Search This Blog

Friday 30 December 2022

KIAPO CHA MFUNGWA (6) - 5

    

Simulizi : Kiapo (Mtetezi Wa Kinte) (6) 


Sehemu Ya Tano (5)



'huyu Mshenzi Najua hana nia nzuri na mimi, laiti kama angekuwa mzur asingenificha hili angeniweka wazi kuwa nilitekwa na mafia ikawa hivi,kikafatia hiki tujue jinsi ya kufanya ila eti wanakubaliana kaz ikikamilika anaruhusu waniue kwel mfadhili mbuz binadamu ana maudhi,'



Zidu alizidi kuwaza,ila ghafla alihisi kuna gari ilikuwa ikimfata kwa nyuma,kwa makusudi akaiacha barabara ile ielekeayo Ikulu Na Kukata Kushoto Kama Anaelekea Jijini Wami,alifata Lami Mpaka Katika Njia Panda Moja Akaiacha Njia Ya Wami Akachukua Njia Ya Msovero,bado gari ile ilikuwa ikimfata kwa nyuma!,akaachia cheko la dharau



"bila shaka hawa ni maadui wengine sijui nimewakosea nini mimi"



Zidu aliongea kwa sauti kama anaongea na mtu mule ndani,ila ukweli alikuwa peke yake,akaishika silaha yake,taratibu aka anza kupunguza mwendo gari ile ikamfikia na kumuwashia taa za kumuomba kumu ovartake akaruhusu,kama alivyotegemea gari ile ikamzuhia kwa mbele ikabidi asimamishe gari yake,mkono wake wenye silaha akauelekeza mbele tayari kwa lolote,zilipita kama dakika tatu pasina chochote kuendelea ni kama walikuwa wakitegeana ni nani aanze!,naye akuwa mpumbavu kushuka alisubiri kuona mwisho wao ni nini!



Kama Ni Kushambulia,alisubiri Wamuanze Naye Awaoneshe Uwezo Wake!...



Ghafla Upande Wa Kushoto Anapokaa abiria ukafunguliwa,Zidu macho akayakaza kuangalia ni nani anatoka!



Ghafla alishtuka,na silaha ikamponyoka,macho akayatoa pasina kuamini kile akionacho!...



Mbele Yake Alitazamana Na Mtutu Wa Bastola!



Alianza Kutetemeka,na Mwili Kumsisimka,akataka kufumbua mdomo wake kutamka kitu akashindwa,akabaki kaganda huku akitetemeka!



Mtu Yule akawa akimsogelea taratibu huku akitabasamu!



*NI NANI MTU HUYO*



Hili bado alikujulikana...



***



HIMAYA YA MAJINI



KUZIMU LAND



Ni chini kabisa ya Ardhi, kupitia njia ya msitu mtimbuyu,vilio vilisikika,

mmoja wapo wa wafalme wa familia kubwa iitwayo kidombokwezo,alikuwa amefariki na simanzi zilitawala katika kasri yote ile!



Upande Wa Wajomba Wa Marehemu Na Mashangaz Waliketi Katika Kikao Kidogo



"tumetuma Masowati Wakamlete Binadamu Alousika Na Mauaji Ya Ndugu Yetu Lazima tumle nyama na damu yakendo kinywaji chetu!

"ha ha ha ha"

maviumbe wale walicheka ghafla masowati hao waliotumwa wakatokea wakiwa na mwili wa marehemu mfalme wao pamoja na muuaji Fatma,alokuwa akilia na kushangaa kule alipokwepo!



vibwengokwezo ilikuwa ni jamii ya majini wafupi wapatikanao huko ujinin wenye damu nyeusi...



Mfalme Wao Ndiyo alomwingilia Olomy Na Kumwangamiza Odovy,akamkimbiza Fatma Na Kumbaka Lakin Kwa Bahati Mbaya Alikufa,na Vibwengo Wale Wakamteka Fatma Na Kumpeleka Kule Himayan Mwao!



Baada Ya Viongozi Wale Kumfikisha Katika Wanakoo Wa Koo Ile Kubwa Wanakoo Wajomba Na Mashangaz Wakamtoa Nje Palipo Na Koo Nzim a ile ya vibengokwezo,wote waliwapokea kwa kilio,na hasira,walikuwa na jazba,Fatma alijua kupona kwake ilikuwa ngumu kwa mazingira yale,akasubiri kuona kitakachotokea...



wakawasha moto mkubwa wakaweka sufuria la mafuta,yakachemka,sasa wakambeba Fatma kwa lengo la kwenda kumdumbukiza wamchome mzima mzima na kuitafuna nyama yake!...



Fatma alilia akirusha miguu huku na kule ila awakumwachia,walimshika madhubuti...

wafafika katika sufuria lile wakamdondoshea....



*DAH SIJUI KAMA ANGESALIMIKA*



MSITU PANDE



Gambi alifumbua macho kichwa kilikuwa kizito ni sauti za nzege na ndege ndizo alizozisikia zikilia,a kanyanyuka na kukaa kitako!

akawa akishangaa maeneo yale alokwepo,akajaribu kuvuta kumbukumbu,



AKAKUMBUKA



Ghafla akasimama taratibu na kuanza kurudi nyuma akiushangaa ule mti...



"ha ha ha kimbiaaa Nimekwambia kimbiaaaaa"



Ghafla akashtuliwa na sauti kali,pale pale acha aanze kukimbia ghafla akapamia kitu kama kisiki akaenda chini kuinua kichwa akuamin kile alichokiona,ni kile kibwengokwezi,akakipiga teke akiwa palepale chini akanyanyuka na kuanza kukimbia,kiumbe kile kilizidi kumkimbiza japo akikuwa na spidi mwisho akakipoteza,kwa kuwa alikuwa amechoka,akaketi mahali kwa lengo la kujipumzisha...





Gambi Pale alipolala aligundua si mahali salama sana!,kwa Kuwa Palikuwa Na Uwazi Na Miti Kidogo Ilikuwa Mbali Mbali Ivyo akaona ni rahisi kukutwa na vile viumbwe vibwengokwez akanyanyuka na kuendelea na safari!,ghafla akahisi hatua nyuma yake kugeuka ni vibwengo ila vilikuwa mbali sana safari hii vilikuwa vingii kitendo cha kugeuka tu vikaanza kucheka!,...



Kufumba Na Kufumbua hivyo hapo,"umeniona wapi?"

Vikamuuliza,gambi Akujibu akabaki tu kapigwa na butwaa kwa haraka vikaweka duara,gambi kati vitatu vikapandiana ndo vikafika urefu wa Zidu Yule Wa Juu Akamtandika Kibao shavuni huku akifoka "nakuuliza umetuonea wapi?!"



Gambi akavisukuma vikadondokea kule akaruka katik ya mikono ya wawili waloshikana acha aanze kukimbia,vile vikawazingira wenzao walodondoka kila kiumbe kikawa kikiongea chake kwa mfumo wa manung'uniko...



Gambi akazidi kimbia katikati ya ule msitu,ghafla akakanyaga mahali kumbe palikuwa na shimo,akaanza kwenda chini akiachia yowe...



*****************



Kule Upande Mwingine Fatma baada ya kunyanyuliwa juu juu wakamrushia ndani ya pipa lililo chemka mafuta,ila kabla ajatua pipani ghafla akanata na kuja juu ni kama alikuwa akivutwa na nguvu flani akavutwa mpaka juu na kutupwa chini,vile viumbe sasa vikawa kwenye mshangao ghafla ikasikika sauti...



"nikosa kubwa sana mnalofanya hanakosa huyo binadamu kivipi mumuhukumu?"



"katuulia mfalme wetu kivipi tumuache hai"



Kwa Pamoja Vile Viumbe Vikaijibu Ile Sauti Nayo Ikajibu...



"nasema Mnakosea Sana,ana hatia huyo binti na wala si yeye aliyemuua mfalme wenu,hawa walikuwa wakija kwangu kwa bahati mbaya nyie mkawa ingilia na mfalme wenu akaingia katika mwili wa mmoja wao na kumtuma apambane na mwenzake akamuua,huyo fatma kuona ivyo akakimbia mfalme wenu akaanza mkimbiza kwa bahati mbaya binti alidondoka ndipo kibwengo mkuu alipomwingilia akisahau kwamba huyu ni binadamu,na nyinyi ampaswi kufanya mapenzi na binadamu ni kifo ivyo huyo binti ana hatia na ikiwa mtamwangamiza mtapata laana katika kizazi na kizazi mwonesheni huyo binti njia ya kufika hapa nilipo"



Sauti Ile Ikakata,minong'ono Ya Chini Kwa Chini Ikaanza,hatimaye Viongoz Wa Koo Ile Wakakaa Chini Kuongelea Jambo Lile,mwisho Wakaafiki Kumpeleka Fatma Mahal Alipo Mganga Ndumbwendumbwele,ni Mtu Waliyemuheshimu Na Kumsikiliza Kwa Kila Akisemacho,akapewa Watu Wawili Safari Ikaanza...



********



Zidu K ' akabaki akimwangalia yule mtu akija ile gari ilomleta ikageuza na kuondoka



"ka..ka.katarin?"



Zidu akaita pasina kuamini,kama yule alokuwa akimjia ni mke wake Katarina alitegemea muda huo angekuwa nyumban kumbe anamfatilia...



Akarudisha Silaha Yake Mahali Pake,katarina Akafungua Mlango Na Kuingia Akaketi



"una Nin Mume Wangu?!"



"Raisi Mimi Wa Kunifanyia hivi?"



Ikabidi Zidu aanze kumsimulia mke wake kila kitu alichogundua katika zile audio kule kwenye mitandao ya simu



"mh! kwa hiyo kumbe Rais anataka akutumie tu ukishamdhibiti gambi awaachie mafia wakwangamize"



"na ndo maana nataka kwenda kumuua mwanaharamu huyo"



Zidu akaongea kwa jazba akijiandaa kuliwasha gari lake ila Katarina Akamzuhia



"hapana mume wangu,punguza jazba,wewe ni usalama wa taifa my tena explores kwanin unakuwa ivyo,je kama rais kawalaghai tu ili wa kuachie?"



"kuwalaghai si lazima angeniambia nilitekwa na watu gan na kaniokoa kwa makubaliano gan kusudi nijipange lakin yey mpaka sasa ajanambia..."



"ungekurupuka Zidu Kuwakabili Ukisahau Kwamba Una Kaz Ya Rais,jua Ilo,ivyo Rais kukuficha siyo kwamba ana malengo ya kukugeuka kikubwa tuliza akili fanya kazi yake kwa umakin huku naye ukimchunguza kujua kusudio lake!"



"mmmh!,lakin ni kwel,haya nambie na wewe kisa cha kunifatilia mpaka kufika hapa"



Katarina akacheka kidogo,kisha aka endelea...



"cp Magreth ndo kanitext alikuwa pale bar akanambia laaziz wako shoga sijui kakumbwa na nin anapuliza hizo chupa,chukua boda boda haraka njoo,ndo nkachukua bodaboda kufika tu pale bar nawe ndo unaondoka nikamwambia Mage akufate ndo mpaka hapa akakutanga kwa mbele mi nikashuka twende zetu nyumbani mume wangu"



Zidu akawa kashaelewa, akaliwasha gari na kurejea alipotoka,aliamua kumsikiliza mke wake...



Akaamua Kuendelea Na Opereshen Ya Kumsaka Gambi Wakati huo huo akimchunguza na raisi,



TUTASONGA HAKUNA NAMNA







wakati Gambi anakimbia mara ghafla alikanyaga sehemu iliyotitia akadondoka kisha akatumbukia ndani ya shimo refu sana Tiiiiii



Akapoteza fahamu



alipozinduka alishangaa kujikuta amelala chini alipatazama upande wa juu aligundua kuwa yumo ndani ya shimo...



'Sasa nimefikaje humu' Gambi alijiuliza ndipo kumbukumbu ikarudi alikumbuka kuwa alikuwa anawakimbia viumbe wa ajabu ambaye hata yeye mwenyewe hakufanikiwa kuvitambua viumbe hao...



Viumbe vifupi vyenye roho mbaya Gambi alijikuta akiogopa sana alipotazama vizuri aliona kama kunauwazi sehem akaamua kupita kwenye uwazi huo.....



aliifuata njia hiyo ambayo ilikuwa iko chini ya aridhi....



wakati anazipiga hatua alikuwa anajiuliza maswali njia hii itatokezea wapi???



lakini alijipa moyo bila shaka hili ni handaki hivyo basi lazima kutakuwa na njia ya kutokezea nje..



baada ya kuwaza hivyo alianza kuzipiga hatua za harakaharaka..kutokana na giza lililokuwemo humo ndani ya hiyo njia ya chini kwa chini ya aridhi....kidume Gambi alijingonga gonga kwenye kingo za njia ile



alianza kuona mwanga



alipotazama kwa makini aliona ni mwanga wa Jua....



akaanza kuzipiga hatua za haraka haraka kuelekea kunako mwanga huo...alipoukaribia aliona njia ikionesha upande wa nje aliona miti alifurahi sana kisha akaifuata njia ile ili atoke nje....



kabla ya kutoka ghafla alipiga breki mdomo akauachama kwa khofu macho yake aliyatoa Pima akitazama nje kwa uoga



Alitazama kwa makini mti mmoja ndipo alipogundua mti ule ulikuwa ukijongea..



Kumbukumbu za ule mti alowah kuupanda ukaanza kutembea akaruka zikamjia ila mti ule alokuwa akiutazama ulikuwa mdogo



'Nipo katika dunia gani mimi jamani?!'



Gambi akawaza akizidi kujibanza zaidi katika kingo za shimo lile macho yake yakiangalia nje upande anapoelekea kiumbe Yule jamii ya mti



Baada ya kiumbe kile kupotea machoni mwake Gambi kabla ajatoka akaanza kuangaza angaza macho yake alipo tazama kwa mbali alishtuka kuona mafuvu na mifupa mingi ya binadamu......



Gambi aliogopa sana akajua siku ile ndio mwisho wa uhai wake....



Inamaana kuna binadamu walishafikaga huku na kuuwawa mifupa yake na mafuvu ya vichwa vyao vikaifadhiwa pale?!



Gambi aliwaza akikumbuka pia alipompoteza mwenzao Odovy baada ya kushambuliwa na Olomy bila shaka naye fuvu na mifupa yake ingeletwa pale



Akujua kama Odovy alishakufa wala hakuwa na habari na Fatma



Ila alipofikiria kutoka nje,moyo ulisitq



Gambi aliogopa kutoka nje akutaka kuzibishia hisia zake aliamua kubaki kulekule ndani ya shimo ...



Aliikaa kwa muda kama wa lisaa limoja alipoona pako kimya ndipo alipoamua kutoka aondoke eneo lile



Ile anaotoa mguu wake nje ghafla alimuona yule kiumbe wa ajabu anayefanana na mti anarudi huku ameninginiza kiwiliwili cha binadamu...



kiwiliwili hicho kilionekana kuanzia upande wa tumboni kuelekea kichwani...bila kuwa na sehemu ya chini yani kiuno na miguu....



Gambi aliogopa sana.



kiumbe kile kadri kilivyokuwa kikisogea na Gambi kukitazama alishtuka akuamini macho yake kwa kile alichokiona.....



Aliogopa zaidi baada ya kuona kiwiliwili hicho kilikuwa ni Odovy



Hasira zikampanda,ujasiri ukamvaa akajikuta woga ukimtoka na kutoka ndani ya shimo lile huku akiwa kakunja sura alijua yule kiumbe ndicho kilichompoteza rafiki yake yule



Kitendo cha kupiga kelele za jazba kilimshtua yule kiumbe akajikuta akiuachia ule mwili na kumwangalia Gambi kwa mshangao jinsi alivyokuwa akimfata



Gambi kumfikia akamtandika teke ila ilikuwa ni kama kuupiga mti teke akajikuta akiumia mwenyewe mti ule aukutetereka



Akajaribu kuukamata eneo la juu na kuutingisha aukutingishika



Sasa akaugeukia mwili wa Odovy na kuufata akaanza kuulilia

Alijua kijana yule alikufa kwa ajili yake



Kwa ajili ya kisasi chake wakati akiendelea kulia ghafla ule mti ulokuwa nyuma yake mkono wake ulirefuka mpaka ilipo shingo ya Gambi na kumnyanyua juu



Huku akicheka akaanza sasa kumnyonga,alimnyonga bila huruma Gambi alitupa tupa miguu ila mti ule ulizidi mnyonga ghafla giza likaanza kutanda kwenye macho yake



Pumzi zikaanza kumkata ni wazi ule sasa ndo ulikuwa mwisho wa maisha yake....







Wakati Viumbe Vile Vyenye Umbo La Mti Vikiwa Vimemzingira Gambi Mara ghafla vikatoweka na kumuacha gambi katika mshangao,wakati akiwa katika mshangao mara viumbe vingine vikamtokea na kumzunguka,vilikuwa ni vibwengokwezi,



Viumbe Vile Vyenye Asili Ya Mti Na Vibwengo Mara Nyingi Vimekuwa avipatani,ni kama paka na panya vibwengo walikuwa wakivikuta vilamwi ilikuwa lazima waviangamize na vilamwi walivigundua vibwengo kwa harufu yake ndipo vilipotoweka punde tu vibwengo vikatokea na kumzunguka Gambi Vikawa Vikizungumza Lugha Isiyoeleweka Huku Vikionekana Kuwa Na Furaha,gambi alikumbuka jinsi alivyovitoka ile le mara ya kwanza wakati walipo mzunguka na baadhi kubebeshana,



Safari hii avikumpa muda mmoja wako akampiga kombora wakatoweka wote!...



***



Macho Yalikuwa Mazito Kufumbuka,alihisi Maumivu Makali Ya Kichwa,hivyo Hivyo akajitahidi kuyafumbua macho yake kwa shida sana yakafunguka...

akapeleka mkono wake kwenye macho akakutana na lindi la matongo tongo,akajitahidi kuyatoa hivyo hivyo kwa shida huku akijitahidi kukumbuka kilichotokea



'nipo wapi?!' wazo hilo likapenya katika mawazo yake na kumfanya ajaribu kuamka pale alipolala,



Alikuwa Ndani Ya Chumba Kimoja Kidogo,akiwa Kalala Juu Ya Kitanda Chakamba ambacho kilikuwa kimetandikwa ngozi ya kulalia,gambi akakaa kitako,macho yake akaya angaza kukisanifu chumba kile,kilikuwa na mwanga kidogo,ulopitisha hewa pia kule ndani kulikuwa na vyungu viwili vikubwa ambavyo akuweza kung'amua mara moja vyungu vile vinanin ndani,na wala akuwa na muda wa kutaman kujua hilo...



Akili yake alikuwa akiishurutisha kujaribu kuilazimisha akumbuke ni wap pale alipo na nin kilicho mtokea mpaka kuwa pale,baada ya kujaribu kuvuta sana kumbukumbu mara akakumbuka alipokuwa akikimbizwa na vile viumbe wa ajabu vyenye umbo la mti,vikamuweka kati ila ghafla tu vikatoweka na kablajafanya kitu viumbe vingine ambavyo alivitambua kwa jina la vibwengo vikatokea na kumuweka kati ghafla kimoja kilimnyooshea mkono akahisi kizunguzungu,akujua kilichoendelea...



Wakati akiendelea kutafakari,mara ghafla mlango ukafunguliwa,gambi akakaza macho kuangalia ni nani alokuwa akiingia,ghafla aliyatoa macho ya mshangao pasina kuamin kile akisemacho...



"fa..fat..fa.fatma..ni wewe?!"



Akajikuta akiongea kwa kigugumizi pasina kuamini kile akionacho,binti yule kwa furaha akapiga hatua ndefu ndefu mpaka alipo Gambi akamkumbatia



"nimefrah umezinduka Gambi,"



"upo hai Fatma?"



Gambi aliuliza pasina kuamini kile akisemacho,



"nipo hai Gambi furaha yangu kuona nawe upo hai na umezinduka"



"kwan Hapa tupo wapi Fatma na ulinikuta wapi maana mi sikumbuki kitu?!"



"ni stori ndefu sana Gambi lakin tambua upo mahali salama tupo kwa maganga ndumbwe ndumbwele"



Gambi akatabasamu,



"nimefikaje sasa hapa?!" akauliza sasa akiwa mwingi wa furaha,



Ikabidi Fatma aanze kumsimulia toka pale walipoachana kila mmoja kukimbilia njia yake,jinsi Olovy alivyobahatika kumkamata na kumbaka,alivyokufa,viumbe wale vibwengokwezi walivyomtokea na kumbeba walivyotaka kumla nyama ndipo mganga yule alipopaza sauti yake kumtetea, akaamrisha apelekwe

Baada Ya Kupelekwa Kwa Mganga Ndumbwendumbwele Ndipo Nilipokuombea Nawe Mganga alipotazama aligundua unakimbizwa na vilamwi ndipo alipoviagiza hivi vibwengo vikakulete,vilamwi viliposikia harufu ya vibwengo vilitoweka na kukuacha ndipo vibwengo vilikuchukua na kukuleta huku!...



Gambi alista ajabu maongezi yale ilikuwa ni kama akisimuliwa riwaya ya kufikirika au alijihisi yupo ndani ya ndoto ila akuweza kuubadilisha ukwel ule kuwa ndoto kama alivyofikiria...



"nataka kwenda kumuona huyo ndumbwendumbwele"



Akapeleka Ombi Lake,akinyanyuka Fatma hakuwa mbishi,akamkubalia wakatoka nje!



Nje kulikuwa na nyumba za makuti kadhaa,wakaongoza mpaka katika nyumba moja kubwa,walipishana na vile vibwengokwez na viumbe vingine vya ajabu ila kila mmoja alikuwa na mishe yake wakaingia mpaka ndani ambapo walimkuta mzee mmoja ambaye nywele zake zote zilitawala mvi,huyu ndo mganga ndumbwe ndumbwele,mganga jini alochanganyikana na ubinadamu alougawanya mwaka wake,mwaka mmoja kufanya kazi duniani mwaka unaofatia kufanya kazi ujinini,unaofatia duniani,kisha ujinini



ila mara nyingi miaka alokuwa akifanya kazi duniani majin wenye shida zao pia walimtembelea ambapo aliwasaidia,hivyo wakati akiwa ujinin kupitia njia ya msitu pande

(hazina ya kuzimu) Pindi alipojua juu ya ujio wa Fatma Na Gambi Ni Kuitaji Msaada Wake alishika dhima ya kuwasaidia...



Kwa Kuwa hiyo ni kazi yake....



Baada Ya Kusalimiana Na Kujuliana hali sambamba na kupeana pole hapakuwa na muda wa kupoteza,tiba ikaanza ikiwemo ya kuchanjwa na kupakiwa dawa kwa kila mmoja,

dawa itakayo mfanya atoweke pale atakapo nuia maneno kadhaa waliyokaririshiwa



pia walimezeshwa irizi ambazo hata wangepigwa risasi ingedunda na wala isingeweza kuingia ndani ya miili yao!



Baada Ya tiba ile walishukuru,walipoitaji kulipa ndumbwendumbwele alicheka sana akawaambia malipo yake ni misukosuko walokumbana nayo njiani ,wote walifrah wakamshukuru...



"Kuna Dawa Nyingine Ntawapa Mtajipaka Hii Mkijipaka Amtaonekana,wachawi Wengi Utumia hii,na pindi ukijipaka utaweza pita popote hata katikati ya ukuta,embu chovya kidogo mjipake"



Wakachovya Na Kujipaka



"vizuri Hapo Binadamu Yoyote Awezi Kuwaona Ukitaka Kuonekana Nuia tu NIONEKANE papo hapo utaonekana"



Gambi Na Fatma Walfah Sana Tena Sana Kila Dawa Walokuwa Wakipewa Kwao Ilikuwa Nzuri...



NDUMBWE NDUMBELE akatoa nyungo mbili akawa ambia wakae wafumbe macho wasifumbue mpaka atakapowapa ruksa



WAKATII



Walihis Kama Upepo Mkali Ukiwapiga Machon Na Kama Walikuwa wakipelekwa



"FUMBUA"



Kila Mmoja Kwa Upande Wake Wakasikia Wakinong'onezwa Ile Kufumbua Walikuwa Katikati Ya Soko Tena Juu Ya Nyungo Zao Wakiwa Wamesimama Wima na manguo yao meusi dah



Wote Wakabak Katika hali ya mshangao



duh!...



Embu vuta picha viumbe hawa Gambi na mpz wake Fatma wakipigwa risasi aziwadhuru pia wanauwezo Wa kupotea pindi wakinuia wapotee na wanauwezo Wa kuto onekana pindi wakitaka wao



ZIDU NA KATARINA WAKE watauweza huu mziki?!.....



Mambo ndo kwanza yanaanza



Team Katarina\Zidu



Huku team Gambi \ Fatma







Gambi anaonekana kujiamin kupita maelezo,japo Fatma anajaribu kumshauri gambi anapinga vikali je nin kitaendelea songa nayo...



"Sijakataa Fatma Uwezo huo wa kumuua kimyakimya ninao,ila huo ni udhaifu my,sipaswi kumuua hivyo yapaswa nimuue akiniona tena kwa mateso makali..."



"itakuwa ngumu gambi?"



"kwa nini iwe ngumu?"



"kwa Saivi Rais anaulinzi mkali,na dawa tulopewa ni yakuzuia kuonekana kwa kila mtu unahisi itakuwaje hapo ikiwa utataka kumuua kama unavyotaka?"



Gambi akacheka,tena akacheka sana kicheko cha dharau



"kuna kitu kinaitwa mshtuko wa butwaa,pindi ntakapotokea mbele ya raisi mule ikulu naimani walinzi wake wataupata huo ugonjwa,kwa maana hiyo muda huo ndipo ntakapotekeleza jambo langu,na kingine jambo watakalofikiria kwa muda huo ni kunipiga risasi lakin cha ajabu zaidi hata risasi zao pia zitadunda na azitazama katika mwili wangu kitengo kitakachowazidishia mshangao,namaliza kazi yangu mwanaume natoweka"



Gambi aliongea kwa furaha,ila Fatma bado alitilia shaka wazo lake



"si rahisi kama ufikiriavyo Gambi,ila Kama Umeamua Sawa Nakutakia Kila La Kheri"



Gambi akacheka tena muda huo huo akachukua simu yake akabonyeza tarakimu kadhaa,



"unataka kumpigia nani?"



Fatma akahoji kwa wasiwasi,



"rais,naitaj kumwambia ajiandae ujio wangu!"



"ooh camon Gambi Unataka Kufanya Nin?!...



Fatma aliongea kwa hasira aking'ata mdomo,ila hiyo aikusaidia tayar Rais alishapokea simu...



Zidu K' aliketi ofisini kwake kichwan kwake alikuwa na mawazo sana,hasa toka amegundua juu ya makubaliano ya mafia na mh rais,pia mawazo yake yalikuwa kwa gambi,mpaka muda huo akuwa na taharifa naye,japo vijana wake walizidisha msako nyumba kwa nyumba,vituo na stendi za mabasi,bandarini,viwanja vya ndege mitahani mahotelin,gest bubu ila Gambi akuonekana...



Wakati akiwa katika tanuri lile la mawazo ghafla simu yake ikaita

kucheki,ni divert for prisdent alielewa akushtuka sana kwani ni namba nyingi alishazipokea za rais akiongea na watu mbalimbal, viongozi wa nchi mbalimbali, makada wa chama,viongozi wake,ivyo alipokea tu basi kwani alishakata tamaa na kazi ile,



Akaweka Simu Masikioni,



"mh Rais,gambi hapa...



Si Kwa Rais Pekee Aloshtuka hata kwa Zidu Naye alishtuka mwili wote ulimsisimka kusikia lile jina,palepale akaunganisha simu yake na gprs ilo nasa mnara wa upande wa alipo Zidu akaweka loud spiker simu yake akajaribu kusachi eneo simu ilipotoka,akaigundua ile hotel,ikiwa ni kitendo tu cha dak 2

akachomoa simu yake pale katika 'special computer' yake akavaa earphone akatoka



"stan embu nifate!"



Akamwita Askar Mmoja Alokuwa Akishangaa Shangaa Pale Nje Wakaelekea Kwenye Pikipiki,



"giraffe Hotel Fastar"

Akampa amri muda ule ule pikipiki ile ikatoka kwa spidi ikiacha wanausalama wengine wakishangaa,



...NILIAPA SIKU MOJA LAZIMA NITALIPIZA KISASI KWA WOTE WALE WALOUSIKA NA KIFO CHA WAZAZI WANGU NIMEFANIKIWA UMEBAKI WEWE TU,NAJUA MNANISAKA SANA ILA TAMBUA NI VIGUMU KUNIPATA UNA MASAA KADHAA TU YA KUISHI MH RAIS KIKUBWA TOA SADAKA MALI ZAKO SAA NNE KAMILI USIKU NITAKUWA HAPO KUYAONDOA MAISHA YAKO...



Sauti Ya Gambi Ilizidi Kusikika Kwa Wawili Wale,ambapo Rais akujua kama kuna mtu alikuwa akiwasikiliza na alikuwa akielekea eneo la tukio kwa ajili ya kumtia nguvuni gambi,pia gambi mwenyewe akujua juu ya ilo,



Mwili Wote Ulimloa Jasho Mh Rais alishindwa kuongea akabaki kayatoa macho ya mshangao mwili ukimtetemeka,gambi alizidi kumtia khofu,



Wakati huo Zidu alifikia hotel ile kabla pikipiki ijasimama vizuri mwanaume tayari alisharuka akaelekea ndani ya hoteli ile...



Wala Akuangaika Kuwasemesha Mapokezi Zaid Ya Kuonesha Kitambulisho Hao Wakapanda Juu



Wakwanza Kushikwa Na Machale Ni Fatma Alihisi Mchakacho usio wa kawaida nje ya chumba chao,haraka akajivuta mpaka nyuma ya mlango wakati alipoufikia tu mlango,muda huo huo mlango ukafunguliwa na kumficha kidume kikazama...



"hapo hapo ulipo upo chini ya ulinzi weka simu chini usiguse kitu..."



Zidu akakoroma...



Rais Kule alipo alishtuka baada ya kumsikia Gambi Kakamatwa Kaubaridi Kakaupiga Mwili Wake,aman Sasa Ikamtawala,simu Ile Ikakatwa...



Gambi Naye Pia Alipigwa Na Butwaa,akutegemea askar Kumvamia Muda Ule Alipogeuka Fatma Akumuona Akajua Huyo Alishatoweka Ivyo Naye Palepale Akanuia NITOWEKE, ila ilishndikana akakumbuka akujipaka ile dawa kwa siku hiyo ivyo ilipaswa apambane yeye kama yeye,



Zidu akapiga hatua zake taratibu kumfata Gambi Pingu Ikiwa Mkononi,stan Yeye alisimama mlangon bastola mkonon akiwa kaielekeza mbele, Gambi akuijal sana ile bastola alijua isingemdhuru yeye alisubiri mtu wake amfikie amwoneshe uwezo wake...



Zidu akazidi kusogea,ila ghafla fatma nyuma ya mlango akausukuma kwa nguvu ule mlango ukampiga stan na kumtupa nje katika korido akaruka na kumtandika teke Zidu,



Akaenda kule,muda ule ule kule nje stan alijinyanyua akaiokota silaha yake na kuingia ile anaelekeza mkono wake akakutana na pigo kali la teke katika kitanga cha mkono silaha ikaenda kule sasa mwanadada machachari alikuwa mbele yake kakaa kimapigano, huku Gambi Naye Akiwa Mbele Ya Zidu Kila Mmoja Kakaa Kimapigano,ilipaswa Wazicheze Kavu Kavu...



Gambi Na Zidu Kwa Mara Ya Kwanza Wakutana,nani Ataibuka Mbabe?!



********************MWISHO*********

0 comments:

Post a Comment

Blog