Search This Blog

Thursday 29 December 2022

C.O.D.EX 4 (A MISSING SOLDIER) - 3

 

  Simulizi : C.o.d.ex 4 (A Missing Soldier)

Sehemu Ya Tatu (3)

alionesha kukata tamaa.

“Nakupa dakika moja ya kusimamisha gari lenu wanajeshi,” Uzo akasikika tena na si Merice wala Idris ambaye hakuwa akitokwa na jasho ukiachana na Limasi ambaye alikuwa analia kama mtoto mdogo. “Bado sekunde thelathini.” Uzo akaongea tena na hilo likawafanya Merice na Idris kuangalia wakitaka kufanya shauri la mwisho.

Idris alivyoona kama anaweza kuzidiwa, haraka alifungua mikanda ya siti za kiti na kujitupia siti ya nyuma ambapo alikuwepo Limasi. Akachomoa bunduki yake ambayo ilikuwa na uwezo wa kutoa risasi kwa juu na chini yake mabomu, wanaziita M-16 bunduki hizo. Akaiweka kwenye usawa kioo cha nyuma ya gari lile.

“Fungua mlango wa nyuma Merice. “Alibwata Idris na wakati huo gari la mbele la maadui zake, lilifanya tendo lilelile na mlango wa nyuma ulifunguliwa na yule bwana mwenye kombora alionekana kalikamata tayari kwa kuliachia lakini kwa bahati mbaya alichelewa kuliachia kwani Idris alikwishaachia lake mapema na kumkuta kifuani yule bwana. Likamrudisha ndani na kwa bahati mbaya bwana yule akadondokea mgongo na kombora alilokamata, likafyatuka na kumpiga dereva wa gari lile na kumtolea dirishani huku lile bomu alilopigwa kifuani, nalo likilipuka na kupoteza kabisa muelekeo wa gari.

“Mmekosea sana.” Uzo aliongea na lile gari la nyuma likatoka lilipo na kuchukua nafasi ya lile lililopoteza muelekeo. Idris akawa hana jinsi, mbinu zake zote zilikuwa zimetumika na sasa alikuwa anasubiri litakalotokea tu!

Akamuangalia mpenzi wake na kumkumbatia kwa nguvu na wakati huohuo, lile gari lililochukua nafasi ya lile lililopoteza muelekeo, lilikuwa linajigeuza na watu wawili wenye makombora walijitokeza tayari kwa kufyatua makombora yao.

Lakini kabla hawajafanikiwa kufanya hivyo, masikioni mwao walisikia sauti zinazofanana na nzi na vyumavyuma fulani ambavyo kama vilikuwa vinagongana. Hawakujua ni vitu gani, lakini mambo yalibadilika ndani ya sekunde chache baada ya kusikika sauti hiyo.

ITAENDELEA.




“Mmekosea sana.” Uzo aliongea na lile gari la nyuma likatoka lilipo na kuchukua nafasi ya lile lililopoteza muelekeo. Idris akawa hana jinsi, mbinu zake zote zilikuwa zimetumika na sasa alikuwa anasubiri litakalotokea tu! Akamuangalia mpenzi wake na kumkumbatia kwa nuvu na wakati huohuo, lile gari lililochukua nafasi ya lile lililopoteza muelekeo, lilikuwa linajigeuza na watu wawili wenye kombora walijitokeza tayari kwa kufyatua makombora yao.

Lakini kabla hawajafanikiwa kufanya hivyo, masikioni mwao walisikia sauti zinazofanana na nzi na vyumavyuma fulani ambavyo kama vilikuwa vinagongana. Hawakujua ni vitu gani, lakini mambo yalibadilika ndani ya sekunde chache ya kusikika sauti hiyo.

ENDELEA.

Kwa hali ya kushangaza, wale wanajeshi walijikuta wanafungwa mikono yao iliyokamata makombora. Hawakuweza kufyatua wala kufanya lolote. Mikono yao ilikuwa migumu kufanya tendo hilo. Pini za Agent ambaye bado alikuwa hajaonekana, ziliwabana vilivyo kwenye vidole vyao pamoja na sehemu ya kuvalia saa. Na kibaya zaidi, pini zile zikaanza kuwavuta waingie ndani na makombora yao. Hawakuamini kinachowatokea katika maswala yao.

“Mbona sioni matokeo?” Alibwata Uzo.

“Kuna vichuma vimetukamata mikononi.” Alijibu mwanajeshi mmoja huku akijaribu kukataza mikono yake isizunguke na kuelekea upande wa dereva lakini haikuwa hivyo. Mwisho wake ulikuwa ni kumlenga dereva upande wa mgongoni na kisha pini zile zikalazimisha kubonyeza kifyatulio. Kombora likachomoka na kumtoa dereva kupitia kioo ambacho kilipasuka vibaya. Uzo akashuhudia dereva wa gari lililokuwa mbele yake akija na kutua kwenye boneti. Akiwa haelewi kinachoendelea, mara yule mwanajeshi mwingine naye alianza kulenga gari la uzo na kufyatua kombora ambalo kwa haraka, Uzo alipindisha gari lake na kombora lile likapita pembeni huku gari la wahusika wenye makombora, likipoteza njia na kwenda kupindukia pembeni ya barabara na kulipuka vibaya kwa sababu lilikuwa kwenye mwendo wa kasi.

“Nini kinatokea tena? Mbona wanapoteza muelekeo wenyewe?” Akauliza Merice na swali hilo likamfanya Idris amuachie Limasi na kutazama kilichotokea. Hata yeye hakuamini hali ile. Akajikuta anatabasamu peke yake.

“Sijui ni nini kinatokea lakini ni afadhali maana haya magari mawili yaliyopinduka ndio silaha kubwa ya mtindo ule wa kisu, kwa hiyo kwa sasa, tunaweza kupambana na hawa wengine.” Idris aliongea kwa furaha.

Wakati hayo yanajiri ndani ya gari la Idris, Uzo alikuwa mwenye kiwewe kikubwa akiwa hafahamu ni nini ambachoo kinatokea kwenye nyakati zile ambazo alikuwa karibu sana kuwakamata wanajeshi wake.

Akiwa katika hali hiyo ya taharuki, mara vumbi zito likaanza kuonekana pembeni ya barabara ile ya rami. Uzo akatazama vema. Na vumbi lilipotulia, aliweza kuona ndege kubwa ya kivita, pembeni imeandikwa Jet P112 FISSA, na kisha mlango wake wa nyuma ulifunguka na katika hali ya kupendeza, pikipiki kubwa ilichomoka ndani ya ndege ile na kutua ardhini hadi cheche kuonekana japo jua tayari lilikuwa limechukua nafasi yake kwa kiasi kikubwa.

Ndege iliondoka kwa kasi na kuacha pikipiki ile ambayo ilikuwa inaendeshwa na mtu aliyekuwa katika mavazi meusi na kichwani kwake kavaa kofia ya pikipiki, ikiwa rangi hiyohiyo nyeusi, ikiingia barabarani kwa mbwembwe nyingi sana.

Mtu yule alisogeza pikipiki yake hadi mbele ya gari la Uzo ambaye kwa wakati huo alikuwa mbele kuliko wale wenzake. Na mbele kabisa alikuwepo Idris na kundi lake, hivyo bwana mwenye pikipiki yeye alikuwa katikati ya Uzo na Idris.

Mwenye pikipiki akageuka nyuma na kulitazama gari la Uzo, kisha akafungua kioo cha kofia ya pikipiki. Macho yake yakakutana na Uzo ambaye alirudisha haraka mgongo wake kwenye kiti alichokalia.

“Agent Zero.” Maneno yakamtoka na ni kama yalisikika kwa Agent Zero, kijana tegemezi wa Rais wa Tanzania. Akafunga kioo cha kofia yake baada ya maneno ya Uzo, na kisha akanyoosha mkono wake kuelekea gari la Uzo. Uzo alipotazama mkono wa Agent Zero, aliona kidole kikubwa kikimtazama. Akachoka zaidi.

****

“Ni The Undercover Agent huyu.” Aliongea Idris baada ya kuona pikipiki ile. Japo hakuona sura, ila alikuwa kalikariri vema umbo la Agent Zerio.

“Ndiye nani huyo?” Aliuliza Merice.

“Ni yule jamaa aliyenikamata kule barabarani.” Idris akajibu. “Jamaa kama si mtu aisee, sijawahi kupambana na binadamu mbishi kama huyu.” Akaongeza.

“Ahaa! Ni yule mshenzi?” Akauliza tena kwa nyodo, Merice.

“Naona safari hii kaja kutusaidia maana ndiye aliyewasambaratisha hawa wajinga. Anasayansi za ajabu sana. Sijamuelewa hadi sasa hivi.” Akasifia Idris na wakati huo Agent Zero alichanganyia pikipiki yake hadi upande wa kushoto wa gari la Idris na kisha akafungua kioo cha kofia yake na kugonga kioo cha sehemu aliyokaa Idris. Idris akafungua kioo hicho.

“Nasikia kuna Mtanzania humu kwenye gari lenu.” Ndilo swali la kwanza ambalo aliuliza Agent Zero kwa sauti ya juu ili asikike sababu upepo ulikuwa mkali.

“Ndio. Ni mke wangu.” Akajibu Idris.

“Shukuruni MUNGU amewaokoa.” Agent Zero akafunga kioo cha kofia yake na kupunguza mwendo ambapo gari la Idris likatangulia na Agent Zero akageuza haraka pikipiki yake na sasa akawa anawatazama Uzo na jeshi lake ambapo gari tano ndizo zilibakia.

Mtindo wake uleule wa kutupa pini, ndio alioutumia na pini zile zikaenda kwenye vioo vya magari matatu na kunata hapo. Agent kwa haraka akageuza pikipiki yake na kisha akabofya saa yake ambayo ilikuwa ni maalumu kwa ajili ya kuendesha zile pini, vioo vyao vya mbele vikapasuka vibaya mno. Na wakati huohuo, alirusha pini zingine nazo zikaenda kunasa kwenye mikono ya madereva. Akabofya saa yake kama kawaida, na pini zile zikalazimisha kupindisha usukani wa magari yao. Yakagongana gongana na kuwa mtafaruku mwingine mkubwa sana.

Idris ambaye alikuwa anachungulia shughuli ya Agent Zero, aliweza kuona mtafaruku ule na kwa kusaidia tu, alimrushia Agent Zero mabomu ya sumaku pamoja na bunduki yake ambavyo vilikuwa vinaelekea pembeni kabisa, yaani vilikuwa haviendi kwa Agent Zero lakini Agent yule, alituma pini zake na vifaa vile vikavutwa hadi mkononi kwake.

Akatupa mabomu yale mawili na Idris naye akabofya peni yake. Mlipuko mzito ukatokea eneo lile ukiacha magari ya wanajeshi wa Uzo yakipaishwa angani kama ndege inayopaa.

“Simamisha magari.” Uzo alifoka kwa kiwewe baada ya kushuhudia hali ile. Magari yakasimama likiwepo na la kwake. Kutahamaki, yalikuwa yamebaki mawili tu. Lake na la wanajeshi ambao walikuwa watano kati ya wengi aliowaagiza waje Tanzania. “Watatumaliza hawa. Huyu Agent wao si mzui. Anahitajika kupotezwa au tumsikilize Rais wao anataka nini.” Akaongea Uzo.

Pikipiki ya Agent Zero ikaendelea na safari ikiwa inatoa ulinzi mkubwa wa gari la Idris ambalo lilikuwa linaelekea Moshi kwenye nyumba yake nyingine.

****

“Samahani mkuu, nimekukosea sana. Mtu wako kaja kutuharibia kazi ambayo tulianza kufanikiwa.” Uzo aliongea kwenye simu.

“Nilikwambia sitaki uwadhuru Watanzania wangu, lakini ukakjidai nunda. Unajua kwenye gari kuna Mtanzania mle? Mke wa Idris?” Rais akafoka.

“Sikujua mkuu. Naomba unisamehe.” Akaongea Uzo kwa huruma.

“Sikutaki nchini kwangu. Ukijidai mjuaji tu, namtuma huyo mwanaume aje akufanyie uchafu. Huwa hakosei kazi.” Akatishia Rais.

“Tutaondoka lakini ukiniahidi kitu kimoja.” Akatoa pendekezo Uzo na Rais akawa tayari kumsikiliza.

“Nataka utuletee hawa wanajeshi wetu Marekani. Vinginevyo, tutashusha C.O.D.EX wote nchini kwako, tuone kama huyo Agent atapambana mikoa yote.” Bado kiburi alikuwa nacho Uzo.

“Usinitishe. Nina jeshi lenye roho mbaya kama simba mwenye njaa. Lakini sitaki tu! Ondoka nchini kwangu na wanajeshi wako utakutana nao huko kwenu.” Rais akakata simu baada ya maneno hayo. Uzo akashusha pumzi ya nguvu.

****

Gari la Idris lilifika Moshi mapema na hawakupata tena vikwazo vya wale wanajeshi wa Uzo ambao walionekana wazoefu kwenye kazi zao za kupambana. Agent Zero ambaye naye alikuwepo kwenye msafara ule, aliingiza pikipiki yake ndani ya geti la nyumba ya Idris na kisha kushuka kumuangalia Limasi ambaye ndiye Mtanzania aliyemfanya aingilie ule ugomvi kwa mara ya pili.

“Upo sawa dada?” Akauliza Agent Zero.

“Nipo vema. Ahsante kwa msaada wako.” Limasi alishukuru.

“Ni kazi yangu. Yatupasa tuondoke hapa haraka sana kabla ya wanajeshi wa yule bwana kuja tena.” Aliongea Agent Zero.

“Hapana.” Limasi aliongea kwa sauti ya juu kidogo na kumfanya Idris naye asogee eneo la tukio. “Siwezi kuondoka bila kujua usalama wa mume wangu.” Akaongeza.

“Hawa ni wanajeshi hatari kupata tokea duniani. Wanaweza kuungua na kujirudi vilevile. Wanaakili nyingi na uwezo mkubwa wa kupambana na kitu chochote. Huna haja ya kuwa na wasiwasi hivyo.” Agent Zero alimuweka sawa kiakili, Limasi.

“Hata kama. Lakini mume wangu si mmoja wa wanajeshi hao hatari. Ni mpole na muelewa. Hana hizo sifa unazozitaja.” Limasi alimuambia Agent Zero huku Idris akiwa makini kupata hili na lile.

“Unakosea sana mwanadada.” Akaongea Merice huku naye anasogea eneo la tukio. “Mmeo si kama unavyodhani. Kaundwa kwa njia za tofauti sana na sisi. Sisi uwezo wetu si kama wa mumeo. Huyu ni hatari kuliko sisi. Sisi ni jeshi lingine la maangamizi lakini huyu, ni jeshi moja la kipekee. La ukombozi na pia maangamizi. Baba yangu alimuunda kitaalamu sana. Kuna wanajeshi wengine ambao hata mmoja hajaja huku, hao ndio wanaoweza kupambana na huyu mumeo.” Merice akaongeza.

“Embu twendeni ndani kwanza maana hapa naona mnaanza kunichanganya.” Idris aliweka wazi hasa baada ya yale maongezi ambayo yalikuwa yanamuhusu yeye kwa asilimia kubwa. Wote wakaingia ndani na kuanza kuongea mengi juu ya wao.

****

“Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa nina uwezo mkubwa kuliko nyie?” Baada ya maongezi marefu, Idris aliuliza swali hilo kwenda kwa Merice.

“Ndio.” Akakubali lile swali. Kuna video iliachwa na Baba yangu, nadhani kuwatisha wakina Uzo, inaonesha uwezo wako. Na nilishangaa sana kukutwa umekamatwa na huyu kijinga vile.” Merice aliongea.

“Huyo hawamuwezi wanajeshi wenu tu! Hapa kwangu ni mchuzi.” Agent Zero akaongea kwa dharau.

“Umekosea. Idris angekuwa anajitambua yeye ni nani, wewe ungekuwa maiti.” Merice akajibu nyodo za Zero.

“Unataka kusema kuwa jamaa hajitambui?” Agent akauliza huku ametabasamu. Idris naye akamuangalia Merice kuonesha kuwa naye anataka jibu la swali hilo.

“Hajitambui uwezo wake. Labda tumuulize tu, tangu aje Tanzania, kafanya jitihada gani kujua nguvu zake na uwezo wake? Huyu kapachikwa hadi chipu ya kuweza kubadilisha lugha, kawekewa chipu ya kujua mapigo ya mapambano, anachipu ya kujilinda mwenyewe, anachipu ya kuruhusu mabomu ya nyuklia kulipuka na anachipu ya kumbukumbu na huruma. Mimi nina chipu ya lugha, mapigo na ukatili pekee.” Merice akawatazama wenzake ambao walikuwa kimya.

“Ni kweli asemacho. Sijawahi kufanya majaribio yoyote juu ya nilichonacho mwilini. Ila nakumbuka, niliweza kujua haraka kucheza muziki wa kileo, kufanya mapenzi kwa mitindo tofauti tofauti, na mambo mengine ya kidunia. Nilijua haraka sana.” Kauli hiyo ikamfanya Agent Zero acheke kidogo.

“Unacheka nini?” Akauliza Limasi.

“Hamna dada yangu. Ila kaniacha hoi hapo kwenye kufanya mapenzi kwa mitindo mbalimbali. Kwa hiyo hata ile staili ya…..” Hakumaliza kauli yake, Limasi akampiga ngumi ya mbavu. “Auwuu!” Sauti ya kuumia ikamtoka Agent Zero. “Vipi mbona wanipiga lingumi?” Badala ya Limasi kujibu, akaweka kidole chake kwenye midomo yake akimaanisha akae kimya.





“Ni kweli asemacho. Sijawahi kufanya majaribio yoyote juu ya nilichonacho mwilini. Ila nakumbuka, niliweza kujua haraka kucheza muziki wa kileo, kufanya mapenzi kwa mitindo tofauti tofauti, na mambo mengine ya kidunia. Nilijua haraka sana.” Kauli hiyo ikamfanya Agent Zero acheke kidogo.

“Unacheka nini?” Akauliza Limasi.

“Hamna dada yangu. Ila kaniacha hoi hapo kwenye kufanya mapenzi kwa mitindo mbalimbali. Kwa hiyo hata ile staili ya…..” Hakumaliza kauli yake, Limasi akampiga ngumi ya mbavu. “Auwuu!” Sauti ya kuumia ikamtoka Agent Zero. “Vipi mbona wanipiga lingumi?” Badala ya Limasi kujibu, akaweka kidole chake kwenye midomo yake akimaanisha akae kimya.

ENDELEA.

“Sikilizeni.” Merice akawatoa wale Watanzania kwenye hali yao na wote wakawa tayari kumsikiliza. “Dada hapo, utaondoka na kaka yako. Tuache sisi tupambane. Huo ndio usalama wako. Leo hii hii yakupasa uondoke.” Merice akaweka wazo lake mezani.

“Upo sahihi mwanadada. Huyu naondoka naye sasa hivi. Mi’ nawaacha na majitu yenu.” Akaongeza Agent Zero.

“Kweli Lim. Usalama ni mdogo sana kwako. Naomba uende penye usalama. Ila hayo niliyokupa, kayafanyie kazi.” Idris naye akaongeza na mara simu ya Agent Zero ikaita. Akaichomoa na kuanza kuongea na upande wa pili.

“Yupo salama, mkuu.” Akajibu na kusikiliza upande wa pili wa mpiga simu. “Ndio, nipo nao hapa.” Akaongeza tena na kisha akampa simu Limasi.

“Sawa mkuu. Tumekubaliana kuwa nirudi.” Akaongea Limasi na kusikia upande wa pili utakachomwambia. Na baada ya majibizano hayo, akampa simu Idris.

“Sawa Mkuu. Tutafanya hivyo.” Ndilo jibu alilolitoa Idris baada ya dakika zipatazo tatu za kuisikiliza simu ile upande wa pili unachoongea. Simu ikakatwa na Idris akamtazama Limasi na kisha Merice. “Uzo na jeshi lake wametaka sisi turudishwe Marekani. Na Rais kakubaliana na hilo kwa sababu hapa tunawaletea matatizo wananchi wake.” Idris akaanza kuweka bayana aliyoongea na Mkuu wa Nchi.

“Yupo sahihi. Lakini huko tunapoenda, hawawezi kutukamata kirahisi?” Merice akauliza.

“Kasema atatusaidia kuingia Marekani bila Uzo kujua. Najua ananjia nyingi, atafanya hivyo na hawezi kutusaliti. Na kasema baada ya sisi kuingia Marekani tumtaarifu ili awape taarifa wakina Uzo kuwa tumeingia. Anataka watutafute wenyewe na si kutupeleka kirahisi rahisi tu.” Idris akamfanya Merice ameze mate kwa maneno hayo. Ahueni ikamkumba.

“Hapo sawa. Tutapanga cha kufanya tukiingia huko.” Merice aliongeza na wakati huo Agent aliinuka na kuanza kuitamaza ile nyumba kwa makini. Hakuna ambaye alimtilia maanani kwa sababu akili za wote mle zilikuwa zipo katika mawazo ya kurudi Marekani.

Agent akiwa anatazama huku na huko na kushindwa kuelewa muundo wa nyumba ile, alienda hadi sehemu ambapo kuna kabati kubwa la vitabu. Akalitazama kwa muda huku anasoma kitabu kimoja baada ya kingine. Mara macho yake yakatua kwenye kitabu kimoja ambacho kilifanya macho yake yakitazame kwa muda mrefu kabla hajawageukia wenzake.

“We’ Idris, umesema unaitwa nani jina lako lote?” Akauliza kwa wahka Agent Zero.

“Idris Iris. Kuna nini?” Idris akajibu huku wote wakiinuka na kwenda pale ambapo Agent kasimama.

“Hii ni nyumba ya nani?” Akauliza tena Agent baada ya wote kufika pale alipo.

“Ni ya Dokta Ice. Anayo hii na ile ya Arusha.” Akajibu na Agent Zero akamuonesha kile kitabu kilichomfanya aulize jina lote la Idris.

Idris naye akasogea akiwa kama haamini kile akionacho. Kitabu alichokuwa anakitazama, kilikuwa kinamaandishi makubwa yanayosomeka ‘IDRIS IRIS’.

“Ni nini hii?” Akauliza huku anasogea kwenye kabati na kutaka kukichomoa kile kitabu na hapo ndipo maajabu ya nyumba ile yakaonekana.

Nyumba yote ikafungwa vioo vyake na kuwa giza totoro. Na baada ya hali hiyo, wakaanza kusikia sauti za vitu kujivuta na baadaye kwenye kuta za nyumba zile, zikatokea kompyuta nne na kwa chini yake kulikuwa na majokofu manne. Yaani kila jokofu moja lilikuwa na kompyuta moja. Na vyote vilikuwa vinatoa mwanga mkali kiasi.

Baada ya majokofu na kompyuta zile kusogea na kutulia, kwenye ukuta mwingine, ikatokea runinga kubwa na kujiwasha yenyewe na kisha Dojta Ice alionekana na kuanza kuongea mambo ambayo hapo mwanzo Idris hakuwa na taarifa nayo.

“Idris. Huyu ni wewe. Nimekutengeza kwa lengo jema na si kwa malengo mabaya kama wale wa mwanzo niliyowatengeneza. Sikukupa taarifa za jinsi ya kuutumia uwezo wako lakini hapa, ndipo utaanza kujua uwezo wako ambao si rahisi wewe kuujua.” Alianza hivyo Dokta Ice na wakati huo, wote walikuwa kimya kumsikiliza. “Hayo majokofu unayoyaona, ndio uwezo wako na nguvu zako. Utakapoingia humo, tayari utakuwa unachaji nguvu zako na tayari kuzitumia dhidi ya wabadhilifu wa dunia hii. Naamini wewe ni mwanajeshi imara, na haya majokofu nimeyaunda kwa ajili yako wewe tu! Nilijua ipo siku utafika huku. Naomba utumie nguvu utakazozipata katika jema.” Dokta Ice aliongea hayo machache na kisha runinga ile ikaanza kuonesha jinsi majokofu yale yanavyoweza kufanya kazi ili kumpa Idris nguvu alizoumbwa nazo. Baada ya dakika kadhaa, video ikaisha na taa nyeupe zikawaka na mle ndani pakawa mfano wa Maabara kubwa sana ya kufanyia sayansi.

“Nimepapenda humu.” Agent Zero aliongea huku katabasamu.

“Patakuwa pako kama utatusaidia mambo tunayoyataka.” Agent Zero akatoa macho baada ya kauli ya Idris. Agent anamapenzi makubwa sana na ya Sayansi. Hivyo kwa muonekano ule wa ile nyumba, tayari moyo wake uliingia tamaa ya kutaka kumiliki mambo kama yale.

“Ni ndoto zangu kumiliki kitu kama hichi. Nipo tayari kuwasaidia kama kitakuwa ndani ya uwezo wangu.” Agent Zero akajibu kwa furaha.

“Utaweza tu. Nimeona silaha zako za Kisayansi. Najua utafanya vema kuweza kututengenezea zetu zitakazo tusaidia huko.” Idris hakukwepesha kumpa alichokiwaza.

“Hilo tu! Halina shida. Nitafanya kazi yako kwa sababu nina kila kitu hapa.” Agent aliongea kwa furaha.

“Kazi ianze mara moja. Zima na simu yako. Nataka haya yafanyike ndani ya siku hizi na yawe yamekamilika.” Idris aliongea na Agent Zero akakubali kufanya alichoambiwa.

Cha kwanza alichukua damu za Merice na Idris, kisha akawaruhusu watoke ndani ya maabara ile ili afanye kazi yake bila bugudha. Wakatoka mle ndani na cha kushangaza, badala ya kutokea chumba kingine, wakajikuta kwenye sebule ambalo waliingia mwanzo na kujadiliana mambo kadhaa na lile kabati waliliona lakini bila kitabu kilichoandikwa IDRIS IRIS.

“Dokta hakuwa mtu wa mchezo mchezo.” Idris akaongea huku ametabasamu.

“Ni baba yangu.” Merice naye akajibu akilazimisha tabasamu limtokee. Limasi akaamua umvute Idris na kumuacha Merice peke yake. Wivu ulimuingia ghafla. Wakaenda chumba kingine na kuanza kuongea mambo kadha wa kadha na wakati huo, Merice alitoka nje na kuanza kuikagua nyumba ile kuona kama kutakuwa na jipya lolote kwa sababu baba yake, alikuwa ni mtaalamu si kitoto. Yawezekana akagundua lolote lakini haikuwa rahisi kwake kung’amua hilo.

Usiku uliingia. Agent Zero aliweza kutoka na kupata chakula na kuwapa matokeo kidogo huku akiwaahidi kuwa atafanikiwa japo kazi yake ilikuwa ngumu sana.

Idris na Limasi, walienda kulala kwa pamoja huku Merice akilala chumba kingine na wakati huo, Agent Zero, Kijana ambaye yupo ladhi kukesha kwa sababu ya Sayansi, aliingia maabara na kuendelea kufanya kazi ambayo kapewa.

*****

Ndani ya siku tatu, Rais hakupata mawasiliano yoyote toka kwa kijana wake. Wasiwasi ulimuingia na wakati huohuo, CIA na Uzo, walikuwa wanamuulizia kuhusu wanajeshi wao. Rais alikuwa hana jibu la uhakika na wakati huo alikuwa makini sana kutowapa taarifa kuwa kijana wake kapotea kwani wakina Uzo wangekuja na kufanya vurugu.

“Huyu kijana wamemteka nini? Maana hawa wanajeshi siwaelewi hata kidogo. Simu yake haipatikani na wala haoekani kwenye satelaiti yetu. Nini kimempata?.” Akajiuliza Rais huku akikaa kwenye kiti cha ofisini kwake. Mawazo tele yakamjaa. Amekwishatuma wapelelezi kibao waende Moshi kumtafuta lakini hamna aliyemuona yeye na hata wale wanajeshi wa C.O.D.EX. “Asije akanifanya nikamuita The Last.” Akajionya.

Wakati Rais anawaza hayo, Agent Zero alikuwa amejawa na furaha baada ya kukamilisha kazi aliyoombwa na Idris. Aliwaita kwenye maabara na wote walifika akiwemo Limasi. Wote kwa pamoja walishangaa kukuta ambacho Agent Zero kakifanya.

Waliweza kuziona nguo zikiwa kwenye chumba cha kioo na nguo hizo zilikuwa ni za kike na za kiume. Pia mezani kulikuwa na bunduki pamoja na risasi zilizokuwa na kimiminika ndani yake. Waliona mabadiliko makubwa ndani ya maabara ile. Walikuwa hawaamini kama kazi ile kaifanya mtu mmoja.

“Sasa wazee, hizi ni silaha zenu.” Akawaonesha bunduki mbili pamoja na risasi zake. Vilikuwa mezani. “Risasi hii moja, inaweza kukuua wewe, na kukuharibu kabisa. Hunyanyuki. Ni mchanganyiko wa kemikali zilizowatengeneza na kemikali zingine ambazo ukizichanganya kwa pamoja, unatengeneza kifo. Yaani kemikali zenu, zikichanganywa na kemikali fulani, zinatengeneza mlipuko mkubwa sana. Ndicho nilichoweka humo.” Akaeleza kwa kifupi na kuchukua risasi moja ambayo ilikuwa inaonekana kama inamaji ndani yake. Akaitikisa na maji yale yakabadilika na kuwa mekundu. “Hapa ukimtungua mwanajeshi mmoja, akinyanyuka, njoo uchukue nyumba yako.” Akaongea na kuitikisa tena, ikawa ya blue. “Hapa anaweza kunyanyuka, lakini anakuwa hana uwezo wa CODEX tena. Itategemea umempiga wapi. Hayo ndio matumizi yake.” Akamaliza kwenye upande wa risasi. Akabonyeza kiparaza cha kompyuta iliyokuwepo mezani, na meza ile ikafunguka mitoto (droo) yake ambayo ilikuwa kumi. Kila mtoto wa meza ile, ulikuwa unaboksi la risasi nyingi sana pamoja na mabomu ambayo nayo alielezea madhara yake kwa watu wanaoenda kupambana nao.

Pia kulikuwa na visu na silaha nyingi za kivita ambazo wakina Idris, walikubali kuwa kazi yao itaenda kuwa rahisi.

“Hapa ndipo napopataka sasa.” Akaongea Agent huku anaelekea kwenye kabati moja la kioo ambalo lilikuwa na nguo alizoziunda. “Hizi ni nguo ziwezazo kuwasaidia sana katika mapambano yenu. Haziingizi moto, risasi wala haudhuriki kwa njia yoyote labda kwa hizo risasi ambapo napo, ni lazima mpigaji wa risasi akumendee.” Akaelezea kidogo na kubonyeza vitufe vya kompyuta iliyombele ya nguo mojawapo. Suti ile ikasogea mbele.

“Hii inauwezo wa kuhisi hatari inayokufuata na kuizuia. Yaani kama kuna risasi, basi yenyewe inageuka kuwa chuma na kuzia risasi hiyo. Pia kama kuna moto unakuwakia, inaweza kuuizima bila shida. Inaulinzi madhubuti na inaweza kugeuka parachuti kwa wale wa angani. Yaani unaweza kuifanya itokee mabawa na hiyo kukusaidia kushuka hadi sehemu unayoitaka. Kwa kifupi, inavitu vingi ambavyo vinaongozwa na hii saa.”Akawaonesha saa ambayo ilikuwa kwenye ya suti ile rangi nyeusi.” Si Idris wala Merice ambao hawakufurahia uwezo wa Agent Zero.

“Baada ya hili, naomba niwashe simu ili kumtaarifu Rais wangu uzima wangu.” Akaongea Agent na kuwasha simu na kuanza kuongea na Rais ambaye alishukuru kwa kijana wake kuwa salama na wakati huo, alimpa maelekezo kuwa anatakiwa kuiandaaa ndege maalumu kwa ajili ya kuingia Marekani na si ndege ya abiria. Hilo likapita na Rais akamwambia Jet P112 itakuja kuwabeba hapo Moshi na kuwapeleka hadi Dar es Salaam kabla ya Limasi kupelekwa Arusha kwa dada yake. Wote wakakubali.





“Hapa ndipo napopataka sasa.” Akaongea Agent huku anaelekea kwenye kabati moja la kioo ambalo lilikuwa na nguo alizoziunda. “Hizi ni nguo ziwezazo kuwasaidia sana katika mapambano yenu. Haziingizi moto, risasi wala haudhuriki kwa njia yoyote labda kwa hizo risasi ambapo napo, ni lazima mpigaji wa risasi akumendee.” Akaelezea kidogo na kubonyeza vitufe vya kompyuta iliyombele ya nguo mojawapo. Suti ile ikasogea mbele. “Hii inauwezo wa kuhisi hatari inayokufuata na kuizuia. Yaani kama kuna risasi, basi yenyewe inageuka kuwa chuma na kuzia risasi hiyo. Pia kama kuna moto unakuwakia, inaweza kuuizima bila shida. Inaulinzi madhubuti na inaweza kugeuka parachuti kwa wale wa angani. Yaani unaweza kuifanya itokee mabawa na hiyo kukusaidia kushuka hadi sehemu unayoitaka. Kwa kifupi, inavitu vingi ambavyo vinaongozwa na hii saa.”Akawaonesha saa ambayo ilikuwa kwenye ya suti ile rangi nyeusi.” Si Idris wala Merice ambao hawakufurahia uwezo wa Agent Zero.

“Baada ya hili, naomba niwashe simu ili kumtaarifu Rais wangu uzima wangu.” Akaongea Agent na kuwasha simu na kuanza kuongea na Rais ambaye alishukuru kwa kijana wake kuwa salama na wakati huo, alimpa maelekezo kuwa anatakiwa kuiandaaa ndege maalumu kwa ajili ya kuingia Marekani na si ndege ya abiria. Hilo likapita na Rais akamwambia Jet P112 itakuja kuwabeba hapo Moshi na kuwapeleka hadi Dar es Salaam kabla ya Limasi kupelekwa Arusha kwa dada yake. Wote wakakubali.

ENDELEA.

Makubaliano hayo, yalikuwa ndio mwanzo mpya wa Idris kuanza kutaka kujua nguvu zake siku hiyohiyo kabla ya kuanza safari hiyo. Aliingia kwenye jokofu la kwanza, na Agent kupitia maelezo ya Dokta Ice, aliweza kufanya kazi mwanana ya kumjaza nguvu ambazo Dokta Ice alisema kuwa zipo. Ndani ya jokofu, Idris aliweza kuona picha nyingi wakati anajazwa nguvu hizo muhimu kwenye mapambano yake.

Kumbukumbu za akiwa mtoto na picha ya Uzo, iliendelea kuandama. Na kwa kuwa nguvu zile zilikuwa zinaingilia kwenye mishipa ambayo kemikali za C.O.D.EX ndimo zilipandikizwa, Idris alijikuta akiumia sana lakini hakuwa na uwezo wa kutoka hadi kompyuta ya jokofu lile ilipoandika ‘finish 100%’.

Hamna aliyejua maumivu yaliyompata Idris ndani ya jokofu lile kwa sababu kelele zake zilikuwa hazitoki nje. Na yeye hakutaka kuonesha kuwa ameumia, akaingia jokofu lingine na Agent Zero alifanya yaleyale. Hali ikawa ileile kwa Idris hadi alipoingia jokofu la tatu na baadae la mwisho.

Humo kulikuwa na ubaridi wa raha. Misuli yake ilipoozwa na kumpa amani tele. Alitamani akae humo daima. Alifungua macho yake na kutabasamu kwa sababu ya raha azipatazo humo. Akiwa katika tabasamu, kioo cha jokofu hilo kikafunguka runinga ndogo na kuanza kuonesha nguvu ambazo anazo Idris baada ya kuingia kwenye majokofu yote manne. Aliweza kushuhudia uwezo wake na akili yake ikaanza kunakili haraka sana yale ambayo anaweza kuyafanya. Yalikuwa mambo mengi ya kufurahisha na kumpa ujasiri na alitokea kufurahia sana uwezo ambao kaumbwa nao kwa kutumia video ile.

“Download Complete.” Sauti ilisikika na jokofu la mwisho likafunguka na kutoa moshi wa baridi kisha Idris alitokeza akiwa na mwili mpya, mwili ambao safari hii ulijaa kidogo na kuwa mzuri zaidi kuliko wa mwanzo.

“Nipo tayari sasa. Nipo tayari kupambana hata na wewe Agent Zero.” Idris aliongea kwa utulivu akiwa kavaa ‘boxer’ pekee. Agent akatabasamu kwa kauli Ile na kwa kasi ya ajabu na ya kushtukiza, alichomoa visu vidogo viwili na kuvirusha kwa pamoja. Idris akawa anaviona kwa uzuri na kwa jicho la tatu zaidi, yaani hadi kasi ya visu vile alivisoma kupitia akili yake. Vilivyofika karibu yake, Idris akakinga mkono wake na ile sehemu ambapo palitakiwa kuchomwa na visu vile, pakawa chuma, visu vikadunda na kudondoka chini. Akamtazama Agent na wakati huo, ikabidi Merice na Limasi watoke nje ya maabara ili wawaache wababe wale wapambane.

Agent akatoka nyuma ya meza ya kompyuta na kitendo kingine cha kushtukiza, akakifanya yule kijana. Safari hii alirusha visu vitatu. Na wakati visu vile vinamuelekea Idris, vikajitengua na kuzaa visu vingine vitatu na kumfanya hesabu za Idris kuvurugika kwa sababu yeye aliona vitatu. Akajaribu kuvikwepa kwa sarakasi mwanana, lakini kimoja kiliweza kumpata mkononi.

“Hivyo visu pia ni silaha hatari sana katika kuwaua wanajeshi. Hapo kimekuchoma, nikibonyeza saa yangu hapa, vinatoa kemikali ambayo inaweza kukudhuru. Endelea kufanya mazoezi kuhusu kuzuia na suti hii, ni muhimu kwako kwa sababu yakupasa kwenda kupambana sasa.” Agent aliongea na wakati huo Idris alivimba kidogo na kisu kile kikachomoka bila kuguswa. Jeraha lake likajifunga.

“Hapana, hapo nimetumia silaha ya kwanza kati ya kumi na tano nilizonazo. Nataka kukuonesha kazi Agent.” Aliongea Idris.

“Karibu kwenye mpambano.” Agent Zero bila uoga aliongea na kitendo bila kupoteza muda, alichomoka kwa kasi kwenda kwa Idris na wakati huo alikuwa anarusha visu vyake na kuvitengua tengua na kuwa vingi lakini safari hii Idris aliviona vema yeye akawa anamfuta Agent huku anarusha vichuma ambavyo viligongwa visu vile na kuvipotezea lengo la kumdhuru. Wakakutana katikati na Agent akawa wa kwanza kurusha ngumi lakini Idris aliidaka na kumrusha juu Agent aliyebamiza vibaya mgongo wake.

Idris hakuishia hapo, akatumia silaha nyingine ya mwili wake. Akapotea ghafla, na alipoibuka, alikuwa mbele ya Agent. Akamnyanyua kwa mkono mmoja na kumtupa tena ukutani. Agent akawa anagaa gaa kwa karaha na maumivu lakini hilo halikumshutua sana Idris ambaye alidhamiria kumfundisha adabu Agent Zero. Akamkamata shingo kwa mkono mmoja na kunmyanyua juu, Agent akawa kama anaelea angani. Na mara akajipapasa kiunoni na kuchomoa bastola kuanza kuifyatua kwenye mkono wa Idris. Haraka Idris akamuacha na mkono ule ukabadilika na kuwa na rangi nyekundu na kisha ukaanza kuwaka moto. Moto ulipozima, hali yake ikarudi vilevile.

Lakini wakati anakaa sawa, masikioni mwake akaanza kusikia sauti kama ya nzi wa chooni. Kwa haraka, akageuza mwili wake na kuwa chuma. Pini za Agent Zero zikashika shingo yake na ghafla vikalipuka na kumrudisha Idris katika hali yake huku akiwa katika maumivu makali.

“Nimeviongezea vikorombwezo aisee. Bado hii suti unaihitaji sana tu.” Agent aliongea huku akijaribu kuinuka baada ya kupata kichapo kizito toka kwa Idris.

“Hapana. Wewe huwezi kunishinda kirahisi namna hii. Ngoja nikufundishe adabu sasa.” Idris aliongea na kichwani mwake, akiruhusu kutumia chipu mbili, ya kupigana na kuzuia. Hapo ndipo Agent aligundua kitu kingine cha hatari toka kwa Idris.

Hakupewa nafasi ya kurusha ngumi wala kurusha silaha zake. Kipigo alichokipokea kilikuwa ni cha mbwa mwizi. Idris alikuwa anapotea, na kurudi akiwa karibu na Agent na aliweza kumsoma Agent haraka kwa kitendo ambacho anataka kukifanya. Kuna muda alimsoma anataka kuchomoa bastola, alimuwahi kumkamata mkono na kisha kuuzungusha kama anataka kuuvunja. Alimzidi vitu vingi vya kijanja.

Agent ni wazi alikuwa kazidiwa lakini naye hakutaka kukubali kirahisi kama kawaida ya Watanzania wengi, huwa hawakubali kushindwa hadi wapoteze kiungo kimoja au kufa kabisa. Mikono ya Agent ikatokeza ‘groves’ fulani ambazo ziliacha vidole nje. Mara nyingi huvaa wanamieleka au wapigana judo na karate. Tendo hilo alilifanya alipobonyeza saa yake. Na grovu zile zikaanza kumsaidia katika kurusha ngumi zenye nguvu kwa sababu nazo zilitengenezwa Kisayansi.

Ngumi za nguvu alizirusha na kuna muda alitoa hadi moto kwenye grovu hizo lakini kwa Idris hazikuwa kitu. Idris akawa anawaka na kuzima, yaani aliweza kupotea na kutokea ghafla mbele ya Agent ambaye naye kwa kasi hiyohiyo aliweza kuchomoka kwa kutumia sayansi yake aliyoibuni.

Idris akapotea tena na alipoibuka, akamkamta Agent shingo yake na kumrusha kwenye ukuta. Agent akagugumia kwa maumivu na wakati huo Idris alipaa juu na kukita kwenye tumbo lake na kisha akaanza kumtwanga makonde ya nguvu usoni. Uso wa Agent haukuwa wake tena kwa sababu kuna kinyago cha uso ‘Mask’ kilijifunga usoni kwake wakati Idris anafanya makeke yake. Kila Agent akijitahidi kumtoa Idris mwilini mwake, hakuweza na makonde yaliendelea kumuandama kwa kasi.

Ni simu ya Agent ndio ilimfanya Idris amuache Agent ambaye alipoachwa alianza kugaa gaa kwa maumivu makali sana.

“Mbwa wewe unataka kuniua?” Akauliza kwa maumivu makali Agent Zero.

“Yule wa kule barabarani si huyu tena. Nitakuua mimi. Pokea simu yako.” Agent akafunguka kinyago chake na kwenda iliposimu yake.

“Nyie mnakuja saa ngapi huku?” Rais alifoka baada ya Agent kupokea simu.

“Tunasubiri ndege mkuu. Hatuioni.” Ikabidi aongee kana kwamba yupo tayari. Rais akakata simu. Agent akavua shati lake na kubaki kavaa suti kama ile aliyowatengenezea wakina Idris. “Bila hii, ningekuwa marehemu leo. Imenisaidia sana. Nashauri nanyi kuwa nazo.” Alimwambia Idris akimuonesha ile suti yake. Idris akacheka na kutoamini ujanja wa Agent yule. Yeye alidhani ni ukomavu wake, na kumbe alivaa kitu cha kumsaidia.

Agent akiwa anachechemea huku kakamata kiuno chake, alianza kutoka ndani ya maabara ile huku maumivu yakiandama mwili wake kwa asilimia kubwa.

“Kusanyeni silaha zenu. Mimi za kwangu ninazo.” Alipofika mlangoni alimwambia hayo Idris na kisha akafungua mlango na kutoka.

****

Jet P112 ilifika walipokuwepo wakina Idris na kuwachukua ambapo baada ya kuwachukua ilienda hadi makao makuu ya FISSA. Huko walielekezwa watakapoachwa ambapo palikuwa porini nao iliwapasa waende hadi mjini kuwatafuta wanajeshi wenzao.

Limasi aliweza kuagana na Idris na kuachwa mikononi mwa maafisa usalama wa FISSA.

“Sawa mkuu, ahsante kwa msaada wako.” Idris alimshukuru mkuu wa FISSA,

“Niite Malocha Malingumu. Huna haja ya kuniita mkuu.” Malocha alimwambia Idris na Idris alitabasamu.

“Huyo Agent Zero yeye alikataa kujitambulisha.” Akamnyooshea kidole Agent Zero ambaye alikuwa nyuma ya Malocha.

“Ahaa! Huyu ni Agent Zero. Ni The Under Cover Agent wetu. Huwa tunamuita kwa kazi maalumu kama hizi. Yeye anaitwa Prince Mubarak au Mubah. Ni kijana wetu lakini anamkuu wake ambaye yeye ni chaguo la pili kama huyu atashindwa. Huyo naye ni The Under Cover Agent na ndio jicho letu hapa. Kama mlimshindwa huyu, basi yule sidhani kama mngemuweza.” Aliongea Malocha huku katabasamu.

“Huyu hajatushinda. Muulize.” Akaongea Idris huku katabasamu. “Na huyo Under Cover mwingine yupo wapi?” Akauliza.

“Yupo. Lakini hatujui yupo wapi. Huwa hatakagi kujulikana alipo. Yeye huwa na kazi maalumu tu. Kama huyu lakini huyu ukija humu utamkuta.” Akajibu Malocha.

“Anaitwa nani huyo mwingine?” Akauliza Idris.

“Huyo anajiita Man’Sai. Au The Last, yaani yeye ni Agent asiye na namba na ndio maana yupo huru na hata hapa hayupo.” Akajibu Malocha na mara mlango wa ofisi ulifunguliwa na aliingia mwanamama mmoja wa makamo na mwenye kupendeza.

“Samahani jamani. Nimewakatiza.” Aliongea yule mwanamama na kisha aliinama na kumnong’oneza jambo Malocha. Malocha akatikisa kichwa kukubali alichoambiwa sikioni. Mwanamama yule akasimama wima na kuomba tena msamaha kwa kuwaingilia,

“Huyu anaitwa Lisa Lindsay. Pia ni askari wetu. Mume wake ndiye The UnderCover Man’Sai. Naye ni muhimu sana kwetu.Alikuwepo siku ile Agent Zero alipokukamata. Yeye alikuwa mdunguaji na alimpiga mwanajeshi wenu mmoja risasi. Msimuulize mume wake yupo wapi tafadhali.” Malocha akamtambulisha Lisa ambaye utamuona kwenye riwaya kali ya Jina na Duka la Roho ambazo kaziandika mwandishi wa watu, Frank Masai.

Idris. Limasi na Merice wakashukuru kuwafahamu baadhi ya wapelelezi wa shirika la kijasusi la siri la nchini Tanzania, FISSA (Federal Interigency Secret Services Agency).




“Samahani jamani. Nimewakatiza.” Aliongea yule mwanamama na kisha aliinama na kumnong’oneza jambo Malocha. Malocha akatikisa kichwa kukubali alichoambiwa sikioni. Mwanamama yule akasimama wima na kuomba tena msamaha kwa kuwaingilia,

“Huyu anaitwa Lisa Lindsay. Pia ni askari wetu. Mume wake ndiye The UnderCover Man’Sai. Naye ni muhimu sana kwetu. Alikuwepo siku ile Agent Zero alipokukamata. Yeye alikuwa mdunguaji na alimpiga mwanajeshi wenu mmoja risasi. Msimuulize mume wake yupo wapi tafadhali.” Malocha akamtambulisha Lisa ambaye utamuona kwenye riwaya kali ya Jina na Duka la Roho ambazo kaziandika mwandishi wa watu, Frank Masai.

Idris. Limasi na Merice wakashukuru kuwafahamu baadhi ya wapelelezi wa shirika la kijasusi la siri la nchini Tanzania, FISSA (Federal Interigency Secret Services Agency).

ENDELEA.

Wakatembezwa ndani ya Shirika lile la kijasusi na kutambulishwa maeneo mbalimbali na mwisho wa yote, ilikuwa ni kwa wao kuondoka Tanzania na kurudi Marekani huku Idris akimuahidi mke wake, Limasi kufanyia kazi vitu alivyompa na zaidi, akimuahidi kuwa atarudi Tanzania kumchukua ili wakaishi wote huko Marekani.

Limasi alikuwa ni mtu wa huzuni pale aliposhuhudia mume wake akipanda ndege aina ya Jet P112 ambayo imeelezewa vizuri sana uwezo wake kwenye riwaya kabambe ya Duka la Roho. Ila kwa kifupi, Jet P112 ni ndege mojawapo yenye kasi kubwa sana. Ni ndege inayoweza kuhama nchi hadi hadi ndani ya dakika kadhaa. Mwendo wake ni sawa na ndege zinazokwenda kwenye sayari zingine. Hujichochea na baadae huchomoka kwa kasi na kupotea. Huja kuonekana baada ya kufika eneo la tukio.

Naam. Merice na Idris walikwea ndani ya ndege hiyo wakiwa na silaha zao ambazo zIlitengenezwa na mtundu Prince Mubarak, au Agent Zero. Wakaaga ardhi ya Afrika rasmi baada ya Jet P112 kuondoka ndani ya FISSA.

“Watakuwa salama tu! Usihofie sana.” Aliongea Malocha huku akiondoka na kumuacha Limasi bado kasimama mbele ya kioo ambacho kilikuwa kinazuia moshi na kelele za Jet P112 pale inapoondoka.

“Nakusubiri Id. Nenda katafute haki zako.” Limasi aliongea peke yake na kuondoka eneo lile tayari kwa kupanga safari ya kurudi kwao.

****

CALIFORNIA, MAREKANI.

Kwa mbali anaonekana Idris na Merice wakishuka toka angani huku wamevaa suti ambazo walitengenezewa na Agent Zero. Kwenye makwapa ya suti ile, kuliwa na kitambaa ambacho kilizuia upepo na kuwafanya waweze kuhimili kushuka chini bila kudhurika. Katika mashamba makubwa ya mahindi yaliyopo hapo California, Idris na Merice wanaweza kutua salama na kisha wanaangalia huku na huko na kuanza kuvaa mavazi ya kiraia juu ya zile suti zilizotengenezwa na Agent.

Wanaweka vema silaha zao zilizokuwepo kwenye mabegi na kisha wanaanza kukimbia katikati ya mashamba yale ambapo kulikuwa na mahindi marefu na yamekauka. Yalikuwa ni mashamba makubwa na walitumia muda mwingi kukimbia bila kutokea sehemu yenye uwazi.

Ndani ya lisaa limoja, ndipo walitokea sehemu moja na kuona gari la kizamani likiwa limepakia mabua ya mahindi. Gari hilo aina ya Pageuot lilikuwa imesimama peke yake na injini yake kuunguruma. Idris na Merice walitazama huku na huko kuona kama kuna mmiliki, lakini hawakuona lolote. Wakaamua kulivamia na kuiondoa eneo lile kwa kasi huku wakiacha mabua yakidondoka huku na kule.

Muda kidogo, waliweza kuingia barabara moja ya vumbi na kwa kasi ileile, waliikanyaga barabara ile na kusababisha vumbi kubwa sana. Idris akiwa kashikilia usukani, alikuwa anaongeza mwendo kila alipopata wasaha wa kufanya hivyo, hilo ndilo likawa nyenzo kubwa ya yeye kufika anapotakambapo ilikuwa ni barabara ya rami, na kwa kasi ileile waliingia na kuanza kuisakama rami ile kwa mwendo wa kushangaza.

Katika masaa mawili, walikuwa wameweza kukata kilometa nyingi sana huku lengo likiwa kufika Los Angeles kabla ya usiku, na baadaye kupata usafiri utakaowapeleka hadi New York, yalipokuwa makao makuu ya C.O.D.EX. Walisimama vituo kadhaa na kujaza mafuta na kisha kwa mwendo uleule, waliweza kuondoka.

Saa kumi na moja ya jioni, ndipo walipofanya kosa dogo la kupita kwa kasi sehemu ambayo kuna askari wa barabarani.

“Code One Six, One Six.” Askari mmoja wa kikosi cha barabarani aliongea kwenye simu ya upepo iliyokuwepo kwenye gari lake ili kuwasiliana na wenzake wa mbele waweze kulisimamisha gari hilo lililompita kwa kasi ya mshale. Wenzake wakakubali na kwa haraka, na yeye alikwea ndani ya gari yake ya kazi na kuanza kuifukuzia ile ya Idris na Merice huku zile kelele za kipolisi, nazo zikiongezwa.

“Idris tunafukuzwa na polisi.” Merice aliongea baada ya kusikia ving’ora vya gari la polisi kwa mbali vikija.

“Unajua la kufanya. Hawa hawawezi kutusimamisha lengo letu kwa muda kama huu.” Idris aliweka msimamo wake na Merice alitoa bunduki moja kubwa kiasi na kupachika mabomu mawili na kuikoki bunduki ile tayari kwa mashambulizi.

Gari la polisi lilizidi kusogelea gari alilokuwa anaendesha Idris ambalo sasa lilikuwa halina yale mabua ya mahindi kwa sababu yalimwagika kwa ule mtikisiko wa kurukaruka kwa gari.

Polisi yule wa Los Angeles akiwa kabakiza hatua chache kulifikia gari la akina Idris, aliweza kumshuhudia Merice akiibuka toka kwenye kioo cha gari lao akiwa na bunduki na kisha akafyatua bomu moja lilienda kunasa kwenye bonet ya gari la polisi yule.

“Shit. Magnetic Boom.” Aliongea yule askari huku akili yake ikihama katika kuwafukuzia wakina Idris na kuliangalia lile bomu ambalo lililipuka pale kwenye boneti na kuifanya gari ile ipae juu na kutua chini kama mzigo. Kisha injini yake ilianza kuungua na wakati huo polisi aliweza kutoka na kuanza kukimbia akiacha gari yake ikilipuka na kusababisha mtafaruku mkubwa eneo lile.

“Safi. Hapo nadhani ujumbe utawafikia wahusika na wataanza kutufuatilia.” Idris aliongea na wakati huo aliangalia pembeni baada ya kuona kituo cha mafuta na watu kadhaa wakikimbilia kule ambapo mlipuko umetokea. Akapiga kona ya ghafla na kwenda hadi kituo kile kisha kwa haraka akashuka pamoja na begi lake na silaha, huku Merice naye akifanya vivyo hivyo.

Waliona Range Rover Sport nyeusi ikiwa imesimama hapo na mpira wa kujazia mafuta ukiwa bado kwenye tundu la kuwekea mafuta. Idris akafungua gari lile na kutupia begi lake la silaha na kisha kujaza mafuta ya kutosha. Ilionekana wazi muhusika wa gari lile alikuwa amekimbilia kule kwenye mlipuko au amekimbia mbali kutoka eneo lile kwa sababu ya vitisho vya kigaidi vilivyokuwa vinaendelea nchini Marekani.

Baada ya kufanikiwa kujaza mafuta, Idris na Merice walikwea ndani ya Range ile na kuitoa kwa kasi yao ya mwanzo na wakati huo muuza mafuta wa eneo lile akianza kulalamika kuwa wanaondoka bila kufanya malipo. Alichofanya muuzaji yule ni kunakiri namba za gari haraka na kupiga simu polisi, kisha akatoa taarifa. Naye alikuwa anashangaa mlipuko ule hivyo hakuona wakati wakina Idris wanafanya yao.

“Umesema wapo wangapi?” Akauliza Askari wa usalama baada ya simu ya yule mhudumu.

“Sijajua, ila nahisi wawili. Tena naona gari lao wameliacha hapa na wameiba hili la Range.” Yule bwana aliongea huku akiliangalia lile gari walilokuwa wameliacha wakina Idris.

“Gari aina gani na namba zake ni zipi?” Akaulizwa tena.

“Ni Peugeot ……” Akajibu na kutaja namba za usajili wa gari lile na plate namba zake. “Old Model” Akaongeza.

“Okay. Sasa kuwa makini na usiguse gari hilo. Hao ndio wamesababisha huo mlipuko na taarifa zao tunazo kwani askari aliyelipuliwa gari lake, katuambia. Hivyo kaa mbali na gari hilo, hao ni wavamizi hatari na wanasilaha za hatari sana.” Akaonya mwanausalama.

Muhudumu wa sheli ile ambayo iliunganika na supa maketi moja ndogo, akasogea mbali kabisa na gari ile huku akiwasubiri wanausalama waje.

Rage Rover Sport, ilikuwa imekamata barabara ya kuelekea mjini Los Angeles na ilikuwa inayapita magari kadhaa makubwa kwa madogo kwa kasi ya ajabu. Kasi ambayo iliwashangaza madereva wengine.

Wakiwa katika mwendo huo, helikopta mbili zilijitokeza angani na kuanza kutangaza kwa kipaza sauti kuwa gari ile isimame yenyewe kabla ya polisi hawajaivamia. Idris akatabasamu na kwa makusudi alimwambia Merice achomoe uso wake kwenye kioo cha dirisha ambapo kwa wakati huo lilikuwa limefungwa kwa vioo vyeusi.

Merice akafungua kioo kimoja na alijua nia na sababu ya Idris kufanya hivyo. Akaangalia helikopta moja kwa dakika moja na kisha akarudisha uso wake ndani. Polisi waliokuwepo kwenye ile helikopta, waliweza kuinasa sura yake kwa haraka na kuiingiza kwenye kompyuta yao tayari kutaka kujua wale ni wakina nani lakini kulikuwa hamna taarifa zozote kuhusu Merice, hivyo picha zile zilitumwa hadi makao makuu ya CIA. Huko zikatazamwa kwa muda na baadaye kutumwa hadi makao makuu ya C.O.D.EX. Macho yakamtoka Uzo baada ya kushuhudia uso wa Merice.

“Wajinga wapo mjini.” Uzo aliongea huku akibonyeza kompyuta yake na kumuangalia vema Merice. “Karibuni nyumbani wanajeshi wangu.”Akaongeza Uzo na kisha akatoka eneo lile na kwenda hadi maabara ambapo aliamuru wafanye kazi yao.

“Simeria.” Akamuita kimada wake. Naye yule mwanamama ambaye alikuwa mzazi halisi wa Merice, aligeuka na kumuangalia mwanaume wake kama ishara ya kuitikia wito. “Merice amefika lakini hayupo upande wetu.” Akampa taarifa lakini mwanamama yule hakuonekana kushtuka.

“Kwa hiyo nini kinachofuata?” Akauliza.

“Unajua kinachofuata. Ni muda wa kuona uwezo wa wanajeshi wako.” Uzo akamwambia na mwanamama yule alitabasamu na kuelekea hadi ilipo maabara kuu. Akaanza kubofya viparaza vya kompyuta yake, nayo ikakubali kubonyezeka. Majokofu yapatayo kumi na tano yalianza kuchemka maji yake na baadae ilisikika sauti ya kike ikisema ‘upload complete’ ikimaanisha kuna vitu vilikuwa vinaingizwa kwenye miili ya wanajeshi waliokuwepo kwenye yale majokofu kukamilika.

Baada ya hapo, yakafunguliwa na wanajeshi imara wakajitokeza wakiwa hawana vazi lolote miilini mwao na sura zao zilikuwa za kazi tu. Simeria akawataka waende chumba fulani ambapo huko walikuta mavazi na silaha zao, wakavaa kwa pamoja haraka haraka na kumaliza sawa sawa na kisha wakapanga mstari.

Uzo akatokea na kuwapa majukumu ya kwenda kufanya huku akiwataka kuwa makini kwa sababu ya watu wanaoenda kupambana nao.

“Kutakuwa hamna kiongozi, ni nyie wenyewe ndio mnatakiwa cha kufanya. Sisi tutakuwa tunaongea nanyi kwa kutumia hizo simu za sikioni. Sawa?” Akauliza na wanajeshi wale wakajibu kiukakamavu kuwa wameelewa.

Wakaruhusiwa kutoka ndani ya chumba kile na walitoka huku wanakimbia hadi nje na kisha wakapanda helikopta moja kubwa ya kivita ambayo nayo si haba kwa kasi yake kwani ndani ya dakika kadhaa, ilikuwa ipo barabara kuu.

Gari alilokuwa anaendesha Idris, lilikuwa linakuja kwa kasi na mbele yao kulikuwa na magari mengi ya polisi yaliyozuia barabara huku polisi hao wakiwa wamelenga kule gari ya Idris inapotokea kwa kutumia bastola zao ndogo.

Idris akiwa kadhamiria kwenda kukatisha katikati ya magari ya polisi wale, kwa kutumia macho yake ambayo yalikuwa yanadarubini ya kujitegemea, darubini ambayo ilikuwa inaweza kuona hadi kasi ya silaha, safari hii aliweza kuona wanajeshi wa C.O.D.EX wakiwa wanashuka kwa kutumia kamba nyuma ya polisi wale wa Los Angeles.

“C.O.D.EX advanced wameagizwa.” Alimwambia Merice ambaye alisogea karibu na kuweza kushuhudia wale wanajeshi wakianza kusogea mbele lakini Idris hakupunguiza mwendo.

Zikiwa zimebaki mita zipatazo mia mbili ili gari la Idris ifike kwenye gari za polisi, wanajeshi wa C.O.D.EX walisogea mbele ya gari zile za polisi wakiwa na mitutu yao na kuanza kushambulia kwa risasi nyingi gari la Idris na Merice.



Idris akiwa kadhamiria kwenda kukatisha katikati ya magari ya polisi wale, kwa kutumia macho yake ambayo yalikuwa yanadarubini ya kujitegemea, darubini ambayo ilikuwa inaweza kuona hadi kasi ya silaha, safari hii aliweza kuona wanajeshi wa C.O.D.EX wakiwa wanashuka kwa kutimia kamba nyuma ya polisi wale wa Los Angeles.

“C.O.D.EX advanced wameagizwa.” Alimwambia Merice ambaye alisogea karibu na kuweza kushuhudia wale wanajeshi wakianza kusogea mbele lakini Idris hakupunguiza mwendo. Zikiwa zimebaki mita zipatazo mia mbili ili gari ya Idris ifike kwenye gari za polisi, wanajeshi wa C.O.D.EX walisogea mbele ya gari zile za polisi wakiwa na mitutu yao na kuanza kushambulia kwa risasi nyingi gari la Idris na Merice.

ENDELEA

Gari la Idris hadi linafika pale walipo wanajeshi wa C.O.D.EX, lilikuwa limechakaa kwa risasi na kioo cha mbele kupasuka vibaya sana. Endapo kungekuwa na binadamu wa kawaida, basi ni damu pekee ndiyo ingekuwa imetapakaa barabara nzima.

Gari la Idris likasimama mbele ya wale wanajeshi likiwa hatua kama kumi toka pale walipo. Polisi walikuwa hawana la kufanya na walikuwa hawaelewi ni nini kinaendelea kwani ni tukio la haraka sana limetokea.

“Nendeni watatu mkaangalie watuhumiwa wetu.” Sauti ilisikika sikioni mwa wanajeshi wale na wao wakaitii na kusogea haraka pale gari liliposimama. Idris alikuwa katanua mikono yake kama aliyekufa na wakati huo Merice naye alikuwa katulia tuli huku kichwa chake amekilaza nyuma ya kiti alichokalia.

Macho ya wale Wanajeshi yakaanza kuwaskani Idris na Merice bila kuwagusa ili kuona kama wapo hai au ni wafu.

“Wanaonesha hawana mapigo ya moyo hawa.” Mmoja wa wanajeshi wale waliokwenda kuwatambua Idris na Merice, aliongea kupitia kipaza kilichoungana na kisikilizo cha sikioni.

“Angalieni vizuri. Sii rahisi hivyo.” Uzo akaongea na yule mwanajeshi akaanza kuskani tena kuanzia kiunoni kwa Idris, akaja tumboni, akafika kifuani ambapo ndipo penye moyo. Bado kulikuwa hamna mapigo ya moyo. Ikabidi apande hadi shingoni na baadae akatua usoni ambapo alikutana na kitu asichokiamini katika macho yake.

****

Nchini Tanzania, mwanadada Limasi, anafanikiwa kurudishwa hadi kwa dada yake Timasi ambaye alipomuona tu! Alimkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu huku akimpa pole kwa yote yaliyomkumbuka.

“Ahsante Dada, nipo salama mdogo wako.” Limasi aliongea wakati kapewa pole na Dada yake, Timasi.

“Karibu tena nyumbani dada yangu.” Timasi akamfariji na wote wakaingia ndani wakiwa na baadhi ya mizigo, huku wakiliacha gari toka ikulu, likiondoka eneo lile.

Ndani ya nyumba anayoishi, walikutana na mume wa Timasi ambaye alijulikana kwa jina la Bwana Sema au Shelanga Sema, lakini hakutaka sana kujitambulisha jina lake halisi bali ubini wake ndio ulinakiriwa katika vinywa vya wengi.

“Karibu shemeji,” Alimkaribisha Limasi, Bwana Sema. Na mwanadada yule alishukuru huku akitua baadhi ya mizigo midogo aliyoingia nayo ndani. “Pole sana kwa matatizo.” Akaongeza Bwana Sema.

“Ahsante sana Shemeji. Nashukuru MUNGU kwa upande wangu nipo salama. Ila sifahamu kitakachoendelea kwa mume wangu.” Aliongea Limasi kwa huzuni.

“Naaminii atakuwa salama. Tuzidi kumuomba Mola, amfikishe huko alipo na atimize jukumu lake.” Sema, akampa moyo shemeji yake wa pekee.

“Amen.” Timasi akaongeza maneno ya kusindikizia sala ndogo ya mumewe. Na kimya kikafuata kabla ya Limasi ajaanza kuhadithia mengi ambayo hawayajui Timasi na Mumewe.

“Ujue kama sijakuelewa Shem,” Sema, mume wa Timasi alikaa kitako baada ya hadithi nzima kuisha. “Yaani jamaa yeye aliuawa. Kisha akaingizwa hayo makemikali, akafufuka.” Akarudia yale aliyoelezwa. Limasi akajibu ndio.

“Hiyo inamaanisha kuwa jamaa si yeye. Yaani si binadamu. Ni kama roboti au wale watu wa kwenye muvi za kufikirika.” Akaongeza mawazo yake. “Halafu cha kushangaza, akakupenda, akakuthamini mpaka akakuoa….”

“Na nina mimba yake. Ya miezi miwili.” Akaweka taarifa mpya aliyokuja nayo.

“Eheee! Na kakupa mimba tena?” Akazidi kushangaa Bwana Sema.

“Ila hata mimi nashangaa Lim. How this happens?” Akaweka bayana Timasi.

“Ni kwamba hamniamini?” Akauliza Limasi kwa mshangao.

“Ni ngumu sana Shemeji. Yaani ni ngumu kukubali kuwa mtu aliyefufuliwa, akaingizwa madawa mwilini mwake. Ni kama zombie au labda ni vamp…” Maneno hayo hayakumuisha Sema, yakamfanya Limasi avute begi mojawapo lililokuwepo mahali pale ambapo bado mizigo ile haikuwa imeingizwa chumbani.

Akatoa kompyuta ambayo aliachiwa na Idris. Akaifungua na kuingiza neno siri. Kompyuta ikafunguka na bila kuchelewa, alifungua faili moja. Video kadhaa zikaonekana, akacheza moja na kuwawekea mbele wale ndugu zake muhimu.

“Naitwa Idris. Ndivyo navyojulikana japo jina langu halisi ni Best Bouncher. Mtoto wa Hayati Bouncher. Mmarekani aliyeshiriki kutengeza tena kanuni mpya ya kemikali hatari ya C.O.D.EX” Video ikaanza kwa utambulisho. Hapo ikawaweka kitako Timasi na Sema. “Ni mmoja wa waliyopandikizwa kemikali zile ambazo zinatupa uwezo wa ajabu.” Mara video ikaanza kuwaonesha wanajeshi wa C.O.D.EX wanavyopambana. Wakipigwa risasi, wanalala dakika kadhaa, kasha wanainuka wakiwa hawana jeraha hata moja. Wanaendelea kupambana.

Macho yakawatoka Timasi na Sema lakini wakakaa kimya kuona nini kitafuata. “Na mimi nipo hivyo unavyoona.” Video ile ikamuonesha Idris akisimama na kuchukua kidumu cha lita tano na kukifungua ambamo ndani yake kulikuwa na kimiminika. “Hii ni petrol.” Akaonesha huku anajimiminia kichwani. Kisha akachukua kiberiti cha gesi na kuanza kukiwasha. Zile cheche pekee, zikatosha kumuwasha Idris na kuanza kuungua.

“MUNGU wangu weee.” Timasi akapiga ukulele mkubwa huku akijificha asiweze kuona ile video. Sema alikuwa anaangalia lakini akiwa haamini kama mtu yule atapona. Ila alichokuwa anashangaa, Idris alikuwa hapapariki wala kuonesha kuwa anaumia au kujali kuhusu ule moto mkubwa uliomkumba.

Baada ya dakika tano, Idris alikuwa mweusi kama mti uliokuwa unachomwa ili kwanza ufe matawi yake au labda wadudu wakali waondoke kwenye mti ule. Kimya kikatanda kwenye video ile. Timasi akajaribu kuangalia ni nini kinaendelea, lakini bado picha ile ikamtisha. Akaendelea kujificha na wakati huo, Limasi alikuwa kimya akisubiri waone majibu.

Ghafla mwili wa Idris ukaanza kujirudi katika hali yake. Ngozi ikaanza kujitandika kwenye mwili wake kama vile mtu avaliswaye nguo zake.

“Shit. This is impossible.” Alihamaki Sema akimaanisha kuwa ile ilikuwa haiwezekani. Maneno hayo yakamfanya Timasi naye aangalie. Na aliona jinsi kichwa cha Idris kinavyojitengeneza hadi akarudi katika hali yake na kuchanua tabasamu mwanana. Sema akaifata kompyuta na kuirudisha nyuma kidogo hasa pale wakati anajiunga. Limasi akaacha afanye anachotaka kufanya.

“Shit. No editing. It’s real.” Akabwatuka baada ya kuiangalia video ile kwa umakini zaidi. Alikubali kuwa ile video hamna kilichohujumiwa, vyote vilikuwa ni kweli. “Ina maana haya mambo yapo kweli dunia hii?” Akajiuliza lakini hamna aliyejibu.

“Si kuungua tu. Ningeamua ningejizima mwenyewe. Lakini hii niliyowaonyesha, nilitaka muone ni kiasi gani tunauwezo wa kufanya mambo haya ambayo wengi wenu ni ngumu kuamini.” Video ile ikawatoa kwenye mawazo mengine. “Nataka muijue siri ya wanajeshi hawa, na ninataka mfanyie kazi siri hii.” Kabla video ile haijaendelea, Sema akaingilia kati.

“Ngoja, ngoja, ngoja.” Akamfanya Limasi asimamishe ile video. “Ngoja kwanza.” Akazidi kuwamakinisha Limasi na Timasi. “Anataka wakina nani wajue hapo?” Akauliza. Limasi akamtazama.

“Anataka dunia ijue.” Akajibu Limasi kwa kifupi.

“Kivipi sasa? Tukapeleke habari na video hii kwenye vituo vikubwa vya habari? Au wajue vipi?” Akauliza tena.

“Vyovyote vile. Na ni kheri tupo hapa.” Akaongea Limasi.

“Kwa Marekani hii. Na Wamarekani hawa. Na wakijua tu kuwa sisi ndio tumesambaza, mbona tutakiona?” Akaweka hisia zake Bwana Sema.

“Shem!” Limasi akashangaa kwa yale maneno.

“Kweli nakwambia Shemeji. Tutapotezwa mapema. Na sitamuona mwanangu wa tumboni mwako.” Akazidi kutabainisha.

“Kwa hiyo kutomuona Id kwako ni sawa tu?” Limasi akaja juu kidogo.

“No. I didn’t mean that, Shem….” Akataka kujitetea kuwa hakumaanisha vile alivyofikiria Shemejiye lakini Limasi akamkata.

“So, what do you mean?” Limasi akamuuliza kuwa anamaanisha nini sasa. Sema akabaki na kigugumizi asijue alikuwa anamaanisha nini. “Mbona unauoga wa ajabu sana Shemeji?” Akauliza kwa kukata tamaa, Limasi.

“Lim.” Timasi akamuita pacha wake kwa upole. “Sivyo unavyochukulia haya mambo. Ni magumu kupindukia. A time utakapoweka hadharani haya mambo, eidha utachekwa kwa kupeleka filamu na kisha baada ya kuchekwa,itafikia zamu ya kutafutwa na kuangamizwa ukidhaniwa kuwa unajua mengi sana kuhusu hiyo Protex.

“Siyo Protex na wewe.” Akamkatisha dada yake.

“Eee! Hiyo hiyo sijui phonex au sijui mwatex,” Akawafanya wengine wacheke kwa sababu ya kuchanganya majina.

“Ni C.O.D.EX bwana Dada. Hahahaa.” Limasi aliongea huku hana mbavu.

“Ni hatari hiyo kwako. Heri umuache Id apambane huko alipo. Akirudi, yeye atajua afanyaje.” Akaongeza baada ya kurekebishwa.

“Yaani umenifanya nicheke hadi utumbo kudunda dunda.” Limasi akiwa ndani ya kicheko, sijui kama alisikia ule ushauri wa Timasi. “Hata hivyo nimewaelewa lakini. Nahitaji kufanya jambo ambalo litamsaidia mume wangu.” Akaongeza baada ya kicheko kupoa.

“Jambo gani Limasi. Embu achana na hayo. Ama la! Basi peleka hayo mambo kwa Rais wan chi. Labda hapo kidogo nitakuunga mkono.” Sema akaongea kwa hisia.

“Najua unanijali Shem. Ila huyu ni mume wangu. Yupo vitani sasa. Sijui kama atatoka salama, ila namuombea heri tu. Kitakachotokea, nitamshukuru maulana. Ila sitakaa hivi hivi, kuna jambo nahitaji kulifanya na ninaomba kutopingwa kwa hili.” Limasi akaacha nafasi ya kupokelewa maneno ya familia yake.

“Mi’ kama hayana mashiko kwangu, kwa kweli nitaweka doubt (kikwazo) tu.” Akaongea Bwana Sema.

“Najua ni lazima uogope haya mambo Shem. We’ siyo wale hata kidogo. Japo unatengeneza filamu kama zile, lakini naona wazi, hutaki yatokee kiukweli ukweli.” Limasi aliongea huku akiunganisha na kazi ambayo Shemeji yake anaifanya. Kazi ya kutengeneza filamu za kisasa.

Bwana Sema, akaafiki maneno yale kwa kichwa, lakini Limasi akaendelea. “Ila huyu ni mume wangu. Nampenda mno na anakiumbe chake kwangu. I can’t wait for him to return wakati nina uwezo wa kufanya jambo litakalo muweka pazuri hata pale atakaporudi. Anaweza akashinda vita ambayo anahangaika nayo huko, lakini je? Atamaliza maadui zake wote?” Akauliza lakini swali lake ni kama alikuwa anajiuliza mwenyewe. Kila mmoja aliyekuwepo mle, alikuwa anataka kusikia ni nini hasa anataka kufanya. “Hawezi hata kidogo. Ila mimi nina uwezo wa kuwapunguza baadhi.” Akaongea maneno ambayo yakazidi kuwashangaza wenzake.

“Lim. How can you…” Timasi akabaki anazungusha mkono akiwa anashindwa atumie neno gani zuri kumaanisha anachotaka kukisema. “I mean, unawezaje kupambana na hao watu?” Akauliza. Hakutaka jibu hata hivyo. “Ni wagumu hao. Kwanza hawafi na wala hawana mpango wa kufa. Wanawezana wao tu. Lim, tafadhali embu ongea mambo ya kujenga akili kuhusu suala hili na si kutaka kupambana. Kumbuka ni wewe ndiye nakuona kama baba na mama leo hii, nikikupoteza je? Hapana Lim, hapana kabisa.” Timasi, dada wa Limasi. Akaonesha kutokubaliana na akili ya mdogo wake. Limasi akatikisa kichwa kwa masikitiko.





“The problem is….” Akasita kidogo, kisha akaendelea. “Mnadhani kuwa kila kitu ‘kinasoviwa’ kwa kumwaga damu….” Hakumaliza kauli yake, Timasi akawa kamdakia.


“Kumbe..” Timasi akauliza huku anamtazama dada yake ambaye hakupata nafasi ya kuongea. “Unadhani kuna njia gani ya ‘kuyasovu’ haya mambo kwa kutumia mashairi au nyimbo?” Akauliza huku bado kamtazama dada yake.


“Hamna.” Mumewe akajibu. Kisha akaendelea, “No way. Hamna njia yaani, ni lazima ushike mtutu wa maana na kupigana nao. Limasi, you can’t.” Bwana Sema akakataa kabisa kwa shemijiye kuingia vitani na watu wale wa hatari.


“Ujue mnanishangaza,” Limasi akaongea huku anamtazama mmoja baada ya mwingine. “Yaani ni watu wasomi lakini nashindwa hata kutumia elimu zenu,” Wote wakawa kimya wanamtazama kwa makini. “Wewe ni mtu wa kutengeneza ‘mavideo’, umesomea huko Marekani kwa miaka zaidi ya mitano...” Aliongea hayo huku anamtazama Sema, mume wa Timasi. Kisha akamgeukia Timasi. “Na wewe umesomea mambo ya usalama na uhamiaji. Miaka karibu sita. Na wote mnatumia elimu yenu sehemu stahiki. How about me?” Akabakiza swali akiuliza vipi kuhusu yeye na elimu yake?


“Unataka kusema kuwa, utafungua mashitaka juu ya haya mambo?” Akauliza dada yake baada ya kung’amua maana ya dada yake.


“Hilo si swali tena. Linahitaji baraka zenu tu hapa.” Akajibu Limasi na kumfanya Timasi atikise kichwa kwa masikitiko huku anainamisha kichwa chake na tafakari zito likaanza kutembea katika ubongo wake.


“Lim,” Timasi akamuita dada yake baada ya kimya kifupi. Dada yake hakuitika bali kumuangalia akiwa tayari kusikia kauli yake. “Sawa wewe pia ni msomi wa Sheria. Lakini hapo unapotaka kuanzia kuonesha elimu yako, ni pagumu na pabaya pia.” Akaongea kwa upole dada yake, kuliko safari ya kwanza.


“There’s no easy way when you are starting sis. (Hamna njia rahisi kwenye kuanza Dada)” Limasi alishuka toka kwenye kochi lake na kupiga magoti mbele ya dada yake na kuikamata mikono yake. Uso wake akiuweka kwenye bembelezo mbele ya macho ya dada yake. “Hivi ndivyo nitavyoanza dada. Just give me a chance...” Akasisitiza. Timasi akabaki anakigugumizi. “Najua wanipenda na hutaki kusikia baya likinifika, lakini, I have no choice.” Akaongea hayo akimaanisha kuwa hana chaguzi zaidi ya kufanya kile alichokusudia. Timasi akapumua pumzi ndefu na mikono ya dada yake akiwa bado kaikamata.


“Nashindwa Limasi. Nashindwa kukuzuia lakini bado nakupenda na nakuhitaji sana Lim, please.” Timasi aliongea kwa huzuni na wakati huohuo, mume wake akamshika bega na kumfinyanga kidogo kwa kumfariji.


“Tim mke wangu. Wewe unampenda dada yako. Naye anakupenda sana. Lakini tayari anatakiwa kuanzisha familia yake. Awe na watoto na mume. Ingekuwa anaenda vitani na bunduki na mabomu, hata mimi ningekataa. Lakini anaenda kufuata sheria ili amuokoe mumewe, waje walee familia. Upendo wake kwako, upo daima, lakini anatakiwa kumpenda zaidi mumewe na familia yake atakayoanzisha. Ni sawa na wewe, leo hii nikipatwa na la kupatwa, hutomsikiliza Dada yako, lazima upigane ili niwe sawa.” Sema, mume wa Timasi akaongea kwa kubembeleza. Timasi akamuangalia mumewe na kisha akamuangalia Limasi.


“Dada.” Timasi akaita.


“Abee.” Naye Limasi akaitika.


“Unataka nini kumuokoa Idris wako?” Akauliza Timasi. Badala ya Limasi kujibu, akainuka na kumkumbatia kwa nguvu dada yake na machozi ya furaha yakimbubujika. Sema akawa anawatazama na kutabasamu bila kupanga kufanya hivyo.


“Ushauri wako pekee, unatosha sana dada yangu. Nitawasiliana na marafiki zangu wa huko nje, tutaifumua hii kesi. Nadhani hawatakataa kwa sababu watapata umaarufu mkubwa sana baada ya kufanikiwa kuwatia mbaroni hawa wajinga na mume wangu kuwa huru.” Limasi aliongea huku bado akiwa kamkumbatia dada yake.


“Fanya hivyo dada. Kwa lolote, usisite kunieleza.” Timasi akampa rasmi uhuru dada yake ili afaniikishe kumuokoa mumewe.

Baada ya hapo. Limasi aliamua kuwapa mkakati wake na kisha akawaonesha video zote ambazo aliachiwa na Idris Iris. Walizitizama kwa pamoja na kunukuu baadhi ya mambo ambayo yatasaidia sana ile kesi. Wakasoma pia nyaraka zilizokuwepo na kujipa moyo kuwa watafanikiwa kuliko hapo mwanzo walivyokuwa wanafikiria.


“Lini utaanza kazi hii Limasi.” Mume wa Timasi aliongea baada ya masaa karibu manne ya kutazama zile video na kusoma makaratasi yaliyoachwa na Idris.


“Kesho nitawasiliana na marafiki zangu popote walipo. Nadhani watakuja Tanzania kwa sababu wanajua sana ubora wangu na wanatamani sana kufanya kazi na mimi.” Akajibu Limasi.


“Okay. Pia na mimi nitawasiliana na kampuni moja ya Uwakili na Sheria za makosa ya jinai iliyopo Afrika Kusini, nadhani itawasaidia sana.” Akaongeza mume wa Timasi.


“Hapo utakuwa umecheza vema sana Shem maana vikampuni vyetu vya hapa, hamna kitu. Ila tukianzia South, itakuwa poa sana.” Limasi akaongezea kuhusu hilo.


“Nitakupa website yao ili uone utendaji kazi wao na kama utaridhika, nitakuunga nao ili ukapambane. Najua utafanikiwa tu.” Sema, akampa moyo zaidi na Limasi akapokea ujumbe ule kama habari njema kwake. Akamshukuru shemeji yake.

****

Mwanajeshi aliyekuwa anamkagua Idris, alijikuta amekutana na macho makali sana ya Idris. Macho ambayo kwa yeyote mwenye roho ndogo, anaweza kukimbia au kutoa hewa chafu.


“Oh! Oh!.” Mwanajeshi yule alijikuta akishangaa wakati Idris alipotoa bunduki yake ghafla na kulenga kichwa chake. Mlipuko mkubwa ukasikika ukifuatiwa na mwanajeshi yule mwenye sura mbaya kurushwa mbali akiwa hana kichwa ambacho kilichobongonyolewa vibaya kwa bunduki ya kisasa aliyoiunda Agent Zero.


Kazi ikaanza tena kwa wale wanajeshi wengine kufyatua risasi zao na mabomu kwa ujumla. Hali ikawa tete lakini Idris na Merice hawakuthubutu kujibu mapigo yale.


Baada ya dakika mbili, ukimya mkubwa ukatanda tena na macho ya Uzo yakawa kwenye runinga za mle ofisini mwake ambapo zilikuwa zinaonyesha vema gari la Idris lililokuwa limetobolewa vibaya na wakati huo moto mkubwa ukiwa unawaka kwenye injini ya gari hilo.


Polisi walikuwa mbali na eneo lile na hawakuthubutu kusogea bali kutazama kwa mbali jinsi wanajeshi wale walivyokuwa wanafanya kazi waliyoagizwa.


Sekunde kadhaa mbele, mlipuko mkubwa ukasikika toka kwenye lile gari. Gari likarushwa juu kwa sababu ya mlipuko huo. Na wakati lipo juu, huku chini, mwanadada Merice alibiringita kwa pembeni na kusogea mbali kidogo na eneo lile na hamna aliyemuona kwa sababu ya moshi mkubwa uliyokuwa umetanda muda ule.


Wakati gari lao linashambuliwa kwa risasi, Merice alichomoa bunduki ndogo yenye gesi na kuanza kutoboa kwa gesi sehemu ya kuwekea miguu ya gari alilopanda. Pale lilipoanza kushika moto, yeye alipita kwenye tundu hilo na kulala kwenye rami, kisha akapandikiza bomu moja la kulifanya gari lile lipae angani wakati linalipuka. Na alifanikiwa hilo.

Pale alipoona ni muda wa kulipuka gari lao, alibonyeza kifyatulio cha bomu lile, na bomu likarusha juu zaidi gari na kumpa nafasi yeye ya kuchomoka pale chini na kwenda pembeni ambapo hapatamdhuru kama gari litadondokea hapo.


Mshindo mkuu ukasikika wakati gari lile lilipotua chini likiwa linawaka moto kama nyumba ya nyasi iliyomwagiwa petroli na kurushiwa njiti ya kiberiti iliyowashwa.

Moto ule mkubwa uliendelea kuwaka lakini mara ukaanza kupungua taratibu kama vile mwanga mkali, halafu ghafla ukaanza kufifia labda kwa sababu ya kuishiwa nguvu ya umeme.

Ndani ya dakika mbili, tayari moto ule ulikuwa umepungua kabisa na alionekana Idris akiwa kapiga goti kwa mguu mmoja, mkono wake wa kushoto kakamata bunduki yake ya kisasa, M-16 202 Advance Grade ambayo aliifanya kama fimbo ya kutembelea jinsi alivyoikita kwenye rami na wakati huo, mkono wake wa kulia alikuwa kakunja ngumi nayo ikiwa imekita ardhini.


Wanajeshi wa Uzo wakakoki silaha zao na kujipanga vema kimakabiliano. Nyama za mwili wa Idris zikaanza kujirudi kwa haraka wakati bado kaweka pozi lake la mapigano na mwili wake ukiwa mwekundu sana kama kijinga cha moto. Ngoma iliwaduwaza wote waliokuwa wanaitazama.


“Bidhaa bora ya Dokta Ice.” Uzo alijikuta akiropoka maneno hayo bila kutegemea akiwa kakubali kile ambacho alikiunda Dokta Ice.


Idris akajiunga na kurudi akiwa katika hali yake ya mwanzo ndani ya nguo za kijeshi na zilizokuwa zimependeza sana. Taratibu akiwa kainamisha kichwa chake, akaanza kukinyanyua na kuwaelekea wale wanajeshi wa Uzo ambao walikuwa wamemuweka ‘tageti’ kwa bunduki zao za hatari kwa binadamu wa kawaida.


Kichwani mwa Idris, akaziseti chipu zote za mapambano, kujilinda, ukatili, na yote ambayo alikuwa anaweza kuyafanya. Akatabasamu pale alipoona wanajeshi wamemuelekezea silaha bila kujua wanapambana na kiumbe wa aina gani.


Katika hali ya kushtukiza, Idris akapotea eneo lile na alipoibuka, alikuwa mbele ya mwanajeshi mmoja huku M-16 yake toleo bora iliyoongezewa ubora na Agent Zero, ikiwa kichwani kwa bwana yule ambaye hakuamini kama kuna binadamu kama Idris kwa dunia ambayo amekuja kuishi.


Mlipuko mkubwa ulisikika na wakati huo damu zikiruka kwa nyuma na tobo kubwa likionekana kwenye paji la uso la yule mwanajeshi. Wenzake wakashtuka na kumtazama na walikutana na risasi nyingi za Idris ambaye alikuwa anazimwaga huku anajirusha upande mwingine wa barabara ile. Alipotua chini, akarusha bomu fulani dogo ambalo ndani yake lilikuwa linagesi hatari sana inayoweza kuteketeza wanajeshi wengi wa C.O.D.EX na binadamu wa kawaida.


CARBO-NITRO. EX, ni bomu dogo aliloliunda Agent Zero. Limechanganywa baadhi ya hewa ambazo zinaweza kuwanyong’onyeza maadui ndani ya sekunde kadhaa. Bomu hilo dogo, mfano wa yai la kisasa, hudondoka na kupasuka lenyewe kisha moshi mzito hutokea na uvutapwo na uliyemdhamiria auvute, basi kifo ni halali yake.


Idris akadondokea mbali kidogo na wanajeshi wale ambao walikuwa wamepigwa risasi za hatari za kifuanii na walikuwa wanagaa gaa kama wachawi waliokuwa wamepata maombi ya kichungaji.

Bomu dogo nalo likafunguka na kuanza kutoa moshi ambao wanajeshi wale waliuvuta na taratibu wakaanza kujifinya finya ngozi zao na baadae kukauka kabisa. Ngozi ikashikilia mifupa ya miili yao huku macho yakigeuka na kuwa meusi.


Moshi ulipotulia, Idris alisogea hadi kwa mwanajeshi mmoja na kutoa kifaa kilichokuwa jichoni kwake. Kifaa hicho ndicho kilikuwa kinapeleka mawasiliano ya picha hadi kwa Uzo. Idris akakitazama kifaa hicho na wakati huo Uzo alikuwa anamtazama pia. Hivyo picha ilivyokuwa imejengeka baina yao, ilikuwa kama wanaangaliana kwa uchu.


Baada ya kitendo hicho, Idris bila kusema neno, alikidondosha kile kifaa mfano wa kamera ndogo inayokaa jichoni. Akakikanyaga kwa nguvu na kukivunja. Kule kwa Uzo, runinga aliyokuwa anaiangalia, ikakumbwa na chenga nyingi sana. Uzo akasonya kwa kiburi.





Baada ya Idris kukanyaga kamera ile, aliangalia huku na huko kuona kama kuna tatizo au kizuizi chochote, lakini hakuona kibaya cha kumzuia zaidi ya polisi kadhaa ambao bado walikuwa wamepigwa butwaa na hawaamini kile walichokishuhudia muda mdogo uliopita.


Idris kwa kutumia macho yake, aliweza kuwaona polisi wale walivyokuwa wanaogopa. Na yeye akaamua kutumia mwanya huohuo kwenda kuchukua moja ya magari yao. Wakati anaelekea huko, mwanadada Merice naye alitokea pembeni na kuungana naye kufuata usafiri mpya, tayari kwa kuendeleza kazi ambayo wameianza.

****

“Anajidai tayari ameshinda hii mechi,” Uzo aliongea wakati huo mwanamama Simeria alikuwa amesimama nyuma yake. “Anajiona ninja na kumbe ni katuni tu.” Akaongeza na msonyo mrefu uliomfanya Simeria agune. “Na wewe unaguna nini sasa?” Akauliza baada ya mguno huo wa hawara yake.


“Unajua umeonesha tabia za Kiafrika kabisa?” Uzo ambaye alikuwa ni mzungu halisi kabisa. Akamtazama mwanamke anayempa raha ikifika mida ya raha. “Tena tabia zenyewe ni za Kitanzania.” Akaongeza.


“Usinitajie hiyo nchi hata kidogo. Bora utaje hata habari za mimi kutafuna na kunywa damu za watu.” Akaongeza kwa kisirani Uzo.


“Kisa nini? Halafu huijui Tanzania tu. Ni wakarimu, waelewa na wapenda amani.” Mwanamama Simeria, aliongea huku akiwa anamtazama bwana wake.


“Yote hayo unayajua kwa sababu ya mumeo Ice ambaye sasa ni mifupa chini ya mchanga wa moto.” Akaongea Uzo.


“Upande mwingine naweza sema hilo ni jibu, ila kwa upande mwingine, hata Jografia inalitambua hilo.” Simeria alimuelimisha Uzo kuhusu nchi yenye amani na upendo ya Tanzania. “Labda uwachokoze ndio utawaona ubaya wao.” Wakati anamaliza maneno hayo, alikuwa anaondoka eneo lile.


“Sasa unaelekea wapi?” Uzo akauliza.


“Naona unanichanganyia mafaili tu hapo.” Simeria akajibu baada ya kugeuka na kumtazama mwanababa wa kizungu, mwenye mamlaka na jeshi la C.O.D.EX.


“Hatujamaliza hapa, kuhusu huyu mbuzi.” Sauti ya Uzo iliambatana na kumuonyesha kioo cha runinga mle ndani, akimaanisha mbuzi ni Idris.


“Ndio useme sasa na si kuanza porojo za mimi na Ice. Am done with him.” Hasira zilijionyesha wazi kwenye uso wa Simeria.


“Waandae Pro Soldiers.” Ndiyo maneno ya Uzo ammbayo yalimfanya mama yule aondoke eneo lile bila kusema chochote.

****

Huko Tanzania, Limasi na familia yake, hawakulala kabisa siku hiyo. Usiku kucha wakawa wanatuma barua pepe kwenda kwa watu ambao waliamini kuwa watakuwa msaada mkubwa sana kwao. Barua zilienda kwa Wanasheria wakubwa duniani na makampuni ambayo yanaaminika katika kufanya kazi za kisheria.

Limasi kwa upande wake, aliweza kuwaandaa Wanasheria watano aliomaliza nao huko India. Kazi waliyoipanga, walihitaji kuifanya haraka kabla hata mambo hayajawa mabaya kwa Idris Iris ambaye kwa wakati huo alikuwa ameanza kuuwasha moto wake ndani ya nchi kubwa na babe duniani, Marekani.


Hadi inafika siku nyingine, tayari Limasi alikuwa anauhakika wa watu aliowataka kuja kumsaidia katika kesi ya kuwatuhumu watengenezaji wa kemikali walizozipa jina la C.O.D.EX. Alifurahi zaidi alipoahidiwa na watu hao kuwa watafika Tanzania siku mbili mbele baada ya kukamilisha masuala yote ya kusafiri nje ya nchi.


Na wakati huohuo, mume wa Timasi, Bwana Sema alikuwa bado hajajibiwa maombi ya kampuni kubwa za kisheria alizozihitaji katika kusimamia kesi ambayo Limasi anaenda kuifufua. Hilo halikuwa lina shida sana kwa sababu ilikuwa mapema sana kwa wao kupata majibu. Ilikuwa ni uhakika kupata kampuni ya kisheria nzuri kwa sababu kesi yenyewe inagusa nchi kubwa na endapo watashinda, watapata umaarufu mkubwa sana. Hiyo ni kutokana na wanasheria wengine kushindwa kuitetea kesi ile hasa kwa sababu ya vitisho mbalimbali walivyokumbana navyo, ikiwemo mauaji makubwa.

****

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog