Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

SHE IS MY WIFE - 3

   

Simulizi : She Is My Wife

Sehemu Ya : Tatu (3)


Mshangao wa askari, wanao zishangaa sehemu za siri na Anna, ikawa ni nafasi nzuri kwake kuwafyatuli risasi zisizo na idadi askari hawa na kuwasababishia kifo tulivu kwenye maisha yao.

“Shabaha nzuri my baby”


Anna alizungumza huku akiibusu bastola zake na kuwaruka askari walio anguka chini na kwenda katika sehemu kilipo chumba walipo wezake, mwendo wake wa umakini ulimuwezesha kumuangamiza kila askari ambaya anakatiza mbele yake hadi akafanikiwa kufika kwenye chumba walichopo wezake, akamkuta Fetty amesimama huku akitazamana na askari aliye kunja ngumi

Fetty baada ya kumuona Anna akiwa amesimama nyuma ya askari anaya tazamana naye akaamua kushusha mikono yake chini na kumkonyeza Anna

“Oya broo”


Anna alizungumza huku bastola yake moja akiwa ameielekeza kwenye kichogo cha askari huyu, ambaye aligeuka haraka na kukutana na sura ya Anna akitabasamu

“Kwaheri”

Anna akafyatua risasi moja aliyoingia kwenye kichwa cha askari na kumfaya aanguke chini kama mzigo

“Poleni mashoga zangu”


Anna alizungumza huku akisaidia na Fetty kuwafungua pingu za miguuni na mikononi Halima na Agnes

“Asanteni”

Agnes alishukuru baada ya mikono yake kuwa huru, Anna akawakabidhi wezake kila mmoja bastola yake ambayo ameichukua

“Na hilo shati vibi shosti”

Halima alizungumza huku akitabasamu

“Huu ni muda wa kazi Halima, maswali mengi baadaye”


Anna alizungumza huku akimtazama Halima, Anna akasaidiana na wezake kumvua nguo, askari mmoja waliye muua kisha akazivaa pamoja na viatu vyake.

“Jamani, hapa tulipo tupo chini ya maji, hili ni manoari ambayo ndio inatumika katika kutusafirishia.Maana yangu ya kuzungumza hivyo nikwamba tuwe makini sana kwa kila hatua ambayo tunapiga”

Anna alizungumza kwa umakini huku akiwatazama wezake ambao kila mmoja alionekana kuwa makini kwa maelezo anayo yapata kutoka kwa Anna

“Tumekusoma”


Agnes alizungumza, Fetty akapiga hatua hadi mlangoni na kuchungulia nje ambapo, akatazama kila kona ya nje, hakuona dalili yoyote ya kuwepo na watu zaidi ya miili ya askari walio uliwa na Anna wakiwa wamelala chini, Fetty akanyoosha kidole kimoja akiashiria kwamba mmoja atoke nje, Anna bila kusita akatoka na kwa mwendo wa umakini wakaanza kutembea kuelekea chumba cha manahodha.Kila askari ambaye wanakutana naye hawakusita kumshambulia kwa risasi, haikuwa kazi ngumu sana kwao kufika kwenye chumba cha manahodha na kuwakuta wakiwa wawili, wakijitahidi kufanya mawasiliano na makao makuu ya jeshi la maji, juu ya kuangamizwa kwa wezao wengi

Kutekwa kwa nyambizi(Submarine), ya jeshi la maji, ikawa ni pigo jengine jipya kwa wakuu wa jeshi ambao hadi muda huu wanapambana kupata kujua ni wapi wanaweza kuyapata mabaki ya ndege ya raisi wa Tanzania, sehemu ilipo anguka.

“Haoo waalifu je, wamo?”

Mkuu wa jeshi la maji bwana Lissu alimuuliza mmoja wa manahodha baada ya kuipokea simu yake,

“Ndio tupo”

Sauti ya Fetty alisikika masikiono mwa bwana Lissu, ambaye alianza kuchanganyikiwa na mwili mzima ukaanza kumtetemeka


“Mipango yenu imeoza na hatuna jinsi zaidi ya kuwarudia nyinyi, what goes around, always comes around”

Fetty alizungumza kisha, akafyatua risasi mbili zilizo zidi kumstua sana bwana Lissu na kujikuta mwili wake mzima ukimtetemeka huku akiitazama simua yake, ambayo inatoa mlio wa kukatw

“HAHAHAAAAAAAAAAA”

Samson akazidi kucheka kwa dharau huku akikitazama kioo cha computer kinacho onyesha mlipuko, ambao hadi sasa Watanzania wengi wanaamini ya kwamba raisi wao ameshafariki dunia

“Nahisi watu wako kwa sasa watakuwa wanamwagikwa na machozi, etiiii?”

Samson alizungumza huku akikinyanyua kichwa cha raisi Praygod Makuya, kwa kutumia bastola yake aliyo ishika.

“Your son of bitch”


Raisi alitukana huku akimtemea mate ya uso, Samson.Rahab akabaki akimtazama Raisi Praygod jinsi anavyo vuja damu nyingi usoni mwake kutokana na kipigo kikali alicho kipata kutoka kwa Samso ambaye muda huu anayafuta mate yaliyo tua usoni mwake kwa kutumia kiganja chake cha mkono wake wa kushoto, kisha tataribu akayalamba mate ya raisi Praygod Makuya


“Mmmmm, mate yako ni mazuri sana, ninaimani kama ungekuwa ni mwanamke ungekuwa so mwaaaaa”

Samson aliendelea kuzungumza kidhara, Samson akaka kwenye kiti cha kuzunguka na kuanza kuzunguka taratibu huku akiichezesha chezesha bastola yeka aliyo ishika mkononi mwake


“Samso ni kitu gani ambacho kitaendelea”

Rahab alizungumza huku akimtazama Samson aliye fumba macho yake huku akizunguka zunguka kwenye kiti alicho kikalia


“Wewe unahisi nini?”

“Samson hilo sio jibu”

“Unataka jibu halisi?”

Samson alimjibu Rahab kidharau jambo lililo anza kumkera Rahab, ambaye hadi muda huu ameshaanza kupoteza imani na Samson

“Ndio”


Samson akainyanyua bastola yake na kuikoki vizuri kisha akaielekezea sehemua alipo kaa Raisi Praygod,

“Moja, mbili, ta….”

“Ngoja kwanza, unataka umfanyaje huyo Raisi?”

Rahab alizungumza huku mapigo ya moyo yakimyuenda kasi, kwani moyoni mwake amesha anza kumuonea haruma muheshimiwa riasi

“Namuua”

“Huwezi kumuua raisi kiraisi hivyo”

“Ahaaaaa powa”


Samson akamuelekezea Rahab bastola, jambo lililo mstua Rahab moyo wake, kabla Rahab hajafanya chochote Samson akafyatua risasi zilizo tua kifuani mwa Rahab na kumuangusha chini, jambo lililo mstua Raisi Praygod Makuya

“Huwa sipendagi dharau nawatoto wa kike”


Samson alizungumza huku akinyanyuka kwenye kitia alicho kikalia , kwa hatua za taratibu akatembea hadi sehemu alipo lala Rahab, ambaye hajafariki dunia na wala risasi hazijaingia mwilini mwake kutokana na jaketi la kuzuia risasi alilo kivaa.Kwa haraka Rahab akarusha teke lililo ichota miguu yote miwili ya Samson na kumuangusha chini kama mzigo, muheshimiwa raisi akabaki akishangaa, Rahab akanyanyuka kwa haraka na kuipiga teke bastola ya Samson na ikaangukia miguuni mwa muheshimiwa raisi

“Waooo kumbe upo hai”


Samson alizungumza huku akijinyanyua na kuanza kujipangusa pangusa kwa dharau, Rahaba akarusha ngumi kashaa kwa Samson ambazo, zote Samson aliweza kuzipangua kwa mikono yake mikakamavu, kisha akamtandika ngumi moja Rahab aliyo myumbisha mithili ya mlevi wa pombe za kienyeji.Rahab akakitingisha kichwa chake, ili kukilazimisha kizunguzungu alicho kipata gafla kukata.Samson akarusha teke ambalo Rahab aliweza kuliona likija na kuamua kulikwepa kwa kupiga msamba, Ngumi nzito ikatua sehemu za siri za Samson na kumfanya ajikunje huku akitoa mguno mkali wa maumivu.Ikawa ni zamu ya Rahab kupeleka mashambulizi ya ngumi nzito zilizo tua usoni mwa Samson

“Ulikuwa hunijui vizuri”


Rahab alizungumza huku akipeleka mashambulizi ya haraka yasiyo na idadi mwilini mwa Samson, ambya damu zilisha anza kumvuja puani. Samson akasimama na kuitunisha misuli yake ya mwili mzima, kila ngumi na teke ambalo Rahab aliyepiga, alishangaa kumuona Samson akiwa hatetereki wala kuhisi maumivu ya aina yoyote

“Hhaaaaaa, piga teke jingine la mwisho”


Samson alizungumza huku damu zikimwagika puani mwake, Rahab akajirusha hewani na kumpiga Samson teke shingo, lililo myumbisha kidogo Samson, Rahab akajaribu kujirusha hewani ila ngumi kali iliyo tua puani mwake ikamfanya aanguke chini na kuanza kuvuja damu, wakati mapambano yakiendela kati ya Samson na Rahab, muheshimiwa Raisi akawa na kazi ya kujitahidi kuifungua mikono yake, iliyo fungwa na gundi kubwa, inayotumika kufungia maboksi makubwa ya kusafirishia vitu mbalimbali kama Tv.


Samson akamkalia Rahab tumboni mwake na kuanza kumshindilia mangumi mazito yasiyo na idadi, tararibu Rahab akaanza kujitahidi kukichomoa kisu alicho kichomeka kwenye kiatu chake cha jeshi alicho kivaa, akfanikiwa kukichomoa na kwaharaka akakikita kisu kwenye mbavu za Samson aliye toa ukelele mkali wa maumivu na akamsukumiza pembeni.


Rahab akasimama huku akiyumba yumba na kwenda sehemu alipo muheshimiwa Raisi, akachimoa kishu kinginge kidogo alichokuwa anekiweka kwenye mfuko wa suruali aliyo ivaa, na kuikat gundi aliyo fungwa Raisi kwenye mikono yake na miguu yake

“Upo salama muheshimiwa raisi?”

Rahab alizunngumza huku akimsaidia muheshimiwa Raisi kunyanyuka

“Ndio, asante binti”


Rahab akamgeukia Samson na kumkuta akijitahidi kukichomoa kishu alicho mchomo kwenye mbavu, Rahab akaiokota bastola iliyokuwa chini ya miguu ya muheshimiwa raisi na kupiga hatua na kwenda sehemua alipo lala Samson

“Tutaonana kuzimu”


Kabla hata Rahab ajafyatua risasi ya aina yoyote ndege ikayumba gafla na kuwaangusha raisi na Rahab, kutokana na Samson kuifunga mitambo yote ya ndege, ikiwemo mashine baadhi za uendeshaji wa ndege, zimesababisha marubani kushindwa kuikwepa ndege ya abiria ya shirika la Fly Emirates, ambayo zimekutana kwenye njia moja, marubani wa ndege ya abiria hawakuweza kuiona mapemba ndege ya Raisi wa Tanzania, kutokana na kushindwa kuiona kwenye rada zao, na wakajikuta wakiingonga, ndege ya raisi wa Tanzania kwenye ubavu wa nyuma wa ndege na kuisababisha kugeuka mara mbili na kuanza kwenda chini kwa kasi sana, huku ndege yao ya abiria ikiianza kuwaka moto...



ITAENDELEA....



ILIPOISHIA

“Tutaonana kuzimu”

Kabla hata Rahab ajafyatua risasi ya aina yoyote ndege ikayumba gafla na kuwaangusha raisi na Rahab, kutokana na Samson kuifunga mitambo yote ya ndege, ikiwemo mashine baadhi za uendeshaji wa ndege, zimesababisha marubani kushindwa kuikwepa ndege

ya abiria ya shirika la Fly Emirates, ambayo zimekutana kwenye njia moja, marubani wa ndege ya abiria hawakuweza kuiona mapemba ndege ya Raisi wa Tanzania, kutokana na kushindwa kuiona kwenye rada zao, na wakajikuta wakiingonga, ndege ya raisi wa Tanzania kwenye ubavu wa nyuma wa ndege na kuisababisha kugeuka mara mbili na kuanza kwenda chini kwa kasi sana, huku ndege yao ya abiria ikiianza kuwaka moto



ENDELEA

Kelele za abiria zilizo andamwa na vilio vya uchungu, ziliendelea kusikika kwenye ndege ya raisi wa Tanzania bwana Ptraygod Makuya, kwajinsi ndege inavyozidi kwenda chini ndivyo jinsi ilivyozidi kuwaka mato mwingi na kuendelea kupasuka baadhi ya sehemu na kuzidi kulete maumivu makali kwa kila abiria aliye kubwa na kitu chochote kikali, ambacho kinaugusa mwili wake na kuzidi kumuumiza, huku wengine wakijikuta wakipoteza viungo vyao vya mwili.Hali hii inaendelea sawaswa na hali iliyopo ndani ya ndege ya abiria iliyo gonga sehemu ya nyuma ya ndege ya Raisi.Ndani ya chumba walichopo Samson, Rahab na rais Praygod, hali inazidi kuwa mbaya, kwani computer zote zinaanza kulipuka moja baada ya nyingine, kwa haraka Rahab anajitahidi kushikilia moja ya nguzo ya chuma, huku mkono wake mmoja akimshikilia Raisi ambaya anavutwa na upepo mwingi, unaoingia kwenye chumba chao, ukitokea nje kutokana na ukuta wa chumba chao kutoboka kutokana na motom mkali unaoendelea kuiteketeza ndege



“Muheshimiwa Raisi endelea kujikaza”



Rahab alizungumza kwa sauti ya juu huku mkono wake wa kulia, akiendelea kumshikilia Raisi, huku mkono wake wa kushoto pamoja na mguu wake wa kulia kwa pamoja vikiwa vimezunguka kwenye nguzo ya chuma inayo endelea kumsaidia asitoke nje ya chumba hicho.Hali kwa upande wa Samson inazidi kuwa ngumu sana kutokana na upepo mwingi kuendelea kuingia ndani ya ndege, kutokana na kipigo kikali alicho kipata kutoka kwa Rahab, ambacho kimempelekea mikono yake kukosa nguvu ya kushikilia kwenye baadhi ya vitu vilivyomo ndani ya ndege.Samson anajikuta akiachia kwenye moja ya sehemu aliyo ishikilia na upepo mkali unamtoa nje, huku akipiga kelele za kuomba msaada, Ndege nayo ikazidi kwenda chini kwa kasi kubwa huku, ikizidi kuchanguka baadhi ya maeneo yake



***

Baada ya Fetty kukata simu anawageukia manahodha wawili wanao kiendesha chombo cha kivita kijulikanacho kwa jina la ‘Sabmarine’ au Nyambizi, huku mkononi mwake akiwa ameishika bunduki yake aliyopiga risasi kadhaa pembeni



“Mutafanya kile ambacho mimi nitawaelekeza, Sawa?”



Fetty alizungumza huku bunduki yake akiwa ameielekeza kwa wanahodha hawa, ambao nao ni wanajeshi wa wajeshi la maji nchini Tanzania,



“Sa…wa”



Mmoja alijibu huku mwili wake ukimtetemeka sana, hadi haja ndogo akaanza kuihisi ikimwagika



“Kwanza hapa tulipo ni wapi?”



Anna aliuliza kwa sauti ya ukali



“Hapa tupo bahari ya Pasifiki maharibi kwa bara la Asia, katika nchi ya Australia”



Nahodha mmoja alizungumza huku akitazama kifaa maalumu ambacho kina namba nyingi, ambazo kwa mtu wa kawaida si rahisi kuweza kugundua ni nini kinacho tazwamwa



“Mmmmmmm…..!!”



Halima aliguna huku akiwatazama wezake kwani hakuelewa kitu kinacho zungumzwa hapo ni kitu cha aina gani



“Tutarudi vipi Tanzania?” Agnes aliiuliza



“Tanzania tumeiacha mbali sana?”



“Ndio tutarudi vipi Tanzania” Fetty aliuliza kwa sauti ya ukali, na kuwafanya manahodha kuzidi kutetemeka



“Tutar….”



Kabla nahodha mmoja ajamalizia sentesi yake, akastushwa na kingora kilichopo pembezoni mwa chumba chao kikianza kulia huku kifaa kingine mbele yao chenye kioo kikukubwa mithili ya simu aina za I pad, kikianza kuonyesha vitu vilili virefu vyenye rangi nyekundu vikija kwa kasi sana



“Mungu wangu, ni mabomu haya”



Nahodha mmoja ambaye umri wake umekwenda kidogo alihamaki huku kajasho kakianza kumwagika usoni mwake akitazama kioo hicho kwa macho yake makubwa kiasi



“Mabonu……!!?”



Anna aliuliza huku naye macho yakiwa yanamemtoka



“Ndio, tumeshakamtwa kwenye rada ya nchi ya Australia”



Kila mmoja akaanza kuomba sala yake ya mwisho, kutokana na mabomu hayo kuzidi kuja kwa mwendo wa kasi huku yakionekana kukilenga chombo chao ambacho kinapita kwa siri chini ya bahari hii kubwa ya Pasific, katika eneo la jeshi la nchini Australia



***

Makamu wa Raisi wa Tanzania bwana Gift, anaendelea kujipongeza kwa kuona kifo cha raisi Praygod, kikiwa kimetokea katika wakati muafaka, kwani ni kipindi kifupi tangu waingie madarakani baada ya kushinda uchaguzi kwa kishindo kikubwa, kama chama pinzani cha YRPP(Youth Revolution Political Party), ambacho muundo wake mkubwa unaongozwa na vijana wengi akiwemo Raisi wao kijana bwana Praygod Makuya



“Vipi mume wangu mbona unashangilia?”



Mke wa makamu wa Raisi alimuuliza mume wake, baada ya kurudi nyumbani kwake akiwa na tabasamu kubwa usoni mwake akitokea ofisini kwake, alipo kaa kwa siku mbili mfululizo pasipo kurudi nyumbani kutokana na swala zima la kujaribu kuitafuta ndege ya raisi Praygod Makuya



“Nina furaha sana, mke wangu yaani leo naamini nitakupiga hata vitano”



Maneno ya Gift yakazidi kumshangaza Magnalenar ambaye ni mke wa Raisi



“Sasa, mbona unanishangaza mume wangu, nchi ipo kwenye maombolezo ya kufiwa kwa rafiki yako mkubwa, wewe unashangilia”



“Mke wangu kwangu nifuraha ndio, kwani kufa kwake ndio mafanikio yangu”



“Unashangilia kwa kuwa raisi au?”



Magnalener aliuliza huku sura yake akiwa ameikunja akimtazama mume wake ambaye ameanza kuserebuka ndani ya chumba chao, huku shati lake akiwa amelifungua vifungo vyote na mkononi mwake akiwa na chupa ya whyne



“Achilia mbali kuwa raisi, ila ninafuraha sana kwa Praygod kufariki”



“Nahisi umepagawa wewe, mtu aliye kutoa kwenye ubunge hadi kukupa umakamu wa Raisi, leo hii amefariki wewe unashangilia?”



“Haaaa wewe kinacho kuuma ni nini?”



Magnelener akaachia msunyo mkali huku akipanda kitandania na kujifunika shuka akiendelea kumtazama mume wake anaye andelea kugumumia mapafu ta whyne



“Jiandae kwa vitano”



“Nimechoka na sitaki uniguse na hizo pombe tano, mtu huna hata huruma kwa rafiki yako, sijui wewe upojee, muone na hili jitumbo lako kama…..”



Magnalener alizungumza huku akiachia msunyo mkali na kumfanya Gifti kuachia tabasamu pana na kushusha mafumba mawili ya whyne kwa haraka haraka



“Asante sana Samson, mwanangu kwa kuniondolea huyo mwehu duniani”



Gift alizungumza huku akipiga hatua kwenda kwenye kitanda alicho lala mke, taratibu akazivua nguo zake na kubaki kama alivyo zaliwa na kujirusha kitandani,



“Samson yupi huyo aliye muua raisi?”



“Hakuuhusu”



“Ahaa kumbe wewe na Samson ndio mumeshirikiana katika hili”



Magnalener alizungumza huku akikaa kitako kitandani akimtazama mume wake kwa jicho kali sana, Gift akaupeleka mkono wake wa kulia kwenye ziwa la upande wa kushoto la mke wake na kustukia akizwabwa kibao kikali cha shavu kilicho muacha mdomo wazi akishangaa




SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……24


“Gift ukiendelea kunisumbua na mapombe yako tutaonana wabaya”



Magnalener alizungumza huku akiufunika mwili wake vizuri pasipo tatizo la aina yoyote, taratibu Gift akajilaza upande wa pili wa kitanda chake kwani anamuelewa kabisa mke wake ni mkorofi, na akizungumza huwa anamaanisha na kitu amabacho anakizungumza kwa wakati huo



***

Upepo mkali na uzito wa mwili wa Raisi Praygod vikazidi kupambana na nguvu za Rahab, ambazo taratibu zikaanza kumuishia mwili mwake na kujikuta akianza kuuchia taratibu nguzo aliyo ishikilia



“Muheshimiwa Raisi, nimechoka”



Rahab alizungumza kwa sauti kubwa huku upepeo ukiendelea kumpiga usoni mwake na kujikuta akizidi kuchanganyikiwa na kujihisi vibaya.Raisi Praygod Makuya akamtazama Rahab vizuri kwa jinsi anavyo jitahidi kuyaokoa maisha yake, machozi ya uchungu yakaanza kumwagika.



“Binti ninakuomba uniachie niende”



“Hapana muheshimiwa Raisi siwezi kufanya hivyo”



“Unaweza binti tafadhali ninakuomba ufanye nilivyo kuagiza”



“Wewe ni Raisi wa nchi yenye watu si chini ya milioni thelathini na nne, huwezi kufa kirahisi, unahitaji msaada wangu.Na nitakupigania kama raisi wangu”



Rahab alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, huku hali ya rangi ya mwili wake ikianza kubadilika na kuingia uwekundu fulani, uliao changiwa na maumivu makali yanayo yapata kwa kumshikulia Raisi mwenye kilo si chini ya sabini.Maneno ya kujiamini kwa Rahab, yakaanza kumpa matumaini mapya Raisi Praygod, ya kuoko kutoka kwenye ajali hii ya ndege yake, Macho ya Rahab yakatazama kwenye shimo ambalo muda mchache ulio pita Samson alichomolewa kwa upepo mkali kiasi cha kuto julikana ni wapi alipo kwenda kuangukia



“Muheshimiwa unaona hilo shimo chini yako?”



Rahab alimuuliza Raisi Praygod Makuya kwa sauti kubwa sana, na kumfanya Raisi kutazama chini nakuona shimo kubwa likiingiza upepo mkali ukitokea nje, raisi akajibu kwa kutingisha kichwa akiashiria kwamba ameliona shimo hilo



“Sasa ninakuachia, na mimi ninafwata kwa nyuma”



Rahab alizungumza kwa kujiamini, huku akitazama baadhi ya vitu vikiendelea kuteketea kwa moto ndani ya chumba walichopo, Raisi akameza fumba la mate akarudia tena kulitazama shimo ambalo Rahab amemuomba aweze kutoka. Kisha akayarudisha macho yake upande wa Rahab, wakatazama kwa muda usoni huku kila mmoja akiwa haliamini jaribio wanalo lifanya, ila hapakuwa na jinsi nyingine zaidi ya kufanya hivyo kuliko kuteketea kwa moto mkali unaozidi kuwaka ndani ya ndege yao.



Raisi Praygod akajiachia mikononi mwa Rahab, upepo mkali ukamvuta kwenda nje, Rahab naye, akaiachia nguzo ya chuma aliyo ishikilia na upepo mkali ukamvuta kwenda nje, wapambe wa Raisi Praygod Makuya, wakiwemo washauri wake wakuu pamoja na walinzi wake, wakajikuta wakilipuka na ndege ya raisi na kupoteza maisha yao, huku wengine wakiwa wameshasali sala zao za mwisho huku wengine wakiyaita majina ya mama zao wakiomba wasaidiwe



***

Kila mmoja ndani ya Submarine(Nyambizi) amayafumba macho yake akisubiria kulipuliwa na mabomo hayo yaliyo kilenga chombo chao, ndani ya dakika kumi nzima wakawa bado wameyafumba macho yao wakiusikilizia mlipuko huo, ila sivyo kama walivyo dhani, mtu wa kwanza kuyafumbua macho yake ni Halima, hii nibaada ya kungojea kwa muda mrefu, pasipo mabomo hayo kufika kwenye nyambizi yao, kwani kwa mwendo kasi wa mabomo hayo ilionyesha kwamba zimesalia sekunde 59 hadi mabomo hayo kuwafikia sehemu walipo



“Jamani mbona sioni chochote?”



Halima alizungumza na kuwafanya wezake wote kiyafumbua macho yao, ila kitu ambacho bado kinaendela kuwapa wasiwasi ni jinsi king’ora kilichopo ndani ya chumba chao kikiendelea kulia kwa sauti ya juu



“Kuna tatizo gani, nyinyi?”



Fetty alizungumza kwa hasira huku bastola yake akiwa amewaelekezea manahodha wa meli hii ya kivita inayo tembea chini ya maji



“Hata sisi hatujui” Nahodha mmoja alijibu huku jasho jingi likimwagika kwa wingi mwlini mwake



“Hii ni amri fanyeni haraka muturudishe Tanzania”



Agnes alizungumza huku akiwatazama manahodha hawa walio valia nguo za jeshi la maji, hapakuwa na jinsi zaidi ya wao kugeuza submarine yao na kuanza safari ya kurudi Tanzani, umbali wa kilomita zipatazo themanini na nne(84), gafla submarine yao ikatingishika



“Ni nini hicho?” Halima aliwauliza manahodha



“Tumekwama kwenye, mwamba wa barafu”



Nahodha alizungumza huku akiwaonyesha, mwamba mkubwa wa barafu, uliopo kwenye bahari waliyopo ya Atilantic, inayosifika kwa kuganda kwa barafu katika kipindi kirefu.



“Kwahiyo kama tumekwama?” Anna aliuliza



“Hatuwezi kusonga mbele, itatulazimu kukaa hapa kwa kipindi kirefu hadi hizi barafu ziyayuke”



Nahodha mmoja alizungumza huku akishusha pumzi, akiwatazama Fetty na wezake jinsi walivyo jawa ha mshangao mkubwa



“Sasa itakuwaje?”



“Hatuna jinsi, huchi nikipindi cha baridi, itatulazimu kukaa hapa si chini ya miezi mitatu hadi miinne hadi barafu zima liyanyuke, kipindi tunapita kwa mara ya kwanza ndio tulikuwa tunamalizia msimu wa barafu ila kurudi kwetu ndio, kosa tulili lifanya”



Karibia wote wakajikuta wakishusha pumzi zao, kila mmoja akihofia juu ya maisha yake, baridi kali ikaanza kupenya kwenye ngozi zao, jambo lililoanza kuzua wasiwasi mwingi sana kweye maisha yao



“Itatubidi chombo kitokeze kwenye usawa wa bahari la sivyo tutakufa humu ndani”



Nahodha mkuu alizungumza



“Kikitokeza usawa wa bahari hakutakuwa na madhara yoyote kwetu?” Agnes aliuliza huku akijikunyata



“Ndio, ila kuna makoti makubwa yapo humu ndani itatulazimu kuyatumia, kwa ajili ya kujikinga na baridi iliopo humu ndani”



Halima na Anna wakaondoka na nahodha mmoja wakaingia ndani ya chumba cha kuhifadhia makoti makubwa yanayotumika katika kipindi cha baridi kali.Wakachukua makoti yaliyo sawa na idadi yao, na kurudikatika chumba maalumu walipo Fetty na nahodha mkuu.Submarine yao ikaanza kupanda kwenda juu tataribu taratibu, hadi kikatokezea usawa wa bahari, na katika eneo zima walilopo limeganda kwa barafu kubwa.



“Itatubidi kuitoa miili ya watu walio kufa humu ndani, isije ikatuozea” Anna alitoa wazo



“Kwa baridi hii wataoza kweli?” Halima alizungumza



“Kuoza wanaweza wasioze ila ni kinyaa, unataka kusema tutakaa na maiti tukionana nazo zaidi ya mwezi humu ndani, hembu tusidanganyane hata kama sisi ni makatili ila kuishi na maiti ndani mimi wala siwezi” Fetty alizungumza



“Powa nimewaelewa, tunazitoa saa ngapi?” Halima aliuliza



“Sasa hivi?”



“Mmmmm” Agnes alijikuta akiguna tuu



“Sawa”



Kwa kushirikiana na manahodha wakaanza kutoa mwili mmoja baada ya mwengine wa askari wote walio waua ndani ya Submarine(Nyambizi), kutokana na wingi wa miili ya askari walio fariki ndani ya Submrine ikawalazimu kutumia masaa mengi



“Ahaaaaaa”



Agnes alishusha pumzi nyingi, huku akiutazama mwili wa maiti alio uatupa mbali kidogo na sehemu kilipo chombo chao, kutokana kwa kuganda kwa barafu wanaweza kutembea juu y barfu pasipo tatizo lolote.Agnes akaanza kuifikicha fikicha mikono yake aliyo valia gloves nyeusi, zinazo zuia kupitisha ubaridi, huku pumzi anayo itoa mdomoni mwake ikijawa na mvuke mwingi



“Mmmm, hii baridi si mchezo”



Alizungumza taratibu akipiga hatua za kurudi ilipo Submarine, kabla hajapiga hatua hata nne akastukia kuona kitu kikitua kwenye barafu kwa ngufu kikitokea juu, ikamlazimu kutazama juu na hakuona kitu cha aina yoyote zaidi ya ukungu mwingi, ulio tawala juu ya anga la bahari.Akatazama upande kilipo anguka kitu hicho na taratibu akaanza kupiga hatua za taratibu, huku basstola yake ikiwa mkononi mwake, akafika sehemu kilipo anguka kitu hicho na kukuta mwili wa mtu ukiwa unavuja damu, sehemu za tumboni mwake huku, huku akiheme kwa mbali akionekana bado yupo hai



***

Upepo mkali ukazidi kumpeleka chini Rahab, huku muda mwini akijitahidi kuvuta pumzi, ila anashindwa kutokana na hewa ya sehemu alipo kuwa ni nzito sana,



“Ohooo Mungu wangu ninakufa mimi”



Rahab alizungumza huku, akibana pumzi zake, kwa mbali akamuona Rais Praygod akizidi kwenda chini kwa kasi, Rahab akaibana mikono yake usawa wa mwili wake kuelekea nyuma, huku miguu yake akibananisha kwa pamoja, akajikuta akipata uwiano wa kuweza kwenda chini, kwa mwendo wa kasi pasipo kuyumba, kwa mtindo wa kwenda chini ali ufanya Rahab ukamsaidia kumfikia karibu muheshimiwa Raisi ambaye hadi kwa wakati huu amepoteza fahamu, Rahab akafanikiwa kumshika Raisi Praygod Makuya kiuno chake, na wote wakajikuta wakienda chini na kuingia kwenye maji mengi ya bahari.Rahab akajitoa kwenye usawa wa brahi huku akiheme kwa nguvu, hii ni kutokana na kuishiwa na pumzi, aliyokuwa ameibana kwa muda mrefu



“Raisi……!!”



Rahab alizungumza baada kwa mshangao baada ya kutokumuona Raisi Praygod kwenye usawa wa bahari jambo lililoanza kumpa wasiwasi mwngi.Ikamlazimu kurudi tena ndani ya maji, kutazama kama anaweza kumuona raisi, ila hakumuuona



“Mungu wangu!!”



Rahabu alizungumza kwa kuhamaki baada ya kuona kitu kikija kwa kasi katika upande aliopo yeye, kwa haraka haraka akagundua kwamba ni samaki mmoja hatari aina ya Papa, ndiye anaye karibia kufika katika eneo alilopo



ITAENDELEA....




ILIPOISHIA....

“Raisi……!!”

Rahab alizungumza baada kwa mshangao baada ya kutokumuona Raisi Praygod kwenye usawa wa bahari jambo lililoanza kumpa wasiwasi mwngi.Ikamlazimu kurudi tena ndani ya maji, kutazama kama anaweza

kumuona raisi, ila hakumuuona

“Mungu wangu!!”

Rahabu alizungumza kwa kuhamaki baada ya kuona kitu kikija kwa kasi katika upande aliopo yeye, kwa haraka haraka akagundua kwamba ni samaki mmoja hatari aina ya Papa, ndiye anaye karibia kufika katika eneo alilopo.


ENDELEA.....

Rahab akaanza kujipapasa mwiki mwake kwa haraka, kwabahati nzuri akakikuta kisu kwenye mguu wake wa kulika katika sehemu ya kiatu alipo kichomeka kipindi alipokuwa akivaa, nguo alizo nazo kwenye chumba maalmumu cha kuhifadhia nguo katika ndege ya raisi iliyo anguka muda mchache uliopita.



Akajiweka tayari kwa kupapambana na samaki huyu anaye mfwata kwa kasi katika eneo ambalo ameangukia, kufumba na kufumbua samaki huyu tayari akawa aweshafika katika eneo alipo Rahab, kwa ustadi wa hali ya juu Rahab akajigeuza ndani ya maji na kushuka kwa kasi ndani ya maji, na kusababisha samaki huyu mkubwa kupita juu yake, kwa kasi jambo lililo zidisha ukali wa samaki huyu mwenye uchu wa kutafuna kiumbe chochote kitakacho ingia kwenye enoa la bahari alipo yeye


Rahab akakishika vizuri kishu chake chenye ncha kali, na kutazama jinsi samaki huyu anavyo kunja kona na kurudi katika eneo alipo kwa kasi kubwa, samaki akamfikia Rahab kwa karibu kabla samaki hajafanya maamuzi ya aina yoyote, Rahab akamuwahi kumchoma kisu kwenye eneo la tumbo la samaki huyu, lenye ngozi laini na kuanza kulichana kwa kutumia nguvu nyingi, jambo lililo sababisa damu nyingi kutapakaa katika enoa la sehemu walipo, huku utumbo mwingi wasamaki huyu ukitapakaa kwenye maji

“Haaaaaaaa”


Rahab alizungumza huku akichomoza kichwa chake kwenye maji, huku akivuta pumzi kwa wingi, akajilegeza mwili wake na kuufanya uanze kuelea elea juu ya maji, huku akitazma juu mwili wake ukiwa umechoka sana

Agnes akamgeuza mtu aliye anguka na kumchunguza vizuri na kugundua kwamba anamajeraha kadhaa kwenye mwili wake, Agnes akapiga mluzi ulio mfikia Halima aliyekuwa katika eneo la karibu, Halima akapa hatua za haraka hadi katika sehemu alipo simama Agnes

“Best kuna mtu hapa nimemuona”


Agnes alizungumza huku akimgeuza mtu aliye lala chini huku damu zikimvuja, Halima akamtazama mtu aliye lala chini kwa umakini, pasipo kuzungumza kita cha aina yoyote, kiasha akaikoki bastola yake akiziweka risasi zilizopo kwenye magazine yake, kuwa tayari kutoka nje, kitu kikubwa alicho kibakisha ni kuivuta traiga ya bastola yeka kuziruhusu risasi atakazo zihitaji kutoka nje


“Halima unataka kufanya nini?”

“Hastahili kuishi, mtu mwenye ni mfu huyu”

“Hembu ngoja kwanza?”

“Nini?”

“Usimuue?”

“Sasa anabaki duniani wa kazi gani, unamtambua huyu mtu”

Halima alizumgumza kwasauti iliyo jaa msisitizo mwingi

“Hata kama, simfahamu ila kuna kitu ninacho kihisi kwa huyu jamaa”


“Kwanza ametokea wapi?”

“Mimi sifahamu, ila nilisikia kishindo, nilipo kuja hapa ndipo nilipo muona huyu jaamaa akiwa amelala hapa”

Halima pasipo kuuuliza akafyatua baadhi ya risasi, jambo lililo muudhi sana Agnes na kumfanya amsukume Halima na kuangukia pembeni


“Mbona unakuwa mpumbavu wewe, nini unafanya”

Agnes alizungumza kwa hasira huku akimfokea kwa nguvu Halima aliye angukia pembeni, kwa bahati nzuri risasi alizo zifyatua Halima alizipiga pembeni ulipo mwili wa jamaa na hapakuwa na risasi iliyo ingia katika mwili wa mtu waliye muona.



Milio ya risasi ikawastua Fetty pamoja Anna ikawalazimu kutoka nje ya ‘submarine’ na kuelekea sehemu walipo isikia milio ya risasi huku wakiwa makini sana, kila mmoja akiwa ameishika bastola yake mkononi, waakawakuta Agnes na Halima wakiwa wanafokeana huku kila mmoja akionekana kuwa na jazba ya ajabu, Fetty akafyatua risasi mbili hewani nakuwafanya Agnes na Halima kunyamaza

“Nyingi mumechanganyikiwa?”

Fetty aliuliza kwa sauti juu huku akiwatazama Halima na Agnes


“Si ninazungumza na nyinyi, hamuoni shida tulizo nazo ila bado munagombana kwa kitu kipi?”

Halima hakujibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuondoka na kuwaacha wezake wakimtazama kwa macho yaliyo jaa mshangao mwingi

“Agnes kuna nini?”

Anna aliuliza huku akimtazama Agnes aliye fura hasira nyingi


“Kisa ni hyo jamaa aliye lala chini hapo”

Fetty akapiga goti moja chini na kumshika shingo, mtu aliye anguka chini ya akiwa anavujwa na damu za puani

“Ametokea wapi?” Fetty aliuliza

“Sifahamu, ila nimemuona akiwa ameanguka tu”

“Ameanguka kutoka wapi?”

“Kutoka juu”

“Juuu?”

“Ndio”

“Hembu shika huko”


Fetty alimuomba Anna kuweza kumshika mtu aliye anguka katika eneo la miguu, kwa kusaidiana wote watatu wakamnyanyua juu, na kumpeleka ilipo manohari, wakamuingiza ndani na kunaza kumfanyia huduma ya kwanza, jambo lililo zidi kumkera Halima ambaye hakuhitaji kumuona mtu asiye mfahamu akiwa upende wao

“Raisi”


Rahab alizungumza huku akiingiza miguu yake kwenye maji, na kubakisha kiwiliwili cha juu na kuanza kuangaza kila kona ya eneo alilopo ila hakumuona Raisi Praygod, umbali kidogo kutoka katika sehemu alipo, akaona miti mingi ikiashiria kwamba kuna kisiwa, akavuta pumzi nyingi na kunza kuogelea huku akiendelea kutazama kila eneo, akihisi kwamba anaweza kumuona muheshimiwa raisi, hadi anafika kwenye ukingo wa bahari, ambapo emetumia takribani dakika ishirini na sita kufika alipo, akiajilaza kwenye mchanga mwingi, wenye rangi nyeupe huku akiwa wamechoka mwili wake kupita maelezo

“Ohooo mama yangu nakufa mie”


Rahaba alizungumza huku akihema mithili ya bata mzinga aliye kimbia kwa umbali mrefu, akajilaza kwa dakika kumi, kisha akasimama na kutazama kila upande wa kisiwa hichi, chenye miti mingi mirefu iliyo fungamana kwa ukaribu, na kwambali kukiwa na sauti nyingi za ndege wenye milio mizuri

“Hapa ni wapi?”


Alizungumza huku akitembea tembea katika eneo hili lenye mchanga mwingi wa bahari, ambao kwa mtu aliye choka humuwia ugumu mwingi kutembea, njaa kali haikucheza mbali katika tumbo la Rahab, kila jinsi anavyozidi kwenda mbele ndivyo jinsi alivyoaanza kujihisi mwili kunyong’onyea na kumuishia nguvu, kwa mbali akaliona koti jeusi ambalo alikuwa amelivaa Raisi Praygod Makuya likiwa pembezoni mwa bahari, akapiga hatua za kiuvivu uvivu hadi lilipo koti na kuliokota, akatazama kila upande na hakuuona mwili wa Raisi, akiwa amesimama akasikia sauti ya mtu akikohoa kwenye moja ya kifusi kikubwa kilicho hatua chache kutoka sehemu alip simama, akakimbia hadi kilipo kifusi na kumkuta Raisi Praygod Makuya akiwa amefunikwa na mchanga mwingi wa kuanzia tumboni hadi miguuni huku maji yakiendelea kuipiga miguu yake taratibu na kurudi baharini


Kitendo cha kuzama ndani ya maji, baada ya kudondoka kutoka kwenye maji, raisi Praygod Makuya akanyanyuliwa na wimbi kubwa lililoanza kumpeleka usawa wa kisiwa, kwa uzito wa maji na kasi yake kubwa, akajikuta akiupwa pembezoni na bahari, mchanhg mwingi ukamfunika, huku koti lake likipelekwa na maji na kukwama kwenye moja ya vimawe mawe vilivyoopo pembezoni mwa bahari, baada ya jua kali lililokuwa likimpiga usoni mwake, ufahamu ukaanza kumrudia na kujikuta akianza kukohoa taratibu taratibu, gafla akahisi mtu akimgusa, akayafumbu macho yake yaliyo jaa ukungu mwingi, kwa mbali aliweza kuiona sura ya Rahab, ila kutokana na ukungu ilio tanda kwenye macho yake hakuwa na uhakika kamili kama ni Rahab mwenye au ni mtu mwengine


“Raisi”

Sauti ya Rahab ikumuita ikaanza kumpa matumanini na kuamini kwamba ndio Rahab mwenyewe aliye muita.

“Ni mimi Rahab”


Rahab alizungumza huku akiendelea kuutoa mchanga ulio mfunikaka Raisi, akafanikiwa kumaliza kuutoa mchanga wote, akaishika mikono ya Raisi na kumnyanyua juu, raisi akafanikiwa kumuona Rahab vizuri na kujikuta akiachia tabasamu pana usoni mwake

“Asanye binti”

“Sa…”


Kabla Rahab hajamaliza sentensi wake wakastukia kuona kundi kubwa la watu walio valia ngozi za wanyama wa msituni, wakija kwa kasi katika sehemu walipo simama huku wakipiga vigelele gele na mikononi mwao wakiwa wameshika minyale na mikuki mingi, wakiashiria kwamba wapo tayari kwa kuwashambulia Raisi na Rahab, ambaye amejipapasa mwili mzima na kujikuta akiwa hana silaha hata moja

*****Je watasalimika mikononi mwa hawa watu, usikose toleo lijalo hapa hapa kwenye hii page****


SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……26


Watu hao wakawazingira Rahab na Raisi Praygod, huku wakiendelea kupiga kelele za ajabu, pamoja

huku mikuki na mishale yao wakiielekezea kwa Rahab na Raisi Praygod

“Binti kuwa mpole”


Raisi Praygod alizungumza huku akiinyoosha mikono yake juu, Rahab naye akatii kunyoosha mikono yake juu, jamaa wawili wenye misuli wakawasukuma Rahab na Raisi Praygod, wakaanguka chini, wakafungwa kamba za miguuni na mikononi, kisha wakanyanyuliwa na kubebwa juujuu, wakipelekwa wasipo pafahamu.



Wakafikishwa kwenye moja ya kijiji chenye watu wengi, huku nyumba zao zikiwa zimetengenezwa kwa nyasi pamoja na miti, hazikuwa na urefu sana, kwenda juu, huku milango yao ikiwa ni midogo katika sehemu ya kuingilia.Rahab na Raisi Praygod, wakafungwa kwenye moja ya mti mkubwa, huku miili yao ikizungushiwa kamba ngumu, iliyo zunguka kwenye mti huo.



Giza likaingia pasipo, kujua ni kitu gani kinacho endelea, watu hawa wenye kuzungumza lugha ya ajabu, hawakuwa na muda kabisha na Rahab pamoja na Raisi Praygod, kila mmoja anaonekana kuwa bize na shughuli yake, wakaanza kusikia mlio wa ngoma, ulio changanyikana na kelele za ajabu, ikionekana watu hao wakiwa wapo katika kusherehekea


“Hawa ni watu gani?”

Ragab alimuuliza Raisi Praygod

“Hata mimi sifahamu, ndio mara yangu ya kwanza

kuwaona watu wa aina kama hii”


Wakastukia kuona kundi kubwa la wanaume wakija huku mikononi mwao wakiwa wameshika miti ambayo juu yake imefungwa matambaa yanayo waka kwa moyo mkali.Wakawafungua na kuwabeba juu juu kama walivyo waleta pale awali, wakatupwa chini pembezoni mwa jungu kubwa lililo wekwa kwenye mafiga matatu, huku likitoa mvuke mwingi, ikiashiria kuna maji mengi yanayo chemshwa.



Macho ya Rahab yakawa na kazi ya kutazama watu walio wazunguka, wanawake wa watoto, wakiendelea kushangilia, huku waume zao wengine wakipiga ngoma, huku wengine wakiwa na kazi ya kuhimarisha ulinzi uliopo kwenye eneo hili, akasimama mzee mmoja aliyekuwa amekalia kiti kilicho tengenezwa kwa ngozi ya chui.Mwili wa mzee huyo anaye onekena ni mkubwa sana kiumri, umevishwa dhahabu nyingi kuanzia kichwani hadi miguuni, zilizo tengenezwa katika mionekano tofauti ya hereni, cheni na bangili.



Ukimya ukatawala baada ya mzee huyo kunyanyua mikono yake juu akishiria watu wote kukaa kimya.Akawatazama Rahab na Raisi Pyaygod ambao, wamelala chini huku nguo zao zikiwa zimechafuka kwa vumbi jingi lililopo katika sehemu hiyo.


“Lajmet e juaj?”(Habari zenu)

Mzee huyo aliwasalimia watu wake kwa saut ya upole nyenye kukwaruza kwaruza

“Wanazungumza lugha gani?” Rahab aliuliza

“Wanazungumza ki Albania”

Raisi alijibu kwa sauti ya chini huku akimtazama mzee huyo

“Te sigurt Pergjithshem”(Salama mkuu)

Watu wote walijibu kwa pamoja huku wakiinamisha vichwa vyao chini, kama ishara ya kumuheshimu

mzee huyo


“Sot eshte nje dite e mire dhe e kendshme”(Leo nisiku nzuri ya kupendeza)

“Ku gjalle yne I ri na kane sjelle ushgimin me te mire per shendetin tone”(Ambapo vijana wetu, mahiri wametuletea chakula bora kwa afya zetu)

Raisi Praygod akastuka baada ya kusikia chakula bora, kwa mahesabu ya haraka haraka yaliyo mjia

kichwani anatambua kwamba chakula kinacho zungumziwa hapo si kingine ila ni miili yao


“Hawa watu wanakula nyama za watu”

“Nini?”

“Ndio, hapa wapo kwenye mikakati ya kutaka

kutula sisi nyama”

“Mungu wangu”

Japo kuna hali ya ubaridi ila kajasho kembamba kakaanza kumchuruzika raisi Praygod, huku

mapigo yake ya moyo yakaanza kwenda mbio, akili ya Rahab ikaanza kufanya kazi kwa haraka akijaribu kutafuta jinsi ya kujiokoa kutoka mikononi mwa watu hao.Akatazama kila sehemu, hakuona


sehemu yoyote yenye upenyo wa kutokea, wanume wanne walio jazia miili yao kwa misuli iliyo

kakamaa, wakasimama pembeni ya Raisi Praygod na Rahab, huku wakiwa wamevali ngozi za

wanyama na mikononi mwao wakiwa na visu vikali wakisubiria kupata amri kutoka kwa mkuu wao

“Eshte koha tani per te vlim ushgimin tone”(Ni wakati sasa wa kuchemsha chakula chetu)


Mzee huyo alitoa amri kwa vijana wake, na kuwafanya watu waliopo katika eneo hilo kushangilia kwa furaha, huku vijana hao wanne wakianza kuzikata kamba walizo wafunga Rahab na Raisi Praygod tayari kwa kutatumbukiza katika jungu hili kubwa, lenye maji yanayo chemka sana


Kwa dawa walizo mpatia mtu waliye muokota, zikaanza kuzaa matumaini kadri masaa yalivyo zidi kukatika, mtu huyo akaanza kupata nafuu iliyo pelekea kuyafumbua macho yake kutazama ni wapi alipo


“Unaitwa nani?”

Fetty alimuuliza mtu huyo, anaye onekena kuendelea kushangaa shangaa ndani ya chumba alipo, akatazma akila pande, nakuona wasichana watatu wakiwa wamesimama pembeni yao, huku wakiwa na bastola kwenye viuono vyao, akataka kunyanyuka ila Anna akamuwahi kumrudisha kitandani


“Tulia, upo sehemu salama, je unajua kuzungumzaKiswahili?” Anna alimuuliza

“Ndio”

Mtu huyo alijibu kwa sauti ya chini na kuwafanya, Anna kuwatazama wezake

“Unaitwa nani?”

Anna alimuuliza tena mtu huyo

“Sa….m”

Alijibu kwa kifupi, huku akionekana kupata shida sana katika kuzungumza kwake

“Sam, ndio nini?” Agnes aliuliza

“Samson”


“Ahaaaa, umetokea wapi?” Fetty aliuliza

“Munamuuliza maswali mengi ya nini?”

Sauti ya Halima ilisikika kutoka mlangoni, alipo simama akiwatazama wezake hawa wanamshuhulikia mtu waliye muokota, Fettyakamtazama Halima kwa macho makali kisha akaachia msunyo mkali, akishiria kukasirishwa na swali la Halima


“Halima ninakuomba utoke humu ndani?”

Fetty alizungumza kwa sauti nzito iliyo jaa ukali fulani ndani yake

“Eheeeee,”

Halima alicheka kwa dharau huku akipiga hatua za taratibu na kuondoka katika chumba walipo wezake

“Ana nini, huyu?”

Agnes aliuliza huku akimtazama Halima anaye potelea mbele ya macho yao

“Hembe, tuweni makini naye, Sawa?” Fetty alizungumza

“Sawa”


Halima, akaelekea moja kwa moja katika chumba walichopo manahodha wa nyambizi(submarine) hii,

akawakuta wakiwa wanajaribu kutafuta mawasiliano kisiriri siri, ili kuweza kujitoa mikononi mwa hawa watekaji, walio waua wezao bila yahuruma, Halima akawatazama kwa umakini, pasipo wao kugundua uwepo wa Halima katika chumba hichi, ambaye amesimama nyuma yao


“One, nine, nine, nine Over”(1, 9, 9, 9, Over)

Nahodha mmoja alizungumza kwa kupitia kifaa maalumu cha mawasiliano, huku mwenezake

akionekana kuhangaika na simu kubwa iliyo jaa batani nyingi

“I repeat One, nine, nine, nine. Over”(Ninarudia, 1,9,

9, 9, Over)

Halima akaendelea kuwatazama jinsi manahodha hawa wanacho kifanya, akatoa bastola yake, akatoa magazine na kukuta risasi za kutosha

“Hei….”


Halima alizungumza na kuwastua manahodha hao, pasipo kuwa na huruma, Halima akafyatua risasi

moja iliyotua kichwani mwa nahodha mkuu ambaye alikuwa akihangaika kuminya minya batani nyingi zilizopo kwenye simu hii ya kijeshi, inayo tumika kwa mawasiliano ya masafa marefu

“Endelea……”


Halima alimuambia nahodha msaidizi, ambaye mwili mzima umeanza kumtetemeka kwa woga baada ya kumuona mkuu wake akiwa ameanguka chini, huku damu zikiwa zinamvuja kwenye kichwa chake, na taratibu akiiaga dunia. Mlio wa risasi, ukawastusha Fetty na wezake walipomo kwenye chumba cha kuhudimia wagonjwa, kwa haraja Fetty akatoka pamoja na Anna kwenda kutazama ni nini kilicho tokea huku, Agnes akibaki na mgojwa.Wakamkuta Halima akiwa amemnyooshea nahodha msaidizi bastola, huku nahodha mkuu akiwa ameanguka chini, akiwa amepoteza maisha tayari


“Weka bastola yako chini”

Fetty alizungumza kwa msisitizo huku bastola yake akiwa amemnyooshea Halima, Halima akamgeukia Fetty na kumtazama kwa macho ya mshangao


“Halima, sinta rudia nimekuambia weka bastola yako chini, kabla sijausambaratisha ubongo wako”

“Khaaaa, Fetty unatania eheee…!?” Halima aliuliza kwa mshangao

“Halima sitanii, moja, mbili,………..”

Halima akaitupa chini bastola yake, na kuipiga teke, akimsogezea Fetty sehemu alipo simama, Anna akaiokota bastola ya Halima, kisha akapiga

hatua hadi sehemu alipo anguka nahodha mkuu “Ameshakufa”


Anna alizungumza baada ya kuuweka kiganja chake kimoja kwenye kifua cha nahodha huyo

“Kwanini umemuua?”

Fetty aliuliza kwa hasira, huku bastola yake akiinyooshea kwa Halima, anaye onekana kuto kustushwa na tukio lililo tokea mbele yao

“Nakuuliza wewe, Malaya kwanini umemuua huyu mzee?” Fetty aligomba


“Mimi Malaya?”

“Ndio wewe, Malaya tena uliye kubuhu”

Halima akacheka kicheko cha dharau na kuanza kupiga hatua za kuelekea mlango wa kutoke nje ya chumba hicho

“Simama, ukipiga hatua ninakuua”


Fetty alizungumza kwa msisitizo, Halima akasimama, taratibu akageuka na kumtazama Fetty, akapiga hatua za taratibu hadi sehemu alipo simama Fetty, kisha kwa hasira akishika bastola ya Fetty na kuilekeza kwenye paji la uso wake, huku akiigandamiza kwa nguvu zake zote

“Si unataka kuniua? Niue sasa”


Halima alizungumza kwa hasira huku ameyang’ata meno yake, akimtazama Fetty anaye tetemeka kwa hasira kali, iliyo pelekea sura yake kukunjana na kutisha mithili ya chui jike, aliye uliwa watoto wake akishuhudia.Gafla mlio wa risasi ukasikika huku kishindo kikubwa cha mtu kuanguka chini kikisikika

ndani ya chumba walichomo....

ITAENDELEA



ILIPOISHIA

“Si unataka kuniua? Niue sasa”

Halima alizungumza kwa hasira huku ameyang’ata meno yake, akimtazama Fetty anaye tetemeka kwa hasira kali, iliyo pelekea sura yake kukunjana

na kutisha mithili ya chui jike, aliye uliwa watoto wake

akishuhudia.Gafla mlio wa risasi ukasikika huku kishindo kikubwa cha mtu kuanguka chini kikisikika

ndani ya chumba walichomo.



ENDELEA

Wote macho yao wakayapeleka sehemu alipo angukia mtu huyo, aliye pigwa risasi na kukuta ni yule nahodha msaidizi akiwa chini amelala huku, damu zikimtoka kifuani mwake na kwenye mkono wake wakulia akiwa ameshika bastola ikiashiria kwamba alitaka kuwashambulia wote waliomo ndani ya chumba ila Anna alimuwahi.


Halima akatoka na kuwaacha wezake kwenye chumba walichopo, akatoka nje ya manohari na kupanda juu kabisa, akawasha sigara yake taratibu na kuanza kuvuta, huku akijaribu kuishusha hasira yake iliyo tokana na wezake kumuamini Samson, ambaye hataki hata kumuona kwenye macho yake.

*********

Rahab na raisi Praygod Makuya walipo malizwa kufunguliwa kamba zao kwa ajili ya kudumbukizwa kwenye jungu kubwa lenye maji yaliyo chemshwa kwa ajili yao. Rahab akamkonyeza muheshimiwa raisi na hapo hapo, wakaanza kupambana na vijeba hivyo vipatavyo sita, na kuwafanya watu wengine walio kusanyika katika eneo la uwanja kushuhudia kuuawa kwao, ili wawale wakaanza kuchanganyikiwa kwani kwa mapigo aliyo kuwa akiyapiga Rahab, yalimshangaza hadi chifu wao, hakuamini kuona mtoto wa kike akipambana kwa kiasi cha kuwaangusha vijeba wenye miraba miine.

“Twende muheshimiwa”


Rahab alizungumza baada ya kupata kijinafasi cha kukimbia kutoka kwenye kundi kubwa la watu hawa. Wakaanza kukimbia kuiingia msituni huku wakifwatwa kwa nyuma na kundi la askari wa kijiji hichi ambao wanatumia mishale na upendi katika kuwashumbulia. Kila walivyo kimbia ndivyo kundi la askari hao lilvyo zidi kuwafukuzia, na mbaya zaidi, mwanga wa mbalamwezi ulimulika kila upende wa anga na kuwafanya washinde kujificha kwenye vichaka kuhofia kuonekana na kukamatwa tena.

“Nimechoka…..”


Raisi alizungumza huku akionekana kukatishwa tamaa na kukimbia huko, Rahab akamshika mkono raisi na kuendelea kukimbia, kwa bahati nzuri wakakuta moja ya pango, wakaingia pasipo kuchunguza ndani ya pango hili kutakuwa na kitu gani. Askari hao waliokuwa wanawakimbiza wakapita kwa spidi katika pango hilo pasipo kuchunguza sana kama watu wanao wakimbiza watakuwa wameingia ndani ya pango hilo.

“Asante tena binti”


Rahisi alizungumza huku akiendelea kuhema kwa fujo, akionekana dhahiri kwamba hakuwa ni mtu wa mazoezi. Hawakuwa na sababu ya kuendelea kukaa tena ndani ya pango hilo baada ya kikundi hicho cha askari kupita kwa kasi katika eneo hilo. Wakabadilisha muelekeo na kupita katika njia tofauti na walio kwenda askari hao, ambao laiti wakitiwa mikononi basi hukumu yao ni ile ile ya kwenda kutafunwa nyama. Usiku mzima wakautumia kukimbia, na kutembea pale ilipo walazimu kufanya hivyo, hadi kunapambazuka bado wapo kwenye msitu huu ambao hawaelewi wanaweza kujitoa.

“Tunaweza kupumzika sasa”


Rahab alimuambia muheshimiwa Raisi, baada ya kupata eneo lililo tulia na lina maficho ya wao kupumzika. Raisi Praygod hakuwa na kipingamizi zaidi ya kutafuta sehemu na akajibwaga kama mzigo, miguu yake yote ikawa inawaka moto kwa jinsi alivyo kimbia na kutembea kwa muda mrefu, akavivua viatu vyake na kuviweka pembeni kisha akajilaza.


Rahab akasimama na kuanza kulichunguza eneo zima, kuhakikisha kama wanaweza hata kujilaza kidogo katika sehemu hiyo pasipo buguzi. Akiwa katika kuchunguza chunguza sehemu akabahatika kupata kuona mti wenye matunda mengi makubwa na mazuri, akausogelea na kulichuma tunda moja, akalipasua na kulilamba. Akapata laza tamu ya tunda hilo ambalo hakujua ni tunda la aina gani. Akaanza kulitafuna taratibu kusikilizia kama kuna madhara yoyote atakayo yapata, ila haikuwa hivyo kadri jinsi alivyo zidi kulila ndivyo jinsi alivyo zidi kunogewa na tunda hilo, na wala hakusikia mabadiliko yoyote katika mwili wake. Akachuma mengi kidogo na kurudi sehemu alipo lala muheshimiwa raisi Praygog.


“Muheshimiwa amka”

Rais akajinyanyua kivivu na kukaa kitako, huku akipiga miyayo, akiashiria kwamba yupo katika hali ya uchovu mkubwa. Rahab akampa tunda moja muheshimiwa kwa ajili ya kupunguza njaa ambayo inaendelea kukwangua matumbo yao, muheshimiwa raisi akaanza kula matunda hayo.

“Matunda gani haya?”


“Mimi wala sijui ni matunda gani nimeyachuma hapo mbele”

“Aiseee nimatamu sana, sijawahi kula matunda matamu kama haya”

“Yapo mengi, nikayachume mengine?”

“Twende tukachume”


Raisi akavaa viatu vyake na kwenda ulipo mti huo wenye matunda, wanayo kula. Wakaanza kuyachuma na kuendelea kuyala. Wakiwa katikati ya kuyashambulia matunda hayo, kwa mbali wakaisikia milio ya mingurumu ya magari.

“Ina maana hapa kuna barabara?”

Raisi alimuuliza Rahab, ambaye aliacha kutafuna tunda alilo kua kitafuna kipande kidogo ndani ya mdomo wake na kusikilizia sauti ya mingurumo hiyo ya magari ni wapi inapo toke.


“Ndio nahisi kuna sehemu ipo barabara”

“Twende tuiwate”

Wakabeba matunda ya ziada, na kuanza safari ya kufwatisha inapo tokea milio hiyo ya magari, haikuwa safari ndogo kuitafuta barabara hiyo inayo pitisha magari, ili waweze kuomba msaada wa kuweza kuwafikisha wanapo kwenda. Ikawachukua zaidi ya lisaa zima, kufika wanapo sikia milio hiyo ya magari. Haikuwa ni barabara kama walivyo zania, wakakuta uwanja mkubwa ambao una watu wengi walio jichora michoro tofauti tofauti kwenye miili yao, huku wakiwa uchi, wanaume kwa wanawake. Magari yao hayakuwa ni magari kama waliyo yazea kuyaona yanayo tumiwa na watu wa kawaida. Magari yao yametengenezwa kwa vyuma vigumu na yana miundo ya ajabu, na mengi yanafanania na magari yaliyo tumika katika filamu ya ‘DEATH RACE’.


Michezo iliyo kuwa inafanywa na watu hao wasio na aibu hata kidogo, baadhi yao kushindana na magari yao kwenye uwanja wao kwa mtindo wa kugongana magari

“Hawa ni watu gani…….!!!?”


Rahab aliuliza huku akiwa ameshangaa, kabla raisi hajajibu kitu chochote wakastukia risasi ikipiga kwenye mti walio kuwa wamejibanza wakishangaa kundi hilo la watu, wasijue ni wapi risasi hiyo imetokea

********

Hali ngummu ya hali ya hewa ya baridi kali, ikaendelea kuuimiza miili ya Fetty, Halima, Anna, Agnes na Samson, walio jifungia ndani ya manohari kwa siku kadhaa wakisubiria barafu lililo ganda baharini kuyayuka na kuendelea na safari yao, huku Samson akiwaeleza yeye ni mtaalamu mkubwa wa kuendesha vyombo kama hivyo.

“Sijui Rahab kwa sasa yupo wapi best yetu”


Agnes alizungumza, wakiwa wamekusanyika pamoja kwenye chumba, chenye joto kidogo kwani hali ya nje ya chombo chao ilizidi kuwa mbaya sana. Samson akastuka baada ya kulisikia jina la Rahab, ila akajikausha kukaa kimya ili asistukiwe, kwani yeye anajua yote yaliyo tokea kati yake na Rahab.


“Sijui amekufa au yupo mafichoni?”

“Weee Rahab si rahisi kufa kwa maana namkubali”

“Ila itabidi tufanya mpango wa kujikomboa huku, ili tuweze kumpata mshikaji wetu kwa maana anasiri zetu nnyingi na endapo hatuta mpata siku akitiwa mikononi inaweza kuwa hali ngumu kwetu”


“Kama sisi tulikamatwa basi, hatukuweza kuzungumza kitu cha aina yoyote sidhani kam Rahab anaweza kuzungumza chochote pale atakapo kuwa amekamatwa”

Fetty na wezake wakaendelea kuzungumza, ila Samson hakuchangia chochote juu mada inayo muhusu Rahab

*******

Hali ya masikitiko ikaendelea kuzizimi katika nchi ya Tanzania, hii ni wananchi kuiona taartifa ikionyesha ndege ya raisi kwamba imetekwa na magaidi na kutegwa bomu lililo lipuka, wakilishuhudia kupitia televishion zao. Kitu kilicho zidi kuwachanganya viongozi wa serikali ni pamoja na mabaki ya ndege yaliyo onekana katika bahari na Pasific, yakielea elea juu ya maji, huku kukiwa hakuna mtu hata mmoja aliye weza kusalia kwenye ajali hiyo, iliyo wahuzunisha watu wengi si wananchi wa Tanzania peke yao bali hata mataifa majirani waliweza kuguswa na kifo hicho cha Raisi Praygod Makuya na watu wake.


“Ndugu wananchi, kwa masikitiko yaliyo makubwa, ninatangaza siku kumi na nne za maombolezo ya raisi wetu pamoja timu yake, waliop pata ajali kwenye ndege. Iliyo shambuliwa na…….”


Sauti ya makamu wa Raisi, ilisikika katika vyombo vyote vya habari, Redio na Tv. Kila mwananchi hakusita kujiweka karibu na kitu ambacho alihisi kinaweza kumpatia habari juu ya tukio zima.


Wenye maduka, maofisi, mashule na kadhalika, waliweza kuzisimamisha kazi zao kufanya maombolezo ya kifo cha raisi wao mpendwa ambaye alikuwa bado ni kijana mdogo sana mweney umri wa miaka thelethini na tano.


Mitaa yote ya jiji la Dar es Salaam ilikuwa kimya, hata mtaa wa Kariakoo, unaosifika kuwa na watu wengi, katika siku zote za wiki, ulitawaliwa na ukimya wa hali ya juu, watu wengi wanakumbuaka hali kama hii ilisha wahi kujitokeza mwaka 1999, alipo fariki Raisi wa kwanza, ambaye ni baba wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius K.Nyerere.

**********

Kiwewe cha risasi iliyo piga kwenye mti kikazidi kuwachanganya Raisi Praygod Makuya na Rahab, ambao walitazama kila kona ya sehemu walipo ila wasione mtu anaye walenga kwa silha. Watu walio kwenye uwaja, wakaendelea na mashindano yao kama kawaida, wasijali mlio huo wa bunduki.



Risasi zikaanza kumiminika katika eneo walilo jificha Rahab na Raisi Praygod Makuya. Ikawalazimu kuanza kukimbia kuelekea ulipo uwanja, kwani risasi hizo zilikuwa zikitokea nyuma yao, kulipokuwa walenga shabaha wapatao wanne wanao linda uwanja huo, cha kushangaza zaidi nao wapo uchi kabisa, lengo lao halikuwa si kuwaua Rahab na raisi Praygod, ila walihitaji kukajumuike na wezao wanao endelea na michezo hiyo.


Rahab na raisi Praygod wakajikuta wakiwa wamesimama kwenye uwanja huo, watu wote waliopo kwenye uwanja huo wakakaa kimya wakiwashangaa kwa jinsi walivyo valia nguo zao.

“Muheshimiwa hapa tutafanyaje?”


Rahab alizungumza huku akihema sana kwa wasiwasi akiwatazama watu hawa wanao onekana kama wametokea kuzimu, hii ni kutokana na michoro ya ajabu waliyo ichora kwenye miili yao.

“Tuvue nguo”

Raisi alizungumza huku, akianza kufungua vifungo vya shati lake jeupe lililo chafuka hadi, limepoteza taswira nzuri ya muonekano wake kama lilivyo kuwa hapo awali.


SHE IS MY WIFE(28)



Wote wakajikuta wakiendelea kuchojoa nguo zao hadi wakabaki watupu, chakushangaza hapakuwa na mtu aliye onekana kuwajali kwa kitendo walicho kifanya zaidi ya watu hao kuendelea kushangilia mashindano yao ya magari. Raisi Praygod akamshika mkono Rahab na wakakatiza katikati ya kundi la watu hao, hadi wakatokea upande wa pili wa uwanja na kundelea kukimbia kwenda wasipo pafahamu,

“Nguo!?”


Rahaba alizungumza kwa mshangao mkubwa huku akihema sana. Raisi hakuwa hata na muda wa kuzifikiria nguo zake. Alicho kifanya yeye ni kuendelea kupumua kwa nguvu huku mikono yake akiwa ameshika magotini mwake. Wakaendelea kujipumzisha kwamuda hadi walipo pata nguvu nyingine ya kuendelea kupiga hatua kusonga mbele.


Hakuna ambaye aliweza kumtamani mwenzake zaidi kila mmoja alicho kifikiria kwa muda huo ni jinsi gani wanaweza kutoka ndani ya msitu huo wenye hali ngumu ya kutisha. Kwa bahati nzuri wakafanikiwa kufika kwenye moja ya kijiji, majira ya saa tatu usiku, kutokana na mwanga wa mbalamwezi waliweza kuzihesabu vijumba vichache vipatavyo kumi na mbili, vilivyo tengenezwa kwa mbao. Kwa mwendo wa tahadhari wakakatiza kwenye nyumba hizo ambazo zinaonekana hazina uwepo wa watu ndani.


Wakasikia sauti ya luninga ikitokea kwenye moja ya nyumba kati ya hivi vinyumba vilizopo, kwa mwendo wa tahadhari wakakisogelea kijumba chenye kusikika sauti ya kubinga hiyo, wanayo hisi kuna mechi ya mpira wanatazama. Wakachungulia dirishani huku wakionekana kuwa na wasiwasi mwingi kwani hapakuwa na aliye kuwa na uhakika kama kuna usalama katika sehemu waliyopo.

“Mbona ndani hakuna mtu”


Rahab alizungumza huku akichungulia ndani kupitia kajidirisha ka kioo, kilicho jaa vumbi jingi.

“Hembu tazama tazama vizuri”

“Kweli muheshimiwa ndani hakuna mtu”

“Hembu tuzunguke kwenye mlango”

Wakazunguka hadi kwenye mlango, Rahab akataka kugonga ila Raisi Praygod akawahi kumzuia asifanye hivyo, taratibu Raisi Praygod akausukuma mlango na wakaingia ndani huku wote wakionekana kuwa makini kwa lolote litakalo jitokeza mbele yao.


Wakafanikiwa kuingia ndani, cha kushangaza hawakuweza kumkuta mtu yoyote zaidi ya luninga hiyo inayo toa sauti kubwa, huku ikiwa imejawa na vumbi jingi sana.

“Nahisi watu walio kuwa wanaishi hapa walishahama siku nyingi”

Raisi Praygod alizungumza

“Unauhakika gani kumeshimiwa kama watu hao watakuwa wamehama siku ningi?”

“Tazama mazingira ya humu ndani jinsi yalivyo jaa vumbi jingi, nilazima watakuwa wamehama siku nyingi”

Wakaendela kutazama kila chumba ila hawakufanikiwa kuweza kuona mtu yoyote zaidi ya vitu vilivyomo humu ndani vikionekana kutelekezwa kwa siku nyingi sana. Rahab akalisogelea friji lililopo hapa sebleni kutazama kama kuna kitu chochote cha kuingiza mdomoni. Gafla kabla hajalifungua wakasikia mngurumo wa gari ukitokea kwa nje.

Wote kwa pamoja wakajikuta wakikimbilia dirishani kutazama ni kina nani walio wasili muda huu wa usiku. Wote wakajikuta wakiwa midomo wazi baada ya kuona watu wenye sura za kutisha zilizo kunjamana kunjamana wakishusha miili ya watu, walio fariki kwenye gari lao kubwa aina ya FYATA, huku wakionekana kushangilia.

“Ni kina nani……!!?”


Rahab aliuliza huku akiwa na wasiwasi mwingi usoni mwake

“Hata mimi siui ni kina nani”

Wakawashuhudia watu hao wakiingizwa kwenye moja ya kijumba kilichopo jirani na kijumba walipo wao, wakazidi kuchanganyikiwa baada ya kumuona mtu mmoja kati ya hao wanao tisha akilitoa jicho la mmoja wa marehemu walio kuja nao na kuanza kulivyonza vyonza na taratibu akaanza kulila.

“Haaaaaa……!!!”


Rahab alimaka kwa sauti ya juu ila Raisi Pragod akawahi kumziba Rabab mdomno, sauti ya Rahab ikasikika moja kwa moja kwa mtu wa ajabu aliye kuwa anakula jicho la marehemu.

“Wametusikia tujifiche”


Raisi Praygod alizungumza huku akianza kung’aza ng’aza macho yake ndani kutafuta ni wapi wanaweza kujificha, hapakuwa na sehemu yoyote ya kujificha zaidi ya nyuma ya mlango, wote kwa pamoja wakasimama nyuma ya mlango na kujikausha kimya, mlango ukafunguliwa kwa nguvu na kuwabamiza kwenye vifua vyao huku, mtu huyo mwenye sura ya ajabu akiwa amesimama katikati ya mlango huku mkononi mwake akiwa ameshika bunduki aina ya gobore, huku macho yake akiyazungusha zungusha kila segemu ya seble hii.

***

Kutokana na ujuzi mkubwa wa Samson katika kuendesha manohari pamoja na ndege, akaanza kazi ya kuibabadua manohari hii iliuyo ganda kwenye barabu kubwa katika bahari ya Atelantic, Ikawachukua masaa takribabani sita kuweza kuibabadua manohari hii ya kivita, inayo endelea kutafutwa na majeshi ya Tanzania wakisaidia na jeshi la Marekani, huku pia wakijitahidi kutafuta mabaki ya ndege ya muheshimiwa raisi bwana Praygod Makuya.


Taratibu wakaainaza safari huku Samson akiwapa kila mmoja majukumu yake katika kuifanya manohari hii kuweza kuendelea kupasua miamba ya barabu iliyopo kwenye bahari hii. Kadri jinsi walivyozidi kuiendesha ndivyo jisni walivyo zidi kufanikiwa kuweza kupasua miamba na kuzidi kwenda chini ya bahari ambapo hapakuwa na barafu kubwa sana.


Wakafanikiwa kufika kwenye ukanda ambao hauna barafu kabisa, ikawa ni kazi rahisi kwao kuendelea na safari yao. Furaha ikazidi kutawala ndani ya mioyo yao, huku Fety kila muda akionekana kuwaza kujua ni nini anapaswa kufanya.

“Jamani naomba tusikilizane”


Fety alizungungumza huku akiendelea kuwatazama wezake wanaoendelea kujiburudisha na vinywaji vikali vilivyomo ndani ya manohari hii.

“Tunakusikiliza kiongozi sema mama”

Agnes alizungumza kwa sauti iliyo jaa pombe

”Kurudi Tanzania hatuwezi, kwa sasa, kutokana tumekuwa ni maadui namba moja wa nchi hiyo”


“Sasa tutakwenda wapi, wakati Tanzania ndio nyumbani?”

Anna aliuliza huku akijitahidi kuyafumbua macho yake yalivyo zidiwa kwa pombe nyingi aliyo kunywa.

“Nimeona ni bora tukashauiriana kwenda kwenye nchi ambayo. Tutaomba hifadhi kwa muda huku tukikubaliana na serikali hiyo kuiuza hii manohari”

“Aisee wewe Fetty mbona unamaswala ya ajabu, hivi ni nchi gani ambayo itakubali kuuziwa hii manohari tena ya Tanzania. Hivi unajua kwamba Tanzani ina marafiki wengi kila kona ya dunia?”


Halima alizungumza huku akimkiendelea kushusha mapafu ya mzinga wa whyne alio ushika mkononi mwake. Fetty hakuwa na lakuzungumza ziadi ya kukaa kimya akiendelea kuyatafakari maneno aliyo yazungumza Halima

“Ngoja niwashauri kitu ndugu zangu”

Samson alizungumza kwa sauti ya chini huku akiwatazama wote.


“Miimi nina rafiki zangu katika nchi ya Russia, ila wao ni waasi wan chi hiyo na wamejitenga kwenye moja ya kisiwa kilicho mbali kutoka katika nchi yao.”

“Ningependekeza kwamba kama tunahitaji kuweza kuiuza hii manohari, ni vyema kwenda walipo wao kisha tukazungumza nao bei, wakatupatia pesa kisha sisi tukatafuta sehemu ya maficho na kuendelea na maisha yetu ya kawaida”

“Hilo wazo nalo ni zuri, ila watu wenyewe kama ni waasi, kweli hawawezi kutubadilikia?”


“Mimi kiongozi wao mkuu ni rafiki yangu mkubwa sana, ambaye ni miongoni mwa watu walio nifundisha mimi kazi hii na kunipa ujuzi wa kuendesha vyombo mbalimbali vya kijeshi”

“Sawa, tutafikaje hapo?”

“Kutoka hapa tulipo sio mbali sana kikubwa ni kuweza kuamua kwamba tumekubaliana kwa pamoja kuweza kulitelekeza hilo, kisha mimi niweze kufanya mawasiliano na kiongozi wao”


Ukimya ukatawala kati yao huku kila mmoja akionekana kutafakari juu ya wazo la Samson, japo wote akili zao zina pombe kiasi ila kila mmoja alijitahidi kwa uwezo wake kuweza kuifuta pombe hiyo kichwani mwake na kuweza kutafakari kile alicho kisikia kutoka kwa Samson.

“Tutakuamini vipi kama huto tubadilikia hapo mbeleni?”

Fetty alimuuliza Samson huku akiwa amemkazia macho

“Niamnini, kwani nyinyi ni watu ambao mumuweza kunitendea mema na laity kama mungehitaji kunifanyia mabaya mungenisha nifanyia. Niwakati wa mimi kuweza kulipa wema kwenu”


“Sawa kama ni hivyo twendeni jamani, ,mimi nimeshachoka kukaa ndani yta maji kama samaki”

Halima alizungumza kwa msisitizo wote kwa pomoja wakakubaliana kuweza kulifwata wazo la Samson, Kila mmoja akajiegesha sehemu yake na kulala huku akisubiria masaa yakatize pombe ziwatoke kichwani waendelea na mpango wa kuwasiliana na hao watu wa Samson.


Anna akawa ni wakwanza kustuka, taratibu akanyanyuka huku akiwa amejawa na mawenge ya usingizi, akawatazama wezake, kwa mwendo wa kivivu vivu akaelekea chooni ambapo, alijisaidia haja ndogo kisha na kurudi walipo wezake.



Akaanza kuwaamsha mmoja baada ya mwengine, walipo amka kila mmoja akaanza majukumu yake aliyo kuwa amekabidhiwa na Samson, kuhakikisha chombo hicho kimazidi kusonga mbele.



Wakaanza kufanya mawasilianao na kikosi hicho cha kigaidi ambacho kimeiasi nchi yake ya Rusia. Kwa bahati nzuri wakafanikiwa kupata mawasiliano na kiongozi wa kikundi hicho aitwae Rusevu.



Wakakubaliana naye kuweza kufika kwenye ngome yake siku mbili mbeleni wakiwa na manohari hiyo yenye uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi makubwa ndani ya maji. Mazungumzo ya Rusev na Samson yakazaa matumaini mapya ya utajiri kati ya Fetty na wezake kwani yote waliyo kuwa wakiyafanya ni kutokana na kuweza kupata pesa zitakazo wakimu kimaisha.


“Jamani kama hii dili, ikisimama mimi na ujambazi basi:

Fetty alizungumza, huku akiwa na furaha kubwa moyoni mwake

*******

Mtu huyo wa ajaba akaendelelea kutazama tazama kila kona ya sable hii, akapiha hatua mbili mbele na kuzama ndani kabisa ya sable hii, na kuwapa mgongo Rahab na Raisi Praygod walio simama nyuma yake.



Akaendelea kuvuta vuta pumzi, iliyo muashiria kwamba humu ndani kuna binadamu waklio hai, akalikoki bunduli lake aina ya gobore na kulishika vizuri huku kidole chake kimoja akiwa amekizamisha kwenye traiga, kwa haraka akageuka nyuma na kuwaona Rahab na Raisi Praygod wakiwa nyuma yake wanamtazama




ITAENDELEA 




ILIPOISHIA

Mtu huyo wa ajaba akaendelelea kutazama tazama kila kona ya sable hii, akapiha hatua mbili mbele na kuzama ndani kabisa ya sable hii, na kuwapa mgongo Rahab na Raisi Praygod walio simama nyuma yake.

Akaendelea kuvuta vuta pumzi, iliyo muashiria kwamba humu ndani kuna binadamu waklio hai, akalikoki bunduli lake aina ya gobore na kulishika vizuri huku kidole chake kimoja akiwa amekizamisha kwenye traiga, kwa haraka akageuka nyuma na kuwaona Rahab na Raisi Praygod wakiwa nyuma yake wanamtazama



ENDELEA

Kwa haraka Rahab akaruka hewani na kuipiga teke bunduki ya mtu huyu mwenye muonekano wa ajabu sana, bunduki yake ikaanguka chini na kumpa nafasi nzuri Raisi Praygod kumrukia mtu huyo kwa kutumia bega lake lililo tua begani kwa mtu huyo na wote wawili wakaanguka chini.


Rahab kwa haraka akaiokota bunduki ya mtu huto na kwakutymia kitako cha bunduki hiyo aina ya gobore akampiga nayo kichwani zaidi ya mara kumi mtu huyo, na kupelekea kichwa cha mtu huyo kupasuka kwa na kuvuja damu yenye rangi nyeusi ti.

“Mtu gani huyu….?”

Rahabu aliuliza huku akihema kwa nguvu akionekana kuchanganyikiwa kwa kumuona mtu wa aina hii ambaye tangu azaliwe hajawahi kumuona.


“Tuondike hakuna haja ya kuendelea kukaa hapa”

Raisi Pragod alizungumza huku akichungulia mlangoni kutazama kama wale watu wengine wa kutisha wamesha ingia ndani walipo kua wakiingiza mizoga ya watu walio waua. Wakatoka nje wakiwa katika tahadhari kubwa huku Rahab aklwa ameishika bunduki ya mtu huyo.


Wakafanikiwa kutoka nje pasipo kuonekana na watu hao ambao wapo ndani ya kijumba chao wakiendelea kuwakata kata vipande marehemu walio wachukua na kuwafanya ndio chakula chao cha usiku. Wakaanza kutokomea porini huku wakimuomba Mungu waweze kutoka kwenye msitu huu ambao bado haujawapa matumaini ya kuweza kuziokoa nafsi zao zilizo kwenye matatizo makubwa


Hasili ya watu hawa wa kutisha wanajulikana kama Mazombi, walio anza kujitokeza mwaka 1819 katika bara la ulaya. Inasemekana watu hawa ni wale walio weza kupoteza maisha kwa sumu zenye kemikali kubwa na waliweza kurudi katika ulimwengu huu wakiwa katika hali hiyo ya kutisha na kuweza kuwafanya wanadamu halisi kama ndio vitoweo vyao vya kila siku.


Rahab na Raisi Praygod wakaendelea kukata mbuga pasipo kuchoka, japo wanatamani kuweza kupata japo dakika waweze kupumzika, ila kila walipo kumbuka maiti za watu walio waona wakishushwa na mazombi hayo hawakutamani kamwe kuweza kusimama.


Hali ya majonzi ikawatawala mazombi walio mshuhudia mwenzoa aliye pasuliwa kichwa na kusababisha ubongo wote kumwagika nje. Hawakua na hamu hata ya kuendelea kupata vitoweo walivyo kuja navyo na ziadi kila mmoja akachukua silaha yake na kuingia msituni kufwatilia watu hao walio sababisha mauaji ya mmoja wao. Kutokana na kuufahamu vizuri msitu wao, wakajigawa kwenye makundi ya mazombi wawili wawili na kupelekea kuwa na vikundi vinne. Kila mmoaja akajiapiza kuweza kufanya mauaji ya kikatili kwa watu walio sababisha mauji ya mpendwa wao

***

Samson na wezake wakafanikiwa kufika katika kiswa cha Kunashir nchini Russia, kwa bahati nzuri wakafanikiwa kupokelewa na mkuu wa kikiso kilicho asi nchi ya Russia bwana Rusev, Wakapelekwa moja moja kwa moja kwenye jengo lenye ofisi za kikundi hichi kinacho endelea kufanya mapinduzi kwenye nchi yake ikiitaka serikali kuweza kuunda serikali mbili, ili wao wajipatie mamlaka ya kuweza kutengeneza silaha hatari za nyuklia.


Kila mmoja akakabidhiwa kinywaji alicho kihitaji yeye, ili kuweza kujipozwa kwa uchovu mwingi wa safari yao ndani ya maji, tangu pale walipo kamtwa na jeshi la polisi nchini Tanzania. Fetty na wezake hawakuwa na uwezo wa kuielewa lugha ya kirusi, ambayo Samson yeye aliweza kuizungumza vizuri pasipo matatizo ya aina yoyote. Alicho kua akikifanya Samson ni kuwatafsiria kila kitu ambacho alicho kua akikizungumza na bwana Rusev.


“Jamaa anauliza eti, tunaweza kujiunga na kundi lake?”

“Mmmm……!!” Anna aliguna

“Hatuwezi sisi tupo hapa kwa ajili ya biashara”

Samson akamjibu bwana Rusev kitu alicho kizungumza Fetty anaye onekana kuto kubaliana na swala zima la wao kujiunga na kundi la bwana Rusev

“Je anauliza tunahitaji kiasi gani cha pesa ili tuweze kumkabidhi hii manohari?”

“Sasa hapo ndio umenena la maana” Halima alizungumza huku akitabasamu

“Anatulipa kwa dola au shilingi?” Agnes aliulza

“Hembu na wewe acha ushamba wako, huku shilingi aitolee wapi?” Fetty alimkosoa mwenzake

“Haya yaishe kiongozi Fetty”

“Muambia sisi tunataka dola milioni mia zinatutosha”

Samson akamgeukia bwana Rusev na kumueleza kiasi walicho kitaja wezake na bwana Rusev hakuwa na hiyana zaidi ya kukubali kuwalipa kiasi hicho.


“Anauliza tunataka cashe au hadi benki?”

Anna akashusha pumzi na kubugia fumba moja la juisi anayo kunywa

“Hapa cha msingi kila mmoja apewe kiasi chake mkononi, tusepe” Halima alizungumza huku akiwatazama wezake machoni

“Ujue hizo pesa ni nyingi sana, na kama kuzibeba itakua ngumu?” Fetty alishauri

“Sawa Fetty, haya tukisema tupewe kwenye, akaunti namba tutazitolea wapi, hiyo moja, mbili sisi site hapa tunatafutwa karibia dunia nzima, ni benki ipi tutazipeleka sura zetu na kwenda kuitoa hiyo pesa?”


“Kumbe siku moja moja na wewe. Anna unazungumzaga poiti. Kikubwa hapo Samso muambie huyo mtui wako tunahitaji cashe hapa hapa, kam ni kwenye mabegi tutabeba, cha msingi ni kupewa pesa na kwenda kuanza maisha mapya mbele ya safari”

Agnes alizungumza na wote wakakubaliana waweze kukabidhiwa pesa zao mkononi, Samson akamueleza bwana Rusev maamuzi waliyo yafanya wezake. Bwana Rusev akanyanyua mkonga wa simu yake ya mezani, akaminya namba kadhaa na kumpa maelekezo mlinzi wake, pamoja na muhasibu wake.


“Jamaa anasema pesa inakuja”

Kila mmoja akajiweka mkao wa kupokea kitita chake, ili aweze kuendelea na maisha yake mbele ya safairi. Baada ya dakika kumi na tano kukatika kundi kubwa la watu wapatao kumi, wenye bunduki wakaingia ndani ya ofisi ya bwana Rusev, jambo lililo anza kuwapa wasiwasi Fetty na wezake ambao hawakueelewa ni kitu gani kinacho endelea kwani, watu hao wameingi gafla na moja kwa moja wakamzingira bwana Rusev.

***

Kitendo cha Rahab kujikwaa na kuanguka chini, ikawa ni bahati nzuri kwake, kwani mshale ulio kuwa umelengwa na zombi mmoja ulipita juu yake na kugonga kwenye mti uliopo mbele yake.


“Haaa……!!!”

Rahab alijikuta akiduwaa na kutazama nyuma, kwa mbali akamuona mtu huyo aliye fura hasira akija kwa kasi ya ajabu, kwa haraka Rahab akaikota bunduki yake, kwa bahati nzuri akakuta kuna risasi moja, akaikoki kwa haraka na kumlenga zombi huyo anaye mfwata kwa kasi. Kama kawaida yake Rahab, hakukusoea kuifyatua risasi hiyo iliyo tua kichwani mwa zombie huyo na kumpua kchwa na kugawanyika vipande vipande. Raisi Praygod akaendelea kushangazwa na uwezo mkubwa wa upambanaji alio kua nao Rahab ambaye hakumdhania kwamba anweza kuja kuwa msaada mkubwa sana kwenye maisha ya kuiokoa roho yake. Rais Praygod akampa mkono Rahab na kumnyanyua kutoka chini alipo kua ameanguka. Wakaendelea na kukimbia.


Mlio wa bunduki, ukawastua mazombi wote walio kua kwenye msitu huu, wakafahamu ni wapi mlio huo wa bunduki ulitokea, walicho kifanya ni kubadili mielekeao yao na kwenda sehemu ya tukio huku akijifariji kwamba watu wanao wawinda watakua wamekamatwa na mmoja wao. Wote wakajikuta wakishikwa na butwaa baada ya kumkuta kiongozi wao akiwa amechanguliwa kichwa chake kama ilivyo kua kwa mwenzao waliye mkuta ndani ya kijumba akiwa amekufa, Baadhi yao hawakuweza kuyazuia machozi yao kuweza kumwagika kwani kiongozi wao huyo ndio kila kitu katika maisha yao.


Rahab na Raisi Praygod wakaendelea kutokomea msituni, huku mwanga wa mbalamwezi ukizidi kuwapia uwezo wa kuweza kuona ni wapi wanapo kwenda na niwapi wanapo tokea. Wakafanikiwa kufika barabarani ambapo wakalikuta gari la watu hao wa ajabu, likiwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara. Wakaanza kulinyatia taratibu, huku kila mmoja akiwa amepita upande wake. Wakafanikiwa kufika mbele, kwenye kichwa cha dereva, wakachungulia ila hapakuwa na mtu wa aina yoyote zaidi funguo inayo ning’inia pembeni ya mskani


“Panda”

Raisi Praygod alimsisitiza Rahab ambaye alikua akiendelea kulichunguza gari hilo linalo toa harufu kali ya mizoga iliyo kufa. Rahab akafungua mlango na kuingia, Raisi Praygod akawash gari, taratibu wakaanza kuondoka katika eneo hilo huku, raisi akijitahjidi kuongeza mwendo wa gari hilo linalo toa mgurumo mbaya, kama mabati yanayo gonganga kwa nguvu


Mlio wa gari, ukawastuaa mazombi hao walio kua wakiendelea kusononeka na kuomboleza kifo cha kiongozi wao. Wanne kati yao, wakakimbilia sehemu mlio wa gari unapo tokea huku wengine wakiubeba mwili wa mkuu wao kuurudisha kwenye makazi yao.


Gafla raisi Praygod akajikuta akifunga breki kali, baada ya kuwaona mazombi wanne wakiwa wamesimama katikati ya barabara huku kila mmoja akiwa ameshika bunduki aina ya gobore, wakiwa wamezielekezea kwao, wakiwa tayari kwa kuwalenga Raisi Praygod na Rahab.


***

Wanajeshi wa bwana Rusev walio mzingira, wakamnyanyua kiongozi wao, huku wakimuhitaji aweze kukumbia kwani kuna mashambulizi ya ndege za kijeshi la Russia yanaweza kufanyika ndani ya dakika kadhaa zinazo kuja. Wakatoka kw mwendo wa kukimbia huku wakiwa wamemzingira kiongozi wao huyo wanaye mtukuza kama muumba wao.

“Jamani inakuwaje, mbona tumeachwa peke yetu?”

Anna aliuliza huku akiwa amesimama wima akichungulia mlangoni na kumuona kiongozi huyo akiingia kwenye lifti yeye na wanajeshi wake na kushuka chini.


“Tuondokeni”

Samson alizungumza huku akiongoza msafara wa kuelekea walio elekea bwana Rusev na wanajeshi wake, kwa mwendo wa haraka wakafanikiwa kufika kwenye lifti, ikawalazimu kuweza kusubiri baada kwa muda kidogo kwani bwana Rusev na watu wake walikua wanaelekea chini wakitokea gorofa ya tano. Baada ya muda lifti ikafunguka na wote watano wakaingia ndani na Samson akaminya kitufe cha kuelekea chini. Wakiwa katika gorofa ya tatu, mtikisiko mkubwa, wa bomu ukatokea na kuisababisha gorofa hilo kuyumba na umeme ukakatika na kuipekea lifti hiyo kusimama na kumfanya Agnes kupiga ukelele mkali, kwani gorofa lilianza kuteguka vipande vidogo vidogo likielekea kuanguka chini.


SHE IS MY WIFE(30)


Mtikisiko ukaendelea kulitetemesha jengo lihi ambalo lilipigwa kombora na ndege ya jeshi la Russia, ikiwa ni shambulizi la kustukiza kwenye kikosi hichi kinacho itesa serikali kwa kipindi kirefu. Kwa bahati nzuri mlango wa lifti ukaweza kuachia upenyo mdogo, kwa kutumia nguvu Samson akaanza kuufungua hadi ukafunguka, kwa bahati nzuri sehemu lifti ilipo kwamba ni gorofa ya pili, wakatoka wote kwa pamoja na kutafuta eneo lenye ngazi za kushukia. Kwa bahati nzuri eneo la ngazi halikua mbali sana na eneo zilipo lifti.


Milio ya risasi, ikaanza kusikika vizuri masikioni mwao, ikitokea nje, hhuku kindi la Mr Rusev likipambana na wanajeshi walio kuja kuvamia katika kisiwa hicho, wakafanikiwa kutoka nje huku gorofa hilo wakiliacha likendelea kumeguka vipande vidogo vidogo.


“Twendeni huku”

Samson alikua kiongozi wa wengine, na hapakuwa na wakumuuliza kwamba ni wapi wanapo elekea kwani kila mmoja alihitaji kuyaokoa maisha yake au kuuokoa usalama wake kutoka mikononi mwa jeshi la serikali hiyo inayo linalo sifika kwa maamuzi magumu pale wanapo mkamata mtu anaiye jihusisha na ugaidi, na mara nyingi wa wa namna hiyo wameweza kuambulia kifo kwa kupigwa risasi nyini zisizo na idadi mwilini mwaoa kama alivyo fanyiwa kiongozi Saddam Hussein.


Wakafanikiwa kufika kwenye moja ya jengo, ambalo milango yake yote imefungwa kwa makufuli makubwa

“Samson tunafanyaje sasa?”

Halima aliuliza huku macho yakimlenga lenga. Samson hakumjibu chohote Halima zaidi ya kuziangalia ndege za jeshi, aina ya Jet zikipita kwa kasi katika eneo mbali kidogo na sehemu walipo, huku zikimwaga risasi nyingi kwa wanajeshi wa Bwana Rusev. Hapa ujambazi wao wakauona haufui dafu mbele ya shambulizi hili lililo wapagawisha akili zao huku kila mmoja asijue ni wapi kwa kwenda.


Kwa bahati nzuri bwana Rusev akafanikiwa kuingia kwenye manohari walio kuja nayo Samson na rafiki zake, akiwa na kundi la wanajeshi wake walio kuja kumchukua ofsini kwake. Hapakupoteza muda zaidi ya kuondoka katika eneo la kisiwa ambacho kwa sasa hali yake imekua mbaya zaidi ya kuzimu. Ila nafsini mwake bwana Rusev akatokea kuwaonea huruma sana Samson na mabainti wadogo alio kuja nao, ambao Samson aliwaeleza walikuwa ni magaidi wanao anza kuchipukia katika swala zima la kigaidi.


Kazi ikawa ni ngumu kwa Samson na wezake ambao hadi sasa hivi hali inazidi kuwa tete kwao, hawakujua ni wapi waende kukweukwepa mkono wa serikali, mfano mzuri wanaouona kwa askari wa bwana Rusev wanavyo angushwa chini kama kuku wenye videri kwani, risasi kutoka kwenye ndege hizo za jeshi hazikukosea wapi kwa kupiga.

“Jamani hapa hatuna la kufanya, kila mmoja atawanyike kivyake akaokoe maisha yake mbele ya safari”

Samson alizungumza huku akihema kwa nguvu

“Nyoo atawanyiki mtu hapa, wewe ndio umetuleta na wewe ndio utatuokoa”


Agnes alizungumza kwa hasira akionekana kumpiga Samson vikali, kwa wazo lake alilo liropoka

“Sikia SAMSOM. Nahisi hutujui vizuri wewe eheee?”

Fetty alizungumza huku sura yake ikiwa imebadilika kabisa, akionekana anaweza kufamfanya Samson kitu chochote muda wowote kuanzia sasa. Samson ikambidi awe mpole kana ni uwezo wa kupigana na Fetty na wezaka anao, ila hajui ni watu wa aina gani hadi wanajiamini kiasi hichi na kuwa magaidi wanao sakwa na jeshi la polisi Tanzania.


“Twendeni huku”

Ikamlazimu Samson kuwa kuanza kukimbia kuelekea asipo pajua, ila alihitaji kuepukana na varangati la Fetty na wezake, kwani anafahamu varangati la Rahab, alilo anzishiwa siku alipo kua naye chumbani, na hawa ni rafiki wa Rahab, ina maana wote varangati lao si lakitoto. Wakazidi kukimbia huku wakimfata Samson kwa nyuma. Kila walio ona mwili wa askari aliye fariki hawakusita kuiokota bunduki ya askari huyo, Wakaingia kwenye msitu uliopo kwenye kisiwa hicho, Kila mmoja akajitahidi kufyatua risasi pale walipo weza kupata nafasi ya kufanya hivyo kwa wanejeshi wa serilali walio anza kuingia kisiwani wakitokea kwenye boti zao walizo kuja nazo kupitia baharini.


Hapakuwa na muda wa masihara tena zaidi ya wao kufanya kazi moja tu ya kuua kila mwanajeshi aliye jitokeza kwenye macho yao. Mashambulizi ya ndege za kivita yalisitishwa kutokana na wanajeshi kuingia ndani ya kisiwa, kwahiyo ingewawia ngumu marubani wa ndege hizo aina ya Jeti kuendelea kufanya mashambulizi ambayo yangeweza kuwadhuru hadi wezao. Hiyo ikawa ni nafuu kubwa sana kwa Samson na wezake.


Wakafanikiwa kufika ufukweni ambapo, wakaweza kukuta nguo maalumu za kuogelea, zilizo vuliwa na wajeshi baadhi walio tumia njia ya kuogelea kuingia ndani ya kisiwa hicho na kuanza kufanya mashambulizi ya kimya kimya. Wakayavua mavazi yao waliyo yavaa, wakavaa mavazi hayo ya kuogelea ambayo yana mitungi midgo ya gesi inayo valiwa mgongoni, huku ikiwa na shivikizo vidogo. Kisha wakakimbilia ndani ya maji na kuanza kuogelea kwa kasi kila mmoja anayo imudu yeye.

***

“Usipunguze mwendo muheshimiwaaaaa”

Rahab alizungumza kwa sauti kali, iliyo mbadilisha mawazo Raisi Praygod, na kumfanya ausogeze mguu wake kwenye brake na kuongeza mwendo huku wakiinama chini. Mazombi hawa kwa hasira wakaanza kufyatua risasi kwenye kioo cha gari pasipo kulipisha, Raisi Praygod akazidi kuongeza mwendo, hadi misuli ya mwili wake ikakaza kabisa, huku akiwa amayang’ata meno yake kwa nguvu akihakikisha anawafikia mazombi hao walio endelea kupiga risasi.


Kwa bahati nzuri gari hilo likawaponda ponda vibaya mazombi hao walioweka mgomo wa kulipisha gari hilo na kupelekea kuwaponda ponda vibaya na kufafa. Kwa haraka Raisi Praygod akajiweka sawa kuendelea kuliendesha gari hili linalo kwenda kwa kasi, wakaendelea kuifwatisha barabara hiyo ya lami ambayo ni ndefu sana na haina kona nyingi sana, na ipo katikati ya msitu huu mnene na wakutisha.


Wakafanikiwa kukuta kibao kilicho andikwa kwa herufi kubwa za kushongesha ‘GOOD BYE BLACK FOREST’ Ikiamaanisha kwamba msitu huo ndio jina lake, kabdi walivyo zidi kwenda ndivyo walivyo zidi kuoata matumaini ya kuingia kuokoka kwani, waliweza kukutana na barabara nyingine, ambazo zina magari ya watu wa kawaida.

“Asante Mungu”

Rahab alizungumza huku akionekana kuto kuoamini kwamba wapo salama wakitokea kwenye mikono ya watu ambao walihitaji kuzitoa roho zao. Taratibu gari hilo likaanza kupunguza mwendo kasi wake, likiashiria kuishiwa na mafuta

“Vipi….?”

Rahab aliuliza huku akimtazama Raisi Pragod usoni

“Yatakua ni mafuta yamekwisha”


“Ohooo itakuaje sasa”

“Kwa hapa hakuna tatizo kutokana kuna magari yanayo pita tunaweza tukaomba msaada na kuchukuliwa”

“Mmmmm”

Raisi Praygod akalisogeza gari hadi kando kando ya barabara na kuliegesha, kisha wao wakashuka huku wakiwa wamevalia magauni, waliyo weza kuyapata usiku ulio pita. Magari yakazidi kukatiza kwenye barabara waliyo kuwepo, hii ni kutokana na kupambazuka, na mwanga wa juu kuchukua nafasi yake katika dunia. Mwanga wa juu la asubuhi, likaendelea kupiga kwenye miili yao, na kuwafanya wajihisi vizuri kwenye miili yao, ila njaa kwa mbali zikaanza kuyasumbua matumbo yao yaliyo kosa chakula kwa masaa mengi.

“Muheshimiwa hapa tunaelekea wapi kwa maana sielewi elewi”


“Tusimamishe simamishe magari tutajua pa kwenda, kikubwa tumetoka kwenye hatari”

Wakaanza kazi ya kuyasimamisha magari yanayo katiza kwenye barabara waliyopo, kila mmoja aljitahidi kupunga mkono kwa kila gari lililo kua likikatiza ila madereva wa magari hayo hawakuweza kusimamisha magari yao kuhofia jinsi watu hao walivyo vyaa, wakihisi ni wendawazimu.

“Tutembee tembee mbele”

Raisi Praygod alishauri na wote wakaanza kutembea, huku wakiendelea kuyasimamisha magari hayo pasipo kufanikiwa.

“Muheshimiwa nikuulize kitu?”

“Uliza tu”

“Unavyo hisi kwa sasa, Tanzania, itakua inaongozwa na nani?”

“Aisee, hata mimi sijui ila kisheria makamu wangu, ndio anaweza kukaimu kiti changu cha uraisi hadi zipite siku tisini ndio wanaweza kufanya uchaguzi wa kumchagua raisi mwengine, kama mimi sinto jitokeza”

“Ila inabidi uwahi kurudi nchini, ninaimani kwamba watu watakua wanahisi umefariki”


“Ni kweli, ila kwa sasa inanilazimu kuweza kupumzisha akili yangu, kabla ya siku tisini ninaweza kurudi nchini Tanzania”

“Sawa, je familia yako nayo si itakua na majonzi makubwa?”

“Yaaa, ila mke wangu alishafariki mwaka sasa umepita”

“Alaa, sijawahi kuisikia hiyo?”

“Ulikuwa wapi?”

“Aisee kipindi hicho mimi wala sikuwa ninajihusisha na maswala ya serikali, nilikua nikitafuta pesa kwa shida kubwa sana”

“Kwani ulikua unafanya kazi gani?”

Rahab akakaa kimya kuweza kutafakari ni nini amjibu Raisi Praygod, ambaye bado ni kijana mdogo wa miaka thelathini na tano. Rahab aliwaza endapo atamuambia kwamba alikua akifanya kazi ya kuuza mwili wake, atajishusha thamani. Pia akahisi akimueleza kwamba alikua ni jambazi inaweza kuleta picha tofauti


“Vipi mbona kimya, haujibu swali langu?”

“Ahaaa, kusema kweli muheshimiwa mimi, nilikua ni miongoni mwa wale wasichana watano majambazi walio isumbua serikali kwa matukio ya uvamizi wa benki”

Raisi Praygod akastuka kidogo, ila akajitahidi kuuficha mstuko wake, akaachia tabasamu pana kiasi usoni mwake na kumfanya Rahab, asihisi kitu chochote kinacho endelea kwa Raisi huyo


“Sasa kwa nini muliamua kufanya ujambazi?”

“Kusema kweli sisi tulichukuliwa na mzungu mmoja, aliye kua akifanya kazi kwenye hospitali ya jeshi kama daktari mwalimu wa kuwafundisha madaktari wa jeshi kutengeneza sura bandia. Ambao yeye alikua akitufundisha kisha na kutupa kazi ya kuweza kuua baadhi ya watu maarufu”

Hadi kufika hapa Raisi Praygod akawa amemuelewa Rahab, nini anacho kizungumza kwani kazi hiyo yeye ndio alipanga ianyike, akishirikiana na rafiki yake Dokta William, kutokea Israel, kwa lengo la kuweza kuwaangamiza watu wote wanao enda kinyume na serikali kwa kipindi hicho. Ila hadi wasichana hao kuigeuka serikali hakufahamu kuna kitu gani kilicho kua kikiendelea katikati.


“Ahaaa, ila kwa sasa si umeuacha?”

“Sina haja tena inabidi, nifanye kazi halali, kwani hata yule daktari hatujui ni wapi alipo. Wezangu nao ndio hivyo wamekamatwa, nahisi watakua wemesha nyingwa. Kwani kwa makoso tuliyo yafanya sidhani kama wataacha hai”

Raisi Praygod hakuzungumza chochote zaidi ya kuangaza angaza tena macho yake barabarani, akaona gari kubwa aina ya scania, likija kwa mwendo wa kawaida, akalipungia mkono, ila likawapita pasipo kusimama. Kufika mbele kidogo dereva huyo akalisimamisha gari hilo, na kuwapigia honi Rahab na Raisi Praygod, waende wakapande.


Raisi na Rahab wakalikimbilia gari hilo hadi sehemu lilipo simama, ambapo dereva wa gari hilo wakakuta ni mtu mwenye asili ya Afrika. Mtu huyu akaonekana kumtazama Raisi Praygod kwa muda kisha, huku akiwa haamini macho yake

“Wewe si raisi wa Tanzania, bwana Praygod Makuya……!!?”

Mtu huyo alizungumza kiswahili, sahihi akiashiria kwamba yeye ni mtanzania, Rahab akamtazama Raisi aliye pata kigugumizi cha gafla, ila akajikaza hivyo hiyo kumjibu mtu huyo

“Ndio, ndio mimi”

“Ingieni ndani”

Mtu huyo alizungumza kwa furaha, na kuwafanya Rahab na Raisi Praygod kuingia ndani ya gari na kukaa kwenye siti mbili zilizo kua wazi.


“Mimi ninaitwa Azaria, ni mtazania”

“Tunashukuru kukufahamu, hivi hapa ni wapi?”

“Huku ni Mexco, kidogo nimekuja kutafuta tafuta maisha, nimepata kazi kwenye kampuni hii ya kusafirisha mafuta. Vipi tena mbona huku?”

“Tulipata ajali ya ndege, mimi na huyu binti ndio tumefanikiwa kupona”

“Aisee poleni sana wapendwa, unajua mara yangu ya mwisho kuondoka Tanzania ndio kilikua kipindi cha kupiga kura. Nilikupa kura yangu muheshimiwa”

“Asante sana, pia asante kwa kuweza kutusaidia”

“Aisee poleni sana, pia muna bahati hapa ninaelekea mjini, ninapo ishi. Ninatoka mikoa ya chini huko kupeleka mafuta”

“Ahaaa asante sana, huyu ni msaidizi wangu anaitwa Rahab”


“Nashukuru kukufahamu dada Rahab”

“Asante na wewe pia kaka Azaria”

Wakafika kwenye mmoja wa mgahawa ambapo Azaria akashuka na kwenda kuwanunulia chakula pamoja na vichwaji, kisha akarudi navyo kwenya gari na kuwakabidhi Raisi Praygod na Rahab ambao wanaonekana kuchoka sana, kwani tangu walipande gari hilo yamekatika masaa sita wakiwa barabarani. Wakaanza kukila chakula hicho taratibu huku wakionekana kuwa na hamu kubwa ya kula chakula kizuri kama hicho.


“Hii safari itachukua muda gani kufika jijini Mexco City?”

Raisi Praygod alizungumza huku akiwa amefundia kipande cha paja la kuku, lililo nona sana

“Hapa bado sana itatuchukua masaa mengine kama saba, hivi. Tuombe Mungu tusisimamishwe na askari kwa maana huku wanajali sana kukagua passport”

“Aisee kumbe ni kurefu sana?”

“Sana tu, kwa dereva ambaye si mzoefu anaweza kulitupa gari, nje ya barabara. Ila kwa sisi wazoefu tunaona ni jambo la kawaida.”


Kutokana na kushiba, uchovu mwingi ukamtawala Rahab na kujikuta akilala fofofo huku, akiwaacha Raisi Praygod na Azaria wakiendelea kubadilishana mawazo ya hapa na pale.

“Muheshimiwa inatubidi kuweza kulala kwenye Motel moja hapo, mbele, kwani hapo mbele kuna kizuizi cha ukaguzi, na jinsi ninyi mulivyo watatupa shida na giza limesha ingia muda huu”

“Sawa hakuna shida, tena umefanya la maana, kwani kuna rafiki yangu yupo hapa Mexco ninaweza wasiliana naye akanipa hifadhi kwa muda”

“Kwa nini usiupigie ubalozi wa Tanzania ukakuletea msaada?”

“Kwa sasa sihitaji msaada wa kiserikali kuna mambo inanilazimu niyakamilishe kabla sijarudi nchini kwangu”

“Sawa muheshimiwa Raisi”



Wakafika kwenye moja ya Motel iliyopo mbembezoni mwa barabara, na kuna magari mengi makubwa, ikiashiria hapo ni sehemu ya madereva wengi kuweka vituo vyao, ili kuendelea na safari zao muda walio upanga wao wenyewe. Azaria akamuomba Raisi abaki ndani ya gari, kisha yeye akashuka kwenda kukata vyumba vitatu, kisha akarudi akiwa na funguo mkononi

“Tunaweza kwenda”

Raisi Praygod akamuamsha Rahab ambaye muda wote alikuwa amelala fofofo, hii ni kutokana na kukesha siku nyingi pasipo kulala.


“Ehehee….”

Rahab aliweweseka kwa wenge la usingizi, huku akijitahidi kuyafumbua macho yake kuweza kutazama ni wapi walipo.

“Tumefika, shuka twende”

Raisi Praygod akamsaidia Rahab kushuka ndani ya gari na wote wakaongozana na Azaria hadi kwenye vyumba vyoa, huku kila walipo pita baadhi ya watu waliwatazama RaisI Praygod na Rahab kwani wemechafuka sana, huku miili yao wakiwa wameisitiri kwa magauni yaliyo chafuka.

Wote wakaingia kwenye chumba kimoja cha Raisi, ambapo kuna simu maalumu, yenye uwezo wa kupiga sehemu mbalimbali.


“Muheshimiwa niwaletee vyakula tena?”

“Hapana kwa mimi nipo sawa, labda kwa huyo bibie”

“Mimi ninausingizi mwaya, asanteee”

Rahab alizungumza huku akipiga miyayo na kujirusha kitandani, hakujua kwamba hichi chumba si chake. Azaria akataka kumuamsha ila Raisi Pragod akamzuia.

“Wee muache tuu hakuna shida, akilala hapa”

“Sawa muheshimiwa ngoja mimi niende chumbani kwangu”

“Sawa na uwe na usiku mwema”

“Sawa muheshimiwa”

Azaria akatoka na kumuacha Raisi Praygod akiendelea kuminya minya baadhi ya batani za simu akijaribu kukumbuka namba za rafiki yake huyo aliye soma naye kipindi cha nyuma nchini Canada. Kwa bahati nzuri akakuta namba ya rafikia yake huyo ipo hewani, ikaita kwa muda, kisha ikapokelewa.


“Who?”(Nani?)

Sauti nzito ya kiume ilisikika upande wa pili wa simu

“Praygod Makuya hapa vipi wewe”

“Ahaaaa kaka, upo Mexco nini?”

“Ndio mskaji wangu, nipo kwenye motel moja hivi nimechili”

“Raisi unakaa kwenye Motel, vipi bwana mbona kuna mijihoteli mingi mikubwa kwa hadhi yako”

“Kaka yaliyo nikuta wewe acha tu?”

“Vipi kuna tatizo?”

“Yaaa tena si dogo, ila kukipambazuka tu nitakupigia ujue ni wapi nilipo uje kunifwata”

“Ahaaa kaka kwanini usiniambie sasa hivi nije kukuchukua. Kwa maana usakama wako wewe unahitajika na mimi ninavijana wengi tu wa kukulinda”

“Hapana Frednando, tusubiri kupambazuke nitakupigia au wewe unaweza kupiga kwa namba hii, nitakuambia ni wapi nilipo”

“Sawa kaka, haina shida, ngoja niweke mazingira vizuri”

“Sawa”


Raisi Praygod akakata simu na kuanza kushangilia kwani matumaini ya usalama wake kwa ujumla yamesha rudi, kwani rafiki yake ni miongoni mwa matajairi wakubwa ndani na nchi ya Mexco. Macho ya Raisi Praygod yakatua kwenye mapaja ya Rahab, aliye lala kifudi fudi, na kuacha makalio yake makubwa kiasi kuonekana vizuri. Taratibu Rais Praygod akamsogelea Rahab, akachuhuka shuka kubwa na kumfunika. Rahab taratibu akajigeucha na kumtazama Raisi Praygod.

“Wewe hulali?”

Rahab aliuliza kwa sauti ya unyonge, huku akimtazama Raisi Praygod kwa macho yaliyo jaa usingizi, hadi akajikuta akirembua.


“Nataka nikaoge” Rais Praygod akapiga hatua moja, ila Rahab akamshika mkono na kumvuta kwa nguvu na kuangukia kitandani. Rahab kwa haraka akausogeza karibu mdomo wake kwa Raisi Praygod na wakaanza kunyonyana, huku wakionekana kuwa katika hisia kali. Raisi Praygod akalivua gauni lake na kulitupa pembeni. Akalishika la Rahab na akamvua, wote wakabakiwa kama walivyo zaliwa.



ITAENDELEA 




ILIPOISHIA

“Wewe hulali?”

Rahab aliuliza kwa sauti ya unyonge, huku akimtazama Raisi Praygod kwa macho yaliyo jaa usingizi,

hadi akajikuta akirembua.

“Nataka nikaoge”

Rais Praygod akapiga hatua moja, ila Rahab akamshika mkono na kumvuta kwa nguvu na kuangukia kitandani. Rahab kwa haraka akausogeza karibu mdomo wake kwa Raisi Praygod na wakaanza kunyonyana, huku wakionekana kuwa katika hisia kali. Raisi Praygod akalivua gauni lake na kulitupa pembeni. Akalishika la Rahab na akamvua, wote wakabakiwa kama walivyo zaliwa.



ENDELEA

Hapakuwa na mtu aliye weza kumuonea mwenzake aibu zaidi ya wote kushiriki tendo la ndoa ipasavyo. Rahab akazidi kujituma kitandani kumpa muheshimiwa Raisi mambo matamu ambayo hata Raisi Praygod, hakuwahi kuyapata kutoka kwa mwanamke wa aina yoyote tangu azaliwe. Hata marehemu mke wake, hakuweza kufikia hata aslimia kumi kwa mambo ambayo Rahab anamfanyia juu ya kitanda. Wote wakajikuta wamesahau kwamba wanapita katika kipindi kigumu cha matatizo.

“Rahab”

Raisi Praygod alimuita Rahab, aliye mkalia juu ya kiuno chake akizidi kukatika kadri ya uwezo wake.

“Mmmmmm”


Rahab aliita huku akiwa amebana pumzi zake, huku jasho kwa mbali likimwagika na nywele zake ndefu zikiwa zimekaa shaghala baghala.

“Nataka nikuoe”

“Kweli?”

“Ndio nahitaji uwe mke wangu, wa ndoa”

Rahab kuambia wahivyo hakujibu kwa sauti, ila akajibu kwa vitendo, vilivyo mfanya Raisi kusahau matatizo yote na kuzidi kuchanganyuikiwa kwa penzi hilo la binti mdogo mwenye mwili mwembamba, fulani, ila si shuuhuli ya kupambana pekee yake na maadui, ila hata shughuli ya kitandani anaiweza kwa asilimia mia moja. Hadi wanafikia kileleni wote kwa pamoja wakajikuta wakicheka huku wakiamini kwamba walicho peana kilistahili kwa wao kuweza kukipata kwa wakati huo.


“Nakupenda sana Rahab”

Raisi Praygod alizungumza huku akihema mithili ya mwana riadha wa mwisho kwenye mbio ndefu, aliyekua na kibarua kirefu cha kuwakimbiza wezake wanao kwenda kwa mbio ndefu sana.

“Nakupenda pia Praygod”

Kwa mara ya kwanza Rahab kufungua kinywa chake na kuliita jina la Raisi, kwani siku zote alizoea kumuita muheshimiwa Raisi. Taratibu Rahab akajilaza kifuani mwa Raisi Praygod, huku taratibu akiupa kazi mkono wake wa kushoto kuchezea nywele nyini lizizopo kifuani mwa raisi Praygod.


“Twende tukaoge”

Raisi Praygod alizungumza, na taratibu wote wakashuka kitandania, wakaingia bafuni na kila mmoja akawa na kazi ya kumuogesha mwenzake kwa kila kona ya mwili. Ukawa ndio mwanzo mpya wa mahusiano kati ya Raisi Praygod na Rahab, kila mmoja aliweza kuufungua moyo kwa mwenzake na kuamini upendo wao umeendana kwa asilimia kubwa sana.

***

Kila jinsi walivyo zidi kuogelea ndivyo jisi walivyo zidi kwenda mbele, huku mara kwa mara wakiwa wanajitokeza kwenye usawa wa bahari kutazama ni wapi wanapo elekea. Ikawachukua muda mrefu sana kuweza kufika pembezoni mwa fukwe za bahari, katika eneo ambalo limetulia sana. Wote wakaivua mitungi ya gesi ambayo walikuwa wameivaa migongoni mwao. Kila mmoja alijihisi njaa kubwa kwenye tumbo lake, kwani waliweza kudumu ndani ya maji takribani masaa nane, wakiwa wanatoroka kutoka sehemu mmoja kwenda nyinine


“Ahaaa kudadadeki, kweli ng’ombe wa masikini hazai”

Halima alizungumza kwa sauti kubwa huku akijilaza kwenye mchanga mweupe ulio kua pembezoni mwa bahari hii kubwa. Hakuna aliye mjibu zaidi ya wezake kuendelea kutazama kila eneo la fukwe hizi zinazo pendeza kuvutia sana.

“Jamani inakuaje?”

Anna aliuliza kwa sauti ya unyonge, dhairi akionekana kuchoka sana.


“Nahisi hapa kwenye fukwe kunaweza kua na nyumba tutembeeni tembeeni, tunaweza kupata msaada”

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog