Search This Blog

Wednesday 29 March 2023

PENIELEA (5) - 1

 

IMEANDIKWA NA : PATRICK CK




*********************************************************************************



Simulizi : Peniela (5)

Sehemu Ya Kwanza (1)

“ Dr Joshua is here? Akamuuliza Yule 
mlinzi 
 “ Yes he’s here and I’m going to ask him if 
he knows you.Kama umedanganya utakuwa 
umejiweka katika matatizo makubwa sana kwa 
kuhatarisha usalama wa rais.” Akasema Yule jamaa na kumkabidhi Peniela kwa mlinzi 
mwanamama ili amkague na alipohakikisha hana 
silaha yoyote akaelekea ndani 
 “ Stay Calm Peniela.Usionyeshe woga wa 
aina yoyote” Mathew akamwambia peniela kupitia 
kifaa cha mawasiliano Peniela alichokivaa sikioni. 
ENDELEA SEASON 5 
 “ Dr Joshua “ akasema Donald baada ya 
chumba kutawaliwa na ukimya 
 “ Baada ya kukueleza suala la pili lililonileta 
hapa, sasa turejee katika suala la kwanza.” 
Akasema Donald 
 “ Sawa endelea” akasema Dr Joshua 
 “ Awali nilikueleza kwamba tayari 
tumekwisha fanya mipango yote ya kumuua 
Andrew Rodney na Deus Mkozumi na kazi hiyo 
itafanywa na Alqaeda na litaonekana ni shambulio 
la kigaidi.Serikali ya Tanzania wala Marekani hazitahusishwa kabisa na tukio hilo badala yake 
nchi zote zitaulaani kwa nguvu mtandao wa 
Alqaeda kwa kitendo hicho.” Donald akanyamaza 
kidogo halafu akaendelea 
 “ Ili kuutekekeleza mpango huo,Alqaeda 
wametoa masharti mawili.Sharti la kwanza 
tumuachie huru mmoja wa watu wao muhimu 
ambaye tunamshikilia katika mojaya magereza 
yetu.Hilo tayari tumelikubali na tutamuachia huru 
kiongozi wao.Sharti la pili kuna kiongozi wao 
muhimu sana anashikiliwa nchini Saudi Arabia 
ambaye wanataka aachiwe.Serikali ya Saudi 
Arabia haiku tayari kumuachia kiongozi huyo kwa 
hiyo Alqaeda wanataka kuilazimisha serikali ya 
Saudi Arabia kumuachia kiongozi wao na hilo 
wataklifanya kutokea hapa nchini Tanzania” 
 “ Tanzania tena??!!...Dr Joshua akauliza 
 “ Ndiyo .Wanataka jambo hilo lifanyikie 
hapa Tanzania” akasema Donald na kukawa 
kimya.Mara mlango ukagongwa Dr Joshua 
akaenda kuufungua.Alikuwa ni mmoja wa walinzi 
wake Unasemaje Peter? 
 “ Mzee kuna kitu kimetokea hapa nyumbani 
sasa hivi” 
 “ Kitu gani? akauliza Dr Joshua kwa wasi 
wasi 
 “ Kuna mwanamke mmoja amefika hapa 
anasema anaitwa Peniela na anadai kwamba 
anaishi hapa na anakufahamu na wewe ndiye 
uliyemruhusu aishi hapa” 
 Mwili wa Dr Joshua ukastuka kama vile 
umepitiwa na chaji za umeme 
 “ Peniela ???..where is she? Akauliza 
 “ Yuko nje tunamshikilia” 
 “ Muachieni haraka aingie ndani ila mpitishe 
kwa mlango wa nyuma aende moja kwa moja 
chumbani kwake na asiruhusiwe kutoka hadi 
nitakapomaliza maongezi na mgeni 
wangu”akaamuru Dr Joshua 
 “ sawa mzee” akajibu Peter na kuanza 
kuondoka Dr Joshua akamuita 
 “ Peter sitaki jambo hili alifahamu mtu 
mwingine zaidi ya ninyi mlioko hapa.Kuhusu wale polisi pale getini tafuta namna yoyote ya 
kuwadanganya .Tell them she’s my relative or 
anything.” 
 “ Sawa mzee nitafanya hivyo” akajibu Peter 
kwa adabu 
 “ Another thing,umewasiliana na Kareem? 
Akauliza Dr Joshua 
 “ Ndiyo mzee nimewasiliana naye 
ameniambia kwamba yuko maeneo ya kule 
msibani” 
 “ Ok Good” akasema Dr Joshua na Peter 
akaondoka 
 “ Peniela !!!.Finaly I’ve got her...” akawaza 
Dr Joshua huku akihisi mwili unamtetemeka kwa 
ndani kiasi cha kumshangaza hata yeye 
mwenyewe ... 
 “ Sijui kwa nini kila ninapolisikia jina 
Peniela,mwili wote hunitetemeka.Ngoja kwanza 
nimalize maongezi na Donald halafu nitakwenda 
kuonana naye nifahamu kitu gani kilichomleta 
hapa.Nashukuru amejileta mwenyewe ,nilikuwa 
naumiza kichwa ningempata wapi.Nilikwisha sahau kabisa kama nilimkabidhi nyumba hii aishi.” 
Akawaza Dr Joshua aliyekuwa amesimama karibu 
na mlango mara akastuliwa na Donald 
 “ Dr Joshua kuna tatizo lolote limetokea? 
Mbona umebadilika ghafla? 
 “ Oh hapana Donald…Tuendelee na 
maongezi yetu.Tuliishia wapi? 
 “ Nilikueleza kwamba Alqaeda wana 
kiongozi wao anayeshikiliwa nchini Saudi Arabia 
na wanataka kuishinikiza serikali ya Saudi Arabia 
imuachie huru na jambo hilo litafanyika kutokea 
hapa Tanzania” akasema Donald 
 “ Naomba unifafanulie vizuri 
Donald.Wanataka kufanya nini kuishinikiza serikali 
ya Saudi Arabia imuachie kiongzo wao? Akauliza 
Dr Joshua ambaye macho yake yalionyesha wazi 
alikuw ana wasi wasi mwingi 
 “ Binti mfalme wa Saudi Arabia aitwaye 
Salhat Abdullah atatembelea Tanzania kwa 
mwaliko wa rafiki yake ambaye ni Dr Lucia 
Mkozumi .Salhat na Dr Lucia wanafanya kazi 
pamoja katika shirika la fedha la umoja wa mataifa kwa hiyo ni marafiki wakubwa.Binti mfalme huyo 
ambaye anapendwa mno na baba yake 
atakapofika hapa Tanzania atatekwa nyara na 
atatumika katika kuishinikiza serikali ya Saudi 
Arabia imuache kiongozi wa Alqaeda ili Salhat 
aachiwe huru.Kwa jinsi Salhat anavyopendwa na 
baba yake lazima atakubaliana na matakwa ya 
Alqaeda tu.”akasema Donald 
 “ Wanataka kumteka mtoto wa mfalme? 
Hebu nifafanulie Donald watafanyaje hilo? Mbona 
mambo mengi yanataka kutokea hapa nchini 
ndani ya kipindi kifupi? 
 “ Mpango mzima uko hivi.Lucy ambaye 
ndiye aliyemualika salhat kuja hapa nchini 
ataongozana naye hadi katika jengo la biashar ala 
Dar city shopping mall kwa lengo la kufanya 
manunuzi ya vitu mbali mbali kwa ajili ya kupeleka 
zawadi katika vituo vya watoto wanaoishi na virusi 
vya ukimwi kwani Salhat anayo taasisi yake 
inayojishughulisha na kuwahudumia watoto wa 
aina hiyo .Katika msafara huo Dr Lucia anapaswa 
kuhakikisha kuwa baba yake Deus Mkozumi anaambatana nao .Wakati manunuzi yakiendelea 
Lucia atampeleka Salhat katika duka moja 
linalouza vinyago..Atakapofika huko Alqaeda 
watalivamia jengo hilo na kuwachukua mateka Dr 
Lucia na Salhat na hapo ndipo Deus Mkozumi 
atakapouawa” 
 Dr Joshua akatoa kitambaa na kujifuta 
jasho lililoanza kumtoka usoni.Alihisi joto kutokana 
na mambo mazito aliyoelezwa na Donald 
 “ Nini kitafuata baada ya hapo? Akauliza Dr 
Joshua kwa wasi wasi 
 “ Dr Lucia Mkozumi ataachiwa huru,Salhat 
ataendelea kushikiliwa na magaidi na ili aachiwe 
huru watashinikiza kuachiwa huru kwa kiongozi 
wao kwanza” akasema Donald 
 “ Itakuaje endapo madai yao 
yasipotimizwa? Akauliza Dr Joshua 
 “ Ikitokea kwamba madai yao yasipotimizwa 
wataondoka na Salhat na itakulazimu kuwasaidia 
kuondoka hapa nchini lakini kwa utafiti uliofanyika 
tunaamini lazima madai yao yatatekelezwa kwani 
mfalme anampenda mno mtoto wake.Kiongozi wao atakapoachiwa huru watamuachia Salhat na 
watapotea zao” 
 Dr Joshua akafikiri kidogo halafu akasema 
 “ Nina wasiw asi katika shambulio hilo 
litakalofanyika Dar city shopping mall,watu wasio 
na hatia watapoteza maisha yao.” 
 “ Ni kweli hilo unalolisema Dr Joshua na 
haliwezi kuepukika.Lazima watu wapoteze 
maisha .Nadhani unafahamu namna 
mashambulizi ya kigaidi yanavyokuwa,lazima 
idadi kadhaa ya watu wapoteze maisha” 
 “ Naogopa sana Donald kusema chochote 
kwa sasa hasa nikivuta picha ya watu wasio na 
hatia wakiwa wamelala chini hawana 
uhai...Inaniogiopesha sana.Damu ya watu hao 
wasio na hatia itatuandama sisi tuliosaidia 
kufanikisha shambulio hilo.” Akasema Dr Joshua 
 “ Usiogope Dr Joshua.Kazi ya urais ni 
ngumu na kuna nyakati unatakiwa kufanya 
maamuzi magumu sana kwa maslahi mapana ya 
nchi.Wakifa watu kumi au ishirini si kitu kwani 
kuna mamilioni ya watu waishio vijijni watakwenda kunufaika na huduma za maji,afya,elimu,kilimo 
n.k.Kwa hiyo usiogope Dr Joshua kufanya 
maamuzi kwani maamuzi utakayoyafanya leo 
yanaakisi maendeleo makubwa kwa Tanzania 
kwa miaka mingi ijayo.Nakuhakikishia Dr Joshua 
baada ya miaka kumi Tanzania hii uionayo sasa 
haitakuwa kama unavyoiona leo.Itakuwa na 
mabadiliko makubwa mno lakini haya yote 
yanategemea maamuzi utakayoyafanya kuhusu 
suala hili” akasema Donald.Dr Joshua 
akainamisha kichwa akiwaza na baada ya muda 
akasema 
 “ Dr Lucia Mkozumi anafahamu kuhusiana 
na baba yake kutakiwa kuuawa ? 
 “ Anafahamu kila kitu na ameshiriki katika 
kuandaa mpango huo.Dr Lucia mkozumi 
hafahamiki kabisa hapa nchini na tukio hili 
litachangia sana katika kumtangaza.Dunia yote 
watamfahamu yeye ni nani ndani ya kipindi kifupi 
sana na atakapotangaza kuwania urais wa 
Tanzania haitakuwa kazi ngumu kumnadi.Dr 
Joshua kila jambo lina sadaka yake na Dr Lucia Mkozumi yuko tayari kwa lolote ili aweze kuupata 
urais wa Tanzania” akasema Donald..Dr Joshua 
akakosa neno la kusema 
 “ Dah ! huyu Lucia lazima atakuwa ni 
mwanamke mwenye roho ngumu sana.Kama 
kweli amekubali baba yake auawe na magaidi 
basi ni mwanamke anayefaa kabisa kuwa rais 
kwani urais unahitaji mtu mwenye kuweza 
klufanya maamuzi magumu kama aliyofanya Dr 
Lucia.She’s a monster just like me.Lakini hata 
hivyo siwezi kuukataa mpango huu kwani 
umekuja kwa wakati muafaka kabisa.Kwa muda 
mrefu nimekuwa nkitafuta namna ya kumuondoa 
Deus Mkozumi kwani amekuwa akiingilia sana 
mambo yangu na sasa nafasi hiyo imejitokeza na 
siwezi kuiacha.Nitaitumia fursa hiyo kumuondoa si 
Deus Mkozumi peke bali na mke wake Rosemary 
Mkozumi.I hate that woman so much.Najua 
atakuwa ni kikwazo kikubwa kwangu kufanikisha 
mambo yangu .Lazima nimuondoe haraka sana 
Yule mwanamke ili mpango huu usiingiliwe na 
kikwazo chochote”  “ Dr Joshua !!” akaita Donald na kumstua 
Dr Joshua toka mawazoni 
 “ Donald mambo uliyonieleza ni makubwa 
na mazito sana lakini ninaiona faida kubwa mbele 
yake.Japokuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa 
kasi kubwa lakini idadi kubwa ya raia wake bado 
masikini na kwa ahadi hizi ambazo serikali ya 
Marekani imeziahidi ninayaona mabadiliko 
makubwa kwa Tanzania.Kwa upande wangu mimi 
sina tatizo katika hili ilimradi tu ahadi zote 
zuilizoahidiwa zitekelezwe.Najua baada ya 
matukio hayo kutokea mtikisiko kidogo wa 
uchumi lakini nina imani ndaniya kipindi kifupi hali 
tarejea kuwa ya kawaida.” Akasema Dr Joshua 
.Donald kwa furaha aliyoipata akainuka na kumpa 
mkono Dr Joshua 
 “ Hongera sana Dr Joshua.Wewe ndiye rais 
unayeona mbali.Una mtazamo mpana sana kwa 
nchi yako.Ninakuhakikishia kuwa maamuzi yako 
ya leo yatakuwa na faida kubwa sana kwa nchi 
yako siku za usoni.Nakuhakikishia wananchi wa 
Tanzania watakukumbuka daima kwa kuwaachia rais kama Dr Lucia ambaye wakati wa uongozi 
wake serikali ya Marekani itamwaga misaada 
mingi sana kwa serikali yake itakayowanufaisha 
mamilioni ya watanzania.Nataka nikuondoe wasi 
wasi pia kwamba mambo yote yatakayotokea si 
Tanzania wala Marekani watakaolaumiwa bali ni 
mtandao wa Alqaeda.Wakati dunia ikiwalaani 
magaidi ,mamilioni ya watanzania watakuwa 
wanapata huduma za maji safi ya 
kunywa,huduma bora za afya,elimu nishati ajira 
pamoja na mambo mengine mengi toka kwa 
serikali ya Marekani.Kwa kauli yako hiyo 
mheshimiwa rais unaniruhusu niwataarifu 
wakubwa zangu kwamba umekubali ili tuweze 
kuendelea na hatua inayofuata? 
 “ Bila shaka Donald,unaweza kuendelea na 
hatua inayofuata.Nini kinachofuata baada ya 
hapa? 
 “ Hatua inayofuata ni kumleta nchini rais 
mtarajiwa Dr Lucia Mkozumi na tutakuwa na 
maongezi ya pamoja mimi,wewe,Dr Lucia pamoja 
na mratibu wa mashambulio mawili toka Alqaeda  Dr Lucia yuko nchini Afrika ya kusini akiwa 
ameambatana na binti mfalme Salhat 
nitawasiliana naye usiku huu na kesho atakuwa 
hapa nchini na kesho hiyo hiyo jioni tutakutana 
hapa kwa ajili ya kukaa kikao kizito cha kupanga 
mikakati ya utekelezaji wa matukio yote.” 
Akasema Donald. 
 “ Sawa Donald.Tutaonana hiyo 
kesho.Tutakutana hapa hapa kwani ndiyo sehemu 
salama zaidi kwa sisi kuongea na kupanga 
mipango yetu” akasema Dr Joshua na kuagana 
na Donald akamsindikiza hadi lilipo gari lake 
akaondoka zake na Dr Joshua akarejea sebuleni 
akaketi sofani 
 “ Mambo aliyotumwa Donald aje anieleze 
ni mambo mazito mno lakini endapo yatafanikiwa 
kutekelezwa basi nchi yetu itapata manufaa 
makubwa kuliko athari zitakazojitokeza katika 
utekelezaji wake .Nchi itayumba kidogo lakini 
ndani ya kipindi kifupi itakaa sawa na wananchi 
watasahau kabisa matukio yote.Suala hili 
ukilitazama kwa upana wake ni kweli Marekani wanastahili kulinda maslahi yake kutokana na 
kufanya uwekezaji mkubwa sana hapa nchini 
kuliko nchi nyingine yoyote afrika.Uwekezaji huu 
unawapa nguvu ya kuweza kuingia hadi katika 
siasa zetu na kuchagua rais wanayemtaka 
ambaye wanaamini atakuwa na manufaa 
kwao.Hili si tatizo as long as wananchi wetu 
wananufaika kwa misaada mikubwa itakayotolewa 
na Marekani.Kipindi changu cha uongozi,serikali 
ya Marekani wamekuwa ni wafadhili namba moja 
wa bajeti yetu ya serikali na miradi mingi ya 
maendeleo na endapo nikifanikisha Dr Lucia awe 
rais kama wanavyotaka misaada itaongezeka 
maradufu” akawaza Dr Joshua na kukumbuka kitu 
akatabasamu 
 “ Dr Lucia Mkozumi,huyu mwanamamama 
japokuwa sijabahatika kuonana naye lakini 
anaonekana anafaa sana kuwa rais.Anaonekana 
ni mtu jasiri na asiyesita kufanya maamuzi 
makubwa “ akawaza Dr Joshua akajimiminia 
whisky katika glasi na kunywa funda kadhaa  “ Kwa upande wangu nimeahidiwa mambo 
mengi makubwa .Kikubwa zaidi ni fedha nyingi.It’s 
a lot of money.Maisha yangu baada ya kustaafu 
yatakuwa mazuri mno.I’ll be like an angel in 
heaven.Laiti kama jambo hili lingekuja mapema 
kabla sijaanza mchakato wa kukiuza kirusi Aby 
katu nisingeuza kitu kile kilichojaa mikosi na hadi 
sasa mke wangu na mwanangu Flaviana 
wangekuwa bado hai..” 
 Mara wazo likamjia Dr Joshua 
 “ Kwa kuwa kuna huu mpango mpya 
umekuja ambao unaonekana ni bora zaidi na una 
maslahi mapana kwangu na kw anchi kwa nini 
nisiachane na mpango ule wa kukiuza kirusi 
Aby?.Kirusi kile naona kama vile kina mkosi kwani 
mpaka sasa tayari nimemkwisha wapoteza watu 
wangu wawili wa karibu sana halafu kitu kingine ni 
kwamba sifahamu Hussein anataka kukitumiaje 
kirusi hicho.” 
 Dr Joshua akanywa tena funda la mvinyo 
 “ Hapana siwezi kumpa Hussein kile 
kirusi.NItamrejeshea fedha zake zote .Najua itakuwa ngumu lakini hakuna namna nyingine 
lazima niachane na mpango ule na nielekeze 
nguvu katika mpango huu wa Marekani ambao 
una maslahi manono kwangu..” 
 Akatulia tena akanywa funda lingine la 
mvinyo 
 “ Dah ! Imekuwa ni siku ndefu sana 
iliyokusanya mambo mengi na kichwa changu 
kimechoka.Nahitaji kupumzika lakini kabla ya yote 
lazima nikaonane na Yule shetani wa kike 
Peniela.Nashukuru amejileta mwenyewe.” 
Akawaza Dr Joshua halafu akakumbuka maneno 
aliyoambiwa na jaji Elibariki kuhusu Peniela 
akapandwa na hasira na kutoka mle sebuleni kwa 
hasira akaelekea katika chumba alimokuwamo 
Peniela akaminya kitasa lakini mlango ulikuwa 
umefungwa kwa ndani.Akagonga kwa nguvu na 
taratibu mlango ukafunguliwa akajikuta 
akitazamana na sura yenye tabasamu ya Peniela. 



Halow my love” akasema Peniela.Dr 
Joshua akavuta pumzi ndefu baada ya 
kumshuhudia Peniela akiwa amesimama mlangoni akiwa na nguo ya ndani peke.Mapigo ya 
moyo wake yakabadilika na kuanza kwenda kwa 
kasi alipoushuhudia mwili ule mwororo .Kwa 
sekunde kadhaa wakabaki wanatazamana. 
 “ Karibu ndani mpenzi wangu” akasema 
Peniela kwa sauti laini.Dr Joshua hakujibu kitu 
akaingia ndani Peniela akaufunga 
mlango.Akamfuata Dr Joshua aliyekuwa 
amesimama 
 “ My love sikujua kama uko hapa..” 
akasema Peniela lakini Dr Joshua akamkatisha 
 “ Stop calling me yur love ,you evil witch!!! 
Akasema Dr Joshua kwa ukali huku akimsukuma 
Peniela akaangukia kitandani.Peniela akainuka na 
kumfuata Dr Joshua 
 “ Whats wrong my love??? 
 “ Don’t touch me you devil !!! akaendelea 
kufoka Dr Joshua huku akimtazama Peniela kwa 
macho makali yaliyojaa hasira. 
 “ Shhh..!!My love I’m not here to 
fight.Please calm down and tell me whats wrong 
with you and why you are so angry at me today.Sijawahi kukuona ukiwa katika hali hiyo 
hata siku moja.Lakini kabla ya yote tafadhali 
naomba nikupe kile ambacho umekuwa unakihitaji 
sana.” Akasema Peniela na kumkumbatia Dr 
Joshua na kuanza kumwagia mabusu mfululizo.Dr 
Joshua akakosa cha kusema kwani hasira 
zikampotea ghafla na kujikuta akipandwa na 
mdadi na kumkumbatia Peniela.Peniela 
anamfahamu Dr Joshua na anayafahamu maeneo 
ambayo yanampa uchizi mzee huyu hivyo 
akayatumia vyema kumpagawisha na kumfanya 
atoe miguno. 
 “ You called me devil,I’m going to show you 
I’m a real devil” akawaza Peniela na kumsukumia 
Dr Joshua kitandani akaanza kumchojoa nguo 
moja moja na kuendela na utundu wake huku Dr 
Joshua akilalama kama mtoto na kuongea 
maneno ambayo hayakuwa yakisikika vizuri,yote 
hii ilisababishwa na raha alizozipata.Peniela 
alipohakikisha Dr Joshua amepagawa vya 
kutosha akajiweka tayari kwa ajili ya mtanange. Mtanange wa dakika thelathini ulimuacha 
Dr Joshua akivuja jasho kama mkimbiaji wa mbio 
ndefu. 
 “ This woman is real amazing.Kila 
ninapokutana naye ananifanyia vitu ambavyo 
sijawahi fanyiwa na kuzidi kunipagawisha.Sijui ni 
uchawi gani anaoutumia kunivuruga akili yangu 
namna hii.Mambo aliyonifanyia leo yamenifanya 
hata hasira zangu zote nilizokuwa nazo juu yake 
zipotee.I think I still love this woman so 
much.Pamoja na yote ambayo jaji Elibariki 
alinieleza kuhusu Peniela but I still love her and I 
don’t know what I’m going to do because I cant let 
her go..Mara ya kwanza alinisaliti kwa kuanzisha 
mahusiano na Edson na kwa namna alivyoniudhi 
nilitamani afungwe kifungo kirefu gerezani ili 
apotee kabisa lakini ikashindikana na nilipokuja 
kuonana naye tena hasira zangu zote juu yake 
zikapotea na nikajikuta nikimpenda zadi na 
zaidi.Safari hii tena baada ya kupata taarifa za 
anachokifanya dhidi yangu nilimchukia na 
nikamuweka katika orodha ya watu ninaotaka  kuwashughulikia lakini baada ya kuonana naye 
hasira zote zimepotea na kwa mara nyingine 
ninajikuta nikizidi kumpenda Peniela.Mapenzi 
niliyonayo kwa Peniela ni makubwa mno na sijui 
kwa nini ameshindwa kulitambua hilo.Ni kiasi gani 
anacholipwa na hao watu wanaomtumia? 
Ninaamini hakuna kiasi anachoweza kulipwa 
kinachoweza kulingana na upendo wangu kwake” 
akawaza Dr Joshua na kugeuka akamtazama 
Peniela 
 “ Muda si mrefu nitamaliza kipindi changu 
cha uongozi na kwenda kuishi nje ya nchi.Nitaishi 
maisha ya kifahari mno kwa nini basi nisiende 
kuanza maisha yangu mapya na mrembo huyu 
ambaye ametokea kunipagawisha kuliko 
wanawake wote hapa duniani? Siwezi kumfanya 
chochote Peniela hata kama ni kweli amekuwa 
anatumika na watu kutaka kunihujumu kwa 
sababu bado ninampenda sana.Ni mwanamke 
pekee ambaye ananifanya nijione nina miaka 
ishirini kila ninapokuwa naye.Lazima nifanye kila 
ninavyoweza mpaka niondoke naye.Utajiri wote nitakaokuwa nao hautakuwa na maana kama 
sintakuwa na Peniela..” 
 “ Dr Joshua ..!!” akaita Peniela kwa sauti 
laini na kumuondoa Dr Joshua mawazoni. 
 “ Unasemaje Peniela? Akauliza Dr Joshua 
 “ Earlier you called me evil witch ,what was 
the meaning to call me that? Am I a witch to you 
now? Akauliza Peniela Dr Joshua hakumjibu kitu 
akamkazia macho 
 “ Sikutegemea kabisa kama siku moja Dr 
Joshua ungeweza kunitamkia maneno kama 
yale.Kitu gani kibaya nilichokufanyia mpenzi 
wangu kiasi cha kuniita majina yale mabaya? 
Tafadhali nieleze Dr Joshua kama kuna chochote 
nilichokukosea” 
 Dr Joshua akainuka na kukaa kitandani 
 “ Peniela you you know how much I love 
you,right? Akauliza Dr Joshua 
 “ Yes I know?” akajibu Peniela 
 “ Toka tumekuwa na mahusiano nimekuwa 
tayari kukufanyia jambo lolote ili kukuonyesha ni 
kwa namna gani ulivyo muhimu kwangu.Hukuwahi kuniambia chochote nikasema hapana lakini 
pamoja na kukupenda kote kwa nini unanifanyia 
hivi? Akauliza Dr Joshua 
 “ Nimekufanyia nini Dr Joshua? Peniela 
naye akauliza 
 “ Usitake kuniudhi Peniela.How much do 
they pay you? Tell me please how much?? 
Akasema Dr Joshua kwa ukali 
 “ Nani hao? Mbona sikuelewi Dr Joshua ?? 
akauliza Peniela 
 “ Team SC41.How much do they pay you? 
 Peniela akavuta pumzi ndefu na kusema 
 “ Team SC41 ni nini? Akauliza 
 “ Tuokoe muda Peniela.Ninafahamu kila 
kitu kuhusu wewe.Ninafahamu kwa nini uko na 
mimi na kitu gani unakihitaji toka 
kwangu.Nimeskitika sana Peniela baada ya 
kufahamu jambo unalonifanyia na ndiyo maana 
ninataka kufahamu unalipwa kiasi gani na hao 
waliokutuma kwangu? 
 “ Dr Joshua nashindwa kukuelewa 
unazungumzia kitu gani kwani hiyo team sijui nini 
sifahamu ni kitu gani na wanahusika na nini? 
Umetoa wapi taarifa hizo? 
 “ Peniela najua machoni unakataa lakini 
moyoni umestuka sana na unajiuliza nimefahamu 
vipi.Just tell me how much they pay you and I can 
pay you back a hundred times.” 
 “ Dr Joshua I don’t understand what you are 
talking about” akasema Peniela.Dr Joshua 
akamtazama Peniela kwa sekunde kadhaa na 
kusema 
 “ Kwa nini unanifanyia hivi Peniela? kwa 
nini unataka kunifanyia ukatili huu wakati mambo 
ninayoyafanya ni kwa ajili yetu sote? Ninataka 
nitakapomaliza kipindi changu cha uongozi mimi 
na wewe tuishi maisha kama ya mfalme lakini kwa 
nini hutaki kulielewa hilo na kutaka kuvuruga 
mipango yangu? Nilikupa nafasi ya kuchagua 
sehemu yoyote duniani unayotaka kwenda kuishi 
ili tukaishi nitakapomaliza kipindi changu cha 
uongozi lakini yote haya umeyaweka pembeni 
..Why Peniela??  “ Dr Joshua I real don’t understand 
you.Mambo unayonieleza ni mambo mageni 
kabisa kwangu na siyaelewi.” 
 “ Peniela ninakupenda sana ndiyo maana 
nnakwambia haya ili ufahamu nina lengo zuri na 
wewe.Mimi ni rais wa nchi na ninafahamu kila mtu 
aliye karibu yangu.Ninafahamu kila 
kinachoendelea.Uko hapa na mimi muda huu kwa 
sababu nimetaka iwe hivyo kutokana na upendo 
mkubwa nilionao kwako vinginevyo muda huu 
usingekuwapo katika ulimwengu huu” 
 Peniela akamtazama Dr Joshua huku 
machozi yakimchuruzika akasema 
 “ Dr Joshua ninaomba unieleze ni nani 
aliyekuambia maneno hayo? Ni nani huyo 
asiyetutakia mema katika mapenzi yetu na 
anataka kukutenganisha? Do you believe them 
than me?? 
 “ Peniela mimi ni raisi na ninazungukwa na 
watu ambao wamekula kiapo cha kunilinda hata 
kama ikiwabidi kuyatoa maisha yao kwa ajili yangu hivyo ninawaamini kwa kila 
watakachioniambia” 
 Peniela akamtazama na kutikisa kichwa 
 “ Siamini maneno hayo kama yanatoka 
kwako.Lini Dr Joshua utaniamini? 
 “ How can I trust you Peniela? You are a 
professional liar.A cheater !!” akasema Dr Joshua 
kwa ukali.Peniela akamnasa kibao 
 “ Iwe ni mara ya kwanza na ya mwisho 
kunitamkia maneno hayo machafu.Kama 
ningekuwa nina nia mbaya ningekwisha kufanyia 
kitu kibaya muda mrefu .You killed Edson na kesi 
ikaniangukia mimi.NiIiifahamu wewe ndiye 
uliyemuua Edson lakini sikufumbua mdomo 
wangu kusema chochote.Nimeteseka gerezani 
mwaka mzima lakini sikuwahi kuufungua mdomo 
wangu na kutamka neno lolote la kukuhusisha 
wewe na kifo cha Edson.Iweje leo hii unitamkie 
maneno hayo machafu? Akauliza Peniela huku 
akilia  “ Do you have any proof? Una ushahidi 
kwamba ninahusika katika kifo cha Edson? 
Akauliza Dr Joshua 
 “ Na wewe una ushahidi wa hayo 
unayonituhumu kuyafanya? Akauliza Peniela 
 “Ndiyo nina ushahidi .Usitake niyaanike 
mambo yako Peniela.Ninafahamu kila kitu 
unachokifanya.Ninaifuatilia kila hatu unayopiga 
kwa hiyo ninakufahamu zaidi ya 
unavyojifahamu.Nafahamu umetumwa kwangu na 
Team SC41,ninafahamu unashirikiana na mtu 
anayeitwa Mathew ambaye aliwahi kufanya kazi 
katika idara ya usalama w a taifa .Nafahamu 
umetembea na Dr Kigomba na ulimtumia ili 
kufanikisha mipango yenu.Ulimpa saa ya mkononi 
mliyoiwekea kifaa maalum cha kuweza kutambua 
kila mahala alipo .Kama haitoshi mliunganisha 
simu yake na mtandao wenu na mkayasikia 
mawasiliano yake yote.Peniela ninazifahamu 
mbinu zako zote chafu..” akasema Dr Joshua 
.Peniela akamtazama na kusema “ Dr Joshua kitu gani unakitafuta toka 
kwangu? Kwa nini umeukubali uongo huu bila ya 
kufanya kwanza uchunguzi? Watu unaosema eti 
ninashirikiana nao ni mara yangu ya kwanza 
kuwasikia leo hii.I don’t know them.Halafu 
unasema eti nilikuwa na mahusiano na Dr 
Kigomba? Mimi Peniela naweza kumuonyesha 
utupu wangu mtu kama Yule? Sikutegemea 
kabisa mtu kama wewe unaweza kuwa mwepesi 
kusikia na kuamini maneno ya watu wasiokutakia 
mema” akasema Peniela 
 “ Peniela mambo haya nimeyapata toka 
kwa mtu ninayemuamini na ambaye mlikuwa 
mnashirikiana naye katika mipango yenu bila ya 
ninyi kufahamu kuwa alikuwa ni m tiifu 
kwangu.Hamkuwa mkijua kama jaji Elibariki ni mtu 
wangu.Hahahahaaa…” akasema Dr Joshua na 
kutoa kicheko cha dharau 
 “ Jaji Elibariki ???..Peniela akashangaa 
 “Ndiyo.Mbona umestuka ? Humjui?  “ Jaji Elibariki Yule aliyehukumu kesi yangu 
na kuniachia huru ndiye aliyekuletea habari hizi? 
Akauliza Peniela na kutoa kicheko kidogo 
 “ Nilijua tu kitu kama hiki lazima 
kitatokea.You are so fool Dr Joshua.Jaji 
Elibarikiamekuingiza katika mtego na wewe kwa 
kutokuwa na umakini umeingia katika mtego 
wake..” akasema Peniela na kutoa kicheko 
kidogo.Dr Joshua hakusema kitu akabaki 
anamtazama 
 “ Ni hivi naomba unisikilize vizuri Dr 
Joshua” akasema Peniela 
 “ Nilikuwa najiuliza sana ni nani ambaye 
anaweza kunitungia uongo mkubwa kama huu? 
Nilijua tu lazima mtu ambaye amenitungia uongo 
mkubwa kama huu atakuwa na lengo baya na 
mimi la kuniharibia maisha yangu kwa kutaka 
unichukie na uniache kumbe ni jaji Elibariki 
!!!!..akasema Peniela na kutulia kidogo halafu 
akaendelea 
 “ Nilimfahamu Elibariki alipoanza kusikiliza 
shauri langu .Mahakama haikunikuta na hatia na nikaachiwa huru.Baada ya kuachiwa huru jaji 
Elibariki akanifuata na kuanza kunitongoza akidai 
kwamba yeye ndiye aliyeniweka huru.Aliendelea 
kunisonga sana na siku moja usiku alikuja kwangu 
akiwa ametapakaa damu akaniomba nimuhifadhi 
kwa madai kwamba kuna watu wanamtafuta na 
wanataka kumuua.Nilimuonea huruma 
nikamruhusu alale pale kwangu na kesho yake 
asubuhi wakati nikioga alinivamia bafuni.Unajua 
alinifanya nini?? Akauliza Peniela kwa hasira.Dr 
Joshua hakujibu kitu akabaki anamtazama 
 “ He raped me !!!!..akasema huku machozi 
yakimtoka.Maneno yale yalimfanya Dr Joshua 
astuke kidogo na kumtazama Peniela kwa hasira 
 “ Nilikasirika sana na nikamuweka wazi 
kwamba lazima nikueleze kuhusu jambo lile 
akanitolea vitisho vingi kwamba nikithubutu 
kukueleza chochote ataniua.Alipoona nimeshikilia 
msimamo wangu wa kuja kukueleza akaondoka 
na baadae akarudi akiwa ameongozana na mke 
wa rais mstaadfu Rosemary Mkozumi .Kwanza 
aliniomba msamaha halafu akaniambia kwamba amemleta Rosemary mkozumi kwangu kuna 
jambo wanataka kuzungumza nami.Rosemary 
Mkozumi akaniambia kwamba kuna jambo 
wanataka kunishirikisha ambalo endapo 
litafanikiwa nitapata fedha nyingi sana.Nilitaka 
kufahamu ni jambo gani hilo na wakanieleza 
kwamba kuna kifaa Fulani unacho ambacho 
natakiwa kufanya jitihada nikipate na nkifanikiwa 
basi nitakuwa bilionea.Waliniahidi kunipa shilingi 
bilioni kumi endapo ningefanikiwa.Nilitaka 
wanifafanulie ni kitu gani hicho lakini hawakuwa 
tayari na kwa kuwa tayari jaji Elibariki alikwisha
nifanyia kitendo kibaya cha udhalilishaji mkubwa 
sikuwa tayari kushirikiana nao kwa lolote.Baada 
ya jitihada zao zote za kunishawishi kushidnikana 
wakanitolea vitisho na kunipa muda wa kutafakari 
na kufanya maamuzi na wakanionya kwamba 
nisithubutu kufungua mdomo wangu na pindi 
nikikifanya hivyo wataniua.Pamoja na kitisho cha 
kuniua lakini sikukubaliana nao na kama 
utakumbuka nilikupigia simu na nikakwambia 
kwamba ninataka kuonana nawe lengo lilikuwa ni kukueleza kuhusu jambo hili lakini hatukuweza 
kuonana kutokana na msiba wa Flaviana.Juzi 
usiku nilivamiwa na watu ambao nina hakika 
walitumwa kuja kuniua kwa bahati nzuri 
nilifanikiwa kutoroka na nyumba yangu 
ikachomwa moto.Nilijihifadhi kwa rafiki yangu na 
leo hii nimeamua nije katika hii nyumba uliyonipa 
niishi.Kwa hiyo Dr Joshua mambo aliyokwambia 
jaji libariki hayana ukweli hata kidogo.Amewahi 
kuja kwako na kukupa uongo huu mkubwa kwani 
alijua lazima ningekuja kukuona na kukueleza 
mambo haya.He lied to you na wewe ukawa 
mwepesi kuamini.Dr Joshua mimi sina mpango 
wowote mbaya nawe ila nisikilize vizuri ,jaji 
Elibariki na Rosemary Mkozumi kuna jambo baya 
wanalipanga dhidi yako,kuna kitu wanakitafuta 
toka kwako.Sikulazimishi uniamini huo ni uamuzi 
wako.Mimi nimekwisha kueleza ukweli wangu na 
utapima nani mkweli kati yangu mimi au Elibariki” 
akasema Peniela 
 Mathew na Anitha waliokuwa garini 
wakifuatilia mazungumzo yote kati ya Peniela na Dr Joshua kupitia kifaa cha mawasiliano 
alichokivaa Peniela sikioni,wakatazamana na 
Mathew akatabasamu 
 “ Peniela is real a professional 
liar.Sikutegemea kama angeweza kutunga uongo 
ule mkubwa kwa haraka” akasema Mathew Anitha 
hakujibu kitu naye akatabasamu 
****************** 
 Maneno aliyoambiwa na Peniela yalimfanya 
Dr Joshua abaki kima akitafakari. 
 “ Kwa hiyo Dr Joshua “ akasema Peniela 
na kumfanya Dr Joshua ainue kichwa 
 “ Ni juu yako kuchagua na kuamini yupi 
mkweli kati yangu na jaji Elibariki” 
 Dr Joshua akavuta pumzi ndefu na kusema 
 “ I don’t know anymore the meaning of 
these two words,believe and trust.I don’t know 
who to believe or who to trust.” Peniel akamtazama kwa makini na kusema 
kwa sauti ndogo ya kimahaba 
 “You don’t believe even the woman you 
love the most as you always say? You don’t 
believe me? That’s too bad.” 
 Akamtazama tena Dr Joshua na kusema 
“Kila siku umekuwa unaniambia kwamba 
unanipenda na uko t ayari kwa lolote kwa ajili 
yangu sasa ni wakati wako wa kulithibitisha hilo 
kwa vitendo.Nitaumia mno endapo utashindwa 
kuniamini na kuchagua kumuamini mtu ambaye 
ana lengo la kukuangamiza.One more thing,if y u 
choose not to trust me today then there is no any 
meaning for us to contnue with our 
relationship.We have to put an end to us 
!!!!..akasema Peniela kwa ukali kidogo 
 “ Peniela my love,si kwamba sitaki 
kukuamini lakini ….” Dr Joshua akasita 
 “ Lakini nini Dr Joshua? Unashindwa kweli 
kuniamini mimi? Nasikitika sana kwa hilo.Sasa 
nimegundua yale maneno yote uliyokuwa 
unaniambia kila siku kamba unanipenda hayakuwa ya kweli.Lengo lako lilikuwa ni kutimiza 
tu haja zako za mwili na si kweli kwamba ulikuwa 
na nia ya dhati ya kufanya jambo lolote kwa ajili 
yang….” 
 “ Peniela stop !!” akasema Dr Joshua 
 “ Kwanza naomba samahani sana kwa 
maneno yale niliyoyatamka mwanzo.NIsamehe 
sana Peniela.Nilitamka maneno yale kutokana na 
hasira nilizokuwa nazo juu yako kwa sababu ya 
maneno niliyolishwa na jaji Elibariki na mimi 
nikayaamini.Maneno uliyonieleza ni mazito na 
ninakuahidi nitayafanyia kazi kwa haraka na hawa 
wote wanaojifanya ni watu wangu wa karibu 
kumbe ni chui wanaoiwinda damu yangu 
watakiona cha moto” akasema Dr Joshua halafu 
akamtazama Peniela kwa sekunde kadhaa 
akamsogeza karibu yake akambusu 
 “ Peniela nakupenda sana malaika wangu 
zaidi ya n inavyoweza kukueleza.Sikumbuki ni 
mara ngapi nimekutamkia neno hili kwamba 
ninakupenda lakini usiku wa leo nataka 
nikukumbushe kwamba ninakupenda kuliko chochote hapa duniani.Japokuwa kuna nyakati h 
uwa unaniudhi mfano ulipoanzisha mahusiano na 
Yule kijana Edson nilichukia sana lakini kila pale
ninapokuwa na hasira juu yako ninapokuona tu 
hasira zote hupotea na hutabasamu 
tena.Nakuomba Peniela usiwe na shaka yoyote 
juu ya upendo wangu kwako na kwa ajili yako niko 
tayari kwa lolote “ akasema Dr Joshua na 
kumbusu tena Peniela 
 “ Peniela muda wangu wa uongozi 
unakaribia kumalizika .Utafanyika uchaguzi na 
atapatikana rais mpya na mimi nitaenda 
kupumzika.Ninao u tajiri mkubwa sana ambao 
utanifanya niishi maisha mazuri ya kifahari baada 
ya kustaafu hadi siku ninaingia kaburini .Hivi 
karibui ninatarajia kupata ukaazi wa kudumu 
nchini Marekani kwa hiyo baada tu ya kustaafu 
nitakwenda kuishi huko.Sintokwenda huko 
mwenyewe bali nitaongozana nawe malaika 
wangu unayejenga tabasamu usoni pangu kila 
niionapo sura yako.Peniela una nafasi ya pekee 
kabisa katika moyo wangu kwa hiyo kokote niendako nitaambatana nawe.Nataka tuishi 
maisha yenye furaha ,tuzunguke dunia nzima 
tukistarehe na kuyafurahia maisha.” Akasema Dr 
Joshua na kumbusu Peniela 
 “ Peniela sitaki kukupoteza wala kuruhusu 
jambo lolote baya likutokee.Kwa Elibariki na 
mshirika wake Rosemary Mkozumi ntajua n ini 
cha kuwafanya .Kwa hiyo basi kuanzia sasa hadi 
hapo nitakaporidhika kwamba hakuna shaka ya 
usalama wako utakaa humu ndani na hutatoka 
hadi hapo nitakapokuruhusu kutoka.” 
 “ No !Dr Joshua yu cant do that to me 
!!.akasema Peniela 
 “ Yes you will.Thats an order!!! Akasema Dr 
Joshua kwa sauti ya ukali 
 “ Peniela I’m doing this for you,for us,kwa 
hiyo naomba usikasirike wala usinione mimi 
mkatili .Maisha yako yana thamani kubwa kwangu 
na jambo hili ni la muda tu na nitakapohakikisha 
hali ya usalama imeboreka basi utakuwa huru 
.Utapata kila unachohitaji na ulinzi nitauimarisha
zaidi hapa.Nitakuelekeza Kareem ahakikishe kunakuwa na ulinzi wa kutosha hapa.Kila jioni 
nitakuwa nakuja hapa na tunapata wasaa wa 
kuwa pamoja.Peniela this is our moment to be 
happy.Give me a chance to show you how much I 
love you.Mwanamke kama wewe unapaswa kuishi 
zaidi ya malkia” akasema Dr Joshua .Peniela 
akaachia tabasamu kubwa akambusu Dr Joshua 
na kusema 
 “ Dr Joshua nafahamu unanipenda na una 
nia nzuri na mimi hasa kwa wakati huu ambao 
usalama wangu uko shakani lakini siwezi kukubali 
kufungiwa humu ndani.Nahitaji kuwa huru mpenzi 
wangu” 
 “ Usijali Peniela.This is just for few 
days.Nataka ukitoka hapa japokuwa si rasmi 
lakini uishi kama mke wa rais kwa hiyo naomba 
unipe siku chache tu niweze kuyafanya mambo 
makubwa ambayo nataka kukufanyia.Sawa 
malaika wangu? Akasema Dr Johsua.Peniela 
akatabasamu na kwa sauti laini akasema 
 “ Dr Joshua you’re the king 
here.Nitatekeleza yote unayoyasema but I have one request na endapo utanitekelezea hilo 
nitaamini kwamba kweli unanienda and I’ll go with 
you anywhere you wat us to go” 
 “ Peniela,neno lako ni amri 
kwangu.Tafadhali nieleze chochote 
nitakutekelezea bila kusita” akasema Dr Joshua 
kwa kujiamini 
 Peniela akainamisha kichwa na alipoinua 
kumtazama Dr Joshua macho yake yalijaa 
machozi.Dr Joshua akastuka 
“ Whats wrong my queen? Akauliza Dr 
Joshua 
 “ Dr Joshua nimedhalilishwa sana na jaji 
Elibariki .He raped me.He raped the woman you 
real love.I want him for what he did.Can you help 
me make him pay? 
 Dr Joshua akamkumbatia Peniela na 
kusema 
 “ My dear Peniela,siwezi kukueleza ni 
namna gani nimeumizwa na taarifa hizo za 
kitendo kiovu alichokifanya Elibariki.Edson 
nilimuondoa kwa sababu moja tu ya kuwa na mahusiano na mwanamke wangu ninayempenda 
kuliko wote.Peniela you are mine and mine alone 
kwa hiyo yeyote atakayekuumiza wewe atakuwa 
ameniumiza mimi pia.Nakuahidi Peniela, Elibariki 
will pay very dearly !!!!... akasema Dr Joshua 
huku akiuma meno kwa hasira. 
 “ Ahsante sana my love.Sasa naamini 
maneno yako kwamba unanipenda,Unajua 
sikuwahi kufikiri hata siku moja kama ninaweza 
kudhalilishwa kiasi kile.Inaniumiza sana na sijui 
nitafanya nini ili niweze kuliondoa jambo hili katika 
akili yangu” 
 “ Peniela I’m right here.Nitakufuta machozi 
na kukusahaulisha jambo hili.Narudia tena 
kukuahidi jaji Elibariki lazima atalipa uovu wake..!” 
 Peniela akaanza tena utundu wake na Dr 
Joshua akazidi kupagawa 
 “ Dah ! hatimaye nimefanikiwa kumteka akili 
huyu mzee.Elibariki alifanya kosa kubwa sana 
kutusaliti.Nitahakikisha anakosa kila kitu.Dr 
Joshua hana tena kauli yoyote kwangu na lazima 
mipango yetu yote iende kama tunavyotaka.Kwa kuwa amenitaka nisitoke nje ya nyumba hii ngoja 
nimkubalie matakwa yake lakini natakiwa kutafuta 
namna ili niweze kulichukua kasha langu na 
kuwapelekea akina Mathew.Kitu kizuri ni kwamba 
anasema Kareem ndiye atakayekuwa hapa 
nyumbani akihakikisha ninakuwa salama.Kareem 
hana kauli kwangu atafanya kila 
nitakachomuamuru kufanya.” Akawaza Peniela 
huku akiendelea kumfanyia Dr Joshua 
utundu,ambaye alikuwa anaguna kimahaba kwa 
mambo aliyofanywa na muda si muda wakaingia 
katika mzunguko wa pili.Peniela akashika usukani 
alimpeleka vilivyo Dr Joshua na kumfanya alalame 
kama mtoto mdogo.Hadi mzunguko wa pili 
unamalizika Dr Joshua alikuwa hoi amechoka 
kupita maelezo. 
 “ I swear Peniela sintamuacha hata itokee 
nini.Huyu binti ananipa raha ambayo siwezi 
kupewa na mtu yeote.Nitafanya kila 
linalowezekana hadi niw…..” Dr Joshua 
akashindwa kuendelea kuwaza akapitiwa na 
usingzi. 
 “ Dr Joshua!!.Dr Joshua .!!” akaita Peniela 
lakini tayari D Joshua alikuwa katika usingizi 
mzito. 
 “ Kwisha habari yake” akawaza Peniela na 
kuinuka akaelekea chooni akakigonga kile kifaa 
cha kuwasiliana alichokiweka sikioni. 
 “ Hallow Mathew,can you hear me?!!! 
Akauliza Peniela. 
 “ Ndiyo Peniela.Tumesikia kila 
kilichoendelea hapo ndani.Good job” akasema 
Mathew 
 “ Ahsante.Kama mlivyosikia huyu mzee 
hataki nitoke humu ndani . What are we going to 
do? Tunatakiw akuonana na Deus Mkozumi,right? 
 “ Usijali kuhusu hilo tutatafuta namna 
nyingine ya kufanya kuweza kuonana na Deus 
Mkozumi ila kwa sasa wewe endelea kukaa humo 
humo ndani kama anavyotaka.Endelea kumfanya 
akuamini tena na wakati ukiwa hapo ndani jaribu 
kutafuta chochote kinachoweza kutusaidia katika 
mpango wetu wa kukipata kirusi Aby”  “ Sawa Mathew,nitafanya nhivyo ila kesho 
nitamtuma Kareem alete ule mzigo hapo 
nyumbani. Mathew,tutawasiliana kesho.Good 
night”akasema Peniela na kurejea chumbani 
ambako Dr Joshua alikuwa amelala fofofo. 
 “ Nini kinafuata baada ya hapa? Akauliza 
Anitha wakiwa ndani ya gari baada ya Peniel 
kumaliza kuongea na Mathew 
 “ Tunarudi nyumbani kwani Peniela hawezi 
kutoka mle ndani leo,kwa hiyo hatuna haja ya 
kuendelea kukaa hapa” 
 “ Are you sure she’ll be ok? Ninawasi wasi 
kidogo kwani mchezo anaoucheza ni wa hatari 
sana.Anacheza na akili ya Dr Joshua,unadhani 
nini kitatokea endapo dr Joshua atagundua kuwa 
Peniela anamdanganya? Akauliza Anitha 
 “ Hilo haliwezi kutokea kabla 
hatujakamilisha mpango wetu.Peniela ni mjanja 
mno.Akili yake inafanya kazi haraka sana na 
anaweza kufanya jambo lolote muda 
wowote.Amenishangaza sana kwa namna 
alivyoweza kubadili upepo kati ya Dr Joshua na jaji Elibariki.Ameweza kuuvaa vyema uhusika na 
mtu yeyote angeweza kumuamini alichokisema” 
akasema Mathew kisha wakaondoka kurejea 
nyumbani. 
***************** 
 Watu hawakuwa wengi nyumbani kwa rais 
usiku huu uliko msiba wa Flaviana.Wengi wa 
waliobaki ni ndugu na watu wa karibu na familia 
ya rais.Anna akamuulizia Jaji Elibariki akaambiwa 
kwamba ameondoka ameelekea nyumbani kwake 
kupumzika 
 “ Nitamfuata huko huko nyumbani kwake” 
akawaza na bila kupoteza wakati akaelekea katika 
gari lake na kuondoka kumfuata jaji Elibariki 
nyumbani kwake 
 “ Leo lazima nifahamu ni kitu gani 
kinachoendelea kati ya baba na jaji Elibariki.Kama 
alivyonieleza Mathew lazima kuna kitu 
kinachoendelea kati yao.I must find out” akawaza
TUKUTANE SEHEMU IJAYO...


 “ Dr Joshua!!.Dr Joshua .!!” akaita Peniela 
lakini tayari D Joshua alikuwa katika usingizi 
mzito. 
 “ Kwisha habari yake” akawaza Peniela na 
kuinuka akaelekea chooni akakigonga kile kifaa 
cha kuwasiliana alichokiweka sikioni. 
 “ Hallow Mathew,can you hear me?!!! 
Akauliza Peniela. 
 “ Ndiyo Peniela.Tumesikia kila 
kilichoendelea hapo ndani.Good job” akasema 
Mathew 
 “ Ahsante.Kama mlivyosikia huyu mzee 
hataki nitoke humu ndani . What are we going to 
do? Tunatakiw akuonana na Deus Mkozumi,right? 
 “ Usijali kuhusu hilo tutatafuta namna 
nyingine ya kufanya kuweza kuonana na Deus 
Mkozumi ila kwa sasa wewe endelea kukaa humo 
humo ndani kama anavyotaka.Endelea kumfanya 
akuamini tena na wakati ukiwa hapo ndani jaribu 
kutafuta chochote kinachoweza kutusaidia katika 
mpango wetu wa kukipata kirusi Aby”  “ Sawa Mathew,nitafanya nhivyo ila kesho 
nitamtuma Kareem alete ule mzigo hapo 
nyumbani. Mathew,tutawasiliana kesho.Good 
night”akasema Peniela na kurejea chumbani 
ambako Dr Joshua alikuwa amelala fofofo. 
 “ Nini kinafuata baada ya hapa? Akauliza 
Anitha wakiwa ndani ya gari baada ya Peniel 
kumaliza kuongea na Mathew 
 “ Tunarudi nyumbani kwani Peniela hawezi 
kutoka mle ndani leo,kwa hiyo hatuna haja ya 
kuendelea kukaa hapa” 
 “ Are you sure she’ll be ok? Ninawasi wasi 
kidogo kwani mchezo anaoucheza ni wa hatari 
sana.Anacheza na akili ya Dr Joshua,unadhani 
nini kitatokea endapo dr Joshua atagundua kuwa 
Peniela anamdanganya? Akauliza Anitha 
 “ Hilo haliwezi kutokea kabla 
hatujakamilisha mpango wetu.Peniela ni mjanja 
mno.Akili yake inafanya kazi haraka sana na 
anaweza kufanya jambo lolote muda 
wowote.Amenishangaza sana kwa namna 
alivyoweza kubadili upepo kati ya Dr Joshua na jaji Elibariki.Ameweza kuuvaa vyema uhusika na 
mtu yeyote angeweza kumuamini alichokisema” 
akasema Mathew kisha wakaondoka kurejea 
nyumbani. 
***************** 
 Watu hawakuwa wengi nyumbani kwa rais 
usiku huu uliko msiba wa Flaviana.Wengi wa 
waliobaki ni ndugu na watu wa karibu na familia 
ya rais.Anna akamuulizia Jaji Elibariki akaambiwa 
kwamba ameondoka ameelekea nyumbani kwake 
kupumzika 
 “ Nitamfuata huko huko nyumbani kwake” 
akawaza na bila kupoteza wakati akaelekea katika 
gari lake na kuondoka kumfuata jaji Elibariki 
nyumbani kwake 
 “ Leo lazima nifahamu ni kitu gani 
kinachoendelea kati ya baba na jaji Elibariki.Kama 
alivyonieleza Mathew lazima kuna kitu 
kinachoendelea kati yao.I must find out” akawaza  na kuanza kuyakumbuka maneno aliyoambiwa na 
Mathew 
 “ Kila nikiyakumbuka maneno ya Mathew 
kuhusu baba,mwili wote unanisisimka.Ni mambo 
mazito mno.Hatua aliyofikia baba si hatua ya 
ubinadamu.Amefikia hatua ya ukatili 
uliopitiliza.Amebariki mke wake na mwanae 
wauawe kwa sababu ya pesa???..!! Atapata raha 
gani kama atazipata hizo pesa lakini hana mtu wa 
kutumia naye? Ni ujinga mtupu” akawaza Anna 
akiwa katika mwendo mkali akielekea nyumbani 
kwa jaji Elibariki 
 “ Kwa kila nitakavyoweza lazima nimsaidie 
Mathew kuhakikisha baba na genge lake wote 
wanafikishwa katika vyombo vya sheria ili na 
kupata dhabu stahiki.Siwezi katu kulifumbia 
macho suala hili kwa vile muhusika mkuu ni baba 
yangu.Nitapambana bega kwa bega na Mathew 
mpaka tuhakikishe tunashinda” akawaza Anna na 
sura ya Mathew ikamjia kichwani 
 “ Mathew ni mtu shujaa ambaye anastahili 
sifa za kipekee kabsa.Ameweza kufukunyua na kugundua mambo mazito kama haya .Lazima 
nimuunge mkono.Nadhani nikiwa karibu naye 
nitafahamu mambo mengi zaidi.Anaonekana ni 
mtu anayefahamu mambo mengi sana mabaya 
yanayofanywa na watu mbali mbali wa hapa 
nchini.Natakwa kutafuta namna ya kumfanya 
aniamini.Halafu kuna kitu Kareem aliniambia ,eti 
Mathew na Anitha ni mtu na mpenzi wake.Kuna 
ukweli wowote katika hili? Nitamuuliza Mathew 
nikionana naye” akawaza 
 “ Lakini kwa nini nifuatilie mambo binafsi ya 
Mathew na Anitha? Kama ni wapenzi mimi 
inanihusu nini? Kazi yangu mimi ni kumsaidia na 
kuhakikisha tunawafikisha mbele ya sheria baba 
na mtandao wake.Lakini mhhh!!Mathew 
amenivutia sana.He’s real a gentleman.Anajiamini 
na kwa namna nilivyomsoma kwa haraka ni 
mwanaume ambaye hana tamaa na wanawake 
kama hawa wanaume wengine ..” 
 Anna aliwaza mambo mengi sana akiwa 
njiani kuelekea nyumbani kwa jaji Elibariki.Alifika
katika makazi ya jaji Elibariki ,akasimamishwa na askari wawili wenye silaha ..kulikuwa na ulinzi 
mkali eneo lile.Anna akawasalimu askari wale na 
kujitambulisha kwao.Mmoja wa askari wale 
akaenda kumfahamisha jaji Elibariki kuhusu ujio 
wa Anna.Jaji Elbariki akatoa ruhusa Anna 
aruhusiwe kuingia ndani.Anna akashuka garini na 
kulakiwa na jaji Elibariki akamkaribisha sebuleni. 
 “ I’m sorry Anna,sina kinywaji kingine 
chochote kikubwa humu ndani zaidi ya hii whysky 
ninayokunywa” akasema jaji Elibariki ambaye 
macho yake yalikuwa mekundu kwani toka 
aliporejea amekuwa akinywa pombe kali 
 “ Usijali Elibariki hata kama kungekuwa na 
vinywaji nisingekunywa.Look,Im here for one 
reason only.I want to know whats going on 
between you and my father? Akauliza 
Anna.Elibariki akamtazama kwa sekunde kadhaa 
na kusema 
 “ Anna imekuwa vizuri umekuja .Kuna 
mambo kadhaa ambayo nataka tuongee na 
itakuwa vyema kama tutautumia usiku hu wa leo 
kuongea kila kile kinachotuhusu lakini kabla sijasema chochote naomba kwanza nitumie nafasi 
hii kukupa pole sana kwa kifo cha dada 
yako.Nimeumizwa mno kwa kifo cha mke wangu” 
akasema Elibariki na kuinamisha kichwa. 
 “ Elibariki I think you know me,huwa si mtu 
wa kutaka hadithi nyingi.Nahitaji uende moja kwa 
moja kujibu swali langu nililokuuliza,whats going 
on between you and my father? Jeshi la polisi 
walitangaza msako mkali dhidi yako kwa 
kusababisha kifo cha Flaviana.Nikiwa Afrika ya 
kusini nilikupigia simu na ukanihakikishia kwamba 
hauhusiki kabisa na hicho kinachodaiwa na jeshi 
la polisi halafu nikakuuliza kama baba anahusika 
katika matukio ya vifo vya mama na dada 
ukakubali kwamba ni kweli baba ndiye muhusika 
mkuu wa vifo hivyo na kwamba hata wewe 
umejificha kuepuka kuuawa kwa vile tayari 
unayafahamu madhambi ya baba.Ghafla bila 
kutegemea umeibuka toka mafichoni na 
unaonekana ukiwa umeongozana na baba mtu 
ambaye ulidai anataka kukuua.Na kama 
haitoshi,jeshi la polisi lililokuwa linakusaka kwa udi na uvumba wanadiriki kujitokeza mbele ya 
watanzania na kukusafisha kwamba ulikuwa 
umetekwa na majambazi na kwa hiyo tuhuma 
ulizokuwa ukitafutwa kwazo hauhusiki 
nazo.Nataka uniondolee hizi picha picha kichwani 
kwangu na unieleze ukweli wa nini kinaendelea 
kati yako na baba? Nataka unieleze ukweli 
wote.You know I do trust you with all my heart so 
tell me nothing but the truth.Nataka ukiri tena ile
kauli yako uliyonieleza kwamba baba anahusika 
na vifo vya mama na dada.If you real love my 
sister you are going to tell me the truth” 
 Jaji Elibariki akanywa whysky halafu 
akainamisha kichwa na alionekana kuzama katika 
mawazo mengi.Baada ya ya kufikiri kwa muda 
akasema 
 “ Ok I’m going to tell you the truth” 
 Jaji Elibariki akainamisha tena kichwa 
alionekana kuwa katika majonzi mazito… 
 “ Anna kwanza kabisa nataka nikiri tena 
kwamba yale maneno niliyokwambia ukiwa afrika 
kusini kuhusiana na baba yako ni ya kweli kabisa.Yeye ndiye muhusika mkuu wa vifo vya 
mama na dada yako.” Akanyamaza akainamisha 
kichwa kidogo halafu akainua kichwa na 
kumuelea Anna kila kitu kilichotokea toka mama 
yake alipofariki .Maneno aliyoyasema jaji Elibariki
ni sawa na yale yale kama Anna aliyoambiwa na 
Mathew. 
 “Kwa hiyo Anna hivyo ndivyo ilivyokuwa” 
Mathew akaendelea 
 “ Baada ya Dr Joshua na kundi lake 
kugundua kwamba tayari nimefahamu 
wanahusika katika kifo cha Dr Flora wakasuka 
mpangowaniue.Nilinusurika katika shambulio 
lililoratibiwa na mtandao wa Dr 
Joshua.Nawashukuru sana Mathew na wenzake 
kwa jitihada zao hadi leo niko hai” akainama 
akawaza kidogo kisha akaendelea kumsimulia 
Anna kila kitu bila kumficha.UKimya ukatanda 
pale alipomaliza.Anna alimtazama Elibariki kwa 
jicho la chuki  “Kwa hiyo Anna baada ya matukio haya 
yote nikajikuta maisha yangu yakibadilika ghafla” 
akaendelea jaji Elibariki 
 “ Sikuwa na muelekeo na nilipoteza kila kitu 
katika maisha yangu.Niliishi bila kuifahamu kesho 
yangu.Kwa ufupi nilikuwa nimekwama na sikuwa 
na namna nyingine ya kujikwamua ili maisha 
yangu yasonge mbele kwani nilikuwa sawa na 
mtu asiye na uhai na ndipo nilipoamua kufanya 
jambo ambalo kila ninapolifikiria nahisi kama 
moyo wangu unakatwa katwa na kisu kikali” 
akasema jaji Elibariki na kuinama akashika mahali 
ulipo moyo wake 
 “ Moyo unaniuma sana kwa jambo 
nililolifanya” akasema jaji Elibariki 
 “ Ulifanya nini” akauliza Anna 
 “ Baada ya kuona nimekwama na maisha 
yangu yamekwama nililazimika kutafuta namna ya 
kujikwamua na njia pekee ya kurejesha tena 
maisha yangu ni kwa kujisalimisha kwa Dr 
Joshua.Niliwasaliti wenzangu na kwa kumtumia 
Rosemary Mkozumi ambaye nilimfungua toka  
mahala pa siri alipokuwa amefichwa na 
Mathew,nilifanikiwa kuonana na Dr Joshua 
,nikaongea naye na ili anisamehe nikalazimika 
kumueleza kila mpango mimi na wenzangu 
tuliokuwa tumeupanga dhidhi yake.Dr Joshua 
alifurahi kwa niliyomuleleza akanisameheh 
tukaufungua ukurasa mpya.I’m free now” 
 Anna akamtazama kwa hasira na kusema 
 “ Hukupaswa hata kumuoa dada yangu mtu 
kama wewe.Kwa nini ukafanya jambo kama hilo la 
kijinga Elibariki? Baada ya kufahamu yote ambayo 
baba ameyafanya na hadi kuhusika katika 
kusababisha kifo cha mkeo kwa nini badala ya 
kumfikisha mbele za sheria ukawageuka wenzako 
na kuungana na muuaji? Wewe na yeye nyote 
mko sawa..You are both monsters!!! Akasema 
Anna 
 “ Yes I’m a monster!! Akasema kwa ukali 
jaji Elibariki. 
 “ I had no choice.Nilifanya kile ambacho 
mtu yeyote kama angekuwa mahala pangu 
angekifanya.Hupaswi kunilaumu mimi kwani niFlaviana ndiye aliyeniingiza katika vita dhdi ya 
rais na baada ya kufariki sikuona sababu ya 
kuendeleza vita ile ambayo hata ningefanya nini 
nisingeshinda,nikaamua kujisalimisha” 
 “Is that all you wanted ?only to be free” 
akauliza Anna 
 ‘” Nilichokuwa nakihitaji sana nI kuwa huru 
ili niendelee na maish a yangu ya kawaida lakini 
baada ya kumueleza Dr Joshua mambo yale 
makubwa yaliyopangwa dhidi yake amefanya 
maamuzi .Anataka niwe rais ajaYe wa Tanzania 
baada ya yeye kumaliza muda wake wa uongozi” 
akasema jaji Elibariki huku akitabasamu kidogo 
 “ What??!! Anna akapatwa na mshangao 
mkubwa 
 “ Tell me it’s a lie!! Akasema 
 “ Its true Anna.I’m going to be the next 
president” Anna aliyekuwa amekunja sura 
akalazimika kutoa kicheko kidogo. 
 “ Ama kweli dunia inaelekea ukingoni.You 
?? Next president?? That cant be” akasema Anna  “ Anna utake usitake nitakuwa rais wa 
jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya 
baba yako kumaliza muda wake hiyo ni ahadi 
aliyonipa.Kwani siwezi kuongoza nchi? Akauliza 
Elibariki 
 “ Kama umeshindwa kuvumilia na 
ukawasaliti wenzako itakuwa nchi? Si utaiuza nchi 
na watu wake wewe?? Hebu acheni hayo 
masihara “ 
 “ Si masihara Anna.Hili ni jambo la kweli na 
ndivyo itakavyokuwa” 
 “ Hivyo ndivyo baba alivyokudanganya? 
 “ Hajanidanganya .He’s going to make me 
the next president .Right now I’m the only one he 
trust the most” 
 “ Elibariki kitu gani kimekuingia kichwani na 
kukubadilisha kiasi hiki? I know me and you we 
never seen eye to eye but down deep I know you 
are a good guy,what turns you to a monster? 
 “ I’m serving a monster so I have to be a 
monster too!! Akasema jaji Elibariki kwa sauti ya 
juu akionekana kukerwa na maneno yale ya Anna  “ Sikiliza Anna.Hakuna ubishi kwamba 
nitakuwa rais ajaye wa Tanzania kwa hiyo badala 
ya kunikashifu na kunivunja moyo unapaswa 
kuniunga mkono kwani mimi na wewe tuna 
maisha marefu huko mbeleni” 
 “ What do you mean ?? akauliza Anna 
akimtazama Elibariki kwa hasira 
 “ Sikiliza.Kwa sasa sisi sote tumewapoteza 
wapenzi wetu.Umempoteza Edson na mimi 
nimempoteza Flaviana hivyo basi kwa kuwa 
ninaelekea kushika wadhifa mkubwa na wa juu 
katika uongozi nahitaji kuwa na mwenza na kwa 
vile kwa sasa uko mwenyewe basi si vibaya kama 
tukianzisha mahusiano na baada ya mimi kushika 
urais you are going to be the first lady” ak asema 
Elibariki .Ana akamtazama kwa hasira na kusema 
 “ You are sick Elibariki and you need 
treatment.Hivi unathubutuje kutamka maneno 
kama hayo? Unafahamu kabisa kwamba 
ninakuchukua sana sana na kwa hili ulilolifanya 
limenifanya nikuchukie hata zaidi kwa hiyo naomba usirudie tena kunitusi kwa kunitamkia 
maneno hayo ” akafoka Anna 
 “ Hata mimi si kwamba ninakupenda Anna 
bali huo ni ushauri toka kwa baba yako na ndivyo 
anavyotaka iwe.Anataka familia yake iendelee 
kushika nafasi za juu za uongozi na mimi siwezi 
kuipinga kauli yake” 
 “ You are both devils !!! I’m out of here but 
I’ll come back again .Our conversation is not over
yet!! 
 Akasema Anna na kutoka kwa hasira hadi 
katika gari lake akaondoka 
 “ Dah ! kweli haya ni maajabu ya 
Musa.Haya mambo yanayotokea ni kama vile 
filamu lakini ni ya kweli kabisa.Is my father a real 
human? Akajiuliza Anna akiwa garini 
 “ mambo anayoyafanya baba yananipa 
wasi wasi na wakati mgumu kumuelewa ni kiumbe 
mwenye damu ya namna gani.Kwa kumtazama 
anaonekana ni mtu mwema lakini kwa ndani ana 
moyo wa kishetani.Yaani kwa tamaa ya pesa 
anadiriki bila huruma kuutoa uhai wa mwanamke aliyenileta duniani ambaye nilimpenda kuliko wote 
.I’ll never forgive him for that.Kwa kusababisha 
vifo vya mama na dada amechukua kila kitu cha 
thamani katika maisha yangu na lazima 
nihakikishe hafanikiwi katika mipango yake 
yoyote” akaendelea kuwaza Anna 
 “ Halafu kituko kingine bila hata ya aibu eti 
anataka kumfanya Elibariki awe rais wa Tanzania 
baada ya yeye kumaliza muda wake.Hiki ni 
kichekesho kabisa.Kwa kuwa Elibariki naye 
ameamua kushirikiana na baba naye pia lazima 
nihakikishe anaozea gerezani.Hakuna 
atakayesalimika” 
 Anna alifika nyumbani kwao na kukuta 
tayari watu wamekwisha lala .Ni watu wachache 
tu waliokuwa wamekaa kivikundi wakiongea hili na 
lile huku wakiendele a na vinywaji.Alimtafuta baba 
yake lakini aliambiwa kwamba alitoka muda mrefu 
.Kwa kuwa alikuwa tayari na uchovu mwingi moja 
kwa moja akaelekea chumbani kwake 
kupumzika.Kabla ya kulala akamtumia baba yake  ujumbe katika simu akamtaka waonane asubuhi 
kuna jambo la maana sana anataka waongee. 
***************** 
 Mathew na Anitha waliwasili katika makazi 
yao na moja kwa moja Mathew akaenda sebuleni 
akajitupa sofani .Alionekana kuwa na mawazo 
mengi.Anitha akamtazama kwa sekunde kadhaa 
na kusema 
 “ Unaonekana hutaki kabisa kupumzika 
siku ya leo.Its been a long day Mathew let us take 
some rest” 
 “ Sina hakika kama jicho langu litafumba 
leo” 
 “ Kwa nini Mathew” Kitu gani kinakunyima 
usingizi? Akauliza Anitha 
 “ Nitawezaje kupata usngzi wakati sina 
hakika na usalama wa Peniela? Ni vipi kama Dr 
Joshua atagundua wamba Peniela 
anamdanganya? Suala hili linaniumiza mno 
kichwa changu.I will never forgive myself if anything bad happens to Peniela” akasema 
Mathew.Anitha akatumia sekunde kadhaa 
kumtazama Mathew halafu akasema 
 “ Mathew kuna kitu nataka kukuuliza and 
please be honest with me.” 
 “ Uliza Anitha” 
 “ Ni kuhusu wewe na Peniela.Nikiwatazama 
ninyi wawili kuna vitu Fulani naviona kwenu 
vinavyonifanya nijiulize maswali mengi.Is there 
anything going on between you two? 
 Mathew akatabasamu kidogo na kusema 
 “ Hakuna chochote kinachoendelea kati 
yetu.” 
 “ Kama hakuna kinachoendelea kwa nini 
kila linapokuja suala la Peniela kutumia mbinu 
yake ya kuutumia mwili waake kufankisha jambo 
Fulani umekuwa unapinga sana? Unaonekana 
kuumia moyoni.Do you love her? 
 “ Anitha its like this .Peniela ni mtu ambaye 
tunamtegemea mno katika operesheni hii kwa 
hiyo lazima niwe makini sana kuhusu usalama 
wake.Tukimpoteza yeye tumepoteza kila kitu.Kuhusu kutembea na watu mbali mbali ili 
kupata taarifa za muhimu na kufanikisha baadhi 
ya mambo ni kweli imetusaidia sana lakini toka 
ndani ya moyo wangu sifurahii kabisa hali 
hii.Peniela hastahili maisha kama haya ya 
kuutumia mwili wake kama chambo.Ni jambo la 
hatari sana kwake.Ndoto yangu kubwa toka 
nilipoyafahamu maisha yake ni kumsaidia aanze 
maisha yake yenye staha na amani.Nataka 
nimtoe na kumsahaulisha kabisa maisha yake ya 
sasa.Kujibu swali lako kama ninampenda Peniela 
au la,ni kwamba ninampenda Peniela kama 
ndugu yangu,kama mdogo wangu,kama 
binadamu wengine na si vinginevyo.Natumai 
umeridhika Anitha” 
 “ Ndiyo Mathew na samahani sana kwa 
mawazo niliyokuwa nayo juu yenu.Pamoja na 
hayo narudia tena kukuomba kama una hata 
chembe moja ya mawazo kuhusu kuwa na 
mahusiano na Peniela naomba ufute kabisa wazo 
hilo.Peniela is not good for you”  “ Ahsante kwa ushauri wako Anitha” 
akasema Mathew halafu ukimya ukapita 
 “ Mathew !! akaita Anitha 
 “ Kwa sasa wakati tuko peke yetu kuna 
jambo nataka kulifahamu” 
 “ jambo gani hilo Anitha? 
 “ Kabla hajaaga dunia ,John Mwaulaya 
alitaka kuonana nawe na mpaka leo hii hakuna 
anayefahamu wewe na John mliongea kitu 
gani.Mathew umekuwa ni mtu wangu wa karibu 
kupita wote katika hii dunia na hata siku moja 
hujawahi kunificha jambo lolote.I think I deserve to 
know what you and John Mwaulaya talked” 
 Mathew akafikiri kidogo na kusema 
 “ Ok nitaueleza uweli” akasema na 
kunyamza tena halafu akaendelea 
 “ Kwanza haikuwa rahisi kukubali wito ule 
wa John Mwaulaya kutokana na historia yangu 
naye kuwa si nzuri.Nafsini mwangu nilichokuwa 
nakiwaza ni kisasi tu.Baada ya kutafakari 
nikaamua kwenda kumuona.Nilipofika nilikuwa na 
hasira na akalitambua hilo akaniomba nisiwe na   
hasira kwani anayotaka kunieleza ni ya muhimu 
sana kwangu” Mathew akatulia baada ya sekunde 
kadhaa akaendelea 
 “ Kwanza alianza kwa kuniomba samahani 
kwa kile kilichotokea wakati ule na kusababisha 
mimi na yeye kuwa maadui.John alikuwa katika 
maumivu na alikuwa anapumua kwa 
shida.Nilimuonea huruma nikamtaka anieleze 
alichoniitia pale.Aliniambia kwamba kuna mambo 
mawili ,kwanza ni kuhusu Peniela.Alisema 
kwamba yeye atakufa na hataweza kuitimiza 
ndoto yake ya kubadili maisha ya Peniela kwa 
kumtoa Team SC41 ili aweze kuishi maisha ya 
kawaida .Alikiri kwamba alikosea sana 
kumuingiza Peniela Team SC41 na kuziharibu 
ndoto zake nyingi za maisha.kwa hiyo alinikabidhi 
mimi jukumu la kwaza kuhakikisha ninamsaidia 
Peniela atoke Team SC41 na pili kuhakikisha 
Team SC41 inatoweka katika ardhi ya 
Tanzania.Kuhusu Peniela aliniambai kwamba 
kuna mamo ya siri yanayomuhusu ambayo 
ameyaweka katika kisanduku alichompatia akihifadhi.Alisisitiza kwamba katika kisanduku 
hicho kuna mambo muhimu na ya msingi ambayo 
hatakiwi mtu mwingine kuyafahamu zaidi ya 
Peniela na mimi.Alirudia kunisisitiza kwamba 
nimlinde Peniela zaidi ya mboni yangu ya jic ho 
kwani ni binadamu mwenye thamani kubwa 
.NIlimtaka anifafanulie ana maanisha nini kwa 
kauli hiyo akasema kwamba kila kitu alichokisema 
kimo ndani ya sanduku alilompa 
Peniela.Alinielekeza kwa Askofu Edmund Dawson 
kwamba ni mtu muhimu na msaada mkubwa 
kwetu.Alinipa maelekezo namna ya kufika kwa 
askofu Edmund ambaye ndiye aliyetusaidia hadi 
hapa tulipofika” akatulia kidogo kisha akaendelea 
 “ John Mwaulaya alinieleza jambo lingine 
linalonihusu mimi” akasema Mathew 
 “ Jambo gani hilo? Akauliza Anitha.Mathew 
akainamisha kichwa 
 “ tell me Mathew.Ni jambo gani hilo 
alilokwambia John? 
 “ John…John..” Mathew akababaika “ Niambie Mathew.John alikueleza nini? 
akasisitiza Anitha ,akaingiwa na hofu 
akamsogelea Mathew karibu zaidi 
 “ Mathew kuna tatizo gani? John alikueleza 
nini? 
 “ Its about my family” 
 “ Alikueleza nini kuhusu familia yako? 
 “ Familia yangu bado iko hai.My wife and 
children are all still alive” 
 “ Whats ?? Anitha akashangaa 
 “ No ! that’s not true.Ulitueleza kwamba 
familia yako yote iliteketea kwa moto” 
 “ Hata mimi nilijua hivyo lakini kumbe 
haikuwa hivyo.” 
 “ What real happened?haya mbona kama 
mazingaombwe? Waliotekete katika nyumba yako 
kama si familia yako ni akina nani basi? 
 “ John alisema kwamba lengo lao lilikuwa si 
kuiteketeza familia yangu kwani hawakuwa na 
kosa ila walitaka kunichanganya akili kwa 
kunifanya niamini familia yangu iliteketea kwa 
moto ili wanikamate kirahisi.Alisema kwambawatu waliokutwa wameteketea mle ndani yan 
nyumba ni maiti walizozitoa katika chuo kikuu cha 
utabibu.Kwa hiyo Anitha familia yangu iko salama 
kabisa” 
 “ Jesus Christ !! Anitha akapatwa na 
mshangao mkubwa 
 “ So where are they now? 
 “ Wanaishi Marekani .Alinipa anuani ya 
mahala wanakoishi endapo nitahitaji 
kuwatafuta.Kwa bahati mbaya…” Mathew 
akainaisha kichwa 
“ bahati mbaya gani tena Mathew? 
“ Its complicated” akasema Mathew 
 “ How ? 
 “ Mke wangu tayari amekwisha olewa na 
ana watoto wengine wawili kwa mume wake wa 
sasa.” 
 “ Oh jamani….! Nimeishiwa maneno ya 
kuongea.Dunia hii imejaa watu makatili sana.kwa 
nini wakakufanyia hivi Mathew? I hope right now 
John Mwaulaya is burning in hell for all that he did 
” akasema Anitah kwa hasira “ Naye mkeo kwa nini alikubali kuolewa 
tena? Nini hasa kilimshawishi afanye hivyo? 
Akauliza tena 
 “ John alikuwa ni mtu mwenye roho mbaya 
lakini katika hili ninamshukuru kwani 
hakuiteketeza familia yangu.Alikuwa na uwezo wa 
kuwateketeza wote lakini akaingiwa na moyo wa 
huruma akawaacha hai na kuwatafutia mahala 
kwingine kwa kuishi nje ya nchi ambako wanaishi 
maisha yaliyojaa furaha hivi sasa.Mke wangu 
naye sipaswi kumlaumu kwa sababu sielewi ni kitu 
gani hasa kilichomfanya anisahau na aamue 
kuolewa tena” akasema Mathew na kuinama 
chini.Anitha akasema 
 “ So what are you going to do? When this is 
over are you going to find them? 
 “ I cant..They’ve moved on with their life 
and they are happy.Sitaki kuyavuruga maisha yao 
ya furaha waliyonayo sasa” 
“ Mathew una hakika hutaki kuwatafuta na 
kufahamu kilichosababisha mkeo aamue kuolewa 
tena?  Anitha kwa sasa tuna kazi moja tu kubwa 
iliyoko mbele yetu,kirusi Aby kiko katika hatari ya
kutua kwenye mikono isiyo salama ya watu 
wenye lengo la kufanya maangamizi makubwa 
.Me ,you,peniela and Anna we’re the only people 
who can save the world.Tunatakiwa kufanya kila 
tuliwezalo kuiokoa nchi yetu na dunia toka katika 
maangamizi makubwa yanayoweza kutokea 
endapo kirusi Aby kitasambaa hewani.Ni jukumu 
zito sana kutokana na watu tunaopambana 
nao.Baada ya kulikamilisha jukumu hilo ndipo 
hayo mambo mengine yatafuata ila kwa sasa 
nataka akili yangu niielekeze sehemu moja tu 
mambo ya familia yatafuata baadae kwa hiyo 
naomba tusiongee chochote kuhusiana na suala 
hilo la familia.” Akasema Mathew 
“ Sawa Mathew nimekuelewa ila naomba 
uniahidi kwamba baada ya mambo haya 
kumalizika mimi na wewe tutapata wasaa wa 
kuzungumzia suala hili “ 
 “ sawa ninakuahidi hivyo Anitha”  “ Thank you.Now let us g to sleep.I’m 
sleeping with you tonight” 
 “ Nini ? Mathew akashangaa 
 “ Mbona umeshangaa Mathew niliposema 
kwamba nitalala nawe usiku wa leo? 
 “ Lazima nishangae Anitha.Kwa nini tulale 
wote wakati k ila mmoja ana chumba chake? 
 “ Mathe I’m sorry to say this but you and I 
we’ve been in a sea of loneliness.Toka 
tumefahamiana sijawahi kukuona hata mara moja 
na mwanamke halikadhalika hujawahi kuniona au 
kusikia nina mpenzi.Sote tulichagua kuishi 
maisha haya ya upweke kutokana na mambo 
tuliyoyapitia.Baada ya kifo cha Noah nilijifunza 
kwamba maisha ni zawadi na ni mafupi 
sana.Noah died so yung.What happened to Noah 
can happen to us at anytime” 
 “ Unamaanisha nini Anitha? 
 “ Ninamaanisha kwamba tumeelekeza 
nguvu na akili zetu zote katka kazi na tumejisahau 
wenyewe.Kazi zetu zina mafanikio na tunapata 
pesa nyingi za kutuwezesha kuishi maisha mazuri but we’re not happy.All we think day and night is 
work,work,work,nothing else.Kama si kwa nguvu 
ya Mungu pengine hivi sasa ningekwisha kuwa 
marehemu.Tayari Rosemary angekwisha 
niua.Baada ya kunusurika katika mikono ya Yule 
shetani mla watu, nimefanya maamuzi.” Akatulia 
kidogo na kuendelea 
 “ Baada ya mambo haya kukamilika vizuri 
na kama tutajaaliwa kubaki salama nitaachana na 
hizi kazi.Nataka kuanza aina mpya ya maisha .I’m 
dreaming to have a family and be 
happy.”akasema Anitha.Ilimkuchukua Mathew 
zaidi ya dakika moja kusema chochote kuhusiana 
na kauli ile ya Anitha 
 “ I’m glad to hear that.Its a good 
idea.Unachokisema ni cha kweli kabisa.Mawazo 
yako ni kama ya kwangu.Hata mimi zaidi ya mara 
moja nimekuwa nafikiria kuachana na shughuli 
hizi na kuanza maisha mapya” 
 “ Wow Mathew.Ahsante sana kama nawe 
umeliona hilo .We both need to be happy 
again.Kwa kuwa sote tuna mawazo yanayofanana,tonight we’re going to sleep 
together We weed to comfort each other.Please 
Mathew don’t say no to this.I need someone to 
comfort me tonight so do you.I need strong arms 
to hug me tight tonight and tell everything will be
ok.I need you Mathew” akasema Anitha.Mathew 
akajikuta akishindwa kumkatalia Anitha kwani 
naye alihisi kuhitaji faraja kwa usiku ule.. 
Tukutane sehemu ijayo...


“ Wow Mathew.Ahsante sana kama nawe 
umeliona hilo .We both need to be happy 
again.Kwa kuwa sote tuna mawazo yanayofanana,tonight we’re going to sleep 
together We weed to comfort each other.Please 
Mathew don’t say no to this.I need someone to 
comfort me tonight so do you.I need strong arms 
to hug me tight tonight and tell everything will be
ok.I need you Mathew” akasema Anitha.Mathew 
akajikuta akishindwa kumkatalia Anitha kwani 
naye alihisi kuhitaji faraja kwa usiku ule.. 
Endelea.....
Tayari usingizi ulikwishaanza kumchukua 
Peniela lakini alifumbua macho baada ya kusikia 
mlio wa simu ya mkononi mle chumbani.Akainuka 
na kumtazama Dr Joshua aliyekuwa amelala 
fofofo anakoroma.Akainuka taratibu na kuzifuata 
nguo za Dr Joshua ambako mlio ule wa simu 
ulitokea.Ndani ya koti akatoa simu na ilionyeshga 
mpigaji alikuwa ni Abel Mkokasule 
 “ Abel Mkokasule,ni nani h uyu? Akajiuliza 
Peniela na kwenda kumuamsha Dr Joshua 
ambaye alifikicha macho na kutazama katika kioo cha simu na alipoona jina la mpigaji akainuka 
haraka haraka na kubonyeza kitufe cha 
kupokelea. 
 “ Hallow Abel” akasema Dr Joshua 
 “ Mzee samahani kwa usumbufu” 
 “ Bila samahani Abel” 
“ Mzee nimekupigia kukutaarifu kuhusu Dr 
Kigomba na Jacob Kateka.” Akasema Abel 
Mkokasule .Dr Josha akagundua kwa sauti ya 
simu ilikuwa kubwa na Peniela alikuwa akisikia 
walichokuwa wanakiongea ,akainuka pale 
kitandani na kwenda chooni hakutaka kabisa 
Peniela kusikia chochote. 
 “ Nipe taarifa Abel” akasema Dr Joshua 
 “ Dr Joshua tumeendelea na zoezi la 
kumfuatilia Dr Kigomba na usiku huu amekuwa na 
maongezi marefu na Jacob Kateka hapa 
Mananzana Royal Club.Mzee hisia zako zinaweza 
kuwa sawa kutokana na maongezi yao yalivyo 
wanaonekaa kuna kitu kikubwa wanakipanga.” 
 Dr Joshua akavuta pumzi ndefu na kusema  “ Mmeweza kunasa sauti zao kufahamu 
wanachokiongea? 
 “ Hapana mzee hatujafanikiwa kwa hilo 
lakini wanaonekana kujadili mambo kwa kina 
sana.Kama kuna jambo wanalipanga basi 
litakuwa kubwa” 
 Dr Joshua akafikiri tena kidogo na kusema 
 “ Sikiliza Abel” 
 “ nakusikiliza mzee” akasema Abel 
 “ Edeleeni kuwafuatilia na watakapoondoka 
hapo ,take down Jacob Kateka but do it ina 
professional way,make it like an accident” 
 “ What about Kigomba? Akauliza Abel 
 “ Kigomba muache kwa sasa.Abel nataka 
tukio hilo liwe ni habari kuu ya kesho 
asubuhi.Umenielewa? 
 “ Nimekuelewa mzee,tutalitekeleza kama 
ulivyoagiza” 
 “ Good” akasema Dr Joshua na kukata 
simu 
 “ Nikiwachia Kigomba na Jacob wanaweza 
kuniharibia kila kitu.Lazima niwawahi kabla hawajaniwahi.Jacob nimekuwa namtafuta siku 
nyingi kwani ni mtu ambaye hatuelewani na 
amekuwa akinifuatilia sana katika shughuli zangu 
sasa Muda wake umefika na lazima nimuondoe” 
akawaza Dr Joshua na kutoka mle chooni na 
kuelekea moja kwa moja zilipo nguo zake 
akaanza kuvaa 
 “ Peniela I have to go now” akasema 
 “ Ouh Dr Joshua my love kwa nini 
usiendelee kukaa nami hadi asubuhi? I need you 
darling” 
 “ Peniela mimi ni rais na muda wote niko 
kazini.Kuna masuala muhimu natakiwa 
kuyashughulikia usiku huu.Tutaonana kesho 
jioni.Nitakuwa na wageni wangu muhimu kesho 
jioni hapa hapa kwa hiyo baada ya kuzungumza 
nao nitapata tena wasaa wa kukaa nawe 
ikiwezekana hadi asubuhi.Usalama hapa ni 
mkubwa na kesho asubuhi Kareem atafika hapa 
kuhakikisha unakuwa salama na unapata kia 
unachokihitaji ila naomba uzingatie jambo 
nililokueleza kwamba usithubutu kutoka humu ndani hadi hapo nitakapokuruhusu.Lengo langu ni 
kukutengenezea mazingira mazuri ya maisha na 
usalama wako kwani wewe ni mke wa rais ingawa 
bado si rasmi.” Akasema Dr Joshua huku akivaa 
nguo zake.Peniela akambusu wakaagana 
akatoka.Dr Joshua akatoa maelekezo ya kubaki 
askari wawili kulinda nyumba ile na kuhakikisha 
Penila anakuwa salama. 
 “ Kama si Peniela kuniamsha baada ya 
Abel kupiga simu ningejikuta nimelala hadi kesho 
saa mbili asubuhi.Na hii imesababishwa na 
mambo aliyonifanyia Peniela.Yule mmwanamke 
anajua mno kunipa raha.Anajua kucheza na mwili 
wangu.Naapa sintomuacha Peniela hata 
iweje.Yeye ndiye mwanamke pekee ambaye 
ninataka kuishi naye baada ya kumaliza kipindi 
changu cha uongozi lakini…” Akawaza Dr Joshua 
na kitu Fulani kikamstua alipokikumbuka 
 “ Yale maneno aliyonieleza Peniela kuhusu 
Elibariki ni ya kweli? Nani nimuamini kati ya 
Elibariki na Peniela? Akajiuliza “ lakini namuamini Peniela Hawezi 
kunidanganya.Maneno yote aliyonieleza Elibariki 
ni ya uongo kutaka kunifarakanisha na 
mwanamke ninayempenda kumbe wao ndio 
wenye nia ovu na mimi.Elibariki ni chui mwenye 
ngozi ya Kondoo.Sikupaswa kabisa 
kumuamini.Hata mimi ni likuwa na mashaka naye 
sana.Kumbe yeye na Rosemary Mkozumi 
wanashirikiana kunihujumu? Hili ninaweza kabisa 
kuliamini.Dah ! yaani kila mtu anayenizunguka ni 
msaliti nani nitamuamini? Kigomba nae 
nilimuamini mno lakini kumbe naye ana mipango 
yake ya siri ya kunizunguka na Jacob 
Kateka.Haya yote yanatokea kwa sababu ya 
kirusi kile.Nahisi kina laana na ndiyo maana toka 
nilipoanza mchakato wa kukiuza matukio 
yamekuwa yanatokea mfululizo.Nimempoteza 
mke wangu,mwanangu na watu wangu wa karibu 
niliowaamini kama Captain Amos ambao 
waligeuka wasaliti.Ngoja nifanye haraka haraka 
nimpatie Hussein mzigo wake ili nipate nafasi 
nzuri ya kulishughulikia lile suala la serikali ya Marekani” akawaza Dr Joshua akiwa garini 
kurejea nyumbani. 
 “ Abel Mkokasule ….” Peniela akasema 
kwa sauti ndogo akiwa amekaa kitandani baada 
ya Dr Joshua kuondoka. 
 “ Ni nani huyu Abel Mkokasule? Kabla Dr 
Joshua hajainuka na kwenda kujificha bafuni 
nilisikia huyo mtu anasema kwamba anataka 
kumpa taarifa kuhusu Kigomba na Jacob 
Kateka.Who is Jacob Kateka? Ana mahusiano 
gani na kigomba? Is Dr Joshua spying on 
Kigomba? Nahisi hivyo.Kama ni kweli Dr Joshua 
anamchunguza Kigomba ambaye ni mshirika 
wake wa karibu basi lazima kuna jambo 
linaendelea kati yao.Mathew anatakiwa 
kulifahamu jambo hili alifanyie uchunguzi “ 
akawaza Peniela na kulala. 
**************** 
 Mlio wa simu ulimuamsha Dr Joshua toka 
usingizini.Tayari imekwisha timu saa kumi na dakika nane za alfajiri.Mpigaji alikuwa ni Dr 
Kigomba. 
 “ Hallow Kigomba” akasema Dr Joshua 
 Mheshimiwa samahani kwa kukupigia 
muda huu bu I have a bad news” akasema Dr 
Kigomba 
 “ Kuna taarifa gani mbaya Kigomba? 
 “ Nimepigiwa simu sasa hivi Jacob Kateka 
mkuu wa idara ya usalama wa taifa amepata ajali 
mbaya usiku huu wakati akirejea nyumbani kwake 
na inasemekana yeye na dereva wake hali zao ni 
mbaya sana na tayari wamekimbizwa hospitali 
.Mimi niko njiani sasa hivi naelekea huko hospitali
kupata uhakika wa hali zao” 
 Dr Joshua akavuta pumzi ndefu akakaa 
kimya kidogo na kusema 
 “ Hizi ni taarifa za kustusha sana 
.Nashangaa kwa nini mpaka sasa sijataarifiwa 
kuhusu suala hilo.Naomba unipe taarifa za hali 
zao mara tu utakapowasili hospitali ” akasema Dr 
Joshua “ Sawa mzee nitakutaarifu mara moja 
nitakapofika hospitali” akasema Dr Kigomba na 
kukata simu.Dr Joshua akatabasamu 
 “ Good job Abel.Napenda sana kuwatumia 
vijana wachapakazi kama huyu.Kazi yoyote 
ukimpatia unakuwa na uhakika itakamilika kama 
unavyotaka.I hope Jacob is dead.Mipango yao 
yote waliyoipanga na Kigomba imekwama na 
ndiyo maana Kigomba amechanganyikiwa .Na hii 
ni taa nyekundu kwake asipobadilika naye lazima 
nitamuondoa.He should never try to cross me !!” 
Dr Joshua akainuka kitandani na kwenda katika 
kabati dogo zilimo chupa kadhaa za mvinyo 
,akamimina mvinyo mkali katika glasi na 
kugugumia wote huku amefumba macho 
 “ Sasa baada ya Jacob ,watakaofuata ni 
Elibariki na mshirika wake Rosemary 
Mkozumi.Hawa wawili wanajifanya wema kwangu 
kumbe ni nyoka wa vichwa viwili.Hawa nao 
natakiwa kuwaondoa haraka sana” akawaza Dr 
Joshua na kuchukua simu akampigia Abel 
Mkokasule “ Hallow mzee” akasema Abel baada ya 
kupokea simu 
 “ Abel nimepokea taarifa usiku huu kuhusu 
Jacob” 
 “ Samahani mzee kwa kutokutaarifu 
mapema kuhusu kazi uliyonituma hadi ukapata 
taarifa toka kwa watu wengine.” 
 “ Usijali kuhusu hilo.You did a good 
job.Nashukuru sana kwa kazi uliyoifanya.Hata 
hivyo bado nataka uendelee kuwafuatilia 
Kigomba na jaji Elibariki.Kwa jaji Elibariki nataka
uchunguze anakutana na akina nani na halafu 
nitakupa maelekezo nini cha kufanya” 
 Sawa mzee nitafanya hivyo.” Akajibu Abel 
 “ Once again,thank you Abel.Thank you so 
much.” Akasema Dr Joshua na kukata simu na 
ndipo akakumbuka kusoma jumbe kadhaa katika 
simu yake ambazo hakuwa amezisoma 
bado.Moja ya ujumbe ulitoka kwa Anna ,akimtaka 
waonane asubuhi kuna jambo la muhimu la 
kuzungumza. “ Anna mwanangu amebaki na ukiwa 
mkubwa sana baada ya kuondokewa na mama na 
dada yake.Natakiwa kufanya kila linalowezekana 
kuhakikisha kwamba anakuwa na furaha tena” 
akawaza Dr Joshua na kurejea tena 
kitandani.Baada ya dakika kumi Dr Kigomba 
akampigia simu na kumtaarifu kwamba Jacob 
Kateka na dereva wake wamefariki dunia mara tu 
baada ya kufikishwa hospitali.Uso wa Dr Joshua 
ukachanua kwa tabasamu . 
*************** 
 Mlango wa chumba cha Anna ukagongwa 
akainuka na kwenda kuufungua akakutana na 
baba yake wakasalimiana kisha Anna akawaomba 
radhi marafiki zake watatu waliokuwamo mle 
chumbani kumfariji watoke kidogo kwani ana 
maongezi muhimu na baba yake. 
 “ Vipi maendeleo yako Anna? Akauliza Dr 
Joshua baada ya kubaki wawili mle chumbani  “ Ninaendelea vizuri japokuwa siko sawa 
kama nilivyokuwa kabla ya matukio haya mfululizo 
kutokea.” Akasema Anna 
 “ Yes I k now.Hii ni mipango ya Mungu na 
mafundisho yanatufundisha kwamba tujifunze 
kushukuru kwa kila jambo.Tushukuru kwa haya 
yaliyotupata katika familia yetu.Anna haya ni 
mapito tu katika maisha and I promise you that Im 
with you and we’ll get through this together.’ 
Akasema Dr Joshua 
 “ Muangalie kwanza anavyoongea kama 
malaika lakini kumbe ni shetani mwenye mkia” 
akawaza Anna akimtazama baba yake kwa 
macho makali 
“ Anna leo tunamalizia shughuli za hapa na 
tutarejea ikulu kuendelea na maisha yetu ya 
kawaida.Asubuhi hii tutakwenda kuwasha 
mishumaa katika kaburi la dada yako halafu 
tutarejea hapa kumaliza taratibu kisha tutakwenda 
ikulu.Nimepata ujumbe wako unasema kuna 
jambo la muhimu la kuongea.I’m here now tell me”  “ Ndiyo baba kuna jambo nataka 
tuzungumze” akasema Anna 
 “ Ok karibu .I’m here to listen” 
 “ Ni kuhusu Elibariki” akasema Anna na 
kumstua Dr Joshua 
 “ Nimeonana na jaji Elibariki jana 
usiku.Nilitaka kufahamu kuhusu kilichotokea 
kwani siku chache zilizopita alikuwa anatafutwa 
na jeshi la polisi kwa kusababisha kifo cha dada 
lakini ghafla amejitokeza toka mafichoni na 
zikafuata taarifa toka jeshi la polisi kwamba 
alikuwa ametekwa na majambazi waliokuwa 
wanamtumia kwa lengo la kujipatia fedha na 
akafanikiwa kutoroka.” Anna akanyamaza kidogo 
akameza mate kulainisha koo lakini kabla 
hajaendelea Dr Joshua akasema 
 “ Do you believe him? 
 “ Yes I do.I believed him because you did 
too” akasema Anna 
 “ Good” akajibu Dr Joshua kwa sauti ndogo  “ Kuna kitu Elibariki aliniambia ambacho 
kimenifanya nitake kuonana nawe asubuhi hii ya 
leo” akasema Anna 
 “ Amekwambia kitu gani? Akauliza Dr 
Joshua kwa sauti yenye kuonyesha wasi wasi 
kidogo 
 “ Ameniambia kwamba umemuahidi 
atakuwa rais wa Tanzania baada ya wewe 
kumaliza kipindi chako cha uongozi.Is that true? 
 “ You know uhhmmm…I.. I Told hime that 
in order..” Dr Joshua akajikanyaga katika kujibu 
swali lile 
 “ Kama hiyo haitoshi Elibariki aliniambia eti 
mmepanga mimi na yeye tuwe na mahusiano na 
tuoane.Hilo nalo ni la kweli? 
 “ Listen my dear Anna,alichokwambia 
Elibariki ni kitu cha kweli kabisa.Ni kweli alikuwa 
ametekwa na majambazi ambao walimtumia 
kutaka kujipatia pesa.Baada ya kufanikiwa 
kuwatoroka alinifuata akanieleza nami nikampigia 
simu mkuu wa polisi kanda ya Dar es salaam 
nikamueleza kuhusiana na watu hao na usiku huo huo polisi wakapambana na watu hao 
wakafanikiwa kuwaua baadhi na wengine 
wakatoroka na hadi sasa msako unaendelea.Kwa 
kitendo cha kishujaa alichokifanya niliona ni mtu 
anayefaa kabisa kuwa mrithi wangu baada ya 
kumaliza kipindi change cha uongozi kwani katika 
chama tumeazimia sasa hivi kuwa na mgombea 
kijana kabisa.Niliahidi kulifikisha suala hilo kwa
wadau ila sikumpa uhakika wa moja kwa moja 
.Kuhusu yeye na wewe kuwa na mahusiano 
nilifikiria hilo ili kuifanya familia yetu iendelee 
kuwa katika nafasi za juu za uongozi.” 
 “ Kwa nini ukafanya hivyo baba? Kwa nini 
ukataka kuyaingilia maisha yangu na kupanga 
mambo bila kunishirikisha?I’m not a child 
anymore..” 
 “ Anna I’m sorry .I don’t know what I was 
thinking at that time.I Think I was drunk.But forget 
about that because it wont happen 
anymore.Siwezi tena kumfanya Elibariki awe rais 
wa nchi hii.Baada ya kutafakari kwa kina nimeona 
hana sifa za kuwa rais kwa hiyo sahau kabisa suala la wewe na yeye kuwa na mahusiano.” 
Akasema Dr Joshua kwa ukali kidogo.Anna 
akamtazama na kuuliza 
 “ Endapo Elibariki angekuwa chaguo lako 
la kurithi kiti cha urais ,bado ungesisitiza mimi na 
yeye tuwe na mahusiano” 
 Dr Joshua akakuna kichwa na kusema 
 “ Ndiyo.Ingekuwa ni kwa faida yako Anna” 
 “ Faida yangu? What kind of a father are 
you? Yaani kulazimisha niwe katika mahusiano na 
mwanaume ninayehisi kutapika nikimuona kwa 
sababu ya maslahi yako unasema ni faida 
yangu?Akauliza Anna kwa ukali 
 “ Anna tafadhali usiongee na mimi katika 
lugha ya namna hiyo.I’m your father and I’m the 
one who decides whats good for you so if I want 
you to be with Elibariki or whoever I want you cant
say No!!! akasema D Joshua kwa ukali 
 “ A father? Have you been a father to us? 
Where were you when me and my sister needed a 
father? Muda wote unashughulika na mambo 
yako yenye faida kwako..”“ Stop that Anna!! Akafoka Dr Joshua na 
kusimama akamtazama Anna kwa hasira 
 “ Don’t you dare talk to me like that 
again.Leo unadiriki kusema eti I wasn’t there 
when you needed me,are you sure?? Akauliza Dr 
Joshua kwa ukali.Anna hakujibu kitu 
 “ Anna my dear,ndani ya kipindi kifupi 
familia yetu imepitia mambo magumu sana.Hii ni 
mitihani na ili tuishinde mimi na wewe lazima 
tushikamane.Kuna mambo mengi makubwa na 
mazuri yanakuja kwa ajili yako.Wewe pekee 
ndiye uliyebaki furaha yangu.Nitakulinda zaidi ya 
mboni yangu ya jicho.Si muda mrefu topka sasa 
nitamaliza kipindi changu cha uongozi na kwa 
pamoja tutaizunguka dunia tukifurahia uumbaji wa 
mwenyezi Mungu.Kitu kingine ambacho nataka 
nikuahidi ni kwamba sintoingilia tena masuala 
yako ya kimahusiano .Mwanaume yeyote ambaye 
utampenda mimi nitamridhia kwani nahitajhi uwe 
na furaha” akasema Dr Joshua .Akamtazama 
Anna kwa sekunde kadhaa na kusema  “ Now get ready,tunakwenda makaburini 
muda si mrefu” akasema Dr Joshua na kutoka 
mle chumbani . 
 “ Nasikitika sana kuwa na baba kama huyu 
ambaye hana roho ya ubinadamu hata 
chembe.Anyway siku zake zinahesabika,lazima 
akumbane na mkono wa sheria.Ngoja nimjulishe 
Mathew kwamba nitakwenda kuonana naye 
baadae baada ya kutoka makaburini” akawaza 
Anna na kumuandikia Mathew ujumbe mfupi 
akimfahamisha kwamba wataonana baadae 
******************* 
 Mlio wa ujumbe wa simu ,ulimstua Mathew 
akafumbua macho.Pembeni yake alilala Anitha 
.Wote walikuwa watupu 
 “ Dah ! siamini kama kweli nimelala na 
Anitha mwanamka ambaye ni rafiki yangu 
mkubwa.Sifahamu nilikuwa nawaza wapi hadi 
nikakubali kufanya kitu kama hiki.Hata hivyo 
baada ya miaka zaidi ya kumi kupita bila kukutana na mwanamka yeyote kimwili,usiku wa jana 
niliona kama siko katika ulimwengu huu.Anitha 
amenifanya nijione mimi ni mwanaume wa 
shoka.Aliniondoa katika dunia ya upweke 
mkubwana kunirejesha katika dunia ya 
kawaida.Last night was my beautiful night ever 
since I lost my wife.Anitha amenikumbusha 
umuhimu wa kuwa na familia tena” akawaza 
Mathew na kumtazama Anitha ambaye bado 
alikuwa amelala 
 “ She’s beautiful.Ujuzi wake si katika 
teknolojia tu bali hata kitandani mambo 
anayaweza lakini sitaki turudie tena mchezo 
huu.Mambo tuliyoyafanya jana usiku yataishia h 
apa kwani tukiendelea tunaweza kujikuta 
tumezama mapenzini na mimi sitaki kuingia katika 
mapenzi na Anitha.She deserve a better man than 
me” akawaza na kukumbuka kilichomstua 
usingizini ni ujumbe wa simu.Akaichukua simu 
akaufungua ujumbe ule uliotoka kwa Anna 
akimjulisha kwamba wataonana baadae  “Namuonea huruma sana Anna kwa 
mambo yaliyomkuta.Baada ya kuufahamu upande 
wa pli wa baba yake ameumia zaidi lakini 
hakukuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya 
kumueleza ukweli ili aweze kutusaidia” akawaza 
Mathew na kuinuka akatoka mle chumban na 
kwenda kufanya mazoezi mepesi ya viungo halafu 
akaingia jikoni kuandaa kifungua kinywa.. 
 “ Natamani kujua Penila 
anaendeleaje.Endapo hadi mchana wa leo 
hatakuwa ametujulisha chochote kuhusu 
maendeleo yake nitakwenda kumtoa ndani ya lile 
jumba mimi mwenyewe.I don’t care what will 
happen ila jukumu langu ni kuhakikisha Penila 
yuko salama.Lakini alisema wamba atamtuma 
kareem leo alete kasha alilopewa na John 
mwaulaya.Halafu siku ya leo alitakiwa aongee na 
Deus Mkozui ili tuone kama anaweza kutuelekeza 
chumba kilimohifadhiwa kirusi aby lakini kwa k 
uwa Peniela ndiye aliyepaswa kwenda kuonana 
na Deus na kwa kuwa hawezi kutoka ndani ya 
jumba lile itabidi kazi hiyo niifanye mimi na Anitha.Tutakwenda kuonana na Deus Mkozumi” 
akawaza Mathew wakati akiandaa mlo wa 
asubuhi .Kisha maliza kuandaa akamfuata Anitha 
chumbani akamuamsha. 
 “ Wake up pretty angel ….” Akasema 
Mathew.Anitha akafumbua macho na kutabasamu 
 “ C’mon Mathew I was dreaming..” 
akasema kwa sauti laini 
 “Umeiharibu ndoto yangu” 
 “ I’m sorry Anitha muda wa ndoto 
umepita.Huu sasa ni muda wa kazi so wake up” 
akasema Mathew.Anitha akainuka huku akiona 
aibu kidogo kwani alikuwa mtupu.Akavaa nguo na 
kumtazama Mathew 
 “ Thank you Mathew.Sijawahi kuwa na 
usiku mzuri kama wa jana.You are real 
amazing.Last night I felt like….ouh gosh I dont 
know how to explain it” akasema Anitha.Mathew 
akatabasamu na kusema 
 “ Thank you too but that wont happen again 
Anitha.Let us forget what happened and pretend 
like nothing happened” “ Its ok Mathew it wont happen again .Lakini 
narudia tena kukushukuru kwa namna 
ulivyoufanya usiku wangu kuwa mzuri.Leo 
nimeamka vyema na akili yangu imetulia na tayari 
kwa kazi.Lets get back to work” akasema Anitha 
 “ Breakfast is ready” akasema Mathew na 
baada ya Anitha kujiswafi wakaelekea kupata 
kifungua kinywa. 
 “ Any news from Peniela or Anna? 
Akauliza Anitha. 
 “ Anna kanitumia ujumbe kanitaarifu kuwa 
atakuja baadae ila kwa Peniela bado sijapokea 
taarifa yoyote toka kwake kwani hakubeba 
simu.Nina wasi wasi sana na usalama wake ndani 
ya jumba lile” 
 “ She’ll be fine don’t worry.If anything 
happens she can handle it” akasema Anitha 
 “ Lazimaniwe na wasi wasi kwa sababu 
John Mwaulaya kabla ya kifo chake alinisisitiza 
kwamba kwa namna yoyote ile hata ikibidi kuweka 
rehani maisha yangu nihakikishe Peniela yuko 
salama kwa hiyo endapo mpaka mchana wa leo sintapata taarifa yoyote toka kwake itakwenda 
kumtoa mle ndani mimi mwenyewe.I don’t know 
wh….” Kaba hajamaliza sentesi yake kengele ya 
getini ikalia.Mathew akainuka na kwenda katika 
chumba chenye luninga zilizounganishwa na 
kamera za ulinzi 
 “ Kareem !! akasema Mathew na kutoka 
akaelekea getini akamfungulia Kareem geti 
akaingia 
 “ Karibu Kareem.Naamini Peniela 
amekutuma” akasema Mathew 
 “ Ndiyo nimetumwa na Peniela” 
 “ Anaendeleaje? Is she safe there? 
 “ She’s mopre than safe.Amenituma 
nikuletee huu mzigo na h ii bahasha” akasema 
Kareem na kutoka kuondoka Mathew akamuomba 
asubiri akaenda chumbani na kuchukua simu 
akampatia 
 “ Mpe Peniela hii s imu” 
 Kareem akaondoka ,Mathew na Anitha 
wakaelekea katika ofisi yao na kitu cha kwanza ilikuwa ni kuifungua ile bahasha iliyokuwa na 
karatasi ndogo ndani yake iliyoandikwa 
 “ ABEL MKOKASULE..Find out who is he? 
 Mathew na Anitha wakatazamana. 
*************** 
 Taratibu za mwisho za kimila zilikamilika 
nyumbani kwa Dr Joshua na hivyo kumpa nafasi 
Dr Joshua ya kuondoka kuendelea na majukumu 
mengine ya kitaifa.Mtu wa kwanza kuonana naye 
baada ya kurejea ikulu ni Dr Kigomba 
 “ Kigomba nimekuita hapa kuna mambo 
kadhaa ambayo nataka tongee” akaanzisha 
maongezi Dr Joshua 
 “ Kwanza kabisa nataka nikupe pole sana 
kwa kifo cha Jacob Kateka.Nafahamu wewe na 
Jacob mlikuwa marafiki wakubwa .Hata mimi kifo 
chake kilimuumiza sana.Nasubiri taarifa za 
uchunguzi wa kifo chake ili tufahamu nini 
kilisababisha hiyo ajali.Tumempoteza mchapakazi 
mzuri sana.Mungu amempumzisha mapema” akasema Dr Joshua halafu ukapita ukimya mfupi 
akaendelea 
 “ Tukiachana na taarifa hizo za kustusha za 
kifo cha Jacob ,ninataka nikushukuru binafsi kwa 
ushirikiano wako mkubwa katika msiba wa 
mwanangu.Kazi uliyoifanya ni kubwa na mimi na 
familia yangu tunawiwa deni la shukrani.Kwa 
niaba yao nasema ahsante sana Kigomba .Wewe 
ni rafiki wa kweli.” 
 “ Nashukuru sana mheshimiwa rais.Ule 
ulikuwa ni msiba wetu sote kwa hiyo juhudi za kila 
mmoja wetu zilihitajika” akasema Kigomba 
 “ Jambo lingine ni kuhusiana na 
sintofahamu iliyojitokeza katika ule mpango 
wetu.Yalijitokeza mambo kadhaa likiwamo na hili 
la msiba na ndiyo maana nikasimamisha zoezi 
zima” 
 “ Tukiachana na hilo la msiba ,nini kingine 
kilitokea? Nahitaji sana kufahamu” 
 “ Kama utakumbuka usiku ule tukiwa 
msibani,niliondoka ghafla bila kukutaarifu 
naelekea wapi.Nilipigiwa simu na Rosemary Mkozumi akanitaka niende nyumbani kwake 
haraka kuna jambo la maana sana anataka 
kunieleza.Nilipofika kwake akanikutanisha na jaji 
Elibariki.Aliniambia kwamba jaji Elibariki ana 
mambo makubwa ya kunieleza.Niliondoka naye 
hadi msibani na baadae usiku ndipo nikakaa naye 
akaanza kunieleza mambo.Alisema kamba baada 
ya kumuacha huru Peniela alitaka kufahamu 
kuhusu nani hasa aliyemuua Edson na ndipo 
alipoanzisha uchunguzi.Kazi hiyo alimpa rafiki 
yake aitwaye Mathew ambaye aliwahi kufanya 
kazi katika idara yetu ya usalama wa taifa na 
aliacha baada ya familia yake kuteketea kwa 
moto.Wakati rafikiye huyo akiendelea na 
uchunguzi Dr Flora akafariki na Flaviana 
akamuomba Elibariki amsaidie kwa kila nama 
awezavyo kufahamu kilichomuua mama 
yake.Elibariki naye akamkabidhi kazi hiyo Mathew 
ambaye alifanikiwa kugundua kilichomuua Flora 
na ndipo akatuletea ile ripoti tuliyoikataa.Mpango 
wa kumuua ulishindwa kwani aliokolewa na Jessica Yule aliyewahi kuwa mlinzi wangu kama 
unakumbuka” 
 “ Jessica? Kigomba akashangaa 
 “ Ndiyo,aliokolewa na Jessica” 
 “ How? Jessica alifahamuje kuhusu 
mpango ule wa kumuua Elibariki? 
 “ Alielekezwa na Amos.He was a 
traitor.Amos alikuwa anafanya kazi na Team 
Sc41” 
 “ Team Sc41? Ni kampuni gani hiyo? 
Akauliza Dr Kigomba 
 “ Hii si kampuni .Hiki ni kikundi 
kinachofanya kazi kwa siri hapa nchini kwa ajili ya
kulinda maslahi ya Marekani.Hata mimi bado 
sijakifahamu kiundani zaidi naendelea kutafuta 
taarifa zake.Kwa mujibu wa Elibariki hawa Team 
SC41 wanakitaka kile kirusi na Amos ndiye 
aliyekuwa mtu wao waliyempandikiza.Si yeye 
peke yake bali na Peniela”. 
 “ Ndiyo Peniela “ akasema Dr Joshua na 
ukimya mfupi ukapita  “ kwa mujibu wa Elibariki walikuwa na timu 
yao ya kuhakikisha nao wanakipata kirusi 
Aby.Timu hiyo iliongozwa na huyo 
Mathew,akawepo pia Elibariki mwenyewe,Peniela 
na msichana mwingine nimesahau jina.Elibariki 
alidai kwamba baada ya kutafakari sana aliona 
hataweza kupambana na mimi kwa hiyo akaamua 
kuwasaliti wenzake na kumuachia huru Rosemary 
mkozumi ambaye alikuwa anashikiliwa katika 
jumba la Mathew.Alimtumia Rosemary ili kunifikia 
mimi.Alinielezea mipango yote waliyokuwa 
wameipanga ili kukipata kirusi hicho na ndiyo 
maana nikachukua tahadhari kwa kusitisha kila 
kitu hadi hapo tutakapojipanga upya vizuri 
ikiwamo kumuondoa Hussein na ujumbe wake 
pale walipokuwa wamefikia na kuwapeleka 
sehemu nyingine.Kwa hiyo Kigomba hiyo ni 
sababu kuu iliyonipelekea nisitishe kila kitu hadi 
hapo tutakapojipanga upya” 
 Ukimya ukatawala mle ofisini,baada ya 
dakika mbili Dr Kigomba akasema  “ Ahsante sana Dr Joshua kwa kueleza 
mambo hayo mazito lakini kwa nini unieleze 
sasa? Nilikufuata zaidi ya mara moja kutaka kujua 
nini kimetokea na hukuwa tayari kunieleza 
chochote.You didn’t even trust me” akasema Dr 
Kigomba 
 “ What do you expect me to do Kigomba? 
I’m surrounded by traitors so I chose not to trust 
anybody especially you Kigomba!! Dr Joshua 
akawa mkali kidogo 
 “ I sent you to spy n Peniela,what did you 
do? Akauliza Dr Joshua. 
 “ Nothing…I didn’t do anything wrong Mr 
President”akajibu Dr Kigomba.Dr Joshua 
akamtazama kwa macho makali na kusema 
 “ Kigomba wewe ni mmoja wa watu wangu 
wa karibu sana.Please tell me the truth.Ulitembea 
na Peniela na akakupa ile saa ya dhahabu kama 
zawadi .Is that that true? 
 Dr Kigomba akamtazama Dr Joshua kwa 
macho makali na kuuliza 
 “ Elibariki ndiye aliyekueleza hivyo? Do you 
believe him? After all that you and I we’ve been 
through you choose not to trust me and you trust 
that good for nothing judge?Ahsante sana Dr 
Joshua.Ahsante sana kwa kuchagua kumuamini 
Elibariki.Kesho asubuhi nitawasilisha kwako barua 
yangu ya kujiudhuru ili nikupe nafasi ya kufanya 
kazi na watu unaowaamini” akasema Dr Kigomba 
na kuinuka akataka kuondoka 
 “ It’s not like that Kigomba.Please sit 
donw.Usiwe mwepesi kukasirika kiasi hicho” 
akasema Dr Joshua lakini bado Dr Kigomba 
alikuwa amesimama 
 “ Sit down Kigomba” akaamuru Dr Joshua 
na Kigomba akaketi 
 “ Nisamehe Kigomba kama maneno 
niliyoyatamka yamekukwaza.Sikuwa na lengo 
hilo.Naomba nikuweke wazi Kigomba kwamba 
Peniela ni mwanamke wangu.” Dr Kigomba 
akastuka sana akamtazama Dr Joshua kwa 
sekunde kadhaa kisha akasema 
 “ I didn’t know that”  “ I’m telling you now” akasema Dr Joshua 
 “ Elibariki aliponieleza kuhusiana na wewe 
kutembea na Peniela nilichukia sana sana.I love 
Peniela so much and she’s mine alone” 
akanyamaza akamtazama Kigomba na kuendelea 
 “ Jana nimekutana na Peniela akanieleza 
ukweli wote” 
 “ Amekueleza nini? akaulizia Kigomba kwa 
wasi wasi. 
 “ She told me the truth” 
 “ What truth Dr Joshua? Akauliza Kigomba 
huku wasi wasi ukimzidi 
 “ Kuhusu Elibariki.Yale yote aliyonieleza 
Elibariki ni uongo mtupu.Kumbe amekuwa 
akishirikiana na Rosemary Mkozumi kupanga 
mipango ya kunihujumu.Wanapanga mipango ya 
kukipata kirusi na kibaya zaidi alichokifanya 
Elibariki amekuwa akimtaka peniela kimapenzi 
kwa kisingizio eti yeye ndiye aliyemuachia 
huru.Baada ya peniela kumkatalia ,jaji Elibariki 
alimbaka!!!!..Sura ya Dr Joshua ikabadilika na 
hasira za wazi wazi zikaonekana  “ Kibaya zaidi baada ya kumbaka alimtolea 
vitisho vya kumuua endapo atanieleza suala 
hilo.Juzi usiku Peniela alivamiwa na watu 
nyumbani kwake waliokuwa na lengo la kumuua 
lakini akafanikiwa kutoroka na watu wale 
wakaichoma moto nyumba yake wakateketeza 
kila kitu.Elibariki is a snake!!! Akasema Dr Joshua
kwa hasira 
 “ Peniela anaishi wapi kwa sasa? 
 “ Anaishi kwenye ile nyumba yangu ya 
ufukweni.Elibariki ameniudhi sana na nitamfunza 
adabu.Alinifanya niwachukie watu wangu wa 
maana kwa maneno yake ya uongo” akasema Dr 
Joshua na kumfanya Dr Kigomba ashushe pumzi. 
 “ Wakati mwingine ukiletewa taarifa kama 
hizo unatakiwa kujadiliana kwanza na wenzako” 
akasema Dr Kigomba 
 “ Usemayo ni ya kweli Kigomba.Mambo 
yetu mengi yamekwama.Hivi sasa tayari 
tungekwisha maliza biashara yetu na Hussein.”  “ Baada ya kuufahamu ukweli nini 
kitafuata? MIpango yetu inaendelea ? akauliza 
Kigomba 
 “ Tutaendelea Kigomba ila si sasa 
hivi.Tutasubiri kidogo mambo yatulie ili tuendelee 
na mpango wetu.Macho ya wengi tayari yameona 
kwa hiyo ni hatari kwetu.Nahitaji muda wa 
kusafisha kwanza njia ndipo tuendelee na 
mipango yetu tukiwa na uhakika kuwa hakuna mtu 
yeyote atakayekuwa kikwazo 
kwetu.Nitazungumza na Hussein ili nimfahamishe 
kuhusu maamuzi haya na ninaamini atanielewa 
na atasubiri.Endapo hatanielewa basi sintakuwa 
na namna nyingine ya kufanya zaidi ya 
kumrejeshea fedha zake” 
 “ Dr KIgomba najua maamuzi haya 
yamekunyong’onyeza sana kwani tumetoka mbali 
na jambo hili na mengi yametokea hadi hapa 
tulipofika lakini hakuna namna nyingine ya 
kuendelea na jambo hili kabla kwanza ya 
kusafisha njia kwa kuwaondoa njiani wale wote 
ambao wanaonekana kuwa kikwazo kwetu.Usiogope Kigomba hata kama jambo hili 
halitawezekana mimi na wewe bado tuna fursa 
nyingi za kutengeneza fedha nyingi za 
kutuwezesha kuishi kama malaika baada ya 
kustaafu.Nipe muda kidogo Kigomba na 
nitakushirikisha katika jambo Fulani kubwa zaidi 
ya hili la kirusi” akasema Dr Joshua 
 “ Dr Joshua mimi sina kipingamizi chochote 
na maamuzi yako.Ni kweli tumetoka mbali na 
suala hili na kweli mengi yametokea huko njiani 
hadi hapa tulipofika na kwa hali ilivyo nakuunga 
mkono kwamba tusimamishe mipango yetu kwa 
muda .Ni hasara kubwa lakini hatuna namna 
nyingine ya kufanya” akasema Dr Kigomba na 
kumfanya Dr Joshua atabasamu 
 “ Nafurahi sana kusikia kauli hiyo 
Kigomba.Pamoja na hayo kuna jambo moja bado 
nahitaji msaada wako” 
 “ Sema chochote unachohitaji Mr President” 
 “ Leo jioni nitaonana na Donald pale pale 
nyumbani kwangu ufukweni kwa hiyo naomba 
unifanyie maandalizi kama uliyoyafanya jana.Nataka kiandaliwe chakula cha usiku kwa ajili 
ya watu wanne kwani nitakula chakula cha usiku 
na wageni wangu usiku wa leo” 
 “ Sawa mheshimiwa rasi nitalifanya hilo” 
akasema Dr Kigomba kisha wakaagana akatoka ili 
kwenda kufanya kazi aliyotumwa.Mara tu baada 
ya Dr Kigomba kutoka Dr Joshua akachukua simu 
na kumpigia Kareem 
 “ Hallow mzee” akasema Kareem baada ya 
kupokea simu 
 “ Kareem Peniela anaendeleaje? 
Amekwisha amka? Amepata kila anachokihitaji? 
Akauliza Dr Joshua 
 “ Ndiyo mzee.Peniela anaendelea vizuri 
,tayari amekwisha amka na amepata kila 
alichoagiza” akajibu Kareem 
 “ good to hear that.Kareem nitakuwa na 
wageni wangu hapo nyumbani usiku w a leo na 
nitakula nao chakula cha usiku hapo hapo 
nyumbani.Nimemtuma Dr Kigomba yule katibu 
wangu aje afanye maandalizi,please please 
hakikisha hamkaribii Peniela.Umenielewa 
kareem? 
 “ Nimekuelewa mzee,Nitalitekeleza hilo” 
 “ Good” akasema Dr Joshua na kukata 
simu.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO...
PENIELA SEASON 5
SEHEMU YA 5
ILIPOISHIA
Kareem Peniela anaendeleaje? 
Amekwisha amka? Amepata kila anachokihitaji? 
Akauliza Dr Joshua 
 “ Ndiyo mzee.Peniela anaendelea vizuri 
,tayari amekwisha amka na amepata kila 
alichoagiza” akajibu Kareem 
 “ good to hear that.Kareem nitakuwa na 
wageni wangu hapo nyumbani usiku w a leo na 
nitakula nao chakula cha usiku hapo hapo 
nyumbani.Nimemtuma Dr Kigomba yule katibu 
wangu aje afanye maandalizi,please hakikisha hamkaribii Peniela.Umenielewa 
kareem? 
 “ Nimekuelewa mzee,Nitalitekeleza hilo” 
 “ Good” akasema Dr Joshua na kukata 
simu 
 “
Endelea....
   “ Ingawa hakutaka kuonyesha wazi wazi 
lakini Dr Kigomba amestushwa sana na maamuzi 
yangu ya kusitisha ile biashara yetu ya 
kirusi.Sitaki kabisa kushirikiana chochote na Yule 
msaliti.Nina hakika yeye na Jacob kuna njama 
walikuwa wanaipanga dhidi yangu.Hata yeye 
Kigomba naamini siku zake zinahesabika kwani 
nafahamu namna alivyo na kiu ya pesa atatafuta 
kila namna ili aweze kupata pesa nyingi kupitia 
kirusi kile.Nilifanya kosa kubwa kumshirikisha 
katika mpango ule .” Simu ya mezani iliyoita 
ikamtoa Dr Joshua katika mawazo akaipokea 
 “ Mheshimiwa rais kuna mtu anahitaji 
kuzungumza nawe katika laini ya simu namba 
moja” akaambiwa Dr Joshua na bila kupoteza 
muda akabonyeza laini namba moja 
 “ Hallow !! akaita “ Hallow Dr Joshua.It’s me Rosemary 
Mkozumi.Vipi maendeleo yako? Nimekuwa 
nakutafuta niongee nawe jambo la muhimu lakini 
sikupata nafasi hii hadi sasa nilipoomba sana 
wasaidizi wako wanisaidie niongee nawe.” 
 Dr Joshua akavuta pumzi ndefu na kuuliza 
 “ What do you want Rose? 
 “ Dr Joshua I need your help.Something 
happened yesterday here at my place” 
 “ Kitu gani kilitokea? 
 “Unakumbuka kuna Yule msichana 
niliyekuambia kuwa anashirikiana na Mathew na 
Peniela ambaye nilikuwa namtegemea sana 
atueleze mahala alipo Mathew? 
 “ Ndiyo nakumbuka ulinieleza kitu kama 
hicho.” 
 “ Basi Yule msichana ametoroka na sijui 
nitampataje.Ninaomba msada wako ili aweze 
kupatikana kwani anahatarisha usalama 
wetu.Mipango yetu yote haitaweza kufanikiwa 
endapo huyu msichana hatapatikana.She knows too much” akasema Rosemary.Dr Joshua 
akapatwa na kigugumizi akashindwa aseme nini 
 “ Dr Joshua are you there? Akauliza Rose 
baada ya kuona kumekuwa kimya 
 “ Uhhmm Rose are you sure about that? 
 “ About what? 
 “ About that woman.Is she real? 
 “ Dr Joshua how come you ask me such a 
silly question.You don’t trust me now? You think 
I’m lyin g? akauliza Rosemary mkozumi kwa ukali 
 “ Sikiliza Rose,kwa sasa nina mambo 
mengi ya kushughulikia.Tafadhali naomba mambo 
yako yashughulikie mwenyewe.If that woman real 
do exist find her by yourself” akasema Dr Joshua. 
 “ Dr Joshua ni wewe kweli unayethubutu 
kuniambia maneno hayo leo? Akaulizia Rose kwa 
ukali.Dr Joshua hakutaka kuendelea na 
maongezi akakata simu 
 “ Huyu naye ni miongoni mwa watu 
waliomo katika orodha ya watu wanaotakiwa 
kuondolewa.Yeye na mumewe Deus ni vizingiti 
vikubwa katika kufanikisha mipango yangu.Katika mpango wa kumuua Deus Mkozumi huyu naye 
lazima awepo” akawaza Dr Joshua na 
kutabasamu 
 “ Ngoja nijiandae nikaonane na 
Hussein,nimfahamishe kwa kina ugumu uliopo 
kwa sasa katika kuufanikisha mpango wetu na 
kama ikiwezekana basi anisubiri na kama hataki 
kusubiri basi nimrudishie pesa zake zote 
alizotoa.Sintaathirika na chochote kwani tayari 
serikali ya Marekani imeleta mpango 
utakaoniingizia fedha nyingi mno kwa hiyo 
sibabishwi na pesa zake”s akawaza Dr Joshua. 
*************** 
 “ Dr Joshua ni shetani.Najuta kushirikiana 
na mtu kama Yule. Nina hakika kabisa anataka 
kunizunguka na kuchukua pesa zote 
mwenyewe.No! I wont let him do that 
.Nitapambana naye!! Akawaza Dr Kigomba akiwa 
garini kuelekea nyumbani kwa Dr Joshua kufanya 
kazi aliyotumwa.  “ Tayari nina mipango mingi mikubwa ya 
kufanya baada ya kuzipata zile fedha na kwa hiyo 
nisipozipata mipango yangu yote itakuwa 
imeyeyuka.Hapana siwezi kukubali hilo.Nimefanya 
kazi kubwa kuhakikisha jambo hili linafanikiwa 
lakini leo baada ya pesa kuwasili Dr Joshua 
ananiondoa kimya kimya katika mpango kwa 
sababu ambazo hazina kichwa wala 
miguu.Anadai eti kuna tishio la usalama na eti jaji
Elibariki na Rosemary Mkozumi tayari 
wanafahamu kuhusu mpango huu na kwamba eti 
wana njama za kumzunguka na kuuchukua ule 
mzigo,that’s a big lie.Najua lazima kuna kitu 
kinachoendelea kati yake na jaji Elibariki 
.Nitautafuta ukweli” akawaza Dr Kigomba na mara 
akakumbuka kitu. 
 “ Peniela !!..oh my God..Dr Joshua na 
Penila kumbe ni wapenzi.Kwa nini hakunieleza 
kuhusu jambo hili wakati ananituma 
nikamchunguze? Inawezekana kweli Peniela na 
Elibariki wakawa wanafahamiana kwa sababu 
mambo ambayo Elibariki alimueleza Dr Joshua ni ya kweli k abisa.Ni kweli nilitembea na Peniela na 
akanipa zawadi ya saa ya mkononi.Lakini je ni 
kweli saa ile aliyonipa Peniela ilikuwa ni mtego? Ni 
kweli yeye na wenzake anaowasema Dr Joshua 
walikuwa wakifuatilia maongezi yangu ya 
simu?.Dr Joshua amesema pia eti Peniela na 
Amos walikuwa wanafahamiana na kwamba eti 
walikuwa wanashirikana sijui na kikundi gani 
nimekisahau jina lake.Haya yote ni ya kweli? 
Akaendelea kujiuliza Dr Kigomba. 
 “ Mmmhhh ! naanza kupata mashaka 
kidogo kuhusu huyu Peniela.Lazima kuna kitu 
kinachoendelea kati yake na Elibariki.Nani mkweli 
k ati yao? Nadhani natakiwa kuonana na Elibariki 
.Anaweza akanipa ukweli .Kabla ya kwenda 
kuonana naye natakiwa kwanza kutafuta mahala 
Dr Joshua alikompeleka Hussein.Natakiwa 
kuongea naye kufahamu kinachoendela kati yake 
na Dr Joshua na kama ameshakabidhiwa mzigo 
wake ama bado.Najua hawezi kunificha chochote 
kwani anafahamu mimi na Dr Joshua ni washirika 
na mimi n diye niliyefanya naye mchakato mzima hadi hapa tulipofika.Nitamuonyesha Dr Joshua 
kuwa mimi nina akili zaidi yake.” Akawaza Dr 
Kigomba 
**************** 




ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog