Search This Blog

Thursday 29 December 2022

KIAPO (AGANO LA DAMU) - 5

   

Simulizi : Kiapo (Agano La Damu) 

Sehemu Ya Tano (5)




"kama umeamua hivyo sina shaka mzee! ila ombi langu ongea na huyo mtu wako wa polis aibe huo ushahidi wa sura yangu"




"usijali kijana!"




Zidu Katili Akaaga Na Kuondoka Zake Mafichoni Kwa Miezi Ile Mitatu Ya Kampen Na Uchaguzi!




Huku Nyuma Afande Kisogo Aliiba Ile Flash Ofisini,nurdin Akujua Ninan Aloiba Flash Ile!,siku Zikasogea Pasina Mwindaji Alowindwa Kunaswa,hatimaye Wakamsahau!,kampeni ikapamba moto!,mzee alex alikubalika sana katika jimbo lake lile! na alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda ila je angeshinda?!...




*****




SURA YA TISA




KWA muda Ule Ndani Ya Ofisi Ile Mida Ile Ya Saa Kumi Kulikuwa Na Walimu Wawil Tu Na Mtoto Mdogo Isach,


Sar Gibson Alikuwa Akisahihisha Mitihan Ya Wanafunzi Huku Mwalimu Jane Akimfundisha Isack!,ghafla Madam Akanyanyuka Ni Kama Alikuwa Akielekea Chooni!




"samahan Isack Embu Chukua Hii Ela Kanletee Sigara Cm Moja Na Chenji Nunua Kipotabo Chako Sawa?"




Isack Alifurah Akanyanyuka Na Kuchukua Ela Ile!,akatoka Kuelekea Nje,duka Alikuwa Mbali sana na pale!,kitendo tu cha kunyanyuka mwalimu gibson akavamia begi la madam jane na kufungua zipu akaitoa simu mbili apple moja na sumsung akazipachika mfukoni akuishia hapo alikuta elfu sitin akazichimbia mfukoni kisha akuwa na muda wa kuendelea kukaa pale ofisini huyooo akaondoka zake




'kwisha habar yako isack'




njian alijiwazia! moyon akiwa na furaha!...




madam jane aliporejea alishtuka kutomkuta mtu ofisini si isack wala mwalim gibson akujal akaketi na kuendelea kusoma kitabu kile alichokuwa akimfundishia mtoto isack




baada ya kama dakika tano isack akarejea mkonon akiwa na sigara na kipotabo!.




alipofika kwanza alishtuka alipomkuta sir gibson ayupo akujal akaenda kuket na kipotabo chake akakifungua na kuanza kunywa sigara akawa kazishika vilevile,akitegemea mwalimu hitlar atakuja ampe!


madam napo akuangaika kuulza chochote japo moyon alijiuliza mtoto yule kapata wap ela ya kununulia kipotabo?!


akapotezea!,akaendelea kumfundisha...




walifunga masomo madam alishasahau juu ya sigara isack alizozishika na kuziweka mfukoni madam akachukua pochi yake wakaongozana mpaka ndani ya gari wakaingia pasina madam kukagua begi lake haooo wakaondoka kuelekea nyumbani!










Maisha Ya Mtoto Isack Bado Yapo Kwenye Mtihani Mzito,mengi Anakumbana Nayo Mengi Magumu Anayapitia Na Hata Mengine Yanatishia Maisha Yake Je Nin Hatma Ya Maisha Yake Hayo?! Twende Pamoja




*NA HII NI SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA*




Wakati wakiwa ndani ya gari ndipo madam Jane alipokumbuka simu zake,akafungua pochi yake ghafla alitoa macho ya mshangao pasina kuamin kile akionacho akajaribu kuchakura chakura ila hapakuwa na simu wala ela!


madam alionekana wazi kuchanganyikiwa akashuka kwenye gari haraka na kurudi ofisini bado akufanikiwa kuviona vitu vyake vile je vimeenda wapi?! swali hilo alikuweza kujibika kwenye kichwa chake,akarudi zake kwenye gari na kuliwasha kichwani akiwa na mzigo wa mawazo!




"madam kuna nini madam?!"




isack alijaribu kumuuliza madam wake ambapo madam alimwambia waz kuwa kaibiwa ela na simu zake mbili pale ofisini




kamwe madam jane akutaka kuamin kwamba walimu wenzake ndiye waliyemwibia,sasa ni nani?! akajiuliza pasina jibu...




Safari Ikaendelea Ya Kuelekea Nyumbani Kwenye Gari Wote Wakiwa Kimya!




*****




Kesho Yake Asubuh Mwalimu Gibson Alimtafuta Brayson Rafiki Yake Na Isack Chemba Wakazungumza


"kuna Kitu Nataka Unsaidie Mtoto Mzuri Ntakupa Zawadi Na Sitokuchapa Ila Iwe Siri yako"




"kitu gani sar"




"ewaaaa!,kuna vitu nataka nikupe ukaweke kwenye begi la isack mtu yoyote asione sawa?!"




Bray akashtuka wasiwasi ukamvaa,akajikuta pasina kupenda swali likamponyoka!




"vitu gani mwalimu!"




Gibson akaachia tabasamu lakumtoa wasiwasi kijana yule kisha akaingiza mkono mfukon na kutoa miatano akampa




"hii yako utanunua vitu utakavyo ila chukua huu mfuko usiufungue wakati watu wote wakiwa mistarin we kauweke kwenye begi la isack pasina yeye kujua sawa?"




Bray akatingisha kichwa kuafiki akaupokea ule mfuko mweusi,ghafla kengele ya mistarin ikagongwa




"ngoja kwanza wanafunz wote waende mistarini"




Baada ya dakika kama tano hivi mwalimu Gibson Akamruhusu Bray Akafanye Kazi Ile!


Bray Naye Akaenda Kuitekeleza!




OFISINI KWA WALIMU




Ndani ya ofisi ile ya walimu kulikuwa kuna mjadala mzito juu ya kupotea kwa simu mbili za madam na pesa zake


"eti walimu! hapa ofisini tulikuwa watatu tu nyote mlishaondoka jion ile au unataka kuniambia ivyo vitu vilipotea kabla walimu awajatoka?"




"hapana,vitu vile vimepotea muda ambao tulikuwa wawili hapa!"




"kwa hiyo unataka kusema mimi ndo nloiba?!"




mwalimu gibson akaja juu,hali ya hewa ikachafuka ofisini mule




"mi nahis kale katoto chako ndo kajiz"




"ishia hapo hapo isack ana tabia ya uwizi na awe ameniibia sa ngapi?!"




madam jane akajaribu kumtetea isack




"baada ya wewe kwenda chooni nami nlitoka nikakaacha chenyewe je muda ule awez kukuibia?!"




Madam Jane Akashtuka Akavuta Kumbukumbu Na Kukumbuka Muda Ule Alienda Kweli Chooni Aliporudi Akumkuta Isack Wala Mwalimu Yule,ila Baadaye Isack Alirejea Na Kipotabo Na Sigara,je Alipata Wapi Ela?!




"kakasachiwe Begi Lake.."




Wakati Mwalimu Isack Akiongea Hivyo Ghafla Kuna Mwanafunz Mmoja Akaingia Kuchukua Daftar Zilizokwisha Sahihishwa


"we Zahra Mwambie Isack Aje Na Begi Lake Huku"


Mwalimu Mwingine Wa Kike Kutoa Utata akamwagiza yule mwanafunz ambaye aliingia darasani na kumwambia isack anaitwa ofisini kwa walimu na begi lake!




maskin isack,pasina kujua tena akiwa na tabasamu akijua pengine madam anaenda kumfundisha pasina kufungua ata begi lile akalinyanyua na kulivaa huku akiruka ruka akakimbia kuelekea ofisini




ile kuingia tu walimu wote wakanyamaza na kumwangalia!




"embu lete begi lako hapa isack"




isack akampelekea madam jane begi lake lile madam akalifungua maskin akatoka na mfuko ule!




akaufungua taratibu!,bado isack akujua kinachoenda kutokea wala akujua kile kilichotokea




binadamu wabaya!,wanataka kuyaharibu maisha ya mtoto yule yatima je kawakosea nini mpaka kumfanyia visa vibaya namna ile mtoto mdogo vile?!




madam akuamin!




mtoto alompenda,alomlea kama mtoto wake,bado afadhiliki,bado anamuibia,na mbaya zaid ela ile ilikuwa imechenjiwa na si elf arobain bal ni elf thalathin na tisa na mia mbili akimaanisha kwamba mia tano ndo kanunua kipotabo na mia tatu ndo ya zile sigara mbili alizokuwa kashika!




'ahaaa ndo maana alivyorud na kunikuta alishtuka vile,kwa unyonge akaficha zile sigara eeh'




madam jane akawaza huku akiwa anapandisha hasira




'ama kwel bora umfadhil mbuzi utamnywa mchuzi binadamu wanamaudhi'.




Madam Akawaza Akipandisha Hasira Akanyanyua Uso Wake Kumtazama Isack!,machozi Yalimtawala Mtoto Yule Katika Paji Lake La Uso!




madam akaunyanyua mkono wake kwa nguvu akaushusha katika shavu la mtoto yule maskin!




paaaaaaa




Kilikua ni kibao kitakatifu,kilicho mfanya isack akapepesuka,nyotanyota akaziona hewani




"mtoto mpumbavu sana wewe nakuokoa kwa mangapi bado unaniibia nikuleaje lakini mimi isack,inafikia nayaweka maisha yangu rehani kwa ajili yako uthaminiki wewe si bora wangekuua tu wewe sasa inatosha ulimwengu utakufunza wewe..."




madam jane aliongea kwa ukali machoz yakimtiririka,akutegemea kama isack angeweza kumuibia yeye!,isack akapiga magoti huku akilia




"sijakuibia mimi mwalim"




"ni nani sasa?! vimefikaje huku katika begi lako kwanza njoo"




madam akamuinua na kuanza kumsachi akatoka na zile sigara!,kwani alizisahau katika mfuko wa suruali




walimu wakayatoa macho ya mshangao




mtoto wa darasa la nne anavuta sigara!




"hapana hizi ni mwalimu jana alintuma"




"mwalimu nani?!" mwalimu mwingine akauliza




"mwalimu gib.."




kabla hata ajamalizia gibson akadakia!




"akaaa we mtoto mimi nikutume wewe?,yani nilishasema hili toto chonganishi..."




"mwalimu wa nidhamu nakuachia kazi yako na isack kwanzia leo navunja msaada wangu wote juu yako,utatafuta pakuishi,pakula na utatafuta wa kukusomesha siwez lea jizi"




madam jane aliongea kwa hasia,isack alilia akipiga magoti asamehewe! mwalimu Gibson Akafungua Kabati Lililopo Ofisini Mule Na Kutoka Na Rundo La Fimbo Akamkabidhi Kila Mwalim Fimbo Yake




Isack Akaanza Kuchapwa!




Mwalimu Mkuu Akapewa Taharifa Ya Uwiz Aloutenda,kengele Ikagongwa Wanafunz Wote Wakakusanyika Mistarini Isack Akiwa Anachechemea Kwa Kipigo Kikali Alichopewa Akasimama Mbele Ya Wanafunzi Wote




Mwalimu Mkuu Akaruhusiwa Aongee!




Akaeleza Wazi Kumfuta Shule Isack Kwa Kitendo Chake Cha Uwizi!!...




Isack Alilia,alilia Kwa Uchungu Wanafunzi Wakamzomea




"mwanangu Hatuna Urithi Wa Kukupa Zaidi Ya Elimu Pekee,soma Kwa Bidii Ndiyo Ufunguo Wa Maisha Yako"




Akakumbuka Kauli Aloambiwa Na Baba Yake Mzee John! Leo Hii Anafukuzwa Shule Kwa Kosa La Wiz Ambalo Hata Ivyo Akulitenda Yeye!...




Taratibu Akapiga Magoti Mbele Ya Wanafunzi Wote




"walimu Wangu,wanafunzi Wenzangu Mimi Ni Yatima Nisiye Na Kimbilio Zaid Ya Elimu Pekee Nisameheni Sijaiba Wala Sina Tabia Hiyo Madam Nisamehe Mama"




"ni Ndani Ya Dakika Tano Inapaswa Usionekane Hili Eneo La Shule Tofaut Na Ivyo Tutapiga Simu Polisi Watakuja Kukuchukua Hapa Haya Wanafunzi Darasani"




Mwalimu Mkuu Akamaliza! Wanafunz Wakatawanyika Kurudi Madarasani




Isack Akaelekea Lilipo Geti La Kutokea Akatoka Zake Kila Mara Akigeuka Nyuma Kuitazama Shule Kama Kwamba Shule Ile Ingemwita


Alijidanganya Sana Kudhani Ivyo!


Shule Ilimuaga!...




Je Angeenda Wapi?!,angekimbilia Wapi!




Bila Ridhaa Ya Miguu Yake Akazidi Kusonga Kutoka Mtaa Ule Wa Shule!,alikuwa Akielekea Makaburini Kwa Wazazi Wake Akazilaumu Mait Za Wazaz Wake Kwa Kumzaa Na Kumuacha Katika Mateso Makali Kiasi Kile!...Akazidi Kusonga Dukuduku Likiwa Limemkaa Kooni








Maisha ya kijana Isack bado yamezungukwa na wimbi la mateso!,msaada pekee alokuwa akiutegemea nao umemtosa je ninin hatma ya maisha yake baada ya kufukuzwa shule na nyumbani kwa madam jane? twende pamoja kujua hatma ya mtoto huyu




*NA HII NI SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE*




Alizidi kupiga hatua zake fupi za kinyonge kuelekea yalipo makaburi ya wazazi wake!


alipofika aliinama kwanza akakata majani yalo ota juu yake! baada ya kuwaliza akiwa kapiga vilevile magoti akiwa katikati ya makaburi yale mawili akaanza kuongea kwa hisia akilitoa dukuduku lile lililokaa moyon...




"baba!,mama bila shaka uko mlipo mmepumzika,mmepumzika sijui kama mnajua maisha mwanenu ninayoishi,sidhani kama mngekuwa mnajua mngeniacha yatima niteseke kiasi hiki,roho yangu inasakwa itolewe kosa nikiwa silijui,eti baba! hata ule ufunguo wa elimu uloniachia nimenyang'anywa,nimefukuzwa shule baba,je ni upi urithi wangu sasa?!,nakuwa chokoraa mamaa wakat ulinikataza hata nisicheze nao mtahan leo naenda kuwa miongon mwao,ntafanyaje mama yang kwa nin mmeniachaaaa iiiii..."




Isack Akashindwa Vumilia Akaangua Kilio,alilia Kwa Uchungu,aliendelea Kulalamika Lakin Hapakuwa Na Lolote La Ziada Lililoendelea Taratibu Akajiinua Na Kuingia Rasmi Mtahani!...




jua lilikuwa kali,kila mtu akiendelea na shughuli yake pilikapilika zikitawala katikati ya jiji!




kutokana na kutembea sana kuchomwa na jua lile uchovu njaa vilimtawala,Isack akatafakari ale wapi kupambana na lile baa la njaa lilitoutafuna utumbo wake,akakosa jibu akuwa hata na sent tano mfukoni pengine angenunua chakula akala!,wazo lililo mjia ni kuingia kwenye magenge na kuomba apewe hata makoko!




kila genge aliloingia aliambiwa akale shule ama nyumbani kwao


jua lilikuwa kali,kila mtu akiendelea na shughuli yake pilikapilika zikitawala katikati ya jiji!




kutokana na kutembea sana kuchomwa na jua lile uchovu njaa vilimtawala,Isack akatafakari ale wapi kupambana na lile baa la njaa lilitoutafuna utumbo wake,akakosa jibu akuwa hata na sent tano mfukoni pengine angenunua kitu akala




,isack alikosa msosi,akatafuta mti wenye kivuli akaketi!




Bado Machozi Yalimchuruzika Kufikiria Hatma Ya Maisha Yake!




Je Usiku Ungefika Angejii hiifadhi wapi na kulala nje akuzoea?!




akavua begi lake na kutoa madaftari akaanza kukagua,alikuwa na hati nzur makosa ayakuonekana kwenye madaftar yale na tiki zilitawala!,alijijua kama angesoma lazima angefika mbali,ila aliishughudia elimu yake ikiishia pale!




tumbo lilinguruma kuitaji kitu,angelilisha nin,bila ridhaa ya mikono yake akaanza kuchana karatasi moja moja na kulitafuna,akalimeza,aliona makaratasi yale ndo chakula pekee! kwa muda ule ayakuwa na umuhimu tena!




"we mtoto wenzako wako shulen saiv wewe unadhurura mtahani!"




ghafla akashtuliwa na sauti kali ya mzee mmoja aliyekuwa akija uelekeo wake




tena mkononi alishika fimbo ilo nyooka baraabarra




mzee yule alikuwa na kumbukumbu katika kikao cha wananchi kilichofanyika wiki mbili kadhaa nyuma kutokana na utoro wa wanafunz mashuleni basi kila mzazi akimuona mtoto mtahani anadhurura amchape na ikiwezekana amrejeshe shuleni na isack bado alikuwa na 'uniform' tena zikiwa bado safi!




Isack Baada Ya Kumuona Mzazi Yule Akimjia Kwa Kasi Huku Kashikilia Fimbo Akajinyanyua Kwa Haraka Pasina Kujali Begi Lake Akaanza Kukimbia Mzaz Yule Akaokota Lile Begi Na Kuondoka Zake Akuwa Na Muda Wa Kumfukuzia Isack...




Jioni Mtoto Wake Aliwasili Akitokea Shuleni!,.




"pole na masomo mwanangu na leo nimekununulia begi na madaftari ulokuwa ukinsumbua kila mara!"




Mzee Yule Aliongea Akishika Begi Lile Lililokuwa La Isack Aloondoka Nalo Kule Mtahani!




Mtoto Wake Yule Akaachia Tabasamu!




"tena Baba Begi Kama La Rafiki Yangu Isack!"




Mtoto Yule Akaongea Kwa Furaha Akilitazama Begi Lile,na Ghafla Akakunja Sura!




Ni Kama Alikumbuka Kitu!,ndiyo Alimkumbuka Rafiki Yake Isack Alokuwa Kafukuzwa Shule Kwa Madai Ya Wizi,mtoto Yule Alijua Kila Kitu!




"mh Bray Nin Tena Mbona Ghafla Umebadilika?!"




Baba Yake Akauliza Baada Ya Kuona Mabadiliko Ya Mwanae,




"hapana Baba Amna Kitu!".....




Bray Akajibu Kwa Wasiwasi Akafungua Begi Lile Na Kutoa Daftar Ambapo Alizijua Fika!




"baba Umetoa Wapi Hili Begi La Isack?!"




"isack?,isack Gani!"




Baba Yake Bray Akauliza Aibu Ikianza Kumtawala Kwa Kugunduliwa Uongo Wake Na Mwanaye




"alikuwa Rafiki Yangu Baba Ila Leo Asb Kafukuzwa Shule Na Mwalimu Mkuu Baada Ya Kumuibia Mwalimu Simu Na Ela."




Bray Akajibu Akiukwepa Kuusema Ukwel Kwamba Ela Na Hata Simu Zile Alipewa Na Mwalimu Gibson Amwekee Mtoto Yule Ili Yeye Aonekane Mwizi Akihofia Kupokea Kipondo Kikali Kutoka Kwa Mzee Wake!




"ni Mara Ngapi Nimekukataza Kuunga Urafiki Na Watoto Wezi?!"


Mzee Akauliza Kwa Ukali!




"nisamehe Baba"




"Basi Sawa,ilo Jizi Nimelikuta Mtahani Nilipotaka Kumfata Ndipo Likakimbia Na Kuacha Begi Lake Siyo Ishu Utachomoa Dalajio Lake Utaweka Lako Na Hizi Karatasi Alizoandikia Utazichana Sawa?!"




"sawa Baba!"




Bray Aliitika Huku Akibandua madalajio yaliyojaladia madaftari yale!;...




ISACK MTAHANI:




Mpaka Muda Ule Wa Jion Isack Alikuwa Bado Ajatia Kitu Mdomoni,


Kila Alipopita Kuomba Chakula Alinyimwa Na Mwisho Aliamua Kuomba Vibarua Kama Kuosha Vyombo Kudeki Na Mshahara Apewe Tu Chakula Lakin Akuna Alomjali!




"we Mtoto Tena Mwanafunzi Upewe Kaz?! Embu Nenda Nyumbani Unatafutwa Sasa"




Kila Alipopita Kuomba Aliishia Kuambiwa Ivyo Na Kuchekwa Hiyo Yote Ni Kutokana Na Utanashati Alokuwa Nao Sindo Siku Ya Kwanza Hata Kuchafuka Ilikuwa Ajachafuka




Jioni Ile Hali Ya Hewa Ilianza Kubadilika,wingu Zito Kutanda,upepo Mkali Ulivuma,isack Alianza Kutetemeka Pasina Kujua Kama Mvua Ile Inges




huka ni wapi angejistiri!




'isack! mwalimu ni mpole anakupenda nenda kamwambie ukweli mbona atakuelewa tu'




nafsi yake ikamsihi akawaza kidogo,akaona aifate nafsi ile,taratibu akaanza kusonga kuelekea makazi ya madam wake!




ghafla radi likaanza kupiga na taratibu mvua kubwa ikaanza kunyesha!,




Isack Akaona Bora Sasa Akimbie Ile Si Mvua Ya Kukata!,akakata Mitaa Miwili Mitatu Akaingia Katika Mtaa Wa Mwalimu Wake Yule!




Madam Jane!




Madam Pekee Alomtegemea,akalifikia Geti Kwa Bahati Nzur Lilikuwa Waz Akazama Ndani! Alipopokelewa Na Ua Mkubwa,




Akaelekea Katika Mlango Wa Kuingilia Varandan Na Kuugonga Huku Akitetemeka!,akimuomba Mungu Kimoyo Moyo Madam Amwelewe Tu!




SURA YA KUMI




SEBULENI KWA MADAMU




Ni Hali Ya Kutokuweza Kuamini Kwako Ndugu Msomaji! Ila Ndo Hali Halisi,


Sebuleni Kwa Madam Jane Katika Kochi Walikwepo Watu Wawili Jinsia Tofauti Katika Hali Ya Kimapenz Wakifuraishana Juu Ya Kochi Lile




Wakiume Alikuwa Ni Mwalimu Gibson Wakike Akiwa Ni Madam Jane!,penzi Lao Lilianza Siku Hiyo Hiyo Ila Utadhan Ni Watu Waliyozoeana Muda Mrefu




"mmmh Mwalimu Kumbe Ulikuwa Una Haki Ya Kumchukia Yule Mtoto Mwanzo Alikuwa Akivuta Bangi Nikamsema Nikajua Kaacha,kumbe Anavuta Sigara Na Mpaka Anadiriki Kuniibia?!...




Madam Jane Aliongea Kwa Uchungu Akiwa Kalala Mapajani Kwa Mwalimu Gibson Naye Akizichezea Nywele Zake Taratibu




"mimi Naijua Saikology Vizur Mpz!,na Ndo Maana Hata Hisia Zako Kwangu Nilizitambua Mapema,na Kama Si Yeye Mapema Tu Tungeshakuwa Wapenz Ila Yeye Alizifunika Hisia Zangu Kwako Mim Nilikuwa Katika Kumjenga Madam.."




"kwa Sasa Atengenezeki Yule,wazaz Wake Wamemshindwa,mimi Nimemshindwa Jamii Sasa Itamfundisha Ningeendelea Kumfuga Si Angeniibia Mpaka Vitu Ndani"




"haswaaa!...,kabla Mwalimu Gibson Ajaongea Jambo Jingine Wakaskia Mlango Kugongwa Madam Akanyanyuka Ila Gibson Alimvuta Mkono Akamkalisha,




" wacha nikafungue Mimi"






Jinamizi La Mateso Bado Linazidi Kumuandama Mtoto Isack,anakosa Shule,anakosa Pa Kulala Mtoto Yule,anakosa Chakula,anakosa Hata Wa Kumfariji,kimbilio Pekee Ana Amua Kurudi Kwa Madam Jane Mvua Kubwa Ikiwa Inanyesha Anabisha Hodi Mlango Unafunguliwa Ni Mwalimu Hitlar Je Nin Kitaendelea?! Twende Pamoja Kujua Hatma Ya Maisha Ya Mtoto Huyo




*NA HII NI SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA*




"ehe wewe mtoto unataka nini hapa?!"




mwalimu Gibson Akapayuka Kwa Ukali Akionekana Wazi Kukasirika


"nisamehe Mwalimu,naomba Niombee Msamaha Kwa Madam Ansamehe Mimi Si Mwizi!"




"ishia Hapo Hapo Nlisha Kukataza Kuja Hapa Kwangu Naomba


uondoke haraka sana,"




madam aliongea kwa ukali,Isack Akakimbia Kupiga Magoti Akimshika Mwalimu Yule Miguu Huku Akilia!




"nisamehe Madam Kwel Mimi Sikukuibia,sina Tabia Hiyo Mimi Ntaenda Wapi Sasa Niurumie Madam"




"kwani Mimi Nisingekwepo Ungeenda Wapi?!,kama Leo Hii Unaniibia Si Utaniibia Mpaka Ndani?,sasa Dunia Itakufunza Nakwambia Mpz Tuondoke Zetu!"




Kabla Ajageuka Madam ,isack Akamdaka Siketi Yake,madam Huku Akiwa Kakunja Sura Akageuka Na Kumpiga Kibao Sambamba Na Kumsukuma Isack Akadondokea Kwenye Mvua Madam Akaingia Ndan Wakiubana Mlango!




"hivi Kwel Mungu Upo? Kwanin Unaruhusu Mateso Kama Haya Kwangu mja wako,kosa langu lipi hasa?!,mvua ni yang lipi kusudio lako kwangu Mungu Wangu,natanga Na Njia Naangaika Lakin Mungu Ukoo Tabu Juu Ya Tabu Mateso Juu Ya Mateso..."




Isack Aliendelea Kuomboleza Akiwa Katikati Ya Mvua Kapiga Magoti Chini Machozi Yakimchuruzika Kama Bomba La Maji!




Angekimbilia Wapi Sasa?!,angejificha Wapi Sasa Dhidi Ya Mvua Ile,akanyanyuka Na Kwenda Taratibu Mpaka Ndani Ya Banda La Kuku Alokuwaga Akilifanyia Usafi Akalifungua Na Kuingia Hata Alale!




Kuku Si Wakaanza Kupiga Kelele Bwana,awana Siri Wale Viumbe Kama Ukiingia Kwenye Himaya Yao!...




Madam Jane Wakiwa Bado Wanakula Raha na mwalimu Gibson,wakiifurahia Mvua Ile Ghafla Wakasikia Kuku Wakilia!




"atakuwa Ni Paka Nin?"




Mwalimu Gibson Akatamka,kwa Wasiwas




"paka Atoke Wap Litakuwa Ni Lile Jizi,linaiba Kuku Embu Twende"




Wakajinyanyua Kuelekea Sebuleni Wakafungua Mlango Mwalimu Gibson Akachukua Fimbo Kubwa,kuni,huku Akinyata Akaelekea Lilipo Banda La Kuku




Ni Mwalimu Alojaliwa Roho Mbaya Tena Ilopitiliza!




"haya Toka Acha Awo Kuku Toka Haraka Alaaa"


Akapayuka Isack Taratibu Akatoka Ila Mwalimu Alimdaka Na Kumshushia Lile Fimbo Kisogon Isack Akatua Chini Kama Mzigo,akatulia Tuli!




"umeua Mwalimu"




Madam Jane Aliongea Kwa Sauti ndogo ilojaa uwoga!




"shhhh!!! nyamaza hii kesi yetu sote tutafute jins ya kuuzika u mwili"


mwalimu gibson akaongea kwa kujiamin jambo lililozidi kumtia khofu madam yule!


"tutamzika wapi sasa?!"




"maneno si ndo hayo!,lete sururu nikachimbe huko nyuma ya nyumba usiku huu huu tunamzika"




"hakuna kuna jembe tu"




"lete hata ilo haraka muda unazidi kwenda"




madam haraka akaingia ndani alipotoka alikuwa na jembe akamkabidhi mwalimu gibson jembe lile




pasina kujal mvua akatoka nje na kuanza kuchimba shimo nje nyuma ya nyumba ile!...




kutokana na khofu akuchimba shimo kubwa sana akarudi ndani alipombeba mtoto yule begani na kutoka naye nje!




alimtua kwenye shimo lile ila kabla ajamfukia,ghafla isack akafumbua macho!




mwalimu gibson alishtuka,pasina kuamin kile kilichotokea,ujasiri ukamtoka na ghafla woga ukamvaa akajikuta akikimbilia ndani




Isack Akujua Kile Kilichotokea Akajinyanyua Katika Shimo Lile,pasina Kuamin Macho Yake Alijua Waz Yeye Ndo Ilipaswa Afukiwe,baada Ya Kupoteza Fahamu,kichwa Kilikuwa Kizito Taratibu Akaunyanyua Mguu Wake Kuondoka Eneo Lile,alimchukia Mwalimu Gibson,alimchukia Madam Jane,aliwachukia Binadamu Wote!




Aliamua Kuyakabili Maisha Ya Mtahani Itakavyokuwa Na Iwe,alijua Mungu Anamakusudio


ya kumuacha hai mpaka muda ule!,alienda akasimama kwenye baraza ya nyumba moja ,akajikunyata,alitetemeka kwa baridi,nguo zote zililoa na zilinyunyuzika maji aliamua kutulia pale pale! mpaka kutakapopambazuka acheki ustaharabu mwingine!




mwalimu gibson aliingia ndani akaufunga mlango madam jane alimshangaa!




"nini sasa babaa"




madam jane akamuuliza nay akianza kushikwa na wasiwasi!




"yule mtoto kabla sijamfukia si kafufuka!"




"atii?,kafufuka?!, kafufukaje?"




ikabidi mwalimu gibson aanze kumsimulia madam jane akaachia kicheko!




"itakuwa akufa yule alizimia tu nasi kwa kuwa tulipeleka mawazo kule tukajua amekufa Ana Mungu Yule"




Gibson Naye Akaachia Kicheko,




"aswaaaa Ndivyo Ilivyokuwa!..."




"basi Mpz Wangu Vua Hizo Nguo Sasa Zimeloana Sana Sijui Kesho Utavaa Nin!..."




Mwalim Gibson Akapewa Taulo Akavaa Nguo Zikaanikwa Bafuni!




Wakaelekea Chumbani Kulala




Asb Wakwanza Kuamka Ni Madam Jane Akaelekea Mpaka Bafuni Bado Nguo Zilikuwa Mbichi Akazitoa Nje Na Kuzianika,muda Ule Ule Akapanda Gari Mpaka Duka La Nguo Akanunua Shati La Bei Ghal Zuri,suruali,na Viatu Pasina Kusahau Soksi


Akarudi Nyumban Akavipiga Pasi,na Kuviandaa




Akaelekea Ndani Ambapo Mwalim Gibson Bado Alikuwa Kalala Akamuamsha!


gibson Kitu Cha kwanza kutazama ni nguo zake!,alishtuka alipozikuta bado mbichi!




"usijal mume wangu utavaa hiz" alishtushwa na sauti ya madam jane,akaachia kicheko hafifu na kwenda kumkumbatia mwanamke wake yule




"hakika wewe u mwanamke bora tena unajua wajib wako nakupenda jane"




Jane akaishia tu kutabasamu,mwalimu Gibson Akaingia Bafuni Akaoga Akavaa Wakakaa Mezani Kupata Chai Na Baada Ya Hapo Wakaingia Kwenye Gari La Madam Jane Tayari Kwa Safari Ya Kuelekea Shuleni!




"vipi Madam Mbona Ujanipa Ripoti Zozote Kuhusu Yule Mtoto?"




Ghafla Meseji Ikaingia Katika Simu Ya Madam Jane Alikuwa Ni Insp Nurdin,madam Akaisoma Na Kuachia Mguno




"mbona Unaguna Mpz"




Mwalim Gibson Akamuuliza Kwa Sauti Nzito Na Kabla Ajajibu Insp Nurdin Akampigia Kabisa




"yule Mtoto Sipo Nae Tena,kawa Jambazi,mdokoz Shule Kafkuzwa Na Kwangu Pia Nimemfukuza"




"astaghafirullah Madam Lakin Si Unajua Anasakwa Yule Atauwawa Eti!?"




"wamuue Tu Ila Mi Siwez Kulea Jizi!"




"ungemleta Kwangu Nimnyooshe Lakin Si Kumfukuza Hali Ya Kuwa Unajua Fika Maisha Yake Yapo Hatarin"




"bwana Eeeh Kamsake Mtahan Ukae Naye Mbona Hata Wewe Waweza Kumlea?"




Baada Ya Maneno Yale Madam Yule Akakata Simu!,




"ninin Mpz?!" Mwalim Gibson Aliyekwepo Pembeni Yake Akamuoji Jane Ikabidi Amsimulie!


"akamtafute amlee basi kama ana uchungu nae"


baada ya kusimuliwa kila kitu mwalim gibson akaongea kwa kujiamin! walikaribia kufika shuleni:




****




Insp Nurdin Alichukia Kwa Kile Alichoambiwa Na Madam Jane Binafsi Alijikuta Akihitaji Kumsaidia Yule Mtoto,akiwa Baba Wa Mtoto Mmoja Aloitwa Ramadhani Aliish Yeye Na Mke Wake Bi Saumu Katika Nyumba Ya Kota Pango La Maaskari,aliamua Kuingia Rasmi Uraiani Kumsaka Isack Kusudi Aishi Naye Mtoto Yule Kukaa Mtahan Alijua Maadui Zake Wangemuua Kirahisi Alimjua Fika Zidu K Na Alikuwa Akimsaka Kwa Muda Mrefu! Je Angempata Uko Mtahani?!...




***




MCHANA




Njaa sasa ilimuuma,toka jana yake asb ndo aliweza kuingiza kitu mdomon mpaka muda huo akula na wala akujua angekula nin!


alikaa pemben ya dampo na watoto wengine wakisubiri magari ya mataka taka yaje yamwage uchafu wagombanie machakula ndo wale! ni maisha alopaswa ayazoee hayo!




wakati wewe ukitupa chakula eti umeshiba,jua yupo anaekitafuta na anakikosa!




wakati wakiwa katika subira ile ghafla ikaja gari nyeus yenye vioo vya tinted watoto wote wakaikimbilia ile gar wakitaja anko kinampa huyo isack akuwa nyuma kuunga tela




"leo nataka mtoto mmoja tu"




kijana mmoja alokuwa ndan ya gari ile baada ya




kushusha kioo akatamka kwa furaha watoto wakadakia wakisukumana




"mimi anko,..mimi..,mimi mim anko"




Isack akabaki ametumbua macho akishangaa akujua anko yule ninin watoto wanachompendea




"ok! leo namchukua yuleee mdogo kuliko wote"




jamaa yule kwenye gari akaongea akimnyooshea kidole Isack!




Isack Akabak Ameganda




Akapiga Hatua Kulisogelea Gari Akapanda,vioo Vikafungwa Gari Ilooo Likaondoka!.








Nikijana Alizekuwa Na Ndoto Kubwa Sana Maishan Kwa Miaka Ya Badae Ila Binadamu Wanazikatisha Ndoto Zake Na Hatimaye Kuangukia Kuwa Mtoto Wa Mtahani Alimaharufu Kama Chokoraa! Je Unajua Ni Nin Hatma Ya Maisha Yake?! Twende Pamoja Kuimalizia Hii Sezon One Kujua Nin Kilichoendelea




*NA HII NI SEHEMU YA THALATHIN*




"Kaka kwani ni wapi tunaenda?!"




ilibidi isack aulize baada ya kuona wanazidi kuelekea katikati ya jiji!,kinampa akamkata jicho hapo hapo akatabasamu kumtoa khof




"una muda gani toka uingie mtahani!"




badala ya kujibu swali la mtoto yule naye akampachika lake!




"ni leo tu!"




Isack Akajibu Haraka!..




Kinampa Akaachia Tabasamu!




"nadhani Wenzako Awajakupa Maelekezo Sawa Ni Kwamba Kuna Kaz Utansaidia Na Ntakusaidia Vizuri Ok?!"




"kaz Gan Anko?!"




Isack Akaoji Kwa Wasiwasi!




"usijal Utaijua Tu!"




Kinampa Akajibu Akisimamisha Gari Lake Katika Duka Flan La Jumla Akatoka Na Kuingia Ndani Ya Duka Lile Dakika Chache Aliporejea Alikuwa Na Box Kubwa Yale Ya Tv Akaliweka Ndan Ya Buti Akawasha Gari Na Kuondoka!




Safar Yake Iliishia Katika Nyumba Yake Kubwa,akamkaribisha Isack Sebulen,kinampa Naye Aliishi Peke Yake Katika Jumba Lile!




"pumzika Hapo Uangalie Tv Mi Nishughulikie Msosi!"




Kinampa Akaingia Jikoni,nusu Saa Badaye walikuwa mezani wakipata chakula,




"umeona lile box mdogo wangu?"




Isack Akatingisha Kichwa Kuafiki




"unajua Kwa Nini Nimekuchagua Wewe Na Sijawachagua Wale?"




"hapana Anko"




"kwa Kuwa Wewe Ni Mdogo Na Unaenea Vizuri Kwenye Lile Box Ntakuingiza Ndan Ya Box Lile Na Kuna Duka Uck Ntakupeleka Na Kukuombea Kukuifadh Kama Bidhaa Ukiwa Ndan Uck Huo Unatakiwa Utoke Uibe Pesa Zote Na Urudi Ndan Ya Box Asb Ntaja Kukuchukua Sawa?"




Isack Alitingisha Kichwa Kuafiki Ila Moyon Mwake Alitetemeka,akujua Kama Angeweza Fanya Kazi Ile,akuamin Kama Hiki Ndicho Watoto Walichompendea Kinampa!




Ilipofika Usiku Kwel Akaingizwa




Ndani Ya Box,kijana Yule Wa Mjini Akabeba Box Lake Na Kulisweka Ndani Ya Buti Akaingia Ndani Ya Gari Yake Na Kuliondoa Gari Kwa Kasi Kuelekea Katikakat Ya Jiji!




Lilikuwa Ni Duka Kubwa Lililomilikiwa Na Muhind Rajit Sanjeed Duka Hilo Liliuza Tv,laptop,kompyuta,redio Aina Ya Sabufa,deki Mbalimbali Mida Hiyo Ya Saa Tatu Usiku Kinampa Alishuka Kwenye Gari Yake Na Kuingia Ndani Ya Duka Lile,akachagua Tv Nzuri Akailipia Kabisa!


"sasa Mzee Ntakuja Kuichukua Kesho Asb Na Na Tv Nyingine Naomb Niifadhie"




"sawa! Sawa Hapana Kuwa Na Shida Yoyote We Lete Tu!"




Kinampa Akaliendea Gari Lake Akafungua Buti Na Kutoka na


box lile ambalo ndani alimuifadhi mtoto isack!,muhindi yule akamuonesha mahali pa kuliweka akiliweka juu ya lile alilolinunua




kijana wa mjin kinampa akaaga na kuondoka,




Hata Ivyo Ulikuwa Ndo Muda Wa Muhindi Yule Kufunga Duka Lake Lile,akafunga Hesabu Na Kufunga Duka Huyo Akaondoka Zake!




Usiku Isack Akatoka Ndani Ya Box Lile Na Ufunguo Malaya Wake Alopewa Na Kijana Wa Mjini Anko Kinampa! Akalifuata Droo Na Kulifungua Akuamin Alichoona,akajaza Kwenye Mfuko Wa Malboro Kisha Akafunga Kama Alivyokuta Na Kurudi Ndan Ya Box!




Asb Na Mapema Hata Kabla Muhindi Yule Ajaja Kinampa Alikuwa Nje Ya Geti Ya Duka


Lile,lililomilikiwa Na Muhindi Rajit Baada Ya Kama Robo Saa Hivi Muhindi Yule Aliwasili Kwenye Gari Yake




"naona Iko Wai Sana Wewe"




Muhindi Yule Alimsemesha Kinampa Akiwa Katika Tabasamu! Huku Akiliendea Geti La Duka Lake Na Kulifungua




"yah Mzee Si Unajua Sa Mbili Naingia Kazini Na Kutoka Usiku Ivyo Nimeona Niwai Kuchukua Nipeleke Nyumban Kabla Sijaenda Kazini"




"iko Fanya Vizur Sana Aya Box Yako Mbili Ile Pale"




Mhindi Rajeet Alitamka Akimnyooshea Kidole Box Mbili Kinampa Akazifata Na Kubeba Ya Juu Akaenda Kuiweka Katika Buti Akarudia Box Lile La Tv Nalo Akalibeba,akafunga Buti Na Kuliondoa Gari Lake Kutoka maeneo yale,




huku nyuma muhindi rajeet alipofungua droo zile akuamin alichokiona droo zilikuwa tupu,ni zaidi ya milioni tano,akujua aliibiwaje,katu akumfikiria kinampa,akuona pia sababu ya kwenda polis ni vipi angetoa maelezo?,akabaki katika simanzi,akiushirikisha na moyo wake!




kwa upande wa kinampa alifrah sana dili lake lilienda kama alivyopanga!




"vizuri sana mtoto sasa shika hii itakusaidia siku mbili tatu nikiwa na shida na wewe ntaja kukuchukua tena pale maskan sawa?"


kinampa aliongea kwa furaha akimpa elf thalathin kumi kumi tat




"asant anko"




"si umeshiba lakini?"




"ndiyo anko"




"uifadhi ela yako vizuri uwasaidie na wenzako sawa?!"




"sawa mjomba"




wakaingia ndani ya gari,tayari kinampa kumrejesha Isack Kule Alipomtoa!




Hii Ndo Ilikuwa Kawaida Yake Akiwatumia Watoto Wale Wa Mtahani Kwa Maslah Yake Binafsi Akiwatoa Kiasi Kidogo Cha Ela!


Alipofika Katika Dampo Lile Alishuka Kwenye Gari Akishangiliwa Na Wenzake,kinampa Akaondoka Akihaidi Kurejea Siku Ingine!




Watoto Wale,walo Litawala Dampo Lile Walikuwa Jumla Ya Kumi,waliishi Kwa Upendo Ivyo Isack Alinunua Mikate Na Juisi Za Miatano Miatano Wakafrah!




Isack Alikuwa Ndo Mdogo Kati Ya Wote,mkubwa Wao Kabisa Alitambulika Kwa Jina La Bedu




hakuna alojua jina lake kamili,na hata historia ya maisha yake ilikuwa siri yake,bedu aliyekuwa na miaka kama kumi na tano alikuwa na wadogo zake wawil wa kike!,sita walobakia wote walikuwa wakiume wote wakiwa ni mayatima walokosa msaada katika familia zao!




"isack!" bedu akaita




"naam kaka!" isack akaitika kwa upole alimheshimu sana kaka yao yule alodumisha upendo katika dampo lile




"jana baada ya wewe kuondoka na anko si alikuja pai hapa kuku ulizia na ana kusaka kinyama"




isack alishtuka!,ni kwel baada ya yeye kuondoka na kinampa aliwasili insp Nurdin Akiwa Katika Sare Za Jeshi Kumuulizia! Wote Walikana kumfahamu lengo kumlinda hakuna alohis kwamba insp nurdin alimuhitaj isack kwa kumsaidia!




"uwe makini katika mienendo yako"




BEDU akazidi mshauri isack,siku zikaenda hatimaye ela ile ya Isack Ikaisha,maisha Yakaanza Kubana




"ndugu Zangu!.."




Bedu Akawaita Ndugu Zake,ni Kijana Ambaye Muda Mwingi Alikuwa Na Mawazo Vijana Wote Wakasogea Kumsikiliza Bedu Akaendelea...




"mdogo Wangu Ana,selina,john,isack,mkude,martin,juma,samwel Na Wewe Samson Nadhan Mnaona Jins Jamii Ilivyotutenga,mim Nadhan Ndo Mkubwa Wenu Na Mnanitegemea Tutaish Hivi Mpaka Lini Tunakula Vizur Siku Tatu Tunateseka Miez,jamii Ishatutenga sisi hata tukiomba hatupewi je tutaish hivi mpaka lini?!,kama wametutenga nasi tubadilike,tusicheke na kiumbe atakayepita kona hii ama zake ama zetu kila atakachokuwa nacho halali yetu ndo maisha tutakayoamua kuishi ama mnasemaje?"


bedu akamaliza,wote awakuwa wapinzani wakaungana mkono kuianza kazi!




"na kazi tunaianza muda huu apitaye ama zake ama zetu"




wakakubaliana na kwa bahati kuna mdada aliyekuwa akija kashika simu na ki begi wakapeana ishara dada yule alipowafikia wakamzunguka na kuanza kumtisha kabla awajamuibia yule mdada akaanza kupiga kelele mwizi raia wakawa wakija kwa kasi,machokoraa wale kuona vile wakakimbia ila kwa bahati mbaya isack akakamatwa! na yule dada si ndo alikuwa mdogo kuliko wote!




raia wakamzunguka,akaanza kupigwa


wakati akiendelea kupigwa gari ya kifahari ikasimama madam jane akashuka pemben yake akiwepo mwalimu gibson,awakupiga hatua wakasimama palepale nje ya mlango wa gari lao!




"ama kwel asiye funzwa na mama ufunzwa na ulimwengu"




madam jane akaongea kwa sauti akiangalia jinsi isach alivyokuwa akiadhibiwa!




mwalimu gibson akatabasamu akashika simu yake kuchukua video tukio lile,kuna mtu alitaka amtumie!...




kelele zikaendelea




"leten tairi tumchome!"




sauti kali ikaskika,akuwa mwingine alotoa sauti ile zaidi ya zidu,ndiyo Zidu Katili,madam Jane Akamchek Akamkumbuka Akaishia Kucheka Na Kwenda Nyuma Ya Gari Yake Akatoa Tairi Spea! Na Petrol Akampa Mwalimu Gibson Apeleke




Mwenyewe Akutaka Kushughudia Tukio Lile La Kuunguzwa Mtu Huyooo Akawasha Gari Na Kuondoka!




Huku Nyuma Sasa Isack Akavalishwa Tairi!...




Akamwagiwa Petrol!




Zidu Akawasha Njiti Kwenye Kiberiti Akatupa Kwenye Tairi Lile Alovalishwa Isack Watu Wote Wakasambaratika Wakiacha Moto Ukiwaka Mkubwa!




MWISHO




HII NDO MWISHO WA SEAsON NO MOJA ENDELEA KUSOMA SEASON 2


0 comments:

Post a Comment

Blog