Search This Blog

Wednesday 29 March 2023

PENIELEA (3) - 4

  





Simulizi : Peniela (3)

Sehemu Ya Nne (4)



“ Amos is dead” “Amos is dead? how?Who killed him?

“ Mpaka sasa haijafahamika ni nani lakini inaonyesha aliyemuua is very professional assassin”

“ Mungu wangu ! !!Dr Joshua akastuka

“ tuki hilo limetokea muda gani? Mbona asubuhi ya leo nimewasiliana na Amos ?

“ Tukio limetokea mchana wa leo Mlimba lodge”Zikapita sekunde kadhaa kisha Dr Joshua akasema “Nimestushwa sana Kigomba kwa taarifa hizi.Ngoja nizungumze na mkuu wa polisi nifahamu kama kuna hatua yoyote imefikiwa kuchunguza waliomuua Amos.Kigomba kwa mara ya kwanza nimeogopa sana.Kama Amos ameuawa basi watu walionfaya hivyo wako karibu sana kutufikia na sisi pia.Please make sure hakuna kitu chochote ambacho kinaweza kutuunganisha sisi na Amos.Kigomba this is a very serious matter and take it very seriously.Nitakupigia baada ya masaa mawili kujua kinachoendelea na tutaongea zaidi”

“ sawa Mr President lakini wa mujibu wa taarifa za polisi watu waliofanya mauaji hayo wameondoka na kompyuta na simu ya Amos.” “Kigomba something is going on.Kuna kitu kinatafutwa kwa Amos.We need to hurry.Tunatakiwa tuimalize biashara yetu haraka iwekanavyo .Ntakupigia tena baadae kidogo”akasema Dr Joshua na kukata simu.



“ Vifo vilivyotokea mfululizo vimemuogopesha sana Dr Joshua nandiyo maana anataka kuitoa package hiyo haraka kwani ana wasiwasi kwamba kuna watu wengine wanaoitolea macho package hiyo.Kwa maelezo yake mwenyewe alikiri kwamba anataka makabidhiano yafanyike haraka pindi tu akirejea kutoka afrila ya kusini kwani tayari pesa imekiwsha ingizwa katika akaunti zao za sri walizofungua nje ya nchi.Amemtaja Hussein kwamba atawasili kesho jioni na huyu inaonekana ndiye ambaye anakuja kukabidhwa package hiyo.Kwahiyo jamani ile kazi yetu ya msingi iko mbioni kukamilika.Umakini wa hali ya juu sana unahitajika.Tutakaa na kulijadili hilo baadae kidogo lakini kwa sasa tuanze kumuandaa Peniela kwa ajili ya kwenda kuonana na Deus Mkozumi.” Akasema Mathew kisha akamuomba jaji Elibariki aongozane naye wakaelekea katika chumba alimo Rosemary.Mara tu walipoingia mle chumbani Rosemary akastuka sana baada ya kumuona jaji Elibariki “I know you !! akasema Rose. “ unanifahamu? Akauliza jaji Elibariki.Hakutegemea kama Rose angemtambua

“ Elibariki ,right? Jaji Elibariki..Ninakufahamu sana.Kumbe na wewe uko na hawa mashetani.Who are you guys? Akauliza Rose akishangaa sana kumuona jaj Elibariki pale. Mathew akafungua mlango uliokuwa pembeni na ndani ya chumba kile kukaonekana vifaa mbalimbali akatoa kiti cha magurudumu na kukisogeza karibu na kitanda alicholazwa Rose.Akamfungua pingu na kumuomba Elibariki amsaidiea kumuinua Rose wakamuweka katika kile kiti.

“ Mnanipeleka wapi? Akauliza Rose.Mathew akakisukuma kiti kile hadi chumbani kwake halafu akaenda katika kisanduku Fulani kilichokuwa ukutani kilichokuwa na muundo kama simu akabonyeza namba kadhaa na mara kabati kubwa la vitabu likasogea pembeni na ukaonekana mlango.Mathew akaufungua ule mlango nakulionekana kuna ngazi za kushuka chini.Mathew akamuamuru Elibariki amfuate waksshuka ngazi kuelekea chini..Elibariki na Rose wakabaki wanashangaa.

“ who are you ? Hii nyumba ya chini ni kwa ajili gani?akauliza Rose lakini Mathew hakumjibu kitu..Waliingia katika chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na kitanda kikubwa meza ya kulia chakula,meza ya kusomea,kabati kubwa la nguo bila kusahau Luninga kubwa iliyokuwa ukutani.Wakamnyanyua Rose na kumuweka kitandani.

“ Rose suala lako uliloliomba tunalishughulikia na litakapokuwa tayari tutakutaarifu lakini mpaka wakati huo this will be your new home.Hii ni nyumba iliyoko chini ya ardhi .Nobody will know you are here.Usihofu sisi si watu makatili kama unavyodhani lakini huwa tunalazimika kuwa wakali kwa watu kama ninyi ambao mnashirikiana na magaidi.Kwa sasa pumzikanitakuwa na maongezi nawe baadae” Akasema Mathew huku akimfunga pingu za mikono na miguu.

“ Mpaka lini mtaendelea kunifunga pingu hizi ? akauliza kwa ukali Rose

“ Mpaka hapo tutakapopata kila tunachokihitaji toka kwako”akasema Mathew.

“ tafadhali naomba msinifunge namna hii,.Mnanitesa sana.Vipi kama nikihitaji kujisaidia “ akaomba Rose

“ Jisaidie hapo hapo.You deserve to be in chain mpaka hapo rais atakaporejea na hatujui atarejea lini yawezekana ikawa ni kesho,wiki ijayo,baada ya miezi au hata mwaka “ akasema Mathew na kisha wakatoka mle chumbani wakimuacha Rose akiangua kilio

“ Mathew umejiandaa sana.Sikutegema kama nyumba yako inaweza kuwa na mambo mengi ya siri namna hii”akasema Elibariki

“ Kutokana na kazi ninayoifanya,nimelazimika kutengeneza nyumb aiwe namna hii ili kuniwezesha kufanya kazi zangu bila wasiwasi.”akasema Mathew wakati wakipanda ngazi kurejea sebuleni.Wakaelekea ofisini alikuwemo Anitha peke yake.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ peniela yuko wapi? akauliza Mathew

“ Nimempeleka chumbani anajaribu mavazi,can you check on her Mathew if she’s ready ? kuna kitu ninamalizia katika komyuta hapa”akaomba Anitha..Mathew akatoka na kuelekea katika chumba cha Anitha akaufungua mlango na kuchungulia ndani.Akapatwa na mstuko wa ghafla kwa alichokiona ndani..Peniela alikuwa amegeukia katika kioo akijipodoa.Alikuwa na nguo za ndani pekee.

“ ouh my gosh ! akasema Mathew kwa sauti ndogo na kubaki anamkodolea macho binti Yule mwenye uzuri usioelezeka..

“ Ndiyo maana kumbe wanaume wanachanganyikiwa kwa ajili yake.She’s hot !!

akawaza huku akiwa amejisahau kabisa akiendelea kumtazama Peniela..Kupitia kioo cha kujitazamia Peniela alimuona Mathew namna alivyostuka baada ya kumkuta katika hali ile.Hakutaka kumstua akamuacha aendelee kumtazama. kwa makusudi akainama kujipaka mafuta miguuni.Mathew akaufunga mlango na kusimama pale nje kwa sekunde kadhaa

“ Dah ! Kitu gani kimeniambia nije huku chumbani hadi nimekutana na mambo haya? Nimekwisha mzoea Anitha mara nyingi tu huwa ninamshuhudia akiwa mtupu lakini hakuna chochote kinachonitokea ila kwa peniela imekuwa tofauti kabisa.Nimepata msisimko wa ajabu.This woman have got smething special to attract men” akawaza na kupiga hatua za haraka haraka kuelekea chumbani kwake kwani tayari ikulu kulikwisha kasirika na mambo yalikwisha haribika..Haraka haraka akaingia bafuni akaoga na kubadili nguo kisha akafungua kasiki lake ambalo huhifadhia vifaa mbalimbali na silaha akachagua vitu ambavyo wangevihitaji kwa usiku ule na kutoka akaeleka ofisini ambako Anitha alikuwa anamalizia kuweka sawa program kadhaa katika kompyuta yake..

“ is everything ready? akauliza Mathew

“ Nimeshamaliza kuweka kila kitu tayari.” Akasema Anitha. Na mara akatokea Peniela akiwa katika gauni jeusi la Anitha lililomkaa vyema sana.

“ dah ! Peniela !! Huyu mwanamke amebarikiwa uzuri wa ajabu sana.Sikuwahi kuifahamu siri yake ya kuwadatisha wanaume kiasi hiki leo nimegundua.Mtoto huyu akiwa hana nguo huwezi amini ni binadamu wa kawaida.She looks like an angel”akawaza Mathew huku akimtazama Peniela

“ hello Mathew How do I look?akauliza Penela

“ You look wonderful..unafanana sana na malaika” akasema Mathew na wote wakacheka.

“ Anitha mimi niko tayari sasa ni zamu yako kuniandaa”akasema Peniela.Anitha akafungua kisanduku kidogo akatoa vidude Fulani vinne kama vispika vidogo akachukua kimoja na kukipachika sikioni kwa Peniela halafu kingine akampatia Mathew na kingine akaweka katika sikio lake

“Hivi ni vifaa vya mawasiliano ambavyo vitawezesha kuwasiliana .Kupitia vifaahivi tutasikia kila utakakachokiongea na Deus na sisi tutakuongoza nini ukiseme .Usifanye chochote bila ya maelekezo yetu.”akasema Anitha halafu akafungua kiboksi kidogo akatoa kijiua kidogo cheusi akakipachika katika sehemu ya titi la kulia .

“ Hili ukilitazama ni kama ua linaloongeza urembo katika nguo uliyovaa lakini kidude hiki katikati ya ua kinachoonekana kama pini ya ua ni kamera ambayo ndiyo itatuwezesha sisi kutazama kila kitu kitakachofanyika ukiwa na Deus.Kwa kujaribu Mathew mpeleke chumbani kwa Naomi akaongee naye jambo lolote ili tuijaribu kamera” .Akasema Anitha

“ Lets us go.I’ll show you the room” akasema Mathew na kumuongoza Peniela kueleka katika chumba cha Naomi akagonga mlango Naomi akafungua Peniela akaingia Kila walichokiongea Peniela na Naomi kikaonekana katika kompyta ndogo ya Anitha

“ Kila kitu kinakwenda vizuri .kwa upande wangu nimemaliza”akasemaAnitha.Mathew akamfuata Peniela chumbani kwa Naomi akamtaarifu kwamba kila kitu tayari na wanaweza wakaondoka halafu akaongea na Naomi akamfahamisha kwamba wanatoka kidogo kuna mahala wanaelekea na watarejea baadae kisha akatoka hadi katika nyumba yake ya magari akatoa gari moja ambao hulitumia mara chache sana.Mle ndani alikuwa na magari sita

“ hili ndilo gari analostahili kulitumia Peniela leo.Anastahili gari kama hili.She’s ana angel”akawaza Mathew akilijaribu gari.Aliporidhika liko vizuri akarejea ndani.

“ Kila kitu tayari we can leave now.Elibariki utaangalia kila kitu hapa ndani.Utamuangalia Naomi na endapo kuna tatizo lolote utatujulisha mara moja kwa kutumia simu ile ofisini” akasema Mathew

“ Mathew tafadhali kuwa makini sana.Take good care of peniela. “ akasisitiza Elibariki “ I will” akasema Mathew.Elibariki na peniela wakakumbatiana kwa muda

“ Please be carefull Peniela.”akasema Elibariki

“ I will Eli” akajibu Peniela akumbusu Elibariki kisha akaongozana na Mathew na anitha kueleka nje.Peniela akaingia katika gari aliloandaliwa na kutangulia.Mathew na Anitha wakafuata nyuma yake.Elibariki akafunga geti na kurejea ndani akajilaza sofani. Mawazo mengi kuhusiana na kinachoendelea.

“ Sikuwahi kuota kama siku moja maisha yangu yanaweza yakabadilika na kuwa hivi..Mtu niliyekuwa ninaheshimika leo hii nimejificha humu ndani ninasakwa kila kona ya nchi..” Mara Elibariki akastuliwa toka mawazoni na mtu aliyeingia pale sebuleni alikuwa ni Naomi.

“ Hallow” akasema Naomi

“umenistua sana ,nilikuwa nimezama katika mawazo mengi.”akasema jaji Elibariki.

‘” Pole..”akajibu Naomi huku akicheka kidogo kisha akaenda kuketi sofani

“ Wamekwenda wapi akina Peniela?akauliza Naomi

“ Kuna mahala wamekwenda na watarejea muda si mrefu sana.Kuna kitu unahitaji? Chakula tayari kipo jikoni.Mfumo wa hapa ukihisi njaa unakwenda mwenyewe jikoni unatafuta chakula unachokitaka unakula.Vyakula vingi vya hapa ni vya maboksi .Ndani ya nyumba hii watu wanafanya kazi muda wote kiasi kwamba hawakumbuki hata kula kwa hiyo kama unahisi njaa tafadhali nenda jikoni utaangalia wewe mwenyewe unataka kula kitu gani” akasema jaji Elibariki.

“ Nadhani nyumba hii mnahitaji sana mtu wa kuwasaidia,kuwapikia n.k.Sura zote zinaonekana sura za kazi .Kesho nitakwenda kununua mahitaji ya ndani.Hamuwezi mkafanyakazi mkasahau kula..Anyway tuachane na hayo wewe ni jaji si ndiyo?

“ Ndiyo mimi ni jaji wa mahakama kuu.naitwa jaji Elibariki.”

“ Nimefurahi kukufahamu.Mbona hukuambatana na akina Mathew? Akauliza Naomi

“ Sitakiwi kuonekana huko nje”akajibu Elbariki kwa ufupi

“ Unatafutwa? Ulifanya nini?

“ Ni hadithi ndefu sana ambayo siwezi kukuelezea kwa sasa” akajibu Elibariki.Kikapita kimya kifupi Naomi akauliza

“ Mke wako anafahamu kama unaishi hapa?

“ Sina mke” akajibu Elibariki

“ Huna mke? Naomi akashangaa

“ Ndiyo sina mke kwa sasa.She’s dead”akasema Elibariki.

“ Pole sana jaji .Sikulifahamu hilo.” Akasema naomi

“ yah ni mapenzi ya Mungu.”

" Kwa hiyo una mpango gani hivi sasa kuhus maisha yako? Hufikirii kuoa tena?bado kijana sana” Akauliza Naomi

“ kwa sasa ni mapema sana kusema chochote kuhusu mpango wa kuoa tena kwa sababu hata mke wangu bado hajazikwa” akasema Elibaliki na kumstua sana Naomi

“Ina maana amefariki si muda mrefu?

" Asubuhi ya leo” akajibu Elibariki “leo ?!! Naomi akazidi kushangaa “Ndiyo .”

“ Kwa hiyo huruhusiwi hata kuhudhuria msiba? “ kama nilivyokwambia awali kwamba siruhusiwi kabisa hata kuonekana huko nje.Ninasakwa kila kona”

“Ulifanya nini?

“ni hadthi ndefu sana .Nitakusimulia siku nyingine.”

“ jamani pole sana jaji.Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu.” Akasema Naomi na kuinuka akelekea jikoni akafungu fungua makabati kuangalia kuna kitu gani ambacho wanaweza kula kwa usiku ule

“ Kweli hii ni nyumba ya watu wa kazi .Vyakula vyao vyote ni vile vya makopo.Nataka nimtengenezee jaji Chakula aweze kula..Kwa hali aliyo nayo anatakiwa apate chakula ili awe na nguvu.Namuonea huruma sana yule kaka.Kufiwa si jambo dogo” akawaza Naomi huku akiwasha jiko na kuanza kutengeneza chakula.

“ Ninamshukuru sana Mathew kwa kuniweka huru kasi hiki.Nitafurahi sana kama nikiendelea kukaa hapa kwake siku zote.Ninahisi amani sana nikiwa ndani ya numba hii.Mathew ni mtu mzuri na ana moyo wa huruma.Hata watu anaofanya nao kazi vile vile ni watu wazuri sana.” Akawaza Naomi na mara akamkmbuka Elibariki

“He’s so handsome…sijui kwa nini ametokea kunivutia sana yule jaji...Nitajitahidi nijenge ukaribu naye..” akaendelea kuwaza Baada ya kama dakika kumi na tano chakula kikawa tayari akabeba sahani mbili na kwenda nazo sebuleni.

‘” jaji karibu chakula” akasema “ Wow Naomi kumbe ni mpishi mzuri .Chakula kinanukia sana.lakini hata hivyo ahsante sina hamu ya kula.” Akasema jaji Elibariki

“ jaji lazima ule chakula ili upate nguvu ya kukabiliana na wakati huu mgumu ulio nao” akasema Naomi

“ Naomi najitahidi sana kujilazimisha lakini chakula hakipiti.” Akasema Elibarii

“ sawa jaji naomba nikulishe mimi kwa mkono wangu kitapita tu”akasema Naomi na kwenda kukaa karibu na jaji Elibariki akachukua kijiko na kumuwekea jaji Elibariki chakula mdomoni.Elibariki akacheka kidogo kisha akasema

“ Ahsante sana Naomi.naomba niendelee kula mwenyewe.” Akasema jaji Elibariki

“ hapana jaji.Kaa utulie .Nataka nihakkishe umekula chakula chote hiki umekimaliza” akasema Naomi na kuendelea na zoezi lake na akahakikisha Elibariki amemaliza chakula chote

“ nashukuru sana mdogo wangu kwa chakula.Bila wewe nisingekuwa na nguvu ya kutia chochote tumboni.”akasema jaji Elibariki. Waliendelea kukaa pale sebuleni wakitazama filamu kisha Naomi akasema

“ Its bored in here.twende tukakae pale katika bwawa la kuogelea” Jaji Elibariki hakupenda kwenda nje lakin Naomi akamshika mkono akamvuta naakakubali kuinuka wakaeleka katika bwawa la kuogelea ,. “ Unajua kuogelea? .” akauliza Naomi

“ ndiyo ninaweza lakini nina muda mrefu sana sijaogelea”

“ Ok let’s swim.” “Not today naom......“ Kabla hajamalizia sentensi yake Naomi akamsukumia Elibariki ndani ya maji naye akajitupia majini na kuzama chini kisha akaibuka na kumfuata Elibariki aliyekuwa amejiegemeza katika kingo za bwawa lile

“ Naomi mbona we mtundu sana.Nimekwambia leo sijisikii kuogelea” akasema jaji Elibariki

“ najua una matatizo jaji hata mimi nina matatizo yangu tenamakubwa tu lakini pamoja na matatizo tuliyonayo ninataka uchangamke na uondoe mawazo.Maisha lazima yaendelee.”akasema Naomi na kumsogelea Elibariki.Wakaangaliana usoni kwa sekunde kadhaa.halafu kiuchokozi akaupeleka mkono wake kunako ikulu ya Elibariki

“ Naomi unafanya nini?

“ Shhhhh !!!.akasema Naomi

“ watu wote hawapo tuko peke yetu hakuna ubaya kama tukistarehe nakupunguza mawazo tuliyo nayo.” Akasema Naomi huku akiendelea kumchezea Elibariki maungoni



“ Naomi unafanya nini? Tafadhali acha huo mchezo “ akasema jaji Elibariki na kuutoa mkono wa Naomi uliokuwa katika maeneo yake nyeti. “ Naomi tafadhali jaribu kuwa na heshima.Huu ni ukosefu mkubwa wa adabu.Mimi ni kaka yako mkubwa na hutakiwi kabisa kufanya hivi unavyofanya” akasema jaji Elibariki

“ Jaji unaogopa nini? Usiogope jaji tuko peke yetu na hakuna mtu yeyote atakayetuona wala atakayefahamu suala hili.Jaji mwenzio mwili unawakA moto.Nimefungiwa ndani kwa zaidi ya miaka minne na kwa muda huo wote sijawahi kukutanA na mwanaume yeyote Yule.Jaji tafadhali naomba unisaidie mwenzio nina hali mbaya sana” akasema Naomi huku akiweweseka.Alionyesha wazi kwamba alihitaji sana kukifanya kitendo kile kwani tayari alikwisha vua nguo zake na kubakiwa mtupu na sasa alianza kuivua nguo ya jaji Elibariki.

“ Hizi balaa gani ninakutana nazo jamani? Yaani kila kukicha kuna mambo mapya yanaibuka.Kabla hili halijamaliziKa lInaibuka lingine.Wakati hata machungu ya mke wangu hayajanitoka tayari ameibuka huyu mtoto ambaye sijui katokea wapi na anataka aniongezee matatizo” akawaza jaJi Elibariki huku Naomi akiendelEa kuufungua mkanda wa suruali yake na kuishusha halafu akamrukia.Kwa nguvu jaji Elibariki akamsukuma Naomi akaangukia ndani ya maji kisha akatoka nje ya bwawa .

“ Naomi naomba tafadhali ukitaka kuishi kwa amani humu ndani jitahidi uwe na heshima kwa watu wote na usilete tabia zako mbovu humu ndani.Humu ndani sote ni watu na heshima zetu na heshima imetawala kwa hiyo naomba sana ujiheshimu” akasema jaji Elibariki kwa ukali huku akielekea ndani akiwa ameloa chapa chapa.Naomi naye akatoka majini akaelekea ndani .Alikuwa mtupu kabisa.

“ Miaka zaidi ya minne sijakutana na mwaume ,leo sintakubali lazima Elibariki aniondolee kiu yangu hii.Mwili wote unanichemka na siwezi kulala na hali hii.I swear Elibariki akikataa nitaruka hata geti niende nje nikatafute mwanaume yeyote Yule anitimizie haja zangu “ akawaza Naomi na kwenda hadi katika mlango wa chumba cha jaji Elibariki akagonga .. “ Naomi unataka nini lakini we mtoto? Akasema jaji Elibariki kwa ukali

“ jaji fungua tuongee,usinifanyie hivyo” Akasema Naomi

“ Naomi tafadhali naomba uende chumbani kwako ukalale usinitafutie matatizo zaidi wakati huu ambao nina matatizo lukuki.Matatizo niliyonayo yananitosha naomba tafadhali usiniongezee matatizo zaidi ” akasema jaji Elibariki

“ Jaji naomba unisaidie mwenzio nina hali mbaya .Ninahitaji sana mtu wa kuniondolea taabu hii leo.Siwezi kulala na hali hii leo.Tafadhali jaji naomba unisaidie.” Akasema Naomi huku akiendelea kuugonga mlango wa jaji Elibariki.Kwa hasira jaji Elibariki akaufungua mlango na kustuka sana alipomkuta Naomi hana nguo hata moja

“ Naomi hii ni tabia gani ya kuvua nguo na kubaki mtupu? Tafadhali usitulete tabia zako za huko mtaani humu ndani.Hakuna mtu anayevuta unga humu ndani .Vaa nguo zako haraka sana” akasema kwa ukali jaji Elibariki

“ Elibariki kwa nini unanitukana kiasi hiki? Kwa kuwa umenitukana na kunikashifu basi utaamini kwamba mimi ninakula unga.Nitakaa hivi hivi hadi Mathew atakaporejea na nitamueleza kwamba ulitaka kunibaka” akasema Naomi huku akielekea sebuleni

“ Mungu wangu haya ni mambo gani yananitokea mimi? Kwa nini kila wakati ni majaribu tu yananijia? Akasema jaji Elibariki.

“ Mathew kamtoa wapi huyu mtoto nusu kichaa? Kwa nini anataka kunisababishia matatizo? Akawaza Elibariki na kuufunga mlango wa chumba chake na kukaa kitandani “ Naomi ni binti mzuri sana lakini kwa nini anakuwa na tabia chafu kiasi hiki.Hana aibu hata chembe.Haogopi hata utofauti wa kiumri kati yetu ananiona ni kama mtu wa rika lake na anasisitiza kabisa kwamba lazima nifanye naye mapenzi.Ee Mungu nisaidie niweze kutoka haraka ndani ya jumba hili.” Akaendelea kuwaza jaji Elibariki na mara akainuka kitandani “ Naomi anaweza kweli akaja kumweleza Mathew kwamba ni kweli nimetaka kumbaka.Hana aibu Yule mtoto.Na kwa mazingira watakayomkuta nayo lazima wataamini kwamba ni kweli nimetaka kumbaka Yule mtoto.Nafahamu hata kama nikijitetea vipi hawatanielewa kabisa.Sasa nitafanya nini? Akajiuliza akatoka mle chumbani akamfuata Naomi sebuleni.

“ Naomi naomba uvae nguo zako tafadhali.Jiheshimu na usifanye ujinga huo unaotaka kuufanya” akasema jaji Elibariki

“ Jaji umenidharau sana na kunitusi pia sasa nataka nikuonyeshe kwamba mimi na wewe nani ana akili kumshinda mwenzake.Nitakaa hivi hivi hadi hapo Mathew na dada Anitha na Peniela wakatakaporejea nitawaeleza kwamba umetaka kunibaka ndani ya bwawa la maji.” Akasisitiza Naomi

“ Naomi kwa nini lakini unafanya hivi? Kwa nini unataka kunichafulia jina na heshima yangu?

“ Jaji naomba uondoke mbele yangu na tusubiri hadi Mathew arudi” akasema Naomi huku akitanua miguu yake.Jaji Elibariki mwili ukamsisimka.

“ Naomi anataka nifanye kitu ambacho sikuwa nimetaka kukifanya.Kwa kuwa ametaka mwenyewe ngoja nimuonyeshe kazi” akawaza jaji Elibariki na kuivua bukta aliyokuwa ameivaa akaitupa pembeni akamfuata Naomi pale katika sofa kama mbogo majeruhi akamuinua . “ Si umesema unataka nikukate kiu yako ya miaka minne? Haya njoo nikuonyeshe kazi” akasema jaji Elibariki na bila kukawia akaanza shughuli kwa kasi ya ajabu.Naomi alitoa kilio kikubwa kama vile anapigwa.



********************



Iyumba country club ni moja ya klabu ambayo huwakutanisha mabilionea na vigogo wakubwa wa serikali . Ulinzi nje na ndani ya klabu hii ni mkubwa sana na walioruhusiwa kuingia ndani ya klabu hii ni wanachama waliosajiliwa tu ambao huilipa kiasi kikubwa cha ada kila mwaka.

“ Mathew nimefika katika kibao cha Iyumba country club.Ninakata kushoto na kuishika bara bara inayoelekea klabuni” Paniela akawataarifu akina Mathew.

“ Ok Peniela tuko nyuma tunakufuata.Tunaangalia kila kitu kwa umakini” akasema MathewPeniela akaukunja kushoto na kuifuatilia bara bara iliyokuwa inaelekea Iyumba country club.Barabara ilizungukwa na taa za rangi mbali mbali na maua ya kupendeza.

“ Ninakaribia geti la kwanza” akasema Peniela na kupunguza mwendo wa gari katika kizuizi cha kwanza.Kulikuwa na walinzi zaidi ya watano na wote walikuwa na silaha.Peniela akashusha kioo cha gari baada ya mlinzi mmoja kumsogelea.Akamsalimu kwa adabu sana na kumuomba kadi yake

“ Mgeni namba ishirini na saba.” Akasema Peniela na yule jamaa akamruhusu apite

“ Jamaa wamejizatiti sana kiulinzi .Hii ni kwa sababu watu wanaokuja hapa ni watuwenye nyadhifa na uwezomkubwa.” akawaza Peniela na baada ya mwendo mfupi akakutana tena na kizuizi cha pili.Akataja namba ya utambulisho na akaruhusiwa kupita .Hatua kadhaa mbele akakutana na kizuizi cha tatu.Kama kawaida akataja namba ile ya utambulisho akaelekezwa sehemu ya kwenda kuegesha gari.Geti likafunguliwa akingia ndani.Ilikuwa ni sehemu nzuri mno yenye mandhari ya kuvutia sana. Magari ya kifahari yalikuwa yamejipanga. I’m getting out of the car now.” Peniela akawataarifu akina Mathew kisha akaufungua mlango wa gari akashuka.Mara tu aliposhuka akakutana na mwanadada mmoja mrembo sana aliyevalia nadhifu ambaye alikuwa tayari kumpokea na kumpeleka sehemu anayotakiwa.Mwanadada Yule akamsalimu kwa adabu kubwa na kumuuliza alikuwa anaelekea wapi.Peniela akajitambulisha kisha yule mwanadada akamchukua hadi sehemu ya mapokezi ambako alikabidhiwa kwa mwanadada mwingine ambaye akamuomba waongozane kuelekea mahala anakohitajika .Sura zilizoonekana humu ni sura za matajiri .kulikuwa na burudani ya kila aina Walivuka vyumba kadhaa halafu akatokeza katika mlango mkubwa wenye maandishi VVIP.Yule mwanadada akawasalimu walinzi waliovalia nadhifu wakaufungua mlango wakaingia na kuelekea moja kwa moja katika chumba chenye namba ishirini na saba,Nje ya chumba kile kulikuwa na walinzi wawili ambao walimsalimu Peniela kwa adabu kisha mmoja wao akachukua kifaa cha kukagulia akamkagua Peniela kama alikuwa na silaha yoyote na waliohakikisha kwamba hana silaha yoyote akaufungua mlango wakaingia ndani. Chumba kilikuwa na mwangaza mwekundu na masofa mazuri meupe.Katika mjawapo ya sofa mzee mmoja alikuwa amezungukwa na wanawake wawili.Mara tu mlinzi wake alipingia mle ndani akiwa ameogozana na Peniela mzee yule akawaamuru wale wanawake aliokuwa nao watoke nje kwa muda kwani ana mgeni muhimu .Wasichana wale waliovalia mavazi mafupi wakamtazama Peniela kwa macho makali kisha wakatoka nje.

“ Hallow Peniela” akasema Yule mzee “ Deus Mkozumi.Shikamoo” akasalimu Peniela.Deus akamfanyia ishara mlinzi wake naye atoke nje wakabaki wawili tu mle chumbani.

“ Shikamoo mzee “ Peniela akamsalimu Deus

“ Marahaba Peniela.Karibu sana”

“ Ahsante sana” akasema Peniela na kuketi katika sofa lililotazama na Deus.

“ Welcome to Iyumba country club.We call this a paradise on earth.Have you ever been here before? Akasema Deus

“ hapana Deus sijawahi kufika hapa hata mara moja.Ni mara yangu ya kwanza leo kufika hapa.Its a nice place nimepapenda sana:”

“ Ndiyo maana inaitwa Eden ya duniani. kila aina ya starehe unayoifahamu katika hii dunia hii inapatikana humu..Karibu sana Peniela.Nimefurahi sana kukutana nawe jioni ya leo na ninaweza nikasema ni bahati sana kukutana na malaika kama wewe sehemu kama hii.Unatumia kinywaji gani? Akauliza Deus Mkozumi.

“ Mvinyo mwepesi tafadhali” akasema Peniela.Deus akainuka na kuchukua chupa ya mvinyo akamimina katika glasi na kumpatia Peniela ambaye alitoa tabasamu pana sana

“ What a beautfull lady.Nilikuwa ninamsikia tu lakini sikuwahi kukutana naye ana kwa ana.Ninakiri kwamba msichana huyu ni mzuri na ndiyo maana hata Dr Joshua alichanganyikiwa kwa uzuri wake.lakini pamoja na uzuri wake huu she’s a snake !!” akawaza Deus akiendelea kumkodolea macho Peniela

“ Can you have a sit Mr President so that we can talk? Akasema Peniela na kumstua Deus

“ Ouh Sorry.” Akasema Deus na kuketi sofani akaendelea kumtazama Peniela “ Mr Presdient” akasema Peniela.

“ No peniela just call me Deus.Tukiwa sehemu kama hii hatutumii vyeo vyetu.Only Deus inatosha sana na nitafurahi kama ukiniita hivyo”akasema Deus .Peniela akatabasamu na kuipeleka glasi ya mvinyo mdomoni akanywa kidogo.

“ Peniela ! akaita Anitha.

“ We’re watching everything.Deus tayari ameonyesha matamanio .Amekwisha onyesha udhaifu mapema sana itumie vizuri nafasi hiyo.make him fall for you” akasema Anitha akiwa na Mathew ndani ya gari wakifuatilia kila kinachoendelea kati ya Peniela na Deus kupitia kamera ya siri aliyoivaa Peniela.Huku akitabasamu Peniela akaupandisha mguu wake wa kulia juu ya mguu wa kushoto na paja lake likaonekana .

“ Wow ! Huyu msichana anajua sana kuchota akili za watu.Mbona ninachanganyikiwa mapema namna hii? Akawaza Deus baada ya kuushuhudia upaja wa Peniela

“ Deus ! akasema Peniela

“ kwanza kabisa ninakushukuru sana kwa kuacha shughuli zako nyingi na kuitika mwito wangu.Umenipa heshima kubwa sana.Mtu mkubwa kama wewe kuahirisha shughuli zako zote na kuja kuniona mtu kama mimi si jambo dogo.Ahsante sana kwa hilo “akasema Peniela

“ Peniela nisingeweza kukosa kuja kuonana na malaika kama wewe .Nimefurahi sana kukutana nawe.Nilikuwa ninakusikia tu lakini leo hi nimepata bahati ya kuonana nawe ana kwa ana,moyo wangu umejaa furaha sana.Nimekubaliana na yale yote niliyokuwa ninaambiwa kuhusu wewe” akasema Deus

“ mambo gani uliyoambiwa kuhusu mimi?

“ Niliambiwa kwamba peniela ana uzuri wa kipekee kabisa na kweli nimelithibitisha hilo.You are a living angel” akasema Deus na kumfanya Peniela atabasamu “ Thank you.”

“ Peniela go straight to the point.Usimpe nafasi kubwa ya kujieleza hisia zake.”Anitha akamwambia Peniela

“ Deus ,kama nilivyokueleza simuni kwamba nina mambo ya msingi sana ambayo ninataka kuzungumza nawe.”akasema Peniela

“ Ndiyo peniela ninakusikia.” Akasema Deus “Nilipewa mawasiliano yako na captain Amos” akasema Peniela na Deus akaonyesha mstuko kidogo

“ Amos yupi? Akauliza Deus

“ Amos ambaye umekuwa unamtumia kupata habari na taarifa toka ikulu “ akasema Peniela

“ I don’t know any Amos” akasema Deus.

“ Peniela muulize kama kuna kamera yoyote humo chumbani” Mathew akamuelekeza Peniela

“ Deus is there any camera in this room? Peniela akauliza

“ no ! why? Akauliza Deus

“ Ninataka tu kufahamu kama kuna kamera inayokufanya uogope..Kama hakuna kamera basi tuongee kwa uwazi I’m here because I know something you don’t know and I want something from you.Kwa hiyo hiki ni kikao chenye faida kwetu sote” akasema Peniela.Deus akanywa mvinyo kidogo na kusema

“ Peniela narudia tena kukuhakikishia kwamba simfahamu huyo Amos unayemsema na kama alikwambia lolote kuhusu mimi alikudanganya.Naomba tuongee mambo mengine yanayohusu maisha yetu.Kwa sasa unafanya kazi gani? Akauliza Deus

“ Unanifurahisha sana Deus.Well ! let me be honest with you.Nina ushahidi wa mawasilino yako yote na Amos,ninaufahamu mpango wenu wa kuipata package muhimu toka kwa Dr Joshua.Ninamfahamu aliyemuua Amos,ninafahamu mahala alipo mke wako wa zamani Rosemary Mkozumi ,ninayafahamu mambo anayoyafanya kwa ujumla ninafahamu mambo mengi kuhusu wewe.kwa nini basi tusiokoe muda na kuzungumza mambo ya msingi ? akasema Peniela.Deus akabaki kimya akimtazama akainua glasi yake akanywa na kusema

“ Nimefurahishwa na ujasiri wako Peniela.Sijawahi kukutana na msichana jasiri na mwenye upeo kama wewe.Hii inanifanya nikupende zaidi na zaidi ”akasema Deus na kunywa funda la mvinyo.

“ Kama ulivyosema kwamba hatuna sababu ya kupoteza muda,tuendelee na mambo ya maana.Kama wewe unavyonifahamu vizuri Peniela hata mimi ninakufahamu vizuri pia.Ninafahamu unashirikiana na Team SC41 ,ninazifahamu kazi zenu na toka nikiwa rais nilikifahamu kikundi hiki na ni mimi niliyetoa ruhusu kifanye kazi hapa nchini ya kusimamia uwekezajimkubwa uliofanywa na serikaliya marekani lakini kwa usiri mkubwa bila kuvunja sheria za nchi.Ninafahamu matatizo uliyoyapata ya kusingiziwa kesiya mauaji,ninafahamu kwa sasa uko katika mahusiano na jaji Elibariki,ninamfahamu Johnmwaulaya alikuwa ni rafiki yangu wa siri na wakati wa uongozi wangu alinisaidia mambo mengi niliyohitaji kuyafanya kwa siri.kwa ujumla ninafahamu mambo mengi kuhusu wewe” akanyamaza akanywa pombe yake katika glasi na kuendelea.

“ Amos amekuwa ni kijana wangu kwa muda mrefu na kifo chake kimeniumiza sana.Amekuwa akinipa kila taarifa za kinachoendelea ikulu na siku kadhaa zilizopita alinipa taarifa kwamba kuna watu ambao wanataka kumuua jaji Elibariki nikampa maelekezo kwamba afanye kila linalowezekana ili kumuokoa Elibariki kwani tuna mipango naye mikubwa.Amos alijitahidi kwa kila alivyoweza na kufanikiwa kumuokoa Elibariki akamkabidhi kwako” akasema Deus.

“ You knew about that? Akauliza Peniela kwa mshangao

“ Yes I knew na mimi ndiye niliyetoa amri Elibariki aokolewe.” Peniela akabaki anashangaa.Mathew na Anitha ndani ya gari pia wakatazamana.



“ Elibariki was saved by a woman.Do you know her? Akauliza Peniela

“ Nilimpa maagizo Amos ya kuhakikisha kwamba Elibariki hadhuriki katika tukio hilo lililopangwa na watu wa Dr Joshua kwa hiyo sifahamu aliokolewa vipi na nani.Nilichohitaji mimi ni jaji awe mzima tu so to answer your question I don’t know her” akajibu Deus.Peniela akanywa mvinyo kidogo kisha akauliza

“ Why you saved him? Deus Mkozumi akamtazama Peniela kisha akainuka akaeleka katika kabati la kioo lililokuwa na chupa kadhaa za pombe kali akalifungua na kuchukua chupa moja akaitazama na kutabasamu

“ This whisky is called Labellion.Its one among the expensive whisky on earth.,”akasema na kuitazama tena ile chupa.

“ Aliyeitengeneza whisky hii anaitwa David Labellin aliyekuwa mwanajeshi mstaafu wa jeshi la ufaransa na mpaka leo anaheshimika duniani kote kwa umahiri wake wa kutengeneza kinywaji kama hiki. Whisky hii hunywewa na watu maarufu duniani.Most of them are leaders of powerfull nations on earth .Would you like to try it? Akauliza Deus.Peniela akatabasamu na kutikisa kichwa.Amos akamimina katika glasi mbili na moja akampatia Peniela kisha akanywa pombe yote iliyokuwamo katika glasi kisha akafumba macho kwa sekunde kadhaa na kusema “ Kama nilivyokwambia kwamba marais wenye nguvu kubwa duniani hupendelea sana kutumia kinywaji hiki and I’m happy that I’m one of them.Pamoja na kwamba nimemaliza uongozi wangu lakini bado ni mtu mwenye nguvu katika taifa hili..” akanyamza na kumtazama Peniela halafu akaendelea

“ Nilipokaribia kumaliza uongozi wangu nilimpendekeza Dr Joshua aweze kunirithi nikiamini kwamba ni mtu sahihi na ambaye anaweza akafuata misingi ile mizuri ya uongozi niliyoiweka.Kwa bahati mbaya alipoingia madarakani Dr Joshua alibadilika na hakufuata kabisa kile ambacho sote tuliomuweka pale tulitarajia.Uongozi wake umekuwa na kasoro nyingi sana kiasi kwamba lawama zote zinakuja kwangu kwa sababu ni mimi niliyempendekeza ndani ya chama na nikawahakikishia watu kwamba anafaa kupewa dhamana hii kubwa ya kuwatumikia watu.He failed me.” Deus akanyamaza kidogo akamimina tena mvinyo kidogo akanywa na kuendelea

“ Dr Joshua anakaribia kumaliza muda wake wa uongozi na ni nafasi yangu tena kutafuta mtu ambaye nina hakika kabisa kwamba anaweza akaiongoza nchi hii vizuri kwa namna ninavyotaka mimi.Nimejaribu kuangalia sana watu mbali mbali nani ambaye anaweza akafaa kuongoza nchi nikampata jaji Elibariki.Ni mtu ambaye binafsi nina uhakika naye mkubwa sana kwamba anaweza akafaa kupewa nafasi kama hii baada ya Dr Joshua.Hiyo ni sababu sikutaka jaji Elibariki auawe.”akasema Deus.

“ peniela muulize nini sababu ya Elibariki kutaka kuuawa? Mathew akamwambia Peniela

“ Deus unafahamu ni kwa nini jaji Elibariki alitakiwa auawe? Akauliza Peniela.

“ Ni kwa sababu aliufahamu ukweli ambao hakutakiwa kuufahamu na ndiyo maana ikatolewa amri auawe ili siri aliyoigundua isivuje” akasema Deus “ aligundua kitu gani? Akauliza Peniela

“ Ouh peniela mbona una maswali mengi ? Elibariki aligundua siri ya kuhusu kifo cha Dr Flora mke wa Dr Joshua.”

“ Unataka kuniambia kwamba Dr Flora aliuawa? Akauliza Peniel

“ yes Dr Flora aliuawa .”

“ who killed him?

“ Amos did.Captain Amos ndiye aliyemuua Dr Flora kwa amri iliyotoka kwa rais mwenyewe.”

“ Ouh my gosh ! so he killed his own wife? But why would he do that? Akauliza Peniela

“ Dr Flora aligundua kuhusu jambo fulani kubwa analotaka kulifanya mumewake na hakukubaliana naye hata kidogo na ndiyo maana suluhisho peke likawa ni kumuua” Deus akanyamaza halafu kikapita kimya kifupi akasema

“ Kuna uovu mwingi ambao umefanyika wakati wa kipindi cha Dr Joshua na ndiyo maana safari hii ninataka mtu ambaye ni msafi na hawezi kufanya mambo kama aliyoyafanya Dr Joshua.Ninamtaka jaji Elibariki.I want to make him very powerfull president na wewe ukiwa kama mwandani wake you’ll be the next first lady.Hiyo ndiyo mipango tuliyonayo juu yako wewe na jaji Elibariki ambao Amos alitaka kukwambia. Both of you will be very powerfull..What do you think about that? Picture yourself being a first lady ,what do you see? Akauliza Deus Peniela akatoa tabasamu pana sana halafu akapeleka glasi ya mvinyo mdomoni akanywa kidogo

“ What a beautifull lady..akitabasamu anafanana na wale viumbe wazuri wanaotajwa katika simulizi za kale.I’ve never met with such a beautifull queen like this one.She deserve to be the next first lady””akawaza Deus kisha akasema

“ Natumai tayari umekwisha pata picha ni namna gani utakavyokuwa ukiwa mke wa rais.Do you like to be in that position? Akauliza dues

“ Kila mtu anapenda kuwa katika madaraka na nafasi fulani lakini katika hili ulilolisema ninaomba muda wa kulifikiria.”

“ Good. You have all the time in the world to think about it..what do you say about elibariki.Do you think he can agree to be the next president? Akauliza Deus

“ I don’t know..” akajibu Peniela

“ Anyway where is he now? Can you tell me? Akauliza Deus “ Siwezi kukwambia kwa sasa yuko wapi kwa sababu anatafutwa kila kona akihusishwa na shambulio lililosababisha kifo cha mke wake”akasema Peniela

“ Ouh I heard about that and I’m so sorry for his loss lakini hizi zote ni njama za Dr Joshua na genge lake.Wanamtafuta Elibariki kwa udi na uvumba kwani wanafahamu yeye ni kikwazo kikubwa katika kufanikiwa mambo yao. Anyway tell me ,huko aliko Elibariki is he well protected? Akauliza Deus

“ yes he’s safe and well protected”akajibu PenielaDeus akachukua tena ile chupa ya Labellion na kumimina katika glasi yake kisha akamtazama Peniela

“ More whisky?akauliza

“ Yes ofcourse”akajibu Peniela na Deus akamimina tena whisky kidogo katika glasi yake.

“ Deus kuna kitu ninataka kukifahamu kutoka kwako.”

“ Ouh Peniela una maswali mengi sana leo.Ok ninakupa nafasi ya maswali matatu tu ya mwisho “akasema Deus

“ Ok thank you Deus”akajibu Peniela na kunywa whisky kidogo kisha akauliza

“ Amos alikuwa mtu wako ndani ya ikulu na alikuwa akikupa taarifa za kila kinachoendelea kule.Hivi sasa,Dr Joshua anataka kuiuza package ambayo imehifadhiwa ikulu .Wewe umekuwa mstari wa mbele sana katika kuzuia jambo hili lisifanyike.Nataka kufahamu nini kilichomo ndani ya package hiyo? Deus akamimina tena whisky katika glasi akanywa na kusema

“ Nilipokabidhiwa ofisi na rais aliyenitangulialia mojawapo ya vitu ambavyo nilikabidhiwa ni hicho kitu anachotaka kukiuza Dr Joshua.Japokuwa hakuna kiapo rasmi lakini niliapa kwamba nitailinda package ile kwa nguvu zangu zote na wala sintathubutu kwa namna yoyote ile kuruhusu iguswe na mtu mwingine yeyote na wala kufahamika mahala ilipo .Nilitimiza kiapo change kwani hadi ninamaliza uongozi wangu package ile haikuwa imeguswa na mtu yeyote..Nilipomkabidhi Dr Joshua ofisi nilimkabidhi pia na package ile ailinde kama mboni ya jicho lake .Aliapa kufanya hivyo lakini aliingiwa na shetani wa tamaa na sasa anataka kuiuza .Nimekuwa mstari wa mbele sana kuzuia jambo hili lisifanyike na si mara moja nimewahi kumpigia simu na kumfahamisha kwamba ninafahamu mambo anayoyafanya na kumtaka aache kabisa mipango yake hiyo ya kutaka kuiuza package ile. Badala yake ameniweka katika kundi la maadui zake na tayari alianza kusuka mipango ya kuniua kwa bahati nzuri mtu ambaye alitaka kumtumia katika mpango huo ni kijana mtiifu kwangu . Kuhusu nini kilichomo ndani ya hiyo package sintaweza kukwambia kwani ni siri niliyoapata kuilinda hadi ninaingia kaburini.”akasema Deus akanyamaza kidogo na kusema

“ second question “ “ Kuna nyaraka za siri ziliibwa ikulu na aliyeziiba ni Amos akishirikiana na kijana mmoja anaitwa Edson na aliyekuwa nyuma ya mpango huu wote ni Rosemary Mkozumi mke wako wa zamani.Nyaraka hizo zina kanuni ambazo zinaelekeza namna ya kutengeneza kirusi hatari na kinachoweza kusababisha maangamizi makubwa sana.Unafahamu chochote kuhusu jambo hili? Swali lile likamstua sana Deus

“ What ?! I didnt know anything about that.Nyaraka zile zimeibiwa? Deus akashangaa sana

“ Ndiyo Deus na kinara wa mpango huo ni mkeo “ akasema Peniela na Deus akasimama.

“ Amos was a devil.Sikutakiwa kumuamini kiasi kile !! akasema Deus

“ Amos was working with your wife “ akasema peniela

“ peniela naomba niweke rekodi sawa.Yule si mke wangu.Mimi na yeye tumekwisha tengana kitambo kwa hiyo haipendezi kumtaja kama mke wangu.Nilimuamini sana Amos na sikutegemea kama angeweza kunigeuka na kushirikiana na mke wangu.Nyaraka hizo unazozisema ni moja wapo ya vitu ambavyo niliapa kuvilinda kwa nguvu zangu zote kwani ni mojawapo ya nyaraka hatari sana na ndiyo maana zikafichwa ikulu sehemu ya siri kabisa .Amos hakuwahi kuniambia kama nyaraka zile zimeibwa na wala sikujua kama anashirikiana na Rosemary.Laiti ningelifahamu jambo hili toka mapema basi ningemuondoa mapema sana.Rosemary ni mtu hatari sana na ndiyo maana mimi na yeye kwa hivi sasa ni chui na paka.Niliishi naye ikulu na anayafahamu mambo mengi ya ikulu kwa sababu nilimshirikisha kwa kuwa nilimuamini kama mke wangu lakini baadae niligundua kwamba nilikuwa ninaishi na nyoka na si binadamu na ndiyo maana nikatengana naye.”akasema Deus kwa hasira kali kisha akamimina tena mvinyo katika glasi akanywa kwa fujo

“ Peniela muulize kuhusu Hasheem Abdullah” Mathew akamwambia Peniela

“ Do you know someone called Hasheem Abdullah ? akauliza Peniela na kumstua sana Deus “ Hasheem Abdullah ?!! Do you know him? Akauliza Deus. “ Hasheem is working with Rosemary Mkozumi” akasema Peniela.Deus akamtazama kwa makini sana na kusema

“ Peniela who are you working with?

“ kwa nini unauliza Deus?

“Ninahitaji kufahamu.Ninajua unafanya kazi na Team SC41 lakini na hakika kanisa kwamba mambo haya unayonielea hayajatoka katika Team SC41.” Akasema na kumtazama Peniela “ Whoever you are working with ,they must be a very professional people..”akasema Deus.

“ This guy Hasheem do you kow him? Akauliza peniela.Deus akanyamaza kidogo akafikiri kisha akasema

“ Hasheem Abdullah ndiye aliyetufanya mimi na Rose tukatengana.Niligundua kwamba Rose alikuwa na mahusiano na mtu huyu hatari ambaye anayetajwa kufadhili vikundi vya kigaidi.” akasema Deus

“ Do you know that your wife is working with terrorists? Akauliza Peniela

“ I’ve answered your three questions now its my turn to ask” akasema Deus “ Kitu cha kwanza ninachotaka kufahamu ni kuhusu zile nyaraka ,mmefahamu mahala zilipo? Akauliza Deus

“ usihofu Deus nyaraka zile tayari tunazo mikononi mwetu na tuliziwahi kabla hazijauzwa kwa mtu mmoja anaitwa Habib soud raia wa Saudiarabia ambaye anatajwa kufadhili vikundi vya kigaidi.Ziko salama ” akajibu Peniela

“ Thank you Lord ” akasema Deus

“ Second question.Uliniambia kwamba unamfahamu aliyemuua Amos?

“ yes I know her.Ni yule mwanamke aliyemuokoa Elibariki ” akasema Peniela

“ The same woman? Are you sure Peniela ? akauliza Deus

“ yes I’m sure.I saw her face that night and I saw her face today, its her” “ Ouh my God .kwa nini alimuua?

“ Sifahamu kwa nini alimuua lakini inaonekana wazi kwamba hakutaka Amos anieleze kuhusiana na mipango mliyonayo juu yangu na Elibariki.”

“ Ninashindwa kupata jibu kwa nini hakutaka kufahamu kuhusiana na mpango huu? What’s going on? Akauliza Deus.

“ Anyway nitafanya uchunguzi wangu na kufahamu undani wa jambo hili.Naomba unieleze ni wapi alipo Rosemary? Nani anayemshikilia na kwa nini? Akauliza Deus

“ Sintaweza kukueleza ni akina nani ambao wanamshikilia Rosemary lakini yuko sehemu ambako si rahisi kufikiwa na watu anaoshirikiana nao .Anahojiwa kuhusiana na kushirikiana na magaidi.I’m sorry Deus but your wife is very dangerous.“ akasema Peniela

“ Ninalifahamu hilo na ni mojawapo ya sababu iliyonifanya nikaachana naye na hasa nilipogundua kuhusu mahusiano yake na Hasheem ,lakini sikutegemea kama itafikia hatua hii aliyofika.Amefikia hatua mbaya sana.Naomba sana Peniela kama unafahamiana na watu ambao wanamshikilia Rosemary waambie tafadhali wasimuachie kabisa Yule ni mtu hatari sana.In anyway Rosemary hatakiwi kabisa kuachiwa.Ninawapongeza sana waliomkata kwani ana mtandao mkubwa na amekwisha jihakikishia kwamba hawezi kukamatwa. Mtandao wake wote unatakiwa ufahamike na watiwe nguvuni.Rosemary ni mtu muhimu sana ambaye anaweza akawaongoza na kufanikisha kuufumua kabisa mtandao wa kigaidi hapa nchini .” akasema Deus akamtazama Peniela kwa makini na kusema

“ Jambo lingine.Nilimtegemea sana Amos katika kupata taarifa kuhusiana na package anayotaka kuiuza Dr Joshua lakini kwa sasa baada ya Amos kuuawa I don’t have any connection with the president kwa hiyo sintajua kinachoendelea.Package ile haitakiwi kutua mikononi mwa mtu yeyote Yule.Inatakiwa ihifadhiwe sehemu salama sana .Ninafahamu wewe na team Sc41 mko pia katika harakati za kuipata package hiyo lakini ninakusihi Peniela usiache package ile ikatua mikononi mwa team SC41.fanya kila uwezavyo kuweza kuipata wewe mwenyewe na kisha unikabidhi mimi niihifadhi sehemu salama ambako nina uhakika kwambaitakuwa salama.Endapo utahitaji msaada wowote ule mimi niko tayari kukusaidia ili package hiyo isipotee .We’re doing this for our country,our children’s children and for the whole world..Can I trust you on this?

“ Yes you can.I’ll try to do that “ akajibu Peniela

“ Good.sasa tuachane na hayo tuzungumzie masuala yetu ya msingi.”

“ masuala gani hayo Deus? Akauliza Peniela.Deus akamsogelea Peniela pale sofani. “ about me and you” akasema Deus na Peniela akatabasamu

“ Peniela I want to make you the most powerfull woman in this country.I want to make you the first lady.Every woman wants to be the first lady so I want to make your dream come true.Utatembea na msafara ,utakuwa na walinzi na utapata kila unachokitaka.Hii ni fursa ya kipekee kabisa unaipata.tafadhali usiiache na ninajua kabisa kwamba huwezi kuikataa.. “ “ Peniela mkubalie anachokitaka.mwambie uko tayari” Mathew akampa peniela maelekezo

“ Ok Deus siwezi kuikataa nafasi kama hii adimu kabisa kupatikana.” “ Good.I’ll make you the first lady.But I need something in return” akasema Deus

“ What do you need in return Deus? Akauliza Peniela

“ I need you.!akasema Deus “ Me?! Peniela akashangaa

“ yes I need you.I want to spend time with you especially tonight.I need ypu so badly..”akasema Deus

“ peniela mkubalie lakini mwambie na wewe kuna kitu unataka kutoka kwake” amathew akamwambai peniela

“ Ouh Deus ,utaniweza mtu kama mimi..?akaulzia Peniela

“ kwa nininisikuweze peniela?

“ Ok tutaona lakini mimi niko tayari kukuachia mwili wangu but I also need onething in return”akasema peniela

“ What do you need beautiful angel?

“ mwambie akwambie nini kilichomondani ya package” akasema Mathew

“ I want you to tell me whats in the package”

“ peniela ! peniela..nimekwisha kwambia kwamba hii ni siri yangu hadi siku ninaingia kaburini.tafadhaliombakitu kingine chochote na si hicho.Katu sintaweza kukuambia” akasema dues

“ peniela wakati wa kuondoka sasa.”Mathew akamwambia peniela

“ Deus ninashukur sana kwa kuipata nafasi hii ya kukaa nawe japo wa dakika chache.Ninashukuru kwa ushirikiano wako na kama Mungu akipenda tutaonana tena.Niko tayari kukaa nawe hata kwa usiku mzima lakini hadi pale tu utakaponieleza kuhusu kilichomo ndaniya package.” Akasema peniela huku akiinukana kuuchukua mkobawake tayari kwa kuondoka



“ Peniela not so fast my lady ! akasema Deus huku akitabasamu



“ Deus we’re done in here so I have to go” akasema Peniela

“ Not yet Peniela.The night is still so young.Tunahitaji kufahamiana zaidi hasa kwa usiku huu wa kwanza mimi na wewe kukutana.Dont you want to spend time with the person who wants to make you the next first lady? Akauliza Deus.Peniela akatabasamu

“ Deus tumekwisha fahamiana vya kutosha tayari . Tutatafuta tena siku nyingine ambayo tutakutana na kuendelea kufahamiana zaidi.” Akasema Peniela akionekana kuushikilia msimamo wake wa kutaka kuondoka.Deus akanywa whisky kidogo na kusema



“ Peniela unajua sisi tuliobobea katika masuala ya siasa we’re not good in convincing women and tonght I don’t know how to convince you to spend the night with me.” Akasema Deus Peniela akamtazama na kutabasamu



“ Peniela mwambie uko tayari kwa kile alichokiomba lakini mpaka akwambie kile kilichomo katika package ” Mathew akampa maelekezo.Peniela akasita kidogo

“ Peniela do it ! akasema Mathew.Peniela akasema



“ Deus , I would like to spend the night with you “ akasema Peniela na kuuweka mkoba wake chini akamfuata akaupeleka mkono wake shavuni kwa Deus akambusu kisha akamtazama na kusema



“ I’m ready to give you what you want,but you’ll have to tell me what is in that package ? akasema Peniela. Deus akaiweka mezani glasi yake ya mvinyo na kumtazama

“ Kwa nini unataka kufahamu kilichomo ndani ya hiyo package ?



“ Kwa sababu mimi na wewe tuna lengo moja la kuhakikisha kiwamba package hiyo haitui mikononi mwa watu wabaya kwa hiyo ninahitaki kufahamu ni kitu gani kiko ndani ya hiyo package na kwanini watu wamekuwa wakiitafuta kwa pesa nyingi kiasi hiki? Is it a bomb? I want to know Deus”

Peniela akamkumbatia tena na kuanza kumchezea Deus maeneo nyeti ambayo ghafla yakafura kwa hasira kali.

“ I know This is what you want Deus so tell me everything that I want to know and I’ll be yours tonight and many nights to come “ akasema Peniela na kumchanganya zaidi Deus



“ Peniela kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nimekutana na mwanamke ambaye amenifanya niende nje ya msimamo na kiapo changu.Nitakueleza kila kitu,lakini tafadhali naomba uniahidi kwamba hii itabaki kuwa ni siri yako na hatafahamu mtu mwingine yeyote Yule.What am about to tell you it’s a very very big secret.” Akasema Deus.Peniela akamsogelea akamkumbatia na kuanza kumpapasa maungoni



“ That secret is safe with me.” Akasema Peniela na kuipeleka ncha ya ulimi wake katika sikio la Deus na kumfanya atoe mguno kwa msisimko alioupata.Deus akamuinua Peniela kwa nguvu na kumtupa kitandani kisha akaanza kuvua nguo zake haraka haraka na kupanda kitandani.

“ Peniela kuwa makini sana na Deus.Usifanye naye chochote kabla hajakueleza kile tunachokitaka” Mathew akamuelekeza Peniela.Deus akaanza kumbusu Peniela kila sehemu

“ Ouh C’mon Deus not so fast my dear. First thing first Mr President.Why don’t you start by telling me what I want to know before I undress ? Akasema Peniela kisha akamvuta Deus na kumbusu huku akiendelea kumpapasa sehemu mbali mbali za mwili wake.

“ She’s so good at this “ Anitha akamwambia Mathew wakiwa garini wakiendelea kufuatilia kila kinachoendelea kati ya Deus na Peniela

“ yah .She good.Very good.” Akasema Mathew.Anitha akamtazama kwa makini na kusema

“ Mathew can I ask you something?

“ Yes ask”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Unakumbuka tukiwa nyumbani nilikuelekeza kwamba uende chumbani ukamtazame Peniela kama amemaliza kuvaa.What happened in there?

“ kwa nini umeuliza hivyo Anitha?

“ Ninahitaji tu kufahamu kwa sababu baada ya kutoka kule chumbani ulionekana tofauti kidogo,the way you were looking at her..tell me, did something happen in there? Akauliza Anitha.Mathew akatabasamu na kusema



“ Nothing happened”

Anitha akamtazama tena usoni na kutabasamu kisha akasema

“ You saw her naked right? Do you like her? Akauliza Anitha



“ Anitha lets not talk about that” akasema Mathew



“ Mathew wewe ni rafiki yangu na ninakupenda na ndiyo maana ninataka kukupa ushauri mdogo.Tafadhali ifute kabisa picha ya Peniela kichwani kwako.She’s not good for you..”akasema Anitha



“ Deus anataka kumweleza kitu Peniela

“ Mathew akamwambia Anitha wote wakaelekeza macho katika kompyuta kusikiliza kile ambacho Deus anataka kumweleza Peniela

“ Ok Peniela you won .I’m going to tell you what’s in there” akasema Deus akamtazama Peniela kwa sekunde kadhaa na kusema

“ Kilichomo ndani ya hiyo inayoitwa package ni kirusi kilichopewa jina la Aby 16.”

“ A virus ?!!! Peniela akashangaa

“ Yes it’s a virus and not only a virus but a very very very dangerous virus ever made by a man” akasema Deus.

“ ouh my gosh ! akasema Peniela



“ Kirusi hiki kama kitaachiwa husambaa kwa njia ya hewa na ndani ya dakika kinaweza kusambaa kwa maelfu ya watu na kusababisha homa kali ambayo mgonjwa asipotibiwa ndani ya saa moja toka alipopatwa na ugonjwa huo atapoteza maisha.Kibaya zaidi ni kwamba mpaka hivi sasa kirusi hicho hakijawahi kupatiwa kinga yake kwa hiyo ni kitu hatari sana kwa usalama wa nchi yetu na dunia kwa ujumla na ndiyo maana kinahifadhiwa ikulu mahala ambako hakuna mtu wa kawaida anaweza akapafikia.Kwa bahati mbaya taarifa za uwepo wa kirusi hiki katika Ikulu ya Dar es salaam zimevuja na hivyo kuyavutia sana mataifa mbalimbali kutaka kukipata kirusi hiki kwa gharma zozote zile.Serikali ya Marekani inakitumia kikundi cha Team SC41 ili kuweza kukipata kirusi hicho lakini kibaya zaidi ni kwamba hata mitandao ya kigaidi wamekuwa wakikitafuta kirusi hiki kwa nguvu sana ili kuweza kukitumia katika mashambulio yao ya kigaidi.Mataifa makubwa yenye viwanda vikubwa vya kutengeneza dawa nao pia wanakitafuta kirusi hiki kwa udi na uvumba ili waweze kutafuta dawa yake na kisha kukiachia ili wafanye biashra ya dawa.Kwa bahati mbaya sana Dr Joshua ameingiwa na tamaa ya pesa nyingi na ndiyo maana anataka kukiuza kirusi hicho kwa namna yoyote ile bila kujali madhara yake.Wakati wa uongozi wangu hata mimi nimeshawishiwa sana kuuza package hiyo kwa matrilioni ya pesa lakini sikuwa na tamaa na pesa .” akasema Deus.Kikapita kimya kifupi Peniela akauliza

“ Deus hebu nifafanulie kirusi hicho kimefikaje katika ikulu yetu ya Dar es salaama ? Nani alikitengeneza? Yuko wapi? Karatasi zile zilizoibwa ikulu na akina Rosemary na kutaka kuuzwa kwa magaidi zinahusiana kwa namna yoyote na kirusi hiki?



“ Peniela ulitaka kufahamu kuhusiana na pachage hiyo anayotaka kuiuza Dr Joshua ina nini ndani yake na nimekueleza kilichomo kwa hiyo nadhani nimejibu swali lako .Kuhusu kimetoka wapi na nani aliyetengeneza kwa kweli sintaweza kukujibu kwa sababu hata mimi sifahamu.Mimi pia nilikabidhiwa bila kupewa historia yoyote ile.Kuhusu karatasi zile kama zinahusiana na kirusi kile jibu ni ndiyo.Kanuni zile ndizo zinazoelekeza namna ya kukitenegeneza kirusi hicho lakini bado hazijakamilika ,bado kuna karatasi nyingine zimehifadhiwa sehemu nyingine na ili uweze kukamilisha kutengenza kirusi kamili unatakiwa uzipate karatasi hizo zote.” Akasema Deus



“ Peniela nadhani sasa umefahamu ni kwa nini watu wanaitafuta package hiyo kwa udi na uvumba.Kwa nini watu wako tayari kutoa pesa nyingi mno kwa ajili ya kukipata kirusi hicho .Ninakuhakikishia kwamba endapo kirusi hicho kikifanikiwa kutoka mahala kilipohifadhiwa na kutua mikononi mwa watu wenye uchu wa kukipata dunia haitakuwa sehemu salama tena .Hili si suala dogo kama unavyodhani . Kitu anachotaka kukifanya Dr Joshua kwa tamaa ya fedha ni kitu kinachoweza kusababisha maangamzi makubwa sana duniani.Endapo kirusi hicho kikitua mikononi mwa mitandao ya kigaidi unadhani nini kitakwenda kutokea? Yatakuwa ni maangamizi makubwa ambayo hayajawahi kutokea katika historia ya dunia.Endapo kirusi hiki kitatua katika mikono ya mataifa makubwa yenye viwanda vikubwa vya kutengeneza dawa lazima watakuja kukitupa kirusi hiki huku Afrika kwa ajili ya kufanya majaribio na kuuza dawa zao.Watu wengi sana watapoteza maisha yao kwa hiyo kirusi hiki hatari kinatakiwa kuendelea kuhifadhiwa katika sehemu salama” akasema Deus.

Ndani ya gari Mathew akachukua kitambaa na kujifuta jasho.Mambo waliyoyasikia toka kwa Deus yalimsisimua sana.

“ Peniela ,nadhani Deus hataweza kutoa tena maelezo mengine zaidi ya hayo aliyoyatoa.Mpatie anachokihitaji halafu uondoke “ akasema Mathew

“ Deus thank you for this information.Sikuwahi kuhisi kabisa kama package hiyo itakuwa na kitu cha muhimu kama hiki.Nikuahidi nitahakikisha haitui katika mikono ya mtu yeyote Yule mwenye nia mbaya na itaendelea kuwa salama”



“ Thank you Peniela.Thank you so much” akasema Deus



“ Now come here and get what you need” akasema Peniela huku akilipandisha juu gauni lake na nguo yake ya ndani ikaonekena.Deus akaonekana kuchanganyikiwa.Taratibu Peniela akaanza kuishusha nguo ile ya ndani, na kuiweka pembeni akamfanyia ishara Deus amsogelee.

“ Switch it off “ akasema Mathew ndani ya gari

“ kwa nini Mathew? Lazima tuangalie kila kinachoendelea mle ndani ili tujue kama Peniela yuko salama “ akasema Anitha



“ Japokuwa tumepata taarifa tulizokuwa tunazihitaji lakini sifurahii na njia tuliyoitumia kuzipata.” akasema Mathew.

“ Usijali Mathew .Kitu cha msingi ni kwamba tumefanikiwa kupata taarifa muhimu.” akasema Anitha.

Ndani ya chumba haikuchukua zaidi ya dakika sita Deus kufika mshindo akaanguka pembeni.

“ Gosh ! mzee mwenyewe hajiwezi halafu anataka kukesha na mimi .Dakika tano tu ameanguka kama kuku “ akawaza Peniela huku akivaa nguo yake ya ndani akambusu Deus na kusema



“ Deus nadhani tayari umekipata kile ulichokuwa unakihitaji.I can go now. ” akasema Peniela

“ Ouh Peniela I’m so sorry kwa hali hii.Leo siko vizuri na ndiyo maana sijaweza kwenda mwendo mrefu” akasema Deus



“ Its ok Deus.I’ll call you again” akasema Peniela.

“ Ngoja kwanza Peniela niwaite walinzi wakuongoze kutoka humu ndani” akasema Deus na kuvaa kisha akabonyeza kitufe Fulani na mara mlango ukafunguka akaingia mtu mmoja aliyevalia nadhifu suti nyeusi.Deus akampa maelekezo amuongoze Peniela hadi katika gari lake .

“ Nimemaliza kazi and now I’m on my way out

“ Peniela akawataarifu akina Mathew baada ya kuingia garini



“ Thank you Peniela and good job.” Akasema Mathew.Peniela akawasha gari na kuondoka







********





Peniela ndiye aliyekuwa wa kwanza kuwasili nyumbani kwa Mathew na baada ya dakika mbili wakawasili Mathew na Anitha.Mathew akashuka garini na kwenda kulifungua geti



“ Elibariki amepitiwa na usingizi ? Mbona hafungui geti “ Akauliza Mathew.



“ Sielewi kwa sabau nimejaribu kupiga honi mara kadhaa hakuna aliyejitokeza kufungua geti” akasema Peniela

. Kwa kutumia remote control Mathew akalifungua geti na magari yakaingizwa ndani .Mara tu Peniela aliposhuka garini Mathew akamfuata na kumkumbatia.

“ Peniela you did a good job today.Bila wewe katu tusingeweza kuzipata taarifa zile nzito” akasema Mathew.Peniela akatabasamu



“ Ahsanteni pia kwani tumeifanya kazi hii pamoja.Bila ninyi hakuna kitu kingeweza kufanikiwa.” Akasema Peniela halafu wakatazamana kwa sekunde kadhaa wakastuliwa na Anitha



“ Jaji yuko wapi ?Mbna nasikia sauti kubwa ya muziki ? akauliza Anitha



“ Inawezekana amepitiwa na usingizi” akasema Mathew kisha wote wakingia ndani.

Anitha na kwenda kupunguza sauti kubwa ya muziki .Baada ya kupunguza sauti wakasikia sauti ya kilio cha mtu.



“ Who is that? Akauliza Peniela

Mathew akatoa bastora yake na kuanza kufuatilia ilikotoka sauti ile ya mwanamke huku Anitha na Peniela wakiwa nyuma yake.Sauti ile ilitoka katika chumba cha jai Elibariki.Ilikuwa ni sauti ya Naomi.Haikuwa siri tena kwani sauti ilionyesha kwamba Jaji Elibariki na Naomi walikuwa wanafanya mapenzi.

“ Peniela,Anitha nendeni ofisini ninakuja muda si mrefu” akasema Mathew

“ No Mathew ! I want to see everything “ akasema Peniela kwani alikwisha jua nini kilichokuwa kinaendelea mle chumbani.



Mathew akavuta pumzi ndefu na kisha akagonga mlango lakini ilionekana waliokuwemo mle chumbani hawakusikia,akagonga tena safari hii kwa nguvu zaidi na ghafla kukawa kimya.Mathew akagonga tena na baada ya sekunde kadhaa mlango ukafunguliwa na jaji Elibariki ambaye licha ya kjaribukujifuta jasho bado liliendelea kumtiririka usoni..Alipatwa na mstuko mkubwa baada ya kukuta watu wote wako pale mlangoni wakimtazama akiwamo Peniela..

“ Mathew !.I can Explain this !!akasema jaji Elibariki huku akimtazama Peniela aliyekuwa anamuangalia kwa macho makali sana.

“ I can..I can explain this..akajitetea.



“ tell her to go to her room” Mathew akamwambia jaji Elibariki.Akaufunga mlango na kukasikika mabishano mle chumbani kati yakena Naomi na baada ya dakika mbili mlango ukafunguliwa na Naomi akatoka akiwa amejifunika shuka.uso wake ulijaa aibu.Alipotazamana na Mathew akarudi tena ndani na kuufunga mlango.Michirizi ya machozi ikaonekana machoni mwa Peniela ,akaondoka kwa kasi kuelekea sebuleni,Mathew akamfanyia ishara Anitha amfuate halafu akaufungua mlango na kuingia mle chumbani.Naomi alijibanza pembeni ya kabati na jaji Elibariki alikuwa amejinamia kitandani .

“ Mathew naomba unisamehe ..”akasema Naomi.

“ Naomi nenda chumbani kwako haraka sana”akasema Mathew..Naomi akatoka na kuchungulia nje kama akina Peniela wapo pale mlangoni kisha akatoka mbio kuelekea chumbani kwake.Mathew na Elibariki wakatazamana..



“ Mathew I can explain this..”akasema jaji Elibariki



“ Explain? Akasema Mathew ambaye hakuonekana kufurahishwa na kitendo kile

“ Sikutegemea kabisa kama unaweza ukafanya kitendo kama hiki Elibariki.na hasa kwa wakati huu zaidi ya yote na Naomi ”

“ Mathew najua nimechafua taswira yangu kwenu lakini naomba unielewe ndugu yangu kwamba sikufanya hivi kwa ridhaa yangu..”akasema jaji Elibariki na kumfanya Mathew acheke kidogo

“ Hukufanya kwa ridhaa yako? Unataka kuniambia kwamba Naomi alikubaka? Akauliza Mathew



“Mathew ni hadidthi ndefu na ninaomba tafadhali unipe nafasi nikueleze kila kitu” akasema jaji Elibariki



“ Elibariki mimi sina haja ya simulia yako unayetakiwa kumueleza ni Peniela na si mimi.Umemuumiza sana mtu ambaye tunamtegemea katika kazi yetu.Nenda kamueleze hayo unayaotaka kunieleza ”akasema Mathew na kutoka akaelekea katika chumba cha Naomi akagonga mlango Naomi akafungua.Uso wake ulijaa aibu na hakuthubutu kumtazama Mathew usoni



“ Mathew naomba unisamehe kaka yangu.Ni shetani tu alitupitia tukashindwa kujizuia” akasema Naomi huku akilia machozi



“ Isingekuwa kama nilikuahidi kukusaidia basi usiku huu huu ningekutimulia mbali.Kwa nini ukakubali kufanya uchafu ule katika nyumba yangu Naomi ?

“ Nisamehe Mathew, sintarudia tena” akalia Naomi.Mathew akamtazama kwa hasira.Na mara akakumbuka namna alivyoachia risasi zilizomuua Henry baba yake Naomi.

“ I killed her father.kwa namna yoyote ile natakiwa kumsaidia.Namuonea huruma sana huyu binti kwani hajui hata kama baba yake amefariki dunia..”akawaza Mathew na kumshika mkono Naomi akamuinua.Uso wake ulijaa machozi.

“ Naomi nimekusamehe kwa kitendo hiki cha leo lakini ninakuomba kitendo kama hiki kisijirudie tena.Mimi na wenzangu tumejitolea kukusaidia ili uweze kuanza upya maisha yako kwa hiyo tafadhali naomba sana jitahidi kutunza heshima yako.Wote unaowaona humu ndani ni watu na heshima zao na kwa kitendo ulichokifanya leo hii kimekushushia sana heshima thamani yako kwao kwa hiyo jitahidi kwa kila uwezavyo kuhakiksha wanakuamni tena.Tumeelewana Naomi? Akasema Mathew

“ Nimekuelewa Mathew.Ninakuahidi kwamba sintarudia tena kitendo kama hiki na ninaomba unisamehe sana na uniombee msamaha kwa dada Anitha na Peniela “

“ sawa nitajaribu kuwaelewesha .”akasema mathew na kutaka kutoka mle chumbani Naomi akamuita



“ Unasemaje Naomi ?akauliza Mathew



“ Mathew naomba msimlaumu jaji kwani ni mimi ndiye niliyemshawishi hadi akakubali kufanya name mapenzi.Hakuwa anataka kufanya jambo hilo ila mimi nilimlazimisha kwa kumpa vitisho ” akasema Naomi.Mathew akamuangalia na kutikisa kichwa



“ Mathew usinielwe vibaya kaka yangu lakini nilijikuta tu nikipatwa na tamaa baada ya kubaki sisi wawili tu humu ndani na kwa muda wa miaka zaidi ya minne sikuwa nimekutana na mwanaume yeyote Yule.Nisamehe sana mathew najua hata kama ni wewe au mtu mwingine yeyote angekuwa katika nafasi kama yangu nina hakika kabisa kwamba angeweza kufanya jambo kama nililolifanya”akasema Naomi.Mathew hakusema kitu akafungua mlango na kutoka akaelekea chumbani kwake akafungua kasiki lake na kurejesha silaha na baadhi ya vifaa alivyokuwa amevichukua kisha akaenda kukaa kitandani.Alionekana kuwa katika mawazo mengi sana.Mara mlango ukagongwa akaenda kufungua na kukutana na Anitha akamkaribisha ndani

“ Nimewapa nafasi Elibariki na Peniela ya kuzungumza kwa uhuru ila Peniela ameumizwa sana na kitendo cha aibu alichokifaya jaji Elibariki.Nilimuamini sana Eli na sikutegemea kama angeweza kufanya kitendo kama kile.” Akasema Anitha,Mathew akamtazama na kusema



“ Naomi alifungiwa ndani kwa zaidi ya miaka minne na kama binadamu wengine naye alikuwa na matamanio.Alipogundua kwamba amebaki yeye na jaji Elibariki pekee akaingiwa na tamaa na ndiyo yakatokea yale yaliyototokea.Nimeongea naye na amekiri kwamba ni yeye ndiye aliyemshawishi jaji Elibariki wakafanya mapenzi .”

“ Do you believe her?akauliza Anitha

“ yes I do .Hata hivyo Naomi bado anahitaji sana msaada wetu.Kazi kubwa inatakiwa kufanyika ili kumtoa katika maisha yake ya awali aliyokuwa akiishi na kumlata katika maisha ya kawaida.”akasema Mathew



“ Tayari umemfahamisha kuhusu kifo cha baba yake? akauliza Anitha

“ hapana bado sijamwambia.Ninasubiri muda muafaka ukifika nitamweleza.”akasema Mathew.



“ Ok tuachane na hayo..Usiku wa leo naweza kusema ni usiku mkubwa sana kwetu kwani tumefanikiwa kugundua suala kubwa na zito.hatimaye leo hii kitendwili kimeteguliwa.Tumefahamu nini kilichomo ndani ya hiyo package.Mathew mpaka sasa mwili wote bado unanitetemeka sana baada ya kufahamu pachage hiyo ina kitu gani ndani yake. Sikuwahi kuota kama kungekuwa na kitu kibaya na cha hatari kama hiki.”akasema Anitha .Akanyamaza kidogo na kuendelea

“ kwa hiyo nini kinafuata baada ya hapa?

Mathew akafikiri kidogo na kusema

“ Anitha kwanza kabisa ninapenda nikushukuru sana na kwa dhati kwa msaada mkubwa uliotuwezesha kufika hapa.Bila wewe juhudi zetu zote zingekuwa bure.Utaalamu wako wa hali ya juu wa teknolojia unaifanya kazi yetu isiwe ngumu sana.pamoja na hayo kuna jambo ninataka nikiri kwako na nina omba unisamehe kwa hilo”

“Ni jambo gani Mathew?akauliza Anitha kwa wasiwasi

“ I knew about that virus before”

Anitha akamtazama Mathew kwa sekunde kadhaa halafu akainuka na kujishika kiuno



“ You knew? And you didn’t tell me?

“ I’m sorry for that Anitha” akasema Mathew

“ Mathew sijui niseme nini lakini umenishangaza sana.Tunahangaika kila siku kutaka kujua nini kilichomo ndani ya package hiyo kumbe wewe unafahamu na hutaki kutueleza !! why Mathew why ?!!..Ulifurahi kumuona peniela akiuza utu wake kwa Dues wakati unafahamu alichokuwa anakitafuta?akauliza Anitha kwa ukali



“ Calm down anitha “akasema Mathew



“ John told me !..

“ John Mwaulaya? Akauliza Anitha

“Ndiyo.John mwaulaya ndiye aliyeniambia kuhusiana na suala hili.,Usiku ule aliponiita nikaonane naye hospitali alinieleza kila kitu kuhusiana na package hiyo na kwa nini ni kitu cha muhimu sana ambacho kwa namna yoyote ile hatupaswi kukiacha kitue mikononi mwa watu ambao wana lengo la kukitumia kwa matumizi yasiyofaa”akasema Mathew



“ Kwa nini basi hukutuambia?

“ Nilihitaji kupata uthibitisho kutoka kwa Deus.Sikumuamini John Mwaulaya mojakwa moja ”akasema Mathewm.Anitha akamtazama na kuuliza



“ Kitu gani kingine alikwambia na hujatuambia?akauliza Anitha

“ Ni hilo tu”



“ Are you sure?akauliza Anitha



“ Yes I’m sure.” Akajibu Mathew



“ Once I find out that you’ve been lying to me I’ll never forgive you Mathew.Why don’t you trust me? Akauliza Anitha..

“ Anitha I do trust you with my life..”akajibu Mathew na kumfanya Anitha atabasamu



“ So what’s next?

“ Tulikuwa tunapambana kuipata package ambayo hatukujua ina nini ndani yake.kwa sasa baada ya kufahamu kila kitu kuhusiana na package hiyo tunapaswa kuongeza nguvu na mikakati katika kuhasikisha kwamba kwa gharama yoyote ile tunaipata hiyo package.Vyovyote vile itakavyokuwa lakini tunatakiwa kuhakikisha kwamba Dr Joshua hafanikishi lengo lake la kuiuza package hiyo.Tutatumia kila aiana ya mbinu tuliyonayo katika kuhakikisha kwamba jambo hili halifanikiwa.Mtu wa muhimu sana ambaye atatusaidia katika kulifanikisha hili ni peniela pekee.Ndiyo maana sikufurahishwa kabisa na kitendo alichokifanya jaji Elibariki ambacho kimemuumiza sana Peniela na kumtoa nje ya mstari..She loves him so much .Kwa kitendo cha kumfumania na mwanamke mwingine kimemuumiza sana.Inatakiwa ifanyike juhudi ya makusudi kumrudisha Peniela katika hali yake ya kawaida ili tuweze kuifanya kazi.Dr Joshua anarejea kesho na kwa mujibu wa mawasiliano yake na Kigomba ni kwamba anataka jambo hili limalizike haraka iwezekanavyo kwani mchakato wake umeingiliwa na watu wengi.kwa mujibu wa maelekezo yake kwa Kigomba ni kwamba kesho atawasili Hussein ambaye nina uhakika mkubwa kwamba ndiye anayekuja kuuchukua mzigo huo na hivyo kumfanya kuwa mtu muhm,u sana kwetu ” akasema Mathew.

“ Katika hili“Mathew akaendelea

“ Peniela ana nafasi kubwa sana kwani tunatakiwa tumfahamu huyo Hussein ni nani na njia pekee ya kumfahamu Hussein ni kwa kuipata simu ya Dr Joshua na mwenye uwezo wa kuipata simu hiyo ni Peniela pekee.”



“ kesho mwili wa Flaviana utawasili kwa hiyo itakuwa ni siku yenye pilika pilika nyingi sana na wageni watakaofika kwa ajili ya kumpa pole Dr Joshua ni wengi na miongoni mwa wageni hao ni huyu Hussein ambaye tunatakiwa kumfahamu na hata kuipata sura yake ili tuweze kumfuatilia toka anapowasili uwanja wa ndege. Nina uhakika mkubwa kwamba huyu ndiye anayekuja kuuchukua mzigo huo kwa hiyo jicho letu halitakiwi kubanduka kabisa kwake”akasema Mathew

“ kama nilivyokwambia awali kwamba ni Peniela pekee anayeweza kutusaidia kulifanikisha hili suala.Ni yeye pekee anayeweza kuipata simu ya Dr Joshua” akasema Anitha

“ Nakubaliana nawe Anitha.Katika hili tunamuhitaji sana Peniela .Ngoja nikajaribu kuongea naye nimuweke sawa ili aweze kuirejesha akili yake katika jambo la msingi linalotukabili”akasema Mathew na kutoka mle chumbani akaelekea sebuleni lakini peniela hakuwepo.Akachungulia ofisini lakini hakuwepo pia akatoka nje na kumuona akiwa amekaa pembeni ya bwawa la kuogelea akamfuata na kuketi pembeni yake.Peniela alikuwa anatazama angani huku analia.Mathew akatoa kitamba cha mfukoni akampatia.

“ take this”akamwambia.paniela akastuka kidogo

“ Take it it’s clean.Futa machozi yote”akasema Mathew



“ Mathew why always me? Akauliza Peniela huku akishindwa kujizuia kulia kwa nguvu.Mathew akauzungusha mkono wake shingoni na kumkumbatia.Peniela akakilaza kichwa chake kifuani kwa Mathew na kuendelea kulia .



“ Its ok peniela..its enough now” akasema Mathew.



“ Inaniuma sana Mathew kwani nilimpenda sana Elibariki na niliamini kwamba ni mwanaume ambaye nitaanza naye maisha mapya baada ya skata hili kumalizika .Yeye ni sababu kubwa inayonifanya nipambane kufa na kupona katika kuhakikisha kwamba tunashinda vita hii na mimi kubaki huru but he did in return, he broke my heart!!..akasema Peniela kwa uchungu mkubwa

“ Peniela kitendo kile cha Elibariki kimetuudhi sisi sote lakini hta hivyo kwa sasa tuko kati kati ya vita na tunatakiwavkuishinda vita hii kwa hiyo ninakuomba japo kwa siku mbili tatu zilizobaki ,yaondoe mawazo yako kwa Elibariki na tuelekeze nguvu zetu katika suala zito lililoko mbele yetu.Baada ya kulimaliza suala hili tutapata wasaa wa kukaa na kuzungumza jambo lililotokea leo. Ninajua umeumia Peniela lakini maumivu haya yaelekeze katika jambo lililoko mbele yetu ambalo ili lifanikiwe linakuhitaji sana wewe.Kuna mambo mengi mazuri yanakuja mbele yako iwapo suala lililoko mbele yetu litafanikiwa kumalizika na sisi tukaibuka washindi.Ukumbuke vile vile kwamba kuna mpango mkubwa wa kukufanya mwanamke mwenye nguvu au the next first lady..”akasema Mathew.Peniela akamtazama na kusema

“ Mathew unaweza ukanieleza ukweli?

“Ukweli upi Peniela?

“ Ninataka unieleze ukweli bila kunificha.Ukiniangalai mimi unanionaje? Ninaonekanaje mbele zawatu? Ninaonekana kama kahaba? mwanamke nisiye na heshima yoyote,mwanamke ambaye kila mwanaume anaweza akamtumia? Akauliza Peniela.Mathew akamtazama kwa makini usoni

“ Tell me the truth Mathew “ akasema Peniela.mathew akakohoa kisogo na kusema

“ Mtazamo wangu kwako unawakilisha mtazamo wa watu wengi na si mtazamo tu bali ni ukweli halisi.Nikuonapo ninamuona mwanamke jasiri,mwenye ndoto na ambaye yuko tayari kwenda hadi ncha ya mwisho wa dunia ili azitimize ndoto zake,mwaname asiye kata tamaa ,mwanamke mwenye nguvu kubwa ndani yake licha ya mwili wake kuwa mdogo, mwanamkemwenye sauti laini lakini inayoweza kupenya hadi ndani ya mioyo ya watu wenye nguvu na wakavifunga vinywa vyao kumsikia,sifa ni nyingi za mwanamke ninayemuona nikuonapo lakini kubwa zaidi ya yote mwanamke mwenye uzuri wa asili wa ndani na wa nje ambao unaweza kujaza kitabu cha kurasa mia mbili kuuelezea. Huyu ndiye mwanamke ninayemuona nikikutazama.thats you Peniela.” Akasema Mathew.Uso wa Peniela ukatabasamu na kisha akasema



“ Ahsante Mathew kwa kunieleza ukweli.Kwa miaka mingi nilitafuta mwanaumeambaye atanieleza ukweli kuhusu mimi.Maneno uliyoyatamka yametoka ndani kabisa mwa moyo wako na ninayaamini ni sahihi na wala hujayatamka kwa kunifurahisha so thank you Mathew,thank you so much.I’m so lucky to have you..”akasema Peniela na kumbusu Mathew shavuni.



“ Now lets get back to work” akasema Peniela huku akiinuka na kumuacha Mathew bado amekaa katika bwawa akiwa ni kama vile amepigwa na butwaa .

“ Mathew we have a job waiting for us “ akasema Peniela na Mathew akainuka kisha wakaelekea katika chumba cha ofisi ambamo walimkuta Anitha



“ Elibariki yuko wapi? Akauliza Mathew



“ Yuko chumbani kwake”akajibu Anitha



"Go call him.we need him here”akasemaMathew na Anitha akatoka .Baada ya dakika mbili akarejea akiwa na Elibariki.

“ Jamani tumekutana tena hapa ili tuweze kujadiliana masuala ya muhimu kuhusiana na kile tulichokipata usiku huu..”Mathew akaanzisha maongezi lakini Elibariki akaingilia kati



“ Ndugu zangu kabla hatujaendelea naomba dakika kama mbili tu niweze kuwaelezea kile kilichotokea.” Akasema jaji Elibariki

“ Eli,utapata nafasi lakini si sasa.kwa wakati huu tuna masuala mazito yaliyoko mbele yetu”akasema Mathew.Akawatazama wote usoni halafu akaendela

“ usiku wa leo tunaweza kusema kwamba ni usiku wa kipekee kabisa kwa sababu tumefanikiwa kulifahamu jambo kubwa sana.Tumefahamu nini hasa hiyo package ambayo Dr Joshua anataka kuiuza.kwa vile sisi sote tayari tunafahamu,naomba nikufahamishe Elibariki kwamba kilichomo katika hiyo package ni kirusi hatari ambacho kinaitwa Aby 16.Hiki ni kirusi hatari sana na kinachoweza kusababisha maangamizi makubwa sana.” Mathew akaendelea kumuelezea Elibariki kila walichokipata toka kwa Deus kuhusiana na kirusi hicho.



Jaji Elibariki alibaki kinywa wazi baada ya maelezo yale ya Mathew.Akashusha pumzi



“ Kwa hiyo maelezo yale ya Josh Yule rafiki yako wa Israel kuhusiana na kirusi kile yalikuwa sahihi kabisa .” akasema Elibariki

“ Ndiyo Eli. Josh alikuwa sahihi kabisa .Kilichoandikwa katika nyaraka zile ni kanuni za kutengeneza kirusi Aby 16.Kwa bahati mbaya kirusi hicho tayari kimekwisha tengenezwa na kinahifadhiwa katika ikuluya dare s salaam na kwa hivi sasa kinagombaniwa na watu mbali mbali na wengi kati yao ni watu wenye nia ovu na wanaotaka kukitumia kusababisha maangamizi makubwa ” Akasema Mathew

“ Mathew ambacho bado sijakielewa mpaka sasa na sijasikia ukikisema.Kirusi hicho hakikujitengeneza na wala hakikujileta chenyewe pale ikulu bali kimetengenezwa na mtu na kikafikishwa pale ikulu na mtu.Ninachotaka kufahamu ni nani aliyekitengeneza na yuko wapi? Kilifikaje pale ikulu ? Akauliza jaji Elibariki

“ Elibariki maswali hayo ni magumu hakuna anayeweza kutupa majibu yake kwa sasa.Kilichopo mbele yetu baada ya kufahamu kwamba package tunayoitafuta ni kirusi Aby 16 ni kuhakikisha kwamba tunakipata kirusi hicho kwa gharama zozote zile.Tukirejea mazungumzo ya Dr Joshua na Kigomba ni kwamba wanataka kulimaliza suala hili haraka kwani tayari limekwishaanza kuiingiliwa na watu wengi.Kesho mwili wa Flaviana utarejeshwa nyumbani kutokea afrika ya kusini kwa hiyo itakuwa nisiku yenye shughuli nyingi kwa Dr Joshua na sina hakika kama ataweza kushughulika na suala hili.Nina hakika baada ya shughuli za mazishi kukamilika basi wataifanya biashara hi haraka sana.” Akasema Mathew akanyamaza kidogohalafu akaendelea.

“ Dr Joshua alimtaarifu Dr Kigomba kuhusu kuwasili kwa mtu aliyemtaja wka jina moja tu la Hussein.Si mara ya kwanza kwa Dr Joshua akumtaja mtu huyu mtu na nina hisi kwamba ana nafasi kubwa sana katika jambo hili.Hussien anategemea kuwasili kesho jioni .Hatufahamu ni raia wa nchi gani na hata sura yake hatuifahamu lakini ni mtu muhimu sana ambaye tunatakiwa kumfahamu na kumfuatilia kwa karibu sana toka dakika ambayo ataingia nchini.Nina uhakika mkubwa kwamba mtu huyu kama si yeye aliyekuja kuuchukua mzigo huo basi ni wakala kwa hiyo jicho letu halitakiwi kubanduka kwake.” Mathew akanyamaza akawatazama wenzake waliokuwa kimya wakimsikiliza kisha akaendelea.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ ili kumfahamu Hussein ni nani tunapaswa kuipata namba yake ya simu toka katika simu ya Dr Joshua na anayeweza kuipata simu ya Dr Joshua na akatupatia namba ya Hussein ni Peniela pekee.Zoezi la kuipata namba hiyoya simu toka katika simu ya Dr Joshua linatakiwa lifanyike kesho ili tuweze kumfahamau Hussein na kumfuatailia toka dakiak ya kwanza anapoingia nchini.Unasemaje kuhusu hilo peniela linaweza ufanyika kesho? Akauliza Mathew

“ Usihofu Mathew,ninaweza kuifanya kazihiyokesho.Najua Dr Joshua kwa siku ya kesho atakuwa na pilika nyingi za msiba lakininitahakiksha kwamba ninakutana naye na ninaipata simuyake na kuichukua hiyo namba ya Hussein tunayoitaka” akasema peniela

“ Are you sure peniela? Hatutaki kukuweka katika hatari” akasema Mathew



“ Usiogope Mathew.Nitakupatia hiyo namba kesho..” Akasema peniela



“ Thankyou so much Peniela “ akasema Mathew



“ Nini kitafuata baada ya kumfahamu Hussein? Akauliza Peniela

“ Kama nilivyosema awali kwamba Dr Joshua amemtaja Hussein zaidi ya mara moja kuhusiana na mpangohuu.Mara ya kwanza alimfahamisha Kigomba kwamba amezungumza na Hussein na amemfahamisha kwamba tayari pesa imekwisha ingizwa katika akaunti walizofungua nje ya nchi.Katika maelezo mengine Dr Joshua amemtaarifu Kigomba kwamba Hussein atawasili kesho na inaonyesha wazi kwamba ujio wake huu ni wa kuja kukamilisha biashara yao na ikiwezekana kuondoka kabisa na kirusi hicho. Dr Joshua atamkabidhi Kigomba package hiyo na ambaye ndiye atakayefanya makabidhiano na wanunuzi .Nina hakika kabisa kwamba makabidhiano hayo yatafanyika sehemu fulani ambako wanunuzi itawalazimu wahakikishe kwamba kitu walichouziwa ni chenyewe .Hili litafanyika sehemuya siri sana .Kwa kuwa sisi tayari tunamfuatilia Kigomba kila aendako basi itakuwa rahisi kujua yuko wapi na tutamdhibiti na kuichukua hiyo package. Wakati huo huo Hussein naye atadhibitiwa kikamilifu ili asije akatoroka kwani mtandao huu wote unatakiwa utiwe nguvuni.Huo utakuw amwisho wa mchezo.”Mathew akasema halafu akafikiri kidogo na kusema



“ Kwa namna yoyote ile nilazima tupate mtu ambaye anaweza akatusaidia kwa upande wa kumdhibiti Hussein.Ni nyakati kamahizi ninakumbuka sana Noah”akasema Mathew



“ Josh can do that”akasema Peniela

“Josh ?!

“ Ndiyo .Ni kijana mwenye uwezo mkubwa sana anafuata maelekezo na anaweza akaifanya kazi hii bila matatzo”

“ Are yu sure we can trust him? Akauliza Mathew



“ Bila wasiwasi.Josh aliaminiwa sana na John Mwaulaya na alikuwa akimtumia sana katika shughuli zake mbali mbali na kama alikuwa akihitaji kumshughulikia mtu Fulani basi alikuwa akimtumia josh.NI kijana ambaye ana malengo ya kuachana na team SC41 na kuanza maisha mapya kwa hiyo anaweza akatufaa sana” akasema Peniela



“sawa.Tutampataje Josh?akauliza Mathew

“kesho asubuhi nitalazimika kwenda nyumbani kwa John kuonana na Team SC41 na kujua ni kitu gani ambacho wamekipanga kuhusianana na msiba wa john.Nina hakika mpaka mida hiii watakuwa wamejiuliza maswali mengi sana kuhusiana na kutoonekana kwangu.Baada ya kifo cha amos ,mimindiye wananitegemea sana katika suala hii.Ninataka nifahamu pia kuhusiana na mipango yao ya kuipata package na nitawataarifu ” Akasema Peniela

“ Ok jamani nadhani tumeelewanatutapanga zaidi kesho.Siku ya leo imekuwa ni ndefu sana kwetu kwa hiyo niwakatiwa kwenda kupumzika na kujiandaa kwa ajili ya kesho.” Akasema Mathew



“ Kabla hatujaondoka humu kuna suala ninataka kuuliza”akasema jaji Elibariki



“ Uliza Eli” akasema mathew

“ Tunaye Rosemary Mkozumi humu ndani tunaendelea kumshikilia ,nini hatima yake? Suala lake linashughulikiwa vipi?



“ Suala la Rosemary ni kubwa na linatakiwa kushughulikiwa kwa upana wake.Tumeliweka pembeni kidogo tumalize kwanza suala la Dr Joshua na ndipo tutaendelea na suala la Rose.Tutaendelea kumshikilia hapa ambayo ni sehemu salama zaidi.Vile vile kuna suala la Deus alilomweleza Peniela kuhusiana na mipango waliyonayo juu yako Elibariki na Peniela.Yote haya tutayaweka pembeni kwa muda ili tushughulikie kwanza hili kubwa “ akasema Mathew

“ Mathew mimi sintalala hapa ninaomba niondoke niende nyumbani nikapumzike ili kesho niamkie katika masuala mengine.Tutawasiliana kuhusiana na kinachoendelea..” akasema Peniela.

“ Hapana peniela.Tayari umekwisha kuwa usiku mwingi.Hapa kuna nafasi ya kutosha na zaidi sana ni sehemu salama .Utalala hapa” akasema Mathew

“ Mathew dhumuni la kutaka kwenda nyumbani ninataka kufanya mawasiliano na Dr Joshua usiku huu .Simu ninayotumia kuwasiliana naye iko nyumbani so I must go there” akasema Peniela.

“ Ok sawa.Kama umesisitiza kwamba unataka kwenda basi nitakupeleka ukaichukue hiyo simu kisha tutarejea hapa.Peniela wewe ni mtu muhimu sana kwa sasa na siko tayari upatwe na tatizo lolote.” Akasema Mathew.Peniela akatabasamu na kutikisa kichwa kukubalianana Mathew kisha wakaingia katika gari la Mathew na kuondoka kuelekea nyumbani kwa Peniela

“Mathew imekuwa vizuri sana nimepata nafasi hii ya kuwa nawe kuna mambo mawili ninataka tuyajadili.” Akasema peniela

“Nakusikiliza Penny”akasema Mathew.

“usijali Mathew tutajadili tukifika nyumbani” akasema Peniela kisha wakaendelea na safari.

“ Mathew kwa nini hukutaka nije kulala nyumbani kwangu wakati unafahamu kabisa kwamba ni vigumu tena mimi kuwa karibu na Elibariki hasa kwa kitendo alichokifanya? Akauliza Peniela.



“ Peniela tulikubaliana kwamba masuala yale yaliytokea yawekwe pembeni kwanza kwa muda hadi tutakapomaliza masuala mazito yanayotukabili”akasema Mathew.Peniela akamtazama na kuuliza

“ Mathew toka alipofariki mkeo,have you ever been in love?

“ There is only one woman I Ever loved on earth.Thats my wife ..She died with all the love I had inside me so my heart is empty.Kujibu swali lako ni kwamba sijawahi kuzama mapenzini kwa mwanamke yeyote Yule toka alipofariki mke wangu”akasema Mathew



“ That’s why you don’t know the pain I’m feeling right now.” akasema Peniela.

“Umesemaje?!! Akauliza Mathew

“ Nimesema kwamba bado huyafahamu maumivu ya kumpenda mtu halafu akakufanyia kama alivyonifanyia Elibariki” akasema Peniela

“ Peniela nimepitia mambo mengi zaidi yako.Ninayafahamu mapenzi zaidi ya unavyoyafahamu wewe.Nimeumizwa na mapenzi zaidi ya ulivyowahi kuumizwa wewe na ndiyo maana nikasema kwamba suala lako na Elibariki nisuala dogo na linaweza kumalizika.Are you sure that you love him? Are you sure that he loves you? Unatakiwa ujiulize maswali haya kabla ya kuuruhusu moyo wako uumie kwa sababu ya mtu Fulani.Anastahili machozi mtu Yule ambaye una hakika kwamba uko tayari hata kufa kwa ajili yake lakini kama huna uhakika na hilo just let this go” Akasema Mathew

“ Do you think it’s easy to let this go Mathew? I love Elibariki with all my heart na ndiyo maana nimeumia sana kwa kitu alichonifanyia.Sikutegemea kama angeweza kunifanyia kitu kama kile.” Akasema Peniela.

“ Peniela forget what happened and move on.Thats my advice to you”akasema Mathew

“ I don’t know if I’ll move on without him.I love him so much”



“ If you do love him that much then forgive him” akasema Mathew kisha safari ikaendelea kimya kimya.Baada ya muda Penieal akasema

“ Mathew kuna jambo lingine nataka kukuuliza “ akasema Peniela

“ Uliza peniela hii ni fursa yako” akajibu Mathew



“ wakati tukijiandaa kwenda kwa Deus usiku huu ,ulikuja chumbani kwa Anitha na ukafungua mlango ukanikuta nikiwa mtupu ninavaa .Nilijua ni bahati mbaya labda hukujua kama ninavaa na nilitegemea ungefunga mlango mara moja na kuondoka na baadae ungeniomba samahani lakini hukufanya hivyo badala yake ukaendelea kusimama pale mlangoni unanitazama .Nilikuona na sikutaka kukusemesha.Nataka kujua Mathew kwa nini ulifanya vile? akauliza peniela.

“ I’m sorry for that peniela.Sikujua kama ulikuwa unavaa” Akajibu Mathew



“ Mathew si suala la kuomba msamaha na wala hii si kesi.Ninachotka kusikia toka kwako ni kwa nini baada ya kunikuta ninavaa hukuufunga mlango na kuondoka badala yake ukabaki unanitazama? Mathew ninakuamini wewe ni muwazi na huwezi kunificha kuhusu hili.Be honest with me” akasema peniela

“ Kumbe aliniona?!!..dah !aibu gani hii..” akawaza Mathew

“peniela naomba tafadhali tusiongele suala lile la aibu.Samahani sana kwa kitendo kile cha aibu nilichokifanya and please don’t tell anyone” akasema Mathew



“ Mathew naona hujanielewa.Ni kwamba sikulaumu kwa kitendo kile na wala sijakasirika na wala sioni aibu kwa sababu najua mwili wangu wote umekwisha uona ukiwa mtupu. Ninachotaka kufahamu ni kwa nini ulisimama mlangoni na kunitazama? Do you like my body when naked? Akauliza Peniela na kumpa wakati mgumu Mathew kujibu.

“ peniela naomba tafadhali tusiliongelee suala hilo” akasema Mathew.Peniela akatabasamu na kusema

“ Mathew ninajua unachokiogopa kukisema.Let me answer for you.You liked me ,right? Akasema peniela Mathew akabaki kimya.



“ Ever since we met I knew you liked me but you are scared to let me know.Ulitakiwa kuniambia ukweli wako Mathew because even me I’ve started to like you” akasema peniela.



“ Peniela tafadhali naomba tuachane na mambo hayo.”akasema Mathew



“ I’ve been in many places around the world and I’ve met so many guys lakini sijawahi kukutana na mtu kama wewe Mathew.You are a real gentleman.”akasema peniela .

“ peniela ni mwanmke mwenye majaribu makubwa sana.Ana maneno matamu ambayo yanaweza kukufanya akili yako yote isiwaze kitu kingine chochote zaidi yake yeye tu. Nimekwisha fahamu anachokitaka na siwezi kumpa nafasi. “ akawaza Mathew



“ Pamoja na hayo lazima nikiri kwamba Peniela amependelewa uzuri wa kipekee kabisa.Anasisimua mno na ndiyo maana nilipomkuta akiwa mtupu mle chumbani nilijikuta nikisisimkwa na nikashindwa kubandua mguu pale mlangoni..She’s hot” akawaza Mathew

Walifika nyumbani kwa Peniela wakaingia ndani.Nyumba ilikuwa tulivu sana



“ Home sweet home.I missed my house so much”akasema Peniela na kumkaribisha Mathew sofani.Peniela akafungua kabati kubwa ambalo hulitumia kuhifadhia mvinyo akatoa chupa kubwa ya mvinyo na kuiweka mezani



“ Mathew imekuwa ni siku ndefu sana na mambo mengi yametokea siku ya leo.Kwa nini tusiitumie nafasi hii kutuliza akili wakati tukijiandaa na kesho?akasema Peniela huku akimimina mvinyo katika glasi na kumpatia Mathew

“ Ulisema kuna mambo ambayo unataka kuniuliza ? akauliza Mathew



“ Ndiyo Mathew but before that I’m hungry ,why don’t we make something to eat? Aren’t you hungry? Akauliza Peniela



“ hata mimi ninahisi njaa” akasema Mathew.



“ Wakati ninaandaa chakula kwa nini usiende kuoga na upunguze uchovu? Akasema Peniela

“ Hilo ni wazo la msingi .Ninahisi uchovu mwingi sana.” Akasema Mathew.

Penela akamshika mkono Mathew na kumuogoza hadi chumbani kwake akamuingiza katika bafu lake kubwa na zuri akamuacha humo kisha akaenda jikoni kuendelea kuandaa chakula.



“ Elibariki amenifanyia kitendo cha aibu sana na ameniumiza mno.Nilimpenda sana lakini kwa kitendo alichokifanya sitaki tena kuendelea naye.Nimeanza kuvutiwa na Mathew.Ni kijana mzuri anajitambua na kujiheshimu tofauti na Elibariki ambaye anaonekana kuwa na tamaa.Mathew anaonekana ni mtu mwenye msimamo kwani toka mke wake alipofariki hajawahi kujiingiza tena katika mapenzi na mwanamke mwingine .Sina hakika kama ananipenda lakini nina hakika na kitu kimoja kwamba ana hisa Fulani juu yangu.Nina uhakika huo kutokana na namna alivyokuwa ananiangalia .Hii ni sehemu nzuri kwa kuanzia .” akawaza Peniela.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Aliandaa chakula chepesi haraka haraka kisha akarejea chumbani .Bado Mathew alikuwa amekaa katika jaccuzi akioga.Kichwa chake kilijaa mawazomengi sana.Mara mlango wa bafu ukafunguliwa akaingia peniela akiwa amejifunga taulo.Mathew macho yakamtoka pima.Peniela akamtazama akatabasamu na kusema

“ Mbona umestuka Mathew? Umestuka kuniona hivi? Akauliza Peniela huku akitoa kichekokidogo

“ Usiogope Mathew kwani hakuna kitu ambcho hujakiona.”akasema Peniela na kuliangusha taulo akabaki mtupu.








“ Ouh my God !!..Huyu Peniela anataka kufanya nini ? Mbona ananiingiza katika jaribu kubwa ? Akawaza Mathew huku mwili ukimsisimka kwa kuushuhudia wazi wazi mwili ule mwororo wa Peniela uliokuwa uking’aa kama malaika.

Huku akitabasamu,Peniela akaingia ndani ya jaccuzi ,Mathew akabaki anamtazama.Ghafla Picha ya moto mkubwa ukiiteketeza nyumba yake ambayo ndani yake walikuwemo mke wake na wanae wawili ikamjia tena kichwani , akainuka na kutoka ndani ya jaccuzi akaelekea chumbani na kuvaa nguo zake.Peniela akashangaa sana naye akatoka ndani ya jaccuzi akamfuata Mathew chumbani.Alikuwa mtupu.Mathew akachukua taulo na kumvalisha



“ Mathew what’s wrong? Unaogopa nini? Akauliza Peniela huku akionyesha kushangaa



“ C’mon Mathew.Usiogope tafadhali “ akasema Peniela.



“ I cant do that Peniela .Tafadhali nenda kaoge kisha tuondoke “ akasema Mathew



“ Mathew usiwe muoga namna hiyo.No body is watching us.Its just me and you.Tafadhali Mathew naomba unisaidie kuniondolea machungu ya kuumizwa na Elibariki.I need you just for few minutes”

“ Peniela naomba unielewe kwamba siwezi kufanya kitu hicho unachotaka tufanye” Mathew akaendelea kusisitiza.Peniela akamfuata na kusimama karibu yake akamtazama kwa macho yake malegevu na kusemahttp://deusdeditmahunda.blogspot.com/



“ Mathew its been years since your wife passed away so you need this.Najua unahitaji sana kufanya mapenzi na mimi na ndiyo maana hata sasa nyeti zako zimefura.Tafadhali usiendele kujitesa Mathew.Let us do it”



“ Peniela nimekwisha kwambia kwamba siwezi kufanya hicho kitu.Ni kweli mke wangu amefariki muda mrefu sasa na toka alipofariki sijajihusisha tena katika mahusiano na sitaki kufanya hivyo.”

“ Kwa nini Mathew unajitesa hivyo? Akauliza Peniela



“ Because I still love her !! akajibu Mathew



“ Hahahaha Mathew ,your wife is gone and she will never come back so you have to move on.Mathew naomba nikuweke wazi kwamba ninakutamani sana na mwili wangu uko tayari kwa ajili ya kukufurahisha .Please Mathew…” akasema Peniela.Mathew akaitazama saa yake na kusema

“ Peniela muda unakwenda sana.Kesho ni siku ndefu na tuna kazi nyingi kwa hiyo jiandae tuondoke.Utanikuta ninakusubiri sebuleni” akasema Mathew na kuanza kupiga hatua kuondoka mle chumbani.Peniela akamuita

“ Mathew !!..

Mathew akageuka na kumtazama



“ Mathew are you sure that you don’t want to make love with me? Akauliza Peniela.Mathew akamtazama na kusema



“ Yes ! I’m sure”

Peniela akamsogelea na kusema



“ Ninajifahamu mimi ni mzuri na uzuri wangu ni kama ua lenye harufu nzuri ambalo huwavutia nyuki kutua na kuling’ang’ania .Sifahamu ni kitu gani ninacho ambacho huwafanya wanaume wachanganyikiwe na mimi na hiyo imenifanya niamini kwamba hakuna mwanaume ambaye nitamtaka katika hii dunia ataniambia hapana na haijawahi kunitokea kwa mwanaume kuniambia hapana lakini kwa usiku wa leo kwa mara ya kwanza nimekutana na mwanaume ambaye amenitazama nikiwa mtupu akanitazama machoni na kuniambia Hapana.Si kunitamkia tu neno hilo bali ameokota taulo na kunivisha ili asiendelee kunitazama nikiwa mtupu.Wanaume wengine wote hufurahi na kuchanganyikiwa wakiniona nikiwa mtupu lakini kwako imekuwa tofauti.Mathew thank you so much.Kitendo cha kunikatalia kufanya mapenzi usiku huu kimeonyesha ni namna gani unavyonithamini.Uliokota taulo na kunivisha kunionyesha kwamba mwili wangu una thamani kubwa na hautakiwi kuachwa utupu bila sababu.Mathew wewe ni wa kipekee kabisa na kitendo hiki cha leo kimenifanya nizidi kutamani kukufahamu zaidi kwani nahisi bado sijakufahamu vizuri wewe ni mtu wa aina gani.You are different from all men I know ” akasema Peniela.Mathew akamtazama na kusema

“ Tukiwa nyumbani uliniuliza swali ni mwanamke wa aina gani ninayemuona ndani yako na nikakujibu kwamba ninapokuona ninamuona mwanamke jasiri,mwenye ndoto na ambaye yuko tayari kwenda hadi ncha ya mwisho wa dunia ili azitimize ndoto zake,mwanamke asiye kata tamaa ,mwanamke mwenye nguvu kubwa ndani yake licha ya mwili wake kuwa mdogo, mwanamke mwenye sauti laini lakini inayoweza kupenya hadi ndani ya mioyo ya watu wenye nguvu na wakavifunga vinywa vyao kumsikia.Mwanamke wa aina hii ni mwanamke ambaye binafsi ninamuheshimu sana zaidi ya ninavyoweza kueleza na sistahili hata kuugusa mwili wake.Peniela hata mimi ni binadamu na nina matamanio kama wengine na ninakiri kwamba hili ni jaribu langu kubwa sana kuwahi kunitokea lakini siwezi kuuchezea mwili wako kwa sababu ninakuheshimu sana ,na ninaomba nikuweke wazi kwamba moyo wangu unaniuma sana pale ambapo mwili wako hutumika kufanikisha baadhi ya mambo kama ilivyotokea leo kwa Deus.Ili kupata taarifa tulizohitaji ulilazimika kuutoa sadaka mwili wako na ndipo akakueleza kile tunachokitaka.Mwili wako umegeuzwa bidhaa and no body cares..jambo hili linaniumiza sana na ndiyo maana ninasema kwamba muda sio mrefu jambo hili litafikia mwisho na utaishi maisha yako kwa uhuru na amani na wala hutalazimika tena kuutumia mwili wako huu wa thamani kubwa kwa ajili ya kupata taarifa mbali mbali kama ufanyavyo sasa kwani katika wakati huo hakutakuwa tena na team SC 41. “ akasema Mathew . Peniela akashindwa kujizuia akamfuata na kumkumbatia kwa nguvu huku machozi yakimtoka.

“ Mathew ulikuwa wapi? Wewe nI mwanaume ambaye nilikuwa ninakuhitaji sana katika maisha yangu.Ee Mungu Ahsante sana kwa kuniletea kijana huyu ambaye ndiye haswa niliyekuwa ninamtafuta katika maisha yangu.Ananijali na kunithamini huyu ndiye atakayenifaa . Huyu ndiye mwanaume wa maisah yangu. “ akawaza Peniela

“ Thank you Mathew.Thank you so much.Sina neno la kusema kwa hayo maneno mazito uliyoyatamka” akasema Peniela huku machozi yakimdondoka.Mathew akamfuta machozi na kusema

“ Peniela muda unakwenda kwa kasi kwa hiyo jiandae ili tuweze kuondoka” akasema Mathew na kuitoa mikono ya Peniela iliyokuwa imeng’ang’ania halafu akafungua mlango wa chumbani na kutoka akaelekea sebuleni

“ Ee Mungu ahsante kwa kunipa nguvu ya kulishinda jaribu hili kubwa.Haikuwa rahisi ,Ilihitaji nguvu ya ziada kuweza kulishinda .Hata Peniela mwenyewe ameshangaa sana na kushindwa kuamini kwamba nimekataa kufanya naye mapenzi licha ya ushawishi wote alioufanya.kwa maelezo yake mwenyewe ni kwamba hajawahi kukutana na mtu ambaye ameuona mwili wake na akakataa kufanya naye mapenzi.” Akawaza Mathew wakati akielekea sebuleni



“ Team SC41 wamemfanya Peniela aondoe kabisa thamani ya utu wake na ndyo maana yuko tayari kuutoa mwili wake kwa mwanaume yeyote Yule ili mradi kuna kitu anakkitaka kwake.Peniela ni mwanamke mzuri na anayestahili heshima kubwa na hapaswi kuuchezea mwili wake kama afanyavyo sasa.Nitahakikisha anakuwa na maisha yake ya kawaida ambayo hayatamlazimu kuutumia mwili wake kama chambo” akawaza Mathew.Akaketi sofani na kujimiminia mvinyo kidogo katika glasi akanywa

Baada ya dakika kumi Peniela akatokea .Alikuwa amependeza sana.

“ Dah ! mwanamke huyu ana uzuri wa ajabu sana. Kila ninapomuona mwili wote unanisisimka.Nina wasiwasi kwamba nisipokuwa makini yawezekana na mimi nikajikuta nimeanguka na kuzama katika penzi zito na malaika huyu..” akawaza Mathew



“ Mathew samahani sana kwa jambo lililotokea chumbani.” Akasema Peniela

“ Usijali Peniela.Ni jambo la kawaida.”

“ Mathew kuna jambo ninataka kuliomba toka kwako.”

“ Jambo gani?



“ Ninaomba baada ya mambo haya kumalizika ,mimi na wewe tupate nafasi ya kwenda mahala na kupumzika hata kama ni nje ya nchi .I want to spend much time with you.I want to know you better” akasema Peniela,.Mathew akatabasamu na kusema



“ Tutaangalia kama itawezekana .”

“ Thank you Mathew “ akasema Peniala na kuchuua simu ambayo huitumia kuwasiliana na Dr Joshua akabonyeza namba Fulani na kuiweka sikioni.

“ namba yako ya utambulisho tafadhali ” ikasema sauti ya upande wa pili iliyopokea simu.

“ pkp46 “ akasema Peniela

“ Ok subiri kidogo” akasema yule mwanadada aliyepokea simu.Baada ya kama dakika moja hivi sauti nzito ya kiume ikasikika katika simu

“ Hallow Peniela” ilikuwa ni sauti ya Dr Joshua



“ Dr Joshua “ akasema Peniela



“ Hallo my queen..Unaendeleaje? Nimestuka kidogo ulipoamua kutumia njia hii ya dharura.” Akasema Dr Jshua

“ Dr Joshua najua si matumizi sahihi ya simu hii ya dharura lakini sikuwa na namna nyingine ya kuweza kuwasiliana nawe .Lengo langu ni kutaka kukujulia hali na kukupa pole sana kwa kifo cha Flaviana.Nimesikitishwa mno na kifo hiki.Pole sana my love” akasema Peniela

“ Peniela ahsante sana.Madaktari walijitahidi kwa kila namna walivyoweza lakini ikashindikana haikuwezekana kupona.”

“ Pole sana Dr Joshua.”



“ Ahsante sana Peniela”



“ kwa hiyo lini mwili wa Flaviana utarejeshwa nchini kwa mazishi? Akauliza Peniela



“ Kesho saa tano asubuhi mwili wa Flaviana utarejeshwa nyumbani kwa ajili ya maandalizi mazishi.”



“ Ahsante kwa taarifa Dr Joshua.Tutashirikiana pamoja katika kuupokea mwili na hadi tutakapohitimisha safari ya mwisho ya Flaviana.”

“ Ahsante sana Peniela"



“ Pamoja na hayo Dr Joshua nina ombi moja kwako”

“ Peniela nimekwisha kupa ruhusa ya kuomba chochote kile unachokitaka bila hata ya kuniuliza kwanza”

“ Ahsante Dr Joshua.Nnajua kesho utakuwa na shughuli nyingi lakini ninataka utafute nafasi tuonane hata kwa dakika ishirini tu.Nina maongezi nawe na ninataka nitumie dakika hizo chache kukufariji mpenzi wangu.Nataka tukutane katika ile nyumba yetu kule ufukweni” akasema Peniela

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Uliponiambia kuna kitu unataka kuniomba nilidhani kuna jambo kubwa na zito kumbe ni hilo tu,basi usijali Peniela kesho mara tu baada ya kutua na kuelekea nyumbani nitatafuta muda na tutaonana.Saa saba za mchana tutaonana.Hata mimi nina hamu sana ya kukuona malaika wangu.Ninahitaji sana faraja yako na vile vile kuna jambo ninataka tuongee mimi na wewe linalohusu maisha yetu” akasema Dr Joshua

“ Ahsante sana kwa kunikubalia ombi langu mpenzi wangu.Basi naomba nikutakie usiku mwema na safari njema hiyo kesho.Tutaonana hiyo kesho.I love you so much” akasema Peniela na kukata simu kisha akaitupa pembeni na kumtazama Mathew



“ Samahani Mathew kwa kusikia maongezi yangu na huyu mzee lakini hivi ndivyo huongea naye.Anachotaka kukisikia Dr Joshua toka kwangu ni kwamba ninampenda sana nami siku zote huwa ninajaribu kumuhakikishia kwamba ninampenda lakini laiti angeweza kuusoma moyo wangu na namna ninavyomchukia angeniogopa kama kifo.Ninamchukia sana Yule mzee lakini sina namna nyingine ya kuweza kumuepuka lazima nikubali kumpenda ili mipango yetu ifanikiwe.” Akasema Peniela

“ Usijali Peniela.Mambo haya yatakwisha muda si mrefu.” Akasema Mathew.

“ Huyu mwanamke ana kitu gani anachokitumia kuwachanganya wanaume akili kiasi hiki? KIla mwanaume anayetembea naye anachanganyikiwa kabisa kama alivyomchaganya rais wa nchi.Peniela ni mwanamke mwenye uwezo wa kipekee na ni hatari zaidi ya watu wanavyomchukulia.Kama ameweza kupenya hadi kujenga mahusiano na rais wa nchi basi anaweza kuingia sehemu yoyote ile na akafanya chochote .Kuna nyakati hata mimi mwenyewe ninamuogopa kutokana na uwezo alionao wa kushawishi mtu yeyote Yule.Wasiwasi wangu ni kwamba hata mimi najihisi kwamba muda si mrefu ninaweza nikajikuta nimeshindwa kuendelea na msimamo wangu na kujikuta nikizama mapenzini na kimwana huyu kwani kadiri ninavyozidi kukaa naye karibu ndivyo ninavyojikuta nikizidi kuvutiwa naye na kutamani kuwa naye karibu zaidi na zaidi…………..” akawaza Mathew kisha akasema.



“ Peniela jambo kubwa lililotuleta hapa kwako ni kuzungumza na Dr Joshua na tayari umekwisha ongea naye.Nadhani sasa tunaweza kuondoka.” Akasema Mathew



“ Mathew are you sure you don’t want to spend time here at my house? Usihofu hapa ni sehemu salama sana “ akasema Peniela

“ Hapana Peniela tunatakiwa turejee nyumbani kwangu .Ninaamini sana usalama ulioko pale kuliko sehemu nyingine yoyote ile.” akasema Mathew.Peniela akaenda kufunga chumba chake halafu wakaingia garini na kuondoka

“ Peniela kuna mambo uliniambia unataka tuyajadili,mbona hukunikumbusha tena ili tujadili? Akauliza Mathew wakiwa garini



“ Ah ! usijali Mathew tutajadili siku nyngine tena kama tukifanikiwa kupata nafasi nzuri kama tuliyoipata leo.” Akasema Peniela na Mathew akatabsamu

“ Tutapata nafasi Peniela usijali.Bado tuna muda mwingi wa kuweza kukaa na kujadili mambo mengi tu “ akasema Mathew na mara simu ya Mathew ikaita.Alikuwa ni Anitha



“ Hallow anitha.Bado hujalala mpaka mida hii? Akaulzia Mathew



“ Nitalala vipi bil akuhakikisha umerejea salama? Akasema Anitha



“ Ahsante sana Anitha kwa kunijali.Kuna jambo jipya?

“ Mathew unakumbuka kuna wanati Peniela alitumia simu ya hapa ndani kumipigia mtu wake na kumfahamisha kwamba hatarejea leo?

“ Ndiyo ninakumbuka ,alimpigia Josh” akasema Mathew

“ Basi kijana Yule yuko katika laini ya simu anataka kuongea na Peniela” akasema Anitha.Mathew akampa simu Peniela

“ Josh wants to talk to you” akasema Mathew

“ Hallow” akasema Peniela.



“ Peniela ngoja nikuunganishe na Josh anataka kuongea nawe” akasema Anitha na kumuunganisha josh na Peniela

“ hallow Peniela” akasema Josh

“ Josh,is everything ok? Akauliza Peniela



“ Peniela you are being followed “ akasema Josh

“ Followed by whom? Peniela akashangaa

“ Ulionekana kupitia kamera zilizofungwa nyumbani kwako ukiingia kwako usiku huu ukiwa umeongozana na Mathew na hivyo wakatuma watu kuja kukuchunguza ulikuwa wapi na unafanya nini.Wako nyuma yako wanakufuatilia.Kuwa makini sana” akasema Josh



“ Ouh my gosh !! akasema Peniela

“ Peniela kuna nini?



“ Team SC41 wanatufuatilia” akasema Peniela.Nikweli kupitia kioo cha pembeni Mathew akagundua kwamba kuna gari lilikuwa linawafuatilia .

“ Hata mimi nilihisi kuna gari linatufuatilia toka tulipoondoka nyumbani kwako.Get ready.We must do something…” akasema Mathew na kuongeza mwendo wa gari.



“ Wewe na Amos mlikuwa ni watu muhimu na mnaotegemewa sana na Team Sc41 katika zoezio zima la kuipata package na baada ya Amos kuuawa ,umebaki peke yako .Uliondoka bila kuwaaga na hawajui umeelekea wapi .Tayari team SC41 wamekwisha anza kuwa na wasiwasi na wewe na ndiyo maana wanakufuatilia ili wazifahamu nyendo zako.Tayari wamehisi kuna kitu hakiko sawa ” Akasema Mathew

“ kwa hiyo tutafanya nini Mathew? Hata mimi nina wasiwasi kwamba tayari wamekwisha gundua kwamba nina shirikianananyi kwani Dr Martin aliwaambia wale madaktari waliotoka Marekani kwamba haliya John ilibadilika baada ya wewe kumtolea vitisho.Walitaka sana kukufahamu na wakamuhoji Josh maswalimengi kama anakufahamu lakini alikana kukujua na akasema kwamba mimi ndiye ninayekufahamu kwa hiyowalikuwa wanatafuta nafasi ya kunihoji.Nilipoondoka kule hospitali bila kuaga kumewapa maswali mengi na kuwafanya waamini kwamba ni kweli kuna watu ninashirikiana nao.Mathew watu hawa ni hataisana na tusipojitahidi wanaweza wakatuua.” Akasema Peniela kwa wasi wasi huku akilitazama gari lile lililokuwa linawafuata nyuma yao.

“ Siku zote usihofu unapokuwa karibu na mimi” akasema Mathew na kufungua droo ya gari kulikuwa na bastora nne.Peniela akachukua mbili na kumpatia Mathew mbili.

“ Utafuata kile nitakachokuelekeza sawa? Akasema Mathew

“ Sawa Mathew.” Akajibu Peniela lakini kabla hawajafanya lolote zikatokea gari mbili mbele yao ambazo zilikuwa zinakuja kwa kasi huku zikiwasha taa zote kubwa na kumfanya Mathew apate ugumu kuona mbele



“ Damn it !!..akasema Mathew na kufunga breki za ghafla ,akageuza shingo ili aweze kulitazama gari lile lililokuwa linawafuatilia nyuma,lilikuwa karibu sana.Pembeni ya bara bara kulikuwa na vibanda vitatu ambavyo vilionekana ni kama vya wafanya biashara ndogo ndogo.

“ Peniela nahisi hizi gari mbili zinazokuja mbele yetu ni za kwao pia.Hatuwezi kuendelea mbele wametudhibiti kila kona.Shuka garini nenda kajifiche katika kibanda kimoja wapo kuna kitu ninataka kufanya.” Akasema Mathew na bila kupoteza hata sekunde Peniela akafungua mlango na kukimbia hadi katika kibanda kimoja wapo akajificha.Mathew akaliona tofali pale karibu yake akafungua mlango na kulichukua tofali kisha akaiganzamiza pedeli ya mafuta kwa kutulia tofali lile na yeye akaruka nje.Gari ilifyatuka kwa mwendo mkali sana nazile gari mbilizilizokuwa zinakuja mbele yao zikasimama na haraka haraka milango ikafunguliwa watu wakashuka na mara ikaanza kusikika milio ya risasi ,wale jamaa walianza kulimiminia risasi gari la Mathew wakiamini kuna mtu ndani na ghafla kikasikika kishindo cha magari kugongana.Garila Mathew liligonga mojawapo ya zile gari mbili.

.Mathew alitoka mtaroni alikoangukia mara aliporuka garini na kuelekea nyuma ya kibanda alichokuwa amejibanza Peniela.Baada ya kishindo kile wale jamaa wakalizunguka gari la Mathew an kuchungulia ndani lakini hakukuwa na mtu yeyote.Lile gari lililokuwa likiwafuata nyuma akinamathew likasimamana wakashuka watu wanne na kuanza kukimbia kuelekea mahala walipokuwa wenzao.walijadiliana kwa sekunde kadhaa kisha wakaanza kuwatafuta akina Mathew.

“ Hawako mbali na hapa.lazima watakuwa maeneo ya karibu i”akasema mmoja wao



“Wanatutafuta.Tunatakiwa tuwastukize “akasema Mathew na kisha akainuakichwa na kuchungulia nakwa kasi ya ajabu wote wawili wakasimama na kuanza kuwachafua wale jamaa kwa risasi.lilikuwa ni shambulio ambalo hawakulitarajia ,watu wanne wakaanguka chini .

“ Tayari wamekwisha tuona tulipokaa,let us get out of here”akasema Mathew na kabla

na hawajaondoka akapigwa risasi akaanguka chini

“ Aaaaaghhhhh !!!..akatoa mguno na kuanguka chini,



“ Mathew ! Mathew !..akaita Peniela huku akimtingisha Mathew aliyekuwa akigala gala kwa maumivu .



“ Nyuma yako Penny!!!.” Mathew akapaaza sauti.Penny akageuka na kumuona mtu mmoja akiwa amesimama nyuma yao akiwa amewaelekezea bastora.

Kwa kasi ya aina yake ambayo Mathew hakuitarajia Peniela akanyakua bastora yake na kumchakaza Yule jamaa kwa risasi akaanguka chini.Mivumo ya risasi ikaanza kusikika kuelekea kule mahala waliko.Mathew akainuka na kuegemea kibanda ,Peniela akamsaidia kuinuka wakaenda kujificha nyuma ya kizimbacha kuusanyia taka taka.

“ Mathew are you hurt? Akauliza Peniela

“ I’m ok Peniela.Risasi haijagusa mfupa imepita kwenye nyama” akasema Mathew na mara gari tatu nyingine zikawasili



"wanaongezeka.Bastora yangu imebakiza riasi chache sana” akasema Mathew



“ Me too.. I’m empty” akasema Peniela

“ we have to get out of here.Tusipo harakisha kutoka eneo hili wanaweza wakatuua hawa jamaa.Risasi tulizo nazo hazitoshi kupambana nao.Tuitumie nafasi hii ambayo wanajipanga tuondoke eneo hili” akasema Mathew kisha akachungulia na kwa msaada wa taa ya gari akaweza kuwaona watu zaidi ya sita wakiwa wamesimama wakijadiliana jambo

“ Mathew jereha lako linatoa damu nyingi,kutoka hapa hadi nyumbani kwangu hakuna umbali mrefu.Turejee nyumbani tukatibu jeraha hilo na kuchukua silaha .Ninazo silaha pale ndani”akashauri Peniela.Mathew akamtazama na kusema

“ Tutambae chini ya mtaro tutokee upande wa pili hahafu tupotee kabisa eneo hili.Tangulia.I’ll cover you” akasema Peniela akaanza kutambaa taratibu na kuingia mtaroni Mathew naye akafuata.Bado wale jamaa walikuwa wamesimama wakijadiliana jambo yawezekana hawakuwa wametegemea kupata upinzani mkali kiasi kile.

Mathew na Peniela wakatambaa katika mtaro ule wa maji machafu yaliyokuwa na harufu kali na kutokea upande wa pili wa bara bara kisha wakaambaa ambaa na mtaro hadi usawa wa nyumba moja kubwa nyeupe .Wakatoka mtaroni na kupita katika uchochoro uliokuwa pembeni ya nyumba ile kisha wakaanza kukimbia na kutokea katika mtaa wa pili .



“ Mathew unavuja damu sana.” Akasema Peniela.

“UsijaliPeniela.” akasema Mathew wakaendelea kutembea kwa kasi kubwa.Ni sauti za mbwa ndizo zilisikika.Ghafla Peniela akasimama baada ya kuona miale mikubwa ya moto katika mtaa unaofuata iliko nyumba yake.

“ Mathew kuna moto mkubwa unaonekana mtaa wa pili”akasema peniela.



“ Yawezekana kuna nyumba inaungua”akasema Mathew kisha wakapita katika nyumba moja yenye maduka manne na kutokea katika mtaa iliko nyumbaya Peniela.Taratibu Peniela akaishiwa nguvu na kuanguka chini.Nyumba ya Peniela ilikuwa inawaka moto



“ Peniela ! peniela ! akaita Mathew…







******



http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Jaji Elibariki alikaa kitandani na kuinamisha kichwa halafu akasimama akaenda dirishani akachungulia nje.Kulikuwa kimya kabisa.Akarudi kukaa kitandani

“ Lazima nikubaliane na ukweli kwamba maisha yangu tayari yame haribika .Sifahamu ni lini nitatoka humu ndani na hata kama nikitoka sijui hatima yangu ni nini kwani tayari jina langu limekwisha chafuka na ninasakwa kila kona ya nchi hii kwakosa la kusababisha mauaji .Mathew anajitahidi sana kuhakikisha suala hili linafika mwisho lakini kila anapopiga hatua fulani jambo lingine linaibuka.”akawaza na akainuka tena na kusimama dirishani.



“ maisha yangu yameharibika .Nimempoteza mke wangu,nimepoteza kazi,nimepoteza kila kitu.Sina tena muelekeo katika maisha yangu .Kinachoniumiza zaidi ni kitendo cha kukutwa na Naomi .Sijui ni shetani gani alinipitia na nikajisahau kabisa hadinikakutwa na akinaMathew.Heshima yangu imeshuka mbele ya Peniela kwa sababu ya huyu kahaba Naomi.Ninampenda sana penela na tayari nilikuwa na mipango naye mingi tu baada ya mambo haya kumalizika lakini sina hakika tena kama kuna kitu kitakachoendelea tena kati yetu baada ya tukio la leo.Nimejidhalilisha sana kwa watu walioniheshimu na kunithamini ,walioyatoa maisha yao kunisaidia.Hakuna namna ninayoweza kuwaeleza na wakanielewa kwamba haikuwa ridhaa yangu mimi kufanya vile na kujishushai heshima kiasi hiki. “akaendelea kuwaza jaji Elibariki.

“ Mathew alisema kwamba Deus Mkozumi alikuwa na mpango mkubwa juu yangu na hakunieleza kwa kina ni mpango gani huo ila alisema kwamba ni mpango wa kutufanya mimi na Peniela wenye nguvu.Mpango huu utawezekanaje wakati ninaishi kama mfungwa.Natamani sana kuufahamu mpango huo , anaMathew ameonekana kama vile hataki kunieleza na kwa kuw ampangohuo unatuhusu mimi na peniela sidhani kama mpangohuo utawezekana tena kwani Peniela amekwisha vunja rasmi mahusiano yangu na yeye.Natakiwa kuonana na Deus mkozumi mimi mwenyewe ili aniambie ana mpango gani kuhusu mimi.Natakiwa kutafuta namna ya kutokahumu ndani ili ili niweze kunana na Deus nijue ana mipango gani juu yangu. “ akawaza Elibariki



“ Ninahitaji kumpata mtu ambaye atanisaidia kutoka hapa nilipo ,niweze kusafisha jna langu na mwisho maisha yangu yaweze kurejea kama awali.Ni nani ambaye anaweza akanisaidia katika jambo hili? Akaendelea kujiuliza na kushindwa kupata jibu akaenda kukaa kitandani

“ Nisipofanya bidii nitakwama hapa nilipo na maisha yangu yatahamia ndani ya nyumba hii.Dr Joshua na wenzake wamenitengenezea kesi mbaya sana ya kusababisha kifo cha Flaviana na kwa vyovyote vile endapo nitakamatwa hata kama sina hatia nilazima nitasota gerezani kwa kipindi kirefu kwani watu wanaonitafuta niwatu wenye nguvu sana na watatengeneza kila aina ya ushahidi mpaka wahakikshe nimekutw ana hatia na kufungwa.. Lazima nikiri kwamba hapa sina ujanja tena kwani siwezi kuepuka kukaa gerezani .Jaji wa mahakama kuu na mwenye heshima kubwa sana nchini,nitatuhumiwa na kesi ya kumuua mke wangu tena mtotowa rais.Dah ! balaa gani hili” akaendelea kuwazua jaji Elibariki



“ Naona akili yangu imefikia mwisho wake wa kufanya kazi na sioni msaada wowote tena ambao unaweza ukanitoa hapa nilipo na kunirudisha katika maisha yangu ya kawaida.Najuta ni kwa nini nilijiingiza katika mambo haya.Awali nilikuwa na maisha mazuri tu na kama nisingejingiza katika masuala haya basi nisingefika hapa nilipofika sasa hivi.Lakini haya yote yamesababishwa na Peniela.Nilitaka nimtafute muuaji wa Edson ili nimuonyesha peniela ni namna gani ninamjali na ili niweze kulisafisha jina lake katika jamii.Nilimpenda Peniela na ndiyo maana nikajitolea kufanya haya yote kwa ajili yake lakini mambo yamebadilika.Peniela nimemkosa na jina langu limechafuka na sijui nitumie njia gani kulisafisha tena.Najuta sana kujiingiza katika mapaambanohaya na watu wenye nguvu..” akatoka mle chumbani na kuelekea jikoni katika kabati ambalo huhifadhiwa chupa za pombe akafungua na kuchukua moja.wakati anatoka mle chumbani akakutana na Anitha



“ Elibariki hujalaa bado? Akauliza Anitha



” Hapana Anitha ,nimekosa usingizi kabisa .Nataka nipate mvino kidogo labda ninaweza kupata usingizi” akasema jaji Elibariki na kuelekea chumbani kwake akaanza kunywa pombe ile kali



“ Kuna wazo limenijia ,kwa nini nisitafute muafaka na rais? Akasimama na kutabasamu



“ Hili ni wazo zuri sana.Hakuna ubaya wowote kama nikijishusha na kuomba msamaha kwa rais na mambo haya yakaisha.Bila ya kufanya hivyo katu hakutakuwa na muafaka wowote ule.kwa kuwa yeye ndiye aliyeviagiza vyombo vya usalama vinisake kila kona ya nchi anaweza akaviamuru viachane na msako huo ,kesiyangu ikafutwa na jinalangu likasafishwa.Nitarejea kazini na maisha yangu yataendelea kuwa ya kawaida kama zaman japokuwa nitakuwa na maumivu ya kumpoteza mke wangu Flaviana na peniela pia.” Uso wa jaji Elibariki ukapambwa na tabasamu baada ya kupata wazo lile.Akachukua chupa ya mvinyo akanywa kidogo



“ hakuna ujanja mwingine , lazima nionane na Dr Joshua nimuombe msamaha ili mambo haya yamalizike.Natumai endapo nikimuangukia na kumuomba msamaha atanielewa na anaweza akanisamehe na mambo haya yatakwisha.Lakini endapo nikionana na Dr Joshua ina maana lazima niwasaliti wenzangu kwa kuianika mipango yao yote wanayoipanga kwa Dr Joshua ili aweze kuniamini . Huu ni usaliti mkubwa sana lakini nitafanya nini? Sina namna nyingine ya kufanya.” Akaendelea kuwaza.

“ Elibariki na wenzake wamenifanyia mambo mengi makubwa hadi hapa tulipofika na kuwasaliti itakuwa ni dhambi mbaya sana.lakini nitaendelea kukaa humu ndani hadi lini? Nitaendelea kujificha hadi lini wakati sina kosa? Nitakubali maisha yangu yaharibike na niendelee kuwa mkimbizi hadi lini? Elibariki akachukua mvinyo akanywa na kuendelea kutafakari

“ Hapana siwezi kukubali maisha yangu yaharibike kiasi hiki.I must do something to save myself.Hakuna ambaye atanisaidia kunikwamua ..Mathew ana mambo mengi sana ya kushughulikia na nisipo jihangaikia mwenywe nitaozea humu ndani.Ni lazima nifanye maamuzi magumu kwa ajili ya mustakabali mzima wa maisha yangu ya sasa na yajayo.”akaenda dirishani akatazama nje



“ Moyo unaniuma sana lakini nitafanya nini wakati sina ujanja tena .Nililianzisha jambo hili na mimi ndiye nitakayelimaliza na ili kulimaliza hakuna namna nyingine ya kufanya zaidi ya kutafuta muafaka na Dr Joshua.Tayari amekwishanizidi nguvu na sina namna ya kupambana naye tena.Ninafahamu maovu yake ,ninafahamu kamuua mke wake,na amesababisha kifo cha mkewangu Flaviana lakini sina namna zaidi ya kumuangukia kwani nikiendelea kupambana naye ni sawa na kupambana na ukuta nitajiumiza mwenyewe.Potelea mbali litakalokuwa na liwe tu lakini sitaki tena kuendelea kuishi maisha haya.Acha tu niibebe dhambi hii ya usaliti lakini lazima nirejee katika maisha yangu ya kawaida.” Akawaza Elibariki

“ Lakini nitaonana vipi na Dr Joshua? Si rahisi kuonana naye hivi hivi lazimaawepo mtu wa kuniunganisha naye .Ni nani basi ambaye anaweza kunisaidia kwa hili? Akajiuliza na kutafakari kwa sekunde kadhaa halafu akapata wazo

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ Rosemary Mkozumi.Huyu anaweza akanisaidia sana kuniunganisha na Dr johua.Huyu mwanamke ana mtandao mkubwa wa watu na anaweza kuwa na msaada mkubwa kwangu.lakini ili anisaidie lazima nimfungue kule chini alikofungwa.Nafahamu Rosemary ni mtu hatari sana na anashirikiana na magaidi lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kumuachia huru ili aweze kunisaidia.Ninakumbuka kila kitu alichokifanya Mathew wakati tunamuingiza Rosemary kule chini.Ninazikumbuka namba alizobonyeza na mlango ukafunguka.Ninachotakiwa kufanya ni kumdhibiti kwanza Anitha “

Jaji Elibariki akaufungua mlango akachungulia nje.Nyumba yote ilikuwa kimya kabisa akatoka akaelekea katika chumba cha ofisi akachungulia na kumuona Anitha amekaa akiendelea na kazi akaufungu amlango na kuingia mle ofisini.Anitha akastuka



“ Jaji hulali leo? Akauliza

“ Nimekosa usingizi kabisa.Mathew na Peniela hawajarejea?



“ Hapana bado hawajarejea.Kuna tatizo limetokea”



“ Pole sana Anitha.let me make you a coffee”akasema Mathew



“ No thankyou Elibariki.situmii kahawa tafadhali” akasema Anitha na mara simu ikaita..

“halow Mathew.What happened? akasema Anitha kwa wasi wasi

“Hii ni nafasi ambayo natakiwa kuitumia vizuri”akawaza Elibariki na kwa kasi ya aina yake akakinyakua chungu cha maua kilichokuwa karibu yake na kumpiga nacho Anitha Kichwani akaanguka na kupoteza fahamu.Akaikanyaga kanyaga simu ile akakimbia hadi katika mlango wa chumba cha Mathew na kujaribu kuufungua.Ulikuwa umefungwa.Akarudi nyuma hatua kadhaa na kuurukia teke mlango ule ukafunguka akaingia ndani na moja kwa moja akaeleka katika kile kisanduku chenye namba.Akabonyeza namba alizozikumbuka lakini mlango haukufunguka.



“ C’mon nimekosea wapi? Mbona namba alizobonyeza Mathew ni hizi hizi? Akajaribu tena lakini bado mlango haukufunguka

“Nimekumbuka kulikuwa na namba mbili mwisho nasi namba tano.”

Akarudia tena kubonyeza na safari hii kabati kubwa la ukutani likasogea pembeni na mlango ukafunguka kwa akaanza kushuka kuelekea chini





Jaji Elibariki akaufunguua mlango wa chumba alimowekwa Rosemary akaingia.Tayari Rosemary alikwisha pitiwa na usingizi. Elibariki akamuamsha.Rose akafumbua macho na kupatwa na mshangao mkubwa kwa kumuona Elibariki mle chumbani

“ Jaji ?!! akashangaa Rose

“ Rosemary amka” akasema Elibariki

“ jaji unafanya nini huku?

“ Rose I’ve come to free you” akasema jaji Elibariki huku akiangaza angaza kama angeweza kupata kitu chochote cha kumuwezesha kufungulia pingu alizofungwa Rosemary

“ You want to free me?akauliza Rosemary kwa mshangao

“ Ndiyo.Nataka nikuondoe hapa.”akajibu jaji Elibariki



“ jaji mbona sikuelewi? Unataka kunifungua? Unataka kunipeleka wapi?



“ Sikiliza Rose,hatuna muda mrefu hapa.Elibariki anaweza akatokea muda wowote na akinikuta huku tumekwisha kwa hiyo acha kuuliza maswali na unisadie mawazo namna ya kufungua pingu hizi ulizofungwa” akasema Elibariki



“ Hebu subiri kwanza jaji .Bado sijakuelewa unataka kufanya nini.Umesema unataka kunifungua? Unataka kunipeleka wapi? Akauliza Rose



“ Mathew hajanituma nikufungue lakini nimeamua mimi mwenyewe nikusaidie uweze kutoka humu ndani.Mathew hafahamu chochote juu ya hiki ninachokifanya”

“ Mathew hayupo?akauliza Rose



“Mathew hayupo ndiyo maana nimepata nafasi ya kuja humu.Unadhani angekuwepo ungeniona humu? Akauliza jaji Elibariki



“ jaji natamani sana nikuamini lakini ninasita.Wewe ni mshirika mkubwa wa Mathew unanishangaza sana kwa kitu unachotaka kukifanya.Are you betraying your friends? Akauliza Rose.Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu na kusema



“ Rose acha kuuliza maswali mengi .Ninataka nikutoe humu.Unahakika Mathew atakuachia? Nakuhakikishia kwamba hanampango wowote wa kukuachia huru kwa hiyo naomba tafadhali ukubali nikusaidie.”akasema Elibariki.

“ kwa nini unafany ahivi Elibariki? Kwa niniunawasaliti wenzako kwa sababu yangu? Akauliza Rosemary.

“ Rose nina tatizo kubwa na nimeona ni wewe pekee unayeweza kunisaidia ndiyo maana nimelazimika kufanya hivi ..Kabla sijakufungua ninataka unihakikishie kwamba utanisaidia tatizo langu.”

“Ni tatizo gani ulilonalo na unalotaka nikusaidie?akauliza Rose

“ hatuna muda wa kupoteza Rose.Mathew anaweza akatokea hapa muda wowote kwa hiyo nitakueleza baada ya kuwa tumetoka hapa.”akasema jaji Elibariki.



“ Ok jaji tafuta kitu kidogo kama waya au sindano nikuonyeshe namna ya kufungua” akasema Rose.jaji Elibariki akatoka kwa kasi mle chumbani hadi katika chumba cha Mathew akaanza kupekua sehemu mbali mbali akitafuta kitu cha kumuwezesha kufungua pingu zile alizofungwa Rose.Katika mojwapo ya droo akaziona funguo ambazo alihisi zinaweza kuwa ni zakufungulia pingu zile.Kwa kasi akarejea chini na kweli kama alivyokuwa amehisi funguo zile ziliweza kufungua pingu na Rosemary akabaki huru.Alikuwa amechubukana mwli wake wote umatapakaa damu.

“ I’m free now”akasema Rosemary.



“ Lets get out of here” akasema jaji Elibariki akamsaidia Rose kushka katika kitanda hlafu akamtegemeza wakatoka mle ndani.Rosemary alikuwa akihisimaumivu makali kutokanna kukatwa vidole na Mathew.Walielekea hadi katika chumba cha ofisi.Rosemary akastuka alipomuna Anitha amelala sakafuni hana fahamu



“ Na huyu naye vipi?akauliza

“ Huyu ndiye aliyekuwepo humu ndani na alikuwa ni kikwazo kikubwa kwangu hivyo nikampiga na mtungi wa maua kichwani akazimia.Tusipoteze muda wapigie watu wako waje watuchukue haraka kabla Mathew hajarejea.” Akasema Elibariki huku akichukua waya na kumfunga Anitha miguu na mikono

Juu ya meza Rose akaiona simu yake pamoja na kompyuta yake akaichukua simu akaiwasha na kuongeana mtufulani simuni akamuhakikshia kwamaba yuko salama na akamuomba waje haraak wamchukue.Rose hakuwa akipafahamu mahala walipo,hivyo akampa Elibariki simu ili amuelekeze Yule jamaa..

“Mathew kaenda wapi? Akauliza Rose

“ Aliondoka na Peniela na sijui wameelekea wapi.” Akajibu Elibariki.

“ watu wako watachukua muda gani kufika hapa?akauliza Elibariki



“ Sijui watatumia muda gani lakini watajitahidi sana kufika ndaniya muda mfupi.” Akasema Rose huku akiichukua kompyuta yake

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“ washenzi sana hawa vijana.Sintawasamehe kabisa kwa jambo walilonifanyia. “ akasema Rose

“ jaji kwa kitendo hiki ulichokifanya ujue umewasaliti wenzako na watakutafuta kila kona ya nchi hadi wahakikishe wamekupata.Una hakika kwamba unataka kufanya jambo hili? Akauliza Rose



“ Najua nimefanya jambo baya la kuwasaliti wenzangu lakini sina namna nyingine ya kufanya kutokana na matatizo niliyonayo ndiyo manaa nikaamua kukusaida kuwa huru ili na wewe unisaidie.”akasema Elibariki

“ Jaji umenifanyia jambo kubwa sana na lazima na mimi nikusaidiae katika matatizo yako.Watu wangu wanaweza kufika hapa muda wowote kwa hiyo nenda getini ukawasubiri ili wasipotea” akasema Rose na Elbariki akatoka mle ndani akaenda getini.



“ Nimewasaliti rafiki zangu .Nimefanya jambo baya sana lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya hivi nilivyofanya.Siwezi kukubali maisha yangu yawe niya kujificha humu ndani.”akawaza jaji Elibariki.



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog