Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

SHE IS MY WIFE - 2

   

Simulizi : She Is My Wife

Sehemu Ya : Pili (2)


Akapewa Helment na kulivaa, safari ikaanza huku kila mmoja akiwa kimya.

“Kaka usipeleke kasi sana,nyinyi waendesha pikipiki siwamini”


“Kwa nini hutuamini?”

“Ahaaa nyinyi bwana pikipiki munajifunza leo kesho muingia barabarani”

“Ahaaa,wanao pataa ajali ni wale wazembe, utakuta mtu anaendesha pikipiki huku akiwa amekunywa konyagi, sasa ni kwanini asipate ajali”


Anna akalitazama eneo la kituo cha gesi ambacho jana walifanya tukio, na kuwaona baadhi ya askari wakifanya fanya uchunguzi wa vitu vidogo vidogo

“Ahaaa jana hapa kulichimbika” Dereva pikipiki alizungumza

“Kulikuwa na nini?” Anna aliuliza kama vile hajui kilicho tokea

“Ahaa nasikia kuna majambazi walifunga mtaa jana, hapakuwa na askari aliyekurupuka”


“Ahaaaa......!!”

“Ina maana jana hukusikia?”

“Mimi ninatokea,turiani Morogoro na wala sijasikia”

“Ahaaa,jana basi askari wengi wamekufa pale kwa kulipukiwa na gesi”

“Kisa nini hadi wakafa?”

“Ahaaa nasikia kuna sister mmoja ambaye ni jambazi, askari walimshika.Kumbe yule dada ni mafia katika kupambana pambana nao basi akawatoka polisi na sijui alifanyaj fanyaje hadi akailipua mitungi ya gesi”

“Ahaaa masikini weee”

“Ahaaa wee acha tuu, hapo ndipo nimeamini kuwa Tz kuna watu m agaidi kama huko Lebanon”

“Ahaaa pole yao”


Anna akaendelea kuzungumza na muendesha pikipiki hadi wanafika Kariakoo, Anna akatoa noti tatu za elfu kumi na kumkabidhi muendesha pilipiki

“Kaa na chenchi kwani safari ni ndefu”

“Asante dada yangu,Mungu akubariki”

“Amen”

Anna akaingia kwenye duka analo hitaji kununu vifaa na kumuacha muendesha pikipiki akiondoka zake.


Dokta William baada ya kumaliza kikao na viongozi wa polisi, akawaomba wampe muda kuweza kufikiria juu ya ombi lao la kuunda kikosi kipya cha uchunguzi ambacho kitawatafuta majambazi walio sababisha tukio la askari na wananchi kufariki.Kwa bahati nzuri likizo ya Dokta William inaanza sikuinayo fwata, kwa kigezo hichi akatumia kaondoka nchini na kuelekea Israel sehemu ilipo familia yake.


                                             ***


Anna akafanikiwa kununu manunuzi yote aliyo agizwa na wezake, akaelekea sehemu ya kununulia magari ambapo akaanza kutazama ni gari gani ambalo anaweza kununua,kwa bahati nzuri akabahatika kupata gari aina ya corora ambayo imetuka kidogo kwa kiasi cha pesa alicho nacho.


Akamaliza makabidhiano na wauzaji kisha akaondoka na kutafuta baa iliyopo karibu na sehemu ya kuuzia magari, hii ni kuepukana na kukamatwa na askari wa barabarni kwani gari lake bado halijamaliziwa kukamilisha baadhi ya usajili

Akaagiza soda na kunywa kunywa akivuta muda ifike saa mbili usiku aanze safari kurudi sehemu anapoishi, Simu ya ana ikaita na kuona ni namba ya Halima


“Wewe, mbona hurudi?”

“Nipo sehemu nimekaa nasubiri muda uende ende kidogo,kwani barabarani kumechafuka sana”

“Sasa ungesema sio kukaa kimya kutuweka sisi matumbo juu bwana”


“Musijali”

“Hili gari umesha lipata?”

“Ndio”

“Ni zuri au ni kimeo?”

“Zuri kiasi chake”

“Wewe sema zuri kiasi chake, utujie na kimeo hapa utakiendesha wewe mwenyewe”

“Haaa wasi wasi wenu wa nini sasa”

“Powa, jipya?”

“Jipya hakuna ni ishu ya jana ndio top story hapa mjini”

“Ahaaa powa mwaya”

“Ok”


Anna akakata simu na kuendelea kupata kinywaji,hadi in atimu mida ya saa tatu kasoro usiku akalipa pesa ya vinywaji alivyo kunywa na kuingia ndani ya gari,akapitia kwenye moja ya sheli na kujaza mafuta yatakayo mtosha kwa safari.Mwendo wa masaa mawili ukamtosha kufika kwenye handaki lao


“Nice job baby”(Kazi nzuri mtoto)

Rahab alizungumza huku akimpiga piga Anna mgongoni, usiku mzima wakawa na kazi ya kupanga mipango jinsi ya kwenda kuvamia benki ya taifa na muda maalumu walio upanga ni saa sita mchana siku inayo fwata


Kila mmoja akaamka asubuhi akiwa na shauku ya kufanya tukio la kwenda kupora pesa,Fetty akajitolea kuuvaa mwili wa jimama ambalo likambadilisha na kumfanya aonekane ni  mama mtu mzima mwenye familia kubwa.Kila mmoja akajiandaa na kuchukua silaha zake ambazo zitamsaida katika tukio zima,Kabla hawajatoka simu yao ya mezani ikaita 


“Pokea”

Anna akamuomba Rahab kuipokea simu hiyo

“Haloo”

“Dokta Will hapa nazungumza”

“Dokta vipi, mbona umetupiga na simu ya mezani?”

“Hilo halina tatizo sana, kikubwa nataka kuwaambi kuweni makini kwani kuna wanajeshi wametumwa kuja kuukagua huo msitu munapo ishi”

“Lini?”

“Unauliza lini? Wanakuja sasa hivi na wapo njia na hii taarifa nimepewa na kiongozi wao”


 ITAENDELEA....


 

ILIPOISHIA....

Anna akamuomba Rahab kuipokea simu hiyo

“Haloo”

“Dokta Will hapa nazungumza”

“Dokta vipi, mbona umetupiga na simu ya mezani?”

“Hilo halina tatizo sana, kikubwa nataka kuwaambi kuweni makini kwani kuna wanajeshi wametumwa kuja kuukagua huo msitu munapo ishi”

“Lini?”

“Unauliza lini? Wanakuja sasa hivi na wapo njia na hii taarifa nimepewa na kiongozi wao”


ENDELEA....

“Sawa nimekupata dokta”

“Cha kufanya ni kufunga handaki na nendeni mbali na lilipo”

“Hapa tulipo, ndio tulikuwa tunatoka, tunakwenda kuv......”

Fetty akamziba mdomo Rahab kabla hajaimalizia sentensi yake

“Mnakwenda wapi?”

“Kununua nguo za kuvaa”

“Sawa”

Rahab akakata simu


“Unajua wewe mtoto ni mwehu” Fetty alizungumza huku amemtolea macho Rahab

“Uwehu wangu upo wapi?”

“Unataka kumwambia kuwa tunataka kwenda kuvamia, hujui mazugumzo yote yanasikiwa kwenye mitandao ya simu”

“Ahaa, nilipitiwa”

“Sio kupitiwa, uacha hilo domo lako kubwa”

“Jamani hebu acheni kurumbana, ehee tuambie kuna ishu gani?”


“Anasema kuwa kuna wanajeshi wanakuja kuukagua huu msitu, na wapo njiani”

“Ahaaaa sasa inakuwaje?” Anna alizungumza

“Dokta amesema tufunge handaki na kuondoka, twende mbali na hapa”

“Mpango umeshakufaa huu” Halima alizungumza

“Sasa, mbona Ni shidaaaa” Agnes alizungumza huku akikaa kwenye kiti


“Jamani, tusiakate tamaa, kikubwa ni kuamua lile tunalo lihitaji” Fetty alizungumza

“Sawa, tunaamua je akili na maarifa yetu yanafikiria kile tunnacho taka kukifanya au tunaamua tuu, mwisho wa siku tufaye madudu ambayo yatatucost kwenye maisha yetu” Agnes alizungumza


“Nyinyi mbona waoga sana, kama maji tumeyavulia nguo tunapaswa kuyaoga” Rahab alizungumza

“Wewe acha misemo yako iliyopitwa na wakati, maji ukiyavulia nguo, ukiona yanazingua si unavaa na kuondoka.Kwani ni lazima kuoga” Anna alizungumza.


“Sikieni,dili limesha kufa kwa maana hapa kila mmoja anazungumza lake.Wapo wanao taka kufanya na wanao kataa.Sasa tuwafikirie hawa nguruwe wanao kuja huku”

 Fetty alizungumza huku akiwatazama wezake, hakuna aliye zungumza zaidi ya kufikiria cha kuzungumza.


“Watu wanasema, mwanaume hakimbii nyumba yake, bali anapambana kuhakikisha analinda mali zake na familia yake.Sisi sasa hivi ni sawa sawa na wanaume.Hapa ndio kwetu, hapa ndio tunapo ishi kwa amani.Hakuna aliyekuwa na kwake zaidi ya kutegemea maisha ya kuliwa na wanaume na kumnufaisha mwehu mmoja” Fetty alizungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo na msimamo


“Tunatakiwa kupambana, tunatakiwa kujilinda, Hatupaswi kukimbia makazi yetu.Kikubwa ni kuanyanyuka na kwenda kupambana na hao wanao jaribu kupambana na sisi.Hatuna uchaguzi mwingine.Simama lady’s”


Fetty alizungumza na kuwaamsha wezake walio kaa,wakazunguka duara moja na mikono yao ya kulia wakaikutanisha pamoja, huku wakiwa wamekunja ngumi.


“Tunatoka watano, tunarudi watano”  Agnes alizungumza

“KWA UMOJA TUNAWEZA”

Walizungumza kwa pamoja, kiasha wakaachiana, Kila mmoja akahakikisha silaha take ipo sawa

“Jamani ninapendekeza, tuvae vinasa sauti kwa ajili ya kuwasiliana kwa pamoja” Agnes alizungumza

“Hapo umenena wangu” 


Anna alizungumza, akafungua kabati ambalo wameweka vinasa sauti, kila mmoja akachukua cha kwake na kukiweka kwenye masikio.Kila mmoja akahakikisha kinasa sauti chake kinafanya kazi


“Mnanisikia?” Halima alizungumza

“Ndio dada Halima” Rahab alijibu

“Fetty si ulivue hili jimwili” Agens alizungumza

“Nitapambana nalo hivyo hivyo”

“Mmmmm, haya big mama”


Wakacheka kwa pamoja na kutoka ndani ya pango,kila mmoja akaende njia yake huku wakiwa wameuzingira msitu wao.Kila mmoja akakaa kwenye nafasi ambayo angeweza kuona uingiaji wa wanajeshi hao waliotumwa kuja kufanya uchunguzi kwenye msitu.Kila mmoja akawa na hamu ya kutumia silaha yake, ambayo ameijaza risasi za kutosha.Masaa yakazidi kukatika pasipo kuona dalili yoyote ya majambazi kutokea kwenye msitu walio kuwepo.


“Jamani, mbona kimya? Agnes aliwauliza kupitia kinasa sauti chake

“Jua ndio linazama hivi” Rahbu alijibu

“Tuvuteni subira, kwa maana inaweza nao wamepanga kuvamia usiku” Fetty alizungumza

“Ahaa, jamani mimi njaa inaniuma” Anna alizungumza

“Wezako tunazungumza la maana wewe unazungumzia njaa hapa” Rahab alijibu


“Kwani kusema njaa, ndio nimekosea jamani?”

“Hujakosea ila ngoja tukamilishe hii kazi kwanza”

“Jamani kila mmoja awe makini kwenye pozi lake tunaumizana masikio” Halima alizungumza

“Powa bwana” Anna alizungumza

Masaa, yakazidi kukatika, hapakuwa na dalili yoyote ya mwanajeshi kutokea katika msitu wao.Hadi inatimu mida ya saa saa tano usiku hali ikaendela kuwa ya ukimya.


”Nimevumilia nimeshindwa, kama ni kuja waje tuu, Mimi ninakwenda kula jamani”

Anna alizungumza huku akisimama

“Hata mimi jamani” Rahab alizungumza

“Wewe si ulisema, tunazungumza ya maana subiri hao jamaa zako”

“Rahab na Anna tuachieni kelele” Agnes alizungumza

“Powa”


Anna akaanza safari ya kurudi lilipo handaki lao, hakuchukua muda sana akafanikiwa kufika kwenye handaki.Mazingira ya handaki akayakuta kama walivyo yaacha.Akafungua mfuniko wa handaki ambao ni wachuma na kushuka chini, huku bunduki yake ikiwa mkononi.Akawasha taa zote na kujirusha kwenye moja ya sofa huku akiwa amejichokea sana, Simu ya mezani ikamstua na taratibu akanyanyuka na kuifwata sehemu ilipo na akaipokea

“Hallo”

“Dokta Wille nazungumza”

 “Eheee”


“Ahaa samahani jamani, ile habari ilichanganywa na haukuwa msitu huo.Nilijaribu kuwatafuta kwenye simu zenu za mikononi na ila hazipatikani”

Anna akajizuia kuliachia tusi ambalo, ni languoni, akaendelea kuushika mkonga wa simu pasipo kuzungumza kitu chochote

“Anna unanisikia?”

“Umemaliza?”

“Samahani jamani”

Anna akairudisha simu sehemu alipo ichomoa, macho yake akayagandisha kwa sekunde kadhaa kwenye simu ya mezani kisha akaachia msunyo mkali


“Oya rudini mlale” Anna alizungumza

“Kuna nini?” Halima aliuliza

“Hakuna jipya, huyo mwehu anasema eti alikosea kutoa taarifa”

Kila mmoja akajikuta akiachia matusi mfululizo na misunyo mingi ya kuonekana kukasirishwa kwa kitendo cha dokta William kutoa taarifa iliyo ya uongo.Wakarudi wote wanne wakiwa wamechoka kiasi kwamba hakua aliye kuwa na hamu ya kuingia jikoni kupika.


“Oya huyu mzee tumfanye nini?” Rahab alizungumza

“Mkaushieni” Halima alizungumza

“Haki ya mama naapa, siku akija akisema, oohh sijui ninakazi, ohaa sijui nini, haki ya mama sifanyi”

 Agnes alizungunza kwa uchungu huku machozi yakimlenga lenga kwa hasira.Fetty akawa na kazi ya kuachia misunyo isiyo na idadi huku akiwa ametizama chini.


“Katika maisha yangu, sipendi kupotezewa muda kabisa”

Halima alizungumza kwa sauti nzito kidogo, iliyo jaa hasira hadi wezake wakamtazama

“Nina hamu na pombe, ninataka ninywe hasira iniishe” Fetty alizungumza

“Twende zetuni town” Anna alizungumza

“Kwani, saa hizi ni saa ngapi?” Rahab alizungumza

“Saa hizi ni saa sita” Anna alijubu

“Tuvaeni basi tuondoke”


Kila mmoja akaingia kwenye chumba chake na kuvaa jinzi iliyo mbana na kwa jinsi walivyo barikiwa maumbo mazuri, mtu huwezi kuamini kama wao ni watu hatari katika swala zima la maangamizi.Kila mmoja alipo hakikisha ametoka chikopa, wakatoka kwenye handaki na kuingia kwenye gari lao huku kila mmoja wao akiwa na bastola yake akiwa ameichomeka kwenye sehemu ambayo anaamini hakuna mtu anayweza kuiona.


Kama kawaida Agnea ndio dereva wao, hadi inatimu saa saba usiku wakawa wamesha fika kwenye ukumbu wa ‘MAISHA CLUB’.Wote kwa pamoja wakashuka kwenye gari huku Fetty akiwa amevalia kofia na kuziachia nywele zake ndefu zikikizunguka kichwa chake na kumfanya sura yake isionekane vuzuri.Wakatafuta meza isiyo na watu na kukaa,wakaagizia vinywaji na taratibu wakaendela kuburudika huku wakiwatazama tazama watu wanao cheza mziki


Uwepo wa kundi la wasichana wapya watano kwenye ukumbi, wenye mvuto sana kupita maelezo, ukaanza kuinua hisia za matamanio kwa mapendeshee waliopo kwenye ukumbi huu.Kila pedeshee mwenye pesa zake hakusita kupeleka ofa ya bia kwenye meza waliyokaa Rahab na wezake.


“Samani dada zangu, yule mzee pale ameniagiza nilete hivi vinywaji”

Muhudumu alizungumza huku akiweka chupa za bia zipatazo kumi,

“Sikia, toa uchafu wako.Mwambie hizo bia anywe yeye, na mimi nimalipia”

Fetty alijibu kwa dharahu huku akitoa nito kumi za elfu kumi na kuziweka kwenye kisahani cha muhudumu


“Fetty wacha bwana tuzipige” Anna alizungumza

“Nyamaza wewe, kwani sisi ni Malaya hadi tulipiwe bia.Wewe kaka hebu ondoka na uchafu wako kabla sijabadilisha maamuzi yakawa mengine”


Muhudumu akaanza kutoa chupa zake, moja baada ya nyingine na akapeleka jibu kwa bwana Turma ambaye ni meneja wa benki ya CNB.Akamwambia jinsi alivyo ambiwa

“Hembu nipe kikaratasi na kalamu” 


Bwana Turma alizungumza, muhudumu akampatia kile ambacho aliomba, wbwana Turma akamkabidhi kikaratasi muhudumu na akamuonyesha ampe dada aliye valia kofia.Muhudumu akamkabidhi Fetty kikaratasi.


“Mizee mingine bwana”

 Fetty alizungumza huku akisunya, akataka kukichana ila Anna akamzuia

“Hembu kisome bwana”

“Atakuwa kaandika ujinga”

“Huwezi jua kilicho andikwa” Agnes alizungumza

“Ahaaaa”


Fetty, akakifungua kikaratasi alicho pewa na muhudumu na kukifungua na kuanza kusoma maandishi yaliyo andikwa

{NAITWA TURMA, MIMI NI MENEJA WA BENK YA CBN, SEMA CHOCHOTE NITAKUPA MTOTO MZURI}

Fetty akawaonyesha wezake kikatasi alicho pewa, na kila aliye kisoma akajikuta akitabasamu


“Fetty tumtekeni” Rahab alizungumza

“Eti eheee”

“Ndio”

“Powa niachieni hiyo kazi”

Fetty alizungumza huku akiupeleka mkono wake kwenye mguu wake wa kushoto ulio vaa kiata kirefu aina ya Travota na taratibu akaanza kuichomoa bastola yake


             SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……12


Anna akaliona tukio la Fetty kuichomoa bastola yake

“Wee Fetty unataka kufanya nini?”

“Hakuna”

“Sio hakuna hebu acha ujinga, hiyo bastola watu wakiiona itakuwa ni shida bwana”

Fetty akairudisha bastola yake kwenye mguu wake, kisha akanyanyuka kwenye kiti alicho kikalia, akawaaga wezake na kuondoka kwa mwendo wa taratibu uliojaa madaha yalio wafanya watu wanaume wengi kumkodolea mimamcho, huku wengine wakianza kuimba wimbo


“Hamsini, hamsini, Mia”

Wakiendana na jinsi makalio ya Fetty yanavyokwenda.Fetty akafika kwenye meza ya bwana Turma na kukaa karibu yake huku sura yake akiwa ameiinamisha chini

“Habari yako mrembo?”

“Salama, tu”


“Mbona unaaibu kiasi hichi,”

“Hapana, sijazoea mazingira haya”

“Ahaa, tunaweza pia kuondoka”

“Tukaenda wapi?”

“Ni wewe tuu,sehemu nzuri ambayo mtoto mzuri kama wewe inaweza ikakufaa”

Bwana Turma alizungumza kwa madoido makubwa, hukua akijitutumua akiamini usiku wa leo utakuwa ni mzuri sana kwenye maisha yake kwa kulala na mtoto mzuri kama huyu


“Popote tu”

“Ahaa basi twende kwenye hotel moja hivi ya kifahari”

Bwana Turma akatoa simu yake kwenye mfuko wa koti la suti yake na kuminya namba fulani na kuiweka sikioni simu yake

“Habari yako Luka”

“Salama tuu”

“Hapo kwako kuna vyumba vizuri”

“Vipo mzee wangu”

“Basi niwekee chumba chenye hadhi ya uhakika”


“Sawa mzee”

Bwana Turma akakata simu

“Tunakwenda Hoteli gani?”

“Inaitwa White Sandas Hotel and Resort, naamini hapo utapapenda, pametulia sana, patakufaa wewe mtoto mzuri”

“Sawa, ngoja niwaage wenzangu”

“Sawa, kwani ni nani zako wale?”

“Ni ndugu zangu”

“Sawa mtoto mzuri”


Fetty akanyanyuka na kwenda walipo wezake, ambao wanaendelea kukata kinywaji kwa kwenda mbele

“Sikieni nyinyi, acheni kunywa, tangulineni kwenye hoteli ya White Sandas Hotel and Resort, Mnapajua?”

“Ndio” Anna akajibu

“Sasa, huyu mzee kaingia kumi na nane zangu cha msingi ni kuwa makini kama ni pombe bebeni mtakunywa baadaye”

“Powa tumekusoma kiongozi” Agnes alizungumza


Fetty akaondoka na kumfwata bwana Rurma alipo, wakatoka nje na kuelekea sehemu ya maegesho ya magari.Bwana Turma akaingia kwenye gari lake aina ya Range rover yenye, nyeusi na inavyoonekana ni mpya.Wakaingia ndani ya gari na dafari ikaanza, huku Fetty akikaa mikao ya hasara hasara kumdatisha Bwana Turma anayemtolea jicho la uchu.


“Hii gari yako umenunua shilingi ngapi?”

“Ahaaa, hii gari nimenunua milioni mia nne hamsini”

“Mbona pesa nyingi, hivyo baby?”

“Ahaa, hizo mbona pesa za madafu.Ninapesa nyingi zaidi ya hizo”


“Ahaaa, ulisema unafanya kazi wapi?”

“Mimi ni meneja wa benki ya CBN”

“Je nikitaka kufungua akaunti, nitaruhusiwa?”

“Kwa swala la akaunti usijali mpenzi wangu, asubuhi nikifika kazini nitakufungulia akaunti yako na kukuingizia milioni hamsini”


“Kweli baby?”

Fetty alizungumza huku akitabasamu

“Ndio mpezi wangu, nitakujengea nyumba kama utahitaji”

“Nitashukuru sana mpenzi wangu”

Kwa kumpagawisha zaidi Bwana Turma, Fetty akampiga busu zito la mdomo bwana Turma

“Baby ninaendesha gari”

Kutokana ni usiku hawakuchukua muda mwingi sana katika kufika hotelini,

“Baby shuka kwenye gari basi”

“Naona aibu, wewe nenda tuu alafu utanijulisha ni chumba gani upo”


“Sawa, nipe namba yako”

Fetty akampa namba ya simu bwana Turma

“Nitakupigia sasa hivi”

Bwana Turma akaondoka hadi kwenye chumba alicho wekewa na Lukas, mkurugenzi msaidizi wa hoteli hii ya kitalii, yenye hadhi ya kitalii.Fetty akatoa simu yake na kumpigia Rahab

“Mupo wapi nyinyi?”

“Sisi ndio tupo Mikocheni sasa hivi” Rahab alizungumza kwa sauti iliyo jaa pombe


“Ahaaa saa zote mlikuwa wapi?”

“Tulikuwa, tunamalizia bia zetu”

“Anaye endesha gari ni nani?”

“Anna”

“Amelewa?”

“Ana unaulizwa na Fetty umelewa?”

Rahab alizungumza huku, akimtazama Anna aliye kaa pembeni yake akiendesha gari


“Hapana”

“Anasema ajalewa”

“Mpe simu nizungumze naye”

Rahab akamuweka simu sikioni Anna

“Anna shosti fanya, mpango mrudi home”

“Kwani vipi?”

“Hao wenzako wamelewa sana, si unajua hali yetu”

“Sawa, ngoja nigeuze gari”

“Nakuomba sana, msirudi club”

“Sawa”


Fetty akakata simu yake, hakukaa sana simu yake ikaita, akapokea na kuisikia sauti ya bwana Turma.Akamuomba aingie chumba namba 27.Akamuelekeza Fetty sehemu ya chumba hicho kilipo na kukata simu,Fetty akashuka kwenye gari na kwenda sehemu alipo elekezwa

                                                                                                 “Anna mbona unageuza gari?”

Rahab aliuliza kwa sauti ya kelele

“Tunarudi home”

“Ahaa, twende bwana”

“Hatuwezi kwenda”

Agnes na Halima wao hawakuwa na usemi wowote, kila kinacho endelea kwao wanaona ni sawa, hii nikutokana na kunywa pombeni nyingi kupita maelezo.


“Kwa nini sasa hatuendi?”

“Rahab umelewa sana, twendeni home tukalale tu”

“Kweli bwana, tukalale”

 Agnes akaunga mkono na kumfanya Rahab kukubaliana na hali halisi.Kwa mwendo wa kasi wa gari yao hawakuchukua muda mwingi sana kufika kwenye handaki lao, kila mmoja akaingia kwenye chumba chake na kulala

                                                                         

Fetty akaingia kwenye chumba ambacho ameelekwezwa, akamkuta bwana Turma amevua nguo zake na kubaki na bukta huku akiwa amejilaza juu ya kitanda.Kwa ukubwa wa tumbo la bwana Turma ukamfanya Fetty kuangua kicheko cha chini chini

“Bab mbona unacheka?”

“Hapana mpenzi wangu, wale wezangu nilizungumza nao wakaniambia kuwa mmoja wao ametapika kwa pombe, hapa ndio ninacheka”

“Ahaa, ni mgeni kwenye pombe?”

“Hapana,ila leo amechanganya pombe”


Fetty alimdanganya bwana Turma ambaye, alisha agizia mzinga wa pombe kali.Fetty taratibu akavua nguo yake ya juu na kubaki na sidiria.Taratibu akakaa kitandani, bwana Turma akaanza kufakamia mipombe mingi akiamini mechi atakayoipiga itakuwa ni motomoto, itakayo mpagawisha Fetty


“Alafu hukuniambia jina lako”

“Ninaitwa Faudhia”

Fetty alimdanganya bwana Turma

“Unafanya kazi gani”

“Mimi nipo tuu nyumbani, wazazi wangu wanakaa Afrika kusini, ila kwa sasa wapo nyumbani likizo”

“Ahaa, wanafanya kazi gani?”

“Wao kule ni madaktari”

Kila anacho kizungumza Fetty ni uongo ulio kubuhu, ila unaendana na ukweli


“Baby benki kwenu mna pesa nyingi eheee?”

Fetty aliuliza kwa sauti ya mitego

“Ndio, tena kesho asubuhi inabidi niwahi ofisini kwani kunapesa nyingi sana inaletwa na wafanya biashara”

“Ni kiasi gani?”

“Ni zaidi ya Bilioni mbili, na ushee hivi”

“Ahaaa, zinaletwa saa ngapi?”

“Mida ya saa moja na nusu watakuwa tayari wameshazileta”

“Ahaaa, ila baby nikuombe kitu?”

“Kitu gani?’


“Mimi, asubuhi naomba niende na gari lako nyumbani kwa maana wazazi wangu ni wakali sana.Wakiniona na gari kama hiyo yako, hata nikiwaambia kuwa ni yarafiki yangu hawata nigombeza sana”

“Ahaaa, sawa.Nitampigia dereva wangu wa kazini aje kunichukua asubuhi”

“Sawa, asante baby”

“Usijali ni vitu vidogo sana kwangu”


Ikawa ni hatua moja aliyoifanya Fetty katika upelelezi wake, Fetty kutokana si mgeni na kazi ya kuuza mwili wake akaanza madoido ya kuzichezea chezea sehemu za siri za bwana Turma na kumfanaya aanze kuweweseka na kutoa vilio vya raha.Kwa jinsi ya utundu wa Fetty katika kuwapagawisha wanaume hususani kama bwana Turma mwenye maumbile madogo ya bunduki zao.Akadumbukiza bunduki ya bwana Turma kwenye mdomo wake na kuanza kuichezea kwa jinsi anavyoweza, bwana Turma akajikuta akipanda mlima Kilimanjaro bila kupenda.

“Baby asante, naomba tulale”


Bwana Turma alizungumza huku akihema kama bata mzinga, Ikawa ni nafuu kwa Fetty, bwana Turma akajigeuza upande wa pili wa kitanda na kulala.Fetty akayatupia macho yake kwenye saa ya ukutani, na kukuta ni saa kumi usiku.Hakuona haja ya kulala zaidi ya kusubiria muda usogee sogee amuamshe bwana Turma.


Saa kumi na mbili alfajiri akamuasha bwana Turma, ambaye amejawa na uchovu mwingi sana na wenge la pombe

“Baby nataka kuwahi nyumbani”

“Nyumbani”

“Ndio, nataka niwahi kabla hata baba na mama hawajaamka”

“Ahaa, hembu niletee hiyo suruali yangu hapo”


Fettya akashuka kitandani na kuichukua suruali ya bwana Turma, iliyoning’inizwa nyuma ya mlango kwenye kijisumari.Bwana Turma akaingiza mkono kwenye surua yake na kutoa kibunda cha pesa, akahesabu noti thelasini na tano za shilingi ellfu kumi kumi, ikiwa ni wasa na shilingi laki tatu na nusu.Akamkabidhi funguo ya gari Fetty

“Baby leo naomba, mida ya jioni urudi tena kwenye hii hoteli sawa”


“Sawa baby, kwani hata mimi sijaridhika”

“Nikitoka kazini nitakuja, tukamuane sana”

Bwana Turma alizungumza huku akipiga miyayo ya uchovu

“Sawa mume wangu”

“Gari hiyo tumia, siku nzima.Kwani mafuta yake ni yakutosha”

“Sawa baby, asante”

“Sawa, na nikija jioni nitakujia na kikadi chako cha benki, nitakufungulia akaunti kwa jina jengine, au wewe unasemaje?”

“Sawa mpenzi wangu”


Fetty akampiga busu bwana Turma na kuvaa nguo zake, kisha akarudia kumpiga busu la mdomo bwana Turma na kuzudi kumchangaya mzee wa watu.

“Yaani kwa ulivyo nifanya jana nipo tayari hata kukuoa wewe mtoto”

“Usijali tutalizungumza vizuri, jioni.Utanikuta humu ndani”

“Sawa nitalipia chumba kwa siku tano”

“Itakuwa vizuri”


Fetty akamuaga bwana Turma na kutoka ndani, moja kwa moja akaelekea sehemu lilipo gari la bwana Turma na kupanda na kuondoka kwa mwendo wa taratibu ili asistukiwe na watu waliopo kwenye hii hoteli.Safari ikaanza huku akiwahi foleni ya magari yanayokwenda mikoani asubuhi.Akafanikiwa kufika kwenye handaki lao, Akawakuta wezake wakiwa wamelala, akaanza kuwagongea mmoja baada ya mwengine


“Jamani, kuna dili la pesa ndefu” Fetty alizungumza

“Ya kiasi gani?”

“Bilioni zaidi ya mbili, pia ni benki tunayo kwenda kuvamia.Sasa ule mpango wa jana tunauhamishia benki hii”

“Benki gani?” Halima aliuliza

“CBN, kila kitu kipo katika mpango.Jamaa jana kanieleza kila kitu, hadi gari ameniachia”


“Wee....!!” Agnes alihamaki

“Ndio, ipo hapo nje”

Wakatoka na kuliona gari la kifahari alilo kuja nalo Fetty.Wakaanza kulikagua huku kila mmoja akiwa amejawa na furaha sana

“Sasa, kazi ni moja.Pesa pale inapelekwa mida ya saa mbili, sisi tunatakiwa kwenda pale mida ya saa tono, au sita”

“Etii eheee”

“Ndio”


Wakanywa chai ya nguvu kuyapa matumbo yao uhai, wakaanza kujiandaa kila mmoja akahakikisha anachukua silaha yake anayo weza kuitumia, wakachukua mifuko mikubwa, ilio tengenezwa kwa nguo kisha wakaingia kwenye gari na safari ikaanza


“Jamani, umakini ni muhimu sana, kulinda ni kitu kikubwa, Ndani ya benki wataingia wawili, nje watabaki watatu”

Fetty alitoa maelezo yaliyo sikilizwa na kila mmoja.Wakafanikiwa kufika nje ya benki na Fetty akalisimamisha gari kwa kasi na wote kwa pamoja wakashuka kwa haraka, na kuaanza kufyatua risasi hewani, zilizo wachanganya wananchi waliopo kwenye eneo la benki

                                                                                       

 Bwana Turma akafika benki, kwa kutumia gari ya benki moja kwa moja akaingia ofisini kwake na kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.Wafanya biashara watatu, wakafika benki kama walivyo weka ahadi yao juzi.Wakakutana na bwana Turma na kuhifadhi kiasi chao kikubwa cha pesa walicho kuja nacho kisha wakaondoka.Fedha zikahifadhiwa kwenye chumba maalumu, ambapo kuna pesa nyingine.Akarudi ofisini kwake, mfanyakazi wake akamuarifu kuna mgeni amekuja kumtembelea.Akaingia kijana aliye valia nguo za kipolisi huku mkononi mwake akiwa ameshika begi, bwana Turma akatabasamu baada ya kumuona kijana huyo akiwa amevalia mavazi ya polisi.


“EDDY, UMEKUWA ASKARI?”

 “HAPANA MJOMBA”

“ILA?”

“AHAA VIJIMAMBO TU,”

“ILA NINASIKIA UNATAFUTWA NA POLISI”

“NDIO, ILA MJOMBA NINAOMBA MSAADA WAKO”

“MSAADA GANI?”

“KUNA HAYA MADINI, YANADHAMANI KUBWA SANA.NINAOMBA NIWAUZIE NYINYI KAMA BENKI NA PESA YANGU MUIWEKE HUMU NDANI, IPO SIKU MUNGU AKIBARIKI, MIMI AU MWANGU ANAWEZA AKASAIDIWA NA HIYO PESA”


Bwana Turma akamtazama Eddy kwa umakini kisha akamuomba Eddy amuonyeshe hayo madini, Eddy akaweka begi juu ya meza na kulifungua na kumfaya bwana Turma kushangaa.


“UMEYATOA WAPI?”

“HII NI MALI YA MAMA, NINAKUOMBA SANA UNIWEKEE”

“WEWE ULIKUWA UNAYAUZA KWA KIASI GANI?”

“BILIONI MOJA NA NUSU SHILINGI”

“MBONA NYINGI SANA”

“HATA HAYA MADINI, YANADHAMANI KUBWA SANA.NIKISEMA NIUZE KWA MASONARA SI CHINI YA BILIONI TANO”

“SAWA MJOMBA NIMEKUELEWA, NGOJA NIKAWAITE WAHASIBU NA WANASHERIA WA BENKI TUWEZ KUFANYA BIASHARA”

“SAWA MJOMBA”    


Bwana Turma akatoka na kwenda kwenye ofisi ya muhasibu, akakubukua kwamba hajamfungulia kipenzi chake akauti kama alivyo muhaidi.Akaanza kumpa maelekezo muhasibu wake juu ya ufunguaji wa akaunti anayo itaka

“Meneje hizo pesa nitoe za benki au zako binafsi?”

“Toa za benki mtu akikuuliza, muambia aje kwangu”

Bwana Turma akiwa anasubiria zoezi la kufungiliwa akauti, gafla milio mingi ya risasi ikaanza kusikika ikitokea nje na kuanza kuwachanganya bwana Turma na muhasibu wake

 

 ITAENDELEA....





ILIPOISHIA....

“Meneja hizo pesa nitoe za benki au zako binafsi?”

“Toa za benki mtu akikuuliza, muambia aje kwangu”

Bwana Turma akiwa anasubiria zoezi la kufungiliwa akauti, gafla milio mingi ya risasi ikaanza

kusikika ikitokea nje na kuanza kuwachanganya bwana Turma na muhasibu wake



ENDELEA......

Kitendo cha wasichana, makatili kuiingilia bank ya CNB, na kuwazalilisha wananchi walio kuwemo ndani ya benki kwa kuwatoa nje uchi kinazidi kuiumiza serrikali.Isitoshe inamuwia ugumu Bwana Turma, na akashikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano maalumu kwani gari lake la thamani, limehusika katika matumizi ya uvamizi wa Benki.


Dickson anatoa nje ya kibanda chake, huku akiwa na wasiwasi mwingi akiwatazama askari wawili wanaokuja kwenye kibanda chake

“Habari yako kaka?”

Askari mmoja alimsalimia Dickson

“Salama tuu mambo vipi?”


Dickson alizungumza kwa kujikaza tuu, kuuficha wasiwasi wake kwa maana msichana ambaye ni Rahab aliye muacha ndani anaonekana hana masihara kabisa katika matumizi ya silaha


“Hukuona, msichana aliye vaa akipita katika maeneo haya?”

“Ahaaa kusema kweli, sijamuona kwa maana hizi bunduki kwa jinsi zilivyokuwa zikinguruma huko nje sikudhubutu hata kuitoa miguu yangu”


Askari wakamtzama kwa umakini Dickson, ambaye anazungumza kwa kubabaika

“ Basi tunakuomba ufunge duka lako”

“Sawa”

Askari wakaanza kuondoka na kurudi katika eneo walipo wazao, Dickson akarudi ndani huku jasho jingi lkimwagika mithili ya maji.

“Waameniambia nifunge”


Dickson alimsemesha Rahab ambaye kichwa chake amekiinamisha kwenye ukuta huku sura yake ikitazama juu.

“Dada, dada.Wamesema nifunge duka langu”

Rahab hakujibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya, huku akimtazama Dickson jinsi sura yake inavyo mwaga jasho jingi

“Powa”

Rahab alijibu kwa kifupi, na kuzidi kumchanganya Dickson

“U...takaa humu ndani?”

“Ndio wewe funga”

“Mmmm”


Dickson akabaki akiwa anashangaa shangaa, Rahab akainyanyua bastola yake na kumuwekea Dickson ya kichwa, mwili mzima wa Dickson ukawa kama umepigwa na shoti ya umeme, taratibu suruali yake ikaanza kutengeneza mchoro sehemua ya zipu, kwani woga umemfanya hadi ameshindwa kuzuia haja ndogo

“Huwa sipendi, nizungumze mara mbili mbili.Potea”


Rahab alizungumza huku sura yake akiwa ameikunja, na anaonekana kuwa na hasira kali.Kwa hahara Dickson akatoka nje ya kibanda chake, na kuaanza kufunga geti la kaduka kake hata baiskeli anazo zitengeneza hakukumbuka kuziingiza ndani.Kwa kuchanganyikiwa akajikuta akitembea asijue ni wapi anaelekea


Wote wanne wakiwa na bunduki zao mikononi, wakawa wanaitazama njia ambayo ni yakuingilia kwenye eneo lao la handaki.

“Tutawanyike wawili wawili”


Fetty alizungumza huku akiikoki bunduki yake, Anna akamfwata Fetty huku Halima na Agnes wakiwa wamesimama sehemu moja.Wakatazamana kwa muda pasipo mtu yoyote kuzungumza neno , kisha wakaanza kukimbia mtuni, wakiwa wameganawana kila watu wawili sehemu yao.Fetty na Anna walielekea magharibi mwa msitu wao, huku Agnes na Halima wakielekea Mashariki mwa msitu wao.


Askari wakiongozwa na mbwa wao, walio fundishwa mafunzo maalumu ya kunusa kila sehemu ambayo amepita mtu ambaye askari wanamuhitaji, ndivyo walizidi kuendelea kuingia msituni wakiwa na bunduki zao.Huku kila mmoja akiwa na hasira kali juu, ya maauaji yaliyo tokea siku chache zilizo pita juu ya wezao walio uwawa kwenye kituo cha gesi kwa mlipuko mkali.Amri mmoja iliyo tolewa na mkuu wa jeshi la polisi Bwana Gudluck Nyangoi ni kwamba wahakikishe wanawatia nguvuni ili wahukumiwe kifungo kikali kitakacho ishangaza dunia


Askari wakiongozwa na Kamishina Msaidizi wa Polisi(ACP) Ngurumo, wanaendelea kuuzingira msitu huku wakiwa na imani ya kufanikiwa na abushi yao wanayo kwenda kuifanya kwenye msitu unao sadikika ndipo walipo ingia majambazi kipindi wakitokea kufanya tukioa benki, na maelezo haya yalitolewa na msamaria mwema ambaye, gari lao lilisimamisha kipindi askari wa usalama barabarani walipokuwa wakifanya uchunguzi kwa kila gari ambalo lilikuwa likikatiza katika barabara kuu ya kuelekea mikoa ya Tanga na Arusha


Wakiwa katikati ya msitu, mbwa wao wakaanza kubweka kwa sauti ya juu, na kuzidi kuwastua askari na kuamini kuna jamba ambalo lipo kwenye eneo ambalo wamefika.

“Waachie mbwa”


ACP Ngurumo aliwaamrisha askari sita walio washika mbwa wao, Mbwa wakaanza kuelekea katika maeneo walipo Fetty na Anna, ambao bunduki zao wameziweka tayari kwa kila kitu. Kwa kutumia bunduki zao zenye lensi ya kuvuta mtu kwa ukaribu sana, Fetty akawashuhudia mbwa wakiwakaribia katika eneo walilo jificha huku kwa nyuma kukiwa na kundi la askari wapatao sita, wakiwa na bunduki mikononi mwao.Anna akaishika bunduki yake, kabla hajafyatu risasi Fetty akamzuia

“Ngoja nikuonyeshe mchezo, wasikumalizie risasi zako”

Fetty alizungumza huku akikichomo kisu chake, kikali na kirefu sana mfukoni,

“Anna nilinde”

“Powa”


Fetty akaanza kutambaa kwa haraka kuuelekea mbwa wanapo tokea na na askari wao, akajibanza kwenye mti mkubwa ambao ndio njia ambayo mbwa na askari ndio wanatokea, Macho ya Anna yakawa na kazi ya kuwatazama askari wanao kimbia kwa kasi wakiwa nyuma ya mbwa wao, Fetty akachomoa kisu kingine kinacho fanana na kisu alicho kishika mkono wake wa kulia, Akashusha pumzi kidogo kisha akachungulia kidogo sehemu wanapo tokea mbwa na kuwaona wakiwa wamebakisha hatua chache kutoa sehemu alipo jificha

“It’s My time now”(ni wakati wangu sasa)


Fetty alizungumza huku akishusha pumzi nyingi, kwa haraka akachuchumaa chini, kitendo cha mbwa wa kwanza kujitokeza sura yake usawa wa Fetty, ikawa ndio muda wa mbwa huyo mwenye kasi kupita wezake, kukumbana na kisu cha koo na kumfanya kutoa ukelele mmoja tuu, mithili ya panya aliye banwa na kitu kizito na kutulia kimya.Akaskari wakasimama baada ya kuona mbwa wa kwanza akiwa amepotea gafla, kasi ya mbwa wengine watano ikaanza kupungua na kuwa ya kusita sita baada ya kumuona mwenzao akiwa ametupwa katika njia waliyo kusudia kupita, huku akiwatokwa na damu nyingi.


Askari kwa kuchanganyikiwa wakaanza kufyatua risasi pasipo kuwa na mpangilio maalumu, kwani hawakujua ni wapi alipo jifich mtu aliye sababisha kifo cha mbwa huyo, ambaye anaaminika sana kupita mbwa wote.Fetty akaachia tabasamu pana, huku akiwa amejibanza kwenye mti aliopo wenye unene kiasi, unao msaidia kutokuweza kuonekana, wala risasi kumfikia alipo.


“Nyinyi kuna kitu gani kinacho enelea huko.OVER”

Sauti ya Kamishina Msaidizi wa Polisi(ACP) bwana Ngorumo ilisikika kupitia simu ya upepo, hii ni baada ya kusikia milio ya risasi nyingi zikimiminika.

“Wapo, huku mkuu, Over”

Askari mmoja alizuingumza huku akiendelea kufyatua fyatua risasi ovyo

“Tunakuja, Over”


Macho ya Anna yakakutanana na macho ya Fetty ambaye, akaendelea kumkonyeza asifanye kitu chochote cha kijinga.Anna akazidi kupatwa na wasiwasi kwani akujua ni kitu gani kinachompa ujasiri Fetty kuendelea kung’ang’ania nyuma ya mti alio uegemea


Fetty akatupa visu vyake chini na kuchomoa bastola mbili kwenye viatu vyake, ambazo zimejaa risasi za kutosha, kwa ishara ya mmdomo pasipo kuzungumza kwa sautia, Anna akamtaarifu Fetty kwamba askari wameongezeka katika eneo walilopo.Askari walioongezeka kwenye eneo walipo wezao, bila hata ya kuuliza ni wapi walipo majambazi, wao wakaanza kufyatua risasi zao wakishambulia kile eneo


“Zima motoo”

ACP Ngurumo alizungumza kwa sauti ya juu, baada ya kuona risasi zao zikiendelea kumiminika pasipo kuwa na mafanikio yoyote ya kuua majambazi

“AK47 tangulia mbele”


Aliwaamrisha askari wenyebunduki aina ya AK47 kupita mbele, huku wengine wanye bunduki aina ya SMG wakiwa wamebaki nyuma ya wezao huku wamelala chini.Askari wapatao nane wenye bunduki aina za AK47, wakaanza kutembea kwa kunyata wakielekea ulipo mti ambao pembeni kuna mbwa wao aliye lala chini, tayari akiwa amekata roho.



Kwa kutumia ishara ya vidole Fetty akaanza kunyanyua kimoja, kikafwata cha pili, hadi cha tatu anakinyanyua, Anna akaanza kufyatua risasi mfululizo kwa askari wote nane wenye bunduki aina ya AK47, na hakuna hata mmoja aliye baki akiwa amesimama kwani, risasi zote alizo zifyatua kwa kutumi bunduki yake aina ya ‘M8AI’, zilitua vichwani mwa askari hao.


Askari walio lala chini wakaanza kuchanganyikiwa kwa shambulizi walilo fanyiwa wezao, wakaanza kufyatua risasi kuelekea sehemu yenye jiwe kubwa alipo lala Anna, na kusahau kuuangalia mti ambao askari nane walio uwawa walikuwa wakinyata,Fetty kwa kutumia bastola zake mbili, moja ikiwa aina ya ‘COLT 1911’ huku nyingine aina ya ‘DESERT EAGLE’ akaanza kuwashambulia askari kwa nyuma, walio kuwa wameelekea upande alipo jificha Anna.Kila mmoja akaanza kuchanganyikiwa kwani kila alipojaribu kufyatua risasi walipo majambazi ndivyo alivyo jikuta akianguka chini na kupoteza maisha yake hapo hapo.


Hadi shambulizi linazima, akabaki Kamishina Msaidizi wa Polisi(ACP) Ngurumo akiwa amelala chini akiwashuhudia maiti za askari wake wakiwa wamelala chini, wakivunjwa na damu nyingi mwili mzima.Fetty akapiga hatua za umakini hadi sehemu alipo lalaa ACP Ngurumo, na kumuwekea risasi ya kichwa

“Fetty”


Anna aliita kwa sauti ya juu, na kumfanya Fetty kutazama sehemu alipo Anna na kumuona akiwa amesimama huku akiwa anavujwa na damu za paja lake la kushoto, ikiashiria katika risasi zote zilizo fyatuliwa na askari hao kuna iliyo mpiga kwenye mguu wake


Agnes na Halima waliendelea kuzisikia kelele za risasi nyingi, ila hawakudhubutu kunyanyuka sehemu walipo kwenda kwani hawakujua ni wapi risasi hizo zinapo tokea.Kila wanapojaribu kutazama sehemu zote za msitu wanaona ukimya mwingi baada ya risasi nyingi zilizo fyatuliwa zaidi ya nusu saa


“Mbona mapigo yangu ya moyo yanakwenda kasi”

Halima alizungumza huku akinyanyua kichwa chake akitazama mbele yao, pasipo kuona kitu chochote

”Acha uoga chost” Agnes alijibu

“Sio woga, ila mapigo yanakwenda mbio, haijawahi kutokea siku hata moja”

“Hembu ngoj.......”


“WEKENI SALAHA ZETU CHINI, WANAHARAMU NYINYI”

Kabla hata Agnes hajamalizia sentesi yake sauti ya ukali ikawamrisha nyuma yao, wakageuka kwa haraka na kukutana na kundi la askari wapatao kumi wenye bunduki mikononi mwao, huku bunduki zao zote zikwa zimeelekea upande wao, na sura za askari hawa zimejaa mikunjano inayo ashiria hasira kali walizo nazo....



SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……14


.....Taratibu Halima na Agnes wakaweka silaha zao chini, kila mmoja akanyoosha mikono juu, kutokana na amri waliyo pewa na askari hao wenye hasira kali kupita maelezo.Askari wawili wakawasogelea Agnes na Halima na kuwafunga pingu, za mikononi


Katika maisha yao Halima na Agnes hawakutarajia kama ipo siku watakuja kukamatwa kizembe kama hivi walivyo kamatwa.Askari wakamchukua Halima na Agnes na kuwapeleka kwenye magari yao walipo yaacha, huku wakijawa na furaha sana, juu ya kuwakama wasichana makatili walio itingisha nchi kiasi kwamba viongozi wa ngazi za juu kila mmoja alihisi kuchanganyikiwa kwa matukio makubwa yaliyo tokea katika wiki mmoja mfululizo.Moja likiwa ni tukio la askari wengi kuuawa katika kituo cha gesi huku benki ya biashara kuvamiwa na pesa nyingi kuuawa


Hasira nyingi ikazidi kumpanda Fetty, baada ya kumuona Anna akivujwa na damu kwenye paja lake, Fetty akaishika vizuri bastola yake na kunyanyua kwa nguvu (ACP) Ngurumo na kumpiga kabali kwa nyuma


“Unaona washenzi wako walicho kifanya kwa rafiki yangu”

Fetty alizungumza huku akiendelea kuishika bastola yake akiikandamiza kichwani mwa ACP Ngurumo, ambaye mwili mzima unamtetemeka kwa woga, japo amefanya kazi kwa kipindi kirefu ila hajawahi kukutana na wanawake makatili kama Fetty na Anna.Anna taratibu akaanza kujikongoja hadi sehemu walipo simama Fetty na ACP Ngurumo

“Chukua mkanda ujifunge kwenye paja damu zisiendelee kukumwagika”


Fetty alimuambia Anna naye akafanya kama alivyo ambiwa, akauchomo amkanda mmoja wa askari aliye fariki na kuufunga kwenye paja, akiwa anaendelea kujifunga simu ya upepo ya ACP Ngurumo ikaanza kukoroma ikiashiria kuna simu inaanza kuingia

“Ipokee, na ole wako uropoke nauchangua ubongo wako”

Fetty alizungumza huku akiichomoa simu ya upepo ya ACP Ngrurumo aliyo ichomeka kiunoni

“115 Kikosi, OVER”


Sauti kutoka upande wa pili kwenye simu ya upepo ilisikika

“Ninakusikia Over” ACP Ngurumo alijibu

“Mkuu tumewakamata majambazi wawili, Over”

ACP Ngurumo akanyamaza kimya, huku akiwatazama Anna na Fetty, ambao wanaonekana kustushwa na taarifa ya wezao kukamatwa

“Waulize wapo wapi?”

Fetty alizungumza kwa sauti ya chini sana, ambayo si rahisi kwa mtu aliyepo upande wa pili wa simu kuweza kuisikia


“Mupo wapi. Over?”

“Tupo kwenye point B, Over”

“Nimewapa” Simu ya upepe ikakatwa

“Ongoza njia hadi kwenye point B yenu”

“Fetty, mimi sinto weza kwenda mbele”

Anna alizungumza huku machozi yakimlenga lenga kwani maumivu anayo yapata ni makali sana kupita maelezo

“Jikaze mpenzi”

“Siwezi Fetty, amini kwa kitu ninacho kuambia”


Fetty akamtazama ACP Ngurumo kwa macho makali, gafla Fetty akafyatua risasi moja iliyo tua kwenye paja la ACP Ngurumo na kumfanya atoe ukelele mkali ulioambata na kilio cha maumivu na kuanguka chini, Fetty akataka kufyatua risasi nyingine kwenye mwili wa ACP Ngurumo ila Anna akamkataza

“Usimuue, tafadhali” Anna alizungumza huku machozi yakimlenga lenga

“Anafaida gani, jiangalie wewe sasa hivi unavyo mwagikwa na machozi ya maumivu laiti ingekuwa sio wao, sasa hivi ungekuwa unalia?”


Fetty alizungumza huku machozi ya hasira yakimwagika

“Fetty najua kwamba, unaupendo na mimi na sisi sote tunapendana ila tafadhali usimue huyo baba, tambua yeye anaweza kuwa na mke na watoto wadogo sana, wanaoweza kuhitaji maleli ya baba na mama”


“Anna acha ujinga, wewe upo tayari kwenda kufia segerea?”

“Hata kama sipo tayari kwa hilo ila kwa......”

Fetty akajikuta akifya risasi mbili zilizo tua kifuani mwa ACP Ngurumo na kumfanya apoteze maisha hapo hapo,

“Mbona sasa umemua?”

Fetty alimuuliza Anna

“Alitaka kukupiga risasi”

Anna alizungumza huku akimtazama ACP Ngurumo aliyekuwa ameishika, bastola yake kwenye mkono wa kushoto


Makao makuu ya jeshi la polisi ikazidi kuwaongezea nguvu askari walipo, msituni wanao endelea kuwasaka majambazi sugu walio fanya tukio la kulidhalilisha jeshi hilo la polisi, Askari wapatao arobaini wa kikosi maalumu, wakaingia kwenye msitu wa Maliga pasipo wezao kufahamu, uwepo wapo.Wakafanikiwa kuuzingira msitu mzima ambao katikati wapo wezao wakiendela kuwasaka wasichana watano.Wakazidi kuingia ndani ya msitu na kufanikiwa kufika katika enoa walilo simama wasicha wawili wakiwa wamesimama huku kila mmoja akiwa na bunduki yake mkononi


Kitendo cha kufumba na kufumbua Fetty na Anna wakajikuta wakiwa wamezingirwa na kundi kubwa la askari walio valia nguo za jeshi huku sura zao zikiwa zimefuchorwa chorwa na rangi nyeusi.

“Anna, tumekwisha”


Fetty alizungumza huku macho yake yakiwatazama askari wanao zidi kuwasogelea kwa umakini, machozi yakazidi kumwagika Anna kwani hakutaraijia kama naye ipo siku atakuja kukamatwa na polisi, tartibu Fetty na Anna wakapiga magoti na kujisalimisha mikononi mwa askari

****


Kila Samson anavyo jaribu, kujilaza kwenye kitandani, anajikuta akikosa usingizi kutokana na kumuwaza msichana aliye mfungia ofisini mwake.Akaichukua simu yake aina ya nokia tochi, akaiminya kitufe kilicho kifanya kioo kidogo cha simu hiyo kuwaka mwanga hafifu, saa iliyopo kwenye simu yake ikamuonyesha kwamba muda wa sasa ni saa sita na dakika mbili usiku.Taratibu akajiinua kitandani mwake na kuutazama mlango wake alio jaa nguo nyingi chafu alizi zinging’iniza kwenye misumari iliyopo nyuma ya mlango wake


Akatoka kwenye neti yake na kusimama pembeni ya kitanda chake na kuanza kujivuta vuta viungo vyake, kisha akaichukua suruali mmoja aina ya jinzi na kuivaa mwilini mwake, akachukua tisheti yake na kuivaa, akainama na kutoa viatu chini ya mvungu wa kitanda chake na kuvivaa

“Potelea pote”


Samson alizungumza mwenyewe na kuichukua, baiskeli yake aina ya ‘Oscar Chopa’ na kufungua mlangoa wa chumbani kwake na kutoka nje, akashusha pumzi zake na kuangalia angani na kukuta mawingu mengi yamejikusanya kwa pamoja ikiashiria muda wowote mvua inaweza kunyesha, akapanda kwenye baiskeli yake na taratibu akaanza kuiendesha huku taa ndogo ya baiskeli hiyo ikimsaidia kuyakwepa mawe na vishimo vidogo vidogo vilivyopo barabarani.



kila jinsi anavyozidi kuongeza mwendo wa baiskeli yake ndivyo jinsi anavyozidi kuikaribia sehemu anayo fanya kazi, mwendo wa dakika ishirini barabarani, ukamsaidia kufia kwenye kibanda chake.Cha kumshukuru Mungu baiskeli zake zote alizo ziacha nje amezikuta, akashuka kwenye baskeli yake, akatazama pande zote za eneo kilipo kiduka chake hakuona dalili yoyote ya kuwa na mtu wa ina yoyote.


Akajikoholesha kidogo na kuitoa funguo ya geti la kibanda chake na kufungua, mlango, akaingia ndani na ngumi kali ikatua kwenye uso wake na kujikuta akianguka chini

“Ni mimi”

Alizungumza huku akimtazama Rahab aliye shika bastola, akimnyooshea


“Samahani”

Rahab alizungumza huku akiirudisha bastola yake kiunoni, kwani tayari amevaa nguo zake tarari alizo kuwa amezivua kipindi akikimbilia ndani ya kibanda hicho walipo toka kuvamia benki

“Nimekuja kukuchukua” Samso alizungumza

“Kwani, huko nje hakuna watu?” Rahab alizungumza

“Ndio, ila ngoja niingize baiskeli zangu”

“Fanya fasta basi”


Samson akatoka nje huku akiishika shika pua yake iliyo jaa maumivu ya kupigwa ngumi na Rahab, Samson akaingiza baiskeli ya kwanza na kutoka nje akiwa ameishika baiskeli ya pili akitaka kuingia ndani, gafla breki za gari aina ya Defender yenye askari wa kikosi cha F.F.U wapatao sita wakashuka kwenye gari kwa haraka huku wakiwa na bunduki na kunza kumfwata Samson sehemu alipo simama....


ITAENDELEA... 




ILIPOISHIA

“Fanya fasta basi”

Samson akatoka nje huku akiishika shika pua yake iliyo jaa maumivu ya kupigwa ngumi na Rahab, Samson akaingiza baiskeli ya kwanza na kutoka nje akiwa ameishika baiskeli ya pili akitaka kuingia ndani, gafla breki za gari aina ya Defender yenye askari wa kikosi

cha F.F.U wapatao sita wakashuka kwenye gari kwa haraka huku wakiwa na bunduki na kunza kumfwata Samson sehemu alipo simama



ENDELEA

“Unafanya nini hapo?”

Askari mmoja alizungumza kwa sauti ya ukali na kumfanya Samson kuanza kutetemeka mwili mzima

“Husikii au?” askari aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ukali


“Ni..ninaingiza baiskeli zangu ndani”

“Wewe kama nani?”

“Mimi, ni mmiliki wa hapa, mchana nilikimbia kutokana na tukio la majambazi”

Mazungumzo, yote yanavyo endelea nje Rahab anayasikiliza kwa umakini wa hali ya juu, huku bastola yake ikiwa mkononi mwake

“Mkuu tukague ndani”

Ombi la askari huyu mwenye alama ya ‘V’ kwenye bega moja, likamfanya Samson kubaki akiwa anaduwaa, ila akajikaza asiuonyeshe mstuko wake kwani hakujua kitatokea nini baada ya askari hao kuingia ndani ya duka lake na kumkuta Rahab

“Kuna vurugu, maeneo ya Sinza kwa Remy, OVER”

Ilisikika sauti kupitia redio ya upepo aliyo ishika mkuu wao na kusababisha, kuto kulijibu ombi la asakri wake

“Tunakuja Over”


Alijibu, huku akiiwatazama askari wake na wote kwa pamoja wakarudi kwa haraka kwenye gari lao na kuondoka kwa kasi kubwa.Sammso akashusha pumzi nyingi, kwa haraka akaanza kuingiza baiskeli zake zote

“Tuondoke, tayari nimesha maliza”

Samson alimuambi Rahab na wote wakatoka nje kwa umakini, huku wakichunguza kila eneo la nje.Samson akapanda kwenye baiskeli yake

“Panda twende”

Rahab akaitazama baiskeli ya Samson kwa umakini,

“Siwezi kukivunja kiti chake”

“Wewe panda twende kwani kikivunjika tutajua mbele ya safari, isije hawa jamaa wakarudi na kunikuta tupo pamoja hapa sijui itakuwaje”

“Mmmm!!”


Rahab akapanda kwenye baiskeli na taratibu Samson akaanza kubadilisha gia moja baada ya nyingine zilizopo kwenye baiskeli yake kutoka gia laini kuelekea gia ngumu, na jinsi anavyozidi kuendesha baiskeli ndivyo mwendo wa baiskeli yake inavyozidi kuongezeka.Ndani ya dakika kumi wakawa wamefika nyumbani kwa Samson, wakaingia ndani kisiri pasipo mtu yoyote kuwaona


Ukimya ukatawala kati yao, na hakuna mtu aliye msemesha mwenzake kwa wakati huu, alicho kifanya Rahab, akavua viatu vyake na kupanda kitandani na kumfanya Samson kuendela kusimama akimtazama Rahab jinsi alivo jilaza chali akitazama paa la chumba chake


“Panda ulale”

Rahab alizungumza huku akimtazama Samson usoni

“Ahaa, mimi nitalala hapa chini”

“Wewe vipi, kinacho kuogopesha wewe ni nini?”

“Siogopi”

“Sasa kinacho kubabaisha ni nini, hebu acha ufala panda kitandani kwako ulale, ila onyo lala usiniguse mwili wangu”

“Mmmmm”

“Guna, tu”

“Ndio maana ninakuambia kwamba nitalala hapa chini”

“Sijawai kuona dume zima likiwa linaogopa kulala na mwanamke kitanda kimoja”


Samson akamtazama Rahab kwa umakini kisha akapanda juu ya kitanda na kuchukua mito miwili na kutengeneza mpaka kati yao ambao hakuna mtu ambeye angeweza kumgusa mwengine, Samson taratibu akajikuta akiaanza kutawaliwa na hisia za mapenzi juu ya Rahab ambaye anaonekana kawa si mtu wa masihara hata kidogo.Samson akauingiza mkono wake mmoja chini ya mto, na taratibu akanza kuupeleka katika eneo alilo lala Rahab.Akafanikiwa kuufikisha mkono wake alipo lala Rahab, akamminya kwenye maeneo ya mbavu , ila Rahab akatulia kimya na kujifanya kama amelala, Samson akarudia tena kumminya Rahab eneo la mbavu na Rahab hakuonyesha mtikisiko wowote


“Kitu kimelinki”

Samson alizungumza kimoyo moyo, huku usoni mwake akiachia tabasamu pana lililojaa uchu mkali wa mapenzi, akajigeuza na kujilaza kiubavu, taratibu mkono wake mmoja ukaanza kupandisha hadi kwenye chuchu ya Rahab, hata kabla Samson hajaukandamiza mkono wake vizuri kwenye chuchu ya Rahab, gafla macho yake yakakutana yakitazamana na jicho la bastola, aliyoishika Rahab kwa umakini

**************

Vyomo vingi vya habari ndani na nje ya nchi ya Tanzania vimepambwa na taarifa juu ya kukamatwa kwa majambazi sugu walio walaza askari wengi macho kwa kazi moja ya kuwatafuta popote walipo, usiku na mchana.Sura za Fetty, Anna, Halima na Agnes zimepamba magazeti mengi ikiwemo hata magazeti ya udaku,askari walio fanikisha kukamatwa kwa majambazi hawa, ikawa ni moja ya ofa kubwa katika maisha yao kwa kila mmoja kupandishwa cheo kimoja kutoka sehemu alipo hadi sehemu ambayo mkuu wa majeshi Raisi wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania alihisi inastahili kwao.


Japo kuna misiba mingi ya askari walio kufa katika oparesheni kimbunga ya kuwavamia majambazi hao, familia za askari walio kufa zikapewa kiasi cha shilingi milioni mia moja, pamoja na bima za matibabu kwa wale askari wote walio na tattoo chini ya umri wa miaka kumi na nane


Ila haikuwa furaha kwa dokta Wiliam ambaye yupo nchini mwao kwa ajili ya likizo ya muda mrefu, jambo ambalo linazidi kumuumiza kichwa ni kuhusu mahali alipo jificha Rahab kwani hakuwepo katika orodha ya walio kamatwa, akaitoa simu yake ya mkononi na kuingiza namba za rais wa Tanzania, kabla hajapiga akaanza kujiuliza mswali yasiyo na majibu kichwani mwake


“Nikimpigia ninamuambia nini, je akiniuliza ilikuwaje nikawaagiza kwenye tukio hilo walilo lifanya itakuwaje?”

Dokta William alijiuliza swali ambalo akabaki akiitazama namba ya rais, taratibu akakishusha kidole gumba cha mkono wa kulia, ulio ishika simu yake na kuiminya batani yenye alama ya kijani, inayo ashiria kuwa ndio batani ya kupiga simu, akaiweka sikioni simu yake huku mwili ukimtetemeka kiasi kwamba akabaki akiwa anameza mafumba ya mate mengi, ndani ya sekunde kadhaa sauti nyororo kutoka upande wa pili wa simu ukaanza kusikika

“MTUMIAJI WA SIMU UNAYE MPIGIA, ANAONGEA NA SIMU NYINGINE. TAFADHALI SUBIRI AU KATA SIMU NA UPIGE TENA”


Dokta William akakata simu yake na kushusha pumzi nyingi huku akiitazama, akaiingiza simu yake mfukoni na kunyanyuka kwenye kochi lake alilo likalia, kabla hajafanya chochote akasikia simu yake akiita, kwa haraka akaitoa na kukuta namba ya rais ikiingia, akaipokea na kuiweka simu yake sikioni


"Ndio muheshimiwa raisi"

"Niliona simu yako ikiingia Dokta William"

"Ndio muheshimiwa, ila nilitaka tuzungumze kuhusiana na hao mabinti walio kamatwa napolisi"


"Una maoni gani juu yao?"

"Hao ndio wale vijana ulio niagiza kufanya nao kazi ya kuwasaka wote, wanao isumbua serikali yako"

"Kwa hiyo mimi nifanyeje?”


"Usiwachukulie sheria kali bado tunawahitaji"

"Siwezi kufanya ujinga kama huo kwasababu wametugharimu sana serikali yetu"

Raisi alizungumza kwa hasira kisha akakata simu, na kumuacha Dokta William akibaki akiitazama simu yake pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote



******

Mwili wa Samson ukaanza kutetemeka, baada ya macho yake kutazamana na bastola ya Rahab

“Nilikuambia usiniguse, mimi sio Malaya sawa?”

Rahab alizungumza kwa sauti ya ukali

“Sawa mama”


Samson ili kuepukana na dhahama ya kupigwa risasi na Rahab taratibu akajishusha chini, akachukua taulo lake na kulilaza sakafuni na kujilaza.Masaa yakazidi kutakika hadi asubuhi ambapo Samson akawa wa kwanza kustuka kutoka usingizini, hii ni kutokana na ubaridi mkali uliompiga kwenye sakafu, akatoka nje na moja kwa moja akakimbilia chooni kutoa haja ndogo iliyo mbana sana kisha akarudi chumbani kwake


Akamkuta Rahab akiwa, anajinyoosha nyoosha huku akipiga miayo, Samson akamsalimia Rahab ila hakujibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kumtazama tu.

“Simu yako ina redio?” Rahab aliuliza

“Ndio”


“Inashika stesheni gani?”

“TBC FM, Redio One , Clouse”

“Weka TBC”

Samson hakuwa mbishi zaidi ya kuiwasha simu yake, sehemu ya redio, wakakuta miziki ikiwa imerindima kwenye kituo hicho

“Weka stesheni nyingine”


Samson akatii na kuweka stesheni nyingine, hakuna stesheni iliyokua na kitu cha maana na kumfanya Rahab kujipa matumaini wenzake wapo katika hali salama.Samson akamuomba Rahab amsubirie anakwenda kuchukua kifungua kinywa

“Unakwenda kununua nini?”

“Mihogo ya kukaanga”

“Powa, chukua na gazeti”

“Gazeti la kufungia hiyo miogooo au gazeti la kusoma?”

“Wewe unaona gazeti gani?”

“Powa nimekuelewa”


Samson alizungumza huku akitabasamu, akatoka ndani kwake a kwenda mtaa wa pili ambapo kuna biashara za mihogo ya kukaanga, kifungua kinywa ambacho Samson anakipenda na pia kinarahisisha matumizi ya pesa yake, hii ni kutokana na kipande kimoja cha muhogo kuwa ni shilingi hamsini ya kitanzania, Samson akanunua magazeti mawili yaliyo na picha za wasichana ambao moja kwa moja akawatambua ni wale walio kuwa wakizipiga risasi kama wendawazimu.


Kwa mwendo wa haraka huku mkono wake mmoja akiwa ameshika kifuko chenye mihogo ya elfu moja na mkono wake mwingine akiwa na magazeti akafika nyumbani na kuingia ndani


“Oya kuna habari hapa sio nzuri”

Samson alizungumza huku akimpa gazeti, Rahab

“Habari gani?”

Rahab akachukua gazeti la Mwananchi na kuligeuza kurasa ya kwanza na kuwaona wezake wakiwa wapo chini ya ulinzi wa polisi, jasho jembamba lililo endana na mapigo ya moyo ya kasi vikaanza kuchukua nafasi kwa wakati mmoja, hakuamini kama wezake wamekamatwa, akafungua kurasa ya ndani na kushuhudia picha za wenzake wakiwa wanapandishwa kwenye magari ya polisi


“Inabidi tufanye kitu chochote kuweza kuwaokoa wezangu”

Rahab alizungumza huku mwili mzima ukiwa unamtetemeka

“Ufanye na nani?”

“Na wewe”

“Mimi?”

“Ndio”

“Siwezi”

Kwa haraka Rahab akasimama na kuichomoa bastola yake na kuiweka kichwani mwa Samson, huku mwili mzima ukiendela kumtetemeka kwa hasira kali, iliyomfanya kuyang’ata meno yake kwa nguvu zake zote




SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……16


“Basi basi, nitafanya”

Samson alizungumza kwa sauti ya kukata roho na kumfanya Rahab kumuachia, na kukaa pembeni, ukimya ukaanza kutawala kati yao, huku Samson macho yake yote yakiwa kwa Rahab aliye kaa kitandani huku amejiinamia chini

“Unaweza kutumia silaha?”

“Hapana”

Rahab akaachia msunyo mkali huku akimtazama Samson

*******

Mipango ya kuwapeleka Fetty na wenzake katika mahakama kuu inayoshuhulika na maswala ya kigaidi ‘THE HUNG’, ikaanza kufanyika kwa ulinzi mkali wa vikosi vyote vya ulinzi vilivyopo nchini Tanzania, tangu kukamatawa kwao maisha yao yamekuwa ni yakufungwa vitambaa vyeusi katika macho yao pamoja na kufungwa pingu ambazo ni toleo jipya na mara nyingi hutumika katika mataifa makubwa kama Marekani na Uingereza katika swala zima la kuwafunga wahalifu walio shindikana na serikali zao, wanao hesabiwa kama magaidi.


Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali duniani wameweka kambi nje ya makao makuu ya jeshi la polisi, kila mmoja akisubiri kunasa habari ya ni siku gani magaidi hao wa kike watasafirishwa kupelekwa mahakamani, kwani kila mmoja anahamu sana ya kuwaona wasichana hao wanafananiaje kwani matukio waliyo yafanya tangu nchi ya Tanzania ipate uhuru mwaka 1961, hapakutokea kundi au watu walio iumiza serikali kwa kiasi kikubwa sana katika kuua idadi kubwa ya polisi kama walivyo fanya Fetty na wenzake


IGP bwana G.Nyangoi kwa mara ya kwanza anajitokeza mbela ya waandishi wa habari huku akiwa ametawaliwa na tabasamu kubwa, kwani kuwakamata magaidi hawa kwake ni jambo kubwa la kufurahisha na ni miongoni mwa ushindi mkubwa tangu akabidhiwe kiti cha kuliongoza jeshi la polisi

“Nitakaribisha, maswali yasiyo zidi matano tu, ili kuokoa muda”


Bwana G.Nyangoi alizungumza mbele ya waandishi wa habara walio zitega kamera zao za aina mbali mbali 


“Mimi ni Jonh kutoka shirika la utangazaji la BBC Swahili, Ningependa kufahamu kama jeshi la polisi ni hatua gani ambazo mmepanga kuzichukua kwa askari wote walio kufa katika harakati za kuwakamata hawa magaidi?”


“Nilisha zungumza hapo awali, kwa wale askari wangu wote walio fariki katika tukio zima la kuwatafuta hawa magaidi, familia zao zimelipwa kiwango cha shilingi milioni mia moja, huku wale wenye watoto wao watasomeshwa na serikali kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu”


“Je, magaidi hao mmepanga kuwasafirisha kwa usafiri gani?”

“Magaidi, watasafirishwa kwa kutumia ndege”

“Ndege gani?”

“Ndege za jeshi zitahusika katika kuwapeleka mahakama kuu ya magaidi”


“Je, kwa nini wasihukumiwe hapa hapa nchini Tanzania hamuoni, kuwapeleka huko inagharimu kiasi kikubwa cha pesa?”


“Kwakiwango walicho kifikia hawa mabinti ni kikubwa sana na kimefikia kiwango cha kuhesabiwa kama magaidi wa kimataifa na sisi kama washiriki wa umoja wa mataifa tunawaachia umoja wa mataifa kufanya kazi juu ya hawa watu, Asanteni sana kwa maswali yenu”


“Muheshimiwa swali moja la mwisho”

“Ehee uliza, ila hili ndio litakuwa swali langu la mwisho, ninawahi kikao sawa jamani”


“Tumesikia kwamba mmeshirikiana na FBI katika kuwakamata hawa mabinti , nyinyi mlishindwa kufanya hiyo kazi?”


“Hapana, vijana wetu wenye mafunzo kamili ndio wameifanya hiyo kazi, Asanteni sana”

IGP Bwana G.Nyangoi akawaaga waandishi wa habari na kuingia zake ndani na kuwaacha wakiwa wanaulizana maswali wao kwa wao

********

“Shiti…, huu ni ujinga”

Rahab alizungumza huku akiitazama Tv ndogo iliyomo kwenye chumba cha Samson, kwa kupitia chaneli ya Star Tv aliweza kuyaona mahojiano ya waandishi wa habari na mkuu wa jeshi la polisi bwana G.Nyangoi


“Tutafanyaje, wakati watu ndio hao tayari wamekamatwa?”

Samson aliizungumza huku akimtazama Rahab aliye ikunja sura yake, Rahab akainyanyua sura yake na kumtazama Samson kisha akairudisha kwenye Tv inayoonyesha miziki ya bongo Flevar

“Tunaweza kuwapata”

“Tutawapataje?”

“Nitakuonyesha jinsi ya kuwapata”



************

Rahab anafanikiwa kufika katika uwanja wa ndege wa Julias Kambarae Nyerere, bila ya mtu yoyote kuweza kumgundua, kwa jinsi alivyo jitanda mtandio kichwani na kujipara vilivyo, haikuwa rahisi kwa mtu yoyote kuhisi kama yeye ni jambazi, kitu cha kwanza kukifanya anamtafuta Ludovirk mwanaume ambaye alishawahi kulala naye kipindi cha nyuma akiwa anafanya kazi ya kujiuza mwili wake, na Ludorvick anahusika katika kitengo cha ukaguzi.


Kwa bahati nzuri akamuona Ludorvick akiwa amesimama kwenye moja ya nguzo, huku akizungumza na simu.Kwa mwendo wa umakini Rahab akatembea hadi sehemu alipo simama Ludorvick na kumgusa bega kwa nyuma

“Ludo”

Rahab aliita kwa sauti ya uchokozi ambayo ni nyepesi sana, na iliyo legea.Ludovick akageuka na kukutana na Rahab

“Sawa ngoja nitakupigia kuna kazi ninaifanya mara moja hapa”


Ludorvick alimjibu mtu anaye zungunza naye kwenye simu, akaikata simu yake na kumkumbatia Rahab kwa nguvu

“Upo wewe?” Ludorvick alizungumza kwa sauti ya mshangao, na iliyo jaa furaha sana

“Ndio nipo”

“Umezidi kupendeza, mpenzi wangu”

“Asante”


“Twende ofisini, hapa si unaona jinsi watu walivyo wengi”

Ludorvick akaongozana na Rahab hadi ofisini kwake, huku njiani Rahab akiwatazama askari kwa umakini na hakuna ambaye anamfwatilia, wakaingia ofisini mwa Ludorvick, kitu cha kwanza alicho kifanya Ludorvick ni kuanza kuing’ang’ania midomo ya Rahab na kuanza kuinyonya kwa fujo, huku akiachia pumzi nyingi.Rahab hakutaka kujibana na akamuacha Ludorvick kufanya yake

“Mmmm, baby tupo ofisini banaa”

Rahab alizungumza kwa sauti ya kudeka

“Ngoja kwanzaa, kidogo”


Ludorvick alizungumza huku akiaanza kuvua koti lake la suti

“Jamani baby ngoja kwanza tuzungumze, leo nitalala na wewe usiku kucha”

“Kweli” Ludorvick alizungumza huku akihema kama bata mzinga

“Ndio baby, usijali kwa hilo”


Rahab alizungumza kwa sauti ya kudeka na kuzidi kumpagawisha Ludorvick, mchaga huyu anaye babaika sana kwenye swala zima la mapenzi, na kila anapovuta hisia siku aliyo pewa penzi motomoto na Rahab basi anajikuta mwili mzima ukimsisimka.


Ludorvick akaliokota koti lake la suti, alilokuwa amelitupa chini, Rahab akakaa kwenye kiti kilichopo karibu na meza ya Ludorvick

“Niambie mke wangu”

“Safi, tuu.Mume ninishida”

“Unashida gani mke wangu, mtoto mzuri kama wewe?”

“Mmmm, kuna shida nahitaji unisaidie”

“Zungumza, kama ni pesa wewe niambie tu nitakupa kiasi chocote utakacho kihitaji”


Kabla Rahab hajazungumza kitu simu ya mezani mwa Ludorvick ikaita na kumfanya Ludorvick kuachia msonyo mkali na kuipoke na kuminya kitufe cha kuifanya sauti kuwa kubwa(Luodspeker)


“Ludorvick andaa ndege yangu, ninasafari saa mbili na nusu usiku, hakikisha inakaguliwa vya kutosha”

Sauti nzito ilizungumza kutoka upande wa pili wa simu

“Sawa sawa, mheshimiwa Raisi”

Simu ikakatwa na Ludorvick akabaki akiwa ameduwaa kwani hakutegemea kupokea simu ya Raisi kwa wakati kama huu,

“Nani?’

“Raisi”

“Mmmmm”

“Yaani hapa amesha nivunja nguvu mke wangu?”

“Kwa nini?’

“Ndio nilikuwa ninataka kutoka kazini, hapa itanibidi nikasimamie zoezi zima la ndege yake kukaguliwa , hadi aondoke nchini na sijui anakwenda wapi”



“Twende nikakusaidie mpenzi wangu, uku unafanya kazi ninakupeti peti”

“Eti eheee”


“Ehee, kwani sipaswi kuwa karibu nawe?”

“Unapaswa, ngoja niwapigie simu wakaguzi wangu”

Ludorvick akawapigia simu wakaguzi wake wanaohusika katika ukaguzi wa ndege na kuwapa kazi hiyo na kuwaamuru waanze mara moja pasipo kupoteza muda.


Ludorvick akatoka na Rahab hadi sehemu ya maegesho ya ndege ya Rais na kuwakuta watu wake akiwa katika kazi ya ukaguzi wa ndege ya Rais Praygod Makuya, ambayo ni aina ya ‘Air Force’ aliyopewa na serikali ya Marekani, katika kuimarisha ulinzi katika safari zote za raisi wa Tanzania


“Kumbe Raisi anandege kubwa kama hii?”

“Ndio, hii Raisi alipewa kama msaada, si unajua Marekani na TANZANIA tunashirikiana katika mambo mengi”

“Ahaaaa, kwa hiyo humo ndani anaingia Raisi peke yake au?”

“Humo anaingia Raisi na wajumbe wake wote”

“Ahaaa”


“Twende ukaone ndani”

Ludorvick alizungumza huku akiongozana na Rahab kupandisha ngazi ndefu kuelekea juu ulipo mlango wa kuingilia ndani kwenye ndege kubwa, ambayo ukiachilia ukubwa na ubora wa ndege anayo tembelea Raisi wa marekani, inayo fwata ni ndege hii anayo tembelea Raisi wa Tanzania Dokta Praygod Makuya.


Macho ya Rahab yakawa na kazi ya kutazama sehemu zote za ndani ya ndege

“Hii ndege, wamarekanai wameweza kutengeneza, kwa maana inavitu vingi sana vya kumlinda Raisi”

“Ahaaaa, natamani niipande na mimi kuwa miongoni mwa abiria”


“Ahaaa hii huwezi kupanda, ukiachilia ikulu ya raisi, akiwa hewani Raisi Ikulu yake inakuwa humu ndani na ndani ya hiyo ofisi anaweza kufanya kazi zake zote kama akiwa ardhini”


Ludorvick akaendelea kumuelekeza sehemu mbali mbali za kwenye ndege hii ya kisasa ya Raisi wa Jamuhuri wa muungano wa Tanzania bwana Praygod Makuya.Pasipo Ludorvick kuona,

“Baby ninakuomba niingie chooni”

“Sawa ngoja mimi niingie kwenye chumba cha marubani niaangalie kama kuna usalama”

“Sawa”


Rahab akachukua nguo nne za wahudumu wa ndege ya Raisi na kuingia nazo chooni pasipo Ludorvick kuona tukio hilo, akazikunja vizuri na kuzificha kwenye makalio yake kisha alipo hakikisha kwamba yupo vizuri akatoka chooni na kumkuta Ludorvick akimsubiria

“Umeona hivyo vyoo vilivyo vizuri”

“Ndio, hivi wahudumu wa Raisi wanaingia saa ngapi ndani ya ndege?”

“Lisaa limoja kabla ya raisi kuingia ndani ya ndege”

Ludorvick na Rahab wakatoka kwenye ndege na kwenda sehemu ya kutokea, nje ya uwanja wa ndege kwa kupitia geti la nyuma ya uwanja

“Baby ngoja nikupe pesa, uchukue taksi mimi ngoja nirudi nikawasimamie hawa vijana”

“Sawa”


Ludorvick akatoa laki mbili na kumkabithi Rahab

“Alafu sijachukua namba yako ya simu”

“Sina simu mume wangu”

“Ohooo basi ngoja nikuongezee pesa ukanunue nyingine”

“Sawa nitashukuru”

Ludorvick akatoa laki na nusu na kumkabithi Rahab kisha akamtajia namba yake ya simu na Rahab akaahidi kuishika kichwani mwake

“Sawa baby nitakupigia”

Rahab akaondoka huku akiwa na furaha kubwa moyoni mwake, akachukua taksi hadi nyumbani kwa Samson na kumkuta Samson akiwa amejilaza kitandani huku akionekana kuwa na mawazo mengi

“Umetoka wapi?”

Samson alizungumza kwa sauti ya ukali, huku akimtumbulia mimacho Rahab


“Unaniuliza wewe kama nani?”

“Sio ninakuuliza kama nani, ila nataka kujua unatatoka wapi kumbuka kwamba hapa upo kwangu?”

“Hupaswi kujua, mwehu nini wewe?”

Samson akanyanyuka kwa hasira na kumzaba Rahab kibao cha shavuni kilicho myumbisha hadi kikamuangusha chini


ITAENDELEA... 



ILIPOISHIA...

Samson alizungumza kwa sauti ya ukali, huku akimtumbulia mimacho Rahab

“Unaniuliza wewe kama nani?”

“Sio ninakuuliza kama nani

, ila nataka kujua unataoka wapi kumbuka kwamba hapa upo kwangu?”

“Hupaswi kujua, mwehu nini wewe?”

Samson akanyanyuka kwa hasira na kumzaba Rahab kibao cha shavuni kilicho myumbisha hadi kikamuangusha chini


ENDELEA...

Rahab akasimama kwa hasira, akarusha ngumi ambayo Samson aliidaka kwa mkono wake mmoja na kuachia kibaoa kingine kizoto kilicho myumbisha Rahaba na kumuangusha chini.

“Sikiliza wewe mwanamke, hata siku mmoja huto weza kunipiga sawa”

Samson alizungumza kwa kujiamini huku akimtazama Rahab anaye jifikiria kunyanyuka kutoka katika sehemu aliyo angukia.Rahba akarusha teke akikusudia kuipiga miguu ya Samson, ila Samsona akaruka juu na kutua chini, akamnyanyua Rahab kwa mkono mmoja na kumvuta karibu yake

“Nitakuumiza”


Rahab akajaribu kumpiga Samson igoti cha tumbo ila Samson akawahi kurudi nyuma, huku akimsukumiza nyuma Rahab.Rahab kwa hasira akarusha teke, akiwa hewani Samson akamuwahi kwa kupiga tele la mbavu lililo sababisha Rahab kuangukia kitandani huku akihema

“Usijaribu tena siku nyingine”


Samson alizungumza huku akimtazama Rahab anaye ugulia maumivu ya mbavu zake.Rahab akamtazama Samson kwa jicho kali lililo jaa maswali na mashaka mengi juu ya Samson kwani kwa jinsi alivyokuwa anamchukulia sivyo jinsi Samson alivyo


“Wewe ni nani?” Rahab aliuliza

“Mimi ni Samson, au unahisi mimi ni nani?”

“Ninamaanisha unafanya kazi gani?”

“Haaaa mimi si fundi baiskeli”


Samson akafungua boksi lake la kuhifadhia nguo zake, akatoa bastola mbili na kumkabidhi Rahab,

“Nenda kafanye kazi yako kwa umakini”

Samson alizungumza huku akijilaza pembeni ya Rahab, huku akijifungua vifungo vya shati lake.Rahab akaichunguza moja ya bastola zake na kuikuta ikiwa na risasi za kutosha, kwa haraka akajigeuza na kumkala tumboni Samson na kumuweka bastola ya kichwa.

“Sema wewe ni nani?”


Rahab alizungumza huku jasho jingi likimwagika, Samsona akamtazama kwa umakini Rahab kisha akaunyanyua mkono wake wa kushoto pasipo kuwa na waga na kuushika mkono wa Rahab alio shika bastola yake na kuusogeza pembeni, mkono wa kulia wa Samson ukapakishika kiuno cha Rahab na kumvuta chini taratibu na sura zao zikawa zimesogeleana kwa ukaribu sana

“Mimi ni fundi baiskeli”


Samson alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa hisia nyingi za mapenzi, kisha taratibu akaukutanisha mdomo waka nawa Rahab, na kuanza kubadilishaa ladha ya mate yao, kila mmoja akajikuta mwili wake ukisisimka kwa kiasi cha kuzidi kuziinua hisia zao za mapenzi huku kila mmoja akijitahidi kumnyonya mwenzake vilivyo, wakaanza kuvuana nguo moja baada ya nyingine na kujikuta wakizama katika dimbwi kubwa la mapenzi, huku kila mmoja akionekana kuwa na furaha ya kupata penzi la mwenzake


Ndege maalumu ya jeshi ikawekwa tayari kwa safari ya kuwasafirisha Fetty, Halima, Anna na Agnes, ambao tangu wakamatwe maisha yao yamekuwa ni yakufungwa vitambaa vyeusi machoni, huku mikononi na miguuni wakiwa wamefungwa cheni nzzito ambazo si rahisi kwa wao kuweza kuzifungua.Wakavalishwa mavazi ya rangi ya chungwa, yanayo endana na mavazi ya mafundi gereji wengi.Safari ikapangwa kuondoka nchini usiku wa saa nne


Waandishi wa habar pamoja na wananchi wenye hasira kali na wasichana hawa, wamejipanga pembezoni mwa barabara wakisubiria kuwaona wasichana hao wakipelekwa katika uwanja wa ndege kwa ajili ya kuanza safari ya kupelekwa mahakama kuu ya magaidi.Kila mmoja moyoni mwake akawa na sala kubwa ya kuomba wahukumiwe kifungo cha maisha kwani ukatili ambao wameufanya ni mkubwa, ambao haukuwahi kutokea katika nchi inayosifika kwamba ni nchi ya amani.


Kikosi maalumu cha wanajeshi wapatao ishirini na tano, wakiwa na bunduki zao mikononi, wamesimama nje ya magari kumi aina ya GVC yanayotumiwa kusafirishia wahalifu harari, Sifa ta magari haya ni kwamba hayaingii risasi na yametengeneza kwa uwezo mkubwa wa kuhimiili mikiki mikiki ya majambazi endapo wanaweza kuvamia msafara wao.Nitukio la kihistoria nchini Tanzania kwani haijawahi kutokea ndio maana watu wengi pamoja na waandishi wa habari wanaamu ya kushuhudia jinsi msafara huo utakavyokuwa na ulinzi mkali kupita misafara yote ya magaidi walio wahi kukamatwa na jeshi la polisi


Magari yote kumi yakawa yapo tayari kwa safari, wanajeshi hao wakiwa wanasubiria kuletwa kwa magaidi hao walio chini ya ulinzi mkali wa askari.Simu ya IGP Bwana G.Nyangoi inata zikiwa zimesalia dakika tano tu kabla hawajawafungulia magaidi kutoka kwenye chumba maalimu kilicho tengenezwa kwa kuta za chuma, na kuwakabidhi katika kikosi maalumu cha jeshi


“Ndio mkuu” Bwana Nyangoi alizungumza baada ya kuipokea simu yake

“Wahalifu , wabadilishieni msafara”

“Muheshimiwa mbona kila kitu tumeshakiweka kwenye utaratibu”

“Hii ni amri na sio ombi, wasafirisheni na sabmarine”


Rahab na Samson, wakiwa wamevalia nguo za wahudumu wa ndege ya raisi aina ya Air Force, wanafnikiwa kuingia katika ndege, pasipo kustukiwa huku Samson akiwa ametengeneza vitambulisho bandia vinavyo endana na wahudumu kwenye ndege ya Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dokta Praygod MakuyaMbaya zaidi katika siku hii, mtaalamu anaye kagua watu wanao ingia kwenye ndege ya raisi kwa kutumia mashine maalumu, anaumwa sana kiasi kwamba ameshindwa kuwemo katika ndege hii ya raisi, na watu wengine hawana utaalamu wa kuitumia mashine hii kutoka ndege ni mpya katika maisha yao.Samson katika mfuko wake wa nyuma wa suruali ameweka kipakti kidogo chenye madawa ya kulevya yenye nguvu kubwa ya kumlewesha mtu katika muda wa dakika tano tuu


Watu wengi wamezoea kumuona Samson kama fundi baiskeli, na ndivyo jinsi watu wengi wanavyo aminni katika hilo, ila sivyo kama watu wengi wanavyo dhania.Samson ni miongoni mwa wapelelezi wa hatari kutoka nchini Somalia katika kundi la Al-Shabab, Wazazi wake ambao kwa sasa ni marehemu ni watanzania na ameishi Tanzani tangu akiwa mtoto mdogo na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya St. Mary, ila alipo timiza umri wa miaka kumi na mbili aliwashuhudia wazizi wake, baba na mama wakiuwa kinyama na Bwana Praygod Makuya ambaye kwa kipindi hicho alikuwa ni waziri wa mambo ya nje, wazazi wake walikuwa ni walikuwa ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Tanzania kutoka katika chama pinzani, kinachokichua chama kilichopo madarakani katika nafasi za kugombania madaraka ya uraisi.


Kitendo cha wazazi wake kuuawa kikatili katika jumba lao la kifahari lililopo maeneo ya Mbezi beach anaamua kukimbilia nchini Somalia alipo olewa dada yake, alijikuta akivutiwa sana na taarifa za kikundi cha kigaidi kinacho isumbua serikali ya Somalia, ndipo alipo amua kutafuta uwezekano wa yeye kujiunga na kikundi hicho pasipo kumueleza dada yake juu ya nia yake, anafanikiwa kujiunga na kikundi cha Al-Shabab na anapata mafunzo kwa miaka zaidi ya kumi, na anarudi Tanzania na kuanza kujihusisha na utengenezaji wa baiskeil na ukodishaji, na anakuwa ni miongoni mwa mafundi maarufu sana katika mitaa ya Post.


Kazi yake kubwa ambayo amepewa kuifanya ni kuchunguza mfumo mzima wa wapi wanweza kuteka na kusababisha maafa makubwa katika nchi ya Tanzania ndio maana anamua kufanya shuhuli zake nyingi karibu na majengo ya kibiashara ili kujua mfumo mzima wa shuhuli zinazo husika katika maeneo hayo.Utaalamu mkubwa wa utengenezaji wa vyeti au hati bandia, unamuwezesha kufanikiwa kutengeneza vitambulisho vya wafanyakazi katika ndege ya Raisi kwa muda mchache tu, baada ya kuelezwa kila kitu na Rabab, walipo maliza kupeana raha za kitandani


Ndani ya ndege hakuna mtu ambaye alikuwa na shuhuli nao, kila mmoja alikuwa bize na kazi zake, zilizo mpeleka ndani ya ndege hiyo, majira ya saa mbili masafara wa Raisi ukafika uwanja wa ndege na raisi akaingia ndani ya ndege, huku akiwa na furaha kubwa kwa kufanikiwa kuwakamata magaidi walio iaibisha nchi yake na kuonekana ni wazembe katika swala zima la ulinzi


“Tunatakiwa kuwa makini”

Samson alizungumza kwa sauti ya chini, akimnong’oneza Rahab abaada ya watu wote kuombwa na rubani kukaa kwenye viti vyao kwani ndege inajiandaa kuruka hewani, muda mchache kutoka sasa

“Sawa”


Ndege ikaanza kuondoka taratibu kwenye uwanja wa taifa wa mwalimu Julius K.Nyerere, na muda mchache kidogo ikaanza kupaa hewani.Baada ya ndege kukaa sawa hewani watu wakaruhusiwa kuendelea na shuhuli zao, Rahab na Samson wakaingia kwenye chumba kinacho tumika kama baa, na kukaa kama wahudumu wa sehemu hiyo, na kuanza kuwahudumia baadhi ya watu wanao hitaji vinywaji kutoka kwao


“Una simu?”

Samson alimuuliza Rahab

“Hapana, unataka ya nini?”

“Ahaaa, basi”


Wakasitisha mazungumzo yao baada ya Raisi kuingia akiwa na jopo la walinzi wake wapatao sita pamoja na washauri wake wawili.Raisi na washauri wake wakatafuta sehemu na kukaa huku walinzi wake wakiwa wemeizunguka wakiwa makini kwa kila kitu kinacho endelea, Samson akawafwata kwa heshima kubwa, akiwauliza awasaidie kitu gani, kila mmoja akaagizia kinywaji chake, isipo kuwa raisi.Samson akarudi sehemu alipo Rahab na kuchukua vinjwaji alivyo agizwa


“Muheshimiwa wewe hunyi leo?” Mshauri mmoja wa raisi alimuuliza raisi

“Hapana, sijisikii kunywa leo”

“Hivi wale wasichana wanasafiishwa kwa ndege?” Mmoja aliuliza


“Ndio, hapa ndio ninawaza endapo ndege ikianguka itakuwaje?”

“Muheshimiwa raisi, itatubidi tufanye jitihada za za kubadilisha usafiri wao, na mbaya zaidi nasikia wanapitishwa kwenye barabara hizi zetu, je msafara ukivamiwa?”

“Ndio hapa, ninaumiza kichwa changu kujua nini nifanye, nisije nikaingia aibu”


“Ila muheshimiwa, unaonaje wakatumia usafiri wa majini?”

“Maji, maji etii ehee?”

“Ndio kwa maana majini kuna usalama zaidi kuliko angani, kwa maana wanaweza kutunguliwa, huwezi jua wanamtandao gani wale mabinti”

“Karibuni vinjwaji” Samson alizungumza kwa sauti ya upole na kuondoka zake


“Hi naomba muniletee simu”

Raisi alizungumza na mmoja wa walinzi wake akaondoka na kwenda ofisini kwake, baada ya muda kidogo akarudi akiwa ameshika simu.Raisi akaminya baadhi ya namba na kisha akaiweka sikioni simu yake

“Andaeni, submarine(Nyambizi), wasichana nahitaji muwasafirishe nyinyi sawa?”


“Ndio muheshimiwa Raisi”

Raisi akakata simu, na kuminya baadhi ya namba na kumpigia IGP Bwana G.Nyangoi

“Na huo msafara uende kama mulivyo panga, ila mabinti wachukuliwe na kikosi cha majini sawa”

“Ndio muheshimiwa raisi”

Muheshimiwa Raisi akakata simu huku akiwa na jazba kidogo


“Vipi mbona umekasirika?”

“Huyu nyangoi ninamuambia afanye ninavyo taka mimi anadai kila kitu wamekipanga kimekamilika”

“Haaaa…..!!”


“Huyu naye dawa yake inachemka, nitavua madaraka”

“Usifanye hivyo muheshimiwa mpe muda kidogo”

Samson akaachia tabasamu pana baada ya kusikia kwamba wasichana walio kamata wanasafirishwa kwa Sabmarine.

“Nakuja”


Samson alimuaga Rahab na moja kwa moja akaelekea kwenye chumba cha mawasiliano, na kuwakuta wwatu wanao husika kwenye chumba hicho wakiwa wanaendelea na kazi yao

“Munahitaji vinjwaji wapendwa?”


Samson aliwauliza, na watu wanne walipo humo walimtazama kila mmoja akatingisha kichwa akiomba kuletewa chochote kitu, Samson akarudi sehemu ya vinjwaji na kuchukua vinjwaji alivyo ona vitawapendeza watu hao, akajibanza sehemu na kutoa pakti yenye unga kidogo wa madawa ya kulevya na kuweka kwenye kila glasi pasipo mtu yoyote kuona na kuwapelekea.Akawakabidhi kila mmoja glasi yake kisha akatoka na kuanza kuzuga nje ya mlango wa chumba hicho, ndani ya dakika kumi akarudi ndni ya chumba na kuwakuta wote wakiwa wamepitiwa na usingizi fofofo.


Akakaa kwenye moja ya kiti na kuchukua moja ya laptop na kuandika ujumbe mfupi wa meseji kwenda katika makao makuu ya kundi lake la kigaidi la Al-Shabab


SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……18

Samson kabla hajautuma ujembe kwenye kundi la Al-Shabab akapata wazo, akasimama kwenye kiti huku akitabasamu, akawatizama watu wote waliolala kwa kunywa vinjwaji alivyo wapa, akawachukua mmoja baada ya mwengine na kuwiangiza kwenye kijichumba kidogo na kuwafungia.Kisha akarudi kwenye mitamba na kukaa.Kwa elimu ya maswala ya maswasiliana aliyo ipata katika chuo kimoja Afrika kusini alipo pelekwa na kundi hilo la kigaidi la Al-Shabab.Ikamsaidia sana kuweza kukata mawasiliano ya Satelie yanayo ionyeshesha ni wapi ndege ya raisi ipo.


Alipo fanikiwa katika hilo, akafungua moja ya computer inayo shuhulika na maswala mazima ya mfumo wa ndege hii ya raisi, kuanzia kwenye injini ya ndege hadi chumba cha marubani.Kitu alicho anza kukifanya ni kutafuta ni wapi kilipo chumba cha kuhifadhia silaha, na kufanikiwa kukiona, akazitafuta ‘seria number’ za mlango wa chumba hicho, na kufanikiwa kuuufungua.

Marubani wa ndege ya raisi wanaanza kuchanganyikiwa baada ya ramani, inayo waongoza wanapo elekea kufutika kwenye kioo chao, kilichoo pembeni yao.

“Shitii ramani imepote”


Rubani mmoja alizungumza huku akiitazama kioo, wakaanza kufanya kila wanacho jaribu kufanya ila mambo yakawa magumu, wakajaribu kufanya mawasiliano na makao makuu ya uwanja wa ndege wa mwalimu Julius K.Nyerere ila simu zote hazikuweza kwenda sehemu yoyote.


“Jamani tunafanyaje?”

Rubani mmoja alizungumza huku akiwatazama wezake watatu waliopo kwenye chumba chao cha kuiongoza ndege hiyo a raisi ambayo ni yakisasa sana

“Tusimuambie yoyote tuendelee kufanya liwezekanalo?”

“Mmoja aende chumba cha mawasiliano kuangalia kuna nini?”


“Jaribu kuwapigia simu kwanza”

Mmoja wa marubani akachukua simu iliyopo pembeni yake na kujaribu kuwapigia ila hapakuwa na mawasiliano yoyote zaidi ya simu hiyo kutoa mlio wa kukatika

“Simu hazitoki”

“Ngoja niende kutazama kinacho endelea”

Rubani mmoja akatoka ndani ya chumba chao na kuanza kuelekea chumba cha mawasiliano ambacho kipo mbali kidogo na sehemu walipo wao


Hapakuwa na ubishi zaidi ya kamanda mkuu wa polisi kukubaliana na amri ya Raisi Praygod Makuya, akaagiza misafara kupangwa kama kaaida, huku kikosi cha wanajeshi watano wa majini, ambao wanaaminika sana, wakawasili kwenye makao makuu ya jeshi la polisi pasipo mtu raia wa kawaida kuelewa jambo linalo endelea,


Gari zilizo kuwa zimeandaliwa kwa safari ya kuelekea uwanja wa ndege zikaanza kutoka moja baada ya nyingine, huku helcoptar zipatazo sita zikiwa juu angani, zikilinda ulinzi wa magari hayo yanayo tembea kwenye msururu mmoja, huku pembeni wakiwa wamening’inia wanajeshi wawili wawili wakiwa wameshika bunduki zao.



Kila mwenye kamera yake, iwe ya simu au kamera halisi, hakusita kuchukua video au kupiga picha msafara huo ambao, una ulinzi mkali na kwatanzania haikuwahi kutokea tukio la namna hii, tangu nchi kupata uhuru na watu wengi wamezoea kuona misafara ya maraisi haswa maraisi wa marekani kuwa na ulinzi mkali wa namna hii,


Fetty, Halima, Anna na Agnes wakaingizwa kwenye moja ya gari ambalo hutumiwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kusafirisha kiasi kikubwa cha pesa kutoka benki moja kwenda benki nyingine, sifa ya gari hili, halipitishi risasi hata moja, kwani limetengenezwa kwa kiwango cha bati gumu, lisilo weza kutetereka kiraisi kwa kupigwa risasi, matairi yake yametengenezwa pira gumu lisilo jazwa upepo wa aina yoyote.



Safari ikaanza huku wakiwa wamevalishwa vitambaa vyeusi kichwani mwao, kila mmoja wao mikononi mwake amefungwa pingu ngumu isiyo weza kufunguka kirahisi, miguuni mwao wamefungwa nyororo ya pamoja inayo walazimu kutembea kwa mstari mmoja.Mwendo wa kufika bandarini haikuchukua muda mrefu sana, huku wakiwa chini ya ulinzi wa askari hao wa majini.Wakashushwa kwenye gari pasipo wao kujua ni wapi wanapo elekea


Wakaingizwa kwenye moja ya boti ya jeshi iliyokuwa ikiwasubiria, na boti hiyo ya jeshi ikaelekea kwa umbali wa kilomita kumi na tano kutoka ilipo ichi kavu, na kukuta, meli ya kijeshi inayo pita chini ya maji(Nyambizi au submarine) ikiwasubiria,

“Jamani tunaelekewa wapi?”

Anna aliuliza kwa sauti ya chini, ila akastukia akibipigwa ngumi ya mgono na askari mmoja

“Munakwenda kuzimu”


Askari alimjibu Anna kwa dharau kubwa, wakawapandisha kwenye meli hiyo ya kivita, na kuwaingiza ndani kwenye moja ya chumba ambacho sio rahisi kwa wao kutoka,Taratibu meli ikawashwa, ilipo anza kuchanganya, ikaanza kuzama ndani ya maji taratibu na kushuka kina kirefu na kuanza safari

Kupotea kwa mawasiliano kwa ndege ya raisi inaanza kuwaumiza kichwa, viongozi wa kitengo mawasiliano kilichopo kwenye uwanja wa ndege wa mwalimu Juliusi Kambarage nyerere, wanajaribu kuseti mtambo wao wa rada vizuri kuona ni kitu gani kimeipata ndege ya raisi ila wanashindwa, wanafanya mawasiliano na serikali ya Marekani kuomba msaada wa kijeshi kuitafuta ndege ya raisi wa Tanzania.



Kutokanana ushirikiano mzuri wa serikali mbili hizi, ombi lao linafanyiwa kazi mara moja na wanaanza kutumia Satelaiti zao kuitafuta ndege ya raisi ila wanashindwa kufanikiwa, kila mbinu na jitihada za kuitafuta ndege hiyo inashindikana, jambo linaloanza kuzua hofu miongoni mwa viongozi wa nchi mbili hizi.


“Ni kitu gani tunaweza kufanya?”

Ni swali la mkuu wa jeshi wa anga wa Tanzania akizungumza na mkuu wa jeshi la anga nchini Marekani kwa kutumia simu

“Tumefanya kila liwezekanano kuhakikisha tunaipata ndege ya raisi ila imeshindikana, laiti kama ingekuwa imeanguka tungefahamu”


“Sasa inakuwaje?”

“Tuendeleeni kufanya jituhada za kuitafuta, kwani ningesema nitume ndege zangu za kijeshi kwenda kuitafuta itakuwa ni ngumu, kutokana hatujui ni wapi ilipo”

“Sawa tutaendelea kuwasiliana kwa kila ambalo litakuwa linaendelea”

“Sawa”


Mkuu wa jeshi anga la anga la Tanzania anakata simu na kumgeukia makumu wa Raisi wa Tanzania, ambaye ameitisha kikao cha dharura kwa wakuu wote wa jeshi na mawaziri, baada ya kupokea taarifa ya kupotea kwa ndege ya raisi.

“Hawajaipata bado”

“Tunafanye nini?”

“Mkuu hata mimi, sifahamu, vijana wanaendelea kucheza na mitambo kujua ni kitu gani ambacho kinaendelea”

Rahab baada ya kuona, Samson anakawia kurudi kwenye chumba cha mawasiliano kama alivyo muaga, anaondoka na kwenda kilipo chumba hicho kabla hajaingia anakutana na rubani, akitaka kuingia kwenye chumba hicho

“Samahani kaka yangu”


Rahab anazungumza huku, akifungua kifungo cha shati lake alilo livaa na kuyapandisha maziwa yake juu kidogo na kumfanya rubani, huyo kubaki akiwa ameshika kitasa cha mlango pasipo kufungu, huku mimacho yake yote akiwa ameyatulisha kwenye kifua cha Rahab.


“Bila samahani?”

“Umemuona kaka mmoja, mrefu hivi?”

“Hapana”

Mazungumzo ya Rahab na rubani nje ya mlango yanamstua Samson, anaye endelea kufunga mawasiliano ya ndege hii ya raisi kwa kutumia utaalamu mkubwa alio nao.

“Shiti amekuja kufanya nini huyu?”


Samson alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti alicho kikalia, akapiga hatua hadi mlangoni na kufungua mlango na kumkuta rubani akiwa amesimama na Rahab, Samson hakutaka kuuliza na alicho kifanya ni kumvuta ndani rubani, huyo, na pasipo kuwa na haruma akamvunja shingo rubani na kumuua hapo hapo

“Funga mlango kwa ndani”


Rahab akabaki akiwa ameduwaa, kwani tukio la kuuliwa kwa rubani huyo limechukua sekunde kadhaa.Rahab akafanya kama alivyo agizwa na Samson, ambaye alishaanza kuvuta rubani huyo na kumuingizwa kwenye chumba cha alicho waingiza wahudumu wanao shuhulika na mawasiliano

“Unaweza kutumia computer?”

Samson alizungumza huku jasho likimwagika

“Kidogo?”

“Kama huwezi, kaa uangalie ninicho kifanya”


Samson akaka kwenye moja ya cumputer inayo onyesha mfumo wa vyumba vyote kwenye ndege, akaanza kufunga mlango wa chumba cha marubani, na kubadilisha namba za siri za kufungulia mlango huo.Ukafwatia mlango wa chumba alichopo raisi na watu wake, pasipo wao kujua.Akaangalia kwenye computer nyingine inayo onyesha picha za rada(kamera za ulinzi) zilizopo kwenye ndege hiyo, akaaona idadi kubwa ya watu wamelala, kwenye siti zao.

“Unaona hii ni chumba namba moja, ninafunga, milango yao, hakuna mtu kutoka.Kina abiria saba”


Samson alizungumza, huku akimuonyesha Rahab jinsi anavyo fanya.Na kila kitu anacho kifanya Samson ni kigeni mwachoni mwa Rahab, hadi sasa hivi haamini kwamba Samson anaye mjua ndio anayefanya kazi kubwa kiasi hichi.Samson baada ya kukamilisha zoezi zima la kufunga milango yote kasoro chumba cha kuhifadhia silaha akamuagiza Rahab


“Hili chumba kipo chini, unapita kwenye hii kordo kunangazi utaziona za kushuka chini, hapo ndipo utakapo shuka na kukikuta hichi chumba, chukua bunduki unazo ona zitatutosha sawa”

Samson alizungumza huku akimuonyesha Rahaba sehemu anayo paswa kwenda kupitia kwenye computer

“Dakika tano uwe umesharudi hapa”

“Sawa”


Rahab akatoka na kwenda sehemu kilipo chumba cha kuhifadhia silaha, akaanza kuchagua bunduki moja baada ya ningine, akaziweka kwenye mfuko mkubwa alio uona pembeni ya chumba hicho, ulio tengenezwa kitambaa kigumu.Akaweka na boksi nyingi za risasi pamoja na magazine zake.Kabla hajatoka akaona nguo za kijeshi pamoja na majaketi ya kuzuia risasi, akavua nguo zake na kuvaa nguo alizo ziona kisha kabeba na nguo za Samson na kurudi kwenye chumba hicho.Akamkuta Samson akiitegesha video camera vizuri

“Hiyo nayo ni yakazi gani?”

“Kuna kitu nataka kufanya”


Samson akavaa nguo alizo pewa na Rahab na kujiweka sawa, na kuiwesha video camera hiyo na kukaa kwenye moja ya kiti huku Camera hiyo ikianza kuchukua picha kuanzia kifuani hadi miguuni.Video zote zilizopo ndani ya ndee zikakata vipindi vinavyo onyesha na kuonyesha video ya mtu anaye onekana kuanzia kifuani hadi miguuni


“NDUGU ABIRIA, NIFURAHA YANGU KUWA NANYI KATIKA SAFARI HII, NIMETOA LISAA MOJA KWA KILA ABIRIA KUSALI SALA YAKE YA MWISHO KWANI NDEGE INAKWENDA KULIPUKA NDANI YA LISAA HILO KUTIMIA KAMA HUAMINI, TIZAMA HII”

Samson akaishika camera na kuigeuzia kwenye computer aliyo iietega mwendo kasi wa saa, unao onyesha dakika zake zikirudi nyuma, kwani ikifika ndani ya muda alio upanga, mfumo mzima wa ndege unakwenda kuzima, na litakalo tokea hapo ni ndege kulipuka, jambo lililo anza kumuogopesha kila mmoja aliyomo ndani ya ndege hadi raisi mwenyewe

 ITAENDELEA....




ILIPOISHIA...

“NDUGU ABIRIA, NIFURAHA YANGU KUWA NANYI KATIKA SAFARI HII, NIMETOA LISAA MOJA KWA KILA ABIRIA KUSALI SALA YAKE YA

MWISHO KWANI NDEGE INAKWENDA KULIPUKA NDANI YA LISAA HILO KUTIMIA KAMA HUAMINI, TIZAMA HII”


Samson akaishika camera na kuigeuzia kwenye computer aliyo iietega mwendo kasi wa saa, unao onyesha dakika zake zikirudi nyuma, kwani ikifika ndani ya muda alio upanga, mfumo mzima wa ndege unakwenda kuzima, na litakalo tokea hapo ni ndege kulipuka, jambo lililo anza kumuogopesha kila mmoja aliyomo ndani ya ndege hadi raisi mwenyewe


ENDELEA...

Samson akaigeuzia kamera alipo na kuznedelea kuzungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo

“NAJUA MUTASHANGAA, ILA NI KWAMBA NITAHITAJI RAISI KUFANYA HAYA YOTE AMBAYO NITAMUAGIZA KUFANYA LA SIVYO PUUUUUUU, SOTE TUTAKUFA HAHAHAAAAA”

Samson akaanza kucheka kicheko kilicho muacha mdomo wazi Rahab ambaye hadi sasa hivi amuelewi Samson anamalengo gani na roho yake


Fetty, Anna, Agnes na Halima hawatambui ni wapi wanapo elekea, kila mmoja akabaki akiwa na wasiwasi moyoni mwake kwani, nyuso zao bado zimefunikwa na vitu mifuko mnyeusi, isiyo wapa uwezi wa kuona kinacho endelea zaidi ya pumzi zinazo ingia kwenye pua zao.Kila mmoja anahofu ya kuuliza ni wapi wanakwenda kutokana kila jibu walilo pewa apo awali ni kwamba wanaelekea kuzimu.Wakasikia mlango wa chuma ukifunguliwa kwenye chumba walichopo.

“Yupi mkuu”


Sauti ya mwanaume ilisikika kwenye masikio yao, na hawakujua ni nani anaye uliziwa

“Huyu mwenye mahipsi makubwa”

Mkuu wa askari alijibu kupitia redia ya upepo, huku akitazama kwenye moja ya Tv iiyopo kwenye chumba chake, ikionyesha video za kamera za ulinzi zilizopo kwenye chumba walichopo Fetty na wezake


“Ahaa sawa mkuu”

Askari aliye agizwa na mkuu wake wa kikosi, akamkamata Anna, na kumnyanyua juu

“Jamani munanipeleka wapi?”

Anna alizungumza huku akijitahidi kujitoa mikononi mwa askari huyo

“Tulia wewe, nitakuua malaya mkubwa wewe”

Askari huyo akamnyanyua Anna na kumuweka begani mwake, na kutoka kwenye chumba na kuuamiza mlango kwa nguvu

“Hakikisheni hatoki mtu hapa”


Askari huyo aliwaagiza askari wengine wawili, walio simama kwenye malango wakilinda chumba walichopo majambazi hawa wa kike.Askari aakendelea kumbeba Anna ambaye anaendelea kufurukuta kwenye bega lake alipo muweka, kutokana na ukubwa wa misuli yake iliyo jengeka vizuri kutokana na mazoezi ya kijeshi anayo yafanya, Anna hakumsumbua kabisa kuchomoka kwenye mikono yake.Wakafika kwenye moja ya chumba ambacho yupo mkuu wake wa kikosi bwana Mathiasi Reymond na kumuingiza Anna na kumkalisha kwenye kiti

“Tulia kama ulivyo la sivyo tutakunyonga”


Anna aliendelea kupokea vitisho kutoka kwa askari aliye mtoa kwenye chumba alicho kuwepo na wezake.Mathiasi Reymond, tayari amesha vua ngua zake na kubaki na bukta yake ya ndani kwa ajili ya kufanya kazi moja tu, yakumuingilia kimwili Anna, msichana mzuri aliye umbika kila idara ya mwili wake.


Fetty akanyanyuka kwenye kwenye sehemu aliyo kaa, lengo lake ni kusikiliza kama atapokea amri yoyote ya kuambiwa kukaa kwenye sehemu yake, ila ukimya ukatawala.Akapiga hatua za taratibu akizunguka kwenye chumba akijaribu kujua ni kitu gani kinacho endela ila hakusikia chochote.


“Jamani mupo”

Fetty alizungumza kwa sauti ya chini

“Ndio, ila tupo wa tatu”

Halima alijibu kwa sauti ya kunong’oneza

“Nalijua hilo, Anna atakuwa amepelekwa wapi?”

“Yaani hata mimi mwenyewe sielewi?” Agnes alijibu

“Sijui hapa ni wapi jamani” Agens aliiuliza

“Cha msingi ni kujua nini tunatakiwa kukifanya na amini mumenielewa”


Fetty alizungumza huku akijiegemeza kwenye ukuta wa chumba alichopo, kutokana na mikono yake kufungwa kwa nyuma kwa pingu na kugundua si ukuta wa kawaida


Mathiasi Reymond akamuamuru mlizi wake, kumfungua vipingu za mikononi na minyororo aliyo fungwa Anna kwenye miguu yake na mlinzi wake akafanya kama alivyo agizwa na bosi wake.Baada ya mlinzi wake kumfungua Anna akatoka ndani ya chamba na kumuacha bosi wake na Anna


Vichwa vya viongozi wa pande zote mbili Tanzania na Marekani vinazidi kuuma, kila mmoja akijaribu kutafuta mbinu na njia za kuweza kuipata ndege yenye thamanini sana aina ya Air Force inayomilikiwa na serikali ya nchini Tanzania huku ndani mwake ikiwa imembeba raisi pamoja na viongozi wapambe wake.Juhudi za Satelait katika kuinasa ndege ya raisi na kutambua ni wapi ilipo inafua dafu, jambo linalo zidi kuwachanganya sana viongozi wa pende zote mbili.


Wanacho kihofia viongozi wa nchini Tanzania ni kumpoteza raisi wao mpendwa bwana Praygod Makuya, huku serikali ya Marekani ikihofia kupoteza moja ya ndege zake ambazo ina uwezo mkubwa wa kuhimili mikiki mikiki ya vita ya anga japo imetengenezwa kistarehe zaidi kwa ajili ya kumbeba raisi huyu wa Tanzania aliye jijengea umaarufu mkubwa sana kutokana na ucheshi wake na ushirikiano wake kwa wananchi na vingozi mbali mbali duniani, katika mataifa tajiri na mataifa masikini


“Inatuazimu kutumia, mpango namba mbili(Plan B)”

Mkuu wa jeshi la anga alizungumza na mkuu wa jeshi la anga nchini Tanzania kwa kupitia mtandao wa kuonana moja kwa moja katika vioo vya Tv zao kubwa zilizopo kwenye maofisi yao ya jeshi.


“Njia gani?”

“Nimezungumza na raisi wangu, amenipa ruhusa ya kutuma ndege zangu za kijeshi kufwatilia mzunguko mzima wa ndege ya raisi ilipo pitia”

“Asante sana, nitashukuru kama ukifanya hivyo”

“Sawam na pia nitahakikisha kwamba, hakuna kitu kitakacho kwenda kinyume na mpango, na kama itakuwa ipo chini ya watekaji, kikubwa ni kumuokoa raisi tu”

“Sawa”


“MOJA, NINAHITAJI RAISI, KUJA KATIKA CHUMBA CHA MAWASILIANO, AKIWA PEKE YAKE NA PASIPO KUWA NA SILAHA YA AINA YOYOTE”

“MBILI…..OOOHH NITAZUNGUMZA BAADAYE, MUHESHIMIWA RAISI NINAKUPA DAKIKA TATU KUANZI SASA HIVI, NA NINAKUONA HAPO ULIPO NA USIJARIBU KUFANYA UJINGA WOWOTE LA SIVYO UTAANGAMIA”

Samson akazima kamera yake na kumtazama Rahab ambaye muda wote Samson alipokuwa akizungumza yeye alikuwa yupo kimya


“Hilo ni bomu?”

Rahab aliuliza huku sura yake kwa mbali ikionyesha wasiwasi wa kuangamia, Samason akamtazama kwa muda Rahab jinsi anavyo hema japo anajaribu kujikaza


“Kwa nini una wasiwasi?”

“Nimekuuliza tu, ila sina wasiwasi”

“Ndio ni bumu, unaogopa kufa”

Samson alizungumza huku akimsogelea taratibu Rahab, kisha akamshika Rabab kidevu na kutazamana naye kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kuinyonya midomo ya rahab taratibu


“Nakupenda Rahab wangu”

Samson alizungumza kwa sauti iliyo jaa mahaba, ila Rahab kichwani mwake akaanza kupanga mpango tofauti na Samson, kwani hadi sasa hivi aelewi ni kitu gani anacho kifikiria Samson kwenye mpango waliio upanga


Kwa utaratibu mkubwa, huku akishusha pumzi zake, bwana Mathiasi Reymond akaanza kumpapasa Anna mapaja yake, huku kila mara akimeza mafumba ya mate, akazidi kuipandisha mikono yake taratibu hadi kwenye kiono cha Anna na kuendelea kukitomasa, jambo lililo anza kumoa wasiwasi mwingi Anna.Akaendelea kuipandisha mikono yake hadi kifuani mwa Anna na kuzidi kumtomasa kwa nguvu Anna kwenye maziwa yake.Mathiasi Reymond, akamvua fuko jeusi alilo vishwa Anna kichwani na kukutana na sura ya binti mrembo, ambaye ukiambiwa kwamba ni jambazi tena hatari ni lazima ukatae tena kwa nguvu zote


Macho ya Anna yakazidi kulishangaa jitu kubwa. Lenye tumbo kubwa lililo shikana na mijiziwa mikubwa inayo ning’inia mithili ya kifua cha mama anaye nyonyesha, rangi yake ya mwili ikiwa ni nyeusi ikikimbizana na mkaa ulio pauka.Mihemo ya bwana Mathiasi Reymond, inazidi kumchefua Anna ambaye tayari bwana Mathiasi amesha mfungua, vifungo vya nguo lake alilo valishwa

“Wewe ni mzuri sana”


Bwana Mathiasi alizungumza huku mikono yake akiipeleka kichwani mwa Anna, na kwakutumia nguvu zake zote akaivuta shingo ya Anna karibu yake, na kuanza kumng’anganiza kuikutanisha midomo yao.Kutokana na uchovu na kuzidiwa nguvu na Bwana Mathiasi Reymond, Anna akajikuta midomo yake ikitua kwenye midomo ya Bwana Mathiasi na kiasi cha mate ya bwana Mathiasi kikiaanza kuingia kinywani mwake.Anna taratibu akaanza kujilegeza, na kumfanya bwana Mathiasi kupunguza kiasi kikubwa cha nguvu anazo zitumia.


Gafla Anna kwa nguvu zake zote alizo jaliwa na Mungu, akaing’ata midomo ya chini ya bwana Mathias Reynmond, na kujikuta akipokea ngumi nzoto, iliyo tua tumboni mwake na kumlegeza mwili...


SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……20


....Mathis Reymod akamnyanyua Anna na kumtupia kitandani, kwa kutumia minguvu yake mingi akalichana vazi alilovaa Anna

“Tulia wewe”

Mathis alizungumza huku akihema sana mithili ya bata mzinga aliye kimbia kwa umbali mrefu, akaendela kuyachezea maziwa ya Anna ambaye muda wote anajitahidi kuulinda utu wake kama mwanamke anaye jiheshimu mbele ya mwanaume asiye mpenzi wake.Kibao kikali kikatua shavuni mwa Anna na kumfanya atokwe na kiasi cha damu kadhaa kwenye mdomo wake, hii ni baada ya meno yake kuung’ata ulimi wake kwa bahati mbaya baada ya kutandikwa kibao na Mathia Reymond.Anna akaanza kujilegeza huku nguvu za mwili wake zikianza kumuishia taratibu, akajikuta akimuacha bwana Mathias kufanya anacho jisikia kufanya katika mwili wake.


Kwa bahati mbaya ama nzuri kwa Anna, uume wa Bwana Mathias Reymond, hajaweza kusimama kama kawaida yake, jambo ambalo likaanza kufedhehesha bwana Mathias, kila mbinu aliitumia ila kuusimamisha mpigo wake, haikuwezekana na kujikuta jasho jingi likimwagika, huku macho ya uchu yakiwa yametua kwenye mwili wa Anna, ambao hauna nguo hata moja.



Anna akayanyua macho yake kwa uchovu mwingi, huku yakiwa yamejawa na ukungu wa machozi yaliyokuwa yakimwagika kimya kimya, akamkuta bwana Mathias Reymond akiendelea kuuchua mpingo wake, ambao hadi sasa hivi umeelekea chini, ukikataa kabisa kufanya shuhuli aliyo ikusudia kuifanya kwa binti mrembo Anna

“Ni ingize sasa”


Anna alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, sauti yake ya uchungu ikazidi kuusisimua mwili wa bwana Mathias Reymond na kujikuta akitoka kwenye umakini wa kuzifuta hisia zake ili kuusimamisha mpingo wake.Anna akanyanyuka na kumlaza kitandani bwana Mathias Reymond, kisha akamkalia kwenye kiuno chake

“Wewe si unataka kunifanya, nifanye sasa”


Anna alizidi kumtia uchungu bwana Matias ambaye hadi sasa hivi, mapigo yake ya moyo yanakwenda kasi huku jasho jingi likimwagika.Anna akaanza kazi ya kumkomoa bwana Mathias, akaushika mpingo wa bwana Mathias Reymond na kuanza kuuchezea tararibu, ila haukufanya kazi,


“Nyanyuka na ukae”

Anna alizungumza na bwana Mathias Reymond akatii, Anna akamkalia bwana Mathias kwenye mapaja kisha akaipitisha miguu yake na kukutana mgongoni mwa bwana Mathias Reymod

“Unanipenda?”

“Ndio”


Mathias alijibu huku wasiwasi mwingi ukiendelea kumsumbua, na mawazoni mwake akijikuta akijutia ni kwanini alimchukua mwanamke huyu kwani, ni moyo ya aibu kubwa ambayo ameipata mbele ya binti mbichi kiasi hichi, isitoshe na hii ndio mara yake ya kwanza kukutana na binti huyu na mbaya zaidi alitumia nguvu nyingi sana, ila ndio hivyo hadi sasa hivi hajaweza kufaidika na chochote.


Anna akaanza kuinyonya midomo ya bwana Mathias Reymond na kuzidi kumchanganya, kwa kutumia nguvu zake zote za minguu, Anna akaanza kuzibana mbavu za bwana Mathias Reymond, na kumfanya anza kuhisi maumivu.Anna akaendelea kufanya zoezi lake la kazibana mbavu za bwana Mathis Reymond, huku mdomo wake ukiendela kuirudisha pumnzi ya bwana Mathias ndani, ambayo anajaribu kuitoa kwa wingi kupitia mdomo wake

“Uu..naaniu……aaaa”


Bwana Mathias Thomas alizungumza kwa shida nyingi sana, huku machozi yakianza kuwamwagika, akili na mawazo yake yote ameyapelekea kwamba ni miongoni mwa mchezo wa kitandani, utakao msaidia kuufanya mpingo wake kusimama na kufaidi tunda la Anna.Ila sivyo kama anavyo wazia kwani Anna, akilini mwake anawaza kumuangamiza bwana Mathias kwa mfumo huu alio uchagua, wa kumuua kimya kimya.Bwana Matias akaanza kutoa sauti iliyo jaa mikwaruzo, huku macho yake yakiwa yamemtoka mithili ya mtu anaye karibia kukata roho.



Anna akazidi kuongeza juhudi ya kuendela kuzibana mbavu za Mathias hadi akasikia mlio wa kuvunjika kwa mbavu za bwana Mathias Thomas, ndipo alipo chukua uamuzi wa haraka wa kuivunja shingo ya bwana Mathis Thomas na kumsababishia kifo cha kimya kimya bila mtu yoyote kusikia


“Ahaaaaa”

Anna alihema huku akijilaza pembeni ya kitanda, mwili wake wote ukiwa umelowana kwa jasho jingi lililotokana na shuhuli pevu aliyo ifanya


Ndege za jeshi la Kimarekani aina ya Jet, zinazo ingia marubani mmoja, zipatazo sita zikaanza kazi ya kutafuta ni wapi ilipo ndege ya raisi wa Tanzani bwana Pyagod Makuya ambaye hadi sasa hivi hijulikani ni wapi ilipo, marubani hao kazi yao kubwa waliyo pewa ni kumuokoa raisi huyo tu.Mwendo kasi wa ndege zao unawadaidia sana katia kulizunguka anga katika muda mchache, huku wakiendelea kuitafuta ndege ya raisi wakisaidiwa sana na satelaiti


Samson anamuachia Rahab na kwenda kusimama kwenye compter inayoonyesha maeneo mbalimbali ndani ya ndege ya raisi kupitia kamera za ulinzi zilizo fungwa kila sehemu ya eneo la ndege.Anaminya batani kadhaa kwenye moja ya computer na kuuruhusu mlango wa chumba ambacho yupo muheshimi Rais, kisha akaiwasha video kamera yake na kusimama kama alivyokuwa amesimama hapo awali

“Muheshimiwa raisi sasa ni muda wako kutoka, unadakika tatu kufika hapa”


Samson alizungumza kwa ufupi na kuizima video kamera yake, kisha akarudi kwenye computer inayo onyesha picha za video.Akamuona raisi akitoka kwenye chumba alichopo na kuanza safari kuelekea kwenye chumba walipo yeye na Rahab, kisha Samson akaufunga mlango wa chumba alicho toka raisi ili kuwazuia walinzi wake kuweza kutoka nje.


“Samson, hilo bomu dakika zake si zinazidi kuyoyoma?”

“Ndio kwani vipi?”

“Mpango wetu si kulipuka na hawa watu, mpango wetu ni kumteka raisi ili wezangu wa waweze kuachiwa huru, hivi unadhani tukilipuka itakuwaje”


“Ila na wewe hukuniuliza mimi nina mpango gani katika hili”

Samson alizungumza kwa kujiamini sana

“Sikia Samson, mimi sijali kwamba una mpango gani, ila mimi ninacho kihitaji ni wezangu kuachiwa huru”

“Na mimi ninacho kihitaji ni kufa na raisi wa jamuhuri ya Tanzania.Huo ndio mpango wangu nilio nao kichwani mwangu”


“Samson zima bomu lako”

Rahab alizungumz kwa sauti ya ukali, hii ni baada ya kumuona Samson akiwa na kiburi juu ya maamuzi yake

“Sikuzote mwanamke yupo chini yangu, na utafwata kile nilicho kihitaji mimi sawa”

Samson alizungumza huku akimsogela kwa karibu sana Rahab

“Hata mimi pia ninamaamuzi yangu, na wanaume atafwata kile nilicho ninacho kihitaji mimi sawa”


Rahab alizungumza kwa kujiamini, huku sura yake akiwa aimesogeza karibu sana na sura ya Samson.Wakaendelea kutazama kwa muda, wakasikia mlango ukigongwa kwa nje na kumfanya Samason atabasamu kisha akayatupia macho yake kwenye computer inayoonyesha picha za video, akamuona raisi akiwa amesimama nje ya mlango wa chumba walichopo, akapiga hatua za kuelekea kwenye sehemu mlango unapo gongwa

“Karibu muheshimiwa Raisi”


Samson alizungumza huku bastola yake akiwa ameielekeza kwenye tumbo la muheshimiwa raisi.Akamuamuru kuingia ndani ambapo moja kwa moja akamuelekeza kukaa kwenye moja ya kiti ambacho ni chakuzunguka.Akachukua gundi kubwa lililokuwa juu ya meza iliyopo ndani ya chumba hicho, kisha akaanza kumfunga Raisi mikono yake pamoja na miguu.


“Habari yako muheshimiwa Raisi”

Samson alizungumza huku akiwa amekaa kwenye meza akimtazama Raisi Praygod Makuya kwa macho yaliyo jaa kejeli


“Ohoo nimesahau kitu kimoja muheshimiwa Raisi, bumu letu limebaki dakika kumi na nane, kabla hatujafanya puuuuuuu”

Macho ya Rahab yaliyo jaa hasira yakatua usoni mwa Samson anaye zungumza kwa dharau mbele ya Raisi


“Unanikumbuka?”

“Hapana”

“Aaahaa sasa kuna ishu moja nahitaji umsaidie huyo mke wangu hapo, anaonekana kununa sana kutokana na nyinyi kuwateka wezake”

Rahab akashusha pumzi kidogo baada ya kusikia swala la wezake likizungumzwa


“Kuna wasichana wanne ambao mumewateka, ambao ni nani vilee”

“Ni Fetty, Agnes, Anna na Halima”

Rahab alijibu huku naye akipiga hatua akielekea alipo simama raisi na Samson.

“Hao mimi ni vijana wangu na ninahitaji uweze kuwaachia huru sawaa”


“Niliapa kuitumikia nchi yangu, na kuilinda katiba ya nchi yangu siwezi kufanya jambo kama hilo katika maisha yangu”

Raisi Praygod alizungumza kwa kujiamini sana huku akimtazama Samson na Rahab, ambao baada ya kusikia jibu hilo sura zao zikaanza kujaa mikunjano huku kila mmoja akikasirishwa na jibu hilo


“Etii eheee”

Samson alizungumza kwa dharau

“Ndio, kama munaniua niueni tu, naju nitakufa kwa ajili ya nchi yangu.Ila siwezi kubadilisha mawazo juu ya hilo swala munalo lihitaji nyiniyi”


Rahab akaachia kofi zito lililo tua shavuni mwa Raisi hadi, Raisi akaanza kujihisi kizunguzungu

“Utawaachia au uwaachii?”

Rahab aliuliza kwa hasira huku bastola yake akiwa ameishika vizuri kwenye mikono yake akiielekezea kichwani mwa Raisi

“Nenda kuzimu, malaya mkubwa wewe”


Raisi alimtukana Rahab huku akimtemea mate yaliyo tua juu ya uso wa Rahab na kuzidi kumpandisha hasira zaidi.Rahab akawa kama mbogo jike aliyejeruhiwa kwa risasi, akamtandika kichwa kikali raisi, cha pua, huku akiachia ngumi nyingi zilizo tua kwenye kifua cha Raisi

“Utawaachia uwaachii?”


Rahab aliendelea kuzungumza kwa hasira, huku muda wote Samso akawa na kazi ya kufunga mitambo yake ya kamera, na kuminya moja ya computer iliyopo katika eneo hilo

“SIWATOI”

Rahab bila ya huruma akaendelea kumtembezea Raisi mkong’oto mkali, jambo lililo zidi kumfurahisha Samson

“Ohooo baby punguza jazba”


Samson alizungumza huku akimshika kwa nyuma Rahab na kumsogeza katika eneo ambalo yupo Raisi, mikono yote ya Rahab imejaa damu za Raisi Praygod, ambaye hadi sasa hivi sura yake imejaa damu nyingi, huku baadhi ya sehemu za mwili wake zikiwa zimevimba kwa kiasi kikubwa,

“Tulia baby”


Samson alizungumza kwa sauti ya upole na kumfanya Rahab kutulia, Samso tayari ameiunganisha mitambo yake moja kwa moja na chanel zote nchini Tanzania, na kuzima mitambo yote ya Tv hizo na picha inayo onekana ni picha za Camera yake.Samson akasimama mbele ya kamera yake ambayo inammulika kuanzia kifuani hadi miguuni


“NDUGU WANANCHI, TANZANIA, NINAIMANI KWAMBA HII NI ALFAJIRI TAKATIFU KWENU, NA KILA MMOJA ANAJIANDAA KWENDA KWENYE MIZUNGUKO YAKE YA KUMPATIA CHOCHOTE KITU, ILA MIMI NAMI NINAOMBA LEO NIWAPATIA CHOCHOTE KITU, ILI SIKU YENU NZIMA IPATE KUWA NJEMA NA YAKUPENDAZE”


Samson alizungumza, jambo ambalo liliwastua wananchi wengi nchini Tanzania, ambao wamefungulia Tv zao asuabuhi wakijiandaa kwenda makazidi.Kila ambaya amewasha Tv yake akawa na shauku ya kutaka kujua ni kitu gani ambacho mtu huyo anakizungumza kwa maana chaneli ambayo inaonekana muda huu, haina jina na ndio mara ya kwanza kuonekana.Kila mwenye mtambo wa Tv yake anajaribu kuitoa chanel hii inayo onekena ila anashindwaa.


“OHOO, MUSIPATE SHIDA KWA KUITOA HII CHANEL KWENYE VYOMBO VYENU VYA HABARI, KWASABABU HII INATOKA MOJA KWA MOJA ANGANI KWENYE DEGEEE KUBWAAAAA LA RAISI WENU MPENDWA PRAYGOD”

“NINATAKA MUONE MUMUONE RAISI WENUA ANAVYO FANANIA”


Samson akaishika video kamera yake na kuielekezea alipo kaa raisi Praygod Makuya, miooyo ya watu wengi ikastuka baada ya kumuona raisi wao akiwa anavuja damu nyingi usoni mwake, Viongozi wa jeshi na mawaziri wakabaki midomo wazi, kwani hawakutegemea hali ya raisi itakuwa kama wanavyo iona hivi sasa kwenye Tv yao kubwa iliyopo kwenye ofisi walishinda macho usiku kucha wakijitahidi kutafuta niwapi ilipo potelea ndege ya raisi.


“HUYO NDIO RAISI WENU, NIMEMUOMBA AWEZE KUWAACHIA WATU WANGU WALIO KAMATWA ILA KAKATAA NA MIMI SINA JINSI NIMEONA NI VYEMA RAISI NA WATU WOTE WALIOMO NDANI YA HII NDEGE TUFE KAMA HIVI”


Samson akaigeuza kwa haraka video camera yake sehemu ilipo computer yake inayo onyesha jinsi bomu linavyopunguza dakika zake kwa kasi na hadi sasa hivi zimebaki sekunde tatu ambazo Samson aliza kuzihesabu zikirudi nyuma

“TATU, MBILI, MOJA”


Mlipuko mkubwa ulio ambatana na moto ukasikika machoni masikioni na watazamaji wa Tv walio kuwa wakilifwatilia tukio zima, na Tv zao zote, ndani ya sekunde mbili zikabadilika na kuwa chenga jambo lililo waacha midomo wazi Watanzania wengine na wengine kushindwa kustamihili ujasiri na kujikuta wakiangua vilio hadharani


ITAENDELEA...



ILIPOISHIA...

“TATU, MBILI, MOJA”

Mlipuko mkubwa ulio ambatana na moto ukasikika machoni masikioni na watazamaji wa Tv walio kuwa wakilifwatilia tukio zima, na Tv zao zote, ndani ya sekunde mbili zikabadilika na kuwa chenga

jambo lililo waacha midomo wazi Watanzania wengine na wengine kushindwa kustamihili ujasiri na kujikuta wakiangua vilio hadharani


ENDELEA...

Ukimya ukatawala miongoni mwa watu wengi walio kuwa wakitazama taarifa ya hivi punde, juu ya Raisi Praygod Makuya kutekwa na kulipuliwa kwenye ndege yake na watu ambao hadi sasa hivi hawajajulikana ni kina nani.Kila mmoja akaanza kuhisi kwamba ni ndoto ya asubuhi ila ndio ukweli halisi kwao, Tv zao zote zikaendelea kuonyesha chenga, jambo ambalo kwa kipindi hicho cha nchi ya Tanzania kutumiamfumo wa ‘Digital’ ni ngumu sana, kuziona chenga za namna hii kama ilivyo kuwa kipindi cha ‘Analogia’


Viongozi wote walio kuwa wamejikusanya kwenye chumba cha mikutano wakifanya wawasiliano namkuu wa jeshi la anga nchini Marekanani, wanabaki midomo wazi huku wengine wenye mioyo myepesi wakijikuta wakimwagikwa na machozi pasipo wao kutarajia.


“Mmmm”

Makamu wa raisi bwana Gift Kalunde anaguna nia yake ni kuwastua ambao bado wamepigwa na bumbuwazi.

“Jamani, kila mmoja amejionea kilicho tokea.Ila niawaomba muendelee na kazi”


Muheshimiwa Gift alizungumza kwa sauti ya unyonge yenye simanzi ndani yake, akajizoa kimya kimya na kutoka ndani ya ukumbi na kuingia kwenye moja ya chumba akajifungia na kuanza kushangilia hadi jasho la mwili likaanza kumwagika.Furaha yake si kuwa raisi wa muda ila furaha yake ni kuona adui yake namba moja ameondoka kwenye hii dunia.

Anna baada ya kuvuta pumzi ya kutosha akajinyanyua na kushuka kitandani, akapiga hatua hadi mlangoni, akaufunga mlango kwa ndani kisha akarudi kwenye meza yenye computer kadhaa, akazitumbulia mimacho na kuwaona wezake wakiwa kwenye moja ya chumba, akaaendelea kuchunguza chunguza kwenye kila computer, akagundua wapo kwenye Nyambizi ya kijeshi(Submarine)

“Tutatokaje humu?”


Anna alijiuliza swali, huku akitazama kila sehemu ya chumba alichopo, akapiga hatua hadi kwenye moja ya kabati kubwa, akalifungua na kukuta shehena kubwa ya silaha zilizo pangwa vzuri, akachukua moja ya bastola aina ya ‘browning SFS’ na kuichomoa magazine akakuta risasi za kutosha, bila ya kupoteza muda akaanza kukusanya bastola ambazo anaweza kuzibeba kwa wakati mmoja, ambazo zote ni zaaina moja, akaiokota nguo yake na kukuta ikiwa imechanika sana kiasi cha kutowezekana kuvaliwa, Akayazungusha macho yake kwenye kila pande ya chumba na kukuta nguo za Mathias ambazo ni za jeshi zikiwa zimening’inizwa kwenye moja ya msumari, akachukua shati moja, na kulivaa, ambalo ukubwa wake kwake ukawa kama gauni,

“Ni nzuri”


Anna alijisemea mwenyewe kimoyo moyo huku akijitazama kwenye kioo kikubwa cha kabati.Akachukua mkanda wa suruali wa Mathias na kujifunga kiunoni, kutokana na wembamba ikamlazimu kutoboa tobo jipya katika mkanda huo, ili umbane vizuri.Akazichomeka bastola nane kiunoni mwake zote zikiwa zimeajaa lisaha za kutosha, kisha yeye mwenyewe akashika bastola mbili mkononi mwake ambazo zimefungwa viwambo vya kuzuia mlio.

“Bye muheshimiwa tumbo”


Anna alizungumza huku akifyatua risasi kadhaa zilizo tua kwenye tumbo la Mathias Reymond ambaye hadi tayari amesha fariki dunia, alipo ridhika, akashusha pumzi nyingi na kuanza kupiga hatua za haraka kuelekea ulipo mlango, akakishika taratibu kitasa cha mlango na kuanza kuuvuta polepole, akachungulia na kumkuta askari mmoja mwenye mwili mkubwa akiwa amesimama nje ya mlango huku mikono yake akiwa aimeweka kwa nyuma, kama sheria mojawapo ya kijeshi.

“Huyu ndio aliye nileta humu”


Anna alijisemea kimoyo moyo, bila hata ya kupoteza muda akafyatua risasi mbili zilizo ingia kwa nyuma kwenye kichwa askari huyo, na akaanguka kama gunia la chumvi huku kichwa chake kikichanguka kwa nyuma.Anna akaanza kutembea kwa umakini akiifwata njia iliyo nyooka yenye vyumba huku na huku, akiwa katikati ya kordo ndefu gafla mlio mkali wa sauti ya king’ora cha hatari, ikaanza kulia kwa nguvu akaanza kukimbia kabla hajafika mbali. 



Gafla akakutana na askari wanne wakiwa na bunduki mikononi mwao na kumuamrisha Anna kunyoosha mikono juu, wazo la haraka likamjia Anna kichwani mwake, akapandishia shati lake juu, na kuziacha sehemu zake za siri wazi na kuwafanya askari hao kubaki wakishangaa, huku baadhi wakimeza mafumba ya mate kwa uchu mkali wa kuto kukutana na mwanamke kimwili katika kipindi kirefu cha wao kushinda ndani ya maji baharini kwenye nyambizi yao.



Sauti ya king’ora cha hatari kikaanza kuwastua Fetty na wezake wawili ambao hadi sasa hivi wapo ndani ya chumba ambacho hawajui ni wapi, walipo

“Nini hicho?” Halima aliuliza

“King’ora cha hatari hicho”


Fetty alijibu huku akiandelea kusimama katikati ya chumba, huku kichwa chake kikiwa bado kimefunikwa na kofia jeusi, ambalo hadi muda huu wameshindwa kujivua kutokana na mikono yao kufungwa kwa nyuma na pingu.

Askari mmmoja akafungua ndani ya chumba walipo Fetty na wezake kuangalia kama wapo, 

“Wewe mpumbavu rudi ukae chini”


Askari alizungumza huku akimfwata Fetty kwenye sehemu aliyo simama, kitendo cha kumsogelea Fetty ikawa ni koso lake kubwa, kwa kutumia hisia kali Fetty aliweza kujirusha na kumtandika askari kichwa kimoja kikali cha pua na kumfanya aanguke chini, kwa hasira askari akampiga mtama Fetty na kumuangusha chini, akamkalia Fetty tumboni na kunza kumshambulia kwa kumtandika vibao mfululizo vya kichwani.



Pesi wa miguu ya Fetty, ukamsaidia katika kuipitisha miguu yake yenye nyororo ndefu shingoni mwa askari huyo na kumvuta kwa nyuma, na kuanza kumkaba kwa nguvu zake zote.Askari akajikuta akianza kufanya mawasiliano na mtoa roho, kwani kila anavyo jaribu kuitoa nyororo hiyo iliyo mpiga kabali, anashindwa na taratibu anajikuta akianza kuishiwa na nguvu, huku pumzi ikikosekana kwenye mzunguko wa mapafu yake na mwisho wa siku anakata roho taratibu


“Hei”

Fetty aliwaita wezaka baada ya kuhisi askari huyo ametulia kimya

“Tupo” Agnes alijibu

“Acheni kuzubaa sasa, njooni hapa tumpapase kama anafunguo”


Fetty alizungumza huku akiitoa mkiguu yake kwenye shingo ya askari huyo, Halima na Agnes wakaanza kutambaa chini kwa kutumi makali pamoja na mikono yao iliyo fumgwa pingu kwa nyuma, japo wanapata tabu kufika walipo lala Fetty na askari, ila wakafanikiwa kupafika.Wakaanza kumpapasa askari huyo kuanzia miguuni hadi kiunoni na Agens akafanikiwa kupata funguo nyingi 

“Nimepeta funguo sijui ndizo zenyewe”

“Jaribisha sasa” 


Fetty alizungumza huku jasho jingi likimwagika kutokana na shuhuli pevu aliyo ifanya, Agnes akaanza kuichunguza funguo moja baada ya nyingine, na kupata kifunguo kidogo cha pingu

“Nimepata kafunguo”

“Hembu ngoja nikusogelee”


Fetty akajiburuza hadi sehemu alipo Agnes, wakaegemeana migongo na Agnes akaanza kumfungua Fetty pingu za mikono yake, cha kushukuru MUNGU, pingu ya Fetty ikafunguka

“Yeaaahh”


Fetty alishangilia kwa haraka akaitoa pingu kwenye mikono yake, kisha akafungua mikanda nya mikofia waliyo vishwa, furaha yake yote ikaingia shubiri baada ya macho yake kukutana na mdomo wa bunduki aina ya SMG ikimtazama huku macho makali yaliyo jaa hasira na jazba ya askari aliye uliwa rafiki yake yakimtazama Fetty....


SHE IS MY WIFE (NI MKE WANGU)……22


.....Fetty hakutaka kumpa nafasi askari huyo kuchukua maamuzi yoyote katika kitendo chake cha kumnyooshea bunduki aliyo ishika, kwa haraka Fetty akaibeta bunduki ya askari huyo na kuangukia pembeni, jambo lililompa kiwewe askari huyo, Fetty akasimama huku mikono yake akiikunja ngumi akisubiria shambulizi kutoka kwa askari huyu, ambaye hadi muda huu macho yake yote aliyapeleka kwenye bunduki yake ilio anguka chini


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog