Search This Blog

Wednesday 22 March 2023

SHE IS MY WIFE - 4

   

Simulizi : She Is My Wife

Sehemu Ya : Nne (4)


Samson aliwashauri wezake

“Lakini jamani, hembu kuweni makini. Hapa tulipo fika sote hatupajui. Isije ikawa fukwe ya jeshi ikala kwetu ohooo”

Halima alizungumza huku akijigeuza geuza kwenye mchanga

“Sasa Halima wewe unataka tuendelee kukaa hapa si ndio?”

“Hapana sijasema hivyo Fetty, ila ninacho sema mimi, tuwe makini tusiwe vihere here. Kama pesa tumezikosa, lile lidude nalo limechukuliwa. Yote kwa tamaa zetu”

“Halima huu muda sio wa kulaumiana bwana”

Agnes alizungumza kwa hasira kali.


“Hata kama, jamani lakini hua siku zote nikizungumzaga ukweli, munaniona mimi fala. Sasa huyo Samson tuliye msaidia naye katuileta huku, nilipo kua ninamkatalia tusiwe pamoja naye mimi nilijua tuu haya yatatokea. Haya baba Samson tuambie tunaelekea wapi?”

“Maneno ya Halima, yakamkera kila mtu ambaye, alionekana kuchoka sana kwa shuhuli nzima waliyo ifanya ya kujioko kutoka kwenye jeshi la nchi ya Russia


Wakaanza kutembea kwa umakin, huku wakitazama kila eneoa la fukwe hii. Kigiza kilisha anza kuchukua nafasi yake huku kila mmoja akaizidi kunyong’onyewa kwa kuchoka sana. Hawakukata tamaa zaidi ya kwenda mbele kubahatisha kama wanaweza kupata sehemu ya kujistiri. Hadi inagonga mishale ya saa mbili usiku hapakuwa na mtu aliye baatika kuona nyumba ama uwepo wa watu katika eneo hilo

“Jamani tupumzikeni bwana na kama kuendelea tutaendelea kutembea tukiwa na nguvu”


Halima alizungumza huku akiwa amesimama, wezake wote wakamgeukia na kumkodolea mimacho. Kila mtu akakubaliana na wazo la Halima, wakatafuta moya ya jiwe kubwa lililo toboka na kuweka kijichumba kidogo, wote wakaingia na kukaa humo. Mwanga wa mbalamwezi uliweza kuwaonyesha ndani ya jiwe hilo kubwa, hapakuwa na kitu chochote kinacho weza kuwadhuru.



Baridi kali kwao ndio ikawa ni changamoto kubwa sana iliyo weza kuwatesa miili yao, isitoshe nguo walizo zivaa zilizo tengenezwa kwa material ya mpira hazikuweza kabisa kuizuia baridi hiyo kuendelea kuwapiga kwenye miili yao.


“Mmmm hili puku ni balaaa”

Agnes alizungumza huku akijikunyata, taratibu Samson akatoka ndani ya jiwe na kusimama nje, akatizama kila kona ya fukwe hakuona mtu yoyote, akazunguka nyuma ya jiwe na kujisaidia haja ndogo ambayo ilikuwa imememkamata kwa kipindi kirefu sana. Akiwa katikati ya kujisaidia haja ndogo kwa mbali akaweza kuona mwanga wa taa ukitokea kwenye moja ya nyumba iliyo mbali kidogo toka hapo walipo, kwa haraka akamaliza haja yake na kuzunguka walipo wezake


“Jamani kuna kitu nimekiona tokeni haraka”

Fetty na wezake wakatoka kwa haraka, Samson akawaonyesha mwanga wa taa hiyo . Kwa haraka bila hata ya kujiuliza wakanza kukimbia kuelekea kwenye nyumba hiyo. Kila walivyo zidi kwenda ndivyo walivyo zidi kuiona mandhari ya nyumba hiyo, ambayo ni kubwa kiasi na yagorofa. Wakafanikiwa kufika kwenye uwanja wa jumba hilo linalo onekana ni jumba la kifahari, ila nje hapakua na taa ya aina yoyote, zaidi ya taa inayo waka kwenye chumba hicho kimoja.


“Jamani, tuweni makini naona tunaenda tu”

Halima alizungumza, kwa kujiamini. Wote wakasimama kutazama mazingira ya jumba hili lililo zungukwa na miti mingi ya minazi. Kwa mbali wakasikia mngurumo wa gari ukiwa unakaribia kufika kwenye jumba hili, kwa haraka wakatafuta sehemu ya kujificha ambayo iliwawezesha kuona mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya jumba hilo.


Gari moja ya kifahari aina ya Jaguar, ikasimama nje ya jumba hili. Wakashuka watu wawili walio valia suti huku mikononi mwao wakishika bunduki aina ya Short gun. Mmoja akazunguka upande wa pili wa gari ambapo akaufungua mlango wa gari hiyo. Wote wakamshuhudia bwana Rusev akishuka kwenye gari hilo la kifahari huku akionekana kutazama kila upande wa jumba hilo.


‘Asante Mungu’

Samson alizungumza kimoyo moyo, kwani amemuona rafiki yake huyo. Waliye toka kupotezana masaa machache ya nyuma. Samson kwa haraka akanyanyuka na kuanza kukimbilia sehemu alipo Rusev, jambo lililo mfanya Agnes naye atake kunyanyuka kutoka katika sehemu waliyo jificha ila Fetty akamzuia.


Bwana Rusev na watu wake wakaonekana kusthushwa na uwepo wa Samson katika eneo hilo, ambalo kwao ni eneo la maficho la kiongozi huyu. Kabla Samson hajafika alipo bwana Rusev, akachomoa bastola yake moja na kumtandika Samson, ya kwenye mguu, na kumuangusha Samson chini akiwa haamini kama Rusev anaweza kumfanyihi hivyo.

***

Kitu cha kwanza kukifanya Raisi Praygod baada ya kuamka asubuhi akaichukua simu iliyopo mezani na kimpigia rafiki yake Frednando, akampa jina la Motel walipo fikizia, na akamuomba aje na nguo za wao kuvaa.

“Umeakaje mpenzi”


Rahab alizungumza kwa sauti ya uchovu huku akimtazama usoni Rais Praygod aliye achia tabasamu pana usoni mwake.

“Mimi nimeamka salama”

Rahab taratibu akajivuta karibu na sehemu alipo kaa Raisi Praygod, pembezoni mwa kitanda na kumpiga busu moja la mdomoni. Kisha akajilaza kwenye mapaja ya Raisi Praygod.

“Wewe ni mzuri sana Rahab”


“Kwa nini unasema hivyo?”

“Umenifanya sasa, nijisikie kua ni mwanaume mwenye bahati, kumpata mwanamke ambaye siku zote kwenye maisha yangu nilikua nikumuwazia”

“Kweli?”

“Ndio, yaani umenipa kitu ambacho sijawahi kupewa tangu nitoke tumboni mwa marehemu mama yangu”

Rahab akatabasamu, taratibu akajinyanyua mapajani mwa raisi Praygod, na kuanza kumnyonya midomo yake, taratibu wakajikuta wakiingia kwenye dimbwi jengine zito la mahaba, ambapo kama kawaidia yake Rahab, alijua ni nini cha kufanya kuzidi kumpagawisha rasi Praygod, ambaye tayari anaonekana amenogewa na utamu wa penzi la Rahab, binti aliye mpita miaka kumi.


Azaria akagonga mlango akimuashiria Raisi Praygod kwamba, ni muda wa wao kuweza kupata kifungua kinywa. Ila hapakuwa na jibu lolote kutoka kwa raisi, ikamlazimu Azaria kuweka sikio lake moja mlangoni kusikiliza ni kitu gani, kinacho endelea. Akajikuta akitabasamu, baada ya kusikia vilio mchanganyiko kati ya Rahab na Raisi Praygod.

“Mmmm huyo ndio raisi”


Azaria alizungumza kwa sauti ya chini na kuondoka katika mlango na kurudi chumbani kwake kuvuta vuta pumzi akisubiria mtanange wa kukata na shoka uliopo ndani ya chumba cha Raisi Praygod uweze kumalizika.

Ikawachukua takribani dakika arobaini, kumaliza mtanange woa. Raisi kambeba Rabab na kuingia naye bafuni ambapo waliweza kuoga kwa pamoja kisha wakajifunga mataulo yao. Kabla hawajaendelea kufanya kitu kingine, mlango ukagongwa tena.


“Who?”(Nani?)

Raisi Praygod aliuliza kwa sauti ya kujiamini.

“Ni mimi muheshimiwa, Azaria”

“Ahaaa”

Raisi Praygod akapiga hatua hadi mlangoni ambapo, akaufungua kwa funguo iliyokuwa imening’inia kwenye kitasa cha mlango huo. Akamkuta Azaria akiawa amesimama huku mkononi mwake akiwa ameshika chupa mbili za juisi pamoja na kifuko cha rangi ya kaki.

“Muheshimiwa kifungua kinywa”

Azaria alizungumza huku akiwa amesimama nje ya mlango

“Karibu ndani”

Azaria akaingia ndani na kumkuta Rahab akiwa amesha jifunga taulo, na kukaa kitandani, simu ya mezani ikaita na kumfanya Raisi Praygod kuipokea

“Nimesha fika kaka”

Sauti ya Frednando ilisikika kwenye simu

“Ahaaa, kuna kijana wangu hapo anakuja kukuchukua, akulete chumbani”

“Sawa kaka”


Frednando alizungumza kwa sauti ya furaha, kwani ni muda mrefu umepita sasa tangu aonane na rafiki yake huyu. Raisi akamuomba Azaria kwenda kumpokea rafiki yake huyo kipenzi. Azaria akatoka nje, na kukuta gari za kifahari sita zikiwa zimesimama nje ya moteli hiyo, kutokana alielekezwa Frednando anafanania vipi, moja kwa moja akamfwata na kumuomba waweze kuongozana hadi sehemu alipo Raisi Praygod.



Frednando akaongozana na walinzi wake wawili walio beba suti mbili kwenye mifuko yake maalumu, suti hizo zenye gharama kubwa. Wakafika kwenye chumba alipo raisi Praygod. Ikawa ni shangwe kubwa kwa Frednando na Raisi Praygod, vituko vya kusalimiana kwao unaweza kusema kwamba sio waheshimiwa wanao kubalika sana mbele ya macho ya wanajamii wengi.


“Ebwanaa kaka ni more than, miaka kumi na tano hatujaonana eheee?”

“Yaa kaka, kweli Mungu ni mwema”

“Kweli ndugu yangu, nakumbuka kipindi kile ulikua unaniambia utakua raisi na kweli, leo wewe ni raisi”

“Kweli ndugu yangu ndoto zimekua kweli”

Fredinando akawageukia walinzi wake na kuwaambia kwa lugha ya kispain kwamba Praygod ndio mtu alimfundisha lugha ya kiswahili ambayo hadi leo imekuwa ni lugha anayo ipenda sana, japo yeye ni mmexco.

“Kutana na shemeji yako, anaitwa Rahab”

“Ohoooo Rahab, nashukuru kukufahamu”

“Nawe pia”

“Rahab huyu ni Frednando, ni ndugu yangu sana tumesoma chuo kimoja, tumalala chumba kimoja”

“Pia kula tulikua tunakula pamoja”


Frednando alidakia na kuwafanya wote kucheka. Wakawakabidhi suti walizo kuja nazo, kisha wao wakatoka nje na kuwasubiria Rahab na Raisi Praygod waweze kuvaa nguo hizo. Kila mmoja akvaa suti aliyo letewa, kama vile Frednando aliotea, suti hizo ziliwatosha vizuri sana Rabab na Rais Praygod. Wakakabidhiwa viatu vilivyo kua vimesaulika ndani ya gari moja waliyo kuja nayo. Wakatatoka ndnai ya chumba na kukuta Azaria akiwa amewasubiria nje.

“Azaria tunashukuru sana, Mungu akubariki katika kila jambo ambalo unakwenda kulifanya”


“Kwani huyo ni nani?”

Frednando aliuliza, huyu anaitwa Azaria alitusaidia barabarani, akatununulia chakula na kutulipia hadi hapa tulipo lala”

“Ohooo, ngoja basi”

Frednando akamngong’oneza mlizi wake, ambaye akatoa kitabu kidogo cha benk, pamoja na kalamu. Frednando akamuandikia Azaria cheki ya shilingi dola kali mbili na kumkabidhi. Azaria hakuamini machi yake kwani, tangu azaliwe hakuwahi kufikiria kwamba ipo siku atapata mkwanja mrefu kiasi hicho. Wakaagana na Azaria, kisha safari ya kuelekea kwenye jumba la Frednando ikaamza


***

Fetty na wezake wakajikuta wakimshangaa, Samson anaye garagara chini kwa maumivu makali ya risiasi aliyo pigwa na bwana Rusev.

“Jamani itakuaje?”

Agens alizungumza kwa sauti ya chini, huku wakiendelea kumtazama bwana Rusev akifoka kwa sauti ya juu huku akimtazama Samson aliye lala chini.


Mawazo yote ya bwana Rusev alihisi kwamba Samson yeye ndio chanzo kikubwa cha yeye kuvamiwa na wanajeshi wa nchi yake. Kwani uchunguzi walio weza kuufanya wakiwa ndani ya manohari ambayo walilitewa kwa ajili ya kuuziwa, kulikuwa na kifaa cha GPR’s, ambacho kiliweza kuionyesha manohairi hiyo ni wapi ilipo, kifaa kilicho washwa na Halima pasipo yeye kujijua, kina kazi gani katika manohari hiyo, iliyokuwa hainaswi na satalaiti zozote za nchi waliyo kuwepo.

Bwana Rusev akaanza kumshushia kipigo kikubwa, Samson ambaye muda wote aliendela kulia kwa maumivu makali.


“Tuondokeni jamani”

Halima alizungumza huku akianza kutambaa kurudi rudi nyuma, kutoka katika bustani kubwa yenye maua waliyo lala.

“Tutakwenda wapi unadhani?”

Anna aliungumza

“Hembu acha ujinga wewe, sasa unataka tukae hapa ili iweje?”

“Na Samson je?”

“Kwani ni bwana wetu huyo, acheni afe mwenyewe bwana, sisi tunajua ni wapi tunatoka, mi naona anatupeleka peleka tu”


Halima alizungumza kwa hasira, kwani tangu siku ya kwanza kumuona Samson, damu zao hazikulandana kabisa, kiasi cha kumfanya Halima kumchukia Samson, hata kama walizungumza, ila moyo wake ulijawa na mashaka na Samson.


“Hembu Halima acha roho mbaya, tumekuja pamoja tutaondoka pamoja haiwezekani tumuache mwenzetu hapa”

Fetty alizungumza kwa msisitizo na kuzidi kumchefua Halima. Bwana Rusev akamuamrisha askari kuwasiliana na wezao walio ndani, naye akafanya hivyo kupitia simu ya upepo. Taaa zote nje ya jumba hili zikawashwa, na kuwafanya Fetty na wezake waonekane waliopo, Walinzi wapatao hamsini, wakiwa na bunduki, waliiekekeza mitutu yao katika eneo walilo lala Fetty na wezake na kuwafanya wanyanyuke taratibu huku mikono wakiwa wameinyanyua juu.


SHE IS MY WIFE(32)


Hapakuwa na mtu aliye weza kumuonea mwenzake aibu zaidi ya wote kushiriki tendo la ndoa ipasavyo. Rahab akazidi kujituma kitandani kumpa muheshimiwa Raisi mambo matamu ambayo hata Raisi Praygod, hakuwahi kuyapata kutoka kwa mwanamke wa aina yoyote tangu azaliwe. Hata marehemu mke wake, hakuweza kufikia hata aslimia kumi kwa mambo ambayo Rahab anamfanyia juu ya kitanda. Wote wakajikuta wamesahau kwamba wanapita katika kipindi kigumu cha matatizo.


“Rahab”

Raisi Praygod alimuita Rahab, aliye mkalia juu ya kiuno chake akizidi kukatika kadri ya uwezo wake.

“Mmmmmm”

Rahab aliita huku akiwa amebana pumzi zake, huku jasho kwa mbali likimwagika na nywele zake ndefu zikiwa zimekaa shaghala baghala.


“Nataka nikuoe”

“Kweli?”

“Ndio nahitaji uwe mke wangu, wa ndoa”

Rahab kuambia wahivyo hakujibu kwa sauti, ila akajibu kwa vitendo, vilivyo mfanya Raisi kusahau matatizo yote na kuzidi kuchanganyuikiwa kwa penzi hilo la binti mdogo mwenye mwili mwembamba, fulani, ila si shuuhuli ya kupambana pekee yake na maadui, ila hata shughuli ya kitandani anaiweza kwa asilimia mia moja. Hadi wanafikia kileleni wote kwa pamoja wakajikuta wakicheka huku wakiamini kwamba walicho peana kilistahili kwa wao kuweza kukipata kwa wakati huo.


“Nakupenda sana Rahab”

Raisi Praygod alizungumza huku akihema mithili ya mwana riadha wa mwisho kwenye mbio ndefu, aliyekua na kibarua kirefu cha kuwakimbiza wezake wanao kwenda kwa mbio ndefu sana.

“Nakupenda pia Praygod”

Kwa mara ya kwanza Rahab kufungua kinywa chake na kuliita jina la Raisi, kwani siku zote alizoea kumuita muheshimiwa Raisi. Taratibu Rahab akajilaza kifuani mwa Raisi Praygod, huku taratibu akiupa kazi mkono wake wa kushoto kuchezea nywele nyini lizizopo kifuani mwa raisi Praygod.


“Twende tukaoge”

Raisi Praygod alizungumza, na taratibu wote wakashuka kitandania, wakaingia bafuni na kila mmoja akawa na kazi ya kumuogesha mwenzake kwa kila kona ya mwili. Ukawa ndio mwanzo mpya wa mahusiano kati ya Raisi Praygod na Rahab, kila mmoja aliweza kuufungua moyo kwa mwenzake na kuamini upendo wao umeendana kwa asilimia kubwa sana.

***

Kila jinsi walivyo zidi kuogelea ndivyo jisi walivyo zidi kwenda mbele, huku mara kwa mara wakiwa wanajitokeza kwenye usawa wa bahari kutazama ni wapi wanapo elekea. Ikawachukua muda mrefu sana kuweza kufika pembezoni mwa fukwe za bahari, katika eneo ambalo limetulia sana. Wote wakaivua mitungi ya gesi ambayo walikuwa wameivaa migongoni mwao. Kila mmoja alijihisi njaa kubwa kwenye tumbo lake, kwani waliweza kudumu ndani ya maji takribani masaa nane, wakiwa wanatoroka kutoka sehemu mmoja kwenda nyinine


“Ahaaa kudadadeki, kweli ng’ombe wa masikini hazai”

Halima alizungumza kwa sauti kubwa huku akijilaza kwenye mchanga mweupe ulio kua pembezoni mwa bahari hii kubwa. Hakuna aliye mjibu zaidi ya wezake kuendelea kutazama kila eneo la fukwe hizi zinazo pendeza kuvutia sana.


“Jamani inakuaje?”

Anna aliuliza kwa sauti ya unyonge, dhairi akionekana kuchoka sana.

“Nahisi hapa kwenye fukwe kunaweza kua na nyumba tutembeeni tembeeni, tunaweza kupata msaada”

Samson aliwashauri wezake

“Lakini jamani, hembu kuweni makini. Hapa tulipo fika sote hatupajui. Isije ikawa fukwe ya jeshi ikala kwetu ohooo”

Halima alizungumza huku akijigeuza geuza kwenye mchanga

“Sasa Halima wewe unataka tuendelee kukaa hapa si ndio?”

“Hapana sijasema hivyo Fetty, ila ninacho sema mimi, tuwe makini tusiwe vihere here. Kama pesa tumezikosa, lile lidude nalo limechukuliwa. Yote kwa tamaa zetu”


“Halima huu muda sio wa kulaumiana bwana”

Agnes alizungumza kwa hasira kali.

“Hata kama, jamani lakini hua siku zote nikizungumzaga ukweli, munaniona mimi fala. Sasa huyo Samson tuliye msaidia naye katuileta huku, nilipo kua ninamkatalia tusiwe pamoja naye mimi nilijua tuu haya yatatokea. Haya baba Samson tuambie tunaelekea wapi?”


“Maneno ya Halima, yakamkera kila mtu ambaye, alionekana kuchoka sana kwa shuhuli nzima waliyo ifanya ya kujioko kutoka kwenye jeshi la nchi ya Russia


Wakaanza kutembea kwa umakin, huku wakitazama kila eneoa la fukwe hii. Kigiza kilisha anza kuchukua nafasi yake huku kila mmoja akaizidi kunyong’onyewa kwa kuchoka sana. Hawakukata tamaa zaidi ya kwenda mbele kubahatisha kama wanaweza kupata sehemu ya kujistiri. Hadi inagonga mishale ya saa mbili usiku hapakuwa na mtu aliye baatika kuona nyumba ama uwepo wa watu katika eneo hilo

“Jamani tupumzikeni bwana na kama kuendelea tutaendelea kutembea tukiwa na nguvu”


Halima alizungumza huku akiwa amesimama, wezake wote wakamgeukia na kumkodolea mimacho. Kila mtu akakubaliana na wazo la Halima, wakatafuta moya ya jiwe kubwa lililo toboka na kuweka kijichumba kidogo, wote wakaingia na kukaa humo. Mwanga wa mbalamwezi uliweza kuwaonyesha ndani ya jiwe hilo kubwa, hapakuwa na kitu chochote kinacho weza kuwadhuru. Baridi kali kwao ndio ikawa ni changamoto kubwa sana iliyo weza kuwatesa miili yao, isitoshe nguo walizo zivaa zilizo tengenezwa kwa material ya mpira hazikuweza kabisa kuizuia baridi hiyo kuendelea kuwapiga kwenye miili yao.


“Mmmm hili puku ni balaaa”

Agnes alizungumza huku akijikunyata, taratibu Samson akatoka ndani ya jiwe na kusimama nje, akatizama kila kona ya fukwe hakuona mtu yoyote, akazunguka nyuma ya jiwe na kujisaidia haja ndogo ambayo ilikuwa imememkamata kwa kipindi kirefu sana. Akiwa katikati ya kujisaidia haja ndogo kwa mbali akaweza kuona mwanga wa taa ukitokea kwenye moja ya nyumba iliyo mbali kidogo toka hapo walipo, kwa haraka akamaliza haja yake na kuzunguka walipo wezake


“Jamani kuna kitu nimekiona tokeni haraka”

Fetty na wezake wakatoka kwa haraka, Samson akawaonyesha mwanga wa taa hiyo . Kwa haraka bila hata ya kujiuliza wakanza kukimbia kuelekea kwenye nyumba hiyo. Kila walivyo zidi kwenda ndivyo walivyo zidi kuiona mandhari ya nyumba hiyo, ambayo ni kubwa kiasi na yagorofa. Wakafanikiwa kufika kwenye uwanja wa jumba hilo linalo onekana ni jumba la kifahari, ila nje hapakua na taa ya aina yoyote, zaidi ya taa inayo waka kwenye chumba hicho kimoja.


“Jamani, tuweni makini naona tunaenda tu”

Halima alizungumza, kwa kujiamini. Wote wakasimama kutazama mazingira ya jumba hili lililo zungukwa na miti mingi ya minazi. Kwa mbali wakasikia mngurumo wa gari ukiwa unakaribia kufika kwenye jumba hili, kwa haraka wakatafuta sehemu ya kujificha ambayo iliwawezesha kuona mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya jumba hilo.


Gari moja ya kifahari aina ya Jaguar, ikasimama nje ya jumba hili. Wakashuka watu wawili walio valia suti huku mikononi mwao wakishika bunduki aina ya Short gun. Mmoja akazunguka upande wa pili wa gari ambapo akaufungua mlango wa gari hiyo. Wote wakamshuhudia bwana Rusev akishuka kwenye gari hilo la kifahari huku akionekana kutazama kila upande wa jumba hilo.


‘Asante Mungu’

Samson alizungumza kimoyo moyo, kwani amemuona rafiki yake huyo. Waliye toka kupotezana masaa machache ya nyuma. Samson kwa haraka akanyanyuka na kuanza kukimbilia sehemu alipo Rusev, jambo lililo mfanya Agnes naye atake kunyanyuka kutoka katika sehemu waliyo jificha ila Fetty akamzuia.


Bwana Rusev na watu wake wakaonekana kusthushwa na uwepo wa Samson katika eneo hilo, ambalo kwao ni eneo la maficho la kiongozi huyu. Kabla Samson hajafika alipo bwana Rusev, akachomoa bastola yake moja na kumtandika Samson, ya kwenye mguu, na kumuangusha Samson chini akiwa haamini kama Rusev anaweza kumfanyihi hivyo.

***

Kitu cha kwanza kukifanya Raisi Praygod baada ya kuamka asubuhi akaichukua simu iliyopo mezani na kimpigia rafiki yake Frednando, akampa jina la Motel walipo fikizia, na akamuomba aje na nguo za wao kuvaa.

“Umeakaje mpenzi”

Rahab alizungumza kwa sauti ya uchovu huku akimtazama usoni Rais Praygod aliye achia tabasamu pana usoni mwake.

“Mimi nimeamka salama”

Rahab taratibu akajivuta karibu na sehemu alipo kaa Raisi Praygod, pembezoni mwa kitanda na kumpiga busu moja la mdomoni. Kisha akajilaza kwenye mapaja ya Raisi Praygod.


“Wewe ni mzuri sana Rahab”

“Kwa nini unasema hivyo?”

“Umenifanya sasa, nijisikie kua ni mwanaume mwenye bahati, kumpata mwanamke ambaye siku zote kwenye maisha yangu nilikua nikumuwazia”

“Kweli?”

“Ndio, yaani umenipa kitu ambacho sijawahi kupewa tangu nitoke tumboni mwa marehemu mama yangu”

Rahab akatabasamu, taratibu akajinyanyua mapajani mwa raisi Praygod, na kuanza kumnyonya midomo yake, taratibu wakajikuta wakiingia kwenye dimbwi jengine zito la mahaba, ambapo kama kawaidia yake Rahab, alijua ni nini cha kufanya kuzidi kumpagawisha rasi Praygod, ambaye tayari anaonekana amenogewa na utamu wa penzi la Rahab, binti aliye mpita miaka kumi.


Azaria akagonga mlango akimuashiria Raisi Praygod kwamba, ni muda wa wao kuweza kupata kifungua kinywa. Ila hapakuwa na jibu lolote kutoka kwa raisi, ikamlazimu Azaria kuweka sikio lake moja mlangoni kusikiliza ni kitu gani, kinacho endelea. Akajikuta akitabasamu, baada ya kusikia vilio mchanganyiko kati ya Rahab na Raisi Praygod.

“Mmmm huyo ndio raisi”


Azaria alizungumza kwa sauti ya chini na kuondoka katika mlango na kurudi chumbani kwake kuvuta vuta pumzi akisubiria mtanange wa kukata na shoka uliopo ndani ya chumba cha Raisi Praygod uweze kumalizika.

Ikawachukua takribani dakika arobaini, kumaliza mtanange woa. Raisi kambeba Rabab na kuingia naye bafuni ambapo waliweza kuoga kwa pamoja kisha wakajifunga mataulo yao. Kabla hawajaendelea kufanya kitu kingine, mlango ukagongwa tena.

“Who?”(Nani?)

Raisi Praygod aliuliza kwa sauti ya kujiamini.

“Ni mimi muheshimiwa, Azaria”

“Ahaaa”

Raisi Praygod akapiga hatua hadi mlangoni ambapo, akaufungua kwa funguo iliyokuwa imening’inia kwenye kitasa cha mlango huo. Akamkuta Azaria akiawa amesimama huku mkononi mwake akiwa ameshika chupa mbili za juisi pamoja na kifuko cha rangi ya kaki.


“Muheshimiwa kifungua kinywa”

Azaria alizungumza huku akiwa amesimama nje ya mlango

“Karibu ndani”

Azaria akaingia ndani na kumkuta Rahab akiwa amesha jifunga taulo, na kukaa kitandani, simu ya mezani ikaita na kumfanya Raisi Praygod kuipokea

“Nimesha fika kaka”

Sauti ya Frednando ilisikika kwenye simu

“Ahaaa, kuna kijana wangu hapo anakuja kukuchukua, akulete chumbani”

“Sawa kaka”

Frednando alizungumza kwa sauti ya furaha, kwani ni muda mrefu umepita sasa tangu aonane na rafiki yake huyu. Raisi akamuomba Azaria kwenda kumpokea rafiki yake huyo kipenzi.



Azaria akatoka nje, na kukuta gari za kifahari sita zikiwa zimesimama nje ya moteli hiyo, kutokana alielekezwa Frednando anafanania vipi, moja kwa moja akamfwata na kumuomba waweze kuongozana hadi sehemu alipo Raisi Praygod.



Frednando akaongozana na walinzi wake wawili walio beba suti mbili kwenye mifuko yake maalumu, suti hizo zenye gharama kubwa. Wakafika kwenye chumba alipo raisi Praygod. Ikawa ni shangwe kubwa kwa Frednando na Raisi Praygod, vituko vya kusalimiana kwao unaweza kusema kwamba sio waheshimiwa wanao kubalika sana mbele ya macho ya wanajamii wengi.

“Ebwanaa kaka ni more than, miaka kumi na tano hatujaonana eheee?”


“Yaa kaka, kweli Mungu ni mwema”

“Kweli ndugu yangu, nakumbuka kipindi kile ulikua unaniambia utakua raisi na kweli, leo wewe ni raisi”

“Kweli ndugu yangu ndoto zimekua kweli”

Fredinando akawageukia walinzi wake na kuwaambia kwa lugha ya kispain kwamba Praygod ndio mtu alimfundisha lugha ya kiswahili ambayo hadi leo imekuwa ni lugha anayo ipenda sana, japo yeye ni mmexco.

“Kutana na shemeji yako, anaitwa Rahab”

“Ohoooo Rahab, nashukuru kukufahamu”

“Nawe pia”

“Rahab huyu ni Frednando, ni ndugu yangu sana tumesoma chuo kimoja, tumalala chumba kimoja”


“Pia kula tulikua tunakula pamoja”

Frednando alidakia na kuwafanya wote kucheka. Wakawakabidhi suti walizo kuja nazo, kisha wao wakatoka nje na kuwasubiria Rahab na Raisi Praygod waweze kuvaa nguo hizo. Kila mmoja akvaa suti aliyo letewa, kama vile Frednando aliotea, suti hizo ziliwatosha vizuri sana Rabab na Rais Praygod. Wakakabidhiwa viatu vilivyo kua vimesaulika ndani ya gari moja waliyo kuja nayo. Wakatatoka ndnai ya chumba na kukuta Azaria akiwa amewasubiria nje.

“Azaria tunashukuru sana, Mungu akubariki katika kila jambo ambalo unakwenda kulifanya”


“Kwani huyo ni nani?”

Frednando aliuliza, huyu anaitwa Azaria alitusaidia barabarani, akatununulia chakula na kutulipia hadi hapa tulipo lala”

“Ohooo, ngoja basi”

Frednando akamngong’oneza mlizi wake, ambaye akatoa kitabu kidogo cha benk, pamoja na kalamu. Frednando akamuandikia Azaria cheki ya shilingi dola kali mbili na kumkabidhi. Azaria hakuamini machi yake kwani, tangu azaliwe hakuwahi kufikiria kwamba ipo siku atapata mkwanja mrefu kiasi hicho. Wakaagana na Azaria, kisha safari ya kuelekea kwenye jumba la Frednando ikaamza


***

Fetty na wezake wakajikuta wakimshangaa, Samson anaye garagara chini kwa maumivu makali ya risiasi aliyo pigwa na bwana Rusev.

“Jamani itakuaje?”

Agens alizungumza kwa sauti ya chini, huku wakiendelea kumtazama bwana Rusev akifoka kwa sauti ya juu huku akimtazama Samson aliye lala chini.


Mawazo yote ya bwana Rusev alihisi kwamba Samson yeye ndio chanzo kikubwa cha yeye kuvamiwa na wanajeshi wa nchi yake. Kwani uchunguzi walio weza kuufanya wakiwa ndani ya manohari ambayo walilitewa kwa ajili ya kuuziwa, kulikuwa na kifaa cha GPR’s, ambacho kiliweza kuionyesha manohairi hiyo ni wapi ilipo, kifaa kilicho washwa na Halima pasipo yeye kujijua, kina kazi gani katika manohari hiyo, iliyokuwa hainaswi na satalaiti zozote za nchi waliyo kuwepo.

Bwana Rusev akaanza kumshushia kipigo kikubwa, Samson ambaye muda wote aliendela kulia kwa maumivu makali.


“Tuondokeni jamani”

Halima alizungumza huku akianza kutambaa kurudi rudi nyuma, kutoka katika bustani kubwa yenye maua waliyo lala.

“Tutakwenda wapi unadhani?”

Anna aliungumza

“Hembu acha ujinga wewe, sasa unataka tukae hapa ili iweje?”

“Na Samson je?”

“Kwani ni bwana wetu huyo, acheni afe mwenyewe bwana, sisi tunajua ni wapi tunatoka, mi naona anatupeleka peleka tu”

Halima alizungumza kwa hasira, kwani tangu siku ya kwanza kumuona Samson, damu zao hazikulandana kabisa, kiasi cha kumfanya Halima kumchukia Samson, hata kama walizungumza, ila moyo wake ulijawa na mashaka na Samson.


“Hembu Halima acha roho mbaya, tumekuja pamoja tutaondoka pamoja haiwezekani tumuache mwenzetu hapa” Fetty alizungumza kwa msisitizo na kuzidi kumchefua Halima. Bwana Rusev akamuamrisha askari kuwasiliana na wezao walio ndani, naye akafanya hivyo kupitia simu ya upepo. Taaa zote nje ya jumba hili zikawashwa, na kuwafanya Fetty na wezake waonekane waliopo, Walinzi wapatao hamsini, wakiwa na bunduki, waliiekekeza mitutu yao katika eneo walilo lala Fetty na wezake na kuwafanya wanyanyuke taratibu huku mikono wakiwa wameinyanyua juu.




ITAENDELEA 




ILIPOISHIA

“Hembu Halima acha roho mbaya, tumekuja pamoja tutaondoka pamoja haiwezekani tumuache mwenzetu hapa”

Fetty alizungumza kwa msisitizo na kuzidi kumchefua Halima. Bwana Rusev akamuamrisha askari kuwasiliana na wezao walio ndani, naye akafanya hivyo kupitia simu ya upepo. Taaa zote nje ya jumba hili zikawashwa, na kuwafanya Fetty na wezake waonekane waliopo, Walinzi wapatao hamsini, wakiwa na bunduki, waliiekekeza mitutu yao katika eneo walilo lala Fetty na wezake na kuwafanya wanyanyuke taratibu huku mikono wakiwa wameinyanyua juu.



ENDELEA

“Hichi ndicho mulichokua mukikihitaji?”

Halima alizungumza kwa sauti ya kunong’oneza akionekana kukasirishwa na kitendo hicho cha wezake kuwa wabisha hadi wametiwa nguviuni na wanajeshi hjao wa bwana Rusev ambaye kwa mara ya kwanza walimuona ni mtu mwema kutokana na ukarimu wake alio waonyesha kipindi akiwapoke na kuzngumza nao hukusiana na biashara ya kuuza manohari waliyo fanikiwa kuiteka kutoka katika jeshi la wana maji wa Tanzania.


Wakaamrishwa kuelekea sehemu ambapo yupo Samson, akiendelea kulia kwa maumivu makali aliyo yapata kutokana na risasi aliyo pigwa mguuni mwake.


Mr Rusev akaagiza wapelekwe kwenye chumba chenye giza zito na wafungiwe humo hadi kutakapo pambazuka ndipo ajue ni nini awafanye kwani siku zote hua hapendelei mtu kugundua siri zake na isitoshe wao ndio walio sababisha kwa makao makuu ya vikosi vyake kuweza kuvamiwa na jeshi la nchi yake ya Russia na kusababisha vifo vya wanajeshi wake wengi sana.


Fetty na wezake wakingizwa kwenye chumba chenye giza zito, hata kam ni jasiri kiasi gini giza la chumba hicho ni lazima uogope kwani hata mtu wa pembeni yako ha ta hauwezi kumuona zaidi ya kuisikia sauti yake.


***

Wakafika kwenye jumba la Frednando, ambalo lipo katikakti ya jiji la Mexco, Raisi Praygod na Rahab wakapokelewa kwa heshimwa kubwa na wafanyakazi wa Frednando ambao alisha wapa taarifa juu ya ugeni huo wa rafiki yake kipenzi. Wakakaribishwa kwenye moja ya seble ambayo kuta zake zimepabwa na madini ya dhahabu, huku sofa zake zikiwa zimetengenezwa kwa mtindo ambao Raisi Praygod hakuwahi, kuuona katika maisha yake


“Kaka uajua jumba lako ni zuri kuliko ikulu yangu?”

“Weee, acha utani kaka”

“Kweli vile Frednando, inanibidi nikirudi hivi Tanzania ikulu yangu niweze kuibadilisha, kidogo mfumo uwe kama huu wako”

“Ila unakumbuka kwamba ikulu si yako, ukimaliza kipindi chako anakuja mwengine?”

“Hata kama ila, kwa kipindi nitakacho kuwepo mimi itanibidi nikae kidogo sehemu ambayo ninaihitaji mimi”


Wakiwa kwenye maongezi ya furaha, wahudumu wakawa na kazi ya kuandaa chakula na vinywaji, kwa ajili ya wageni hawa. Kwa upende wa Rahab, kila kinacho tokea kwake anaona kama ni ndoto, kwani hakutarajia ipo siku atakuja kuishi maisha ya kuheshimiwa kama haya. Moyo wake ukajikuta ukiuchukia ujambazi ambao alikuwa anaufanya na rafiki zake ambao hadi sasa hivi ajui kama wapo hai, kwani kwa fununu alizo kua akizisikia, ni kwamba marafiki zake hao nilazima waweze kunyongwa, hii ni kutokmna na uhalifu mkubwa walio ufanya wa kuwaua askari wengi wa jeshi la polisi.


“Kuna klitu Frednando nahitaji kukifanya hivi karibuni?”

“Kitu gani?”

“Ninahitaji kumuoa Rahab wangu”

Rahab akastuka kusikia hivyo kwani hakutegemea kwamba inaweza kuwa jambo la haraka kama anavyo hitaji Raisi Praygod

“Waooo, kaka hilo ni jambo jema, tena unaonaje ukalifanya hapa hapa kwangu”

“Ndio maana nikakuamnbia nahitaji kulifanya siku hizi za karibu, kutokana nampenda sana Rahab, bila yeye nahisi kwa sasa ningekua marehemu”

“Kweli kaka, wewe sema ni lini unahitaji kumuoa, niweke mambo sawa si unajua tena”

“Huyu hana siku nyingi hata siku mbili hizi zijazo pia itakua ni sawa”


Rahab akaachia tabasamu pana lililo zidi kuipendezesha sura yake iliyo teumbwa vizuri kwa haraka haraka ukimtamza unaweza kusema ni binti wa kirwanda aliye changanyia na msukuma, kwa maana, urefu amepewa, sura ndio usiseme, hicho kiuno chake sasa, kimefungashia mzigo wa wastani wa makalio yanayo mfanya awe na sifa zaidi ya sifa wanazo pewa asichana wengine.


Raisi Praygod na Rahab wakapewa chumba cha kupumzikia ambacho kina kila sifa ya kuitwa chumba cha kuweza kulala Raisi Praygod pamoja na mkewe mtarajiwa. Furaha ikazidi kutawala mioyoni mwao, kwani kila walipo kua pamoja hawakusita kuipa miili yao burudani ambayo, Raisi Praygod, alijikuta akizidi kuipenda kwani, mburudishaji alimjulia jinsi ya kumburudisha.


***

Siku iliyo fwata, Fetty pamoja na wezake wakatolewa kwenye chumba ambacho walifungiwa, hawakujua ni wapi alipo Samson, ambaye walimuacha nje kipindi wakipelekwa kwenye chumba hicho. Wakafunga pingu mikononi mwao pamoja na nyororo ndefu miguuni mwao. Wakapelekwa kwenye moja ya chumba chenye kuta za vioo vigumu ambavyo si rahisi kuwez kumuona mtu wa nje, ila mtu aliyopo nje unaweza kumuona.


Chumba hicho hakikuwa na kitu cha aina yoyote, jambo lililo wapa alama ya kuuliza kila mmoja kwamba humo ndani wameletwa kufanya nini. Mr Rusev akaamrisha baunsa mmoja kuingia ndani ya chumba hicho kuweza kuwapa mkong’oto mkali Fetty na wezake ambao wanaendele kushangaa shangaa.


Halima akawa wa kwanza kuliona jitu refu si chini ya Futi nane likiingia ndani ya chumba hicho, huku likiwa limejengeka kwa misuli mikubwa, huku likiwa tumbo wazi na suruali ndefu, aaliyo ichimeka kwenye mabuti yake makubwa ya kijeshi.


“Hei jamani chekini kule”

Halima aliwaambia wezake ambao walikuwa wametazama pande nyingine ya chuma hicho, kila mmoja akajikuta akitawaliwa na woga mwingi kiasi kwamba wakaanza kurudi nyuma nyuma, huku wakilihofia jitu hilo linalo toa mihemu mizito kana kwamba limetoka kukimbia safari ndefu.

“Jamani tuweni pamoja”


Fetty alizungumza na kuwafanya wote wanne wajiweke sehemu moja huku wakiwa na wanalitazama kwa umakini jitu hilo lililo anza kupiga hatua za taratibu kuwafwata walipo.

Jitu hilo likarusha ngumi ambayo, ilimpata Anna na kumuangusha chini huku akitoa ukelele mkali, wa maumivu kwani ngumi hiyo ilimpata begani. Mr Rusev na watu wake waliopo nje ya chumba hicho wakashangilia kwa kitengo cha jitu hilo walilo lipachika jina la Great Lundark.

“Anna nyanyuka”

Halima alizungumza huku akimpa mikono yake miwili, Anna na kumnyanyua kutoka katika sehemu ambayo ameanguka.

“Jamani tuweni makini, tutawanyike”


Fetty alitoa agazo ambalo kila mmoja alilitekeleza na kumzunguka jitu hilo, kutokana na minyororo mirefu waliyo fungwa miguuni iliwasaidia kuweza kupiga ndefu kiasi, Fetty akajirusha juu na kwakurumia pingu yake, akaipitisha kwa haraka kwenye kichwa cha jitu hilo, na kuanza kuning’inia kwa kwa mgongoni, na kulifanya jitu hilo kuanza kutapatapa, huku likijaribu kuiweka mikono yake shingoni, ili pingu hiyo isiendelee kumuumiza kuromeo lake. Halima na Agnes wakawa na kazi la kupiga magoti ya jitu hilo na kulifanya lianza kuyumba.



Anna kwa hasira akalisogelea na kwakutumia mikono yake akalibamiza kwenye sehemu zake za siri na kulifanya litoe ukelele mkali. Anna akarudia tena kulibamiza kwenye sehemu za siri na kuzidi kulifanya jitu hilo kuyumba yumba. Fetty akazidi kutumia nguvu zake kuendelea kuivuta kwa nyuma shingo ya jitu hilo, huku miguu yake akiwa ameikunja na kukanyaga kwenye makalio ya jitu hilo, lililo anza kuishiwa nguvu.


Kwa usirikiano wao wakaweza uliangusha chini jitu hilo, hapo ndipo ikawa nafasi nzuri kwa Fetty kuimalizia kuivunja shingo ya jitu hilo na kuwashangaza bwana Rusev na watu wake waote ambao hawakutegemea kwamba jitu lao linaweza kufa.


Bwana Rusev akaagiza wapelekewe majitu mengine mawili yanayo fanana na jitu hilo walilo liua. Majitu mengine ambayo kwa jinsi yalivyo unaweza kuyapa jina la magoliati, hii ni kutokana na urefu wao na miili mikubwa waliyo nayo. Ikaingia ndani ya chumba huku ikiwa imeshika silaha mikononi mwao, huku wakionekana kuwa na hasira kali ya mwenzao kuuawa.


SHE IS MY WIFE(34)


Ikwa ni kazi kubwa sana ya Fetty na wezake kujiweka sawia kuhakikisha wanapambana na mijitu hiyo ambayo kusema kweli, ikikubahatisha kukutandika konde moja litakupa maumivu makali sana ambayo kuyavumilia kwake ni lazima machozi yakulenge lenge.


Fetty na Anna wakajiunga kupigana na jitu moja, huku Halima na Agnes wakaungana kupambana na jitu la pili. Haikuwa kazi rahisi kwako kuweza kupambana na majitu hayo yenye yenye silaha mikononi. Kwa bahati mbaya Fetty akatandikwa ngumi moja kifua iliyo muangusha chini na kujkikuta damu zikimtoka mdomoni.



Anna kuona hivyo akarusha teke kali lililo piga sehemu za siri za jitu hilo na kulifanya litoe mguno wa maumivu huku likijikunya na kumpa nafasi nzuri Anna kuweza kuufikia uso wake. Kwa kutumia vidole viwili vya mkono wa kulia, Anna akavisokomeza kwa nguvu kwenye jicho la kushoto la jitu, akavitoa kwa nguvu na kuchomoka na jicho lote jambo lililo wastua bwana Rusev na wanajeshi wake

“Arrhgaagaa”


Jitu hilo lilitoa mlio wa maumivu huku, likiitupa silaha yake chini, na kupiga goti moja chini, huku likiendelea kulia kwa maumivu makali

Anna akaokota panga kubwa la jitu hilo na kulishika kwa mikono miwili, hii ni kutokana na uzito wake, akamtazama jitu hilo linalo endelea kuvujwa na damu nyingi kwenye jicho lake alilo lichomoa dakika mbili zilizo katiza.


“Mother Fu….”

Jitu hilo lilimtusi Anna na kumpa hasira kali ya kulipitisha panga hilo kwenye shingo yake na kulitenganisha jitu hilo kichwa na kiwiliwili, jambo lililo zidi kumuogopesha bwana Rusev na watu wake na kujiuliza hawa wasichana ni watu wa aina gani.

Jitu linalo pambana na Agnes na Halima, likazidi kuwaadamisha mabinti hawa, kila mmoja amemshika shongoni mwake na mkunyanyua juu na kuendelea kuwababiza ukutani mwa chumba hichi kilicho tengenezwa kwa vioo vigumu sana.


Kila walipo jitahidi kujitoa mikononi mwa jitu hili walishindwa, na kila wanapo bamizwa ndivyo nguvu za mwili zinavyo waishia na kujikuta wakitokwa na damu za pua.

“Ha..lima na Ag..nes wana…kufa kule”

Fetty alizungumza kwa sauti ya kukata kata huku akinyanyua mkono wake wa kulia akimuonyesha Anna kwa kutumia kidole sehemu wanapo sulubiwa wezao hao wawili ambao wapo kwenye hatari ya kupoteza maisha.


Anna kwa haraka akaanza kutembea huku mkono wake mmoja ukiliburuza panga hilo refu kuelekea walipo wezake, kitendo cha Anna kulikaribia jitu hilo, akaushirikisha mkono wake wa pili kulikamata panga hilo, na kwakutumia nguvu zake zote akalipeleka kwenye mguu wa kushoto wa jitu hilo, akautenganisha na mwili wa jitu hilo na kumfanya awaachie Halima na Agnes, na wakaanguka chini. Kwa hasira kali Anna akaanza kulikata kata jitu hilo kwa panga hilo kali, akazidi kulilarua huku akipiga makelele ya uchungu, kiasi kwamba akazidi kulitesa jitu hilo, linalo endelea kupiga makelele ya kuomba msaada wa walipo nje


“Ahaaaaaagrahhh”

Anna alipiga ukelele huku akilishusha kwa nguvu zake zote panga kwenye shingo ya jitu hilo na kulitenganisha kabisa kichwa mwili wake. Anna akalitupa panga hilo chini na kujikongoja hadi walipo Halima na Agnes, ambao kila mmoja anahema juu juu, kiasi cha kuwa katika hali mbaya sana. Fetty taratibu akajinyanyua na kwenda walipo wezake na kukumbatiana kwa pamoja huku machozi yakiwamwagika kwa uchungu mwingi, kwani wanapitia katika kipindi kigumu cha maisha.


”Bosi tuwapige risasi wafe?”

Mlinzi wa bwana Rusev aliuliza kwa lugha ya kirusi, bwana Rusev hakutoa jibu lolote zaidi ya kuendelea kuwafikiria wasichana hawa jinsi walivyo majasiri katika kupambana.

“Mkuu tuwaue tu hawa”

Askari mwengine alizungumza kwa hasira huku akionekana akiikoki bunduki yake. Kwa haraka bwana Rusev akachomo bastola yake na kumtandika risasi ya kichwa askari huyo, aliye koki bunduki yake kwa ajili ya kutaka kwenda kuwaua Fetty na wezake. Askari wote wakashangaa, na kujikuta wakimtazama mwenzao huyo aliye lala chini huku damu zikumvuja kichwani


“Kuna mwengine anaye taka kwenda kuwaua hao mabinti”

Bwana Rusev alizungumza kwa sauti ya ukali kwa lugha ya kurusi na kuwafanya askari wake wote kukaa kimya, huku wakimtazama bosi wao huyo aliye badilika na kuvimba. Bwana Rusev akapiga hatua hadi kwenye kitasa cha mlango wa kuingilia ndani ya chumba hicho. Akakishika kwa nguvu na kuufungua mlango huo na kuingia ndani huku bastola yake ikiwa mkononi, akawafanya Fetty na wezake kustuka, na kujikuta wakimtazama bwana Rusev, wakisubiri kupata hukumu yao kwa kuwaua majitu hayo


***

Siku ya harusi ya Raisi Praygod na Rahab, ikawadia huku ikiwa imeudhuriwa na wasio zidi ishirini. Rahab katika siku alizo weza kujikubali kuwa yeye ni mzuri, ni hii siku aliyo weza kuvishwa shele lenye dhamani kubwa sana ya pesa. Aliweza kupambwa na mwanamitindo waliye mpa kazi hiyo kutokea nchini Italia. Huku Raisi Praygod, akiwa ndani ya suti nzuri iliyo tengenezwa na kiwanda maarufu nchini Italia, na suti hiyo ina sifa za kipekee, ambayo mara nyingi huwa anaivaa raisi wa Marekani.


Kwana suti hiyo ina mionzi ambayo inaweza kuzuia risasi, ya aina yoyote kuweza kumfikia mvaaji wa suti hiyo, pili ni suti ambayo inaweza kuhimili mazingira yote ya hali ya hewa, kukiwa na joto sana inaweza kukuba ubaridi kwenye mwili, kukiwa na baridi sana kunaweza kukupa ujoto kwenye mwili wako.



Hawakuamua kwenda kufunga sherehe hiyo kanisani bali walicho kifanya ni kumchukua mchungaji ambaye akawafungisha harusi hapo hapo nyumbani, baada ya tukio hilo muhimu la kufungishwa ndoa, wakafanya sherehe iliyo furahiwa na kila mmoja, ni mpiga picha mmoja tu aliye kodishwa kwa kuifanya kazi hiyo, huku watu wengine wakikataza kupiga picha hizo kutokana Raisi Praygod hakuihitaji kuweka wazi uwepo wake kama yupo hai. Furaha kubwa ikaendelea kutawala kwenye moyo wa Rahab ambaye hadi sasa hivi anajiona mwanamke wa kipekee sana kwenye maisha yake kwa kumpata raisi Praygod


Frednando akajitole kumzawadia rafiki yake huyo ndege aina ya Jet, aliyo inunua siku chache kabla ya harusi kimya kimya, pasipo mtu yoyote kulifahamu hilo. Ndege hiyo yakifahari ambazo zinamilikiwa na matajiti wachache duniani, hua zinaingia abiria wasio zidi watano, huku kiwa inaendesha wa marubani wawili, na nindege ambazo zinakwenda kwa kasi sana, na huwa imekamilika kwenye idara kuanzia idara ya kujulinda kwa kuweza kufungwa mitambo ambayo inazuia risasi na mabomu pale inapo kuwa imevamiwa angani.


“Rafiki yangu, hii ndio zawadi yangu kwako na shemeji yangu”

Bwana Frednando alizungumza wakiwa wamesimama kwenye kiwanja cha ndege kilichopo kwenye kwenye eneo la jumba lake hili lakifahari. Wote watatu wakaingia ndnai ya ndege hiyo huku wakiwa na furaha. Frednando akawatambulisha raisi Praygod na Rahab kwa marubani wao ambao, wameajiriwa kwa kazi ya kuiendesha ndege hiyo popote pale ambapo Praygod na mke wake watahitaji kwenda.


“Tuzungusheni kidogo angani, ili wafaidi utamu wa ndege yao”

Bwana Frednando alizungumza kwa lugha ya kimexco, marubani hao wakaifanya kazi yao iliyo wafanya wawe hapo. Taratibu mashine za ndege zikaanza kunguruma zikiashiria kwamba zinajiweka sawa kwa safari. Taratibu ikaanza kutembea kwenye kiwanja hichi ambacho nikikubwa kiasi. Jinsi ilivyo zidi kuongeza mwendo kasi ndivyo ilivyo anza kuiacha ardhi, huku kila mtu akiwa amekaa kwenye kochi lake, lililo lililo tengenezwa vizuri, huku pembeni kukiwa na kijimeza cha kuwekea juisi


“Unajua hii ndege, nimeinunua Dola milioni thelathini na tano”

“Duuu mbona pesa nyingi, hiyo inalisha nchi yangu”

“Ahaa kawaida ndugu yangu kwa maana, kuna yakwangu kama hii nayo niliinunua kwa bei kama hiyo seme zimetofautiana rangi, yangu ni nyeusi, nakumbuka kuna siku uliniambia kwamba unapenda sana rangi ya silva, nikaamua kukukamilishia moja ya ndoto zako”


“Asante sana Fred”

Wakiwa juu angani, wakaendelea kupata vinywaji mbalimbali, huku wakitazama baadhi ya chanel, za tv ndogo iliyopo kwenye kila meza ya safa lililopo ndani ya ndege hiyo ya kifahari. Gafla Rahab akaanza kujihisi vaibaya vibaya, huku mara kadhaa, akawa anajikaza ili Praygod asijue ni kitu gani kinacho endelea, ila gafla akajikuta akianza kutapika na kulichafua gauni lake alilo livaa



ITAENDELEA





ILIPOISHIA

“Asante sana Fred”

Wakiwa juu angani, wakaendelea kupata vinywaji mbalimbali, huku wakitazama baadhi ya chanel, za tv ndogo iliyopo kwenye kila meza ya safa lililopo ndani ya ndege hiyo ya kifahari. Gafla Rahab akaanza

kujihisi vaibaya vibaya, huku mara kadhaa, akawa anajikaza ili Praygod asijue ni kitu gani kinacho endelea, ila gafla akajikuta akianza kutapika na kulichafua gauni lake alilo livaa



ENDELEA

Furaha ikabadilika na kuwa mshike mshike ndani ya ndege kwani kadri muda ulivyo zidi kwenda hali ya Rahab ikaanza kubadilika na kujikuta mwili mzima ukianza kumtetemeka, na kutoa mapuvu mdomoni mwake. Frednando akawaamuru marubani wairudishe ndege haraka kwenye kiwanja cha nyumba kwake ili kumuwahisha Rahab, aweze kuonana na madktari.



Macho ya Rahab yakabadilika na mboni zake nyeusi zikapotea na kubaki weupe kwenye macho yake jambo lililozidi kumchanganya raisi Praygod pamoja na Frednando ambaye hakujua ni ugonjwa gani ambao bibi harusi ameweza kuupata.

Haikuchukua muda mwingi, matairi ya ndege yakawa yanaserereka kwenye ardhi ya uwanja wa nyumbani kwa Frednando, ambapo Alisha waeleza madaktari wake wawe tayari kwa kumpokea mgonjwa.


Kwa kushirikia na Frednando, wakambeba Rahab na kumtoa nje ya ndege na kumuingiza kwenye gari maalumu la wagonjwa lililokuwa likiwasubiri. Moja kwa moja Rahab akakimbizwa kwenye jingo linalo tumiwa na Fredando kama hospitali inayo mtibu yeye na familia yake pale wanapo patwa, na hali yoyote ya kuumwa. Uzuri wa eneo lilipo jumba la Frednando, aliweza kuwekeza pesa nyingi kujijengea vitu muhimu kwa mahitaji yake, ikiwemo jengo la hospitali, lenye madaktari bingwa ambao Fredinando anawaamini sana


“Kaka hivi mke wangu atapona kweli?”

Raisi Praygod alizungumza huku machozi yakimlenga lenga, akamshuhudia mke wake akipakizwa kwenye kitanda cha matairi baada ya kushushwa ndani ya gari, na moja kwa moja akaingizwa kwenye chumba kilicho jaa vifaa muhimu kwa kumuhudumia mgonjwa mahututi


“Atapona tu, usijali rafiki yangu”

Fredinando alimfariji raisi Praygod, lakini yeye mwenye amechanganyikiwa kwani hakuamini kama siku kama hiyo kutajitokeza jambo kama hilo la kuhuzunisha. Wakiwa wamesimama kwenye nje ya mlango wenye kioo kikubwa, wakawashuhudia madaktari wakitumia mashine za kustulia mapigo ya moyo wakiziweka kwenye kifua cha rahabu ambaye amezima kabisa mapigo yake ya moyo.

Machozi taratibu yakaanza kumtoka raisi Praygod, hakuamini uzuri wote wa Rahab, unaweza kupotea muda wowote kuanzia sasa.


“Kaka jikaze”

Frednando alizungumza huku, naye machozi yakiwa yanamtiririka, uchungu anao upata rafiki yake, nao unaugusa moyo wake, kwani ni dakika chacha tu wametoka kucheka na kufurahi na shemeji yake ambaye muda mwingi anapenda kumtania kwa jina la ‘AFRICAN QUEEN’. Mashine zakupulia zinazo soma mapigo ya moyo jinsi yanavyo kwenda yakazidi kuwachanganya madaktari hawa wane, kwani ni mstari mmoja ulio nyooka ndio unakatiza kwenye mashine hiyo, huku kukisomeka sifuri mbili za rangi nyekundu zikiashiria kwamba Rahab mapigi ya moyo hayafanyi kazi, moja inawezekana amesha fariki au moyo wake upepata mstuko mkubwa

***

Si Fetty wala mwenzake yoyote aliye weza kujinyanyua kutoka kwenye sakafu walipo kaa, kila mmoja macho yake yaliyo jaa machozi, wakawa wanaitazama sura ya kipande cha mwanaume, aliye fura kwa hasira na si mwingine bali ni bwana Rusev, aliye simama huku bastola yake ikiwa mkononi mwake. Kila mmoja akatamani kujitetea, ila nguvu hakuwa nazo za kutosha kusema anaweza kupambana na bwana Rusev, anaye onekana kuchukia baada ya mapiganaji yake matatu kuuliwa kinyama

“Hatuna tulicho kibakisha tena duniani, tumekuwa ni watu waovu. Hatuna pa kwenda zaidi ya kaburini. Tuue sisi yupo tayari”

Anna alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, huku mikono yake yenye kufungwa pingu akiendelea kumshika Halima, aliye kwenye hali ngumu sana.

“Ehee Mungu zipokee roho zetu, na utusamee makosa yetu tuliyo yafanya. Amen”


Anna alizungumza kwa sauti ya unyonge iliyo wafanya wezake kuendelea kulia kwa uchungu, kwani hakuna aliye tarajia kwamba maisha yake yatakuwa hivyo. Maneno ya Anna, yakamfanya bwana Rusev, kumwagikwa na chozi lililo washangaza askari wake waliopo nje wakiwatazama.

Bwana Rusev akawamrisha askari wake kuingia ndani na kuwechukua Fetty na wezake, ambapo akawaamrisha wavalinye vipande vya vigunia vyuesi kwenye vichwa vyao wasijue ni wapi wanapelekwa.


Wakatolewa ndani ya chumba hicho huku wakiwa wamebebwa, kwenye mabega ya askari walio jazia miili yao kwa mazoezi magumu wanayo yafanya kila kukicha. Moja kwa moja wakawatoa nje ya jumba hilo na kuwaingiza kwenye helcoptar ambapo bwana Rusev naye akaingia ndani ya helcoptar hiyo. Mtiani mkubwa kwa Fetty na wezake ni kujua ni wapi wanapo kwenda, kutokana hawakuwa na jinsi yakufanya huku mikono yao ikiwa imefungwa pingu na miguu yao ikiwa imefungwa minyororo mirefe.


Mwendo wa lisaa zima wakawa wapo angani, ambapo moja kwa moja wakafika katikati ya kina cha bahari, ambapo helcoptar hiyo taratibu ikaanza kushuka chini. Kutokana haoni chochote ikawa ni ngumu kujua ni kitu gani kinacho fwata mbeleni. Jinsi helecoptar hiyo, ilivyo zidi kushuka chini ndivyo sehemu hiyo kubwa ya maji ilivyo anza kujigawa. Maji ya sehemu kubwa yakatawanyika na mfuniko mkubwa wa chuma ukafunguka na kuiruhusu helcoptar hiyo kuingia ndani, ambapo ndipo kuna kambi kubwa ya silaha ya bwana Rusev, ambayo si rahisi kwa mtu kuweza kugundua swala hilo.



Kutona na utaalamu mkubwa waliweza kujenga ngome kubwa chini ya bahari ambapo, ipo ndani ya miamba. Ambapo wameweza kutengeneza hewa ya oksijeni, wanayo weza kuitumi ndani ya miamba hiyo mikubwa huku taa kubwa za umeme zikiwa zinawaka masaa 24.



Wanajeshi wote wanao ishi kwenye ngome hiyo ni makomandoo na niwatu wenye vipaji maalimu, ambao bwana Rusev aliweza kuwachukua sehemu mbalimbali dunia, na kuwaweka pamoja na kuanza kutengeneza silaha ambazo ni adimu sana duniani. Huku siku hadi siku wakitengeneza mabomu ya nyuklia, ambayo ni hatari pale yanapo tumiwa kwenye kushambulia sehemu yoyote kwenye kiumbe, hai nilazima kitaatjirika vibaya.


Fetty na wezake wakapokelewa na wanajeshi, wakapelekwa kwenye wodi, kabla hawajatolewa vipande vya magunia kwenye vichwa vyao, wakachomwa sindano za usingizi, ambazo zikawafanya wapoteze fahamu na kulala fofofo. Wakaanza kuhudimiwa kwenye majeraha yao yote pasipo wao kujigundua.

“Mkuu hawa ni kina nani?”

Daktari mmoja aliuliza kwa lugha ya kirusi.

“Hawa mabinti wananifaa sana kwenye kazi yangu, hakikisheni afya zoa zinatengemaa na kuwa katika hali nzuri sawa”

“Sawa mkuu”

Bwana Rusev akatoka kwenye wodi walipo lazwa Fetty na wezake kisha na kwenda kufwatilia utendaji wa kazi wa vijana wake ndani ya ngome yake hiyo.

***

Taratibu vimistari vya mashine, iliyopo pembei mwa kitanda alicho lazwa Rahab, ikaanza kuonekana vikiwa vimepinda pinda, ikiashiria kwamba ameanza kupumua hii ni baada ya madaktari kuendelea kuustua moyo wake kwa kutumia mashine maalumu za kuweza kustulia mapigo ya moyo. Ikawapa nafasi madakari kuweza kufanya uchunguzi wa kina juu ya tatizo lililo mkumbwa Rahab.


Raisi Praygod akazidi kumuomba Mungu, huku macho yake akiwa ameyatoa kwenye mashine iliyo endelea kuonyesha vimistari vidogo vya kijani ikiashiria kwamba mke wake ameanza kupumua. Baada ya kusimama kwa muda mrefu, Fredando akamchukua raisi Praygod hadi kwenye moja chumba cha mapumziko, ambacho mara nyingi hukitumia pale anapokuwa anazungumza na madaktari wake.

Matokeo ya majibu ya vipimo, ikawa ni jambo la kustaajabisha kwa madaktari ambao wakaanza kujiuliza ni nani ambaye amehusika na ugonjwa wa rahabu


“Wewe umezoeana na baso, peleka majibu”

Mmoja wa madaktari alipendekeza daktari Canter, mwanamama mpole na mchishi kuweza kupelea majibu hayo

“Hivi jamani, ni kweli haya majibu yapo sahihi”

“Jamani si sote hapa tumepima na majibu kuwa hivyo, na tukarudia kwa kipomo kingine majibi yamekuja hay ohayo”

“Wewe peleka sisi huku tuendeleaa kumugudumia mgonjwa”

Bi canter akatoka kwenye chumba alipo lazwa Rahab, moja kwa moja akaelekea kwenye chumba mara nyingu hukitumia kuzungumza na bosi wao. Baada ya kuingia ndani ya chumba hicho raisi Praygod, akanyanyuka kwenye kiti alicho kaa, na kumpokea daktati huyo kwa macho makali yaliyo jaa wasiwasi. Frednando akamuomba daktari kukaa kwenye kiti cha pembeni


“Mke wangu anatatizo gani dokta?”

“Kaa chini kaka”

Frednando alizungumza huku akimshika mkono raisi Praygod na kumkalisha kwenye kiti alichokua amekikalia

“Tumeweza kumfanyia mgonjwa uchunguzi wa kina, na tumeweza kugundua kwamba……”

Baada ya kfika sehemu ya tatizo linalo msumbu Rahab, dokta Canter akanyamaza na kuwatazama matajiri wake hao, ambao wote wamemtumbulia mimacho

“Mke wako muheshimiwa, tumemkuta na….. na sumu nyingi”

“SUMUU…..!!!”

Raisi Praygod alizungumza huku akiwa anashangaa swala hilo

“Ndio sumu ambayo inaoenekana iliwekwa kwenye kinywaji alicho kunywa dakika chache kabla ya kuanza kufanya kazi mwilini mwake”


SHE IS MY WIFE(36)


Raisi Praygod akamgeukia rafiki yake kipenzi Frednando, na kumtazama kwa macho makali ambayo alianza kumtilia mashaka rafiki yake huyo, ila Frednando naye alionekana kuwa hatambui lolote lililo jitokeza katika hili swala kwani muda mwingi walikuwa pamoja.

“Ila tunaendelea kuitoa sumu iliyo ingia mwilini mwake”

“Sawa”

Frednando alimjibu dokta Canter na kumfanya dokta huyo kuomba kunyanyuka na kuondoka ndani ya chumba hicho huku akiwaacha Raisi Praygod na Frednando wakiwa na maswali mengi juu ya nani ni aliye weka sumu kwenye kinywaji cha Rahab.


**(MASAA MACHACHE KABLA)**

Kila alipo yatupa macho yake usoni mwa raisi Ptagod Makuya na mke wake Rahab, roho ikazidi kumuuma Mercy, binti mrembo, ila ni mfanyakazi hodari wa kupika katika jumba hili la tajiri Frednando, tangu siku ya kwanza kumuona Praygod kuingia katika jumba hili moyo wake ulipata shinikizo kubwa la maumivu yaliyo changanyikana na upendo mkubwa. Japo asili yake ni mmexco halisi, ila alijikuta akimpenda mwanaume mwenye ngozi nyeusi kama Praygod.


Halikuwa ni jambo rahisi kuweza kulitamka swala la kumpenda Praygod kwa mtu yoyote ndani ya jumba hili kwani alihisi kwamba itakuw ni hatari kubwa sana kwake, kwani akilini mwake alisha anza kufikiria jambo ambalo lingemfanya akiuke maadili ya kazi yake pamoja na sheria za nchi yake. Ila hakuwa na jinsi zaidi ya kupanga mipango mizito kichwani mwake ya kumuondoa duniani Rahab, ili we rahisi kwake kujiweka karibu na Raisi Praygod, anaye onekana kudatishwa na penzi la Rahab.


Macho ya Mercy, yaliendelea kuwashuhudia Rahab na Praygod jinsi wanavyo endelea kufurahi wakiwa katika mavazi yakuependeza, ikiashiria kwamba kwa sasa ni mke na mume.


Japo ni wafanyakazi wengi wakiume waliendelea kumtamani Mercy ila hapakuwa na aliye ambulia hata kupewa matumaini ya kuoenyeshwa kwamba amependwa na binti huyo. Kila mmoja alijikuuta akijibiwa mbona na binti huyo mrefu, mwenye nywele ndefu zinazo fika mgongoni, huku akiwa na umbo fulani jembamba la kimisi, ila lenye mvuto kwani liliweza kuchukua vazi lolote litakalo mpendeza.


Macho ya Mercy hayakucheza mbali na Rahab, aliye shika kinywaji chake mkononi, huku pembeni yake kukiwa na mumewe aliye endelea kuachia tabasamu pana lililo mfanya azidi kuwa mzuri na kumchanganya Mercy.

“Oooh Mungu wangu nisaidie mimi”


Mercy alizungumza huku mkoni mwake akiwa ameshika kitambaa alicho saga, kidonge komoja cha sumu, kali sana inayo tumika katika kunyunyizia katika mimea ya matunda aina ya apple, ambalo ni zao kubwa sana linalo patikana katika nchi ya Mexco. Mercy akaanza kutafuta uwezekana na kuweza kumuwekea unga huo Rahab kwenye kinywaji alicho kishika kwenye mkono wake. Wakati wa kuwasalimia maharushi na kuwapa mikono ikawa ndio nafasi ya pekee kwa Mercy kuweza kutimiza adhima yake kwa Rahab.



Wakatu wakaanza kupita walio maharusi, huku wengine wakiwakumbatia maharusi kwa ishara ya kuwapongeza. Mercy akaanza kumkumbatia raisi Praygod huku kwenye vidole vyake akiwa ameshika chenhachenga kidogo za unga wa sumu, alipo mfikia Rahab, akamkumbatia na kupata nafasi ya kunyunyiza unga wa sumu kwenye kinywaji cha Rahab pasipo mtu yoyote kuweza kushuhudia tukio hilo, akampiga mabusu kadhaa Rahab ya mashavuni, huku moyoni mwake akiwa akiwa na furaha kwani Rahab kwa muda wowote anaweza kuja na kuwa marehemu mtarajiwa.


Kitu kilicho anza kumshangaza Mercy ni jinsi Rahab alivyo anza kupata ugumu wa kunywa kinywaji hicho, kwa mara kadhaa Rahab alikipeleka kinywaji hicho hadi mdomoni mwake ila akakirudisha na kujikuta akizungumza au akitabasamu na memewe aliye onekena kujawa na furaha sana.


“Foolish”(Pumbavu)

Mercy alizungumza baada ya kusikia kwamba bosi wao amewakabidhi ndege ya kifahari Raisi Praygod pamoja na Rahab. Akawashuhudia Rahab, Praygod na Frednando wakielekea kwenye ndege na kuingia. Mercy akaondoka kwa hasira eneo la sherehe na kuelekea chumbani kwake, akajifungia na kujirusha kitandani mwake na kuanza kupiga piga mto wake kwa ngumi, kwani ni maumivu mazito ya mapenzi yaliuchoma mayo wake hadi jasho jembamba likaanza kumwagika.


Ndani ya nusu saa akaanza kusikia ving’ora vya gari la wagonjwa, kwa haraka akakimbilia dirishani na kufungua kutazama nje, kutokana na chumba chake kuwa gorofa ya nne kwenda juu, aliweza kushuhudia jinsi madaktari wao wakifanya juhudi za kumpa huduma ya kwanza Rahab, mara baada ya kumshusha kwenye ndege.


“I win”(Nimeshinda)

Alizungumza huku tabasamu akiendelea kuliachia, sasa akilini mwake akatambua kwamba kinacho fwata hapa ni yeye kuanza kujiweka karibu na Praygod kwani amefanikiwa kumuondoa adui yake namba moja, japo Rahab hakuwahi kumfanyia jambo lolote ambalo alipaswa kumlipizia kisasi kwa kumsababishia kifo.

***

Frednando akamuaga Rais Praygod, akatoka nje ya jengo la hospitali huku moyoni mwake akiwa amefadhahika sana kwa kile kilicho tokea kwa mke wa rafiki yake kipenzi Praygod.



Akaingia kwenye gari lake na kumuamrisha dereva aendeshe kwa kasi gari hilo hadi nyumbani kwake, huku akipiga simu kwa msimamizi mkuu wa jumba lake aweze kuandaa kikao kikubwa na wafanyakazi wote walio hudhuria kwenye sherehe ya harusi muda mchache ulio pita.



Ndani ya dakika kumi akawa amefika kwenye jumba analo ishi, kuingia sebleni akawakuta wafanyakazi wake wote wakiwa kwenye mkao wa kumsubiria bosi wao huyo, ambaye huwa mara nyingi hapendi ujinga na swala la kumuondoa mtu duniani kwa kumtandika risasi ni dogo sana kwake, endapo mtu huyo ataonekana kuenenda kinyume na taratibu zake alizo ziweka kwa wafanyakazi wake hao.


Frednando akapita katikati yao huku akioenekana kukasirika hadi rangi ya ngozi yake kubadilika na kutawaliwa na uwekundu fulani. Akawatazama wafanyakazi wake karibia wote kutokana na wingi wao, hakuweza kuzitazama sura zote.


“Esto es ridiculo”(Huu ni ujinga)

Frednando alizungumza kwa lugha ya kispain, huku akiwfoka kwa sauti ya juu, na kuzidi kuwaogopesha wafanya kazi wake hao, ambao wengi humuogopa sana bosi wao.

“Quien habla puesto veneno en ;a bebida de Rahab”(Ni nani aliye weka sumu kwenye kinywaji cha Rahab?)


Ukali was suati ya Frednando, ikapenya masikioni mwa Mercy aliyekuwa akishuka ngazi kuja chini sebleni kusikiliza kikao walicho itiwa na bosi wao huyo. Ikambidi asimame kuchungulia chini na kuona wezake wakiwa wamesimama kwenye kundi kubwa hku kila mmoja akionekana kuwa makini na kumsikiliza bosi wao


“Jefe habria sido mejoe si vemos los videos gue se graban en toda la boda sel acontencimento”(Bosi itakuwa ni vizuri tukitazama viseo zilizo rekodiwakwenye tukio zima la arusi)

Mshauri wa Frednando alitoa wazo ambalo kila mmoja alionekana akingong’ona akiamini hiyo itakuwa ni njia mafaka kwa wao kuweza kumjua ni nani muhusika. Wazo hilo likamfanya Mercy kuanza kutetemeka mwili mzima na kushindwa kushuka chini zaidi ya kujibanza kwewye sehemu alipo simama na kuendelea kutazama ni nini kitakacho fwata.



Mafundi mitambo walio husika na swala zima la kurekodi matukio yaliyo tokea kwenye harusi, wakaunganisha picha za matukio yote kwenye mkanda mmoja kisha na kuuweka kwenye kifaa maalumu cha kuwezesha mkanda huo kuonyesha katika tambaa kubwa lililopo sebleni, taa zote zikazima na kubakiwa na mwanga wa mkali wa kifaa kilicho kuwa kinamulika kwenye tambaa hilo na kuonyesha matukio yoyote.


Mercy naye hakuwa mbali katika kutupia macho yake kwenye video hiyo inayo onekana na wezake wote pamoja kwenye seble hiyo kubwa. Ikafika wakati wakiwapa mikono maharusi kwa ishara ya kuwapongeza. Mercy akajiona akipita kwa Raisi Praygod kisha akafika kwa Rahab na kumkumbatia huku akipimpiga mabusu.


“Detener inmediatemente”(Simamisha hapo hapo)

Frednando alizungumza kwa sauti ya juu na kumfanya muongozaji wa video hiyo kusimamisha sehemu inayo muoenyesha Mercy akimkumbatia Rahab kwa furaha. Mercy akajikuta akiitumbualia macho sehemu hiyo iliyo simamishwa huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana. 




ILIPOISHIA

“Detener inmediatemente”(Simamisha hapo hapo)

Frednando alizungumza kwa sauti ya juu na kumfanya muongozaji wa video hiyo kusimamisha sehemu inayo muoenyesha Mercy akimkumbatia Rahab kwa furaha. Mercy akajikuta akiitumbualia macho sehemu hiyo iliyo simamishwa huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana.



ENDELEA

Kila mmoja aliweza kulishuhudia tendo la Mercy kumimini kiasi cha unga unga mweupe kwenye kinywaji alicho kishika Rahab, pasipo watu wengine kuweza kumuona wakati wa sherehe hiyo kuweza kufanyika. Walio na roho nyepesi wakajikuta wakimaka kwa sauti ya juu, Mercy baada ya kuona kwamba ameweza kugundulika kwa haraka, akapandisha juu gorofani na kuingia chumbani kwake kwani anagundua kinacho kwenda kutokea ndani ya masaa machache mbeleni hakitakuwa ni kizuri kwani anautambua vizuri ukatili wa bosi wake.


Mercy akafungua kabati lake na kutoa begi dogo la mgongoni na kuanza kuingiza kiasi cha pesa alicho kuwa amekihifadho ndani ya kabati hilo kisha kwa haraka akafungua dirisha na kusimama, kabla hajafanuya chochote mlango wake ukapigwa na teke wakaingia walinzi wawili wa Frednando wakiwa na bunduki mikononi mwao


***

Hali ya Fetty na wezake, zikazzidi kushuhulikiwa na madaktari bingwa waliomo ndnai ya ngome ya bwana Rusev, komandoo wa nchi ya Rusev aliye weza kuisaliti nchi yake na kuunda kikosi chake alicho kipa jina la R.U.P.P(Rusev United Power of People). Kikundi hichi aliweza kukianzisha kwa siri kubwa tangu akiwa ndani ya jeshi pasipo watu wengine kuweza kukifahamu kwa haraka.



Akaweza kutengeneza kambi yake chini ya bahari kaskazini mwa nchi yake ya Urusi, haya yote aliweza kutafanya kwa siri kubwa akishirikia na baadhi ya viongozi wa juu serikalini walio kuwa na uchu mkubwa wa madaraka. Mbaya zaidi ni kwamba viongozi hao walitaka kumgeuka, ila kwa kutumia umahiri wake aliweza kuwaangamiza kwa mkono wake mwenyewe kuhakikisha kwamba siri yake haiwezi kuvuja kwa mtu wa ina yoyote kwamba yeye anamiliki jeshi kubwa la vijana kinyume na sheria za nchi yake..


R.U.P.P, ikazidi kukua miaka kwa miaka na kuzidi kupata wataalamu wakubwa wa mitambo na kuanza kutengeneza silaha za nyuklia kisiri sana.

Ndani ya miaka ishirini ya usiri, siku moja bwana Rusev aliweza kuja kujikuta siri yake ya kuwa ni muasi ndani ya nchi yake ikagundulika, hii ni baada ya siku hiyo kunywa kiasi kikubwa sana cha pombe na kujikuta akilala ma malaya mmoja aliye weza kumpa penzi tamu, hadi akajikuta akianza kumuambia mambo yake ya ndani huku akimuahidi kumpa nafasi ya kuweza kufanya naye kazi.


Binti huyo pasipo kuwa mvumilivu akajikuta akijinadi kwa rafiki zake, juu ya kupata nafasi ya kuajiriwa na bwana Rusev katika kikosi chake cha siri cha R.U.P.P, hii ni mara baada ya binti huyo kutoka kulala na bwana Rusev ambaye kwa kipindi hicho bado alikuwa ndani ya jeshi la nchi ya Rusia.


Bwana rusev hakuwa na jinsi zaidi ya kuamua kuiasi nchi yake mara baada ya serikali kuanza kumfwatilia na kumuwekea vikwazo vingia hadi kutaka kumuhukumu adhabu ya kunyongwa hadi kufa, ila haikuwa ni rahisi kwa serikali, kwnai watu wa bwana Rusev waliweza kumtorosha kiongozi wao huyo walio muabudu kama Mungu wao, na kuweza kumuweka katika mazingira salama ambayo ni ngumu sana kwa mtu yoyote kuweza kumfikia na kumdhuru.

“Jamani tupo wapi?”


Anna alikuwa wa kwanza kuzungumza mara baada ya kuzinduka kutoka usingizini. Akashangaa eneo zima la chumba kikubwa walicho lazwa na kilicho tawaliwa na rangi nyeupe kwenye kuta zake kuanzia chini, pembeni hadi juu. Akawatazama wezake na kuwakuta bado wakiwa wamejilaza kitandani, huku wakiwa na madripu ya maji. Anna akajitazama na yeye na kujikuta akiwa na dripu kwenye mkono wake wa kushoto, nguo walizo kuwa wamezivaa mara ya mwisho hawakujikuta nazo, alijishuhudia akiwa amevishwa mavazi meupe yanayo fanana na wezake.

Baada ya muda kila mmoja akazinduka na wote wanne wakajikuta wakipiwa katika hali ya kuto fahamu ni kitu gani ambacho kinaendelea katika eneo walilo kumbuka.


“Jamani hapa tulipo tunaonekana kila kona”

Fetty alizungumza baada ya kuzitazama kamera za ulinzi zilizo kuwa katika kona nne za chumba walichomo.

“Sasa kamani tutafanyaje, kwa mana hapa mimi sielewi?”

Halima aliuliza akiendelea kuyapepesa macho yake

“Kikubwa tuweni wapole, kwa maana kama hawa watu wangekuwa ni wabaya kwetu wanegesha tuu, ila wemeweza kutuhudumia hadi hapa”

Fetty aliwasisitiza wezake, kabla Agnes hajazungumza, bwana Rusev akaingia huku akiwa ameongozana na walinzi wake wawili pamoja na daktari mmoja, mwenye umri mkubwa kiasi.


“Munaendeleaje mabinti”

Bwana Rusev alizungumza kiswahili fasaha kilicho wafanya wote wanne kushangaa na kumtumbilia macho kwani siku zote walikuwa wanajua kwamba mzee huyo atambui kishwahili

“Munanishangaa mimi kuzungumza kishwahili? Ok tuachane na hayo, kama munavyo weza kujionea mupo katika mikono salama sana, na kwaupande mwingine pia si salama”

Fetty na wezake wakatazama kwa macho yakujiiuliza ni kwanini Bwana Rusev anasema sehemu hiyo ni salama ama si Salama, hapakuwa na aliye kuwa na jibu la kuzungumza kwa mwenzake zaidi ya kukaa kimya kusubiri ni kitu gani ambacho bwana Rusev atazungumza.


“Natambua kwamba nyinyi ni miongoni mwa mabinti mahiri mulio weza kufanya matukio kadhaa kwenye nchi ya Tanzania, na pia hadi sasa hivi bado munaendelea kutafutwa si ndio?”

Anna akajibu kwa kutingisha kichwa akikubali kwamba ni kweli bado wanatafutwa

“Sawa sasa ni hivi, nawapa uchaguzi wa haya nitakayo kwenda kuyazungumza. Kwanza mukikubali kuwa na mimi nitawapa nafasi kubwa ya kuyatambua mambo mengi ambayo hamjawahi kuyajua. Pili mukikataa kuwa na mimi miili yenu itakuwa ni chakula cha papa walio zunguka eneo hili.”


“Wakati ni wenu kukubali au kukataa”

Bwana Rusev alizungumza na kutoka nje ya chumba hicho. Ukimya ukatawala ndani ya chumba huku kila mmoja akiwa na maswali mengi kichwani mwake.

“Jamani mimi nipo tayari”

Halima alizungumza huku akinyanyuka kwenye kitanda alicho kaa na kusimama wima, wezake wote watatu wakamkodolea mimacho wakimshanga


“Musinishangae bwana, hivi munahisi kuna mtu anaye weza kutoka hapa, ni bora kuwa wapole na hii siku nyingine tujifunze kukurupuka kama angekuwa si yule mwehu Samson, leo tusinge kuwa hapa”

Halima alizungumza kwa kujiamini, huku jazba ikianza kumpanda taratibu, Anna naye taratibu akasimama wima na kupiga hatua hadi sehemu alipo simama Halima

“Hata mimi nimekubali”

Fetty na Agnes wakatazamana kwa macho ya kunto fahamu, nafsini mwao kila mmoja alijihisi kuwaona Halima na Anna kuwa ni wadhaifu na kujirahisisha na kuwa watumwa wa bwana Rusev.


“Kwa nini munafanya hivyo”

Fetty aliuliza kwa sauti ya chini, iliyo jaa majonzi kiasi

“Tumeamua kuwa wapole kama ulivyo tusisitiza, hatuna njia nyingine zaidi ya hii”

Halima alijibu huku akimkazia macho Fetty ambaye kwa muda wote amekuwa kama kiongozi wao, ila kwa sasa hawakuhitaji kusikiliza amri ya mtu yoyote zaidi ya kuamua kufwata akili zao. Agnes akanyanyuka taratibu na kusogea walipo simama Halima na Anna. Fetty akabaki peke yake kitandani huku akiwashangaa wezake. Kwa upole Agnes akanyoosha mkono wake wa kulia na kumuomba Fetty kuwa pamoja na nao.


Fetty akainamisha kichwa cheke chini, huku akijifikiria kwa mara kadhaa, akaunyanyua uso wake ulio jaa machozi yaliyo tapakaa usoni mwake, kwa kasi akanyanyuka na kukumbatiana na wezake huku akiendelea kumwagikwa na macho mengi.

“Sisi ni timu moja, hata kama tupo chini ya mtu tusiachene”

Agnes alizungumza huku mkono wake mmoja ukimpiga piga Fetty mgongoni.


***

Mercy akatazamana kwa muda na askari walio ingia chumbani kwake wakihitaji kuweza kumkamata na kumpelekea mbele ya bosi wake ambaye kwa muda huu amefura kwa hasira kali. Miguu na mwili mzima vikaanza kumtingishika kwa muda, askari mmoja akapiga hatua za haraka kwenda dirishani alipo simama, kabla hata hajamfikia, Mercy akaamua kujirusha kutoka juu gorofani na kwabahati mbaya, akageuka hewani, na kichwa chake kikatangulia chini na kutua kwenye sakafu ngumu iliyopo nje, na hapo hapo Mercy akapoteza maisha.


Ripoti ya Mercy kujiachia gorofani ikamfikia Frednando, kwa haraka akatoka nje akiwa na walinzi wake pamoja na wafanyakazi wengine waliio kuwa wakimsubiria Mercy kuletwa sebleni, kwani yeye ndio muhusika aliye weka madawa ya kulevya kwenye kinywaji cha Rahab.

Hakuna aliye weza kuamini kuweza kumkuta binti mzuri kama Mercy akiwa amepoteza maisha yake kwa jambo ambalo wote walipelekea kuliwaza kwamba ni vivu wamapenzi

“Mtoeni, apelekwe hospitalini kuhifadhiwa”

Frednanando alizungumza kwa lugha ya kimexco, kisha akandoka huku akijifuta jasho jingi lililo kuwa likimwagika usoni.


***

Gafla Rahab akazifumbua macho, na kuanza kuyapepesa kila upande wa chumba alichopo, akakutana na sura ngeni, kwa haraka akawatambua watu hao kwamba ni madaktari, kwani mavazi yao meupe na marefu kiasi yalikuwa ni kielelezo tosha kwa wao kuweza kujulikana

“Nipo wapi hapa”


Rahab alizungumza kwa sauti ya kukwaruza kiasi, nesi akaagizwa na daktari kuweza kwenda kumuita Raisi Praygod Makuya

“Unaitwa”

Nesi alizungumza kwa lugha ya kingereza, Raisi Praygod kwa haraka akanyanyuka katika sehemu aliyo kuwa amekaa na kwenda katika chumba alicho mke wake, kitendo cha kuingia macho yake akayatupia kitandani na kumkuta mke wake akiwa ameketi huku akiwa katika wasi wasi mwingi. Raisi Praygod akamsogelea Rahab na kumkumbatia kwa nguvu huku machozi yakimwagika.


“Praygod nipo salama mume wangu?”

“Kweli?”

“Ndio mume wangu, najisikia vizuri”

Madaktari wote ndani ya chumba wakabaki wakiwa wamemshangaa Rahab kwani utafiti wao unaonyesha amepewa sumu kali sana ila chakushangaza mngonjwa amestuka na kuwa mzima kama si yeye aliye letwa akiwa katika hali mbaya.

“Hapa kuna kitu kinacho endelea, si rahisi akaamka kama hivi”

Daktari mmoja alimnong’oneza mwenzake kwa lugha ya kispain, huku wote macho yao wakiwa wamemtama Rahab anaye tabasamu huku akimkumbatia mume wake.


SHE IS MY WIFE(38)


Madaktari wakaomba nafasi ya kuweza kumpima tena, Rahab kuhakikisha kwamba yupo salama kama anavyo dai, Praygod hakuwa mbisha zaidi ya kusogea pembeni huku akiwa na furaha kubwa sana moyoni mwake kwani mke wake kwa sasa yupo katika hali ya usalama. Wakamchoma Rahab sindano kwenye mkono wa kushoto, wakatoa damu kiasi na kuiweka kwenye chupa, kisha madkatari wawili wakelekea kwenye chumba cha maabara ili kuanza kuifanyia uchunguzi damu ya Rahab


“Mume wangu mbona una wasiwasi mwingi kiasi hicho?”

Rahab aliuliza kwa sauti ya mahaba iliyo jaa unyonge ndani yake

“Nilikuwa na wasiwasi mwingi mke wangu nilihisi kama nimekukosa wakati bado ninakuhitaji”

“Usijali mume wangu mimi nipo salama”

Rahab alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake.


Madaktari walio chukua damu ya Rahab na kuipia wakajikuta wakipatwa na wasiwasi mwingine ambao, mmoja wao Alisha hisi kwamba kuna kitu ambacho kinaendelea na nitofauti sana na walivyo hisi. Walicho kiona ni virusi ambao hawakujau hata wamatokea wapi kwani ni wadogo wadogo na wanazunguka kila kona ya damu. Uchunguzi ukazidi kuendelea huku wakijaribu kutafuta dawa ambayo inaweza kuua virusi hao waliopo kwenye mwili wa Rahab.

“Jamani, tumejaribu kila aina ya dawa kuwaangamiza hawa virusi ila hawajafa”


Doktari mmoja alizungumza baada ya kumaliza majaribio yote katika kutafuta dawa ya kuangamiza virusi hao.

“Jamani nimepata wazo”

“Wazo gani?”

“Hembu tuchukue kiasi kidogo cha hii damu kisha, tuiingize kwa mbwa, ili kuweza kutambua kwamba je vinamadhara au laa”

Wazo la daktari huyo wa kike halikuweza kupingwa, kwa haraka wakatafuta mbwa, kisha wakamchunguza hana magonjwa yoyote, walipo ridhika, wakachukua damu kidogo ya Rahab na kuichoma kwa mbwa huyo kisha wakamfungia kwenye moja ya chumba ambacho kimezungukwa na vioo na nirahisi kwao kuweza kumuona mbwa huyo na endapo atakuwa na mabadiliko ya aina yoyote basi itakuwa ni rahisi kwao kuweza kugundua madhara ya mbwa huyo.



Frednando akafanikiwa kufika hospitalini huku, akiwa katika hali ya furaha baada ya kusikia kwamba mke wa rafiki yake amzinduka kutoka katika hali ngumu na mbaya aliyo kuwa nayo. Frednando hakuamini kumkuta Rahab akiwa anazungumza huku anacheka kwa furaha kama alivyo weza kumuona akiwa katika furaha hiyo masaa mengi yaliyo pita kwenye arusi yao.


“Imekuaje kaka?”

“Yaani hata mimi sifahamu kaka, mimi nahisi ni miujiza ya Mungu kwa maana ikutegea kama mke wangu atazinduka”

“Aisee shemeji pole sana”

“Asante shemeji yangu”

Furaha ikarudi upya kwa watu hao watatu, ila Frednando hakuzungumza chochote kuhusiana na jinsi Mercy alivyo husika katika kutaka kumuu Rahab, kwani tayari muhusika amejiangamiza yeye mwenyewe.

“Ila madaktari wamechukua damu ya mke wangu wanaifanyia uchunguzi, kwani nao hawakuamini kama ataweza kuamka muda huu”


“Mmmm……!!”

“Ndio tunasubiria waweze kutupa majibu”

“Sawa, amekula lakini?”

“Hapana shem, nipo vizuri tu”

Rahab alizungumza kwa furaha ambayo Frednando na Raisi Praygod wakabaki wakiwa wametazamana, kisha wakaaungana na Rahab kuachia tabasamu.

Mbwa aliye wekewa damu ya Rahab akaanza kutokwa na puvu jingi mdomoni mwake, huku akirusha rusha miguu, baada ya hapo akatulia sakafuni tuli, jambo lililo wafanya madaktari kuzidi kuchanganyikiwa kwani mbwa huyo tayari amesha fariki. Kila mmojaa akabaki kimya akiwa amemkodolea mbwa huyo macho, wasiwasi mwingi ukaanza kuwavaa kila mmoja kwani kila mmoja alianza kupatwa nahisia mbaya dhidi ya Rahab.


“Jamani oneni kule”

Daktari mmoja alizungumza huku akikinyooshea kidole chake shemu alipo lala mbwa, aliye anza kujitingisha mguu mmoja, baada ya hapo mbwa huyo akanyanyuka na kukaa sawa, kama alivyo kuwa hapo awali

“Jamani ni nini hichi?”

Daktari mwengine aliuliza kwani kila linalo tokea hapo ni muujiza kwao kwani mbwa huyo waliamini kwamba amesha aga dunia. Wakiwa katika kushangaa shangaa, mlango wa maabara ukafunguliwa na Rahab akaingia na kusimama katikati ya mlango huo, huku macho yake akiwa amewakazia madaktari hao walio anza kutetemeka kwa woga.


***

Fetty na wezake baada ya kukubaliana kuungana na bwana Rusev wakaanza kutembezwa katika vitengo mbali mbali ndani ya ngome hii, iliyopo chini ya bahari. Hapo ndipo wakagunduka kwamba wapo chini ya bahari na ningumu sana kwa wao kuweza kutoka katika eneo hilo lenye vifaa vingi ya ulinzi ikiwemo kamera na askari wanao linda kila kona kwa masaa ishirini na nne.



Fetty akajikuta akivutiwa sana katika kitengo cha watu wanao tengeneza silaha za nyuklia, bwana Rusev baada ya kuligundua hilo akaamuru Fetty kuweza kufundishwa mara moja jinsi ya kutengeneza silaha hizo ambazo wanazitengeneza kwa wingi katika eneo hilo.



Halima na Anna wakajikuta wakipenda kuendesha ndege za kivita ambazo zimo ndani ya eneo hilo. Bila kinyongo bwana Rusev akahitaji mabinti hao kuweza kuwa kaatika kundi hilo. Agnes, kwa umahiri wa kulenga shabaha kwa kutumia bunduki, akajikuta akiingia katika kikosi cha subshotter, watu wanao lenga shabaha kwa masafa marefu. Ubora wa Agnes uliweza kuwapita watu wote walio kuwemo katika eneo hilo, jambo lilizo kumpa sifa nyingi Agnes.


Kuingia kwa mabinti hao wanne ndani ya kngome ya bwana Rusev, kukaleta mabadiliko yaliyo makubwa sana, kila mmoja akajikuta akiwa anafanya kazi kwa juhudi ili wasiweze kupitwa na mabinti hao ambao mara nyingi bwana Rusev aliweza kuwamwagia sifa kwamba ni mahiri sana katika kazi zao. Kitu kingine kilicho zidi kuwapa sifa Fetty na wezake ni jinsi uwezo wao wa kupigana pasipo kutumia silaha, ulivyo mkubwa, hadi wakaanza kuwa ni tishio kwa wababe waliomo ndani ya kambi hiyo.


“Kuna kazi”

Bwana Rusev alizungumza baada ya kuwaita Fetty na wezake ndani ya ofisi yake, mara baada ya kuridhika na jinsi wasichana hao walivyo weza kufanya juhudi katika mafunzo yao.

“Kazi gani?”

Agens aliuliza huku akiwa amemtazama bwana Rusev machoni mwake

“Kazi nyenyewe inakuhusu sana wewe, Agnes, baada ya wiki mbili waziri wa mambo ya nje nchini Marekana atakuja hapa Russia na atafikizia kwenye jiji la Mossow.”

Bwana Rusev akameza mate kidogo kisha akanedelea kuzungumza


“Lengo lake kubwa kuja katika nchi hii, anahitaji kuweza kuingia makubaliano na serili yetu kuweza kusaidiana nao katika swala zima la kuzuia sila za nyuklia zisitengenezwe duniani kote”

“Picha zake zipo?”

Fetty aliuliza

“Ndio zipo”

Bwana Rusev akaminya kitufe kidogo kilichopo kwenye meza yake, chumba kizima kikawa na giza jingi, mwanga wa Tv kubwa iliyomo ndani ya chumba hicho ikawaka, bwana Rusev akanyanyuka na kuisogelea kwenye ukuta ilipo wekwa. Akaanza kuminya minya kwenye kioo cha Tv hiyo, na picha za waziri huyo zikatoke.

“Kwa jina anaitwa bwana Paul Henry Jr. Ni miongoni mwa viongozi ambao wanalindwa sana katika dunia hii, ukiachilia Raisi wao na makamu wake, huyu ndio anafwatia kwa kulindwa sana”


“Atakuja tarehe 22 ya mwezi huu, ataongozana na walinzi zaidi ya mia moja. Watakao mzingira katika msafara wake watakuwa zaidi ya thelathini”

“Hili ndio njengo ambalo atafikia, ni hotel ya kitalii na iliyo anza kuwekewa ulinzi kuanzia sasa hadi hapo atakapo kuja”

Bwana Rusev aliendelea kutoa maelezo ya Hotel atakayo fikizia bwana Paul Henry Jr, akaonyesha kila sehemu ambayo bwana Paul Hery Jr atapita akiwa na watu wake wanao mlinda. Hadi mwisho wa maelekezo yake, wote wakawa wamemuelewa vizuri bwana Rusev.

“Agnes hii ni kazi yako ya kwanza na sinto hitaji ukosee, ninakuamini sana”


“Usijali mkuu nipo kwa ajili yako”

“NITAHITAJI UMUUE KIONGOZI HUYU IWE TISHIO KWA NCHI HII NA DUNIA NZIMA”

“SAWA MKUU”

Agnes alijibu huku akiinamisha kichwa chake chini kama ishara ya kumuheshimu bwana Rusev, kisha bwana Rusev akachuku moja ya chini yenye alama ya X na kumvisha Agnes shingoni, akampa Baraka kwa ajili ya kuitekeleza kazi hiyo hatari sana kwa maisha yake.


==> ITAENDELEA


ILIPOISHIA

Bwana Rusev aliendelea kutoa maelezo ya Hotel atakayo fikizia bwana Paul Henry Jr, akaonyesha kila sehemu ambayo bwana Paul Hery Jr atapita akiwa na watu wake wanao mlinda. Hadi mwisho wa maelekezo yake, wote wakawa wamemuelewa vizuri bwana Rusev.

“Agnes hii ni kazi yako ya kwanza na sinto hitaji ukosee, ninakuamini sana”

“Usijali mkuu nipo kwa ajili yako”

“NITAHITAJI UMUUE KIONGOZI HUYU IWE TISHIO KWA NCHI HII NA DUNIA NZIMA”

“SAWA MKUU”

Agnes alijibu huku akiinamisha kichwa chake chini kama ishara ya kumuheshimu bwana Rusev, kisha bwana Rusev akachuku moja ya chini yenye alama ya X na kumvisha Agnes shingoni, akampa Baraka kwa ajili ya kuitekeleza kazi hiyo hatari sana kwa maisha yake.


ENDELEA

Agnes akaanza kazi moja ya kulenga shabaha kwa masafa ya mbali pasipo kutumia lensi inayo saidia kuweza kuvuta vitu karibu, kila anacho kilenga kwa kutumia bunduki yake aina ya AS50 Sniper rifle, yenye uzito wa kila zaidi ya kumi na tano ikiwa na risasi zilizo jaa, akahakikisha anakipata vizuri huku akiwa ameishika mkononi mwake, jambo ambalo lilizidi kuwashangaza wengi kwani, hii ni bunduki ambayo mara nyingi mtu huwa anaiweka chini na kuisimamisha kupitia vimiguu viwili vya chuma, ili kuweza kulenga shaba.


“Waooooo”

Fetty alimpigia makofi Agens, baada ya kumkuta akiwa analenga vitu vya mbali kwa bunduki hiyo. Agnes baada ya kumuona Fetty akaacha zoezi lake ambalo analo kifanya

“Mwanangu kweli unatisha, hii ngoma ni nzito”

Fetty alizungumza huku akiinyanyua bundiki aliyo ishika Agnes

“Inahitaji mazoea kuweza kuitumia la sivyo unaweza ukafa, kwa maana ninapiga hadi nasikia mapigo ya moyo yanacheza kama kitenesi”


“Hahahaa, sas mtu wangu si uiweke chini ndio upige?”

“Ahaaa chini najiona kama nakosa shabaha vile”

“Ok tuachanane na hayo, vipi maandalizi yako ya kwenda kwenye hiyo mission?”

“Ndio kama hivi unavyo niona nazidi kujikaza, kwa maana nikicheza vibaya nakufa au nakamatwa na nisinge penda kukamatwa na wamarekani, ni bora nijipige risasi nife hapo hapo”

Maneno ya Agens yakamfanya Fetty kukaa kimya huku akimtazama Agnes usoni mwake, jinsi anavyo mwagikwa na jasho jingi.

***

Kila mmoja ndani ya maabara akaka kimya huku akimtazama Rahab, jinsi anavyo mchunguza mtu mmoja baada ya mwengine. Rahab akaachia tabasamu pana kisha akapiga hatua na kuingia ndani kabisa ya maabara huku nyuma yake akiingia mume wake pamoja na bosi wa bwana Frednando


“Jamani asanteni kwa ushirikiano wenu kwa kuweza kunihudumi hadi nimekuwa sawa”

Rahab alizungumza kwa furaha kubwa, ikamlazimu Frednando kuweza kuitafsiri kwa kispain. Madaktari walitabasamu kwa uwoga ila mioyoni mwao kila mmoja alikuwa akiliwazia lake kuhusiana na mbwa aliye fufuka dakika chache zilizo pita. Rahabu pasipo kuambiwa na mtu yoyote akaingia kwenye chumba alicho fungiwa mbwa huyo na kumchuku.


“Jamani mbwa huyu nimependa, anaitwa nani?”

Rahab akawauliza madaktari walio baki na mshangao mkubwa, kwa kingeraza ila mmoja wao akajikaza na kuzungumza kwa sauti ya utaraitibu.

“Anaitwa Charity”

“Waoo nitamchukua nimempenda sana”

Hakuana aliye kuwa na ubishi kuhusiana na kuchukuliwa kwa mbwa huyo, waliye mfanyia majaribio, ila kila daktari akabaki kimya. Hapakuwa na daktari aliye weza kuzungumza kwa kile walicho weza kukiona.


Wakarudi katika jumba la Frednando ambapo ikawalazimu kuwasiliana na ubalozi wa Tanzania uliopo nchini Mexco. Balozi baada ya kupokea simu ya raisi Praygod Makuya, ikamlazimu kuongozana na baadhi ya askari wa jeshi la Tanzania hadi kwenye jumba la Frednando, baada ya kufika wakapokelewa vizuri kama ilivyo kuwa kwa raisi wao.

“Yaani raisi siamini kama upo hai?”

Bi Joyce Maagi alizungumza huku akimtazama raisi Praygod machoni mwake.


“Nipo hai, nasikia nchini watu wapo kwenye maombolezo ya kifo change?”

“Ndio muheshimiwa hapa mwenyewe nilikuwa nimebakisha siku mbili niende kwenye msiba wako”

“ Ok ila sinto hitaji muweze kuzungumza kitu chochote kuhusiana na kuniona kwangu, nitahitaji kurudi siku ya mazishi yangu ninaamini nitakuwa Tanzania”

“Ila kikubwa ninacho hitaji wewe kukifanya nitengenezee mazingira katika uwanja wa ndege kwani nitakuja na private airplane(Ndege binafsi), wajulishe baadhi ya watu watakao nipokea kisiri mimi na mke wangu pasipo watu wengine kuweza kutambua lolote”


“Sawa muheshimiwa ila kuna swala la mke, si tayari amesha fariki au kuna mwengine”

“Yupo”

Raisi Praygod akamngong’oneza mmoja wa wahudumu Frednando na kumuagiza akamuite Rahab, naye akafanya hivyo. Baada ya muda Rahab akafika sebleni, akiwa amevalia gauni jeupe na refu lililo mpendeza sana. Bi Joyce Maagi akusita kumshangaa Rahab, kwani picha yake ipo kwenye moja ya watu wali angamia na ndege ya raisi.


“Huyu binti naye pia amepona?”

“Ndio amepona, ni mmoja wa watu walio weza kuyapigania maisha yangu hadi hapa nilipo”

“Ahaa”

Bi Joyce Maagi akanyanyuka na kwenda kusalimiana na mke wa rais, kwa heshima zote. Wakaendelea na mazungumzo ya kawaida. Siku iliyo fwatia Bi Joyce Maagi akaondoka akiwa na masafara wake kuelekea nchini Tanzania, kitu cha kwanza baada ya kutua katika uwanja wa mwalimu Jk Nyerere, akafanya maagizo yote aliyo agizwa na Raisi Praygod Makuya, japo baadhi ya watu walishangaa kusikia kwamba Raisi Praygod yu hai.


Maandalizi ya safari ya kurudi Tanzania, yakawekwa tayari na Frednando, akahakikisha kwamba kila kitu kipo salama na hakuna jambo baya ambalo litamdhuru raisi Praygod Makuya pamoja na mke wake. Ikawa ni siku nyingine ya huzuni kwa marafiki wawili Praygod na Frednando, kila mmoja Alisha mzoea mwenzake kwa kipindi kifupi walicho ishi, ila hapakuwa na jinsi yoyote yakufanya. Iliwalazimu kuweza kutengana tena na kila mmoja aweze kuendelea na majukumu yake anyo yafahamu.


“Shem siku une ikuli Tanzania”

Rahab alizungumza kwa furaha baada ya kuwaona Praygod na Frednando wakiwa wanalengwa lengwa na machozi ya uchungu

“Usijali Shem, nitakuja siku naamini nikija mutakuwa mumepata kijana mdogo”

“Hahaaa Mungu ni mwema, ombeni Mungu niwazalie kijana wa kiume ili aja kuwa raisi kama baba yake”

“Kwa nini usituzalie wa kike ili awe raisi labda wa kwanza, mwanamke kwa miaka hiyo ijayo?”

“Sawa Mungu ni mwema anaweza kutuwezesha katika hilo”

“Haya jamani niwatakie safari nje, ndege imesha washwa, hiyo mutaitumia katika matumizi yenu binafsi”


“Asante sana Frednando ndugu yangu”

“Na hao marubani kama nilivyo kuambia, nitawalipa mimi”

“Sawa kaka”

Raisi Praygod na Rahab wakaingia kwenye ndege, taratibu ndege hiyo yakifahari ikanza kuiacha ardhi ya Mexco na ndani ya dakika kadhaa ikawa angani. Raisi Praygod kila alipo mtazama mke wake, hakusita kuachia tabasamu pana usoni mwake, kwani uzuri wa mke wake mara nyingi ulimpa kujiamini na kujiona ni mwanaume kwenye bahati kwa kuweza kumpata msichana mzuri kama Rahab.


***

Ukimya mkubwa, umetawala kwenye kiwanja cha mpira, jijini Dar es Salaa, viongozi wote wa nchini Tanzania na wengine wakitoke nchi jirani pamoja na wananchi wengi wakiwa katika kuyaaga mabaki ya miilii ya waanga walio fariki katika ajali ya ndege ya Air foce, huku wakiamini kwamba kati ya miili hiyo iliyo ungua vibaya hadi haitazamiki, mwili wa Raisi Praygod Makuya utakuwepo miongoni mwa hiyo. Viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali nao hawakuwa nyuma katika kusali sala ya mwisho ya miili hiyo.


Vilio vya wamama hadi wanaume walio shindwa kuzuia vilio vyao, viliendelea kusikika katika sehemu mbalimbali za uwanja. Wanajeshi wa kulinda usalama pamoja na jeshi la polisi nao waliweza kukusanyika katika eneo la viwanja huku kila mmoja akiwa katika kuangalia usalama wa viongozi katika eneo hilo unaenenda vipi.



Majira ya saa sita machana ndege ya raisi Praygod Makuya ikatua kwenye uwanja wa mwalimu Julius K. Nyerere, kwa usiri mkubwa alio weza kuutengeneza balozi bi Joyce Maagi, aliweza kumpokea Raisi Praygod Makuya, na moja kwa moja akampeleka nyumbani kwa waziri Mkuu, Bi Magret.


Wakapolekewa nyumbani kwa waziri mkuu ambae alisha arifiwa kuhusiana na ugeni huo, na kipindi ambacho watu wapo viwanjani aliweza kuigiza kupoteza fahamu, ambapo aliweza kukimbizwa hospitalini, akiwa njiani akazinduka na kumuomba dereva ampeleke nyumbani kwake ili akajipumzishe na hakuona sababu ya yeye kwenda hospitalini.



Alipo fikishwa nyumbani kwake akamuru madaktari walio mleta waweze kuondoka, huku moyoni mwake akiwa na siri kubwa ya ujio wa raisi Praygod Makuya.

Ndani ya muda mchache, gari mbili nyeusi aina ya arstorn martin, zikaingia kwenye geti la jumba lake lakifahari. Akiwa pamoja na wafanya kazi wake wa ndani pamoja na mke wake wakasimama sehemu gari hizo zitasimama. Raisi Praygod akashuka ndani ya gari akiwa na mke wake Rahab. Bi Magret hakuamini ujio wa raisi huyo ambaye anamchukulia kama mwanaye kutokana na upendo alio weza kumfanyia na kumpa cheo cha uwaziri mkuu.


Wakakaribishwa ndani, huku Bi Magreti akionekana kuwa na furaha kubwa sana, wakapata chakula cha mchana huku wakitazama jinsi mambo yanavyo endelea kwenye uwanja taifa wa mpira.

“Aloo kumbe watu wananipenda sana ehee”

“Sana tuu muheshimiwa, yaani mimi nilipo pokea kuhusiana na swala la msiba wako nilijisikia vibaya sana”

“Aisee pole sana mama yangu, huyu ni mke wangu anaitwa Rahab”


“Ahaa karibu sana mke mpya wa raisi”

Bi Magreti alizungumza kwa furaha na kuwafanya watu wote waliopo sebleni kucheka. Rahab katika kuzungusha zungusha macho yake sebleni akaiona picha kubwa ukutani ya kijana aliye ustua moyo wake.

“Yule ni nanii ukutani kwenye ile picha?”

Rahab aliuliza huku akiinyooshea kidole picha hiyo

“Yule ni mtoto wangu anaitwa EDDY GODWIN, na yule binti pale ni Mke wake mtarajiwa anaitwa SHEILA”

Bi Magret alizungumza kwa furaha, huku akichia tabasamu pana usoni mwake, jambo lililo uchoma moyo wa Rahab pasipo mtu yoyote kuweza kugundua hilo


SHE IS MY WIFE(40)


“Ila kwa sasa kijana huyo hayupo ndani ya nchi hii”

Bi Magret alizungumza huku kidogo tabasamu lake likipungua usoni mwake, Rahab akataka kuuliza kitu ila akanyamaza na kumtazama mume wake.

“Ok jamani tunafanyaje kwa maana ninahitaji kwenda kuzungumza na wananchi wangu niwezee kuwapa ukweli kuhusiana na kilicho tokea”


“Itabidi tuwasiliane na makamu wa raisi”

“Hapana sihitaji uwasiliane naye”

“Kwa nini muheshimiwa nisiwasiliane naye?”

“Kuna sababu nyingi tu zinazo pelekea usiwasiliane naye ila utakuja kuzifahamu baadaya usijali kwa hilo, ila ninacho hitaji ni kwenda kwenye uwanja wa taifa”

“Muheshimiwa huoni kama itakuwa ni harari sana kwa maisha ya wananchi walio kuwepo katika eneo lile wengine wanaweza kuona kama ni mzimu umefufuka kutoka kuzimu”

Balozi Joyce Maagi alitoa wazo

“Hapana, nahitaji kuingia uwanjani kisiri pasipo mtu yoyote kuweza kugundua, na nitahitaji kuweza kufika katika eneo walio kaa viongozi wa juu au nifike ile sehemu ambayo kuna kipaza sauti”


Kila mmojaa akaka kimya akimtazama Raisi Praygod alicho weza kukiamua.

“Basi inabidi ubadilishe mavazi muheshimiwa, ili usiweze kugundulika”

“Sawa nitafutieni kofia pamoja na tisheti hii hizi walizo vaa waombolezaji”

Raisi Praygod akaletewa ngua ambazo ziliweza kumbadilisha muonekano wake na kuwa kama mtu wa kawaidia sana. Hakutaka kwenda na Rahab, alicho kifanya akaomba kuongozana na dereva wa waziri mkuu ila watumie gari moja kati ya magari mengi yanayo tumika hapo nyumbani kwa waziri mkuu.


“Mutaniona kwenye kideo nyinyi subirini”

Maneno ya Raisi Praygod Makuya yakamchekesha kila mmoja aliye weza kuwa katika eneo hilo, akaingia ndani ya gari na kuondoka, njia nzima Raisi Praygod akawa anapangilia ni maneno gani ambayo atakwenda kuyazungumza mbele ya wananchi wake. Kutokana ni siku ya majonzi, yaliyo tawala nchi nzima, ndani ya jiji la Dar es Salaam, foleni haikuwa kubwa, askari wa ulinzi barabarani wametanda kila mahali wakihakikisha kwamba hakuna ujinga wowote ambao utajitokeza katika siku nzima ya leo.


Wakafanikiwa kufika katika uwanja wa taifa wa mpira, akamuamuru dereva kusimamisha gari kwenye maegesho ya watu wa kawaidia, kisha akashuka kwenye gari, akatazama kila pande, alipo weza kuona hakuna anaye mfwatilia zaidi ya askari wakiendelea kuzunguka zunguka wakiwa na mbwa wanao nusa harufu. Akaanza kupiga hatua za kawaidia kuelekea kwenye geti la kuingilia kiwanjani ambalo ni geti lililo pita magari ya waheshimiwa, na askari wengi waliweza kulinda geti hilo kwani hapakuwa na mtu aliye weza kuruhusiwa kuingia katika geti hilo. Akafika getina na mwanajeshi mmoja akamzuia


“Sahamani hakuna anaye ruhusiwa kupita katika geti hili, zunguka upande ule ndipo kwenye mageti yakuingilia wananchi wa kawaidia”

Mwanajeshi huyo alizungumza kwa lugha ya utaratibu huku kwenye mkono wake wa kushoto akiwa amejifunga kitambaa cheusi akishiria kwamba anaadhimisha msiba.

“Mimi nataka kupita hapa hapa”


“Samahani ndugu, nisinge penda kuweza kutumia nguvu kubwa ya kukutoa hapa. Tafadhali fwata maelekezo niliyo kuagiza uweze kufwata”

Raisi Praygod akatabasamu kisha akaipandisha kofia yake juu taratibu, jambo lililo mstua mwanajeshi huyo.

“Shiiii….usistuke mimi nipo hai, ila nahitaji msaada wako wakuingia humu ndani kupitia geti hili kwani itakuwa raisi kwa mimi kuweza kufika kwenye kipaza sauti. Ila tafadhali usimuambie mtu yoyote kama umeniona sawa”


Mwajeshi huyo akataka kupiga saluti lia Raisi Praygod akamkataza asifanye hivyo, akamsisitizia nia yake ni kuweza kufika kwenye kipaza sauti.

“Muheshimiwa mimi hapa cheo change ni kidogo, kama unavyo nioana wewe mwenyewe. Sina mamlaka ya kukupitisha pele labda nimuite mkuu wangu aje”

“Mimi nimekuomba wewe na si wale wengine fanya uwezalo niingie uwanjani. Kwanza jina lako unaitwa nani?”

“Thomas Makengele”

“Sawa bwana Makengele, fanya kazi niliyo kuagiza kuifanya”

“Sawa nisubiri dakika moja”


Thomas akakimbia hadi kwenye kibanda cha dharula kilicho yengenezwa pembeni ya geti akamuomba mkuu wake na kumuongopea kwamba kuna ndugu yake anahitaji kuingia ndani ya uwanja kwani mageti mengine watu wamejaa

“Sasa unataka kumruhusu akakae wapi, wakati geti hili ni kwaajili ya VIP tu”

“Nakuomba tu mkuu, atasimama hata pembeni ili kuweza kushuhudia kinacho endelea”

“Usije ukawa unatuuingizia jambazi, badae tuje kulamiana?”

“Hapana mkuu, nilikula kiapo kuitete, kuilinda nchi yangu na katiba yake. Siwezi kufanya ujinga kama huo”


“Mruhusu, tena hakikisha unamsindikiza hadi atakapo kaa, kwa maana na ushamba shamba wake anaweza kwenda sehemu ambayo mtu kama yeye haruhusiwi kwenda”

“Sawa mkuu asante sana”

Thomas akatoka akiwa na furaha kubwa moyoni mwake, kwani uongo wake umeweza kukubalika. Akamfwata raisi Praygod sehemu alipo simama.

“Muheshimiwa twende nikupeleke ndani”

“Sawa”

Kutokana na amri ya mkuu wa geti hilo, Thomas akafanikiwa kuingia ndani ya uwanja akiwa na Raisi Praygod ambaye hadi sasa hivi hajajulikana kama ni yeye


***

Jiji zima la Mossco nchini Rusia, limezungukwa na wanajeshi wa Marekani wakisaiidiana na wanajeshi pamoja na polisi wa nchini Rusia, kuendeleza kulinda usalama jiji zima, kwani ni masaa machache yamesalia kiongozi mkubwa dunia waziri wa mambo ya nje nchini Marekani bwana Pual Henry Jr. Kuingia katika jiji hili, kwa madhumuni ya kikako kikubwa ambacho ni moja ya kauli mbiu ya Marekani, kuyazuia baadhi ya mataifa yanayo jaribu kutengeneza silaha za nyukilia, kuachana mara moja na mpango huo, kwani ni harati kwa dunia nzima, endapo silaha hizo zitaweza kutumiwa.


Kila mwananchi aliweza kukaguliwa kwa vifaa maalumu, na askari ambao kila wakati hawakuhitaji kuona kuna jambo baya linaweza kutoke kwa kiongozi huyo mkubwa.

Agnes akiwa katika hali ya umakini mkubwa, akafanikiwa kuingia kwenye jiji la Mosscow, pasipo kuweza kukutana na kuzuizi cha aina yoyote. Kitu cha kwanza kuweza kukifanya, akaanza kutafuta ni wapi kwenye gorofa refu linalo karibiana na Hotel atakayo fikikizia bwana Paul Henry Jr. Akafanikiwa kuona moja ya gorofa lenye urefu wa gorofa zipatazo stini. Kwa kulichunguza kwa haraka haraka akagundua ni moja ya gorofa lenye ofisi nyingi za watu binafsi.


“Nitafanyaje?”

Agnes alizungumza huku akiwa amesimama nje ya jengo hilo, lenye watu wengi wanao ingia na kutoka. Kabegi kadogo alicho kavaa mgongoni, haikuwa ni rahisi kwa mtu kumstukia kwamba amebeba bunduki yenye uwezo mkubwa sana, kwani aliweza kuigawanya gawanya na kuwa ndogo sana inayo weza kubebeka ndani ya kibegi hicho kidogo.


Akaingia ndani ya jengo hilo, akaingia kwenye moja ya lifti na kiminya batani iliyo andikwa namba stini. Lifti hiyo ikaanza kwenda juu kwa kasi, hadi ikafika katika gorofa namba stini, mlango ukafunguka, kabla hajatoka akachunguza kordo nzima, akamuona dada mmoja akiwa anafanya usafi kwenye kordo hiyo, huku akiwa amevalia mavazi yanayo muonyesha ni muhudumu katika eneo hilo. Akatoka na kuanza kuelekea alipo dada huyo, huku akizitazama kamera za ulinzi zilizo tegwa kwenye eneo hilo.

“Samahani”

Agenes alizungumza kwa kingereza na kumfanya dada huyo kuacha alicho kuwa anakifanya na kumtazama

“Unajua kuzungumza kingereza?”


“Ndio zungumza tu”

“Nahitaji kwenda chooni, tafadhali naomba unisaidie”

“Ohooo, ofisi zimesha fungwa dada yangu, na kila ofisi ina choo cheke labda nikusaidie kwenye moja ya ofisi ambayo ndio ninakwenda kuifanyia usafi”

“Sawa nitashukuru”

Dada huyo akabeba vifaa vyake vya usafi, wakaongozana na Agnes hadi kwenye moja ya ofisi, wakaingia ndani.

“Kuna choo kile pale waweza kujisaidia”

“Ila kwa nini watu wamefunga ofisi mapema hivi?”

“Leo ni siku ya kuja kwa kiongozi mkubwa, basi watu tunakwenda kumpokea ndio mana ofisi nyingi zimefungwa mapema hii”


“Ahaaa sawa”

Agnes akaingia ndani ya choo alicho elekezwa, akavua koti lake dogo alilo livaa kutokana na baridi kali, kisha akavua na gloves nyeusi alizo zivaa. Akaminya kitufe kwenye choo cha kukalia na kuyafanya maji kuweza kuzunguka, ili kumdanganya dada huyo kwamba amemaliza haja yake ya kujisaidia.


Kabla hajatoka akasikia mlango ukigongwa, jambo lililo mfanya kujiandaa na kujiweka tayari kwa lolote kisha akamruhusu mtu anaye gonga kuweza kuingia ndani. Akaingia dada mfanyakazi huku akiwa na vifaa vyake, gafla Agnes akampiga ngumi nzito shingoni dada huyo na kumfanya aanguke mzima mzima kama mzoga.

 


ILIPOISHIA

Agnes akaingia ndani ya choo alicho elekezwa, akavua koti lake dogo alilo livaa kutokana na baridi kali, kisha akavua na gloves nyeusi alizo zivaa. Akaminya kitufe kwenye choo cha kukalia na kuyafanya maji kuweza kuzunguka, ili kumdanganya dada huyo kwamba amemaliza haja yake ya kujisaidia.


Kabla hajatoka akasikia mlango ukigongwa, jambo lililo mfanya kujiandaa na kujiweka tayari kwa lolote kisha akamruhusu mtu anaye gonga kuweza kuingia ndani. Akaingia dada mfanyakazi huku akiwa na vifaa vyake, gafla Agnes akampiga ngumi nzito shingoni dada huyo na kumfanya aanguke mzima mzima kama mzoga.



ENDELEA

Akamvuta dada huyo na kumuingiza ndani ya choo. Akatoka ndani ya choo na kuufunga mlango kwa ndani wa kuingilia ofisini hapo, kisha akasimama kwenye moja ya dirisha na kuangalia nje. Kwa bahati nzuri katika sehemu alipo simama anaweza kuona vizuri kwenye mlango wa hotel atakayo ingilia kiongozi huyo, ambapo kumejaa wananchi wengi wakiwa wamejipanga kwa kumpokea kiongozi huyo. Akachukua darubin yake, akatazama kila sehemu ya magorofa ya pembeni ili kuhakikisha usalama wake kama upo.



Alipo ridhika hakuna walenga shabaha wa serikali ambao mara nyingi hujitegega kwenye magorofa makubwa kama hayo. Akafungua kabki kake na kuanza kuchomoa kipande kimoja baada ya kingine cha silaha yake. Akaanza kuiunga kwa utaalamu mkubwa hadi ikakamilika. Akaweka magazine yenye risasi ishirini, kisha akafunga kiwambo cha kuzuia sauti.


Akasimasa kwenye moja ya sehemu ambapo si rahisi kwa mtu wa nje kuweza kumuona. Saa yake ya mkononi akaiweka vizuri, huku ikionyesha zimesalia dakika kumi kabla ya kiongozi huyo kuweza kufika katika eneno hilo.


“Mmmmmmmm”

Agnes aliguna badaa ya kuanza kuona magari meusi yakianza kusimama katika eneo alipo ielekezea bunduki yake, kwa kutumia lensi iliyopo juu ya bunduki yake, akaona baadhi ya walinzi wa waziri huyo wakishuka kwenye magari hayo aina ya GVC. Walinzi hao wakaendelea kuwa macho huku wakijipanga mstati mmoja kuhakikisha kwamba waziri wao anakuwa salama. Kajasho kembamba kakaanza kumchuruzika Agnes, huku mapigo ya moyo yakinza kumpiga kwa mbali jambo lililo anza kumpa wasiwasi kwani katika kazi kama hiyo mtu hutakiwi kuwa na wasiwasi wa aina yoyote.


“Shitiiii!!!!”

Agnes alizungumza huku akitingisha kichwa chake, akijitahidi kutoa wasiwasi mwingi alio kuwa nao. Gari ndefu yene milango sita, ikasimama kwenye zulia jekundu la kuingialia kwenye hoteli hiyo. Walinzi wanne walio valia suti nyeusi wakaufwata mlango wa nyuma wa gari hiyo, mmoja akashika kitasa na kuufungua.


Agnes akashuhudia mguu mmoja ukitangulia kutoka kwenye gari hiyo, akatulia kidogo kutazama vizuri. Akamuona kiongozi Bwana Paul Henry Jr, akitoka kwenye gari hilo, huku akizungukwa na askari hao wanne. Mapigo ya moyo yakazidi kumuenda mbio Agnes baada ya kumuona mtoto mdogo wa kike mwenye umri wa miaka kama nane akitoka ndani ya gari hilo, na mtoto huyo anafanana sana na bwana Paul Henry Jr.

Agnes akataka kufyatua risasi ila akajihisi vibaya sana huku pumzi akiihisi inakwenda kumuishia, kila allipo jaribu kuiweka sawa bunduki yake, mikono yote ikamtetemeka, akajikuta akiwa ameduwaa akimtazama mtoo huyo aliye nyanyuliwa na bwana Paul Henry Jr na kumbeba kifuani mwake.


Bwana Paul Herny Jr akaendelea kuwasalimia wananchi walijitokeza kumpokea, huku akiwa amembeba mwanaye anaye mpenda kuliko kitu chochote na mara nyingi huwa anapenda kwenda naye kwenye dhiara kubwa kama hii ya hapa nchini Russia.

Mlio wa simu ukamstua Agnes, kwa haraka akachukua ear phone na kuiweka sikioni kisa akaminya kitufe kilichopo kwenye hiyo earphone na kuipokea simu hiyo.


“Unafanya nini wewe, muue huyo”

Sauti ya bwana Rusev alisikika kwenye simu hiyo akizungumza kwa kufoka. Agnes hakujibu kitu chochote zaidi ya kuishika bunduki yake vizuri, akayang’ata meno yake kwa nguvu na kuikaza misuli yake, ili kuuzuia wasiwasi mwingi ulio mtawala.

“Uaaaaaa”

Sauti ya bwana Rusev ikaendelea kumshawishi Agnes kufanya tukio alilo tumwa kuweza kulifanya, mshale wa msalaba uliopo kwenye lensi ya bunduki yake, ukatua kichwani bwana Paul Henry Jr, tayari kwa kufyatua risasi.


***

Baada ya Raisi Praygod kuondoka, Rahab akaendelea kuitazama picha ya Eddy, iliyopo sebleni. Jambo lililo mfanya Bi Magret kugundua hilo.

“Muheshimiwa, kuna tatizo kwenye picha ya mwanangu?”

Bi Magret alimuliza Rahab kwa sauti ya chini pasipo mtu mwengine kusikia.

“Naomba tuzungumze”

Rahab alizungumza huku akitoka nje ya jumba hilo, bi Magret akafwa kwa nyuma huku akiwa na wasiwasi na maswali mengi juu ya mwanaye huyo.

“Umesema mwano yupo nje ya nchi?”


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog