Search This Blog

Thursday 23 March 2023

HUBA LA MISS TANZANIA - 3

  

Simulizi : Huba La Miss Tanzania

Sehemu Ya : Tatu (3)




Nimeambiwa masurufu yangu ya safari yapo tayari! " ilikuwa ni kifungua mazungumzo cha Shebby baada ya kusalimiana na mhasibu mkuu wa kampuni. "Hewala! Upo sahihi, tia saini yako hapa, ni masurufu ya siku tano sawa na shilingi laki tano na milioni moja ya kujaza mafuta ya kwenda na kurudi na tahadhari kwa tatizo lolote litakalotokea huko" akielekeza mhasibu huku anampa kitabu cha kuweka saini ya kuchukua pesa hizo. Shebby akasaini kitabu hicho huku akiwa na furaha sheshe ya kusafiri kuelekea pori. "Unawapeleka warembo waliofanikiwa kuingia fainali za Miss Tanzania kwenye hifadhi ya wanyama ya Selous. Maelekezo yao ni kuwa uwafuate kesho kambini kwao Hyatt Regency, The Kilimanjaro hotel saa 12:00 asubuhi" alimfafanulia hizo pesa ni za shughuli gani. Shebby akawa ametega sikio ndi hataki apitwe na neno huku akiwa amenyamaza zii. "Ok..nimeelewa, kwa maana nikichomoka nao kesho Jumapili, Alhamisi usiku natakiwa niwarudishe jijini sio ndio Kiongozi? " aliuliza swali kutaka uhakika. "Ewaa! Ndio maana yake, maana watapumzika Ijumaa na Jumamosi, Jumapili ndio fainali yenyewe ya walimbwende, ngoma uwanjani! " alitilia tashididi maelekezo yake. Wakaelewana na kuagana. Siku ya siku ikafika msafara wa kuelekea Hifadhi ya Selous na walimbwende wa nchi nzima ukaanza. Msafara ulianzia kambini kwao niliwadamkia asubuhi na mapema, nikawa nawasaidia kuwaingizia mabegi yao kwenye gari. Mbwembwe zao za miondoko yao katika kutembea ilikuwa ni burudani tosha, wapo waliokuwa wanatembea kwa kutetemeka kama upanga uliotiwa tahabibu. Kwa kawaida safari ya mbugani huwa ni safari ndefu na yenye kuchosha lakini uwepo wa visura wale wacheshi na wachangamfu ambao wakikupa tabasamu hata kama ulikuwa na njaa tumbo unalihisi limejaa kwa shibe. Selous ni pori la akiba kubwa kuliko yote nchini Tanzania, pia ni ya pili kwa ukubwa duniani baada ya hifadhi ya Yellowstone iliyopo nchini Marekani. Hifadhi hii ipo katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma. Eneo hilo la hifadhi ni kubwa kwa makadiro kushinda nchi 70 duniani ikikadiriwa kuwa na eneo sawa na nchi ya Kostarika (Amerika ya Kati) na takribani mara mbili kuliko nchi ya Ubelgiji. Nikiwa fani yangu ni kama dereva na muongoza watalii (tour guide) na mpishi wangu nikiambatana na walimbwende kumi na Matroni wao wawili jumla tukiwa msafara wa watu kumi na nne nikaamua niwafikishe Selous kupitia barabara ya Kibiti-Lindi kwenye lango la Mtemere. Kulikuwa na njia ya mkato ya kupitia Kisarawe yenye umbali wa kama kilomita 150 lakini barabara ilikuwa ni mbovu na ulikuwa ni msimu wa masika, hivyo nikahofia hatari ya kunasa kwenye matope. Tulivyoanza safari walikuwa na mbwembwe na shamrashamra nyingi lakini safari ilivyokolea wengi wao walikuwa wamelala usingizi wa pono. Maajabu ni kuwa mrembo mmoja jina lake Zabibu muda mwingi alikuwa anajisomea kijitabu chake kidogo cha sifa za wanyama mwitu, kuonyesha yupo makini na ziara ile. "Sasa kaka Shebby naskia hifadhi hii inaitwa kiutani shamba la bibi kwanini mpaka imepewa jina hilo? " ilikuwa ni sauti nyororo ya kama ndege zuwaridi toka kwenye kinywa cha Zabibu ilipenya kwenye ngoma za masikio yangu akifanya udadisi. Sauti yake Zabibu na umbile lake vilikuwa vinashabihiana kwa uzuri. Uzuri wa Zabibu hausimuliki wala kuandikika kwenye vitabu ukaumaliza, tosheka tu kujua alikuwa na ngozi laini kama sufi, nyeupe kama mchanga wa peponi yenye kumeremeta hata akiwa kwenye giza totoro la usiku wa maneno, pua yake ya upanga na shingo yake ndefu kama twiga ilimfanya kila mwanaume rijali mwenye kumtupia jicho kwa mara ya kwanza atarudia tena na tena bila kuchoka kumtazama kama ilivyo chovya chovya inavyomaliza buyu la asali"Swali zuri, ni kweli hii hifadhi ya Wanyapori Selous ilijulikana kama shamba la Bibi enzi za wakoloni. Hii ni kutokana na mtawala wa Kijerumani aitwaye Kaiser Wilheim II ambaye alimzawadia mkewe hifadhi hii kama kumbukumbu yake ya kuzaliwa" alijibu Shebby kwa maelezo safi kama msahafu huku sasa wakiwa wameshatembea karibia masaa 6 barabarani umbali wa zaidi ya kilomita 250. "Daah...natamani niuone uzuri wa Selous mpaka wapendanao wanazawadiana, maana kaacha kumpa mbuga ya Serengeti, Manyara, Mikumi, Tarangire na nyinginezo kaamua kumpa Selous kwa vyovyote vile ina kitu Special" alijibu Zabibu, huku wakicheka kwa pamoja. "Lo lo lo! miaka yote kumbe ulikuwa hujui kama Selous ndio baba lao, ila tu bado haijatupiwa jicho la pekee" alikubaliana na mawazo ya Zabibu juu ya uzuri wa hifadhi hiyo. Wakawa ni mwendo wa stori mtindo mmoja kama vile wamejuana kitambo kirefu sana. Sasa warembo wale walianza kuchangamka baada ya kuuona mji wanakaribia kufika. Baada ya muda wa nusu saa tukawasili Behobeho /Cordura Camp ambapo hapo ndipo tulipanga tupate mlo wa mchana, na muda huo ulikuwa ni adhuhuri tayari. Hapo tulikuta wazungu wengi wameshaanza eneo hilo. "Muongozaji hapa pana kitu gani mbona watu wamejaa fori fori?" aliuliza mmoja wa matroni wa warembo wale. "Hapa ndio kuna kaburi la muasisi wa hii hifadhi. Jina limetokana na Mwingereza Frederick Selous aliyekuwa mwindaji wakati wa kuanzishwa kwa ukoloni katika Afrika ya Kusini na Mashariki na ambaye aliuawa katika Tanzania ya leo akiwa mwanajeshi wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia" nilimjibu yule matroni. Tukatelemka wote kasoro Zabibu peke yake alibakia ndani ya gari. "Zabibuu...mbona unatutenga hivyo hutaki kula pamoja na sisi eeh..." nilimtania huku nikimaanisha kweli ashuke tukale wote tayari alishanikamata mawazoni ndi ndi ndi, kila wakati namuwaza yeye na kujiona ni kiumbe mwenye bahati sana kuwahi kuwa karibu na Zabibu. Nikakumbuka methali kule shule ya msingi isemayo Bi Mariamu hana siri, wakimaanisha mapenzi ni kikohozi hayafichiki. "Aah...najisikia nimeshiba, ukila wewe Shebby ndio na mimi nimeshiba tayari" alizungumza kiutani huku akiachia tabasamu pana lililouacha mwanya wake katika meno yake mazuri ukioneka dhahiri shahiri. "Huyu binti ni mrembo wa Shani, akilikosa hilo taji la Miss Tanzania nitajua kweli uchawi upo! " niliwaza kichwani mwangu huku nikimtabiria ushindi mchana kweupe. Tukamuacha Zabibu tukaelekea hotelini kabla ya kuanza rasmi kuzunguka mbugani. Baada ya kumaliza mlo wangu, nikaamua kufungasha chips kavu na kuku wa kukaanga nikamletea Zabibu. "Pori ni pori dada yangu, nimekuletea hivyo ukitaka vitupe lakini nimetimiza wajibu wangu" nilisema kumuambia Zabibu wakati namrushia kifuko cha chakula pale kwenye siti yake alipokaa huku akabaki ananiachia tabasamu moja matata sana huku macho yake makubwa kayalegeza kama mwali amekula kungumanga anasubiria kutambulishwa kwa mchumba wake. Moyo wangu mapigo yake yakawa yanapiga duku duku kama saa mbovu, nguvu ya huba ikawa imeanza kupenya. Nikaanza kumlaani shetani kwa pepesi zake za tashwishi anazozivuvia kwenye moyo wangu. "Shebby unaota ndoto za alinacha mchana kweupe wa jua kali, huyo Zabibu hauna kufu nae, hadhi yake ni kama mwezi angani humfikanii kamwe, huyo atakuwa anamegwa penzi lake na kigogo mkubwa, musharafu katika jamii, achana nae" nilikuwa ninawaza, mawazo yaliyonisaidia kunirudisha kwenye hali yangu ya kawaida nikafutika futi moyoni mwangu tamaa yangu ya mwili kwake. "Ahsante kaka yangu Shebby kwa ukarimu wako ubarikiwe kwa kujali" alishukuru Zabibu kwa zawadi ile ya kipaseli cha kuku na chips kavu. "Usijali, take easy.." alijibu Shebby huku tayari akiwa analiondosha gari sasa wanaitafuta Matobwe umbali wa zaidi ya kilomita 86 mbele yao. Mpishi wangu mzee Shukuru akawa ametingwa na kukata mananasi kwa ajili ya kuwapa Mamiss wale washushie mlo wao kwa matunda. "Naomba ndugu muongoza watalii uwaelezee warembo wangu wanategemea kuona nini pindi wakiwa ndani ya hifadhi katika siku zote tutakazokaa humu ndani?" aliuliza mmoja wa matroni wao huku warembo wale wakiwa wamekaa mkao wa kuniazima masikio yao niwape shule. "Ahsante kwa swali, hifadhi hii ya Wanyamapori ya Selous inasifika kwa kuwa na Mandhari tulivu naya kuvutia (total wilderness). Uoto wa asili wenye mbuga za wazi na uwanda wa miombo umeenea karibu robo tatu ya hifadhi, ukiwa na miti aina ya mitunduru, mininga na milama. Magharibi mwa hifadhi hii kuna mbuga za nyasi pamoja na miti ya mitagalala.Aidha kuna mikoche ambayo inaweza kufikia urefu wa mita 25. Mikoche hiyo huonekana kwa wingi kando kando ya mto Rufiji. Selous ina idadi kubwa ya wanyamapori wa aina mbalimbali hususani, tembo, simba, chui, nyati, nyumbu, pundamilia, ngiri, twiga, fisi, kongoni, pofu, pongo, kuro utepe mweupe, tandala, ndege wa aina mbalimbali zaidi ya spishi zipatazo 450, nyoka wa aina mbalimbali ambao huonekana kwenye misitu na kwenye mito.Viboko na mamba huonekana kwa wingi wakivinjari ndani ya mto Rufiji na kwenye maziwa ndani ya hifadhi. Sifa hizo zimeifanya hifadhi hii tangu mwaka 1982 imeingizwa katika orodha ya UNESCO ya Urithi wa Dunia", nikawapa jibu maridhawa ambalo walikubaliana na maelezo yangu kutokana na uzuri wa mandhari wanayoiona. Maswali yakawa ni bandika bandua sasa ili mradi wakati kiu yao ya utalii. Nilikuwa natembea mwendo mdogo mdogo ili wapate kuishuhudia mandhari kwa uzuri zaidi. Walikuwa visura wale wameshughulishwa na kupiga picha wanyama kwa kamera zao na wengine kwa kutumia simu zao. Hali ikawa si hali ilipofika majira ya alasiri, ghafla bin vuu tembo mkubwa akiwa ameongozana na mtoto wake alikuwa anakuja wangu wangu mbele yetu. "Tafadhalini kaeni kimya, kila mtu aombe kwa imani ya dini yake tupo kwenye hatari, na hamna tena kula mananasi, harufu ya mananasi inawavutia sana tembo" nilitoa amri kama tupo jeshini inayohitaji utekelezaji tu bila kuanza kuhojihoji kwanini.
PICHA CHINI DEREVA SHEBBY AKIWA JUU YA KABURI LA MGUNDUZI WA MBUGA YA SELOUS



Hali ikawa si hali ilipofika majira ya alasiri, ghafla bin vuu tembo mkubwa amekuwa ameongozana na mtoto wake alikuwa anakuja wangu wangu mbele yetu. "Tafadhalini kaeni kimya, kila mtu aombe kwa imani ya dini yake tupo kwenye hatari, na hamna tena kula mananasi, harufu ya mananasi inawavutia sana tembo" nilitoa amri kama tupo jeshini inayohitaji utekelezaji tu bila kuanza kuhojihoji kwanini. Nikaanza kulirudisha gari langu kwa revasi, kinyumenyume huku tembo yule anatufuata bila kuchoka. Wawindaji haramu, waliifanya hifadhi ya Selous kuwa shamba la bibi kweli, kwa kujiwindia tembo, nyati na wanyama wengineo vyovyote wanavyopenda. Udhibiti juu ya majangili hao ulikuwa mgumu kutokana na ukubwa wa hifadhi hiyo iliyokusanya zaidi ya vijiji 89 katika hiyo mikoa minne. Mpaka nilipopata upenyo wa kugeuza gari nikaligeuza haraka haraka na kurejea kule tulipotoka. Wale warembo wote walikuwa wapo kimya, wamepigwa na taharuki ya uoga. Jioni kabisa tukaianza tena safari ya kuelekea kule tunakokukusudia, tukafanikiwa kufika salama kijiji cha Tagalala ambapo hapo ndio ilikuwa kambi yetu tuliyoichagua. Ziara yetu ilikuwa ni yenye kufana sana. Niliwatembeza maeneo tofauti kuanzia maporomoko ya maji ya Stieglers katiika mto Rufiji, ziwa Tagalala, Mnze, Nzelekela, Siwandu, Utunge na Mzizimia na Maji moto ambavyo vyote ni vivutio muhimu kwa utalii na kuvua samaki Sport fishing katika hifadhi ya Wanyamapori Selous. Nikawatembeza
maeneo mengine yanayotumika kwa ajili ya uwindaji wa kitalii. Baadhi ya sehemu za shughuli za utalii wa kuona wanyama (Game viewing), utalii wa kutembea, utalii wa boti. Mpaka ukatimu muda wa kurejea jijini Dar es Salaam. Ila penzi ni kikohozi halijifichi, wenzake na Zabibu walikuwa wameshanizoea wananitania shemeji shemeji. Waliona tuna ukaribu usio wa kawaida kati yangu na Zabibu. Alikuwa kila wakati wa kula chakula lazima awe pembeni yangu, na kwenye kila jambo alikuwa hakubali kuwa mbali na mimi. Siku ya Alhamisi mchana tukaanza msafara wa kurejea Jijini Dar es Salaam, mpaka kufikia majira ya usiku mbichi nikawarejesha kambini kwao. Wakati najiandaa kulitoa gari kwenye maegesho ya Hyatt Regency ili kukirejesha gari langu ofisini nikakabidhi gari. Nikashtukia Zabibu kachomoka kutokea eneo la mapokezi ya hoteli ananifuata, "Shebby......Shebby.....nisubiri pleaaase....! " nilimsikia vizuri nilikuwa bado sijapandisha kioo cha gari upande wa dereva. Nikazima gari kisha nikashuka chini, sikutaka mazungumzo yetu mpishi mzee Shukuru ayasikie maana nae alikuwa mpambe wa Bosi, akifika kazini anaweza kutapika kila kitu bila kusaza kitu. "Shebby.....ahsante kwa ukarimu wako nimefurahia sana safari, ila nakualika kwenye hafla ya fainali ya Miss Tanzania siku ya Jumapili tafadhali usikukose kuja kwako ndio furaha yangu. Nimekuletea hii kuponi ya tiketi utakayoitumia kukaa V. I. P. pale hivyo usipokuja nitakuona tu na utakuwa umeniangusha" alizungumza Zabibu kwa sauti ya kubembeleza huku ameinamisha shingo yake pembeni kwa huruma. " Duuuh....lakini......" alianza kujibu Shebby, "Lakini nini....sitaki kusikia cha lakini,faraja yangu ni kukuona basi, kwaheri" alimkatiza mazungumzo yake Shebby huku akimzuia kuzungumza kwa kidole chake cha shahada. Kisha akaaga haraka haraka kuanza kukimbilia ndani ya hoteli kwani kwa sheria za kambi hakutakiwa kuwa nje ya kambi. Shebby alibaki ameganda kama sanamu la chumvi lililogandishwa, akawa kama kapigwa shoti ya umeme, haamini anachokishuhudia machoni mwake. Zali la mentali la kupendwa na kisura mwenye viwango vyake vya ubora unaokubalika kimataifa. Kisura ambaye hana kasoro kuanzia kwenye unyayo mpaka kichwani kwenye nywele zake. Tofauti na wasichana wa uswazi aliozoea kukimbizana nao kila siku uzuri wao ni wa kutafuta na tochi. "Uswazi kwetu ukimkuta binti ana sura nzuri, basi matiti yake makubwa kama ananyonyesha kambi ya yatima, sio wakamilifu kwenye kila idara kama Zabibu toto la Kitanga" niliwaza nikiwa nimesimama pale pale nje ya gari pembeni kidogo namsindikiza kwa macho Zabibu. Mpaka alipofungua mlango wa hoteli na kunipungia mkono, na mie nikampungia na kurejea kwenye gari kiunyonge kulirejesha ofisini.

Usiku wake siku hiyo ya Alhamisi tulikesha tunatumiana meseji za chombezo zenye ujumbe wa mahaba na Zabibu mpaka manane ya usiku. Sasa ikawa rasmi Zabibu ni mpenzi wangu mpya, ameshaingia kwenye himaya yangu nikaona kama nimeokota embe dodo chini ya mti wa mwarobaini au kama vile nimeokota madini ya lulu pembezoni mwa ufukwe wa bahari. Katika dunia hii kila jambo hutanguliwa na ishara, hata mvua huwa hainyeshi ghafla, utaziona ishara za mawingu. Na huba mwanzowe ni jicho, kisha hufuata maneno matamu matamu ya kunawirisha nyoyo mpaka mnafanya maagano ya kuwa pamoja. Wahenga walituambia, kuwa ukiona zinduna na ambali iko nyuma. Hivyo nilishajiona Zabibu na mimi tutafika mbali sana katika penzi letu. Kama kanikubali nikiwa kapuku, kipato cha wastani huku akiwatolea mbavuni vigogo wenye pesa sufufu na madaraka yao, akaamua kunichagua mimi ninayeganga maisha, kweli amenipenda kwa dhati furaha ya kweli inakuja katika maisha yangu.
Usiku wa fainali za Shindano la Miss Tanzania ukawadia lilofanyika usiku wa Jumapili yake na kushuhudia Queen Zabibu Shamsi Sakuzindwa kuibuka na ushindi katika mashindano hayo na kutawazwa rasmi kuwa ni Miss Tanzania.
Tukio hilo nalikumbuka vizuri sana kama vile ninashuhudia jua la utosini la saa 6 mchana.
Ilikuwa ni Jumapili ya usiku mbichi kuanzia saa 1:30 usiku, washabiki walianza kumiminika katika ukumbi maarufu kwa burudani wa Mlimani City Hall. Watanzania wengi walitamani kuhudhuria siku hiyo ila viingilio vilikuwa ni vya bei ya kupaa. Wale wenye vipato vya pangu pakavu tia mchuzi hapa, ikabidi wakabaki majumbani mwao wanafuatilia kwenye runinga zao huku wanalaumu kuwa Kamati ya Miss Tanzania imeweka mbele tamaa ya pesa kwa kuweka kiingilio cha fainali hizo kuwa ni kati ya shilingi 100,000 na 200,000, kiasi ambacho ni kikubwa mno kwa Mtanzania wa kawaida. Mpaka kufika saa 2:00 usiku, ukumbi ukawa umejaa pomoni hamna hata pa kutema mate. Mimi niliwasili ukumbini mapema kidogo ingawa nilipata rabsharabsha za hapa na pale. Walinzi wa ukumbi na wakaguzi wa tiketi hawakuamini kama ni tiketi yangu kweli ile inayoniruhusu kwenda kukaa viti vya V. I. P. maana viti hivyo vilitawaliwa na mawaziri, wafanyabiashara wakubwa na watu mukhtari wenye wadhifa wao katika nchi za Watanzania. Na kila wakati kamera za waandishi wa habari zilikuwa zinawamurika watu wao wenye sharafu zao. Mwanzoni wakahisi labda nimemuibia mtu au nimeokota hiyo tiketi. "Kijana sema ukweli wako ni yako kweli au umeiokota? Usije pata matatizo bure mwenyewe akifika! " aliniuliza mmoja wa wakaguzi huku ananikazia macho. "Ni tiketi yangu kabisa, wewe kazi yako ni ukaguzi wa uhalali wa tiketi, usiingilie undani wa mtu! ' nilimjibu kwa ufedhuli,maana dawa ya moto ni moto. "Achana nae Bwana mruhusu, pesa za siku hizi hazina adabu, tofauti na pesa ya zamani ilikuwa ina watu na ukoo maalumu" alizungumza mkaguzi mwenzake aliyeonyesha busara kubwa. Ndipo nikaruhusiwa kupita mlango maalumu wa V. I. P. Tayari mashindano hayo yalishanitumbukia nyongo kwa dharau niliyoonyeshwa mlangoni, nusura nifanye maamuzi magumu ya kurudi zangu maskani. Ila nikawa namfikiria mpenzi wangu Zabibu nitamuumiza vibaya sana, hasa ukichukulia wenzake wote tiketi zao waliwapa familia zao ili waje kuwatia hamasa ya ushindi pindi wakiwaona, ila yeye Zabibu kaamua tiketi yake anitunuku mimi nije kumtia nguvu akiwa jukwaani. Nilipokaa kwenye eneo hilo la viti vya V. I. P nilikuwa mdogo kama kidonge cha piritoni, maana nilizungukwa na vigogo kila pande yangu ya shimaali, yamiini, mbele na nyuma yangu. Maongezi yao yalikuwa ni ya biashara kubwa kubwa za bilioni za pesa, nikabaki nimebung'aa tu nakodoa macho,nabaki nachezea simu yangu Tekno ya Mchina, ikabidi na sauti niipunguze kabisa, isije kuita mbele yao nikawasumbua wanene wa nchi. "Kijana changamkieni fursa za biashara, leo ofisini kwangu zimekuja kampuni za kutoka Uarabuni, Saudi-arabia na Qatar wanahitaji mbuzi wenye thamani ya bilioni 50 kwa mwezi, kama unaweza kuchangamkia hiyo fursa tuonane kesho ofisini" alinizungumzusha waziri wa biashara huku akinikabidhi kadi yenye mawasiliano yake. Nikaipokea na kubaki najilazimisha kutabasamu. Maana nilikuwa naona kama ananichezea shere, ananieleza fursa za mabilioni ya pesa wakati ndio kwanza nimenunua kagari cha biashara ya taksi- UBBER cha mkopo kazini kwa dhamana ya nyumba ya familia. Mambo yalimuendea sheshe mpenzi wangu Zabibu, akafanikiwa kuingia kwenye tano bora ya wale wanaowania taji hilo. Minong'ono ya Mapredeshee niliokaa nao jirani nao, ilinivunja nguvu kabisa ya kufanya mahusiano ya kwelikweli na Zabibu. Nilipanga nikitoka pale ukumbini namtumia meseji kuwa mimi na yeye mahusiano yetu yafe. Ilihitaji roho ya paka kuweza kuvumilia njama zilizokuwa zinapangwa na wale vigogo bila kujua kuwa Zabibu ni mpenzi wangu." Huyu mrefu kuliko wote mwenye jina tamu kama zabibu zenyewe huyu wangu. Nakula nae sahani moja, nampa mkataba wa kutangaza bidhaa za kampuni yangu, safari za China nyingiii naenda kumla huko huko ha...ha..ha..." alizungumza tajiri mmoja mwarabu mwenye kampuni ya kuuza vifaa vya umeme vya majumbani. "Ha.. ha.. ha..mwenye kisu kikali ndio atakula nyama, mie nataka nitafune wote hawa tano bora kabla hawajachakaa maana mashindano ya mwakani vinakuja vipuri vipya vyenye kilomita sifuri" akachagiza mwenzake huku wanapongezana kwa ujinga wao kwa kugongesheana glasi ya vinywaji vyao. Aheri nivunje nae uhusiano kabla sijafika nae mbali huyu Zabibu ni bahari kubwa anagombewa na watu wazito. Ikafika kipindi cha maswali kila mrembo anachagua swali la kujibu, kati ya linalohusu sekta ya afya, utalii, haki za watoto na akina mama, ajira kwa vijana na uchumi wa nchi. Zabibu akachagua swali la masuala ya utalii, ambapo aliulizwa kama angekuwa waziri wa utalii angefanya mbinu gani ili kupandisha idadi ya watalii wanaoitembelea nchi yetu?. Akalijibu kiufasaha mkubwa swali hilo ukumbi mzima ulisimama huku unapiga makofi kuashiria kawabwaga wenzake vibaya sana. Muda ukafika wa kumtangaza mshindi wa taji hilo baada ya kujumlisha idadi ya kura toka kwa majaji watano. Mshereheshaji wa sherehe akamtangaza Zabibu Shamsi kuwa ndio mshindi wa taji hilo la Miss Tanzania kwa mwaka huo. Ukumbi mzima ukaripuka kwa mayowe, shangwe na vigeregere kuonyesha wamekubaliana na na maamuzi ya majaji hamna upendeleo wowote uliofanyika. Zabibu alikuwa na furaha isiyomithilika mpaka akawa anamwaga machozi ya furaha, huku wale Mapredeshee wanahangaika kuwatafuta waandaaji wa mashindano hayo kwa malengo ya kunasa namba za simu za warembo hao. Zabibu akafanya tukio ambalo lilinipaisha ukumbi mzima na kila mtu kujiuliza mimi ni nani katika jamii mpaka nimeopoa mlimbwende wa nchi kama yule. Kabla hajavikwa taji lake la kichwani na mgeni rasmi ambaye alikuwa ni Naibu Waziri Mkuu wa nchi. Alichomoka kule stejini na kuja mpaka pale nilipokaa mimi akaninyanyua kitini na kunikumbatia kwa furaha. "Ahsante Honey...kwa kuja, sikutegemea kama utakuja kunitia nguvu, pia nashukuru sana maelezo yako mazuri kule kwenye hifadhi ya Selous ndio yameniwezesha kujibu swali la masuala ya utalii kiufasaha mkubwa, bila wewe hili taji nisingelipata. Usiniache usiku huu naondoka na wewe Mwaaaaah....Mwaaaah...!" alininong'oneza sikio kisha akanipa mabusu mawili motomoto ya shavuni kisha akaniachia na kurudi stejini. Macho ya ukumbi mzima yakawa yamenigeukia mimi, huku vyombo vya habari nao wakiwa ndio wamepata habari ya kuandika, wakinimulika na kamera zao. Mgeni rasmi akamkabidhi zawadi yake ya gari aina ya 'Toyota Highlander New Model'. Baada ya hapo akaanza kuhojiwa na vyombo vya habari mubashara anaonekana Tanzania nzima.



Mbele ya wafanyakazi wenzangu nilijipiga kibobwe nikajifanya sijali kufukuzwa, lakini nilipotoka nje ya jengo la RAJA SAFARI TOURS na kukanyaga tu lami ya barabarani machozi yakaanza kunimwagika kwa uonevu niliofanyiwa. Nikafanikiwa kupata daladala ya kuelekea nyumbani Mwembechai, lakini kimwili nilikuwa ndani ya daladala ila kimawazo nilikuwa nipo kwenye nyumba ya familia Kariakoo, ninawaza hali itakavyokuwa siku ya mnada hapo kesho, jinsi dalali atakavyokuwa anatamba kwa mbwembwe, huku akijitawanya kwa mapana na marefu na kipaza sauti chake. "Milioni 7 mara ya kwanza, milioni 7 mara ya pili, milioni 7 mara ya tatu....tooop top..! , ameshinda mpeni nyumba yake, hongera sana kalipie kwa keshia asilimia 25% zako" . Nikawa navuta taswira jinsi mama yangu, ambaye ni kikongwe atakavyokuwa anatoa machozi kwa kujutia kwanini alikubali kunipa hati ya nyumba kwenda kukopea, huku ndugu zangu wakinilalamikia kwa kuwasababishia nyumba yao ipigwe shoka. Ilifika hatua nikawa natamani baragumu la siku ya kiama lipulizwe muda huo huo ili dunia iwe ndio mwisho niepuke fedheha iliyopo usoni mwangu. Mbona mimi sina tabia nzito kama zamani sasa ni mtu mwema ninayeweza kusuhubiana na mtu yoyote, lakini yule ponjoro nimemkosea nini lakini, ya rabi stara!. Sina roho choko, naridhika na kile ninacholipwa sijawahi hata kupiga nyoka mafuta ya gari kama wafanyavyo madereva wasio waaminifu" mawazo yaliendelea kujikita mizizi akilini mwangu. "Mwembechai washukajii piga chiniii....Mwembechai waendaji choma ndani..." nilishtuliwa kutoka kwenye dimbwi hilo la mawazo na sauti ya mvumo wa radi ya kukwaruza ya kondakta wa daladala ile. Ndipo nikatanabahi kuwa nimeshafika maeneo ya nyumbani kwangu. Nikajizoazoa hima hima toka kitini na kuharakia mlangoni kabla daladala halijaondoka. Nikavuka barabara bila hata kuangalia vizuri magari yanayopita kwa kasi, nusra nigongwe na lori la kusambaza bidhaa madukani. "Wewe mshambaaa....utakufaaa, ndio nyie mliokuja mjini kwa mbio za mwenge" niliporomoshewa maneno ya kejeli ya kila sampuli na walimwengu wasio na hata chembe ya huruma. "W-houf...!" nilishusha pumzi ndefu sikuwajibu kitu zaidi ya kumshukuru Rabana kwa kuniepusha na ajali ya asubuhi asubuhi, nilikuwa nimepatwa na pumbao la nafsi sijielewi. Laiti wangeingia kichwani mwangu na kukuta mambo yalivyo tumbi tumbi wasingenihukumu kwa kosa za uzembe barabarani. Yalikuwa ni makosa yangu kushuka bila kuchukua tahadhari kwa umakini lakini hiyo yote ilitokana na mazonge kichwani ya kufukuzwa kazi. Nikawa ninawaza Jiji hili lilivyo gumu kuishi bila kazi sijui maisha yatakuwaje!."Hivi tu mtu utakuta ana ajira lakini maisha yake vuru vuru sasa sembuse upo benchi apeche alolo huingizi hata senti tano nyeusi!" bado lundo la mawazo lilikuwa limetawala kichwani mwake. Nilipokuwa nakaribia kufika nyumbani nikaona mtiti wa akina mama nyumbani kwangu nilipopanga, mpaka nikadhania labda ni msiba. Walikuwa wamejikalia kibarazani pote sambejambe bila nidhamu wala taadhima. Ikabidi nichepuke kidogo kwenye kiduka cha Mangi nyumba ya jirani nijitie nakunywa soda ili niyasome mazingira kunani pale nyumbani. Ndipo nikawasikia mazungumzo yao waziwazi kumbe yalikuwa ni vijembe tu dhidi yangu na Zeddy wangu. "Mama Sele nakuambia huyu mzaramo mwenzako ametushinda tabia, mchawi kabisaa kamuendea kwa kalumanzila binti wa watu mpaka amezuzuka zuzu, haiwezekani Miss Tanzania wetu jana tumekesha tunamshangilia kwenye runinga leo aje kuamkia usingizini kwenye mabanda yetu haya ya uswahili tena analishwa misumari akitoboko utumbo akatutie aibu huko Miss World ha ha haaaaa...hoi.. hoi.. hoi.. hallo.. hallo.. ya dagaa kauzu kwa teeembeleee" alizungumza mama mmoja wapo mpangaji mwenzangu ambaye nilikuwa namheshimu sana, nilijua ni jirani wa huba na hawa, kumbe jirani mnafiki sikutegemea abadaan kataan kama ipo siku atanisengenya na kunikebehi nyuma ya mgongo wangu." Mie kuhemwa naona mrembo anakuja kibarazani kwangu chaka chaka kupima mkaa wa kikopo, kumbe ndio mchumba wa Shebby..sasa atatulizana maana walikuwa wanakuja wanawake wa kila sampuli yeye ni zoa zoa tu. Ila yatamkuta mambo hao Mamiss wanahitaji matunzo hana pesa za kumuengaenga binti mrembo kama yule" alizungumza maneno ya uwongo, uzandiki na uzushi mtupu mama Sele kuwa mimi ni mpenda vidosho wakati hasha lillahi! sipo hivyo. Walizama kwenye porojo zao za hamrere hamrere, bandika bandua ili mradi baraza lao la umbea lilichachamaa kwa vijembe. Nikachomoka pale dukani kwa Mangi kwa kasi huku nikiwa na soda yangu mkononi na kuwapita kwa kupasua kati kati yao bila salamu yoyote kwao. Kwa ghaidi nilizokuwa nazo, ningewakwapua mikwaju laiti angethubutu mmoja wao kujishaua kunisalimia. Wakabaki wameduwaa,wameshukwa na nyuso zao, wamenitumbulia macho kwa uoga utasema wanaaga maiti. Hawakutegemea kuniona wakati ule kurudi nyumbani. Walijua fika kuwa nimewasikia kila kitu walichosema, maana walimuona mtu amesimama pale dukani kawapa mgongo ila hawakujua kama ndio mimi. Wakatawanyika kla mmoja akashika njia yake anayoijua mwenyewe. Siku zote mwisho wa ubaya ni aibu na fedheha isiyobebeka machoni mwa waja. Namshukuru Mwenyezi Mungu alinipa stahamala ya uvumilivu ningewashushia kipigo ningekuwa nimepanda kimbunga kwa lengo kuvuna tufani"Hodii ngo ngo ngo Hodii ngo ngo ngo," nilibisha hodi mlango wa kuingia kwenye chumba changu. Zabibu alikuwa ametulizana chumbani Anachambua dagaa kauzu wa Mwanza raha mustarehe kama sultan bin Jerehe habari hana huku anaangalia vipindi vya televisheni. "Oooh..! Waaaoh baby huyoo, karibu tena " alikurupuka na kufungua mlango Zabibu na kunikaribisha ndani. Alikuwa amevalia jezi zangu za timu ya Chelsea na trakisuti yake maana hakuwa na nguo za kubadilisha. "Ahsante my love, umeshindaje lakini" nilijikaza kisabuni kwa kujibu salamu yake kiuchangamfu." Mbona hunisifii nimetinga jezi za vijana wa darajani au sijapendezaa?" alijilalamisha kwa kudeka huku anajigeuzageuza mwili wake kimadoido. "Oooh! Sorry baby nimesahau mawazo mengi , bundi analia....upande wangu. " nikajibu kwa ufupi na kwenda mubashara kukaa pwetepwete kwenye kochi mojawapo kisha nikaendelea kumpa ufafanuzi . "Mambo hamkani si shwari tena!, nimefukuzwa kazi bila utetezi wowote". Nikawa nimejiinamia kwa kushika tama mashavuni mwangu nimeishiwa mipango sina alifu wala bee, kilichokuwa kinanitesa zaidi suala la nyumba ya familia basi hamna kingine. Hasa nikikumbuka nilianza maisha ya ununda ya kutoroka nyumbani na kurejea tokea nikiwa darasa la saba, hivyo suala la ajira haikuwa shida kubwa sana, tatizo sasa lilikuwa kwenye mnada. "Beeebi...umefukuzwa kwa kosa gani, mbona kama ujio wangu kwenye maisha yako kumefungua balaa, nuksi na fali mbaya kwako nisamehe bebiiii.....sio kosa langu ni kosa la moyo wangu kukupenda" akawa Zabibu ameingiwa na kimuyemuye huku akaanza kuangusha kilio cha kwi kwi, huku ananipigia magoti. "Acha dhana za kufikirika hizo my love!, mie tatizo langu linaloniny'ong'onyesha ni mkopo wa lile gari langu ninalolifanya UBBER, nimeambiwa mpaka kesho saa 4:00 niwe nimerejesha la sivyo nyumba ya familia kule Kariakoo inapigwa mnada, hicho ndicho kinaninyima raha mpenzi wangu!" nilijikaza kuzungumza baada ya kuona mpenzi wake kumbe nae ni moyo wa wake ni nyumba ya udongo hauwezi kuhimili vishindo. "Kuna kitu nimekumbuka mpenzi wangu ngoja nimeagizia begi la nguo zangu toka kwa shoga yangu, mchana nina kipindi chuo usiku nitakuja tena kukupa jibu kama ninaweza kukusaidia au laah!" alipata ujasiri wa ghafla Zeddy akafuta machozi yake na kunipa matumaini ya msaada. "Kweli mpenzi wangu Zabibu alinisaidia kwa hali na mali nyumba ya familia haikuuzwa" nilikuwa ninanong'ona kwa sauti ya chini huku usingizi ukinivamia kwa nguvu bila huruma, haukutaka usingizi huo kuniacha niendelee kumaliza kumbukizi zangu zote za maisha ya misukosuko, yenye milima na mabonde niliyoyapitia na mchumba wangu Zabibu tokea nakutana nae mpaka anachukua maamuzi ya kujitoa uhai wake.

Shebby alikuwa yupo katika ofisi za Mkurugenzi wa Kampuni ya Firdaus Trading and Shipping LTD zilizopo barabara ya Kawawa nyuma ya majengo ya Chuo Kikuu Huria. Ofisi hizo zilikuwa zinajishughulisha na biashara ya mbalimbali ikiwemo ya kuuza na kununua madini ndani na nje ya nchi. Ilikuwa inamilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania Bwana Nadeem Massawe. Lengo, madhumuni na nia ya kukanyaga ofisi hizo lilikuwa ni kutaka kuonana uso kwa uso na mkurugenzi mkuu huyo wa kampuni bwana Nadeem. Ugumu sasa ulikuwepo kwenye kuonana nae bwana mkubwa huyo. Mara nyingi shida za wenye kutaka kuonana nae zilimalizwa na wasaidizi wake. Hakuwa mtu wa kujichanganya na watu wala vyombo vya habari. Watanzania wengi walikuwa wanamjua kwa matendo yake mema kwa jamii lakini hawamjui kwa sura. "Kuna nini mbona watu wamejazana hapa chini" lilikuwa ni swali la kwanza kuuliza Shebby baada ya kuwasili ndani ya uwanja uliozungukwa na geti, uwanja ambao ndani yake kulikuwa na majengo pacha ya roshani 10. "Wewe itakuwa mgeni hapa eeh..! Hapa hali ipo hivi karibia mwaka wa tatu, kila ikifika siku ya Ijumaa, siku ya ibada kwa waumini wa kiislamu, bwana mkubwa huyu Mwenyezi Mungu amuingize peponi huwa na tabia ya kutoa sadaka kwa mafukara, masikini, yatima na wajane" alijibu mmoja wa watu wazoefu wa mazingira yale. "Kupata tajiri mwenye uchamungu kama huyu ni nadra sana, Allah amlinde na amkuzie mali zake, amuepushe na husuda za mahasidi-Amiiin..." mzee mmoja wa makamo alishadidia mazungumzo hayo huku mkononi akiwa amefumbata burungutu la pesa kuonyesha tayari kashapata kamgao chake. Shebby alikuwa anachekea tumboni kimoyomoyo alivyosikia Nadeem anasifiwa uchajimungu. Kwa umati ule wa watu, Shebby akaona itakuwa ngumu kuonana nae bwana Nadeem. Inasemekana watu huanza kufurika hapo kuanzia manane ya usiku kupanga foleni, nae Mkurugenzi mwenyewe anawasili baada ya kusali swala ya Alfajiri. "Kwa hiyo siwezi kumuona Kabisa kwa leo? " aliuliza Shebby akiwa ameshaanza kukata tamaa, hasa ukichukulia kuzipata zilipo ofisi hizo imemchukua karibia siku tatu kudodosadodosa. "Siku zingine rahisi kumpata ni siku za Jumatatu na Alhamisi, siku hizo anarudi nyumbani kwake mapema sana kwa sababu anafunga swaumu za sunnah hivyo anawahi kufuturu" alisema mmoja wa wasimamia usalama wa eneo lile. Shebby akaondoka eneo lile kiunyonge huku akiwaza na kuwazua jinsi atakavyojipenyeza mpaka afanikiwe kumuona. Wakati anataka kuondoka akapata mawazo mapya, "leo ni siku ya Ijumaa kwa vyovyote ataende msikitini kuswali pindi atakaporudi nitamvizia kwenye lifti nipande nae hapo ndio nitatapika dukuduku langu kwake. Barua iliyoachwa na marehemu Zabibu ndio iliyompelekea Shebby kuwa na uhitaji wa kuonana na Kibosile Nadeem. Akajibanza kwenye moja ya mahema yaliyojengwa kwa ajili ya kupumzikia wageni wanaotembelea eneo hilo. Akiwa pale anasomasoma magazeti aliyokuwa ameyanunua siku hiyo akamuona kwa mbali Kibosile Nadeem akiwa na mlinzi wake binafsi anapanda gari kuondoka eneo lile la maegesho, akatabasamu, alipoangalia saa yake ya mkononi ilikuwa ni saa 6:00 kamili mchana, akajua sasa lazima tu atakuwa anaelekea msikitini kuswali swala ya Ijumaa. Shebby alikuwa ni tariku swala, msikitini kwake ni kama kituo cha polisi, mara ya mwisho ni siku aliyotaka kumuona Zabibu. Alikuwa hajali cha siku ya Ijumaa, wala mwezi wa ramadhani wala sikukuu ya Eid alikuwa na mzio mkubwa na msikiti. Maisha yake ya kushinda mbugani na wanyama, nae kulimfanya awe kama hayawani hajali mambo ya ibada. Mpaka kufika majira ya alasiri, Bwana Nadeem alikuwa bado hajatia mguu ofisini kwake. Shebby akaanza kuwa na wasiwasi huenda ndio kakitoa kimoja hatorudi ofisini. Pesa ziliendelea kutolewa kwa wenye mahitaji maalumu na wasaidizi wake. Ilipofika majira ya saa 11:00 jioni akakata tamaa kabisa ya kuonana nae kabisa. Akanyanyuka kwenye kiti na bahasha yake ya kaki mkononi na magazeti yake akijongea getini tayari kwa kuondoka eneo lile akajipange upya. Hakupiga hata hatua tano akasikia mvumo wa gari la Bwana Nadeem linataka kuingia kwenye jengo lile. Chapuchapu Shebby akabadili uelekeo na kwenda kwenye moja kwa moja kwenye jengo la ofisi kwa ajili ya kumvizia kwenye lifti." Kijana mbona umesimama hapo kwenye lifti muda mrefu kulikoni? " walikuja wana usalama wawili wakimzongazonga Shebby baada ya kumuona kwenye kamera za ulinzi za jengo.


Mbele ya wafanyakazi wenzangu nilijipiga kibobwe nikajifanya sijali kufukuzwa, lakini nilipotoka nje ya jengo la RAJA SAFARI TOURS na kukanyaga tuwlami ya barabarani machozi yakaanza kunimwagika kwa uonevu niliofanyiwa. Nikafanikiwa kupata daladala ya kuelekea nyumbani Mwembechai, lakini kimwili nilikuwa ndani ya daladala ila kimawazo nilikuwa nipo kwenye nyumba ya familia Kariakoo, ninawaza hali itakavyokuwa siku ya mnada hapo kesho, jinsi dalali atakavyokuwa anatamba kwa mbwembwe, huku akijitawanya kwa mapana na marefu na kipaza sauti chake. "Milioni 7 mara ya kwanza, milioni 7 mara ya pili, milioni 7 mara ya tatu....tooop top..! , ameshinda mpeni nyumba yake, hongera sana kalipie kwa keshia asilimia 25% zako" . Nikawa navuta taswira jinsi mama yangu, ambaye ni kikongwe atakavyokuwa anatoa machozi kwa kujutia kwanini alikubali kunipa hati ya nyumba kwenda kukopea, huku ndugu zangu wakinilalamikia kwa kuwasababishia nyumba yao ipigwe shoka. Ilifika hatua nikawa natamani baragumu la siku ya kiama lipulizwe muda huo huo ili dunia iwe ndio mwisho niepuke fedheha iliyopo usoni mwangu. Mbona mimi sina tabia nzito kama zamani sasa ni mtu mwema ninayeweza kusuhubiana na mtu yoyote, lakini yule ponjoro nimemkosea nini lakini, ya rabi stara!. Sina roho choko, naridhika na kile ninacholipwa sijawahi hata kupiga nyoka mafuta ya gari kama wafanyavyo madereva wasio waaminifu" mawazo yaliendelea kujikita mizizi akilini mwangu. "Mwembechai washukajii piga chiniii....Mwembechai waendaji choma ndani..." nilishtuliwa kutoka kwenye dimbwi hilo la mawazo na sauti ya mvumo wa radi ya kukwaruza ya kondakta wa daladala ile. Ndipo nikatanabahi kuwa nimeshafika maeneo ya nyumbani kwangu. Nikajizoazoa hima hima toka kitini na kuharakia mlangoni kabla daladala halijaondoka. Nikavuka barabara bila hata kuangalia vizuri magari yanayopita kwa kasi, nusra nigongwe na lori la kusambaza bidhaa madukani. "Wewe mshambaaa....utakufaaa, ndio nyie mliokuja mjini kwa mbio za mwenge" niliporomoshewa maneno ya kejeli ya kila sampuli na walimwengu wasio na hata chembe ya huruma. "W-houf...!" nilishusha pumzi ndefu sikuwajibu kitu zaidi ya kumshukuru Rabana kwa kuniepusha na ajali ya asubuhi asubuhi, nilikuwa nimepatwa na pumbao la nafsi sijielewi. Laiti wangeingia kichwani mwangu na kukuta mambo yalivyo tumbi tumbi wasingenihukumu kwa kosa za uzembe barabarani. Yalikuwa ni makosa yangu kushuka bila kuchukua tahadhari kwa umakini lakini hiyo yote ilitokana na mazonge kichwani ya kufukuzwa kazi. Nikawa ninawaza Jiji hili lilivyo gumu kuishi bila kazi sijui maisha yatakuwaje!."Hivi tu mtu utakuta ana ajira lakini maisha yake vuru vuru sasa sembuse upo benchi apeche alolo huingizi hata senti tano nyeusi!" bado lundo la mawazo lilikuwa limetawala kichwani mwake. Nilipokuwa nakaribia kufika nyumbani nikaona mtiti wa akina mama nyumbani kwangu nilipopanga, mpaka nikadhania labda ni msiba. Walikuwa wamejikalia kibarazani pote sambejambe bila nidhamu wala taadhima. Ikabidi nichepuke kidogo kwenye kiduka cha Mangi nyumba ya jirani nijitie nakunywa soda ili niyasome mazingira kunani pale nyumbani. Ndipo nikawasikia mazungumzo yao waziwazi kumbe yalikuwa ni vijembe tu dhidi yangu na Zeddy wangu. "Mama Sele nakuambia huyu mzaramo mwenzako ametushinda tabia, mchawi kabisaa kamuendea kwa kalumanzila binti wa watu mpaka amezuzuka zuzu, haiwezekani Miss Tanzania wetu jana tumekesha tunamshangilia kwenye runinga leo aje kuamkia usingizini kwenye mabanda yetu haya ya uswahili tena analishwa misumari akitoboko utumbo akatutie aibu huko Miss World ha ha haaaaa...hoi.. hoi.. hoi.. hallo.. hallo.. ya dagaa kauzu kwa teeembeleee" alizungumza mama mmoja wapo mpangaji mwenzangu ambaye nilikuwa namheshimu sana, nilijua ni jirani wa huba na hawa, kumbe jirani mnafiki sikutegemea abadaan kataan kama ipo siku atanisengenya na kunikebehi nyuma ya mgongo wangu." Mie kuhemwa naona mrembo anakuja kibarazani kwangu chaka chaka kupima mkaa wa kikopo, kumbe ndio mchumba wa Shebby..sasa atatulizana maana walikuwa wanakuja wanawake wa kila sampuli yeye ni zoa zoa tu. Ila yatamkuta mambo hao Mamiss wanahitaji matunzo hana pesa za kumuengaenga binti mrembo kama yule" alizungumza maneno ya uwongo, uzandiki na uzushi mtupu mama Sele kuwa mimi ni mpenda vidosho wakati hasha lillahi! sipo hivyo. Walizama kwenye porojo zao za hamrere hamrere, bandika bandua ili mradi baraza lao la umbea lilichachamaa kwa vijembe. Nikachomoka pale dukani kwa Mangi kwa kasi huku nikiwa na soda yangu mkononi na kuwapita kwa kupasua kati kati yao bila salamu yoyote kwao. Kwa ghaidi nilizokuwa nazo, ningewakwapua mikwaju laiti angethubutu mmoja wao kujishaua kunisalimia. Wakabaki wameduwaa,wameshukwa na nyuso zao, wamenitumbulia macho kwa uoga utasema wanaaga maiti. Hawakutegemea kuniona wakati ule kurudi nyumbani. Walijua fika kuwa nimewasikia kila kitu walichosema, maana walimuona mtu amesimama pale dukani kawapa mgongo ila hawakujua kama ndio mimi. Wakatawanyika kla mmoja akashika njia yake anayoijua mwenyewe. Siku zote mwisho wa ubaya ni aibu na fedheha isiyobebeka machoni mwa waja. Namshukuru Mwenyezi Mungu alinipa stahamala ya uvumilivu ningewashushia kipigo ningekuwa nimepanda kimbunga kwa lengo kuvuna tufani"Hodii ngo ngo ngo Hodii ngo ngo ngo," nilibisha hodi mlango wa kuingia kwenye chumba changu. Zabibu alikuwa ametulizana chumbani Anachambua dagaa kauzu wa Mwanza raha mustarehe kama sultan bin Jerehe habari hana huku anaangalia vipindi vya televisheni. "Oooh..! Waaaoh baby huyoo, karibu tena " alikurupuka na kufungua mlango Zabibu na kunikaribisha ndani. Alikuwa amevalia jezi zangu za timu ya Chelsea na trakisuti yake maana hakuwa na nguo za kubadilisha. "Ahsante my love, umeshindaje lakini" nilijikaza kisabuni kwa kujibu salamu yake kiuchangamfu." Mbona hunisifii nimetinga jezi za vijana wa darajani au sijapendezaa?" alijilalamisha kwa kudeka huku anajigeuzageuza mwili wake kimadoido. "Oooh! Sorry baby nimesahau mawazo mengi , bundi analia....upande wangu. " nikajibu kwa ufupi na kwenda mubashara kukaa pwetepwete kwenye kochi mojawapo kisha nikaendelea kumpa ufafanuzi . "Mambo hamkani si shwari tena!, nimefukuzwa kazi bila utetezi wowote". Nikawa nimejiinamia kwa kushika tama mashavuni mwangu nimeishiwa mipango sina alifu wala bee, kilichokuwa kinanitesa zaidi suala la nyumba ya familia basi hamna kingine. Hasa nikikumbuka nilianza maisha ya ununda ya kutoroka nyumbani na kurejea tokea nikiwa darasa la saba, hivyo suala la ajira haikuwa shida kubwa sana, tatizo sasa lilikuwa kwenye mnada. "Beeebi...umefukuzwa kwa kosa gani, mbona kama ujio wangu kwenye maisha yako kumefungua balaa, nuksi na fali mbaya kwako nisamehe bebiiii.....sio kosa langu ni kosa la moyo wangu kukupenda" akawa Zabibu ameingiwa na kimuyemuye huku akaanza kuangusha kilio cha kwi kwi, huku ananipigia magoti. "Acha dhana za kufikirika hizo my love!, mie tatizo langu linaloniny'ong'onyesha ni mkopo wa lile gari langu ninalolifanya UBBER, nimeambiwa mpaka kesho saa 4:00 niwe nimerejesha la sivyo nyumba ya familia kule Kariakoo inapigwa mnada, hicho ndicho kinaninyima raha mpenzi wangu!" nilijikaza kuzungumza baada ya kuona mpenzi wake kumbe nae ni moyo wa wake ni nyumba ya udongo hauwezi kuhimili vishindo. "Kuna kitu nimekumbuka mpenzi wangu ngoja nimeagizia begi la nguo zangu toka kwa shoga yangu, mchana nina kipindi chuo usiku nitakuja tena kukupa jibu kama ninaweza kukusaidia au laah!" alipata ujasiri wa ghafla Zeddy akafuta machozi yake na kunipa matumaini ya msaada. "Kweli mpenzi wangu Zabibu alinisaidia kwa hali na mali nyumba ya familia haikuuzwa" nilikuwa ninanong'ona kwa sauti ya chini huku usingizi ukinivamia kwa nguvu bila huruma, haukutaka usingizi huo kuniacha niendelee kumaliza kumbukizi zangu zote za maisha ya misukosuko, yenye milima na mabonde niliyoyapitia na mchumba wangu Zabibu tokea nakutana nae mpaka anachukua maamuzi ya kujitoa uhai wake.

Shebby alikuwa yupo katika ofisi za Mkurugenzi wa Kampuni ya Firdaus Trading and Shipping LTD zilizopo barabara ya Kawawa nyuma ya majengo ya Chuo Kikuu Huria. Ofisi hizo zilikuwa zinajishughulisha na biashara ya mbalimbali ikiwemo ya kuuza na kununua madini ndani na nje ya nchi. Ilikuwa inamilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania Bwana Nadeem Massawe. Lengo, madhumuni na nia ya kukanyaga ofisi hizo lilikuwa ni kutaka kuonana uso kwa uso na mkurugenzi mkuu huyo wa kampuni bwana Nadeem. Ugumu sasa ulikuwepo kwenye kuonana nae bwana mkubwa huyo. Mara nyingi shida za wenye kutaka kuonana nae zilimalizwa na wasaidizi wake. Hakuwa mtu wa kujichanganya na watu wala vyombo vya habari. Watanzania wengi walikuwa wanamjua kwa matendo yake mema kwa jamii lakini hawamjui kwa sura. "Kuna nini mbona watu wamejazana hapa chini" lilikuwa ni swali la kwanza kuuliza Shebby baada ya kuwasili ndani ya uwanja uliozungukwa na geti, uwanja ambao ndani yake kulikuwa na majengo pacha ya roshani 10. "Wewe itakuwa mgeni hapa eeh..! Hapa hali ipo hivi karibia mwaka wa tatu, kila ikifika siku ya Ijumaa, siku ya ibada kwa waumini wa kiislamu, bwana mkubwa huyu Mwenyezi Mungu amuingize peponi huwa na tabia ya kutoa sadaka kwa mafukara, masikini, yatima na wajane" alijibu mmoja wa watu wazoefu wa mazingira yale. "Kupata tajiri mwenye uchamungu kama huyu ni nadra sana, Allah amlinde na amkuzie mali zake, amuepushe na husuda za mahasidi-Amiiin..." mzee mmoja wa makamo alishadidia mazungumzo hayo huku mkononi akiwa amefumbata burungutu la pesa kuonyesha tayari kashapata kamgao chake. Shebby alikuwa anachekea tumboni kimoyomoyo alivyosikia Nadeem anasifiwa uchajimungu. Kwa umati ule wa watu, Shebby akaona itakuwa ngumu kuonana nae bwana Nadeem. Inasemekana watu huanza kufurika hapo kuanzia manane ya usiku kupanga foleni, nae Mkurugenzi mwenyewe anawasili baada ya kusali swala ya Alfajiri. "Kwa hiyo siwezi kumuona Kabisa kwa leo? " aliuliza Shebby akiwa ameshaanza kukata tamaa, hasa ukichukulia kuzipata zilipo ofisi hizo imemchukua karibia siku tatu kudodosadodosa. "Siku zingine rahisi kumpata ni siku za Jumatatu na Alhamisi, siku hizo anarudi nyumbani kwake mapema sana kwa sababu anafunga swaumu za sunnah hivyo anawahi kufuturu" alisema mmoja wa wasimamia usalama wa eneo lile. Shebby akaondoka eneo lile kiunyonge huku akiwaza na kuwazua jinsi atakavyojipenyeza mpaka afanikiwe kumuona. Wakati anataka kuondoka akapata mawazo mapya, "leo ni siku ya Ijumaa kwa vyovyote ataende msikitini kuswali pindi atakaporudi nitamvizia kwenye lifti nipande nae hapo ndio nitatapika dukuduku langu kwake. Barua iliyoachwa na marehemu Zabibu ndio iliyompelekea Shebby kuwa na uhitaji wa kuonana na Kibosile Nadeem. Akajibanza kwenye moja ya mahema yaliyojengwa kwa ajili ya kupumzikia wageni wanaotembelea eneo hilo. Akiwa pale anasomasoma magazeti aliyokuwa ameyanunua siku hiyo akamuona kwa mbali Kibosile Nadeem akiwa na mlinzi wake binafsi anapanda gari kuondoka eneo lile la maegesho, akatabasamu, alipoangalia saa yake ya mkononi ilikuwa ni saa 6:00 kamili mchana, akajua sasa lazima tu atakuwa anaelekea msikitini kuswali swala ya Ijumaa. Shebby alikuwa ni tariku swala, msikitini kwake ni kama kituo cha polisi, mara ya mwisho ni siku aliyotaka kumuona Zabibu. Alikuwa hajali cha siku ya Ijumaa, wala mwezi wa ramadhani wala sikukuu ya Eid alikuwa na mzio mkubwa na msikiti. Maisha yake ya kushinda mbugani na wanyama, nae kulimfanya awe kama hayawani hajali mambo ya ibada. Mpaka kufika majira ya alasiri, Bwana Nadeem alikuwa bado hajatia mguu ofisini kwake. Shebby akaanza kuwa na wasiwasi huenda ndio kakitoa kimoja hatorudi ofisini. Pesa ziliendelea kutolewa kwa wenye mahitaji maalumu na wasaidizi wake. Ilipofika majira ya saa 11:00 jioni akakata tamaa kabisa ya kuonana nae kabisa. Akanyanyuka kwenye kiti na bahasha yake ya kaki mkononi na magazeti yake akijongea getini tayari kwa kuondoka eneo lile akajipange upya. Hakupiga hata hatua tano akasikia mvumo wa gari la Bwana Nadeem linataka kuingia kwenye jengo lile. Chapuchapu Shebby akabadili uelekeo na kwenda kwenye moja kwa moja kwenye jengo la ofisi kwa ajili ya kumvizia kwenye lifti." Kijana mbona umesimama hapo kwenye lifti muda mrefu kulikoni? " walikuja wana usalama wawili wakimzongazonga Shebby baada ya kumuona kwenye kamera za ulinzi za jengo.


Kijana mbona umesimama hapo kwenye lifti muda mrefu kulikoni? " walikuja wana usalama wawili wakimzongazonga Shebby baada ya kumuona kwenye kamera za ulinzi za jengo. "Nilikuwa nina shida ya kuonana na Bwana Nadeem sasa kila ninavyojitahidi sipati nafasi ndio nikaamua bora nije nimtegee hapa, samahani sana nimekosa" alijieleza kwa ufasaha alishajua kimenuka tayari. "Angalia bwana mdogo utapata matatizo bure Bosi anatumia lifti ya peke yake inayoenda moja kwa moja mpaka ndani ya ofisi yake. Kama una shida nae rasmi nenda kwa sekretari wake uombe nafasi utakuja kupata matatizo bure" aliongea mmoja wa wale wana usalama. "Haya potea haraka sana eneo hili mara moja" alitoa amri mlinzi mwingine, amri ambayo ilimfanya Shebby aondoke haraka eneo lile la jengo akiwa ameshakata tamaa. Kigiza cha magharibi kilikuwa kinaanza kuinyemelea anga.
ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog