Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

SHE IS MY WIFE - 1

  

IMEANDIKWA NA : EDDAZARIA G  MSULWA

***********************************************

Simulizi : She Is My Wife

Sehemu Ya : Kwanza (1)



 Mioyo ya watu wengi wanao jishuhulisha nje ya eneo hili la Benki hii ya kijamii baada ya kundi la wasichana wapatao watano wakiwa na  bunduki zenye uwezo mkubwa wakiwa na kazi moja iliyo wapeleka katika eneo hili ambayo si nyingine zaidi ya kushambulia askari yoyote atakaye jipendekeza katika shuhuli ya uibaji wao wa fedha ambao wameidhamiria kwa siku nyingi na leo ndio hitimisho la mipango yao.Wamejitolea kufa na kupona huku kila mmoja akiwa makini sana na upigaji wake wa risasi zinazo toka kweye unduki zao za kila aina.


Wasichana wawili wakaingia ndani na mkuwalaza chini wahudumu wote wa benki pamoja na wateja ambao wapo ndani ya benk hii na hawakuwa na huruma kwa yoyote aliye inyanyua shingo yake kwa madai ya kuwatazama ni kina nani ambao wanafanya kazi hiyo na ambaye alijaribu kufanya hiyo basi risasi kadhaa kama si mbili basi ni zaidi ya mbili zinatua kwenye mwili wake


Wakamkamata meneja wa benki na kumuamrisha awapekeke kwenye chumba cha kuhifadhia pesa hizo na bwana Turma hakuwa na ubishi zaidi ya kuongoza hadi kwenye chumba wanacho hifadhia pesa pamoja na vito vya dhamani kama madini ya kila aina yenye dhamani kubwa sana katika mauzo yake.


Agnes akashusha mabegi makubwa matatu chini alilokuwa ameyabeba mgongoni na akayafungua na akaanza kazi ya kuviingiza vibunda vya pesa pamoja na vipande vya madini,begi lakwanza likajaa na akahamia kwenye begi jengine na kazi ikawa ndio hiyo hiyo ya kuweka pesa kwenye mabegi hadi mawili yakajaa babisa na jengine likafika nusu

“Anna take it”(ana chukua hilo)


Agnes akamsukumia Anna begi moja ambaye kwa wakati wote alikuwa amaishika bunduki yake kiumakini na kuielekezea kwa bwana Turma.Wakati ndani yakiendelea Alima,Rahab na Fety kazi yao ikwa nikuhakikisha hakuna kiumbe yoyote ambaye anaweza kujipenyeza na kufika katika eneo la nje ya banki.Gari tatu za watu binafi zilizo kuwa zinajaribu kukatisha katika eneo la karibu yao wakijifanya ni vichwa ngumu hawaelewi ni kitu gani kinacho endelea walizishambulia kwa risasi nyingi na kuwaua madereva pamoja na watu walimo ndani ya gari hizo

“R nenda kacheki ndani waambie waache pozi hapa nje hali ishakuwa tete”


    Fety alizungumza huku sura yake akiwa ameiziba na kofia maalumu ambalo limetobolewa sehemu za macho tuu na kofia lake linafanana na wezake wote waliomo ndani huku wakiwa wamevalia majaketi maalumu ya kuzuia risasi kupenya(bullet proof) huku suruali zao zikiwa ni nyeusi zenye mifuko mingi pamoja  na viatu vyeusi vya jeshi.


Rahab akaingia na kumuona askari mmoja akijaribu kunyata akielekea kwenye chumba cha kuhifadhia pesa huku akiwa na bunduki mkononi,Rahab hakufanya masihara zaidi ya kufyatua risasi zipatazo tato zilizo ukatisha uhai wa askari huyo na kumuangusha sakafuni kama mzigo na watu wengine wakavifunika vichwa vyao huku baadhi yao wakishindwa kuzizuia haja zao ndogo


Ikamlazimu Anna kuchungulia baada ya kusikia milio ya bunduki na kumuona Rahab akiwa anamgeuza geuza askari ailiye mpiga risasi kwa kutumia mguu kuhakikisha kama amefariki dunia au laa.


“Oya best fanyeni fasta tuibuke zetu hao machalii huko nje wamesha aanza kubweka kama bweha si munajua tena”

“Ndio tumemaliza njoo unyanyue hii ishu hapa”

Rahab akaingia na kuchukua begi lenye pesa nusu na kuliweka mgongoni na wakatoka wakiwa wameongozana huku kila mmoja akiwa ameishika bunduki yake vizuri

“Simameni juu wote”


Rahab alizungumza na kuwafanya wezake kushtuka

“Wewe unataka kufanya ishu gani tena twende zetu”

“Ngojeni musiwe na papara wanangu huko nje kimesha nuka na tukitoka hivi hatuwezi kufika mbali”


Wakamuacha Rahab afanye anacho taka kukifanya,Rahab akawaamrisha watu wote kuvua nguo zao hakujali kama kuna mkubwa au mdogo,msichana au mvulana wote jukumu lilikwa ni moja.Watu wote wakavua nguo zao zote na kubakiwa kama walivyo zaliwa na wote akawaamuru kufungua milango ya benki na kutoka nje na kukimbia la sivyo wote atawachakaza kwa risasi.


Alima na Fety wakashangaa kuona kundi kubwa la watu wakitoka wakiwa wapo uchi wakikimbia,Rahab,Anna na Agnes wakatoka wakijichanganya kwenye watu hao na Rahab akamrushia begi Fety na akaanza kuwashambulia askari ambao ndio wanasimamisha gari lao ili wapambane nao.


Rahab akaendelea kuwashambulia askari wapatao wanne na kuwafanya wapoteze maisha na wezake tayari walisha ingia ndani ya gari lao aina ya Rage rover,Idadi kubwa ya watu waliomo kwenye eneo hili wakaanza kutawanyika kila mmoja kuyanusuru maisha yake na kama mtu alihisi kama hayapendi maisha yake basi alijikuta akijerushiwa na wasichana hawa wenye roho za kikatili huku wakirusha mabomu ya machozi yapatayo kumi yaliyosababisha moshi mwingi katika eneo hili na watu wengi wakajikuta wakitokwa na machozi pasipo kupenda 


Rahab akatupa bunduki yake na kuichomoa bastola yake na kujichanganya kwenye watu wanao kimbia kimbia wakiwa wamechanganyikiwa huku wezake wakiwasha gari lao na kutokomea wasipo pajua.


Dickson fundi maarufu wa baiskel eneo la benki ya biashara iliyo vamiwa na majambazi,naye akawa ni miongoni mwa watu walio jilaza ndani ya kiduka chake huku wakisubiria heka haka za majambazi kutoweka isitoshe moshi wa mabomu ya machozi ukiwaadhiri sana.Akastukia msichana akiingia ndani ya kiduka chake cha na kumuomba hifadhi ya muda,Dickson hakuweza kubisha kutokana na msichana huyo kushika bastola mkononi na kwa haraka akatambua ni miongoni mwa wale majambazi walio ivamia benki


“Ingia humo ndani”

Dickson akamuongoza Rahab kuingia ndani ya kijichumba anacho hifadhia spea mpya za baiskeli anazo ziagizia kutoka Zanzibar.

“Kaka ninakuomba usiseme chochote kwa mtu yoyote sawa”

“Sawa nimekuelewa”


Katika siku ambayo Polisi wanapata shida sana ni siku hii ambayo Benki ya CNB kuvamiwa na majambazi na kushindwa kumkamata jambazi hata mmoja na isitoshe wananchi wamedhalilishwa kwa kutembezwa uchi .Msako mkali ukaanza kufanyika katika jiji la Dar es Salaam na kila gari zinazo kwenda mikoani ni lazima zikaguliwe na kitu ambacho kinawaumiza akili askari ni kutoweza kuwafahamu majambazi hao japo kila wanapo wahoji hoji wahanga wa tukio hilo akiwemo meneja wa Benk ambaye muda wote analia kama mtoto mdogo anadai kuwa majambazi hao ni wasichana tena wanao onekana kuwa na umri wa miaka kati ya 21 hadi 25


“Huko nje vipi polisi wapo bado?”

Rahab alimuuliza Dikson ambaye anakazi ya kuchungulia nje kuangalia ni kitu gani ambacho kinaendelea

“Ndio wapo wanatoa toa maiti za watu walio kufa na kuweka mikanda ile ya njano”

“Ahaa powa”


Rahab akaanza kuvua nguo moja baada ya nyingine na kubakiwa na boxer na kumfanya Dikson kumshangaa jinsi uzuri wa Rahab ulivyo kwani ni mrefu kiasi,sura yake ndogo iliyo jengwa na macho malaini na mazuri ya kuvutia,pua ndogo iliyo chongoka kidogo na unaweza kusema ni jamii ya mabinti warembo wa kisomali,Wembamba wake unavigezo vya kumfanya kuwa miongoni mwa wasichana wanao stahili kugombania umisi Tanzania hata umisi wa Dunia.


Rangi yake ya mwili ya kahawia inazidi kuufanya mwili wake kuwa kivutio kizuri mbele ya macho ya Dikson na kumfanya abaki akiwa amemtizama kwa dakika kadhaa gafla akajikuta akitazamana na mdomo wa bastola iliyo shikwa na Rahab

“Usishangae sana kijana”


Rahab alizungumza huku akiishusha bastola yeke chini na kumafanya Dickson kuirudiasha sura yake kwenye tukio la askari wanaondelea kufanya mahojiano na watu walio kuwepo katika eneo hili.Dickson akamshuhudia bodo boda mmoja wa pikipiki akizungumza na askari wawili ambao akanyoosha kidole chake kilipo kiduka chake akiashiria kuna kitu wakakitazame ndani ya kiduka hiki na taratibu askari wakaanza kupiga hatua za kuelekea kwenye kaduka ka Dikson


“Shiiti polisi wanakuja huku”

“Wapo wangapi?”

“Wawili”

“Wameshika bunduki mkononi”

“Sasa wewe jikaushe na atakaye ingia humu ndani halali yangu”

“Mmm”

Tayari polisi wamesha fika nje ya duka la Dickson na kuanza kulitazama tazama kwa umakini


                                         ****


Fety anaendelea kukanyaga mafuta ya gari lao akizidi kuliacha jiji la Dar es Salaam na kuutafuta mji wa bagamoyo na ndani ya dakika ishirini wanaingia kwenye mmoja wa msitu  mnene ambao mara nyingi watu hawautembelei na wakalisimamisha kwenye kibanda kimoja kidogo na wakashuka ndani ya gari na Agnes akafungua mfuniko wa chuma ulio jengewa chini ambapo ndipo ilipo kambi yao ya maficho.Kila mmoja akili yake ikawa na kazi ya kumuwazia Rahab ambaye wamemuacha jijini Dar es Salaam

“Jamani kwa mfano R akakamatwa hamuoni kama itakuwa ni shida kubwa sana kwentu?”


Fety alizungumza huku akiliweka chini begi lililo jaa pesa na madini

“Mimi mwenyewe ninogopa asije akatutaja na kila kitu kikaingia dosari”

“Sasa tutafanyaje kwa maana kama ni simu tuliziacha huku na hapa hatuna mawasiliano naye”

“Masikini R wetu cha msingi tumuombee kwa Mungu isiwe kama tunayo fikiria”


Anna akapiga hatua hadi kwenye Tv kubwa iliyopo kwenye handaki lao na kuiwasha na kuanza kutafuta chanel yoyote ya Tanzania ambayo inaonyesha tukio la uvamizi wao.Akafanikiwa  kuiona taarifa ya habari inayorushwa na kituo cha taifa TBC 1 na wote wakakaa kimya huku macho yao na masikio vikiwa vimeelekea kwenye Tv hiyo.


{HADI SASA MAJAMBAZI HAO HAWAJULIKANI NI WAPI WALIPO ILA KWA MUJIBU WA KAMANDA MKUU WA POLISI BWANA IZAK KIMARIO AMEKIRI KWAMBA MAJAMBAZI HAO WALITUMIA BUNDUKI ZA KIVITA NA PIA WAMEWAUA WATU NANE AKIWEMO POLISI MMOJA}

(“Tutahakikisha majambazi hao tunawatia nguvuni kwa maana hili ni tukio ninaliita ni tukio la kigaidi ambalo sisi kama jeshi la polisi hatuta lifumbia macho hata kidogo)


Anna akazima Tv na kuwageukia wezake ambao kila mmtu amekaa kwenye mkao wake  wa kufikiria nini cha kufanya.

“Jamani cha msingi nikuweza kuwasiliana na Dokta Wiliam aje atufanyia upasiaji wa hizi sura za bandia alizo tuvisha”

“Hilo ndio la msingi inatubidi tusitoke nje hadi uweze kufanyiwa upasuaji wa sura zetu”


Agnes akakubaliana na wezake na ajachukua jukumu la kumpigia Dokta Wiliam kutoka nchini Israel na wakampa taarifa juu ya kazi wanayo hitaji kufwanyiwa.Wakakubalina na dokta Wiliam aweze kutuaTanzania na uzuri ni kwamba dokta Wiliam anapafahamu kwenye makazi yao.


Wakiwa wamo ndani ya handaki lao gafla mlio wa hatari ukaanza kulia kwenye moja ya king’ora walicho kiweka kwenye kona ya handaki lao,Kwa haraka Halima akanyanyuka na kusimama kwenye meza yenye kompyuta zipatazo nne na akaziwasha na kuona askari wengi wakiwa na mbwa wakishuka kwenye magari yao mwanzo wa msitu.Picha za video za askari wanao ingia kwenye msitu huu zinaonyeshwa na kamera za ulinzi walizo zifunga kwenye miti umbali mkubwa kutoka katika sehemu lilipo handaki lao.


Wakakumbatiana kwa pamoja huku machozi yakiwamwagika kwa uchungu kwani siku ya leo wanahisi wanaandika historia nyingine mpya tofauti na walizo wahi kuzipitia huko nyuma.

“Sisi ni familia moja endapo itatokea tukafariki basi ninaamini tutakwenda kuonana mbinguni”


Agnes alizungumza huku akijikaza katika kuzungumza kisha kila mmoja akambusu mwenzake kwenye paji la uso na wakaokota bunduki zao na mabegi ya pesa wakaficha kwenye moja ya chumba na kutoka nje ya handaki wakiwa wamejiandaa tayari kwa mapambabo ya kufa na kupona


                                        ****


Ni kikundi kidogo cha watoto wa kike wa mitaani wenye umri isiyo pishana sana kiasi kwamba wanajikuta kutengeneza ushirikiano wao kwenye kuanza kuzitafuta kazi ili kuweza kuyasongesha maisha yao mbele.Hawa si wengine bali ni Agnes,Ana.Alima,Fety na Rahabu ambao wote wazazi wao wamefariki dunia katika mazingira tofauti tofauti.


Wanakutana kwa mama mmoja kwa jina Maafufu mama Bonge ambaye ana nyumba yake maeneo ya Magomeni na huwatumikisha wasichana wadogo katika kuuza miii yao.Agnes na wezake ni miongoni mwa wafanya biashara wa kuiuza miili yao na pesa zote wanazo zipata wanamkabithi mama Bonge na yeye anawafadhili sehemu ya kulala pamoja na chakula na malipo yao kwa siku ni shilingi elfu moja ambayo haijawatosha katika kununua sabuni za kufulia nguo zao.


“Jamani mimi nimechoka na haya maisha ya unyanyasaji…..Miili tunakwenda kuuza sisi alafu tunamnufaisha mtu mmoja tu”


Anna alizungumza huku machozi yakimlenga lenga akiwa na wezake katika eneo la kujiuza usiku wa saa nne”

“Anna unadhani yutafanyaje wakati sote hapa mjini hatuna baba wala mama”

“Hata kama jamani,wangapi hawana baba wala mama na wanaishi vizuri tuu na wanakazi nzuri na maisha mazuri sisi kweli tunashindwa kabisa kujitoa kwa lile jimama na kuanza maisha yetu?”


“Unacho kiongea Anna ni kweli mimi pia nimechoka na nilikuwa nikisubiria kupata wezangu ambao wataungana na mimi katika kuachana na hii kazi”

“Jamani anaye ungana na mimi anifwate twende tukachukue nguo zetu kwa lile jimama na tukatafuta pa kuishi”


Anna akajitenga peke yake na wezake wanne ambao ni Alima,Rahab,Fety na Agnes wakamfwata na kuwaacha wasichana wengine ambao kwa madai yao wanamuhofia mama Bonge.Wakaanza safari ya kurudi nyumbani kwa Mama Bonge na hadi wanafika ilisha timu saa sita kasoro usiku.Wakagonga na Mama Bonge akawafungulia na akaonekana kushanga kuona kundi la wasichana hao wakiwa wamesimama mbele yake

“Nyinyi vipi kazi imewashinda hadi munarudisha vikwato vyenu huku?”


Mama Bonge alizungumza huku akifoka na akastukia Agnes akimsukuma na akawapisha mlangoni na wote wakaingia ndani na kuingia kwenye vyumba wanavyo shindia na kuchukua nguo zao na wakamkuta Mama Bonge akiwa amesimama mlangoni huku akiwa ameufunga kwa funguo huku mkononi akiwa ameshika bastola

“Sasa ole wenu nione mtu anatoa kwato zake hapa pasipo kuwa na sababu ya msingi”


Mama Bonge alizungumza huku bastola yake akiwa amewaelekezea,Rahab akapiga hatua mbili mbele na  kuwaacha wezake nyuma na kumtazama mama Bonge kwa macho makali yaliyojaa hasira,Taratibu wakaanza kumzunguka mama Bonge na wote kwa pamoja wakamvamia na kumuangusha chini huku bastola yake wakiitupa mbali na wakaendelea kumpiga huku wakimziba mdomo mama Bonge.Rahabu akanyanyuka na kuelekea jikoni na akaangaza angaza na kuliokota shoka wanalo litumia kuchanjia kuni na kurudi nalo sebleni


“Nipisheni”   

Wezake wakampisha na kwa kasi ya ajabu akalishusha shoka kwa nguvu na likatua kichwani kwa mama Bonge na kukipasua kichwa cha mama Bonge na ubongo wake ukamwagika chini huku damu nyingi zikisambaa kwenye sakafu


             SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……2


 Wezake wote wakahamaki kila mmoja hakuamini kuona tukio lililopo mbele yao,Rahab akatupa shoka chini na kuwatazama wezake usoni kwa umakini

“Munacho ogopa nyinyi ni nini?”

“Ehee ahaaa hapana” Halima alijibu kwa kubabaika

“Tuutoeni sasa huu mwili”

“Tutaupeleka wapi?”

“Mimi ninaona tukodishe taksi”

“Dereva gani ambaye atakubali kubebea maiti?”

“Sasa itakuwaje?”

Wote wakakaa kimya wakitafakari ni nini cha kufanya,Fetty akawatazama wezake kwa umakini kisha akazungumza kwa sauti ya kujiamini


“Nisikilizeni....Cha msingi ni kumkata kata kama nyama ya bucha kisha tunamuweka kwenye kisafleti na kwenda kumtupa tunapo pajua sisi”

“Mmmmm”

“Agnes usigune unadhani kuna mtu anataka kwenda jela wakati kama huu....mimi bado ninayapenda miasha ya uraiani japo yanachangamoto kama hizi”

“Basi  tuanzeni kuifanya hiyo kazi”


Wakavua nguo zao na kila mmoja akabakiwa na chupi na sidiria na kila mmoja akachukua kitu ambacho anaamini akikata kwenye mwili wa binadamu kitakata,Wakambeba Mama Bonge hadi bafu lililomo ndani ya nyumba na kuanza kumkata kata kiungo kimoja bila huruma

“Angekuwa ngombe huyu mama nahisi saa hizi si chini milioni tungekuwa tumesha pata”


“Anna hembu acha uchizi wako”

“Kweli nawaambia...Huyu mama angekuwa ni ng’ombe ahaa mbona tungepata mshiko wa maana”

“Alafu si ninasikia kuna makabila wanakula nyama za watu?”

“Mmmmm kabila gani hizo?”

“Wapo ila nahisi Tanzania hakuna”

“Tanzania mbona wapo?”

“Kabila gani?”

“Wachawi”


Agnes akaachia msunyo baada ya Fetty kuzungumza pointi isiyo na msingi wowote,Wakaendelea kumkata kata mama Bonge huku wakipiga story za aina mbalimbali hadi wakamaliza kumchangua changua,wakachukua safleti pamoja na vifuko vya nailoni na kuweka viuongo kadhaa kwenye kila kifuko na kuvifunga na vyote kwa pamoja wakavidumbukiza kwenye safleti.


Wakaanza kufanya usafi kila sehemu yenye damu na wakamaliza.Wakaoga kwa pamoja na kuvaa nguo nyingine zilizo watoa tofauti na laiti ukikutana nao barabarani huwezi kujua kama niwauaji

“Jamni safari ya wapi?”

“Kuna mzungu mmoja juzi kati nililala naye yupo maeneo ya mbezi bichi twendeni kwake”


Rahab alizungumza na wote wakakubaliana,wakakodi taksi huku safleti yao wakiingia nayo ndani ya taksi na dereva hakuelewa chochote kinacho endelea.Wakamlipa ujira wake dereva na Rahab akampigia simu dokta William ambaye yupo Tanzania kwa kazi maalumu ya utoaji wa mafunzo ya oparesheni za sura kwa madkatari wa jeshi tu,Dokta Wiliam akaminya kitufe kinacho liruhusu geti la mlangoni kwake kufunguka na Rahab akawa kiongozi wa masafara na wote wakaingia ndani.


“Mmmm Jamani hapa kama ulaya geti linajifungua lenyewe”

“Anna acha ushamba unataka kusema kutembea kuto huko hujaona geti kama hili?”

“Sijawahi”

“Ahee shosti nawe umezidi ushamba”

“Tuachene na hilo je hii safleti niiweke wapi kwa maana nimechoka kuibeba”

“Idumbukize hapo kwenye hayo maua”

Halima akaidumbukiza safleti kwenye maua yaliyo tengenezwa vizuri kisha wakaingia kwenye jumba la dokta Wiliam.


“Ohhh karibuni warembo”

Dokta William alizungumza kwa Kiswahili cha kujing’ata nga’ta na Rahab akamkumbatia Dokta William na kumpiga mabusu ya kinafki kisha wakajibwaga kwenye masofa ya dhamani yaliyomo mule ndani

“Rahab ona wewe leo fanyia mimi Suprize”


“Ndio mpenzi wangu nimekuja kukufanyia Suprize na wezangu ili kama tukikukuta na msichana tumpige sana”

“Mimi wezi saliti wewe kutokana moyo wangu penda sana wewe,shindwa hata fanya kazi kwa mambo yako ya kukatika kitandani fanya mimi Crayz”

Wote wakacheka huku wakimtazama Dokta William

“Usijali kama ni kiuno tuu utakipata leo hadi uimbe wimbo wa Taifa la nchi yako”


“Kweli?”

“Ndio kwani kuna siku ambayo nimeshawahi kukudanganya?”

“Ahhaa utafanya mimi nisirudi nyumbani maana nyinyi Afrika munajoto sana tofauti na wanawake ngozi nyeupe wao baridi sana kama amfibia(viumbe wenye asili ya kuishi kwenye maji)”


“Tuachane kwanza na hilo.....sisi tumekuja kuhamia kabisa hapa kwako na kama unavyo tuona na vibegi vyetu hatuna sehemu sisi ya kwenda wala ya kulala”

“Kuna mashaka jumba lote hili kaa mimi peke yangu tena ona raha kuona sichana rembo kama nyinyi kuja kaa na mimi nitapata burudani kedekede”


“Ni wewe tu ila ninaombi jingine?”

“Ombi gani?”

“Tunaomba gari yako hiyo ya UN twende nayo sehemu mara moja kisha tunarudi?”

“Mbali sana na hapa?”

“Hapana sio mbali kivile na hapa”


“Basi ngoja niwapeleke turudi tufanye sherehee kubwaa”

Rahab akawatazama wezake na wakakubaliana kwa ishara na wote kwa pamoja wakasimama na kuacha vitu vyao,Agens akaichukua safleti yenye mwili wa mama Bonge na wakaingia kwenye gari aina ya pick up Ford na wakamuomba dokta William waelekee nje ya jiji kidogo.


“Sasa hivi saba usiku huko kwenda fanya nini?”

“Kuna mzigo tunakwenda kuutupa”

“Nini tena?”

“Ni mwi......”

“Rahab”

Fety alimzuia Rahabu hakumalizia anacho taka kukizungumza kwa maana kinaweza kikaleta mtafaruku baina yao na mzungu huyu.


“Zigo gani hiyo?”

Dokta William aliuliza huku akiongeza kasi ya gari hadi na kuliacha jiji la Dar es Salaam,

“Ahaa ni mzigo wa kawaida tuu mpenzi wangu wala usijali katika hilo”

“Isije ikawa dawa kulevya”

“Ahaa mpenzi wangu umeona wapi mtu akatupa dawa za kulevya wakati ni dili kabisa hilo”

“Mbona wezako kaa kimya hawapigi story”


“Ahaa wemejichokea kwa maana mama mwenye nyumba wetu leo ametutimua ndio hivyo hatuna pa kwenda”

“Ahaa sasa mimi huku Pwani kuna handaki langu kubwa kama hamtojali nyinyi kaa humo kwa siku kama mbili tatu kisha rudi mjini kwa maana pale nyumbani kwangu kesho fika wakuu wangu toka state of America sasa shindwa nyinyi jui wapi kaa”

“Ehee tena itakuwa vizuri”

“Eti warembo nyinyi mpo tayari kukaa kwenye handaki?”

“Ni wewe tu”


Ndani ya nusu saa gari yao ikaingia kwenye msitu mnene na kutokana na uwezo wa gari haikuweza kukwama kwenye matope yaliyo sababishwa na mvua iliyokuwa ikinyesha asubuhi.Wakasimama kwenye moja ya mti na Dokta William akashuka ndani ya gari na kutembea hatua chake na kufungua mfuniko mmoja wa chuma ambao juu yake kulikuwa  na majani mengi ambayo sio rahisi kwa mtu kuuona mfuniko huo,Akawaita Rahab na wezake na wote wakashuka kwenda chini kwa kutumia ngazi zilizopo kwenye eneo hilo.


Dokta William akawasha taa zenye mwanga mweupe unao kufanya uone kama ni mchana kweupe,Akawasha mashine inayo sambaza hewa ya oksijeni kwenye eneo zima la handaki,Katika handaki lake kuna vyumba nane ambavyo vinne ni vyakulala na vitatu vimehifadhia vifaa vingi ikiwemo bunduki za kivita.


Kila huduma inayo hitajika kwenye nyumba kwenye hili handaki ipo na zimetengenezwa vizuri na kutakufanya ukiishi ndani humo usiwazie kama upo ndani ya pango,Dokta William akawaelekeza jinsi ya matumizi ya badhi  ya vitu ikiwemo jinsi ya kuzitazama kamera za ulinzi zilizo fungwa mbali na eneo la kuingilia hapa msituni kwa kupitia computer zilizomo humu ndani.Dokta William akaondoka alfajiri na mapema kurudi zake Dar es Salaam na ikawa ni nafasi nzuri ya Rahab na wezake kuvizika viungo vya mama Bonge 


                                           *****

Maisha yakazidi kwenda mbele huku kila siku jioni Dokta William akija kuwatembelea Rahab na wezake na kuwafundisha baadhi ya mbinu za kijeshi kwani Dokta William na miongoni mwa wanajeshi wanaotegemewa sana katika jeshi la umoja wa mataifa UN.Kadri siku zinavyo zidi kwenda ndivyo jinsi Rahab,Agnes,Anna,Halima na Fety walivyo zidi kukomaa katika mafunzo ya kijeshi ambayo Dokta William aliamua kuwafundisha ili kuwatumia katika biashara zake haramu anazo zifanya akishirikiana na baadhi ya viongozi serikalini.


“Amini sasa nyinyi kuwa wanajeshi kamili si ndio?”

“Ndio”

“Sasa hapa kuna kazi moja taka nyinyi anza kuifanya kwa umakini na umahiri wa hali ya juu...”

Dokta William alizungumza huku akiwa amesimama kwenye kitambaa cheupe kikubwa huku mwanga mkali unaotoka kwenye kifaa kidogo(projectar) na kuna picha mbili za wanaume zikiwa zinaonekana kwenye kitambaa hicho.


“Hapa kuna watu wawili.....Huyu mmoja anaitwa Karim Yussuf  ni mmiliki wa Sheli za Total kwa hapa Tanzania.....na huyu namba mbili yeye itwa Mansuri ni mfanya biashara wa madini mkoani Arusha na kabla ya kesho kutwa mimi sitaki waona hawa watu kwenye dunia hii”

“Dokta kwahiyo unataka sisi tuwaue hao?”

“Ndio nataka ua huyo Karim sasa hivi yeye yupo Dar kwenye hoteli Serena na huyu Mansuri yeye yupo Tanga hoteli moja itwa Tanga bich resolt”


“Cha kufanya ni nyinyi kwenda kukamilisha hii kazi ndani ya masaa 20 yajayo hawa watu wawe wamefutika kwenye ramani ya dunia”

“Samahani Dokta je hawa watu wana makosa gani hadi sisi tuwaue hilo ni swali namba moja,swali namba mbili je utatuhakikishia vipi usalama wetu na tatu malipo yatakuwaje?”


“Swali zuri Anna...Malipo kila mmoja wenu nitampa milioni kumi shillings na kwakitangulizi nitawapa milioni tano tano kila mmoja,Mbili usalama wenu upo sababu hiyo kazi si yangu ila imetoka ngazi za juu na tatu hata mimi nilipo uliuliza ni kosa gani walilo fanya hawa watu nikaambiwa nikafanye kazi hiyo”

Halima akashusha pumzi nyingi huku akiwatazama wezake ambao wameridhika na kazi hiyo ya mauaji.


“Hakikisheni munafwata kanuni zote za nilizo wafundisha katika mauaji ya kimya kimya kama mutashindwa basi tumieni silaha zozote na hakikisheni mikono yenu munaivalisha gloves ili kuepuka kuacha alama za vidole kwa hao maiti”

“Je na sura zetu tuzaziwekaje?”

“Agnes hapo mutajua ni jinsi gani ya kucheza huo mchezo wa sura zenu na hizi ndizo namba zao za simu”


Dokta William akawatajia namba za simu za watu wanaopaswa kuuawa ndani ya masaa 20.Rahab na Agnes wakapangiwa kwenda Tanga kwenda kumuua Mansuri.Halima,Anna na Fety wakapangiwa kwenda Dar es Salaam kumuua Karimu.Dokta William akawakabidhi gari Rahab aina ya Verosa yenye rangi nyeusi kisha Walio baki akaongozana nao hadi Dar es Salaam huku wote wakiwa amekamilika katika swala zima la silaha.


                                         ******

Kwa mwendo wa masaa manne kutoka mkoa wa Pwani hadi Tanga ukawafanikisha Rahab na Agnes kufika Tanga na moja kwa moja wakaelekea kweneye Hotel ya Tanga beach Resolt na wakachukua chumba kimoja na kuanza kumtafuta Muntar ni wapi alipo.Wakiwa wamejipumzisha pembezoni mwa swimming pool lililopo kwenye hoteli hii wakamuona Muntar akiingia hotelini akiwa ameongozana na wapambe wake wapatao sita wanao mlinda na wanaonekana wapo makini sana kwa kila mtu ambaye anapita karibu na bosi wao.


“Ag mtu mwenyewe ndio yule pale”

“Nimemsoma wangu so tunalianzisha sasa hivi?”

“Hapana tutumie akili nyingi kumuua la sivyo hatuto toka salama humu ndani”

“Una wazo gani kichwani?”

“Uzuri wetu unaweza pia ukampagawisha?”

“Je ni mtu wakupenda wanawake isije tukajipendekeza ikala kwetu”

“Ngoja tuyasome mawazo yake”


Agnes na Rahab wakaanza kumfwatilia Muntar na watu wake kwa kutumia macho ya wizi ambayo wanahakikisha hakuna anaye weza kugundua juu ya swala hilo.Muntar na watu wake wakatafuta sehemu iliyo tulia na kukaa na kuagiza vinywaji.Agnes akasimama na kuishusha suruali yake ya jinzi chini kidogo na kuziachia shanga zake za kiunoni kuonekana vizuri na kwamwendo wa madaha akajipitisha pembeni ya meza ya Muntar na watu wake na kuwafanya watu wa Muntar wabaki wakimkodolea macho ya uchu Ages.


“Hakikisheni huyu dada nina lala naye usiku wa leo sawa”

Muntar aliwaamrisha wapambe wake na wakamtii na mmoja wao akanyanyuka kwenda kumfatwa Agnes kwenye eneo la kuuzia vinywaji ili kuzungumza ombi la bosi wake analo lihitaji...


ITAENDELEA...



ILIPOISHIA

“Hakikisheni huyu dada nina lala naye usiku wa leo sawa”

Muntar aliwaamrisha wapambe wake na wakamtii na mmoja wao akanyanyuka kwenda kumfatwa Agnes kwenye eneo la kuuzi vinywaji ili kuzungumza ombi la bosi wake analo lihitaji


ENDELEA

“Habari yako dada?”

Kijana wa Muntar alimsalima Agnes ambaya kwa haraka akaliachia tabasamu lake mdomoni na kuufanya uso wake kuzidi kunawiri kwa uzuri

 

“Salama mamo vipi?” Agnes alizungumza kwa sauti nyororo ya kuvutia hadi muhudumu kiume wa vinywaji akaguna

“Salama.....kwa jina mimi ninaitwa Kibopa na yule pale alavalia cheni nyingi ni bosi wangu anaitwa Muntari”

“Aahaa nashukuru kuwafahamu,Samahani kaka ninaomba unipatie Red’s mbili za baridi kiasi”

“Muhudumu mpe katon nzima pesa nitalipa mimi?”

“Jamani kaka yangu mimi sio mnywaji sana”

“Ahaa usijali nyingine unaweza kunywa leo au hata kesho”

“Asante sana”

 

Muhudumu akamkabidhi Agnes katoni ya kinywaji alicho muagizia na kibopa akatoa pesa na kumlipia muhudumu.

“Sasa sister kama huto jali ninaomba namba yako ya simu”

Agnes bila wasiwasi akamtajia Kibopa namba yake ya simu,wakaagana ana Agnes akarudi sehemu alipo Rahab

“Jamaa ameshaingia mkenge sasa kazi ni moja sawa”

“Hapo ndipo ninakupendea Ag”

“Chezea mimi wewe,kumbe mtu ukiwa na kalio kubwa nalo linasaidia”

Wakacheka na kufungua vinywaji na kuanza kunywa taratibu.Muntar akakabidhiwa namba na Kibopa na akaipiga na Agenes akaipokea na kama kawaida na sauti yake nyororo aliyobarikiwa kutoka mbinguni akazungumza

“Nani mwenzangu?”

“Ukigeuka upande wako wa kushoto utaniona nimevaa shati jeupe na cheni za dhahabu”

Agnes akageuka na kumfanya Muntar kupunga mkono akimuashiria kuwa ni yeye ndiye aliye mpigia simu

“Mrembo nakuomba basi uje kujumuika name hapa?”

“Naona aibu labda nije na mwezangu”

“Hilo tuu hakuna tatizo ni wewe tuu”

“Sawa ninakuja”

 

Agnes akakata simu na kumtazama Rahab kwa pamoja wakatabasamu na wakasimama na kuanza kutembea kwa mwendo wa maringo na kupishwaviti na wapambe wa Muntar kisha wakakaa

                                                                       ***

Dokta Wiliama akawashusha kwenye gari Anna,Halima na Fety mbali kidogo na hotel ya Serena huku kila mmoja simu yake ikiwa na salio la kutosha pamoja na picha ya Karim Yussuf kijana mwenye umri mdogo ila anasifika sana kuwa na utajiri mkubwa kutokana na Sheli za mafuta anazo zimiliki kila kona ya mikoa ya Tanzania.Kila mmoja akaingia Hotelini kwa muda wake na kuelekea kuketi katika upande wake ila kwa pamoja wakawa na mawasiliano ya ujumbe mfupi wa meseji.Kutokana ni muda wa jioni hawakuwa na papara kwani watu wengi bado hawakuwa wameingia Hotelini kuendelea na starehe zao.Macho ya Fety yakatua kwa jamaa anayeingia kwenye  mlango wa kuingilia akiwa ameongozana na mwanamke mrembo

{Nimemuona}

 

Fety akausamba ujumbe kwa wezake ambao wapo maeneo ya tofauti kwenye hoteli na taratibu simu yake akaichomeka kwenye suruali yake na kuendelea kumtazama Karim ambaye moja kwa moja aka anaelekea sehemu yenye milango ya lifti zinazo kwenda juu  na kushuka chini,Kutokan-a na Lifti kutumika ikamlazimu Karimu na mpenzi wake kusimama kwa muda kuzisubiria.Kwa haraka Fety akasimama na kupiga hatua za haraka kabla hajafika sehemu alipo Karimu,lifti ambayo wanaisubiria ikafunguaka,Karim na mpenzi wake wakingia ila kabla haijajifunga Fety akawahi kuizuia na kuingia

“Habari zenu?”

“Salma”

 

Karimu kutokana na kutokuwa na aibu akaanza kumshika shika mpenzi wake na kuchezeana katika sehemu zao nyeti.Mcho ya Fety yakawangalia kwa umakini kisha akayahamishia masho yake kwenye kamera mbili za ulinzi zilizopo ndani ya lifti kabla hajafanya kitu chochote akastukia lifti ikisimama hii ni baada ya mpenzi wa Karimu kuminya kitufe cha kuisimamisha lifti.Kufuma na kufumbua Fety akastukia ngumi kutoka kwa mpenzi wa Karim ikitua kwenye shavu lake na kumsfanya kuweweseka kasha akaanza kuikwepa mikono inayoimjia mwilini mwake kutoka kwa Karimu na mpenzi wake Shamsa mwenye asili ya kiarabu.

                                                                           **

Karimu na Shamsa wanaasili ya Oman japo wanauraia wa nchi zote mbili Tanzania na Oman,japo watu wengi waliwaona machoni mwao wanadhani ni watu wema hii ni kutokana na jinsi wanavyo jitoa katika shughuli mbali mbali za kijamii na mara nyingi huwa wanawasaidia wasio jiweza kila siku ya Ijumaa na jumamosi nje ya jumba lao lililopo maeneo ya Mbezi beach.Japo wanautajri mkubwa wa magari ya kifahari,masheli,maduka na mahoteli ya kifahari ila  bado hawaridhiki na utajiri huo na wanaendelea kufanya kazi za haramu ili kuzidi kuuongeza utajiri mara dufu.Jambo la kuua kwao ni sawa na mtu kumchinja kuku siku ya sikuku.

 

Hadi wakati huu Serikali ya Tanzania inashindwa kutambua ni jinsi gani wanaweza kuwatia nguvuni Karimu na mpenzi wake wakiwa katika kidhibitisho kitakacho wawezesha kuwastaki katika mahakama kuu ya Tanzania na kuwatupilia jela.Kila mbinu ambazo serikali waliitumia wakajikuta wakishindwa hii ni baadhi ya viongozi wasio waaminifu kuwapenyezea siri Karim na Shamsa  na hujipanga upya katika kuwatoroka askari.


Amri ya kuwaua watu waote wanaoshindikana kukamatika na kirahisi ilitolewa ma raisi tena kwa siri kubwa na watu walio husishwa katika kazi hiyo ni Dokta William na Mkuu mstaafu wa jeshi bwana Clinton Tony ambao wote ni miongoni mwa watu wa karibu sana wa raisi na mara nyingi humshauri riasi katika maswala mengi ya kukabiliana na ugaidi hii ni kutokana na ujuzi wao katika maswala ya kigaidi

 

Pasipo wao kujua Agnes,Anna,Rahab,Fetty na Halima wanatumiwa na serikali kisiri na kwaimani yao wanatambua kuwa mtu anaye waagiza kazi hiyo ni dokta Williama ambaye amewafundisha mbinu nyingi za kigadi ili kupambana na magaidi wanao itesa serikali ya Tanzania pamoja na jeshi la polisi.

 

***********

Fetty anajipanga vizuri na kuanza kupambana nao kufa na kupona kutokana na ujuzi mkubwa wa kukabiliana na adui anafanikiwa kumpiga Shamsa ngumi kadhaa sehemu ya shingo na kumfanya apate wenge linalo mkalisha chini huku machoni mwake akiona nyota nyota nyingi.Karimu anashangaa kukutana na msichana jasiri anaye vumilia makonde ya mazito kutoka kwake na kwa haraka anamisha kitufe na lifti inaanza kwenda juu huku akiendelelea kuyapangua mateke ya Fetty kwa kutimia mikono yake iliyo komaa.


Lifti inafunguka gorofa ya tano na Karimu anajirusha nje kabla Fetty hajapiga hatua anastukia akishikwa mguu na kuvutwa chini na Shamsa na kuangukia uso na kumshuhudia Karimu akichanganya miguu kwa kasi kubwa na kupolelea anapo pajua mwenyewe.Shamsa akamkalia kwa haraka Fetty mongoni na kuanza kumvuta nywele huku akijaribu kukipigisha kichwa cha Fetty chini.Kwa nguvu zake zote Fetty akajikaza mwili wake kuanzia juu hadi chini na kujinyanyua kwa nguvu hadi akasimama ila Shamsa akaendelea kumng’angania mgongoni huku mkono wake ukiwa umeikaba kwa nguvu zake zote shingo ya Fetty.

                                                                                   ***

Simu za Fetty,Halima na Anna zina Software ambayo kila mmoja wao anapo kwenda ni lazima simu zao ziingize ujumbe katika simu za wezao kuwa ni sehemu gani alipo mmoja wao.Anna akampigia simu Halima na kumpa taarifa Anna wakutate katika milango ya kiingilia kwenye lifti

“Anna,Fety yupo kwenye matatizo ninavyohisi kama unaweza kuiona simu yako inavyoonyesha kuwa yupo eneo maoja  tuu kwa zaidi ya dakika kumi sasa”

“Location inaonyesha yupo gorofa namba tano”

“Sasa tujigawe,wewe pita kwenye ngazi na mimi nitumie lifti”

“Sawa”

 

Halima akaingia kwenye lifti na kuminya kitufe cha gorofa ya tano,huku alima naye akaanza kuzipandisha ngazi kwa haraka kuelekea juu gorofa ya tano japo ni ndefi ila akajikata kutembea kwa mwendo wa kukimbia

 

                                                                                     ***

Kwa haraka wazo lililo mjia Karimu ni kushuka kwa kupitia ngazi kuepukana na kukutana na Fetty ambaye tayari alisha mzidi ujanja na maarifa ya kila aina.Karimu akaanza kushusha kwenye ngazi huku akikimbia na kutazama tazama juu kama Fetty akamfwata ajue ni jinsi gani ya kuongeza juhudi za kukimbia.Macho ya Anna yakamshuhudia jinsi Karimu anavyoshuka kwa kasi huku hasho jingi  likimwagika na shati lake likiwa limejikunja kunja kama limetafunwa na ng’ombe mwenye njaa kali,Anna akapunguza mwendo na hadi Karimu anamfikia kwa ustadi mkubwa wa hali ya juu akampiga teke la miguu Karimu na kumfanya aanguke vibaya na kuanza kubingiria kwenye ngazi akielekaea chini akitoa kelele kali za vilio.

 

                                                                          ***

Fetty akaanza kuishiwa na pumzi mwilini mwake kutokana na kabali takatifu aaliyo pigwa na Shamsa msichana ambeye kwenye maeneo mazima ya kupiga anayapenda tangu akiwa mtoto mdogo wa miaka mitano.Fetty kila alipo jaribu kuitoa mikono ya Shamsa akajikuta akishindwa kwani Shamsa anahakikisha kuwa anaondoka na roho ya Fetty,taratibu Fetty akaanza kushuka chini huku jicho likiwa linaanza kumtoka akimshuhudia mtoa roo akiinyemelea roho yake.Mlango wa lift aliyo panda Halima ukafunguka na akatoka nje akatazama pande zote za kardo akaona hakuna dalili yoyote na mtu,Akasikia kishindo na kukuroma kwa mtu kwenye mlango wa pili wa lifti ambao unshindwa kujifunga kutokana na kiatu chekundu lilicho zuia katikati na kuifanya milango hiyo kujisogeza na kurudi inapotoka.Halima akamshuhudia Fatty akilazwa chini na msichana anaye miminika kwa jasho jingi japo ndani ya lifti hii kuna hewa ya kutengenezwa AC(air condion)

 

Halima hakupoteza muda,akaingia na kuzishika nywele za Shamsa na kumvuta nje kwa nguvu zake nje na kumfanya Shamsa kuburuzika kwenye sakafu iliyotengenezwa vizuri na kufanania na kioo.Akamgauza Faetty na kumkuta akikohoa kohoa akiyaruhusu mapafu yake kuingiza hewa ya kutosha.Shamsa akasimama na kuanza kukimbia kujiokoa maisha yake

“A....nak....imbi....a.”

Fetty alizungumza kwa shida huku mkono wake mmoja akimnyooshea Shmsa anayechanja mbuga

“Upo vizuri lakini?”

“Nd...io muwah....i anatoroka”

 

Halima akamtazama vizuri Fetty na kuridhishwa na afya yake na akasimama kwa haraka na kuanza kumkimbiza Shamsa.Shamsa hakuona sehemu nyingine ya kukimbilia zaidi ya kujirusha kwenye mlango mmoja uliopo mbele yake na kwabahati nzuri mtu aliyopo ndani ya chumba hicho ndio alikuwa ameufungua na kukishika kitasa cha mlango wake kwa ajili ya kutoka nje.


Kikumbo cha Shamsa kikamfanya mwenye chumba kuanguka chini pamoja na simu yake ambayo alikuwa anasoma meseji iliyomfanya asimame kwenye mlango huku akiwa ameshika kitasa.Shamsa hakuona sehemu nyingine ya kukimbilia zaidi ya bafuni ambapo Halima naye akaingia na kwa haraka Shamsa akachukua kibakuli chenye sabuni ya unga na kumbwagia Halima ya uso

                                                                             ***

Muntar na watu wake wakazidi kunywa pombe na kuwaomba Agnes na Rahabu wawe wageni wao kwa usiku wa leo.

“Jamani sisi hatuhitaji kulala kwenye hoteli hii.” Agnes alizungumza huku akikichezea kifua cha Muntar ambaye muda wote anakazi ya kutabasamu tabasamu

“Nyinyi mutanata wapi watoto wazuri?”

“Hoteli yoyote ila si hapa”

“Wee kibopa fanya mpango wa kutafuta vyumba vya mjini kwenye hoteli nzuri nzuri unazo zijua”

“Bosi hotel ambayo ipo powa kwa haraka haraka ninaona ni Mtendele”

“Ipo wapi hiyo?”

“Maeneo ya Chuda raha”

“Sawa twendeni”

 

Wakasimama na wote wakatoka nje,Rahabu na Agnes wakaingia kwenye gari lao na Muntar na wapambe wake wakingia kwenye gari yao aina ya HAICE na taratibu wakaanza safari ya kuelekea katika Hotel ya Mtendele

“Ag hawa watu tunawaua kwa nama gani?”

“Una maana gani?”

“Namaanisha kwa kuwanyonga au kwa kuwapiga risasi?”

“Lengo letu sisi ni huyo Muntar hao wengine tuwapotezee”

“Huoni watakuwa ni watu wa kwanza katika kutusaka sisi?”

“Sawa ila tutajua ni jinsi gani ya kuwaua endepo nao wataingia kwenye kumi na nane zetu”

“Powa hii ishu tuifanye usiku huu huu na turudi zetu kambini”

 

“Powa ni wewe tuu kikubwa ni umakini na hiyo bastola yako ikoki tayari kwa mashambulizi”

                                                                 ***

Muntar na wapambe wake wanaendelea kuburudika na mziki gafla Muntar akazima redio ya gari na kuwafanya wapambe wake kumtazama

“Sikilizeni nyinyi....mpango wetu ni kama munavyo ujua,Sisi mwanamke kwetu ni begi la safari na hawa pia iwe hiyo hivyo”

“Sawa bosi ila mimi sijaelewa kidogo hapo kwa maana hawa nao pia tunatakiwa kuwaua?”

“Ndio ni lazima wafe”

“Ahaaa bosi huoni maduu wazuri kama hawa pia tuwauee ,Acha basi tuspend nao kama siku mbili tatu nne hivi”

Kwa haraka Muntar akachomoa bastola yeka na kumelekezea Kibopa ambaye muda mwingi anapenda sana wasichana wazuri

 

“Katika wakati wa kazi huwa sipendi masihara.....na ole wenu miongoni mwenu nione mtu anajipendekeza kwa msichana yoyote nitamtoa roho,Tuna wakamata na kuwachinja na ndani ya matumbo yao tunadumbukiza shehena yote ya madawa ya kulevya tuliyo nayo.SAWA?”

“Sawa bosi’

Wote wakaitikia kwa woga huku Kibopa mwili wake wote ukiwa unamtetemeka kwani Muntar ni mwanaume asiye na huruma kwa mtu wa aina yoyote katika swala zima la biashara zake haramu.Usemi wake mkubwa ni bora punda afe ili mzigo ufike


       

SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……4


Kwa bahati mbaya katika maeneo ya barabara ya Railys,wakakuta ajali  ya daladala iliyosababisha magari mengi kusimama kwa muda,Kutokana hawakuwa na haraka ikawalazimu kupanga foleni na kuwaacha askari wa usalama barabarani kumaiza vipimbo vyao.

“Rahab nahisi kuna kitu kwenye gari la kina Muntar.” Agnes alimuambia Rahabu

“Kitu gani?”

 

“Kama wanakitu wanakijadili na ona oana jinsi Muntar anavyo zungumza huku akiichezesha chezasha mkono wake ulioshika bastola?” Agens alimuonyesha Rahab na kwakusaidiwa na mwanga wa taa za magari mengine waliweza kuliona tukio la ndani ya gari

Rahab akaitoa bastola yake na kuifunga kiwambo cha kuzuia sauti,akataka kushuka kwenye gari ila Agnes akamzuia

 

“Mbona unakuwa kama mjinga unataka kwenda wapi?”

“Tuwafyatue tusepe zetu”

“Huoni hao askari hapo au unataka tukimbizane kimbizane?”

Wote wakajikuta macho yao yakimsindikiza askari anaye gongwa kwenye kioo cha gari walilomo Muntar na watu wake

 

                                                      ***

Muntar akamtazama askari anaye gonga kioo cha gari lao,Akaitazama astola yake na kukishusha kioo taratibu

“Shukeni ndani ya gari.” Askari aliwaamrisha na kuwamfaya Muntar kufyatua risasi mbili kwa haraka,milio ya risasi ikawafanya watu waliopo kwenye eneo kuanza kutawanyika kuokoa maisha yao.Askari wengine watatu waliopo katika eneo la tukio wakajibanza kwenye magari mengine wakiwa na bunduki zako na kuanza kujibu mashambulizi kuelekea kwenye gari la Muntar

 

“Rudisha nyuma gai hilo.”

Muntar alimuamuru dereva wake na akatii,Wakaligonga gari walilomo Agnes na Rahab na kulifanya lirudi nyuma na kuyagonga magari yaliyopo nyuma yetu.Rahab akaanza akaanza kufyatua risasi katika matairi ya gari la Muntar na kulifanya lipoteze muoelekeo hii ni baada ya breki za gari lao kushindwa kukamata vizuri na kugonga kwenye vyuma vya reli.Watu wa Muntari,mmoja baada ya mwengine wakaanza kujirusha nje ya gari wakiwa na bunduki zao aina ya ‘Short gun’ na kuendelea kufanya mashambuliza kwa askari.

 

Agnes akafungua mlango wa gari lao na kupiga goti moja chini,Bastola yake ikawa na kazi mija tuu ambayo ni kufyatua risasi kwa kila mtu wa Muntar.Muntar akazidi kuchanganyikiwa baada ya watu wake kuwaona wakiwa wanaanguka mmoja baada ya mwengine.Hadi akabaki akiwa na Kibopa ambaye wakati wote wezake wakipambana yeye alikuwa na kazi ya kujibanza kwenye gari lao

 

Muntar akaona nafasi pekee ni kukimbia,kwa bahati nzuri pembeni kuna pikipiki iliyo acha na raia aliyekuwa akijiokoa maisha yake kwa kuiamini sana miguu yake kuliko pikipiki.Akapanda na Kibopa akadanda kwa nyuma wakaondoka kwa kasi wakikatiza katokati ya njia za reli.

 

Agnes na Rahab wakaingia ndani ya gari,Agnes akalirudisha gari lao nyuma na kupata upenyo wa kuiwezesha gari yao kupita na kupita njia ambayo Muntar amekimbilia.Askari wakashindwa kufyatua risasi kwatika gari linalo wafukuzia majambazi kwani hawakujua walio wasaidia ni kina nani.

 

Muntar akazidi kukanyaga mafuta na kuingia barabara inayokwenda mikoani akikatiza katika kiplefti cha kwaminchi,Agnes akawa na gazi ya kupiga honi akiashiria watu waliopo barabarani kuwapiasha.Akazidi kukanyaga mafuta kwa kasi huku akiikaribia pikipiki ya Muntar.Kibopa akaanza kufyatu risasi kuelekea lilipi gari walilopo Agens.

 

“Shiti....” Rahab alizungumza huku akinang’ata meno yake,alikataka kujitokeza kwenye kioo cha gari ila akarudi ndani kwa haraka baada ya kioo kidogo cha pembeni kuvunjwa kwa risasi anazo zipiga Kibopa pasipo kuwa na utaratibu wowote.Gafla kibopa akalikwepa Scania linalo toka kwenye kiwanda cha unga Pembe maeneo ya Kange na karibia robo mbili ya gari imeziba barabara na kuachanisha uwazi mdogo unao weza kuiruhusu pikipiki kupi na kuendelea mbele kwa kasi.Agnes akafunga breki za gari lake kwa kasi na kuiingiza upande wa kulia kwake kukikwepa kichwa cha gari kubwa la unga,Gari karerereka pembeni ya barabara na kwakusadiana na Rahab wakaushika mskani wa gari na kuurudisha upande wa kulia 

 

Gari ikakaa sawa barabarani,kutokana na mstuko katika injini,gari ikazima katikati ya barabara na milago yote kujifunga.Kwa kutumia vitako vya bastola zao wakapasua vioo vya madirisha ya magari na kujitoa ndani ya gari lao,linalo toa mlio wa kuashiria linaitilafu sehemu

“R...itakuwaje sasa?”

“Ndio hivyo jamaa wamesha sepa.”

“Ngoja kwanza.” Agnes akaenda eneo lenye maegesho ya boda boda(waendesha pikipiki),

“Ni kina nani wanaweza kuendesha pikipiki kwa kasi kubbwa?”

 

Kila muendesha pikipiki akaa kimya huku macho yao wakiitazama bastola ya Agnes.

“Ohoo nahisi munaiogopa hii bastola? Mimi ni raia mwema ninaomba masaada wa kuwakimbiza wale watu walio pita hapa?”

”Dada mimi piki piki yangu haina mafuta?” Jamaa mmoja alizungumza huku akilivua kofia lake,wengine wote wakakataa.Rahab akafika eneo alipo Agnes

“Ag wanasemaje?”

“Hawataki?”

 

Rahab akapiga risasi moja hewani,kila dereva aliye ipenda rogo yake akaaruka kwenye pikipiki yake na kuchanganya kwato zake kuooa maisha yake.Rahabu akapanda kwenye moja ya piki piki aina ya Boxer,ambayo dereva wake aliisahau funguo yeke.Muntar kadri anavyozidi kuendesha pikipiki ndivyo jinsi mafuta yaliyozidi kuteketea,na taratibu piki piki ikaanza kugoma na mwisho wa siku ikagoma kabisa hata kusogea hatua mbele.Rahab akazidi kuvuta mafuta ya pikipiki waliyo panda,kwa mbali wakawaoana Muntari na Kibopa wakishuka kwenye pikipiki yao na kuinga pori.

 

                                                                                     ***

Shamsa baada ya kumuona Halima anaanza kuhangaika kwa sabuni ya unga aliyo mwagia usoni,kwa haraka akafungu mlango wa chumba na kuaanza kukimbia kuelekea zilipo ngazi za kushuka.

 

Anna kwa haraka akashuka kwenye ngazi na kuanza kumshindilia mateke Karim ambaye amechoka kwa kiasi kikubwa sana.Karim akajihahidi kujiinua ila Anna akawa makini kwa kila jambo na kwa haraka akaiwahi shingo ya Karimu na kuizungusha kwa nguvu na kuivunja.Kitendo cha Karimu kuuawa kikashuhudiwa na Shamsa ambaye ndio yupo kwenye harakati za kujiokoa kutoka mikononi mwa Halima.

 

Anna hakumjali Shamsa ambaye amesimama kwa mshangao akiwa haamini kwa kitu kilicho tokea kwa mpenzi wake anaye mpenda kuliko kitu cha aina yoyote.Kwa haraka Shamsa akashuka kwenye ngazi kwa hasira na kumrukia Anna ambaye akajibamiza kwenye ukuta,Shemsa akajaribu kumrukia Anna ambaye alifanikiwa kumkwepa na kwa bahati mbaya Anna akamsukuma Shamsa ambaye akaanza kwenda chini kutoka gorofa ya nne hadi kwenye sakafu na kichwa chake kikapiga chini na kikapasuka mbele ya macho ya polisi na baadhi ya wateja wengine

 

Anna taratibu akapiga hatua na kuchungulia sehemu aliyo angukia macho yake yakakutana na askari tishio ambaye ni mpelelezi wa kutegemewa nchini bwana Jackson Luther

 

                                                                                      ***

Rahab anazidi kuvuta mafuta ya pikipiki hadi kwenye njia walio ingilia Muntar na KIbopa mbao walizidi kuongeza mwendo wa kukimbia baada ya kuiona pikipiki ikiwafwata kwa kasi nyuma yao.Kwa bahati mbaya Muntar  na  Kibopa waliishiwa risasi katika silaha zao,kila mmoja akakimbia kwa upande wake anao ujua yeye ili kutaokoa maisha yake,Rahabu akapunguza mwendo wa pikiki na Agnes akaruka na kukimbilia njia aliyo kwenda Kibopa,Rahab akapita njia aliyo kwenda Muntar.


Muntar akajibanza kwenye mti na kuokota gongo kubwa na kulishika kwa umakini.Gafla Rahab akajikuta akiichia pikipiki na kuanguka chini hii ni baada ya kupigwa gongo la kifua na Muntar akajitokeza mbele yake huku akiwa na gongo mkononi



ITAENDELEA....




Ilipoishia....

.....Rahabu akapunguza mwendo wa pikipiki na agnes akaruka na kukimbilia njia aliyo kwenda kibopa,rahab akapita njia aliyo kwenda muntar.Muntar akajibanza kwenye mti na kuokota gongo kubwa na kulishika kwa umakini.Gafla rahab akajikuta akiichia pikipiki na kuanguka chini hii ni baada ya kupigwa gongo la kifua na muntar akajitokeza mbele yake huku akiwa na gongo mkononi....


Edndelea....

.....Rahab akanyanyuka haraka,akamtazama muntar ambaye alianza kucheka kwa dharau akimtazama rahab kuanzia juu hadi chini.Muntar akarusha gongo kwa kutumia nguvu nyingi,rahab akalikwepa na kurusha teke lililotua shingoni mwa muntar na akaayumba,kabla hajajiweka sawa rahab akampiga muntar ngumi kadhaa za kifua na kuzidi kumfanya muntar kuyumba mithili ya mtu aliyelewa kwa pombe za kienyeji.(mataputapu).

Muntar akajaribu kurusha ngumi ila rahab akafanya maamuzi ya haraka katika kuudaka mkono wake wa kulia,akajigeuza na kwakutumia bega lake akauvunja mkono wa muntar.Kilio cha maumivu makali kikamkumba muntar.Pasipo kuwa na huruma rahab akampiga mtama muntar na kumfanya aliachie gongo alilolishika.Rahab akaliokota gongo na kuanza kumpiga muntar gongo la kichwa hadi damu nyingi zikaanza kutoka nje kwa kasi kama bomba la maji lililo pasuka sehemu ndogo.


 Kibopa akafunga breki za miguu yake baada ya kukutana uso kwa uso na agnes.Kibopa akameza funda kubwa la mate huku mwili wake ukimtetemeka kiasi kwamba akabaki akiwa hajajua nini la kufanya.Agnes akaachia tabasamu pana baada ya kuiona surulia ya kibopa ikianza kuchora ramani ya kutota kwa mikojo aliyo shindwa kuizuia.

“ni....Iisssa...Mehe”


Kibopa alizungumza kwa kigugumizi kikali,agnes akapiga hatua hadi alipo simama kibopa na akamtisha kama anampiga ngumi ya uso,kwa woga uliokithiri ukammdondosha kibopa chini kama mzigo na akaanza kulia kama mtoto mdogo

“khaa wewe si jambazi,mbona unalia sasa?”


“mimi ni nilikuwa kibaraka waoo tuu,sioooo jambaazzziiii” kibopa alizungumza kwa kuyavuta vuta maneno kama amemeza fumba la uji wa moto na anashindwa kuumeza.Agnes akamtazama kwa huruma kipopa ambaye taratibu alianza kupiga magoti akimuomba msamaha.Agnes akampiga kofi la shavu kipopa na kumuamuru kusimama

“wenzenu wapo wapi?”

“wameshakufaa”

“changanya mbaliga zako,kabla sijabadilika”

“eheee....!!”


Agnes akampiga kibopa teke la makalio huku akimsindikiza na kofi la mgongoni na kumfanya kibopa aanze kukimbia kwa kasi kubwa.Agnes akabaki kucheka kwani hakutarajia kama ataweza kukutana na mwanaume muoga kama kibopa.


                                          *****


Jackson luther mpelelezi anaye sifika kwa kazi yake nzuri akaanza kupandisha ngazi kwenda juu alipo anna kwa lengo la kumtia nguvuni kwa kosa la mauaji.Anna akaanza kukimbia akipandisha ngazi kwa kasi hadi akafika alipo waacha wezake.

“tuondokeni kimenuka”


Wakasaidiana kumkokota fety ambaye amechoka sana kwa kazi ya kupambana na karim pamoja na shamsa.Wakaingia ndani ya lifti na kushuka hadi gorofa ya kwanza,jackson akaitoa bastola yeka na kuwa makini zaidi,taratibu akaanza kuuunguza mwili wa muntar na kuhakikisha kwamba uhai wa mwili huo umesharudi kwa Mungu baba.

Kitu ambacho kinamchanganya jackson luther ni juu ya nani aliyeweza kumuua karim kwani ni miongoni mwa majambazi ambao alijaribu kuwafuatilia kwa kipindi kirefu pasipo kupata mafanikio ya aina yoyote katika kazi ya uchunguzi wake.Akapandisha hadi gorofa ya tano alipomuona anna akimalizikia na akakuta korido ikiwa haina mtu hata mmoja.


Akachunguza sehemu yote na kumkuta mtu aliye anguka chini akiugulia maumivu na mlango wa kuingilia chumbani kwake ukiwa upo wazi, akamsogelea na kumpa mkono na kumuinua kutoka alipokuwa.


“umepatwa na nini?”

“kuna wadada bwana hapa,walikuwa wakipigana na kuniangusha”

“umeumia?”

“ndio nimepiga kiuno chini.”

“wameelekea wapi?”

“hata sijui wametoka vipi humu ndani kwangu”

“sawa”


Anna,fetty na halima wakaingia kwenye jiko kuu la kupikia vyakula kwa kutumia mlango wa chini wakashuka kwenye ngazi na kutokezea upande wenye maswimcming pool katika hotel,wakawatizama watu waliomo ndani ya hotel na kuona hakuna anayewatilia mashaka kwa mwendo wa umakini wakaanza kuelekea kwenye sehemu lilipo gati la kuingilia hotelini.Kabla ya kutoka nje ya geti walinzi wakawasimamisha,kwa jicho la kuiba fetty kwa kupitia kioo cha dirisha la kijumba cha walinzi akaona video inayomuonyesha akipambana na shamsa kupitia kwenye tv ndogo iliyopo kwenye kijumba cha walinzi


                                            *****


Rahab alipo hakikisha amekipasua kichwa cha muntar kwa kukipiga magongo,akatafuta sehemu chini ya mti na kukaa huku akiyasikilizia maumivu makali ya kifua aliyopigwa kutokana na kupigwa gongo.Agnes akaanza kumtafta rahab na kwabahati nzuri akamkuta akiwa amekaa chini ya mti

“shost umempata huyo mjinga?”

“ndio”

“umemuua?”


“hapana,nimemuachia aende zake kwa maana nimeona hana hatia.”

“mpumbavu kweli wewe,unadhani atashindwa kwenda kujipanga na kuja kutudhuru?”

“atatupatia wapi?”

“wewe mjinga nini?” rahab alizungumza kwa hasira kubwa.

“mpumbavu mwenyewe unadhani kila mtu ni wakumuua,mtu gani huna roho ya huruma”

“ila kumbuka ni nini tulichoamua”


“si tumesha kamilisha kama ni muntar kufa umesha muua,sasa kwa nini damu nyingine zije juu yetu pasipo kuwa na sababu ya msigi”

“katika siku ambazo ag nikuona kuwa wewe ni mjinga,limbukeni,poyoyo ni leo”

Rahab aliendelea kuzungumza kwa dharau iliyo changanyikana na hasira kali

“mimi poyoyo si ndio?” agnes alizungumza kwa hasira

“ndio wewe poyoyo”


Agnes akamsukuma rahab na kumfanya rahab kunyanyuka kama mbogo mkali aliye punyuliwa na risasi,akamrukia agnes kwa kutumia teke lake na kumuangusha agnes chini.Agnes akampiga mtama rahab na kumuangusha chini,wakaanza kushikana nywele zao na kuanza kuminyana huku wakipiga piga kelele.


“rahab nitakuua”

“niue kama unaweza”

Agnes akamuachia rahab nywele na akasimama.Rahab akamtazama kwa jicho kali agnes na akachia msunyo mkali

“rahab hebu tuache maswala ya kitoto,sisi ni marafiki kitu kinacho tufanya haswa tugombane ni nini?”


“wewe si ndio mzembe,unafanya vitu vya kijinga”

“sio vitu vya kijinga,kuna mambo yakufanya na mengine sio ya kufanya.Hivi rohoni mwako unaroho gani hadi umuue mtu asiye ha hatia”

“agnes hebu mtazame yule mjinga alivyokuwa akitumiminia risasi,unadhani angetuua ingekuwaje?”


‘ila haijawa,cha msingi tufanya mpango turudi tunapo ishi”

Agnes akampa mkono rahab na kumnyanyua,wakauvuta mwili wa muntar na kuuficha kwenye kichaka.Agnes akaikagua pikipiki na kukuta haijaharibika sana zaidi ya kuvunjika kioo cha pembeni cha upande wa kushoto.Agnes akaiwasha pikipika na rahab akapanda kwa nyuma na kuondoka porini na kutokea barabara kuu iendeyo mikoani na safairi ikaendelea                                                                                                                                                                                                                    

                                          *****

 

“hamruhusiwi kutoka humu ndani”

Mlinzi mmoja alizungumza huku akiwazuia anna,fetty na halima wasitoke,wakaongezeka walinzi wawili wakasimama mbele yao huku mikononi wakiwa na bunduki zao

“kwa nini,huturuhusiwi kutoka?” anna aliwahoji

“kwa sababu maalumu.Tunawasubir......”


Fetty hakumuacha mlinzi kumaliza sentensi yake,akamtwanga kichwa kilichomfanya mlinzi kuishika pua yake iliyoanza kuvuja damu.Kwa shambulio hilo walinzi wengine wakawa wameduwaa kumuona mkubwa wao akivujwa na damu.Anna na halimwa kwa utaalamu mkubwa wakawapokonya walinzi bunduki zao,

“polisi”


Sauti ya jackson luther ikasikika kwa nyuma ikiwaamrisha fetty na wezake kutulia kama walivyo huku akiwa ameishika bastola yake kwa umakini.Anna akageuka kwa haraka na kufyatua risasi moja iliyompiga jackson luther kwenye paja la mguu wa kushoto na kumfanya aanguke na bastola ikaangukia mbali na alipo.

Mlinzi mmoja akajaribu kumrukia halima ila risasi ya bunduki  iliyotua tumboni mwake ikamfanya arudishwe nyuma na kuanguka kama mzigo wa kuni.Macho ya jackson luther yakatazama na macho ya anna akajaribu kuunyoosha mkono wake kwenye bastola yeka ila akastukia risasi nyingine ikitua kwenye mkono wake na kumfanya jackson luther kutoa ukulele mkali wa maumivu.

Fetty akamvuta kwa haraka askari aliye mpiga kichwa na kumchomolea bastola iliyopo kiunoni mwake.

“waamrishe wezako kutufungulia geti”


Fetty alizungumza huku bastola akiwa ameielekezea kwenye kichwa cha mkuu askari wa hoteli,akawaamrisha wezake waliopo kibandani na wakalifungua geti linaloendeshwa kwa umeme.Wa kwanza kutoka akawa ni halima,akawaamuru watu waliomo ndani ya gari la kifahari aina ya range rover linalo ingia kwenye hoteli.

Vijana wawili wa kiarabu waliomo ndani ya gari wakashuka na kulala chini.Halima akaingia na kuwasubiria fetty na anna ambao nao wakingia kwa na kuondoka hotelini wa kasi,gari mbili za polisi zilizokuwa zinafika hotelini baada ya kupigiwa simu na wasamaria wema zikaanza kuwafukuzia kwa nyuma.

Wakiwa ndani ya gari fetty akatoa simu na kumpigia dokta willim huku akizitazama kwa nyuma gari za polisi zinazo kuja kwa kasi

“vipi kazi imekwenda vizuri?”

“ndio ila kuna tatizo limetokea”

“tatizo gani?”

“tumezidiwa ng............”


Fetty hakumalizia sentesi yake na akajikuta akijigonga kichwa kwenye kioo na gari yao ambayo ilikumbwa na lori la kubebea mchanga ambalo halima ajiribu kulipita kwa kupitia upande wa kushoto kinyume na sheria za barabara,gari ikaanza kuserereka ndani ya mtaro kwa kasi ya ajabu kwa ubavu wa kustoto aliopo fetty na kugonga kwenye karavati la barabara na kusababisha gari kuminyika minyika vibaya sana  na gari moja ya polisi ikamshinda dereva wake kuwahi kufunga breki na ikajikuta ikiligonga lori kwa nyuma na kupenya chini ya uvungu wa lori na kusababisha askari wote sita waliopo ndani ya gari,miili yao kugawanyishwa vipande viwili


                  She is my wife(ni mke wangu)……6


Ajali hii mbaya ikaanza kuwakusanya wananchi waliopo jirani na eneo la ajali,kila mmoja akijaribu kujua ni nini kinacho endelea.Halima akawa wa kwanza kujichomoa ndani ya gari,sehemu kidogo ya paji lake la uso ikiwa imechanika kidogo na kumwaga damu.Anna akajiminya minya kwenye siti aliyoikalia na kufanikiwa kutoka nje ya gari.Ila ikawa ni tofauti kwa fetty ambaye amepoteza fahamu.Kabla hawajaanza kumsaidia kumtoa fetty wakashuhudia gari la polisi likisimama sehemu walipo pata ajali wezao na askari wote wakaruka ndani ya gari lao wakiwa na bunduki mikononi

“anna tuondoke”

“na fetty je?”

“twende nimekuambia tutarudi kumchukua”


Halima hakuwa na haja ya kubaki eneo la tukioa kwa maana tayari askari walishaanza kuwasaka.Wakajichanganya katikati ya askari na kuanza kukimbia kwa wakikatiza mitaani.Wakafanikiwa kufika nje ya baa moja na kumkuta mtu mmoja akishuka kwenye gari lake.Kabla hajaufunga mlango wa gari lake wakamvamia na kumuamrisha atoe funguo za gari lake

“nyinyi kama kina na......”


Jamaa hakumalizia sentesi yake akapigwa kigoti ya tumbo na anna akabaki akiwa amejishika tumbo,akazitoa funguo za gari lake aina ya ‘premore’.Anna akazichukua funguo za gari na wote wakaingia na kuondoka na kumuacha jamaa akipiga kelele za mwizi


“gari yangu ya mkopo ina wiki ya pili ile” jamaa alizungumza huku akimwagikwa na machozi,mbaya zaidi hakuna mtu aliyepo katika eneo la baa aliyeweza kutoa msaada wowote kwao


                                                  *****


Askari  wakamchomoa fetty ndani ya gari na kumfunga pingu japo ajitambui kwa lolote.Wakamuingiza ndani ya gari lao na kumpeleka hospitali ya taifa muimbili huku akiwa chini ya ulinzi mkali.Wakamkabidhi kwa madaktari ambao pasipo kupoteza muda wakaanza kummuhudumia


“tunaomba mumfungue pingu za mikononi”

Daktari mmoja alizungumza na askari mmoja akatii ombi la daktari.Matibabu yakaanza kufanyika kwa haraka.Wakagundua fetty amepeta mstuko tuu uliomfanya kuweza kupoteza fahamu.


                                           ****


Pikipiki waliyopanda rahab na agnes haikuwa na mafuta ya kutosha,ikawazimikia maeneo ya saruji na kwa bahati nzuri wakapata lori linaloelekea dar es salaam ambalo linasafirisha mifuko ya saruji(cement).Wakafika eneo la kuingilia kwenye msitu kulipo na handaki lao.

Wakamuomba dereva kuwashusha,wakawashukuru na kuanza kutembea kwa miguu kuelekea ndani ya msitu, hii ni baada ya gari walilolipanda kuondoka.Japo kuna giza ila wakajiamini sana,wakiwa njiani gafla wakaona taa za gari zikija kwa nyuma yao.Gari ikasimama pembeni yao,anna akafungua kioo cha gari 


“vipi nyinyi?”

“safi”

“ingieni ndani ya gari”

Rahab na agnes wakaingia ndani ya gari na safari ikaendelea.

“jamani fetty yupo wapi?” agnes aliuliza

“wee acha tuu,tumepata ajali mbaya”

“amekufa......!!?” rahab aliuliza kwa mshangao

“hajafa ila alipoteza fahamu na isitoshe,askari walikuwa wanatufukuza

“sasa itakuwaje jamani?”

“mmmm hapa nilipo mimi nimechanganyikiwa”


Wakafika kwenye handaki na kitu cha kwanza kukifanya ni kufungua tv yao kuangalia kama kuna taarifa yoyote inayo endelea.Hawakukuta chohote kinachoendelea

“hivi vyombo vya abari vya ajabu kama nini?”

Rahab alizungumza huku akiachia msunyo mkali na kuingia chumbani kwake.Agens akaanza kuwahudumia wezake majeraha waliyo yapata


“jamani tunafanyaje?”

“inabidi tujue ni wapi alipo fetty,ikiwezekana tukamuokoe sisi wenyewe pasipo msaada wa mtu yoyote”

Anna ilo ulilolizungumza ni kweli,ila ni wapi tutapata magari ya kutumia kwa maana hapa yanaitajika magari si chini ya matatu”


“mumezungumza na huyo babu?”

“nani?”

‘si huyo dokta”

“fetty ndio alikuwa akizungumza naye kabla ya ajali,ngoja”

Anna akatoa simu yake mfukoni na kumpigia dokta william

“anna mbona mmekuwa wazembe kiasi hicho?”

Sauti ya dokta william iisikika kwenye simu baada tu yakuipokea


“badala ya kutuuliza tunaendeleaj,wewe unajidai ukituambia kuwa sisi ni wazembe.Si ungeifanya kazi yako wewe mwenyewe?”

Anna naye alizungumza kwa hasira

“hata kama sijawafundisha hivyo,nyinyi mlitakiwa mtumie akili”

“akili ehhee”


Halima akampokonya anna simu na kuiweka sikioni mwake

“nisikilize wewe mzee kwa umakini,sisi hatukuwa na la kufanya zaidi ya kufanya kile tulicho kifanya.Sasa ni hivi tunakupa masaa mawili uje huku ukiwa na jibu ni wapi alipo pelekwa fetty la sivyo......Utaisoma namba kama ni ya kirumi,kichina au kimakonde.”


Halima akaikata simu na kumrudishia halima.

“jamani,mimi nimechoka ngoja nijipumzieshe”

Agnes alizungumza na kuingia ndani kwake.Anna na halima wakabaki wakiwa amejilaza kwenye masofa,kila mmoja akitafakari kitu cha kufanya akilini mwake


Asubuhi na mapema dokta william akawasili kwenye handaki.Hadi anaingia hakuna aliye msalimia zaidi ya kutazamwa kama kinyago

“habari yenu”

“salama”

“ehee agens vipi kazi ya tanga mmeifanikisha?”

“ndio ila kwa shida kubwa”

“ehee na nyinyi?’

“kwani hujui”


Anna alijibu kwa dharau huku akitafuna taratibu popkone zilizopo kwenye kifuko.Dokta william akashusha pumzi nyingi huku akiwatazama halima na anna.

“fetty yupo katika hospitali ya taifa muhimbili,ila yupo chini ya unagalizi mkubwa wa madaktari na askari wenye silaha kali”

“tutampataje?” anna aliuliza

“kikubwa ni kusubiri siku ambayo atasafirishwa kupelekwa gerezani

“alafu.....”


“ndio tunaweza kufanya harakati za kumuokoa”

“dokta hivi unadhani,mwezetu atajisikiaje.Kama atakaa hospitali mwaka basi tusubirie tuu?” anna alimuuliza dokta william huku akimtazama kwa macho makali

“sijamaanisha hivyo....”

“kwani hapa ulisemeje? Si umesema hadi siku atakayo pelekwa hospitali ndio tukamuokoe au?”

“anna kuwa mpole,”

“sio niwe mpole.Fetty kwetu ni muhimu sana kuliko unavyo fikiria”


“oya anna kausha mwanagu tumsikilize dokta atakacho kizungumza,kupanick haisaidii kitu” rahab alimkanya anna na akakaa kimya

“sikilizeni,fetty anataokolewa kesho hospitalini.Atasafirishwa muda wa saa mbili usiku kupelekwa gereza la segerea”

‘”ngoja kwanza,watapitia njia ipi?”

“kwa njia bado sijafahamu,ila watatumia magari matatu yanayo fanana.Gari moja atakuwepo fetty na gari mbili watakuwepo midoli inayo fanana na fetty”

“sasa hapo itakuwa vipi?”


“muda wote mutawasiliana na mimi,kutokana mimi ndio ninaye shughulika na utengenezaji wa madoli yanayo fanana na fetty”

“je niwapi sisi tutapata usafiri?”

“kuhusiana na hilo wala musijali,kikubwa ni kuwa makini kwa kila jambo na kitu kikubwa ni kujipanga vizuri.Sitaki kutoke tatizo la kijinga”

“sawa”

Dokta william akaondoka zake na kurudi jijini dar es salaam


                                           *****


Gari tatu aina ya gvc zilizotolewa kama msaada kutoka katika serikali ya marekani na kukabidhiwa katika jeshi la polisi nchini tanzania.Zipo tayari nje ya hospitali ya muhimbili kwa ajili ya kumsafirisha fetty ambaye anahesabiwa kama jambazi sugu.Ulinzi mkali unazidi kuhimarishwa kwenye eneo zima la hospitali ya muhimbili kila gari linaloingia na kutoka ni lazima liweze kukaguliwa na askari.

Kuanzia majira ya saa kumi na mbili asubuhi waandishi wa habari wamepiga kambi katika hospitali ya taifa muhimbili kusubiria kumuona fetty ambaye amepata umaarufu katika wakati mchache,hii ni kutokana na mkuu wa jeshi la polisi kutoa siku kumi na mbili za kujisalimisha kwa halima na anna.


Anna,rahab,agnes na halima wapo tayari kwa ajili ya kazi moja tuu,yakumuokoa fetty kutoka mikononi mwa askari.Wote wanne wamevalia nguo nyeusi na viatau vya jeshi vyenye rangi nyeusi.Vifuani wamevalia majaketi ya kuzuia risasi kupenya.Kila mmoja katika suruali yake aliweza kuchomeka magazine zipatazo kumi zilizo jaa risasi za kutosha.Mabomu ya kurusha kwa mkono kila mmoja aliweza kubeba ya kutosha kadri ya mtu alivyo kadiria kuona yanamtosha kwa kazi iliyopo mbele yao.Kila mmoja alachukua bunduki anayo ipenda yeye mwenye.

“kila mmoja yupo tayari?” rahab aliuliza

“ndio”


Kwa pamoja wakaikutanisha mikono yao ya kulia wakiwa wakekunja ngumi huku viganja vyao vikiwa vimefunikwa na gloves ngumu za rangi nyeusi tuu

“kwa umoja tunaweza”

Waliizungumza kauli mbiu yao,inayowafariji kila wanapofanya jambo la pamoja

“jamani msiniache nife usiku wa leo”

Rahab alizungumza huku akiwatazama wezake machoni kwa umakini

“hakuna atakaye kufa,tunakwenda wanne na tunarudi watano” halima aliweka msisitizo


Wakakumbatiana kwa pamoja kisha wakaachiana.Wakaanza kutoka ndani y a handaki lao mmoja baada ya mwengine.Wakazitazama gari tatu zilizopo mbele yao aina ya ferrali zilizo letwa na dokta william alizoziagizia kutoka nchini china.Kutokana na uwezo wa kifedha alio nao dokta william gari hizo ziliweza kusafirishwa kwa haraka na kuingizwa tanzania kwa njia magendo zikipokelewa mpakani mwa kenya na tanzania uliopo mkoani tanga.Kila dereva ambaye aliweza kuzifikisha gari hizo kwenye handaki aliuawa kwa kupigwa risasi dokta william kwa lengo la kuficha siri ya lilipo handaki lao

“hei mnanisikia” 


Anna alizungumza huku akikirekebisha kinasa sauti chake alicho kichomeka sikioni.Kila mmoja akamjibu amemsikia kutokana wote walikuwa na vinasa sauti hivyo ambavyo vinaweza kuwasaidia katika mawasiliano kati yao pamoja na dokta william.Wakaingia kwenye magari yao huku anna akiwa gari moja na agnes.Halima na rahab kila mmoja akiwa ndani ya gari lake.Saa zao za mikononi zinawaashiria ni saa moja na nusu usiku.Na muda uliopangwa kwa fetty kupelekwa gerezani ni saa mbili na dakika tano usiku.


Kwa mwendo kasi wa gari zao wakafika maeneo ya muhimbili na gari zao wakazisimamisha umbali kidogo kutoka lilipo geti la kuingilia hospitaini.Rahab kwa kutumia darubin akaweza kuyaona magari matatu meeusi yakitoka katika geti la hospitali huku mbele yao zikiwa zimetangulia pikipiki tatu za polisi.Gari zote zimefungwa vioo ambavyo ni vyeusi

“mnanisikia mabinti”

Sauti ya dokta william ilisikika katika vinasa sauti walivyo vichomeka masikioni mwa


“ndio”

“sasa sijui mumeshafika eneo la tuukio”

“ndio”

“mumeziona hizo gari zinazo toka?”

“ndio”

“zote zinamidoli,inayo fanana na fetty”

“sasa dokta mbona unatuchanganya sasa”

“tuli,kuna kagari chenye bodi chakavu aina ya taksi kitatoka kama dakika tano zijazo”

“hicho kigari ndipo alipo fetty”

“hapana”

“ila?”


“hicho kina askari wapelelezi wapatao wanne,ambao wao watapita njia za panya kuhakikisha wanakwenda kumpokea fetty maeneo ya kimara na fetty anapelekwa iringa na sio segerea kama tulivyo tarajia”

Anna akashusha pumzi nyingi kila mmoja hakujua kama lengo litabadilika

“hiyo ni plan b iliyo badilishwa muda mfupi kabla ya fetty kupelekwa segerea”

“yeye fetty anatapitishwa njia gani?”

“kuna bomba la maji machafu lililopo chini ya ardhi ndilo atakalo pitishwa fetty,askari waliopo kwenye bomba hilo wapo sita.Na wanatembea kwa miguu”


“duu,na zile gari tatu?”

“zile ni danganya toto.Na zile zote zinakwenda segerea na zitapita njia tofauti.Ninacho waambia mimi kiaminini”

“ni muda gani watatumia hadi kufika kimara?”

“kama lisaa na nusu kutokana wanatumia miguu”

“hiyo nayo ni mpya,sasa ni kimara gani kwa maana zipo nyingi?”


“kikubwa ifwateni hiyo taksi tena kwa umbali mkubwa na ikiwezekana muifwate kwa gari moja tuu ili wasistuke kwani wote waliopo humo ni watu hatari sana”

“tumekupata,baby’s kazi ni kwetu tondokeni” rahab alizungumza na gari zao wakaziwasha na kuondoka kwa mwendo wa kawaida


                                             *****


Hata fetty mwenyewe hakutarajia kama atapitishwa kwenye bomba kubwa la maji machafu,ambalo maji yake yalizuiwa kwa muda ili kuwafanya wao kupita kiurahisi.Fetty akiwa kwenye vazi la kiaskari aliweza kufanana mavazi na askari wanao mshikilia.Tofauti yao iliyopo kati yao ni fetty yeye ni mualifu amefungwa pingu za mikononi na kufungwa cheni nene na ndefu miguuni ila askari wangine watano ni wanaume wenye silaha huku askari mwengine wa kike aliye tengenezwa sura kama fetty na kimo kikiwa ni sawa,ni tofauti sana kwa mtu yoyote kuweza kumgundua.Isitoshe na yeye amefungwa pingu za mikono ila miguuni hakufungwa kitu cha aina yoyote


Harufu ya maji machafu haikuwazudia wao kusonga mbele wakitumia tochi kubwa zilizo wasaidia kuona mbele.Akili ya fetty ikawa na kazi ya kumchunguza mmoja baada ya mwengine na akaapia akipata nafasi yoyote ni lazima ajiokoe kuliko kwenda kunyongwa kisiri kwani ndio mazungumzo aliyoyasikia wakizungumza askari kipindi amelazwa wodini.Gafla fetty akajiangusha na kujifanya amepoteza fahamu,kwa umahiri mkubwa akazibana pumzi zake na kuyafanya mapigo yake ya moyo kupoteza muelekeo.


“bosi tumepata tatizo,over”

Askari mmoja alizungumza kwa kutumia simu ya upepo

“tatizo gani? Over”

“amepoteza fahamu huyu binti,over”

“fanyeni chochote,ila muhakikishe munatoka naye,over”

“sawa mkuu.Over”


Askari mmoja mwenye mwili mkubwa akamnyanyua fetty na kunuweka begani mwake na safari ikaendelea.Fetty akayafumbua macho yake na kuona askari aliye mbeba ndio wa mwisho katika mstari wanao tembea,kwa ustadi wa hali ya juu,fetty akaichomeka mikono yeke katikati ya shingo ya askati,kwakutumia pigu akaanza kumnyonga askari huku akiwa ameninginia kwa nyuma.Mikoromo ya asakri ikawastua wezake waliopo mbele kitendo cha wao kugeuka wakamkuta mwenzo ndio yupo kwenye hatua za mwisho huku macho yake akiwa ameyatoa nje....


Itaendelea.......




Ilipoishia

Askari mmoja mwenye mwili mkubwa akamnyanyua Fetty na kumuweka begani mwake na safari ikaendelea.Fetty akayafumbua macho yake na kuona askari aliye mbebe ndio wa mwisho katika mstari wanao tembea,Kwa ustani wa hali ya juu Fetty akaichomeka mikono yeke katikati ya shingo ya askati,kwakutumia pigu akaanza kumnyonga askari huku akiwa amening'inia kwa nyuma.Mikoromo ya asakri ikawastua wenzake waliopo mbele kitendo cha wao kugeuka wakamkuta mwenzo ndio yupo kwenye hatua za mwisho huku macho yake akiwa ameyatoa njee


ENDELEA

Askari mmoja akataka kufyatua risasi ila mkuu wa masafara akamzuia,Fetty akaiachia shingo ya askari huku akiwa amehakikisha kwamba askari huyo yupo kwenye hali mbaya sana.Askari mmoja akampiga Fetty kwa kutumia kitako cha bunduki na kumfanya  Fetty ajikunje huku akitoa mguno mkali wa maumivu

“Kumbukeni kuwa,anahitajika akiwa hai”

Mkuu wao alizungumza

 

“Sawa mkuu,ila anahitaji kupata kibano kidogo”

Wakaendelea kumtazama mwenzo,ambaye hadi hapa alipo hali yake haipo vizuri sana.Vichwa vya askar vikaanza kupata moto kwani mwenzao ambaye alikuwa anakaribia kunyongwa ndio anaye fahamu njia ya bombo hilo japo imenyooka ila kuna sehemu mbele imegawanyika katika njia nne.Mwenzao anayejulikana kama inspector Julio hawezi kuendelea mbele na safari

 

“Mkuu kuna tatizo jengine limejitokea,Over”

“Nini tena inspector John? Over”

“Huyu binti alimkaba Inspector Julio,Over”

“Nyinyi mulikuwa wa hadi mwenzetu akabwe?”

Sauti ya mkuu wao ilizungumza huku akiwa anafoka,

“Mkuu alizimia,ndipo inspector Julio alipo amua kumbeba”

“Pumbavu zenu.Hakikisheni anatoka huyo binti,akiwa hai na Julio naye akiwa hai”

 

Fetty akatabasamu huku akiwatazama askari,kwani kwake kazi yake imeshaanza kuwa nyepesi kwani mtu ambaye anamuhofia ni huyu Inspector Julio,ambaye kwa mtazamo wake tu anaonekana ni mtu hatari sana katika swala zima la kutumia silaha.Askari mmoja akasimama mbele ya Fetty huku akiwa amempa mgongo akisaidiana na wezake katika kumpa huduma Inspector Julio,huku kazi yake ikiwa ni kuzifungua kamba za viatu vya Julio

 

Kwa umakini wa hali ya juu,Fetty akazichomoa funguo nyingi zinazo ning’inia kiunoni mwa askari huyo pasipo yeye mwenyewe kujua.Kwa bahati nzuri katika wingi wa funguo hizo zipatazo kumi na mbili,mbili ni funguo za pingu.


Macho ya Fetty yakawa na kazi ya kuwatazama askari jinsi wanavyo pata shida katika kumsaidi mwenzao ambaye hali yake inazidi kuwa mbaya.


Hakuna askari aliye kuwa na muda wa kumtazama Fetty kwani wanaamini kile kitako cha bunduki alicho pigwa kwenye tumbo,bado anaendelea kukisikilizia maumivu yake.Fetty akafanikiwa kufungua pingu za mikono pasipo askari yoyote kugundua.Akajaribisha kufungu mnyororo wa miguni ila akashindwa kwani hakuna funguo inayo ingiliana na kufuli alilo fungwa miguuni.

 

“Ja............ama..ani mmmim...i siwezi ku...pona.Ila,njia uki...oony......sha utaku...nja kulia...kwenye shimo lenye mlang....o wa....”

Inspector Julio alizungumza kwa shida na hakuweza kumalizia sentesi yake,mauti yakamchukua.


Inspector John akanyanyuka kwa hasira na kumfwata Fetty sehemu aliyo kaa.Kufumba na kufumbua akajikuta akirushwa juu kimo cha mbuzi  tena beberu na kutua chini kama mzigo.


Hii ni baada ya Fetty kuikutanisha miguu yake kwa pamoja,Kisha mikono yake aliikita chini na kujizungusha kwa kasi kubwa.Askari walio salia wakiwa wanamtizama mkuu wao.Fetty akajinyanyua kwa haraka na kumvaa askari aliye mchomolea funguo,akaichomoa bastola ya askari huyo ambaye alijitahii kumpiga ngumi  za mbavu Fetty

 

Bila ya huruma Fetty akafyatua risasi iliyo penya kwenye kichwa cha akari anayepambana naye na kumtuliza kimya.Askari watatu wa kiume wakazikoki kwa haraka bunduki zao na kuanza kuzifyatua risasi,ila kwa haraka sana kama tairi la gari liendalo kwa kasi sana,akawa na kazi ya kubiringika huku akiwafwata askari kwenye miguu yao mita chache kutoka alipo.


Akiwa anabiringika, bastola iliyopo mkononi mwake ikawa na kazi ya kufyatua risasi zilizo waangusha askari watatu chini na akabaki Inspector John na askari wa kike aliyetengenezwa kama yeye,na wakati wote tukio  la wezake kuangamizwa lilimpa kiwewe hadi akawa na kazi ya kuyaziba masikio yake akiziba asisikie milio ya risasi.Fetty akalala katikati ya miguu ya Inspector John huku mdomo bastola yake akiwa ameuweka kwenye sehemu za siri za Inspector John.Bunduki ya inspector John akawa ameilekezea kwenye kichwa cha Fetty ambaye macho yake yanatazamana na macho ya Inspector  John

“Shoot ni kushooti”

Fetty alizungumza huku akitabasama,na bastola yake akawa na kazi ya kuigusisha gusisha kwenye vitenesi vya Inspector John


 *************

Gari waliyopanda askari wapelelezi ikazidi kuongeza mwendo,huku kila mmoja akiwa na bastola yake mkononi.Kwa uelewa wao mkubwa katika kazi yao ya upelelezi wakagundua kuna gari tatu ambazo kwa Tanzania ni watu wachache sana ambao wanazimiliki kutokana na gharama zake kuwa ni kubwa sana.

“T upo tayari?”

“Ndio Y”

“l je?”

“Ndio Y”

“X je?”

“Ndio Y”

 

Askari hawa waliweza kupeana herufi za moja moja kurahisishana kuitana majina waliyo pewa kazini au na wazazi wao.


Y ndio kiongozi wao mkubwa ambaye ndio dereva wa gari hili ambalo kwa mtazamo wa bodi(umbo) lake la nje,inaonekana ni chakavu Ila injini yake na vifaa vingine ni vipya na inauwezo wa mwendo kasi 250 KM/H.


Kila mmoja akawa na kazi ya kuzitazama gari hizo zinazo wafwata kwa mwendo kama wanao kwenda nao

Rahab akiwa ametangulia gari lake mbele akawawashia wezake taa  huku akikanyaga breki za gari lake,akiwaashiria wapunguze mwendo.

 

“Baby’s munanisikia?” Rahab alizungumza kwa sauti ya kawaida

“Tunakupata”

“Wale jamaa,ninamashaka nao wamestukia dili”

“Kwa nini?” Ann aliuliza

“Kwa maana mwendo wao ni wamashaka mashaka”

“Haya sasa,Plan B yetu ni nini?” Halima aliuliza

“Kuwavamia bwana kwa pamoja” Agnes alishauri

“Tukiwavamia tutampataje Fetty?”

“Sasa ishu inakuwa vipi?” Rahab alizungumza

“Tuwafwateni tu” Anna alishauri

“Oya gari zetu,si zina map direction?”

“Ndio”

 

“Rahab wewe uliopo mbele tuambie,namba za gari la hao jamaa ni ngapi?”

“T234KSJ”

“Tuiingizeni hiyo namba kwenye hizi ramani zetu tutaweza kuiona kwa ishara hiyo gari kila inapo kwenda” Agnes alizungumza

“Sasa Ag wewe ndio mtaalamu wa hivi vitu sisi wezako wala hatujui”

“Ok,ngoja niingize”

 

Agnes akaiingiza namba ya gari na kwamsaada wa satellite aliweza kuiona gari ya wapelelezi kila inapo kwenda huku ikionekana kwa alama nyekundu.


Akawaelekeza wenzake jinsi ya kufanya na kila mmoja pembeni ya mskani wa gari lake kuna kioo kidogo kilicho unganishwa na sateliti na kazi yake ni kuweza kuonyesha ramani ya sehemu ambayo unahitaji kwenda au gari unayo taka kuifwata sehemu ilipo kikubwa ni kuweza kuzitambua namba za usajili wa gari hilo.


Wakaziendesha gari zao kwa mwendo wa kawaida na kuifanya gari ya wapelelezi kuzidi kutokomea,huku wakiwa hawana wasiwasi kuipoteza gari hiyo.


Wapelelezi wakaanza kupata matumaini baada ya gari tatu zinazo wafwata kuziacha nyuma sana.Gari ya wapelelezi ikafika Kimara Gas Station na wakashuka kwa haraka kwenye gari.Rahab na wezake wakalishuhudia gari la wapelelezi likiingia kwenye kituo cha gesi kilichopo Kimara.Wapelelezi wakaingia kwenye msitu wa miti ulipo hapo ambapo ndipo lilipo shimo ambalo wanatarajia kuwapokea Fetty na askari wengine

“Jamani tusishuke kwanza” Agnes alizungumza

“Kwa nini?”

 

“Hamuwezi kujua kama jamaa wamejificha wanatusubiria tushuke watushambulie”

“Hapo,umezungumza point”

Wakazisimamisha gari zao mbali kidogo na kilipo kituo cha gesi,wakisubiria kufanya kazi moja tu ya kuwashambulia askari hao pale watakapo mchukua Fetty


***************

Inspector Julio akaanza kutetemeka huku akimeza mafumba ya mate,kwani ni mwaka wa 25 sasa analitumikia jeshi la polisi,ila hajawahi kukutana na mwanake hatari kama Fetty.Kwa woga akajikuta akiminya kitufe cha kuziruhusu risasi kutoka,kwa bahari mbaya bunduki yake tayari imeisha risasi.

“Kwaheri”

 

Fetty alizungumza huku akiziruhusu risasi mbili kuchomoka kwenye bastola yake aina ya ‘browningu SFS’ na kuzichangua sehemu za siri za Inspector John,Fetty akasimama na kumtazama askari wa kike anaye fanana naye kuanzia mavazi hadi sura ya bandia aliyo valishwa.Fetty akataka kumuua  askari huyo ila akasitisha zoezi lake na kumnyanyua

“Nipe funguo nijifungue”

“Zip.....o kwa inspector John”

 

Fetty akamtazama kwa umakini askari,akachuchumaa kwa umakini huku bastola yake akiielekeza kwa askari huyo anaye itwa Rehema.Akaipapasa mifuko ya Inspector John na kuzitoa fungua nyingi.Akachagua funguo moja inayoweza kufungua kwenye mnyororo,kwa bahati nzuri akaipata.Akajifungua na kumuomba Afande Reheme kutangulia mbele huku akiwa ameshika tochi inayowasaidia kuona mbele.Wakafika kwenye njia nne tofauti,wakabaki wakiwa wamesimama wakiwa hawajui ni wapi waende

“Sema njia  ni ipi?”

“Sujui hata mimi”

 

Fetty akampiga kofi la shavu Afande Rehema huku akiwa amemnyooshea bastola

“Sema ni njia gani la sivyo nakumwaga ubongo?”

“Hii.....”

 

Afande Rehema alizungumza ili mradi aepukane na kifo cha kupigwa risasi.Japo amejitamkia ila njia aliyo ionyesha ndio sahihi.Wakaendelea na mwendo wao hadi wakafika sehemu yenye ngazi za chuma za kutokea nje.Fetty akamtanguliza afande Rehema japo amefungwa pingu za mikononi ila akajitahidi hivyo hivyo kuanza kupanda kwenda juu

 

*****************

Milio ya risasi waliyo isikia kupitia redio ya upepo,iliwachanganya sana wakuu wa polisi na kuwafanya waanze kubabaika na kuwapa taarifa wapelelezi kuwa kuna hali tete ambayo inaendelea chini walipo askari.


Mbaya zaidi kila wanapo jaribu kuwasiliana na wenzao hawakuweza kupata jibu la aina yoyote.Wapelelezi wakajiandaa kwa chochote kitakacho jitokeza kwenye shimo huku bastola zao wakiwa wameziandaa kwa umakini wa hali ya juu

Wakauona mfuniko wa shimo,ukifunguliwa na kichwa cha Afande Rehema kikatokeza,

“Musiniue”

 

Afande Rehema alizungumza huku akijitoa kwa kasi kwenye shimo.Fetty akajua kuna hali ya hatari ipo juu,akaishika bastola yake vizuri na kupandisha ngazi kwa hataka kabla hajajitokeza juu akakiona kichwa cha mpelelezi mmoja akichungulia,Mpelelezi akiwa anashangaa kati ya Rehema na Fetty yupi ni muhalifu kwani wanafanana,akastukia risasi ikipiga kwenye paji la uso wake na kumuangusha chini

 

Milio wa risasi ukawastua Rahab na wenzake,kwa haraka wakawasha magari yao na kuyasimamisha pembeni ya kituo cha gesi.Wakashuka kwa haraka kila mmoja banduki yake ikiwa mkononi.


Walinzi wa kitua cha gesi wakazidi kuchanganyikiwa kwani mlio huo wa risasi umesikika nyuma ya kituo na watu walio ingia kwenye  kituo chao hawaeleweki.Mlinzi mmoja akaikoki bunduki yake aina ya gobora,kitendo cha mlinzi kuishika bunduki yake,Anna alikiona vizuri,pasipo kuuliza ni nini mlinzi anataka kukifanya,akafyatua risasi iliyo muangusha mlinzi chini.Walinzi wengine wakalala chini kwa woga baada ya kumouona mwenzao akivuja damu nyingi

 

Wapelelezi wakabaki katika hali tata,huku kila mmoja akikataa kwenda kuchungulia kwenye shimo asije akakutwa na ktu kilicho mkuta X.


Wakiwa katika taharuki risasi zisizo na idadi zikatua mwilini mwao zikitokea nyuma yao na ukawa ndio mwisho wa maisha yao.Agnes akanza kupiga hatua za haraka akimfwata Afande Rehema aliye lala chini

“Fetty nyanyuka tuondole”

 

Fetty alianza kushua ngazi kurudi kwenye shimo ila baada ya kuisikia milio mingi ya bunduki.

“Fetty twende”

Agnes alizidi kumuita Afande Rehema baada ya kumuona anababaika.Kabla Fetty hajamalizi kushuka kwenye ngazi ya mwisho kuingia kwenye shimo akaisikia sauti ya Agnes.

“Agnes huyo sio Fetty ni polisi mimi nipo humu”

 

Fetty alizungumza huku akianza kupanda ngazi kwa haraka,Agnes akabaki akiwa ameshangaa,akamuona Fetty akichomoza kichwa kwenye shimo.Afande Rehema akajaribu kuiokota bastola ya askari mmoja aliye anguka chini.Risasi kama sita zikatua mgongoni mwake kutoka kwa Rahab.Fetty akamkimbilia Agnes na kumkumbatia

“Pole shosti”

“Asante”

 

Kabla hawajaondoka,mwanga mkali wa helcopar ya polisi iliotumwa kufika kwenye eneo hilo,ukaanza kuwamulika.Wakaanza kukimbia wakielekea mbele ya kituo walipo ziacha gari zao, kitendo cha Halima kujitokeza wakakutana na gari zipatazo kumi za polizi zikiwa zimetanda mbele ya kituo na askari wengi wakiwa na bunduki zao wakiwa wameelekezewa wao.

“WEKENI SILAHA ZENU CHINI”

“Shitii”

 

Wote watano wakabaki wakiwatazama askari huku helcopar ya polisi ikiwa inawamulika kwa mwanga mkali mweupe ambao umelifanya eneo walilo simama wao kuwa kama mchana na endepo watafanya kitu chochote cha kijinga,askari wenye bunduki wapatao thelasini wenye bunduki watazifyatua risasi zao pasipo kuwa na huruma



SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……8



“Nini tunafanya”

Rahab aliwauliza wenzake,huku taratibu mikono yake akiwa anainyanyua juu.Kila kitu ambacho kinaendelea katika eneo la kituo cha gesi,Dokta William anakifwatilia akiwa amelisimamisha gari lake mbali kidogo na eneo walilopo askari.


Kwa haraka alifungua nyuma ya gari lake kwenye buti na kutoa bunduki yake yenye uwezo wa kupiga risasi kwa masafa marefu inayoitwa ‘THE BOR SNIPER’ yenye uzito wa kilo sita na urefu wa milimita 1,038 sawa sawa na nchi 40.9 za urefu.


Akaiweka chini pembeni ya gari lake,kisha akalala na kufungua kifuniko cha lenzi inayoweza kuvuta karibu,Uzuri wa hii bunduki yake unaweza kuona muda wowote hata kama kuna giza ila kwa kutumia mwanga wa kijani uliopo kwenye lenzi yake unaweza kuona vizuri bila shida.


Akaifunga kiwambo cha kuzuia sauti.Alipo hakikisha kila kitu kipo sawa,akwakavuta kwa karibu Rahab na wezake na kuwaona wamenyoosha mikono yao juu .Pembeni na walipo jipanga  askari kuna tanki kubwa la gesi.Akapiga ishara ya msalaba kisha akafyatua risasi moja iliyoingia kwenye tanki la gesi.


Ndani ya sekunde mlipUko mkubwa wa gesi ukawarusha mbali askari karibia wote,mbaya mlipuko huo ukaendelezwa na magari yao yanayo tumia mafuta ya petrol na desel

Haikuwa kwa askari tu kurushwa,ila hata Rahab na wezake wakarushwa na kurudishwa nyuma walipo tokea.Halima akawa wa kwanza kunyanyuka,

“Jamani tuondokeni”

 

Alizungumza akiwahimiza weNzake,wakanyanyuka kwa haraka na kuanza kutokomea kwenye pori.Mitungi iliyo chimbiwa chini ya ardhi ikaanza kupata moto,mwisho wa siku ikaanza kulipuka mmoja baada ya mwIngine na kuzidi kusababisha vifo vya askari.Rubani anaye iendesha helcoptar ya polisi akachanganyikiwa sana,na jinsi moto unavyo waka.


Akaipeleka juu kidogo Helcoptar yake.Dokta William akaona kitendo cha rubani wa Helcoptar kuinyanyua juu.Akamvuta karibu rubani na bila ya huruma akamtandika risasi ya kifua na kumfanya aachie kila kitu alicho kishika na helcoptar ikaanza kurudi chini kwa kasi ya ajabu na kuingia kwenye moto mwingi wa gesi na kuzidi kuongeza mlipuko wa eneo la kituo

 

Dokta William akainyanyua bunduki yake kwa haraka na kuirudisha sehemu alipo itoa kwenye gari kisha akaingia ndani ya gari na kuondoka eneo alilopo,huku akilini mwake akiwa amejawa na mawazo mengi sana kwani kitendo ambacho amekifanya kwanza ni kinyume na sheria za nchi ya Tanzania pamoja na hata nchi yake ya Israel na endapo tukio hili litajulikana kama yeye ndio mtendaji mkuu atahukumiwa kifungo cha maisha jela au kunyongwa mbele ya halaiki ya watu.Kingine kinacho muumiza kichwa ni Fetty na wezake ambao aliwashuhudia wakirushwa na mlipoko wa tanki la gesi

 

Akatoa simu yake ambayo anawasiliana na Rahab na wezake.Akawapigia na kwabahati nzuri akazisikia sauti zao

“Mupo wapi?”

“Tupo kwenye haka kapori kalichopo nyuma ya kituo,tunakaribia kufika kwenye makazi ya watu”

“Sasa nyinyi,katokeeni katika barabara kuu maeneo ya Mbezi”

“Sawa”

 

Rahab na wezake wakabadilisha muelekeo na kuanza kukimbia kuelekea walipo elekezwa na Doktar Willian,ndani ya robo saa wakawa ameshafika Mbezi.Fetty kutokana amevaa nguo za polisi,ikawa ni nafasi nzuri kujitokeza barabarani kutazama ni wapi lilipo gari la Dokta William.

 

Dokta Willim akamuona Fetty  na kumtambua mara moja,akawasha gari lake kwani alikuwa amelisimamisha pembezoni mwa bararaba.Akafika sehemu walipo Fetty na wezake na wote kwa haraka wakaingia ndani ya gari ya dokta William aina ya Ford na kuondoka kwa mwendo wa kasi


***********

Tangu mwaka 1961 nchi ya Tanzania ilipo pata uhuru hapakuwahi kutokea tukio la kinyama lililo husisha mauaji ya askari zaidi ya thelathini kwa wakati mmoja tena wakiwa wanapambana na jeshi la polisi,isitoshe kuna baadhi ya wanachi waliokuwa katika kituo hicho nao pia wamefariki dunia.Tukio hili likaingizwa katika matukio ya kigaidi.Vilio vingi vilitanda kwenye nyumba za askari ambao wamefariki,hivyo hivyo kwa wananchi walio fariki hali ilikuwa ni moja ya kuomboleza vilio

 

Magazeti ya serikali na udaku yakatawaliwa na taarifa ya magaidi kulitingisha jeshi la polisi.Moja ya magazeti linalo itwa Story Za Eddy likatawaliwa na kichwa cha habari kilicho wakera viongozi wengi serikalini

 

(UZEMBE  WAUA ASKARI 30)

“Nitafutieni muandishi wa hili gazeti”

Mkuu wa polisi alizungumza kwa jazba,huku akiwatazama askari wake watatu walio simama mbele yake.Akaendelea kulipitia gazeti moja baada ya jingine kuangalia habari zilizo andikwa kwenye magazeti ya nchi hii.Akakutana na habari nyingine iliyo andikwa

(CHEZEA MAJAMBAWAZI WEWE,WAMEUNYUTI WENYEWE) Huku pembeni kukiwa na picha yake ya kikatuni ikitazama jinsi makatuni askari wakilipuliwa na moto wa gesi.Bwana Gudluck Nyangoi IGP wa polisi ikambidi kufumba macho yake na kuachana na habari ya kuyasoma magazeti ambayo yanazidi kuipandisha hasira yake.Akaitisha kikao cha wakuu wa jeshi la polisi nchi nzima na akawapa masaa manne wote wawe wamefika makao makuu ya polisi,hakujali wengine umbali wa mikoa yao ila tamko lake akaitaji lifanyiwe kazi mara moja

                                                                                           ************

Katika siku walizo amka na furaha ni hii ya leo,Agnes akaingia jikoni na kuwaandalia wezake kifungua kinywa cha nguvu na wote wakakutana katika meza ya chakula,pamoja na dokta William

“Fetty hongera” Agnes alizungumza

“Na nini?”

 

“Nimekukubali sana,wewe ni noma”

“Ahaa mbona kawaida”

“Ahaa,hivi ulisema wale askari uliwafanya nini ndani ya mtaro?”

“Wazembe wale,sema wamekufa ila wangekuwa hawajafa ningewashauri warudi tena mafunzoni”

Wakati Fetty na Agnes wanazungumza,dokta William akawa na kazi ya kupitia habari zinazo endelea kwenye mitandao ya kijami,akianzia na Facebook

 

“Jamani mambo sio mazuri kabisa”

“Kwa nini?” Halima aliuliza

“Huko nje mnatafutwa kama nini”

“Wametujua?”

“Hakuna picha hata moja inayo waonyesha sura zenu ila ni habari tuu”

“Doktar picha ya Fetty je?”

“Huyu picha yeke niliiona tuu,ila haijaandikwa vibaya”

“Imeandikwaje?” Fetty aliuliza

“Iliandikwa anatafutwa”

Wakabaki wakiwa wanacheka na kumfanya Dokta William kushangaa

 

“Mnacheka nini......!!?”

“Si hivyo unavyo sema kuwa haijaandikwa vibaya sana...ila anatafutwa,Doktar sasa hapo unadhani hayo maneno ni mazuri?” Rahab aliuliza huku akicheka

“Sawa tusikilizane,mimi nitaondoka mara moja kwenda Israel nyumbani.Hii ishu ikipita nitarudi”

“Dokta,pesa yetu?”

“Hiyo pesa yenu mimi nitawaingizia kila mmoja kwenye akaunti yake”

 

“Hapa sote unapo tuona hakuna hata mmoja ambaye ana akaunti benki,sasa hatujajua kama kunauwezekano wa sisi kuipata hiyo pesa”

 Anna alizungumza huku sura ya furaha ikiwa imepotea usoni mwake

“Nimewaelewa,kikubwa ni mawasiliano kati yangu mimi na nyinyi kwani hata nikiwa nje ya nchi nitaendelea kuwasiliana na nyinyi”

“Dokta mbona kama sijakuelewea? Ina maana pesa yetu ndio hakuna?”

 

Anna aliuliza huku akijiweka sawa kwenye kiti alicho kalia

“Pesa yenu ipo.Ila kwa kiasi cha pesa mbacho mnanidai chote kipo katika benki ya serikali ambayo kwa sasa akaunti zote zimefungwa kutokana na tukio la jana”

“Wewe kama wewe una kiasi gani kwenye hiyo benki?”

“Milioni mia sita”

“Mmmmm,wataifungua lini?”

“Hata mimi mwenyewe sijui”

“Wewe umejuaje?”

“Kuna mtu alinitumia meseji asubuhi”

“Ni nani?”

 

“Ni kiongozi wa juu,kwenye hiyo benki”

Swala la Dokta William kuto kuwa na pesa ya kumalizia kuwalipa Agnes na wenzake likaanza kumsumbua akili mmoja baada ya mwengine.Anna akanyanyuka na kuingia chumbani kwake na kurudi na bastola na kukaa kwenye kiti alicho kuwa amekikalia

 

“Dokta,tunakuamini tena sana.Ila mimi kwa hili bado hujanishawishi hata kidogo.Kwanza kumbuka sisi ni wasichana wadogo sana ambao kama tungeendelea kufanya kazi yetu ya kuiuza miili yetu tusinge tafutwa kwa mabaya kama hivi sasa.Sasa ninakupauchague vituu viwili,Uzungumze ni lini unatupa pesa yetu au uzungumze na huyu mjamaa hapa”

 

Anna alizungumza huku bastola akiiweka mezani,wenzake wote wakamtazama kisha wakamgeukia Dokta William

“Anna mimi nipeni masaa kadhaa nitawaletea pesa yenu”

“Huyu muongoo” Halima alidakia

“Siwadanganyi jamani”

 

“Mbona saa zote ulikuwa unajikenua kenua mbele yetu tuu?”

“Nilikuwa ninawapima kama mnaniamini au laa” Doktar William alizungumza kwa kujiamini

“Kuna vitu vya kudanganyana na vingine si vyakudanyanyana.Pesa ndio kila kitu bwana”

 

Fetty alizungumza huku akimtazama Dokta William kwa macho makali sana yasiyo na utani hata kidogo.Dokta William akasimama na kutoka nje ya handaki huku nyuma akiwa ameongozana na Fetty.Wakafika chini ya mti mmoja uliopo karibu sana na handaki lao,Dokta William akafukua kidogo na kutoa mfuko wa rambo ulio jaa pesa nyingi za kigeni.

“Duuu kumbe tunaishi na benki hapa ila hatujui chochote kinacho endelea”

 

“Si kutokana na nyinyi sio wachunguzi,mngejuaje”

Dokta Willia akampa mfuko Fetty na wote wakarudi ndani.Dokta William akawalipa kila mmoja kiasi chake anacho hitaji kulipwa.

 

“Jamani ninaondoka Tanzania leo.Mtajua ni nini cha ufanya na hizo pesa.Ila kwa ushauri sasa hivi ninawaomba msitembee tembee sana kwa maana mtakuwa munatafutwa kupindukia”

“Sawa”

Dokta William akandoka na moja kwa moja akafika nyumbani kwake ambapo alichukua nguo baadhi na kuelekea uwanja wa ndege


 

   **************

“Jamani dokta ndio hivyo ameondoka”

Rahab alizungumza huku akiwatazama wezake

“Itakuwaje sasa?”

“Ina bidi madili tujitafutie sisi wenyewe” Anna alizungumza

“Ngoja kaka nilisikia kuwa kuna pesa ambazo zipo benki ya Taifa?”

“Ndio”

 

“Sasa mnaonaje,tukapiga ishu ya mwisho kila mtu akaamua kwenda kivyake kutafuta maisha kwa mbele” Halima alitoa wazo lililo wanyamazisha wezake kwa muda

“Jamani mimi kuishi bila nyinyi mwenzenu wala siwezi” Rahab alizungumza

 

“Sote kuishi mbali mbali hatuwezi”

“Sasa inakuwaje,kwa maana kwa sasa tunatafutwa na vijipesa tulivyo navyo hivi hata tukisema tuondoke nchini huko tuanapokwenda tutapata shida”

 

“Ni kweli hicho ulicho kizungumza Fetty,kama mimi natamani siku na mimi niitwe mama fulani.Niwe na mume wangu tuishi maisha salama tuu” Rahab alizungumza

“Sawa ,ni lini tunapiga hiyo ishu?”

“Tuanze kuitafuta ramani ya benki ambayo tutakwenda kupiga tukio”

 

“Wewe Agnes tunakutegemea wewe ndio fundi mitambo,ingia kwenye kompyuta hizo ututafutie ramani ya benki tukapige tukio”

 

Agnes akasimama na kukaa kwenye kompyuta zilizopo sebleni kwao na kuanza kufanya utundu wake kwenye mtandao,baada ya dakika kadhaa akawa ameipata tamani ya jengo zima la benki kuu ya Tanzania

“Kazi imeanza”

 

 ***********

Ulinzi ukazidi kuimarishwa katika viwanja vya ndege vilivyopo nchini Tanzania,mipaka na bandari zote zipo chini ya uangalizi mkali wa polisi ambao kila unaye muona unatambua ana hasira na majambazi yalio waua wenzao.Hakuna mtu  hata mmoja ambaye alihitaji kutoka nje ya nchi pasipo kukaguliwa.

 

Simu ya dokta William inaita akiwa hatua chache kufika ulipo uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius K.Nyerere.Simu inatoka kwa mkuu wa polisi bwana Gudluck Nyangoi,mapigo ya moyo yanampasuka na kujikuta akiitazama simu kwa muda na anaamua kulisimamisha gari lake pembezoni mwa barabara na kuipokea simu kabla haijakata

“Habari yako dokta William”

“Salama tuu”

“Samahani dokta kwa kukusumbua,”

“Bila samahani”

“Tunakuhitaji hapa makao makao makuu”

“Saa ngapi?”

“Sasa hivi”

 

Simu ikakatwa na kuzidi kumuongezea wasiwasi Dokta William,akaitazama simu yake na kutaka kumpigia mkuu wa polisi bwana Gudluck Nyangoi ila akaacha.Akashuka kwenye gari na kutembea hatua kadhaa hadi ulipo uwanja wa ndege na kuzishuhudia gari nyingi zikiwa kwenye foleni na moja baada ya nyingine inakaguliwa.Akashusha pumzi nyingi huku asijue nini afanye,akarudi kwenye gari lake na kuingia.Nafsi moja inamuambia aende makao ya polisi huku nafsi nyingine ikimuambia asiende.

“Ngoja niende”

 

Akawasha gari lake na moja kwa moja akaelekea makao makuu ya polisi,akasimamisha gari lake kwenye maegesho na kushuka.Akatazama pande zote na kuona polisi wakiwa katika kazi ya kuimarisha ulinzi mkali.Baadhi ya polisi wakawa wanamtazama kwa macho makali.Akajikaza kiume na kuanza kupiga hatua za kawaidia na kungia  ndani ya ofisi

 

“Samahani dada nahitaji kuonana na mkuu” alizungumza na askari mmoja wa kike

“Ingia kwenye lifti pandisha hadi gorofa ya tano,utakunja kulia utaona kibao kidogo juu ya mlango kimendika UKUMBI WA MKUTANO,Utamkuta hapa”

 

“Asante”

Dokta William akaingia kwenye lifti kabla haijafunga wakaingia askari wawilii wenye vyeo vingi kwenye mashati yao.

“Hawa majambazi,tukiwakamata mama yangu nitawanywa damu yao hadharani”

 

“Kweli bwana,yaani nimeacha msiba wa mwanangu ninakuja kwenye hicho kikao.Naapa haki ya Mungu nikimkamata mmoja wao lazima nivunje sheria za nchi”

“Hivi mwanao ni miongoni mwa askari  walio kufa?”

“Ndio,tena ndio kwanza anamwaka wa pili kazini”

“Pole sana”

 

Dokta Williama aliendelea kuwasikiliza wakuu hawa wa polisi ambao vyeo vyao vinawatambulisha kama ma RPC kwenye mikoa yao.Lifti ikafunguka na wote wakatoka ndani ya lifti.Askari hao wakaendelea kwa mwendo wa kasi na kuingia kwenye ukumbi wa mikutano.Dokta William akajiweka sawa nguo zake na kuingia ndani ya ukumbi huu.Gafla macho yake yakatazamana na midomo ya bastola alizo elekezewa na wakuu wa polisi waliokaa kwenye viti vyao huku wakioneka kukasirishwa sana na uwepo wake


Itaendelea.......



Ilipoishia...

Dokta Williama aliendelea kuwasikiliza wakuu hawa wa polisi ambao vyeo vyao vinawatambulisha kama ma RPC kwenye mikoa yao.Lifti ikafunguka na wote wakatoka ndani ya lifti.Askari hao wakaendelea kwa mwendo wa kasi na kuingia kwenye ukumbi wa mikutano.Dokta William akajiweka sawa nguo zake na kuingia ndani ya ukumbi huu.Gafla macho yake yakatazamana na midomo ya bastola alizo elekezewa na wakuu wa polisi waliokaa kwenye viti vyao huku wakioneka kukasirishwa sana na uwepo wake


ENDELEA....

IGP bwana Gudluck Nyangoi akwaamuru wezake kuziweka silaha zao chini na wakati

“Karibu dokra Willian”

Bwana G.Nyangoi alizungumza huku akitabasamu na kumfanya dokta William kushusha pumzi nyingi,kidogo wasiwasi ukaanza kumpungua.


“Jamani huyu ni miongoni mwa wanajeshi wa umoja wa matiafa,yupo hapa nchini kwa ajili ya mafunzo wa madaktari wa jeshi letu juu ya jinsi gani wanaweza kumtengeneza sura bandia”


“Dokta,kwanza samahani kwa kukuvunjia ratiba zako kwa maana haikuwa katika ratiba zako leo kama nitakuitaji hapa”

“Bila samahani mkuu”

“Karibu ukae”


Dokta William akaka kwenye kiti alicho onyeshwa na bwana Nyangoi,akawaytizama makamanda wote waliopo ndani ya ofisi na hapakuwa na hata mmoja anaye mfahamu zaidi ya IGP Gudluck Nyangoi.


“Jamani kama munavyo jua,sisi kama jeshi la polisi tumekubwa na msiba mkubwa sana wakupoteza vijana wetu katika tukio la jana usiku,Pia ni aibu kubwa kwetu sisi kama jeshi la polisi kwa kushindwa kupambana na majambazi ambao,sijajua ni vipi tulishindwa kuwazuia na kusababisha maafa makubwa kama haya”


Ukimya ukatawala,huku akili ya Dokta William ikiwa inajaribu kupanga kitu cha kuzungumza kabla hajaulizwa kwani ametambua umuhimu wake wa yeye kuwa hapa ni kuwashauri viongozi waliopo humu ndani 


“Jamani ninawasililiza,nasubiri maoni yenu.Nini tufanye ili kuwakamata hawa watu na ninavyo sikia wao ni wasichana sasa sijajua inakuwaje wasichana kama hawa wanatushinda kirahisi rahisi?”


“Mkuu mimi ninaona,kwanza tudhibiti mipaka yote ya nchi jirani kwa maana kumbukeni kulikuwa na tishio la kundi la Al-Shabab kuivamia mlimani city.Sasa isije ikwa ndio hao wameanza kutekeleza mipango yao”


“Asante bwana Shaban Mbago,mwengine?”

“Mkuu mimi kuna swala ambalo bado silipatii picha,haiwezekani mpango ule wa kumsafirisha yele binti katika njia ya ardhini ulibumburuka.Swali ni je,ni nani aliye toa siri ile?”


Mapigo ya moyo ya dokta William yakaanza kwenda kasi,ila hakutaka kuiruhusu hali hii kuendelea kuundama moyo wake,akawatazama wakuu wa polisi waliopo eneo hili na kuwaona wengi wapo kimya kila mmoja akikosa cha kuzungumza.Dokta William akanyoosha kidole na bwana G.Nyangoi akampa ruhusa ya kuzungumza

“Wakuu wangu mimi ninajambo moja ninaomba nizungumze”

“Zungumza tuu,kwani ushauri wako ni mkubwa sana”


“Kuna hali ambayo inaendelea ndani ya jeshi lenu,kwa kipindi kifupi nilicho kaa katika nchi hii na kushirikiana na jeshi lenu nikagundua kuna hali amayo sio nzuri na endapo mukiacha ikikua na kukomaa,Siku hadi siku jeshi lenu litazidi kuzalilisha na kuteketea mwisho wa siku ile imani ya kusema kuwa Tanzania ni nchi ya amani itafutika katika vichwa vya watu wengi”


“Viongozi kwa viongozi hamuaminiani,hilo ni la kwanza.Pili viongozi mumekuwa ni watu wakuunda vikundi vikundi vya watu ambao munawatumia kwa maslai yenu binafsi na si ya taifa.Kwa mfano kuna magaidi ambao jeshi la polisi mulikuwa munawatafuta kwa kipindi kirefu sana.


Kutokana na uaminifu finyu wa baadhi ya viongozi magaidi wale wakaendelea kudumu na kuishi kwa kipindi kirefu pasipo serikali kuzungumza kitu cha aina yoyote.Kila mulipo kuwa munajaribu kwenda kuwakama walikuwa wanawakwepa na kubaki mukijiuliza mutafanya nini?”


“Kabla ya hichi kikao kuendelea,jiulizeni je hakuna wasaliti watako vujisha siri juu ya watu muna watafuta? Na kama wapo je kuna haja gani ya hichi kikao kuendelea kuwepo hapa?”


Ukumbi mzima ukakaa kimya,sura za makamanda wote wapolisi zikawa zikimtazama Dokta William ambaye amezungumza maneno ambayo wengi wao hawakuwa wanayafikiria kuyazungumza


“Musikalie kuunda tume kuchunguza vitu ambavyo munajua majibu yake kabla ya kuzungumza.Nyinyi ni jeshi,munatakiwa kuwa kitu kimoja na si kuwa katika mgawanyiko ambao utawakost garama ambazo si za msingi.Jaribuni kuiga baadhi ya mbinu za kijeshi katika mataifa makubwa yaliyo endelea,mfano Marekani na kadhalika.Nitatolea mfano mdogo tuu wa wa wale wanejeshi walio tumwa kwenda kumuua Osama Bin Laden,Gaidi ambaye sisi kama Israel alituumiza pia vichwa jinsi ya kumpata”


“Ila kikosi cha wanajeshi wachache walio tumwa kuumuua Osama,kilikuwa ni cha siri kubwa hata makamu wa raisi wa Marekani hakuwa analifahamu hilo,zidi ya raisi Obama na wasadizi wake,Na tukio zima lilipokuwa linaendelea walikaa kwenye chumba maalumu pasipo na mtu yoyote kuwa na mawasiliano ya simu ya mkononi,hata raisi mwenyewe alizuiwa kuwa na simu.


Huo ni mfano mdogo ila hapa hapa ninashanga muheshimiwa unaendeleza kikao ila kuna huyo bwana hapo anachati na simu chini ya meza,Je kuna umuhimu gani wa hichi kikao?”

Bwana Noel Muro akastuka na kuuingiza simu yake mfukoni baada ya kunyooshewa kidole na Dokta William.

“Muro ninaomba uzime simu yako”


Bwana G.Nyangoi alizungumza huku akimtazama bwana Muro

“Mkuu cha mwisho kukizungumza ninawaomba,muunde kikosi maaalumu cha siri kitakacho wa pambana na hili swala.Asanteni”

Dokta William akakaa kwenye kiti na viongozi wote wakampigia makofi wakimpongeza kwa ushauri wake alio utoa.


“Dokta Willim asante sana kwa ushauri wako mzuri sana.Mimi ningekuomba usaidiane na mimi kuunda kikosi kitakacho weza kuwasaka hawa majambazi.Nipo radhi kuwaishawishi serikali kuongezea mshahara”

Laiti IGP bwana G.Nyangoi angegundua mtu anaye muomba juu ya huo mpango ndio muhusika nambari moja wala asinge zungumza hayo maneno


                                             ***


Kutokana na uelewa mkubwa wa Agnes katika maswala ya usomaji wa ramani akaanza kuwaelekeza wezake jinsi ya kuingia katika benki kuu ya taifa BOT kufanya tukio wanalo taka kwenda kulifanya.Maelekezo yake hayakuwa magumu sana kwa wezake kuyaelewa,Kila mmoja alielewa vizuri na palipokuwa na swali wakawekana sawa

“Ag tumesha isoma ramani nzima je,jinsi ya kuingi hapo itakuwa vipi?” Anna aliuliza


“Hapa kikubwa cha kufanya ni kuvaa miili ya bandia”

“Kivipi tutavaa miili ya bandia?”

“Sio sote tutavaa miili ya bandi,ila kati yetu mmoja atavaa mwili ambao utamfanya aonekane kama bibi kizee,atakwenda ndani ya benki huku katika kifungo cha ngoo yake kuna kamera ndogo ambayo tutaifunga na jinsi anavyo kwenda sisi huku nyuma kupitia simu zetu tutaweza kuona jinsi madhari ya ndani na jinsi ulinzi ulivyo”

“Agnes naamini leo tutakuchosha na maswali mengi,je hiyo kamera itakuwaje kuwaje?” Rahab aliiuliza


“Ngoja nimsaidie kujibu,Kamera ambayo itatumika ni ndogo sana na ipo kama jicho fulani hivi ambako tunaweza kulibandika kwenye kifugo cha nguo pasipo mtu yoyote kujua”

Fetty alimjibu Rahab

“Kamera na mwili huo vitapatikana wapi?”

“Kuna muarabu mmoja pale kariakoo anauza hivi vitu  ila ni kwa siri sana,Japo duka lake linauza urembo wa vitu vya kupambia nyumba” Agnes alizungumza


“So ni nani atakwenda kununu?”

Wakaa kimya huku kila mmoja akiwa kimya.

“Mimi nitakwenda?” Halima alizungumza na kuwafanya wezake kumtazama

“Sawa,itabidi tukafanyie make up itakayo kubadilisha hata muonekano wako”  Anna alizungumza

“Mimi nitakufanyia make up” Rahabu alizungumza 


“Ok kazi inafanyika lini?” Agnes alizungumza

“Kazi ya kununu vitu inaanza leo”

“Je siku ya kwenda kupiga tukio ni lini?” Halima aliuliza

“Hata kesho ikiwezekana kikubwa ni kuwa makini na lile ambalo tunalifanya”

“Mmmm,tuacheni hali huko nje itulie”

“Tukiwaacha wakijipanga itatuwia vigumu.Kikubwa ni kupiga tukio litakao waliza miaka yote” Fetty alizungumza huku akiwatazama wezake


Wakaanza kazi ya kumfanyia ‘make up’ Halima,wakamvalisha wigi la nywele lilo mbadilisha muonekano wake na kuzidi kuwa mzuri zadi,wakamuweka nyusi bandia zilizo zidi kumpendezesha.Hadi wanamaliza Halima akawa tofauti sana na jinsi alivyo,akavalia suruali iliyo mbana makalio yake ya wastani na kuziachia hipsi zake kuonekana vizuri


“Haki ya nani,ningekuwa mwanaume Halima ningekutongoza”

Rahab alizungumza na kuwafanya wezake kucheka

“Kweli vile,cheki mtoto alivyo bomba.Unaweza kusema ameshushwa kutoka mbinguni kumbe kwa shabaha za bunduki ni mwengine kabisa”

“Hembu Rahab acha ujinga bwana”


“Sasa hivi ni saa tano asubuhi,tukikusindikiza hadi pale barabarani itatuchukua kama dakika ishirini si ndioa?” Fetty alizungumza

“Ndio”

“Oya shosti kama kuna uwezekano utujie na gari basi”

“Gari bila hela litatokea wapi,Mbinguni?”

“Ahaaa tuchangeni changeni hata kaVitz kamilioni tano” Rahab alizungumza

“Ok kila mmoja atoe Milioni moja”


Wakakubaliana kila mmoja akatoa milioni moja moja na kumkabidhi Anna,Safari ya kumsindikiza mwenzao ikaanza huku njia nzima wakiwa wanazungumza na kila mmoja akiwa na bastola yake kiunoni.Njia nzima wakawa na kazi yakusimuliana stori zisizo na kichwa wala migu,wakafanikiwa kufika barabarani na wao hawakutoka kabisa barabarani na kumuacha Anna asimame mwenyewe barabarani huku akiwa na pochi ndogo aliyo ining’iniza kwenye kwapa lake


Anna akaisimamisha gari ndogo,kwa bahati nzuri gari ikasimama,akapiga hatua za haraka hadi sehemu ilipo simama na kuzunguka upende wa dereva na kuwakuta vijana wawili

“Samahani kaka zangu?”

“Bila samahani mrembo?”

“Ninaombeni lifti mimi ninakwenda Dar es Salaam”

“Ingia twende kwani na sisi tunakwenda Dar”


Anna akaingia siti ya nyuma na gari ikaondoka,Rahab na wezake wakarudi kwenye handaki.Anna akamtumi wezake meseji

(JAMANI HAWA WAKAKA WANAVUTIA)

(Umeshaa anza,jua kilicho kupeleka achana na hizo habari) Halima akawa wa kwanza kuijibu meseji

“Sister unaitwa nani?” Jama mmoja aliye kaa pembeni ya dereva alizungumza


“Mimi ninaitwa,Hilda” Anna alidanganya

“Ahaa mimi ninaitwa Jackson na huyu kaka yangu anaitwa John”

“Nashukuru kuwafahamu”

“Wewe unafanya kazi gani?”

“Mimi ni mke wa mtuu,najaa nyumbani kwa mume wangu”

“Ahaa,daa kweli wewe ni mke wa mtu kwa maana unavutia sana”


“Asante”

“Sisi bwana ni waanya biashara wa madini,Tunatokea mererani”

“Ahaa hongereni”

“Sasa sijui leo tunaweza kuwa pamoja”

“Ahaa mume wangu bwana ana wivu sana”

“Ahaaa,kawaida mbona.Kila mmoja na chake”


Wakaendelea kuzungumza hadi wanafika maeneo ya Mbezi wakakuta msururu mrefu wa magari,Anna akastuka baada ya kuona askari wengi wakiwa wanakagua gari mmoja baada ya jengine.Askari wawili wafika wenye gari alipo Anna na kuwaomba wote watatu kushuka ndani ya gari jambo lililo anza kumuogopesha askari mmoja akawa amemkazi macho sana Anna akionekana kumtilia mashaka......


            SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……10


......Redio za upepo za polisi zikaanza kusikika zikiokoroma na sauti kali ikasikika

“Kunaajali ya moto huku kwenye magari ya mbele,Over”

“Tunakuja.Over”


Askari mmoja alijibu na kuwaacha Anna,John na Jackson wakirudi ndani ya gari.Wakisubiria foleni iweze kusogea.

“Hivi jamaa alisema kuwa kuna moto mbele” John aliuliza baada ya kuona watu wengi wakikimbilia mbele

“Hembu,ngoja”

Jackson akashuka ndani ya gari na kukimbilia mbele,akakuta gari moja ndogo aina ya Subaru ikiwaka moto na wananchi wakijitahidi kuzima gari hiyo.Jackson akarudi kwenye gari


“Kuna gari hapo mbele inateketea”

“Ipo kwenye foleni” Anna aliuliza

“Ndio Hilda”

“Hakuna aliye jeruhiwa”

“Sidhani kwa maana hakuna mtu yoyote ndani ya gari”

Hali ya foleni ikazidi kuongezaka na kusababisha msongamano mkubwa wa magari

“Napoteza muda tuu”


Anna alijiseme kimoyo moyo huku akitazama nyuma kuyaangalia mabasi mengi yanayo tokea mkoani yakiwa yemejipanga kwa wingi yakisubiria gari za mbele kusogea.

“Jamani ngoja nikanunue maji pale dukani”

“Lete pesa yako nikakununulie,maji” Jackson alizungumza

“Hapana wee acha tuu nitanunua tu hapo juu”


Anna akashuka kwenye gari na kuvuka upande wa pili wa barabara huku akiwa makini asiweze kugundulika kirahisi, kwa kuzuga akaingia kwenye duka moja na kuagiza maji makubwa ya chupa, akiwa anasubiria kukabidhiwa maji na muuzaji akastuka baada ya kuona picha ya Fetty ikitangazwa kwenye taarifa ya habari kwenye kituo cha ITV


(JAMBAZI HUYU, NA WENGINE BADO WANAENDELEA KUTAFUTWA NA JESHI LA POLISI.KIKOSI MAALUMU.UKIMUONA SEHEMU YOYOTE TUNAKUOMBA UWASILIANE NA JESHI LA POLISI KUPITIA NAMBA YA SIMU +225 657072588)


Muandishi wa habari alizungumza na kumfanya Anna kubaki akitazama chini, akakabidhiwa maji na kutoa noti ya shilingi elfu kumi na kuondoka kabla hajapia hatua hata tano akastukia akiitwa na sauti ya kiume nyuma

“Dada umesahau chenchi yako”


Jamaa mmoja, aliye simama kando ya duka alimuambia Anna ambaye anatumia jina la bandia la Hilda.Anna akarudi haraka haraka hadi dukani na kuichukua.Akawatazama Jackson na John ndani ya gari na kuwaona wamejilaza kwenye siti zao huku kila mmoja akiwa amejochokea kiasi kwamba anatamani gari lake liruke hadi mbele kusipo kuwa a foleni na kuendelea na safari zake.


Anna akaanza kutembea kuelekea mbele kulipo tokea janga la moto huku macho yake yakiwa makini sana na polisi wanao wazudia watu kuisogelea sehemu ambayo gari linaungua na kuwaacha askari wa zima moto kufanya kazi hiyo.Akafanikiwa kupita pembezoni mwa barabara hadi sehemu walipo waendesha pikipiki(bodaboda)


“Kaka hapa hadi kariakoo ni bei gani?”

“Ahaaaa dada hapo kwa kumi natano”(elfu kumi na tano)

“Powa twende”

Anna akapanda kwenye pikipiki

“Naomba Helmet”

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog