Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

SHE IS MY WIFE - 5

   

Simulizi : She Is My Wife

Sehemu Ya : Tano (5)


“Ndio muheshimiwa”

“Nchi gani?”

“Mmmm kusema kweli ni historia ndefu sana, kwa maana Eddy nilipotezana naye kwa kipindi kirefu sana. Na hadi ninavyo zungumza kwa sasa sijui yupo nchi gani”

“Ila wewe kama mama unatakiwa kutambua kwamba mwanao yupo wapi, isitoshe una mamlaka makubwa sana kwenye hii nchi”

“Kweli ila hata mimi ninatamani sana kuweza kuwa na mwanagu kwa wakati huu ila ndio hivyo sijapata nafasi hiyo”

Rahab akayafumba macho yake kwa muda huku akilini mwake akiivuta taswira ya picha ya Eddy alipo. Virusi vilivyo ingia mwilini mwa Rahab, vimemfanya kuwa ni binadamu wa tofauti na mwenye uwezo mkubwa sana wa kuweza kujua ni wapi mtu alipo.



Kitu kilicho weza kutokea baada ya Rahab kunywa sumu na kuwahishwa hospitalini. Uhai wake uliweza kupotea, na uhai unao ongwazwa na virusi hivyo ambavyo hadi sasa hivi havijajulikana jina lake, ukachukua nafasi katika mwili wa Rahab, ambaye Rahab halisi tayari roho yake imesha rudi kwa muumba wa mbigu na ardhi, na aliyepo sasa ni Rahab anaye ongozwa na virusi japo mwili, kumbukumbu na akili yake ni ile ile.


“Waoooo mwano ni mzuri sana”

Rahab alizungumza huku akiwa ameyafumba macho yake.

“Anauwezo mkubwa wa kupambana, naona sasa hivi anapambana na magaidi anamuokoa waziri wa marekani na familia yake”

Bi Magret akabaki akiwa ameduwaa akimtazama Rahab machoni asipate kumuelewa ni nini anacho kizungumza kwa wakati huo.

“Mwanao yupo Mexco na kwasasa yupo mikononi mwa wanajeshi wa Marekani fanya uwasiliane na ubalozi wa Marekani hapa Tanzania waweze kumfwatili mwanao. Huo ndio msaada wangu kwako”

Rahab akayafumbua macho yake na kutabasamu kisha akaondoka na kumuacha Bi Magret akimshangaa.

***

Raisi Praygod na Thomas wakafika kwenye eneo ambalo, yupo muongoza shuhuli(MC), aliye pewa jukumu la kuongoza ratiba nzima inayo endelea.

“Samahani MC unaitwa pale”

Thomas alimnon’oneza MC huyo ajulikanaye kwa jina la Maulid, mtangazaji wa kituo cha televishion ya Taifa.


“Na nani?”

Alizungumza huku maiki yake akiwa ameiweka pembeni, ili sauti isisikike kwa watu walio jumuika katika uwanja huu.

“Wewe nenda tu utamuona”

“Basi ngoja mara moja”

Maulidi alizungumza huku akiitazama karatasi aliyo ishika mkononi mwake, akamtazama mchungaji aliye maliza kufanya sala kisha akaisogeza maiki yake karibu na mdomo wake na kuzungumza.

“Anaye fwata sasa ni shehe mku bwana Seif Suleiman”

Baada ya kumkaribisha kiongozi huyo bwana Maulid akapiga hatua hadi alipo simama Thomas pamoja na mtu ambaye hakuweza kumfahamu mara moja kwamba ni nani.


“Kijana habari yako”

Raisi Praygod alizungumza huku akiivua kofia yake na kumfanya bwana Maulid kustuka kidogo, huku macho yake akiwa amemtumbulia Raisi Praygod Makuya.

“Usiogope kijana, ni mimi”

“Mumuuu….hee heeshim…iwa shikamoo”

Bwana Maulid alibabaika huku akiendelea kutetemeka. Raisi Praygod akaivaa kofia yake na kutazama pende zote za uwanja wa taifa, akawaona jinsi wananchui walivyo furika na sura zao zikiwa zimejawa na huzuni huku wengine wakiwa wanamwagikwa na machozi. Akameza fumba la mate kisha akamtazama bwana Maulid.


“Nahitaji maiki yako”

Bwana Maulid akaitoa maiki aliyo ishika pasipo kujishauri mara mbili, akamkabidhi Raisi Praygod Makuya, kisha akasimama pembeni akisubiria kuona ni kitu gani ambacho raisi atakizungumza. Raisi Prargod akanyamaza kimya huku akisikiliza sala anayo ifanya shehe Seif Suleima. Baada ya dakika kumi na tano shehe huyo akamaliza kusali na kutoa risala fupi aliyo iandaa, ambayo iliwahusia watanzania kwa ujumla kuweza kuendelea kufanya ibada kwa bidii kwani kifo kipo kwa kila mmoja na haijalishi uwe kiongozi, tajiri au fukara.



Uwanja mzima ukakaa kimya huku vilio vya chini chini vikiendelea kwa wamama baadhi walio kusanyika katika uwanja. Kila mmoja akawa anamsubiria MC kuweza kusoma ni nani anaye fwata kutua maneno yamwisho kwa majeneza karibi kumi na sita yaliyo wekwa sehemu maalumu kwa ajili ya kuagwa.



Baadhi ya waandishi wa habari wa televishion, ikawalazimu kuzielekezea camera zao sehemu alipo simama bwana Maulid, kwani wengi wao walihisi ukimya wake unaweza kutokana na mawaidha aliyo yatoa shehe mkuu. Kila mchukua video akabaki akiwa na kigugumizi, kwani walihisi kama walicho kichukua katika sehemu alipo simama bwana Maulid ni miujiza ambayo hakua aliye ifikiria.


Si waachukua kamera tu walio weza kushangaa, bali hata wananchi wanao fwatilia tukio zima kupitia luninga zao za majumbani walibaki wakiwa na mshangaa. Tv kubwa lililopo uwanjani likaionyesha sura ya Raisi Praygod akiwa anamwagikwa na machozi, ya huzuni. Viongozi walio kuwa wamekaa katika sehemu maalumu wakasimama kwa mashangao huku kila mmoja akiwa haamini kitu alicho kiona. Raisi Praygod akajifuta machozi kisha akakohoa kidogo na kuzungumza.


“Ndugu wananchi”

Sauti ya Raisi Praygod Makuya ikawafanya watu wote kuamini kwamba wanacho kiono ni kweli, walio na udhaifu wa miili yao, nguvu ziliwaishia na kuanguka chini na kupoteza fahamu. Wengine wakachia matabasamu pana kwenye mioyo yao, wakifurahi uwepo wa kiongozi wao waliye mpenda yu ngali hai. Hali ikawa toauti kwa makamu wa raisi, hasira kali ikamkamata na kumnong’oneza mlinzi wake atoe amri kwa askari raisi Praygod Makuya akamate mara moja.


SHE IS MY WIFE(42)


“Ni huzuni kubwa kwa kila mmoja aliye weza kukusanyika katika uwanja huu kuweza kuiaga miili ya wapendwa wetu”

Raisi Praygod Makuya alizungumza huku akipiga hatua kwenda katika jukwaa lililopo katikati ya uwanja. Askari walio tumwa na makamu wa raisi wakafika hadi sehemu alipo Raisi Praygod Makuya. Badala ya kufanya walicho agizwa na makamu huyo, waliamua kumzingira Raisi Praygod Makuya na kuimarisha ulinzi wake, ili bada lisiweze kutokea. Raisi Praygod akapanda kwenye jukwaa hilo, akatazama kila kila upande wa uwanja na kuona jinsi wananchi walivyo katika hali ya mshangao mkubwa.

“Ndugu wananchi, ni stori ndefu iliyo weza kunikuta mimi kama kiongozi wenu, na nitumie fursa hii kuweza kuwasimulia kabla sijaendelea na mambo mengine”


***

Agnes kila alipo mtazama mtoto mzuri wa bwana Paul Henry Jr, roho ya huruma ikamtawala, akaona hakuna haja ya yeye kuweza kufanya mauaji kwa kiongozi huyo ambaye bado upendo wake unahitajika kwa mtoto wake huyo. Agnes akaiweka bunduki yake chini, akamtazama bwana Paul Henry Jr, jinsi anavyo malizia kuagana na wananchi kisha akaingia ndani ya hotel hiyo huku walinzi wake wakiendelea kuimarisha ulinzi.

“Agnes ni nini umefanya?”

Bwana Rusev alizungumza kwa sauti ya upole, iliyo jaa msisitizo mkubwa.

“Target ilikaa vibaya muheshimiwa, ila nipe dakika kadhaa nitafanya”


“Una dakika kumi kuweza kulitekeleza hilo”

“Sawa muheshimiwa”

Agnes akavua kifaa cha mawasiliano alicho kichomeka kwenye sikio lake, kisha akaingia chooni na kumkuta dada mfanya usafi akiwa bado hajielewi. Akaanza kumvua nguo zake zote kisha naye akavua za kwake na kuzivaa nguo za dada huyo.


Akajitazama vizuri kwenye kioo na kuona anafananiana na wafanya usafi katika ofisi hizo. Akaziweka nywele zake ndefu mgongoni, kisha akatoka na kusimama kwenye dirisha akatizama nje kwenye gorofa la Hotel alipo fikizia kiongozi huyo. Hakuona kitu chochote kinacho endelea zaidi ya wananchi wali kusanyika wakianza kutoka mmoja baada ya mwengine. Akaichukua bunduki yake na kuishika vizuri, akayatazama magari magari baadhi yaliyo simama nje ya hotel hiyo.


Akafyatua risasi moja kwenye tank la moja ya gari na kulifanya lilipuke. Wananchi wakanza kutawanyika kuyaokoa maisha yao, magari yaliyo pembeni nayo yakaanza kulipuka baada ya kukutwa na moto wa gari hilo lakwanza. Agnes akaichangua bunduki yake kisha akairudisha kwenye kibegi chake, akakibeba mdongoni na kutoka kwenye ofisi hiyo.


Askari wakuimarisha ulinzi wakanza kuchanganyikiwa kwani hawakujua mlipuko huo umesabishwa na nini. Agnes akaingia kwenye lifti na kushika hadi chini. Akataka kwenye goroafa hilo, akakutana na wananchi wengie wakijaribu kuyaokoa maisha yao. Akaanza kukimbia kuelekea kwenye hoteli hiyo, huku akiwa makini akitazama kila kona walipo askari.


Mlipuko wamagari, ukawafanya askari wote wanao mlinda bwana Paul Henry Jr pamoja na raisi wan chi hiyo wawazunguke viongozi wao na kuwawekea ulinzi ulio imara ziaid huku kila mmoja bunduki yake ikiwa mkononi, kwani hali ya hatari tayari ilisha jitokeza nje ya Hotel. Moja kwa moja wakawaingiza kwenye moja ya chumba ambacho kimetengenezwa maalumu kwa ajili dharura, kama hizo. Chumba hicho kuta zake, milango na madirisha hayaingizi risasi ya aina yoyote.


“Waheshimiwa mupo salama humu ndani”

Mkuu wa ulinzi aliwaambia viongozi hao, walio tawaliwa na wasiwasi mkubwa. Agnes akafanikiwa kufika kwenye mlango wakuingia kwenye hotel hiyo, ambapo askari wakawaida walisimama mlangoni wakizuia wananchi wasiweze kuingia ndani ya mlango huo, kwani hawakujua ni nani mbaya aliye sababisha tukio hilo.



Agnes akatazama gari zipatazao nne za zima moto zikiwa zimesimama kwenye eneo hilo wakijitahidi kuzima moto wa magari hayo. Akakimbia hadi sehemu yalipo, akazunguka nyuma ya moja ya gari na kumkuta kijana mmoja, zima moto akiwa amechuchumaa akiunganisha moja ya bomba lililo lete itilafu


“Miss……”

Kijana huyo hakumalizia sentesi yake, tayari teke zito lilitua kwenye shingo yake na kumlaza kwenye barabara. Agnes akatazama kila kona, hakuona mtu aliye weza kumfwatilia. Kwa haraka akamvua kijana huyo mavazi yake kisha akavaa juu ya nguo alizo zivaa.



Akavaa likofia la kijana huyo, ambalo lina kioo mbele. Alipo jihakikisha anafanania na zima moto wengine, akasukumia kijana huyo aliye muacha na boxer chini ya gari hilo. Alicho kifanya ni kuchukua kisu kidogo kwenye kabegi kake kisha akakaingiza kwenye mfuko wa jinguo hilo alilo livaa.



Akawaona baadhi ya zima moto wakiingia kwenye mlango wa Hoteli hiyo, kibegi kake akakirusha juu ya gari hilo, kisha akachukua kiboksi kidogo cha chuma, ndani chenye vifaa maalumu kwa kazi hiyo ya zima moto. Akakimbilia hadi kwenye mlango wa kuingilia kwenye hotel, pasipo kustukiwa akaingia ndani ya Hotel hiyo. Kutokana maelekezo yote alisha yapata kwa mkuu wake bwana Rusev aliweza kulijua eneo zima la Hotel hiyo, kazi aliyo anza kuifanya ni kumtafuta ni wapi alipo Bwana Paul Henry Jr.

***

Rahab akamchukua mbwa wake, na kuomba chumba ambacho anahitaji kupumzika, akapelekwa kwenye chumba chawageni. Akakichunguza chumba kizima, alipo hakikisha kipo salama akajitupa kitandani huku akiwa amembema mbwa wake.


“Heii mamy nataka kupumzika, lala eheee”

Rahab aliuzungumza huku akiwa amembeba mbwa wake na kumlaza kifuani mwake. Akakabembeleza kambwa kake hadi kalala. Alipo hakikisha kamelala, akajaribu kuyafumba macho yake, ila sura ya Eddy ikamjia machoni mwake. Moyo wake ukajikuta ukiwa katika shinikozo kubwa la kuhitaji kukutana na Eddy, ila kwawakati alio kuwa nao ni ngumu sana, kwani tayari amesha kuwa mke wa mtu anaye heshimiwa kupita watu wote nchini Tanzania

“Nitahakikisha unakuwa wangu, maisha yangu yote”

Rahab alizungumza kuku akiachia tabasamu pana usoni mwake, na akilini mwake mume wake alianza kupotea taratibu taratibu.

***

Makamu wa raisi akawatumbulia macho askari alio waagiza kufanya kazi ya kumkamata Raisi Praygod, mapigo ya moyo yakamuenda mbio baada ya kuwaona askari hao wakiimarisha ulinzi wa Raisi Praygod Makuya, na wasifanya kile alicho waagiza.


“Pumbavu……”

Alitoa maneno hayo huku akikaa kwenye kiti chake na macho yake akimtazama raisi Praygod Makuya jinsi anavyo waadisia wananchi mambo yote yaliyo toke kwenye ndege hadi alipo pata msaada wa mke wake wa sasa ambaye ni Rahab. Wananchi walio adisiwa stori hiyo ya kusisimua, machozi yafuraha yaliwamwagika kila mmoja akajawa na furaha ya kiongozi wao huyo waliye mpenda na kumuona kwamba yupo hai na katika hali ya furaha.


“Leo nimezidi kuamini kwamba munanipenda sana, na kuuthamini mchango wangu kwenye maisha yetu yakila siku”

Raisi Praygod Makuya alizungumza huku akiunyanyua mkono wake wakulia kuwasalimia wananchi wote jambo lililo nyanyua shangwe na nderemo kwenye uwanja mzima wa taifa. Shangwe na nderemo zilivyo zidi kuendelea, mtu mmoja aliye valia kofia na nguo nyeusi kama waaombolezaji wengine, alifanikiwa kuruka fensi za kuingilia uwanjani na kuanza kukimbia kuelekea alipo Raisi Praygod Makuya huku akimtaja jina lake.

“Muheshimiwa Praygod Makuya, Muheshimiwa Praygod Makuya”

Askari walio na bunduki wakamuwahi kumdaka kijana huyo na kumuangusha chini. Wakampiga pingu za mikononi.


“Muacheni tafadhali”

Raisi Praygod Makuya alizungumza na kuwafanya askari hao kumuachia na kuifungua pingo ya mikono mwake, kijana huyo akakimbilia hadi kwenye jukwaa kisha akaivua kofia yake, ndevu nyingi zilizo tanda kwenye sura yake, zilimfanya kuonekana kama mzee wamiaka stini na kitu, kumbe nikijana mdogo mwenye miaka ishirini na saba.


Kwanza kijana huyo akamkumbatia raisi Praygod Makuya, nakumfanya raisi Praygod Makuya kujitahidi kuvuta kumbukumbu zake niwapi alipo muona kijana huyu anaye mwagikwa na machozi. Kumbukumbu za raisi Praygod Makuya zikagota kwenye ndege na kukumbuka kijana huyu ndio yule aliye kuwa akishirikiana na Rahab.


“We…weee si…”

Raisi Praygod alizungumza kwa kigugumizi, kwani kama kijana huyu alimkosa kwenye ndege basi leo amekuja kumuua kwenye alaiki ya watanzania.

“Samson, Samson muheshimiwa.”

Samson alizungumza huku machozi ya uchungu yakimwagika, akazidi kumkumbatia Raisi Praygod Makuya kwa nguvu zake zote.

==> ITAENDELEA




ILIPOISHIA

Kwanza kijana huyo akamkumbatia raisi Praygod Makuya, nakumfanya raisi Praygod Makuya kujitahidi kuvuta kumbukumbu zake niwapi alipo muona kijana huyu anaye mwagikwa na machozi.

Kumbukumbu za raisi Praygod Makuya zikagota kwenye ndege na kukumbuka kijana huyu ndio yule aliye kuwa akishirikiana na Rahab.

“We…weee si…”

Raisi Praygod alizungumza kwa kigugumizi, kwani kama kijana huyu alimkosa kwenye ndege basi leo amekuja kumuua kwenye alaiki ya watanzania.

“Samson, Samson muheshimiwa.”

Samson alizungumza huku machozi ya uchungu yakimwagika, akazidi kumkumbatia Raisi Praygod Makuya kwa nguvu zake zote.


ENDELEA

Raisi Praygod Makuya akajaribu kujitoa mikoni mwa Samson ila akajikuta akishindwa kwani Samson alizidi kumkumbata kwa nguvu

“Naoamba unisamehe muheshimiwaa”

Samson alizungumza huku akiendelea kumwagikwa na machozi mengi. Makamu wa rais baada ya kumuona Samson, ikanyanyuka kwenye kiti chake huku macho yakiwa yamemtoka. Woga wa siri yake kuweza kufichuliwa na mjomba wake huyo ukaanza kumtawala.


“Muheshimiwa natambua kwamba nilikukosea, ila si kosa langu mimi”

“Nilitumwa niweze kukuangamiza, na mjomba wangu ili kiti chako cha uraisi kiweze kukaliwa na mjomba wangu ambaye ni makamu wa raisi wa sasa”

Maneno ya Samson yakamfanya raisi Praygod kuweza kumtazama makumu wa raisi aliye keti kwenye jukwaa. Sura ya makamu huyo ikamuashiria raisi Praygod kwamba ina hasira dhidi yake.


“Nimekuelewa kijana, unaitwa nani?”

“Samson”

“Sawa Samson nitalifanyia kazi”

“Kabla ya hayo kuna jengine muheshimiwa nahitaji kukuambia”

Makamu wa raisi alipo zidi kumuona Samson anazungumza na Raisi Praygod, akazidi kushikwa na hasira akiamini kwamba kila kitu kimesha haribika, akaangaza macho yake huku na huku, akamuona mlinzi wake aliye simama pembeni, bastola ikiwa imechomekwa kiunoni. Kwa haraka makamu wa Raisi akaichomoa bastola hiyo bila hata yakufikiria mara mbili, akafyatua risasi ambazo kwa haraka Samson aliweza kuliona tukio hilo, alicho kifanya ni kumsukumia pembeni Raisi Praygod, na risasi hizo mbili zikaingia mwilini mwake na kumuangusha chini.


Mlio wa bastola hiyo, ukazua hali ya taharuki kwa kila aliye kuwa katika uwanja wa taifa, kila mmoja akafanya jinsi akili yake ilivyo muagiza kuweza kufanya, wapo walio weza kuchanganya miguu yao na kukimbia hovyo hovyo, wengine waliweza kupoteza fahamu, wengine waliweza kukanyagwa vibaya pale walipo zidiwa nguvu na wale walio hitaji kuokoa nafsi zao. Askari na walinzi wa viongozi waalikwa wakawa na kazi moja tu, yakuwaokoa viaongozi wao waliomo ndani ya kiwana hichi kikubwa cha mpira. Hali ikazidi kuwa mbaya kwani hapakuwa na aliye weza kuvumilia. Walinzi wengi wakamzunguka Raisi Praygod, wakamtoa uwanjani huku wakiwa wanamkimbiza, baadhi ya wanajeshi wakaweza kumtia nguvuni makamu wa raisi aliye weza kufanya tukio lakinyama.


Hali ya Samson, ikazidi kuwa mbaya huku macho yake akimtizama jinsi Raisi Praygod anavyokimbizwa na askari kuyaokoa maisha yake, Samson akaachia tabasamu pana, huku taratibu macho yake yakiingiwa na ukungu ulio pelekea kuyafumba macho yake na kutulia tuli.

***

Moja kwa moja Agnes akakimbilai kwenye chumba amacho aliamini kiongozi anaye muhitaji ni lazima atakuwa amepelekwa huko baada ya milipuko hiyo ya magari kuweza kutokea. Akafanikiwa kufika kwenye kordo yakuelekea kwenye chumba hicho kilichopo chini ya ardhi. Walinzi walio valia suti nyeusi pamoja na miwani nyeusi wapatao kumi na tano, wakawa wamesimama nje ya mlango huo huku macho yao yote wakimtupia Agnes anayekuja kwa kasi huku akiwa amejiamini sana.


Kila mmoja akabaki kuwa na alama ya kujiuliza kwani mavazi aliyo yavaa Anges ni ngumu sana kumtilia mashaka kwani akafanana sana na wahudumu wa kikosi cha kuzima moto. Muonekano wa umbo dogo dogo la Agnes, likawapa imani kwamba binti huyo anaye kuja kasi huku akiwa amenyanyau mikono yake juu, hana madhara yoyote kwao.


“Naomba muwatoe viongozi nje, jengo limeanza shika moto”

Kauli ya Agnes aliyo izungumza kwa lugha ya kirasia, ikawafanya walinzi wote kuchanganyikiwa, ikawalazimu kuwasiliana na wezao waliomo ndani ya chumba kuweza kuwatoa viongozi hao haraka iwezekanavyo. Bwana Paul Henry Jr pamoja na Raisi wa Russia wakatolewa ndani ya chumba hicho kuku wakiwa wamezungukwa na walinzi wao wapatao ishirini.


“GO GO GO….!!!”

Mlinzi mmoja alizungumza huku akionekana ndio mkuu wa kikosi hichi maalumu chakuwalinda viongozi hawa. Agnes akatazama jinsi walinzi hawa walivyo makini na kuwalinda viongozi hawa.

“Hapa hapa”

Agnes akawaacha viongozi hao kupiga hatua nyingi mbele, kisha kwa kasi akanza kukimbia na kuwafwata kwa nyuma, akamfikia mmoja aliye ishika bastola yake na kuitanguliza mbele. Kwa kasi ya ajabu Agnes akajigeuza kwenye shingo ya mlinzi huyo na kuivunja, kabla hajaanguka chini, tayari akawa ameikamata bastola ya mlinzi huyo.


Kwa mafunzo ya uharaka na umahiri wake katika kutumia silaha hizi za bunduki, Agnes, akaanza kuwaangusha chini walinzi hao, walio changanyikiwa kwani, kitendo cha mtu kujaribu kufanya shambuliza tayari umesha vamiwa na kuangushwa chini.

Agnes akafanikiwa kusimama nyuma kwa bwana Paul Henry Jr, akampiga kabali huku bastola yake akiwa ameiweka sikioni mwa kiongozi huyo. Macho yake kwa haraka aliweza kuona miili ya walinzi wapatao kumi na sita wakiwa chini wamekufa huku wanne wakiwa wamesimama huku wamenyooshea bastola zao.


Rasi wa Russia hakuweza kuamini uwezo aliokuwa nao msichana mdogo kama huyo aliye anzisha varangati la kufa mtu na kuwaweka chini watu wazima na kuwa kimya.

“Nipisheni”

Agnes alizungumza kwa kujiamini, kiasi kwamba hapakuwa na mlizi aliye weza kufanya kitu chochote. Askari na kikosi cha zima moto nje wakawa na kazi moja ya kuendelea kuwasogeza watu wasiweze kuingia ndani ya hoteli hii kwani ni hatari kwa maisha yao. Hapakuwa na askari aliye weza kujua ni kitu gani ambacho kinaendelea huko ndani.


“Binti tutakupa chochote ili mradi umeachie huyo kiongozi”

Raisi wa Russia alizungumza huku akiwa anatetemeka sana, Agnes hakuhitaji kumsikiliza hata kidogo, akampiga risasi ya mguu raisi huyo, akamfanya aanguke chini na kutoa ukelele mkali wa maumivu, walinzi wake wakiwa katika mawenge mawenge, Agnes akajaribu kufyatua risasi, akagudua risasi zilizomo ndani ya bastola yake zimekwisha. Agnes akiwa katika hali ya kuishangaa mlinzi mmoja akawa amefanikiwa kuligundua hilo.

***

Raisi Praygod akingizwa kwenye gari, akapelekwa moja kwa moja Ikulu, kwa ajili ya mapumziko huku askari wengine wakimpeleka makamu wa raisi katika kambi ya jeshi huku wakimuweka chini katika ulinzi mkali. Gari tano za jeshi zilizo jaa askari, zikajikuta zikifunga breki katika maeneo ya mwenge, baada ya kukuta foleni kubwa ya magari ya wananchi.


Wanajeshi wapatao sita wakiwa na bunduki wakashuka kwenye magari hayo na kuanza kufanya kazi ya kuwaamrisha wenye magari yao kuweza kuyasogeza pembeni, ikiwa ni amri na si ombi, kwani wanamualifu mmoja waliye hakikisha kwamba hachomoki kwenye mikono ya serikali kwani ameshababisha maafa makubwa kwa raisi pamoja na viongozi walio weza kuingia katika uwanja wa mpira wa taifa.


Gari mbili nyeusi aina ya VAN, zikasimama katikati ya sehemu ambayo magari hayo yalipaswa kuweza kupita. Wakashuka vijana watatu walio valia mavazi meusi pamoja na vinyago usoni mwao. Kila mmoja akiwa na bunduki aina ya AK47

Hapakuwa na aliye weza kuuliza, walicho kifanya ni kuanza kuwashambulia wanajeshi wote walio weza kutoka nje ya magi yao, wakihitaji kuweza kupishwa na waendelea na msafara wao. Kila raia aliyekuwa ndani ya gari liwe lake au daladala, waliweza kuchomoka kila mmoja kuyaokoa maisha yake.


Vijana hao walio valia sura za vinyago hawakuwa na woga wa ana yoyote, walizidi kusonga mbele kwenda zilipo gari za jeshi. Wanajeshi waliomo ndani ya magari, wakajirusha nje huku kila mmoja akiwa ameikamata bunduki yake sawia kuhakikiusha kwamba wanapambamba vilivyo hadi dakika ya mwisho.

Hapakuwa na alie jua kuwa wavamizi hao wanajiamini kwa kitu gani, kwani waliweza kusonga mbele pasipo kuogopa, wanajeshi walio jibanza kwenye magari yaliomo barabarani, wakajikuta wakianza kuangushwa mmoja baada ya mwingine, huku risasi zinazo zidi kuwateketeza wasitambue ni wapi zilipo tokea.


SHE IS MY WIFE(44)



Wadunguaji, walenga shabaha ya masafa ya mbali wapatasi sita wakiwa wamesimama katika magorofa kadhaa yaliyopo katika makutano ya magari ya mwenge, waliweza kufanya kazi yao sawia, kila mwanajeshi aliye weza kuonekana maisha yake yaliondolewa kwa risasi za vichwa.


“No one Clear”

“Two Clear”

“Three Clear”

“Four Clear”

“Five Clear”

“Six Clear”

Wadunguaji wote waliweza kuwasiliana kwa vifaa vyao maalumu vya kunasia sauti, huku kila mmoja akidai hakua mwanajeshi anaye onekana kwenye eneo hilo. Watau walo chini wakakimbia kwa haraka hadi sehemu zilipo gari za wanajeshi, wakafungua kari mmoja wakamkuta makamu wa raisi akiwa amefungwa pingu pamoja na kivishwa kipande cha gunia cheusi. Wakamfunua kipande hicho


“Muheshimiwa tupo hapa kwa ajili yako”

Mmoja alizungumza kwakujiamini na kumfanya makamu waraisi kuweza kutabasamu. Mlio wa helcoptar ukasikika, mmoja akatoka nje ya gari hilo. Akawasiliana na wezao waliomo ndani ya helcoptar hiyo, ambayo kwa uwezo wake mkubwa, ikaweza kushuka karibu sana na eneo ambalo gari hilo lipo. Makamu wa raisi akatoka ndani ya gari akadandia ngazi aliyo teremshiwa na kuanza kuiparamia hadi juu. Wavamizi hao watatu nao wakapanda kwenye helcoptar kwa kutumia vingazi hivyo walivyo shushiwa kisha wakaondoka zao katika eneo la tukio.


***



“Shitii”

Agnes alizungumza, akamsukumia bwana Paul Henry Jr mikononi mwa walinzi wake hao watano, wakajaribu kumdaka kiongozi wao asianguke chini, hapo ndipo ikawa nafasi kwa Agnes kuchuchumaa kwa haraka chini, kunyanyuka juu mikono yake milili iliweza kuwa na bastola alizo ziokota chini kwa walinzi walio kufa. Hakuhitaji kufanya makosa. Akawaogesha walinzi hao mvua ya risasi wakabaki viongozi wawili Bwana Paul Henry Jr pamoja na Raisi wa Russia.

Jasho likiwa linamwagika usoni Agnes akamtizama kiongozi huyo wakimarekani, alicho kifanya, akafyatua risasi tano mfufulizo zilizo tua kifuani kwa kiongozi huyo bwana Paul Henry Jr na hapo ndipo ukawa mwisho wa maisha ya kiongozi huyo.


“Mission yangu ilikuwa ni kwa huyu wewe leo umepona”

Agnes alizungumza huku akiwa amemuinamia muheshimiwa Raisi, kwa kutumia kitako cha bastola akampiga nacho cha kichwa, raisi akazimia hapo hapo.

“Mission complite”

Agnes alizungumza huku akiitazama miili ya marehemu ali wapa tiketi ya kuwahi kwenda mbinguni siku ya leo. Kwa haraka akatoka katika eneo hilo lililopo chini ya ardhi, akatoka nje ya hoteli pasipo kujulikana, akakimbia hadi kwenye gari alilo acha kibeki chake, kwa bahati nzuri akafanikiwa kuweza kukiona. Akakichukua, akayavua mavazi ya zima moto, kisha akakimbia akiungana na wananchi wengine.

***

“Madam tumeagizwa kuja kukuchukua kukupeleka ikulu”

Wanausalama wapatao wanne walisimama mbele ya Rahab, aliye toka usingizini asijue ni kitu gani kilicho weza kutokea.

“Nitaamini vipi nyingi ni watu wazuri”

Kila mmoja akatoa kitambulisho chake na kumuonyesha Rahab, vitambulisho vyao viliwaonyesha wao ni miongoni mwa walinzi wanao fanya kazi ndani ya ikulu.


“Sawa twendeni”

Rahab akaagana wa waziri mkuu aliye jawa na huzuni usoni mwake, Rahab hakuhitajii kujua ni kiupi kinacho mfanya mama huyo kuwa katika hali kama hiyo. Akaingia ndani ya gari, huku macho yake akiwa amemkazia Sheila, taratibu gari zikaanza kuondola

‘Wewe mama huyu binti atakuja kukuliza siku’

Rahab alizungumza kimoyo moyo huku akiendelea kumuangalia Sheila ambaye alisha anza kujenga moyo wa chuki dhidi ya Rahab, mara baaya ya kuhisi kwamba Rahab anaweza kumuhitaji Eddy ambaye hadi sasa hivi hajulikani ni wapi alipo. Wakafika ikulu salama salimi, Rahab akakutana na mumewe Raisi Praygod, ambaye kwa haraka alipo mtazama machoni mwake akatambua kuna kitu ambacho nikibaya kiliweza kutoka kwa mume wake.


Rahab akayafumba macho yake kwa haraka, hisia kali alizo weza kuwa nazo kwa kipindi hichi, zikaanza kumjia kichwani kwake, akayaona matukio yote yaliyojitokea masaa ya nyuma. Akazidi kuvuta hisia ambazo zikampeleka hadi kwenye tukio la kijana aliye yaokoa maisha yake.

“HAHhahahaha….”

Rahab alistuka, huku akihema hii ni baada ya ya kuweza kuona mambo yakutisha kwa ambayo kijana huyo anaweza kuyafahamu vizuri na pasipo kuweza kuyazuia mapema basi nchi inaweza kuingia katika matatizo makubwa.


“Baby vipi unatatizo?”

Raisi Praygod alimuuliza Rahab baada ya kumuona anahema sana, huku macho yake kama yakiwa na uwekundu kama mtu aliye ingiwa na moshi mwingi wakuni.

“Nipo sawa tu”

“Twende chumbani kwanza”

Raisi Praygod akamuondoa katika eneo la sebleni Rahab, akampeleka chumbani kwake ambapo kwa rahab ndio mara yake ya kwanza kuweza kuingia katika chumbacho analala muheshimiwa raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania bwana Praygod Makuya.

“Mke wangu ninavikao vya dharura sijui unaweza kunisaidia kunisubiri kwa muda kadhaa”

Raisi Praygod alizungumza mara baada ya kumpandisha Rahab kitandani ili ajipumzishe

“Au nimuite doktar aje kukutibu”

“Hamna haja nipo sawa”

“Basi mke wangu ninaomba nielekee kwenye chumba cha mkutano”


“Usiku saa hizi”

“Ndio ni dharura”

“Sawa”

Raisi Praygod akainama na kumbusu mke wake mdomoni, kisha akatoka kwenye chumba hicho kwa haraka haraka akaelekea kwenye chumba cha mkutano ambapo alihitaki kuweza kukutanza na viongozi majeshi wote ilii kuweza kuhakikisha wanaiweka nchi katika hali ya usalama.

“Kilicho tokea muheshimiwa tunaomba utumiwe radhi kwani kikosi changu ndicho kilikuwa na jukumu la kuhakikusha makamu wa raisi anafika kwenye mikono ya ulinzi”

Mkuu mmoja wa jeshi la nchi kavu aliweza kuzungumza kwa niaba ya viongozi wengine wa jeshi. Raisi Praygod hakuzungumza kitu chochote zaidi ya macho yake kuyagandisha kwenye sehemu mmoja huku akijaribu kuyakumbuka maneno ya Samson

‘Kabla ya hayo kuna jengine muheshimiwa nahitaji kukuambia’

Kumbukumbu za Raisi Praygod zikakwamia hapo, akajikuta akiyafumba macho yake kwani hiyo ni ya jambo lililo muumiza kichwa.


“Jengine, Jengine lipi…………….?”

Raisi Praygod alizungumza kwa sauti iliyo wafanya wakuu wengine wote kumtazama, wasijue ni kitu gani ambacho muheshimiwa anakizungumza.

“Kuna yule kinaja ambaye alionikoa, fanyeni mawasiliano mujue ni wapi alipo sawa”

“Sawa mkuu”

“Hakikisheni munahimarisha ulinzi kila kona ya mipaka, viwanja vya ndege bahari pamoja na pengineo kwani bila kufanya hivyo hali itakuwa ni tete”

“Sawa muheshimiwa.”

“Muheshimiwa, yule kijana yupo Muhimbili anafanyiwa matibabu”

Secretary wa raisi alimnong’oneza raisi baada ya kupewa jukumu kukufwatilia ni pasi Samson alipo pelekwa.


Rahab hakuweza kufumba jicho laka na kulala, kitu alicho weza kukiona kwenye hisia zake kikamnyima raha, akatamani akiseme kwa mume wake, ila akahofia kuweza kutiliwa mashaka kwani tayari Rahaba amesha anza kujihisi kwamba yeye si mwanadamu wa kawaida. Rahab akanyanyuka kitandani, akaitupia macho saa ya ukutani inaonyesha ni saa saba kamili usiku, akiwa kaatika kuzunguka zunguka ndani ya chumba, mlango wa ndani kwake ukafunguliwa.

AkaingiaRaisi Praygod huku akionekana kuonakana kama mtu mwenye haraka ya kuhitaji kufanya jambo fulani.

“Munataa kwenda hospitalini?”

Rahab alimuuliza mume wake jambo lililo mfanya raisi Praygod kushangaa kidogo kwani jambo alilo liuliza mke wake hakuhitaji kumuambia.


“Umejuaje?”

“Wewe niambie tu kwani na mimi nahitaji kuonana na yule kijana”

“Unamfahamu?”

“Simfahamu ila ninakuomba tu mume wangu tuweze kwenda pamoja”

Raisi Praygod akamtazama Rahab usoni kwa sekunde kadhaa, kisha akakubaliana naye kwani hapakuwa na sababu ya msingi ya yeye kumkataza mke wake kwenda huko kwani anamtambua vizuri kwamba ni mpiganaji mzuri aliye weza kuyaokoa maisha yake kwa kiwango kikubwa sana.

“Jiandae”

Raisi Praygod alizungumza huku akisimama kwenye moja ya picha yake kubwa iliyo wekwa ndani ya chumba chake, akaitoa na kuiweka chini, hapo ndipo rahaba akagundua kwenye picha hiyo kuna mlango wa chuma, huku pembeni kukiwa na batani kadhaa ikashiria mlango huo unafunguliwa kwa namba za siri ambazo anazifahamu raisi peke yake.


Raisi Praygod hakuwa na wasiwasi wowote dhidi ya mke wake, akaingiza namba za siri, baada ya hapo akaweka kiganja chake pembeni ya namba hizo, kwenye kijikioo chenye usawa na kiganja chake. Mstari mwekundu ukapita mara mbili ukitokea juu kwenda chini, ukikagua kiganja hicho, baada ya kufanya hivyo mstari wa kijani ukaweza kupita ukitokea chini kwenda juu, na hapo mlango ukafunguka.

Raisi Prayogod akaingia kwenye chuma hicho chenye taa nyeupe tupu, Rahab hakutaka kubaki nyuma naye akaingia kuangalia ni kitu gani ambacho mume wake akemkifwata humo ndani.


“Unafanyaje baby?”

“Ngoja”

Raisi Praygod akaminya batani nyekundu iliyomo katikati ya chumba hicho, hapo ndipo kuta zote za chumba hicho zikafunguka, Rahab hakuamini baada ya kukutana na silaha nyingi ambazo baadhi anazifahamu kutokana na mafunzo aliyo weza kuyapita kipindi cha nyuma akiwa na wezake ambao hadi sasa hivi hatambui ni wapi walipo.

“Waoooooo………!!!!”

Rahab alishangaa sana, akataka kugusa bunduki moja ila raisi Praygod Makuya akamzuia asiiguse

“Usiguse, vitu vyote humu ndani zina alama za vidole vyangu, na endapo ukigusa kimoja pasipo mimi kukitoa kwenye sehemu kilipo mlio wa hatari nilazima ulie ndani ya chumba hichi”

Rahab akawa amelielewa hilo, Raisi Praygod akavua nguo na kubakiwa na nguo za ndani, akachukua moja ya suta ya bandi kati ya sura nane zilizomo ndani ya chumba hicho, akaivaa, akamuomba Rahab aweze kumuweka vizuri.

“Inanibidi nifanya hivi”


“Kwa nini?”

“Nchi kwa sasa haipo kwenye usalama na kumbuka ninawindwa na yule mshenzi aliye taka madaraka kwa nguvu amesha toroshwa”

Raisi Praygod alizungumza huku akivaa jaketi la kuzuia risasi, akachukua nguo nyeusi zilizo kwenye moja ya kabati, akazivaa vizuri huku muda wote Rahab, aliendela kumsaidia mume wake pasipo kumuuliza maswali mengi.

“Kama tunakwenda basi vaa bullet proof”

“Halina haja ya mimi kulivaa”

“Kwa nini?”

“Hamna, nisadie bastola moja”

Raisi Praygod akatazama tazama kwenye bastola zake kadhaa anazo zipenda, akachomo moja yenye rangi nyeupe, akamkabidhi mke wake. Wakatoka ndani ya chumba, kila mmoja akiwa tayari kwa safari ya kuelekea kwenye hospitali ya taifa Muhimbili.


“Muheshimiwa hadi mke wako anakwenda?”

Mmoja wa walinzi wakaribu akamuuliza raisi kwa kumnong’oneza kwenye sikoo lake, hii ni baada ya Rahab kuingia kwenye gari alilo andaliwa raisi.

“Ndio”

“Ila muheshimiwa hali ya usalama bado si nzuri”

“Hakuna litakalo tokea”

Mlinzi huyo aliye pewa jukumu la kumlinda raisi hakuwa na kipingamizi cha aina yoyote kwani hiyo ni amri ya kiongozi wake. Safari ikaanza huku gari nne nyeusi, zilizo bandikwa plate number, za kawaidia zikatoka katika geti la ikulu na kuelekea hospitali ya Muhimbili.

***

“BADO YUPO HAI…………!!!”

Makamu wa raisi aliye weza kumsaliti Raisi Praygod Makuya, alishangaa baada ya kuletewa taarifa kwamba Samson, kijana wake yupo hai.

“Ohooooo sasa itakuwaje, atatoboa siri”

“Ndio hivyo muheshimiwa”

Mlinzi anaye muamini alimjibu kwa usikivu mkubwa sana. Ukimya wa gafla ukatawala ndani ya chumba hichi cha hotel, iliyopo nchini Kenye maeneo ya Malindi. Ukimya huo ukakatishwa na simu ya mlinzi huyo, kwa haraka akaipokea


“Ndio”

“Nimekuelewa”

“Asante”

Majibu ya mlinzi huyo mwenye roho ya kikatili sana, yakaustua moyo wa makamu wa raisi kwani ameamini kwamba taarifa hiyo si nzuri kwa upande wake.

“Raisi Praygod Makuya anaelekea hospitalini kuonana na Samson”

“WHAT………!!!” Makamu wa raisi alijikuta akiishiwa na nguvu, akajibwaga kwenye sofa lililopo karibu yake akibaki amemtumbulia mimacho mlinzi wake huyo.


==> ITAENDELEA



ILIPOISHIA

Majibu ya mlinzi huyo mwenye roho ya kikatili sana, yakaustua moyo wa makamu wa raisi kwani ameamini kwamba taarifa hiyo si nzuri kwa upande wake.

“Raisi Praygod Makuya anaelekea hospitalini kuonana na Samson”

“WHAT………!!!”

Makamu wa raisi alijikuta akiishiwa na nguvu, akajibwaga kwenye sofa lililopo karibu yake akibaki amemtumbulia mimacho mlinzi wake huyo.


ENDELEA

Makamu wa raisi akakaa kimya kwa muda akifikiria ni kitu gani anaweza kukifanya, gafla akasimama huku akitabasamu

“Bimgo”

Alizungumza huku akimuomba mlizi wake simu. Akaminya baadhi ya namba kisha akaiweka simu yake sikioni, baada ya dakika kadhaa ikapokelewa na sauti nzito ya kiume.

“Yaa ni mimi”


Makamu wa raisi alizungumza, na kumfanya mtu aliye ipokea simu hiyo kuweza kujua anazungumza na nani.

“Kuna mgonjwa hapo hospitalini kwako, somebody Samsoni. Ninahitajia umuondoe kwenye ramani ya dunia”

“Sawa nimekuelewa muheshimiwa, uishi daiama”

“Asante”

Makamu wa raisi akakata simu huku akiwa katika tabasamu pana. Ulinzi kwenye hii hoteli yake aliyo ijenga kwa usiri mkubwa pasipo serikali ya Tanzania kuweza kuifahamu, uliendelea kuimarika kila kona huku vijana wake wanao muunga mkono wakiwa makini sana kuhakikisha kwamba hakuna mtu anaye weza kufahamu kwamba kiongozi huyo anaye tafutwa na serikali ya Tanzania yupo kwenye hoteli hii kubwa ya kitalii.

***

Tayari mawasiliano yalisha fanywa kwenye hospitali ya Muhimbili, ili chumba alicho lazwa Samson kifanyiwe ulinzi wa hali ya juu. Askari wenye bunduki nzito walisha weka ulinzi eneo zima la hospitali wakihakikisha kwamba anapofika Raisi Praygod Makuya, kila jambo linakuwa kwenye mstari na hakuna tatizo la kijinga litakalo kwenda kujitokeza.


Hali ya Samson, kidogo inaleta matumaini kwa madaktari, hii ni baada ya kutolewa risasi mwlinini mwake, ambazo kwa bahati nzuri hazikuweza kuleta madhara makubwa sana kwenye mwili wake.

“Nahitaji kumcheki mgonjwa”

Daktari mkuu wa kitengo cha upasuaji aliwaambia askari wawili walio simamam mlangoni mwa chumba alichopo Samson. Mmoja wa askari akachukua kitambulisho kinacho ning’inia kwenye kifua cha daktari huyo na kulisoma jina lake, ili kudhibitisha kwamba kweli ni daktari wa hospitali hiyo, alipo jiridhisha akamruhusu daktari huyo kuingia ndani ya chumba hicho.


Dokta Maliki, akasimama pembeni ya kitanda alicho lalala Samson, anaye hemea kwa mashine maalumu za kupumulia.

“Nilazima umfe mwanaharamu wewe”

Dokta Maliki alizungumza huku akivaa gloves zake nyeupe kwenye viganja vyake, ili kutoweza kuacha alama za vidole pale atakapo fanya mauaji yale alio agizwa na Makamu wa raisi. Alipo hakikisha gloves zake zipo vizuri, akachomoa mashine iliyo wekwa kwenye kinywa cha Samson, akasababisha Samson kuanza kujitingisha tingisha taratibu, akijaribu kuipigania roho yake na umauti kwani hewa iliyokuwa inaingia kwenye mapafu yake imekatishwa.

***

“Endesheni haraka”

Rahab alizungumza huku akihangaika hangaika kwenye siti aliyo kalia hadi Raisi Praygod akamshangaa kwani ni kama mtu anaye hitaji kuweza kuliwahi jambo fulani.

“Kwani vipi mke wangu?”

“Kuna tatizo fanyeni haraka”

“Wapi…!!?”


“Dereva ongeza kasi tafadhali”

“Madam sote tunakwenda kwenye mwendo mmoja nikiongeza kasi mimi naweza kusababisha ajali”

Dereva anaye waendesha alizungumza kwa ukanini wa hali ya juu kwani ndivyo sheria ya kazi yake inavyo zingatia, kwenye msafara kama huo wote huwa wanaendesha katika mwendo kasi unao fanana.

“Lakini tunakaribia kufika mke wangu”

Raisi Praygod alimtoa wasiwasi Rahab, aliye yafumba macho yake kwa haraka, kama mtu anaye jaribu kuvuta hisia ya jambo fulani. Kila alipo jaribu kuvuta hisia dhidi ya jambo linalo kwenda kumtokea Samson, akashindwa kuona ni nini kinacho kwenda kutokea.


“Pleaseeeee”

Rahab alizungumza kwa sauti ya juu huku akizidi kuyafumba macho yake kwa nguvu, hadi damu za puani zikaanza kumchuruzika taratibu, Raisi Praygod akajaribu kumshika mkono mke wake kutazama ni nini kinacho msumbua, ila akajikuta mkono wake ukisogezwa kwa nguvu na mke wake huyo hadi akabaki ameduwaa.

Rahab, akashuhudia jinsi shingo ya Samson inavyo kandamizwa kwa nguvu na mtu aliye valia mavazi meupe, baada ya muda kidogo Samson akatulia kimya, ikiashiria tayari amesha yapoteza maisha yake. Rahab akayafumbua macho yake huku akishusha pumzi taratibu, machozi ya uchungu yakaanza kumwagika usoni mwake.


“Mke wangu unatatizo gani?”

Raisi Praygod aliuliza huku akiwa na wasiwasi mkubwa, Rahab akatingisha kichwa akidai hakuna tatizo ambalo limejitokeza. Rahab akajifuta damu zilizo kuwa zikimwagika, huku akiamini kwamba safari wanayo iendea haina umuhimu tena kwao. Kwani mtu wanaye mfwata tayaria amesha uawa kinyama, na mtu amabaye hakuiona sura yake.

***

Dokta Maliki, alipo hakikisha kwamba tayari amesha muua Samson kwa kuiminya shingo yake, akarudishia kila kitu alicho kitoa kwenye mwili wa Samson, ikiwemo mashine inayo msaidia kuhema. Baada ya mashine hiyo kurudishiwa kwenye mdomo wa Samson, ikaaonyesha mstari mwekundu ulio nyooka, ukiashiria kwamba mtu huyo tayari amesha poteza maisha. Dokta Maliki akatoka ndani ya chumba hicho.

“Hakikisheni hakuna anaye ingia humu ndani, mgonjwa anahitaji kupumizika”


Aliwaambia askari hao ambao hakuna aliye kuwa akifahamu ni kitu gani kinacho endelea, Dokta Maliki akaanza kutembea kwenye kordo ndefu kuelekea nje, na muda huu hakuhitaji kukaa tena hospitalini kwani tayari anatambua ni kitu gani alicho kifanya na endapo atajulikana kama yeye ni muuaji, basi adhabu kali itaambatana naye.

Akiwa katika eneo la maegesho ya magari, gari kadhaa zinazo ashiria zimembeba kiongozi mkubwa zikasimama, ikamlazimu kuangalia ni kiongozi gani ambaye anashuka. Mlango wa gari moja ukafunguliwa akashuka binti mmoja pamoja na jaama ambaye ni mara yake ya kwanza kuiona sura yake


“Huyu ni nani?”

Alijuliza, huku akiendelea kumtazama jamaa huyo anaye wekewa ulinzi mkubwa kama kiongozi wa nchi. Macho ya dokta Maliki yakagongana na macho ya Rahab, aliye mtazama kwa muda huku akionekana kama msichana huyo anamtambua Dokta Maliki. Raisi Praygod baada ya kumuona mke wake anamshanga sana dkatari aliye simama kwenye moja ya gari huku akiwa na funguo mkononi, ikambidi amshike mke wake mkono.


“Baby twende ndani”

Rahab akaondoka na Raisi Praygod ambaye sura yake halisi imefunikwa na sura bandia ambayo hakuitaji sura yake iweze kuonekana na mtu wa iana yoyote zaidi ya walinzi wake wanao fahamu kwamba ni yeye. Dokta Maliki akiingia ndani ya gari lake na kuondoka katika eneo la hospitali ya Muhimbili huku moyoni mwake akiwa na furaha ya kuweza kukeleza kazi ya kiongozi wake anaye mtumikia.


Raisi Praygod moja kwa moja akapelekwa kwenye chumba alicho lazwa Samson, huku akiwa na mke wake pamoja na daktari mkuu wa zamu, aliye weza kuitambua sauti ya raisi Praygod.

“Samahani dokta. Dokta Maliki ameagiza asiingie mtu ndani ya chumba hichi”

Askari walio achiwa jukumu la kulinda katika chumba hicho waliwazuia Raisi Praygod, Rahab pamoja na daktari huyo wa zamu pasipo kufahamu kwamba huyo wanaye mzuia ndio raisi wao

***

Baada ya hali kutulia, kwenye hoteli alkliyo fikizia waziri wa mambo ya nje ya Marekani, mkuu wa askari nchini Russia akiwa ameongozana na vijana wake wawili, wakaelekea sehemu walipo fichwa viongozi hao wawili. Kila mmoja akashikwa na butwaa baada ya kukuta miilii ya walinzi wote ikiwa imezagaa chini huku ni raisi wao akiwa amekaaa kwenye sakhafu huku akiendelea kuugulia maumivu makli ya jeraha la risasi aliyo pigwa.


Kwa haraka wakafanya mawasiliano na askari wengine wa markani waliopo nje ya hoteli hiyo wakiendeleza ulinzi. Kuhakikisha kiongozi wao anaye lindwa ndani hapatwi na tatizo lolote. Kitendo cha kukuta kiongozi wao ameua, kila mmlinzi akajikuta akichanganyikiwa, kwani hakuna aliye elewa tukio hilo limefanywa na nani, huku walinzi wote wakuaminika wakiwa wameuwa kikatili.


Wakafanya mawasiliano haraka moja kwa moja kwenye ikulu ya Marekani na kutoa taarifa hiyo iliyo wachanganya kuanzia raisi pamoja na jopo lake zima la ulinzi. Uchunguzi wa kina ukaanza kufanyika kwa kina, huku kamera za eneo hilo zikichunguzwa kujaribu kumuona nani ameusika na mauaji hayo. Cha kushangaza kamera zote za eneo lililo tokea maauji, hazikuweza kuonyesha tukio hilo, hapo ndipo wakagundua kuna mchezo ambao umefanyika.


(muda mchache kabla ya tukio)

Baada ya Agnes, kushindwa kumuua waziri wa mambo ya nje wa Marekana, akiwa mbali kwenye sehemu walipo jificha, akili ya Anna ikatambua moja kwa moja ikatambua kwamba ni lazima Agnes atashuka na kwenda kutekeleza tukio hilo kwenye hoteli hiyo. Kifaa maalimu kilicho ingizwa mwilini mwa Agnes, kiliweza kumuonyesha kila sehemu anayo kwenda.

Anna akaomba kupewa kazi moja ya kumlinda rafika yake huyo ambaye anaiendea kazi moja ya hatari sana.

“Utamsaidiaje?”


Bwana Rusev alizungumza huku akimtazama Anna machoni. Anna akamuomba muendesha mitambo katika chumba hicho walichopo aweze kumpisha kwenye kiti kwani kuna kazi anahitaji kuweza kuifanya. Kwa utaalamu alio kuwa nao Anna, akaanza kucheza na kamera za ulinzi zilizopo kwenye eneo hilo kwa kutumia computer iliyo unganishwa mitambo ya Satelaite, alicho anza kukifanya ni kutafuta namba za siri ambazo zinaongoza kamera zote zilizopo kwenye eneo hilo, kwa bahati nzuri akafanikiwa kuzipata, alicho kifanya ni kuweza kugandisha kila kamera anapo pita Agnes, jambo ambalo halikuweza kustukiwa na wataalamu walipo kwenye chumba maalumu kwenye hoteli hiyo katika kuongoza kameza zaidi ya alfu moja zilizopo katika eneo zima la hoteli.


Tukio la Agnes kumteka kijana mwenye mavazi ya zima moto halikuweza kunaswa na kamera za hoteli, zaidi ya wataalamu hao kunao kila eneo lipo salama kupitia tv zao nyingi zilizomo ndani ya chumba hicho.


Agnes anaingia kwenye eneo walilopo viongozi, camera zote ziliweza kugandishwa na Anna, zikawa zinaonyesha uneo hilo likiwa limetulia, kumbe walinzi wanao walinda viongozi wao wapo kwenye wakati mgumu, wakiadamishwa na binti mmoja ila mwenye uwezo mkubwa kupita maelezo.

Hadi Agnes anatoka katika eneo hilo hapakuwa na camera iliyo weza kumnasa sura yake, na hapakuwa na mtu aliye weza kustukila swahala hilo. Watu waliomo ndani ya chumba hicho wakajikuta wakipiga makofi kwani kwa kazi waliyo ifanya mabinti hao, ni kazi kubwa sana yakutumia akili pasipo nguvu nyinngi.

***

Mahojiano ya haraka yakafanywa kwa Raisi wa Russia aweze kueleezea muuaji huyo wa kike anaonekana vipi. Huku akiendelea kufanyiwa matibabu na madaktari bingwa. Raisi akaendlea kutoa maelezo jinsi binti huyo anayo onekana. Wataalamu wa kuchora waziadi kuendela kuichora sara ya binti huyo hadi ikakamilika na kupata sura halisi ya Agnes. Picha hiyo kwa haraka ikatuma makao makuu ya ujasusi nchini Marekani Washinton DC. Sura hiyo ikaningizwa kwenye mitambo maalumu ambapo, kwa kutimia satalaite wakaanza kuitafuta ni wapi sura hiyo inapaikana.

“BINGOOOO”


Mtaalamu mmoja alizungumza baada ya kumpata msichana huyo ambaye bado anaonekana hajatoka kwenye nchi ya Rusia. Kila kona ya mipika picha ya Agnes ikasambazwa kwa haraka kwa kila askari, vituo vyote vya mabasi, reli, anga pamoja na bandari. Vikaimarishwa ulinzi mkali, huku askari wa kutosha kutoka Marekani, wakihakikisha wanamtia nguvuni binti huyo anaye onekana ni gaidi wa kimataifa.


Agnes pasipo kufahamu chochote kinacho endelea, akiamini kwamba kila kitu kipo sawa, akafika kwenye kituo cha treni. Akiwa katika moja ya dirisha la kukatia tiketi za treni, wanajeshi wawili wa kimarekani, wakiwa na mbwa wakasimama mbele yake huku wakimkazia macho, huku mmoja wao akijaribu kuchomoa bastola yake kwa ajili ya kumdhibiti Agnes kwani tayari wamesha mtambua yeye ndio muuaji wa kiongozi wao bwana Paul Henry Jr.


SHE IS MY WIFE(46)


Gafla, wanajeshi hao wawili walio simama, mbele ya Agnes, wakaanguka chini huku wakitoa milio mikali ya maumivu, mbwa walio washika wakatoa milio mmoja na kuanguka nao chini. Hata Agnes mwenyewe akabaki ameduwaa kwania hakujua ni nani aliye weza kulifanya tukio hilo la kuwaangamiza wanajeshi hao walio anza kuvuja damu kwenye miili yao.



Wananchi walipo karibu wakaanza kupiga makelele huklu wakikimbia kimbia. Makelele hayo yakawafanya askari pamoja na wanajeshi wengine kwenye eneo hilo kukimbilia katika sehemu kelele hizo zinatokea. Agnes akataka kujijichanganaya na wananchi hao, gafla akadakwa mkono wake kwa nyuma, akageuka kwa haraka huku akiwa emerusha ngumi iliyo pita hewani baada ya mtu huyo kuweza kuikwepa kwa kubonyea chini kidogo kwa umakini mkubwa alio kuwa nao aliweza kuiona ngumi hiyo inavyo kuja kwa kasi.


Macho ya Agnes yakakutana na macho ya mtu aliye vaa kinyago, huku sura yake yote ikiwa imefichwa na kinyago hicho cheusi. Mavazi ya mtu huyo yanarangi nyeusi tupu kuanzia chini hadi juu. Mgongoni mwake amechomeka sime ndefu iliyopo kwenye sehemu yake maalumu.

“Twende huku”


Hapo Agnes ndipo aliweza kumtambua mtu huyo ni msichana, hii ni baada ya kumuambia maneno hayo kwa lugha ya kiswahili sahihi. Agnes akataka kusita ila binti huyo akamvuta kwa nguvu, wakanza kukimbia wakikatiza katika kwenye kundi la watu wanao kimbia kimbia pasipo kujielewa.

Kundi la askari wapatao sita wakasimama mbele yao wakiwa na virungu, Binti huyo akamuachia Agnes mkono, kwa kasi ile ile walio kuwa wanakimbia nayo, akajirusha hewani mita nne kwenda juu, huku akijiviringisha kwa sarakasi, akawapita askari hao kwa juu, akatua nyuma yao nakuwafanya askari hao kupagawa. Kila askari aliye jaribu kurusha kirungu, aliweza kukutana na teke zito lililo muangusha chini. Agnes baada ya kuona msichana huyo anamsaidia, naye akawajibika katika kujibu mashambulizi ya ngumi zinazo pigwa na askari hao walio chapika kisaswa sawa kama watoto wadogo.

Ndani ya dakika mbili, hapakuwa na askari aliye weza kusimama, kila mmoaja aliweza kushikilia kiungo alicho weza kuvunjwa.


Kwa bahati nzuri, kuna treni inayo kwenda kwa mwendo kasi ikawa imefika katika kituo hicho, abiria wakushuka wakashuka na abiria wakupanda nao wakapanda. Agnes na binti huyo wakajichanganya na kuingia ndani ya treni hiyo, hadi askari wanagundua hilo tayari terni hiyo ilisha anza kuondoka taratibu kwenye kituo hicho. Jambo ambalo liliwawia ugumu askani ni kuisimamisha terni hiyo kwani kwa mujibu na sheria ya treni hizo, hazipaswi kusimama pale zinapo ondoka, kutokana kufanya hivyo kunaweza kusabibisha treni inayo kuja kwenye kitua hicho kuweza kugongana na kusababisha ajali kukbwa na ubaya zaidi treni hizo huwa zinatumia dakika tano tano kukaa kwenye kituo.


Kila abiria aliye waona Agnes na mtu huyo aliye valia ninja na kuificha sura yake, alikaa kimya huku kila mmoja akiwa na woga kwa upande wake, kwani wanaonekana ni watu hatari.

“Hii sio sehemu salama”

Binti huyo alizungumza huku akichungulia nje ya treni kwa kutumia vioo vilivyopo pembeni.

“Kutoka hapa hadi kituo kingine kuna msitu katikati, itatubidi kutoroka la sivyo kituo kinacho fwata nilazima tutakamatwa”

Sauti ya msichana hiyo ni ngeni masikioni mwa Agnes.

“Tunafanyaje sasa?”

“Twende juu”

“Juu…..!!!”


Agnes aliuliza huku akiwa amemtumbulia macho binti huyo, kwani mwendo wa treni hiyo ulivyo mkubwa ni hatari sana mtu kufungua hata kioo..

“Ndio twende juu”

Binti huyo alizungumza huku akichomoa jambia lake refu, watu wote waliomo ndani ya behewa hilo wakaka kimya kwani mlio wa kuchomolewa kwake tu, ulimstua kila mmoja. Binti huyo akapiga hatua mbili mbele kutoka katika sehemu alipo simama yeye na Agnes.

“KAMA UNAHITAJI KUISHI TOKA NDANI YA HILI BEHEWA”

Alizungumza kirusi, abiria wote wapatao kumi na tano wakaanza kutafuta ustaarabu wa kuingia katika mabehewa ya mbele au ya nyuma. Ndani ya dakika wakabaki wao wawili tu ndani ya behewa hilo.


“Ngoja kwanza wewe ni nani?”

“Hupaswi kunifahamu muda huu”

“Nani aliyeku………….”

Agnes hakuimalizia sentesi yake, jambia hilo linalo meremeta kama kioo, likawa limesimamishwa sentimita chache kutoka shingoni mwake.

“Huwa sipendi maswali ya kipuuzi nikiwa kazini”

Agnes akameza fumba la mate kwani tayari amesha gundua mwanamke mwenzake huyo ana uwezo mkubwa sana kuliko yeye na endapo atajaribu kupimana naye uwezo wa kupigana itakula kwake.

“Fwata nitakacho kuambia”

Alizungumza huku alilishusha chini jambia lake hilo, Agnes akashusha pumzi kubwa kwani shingo yake ingegawanyishwa vibaya.

***

Kwa haraka, Rahab akarusha ngumi za kasi zilizo tua shingoni mwa askari mmoja aliye kuwa kiherehere kuwazuia kuingia ndani ya chumba hicho. Mwengine kabla hajafanya chochote Raisi Praygod Makuta akampuka kiwiko cha uso askari huyo nakumfanya mikono yake yote aipeleke usoni mwake kwani giza la gafla liliyafunika macho yake. Rahab akaingia ndani ya chumba huku raisi Praygoda akifwatia kuingia

“Mambo mengine munajitakia wenyewe”

Daktari huyo wa zamu alizungumza huku akimsukumia pembeni askari aliye ufunika uso wake kwa viganja vyake. Dokta baada ya kuingia ndani ya chumba hicho na kukuta mashine ya kupumulia inaonyesha mstari mmoja mwenkundu ikiashiria mgonjwa huyo amefariki, akajikuta amechanganyikiwa.


“Si alikuwa hai huyu”

Daktari alizungumza huku akijaribu kumminya Samson kifuani mwake. Rahab akamshika mikono daktari huyo na kumzuia kufanya akacho kifanya

“Tayari ameshakufa ila naomba sindano”

“Sindano………!!!?”

“Ndio sindano”

Daktari huyo akajipapasa pasa kwenye mifuko yake, hakukuta sindano

“Dakika moja”

Akatoka kwa kasi na kuelekea sehemu ambapo anaamimi nanaweza kupata bomba la sindano. Rahab baada ya daktari huyo kutoka, akaufunga mlango kwa ndani na kusimama pembeni ya kitanda alipo simama mumewe.

“Sasa tunafanyaje na mgonjwa amesha kufa?”


Raisi Praygod aliuliza huku akiwa amekata kabisa matumaini yakundelea kukaa ndani ya chumba hicho.

“Ngoja nikuonyeshe kitu ila ninaomba iwe siri yako mume wangu”

“Siri? Kitu, kitu gani?”

“Subiri”

Rahab akachomoa bastola yake, akatoa magazine. Kwakutimia ncha ya kali ya chini ya magazine hiyo inayo hifadhia risasi, akajikata kwenye mkono wake wa kushoto sehemu yenye mshipa wa damu.

“Unataka kufanya nini mke wangu!!?”

“Subiri utaona mume wangu”

Rahab akamfunua Samson kinywa chake, akaanza kuyanyunyuzia matone ya damu yake kwenye kinywa cha Samson, baada ya kuridhika kiasi cha damua alicho kiingiza mdomoni mwa Samson kinatosha, akachanan kipande cha shuka, akajifunga sehemu ambayo damu inatoka. Akamsogelea Samson karibu, akampulizia pumzi kiasi Samson. Taratibu vidole vya miguu vya Samson vikaanza kucheza, ikiashiria uhai wake umesha rudi.


“Samson, Samson, Samson”

Rahab aliita mara tatu, Samson akayafumbua macho yake, huku macho yake yote yakiwa mekundu sana. Rahab akamkazia macho Samson, kila walivyo zidi kutazamana ndivyo jinsi macho ya Samson yalivyo rudi katika hali yake ya kawaidia. Raisi Praygod Makuya, na ujasiri wake wote akajikuta akitetemeka kwani tangu azaliwe hakuwahi kusikia kama kuna binadamua anaye weza kufufua binadamu mwengine.


“Fungu mlango”

Rahab alizungumza kwasauti nzito kidogo, iliyo mfanya Raisi Praygod kukimbilia mlangoni, kitendo cha kuufungua mlango dokta wa zamua akaingia, alipo muona Samson akinyanyuka na kukaa kitako kitandani, akajikuta akidondosha bomba la sindano. Mwili mzima ukamuishia nguvu akaanguka chini na kupoteza fahamu.

“Amezimia tu”

Rahab alizungumza huku akimtazama dokta huyo aliye lala sakafuni.

“ASANTE MADAM RAHAB”

Samson alizungumza kwa sauti nzito kiasi, Rahab akaachia taasamu pana akiamini jaribio lake limefanikiwa.

“Niagize chochote nitafanya Madam Rahab”

Samson aliendelea kuzungumza huku akimtazama Rahab aliye simama mbele yake.


“Twende nyumbani sasa”

Rahab alizungumza. Sasmso akasimama wima akajigeuza geuza akiashiria yupo safi. Rahab akalishika la hospitalini alilo valishwa Samson, akalichana kwa nguvu na akabaki tumbo wazi. Hapakuwa na jeraha lolote mwilini mwa Samson. Raisi Praygod akabaki ameduwaa tuu, kwani kila linalotokea kwenye macho yake ni kama ndoto. Rahab baada ya kumtazama mume wake akagundua yupo kwenye hali ya woga. Akasogelea, akanyonya mate, yaliyo ufanya mwili wa Raisi Praygod kushikwa na kijiubaridi, kilicho utoa woga wote na kurudi katika hali ya kawaidia.


“Twende zetu Praygod”

“Sawa”

Wakatoka wakiwa wameongozana na Samson, askari wanao endelea kuugulia maumivu, baada ya kuona mgonjwa waliye amini ni mahututi akitoka anatembea huku akiwa hana hata bandeji moja mwilini wake wala kidonda, wakabaki wakiwa wameduwaa kila mmoja akiwa haamini wanacho kiona.

***

“Muheshimiwa kazi yako nimesha imaliza”

Dokta Maliki alizungumza kwa kutumia simu yake ya mkononi huku akizidisha mwendo kasi wa gari gari lake.

“Unauhakika kama Samson amefariki?”

Makamu wa raisi alizungumza kwa kufoka sana hadi dokta Maliki akashangaa kwani si kawaidia ya kiongozi wake huyo kuzungumza kwa sauti ya ukali kama hivyo

“Ndio muheshimiwa”

“Pumbavu wewee, mtu hajakufaa unaniletea ujinga unjingaa hapaaa”

Makamu wa raisi alizungumza kwa kufoka, hadi dokta Maliki akajikuta akifunga breki za gafla, na kusimamisha gari lake pembeni ya barabara


“HAJAKUFAA……!!!?”

“Fala wewe, unamuuliza nani”

Makamu wa raisi akakata simu. Dokta Maliki akabaki anaishangaa simu yake, kila alvyo jaribu kuvuta kumbukumbu zake, anakumbuka aliweza kumnyonga Samson hadi amefariki, sasa inakuwaje makamu wa raisi aseme Samson yupo hai.


Akiwa katika dimbwi la mawazo ujumbe wa meseji kupita whatsapp, ukaingia kwenye simu yake, kwa haraka akaufungua na kukutana na namba ngeni iliyo tuma picha ambayo bado inaendela kusoma kwa ajili ya kufunguka.

“Comen comennnn”


Dokta Maliki alizungumza na simu yake hiyo, mara baada ya kuona picha hiyo inachelewa kufunguka kutokana na mtandao wa internet katika sehemu alipo kuwa ni mdogo. Picha hiyo ikafunguka hapo ndipo dokta Maliki alipo amini kwamba Samson yupo hai. Kwani picha hiyo inamuonyesha Samson akiwa ameongozana na watu watatu ambao alipishana nao mara baada ya kuwaona wakiingia hospitalini.

“Shitiiiiiii Fuc**………..!!!!!”


Dokta Maliki alijikuta akipiga mgumi nzito kwenye mskani wake hadi honi ya gari lake ikalia kwa nguvu. Gafla taa za mbele za gari yake zikafifia sana, akaiweka pembeni simu yake kwani kufifi kwa taa za gari yake hiyo mpya aina ya Breves, kilimstua akafungua mkanda wa siti yake, gafla taa zake zikarudi katika hali ya ukawaida, cha kumshangaza zadia mbele ya gari lake amesimama mtu aliye mpa mgongo, jambo lililo mtisha Doktar Maliki.


Akaminya honi zake kwa nguvu ili mtu uyo kuweza kupisha njiani, na mbaya zaidi dokta Maliki aligundua amasimama katikati ya daraja la Sarenda. Kwa haraka akilini mwake akahisi ni majini ambao mara kwa mara inasadikika yanaonekana kwenye daraja hilo. Akawasha gari yake ila haikuwaka akajaribu kuliwasha gari lake ila halikuwaka kabisa.


Mtu aliye simama mbele ya gari lake taratibu akaanza kugeuka huku sura yake akiwa ameiinamisha chini. Alipo inyanyua sura yake, macho ya Dokta Maliki yakamuona vizuri Samson akiwa amsimama mbele yake, huku akiwa tumbo wazi, mikononi mwake akiwa amshika bastola mbili zilizo elekea chini.


==> ITAENDELEA



ILIPOISHIA

Akaminya honi zake kwa nguvu ili mtu uyo kuweza kupisha njiani, na mbaya zaidi dokta Maliki aligundua amasimama katikati ya daraja la Sarenda

. Kwa haraka akilini mwake akahisi ni majini ambao mara kwa mara inasadikika yanaonekana kwenye daraja hilo. Akawasha gari yake ila haikuwaka akajaribu kuliwasha gari lake ila halikuwaka kabisa. Mtu aliye simama mbele ya gari lake taratibu akaanza kugeuka huku sura yake akiwa ameiinamisha chini. Alipo inyanyua sura yake, macho ya Dokta Maliki yakamuona vizuri Samson akiwa amsimama mbele yake, huku akiwa tumbo wazi, mikononi mwake akiwa amshika bastola mbili zilizo elekea chini.


ENDELEA

Samson hakuhitaji kumuacha hai dokta Maliki, akafyatua risasi zipatazo ishirini, zilizo vunja kioo cha gari ya dokta Maliki, na nyingi zikatua kifuani kwake na huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya dokta Maliki. Samson akapiga hatua hadi kwenye gari la Dokta Maliki, akafungua mlango wa gari hilo ili kuhakikisha kwamba adui yake amesha poteza maisha. Alipo hakikisha dokta Maliki tayari amekuifa, akarudi kwenye gari walipo raisi Praygod pamoja na Rahab.


“Tayari Madam Rahab”

“Kazi nzuri”

Wakaondoka katika eneo la daraja ili kuto kuweza kuingia mikononi mwa askari ambao hawakujilikana watafika muda gani kwenye eneo hilo, kwani ni tayari askari wa nchi nzima walipewa jukumu la kuimarisha ulinzi masaa ishirini na nne, kwani usalama wa nchi bado ni hali tete.

***

Agnes akiwa katika wazo la kufikiria kutoka nje ya treni hiyo inayo kwenda kwa kasi, binti huyo akavunja kioo kimoja kwa kutumia kishikizo cha jambia lake. Upepo mwingi ukaanza kuingia ndani ya treni hiyo


“Tunatoka sasa”

Binti huyo alizungumzakwa sauti ya juu kutokana na upepo huo mwingi. Binti huyo akachungulia nje, alipo ona kuna usalana, hakuhitaji kupoteza muda akapanda kwenye dirisha hilo huku akiwa ameshikilia vizuri kwa ndani. Kabla ya kupanda juu, akamtazama Agnes ambaye anaonekana kuhofia kitendo hicho.

“Hei jikaze, unahitaji kukamatwa?”

Binti huyo alizungumza huku akimtazma Agnes. Hapakuwa na jinsi yoyote ya kuweza kufanya, binti huyo akatoka ndani ya behewa hilo na kwautaalamu mkubwa alio nao akapanda juu ya behewa hilo. Agnes akashusha pumzi kuuondoa woga, akafanya kama alivyo fanya binti huyo, chakushukuru Mungu akafanikiwa kupanda juu ya behewa hilo alipo mwenzake.


“Tunafanyaje sasa?”

Agnes aliuliza kwani hakuelewa ni kitu gani ambacho kinakwenda kutokea kwa wakati huo, na jinsi akitazama mwendo kasi wa treni hilo akajikuta akizidi kuchanganyikiwa.

“Tunaruka”

“TUNARUKAAA…..!!”

“Ndioo”

“Ahaaa siwezi kufanya hivyo, nitakufaaa”

“Tunafanyaa jiamini, pale mbele kuna daraja chini kuna mto mkubwa”

“Ndio turuke………?”

Wakiwa katika kujadiliana ni nini cha kufanya, kwa mbali wakaiona helcoptar ikija kwa kasi ikitokea nyuma, kwao treni inapo tokea. Katika kuitazama vizuri binti huyo akagundua kwamba ni helcoptar ya jeshi la Marekani.


“Shitii…..”

Akamkumbatia Agnes, kisha kwakutumia nguvu, akajirusha naye kuelekea kwenye mto mkubwa unao pitisha maji mengi. Agnes akawa na kazi ya kupiga makelele kwani hakujua watakapo fika chini watakuwa hai au laa. Kila mwanajeshi aliye kuwa kwenye helcoptar hiyo, walio pata habari juu ya uvamizi wa mabinti hao, alijikuta akishangaa kitendi hicho, kwani kuruka kutoka juu ya treni hadi kwenye mto huu kuna urefu mkubwa sana, ambao kama mtu akiruka ni lazima atakutana na mauti yake ndani ya mtu huo.

Wakawashuhudia mabinti hao wakidumbukia ndani ya maji hayo mengi yanayo kwenda kwa kasi sana.

“Sir tunafanyaje?”

Mwanajeshi mmoja alimuuliza mkuu wao wa kikosi waliye kuwa naye ndani ya helcoptar hiyo.

“Peleka helcoptar karibu na mtu huo”

“Sawa mkuu”

Rubani huyo akafanya kama alivyo agizwa na mkuu wake, kutokana na uwezo wa helcoptar hiyo aliweza kuishusha karibu sana na mtu huo kuangalia kama mabinti hao wapo hai au wamesha kufa. Hawakufanikiwa kuwaona wasichana hao ambao hakuna aliye weza kujua kama wamechukuliwa na maji au kufia ndani ya mto huo.


“Wasiliana na kikosi cha maji waje kutoa msaada”

Mkuu huyo alimuagiza msaidizi wake, akafanya kama alivyo agizwa, kwani hawakuhitaji kuweza kuwapoteza wasichana hao, haswa Agnes aliye weza kufanya mauaji ya kiongozi wao, jambo lililo zua simanzi kubwa sana kwa wamarekani wengi, ukiachilia simanzi iliyo wakumba pia ni aibu kubwa sana kwa nchi kubwa iliyo endelea kama hiyo, kiongozi wao mapoja na askari walio aminika kumlinda kiongozi wao nao pia waliuawa kikatili

“Hawa malaya nilazima tuwakamate”

Mkuu huyo wakikosi alizungumza huku akiwa amekunja ngumi ya mkono wake wa kulia akiwa na hasira kali, kwani masaa ishirini na nne waliyo pewa na raisi wao ya kumkamata binti huyo yanazidi kuteketea pasipo mafanikio ya aina yoyote.

Baada ya muda mchache, wanajeshi wa majini wakafika katika sehemu walipo ingia mabinti wanao watafuta, kazi ya kuwasaka ikaanzia hapo, huku kila mmoja akijitahidi kufanya anacho weza kuwatia nguvuni wasichana hao.

***

“Muheshimiwa kuna barua ujumbe wako”

Msemaji wa ikulu alimfwata raisi Praygod Makuya, mara baada ya kufuki ikulu wakiwa wameongozana na mke wake pamoja na Samson.

“Umetoka wapi?”

“Whait House Marekani”

Raisi Praygod hakuwa na wasiwasi mkubwa, kwani Tanzania inaushirika mzuri sana na nchi hiyo kubwa duniani na alicho weza kukiamini, ujumbe huo utakuwa ni wapole kwa yale yaliyo weza kujitokeza.


“Baby muangalie mtu wako”

“Sawa”

Raisi Praygod akaondoka na kumuacha Rahab na Samson wakipelekwa kwenye chumba kingine kwa kuweza kuzungumza. Raisi Praygod alicho weza kukifanya ni kuweza kuivua sura ya bandia aliyo weza kuivaa, moja kwa moja akaongozana na msemaji wa ikulu, hadi ndani ya ofisi maalumu ya mawasiliano. Tv kubwa zote zilizomo ndani ya chumba hicho zikawashwa, ili kuweza kufanya mawasiliano na kiongozi mwenzake wa nchi hiyo kubwa. Kutokana na urafiki wao wakaribu, wakasalimiana kwa furaha, huku raisi wa Marekani akimpa pole raisi Praygod kwa yale yaliyo weza kujitokeza.

“Ila ninatatizo kubwa kuliko hata hilo lakwako”

Raisi wa Marekani alizungumza, huku wakitazama Raisi Pragod Makuya kwa kupitia Tv hizo kubwa


“Tatizo gani ndugu yangu?”

“Waziri wa mambo ya nje bwana Paul Henry Jr ameuawa”

“Weee Paul amefariki…….!!?”

“Ndio tena ameuawa na kijana kutoka nchini kwako?”

“Nchini kwangu!!?”

“Ndio, tena ni msichana mdogo tu mwenye umri kama miaka ishirini na nne au tano”

Raisi Praygod akajikuta akichoka kwa taarifa hizo, kwani Mtanzania huyo hakujua anauwezo gani wa kuweza kufanya mauaji makubwa ya kiongozi anaye lindwa sana

“Praygod, kwa hili nimeamua kulishikilia mimi mwenyewe, ila kutokana wewe ni mtu wakaribu ninakuomba kitu kimoja. Nitakapo mkamata huyu msichana, nimuue”


Raisi wa Marekani alizungumza maneno yaliyo mfanya Raisi Praygod Makuya kukaa kimya huku akimtazama kiongozi mwenzake.

“Hembu naomba hiyo picha niiione yahuyo muuaji”

Picha hiyo ikatumwa kwa njia ya emali, msemaji wa raisi akaitoa picha hiyo na kumkabidhi raisi Praygod, aliye jikuta akiitumbulia macho picha ya msichana huyo kwani kati ya wasichana wanne walio isumbua nchi ya Tanzania katika swala la ujambazi huyu ni miongoni mwao.

“Je unaniruhusu kumuondoa duniani huyu muadiani?”

“Utakapo mkamata, nitakuomba kama rafiki yangu tuweze kukutana kulizungumze hili”

“Sawa ni kutokana ni wewe, laiti angekuwa anatokea nchi nyingine nisinge omba hata kibali cha kuweza kumuua, kwani ameua vijana wangu kama ishirini”


“Ishirini…..?”

“Ndio ishirini wale wote walio kuwa wakimlinda Paul, kwani wote walikuwa Russia kwenye ziara ya kikazi”

“Sawa tutashirikiana kwani mimi pia ninawatafuta hao mabinti waliniulia wanajeshi wangu wengi”

“Basi mimi na wewe ni kitu kimoja, tuendele kuwasaka”

“Sawa”

“Basi tunaendelea kufahamishana kila linalo endelea”

“Sawa”

Mawasiliano yakaishia hapo, Raisi Praygod akaitazama vizuri picha ya Agnes

“Hawa mabinti kumbe bado wapo?”

“Hata mimi nimeshangaa muheshimiwa”

“Ngoja nikapumzike, kesho nitahitaji viongozi wote wa usalama wa taifa wafikie ofisini kwangu”

“Saa ngapi?”

“Saa moja asubu wawe hapa, fanya nao mawasiliano”

“Sawa muheshimiwa”

Raisi Pragod akaondoka na kuelekea kwenye chumba walipo Samson na Rahab, akawakuta wakiendelea na mazungumzo.


“Mumefikia wapi?”

Raisi Pragod alizungumza mara baada ya kukaa kwenye moja ya kiti kilicho pembeni mwa meza hiyo.

“Ni mengi ambayo tumeyazungumza, labda wewe useme unahitaji kuyasikia yapi?”

Rahab alizungumza huku akimtama mume wake

“Ahaaa mwaka huu nitachanganyikiwa”

“Kwa nini?”

“Kuna kiongozi wa Marekani ameuawa”

“Kisa?”

“Hata sifahamu, ila muuaji ni huyu hapa”

Raisi Praygod akampa picha mke wake. Rahab akashtuka mara baada ya kukuta ni Agnes rafiki yake wakaribu sana.

“Agnes…….!!”

Samson baada ya kusikia jina la Agnes, akaichukua picha ya aliyo ishika Rahab kwa haraka na kutazama ni Agnes anaye mfahamu au laa. Hakuwa ni mwengine bali ni Agnes kati ya mabinti alio kuwa akishirikiana nao.

“MUNGU WANGU………!!”

Samson alizungumza huku akitetemeka mwili mwimza hadi Rahab na Raisi Praygod Makuya wakalistukia hilo.


“Vipi unamfahamu?”

Rahab aliuliza

“Ndio nimefanya nao kazi, na kwasasa wapo chini ya gaidi la kimataifa bwana Rusev”

“Rusev, Rusev ndio nani?”

“Ni mmoja ya magaidi wanao taka kuipindua nchi ya Rusia na kama kuna uwezekana kuishikilia dunia kwa ujumla”

“Mmmm kuishikilia dunia!!?”

Raisi Pragod aliuliza kwa mshangao mkubwa sana kwani kinacho weza kuzungumza na Samson ni kitu cha kustaajabisha sana.

“Ndio, kuna maraisi Kumi na tano wanatakiwa kufa”

Samson alizungumza huku akimtazama raisi Praygod Makuya.

“Kati ya hao kumi na tano, wewe pia ni mmoja wapo”

Raisi Praygod akajikuta akijichokea, kwa mbali machozi yakaanza kumlenga lenga, kwani kama kiongozi huyo wa Marekani ameuawa, na muuaji hakuweza kukamata kiurahisi, basi hata yeye anaweza kuuwa muda ni siku yoyote


SHE IS MY WIFE(48)



“Usijali sana mume wangu nitakulinda”

Rahab alimfariji mume wake baada ya kuona amefadhaishwa na taarifa alizo weza kuzitoa Samson.

“Twende tukapumzike”

Raisi Praygod alizungumza huku akiondoka ndani ya chumba, huku sura yake dhahiri ikioshesha hana furaha hata kidogo.

***

Kwa uwezo mkubwa aliokuwa nao binti aliye weza kumsaidia Agnes, aliweza kuendelea kupambana na maji mengi yanayo kwenda kwa kasi huku akiendelea kumshikilia Agnes vilivyo. Ili kuto kuweza kumpoteza Agnes ambaye kwake ni muhimu sana kwa lile ambalo anahitaji kwenda kulifanya na binti huyo.


Kwa bahati nzuri maji hayo yakawapeleka hadi kwenye moja ya mto mkubwa uliotulia na unao katika katika msitu mmoja mkubwa. Akamtoa Agnes nje ya maji, ambaye hali yake ni mbaya kiasi, hii ni kutokana na kushindwa kuweza kuhimili msukomo wa maji hayo ambayo yalikuwa yakiwapeleka kwa kasi. Akampa huduma ya kwanza Agnes, huku akiendela kuuchunguza mwili wa Agnes.

“Shit….”

Msichana huyo alizungumza huku akichomoa kisu chake kidogo kwenye mguu wake wa kushoto, akaushika vizuri mkono wa kulia wa Agnes na taratibu akakipitisha kisu chake kwenye maeneo ya bega la Agnes na kumfanya akurupuke

“Unataka kufanya ni……..?”

“Tulia”

Msichana huyo, akatoa kipande kigogo ya mawasiliano alicho kuwa ameingiziwa Agnes kwenye bega lake na bwana Rusev ili kila anapo kwenda aweze kuonekana.

***

Kila aliye kuwa kwenye chumba cha wamaasilano alijikuta akitumbilia macho computer kubwa iliyomo ndani ya chumba hicho, kwani ni mawasiliano yao na Agnes yaliweza kukatika gafla

“Ni nini kumetokea?”

Bwana Rusev aliwauliza watu wake wa mawasiliano kwa kufoka

“Ku….kuu…kuu kuna tatizo”

Mmoja alijibu kwa kubabaika

“Nini wewe, tumempotezajee”

Bwana Rusev aliendelea kubabaika kwa kufoka sana, kila mmoja akaendelea kuhangaikia jinsi wanavyo weza kumpata Agnes kwenye mitambo yao kwani maandishi makubwa yasomekayo NO SIGNAL, yalijitokeza.

Swala la Agnes kutoweka, likazidi kuwachanganya Fetty, Halina na Anna. Kila mmoja wasiwasi mwingi ulimjaa dhidi ya rafiki yao huyo, hawakuhitaji kupungua zaidi ya hapo walipo fikia, kwani rafiki yao kifpenzi Rahab hadi leo hawafahamu yupo wapi.


“Bosi tunaomba kazi ya kwenda kumtafuta Agnes”

Fetty alizungumza kwa kujiamini, akiwa amesimama wima na mikono yake akiwa ameirudisha nyuma. Bwana Rusev akaka kimya pasipo kujibu kitu chochote, akili yake haikuwa na kitu chohote cha kuwaza zaidi ya kumfikiria Agnes, binti aliye tokea kumpenda na kumuamini kati ya mabinti wote wanao mtumikia.

“Mutampatia wapi?”

“Inabidi kuweza kutambua mto huo upo eneo gani?”

“Nyinyio tafuteni eneo la mto lilipo”

Bwana Rusev aliwaamrisha mafundi mitambo wake ndani ya chumba hicho cha mawasiliano.

“Sir mto huo unaitwa AMUR, ni sawa na kilometer 260 kutoka hapa tulipo”

“Toeni ramani ya mto huoo”

Ramani ikatolewa kama alivyo agiza bwana Rusev, akawakabidhi Fetty na wezake wawili, walio ipita kwa muda, kisha wakaelekea kwenye vyumba vyao kwenda kujiandaa na kazi hiyo ambayo kila mmoja aliamimi itakuwa ni ngumu kwake.


“Tuhakikishe tunarudi wote salama salimini sawa”

Fetty alizungumza huku akifunga kamba za buti yake ndefu aina ya travota

“Sawa, je situchukue vijana wawili watusaidie katika hili?”

“Anna sisi tunatosha kuikamilisha hii kazi”

“Ila Fetty alicho kisema Anna kina maana si kila kitu sisi tunaweza kukifanya kumbuka kwamba hii si Tanzania ambayo tumeizoea, tupo ugenini huku”

Maneno aliyo yazungumza Halima yakamfanya Fetty kuwa muelewa, kwani ukitazama leo ndio siku yao ya kwanza kutoka nje tangu walipo ingia kwenye ngome hii, iliyopo kwenye miamba mikubwa chini ya bahari. Kila mmoja alipo hakikisha kwamba amebeba silaha yake, aliyo ona inafaa kwenye zoezi zima la kwenda kumtafuta Agnes, wakatoka ndani cha chumba na kurudi chumba cha mawasiliano na kumkuta bwana Rusev akiendelea kuweweseka kwa wasiwasi mkubwa, kwani mtu aliye mchukua Agnes hadi sasa hivi hawatambui ni nani.


“Tupo tayari”

Fetty alimuambia bwana Rusev, akawatazama jinsi wasichana hao wanavyo jiamini kisha akashusha pumzi nyingi akitafakari cha kuzungumza.

“Ahaa…ahaa hakikisheni munarudi wote”

“Sawa mkuu”

“Ila mutaidi muwe na vifaa maalumu tuwe tunawasiliana”

Kila mmoja akafungwa kifaa cha mawasiliano, kila mmoja alipo kamilika wakatoka na bwana Rusev kwenda kwenye eneo lenye maegesho ya helcoptar zakijeshi. Wakakuta vijana wengine wanne walio jiandaa tayari wakiwasubiri.

“Mutaongozana na hawa vijana”

“Sawa mkuu”

“Nawatakia kila laheri katika kazi yenu”

“Asante mueheshimiwa”

Wote wakaingia kwenye helcoptar hiyo, kwa kutumia mitambo mikubwa, sehemu ya juu ya eneo hilo ikafunguka na taratibu helcoptar hiyo ikatoka na kuanza safari ya kuelekea kwenye mto Amur.

***

“Tuondoke hili eneo”

Binti huyo alimuamrisha Agnes, baada ya kukifunga kwa kitambaa sehemu alipo mchana na kiu na kutoa kifaa malumu kilicho mfanya kuweza kuonekana kila anapo kwenda kw akutumia mitambo ya Satelaite.

“Tunakwenda wapi?”

“Utafahamu ni wapi tunapo elekea”

“Ila samahni, nahitaji kujua wewe ni nani?”

“Utanijua hapo baadaye, ila kwa sasa tunahitaji kusonga mbele, kumbuka kwamba unatafutwa na jinsi tunavyo endelea kukaa hapa ndivyo jinsi tutakavyo jikuta tunakamatwa”


Agnes hakuwa na pingamizi zaidi ya kuongozana na binti mwenzake kuingia kwenye msitu huo wenye miti mirefu sana kwenda juu. Masaa na majira yakazidi kukatika hadi kigiza kikaanza kutawala anga, wakazidi kutembea kusonga mbele pasipo kuchoka, hadi wakafanikiwa kufia kwenye moja ya kijiji, ambacho binti huyo aliweza kuongoza na Agnes mpaka kwenye moja ya nyumba, iliyo tengenezwa kwa mbao na wote wakaingia. Wakamkuta mmzee mmoja mwenye nywele ndefu, na sutra ya kichina akiwa amekaa chini na kukunja miguu yake pamoja na mikono akionekana kama yupo kwenye ibada.

Wakasimama nyuma yak kumsubiria mzee huyo kuweza kumaliza anacho Sali, baada ya muda mzee huyo akawageukia na kuwatazama.

“Monk nimerudi”

Binti huyo alizungumza kwa lugha ya kijapani na kumfanya Agnes asiweze kuelewa kitu cha aina yoyote.

“Kazi nzuri, muandalie sehemu mzuri ya kulala”

“Sawa Monk”

Binti huyo akatoa heshima kama alivyo zoea ufanya kwa watu kama hao ambao ni wacha Mungu, ila pia ni watu hatari sana kwenye maswala ya kupigana. Akamuandalia Agnes chumba ambacho angeweza kujipumzisha kisha akarudi sehemu alipo waacha yeye na Monk.


“Tayari Monk”

“Je ameiona sura yako?”

“Hapana”

“Unaweza kumuonyesha”

Msichana huyo, taratibu akaivua kitambaa kilicho funika kichwa chake pamoja na sura yake, Agnes akabaki akiwa amemtumbulia mimacho kwani ni binti mwenye asili ya kiafrika, isitoshe ana kifahamu kiswahili vilivyo.

“Naitwa JACKLINE”

Binti huyo alijitambulisha mbele ya Agnes huku akimpa mkono wa salama, Agnes taratibu naye akaopokea mkono huo na kusalimiana naye.

“Mimi ni mtazania kama ilivyo kuwa wewe, ila ninakufahamu ndio mana nikaamua kukuleta sehemu kama hii”

Jackline alizungumza maneno yaliyo muacha Agnes mdomo wazi kwani hakujua ni jinsi gani Jackline aliweza kumfahamu yeye pamoja na mipano yake yote aliyo kuwa akiifanya.


***

Giza kila lilivyo zidi kwenda ndivyo jinsi Fetty na wezake walivyo zidi kuendelea kutafuta sehemu alipo Agnes, kila mmoja alijitahidi kuchunguza kwa umakini katika eneo la mto huo wenye maje mengi yaendayo kwa kasi.


Wakiwa katika msako, kwa mbali wakasikia milio ya mbwa wanaokuja katika eneo walipo.

“Kuweni makini”

Wote kwa pamoja wakaingia msituni na kujibanza kwenye miti kutazama ni kina nani wana kuja katika enoo hilo. Mianga ya tochi nyingi ikaanza kuonekana kwa mbali, ikitokea usawa wa mto huo.

“Ni wanajeshi”

Anna alizungumza huku bunduki yake akiwa ameishika vizuri na kuielekezea sehemu ambapo wanatokea wanajeshi hao, wanao endelea kuwatafuta wasichana wawili kwa udi na uvumba. Msako huo uliundwa na majeshi ya Marekana pamoja na majeshi ya Riussia. Kila watu walina maumivu kwa upande wao haswa Wamarekani.


Wakafanikiwa kufika kwenye sehemu walipo fika Agnes na Jackline. Wakasimama katika eneo hilo huku wakiendelea kuchunguza eneo hilo kwa umakini wa hali ya juu.

“Hapa ndipo walipo kuwa, inaoenekana wapo ndani ya huu msitu”

Mtaalamu mmoja wa kuchunguza mambo ya kitaalamu alizunungumza huku akishika udongo wa eneo walipo kuwa Jackline pamoja na Agnes.

“Wapo kumi na tano”

Fetty alizungumza kila mmoja akiwa na kifaa chake cha mawasiliano masikioni mwake, aliweza kuisiskia sauti hiyo iliyo kuwa ikizungumzwa na kiongozi wao wa msafara.

“Tuwafanyaje mkuu?”

Jamaa mmoja aliuliza, huku bunduki yake ikiwa wameielekeza walipo wanajeshi hao

“Ngojeni kwanza, musifanye chocho”

“Ila sister, inaoenekana wameingia kwenye mission moja na sisi”


“Sawa, tuwaache ache kwanza, tunaweza kuwaona wapo wachachche kumbe kuna wengine”

“Ila Fetty siku hizi umekuwa mzito sana, tazama jisni wanavyo tizama tizama huku, wasije kutuona”

“Cheki wanavaa miwani za usiku tutakwisha”

Jamaa mmoja alizungumza, bila hata kusubiri amri ya Fetty, akaanza kufyatua risasi, zilizo anza kuwapeleka baadhi ya wanajeshi chini. Kitendo hicho kikawafanya baadhi ya wanajeshi kutawanyika na kujificha kwenye majabali, makubwa na kuanza kujibu mashambulizi hayo. Kazi ikawa ni moja tu, kuhakikisha wanawazidi wanajeshi hao, walio jipendekeza katika kazi yao.

“Tunahitaji msaada, narudia tena tunahitaji msaada”

Mwanajeshi mmoja alipiga simu makao makuu, kuomba msaada wa wanajeshi wengine kwani tayari wanajeshi wao kama saba wamesha iaga dunia.


“Tumekupata”

Alipokea jibu mmoja kutoka, makao makuu. Wakaendelea kujibu mashambulizi ya watu hao ambao wamewavamia na hawakujua niwatu wangapi. Hali katika eneo la mto ikazidi kuwa mbaya zaidi milio ya bunduki, ilizidi kurindima kila kona.

“Helcoptar…..!!!”

Anna alishangaa baada ya kuona helcoptar zipatazo sita za jeshi la marekani zikifika katika eneo hilo, huku wajeshi wengi wakishuka kwenye helcoptar hizo zilizopo hewani, kwa kutumia kamba ndefu hadi chini.

‘Tunakufa leo’

Halima alijisemea kimoyo moyo huku akiendelea kuftyatua risasi nyingi kuelekea walipo wanajeshi hao.


==> ITAENDELEA



ILIPOISHIA

“Tumekupata”

Alipokea jibu mmoja kutoka, makao makuu. Wakaendelea kujibu mashambulizi ya watu hao ambao wamewavamia na hawakujua niwatu wangapi. Hali katika eneo la mto ikazidi kuwa mbaya zaidi milio ya bunduki, ilizidi kurindima kila kona.

“Helcoptar…..!!!”

Anna alishangaa baada ya kuona helcoptar zipatazo sita za jeshi la marekani zikifika katika eneo hilo, huku wajeshi wengi wakishuka kwenye helcoptar hizo zilizopo hewani, kwa kutumia kamba ndefu hadi chini.

‘Tunakufa leo’

Halima alijisemea kimoyo moyo huku akiendelea kuftyatua risasi nyingi kuelekea walipo wanajeshi hao.



ENDELEA

“Sister nguvu yetu imesha anza kuwa ndogo tunafanyaje”

Jamaa mmoja alizungumza huku akibadili magazine ya mwisho katika bunduki yake na endapo risasi zitakwisha kwenye magazine hiyo, basi hatokuwa na msaada wowote.

“Endelea kupambana hatuwezi kurudi nyuma”


Fetty alizungumza huku akizendelea kufyatua risasi kuelekea walipo wanajeshi hao

“Fetty eheee omba msaada kwa mkuu, lasivyo tutakufa humu”

Halima alilalamika kama kawaida yake, Fetty kutazama idadi ya wanajeshi wanao shuka kwenye helecoptar hizo kubwa za kijeshi, ikambidi awasilianen na bwana Rusev.

“Muheshimiwa wanajeshi wa Marekani wametuvamia”

“Endeleni kupambana”

“Sawa muheshimiwa ila tunahitaji msaada wa vijana wengine”


“Msaada….. Masaada wa nini pambaneni”

Majibu ya bwana Rusev, yakamtia hasira Fetty aliye jibanza kwenye mti huku akisikilizia jinsi risasi hizo zinavyo zidi kupigwa kwenye sehemu walipo.

“Muheshimiwa nakuheshimu, ila narudia tena nahitaji msaada wako”

“Kama hamjampata Agnes basi, hakuna cha msaada wowote kutoka kwangu”

Mawasiliano yakakatwa, Fetry akabaki aking’ata meno yake kwa hasira. Kumbukumbu ya tukio hili likamrudisha miaka ya nyuma, jinsi siku wanajeshi wa Tanzania walivyo vamia kwenye kambi yao, na kuwashambulia sana kisha wakaingia mikononi mwao wanajeshi hao, hapo ndipo ulipo kuwa mwisho wa maisha yao ya furaha na amani na wakajikuta wakiwa wanaishi kama wakimbizi na kukubali kufanya kazi na watu ambao ni magaidi wa kidunia, ili mradi waweze kuendelea kuishi kwenye maisha haya.


Fetty akiwa katika mawazo hayo, akamshuhudia kijana mmoja wa bwana Rusev akianguka chini, baada ya kupigwa risasi ya kichwa, akiwa anashangaa tukio hilo, kijana mwengine akajitokea kwa hasira kwenye mti alio kuwa amejificha huku akiwa na bastola mbili mkononi mwake, akifyatua risasi zisizo na idadi, ila alicho weza kukutana nacho, ni mvua ya risasi zizizo toka kwenye jeshi lilio wazidi nguvu.

“Fetty amesemaje”

Halima alizungumza huku machozi yakimlenga lenga.

“Mmmmmm…….”

“Amesemaje mkuuuuuu…..”

“Hana msaada na sisi, tupambane kama kufa tufe ila si kukamatwa”


“Mungu weeeee, nini sasa hichi”

Halima alizungumza huku machozi yakimwagika, akachomo magazine kwenye bunduki yake na kukuta ikiwa na risasi chache, akajipapasa hana tena magazine. Akageuza kichwa sehemu alipo Anna, akamkuta akiendelea kufyatua risasi pasipo kuangalia wezake wapo katika hali gani. Vijana wawili wa bwana Rusev walio bakia, wanazidi kuyapigania maisha yao kwani ni heri kufa kuliko kukamatwa na jeshi hilo.

“Nakupenda Anna, Fetty”

Halima alizungumza kwa sauti ya unyonge, akairudishia Magazine yake kwenye bunduki, akapiga goti mmoja chini, akawatazama jinsi wanajeshi wa wanavyo zivurumisha risasi katika eneo walipo.

“One one one bullet”(Mtu mmoja, risasi moja)

Halima alizungumza huku akiendelea kufyatatua risasi kwa kila aliye weza kumuona kwa wakati huo. Ila zilipo fika risasi kumi na mbili, bunduki yake ikagoma kutoa risasi, ikiashiria kwamba hakuna risasi nyingine ndani ya bunduki hiyo aina ya AK47, zinazo tumika sana nchini Russia.

***

Asubuhi na mapema, raisi Praygod akakurupuka kitandani, akaka kitako huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana. Rahabu taratibu akajinyanyua na kumtazama jinsi anavyo tokwa na jasho jingi mwilini.

“Una tatizo gani mume wangu?”

“Naota mandoto mabaya mabaya tu”

“Ohoo pole mume wangu”


Rahab alizungumza huku akimkumbatia raisi Praygod, taratibu akaanza kumpapasa kifuani mwake, hisia za mapenzi zikaanza kuusisimua mwili wa raisi Praygod, taratibu akajikuta akianza kumnyonya mke wake mdomo, baada ya muda wakajikuta wakizama kwenye dimbwi zito la kupena haki ya wanandoa.

Baada ya kumaliza wakaingia bafuni kuoga, Rahab akamuandalia mume wake nguo za kuvaa kwenye kikao anacho kwenda kukifanya na wakuu wote wa kitengo cha usalama wa taifa.

“Leo nitapendeza sana mke wangu”

“Kwa nini?”

“Umenichagulia nguo wewe”

“Ahaaa si kawaida”

“Sawa ila utapendeza sana, siku zote nimezoea kujichagulia nguo mwenyewe”


“Ila si una wafanyakazi wenye jukumu hili?”

“Ndio ila mke wangu upo kwa nini nichaguliwe na mfanyakazi”

“Hapa utakuwa poa sana”

Rahab alizungumza baada ya kumfunga tai raisi Praygod, akampiga busu la mdomoni

“Twende tukapate kifungua kinywa pamoja”

Wakatoka na kwenda kwenye sebla yao, ambapo wakakuta chakula tayari kimesha andaliwa na kukaguliwa na daktari maalumu anaye weza kukagua chakula cha raisi kabla hajakila. Wakapata chakula baada ya kumaliza akaomba kuweza kuitiwa wafanyakazi wote wa ikulu, ikawa kama alivyo agiza.

“Nimewaita hapa kutokana nahitaji kuwatambulisha mama yenu, so mukimuona huko nje misije mukamdharau.”

“Muheshimuni kama munavyo niheshimu mimi, mpendeni kama munavyo nipenda mimi. Nisinge penda mtu yoyote kuweza kuona mtu ana….ana anaa mkosea adabu”

“Mumenielewa”


Ndio muheshimiwa”

Baada ya utambulisho huo, raisi Praygod akawaamuru wafanyakazi wake kuweza kuondoka, akabaki na mke wake. Akamtuma mmoja wa walinzi wake kwenda kumuita Samson kwenye chumba chake. Samson akafika katika sehemu walipo.

“Umeamkaje muheshimiwa”

Samson alisalimia kwa heshima

“Salama tu kaa”

“Madam Rahab je wewe umeakaje?”

“Nipo salama”

Kwa nguvu aliyo weza kumuwekea Samson. Rahab anamamlaka makubwa ya kuweza kumuamrisha Samson, akafanya kile alicho weza kumuambia.

“Jiandaeni kwani nitawahitaji kwenye kikao baada ya muda fulani hivi”

“Baby kwa nini sisi?”

“Nahitaji tusaidiane katika kuirudisha heshima ya nchi, pia kesho tutakwenda kwenye misiba ya wanajeshi wali fariki walipo kuwa wakimsafirisha makamu wa raisi”

“Kwani hawakuzikwa?”


“Ndio, hawajazikwa, nimeagiza kwamba iwe siku ya maombolezi kwani pia wale wananchi walio poteza maisha uwanja wataifa inabdidi kuzikwa kesho”

“Sawa”

Raisi Praygod akawaaga, akaongozana na walinzi wake wawili hadi chumba cha mkutano.

“Hivi umempataje pataje raisi?”

Samson alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake

“Ni story ndefu sana, tangu tuachane pale kwenye ndege basi ikawa ndio siku ya mimi kuweza kuonana na raisi Pray”

“Ahaaa maisha haya bwana, adui yako amekuwa mume wako”

“Usiongee kwa sauti kubwa, tusije kuhisiwa vibaya. Ila kusema kweli ninampenda mume wangu”

Samson hakuwa na chakuzungumza zaidi ya kuanza kupata kifungua kinywa, Rahab akaondoka na kuelekea chumbani kwao kujiandaa na kikao ambacho mume wake alimuhitaji kuweza kufika.

***

“Kila mmoja ninaamini ameyaona yaliyo jitokeza.”

“Nchi imepata fedheha mbele ya wageni, walio huzuria msiba ulio kuwa wangu pamoja na wahanga wengine. Kiongozi mkubwa wa nchi kuweza kufanya mambo ambayo yangefanywa na wagaidi ameweza kuyafanya yeye.”

“Inaonekana ni jinsi gani, kitengo chenu, kilivyo jisahau kwa asiliimia nyingi tuu kwani hadi inafikia hatua ya matukio ya ajabu kama kushambuliwa kwa wanajeshi na makamu wa raisi kutoroshwa, yote ni uzembe na inavyo onekana anamiliki kundi kubwa la vijana anao weza kuwatumia katika kuleta machafuko kwenye nchi hii.”


Raisi Praygod alizungumza kwa saut iliyo jaa msisitizo mkubwa huku akiwatazama viongozi hao wapatao kumi na mbili walio izunguka meza kubwa katika eneo hilo.

“Yote yaliyo weza kujitokeza, hayaweze kubadilika, ila tunaweza kuyafanya wananchi wakaweza kutuamini na kuishi kwa amani. Kwani inavyo onekana hali ya amni imekuwa tata kwa wananchi.”

“Hivyo basi, nitahakikisha kwamba tunafanya kazi, iliyo wafanya kila mmoja wenu kuwa katika kitengo alicho kuwepo. Hata mimi mwenyewe nitahakikisha kwamba ninafanya kazi zote zakijeshi kama ni kuua basi tuue yule anaye stahili kuuliwa.”

“Sinto kuwa na msamaha kwa mtu ambaye ukimpa nafasi moja, anakuua wewe. Kuanzia sasa nahitaji kusikia ni wapi alipo makamu wa raisi wangu, yeye na kundi lake tuweze kuwatia nguvuni kwa pamoja. Nakaribisha maoni”


Raisi Praygod akazima maiki yake aliyo kuwa akitumia kuzungumzia. Kiongozi mmoja akanyoosha kidole na raisi Praygod akampa nafasi ya kuzungumza

“Muheshimiwa, kwanza tuombe radhi ya yale yaliyo jitokeza. Pili tumeweza kupata sehemu ambayo makamu wako amejificha na kundi lake”

“Ni hapa ndani ya nchi?”

Raisi Praygod alizungumza huku akimtumbulia macho kiongozi huyo.

“Hapana si ndani ya nchi hii, ila yupo nchini Kenya, na taarifa hizi tulizipata kwa wana usalama wa nchi ya Kenya”

“Eheee mu..mu muu mumejipangaje?”

“Tulimesha andaa taskforce kuweza kuvamia katika sehemu hiyo, huku tukishirikiana na interpol”

“Fanyeni mawasiliano na raisi wa Kenya sasa hivi nizungumze naye”

***

“Kwa nini memenisaidia?”

Agnes aliuliza swali baada ya kumaliza kupata kifungua kinywa akiwa na Jackline pamoja na Monk

“Kwani inatubidi kurudi nchini kwetu kuimarisha ulinzi na si kuendelea kutumika katika vikosi vya ajabu”

“Umejuaje kama ni vikosi vya ajabu na umenifamu fahamu vipi mimi?”

Agnes aliendelea kumuuliza maswali Jackline ili kuweza kumfahamu vizuri

“Kipindi nyinyi munakuja kwenye ngome ya bwana Rusev, mimi nilikuwa ni miongoni mwa walinzi wake wakaribu. Wiki moja baada ya nyinyi kufika pale mimi nilipewa kazi ya kwenda kumuangamiza raisi wa Korea kaskazini.”


“Ilikuwa ni kazi ngumu sana kwangu, hii ni kutokana na umahiri wa ulinzi wa kiongozi huyo. Ila nilijaribu kufanya ninacho weza, nikiwa katika sura ya bandia, iliyo nifanya nionekane kama mjapan.”

“Nilizidiwa kwa mashambulizi ya walinzi wa kiongozi huyo. Nilipo jaribu kuomba msaada kwa kiongozi bwana Rusev aliniambia………”

Jackline akashusha pumzi kubwa kisha akaendelea kuzungumza

“Akaniambia niendelee kupambana tu kwani ni kazi ninayo takiwa kuikamilisha mimi mwenyewe.”

“Niijitahidi sana, nikafanikiwa kuwakimbia pasipo kuweza kunikamata, ila niliweza kupata majeraha kadhaa ya risasi mgongoni mwangu”


“Nilikwenda kwenye temple moja ambapo ndipo nilipo kutana na Monk”

“Temple ni nini?”

“Ni nyumba ya ibada, ni sawa na kama kanisa au msikiti”

“Mzee huyu aliweza kunileta huku, aliweza kunitunza kama mwanae, ila aliweza kunitafutia waalimu walio weza kunifundishi ujuzi mkubwa wa kupambana, kuanzia kung fu, kareti, judo, krobariotik, ninja”

“Kwahiyo nimefuzu katika hayo yote, lengo langu kubwa ni kuweza kwenda kuhakikisha siku ninamuondoa dunia bwana Rusev yeye na kundi lake kwani hana msaada wowote kwa sisi waafrika, anawajali sana wa russia wezake”

Hapo kidogo Agnes akaanza kufunguka akili yake, swali alilo anza kujiuliza ni kwa nini alitumwa yeye, na kwa nini alipaswa kwenda kuua viongozi wakubwa kama hao. Swali kama hilo halikuwa na jibu kichwani mwa Agnes.


“Ila hili ni ombi, sinto hitaji kukulazimisha. Kama unahitaji kuwa nawi unaweza kuungana nami na tukarudi Tanzania na ukafanya yaliyo mema kujisafisha jina lako. Ila kama hauto hitaji basi unaweza kurudi kwa Russev na kuendelea kuishi chini ya bahari pasipo kuelelewa dunia inakwendaje”

Jackline alizungumza na kutuka nje ya nyumba hiyo. Agnes akabaki akitazamana na Monk huyo ambaye muda wote yupo kimya. Agnes akanyanyuka na kutoka nje.

“Nahitaji mafunzo”

Agnes alizungumza akimtaza Jacklin usoni mwake

“Je utakuwa tayari kurudi Tanzania?”

“Nipo tayari kurudi Tanzania”

“Basi mazoezi tunaanza sasa”

Jackline alizungumza, akamtisha Agnes kama anarusha ngumi, Agnes akakwepa, kidogo ila akastukia akipigwa teke la kifua lililo muangusha chini.

“Umakini ni muhimu sana”

Jackline alizungumza huku akimpa mkono Agnes na kumnyanyua kutoka chini alipo angukia

***

Hadi kuna pambazuka hapakuwa na msaada wowote kutoka kwa bwana Rusev. Fetty na wezake wakajikuta hali ya mashambulizi ya wanajeshi yakiwazidi na kujikuta wakikata tamaa kabisa. Kijana mmoja wa bwaa Rusev baada ya kuona hali imekuwa ngumu kwa upande wao. Akajichoma kisu cha tumbo na kujiua, jambo lililo zidi kuwachanganya Fetty na wezake.


Wa pili baada ya kuona mwenzake amekufa, akachomoa risasi moja aliyo ihifadhi mfukoni, akaiweka kwenye magazine ya bastola yek iliyo isha risasi, akairudisha magazine kwenye bastola yake, kisha akajipiga risasi ya kichwa na kufa hapo hapo.

Wakabaki Fetty, Anna na Halima wakishangaa tukio hilo, hawakuwa na risasi kwenye bunduki zao, na kila walivyo chungulia wakawaona askari wakizidi kusogea katika eneo walipo



SHE IS MY WIFE(50)


Hapakuwa na aliye weza kumsemesha mwenzake, kwani hali ya hatari tayari kila mmoaja aliweza kuiona. Wingi wa wanajeshi uliwafanya ujasiri wa kuweza kutoroka katika eneo hilo upotee.

“Haya ndio malipo yetu”

Halima alizungumza huku akimwagikwa na machozi mengi, kwani hakuamini kama leo hii anaweza kukamatwa tena, kwenye nchi ya ugenini. Fetty akawatazama wezake, jinsi walivyo wanyonge, taratibu akasimama kisha taratibu akajitokeza kwenye mti alio kuwa amejificha, bunduki za wanajeshi baadhi zikaelekea kwake, akiashiria kwamba yupo tayari kwa kufa

***

Mawasiliano ya kitelejensia yakaweza kufanyika kati ya majasusi wa Kitanzania na Kenya. Vikosi vikaandaliwa kwa ushirikiano mkubwa kwenda kufanya uvamizi kwenye hotel ya makamu wa raisi aliye kuwa msaliti kwenye nchi yake. Kwa usiri wa hali ya juu vikosi hivyo vikaweza kujongea kwenye hotel hiyo, ila chakushangaza ukimya mwingi wa hotel hiyo uliwafanya hata majasusi hao kuweza kushangaa kwani hawakujua ni kwanini eneo hilo lipo kimya kiasi kwamba wasiwasi uliweza kuwaingia.


Wakiwa katika eneo hili, wakaanza kustukia kuona baadhi ya majengo yakianza kulipuka kwa mabomo yaliyo tengwa ndani. Ikawabidi wote kutawanyika ili kuyaokoa maisha yao. Hoteli nzima iliweza kuporommoka kwa mabomu, na kubaki vipande vipande vya kuta ndogo ndogo na chakavu, jambo lililo zidi kuwachanganya majasusi hao

Taarifa za kulipuka kwa hoteli hiyo, zikawafikia maraisi wote wawili wa Tanzania pamoja na Kenye. Raisi Praygod akabaki akiwa amechanganyikiwa asipate kujua ni nini anaweza kuzungumza kwani adui yake hadi sasa hivi hajulikani ni wapi alipo na nilini anaweza kufanya shambulizi litakalo itingisha nchi.


“Hajulikani alipo!!?”

Rahab aliuliza kwa msahangao mkubwa baada ya kupewa taarifa hiyo

“Ndio na hoteli nzima imelipuka”

“Kuna mtu kati ya watu nahisi anaweza kumwaga siri za mipango yenu ambayo munaweza kuipanga”

“Sasa atakuwa ni nani?”

“Kati ya viongozi hao hao wa usalama wa Taifa, ulio panga nao huo mkakati”

Raisi Praygod akajitupa kitandani akionekana kujichokea kisawa sawa, kila alilo lifikiria akaona halina jibu halisi.

“Naomba hiyo kazi uniachie mimi mume wangu”

“Kazi gani?”

“Yakumtafuta adui yako nina imani nitampata nikishirikiana na Samsoan”


“Ila kumbuka wewe ni MKE WANGU, mke wa raisi, sasa utaifanya vipi hiyo kazi”

“Nakuomba unipatie nina imani nitaweza kuifanikisha na wewe utafurahi”

“Ila utaingia matatizoni tena mke wangu, unadhani nitakuwa katika hali gani?”

“Usijali mke wako, tambua mimi ndio nilikulinda kwa uwezo wangu wote hadi leo umefikia hapa”

Raisi Praygod akamtazama mke wake kisha akampa mkono na kumvutia kitandani, akamlaza vizuri kifuani kwake

“Rahab kumbuka ninakupenda sana, tena sana. Sinto hitaji kukupoteza nina imani unalitambua hilo”

Raisi Praygod alizungumza kwa sauti ya unyonge, iliyo jaaa uchungu ndani yake.

“Ndio baby ila amini kwamba ninaweza kuifanya kazi hiyo”

“Sawa”


“Nitakupa vijna wa kukusaidia?”

“Hapana nahitaji kuifanya nikiwa na Samson, ila vijana wawe tayari sisi tukiimaliza kazi hiyo”

Raisi Praygod akashusha pumzi, kisha akamtazama Rahab usoni, taratibu akaendelea kuutadhimini uzuri wa Rahab. Kwa mbali machozi yakanza kumlenga lenga.

“Mbona hivyo baby?”

“Niahidi utaishi mke wangu na huto kufa?”

“Nakuahidi nitarudi, na nitaendelea kuilinda heshima yako pamoja na nchi yangu”


Raisi Praygod akamkumbatia mke wake kwa nguvu, taratibu Rahab akaanzisha uchokozi wa kuupeleka mkono wake katika maficho ya tango la raisi, taratibu Raisi Praygod akanza kutoa miguno ya kimahaba, iliyo zidi kumsisimua Rahab na kumfanya aongeze kasi kubwa katika kulichua tango hilo. Rahab akahakikisha anampa memewe penzi ambalo hakuwahi kulipata tangu wakutane, raisi Praygod, alijikuta akitukana kila aina aina ya tusi kwa jinsi alivyo zidi kuupata utamu wa mke wake kipenzi Rahab.

Baada ya mtanange mkubwa, taratibu Rahab akajilaza kifuani mwa raisi huku akihema taratibu, pumzi nzito iliyo pitapita kifuani mwa raisi Praygod.

“Nakupenda sana mke wangu”

“Nakupenda pia baby”

***

Agnes akazidi kufanya mazoezi kwa juhudi zake zote, huku kila mara akilini mwake akiwakumbuka marafiki zake alio waacha kwenye ngome ya bwana Rusev.

‘Fetty, Anna, Halima ninawapenda sana’

Agnes alizungumza huku akiendelea akupokea mafunzo makali kutoka kwa Jaquline, aliye amua kumfundisha vilivyo Agnes.

“Mbona roho ina niuma hivi?”

Agnes alimuuliza Jaquline, baada ya kumaliza kufanya mazoezi hayo, kwa siku ya kwanza

“Kuna tatizo baya limetokea”

“Tatizo…..!! Tatizo gani?”

“Hata mimi siwezi kufahamu ila ni tatizo ambalo litakuwa ni pigo kubwa sana kwako”

“Mmmmmm…..!!”


“Yaaa huwa ndivyo tunavyo weza kuamini. Na ukipitia katika mafunzo ya unija utaweza kukutana na hisia hizo.”

“Siku zote huwa hisia katika maisha ya binadamu ndio kitu kikubwa sana, kwani zinaweza kukufanya wewe kuepuka kwa jambo baya au kuingia katika jambo baya”

“Sasa nitawezaje kujua mafunzo hayo”

“Juhudu zako katika mazoezi ndizo zitakazo kufanya wewe kuweza kukutana na mafunzo mengine mapya”

“Yatachukua muda gani?”

“Sio muda gani, ila juhudu zako ndizo zitakuwezesha kuwahi au kuchelewa kufanya mazoezi”

Jaquline akaondoka na kumuacha Agnes akiwa anatafakari ni kitu gani ambacho anaweza kukifanya ili kujihimarisha katika mazoezi hayo. Akaitazama njia waliyo pita jana usiku kuingilia kijijini hapo, ambapo kuna nyumba nyingi zilizo tengenezwa kwa miti na kuezekwa kwa nyasi.

“Mungu ibariki Tanzania”

Agnes alijikuta akiyatamka maneno hayo pasipo kudhamiria, taratibu akaingia ndani ya nyumba hiyo.

***

Baada ya siri kuweza kuvuja ya kuweza kuvamiwa katika hoteli yake. Makamu wa raisi, pamoja na vijana wake wapatao kumi na mbili, wakatega mabumu kwenye hoteli nzima. Pasipo kujali ni hasara gani anayo weza kuipata kwenye hoteli hiyo, anayo ishi peke yake na vijana wake tu. Walipo maliza zoezi hilo, wakashuka chini ya ardhi kwenye njia zinazo weza kuwapeleka moja kwa moja hadi nchi ya Somalia, ambapo wanaweza kupotelea katika nchi za uarabuni pasipo kuweza kukamatwa na kuweza kuhukumiwa kifo.


“Wataisoma namba”

Makamu wa raisi alizungumza huku akicheka kwa dharau. Wakaendelea kutembea kwenye njia hizo zilizopo ardhini huku vijana wake wakiendelea kuimarisha ulinzi mkali kila wanapo pita. Matochi makubwa waliyo yabeba yaliweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kuendelea na safari yao hiyo, waliyo weza kukusanya vinywaji na vyakula vya kutusho.

“Yale mabumu uliyatega kwa muda gani?”

Alimuuliza kijana wake mmoja mtaalamu wa maswala ya kutega mabomu na kutegua.

“Niliyatega kwa dakika arobaini na tano”

“Ahaaa safi, kwa umbali huu tulio kwenda hata yakilipuka si hayata weza kutudhuru?”

“Ndio muheshimiwa”

“Basi tutafute sehemu tupumzikeni kwa maana nimechoka sana”


“Ila muheshimiwa kwa usalama inabidi tusonge mbele kwani hatuta weza kujua mabomu hayo kwa pammoja yanaweza kutudhuru sisi, kumbuka tupo chini ya ardhi”

“Sawa”

Wakazidi kusonga mbele huku makamu wa raisi akionekana kuchoka sana, mwili mkubwa wenye kitambi kikubwa, ulizidi kumuelemea na kujikuta akihema kama bata mzinga

“Hembu fanyeni mpango muwasiliane na general Godwin”

Alitoa amri huku akiendelea kuhema na kutembea mwendo wa kivivu vivu, gafla tetemeko la ardhi likaanza kutikisa sehemu walipo, makamu wa raisi akajikuta akistuka sana na kuhofia usalama wake.


“Nini hicho?”

“Mabomu ndio yanaiporomosha hoteli”

“Ohaaa”

Baada ya dakika moja tetemeko hilo kilatulia. Hapo makamu wa raisi hakuwa na hata muda wa kupoteza zaidi ya kuwaamrisha vijana wake waweze kusonga mbele.

“Mzee simu ipo hewani”

Kijana wake akampatia simu, akaichukua na kuiweka sikioni mwake

“Ndio ndugu yangu Godwin”

“Mipango naona imefeli?”

“Ndio kaka, yaani hapa nahitaji vijana wako wanisaidie bwana”

“Usijali mutapokelewa na madam”

“Madam, madam gani tena huyo?”


“Utamuona tu mukikutana mimi nipo mbali na Somalia”

“Sawa muheshimiwa”

Makamu wa raisi akakata simu na kuendelea kutembea, huku akiwa na mawazo mengi ni kwanini jaribio la kuchukua madaraka limeweza kushindwa

‘Nitajipanga tena, lazima niichukue Tanzania’

Alijisemea kimoyo moyo. Akawaamrisha vijana wake waweze kupumzika, ili wajipatie chakula na hata kama kuna uwezekano waweze kulala, kwani kwa jinsi saa yake ya mkononi inavyo muonyesha, wametembea zaidi ya masaa kumi na tatu na muda huo ni wakati wa usiku, japo ndani ya njia hizo kuna giza lisilo weza kuonyesha kwamba muda huu ni mchana au usiku.

***

Rahab hakuwa na muda wakupoteza, akaingia bafuni akaoga kuondoa uchuvu. Kisha akamuomba muwe wake kuweza kumfungulia kwenye chumba ambacho kuna silahan na vitu mbalimbali vya raisi anavyo weza kuvitumia pale panapo jitokeza tatizo la uvamizi wa kivita.

Rahab akachukua mavazi meusi ambayo siku zote ananamini, kwa mavazi kama hayo basi kazi yake huwa ni nzuri, akachukua bastola sita pamoja na magazine zakutosha zilizo jaa risasi.

“Nipo tayari”

Alimuambia raisi Praygod Makuya, aliye baki akimtazama tu, mke wake jinsi alivyo weza kujiandaa


“Kuna kitu umesahau?”

“Nini hicho?”

“Saa ya mkononi”

Raisi Praygod akamkabidhi Rahab saa moja, nyeusi inayo onekana kutengenezwa kwa utaalamu wa hali ya juu

“Saa hiyo, imefungwa, mitambu maalumu kwa kupitia satelait tutaweza kukuona kila unapo kwenda”

“Sawa mume wangu”

Rahab akamkumbatia Raisi Praygod na kumbusu mdomoni. Wakatoka chumbani kwao na kwenda katika chumba, walipo wakuta vijana wawili wa raisi pamoja na Samson wakiwa tayari wamesha jiandaa kwa kazi ya kwenda kumtafuta makamu wa raisi na kuweza kumkamata.

“Ninaimani watanzania wanatamani kuweza kuisikia taarifa ya kukamatwa kwa msaliti wao. Ninawapa baraka zote katika kazi hii munayo kwenda kuifanya”

“Asante muheshimiwa”

Vijana hao waliweza kuzungumza na kumpa heshima raisi Praygod, aliye achia tabasamu pana kidogo akionekana kufurahishwa na vijana hao ambao wamejitolea maisha yao kuweza kulitete taifa lao.


“Si kila kitu kipo tayari?”

Rahab aliuliza, huku akimtazama mume wake machoni?”

“Ndio mutaondoka na helcoptar hadi Kenya, kwenye hoteli ilipo kuwa na mutapokelewa na makamanda nilio waagiza kuwapokea nao bado wapo kwenye oparesheni hiyo”

“Sawa”

Wakatoka hadi kwenye kiwanja kidogo cha helcoptar, wakaingia kwenye moja ya helcoptar inayo kwenda kwa kasi. Safari ikaanza huhu raisi pamoja na walinzi wengine wakiwapungia mkono vijana wao.

“Sasa hivi ni saa nane usiku, hadi saa moja asubuhi oparesheni iwe imekwisha”

“Sawa madam”

Kwa mwendo kasi wa helcoptar hiyo, wakafika Kenye majira ya saa tisa usiku, wakashushwa katika eneo la hoteli ambapo ulinzi wa majasusi wa nchi mbili kati ya Tanzania na Kenye bado unaendelea.

“Mimi ninaitwa kamanda Lawi Okoye”

Kamanda mmoja wa kike alijitambulisha baada ya kuwapokea kutoka katika helcoptar hiyo iliyo waleta

“Mimi ni Mrs President”

“Karibuni”


Samson akabaki akiwa anashangaa, kwani majengo yote ya sehemu hiyo yameanguka chini na nikuta baadhi zimesimama.

“Sasa hapa atakuwa amepona mtu kweli?”

Samson alimuuliza Rahab huku wakiendelea kutembea kuelekea kwenye moja ya kibanda alipo mkuu wa kikosi hicho.

“Ngoja utaona tu”

Tatatibu Rahab, akachuchumaa, mkono wake wa kulia akauweka chini na kugusa ardhi, kwa uwezo na nguvu ya hisia zake, aliweza kugundua kwamba maadui zao wamepita chini ya ardhi na kwamuda huo wapo mbali sana na hapo walipo.

“No tunapoteza muda”

Rahab alinyanyuka haraka, akaanza kukimbia kuelekea porini huku vijana wake wakiwa nyuma wakiwafwata, hadi kamanda Lawi Okoye aliweza kuunga msafara huo.


“Munakwenda wapi hamuja onana na mkuu?”

Kamanda Lawi Okoye aliuliza huku akikimbia

“Hei miss hii ni kazi isiyo kuhusu, ningekuomba uweze kurudi na kuendelea kuimarisha ulinzi katika lile eneo”

Rahab alizungumza huku akimtazama kamanda Lawi Okoye kwa macho makali sana hadi yeye mwenyewe, akamuelewa Rahab pasipo kuuliza swali jengine. Rahab na vijana wake watatu wakendelea kusonga mbele

“Huku”

Rahab alizidi kuwaongoza vijana wake, kwa kufwata usawa wa sehemu ambapo njia hizo zilizopo ardhini zinaweza kupita. Kasi ya Samson na Rahab, ikazidi kuwatesa vijana wa raisi Praygod wanao onekana kuchoka sana kwa kukimbia.

“Wamechoka wale?”

Samson alizungumza baada ya kugeuka nyuma na kukuta vijana hao wamewaacha mbali sana

“Twende mbele, achana nao”

Rahab akazidi kuongeza kasi zaidi hadi vijana hao wakapotezana nao. Wakafika kwenye moja yam lima Rahab akasimama huku akihema sana. Akaitazama saa yake ya mkononi inaonyesha ni saa kumi na moja kasoro alfajiri.

“Hawa washenzi watakuwa wamelekea wapi?”

“Kwa nini?”

“Nimepoteza hisia ya kujua ni wapi walipo kwenda”

“Sasa tutafanyaje?”

“Ngoja”

***

Anna na Halima, wakamshuhudia Fetty akinyoosha mikono yake juu, ikiashiria kwamba amejisalimisha mikononi mwa wanajeshi hao, walio kuwa wanapambana nao usiku kucha. Machozi mengi ya uchungu yakazidi kumwagika Halima. Kwani hakuwa tayari kufa, naye taratibu akajitokeza huku akiwa ameinyoosha mikono yake juu. Anna naye hakuwa na jinsi akafanya kama walivyo weza kufanya wezake.

Ikatolewa amri na mkuu wa vikosi hivyo mabinti hao waweze kukamatwa. Fetty na wezake hawakuwa na ujanja zaidi ya kupiga magoti chini, na kujisalimisha. Wanajeshi wakawazingiza, wakiwa na silaha zenye uwezo mkubwa. Kila mmoja akavishwa pingu imara mikononi na miguuni wakafungwa cheni ngumu sana.


“Kumbe ni wasichana, washenzi sana”

Asakri huyo aliuzungumza huku akimtazama Fetty usuni aliye weza kufumba macho yake akionyesha kububujikwa na machozi ndani kwa ndani. Wakaichunguza miili ya magaidi wengine, wakawakuta wakiwa tayari wamesha poteza maisha. Ulinzi mkali ukaimarishwa hadi helcoptar sita zilivyo weza kufika katika eneo hilo, huku hecoptar moja ikiwa imebeba waandhishi wa habari wa vituo vikubwa viwili vya habari duniani BBC na CNN.

Tukio la wasichana watatu magaidi kukamatwa, likatawala vyombo vingi vya habari duniani, kila wenye vituo vya tv, waliweza kujiunga moja kwa moja na vituo hivyo viwili na kuonyesha hali inavyo weza kundelea katika msitu huo.

Bwana Rusev na watu wake wakashuhudia jinsi Fetty na wezake jinsi wanavyo ingizwa kwenye helcoptar hizo za jeshi.

“Muheshimiwa sasa ni kwanini hukuhitaji tuwapatie msaad……………”

Kabla ya kijana huyo hajamaliza sentensi yake, akapigwa risasi mbili za kifua na bwana Rusev anaye onekana kushikwa na hasira kali sana


“Huo ndio msaada ulio wapatia”

Bwana Rusev alizungumza kwa hasira, hadi vijana wengine waliomo ndani ya chumba hicho ya mawasiliano wakakaa kimya

“Munashangaa nini? Endeleeni na kazi iliyo waweka hapa na toeni hii takataka ya huyu mshenzi mbele ya macho yangu”

Bwana Rusev aliendelea kufoka, vijana wake wanao muogopa kila mmoja akaendelea na kazi yake huku baadhi wakiutoa mwili wa kijana huyo.

Moja kwa moja Fetty na wezake wakapelekwa kwenye kambi ya jeshi ya Marekani iliyopo Russia kwa ajili ya mahojino maalumu.


Wakaingizwa kwenye moja ya chumba, ambacho kimejaa kila aina ya silaha za mateso, wakavuliwa nguo zote na kubaki kama walivyo zaliwa, huku kazi hiyo ikifanywa na majasusi wa kike wakirussia na marekani.

Wakafungwa miguu juu, vichwa chini. Wakamwagiwa mafuta yanayo teleza kwenye miili yao. Kisha majasisi hao watatu walio kabidhiwa kazi hiyo, kila mmoja akakamata fimbo aina ya mkia wa taa na kukaa tayari kwa kuanza kuwapa mateso Fetty na wezake ili waweze kuzungumza ni nani aliye watuma.


Fimbo hizo zenuye miba miba mikali, kila ilivyo tua kwenye miili yao, kila mmoja alikia kwa uwezo wake, fimbo hizo ziliweza kutoka na nyma kila walipo chapwa. Halima, alioenekana kulia kupita wezake wote, ila hakuwa yayari kuweza kuzungumza kitu cha ania yoyote. Mateso yakazidi kuongezwa, huku vyuma vya moto vikibandikwa mara kadhaa kwenye miili yao, kila walipo ulizwa swali na kuto kujibu, vilizidi kuwapa machungu. Fetty kwenye mawazo yake, mara kwa mara aliweza kumfikiria bwana Rusev, kimoyo moyo akajiapisha kumuua kingozi huyo aliye wageuka kwa mkono wake yeye mwenyewe.

Anna, alikaa kama bubu, machozi yakimtiririka, akiamini kukaa kimya kwake hakuto muingiza matatizoni.

‘Bora waniue kuliko kusema’

Alijisemea kimoyo huku akiyasikilizia maumivu ya pasi, ya moto iliyo bandikwa mgongoni mwake na kumfanya ayakaze meno yake.

***

Makamu wa raisi akaendelea kusonga mbele na watu wake, baada ya kujipumzisha kwa lisaa zima, kwa jinsi ramani waliyo nayo inavyo waonyesha, wakafika kwenye moja ya sehemu walipo kuta mgawanyiko wa njia nne.

“Hii inakwenda Somalia”

Msoma ramani aliweza kuwaonyesha ni wapi kwa kwenda nao bila kipingamizi waafwata. Saa ya makamu wa raisi inamuonyesha ni saa kumi na moja na robo, asubuhi, msoma ramani amewaahidi kama watatembea kwa mwendo huyo huo, hadi saa moja kamili asubuhi watatokea kwenye fukwe za bahari na hapo ndipo wataweza kukutana na mtu waliye ahidiwa kuwapokea.


Wakazidi kusonga mbele, jinsi masaa yalivyo zidi kwenda ndivyo kwa mbali walivyo weza kuuona mwanga ulio ingia kwenye nyia hizo.

“Pale ndipo kwakutokea?”

Makamu wa raisi aliuliza kwa furaha sana

“Ndio?”

“Twendeni twendeni”

Makamu wa raisi akazidi kuongeza mwendo hadi vijana wake wakafurahi, kwani anaoenekana kuwa na hamu kubwa sana ya kuweza kutoka kwenye sehemu hiyo.

“Yaani nawaambia siku nikija kuitia Tanzania mikononi mwangu, basi nyinyi nyote nitawapa vyeo vikubwa”

“Sawa mkuu”

“Ndio lazima nifanye hivyo”

Makamu wa raisi alizungumza huku akihema kama bata mzinga, aliye kimbia kwa umbali mrefu sana. Wakafika kwenye sehemu ya kutoke, wakakuta ngazi ndefu kwenda juu. Kijana mmoja akapanda hadi juu, akafungua mfuniko wa chuma uli funika katika eneo hilo, akachungulia nje, akakuta hakuna mtu katika eneo hilo ambalo kidogo lipo mlimani na bahari inaonekana kwa chini kidogo. Akatoka akiwa na bunduki yake, akawaamrisha wengine kuweza kutoka kwani eneo walilopo ni salama kabisa.

***

Rahab akasimama katika eneo hilo zaidi ya nusu saa, akijaribu kuvuta hisia ni wapi walipo watu wao wanao watafuta. Katika eno alipo simama Rahab kwa chini ndipo zilipo njia nne zilizo gawanyika. Akaweka tena mkono wake chini, alipo simama akatazama mbele na kuona mlima mmoja mrefu, wenye majabali makubwa ambao wanapaswa kuuweza kuupanda.

“Twende tukaupande mlima ule”

“Sawa madam”

Wakaendelea kukimbia hadi wakaufikia mlima, taratibu wakaanza kuupanda mlima huo ulio nyoka mithili ya namba moja. Haikuwa kazi rahisi kwao ila wakajikaza hivyo hivyo kuhakikisha kwamba wanapanda mlima huo kwa juhudi zao zote. Ili wagharimu zaidi ya lisaa na nusu kuweza kufika kileleni mwa mlima huo. Hapo ndio wakaweza kuiona bahari kwa chuni.

“Watakuwa maeneo haya”

Rahab alizungumza huku akiangaza angaza macho yake kila kona, kwa bahati nzuri kwa mbali kidogo anaona mtu akichomoza kichwa chake, kwa haraka wakajibanza kwenye moja ya jabali na kumtazama mtu huyo ni nini atakacho kifanya.


“Bingo”

Rahab alizungumza mara baada ya kumuona mtu huyo akioka huku akiwa na bunduki, wakaanza kutoka mmoja baada ya mwengine hadi wakafikia kumi, wa kumi na moja wakamuona makamu wa raisi waliye kuwa wakimtafuta, wakamshuhudia jinsi anavyo cheke cheka na kufurahia kuuona mwanga wa juu. Wakatoka vijana wengine wawili na kuifanya idadi yao kuwa kumi na mbili. Vijana hao wanaendelea kuimarisha ulizni katika eneo hilo huku wakionekana kama kuna kitu wanacho kisubiria.

“Wanafanyaje?”

Samson aliuliza

“Nahisi kuna kikundi kingine kina kuja kuwachukua si unaona zile boti mbili zinazo kuja kwa kasi katika eneo hili?”

“Si tuwavamie?”

“Ngoja tutazame, mchezo”

Boti mbili hizo za kisasa zilizo tokea kwenye moja ya meli kubwa ya kifahari, zikajongea hadi karibu na nchi kavu. Wakashuka vijana wengine nane, huku mmoja wao akiwa mwanamke aliye valia mavazi meusi pamoja na miwani. Makamu wa raisi akaanza kushuka taratibu na vijana wake, huku wakiendelea kuimarisha ulinzi katika eneo. Wakakutana kati kati na kiongozi ambaye aliweza kuagizwa na Mzee Godwin.

“Karibu sana muheshimiwa, jina langu ninaitwa Madam Merry”


“Ohoo asante sana binti”

Makamu wa raisi alizungumza kwa furaha kubwa, huku akimpa mkono Madam Merry. Kabla hata hawajazungumza chochote, vijana wa makamu wa raisi mmoja baada ya mwengine waakanza kuanguka chini huku wakilia kwa maumivu makali ya risasi zinazo waftwa kama mvua. Vijana wa Madam Merry walipo ona hali imebadilika gafla, wakamchukua kiongozi wao kwa haraka na kurudi naye kwenye boti zao, wakaondoka katika eneo hilo kwa kasi ya ajabu sana.

Makamu wa raisi akazidi kuchanganyikiwa kwani vijana wake walizidi kuteketea kwa risasi zinazo fyatuliwa na Samson pamoja na Rahab. Ambao wanazidi kuwafwata katika eneo walipo.


Ndani ya dakika mbili vijana wote kumi na mbili wa makamu wa raisi wamelala chini, akabaki makamu wa raisi peke yake huku akitetemeka mwili mzima, hadi haja ndogo ikaanza kumwagika.

“Samson mjomba wangu…….”

Makamu wa raisi alizunguza kwa kiwewe huku akimtazama Samson anaye mfwata taratibu sehemu alipo simama

“Aha….. aahaa Samson mjombaaa. Naa naaa naaa kuu kuuu kuaaa”

Makamu wa Raisi alizidi kutetemeka, ila Samson hakuweza kumuonyeshea sura ya furaha. Alicho kifanya Samson ni kumtandika teke moja ya miguu, lililo mrusha juu kiashi na kuanguka chini. Makamu wa raisi alishindwa kujizuida kumwaga machozi, hii ni baada ya kuulalia mkono wake wa kulia vibaya na kuuvunja.

“Usimuue”

Rahab alimzuia Samson asimuue makamu wa raisi, kwani sheria itafwata mkondo wake. Rahab akaiminya batani moja ya saa yake ya mkononi ambayo kwa iliweza kumuonyesha sura ya mume wake.


“Hei baby”

Rahab alizungumza kumstua mume wake anaye onekana kumtumbulia macho kama haamini

“Mke wangu”

“Nimefanikiwa mume wangu, muhalifu tupo naye hapa”

Rahab akaigeuza saa yake, na kuielekezea katika sehemu alipo lala makamu wa raisi, akiwa chini ya ulinzi mkali wa Samson. Watu wote waliopo ndani ya chumba cha mawasilino waliweza kushangilia kwa kazi aliyo ifanya mke wa raisi. Wakawasiliana na majasusi waliopo Kenye, haraka wakaomba ruhussa kuweza kuingia nchini Somalia kumchukua mfungwa wao. Serikali ya Somalia haikuwa na hiyana wakaziruhu helcoptar hizi kuweza kuingia nchini mwao.

Wakafika katika eneo walipo Rahab, wakawachukua wote watatu, huku miili ya marehemu ikibebwa na helcoptar nyingine ya jeshi.


Kukamatwa kwa makamu wa raisi vituo vya televishion, TBC, ITV, STAR TV, CHANEL TEN na kadhalika vikishirikiano na vituo vya redio, vikaonyesha jinsi makamu wa raisi akikabidhiwa na vijana wawili Samson na Rahab, kwa jeshi la polisi pamoja na jeshi la kujenga taifa. Kwa ajili ya kumpeleka katika ngazi za mbele za sheria.

Kwenye mitandao ya kijamii, facebook, twitter, whatsapp, immo, tovuti pamoja na blog za watu mbali mbali ikiwemo www.storizaeddy.blogspot.com ziliweza kuweka vipande vya video pamoja na picha zikimuonyesha makamu wa raisi akiwa mikononi mwa wanajeshi pamoja na askari. Heshima kwa vijana wawili Samson pamoja na mke wa Raisi Praygod, ziliendelea kutolewa na watu mbalimbali serikalini. Huku Rahab akionekana ni shujaa aliye weza kumkamata gaidi ambaye angeachiliwa angeweza kuleta madhara makubwa hapo baadaye.

Raisi Pragod akamtangaza Rahab rasmi kwenye vyombo vya habari kwamba ni mke wake halali, akaadisia historia fupi walipo kutana hadi wakaona. Kila mtanzania aliweza kufurahishwa na mahusiano hayo ambayo watu wengi waliyaita ni zali la mentali.

***

Mwaka mzima ukakatiza Fetty na wezake wakiendelea kusota kwenye gereza kubwa la Guantemana, gereza linalo sifika kukusanya idadi kubwa ya wahalifu walio weza kufanya matukio makubwa sana duniani. Hukumu ya wao kupelekwa Gwantemana kuhukumiwa kifongo cha maisha, nikutokana na wao kutoweza kuzungumza kitu cha aina yoyote kwa serikali ya Marekani.

“Hatuwezi kufia humu ni lazima tutoroke”

Fetty aliwaambia wezake, wakiwa katika meza ya kulia chakula

“Tutatorokaje?”

“Musijali ninayo mipango”

Fetty alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake na kuwafanya Anna na Halima kumkodolea macho

***

“Jack inabidi nirudi Tanzania na wezangu”

“Kina nani?”

“Fetty, Anna na Halima”

Agnes alizungumza mara baada ya kufuzu mafunzo ya uninja, na kukamilika na kuwa mpiganaji hatari sana

“Utawezaje kuwatoa Gwantemana”

“Usijali nina mpango madhubuti”

Agnes alizungumza huku akilichomoa panga lake mngoni na kulishika kikamilifu akiashiria amekamilia kwenda kuifanya kazi hiyo iliyo hatari kupindukia katika maisha yake.



MWISHO

 


0 comments:

Post a Comment

Blog