Search This Blog

Friday 30 December 2022

HEKAHEKA MSITUNI - 4

    


Simulizi : Hekaheka Msituni 


Sehemu Ya Nne (4)

  
    

Simulizi : Hekaheka Msituni 

Sehemu Ya Nne (4)





“Kuingia katika kikosi cha waasi halafu na kumchukua mwanajeshi mmoja miongoni mwao. Duh! Jambo hili kweli mtihani mzito sana!” afisa mwingine naye aliongezea kumuunga mkono yule wa mwanzo.



“Kwa hiyo kwa kusema hivyo mnamaanisha nini? Mna maana kwamba tumwache mheshimiwa Rais apoteze maisha?” Chifu aliuliza.



“Hapana, tulikuwa tunajaribu kuweka wazi ugumu wa jambo lililopo mbele yetu” yule aliyetoa kauli mara ya kwanza aliongea.



“Kauli zenu ni za kukatisha tama. Kwa sasa tunatakiwa tufikirie namna ya kulitatua tatizo hili na si kukatishana tama!” Chifu aliongea huku akionyesha wazi kwamba alikuwa amekerwa na kauli za maafisa wale wa mwanzo.



“Tusamehe ndugu!” maafisa wale waliomba radhi.



“Mimi nitakwenda katika misitu ya Masolo. Nitaingia katika kikundi cha waasi cha BMM na nitamleta bwana Martin Samweli hapa!” Inspekta Tom Green aliongea.



Maafisa wote pale walishindwa kuamini kile ambacho walikuwa wakikisikia. Walihisi huenda Inspekta Tom Green alikuwa ameanza kuchanganyikiwa. Haikuwa rahisi kwa mwanadamu wa kawaida kufanya maamuzi yenye kuhatarisha maisha kwa kiasi kile.



Ukiachilia mbali kuhatarisha maisha lakini maamuzi yale yalikuwa hayawezekani. Haikuwa rahisi kwa mtu yeyote kuingia katika kambi ile na akatoka salama kabisa. Kwanza ataingiaje pasi kupoteza maisha kabla hata hajaingia katika kambi ile maana ulinzi ambao ulikuwa katika kambi ile haukuwa wa kawaida. Kauli ya Inspekta Tom Green iliwafanya maafisa wale wapigwe na butwaa la mwaka.



Ni Chifu pekee ndiye ambaye hakushangazwa na kauli ya Inspekta Tom Green. Yeye alimfahamu kijana wake huyu kwamba alikuwa na uwezo wa pekee sana. Alikuwa na uwezo mkubwa sana katika tasnia nzima ya ujasusi pamoja na mapigano.



Alikuwa na uwezo wa kupambana na jeshi kubwa kwa wakati mmoja na akatoka na ushindi. Kwa upoande wake maamuzi ya Inspekta Tom Green aliyabariki kwa moyo mkunjufu kabisa. Hakuwa na wasi hata kidogo katika moyo wake.



“Heeee! Itawezekanaje?” afisa mmoja alishindwa kujizuia na kuamua kuuliza.



“Hili ni jambo la uzalendo linalohitaji moyo wa pekee. Ukiwa na moyo dhaifu huwezi kufanya jambo kama hili. Rais wetu anahitaji msaada kwa sasa katika kuyaokoa maisha yake. Nina imani na kijana wangu. Ataikamilisha misheni hii!” Chifu aliongea.



Maafisa wengine walikuwa bado wameduwaa. Hawakuwa wameyaamini maneno ya Chifu. Waliona jambo lile kama haliwezekani kabisa.



“Nimesema nitaifanya shughuli hii. Wakuu hebu ondoeni shaka zeni na tufokasi zaidi katika afya ya Rais” Inspekta Tom Green aliongea.



“Dokta Morgan naomba schedule to the deadline!” Inspekta Tom Green aliongea akimtazama dokta Morgan ambaye alikuwa ameshikilia nyaraka fulani mkononi.



“Kwa sasa tumefanikiwa kuizuia damu isiendelee kuvuja katika jeraha. Kwa kiwango cha damu kilichopo katika mwili wa Rais, hatakuwa na maisha marefu kama hataongezwa. Kwa makadirio ni masaa tisini na sita. Yaani tuna siku nne kabla ya mheshimiwa Rais hajapoteza maisha kama hatoongezwa damu!” dokta Morgan aliongea.



“Siku nne nyingi sana kwangu. Kabla ya masaa tisini na sita nitakuwa hapa na Martin Samweli. Dokta Morgan trust me. I will bring you Martin Samweli before the deadline!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Nakuamini sana kamanda. Naamini kila kitu kitakwenda salama kabisa na Rais atarejea katika kiti chake salama” dokta Morgan aliongea.



“Wakuu, naomba nikaanze safari. Sina muda wa kuendelea kupoteza!” Inspekta Tom Green aliwaaga wale wakuu wa usalama.



“Nadhani ninahitaji kwenda na kijana wangu kwa maandalizi. Tutakutana baadaye kidogo wakuu!” Chifu naye aliongea akianza kuondoka akiambatana na Inspekta Tom Green.

******

KATIKA OFISI ZA BSA



“Wazee, kama ambavyo nilizungumza hapo awali, nina misheni kubwa sana katika misitu ya Masolo ambako ninatakiwa nimlete bwana Martin Samweli mwanajeshi kutoka kikosi cha waasi cha BMM kwa ajili ya blood donation kwa mheshimiwa Rais” Inspekta Tom Green aliongea.



“Kwa nini tusiende wote mkuu maana misheni hii ni ya hatari” Inspekta John Michael aliongea.



“Kama ulivyokwishasema kwamba misheni hii ni ya hatari sana. Hatutakiwi kukirisk kikosi chote. Acha niende mwenyewe. Ninawamudu wale jamaa katu hawawezi kunipa shida!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Uko sahihi kabisa mkuu. Pekee wawaweza wale jamaa but you need mya company!” Latoya aliongea.



Inspekta Tom Green alibaki kimya akimtazama Latoya. Hakufahamu ajibu nini.



“You don’t have to say no. tutakwenda pamoja!” Latoya alisisitiza.



“Yes boss. Unahitaji kampani ya Latoya!” Hashim naye alisisitiza.



“Ok, hebu kajiandae tuanze safari kwani hatuna muda wa kupoteza. Muda ni finyu sana kwetu!” Inspekta Tom Green aliongea akimtazama Latoya.



“Rodger that boss!” Latoya alijibu na kusimama kwa ajili ya kwenda kujiandaa.

******





“Ok, hebu kajiandae tuanze safari kwani hatuna muda wa kupoteza. Muda ni finyu sana kwetu!” Inspekta Tom Green aliongea akimtazama Latoya.



“Rodger that boss!” Latoya alijibu na kusimama kwa ajili ya kwenda kujiandaa.



SASA ENDELEA



NDANI YA CHOPA



“Kwa jinsi uhitaji wa damu hii ulivyokuwa wa muhimu, tunahitaji kutumia siku moja tu kuhakikisha kwamba tumempata bwana Martin Samweli na kumfikisha Kano” Inspekta Tom Green aliongea.



“Ni kweli usemayo kamanda. Lakini naona mazingira ya kambi ile siyo rafiki kuitimiza misheni hii kwa haraka kiasi hicho” Latoya aliongea.



“Umeongea sahihi kabisa Latoya. Ni kweli katika kambi ile kwa mujibu wa ramani imegawanyika katika sehemu mbili. Kwanza kabisa kuna makazi ya wananchi wa kawaida na upande wa pili kuna kambi ya jeshi. Sasa katika misheni hii tunatakiwa tuvifanye vile visivyowezakana viwezekane. Sisi ni askari wenye mafunzo ya hali ya juu. Naamini hili litawezekana. Kumbuka maisha ya Rais kwa sasa yapo mikononi mwetu!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Kuvamia kambi ni jambo dogo. Ugumu ninaouona hapa ni namna ya kumshawishi askari huyu kuondoka na sisi” Latoya aliongea.



“Hiyo itawezekana tu. Akikataa basi itatubidi kutumia njia ya pili yaani kuhakikisha kwamba anafika Kano ndani ya muda uliopangwa apende asipende!” Inspekta Tom Green aliongea.



Wakati huo chopa iliendelea kukata anga. Rubani alikuwa makini kabisa kuhakikisha kwamba anakiongoza chombo katika hali ya usalama. Kipindi hicho chote Inspekta Tom Green pamoja na Latoya waliendelea luzungumza hiki na kile katika kuiboresha mikakati yao ya uvamizi katika kambi ile ya waasi. Mioyo yao ilikuwa na ari kubwa sana ya kufanya misheni ile kwa mafanikio ili kuyaokoa maisha ya mheshimiwa Rais.



Mwendo wa masaa matano uliwafikisha katika eneo la misitu ya Masolo.



“Nadhani wewe utushushe hapa na ugeuke kurejea Kano. Eneo hili kwa sasa siyo salama kabisa. Haitakiwi waasi hawa wabaini uwepo wetu mapema kabla ya misheni kukamilika!” Inspekta Tom Green aliongea.



“Sawa mkuu!” rubani alijibu huku akiishusha chopa ile mahali fulani ndani yam situ.



Baada ya hapo Inspekta Tom Green na Latoya walishuka. Chopa ilipaa na kurudi ilikotoka.



“Haya mama. Let’s start the game!” Inspekta Tom Green huku akibeba begi lake ambalo lilikuwa na silaha.



“Rodger that darling!” Latoya alijibu huku naye akilibeba begi lake mgongoni.



Baada ya hapo walianza safari ya kusonga mbele huku silaha zao zikiwa mikononi mwao. Walikuwa makini sana kila walipotembea kwani walifahamu kwamba msitu ule ulikuwa ukimilikiwa na waasi hivyo hatari yoyote yaweza kutokea.



Mwendo wa saa moja uliwafikisha katika kijiji ambacho kilikuwa kikimilikiwa na waasi lakini walikuwa wakiishi raia wa kawaida. Hii ina maana kwamba utawala uliokuwepo katika kijiji kile ulikuwa ni utawala wa waasi chini ya Kanali Edson Makoko.



Inspekta Tom Green na Latoya hawakutaka kupita katika kijiji hiki. Hii ilikuwa ni kwa sababu za kiusalama. Walichokifanya ni kuambaa ambaa pembezoni mwa kijiji kile na kuendelea kusonga mbele wakiifuata ramani ya msitu ule ambayo walikuwa nayo.



Baada ya muda fulani wa kutembea, hatimaye walianza kuyaona majengo ya kambi ya jeshi. Majengo hayo vilikuwa ni vibanda ambavyo vilikuwa vimejengwa kwa miti na kuezekwa nyasi wakati vingine viliezekwa kwa bati.



“Haya sweetheart, tumekwishafika tayari. Ngoja tuwaonyeshe shoo moja matata sana!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Yes darling, let’s pop in!” Latoya alijibu.



Walianza kutembea kwa tahadhari kubwa sana mpaka walipokifikia kibanda cha kwanza ambacho kilikuwa kimejengwa miti na turubai.



Walipochunguza vizuri kuna kitu walikigundua. Vibanda vile vilikuwa na majina. Majina yale yalikuwa ni ya askari ambao wanaishi ndani ya vibanda hivyo.



Mungu alikuwa upande wao kwani kibanda ambacho walikuwa wamekifikia kwa mara ya kwanza kilikuwa kimeandikwa Martin Samweli hii ikimaanisha kwamba mtu wao ambaye walikuwa wamemfuata ambaye ni Martin Samweli alikuwa akiishi ndani ya kibanda kile.



Inspekta Tom Green alimwonyesha ishara Latoya kwa kutumia kichwa chake na Latoya alijibu kwa kuonesha idara ya dole gumba. Hii ilimaanisha kwamba alikuwa amemwelewa Inspekta Tom Green. Kwa tahadhari kubwa sana Latoya alizama ndani ya kibanda kile huku Inspekta Tom Green akiwa anaangalia usalama upande wa nje.



Kwa wakati huo yalikuwa ni majira ya saa nane za mchana. Martin Samweli alikuwa amejipumzisha juu ya kitanda chake ndani ya kibanda kile usingizi ukiwa umempitia. Latoya alimgusa Martin Samweli kumuamsha ambapo Martin alishtuka ghafla na kuishika bastola yake mkononi.



“Wewe ni nani na umefuata nini hapa!” Martin Samweli alifoka huku akimtazama Latoya.



“Naitwa Latoya. Ninatoka Kano. Nimekuja hapa kwako kwa sababu nina shida kubwa sana. Na sina muda mrefu wa kuendelea kuwepo hapa!” Latoya aliongea.



Martin Samweli alimtazama Latoya usoni na kuvutiwa na sura nzuri nay a kirembo ya Latoya. Sura ile ilimfanya Martin Samweli apunguze munkari wake kwani aliamini mwanamke huyu hawezi kuwa hatari kwake. Na hili ndilo kosa kubwa sana alilolifanya. Alikosea sana kumwamini Latoya. Hakufahamu kwamba Latoya alikuwa ni mwanamke hatari zaidi ya hatari yenyewe.



“Una shida gani?” Martin Samweli aliuliza.



“Hali ya mheshimiwa Rais ni mbaya sana kwani amejeruhiwa kwa kuchomwa kisu. Kuna uhaba wa damu ya kumwongezea. Rekodi zimeonyesha kwamba damu yako ndiyo inafanana na ya mheshimiwa Rais” Latoya aliongea.



“Unasemaje wewe kenge. Yaani huyo mtu unayemsema ni adui yangu namba moja. Kwanza ilikuwa inafahamika kwamba amekufa, kumbe amenusurika. Halafu nashangaa umefikaje hapa pasi kuonekana!” Martin Samweli aliongea huku sasa akiwa amemwonyeshea Latoya bastola.



“Martin Samweli nadhani kuna mambo mengi sana ambayo mnapotoshwa na huyu kiongozi wenu Kanali Edson Makoko. Yeye anachokitaka ni kuwatumia ili aweze kutekeleza adhma yake ya kuwa Rais wa Bantu. Ninachokuomba kuwa mzalendo na itetee nchi yako!” Latoya aliongea.



“Hebu ondoa ngonjera zako hapa!” Martin Samweli alizidi kufoka.

****





“Martin Samweli nadhani kuna mambo mengi sana ambayo mnapotoshwa na huyu kiongozi wenu Kanali Edson Makoko. Yeye anachokitaka ni kuwatumia ili aweze kutekeleza adhma yake ya kuwa Rais wa Bantu. Ninachokuomba kuwa mzalendo na itetee nchi yako!” Latoya aliongea.



“Hebu ondoa ngonjera zako hapa!” Martin Samweli alizidi kufoka.



SASA ENDELEA



“Hebu fikiria athari zitakazopatikana na vita ambayo mnataka kuianzisha. Hebu fikiri ni maisha ya watu wangapi wasio na hatia ambayo yatapotea. Fikiria kama katika wahanga wa vifo hivyo wanakuwepo watu wa familia yako. Ni uchungu kiasi gani utaupata? Hebu kuwa mzalendo kwa kuokoa maisha ya Rais. Hakika utatangazwa shujaa wa Taifa na makosa yako yote yatafutwa!” Latoya aliongea.



“Nimekwambia nyamaza kunguni wewe. Kwanza inabidi nikuripoti ili uweze kukamatwa na kuuawa kidudumtu wewe!” Martin Samweli alifoka.



“Samahani sana brother. Hilo haliwezi kutokea!” Latoya aliongea.



Wakati huohuo aliipangua bastola ya Martin Samweli na kisha alimbandika ngumi ya uso. Martin Samweli alihisi nyotanyota. Kabla hajatahamaki mateke matatu mfululizo yalitua kichwani kwake na kumbwaga chini.



Baada ya hapo Latoya alimpa Martin Samweli pigo la nyuma ya kisogo ambalo lilimfanya apoteze fahamu. Latoya aliibonya batani Fulani katika saa yake ambapo muda huohuo saa ya Inspekta Tom Green kule nje ilipiga mlio. Inspekta Tom Green aliingia haraka sana ndani ya kibanda kile. Ndani ya kibanda aliweza kuushuhudia muziki ambao alikuwa ameucheza Latoya.



“Ha ha ha haaaaa! You are the beast!” Inspekta Tom Green aliongea huku akimbeba Martin Samweli begani mwake.



Baada ya hapo safari ya kutoka katika kambi ile ilianza. Mwendo ulikuwa ni wa haraka sana. Mbele kidogo waliweza kuliona gari ambalo lilikuwa limeegeshwa. Walimwingiza Martin Samweli ndani ya gari lile. Inspekta Tom Green aliliwasha na kasha waliondoka kutoka eneo lile.

*******

Mwendo wao ulikuwa ni wa kasi sana. Ndani ya muda mfupi walikuwa wamekwishakikaribia kile kijiji ambacho kinamilikiwa na waasi. Pale waliamua kutumia akili ya kikomando. Waliamini kwamba kama wangelipita na gari lile pale kijijini, basi waasi wangeliweza kushtuka na kuanza kuwaandama.



Inspekta Tom Green alichepusha gari kutoka barabarani na kuliingiza ndani ya msitu. Aliliingiza ndani kabisa na kasha alisimama. Kwa wakati huo bwana Martin Samweli alikuwa bado amezirai. Na alikuwa amefungwa mikono yake ili kama ataamka basi asiweze kuleta matata.



“Now we walk!” Inspekta Tom Green aliongea.

“Yes ofcourse!” Latoya alijibu.



Walishuka kutoka kwenye gari. Inspekta Tom Green alimbeba bwana Martin Samweli begani na kisha safari ya kusonga mbele ilianza.

*******

KAMBINI BMM



“Mkuu kuna tatizo limejitokeza!” mwanajeshi mmoja aliongea mbele ya Kanali Edson Makoko.



Hii ilikuwa ni ndani ya ofisi ya Kanali Edson Makoko ambaye alikuwa bize toka asubuhi akiuandaa mpango wa mapinduzi.



“Tatizo gani?” Kanali Edson Makoko aliuliza.



“Martin Samweli ametoroka kambini” mwanajeshi yule aliongea.



“Una maana gani?” Kanali Edson Makoko aliuliza tena.



“Ameasi mkuu. Ameacha ujumbe kwamba ameamua kurudi serikalini na kuomba msamaha” mwanajeshi yule aliongea.



“Shiiiit! Asakwe mara moja na kurudishwa hapa. Anaifahamu siri na mipango yetu mingi sana!” Kanali Edson Makoko alifoka.



Wakati wanaondoka baada ya kumteka Martin Samweli, Inspekta Tom Green aliacha ujumbe kwamba akijifanya ni Martin Samweli ndiye ambaye aliuacha. Kitendo hiki kilikuwa na maana kubwa sana kumbuka kamba maafisa hawa wa BSA kila jambo walitendalo, hulitenda kwa kutumia akili kubwa sana.



“Ita paredi mara moja. Mbwa huyu ni lazima arejeshwe hapa mara moja!” Kanali Edson Makoko alifoka.



“Sawa mkuu!” mwanajeshi yule alijibu huku akipiga saluti na kuondoka mle ofisini.



Baada ya dakika mbili king’ora kilisikika pale kambini. King’ora hiki kiliashiria kwamba kulikuwa na hali ya hatari ambayo ilikuwa imetokea. Wanajeshi kutoka kila kona ya kambi ile walianza kukusanyika katika uwanja mkubwa sana pale kambini ambao hutumika kwa ajili ya paredi.



Baada ya kujipanga katika mistari mingi iliyonyooka, Kanali Edson Makoko aliwasili eneo lile. Kila mwanajeshi alikuwa kimya akiwa na shauku ya kusikia ni nini kilikuwa kimetokea.



“Soldiers, kuna tatizo moja limetokea. Kuna mmoja miongoni mwetu ameasi jeshi na sasa yuko mbioni kwenda kujikabidhi kwa serikali. Mwenzetu huyu ni askari Martin Samweli!” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo.



“Haaaaaa!” wanajeshi wote walishangaa.



“Sasa bwana huyu anazijua siri zetu nyingi pamoja na mipango yetu yote. Akifika mikononi mwa serikali tu, basi itakuwa ni rahisi sana kwa serikali kutuvamia na kutushinda. Hivyo basi ninaagiza kwamba ndani ya muda mfupi bwana huyu awe amerejeshwa hapa akiwa mzima kabisa. Nitamuua kwa mkono wangu!” Kanali Edson Makoko aliongea.



“Haya tawanyikaaaaa!” Kanali Edson Makoko alifoka.



Wanajeshi walianza kutawanyika na kwenda katika ghala la kuhifadhia silaha. Walichukua silaha na kisha waliingia msituni tayari kumsaka bwana Martin Samweli. Kulikuwa na askari wa miguu ambao walikuwa na mbwa maalum, kulikuwa na askari wa anga pamoja na askari wa miguu. Kwa kifupi jeshi la Kanali Edson Makoko lilikuwa limekamilika hasa.

*******

Safari ya Inspekta Tom Green, Latoya pamoja na mateka wao ilikuwa bado inaendelea ndani ya msitu wa Masolo. Mateka wao alikuwa bado yupo katika hali ya kupoteza fahamu. Hii kwa kiasi kikubwa iliwapa urahisi wa kusonga mbele pasi upinzani kutoka kwa mateka wao. Kwa sasa walikuwa eneo ambalo lilikuwa na mto mkubwa sana. Hiki kilikuwa ni kizingiti kikubwa sana katika kuendelea na safari yao.



“Sasa tunafanyaje hapa?” Inspekta Tom Green aliuliza.

“Tunahitaji boti” Latoya aliongea.

*****





“Sasa tunafanyaje hapa?” Inspekta Tom Green aliuliza.

ITAENDELEA

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog