Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

UKURASA WA GAIDI - 2

  

Simulizi : Ukurasa Wa Gaidi 

Sehemu Ya : Pili (2)


iliyojengeka katika mwili wake ule.Usoni

alionekana kama mtu aliye na umri wa miaka

mwishoni mwa arobaini au mwanzoni mwa miaka

hamsini.

Mara mtu huyu alipokanyaga ardhi,watu kadhaa

waliokuwepo mahali hapo wakiwa webeba bunduki

zao, walipiga goti moja chini na kukunja mkono wa

kulia mbele huku wakiinamisha ichwa chini usawa

wa mkono uliokunjwa kama ishara ya heshima

kubwa.Kwa kuwaangalia tu, ilionekana huyu

aliyekuwa mbele yao alikuwa mtu mkubwa na

mwenye kuheshimiwa sana na watu hawa.

Bwana yule akawataka watu wale

wasimame,akawakumbatia kila mmoja na

kuwabusu katika paji la uso huku akizungumza nao

kwa lugha ya kiarabu.Wakati huo huo helkopta

nyingine ikawasili eneo hilo.Hii ilikuwa na chapa

ya shirika la utangazaji la CNN. Bwana mkubwa

yule akaongozwa na watu wake hadi katika

helkopta ile na baada ya kupanda ikapaa na

kutokomea kutoka katika eneo hilo. Sekunde

chache baada ya helkopta ile kupaa, ile helkopta

iliyotumika kubeba gari, ililipuka na kuteketea

kabisa.

*********************************************

*****************************************************

"Breaking news".Ndivyo vioo vya luninga

vilivyosomeka siku hiyo.Vituo mbali mbali vya

televisheni vilikatisha matangazo ya kawaida na

kurusha habari hizi mpya zilizokuwa na msisimko

kuliko habari nyingine.Vituo vikubwa vya

televisheni na radio viliripoti moja kwa moja

kutoka eneo la tukio.Makamanda waliohusika

kuongoza msafara ule walihojiwa nao wakatoa

ushirikiano wa kutosha. Vyombo vya habari vya

kimataifa kama BBC,CNN,ALJAZEERA na Sky News

navyo viliripoti kupitia wawakilishi wake.Dunia

nzima ilipata habari hizi za kuogofya moja kwa

moja kwamba yule gaidi aliyeisumbua dunia kwa

uhusika wake katika matukio mbalimbali bwana

'Omar Al-Mahmood' ametoroka tena kutoka katika

ulinzi mkali sana.

Usiku ulipita,siku mpya ikaanza kwa mchaka

mchaka wa hali ya juu.Jua lilichomoza wakati

makachero wa polisi na wanausalama wa vitengo

na idara mbali mbali wakiwa wamemwagwa kila

kona ya nchi. Wanausalama walipewa maagizo ya

kuacha kazi nyingine zote zisizo na uhitaji wa

haraka na kipaumbele chao kiwe ni kesi hii

iliyokuwa mbele yao. Kesi ya kutoroshwa kwa

gaidi aliyesemwa kuwa ni hatari sana zaidi ya

magaidi waliowahi kutokea katika historia ya bara

la Africa.

Baadhi ya wananchi walisikika wakitoa sifa kwa

kituo cha habari cha CNN kwa kuwahi kuelekea

eneo la tukio kabla hata mapambano hayajapoa

vizuri. Watu wengine walienda mbali zaidi kwa

kusema kuwa vyombo vya habari vya Tanzania

vimelala sana.Wapelelezi waliomwagwa kila kona

ya nchi walisikia habari ya helkopta ya shirika la

habari la ' CNN' kuonekana ikielekea eneo la tukio

kabla hata watu hawajajua ni nini kinaendelea.Lak

ini haikuchukua muda kwa wapelelezi kujua kuwa

ilikuwa ni helkopta ya 'CNN feki'. Magazeti nayo

hayakuwa nyuma kiripoti habari hii.

Gazeti la 'MTANZANIA MZAWA' liliandika " Gaidi wa

kimataifa aliyekamatwa na vyombo vya usalama

vya marekani kwa kushirikiana na Tanzania

ametoroshwa kutoka chini ya ulinzi mkali

alipokuwa anasafirishwa mara baada ya kutokea

mapambano makali sana.Gaidi huyo alikamatwa

katika mpaka wa Tunduma mkoani Mbeya wakati

alipokuwa akitaka kutorokea nchini

Zambia.Mapambano haya yalitokea baada ya

msafara huo kuvamiwa na kundi kubwa la watu

wanaodaiwa kuwa ni magaidi kutoka nchini

Somalia. Aidha maswali ambalo watu wengi

wanajiuliza sasa ni kuwa inawezekana vipi kundi

kubwa la magaidi kuvuka mipaka yetu na kuingia

nchini kwetu bila vyombo vya usalama kung'amua?

Na ni vipi watu hawa wavushe silaha nyingi kiasi

kike bila vyombo vya usalama kuona?"



AGOST 7, 1998

Siku hii ni kati ya siku ambazo wanaafrika

mashariki hawataisahau. Ofisi za ubalozi wa

Marekani nchini Tanzania na ubalozi wa Marekani

nchini Kenya zililipuliwa na Magaidi.Wahusika

walikuwa ni magaidi wa kikundi cha Alquaeda.

Moja kati ya watu waliotekeleza kusuka mipango

ya kufanikisha tukio hilo ni Omar Al-Mahmood.

Waweza kujiuliza Omar Al-Mahmood ni nani

kiundani sana? Ni mmoja wa viongozi wa ngazi za

juu wa Al-shabaab.Anasifika sana kwa kuwa na

ushawishi,utashi na kuwa na misimamo mikali

sana. Wakati wa mkakati wa kutekeleza matukio ya

kigaidi katika balozi za marekani nchini Tanzania

na Kenya, kikundi cha alquaeda kilifanya

mazungumzo na kikundi rafiki cha al-

shabaab.Wakati huo kikundi cha Alshabaab

hakikuwa na umaarufu kama ilivyo sasa bali

kilikuw ndiyo kwanza kinachipua bado.Mawasiliano

haya yalikuwa yamefanyika kwa kuwa iliaminika

Somalia iko karibu na Kenya na Tanzania hivyo

wanafahamu vizuri nchi hizi kuliko alquaeda

ambao makao makuu yao yapo Afghanistan. Omar

Al Mahmood alifanikisha tukio hili kwa mipango

yake yenye utashi na utaalamu wa hali ya juu.

Siku hiyo (August 7, 1998) alfajiri,gari lililobeba

milipuko (mabomu) lilionekana nje ya ubalozi wa

Marekani barabara ya Laiboni mahali ambako

ubalozi huu ulikuwepo.Gari hilo lilikuwa likienda

kasi na kutaka kuingia ubalozini moja kwa moja.

Lakini lilizuiliwa na lori la maji lililokuwa

linamilikiwa na ubalozi huo.Baada ya muda kidogo,

gari hili lililipuka kwa kishindo na kujeruhi na kuua

watu kadhaa.

********:*************

C.T.I

Idara ya kupambana na ugaidi Tanzania iliundwa

mwaka 2002. Hii ilikuwa ni miaka minne imepita

tangu lilipotokea shambulio la ugaidi katika ubalozi

wa Marekani nchini.Mara tu baada ya tukio la

ugaidi kutokea, nchi ya Tanzania iliona ni vyema

kuanzishwa kwa idara hii huru. Hili lilishauriwa na

wakuu wa mambo ya usalama kwa kuzingatia

kuwa ,suala la kupambana na ugaida lilikuwa chini

ya idara ya usalama wa taifa (TISS) ambayo ndiyo

idara kubwa ya intelijensia nchini.Kwa kuwa

Tanzania ilikwishaonja joto la ugaidi wakati huo,

ilionekana ni vyema ikianzishwa idara maalum kwa

ajili ya kupambana na ugaidi pekee. Hapo ndipo

idara hii ilianzishwa ikiwa na mamlaka kamili ya

kupambana dhidi ya ugaidi au tishio lolote la

ugaidi kutoka ndani na nje ya nchi.

Idara ya C.T.I(Counter Terrorism Inteligence),il

iundwa na vitengo vikuu vinne. Wapelelezi

walioenda kufanya kazi kwa vitendo uwanja wa

mapambano ( field agent ), wataalamu wa

teknolojia ya kompyuta(information technology/

data analysis), wataalamu wa maabala na kikosi

cha askari maalum wenye weledi wa hali ya juu

kwa mapambano kinachoitwa E.C.S(Elite Combat

Squad).

OFISI ZA C.T.I DODOMA

Mkurugenzi wa idara hii nyeti bwana Eliakim

Makassy alikuwa ana harakati nyingi sana ofisini

mwake.Hii ilitokana na kazi ngumu ambayo ilikuwa

inaikabili idara hii iliyo chini yake.Tangia hapo jana

alipopata taarifa rasmi ya matukio yote

yaliyojitokeza likiwepo la kutoroka kwa gaidi hatari

zaidi Africa kwa kuratibu matukio mbalimbali ya

ugaidi, hakutulia kabisa. Mara ashike karatasi

hili,mara apige simu pale, mara acheze na

kompyuta iliyokuwapo mezani.Yaani ili mradi

alikuwa bize kuliko kawaida.

Kazi kubwa aliyokuwa anaifanya katika kompyuta

iliyokuwa mbele yake, ni kufuatilia kiumakini zaidi

majina mawili.Omar Al-Mahmood na Abdallah

Yusoof.Si kwamba ilikuwa ni mara ya kwanza

kuwafuatilia watu hawa.La hasha.Hata kuanzishwa

kwa idara hii ulitokana na tukio lililomuhusisha

Omar Al Mahmood.Baada ya kuanzishwa kwa idara

hii, kazi yao kubwa ya kwanza ilihusiana na

kukusanya data mbali mbali kumuhusu Omar.Na

hata wakati wakikusanya data mbalimbali

kumuhusu, ndipo jina La abdallah Yusoof

likajitokeza mara kadhaa ndani ya upelelezi

wao.Kujirudia kwa jina La Abdallah Yusoof katika

matukio yaliyofanywa kwa mipango ya Omar Al

Mahmood, kulisababisha waanze kufuatilia haba ri

zinazomuhusu Abdallah Yusoof. Upelelezi huu

ulipofika hatua kadhaa mbele, ulisababisha Yusoof

awekwe katika vipaumbele vyao kati ya watu

wanaotafutwa zaidi.

Eliakim Makassy alikuwa akichambua taarifa

mbalimbali muhimu kutoka katika taarifa nyingi

walizokuwa nazo ndani ya idara.Pengine inaweza

kushangaza.Kwamba mkurugenzi ni mtu mzito

sana.Kwa nini afanye kazi ya kuchambua taarifa

badala ya kumpa kazi hiyo mtaalamu wa

kuchambua data(data analyst)? Makassy alikuwa

mkurugenzi wa tofauti sana. Kwanza alipenda

kujishughulisha kwa kila jambo ambalo lilikuwa

ndani ya uwezo wake. Yaani wakati mwingine

kama mtu angeingia katika ofisi za idara hii,

pengine angeweza kukaa hata masaa mawili bila

kutambua kuwa mkurugenzi wa idara hii ni

nani.Alijichanganya na maajenti wengine na

kufanya nao kazi kila alipopata nafasi. Lakini mbali

na kupenda kujishughulisha tu,Makassy alikuwa ni

mtaalamu wa mambo ya kompyuta.Hivyo wakati

mwingine maajenti wanaohusiana na utaalamu wa

kompyuta wakiwa na majukumu mengi sana

aliwasaidia kazi hii kwa mikono yake.

"Ngrii ngrii". Simu ya mezani iliita.Makassy ni

kama alitegemea simu hii kuita kwa namna ali

yoipokea haraka kabla haijaita mara ya pili.

"Hallow. C.T.I hapa."

"Unahitajika Ikulu haraka kadri inavyowezekana."

Upande wa pili ukaongea

"Sawa . Niko njiani".Alijibu Makassy.Kisha alipanga

makabrasha mawili matatu na kompyuta mpakato

yake katika begi dogo la mkononi kisha

akatokaofisini kwake.Alielekea moja kwa moja

katika kiwanja kidogo kilichokuwa nje ya ofisi za

C.T.I.Hapo alipanda katika helkopta moja iliyokuwa

imepaki hapo, kisha akaipaisha kuelekea Dar es

salaam.

IKULU.Dar es salaam

Baada ya muda,Makassy alitua helkopta yake

sehemu maalum ndani ya viwanja vya ikulu.Mara

baada ya taratibu mbili tatu kukamilika, aliongozwa

na mtu mmoja anayehusika na usalama ikulu hadi

katika ofisi ya Rais George Katumba.Mara

alipoingia katika ofisi hii, alimkuta rais anaongea

katika simu ya mezani.Zaidi ya raisi pia alikuwepo

waziri mkuu wa Tanzania mheshimiwa Abdulahman

Mohamed, pamoja na waziri wa ulinzi

muheshimiwa Michael Josheph Magombe. Rais

akaonesha kwa ishara tu, kumtaka Makassy akae

kwenye moja ya sofa zilizokuwa katika ofisi

hiyo.Mara baada ya kumaliza kuongea na simu,rais

alisabahiana na Makassy kisha akatoka katika kiti

chake cha kiofisi, na kwenda kukaa katika sofa

nyingine iliyokuwa inamtazama kiupande upande

Makassy.

"Ndiyo bwana Makassy, nadhani utakuwa

umekwisha kuhisi jambo tunaloelekea

kuzungumza.Ama niseme nadhani ulikuwa

unasubiri kusikia kutoka kwangu ili uanze mara

moja kufanya jambo hili linaloihusu idara

yako."Alianza kuongea Rais kisha akaendelea"

Sasa ninaweka suala hili mikononi mwako kuanzia

sasa kazi ianze mara moja. Nimeongea na

Marekani ambao ndiyo walikuwa wanaendesha

oparesheni ya kumkamata Omar Al Mahmood

kabla hajakimbia na kukamatwa mpakani akitaka

kwenda Zambia kisha kutoroshwa tena. Wao

wamesema kuwa kwa kuwa haya ni mambo ya

ndani ya Afrika, yanausikiliza umoja wa nchi za

Afrika utakavyoamua. Nimezungumza na umoja wa

Afrika, tumefikia muafaka.Tumepewa miezi mitatu,

kama hakutakuwa hata na mafanikio kidogo, basi

itabidi tuwaachie Marekani wafanye kazi hii. Kwa

hiyo idara yako inatakiwa kuonesha mafanikio juu

ya kazi hii kabla miezi mitatu haijaisha. Serikali

itakuwa bega kwa bega nyuma yako na itakupa

kila msaada utakaohitaji katikakufanikisha

hili.Tambua Afrika yote, na nchi zote zilizo mstari

wa mbele kupambana na ugaidi ziko nyuma

yako."Alimaliza kuongea rais.

"Ahsante sana muheshimiwa kwa kuiamini idara hii

na kuikabidhi kazi kubwa hivi.Naahidi

hatutakuangusha. Ila ninaomba tu vyombo vingine

vyote vya usalama viendelee na majukumu yao ya

kawaida na waachane na kesi hii, hadi pale idara

hii itakapo hitaji msaada wao".Aliongea Makassy.

"Sawa hilo halina shaka".Aliongea rais.

"Sijui kama kuna la nyongeza"Alihoji rais huku

akiwaangalia waziri mkuu na waziri wa ulinzi.

"Nadhani uko sawa kabisa"Aliongea kwa kifupi

waziri mkuu.

"Hata mimi nadhani muheshimiwa umeongea vizuri

sana.Nadhani hii idara inastahili kabisa kufanya

kazi hii kwa kuwa inaongozwa na mtu makini

sana.Nadhani cha msingi tu kuendelea

kushikamana na kuwasiliana kila mahali ambapo

idara hii itafikia. Nadhani tutalifumbua fumbo hili

kwa ustadi wa hali ya juu." Aliongea pia waziri wa

ulinzi.Mmoja wa mawaziri waliosifika sana kwa

kuwa wazalendo.

Baada ya hapo waliongea kuhusu mipango mbali

mbali ambayo Makassy alikwishafikiria kuhusiana

na suala lililokuwa mbele yao.Baada ya hapo

waliagana, Makassy alirudi Dodoma kuanza

kutekeleza kazi ambayo idara ya C.T.I ilipewa.

HISPANIA

Visiwa ya Ibiza

Jua lisilo na miale mikali liliwaka huku upepo

mwanana wa bahari ukivuma taratibu bila

bugdha.Watu wengi walikuwepo katika eneo la

ufukwe wakipunga upepo ,wengine wakiwa na

wenzi wao na wengine na familia zao.Ilikuwa ni

kipindi cha mwisho wa wiki hivyo watu wengi

walifika pale kwa mapumziko ya wikiendi.

Japo wengine walifika kwa mapumzikobya wiki

endi tu, lakini kuna baadhi ya watu walikuwa katika

mapumziko ya likizo ya muda mrefu.Hasa wale

waliokuwa na pesa za kutosha na waliojua

kuzitumbua pesa hizo walikaa mahali hapa

hadibpake limizo zao zilipokwisha. Mmoja wa watu

hawa ni kijana Mmoja wa Kitanzania.Kwa

muonekano wake ,ni mrefu wa wastani mwenye

sura na haiba ya kuvutia, mwenye mwili wa

wastani uliojengeka kimazoezi. Kwa Jina anaitwa

Mick-Reuben Garino.

Wakati huu alikuwa amejilaza katika mchanga

akiwa na mrembo mmoja wa kihispania ambaye

amekuwa akimpa kampani kwa kipindi chote cha

likizo hii.Hadi sasa,Mick alikiwa ni kijana wa umri

wa miaka 28.

Ni mwezi wa pili sasa tangu Mick afike katika

visiwa hivi na amefanya anasa sana tu. Katika

wakati ambao anakuwa nje ya majukumu yake

halisi, Mick alikuwa ni mfanyabiashara wa madini.

Alikuwa na ofisi yake Dar es salaam Tanzania

ambako watu walienda kuuza na wengine walienda

kununua madini na vito aina mbalimbali, biashara

iliyomuingizia pesa nyingi na kumuweka katika

watu waliokuwa na pesa nyingi.

Lakini kitu ambacho wengi hawakukijua,katika

majukumu yake halisi Mick ni ajenti namba moja

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog