Search This Blog

Friday 30 December 2022

KIAPO (AGANO LA DAMU) (2) - 5

 


Simulizi : Kiapo (Agano La Damu) (2) 

Sehemu Ya Tano (5)


Njaa Ilimuuma Isack Ila Akuwa Na Jinsi Zoez Likaanza,maskin Mpira Wakawa Wakitupiana Wenyewe Kwa 

wenyewe wakim'bagua mtoto yule!



moyo ulimuuma Isack Akatoka Uwanjan Huku Kitu Kikimkaa Kooni Akijiuliza Kwa Nin Anabaguliwa? Kosa Lake 

Lipi Hasa? Ni Kwa Sababu Ya Bray?! Kisa Umaskini Au Kisa Mery?!



Kwakwel Akupata Jibu Sahihi Akawa Analia Kusafisha Uchungu Ulouzunguka Moyo Wake!



"isack!"



Ghafla nyuma yake Akaitwa Kwa Sauti Nyororo Ambayo Ilimlazimu Ainue Kichwa Chake ageuze

Shingo yake Kumtazama Yule Aliyemwita!



Macho Yake Yakakutana Na Tabasamu La Binti Mrembo,tabasamu Ambalo Kwa Kiasi Flani Lilimtoa Katika 

Tanuri La Mawazo Na Mateso Katika Moyo Wake,akabaki Akimshangaa Binti Yule Akasogea na Kuketi, karibu 

Na Isack



"mbona Wewe Ushirikiani na wenzako katika michezo isack!,kwanza kwa nin umevaa ovar rol una nguo za 

mazoez wewe?!"



"wamezichana chana nguo zangu!"



Isack akaongea kwa sauti ya upole



"wamezichana nguo zako kina nani hao?"



binti yule alokuwa na asili ya kizungu akazidi kumuuliza akionekana wazi kuanza kushangaa



"watu nnaoishi nao bwenin wameiba ela zangu zote na kuchana chana nguo zangu azifah tena kuvaa"



"atakuwa ni head boy tu yey si ndo anafunguaga ma bweni na si ndo mnakaa naye?"



"ndiyo! aina tabu embu twende nifate"



Isack Akamfata Binti Nyuma



"nisubiri Hapa"



Binti Yule Akakimbia Kuelekea Upande Wa Mabweni Yao Akukaa Sana akarejea akiwa na kamfuko cha 

nailon,akatoa track tatu na tshart zake



"hizi nguo mpya Isack Sijazivaa,nimezifua Tu hii Moja Utaifanya Ya Mazoez Si Unapenda Mpira Wewe!"



"yah!"



Isack Akajibu Akitabasamu



"basi Na Hizi Mbili Utafanya Za Kushindia! Naskia Kesho Tunamechi Nje Tukitoka Ntakununulia Zingine 

Sawa!"



"asante Alice"



Isack Akamshukuru Binti Yule Alokuwa Akisoma Naye Darasa Moja,alikuwa Ni Binti Mwenye Huruma,na 

Akupenda Jinsi Mtoto Yule Alivyonyanyasika,alijikuta Tu Akimpenda,



"peleka Hizi Nguo Ndani Tutaonana Uwanjani"



Isack Akageuka Kuanza Kukimbia



"isackiii"



Akapiga Breki Baada Ya Kuitwa Akageuka nyuma kumtazama alice,aligundua kitu kwenye macho ya binti yule



Mapenzi!!



Akamnyooshea Mkono Kumwita Ikabidi Isack Arudi!

"ehe Nimekumbuka Ulinambia Umeibiwa Ela Zako Zote Chukua Hii Itakusaidia Mpaka Mwisho Wa Mwez Mzaz Wako 

Akija Kukutembelea!"



Isack Akatoa Macho Ya Mshangao Zilikuwa Ni Ela Nyingi Sana!



"alice Na Wewe Utatumia Nini?!"



"usijal Isack Mimi Nnazo Zangu Hizi Apa!"



Wote Wakacheka!



"kwa Hyo Ndo Unatembea Nazo?"



Alice Akacheka "yah Ili Kukwepa Kuibiwa,hata Sisi Kule Kwetu Wezi Kama Nin"



"asant Nami Ntakuwa Natembea Na Zangu!"



"yapaswa Uwe Makini Zisipotee"



"au Kwa Nin Wewe Usiniwekee alice nkawa natumia kidogo kidogo?"



"na tukigombana je? we weka mwenyewe bhana!"



"sawa wacha nkajiandae tutaonana zoez"



wakatawanyika





*********



kijana alosifika kwa kucheza mpira katika chuo kile ni Brayson,

"dah Kesho Nataman Nimuone Bry Wangu Jins Akitupia Mabao"

Mery Aliongea Kwa Furaha Kumwambia Mdogo Wake Agnes!



Egi Akaduwaa,akikumbuka Jins Bray Alipomwambia Kuwa Mery Ni Mchumba Ake,leo Mery Anadhibitisha Ilo!

"mh Mery Bray Wako Ina Maana Una Mahusiano Na Head Boy?"

"tia Tiki Hapo Yule Ni Wangu Star Wa Football Kisha Hao Maintain Colage Watamjua Vizuri"



"ha ha ha ha kesho huyo bray wako atafuzu kwa bf wangu na nyota yake itazimwa mwaaaaaa"



ghafla ikasikika sauti ya mtu alokuwa akiingia,si mwingine ni Alice Binti Alotokea Kumsaidia 

Isack,aliongea Tu Bas Kujifuraisha Ila Mwenyewe Aliujua Uhodar Wa Bray Katika Kabumbu!



Wote Wakamcheka



"toka Lini Mama Mchungaj Ukawa Na Bf"



Mery Akaongea Kwa Kejeli



"ndo Hapo Kesho Mtakapo Ona Nyota Mpya Itakapo Ng'aa Kwa Leo Twenden Uwanjan Mkajionee



Wote Wakaongozana Kuelekea Uwanjani!



Uwanjan Zoez Liliendelea Kama Kawaida,bray Alishtuka Kumuona Isack Akitokea Akiwa Na Bukta Na Tshart Za 

Mazoez Alikumbuka Si Alizichana?



Akakumbuka Uhodari wa kijana yule Katika Uchezaji Mpira wakati wakiwa gulion akajikuta akikosa raha!



Akajikuta akianza kunyong'onyea



Ticha wa michezo akawapanga ili kuchambua wakucheza mechi kesho na kwa bahat mbaya isack akapangwa 

tofaut na bray yan yey akapangwa amkabe bray akiwa na mpira au bray amkabe isack akiwa na mpira mechi 

ya zoez ikaanza!



isack akapata mpira ila kabla ajapiga akaenda chini watu wote uwanjani wakaangua kicheko Isack

Akaonekana wazi ajui kucheza mpira,mwalimu akamtoa nje!



dah ilimuuma sana!...



je nini kitaendelea chuoni pale,vita ile ya isack na bray itakuaje vp isack atampenda alice?







Tanuri La Mateso Bado Linaya Andama Maisha ya mtoto Isack Furaha Imeenda Mbali Na Upeo Wa Moyo Wake,



Baada Ya Kashkash Ya Mzee Alex Akimtumia Zidu Mara Kadhaa Wakimkosakosa Kumuua Zidu Anaishia Guantanamo 

Gereza La Mateso Kifungo Cha Maisha,Alex kwa uoga anaacha kumfatilia mtoto yule ila sasa furaha yake 

inapokonywa na mtoto mwenzake Bray! Tena Walokuwa Marafiki Wakubwa Tanzania,je Unahis Isack Ataweza 

Kuendelea Kuvumilia Mateso Yale Ikiwemo Kunyanyaswa,kuteswa,kuonewa Na Mambo Mengine Ya Ajabu Kama 

Haya?!



TUSONGE



Vicheko vilivyochanganyikana na miluzi,kuzomewa vilizidi kumsindikiza Isack Kumtoa Nje Ya

uwanja,



"best kama ulikuwa uwezi kucheza si usingeingia Isack Ona Sasa Ulivyoaibika"



Alice Alimwambia Huku Akimfuta Mavumbi



"he he heee aloooh huyo ndo bf wako wakuzima nyota ya Bray Wangu"



Ghafla Ikasikika Sauti Nyuma Yao Akuwa Mwingine Zaidi Ya Mery Kabla Awajamjibu Kitu Ghafla Wakasikia 

Goooh Tayar Bray Alishafanya Yake



"umeonaaa? Yule Ndo Mwanaume Sasa Ila Si Huyu Eti Anazima Nyota Ya Mume Wang Aaah Ndo Kwa Uchezaji Ule 

Anapewa Pasi Tu Chini Yan Kupokea Pasi Tu Matatizo Ndo Ataweza Kubutu



Mery Akazidi Kumtolea Bray Maneno Ya Kukera Yalomchoma Mpaka Ndani Ya Moyo Wake



"hivi Nimekukosea Nin Mery Mbon

unanichukia hivi?"



"ha ha ha ha ha unataka nikupende kwa sura gan hasa ulonayo nampenda mtu mmoja tu naye ni Bray Wewe 

Nakuchukia Unajua Kwa Nin? Kwa Kitendo Chako Cha Kuja Kunikumbatia Mbele Ya Mpenz Wangu Ili 

Untenganishe Naye Siyo Umeshndwa Kaka Wewee Kama Huyu Alice Akutoshelez...



"ishia Hapo Hapo Mery Isack Twende Tuondoke Zetu"



Pale Hapakuwa Eneo Salama Tena Akamchukua Isack Wake Wakatoka Nyuma Wakizomewa Alice Akujal Ilo!



Wakaelekea Zao Restraunt Wakaagiza Chakula Na Kuanza Kula!



"unaweza Kuniadithia Historia Ya Maisha Yako Na Mahusiano Yako Na Mery,bray Na Janeth!"



Lilikuwa Ni Swal La Ghafla Lililomshtua Hata Isack Mwenyewe



"mimi?,historia Ya Maisha Yangu Mimi?!"



Isack Akauliza Pasina Kuamini Tena Kwa Wasiwas Mkubwa,Alice akaachia tabasamu,murua,tabasamu lenye 

lengo la kumtoa khofu Isack Kisha Likafatiwa Na Sauti Nyororo,sauti Tamu! Sauti Ya Kubembeleza 

Ilofanikiwa Kuitoa Khofu Na Wasiwas Uliyokuwepo Moyoni Mwa Isack



"sina Nia Mbaya Isack Lengo Nifahamu Tu Aiwezekani Bray Mtu Mnaotoka Taifa Moja Akuchukie Tu Mery Naye 

Vivyo Hivyo Kunasababu Hapo Katikati Nambie Mim Ndo Rafiki Yako Wa Karibu! Au Uniamini?"



Ghafla Machozi Yakaanza Mtiririka Isack!,jambo Hilo Likamshangaza Zaidi Alice!



"mbona unalia Bray bas kama unahisi nimekosea kukuhuliza ivyo nsamehe..."



Alice Akaongea Kwa Unyonge!



"hapana Ujakosea Kuniuliza Alice Ila Nalia Kwa Uchungu Uliyoko Katikati Ya Moyo Wangu Uwez Amin 

Nikikwambia Bray Tanzania Alikuwa Rafiki Yangu Mkubwa Tena Wa Pekee"



"una Maana Gani Kusema Ivyo?"



"namaanisha Hivi Mimi Nimezaliwa Katika Familia Ya Kimasikini Kuta Yetu Tabu Ila Tuliishi Kwa Raha Na 

Amani,

Kutokana Na Umasikini Mkanda Wa Kaptura Yangu Ulikuwa Malboro Nilivaa Ndala Mimi Kitendo Hiko 

Kikanifanya Wanafunz Wanitenge Ila Si Kwa Bray!



Bray Alinipenda Nilikaa Naye Katika Dawati Moja Yeye Pekee Ndo Alikuwa rafiki yangu!,maisha yalipozidi 

kuwa magumu ada sina nikasimamishwa shule ivyo ikamlazimu baba auze kipande cha uwanja apate ada nirudi 

shule na apate ela ya chakula akamuuzia diwani wetu aloitwa mr alex,ndo baba yake agnes na mery..."



"wachaa wewee embu ngoja ehee ikawaje sasa?"



"mr Alex akajenga nyumba Kubwa Pale Jiran Yetu Akawa Anaishi Na Familia Yake Yey Mke Wake Na Mtoto Wao 

Agnes Mery Kipind Icho Wakiamia Yeye Alikuwa Chuo Hvyo Sikupata Kumuona..



Baba Na Baba Mery Walikuwa Na Ugomvi Ambao Sikujua Sababu Ni Nini Ila Nilikuwa Nikimsikia Baba Akisema 

Mr Alex Kamdhulumu Ardhi Na Hata Kile Kiwanjakumlipa ela yake yote,siku zilivyozidi kwenda ugomvi 

ukazidi kukua mzee alex akitwambia mpaka ile nyumba ni mali yake ivyo akatupa siku kumi tuame akawa 

akituhesabia!



na kwel ile siku ya kumi nilipotoka shule nilishughudia nyumba yetu ikiungua moto aikujulikana ninani 

aloichoma,wazaz wangu wote wakafia ndani!...



Isack Alipofika Hapo Alilia Akikumbuka Wakati Nyumba Yao Ilipokuwa Ikiteketea Akawa Kama Akizisikia 

Sauti Za Wazaz Wake Wakilia Wasaidiwe!



Machozi Yakazidi Mchuruzika! Sasa Alilia Kwa Kwikwi



"hapakuwa Na Wakuwasaidia Wazaz Wangu Mpaka Moto Unazima Ilikutwa Miili Ya Wazaz Wangu Ikiwa 

Imegandana,ilibadilika rangi na kuwa myeusi nilizimia mara kadhaa kila nilipoiona miili ya wazaz wangu!



kwel tuliwazika wazaz wangu na katika kikao ikapendekezwa mi nikaishi kwa diwani alokuwa jirani yangu



maisha ya mwanzo yalikuwa mazur ila kadri siku zilivyokuwa zikienda maisha yalianza badilika mama agnes 

akawa akintesa yey na mwanaye egy napigwa,



nikiomba daftar la shule nanyimwa vita vikaamia mpaka shule nachonganishwa na walimu,mama anakuja 

anansingizia vitu ambavyo sivyo mpaka nachapwa na walimu wote sasa ikawa shule panawaka moto nyumban 

panawaka moto,kwa bahat nzur kuna mwalimu mmoja Mungu Ailaze Roho Yak



mahali pema madam Jane Alitokea Kunipenda,akawa Akinsaidia Madaftari...



Mh! Alice Siku Moja Nilipotoka Shule Kufika Nyumban Nje Nkakuta Gari Kali,kuingia Nikaskia Mgeni 

Akiongea Kuwa Yule Ni Mdogo Wake Na Baba Yangu Yani Bab Mdogo Wang Nlfrah Kumuona Akasema Amekuja 

Kunichukua Wazaz Walonlea Mwanzo Walpinga Anichukue Ila Mwisho Wakakubali,tuka Toka Mpaka Katika Jumba 

Lake Kumbe Mtu Yule Alitaka Kuniua....



"mamaaa Kwa Nin Sasa Mamdogo Wako Atake Kukuua?!"



"sijui Alice Mtu Yule Akaenda Ntupa Porin Nkaokotwa Na Wawindaji Wakanipeleka Mpaka Kwa Madam Jane Ila 

Bab Mdogo Bado Aliendelea Kuniwinda Aniue,akaja akamuua madam jane,na kila nlipomkwepa mara kadhaa 

alinikamata siku ya siku nikagundua kumbe wanashirikiana na baba mery ,



nikiwa simjui mery na nimemsahau siku moja wakat bab yake na zidu wakitaka kuniua alitokea kuniamua 

ivyo tukachanganywa naye wote wawil tukataka kuuwawa ila kuna mtu (kijo) simjui alikuja kutuokoa 

akatupeleka porin alikuwa akiwasiliana na zidu sijui waliongea nin mtu yule akapanda gari akionekana 

wazi kuchanganyikiwa na kuondoka akatuacha pale

mim nlikuwa na hali mbaya Mery Akajitahid Kunsaidia Na Kwa Bahat Nzur Alipata Guda,



"guda! Guda Ndo Nini?"



Alice Akahoji



"guda Ni Kamkokoteni chenye tairi moja mbele akanibeba na kunipandisha akaanza kukasukuma,.."



"mery huyu huyu wa head boy"



"ndiyo huyu huyu!"



"ehe ikawaje maana siamin"



"ndo maana mi mwenyewe nashangaa alice,basi alijitahidi ila naye alikuwa hana nguvu mwisho alishindwa 

akadondoka Akapoteza Fahamu! Tulikuja Okolewa Tukapelekwa Hosptalini! Tukiwa Sote Hatuna Fahamu Huu Ndo 

Ukawa Mwisho Wa Mimi Na Mery Kuonana



Nilipokuja Kushtuka Nilikuwa Npo Hosptalin Madam Jane Akiniangalia Wakisaidiana Na Polis Mmoja Ambaye 

Aliamishwa



Nilikuja Ruhusiwa Nikachukuliwa Na Madam Jane Ila Tulifika Supar Maket Moja Madam Akaniacha Naye Kwenda 

kununua vitu,ile kutoka zidu akaniibukia na kunichukua akanpeleka kwake ambapo alinifungia ktk chumba 

chenye mamba"



"chumba chenye mamba kivipi?"



"yani kile chumba ndani kilikuwa na kisima cha mamba,alokuwa akiwafuga"



"mamaaaaaa mamba hawa hawa"



"yah mamba hawo hawo unaowajua hawa wanne!"



"ilikuwaje sasa ukapona!"



"nilitaka niunde urafiki na wale mamba kama nilivyofunzwa na tartaz kule porin tartzan alinambia ili 

niunde urafiki na wanyama uchawi wao mkubwa nichakula ivyo zidu alivyonletea chakula nikaona niwatupie 

nyama kumbe zinasumu si ndo wakafa nikamwaga kile chakula"



"Mungu wangu jitu lina roho mbaya ilo ikawaje sasa?"



"alipokuja akashkwa na hasira kisa nimemwaga chakula akanshka na kuntupia kisiman niliwe na mamba"



"mamaaaaaa"



alice akatoa macho hayo

ila isack akaendelea



"akaja nichungulia aone ninavyotafunwa na mamba wake si ndo akawakuta wamekufa akatoa bastola akiwa na 

hasira na kunimiminia risasi mingi mingi kifuani damu zikazagaa kisimani alidhamiria kuniua yule mtu"



alice alijikuta akishindwa vumilia na kumkumbatia Isack Kwa Nguvu Huku Akimpa Pole! Machoz 

Yakichuruzika Na Kumdondokea Isack Kifuani Kwake



Dah Kweli Kilimuuma Alice







Mtoto Isack Bado Anapitia Katika Majaribu Magumu!



Ananusurika Kufa Mara Kadhaa Toka Kwa Zidu Katili Anayeishia guantanamo gereza lenye mateso makali



Isack Anapata msaada kwa afisa wa fbi anayemchukulia kama mwanaye! yey na mke wake bi sara wanaamua 

kumpeleka isack chuo huko anaenda kukutana na watu anaowafahamu akiwa rafik yake Bray,Mery na Agnes Cha 

Ajabu Wanamtenga Na Bray Kuanza Kumnyanyasa Ila Alice Binti Wa Kizungu Anatokea Kuwa Karibu Na Bray 

Kumsaidia Na Hata Kumpa Moyo



Bray Anamsimulia Alice Stori Nzima Ya Maisha Yake,stori Inayomuumiza Alice,je Nin Kiliendelea?



NA HII NI SEHEMU YA HAMSINI NA TANO



"pole sana Isack Kwa Yale Yote Yalokukuta,mi Ntaongea Na Mery Nijue Kilicho Mfanya Akuchukie Kuna Kitu 

Hapa Katikati Aiwezekani Apiganie Maisha Yako at the end aje akufanyie hivi!,nimesikitika sana Isack 

mtoto mdogo lakini umepitia mambo makubwa tena ukiwa katika umri mdogo,ila Nikuhaidi Kwa Saivi 

Ntajitahidi Kuwa Karibu Yako,ntajitahidi Uishi Vizuri Hapa Chuoni!...



Kwa Sasa Twende Tu Tukacheki Mpira Mi Ntaongea Na Mery,kingine Isack Nakupenda...



Isack Akaduwaa,alice Anampenda?!,akajikuta Akimwangalia Kwa Mshangao,alice Akaangalia Pembeni Kwa Aibu



"u..u..unasema?!"



Isack Akauliza Pasina Kuamin Kile Alichokisikia kutoka kwa mtoto yule wa kizungu!



"nakupend isack,nimeshindwa kuzizuhia hisia zangu toka nlipokuona mara ya kwanza..."



"ssh alice usiongee sana nimekuelewa mamy wacha ntakujibu wacha saiv nikaingize zile nguo ndani 

zitakuwa zimekauka?"



"nguo? siumesema zimechanwachanwa nguo zako ni nguo zipi hasa unazosemea!"



Isack Akaduwaa, Je Amwambie Ni Nguo Za Wenzak Walomlazimisha Afue Au?



Akabaki Kaganda Pasina Kujua Amjibuje!



"nijibu bas isack wang"



Alice Akazidi Mlalamikia Huku Mkono Wake Akiupeleka Kifuani Kwa Mtoto Yule Na Kupapasa Taratibu Tena 

Kwa Uwoga Wa Mbali,ila Akujal Sana Si Alishazieleza Hisia zake!



"yah zile si zangu waliniomba tu nikawainulie ikiwa zitakauka na wenyewe wako mchezoni"



Isack Akajitahidi Kudanganya



"haaaa We Wawapi Yani Wakunyanyase Na Nguo Uwainulie Achana Na Hiyo Kitu Kabisa Sikushauri Kufanya Ivyo 

We Kwa Saiv Kachukue Daftari Tukatafute Darasa Tujisomee!



Isack alizidiwa wakakubaliana akaenda kuchukua daftar wakachagua darasa moja wapo na kuanza kujisomea!



kesho yake ilikuwa ndo siku ya mechi nje ya chuo,wanafunzi wakajiandaa muda ulipotimia wakaingia ndani 

ya gari kuelekea katika icho chuo walichopanga wapambane nacho



hatimaye mechi ikaanza!,moyo wa Isack Ulimuuma Sana alitamani naye awe mmoja wa wachezaji kwani ni moja 

wapo ya vitu alivyovipenda!



ndani ya dakika 20 Bray Alikiwezesha Chuo Chake Kupata Goli La Kwanza Na Dak 43 Badae Kabla Ya Dakika 

Mbili Za Mapumziko Akaipatia Timu Yake Goli La Pili Vifijo Vilirindima Uwanjani Jina La Bray Likitajwa



Wakati Huo Maskin Isack Alikuwa Pembeni Ya Mwalimu Wake Wa Michezo Akimbembeleza Ampe Nafasi Naye 

Aingie



"aaah We Na Mpira Wapi Na Wapi Jana Tu Kupewa Pasi Kuituliza Unaanguka Utaiwezaje Mechi?"

Mwalimu Yule Wa Michezo Aliongea Kwa Majivuni Mbele Ya Mwalimu Mwenzake Wa Shule Pinzani



Mwalimu Yule Wa Chuo Cha St Mery Alijikuta akimuonea huruma Isack!



Akuona Sababu Ya Mwalimu Yule Kumkataza Mtoto Kucheza Hali Ya Kuwa Ni Mechi Ya Kirafiki Tu!



"mwalimu Namuomba Huyo Mtoto Achezee Timu Yangu"



"ha ha ha isack utaenda kuwapa nguvu hawa muwe kumi na mbili!"



ticha yule akazidi kuongea kwa nyodo,muda ule ule kipenga cha mapumziko kikapulizwa kila wachezaji 

wakakaa upande wao walimu wao wakawafata huku sir Richard Mwalimu Wa St Mery Akimshika Mkono Isack 

Kuelekea Naye Katika Timu Yake!



"ongereni Sana Bray Upo Katika Ubora Wako Kipindi Cha Pili Ongeza Tatu Tano Za Watosha"



"sir Lakin Mbona Kama Yule Mwalimu Kaondoka Na Isack?!"



"yule mtoto nuksi si alikuwa anansumbua aingie na kucheza awezi anataka atutie aibu sasa yule mwalim 

kamtaka nikamuachia waingie 12 tuwaaibishe zaidi"



wachezaji wale wakacheka...



kwa upande wa st Mery Sir Rich Aliwapa Pole Wachezaji Wake Akawa Ambia Wasipaniki,wanafunzi Wa Shule 

Ile Walifundishwa Kupendana,ivyo Awakujal Sana Walipoletewa Isack Mshambuliaji Mmoja Akatoka Na Kumpa 

Nafasi Isack,



Kipenga Kikapulizwa



Wakabadilishana Magoli Kipindi Cha Pili Kikaanza!



Nikatika Dakika Ya Pili Ikiwa Pasi Ya Kwanza Kuipewa Isack Ikazaa Matunda!,akafunga Goli,wanafunzi Wa 

St Mery Walimshangilia,upande Wa Chuo Chake ni mwanamke mmoja tu ndo alikuwa na udhubutu wa 

kumshangilia!



alice!



alishindwa zizuhia furaha yake,mwalimu kwa mara ya kwanza aliushangaa uchezaji wa Isack Chenga Akiwa Na 

Mpira Ukimbiaji Wake,mara Kadhaa Alimuaibisha Bray Alipomkaba Hatimaye Dakika Ya 27 Kipind Kile Cha 

Pili Akafunga Goli La Pili Ikawa Mbili Mbili!



Jina La Bray Sasa Likawa Alitajwi Ni Isack,isack,isack!



"nilikwambia Leo Nyota Ya Mpz Wako Itazimwa Ukuniamini Unaona?"



Alice Akamnong'oneza Mery Ambaye Alisonya Na Kuondoka Pale Alipo Alice!



Katika Dakika Ya Arobaini Na Nne Ikiwa Imebakia Dakika Moja Mpira Uishe Isack Akafunga Goli la tatu!



goli lililo muudhi kila mwanafunz na hata walimu wake pia



mzozo ukaanza eti wamemchezesha mchezaji ambao siyo wao,mvunjiko wa amani ukaonekana waziwazi



hatimaye mpira ukaisha,Bray akiwa kaifungia timu yake goli mbili huku isack alodharaulika nyota yake 

iking'aa akasawazisha goli zile na kuongeza moja la ushindi



Isack alijua kwa kufanya vile atarudisha heshima,kupendwa ila kumbe ndo alizalisha chuki hadi kwa 

walimu wake,



kuifunga timu yake! ilikuwa ni kama tusi ambalo sidhani kama walimu wangelivumilia!



Isack aliwaaibisha!









Nyota ya Isack inang'aa ni baada ya kusinyaa muda mrefu akiandamwa na zimwi la kibinadamu lijulikanalo 

kwa jina la Zidu Katili!



Likiisaka Roho Yak ikiwa ni kazi ya mh alex ila mwisho inamuingiza guantanamo kifungo cha maisha,



ila kupotea kwa jitu lile kunazaa katoto kengine rika lake kanachotaka shindana naye huyu si mwingine 

ni Bray Na Sasa Kwa Mara Ya Kwanza Anafanikiwa Kuizima Nyota Yake Katika Mechi Ya Kirafiki Walocheza Na 

Chuo

Cha Jiran Yao Baada Ya Kuifungia Timu Hiyo Tatu Mbili Je Unahis Nin Kitaendelea?



Songa Kujua Nin Hatma Ya Riwaya Hii



SEHEMU YA HAMSINI NA SITA



Isack alipongezwa,



"helow naitwa melina u handsome naomba namba zako?"



"asant sina simu chuoni aturuhusiwi!"



"bas hata selfie star wetu"



watoto wa kike wa shule ile walishindwa vumilia kutaka mawasiliano na kijana yule



walipiga nae picha wakimshangilia,hatimaye Isack Akaagana Nao Na Kuelekea Walipo Wenzake!



"isaaaaack!"



Alice Alishindwa Vumilia Akaenda Kumkumbatia Isack Kumpongeza,huku Nyuma Visunyo Vilitawala!



"ongera Isack Hakika Wewe Ni Mchezaji Hakika Wewe Ni Mshindi"



Alice Alimpongeza Isack Aliyeishia Tu Kutabasamu,na Kumshukuru Wakaingia Kwenye Gari Safari Ya Kurudi 

Chuo Ikafatia!



"ongera Isack Nilikudharau Bure Kumbe Unaweza Sasa Chuo Chetu Kitakuwa Na nyota wawili Bray Na Wewe"



Mwalimu Laurent Alimpongeza Isack Akijishangaa Kutokitambua Kile Kipaji Mapema!



japo Isack Aliwaaibisha Ila Kwa Sasa Walijivunia Kuwa Nae!...



Hatimaye Wakafika Chuoni Jina Lililokwepo Mdomoni Mwa Wanafunzi Ni Isack! Isack!



Usiku Mery Akiwa Kalala Ghafla Tukio Lile La Mchana Likajirudia Katika Fikra Zake,jinsi Isack 

Alivyokuwa Akicheza Mpira Watu Wakimshangilia,



"nilikuhaidi Leo Isack Ataizima Nyota Ya Bray Umeona"



"noooo Alice!"



Mery Akaongea Kwa Hasira Na Ghafla Akazinduka

Ilikuwa Ni Kama Kumbukumbu Ya Yale Yalotokea Mchana!.



"no No Alice Unaniota Ota Nini?"



Alice Akauliza kwa hasira,Mery akasonya kama kawaida yake na kugeukia upande wa pili!



alianza kuiwaza ile ndoto!



kuna kitu flani alihisi kinamnyemelea,alijihisi kumpenda Isack!,hapana Akajicheka Akiyatupilia Mbali 

Lile Wazo Na Kujiwazia Kuwa Katu Awezi Mpenda Isack



Akisahau Kwamba Ubongo Wake Ndo Ulowaza Vile Ila Si Moyo Wake Ulopenda!



Ndiyo Moyo Wake Ulimpenda Isack Japo Fikra Kutoka Ndani Ya Ubongo Wake Zilipinga Kile Kitokacho Moyoni!



Naam Katika Usiku Ule Vita Kali Ya Kihisia Kati Ya Moyo Na Ubongo Yani Mawazo Vikapigana Katika Mwili 

Wa Mery Naye Kubaki Kati Hali Ya Sintofahamu!



Baada Ya Mawazo Mengi Hatimaye akapitiwa na kausingizi ikiwa ni saa nane na usiku



MIDA ILE ILE YA SAA NANE ZA USIKU KATIKATI YA MJI!



KATIKA JUMBA LA MACDONALD



Nje Ya Jumba Lile Katikati Ya Usiku Ule Ilipaki Pikipiki Kubwa Akashuka Mtu Usoni Alivaa Kizibio Cheusi 

Hata Nguo Alizovaa Ni Nyeusi Mkononi Akiwa Na Gloves Nyeusi Akasonga Kulifata Jumba Lile!



Mkononi Akiwa Kashika Kifaa Flan Kama Kimkebe Ambacho Akikutambulika Kina Nini Ndani

Mtu Yule Kabla Ajalifikia Geti Akakata Kidogo Kielekea Nyuma Ya Nyumba Ile Akafungua Mkebe Wake Na 

Kutoa Vifaa Flani Akauparamia Ukuta Na Kupanda!



Alifanya Alivyojua Yeye Akatua Upande Wa Pili!



Cha ajabu hata mbwa awakubweka!



aikuwa hali ya kawaida ile!



mtu yule akaufata mlango wa ndani akatia funguo yake na kufungua akazama ndani...



dakika tano zilipita mtu yule akatoka! akaruka ukuta na kuifata pikipiki akapanda na kutoweka zake...



ni nani mtu yule?!,na kafanyaje ndan ya jumba lile hii ilijenga hali ya sintofahamu!



NDANI YA USIKU ULE ULE GUANTANAMO



Jitu katili lenye roho mbaya lilionekana Likiingia Katika Chumba Chake Likiwa Limenuna!,aikujulikana 

Sababu



Mikono Yake Ililowa Damu!...



Nikama dakika chache alifanya tukio baya



Likajitupa Sakafuni Tayari Kuusaka Usingizi Moyon Akiwa Na Chuki Kali Dhidi Ya Mtu Fulani!



Jitu Hili Si jingine bali Ni Liji zidu Katili!



"lazima Nitamuua Tu Haiwezekani Niteseke Hivi Kwa Ajil Yake Na Kazi Nishaianza Rasmi"



Lijitu Lile Likawaza Na Kuangua Kicheko kwa nguvu



ha ha ha ha ha ha ha



nikama lilichanganyikiwa!



MAPAMBAZUKO:



Baada ya usiku ule hatimaye kukapambazuka,mazoez ya kukimbia wanafunz wa st lucy kuoga hatimaye kupate 

chai kuelekea darasani ghafla isack akaitwa ofisini kwa mkuu wa chuo



akuwa na shaka anaenda kupongezwa akaenda akiwa na furaha alipofika alishtuka baada ya kumkuta mtu 

alomtambua kama mfanyakaz wao



"unaitwa nyumbani kuna matatizo kidogo"



moyo wa Isack Ukapasuka Paaa



Matatizo?!



Ni Matatizo Gani Hayo?!



Meno mdomoni yakaanza kugongana mawazo juu ya mtu alomtambua kama Zidu Yakajijenga Katika Mawazo Yake!



Mkuu Wa Chuo Alimwangalia Kwa Huruma ilozidi kumwongezea khofu



Isack na mfanyakaz yule Wakaongozana Mpaka Kwenye Gari Wakaingia Garini Na Kuelekea Nyumbani!



Alipofika Nyumbani Alishtuka Kukuta Watu Wengi Wakiwa Wamevaa Nguo Nyeusi Ikiwa Ni Ishara Ya Msiba!



alishindwa kuamini kile alichokisikia,baba yake mlez macdonald na mkewe bi sara wameuwawa kikatili kwa 

kuchomwa visu!



Isack Alilia,akumuwaza Mwingine Zaidi Ya Zidu!,huyu Alikuwa Ndo Muuaji Wake!

"ba Mdogo Sitokuacha Hai Zidu"

Akajikuta Akiweka Kiapo Pasina Kujua Pale Kuna Wapelelez Wa Kutosha Tena fbi walokamilika kiupelelezi



kuuwawa kwa mkuu wao kuliamsha morari ya kumtambua muuaji!



pembeni ya miili ya mr Donald Kulikutwa Picha Tatu Picha Ya Mack Ilowekwa Kosa Kwa Damu Mke Wake Nako 

Iliwekwa Kosa Ya Isack Ikawekwa Alama Ya Ulizo Na Nyuma Ikiandikwa *ANAFATIA*

Ivyo wapelelez wale waliamua kudili naye kumtambua muuaji!



je Muuaji Ni Zidu Kwel Na Katokaje Katika Gereza Lile Lenye Ulinz Mkali Na Ana Hasira Na Mtu Ni Mtu 

Gani Huyo?!



Je Wapelelez Wale Watamtambua Muuaji Hali Yakuwa Isack Anayemuhis Yupo Gerezani?







Mtu Asiyejulikana Anaingia Katika Jumba La Macdonald Usiku Wa Manane Na Kusababisha Mauaji!



Kisha Kutoweka!



Wakati Huo Huo Zidu Aliyefungwa Kifungo Cha Maisha Katika Gereza La Guantanamo usiku ule ule anaingia 

katika selo yake huku mikono yake ikiwa imeloa damu ni kama alitoka kufanya tukio baya



je ni tukio gani na nini kilichoendelea?!



TIRIRIKA NAYO KATIKA SEHEMU HII YA HAMSINI NA SABA



Mheshimiwa Alex akiwa ofisini kwake Mara Ghafla Simu Yake Inaita!



Ksg Ndilo Jina Alilolisevu Katika Simu Yake Na Ndiyo Mpigaji Anayempigia...



akiwa na uso wa tabasamu anapokea simu yile!



"vizuri sana kijana wangu ni mepata habari ya kazi yako ukwenda marekani kushangaa silaha!"



"kuna vingi tutaongea mkuu ila nasikitika yule alikuwa ni bosi wangu mkuu wetu ila nitatengeneza 

mazingira Zidu Aonekane Ndiyo Muhusika Anyongwe Au Unakaz Naye?"



"kwa sasa wewe upo ucwaze kuhusu yeye fanya kaz katika mazngira salama nakuaminia kijana wangu,"



"vizur! sasa kamebakia hako katoto nipe siku mbili"



Baada ya kuongea maneno yale simu ile ikakatwa,mzee alex alifrah sana,kitendo cha Isack Kuwa Hai 

Aikumpa Aman Ya Moyo,ivyo Baada Ya Kijana Wake Yule Alompeleka Masomon Nchini Marekani Kufuzu Vizuri 

Kabla Ajarudi Nchini Ndipo Alipompa Ile kazi,kisogo akaingia kazini!...



ila kwa kuwa alijua kaz ile ni ngumu na ilihusisha wapelelez wa kimataifa ilikuwa lazima atumie akili 

ya hali ya juu

akamkumbuka 'zidu'



ilikuwa lazima amtumie mtu huyu alokuwa gerezani kuiangamiza familia ya Macdonald!



Mapema Siku Ilofatia Akaelekea Katika Gereza Lile Lengo Akakutane Na Zidu! Ampange Kuhusu Kaz Hiyo



Mazishi Yalifanyika,na Baada Ya Mazishi Isack akarudi zake chuo huku nyuma akiacha Kikao Cha Familia Na 

Mali Kugawanywa!



Japo Mali Zile Ziliandikwa Kwa Jina La Isack Mwanasheria Akawekwa Sawa Isack Akawa Atambuliki!...



Moyon Isack alikuwa na uchungu dhidi ya Zidu Akijua Ndo Msababishi Wa mauaji yale!...



Moyon Mwake Aliapa Ipo Siku Lazima Angemteketeza Zidu Tena Kwa Mikono Yake!



Moyon Mwa Mery Akuamin Yale Aliyoyasikia Kutoka Mdomoni Mwa Alice!



Alice Alimsimulia Kila Kitu Alichosimuliwa Na Isack!



"ina Maana Nilipoteza Kumbukumbu?!"



"inawezekana Mery Ulpoteza Kumbukumbu"



"si Kwel Alice Eg Atanieleza Kila Kitu..."



Mery Akaondoka,kichwani Alionekana Kuchanganyikiwa Akuamin Kabisa Kile Alichosikia...

Akamfata Mdogo Wake Na Kumuuliza



"ivi Egy Nishawah Kupotezaga kumbukumbu mimi?"



ndo swali la kwanza alilo muuliza,egy aliduwaa



"hata siku moja usije ukamueleza ukweli dada yako ntawaua sawa?"



kauli ile alowah ambiwaga na baba yake kabla hata awajaenda chuo ikajirudia katika fikra zake Agnes 

Alimuogopaga Sana Baba Yake



"hapana Dada Si Kwel Ujawahig Kupotezaga Kumbukumb Ninan Kakwambia Maneno Hayo!"



"we Egy Kuwa Mkwel Kwa Nin Lakini Unamficha Dada Yako?"



Alice Akaingilia!



"ukwel Upi Unaoujua We Alice Dada Ujawah Potezag Fahamu Nikudanganye Sasa Ili Nifaidike Nin Kuna Kitu 

Huyu Binti Atakuwa Anakitafuta Dhidi Yetu!"



Mery Akasonya Na Kutoka Zake Nje!



Alice alishindwa kuelewa ni kwa nini Mery Akumbuki Na Ni Kipi Kilicho Mkuta Mpaka Akawa Akumbuki Na Kwa 

Nini Egy Anaficha Ukwel?!



Aligundua Ni Wazi Hapo Katikati Kulikuwa Na Kitu,na Nilazima Akaongee Na Isack Juu Ya Jambo Lile!

Ile Aikuwa Hali Ya Kawaida!...



UPANDE WA PILI KWA MZEE ALEX



Kwa mara nyingine tena simu yake ikaita,jina lilikuwa ni lile lile ksg kama alivyosave katika simu yake 

akaipokea...



"nahabari njema!"



"nakusikiliza kijana wangu!"



"baada ya kuifyeka ile familia mali zote zimechukuliwa na ndugu ivyo yule panya ana pa kutegemea tena 

hii itaniwezesha mimi sasa nimuwinde na kumuua kwa urahisi zaidi!"



"kazi nzuri!"



"kwa saivi yupo kule chuoni ila akitoka tu nje ya jengo lile kitakuwa ndo kiama chake!"



upande wa pili ukaendelea ,mh alex alfurah sana



Akakata simu!...



No 58



Maisha yanachangamoto sana,ukifatilia riwaya hii utaamini hili nisemalo hasa kwa maisha alopitia kijana 

Isack,



Kila anayetokea kumsaidia uishia kupoteza maisha na kumwachia ladha chungu hasira zake akibaki 

kumwachia Zidu akijua ndo msababishi wa Yale yote!



Je nini kitaendelea



Tiririka nayo katika SEHEMU HII YA AMSINI NA NANE



lilikuwa ni jopo la wapelelezi kadhaa kutoka shirika la kipelelezi fbi wakijadili walipofikia katika 

uchunguzi wao!



walikuwa ni jumla ya watu tisa wakiizunguka meza kubwa yenye kopo za maji juu yake wanne waliangaliana 

na wa nne wa mbele yao na mbele ya meza ile alikaa aliyeonekana ndiyo kiongoz wao!



"nawasikiliza ndugu wapelelelezi hatuna muda wa kupoteza niwakaribishe tu wale tulowatuma kuchunguza 

vifo vile nianze kwa kumkaribisha bright karibu"



"asante ofisar yah mi nadhan ndo nilikuwa wakwanza kufika eneo la tukio kabla yoyote yule ajafika,na 

wakat nikiwa pale alikuja yule mtoto wa marehemu isack nadhani Nyote Mnamjua Kuna Mtu Alimtaja Kama 

Muhusika,Zidu kuwa yeye pekee ndo hadui yake,na kwel mim na jopo langu tulipozidi kuchunguza tukagundua 

kuwa ni kwel mtu yule ndiye anayeweza kuwa anausika na mauaji hasa kwa kuwa chini pia aliacha picha ya 

mtoto yule akisema wazi ndo anayefatia cha ajabu sasa huyo Zidu Kwa Sasa Yupo Gerezani Kwani Mara Ya 

Mwisho Aliwashambulia Kwa Lengo La Kuwaua Akasekwa Guantanamo Tena Kifungo Cha Maisha"



Jopo Lile La Wapelelezi Lote Likaduwaa,hakuna Asiyepajua Guantanamo Gereza Lenye Ulinzi Mkali,kivipi 

Mtu Yule Atoke Na Kwenda Kusababisha Mauaji?



Ile Ilikuwa Ni Hali Ya Sintofahamu baina yao!



"kuna kitu kinachoendelea kiso tutakutuma ndani ya gereza lile kama mfungwa ukachunguze juu ya hili 

kusanya ushahidi tosha utakaokuwezesha tugundue kila kitu"



pasina kujua kuwa yule wamtumaye ndiyo muhusika mwenyewe wakamtengenezea mazingira mazuri ya kwenda 

kualalisha ubaya wake usigundulike!



kikao kile kikafungwa kwa makubaliano ya kiso kuelekea gerezani kuchunguza na kutafuta ushahidi kuwa 

Zidu Ni Muhusika Au Vipi!



Wakati Yale Yakiendelea Upande Wa Isack Na Alice Walionekana Pamoja Wakijadili Hasa Juu Ya Mery



Hata Isack Mwenyewe Binafsi Akujua Ni Kitu Gani Kilichokuwa Kikiendelea



"isack mpz si unanipenda?"



isack akatingisha kichwa kuafiki jambo lile!



"kama unanipenda kweli basi tuachane na maswala ya mery naamini anajua kila kitu ila wanafanya hivi 

kukufedhehesha!"



"hapana si kwel mi nakataa mery kansaidia sana alice wangu lazima nasi tumsaidie ajitambue anikumbuke"



"ndo kashakataa sasa utafanyaje?"



alice akauliza kwa hasira alisha choka kila siku Mery Hivi Mery Vile,alitaman Kwa Muda Ule Waliendeleze 

Penzi Lao Na Siyo Kuangaika Na Watu Ambao Awaelewani!



"ishia Hapo Hapo Alice Siwez Kuacha Kumfatilia Mery Nishasema!"



Isack Akaongea Kwa hasira Na Kuondoka Zake!



Mawazo Mapya Yakajijenga katika kichwa cha alice,inawezekana Isack Ampendi Na Yeye Anajipendekeza 

Bure,mchomo Mkali Wa Uwivu Ukauchoma Moyo Wake!



'achague Moja Mimi Au Mery Kama Ni Mimi Aache Kufatilia Maswala Ya Mery Tofauti Na Hivi Nipo Tayari 

Kumpoteza Isack Siwez Kwa Kwel Siwez Kuendelea Kuumia Mimi Kisa Mapenzi"

Alice Aliongea Kwa Uchungu Machozi Yakimtiririka Binafsi Aliamua Itakavyokuwa Na Iwe,akaondoka Kumfata 

Isack Akachague Moja



Je Unadhani Isack Angechagua Nin?!...



SURA YA KUMI NA TANO



GUANTANAMO JAIL



Ni katika chumba kimoja katika kiti aliketi jitu la miraba minne alivuliwa nguo zote na kubaki na boxa 

ilobadilika rangi na kuwa nyekundu kwa ajili ya damu,mwili wake wote uliloa damu!



"kwa nini umeua?"



ndo swali ambalo jitu lile liliulizwa lakin akujibu na kuzidisha hasira za wamuadhibuaye na kuzidi 

kumtesa,watu wale waloficha sura zao ila tshart walizovaa ziliandikwa x ikiwa na maana kwao hata kuuwa 

sawa tu!



wakazidi mtesa zidu aeleze kwa nin aliua zidu kimya hatimaye akapoteza fahamu!

watu wale wakatoka miili yao ikiwa imeloa jasho kwa kazi ngumu waloifanya!



"kiburi chake kitaisha atasema tu awamu hii asiposema tumuueni tu"



aloonekana kama kiongoz wao akawaambia wenzake walotingisha kichwa kuafiki

je? ni mtu gani Zidu Aliyemuua Anayekataa Kujibu Sababu Ya Kumuua? Bado Lilikuwa Ni Fumbo Ambalo Ni 

Gumu Kufumbuka!



Baada Ya Masaa Kadhaa Zidu Katili Likazinduka,mwili Ulimuuma Kwa Maumivu Bado Damu Zilimchuruzika



"sema Kwa Nini Umeua?"



Akakumbuka Swali Lile Aliloulizwa Naye Kutabasamu Huku Akitema Damu,basi Akazidi Kupigwa,akajikuta 

Akiwaza Mwenyewe...



'eti Kwa Nini Naua! Wanataka Wajue Ili Iweje Basi Waniue!'



Zidu Likawaza Likikunja Domo Lake Ila Ghafla Lango Likafunguliwa!



Watu Wale Wakaingia...



"kwa Nini Unaua?"



Wakauliza Tena Awamu Hii Wakiwa Wameadhimia Kabisa Zidu Asipojibu Wamuue!



Je Zidu Atajibu Sababu ya kuuwa?,nini kitakachoendelea vipi kuhusu maisha ya isack?

na mahusiano yake ya Alice Na Mery Atachagua Nin?









Mapenzi Ni Kizungumkuti Yanaanza Kumzungusha Binti Alice,wivu Unamtawala,ni Baada Ya Isack Kuelekeza 

Akili Yake Kwa Mery Zaidi Je Unahisi Nin Mwisho Wa Penz Lao?



Pia Kwa Upande Mwingine Jitu Katili Lijulikanalo Kwa Jina La Zidu Linazidi Kuteswa Likiulizwa Hasa 

Sababu Ya Kuua!



Je Ninan Kamuua Na Ataieleza Sababu Ya Kuua?

Twende Pamoja Kujua Hatma Ya Mambo Yote Haya



NA HII NI SEHEMU YA HAMSINI NA TISA



"Muacheni mimi ndiyo niliyouwa!"



ghafla sauti ikasikika nyuma yao,watu wale wakageuka nyuma kumwangalia yule alotoa ile sauti tena kwa 

kujiamini kiasi kile!

hata zidu mwenyewe alishangaa...



katika geti lile la kuingilia katika chumba kile alisimama mfungwa akiwa no 09



"muacheni huyo ahusiki mimi ndiye niliyemuua yule mwanajeshi na si huyu!"



mtu yule aliyeingia akazidi kutoa maelezo yaliyozidi kuwashangaza wale watu!



Zidu Alizidi Kumshangaa Kwa Kuwa Yeye Ndiyo Aliyeuwa Kivipi Mtu Yule Ajibebeshe Mzigo wake!?



Watu Wale Wakamuacha Zidu Na Kumvaa Mfungwa Yule Aloingia Wakamkamata Mmoja Akafunga Lango Lile!



Wakaondoka Na Mtu wao!!!!!



Zidu kule Ndani Akaachia Cheko lake la dharau



'ukistaajabu Ya Musa Utaona Ya Firauni' Akawaza Akikumbuka Jinsi Alivyofanya Tukio Lile ilikuwa 

Hivi....



TURUDI NYUMA KIDOGO JINSI ILIVYOKUWA



Moyoni alikuwa na uchungu, mwaka mmoja na nusu ulishapita akiwa ndani ya gereza lile lenye 

mateso,unyama na manyanyaso ya hali ya juu



akuhamini kama mheshimiwa Alex Angemwacha Ateseke kiasi kile ndani ya gereza lile,Guantanamo apakuwa 

mahali pa kukaa binadamu si komandoo polisi au mjeda



Siku Moja kwake ndani ya gereza lile Ilikuwa Kama Mwaka



Ndipo Kwa Kujua Mh Alex Kamtelekeza Akaweka Kiapo Siku Akitoka lazima alipize Kwa Lile!



Alijikuta Akimchukia Mh Alex,



Siku Zikaenda mpaka Siku ya tukio ambapo siku Hiyo Ikiwa Usiku Wa Manane Alikuja Kutolewa Katika Chumba 

Chake Na Askar Wa Magereza Wakaenda Chobisi!



"na Ujumbe Wako Kutoka Kwa Mh Alex Anaitaji Nikutoe Huku Kwa Siri Uende Uraiani Nikakukutanishe Na Mtu 

Ambaye Kwa Muda Huu Huyo Mtu Anawateketeza Wale Walomsaidia Yule Mtoto Umsaidie Kukaua Kale katoto,then 

baada ya tukio urudi huku kuendelea kutumikia kifungo chako"



Maneno Yale Yalikuwa Kama Tusi Kwa Zidu,yani Atolewe Akafanye Tukio Kisha Arudishwe?!

Badala Ya Kumuokoa Atoke Kule Gerezan!



Mh Alex Alimuonaje Lakini Yeye,aliona Anafaidi Sana Kule Gerezan Au! Yan Amtumie Kisha Amrudishe Kule 

Gerezani!



Akajikuta Anacheka Ghafla Akarukia Kisu Kilichokuwa Mezani Akakishika Sawia Kilikuwa Ni Kitendo Cha 

Haraka!



Mkono Uloshika Kisu Akaurudisha Nyuma Alipoupeleka Mbele Kwa Nguvu Kuelekea Kwenye Mwili Wa Mwanajeshi 

Yule Akakitoa Na Kumchoma Tena!



Alipokitoa Awamu Ya Tatu Mtu Yule Akaporomoka Chini Kama mzigo akatulia tuli!,mwanaume akatoka akarudi 

katika chumba chake akiwa kanuna mikono imeloa damu,likajitupa sakafuni tayari kuusaka usingizi akiwa 

na chuki kali dhidi ya mh alex



(Kama tulivyoona katika Kipande kilichopita)



"lazima nitamuua tu haiwezekani niteseke hivi kwa ajili yake na kazi nishaanza rasmi"



akakumbuka kabisa alijisemea akimaanisha mh alex iweje leo mtu mwingine atokee na kusema wazi ndiye 

aliyeua?



au naye katumwa na huyo mh alex



Jitu lile likacheka baada ya kuwaza ivyo!



'ntawakomesha'



Wakati Huo Huo Wale Wanajeshi Walizidi Kumkokota Mtu Yule Alowavamia Ghafla!



"samahanini Mim Ni Mwanausalama Wa Shirika La Kijasusi Nimekuja Kwa Kazi

Maalumu ndani ya gereza hili,juu ya mtu yule aloenda uraiani na kusababisha mauaji ya afisa wa shirika 

letu ivyo nimekuja kupeleleza nacho omba kwa sasa asiteswe na asiuwawe"



Mtu Yule Aliongea Kwa Kujiamini Huku Akiingiza Mkono Wake Mfukoni Alipoutoa Ulikuwa Na Kitambulisho!



Alikuwa Ni Kisogo Au Kiso,mpelelezi Alousika Na Mauaji Ya Macdonald Na Mke Wake Na Kuja Katika Gereza 

Lile Kwa Lengo La Kumuunganisha Zidu Na Mauaji Yale Pasina Kujua Jitu Lile Lilisha Badilika Na Kwa Sasa 

Toka Mh Alex Amtelekeze Kule Jela Alisha Kula Kiapo Cha Kumuua Ikiwa Atatoka Nje Ya Gereza Lile!



Je Unahisi Akigundua Anataka Alimbikiziwe na kesi isiyo muhusu atachukua maamuzi gani watu wale 

wakaelewa na kumuacha mtu yule baada ya kugundua ni mpelelezi!...



'umekwisha Zidu'



Kiso Akawaza Baada Ya Kuachiwa Na Watu Wale!...



MASAA MATATU BADAE



Moyoni Mwake Kulijaa Simanzi,ugonjwa Ulomsumbua Kwa Muda Mrefu Alijua Siku Yoyote Angeweza Kupoteza 

Maisha



Ukimwangalia Hivi Alionekana Ni Mwanaume Mkakamavu Jasiri Ila Ukwel Aliutambua Ndani Ya Moyo Wake!



Kulitumikia Gereza Lile Ndani Ya Miaka 36 Kama Mlinzi Wa Getini Mwenye Machale Na Shabaha Tosha Ilo 

Mfanya Aendelee Kuaminika Na Kuwekwa Pale,japo Alilipwa Mshahara Mdogo Ambapo

Aukumuwezesha mpaka muda huo kujenga

alijua kansa muda wowote ingemchukua vipi angeiachaje familia yake?...



wakati akiwa katika tanuri lile la mawazo pale getini ghafla akashtuliwa na sauti...



"ni kweli auna maisha mengi ya kuendelea kuish hapa duniani na unajiumiza kichwa ni vipi utaiacha 

familia yako hali ya kuwa maisha yako ni magumu!"



ilikuwa ni kama sauti ya malaika ikimsemesha ila alipofumbua macho akagundua si malaika yule ila ni mtu 

alokuwa amesimama mbele yake!



"kisogo ni wewe?!" alishtuka akauliza pasina kujiamin ni kama walijuana,kisogo akaachia tabasamu!



"ni mimi bhana nipo humu ndani napeleleza ishu flan ila naomb nsaidia henry nami ntaisaidia familia 

yako kipindi ambacho utokuwa hai,nakupa kias cha sh milion mia ikiwa utakubali kuwa ulimpitisha mfungwa 

hapa getini kwenda uraiani kufanya tukio na kurudi



Henry Akaduwaa!



Toka Amewekwa Pale Ajawah Kuwa Msaliti Kivipi Leo Aongope Kitu Ambacho Akukifanya?



Akakumbuka Pia Lakin Kuhusu Familia Yake Muda Wowote Anaenda Kupoteza Maisha Ni Vipi Ingeishi?



Hata Kama Angedanganya Angefungwa Mda Mchache Tu Angekufa Akiacha Familia Yake Katika Maisha Mazuri!

Henry Akatabasamu!



"nimekubali!"



Kiso Akatabasamu Akaanza Chukua Ushahidi Wa Uongo Kwamba Mtu Yule Ndiyo alomfungulia geti Zidu Apite Na 

Kwenda Kusababisha Tukio!



Zidu Akazidi Kuwekwa Sehemu Mbaya Pasina Yeye Mwenyewe Kujua!



FUNZO



Ukimfanyia mwenzako baya utokufa mpaka Nawe Ufanyiwe Vilevile

Malipo Duniani Mbinguni Mahesabu...



No 60



Jumba bovu linaenda kumwangukia Zidu katili,anaenda kupewa kesi ambayo si ya kwake je ataweza 

kujiokoa?!



Pia tumeona kwa upande wa Alice mapenzi yanampeleka puta wivu mkali unaenda kumkamata baada ya kuhisi 

Isack ampendi na anampenda Mery anamfata kwa lengo moja tu aelezwe ukweli kati yake yeye na Mery 

anampenda nani



Amchague yeye aache kufatilia maswala ya Mery au amchague Mery aendelee kufatilia maswala yake naye 

aachane naye unahisi Isack atachagua jambo gani?!....

Kati ya hayo mawili,kumpenda Alice aliyemsaidia hapo chuo au kuendelea kumfatilia Mery na kumpoteza 

Alice?!

Twende pamoja kujua hatma ya kisa hiki....



NA HII NI SEHEMU YA SITINI



Moyoni Mwake Kulijaa Ghadhabu,chuki Na Wivu Mkali,

akazidi kusonga kuelekea mahali ambapo Isack Alielekea!



Isack Aliingia Katika Darasa Moja Ambalo Alikuwa Na Mtu Ndani Yake Lengo Atulize Akili Lakini Mara 

Mlango Ulifunguliwa Na Alice Akaingia,usoni Simanzi Ilimtawala Binti Yule



"naitaji Nibaki Mwenyewe Alice Kwa Saivi Nitulize Akili Pls Pls Pls Nakuomba Utoke!"



Alice Akashtuka,kwel Aliamin Mapenz Kwa Isack Sasa Yaliama Mpaka Anafikia Kumfukuza?



"sawa Ntaondoka Isack Na Kukuacha Lakini Nakuomba Uchague Kitu Kimoja Ubaki Na Mimi Na Maswala Ya Mery 

Kwanzia Sasa Uachane Nayo Ubaki Na Mimi,au Kuendelea Kumfatilia huyo Mery Wako Uniache Mimi Niendelee 

Na Maisha Yangu We Nambie Tu!"



"whatevar U Like We Fanya Ila Sitoweza Kuacha Kumfatilia Mery Kwa Kuwa Ni Mwanamke Alonsaidia!"



Alice Akuamini Kile Alichokisikia,ina Maana Isack Kakubali Kutengana Naye Kisa Mery?



Mchomo Mkali Wa Maumivu Ukamchoma Moyo Wake Machozi Yakaanza Kumtiririka!



Si Yeye Pekee Aloumizwa Na Neno Lile La Isack Hata Kwa Kijana Brayson Alokwepo Nje Ya Dirisha 

Akiwasikiliza!



Ikiwa Isack Kamtolea Maneno Makal Mpz Wake Kisa Mery Ile Ni Dalili Ya Anguko La Penzi Lake Naye Kiukwel 

Alimpenda Mery Akuwa Tayari Kumpoteza!



Ghafla Akapata Wazo,kumpoteza Isack Kusudi Yeye Abaki Na Mery Wake!



Kivipi Sasa?!



Kichwa Chake Kikaanza Kufikiria Njia Ambayo Angeitumia Na Wakati Akifikiria Ghafla Alimshughudia Alice 

Akiwa Na Hasira Akatoka Ndani Ya Chumba Kile!...



Isack Wala Akuangaika Kumfata!,mlangoni Wakati Anatoka Akagongana Na Sparck Rafiki Yake Isack...



Brayson Akutaka Kupoteza Muda Haraka Sana Akachoropoka Pale Kidirishani Akawa Akimfata Alice,alipofika 

Pale Mlangoni Akaufunga Mlango Ule Kwa Nje Na Kuendelea Kumfata Alice!



Alice Pasina Kujua Anafatiliwa Kwa Nyuma,machozi Yakiendelea Kutiririka Katika Macho Yake Madogo 

Akavuka Madarasa Kadhaa Na Kuelekea darasa la mwisho ni darasa alilopenda kulitumia wakati alipokuwa 

mwingi wa mawazo!...



Akaenda Kuketi Mbele Kabisa Dawati La Kwanza Na Kuinamisha Kichwa Chake Akaanza Kulia!



Katu Akujua Pembeni Yake Bray Alikuwa Kasimama Na Kisu Kidogo Mkononi Akimwangalia Kwa Tabasamu Pana!



"alice Malaika Wa Chuo!"



Bray Akaita Kwa Sauti Nene Alice Akainua Kichwa Kumwangalia Aliyemwita



Kosa!



Alipokelewa Na Kofi Moja Zito Lililompa Wenge Kisa Alihisi Mchomo Mkali Katika Kifua Chake Akahisi Kitu 

Cha Unyevu Nyevu Kikitiririka!



Alipopeleka Mkono Akuamini Kile Alichokigusa,akataka Afumbue Mdomo Wake Kuongea Kitu akashindwa!,ghafla 

nuru ikatoweka kichwa akakishusha chini!



Alice Akakata Roho!



Bray Akayatoboa Macho Ya Binti Yule Kupoteza Ushahidi!



Kisha Akatoka Ndani Ya Darasa Lile Tayari Kwenda Kumfungulia Isack!



Ilikuwa Lazima Afanye Kitu Isack Aende Akaingie Katika Kile Chumba Plan Yake Ndo Ilikuwa Hiyo!



Ni Kama Shetani Muda Huo Alikuwa Upande Wake Kumsaidia Kazi Ile Iende Kama Yeye Alivyotaka!



Kwani Baada Ya Alice Kuondoka Na Kupishana Na Spark



"vipi Best Mbona Shem Anatoka Na Mihasira Mmekosana Nini?"



Spack Ikabidi Aulize



"aaah Achana Naye Anataka Aniumize Kichwa Mery Aniumize Kichwa Naye Aniumize dah naitaj mawazo yako 

best!"



"nambie!"



"Ni kama nilivyokueleza kuhusu maisha yangu mi naitaji kujua kilichomkuta Mery Mpaka Kunisahau Je Ni 

Makusudi Au!"



"ilo Swala Niachie Mimi Ntalichunguza Nitaunda Urafiki Wa Kimapenz Na Egy Atanieleza Kila Kitu We Kwa 

Sasa Usimfatilie Kabisa Mery Unamuumiza Mwenzako We Nenda Kambembeleze Yule Mtoto Anakupenda Na Anaweza 

Fanya Chochote Kwa Ajili Yako Eti"



"kwel Eh!"



"yah! Muwah Ukamuombe Radhi Nao Wacha Mimi Nikamsake Huyo Egy!"



"bas Sawa!"



Wakakubaliana Pasina Kujua Mambo Yalishaharibika,alice Akuwa Alice Tena!



Walipoufikia Mlango Walishtuka Kukuta Umefungwa kwa nje kwa akili ya kawaida tu wakajua alice 

aliwafungia pasina kujua kwa jinsi alivyokuwa kachanganyikiwa labda ili Isack Asimfate!



Kwa Dirishan Wakamwita Mwanafunz Mmoja Alokuwa Akipita Wakamwomba Awafungulie!



Wakafunguliwa!



Isack Akaelekea Kushoto,Spack kulia!



"ngoja bas nkamchek huyo mamylo nahs atakuwa darasa la mwisho kule nkaongee nay nimuweke sawa 

tutajulishana itakavyokuwa"



"usijali msalimie bhana"



wakaachana kama ivyo



Bray Ni Kama Shetani Alikuwa Upande Wake Muda Ule Ule Akawachukua Wenzake Kadhaa Na Kuwaomba Wamfate Ni 

Baada Ya Kumuona Isack Kaelekea Kwenye Lile Darasa!



Isack Akazidi lifikia darasa lile pasina kujua yupo katika mtego!



akausukuma mlango na kuzama ndani!



kwanza alishtuka kuiona damu sakafuni tena mbichi ikichuruzika!



akamvamia alice na kukiinua kichwa chake kuangalia uhai wake,akashtuka zaidi baada ya kushughudia macho 

yakiwa yametobolewa na kisu kidogo kikiwa kifuani kwa binti yule



"aliceeeeee!!!..."



akajikuta akiita kwa nguvu na ghafla akaporomoka na kwenda chini!



akapoteza fahamu!



Kina Bray Walipofika Wakijifanya Awajuh Wakaanza Piga Kelele Watu Wakajaa!



Walimu Wakawasili!



Taharifa Ikatolewa Police! Na Kwa Wazaz Wa Alice!



Baba Yake Alice Alikuwa Ni Waziri nchini marekani!,...



"natoa masaa matatu muuaji awe amegundulika"



ndiyo amri aloitoa baba yake alice akiwa mwingi wa uchungu! kumpoteza mwanae tena mauaji ya kikatili 

namna ile mh Alfonsor Akuwa Tayar Kwa Ilo!



Ndani Ya Masaa Matatu Jina Alilopelekewa Kuwa Ndo Muuaji Ni Isack John



"naitaji Kuonana Na Huyo Isack"



Mzee Yule Katili Aliongea Kwa Hasira Na Chuki Alimpenda Sana Mtoto Wake!



Isack Alikuja Fumbua Macho Yake,kichwa Kilikuwa Kizito,mikono Yake Ilibanwa Na Kitu Akupata Tabu 

Kung'amua Kwamba Ile Ni Pingu!



Je Kafanya Kosa Gani?! Na Pale Yupo Wapi!



Kutokana Na Mazingira,harufu Ya Madawa Alijua pale ni wodini,ila kwa nin amefungwa pingu?!...



mwisho kumbukumbu zikaanza mrejea,machozi yakaanza mchurizika!



"zidu!"

akajikuta akitaja jina hili kwani jina hili pekee ndilo alilojua ndo linalohusika kuondoka na furaha 

yake!



"ZIDU UMEUA TENA!"



Akatamka Huku Mdomo Ukimcheza Kwa Hasira!



"sitokuacha Hai Ziduuu!"



Akaongea Kwa Ukali Na Hasira Kabla Ajapoteza Fahamu Tena!



"ZIDU?!" mh Alfonsor Baba Yake Alice Aliongea Huku Akijaribu Kutafakari Kitu!...



Ni juu ya sahihi Ya Kifo Alotia Juu Ya Mtu Huyo 'Zidu' Ndani Ya Dakika Tano Zilizopita Ilipaswa Awe 

Ameshanyongwa!



'kivipi Ahusike Na Mauaji Ya Mtoto Wake?'



HAPA NDO MWISHO WA SEASON TWO VIPANDE VINGINE 30 TUMEMALIZA



TUJIANDAE KWA SEASON 3 NAYAMWISHO KATIKA VIPANDE VINGINE 30



ISACK ASHTAKIWA KWA KOSA LA KUMUUA MPZ WAKE ALICE



ZIDU GEREZANI ILIKUWAJE MPAKA KUONANA NA KITANZI JE ALIKUFA KWA SABABU KUMBUKUMB ZA WAZIR BABA YAKE 

ALICE DAKIKA TANO NYUMA ILIPASWA AFE KWENYE KITANZI IVYO MUDA ULE ILITAKIWA AWE MAITI NAYE ANATAKA 

KUJUA SABABU YA KUMUULIA MTOTO WAKE UNAHIS NIN KITAENDELEA?



VIPI SPARK MERY BRAY NA EGY?



MAJIBU NI KATIKA SEASON 3 ITAKAYOKUJIA BAADA YA KUISHA SIMULIZI YA KWELI YA MAISHA YA DADA SHAA IITWAYO 

MATESO YA MAMA!



NENO LA MWANDISHI



RIWAYA HII NI RIWAYA YANGU YA KWANZA KUIANDIKA KATIKA WAKATI MGUMU SANA,HOSPITALI NILIPOLAZWA 

NILIANDIKA,KAZINI NILIBANA DK NIKAANDIKA KUWAPA BURUDANI WAPENZI WASIMULIZI ZANGU ASANTEN KWA 

WALIONIUNGA MKONO MMENIPA MOYO SANA!



RIWAYA HII NI YAKUBUNI NA SIJACOPY POPOTE!



AHSANTEN SANA



TUJIFUNZE KWA YALE YALOMKUTA DADA SHAAAAAAAA





TWENDE NA SEASON 3 SASA


0 comments:

Post a Comment

Blog