Search This Blog

Sunday 22 May 2022

BARUA NDEFU KUTOKA BAGHDAD - 2

 







    Simulizi : Barua Ndefu Kutoka Baghdad

    Sehemu Ya Pili (2)



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kelele zilianza kusikika kutoka katika vyumba vya jirani. Erick akakurupuka kutoka kitandani kama mtu ambaye alikuwa ameota ndoto mbaya na ya kutisha. Akainuka na moja kwa moja kuwasha taa na kisha kuangalia saa kubwa ya ukutani.

    Saa ilimuonyeshea kuwa ilikuwa saa tatu usiku. Maswali mengi yakaanza kumiminika kichwani mwake kuhusiana na kelele zile alizokuwa amezisikia. Erick akapuuzia kwa kudhani kuwa kelele zile zilitoka nje ya hoteli ile, akazima taa na kuanza kupiga hatua kuelekea kitandani.

    Hata kabla hajafika kitandani, kelele zile zikaanza kusikika tena. Erick akasimama kwa muda, tayari alionekana kuhisi hali ya hatari ikiwa imeanza kutokea ndani ya hoteli hiyo. Akapiga hatua kuufuata mlango wa chumba kile na kuufungua.

    Erick hakuamini macho yake, Wamarekani wengi ambao walikuwa ndani ya hoteli ile walianza kuvutwa na kupelekwa nje na watu ambao walikuwa wameshika bunduki mikononi mwao. Erick akaanza kutetemeka, hali ile ikaonekana kumuogopesha kupita kiasi.

    Jina la kwanza ambalo lilimjia kichwani kwa wakati huo lilikuwa Brian, Mmarekani ambaye alikuwa rafiki yake. Hakuelewa kama katika kipindi hicho Brian alikuwa salama au na yeye alikuwa amekwishachukuliwa na Waarabu wale ambao walionekana kuwa na hasira.

    Erick akaupiga moyo konde, akaufungua mlango kwa mara nyingine na kuanza kupiga hatua kuelekea katika chumba alichokuwa akikaa Brian. Mlango ulikuwa umevunjwa, Erick akapiga hatua na kuingia ndani.

    Kila kitu kilikuwa shaghalabaghala. Akaanza kuliita jina la Brian, aliliita zaidi na zaidi lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia. Wasiwasi zaidi ukazidi kumkamata Erick, tayari akili yake ikamwambia kuwa Brian alikuwa amechukuliwa na Waarabu wale walioingia katika hoteli ile katika kipindi kichache kilichopita.

    “Erick... Erick...” Erick alisikia akiitwa nyuma ya kabati.

    Kwa haraka sana Erick akaanza kupiga hatua kuelekea kule ambako alisikia akiitwa. Brian alikuwa amejificha huku uso wake ukionekana kuwa na hofu tele.

    “Vipi?” Erick aliuliza.

    “Tuondoke. Kuna kitu nimekijua, ila nitataka kukijua zaidi” Brian alimwambia Erick.

    “Kitu gani?” Erick alimuuliza Brian.

    “Kitu kimoja ambacho kila Mmarekani na Muingereza anahitaji kukifahamu” Brian alimwambia Erick

    Erick hakuongea kitu chochote kile, alibaki kimya akimwangalia Brian. Hali ilionekana kutokuwa na usalama wowote mahali hapo lakini baada ya kuona hali imekuwa shwari, wakatoka nje. Michirizi ya damu ilionekana ukutani, hawakuelewa kama michirizi ile ilisababishwa kwa mtu yeyote kupigwa na risasi au kipigo.

    Hawakutaka kupoteza muda kujiuliza maswali ambayo wala hayakuwa na majibu yoyote, wakaendelea kupiga hatua kuelekea nje ya hoteli ile kwa kuanza kushusha ngazi. Erick alibaki akimshangaa Brian. Hakuelewa sababu iliyomfanya Brian kufanya kitendo kama kile ambacho kilikuwa ni hatari kwake.

    “Mbona tunakwenda chini? Haujui kama kuna hatari huko, hasa kwako” Erick alimuuliza Brian ambaye alionekana kutokusikia.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakashuka chini hadi katika ghorofa ya kwanza. Mlinzi alikuwa amefungwa kamba huku watu wengine waliokuwa katika hoteli ile wakiwa wamelala kifudifudi. Erick na Brian walizidi kutembea kuelekea nje.

    Wakaanza kuangalia katika kila upande, magari mawili yaliyokuwa yamebeba Wamarekani na Waingereza kadhaa yalikuwa yameanza kuondoka kuelekea katika Mji wa Al Aziziyah uliokuwa upande wa kusini mwa nchi ya Iraq. Kwa harakaharaka Brian na Erick wakaanza kuifuata teksi moja ya kukodi iliyokuwa mahali hapo na kuingia ndani.

    “Mnakwenda wapi?” Dereva wa ile teksi aliwauliza.

    “Yafuate magari yale” Brian alimwambia.

    “Yale mawili yaliyowabeba Wamarekani?”

    “Ndiyo”

    “Hapana. Siwezi kufanya hivyo. Hii ni hatari kubwa sana. Nikifanya hivyo halafu wakagundua, nitauawa” Dereva yule aliwaambia huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikiongea.

    Brian akakaa kimya kwa muda, alimwangalia Erick katika ishara ya kutaka kufahamu ni kitu gani walichotakiwa kufanya kwa wakati huo ili kumshawishi dereva yule afanye kama kile walichotaka akifanye.

    Neno fedha ndilo ambalo lilimjia Brian kichwani. Kwa harakaharaka akaifungua pochi yake na kutoa noti mbili za dola mia moja na kumgawia dereva yule. Dereva hakuyaamini macho yake, aliziangalia fedha zile mara mbilimbili, kiasi kile kilionekana kuwa kikubwa ambacho ungeonekana kichaa kama ungekikataa.

    “Ulisema magari yale mawili?” Dereva aliuliza huku akiwasha gari.

    “Ndiyo. Fanya haraka kabla hayajatuacha sana” Brian alimwambia dereva ambaye akaanza kuliondoa gari lile na kuyafuata magari yale mawili.

    Magari yale yaliendelea kuelekea katika upande Kusini Mashariki ambapo kulikuwa na Mji wa Wasit. Mwendo wa magari yale ulikuwa ni wa kasi kupita kawaida, barabara haikuwa ya lami, ilikuwa ni barabara ya vumbi ambayo haikuonekana kuwa na uimara mkubwa sana. Alichokitaka Brian mahali hapo ni kuendelea kuyafuata magari yale huku taa za gari lile lao zikiwa zimezimwa kwani hawakutaka watu wale wajue kama walikuwa wakiwafuatilia.

    Safari iliendelea kwa zaidi ya saa moja na ndipo magari yale yakaanza kuingia katika Mji wa Wasit, mji ambao ulikuwa maarufu kwa ajili ya uchimbaji wa mafuta nchini humo. Hali ya hewa katika kipindi hicho ilikuwa ni joto kali sana ambalo lilionekana kuwa zaidi ya lile ambalo lilikuwa likipatikana ndani ya jiji la Dar es Salaam.

    Magari yale yakaanza kuingia katika barabara moja ambayo nayo ilikuwa ni ya vumbi na kisha kuendelea na safari kana kwamba walikuwa wakitaka kuelekea katika Mji wa Thawra, mji ambao ulikuwa maarufu sana kwa upatikanaji wa ngamia.

    Baada ya mwendo fulani, magari yale yakaanza kuingia katika eneo la nyumba fulani ambayo ilionekana kuukuu. Brian na Erick hawakutaka kuendelea mbele, walichomwambia dereva ni kuwashusha na kisha kujua mambo yake.

    “Kuna hoteli hapa?” Brian alimuuliza dereva.

    “Mbali sana kutoka mahali hapa. Mtahitaji mwendo wa dakika kumi kwa miguu” Dereva yule aliwajibu.

    “Hakuna shida. Unaweza kwenda” Brian alimwambia dereva yule ambaye aliondoka mahali pale.

    Waliendelea kusimama mahali pale kwa muda fulani huku wakiangalia katika kila kona mahali pale. Sehemu ile ilikuwa imetawaliwa na giza huku mwanga ukionekana kwa mbali kutoka katika lile jumba kubwa na bovu ambalo magari yale mawaili yalikuwa yameingizwa ndani.

    Hawakujua ni kitu gani ambacho walitakiwa kukifanya kwa wakati huo, hawakujua kama walitakiwa kwenda moja kwa moja ndani ya jumba lile au walitakiwa kubaki kule nje. Bado swali lilikuwa likiendelea kuwa kichwani mwa Erick, hakujua sababu ambayo iliwapelekea kuyafuatilia magari yale ambayo yalikuwa yamewabeba wazungu wale.

    Walisimama kwa muda mahali pale mpaka pale ambapo Brian akashauri kitu kimoja cha hatari kifanyike mahali pale, kuelekea ndani ya jumba lile. Ushauri ule ulionekana kuwa wa hatari sana ambao haukutakiwa kushauri mahali pale, wangeweza vipi kwenda kule na wakati katika kipindi hicho Waarabu walionekana kuwa na hasira kubwa na wazungu? Katika kila swali ambalo Erick alikuwa akijiuliza mahali pale alikosa jibu.

    Brian hakuonekana kuogopa hata kidogo, dhamira yake kwa wakati huo ilikuwa ni kuingia ndani ya lile jumba na kisha kujionea kile ambacho kiikuwa kikiendelea ndani ya jumba lile. Kwa wakati huo alitaka kufahamu kitu kimoja tu kwamba Wamarekani na Waingereza walikuwa wakipelekwa kule ndani kufanya nini. Kadri ambavyo Erick alishauri kutokwenda ndani ya jumba lile, Brian alionekana kupinga sana, alichokuwa akikitaka yeye ni kwenda ndani ya jumba lile.

    “Haiwezekani kwenda hivi! Tunaweza kukamatwa” Erick alimwambia Brian.

    “Unaogopa nini sasa? Wewe ni mwandishi wa habari. Nakuhakikishia kwamba kama tutafanikiwa katika kujua kila kitu kinachofanyika ndani ya jumba lile, tutapata fedha nyingi sana” Brian alimwambia Erick.

    “Na kama tukikamatwa hauoni kama litakuwa tatizo ambalo litaweza kusababisha kuuawa?” Erick alimuuliza Brian.

    “Kufa kwa sababu ya kupata kitu fulani si tatizo. Haiwezekani kuwa na tatizo kabisa kama utakufa huku ukijaribu kufanya kitu fulani” Brian alimwambia Erick.

    Bado malumbano yalikuwa yakiendelea mahali hapo. Kitu alichokuwa akikitaka Brian ni kwenda kuingia ndani ya jumba lile lakini kwa Erick kila kitu kilionekana kuwa tofauti sana. Hakutaka kabisa kuingia ndani ya jumba lile kwani alijua kwa vyovyote vile wangeweza kuonekana na mwisho wa siku kukamatwa na kuuawa.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Bado waliendelea na malumbano mpaka pale Erick aliposhauri kwamba ilikuwa ni lazima kwenda katika nyumba yoyote mahali hapo na kutafuta kanzu pamoja na vilemba kwa ajili ya kuvaa ili wasiweze kugundulika mara moja mara watakapoamua kuingia ndani ya jumba lile. Ushauri huo ukapitishwa na pande zote mbili, wakaanza kuondoka kuelekea katika nyumba ambazo zilikuwa zikionekana kwa mbali sana kutokana na taa ambazo zilikuwa zimewashwa ndani ya nyumba hizo.

    Walipozifikia wakaanza kuzunguka huku na kule na hatimae kuyaona baadhi ya mavazi ambayo yalikuwa yameanikwa kwenye kamba nje ya nyumba moja. Walichokifanya ni kuanza kutembea kwa mwendo wa kunyata mpaka pale ambapo walipoifikia kamba ile na kisha kuchukua nguo ambazo walikuwa wakizihitaji na kuondoka mahali hapo.

    Walipofika umbali fulani wakazivaa kanzu zile na kisha kuanza kulifuata jumba lile huku kwa mbali zikisikika sauti za Wamarekani wakipiga kelele huku wakitukana ovyo. Katika kipindi hicho wakajivika ujasiri, moja kwa moja wakaanza kupiga hatua kulifuata jumba lile ambalo baada ya kuufikia mlango wa kuingia ndani, wakaanza kuingia.

    *****

    Wote wakaanza kuingia ndani ya jumba lile huku kwa mavazi ambayo walikuwa wameyavaa yakiwafanya kuonekana kuwa kama waarabu ambao walikuwa wakiingia ndani ya jumba hilo. Hakukuwa na mwanga mkubwa ndani ya jumba hilo japokuwa kulikuwa na taa ambazo hazikuwa zikitoa mwanga mkubwa.

    Wakaanza kuangalia huku na kule, idadi ya waarabu haikuwa kubwa sana ingawa kila mwarabu ambaye alikuwa mahali hapo alionekana kuwa na jambia pamoja na magobore makubwa huku kanzu zao pamoja na vilemba vikiwa mwilini mwao.

    Brian na Erick wakaanza kupiga hatua kuelekea juu ya ghorofa la jumba hilo kwa kutumia ngazi ambazo zilionekana kuchoka sana. Mwendo wao ulikuwa ni wa kawaida sana lakini Erick alikuwa akionekana kuwa na hofu kupita kawaida. Kelele zile za wala wazungu bado zilikuwa zikiendelea kusikika ndani ya jumba lile.

    Vyumba vingi vilikuwa vikionekana ndani ya jumba lile hali ambayo ikawa ngumu sana kujua vile vyumba ambavyo vilikuwa vikisikika kelele zile. Hawakusimama, wakaendelea kusonga mbele zaidi na zaidi mpaka walipofika katika mlango ambao ulikuwa ni wa mwisho ndani ya jumba hilo. Walichokifanya ni kuufungua mlango huo na kisha kuingia ndani.

    Picha ambayo walikutana nayo ndani ya jumba lile ikaoneonekana kuwaogopesha kupita kawaida. Wazungu wote ambao walikuwa ndani ya chumba kile kikubwa walikuwa wamevuliwa nguo huku wakichapwa mijeredi hali ambayo ilionekana kuwa kama adhabu ya wao kuingia ndani ya nchi ile ambayo haikuwa na mapenzi na Wamarekani wala Waingereza.

    Kelele zile ndizo ambazo zilikuwa zikisikika kwa sauti ya juu sana katika usiku huo. Erick akazidi kutetemeka zaidi, picha ile ikamtia hofu kupita kawaida. Mwili wake ukaanza kutokwa na jasho jembamba hali ambayo ilimfanya kutamani kutoka ndani ya chumba kile.

    “Let get out of here (Tuondoke mahali hapa)” Erick alimwambia Brian.

    “Let’s wait (Tungoje kwanza)” Brian alimwambia Erick.

    Bado walikuwa wakiendelea kuangalia kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea mahali pale. Waarabu wale walionekana kuwa na hasira kupita kawaida. Bado walikuwa wakiendelea kuwachapa huku wakiongea maneno mengi yaliyojaa kejeli.

    “Lets save them (Tuwaokoe)” Erick alishauri huku akionekana kuumia juu ya kile ambacho kilikuwa kikitokea.

    “No! We have no guns (Hapana. Hatuna bunduki)” Brian alimwambia Erick.

    Hawakutaka kuendelea kusimama mahali pale, walichokifanya ni kuanza kutembea tembea ndani ya jumba lile. Waarabu hawakuonekana kuwatambua kabisa, kwanza ilitokana na mwanga hafifu ambao ulikuwepo mahali pale lakini kubwa zaidi ilitokana na kanzu pamoja na vilemba ambavyo walikuwa wamevivaa huku asilimia kubwa ya uso wao ukiwa umezibwa.

    Walipokaa ndani ya chumba kile kwa muda fulani, hapo hapo wakatoka na kisha kuanza kuelekea katika chumba kingine. Huko hali ilionekana kuwa kama ile iliyokuwa kule. Wamarekani wengi pamoja na Waingereza walikuwa wametekwa na kuwekwa ndani ya chumba hicho. Haikujalisha kama ulikuwa mwanaume au mwanamke, wote walikuwa watupu kabisa.

    Mijeredi bado ilikuwa ikiendelea mahali hapo huku picha kubwa ya gaidi la kimataifa ambalo lilikuwa likitafutwa sana na Wamarekani, Yousouf ikiwa mbele kabisa ya kila chumba ndani ya jumba lile. Vyumba vile vilionekana kuwa vyumba vilivyojaa maumivu makali, wazungu wengi walikuwa wakiuawa ndani ya vyumba vile.

    Vyakula havikuwa vikiletwa ndani ya vyumba vile na kama vilikuwa vikiletwa basi vilikuwa vidogo sana tena huku vikiwa haviwatoshi kabisa. Lengo kubwa la kuwateka watu hao lilikuwa ni moja tu, kuwaua kwa maumivu makali, yaani mtu kufa huku akijiona kwamba alikuwa anakufa.

    Lengo la waarabu lile lilikuwa limefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, wazungu wengi walikuwa wakifa kila siku jambo ambalo lilionekana kumtsha kila mtu. Hakukuwa na taarifa yoyte ile ambayo ilikuwa ikijulikana hasa juu ya kile ambacho kilikuwa kikiendelea ndani ya jumba lile. Kila kilichokuwa kikiendelea ndani ya jumba lile kilionekana kuwa siri kubwa.

    Wamarekani na Waingereza hawakutaka kukata tamaa, mara kwa mara walikuwa wakiwatuma wapelelezi wao kuelekea katika nchi ya Iraq hasa katika jiji lile la Baghdad kwa ajili ya kuangakile na kujua kile ambacho kilikuwa kikitokea lakini mwisho wa siku hata wapelelezi wale walikuwa wakikamatwa na kuuawa jambo ambalo liliwafanya kutokujua ni mahali gani Wamarekani na Waingereza walipokuwa wakipelekwa.

    Brian na Erick hawakutaka kuendelea kukaa ndani ya chumba kile, kitu ambacho walikuwa wamekipanga mahali hapo ni kuodoka na kuelekea mjini ambapo huko wangefanya mawasiliano na jeshi la Marekani na kisha kuwaambia kile ambacho kilikuwa kimeendelea nchini Marekani.

    Erick akaonekana kushangaa, alijua fika kwamba kama taarifa ile wangeitoa katika jeshi la nchini Marekani basi nao wasingeweza kukaa ndani ya nchi ile jambo ambalo lingewafanya kuondoka na kuelekea Marekani huku akiwa hajaifanya hata ile kazi ambayo aliambiwa kuifanya nchini Iraq.

    “We don’t have to tell them (Haitupasi kuwaambia)” Erick alimwambia Brian ambaye alionekana kushtuka.

    “Why? (Kwa nini?)”

    “We are Journalist, right? (Sisi ni waandishi wa habari, sawa?)” Erick aliuliza.

    “Right (Sawa)

    “We have to proceed with our works that brought us in here (Inatupasa tuendelee na kazi yetu ambayo ilituleta mahali hapa)” Erick alimwambia Brian.

    “Which work? (Kazi gani?)” Brian aliuliza.

    “To write down what we suppose to write (Kuandika kila kitu tunachotakiwa kukiandika)” Erick alijibu.

    “This is the one. Trust me Erick, you are here because they want you to give them feedback about what the hell is going on in here. Journalists were taken to Iraq but they did not succeed. We have to see what is going on here, then we are going back to home (Hiki ndicho chenyewe. Niamini Erick, upo hapa kwa sababu wanataka uwaambie kile kinachoendelea mahali hapa. Waandishi wengi wa habari waliletwa Iraq lakini hawakufanikiwa. Tukiona kile kinachoendelea mahali hapa, kwa hiyo ni lazima turudi nyumbani)” Brian alimwambia Erick.

    “They? Who are they?” (Wao? Wao wakina nani?)

    “Americans” (Wamarekani)CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakukuwa na sababu ya kuendelea kuongea mahali hapo, walichokifanya ni kuanza kuondoka huku wakionekana kutembea kwa mwendo wa kasi. Lengo lao kwa wakati huo lilikuwa ni kufika mjini ambapo hapo wangeelekea hotelini na kisha kupiga simu nchini Marekani na kuwaambia kile ambacho kilikuwa kinaendelea.

    Wakashuka ngazi kwa haraka sana na kisha kuzidi kutembea kwa kasi kupita kawaida. Kitendo kile cha kutembea kwa haraka na ndicho ambacho kikawafanya hata waarabu wengine kuanza kuwatilia mashaka. Huku wakiwa wameufikia mlango wa kutokea nje ya jumba lile, wakaamriwa kusimama lakini hakufanya kile ambacho waliambiwa kukifanya, wakaanza kukimbia jambo ambalo likawafanya waarabu kuanza kuwamiminia risasi ambazo ziliishia kugonga ukutani.

    Milio ile ya risasi ndio ambayo ilionekana kuwashtua waarabu wengine na kutoka hapo nje. Hakukuwa na kitu cha kusubiri, walichokifanya ni kuzishika bunduki zao vizuri na kisha kuanza kuwafukuza huku wakiendelea kuwamiminia risasi mfululizo.



    Erick na Brian walikuwa wakikimbia kwa mwendo wa kasi kuelekea wasipoafahamu, milio ya risasi ilikuwa ikiendelea kusikika masikioni mwao hali ambayo iliifanya kuongeza kasi zaidi na zaidi. Erick alikuwa akikimbia huku akiogopa kupita kiasi, risasi ambazo zilikuwa zikipiga ardhini zilikuwa zikimfanya kuona kwamba mwisho wake ulikuwa ukikaribia.

    Walikuwa wakikimbia kwa umbali mrefu huku kukiwa hakuna hata nyumba iliyoonekana, hali ya jangwa iliyokuwepo katika eneo lile iliwapa tabu kupita kawaida. Walikimbia kwa muda wa dakika kumi na ndipo wakafanikiwa kuiona nyumba moja ambapo wakaifuata na kuingia ndani.

    Ngamia waliokuwa wamefungwa nje ya nyumba ile wakaanza kupiga kelele mpaka wale Waarabu wale walipofika na kugundua kwamba watu wao waliokuwa wakiwakimbiza walikuwa wameingia ndani ya nyumba ile. Wakaufuata mlango wa kuingilia ndani ya nyumba ile na kuanza kuwatafuta.

    Walizunguka katika eneo la nyumba nzima huku wakiwatafuta watu hao. Japokuwa wenyeji walikuwa wameamka na kuanza kuwashangaa lakini hakukuwa na mtu aliywaongelesha, walipoona kwamba wamewakosa, wakawageukia wenyeji wale.

    “Wapo wapi?” Mwanaume mmoja aliuliza kwa sauti iliyojaa ukali.

    “Wakina nani?”

    “Wale tuliokuwa tukiwakimbiza” Mwanaume yule alijibu.

    “Mmmh! Mbona hatujaona mtu humu.”

    “Unasemaje?”

    “Hatujaona mtu humu. Watakuwa wamepita katika mlango ule pale wa kwenda nje upande wa pili” Mwanaume yule alisema hali iliyowafanya Waarabu wale kuufungua mlango ule.

    Macho yao akatua katika ukuta uliokuwa nyuma ya nyumba ile, walipouangalia vizuri ukuta ule, wakaona mikwaruzo ambayo moja kwa moja wakajua kwamba watu waliokuwa wamewafukuza walikuwa wamepanda ukuta na kutokea upande wa pili.

    Hawakutaka kuendelea kubaki mahali pale, walichokifanya ni kuanza kuupanda ukuta ule na kutokea upande wa pili. Wakaanza kuangalia katika kila kona lakini hawakuweza kumuona mtu yeyote yule zaidi ya alama za viatu zilizoonyesha kwamba walikuwa wamekimbilia upande wa mashariki.

    Wakaanza kuzifuata zile alama za viatu kule kulipoelekea, japokuwa walikuwa wamejitahidi sana kuwatafuta lakini hawakuweza kuwapata jambo liliowachanganya sana.

    “Ni lazima tuwapate” Mwarabu mmoja ambaye alionekana kuwa kiongozi aliwaambia wenzake na kisha kutawanyika.

    Tayari akili yao kwa wakati huo ilikwishajua kwamba ni lazima watu wale waliokuwa wameona kila kilichoendelea ndani ya jumba lile wangeweza kwenda kutoa siri kwa Wamarekani ambao wangekuja mahali pale na kuwakomboa Wazungu wengine waliokuwa ndani ya jengo lile.

    *****

    Erick na Brian walitokea upande wa pili wa nyumba ile na kukutana na ukuta, walichokifanya, tena huku wakiwa katika kasi ya ajabu wakauparamia ukuta ule, wakarukia upande wa pili na kuendelea kukimbia mbele zaidi. Hawakutaka kukamatwa na kutiwa mikononi mwa Waarabu wale walioonekana kuwa na hasira mno.

    Walizidi kukimbia zaidi mpaka kuzifikia nyumba zaidi ya ishirini zilizokuwa zimejengwa katika eneo moja, wakaanza kutembea kwa mwendo wa harakaharaka kuzifuata, baada ya kuzifikia, wakaingia ndani.

    Walikuwa wakihema kupita kawaida jambo lililowafanya watu waliokuwa ndani ya nyumba ile kuwasogelea na kuanza kuzungumza nao. Bado Brian alionekana kumshangaza sana Erick, alikuwa akiongea na Waarabu wale kwa lugha ya Kiarabu iliyoonekana kuzoeleka sana mdomoni mwake.

    Baada ya kuongea na wale watu kwa muda wa dakika moja, wakawachukua na kisha kuwapeleka chumbani kwa ajili ya kupumzika. Bado Erick alionekana kumshangaa Brian kwa kile kitendo chake cha kuongea lugha ya Kiarabu kwa ufasaha kwa umahiri mkubwa namba ile.

    “Why do you look me that way?” (Kwa nini unaniangalia hivyo?) Brian alimuuliza Erick

    “Where did you learn to speek Arabic?” (Umejifunza wapi lugha ya Kiarabu?) Erick aliuliza.

    “I learned at school. We had an arabian teacher who always taught us how to speek arabic” (Nilijifunza shuleni. Tulikuwa na mwalimu wa Kiarabu ambaye mara kwa mara alikuwa akitufundisha kuzungumza Kiarabu) Brian alimwambia Erick.

    Siku hiyo walikuwa wakiongea mambo mengi ambayo walipaswa kuogea kwa wakati huo. Muda ulizidi kusogea zaidi na zaidi mpaka kufikia saa kumi alfajiri muda ambao adhana ikaanza kusikika masikioni mwao. Sauti za milango ambayo ilikuwa ikifunguliwa ikaanza kusikika kuonyesha kwamba watu walitakiwa kuwa msikitini kwa wakati huo, msikiti ambao haukuwa mbali kutoka hapo walipokuwa.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Katika kipindi chote walikuwa macho, usingizi, kwao haukupatikana kabisa. Huku watu wakiendelea kutoka nje ya vyumba vyao kwa ajili ya kuelekea msikitini, mara sauti za watu ambao hawakuonekana kuwa wa amani zikaanza kusikika kutoka masikioni mwao jambo ambalo likawafanya kushtuka kupita kawaida.

    Hawakutaka kujiuliza maswali zaidi, tayari walijua kwamba wale watu ambao walikuwa wamewakimbia ndiyo waliokuwa wamekuja mahali hapo. Wote wakaonekana kuingiwa na wasiwasi kupita kawaida, tayari wakaona kwamba walikuwa wameingizwa mikononi mwa Waarabu wale ambao walikuwa wakiwasaka kama lulu kwa ajili ya kuficha siri zao za kuwateka Wamarekani na Waingereza wengi katika jiji hilo la Baghdad.

    “What should we do?” (Tufanye nini?) aliuliza Erick.

    “Lets run” (Tukimbie)

    “What?” (Nini?)

    “Leave it to me. You have to do what I ask you to do, right?” (Niachie mimi. Unatakiwa kufanya kile ninachotaka ukifanye. Sawa?) aliuliza Brian.

    “Right” Erick alisema huku watu wale wakisikika wakiongea kwa nje na Waarabu wengine ambao walikuwa wameamka kwa ajili ya kwenda kumswali msikitini.

    *****

    Mchungaji Joshua na mkewe, Mary walikuwa kwenye maumivu makali, mijeredi waliyokuwa wamechapwa na Waarabu wale iliwaacha wakiwa kwenye maumivu makali. Walikuwa uchi wa mnyama. Muda wote walikuwa wakilia tu huku mchungaji Joshua akijitahidi kumbembeleza mkewe ambaye alikuwa akiugulia kwenye maumivu makali zaidi yake.

    Hakukuwa na tumaini lolote ambalo walikuwa wakilitumainia kwa wakati huo zaidi ya kumuomba Mungu awaokoe kutoka katika mikono ya Waarabu wale waliokuwa na roho iliyojaa ukatili kupita kawaida. Kila alipokuwa akiyapitisha macho yake kwa Wazungu wengine arobaini ambao walikuwa katika chumba kile, moyo wake ulikuwa kwenye masikitiko makubwa.

    Muda wote alikuwa akimshika mke wake mkono huku akimuomba Mungu wake kimoyomoyo afanye muujiza utakaowafanya kutoka salama katika mikono ya Waarabu wale. Ingawa walikuwa wametekwa na kufungiwa ndani ya chumba kile kilichojaa mateso lakini kamwe hakutaka kuusitisha mpango wake wa kufungua kanisa ambao ulikuwa umewafanya kuja nchini Iraq ndani ya Jiji la Baghdad.

    Mipango yake ya kuanzisha kanisa bado ilikuwa moyoni mwake kwa wakati huo, makanisa machache ambayo yalikuwa yakipatikana ndani ya Jiji la Baghdad yalionekana kutokutosha kabisa. Sala zake bado zilikuwa zikizidi kuendelea zaidi na zaidi huku wakati mwingine akisimama mbele ya Wazungu wenzake na kuwaambia juu ya imani kubwa ambayo alikuwa nayo moyoni mwake kwamba ilikuwa ni lazima waokolewe mahali hapo na kurudi nyumbani kwao, nchini Marekani na Uingereza.

    Katika kipindi ambacho Erick na Brian kuingia ndani ya chumba kile, mchungaji Joshua akaonekana kuwa na wasiwasi mwingi kutokana na watu wale kumuangalia sana. Kitendo kile tayari kilikuwa kimemfanya kuwa na mashaka zaidi moyoni mwake. Hakuwatambua kwamba wale walikuwa Erick na Brian ambao walikuja ndani ya jumba lile na kuangalia kila kilichokuwa kikiendelea mahali pale.

    Mpaka Erick na Brian wanaondoka mahali hapo, mchungani Joshua alikuwa na wasiwasi mwingi. Ni ndani ya sekunde chache baada ya Erick na Brian kuondoka ndani ya chumba hicho ndicho kipindi ambacho milio ya risasi ikaanza kusikika nje.

    Kelele zikaanza kusikika ndani ya chumba hicho, kila mtu kwa wakati huo akaonekana kukiogopa kifo, milio ya risasi ambayo ilikuwa ikisikika ilikuwa imeinua hofu kubwa mioyoni mwao. Baada ya dakika kadhaa, kundi la Waarabu watatu wakaingia ndani ya chumba kile huku nyuso zao zikiwa katika hali ya hasira kupita kawaida.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walichokifanya mahali hapo ni kuanza kuwahesabu watu wote waliokuwa ndani ya chumba kile. Kitu ambacho walikuwa wamekijua kwa wakati huo ni kwamba wale watu ambao walikuwa wamekimbia walikuwa miongoni mwa watu ambao walikuwa mateka ndani ya vyumba vile. Walipomaliza kuwahesabu, wakatoka na kuanza kuelekea katika chumba kingine na kuanza kuwahesabu wengine.

    “We are going to leave this room very soon (Tutaondoka ndani ya chumba hiki hivi karibuni)” Mchungaji Joshua aliwaambia wazungu wenzake ambao walikuwa mateka pamoja nao.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog