Search This Blog

Friday 30 December 2022

KIAPO (AGANO LA DAMU) (3) - 4

  


Simulizi : Kiapo (Agano La Damu) (3) 

Sehemu Ya Nne (4)









Hatimaye Bray Na Mery,Agnes wanamaliza masomo yao na kurejea Tanzania!



Bray Na Mery Wakijua Penz Lao Ni Siri Na Alijulikan Na Wazazi Kutua Nchin Wanapokewa Na Wazaz Wao,wanaelekea Hotelin Ambapo Wanakutana Na Sapraiz Wasoitegemea!



Wanatakiwa Wavalishane Pete Ya Uchumba,machoz Yanamtiririka Mery Bray Anashangazwa Na Jambo Lile Je Nin Kitaendelea Songa Nayo!



SEHEMU YA SITINI NA TISA



Moyo wake ulizidi muuma akujua kwa nini anakuwa katika hali ile,



"tunamuona shemeji yetu analia kwa furaha!...



Mc Alimzindua Mery Katika Tanuri Lile La Mawazo Akamrudisha Kiakili Pale!...



"Bi mery tunakumba umpe mkono wako mume wako,akuvishe kitambulisho kitakachokutambulisha kuwa wewe u mchumba wa mtu,



Mery Bas Akuwa Na Budi Kutoa Mkono Wake Akampatia Bray,bray Akaupokea Na Kuuvisha Pete Wageni Waalikwa Wakapiga Makofi kushangilia jambo lile sherehe ikaendelea!



Upande Mwingine Yule Jamaa Alokaa Siti Ya Nyuma Ambaye Mpaka Sasa Akutambulika Masikioni Alivaa Ear Phon Akawa Akiongea Na Baadh Ya Wanausalama Wenzake Kutegua Lile Bomu!



Ilihtajika Wafanye Kwra Sir Sana Hata Mh Max Asigundue Kama Gari Lake Kuna Kitu Alitegeshewa!,dereva Akasaidia...



Yule Mwanausalama Ghafla Akatoa Anjifu Na Kumnusisha Yule Dereva!



Dereva Akatulia akamvuta nyuma naye kukaa kwenye kiti cha dereva!



alifumbua macho akajigundua kafungwa kwenye kiti,mwili wote ulimuuma,akaangaza macho yake kutazama lile eneo alilokwepo



kilikuwa ni chumba ambacho kilikuwa na dirisha dogo tena juu kabisa mfano wa selo,sakafuni palikuwa na simenti ilobondeka bondeka,hata rangi ilopigwa ukutani ilichubuka!



"bila shaka hapa ni selo"



akajisemea akijaribu kukumbuka kilicho mtokea!



ghafla mlango ukafunguliwa na yule alomteka akaingia!



mkononi alishika mkanda wa kijeshi,na tape record akabonyeza kurekodi na kuiweka pembeni!



"kwa kuanza ningependa unambie unaitwa nan,unatokea wapi na ni kwa nin unataka kumuua rais wetu"



"niue sitosema kitu!"



Mtu Yule Akajibu Kwa Kiburi,mwanausalama Akaachia Tabasamu Akaunyanyua Mkanda Wake Juu Akaushusha Mgongoni Kwa Kijana Yule Ukatoka Na Ngozi!

Akaunyanyua Mara Ya Pili Ila Kabla Ajaushusha Mtu Yule Akawa Tayari Kujieleza Huku Akilia!



"jina Langu Naitwa Spack Robert,baba Yangu Ni Balozi Wa Tanzania Nchin Marekani!,



Mwanausalama Yule Akashtuka Alimfahamu Mh Profesa Robert,akaendelea Kumsikiliza...



"ni Mmoja Wa Wanafunz Waloitimu Chuo Cha St Lucy Mwaka Juzi Mwishon Nilimpoteza Rafiki Yangu Kipenz Isack Ikisemekana Kamuua Mpz Wake!



Uongo huo! Bray Ndo Aliyemuua Alice Akasingiziwa Rafiki Yangu Na Hatimaye Akanyongwa Niliapa Kulipiza Kisasi!...



Na Kutegesha Kwangu Bomu Lengo Ni Kumuua Bray



"lakini Uoni Kama Gari Hilo Hilo Ndo Analitumia Rais?"

Mtu Yule Akaoji



"oterval!...Sikujal Ilo Lengo Kiapo Nilichokula Kitimie!"



Mwanausalama Yule Akacheka



"ongera Kijana Kwa Ushujaa Wako Sasa Utapotezwa Hata Mfupa Wako Uto Onekana!,utajuta Wewe!"



Ghafla Kilio Kikali Kikaskika!



Aikujulikana Mwanausalama Alimfanya Nin Mtu Yule Ila Ule Ndo Ukawa Mwisho Wa Spack Wazaz Wake Walimtafuta Wakitangaza Dau Ila Akuonekana Tena!...



Usalama Wa Taifa Tayari Walishampoteza!



Baada Ya Sherehe Kukamilika Waheshimiwa Na Familia Zao Walitoka Wakaingia Ndani Ya Magari Yao,wakiongozwa Na Msafara Bray Na Baba Yak Mh Rais Max Wakaelekea Ikulu

Huku Mery,egy Na Bab Yake Wakielekea Ilipo Nyumba Yao!



Moyo Wa Agnes Ulimuuma,wivu Ulimshika Kwa Sapraiz Alofanyiwa Dada Yake Mery

Akamkumbuka Mpz Wake Spack Akataman Naye Angemfanyia Vile!

Akamtext,mesej Ya Kwanza,yapil,kimya,si Kawaida Ya Spack Kutojibu Sms Zake,wivu Mkali Ukamkamata,akataman Hata Ampigie Ila Angeanzaje Na Yupo Na Baba Yake Ndani Ya Gari! Ilibidi Angojee Tu Afike Nyumbani



Kwel Dakika Chache Baadaye Waliwasili nyumbani,kabla Ya Kwenda Kuoga Eggy Akakimbilia Chumbani Kwake Akamtwangia Simu Spack Kitu Kikiwa Kimemkaa Kohoni!



Simu Ikaita Mpaka Ikakata,akapiga Tena,ikaita Mpaka Ikakata,tena Jibu Likawa Hilo Hilo!



Maumivu Makali Yakauvamia Moyo Wake!

Akapiga Tena,awamu Hii Ikakatwa Na Kuzimwa Moja Kwa Moja!

Namba Ile Aikupatikana Tena Hadi Hivi Leo!,siku Zikasonga!



Badae Eggy Akaja Kupata Habari Ya Kutopatikana Kwa Spack Toka Amalize Chuo!



Ilisemekana Amekimbilia Tanzania,ni Wapi Sasa Yupo!



Maskin,eggy Akujua Kuwa Mpz Wake Alisha Uwawa Na Usalama Wa Taifa Na Kupotezwa!



Yeye Bado Mawazo Yake Yalikuwa Katika Usaliti Ikiwa Imebakia Miez Sita Kumalizika Kwa Mafunzo Ya Jeshi Katika Kambi Moja Nchini Marekani



Stanley Browser Alikaa Katika Bwen Lake Moyon Alikuwa Na Uchungu!



Ni Kwa Nin Yule Apendelewe Wakati Yeye Ni Ndugu Yake Na Yule Ni Mtu Baki?!



Akakumbuka Kosa Alilofanya Miezi Kama Saba Nyuma Ilipaswa Auwawe,lakini Baba Mdogo Wake Akashika Dhima Ya Kumtetea!



Akakumbuka Zawadi Alizoletewa Yeye,mtu Yule Alipewa Mara Mbili Yake!

Hiki Ndicho Kilicho Muuma Stanley



"bila Shaka Hata Urithi Si Ajabu Akampa Wote Yule Kijana"



Mawazo Yake Yakazid Kwenda Mbele,pasina Kujua Ni Kwa Nin Baba Mdogo Wak Alimpenda Isack Zaidi!



Akajenga kisasi dhidi yake!

akaapa kumuua isack! hata hyo miezi sita ilobakia isack asiimalize!



ndiyo!



huyu alikuwa ni stanley mtoto wa mdogo wake mh alfonsor baba yake alice!



mwenye siri nzito na watu wawili Zidu,na Isack Au Richard Mombi Jina Analotumia Kwa Saiv!



Mambo Yameanza Tena,stanley Anaijenga Chuki Dhidi Ya Isack Kisa Ba Mdogo Wake Anampenda Isack Zaid Je Atafanikiwa Hayo Anayoyapanga Dhidi Ya Isack?!...





Ikiwa Imebakia Miez Sita Kuhitimu Mafunzo Yake Ya Jeshi Stanley Mtoto Wa Mdogo Wake Na Alfonsor Anapandikiza Chuki Moyoni Mwake,anakula Kiapo Kumwangamiza Isack Ikiwa Ni Uwivu Tu Usio Na Tija!

Je Unahis Nin Kiliendelea?!

Songa Nayo Katika Sehemu Hii Ya 70



"Morice,sunday,na Patrick Nyinyi Si Kama Ni Rafik Zangu Tu Ni Kama Ndugu Zangu Ninaowaamini!,tuwe Kitu Kimoja Katika Hili,sis Wa Nne Nne Atutomshindwa Yule Mtu Mmoja Tumpe Shambulio La Ghafla!"



Stanley Aliwaeleza Wenzake,walikuwa Ndani Ya Bweni Lao!



"je Tutamuangamizaje Na Saiv Ndo Mchakamchaka Wakuu Wako Makin Na Sis Muda Tunaoupata Ni Hizi ni hizi dakika mbili tu za kula,morice alitoa wazo lake!



"hata ilo mi nishaliwaza,ila wiki moja ya mwisho huwa tunasitisha mazoez na mafunzo tunakuwa tumeshakamilika,tukijiandaa na mahafali ivyo katika kipindi iko ndicho tutakachomwangamiza kingine wakat tukisubir wiki hiyo ifike saiv tupo katika mazoez magumu tumtaftie njia tummalize hata tukiwa ndani ya mazoez ijulikane tu ni bahati mbaya?

majadiliano yakaendelea hatimaye wakamaliza kula wakaendelea na mazoezi wakimsomea isack gepu!



maskin yeye mwenyewe alikuwa ajui kama anawindwa!...



"tukiwa tumebakisha wiki tatu,wiki hii inayoanza kesho atutokula

zaidi ya kunywa maji mara moja tu tena saa maalumu saa saba kutumia kifuniko cha kilimanjaro yani bobo lile dogo la nusu lita ndilo litakalolinda maisha yako ndan ya wiki hiyo,wakat huo kutakuwa na mazoez makali kama ya kuchimba andaki kwa kutumia kijiti maalumu tutakavyowapa,pia kupita juu katika nyaya za umeme zenye shoti kwa gloves maalumu zinazozuhia shoti hiyo!



na wik ya mwisho hiyo inaitwa dangereous wiki yan siku ya kwanza jtatu mtakula kisha zinazofatia zoez letu la maji nusu lita litarudia palepale wiki endi hiyo jumamos na jumapil mtapigana vita ya kwel tutaunda vikosi viwili tutawapa boom,bastola ya kivita atakayeuwawa huo ndo utakuwa mwisho wake vita hiyo itakuwa niya siku mbili itakayoisha jumapil saa tano na dakika 59 saa sita kamil ambapo sasa ni jumatatu itakusanywa miili yote ya maiti kutumwa kwao imekufa mafunzoni,na hapo tutakuwa tumemalizi rasmi mafunzo yetu!



jemedari wao alimalizia kusoma ratiba ile huku akitabasamu,ila hakuna mwanajesh hata mmoja aliyekenua wote walinuna!

wacheke sasa kwa lipi pale,kula walikuwa wakila kwa muda maalumu,wiki hii awali kabisa,kilindacho uhai ni maji tu mwisho wauwane kivip wafrah!



Basi Lililofatia Ni Gwaride Na Mazoez Madogomadogo Wakaruhusiwa Wakapumzike kidogo!



Kundi La Watu Wale Wa Nne Likiongozwa Na Stanley Waliweka Kikao Katika Bwen Lao,tofauti Na Wanafunz Wengine Wao Walifurahia Swala Lile Wao Walijua Pa Kupata Chakula,ila Pia Opereshen Yao Malengo Yao Yalikuwa Ndo Yanaenda Timia!...



Wiki Ijayo Ndo Wiki Rasmi Ya Kumwangamiza Kwa Kuwa Tena Atakuwa Na Njaa Tutamuua Vizur Ila Narudia Tena Jamani Nafas Ikipatikana Alipuliwe ,Patrick jitahidi uwe nae karibu tengeneza urafiki pia itakuwa njia rahis kwetu kufanya tulichopanga!



mh Alfonsor Alijua Wiki Zile Ni Wiki Za Hatari Hasa Kwa Kijana Ake Isack Ilikuwa Lazima Amlinde Kwa Namna Yoyote Ile Kusudiaje alipize kisasi! ivyo alihtaji kufanya kila linalowezekana ampelekee chakula Isack Na Mtoto Wa Mdogo Wake Stanley!



Na Chakula Ilikuwa Lazima Kipitie Kwa Stanley Ndiyo Stanley Ampe Mwenzake,Alfonsor maskin akuijua chuki iliyokuwepo moyon kwa Stanley Dhidi Ya Isack,



Akiwa ndani ya gari lake jeusi alishuka katikati ya pori akatoka na vimfuko viwili kimoja kiliandikwa 'I' Ikimaanisha Isack Kingine Kiliandikwa 'S' ikimaanisha stanley!

kwa kuwa stanley alikuwa wa mwisho akamkonyeza yule mwanajesh alokuwa nyuma kabisa,ambaye walikuwa wakijuana!



Akachoropoka Kikosin Na Kuelekea Pale Kichakan Akachukua Vile vimfuko akavisweka gwandani,wanajeshi awakuwa na tabia ya umbea umbea walipotezea,



Bas Baada Ya Mchakamchaka Ule Wakarudi Kambini Wakapewa Muda Wa Dakika Tatu Tu Ya Kupumzika Wakarudi Bwaloni Wakafungua Kile Chakula Na Kula Chote! Pamoja Na Kile Cha Isack!



Ndivyo Katika Wiki Ile Chungu Alivyokuwa Anafanya Isack Yeye Akujua Kilichokuwa Kikiendelea,



Alishinda Njaa,alilala Njaa,akinywa Maji Kidogo Sana Akujali,alifanya Kazi Ngumu Pasina Kuwa Na Nguvu Zozote!



Ndivyo Wanafunz Wengi Katika Wiki Ile Walivyokuwa Wakiishi!

Wengi Walipoteza Maisha,walojaribu Kutoroka Waliuawa,hatimaye Siku Tano Chungu Zikatimia siku ya sita ilikuwa siku ya kutembea katika waya kwa gloves maalumu zisizopitisha umeme,



"lazima tufanye kitu tujitahidi gloves yake tuiweke ya kawaida afie katika shoti ya umeme au mnasemaje!"



"wazo zuri lakin we unahisi tutabadilishaje?"



"ha ha ha iyo kwangu kazi rahisi mi najuana na kapteni akuna kinachoishinda pesa olways without money uwez fanya kitu"



"do that kile unachoweza kaka kufanikisha malengo yako!"



"right! kwanzia leo twatangaza vita na isack twaanza isaka roho yake vyoo"



"yah ofcorze"



Na Ndivyo Ilivyokuwa Stanley Akaenda Kuongea Na Jemedari Akamkabidhi Gloves Zile Zilizofanana Na Za Isack

wakazibadilisha! lengo isack akivaa zile akagusa nyaya tu za umeme kwanza zingenasa katika nyaya zile zingepitisha shoti,na palepale sekunde ile ile Isack Angepoteza Maisha!...







Kiso Hatimaye Anapewa Uamisho Wa Kurejesha Nyumbani Tanzania Akalitumikie taifa lake,



anashikwa na furaha ya ajabu anarudi zake nyumbani kujiandaa,ila nyumban anakutana na ugeni asioutarajia!,ni lazima apambane kulinda maisha yake dhidi ya mtu yule asiyefahamika!...



songa nayo kujua kilichoendelea!...



Ni Wakati Mwenzako Anapopoteza Nukta Moja Kuwaza Jinsi Ya Kukukabili,ile Ile Nukta Moja Aliyeipoteza Kiso Jamaa Yule Alijirusha Akamtandika Teke La Mbavu Kiso Akasambaratika Chini!



Ila Akutaka Kubaki Palepale Akajinyanyua Na Kukaa Vizuri,akaruka Teke Zake Mbili Ambapo Ya Kwanza Mwanaume Yule Aliinama Chini ikapiga hewa



alipojiinua akakutana na teke la pili ambapo alilipangua kwa mkono sambamba na kurusha ngumi ilotua katika paji la uso la kiso damu zikawa zikimchuruzika katika pembe za mdomo wake!

sasa hasira zikawa zimempanda kaukunja mdomo wake,



Jitu lile lililokuwa likipambana naye lenyewe lilikuwa katika tabasamu baya lengo aendelee kumkasirisha ili apigane kwa kuongozwa na hasira

ilo lile jitu vamizi lilifanikiwa!



Kiso Wa Watu Sasa Akawa Akiongozwa Kwa Hasira,jitu Vamizi Likiwa Nyuma Kidogo Ya Ukuta,kiso Akakusanya Nguvu Akajirusha Akitanguliza Teke,jitu Vamiz Likaenda Tu Pembeni Kidogo Kiso Akauvaa ukuta mzimamzima kisha akaenda chini akisindikizwa na yowe!...


ITAENDELEA

   

Simulizi : Kiapo (Agano La Damu) (3) 

Sehemu Ya Tano (5)



"ha ha ha ulijiona mjanja kuja gerezani kuntengenezea ushahidi wa uongo nionekane ndio muhusika wa vifo vya mac donald na mkewe miss sara,malipo yako ndo haya mwanahizaya wewe!"



jitu vamiz likaongea kwa kiburi akimtazama kwa dharau pale chini!



Kiso Hakuwa Na Ubavu Tena Wa Kunyanyuka Pale!



Kauli Ile Ilimshtua!,ndo Yule Alomuhisi Ila Mbona Sura Tofauti Huyu Ni Zidu?!!...



Ni Kama Jitu Vamizi Lile Lilisoma Akili Yake Nalo Likamjibu Kwa Cheko Lake La Dharau!



"ha ha ha usiumize kichwa kuwaza mim ndiyo siyo,mimi ndiyo yule yule Mzimu Zidu Katili Si Mliniua nyinyi?! nimerudi kwa sura nyingine kulipiza sitowaacha wa zima"



akamalizia na kujirusha juu ya kifua cha kiso guu lake moja lililovaa kiatu kizito chenye soli ngumu akaupachika shingoni kwa kiso,akaanza kuusigina mithili mtu akiua mdodu kwa kutumia mguu chini!



Zidu Akuwa Na Huruma Asee,alisigina Mpaka Alipoakikisha Alomkanyaga Kakata Roho Ndipo Akaruka Toka Juu Ya Kifua Cha Mtu Yule!



Kwa Kutumia Vidole Vyake Akamtoboa Macho Kupoteza Ushahidi!,akaivaa Laptop Ilokwepo Hapo Sebuleni Akaifungua Kwa Kutumia Njia Zake Alizojua Yeye Akafuta Sura Yake Katika Camera Ile!



Akajongea katika ule mwili akaingiza mkono wake katika mfuko wa koti lake lile akatoka na kisu kidogo akamchoma kidogo tumboni damu zikaanza kutoka

Alikuwa na kazi na damu ile



Akachovya kiasi cha damu na kuandikia sakafuni maneno 'kiapo ( agano la damu)' akimaanisha alishakula kiapo yeye na Isack Kwa Kuchanganya Damu Zao Kulipiza Visas Kwa Wote Waliyoyatesa Maisha Yao,na Sasa Yeye Alianza Na Kiso!



Baada Ya Hapo Pasina Kukimbia Mwanaume Akatoka Tena Akipitia Getini,akazunguka Nyuma Ya Nyumba Ile Alipopaki Pikipiki Yake,akajipandisha Na Kuvaa Element Yake Akapiga Kiki,taratibu Mwanaume Akaondoka!...



TANZANIA



IKULU JIJINI DODOMA



Ndani ya ofisi ya rais ndani ya ikulu ile aloishi raisi na familia yake!,

Katika Chumba Cha Ofisi Yake Ile Ndogo Leo Alikuwa Na Ugeni,ni Waziri Wa Ulinz Na Rafiki Yake Kipenz Mh Alex,



Mambo mawili makuu walokuwa wakiyaongea ndiyo yalompa furaha rais yule!



jambo la kwanza ni kuwasili kwa Kiso,alokuwa Inspekta Wazir Wake Akampeleka Nchini Marekani Akajiunga Na Jeshi Kabla Ajajiunga Na Shirika la kijasusi na upelelez fbi akafanya kaz kwa miaka kadhaa,walipomuomba jeshi la marekani lilikataa,ila leo habar nzur alomletea mh Rais Ni Kuwa Shirika Lile Limekubali Kumrejesha Kiso



Na Swala La Pili Ni Tarehe Ya Ndoa Kwa Mtoto Wake Mery Na Bray Vitu Hivi Vilifanya Kikao Chao Kile Kizingirwe Na Furaha!



"huyu Akifika Tumpe Cheo Awe Mkuu Wa Usalama Wa Taifa!"



Mh Alex Akatoa Wazo!



"lakin Mh Asije akawa ni shushushu katumwa akaendelea kulifanyia kazi shirika lake la marekani maana lile taifa Mimi nalijua vizur ni vigumu sana wale kumfundisha mtu mpaka akajua then wakamtoa burebure tu...."



"Hapana mkuu si rahisi Toa mawazo hayo nilianza kuwaomba siku nyingi wanipe kijana wetu.....



Kabla ajaendelea ghafla Simu Yake Ikaita,alitoa Macho Kwa Mshangao Kwa Habari Ile Aloambiwa Ni Juu Ya Kifo Cha Ghafla Cha Kiso Tena Ikisadikika Ameuwawa!



WAKAPIGWA NA BUTWAA!



"hii itakuwa ni wenyewe wamemuua marekani wajanja sana nilijua awawez mfundisha mtu mbinu za kijasusi akaenda kunufaishia nchi nyingine wapumbavu sana hawa watu"

Mh Rais Max Malwale Aliongea Kwa Hasira!



"inawezekana Mkuu Ila Pia Na Mashaka Kwa Kuwa Nimeambiwa Pembeni Ya Mwili Wake Kumekutwa Maandish Yaloandikwa Kwa Kutumia Damu Maneno Kiapo(agano La Damu) Je Uoni Hapo Yapaswa Tuwaze Kwa Jicho La Tatu Mkuu?"



"kiapo?! Nin Agano La Damu? Mbona Kama Sijakuelewa?!"



Rais Max Malwale Aliuliza Akitoa Macho Ya Mshangao,



"Hiki ndo Kitu Ambacho hata mimi sijakielewa hapo mkuu lakin fikra zinantuma hiki ni kisasi aiwezekani muuaji aandike hayo maneno bila sababu na kingine mkuu katika nyumba yake ile cctv camera eti zimefutwa ila za nje zimemuonesha jamaa alovaa jacket la laizar na kofia laizar mbinuko sura aikutambulika,



wamesema wanaendelea na uchunguzi na lazima muuaji abainike?"



dah habari ile ikaleta mkanganyiko katika vichwa vya viongozi wale ila katika mioyo yao awakuhis wala kudhani kiapo kile kiliwahusisha mpaka wao!





Kazi Imeanza Rasmi!,Zidu anafanikiwa kumwangamiza Kiso Tena Kikatili Akiacha Maandish Kwa Kutumia Damu Kiapo 'Agano La Damu'



Habari Ya Kifo Kile Inamfikia Mh Alex Na Rais Max Maliwale Mawazo Yao Wanajua Ni Marekan Wenyewe Ndo Wamemuua Mtu Wao,wanakasirikia Jambo Lile Pasina Kujua Msababishaji Ni Mtu Alokwisha Kula Kiapo Juu Yao,tena Kwa Agano La Damu!



Ni Jeshi La Watu Wawili!

Zidu & Isack Watauweza Mchezo?!







Wanajesh wote walijipanga katika vikosi walivyopangwa,vilikuwa ni vikosi vya watu kumi kumi wanajeshi wote jumla walikuwa mia na arobaini ivyo kila siku wangepanda watu Ishirini Mpaka Siku Saba Wangemalizika Wote



Ambao Wangefuzu Ndo Wangekuwa Wanajesh Kamili!



Zoez Lile La Mwisho Ilipaswa Lianze Siku Hiyo Ambaye Ni Jumatatu Na Kumalizika Jumapili Jumatatu Kila Mtu Kwao!



Isack Ilipangwa Yeye Kundi Lake Ni Jumapili,siku Ya Mwisho,kina Bray Walfrah Kwa Kujua Siku Ya Mwisho Hata Umakini Kwa Usimamiz Usingekuwa Mkubwa Kama Hizi Siku Za Mwanzo Na Za Katikati!...



Vikundi Vikaingia Vitani!,watu Ishirini Wa Mwanzo Wakaingia Vita Vilipaswa Vianze Saa Sita Usiku Yani Kuamkia Jumatat Mwisho Wa Vita Ni Saa Tano Na Dakika 50 Sasa Sita Kamili Kundi Lingine La Siku Inayofatia Linaanza mpaka sita kasoro dakika tano kuamkia siku ingine!



Kundi moja ilipaswa likae upande wa juu lingine upande wa chini!

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog