Search This Blog

Saturday 24 December 2022

TOP SECRET: NYARAKA NAMBA 12333 KUTOKA WHITEHOUSE - 3

   http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/top-secret-nyaraka-namba-12333-kutoka_10.html

Simulizi :  Top Secret: Nyaraka Namba 12333 Kutoka Whitehouse

Sehemu Ya Tatu (3)




Kwa kuzingatia kwamba makala hii inalenga kuzungumzia uhusika wa CIA katika mapinduzi ya serikali ya Iran. Hivyo basi nitatoa mifano michache sana ya oparesheni zilizotekelezwa na kitengo hiki cha SAD ndani ya CIA. Nitaeleza kwa ufupi ili tusitoke nje ya lengo kuu (mapinduzi ya Iran).


Ni idara hii maalumu ya CIA ambayo ilikabidhiwa raia wanne wa Tibet kutoka kwa kaka mkubwa wa kiongozi wa kiroho wa Tibet Mtukufu Dalai Lama ambapo idara ya SAD iliwapa mafunzo ya kikomando watibeti hao kisha wakawarudisha Tibet kutafuta raia wengine 300 ambao SAD iliwapa mafunzo ya kijeshi kwa siri katika kisiwa cha Saipan na mwezi oktoba SAD ikawaongoza wanajeshi hawa mpaka Tibet kuanzisha vuguvugi la kudai kujitenga na China.


Pia ni kikosi maalumu hiki cha idara ya SAD ambacho kilimtorosha kwa siri mtukufu Dalai Lama kwa kupita katikati ya majeshi ya China yaliyokuwa mpakani na kumpeleka India.

Mpaka leo haijulikani ni namna gani waliweza kufanya tukio hili.


Ni idara hii ya SAD ndani ya CIA ambayo ilihusika kuwapatia mafunzo ya kijeshi raia wa Cuba waliokuwa wanaishi uhamishoni na kuwaongoza katika jaribio la kumpindua Fidel Castro. Mapigano haya yakihistoria yalidumu kwa siku tatu na yanajulikana kwa jina maarufu la 'Bay Of Pigs Invasion'.

Jaribio hili la mapinduzi halikuwezekana na ndilo lililochangia kudorara kwa mahusiano kati ya Marekani na Cuba mpaka leo hii.


Kwa mujibu wa nyaraka za siri za CIA zikizowekwa wazi mwaka 2004. Amri ya kumpiga risasi Che Guevara katikakati mwa miaka ya 1960 ilitoka kwa makomado wa SAD.


Ilikuwaje; Jeshi la msituni lililojiita Jeshi la Ukombozi la Bolivia (National Liberation Army of Bolivia) lilianzisha vita dhidi ya serikali ya Bolivia ambayo ilikuwa inaungwa mkono na Marekani. Jeshi hili likuwa na vifaa vya kisasa na liliungwa mkono na mwanamapinduzi Che Guevara.


Katika hatua za mwanzo za mapigano jeshi hili la waasi lilionekana kushinda dhidi ya majeshi ya serikali.

Ndipo hapo CIA wakatuma makomando wa kitengo cha SAD ambao walienda kutoa mafunzo kwa majeshi ya Bolivia katika milima Camiri. Na baada ya hapo wakawaongoza kupigana na waasi na kufanikiwa kuwashinda. Kisha makomando wa SAD wakawaongoza makomando wa jeshi la Bolivia (Bolivia Special Forces) kumkamata Che Guevara ambapo Mara tu baada ya kukamatwa komando wa SAD aliyeitwa Felix Rodriguez akaamuru auwawe.






Hii ni mifano michache kati ya mifano mingi amabayo CIA kwa kutumia kitengo cha SAD wameendesha opesheni maalumu za kijeshi katika nchi nyingi.


Ingawa Rais wa marekani ndiye anayetoa amri ya kufanyika kwa operesheni hizi za kuvamia kijeshi nchi nyingine au kuongoza mapinduzi ya serikali halali duniani kote lakini analindwa na sheria ya Marekani ambayo inampa Rais uwezo wa kukana uhusika wa Rais wa marekani kutoa amri au kufahamu kinachofanywa na kitengo hiki. (Plausible Deniability).


Sheria hii ilitingwa mwaka 1947 inajulikana kama National Security Act. Pia Sheria hii ilitiliwa mkazo na tamko la rais namba 12333 (Executive Order 12333) lenye kichwa cha habari National Intelligence Activities.







Kikaoni Whitehouse..


Rais Eisenhower akakubaliana na mapendekezo ya Mkurugenzi wa CIA Allan Dulles na kumtaka awasiliane na wenzao Idara ya Ujasusi ya Uinhereza MI6 na waanze mikakati Mara moja pasipo kuchelewa.


Lakini kabla hatujazungumza zaidi kuhusu Oparesheni ya kijasusi iloyofuata ambayo ilitekelezwa na Maafisa wa CIA Idara ya SAD ni vyema kujiuliza. Iliwezekana vipi kwa Uingireza kujimilikisha visima vyote vya mafuta nchini Iran.??


Ili kulielewa swali hili ni vyema kuangalia historia ifuatayo kwa ufupi sana..


Miaka ta nyuma, yaani karne ya 18 hadi mwishoni mwa Karne ya 20 Iran ilikuwa inatumia mfumo wa uongozi ambapo viongozi wa juu kabisa wa nchi walitoka katika koo moja (Dynasty) na aliyekuwa na madaraka ya juu kabisa cheo chake kiliitwa 'Shah'. Cheo hiki kilikuwa ni sawa sawa kabisa na cheo cha mfalme katika nchi nyingine.


Mwaka 1901 Shah aliyekuwa anatawala aliitwa Mozzafar al-Din Shah Qajar kutoka koo ya Qajar (Qajar Dynasty). Kipindi Iran bado ilikuwa ni nchi masikini sana na hakukuwa na uzalishaji mkubwa wa mafuta.


Mwaka huo kuna shushushu wa Uingereza aliyeitwa William Knox D'Arcy alifunga safari mpaka nchini Iran kukutana na Shah.


Bw. D'Arcy alijitambulisha kama mwekezaji na alienda na ofa kwa ajili ya Shah. Waingereza walisikoa taarifa kuhusu matamanio ya Shah kutembelea nchi za Ulaya lakini kikwazo chake kikubwa ilikuwa ni uwezo mdogo wa nchi hiyo kugharamia safari hiyo kubwa kwa kiongozi wa nchi na msafara wake.


Hivyo basi D'Arcy alimueleza Shah wa Iran kuwa yeye kama mwekezaji anauwezo wa kugharamia Safari ya Shah pamoja na msafara wake kwenye nchi zote muhimu barani Ulaya ambazo Shah angependa kuzitembelea na akamuahidi kuwa atahakikisha safari hiyo ya Shah inakuwa ni ya kifahari kuakisi cheo chake cha Shah na atatumia ushawishibwake kuhakikisha kuwa kila nchi ambayo Shah ataitembelea basi atapewa mapokezi ya kitaifa kwa kulakiwa na viongozi wa juu kabisa wa nchi husika. Na akamueleza kuwa ametenga kiasi cha Paundi za Uingereza elfu 20 (sawa na Paundi Milioni 10 kwa viwango vya sasa) kwa ajili ya Safari hiyo ya Shah.


Alipoulizwa atahitaji nini kwa kugharamia Safari hiyo ya Shah, akamjibu kuwa anahitaji wampe kibali cha Kutafuta Mafuta katika pwani za bahari pamoja na baharini kwenye kina kirefu.


Na endapo mafuta yakipatikana basi ataleta wataalamu pamoja vitendea kazi ili kuanza shughuli za uchimbaji.


Ndipo hapa ambapo alifanikiwa kumsainisha Shah mkataba ambao unaipa Iran 16% ya faida (pindi kampuni "ikianza kutengeneza faida).


Miezi michache iliyofuata kwa kugharamiwa na shushushu D'Arcy, Mozzafar al-Din Shah Qajar alifanya ziara ya kifahari katika nchi za Ulaya na kukata kiu yake ya miaka mingi.


Baada ya kurejea Iran D'Arcy akaingia na watu wake na mitambo na kuanza kutafuta mafuta katika kina kirefu cha bahari ya Iran.


Si miezi mingi wakagundua kowango kikubwa cha mafuta kwenye kina kirefu na baadae mitambo mizito ya uchimbaji mafuta pamoja na wataalamu wakapelekwa Iran na kazi ya uchimbaji ikaanza.


Siku si nyingi Bw. D'Arcy "akauza" hisa zake zote kwa kampuni ya Kiingereza ya Burmah Oil Company.

Mwaka 1908 hisa zote za Burmah Oil Company nchini Iran "zikanunuliwa" na serikali ya Uingereza na ndipo hapo ikaundwa kampuni mpya ya kiserikali AIOC (Anglo-Iran Oil Company).


Mwaka 1923 Mozzafar al-Din Shah Qajar alifariki na nafasi yake akarithiwa na mtoto wake Ahmad Shah Qajar.

Tofauti na baba yake aliyekuwa ni nguli wa siasa na utawali, Ahmad Shah Qajar alikuwa ni mtu dhaifu na muoga.


Hii ilimfanya apelekeshwe na wanasiasa wakongwe nchini Iran pia alishindwa kustahimili malalamiko ya wananchi kwani ilikuwa kila wananchi walipo lalamika kihusu chochote alikitekeleza.


Mojawapo ya masuala makubwa aliyo yafanya ilikuwa ni kubadili mfumo wa uongozi wa nchi hiyo.

Wananchi walikuwa wanalalamika juu ya ukoo mmoja tu kuongoza nchi na walitaka kama mfumo huo unaendelea basi kuwa na namna ambayo kutakuwa na chombo na viongozi wengine wa kusimamia shugjuli za kiserikali.


Ndipo hapa Shah mpya akaanzisha mfumo wa Majlis.

Majlis lilijuwa ni baraza la Bunge la Iran lililoundwa na Wabunge waliochaguliwa na wananchi.


Pia kwa mujibu wa mfumo huu, wabunge hao walimpigia kura mbunge mwenzao mmoja ambaye anakuwa Waziri Mkuu ambaye ndiye aliongoza shughuli za kila siku za serikali lakini Shah alibakia kuwa kiongozi mwenye mamlaka makuu ya nchi.


Kitendo hiki kilikuwa ni suala chanya kwa siasa za kidemokrasia nchini Iran lakini hakikuwapendeza waingereza kwani walimuhisi Shah mpya kama kiongozi dhaifu.


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog