Search This Blog

Saturday 24 December 2022

WAUAJI WALITUMIA, CHAI, MIAVULI NA HATA SUMU KUWAANGAMIZA WAPINZANI - 2

   http://pseudepigraphas.blogspot.com/2020/06/wauaji-walitumia-chai-miavuli-na-hata_10.html

Simulizi :  Wauaji Walitumia, Chai, Miavuli Na  Hata Sumu Kuwaangamiza Wapinzani 

Sehemu Ya Pili (2)


Chai ya sumu ya Polonium

Kifo cha Alexander Litvinenko's kinadaiwa kuwa cha mtu maarufu katika miaka ya hivi karibuni.


Jasusi huyo wa Urusi alianza kuugua mnamo tarehe 1 mwezi Novemba 2006, saa chache tu baada ya kunywa chai katika hoteli ya Millenium huko Mayfair pamoja na majasusi wenzake wawili.


Baada ya kifo chake majasusi hao ndio waliokuwa washukiwa wakuu katika kifo chake.


Alexander Litvinenko alitiliwa chai iliowekwa sumu ya Polonium 210

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Alexander Litvinenko alitiliwa chai iliowekwa sumu ya Polonium 210


Wakati bwana Litvinenko alipolazwa hospitalini mnamo tarehe 3 mwezi Novemba aliwaambia madaktari amepewa sumu.


Baadaye, alimtaja rais Vladmir Putin akisema ''ndiye aliyesababisha kifo chake''.


Wakati huohuo nywele zake zilianza kuanguka huku viungo vyake vya mwilini vikishindwa kufanya kazi-huku madaktari katika hosptali ya chuo kikuu cha London nchini Uingereza wakishindwa kupata chanzo.


Baadaye ilibainika ni nini kilichomuua kwani wanasayansi bingwa wa Uingereza wanaofanya utafiti wa zana za nyuklia huko Aldermaston walifanikiwa kugundua kwamba tembe ya polonium 210 iliotumika katika bomu la kwanza la nyuklia ndio chanzo cha mauaji hayo.


Hakuna kitu madaktari walichoweza kufanya.


Huenda rais Putin 'aliidhinisha' mauaji ya Jasusi

Bwana Litvinenko aliambia BBC Urusi kwamba alikuwa akichunguza mauaji ya mwanahabari Anna Politkovskaya mwezi uliopita wakati aliposhambuliwa, Alifariki tarehe 23 mwezi Novemba.



ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog