Search This Blog

Friday 30 December 2022

HEKAHEKA MSITUNI - 3

    


Simulizi : Hekaheka Msituni 


Sehemu Ya Tatu (3)


Simulizi : Hekaheka Msituni 

Sehemu Ya Tatu (3)





Kumbe haikuwa imejulikana. Mheshimiwa Rais Ditric Mazimba alikuwa katika hatari kubwa sana. Walinzi hawa wawili ambao walikuwa wakilinda hapa mlangini walikuwa ni wanajeshi kutoka katika kikundi cha uasi cha Bantu Military Movement. Walikuwa hapa kwa shughuli maalum ambayo walitakiwa kuitekeleza kwa haraka sana na kwa ufanisi mkubwa. Kwa mara nyingine tena Kanali Edson Makoko alikuwa amefanya mambo yake.



Mlinzi mwanajeshi mmoja aliitoa kadi yake mfukoni na kuipachika katika mashine maalum ambayo ilikuwa pale mlangoni. Baada ya hapo alibonyabonya namba kadhaa na mlango ulifunguka. Hatimaye mlinzi yule aliufungua mlango ule taratibu na kisha aliingia ndani.



Kwa wakati huo mheshimiwa Rais Ditric Mazimba alikuwa amekwishalala. Askari Yule mmoja aliyekuwemo mle ndani naye alikuwa amepitiwa na kausingizi kidogo hivyo alikuwa amejiegesha kitini.



Bila ya kupoteza wakati mwanajeshi yule alikirusha kisu chake ambacho kilitua katika shingo ya mlinzi yule na kuzama katika koromeo. Mlinzi yule alianguka chini na kuanza kutapatapa huku akikoroma kuupigania uhai wake.



Upande wa nje ya chumba alicholala mheshimiwa Rais Ditric Mazimba yule askari inchaji aliendelea kufanya doria ya kuyazungukia maeneo yote ambayo yalikuwa yamewekewa ulinzi. Ghafla kichwa cha askari yule afisa inchaji wa ulinzi kilichemka haraka haraka, alihisi palikuwa na tatizo katika chumba cha mheshimiwa Rais.



Katika mlango wa chumba kile alionekana amesimama askari mmoja wakati pale walikuwa wamepangwa askari wawili.



“Huyu mwingine ameenda wapi?” inchaji yule alijiuliza swali lile kwa sauti ya chini. Baadaye aliamua kwenda kuangalia palikuwa na tatizo gani pale.



“Mwenzako yuko wapi?” askari yule inchaji aliuliza.

Askari yule ichaji hakupata jibu kutoka kwa mlinzi yule. Alichokipata ni ngumi kali ambayo ilifuatiwa na teke ambalo lilimkalisha chini. Kisu kilirushwa kumfuata pale chini lakini alikiona na kukikwepa. Hapo ndipo askari yule inchaji alipotambua kwamba walikuwa wameingiliwa na maisha ya mheshimiwa Rais yalikuwa hatarini.



Kutoka pale chini alijibinua na kusimama dede tayari kwa mashambulizi. Alijipanga kwa mapigo ya karate ambapo jambazi yule mlinzi naye alifanya vivyohivyo. Jambazi yule alirusha pigo la mkono ambapo askari inchaji alibonyea na kuliepa. Teke kali lilimfuata lakini nalo alilikinga kwa mikono yake yote miwili.



Ndipo naye askari inchaji alipomfyatua teke jambazi yule na kumfya ale mweleka. Alipotaka kusimama alitulizwa kwa ngumi mbili mfululizo ambazo zilifuatia na pigo la karate katika koo lake. Pigo lile lilizikata kabisa pumzi za jambazi yule na hatimaye alikata roho. Kwa kujiridhisha askari inchaji yule alichomoa bastola na kumimina risasi katika kichwa cha jambazi yule.



“Section A ….. Section B …. Section C …. We have the situation! Over!” askari inchaji aliongea katika kifaa chake cha mawasiliano akiwataarifu walinzi wote katika ikulu ile kwamba walikuwa wamevamiwa.







“Section A ….. Section B …. Section C …. We have the situation! Over!” askari inchaji aliongea katika kifaa chake cha mawasiliano akiwataarifu walinzi wote katika ikulu ile kwamba walikuwa wamevamiwa.



SASA ENDELEA



Askari inchaji yule alichomoa kadi yake maalum na kuitumbukiza katika mashine maalum iliyokuwa katika mlango wa chumba ambamo alikuwa amelala mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba. Bastola ikiwa mkononi aliusukuma mlango ule mara baada ya kufunguka na kisha aliingia ndani kwa tahadhari kubwa sana.



Askari inchaji yule hakuamini kile ambacho alikiona mkle ndani. Mlinzi wa Rais alikuwa chini amelala akiwa maiti. Katika kitanda alionekana mheshimiwa Rais akiwa amelala huku mtu mmoja akiwa amekishika kisu kilichokuwa kikimeremeta kwa makali tayari kwa kushusha pigo moja kwa mheshimiwa Rais.



Askari inchaji yule alipiga hesabu za haraka haraka. Kufumba na kufumbua alizimimina risasi mfululizo kuelekea kwa jambazi yule.



Lakini askari inchaji yule alikuwa amechelewa. Kisu kilikuwa kimeshuka na kuzama katika tumbo la mheshimiwa Ditrick Mazimba. Jambazi yule naye alikuwa amepigwa risasi nyingi sana ambazo zilimwangusha chini akiwa maiti.



Tukio lile lilitisha sana. Ikulu ndogo ya Soweni ilikuwa imechafuka. Upekuzi mkubwa sana ulianza kufanyika ili kubaini kama kulikuwa na majambazi wengine ambao walikuwa wamesalia miongoni mwa walinzi wa ikulu ile.



Wakati huo huo hali ya mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba ilikuwa mbaya sana. Madaktari bingwa wa wilaya walikuwa wamewasili pale ikulu na walikuwa wakijaribu kuokoa maisha ya mheshimiwa Rais.



Wakati huohuo kuna helkopta ambayo ilikuwa njiani ambayo ilikuwa inatakiwa imsafirishe mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba kutoka pale Soweni mpaka katika mkoa wa Dolayo ambako mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba angesafirishwa kwa ndege mpaka jijini Kano ambako angepatiwa matibabu.



Taarifa za kuvamiwa mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba pale ikulu ndogo ya Soweni zilikuwa zimefanywa siri kubwa sana. Hii yote ilikuwa ni kwa ajili ya sababu za kiusalama.

*******

“BMM oyeeeee!”

“Oyeeeee!”



“Bantu mpya safiiiiiii!”



“Saaaafiiiiiiiii!”



Hii ilikuwa ni salamu kati ya Kanali Edson Makoko na wanajeshi wake wa BMM pindi alipokuwa amekutana nao kwa dharura. Hii ilikuwa ni pindi alipopata mrejesho wa uvamizi wa kumwua mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba ambao ulikuwa umefanywa na vijana wake.



Kanali Edson Makoko alikuwa na furaha sana. Furaha ambayo alikuwa nayo siku ile hakuwahi kuwa nayo hapo kabla katika maisha yake. Habari ambazo alikuwa amezipata zilikuwa ni habari njema sana kuwahi kutokea katika maisha yake. Habari zile zilikuwa ni muhimu zaidi ya chakula ambacho alikuwa akila.



Wafuasi wa Kanali Edson Makoko walikuwa walimeibaini furaha ambayo bosi wao alikuwa nayo. Hii iliwafanya nao wawe na furaha kubwa sana. Hii ilikuwa ni kwa sababu bosi wao Kanali Edson Makoko anapokuwa na furaha basi hufanya sherehe kubwa sana pale kambini. Watu hunywa na kulewa sana. Pia wanawake Malaya huletwa pale kambini ambapo wanajeshi huburudika kwa kulala nao kimapenzi. Hii ndiyo sababu kuu iliyowafanya wanajeshi wale kufurahi.



“Nina habari njema sana ambazo ninataka niwaletee leo hii!” Kanali Edson Makoko alianza kuongea.



“Kama ambavyo niliwahi kuwataarifu kipindi furani hapo nyuma kwamba Rais Ditrick Mazimba ndiye ambaye alimwua mzee wetu Shukuru Kizibo. Siku zote jambo hili lilikuwa likinitesa sana kwani nilikuwa nikiumia sana kwa unyama huu ambao Rais alikuwa ametutendea. Unyama ule ambao alikuwa ametutendea lilikuwa ni pigo kubwa sana kwetu. Aliturudisha nyuma katika harakati zetu kwa hatua nyingi sana” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo na kuwatazama wanajeshi wao namna ambavyo wanaipokea taarifa yake.



Wanajeshi wote kwa wakati huo walikuwa kimya kabisa. Mioyo yao ilionyesha kuguswa sana na kuchomwa na habari zile ambazo Kanali Edson Makoko alikuwa akiwapa. Hii hasa ilitokana na namna ambavyo walikuwa wamemzoea marehemu mzee Shukuru Kizibo.



“Binafsi sikupenda kuona mwanaharamu yule akiendelea kuvuta pumzi ya dunia hii. Nilitaka na niliazimia kumfanya aulipe uovu wake. Sikutaka kusubiri mpaka siku ya mapinduzi itakapofika. Kwa sababu yeye alikuwa ameyakoroga mambo, basi nasi ilibidi tuyakoroge vilevile” Kanali Edson Makoko aliendelea kumwaga cheche.



Wanajeshi waliendelea kuwa kimya wakiwa na shauku ya kutaka kujua ni jambo gani ambalo limetokea ambalo kiongozi wao Kanali Edson Makoko alikuwa akitaka kuwaambia. Mioyo yao ilikuwa na shauku kubwa sana.



“Basi hapo nilianza kuandaa mpango wa kuhakikisha Rais Ditrick Mazimba anatoweka duniani. Mpango huu nilikaa na kuupanga kwa muda mrefu sana kwani ulikuwa ni mpango ambao ulikuwa unahitaji umakini wa hali ya juu sana hasa ukichukulia hadhi ya mtu ambaye alikuwa akitakiwa kuondolewa duniani” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo.



“Mpango wangu lipokamilika, basi niliuingiza katika utekelezaji. Niliwateua wanajeshi wawili miongoni mwenu kwa ajili ya kuutekeleza mpango huu. Kwanza kabisa ninaleta kwenu habari za huzuni kwani wale wenzetu wawili wameyapoteza maisha yao. Waliuawa wakiwa wanautekeleza mpango huu” Kanali Edson Makoko alitulia kidogo akiwatazama wanajeshi wake ambao waliviinamisha vichwa vyao kwa huzuni.



“Lakini hatupaswi kuhuzunika sana kwa sababu wenzetu wale walikuwa ni wazalendo ambao walikuwa wamejitolea maisha yao kwa ajili ya kuyatetea maslahi mapana ya jeshi la BMM na wananchi wa Bantu kwa ujumla” Kanali Edson Makoko al;itulia kidogo.



“Habari njema ni kwamba mpango wetu huu umefanikiwa kwani wenzetu wale walifanikiwa kumwua Rais Ditrick Mazimba. Hivyo ninatangaza rasmi kwamba Rais Ditrick Mazimba ameuawa na kisasi cha kifo cha kiongozi wetu kimelipwa. Jambo pekee ambalo tutakuwa nalo kwa sasa ni maandalizi ya mpango wa mapinduzi. Tunatakiwa tuifyekelee mbali serikali nzima ya Bantu. Viongozi hawa hawastahili kabisa kuendelea kuwepo madarakani” Kanali Edson Makoko aliongea.



“Hureeeeeeeee!” wanajeshi wote walipiga kelele za shangwe huku wakizinyanyua juu bunduki zao.



Walionyesha kuwa na furaha kubwa sana kwa habari hizi ambazo walikuwa wameletewa na kiongozi wao. Habari hizi ziliwafanya warukeruke kwa furaha. Hawakuamini kama kilio cha kisasi kwa mtu ambaye alikuwa amemwuua kiongozi wao kilikuwa kimesikika.



Lakini wanajeshi hawa hawakufahamu siri kubwa sanaambayo ilikuwa nyuma ya mambo yale. Wao waliendelea kulishwa unga wa sumu ndani ya fikra zao.

*****





Lakini wanajeshi hawa hawakufahamu siri kubwa sanaambayo ilikuwa nyuma ya mambo yale. Wao waliendelea kulishwa unga wa sumu ndani ya fikra zao.



SASA ENDELEA



“Kwa sasa ninatangaza sherehe za ushindi. Kwa muda wa wiki nzima iktakuwa ni sherehe hapa kambini ambapo tutakunywa pombe na kuburudika. Yaani raha na starehe za aina zote zitakuwepo hapa kambini kwa muda wa wiki nzima!” Kanali Edson Makoko aliongea.



“Hureeeee! Long live our Cornel!” wanajeshi walipiga kelele za furaha huku wakimimina risasi ovyo angani.

******

OFISI ZA BSA JIJINI KANO



Habari zakuvamiwa mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba zilikuwa zimeifikia ofisi ya Idara ya usalama wa Taifa ya BSA. Habari hizi hazikuwa njema hata kidogo. Maafisa waandamizi wakiongozwa na mkuu wao yaani Chifu walikuwa wamekusanyana na kujaribu kutafakari ni vipi tukio baya kama lile liliweza kutokea. Hali ya ulinzi na usalama wa Rais ilikuwaje mpaka mahaini hao wakaweza kujipenyeza na kufanya maafa yale?



Waliamini kwamba ni lazima kulikuwa na uzembe katika kikosi cha usalama wa Taifa na kikosi cha ulinzi na usalama wa Rais.



Wakati huu Dokta Morgan aliwasili katika ofisi za BSA kwa ajili ya kufanya mazungumzo muhim sana na Chifu.



“Karibu sana dokta” Chifu alimkaribisha dokta Morgan



“Ahsante sana Chifu” dokta Morgan alijibu.



“Karibu uketi hapo” Chifu alimwelekeza dokta Morgan mahali pa kuketi katika sofa.



“Starehe!” dokta Morgan alijibu.



“Nadhani umekwishasikia kile ambacho kimetokea kwa Rais wa Jamhuri ya Bantu” Chifu alianza kuongea.



“Ndiyo Chifu. Nimesikia” dokta Morgan alijibu.



“Basi hali ni mbaya dokta. Maisha ya mtukufu Rais Ditrick Mazimba yako hatarini sana” Chifu alitulia kidogo na kumtazama dokta Morgan.



“Nimepokea ujumbe kutoka Idara ya usalama wa Rais ikulu. Wananiomba msaada wa kuokoa maisha ya Rais. Hii ina maana kwamba taaluma yako pamoja na umahiri wako katika tiba vinatakiwa sasa katika kuyaokoa maisha ya Rais. Nadhani umenielewa dokta!” Chifu aliongea.



“Nimekuelewa Chifu. Naamini Mungu atasaidia na maisha ya mheshimiwa Rais yatakuwa salama kabisa” dokta Morgan aliongea.



“Ok, basi nifuate kwa zoezi hilo linaanza sasa!” Chifu aliongea.



Chifu alisimama na kuanza kutoka mle ofisini huku akifuatwa na dokta Morgan. Moja kwa moja walienda mpaka mahali ambapo maafisa waandamizi wa BSA walikuwepo wakifanya mazungumzo.



“Attention! Kama vile ambavyo kila mmoja ana taarifa, ni kwamba mheshimiwa Rais amevamiwa na kuchomwa kisu katika ikulu ndogo ya Soweni. Kwa taarifa nilizonazo ni kwamba hali yake mpaka sasa ni mbaya. Kwa sasa yuko njiani analetwa hapa Kano. Atakuwepo katika hospitali ya Kano kwa ajili ya matibabu ya awali kwa ajili ya kuweka afya yake katika hali ya usalama!” Chifu alitulia kidogo na kuvuta funda la mate.



“Nadhani mpaka hapo mtakuwa mmefahamu kazi nzito ambayo iko mbele yetu kama Idara ya usalama wa Taifa. Kwanza kabisa itakuwa ni kuwatafuta watu waliofanya uhaini huo. Na pili ni kuhakikisha kwamba hakuna jambo linguine la hatari ambalo litampata mheshimiwa Rais” Chifu aliongea.



“Sawa mkuu!” maafisa walijibu kwa umoja.



“Kwa sasa Code 001 utakiongoza kikosi. Naomba umfikishe dokta Morgan mpaka katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano ambapo yeye atasimamia matibabu ya mheshimiwa Rais. Wengine wote pia myahakikisha kwamba mnafanya track katika eneo lote la hospitali ile ili kuhakikisha kwamba hakuna hatari nyingine ambayo itakuwa imepangwa. Hii ndiyo misheni ya awali. Misheni nyingine mtapata taarifa” Chifu aliongea kwa msisitizo.



“Sawa mkuu umeeleweka!” maafisa wote walijibu kwa pamoja huku wakionyesha munkari mkubwa.



“Haya nendeni sasa” Chifu aliongea na kasha aliondoka kutoka eneo lile.



Maafisa wale walijiandaa kwa haraka sana. Baada ya kujiandaa walimchukua dokta Morgan na kuanza msafara wa kuelekea katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano.

*******

HOSPITALI YA RUFAA YA TAIFA YA KANO



Mheshimiwa Rais Ditrick Mazimba alikuwa amefikishwa katika hospitali ya rufaa ya Taifa ya Kano. Madaktari walikuwa wakihaha huku na huku katika kuhakikisha kwamba hali ya mheshimiwa Rais inakuwa ahueni.



Dokta Morgan daktari kutoka Idara ya usalama wa Taifa ya BSA ndiye alikuwa daktari ambaye alikuwa ameteuliwa kuhakikisha kwamba maisha ya mheshimiwa Rais yanakuwa salama. Sababu za kumpendekeza na kumteua daktari huyu ilikuwa ni kutokana na umahiri wake katika masuala ya tiba.



Hali ya ulinzi kuzunguka eneo lote la hospitali ile ilikuwa imeimarishwa sana. Askari mbalimbali kutoka katika idara mbalimbali za usalama wa Taifa walikuwa wametapakaa kila mahali katika kuhakikisha hakuna hatari yoyote ambayo inatokea kwa mheshimiwa Rais.



“Hali ni mbaya. Mheshimiwa Rais amepoteza damu nyingi sana. Hivyo anatakiwa kuongezewa damu haraka sana!” dokta Morgan aliongea mbele ya wakuu wa idara mbalimbali za usalama.



“Sasa si aongezewe haraka dokta?” mkuu wa idara ya usalama wa Rais ikulu aliongea.



“Uko sahihi mkuu. Nadhani kila mmoja anawaza kama ambavyo wewe wawaza. Lakini kuna tatizo kubwa sana” dokta Morgan aliongea.



“Tatizo gani dokta?” Chifu aliuliza.



“Damu ya mheshimiwa Rais ipo katika kundi maalum. Watu ambao wana damu ambayo ipo katika kundi hili ni wachache sana. Hivyo hii inaleta ugumu katika upatikanaji wa damu ya kumwongezea mheshimiwa Rais” dokta Morgan aliongea.



“Duh!” wakuu wale wa Idara za usalama wa Taifa walijibu kwa pamoja wakionyesha kuchoka kabisa kwa majibu yale kutoka kwa dokta Morgan.



“Sasa tunafanyaje dokta?” afisa mwingine aliuliza



“Kwa mujibu wa rekodi zilizopo ni kwamba hapa nchini kuna watu sita ambao wana damu ya kundi hili la mheshimiwa Rais. Hawa watano rekodi za upatikanaji wao hazijawekwa vizuri. Lakini yupo huyu mmoja ambaye rekodi zake zipo clear kabisa!” dokta Morgan aliongea.



“Basi huyo aletwe hapa mara moja pasi kupoteza muda” Chifu aliongea.



“Kwa mujibu wa rekodi zilizopo ni kwamba hapa nchini kuna watu sita ambao wana damu ya kundi hili la mheshimiwa Rais. Hawa watano rekodi za upatikanaji wao hazijawekwa vizuri. Lakini yupo huyu mmoja ambaye rekodi zake zipo clear kabisa!” dokta Morgan aliongea.



“Basi huyo aletwe hapa mara moja pasi kupoteza muda” Chifu aliongea.



SASA ENDELEA



“Huyu bwana anaitwa Martin Samweli. Ni askari jeshi katika jeshi la BMM. Hapo awali alikuwa ni mwanajeshi katika Jeshi la wananchi wa Bantu lakini baadaye aliasi na kujiunga na kikundi cha waasi cha BMM” dokta Morgan aliongea.



“Mungu wangu!” wakuu wale waliongea kwa pamoja vinywa vyao vikiwa wazi kabisa kuonyesha kukata tama kabisa.



“Hii ina maana kwamba inatakiwa kwenda katika kikundi hicho cha waasi na kumchukua huyu bwana ili aje awe msaada hapa kwa maisha ya mheshimiwa Rais” dokta Morgan aliongea.



“Aiseee! Hapa tuna changamoto kubwa sana. Litawezekanaje jambo hili?” afisa mmoja alihoji.

ITAENDELEA

   

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog