Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

UKURASA WA GAIDI - 3

  

Simulizi : Ukurasa Wa Gaidi 

Sehemu Ya : Tatu (3)


wa idara ya kupambana na ugaidi Tanzania yaani

C.T.I(Counter Terrorism Intelligence). Ni ajenti

namba moja kati ya maajenti wanaokwenda mstari

wa mbele kufanya kazi kwa vitendo (field agent) na

ni ajenti pekee aliyekuwa na uwezo wa kufanya

upelelezi na hata mapambano peke yake bila ya

kuwa na usaidizi.Mick ni ajenti namba moja kati ya

Maajenti sita wa idara ya C.T.I, maajenti watatu

wakiwa ni wa mstari mwa mbele kivitendo(field

agents) na watatu wakiwa ni maajenti wa usaidizi

(back up) waliofanya kazi zao nyingi ndani ya ofisi

na mara chache sana nje ya ofisi.

JIONI YA SIKU HIYO

Katika moja ya hoteli zilizopo katika kisiwa hiki cha

Ibiza, Mick anaonekana akipata chakula cha

jioni.Wakati huu ndipo alipowasha simu yake ya

mkononi aliyoifunga wiki nzima.Hakutaka

kusumbuliwa katika likizo yake.Hata televisheni na

kompyuta yake,alivitumia kwa nadra sana wakati

kama huu anapokuwa likizo.Alipenda kuishi kiasili

sana anapokuwa likizo. Muda mwingi

alijishughulisha kutembelea vivutio mbali mbali vya

Hispania ikiwapo majumba ya makumbusho ya

kihistoria na kujifunza mambo mbalimbali ya

kihistoria. Wakati mwingine alitembelea nchi

nyingine mbali mbali kama Italia,Ugiriki,

Korea,China na hata Japan.Yaani moja ya starehe

zake ilikuwa ni kujifunza historia mbali mbali na

hasa kwa nchi zilizokuwa na historia ndefu sana

tangu zama za kale(ancient time).Moja ya historia

aliyoipenda sana ni ile ya Korea ya kale na Mataifa

matatu yaliyowahi kuwapo katika nyakati hizo yaani

Koguryeo, Baekje na Silla.Lakini pia aliipenda

historia ya tawala za kirumi.

Wakati huu Mick alipoiwasha simu yake, message

mbalimbali ziliingia katika simu yake.Kulikuwa na

meseji mbali mbali kutoka mitandao ya kijamii na

zile za kawaida. Moja ya message iliyomvutia zaidi

ni ile ya kawaida iliyoingia katika laini yake namba

mbili ambayo hakupenda kuitumia sana na ni watu

wachache sana walioifahamu. Message ilisomeka

kwa Lugha ya kiingereza 'When the house is

burning call the resque team' (nyumba inapoungua

wapigie zimamoto).

"Kumekucha".Alijisemea Mick mara baada ya

kupata meseji hiyo.Dakika kadhaa baadaye Mick

alikwisha kufuatilia habari zaidi na kujua kinaga

ubaga nini kimetokea nchini.Baada ya kufuata

taratibu za kukodi ndege,saa chache baadaye

alikuwa yuko ndani ya 'pipa' ngani akielekea

nyumbani Tanzania, kuungana na idara nzima

kufanya kazi ngumu iliyokuwa mbele yao.

*********************************************

*****************************************************

Ndege aliyopanda Mick iliwasili uwanja wa ndege

wa JKIA(Julius Kambarage International Airport)

saa sita mchana.Mara baada ya kukamilisha

taratibu zote za ukaguzi wa uwanja wa ndege,

alielekea sehemu ya maegesho ya magari ambako

alikuta magari mbali mbali yakiwa yamepaki lakini

yeye akaliendea gari aina ya Range rover sport

nyeusi.Mick alikwenda moja kwa moja eneo la

matairi ya nyuma ya gari hilo, akapenyeza mkono

katika mlsehemu ya juu ya moja kati ya matairi

hayo kisha akapapasa katika.eneo hilo.Hapo

alifanikiwa kupata ufunguo wa gari hilo.

Moja kwa moja Mick alifungua mlango wa gari hilo

na kuingia ndani ambako alifungua droo katika

'dash board' ya gari hilo.Hapo akakuta bastola

mbili moja aina ya Beretta na nyingine ndogo aina

ya 'colt 45', pia kulikuwa na kiwambo cha kuzuia

sauti kwa jija lingine 'sailensa', magazine nne za

'beretta' zilizosheheni risasi, kiboksi cha risasi za

'colt 45'. Pia chini kabisa ya vitu hivyo alikuta

kikaratasi kimeandikwa 'Mahali salama Iringa.

Wengine watafuata'.Hapo Mick aliwasha gari na

kuondoka kwa kasi kuelekea Iringa.

Message iliingia katika simu ya Makassy "IRINGA".

Hapo hapo Makassy akamuita katibu muhtasi wa

C.T.I, Clara Makene. Sekunde chache baadaye

Clara alikuwa mbele ya mkuu wake wa kazi

akipewa maagizo. "Andaa kikao Maajenti wote

wahudhurie.Pia wasiliana na Kamanda wa E.C.S

( Elite Combat Squad). Mwambie nahitaji kuonana

naye masaa matatu kuanzia sasa.Ila kikao hiki

kiandae sasa hivi. Ndani ya nusu saa maajenti

wote muwe ndani ya chumba cha mikutano."

Alizungumza Makassy.

"Sawa boss". Alijibu Clara,katibu muhtasi wa C.T.I.

Wakati ambao idara ya C.T.I haikuwa na kazi

maalum zaidi ya upelelezi ule wa kung'amua kama

kuna tishio lolote la ugaidi linalotishia taifa, Clara

Makene alifanya kazi kama katibu muhtasi wa

C.T.I. Lakini kwa nyakati kama hizi ambazo

kulikuwa na kazi maalum iliyohitaji kupewa

kipaumbele , Clara alikuwa ni ajenti aliyepewa

namba nne katika idara ya C.T.I na namba moja

katika utaalamu wa teknolojia ya kompyuta.Clara

alikuwa na shahada ya pili ya teknolojia ya habari

na mawasiliano (information and communication

technology) aliyoipata katika chuo kikuu cha M.I.T

huko Marekani.Pia alikuwa ni mtaalamu wa 'data

analysis' kwa hiyo alikuwa ni data analyst

(mchambua data) wa C.T.I .Wataalamu wengine wa

kompyuta walikuwa ni ajenti Morris ambaye pia

alibobea katika masuala yote ya maabara na ajenti

Rachel ambaye pia alikuwa Daktari wa idara.

*************************************

Nusu saa baadaye, chumba cha vikao ndani ya

ofisi za C.T.I, maajenti wote kasoro ajenti Mick,

walikwisha kufika na kukaa katika viti vilivyomo

humo ndani. Zaidi ya ajenti Clara, Ajenti Morris na

Ajenti Rachel ; pia alikuwemo Paul Kumwembe,

ajenti namba mbili wa C.T.I ambaye alikuwa ni

ajenti wa mstari wa mbele(field agent) ambaye pia

alikuwa ni mtaalamu aliyebobea katika masuala ya

ulengaji wa shabaha, na mwisho alikuwepo ajenti

Jackline, ajenti namba tatu kati ya maajenti wa

mstari wa mbele( field agent) ambaye pia ni

mtaalamu wa kupangilia vikosi vya kimapigano.

Jukumu namba mbili Jackline lilikuwa ni kumsaidia

kiongozi wa kikosi maalum cha mapigano cha

C.T.I cha E.C.S kamanda Joshua Mwambinga

katika uwanja wa vita.Kwa lugha ya kitaalam

Jackline alikuwa ni 'Second in comand' wa E.C.S.

"Nadhani wote mumekwisha kuhisi sababu ya

kuwaita katika kikao hiki. Tukio lililotokea hapa

nchini ni tukio linalotuhusu sisi kuliko mtu

mwingine yeyote. Idara hii ilianzishwa ili ilifae taifa

kwa nyakati kama hizi.Kwa sababu hiyo ,tuna

sababu ya kuanza kazi mara moja.Tunaachana na

masuala mengine yote ya kiusalama na tunalipa

suala hili kipaumbele. Tuna chini ya miezi mitatu

kukamilisha kazi iliyo mbele yetu. Nimeongea juu

juu kwa kuwa Clara atatueleza mambo haya yote

kwa kina."Aliongea Mkurugenzi Eliackim Makassy.

Clara Makene, binti mzuri na mrembo kwelikweli,

alitembea kutoka alipokaa na kwenda katika meza

iliyokuwa mbele yake umbqli wa mita kama sita

hivi mbele yake. Juu ya meza hiyo kulikuwa na

kompyuta mpakato pamoja na 'projector'.Clara

akachomeka waya maalum wa 'AVG' upande

mmoja katika 'projector' na upande mwingine

katika kompyuta mpakato. Kisha akabonyeza hapa

na pale katika vifaa hivi vilivyokuwa mbele

yake,'projector' na kompyuta vikawaka.Taa katika

chumba hicho zikazimwa nakufanya 'projector'

kufanya kazi yake vizuri zaidi. Kilichokuwa

kikionekana katika kompyuta ile kilionekana katika

ukuta mweupe , mbele walikokuwa wanatazama

maajenti wote wa C.T.I.Taswira mbili zilionekana

ukutani kwa msaada wa 'projector'.Picha za Omar

AL-Mahmood na Abdallah Yusoof zilionekana

vizuri kabisa mbele yao wote.

"Omar Al Mahmood,mrefu wa futi nane,mtaalamu

wa kutengeneza milipuko ya aina mbalimbali

kutoka huko Urusi.Amewahi kufanya kazi katika

idara ya kipelelezi ya KGB enzi za serikali ya ki-

SOVIET. Alikuwa ni 'special agent' na pia 'head of

field operations' ndani ya KGB kabla ya

kubadilishiwa majukumu na kuwa mkufunzi wa

'martial arts' na matumizi ya silaha kwa maajenti

wanafunzi.Aliondoka katika nchi ya Urusi mara tu

baada ya USSR( United States ofSoviet Repablic)

kuvunjika mwanzoni mwa miaka ya 90 kwa kuwa

alikuwa mkereketwa wa sera za ki-soviet.Alirudi

katika asili yake na alikozaliwa nchini

Afghanistani.Alipotea machoni pa wengi kabla ya

baadaye kusemekana kuwa amejiunga na kikundi

cha kigaidi cha Alquaeda.kisha baadaye kuhamia

Somalia kama moja ya viongozi wa ngazi za juu

na waanzilishi wa kikundi cha kigaidi cha

Alshabaab." Aliongea Clara kisha akakohoa kidogo

kuiandaa sauti yake kuanza kutoa maelezo

mengine tena.

Ajent Clara akaanza kubonyeza keyboard ya

kompyuta ile tena.Mara baada ya kubonyeza hapa

na pale,picha ya Omar Al Mahomood

ikapotea,picha nyingine ikajitokeza kwa ukubwa

kama ile picha iliyopita.

"Mtuhumiwa namba mbili, Abdallah Yusoof

Fatawi.Mtaalamu wa teknolojia ya habari na

mawasiliano ama 'ICT' aliyebobea sana na

mtaalam wa mambo yote ya kompyuta

kiujumla.Amekwisha wahi kufanya kazi idala ya

inteligensia ya ISI(Inter Service Intelligegence) ya

huko Pakistani.Alitoroka na kukimbilia India baada

ya kugundulika kuwa anavujisha siri za ki-

intelijensia za Pakistani kwa idara ya kipelelezi ya

nchi ya india 'RAW'.Baada ya kukaa kwa muda

nchini India, Yusoof alihamia Afghanistani na

kulowea huko kwa muda mrefu kabla hajajiunga na

kikundi cha kigaidi cha Alquaeda. Mara utaalamu

na ujuzi wake ulipoonekana kuwa na tija ndani ya

kikundi hicho,alipandishwa na kuwa katika uongozi

wa juu wa Alquaeda. Alikuja kuhamishiwa Somalia

baada ya miaka kadhaa ili kukiongeza nguvu

kikundi cha Alishabaab. Yusoof ni mtaalamu pia

wa mapigano ya mwili kwa mitindo ya

karate,taekwondo na kick-box , mrefu wa futi 7.8

na kati ya waharifu hatari zaidi na asiyewahi

kukamatika duniani".Akamaliza kuongea

Clara,kisha akarudi mahali alipokaa mwanzoni.

Kikao kiliendelea kwa kuongelea na kupanga

mambo mbalimbali kuhusiana na kazi iliyokuwa

inaikabili idara hii nyeti.

"Jambo la muhimu ni kuwatambua hawa walengwa

wetu wakuu kwa sasa.Tufanye jitihada za hali ya

juu kuwatambua mahali walipo ili hatua nyingine

zifuate.twapaswa kutambua kuwa tunaenda

kupambana vita nzito sana na hawa wahalifu wa

kimataifa."aliongea mkurugenzi kisha akaendelea

"Kwa kuhitimisha naomba tujiandae kwa safari ya

kwenda 'safe house' ya Iringa ambako ndiyo

kitakuwa kituo chetu kikuu katika kesi hii.Tukutane

Iringa kesho asubuhi na pia bila kusahau,tumepew

a miezi mitatu tu kukamilisha suala hili.Miezi hii

ikiisha basi tutanyang'anywa hili suala na kisha

litakuwa mikononi mwa Taifa la Marekani.Hii

itakuwa aibu kwetu.Kwa hiyo kabla miezi mitatu

haijaisha angalau tuwe na uelekeo wa kung'amua

wahalifu hawa walipo."Alimaliza kuongea

mkurugenzi na kikao kikaahirishwa.

Baada ya muda mkurugenzi Makassy alikuwa na

kikao na kamanda wa kikosi cha ECS , Kamanda

Joshua. Waliongea wakipanga hili na lile kisha

wakaagana.Kamanda wa ECS(Elite Combat Squad),

akaenda kupangilia askari wake wa weledi kwa ajili

ya safari ya kuhamia Iringa pamoja na kuwaweka

tayari kimapigano wakati watakapohitajika kufanya

hivyo



IRINGA

SAFE HOUSE

Hadi kufikia siku iliyofuata asubuhi, idara yote ilikuwa imehamia Iringa katika moja ya nyumba ambazo inazimiliki Tanzania. Katika mikoa yote iliyo jirani na mikoa iliyo mpakani mwa nchi,C.T.I ilimiliki nyumba moja kama hii. Kwa kuwa mkoa wa Mbeya unapakana na nchi ya Malawi na Zambia, nyumba ilijengwa katika mkoa jirani wa Iringa.

Kiuhalisia si kwamba nyumba ilikuwa mpya. Nyumba ile ilikuwa imefanyiwa ukarabati kutoka kuwa ghala la chakula na kurekebishwa kuwa jumba la kisasa sana.Jumba hili lilikuwa na vyumba kadhaa vya kulala pamoja na ofisi kubwa na ofisi ndogo ndogo pamoja na vitu vingine vingi sana.Hata namna ya kuingia katika nyumba ile haikuwa kazi nyepesi. Kulikuw na vitasa vya kisasa katika nyumba hii ambavyo vilihitaji namba ya siri, alama za vidole pamoja na mtazamo wa mboni ya jicho ili kufungua.Walio weza kuingia ndani ya nyumba hii ni wale wahusika tu. Hawa ndio pekee ambao teknolojia inayohusika kwa sababu za usalama katika nyumba hii ilikuwa imelishwa taarifa zao.

Maajenti wa idara hii ya CTI,walikuwa wamekusanyika katika ofisi kubwa ya pamoja wakifanya hili na lile pamoja na kupanga hiki na kile ili mradi kuweka mambo sawa.Chumba hiki cha ofisi, kilikuwa kimetawaliwa na kompyuta kadhaa zilizounganishwa kwa utaalamu wa hali ya juu huku zikitumia 'soft wares' za kisasa kabisa zinazohusika na kazi hii ya upelelezi. Yaani kwa kifupi kazi ilikuwa inaanza kuoamba moto rasmi wakati huu.

********************************************************

"Clara, hebu jaribu ku-hack mfumo wa kamera za CCTV za jeshi kikosi cha jkt Mafinga uangalie kilichorekodiwa kwa muda wa wiki moja nyuma kabla ya tukio kutokea." Aliongea Mick na kusikika kwa ajenti Clara upande wa pili kupitia kifaa cha mawasiliano alichokivaa sikioni.

"Ok acha nifanye yangu ".Alijibu Clara kutoka upande wa pili na kisha sauti ya vitufe vya kompyuta ikaanza kusikika ikibonyezwa bonyezwa kwa kasi ya ajabu.

Wakati huu ambao wawili hao walikuwa wanawasiliana, Clara alikuwa yupo ofisini wakati Mick yupo msituni,mahali ambapo palitokea tukio siku mbili tatu nyuma.Tukio lililosababisha wanaidara wa C.T.I kujikuta wana jukumu zito la kufanya mara baada ya kuwa na majukumu ya kawaida tu kwa muda mrefu.

Tangu asubuhi,wakati idara yote ya C.T.I ilipokuwa imewasili katika eneo hili, Mick alikwenda mahali pale na kuanza kazi yake eneo la tukio mara moja.Akiwa amekwishapata taarifa za awali za nini kilichojiri,moja kwa moja Mick alijua ni wapi pa kuanzia. Alikumbuka moja ya kauli mbiu ya idara yake iliyosema "katika tukio lolote, ni vizuri na lazima upelelezi uanzie eneo la tukio kwa sababu ndiyo mahali pekee ambapo utapata ushahidi au fununu zitakazokupeleka kwenye ushahidi". Na ni ukweli mtupu unaoongelewa katika kauli mbiu hii.Idara yoyote ya usalama duniani inapofanya upelelezi wa tukio fulani,ni lazima itafika eneo la tukio kwa sababu ya mambo mawili.Ushahidiau fununu au kama mataifa ya magharibi yaliyotufundisha mambo haya wanavyosema kwa lugha yao 'either clue or evidence'.

Kwanza kabisa baada ya kufika eneo la tukio,ajenti Mick alimuhoji mmoja wa askari waliokuwa wanalinda eneo hilo.Wakati alipomuhoji,Mick aliweza kung'amua kuwa magaidi wale walikhwapo muda mrefu,pengine masaa mawili matatu kabla ya msafara kupita na kushambuliwa.Aling'amua kuwa magaidi wale walikuja kwa pamoja eneo hilo na kisha wakatawanyika kila upande nyuma ya misitu ya eneo lile la tukio na ndiyo maana ilikuwa vigumu kupambana nao.Pia alihisi,kwa jinsi eneo lilivyokuwa msituni basi magaidi hawa yawezekana waliletwa eneo lile kwa usafiri fulani mahali pale.Kwa maelezo ya askari aliyehojiwa Mick ,aliweza kung'amua upande ambao inawezekana ndiko magaidi wale walikoikia kabla ya kutawanyika kuzingira eneo lote.

Ndiyo.Ilikuwa ni rahisi kwa Mick kung'amua mambo haya kutokana na maelezo ya askari yule wa weledi wa E.C.S waliokuwa chini ya C.T.I ambaye alikuwa miongoni mwa askari waliokuwa wakilinda eneo lile la tukio ili ushahidi usipotee.Kilichopelekea askari yule kutoa maelezo kwa kina ni kwa kuwa pia alikuwa ni miongoni mwa askari waliosindikiza msafara uke uliovamiwa.Askari yule alimueleza ajenti Mick upande ambao risasi nzito zaidi kutoka kwa adui ziliwashambulia.Na ni upande huo huo ambako upinzani mkubwa ulitokea kuliko upande wowote.Mick aliposikia hayo aliweza kuhisi kuwa yawezekana upande huo ndiko upande ambao adui walikuwa wengi zaidi.Pia yawezekana risasi nzito kwa maelezo ya askari,zilitokea katika bunduki nzito nzito zilizofungwa katika magari ya adui.Basi kwa kusikiliza hayo na kuyachambua kichwani Mick aliuhisi upande huo na kuanza kufuatilia,akitokea barabara ya lami na kuingia msituni.

Mick alipasua msitu na kuukabili hadi kilometa moja na nusu msitu ukipoishia. Wakati huu wote,alikuwa anafuata njia za vumbi ambazo zilitawaliwa na tope katika msimu huu wa mvua Akitumia gari alilokabidhiwa,aina ya Range rover sport nyeusi iliyong'ara sana,Mick alifuatisha barabara ya vumbi iliyokuwa inapita nyuma,upande wa pili wa msitu huu kwa umbali wa kilomita moja tena. Kama ingepigwa picha kutoka juu sana,ama kama ilivyoonekana kwa picha za satelite, barabara hii ilikuwa upande wa pili wa msitu huu wa 'mipaina' ikionekana kwenda ki-msambamba na barabara ya lami.

Kilomita moja mbele ,Mick aliweza kung'amua alama za matairi ya magari zinazoingia msituni.Kilichompa dukuduku zaidi kuwa huenda hicho ndicho alichokuwa ankitafuta,ni kuwa alama zile zilizojichora katika tope zilionesha kuwa magari zaidi ya nane yalipita eneo hili na kuchepuka kuingia msituni.Alama hizi zilinoga zaidi eneo la miti michanga ambapo miti ilikanyagwa sana.Akiwa ameshuka kutoka garini,kwa miguu yake Mick alipasua pori na kuanza kufuatilia matairi hayo huku bastola yake aina ya bereta ikiwa kiunoni na ile ndogo ya 'colt 45' ikiwa imepachikwa katika soksi mguu wa kulia.Kufuatilia huku kulimpeleka hadi mita 300 ndani ya msitu ule,eneo ambalo alama za matairi ya magari yale ziliishia.Hapo Mick aliona kitu ambacho kilimuhakikishia kuwa adui walifikia katika eneo hili na kisha kutawanyika.Eneo lilikuwa limetawaliwa na maganda ya risasi kwa uwingi hasa. Maganda ya risasi kutoka katika bunduki nzito nzito yalikuwa yametawanyika katika eneo hili.Bunduki ambazo aidha zilikuwa zimefungwa kwenye magari au hata kama zilibebwa na magaidi wale basi wasingeweza kutembea nazo kwa umbali mrefu kutoka katika gari kutokana na uzito wake.Hili nalo lilizidi kumthibitishia kuwa hapa ndipo maadui walifikia nakutawanyika kufanya mashambulizi.

Baada ya kujihakikishia kwa hili,Mick alirudi katika gari lake na kuanza kufuatilia alama zile.za magari zilizokatisha msituni na kuishia mahali alikokuta maganda ya risasi mengi,upande zilikotokea kabla yakukatisha porini hapo.

Akiwa anaendesha gari lake huku akifuatilia alama za matairi za magari haya mahali zilikotokea, alama hizi zilimpeleka kilomita nane mbele,mahali ambako barabara hii ilipita nyuma ya kambi la jeshi la kujenga taifa.Kambi ya Mafinga.

Hapa Mick aliona alama za matairi zikiwa zimechepuka kidogo na kisha mbele kurudi usawa wa mwanzo.Alama hii ilikuwa ni ya matairi ya gari dogo.Mick alipaki gari pembeni, akashuka na kuchuchumaa kuangalia kwa umakini alama zile huku akionekana kutafakari jambo.

"Hapa yalipita magari madogo mawili na makubwa au labda malori sita.Kati ya haya magari makubwa kulikuwa na magari aina ya TATA mawili, IVECO mawili na ISUZU mawili.Hapa alama za matairi zinazoonekana kwenda pembeni kidogo nakisha kurudi usawa wa mwanzo na kutengeneza 'curve', kuna gari moja kati ya magari makubwa lilipaki kando na kisha kuendelea na safari,labda kuna jambo wahusika walifanya nje ya gari."Aliwaza ajenti Mick ndani ya kichwa chake.Kisha akageuka nyuma na kuona ukuta wa fensi upande wa nyuma wa kambi hilo ulivyo mrefu.Kisha baada ya ukuta huo kwa ndani kulikuwa na msitu wa miti mingi aina ya milingoti na miti ya matunda mingi. Majengo hayakuonekana labda utumie kiona mbali kutokana na msitu ulivyoshona mahali hapo,hivyo Mick akatambua kuwa si rahisi kwa walio ndani kujua nini kinaendelea nje.Lakini alipokaza macho vizuri, aliona kamera za CCTV zilizofungwa kwa juu katika jengo hilo ambapo kama si utaalamu na uzoefu wa kazi yake pengine asingeziona.

Na hapo ndipo alipowasiliana na ajenti Clara ili amsaidie kwa utundu wa kompyuta kuingilia mfumo wa kamera hizi na ikiwezekana kuibia mambo yaliyorekodiwa nyakati za tukio lile lilipotokea.

Mara baada ya kuwasiliana na ajenti Clara,Mick alirudi katika gari lake na kuendelea kufuatilia alama za matairi alizokuwa anazifuatilia tangu mwanzo.Alifuatilia zilikotokea kabla ya eneo hili alikotoka.Mbelealimaliza eneo la usawa wa jeshi.Mbele kidogo ya hapo alikutana na magari yanayobeba mbao yakitokea katika upande mmoja wa barabara hii ya tope na kwenda porini kwa kufuata barabara nyingine.Hii barabara iliyofuatwa na malori haya na ile inayotoka nyuma ya jeshi zimeunganishwa kwa barabara moja huko zilikotokea.Kwa sababu hiyo ikawa siyo rahisi kwa Mick kuweza kuendelea kung'amua alama zile za matairi alizokuwa anazifuatilia kwani zilichanganyika na alama za matairi za malori yale naa pengine zilifutwa kabisa na kubaki alama za malori yale.

Akiwa amekata tamaa ya kufuatilia kile alichokuwa anakifuatilia,akaona si vibaya akiuliza kitu kutoka kwa bwana mmoja aliyekuwa akibadilisha tairi katika roli lake lililokuwa tupu.Bwana huyu alionekana kama ndiye dereva wa gari lile na kwa upande ambao gari lake lilitazama,ilionekana kuwa ndiyo anaenda kufuata mzigo wa mbao.

"Samahani braza".Mick alianzisha mazungumzo na dreva yule ambaye ndiyo kwanza alikuwa amegundua kuwa kuna mtu nyuma yake.

"Bila samahani kaka sijui nikusaidie nini".Alijibu kwa staha dreva yule hasa kutokana na unadhifu wa huyu mgeni wa ghafla(Mick).Ama kwa hakika jinsi dreva huyu alivyoongea kwa adabu ungeweza kudhani kuwa madreva wa malori ni watu wa staarabu sana.Lakini kumbe...........

"Hivi ni kwa nini mnapita njia ndefu na malori yenu. Mbona kuna njia fupi hii inayopita nyuma ya jeshi au wajeda wanamaindi nini.?" Alihoji Mick.

Yule dreva aliyeulizwa swali hili akamuangalia Mick usoni kwa sekunde kadhaa kwa kukereka kisha akafungua mdomo wake.

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog