Search This Blog

Saturday 24 December 2022

BEHIND THE CURTAIN: SEPTEMBER 11 - 2

   http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/behind-curtain-september-11.html

Simulizi :  Behind The Curtain: September 11

Sehemu Ya Pili (2)


Osama hakuishia hapo tu katika hii fa'twa, akaenda mbali na kusema kuwa ana taarifa za siri zinazothibitisha kuwa Marekani ina mpango wa kuigawanya Taifa la Sudan na kuwafitinisha Waislamu wa Sudan (jambo hili limetokea miaka michache iliyopita).


Osama akaongelea pia suala lenye utata akidai kuwa, Mauaji ya Kimbari ya Rwanda yalipangwa kwenye ofisi ya balozi mojawapo hapa Afrika ta Mashariki.


Pia akakemea vikali kukamatwa kwa wapiganaji wa Jihad waliokuwa wamejificha nchini Albania na ikasemekana kuwa waliteswa katika jela za siri za CIA mpaka kufa.


Osama akahitimisha fa'twa kwa kuahidi kuwa wako njiani kulipiza kisasi kwa uonevu huu wa wamarekani, na manyanyaso katika "nchi za kiislamu".


Akaahidi kuwa kisasi hicho kitafanyika si siku nyingi.



Na ndani ya miezi michache mwaka huo huo 1998 Marekani ikaanza kushuhudia impact ya hii Fa'twa kutoka kwa washirika wa Al Qaida wakiongozwa na kikundi cha EIJ (Egyptians Islamic Jihad).

Feb 22, 2017

Thread starter

#389

AL QAIDA WANAANZA "KUPASHA" MISULI KUJIANDAA NA 9/11





Shambulizi katika Balozi za Marekani Afrika Mashariki


Siku chache baada ya kutoka kwa fa'twa ya Osama bin Laden, washirika wa All Qaida kutoka kikundi cha kigaidi cha Misri (Egyptian Islamic Jihad) kwa muongozo wa Osama bin Laden binafsi na Al Qaida wakaanza kupanga mkakati wa kuanza kuwaonyesha "advertise" ya uwezo wao wa kufanya mashanbulio na kuwalipiza kisasi.


Mwezi May 1988, Sheikh Ahmed Salim Swedan alipanga chumba katika Jengo la kipato cha kati jijini Nairobi.


Wakati huo huo, bwana mmoja anayejukiakana kama K.K Mohamed naye alipanga nyumba namba 213 iliyoko maeneo ya Ilala jijini Dar es Salaam, nyumba hii ikiwa takribani kilomita sita pekee kutoka Ubalozi wa Marekani.


Nyumba hizi mbili za Dar na Nairobi zilitumiaka kama vituo vya kutengenezea mabomu yatakayo tumika kulilipua balozi za Marekani.


Mabomu haya yaliutengenezwa chini ya uangalizi wa "mtaalamu" Mohammed Odeah.


Bomu la nairobi liliundwa katika mtindo ambao ulitumia zaidi TNT.


TNT (Trinitrotoluene) ni tumawe mawe fulani hivi twenye rangi ya manjano ambayo ni Chemical Compound - C6H2(NO2)3CH3.


TNT huwa inatumiaka kwenye "chemical synthesis" kama "reagent".


Pia hutumika kwenye process za kikemia kutengeneza "charge transfer salts"


Licha ya hivyo kampaundi hii unaewezo mkubwa wa kulipuka na hii ndio sababu hata hutumika kama kipimo cha kupimia uwezo wa vitu vingine kulipuka (standard measure of explosives)


Sasa jijini Nairobi, magaidi hawa wakatumia cylinder mia tano za TNT, pamoja na unga wa Aluminum kuunda mabomu yao ambayo waliyahifadhi katika masanduku ya mbao.


Jijini Dar es salaam Bomu lake lilikuwa tofauti kidogo.


Hili bomu la Dar lilitengenezwa kwa kutumia hiyo hiyo TNT, lakini cylinder zake ziliuungwa kwenye mitungi kumi na tano ya Oxygen na "gas canisters".


Pia kwenye steji ya mwisgo ya upakiaji kwenye gari waliweka na viroba vinne vya mbolea yenye kiwango kikubwa cha Ammonium Nitrate.



Baada ya mabomu kukamilika, magaidi wa Nairobi wakanunua gari aina ya Toyota Dyna na kupakia karibia maboksi 20 yenye milipuko.


Huku Dar, wao walinunua gari aina ya Toyota Atlas, yenye jokofu (refrigeration truck) na wakajaza milipuko waliyotengeneza kama wenzao wa Nairobi.


Siku ya August 7, 1998 siku ambayo ilikuwa ni maadhimisho ya miaka 8 tangu vikosi vya Marekani kuwasili nchini Saudi Arabia, magari haya yenye milipuko yakiendeshwa na kwenda kupaki kwenye balozi za Marekani jijini Nairobi na Dar es salaam.


Mnamo saa nne na nusu asubuhi, mabomu ya Nairobi yakalipuka.


Dakika kumi baadae, yaani saa nne na dakika arobaini asubuhi, bomu mabomu ya Dar es salaam nayo yakalipuka.


Mlipuko wa Nairobi ukisababisha vifo vya watu 213 na kujerehi wengine 4000, huku mlipuko wa Dar ukisababisha vifo vya watu 11 na kujeruhi watu 85 wengine.


Kicha ya vifo hivi vingi, lakini ni Wamarekani 12 pekee walio fariki kutokana na milipuko hii.

Kati ya hao wamarekani 12 waliofariki walikuwemo, makachero wawili wa CIA waliokuwepo Ubalozini Nairobi, kulikuwa na Sajenti mmoja wa US Marine, julikuwa na Marine mwingine aliyekuwa kama mlinzi ubalozini, pia kulikuwa na sajenti wa jeshi (US Army).



embassy1.jpg

Eneo la tukio la mlipuko ubalozini.




Tukio hili ndilo kikifanya kwa mara ya kwanza FBI ikamuingiza Osama katika Orodha ya Most Wanted.


Likaanzushwa "vugu vugu" la kuwasaka waliohusika kutekeleza tukio hili la kulipua balozi.


Lakini bila kujua, wakati vyombo vyote vya usalama na ujasusi nchini Marekani vikihahah na kukuna kichwa kuwatafuta wahusika wa mashambulio haya kwenye balozi wao, ndipo kipindi hiki hiki nchini Afghanistan Osama bin Laden anapokea ugeni muhimj wa kikundi cha wanafunzi wa kiarabu wanaosoma nchini Ujerumani... Vijana ambao Osama alikuja baadae kuwatumia kuwapandikiza nchini Marekani na kutekeleza tukio la September 11.




moga.jpg

Ahmed Ghailani kijana wa kitanzania aliyehusiuka katika shambulio la Balozi ya Marekani.





The Hamburg Cell


Katika jamii ya Ujasusi nchini kuna "kijiwe" cha ugaidi cha wanafunzi ambacho kilikuwa kwenye mitaa ya Hamburg nchini Ujerumani na wamekibati,a jina kama "The Hamburg Cell"


Wanachama muhimu zaidi katika kijiwe hiki walikuwa ni, *Mohamed Atta, Ramzi bin al-Shibh na Marwan al-Shehhi.* hawa watatu walikuwa na uhusika mkubwa katika tukio la September 11.


Lakini pia kijiwe hiki kilikuwa na wanachama wengine kama vile, Said Bahaji, Zakariya Essabar, Mounir el-Mossadeq na Abdelghani Mzoudi.


Kijiwe hiki kina historia ndefu mpaka kufikia kuwepo kwake.



Historia ya kijiwe hiki inaanzia kwa kufika kwa Mohamed Atta nchini Ujerumani.



Mohammed Atta; Kijana pekee wa kiume katika familia ya mwanasheria mahiri nchini Misri Bw. Mohamed el-Amir Awd el-Sayed Atta, alizaliwa September 1 mwaka 1968 katiaka eneo la Kafr el-Sheikh kwenye mkoa wa Delta ya Nile.


Mohamed Atta alikuwa na bahati, kwani alizaliwa kwenye familia yenye kipato kizuri kabisa baba yake akiwa ni mwanasheria mahiri, pia mama yake mzazi alikuwa anatokea kwenye familia ya kitajiri inayojihusisha na kilimo kikubwa.

Atta pia alikuwa na dada wawili wakubwa na wote walikuwa wasomi wa hali ya juu na wenye mafanikio. Dada yake mmoja alikuwa ni Daktari Bingwa na mwingine akiwa ni Profesa wa Chuo kikuu.


Baba yake Atta anajulikana kwa kuwa muisilamu mwenye kuifuata dini mpaka kipindi kingine anazidisha anafanya mambo ambayo labda yanaweza kuonekana sio ya lazima kidini. Hii ilipelekea hata familia yao isiwe karibu na upande wa ndugu wa Mama yake wakiokuwa nabutajiri mkubwa. Wengi wa ndugu hao hawakupendezwa na misimamo ya kidini ya baba yake Atta.


Akiwa na umri wa miaka 10 familia yao ilihamia jijini Cairo ambapo baba yake alimpiga marufuku kujichanganya na watoto wengine wa majirani.


Hivyo Atta alitumia muda wake mwingi wa utotoni akiwa mpweke amejifungia ndani akijisomea.

Lakini hii pia ilimpa faida kwani, alifanikiwa kufaulu vizuri masomo yake na kuchaguliwa kujiunga na Chuo kikuu cha Cairo mwaka 1985 akisomea Uhandisi.


Akiwa katika mwaka wake wa mwisho chuoni, kutokana na kuwa wanafunzi bora kabisa hapo chuo, akaingizwa kusoma programu adhimu kabisa chuoni hapo ya Architecture.

Mwaka 1990 akahitimu chuo.


Baada ya kuhitimi chuo akapata kazi kwa muda katika kituo cha Mipango Miji jijini Cairo (Cairo Urban Development Center) akifanta kazi ya 'Architectural Planning and Building Designing'.


Baadae mwaka 1991 akajiunga na Kituo cha Goethe Institute ili kujifunza kijerumani.


Mwaka 1992 akapata nafasi ya kusoma Shahada ya Uzamiri katika 'Urban Planning' kwenye chuo kikuu cha Hamburg.


Akiwa chuoni hapa kusomea shahada hiyo mwangalizi wake wa masomo (Supervisor) alikuwa anaitwa Dittmar Machule ambaye ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Idara.


Bw. Dmittar anamuelezea Atta kama mwanafunzi mwenye akiki sana lakini alikuwa na misimamo mikali ya kiitikadi.


Kwa mfano; anaeleza kuwa kwenye maongezi ya kawaida (mara chache sana, inaelezwa kuwa Atta hakuwa muongeaji, unaweza kuishi naye nyumba moja wiki nzima asikusemeshe hata neno wala, hata salamu.. Mwanzoni alipoingia Ujerumani aliwahi kufukuzwa kwenye nyumba ya wanandoa fulani waliokuwa walimu wa sekondari kutokana na tabia yake ya ukimya uliopitiliza mpaka kuudhi).. Sasa kwenye maongezi hayo ya bahati nasibh, inaelezwa kuwa Atta alikuwa nanipinga sana Sera ya Marekani kuhusu Mashariki ya Kati.


Si hivyo tu bali pia alipinga Utawala wa 'kifamilia' wa Hussein Mubarak nchini Misri na aliichukia serikali kutokana na kampeni yake ya kutokomeza kikundi cha kisiasa cha Muslim Brotherhood.


Atta alikuwa anapinga hata namna ambavyo miji katika nchi za kiarabu ilovyokuwa "inaharibiwa" kwa kujengwa kwenye mtindo wa kuiga umagharibi.


Bw. Dittmar anaeleza kwa mfano, Atta alichefukwa sana na namna ambavyo maghorofa yalikuwa yakijengwa kimagharibi jijini Cairo kila uchwao.


Hata katika 'thesis' yake, Atta alitafiti ujenzi wa zamani wa mji wa kihistoria wa Aleppo nchini Syria na akaonyesha namna ambavyo mji huo unaharibiwa kwa "usasa"




moata.jpg

Mohammed Atta akiwa na wanafunzi wenzake wa Hamburg University katikasiku zake za kwanza mara baada ya kufika Ujerumani.



Akiwa bado mwanafunzi chuoni, baadae Mohamed Atta akaanza kuhudhuria Ibada katika Msikiti wa Kisunni wa Al-Quds.!


Msikiti huu unajulikana kwa kuwa na mahubiri yenye chuki na hasira dhidi ya mataifa ya magharibi.


Akiwa msikitini hapa ndipo akakutana na Ahmed Maklat, Muonir El Motassadeq na Ramzi bin al-Shibh.


Mwanzoni waliunda urafiki kwa kuunda "kikundi cha maombi" cha pamoja, lakini baadae umoja huu ndio ukaja kugeuka na kuwa kijiwe cha kigaidi maarufu cha "Hamburg Cell".



Mara kadhaa Atta ilimbidi kuhahirisha masomo kwa sababubz kiidini nyingine zikiwa zinaeleweka ila nyingine zilikuwa na mashaka makubwa.


Mfano tarhe 31 october 1995 Atta allihairisha masomo kwa muda na kwenda Hijja, Makka. Hii ilieleweka na ilikuwa na msingi.


Takribani miezi kumi na nane baadae, yaani June 1997 Atta akapotea tena chuoni.

Supervisor wake anaeleza kuwa hii ilisababisha kuwa nyuma ya muda wa kuwasilisha thesis yake (alifanikiwa kuwasilisha thesis mwanzoni mwa mwaka 1999 na kufanya utetezi mwezi August 1999) Dittmar aalipowasiliana nae ili kujua mahali alipo wasiliana nae ili kujua alipo alimueleza kuwa yuko safarini kwenda tena Hiija.


Hii ilitia mashaka kidogo ukizingatia ni miezi 18 tu nyuma alitoka kwenye Hijja.


Atta alikaa kwa muda mrefu huko alipoenda na kurejea mwaka 1998.


Aliporejea alikuwa amebadilika sana kiahiba! Kwanza alikuwa amevuga ndevu ndefu sana na alikuwa mtu 'serious' kuzidi mwanzo.

Pia akaeleza kuwa amepoteza passport yake hivyo hii imembidi kutafuta passport nyingine. Hii ni moja ya mbinu inayotumiwa na watu kutaka kuficha sehemu aliyokwenda.


Kwahiyo kutokana na kwanza kukaa muda mrefu huko alikoenda tofauti na muda halisi wa Hijja, na pia kuficha passport yake kwa makusudi.. Inaaminika kuwa Mohammed Atta alienda kwenye kambi za Al Qaida nchini Afghanistan.



Marienstraße_54.JPG

Muonekano wa Mtaa a Marienstrasse mjini Hamburg, mtaa ambao kulikuwa na apartment ya "Humbarg Cell"




Kijiwe cha Hamburg kinazidi kupata ushawishi


Baada ya Atta, Ramzi na Shehhi kuwa marafiki walioshibana, hatimaye siku ya November 1 mwaka 1998 wote watatu wakapanga 'apartment' moja katika mtaa wa MarienstraBe jijini Hamburg.


Apartment yao ikaja kujipatia umaarufu sana kwa wanafunzi wengi wa kiarabu wenye misimamo mikali waliokuwa Hamburg.

Ilifikia kipindi mpaka karibia wanafunzi 21 wa kiarabu walikuwa wameandikisha apartment hiyo kama "address" yao rasmi kwenye nyaraka mbali mbali.


Kulikuwa na ratiba ya mijadala kwa wiki mara tatu au nne na mijadala hii yote ilihusu Marekani na Israel na jinsi wanavyogandamiza waislamu.


Kadiri muda ulivyoenda, kijiwe hiki kilianza kuwavutia hata "magaidi" halisi.


Inaelezwa kwamba hata Khalid Sheikh Mohammed aliwahi kukitembekea kijiwe hiki mara kadhaa kufanya "vetting" kwa ajili ya mpango wa shambulio la kiihistoria,alio uwasilisha kwa Osama, ingawa hawa vijana wenyewe hawakujua nia ya KSM kuwatembelea.




SEHEMU YA NNE 



SEHEMU YA NNE



Katikati ya mwaka 1999, kijiwe hiki kilipata mgeni adhimu kwenye ulimwengu wa watu wenye misimamo mikali, walitembelewa na Khalid al-Masri.


Kama kawaida akaanzisha mjadala kutaka kujua mtazamo wao kuhusu vugu vugu la Jihad lilikuwa linaendeshwa na Waislamu huko Chechnya kupinga eneo hilo kudhibitiwa na Urusi.


Mjadala ulikuwa mkali, ambapo Atta na wenzake walionyesha ni kiasi gani wanaunga mkono vugu vugu hilo.

Mwishoni mwa mjadala wakamuomba Khalid al-Masri awasaidie kuingia Chechnya ili wakajiunge na mapambano hayo ya Jihad.


Khalid akawapa mawasiliano wawasiliane na mtu aliyepo maeneo ya Duisburg anayeitwa Abu Musab.

Atta na vijana wenzake wakafunga safari kumfuata Abu Musab.


Walikuwa hawajui, kumbe huu ulikuwa ni "mchongo" umepangwa kwa umahiri kabisa.


Wakupofika Duisburg na kwenda kuonana na Abu Musab, wakashikwa na butwaa kukuta kumbe Abu Musab lilikuwa ni jina la bandia, ila uhalisia ni kwamba mtu alikuwa ni Mohammedou Ould Slahi moja ya 'makachero' muhimu zaidi wa Al Qaida kwenye nchi za Ulaya.


Slahi akawaeleza vijana hawa, kwamba kwanza ni vigumu mno kuingia Chechnya kutokana na udhibiti mkali wa Urusi.

Lakini pia wanahitaji mafunzo zaidi kama wanataka kujiunga rasmi na Jihad.


Hivyo basi akawashauri waende Karachi, nchini Pakistan na maelekezo zaidi watayakuta huko.


Baada ya Atta na wenzake kukubali, Slahi akawaeleza kuwa wakifika Pakistan waende mpaka kwenye ofisi za Taliban na wamuulizid mtu anaitwa "Umar al Masri".


Atta na wenzake wakayapokea hayo maelezo na kurejea Hamburg.


November 29, mwaka 1999 Atta na Jarrah wakapanda ndege ya shirika la Turkish Airlines, Flight TK1662 kutoka Hamburg kwenda Istanbul. (Shehi aliondoka na ndege nyingine peke yake na bin al-Shibh aliondoka wiki mbili baadae).


Walipofika Istanbul wakapanda ndege nyingine ya Turkish Airlines, Flight TK1056 kutoka Istanbul kwenda Karachi.


Kama walivyoelekezwa na Slahi, wakaelekea mpaka kwenye ofisi za Taliban na baada ya kukaribishwa wakaomba kuonana na "Umar all Masri"!!

Wao hawakujua, wakidhani ni mtu, lakini hili lilikuwa ji neno la fumbo (code word) ambalo kwenye ulomwengu wa siri wa Taliban lilikuwa na maana kuwa hao walikuwa ni wageni wa "Bwana Mkubwa".


Kwahiyo wakachukukiwa kutoka hapa Karachi, Pakistan na kupelekwa Kandahar, nchini Afghanistan.


Wakiwa huku Kandahar, wakapelekwa katika nyumba ya siri, na pasipo kutegemea na kwa mshangao mkubwa... Wakakutanishwa na "Bwana Mkubwa", Usama bin Laden.


Osama akawaeleza kuwa amekuwa anawafuatilia kwa muda mrefu ya vijana hao kupendekezwa kwake na KSM.

Akawaeleza kuwa anataka wawe wahusika kwenye shambulio la kihistoria ambalo litawashikisha adabu wamarekani na hawatasahau maishani mwao mwote, lakini shambulio hilo linahitaji vijana hao wajitoe uhai wao.!! Akawauliza kama wako tayari??


Vijana hao bila kusita sita, wakamueleza kuwa hiyo itakiwa ni heshima kubwa kwao kutekeleza tukio hilo, na wako tayari kuyatoa maisha yao muhanga.


Inaelezwa kuwa Osama "akawaapisha"!

Vijana wakala kiapo cha utii na uaminifu wao kwa Osama na Al Qaida.


Baada ya hapo vijana hawa wakapelekwa kwa kamanda mkuu wa wapiganaji wa Al Qaida, Bw. Mohammed Atef ambaye aliwapa muhtasari kuhusu tukio linahusu nini. Baada ya hapo kwa karibia miezi miwili wakapewa mafunzo ya ukakamavu wa kijeshi na mbinu za mawasiliano ya kijasusi na mbinu za kishushushu.


Kisha, wakapelekwa tena Pakistan ambako huko walikutana na KSM aliyewapa 'specifics' kuhusu mission yote.


Wakiwa tayari wamewiva kwenye kile wanachotakiwa kukifanya, February 24 mwaka 2000 wakapanda ndege ya Shirika la Turkish Airlines, Flight TK1057 kutoka Karachi mpaka Istanbul na walipofika Istanbul wakapanda ndege nyingine ya shirika la Turkish Airlines, Flight TK1661 kutoka Istanbul kurejea Hamburg.


Walipofika Hamburg wakaripoti kuwa wamepoteza Passports ili kuficha walikokuwa wametoka.


Hawakutaka kupoteza muda, siku chache baadae wakajiunga na kozi za Urubani hapo hapo Ujerumani.



Baada ya Atta, al-shehhi, al-shibh na Jarrah kurudi Ujerumani walikuwa na mabadaliko makubwa.


Wengi wanaweza kudhani kwamba labda wangekuwa sasa na misimamo mikali lakini ilikuwa tofauti.


Walikuwa na mabadiliko makubwa ya haiba zao na mtindo wa maisha.


Mfano; waliacha kwenda msikito wa Al-Quds, wakanyoa ndevu walizokuwa wamefuga, wakaacha kuvaa 'kiarabu', na badala yake wakaanza kuvaa kimagharibi.


Pia mtu kama Atta ambaye alikuwa ni mkimya kupindukia akabadilika na kuwa mtu mcheshi.


Hii haikiwa bahati mbaya, walifanya hivi ili wasiweze kutilowa mashaka yoyote na watu pamoja na vyombo vya usalama.


Pia kama kawaida wakaripoti kuwa pasipoti wamezipoteza hivyo wakatengeneza nyingine.

Al-Shehhi yeye kwa kuwa alikuwa ni raia wa UAE, hivyo akaenda huko na kuomba kabisa Visa ya kwenda amarekani.


Baada ya wote kujifunza kozi za mwanzo kuhusu urushaji ndege (Basics) kila mmoja akawa anashawishi 'supervisor' wake amuandikie 'recommendation' ya kwenda kusoma zaidi kozi hizo za urubani nchini Marekani. Na wote wakifanikiwa kupata recommendations!


Baada ya hapo wakaanza kutuma maombi kwenge vyuo mbali mbali nchini Marekani.

Kwa mfano, Atta inakadiriwa alituma karibia maombi 60 kwenye vituo mbali mbali vya kufundisha urubani nchini Marekani.


Baada ya hapo wakaanza michakato ya kupata viza.


Mohamed Atta aliomba viza yake siku ya tarehe 17, mwezi May mwaka 2000 katika ubalozi wa Marekani, nchini Ujerumani.

Kutokana na kusoma kwake Ujerumani kwa kipindi kirefu, hivyo basi akaaminiwa na hakufanyiwa upembuzi wowote wa kina, na akapewa viza siku iliyofuata ya tarehe 18 May, 2000.

Akipewa Viza ya miaka mitano ya kundi la B-1/B-2 (viza ya utalii/biashara).


Kama nilivyoeleza, al-Shehhi yeye viza yake alienda kuichukulia UAE.


Lakini kwa bahati mbaya (au nzuri) rafiki zao al-Shibh na Essabar walinyimwa Viza.


Sababu kubwa ya Al-Shibh kunyimwa Viza ilikuwa ni kutokana na uraia wake wa Yemen.

Kwa miaka mingi, mpaka sasa hivi, ni ngumu mno kwa raia wa Yemen kupata Viza ya Marekani. Sababu kubwa ni vile ambavyo kwa miaka mingi, asilimia kubwa ya raia wa Yemen wakienda nchini Marekani hubakia humo Marekani kimagendo hata baada ya Viza zao kuisha muda. Hii imepelekea mamlaka za Marekani kuwakataa Wayemen wengi wanaoomba Viza kwenda nchini Marekani.


Al-Shibh hakukata tamaa haraka baada ya kukataliwa kupewa viza. Kuna kipindi alituma mpaka ada ya dola elfu mbili kwenye kituo cha urubani cha Florida kilichomkubalia kwenda kusomea urubani na akatumia kigezo hicho kwenda kuombea viza (kwamba akubaliwa na Chuo cha Marekani na elipa ada tayari), lakini bado akakataliwa Viza.

Muda mwingine alideposit hela nyingi kwenye akaunti yake ili kuonyesha hana "njaa" hivyo hawezi kibaki kimagendo nchini Marekani akikubaliwa kuingia, lakini bado ubalozi ukakataa kumpa viza.


Baadae akakubali matokeo na akaamua kubaki Ujerumani wenzakw wakielekea Marekani na akaamua kujipa jukumu la kuwatumia hela wenzake wakiwa huko na pia kuwa kuinganishi kwa wao walioko Marekani na viongozi wao waliopo Ulaya ma Uarabuni.


SEHEMU YA TANO




June 2, 2000 Atta alipanda basi kutoka Ujerumani mpaka Nchini Czech Republic katika jiji la Prague. Kutokea hapo akapanda ndege mpaka nchini Marekani.


Al-Shehhi yeye aliondokea kutokea Dubai ambapo alipitia Brussels na baadae akatua Marekani.


Kumbu kumbu zinaonyesha kuwa al-Shehhi alianza kuwasili na siku chache, mbele Atta naye akawasili, yaani June 3, 2000.

Wote waliwasili kupitia uwanja wa ndege wa Newark Inatenational Airport.


Kwa mwezi mzima walikuwa wanakaa kwenye mahoteli kwenye miji mbali mbali huku wakiendelea kuomba nafasi kwenye vituo mbali mbali vya kufundisha urubani.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa waliwahi kufika hata kituo cha chuo cha Airman Flight School kilichopo Norman, Oklahoma lakini hawakupapenda na wakaendelea "kutalii" kwenye vyuo vingine.


Hatimaye wakapata sehemu waliyoipenda, Venice, Florida ambapo walipata nafasi katika kituo cha Huffman Aviation.

Kwahiyo wakaweka kabisa makazi na kupanga apartment hapa hapa Venice, Florida.


Wote wawili wakafungua akaunti katika benki ya SubTrust na wakawa wanalokea fedha za kujikimu kutoka kwa mtu anayeitwa Ali Abdul Aziz Ali aliyeko UAE. Mtu huyu alikuja kugundulika baadae kuwa alikuwa ni mpwa wa KSM.


Rafiki yao Ziad Jarrah naye alipata kituo cha kujifunza urubani hapa hapa Venice lakini kilikuwa ni kituo tofauti na kile wanachojifunzia Atta na al-Shehhi.



Atta na al-Shehhi walianza rasmi mafunzo tarehe 6 July, 2000.

Inaelezwa kuwa walikuwa na bidii haswa ya kujifunza. Walitrain kila siku asubuhi mpaka jioni kana kwamba hawana kingine chochote cha kufanya au wameletwa duniani kujifunza kurusha ndege pekee.


Mpaka kufikia mwanzoni mwa mwezi August, walikuwa wanaweza kurusha ndege wenyewe bila msimamizi au abiria (solo flight).


Wakaendelea kujifinza kwa bidii kubwa na hatimaye mwishoni mwa mwezi September, 2000 wakapata leseni za Urubani wa ndege binafsi.


Baada ya hapo mwezi October wakahama kituo cha kujifunzia na kwenda katila kituo cha Jones Aviation kilichopo Sarasota.

Lengo lao la kwenda huku ni ili wapatiwe mafunzo ya kurusha ndege kubwa zenye nguvu zaidi (multi-engines planes).

Lakini wakaanza kupewa 'longolongo' kuwa inabidi waanze na videge vidogo kisha baadae wahamoe kwenye midege mikubwa.


Hawakutaka kupoteza muda, mwezi huo huo kati kato wakarudi kwenye kituo chao cha zamani cha kujifunzia cha Huffman Aviation.


Wakaendelea kunifunza kwa bidii zaidi na zaidi na hatimaye mwezi November wakapewa daraja la 'instrument' (instrument rating).


Hawakutaka kubweteka wala kuridhika mapeka, 'wakakaza" zaidi na kuongea juhudi kubwa, na hatimaye mwezi December, 2000 wote wawili wakakabidhiwa Leseni za Urubani wa Ndege za Abiria.


Kwahiyo sasa walikuwa na rihusu kuendesha au kujifunza dege la aina yoyote haijalishi ukibwa wake.


Ndipo hapa kuanzia Desemba 22 hadi 29, wakaenda chuo Eagle International kwa ajili ya mafunzo mafupi ya Kuendesha Madege makubwa.


Kwa kuwa walikuwa wanakimbizana na muda, iliwabidi waanze kujifunza kwa njoo ya 'Mafunzo hisi' (Simulation trainings) ili kuepuka mlolongo wa urasimu wa kupata madege makubwa ya kujifunzia.


Mafunzo haya ya 'simulation' mfano mzuri kuyaelezea unakuwa kwenye chumba maalumu na chenye vifaa maakumu na ukakuwa kama vile "unacheza game" lakini tofauti na "game" za kawaida, hii yenyewe inakuwa ina uhalisia kabisa. Unakuwa kana kwa 100% kama upo kwenye ndege halisi.


Kwahiyo, kwanza wakaenda Opa-locka Airport ambapo hapa walifanya 'simulation training' ya ndege ya Boeing 727 kwa tarehe 29 na 30 ya mwezi desemba, 2000.


Baada ya hapo wakaenda Pam Am International Airport kwa ajili ya 'simulation training' ya ndege ya Boeing 767, hii walifanya tarehe 31 desemba.


Mpaka kufikia hapa walikuwa na ujuzi wote waliokuwa wanahotaji ili kurusha aina yoyote ya ndege.



WASHIRIKA WENGINE WANAWASILI


Jumla ya washiriki wote walihusika kuteka ndege na kuzilipua kwenye majengo siku ya 9/11 jumla yao walikuwa watu 19.


Tukiacha washiriki wakuu watatu kutoka "Hamburg Cell" ambao nimewaelezea kwa kina (Atta, al-Shehhi na Jarrah).. Washiriki wengi wachache waliwasili mwaka 2000 lakingi waliwasili mwanzano na kati kati ya mwaka 2001.


Washiriki hawa wote ni hawa wafuatao;



Nawaf al-Hamzi (miaka 25)& Khalid Mihdhar (miaka 26)


Hawa wawili walikuwa wanahusudiwa sana na bin Laden. Na aliwachagua yeye binafsi wawemo kwenye mpango huu.


Marafiki hawa wawili walipigana kwenye vita ya Bosnia upande wa Waislamu, na walishiri mapigano mengi huko Afghanistan.


Uraia: Saudi Arabia




Wail al-Shehri (miaka 28) & Waleed al-Shehri (miaka 22)


Hawa walikuwa ndugu. Kaka mtu alikiwa ni mwalimu wa shule ya awali na mdogo mtu alikiwa ni mwanafunzi wa chuo.

Walijiunga na kambi za Al-Qaida nchini Afghanistan mwaka 2000 na kuchagulowa kushiriki makakati huu.


Uraia: Saudi Arabia




Abdulaziz al-Omar (miaka 25)


Hakuna kumbu kumbu nyingi kumuhusi huyu, ila inafahamika tu kwamba alikuwa ni Imam na pia alikuwa mlinzi kwenye uwanja wa ndege.


Uraia: Saudi Arabia.




Satam al-Saquami (miaka 25) & Majed Moqed (miaka 24)


Hawa marafiki wote wawili walikuwa ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Saudi Arabia wakisome sheria.

Waliacha chuo mwaka 2000 na kujiunga na kambi za Al-Qaida nchini Afghanistan.


Uraia: Saudi Arabia


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog