Search This Blog

Friday 30 December 2022

KIAPO CHA MFUNGWA (5) - 2

    

Simulizi : Kiapo (Mtetezi Wa Kinte) (5) 


Sehemu Ya Pili (2)




Brown Stanley Mkuu Wa Kikosi Maalum Na Rafiki Yake Kipenzi Zidu ambaye siku za nyuma aliwah kushikilia kesi ya binti black snake kabla ajauwawa akiwa ndani ya gari yake aliongeza mwendo kwa minajili ya kufika nyumbani kwa Zidu,



Brown alikuwa na kawaida ya kumtembelea rafiki yake yule nyumbani na kupiga naye stori mbili tatu,ndani ya gari yake aliburudishwa na mziki laini wa wast life 'my love' naye aliufatisha kwa mluzi kichwa chake akikitingisha taratibu!



Alikata Kulia Kuiacha barabara kuu iendayo katika jiji la Gulisia Na Kuchukua Uelekea Wa Kisangire Dakika Kumi badae alifika nyumba ya Zidu Lakini Kwa mshtuko alishughudia gari la Zidu Ikitoka Kwa Kasi na kilicho mshangaza hata geti alikufungwa,ikabidi apige breki na kuchukua simu yake na kuitafuta namba ya Zidu alipopigwa ikakatwa



Machale Yakamcheza!



Wala akuangaika kushuka wala kuingia ndani akajue kuna nini,akili yake ikamtuma aifatilie ile gari kwa nyuma



Taratibu akaanza kuifatilia ile gari,japo alikuwa nyuma kwa magari mawili alishangaa wakielekea msitu wa Lwana, akashika simu yake na kupiga kwa kamanda Wake,alijua kwa vyovyote Zidu atakuwa Na Matatizo,akatoa Maelekezo gari tano za kijeshi usiku ule ule zikatumwa zikitoka taratibu bila ving'ora kwa lengo la kuwah kumuokoa komandoo na waziri wao,kwan kwa kipindi icho Zidu alikuwa Ni Waziri wa jeshi ulinz na usalama wa taifa,



***



Stanley Brown Macho Yalimtoka Pima hakuamini alichokiona wala aikumwingia akilini,ni mara ya pili sasa alishajitoboa jicho akihisi pengine ni ndoto lakini ukweli ulibaki kuwa ule ule



Rais Mernel ii,alikuwa na bastola kamuwekea Zidu Kwa Lengo La Kumuua



Zidu Kakosa Nini?!,



Mfululizo Wa Maswali Yasiyo Na Majibu Yalitiririka Kichwani Mwake,mshangao alioupata aukuelezeka



Akawa akisikia maneno alokuwa akiongea raisi eti anamuua Zidu Kisa Kukubalika Kwake?!,



Tayari Wanajeshi Walishafika eneo lile na kuwazunguka ila walikuwa mafichon,



Macho Yake Yalishtuka pale aliposhughudia Rais Mernel Wa ii Akishika Silaha Na Kumnyooshea Zidu akaanza kuhesabu



Kama Kompyuta Alishika Silaha Yake Vizuri Na Kuruhusu Mlio Wa Risasi Kuchomoka,risasi Ikaenda Moja Kwa Moja Mpaka Kichwan Kwa Snake Man Ikatawanyisha Ubongo Wake!..



Rais akaidondosha bastola yake chini kwa mshtuko akageuka kusudi akimbie wale vijana wa nne wakashambulia upande mlio wa risasi ulipotokea,ila tayar Brown alisha ama muda huo huo wanajeshi wakajitokeza na kuwaweka watuhumiwa chini ya ulinzi



Rais Mernel ii alichanganyikiwa alipigwa pingu na safari ya kuelekea mjini ikaanza,katarina Na Zidu Wakiwaishwa Hosptalini



***



Swala Lile La Kukamatwa Kwa Rais Mernel ii katika msitu wa lwana akitaka kumuua waziri wake wa jeshi Zidu Kite,na Watu Sita Wa Kundi La Mafia Ilibaki Siri Ya Usalama Wa taifa,



Kwa Usalama Wa Taifa,cha ajabu sasa Zidu alipata nafuu na kumsamehe Mernel Kurudi Ikulu Lakini Jeshi Lililo Ongozwa Na Mkuu Wa Majeshi Jemedar Laizer Nyoshi,mkuu Wa Upelelezi Alex Mbaga,waliasi Na Kuingia Porini Wakimshinikiza Rais Mernel ii ajiuzulu,kwani kama Zidu Kajiuzulu,kwa Nin Naye Asijiuzulu?



Akatoka madarakani?!,mbaya zaid kilichokasirisha jeshi ni kitendo chake cha kuwa achia huru mafia wale wa 4 walobakia



Hali Ya Kisiasa Kinte Ikabadilika,kinte Vita Vya Wenyewe Kwa Wenyewe Vikarudi,ZIDU na mwenzake katarina waliamua kupumzika nchini Tanzani,kwa Kina Isack,kuilea Mimba Changa Ya Mkewe



Zidu Likapata Uraia Wa Tanzania,likaanzisha Biashara,

Kinte Ni Nchi Yake,lakin aliichukia tayari miji mikubwa ya kinte ilishikiliwa na waasi,wakishinikiza Mernel Ajiuzulu



Mernel ii hakuwa tayari kujiuzulu,aliapa kujificha na kuendeleza mapambano mpaka kieleweke mwanaye LAURENT GAMBI alokuwa nchini Kongo Kulinda amani ikabidi aitwe ili ikiwezekana amtoroshe babake hali ilishachafuka



Laurent Gambi kidume cha shoka,roho ya paka alifanikiwa kuingia salama nchini Kinte Na Kufika Mpaka Ikulu Salama Lakini Dakika Chache badae kabla ajamtorosha ikulu ikazingirwa na wanajeshi wale waasi ndo kwanza gambi alikuwa akiwaondoa wazazi wake vita kali ikapigwa kati ya kundi la waasi na walinzi wa ikulu pamoja na wanajeshi wachache wa Serikali



Mbinu Za Kumtorosha Mernel Zikashindikana,



Hatimaye akakamatwa,tena mbele ya macho yake Gambi alimshughudia jemedar Laizar Nyoshi akiwapiga risasi wazazi wake mama yake na baba yake wakafa palepale,gambi Alilia,akaenda Katika Miili Ya Wazaz Wake,akaweka Kiapo LAZIMA NILIPIZE KWA HILI AIWEZEKANI,



"kamata huyo mfungeni pingu sheria itamuhukumu aina haja ya sisi kumuua!"



Laizar Akatoa Amri Gambi Roho Ya Paka,akakamatwa,akatiwa Rumande Kusubiri Kupelekwa Mahakamani



Nchi Ikawa Chini Ya Rais Laizar Nyoshi Alokuwa Jemedar Mkuu Kipindi Cha Mernel ii nchi ikarudi katika amani!



Baada Ya Miez Kadhaa Gambi Akapandishwa Mahakaman Kwa Kushtakiwa Kwa Kosa La Kutaka Kumtorosha baba yake na kuua raia wasio na hatia,kwa jeuri kidume kikakiri mwisho kikahukumiwa kunyongwa hadi kufa chenyewe kikawa kikitabasamu tu,kikapandishwa mpaka ndani ya gari mpaka ndani ya gereza la jehannam jail,gereza la kijeshi,kusubiri siku yake ya hukumu



*"NALA KIAPO KATIKA GEREZA HILI KWA WOTE WALE WALOSABABISHA KIFO CHA WAZAZI WANGU WAKIONGOZWA NA LAIZAR SITOWAACHA HAI,NASEMA SITOWAACHA HAI!,DAMU YENU HALALI YANGU UWAI WENU UKO MIKONONI MWANGU SITOWAACHA HAI NASEMAAA"*



JE UNADHANI KIAPO CHA MFUNGWA HUYU KITATIMIA?!







Lilikuwa Ni Bonge La Jumba,lililo Milikiwa Na Mzungu Henry Leyland,



Katika Chumba Ambacho Mara Nyingi Ukitumia Kwa Mikutano,leo Hii Kimya Kilitawala baina yao,walikwepo wa tatu,mchina King Yao,mzungu mmarekani double killer,na tiger man,



Baada ya kuwapoteza wenzao watatu ambao ni Rich,Snake Garl pamoja na black Snake,baada ya kuachiwa huru watatu wale,walirudi marekani,mpango mahususi ukapangwa juu ya kulipiza kisasi,awakutaka jambo hili kuliachia hivi hivi



"kwa taharifa zilizopo jinsi Kinte Ilivyochafuka,mtu Yule Na Mwenzake Wanaenda Tanzania,watashukia Kwa Kijana Isack,itapaswa nasi tumfate huko huko,bosi mr x katupa siku mbili tu Zidu awe ameuwawa"



Vijana Wale Watatu Wakaangaliana, ghafla Simu Ya Henry Ikaita akapokea!



"anasafiri kwenda Tanzania Kesho Ndege Aina Ya Amerates 115 Akikisha Unatuma Vijana Wa Kummaliza Nishaongea Na Kampuni Hiyo Paspot Watazikuta Hapo!"



"yes Mkuu!"



"fanya Mfanyavyo Mummalize Huyu Mtu!"



Baada Ya Maelekezo Yale Simu Ikakata!



"kama Mlivyosikia Nimeongea Na Bosi Na Katupa Information Zote Juu Ya Mtu Huyo Hivyo Kazi Ni Juu Yetu! Lazima Kesho Kesho tuikamilishe"



Vijana Wale Wote Watatu Walikuwa Na Uchungu Na Zidu,hasira Zao aziandikiki,muda ule ule wakaanza kupanga nguo zao!.



TANZANIA



UWANJA WA NDEGE WA KIA



KILIMANJARO



Zidu Na Mpz Wake Katarina Walishuka Katika Uwanja Wa Kia Mkoani Kilimanjaro,



Lengo Lao Ni Kuja Kuutalii Mlima Huo Wa Pili Kwa Ukubwa Duniani Baada Ya Ule Wa Evarist Ulioko Nchini Marekani



Walichukua Gari Dogo Mpaka Machame Ambapo Walipata hotel ya kilimanjaro,moja wapo ya hotel kubwa zilizopo mjini Moshi,pia Pemben Ya Hotel Hiyo Kulikuwa Na Touwrs Za Kupandisha Watalii Mliman!,



"mpz Wangu Wewe Na Huo Ujauzito Yapaswa Ubaki Hapa Utoweza Kupanda Huko"



Zidu alimshauri mpz we ambaye akuweza kupinga,Zidu akajiandikisha katika kampuni ile kupanda siku saba,akamuaga mke wake siku ya siku akapanda,

Katu akujua wala Kuwatilia Mashaka Majiran Zake,ambao Walikuwa Wakimfatilia Kila alichokuwa akikifanya!



Japo Kila Mmoja alikuwa na chumba chake mara chache walikutana kujidili kipi kifanyike!



kesho anapanda mlima yapaswa kati yetu wawili wapande na mmoja abaki chini kumdhibiti huyu mwanamke wake,



"dah mziki wa huko juu naujua mimi nishajitoa sitopanda mlima nina aleji na hivi vitu!"



King Yao Akajitetea,double K Na Tiger Man Wakacheka Wenyewe Walitaman Sana Kuupanda Mlima,



"bas Siyo Ishu Mimi Na Tiger kesho tutapanda mlima,wewe utamdhibiti huyu mwanamke,sidhani kama utamshindwa,basi poa,ukija mje na habar nzuri mimi huku kesho kesho huyu dada kwisha habar yake" kingyao akajielezea



Kilichofatia Ni Double K Na Tiger Kwenda Kujiandikisha Kuwa Kesho Nao Wanasafiri Wakaandaa Makoti,kesho Yake asb Wakapanda Katika Kosta Moja Na Zidu Kuelekea Mliman



Maskin Zidu akujua amemuacha mke wake katika hatari,tena hatari aswaaa,pia akuweza kubahatika kuiona hatari ilokuwa mbele yake,



JEHANNAM JAIL



Karandika lililompakia roho ya paka,mwanaume wa shoka gambi liliingia ndani ya gereza lile,

gereza lenye ulinzi mkali,mlango wa chuma wa karandinga lile ukafunguliwa ghafla mtu akatupwa,toka juu ya gari lile mpaka chini kwenye changarawe palikuwa na umbali,ni baada ya kutoka kufanyishwa kazi ngumu sasa alikuwa akirejeshwa,miguuni kapigwa pingu mikononi pingu akawa akivutwa sasa,alichubuka mikononi ila hakuna alojali miguno yake ya maumivu akapelekwa mpaka lock up yake akafungiwa huko tena alifungwa kama mbuzi kamba ikiwa mnyororo mzito,ukifungwa kwenye nondo na kufuli kubwa!



Kila Siku alikuwa maaskar wakija kwa zamu jion na usiku kumchapa kwa mkanda wa jeshi,alilala akiwa katika maumivu makali na asb alitolewa chini ya ulinz mkali kupigishwa kazi akisimamiwa na wanajeshi wakutosha!



*'ipo siku yote haya yataisha sitosubiri ninyongwe ipo siku nafasi itapatikana ndipo watakapo mjua gambi ni mtu wa aina gani,naichukia sana Kinte,na Ntaisambaratisha Kama Walivyo Msambaratisha Baba Yangu,'*



Kidume Kiliwaza Kikiachia tabasamu baya,meno mchanganyiko wa njano na nyekundu ya damu yakaonekana,



*'nitaua bila huruma,nitateketeza wote,mbele ya macho yangu wakaua wazaz wangu sitoacha hai hata mmoja nasemaaa,ha ha ha ha,acha wantese,wacha wannyanyase,wacha wafanye wanavyoweza ila ipo siku yao,nasema ipo siku yao wote ntaua ha ha ha ha'*



ilikuwa ni kama kachanganyikiwa ila kile alicho ongea mwanaume yule hatari alikuwa akimaanisha,na kwa kudra za Mungu Nafasi aloihtaji ikapatikana usiku ule ule,



Mwanajeshi Wa Magereza katili aloenda kwa jina la Pinchu alikuwa na cheo kikubwa katika gereza lile,alikuwa na roho ya kikatili hasaa kwake kuua mfungwa ilikuwa ni kitu cha kawaida na kitu kingine mtu huyu alikuwa anapenda sifa,mpaka muda ule alikuwa kashawaingilia kinyume na maumbile wafungwa wote wababe katika gereza lile,jambo lile likazidi kumpa sifa kiburi,pindi roho ya paka alipoletwa kwenye lile gereza,akataka kuendeleza ubabe wake pasina kujua ile ni namba nyingine!



usiku ule ule akatuma vijana wake wamletee ofisini kwake,ili afanye kama alivyozoea!,vijana awakuwa wabishi usiku ule ule wakaenda wakamtoa wakampeleka,



"haya we kidume,mfungulieni hiyo minyororo mumuache huru nimfaidi vizuri,"



Wakamfungua!



Kosa!



Pinchu,msaidizi Wa Mkuu Wa magereza Akiwa Na Kawaida Ya Kuwafanyia Vitendo Vichafu Wafungwa Wababe,hili Naye Aonekane Mbambe anaomba aletewe Gambi Lengo Lake Likiwa Ni Lile Lile Kuiendeleza Rekodi Yake Ya Ubabe,ila Sehemu Anayoingia Ni Nyingine Twende Pamoja Kujua Kilichotokea...



"kwa heshima yako sitokufanya mbele za watu naombeni mtoke mniache naye humu ndani mpaka nimalizane naye"



Wanajeshi Wale Walo Mleta baada ya kumfungua ule mnyororo na zile pingu wakatoka wakimwomba mkuu wao kuwa makini,pinchu yeye alicheka tu kwa dharau alidanganywa na ulinzi ulokwepo pale,akabebwa na jina lake akasahau kwamba si kila binadamu ni mwoga,si kila binadamu anaogopa kufa,



Basi baada ya vijana wale kutoka akamfata Gambi Na Kuanza Kumfungua Vifungo Vya OvarRolly,muda wote Gambi alikuwa kimya ila ghafla aligeuka na kumkamata shingo,kuna mshipa alougusa,jamaa lile palepale akapoteza fahamu,akutaka kumuua taratibu akamsimamishia kwenye meza ya ofisin kwake kutokana na uzito na jinsi alivyo msimamisha ile meza ikawa ikinesa,mwanaume akapanda juu ya siling bord akatambaa taratibu mpaka nje ya vyumba vya magereza,kwa kunyata na kwa spidi akawa akielekea getini,kwa lengo la kutoka nje sasa,



Wanajeshi Walokuwa Nje Ya Mlango waliposikia ndani kuna nesa,wakajua gambi tayari,ila mwanajesh mmoja nje kule akataman kuchungulia kusuji ajue kulikoni,kuchungulia akiwa katabasamu si ndo ghafla akakunja mdomo wake,haraka sana akafungua ule mlango,wenzake wakiwa nyuma yake,



Mkubwa Wao Wa Kazi Alikuwa Kapoteza Fahamu Akinesa Nesa Kwenye Meza Haraka Sana Taharifa Ikasambaa,kengele Ikagongwa,wanajeshi Wote Wakakusanyika Mbwa Wakatolewa tayari kuingia porini kumsaka roho ya paka gambi...

Mkuu Wa Magereza Ndani Ya Usiku Ule Ule Akapiga Simu Kambin Kuitaji Jeshi Liongezwe Ndege Za Kivita Angani Vyote Vikimsaka Mtu Mmoja



MASATI



1:34 am



Moja Wapo Ya Jumba Za Kitajiri,nje Kulikuwa Na Ulinzi Mkali,ndani Ya Chumba Kimoja alilala kijana ambaye aliishi peke yake katika jumba lile,



Wakati Akiwa Katikati Ya Usingizi ghafla simu yake ikaanza kuita akashtuka,macho yake yakadondokea ukutani,ni saa saba za usiku,akanyoosha mkono wake kuchukua simu yake pembeni ya kitanda chake!



akaweka sikioni!



"gambi katoroka,haraka sana njoo uelekeo wa msitu pande mpaka kupambazuke awe kapatikana!"

baada ya maelekezo yale simu ile ikakata!



Hakuwa mwingine zaidi ya rafiki yake Zidu alowah kumuokoa Zidu Kuuwawa Na Rais Mernel ii komandoo Brown Stanley,

Morali ikiwa imempanda akashuka kitandani akavaa tshart yake akanawa uso,haraka akaingia ndan ya gari yake!...



Walinz Wala Awakushtuka Bosi Wao Kutoka Usiku Ni Katika Majukumu Yake Ya Kazi Wakamfungulia Geti Brown Akatoka,tayari Kwenda Kuelekea Katika Pori Lile Kujumuika Na Wenzake Katika Msako Ule,



NDANI YA MSITU PANDE!



Mbwa watatu wa awali walotangulizwa na askar sita wote walikutwa porini wakiwa wamekufa silaha zao pembeni,

ndipo jeshi lilipo ongezwa,ndege angani katika sitelite zao walimuona Gambi Waliporusha Risasi Na Mabomu Alitoweka Katika Mazingira Ya Kutatanisha,

Mpaka Panapambazuka Askar Wengi Walikuwa wamekufa,pasina Gambi Kuonekana,



Taifa Likaingia Katika Uwoga,

Wakati Huo Zidu Alishatoka Katika Msitu Ule Na Kuingia Ndani Ya Kijiji Cha Msinyaa,

Hapo Ndipo Alipoamua Kuweka Makazi Ya Muda,kichwa Chake Kilimuuma,aka Amua Apate Pombe Katika Kilabu Kimoja Kusudi Akili Ikae Sawa,akutaka Kwenda Mjini Kwanza Sehemu Ambapo Alijua Serikali Ingeweka Nguvu Zake Kubwa Katika Kumsaka,na Kweli Katika Vituo Vya Ndege Stendi Za Mabasi,ma Bandarini,msako Ulikuwa Mkali Gambi Asitoke,

Naye Akaamua Kujichimbia Katika Kijiji Kilekile Kilichopo Mpakani Mwa Msitu Kuchaki Gemu Liendavyo!



Mwanaume Brown Stanley Machale yalimcheza,wasiwasi wake ni juu ya kijiji kile,alihis mwanaume atakuwa akutoka pale,na lazima miongon mwa wananchi naye yumo,mwanaume akaamua naye kujichanganya kijijini,



Mpelelezi hatari,akavaa kama wananchi Wa Kijiji Kile,akawa tayari kupeleleza chini kwa chini Gambi Alipo,



Siku Ya Siku Katika Moja Ya Ngoma Za Kijijini Pale,mwanaume Si Ndo Alipo Mfuma Gambi,vurumai Likatokea Mapigano Yakaanza,ghafla Brown Akachomoa Bastola Na Kumtwanga Nayo GAMBI cha ajabu risasi ile ilipoingia tumboni jeraha likajifunga ikatokea upande wa pili napo pakajifunga!...



khaaa,



Brown Akaachia Bastola Na Kukimbia,si Yeye Pekee hata wananchi pia kila mmoja akakimbia upande wake!



Gambi akaachia cheko,kabla ajatoweka!



tena akatoweka kama jini...



makubwa!....



***



TANZANIA



USIKU WA MANANE



Ni ule usiku ambao gambi katoroka katika gereza la jehannam jail nchin Kinte,nchini Tanzania,katika Hotel Ya Kilimanjaro,aliamka Mchina King Yao,akaisweka Bastola Yake Kibindoni,akanyata Kuufata Mlango,akafungua Na Kutoka,akaufunga Taratibu,akakifata Chumba Kinachofatia,ambacho Ndicho Kilichotumiwa Na Katarina,akatoa Funguo Malaya,akachomeka Kwenye Tundu La Funguo Akatokonyoa Mlango Ukafunguka,akashika Kitasa Akafungua Taratibu



akazama ndani bastola mkononi,ghafla akawasha taa,macho kitandani,bastola kashakamata kifyatulio,kutupa jicho kitandani,akajikuta akistop na kusogelea kitanda akatoa net akaitupia kule,shuja zote kule,sasa akawa kamuelekezea bastola katarina tayari kwa kumuua...



Katarina alishtuka toka usingizini wakat mtu yule alipowasha tu taa,akamshughudia akikisogelea kitanda akaitoa neti na mashuka alojifunika,

alijua sasa mwisho wake umefika,tumbo lilikuwa kubwa hakuwa na uwezo wa kupigana,ivyo akafumba macho yake kusubiri risasi zimmalize!







Gambi anafanikiwa kutoroka katika gereza lenye ulinzi wa kutosha,msako dhidi yake unaanza mara moja pasina mafanikio,wanajeshi wanatanda kila kona,



Huku Upande Wa Pili Mpelelezi Wa Kipekee Na Mwenye Uwezo Wa ajabu aliyewah kuwaga rafiki yake mkubwa na Zidu anafanikiwa kukigundua Kijiji Gambi alichokimbilia naye anatua ndani ya kijiji iko na kuanza upelelezi mara moja,siku ya siku anamfuma ila Gambi Anatoweka Katika Mazingira Ya Kutatanisha Je Unahisi Nin Kiliendelea



Twende Pamoja Kubaini Kilichojiri



Macho Yalimtoka Pima Kingyao,mapigo Ya Moyo Yakaanza Kumwenda Mbio mishipa ya kiungo kilicho mpa uanaume ikawa ikitanuka na kujaa,mwanamke yule alokuwa kavaa nguo za kulalia ni kama ziliacha maungo yake yote wazi,



Yeye alibaki kutetemeka akijua muda wowote sasa anaenda kufa pasina kujua hasa ni lipi kosa lake?,ila mabadiliko ya mtu yule aliyaona akapata 'chance' ambayo akutaka kuichezea vibaya,akazidi jifunua akijifanya kuzidiwa na uwoga,



Pasina kutarajia mchina yule akujua ni sangapi silaha ilimponyoka akakivamia kitanda,mwanamke pale chini akampokea wakaanza mashambulizi ya kimapenzi,king tayari akili ilishamuhama,wala akufikiria kwa nin msichana yule alimpokea kwa mikono miwili pasina kipingamizi,akujua tayari yupo katika mtego,wakazidi kupagawishana mabusu moto moto huyu akija juu,huyu naye juu,huyu juu,ili mradi kila mmoja aoneshe uhodari kwa mwenziye!



Kingyao,hisia Zilikuwa Juu,alikuwa akihema kama mtu alotoka kukimbia mbio za riadha,wakati Katarina akiwa juu yake ghafla mikono yake akaipeleka shingoni kwake na kuanza kumnyonga kwa nguvu king yao alipojaribu kufurukuta alishindwa,dakika chache badae Katarina aliiachia ile shingo baada ya kuakikisha mchina yule katulia,



Jasho mwili mzima ulimtoka, akujal ilo,aliwaza kile ambacho kingefatia,ni msala ule angewezaje kuusevu?,ndicho kilicho mpa mawazo kwa muda huo,itakavyokuwa na iwe,kwa kuwa ni usiku akataka kuutoa ule mwili nje aupakize katika gari lake akautelekeze maporini huko!

ITAENDELEA

Simulizi : Kiapo Cha Mfungwa (5) 

Sehemu Ya Tatu (3)





Akatoka kwel kucheki usalama,alirizishwa na hali ya utulivu alokumbana nayo,na hata nje walinzi wawili walikuwa wamekaa kwenye viti wameegemea ukuta wamelala,akarudi ndani chap,kwa nguvu zake zote akaunyanyua ule mwili na kutoka nao,mpaka nje,akauingiza nyuma ya buti la gari akafunga ile anageuka aelekee sasa ndani ya gari lake akuamini kile alichokiona,



Walinzi wale dakika chache walokuwa mamelala walikuwa nyuma yake wakimwangalia kwa tabasamu pana



"upo chini ya ulinzi,kwa tuhuma za mauaji ukipiga hatua moja tu kitakachofatia utopata hata muda wa kujutia,kikubwa nyoosha mikono yako,mshtuko aloupata Katarina ukuwa wa kawaida,



"Mh..."



Akaguna



Wakati akitafakari cha kufanya walishughudia gari jingine la polisi likiwasili , haraka sana maaskari watatu wakashuka na kuja eneo lile



Waliitwa na nani?!,hata wale walinzi awakuwa na jibu ya swali hili,maaskar wale wakapiga simu ambulance ikawasili



"ero Marwa Piga Pingu Iro riuaji Ritaenda Jiereza Kituoni!"



Askar mwingine akaongea akimpa amri askar yule wa pili aloshika pingu!,Kata akutaka kuwa mbishi kupambana tena na maaskari wa kibongo na hali yake ile,hakika alikuwa ni mzito akanyoosha mikono yake akapigwa pingu,Akaingizwa ndani ya gari,safari ya kuelekea kituoni ikafatia!....



Huku maiti ile ikipakiwa katika gari la hospital tayari kwa kwenda kufanyiwa uchunguzi wa awali



Kwa Usiku Ule Katarina alifikishwa kituoni na kutupwa rumande!





Afande Nurdin Akiwa Ofisini Kwake,maaskar Wale Watatu Wakaingia Na Kumpa taharifa mkuu wao juu ya kufanikiwa kumkamata Katarina,



"well,well,well,kazi Njema,"



Rudin Patrol Kesho Uchunguzi Utafatia Juu Ya Mwanamke Huyo,



"sawa Mkuu"



Insp Nurdin baada ya vijana wale kutoka ndipo alipokumbuka robo saa kabla ya tukio lile akiwa ofisin kwake alipopokea simu,alipocheki namba ni mpya!



"kwa muda huu chumba namba 3 katika hotel ya kilimanjaro kunafanyika mauaji mwanadada anaua waini kutoa msaada!"



Insp Nurdin akaduwaa,wewe nani lakini?!



"kwa sasa upaswi kunijua ila kwa kifupi waeza niita mr x"

Upande Wa Pili Ukajibu



"mr X?!" Nurdin Akahoji Kwa Mshangao Ila Simu yake tayari ikawa ishakatwa,



Si Mtu Alokuwa Akidharau Ripoti Alizozipokea Haraka Sana Akawapigia Simu Askar Walioko Chini Yake Na Kuwa agiza katika hotel ile,na kwa bahati nzuri maaskar wale awakuwa mbali ile wanafika pale wakamshughudia mwanadada yule akifunga buti palepale wakashuka na kumuweka chini ya ulinzi,wakawapigia simu wenzao,pamoja na gari la wagonjwa,maiti ikapakiwa kupelekwa hosptal kwa uchunguzi,katarina Akaletwa Pale Kituoni!



Insp Nurdin Akutaka Kujiumiza Sana Kuwaza Yeye alijua kesho yake ndo angejua kila kitu!







Upande Wa Pili,bado Kijana Brown Stanley Alizidi Kumfatilia Kijana Gambi,pasina Gambi Kujua Kama Anafatiliwa,tayar alishagundua nyumba alokuwa anakaa,



ila tatizo Gambi Alikuwa Akamatiki,akuweza Kujua Amuweke Kwenye Kundi gani la binadamu au!..



Wakati Akiwa Katika Mawazo Hayo Alikuwa Pemben Ya Nyumba Ya Gambi Ghafla Macho Yake Yakamuona Gambi Akitoka Katika Chumba Chake,



Akiwa Na Ndoo Ya Maji akaelekea Nyuma Ya Choo Akachuchumaa Akawa Kama Akichimba Chimba Akuelewa Anafanyaje Pale,ghafla Akanyanyuka Na Kuelekea Msalani Kukoga,bafu Ndo Ilo Ilo Choo,haraka Sana Brown Akachepuka mpaka Lile eneo alilochimba chimba gambi akaanza kufukua alihitaji kujua jamaa yule kafukia nini!



ghafla alipigwa na kitu nyuma yake,kugeuka nyuma gambi mkonon kashika li kuni,akalinyanyua ili ampige tena ila safari hii Brown Akalidaka Na Kumsindikiza Na teke



gambi kuleee,akaachia yowe la maumivu,Brown akajirusha,ila gambi akamkwepa sambamba na mwanaume kuinuka,brown naye akakaa sawa,wote wakawa tayari kupambana!



Brown Akawa Sasa Akimfata Kwa Spidi Ila Gambi Alisimama Palepale tabasamu baya mdomon mwake



Brown Ile Anarusha teke patupu ghafla akahis maumivu nyuma yake pemben kiunoni,mwanaume tayar alimtokea kwa nyuma na kumsweka teke,Brown Kulee,sasa Akawa akiona maruweruwe,tena wakija wawili wawili,mdomon wakiwa na tabasamu baya!,



"ndo naenda kufa mimi wallah"



Wazo hili likapita moja kwa moja mpaka kwenye kichwa chake







Baada ya wazungu wale kuondoka wakiwa na Zidu usiku ule katika mahema Yale apakulalika tena



"Tom tukisema tuendelee kukaa kimya mpaka kupambazuke itakuwa hatari zaidi ni bora tuwajulishe walinzi wa mlima huu wawe na taharifa kwamba watalii wametekana"



"Tutawajulisha na nini na mawasiliano hayapatikani"



Tom aliongea huku akionekana kuchanganyikiwa,ghafla walipotupa macho kwenye redio call zao zikapandisha minara ni kama wale watekaji waliachia mawasilino sasa



Na ni kweli baada ya kuakikisha wamemwangamiza Zidu chini ya maporomoko ya jiwe la kubusu wakaachia mawasiliano katika kidude cha kukata mawasiliano 'double' alichokuwa nacho



Vidude hivi vidogo vilitumika sana na magaidi au wapelelezi kukata mawasiliano iwe simu redio au kitu chochote cha kuwasiliana kwa njia ya hewa au minara



Baada ya kuachia mawasiliano viongozi wale wa Kilimanjaro tour wakawapigia walinzi wa mlima ule na kuwapa taharifa dakika chache ndani ya usiku ule ule taharifa ikafikia idara ya jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro



Nao wakalifikisha ngazi ya taifa,ndani ya nusu saa ndege ya kijeshi ilikuwa angani ikipambana na ukungu wa barafu satelite za ulinzi zikimulika chini



Wanajeshi wengine wakisaidiana na askari pori walishuka chini ya maporomoko yale ya jiwe la kubusu wakamtoa Zidu akapakiwa ndani ya ndege ya kijeshi kuwaishwa hospitalin



Double na mwenzake Tiger awakufika mbali wakatiwa nguvuni,awakuamini kama nchi Tanzania ilikuwa na ulinzi kiasi kile,walichukulia ni taifa jepesi pasina kujua hili ni taifa lenye ulinzi mkali hasa kwa Mali na u salama wa raia wake!....



Taifa pole lenye amani ila lenye nguvu na usiri wa hali ya juu hasa katika maswala ya upelelezi



Baada ya upelelezi kufanyika ikagundulika yule mchina alouwawa kilimanjaro hotel ni wamoja tena ni magaidi wa kundi hatari la mafia walokuwa wakisakwa na nchi zao!



Ivyo mwanadada Katarina akaachiwa huru,



Hali Ya Zidu Ilipoleta Matumaini Akaruhusiwa Kutoka Kcmc Isack Akawa Chukua Mpaka Nyumbani Kwake,alipoishi Yeye Na Mke Wake Mery,na Mtoto Wao Mdogo Beatrice



Huku Upande Wa Pili Henry Leyland Mr X alimpigia hasira zikiwa zimempanda akawa akimfokea



"sitaki kuamini kama umeshindwa kumuua huyu mtu,ujui kanipa pigo gani kwenye maisha yangu,ujui kanitesa kiasi gani,nimepoteza fedha zangu mtu huyu afe ila umeshindwa hii kaz ntaifanya mwenyewe ikiwa wewe umeishindwa"



Mr X aliongea kwa hisia,ni wazi alimchukia Zidu Na alikuwa na hasira naye,ni kama aliwah mfanyia kitu kibaya ambacho alishindwa kukisahau kwenye maisha yake ni kitu gani icho?!,



Bado Ilibaki Siri Yake Ambayo Hata Henry Mwenyewe Akuijua,



"nipe Nafasi Ya Mwisho Mkuu,nitaenda Kuifanya hii kazi mwenyewe nitasafir mpaka Tanzania Kummaliza Huyu Mtu! Nipe Masaa 42"



Henry aliongea kwa kubembeleza,



"sawa kaz ipo mikonon mwako ni kijana ninayekuamin hakikisha uui asiyehusika zaidi ya Zidu Pekee Sawa?"



"Sawa Mkuu"



'Mr X' Akakata simu, Henry Leyland Pale Ofisini Kwake Alikuwa Kavimba kwa hasira,akuwah kumuona bos wake akiwa na hasira Kiasi Kile,naye japo akumjua kisura,wala jina lake halisi lakin alimuheshimu zaidi ya kitu chochote!,



Hakuwa Na Muda Wa Kupoteza Akajiandaa Kwa Safari Ya Kuelekea Tanzania!,kuakikisha awamu hii amuudhi mkuu wake "mr x" ndo maana kazi ile akaamua kuifanya mwenyewe



Kwa Upande Wa Zidu Katili Na Mke Wake Katarina Isack Alimfanyia Mchakato Wa Uraia Wa Kudumu,siku Ilofatia Wakaenda Kutembelea Nyumba alizokuwa akimiliki Zidu,zote Zilikuwa Chafu Wakaweka Wafanyakazi Kuzisafisha Ikiwemo Kupiga Rangi Upya Wakati Urepeaji Ukiendelea Zidu Na Mke Wake Waliendelea Kuishi Katika Jumba Lile La Isack

kwa minajili mpaka Katarina atakapojifungua,



Wakati Hayo Yakiendelea Uwanja Wa Ndege Wa Kimataifa Dia Alishuka Mzungu Henry Leyland,moja Kwa Moja Mpaka Nje Ya Uwanja Akachukua Tax Mpaka Katika Hotel Moja Ya Kitalii,baada Ya Kula Akachukua Chumba Na Kujipumzisha



"nimefanikiwa Kuingia Nchini Tanzania Jijini Dar Nipe Maelekezo Mkuu"



Upande Wa Pili Mr X Akamjibu,

"ok Panda Ndege Shukia Mkoa Wa Kilimanjaro Kia Pale Kuna Watu Ntawatuma Wakupokee Maelekezo Mengine ntakupatia ukishafika"



"ok Mkuu!"



Henry akaitika,moyon mwake hasira juu ya Zidu Ikizidi Mara Mbili baada Ya Kuwapoteza Vijana Wake Alowategemea,ilipaswa kwa vyovyote vile afanikiwe ile kazi!



Naam,nusu saa badae alikuwa ndani ya ndege,akielekea katika mkoa wa Kilimanjaro,hamu Yake Pia Ilikuwa Ni Kuuona Mlima Huo,alifika Katika Uwanja Wa Kia Kushuka tu



'Mr Henry Leyland Karibu Tanzania,karibu Moshi'

Kijana 'smart' alovaa suti nyeusi akiwa pembeni ya gari yake nyeus nzur gari za kisasa,mkononi alishika simu ilokuwa na picha ya Mzungu Yule



Henry akatabasamu na kumfata mtu yule,wakakumbatiana,



"m.." Henry Akamnong'oneza



"mafia For Life,itadumu Milele"



Henry akatabasamu,ile ilikuwa ndo kama logo yao ya siri,mwana mafia yoyote ni lazima aijue lau kama jamaa yule asingejibu,machale yangemcheza Henry Na Kung'amua Yule Siyo,yule Jamaa Akafungua Mlango Henry Akazama Ndani,



"naeza Kulijua Jina Lako?"



"yah Naitwa Piter Bosi 'Mr X' Kanambia Kuna Mgeni Wake atakuja nije kukupokea hapa karibu sana"



"ahsante sana!"



Safari Ikaendelea,mpaka Mjini Moshi ambapo alipewa hotel,baada ya yule jamaa kuondoka akiwa ndani ya chumba chake mr Henry akampigia tena bosi wake 'mr x'



"chukua bodaboda,nenda maeneo ya majengo nyuma ya kituo kikuu cha polisi majengo kuna jumba moja la kifahari mbele kuna grosary pemben yake kuna duka la vifaa vya umeme ukivuka barabara upande wa pili kuna soko kuu la majengo hapo katika ilo jumba ndipo anapoishi huyo mtu,Zidu Katili,kuwa Makini Naye,ni Mtu Katili hasa,ni mjanja ana akili na ukimpa nafasi umekwisha,ivyo ukipata nafasi usiipoteze"



'Mr x' akampa tahadhari alionekana ni mtu aliyemfahamu vizur sana Zidu,akaendelea



"katika Ilo Jumba Wanaishi Watu Wa Tano,Zidu na mke wake Katarina Ambaye Ni Mjamzito Na Mimba Yake Inamiez tisa naye ni komando ila kwa uzito alo nao sidhani kama kwako atakuwa kikwazo,ila komando ni komando kama kaweza kumuua kingyao lazima uwe nae makin,pia kuna kijana mwingine anaitwa Isack Huyu Ni Mwanajesh Wa Jwtz Mwenye Cheo Cha Luten Ni Kijana Mdogo hatari,na mwenye mafunzo na mpiganaj mzuri ivyo nyumba unayoingia siyo ya mchezo kuwa makini,"



'Mr X' Akazidi Mtahadharisha Kijana Wake Yule alomtoa khofu mkuu wake yule



"ok kaz njema tutawasiliana"



'Mr X' baada ya kukata simu Henry akachukua silaha yake akaisweka kibindon akachukua bodaboda

"nipeleke majengo polisi,'

Akampa Maelekezo Yule bodaboda akawasha pikipiki safari ikaanza...



Robo Saa Alikuwa Nje Ya Geti La Nyumba Ya Isack,akashuka Katika Pikipiki Na Kumlipa bodaboda ela yake boda boda akaondoka



Akasogelea geti na kugonga kengele ilokwepo ukutani:







X' baada ya kukata simu Henry akachukua silaha yake akaisweka kibindon akachukua bodaboda





"nipeleke majengo polisi,



Akampa Maelekezo Yule bodaboda akawasha pikipiki safari ikaanza...



Robo Saa Alikuwa Nje Ya Geti La Nyumba Ya Isack,akashuka Katika Pikipiki Na Kumlipa bodaboda ela yake boda boda akaondoka



Akasogelea geti na kugonga kengele ilokwepo ukutani:



Baada Ya Kugonga akasubiri kwa sekunde kadhaa geti lifunguliwe,

Na Kweli baada ya dakika chache geti likafunguliwa mbele yake alikwepo Mery,mke Wa Isack,



"nimemkuta Zidu!"



Akaongea Kwa Sauti Kavu,iso Na Mzaha hata chembe



"ndiyo yupo karibu ndani,"



Akakaribishwa taratibu Henry akajongea mpaka ndani!,



Zidu alishangaa kuto mfahamu mtu yule,Henry akakaa kwenye kochi tayari kuanza maongezi,katu akuhisi wala kudhani kwamba yule si mtu mzuri kwake,



Henry alikuwa akisoma ramani maeneo yale ambapo alishagundua Kwa Muda Ule Ndani Walikwepo Watu Wawili tu,japo akujua huko vyumbani,aliyewaona ni Zidu Na Mery Mke Wake Isack,



"kwa Jina Naitwa Sir Richard Mackey nadhani mi ni mgeni kwako!"



Henry Leyland alijitambulisha kwa jina la uongo,muda ule alikuwa akitafakari pale ni kipi cha kufanya,



'sijui nichomoe bastola hapa ghafla nimbutue'



Wazo hilo likakubaliana na akili yake na kwa siri sana akawa akipeleka mkono wake alipoifadhi silaha yake



"ni kweli mimi sikujui na ni mgeni kwenye macho ya.."



Kabla ajamalizia akatazamana na Bastola,ila Sekunde Ile Ile Mwanaume akajirusha na kumpiga teke la mkono bastola ikaruka kule,



Sasa mafahali wawili wakawa wakitazamana,wakiviziana,Zidu akamsogelea na kumrushia teke ambalo Henry aliinama chini teke lile likapiga hewa alipo nyanyuka alisogeza mkono wake nyuma aloukunja na kuutuma mbele kwa nguvu ila Zidu aliona ngumi ile akatanguliza mkono wake mbele kukinga ngumi ile sambamba naye kufyatua yake ilo mpata sawia Henry Usoni,



Mzungu yule akapepesuka,kabla ajakaa sawa Zidu Akamuwah Kwa teke Henry akaenda chini akidondokea meza,akaachia yowe!



Mwanaume Akapiga Hatua Ya Kwanza Ile Ananyanyua apige ya pili Henry akajinyanyua sambamba na kuikwapua meza ya kioo alodondokea hapo awali,



Akamtandika nayo Zidu Kichwani,ikamvunjikia Na Kumuumiza Vibaya Sana,kizunguzungu Kikali Kikamshika Mwanaume akaenda chini,akapoteza fahamu,



Wakati Hayo Yakiendelea Mery alikosa cha kufanya muda huo alikuwa akipanga vyombo kwenye kabati sebuleni pale ivyo wakati mafahali wale wakipigana yeye alibaki kuwatazama tu pasina kujua alipaswa afanye nini,alikuwa Kachanganyikiwa,akili Ilifanya Kazi baada ya Zidu Kupigwa Na Meza Ile,hapo ndipo alipopata wazo la kumpigia simu mume wake Isack Na Kumjulisha Kile Kilichotokea!

Ile anapiga hatua,akashtushwa kwa sauti ya ukali,



"we mwanamke unaenda wapi?!"



Mery akaganda mwili wake wote ulikuwa ukimtetemeka,macho yake yakimwangalia Zidu alolala chini katika dimbwi la damu,akuitaji kipimo cha kumjulisha kuwa yule yupo katika hali mbaya



"usisogee mbele,wala kunyanyua mdomo fata maelekezo yangu ukienda kinyume na mimi sitosita kuacha maiti mbili hapa"



Mzungu Yule akazidi kuongea kwa biti akionekana wazi kuchukia,

Mary akawa mnyonge,nje nimekuta gari tatu hapo nipe funguo ya gari moja na ukanifungulie geti nitoke ufunge,Henry aliongea huku akimfata,wakaongozana mpaka ndani akatoka na funguo,wakarudi Sebuleni Henry akambeba Zidu Mabegani Wakatoka Mpaka Nje Akamuingiza Mpaka kwenye buti akaingia garini na kuliondoa gari kwa spidi!



Huku Nyuma Merry akafunga geti huku akilia akikimbilia ndani akachukua simu yake na kumpigia mumewe ila namba ilikuwa ikitumika akampigia Katarina aloenda zahanat kuangalia ujauzito wake!



Wakati Hayo Yakiendelea,moyoni Mwake Kulijaa Chuki,alimchukia Zidu Zaidi Ya Kitu Chochote Katika Maisha Yake,aliketi Ofisini Kwake Macho Yake Yalikwepo Katika Laptop Yake,



Alikuwa Akishughudia pambano lile lililokuwa likiendelea katika jumba la Isack Kati Ya Mtu Wake,kijana Wake Wa Kazi Henry Leyland Na adui Yake Mr Zidu,ni Wazi Mtu Huyu alifanikiwa kutegesha kamera sebuleni pale pasina kujulikana na mtu yeyote!

'Mr X' alikuwa katika tabasamu zito,ila tabasamu liliyeyuk baada ya kumshughudia kijana wake yule akimbeba Zidu akakunja kite cha hasira!



'haaa huyu kashaua badala asepe aache hiyo maiti humo ndani sijui anaibeba anaipeleka wapi tena'



'Mr X' akawaza wakati Mr Henry alipo mnyanyua Zidu Na Kutoka Naye Nje,kitendo Cha Kutoka Naye Tu Nje Mawasiliano Yakakata Na Kurudi Pale Sebulen Ina Maana Kamera Zile Zilitegeshwa tu sebuleni,



Baada Ya Kama dakika tano simu yake ikaita kumcheki ni Henry,haraka Sana Akapokea...



"umekosea Usingebeba Hiyo Maiti Ungeacha Umo Ndani Ukaondoka Cheki Umejibebesha Mzigo Sasa Nawe Mgeni Hapo Moshi Unafikiri Utaenda Itupa Wapi?!"



Mr X Akamuuliza kwa hasira tofauti na mategemeo yake upande wa pili ukacheka tena kwa kiburi,



"naenda utupa msandaka huko msitu wa ajabu mvuleni najua nifanyacho mkuu!"



Mr X akatoa macho!



"Mvule Wa Ajabu?!,unaufahamu Mvule Wa ajabu wewe"



"Yah Naufahamu Na Kuna Hazina Ya Mababu Yetu Kule Nishakujaga Nikiwa Mtoto,ivyo Damu Ikimwagwa Kuzunguka Ule Mti Ukichimba Pale Kuna Sanduku La Almasi Na Dhahabu"



"wacha Wewe Kwel?!"



"kwel Na damu ya Zidu Ndiyo ufunguo wa hazina hiyo ukushangaa bosi mimi kufanya hii kazi"



"vizur sana kuwa makin kijana,ela yako tayar katika akaunt sasa moyo wangu una amani"



Mr X akamaliza huku akitabasamu, akakata simu,alicheka sana,alikuta missd call 8 za mke wake akaamua kumpigia moyon akiwa na aman kupitiliza baada ya kufanikisha hazma yake!...



Wakat Mr X Na Kijana Wake Wakiwa Katika Furaha Ya Kufanikisha Kumuua Zidu Upande Mwingine Isack Kamishna Wajesh La Polis Aliketi Ofisini Kwake,



Macho Yake Yakiwa Bize Katika Laptop Yake,nikama Alikuwa Akifatilia Kitu Kwa Makin Na Alionekana Kufrahia Sana Kitu Kile,ghafla Simu Yake Ikaita Akaongea Na Mtu Ambaye Aikusikika Aliongea Naye Nin Na Baada Ya Kukata Tu Simu Ya Mke Wake Ikaingia Akapokea...



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog