Search This Blog

Saturday 24 December 2022

LA ULTIMA LETRA - 3

   http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/la-ultima-letra.html

Simulizi :  La Ultima Letra

Sehemu Ya Tatu (3)



Agizo kuu ambalo walikuwa wamepewa ilikuwa ni kusambaratisha mawakala wote wa Sinaloa Cartel ambayo ilikuwa chini ya El Chapo.

Makamanda wa Los Zetas walipoingia katika miji waliyopangiwa walifanya kazi kama Kikosi maalumu cha kijeshi cha wanamaji wa marekani (Navy SEALs) kutokana na mbinu walizotumia na ufanisi wa hali ya juu katika kutekeleza matukio yao.


Kwanza kabisa walikusanya taarifa za muhusika (wakala wa Sinoloa Cartel na wenzanke katika mji husika) kwa mbinu za 'kishushushu'. Walikusanya taarifa na kujua kila nukta ya maisha ya mtu wanayemlenga. Walijua mahali anapoishi, familia yake, sehemu anazopenda kutembelea, mahusiano ya kimapenzi na wanawake wengine zaidi ya mke wake kama ameoa, n.k.


Baada ya kujipatia taarifa za kutosha, Kamanda wa Los Zetas na 'malaika wake' walimteka muhusika na kutokomea nae mahali kusikojulikana. Wakiwa huko, wanamtesa muhusika kwa siku kadhaa ili atoe siri za viongozi wa Sinaloa Cartel pamoja na washirika wao.


Baada ya mateso ya siku kadhaa kinafuata kitendo cha kinyama ambacho ndicho hasa kinaifanya nchi nzima ya Mexico kuwaogopa Los Zetes na kuifanya nchi kuwa kama Jehanum duniani.


Muhusika aliyetekwa pamoja na wenzake wanaingizwa kwenye chumba maalumu wakiwa wamefungwa vitambaa vyeusi usoni. Wanaongozwa mpaka kwenye ukuta mmoja wapo wa chumba hicho ambapo kwente ukuta kunakuwa na kitambaa kikubwa cheupe kimening'ninizwa kwenye kuta kikiwa na maandishi ya kuisifu Los Zetas.

Baada ya hapo mtu huyu na wenzake waliotekwa wanapigishwa magoti mbele ya kitambaa hicho na Camera ya kurekodi video inawashwa.


Baada ya Camera kuwashwa Makamnda wa Los Zetas wakiwa wameficha sura zao kwa kuvaa 'kininja' wanatoa maelezo ya kuwaonya wanachama wengine wa Sinaloa Cartel kuwa kitakachotokea muda huo ndicho hicho hicho pia kitawakuta wanachama wengine wote wa Sinaloa Cartel kwenye kila pembe ya Mexico.


Kisha Makamanda na 'malaika' wao wanachukua sime na kuwakata vichwa mateka wao mmoja baada ya mwingine kama wanachinja Kuku na tukio hili linarekodiwa kwa ufasaha kwenye video na baadae video hiyo inawekwa kwenye mtandao kufikisha Ujumbe kwa ulimwengu mzima na Mara nyingi miili ya waliochinjwa ulitupwa katika barabara kuu au kuning'inizwa kwenye madaraja.


Matukio haya yaliyotekelezwa na Los Zetas yalileta taharuki ndani ya Mexico kwani matukio yalitekelezwa katika tarikbani miji 15 ya Mexico ambapo makamanda hawa na 'malaika' zao walitawanywa.


Ndani ta miezi michache taharuki ilikuwa kubwa kiasi kwamba washirika na mawakala wa magenge mengine ya mihadarati walidiriki kuyakana magenge yao na kujiung na Gulf Cartel kwa kuogopa kuchinjwa hadharani Los Zetas na kikundi cha ulinzi cha Gulf Cartel.


Pamoja na mamilioni ya madola waliyokuwa wanalipwa Los Zetas kutoka kwa Gulf Cartel, wakaamua watumie mbinu na uwezo wao wa kijeshi kujiongezea mamilioni zaidi.


Los Zetas wakaanzisha mfumo ulioitwa "Pisos".

Mfumo ambao ulikuja kuigwa na magenge mengine karibia yote hapo baadae.




SEHEMU YA PILI.


Los Zetas wakaanzisha mfumo ulioitwa "Pisos".

Mfumo ambao ulikuja kuigwa na magenge mengine hapo baadae.

Pisos ulikuwa ni mfumo ambao, Los Zetas katika maeneo yote ambayo walipangiwa kwenda kusambaratisha magenge mengine, hawakuishia hapo tu bali walihakikisha kuwa katika miji yote waliyokuwepo wafanyabiashara wengine wote wanaofanya biashara za haramu (hata kama sio madawa ya kulevya) wanalipa 'kipande' kwao ili waendelee na biashara zao za haramu.


Yaani kwa mfano wamiliki wa madanguro ya makahaba, au watu waliouza bidhaa 'feki' ikikuwa ni lazima wapeleke kipande kwa Los Zetas kila mwisho wa wiki ili waendelee na biashara katika eneo hilo.


Na kwa upande wa biashara ya madawa ya kulevya ni mawakala wa mabosi wao wa Gulf Cartel pekee ndio waliruhusiwa kufanya biashara hiyo kwenye eneo ambalo Los Zetas walikuwepo.



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog