Search This Blog

Sunday 22 May 2022

HATI FEKI - 3

 





    Simulizi : Hati Feki

    Sehemu Ya Tatu (3)



    MOSSES Ndula na wenzake hawakuwa na ujanja tena zaidi ya kutii na kuweka silaha chini na kunyanyua mikono juu. John na Aminata walianza kusogea kuwafuata polisi waliko ili waweze kujitambulisha.



    “Heshima yako mkuu,” Polisi mmoja aliyekuwa amewafuata Aminata na John alitoa saluti kwa Aminata. Aminata alikuwa bado amewaelekezea Mosses na watu wake bastola hadi walipoweka silaha chini baada ya kugeuka na kuwaona polisi nao wakiwa wamewaelekezea mitutu ya bunduki na hivyo wasiweze kukimbia. Polisi waliwashangaa Mosses na watu wake wawili.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Huyu jamaa aliwahi kuja pale kituoni na wanasheria wake,” polisi mmoja alisema huku akistaajabu kulikoni mtu mkubwa vile akimbizwe na gari kama mhalifu.



    “Nyamaza… kila kitu kitajulikana huko huko. Waliwachukua Mosses Ndula pamoja na wenzake hadi Kituo cha Polisi. Mosses hakuonekana kutishika wala kujali. Dereva alikimbilia porini na hivyo hakuweza kutafutwa wala kujulikana.



    Aminata alimfuata kiongozi wa wale polisi na kumsihi wasikubali akatoroka hadi pale watakapofika mjini Arusha kesho yake.

    “Sawa mkuu,” tutawafikisha wote kama amri yako ilivyosema.”



    ****

    Msafara wa kuwapeleka mahabusu Mosses na mlinzi wake ulianza. John na Aminata wao waliamua kurudi. Walielekea Mererani na moja ya magari ya polisi kwani gari lao lilikuwa limepasuliwa tairi wakati wa mashambulizi ya kurushiana risasi wao na Mosses. Waliingia siti ya nyuma wakiendeshwa na mmoja wa polisi waliokuwa wamefika pale.



    “Ninafururaha sana tumekamilisha hii safari yetu ya muda mrefu. Sikutegemea kusambaratisha jeshi zima japo sio kubwa na. kilichobaki sasa ni kujua kama Antony ameshafanikisha kuuzuia mgodi kule Mererani.” Aminata alisema wakati wakiwa njiani kuelekea Mererani kuangalia kilichoendelea usiku huohuo.

    John alitoa simu yake kwa nia ya kumpigia Antony.



    Lakini kabla hajabonyeza namba alisikia ikiita simu yake.



    “Antony anapiga. Utafkiri alijua nataka kumpigia.”



    “Akili zenu sawa, kweli nyie pacha,” John alicheka huku akipokea simu yake.



    “Haloo kaka,” alisema John akiitikia simu ya upande wa pili alipokuwa Antony.



    “Shwari tu kaka. Nawasikilizia nyie. Mnaendeleaje huko?”



    “Tumeshawatia nguvuni wawili japo mmoja kakimbia. Nadhani ni dereva wake. Ila mhusika mkuu tayari tunaye.”



    “Kwa nini msingemuua broo?”



    Polisi waliwahi kumchukua. Hata hivyo hawezi kuleta madhara. Kesho asubuhi tutaenda kwa ajili ya kuanza kumfungulia kesi.”



    “Sawa, sasa wapi mnaelekea sasa hivi?”



    “Tunakuja huko kuangalia usalama.”



    “Huku tumeshikiliwa na polisi. Nadhani Aminata akija itakuwa safi.”



    “Usijali. Tunakuja na gari la polisi. Nadhani kila kitu kitakuwa poa. Baadaye kaka.”



    “Poa Broo.”



    John na Antony walimaliza maongezi yao. Sasa John alimgeukia Aminata ambaye alikuwa amejiegemeza kwenye bega la John na kulala. Alimbusu kwenye paji la uso. Busu lile lilimshtua Aminata na kujikuta akimuuliza John.



    “Vipi, kina Antony wako poa huko?”



    “Ndiyo mpenzi, wanakusubiri wewe ukawanasue maana wako chini ya ulinzi wote. Wamekalishwa chini. Nadhani linasubiriwa karandinga kuwapeleka kituoni.”



    “Haiwezekani bana,” Aminata alisema huku nay eye akitoa simu yake na kupiga makao makuu kwa ajili ya kutoa taarifa za kuwekwa chini ya ulinzi huku akiwataka wasiwaondoe watu hao hadi atakapofika eneo la tukio.



    “Tayari mpenzi. Nimeshawaambia wasiwapeleke kokote hadi nifike.”



    “Asante mpenzi,” John alimshukuru Aminata huku akimvuta na kunanza kumbusu.





    *****

    Wakiwa njiani kuelekea Arusha Mjini kuwapeleka Mosses na mlinzi wake Mahabusu. Polisi hawakujua kwamba Mosses alikuwa na bastola.



    “Samahani mkuu,” kabla sijapatwa na hili janga nililtokea katika starehe zangu. Nahisi kwenda haja ndogo. Tafadhalin,” alisema Mosses huku akiwa amefungwa pingu. Ndani ya koti lake kulikuwa na bastola.



    “Hakuna, mpaka tufike,” Polisi mmoja alisema kwa ukali.

    “Hapana, kwa kuwa tumemfunga. Tumwache ajisaidie,” polisi mmoja aliyekuwa akiendesha gari alisema huku akiegesha gari pembeni ili Mosses ajisaidie.



    “Nshukuru sana,” Mosses alisema huku akitoka nje ya gari.

    Ni katika maeneo ya Tengeru ambapo Mosses anafanikiwa kuwatoroka polisi baada ya kuitoa bastola yake ndogo na kuwapiga nayo.



    Alitokomea kusikojulikana pamoja na yule mlinzi wake ambaye muda wote alikuwa amechoka baada ya damu nyingi kumtoka baada ya kupigwa risasi ya begani.



    Kuona vile, Mosses aliamua kumpiga tena risasi na kumuua kwani aliona atasababisha wakamatwe. Alipita katikati ya mashamba na kutokomea kabisa.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *****

    Asubuhi, watu walikuwa wamejazana katika eneo hilo ambapo miili ya polisi ilikutwa hapo. Polisi watatu wakiwa wamelala chini. Walikuwa wameshakufa. Habari zilienea kila mahali.



    “Aaah. John,” aliita Aminata kwa ukali.



    “Sema mpenzi, nini tena huko?”



    “Huwezi amini…”



    “Nini?” aliuliza John kwa mshtuko.



    “Yule mshenzi, amefanikiwa kutoroka, kawaua wale polisi na sasa hajulikani aliko.”



    “Dah….sasa itakuaje Aminata.”



    “Dah hata….hata sielewi tuanzie wapi tena…tutampataje sasa?” aliuliza Aminata ambaye alikuwa ameshakata tamaa.



    “Ngoja nimshtue Antony,” John alisema huku akiifuata simu yake na kumpigia Antony ambaye alifika pale dakika kumi baadaye ili kujua itakuaje.



    “Itabidi tumtafute wenyewe tena.” Aminata alisema huku akinyanyuka tayari kuvaa kwa ajili ya safari ya kurudi mjini Arusha.

    Antony alitoka na kwenda hadi kwa wale wachimbaji ili kuongea nao. Aliwataka wakae tayari na kujitayarisha tena kuanza kazi kwani wanafuatilia hati miliki na jina la kampuni ili waweze kuendelea na shughuli.



    “Kwa hiyo, tutamtuma kiongozi wenu awataarifu mambo yatakapokuwa mazuri,” alisema Antony huku akishangiliwa na wachimbaji wote.



    “Antony wamemubali sana, naona wanamweshimu. Inawezekana jana usiku aliwatuliza sana,” John alisema akimwambia Aminata wakati wakiwa ndani ya gari la Antony wakimsubiri kwa ajili ya safari.



    “Unajua mmefanana sana na mzee wenu. Ndo maana wamewatambua haraka. Na pia yule jama aliyetutaarifu.”

    “Mbago…au sio?” aliuliza John.



    “Yah, huyohuyo, amesaidia sana jitihada hizi,” Aminata alimaliza kuongea. Antony alikuwa ameshafika kwenye gari na kuanza kuingia.



    “Nitawaendesha mwenyewe waheshimiwa,” wote walicheka na safari ya kuelekea Arusha ilianza.





    *****

    Walifika mjini na kuelekea moja kwa moja hadi nyumbani kwa kina John, Njiro. John na Aminata walianza kuyasahau ya mapambano na sasa waligeukia penzi lao usiku huo. walirudi ndani ya penzi lao zito ambalo kwa muda walilisahau.



    “Mpenzi, nadhani haina haja ya kuchelewesha mipango yetu. Tuoane kabisa,” John alikuwa wa kwanza kumsihi Aminata juu ya ndoa. Hakujua juu ya siri ambayo ilikuwa ndani ya moyo wa Aminata. Aminata alimwangalia sana John kwa shauku ya kumwambia. Alijua atafurahi sana baada ya kumtamkia juu ya ndoa.



    “Sidhani kama kuna pingamizi John. Muda tuliokuwa pamoja ni dhahiri kwamba tumeshajuana na haina haja ya kukawiza,” Aminata alisema huku akimsogelea John ambaye na yeye alimvuta karibu Aminata na kuanza kumshushia mabusu motomoto.



    “John,” aliita Aminata huku akiwa bado kifuani kwa John.



    “Sema mpenzi wangu,” John aliitikia huku akimweka sawa Aminata kusikia kauli ambayo alikuwa anataka kumwambia.



    “Hujui lolote kuhusu mimi?” aliuliza Aminata huku akichezea kideevu cha John aliyekuwa akimwangalia wakati wote.



    “Hapana, sifahamu mpenzi. Nijulishe tafadhali,” John alimsihi Aminata amweleze alichokitaka.



    “Niangalie vizuri utajua.”



    “Aminata….una mimba yangu?” John aliuliza kwa furaha.

    “Ndiyo mpenzi.”



    John alifurahi kupita kiasi. Alimkumbatia Aminata kila wakati. Furaha aliyokuwa nayo hakutamani kumwachia.



    Ilibakia kucheza na kupeana mapenzi motomoto usiku huo. Aminata alijua kuutumia vizuri mwili wa John na hivyo hakumpa nafasi ya kupumzika. Alimshika sehemu zote na kumwonyesha utundu wake. Alitaka kumwongezea furaha zaidi ya ile aliyokuwa nayo ya kufanikiwa kusambaratisha kundi la Mosses na kujua kwamba alikuwa ana mimba yake.





    *****



    John na Aminata walifunga ndoa na kuishi pamoja. Antony alisimama imara hadi kuhakikisha mgodi unaanza tena kazi.

    Miezi mitatu baada ya hali kutulia mgodi ulirudi tena na kuanza kufanya kazi. Waliajiri wataalamu mbalimbali kwa ajili ya kusimamia na kuongeza wachimbaji wengine ambao walikuwa chini ya mbago.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sakata la Mosses lilikuwa limebaki mikononi mwa polisi ambao walikuwa wakiendelea na msako juu yake popote alipo. Walifanikiwa kuweka vizuizi ktika mipaka yote. Mawasiliano yake pia yalirekodiwa pale ambapo aliitaka kuwasilianana na watu aliowafahamu.



    Mosses hakuwa na pakukimbilia zaidi ya kuzunguka tu ndani ya nchi. Hakuna aliyetaka kujihusisha naye kwa kuhofia kukamatwa baada ya kusikia Mosses anatafutwa kwa udi na uvumba na polisi.

    Aliamua kuishi kwa kujificha. Hakuwa na hata pesa kwani akaunti zake zote zilifungwa na kiasi alichokuwa nacho mfukoni kilimalizika.



    Aliishia kushinda maeneo ya Sinoni ambapo huko alifahamiana na vijana wengi aliokuwa akiwatumia kumfanyia biashara ya kusambaza dawa za kulevya kwa kuziuza kwa wateja wake.



    Aliwaza na kumkumbuka Aminata ambaye alishawahi kufika Kambi ya Fisi. Alikumbuka kwamba ni Aminata ndiye aliyesababisha yeye kumuua Dula ambaye ndiye aliyetoa siri za kundi lao.



    “Nitakutafuta wewe mwanamama,” aliwaza huku akitngisha kichwa chake kuonyesha dhamira yake ya kumtafuta Aminata.



    “Nitakuua kabla ya mimi kufa… lazima ufe wewe mama,” Mosses alisema huku akicheka na kuiweka sigara yake mdomoni tayari kwa kuiwasha.





    *****

    Wakiwa ndani usiku. John na Aminata wallikuwa wakifurahia mimba ya Aminata ambayo ilibakiza siku chache tu aweze kujifungua. Aminata alikuwa akipenda sana kucheza na John kla wakiwa pamoja.



    Alimkumbusha shauku yake ya kutaka kumwona Mosses aiwa yuko jela au amekufa. Hilo lilimwingia sana John ambaye pia hakuridhika kusikia Mosses alikuwa ametoroka na hakujulikana aliko.



    “Usijali…cha msingi ni kuwa makini na huyu mtu kwani sidhani kama amekufa bali atakuwa tu mitaani.” John alisema huku akimshika aminata aliyekuw amesuimama akielekea dirishani. John alibaki amesimama huku akimwangalia Aminata akienda kuweka pazia la dirisha vizuri.



    Ghafla Aminata alirudi kasi na kumkumbatia John.



    “Nini Aminata?”



    “Nimemwona mtu….”



    “Mtu gani, acha woga. Aminata.”



    “Mosses, kweli, nimechungulia tu nayeye akaniangalia afu akakimbia.”



    “Sasa we unamwogopa?”



    “John, kwa hali hii..sitaki matatizo. Waniache kwanza nijifungue mtoto wangu.” John alicheka sana na kumbeba Aminata hadi chumbani tayari kwenda kulala.



    (END OF SEASON 1)



    MWISHO WA SEHEMU YA KWANZA



    MOSSES ANAFANIKIWA KUTOROKA. ANAUA POLISI NA KUTOKOMEA. TAARIFA ZAKE ZINAVUMA NA MSAKO MKALI JUU YAKE UNAANZA.



    ANAJIFICHA KILA SEHEMU KUHAKIKISHA HAKAMATWI.

    AMINATA BAADA YA KUWA MJAMZITO ANAOLEWA NA JOHN NA KUISHI PAMOJA HUKU ANTONY AKIRUDISHA HADHI YA MGODI NA KUANZA KAZI.



    AMINATA ANAMKUMBUKA MOSSES NA MARA ANAIONA SURA YAKE NA KUOGOPA WAKATI AKICHUNGULIA DIRISHANI….ANAHISI KAMWONA MOSSES.



    JE HIYO NI SURA HALISI YA MOSSES AU NI TASWIRA TU ILIYOMWINGIA AMINATA KWA WOGA



    HII NI SEHEMU YA MWISHO YA SIMULIZI HII KALI YA HATI FEKI (SEASON 1)



    …. USIKOSE SEHEMU YA PILI (SEASON 2) YA SIMULIZI HII TAMU…..





    ***SEASON TWO***



    Katika RIWAYA hii SEHEMU YA KWANZA (SEASON ONE), John, Antony na Aminata wanaingia katika mtihani mgumu wa kulipa kisasi na kurudisha mali yao ambayo ilichukuliwa kwa hila na Mosses Ndula. Wanafanikiwa kuwatokomeza na kuurudisha mgodi huku John na Aminata nao wakionekana kuimarika katika penzi lao. Aminata anapata mimba ya John.



    Antony baada ya kufanikiwa kurejesha mgodi anaweka mambo vizuri na kisha anarudi Nairobi kuendelea na shughuli zake ambazo zilisimama kwa muda.



    Mosses Ndula, anafanikiwa kutoroka polisi. Anajificha mtaani Sinoni kwa rafiki na vijana wake ambao alifanya nao kazi. Wanamchukua na kumpa hifadhi. Kwa kuonyesha hajaridhika na ushindi wa kina John na Aminata. Anawaza namna ya kuwafuata tena tena na tena.





    SEHEMU HII YA PILI (SEASON TWO) Mosses Ndula anaonekana kufufuka upya. Anakutana na mfanyabiashara mkubwa wa madini na tajiri Steve Mikaeli. Anamchukua Mosses na kufanya naye kazi pamoja na viongozi wengine wa serikali.



    Je, watafanikiwa kuwasambaratisha kina John ambao ndio wapinzani wao wakubwa katika biashara ya madini kama ilivyokuwa kwa mzee Amigolas.



    Endelea…..





    *****



    Biashara ya madini ilikuwa kubwa sana kwa John na Antony. Kulikuwa na ushindani ambao ulikuwa ukiendelea bila John na Antony kufahamu. Hila za kila aina zilikuwa zikifanywa ikiwa ni pamoj na kuwateka na kuwaibia wafanyakazi wa mgodi wa Amigolas.



    Jambo hilo liliwafanya baadhi ya wafanyakazi wa mgodi kushangaa huku wengine wakirubuniwa na kuhamia katika mgodi wa Steve.



    Steve Mikaeli, ambaye baada ya kusikia taarifa za Mosses anaamua kumtafuta na kumficha kabla ya kumwibua tena.

    Katika taarifa zake za kuonekana katika mitaa ya Sinoni. Steve anawatuma watu na siku hiyo hiyo anaonekana n taarifa zinafika polisi ambapo alikuwa akitafutwa huku wengine wakisema kuwa ametoweka na helikopta baada ya kufuatwa na watu wasiojulikana na kupelekwa kusikojulikana.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akiwa tayari amefika na kuongea vizuri na Steve na kuelewana. Sasa Mosses alijua mambo yake yatakwenda vizuri ingawa bado hakuwa amemwambia hadi pale Steve alipomuuliza ili ajue ukweli wa yeye kuwa katika hali ile.



    “Kuna wajinga waliokuwa wakinifuatilia. Wametaka kuharibu maisha yangu lakini hawakuwezaa,” Mosses aliongea kwa hasira huku akionekana kutaka kupiga chochote au yeyote ambaye atakuwa amesimama mbele yake. Hilo lisingewezekana kwa kuwa aliyekuwa mbele yake alikuwa ni bosi wake, Steve.



    Steve alionekana akimsikiliza kwa makini hukun akujua ushindani wake wa ibiashara utaongezeka ikiwezekana kuua kabisa biashara ya madini katika mgodi wa mzee Amigolas kwa kumtumia Mosses. Alitaka kuhakikisha Mosses anawahadaa wachimbaji wa mgodi wa Amigolas na kuwafanya wajiunge na mgodi wake.



    Jambo hilo lilionekana kumfurahisha sana Mosses ambaye alijua wazi hiyo itakuwa mbinu moja wapo ya kuwachokoza John na Aminata ili aweze kuwakamata.



    Aliamini kwa kuwahadaa huko wangethubutu kujitokeza na kwamba huo ndio ungekuwa mwisho wao kwani angewamaliza kabisa. Alifurahia na kujiona mpya kabisa ambapo ka kipindi kirefu alikuwa amesahaulika. Ujio huu ulimfanya afurahie zaidi kwani aliamini atakuwa na sura na mwonekano mpya kwa wale wasiomjua.



    John alikuwa chini ya ulinzi mkali. Ulinzi mkali wa askari wa Mosses Ndula. Hakujua kwa nini wameweza kutekwa kirahisi hadi kujikuta mikononi mwa Mosses. Hawakuweza hata kujiokoa kwani jeshi la Mosses Ndula lilionekana kuwa imara. Alitakiwa kusema ukweli juu ya jambo ambalo Serikali inataka kujua kwani inaonekana kama alitumwa na chombo hicho kikuu cha dola.



    Mosses alijua John na Aminata watakuwa wanatumiwa. Alifahamu sana mambo ya baba yake, Mzee Amigolas ambaye alikuwa yupo karibu sana na viongozi wakubwa wa nchi. Amigolas alijihusisha upande mwingine na serikali. Alisaidia viongozi kila mara wakati wa kampeni.



    Hakutaka wajue kwamba alikuwa anafanya hila za kuwateka na kuwaua kama alivyodhamiria hivyo aliwauliza maswali ili ajue endapo wangekufa asingeweza kutafutwa na polizi zaidi kwani ni miezi michache imepita baada ya kufanikiwa kumaliza tofauti zake na polisi ambao walikuwa wanamtafuta na kusaidiwa kwa kivuli cha Steve ambaye sasa ndiye bosi wake.



    “Tatizo lako John hutaki kuongea ukweli, usipoangalia nitakuangamiza mshenzi mkubwa wewe.” Mosses Ndula alimfokea John. Mlinitafuta mkanipata. Sasa nimewapata mimi. Mi ndio Mosses,” Mosses alisema huku akicheka sana na kumtandika kibao kikali John huku akiendelea kucheka zaidi.



    John alijikuta akisukumiwa ngumi mbili nzito huku ikishuhudiwa na Steve, Bosi huyo mkuu anayemiliki kampuni ya uchimbaji madini huko Mererani. Aliyekuwa mpinzani mkubwa wa mzee Amigolas.

    Aliongoza genge la wahuni waliotaka kuipindua Serikali ya nchi kwa kuwa alikuwa ana uwezo wa kufanya hivyo.



    Alifanya kila njama kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa Serikali ili kufanikisha azma yao. Habari zilienea na kuwapa hofu watu kwamba jeshi la nchi linataka kuipindua Serikali. Habari zilivuma kwamba majeshi ya Serikali ndiyo yaliyotaka kuipindua nchi. Nchi haikukalika hadi pale kiongozi mkuu alipotoa tamko kwamba hakuna habari kama hizo. Nchi ilitulia tena kama kawaida. Vyombo vya habari vilitakiwa kutangaza amani kama ilivyokuwepo awali.



    Ndiye huyo Steve. Hela haimpigi chenga. Tajiri wa kutupwa aliyeweza kununua hata robo tatu ya nchi. Ana uwezo wa kununua chochote atakacho. Aliyemchukua Mosses Ndula na kumweka sawa. Akampa uwezo wa kuamua atakalo kwa masilahi yake na genge hilo ambalo Mosses ndiye aliyelitengeneza na kuunda jeshi. Sasa anafanya kisasi kwa Aminata na John.



    Ililazimika kwa Serikali kufanya kazi ya ziada ya kuweza kuwabaini wahusika wa mauaji yaliyosababishwa na genge la Mosses ambaye alifanya mauaji mengi kwa kutumia kivuli cha Steve na yeye mwenyewe kwa upande mwingine kwa kuwa aliweza kuwa karibu na viongozi wengi hasa waziri wa Ulinzi Steve na Mosses waliweza kuziteka hisia za viongozi wengi na pale walivyotoa wazo kila kiongozi waliyekutana naye alikubaliana nao. Hakuna kiongozi aliyeweza kufika katika ngome ya Steve.



    *****

    Max mmoja wa askari wa upelelezi aliyefanya kazi yake imara. Aliaminiwa sana na serikali na hasa katika matukio aambayo yangehitaji ujasiri mkubwa na mbinu nyingi za kikomando. Aliyafahamu mafunzo imara aliyoyapata katika kambi mbalimbali ambazo amekuwa akizipitia ili kujiimarisha mwenyewe.



    Baada ya kumaliza mafunzo yake nchini Urusi na kurejea nchini, Max alikutana kwa mara nyingine na Aminata. Mwanafunzi mwenzake waliyekuwa wakisoma pamoja katika mafunzo ya askari upelelezi na baada ya hapo Max alichaguliwa kujiunga na kambi ya kijeshi na kufuzu mpaka alipochaguliwa tena akapate mafunzo zaidi nchini Urusi.



    Alipewa jukumu la kufuatilia nyendo za watu mbalimbali wanaoshukiwa ili kujua ukweli wa vikosi hivyo vilivyofanya shambulio la kushtukiza. Shambulio lililosababisha na baruti kulipuliwa katika mgodi wa Amigolas. Ilisemekana ni watu wa Steve wakiongozwa na Mosses ndio waliosababisha mlipuko huo wakati wa usiku baadhi ya wachimbaji wakiwa chini ya ardhi wakitafuta Tanzanite.



    Max alitii amri hiyo na kuahidi kuanza kazi hiyo haraka iwezekanavyo. Baada ya mienzi kadhaa ya kufanya uchunguzi wao Mosses Ndula na Bosi Steve walikuwa tayari wamepata taarifa kutoka kwa baadhi ya makachero wao waliowatega karibu na Serikali ili kujua ni nini kinachoendelea na jinsi ya kuendelea kujiimarisha, pia waliwaweka ili kuhakikisha wanachunguza ni kwa kiasi gani Serikali inajua kuhusiana na genge lao. Kwa uwezo aliokuwa nao Steve, aliongeza ukubwa wa genge lake. Sasa alitawala sehemu kubwa ya watu.



    Wachimbaji wengi walikufa na wengine kujeruhiwa huku mgodi wa mzee Amigolas ukitishiwa kufungiwa. Hata ilipojulikana kwamba ni Steve ndiye aliyeamuru yafanyike mauaji hayo hakuweza kuchukuliwa hatua na hivyo kesi yake kuzimwa na kuonekana ilikuwa ni bahati mbaya kutokana na kushindwa kulipua vizuri baruti katika mgodi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    *****

    “Huwezi kutusumbua wewe mtu mmoja na huyu mke wako leo lazima mtakufa,” Mosses Ndulah alifoka kwa hasira huku amemsogezea John mdomo wa Bastola aliyokuwa ameishika. Kutokana na ngumi mzito aliyopewa na Mosses Ndulah, John damu zilitapakaa usoni. John alikuwa aimwangalia Aminata ambaye alikuwa hajitambui kwani Steve aliyekuwa sambamba kusikiliza kauli za Mosses Ndula alimchapa Aminata kwa kutumia kitako cha Bastola yake na kuzirai.



    Vikosi vya Mosses Ndula vilikuwa vimetapakaa kila mahali kuzunguka jengo kubwa la gharama lililotumiwa na Mosses Ndula katika kuimarisha ngome ya Bosi Steve. Jengo la Bosi Steve lililoko Mererani, hakuna aliyejua ndani ya jengo hili kulikuwa kuna nini kwani hata barabara iliyoelekea katika jingo hilo haikuonekana, lilizingirwa na msitu mkali lenyewe likiwa katikati ya msitu huo mkubwa.



    Si rahisi kuona barabara inakoingia mpaka kwenye jengo hilo kubwa hivyo wapitanjia wa kawaida hawakuwa na urahisi wa kuingia ndani ya jengo hilo japo kwa mbali waliweza kuliona. Wengi walidhani kwamba lilikuwa halikaliwi na mtu. Wengine walijua linakaliwa na majini kama imani zao zilivyowatuma.



    Hata walinzi hawakuweza kuonekana kwa urahisi kwani hawakuwa wakitoka mara kwa mara hasa wakati wa mchana. Wengine walijua ni sehemu ya ajabu kwani wengi walioingia huko hawakurudi waliuliwa ili kuzuia siri kufichuka.



    John na Aminata pia hawakujua wako wapi kwani waliingizwa ndani ya jengo hilo walikuwa wakiwa wamezirai kutokana na kipigo kikali kutoka kwa Mosses Ndula na vikosi vyake.



    Jioni ya saa mbili na nusu walikuwa ndani ya Land Cruser V8 kabla ya kutekwa John na Aminata, walikuwa wakielekea nyumbani kwa Aminata kwa ajili ya mapumziko kwani ilikuwa ni majira ya jioni. Aminata ndiye aliyetoa wazo kwa John kwamba waende kupumzika.



    John alikubali na kuondoka. Walikuwa wakijiburudisha jioni. Hawakuwa na mengi ya kufanya zaidi ya kuwa pamoja.

    Baada ya kujifungua mtoto wao Amigolas, sasa waliishi kwa furaha huku wakiamini kwamba mambo yametulia. Mtoto wao alipelekwa shule za bweni ili kumwezesha asome zaidi. Ni miaka mitano baada ya kuzaliwa na kuifanya familia ya John kuwa na furaha baada ya kumpata Amigolas mpya.



    Sasa waliishi maisha ya wawili. Walifanya hivyo ili kumwepusha mtoto wao na balaa linaloweza kuwatokea kwani Aminata alikumbuka siku aliyomwona Mosses dirishani na kushtuka. Aqalimsihi sana John wampeleke Amigolas shule za bweni ili asije akapatwa na madhara kwani aliamini bado hawajamalizana na Mosses Ndula.



    Wakiwa wanapita barabara iliyotokea Hospitali ya Mount Meru, Aminata alitazama kwenye kioo cha gari na kuona msururu wa magari ukiwafuta huku yote yakiwa yamewasha taa kuashiria jambo fulani.



    “John embu geuka nyuma ujionee hayo magari, sijui yanaelekea wapi,” John aligeuka na kujionea, alihisi jambo hivyo akamwambia Aminata aingilie barabara inayoelekea Kijenge kisha aongeze mwendo. Aminata alimshangaa John kwa maneno aliyoyatoa na kukemea kwa hasira.



    “Kwani umeambiwa wanatufuata sisi?” John alizidi kumsihi afanye hivyo. Aminata alibaki akimwangalia John ambaye hakuwa hata na wasiwasi huku yeye akiendesha gari kama alivyoelezwa. Wakiwa makutano na Barabara ya Kijenge karibu walikuwa tayari wamezingirwa baada ya gari nyingine kutokea upande wa chini wa barabara ya Uhuru.



    Aminata alifunga breki kwa nguvu zote kutokana na gari kuwa katika mwendo wa kasi. Gari zilizokuwa zinakuja mbele yao nazo zilisimama na kisha watu takribani saba waliteremka kuwafuata. John na Aminata hawakuwa na silaha ya aina yeyote hivyo wakajikuta wakiishia katika mikono ya vikosi vya Mosses Ndula.



    “Aminata kwani kuna nini?” Aminata hakujibu kitu bali alikaza macho ili kuwatambua watu waliokuja mbele yao kama aliwajua. Alimwona Mosses na watu wake wakija.



    “Ni Mosses.”



    “What?” John alihamaki baada ya kumwona Mosses akiwafuata huku ameshikilia bastola akifuatana na watu wengine waliokuwa wameshikilia silaha nzito.



    “John tutafanyaje hapa na hatuna hata silaha?” Aminata alisema huku akimwangalia Mosses bila kuamini macho yake kwamba amerudi tena na bado anaendelea na ukatili wake. John kabla ya kumjibu Aminata. Mosses Ndula ndiye aliyekuwa wa kwanza kushika kitasa cha gari la kina John na kumchomoa John kwa nguvu. Alimtupia John ngumi nzito na kuzirai. Bosi Steve alimchapa Aminata kwa kitako cha bunduki na kuzirai.



    Waliwachukua wote mpaka katika jengo lao kubwa lililokuwa kule Mererani. John na Aminata hawakuweza kutambua waliko. John ndiye wa kwanza kuzinduka na kujikuta akivuja damu sehemu za usoni na kwenye jicho la upande wa kulia.



    “Mnataka nini nyie watu, si mseme na mtuachie twende zetu? Kwanza hapa ni wapi”? alifoka John kwa hasira baada ya kumwona Mosses Ndula karibu yake. Mosses Ndula alicheka kicheko cha dharau na kumchapa kibao tena John, wakati huo Aminata alikuwa analia huku kashikiliwa na Bosi Steve.



    “Ulitaka kuchukua mali za baba angu, sasa hujaridhika unataka kunichukulia na mimi” haya fanya uwezavyo.”



    “Unajidai hujui kilichosababisha kuwepo hapa we nyang’au? leo utatutambua kwamba sisi siyo hiyo Serikali yako inayowatuma kufanya uhuni wakati uhuni wenyewe hamuujui” Bosi Steve alimkaripia John na kumchapa tena ngumi ya tumboni.



    “Sisi hatujatumwa na mtu. Wala hatuna tunalolitaka kwenu,” John alisema huku akimwangalia kwa hasira Mosses ambaye alikuwa amemwekea bastola kichwani.



    “Kimya, Malaya mkubwa wewe, unataka kuleta upelelezi wa kizamani hapa, leo na wewe utanitambua, baada ya kufa kwa huyu nyang’au wa kiume utafuata wewe Malaya mkubwa, Bosi Steve alimkaripia Aminata ambaye alikuwa akilia.



    “Chanzo cha yote haya ni huyu mpumbavu mwenzako….wote leo mtakufa. Namkumbuka sana. Alimlaghai mtu wangu ili kujua mambo yangu…sasa atayajulia aghera.”



    Haikuwa rahisi kwa John kuweza kumjulisha rafiki yake Max aje kumwokoa.



    John na Max walijuana baada ya Max kusikia kwamba Aminata ameolewa na John. Yeye alikuwa kwenye mafunzo Urusi na hivyo hakuweza kuhudhuria wala hakujua lolote. Aliukumbuka tu urafiki wake na Aminata wakiwa pamoja chuo.



    Alipotezea hata lile lengo lake la siku moja kumwambia Aminata kwamba anampenda. Sasa aliamua kuacha mambo ya livyo. Aliamua kuwa karibu nao kwani kazi aliyopewa ilikuwa inawahusu wote na hivyo iliwalazimu kujuana.





    Baada ya kurudi walikuwa wakiwasiliana na hapo John alipata kumfahamu na kujua alilokuwa akifanya. Ukaribu wao ulimpa nafasi John kujiingiza katika masuala ya upelelezi hasa baada ya kushawishiwa sana na mke wake Aminata. Aliaanza kujifunza masuala ya jeshi na baadaye alihamia kwenye upelelezi. Alitumia muda mfupi kutokana na kufahamiana na wakufunzi ambao walimfananisha na Antony ambaye aliwahi pia kupitia jeshi. Pia Aminata alimsaidia katika kujua mafunzo ya upelelezi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Katika jumba la Steve John sasa hakuwa na lakufanya zaidi ya kusubiri kama ataweza kujiokoa mwenyewe. Aliona kweli itakuwa vigumu sana kuokoka katika mikono ya wahuni wale lakini akaapa kwamba lazima atajitahidi kujiokoa. Alijua wakiweza kuchukua silaha zao yeye na Aminata wataweza kujikwamua kutoka kwao.

    Alikwisha tambua kwamba genge lile lilikuwa ndiyo lile lililokuwa linasakwa na Serikali na hivyo kutokana na kwamba John alikuwa mmoja wa aliotumwa kulifuatilia alijua itakuwa genge hilo limejua azma ya Serikali juu yao na hivyo kutaka kukomesha matakwa ya Serikali. Alifikiria kama ataweza kuwasiliana na Max lakini hakuona njia yoyote.



    Hakuwahi kufika sehemu ambayo alipelekwa na wala hakujua yuko wapi kwa wakati huo hivyo alihofia pia iwapo akijaribu kujiokoa atapita wapi kurudi kule alikokuwepo awali.



    *****

    Max amekuwa mpelelezi wa Serikali kwa kipindi kirefu na amekuwa akiaminiwa na Serikali juu ya majasusi na maharamia wa nchi ambayo wanataka kuipeleka nchi pabaya. Wauaji na wadhalimu wa mali za walio wengi kwa kutumia mabavu aliweza kuwadhibiti vilivyo kwa kutumia mbinu za kiintelejensia.



    Hakupenda udhalimu wala manyanyaso ya watu wachache dhidi ya raia wasio na hatia.



    Alifurahi kuwa karibu na John pamoja na Aminata. Kazi walizofanya pamoja za kupambana na uhalifu ziliwafany wawe ni watu walioheshimika sana. hata viongozi wan chi waliwajua kwamba waliweza kazi ingawa kulikuwa na matatizo ambayo yalipelekea wafanye kazi kwa ugumu.



    Moja ya kazi ambazo walipewa ni ya kufichua wapi zilipokuwa almasi na kuwashikilia wahusika. Almasi hizo zilikuwa zimefichwa katika kitongoji cha Kigamboni Dar es Salaam.



    Hilo lilifanikiwa kwa hali ngumu kwani walikumbana na mashambulizi ya hatari ambayo yalipelekea Max kuvunjika mkono. Mazx aliipenda kazi yake na hivyo baada ya kupona mkono wake aliamua kurudi na kuendelea na kzi hiyo.



    Habari za kutoweka kwa John zilitawala kila kona, watu waliweka makundi kujadili juu ya habari hizo. Max naye alizipata habari hizo. Alijua lazima na Aminata atakuwa na John kwani mara nyingi walitoka pamoja hasa wikiendi.



    Alijua sasa lazima afanye awezalo ili awasake walipopelekwa. Hakujua juu ya jumba la Steve.



    Ndani ya jengo la Steve, Mosses Ndula na Bosi Steve wakati wote walikuwa wakitaka kujua ni kwa nini Serikali inataka kuwafatilia, hivyo waliendelea kumhoji John wakati wote. John alionyesha ujasiri mkubwa kwa kutokuonyesha ushirikiano wowote kwao.



    Alipewa adhabu mbalimbali ili aweze kusema lakini hakuwaeleza jambo lolote kuhusiana na Serikali akidai kwamba yeye hakufahamu jambo lolote na hivyo wanamwonea tu.



    “Mna uhakika gani kama mimi nimetumwa na Serikali kuja kuwachunguza, kwani ni katika mazingira gani ambayo mmenikamata?”



    “Wewe unataka kutuambia hii picha hapa siyo wewe, au tumeifananisha hiyo sura?” Mosses Ndula alimfokea huku akimkaba John shingoni. Alimwonyesha picha ambayo alikuwa na Aminata wakimpongeza baada ya kuhitimu mafunzo ya upelelezi. John alishangaa sana.



    “Kama mlinikosa mwanzo…..sahauni kuhusu kunipata.”

    “Mimi sina shida na wewe kama unavyofikiria.”

    “Sasa mbona unawachelewesha….fanya kama tulivyokubaliana bwana Mosses. Muda unakwenda,” Bosi Steve alitoa kauli hiyo baada ya kuona hakuna ushirikiano wowote ulioonyeshwa na John na Aminata.



    Moses alkuwa akiwaangalia kwa hasira wote wawili, alishindilia mdomo wa bastola aliyokuwa ameishika juu ya kichwa cha John huku akimkaba shingo kwa nyuma. Hasira zilikuwa zimempanda sana.



    “Leo safari yako ya kuzimu imetimia, lazima ufe ili tuweze kuzima hizo janja zenu za kutaka kutudhibiti, nataka nikuambie kwamba leo wewe na huyo malaya wako mtaongozana kwenda kuzimu kisha itafuata hiyo Serikali yenu. Bosi Steve alimwamuru Mosses Ndula awaarifu vikosi vya mauaji kutekeleza tukio hilo mara moja.



    Mosses Ndula bila ya kuchelewa aliwaamuru kikosi cha mauaji kufanya kile Bosi Steve alichotaka.



    “Wapelekeni nje ya mji karibu na pori dogo na kisha baada ya kuwaua muache miili yao katikati ya barabara. Aliwaamuru wafanye hivyo wakihakikisha kwamba hakuna mtu yeyote atakayewaona wala kuwadhani wakati watakapokuwa wameshafanikisha tukio hilo.



    Bosi Steve na Mosses Ndula walibariki mauaji hayo na kisha kuwaaga askari wa kikosi cha “MALIZA KAZI” ambao ndiyo waliopewa dhamana ya kutekeleza adhabu ya kifo. Walikuwa ni askari watatu waliowachukua John na Aminata mpaka eneo waliloagizwa.



    Wakiwa njiani hali ilikuwa ni shwari kwani hakusikika kiumbe wa aina yeyote aliyelia wakati huo, wakiwa wanatoka waliwafunga vitambaa usoni ili wasitambue walikokuwepo na wanakokwenda, iliwachukua takriban dakika arobaini kufika. Waliwashusha kutoka kwenye gari aina ya MARK II nyeusi na kuwavua vitambaa ambavyo waliwafunga ili wasiweze kutambua eneo waliloko.



    John alitumia ujasiri wake kutaka kuwalaghai askari wale ambao walikuwa watatu. Aliomba afunguliwe mikono ili aweze kuongea mara ya mwisho na Aminata kisha atakuwa tayari kufa.



    Kwa vile askari wale walikuwa wameshika silaha za moto hawakuhofia jambo lolote ambalo John angeweza kusababisha kwani hakuwa na silaha ya aina yoyote wakati huo. Walimfungua John na Aminata kamba walizokuwa wamewafunga mikononi kisha kuwasogeza kando ili waweze kuzungumza maneno ya mwisho kabla ya kifo chao.



    “Usijali Aminata niko kwa ajili yako, hakuna baya litakalokukuta usiku huu, kumbuka kwamba tuko wawili na nina imani kwamba tutashinda. Nakupenda sana Aminata,” alimalizia John huku amemshika Aminata mikono.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Najua unanipenda sana John lakini hadi sasa sioni kama tutasalimika na unaona wamebeba silaha wakati wewe huna hata moja, sijutii kuwa na wewe John hii ni kazi yetu wote, sijui mtoto wetu ataishije bila ya wazizi wake. Najua atapata tabu sana lakini Antony yupo, atakaa na baba mdogo wake. Kwa kuwa nakupenda nitakufuata huko huko kuzi….



    Kabla hajamalizia neno alilokuwa anamwanbia John, John aligeuka na ngumi nzito na kumtupia askari aliyekuwa karibu yao akiwasubiri wamalize kuzungumza. Askari yule alianguka chini na kuzirai na mara moja John aliiwahi silaha yake na kuwamiminia risasi askari wawili waliobaki. John alipata nguvu za kukimbia pamoja na Aminata. Aminata hakuamini macho yake. John alikuwa amemkabidhi Aminata silaha moja kati ya tatu na yeye akabakiwa na mbili. Walipita njia za vichaka hadi walipoona eneo lililokuwa na mwanga.



    Zilikuwa zimepita saa takriban tatu bila ya jibu lolote toka kwa askari wa Mosses Ndula kuhusiana na kifo cha John. Wala hawakuona dalili za askari hao kurudi mapema. Ilibidi watumwe askari wengine wawili kufuatilia juu ya kinachoendelea. Gari la askari waliotumwa lilifika eneo la tukio saa tano na nusu usiku na kushuhudia damu nyingi ikiwa imemwagika.



    Waliona askari wao wakiwa wamelala chini wakiwa hawana hata silaha moja. Walishangaa kuona walikuwa wawili wakati kambini waliondoka watatu. Mara wakasikia sauti ya askari ikilia kwa maumivu makali. Walimfuata na kumbeba na kumwingiza kwenye gari.



    Waliwachukua wale maiti wawili na kuwapakia kwenye gari na kuondoka nao kurudi kambini kwani walijua isingekuwa rahisi kwa wao kuwatafuta John na Aminata wakati huo kwani lazima watakuwa wamejificha mbali sana, hivyo waliona ni bora wakatoe taarifa juu ya kilichotokea.



    Waliwafikisha wale maiti pamoja na yule askari mwingine majeruhi kwa wakuu wao. Bosi Steve alikasirika sana kusikia kwamba John na Aminata walitoroka baada ya kuwashinda askari wake nguvu. Alimmiminia askari aliyebaki risasi na kumuua.



    “Wafuate wenzako mshenzi mkubwa wewe,” alifanya tukio hilo la mauaji kwa askari yule akiwa na hasira sana. Askari wengine waliokuwepo eneo lile walipata woga wakijua kwamba wanaweza wakauawa.



    ”Nataka John na Aminata warudishe hapa haraka sana,” alifoka Bosi Steve.



    Mosses Ndula aliwaamuru askari wavae nguo za kiraia ili waingie katika msako wa kuwatafuta John na Aminata kabla habari hazijazagaa juu ya kutekwa kwao na kutoroka.



    Wakati huo John na Aminata walikuwa wamepata sehemu ya kulala na kupumzika ambapo walijua hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kutambua sehemu waliko. Walikuwa katika hoteli ya MIDLAND.



    Aminata hakuamini kwamba wamepona wakati wote alikuwa anafurahi wakati John yeye alikuwa akitafakari hatari atakayokumbana nayo hapo mbele.



    “Vipi John mbona unaonekana una mawazo mpenzi, sijui hata nikushukuru vipi mpenzi wangu kwa ushujaa uliouonyesha na kupelekea kupona kifo kile, nilijua ni lazima wangetuua mpenzi. Nakupenda sana jasiri na shujaa wangu,” Aminata alimkumbatia John kwa nguvu huku akimtupia mabusu motomoto ambayo wakati huo John hakuwa katika hisia hizo kama alizokuwa nazo Aminata.



    Aminata alishanga kitendo cha John kubaki akimwangalia tuu asijue la kufanya. Wakati huo John alikuwa katika hali ya majeraha makubwa yaliyosababishwa na kichapo kikali alichopata toka kwa Bosi Steve na Mosses Ndula.



    Aminata kuona hivyo mara mija alimtoa John shati alilokuwa amevaa na kuanza kumfuta damu na kuuguza majeraha aliyokuwa nayo japo kuwa nay eye alikuwa akiugulia maumivu aliyoyapata baada ya kupigwa na Steve hadi kuzirai.



    Ni furaha ndiyo iliyommaliza maumivu. Alijihisi mwenye nguvu huku akimhudumia mume wake tayari kwa kumweka sawa.



    “Nadhani maisha yetu yapo hatarini zaidi kuliko hatari tuliyokutana nayo. Hawa jamaa lazima watutafute hivyo Aminata naomba uwe makini sana na tena ikiwezekana usikae mbali na mim,” John alimwambia Aminata ambaye kwa wakati huo alikuwa akimfuta John damu iliyoenea mwilini na kumuuguza majeraha aliyoyapata.



    “Najua John, siko tayari kufa. Ntapambana kama tulivyopambana. Sijasahau kabisa mapambano. silaha tayari tunazo. Tutaweza tu. Huyu Mosses nadhani hatujui… haifai tukamkawiza. Tujipangeni twende.”



    ”Nakupenda sana Aminata,” alirudia tena John maneno yale yale aliyomwambia Aminata wakati wote, ila safari hii ilikuwa ni kumdhibitishia kwamba yuko tayari kufa kwa ajili yake. Aminata alilia kwa uchungu baada ya kukumbuka kwamba walinusurika kifo pamoja, alimvamia John na kumkumbatia kwa nguvu zote huku akimpa mabusu motomoto yaliyomfanya John asahau hata maumivu ya majeraha aliyokuwa nayo.



    Mlango uligongwa ghafla wote wakashtuka. John alificha silaha nyuma na kuelekea mlangoni. Aminata hakujua la kufanya zaidi ya kusubiria kitakachotokea. Alikuwa tayari kashasimama karibu na silaha ingawa hakuichukua. Alikuwa ni mhudumu wa hoteli aliyegonga ili awaulize jambo.



    “Hodi kaka yangu, samahani kwa usumbufu, je mngehitaji chakula?” John aliyekuwa amebeba silaha alirudi nyuma na kuiachilia silaha juu ya kiti jambo ambalo haikuwa rahisi kwa yule mhudumu kugundua ni kitu gani. John alimuuliza Aminata kwamba angependelea chakula gani.



    “Chochote utakachokula mpenzi mimi nitakula.” Aminata alijaribu kumwonyesha John mapenzi ya dhati ilimradi amfurahishe na ajue wazi kwamba anampenda sana. John alimwomba mhudumu awaletee wali na nyama choma pamoja na glass mbili za juice ya Passion. Baada ya dakika kama tano, mhudumu alikuwa amesharejea na alichoagizwa na John.



    Hawakuwa na hela ya kulipia na hivyo John alimkumbuka Max. alitaka amtaarifu aje mahala walipo ikiwa ni pamoja na pesa ya kulipia chumba pamoja na chakula.



    “Aminata, nahitaji kupiga simu kwa Max haraka iwezekanavyo kesho nikutane naye ili tujue la kufanya, hawa washenzi lazima tuwaangamize hata kama wanajeshi la watu milioni kumi,” John alimtaarifu Aminata juu ya alichofikiria.



    “Bila hivyo Aminata sisi tutakufa na ujue kwamba hapa tulipo tupo kazini kwa hiyo kuwaangamiza hao washenzi itakuwa ni sehemu ya kazi yetu. Sitakubali walete madhara kwa wengine kama walivyotaka kuleta kwetu. Nitahakikisha kwamba wanaangamia wote,” John alizidi kuongea kwa hasira. Alimkumbuka Mosses na Syteve. Alijiapiza ni lazima awamalize.



    “Sikiliza John, inabidi tutulie kwanza ili tuweze kuwatafuta wenzatu tujadiliane juu ya hilo suala lakini si kwenda mbio hivyo. Na isitoshe wale inaonekana ni hatari zaidi wanaweza wakatudhuru mpenzi. Mi nna imani akiongezeka Max na Antony tutawamaliza,” Aminata alimsihi John.



    Najua Aminata lakini lazima tuanze hili jambo mapema kabla hawajagundua mipango mingine hivyo ni lazima nikutane na Max mara moja ili tujue tutawafanyaje,” John alimhakikishia Aminata juu ya hilo.



    “Sawa mpenzi lakini nahofia sana maisha yetu, na mi sitakuacha tutaenda wote kila mahali ukifa na mimi nife hapo hapo,” Aminata alimfariji John.



    “Aminata, nimekumbuka kitu,” alisema John.



    “Kitu gani tena mpenzi?” Aminata aliuliza.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mi naona ungeliacha hili suala kwetu sisi. Sitaki mtoto wetu apate shida ya kuwa bila ya wazazi. Nakuomba usiende. Tuachie mimi na Max. Najua tutaweza,” John alijaribu kumshawishi Aminata ili asijihusishe na mpambano ambao alitaka kufanya na Max na Antony bila ya kuwashirikisha wengine.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog