Search This Blog

Saturday 24 December 2022

TOP SECRET: NYARAKA NAMBA 12333 KUTOKA WHITEHOUSE - 5

   http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/top-secret-nyaraka-namba-12333-kutoka_10.html

Simulizi :  Top Secret: Nyaraka Namba 12333 Kutoka Whitehouse

Sehemu Ya Tano (5)



Hivyo basi Kermit akasafiri mpaka Iran kuungana na Donald Wilber shushushu wa CIA aliyepandikizwa Iran Siku nyingi nchini Iran akiwa kama Mwanaikolojia na mtafiti wa mambo ya kale yahusuyo milki ya Persia.


Katika kipindi hiki kikundi cha msimamo mkali cha Fadaiyan e-Islam kilikuwa kimeacha kumuunga mkono Mosaddegh kutokana na Waziri Mkuu huyo kushikilia msimamo wankutenganisha Dini na serikali.


Hivyo basi Mara baada ya Kermit kutua Iran kwa siri na kuungana na afisa mwenzake Wilber wakaenda kuonana na viongozi wa kikundi cha Fadaiyan e-Islam na kiongozi Mkuu wa kikundi kwa kipindi hiki alikuwa ni Mohammad Behbahani na kumueleza shida yao.


Kikundi cha Fadaiyan e-Islam kilokuwa na 'connection' nchi nzima na viongozi wa serikali za mitaa. Hivyo maafisa hawa wa CIA walimuomba Behbahani awasaidie kusambaza fedha kwa viongozi hao ili wasaidie kupotisha viongozi wanaowataka wao (CIA) katika uchaguzi mdofo wa wawaoilishi wa Bunge la Majlis utakaofanyika katikati ya mwaka huo.


CIA wakamuahidi Behbahani kuwa kama atashirikiana nao watahakikisha kuwa Waziri Mkuu Mosaddegh akiondoka madarakani, kiongozi atakayerithi cheo hicho anaifanya Iran kuwa nchi ya kiislamu rasmi na kutimiza matamanio ya kikundi cha Fadaiyan e-Islam.


Behbahani na wafuasi wake wa Fadaiyan e-Islam wakakubaliana na ombi hili na akaanza kazi ya kugawa fedha kwa siri nchi nzima kwa viongozi wa serikali za mitaa.


Wakati zoezi hilo linaendelea wakawasiliana na serikali ya Uingereza watume jeshi lao la Wana maji (Royal Navy) katika pwani ya Iran ili kuzuia njia kwa meli yoyote kutoka Iran iliyobena mafuta isitoke.


Uingereza ikatekeleza agizo hili kwa kusimamia kigezo kuwa, mafuta hayo yanamilikiwa na kampuni ya Ango-Iran Oil Company ambayo serikali ya uingereza ni mmiliki Mkuu wa kampuni. Kwahiyo kitendo cha Iran kuchimba mafuta hayo na kutaka kuyauza kilikuwa ni kiyendo cha "wizi".


Na hili kilifanikiwa, mafuta yalikuwa yanachimbwa lakini hayatoki ndani ya Iran kutokana na kuzibwa njia ya baharini na Royal Navy.


Taratibu uchumi ukaanza kutikisika na ajira zikaanza kuyeyuka kitokana na kutokuuzwa kwa mafuta kwenye soko la kimataifa.


Wakati haya yanafanyika maafisa wa CIA wakakutana na viongozi moja ya kikundi wapinzani wa Waziri Mkuu Mosaddegh, kilichoitwa Tudeh Party.

Hiki kilikuwa ni kikundi cha kikomunisti.


CIA wakawahonga kiasi kikubwa cha fedha na kuwaomba waache kumpinga Mosaddegh na badala yake waanze kumuunga mkono.

Wakapewa hela ya kutosha na wakabadili msimamo na kuanza "kumuunga" mkono Waziri Mkuu Mosaddegh.


Walianzisha maamndamani mitaani kumsifu Mosaddegh na kila Waziri Mkuu alipoitisha mikutano, maelfu ya wanachama wa Tudeh Party walijitokeza.


Hili lilimshangaza hata Mosaddegh mwenyewe kakini hakufikiria mbali, yeye alidhani kuwa labda sera zake zimewakuna wapinzanibwake hao na wameamua waanze kumuunga mkono.


Hakufahamu kuwa suala hili lilikuwa ni mkakati wa kipropaganda kumuangusha.


Ni kwamba; nchi ya Iran ina waisilamu wengi na wengi wao hawapendelei sera za kikomunisti kwa kuhisi kwamba ukomunisti una chembe chembe za kumpinga Mwenyezi Mungu.


Sasa kitendo cha Mosaddegh kutaifisha visima vya mafuta, zilianza kuenezwa propaganda na wapinzani wake kuwa anataka kuifanya Irani kuwa nchi ya kikomunisti. Wananchi walipuuza pripaganda hizi kwa kuwa walimuona Mosaddegh kama shujaa kurudisha visima vya mafuta kwa taifa la Iran.


Lakini kitendo cha Tudeh Party kumuunga mkono na Mosaddegh kushindwa kuwakemea au kujitenga nao, kikaanza kypandikiza hisia kwenye fikra za wananchi kuwa huenda ni kweli Mosaddegh anataka kuitumbukiza Iran kwenye ukomunisti.


Taharatuki ikazidi kuongezeka.

Mafuta hayauzwi.

Ajira zinayeyuka.

Mosadeggh anungwa mkono na makomunisti.


Balaa kubwa zaidi lililokuja kumuwehusha Mossadeggh ni baada ya matokeo ya uchaguzi wa Wawakilishi wa Bunge la Majlis kutangazwa. Chama chake kilikuwa kimeshindwa vibaya. (Kumbuka CIA waligawa fedha kwa kumtumia Behbahani kwa viongozi wengi wa serikali za mitaa wawapendelee wapinzani wa Mosaddegh).


Baada ya kikao cha kwanza cha Bunge jipya kuitishwa, vikaanza kuibuka hoja za kumpigia kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mosaddegh.


Mosaddegh akalisitisha Binge kwa muda na kuitisha kura ya maoni kuomba wananchi wamruhusu kulivja Binge hilo.

Wananchi wakapiga kura lakini Mosaddegh akafanya kosa kubwa la kupika matokeo.


Alitangaza matokeo kwamba 99.9% ya wananchi wamekubali ombi lake la kuvunja Bunge. Hii ilikuwa tofauti kabisa na maoni halisi ya wananchi kwani wengi walitaka Bunge liendelee kuwepo ili limsimamie zaidi Mosaddegh kwani wameanza kukosa imani nae.


Kitendo cha kupika matokeo ya kura ya maoni na kulivunja Bunge na kubaki yeye pekee na baraza lake la mawaziri kuongoza nchi kilipingwa vikali wananchi na wengi walimuona kama amegeuka kuwa Dikteta.


Wapinzani wake wakaanza kuandamana mitaani na Mosaddegh akaamuru wakamatwe na kuswekwa rumande. Hii ilizidi kuchochea hasira za wananchi.


Wakati haya yote yanaendelea, mafisa wa CIA Kermit Roosevelt na Donald Wilber waliagiza makomando kutoka CIA kitengo cha SAD.

Makomando hawa wakachukua mamia ya vijana kutoka Tudeh Party na kuwaingiza kwenye msitu maeneo ya Abadan na kuwapa mafunzo ya kijeshi kwa siri kubwa.


Huko mtaani taharuki iliendelea kuwa kubwa zaidi, na umaarufu wa Waziri Mkuu Mosaddegh ulikuwa umeshuka kwa kiwango kikubwa na uhusiano wake na wananchi wake ulizorotota kupitiliza.


Mafuta yalikuwa hayauzwi kutokana na meli kuzuiwa zisitoke na Royal Navy.

Bunge la Majlis limevunjwa.

Wakomunisti wanamuunga mkono Waziri mkuu Mosaddegh.

Wapinzani wanatupwa gerezani.


Hapa ndipo ambapo CIA wakamuamuru kibaraka wao mtawala Shah Pahlavi kuingilia kati.


Ingawa Mosadeggh alikuwa amefanikiwa kulishawishi Bunge kumpunguzia madaraka Shah wa Iran lakini aliachiwa jukumu la kikatiba la kumuapisha Waziri Mkuu. Hii pia ilimpa uwezo wa kikatiba wa kumuondoa madarakani.


Ndipo hapa katika kipindi ambacho wananchi wengi wa Iran walitamani Mosaddegh kutoka madarakani, Mfalme Mohammad Reza Shah Pahlavi akaandika waraka wa kumuondoa madarakani Waziri Mkuu Mohammad Mosaddegh na kumteua Generali Fezlollah Zahedi.


Waraka huu alikabidhiwa Kanali wa Jeshi la mfalme aliyeitwa Nemattolah Nassiri. Na yeye mwenyewe mfalme akapanda ndege kwenda Uingereza akijua wazi kitakachofuata.

Baada ya kanali Nematollah kufika katika makazi ya Waziri mkuu na kumkabidhi waraka.

Mosaddegh akauchana mbele yake na kuamuru Kanali Nassiri awekwe rumande.


Sikh ya Tarehw 19 August 1953 CIA ikawachukua vijana waliokuwa wanapewa mafunzo ya siri msituni na kuwagawanya katika makundi mawili.


Kundi la kwanza liliingia mtaani asubuhi likiwa na sare za Tudeh Party na kutangaza kuwa linafanya mapinduzi ya kikomunisti kwa kumuunga mkono Waziri Mkuu Mosaddegh.


Walichokifanya walipita mitaani wakiharibu “alama zote za ubepari”.

Hii ilimaanisha kuwa waliharibu kila aina ya biashara waliyoikuta mbele yao.

Mji mkuu wa Tehran ukashikwa na tahatuki kuu.


Ilipofika mchana, CIA wakaruhusu kundi la pili kuingia mtaani.


Kundi hili la pili lenyewe, lilipita nyumba hadi nyumba kuhamasisha wananchi wasikubali kubaki majumbani wakati wanachama wa Tudeh Party wakiharibu mali zao.


Wananchi wengi wakajitokeza na silaha za jadi nabkuandamana mitaani kupambana na "wanachama" wa Tudeh Party.


Mji mzima ukaingia katika machafuko.


Ndipo hapa CIA wakampa maelekezo ya mwisho Generali Fezlollah Zahedi.

Wakamuru huo ndio ulikuwa muda muafaka wa mapinduzi.


Generali akakusanya vikosi vyake, wakaingia mtaani na vifaru na silaha nzito. Wakaelekea kwenye makazi ya Waziri Mkuu.

Hawakumkuta Waziri Mkuu, hivyo ikawalzimu kuwakamata Mawaziri wake. Masaa machache baadae Waziri Mkuu Mohammad Mosaddegh akajitokeza na kujisalimisha.


Mapinduzi yalikuwa yamekamilika.


Siku mbili baadae mfalme, Mohammad Reza Shah Pahlavi alirejea Iran akiwa kwenye ndege binafsi ya kifahari akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa CIA, Allan Dulles.


Tarehe 21 August 1953, akamuapisha Genetali Fezlollah Zahedi kuwa Waziri mkuu mpya na yakafanyika mabadiliko ya kikatiba kumrudishia Shah wa Iran nguvu kubwa zaidi kuamua kuhusu mwenendo wa nchi.


Kutokana na nchi kutokuwa na akiba yoyote ya fedha, serikali ya Marekani wakampatia Shah wa Iran Dola Milioni 5.


Mohammad Mosaddegh akahukumiwa kifungo cha maisha gerezani lakini Shah wa Iran Mfalme Mohammad Reza Shah Pahlavi akampunguzia adhabu kuwa kifungo cha miaka mitatu jela.


Ingawa tukio hili la serikali ya Marekani kwa kutumia CIA, kitengo cha SAD kuongoza mpango wa kuipindui serikali halali ya kidemokrasia kutokea mwaka 1953 lakini ndilo lililofanya kuzorota kwa mahusiano kati yake na Iran mpaka Leo.






Mpaka leo hii tunapojadili hapa, kitengo hiki cha SAD ndani ya CIA kinaendelea na shughuli mbali mbali za siri ulimwenguni kote na ni Tamko/Nyaraka namba PTU12333 kutoka Ikulu ya marekani inayowapa ruhusa ya kutekeleza shughuli hizo.








Mwisho.






The Bold.


0 comments:

Post a Comment

Blog