuwa atalifanyia kazi siku mbili tu suala aliloambiwa likiwa na taarifa inayohitaji vitendo sasa, siku ya jumatatu ya wiki inayokuja mheshimiwa Rais alipanga ndiyo siku atakayo fanya maamuzi ya kuushangaza umma na hata kumshangaza rafiki yake mkubwa na mtu aliyemsaliti mheshimiwa Ceni.

Alexis Carlos Codrado mdogo wake Fernandes Carlos Codrado mambo yamemchachia ameona hawezi kusubiri bakora amekimbilia ilipo ngome yao mkoa wa San Marcos.

Nini kitafuata baada ya haya?



Hapo Alexis alirudi kwenye kiti alichokuwa kakiacha baada ya kupokea simu aliposimama na kusogea pembeni, alipofika kitini akapata wazo apige simu kwingine akanyanyua simu yake na kupiga sehemu ingine.

   “Umeingia ofisini?” Aliuliza swali baada ya kupokelewa na upande wa pili.

   “Ndiyo ndiyo! Niko ofisini nashukuru walinzi wa hapa hawakuwa makini niliwakuta wamelala nimewaua wote watatu na nikafanikiwa kuja hadi ofisini kwako bila tabu nishaanza kufuatilia kazi yako ndugu yangu”

   “Vizuri! Angalia katika droo zangu zote uondoe mafahili yote niliyokuelekeza hayatakiwi kukutwa humo acha ambayo wewe mwenyewe unajua hata ukiyaacha hayatafuatiliwa sana… Kisha ya hapo nenda katika kasiki langu ninalohifadhi nyaraka zangu za hati za nyumba nywila zangu za siri andika neno ‘Angelxis’ ondoa hizo nyaraka zote”

   “Usihofu.. Sijawai potea maelekezo..”

   “Kazi njema!!” Akamalizia mpigaji simu Mr. Alexis Carlos na kukata simu hii ilimaanisha kuna mtu wa kazi amemtuma aende zilipo ofisi zake kati ya ofisi zake ambayo moja ipo hapa San Marcos aliopo kwa sasa na ingine ikiwa huko jijini Guatemala na ndiyo ofisi ambayo katibu wa balozi aliomba iwekewe ulinzi na jeshi la polisi lakini jeshi la polisi ikaweka walinzi walio wazembe kazini na kufanya wavamiwe na mtu mmoja tu akawaua na kuingia ndani na kufanya alichoagizwa na Mr. Alexis.

ENDELEA NA NONDO DODO..!

HOFU NDANI YA TRJ I

JUMAMOSI ASUBUHI

CHIMALTENANGO, GUATEMALA CITY –GUATEMALA

Ni kweli alikuwa akiota kitu kama mbao kinagongwa lakini kila alivyokuwa akiiweka ndoto sawa hili imuelekeze maana kama ilivyo ada yake anapoota ndani ya ndoto humo humo hata kama hisia uwa haziendi mtu atakavyo lakini yeye uruhusu ndoto iende vile inavyotaka lakini uwa anapenda kuifanya ndoto kuendelea kumletea maana kwakuwa yeye Agent Kai ni miongoni mwa watu wale wanaoota ndoto ambazo kama akiikumbuka vizuri umletea yale yanayokuja tena ndani ya siku moja au mbili mbele hivyo anahususdu na kuziamini ndoto kwakuwa hazimdanganyi ilimradi tu aikumbuke amkapo.

Ugongaji wa ubao uliendelea mpaka sasa akaamini hii si ndoto ni mtu anagonga ubao kweli fahamu za kurudiwa na fahamu toka ndani ya lepe la usingizi mzito ilirudi taratibu masikio yaliyokuwa yakipokea yakafunguka zaidi ubongo ukakubaliana na hali halisi ukapeleka taarifa kwenye macho akayafungua taratibu na akagundua haikuwa ndoto ni mtu anagonga mlango taratibu yaani ugongaji wa kutaka aliye katika chumba hiki ndiye asikie lakini si aliye jirani na chumba hiki, Agent Kai akajipindua kutoka kulala kifudifudi akaja chali kisha akainua kiwiliwili chake akawa amekalia matako.

Mgongaji alitulia kidogo kisha akagonga tena vile vile kama alivyokuwa akigonga mwanzo hapo Agent Kai hakuwa na jinsi akafikicha macho yake shuka likasogezwa pembeni akasimama toka katika kigodoro chembamba ambacho ni siku ya pili sasa anakitumia kukilalia anapohitaji kulala akiwa anakiweka sakafuni juu ya zulia katika chumba ambacho ni ofisi yao ya muda kwa shughuli zao mbalimbali za mawasiliano ya timu yake.

Alikuwa amevaa bukta kifuani akiwa hana nguo yoyote lakini hakutaka kuendelea kusubiri kwa hofu pengine mgongaji amegonga kwa muda mrefu, macho aliyatupa kwenye saa ya simu yake ya mkononi ikamuonyesha ni saa kumi na mbili na nusu asubuhi ikiwa ni masaa manne toka aagane na wenzake saa nane na nusu usiku baada ya kikao kirefu hasa wakisikiliza mrejesho wa kitaarifa za ikulu na kikao cha Rais na wenzao kina Kamanda Muniain.

Alisogea kwa mnyato mpaka kwenye kitobo chenye lenzi inayochukua mtu anayegonga mlango upande wa pili (kwenye korido) akachungulia, mtu aliyemuona ilibidi astuke na si kama hamjui la hashaa anamjua ni nani ila hakutegemea asubuhi ya mapema aje kumgongea mlango, alijiuliza kwanini apewe uhuru huu mtu huyu, alimtizama vizuri kupitia tunduni kama ni salama yeye kumfungulia akaona ni salama akajitizama kama kuna umuhimu arudi kuvaa nguo juu hapo aliona umuhimu wake akarudi kwenye meza ambako katika kiti alikuwa ameacha fulana akaichukua na kuivaa.

Kasi akarudi mlangoni akazungusha funguo na kuufungua kwa kasi mlango mpaka mgonga mlango alistuka, alikuwa ni mwanadada Angelica Linares mrembo wa haja amabaye usiku wakati wanafanya kikao wao yeye alikuwa kashaenda kulala kwenye chumba ambacho analala Special Agent Rebecca Smith, Agent Kai alihoji juu ya wenzake kumuamini binti huyu mpaka kumuacha huru sana na jibu alilopewa kuwa msichana huyu hana uwezo wa kufanya baya ametoa siri karibu zote na amekiri kuwa alikuwa amefanya kosa kubwa kuwa kimapenzi na Alexis hakujua uchafu wake alikuwa akijua mchumba wake ni mtu safi mfanyabiashara mkubwa sana anayetokea Mexico.

   “Habari za asubuhi?” Akahoji Agent Kai ‘TSC’ huku akiendela kumsahili chini mpaka juu bibie mrembo.

   “Nzuri kaka… Samahani nimekusumbua usingizini.. Pole sana!” Akaongea binti akitetemeka kama baridi la asubuhi limemkolea.

   “Bila samahani… Nafikiri una jambo zito la kunieleza mpaka ukakosa subira ya kusubiri jua litoke vizuri zaidi… Rebecca bado amelala?” Akajibu na kuhoji ‘TSC’ hakuacha kumkazia macho.

   “Amewai kuamka yuko chumba cha gym.. Nilikuwa naye nimemuacha huko” Akajibu tena binti mrembo.

   “Eeeeh!” Alijikuta anasema hivi ‘TSC’ ‘Ina maana Rebecca anamuamini sana huyu mwanamke?’ Akawaza kwa swali kisha akausogeza mlango zaidi hili binti apite akimsaidia kumuonyesha kwa ishara apite ndani, kabla binti hajapiga hatua mwisho wa korido zikasikika nyayo za mtu anakuja anatokea kwenye korido ingine alipotokea alikuwa Rebecca.

Angelica alishakuwa ameanza kuingia ndani ya chumba Agent Kai alisimama tu walipoangaliana na Rebecca akambonyeza aje walipo kisha akafuata nyuma ya mgeni wake kuingia katika chumba ambacho ni kama ofisi yao kama timu lakini pia yeye alitumia kulala.

Rebecca alifika na kwakuwa ‘TSC’ aliacha mlango wazi haikuwa tabu kwake kupita tu kisha yeye ndiye akaurudisha mlango.

   “Habari za asubuhi? Boss!” Akasalimu Rebecca salamu iliyoenda kwa mshirika wake wa kazi na boss wake Agent Kai.

   “Nzuri kabisa Rebecca! Naona mazoezi yamekolea kijasho chako nakitamani… Vipi mgeni wetu amefanya mazoezi?”

   “Mgeni ameruka kamba tu bado ana kauvivu fulani ila akiendelea kuwa nami kwa wiki tu mazoezi yatakolea.. Heti shosti unaonaje siku yako ilivyoanza?” Akajibu Rebecca kisha papo hapo akatupa swali kwa Angelica.

   “Ukweli ni hivyo unavyosema lakini kunyanyua vile vyuma sijui kama nitaweza..!” Akajibu Angelica na kwa pamoja wote waliopo hapa wakatabasamu.

   “Usijali miss! mazoezi  ni upendo wa mtu si lazima kufanya vile ambavyo mwingine anafanya kama ilivyo vitu vingine vya kimichezo unavyoweza kuona watu wa timu fulani wanafanya au sisi tunaolazimika kuuweka mwili sawa, wale wako kazini na sisi pia bila hivi ubongo unakuwa hauko tayari kwa mikikimikiki” Akaongea ‘TSC’.

  “Kazi yenu inahusika na mikikimikiki muda wote au kwa muda tu?”Akauliza swali Angelica macho yake yakikwepa kuangaliana na macho ya Agent Kai yanayomtizama muda wote.

   “Si kila muda… Muda mwingine inapita mwaka usipate kazi ya kufanya hivyo huwezi kupata na mikiki mikiki lakini mazoezi hata ikiwa hivyo hatuwezi kupumzika mazoezi ni kama chakula kwetu maisha yetu yote mpaka Mungu atakaposema mwanangu njoo upumzike..” Akajibu S.A Rebecca Smith.

   “Ndiyo ndiyo… Kuna jambo lililokufanya unigongee asubuhi hii ya mapema.. Naomba unieleze kwakuwa jana sikupata nafasi ya kuongea nawe nilibanwa na majukumu mengine” Kama kawaida yake mzee kubadili mada ‘TSC’ alibadili mada na sasa walikutanisha macho na mrembo huyu ambaye ni nadra sana kukubali macho yakutane na wanaume waliopo hapa alijitahidi sana kuwaepa na hii kwakuwa alikuwa anajijua alivyo na uzuri ulio na kishawishi kwa mwanaume yoyote yule awe ameoa au hata hajaoa ilimradi awe ni mwanaume aliyekamilika basi hataacha kumtamani yeye kimahusiano.

   “Jana wakati umetoka na dada hapa nilifanya maongezi mengi tu na yule uliyeniacha naye nafikiri alikwambia kile ambacho tuliongea kwa ufupi” Akaanza kueleza kile kilichomfanya atake maongezi na ‘TSC’.

   “Sikupata nafasi ya kuongea na Special Agent Silla.. Na hamu ya kujua mliongea nini?” Akajibu akijifanya hajagusiwa lolote na Silla lakini ukweli wakati wamerudi na kina mzee wao Kamanda Muniain walifanya maongezi kidogo na Silla na walimzungumzia Angelica.

   “Ukweli kaka ni kuwa mimi sina kosa lolote na mambo ambayo mnayafuatilia.. Nimekuwa na Mr. Alexis Codrado mwaka mmoja  na miezi nane mpaka wakati huu sikupata nafasi ya kujua mambo yake ya siri zaidi ya kumjua yeye ni mfanyabiashara tajiri aliyeamia Guatemala kutokea Mexico lakini ana makazi sehemu zote mbili na hata uraia ana uraia wa nchi mbili hizi.. Alianza kunifuatilia miaka miwili iliyopita baada ya kuwa tulikutana katika maonyesho ya mavazi hapa jijini” Alisimama kuongea walipoangaliana na ‘TSC’ akamuona anataka kuuliza kitu.

   “Wewe ni mke au ni mchumba wake au?” Akauliza ‘TSC’.

   “Mimi siwezi kujiweka kwenye uchumba sababu tayari Mr. Alexis ana mke wake huko Mexico City anasimamamia biashara zao ambazo ni supermarket za Dorocorate Supermarket na huyu nafikiri kama mnavyosema Mr. Alexis anajisusisha na biashara zisizofaa basi huyu mwanamke atakuwa anahusishwa moja kwa moja na mumewe” Akajibu Angelica au alivyopenda wamuite ‘Ange’.

   “Hivyo wewe ni kimada wake?” Akahoji tena bwana maswali.

  “Ndiyo hivyo!” Akajibu Ange uso na macho yake akikwepesha pembeni asiweze kuangaliwa hata na mwanamke mwenzie Rebecca.

   “Kawaida hiyo usihofu hatuko uarabuni hapa bibie, mabara yote ya Amerika watu wanachepuka sana na ndoa ni chache sana hivyo hakuna ajabu kwa wewe kuwa kimada na isikuume ila linalotakiwa kukuuma ni kutojua mengi ya Mr. Alexis…. Mimi na timu yangu tunaweza kuwa tunajua machache kuliko wewe unayejua juu ya mwili wake tu” Aliongea Agent Kai na kuongea maneno ya mwisho yenye karaha ndani yake ikiwa anahitaji kuibua jambo lililo ndani ya kifua cha mrembo huyu matata.

   “Siku zote vimada uwa wana sehemu mbili.. Sehemu ya kwanza uwa ile ya kimada mwenye bahati na mwanaume basi kimada huyo ujikuta anapata kila zuri toka kwa mwanaume lakini kuna aina ya pili ambayo uwa ni kimada ambaye mwanaume uogopa kusema ukweli wake wote kwa kuhofu pengine siri itakuwa si mahala sahihi lakini kimada huyu upewa pesa na kila hitaji lake, hivyo ndivyo mimi ninavyojua juu ya vimada..!” Aliongea Special Agent Rebecca huku akitabasamu.

   “Huko sahihi shosti wangu… Mimi naweza nijiweke katika kimada namba mbili kati ya hao vimada uliowafafanua, mimi ni kimada ambaye ninaogopewa na Mr. Alexis hivyo sikuwa naujua upande wa pili wa shilingi yake ingawa hisia za mabaya nilikuwa nao hasa jinsi anavyolindwa na anavyonibagua katika maongezi mara nyingi zaidi ya kawaida kwa kisingizio marafiki zake wengi ni watu wa karibu kibiashara na mkewe… Nachoweza kusema kwenu ni kitu ambacho nilikisema kwa Silla ni kuwa mimi nitaweza kuwasaidia kumpata huyu mtu kwa njia ambazo nyinyi mtaona ni sahihi yaani njia yoyote mtakayopanga kwakuwa nyinyi ni wataalamu wa mambo haya basi nitaifanya njia hiyo msiwe na hofu wala mashaka… Nimechoka kuishi kama digidigi..!”Akaeleza Ange akiwa anawaangalia kwa zamu waliomzunguka kushoto na kulia kwake.

   “Huko siriasi na hili?” Agent Kai akahoji akimkazia macho.

   “Ndiyo kaka yangu niko sahihi kabisa.. Usiku kuchwa limenifikilisha hilo na nikachukua maamuzi haya..!”

   “Basi tutafanya jambo ambalo litasababisha hili… Cha kwanza naomba mnipe muda nioge na kufanya mambo mengine kama muonavyo ni asubuhi sijafanya lolote kisha niandae mpango madhubuti utakaokushirikisha kumpata mtu tunayemuhitaji..”

   “Nitashukuru kwa hili ila nitahitaji sana ulinzi wenu na usalama wangu wa kimaisha kwa wakati wote wa maisha yangu”

   “Usijali juu ya hili kazi ikienda vyema hautaishi tena nchi hizi za ukanda huu labda ukatae ofa ya kuja kuishi Marekani” Alimalizia hivi Agent Kai kisha wakakubaliana yeye ajiswafi mwili kisha ya hapo wapate kifungua kinywa kwa pamoja na ndipo watapanga wakiwa wote kwa ujumla kama timu.

Ilimchukua Agent Kai ‘TSC’ muda wa nusu saa kufanya kati ya matatu manne yanayofanywa maliwatoni muda wa asubuhi ikiwemo kuoga kisha ya hapo akachagua mavazi aliyoona ni swadakta kuvaa kwa siku hii ya jumamosi ndipo akatoka kuelekea sebuleni ambapo aliwakuta watu wa timu nzima katika timu yake wanamsubiri yeye.

  “… Habari zenu timu?” Akatoa salamu ya ujumla huku akielekea kwenye sofa ambalo lilikuwa peke yake hili naye ajumuike kwa maongezi na hata kupata kifungua kinywa kwa kuwa mezani licha ya kuwa si sehemu maalumu ya kulia chakula kulikuwa na bilauri kama tatu za juisi na hata chupa birika ya kahawa na pia vitafunwa mayai ya kukaangwa na kuchemshwa, mikatena keki.

Salamu iliitikiwa na watu wote  kwa furaha ya kumuona yeye na wote kuwa wako fiti wa afya njema wakiwa tayari kiakili na vitendo kwa lolote lile ikiwemo hata mzee Muniain.

   “Naiona hali iliyokuwemo miongoni mwenu ni hali ya ushindi unaokuja soon… Nafurahi sana pale ninapoiona timu ina furaha kama hivi” Tabasamu likiwa limeweka maskani kwenye viunga vya sura yake aliongea tena ‘TSC’ huku akijimiminia juisi katika glasi toka kwenye bilauri hii ni mazoea kwake asubuhi yeye si mtu wa kupenda chai ni mtu wa kupenda kustua mizuka ya tumbo kwa juisi  kana kwamba si mtanzania wa kuzaliwa ingawa kwa sasa si raia wa Tanzania tena akiuacha uraia toka angali mdogo na kuwa raia wa Marekani akitamani katiba ya Tanzania siku moja ingebadilishwa na kuruhusu uraia wa nchi mbili kama baadhi ya katiba ya nchi nyingi kubwa na zilizoendelea zinazoruhusu mfumo wa uraia wa nchi mbili hapo yeye angechukua fursa ya kumiliki uraia wa nchi ya tz na Marekani kwa furaha sana.

   “Nami nilivyofika hapa nilikuta furaha kubwa sana miongoni mwa watu wote na nikasema kama ulivyosema nikajibiwa leo Silla ni siku yake ya kuzaliwa mimaji inamuhusu! Hahahaha hahahaha… “ Akaongea Rebecca na kicheko kikaunganishwa kwa kuvunjwa bei na kila mtu.

   “Khaah! Happy birthday Silla… Kheri ya siku yako ya mfanano wa kuzaliwa jasusi mbobezi na mwandamizi sijachelewa sana nami najiunga kwenye furaha kukupongeza teammate..!” Aliacha glasi iliyokuwa ikitamani kwenda zilipo papi za mdomo wake hili kupeleka burudani shibe tumboni mwake akatoa pongezi iliyoambatana na mkono wake wa kulia kumnyoshea Silla wakakamatana kwa furaha kisha wakainuana na kukumbatiana, furaha iliongezeka miongoni mwao wote wakafurahi sana zikapigwa soga za nusu saa huku wenye kunywa wakiendelea kunywa kinachomvutia mtu kwa asubuhi hii na vitafunwa vyake na hili la birthday ya Special Agent Silla iliweza kunijuza hata nami mwandishi kwanini keki kubwa ilikuwepo mezani ilikuwa si kitafunwa cha asubuhi bali ni pongezi.

   “Furaha imezidi na sasa tunaweza rudi kwenye ajenda kuu ya timu… Silla kijana wangu narudia tena hongera lakini hongera iambatane na bidii ya kazi maana kwa sasa timu yetu iliyo hapa ndiyo timu yenye kikosi muhimu sana kwa maisha ya watu wa ukanda wa Latin Amerika na mabara yote ya jirani” Alibadili mada mzee na mkurugenzi wa ‘Organized Crime Of Latin America’ (OCLA) baada ya kutizama saa yake na kuona muda umetamaladi na kajua kanazidi kushika hatamu ya kuimaliza asubuhi.

   “Naam! Furaha ishafika mahala pake.. Tungefanya mengi zaidi Silla lakini hatuko mahala pakula show ya burudani ya kutufanya tukajisahau nini kilicho mbele yetu tuko GTL kwa kazi ambayo kama mlivyomsikia mzee wetu mzee Muniain… Jana usiku tuliweza kuongea kirefu juu ya maongezi ya Rais na wenzetu wa OCLA na vile ambavyo tunahisi tunaweza tukafanya zaidi ya matarajio ya mheshimiwa juu ya hiki kikosi lakini leo asubuhi mwanadada na shemeji yetu Angelica alinifuata na yeye  ndiyo akaniamsha katika usingizi wa ndoto tamu nikiwa najikumbusha fungate yangu Afrika! Hahahahah! (Aliachia kicheko kidogo) Kwa sasa Ange ni mwenzetu kwa namna moja ama nyingine… Mnaweza kuuliza kwanini mwenzetu?” Nahodha wa timu kijana wa kiafrika raia wa Marekani alielekea alipoelekea Kamanda Muniain kimada ya maongezi.

Mwisho wa sehemu ya sabini (70)

Mpango mkakati umeingia maabara! Majasusi wabobezi wakiongozwa na ‘The Sole Cat’ wako sebuleni wakijadili ingawa mjadala uliingiliana na siku ya kuzaliwa ya Special Agent Silla ambako furaha ililindima ikiambatana na vicheko vya furaha.

Nini kitaendelea sehemu inayofuata?





   “Khaah! Happy birthday Silla… Kheri ya siku yako ya mfanano wa kuzaliwa jasusi mbobezi na mwandamizi sijachelewa sana nami najiunga kwenye furaha kukupongeza teammate..!” Aliacha glasi iliyokuwa ikitamani kwenda zilipo papi za mdomo wake hili kupeleka burudani shibe tumboni mwake akatoa pongezi iliyoambatana na mkono wake wa kulia kumnyoshea Silla wakakamatana kwa furaha kisha wakainuana na kukumbatiana, furaha iliongezeka miongoni mwao wote wakafurahi sana zikapigwa soga za nusu saa huku wenye kunywa wakiendelea kunywa kinachomvutia mtu kwa asubuhi hii na vitafunwa vyake na hili la birthday ya Special Agent Silla iliweza kunijuza hata nami mwandishi kwanini keki kubwa ilikuwepo mezani ilikuwa si kitafunwa cha asubuhi bali ni pongezi.

   “Furaha imezidi na sasa tunaweza rudi kwenye ajenda kuu ya timu… Silla kijana wangu narudia tena hongera lakini hongera iambatane na bidii ya kazi maana kwa sasa timu yetu iliyo hapa ndiyo timu yenye kikosi muhimu sana kwa maisha ya watu wa ukanda wa Latin Amerika na mabara yote ya jirani” Alibadili mada mzee na mkurugenzi wa ‘Organized Crime Of Latin America’ (OCLA) baada ya kutizama saa yake na kuona muda umetamaladi na kajua kanazidi kushika hatamu ya kuimaliza asubuhi.

   “Naam! Furaha ishafika mahala pake.. Tungefanya mengi zaidi Silla lakini hatuko mahala pakula show ya burudani ya kutufanya tukajisahau nini kilicho mbele yetu tuko GTL kwa kazi ambayo kama mlivyomsikia mzee wetu mzee Muniain… Jana usiku tuliweza kuongea kirefu juu ya maongezi ya Rais na wenzetu wa OCLA na vile ambavyo tunahisi tunaweza tukafanya zaidi ya matarajio ya mheshimiwa juu ya hiki kikosi lakini leo asubuhi mwanadada na shemeji yetu Angelica alinifuata na yeye  ndiyo akaniamsha katika usingizi wa ndoto tamu nikiwa najikumbusha fungate yangu Afrika! Hahahahah! (Aliachia kicheko kidogo) Kwa sasa Ange ni mwenzetu kwa namna moja ama nyingine… Mnaweza kuuliza kwanini mwenzetu?” Nahodha wa timu kijana wa kiafrika raia wa Marekani alielekea alipoelekea Kamanda Muniain kimada ya maongezi.

ENDELEA NA NONDO..!!

HOFU NDANI YA TRJ I

JUMAMOSI ASUBUHI

CHIMALTENANGO, GUATEMALA CITY –GUATEMALA

   “Inaweza kuwa swali zuri linalohitaji majibu” Akaongea Kamanda Muniain.

   “Mrembo ni njia ingawa kuna mwingine warembo uwa si njia nzuri kwa sababu wanawake wote duniani katika mambo ya kazi zetu uwa wana mambo yasiyotabirika kama baadhi ya wanaume wenzetu uwa nao hivyo… Ange kwetu anaenda kuwa njia ya tunayohitaji katika misheni yetu” Akafafanua Agent Kai na kuweka kituo apate kumuangalia kila mmoja kati ya wote.

  “Mapema sana umemkubalia aingie kwenye timu… Humu kuna mateka watatu na wote ni muhimu sana kwakuwa wanajua mengi ya kuhusu maadui zetu lakini hakuna uliyesema aingie… Unatuweka njiani sana mkuu, fafanua hili Kai..!” Akaongea Investigator Miller maana yeye alikuwa anahisi kuna mvuto wa kimapenzi kati ya watu hawa waili toka mwanamke huyu aletwe hapa siku ya kwanza akiwa kaongozana na Agent Kai kirafiki zaidi.

   “Kuna mashaka juu ya hili lakini naomba msimfananishe hawa na wale wengine naweza sema hivyo.. Kwanini nasema hivi? Jibu ni kuwa huyu ni mtu ambaye nimemtizama vizuri na kugundua yeye hayumo katika waliokuwa wakitumika wakiwa wanajua kuwa wanatumika kwa Alexis kwa kazi gani! Hivyo huyu si adui yetu ingawa si vya kuamini sana kwakuwa kwenye mapenzi kuna maamuzi ya utata hasa pale mtu anapojua ukweli kuhusu mpenzi wake ukweli aliokuwa haujui hapo kabla.. Wengine uupokea ukweli katika hali ya kutoukubali hata iwe vipi! Na wengine uukubali ukweli huo na kuamua kuwa hata kama si ukweli mzuri kwenye jamii inayowazunguka yeye anasimama alipo mpenzi wake… Hili ndiyo jambo ambalo litatufanya sisi tuwe na Ange kwa tahadhari kubwa lakini haikatazi sisi kumtumia yeye kufanikisha hitaji letu hitaji la kazi yetu” Alifafanua ‘TSC’ macho yake yakizunguka wakati wote kumuangalia kila mmoja kwa zamu akirudia rudia wakati wote anavyoongea ikiwemo Ange anayezungumziwa na uzuri walikuwa wakizungumza kwa kiingereza katika kumjadili maana wote walishaujua udhaifu wake wa kutojua kiingereza kiufasaha tena kwa asilimia kubwa kama ilivyo watu wengi wengi wa Guatemala na nchi nyingine za ukanda wa latin amerika zinazotumia kilatini.

   “Sawa! Tusikie huo umuhimu wake kuingizwa katika timu..!” Akaongea Rebecca lakini huyu alikuwa akijua ishu yote.

   “Sasa hapa kitahusika kilatini ndugu zangu hivyo nabadilika kwa niaba yake..!” Akaongea Agent Kai na kuachia tabasamu wengine nao wakatabasamu kukubali.

   “Ange samahani tulikuacha kidogo tulikuwa tukijadili jambo linalohusiana na usalama wako baada ya yote ambayo tutaenda fanya kumaliza shughuli yetu iliyotukusanya hapa Guatemala… Sasa tunaweza endelea na maongezi yakikujumuisha na wewe.. Kuna maswali ambayo nitapenda kukuuliza na wewe ujibu, maswali hayo na majibu yako yana maana kwakuwa tayari wewe ni mwenzetu nafikiri unafafanua vizuri zaidi” Akaongea Agent Kai sasa akitumia kilatini hili kumjumuisha na Angelica katika maongezi yao.

   “Niko tayari kujibu na kufafanua kwa uzuri kila ninalolijua juu ya Alexis!” Angelica alijibu akiwa sasa amefurahi kuona anahusishwa katika maongezi kwa lugha iliyo ndani ya ulimi wake.

   “Unasema hujui lolote katika biashara zake kwakuwa hakuhusishi na biashara zake ila anakuhusisha katika baadhi mali zake za hapa GTL.. Na..!” Alinyamaza kuangalia upande alipo mzee Muniain sababu simu ya mkononi ya mzee huyu iliita.

   “Mtanisamehe hawa ni vijana wangu wa OCLA wa ulinzi wa nje acha niwasikilize” Akaongea Kamanda Muniain kisha akasimama.

  “Wanajua mahala ulipo?” Akauliza Agent Kai kumuuliza Kamanda Muniain wakiangaliana kwa umakini.

  “Niliwapa taarifa niko mafichoni ila sikusema maficho yenyewe ni wapi!” Akajibu simu ikiwa kiganjani bado inaita.

   “Sawa ila nina wasiwasi kidogo… Pokea tu uwasikilize, tutasubiri umalize kuongea ndipo tuendelee na Ange” Akafafanua juu ya wasiwasi wake kisha akatoa ruhusa aendelee na utaratibu wa kuongea kwa simu na hao vijana wake, watu wote wakawa kimya kusikia Muniain anavyoongea maana Mr. Machale alionyesha wasiwasi juu ya simu hii.

   “Halloo!” Akaongea Kamanda Muniain baada ya kupokea simu.

   “Heshima yako mkuu.. Unaongea na Jairo Jimenez, nimetumia simu ya Austin kuna tatizo kidogo mzee wangu, tumekimbizwa na watu tunaofahamu kabisa ni watu GIS lakini ajabu wametusimamisha tukastuka si watu wazuri kwetu tukaanza kukimbia tukapora pikipiki ya mtu mmoja mtaa wa Horse buggy lakini wakati tunakimbia walitokea watu wengine kama watatu nao wakiwa na pikipiki wakaanza kutukimbiza wakatushambulia katika sehemu ya wazi kabisa maeneo ya watu ambapo si rahisi watu wenye uwoga juu ya maisha yaw engine, walilenga tairi vizuri tukadondoka mimi kwakuwa nilipakizwa nilifika chini bila kupata majeraha makubwa mwenzangu pale pale kwa bahati mbaya amekutwa na umauti kwakuwa hakuwa na element kama ilivyo mimi alidondoka kichwa kilipiga chini vibaya kwakuwa lilikuwa eneo la watu wengi nilifanikiwa kuinuka haraka nikamsachI ndugu yangu kwa haraka nikachukua simu yake kabla hawajafika majahili na kuingia kwenye moja ya vichochoro kuna mtu alinionea huruma na aliona wakati tunashambuliwa na risasi akaniambia niingie kwenye banda lake la biashara ndipo ikawa pona yangu maana naambiwa walitafuta kila sehemu dakika zaidi ya thelathini polisi walipofika wao ndiyo wakaona waondoke nikatoka pale baada ya dakika ishiini ikiwa polisi nao wakiwa washaondoka na pikpiki pamoja na mwili wa Austin… Nimekupigia kukupa taarifa hii mkuu niko kwa rafiki yangu anayefanya kazi hospitali ya jiji ananipatia matibabu ya vidonda..!” Yalikuwa maelezo marefu ya upande uliopiga simu na kwakuwa Kamanda alikuwa ameweka loud speaker kila mmoja aliweza sikia vizuri ikwemo Angelica kwakuwa lugha ilikuwa lugha mtambuka kwake.

   “Pole sana kijana wangu… Nchi hii sasa imekuwa si salama kwa wanausalama walio wema kwa taifa lao yaani hata simu zetu kuongea kwetu imekuwa ni wasiwasi, pata matibabu yako kisha tutawasiliana baadaye kupeana taarifa hali yako unaendeleaje”

   “Ndio mkuu lakini naomba haraka afuatiliwe Jaques Texequela wa GIS amekuwa akiongoza kikosi kinachokufuatilia mkuu wewe na Norman, mkimpata huyu mtapata taarifa nyingi mnazotaka mkuu”

   “Nashukuru kwa taarifa tutaanza kumfuatilia muda si mrefu nachoomba usifanye jambo lolote litakalo hatarisha usalama wako kwa kutoka kwenda mahala popote zaidi ya hapo ulipo, usiwasiliane na mtu yoyote awaye na kusifu kwa ulivyofanya uamuzi wa kijasiri kuchukua simu ya Austin! Mungu amuweke mahala pema peponi” Alimalizia Kamanda Muniain na kisha akakata simu akainua uso wake akiwa amechoka mzee wa watu akakutana na nyuso za simanzi toka watu waliokuwa wakimsikiliza.

   “Jaques Texequela ndiyo nani?” Akauliza Investigator Miller akilenga swali lake kwa Kamanda Muniain.

   “Ni mmoja wa makachero wazuri sana walio Guatemala Intelligence and Security ni jasusi aliyeanzia jeshini kisha Mkurugenzi wa jasusi akamuomba mkuu wa kitengo cha kijasusi cha jeshi kuwa anamtaka huyu Jaques ndipo akatoka jeshini na kuwa jasusi wa GIS kitengo cha kazi maalumu ndicho kinaongozwa na yeye ana miaka miwili toka atoke jeshini kuingia GIS” Akajibu Kamanda Muniain.

   “Vipi msako wa Kamishina tunayemshikilia kuna habari zozote?” Akauliza Agent Kai lakini swali lake kimtazamo lilienda kwa Norman Cabrera kwa jinsi tu alivyokuwa akimuangalia.

    “Polisi wa upelelezi wanaendelea na upelelezi wao na haswa wananitafuta mimi kama nilivyokugusia usiku kwenye kuta za matangazo za ma bar, mistimu na hata vituo vya stendi kuna picha zangu wakisema mimi ni mtu hatari nimemteka Kamishina Alvaro Conedera na kumshikilia bila utaratibu maalumu popote nitakapoonekana itolewe taarifa kwa haraka kwa maafisa wa polisi katika namba ambazo wameweka namba mbalimbali za maafisa kadhaa…. Hizi habari nimepewa asubuhi hii na rafiki yangu ninayemuamini na kufanya naye mawasiliano akiwa ndani ya jeshi la polisi” Akajibu Norman.

   “Dah! Umakini uwepo kwako pia usikose kila unapotoka utoke ukiwa ndani ya sura ya bandia… Nashukuru tumefanikiwa katika kuja kuweka makazi huku nje ya jiji greenhouses…  Leo tutatakiwa kumuongeza Jaques hapa hili tuweze kukusanya ushahidi mzuri juu ya mtu mjanja mjanja kama mheshimiwa Ceni tunahitajika tuwe na ushahidi wa kutosha… Turudi kwenye maongezi juu ya Ange” Aliongea Agent Kai akimuangalia kila mmoja kwa wakati wake alipofika kwa Angelica akakumbuka umuhimu wa kuendelea na maongezi yanayomuhusu.

   “Sawa tuendelee tu!” Ange akaongea kwa sasa akiongea na kauchangamfu kidogo.

   “Hapa Guatemala unawajua marafiki wakubwa wa mpenzi wako?” Akauliza ‘TSC’.

   “Baadhi nawajua lakini wengi wao ni watu wa serikalini na si wafanyabiashara kama wafanyabiashara wengine wanavyoweza kuwa na marafiki wafanyabiashara wenzake lakini yeye ni tofauti marafiki zake ni watu walio na vyeo katika serikali ya nchi hii na wengine siwajui hata wanahusika na nini hapa Guatemala” Akajibu Ange.

   “Ulisema unazifahamu mali zake mtu wako… Je? ni mali gani unaoifahamu ukiacha nyumba yake kule kwake”Akauliza tena Agent Kai ‘The Sole Cat’.

   “Ana magari ya kifahari ambayo mimi nayajua pia ana nyumba ukiacha ile kule anayo ingine mtaa wa Avenida Calle barabara ya kwenda ikulu zone one pia hotel ya Villa Mexico anaimiliki na ndiyo aliniambia ni mali yangu tulikuwa tunataka kuanza taratibu za kuishughulikia kwa mwanasheria nipamiliki kisheria.. Pia ana nyumba aliyoninunulia pia lakini makaratasi yamechelewa kubadilishwa hii ipo huko San Marcos mtaa wa Main kingine ni kitu kikubwa ambacho kila mtu anakijua ni shamba na kiwanda kidogo cha kusindika kahawa huko San Marcos pia ana kiwanda kikubwa ambacho hiki kimeajiri watu wengi huko mji wa Scuintla hapa hapa jijini Guatemala ni hivi ninavyovijua kuhusu Alexis” Alijibu vizuri kiufafanuzi Angelica wengine wakimsikiliza kwa umakini.

   “Hujawai kufika kwenye shamba lake kubwa la Tajumulco huko San Marcos?” Akauliza ‘TSC’ wakitizamana  na Angelica.

   “Nimefika mara zaidi ya tatu huko” Akajibu.

   “Kitu gani cha ajabu unachoweza kumbuka ulikiona ambacho kinaweza kuwa ni tofauti na ukawaida wa mashamba mengine unayoyajua au uliyowai kuyasikia?” Akahoji tena Agent Kai ‘TSC’.

   “Ulinzi na walinzi hao kuwa kwa wingi zaidi anapokuwepo Alexis pale kukutana na ndugu yake Fernandes Carlos Codrado mtu yule uwa anakuja na walinzi wake wengi tu mpaka niliwai kumuhoji Alex juu ya hilo”

   “Alikujibu kwanini inakuwa hivyo?”

   “Alisema inatokana na biashara zake anazozifanya kuwa hazina guarantee ya usalama wake hasa kwa maadui zake na hata serikali mbalimbali hapa duniani hasa Marekani”

   “…Ni hilo tu lililokustaajabisha?”Maswali aliendela kati ya Kai na Angelica tu wengine wakiwa makini kusikiliza.

   “Lingine kuambiwa nisijihusishe na kutembea tembea bila yeye Alex mara zote nilizofika pale kuna chumba maalumu niliachwa yeye akiendelea na kuzunguka zunguka sehemu mbalimbali”

   “Tunaweza pata ramani ya maelekezo kidogo kulivyo?”

   “Sawa nitawachorea na maelekezo ya kimaandishi pia nitatoa vile nijuavyo hasa unavyoingia na mpaka pale kwenye chumba ambacho nakuwa nafikia mimi maana ndiyo mwisho wangu kwengine nakuona kwa mbali na ninapokuwa kwenye chumba ulinzi uimarishwa nikiambiwa nalindwa na wahuni waliopo pale lakini kuna siku nilihisi si kama nalindwa kwa wahuni waliopo pale bali nalindwa nisitoke toke kwenda mahali”

   “Sawa… Maelezo mazuri leo hii tutaenda huko San Marcos hatuwezi endelea kuwepo hapa GTL kwakuwa hapa kazi yake inasubiri maelekezo ya mheshimiwa Rais na itahusu ruhusa yake ya kumvuruga waziri wake anayeharibu nchi hii katika ulinzi na usalama… Jamani maelezo na faida ya kuwa karibu na Angelica Linares mmeyasikia wote kwa ujumla?” Alimalizia TSC akiwatizama timu wote kwa ujumla na kuwauliza kama wameelewa.

   “Kila mmoja ameelewa kwa uzuri.. Upande wangu hakuna swali, nimefurahi sana kusikia nilichosikia… Tajumulco kuna siri kubwa sana na kwa aina ya ulinzi anaosema Ange ni ulinzi ambao hata sisi tuliouona kwa mbali tulipoenda kuchunguza kwa kuuliza uliza wenyeji wa pale” Akaongea Investigator Miller.

   “Ni kweli asemavyo Miller na hata Ange amefafanua vizuri kati ya maswali tuliyojiuliza wakati ule… Shamba lile lina siri za genge la TRJ”Akaongea Special Agent Silla na wengine baadhi yao wakatingisha vichwa kukubali.

   “Usiku wa leo tunaelekea San Marcos kwa kazi maalumu ya kujua pale kuna nini? Kwanini kuwe na ulinzi mkali sana usiofanana na mashamba mengine tunayoyajua, kwanini simu ya mwanamke anayejiita Valentina Aurelia Moschi mnara wa Tajumulco ulituonyesha wakati Jogre anatuma barua pepe kwangu ilitokea pale”Nahodha wa timu alitoa maelekezo ya kazi itakayokuja itakuwa ni mkoa wa San Marcos inakopatikana milima ya milima ya Tajumulco.

   “Kwa sasa hii asubuhi ratiba ikoje?” Akauliza Norman akimtizama Agent Kai kutarajia jibu litoke kwake.

   “Tunamchukua Gadiano Soria kwenda naye mjini kisha tutamwambia ampigie simu mwanamke tunayemtaka kuwa anahitaji kuonana naye eneo la nje ya jiji… Kama tutabahatisha kuja yeye mwenyewe itakuwa vizuri zaidi hata akija na jeshi lote la TRJ tutalidhibiti na kumchukua…!” Akajibu Agent Kai bila kufikiri sana akiwa kainamisha kichwa chini pale alipokaa kama anahesabu kitu.

   “Ulikuwa ushapanga hilo boss?” Akauliza Special Agent Rebecca kwakuwa alistaajabu ratiba hiyo kuingia ghafla sana.

   “Nimeikumbuka Marekani nataka tumalize shughuli turudi kwetu.. Hahahaha…!” Akajibu Agent Kai akitabasamu na kupiga makofi matatu ya kufuatana.

   “Sawa kabisa uchunguzi utaenda na kazi tushachunguza mengi muda wa kazi sasa…” Akasema Silla mtu anayependa kupigana pigana kikawaida yake ikiwa hulka yake.

  “Jiandaeni kwa hilo.. Hapa watabaki Kamanda Muniain, Rebecca na Angelica..!” Alimalizia Agent Kai kisha akamimina juisi kwenye glasi mpaka juu kisha akanywa yote na kuinuka toka sofani akawatizama akiwa anatabasamu na wote wakatabasamu kama yeye na wapo waliotoa vicheko vidogo, alipoanza kupiga hatua kuondoka pale nyuma huku Angelica naye akainuka na kuanza hatua za mbio kumkimbilia mpaka waliowaacha wakaangaliana na kukonyezana, kiwivu kikapanda ghafla kwa swahiba wa Agent Kai mwanadada Rebecca Smith hata mimi sijui kwanini kiwivu kilimpanda.

Mwisho wa sehemu ya sabini na moja (71)

Agent Kai amefungulia kazi baada ya mijadala mirefu ya kiuchunguzi wakijadili jinsi ya itakavyokuwa na kufikia kuwa sasa ni muda wa vitendo usiku wakiamua kwenda kulichunguza eneo la milima ya Tajumulco huko San Marcos.

Je watafanikiwa kumuona mwanamke wanayeijua sauti yake akiongea kwa simu na pia kujua anaitwa Valentina Aurelia Moschi?

Majibu ya yote tukutane sehemu zinazofuata katika Jino kwa Jino!




   “Tunamchukua Gadiano Soria kwenda naye mjini kisha tutamwambia ampigie simu mwanamke tunayemtaka kuwa anahitaji kuonana naye eneo la nje ya jiji… Kama tutabahatisha kuja yeye mwenyewe itakuwa vizuri zaidi hata akija na jeshi lote la TRJ tutalidhibiti na kumchukua…!” Akajibu Agent Kai bila kufikiri sana akiwa kainamisha kichwa chini pale alipokaa kama anahesabu kitu.

   “Ulikuwa ushapanga hilo boss?” Akauliza Special Agent Rebecca kwakuwa alistaajabu ratiba hiyo kuingia ghafla sana.

   “Nimeikumbuka Marekani nataka tumalize shughuli turudi kwetu.. Hahahaha…!” Akajibu Agent Kai akitabasamu na kupiga makofi matatu ya kufuatana.

   “Sawa kabisa uchunguzi utaenda na kazi tushachunguza mengi muda wa kazi sasa…” Akasema Silla mtu anayependa kupigana pigana kikawaida yake ikiwa hulka yake.

  “Jiandaeni kwa hilo.. Hapa watabaki Kamanda Muniain, Rebecca na Angelica..!” Alimalizia Agent Kai kisha akamimina juisi kwenye glasi mpaka juu kisha akanywa yote na kuinuka toka sofani akawatizama akiwa anatabasamu na wote wakatabasamu kama yeye na wapo waliotoa vicheko vidogo, alipoanza kupiga hatua kuondoka pale nyuma huku Angelica naye akainuka na kuanza hatua za mbio kumkimbilia mpaka waliowaacha wakaangaliana na kukonyezana, kiwivu kikapanda ghafla kwa swahiba wa Agent Kai mwanadada Rebecca Smith hata mimi sijui kwanini kiwivu kilimpanda.

ENDELEA NA NONDO …!!

HOFU NDANI YA TRJ II

CHECHE MUNDO PETAPA GARDEN

Gari aina ya Mercedes Benz 2010 ML300 CDI inayoendeshwa na Detective Norman ilifunga breki kwenye maegesho ya bustani ya Mundo Petapa iliyopo eneo la Santa Catarina Pinula barabara ya Zona 10 mji mdogo wa Petapa, bustani hii kushoto kwake kuna chuo kikuu kiitwacho De San Carlos Univesidad.

Ndani ya gari kulikuwa na watu wapatao watano ikiwemo dreva mwenyewe Detective Norman, Agent Kai, Special Agent Fransis Simone Silla, Investigator Joseph January Miller na mtu wa tano alikuwa ni kijana muajiriwa wa genge la TRJ akiwa amepewa kazi ya kumfuatilia Kamanda Muniain kisiri kila anapoenda kisha akaingia katika mikono inayobana kama praizi ya kikosi kazi siku ambayo Agent Kai aliingia jiji la Guatemala na kupokelewa na kazi ya kuwaokoa katika kuzingirwa kina Silla katika mgahawa wa kitalii wa Filadelifia Coffee Resort & Tours.

Wote ndani ya gari walikuwa kimya kila mmoja akiangalia nje ya gari huku na huko kana kwamba wanamtarajia mtu lakini Agent Kai mkononi mwake alikuwa na simu ambayo mmiliki wake ni mateka wao Gadiano Soria, alikuwa akisachi jina ambalo alishaelekezwa na mwenye simu kuwa ndiyo namba ya boss anayemtumia yeye katika kazi maalumu aliyokuwa kapewa.

   “Inasachi.. Ooo.. Inaita.. Shika simu uongee kama tulivyokuelekeza” Agent Kai akaongea na kuondoa ukimya uliokuwa umetamalaki ukimya wa kimaongezi kati yao.

Gadiano alipokea simu toka mkononi mwa Agent Kai huku mikono yake ikitetemeka kama kapewa bomu la kutupwa na hajui kuweza kulifanya likatumika, akaiweka sikioni.

   “Halloo!” Upande wa pili ukaongea kwa sauti iliyojidhihiri mpokeaji naye alikuwa na mashaka na simu hii.

   “Madam! Madam mimi ni Gadi!” Akaongea Gadiano kwa sauti ya kitetemeshi kama ahamini anaongea na mtu anayeongea naye au anamuogopa.

   “Gadi? Gadi gani?” Upande wa pili sauti ya kike ilionyesha mshangao kuwa haitambui sauti ya mpigaji simu wala jina alilotajiwa lakini kwa kina Agent waliokuwa wanatumia vinasa sauti sauti vyao kiteknolojia vya Bluetooth waliweza tambua mpigiwa simu anazuga.

   “Gadiano Soria kijana wako TRJ… Naomba usiwe na hofu siko na watu wa hatari nimetoroka nimewatoroka waliniacha kwenye nyumba waliyokuwa wakinishikilia mateka” Akaeleza tena Gadiano macho yakimtizama kila mmoja aliye ndani ya gari kwa zamu na bado alikuwa anatetemeka kama anasikia baridi kali.

   “Mbona umeanza bila salamu yetu? Haujijui wewe nani?” Akahoji mwanamke ambaye kiukweli aongeapo kwenye simu Agent Kai anaijua sauti kinagaubaga na anaitamani haswa aitengenezee sura yake kimichoro imjulishe ni nani.

   “Siamini madam boss kama nimetoroka ndiyo maana nimejisahau kidogo… Niko mahala nimejificha nahisi kama wananifuata au wananiona” Akaongea Gadi.

   “Mtaa gani upo?” Akauliza mwanamke kwa sauti ya kasi.

   “eneo la Santa Catarina Pinula barabara ya Zona 10 karibu na bustani ya mji mdogo wa Petapa inayoitwa Mundo Petapa nimejificha ndani ya eneo la ndani la hii bustani naomba msaada wako niwe salama sijui nitajisaidia vipi binafsi!” Akaongea Gadiano.

   “Endelea kujificha papo hapo… Nyumba uliyotoroka ipo mtaa huo huo?” 

   “Ndiyo mkuu!”

   “Natuma watu haraka kukuchukua.. Nahitaji maelezo kamili juu ya hiyo nyumba”

Mwanamke alimalizia hivyo na kukata simu kana kwamba kapiga yeye.

   “Plan B inaenda kufanya kazi!” Akaongea Investigator Miller baada ya sekunde za ukimya kuwanyemelea tena.

   “Ndiyo plan B… Hata hivyo kwa tokea mwanzo niliamini kwenye plan hii zaidi… Si rahisi kwa hali ilivo sasa mwanamke huo akafika mwenyewe lazima alikuwa atume watu wake kumfuata Gadiano… Mpango utakuwa vile tulivyokwisha panga mwanzo wewe Gadiano utaenda pale karibu na michikichi ukijfanya umekaa eneo ambalo unahisi kwako ni salama zaidi mpaka pale watakapofika watu watakaotumwa kukufuata eneo la karibu yako atakuwepo Miller karibu na kaunta ya vinywaji atakuwepo Silla huku nje nitabaki mimi na Norman tukitizama watakavyokuwa wamefika… Tafadhali Gadiano usitumie simu kwa namna yoyote ile zaidi ya kupigiwa na watu wako watakaokufuata au huyo Madam wenu…!” Plan B ilipita kwa ‘TSC’ kuipitisha na kuifafanua vizui itakavyokuwa.

Silla alitoa bastola yake toka mahala anapohifadhi akaikagua kidogo na wengine wote wakaiga kufana kama alivyofanya yeye ukiacha Gadiano ambae hakuwa na silaha yoyote.

   “Haya! Muda wa kazi!” Akaongea Miller wakatizamana na wenzake kila mmoja akimtizamna mwenzie wakatabasamu tabasamu la ushindi.

  “Miller utakuwa karibu na mtu huyu akienda tofauti na tulivyopanga mpoteze, hakikisha hatumii simu yake kwa meseji maana akiongea sote tunamsikiliza hivyo hata katika vinasa sauti uwe makini” Agent Kai akatoa maelekezo a mwisho.

   “Niko makini kaka!... US First!”

Miller akamuongoza Gadiano kushuka kwenye gari wakifuatiwa na Silla kwakuwa eneo la ilipo miti ya michikichi lilikuwa eneo linaloonekana tokea huku kwenye lango kuu la kuingilia ndani ya bustani nzuri a kupumzikia watu wa eneo la Petapa likiwa ni eneo lenye mandhari ya kupendeza sana kwa miti mizuri, maua mbalimbali ya kupandwa yanayonukia yenye rangi mbalimbali za kuvutia yalilifanya eneo hili liwe la kuvutia sana kukiwa na mabenchi ya kujengwa kwa simenti maji yanayotoka kwenye mabomba yaliyo kwenye masanamu ya watu na wanyama maji haya yalikuwa yakitoka yanapoenda kutua yanarudishwa ndani ya masanamu ndani kwa ndani kisha yanatoka tena na hii ikiongeza mvuto mwingine hapa kwenye bustani ya Mundo Petapa Garden.

Mgawanyiko wa timu ulifanyika kwa ufasaha vile Kapteni wa timu alivyopanga, zilipita dakika ishiini na tano ukimya ukiwa umetawala kati yao watu wote wakiwa makini kuhakikisha hakisogei kiumbe chochote bila wao kujua.

Wakiwa hivi kuna mwanaume mmoja wa kizungu ambaye alikuwa kavaa suti ya rangi ya kijivu, miwani meusi na kofia aina ya marliboro alitokea kwenye njia  inayojia eneo la bustani  kwa kutokea upande wa chuo.

Alivyojichora chora mwili wake na hereni ndefu za msalaba alizovaa masikio yote mawili zilifanya Agent Kai ainamishe uso kusogeza macho kwenye kisehemu kipenyo katika vioo vya tinted vya gari hili aweze kumuona vizuri mtu huyu katika side-mirror kwakuwa eneo la chuo gari yao kina Agent Kai iliweka eneo lile kwa nyuma.

  “Na wasi wasi na mtu anayetokea eneo la barabara ya kutokea chuo.. Watu wengi wa genge la TRJ wana michoro mingi  tuwe makini naye anakaribia eneo la gari letu kwa nyuma” Akaongea Agent Kai akiwa bado anatizama kioo cha side-mirror jamaa anavyokuja huku mkono wake wa kulia ukiwa umeinuka kwenda sikioni kiganja kimekamatia simu hii ilimaanisha anaongea na mtu mwingine kwa simu yake.

Aliipita gari akiwa kwenye mwendo ule ule na hakuacha kutaka kuona kwenye gari anayoipita kuna watu ama vipi? akachungulia kwa kuibia akaona haitoshi wakati anaendelea na hatua zake akaweka kiganja kwenye paji la uso kuzuia mwanga wa jua kisha akainamisha kichwa chake kwa haraka kuchungulia walio kwenye gari walimuona vizuri sana kama ujuavyo vioo vya tinted vilivyo na hata hawakujishughulisha kuinama ili wasionekane kwani walitambua hawezi kuwaona vizuri ataona vivuli tu.

Ni kweli jamaa aliona vivuli vya watu akazuga na kuendelea na safari yake kuelekea eneo la kuingilia kwenye bustani akasonga kwa mwendo ule ule akijifanya anaongea kwa furaha sana kwa simu kicheko kikianikizwa hili asionekane mtu tofauti kwa kosa lake la kuchungulia kwenye gari.

   “TRJ huyu… Nafikiri washafika” Norman akaongea akimtizama Kai ambaye yeye alikuwa bize kumtizama mtu yule anavyotokomea ndani ya eneo la bustani.

   “Miller kuwa makini kuna mtu tumemshuku anakuja huko.. Nafikiri ndiyo wametumwa na madam” Akaongea Agent Kai akiwa kainua mkono wake wenye saa ya mawasiliano.

   “Yah! Nimemuona na anaongea kwa simu na pia Gadi anaongea kwa simu pia acha tusikilize Gadi anamwambiaje” Akajibu Investigator Miller kisha wote wakatega sikio kusikia Gadi anaongea nini lakini hawakusikia akiongea kitu.

   “Gadi ameinuka toka alipokuwa amekaa anajitokeza hili aonekane kwa mtu aliyefika hapa” Akaongea Miller kwa kasi.

   “Kuna gari inakuja huku kwa mwendo wa kasi.. Shiit! Miller jiandaeni kwa mashambulizi kama kutakuwa na utofauti wowote.. Mchunge Gadiano nahisi kaleta ujanja fulani ..” Aliongea Agent Kai kwa kasi na timu yote ilipata ujumbe macho yake yakikaza kuangalia mbele ambako ilionekana gari aina ya FJ Cruiser Convertible rangi nyeusi na ndani ya gari haikuweza kujificha kwa umbali ule ule Noman na Agent waliweza kuwaona waliomo ndani ya gari wameshika mitutu viganja vyao vikiwa vimevalishwa gloves nyeusi.

   “Hatari Norman… Inabidi tucheze disko sasa, hakuna kuremba… Miller na Silla mnanisikia huko mlipo?” Akaongea kwa kasi Agent Kai kisha akamgeukia Norman wakatizamana kuna ishara akampa papo hapo Norman akawasha gari.

   “Ndiyo! Gadiano katuchezea shere….!” Akaongea  Miller kwa kasi ikionekana sauti yake tu kuwa naye amejificha sehemu kuzuia asishambuliwe.

Gadiano Soria alijifanya kama katulia pale alipokuwa ameamrishwa na Agent Kai kuwa akishaingia ndani ya eneo la bustani akakae eneo linaloonekana kama amejificha kwa woga akihofia asionekane na watu kiurahisi, moyoni mwake alijiambia yeye ni chui mwekundu hatakiwi kuwasaliti wenzake kisa kaambiwa ataachiwa huru, aliweza kutuma meseji kuwa hayuko mahala salama amezungukwa na watu wanaomsaka madam hivyo Madam aliongoza kikosi kazi kilichokuja eneo hili wakimtanguliza mwanamume aliyeonekana na kina Agent Kai ambaye naye alifana kazi nzuri kutoa maelekezo kuwa ni kweli katika gari aina ya Mercedes Benz 2010 ML300 CDI kuna watu wawili washambuliwe haraka.

Gadiano aliwai kujificha nyuma ya mti mkubwa wa mchikichi na hata yule mtu aliyekuwa anawasiliana nae kwa siri kwa meseji naye alijificha karibu na mti mchikichi mwingine katika safu moja a miti hii inayopendezesha eneo hili, kazi ipo!.

Detective Norman alitia gia ya rivasi gari akaachia mafuta akatizama nyuma na kuliacha gari lianze kurudi kasi nyuma lakini alipopindua tu kuliweka sawa kwa eneo la chuo aliziona gari mbili zinazofanana aina na rangi na ile walioiona kwa mbali inakuja.

   “Tumezingirwa Kai!” Akaongea Norman.

   “Aisee wako wengi sana hatuwezi pambana nao kanyaga mafuta ingia eneo la lango la bustani..” Kai nae akaongea akitamani angekuwa yeye ndiyo kashika usukani wa gari, Norman akazungusha usukuni wa gari kisha akakanyaga mafuta kwa kasi likafana kama linaruka akalielekeza alipoambiwa.

Milio ya risasi ikasikika walianza kushambuliwa na wale waliokuwa wanakuja kwa mbele yao kioo cha upande wa Kai kilipasuliwa akainama kwa kasi risasi ikamkosa ikaenda pita juu ya kichwa cha Norman na yeye alimanusura yake aliwai kuinama pale alipoona mwenzake anainama kwa kasi.

   “Ongeza mwendo Norman watatuua hawa.. Miller na Silla tunaingia ndani ya eneo la bustani jamaa wako kama kikosi cha jeshi huku nje!” Ilisikika sauti ya Agent Kai.

Aliweza kujiinua baada ya kuwa gari lao limelipa mgongo gari linalowafukuza huku waliomo garini wanashambulia, kujiinua kwake kulikuwa kumefuatana na kuitoa bastola yake toka kwenye dashboard a gari.

Njia hii wanayojia ilikuwa kaibu na michikichi Agent Kai aliweza kumuona Gadiano alipojificha na hata ule mwingine haraka akapitisha hukumu yao mkono uliinuka akawalenga gari ikiwa kwenye kasi Gadiano aliwai kuona akajitupa chini lakini yule mwingine alipogeuka tu alijikuta akipaishwa juu huku kichwa chake kikichimbwa na risasi pembeni kidogo ya paji la uso alidondoka karibu na Gadiano akaanza kupaparika kama kuku kwakuwa risasi ilivunja juu ya jicho lakini haikugusa ubongo akawa anaitetea roho yake kwa maumivu makali sana mpaka akawa analia kuomba msaada kwa Gadiano alieeogopa kutokeza.

 Investigator Miller alitumia fursa hiyo kubingirika kwa kasi kama tairi linalotembea likiwa tupu alipokuja kukaa sawa ilikuwa hatua nne tu toka alipo Gadiano na jamaa yake anayeaomba msaada, macho yao yakagongana Miller akambinyia jicho la kumkonyeza kisha akabinya kifyatulio cha bastola yake (trigger) akilenga kichwa cha muomba msaada, risasi ya juu ya utosi ilimaliza kelele zake za kuomba msaada Israel mtoa roho aliipitia roho kama kipanga anayenyakua windo lake.

Gadiano macho yakamtoka kama fundi seremala kajigonga na nyundo wakatizamana tena na Miller ambaye sasa akili yake ilikuwa ikifanya kazi mara ya ziada, aliona gari yao ikimpita kwa nyuma kwa kasi kisha gai lingine likatokea kuingia eneo la bustani hapo Miller alifyatua risasi ikaenda ondoa uhai wa Gadiano malipo ya ujanja mwingi mbele giza.

Pale pale alipo Miller alijipindua akaelekeza bastola yake inapotokea gari ya adui ambayo kabla hajaifyatulia risasi katika moja a tairi alilolilenga aliona ikilala upande mmoja ikiwa bado kwenye mwendo kasi hapo akajua kazi ya Special Agent Silla, alichofanya Miller akapiga risasi tairi la mbele upande wake wa kulia alipo ukasikika mlio wa gari za kugongana kwakuwa gari ingine iliingia kwa kasi ikifuata gari hii ya mbele.

   “Simamisha gari tuwasaidie kina Silla..!!” Mashambulizi ya Miller na Silla yalifanya Agent Kai aongee hivi na Norman akafunga breki bila kupunguza mwendo mserereko wa maana wa matairi ya Mercedes Benz 2010 ML300 CDI ukalifanya liyumbe mpaka juu ya kibaraza tuta cha masanamu ya wanyama mbalimbali yanayotema maji, kwa kasi ya mnyama ‘TSC’ akafungua mlango wa gari kisha akashuka na kuufanya mlango kama ngao mkononi akiwa na bunduki aina ya M240 Machine Gun bunduki ya kivita ya kimarekani ambayo kwa Agent Kai ndiyo bunduki aliyoizoea sana kucheza nayo akiwa maeneo ya mashambulizi.

Mwisho wa sehemu ya sabini na mbili (72)

Mundo Patapa Garden hali si shwari! Mafundi wamekutana baada ya mtego waliotaka umnase mwanamke wanayemuwinda kunasuliwa na mtu aliyeandaliwa kama mtego.

Mashambulizi ya ana kwa ana yataleta majibu gani kwa pande mbili zinazoshambuliana?

kwa majibu zaidi sogea mbele kwa pamoja tuweze kusoma na kuona movie inakwendaje?




Investigator Miller alitumia fursa hiyo kubingirika kwa kasi kama tairi linalotembea likiwa tupu alipokuja kukaa sawa ilikuwa hatua nne tu toka alipo Gadiano na jamaa yake anayeaomba msaada, macho yao yakagongana Miller akambinyia jicho la kumkonyeza kisha akabinya kifyatulio cha bastola yake (trigger) akilenga kichwa cha muomba msaada, risasi ya juu ya utosi ilimaliza kelele zake za kuomba msaada Israel mtoa roho aliipitia roho kama kipanga anayenyakua windo lake.

Gadiano macho yakamtoka kama fundi seremala kajigonga na nyundo wakatizamana tena na Miller ambaye sasa akili yake ilikuwa ikifanya kazi mara ya ziada, aliona gari yao ikimpita kwa nyuma kwa kasi kisha gai lingine likatokea kuingia eneo la bustani hapo Miller alifyatua risasi ikaenda ondoa uhai wa Gadiano malipo ya ujanja mwingi mbele giza.

Pale pale alipo Miller alijipindua akaelekeza bastola yake inapotokea gari ya adui ambayo kabla hajaifyatulia risasi katika moja a tairi alilolilenga aliona ikilala upande mmoja ikiwa bado kwenye mwendo kasi hapo akajua kazi ya Special Agent Silla, alichofanya Miller akapiga risasi tairi la mbele upande wake wa kulia alipo ukasikika mlio wa gari za kugongana kwakuwa gari ingine iliingia kwa kasi ikifuata gari hii ya mbele.

   “Simamisha gari tuwasaidie kina Silla..!!” Mashambulizi ya Miller na Silla yalifanya Agent Kai aongee hivi na Norman akafunga breki bila kupunguza mwendo mserereko wa maana wa matairi ya Mercedes Benz 2010 ML300 CDI ukalifanya liyumbe mpaka juu ya kibaraza tuta cha masanamu ya wanyama mbalimbali yanayotema maji, kwa kasi ya mnyama ‘TSC’ akafungua mlango wa gari kisha akashuka na kuufanya mlango kama ngao mkononi akiwa na bunduki aina ya M240 Machine Gun bunduki ya kivita ya kimarekani ambayo kwa Agent Kai ndiyo bunduki aliyoizoea sana kucheza nayo akiwa maeneo ya mashambulizi.

ENDELEA NA MOTO WA MOTO!!

HOFU NDANI YA TRJ III

CHECHE MUNDO PETAPA GARDEN

Detective Norman Cabrera alishuka kwenye gari  akifuatiwa kwa sekunde zipatazo tano ukiacha za ‘TSC’ lakini upende wake ilikuwa kuna ugumu kuona vizuri upande wa hatua kumi toka walipo na gari lao likiwakinga hivyo hakuweka kingo ya mlango alisogea kidogo mbele kupita side-mirror naye mkononi alikamatia ‘mkwasa’ (bunduki) na wote walikuwa wamefunga nyuso zao kwa vitambaa leso vikubwa vikiwa vimeziba kuanzia juu ya pua chini ya macho kuja mpaka shingoni hili wasionekane kwa urahisi kwa watu walio hapa hata maadui zao wanaojibishana nao kwa risasi.

Mgongano wa gari hizi zinazofanana aina na rangi uliotokea mbele kidogo ya kona ya lango kuu la kuingilia ndani ya eneo la bustani halikuwafanya waliomo ndani ya gari zote mbili kuzubaa hata kama wapo waliokuwa wameumia lakini waliokuwa katika hali ya uzima walishuka toka ndani ya gari kwa kila mmoja aliye na uwezo wake wa kinguvu kusukuma iwe kwa mguu au bega upande ilmadi milango iliyokuwa imelock kutokana na mgongano uliosababisha magari yote kubonyezana.

Wawili wa mbele katika siti za dreva wa kila gari waliotokea upande alio Agent Kai msukumo wa nguvu walizotumia uliwatupa chini kwa kishindo kwa macho yake yaliyo makini akiwa kainama na mlango umemziba alimuona wa nyuma damu zikimruka toka mwilini mwake hapo Agent Kai akajua ni kazi ya Miller naye akatumia fursa hiyo kumcharaza risasi tatu za dabodabo (kufuatana) wa mbele umauti uliwafika papo hapo watu wengine waliorukia upande wa kushoto mwa magari yao walikuwa nao wamefanya kazi ya bure hatua nne toka walipodondokea alikuwepo S.A Silla kajificha nyuma ya mti wa mkokono wenye upana wa kumziba mwili wake wote akiwa na bastola zake mbili azipendazo katika kazi zake za kazi kila mkono mmoja moja zote aina ya beretta nano zao la italia akiwa kazifunga kiwambo hakuwaacha hata wajiviingishe kama walivyokuwa wametamani walikula risasi moja moja za kichwa hakuna aliyeomba dua lolote sekunde tu macho yao yalikuwa yakiona giza tupu giza la zito pumzi ikawakata.

Walio ndani ya gari waliona wenzao waliotangulia kushuka kwenye magari kwa mbwembwe za kujifanya wanajua sana michezo ya giza wakilambishwa umauti wakaanza kufyatua risasi kutokea ndani ya magari pia walikuja waliokuwa kwenye gai ambayo hii sasa alikuwemo mwanamke mtafutwa sana na Agent Kai bibie anayemjua kwa jina la Valentina Aurelio Moschi lakini kiukweli ni Koplo msaliti wa jeshi la Mexico aliyejifukuzisha kazi yeye mwenyewe baada ya kusikia anatafutwa kwa tuhuma za kuhusika kughushi hati za kuwaamisha gerezani  wafungwa waliokuwa wanajeshi kabla ya kukutwa na hatia ya kujihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya, Koplo Mariana Caro Funtes.

Kikosi hiki kilichokuwa na watu wanne waliovaa vinyago nguo kama maninja wakiacha macho tu kilishuka toka kwenye gari wakiwa na silaha aina ya bunduki ambazo na wenzao nao walikuwa na aina hizo hizo Norinko QBZ-97 zao la kampuni ya utengenezaji silaha iliyoko uchina, Mariana akiwaongoza yeye na mwenzake wakaenda jificha kwenye nguzo inayoshika bango kuu la kuingia Mundo Petapa Garden sababu bustani hii ilikuwa imewekewa uzio wa wa michongoma maua ambayo yana rangi nyekundu na kijani hapa kwenya barabara ya kuingia ndipo palipo na bango ya kufahamisha hapa ni mahala pa watu kupumzika ni eneo kubwa tu huku wawili wengine wakijiweka nyuma ya gari la wenzao walio watangulia na kuingia kibanoni.

Watu wachache waliokuwepo muda huu wa mchana wa jumamosi eneo hili walishikwa na taharuki kila mmoja akawa anakimbilia anapopaona ni salama kwa maisha yake wapo waliojificha wakiwa katika kujikusana eneo moja hili wasizuliwe pia wapo waliojificha mmoja mmoja na uzuri hakukuwa na watu wengi muda huu kama ambavyo inavyokuwa muda wa jioni unapofika, pia waliokuwepo walioona wasipitwe sana wakatoa simu zao za smartphone na kuchukua video za siri.

Milio ya risasi ya bunduki za walio ndani ya gari zilikuwa zikisikika kwa mtindo ‘cover me’ wakiwa wanajilinda wasishambuliwe hivyo wanapiga tu kule walipoona mashambulizi yaliyoua ndugu zao yametokea, wote risasi zao walizifyatua kuelekea alipo Agent Kai na kushoto kwao alipo Silla aliye nyuma ya mti wa mkokono tena anainuka mmoja tokea mule mule ndani ya gari anafyatua risasi kisha anainama haraka anainuka mwingine au wawili nao wanashambulia wanayemshambulia alikuwa ametumia mlango kama ngao yake, Miller pale alipo alikuwa akiona michezo ile lakini hakuwa na uthubutu wa kushambulia kwakuwa alikuwa kabakiwa na risasi mbili katika bastola yake hapa ndiyo alijuta kwanini alijisahau kuchukua bastola mbili sababu angekuwa na silaha hii angeweza kumuondoa mmoja si kama wawili.

Dakika moja ilipita Miller akachungulia kwa nje kupitia kwenye maua akaona mijongeo ya watu wakijisogeza kutafuta upenyo wapi wataona adui, akatulia kidogo kisha iliposikika milio ya washambuliaji wanaojihami  aliokuwa akiisubiri.

   “Psiii! Psiiii! Psiiii..!” Akapiga mluzi alioakikisha Agent Kai anausikia walipoangaliana tu akamuonyesha ishara aina tatu ambazo zilieleweka na mtaalamu akainua bundukki na kuanza kufyatua risasi mfuatano bila kupumzika kuelekea kwenye zilizpo gari akichakaza vioo na vikirushwa kwa ndani walipo maadui wa genge la TRJ walioufyata chini kila mmoja akijikandamiza asizulike Norman akaongezeka naye akawa anatupa risasi kama afanyavyo ‘The Sole Cat’ ni kelele tu na uvunjikaji wa vitu uliokuwa ukisikika na maa mlipuko wa gai kulipuka ulisikika gari ya mbele ikapaa juu kisha mshindo ukajibiwa na gari ya pili zote zikapaa juu mita kadhaa kutokana na mshindo wa mlipuko alikuwa ni Investigator Miller risasi zake mbili zilizobaki kwenye bastola yake alilenga mfuniko wa tanki la mafuta ya gari la mbele kwa ustadi mkubwa akitumia mwanya wa mashambulizi ya Agent Kai na Norman.

Watu wawili waliokuwa nyuma ya gari wakijificha wakiwa wameongozana na Mariana moto uliwavagaa wakaanza kuwakwa miilini mwao nguo zilishika moto wakawa wanapiga kelelebunduki zao wakazitupa chini, Mariana na mwenzake aliyebaki walipigwa na butwaa kubwa wasijue wafanye nini? Kwa sekunde chache, wakaangaliana kisha bila kuambiana kitu walikimbia ndani ya gari lao ambalo lilikuwa wameliacha kwa kando kidogo na milango hawakuwa wameifunga kana kwamba walijua watazidiwa kama hivi na itawabidi kukimbia, waliruka mtindo kama wanapiga mbizi kwenye maji.

Macho ya Agent Kai aliyekuwa sasa amesimama wima pale pale ulipo mlango wa gari aliokuwa akiufana kinga ya kuzuia mashambulizi ya adui aliweza kuona upande wa pili toka kwenye moshi na moto wa uunguaji magari na watu waliokuwa hawajiwezi wanaungua sambamba na gari roho zinanyofoka wakijiona hakuna utetezi wowote, aliona watu wawili wakijitupa mbizi na kupotelea ndani ya gari katika kuona kwake macho hayakumdanganya aliona shepu ya mwanamke hata kama amevaa suruali ya jeans rangi, ‘kishundu’ (kishepu tako) na nywele zilizotuna ndani ya kofia la ninja alilovaa zilizonekana kwa haraka kwenye macho ya mtaalamu Kai.

Kengele ya michale ikapiga kichwani mwake akainua bunduki yake tena akaanza kufyatua risasi mkono ukisugua kifyatulio kama ana mashine alikuwa akijitahidi kulenga matairi na kioo cha mbelealichoweza kukimwaga kikavunjika kwa mashambulizi ya risasi lakini gari ilishawashwa ikaanza kurudishwa nyuma kwa kasi bila dreva kuonekana, Agent Kai akajitokeza na kuanza kukimbilia kule lakini mara aliouona mdomo wa bunduki ukiinuliwa huku ukiyumbayumba kutokana na gari kuwa linayumba yumba nalo hapo Kai alisimimama akageuza na kuudi mbio lilipo gari lao akaruhusu kitufe cha saa yake aweze kuongea mkono ukasogezwa mdomoni.

   “Mwanamke tunayemtafuta anatoroka njooni kwenye gari tuondoke tuwafukuze” Akaongea kwa sauti kubwa ya kupazwa, wenzake wote wakamsikia.

Miller na Silla wakatokea mbio zao ungeziona ungesema wanamkimbia mnyama simba, tayai kwenye usukani alishakaa Norman na akisubiri wenzao waingie aliondoe gari, wakaingia wote kwa pamoja gari likaondoshwa kwa kasi likilengeshwa kwa pembeni ya magari yanayowaka moto.

Gari aliyopanda Koplo Mariana na Mwanajeshi mwenzie mfukuzwa Stafu Sajenti Morientes Gudrado ambaye ndiye alikuwa kwene mskani ilikuwa ishageuzwa na kuwekwa sawa wakati timu pinzani ikiongozwa na Agent Kai gari wanayotumia ilipokuwa inakunja kona kuingia barabara a Zone 10.

   “Wametuacha mbali Norman ongeza mwendo sisi sote humu tayari maisha yetu yamegongwa mihuri ya kuishi maisha hatarishi hivyo usogope chochote kanyaga mafuta tujaribu kuona pengine leo siku ya kumtia mikononi mwetu mwanaharamu wa kike..” Aliongea Agent Kai huku macho akiwa kakazia kuangalia mita za zaidi ya mia nne na mkimbio wa gari inayokimbizwa na Gudrado, gari aina ya FJ Cruiser Convertible ilikuwa ikikimbizwa kwa spidi kubwa sana hadi Norman moyo wake ukitamani Agent Kai aseme ‘basi tuwaache’.

Kasi kama wako kwenye mashindano walikimbia kutoka Zone 10 hadi barabara ya El Tejar mkia unaofahamika kwao ulikuwa haujaacha kuwafuata kwa kasi ile ile mpaka wanafika hapa na taratibu kutokana na msongamano uliokuwepo kule Zone 10 ilisababisha wanaowafukuza kuwasogeza kutoka mita tofauti na za kwanza wakati wanaondoka eneo la bustani ya Mundo Petapa hapo Marianna akatoa simu yake ya mkononi na akatafuta namba za mheshimiwa waziri Ceni.

   “Mheshimiwa waziri tuko matatani tunafukuzwa na watu waliokuwa wanamshikilia kijana niliyekwambia alikuwa na kazi ya kumfuatilia kwa ukaribu Kamanda Muniain kwa kumuomba kwa Kamishina Canedero baada ya watu wetu kumi na tatu kuuliwa kule Filadelifia Café… Walimtumia kutaka kuninasa mimi maana alinipigia simu anahitaji msaada wangu kumbe waliweka mtego” Akaanza kueleza Marianna baada tu ya mheshimiwa Ceni kupokea simu tena wakiwa hawajasalimiana kama ilivyo kawaida yao.

  “Kwanini hukunipa taarifa kazi ingefanyika kwa ushirikiano wenu na watu wangu wa GIS? Wamewazidi vipi nguvu? Kila wakati Marianna unaharibu, mko wapi? Na msaada gani mnataka?” Aliuliza maswali mengi mheshimiwa Ceni tena kwa kasi kama kameza mwendokasi.

   “Maelezo hayakuwa kamili toka kwa Gadiano, pia aliamini katika kila jambo uwa hatukwami.. Muda wa kulaumiana haupo mkuu fanya msaada wa haraka lasivyo tutazidi kuzungushana tu hapa jijini bila sababu maana sidhani kama wanaweza kata tamaa ukiachilia mbali hujuzi wao wa kukimbiza gari unaonyesha si watu wa kuwapuuza!... Tupo barabara ya El Tejar tunakaribia kulipita eneo la Santiago Sacatepequez tuingie San Lucas Sacatepequez tumeingia huku kukwepa msongamano wa katikati ya jiji” Maelezo yenye jibu moja tu kati ya maswali lukuki yaliyoulizwa na mheshimiwa ambayo kiukweli kwa wakati huu walionao ni kero kubwa kwao.

   “Kwahiyo mnaelekea Chimaltenango?” Akauliza Ceni.

   “Ni kama hivyo ingawa haikuwa nia yetu tufike huko na nia yao kuu ni mimi hawa watu”

   “Hao ni hao wa wamarekani tu wakiwa na Norman.. Haraka natuma kikosi changu cha siri cha GIS kabla hamjafika Arililo Perferico watawadhibiti watakuwa pembeni ya barabara, muda huu walikuwa na kikao chao bustani ya Plaza De La Constitution hivyo ni kama bahati wanashuka tu kuja Arililo Perferico” Akamalizia kwa kutoa matumaini mheshimiwa waziri wa usalama Rafael Valdes Ceni, simu ikakatwa na Maianna kisha akageuka kuona wanaowakimbiza wako umbali gani? Akaona wanazidi kuwavuta mpaka akampiga kibao cha bega dreva S.S Morientes Gudrado.

   “Natamani ningekuwa naendesha mimi… Stafu Sajenti umekuwa dhaifu kwenye uendeshaji wa gari..!” Akaongea huku anafunga mkanda wa siti maana hakuwa ameufunga na barabara waliyoko sasa ina baadhi ya sehemu kuna matuta kutokana walikuwa wanakaribia mzunguko wa Vuelta Grande na Santa Lucia Milpas Altas.

Stafu Sajenti mfukuzwa wa jeshi la wananchi wa Mexico aliongeza mwendo zaidi hili amridhishe Koplo msaliti Marianna Caro Funtes dude likakolea kama linataka kupaa huko nyuma Norman yeye ilikuwa ni kupangua tu gia za gari kwakuwa walioko ndani ya gari walikuwa kama hawana mioyo kwenye miili yao toka kitambo tu katika maisha yao uwa wanafanya mengi ya kustaajabu ambayo mpenda kuishi hawezi kuhisi ipo siku atafanya, dude lao nalo mashaallah lilikuwa linapea na kutereza kwenye lami kama kishada cha umeme magari mengine yalikuwa yakijiweka kando kwa jinsi gari zote hizi zilikuwa zikianikiza sauti ya honi za gari zao bila kuacha ni mwendo wa ‘piiiiiiiii iiiiii!!!! piiiiii iiiiii!!!!! piiiii !!!!! tu non stop hili wapishwe na watumiaji barabara iwe wa miguu hata magari.

Walizunguka mzunguko unaoziunganisha barabara ya Vuelta Grande na Santa Lucia Milpas Altas wakakamata ya Santa Lucia Milpas Altas yenya kona kali zinazofuatana kukwepa mabonde yaliyo pembezoni mwa barabara pande zote kwakuwa ilijengwa kwa kuinuliwa kufuata kilima kona tatu kali zilipoisha hapo walikimbia dakika mbili moja kwa moja wakakutana na mzunguko mwingine unaoziunganisha barabara ya chuo kikuu cha Univesidad De San Carlos De Guatemala na Mixco hapo walipomaliza mzunguko Gudrado akaingia Zona 3 De Mixco hapa sasa walikuwa wanakaribia walipoelekezwa kuwa watu wa GIS wanaokula mshahara wa serikali halali ya Guatemala na mshahara utokao kwenye genge analolihudumu boss wao wa siri mheshimiwa Ceni.

Hapa S.S Gudrado akacheza na akili za wafukuza wao akaanza kupunguza mwendo kuwatamanisha kana kwamba wamekata tamaa fulani waliyokuwa nayo kukimbia mbio zaidi.

   “Kuna kitu… Ni kama wamepunguza mwendo usio ule waliokuwa nao.. Michezo hii.. Kuweni makini maana njia hii tumebaki sisi na wao nina mashaka” Akongea Agent Kai kisha akafungua mkanda wa siti aliokuwa kafunga na kujishika katika kishikio cha juu kilicho juu ya mlango kwa ndani, akageuka siti za nyuma kuwaangalia Investigator Miller na Special Agent Silla ambao muda wote walikuwa kimya wakiwa makini kuangalia hatari ya ajali inayoweza kutokea katika mwendo kasi, majasusi wabobezi hawa tena majasusi wanaokwenda site kupiga kazi si wale wanaokuwa kazi zao kuchunguza tu wakiingia matatani ndiyo wanahusika na kashikashi, wao walikuwa wazoefu sana wenye kufanya kazi hii kiuchunguzi na kivitendo pia ndiyo maana kwao kutolewa katika ‘military intelligence’ si kutolewa katika vyuo vingine vya kijasusi vinavyosimamiwa na mashirika kadhaa ya kijasusi ya Marekani yaliyo chini ya ‘National Security Agency’ (NSA).

Agent Kai alipowaangalia wakakonyezana kisha wote wakatabasamu wakatingisha vichwa vyao wakafungua mikanda yao hakuna aliyekuwa hajaona kama kuna dalili za wazi za wafukuzwa wao kuwa wanapunguza mwendo hivyo kuna ujanja unaenda kutumika unaoweza kuwadhuru na kuwafanya wajutie lolote lile maana hata wakiwa wamekutwa na umauti hakuna anayejua pengine watajutia kwa pamoja wakiwa ndani ya umauti wa roho.

Walipokuwa wanamaliza kilima cha Mixco jambo ambalo uwa ishara ya hatari katika milango yake ya fahamu katika mwili wake Agent Kai ilileta taarifa ambazo uwa hazijawai mdanganya kiwepesi, tumbo lilibana na kutoa muungurumo kama ameshikwa na haja.

   “Shiiiit!.... Fungueni milango turukeeeee eeeh..!” Akapaza sauti Agent Kai kwa mbele yao mita kama ishirini kulikuwa na gari dogo aina ya  volkswagon ya kizamani ambao imechakaa ilikuwa inaingia barabarani kama imesukumwa tu maana licha ya kuwa haikuwa na vioo vya madirishani kotekote pia hakuonekana dreva wake ilikuwa imesukumwa tokea kwa pembeni ya barabara kulikokuwa na kilima na mitimiti ya pembezoni mwa barabara.

Kelele wakati zinapigwa na Agent Kai alishakuwa kafungua mlango akaruka bila kuangalia hata anarukia wapi wakati yupo hewani ndipo akaangalia anapoenda kutua ni salama kwake macho yakakutana naenda kujipiga kwenye mti kati ya miti iliyo pembeni.

Mwisho wa sehemu ya sabaini na tatu (73)

Hatari fire! Moto umewaka ndani ya Guatemala ni mwendo wa jino kwa jino!

Mapigano makali ndani ya eneo la bustani ya Mundo Petapa yamepelekea kufukuzana kwa magari baina ya mwanamke anayetamaniwa sana kuingia katika mikono ya Agent Kai.

Wakiwa wanamaliza muinuko wa Mixco hili wateremke wapate kuingia eneo linaloitwa Arililo Perferico Agent Kai anastuka kuwa kuna mchezo na kuwaambia wenzake waruke toka ndani ya gari.

Itakuwaje kwa majasusi awa? Je mti anaokwenda kuuvamia Agent Kai akiwa kwenye ya kuruka toka ndani ya gari itakuwaje kwake?

Majibu ya yote yanayofuata baada ya hapa yanapatikana katika subira yako na kusogea mbele kuona nini kilijiri machoni na ubongoni mwa mtunzi wako.




Agent Kai alipowaangalia wakakonyezana kisha wote wakatabasamu wakatingisha vichwa vyao wakafungua mikanda yao hakuna aliyekuwa hajaona kama kuna dalili za wazi za wafukuzwa wao kuwa wanapunguza mwendo hivyo kuna ujanja unaenda kutumika unaoweza kuwadhuru na kuwafanya wajutie lolote lile maana hata wakiwa wamekutwa na umauti hakuna anayejua pengine watajutia kwa pamoja wakiwa ndani ya umauti wa roho.

Walipokuwa wanamaliza kilima cha Mixco jambo ambalo uwa ishara ya hatari katika milango yake ya fahamu katika mwili wake Agent Kai ilileta taarifa ambazo uwa hazijawai mdanganya kiwepesi, tumbo lilibana na kutoa muungurumo kama ameshikwa na haja.

   “Shiiiit!.... Fungueni milango turukeeeee eeeh..!” Akapaza sauti Agent Kai kwa mbele yao mita kama ishirini kulikuwa na gari dogo aina ya  volkswagon ya kizamani ambao imechakaa ilikuwa inaingia barabarani kama imesukumwa tu maana licha ya kuwa haikuwa na vioo vya madirishani kotekote pia hakuonekana dreva wake ilikuwa imesukumwa tokea kwa pembeni ya barabara kulikokuwa na kilima na mitimiti ya pembezoni mwa barabara.

Kelele wakati zinapigwa na Agent Kai alishakuwa kafungua mlango akaruka bila kuangalia hata anarukia wapi wakati yupo hewani ndipo akaangalia anapoenda kutua ni salama kwake macho yakakuta anaenda kujipiga kwenye mti kati ya miti iliyo pembeni.

ENDELEA NA DODO ASALI..!!

HOFU PANDE ZOTE I

ZONA 3 DE MIXCO, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Detective Norman akiwa katika spidi ambayo hakika ni spidi zinazokaribia kumaliza spidi mita za gari anayoendesha,  alisikia kelele za Agent Kai na aliliona gari chakavu lilivyokuwa linavyoporomoka mkono wake wa kulia katika siti ya dreva alipokaa ulitakiwa acheze nao kufungua mlango wa gari aweze kuruka lakini akili yake ilichelewa kwenda na spidi ya mwendo alionao hivyo hakuona njia ingine zaidi ya kulizungusha gari kuendea upande wake aweze kulikwepa  gari chakavu au kugongana kwa upande upande ambao alikuwa kakaa Agent Kai ambaye muda huu alikuwa hayupo ndani ya gari, kiukweli ndani ya gari alibaki mwenyewe sekunde hii anafikiria alikuwa anawaona wenzake wanajirusha.

Breki iliminywa bila kupangua gia kisha usukani ukazungushwa kwa nguvu mlalamiko wa msuguano wa lami na kashata za tairi ukasikika mpaka harufu na moshi ukaonekana kati ya lami na matairi ukifuatiwa na mshindo wa mzinga wa mgongano alifanikiwa Norman kulibamiza gari upande lakini hakuweza kuzuia mpinduko na kisha kufuatiwa na kubingirika kwa gari ikiendea kwa pembeni ambako kuna msingi mtaro baada ya hapo kuna miti iliyopandwa kando ya msingi mtaro.

Upande wake Agent Kai aliuona mti ambao kiharaka alijua anaenda kujipiga kichwa asipojiseti vizuri hivyo aliulazimisha mwili kujipindua kwakuwa si mambo mageni kwake na wepesi aliojaliwa na Mungu, tumbo likajipiga katikati ya mti ule kwa nguvu sana kisha mapaja yote mawili nayo yakajipiga kwa maeneo ya mifuko ya mbele ya jeans aliyovaa mpaka akaona nyotanyota machoni kwa maumivu akajikuta anaenda chini akijipiga pia kwa nguvu kwenye kingo ya msingi mtaro kwa mkono wa kulia uliokuwa unatafuta balansi ya kumfanya atue vizuri ulijikunja na kumletea maumivu akabingirika bila kupenda kuelekea kwenye mtaro msingi wa pembeni ya barabara iliyojengwa kwa dhumuni la kupitisha maji ya mvua ambao mruko wake ulikuwa umeuruka kwakuwa ulikuwa unaanza wenyewe ndiyo ufike ilipo miti ya pembeni, mtaro msingi huu ulikuwa mrefu kidogo kwenda chini akatua na kupokelewa na tope maji zito kidogo lililoweza kumpoza asiumie hapo fahamu zilizokuwa zimemuhama kwa mbali zilimrudia kwa tope maji kuwa na ubaridi akajiinua kwa nguvu asizame kwenda chini mwili wote ukiwa na matope.

Akakumbuka wenzake baada ya masikio yake kupokea sauti ya mshindo wa mzinga wa mgongano anaoujua kutokana na uzoefu wake kuwa ni mzinga wa mgongano wa magari, maumivu ya mkono hakujali akasimama kutizama eneo la tukio kwa urefu wake akawa anaona vizuri upande wa kichwa chake ukiwa wote umetokeza.

Alishuhudia gari yao inavyobingirika na kile ki-volkswagon chakavu kikiwa kimeamishwa hatua nyingi toka kilipokuwa kimeporomoshwa, haraka akageuza macho yake upande wa pili wa barabara akawaona kwa pamoja Miller na Silla mmoja akiwa anagaragara kwa kasi kuelekea ulipo msingi mtaro na si kama anapenda ni kasi ya kuruka toka ndani ya gari huyu alimtambua ni Special Agent Silla na upande mwingine Investigator Miller alikuwa naye anabingirika akiwa katikati ya barabara huyu laiti kungekuwa na gari nyuma yake asingepona endapo ungekosekana umakini wa dreva wa gari ambayo ingekuwa kwa nyuma na hata yeye mwenyewe.

Kule ilipotokea gari ndogo chakavu kwa minajili iwasababishie ajali walitokea watu idadi yao kama saba wakiwa wamevaa suruali za jeans nyeusi na makoti ya ngozi rangi nyeusi pia usoni mwao walivaa kofia za kininja wakiwa wanaonekana macho tu, kila mmoja mikononi mwao walikuwa wamekamatia bastola hakuna aliyekuwa na bunduki za kivita.

Kila mmoja alikuwa makini na walikuwa wakitupa macho yao huku na huko kufuatana na vichwa vyao vinavyowapeleka, waliingia eneo la barabara watatu wakakimbilia ilipotuama gari huku wanne wakiinua mikono yao kuweka bastola zao mbele tayari kwa matumizi kumshambulia Miller endapo ataonyesha dalili zozote za hatarishi kwao hakuna aliyekuwa akiangalia eneo alilopo Agent Kai hii ilimaanisha hawakumuona ambaye naye kama paka akainama akibakiza kisehemu cha kuona akishukuru matope yaliyomzunguka uso wote na kumuacha machoni tu pia hawakuwa wakiangalia upande wa msingi mtaro aliotumbukia  Special Agent Silla hii ilimaanisha naye hawakumuona.

Jamaa wanne wanaokuja kwa kunyata kuja alipolala Miller walisogea bastola zao zikiwa zimetanguliza tundu zake mbele wakipiga hatua zinazorandana na hata wale wanaoelekea kule ilipolala gari waliyoitega ikiwa imelalia ubavu sehemu ya mbele imeingia mtaroni nao walikuwa wakinyata kama hawa wanne hakuna alieongea kitu na Agent Kai alikuwa akiona kila kitu tokea ndani ya mtaro.

Investigator Miller si kama alikuwa amezimia au amekufa au amejeruhiwa kiasi cha kushindwa kuinuka toka pale alipo hapana haikuwa hivyo bali alipokuwa akipinduka pinduka kwa kasi ya kuruka toka kwenye gari alipoweza weka kituo tu alijigundua lami imemla sehemu za mikono yake na kumuacha na michubuko kadhaa wa kadha inayovuja damu akiwa ameokolewa na koti alilovaa kwa ajili ya kujikinga na baridi ya Guatemala iliyopo majira haya ya wakati huu ambapo hata mchana uchapa kweli kweli, aliwaona watu wale wakitokea kule ulipotokea mgongano wa gari wakiwa na silaha mikononi mwao hivyo alitambua ujanja wowote atakaoufanya utayagharimu maisha yake kwa kifo, aliona anatakiwa kutulia kana kwamba amepoteza fahamu akiwa kalala kifudifudi kwenye lami katikati ya barabara maana hata bastola yake aliyokuwa kaipachika nyuma ya kiuno ilikuwa imemtoka na kuwa pembeni yake toka alipolala hatua nne hivi.

Wa mbele alipomfikia Miller alimkanyaga kwa mguu wa kulia kisha kwa kutumia mguu wake huohuo akatumia nguvu kumsukuma apinduke chali bastola ikiwa makini kutumika endapo kutatokea janja janja anavyompindua, Miller akapinduka akiwa kafunga macho akijitahidi kupumua kwa mbali ingawa ilikuwa si rahisi sana kuekti hivyo, wakasogea wote wanne na kumzunguka mmoja akamvua kitambaa alichojifunga kujiziba uso sasa wakawa wanamuangalia vizuri.

Agent Kai alishuhudia yote hayo toka mtaroni hatua za mtu mzima zipatazo sita tu akitamani kufanya kitu lakini ilikuwa si rahisi kwake kwakuwa hata bastola ambayo angeitumia kwa umbali huu wa hatua sita hakuwa nayo na yeye ilikuwa imemdondoka na kuzama kwenye tope bila yeye kutambua  wakati anabingirishwa kuja msingini ilishatoka, alichoweza kufanya aliinama zaidi kujilinda asionekane akihofu hata kujisogeza maana matope aliamini yatasahau kama yeye ni ‘The Sole Cat’ na kutoa mlio wa kuinua kwake mguu au kufanya mjongeo.

Kule kwenye gari jamaa watatu walifika na kukuta mlango umembana Detective Norman huyu sasa ni kweli alichelewa kuruka wakati anafanya mgongano wa ubavuni, kubingirika kwa gari kwa mibingiriko kadhaa hivi ilimfanya apoteze fahamu ikiwa bahati yake aliweka mahala palipoweza kumfanya asibanwe zaidi, jamaa walimchomoa kwa kuuvuta mlango kwa nguvu wakamtoa nje ya gari.

Waliwaburuza mpaka eneo walilokutana kwa pamoja kisha mmoja wao akatoa simu yake ya mkononi akatafuta namba aliyohitaji.

   “Halloo mkuu!” Akaongea kwa simu kwa sauti ambayo hata Agent Kai aliisikia toka mtaoni alipo lakini hakuweza sikia wa upande wa pili anajibuje akasikia akiongea tena tu.

   “Norman na mwingine mwenye asili ya rangi ya waafrika na kizungu atakuwa ni chotara huyu..”

Ukimya ukapita kidogo kisha akaongea tena.

   “Nafikiri walikuwa wawili tu sababu kwa mwendo waliokuwa nao na mtego tuliouweka wasingeweza kuruka na kufika chini salama ndiyo maana huyu mmoja aliyeruka naye pia amezimia… Wote wamezimia mkuu!” 

Kikapita kimya kirefu kidogo jamaa akisikiliza kwa umakini wenzake wakiwa wamekaza macho kumuangalia na pia wakiangalia huku na huko, mtaa huu ulikuwa na nyumba zilizoko mbali na barabarani hivyo macho umbeya hayakuwepo na hata waliotamani kushuhudia waliishia huko huko wakihofia kuingia matatizoni.

   “Sawa mkuu.. Tunawapeleka!” Alimalizia hivyo na kukata simu, aliporudisha tu mfukoni akatoa maelekezo kwa wenzake ambayo Agent Kai hakuwa anayasikia ukasikika mlio wa gari ikitokea kule walikoweka mtego kwenye barabara inayochepuka, ikajitokeza ilikuwa ni gari aina ya Lekkon Volkswagon, gari ambazo mtu wa mambo ya usalama katika nchi ya Guatemala akiiona tu utambua walio ndani ya gari hii au kama ameshuka ni wanausalama toka shirika kuu la kijasusi la Guatemala la ‘GIS’, waliwaingiza kwenye gari watu waliowanyanyua wakiamini wote wamezimia kumbe mmoja hajazimia, gari ikatiwa gia na kuondolewa kasi kuelekea ilipoelekea gari iliyowaponza kina Agent Kai wakimfukuzia mwanamke wanayemtafuta kwa hamu zote.

‘The Sole Cat’ akajitoa toka mtaroni akiwa na maumivu makali tumboni yaani kama angekuwa si mtu wa mazoezi naamini yangekuwa makali zaidi anayoyasikia yeye kama si kumfanya ashindwe hata kutoka mtaroni bila msaada wa mtu, mkono wake wa kulia ulikuwa ukipwita kwa maumivu mpaka akawa anang’ata meno kupunguza ukali wa maumivu ya sehemu mbalimbali anayoyasikia.

Alipoanza kuvuka barabara tu hili aende kwenye mtao wa upande wa pili macho yake yakakutana na macho ya Special Agent Silla akiwa naye anajitokeza toka kwenye msingi mtaro aliojikuta akitupwa humo, naye alikuwa aking’ata meno kama anavyong’ata ‘TSC’, ilikuwa ikileta maana kuwa naye alijificha tuli asionekane kwa maadui ila yuko mzima ukiacha maumivu ya kubingirishwa wakati anajitupa toka ndani ya gari.

   “Huko sawa?!” Akauliza Agent Kai akimuuliza akitamani akimbie kumsogelea aweze kumvuta toka msingini lakini na yeye maumivu yake yalimfanya asifanye hivyo.

   “Kabisa! Niko sawa ni michubuko tu, shukrani kwa koti nililovaa kuzuia baridi lasivyo kwa jinsi nilivyojipiga kwenye kingo ya msingi hali ingekuwa tata… Vipi wewe?” Akajibu na kuhoji Silla huku wote wakigeuka kuangalia kwa juu kulikuwa na watu wa nyumba za jirani wanakuja eneo la tukio kushuhudia nao wapate cha kuhadithia kama ilivyo nchi nyingi duniani hali hii ni kawaida ingawa awa ni kama walichelewa kidogo kufika.

   “Tuondoke hapa… Tusipite kufuata barabara kuu , twende yalipo makazi angalau tuombe maji ya kuondoa matope haya!” Akaongea tena S.S Silla akamshika bega ndugu yake wakasaidizana kutembea zinakoonekana nyumba za kando ya barabara.

Walikwenda wakipishana na watu wanaokuja barabarani lakini walikuwa wakipewa pole tu bila watu wale kutaka kuwasaidia angalau kuwakokota, Mungu saidia wakafika kwenye nyumba ya kwanza kabisa wakaomba maji kwa mwanamke waliyemkuta anatoka ndani naye akitamani aelekee barabarani kushuhudia lakini ikambidi aikatizie nia yake akawasaidia maji wakanawa, walipomaliza kunawa matope wakaanza kusikia ving’oa vya gari za polisi.

   “Polisi wanakuja inabidi tuondoke eneo hili sasa.. Tuendelee juu!” Akaongea Agent Kai akiwa sasa anajisikia vizuri mwilini, walimuita mama aliyewasaidia wakatoa noti mbili za Guatemala wakampa kama shukrani kisha wakamuuliza njia nzuri wasiweze rudi barabarani mama hakuwa na hiyana akawaelekeza haraka haraka akiwa na wasiwasi na furaha ndani yake ya kupata kiasi cha pesa alichopewa.

Haraka Agent Kai na S.S Silla waliondoka wakifuata maelekezo nguo zao wote hazikuwa na hafadhali zilikuwa na matope hivyo kila walipokutana na mtu hakuacha kuwakatia shingo wao hawakujali wakawa wanakaza mwendo mpaka walipofika mahala ambapo kulikuwa na barabara ya vumbi wakiacha vinjia vidogowalivyokuwa wanapita.

Hapa walisimama chini ya mti mkubwa wa mkuyu ulioko pembezoni mwa barabara wote bila kuambiana wakajisachi mifukoni na wote wakaibuka na simu wakaangaliana na kutabasamu.

   “Nataka nimpigie simu Rebecca atufuate lakini kumbe hata simu yangu imeharibika nafikiri nilipojipiga kwenye mti mpigo ulivunja nah ii simu na hata ingekuwa nzima jinsi ya kumuelekeza tuko wapi ingeniwia shida kweli..!” Akaongea Agent Kai akiwa anatabasamu simu yake mkononi ikiwa imevunjika kioo.

   “Tumefanya kosa kutouliza kwa mama yule kuwa tuko sehemu gani huku..” Akajibu Silla macho yakiangalia kwa juu inapotokea barabara maana walikuwa wakisikia muungurumo wa gari inajia huku.

   “Tuisimamishe hiyo gari inayokuja.. Saa yangu ya mawasiliano nayo ndiyo naiona imevunjika na kifaa cha masikioni cha Bluetooth earphone sina sikioni” Akaongea Agent Kai akijisogeza usawa wa mti hili wasionekane inapotokea gari uso wake ukiwa unalazimisha tabasamu.

   “Hatari kaka.. Mimi saa nzima lakini pia sikioni sina kitu hata simu kama unavyoona kioo kimeachia chote… Hahahaha.. Sijui itakuwaje lakini nashukuru bastola kubingirika kote ipo kiunoni kana kwamba niliigandisha na gundi” Akaongea Silla kisha akatoa bastola na kuikagua haraka huku anarudi nyuma usawa wa mti kama alivyofana mwenzie.

Gari ilitokea ilipokaribia tu Silla hakusubiri akakimbia katikati ya barabara akiwa anaiangalia gari mkononi bastola ikilenga kioo usawa wa dreva na mkono wa kushoto anamuonyesha ishara asimame lasivyo anaachia risasi.

Dreva wa gari ndani ya gai hakuwa peke yake alikuwa na wenzake wawili mmoja siti ya mbele na mwingine siti ya nyuma ya abiria lakini kuona mdomo wa bastola mbele alisimama tena hakukumbuka kupangua gia hadi gari ilisereresha matairi mpaka hatua nne tu toka aliposimama Special Agent Silla.

  “Wote shukeni kwenye gari!” Akapaza sauti Silla akitumia kilatini mdomo wa bastola ukihimiza kufuata amri ya kiganja cha mkono wake wa kulia ulioshika bastola.

Majamaa wa kizungu wote watatu waliokuwa ndani ya gari walishuka kwa kasi kufuata amri waliyoamrishwa na Silla.

   “Kaeni sehemu moja na mpige magoti” Akasema tena Silla uso akiwa kaukunja ingawa ulikuwa ndani a soksi ninja aliyoishusha wakati anaingia barabarani kuzuia gari.

Agent Kai alijitokeza na wote wawili wakaingia ndani ya gari hii ndogo inayochukua watu wanne aina ya vitara, Kai alishika usukani akatia gia kwakuwa haikuwa imezimwa akaiondoa kasi kuelekea kule walipokuwa wakielekea waliowapora gari yao.

   “Hii kaka! Ukisikia jino kwa jino ndiyo hii.. Khaaah!” Akaongea Silla akijitizama kwenye kioo cha ndani ya gari.

   “Yah! Kile ambacho tulikifanya juzi wakati tunamuokoa Kamanda Muniain ndicho walichofanya wao kutusubiri… Jino kwa jino… Tuna kazi ya kuwaokoa wenzetu ila mkono wangu wa kulia hali tete” Akakubali kuwa ni jino kwa jino Agent Kai.

   “Kawaida hiyo mkuu… Umeumia padogo sana”

   “Yah! Ni kweli kabisa… Wenzetu wameumia zaidi.. Ila jamaa wale hawafanani na TRJ wale watakuwa ni majasusi wa usalama wa GIS, naikumbuka gari ile ni kama ile tuliyoitega kona ya Chimaltenango na Jocotenango nakumbuka Norman alisema ni gari zinazotumika na majasusi wa GIS, waziri wa usalama ameharibu kabisa vyombo vya usalama vya nchi hii, natamani nikamuangamize..” Akaeleza Agent Kai kisha akakunja kona kuingia barabara ya lami ambayo muda si mrefu waliingia matatani, akakunja kuelekea kurudi walikotoka hili wasipotee maana wao si wenyeji na ndiyo maana Norman uwaendesha katika safari zao.

  “Tupite yalipo maduka ya simu tupate simu zingine..!” Akatoa wazo S.S Silla alipoona Agent kai anaitizama simu yake wakati yeye Silla anaitoa laini.

  “Karibu na hotel niliyopanga kuna duka la simu… Jina la mtaa ni 5A Avenida kama sikosei, shida hali tuliyonayo nguo hizi zinanuka tope” Akakubali wazo la Silla lakini akaweka hoja ya nguo na wote wakajiangalia kisha wakacheka kwa sauti na kufanya wapatwe na faraja kubwa sana licha ya kuwa walikuwa na maumivu ya vidonda vya michubuko hasa mikononi.

Mwisho wa sehemu ya sabini na nne (74)

‘GIS’ wamefanikiwa kuwatia maumivu kikosi cha timu ya kina Agent Kai, hasara ya gari na hasara ya kuumizwa miili yao inawakuta baada ya kuingia mtegoni.

Norman na Miller wapi wamepelekwa na watu hawa waliowateka?

Nisimalize muda wako sogea kurasa ingine!




   “Hii kaka! Ukisikia jino kwa jino ndiyo hii.. Khaaah!” Akaongea Silla akijitizama kwenye kioo cha ndani ya gari.

   “Yah! Kile ambacho tulikifanya juzi wakati tunamuokoa Kamanda Muniain ndicho walichofanya wao kutusubiri… Jino kwa jino… Tuna kazi ya kuwaokoa wenzetu ila mkono wangu wa kulia hali tete” Akakubali kuwa ni jino kwa jino Agent Kai.

   “Kawaida hiyo mkuu… Umeumia padogo sana”

   “Yah! Ni kweli kabisa… Wenzetu wameumia zaidi.. Ila jamaa wale hawafanani na TRJ wale watakuwa ni majasusi wa usalama wa GIS, naikumbuka gari ile ni kama ile tuliyoitega kona ya Chimaltenango na Jocotenango nakumbuka Norman alisema ni gari zinazotumika na majasusi wa GIS, waziri wa usalama ameharibu kabisa vyombo vya usalama vya nchi hii, natamani nikamuangamize..” Akaeleza Agent Kai kisha akakunja kona kuingia barabara ya lami ambayo muda si mrefu waliingia matatani, akakunja kuelekea kurudi walikotoka hili wasipotee maana wao si wenyeji na ndiyo maana Norman uwaendesha katika safari zao.

  “Tupite yalipo maduka ya simu tupate simu zingine..!” Akatoa wazo S.S Silla alipoona Agent kai anaitizama simu yake wakati yeye Silla anaitoa laini.

  “Karibu na hotel niliyopanga kuna duka la simu… Jina la mtaa ni 5A Avenida kama sikosei, shida hali tuliyonayo nguo hizi zinanuka tope” Akakubali wazo la Silla lakini akaweka hoja ya nguo na wote wakajiangalia kisha wakacheka kwa sauti na kufanya wapatwe na faraja kubwa sana licha ya kuwa walikuwa na maumivu ya vidonda vya michubuko hasa mikononi.

ENDELEA NA DODO ASALI…!

HOFU PANDE ZOTE II

LAS ANONAS, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Nje ya mji wa Antigua moja ya miji mikubwa inayounda jiji la Guatemala linapatikana eneo linaloitwa ‘Las Anonas’ eneo linakopatikana jengo lenye jengo la juu na chini (handaki) linalotumiwa kwa siri na majasusi walio katika kitengo kisicho rasmi kinachomtumikia mkurugenzi mkuu wa shirika kuu la kijasusi la Guatemala Intelligence And Security (GIS) ambaye ni kibaraka wa mheshimiwa waziri wa usalama Rafael Valdes Ceni.

Jengo hili lililojengwa katikati ya kiwanja kilichozungushiwa senyenge chenye ukubwa wa mita mia moja bila nyongeza lilikuwa ni jengo ambalo miaka kama mitatu iliyopita lilikuwa likitumika kama ghala la kuhifadhia vipuri vya mashine za kiwanda kahawa cha Mr. Alexis baada ya mheshimiwa waziri wa usalama Ceni kuteuliwa kuwa waziri na mheshimiwa Rais basi Mr. Alexis alilitoa jengo hili na eneo kumpa waziri kama zawadi naye akamkabidhi mkuugenzi wa usalama wa taifa anayeongoza GIS naye akaona matumizi yanayofaa ni kuligeuza kuwa jengo la kuwatesea watu wanaoenda tofauti na mambo yao.

Wanaume wa kazi walioongoza shambulizi la kuvizia kwakina Agent Kai huko eneo la Mixco walifika kwenye jengo hili wakiwa na mateka wao wawili ambao ni mtu waliyekuwa wakimtafuta sana Detective Norman wa ‘Oganized Crime Of Latin America’ (OCLA) pamoja na Investigator Miller kwa amri za maboss zao mateka awa iliamriwa waitiwe daktari anayehusika na huduma za watu awa wanaokula mishahara miwili sababu wako serikalini na wapo kitengo cha pembeni cha genge la TRJ.

Daktari alifika kwa muda muafaka akawapa huduma waliyostahili Miller na Norman kisha akawapiga sindano za kutuliza maumivu na sindano ya kufana wapumzike kwa masaa kadhaa hili watakapoamka tu wapelekwe chumba cha mahojiano wakiwa chini kwenye handaki lenye huduma zote kiasi ya kwamba ukifika wewe kwa nje huko juu kama hautaambiwa juu ya uwepo wa handaki hili huwezi kujua kama chini kuna handaki kwahiyo hili jengo ni kama ghorofa la flour (losheni) mbili 

   “Nishawapatia matibabu mmoja ambaye ni mzungu mwenzetu alivunjika mbavu mbili na pia sikio lake kwa pembeni kidogo lilikuwa limevia damu kwakuwa alijigonga wakati wa ajali huyu unafuu wake unaweza kuwa baada ya siku mbili nimemchoma sindano ya usingizi maana akiwa macho anaweza akawa anapiga kelele kwa maumivu.. Yule nigga! Maumivu aliyokuwa nayo ni mikononi na kichwani kidogo huyu akiamka toka katika sindano ya kupumzika niliyomchoma mnaweza anza kumuhoji tu mtakavyo ila msimtese sana kwakuwa kichwa chake kina maumivu makali pale alipo na ndiyo maana nimempiga sindano ya usingizi ingawa yeye si ya kumfanya alale kwa muda mrefu zaidi” Yalikuwa ni maelekezo ya daktari akimuelekeza mtu mmoja mwanaume aliyeshiriki na kuongoza shambulizi la kuvizia kwakina Agent Kai na wenzake.

   “Sawa haina shida.. Mheshimiwa amesema atafika hapa akiwa na kina Gudrado kwa ajili ya kuwahoji hivyo nafikiri kwa muda unaosema wakifika watakuta tayari nigga kaamka” Akakubali maelezo na kisha waliongea mambo mengine kidogo kisha daktari aliondoka akiahidi kurudi kesho asubuhi kufana ukaguzi kwa wagonjwa wake.

Li saa li moja baada tu ya daktari kuondoka na hata baadhi ya watu wengine wa ‘GIS’ kuondoka wakibaki wachache nyuma ya saa kadirio alilokadiriwa na daktari wakati anatoa ripoti yake, Investigator Miller alizinduka. 

Kwa mara ya kwanza aliporejewa tu na fahamu alifumbua macho yake yote na haraka akajiwa na kumbukumbu kuwa hayuko mahala palipo na uzuri kwake hivyo akafumba macho tena kisha akayafumbua taratibu akiacha eneo dogo la kuona kama ujuavyo majasusi awa wana njia nyingi za ujanja ujanja kwenye mambo mengi ya kuwafanya wawe wasanii wa kutupwa mabingwa wa uongo uongo kuliko hata wacheza michezo kama basketball na soka walio na uongo mwingi wanapokuwa wanawachenga maadui zao wanaopambana nao uwanjani.

Mwanga wa taa ulikuwa mkali ukimmulika usoni na kuleta wekundu katika ufungaji wake wa macho kwa ndani akawa anaona hivyo, aliweza kusikia kimtambo alichounganishwa nacho kinachofuatilia mapigo yake ya moyo kikitoa mlio aliouzoea mara nyingi anapozirai na kupelekwa hospitali anapozinduka anakutana na kimtambo hiki na si yeye hata wenzake uwa hivyo.

Alijitingisha pole pole aweze kuona kama amelazwa tu pale kitandani au hajalazwa peke yake amefungwa na vizuizi, aliweza tambua mikono yake imefungwa kila upande husika na vyuma vya pembeni ya kitanda hiki cha chuma hapa akaona kuna kizuizi hakuna analoweza fanya kati ya mengi ambayo angeweza kuyafanya endapo mikono yake ingekuwa huru.

Hakuwa huru! Alikuwa amefungwa kuanzia mikono hadi miguu hivyo akaona hakuna jinsi afungue macho tu hana ujanja, atakuaje na ujanja kwa kufungwa jinsi alivyofungwa tena na minyororo, akafungua macho na kuangalia dari ya chumba alichomo kwakuwa alilazwa chali, chumba kilikuwa na dari ya zege iliyopakwa rangi nyeupe, akarudisha shingo pembeni kulia hakuwa mbali na ukuta wa chumba hatua moja tu hapa akaelewa kitanda alicholazwa kipo pembeni karibu na kona ukutani, akarudisha shingo kushoto kwake hapo hatua nne aliona kitanda kingine hiki kuna mtu amelazwa akiwa kawekewa dripu ya maji dawa, Miller akatikisa kichwa chake na kufinya macho yake akafumbua na kuangalia tena kuhakikisha anachoona hapo aliweza kumuona kiupande aliyelazwa alimgundua ni wa timu moja naye ni Norman aliyelazwa pale akiwa hoi hajitambui maana uso ulionekana umevimba hasa kwenye paji la uso kuja pembeni hadi shavu la upande huu anaouona vizuri Miller.

 Sasa hapa akavuta kumbukumbu ni nini kimewakuta na kuwafanya wawe hapa katika hali hii aliweza kukumbuka kila kitu akikumbuka jinsi walivyoletwa hapa akiwa anajitambua lakini akiwa anaekti amezirai hajitambui, alikumbuka jinsi alivyoletwa katika chumba hiki akiendelea kujizuia kufumbua hata kidogo macho yake maana alikuwa akihisia tu amezungukwa na watu wakijadili mambo ambayo aliyasikia vizuri mwisho wa yeye kuwa na katika kujielewa kwake ilikuwa ni pale alipochomwa sindano aliyohisi ni ya usingizi, swali kuu alilobaki nalo kwa wakati huu wako wapi yeye na Norman? Je kina Agent Kai na mwenzake Special Agent Silla wako wapi? Kwanini wako wao tu hapa? Je Kai na Silla walifanikiwa kukimbia eneo la tukio na kutoonekana na hawa majahili? Haya yalikuwa maswali yaliyomfanya kichwa kiwe kinamuuma.

Alimuangalia tena Norman kisha akatikisa kichwa chake kwa uchungu, moyo ulimuuma sana Investigator Miller akitamani angefanya kitu aweze kuinuka na kwenda kumuangalia vizuri ndugu yake, wakati akiendelea kuwaza akasikia nyayo za mtu anayejongea kutembea kuijia kwa nje ya mlango wa chumba hiki walichomo tena wakiwa wameachwa peke yao muda huu ambao hakuwa anaujua ni saa ngapi, hatua za mtu yule aliyevaa viatu ambavyo milio ya ukanyagi wake kila anapopiga hatua jibu la haraka kwa mtu anayemsikia mtembeaji huyu anaweza kutambua amevaa viatu aina ya skuna kama ni mwanamke na kama ni mwanaume itakuwa dizaini ya moka, hatua ziliacha kusikika ikiwa ni karibu kabisa na mlango hapo Investigator Miller aliukodolea macho mlango kuona ataingia mtu wa aina gani?.

Mlango ulifunguliwa akaingia mwanamke mrefu haraka Miller akafumba macho yake akijifanya hajarejewa na fahamu, mwanamke wa kizungu mrefu aliyevaa suruali ya jeans rangi ya bluu inayobana toka juu mpaka chini akiwa na kiblauzi kitopu cheusi na juu akiweka kikoti cheusi na juu akisindikiza na kikoti cha jeans rangi mfanano na suruali aliyovaa, mkononi mwake alikuwa na kisinia cha pembe nne kikiwa na chupa za dawa pamoja na pakti ya sindano sirynge.

Alisogea alipo Investigator Miller akamuinamia kisha akambinjua kope ya jicho na bwana kuekti alipoguswa tu jichoni akalegeza kope zake kwani alijua mtu huyu anataka nini kwake, kope ilipobinjuliwa hili mwanadada aone ndani bwana kuekti akalifanyisha jicho liwe kama linavyokuwa kwa wanaozirai, mwanadada akaiachia kope akamuwekea kipima katika kifua chake eneo la moyo akampima pima pale kisha akageuka kwenda kwa wa upande wa pili ambaye ni Norman napo akaanza kumpima ndipo Miller akafungua macho na kuigeuzia shingo upande akawa anamsahili vizuri kwa kutokea mgongo wa mwanamke huyu.

Dakika tano mpaka sita zilipita mwanamke akiendela na vipimo vyake kisha akapiga hatua moja ilipo chupa ya dripu hapo akaongeza ongeza baadhi ya vitu katika sehemu inayotumika kwa spidi ya dawa kuporomoka kwenda mwilini kwa mgonjwa, alipomaliza pale akageuka upande wa Miller akiwa ambapo haraka bwana kuekti akajirudisha alivyokuwa.

Mwanadada akasogea hadi pale hii ilimpa uwoga kidogo Investigator Miller kwakuwa hakuna kitu anachokichukia kama kuwekwa dawa mwilini mwake ambazo yeye hatakiwi kuzitumia hata iweje, kurudi kwa mwanadada huyu eneo la kitanda alicho yeye ilimstaajabisha na kumpa hofu hii akatamani afungue macho kuona anataka kumfanya nini? Lakini alijiambia awe na subira hawezi juwa kama itajulikana ameshakuwa tayari na fahamu iliyo kamili watamfanyaje ingawa kiuhalisia wa kazi hizi za kazi kama ajuavyo yeye atatakiwa kwa mahojiano yatakayoambatana na kulazimishwa mengi kati ya wanayoyataka watu hawa iwe kuyajua au kutekelezwa kwa kupitia yeye.

Mwanadada huyu wa kilatini alisimama dakika moja nzima akimtizama Miller mpaka ikawa inazidi kumtatiza Miller pengine amegundulika anaekti au ni nini? Lakini baada ya dakika kupita mwanadada huyu mwenye taaluma ya u ‘medical assistant’ akiwa ameajiriwa na ‘GIS’ kwa shughuli zinazohusu mambo ya tiba za majasusi wa shirika hili lakini vile vile kama walivyo waajiriwa wengi wa ‘GIS’ kuwa pia wanamfanyia kazi mheshimiwa waziri wa usalama Rafael Ceni naye vivyo hivyo alikuwa akimfanyia kazi mheshimiwa hivyo alikuwa akilipwa mishahara miwili kwa mwezi kama wengine wanaofanya kazi huku na huku.

Mwanadada alipiga hatua kama ananyata kuelekea mlangoni ikabidi Miller afumbue macho aone akamuona akinyata kuelekea mlangoni lakini bila kueleweka ananyata kwa sababu gani? Alipofika pale aliubana mlango na komeo kisha akarudi lakini safari hii si kwa kunyata kikawaida ilikuwa kwa kasi mpaka alipo Miller ambaye alishafunga macho yake.

Mwanadada alifikia kwenye shuka alilofunikwa Miller akamfunua eneo la tumboni kuja kiunoni hali ya ubaidi aliyoipata Miller ilimtambulisha amevuliwa suruali yake lakini alikuwa akijihisi tu amevaa chupi yake aina ya boxer ambayo aliivaa asubuhi wakati amemaliza kuoga na kuvaa nguo kama ilivyo ada.

Mwanadada nesi aliposhusha shuka alitupa macho yake kumuangalia Miller ambaye sasa aliamua kufumbua macho kwa mbali kushuhudia anataka kufanywaje na mwanamke huyu, akasikia akishushwa boxer yake na mara akaanza kupapaswa mdudu (uume) wake unaomfanya yeye kuitwa mwanaume, mikono ilikuwa laini sana mpaka ikaanza kumletea msisimko bwana kuekti, mdudu akapapaswa dakika nzima kisha mwanadada akainama na kuanza kuunyonya alipoona unaanza kusimama taratibu, aliunyonya kifundi sana mishipa ya uume wa Mille ikaanza kupokea hisia zilizopelekwa kwenye ubongo wake mpaka akaanza kusisimkwa na kuanza kutamani matamanio ambayo hakutaraji anaweza kuyatamani eneo kama hili lisilo salama kwake na Norman.

Mwanadada nesi alipoona uume wa Mille umesimama vizuri mishipa hadi mzizi wa chini umetuna kiasi kikubwa alianza kuunyonya huku anajichezea tupu (uchi) wake kwa kutumia mkono wake wa kushoto alioutumbukiza kwenye suruali yake baada ya kujifungua zipu na kuishusha suruali mpaka magotini kisha aliishusha na chupi yake aina ya bikini mpaka ilipozuiliwa na suruali jeans yake alianza kujichezea kwa kasi huku mkono wa kulia ukisapoti mdomo wake unaoingiza na kutoa uume wa mgonjwa aliyemtamani toka wapo yeye na dokta wanawapa huduma za kitabibu, uhondo wa unyonyaji huku anajichezea kwa vidole vyake uliendelea kwa dakika mbili spidi ikizidi sana mara akaacha na kumchezea akapanda kitandani.

Uvumilivu ulimshinda Investigator Miller akaona akizubaa anaweza bakwa na kupatwa hata na ugonjwa isivyo na faida kwake ingawa ibilisi wa ngono alishasimama dede katikati ya utosi wake mpaka mate yalimjaa mdomoni akitamani kufilimba tunda (hapana chezea utamu), alijitingisha mwanaume kisha akakohoa kikohozi umbeya maana kilikuwa cha chini kabisa akijifanya ndiyo anazinduka na kurejewa na fahamu.

Nesi alishtuka akashusha mguu wake wa kushoto uliokuwa ndiyo unataka kumruka eneo la kiuno mwanaume hili aanze kujigegedea utamu, akashuka na kusimama mwili ukitetemeka kiasi ambacho kama angekuwa kajificha kichakani kichaka kingejitingisha majani yote na kustukiwa iwapo angekuwa anatafutwa iwe na mapolisi, wanausalama wengine, maadui au vinginevyo, alibaki akitumbua macho kumuangalia Miller usoni huku akipandisha chupi yake ya bikini kwa kasi ikifuatiwa na suruali akamalizia na kufunga kifungo tu akiacha zipu.

Miller akafumbua macho na kumtizama wakagonganisha macho nesi aibu ikamvaa usoni akatupa macho pembeni kisha akavuta shuka lililokuwa pembeni ya Miller kumfunika mahala penye mzizi utamu akisahau kama alikuwa amemvua chupi kaka wa watu.

   “…Eeeeh! …..Umezinduka kaka.. Pole, pole, pole na matatizo kaka, ulipatwa matatizo kidogo… Ulipatwa matatizo ndiyooo…. Eeeeh mimi ni nesi nina ninaye ku ku hudumia…!” Alijikuta anaongea kwa kilatini akibabaika na mwili bado ukiwa unatetemeka sana mpaka Miller akajiongeza akajifanya anauma meno kwa maumivu huku anafinya macho, nesi akanyosha mkono wake kwenye sinia akachukua kipimio cha mapigo ya moyo na mambo mengine kwa wagonjwa.

   “Niko.. Mmmh! Niko, hahaha eeeeh.. niko wapi ha hapa?” Akauliza Investigator Miller bwana maigizo akijifanya kubabaika kana kwamba anasikia maumivu makali sana kwa jinsi alivyokuwa anauweka uso wake na hata mwanga wa taa kali zilizomo chumba hiki ambacho kiukweli kilikuwa hakina madirisha zaidi ya kuta pande zote na ule mlango tu ambao chini kulikuwa na uwazi unaoingiza oxygen ya humu na juu kulikuwa na kadirisha ka nyavu na hii ilitokana kama nilivyoeleza mwanzo ni kuwa jengo hili lina pande mbili huku chini unakoweza sema ni handaki na juu ilipo kama karakana sasa endapo utafika ukiwa hujui yanayohusu hapa utasita kuendelea kuamini hapa ni karakana ya vipuri mbalimbali.

   “Huko… Eeh! Sa, Sa… Samahani mimi pia.. mimi sijui kunaitwaje huku”Alitaka kujibu kiusahihi lakini akastuka na kujirekebisha haraka akajibu alivyoona sawa huku akijutia kwanini mtu huyu amestuka bila yeye kufanya alichotaka kufanya.

   “Wewe.. Wewe ni nesi wa hapa? Ina maana niko hospitali? Imekuwaje kwani?” Akauliza maswali a kufuatana huku akiendela kukunja uso wake kuekti hajisikii vizuri.

   “Ndiyo huko hospitali kaka.. Si hospitali kubwa ni zahanati ndogo tu.. Mlipata ajali ya gari wewe na mwenzako huyu wa kitanda cha pili” Akajibu nesi akiendelea kukwepesha macho yake wasiangaliane maana Miller alikuwa habandui macho usoni mwake.

  “ Eeeeh! Kumbe? Anaendeleaje? Vipi hali yake?” Akahoji maswali ya kufuatana na ndipo wakaangaliana usoni na hapo Miller akaona mwanadada wa kilatini mwenye sura ya kuvutia akatamani angeruhusu kuonja utamu kidogo wa mrembo huyu akavuta hisia wakati mdomo wenye joto ulivyokuwa ukimung’unya uume wake kama mrembo anamung’unya pipi kijiti kubwa, walitamaniana walipotizamana kwakuwa kila mmoja alimeza mate bila kujali wako wapi? na kwanini?.

  “Anaendela vizuri.. Tumewapatia huduma nzuri sana hata wewe ulifika ukiwa katika hali isio nzuri sana..!” Akajibu kiujumla nesi akimfunika vizuri zaidi Miller.

   “Naweza kumuona mwenzangu?” Miller akauliza kisha akajifanya hajui kama mikono na miguu yake amefungwa minyororo akajiinua na kujifanya kashangazwa kuwa amefungwa.

   “Mbona nimefungwa hivi? Hospitali gani mnahudumia wagonjwa huku mmewafunga kwa minyororo kama hivi?”Akauliza huku anamtizama nesi uso kaukunja kuonyesha alivyochukizwa kuwa vile.

Mwisho wa sehemu ya sabini na tano (75)

Sehemu iliyohusika zaidi na kujua walipo Investigator Miller na Detective Norman na ilikuwaje upande wao baada ya kukutwa na masahibu juu yao ya kutekwa kwa kutegeshewa gari chakavu wakiwa wanawafukuza mwanamama ambaye laiti angejua ndiyo hasa sababu ya majasusi wa Marekani kuwa Guatemala basi angejitahidi kujidhibiti katika mawasiliano yake yaliyosababisha kwa asilimia tisini kuwa hivi sasa wakiwa wanajiuliza imekuwaje, kwanini?

Nisikupotezee wakati zaidi kujua nini kiliendelea zaidi fanya kusogea mbele uendelee kupata uhondo wa jino kwa jino unaoelekea kutamu zaidi na kama ujuavyo utamu unapokolea zaidi basi mambo uwa yamekaribia kufika kileleni a.k.a kuvunja dafu.




   “Niko.. Mmmh! Niko, hahaha eeeeh.. niko wapi ha hapa?” Akauliza Investigator Miller bwana maigizo akijifanya kubabaika kana kwamba anasikia maumivu makali sana kwa jinsi alivyokuwa anauweka uso wake na hata mwanga wa taa kali zilizomo chumba hiki ambacho kiukweli kilikuwa hakina madirisha zaidi ya kuta pande zote na ule mlango tu ambao chini kulikuwa na uwazi unaoingiza oxygen ya humu na juu kulikuwa na kadirisha ka nyavu na hii ilitokana kama nilivyoeleza mwanzo ni kuwa jengo hili lina pande mbili huku chini unakoweza sema ni handaki na juu ilipo kama karakana sasa endapo utafika ukiwa hujui yanayohusu hapa utasita kuendelea kuamini hapa ni karakana ya vipuri mbalimbali.

   “Huko… Eeh! Sa, Sa… Samahani mimi pia.. mimi sijui kunaitwaje huku”Alitaka kujibu kiusahihi lakini akastuka na kujirekebisha haraka akajibu alivyoona sawa huku akijutia kwanini mtu huyu amestuka bila yeye kufanya alichotaka kufanya.

   “Wewe.. Wewe ni nesi wa hapa? Ina maana niko hospitali? Imekuwaje kwani?” Akauliza maswali a kufuatana huku akiendela kukunja uso wake kuekti hajisikii vizuri.

   “Ndiyo huko hospitali kaka.. Si hospitali kubwa ni zahanati ndogo tu.. Mlipata ajali ya gari wewe na mwenzako huyu wa kitanda cha pili” Akajibu nesi akiendelea kukwepesha macho yake wasiangaliane maana Miller alikuwa habandui macho usoni mwake.

  “ Eeeeh! Kumbe? Anaendeleaje? Vipi hali yake?” Akahoji maswali ya kufuatana na ndipo wakaangaliana usoni na hapo Miller akaona mwanadada wa kilatini mwenye sura ya kuvutia akatamani angeruhusu kuonja utamu kidogo wa mrembo huyu akavuta hisia wakati mdomo wenye joto ulivyokuwa ukimung’unya uume wake kama mrembo anamung’unya pipi kijiti kubwa, walitamaniana walipotizamana kwakuwa kila mmoja alimeza mate bila kujali wako wapi? na kwanini?.

  “Anaendela vizuri.. Tumewapatia huduma nzuri sana hata wewe ulifika ukiwa katika hali isio nzuri sana..!” Akajibu kiujumla nesi akimfunika vizuri zaidi Miller.

   “Naweza kumuona mwenzangu?” Miller akauliza kisha akajifanya hajui kama mikono na miguu yake amefungwa minyororo akajiinua na kujifanya kashangazwa kuwa amefungwa.

   “Mbona nimefungwa hivi? Hospitali gani mnahudumia wagonjwa huku mmewafunga kwa minyororo kama hivi?”Akauliza huku anamtizama nesi uso kaukunja kuonyesha alivyochukizwa kuwa vile.

ENDELEA NA DODO ASALI…!

HOFU PANDE ZOTE III

LAS ANONAS, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

   “Samahani.. Mimi ni nesi tu! na waliokuleta hapa wakikuondoa eneo ulilopata ajali walisema wanatakiwa kuwafungeni nyote hivi hivyo sina majibu kamili kwanini huko hivyo nachotakiwa ni kuwaangalia nyote nyie kwa ukaribu mpaka afya zenu zitakapotengamaa waliowaleta watakuja kuwachukua kwa shughuli inayowahusu wao si mimi tena maana nitakuwa nishamaliza wajibu wangu nilionao ni huo tu..!” Akajibu nesi akiwa bado na aibu usoni mwake.

  “Vizuri! Umesema wewe ni nesi lakini kwangu mimi nijuavyo mtu yoyote anapokuwa nesi lazima awe mjuzi wa mambo ya matibabu ingawa si kiasi kikubwa kama alivyo dokta anayekuwa anajua zaidi.. Hivi katika huelewa wako uliokuwa nao ni halali mtu aliyenusurika kwenye ajali kufungwa kama hivi nilivyofungwa? Namaanisha nikawa siwezi hata kujilaza kiubavu kwa uhuru? Au vipimo vyenu vimeelekeza tu mimi na ndugu yangu ni wa kulazwa chali tu?”Miller kidogo alipunguza kuigiza akaongea kwa urefu mdogo aweze kuelewekwa kwa mwanadada nesi.

   “Mgonjwa una maswali mengi sana.. Unajua haswa kilichokufanya upate ajali lakini unataka kunifanya mimi mjinga, kifupi hapa ulipo upo eneo ambalo huwezi kuwa huru wewe na hata mwenzako hapa si mahala ambapo mimi naweza kukueleza unayotaka ndugu yangu uvumilie tu na waliokuleta muda si mrefu watakuja kuwakagua walikuwa wakiawasubiri watu maalumu wafike kuja kuwaona ni kwamba wewe umewai kuzinduka tofauti na maelekezo ya daktari na hata sindano niliyoelekezwa nikupige na dokta” Akajibu nesi lakini sasa alikuwa ameweza kumuangalia anayeongea naye bila aibu aliyokuwa nayo dakika chache zilizopita.

  “Ulinichoma sindano gani? Dokta alitaka nilale kwa muda gani?” Akauliza Miller wakitazamana.

  “Ya usingizi hili kukwepa maumivu sidhani kama kuna umuhimu nikakutajia jina aina ya dawa hiyo ya usingizi, nachoomba usiwe na wasi sababu haina madhara na ndiyo maana umeamka ukiwa hauna maumivu uliyokuwa nayo wakati unafikishwa hapa..”Akajibu nesi.

   “Nesi mzuri na majibu yako ni mazuri sana natamani ningekuwa mpenzi kama si mchumba wako… Hakika nimevutiwa sana na uzuri wako… Unajua kwanini nimezinduka kabla ya wakati ulioelekezwa?” Akili ya kazi ya jasusi mbobezi ilianza kuendea alipopaanza tokea anaanza kuuliza maswali yake.

   “Mmh! Mpenzi au mchumba kabisa? Mmh! Hata hivyo na wewe ni mwanaume mzuri unayevutia una mwili uliojengeka vizuri  kimazoezi… Niambie kwanini umewai kuamka kabla ya muda kadiriwa?” Akakubali sifa alizopewa kisha akahoji kule alikoachwa na Miller katika swali jengwa.

   “Ni kwa sababu ulikuwa ukinifanyia jambo tamu sana ambalo limenisisimua mwili wangu sana na kuziamsha hisia zangu za mapenzi.. Natamani ungeendelea lakini nikahofia nitakuwa sifaidi na wewe pia hautafaidi ukiwa unakosa ushirikiano wangu, kama hautajali nisaidie nifike ulipoanza nipeleka nikiwa usingizini mpaka kunipelekea nizinduke..” Aliongea Miller akiwa ‘serious’ kumuangalia kwa macho ambayo anaamini yeye kama yeye kuwa akimuangalia mdada hivi lazima atamvuta zilipo hisia za mapenzi.

Nesi alibaki akimuangalia tu na ghafla akajkuta anameza mate ya tamaa mate yaliyojaa utamu mepesi na mapya toka kwenye vifuko hifadhi vya mate, mkono wake kama unapelekwa na ibilisi la mahaba ulijikuta umetua kifuani mwa Miller na akajikuta anampapasa taratibu mwanaume.

   “Mnatokea wapi?” Akauliza kwa sauti iliyojazwa mahaba sauti nyororo kama imelainishwa kwa mafuta, sauti tamu ambayo unaweza enda benki nayo ukaiweka dhamana kwa meneja wa benki kama ni mwanaume na bila hiyana akasaini karatasi ya kuidhinisha upewe mkopo wa mamilioni (hatari), kuna wanawake wamejaliwa mbwembwe za mahaba na ushetani wao wa vishawishi vyenye kulainisha hatari maana jeki ya asili kwa sauti yake tu inainuka yenyewe bila taarifa, mkono wake hakuacha kumpapasa kifuani bwana maigizo.

   “Ma… Mare… Ma rekani..! Khaaa..!” Akaongea bwana maigizo akijifanya ana hamu kweli kweli ya mapenzi maana hata mikono yake aliyofungwa aliifanya kama nayo inasikia ladha ile.

   “Nyie ni wapelelezi wa DEA?” Akahoji tena nesi mpaka Miller akatabasamu ndani kwa ndani maana ilikuwa kama anatakiwa kujipeleka mahala ambapo watu hawa pengine wanapataka wanamtumia mwanamke huyu kufika huko.

   “Watalii tu… Mimi ni mfanyakazi wa kampuni ya Apple makao makuu na na mwe mwenzangu ni…ni mfanyakazi wa ubalozi wa Marekani hapa Guatemala lakini si mmarekani ni mu Guatemala kama wewe… Au wewe mrembo si mu Guatemala?!” Akahoji Miller na kumbinyia jicho mrembo akiwa kadanganya kazi bila kujali laiti kama nesi huyu anaujua ukweli ama lah.

  “Watalii.. Okay! Mi sina la kusema nataka unisugue na mchi wako mtamu mpenzi..!” Akaongea kwa sauti yake matata kisha akainama kusogeza mdomo wake ulipo mdomo wa Miller ambaye hakuremba akaupokea wakanasishana midomo ikawa ni mwendo wa kubadilishana ladha za mate na vimilio vya kupasua ngoma za masikio, vimilio vitamu vya mabusu membamba na mazito, dakika mbili zilikuwa hizi kila mmoja akisisimkwa mwili na kuingiwa na joto la mahaba lakini ghafla Miller alijiondoa kwa kuupeleka uso kando nesi akainua mwili kidogo kumuangalia kulikoni kwakuwa wakati wakifanya hivyo mikono ya nesi kama ina shoti ya umeme ilikuwa ikipapasa mwili wa Miller kuanzia mapajani kuja juu kifuani kwa miterezo mitamu akipapita kuliko mzizi bila kupagusa ka makusudi (mahaba mubashara).

  “Baby! Mgongo unaniuma naomba nifanyie mpango nikae kidogo huku tunaandaana kabla ya kuanza kufanya..!” Akaongea macho yake yakihakisi akisemacho kuleta maana kwa nesi.

   “Kweli? Sasa mbona funguo sina mimi… Ngoja niangalie kwenye droo..!” Akaongea nesi kisha akakimbia haraka kwenye droo ya meza akafungua na kutoka na funguo, Miller akaona hatua ya kwanza kavuka lakini vile vile kwa mara ya kwanza pale mezani aliweza kuiona saa yake, saa ya Norman zikiwa juu na hata simu ambayo moja aliitambua ni yake lakini ikiwa imepasuka kioo kiasi kikubwa akafikiria jambo kwa haraka akaziangalia saa na kuziona zilivyo kwa kutokea alipo zikampa matumaini kidogo hata kama hakujua uzima wake.

Mwanadada alirudi akiwa mbio mbio za haraka vile vile akaiweka funguo kitandani pembeni ya Miller kisha akafungua kifungo cha suruali yake akaivua suruali ikiambatana na kusukuma viatu vyake virefu vya skuna alivyovaa, akawa sasa amebaki mtupu (uchi kabisa) maana suruali alishusha kwa pamoja na chupi yake ya bikini.

Alivuta shuka lililomfunika mgonjwa wake anayetakiwa kumuhudumia na kwa kuzidi kumroga zaidi pale alipofunuliwa kwakuwa alikuwa anajua chupi yake ilishavuliwa ‘bwana maigizo’ alilinesesha liuume lake kwa mbwembwe kana kwamba lina uchu wa mfungwa aliyetoka gerezani na kwa kweli bwana huyu naye alikuwa amejaliwa sana kitu cha maana, mate ya uchu yalimjaa mwanadada akataka kulikamatia hili alipeleke mdomoni akakatiziwa kwa sauti ya ‘bwana maigizo’.

   “Baby! Subiri.. “ Akaongea hivi na nesi akasimamisha mashambulizi na kumtizama mwanaume huyu wa kichotara.

   “Walionileta hapa walisema wanarudi baada ya muda gani? Namaanisha saa ngapi wanarudi kuniona”

   “…Mmh! Wee nawe una wasiwasi gani? Mi najua nachokifanya usiogope hakuna wa kutufuma hapa… Wakiwa wanakuja lazima wanipigie simu kwanza kuuliza kama mmezinduka hasa wewe kwakuwa wewe ndiyo humo kwenye ratiba ya kufanyiwa mahojiano si huyu mwenzako” Akajibu akionyesha kutopenda swali aliloulizwa tayari uchu ulishasimama kwenye njia yake mwili wote ulikuwa ukinyevua vua.

  “Tafadhali baby! Naomba usidharau hili… Ebu naomba saa yangu ile pale mezani nimeiona.. Mimi ninajijua nilivyo napofanya mapenzi uwa nakadiria muda katika balansi ya kukojoa kwangu kutokana na mahali tulipo kiusalama, sitaki kukuingiza matatani mrembo nataka matatizo yangu yasikuponze mpenzi..” Akaongea kwa sauti bembeleza na lugha anayotumia ya kilatini inavyopendeza kimatamshi katika malavidavi Miller alitia ushawishi alioona haraka umepokewa alivyotaka sababu nesi alisimama akamuangalia wakaangaliana wakiwa na mihemko haswa kila mmoja hii ilikuwa kweli kwa bwana maigizo ni kweli alikuwa akitamani kumgegedua binti wa kilatini mrefu na mwenye umbo zuri pamoja na sura.

   “Saa kumi na mbili na robo bado.. Walisema watakuja kina madam pamoja na mheshimiwa muda huo, muda huu wapo kwenye kikao .. Acha niangalie saa tujue kabisa tunachezaje mpenzi wangu..!” Akajibu akiwa hajui ni mpango mkakati upi huko kwenye kichwa cha jasusi mbobezi, kasi alielekea kwenye meza akainyanua saa mojawapo na ilikuwa kama zali alinyanyua saa husika, saa ya Miller.

   “Haiwaki!” Aliporudi nayo pale kitandani akaongea hivi.

   “Nifungue upande wa kulia pia unifungue na mguu mmoja wakati tunafanya nisilalie mgongo nitakuwa sifurahii kwa raha baby!” Akaongea Miller na bila kujiuliza zaidi nesi mwenye hisia kali za kimapenzi alimfungua kufuli iliyofungwa na minyororo ya mkono na mguu upande wa kulia bwana maigizo akawa huru upande wote kulia kwake akibakia kushoto ndipo kulikokuwa bado kuko kama ilivyokuwa hapa angeweza fanya chochote kwa mwanamke kama kumtoa roho na lingine ambalo angejisikia kumfanya lakini kwake Miller haikuwa wakati sahihi kufanya chochote kati ya mengi ambayo angeweza mfanya mwanamke na hata mwanaume yoyote ikiwa angehitaji.

   “Ahsante mpenzi! Nipe saa niiwashe..!” Akasema kushukuru na kupokea saa akaiwasha sekunde kama thelathini ilikuwa tayari kufanya kazi, akaangalia saa ilikuwa ni saa kumi na moja kasoro dakika ishirini.

  “Mmmh! Muda wao waliosema unakaribia inabidi tufanye haraka ingawa kuna muda wa kutosha kama tutakuwa makini kubalansi muda wakati tunacheza mechi..”Akaongea tena Miller kisha akaiweka saa pembeni yam to aliolaza kichwa chake.

Nesi ni kama hakusikia chochote kilichosemwa tayari aliukamata mzizi nyama wa mwenzie akaanza kuunyonya kwa kasi hapo yaliyoendelea kwangu mimi ingawa nilihadithiwa na aliyekuwepo eneo la tukio naomba tu niishie hapa sababu yalikuwa ni mambo makubwa ya kikubwa wakipeana dozi nzito mpaka nesi wa watu alivunja madafu yasiyo na idadi, wakati wakiendelea nesi aliwekwa stahili ya ‘dog style’ (chuma mboga) uso wake uligeuziwa mlangoni halafu ‘bwana maigizo’alikuwa nyuma yake akampachika kitu wakiwa wanaendelea na ‘pump’ za nje ndani kwa kasi kama wanaekti movie ya ngono ‘bwana maigizo’ alitumia fursa ya mkolezo ule kuchukua saa kisha akatuma meseji kwa Special Agent Rebecca akimuomba afuatilie alipo kwa kufuata signal za saa hii pia alituma na kwa Agent Kai kutaka kujua kama yuko poa? Waliweza kujibishana kwa meseji zaidi ya tatu kila upande bila nesi kujua kisha ya hapo akawaaga akaitupa chini ya kitanda saa ile akiwa hajaizima hili waweze kufuatiliwa walipo kufuata ‘signal’.

‘Bwana maigizo’ aliamua kufika mwisho akasugua mashine kwa kasi akivuta hisia zote na kujikuta anadondosha goli zito sana ndani ya tupu ya nesi.

   “Ahsante sana… Ahsante sana..!” Akaongea nesi kisha akageuka na kumkumbatia Miller wakapigana mabusu pale papo hapo nesi akachukua jukumu la kumfuta futa mwenza wake wa muda mfupi wote walikuwa na fuaha kwa aha walioipitia ingawa kwa upande wa Miller ilikuwa raha iliyoambatana na kazi.

  “Baby! Unaitwa nani?” Akahoji nesi huku anamvalisha ‘boxer’ yake Miller.

   “Jose! Naitwa Jose…. Wewe je?” Akajibu na kuhoji Miller akitaja jina lake la kwanza la ukweli lakini akilikatizia.

   “Avon… Avon Morris.. Nimefurahi sana leo, umenikata kiu yote niliyonayo… Nawapenda sana wanaume kutoka Marekani ndiyo maana nilivyosikia nyinyi wamarekani nikapata hamu ya kuwa kimapenzi na wewe nilifurahi nilivyoambiwa nibaki kuwaangalia” Akaongea ukweli wake nesi akisema jina lake la ukweli.

  “Nimekukata kiu… Kwani kila siku hukatagi kiu yako?” Akauliza swali Miller akiwa anafungwa mkono wake tena kwa minyororo.

   “Mchumba wangu mlevi sana… Wanaume wa nchi hii pombe kwao ni bora zaidi kuliko mapenzi… Mume wangu ni mwanasheria wa ofisi ya waziri wa usalama ni miongoni mwa wanaume wenye kupenda sana kunywa sana hivyo akirudi nyumbani hana muda wa kufanya kitu na mimi licha ya uzuri wote nilionao, huwezi amini tuna miezi miwili hajanigusa kwa kuniridhisha mimi binafsi anajiridhsisha yeye tu kisha analala ananiacha nalia tu” Akajibu Avon.

  “Pole sana! Natamani niishi nawe lakini maisha yangu siijui hatma yake kwa nilivyo hivi na pia kumbe ushaolewa Avon!” Akalainsiha kwa neno hilo.

Kabla Avon hajaongea kitu katika alilolisikia toka kwa Miller, simu iliyokuwa juu ya meza ile ile yenye vitu mbali mbali, ilikuwa ni ile misimu mikubwa kama viredio vidogo lakini si simu ya mezani ila pia si za kutembea nazo mtaani ni kama radio call, walitizamana kisha Avon akainuka alikuwa bado hajavaa suruali yake wala chupi yake ya bikini alikuwa bado anapunga hewa baada ya kusuguliwa msuguliwo haswa, Miller alimtizama anavyoenda akameza mate ya uchu akikubali uumbaji.

   “Halloo!..”Akaongea Avon baada ya kupokea na kuiweka sikioni, ilikuwa ni ngumu kujua mpigaji ni nani kwakuwa ni simu zisizo na kioo cha kujulisha kwa mpigiwa nani anampigia.

   “Tuko njiani tunaenda kukutana na Madam na wenzake wa genge lao kwa maagizo ya mheshimiwa kisha tuje nao huko… Huyo nigga anaendeleaje?” Ukauliza upande wa pili akiwa hajajitambulisha yeye nani.

  “Niko chumba walichomo nimeingia sasa hivi kuwaangalia.. Bado hajaamka” Akajibu uongo Avon akikataa kusema ukweli bila hata kufundishwa na Miller.

   “Tuko na dokta… Atajua afanyaje hili aamke… Madam na watu wake wanataka kumuhoji, mheshimiwa waziri amepatwa dharua hawezi kuja tena huko” Aliongea tena wa upande wa pili kisha akakata simu.

Avon aligeuka alipo Miller wakatizamana uso wa Miller ulionyesha unatamani kujua kilichoongelewa na mpigaji wa simu maana alisikia tu alivyovijibu Avon.

Mwisho wa sehemu ya sabini na sita (76)

Tumeshuhudia Investigator Miller akivunja amri ya sita kwa kuligegedua tunda la nesi anayeitwa Avon ni kweli mwanamke ni mzuri lakini ingekuwa ngumu kwa Miller kukubali kumfilimba katika hali ya kawaida lakini kutaka apate alichoona ni muhimu kufikisha taarifa kwa wenzake aliona hakuna njia ni kufanya vile anavyotaka dada wa watu, akimmwagia ndani mambo yote bila kujali kama anaweza kumpa ujauzito, alichoona yeye ni sahihi mwanamke mwenyewe kuhitaji kufanyiwa alichomfanyia.

Agent Kai na Rebecca wamepata ujumbe kutoka kwa Miller hatua gani itafuata?

Mariana na watu wake nao wanaelekea huko ‘Las Anonas’ walipo kina Miller kwa ajili ya kuhakikisha yanafanyika mahojiano.

Nini kitafuata? Tuweke maneno mengi pambeni, tuweke mziki



   “Mchumba wangu mlevi sana… Wanaume wa nchi hii pombe kwao ni bora zaidi kuliko mapenzi… Mume wangu ni mwanasheria wa ofisi ya waziri wa usalama ni miongoni mwa wanaume wenye kupenda sana kunywa sana hivyo akirudi nyumbani hana muda wa kufanya kitu na mimi licha ya uzuri wote nilionao, huwezi amini tuna miezi miwili hajanigusa kwa kuniridhisha mimi binafsi anajiridhsisha yeye tu kisha analala ananiacha nalia tu” Akajibu Avon.

  “Pole sana! Natamani niishi nawe lakini maisha yangu siijui hatma yake kwa nilivyo hivi na pia kumbe ushaolewa Avon!” Akalainsiha kwa neno hilo.

Kabla Avon hajaongea kitu katika alilolisikia toka kwa Miller, simu iliyokuwa juu ya meza ile ile yenye vitu mbali mbali, ilikuwa ni ile misimu mikubwa kama viredio vidogo lakini si simu ya mezani ila pia si za kutembea nazo mtaani ni kama radio call, walitizamana kisha Avon akainuka alikuwa bado hajavaa suruali yake wala chupi yake ya bikini alikuwa bado anapunga hewa baada ya kusuguliwa msuguliwo haswa, Miller alimtizama anavyoenda akameza mate ya uchu akikubali uumbaji.

   “Halloo!..”Akaongea Avon baada ya kupokea na kuiweka sikioni, ilikuwa ni ngumu kujua mpigaji ni nani kwakuwa ni simu zisizo na kioo cha kujulisha kwa mpigiwa nani anampigia.

   “Tuko njiani tunaenda kukutana na Madam na wenzake wa genge lao kwa maagizo ya mheshimiwa kisha tuje nao huko… Huyo nigga anaendeleaje?” Ukauliza upande wa pili akiwa hajajitambulisha yeye nani.

  “Niko chumba walichomo nimeingia sasa hivi kuwaangalia.. Bado hajaamka” Akajibu uongo Avon akikataa kusema ukweli bila hata kufundishwa na Miller.

   “Tuko na dokta… Atajua afanyaje hili aamke… Madam na watu wake wanataka kumuhoji, mheshimiwa waziri amepatwa dharua hawezi kuja tena huko” Aliongea tena wa upande wa pili kisha akakata simu.

Avon aligeuka alipo Miller wakatizamana uso wa Miller ulionyesha unatamani kujua kilichoongelewa na mpigaji wa simu maana alisikia tu alivyovijibu Avon.

ENDELEA NA DODO ASALI..!

HOFU PANDE ZOTE IV

LAS ANONAS, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

   “Signal inaelekeza dira tuingie kushoto lakini hofu yangu tunakaribia kama inavyoonyesha.. Ebu tusogee mpaka pale njia panda pengine tunaweza tukapata eneo la kuweza kuificha gari yetu miongoni mwa miti ile naona kama kuna miti mingi sana kule.. Kisha tutashuka na kuitafuta nyumba vizuri” Alikuwa ni Agent Kai ‘TSC’ akimuelekeza Special Agent Rebecca asogee mbele na gari iliyokuwa inaendeshwa na mwanadada huyu huku ‘The Sole Cat’ akiwa ameshika kifaa kinachowaongoza kufuatilia saa ya Investigator Joseph January Miller aliye mateka lakini kwa ujanja alitumia fursa ya kutamaniwa kimapenzi na mwanadada nesi Avon kufanya mawasiliano bila mwanadada kujua kama Miller amefanya mawasiliano na wenzake, kwenye siti za nyuma za abiria alikuwepo Special Agent Fransis Simone Silla.

Rebecca aliendesha mwendo wa kubembeleza gari hii haina ya Ford Edge mali toleo la mwaka 2015 ya ubalozi wa Marekani nchini Guatemala, moja ya magari toka yafike ubalozini kwa ajili ya kutumika kwa shughuli za kibalozi ilikuwa imetumika mara chache sana, Agent Kai na mshirika mwenza jasusi wa DEA S.S Silla walivyotoka eneo la Mixco wakinusurika kiajabu kuingia katika mikono ya adui zao waliokosa umakini wa kufanya ukaguzi maeneo ya karibu na tukio na sababu kuu kutokuwa na taarifa kamili ya idadi ya watu waliokuwa katika gari inayowafukuzia Madam Mariana na mwenzake Gudrado. 

Moja kwa moja ‘TSC’ na Silla walikwenda hadi eneo moja ambako kulikuwa na parking ya magari hapo walimpata kijana mmoja aliyekubali kuwapa msaada wa simu waweke laini kama walivyomuomba na walipoweka laini ya Agent Kai cha kwanza alipiga simu kwa katibu wa ubalozi wa Marekani ambapo wakamuomba msaada na ndipo akawafuata katibu mwenyewe katika eneo lile wakaenda hadi ubalozini wakaoga na kupewa huduma za kitabibu sehemu walizoumia wakati wanaondoka wakaomba gari wakakubaliwa na kupewa hili dude la ukweli ‘Ford Edge’rangi ya hudhurungi (blue) inayong’ara, wakarudi maskani kwao sign street eneo la greenhouses kabla hawajapumzika vizuri wakiwa wanaongea na wenzao waliowaacha hapa ambao ni Kamanda Muniain, Special Agent Rebecca Smith wakiwa pamoja na malkia wa urembo Angelica Linares, ujumbe wa meseji uliingia katika saa simu ya Rebecca Smith ambapo akawastua wenzie waliokuwa wamekaa kwenye masofa hawajui wanaanzia wapi katika kutaka kujua wenzao waliotekwa walipo na hata kujua hali zao hii hali iliwafanya wawe wanyonge sana.

Furaha ilitamalaki miongoni mwao baada a majibishano ya meseji baina ya Rebecca na Miller akiwaambia kwa meseji ukweli wa anachofanya kwa wakati na ndicho kinamsaidia yeye kupata fursa ya kuchati naye, haikuishia hapo alichati kidogo na Agent Kai ambaye kwa wakati huo alikuwa kashabadilisha laini iliyokuwa inatumika katika simu saa iliyoharibika kwakuwa toka wanatoka Marekani alibeba saa za mfumo huu kama nane hivi kwa madhumuni hata kama wataunda kikosi kikubwa zaidi waweze kuwasiliana bila shida.

   “Paki mbele ya nyumba hiyo haina haja ya kutafuta pori tufiche gari… Paki hapo tutaongea  na mwenyeji atusaidie kuiangalia pesa sabuni ya roho” Akaongea ‘TSC’ akielekeza kwa kidole hili Rebecca amuelewe na kweli alimuelewa akasogea mbele ya nyumba ambayo ilikuwa kuukuu ikionyesha ni ya muda mrefu katika eneo hili la nyumba chache zilizokaa mbalimbali huku wenyeji wakionekana ni watu wanaojihusisha na kilimo cha wakulima wadogo wadogo na pia eneo hili lilionyesha kwa mtu anayefika kwa mara ya kwanza kutambulisha kuwa ni eneo la makzi yaliyo mapya kwa wakazi maana nyumba nyingine zilikuwa mpya na za kisasa ingawa pia zilikuwepo kama hii inayoonekana kuukuu na chakavu mwenye nyumba haijifichi ni ndiyo wanaoitwa waanzilishi wa maeneo kama haya.

Gari iliposimama tu Rebecca alipiga honi ya gari kumstua aliyeko ndani kama yupo atoke kuwasikiliza kisha ya hapo akazima injini kukawa kimya waliweka subira majasusi awa hakuna aliyeshuka garini.

Ilipita dakika tu akatokea mzee wa kizungu mwenye nywele zenye mvi kichwa chote mashavu yake yalikuwa yamepigika uzee alikuwa amejivalia makoti mawili mzee wa watu, koti zito juu na ndani koti la suti  kwa kweli alikuwa ni mzee haswa aliyekula chumvi haswa ila pamoja na hivyo hakuwa anatembelea fimbo yoyote kumsapoti katika utembeaji wake, alipotoka mlangoni na kuona gari limesimama mbele ya uwanja wake akasita kusogea mbele.

Rebecca akashuka toka ndani ya gari akapiga hatua akiuacha mlango wa gari wazi kuelekea alipo babu lakini hatua zake hazikusogea sana alitokea kijana wa kizungu aliyevaa kaptura ya jeans na fulana aina ya ‘pullneck’ alikuwa na nywele nyingi zilizo katika mtindo maarufu kwa vijana na hata watu wazima eneo la nchi za kilatino mtindo unaoitwa ‘bambucha’  uso wake ulionyesha ametoka kulala muda huo.

   “Karibu!”Akitumia kilatino lugha ya taifa ya nchi hii ya Guatemala alitoa ukaribisho kwa mwanadada anayemuona mbele yake.

   “Ahsante! Habari yako?!!” Uzuri ya majasusi wengi wa Marekani toka mashirika mbalimbali wanazungumza vizuri kilatino na kiingereza lugha zoeleka kwao lugha ya ulimi wa mama zao na walezi wao.

   “Nzuri! Kabisa.. Ni wageni wetu nyinyi?” Akajibu salamu na kuhoji kijana yule akiwa pembeni ya mzee wake aliyekuwa katangulia kutoka ndani pale aliposikia honi tu.

   “Ndiyo… Wageni sisi tunatanguliza samahani kisha tunapenda kusogeza ombi kwenu..!” Akaongea Rebecca usoni akiwa ameachia tabasamu mujarabu kwa kijana wa watu mwenye haiba ya ujanja mwingi usoni mwake na hali ya kuwa ni mpenzi wa pombe kitu ambacho katika Guatemala ni kitu cha kawaida kwa vijana wote ni kama tamaduni yao kuu kwakuwa hata mtu akienda kuposa sehemu katika nchi hii basi katika kikao cha kwanza mposaji utakiwa kuonyesha alivyo vizuri katika unywaji wa pombe huku wakwe wakimuangalia kuwa anamaliza idadi ya chupa ngapi za pombe? Na kumaliza kwake bila kulewa upesi katika idadi aliyoekewa basi umeongezea pointi ya kuonekana kweli yeye kidume cha mbegu kitakacho mtunza vyema binti wa familia aliyoenda kuposa.

   “Naam! Karibu tunakusikiliza ombi lenu”Akakubali kijana kulisikiliza hilo ombi linalotaka kusogezwa kwao kisha likahitaji kufanyiwa kazi.

   “Sisi ni wageni eneo hili ambalo tunalijua kwa jina linaitwa eneo la  Las Anonas lakini kati yetu hakuna aliyewai kufika hapa hapo kabla… Tuna ramani ya mahala tunapoenda lakini mwenyeji wetu alitupa taarifa kuwa eneo alipo gari haiingii kutokana na milima milima iliyopo eneo hili hivyo basi ombi letu kwenu tunaomba tuache gari letu hapa mpaka tutakaporudi kisha sisi tutaenda kwa miguu huko anakotusubiri mwenyeji wetu, hatutawaacha hivi hivi tutaacha na pesa ya malipo kwa kutuangalizia mali yetu husika” Akaongea Rebecca akiwaangalia kwa kuwakazia macho mzee na kijana walio mbele yake.

   “Hilo tu… Halina shida kijana wangu.. Tico! Pokea pesa mjukuu wangu” Babu kwa mara ya kwanza ikasikika sauti yake akitabasamu mipengo kama yote mdomoni.

Kijana ambaye sasa Rebecca alidaka jina lake kuwa anaitwa Tico naye alitabasamu akatamani kujua wanaachiwa Quetzal ngapi? Hii Quetzal ni jina la pesa la nchi ya Guatemala, lakini mkono wa Rebecca ulipozama mfukoni katika mifuko yake ya mbele ya suruali aliyovaa uliibuka na pesa aina ya dola za Marekani akampa noti mbili zikiwa ni dola mia mia hivyo jumla akawa amempa dola mia mbili ambazo kama atazibadili kwenda pesa za nchi yao alikuwa anapata pesa nzuri tu kwa wakati huu.

Furaha ilikuwa kubwa sana maana kijana alikuwa ametoka kufanya mishe zake kibao lakini alirudi nyumbani akiwa mikono mitupu mchana ulipita bila wao kula hivyo kutokea kwa kina Rebecca jioni hii ilikuwa kama zali kwao.

Agent Kai na Silla walishuka ndani ya gari baada ya Rebecca kuwaomba kwa ishara ya mkono kuwa washuke kashaweka sawa mambo, walitoa salamu kwa kijana na mzee wake ambao kwa sasa ilikuwa kama wameshinda bingo meno yao yalikuwa ni kukenuka tu hapana papi (lips) za mdomo kufunika meno kwa wakati huo kwao ni furaha tu uhakika wa chakula na pombe ulikuwa kwa asilimia mia moja kwao.

Waliwaaga wakiwa wameli ‘lock’ (funga) gari lao vizuri wakarudi na njia waliyojia mpaka kwenye njia panda ambako signal zao eneo hili zilikuwa zikionyesha dira kuwa wapande juu kulia kuendelea na safari yao ya kuisaka nyumba ambayo ndani kuna saa simu iliyotupwa chini ya kitanda na Miller.

Walitembea wakifuata barabara za wapita kwa miguu wakiacha barabara kubwa ya vumbi kwa hofu wanaweza kukutana na watu ambao kwao inaweza kuwa tatizo, walifuata njia hizo zilizo nyembamba pembeni huku na huku ni nyasi za magugu, mwendo wa kwa miguu walivyo uliwafana watembee mita za kukadiria kama mia mbili ishirini ndipo kifaa alichokishika Agent Kai kinachodaka signal ya saa ya Miller kilianza kutoa mlio kuonyesha wanakaribia eneo husika hapo ‘The Sole Cat’ akapunguza sauti kabisa ya kifaa kikabaki kinawaka tu.

   “Tahadhari jamani nafikiri tukiibuka toka kwenye hili bonde tukapanda kilima kile tutakutana na mahala tunapotafuta” Akaongea Agent Kai kisha akachomoa bastola yake toka nyuma ya kiuno ikakamatiwa mkono wa kushoto huku wa kulia akiwa na kifaa chake kikiwa kimetangulia mbele na kiji antenna , walipanda toka walipo kwenye bonde na walipoinuka kwenye muinuko macho yao wote mbele yao mita kama thelathini tu yalikutana na nyumba iliyo kama ghala au karakana kwa wakati mmoja ikiwa imezungushiwa uzio wa senyenge ya nyaya ngumu pamoja na wigo ambayo inaonekana haina muda mrefu toka ipandwe maana ilikuwa si ndefu ingawa inaenda vizuri na ina afya ya kutosha, watu hawa wote waliinama kisha wakalala chini wote maana kuna kiumbe kilionekana kama kivuli kinajongea upande wa karibu na kimuinuko walichomo wao.

Eneo hili lilikuwa na miti mingi ya asili sio ya kupandwa ni eneo la misitu iliyokubali ukijani kibichi na kufanya kupendeze sana.

   “Nafikiri tumewai kama alivyotaka Miller kuwa kuna watu watakuja kufanya naye mahojiano… Mungu atakuwa kasaidia wasiwe wamefika” Akaongea Agent Kai shingo yake ikiwa inageuzwa huku na huko kuangalia kila kilicho karibu na mbali ya eneo walilopo, kisha akatoa darubini ndogo lakini yenye uwezo wa kuona umbali wa maeneo haya yote ya karibu aina ya Nautical Pocket Brass Telescope zao la Uingereza.

Alisogea kwa juu kidogo pembeni ya mti wa muembe akiwa ameinama vile vile akaiweka darubini machoni na kuanza kuya vuta maeneo mbalimbali yanayozunguka eneo la mjengo unaonekana kwa ndani a uzio wa sennge na wavu.

   “Senyenge ya wavu imezungushiwa nyaya za umeme pia kuna walinzi wanaolinda kwa ushirikiano na mbwa wanaoonekana wana mafunzo mazuri tu, wanaonekana si walinzi wanaohusikana na genge la TRJ… Hawa ni GIS kama alivyoeleza kwenye meseji Miller” Akaanza kutoa maelezo Agent Kai pale alipo pembeni ya muembe akiwaambia walio nyuma yake hatua tatu tu.

   “Geti la kuingilia eneo la ndani nafikiri litakuwa lipo kule kunakoonekana kuna barabara baada ya miti inayoonekana ilipandwa ukiacha hii inaoonekana ni ya asili… Tutaingia ndani baada ya kuwadhibiti walinzi wa upande huu na mbwa wao” Akaongea tena Agent Kai kisha akarudisha darubini kwenye begi lake la dogo la mgongoni ambalo uwa halikosekani haendapo mahala pa kazi za kazi.

Aligeuka nyuma Agent Kai kuwatizama wenzake kisha akatabasamu wote wakamjibu kwa tabasamu la matumaini ambalo kila mmoja liliyeyuka usoni kwa haraka.

   “Kama kuna swali lolote tuulizane haraka.. Kila mmoja kati yetu ataelekea upande wake.. Ambapo Silla utaenda kule barabarani naamini ukifika pale utaliona geti, Rebecca utaelekea juu kuliko mwisho wa uzio ila ukipita kwa kufuata bonde usitokeze juu mpaka utakapoona huko mahala sahihi kwakuwa mahala kama huku hakukosi cctv kamera… Mimi nitapita hapa” Aliongea kimaelekezo Agent Kai mwisho alimalizia kwa kuonyesha mahala atakapopita ni mbele tu ya walipo.

  “Nakubaliana na wewe lakini nina wazo.. Nahitaji nikishaliona geti nitizame uwezekano niweke mlipuko wa kutega hili nikishalipua iwe rahisi kwenu kuingia ndani maana walinzi wote wataongeza umakini wao kuona kulikoni getini” Aliongea Silla wakitizamana na ‘TSC’.

  “Wazo zuri! Basi mimi nitasogea tu pembezoni mwa uzio kisha nitasubii kusikia jibu la mlipuko utakaotega pia na Rebecca elekea tu mpaka nyuma mlipuko ndiyo utakaokupa go a head kufanya linalowezekana kuingia ndani… Wekeni sawa mambo ya mawasiliano muda wote yawe active!” Agent Kai alikubaliana na wazo la Silla kisha naye akaweka lake likiwa ni la maelekezo zaidi.

Special Agent Silla alitoa begi lake mgongoni kisha akafungua zipu na kuangalia vilivyomo kimoja kimoja hili kuhakikisha atakacho kama kipo alipoona kipo akafunga zipu na kutabasamu kisha akamuangalia Rebecca akamalizia na ‘TSC’ wote wakatabasamu wakashikana mikono kupeana baraka zao kwa kila mmoja wao.

   “Kazi njema… Tukafanye kwa ajili ya wenzetu na taifa letu kwa ujumla.. USA First!” Akaongea Agent Kai huku bado wakiwa wameshikana mikono.

   “Mungu yu nasi.. USA First!” Akaongea Rebecca.

   “Siku zote yuko nasi… USA First!” Akamalizia Silla, wakaachiana na papo hapo Silla akiwa ameinama vile vile akaanza kuufuata uelekeo wake anaotakiwa kwenda.

‘TSC’ naye hakuendelea kuchuchumaa alivyochuchumaa, alikwenda huku ameinama usawa sawa na majani yaliyoachwa yajiotee tu na watu wanaoishi eneo hili lenye jumba hili tu ambalo sasa majasusi hawa wanalijongea kwa minajili ya kuingia na kuwaokoa Miller na Norman wanaoshikiliwa mateka ndani ya jumba hili lililozungushiwa senyenge na wigo wa maua mazuri lakini miti yake ina miiba.

Mwamba alisogea akalala chini sambamba na vigingi vya chuma vilivyochomekwa kwenye msingi uliozungushwa chini kabisa hili kushika senyenge iliyozunguka eneo zima la nyumba ambayo inaonekana iko kwa katikati.

Begi lilitolewa mgongoni kwa utulivu na umakini akafungua zipu na kutoa mkasi wa kukatia nyavu ambao si mkubwa ni mdogo tu lakini wenye makali ya nguvu, taratibu akaanza kukata eneo ambalo aliamini ataweza kupenya kama joka mpaka zilipo wigo, dakika moja ilitosha kukata kwa umakini tundu la kumuwezesha kupenya akarudisha mkasi kwenye begi akafunga zipu na kuzama kwa ndani sasa akawa zilipooteshwa wigo haraka akatoa miwani yake ya kijasusi yenye kazi inayofanana na darubini tena yenyewe ikiwa imeboreshwa zaidi ya unavyoweza kujua kwa kuona maeneo ya karibu kwa uzuri ingawa na yenyewe haiwezi kwenda umbali wa darubini.

Mwisho wa sehemu ya sabini na saba (77)

Majasusi wa kimarekani wako eneo la Las Anonas lililpo jengo lililokuwa la Mr. Alexis kabla hajampa kama zawadi mheshimiwa waziri wa usalama ambaye naye akalifanya liwe eneo la siri la taasisi kuu ya ujasusi katika nchi ya Guatemala (GIS), serikali ilikubali iwe hivyo kwakuwa majumba kama haya yanahitajiwa sana kwa minajili ya kurahisisha kazi zao za kijasusi.

Mariana na wenzake nao wako njiani wanakuja huku huku Las Anonas wakiwa wanataka kuja kumfanyia mahojiano Miller.

Nini kitatokea hapa Las Anonas?




Special Agent Silla alitoa begi lake mgongoni kisha akafungua zipu na kuangalia vilivyomo kimoja kimoja hili kuhakikisha atakacho kama kipo alipoona kipo akafunga zipu na kutabasamu kisha akamuangalia Rebecca akamalizia na ‘TSC’ wote wakatabasamu wakashikana mikono kupeana baraka zao kwa kila mmoja wao.

   “Kazi njema… Tukafanye kwa ajili ya wenzetu na taifa letu kwa ujumla.. USA First!” Akaongea Agent Kai huku bado wakiwa wameshikana mikono.

   “Mungu yu nasi.. USA First!” Akaongea Rebecca.

   “Siku zote yuko nasi… USA First!” Akamalizia Silla, wakaachiana na papo hapo Silla akiwa ameinama vile vile akaanza kuufuata uelekeo wake anaotakiwa kwenda.

‘TSC’ naye hakuendelea kuchuchumaa alivyochuchumaa, alikwenda huku ameinama usawa sawa na majani yaliyoachwa yajiotee tu na watu wanaoishi eneo hili lenye jumba hili tu ambalo sasa majasusi hawa wanalijongea kwa minajili ya kuingia na kuwaokoa Miller na Norman wanaoshikiliwa mateka ndani ya jumba hili lililozungushiwa senyenge na wigo wa maua mazuri lakini miti yake ina miiba.

Mwamba alisogea akalala chini sambamba na vigingi vya chuma vilivyochomekwa kwenye msingi uliozungushwa chini kabisa hili kushika senyenge iliyozunguka eneo zima la nyumba ambayo inaonekana iko kwa katikati.

Begi lilitolewa mgongoni kwa utulivu na umakini akafungua zipu na kutoa mkasi wa kukatia nyavu ambao si mkubwa ni mdogo tu lakini wenye makali ya nguvu, taratibu akaanza kukata eneo ambalo aliamini ataweza kupenya kama joka mpaka zilipo wigo, dakika moja ilitosha kukata kwa umakini tundu la kumuwezesha kupenya akarudisha mkasi kwenye begi akafunga zipu na kuzama kwa ndani sasa akawa zilipooteshwa wigo haraka akatoa miwani yake ya kijasusi yenye kazi inayofanana na darubini tena yenyewe ikiwa imeboreshwa zaidi ya unavyoweza kujua kwa kuona maeneo ya karibu kwa uzuri ingawa na yenyewe haiwezi kwenda umbali wa darubini.

ENDELEA NA DODO ASALI

HOFU PANDE ZOTE V

LAS ANONAS, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Nyasi zilizoko hapa ziliweza kumsaidia Agent Kai kufanya kazi ya kukata senyenge hii kwa mkasi huku mkononi akiwa na gloves za kuzuia umeme kuweza kumdhuru, ikimchukua dakika nne kukata akiwa katika umakini wa hali ya juu kweli kuhakikisha hakuna kinachosogea upande iwe kwa ndani ya uzio au nje bila macho yake kuwa ya kwanza kuona, alipomaliza kazi hii ya ukataji akaurudisha mkasi kwenye begi kisha akapenya kwenye uwazi akitanguliza kichwa miguu ikifuata.

Senyenge na wigo wa miti ya maua mekundu viliachanishwa kwa hatua moja tu hivyo uingiaji wa Agent Kai hapa ulimfanya awe mahala ambapo kwa jinsi umbo lake lilivyo ilimfanya awe anachomwa na miiba katika nguo alizovaa za shati la timberland rangi ya kijani nyeusi na suruali ya jeans kampuni ya CAT, mpaka alipoweza kuvunja vunja baadhi  vitawi ndipo alipoweza kulala kwa chini kuangalia mahala anapoweza kukata baadhi ya matawi kupata nafasi ya kupenya tena kuingia eneo la ndani la uzio, kwa akili ya haraka hapa ilikuwa hana budi kutoa mkasi tena umsaidie kwa kazi aliyokuwa akiifikiri kuifanya.

Upande wa Special Agent Silla alikwenda akiwa anainama kujificha kwa usawa wa nyasi ndefu zilizokuwa zimeota hapa zikiwa zimejichanganya na majanii mengine yaliyo na desturi ya kujiotea tu sehemu ambazo watu hawapiti piti na hakuna huduma ya kufyeka au kuyalima magugu na manyasi kama haya kama lilivyo eneo hili lisilo na makazi ya watu zaidi ya hili jengo lililo kama karakana, alipofika hatua kama nne kuifikia barabara ya vumbi ambayo upana wake machoni mwake ulikuwa ukionekana ni upana wa kuwezesha kupishanisha gari mbili tu kwa muachano mdogo kutegemea na aina za gari husika, umakini uliongezeka maradufu mkononi bastola yake aliyoifunga kiwambo cha kuzuia sauti alijilaza chini kabisa akawa anatambalia tumbo kwa kwenda mbele mpaka alipoifikia barabara yenyewe akaacha kutambaa akiwa kalala vilevile chini kabisa macho yake yaliyo ndani ya miwani yakizunguka kwa kasi huku na huko.

Alijisogeza kiupande upande akiifuata barabara mpaka sasa akaliona geti kuu la rangi nyekundu iliyopaushwa kwa jua pamoja na maji nafikiri ni ya mvua kwa muonekano wake, kwa nje kulikuwa hamna mtu yoyote aliyekuwa anaonekana lakini si kwa mtu kama Silla jasusi mbebezi angeweza kwenda kizembe zembe mpaka lilipo geti bila kujihakikishia usalama wake, aliendelea kutambalia tumbo hadi karibu na geti.

Haikuchukua hata sekunde moja alipolifikia kwa ukaribu wa hatua nne alisikia harufu kama mbili mchanganyiko, moja ikiwa ni harufu anayoijua ni ya sigara na ingine ni ya kilevi kinachovutwa kama sigara nacho ni bangi, moshi uliokuwa ukitokea kwa ndani ukienda juu akiwa anauona kwa upande wa juu wa geti ulimtambulisha upande huu aliolala yeye upande wa kushoto kwake na kulia kwa geti upande huu wan je alipo ndipo kuna mtu au watu wanaovuta hivi vivutwa mchangnyiko.

S.S Silla alitizama saa yake ya mkononi akausoma muda na kuziweka hesabu sawa za toka waachane na Agent Kai akaona ameshapoteza dakika kama kumi sasa alitiza huku na huko kisha akajiburuta tena mpaka lilipo geti akafungua zipu na kutoa bomu dogo la kutegwa linalofyatuliwa kwa rimoti kilipuzi haraka bila kusubiri subiri akalitega chini ya geti upande aliouona ndipo walipo wanaopata burudani ya vivutwa wakiwa kimya maana kiukweli toka afike hapa hakuwa amesikia watu wanaongea ilikuwa ni tulivu kana kwamba hakuna watu lakini moshi na harufu uliweza kuwaumbua walinzi wa geti hawa.

Kazi ya kulipachika bomu si kazi ya kumla muda mtu, Silla alimaliza kusudio lake haraka akainuka akainama kama gendaheka (nyani sokwe) akarudi kinyumenyume mpaka kwenye mti  mmoja ulio kati ya miti kadhaa iliyo kando ya miti hapo akaielekeza rimoti kilipuzi kule lilipo geti akaminya batani rukhsa.

Mshindo mkubwa ulisikika ukiwa umeambatana na kufumuka kwa geti na pia kusambaratika kwa nguzo za zegezinazoshika geti, bomu lilileta tafrani pale getini hakuna kilichobaki salama ni vumbi tu na damu zilizokuwa zimetapakaa wakati huo huo mtaalamu Special Agent Silla aliuzunguka mti akajiweka upande wa pili akiwa tayari kumshambulia yoyote ambaye ataitokeza pua yake kutokea kule lililpokuwa geti na sasa kuko wazi mwaaah!

   “Kazi nzuri Silla..!” Ilisikika sauti ya Agent Kai katika ya wote walio katika mfumo wao wa mawasiliano ‘small call network group’ (SCNG).

Kama ilivyotarajiwa walinzi wa upande wa pembeni ambao ni upande aliokuwa anaunyemelea Agent Kai waliposikia mlipuko kwa pamoja walikimbia kwenda mbele ya jengo hili waweze kuona upande wa getini kuna nini mpaka umetokea mlipuko kama huo, mbwa wao walikuwa wakibweka huku wamewashikilia kwa nguvu wasije wakaenda kule na kuishia kushambuliwa na aliyetelekeza shambulizi la bomu kama si waliotelekeza shambulizi hilo, walienda wakiwa wanajificha kitaalamu katika nguzo za vibaraza za jengo bunduki zao mikononi wote akili zao kwenye geti na hata walio nyuma ye jengo nao walipotezwa maboya wakaondoka eneo wanalolilinda na wao wakaja mbele lakini wakiogopa kwenda kuchungulia kwa nje kama wenzao na pia na wao walikuwa na mbwa wawili kama ilivyo kwa wenzao wa upande huu wa Agent Kai ‘TSC’.

‘The Sole Cat’ mtaalamu na jasusi mbobezi kutoka kitengo maalumu cha majasusi fundi cha ‘Special Activities Division’ (SAD) ni kama alipishana nao walinzi wakati wao wanakimbilia mbele kwa akili ya kusema wanaenda kuweka ‘covering’ yeye naye akiwa kama mtu asiyeacha fursa impitealikuwa usawa wa jengo pembezoni mwa moja ya madirisha makubwa kabisa ya vioo yaliyochakaa kwa kuyatizama ni uchakavu wake na kukosa matunzo ya kuyasafisha uliyafanya yawe kama yamepigwa rangi ya kaki kumbe ni vumbi.

Akitumia kiganja chake alichovaa gloves alifuta sehemu ndogo ya kioo usawa wa kichwa chake akaweza ona ndani hapo akakutana na eneo la wazi likiwa na magari kana kwamba ni gereji ya magari maana kulikuwa na ma oil yaliyomwagika mwagika kuleta weusi chini pamoja na madumu ya ma oil hayo na hata mapipa ya mafuta upande wa juu na hapa anapochungulia Agent Kai, hakuona mtu akizunguka kwa ndani ya eneo hili la ndani wala kusema apite akikimbia kwenda nje kulipoleta taharuki hapo ‘TSC’ aliinua mkono wenye saa yake akabonyeza batani aweze kuongea.

   “Silla piga risasi kwa bunduki yako hili udhidi kuwafanya wafikirie huko tu..” Akaongea akimuelekeza Special Agent Silla.

   “Naam… nilikuwa nasubiri kuona pua ya mtu itokeze.. Sawa sawa!” Akajibu Silla.

   “Rebecca unanisikia huko ulipo?”Akaongea tena Agent Kai kisha akatulia macho yaliyo ndani ya miwani yakisukwa sukwa huku na huko (si mchezo).

   “Nakusikia na ninashukuru plan imeenda kama alivyo plan Silla.. Niko ndani tayari nimepitia mlango wa nyuma kwa kutumia funguo hapa nimejificha chini meza kubwa iliyowekwa masanduku kama ya silaha ndiyo nilikuwa nasikilizia utulivu niweza kuona mengineyo kwa zaidi..!” Alieleza Special Agent Rebecca na kufanya Agent Kai muulizaji na hata Silla aliyekuwa akisikiliza kutabasamu.

   “Safi nami nataka niingie kupitia dirishani kama upo kwa ndani njoo nifungulie haraka..!” Aliomba Agent Kai msaada kwakuwa aliamini dirisha hili litakuwa inawezekana kufunguka kwa ndani.

Mara ilisikika milio ya bunduki kutokea kwa nje ya uzio, risasi zikipigwa kuelekea mahala pawazi palipokuwa na geti awali ilikuwa ni toke nitoke risasi moja inaita ingine ni mwendo wa mfuatano wa milio walinzi waliogopa kwakuwa walikuwa hawajui ni nini haswa wakawa kama wamepigwa misumari waliganda wakijificha vichwa vyao vikichungulia tu upande ulio wazi geti likiwa limevunjwa na kuwa limedondokea kwa ndani.

Rebecca alimuona Agent Kai akiwa katika umakini na tahadhari ya hali ya juu alinyata mpaka pale dirishani akafungua mshirika wake wa karibu na boss wake kama anavyopenda kumpa heshima hiyo akapandisha miguu na kuzama ndani ya eneo hili la gereji, dirisha likafungwa kama ilivyokuwa.

Milio ya risasi za kutoka kwenye bunduki ya Special Agent Silla aina ya M240 Machine Gun bunduki ya kivita ya kimarekani ambayo majasusi wengi wa kimarekani na wanajeshi karibu wote kwa ujumla upenda katika nchi hii upenda kutumia bunduki hizi ingawa zipo zingine na ni nzuri lakini kwao aina hii ndiyo ilikuwa bora zaidi ya nyingine kimatumzi na kimazoea, milio ilikata kwakuwa Silla aliacha kufyatua risasi ambazo kimtizamo walinzi waliweza kutambua zinapigwa na mtu mmoja pia ni muoga hivyo wakashauriana waanze kufanya mjongeo waone ni chizi gani anafanya hivyo.

Kuacha kwake kupiga risasi ilikuwa ni kuacha masikio yake yapate utulivu maana hakuwa ana kizuizi chochote alichoweka masikioni kuzuia asisikie makelele ya bunduki, ilikuwa kafana jambo la maana kwakuwa sekunde ishirini tu alisikia muungurumo kama si miungurumo ya gari ikijongea kujia barabara hii hapo kwa Silla aliona kazi yake ya kuwarahisishia ndugu zake kuingia ndani imeisha haraka aliweka bunduki begani kwakuwa ilikuwa na kamba yake maalumu, kisha akatoa bastola yake toka mahala anapopenda kuweka nyuma ya kiuno akainama akirudi kinyumenyume kurudi kule walipokuwa wameijia milio ya gari ilivyokuwa inazidi kusogea naye alizidisha spidi kisha akaanza hatua kubwa kubwa akaongezea na mbio kulifuata bonde mpaka mahala ambapo kulikuwa na muinuko wa kichuguu akaupanda na kujiweka hapo akitizama barabarani kutokea pale juu ya kichuguu.

   “Kuna gari nne zimeongozana zinakuja huko.. Ndani ya magari kuna watu wengi tu..!” Akaongea Silla akiwa kasogeza saa aliyovaa karibu na mdomo kuwaambia wenzake walio ndani .

  “Sawa! Subiri kuongeza nguvu kikinuka… Kuna mtu tunamuona anakuja huku gereji.. Nitakucheki! Acha tuone kwanza maana mpaka sasa hatuoni wapi tuelekee na Miller hajibu wala hatoi taarifa yoyote” Akaongea ‘TSC’ kwa sauti ya haraka haraka akiweka mkono saa aliyovaa karibu kabisa na papi (lips) zake kabla hajashusha mkono chini akiwa mahala pamoja wamejificha na Rebecca aliona meseji ikiingia katika saa simu yake lakini umakini ulikuwa kumuangalia mtu aliyeingia gereji hii akiwa katika mwendo wa kasi sana huku anaitizama simu yake iliyokuwa inaita, alisogea karribu na walipo kina Kai akapitiliza kidogo kisha akaamua apokee ile simu.

   “Hallow! Mkuu..”Akaongea hivyo kisha akanyamaza kupisha kumsikiliza aliyempigia simu aongee kitu ambacho ‘TSC’ na Rebecca hawakuweza kumsikia wa upande huo.

   “Lilikuwa shambulizi la bomu ndiyo lililosambaratisha geti… Mshambulizi hatujui kama yupo mmoja au wangapi ila mlio wa bunduki wote tulikubaliana ulikuwa ukitoka katika bunduki moja, sielewi zaidi ya hivi” Akaongea tena mtu yule mwanaume wa kizungu aliyevaa full jeans za rangi ya nyeusi na viatu aina ya buti za timberland water proof rangi ya njano, alinyamaza kusikiliza tena upande wa mpiga simu.

   “Hakuna kama icho… Tuko makini kweli kweli walio, nyuma ameenda mmoja kuimarisha ulinzi na pande zote vivyo hivyo” Akanyamaza kusikiliza tena akili na mawazo yake ikiwa kuangalia upande wa mbele tu ambako ni nje ya jengo bila kujua nyuma yake kuna watu wawili watu wa hatari sana wasio na utani kwenye hii game.

   “Ndiyo naingia chini kwenda kukagua cctv kamera.. Nilimuacha kwenye chumba kile Nesi Avon nilimpa maelekezo awe makini kuwaangalia mateka na pia kuangalia skrini zote za cctv” Aliongea kuonyesha anajibu swali kisha akanyamaza tena kusikiliza anaambiwaje.

   “Nilikuwa nafanya ile kazi uliyoniachia kuandika ripoti kama ujuavyo ofisi zenye mashine zinazofanya kazi ziko ofisi ya hapa karakana tu zile za chini bado hatujarekebisha” Akajibu tena kisha akasikiliza na ikaonekana wamemaliza maana alishusha simu yake akaipeleka kwenge mfuko wa mbele wa suruali yake akatizama tena nje ambako kulikuwa kukionekana vizuri kwakuwa kulikuwa na vioo tu kuanzia kuta zake, milango mpaka madirisha, aliporidhika akasogea kwenye ukuta wa ‘block’ ulio nyuma huku ambako kuna mlango ambao ulitumika na Rebecca kuingia akitokea eneo la nyuma ya jengo.

Mtu huyu alisogea katika eneo lililo na box kubwa kidogo la mbao linaloning’inia ukutani ambalo lilijazwa maspana mbali mbali pale akapafunua na kuvuta kitu kama waya hivi ulio katika mkusanyiko wa spana zile alipoacha kuvuta kulitikisika kidogo akasogea pembeni eneo lilelie lenye box la spana zile ulianza kujiachia ukasogea kuelekea kushoto kwake ukaanza kuonekana uwazi uliosogea kwa nafasi pana ya kuweza kupita gari haina ya IST, jamaa akazama ndani na muda wa sekunde tu pakajifunga vile vile Agent Kai na Rebecca wakaangaliana na kubetuliana kope za macho kwa ishara.

Hapo Agent Kai akaifungua meseji aliyotumiwa na kuona ni ya Investigator Miller akimueleza kuwa kafanikiwa kumrubuni nesi aliyekuwa akiwaangalia shida nesi hajui namba za siri za kuweza kufungua mlango wa kuweza kuwatoa toka mahala walipo kwa mujibu wa nesi ni kuwa mara zote hawaruhusu watu wengi kujua namba za siri za kufungua milango miwili ya kuingilia kwenye handaki hivyo yeye Miller anasubiri atokee mtu au watu ajaribu kufanya lolote litakalowezekana na Norman bado hana fahamu.

  “Meseji ya Miller… Kama kawaida penzi siku zote uwa ni kete muhimu sana kwa kazi zetu.. Anasema ameshamrubuni mwanamke aliyekuwa anawaangalia hivyo yupo tayari kwa lolote lakini Norman bado hajarejewa na fahamu..” Akaongea Agent Kai wakiwa wanaangaliana na Rebecca aliyekuwa makini kumsikiliza.

   “Mtu aliyepita atakuwa kashasogea umbali, twen’zetu” Akaongea Rebecca huku tayari ikishaanza kupiga hatua kuelekea pale alipofanya mambo yake mtu aliyetoka kuongea kwa simu muda si mrefu kisha akapotelea ndani, alilifikia box la spana la mbao lililoshikizwa ukutani na kwakuwa waya aliouona ulifanya jambo alikuwa ameukariri aliuvuta na kisha akatulia kusubiri matokeo wakati huo huo Agent Kai yeye alikuwa anaangalia nje jengo walipo walinzi ambao mpaka muda huu wapo waliosogea pembezoni mwa geti na wapo waliobaki wakiwa ilipo baraza ya mjengo huu ambao sasa walijua si gereji ni karakana.

Ukuta ulijiachia box likasogea pembeni kwenda kulia na uwazi ukamalizia kuendea kushoto hapo Agent Kai haraka akapiga hatua kumfuata Rebecca wote wakiwa na bastola zao mikononi, wakati wanapita kuna gari liliingia kupitia uwazi uliokuwa geti waliliona wote kwa pamoja lakini wao ilikuwa wazo lao ni huko wanakoingia sasa kunani.

Walipopita kwa ukutani wakaiona swichi wakaibonyeza pakajifunga na sasa wakawa kwenye korido ndefu sana yenye upana wa mita nne na urefu kwa kukadiia ulikuwa sawa na upana wa jengo la karakana, majasusi wakaangaliana kisha wakafuata kulia kwao wakinyata wakiwa wameongozana mpaka mwisho wa korido wakakuta ngazi wakateremka ngazi zile mpaka mwisho wake hapo wakakutana na mlango geti ambao una kadirisha juu cha vioo Special Agent Rebecca akachungulia na kukutana na kioo kisicho na uwezo way eye wa upande huu kuona ndani kwa pembeni a mlango geti huu kulikuwa na soketi yenye namba 0 mpaka 10.

   “Hamna njia zaidi ya kuharibu soketi kisha tufumue waya na kuziunganisha kijasusi zaidi mlango ufunguke” Akaongea Agent Kai alipoona uso wa Rebecca wenye maswali yenye kuhitaji majibu ukimtizama.

Mwisho wa sehemu ya sabini na nane (78)

Mambo yanazidi kunoga utamu!

Mbinu ya kuzubaisha walinzi zilizofanywa na Special Agent Silla zinawafanya Agent Kai na Special Agent Rebecca Smith kuingia ndani ya jengo bila walinzi kujua kuwa wamevamiwa ndani ya jengo.

‘Bwana muigizaji’ Miller amefanikiwa kumrubuni nesi Avon akitumia kete ya kufanya kwao mchezo mbaya mchezo mtamu unaopendwa na kuchezwa na watu wawili lakini wakiwa wanajificha wakati wanatenda licha ya utamu wake.

Kikosi cha watu mahususi toka TRJ na wengineo wanaomuenyekea sana mheshimiwa waziri nao wamefika Las Anonas kwa ajili ya kumfanyia mahojiano Investigator Miller, wanakuta hali ya sintofahamu.

Je Agent Kai na timu yake akiwemo mgonjwa mahututi Norman watatoka vipi katika jengo hili?



   “Mtu aliyepita atakuwa kashasogea umbali, twen’zetu” Akaongea Rebecca huku tayari ikishaanza kupiga hatua kuelekea pale alipofanya mambo yake mtu aliyetoka kuongea kwa simu muda si mrefu kisha akapotelea ndani, alilifikia box la spana la mbao lililoshikizwa ukutani na kwakuwa waya aliouona ulifanya jambo alikuwa ameukariri aliuvuta na kisha akatulia kusubiri matokeo wakati huo huo Agent Kai yeye alikuwa anaangalia nje jengo walipo walinzi ambao mpaka muda huu wapo waliosogea pembezoni mwa geti na wapo waliobaki wakiwa ilipo baraza ya mjengo huu ambao sasa walijua si gereji ni karakana.

Ukuta ulijiachia box likasogea pembeni kwenda kulia na uwazi ukamalizia kuendea kushoto hapo Agent Kai haraka akapiga hatua kumfuata Rebecca wote wakiwa na bastola zao mikononi, wakati wanapita kuna gari liliingia kupitia uwazi uliokuwa geti waliliona wote kwa pamoja lakini wao ilikuwa wazo lao ni huko wanakoingia sasa kunani.

Walipopita kwa ukutani wakaiona swichi wakaibonyeza pakajifunga na sasa wakawa kwenye korido ndefu sana yenye upana wa mita nne na urefu kwa kukadiia ulikuwa sawa na upana wa jengo la karakana, majasusi wakaangaliana kisha wakafuata kulia kwao wakinyata wakiwa wameongozana mpaka mwisho wa korido wakakuta ngazi wakateremka ngazi zile mpaka mwisho wake hapo wakakutana na mlango geti ambao una kadirisha juu cha vioo Special Agent Rebecca akachungulia na kukutana na kioo kisicho na uwezo way eye wa upande huu kuona ndani kwa pembeni a mlango geti huu kulikuwa na soketi yenye namba 0 mpaka 10.

   “Hamna njia zaidi ya kuharibu soketi kisha tufumue waya na kuziunganisha kijasusi zaidi mlango ufunguke” Akaongea Agent Kai alipoona uso wa Rebecca wenye maswali yenye kuhitaji majibu ukimtizama.

ENDELEA NA DODO ASALI..!

HOFU PANDE ZOTE VI

LAS ANONAS, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Ishara ya kuwa kuna meseji imeingia katika saa yake ilionekana kwa kitaa chekundu kuwaka hapo Agent Kai akauinua mkono wake na kuifungua ilikuwa ni meseji inatoka kwa Miller ilikuwa ni maelekezo kuwa kuna mtu ameingia kwa msaada wa nesi wamemdhibiti wanasogea naye kwenye mlango unaotumia ‘code number’kufunguka.

Alipomaliza kuisoma tu akainua macho yake kumuangalia Rebecca wakiwa bado wanaangaliana mlango wa hapa walipokwama ukaanza kupanda juu ukiacha uwazi wakatamani wajifiche lakini hakukuwa na mahala unaweza sema unaweza kujibanza hata kwa kujiweka kando jinsi kulivyo majasusi hawa haraka walishusha soksi zao kama kofia zilizo kichwani zikafunika nyuso zao na kuacha eneo la macho tu kisha wakainua mikono yenye bastola na kuelekeza eneo husika huku wanarudi nyuma taratibu kuhakikisha nyayo hazisikiki kwenye mijongeo yao.

Mlango ulipomaliza kuzama kwa juu tu wakatokea wanaume wawili mmoja akiwa katangulizwa mbele kisogoni mwake kuna mdomo wa bastola iliokamatwa vizuri na mwanaume aliye nyuma yake walisimama katikati ya kiambaza bila wa mbele kusogea maana alikuta watu wawili nao wameelekeza bastola zao kwao, nyuso zao zikiwa zimefunikwa soksi  zinazowaacha machoni, mtu huu alitamani watu hawa wawe ndugu zake huku hofu yake ikiwa kwenye maisha yake.

Agent Kai alichungulia kuona wa nyuma ni Miller kama meseji ilivyoelekeza akaona ni sahihi akapandisha soksi juu na kushusha bastola yake chini.

   “Nje wamezingira kote.. “ Akaongea kwa kiingereza Agent Kai kumwambia Miller kisha akawaacha wasogee mbele na mateka wao aliyetoa msaada mlango huu maalumu unaotumia mfumo maalumu kufunguka asogee mbele.

   “Norman tumemlaza kwa hapo acha nikamchukue… Kuna haja ya kuendelea kuwa na huyu mateka?” Akaongea Investigator Miller naye akitumia kiingereza lugha yao zoeleka, wote walikuwa hawatulii shingo zao zinazungusha vichwa vyao huku na huko tena kwa kasi kuangalia usalama wao hasa kule kwenye mlango uliowaleta huku kina ‘TSC’.

   “Baba! Habari yako?” Agent Kai akamuuliza mwanaume huyu kwa lugha ya kilatini ambaye muda huu alikuwa amelazimishwa kupiga magoti mbele ya majasusi hawa pembeni yao akiwepo mwanadada ambaye ni nesi akiwa amefumbata mikono yake kifuani mawazo mengi yakiwa yanagongana kichwani mwake kwa aliyoyafanya akikinzana na anavyoviwaza kuwa ni sahihi au pia si sahihi alikuwa katikati, penzi la muda mfupi alilopewa na Miller lilikuwa limeharibu uaminifu wake kwa mabosi zake licha ya kiapo alichoapishwa wakati anaingizwa katika shughuli za mheshimiwa waziri wa usalama.

  “Si nzuri” Akajibu mwanaume huyu wa kizungu.

  “Hatuna muda wa mjadala wala kubembelezana.. Sisi pia hatuna makosa, ndugu zetu walitekwa na wenzako hatujui hata wamekosa nini? Hatuhitaji kujua hili ila tunataka kukuacha wewe na maisha yako ukiwa mzima… Ila si bure ni kwa malipo ya msaada wako, umeshatoa msaada wa kwanza tunataka wa pili utakaokuwa ni wa maelekezo tu, hakuna njia ingine ukiacha ile uliyopita wewe wakati unaingia humu?”Agent Kai akamuuliza bila kujali jibu la salamu yake lilivyojibiwa.

  “Hakuna njia zaidi ya hii tu  kuja huku flour ya chini ya siri.. Kama kuna ulinzi mkubwa nje hakuna namna ya nyie kutoka salama hapa” Akajibu mtu yule na mara Miller akarudi akiwa kambeba kwenye bega Norman wakati huo huo Rebecca alikuwa juu ulipo mwisho wa ngazi akitizama kule ulipo mlango unaoingilia huku kwenye korido.

Akiwa bado anatizama aliona dalili za mwanga wa jua kuanza kuingia hii ilimaanisha mlango ulikuwa ukifunguliwa, akaonyesha ishara kuwa mlango unafunguliwa.

Agent Kai aliwatizama kwa zamu alionao karibu kisha kwa kasi akamtwanga kwa kitako cha bastola kwa nguvu mahala ambapo kifundi anajua lazima akimpiga mtu anapoteza uhalisia wake anapoteza fahamu na kweli jamaa akadondoka chini.

Kule juu Rebecca alipoona mtu wa kwanza anaingia kwa kasi hakuremba aliachia risasi toka kwenye bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti (sailensa) iliyoenda kutua kwenye shavu la mtu yule akarushwa na kujipiga kwenye kingo ya mlango moja kwa moja akaenda chini umauti ukamfika alioongozana nao walistuka hawakusogea mbele tena mlango ukabaki wazi vikawa vinasikika vishindo na minong’ono kwa mbali.

   “Mlaze hapo chini… Kazi imeanza upya muda wa kisasi chako Miller… Jino kwa jino” Akaongea Agent Kai huku anafungua begi lake kwa kasi akatoa bunduki yake ambayo iliikuwa imefunguliwa imekuwa kama vifaa tu akavifunga kwa kasi ile ile kwakuwa kwake mara nyingi ufanya hivi haikumchukua muda mrefu ikawa tayari akapakia ‘magazini’ akapanda ngazi kwenda kwenye kona aliyosimama Rebecca akiwa na morali damu inachemka.

  “Avon.. Unahisi tunatokaje hapa?” Miller akamuuliza mpenzi wake mpya wakiwa wamesimama mahala ilipolala miili miwili ya Detective Norman akiwa kwenye kuzirai na mwingine alieziraishwa na ‘TSC’.

   “Simu yangu unayo?” Akauliza Avon kumuuliza mpenzi wake macho yake na hata ya Miller yalikuwa yamekaza kuwaangalia ‘TSC’ na Rebecca ambaye alimpisha Agent Kai kusimama kwenye ile kona yeye Rebecca akiwa ameshuka ngazi moja chini anaiunda bunduki yake baada ya kuitoa kwenye begi aweze kuitumia vijasho wote vilikuwa vikiwatoka licha ya hali ya hewa kuwa si ya joto huku kwenye ‘flour’ ya chini kulikuwa na joto.

Miller hakujibu swali kwa mdomo akainua kichwa kukubali kisha akazamisha mkono kwenye mfuko wa suruali aliyovaa akatoka na simu aina ya ‘Samsung Pass’ smartphone ya kisasa toka kampuni hii ya vifaa vya kiteknolojia yenye makao makuu huko Korea Kusini  ambayo ni mali ya Avon akampa afanye anachotaka.

Juu pale alipo ‘TSC’ akiwa amejiweka tayari kwa lolote kutokea kule kwenye mlango wa kujia walipo wao alibaki amesimama kwa umakini na mara mlango ukaanza kujifunga kisha likaingia kama kopo likiwa limerushwa alikuwa akilitambua ni kopo la nini? Lilipotua chini baada ya kujipiga ukutani likaanza kutoa moshi  ulioanza kutokea pale ukaanza kusambaa kwa kasi kuja alipo yeye, likatupwa kopo lingine na lingine tena yakawa matatu na moshi kuwa mzito sana makopo yale yakitoa wa kama nyoka swila (black mamba)mwenye hasira.

   “Wametupa moshi wa kulevya.. Wote funikeni pua zenu” Akaongea upesi ikiwa Rebecca kashamaliza kazi ya kuufunga mtutu wa bunduki wakawa wote wanaangalia moshi wenye hewa inayolevya unavyosogea kuja upande wao, hawakusubiri wakarudi nyuma wakifuata ngazi  ujumbe wao ulishasikika na kwakuwa mlango waliokuwa wamefunguliwa na mateka aliye kuzirai sasa ulikuwa na ‘sensor’ unapokuwa umefunguliwa na mtu akiwa hajaondoka eneo la kiambaza au waweza sema eneo la besela basi wenyewe haujifungi mpaka mtu asogee hatua tatu mbele uwepo wa Norman akiwa kalazwa chini pale na hata hatua mbele kuwepo aliyewasaidia kina Miller kuufungua ulifanya pasifunge.

Mbio za kushuka ngazi ziliwafikisha pale kwenye kiambaza moshi nao ukawa unasogea kusambaa kuja walipo, kwa pamoja wakamnyanyua mtu wao Norman na kuzama tena kule walipotoka kina Miller hapo kila mmoja akakumbuka maneno ya mziraishwa aliyesema kama nje kumezingirwa hawawezi kutoka salama.

   “Wakati anafungua ulizishika ‘code number’ za kuufungua huu mlango?” Akauliza Rebecca kumuuliza Miller wakiwa wanamalizia kumshusha chini Norman.

   “Ndiyo! Nazijua.. Acha ujifunge” Akajibu Miller na mlango ukateremka kujifunga moshi ukaja na kukuta mlango ushashuka wote wakawa wamefanikiwa kuukimbia.

   “Hapa hatuwezi kutoka bila msaada wa ubalozi.. “ Akaongea Agent Kai akiwa anawaangalia wenzake wote pamoja naye wakiwa na jasho jembamba linalowaporomoka usoni.

   “Kumekaa vibaya sana..” Akaunga mkono Rebecca akaangalia saa na wote wenye saa wakaangalia ikiwemo nesi Avon ambaye kiukweli alikuwa na uwoga mkubwa sana sababu aliamini hakuna chochote kitakachoweza kufanywa na watu hawa wakatoka salama hapa, hofu ikazidi kuongezeka kuwa kwa usaliti aliofanya atapewa adhabu gani? Ikigundulika alifanya jambo kuwasaidia watu hawa.

   “Silla! Silla..!” Akaita Agent Kai kupitia simu saa aliyovaa mkono wa kulia anaoutumia kuvaa saa ukisogea mdomoni kama ilivyo kawaida yao wakiwa wanawasiliana kwa saa hizi zilizo katika mfumo waliounganisha wao kama kundi.

   “Naam! nakupata nakupata..!” Akajibiwa na Special Agent Silla waliyemuacha huko nje akiongea kwa haraka kama mtu aliyekuwa akikimbizwa jinsi hema yake ilivyokuwa si siri hata anapoongea na simu.

   “Huko salama?” Akahoji ‘TSC’.

   “Naam! Imenibidi niende kwa juu ya bonde maana msako mkali na mbwa unakuja huku naweza anza washambulia tokea huku kwa mbali lasivyo watakuwa wamesogea zaidi kunifikia nilipo kama ujuavyo mbwa” 

   “Hapa ndani tulipo hakuna njia salama kwetu kutoka hivyo wewe ondoka tu hapo kabla hawajakufikia maana kwa nilivyowaona uwingi wao hakuna namna tunaweza pambana nao tukiwa na Norman ambaye amaezirai hivyo basi usijaribu njia ya kuwashambulia watakushinda kwa uwingi wao napiga simu kuomba msaada ubalozini wewe rudi kule kwenye makazi ya wakulima tafuta mahala ujifiche”

   “Sawa na ni kweli gari zinaongezeka tu kuleta watu naona washastuka kuwa msaada wao ni nguvu kazi ya watu’

   “Fanya hivyo!” Akamaliza Agent Kai akiwa amesogea kwenye kitundu kidogo chenye kioo kuangalia upande waliotoka akawaona watu kama sita wa kazi wamevaa ‘gas mask’ usoni mwao mavazi yao wote yakiwa ni suti zinazofanana na wale waliowafanyia mtego kule ‘Mixco’, mikononi wakiwa wameshika bunduki aina ya Norinko QBZ-97 hapo ‘TSC’ akakumbuka siku ya kwanza anaingia Guatemala kilichotokea mgahawa wa Filadelifia akaitumia bunduki haina hii kuwaondoa maadui zao.

Watu hawa walikuwa ndani ya moshi mzito unaozunguka lakini kuwa na ‘mask gas’ iliwafanya wasihofu chochote wakawa wanashuka ngazi taratibu wakifuatana kana kwamba wananyatia lakini ilikuwa ni hofu kwao kuwa wanaweza wakashambuliwa kitu ambacho Kai kikawaida alikuwa akitamani kufanya hivyo ila kwa njia gani alibaki akiwaangalia kwa umakini wanavyosogea kisha bila hata kuacha kuchungulia akamuita kwa ishara Rebecca asogee pale naye hakuremba akasogea akaelekezwa achungulie kuona nyendo hatua gani jamaa wanachukua.

Namba ya simu ya katibu wa ubalozini ilitafutwa kwa haraka kwenye simu ya Agent Kai alipoipata akaruhusu kupiga na kuiweka sikioni.

   “TSC!” Upande wa pili sauti likaunguruma kama inatokea mtungini.

   “Tena hatarini mkuu wangu.. Tumezingirwa na maadui eneo linaloitwa Las Anonas, mwana timu mwenzetu alitekwa tumekuja kumfuata hali imekuwa hivi”

   “Las Anonas ni nje ya jiji huko.. Hili wawai itabidi watumie helkopta..!”

   “Vizuri ikiwa hivyo mkuu.. Nitashukuru sana ikiwezekana muombe balozi amtaarifu Rais wa nchi wa operesheni ndogo hii amwambie ni ya uokozi tu”

   “Hilo halina shida tumtaarifu tukiwa tumemaliza operesheni”

Maelekezo yalikuwa hivyo simu ikakatwa na Agent Kai akawaangalia wenzake wote kisha akatabasamu tabasamu la matumaini.

   “Tunakuja kuondolewa hapa msihofu.. Na jamaa hawawezi kuufungua huu mlango kuingia kutushambulia sababu na wao wanajua kuwa tuna mbinu nyingi za kujihami na pia wanaamini hatuna njia ya kuweza kutufanya tukaondoka hapa hivyo wanachofanya ni kuongeza vikosi vyao kuja huku ni kete nzuri jeshi likifika litapunguza nguvu ya maadui” Aliongea Agent Kai akimtizama Avon wakati anaongea maana alikuwa akitetemeka sana mwanamke huyu nesi asiye na uzoefu na mambo kama haya.

   “Naona wameleta kopo za gesi ya kulevya nafikiri kuna njia wanataka kuitumia” Akaongea Rebecca akiwa hajauondoa uso wake kuchungulia kitunduni.

‘TSC’ akasogea kuangalia na yeye aone pengine kutokana na uzoefu wake angeweza juwa nini kinataka kufanyika, alipochungulia akatathimini na kuona bado hakuna kitakachoweza wafanye wawe ana wasi wasi akainua bunduki ake kisha akakipiga risasi kisoketi chenye namba za kufungulia mlango huu akakivunja chote huku sauti ya mlio wa bunduki ikianikiza ndani mule kwa kujibiwa kwa mwangwi.

Akaishusha bunduki chini akasogea na kuziweka waya anavojua yeye ikawa mlango huu hauwezi kufunguka tena iwe kwa aliye nje na hata wao walio ndani labda mpaka litegwe bomu liweze kuusambaratisha.

Mwisho wa sehemu ya sabini na tisa (79)

Msaada ndiyo umeombwa kwa katibu wa ubalozi baada ya majasusi hawa kuona kwao ingekuwa ngumu kutoka eneo hili wakiwa salama hasa kwakuwa walikuwa na mtu muhimu wanayetakiwa kuondoka naye ambaye hana fahamu (amezirai).

Nisikupotezee muda twende tukaone nini kilifuata sehemu ijayo!




   “TSC!” Upande wa pili sauti likaunguruma kama inatokea mtungini.

   “Tena hatarini mkuu wangu.. Tumezingirwa na maadui eneo linaloitwa Las Anonas, mwana timu mwenzetu alitekwa tumekuja kumfuata hali imekuwa hivi”

   “Las Anonas ni nje ya jiji huko.. Hili wawai itabidi watumie helkopta..!”

   “Vizuri ikiwa hivyo mkuu.. Nitashukuru sana ikiwezekana muombe balozi amtaarifu Rais wa nchi wa operesheni ndogo hii amwambie ni ya uokozi tu”

   “Hilo halina shida tumtaarifu tukiwa tumemaliza operesheni”

Maelekezo yalikuwa hivyo simu ikakatwa na Agent Kai akawaangalia wenzake wote kisha akatabasamu tabasamu la matumaini.

   “Tunakuja kuondolewa hapa msihofu.. Na jamaa hawawezi kuufungua huu mlango kuingia kutushambulia sababu na wao wanajua kuwa tuna mbinu nyingi za kujihami na pia wanaamini hatuna njia ya kuweza kutufanya tukaondoka hapa hivyo wanachofanya ni kuongeza vikosi vyao kuja huku ni kete nzuri jeshi likifika litapunguza nguvu ya maadui” Aliongea Agent Kai akimtizama Avon wakati anaongea maana alikuwa akitetemeka sana mwanamke huyu nesi asiye na uzoefu na mambo kama haya.

   “Naona wameleta kopo za gesi ya kulevya nafikiri kuna njia wanataka kuitumia” Akaongea Rebecca akiwa hajauondoa uso wake kuchungulia kitunduni.

‘TSC’ akasogea kuangalia na yeye aone pengine kutokana na uzoefu wake angeweza juwa nini kinataka kufanyika, alipochungulia akatathimini na kuona bado hakuna kitakachoweza wafanye wawe ana wasi wasi akainua bunduki ake kisha akakipiga risasi kisoketi chenye namba za kufungulia mlango huu akakivunja chote huku sauti ya mlio wa bunduki ikianikiza ndani mule kwa kujibiwa kwa mwangwi.

Akaishusha bunduki chini akasogea na kuziweka waya anavojua yeye ikawa mlango huu hauwezi kufunguka tena iwe kwa aliye nje na hata wao walio ndani labda mpaka litegwe bomu liweze kuusambaratisha.

ENDELEA NA NONDO..!

HOFU PANDE ZOTE VII

LAS ANONAS, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Jitihada za vikosi viwili vyenye ushirikano kuvunja mlango kikawaida hili waingie ndani flour ya chini walipo kina Agent Kai kikawaida ziligonga mwamba hivyo walioongoza vikosi hivi kufika hapa waliitana pembeni huku ulinzi ukiwa umezatitiwa kwa kiasi kikubwa sana pande zote na hata msako wa watu kumi waliokuwa wakiufanya kumatafuta mtu aliyetega bomu na baadaye kupiga risasi kwa bunduki mpaka kupelekea milio ya risasi kuwafanya walinzi wafanye uzembe Kai na Rebecca kuingia ndani ya jengo, msako ulisitishwa baada ya viongozi wao kuwaambia warudi atakuwa kashakimbia mbali kama si na yeye kuwa ndani muda huo na ndiyo analeta tishio.

   “Hawa walioko ndani si watu wa mchezo mchezo ni mafundi kama tulivyo sisi na pengine wanaweza kuwa wametuzidi uzoefu kwakuwa wao ni watu wanaofanyia kazi mambo haya mara kwa mara hivyo tusijiulize sana wamezaje kuingia ndani tunaweza waza jamaa ni washirikina wakati si kweli  wamelisoma eneo letu, wakapanga mbinu kisha wakaifanyia kazi mbinu waliyoi plan na sasa wako ndani na huko ndani si kama wamekaa wanaogopa tu la hashah! Wako wanapanga plan ya watatokaje hapa kwakuwa tumewazingira” Alikuwa ni Stafu Sajenti wa zamani wa jeshi la wananchi la Mexico bwana Morientes Gudrado akianza kutoa maelezo yake wakiwa wamesimama kuizunguka meza watu zaidi ya sita, wanne toka genge la TRJ na wawili kutoka taasisi kuu ya kijasusi ya Guatemala inayosimamia na kuelekeza kwa ukaribu mambo yote ya kijasusi kwa mashirika yote ya kijasusi ya serikali ya nchi hii ya Guatemala lakini hawa maafisa wa Guatemala Intelligence and Security si kama wako hapa ikiwa wanafanya mambo yanayotakiwa na serikali la hashah! Hawajulikani, wako kibatili, wako wakifanya kazi kwakuwa ni washirika wa karibu wa mheshimiwa waziri wa usalama wa nchi hii bwana Rafael Valdes Ceni.

   “Haina budi kulazimisha watoke humu ndani, kumbukeni mheshimiwa Rais wa nchi yuko hapa jijini toka jana hivyo jambo lolote linapotokea kuna watiifu wake wanaompatia taarifa hata kama liko huku pembeni ya jiji na ni sehemu ya siri lakini ni jengo linalofahamika miongoni mwa makachero wengi GIS, TACCG na mashirika mengine, hatuwezi kujipa uhakika kuwa wananchi walio karibu na maeneo ya hili jengo letu kuwa hawajasikia au hawatasikia milio ya bunduki na hawawezi kunyamaza tu kwa nchi ya amani kama nchi yetu lazima watatoa taarifa kuwa kuna milio ya risasi eneo la Las Anonas katika jengo la karakana hapo ndipo mambo yataanza kuharibika..!”Afisa wa GIS aitwaye Eddie Mauro aliongea kwa kirefu kidogo akiwaeleza waliokuwa alio nao hapa kikaoni huku mikono yake ikimsindikiza kwenye kila hatua ya mdomo wake unavyonyanyuka na kushuka.

   “Mheshimiwa waziri amenitumia meseji tutumie kila mbinu watu hawa tuwapate hata tukiwaua kadhaa kati yao ni sawa tu tukimpata mmoja mzima atatusaidia kujua ilkuwaje wamejiingiza katika suala hili na walipanga nini? Tutumie njia ya mwisho kwa kuulipua mlango kwakuwa milango mingine ukiacha huu wa pili katika hii flour ya chini ni milango ya funguo za kawaida na ya alluminium si kazi kwetu kuisambaratisha tukiwafukua kila kona… Yaani bado sijajua wamejuaje walipo wenzao au nesi Avon ametusaliti? Natamani kujua!” Huyu sasa ni kiongozi mkubwa tu ndani ya GIS kutoka mkurugenzi alifuatia huyu kwa cheo akiwa anasimamia operesheni zote za GIS iwe nje au ndani ya nchi anafahamika kwa jina la Donta Fransisco Portu akiwa kavaa miwani ya macho ya kumsaidia kuona kwakuwa kidogo alikuwa na matatizo ya kuona vizuri.

   “Jengo ni lenu… Na kiukweli njia uliyoelekeza ndiyo njia sahihi.. Haraka turuhusu vijana waweke bomu au baruti kulipua mlango wakisikia mlipuko tu watachanganikiwa hapo sisi tutaendela na nmfumo wetu wa kurusha hewa ya gesi ya sumu tena tukizidisha kwa kutupa kwa wingi ikaenee flour yote ya chini” Aliunga mkono mwanadada aliyekuwa akifukuziwa na kina Agent Kai Madam Mariana mwanamke pekee aliyekuwa miongoni mwa watu hawa waliosimama kuizunguka meza iliyo katika ofisi ndogo iliyo katika karakana hii ya magari iliyo na siri kadhaa za kutesa watu na hata kuwatoa kwa kikundi kilicho chini ya mheshimiwa waziri wa usalama.

Maamuzi yalipita wafanye kama walivyoona ni sahihi kulipua mlango aliitwa miongoni mwa watu wa kikosi cha GIS akapewa maelekezo ya nini kifanyike, wakati akitoa maelekezo waliona watu walio nje ya jengo wameanza kukimbia kimbia wakipishana huku na huko ilikuwa si kawaida hivyo walinyamaza kuona kuna nini? Hatari! Wakaanza kusikia milio ya helikopta.

Wakuu hawa wote walitoka mbio kuelekea lango kuu kisha wakatoka nje kwa pamoja hakuna aliyekuwa akiongea kitu ndipo macho yao wote wakaona angani helkopta tatu zikiwa zinakuja eneo hili na dalili zote kuwa hakuna usalama zilionekana kwa watu walio kwene helkopta ingawa zilikuwa angani watu wenye silaha za kivita walionekana.

Mabomu ya kudondoshwa yakaanza kudondoshwa kuanzia kule nje yalipopakiwa magari waliyokuja nayo Mariana kila helkopta ilikuwa inashusha mabomu inapita inakuja ingine inashusha vitu pale ilipoishia ingine zinaenda kupindua mbele na kuanza kudondosha kutokea nyuma ilikuwa ni hali ya hatari kubwa sana ni mwendo wa maiti kuzalika tu miili ikawa inatapakaa yalikuwa ni mabomu mazito yaliyokuwa yakisambaratisha kuta za vioo na madirisha yake.

Eneo lililokuwa na karakana ya magari mabovu washambulizi walishambulia kwa mabomu milipuko mikubwa ilitokea kwakuwa kulikuwa na mafuta ya petrol na diesel katika baadhi ya magari na hata oil safi kwa chafu kukawa kunawaka moto kunalipuka huku kunaendelea kuwaka moto mkubwa tu.

Mariana na watu wengine ambao muda si mrefu walikuwa wanafanya kikao kabla hawajakimaliza wakiwa katika kuelekeza cha kufanyika ndipo uvamizi ulipotokea walikimbia kwenye korido wawili kati yao bahati haikuwa yao walikumbwa na moja ya bomu na kuwafanya watawanywe umauti ukawasomba kwa haraka, wawili walikoswakoswa, majeruhi yalimkumba Stafu Sajenti tako lake la kulia alichomwa na chuma kimoja kilichochongoka kilichosambaratishwa kutoka kwenye moja ya gari, kilizama toka nyuma takoni mpaka mbele katika kibofu cha mkojo ilibidi Mariana na Eddie Mauro wa GIS wamshike huku na huku kumsaidia kusogea naye hadi kule kwenye mlango wa chini wakishuka ngazi huku kulikuwa na zege limeachia kwa mabomu lakini kulikuwa kunapitika na majeruhi mwingine alijeruhiwa mgongoni kwa tofali lililojiachia kutoka ukutani kumpiga mgongoni lakini alikuwa akijimudu kutembea akiwa katika maumivu makali uso wake aliukunja huyu alikuwa ni Donta Fransisco Portu wa GIS.

Waliweka baruti kisha wakaulipua mlango ukavunjika lakini aliyetaka kupita au kutokeza sura yake walibakia wamesimama katikati ya kiambaza na ilikuwa haki yao kufanya hivyo kwakuwa kwenye kona mbili za milango inayoingia katika vyumba kulikuwa na Rebecca Smith akiwa na bunduki mdomo ukielekezwa ulipo mlango mkuu wa kujia ndani ya hii flour kwenye kiambaza cha mlango mwingine ulio karibu na lango kuu lililosambaratishwa alikuwepo Agent Kai kakamatia barabara bunduki tayari kwa matumizi akiwa upande wa kushoto na kulia yupo Miller na bastola huku ndani ya chumba walichosimama mlangoni yupo nesi Avon.

Mariana akatoa kopo moja la gesi ys sumu ya moshi wa kulevya toka kwenye begi ambalo alikuwa amelikamatia mkononi, akalitupia kwa ndani kama kawaida lililpojipiga ukutani likajiachia ilikuwa karibu kabisa na kiambaza cha mlango walichosimama Agent Kai na Investigator Miller ambao wote wawili hakuna aliye mgeni na vitu hivi kila mmoja kwa kasi akaondoka toka waliposimama kukimbilia inapoelekea korido ya hapa wakirudi kinyumenyume, Rebecca alijiunga nao ikawa Agent Kai na Rebecca mkono mmoja umeshika bunduki na mkono mwingine wanachana fulana walizovaa zilizo ndani ya makoti waliyovaa kwa ajili ya kuzuia baridi wakiwa wameyafungua zipu yameachia huku na huku, walikuwa wakichana kwa visu huku Miller ambaye alikuwa amevaa shati la jeans lililokuwa la mtu wa GIS aliyewasaidia kufungua mlango kisha akaziraishwa na Agent Kai kwa kipigo cha kitako cha bastola kwenye kibaraza cha ngazi hivyo yeye alikuwa akirudi nyuma akiwa kaziba pua kwa mdomo nia yake asubiri mmoja ampatie kisu naye achane shati alilovaa.

Walifanikiwa kufanya walichotaka wakajifunga eneo la mdomoni na puani kwa vipande vya fulana walivyovikata toka kwenye fulana na shati, lilitupwa kopo lingine likafuata lingine pote pakawa na moshi kama jalala la taka lililochomwa moto kwa minajili ya kuziteketeza taka zote kwa kuziunguza, timu ya watu watatu ikafika mwisho kabisa wa korido miwani waliyovaa Rebecca na Kai iliwasaidia kuzuia miwasho ya moshi lakini si kwa Miller ambaye hakuwa na miwani macho yalianza kuathirika machozi yakawa yanamtoka.

   “Pole Miller.. Tutakulinda kwa vyovyote vile iwavyo..!” Akaongea Rebecca baada ya kumtizama usoni Miller.

Kujaribu hali ilivyo Mariana alilirusha begi kwa ndani kwa mtindo liende linabingirika hapo lilichakazwa kwa risasi za dabo dabo kama sita hivi toka kwenye bunduki mbili moja ya Rebecca ingine ya Kai hasa kwakuwa kulikuwa na moshi walizubaika wakiona kama ni mtu.

Nje huko helkopta zilishuka chini na kushusha wanajeshi wa kimarekani wakiwa katika mavazi yao ya kivita idadi kama ya watu ishirini toka katika helkopta zote kwa ujumla wakiwa wanaamini washafagia va kutosha kwa mabomu waliyoyashusha, kwa tahadhari na umakini mkubwa walikwenda wakikagua kila mwili wanaouona na kama walikuta ni majeruhi walimalizia kwa kushindilia risasi kuwamalizia wakaingia mpaka karakana nako ikawa vivyo hivyo ukaguzi ukiendelea huku kiongozi wao akipokea maelekezo toka kwa katibu wa ubalozini.

Wanne wa mbele walipoingia kwenye korido waligundua harufu ya mabomu ya gesi ya sumu ya kulevya haraka wote wakajiwai kwa kushusha ‘mask gas’ zao usoni kisha wakaendelea kupiga hatua kusonga mbele.

Wa mbele alikwenda mpaka karibu na kona akasimama na kisha akachukua kifaa ambacho kinaweza chukua jambo la upande wa pili bila mtaka kuona kuutokeza uso wake kilicho kidogo kama peni aina ya ‘Speedo’, akakilaza chini na kukitokeza kidogo kwa chini kisha akachukua ‘tablets’ toka kwenye begi akacheza kidogo akaweza kuwaona vizuri licha ya moshi watu ambao walikuwa kwenye taharuki kubwa katika miili yao kwa jinsi walivyokuwa wakiangalia huku na huko na bunduki zao mikononi mwao.

   “Ni vizuri mkajisalimisha sababu wanajeshi wa marekani wamezingira eneo lote na mliobaki ni nyie tu wanne na wawili kati yenu wanaonekana ni wenye maumivu makali sana majeruhi… Tunatoa dakika mbili kujisalimisha kwenu na kwakuwa hatuna shida na nyie si tumekuja kuwafuata ndugu zetu tu tutawapiga bomu la kutupwa kuwaangamiza wote bila huruma..!” Akaongea kiongozi wa wanajeshi waliotokea ubalozini kuja kufanya operesheni ya uwokozi kwa raia wenzao wa Marekani.

Kupitia kifaa kilichotangulizwa kuwekwa kama peni ya’ speedo’ chini watu hawa wakiongozwa na Madam Mariana mwanamke anayetafutwa kwa udi na uvumba na Agent Kai walionekana wakiangaliana kisha wakaweka silaha zao chini na walio wazima wakanyoosha mikono juu kuonyesha wamesalimu amri (maskini) na majeruhi nao wakajilaza chini wakiwa wamekata tamaa.

Wanajeshi wawili wakajitokeza mitutu ya bunduki ikiwa mbele wamewaelekezea waliojisalimisha.

  “Inukeni mpande juu ngazini taratibu janja janja zote wekeni pembeni” Akaongea kwa sauti inayotoka kwa kuunguruma kama spika mbovu inayokwaruza kutokana na kuwa alikuwa amevaa ‘mask gas’ mwanajeshi kiongozi wa jeshi la Marekani, alieongoza kikosi kilichofika hapa kwenye jengo la siri la ‘GIS’ eneo la ‘Las Anonas’.

Mariana na Eddie Mauro afisa wa usalama wa ‘GIS’ wakiwa wamenyoosha mikono juu walipanda ngazi wakiwaacha majeruhi wao wamelala chini mmoja aliyechomwa kutokea takoni kuja kibofuni damu zilikuwa hazajakata kutoka anasikia maumivu makali sana chuma bado liko vile vile, wakati wao wanapandisha juu mwanajeshi mmoja wa jeshi la Marekani alipishana nao akateremka kasi mpaka kwenye kiambaza akiwaruka majeruhi waliolazwa chini kisha akasimama katikati ya kiambaza akatoa kitambaa kidogo mfukoni mwake alipokikunjua kilikuwa kibendera cha Marekani akautokeza mkono wake upande waliokuwa wakiogopa kina Mariana kuingia akakipepea kitambaa kionekane uzuri.

  “TSC’ code name na wenzako tumefika kuwachukua tunajua mmefanya kazi kubwa kuzuia msiingie matatizoni mimi ni Sajenti Ramazani Asmani wa jeshi la Maji la Marekani katika kituo cha operesheni za dharura ubalozi wa Marekani hapa Guatemala…!” Akajitambulisha mtu yule.

  “Ahsante sana Sajenti.. Nashukuru mmefika wakati mufaka kuokoa maisha yetu” Akajibu Agent Kai kwa tabu kwakuwa ilimbidi ashushe chini tambaa alilokata kwenye fulana alillovaa akaongea haraka kisha akapandisha kurudisha papo hapo mwanajeshi aliyekuwa akiongea akajitokeza na bendera yake mkononi wake wa kulia kushoto bunduki akiwa ameikamatia kwenye ‘magazini’.

Sajenti Ramazani Asmani akiwa kajifunika uso wote kwa ‘mask gas’ hakuna sehemu ya mwili wake iliyokuwa ikionekana maana hadi viganjani alikuwa amevaa ‘gloves’, alipojitokeza yeye wakajitokeza na wengine watatu wote wakasogea kuwapa msaada kina Agent Kai kwakuwa walikuwa washaanza kuingiwa kwa gas ya sumu ya kulevya iliyokuwa inapenya kwenye vitambaa walivyofunika juu ya ‘mask’ zao za kawaida walizovaa kuziba tu uso wakati wanaingia kwenye mjengo huu.

  “Poleni sana mkuu.. Mko nyinyi tu?” Akauliza tena Sajenti Ramazani akiuweka mkono wa Miller katika bega lake kwakuwa huyu hali ya hewa ya gesi ya sumu ilikuwa imemfanya kazi sana hivyo ilitakiwa kwa haraka ampeleke juu aweze kusaidiwa kwa kuwekewa kinga.

   “Chumba hiko hapo kuna mwanamke mmoja na mwanaume mmoja ndiyo tuliowafuata humu wachukueni” Akaelekeza Kai kisha akiwa kainua juu kitambaa kisha akakirudisha kasi akikimbia kwenda juu kuwaacha wanajeshi waendelee na kazi.

Dakika tano mbele wote walikuwa wako nje ya jengo hili ambalo nusu saa iliyopita lilikuwa jengo zuri na tulivu lakini kwa sasa palikuwa kama pagala jinsi kulivyovunjwa kwa mabomu na pia damu za waliouwawa na kujeruhiwa zilikuwa zimetapakaa sehemu kubwa madimbwi  dimbwi, vipande vya miguu, mikono na hata viwiliwili na hata vichwa ama kweli mabomu hayarembi, huduma zilitolewa kwa wote waliokuwa wakijisikia vibaya kwa mbali wakaanza kusikia ving’ora vya magari ya polisi.

   “Tuondokeni!” Akaongea kiongozi wa msafara wa wanejeshi Sajenti Ramazani , kauli yake ikaungwa mkono na wote lakini wakati wanaendelea kuingia kwenye helkopta ikatokea gari ambayo Agent kai na kina Rebecca walipoitazama wakaona ni ‘Ford Edge’ ikiwa inaendeshwa na Special Agent Silla.

  “Sajenti! Ni mwenzetu huyu.. Itatubidi tuondoke naye tungeomba tuondoke na mateka walio katika hali nzuri nyie muondoke na hawa majeruhi” Akaongea Agent Kai kumwambiwa Sajenti Ramazani Asmani ambaye kwa muda huu karibu wote waliweza kuonana sua zao kwakuwa waliondoa ‘mask’ zao, huyu alikuwa ni mmarekani mweusi kama alivyo yeye ‘TSC’.

  “Sawa! Haina shida tunachoweza kusema sisi ni kuwatakia operesheni njema na msisite kutuomba msaada kila pale mtakapokuwa mnauhitaji tupo tayari!” Akajibu ombi lile Sajenti Ramazani.

Agent Kai na timu yake yote wakashuka kwenye helkopta kwa haraka wakiwa na majeruhi wao Norman na hata mwanadada nesi Avon wakapakiana kwenye ‘Ford Edge’ na kuondoka wakipita njia tofauti na ile ambayo inaonyesha wangekutana na msafara wa gari za polisi na helkopta nazo zikapaa angani kuondoka eneo hili.

Mwisho wa sehemu ya themanini (80)

Agent Kai na timu yake wamefanikisha mpango wa kuondoka eneo la hatari kwa msaada wa jeshi dogo la msaada wa dharura lililopo nchini Guatemala likiwa limeweka kambi chini ya ubalozi wa Mareakni nchini Guatemala.

Hali imezidi kuwa ya kuogofya upande wa ‘TRJ’ na washirika wao wanaofanya nao kazi kwa kushirikiana bila kujijua kuwa wanajihatarisha hawa ni baadhi ya watu walio katika usalama wa taifa taasisi inayosimamia ujasusi na ulinzi nchini Guatemala (GIS).

Nini kitajiri sehemu inayofuata ambapo tunakaribia hitimisho la jino kwa jino




  “Poleni sana mkuu.. Mko nyinyi tu?” Akauliza tena Sajenti Ramazani akiuweka mkono wa Miller katika bega lake kwakuwa huyu hali ya hewa ya gesi ya sumu ilikuwa imemfanya kazi sana hivyo ilitakiwa kwa haraka ampeleke juu aweze kusaidiwa kwa kuwekewa kinga.

   “Chumba hiko hapo kuna mwanamke mmoja na mwanaume mmoja ndiyo tuliowafuata humu wachukueni” Akaelekeza Kai kisha akiwa kainua juu kitambaa kisha akakirudisha kasi akikimbia kwenda juu kuwaacha wanajeshi waendelee na kazi.

Dakika tano mbele wote walikuwa wako nje ya jengo hili ambalo nusu saa iliyopita lilikuwa jengo zuri na tulivu lakini kwa sasa palikuwa kama pagala jinsi kulivyovunjwa kwa mabomu na pia damu za waliouwawa na kujeruhiwa zilikuwa zimetapakaa sehemu kubwa madimbwi  dimbwi, vipande vya miguu, mikono na hata viwiliwili na hata vichwa ama kweli mabomu hayarembi, huduma zilitolewa kwa wote waliokuwa wakijisikia vibaya kwa mbali wakaanza kusikia ving’ora vya magari ya polisi.

   “Tuondokeni!” Akaongea kiongozi wa msafara wa wanejeshi Sajenti Ramazani , kauli yake ikaungwa mkono na wote lakini wakati wanaendelea kuingia kwenye helkopta ikatokea gari ambayo Agent kai na kina Rebecca walipoitazama wakaona ni ‘Ford Edge’ ikiwa inaendeshwa na Special Agent Silla.

  “Sajenti! Ni mwenzetu huyu.. Itatubidi tuondoke naye tungeomba tuondoke na mateka walio katika hali nzuri nyie muondoke na hawa majeruhi” Akaongea Agent Kai kumwambiwa Sajenti Ramazani Asmani ambaye kwa muda huu karibu wote waliweza kuonana sua zao kwakuwa waliondoa ‘mask’ zao, huyu alikuwa ni mmarekani mweusi kama alivyo yeye ‘TSC’.

  “Sawa! Haina shida tunachoweza kusema sisi ni kuwatakia operesheni njema na msisite kutuomba msaada kila pale mtakapokuwa mnauhitaji tupo tayari!” Akajibu ombi lile Sajenti Ramazani.

Agent Kai na timu yake yote wakashuka kwenye helkopta kwa haraka wakiwa na majeruhi wao Norman na hata mwanadada nesi Avon wakapakiana kwenye ‘Ford Edge’ na kuondoka wakipita njia tofauti na ile ambayo inaonyesha wangekutana na msafara wa gari za polisi na helkopta nazo zikapaa angani kuondoka eneo hili.

ENDELEA NA NONDO…!

PANDE MBILI ZA SHILINGI I

PETATLAN, GUERRERO-MEXICO

Soledad De Maciel eneo linakopatikana kasri la kifahari la ‘Kingpin’ mkubwa kiongozi mkuu wa genge la ‘TRJ’ Bigedia mfukuzwa wa jeshi la wananchi la Mexico Bwana Fernandes Carlos Codrado, katika manispaa ya mji wa Petatlan hali ilikuwa ya kuogofya miongoni mwa kila anayeingia na kutoka katika kasri hili, moja kasri bora sana na la kuvutia.

Muda wa saa nane na dakika ishirini usiku ikiwa siku ya jumapili ina masaa mawili toka ianze ikiiacha jumamosi iliyokuwa ndefu kutokana na mapambano yaliyoacha makovu ya umauti pamoja na umajeruhi kwa ‘TRJ’ helkopta aina ya Robinson R-22 kati ya helkopta mbili anazozimiliki ‘Kingpin’ wa genge la ‘TRJ’ Bwana Fernandes Carlos Codrado ilitua katika eneo la kiwanja cha kutua ndege ndogo na helkopta kama hizi kilichopo ndani ya kasri la kisasa na kuvutia la ‘Secreto Potential La Feca Palacio’ kwa Kiswahili unaweza kuliita ’Nguvu Ya Siri Ya Kasri La Feca’, Helkopta hii na hata ingine usiku huu zilikuwa zimeruka kwa pamoja katika muda mmoja kuondoka hapa kwenda nje ya mipaka ya Mexico kitu ambacho ni nadra kutokea toka zinunuliwe katika nyakati tofauti tofauti.

Pamoja na kuruka kwa wakati wa muda unaofanana lakini kurudi ilianza kurudi kabla ya hii ya rangi ya njano  ‘Robinson R-22’ kuwa imeingia hapa ambayo yenyewe ni aina ya ‘Robinson R-44 Raven I’ hii ni ya rangi nyeusi na baaadhi ya sehemu kuna mistari meupe hii ni kubwa na bora zaidi ya kwanza ikiwa na kasi zaidi pale inapokuwa mawinguni hii marakwa mara Bwana Feca uitumia yeye, ambayo mara kwa mara kwa matumizi ya watu wengine ‘Kingpin Feca’ upenda watu wa tofauti naye watumie iwe marafiki au ni vipi basi uwaachia watumie ‘Robinson R-22’ Helkopata yake ya kwanza kuinunua katika maisha yake.

‘Robinson R-44 Raven I’ iliondoka kuelekea nchini Canada ambako kiumbali ni mbali kuliko Guatemala lakini ndiyo ilikuwa ya kwanza kurudi kama nilivyokwisha kueleza hapo juu, huko Canada ilikuwa imefuata moja ya viongozi wa juu wa genge la ‘THE RED JAGUAR’ waliokuwa huko wiki zaidi ya tatu wakipata matibabu ambao ni Ivan Albeto a.k.a ‘alto genius’ mzee wa vimemo, Mr. Villa Nandez Guti, Wolfs Klauben Gend a.k.a ‘Monster One’ na Koplo Lavatel Santos. Wote hawa walikwenda Canada ilipo hospital ya genge hili ya siri ikifanya vizuri kwenye jamii lakini pia ikiwa inafanya mambo kwa ajili ya faida ya genge la ‘TRJ’, ikiwa ni moja ya hospitali yenye madaktari bingwa wa kihindi wa magonjwa na operesheni mbalimbali.

   “Karibuni sana ndugu zangu, karibuni sana nyumbani kwenu waheshimiwa mabosi wenzangu” Aliongea Feca mwenyewe akiwa kasimama safu ya mbele kabisa karibu na helkopta hii iliyotua muda si mrefu huku pembeni yake akiwa na watu walio kama wanamzunguka kumbe walikuwa na wao wamesogea hapa kuwapokea watu waliofika hapa na kushuka wakiwa na tabasamu tele kama waliokuwa wanawasubiri.

   “Ahsante sana mkuu.. “Aliyejibu ukaribisho alikuwa ni mtu aliyewastaajabisha wengine wote ambao si washukaji toka kwenye helkopta, alikuwa ni ‘bwana vimemo’ tena aliweka tabasamu kabisa kuonyesha sasa si ‘bwana vimemo’ tena kwa furaha kubwa ‘Kingpin Feca’ alimkumbatia wakakumbatiana wakiminyana kwa nguvu kuonyesha furaha kali waliyonayo.

  “Nina furaha sana leo kwa kurudi kwenu” Akanong’ona Feca mdomo wake akiwa kausogeza kwenye moja ya sikio la Ivan ‘Alto Genius’.

Alipoachiana na ‘Alto’ akasogea kukumbatiana na Mr. Villa Nandez Guti, makamu wa Rais wa genge la ‘THE RED JAGUAR’.

   “Karibu mheshimiwa.. Poleni kwa safari!” Akaongea Feca wakapigana migongoni ishara ya kutiana mioyo.

   “Ahsante sana mheshimiwa.. Nasi tunafurahi sana kurejea Mexico yetu ingawa tunapata habari za kutuchanganya sana toka majuzi toka kwako na wengine” Villa Nandez akajibu ukaibisho kwa kueleza kwa kifupi linaloonekana linamchanganya.

  “Kwa kweli kuna kamtikisiko kanatubabaisha kwa kweli.. Kwakuwa mshafika nafikiri mkishapumzika asubuhi tutaongea mengi zaidi kwenye cha kamati kuu yote ambacho pia mdogo wangu Alexis na mheshimiwa Ceni watakuwepo wameingia muda si mrefu toka GTL” Maelezo ya kutia moyo yakatoka kwa Feca kwenda rafiki yake.

   “Kuna usalama kweli?! Kaka” Akauliza Mr. Guti baada ya kusikia majina yaliyotajwa kuwa pia na wao watakuwa kwenye kikao watakachofanya asubuhi hapa waliachiana wakabaki mikono yao ya kulia imeshikana wanaangaliana kwa sura zisizo na ujasiri ambao uwa wanao mara nyingi.

   “Usiumize kichwa Guti… Najua unatambua tumeshinda vita nyingi sana mpaka kufika hapa, umetoka kwenye matibabu na hata hujapumzika unataka kujiumiza kwa mawazo yasiyotakikana” Akaongea Feca kisha akauachia mkono wa rafiki yake.

Feca akamgeukia mjerumani mwenye roho ya kishetani, roho ya kutamani kuona mtu anavyoumia wakati anamtoa roho Mr. Wolfs Klauben Gend a.k.a Monster One naye wakakumbatiana wakisalimiana kwa mtindo ule ule kama wa wengine waliokwisha salimiana.

    *****  *****  *****

PANDE MBILI ZA SHILINGI II

CHIMALTENANGO, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Jumamosi ilikuwa ndefu sana kwa timu inayoongozwa na Agent Kai kwani walipotoka eneo la ‘Las Anonas’ wakisaidiwa kuokolewa kutoka katika jengo la siri la kikosi kilicho ndani ya taasisi kuu ya kijasusi ya ‘GIS’, kikosi kilichoundwa na mheshimiwa wa waziri wa usalama kwa siri akimshirikisha mkurugenzi wa taasisi hii aminiwa na serikali katika masuala ya nchi katika usalama na hata kuulinda uchumi wa nchi na vyanzo vyake.

Walivyofika maskani kwao ambayo ni maskani iliyoweza vunja rekodi kwakuwa ya usiri mkubwa sana kiasi cha kuwasumbua sana vichwa kikosi cha siri cha waziri wa usalama pamoja na washirika wao wa genge la ‘TRJ’, uchunguzi wao uligonga mwamba kipindi chote kuwa wapi wanapotokea? Wapi wanapojificha? Haya yalikuwa maswali makuu yasiyo na majibu kwao, walipofika Agent Kai na wenzake wakiwa na mwili wa mtu aliye hai lakini yumo ndani ya kuzirai walifanya taratibu wa kumuita daktari ambaye ni daktari wa siri na muaminifu kwa Kamanda Muniain pamoja na kijana wake Norman.

Hakuitwa dokta peke yake waliitwa na vijana wengine waaminifu ambao mara nyingi Kamanda Muniain alikuwa akiwatumia kufuatilia mambo ambayo wao wanakuwa hawataki kuonekana wako nyuma ya jambo hilo, hawakuwa ni vijana wanaojulikana kuwa wako ‘Organized Crime Of Latin America’(OCLA) mwanzoni mwa timu ya Agent Kai kuingia hapa Guatemala tuliona walitumwa kuwafuatilia Investigator Miller na mwenzake Special Agent Silla mpaka waliwastukia na kujikuta wanatekwa na kina Silla na kisha kuokolewa na Kamanda Muniain kwa simu aliyopigiwa kuulizwa ukweli juu yao wanaume hawa wawili mmoja akiitwa Austin Manuel Contreras na mwenzake ni Jairo David Jimenez.

Ilifika alfajiri hakuna aliyelala walikuwa wakipanga mipango mbalimbali huku Kamanda Muniain akifanya mawasiliano kadhaa wa kadha na mheshimiwa Rais wakielekezana mengi hasa maamuzi ya Rais ambayo alimwambia ndugu yake Muniain ameyachukua kuwa kutakapokuchwa tu anahitaji kuonana na wakuu wake wote wa vyombo vya ulinzi na usalama katika nchi yake bila kusita Muniain aliomba mheshimiwa Rais ahaklikishe kabla ya kuwaita watu hao awakamate mheshimiwa waziri wa usalama pamoja na mkurugenzi wa ‘Guatemala Intelligence And Security’ ambao kwa asilimia mia ndiyo wanaongoza kuitumia ‘GIS’ kulinda maslahi yao ya biashara haramu na washirika wao kwa ujumla kwakuwa ilikuwa usiku mheshimiwa Rais aliomba Muniain avumilie kukuche hili yeye atizame nani anaweza ifanya kazi kwa uaminifu maana kila aliyekuwa anamtizama alihisi anaweza kuwa ni timu Ceni na vibaraka wake.

Saa kumi na mbili ndipo watu wa kazi za kazi walikubaliana wapumzike kidogo na daktari walimuomba apumzike papo hapo kwao kila mmoja akaenda kulala anapostahili kulala ikiwemo wote waliongezeka leo katika nyumba hii ambao ni Nesi Avon, Austin na Jairo.

Alitega simu yake  ‘alarm’ itakapofika saa nne kamili asubuhi iweze kumstua na kweli usingizi mzito uliokuwa umemchota na kumfana kuota njozi kadhaa za nyumbani kwake huko Washington DC na hata kwao kwa kuzaliwa huko Tanzania, hatimaye alistuliwa kwenye ndoto hizo kwa ‘alarm’.

Haraka aliamka na kwenda bafuni kuswaki na kutoa haja zinazotakiwa kutolewa asubuhi binadamu anapoamka kisha ya hapo mwili wake ulikuwa unahitaji kufanya mazoezi ya viungo na hata kunyanyua vitu vizito, alipofungua mlango tu akakutana na Special Agent Silla akiwa anasogea mlangoni mwake.

   “Vipi Silla?” Akamuuliza.

   “Saa mbili niliamshwa na Kamanda Muniain akanipa taarifa haraka sana anaitwa ikulu kuna taarifa muhimu huko akataka nimpeleke kwa usalama zaidi nikampeleka kwa gari letu tulilopewa na katibu nilimfikisha nikaambiwa nimsubiri nje na walinzi wa pale hivyo nami nikamuomba nije niwape taarifa kwa mdomo kuwa nimemuacha huko ikulu hapa ndiyo naingia sasa hivi kutoka huko”

   “Hakuna taarifa zake zozote tena?”

   “Bado hajanipigia simu”

   “Vipi mlimuangalia Norman? Kabla hamjaondoka”

   “Hapana sijui yeye Muniain.. Lakini daktari alilala naye kwenye chumba cha matibabu”

   “Twende tukamuone kwanza.. Mwili unaniuma natakiwa nifanye na mazoezi kidogo kisha niongee na familia yangu” Aliongea Agent Kai kisha wakaongozana kwenda chumba ambacho Norman alikitenga kwa ajili ya matibabu kukiwa na vifaa vyote muhimu vya huduma za kitabibu zinazoweza fanyika sehemu kama hii ukiacha hospitali zinakofanyika mambo makubwa zaidi.

Waligonga hodi wakaitikiwa na mtu aliyeonekana naye alikuwa bado anauchapa usingizi wakaingia na kumkuta dokta ndiyo anaamka wao ndiyo wamemstua kwa walivyomgongea.

   “Pole sana dokta.. Za asubuhi?” Akatoa pole na kuuliza hali S.S Silla.

   “Nzuri! Habari zenu wote kwa ujumla? Mnisamehe nimelala muda mbaya kama nyiye lakini mimi sikuwa  na kazi nzito kama nyiye hivyo sikustahili kulala sana” Dokta mwanamume wa makamo akawajibu watu waliosimama mlangoni wakitabasamu kwa anavyoonyesha uoga kwao ambao haukustahili lakini dokta huyu uwa ni muoga awaonapo watu walio na historia ya kuua watu wengine na kina Agent Kai alikuwa akijua ndiyo kazi yao watu hawa na hata alichosikia kwenye vyombo vya habari wakati yuko njiani idadi ya maiti zilizokutwa huko ‘Las Anonas’ zilimfanya kuwaogopa watu wote walio hapa ila uaminifu wake kwa mtu anayemuheshimu sana Kamanda Muniain ilimfanya aendelee kuwepo hapa.

   “Usijali dokta.. Vipi mgonjwa wetu?” Akaongea na kuuliza Agent Kai akiwa kashamsoma dokta kile anachowaza mpaka akawa anahisi dokta huyu asije kuwa amefanya jambo linalohusu usaliti fulani, wakaangaliana na Silla macho yao yakaongea jambo bila dokta kuelewa.

   “Ndiyo nataka nimuangalie ila naamini si leo ambapo ataweza kurejewa na fahamu nafikiri kesho ndipo tutaweza kumuona angalau anafumbua macho kwa uzoefu wangu” Dokta akajibu.

   “Sawa! Vipi wewe leo upo hapa au utatoka kurejea kwako?” Akajibu na kuhoji Agent Kai.

   “Nitatoka mkuu… Familia nayo inahitaji kuniona ila nitarudi jioni kumkagua”

   “Kwanini unaonyesha kama una jambo lisilo la kawaida?” Akauliza ‘TSC’ tena akiwa anamkazia macho dokta.

   “Hapana sina jambo lolote lisilo la kawaida naomba msinielewe vibaya… Kiukweli kuna habari nilisoma kwenye mitandao yetu ya kijamii na blogs mbalimbali za hapa GTL zilinifanya kuogopa sana juu ya mauaji hivyo mzee wangu Muniain alivyoniita tena hapa kuja kwa ajili ya kijana wake Norman nilikuwa na hofu sana, mimi naogopa sana wanajeshi wanaopigana vita au hata wengine wanaofanana nao ni hivyo tu mkuu” Akajitetea dokta akifunguka ukweli wake kwa majasusi hawa ikiwa ni uoga wa dhahiri ulimuumbua katika macho ya watu hawa wa kazi za kazi.

   “Sawa.. Utatoka tu na ukiwa unarudi utawasiliana kwanza na Kamanda Muniain kwa simu yake mnayowasiliana, tunaomba tafadhali jitahidi kutuzoea na kutulinda pia hasa hii maskani yetu dokta wetu, mimi pia nakuahidi kukupatia zawadi Norman akiamka tu kama shukrani yangu kwako” Akaongea Agent Kai huku akimtizama Special Agent Silla anavyoiangalia simu yake inayoita.

   “Kamanda Muniain anapiga..” Akaongea Silla akimtizama ‘TSC’ kisha akaipokea huku wanatoka kwenye chumba cha matibabu.

   “Kamanda!” Akaongea ilipokaa sikioni akiikamata kwa kiganja chake.

   “Kikao ndiyo kimeisha sasa hivi.. .. Mheshimiwa Ceni ametorokea kusikojulikana tena ametoroka na mkurugenzi wa taasisi kuu ya usalama wa taifa, nimewapa orodha ya makamishina wa polisi walio kwenye mtandao wake nao wakamatwe kabla hawajatorokea huko alipokimbilia bwana wao”

   “Duh…. Tumepoteza nafasi yetu ya kumpata yeye na mshirika wake Alexis naye tulimkosa”

   “TSC’ ameshaamka?”

   “Ndiyo! Niko naye anasikiliza tunavyoongea”

   “Mpe simu niongee naye”

   “Sawa!”

Mwisho wa sehemu ya themanini na moja (81)

Mambo yanazidi kuwa mambo, Feca anawapokea watu wake wa karibu waliokuwa wametokea kwenye matibabu huko Canada na inampa faraja ingawa kiukweli moyo wake ulikuwa ukihisi wasiwasi juu ya taarifa anazopokea toka nchini Guatemala nchi ambayo kwa asilimia sabini ndipo aliposimamisha msingi wa biashara zake kwakuwa na mahala ambapo hifadhi ya idadi kubwa ya mizigo yake iko huko na hata kiwanda kidogo cha siri cha kusaga mimea ya madawa ya kulevya kuwa unga wa kulevya kipo huko katika kambi ya siri iliyopo milima ya Tajumulco, katika wageni aliowapokea hawakuwa hawa viongozi waandamizi anaowaamini tu bali walikuwepo na watu waliokuwa wanaiona Guatemala sasa kwao si salama tena baada ya kuvujishiwa taarifa kuwa Rais wa nchi ana maamuzi ameyafikia juu ya wao kuwekwa chini ya ulinzi.

Agent Kai na timu yake mipango yao na wao iko moto huku wakiangalia afya ya mwenzao Norman kuona inakaaje wanaamua kuongeza nguvu kutoka kwa waliokuwa mamesenja wa siri wa Kamanda Muniain lakini kulipokucha Kamanda Muniain anaitwa ikulu ambako anatuma taarifa juu a kutoroka kwa mheshimiwa waziri wa usalama Ceni pamoja na baadhi ya watu wengine muhimu.

Nini kitafuata baada ya taarifa hizi za kutoroka kwa mheshimiwa Ceni?





   “Sawa! Vipi wewe leo upo hapa au utatoka kurejea kwako?” Akajibu na kuhoji Agent Kai.

   “Nitatoka mkuu… Familia nayo inahitaji kuniona ila nitarudi jioni kumkagua”

   “Kwanini unaonyesha kama una jambo lisilo la kawaida?” Akauliza ‘TSC’ tena akiwa anamkazia macho dokta.

   “Hapana sina jambo lolote lisilo la kawaida naomba msinielewe vibaya… Kiukweli kuna habari nilisoma kwenye mitandao yetu ya kijamii na blogs mbalimbali za hapa GTL zilinifanya kuogopa sana juu ya mauaji hivyo mzee wangu Muniain alivyoniita tena hapa kuja kwa ajili ya kijana wake Norman nilikuwa na hofu sana, mimi naogopa sana wanajeshi wanaopigana vita au hata wengine wanaofanana nao ni hivyo tu mkuu” Akajitetea dokta akifunguka ukweli wake kwa majasusi hawa ikiwa ni uoga wa dhahiri ulimuumbua katika macho ya watu hawa wa kazi za kazi.

   “Sawa.. Utatoka tu na ukiwa unarudi utawasiliana kwanza na Kamanda Muniain kwa simu yake mnayowasiliana, tunaomba tafadhali jitahidi kutuzoea na kutulinda pia hasa hii maskani yetu dokta wetu, mimi pia nakuahidi kukupatia zawadi Norman akiamka tu kama shukrani yangu kwako” Akaongea Agent Kai huku akimtizama Special Agent Silla anavyoiangalia simu yake inayoita.

   “Kamanda Muniain anapiga..” Akaongea Silla akimtizama ‘TSC’ kisha akaipokea huku wanatoka kwenye chumba cha matibabu.

   “Kamanda!” Akaongea ilipokaa sikioni akiikamata kwa kiganja chake.

   “Kikao ndiyo kimeisha sasa hivi.. .. Mheshimiwa Ceni ametorokea kusikojulikana tena ametoroka na mkurugenzi wa taasisi kuu ya usalama wa taifa, nimewapa orodha ya makamishina wa polisi walio kwenye mtandao wake nao wakamatwe kabla hawajatorokea huko alipokimbilia bwana wao”

   “Duh…. Tumepoteza nafasi yetu ya kumpata yeye na mshirika wake Alexis naye tulimkosa”

   “TSC’ ameshaamka?”

   “Ndiyo! Niko naye anasikiliza tunavyoongea”

   “Mpe simu niongee naye”

   “Sawa!”

ENDELEA NA DODO ASALI..!

PANDE MBILI ZA SHILINGI III

CHIMALTENANGO, GUATEMALA CITY-GUATEMALA

Simu ikatoka kiganjani mwa Silla kumpatia Agent Kai naye haraka akaipokea.

   “Naam Kamanda mzee wangu” Akaongea ‘TSC’.

   “Kama ulivyosikia kijana wangu.. Hali imekuwa hivi, nchi imekuwa na full msako kila mahala ambapo kunahisiwa kuna maslahi ya mheshimiwa Ceni kunavamiwa kupekuliwa ingawa taarifa ya walinzi wa familia yake nay eye aliopewa na serikali inasema aliondoka kwa helkopta iliyofika saa nane ya usiku kwake akaondoka na mkewe pamoja na watoto wake wote kuelekea huko alikoelekea”

   “Hisia zinaniambia kakimbilia kwa bwana wao kiongozi wa genge la TRJ huko Mexico”

   “Nafikiri… Vipi mmemfanyia mahojiano mwanamke aliyegoma kuongea chochote usiku?”

   “Nataka nifanye mazoezi kidogo kisha tuingie kumuhoji atasema yote tu hana ujanja tutajua kila kitu kwake mwenyewe au hata simu yake itatupa majibu ilimradi tushaanza siku mpya na uchovu wa jana umeondoka”

   “Unahisi yeye ndiye mwanamke mliyesema mnamtafuta kuwa ndiyo kiunganishi wa mtiririko wote?”

   “Sauti yake kwenye simu na hii niliyoisikia jana naunganisha napata jibu ni yeye… Jibu litapatikana tu”

   “Sawa! Mimi nimeongezewa ulinzi na mheshimiwa Rais hivyo msiwe na wasiwasi juu yangu… Muda huu tupo kwenye ukumbi mikutano tunamsubiri afike kuhutubia taifa kupitia waandishi wa habari ajenda kuu juu ya kuzivunja teuzi zake kadhaa za katika ulinzi na usalama”

   “Kazi njema… Maelekezo mengine ni kwamba muelekeze mashirika yote ya ujasusi yamulikwe kwa kiasi kikubwa na kwakuwa sisi huku tunaye mmoja uliyesema ni mmoja wa watu wa juu wa GIS nafikiri tutamkwabua vizuri atabwabwaja listi lote kisha tutawapa serikali waendelee naye, nikutakie muda mwema mzee wangu acha tuendelee na ratiba inavyotaka”

   “Vizuri mkabane aelekeze kila kitu kwa ufasaha kisha mtanitumia listi alilosema muwashirikishe Austin na mwenzake katika kazi ya kuwabana watu hao pia nimeagiza vijana waje wamchukue Kamishina Canedero kwa ajili wenzake walio katika malipo ya Ceni wamemtaja katika listi anatakiwa mara moja niliwapa taarifa ninaye mimi hivyo vijana watakaokuja nimewaelekeza waje hadi ghala la ndizi la kiwanda cha Greenhouse’s hapo watakutana na mtu atawakabidhi Canedero bila kuulizana mambo yoyote nao wataondoka naye”

   “Sawa! Kazi ataifanya mmoja wa vijana wako au unaonaje?”

   “Vizuri angeifanya Special Agent Silla sababu ya umakini na kuepusha kujuana baina ya kina Austin na hao vijana maana watu wa hapa wengi wanajuana juana kutokana na kozi mbalimbali ambazo uwa zinaingiliana baina yao”

   “Okay! Nimekuelewa mzee… Atafanya Silla au hata Miller maana naye nafikiri asubuhi hii atakuwa yuko sawa ingawa sijaonana naye bado”

   “Utakavyoona.. Baadaye kijana wangu! Mheshimiwa anaingia..!”

   “Okay!”

Simu ikakatwa papo hapo Agent Kai akampatia simu yake Special Agent Silla ambaye muda wote alikuwa pembeni yake akimsikiliza kwa umakini ndugu yake.

   “Mtizame Miller chumbani kwake kisha fanya hivyo pia kwa kina Rebecca mi najinosha kidogo gym nitoe jasho kuondoa baridi… Nikimaliza ni mahojiano na wateja wetu, mahojiano yasiyo na huruma wala cheko” Agent Kai akatoa maelekezo yake kwa Silla kisha wakaachana hapo kila mmoja akielekea kutekeleza kilichoelelezewa hapa kwa vitendo.

Ilipita saa nzima na dakika zake kadhaa ndipo Agent Ka alimaliza kila ambacho kilichokuwa katika ratiba yake kuanzia mazoezi hadi simu za kuongea na wapendwa wake kuanzia mama yake hadi mkewe na watoto wake kwakuwa ilikuwa jumapili alipata wasaa wa kuzungumza na watoto wake wote kupitia simu ya mama yao mpendwa kuanzia mtoto wa kwanza binti wa Kai hadi mtoto wa mwisho ukiacha anayesubiriwa kuzaliwa kutoka kwenye ndoa yake mpya na binti wa kiarabu Shufania, kisha simu yake iliendelea kwa kumalizia kuongea na Elizabeth Robert ‘Liz Rob’ ambako kulikuwa na maelekezo ya kazi kwa kila mmoja kutaka alichotaka kwa mwenzie hii ikawa simu ya mwisho kwenda nje ya Guatemala kwa muda huu wa asubuhi.

   “Nishamkabidhi Kamishina Canedero kwa watu waliotumwa na Kamanda Muniain.. Walikuja wanajeshi wa jeshi la wananchi ilinishangaza pia imenifurahisha” Akatoa maelezo Special Agent Silla akiwa amekaa kwenye sofa akiwa na glasi iliyojaa juisi akifyonza kwa mrija taratibu, macho yake yakimuangalia Agent Kai aliyeingia sebuleni kutokea chumbani kwake alipokuwa akitinga mavazi aliyoona yanastahili kuvaliwa siku hii ya jumapili, mavazi yake mara nyingi anapokuwa maeneo ambayo yanamuhitaji yeye kufanya kazi anazoziita kazi za kazi, mavazi ya suruali za timberland zenye mifuko mbalimbali na hata mashati yake uwa kama yale yanayotumiwa na chama fulani cha siasa huko nchini Tanzania na kwakuwa kuna baridi aliongeza koti zito ambalo nalo lilikuwa na mifuko kadhaa ya kuonekana na ya siri.

  “Safi.. Miller vipi hali yako?” Akaitikia maelezo ya Silla kisha akamuuliza Miller ambaye naye alikuwa miongoni ya watu waliopo hapa sebuleni muda huu.

   “Kichwa kinaniuma kwa mbali… Ila si cha kunifanya nishindwe kufanya kazi yoyote ile.. Vipi na wewe?” Akajibu na kuuliza Investigator Miller kisha akajimiminia kahawa kwenye kikombe cha udongo.

   “Na mimi niliamka kichwa kikiwa kinauma kidogo ila mimi ni kwa sababu niliamka nikiwa bado na usingizi.. Sote tutakaa sawa usiku wa leo utakuwa usiku murua sana katika zile usiku zinazopendwa sana na watu wa kazi za kazi kama sisi  hivyo ni muhimu kupumzika mchana wa leo ifikapo usiku tufanye kazi muhimu kwa ukanda wetu wa mabara yetu.. Wageni wetu na nyie vipi hali zenu?!” Akaongea Kai akimalizia na swali kwa wageni walioongezwa usiku uliopita na Kamanda Muniain mamesenja wake hawa, kisha akajimiminia kahawa kwenye kikombe akanyanyua na vipande kadhaa vya mikate akaanza kula.

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog