Search This Blog

Sunday 22 May 2022

JULAI SABA - 4

 







    Simulizi : Julai Saba

    Sehemu Ya Nne (4)



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Adui wa Amata alikua ni mjanja kupita maelezo, alijizungusha na kupiga ngwala ya miguu miwili ule uliotangulia ulipita sentimeta kadhaa kutoa sakafuni na Amata aliukwepa kwa kuruka lakini ule wa pili ulifuatia juu kidogo ya ule wa kwanza, huu ulimpata sawia kabisa katika visigino vyake na kutokana na kasi ya mguu ule, Amata alijikuta akikosa umakini hivyo kwa wakati huo akili yake ilifanya kazi haraka na kujirusha samasoti lakini alisahau kuwa eneo hilo ulikuwa ni ujia mdogo ambao haukuzidi mita moja na nusu kwa upana, so kwa uamuzi wake huo akajikuta akijigonga kichwa ukutanni na kitendo hicho kilifanya kengele za tahadhari za siri katika jingo lile kupata uhai, alipotua chini kama mzigo taa kali ziliwaka katika ujia ule na hakuna aliyeweza kujivuta hata sentimeta kumi, ndipo Amata kwa shida sana aliweza kumuona adui yake, akagundua kuwa alikuwa akipambana na mwanamke wa Kihindi, ShaSha, alimtazama kwa shida huku akiona taswira inayofifia machoni pake, akajitahidi kupambana na hali hiyo lakini haikuwezekana hata kidogo, akapoteza nuru kutokana na kupiga kicha chake kwa nguvu ukutani.



    ˜˜˜



    “Kazi imekamilika bila kuitolea jasho kiongozi,” Shakrum alikuwa akimueleza Shailan huku usoni akionesha furaha ya wazi kabisa isiyofichika, “kamanda Amata, Yule Malaya wa kihindi na mwanamke wa Amata, wote tunao mikononi bila tabu, ni sisi tu wa kutoa hukumu juu yao, nikiwa na maana kuwa siku hizi mbili tulizobaki nazo tuna uwezo wa kuitikisa dunia katika mhimili wake kupitia nchi hii nyonge na dhaifu,” aliendelea kuongea. Shailan alibaki katumbua macho tu kwani hakuamini anachoambiwa kuwa watu hao wote ambao walikuwa wanatishia juhudi za kazi zao sasa wapo mikononi mwao, bado ilikuwa ni kama simulizi ya alfu lela ulela, Shalan hakuamini kama Kamanda Amata wanae.

    “Shakrum, unalolisema lina ukweli au ndio sikukuu yua wajinga?” Shailan aliuliza.



    “Tangu lini nakutaniaga wakati wa kazi muhimu kama hii? Nimepewa ripoti kutoka yadi kubwa kule Bunju hawa jamaa wamejiingiza wenyewe katika mtego huo, na hivi sasa wapo katika chumba cha chini na pingu mbilimbili kila mmoja kuhakikisha hawatoroki,” Shakrum alizidi kusisitiza.

    “Habari njema, basi kwa ujumla tumemaliza kazi yetu kwa urahisi ambao hatukuutegemea. Haya mpe taarifa balozi tukutane pale yadi kubwa haraka iwezekanavyo,” Shailan hakuweza kuificha furaha yake, muda uohuo alituma fax haraka kule Mombasa kwa mkubwa wao naye aliwapongeza kwa hilo akaamuru watu hao wachinjwe mara moja na miili yao ihifadhiwe kwenye kaburi la siri ambalo limejengwa ndani ya yadi kubwa kupitia chumba maalum kilicho ndani ya chini ya ardhi.



    Haikupita hata lisaa limoja timu yote ya kikosi kazi cha ‘Freedom Fighters’ pamoja na balozi wao hapa nchini Mr Scolleti walikuwa wamekusanyika katika chumba maalumu pale yadi kuu, Bunju.

    “Tumepewa Baraka zote, za kuwakata vichwa hawa mabwana, na mi sioni haja ya kupoteza muda kwani kama kutusumbua wametusumbua sana hasa huyu Amata, na huyu nahitaji kumuua kwa mkono wangu huu,” Shailan aliongea kwa jazba mbele ya jopo lote hilo, akatulia kidogo akimtazama mmoja baada ya mwingine kisha akaendelea kusema, “Sasa hakuna po, kukipambazuka ni onyo la mwisho kwa serikali kwani sasa tayari ni wakati muafaka, afunguliwe kaka yetu, mpigania uhuru mwenzetu, anayejua kile anachokifanya, Jegan Grashan, awe huru na keshokutwa turudi naye nyumbani ambako atapokelewa kwa furaha,” akamalizia.

    Baada ya majadiliano machache, wote wakashuka kwa chombo maalum mpaka chini ya ardhi ambako walifika kwenye chumba hicho cha siri, chumba madhubuti kwani mlango wake ulifungwa kwa namba maalum ambazo ni mtu mmoja tu aliyezijua, Shakrum.



    “Ah ha ha ha ha !!!!” lilikuwa cheko la Shailan, cheko la dharau ambalo lilifika moja kwa moja masikioni mwa Kamanda Amata aliyekuwa amelala chini na pingu mbili mkononi mwake, alisikia kwa uzuri kila lizungumzwalo na watu hao lakini alijifanya bado hana fahamu ilhari akijua hila zao, ShaSha yeye alikuwa katulia tuli, hana la kufanya katika hilo maana pingu zile zilikuwa zimeimaban mikono na miguu yake pale chini, alikutana mzcho kwa mzcho na adui yake Scolleti, alyetumwa kwake kuja kuichukua roho yake tu baada ya serikali ya India kuchishwa na malalamiko ya mataifa mbalimbali yaliyopelekea mengine kuwa na mgogoro wa kidiplomasia na taifa hilo.

    Scolleti, alivuta hatua chache sana na akamfikia ShaSha pale alipoketi, akamsukuma kwa mguu wake, ShaSha akainua kichwa na kumtazama mtu huyo.

    “Hivi wewe mwanamke, nchi yako imekutuma na kukuamini kuja kunichunguza mimi, we unanijua mimi wewe, wenzako wote walionifuatilia mpaka sasa hawajulikani walipo, na wewe leo ndio zamu yako kuwafuata, kifo chako hakitakuwa na maazishi, wala maiti yako haitakuwa na mapambo yoyote, nani aliyekwambia binadamu anaweza kufuata nyayo za samba pa si kudhurika? Karibu sana katika himaya ya Shetani, na sisi sote ni wafuasi wake watiifu,” Scolleti aliongea kwa sauti yake nzito, huku akimsukasuka ShaSha. Bila kutegemea, Scolleti alijikuta akitemewa mate usoni na mwanamke huyo jeuri, aliyejiamini hata ndani ya pingu na minyororo ya watesi wake.



    “Hata ukiniua mimi bado wapo wanaokuja kukutafuta, yupo ambaye atakutia mkononi na kuivunja shingo yako hata kama si mimi, Shetani mkubwa wewe, unayepoteza maiSha ya watu kwa kufadhili na kuhifadhi magaidi sehemu mbalimbali duniani, ilahali kule kwetu India unajifanya mwema kuwasaidia masikini na kuwajengea mashule na mahospitali ili kuilagha serikali, sasa umefika wakati, msaada wako ni takataka mbele ya wanaokujua na sasa kinachopangwa na kutenganisha roho yako na mwili wako ambao tungewapa ndege wa angani wafaidi nyama iliyojaa damu ya ibilisi ndani yako,” ShaSha hakumaliza kauli yake kwani teke la nguvu lilitua ubavuni mwake, na kumlete maumivu makali, hajakaa sawa teke lingine na lingine, kisha Scolleti akaenda kwa Shakrum na kumvua mkanda wa kijeshi uliofungwa kiunoni mwake, vichapo kadhaa vilimuacha ShaSha hoi hajitambui, damu zikimtoka puani na kinywani, hasira zilizotawala damu yake zilimfanya ajaribu kujitikisa labda pingu zile zingemuachia huru amuoneshe kazi mzee huyu lakini haiku hivyo alibaki kuuma meno tu. Shakrum akamuendea Scolleti na kumvuta pembeni, “Braza, usifanye kazi ambayo bado muda wake,” alimwambia. Tajan akaingia ndani ya chumba hicho akiwa na dvcam moja iliyofungwa juu ya miguu maalumu ya chuma, akaiweka mbele yake na kuigeuzia kule aliko Amata na ShaSha, Shailan akajifunga kitambaa cheusi usoni mwake na kusimama mbele ya camera ile kisha akaanza kuongea, kutoa ujumbe wakati chombo kile kikinasa picha ile. Nusu saa baadaye walikuwa wamekamilisha zoezi lao, waliamua wawachinje watu hao watatu siku iliyofuata huku wakipiga picha zingine ambazo zingekuwa ni salamu ya mwisho kwa serikali kama wasingekubali kumfungulia ndugu yao, kaka yao, mpigania uhuru mwenzao.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    <<<<<<<>>>>>>



    ASUBUHI ya siku iliyofuata ilimkuta Madam S katika ofisi yake akiendelea na majukumu yake kama kawaida, ndani ya ofisi yake kubwa na nzuri iliyobeba heshima zote za kuitwa ofisi. Kila mara aliangalia saa yake kana kwamba kuna mtu au kitu anachokisubiri ambacho mi na wewe hatukukijua isipokuwa yeye peke yake. Ilipita nusu saa ikawa saa, Madam S aliinua simu yake ya mezani na kubofya namba kadhaa kisha kutega chombo cha kusikilizia sikioni mwake lakini baadae alikishusha na kukiweka palepale alipokitoa.

    Kwngele ya mlangoni kwake ililia, nae kwa kutummia chombo maalum aliweza kumuona Yule anayegonga kengele hiyo, Madam S akabonyeza tarakimu kadhaa zilizotengenezwa maalum juu ya meza yake na mlango ukajiondoa kitasa chake na kuruhusu mtu huyo kuingia ndani.



    DHL, ni kijilebo kidogo kilichoning’inizwa katika box kubwa lililowekwa katika meza ya kando kidogo ofisini mwa Madam S, mlinzi wa getini alilileta ndani humo. Madam S alilisogele na huku akiwa ameshika saa yake akichezea kidubwasha Fulani, alipolikaribia akasimama na kuliangalia vyema, kabla hajalifungua alipiga simu getini na kumuita Yule mlinzi kumuuliza ni nani aliyeleta kasha lile, akajibiwa kuwa ni mfanyakazi wa DHL ambaye alikuwa na pikipiki. Kwa uzoefu wa kazi za kipelelezi kwa maiaka mingi, madam S aligundua wazi kuwa lile kasha halikutoka DHL kwani ufungwaji wake ulikuwa tofauti na ule aliouzoea, alilichunguza tena na tena na kugundua mambo mengi ambayo ni tofauti na utaratibu wa DHL, akalichukua na kuingiza kwenye kikabati maalumu chenye mitambo ya x-ray ili kuweza kuona ndani kuna nini kabla ya kulifungua. Mtambo ule baada ya kuwashwa ulionesha ndani ya kasha lile mlikuwa na kitu mfano wa dvd, akalitoa ndani na kulifungua, hakukosea, ilikuwa ni dvd moja ikiwa katika kasha lake, akaitoa na kuigeuzageuza, kisha akaifuata luninga yake kubwa iliyopo hapo ofisisni na kuitumbukiza dvd ile, akasubiri kuona kitu kitakachofuata.



    Mtu aliyevalia vazi jeusi lililomfunika mpaka usoni, alionekana ametulia tuli, kisha akaanza kuongea kufikisha ujumbe ule alioukusudia. Madam S alisikiliza kwa makini ujumbe huo wenye vitisho vingi vya mauaji ya kutisha kutoka kwa magaidi waliokuwa wakidai kufunguliwa kwa mwenzao Jegan aliyefungwa na serikali ya Tanzania. Mwisho wa dvd hiyo aliziona picha za mateka waliowakamata akiwemo Kamanda Amata, Gina na mwingine asiyemjua. Kijasho kilimtoka Madam S, moyo ulimuenda mbio, akanyanyua simu iliyopo mezani na kubonya namba Fulani Fulani,

    “Yes, nakuja sasa hivi, kuna ujumbe mzito umetufikia asubuhi hii,” Madam S akakata simu baada ya kuongea maneno hayo, alionekana wazi kuchanganyikiwa kwa hilo, akanyanyuka na kuondoka zake.



    Breki ya kwanza ilikuwa katika jengo la wizara ya ulinzi, kwa kasi alishuka katika ngari yake na kuuendea mlango ambao aliufungua bila kubisha hodi, moja kwa moja alikutana na mheshimiwa waziri aliyekuwa akimsubiri kwa hamu.

    “Ndio madam,” alimkaribisha huku akiipokea ile dvd na kuelekea kwenye luninga yake, akatumbukiza kwenye chombo maalum cha kusoma dvd hiyo na kutazama,

    “…tumesema tumechoka, nah ii sasa ni mara ya mwisho, hatutarudia tena, tunaomba mumuachie huru ndugu yetu, mpigania uhuru mwenzetu mliyemfunga katika gereza lenu la Ukonga, Jegan Grashan. Tuliwapa siku saba lakini sasa tumeona wazi kuwa hamna nia ya kutekeleza ombi letu. Basi kama ilivyo ada kwa kuwa imebaki siku moja na masaa machache, matukio mabaya ya kutisha yatakayoondoa roho za walio wengi yatatukia mara tu mmalizapo kutazama dvd hii, watanzania makumi, mamia kwa maelfu watateketea kutokana na ugumu wa mioyo yenu, muachieni huru kaka yetu nasi tuwaachie nchi yenu, la, damu itamwagika na kamwe matukio haya hayatasahaulika katika historia ya taifa lenu, kizazi hata kizazi. Kama mlikuwa mnajidai na mpelelezi wenu kutuharibioa mipango yetu, sasa ni huyu hapa tunae, hata mumtafute vipi kamwe hamtompata, muachieni Jegan tumuachie Kamanda Amata, siku yetu Julai Saba imefika, nchi itatetemeka kwa hofu na kilio kikuu, lakini utangulizi wa yote mtaupata sasa, kaeni chonjo…”

    Ujumbe ule uliishia hapo na mheshimiwa waziri aliona picha ile ya kwa uzuri kabisa, kamanda Amata aliyekuwa hoi bin taaban chini sakafuni, mheshimiwa waziri alionekana wazi akitetemeka.

    “Madam, hapa hatuna ujanja, twende Ikulu haraka,” Mheshimiwa waziri aliyasema hayo huku tayari alikuwa ameitoa ile dvd na kushika njia kuelekea nje, gari yake ikaja jirani mara moja, wote wawili wakaingia na kuondoka.



    KIVUKONI – DAR ES SALAAM



    Honi ya pantoni ilisikika watu walikimbilia na kuingia ndani ya chombo hicho ili wapate kuvuka kutoka Kigamboni kuelekea upande wa pili uliojulikana maarufu kama Ferry. Watu wengi walijaa, wakubwa kwa watoto, wanafunzi, wafanyakazi na wafanyabiashara, wote wakiwa kwenye michakato ya kuwahi shughuli zao za kila siku, nahodha wa chombo hicho alipoona kimejaa na tayari kuondoka aling’oa nanga na pantoni ikaanza kusogea majini taratibu, kwa mwendo wa madaha.

    Katika banda la kupumzikia abiria upande wa Kigamboni, palibaki watu wachache ambao walifika pale dakika kadhaa baada ya kile chombo kuondoka, hivyo iliwapasa kusubiri kitakaporudi.

    “Wewe ni msafiri au? Maana naona umekaa hapa karibu dakika ishirini sasa, wengine wakiondoka na wengine wakifika, we upo hapahapa, hapa si kijiwe cha wavuta bangi kaka, kama huvuki basi uondoke hapa,” Mgambo mmoja alikuwa akimsemesha kijana aliyekuwa ameketi katika moja ya vibench vilivyopo hapo, Yule kijana aliomba samahani na kuondoka eneo hilo, mkononi mwake alikuwa na redio ndogo iliyokuwa ikikoroma kana kwamba haipati mawimbi ya sauti, nay eye alikuwa akijaribu kuirekebisha mara kwa mara, akatoka na kuielekea tax iliyokuwa imeegeshwa jirani kabisa na kituo cha polisi, akaingia na kuketi kiti cha nyuma, akageuza shingo yake na kutazama nyuma kule baharini.



    Muziki wa Bob Marley, ‘So Much Trouble in In the World’ ulikuwa ukisikika kutoka katika spika zilizofungwa juu ya chombo hicho, kilendelea kukata maji kuelekea Ferry, na sasa kilikuwa katikati ya upande wa Kigamboni na Ferry, watu walikuwa wakitazama mandhari safi ya jiji kongwe la Dar es salaam, wakibadilishana mawazo, hili na lile, wanafunzi wakifikiria kufika mashuleni haraka huku wakiwaza jinsi gani watapata usafiri kutokana na manyanyaso ya kondakta dhidi ya wanafunzi, tabia iliyokithiri katika jiji la Dar es salaam, tabia inayopelekea wanafunzi wa kike kupata mimba ovyo kwa sababu ya urahisi wa usafiri hawana budi kujirahisisha ama kwa madereva tax au makondakta wa daladala, serikali inashindwa kuwatetea katika hilo, ikawahi kuanzisha mradi wa mabasi ya wanafunzi uliokuwa ukiendeshwa na vijana wa chama lakini pesa zote zikaliwa na mradi ulikopotelea si mimi wala wewe tunajua.



    Wakiwa katikati ya maji, kitu kisichotegemewa kikatokea, huku walio Ferry wakiitazama pantoni ile ikiwa inakuja taratibu na wale wa Kigamboni wakiiangalia ikiwa inaenda taratibu, sasa zilikuwa zikipishana inayotoka Ferry na inayotoka Kigamboni. Mtu mmoja aliyekuwa akisubiri katika banda la kusubiria usafiri huo upande wa Ferry aliinua mkono wake na kuitazama saa yake iliyomwambia ni saa tatu na nusu asubuhi, aliishikashika saa yake na alipoiachia alishtushwa na mtikisiko mkubwa mkubwa, mlipuko mzito ulioacha kitu kama tetemeko la ardhi la sekunde kadhaa, watu walionekana kutawanyika huku na kule wakiwa hawajui hata wapi wanakimbilia au nini kinawakaimbiza, mji wa Dar es salaam ulizizima kwa kishindo hicho. Moshi mzito, mweusi, uliobebwa na moto mwekundu sana vilionekana katikati ya bahari eneo la kuvukia vyombo hivyo vya usafiri, vilio vilitawala, hakuna aliyejua nini kimetokea.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Zimegongana! Zimegongana!” wengi walisikika wakisema hivo, “Hapana zimelipuka!” wengine walisikika namna hiyo, kizaazaa. Mamia ya wasafiri walikuwa wakiteketea kwa moto, nani wa kuwaokoa, vyombo vyetu vya zimamoto havikuwa na uwezo wa kufika pale, hakukuna na hata meli ya kusogea kufanya uokozi zote ziliogopa mlipuko kwani nazo zinatumia mafuta. Moto mkubwa ulikuwa ukiendelea kuwaka, pantoni zilikuwa zikiendelea kuteketea na abiria wengi walioko ndani, wenye uwezo walijirusha majini, wengine waliojua kuogelea wakafanya hivyo, wenzangu na mimi walibaki wakihangaika kunusuru pumzi zao za mwisho.



    ˜˜˜



    “Hawa jamaa hatuna njia ya kuwadhibiti sasa, kama Amata aliyekuwa akiongoza operesheni hii nae wamemteka, tutafanya nini?” Makamu wa Rais alikuwa akiongea na wadau wa usalama ofisini kwake katika Ikulu ya Tanzania, aliwatazama mmoja mmoja kwa zamu, hakuna aliyeonekana kama ana jipya katika hilo, Madam S, waziri wa mambo ya ndani, waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa, IGP, Mkuu wa majeshi na kamishna mkuu wa Magereza, kimya kiliwakumba, giza likawatawala.

    “Mheshimiwa hayupo, lakini sina budi kufanya maamuzi ya haraka, nitampigia simu na jibu tutatoka nalo sasa hivi kabla hali haijawa mbaya,” makamu wa Rais alipomaliza kusema hayo, aliitazama saa yake ya mkononi na alipoishusha alisikia mtetemo kama kishindo kizito cha kudondoka kitu, picha kubwa zilizokuwako ukutani zianguka na kuvunjika vipande vipande, kisha utulivu ukarejea tena. Jopo lote lililokuwa katika kikao hicho cha dharula lilihamanika kwa kishindo hicho, “Nini?” aliuliza makamu wa Rais, “Bila shaka ni mlipuko mzito umetokea, kwa kishindo hiki, itakuwa ni maili mbili au zaidi,” Mkuu wa majeshi alikuwa akisema hayo huku akinyanyuka kitini, mara simu ya IGP ikapata uhai, akainyakua kutoka mfukoni mwake ili kuizima asiharibu mkutano, lakini alipotazama kioo cha simu hiyo ilijiandika ‘Detective’, akaona ilikuwa ni habari nzito, “Inspector General of police,” IGP aliitikia kwa kujitambulisha cheo chake moja kwa moja, hii ilitokana na uzito wa simu iliyopigwa, simu ambayo inaweza kukaa hata miezi mitatu isipigwe, simu iliyoandikwa ‘detective’, simu nyeti, kwa mambo nyeti.



    “Mlipuko mkubwa umetokea maeneo ya Ferry, pantoni zote mbili zimewaka moto kwa mara moja wakati zikipishana,” ilikuwa sauti ya upande pili, “Umesomeka chukua hatua, nafika sasa hivi,” IGP alijibu na kukata simu. Sura yake iliyojikunja ilionekana wzi mbele yaw engine, akawapa ujumbe na wote wakaonekana wazi kuchanganyikiwa, makamu wa Rais akatoa amri ya kufuatailia swala hilo nay eye akisubiri taarifa hiyo.

    “Ugaidi,” Madam S alisikika akiongea kwa sauti ya chini, akipigisha viganja vya mikono yake kuashiria ameshindwa afanye nini. Iliwachukua dakika tano tu kufika eneo hilo, hali waliyoikuta ilikuwa tete, wapiga mbizi kutoka jeshi la polisi la wanamaji lenye kituo chake jirani kabisa na Ferry wakishirikiana na kikosi cha jeshi la wanamaji kutoka Kigamboni ‘Navy’ walikuwa wakishirikiana katika uokoaji huku gari za zima moto zikiwa zimefika lakini haziwezi kusogea eneo la tukio.

    Vilio vya wenye ndugu vilisikika kila kona, wakati gari za wagonjwa zilipokuwa zikitoka na kuingia kukusanya majeruhi ambao wameopolewa kutoka majini. Siku ilikuwa nzito kwa viongozi wa serikali, hawakuwa na la kufanya zaidi ya kukutana tena na tena kujadili swala hilo, msiba wa kitaifa.



    Madam S alisimama kwenye njia panda ya kuingia Ferry na ile inayokuja Posta ya zamani akiangalia kila kinachoendelea huku akiwa hajui hata wenzake aliokuja naoi wamepotelea wapi, midomo ilimchezacheza kwa hasira, machozi yalimtiririka kwa uchungu, alitamani amuone huyo anayesababisha haya yote ili amfundishe adabu, lakini hakumjua, alimkumbuka sana Kamanda Amata katika sakata kama hili tayari angekuwa amekwishajua fununu za mhusika, maana wakati mwingine alipenda kumuita ‘The black dog’ kutokana na tabia yake ya kugundua vitu haraka, Madam S aliifananisha na kunusa. Hakuwa na uamuzi, ahata alipokuja kushikwa mkono na Chiba kuondolewa eneo lile yeye bado alikuwa hajielewi.

    “Chiba, Kamanda ametekwa!” Madam S alimwambia Chiba wakiwa ndani ya gari.

    “Unasema?” Chiba aliuliza kwa mshtuko, Madam S akamueleza kwa kirefu sana juu ya ile dvd. Chiba alibaki kusikitika, akachukua kompyuta yake ndogo na kuifungua kisha akaanza kubonyezabonyeza namba Fulani Fulani na kufuatilia aina ya mchoro uliokua unajionesha ukijichora kitu kisichojulikana.

    “Unafanya nini Chiba?” Madam S aliuliza.

    “Natafuta uelekeo wa micro chip ya Amata labda itaniambia yuko wapi, ili tujue tunafanya nini,” Chiba alimjibu Madam. Baada ya muda mfupi wa Chiba kuchokorachora kompyuta yake, alimgeukia Madam S, “Madam” Chiba aliita, akamtazama Madam ambaye alikuwa amejiinua kutoka katika siti aliyokuwa amekaa katika mtindo wa kujilaza, “Signal, inanionesha Kamanda yupo maeneo ya Bunju,”

    “Bunju?!” Madam aliuliza.



    “Ndiyo ni Bunju,” Chiba alijibu.

    “Ok, fanya unaloweza ujue alipo na ikiweza upange rescue haraka, hawa jamaa inaonekana wameshatuweza kwa kumteka Kamanda” Madam alimwambia Chiba, mara Simu yake Madam S ikapata uhai kwa mara nyingine, akaichukua haraka kutoka katika mfuko wa koti lake na kutazama, private namba, akaifyatua kitufe cha kusikilizia na kuweka sikioni, ilikuwa ni simu inayomhitaji mkutanoni haraka.



    “Chiba nipeleke ofisi kuu,” aliamuru Madam S na Chiba alitii amri ya boss wake, akawasha gari na kuingia barabarani, muda mfupi baadae alikuwa tayari mbele ya jingo hilo chakavu la kizamani, jingo la mkoloni, city hall.

    “Fanya nililokwambia, kasha nipe mrejesho wa siri,” madam alimwambia Chiba, akashuka na kuingia ndani ya jingo hilo.

    “Mimi nilishasema, hawa jamaa watafanya kitu mbaya, tumuachie huyo mtu wao tuishi kwa amnai, sasa tazama jinsi watu wasio na hatia wanavyotekea, tutafakari mara mbili ndugu zangu, sio tunasikiliza ubishi wa mtu mmoja tena asiye na maamuzi kati jopo hili. Yuko wapi sasa? Si hawa wameshamteka!” alilalama Waziri wa ulinzi mheshiimiwa Maige. Wajumbe wa mkutano huo wote walikuwa kimya hakuna aliyethubutu hata kunyanyua mdomo wake, kila mtu alikuwa akimlaumu mwingine ndani ya moyo wake. Mara mlango ukafunguliwa na katibu wa ofisi hiyo, Miranda, na baada yake akaingia bi mkubwa Madam S, akavuta kiti kilichokuwa wazi na kuketi.



    “Mi nafikiri, sasa turejee uamuzi wetu, kwa kuwa leo ni tarehe sita mapema hii, kesho tarehe saba wanayomtaka mtu wao, hatujui mi na wewe nini wamepanga kufanya hiyo kesho, ina maana ulinzi uliowekwa haukuwa sawa?” mkuu wa majeshi akauliza, IGP akamtazama kwa jicho baya sana.

    “Lazima tujue tunapambana na watu wanaojua medani za vita, wameangalia wapi tumelegeza wametumia nafasi, hatutakiwi kulaumiana ila tunatakiwa tuamue la kufanya kwa kuwa muda ndiyo huo unakwenda na Julai 7 imekaribia.” IGP nae alitoa hoja yake. Mara mlango ukafunguliwa tena akaingia Miranda na karatasi mkononi na kumkabidhi Waziri wa ulinzi, akaitupia macho na kasha akaiweka mezani. “Ripoti ya awali ya ajali hii hapa,” Waziri aliwaeleza wajumbe na kila mmoja aliipitia na kuirudisha mezani.

    “Vijana wetu wa Jeshi la wananchi wameng’amua kuwa mlipuko ule ni wa bomu, na bado wanachunguza ni bomu la aina gani, maiti zilizoopolewa ni kama sabini hivi na majeruhi wengi sana wamekimbizwa hospitali,” waziri maige aliangusha machozi alipokuwa akisema hayo. Wote katika mkutano ule walibaki kimya kwa muda. Mara ngumi nzito ya nguvu ikatua mezani mpaka kufanya glass za maji kuanguka na maji kuwalowesha wajumbe, “Nasema hivi Jegan aachiwe mara moja na watu wake waondoke nchini ndani ya masaa kumi na mawili,” Waziri wa ulinzi alitamka kwa hasira, karatasi ikaletwa na akamkabidhi waziri wa mambo ya ndani aandike hati hiyo ya kuachiwa huru kwa gaidi huyo. Madam S aliinyakuwa ile karatasi na kuikunjakunja kasha akaitia katika chombo cha takataka, kila mmoja akamatazama mwanamke huyu aliyeonekena kuvimba kwa hasira mpaka mishipa ya uso ilidinda.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Tusiamue mambo kama watoto, kwa kutumia hasira, tumuachie!? Na damu za Watanzania hawa zilipwe na nani, na Kamanda Amata yuko wapi? Siafiki, siafiki, lazima tuingie kwenye mapambano ya nkono kwa mkono, kama mnaogopa kikosi changu na mimi mwenyewe tutaingia kazini kuanzia sasa,” Madam S alifoka, baadae kila mmoja akaona usahihi wa maneno hayo. Ulikuwa mvutano uleule ambao ulitokea siku tatu nyuma, kutokuelewana kukaendelea katika hilo. Mwisho wa yote, ikaundwa kamati ya watu watatu ili wakakutane na makamu wa Rais, kutoka kwao watapata lile wanaloona linafaa kuamuriwa.



    ˜˜˜˜



    Sherehe iliendelea katika ukumbi mdogo ndani ya yadi ile ya Bunju, freedom fighters walikuwa wakijipongeza kwa kazi waliyoifanikisha siku hiyo, huku ikiwa tayari kazi ya julai 7 imwkamilika bado kufyatua tu.

    “Sasa vijana, tumefikia tamati ya maafikiano yetu na serikali hii isiyo na masikio, leo tumewapa onyo lakini kesho wataiona kazi yenyewe watakapookota maiti zilizokuwa jivu mia kwa mamia, lazima dunia itikisike. Sasa Shakrum, weka kamera yako tayari twende kuchinja wale mbuzi,” Shailan aliwaambia swhaiba zake, kasha wote wakashuka kwenye kila chumba cha chini, chumba walichomfunga Amata na Yule Mkorea, walipofungua hawakuamini macho yao, hakuna mtu ndani. Shailan na wenzake wote wakajikuta wamepigwa na butwaa hawajui watu wale wametokaje mle ndani, kila mtu alimtazama mwenzie, wote wakatoka tena nje na kuufunga mlango ule. Wakatawanyika na kuwauliza walinzi ambao waliwaeleza wazi kuwa hakuna mtu aliyetoka nje, lazima watakuwa ndani umohumo, msako mkali ukaanza kila pembe ya jengo na kila chumba kilichopo ndani humo.



    Kamanda Amata na Shasha walikuwa wamejificha katika katika bomba kubwa la maji machafu lililopita chini tu ya chumba hicho walimofungiwa. Amata aligundua hilo baada ya kusikia kitu kama maji yanayotembea wakati alipokuwa amelala pale chini, baada ya kutoka wale jamaa, alijivuta mpaka kwa Yule binti wa Kikorea na kumchomoa pini iliyobana nywele zake, maana alijua wazi kutokana na ile shepu ya pini angeweza kufungua pingu walizofungwa, alipoichomoa kwa meno akaibana hivo na kujaribu kuingiza katika tundu la ufunguo la pingu aliyofungwa ShaSha na kufanikiwa kuifungua, kasha ShaSha akamalizia kufungua zilizobaki pamoja na zile za Amata, katika kutazama huku na huko waligundua kuwa kuna mlango uliozibwa kwa mbao laini, wakautoa uzibo huo kwa umakini sana na kujikuta kwenye choo kingine, wakang’oa sinki lake na kupata tundu la kutosha ambalo chini yake kulikuwa na lile bomba kubwa la maji machafu ambalo lilikuwa limekusanya maji ya mtaa huo. Ijapokuwa ilikuwa ni tabu kupita kwa kutambaa na kupambana na harufu mbaya na chafu lakini hawakuwa na budi kujiokoa kwa njia hiyo. Waliendelea kutambaa humo bombani kwenye hewa nzito sana ambayo kama hauna mazoezi ya kutumia pumzi lazima ufie njiani. Mwendo kama wa lisaa limoja walianza kuona mwanga wa jua mbele yao uking’aa kupitia yale maji, hapo wakapata moyo kuwa sasa wamefika nchi kavu, wakaongeza nguvu zilizokuwa zikipungua muda baada ya muda, walitambaa na kujikuta wanatokea baharini, ShaSha na Kamanda Amata walijikuta baharini, hiyo kwao ilikuwa ni faraja sana waliogelea kidogo kuondoa harufu na uchafu uliyowaganda mwilini, wakaogelea kuondoka eneo lile mpaka mbali penye maji safi, wakatoka nchi kavu na kujitupa kwenye mchanga. Kamanda Amata alimgeukia ShaSha, “Wewe ni nani?” alimuuliza,

    “ShaSha, kutoka India” akajibu

    “Unafanya nini hapa? Huoni unahatarisha maisha yako?” Kamanda aliuliza



    “Nipo kazini,” akajibu kwa kifupi huku akijinyanyua kwenye ule mchanga akasimama wima lakini bila kutegemea alijikuta akipigwa ngwala kali na kudondoka, kabla hajafika chini Amata alaijivingiriha na kumdaka kwa ustadi, akamkumbatia.

    “Kuwa muangalifu ShaSha,” akamwambia kasha akamtupia pembeni.

    “Tuko wapi?” ShaSha akauliza

    Amata aliangalia mazingira yale lakini hakuyajua kutokana na mikoko mingi iliyojaa eneo hilo, akampa ishara ya kuondoka, ShaSha akanyanyuka na wote wakafuatana wakitembea juu ya mchanga huo mweupe wakiwa hawajui wapi wanaelekea. Baada ya mwendo mrefu waliona madau ya wavuvi yakiwa yameegeshwa, wakaendelea kusogea mpaka eneo lile, “Bagamoyo,” Amata alimwambia ShaSha. Kisha akaendelea kutembea mpaka nchi kavu na kuyapita yale madau mpaka kwenye barabara kubwa. ShaSha akajiangalia na kujaribu kujinusa hapa na pale, akaona bado ananuka uchafu, akamnusa na Amata vivyo hivyo. Kamanda Amata alaimshika mkono ShaSha na kutembea taratibu wakapita mitaa kadhaa na kutokea katika hoteli kubwa ya Paradise, wakaingia mpaka kaunta, kila mtu aliyewaona akajishika pua kutokana na hali hiyo, mlinzi wa hoteli alaikwenda kuwazuia lakini meneja akampa ishara ya kuwaacha wafike kaunta.

    “Habari Kamanda Amata,” Yule meneja mwenye asili ya kipemba alimsabahi Kamanda



    “Si salama, naomba chumba change cha kawaida tafadhali,” Kamanda alitoa oda, na mara moja wakaongozwa mpaka ghorofa ya pili na kukabidhiwa funguo ya chumba hicho. Kabla ya yote kila mtu alijikuta akiuendea mlango wa bafuni wakakutana mlangoni mikono yao miwili ikiwa imekamata kitasa cha mlango huo. Wakatazamana, macho yakakutana, ShaSha akaona aibu akainama chini, Kamanda Amata akiwa bado kashika kitasa juu ya mkono wa ShaSha akakinyonga na mlango ukafunguka, bafu kubwa la kisasa likawakaribisha, wakaingia na kila mmoja akajitupa ndani ya beseni kubwa linaloweza kuwabeba wote wawili, michezo ya kuogeshana ikaanza na kumwagiana maji, kila mmoja akimmwagia mwenzake mwisho Kamanda Amata alimdaka ShaSha na kumvutia kwake, akamtazama usoni kwa tuo, ShaSha akaelewa lugha inayozungumzwa na macho ya Kamanda, vinywa vyao vikakutana, ndimi zao zikacheza pamoja, miili yao ikakutana, viungo vyao vikabadilishana mawazo, wote wawili wakazama katika bahari ya mapenzi.



    KAMANDA AMATA ALITOKA ndani ya bafu hilo la kisasa katika hoteli ya Paradise pale Bagamoyo, akiwa na taulo kiunoni mwake alipita kabisa na luninga, akili yake ikamtuma kwanza kuwasha luninga hiyo kujua nini kimejiri huko duniani muda ambao yeye hakuwepo huko. Luninga ile ilimkaribisha kwa moshi mzito uliokuwa ukionekana kwenye kioo chake, akatamani kujua kilichotokea akaketi kwenye kitanda na kukodoa macho akiizama ‘breaking news hiyo’, baada ya dakika tatu za kuangalia habari hiyo alikurupuka kama kichaa, ShaSha alikuwa bado akijivuta kama kawaida ya wananawake wengi, kujivutavuta dio mpango mzima kwao.

    Kamanda Amata tayari alikuwa ndani ya suti nyeusi safi iliyomtoa kweli kweli. ShaSha alipofika chumbani alimkuta Kamanda amekwishajiandaa, “Vipi, mi nilijuwa tunakula fungate, mbona mwenzangu hivyo?” ShaSha aliuliza kwa kiingereza chake kilichochanganywa na lafudhi ya kihindi. “Hapana mama hapa ni kazi,” Amata alijibu huku akimuonesha ile luninga pale.



    “Tayari, ugaidi umeshafanyika bila kificho na kesho ni Julai saba, lazima niwahi kuokoa jahazi,” kamanda Amata alimalizia kuongea huku akifunga kiatu cha mwisho, akamwangalia ShaSha pale aliposimama, “Twende au utakuja baadae?” akamuuliza.

    “Hapana tunaondoka wote, habaki mtu hapa,” ShaSha alijibu huku akinyakuwa moja ya gauni zuri la kibuluu lililokuwa limening’inizwa katika vining’inizio kadhaa vilivyowekwa hapo, wakati yeye anavaa, Kamanda Amata alikuwa akishushia glass iliyojaa pombe aina yaVodka ili akili yake ichangamke vizuri.

    Dakika kumi baadae wawili hao walikuwa tayari nje ya hotel hiyo wamekwishakukamilisha itifaki zote. Waliingia ndani ya tax moja ilikuwa imeleta mgeni hotelini hapo, “Bunju tafadhali, karibu na Baobab,” Amata alimwambia Yule dereva, naye akatii bila hata kuuliza. Kutokana na ustadi aliouonesha dereva Yule kwa kuendesha gari, haikuwachukua muda wakafika eneo hilo, ShaSha aliiona gari yake ikiwa imepaki palepale katika ile pub aliyoingia jana yake. Dereva akaegesha gari kwa mbele kidogo, Amata na ShaSha wakashuka, Amata akampa noti za elfu kumi tatu, ambazo alipewa pale kaunta katika hotel ile.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ile pale gari yangu,” ShaSha alimwambia Amata, wakatazamana. “Subiri hapa,” Amata alimwambia ShaSha, akachomoa miwani yake na kuipaika usoni kisha akainedea gari ile mpaka pale, akashika saa yake na kuizungusha katika mtindo Fulani, ile saa ikatoa mlio Fulani hafifu, akarudi kwa ShaSha na kumwamru wasonge mbele kidogo.

    “Vipi mbona umeiacha?” ShaSha aliuliza

    “Imetegwa bomu, haiku salama,” wakatembea mwendo mfupi wakafika kwa jamaa wanaouza na kufyatua matofali, “Subiri hapa,” akamwambia, Kamanda Amata akawasalimu wale vijana na kupita mpaka eneo ambalo wao huwa wanatumia kuteka maji au pi kujipumzisha, pana kijito kilichopita kuelekea baharini lakini kimezungukwa na machaka mengi utafikiri hakuna mtu anayefanya shughuli eneo hilo. Wale vijana wakawa wakimshangaa hawakujua ni wapi anaelekea, “Mheshimiwa choo hiki huku!” mmoja wao alipaza sauti kumwambia Kamanda akijua kuwa kaenda kujisaidia, akapotelea vichakani bila kumjibu yeyote. Aliikuta pikipiki yake ipo salama, akaitazama tena kwa jinsi ileile, akaikuta ko salama kabisa.

    Kutoka ndani ya kichaka, wale vijana walishuhudia bonge la pikipiki la Kirusia likiibuka kama kifaru cha jeshi ‘Cagiva’, “Twende zetu” alimwambia ShaSha aliyekuwa kabaki mdomo wazi, kwa wepesi wake alijirusha na kutua katika kiti cha mashine hiyo huku mikono yake akimutana mbele ya tumbo la Amata. Haikuwa mwendo wa kitoto, dakika chache walikuwa wakiipita Boko na kuitafuta Tegeta ambako hawakujali fole za kuja Mbezi mpaka Mwenge wao walipita pembeni pembeni na kujikuta wakifika katika mataa ya Mwenge mapema kuliko walivyotegemea. Muda wote ShaSha alikuwa kimya ametulia katika mgongo wa Kamanda Amata akisikiliza mlio mzuri wa pikipiki hilo.



    ˜˜˜˜



    Shailan bado hakuamini kile ambacho alikishuhudia, Kamanda Amata amewezaje kutoroka kwa jinsi walivyomdhibiti kwa minyororo na kumuweka katika chumba ambacho kwao kilikuwa ni chumba pekee chenye usalama wa asilimia mia moja. Alikuwa amesimama akiangali nje ya nyumba hiyo kupitia dirisha kubwa lililomruhusu kufanya hivyo. Shakrum alikuwa ameketi katika kiti kingine ndani ya sebule hiyo ndogo. “Tunahitaji kikao cha haraka,” Shailan alimwambia Shakrum, Shakrum ahakuhitaji kuhoji aliiendea meza ya mbele yake na kutuma ujumbe kwa wote wanaohusika kukutana hapo mara moja, na haikuchukua muda ndani ya nusu saa wajumbe wote walikuwa wamekwishafika, na kukusanyika katika meza kubwa ya duara, simu zao zote zilikusanywa na kuzimwa maana hakukutakiwa kuwe na mawasiliano yoyote kutoka nje.

    “Nimekuiteni, ndugu zangu, sina mengi, leo tumefanya kazi nzuri na tumejipongeza lakini kilele cha pongezi zetu kimeingia shubiri, mateka wetu wametoroka,” Shailan aliwaambia wajumbe. Scolleti alikuwa wa kwanza kushtuka akamtazama Shailan kwa jicho kali, “Na Yule msichana wa Kihindi je?” akauliza.

    “Nimesema mateka wetu wote isipokuwa Yule tuliyemhifadhi kule Mabibo,” Shailan aliwaeleza, ukimya ukachukua nafasi yake.

    “Sasa hatujui kama hiyo kesho wanatupatia mtu wetu au la, maana hapa nimeanza kupata wasiwasi.” Shailan aliendelea kuongea kwa huzuni.



    “Shailan, kama tulivyopanga, kesho kila kitu kipo tayari, tumefanya uchunguzi wetu tumeshajua kuwa tukio tunalolitaka litakuwa ni saa nane kamili, na sisi tumeomba watupatie mtu wetu saa saba kamili, wakichelewa tu tunafanya yetu halafu kuanzia hapo ni mashambulizi mfululizo,” Shakrum alizungumza huku akipigapiga meza kwa ngumi yake.

    “Mimi nipo tayari kwa msaada wowote mtakaouhitaji kwa hizo shughuli zote, ila naomba Yule msichana wa Kihindi kihwa chake mniletee,” Scolleti aliongezea.

    “Msiwe na shaka, Amata atakuja tu, maana atakuta ujumbe wake kuwa malaya wake yupo huku,” Tajan aliongeza kuwatia moyo wenzake. Basi kikao kikavunjika, na siku hiyo wote waligawana maeneo ya kufanya kazi zao za kuchunguza mambo mbalimbali.



    ˜˜˜˜



    Gina alirudiwa na fahamu zake baada ya kutoka katika usingizi mzito usiopimika, akajigeuza na kujikuta kwenye sakafu baridi, akiwa amelazwa na minyororo mikononi mwake, alijishangaa, alikuwa kwenye nguo ya kulalia tu, hakuelewa kinachoendelea hapo, aljaribu kutazama na kuchunguza chumba kile, kilikuwa kitupu kabisa hakina samani yoyote, wala hakikuwa na picha wala dirisha la kuwezesha kuona nje. ‘Niko wapi?’ alijiuliza, ‘Nimekujaje?’akazidi kuzama katika maswali yasiyo na majibu. Akatulia chini kwenye sakafu baridi na chumba hicho kilionekana wazi kuwa kilikuwa ni ‘cold room’ chumba cha kuhifadhia nyama na vitukama hivyo. Baridi ya chumba hicho ilimuingia mwilini bila huruma, alihisi kuganda lakini hakuwa na la kufanya. Mara akaona kitasa cha mlango ule mzito wa chuma kikifunguliwa kwa jinsi kilivyokuwa kikiinamia upande wa chini, moyo wake ulianza kwenda mbio kwani hakujua anayeingia ni adui au rafiki, akajituliza palepale, mara kijana mmoja mwenye asili ya kiarabu au kihindi lakini alikuwa na ngozi nyeusi iliyokata tama aliingia kwa mwendo wa kunyata kama anayewinda kitu, alimwogopa nani ilhali alikuwa pekee ndani humo. Alisimama na kumtazama Gina aliyekuwa kajikunyata pale katika kona ya chumba hicho, uso wake ukiwa umekutanishwa na magoti yake, gauni lake la kulalia alilovaa lilimwagika chini na kururuhusu mapaja yake manene kubaki wazi, alijua fika kuwa huo ni mtego tosha kwa kijana huyo, Yule jamaa alimfikia Gina na kuanza kumpapasa kimahaba, Gina aliinua uso wake na kumtazama jamaa huyo alienokana kujawa na mate kinywaji kwa uchu wa penzi laharaka haraka, alianza kumshikashika Gina kwa fujo, mara mapajani mara sijui wapi, huku bastola yake akiwa kaiweka pembeni kabisa, Gina alijifanya kujilegeza na kutoa sauti ya kukataa jambo hilo, Yule jamaa alimbembeleza na kumuahidi kumletea chakula mchana huo kwani yeye ndiye alikuwa kwenye lindo, Gina alimtazama tena na tena jinsi suruali yake ilivyotuna.



    “Sasa tutafanyaje mapenzi huku nina minyororo?” alimuuliza Yule kijana, badala ya kujibu akawa anachekacheka tu alipoanza kuyaona matiti ya Gina sasa yakiwa nje ya kigauni hicho, Yule jamaa alijipapasa mifukoni na kutoa funguo, akaifungua ile minyororo, hakika penzi kitovu cha uzembe. Alipokuwa akiiweka pembeni ile minyororo ndipo alipokutana na kabali maridadi kutoka kwa Gina iliyopigwa kwa miguu yake miwili, Yule jamaa alikukuruka lakini wapi, alikutana na miguu ya Gina yenye nguvu ya ajabu, baada ya dakika mbili alilegea na kutulia, Gina alimuachia taratibu, akamvua fulana yake na kuivaa yeye kwa haraka kisha akamtoa na suruali, akamuacha humo ndani, akaokota ile bastola na kuuelekea mlango kwa hadhari kubwa. Aliufungua taratibu kwa kuuvuta ndani kisha akachungulia akiwa na bastola yake mkononi, akajitokeza na kujibanza pembeni mwa ukuta huo, akaangalia kwa makini ili agundue ni wapi alipo lakini ilikuwa ngumu maana macho yake yalipambana na ngaxi nyingi hata yeye mwenyewe hakujua ni wapi aweze kupita, pale ambapo moyo ulimtuma ndipo alipoikwea ngazi ya mbele yake kwa haraka mpaka korido ya juu, akaambaa na ukuta na kuipita milango kadhaa, mlango mmoja uliokuwa mbele yake alipotaka kuupita alisikia sauti za watu wakiongea, akasimama na kutulia kusikiliza ni nini hasa walikuwa wakiongea. Gina alitulia pale kama dakika tano hivi alivutiwa na mazungumzo ya humo ndani hata akajisahau kama yupo eneo la hatari.



    Kutoka chumba cha usalama katika jengo hilo mtu aliyekuwa akicheza na camera za usalama alikuwa anamuona Gina kila alichokuwa akifanya tangu alipotoka katika chumba cha siri mpaka alipofika hapo, akainua simu yake ya upepo, “Gadi namba sita tafadhali, mateka wetu ametoroka ulinzi, yupo ngazi namba sita katika mlango namba 7 hakikisha hafanyi madhara yoyote, ova” Yule bwana alibonya kitufe kimojawapo katika ile redio yake, “Nimekusoma, linafanyiwa kazi,” Yule mlinzi aliyepigiwa alijibu.

    Gina bado aliganda palepale akisikiliza kile kilichokuwa kikizungumzwa mle ndani, akajisahau kabisa, mara alihisi akiguswa begani, Gina akatulia kisha akageuka kwa kasi na kuachia konde moja ambalo lilimpepesua Yule mlinzi akajibamiza kwenye mlango wa chumba kingine, kabala Gina hajamfikia Yule mlinzi akanyanyuka kutoka pale alipoangukia na kusimama wima lakini bunduki yake ilikuwa iko mbali kidogo, kabla hajaichuku Gina aliruka juu na kutua kifuani mwake kwa miguu miwili, wote wawili wakaanguka chini na kishindo kile kikawashtua wale walio katika ule mkutano, wakatoka na kukuta pigano lile, wote kwa pamoja wakamvamia Gina.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni ngumu kujitutumua, wakamkamata na kumfunga kamba.

    Tajan aliyekuwa katika mkutano huo alimtazama Gina kwa jicho la gadhabu sana, akihema kama mbwa aliyekosa windo lake, alirusha teke likatua shavuni mwa Gina na kumtupa upande wa pili, akamfuta na kumkanyaga kichwani kwa nguvu kisha kuutuliza pale mguu wake. Gina alihisi maumivu makali sana, damu zilimtoka mdomoni, hakuweza kufanya chochote kutokana na zile kamba za mikononi walizomfunga kwa nyuma. Wakamchukua na kuondoka naye.



    ˜˜˜



    Kamanda Amata aliwasili eneo la Kivukoni pale Magogoni mchana ambapo pilikapilika za uokoaji zilikuwa zimekwishapungua ila bado watu walikuwa ni wengi na polisi nao wengi. Aliegesha pikipiki yake na kuteremka akifuatiwa na ShaSha, akavuta hatua kuelekea geti la kuingilia abiria. Ijapokuwa ilikua ni shida kidogo lakini alijitahidi kupenya na hadi kufika ndani ambako miili mingi ya watu waliopoteza maisha ilihifadhiwa, alisimama na kutazama hali ile isiyovumilika, moyo wake ulipata uchungu uliochanganyika na hasira mbaya.

    “Kamanda!” sauti moja iliita kutoka nyuma yake, akageuka na kumuona kijana mmoja aliyevalia sare za kijeshi za kikosi cha wanamaji, wakasalimiana kisha akamvuta pembeni, “Okoa jahazi Kamanda, Watanzania wanakufa kama hivi,” aliongea huku akitoa machozi, Kamanda Amata aligundua kuwa Yule kijana ni daktari wa jeshi baada ya kumuona akiwa na Stetoscope (BP Machine) shingoni mwake.



    “Usijali dokta, ndio nimefika, tutalifanyia kazi,” Kamanda Amata alijibu, akabaki hana la kusema zaidi ya kusikiloiza vilio na kuangalia miili ile iliyolala bila roho kwa dhambi na ukatili wa watu wachache, ‘Jegan Grashan!’ alijisemea huku akiuma meno alipoinua uso wake macho yake yakautana na ule mnara mkubwa wa kuongozea meli uliojengwa kwa mtindo wa meli pale pembezoni mwa soko dogo la samaki, aliutazama na kuutazama, akili yake ikamwambia kitu, akatoka haraka na kuelekea kwenye ule mnara. Alipigana vikumbo na watu ili apate njia, huku akikimbia na huku akitembea, akafika pale mnarani na kuingia katika ofisi za kwanza pale chini kisha akaiendea lifti na kupanda kwenda juu kabisa, alipofika mlangoni akakuta mlango umefungwa, akajaribu kubofya kengele mara ukafunguliwa na akaingia ndani. Katika kile chumba kulikuwa na vijana wawili na msichana mmoja walikuwa kwenye viti wakifanya kazi zao katika mitambo maalum iliyofungwa ndani humo.



    “Karibu, tukusaidie nini?” Yule msichana aliuliza

    “Umeiona ile Pantoni iliyolipuka leo?” kamanda akauliza. “Sidhani kama kuna mtu aliye eneo hili ambaye hakuiona,” Yule mwanadada akaejibu. “Sawa, nahitaji kuona kamera zenu za usalama kabla ya tukio na mpaka dakika kumi baadae, tafadhali,” Kamanda Amata alitoa amri. “Mkuu, utaratibu hauendagi hivyo mkuu, hizi ni ofisi za watu,” kijana mwingine akasema lakini kabla hajamaliza alikatishwa na Kamanda Amata, “Sikia we kijana, hicho kiti unachokalia utakiacha sawa, haya ni amri tekeleza ninalotaka haraka,” wale vijana hawakuwa na jinsi, “Shida mheshimiwa funguo hatukai nazo sisi za hicho chumba chenye hizo tv,” Yule mwanadada akaongezea. Kamanda akaupigab teke ule mlango unaoingia kwenye hicho chumba nao ukaachia, akaingia ndani na kuketi kati kiti akazitazama zile tv zilikuwa kama ishirini hivi zikionesha pande tofauti. Akaangali ile inayopiga picha za Kigamboni, Kivukoni akaipata, akarudisha lile tukio nyuma mpaka dakika mbili kabla na kutazama kwa makini. Aliweza kuona jinsi zile Pantoni zilipokuwa zikitoka mpaka zilipolipuka, haikumpa maana sana, akairudia tena na tena, kitu kimoja kikamjia kichwani, aliona wakati watu wote wakiwa wameingia katika Pantoni upande wa Kigamboni kulikuwa na mtu mmoja aliyebaki, ijapokuwa hakuona vizuri lakini alihisi hivyo, ‘sasa hiki kina maana gani?’ alijiuliza, akaona hakuna chochote cha kumsaidia, alipotaka kuondoka, akasita, akakaa tena, kurudisha ile picha lisaa limoja nyuma, na kutazama safari zingine kama tatu hivi za pantoni ile. Sasa aliona Yule aliyedhania kuwa ni mtu bado akiwa ameketi pale tangu safari tatu nyuma, wasiwasi ukamuingia, ‘Kama si msafiri alikuwa akifanya nini pale,’ akawaza hakupata jibu. Akatoka na kuteremka chini bila kuongea na mtu yeyo mle ndani, safari ya miguu ikamfikisha palepale kivukoni, kichwani akiwa na mambo mawili tu lakini kabla ya kuyatekeleza. Akafika kwenye geti la kuingilia pale wanaposubiria abiria, akapenya na kuifikia ofisi ya mkuu wa kitengo, lakini hakuwa ofisini, akauliza baadhi ya watu aliowaona kuwa ni wafanyakazi wakamuitia. Wakiwa wawili tu ofisini mazungumzo yakaanza.



    “Unaweza kuniambia mlipuko huu ni wa nini?” Kamanda aliuliza. “Kwa kweli sijui, yaani mi nilikuwa ofisini nikasikia tu kishindo, hata wewe mwenyewe tazama vioo vya madirisha jinsi vilivyovunjika,” akajibu Yule mzee alieonekana tangu machoni kuwa hajui lolote lakini pia mwenye hofu kuu na moyo wa kuchanganyikiwa.

    “Sasa sikia, huu ni mlipuko wa bomu, na ni bomu ambalo lilitegwa kwenye Pantoni moja wapo kati ya zile mbili, sasa basi nahitaji orodha ya wafanyakazi wako waliokuwa zamu siku ya jana na leo,” Amata aliongea kwa ukali. Yule mzee akasukuti, akamtazama Kamanda, “Sikia kijana hapa sisi hatuna zamu, tunafika wote na kutoka wote,” akamjibu. “Sawa sasa naomba uniitie wafanyakazi wote hapa ili tuone tunafanya nini kwa pamoja sawa”, zoezi hilo likafanyika mara moja, wafanyakazi walikusanywa wote eneo Fulani, “Wote mpo?” Kamanda akauliza, “Hapana si wote, ukiacha wale waliofariki kwenye ajali ambao ni kama sita hivi hapa sijajua ni nani na nani” alijibu Yule mzee huku akiwa anatokwa na machozi. Kamanda Amata alisogea pembeni na kuonge na OCD wa kituo cha polisi cha kati, akimwambia wale wafanyakazi wopte wapelekwe polisi kuhojiwa haraka iwezekanavyo. Dakika mbili tu gari za polisi zilifika na kuwasomba wote wakaondoka nao. Kamanda Amata sasa alikuwa akifanya jambo la pili, alikiendea kituo cha pilisi cha wanamaji kilichopo hatua chache kutoka Magogoni na kuwaomba wamvushe kwa boti yao ya akiba wakafanya hivyo.



    ˜˜˜˜



    MADAM S alitoka katika kikao na kutokea geti kuu akiwa hajielewi sawasawa baada ya maamuzi yaliyopitishwa katika kikao hicho, waliombwa kukutana tena jioni ya siku hiyo ili kujua nini cha kufanya, wakati huo pia akisubiriwa mkuu wa nchi kufika kwani alikuwa nje kwa ziara ya kikazi.

    Chiba alikuwa tayari amefika katika katika eneo hilo na gari yake, akamchukua Madam S, kisha kwa mwendo wa taratibu akaingia barabarani kama anaelekea stesheni ya treni, kisha akakata kulia na kuzunguka mnara wa saa na kurudi barabar ya Samora kuja picha ya askari, “Yes madam,” Chiba alimchokoza. “Nipe habari za Kamanda,” Madam alirudisha mazungumzo kwa mtindo huu. “Kamanda yupo kazini, kama masaa mawili sasa,” Chiba alijibu, “What? Don’t tell me!!!” (Nini? Usiniambie!!!), Madam S alichanganyikiwa kwa jibu hilo, haraka sana akamuamuru Chiba kuelekea Magogoni, walipofika pale hawakumkuta Kamanda, wakaenda kwa mmoja wa vijana wao, akaweleza Kamanda Amata amevuka ng’ambo mara moja. “Tangu amefika ameshafanya nini?” Madam akauliza. “Kiukweli amefika hapa nilimuona anaongea sana na mtawala wa eneo hili mara baadae kakusanya wafanyakazi wote kapeleka polisi, mwenyewe anajua kwa nini, lakini pia nilimuona akielekea kule kwenye mnara wa kuongozea meli.” Yule kijana alijibu. “Ok asante,” Madam akamalizana na huyo kijana kisha akatoka na Chiba na kurudi garini. “Sasa nina amani, kama kamanda amerudi, lakini nampa pole kwa kuwa Gina ametoweka,” Madam S alizungumza wakati alipokuwa akikaa vyema kitini. “Unasemaje Madam? Gina ametoweka?” Chiba akauliza kwa mshangao, “Ndiyo, nimemtafuta sana lakini sijampata na si kawaida yake msichana huyu,” Madam S alimaliza huku akitafuna jojo yake.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Saa moja baadae, Kamanda Amata alirudi upande wa Magogoni, na mara moja aliigundua gari ya Chiba iliyoegeshwa pembezoni kabisa mwa kituo cha daladala akaisogelea na kumuona akiwa na Madam S, akaufungua mlango wa nyuma na kuketi. Madam S aligeuka ghafla na kukutana na Amata, furaha yake ndani ya tabasamu pana haikuweza kujificha. “Pole sana Kamanda,” Madam alimpoza. “Asante Madam, ndio kazi zetu, unapotea kisha unapatikana lakini inapobidi, unapotea kabisa. Madam tuna kazi ngumu sana na hawa jamaa inabidi tujipange vya kutosha, hiyo kesho sijui itakuwaje, mimi usiku huu lazima nifanye kazi ya ziada kuvuruga mipango yao yote, cha msingi ni kwamba nimeshajua kambi zao zilivyo haitanisumbua, leo ni usiku wa kazi Madam, sehemu zote nyeti ziwekewe ulinzi madhubuti,” Amata aliongea kwa jazba. “Sikia Kamanda, we kapumzike kidogo, kisha jioni saa kumi na mbili tunakutana pfisi kuu, uje tafadhali halafu kutoka pale tutapanga kikosi kazi.” Madam S alimueleza Kamanda, Chiba akavuta droo ya dashboard na kutoa kimkebe kidogo, akampatia Kamanda, wakaagana na kila mtu akashika hamsini zake.



    §§§§§



    “Hatukuwa na jinsi kwa maana watu wetu wanakufa tu, kwa nini tung’ang’anie kukaa na mtu mmoja gerezani wakati mamia yaw a kwetu yanateketea?” Makamu wa Rais alikuwa akiongea Mheshimiwa Rais alipokuwa amerudi ghafla kutoka nje ya nchi kwenye mkutano wa kimataifa wa nchi zinazoendelea.

    “Ok, kama mmeona kwa pamoja na watu wa vyombo vya usalama mi sina neno, mtoeni huyo mtu na hao watu wake waondoke nchini ndani ya masaa machache,” Mheshimiwa Rais alitoa amri.

    Hakukuwa na lingine zaidi ya kutekeleza lililokuwepo, hati ya kuachiliwa Jegan Grashan iliandaliwa na wanaohusika na kazi hiyo.

    Madam S bado alikuwa akiumiza kichwa katika hilo, kwa kuwa ni yeye peke yake ambaye alipinga kuachiwa kwa gaidi huyo hivyo hakuwa na budi kwa sababu Waswahili wanasema wengi wape. Kama alitegemea amri au uamuzi tofauti kutoka kwa mheshimiwa Rais basi haikuwa hivyo kwani uamuzi wake ulipita mlemle ambamo wengine waliamua. Maneno ya Kamanda Amata yalimrudia mara kwa mara akilini mwake, ‘Mkimuachia mi namuua’ lilikuwa likikifanya kichwa chake kutotulia.





    Kamanda Amata alichanganyikiwa kutomkuta Gina nyumbani, alipompigia simu hakumpata, akaingia ndani ya chumba ambacho Gina mara nyingi huwa akilala kila ajapo kumtembelea. Kitanda kilikuwa kama kilivyo, kwa jinsi shuka ilivyobakia, Kamanda Amata alijuwa wazi kuwa Gina hakuamka mwenyewe bali alibebwa na kitu au mtu, akatoka na kuingia kwenye kichumba chake cha siri ambacho humuonesha mambo yote yaliyotukia nyuma, akijifungia kwa ndani na kuwasha viscreen vyake na kutazama matukio yaliyopita hasa kwenye chumba cha Gina, ndipo alipoona nyendo za mtu anayenyata, hila zote alizofanya na kumbeba Gina kisha kuondoka naye.



    Akajaribu kumsogeza uso wake mtu huyo lakini kutokana na giza hakuweza kumuona sawia ila alijua wazi kuwa watakuwa ni wale wale wabaya wake, alipiga ngumi mezani ya hasira, ‘ama zao ama zangu’ akanyanyuka na kuingia chumbani kwake ambako alichukua silaha zake muhimu kwa kazi za usiku, akilini mwake akiiwaza ile Julai saba 7 ambayo jamaa hao wanajivunia, hakujua kwa uwazi ni nini wanataka kufanya. Mara simu yake ya mezani ikaita, akaiendea na kuinyakuwa mara moja, akaiweka sikioni, hakuongea lolote bali alimtegea mtu wa upande wa pili aseme lolote, alisikia sauti ya mtu anayepigwa na kelele za kilio cha kike, aliitambua sauti hiyo kuwa ni Gina, uchungu ukaushika moyo wake, akauma meno kwa hasira.

    “Tunajua kuwa umetutoroka, usalama wa huyu Malaya wako ni wewe kujisalimisha kwetu,” kisha ile simu ikatulia, “Nakuja kujisalimisha kaeni tayari kunipokea,” kisha akakat simu ile.

    Kama kuna kitu ambacho Kamanda Amata alikichukia ni dharau kama hizo, aliitazama saa yake, tayari ilitimu saa 11 jioni, akaendeloea kujiweka sawa. Jambo linguine lilimchanganya ni kuwa wapi Gina atakuwa amefichwa, Bunju au kwenye yadi ndogo Mabibo, hakujua, alihisi wazi kuwa anahitaji msaada, msaada wa mtu mwenye akili kama yake, akamkumbuka ShaSha, yuko wapi, hajui. Alikumbuka tu kuwa mara ya mwisho walikuwa wote pale Kivukoni lakini sasa hajui alipokwenda, ‘atakuwa wapi?’alijiuliza bila kupata jibu.



    §§§§§



    SHASHA baada ya kuona kamanda Amata amegubikwa na mambo mengi pale Kivukoni, akaamua kumtoroka, alitafuta tax na kupata kisha akamuamuru dereva kumpeleka Manyanya hotel, Kinondoni.

    Alipofika jambo la kwanza alifungua laptop yake na kuweka flash yake ili ajue kati ya vile alivyovichukua kwenye kompyuta ya Scolleti kama vina tija. Kompyuta yake ikawaka na kuanza kuonesha mafaili mbalimbali, makabrasha na nyaraka anuai za Scolleti. Kati ya makabrasha hayo, moja lilimvutia zaidi lilionesha habari nyingi za Scolleti kote alikokuwa akipita na kufanya mambo yake, siri ya utajiri wake na mipango anayoipanga, kitu kilichomshtua zaidi ni ufadhili wa pesa nyingi anaoufanya kwa vikundi vya wakorofi sehemu mbalimbali za dunia, kuwapa nguvu kufanya mapinduzi ili yeye afaidi mkataba mnono na wao wakishaipindua serikali au wakisha miliki maeneo Fulani. Alianzia huko Thailand mara tu baada ya kutoka India na kuwa mfanyabiashara maarufu. Pale India katika mji wa Bombay alikuwa akimiliki mahoteli kadhaa aliyoachiwa na wazazi wake na kwa kuwa yeye alisomeshwa maswala ya biashara, ndipo alipoweza kuyaendesha mahoteli hayo na pia kujenga mengine makubwa zaidi ya hayo katika miji mbalimbali ya India kama Delhi, Mumbai, Bangalore na mingine mingi. Kama haitoshi aliamua kuongeza mabishara sasa akaingia kwenye maswala ya uingizaji mafuta ndani ya India kutokea Mashariki ya kati, katika sakasaka zake za biashara hizo ndipo siku moja alipokutana na mtu mmoja aliejulikana kwa jina la Muntazil da Silva, mtu huyo alikuwa ni chotara wa Kihindi upande wa mama na Kibrazil upande wa baba, lakini yeye alikuwa akiishi India na kufanya shughuli zake huko Brazil na Chile.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    SCOLLETI

    MIAKA 25 NYUMA- BOMBAY, INDIA



    ILIKUWA asubuhi ya saa 4:30, katibu wa Scolleti alipompigia simu bosi wake akimwambia kuwa kuna mgeni anayetaka kuonana naye, japokuwa siku hiyo ilikuwa ni siku ambayo Scolleti hakupenda kuonana na wageni lakini ilibidi amkaribishe mgeni huyo baada ya kuwa jina alilotajiwa alilifahamu fika.

    “Karibu sana bwana Muntazil,” alimkaribisha huku akiwa amesimama wakipeana mikono.

    “Kwanza samahani bwana Scolleti, nimekuja bila miadi lakini nilikuwa na jambo muhimu la kukueleza, kesho mimi ninasafiri kwenda Saudi Arabia kwenye mambo yangu ya kibiashara, lakini nimeona nikualike tufuatane ili nawe ukaone nini tunafanya labda utavutiwa kuwekeza katika nyanja kama zangu,” Bwana Muntazil alimueleza kwa tuo bwana Scolleti. Akiwa kimya huku akiandikaandika katika kitabu chake cha kumbukumbu, aliinua uso wake na kumtazama mgeni wake huyo, “Nakusikiliza, bwana Muntazil,” Scolleti alimwambia mgeni wake. “Sasa ujio wangu hapa ukiachilia mbali kuwa nimeonana na wewe, lakini nilitaka kukuomba kufuatana name, kwani mwenzio nilianza hivihivi kwa mahoteli, mashule, maduka, lakini nikaja kuingia kwenye mgogoro na serikali ya Delhi wakataifisha vitu vyote, ndipo nilipoondoka nchi hii na kwenda kwa mama zangu huko Brazil ambako mjomba wangu alinipa mtaji mdogo tu lakini leo hii nimewekeza kwenye Nyanja nyingi huko America ya kusini, Africa na mashariki ya kati, sasa siku moja na wewe utaangukia kwenye mikono hii hii ya dola, unafikiri utajikwamua vipi, twende huku halafu utaamua,” Muntazil alimshawishi Scolleti kwa kina mpaka Scolleti akakubaliana naye na siku hiyo wakapanga safari.

    Siku ilofuata wawili hao pamoja na whudumu wachache walikuwa hewani kwenye ndege binafsi inayomilikiwa na bwana Muntazil wakielekea Saudi Arabia ambako wangekaa siku mbili kisha kuelekea Brazil na Chile kabla ya kurudi India.



    Wakiwa Saudi Arabia, Scolleti alijifunza mengi sana huko mashariki ya kati, biashara ya kusafirisha mafuta na kumiliki visima vya mafuta ambayo bwana Muntazil alikuwa akiifanya na ilikuwa ikimuingizia pesa nyingi sana. Scolleti aliitamani sana biashara hiyo ambayo ilimtoa udenda kwa jinsi ilivyoingiza pesa nyingi kwa muda mfupi. “Bwana Muntazil, biashara hii nimeipenda sana, je waweza kunisaidia nami nipate kama si kumiliki basi kusafirisha,” Scolleti alimwambia Muntazil. “Usijali swahiba, hatujamaliza bado, inawezekana ukakutana na biashara nzuri kuliko hii, subiri tumalize ziara yetu kisha utachagua,” Muntazil akmwambia Scolleti. Baada ya siku hizo mbili waliondoka kwa ndege ileile na kutua Chile, ambako walifikia kwenye nyumba ya kifahari yenye kila kitu ndani yake, wahudumu wa kumwaga wakikuhudumua kila utakalo. Scolleti aliushangaa sana utajiri wa bwana huyo, wakati kule India alikuwa akimiliki shule moja tu lakini ilikuwa yakisasa kuliko shule nyingine yoyote katika nchi hiyo. “Muntazil, hili jumba ni la kwako au umekodi?” Scolleti alimuuliza Muntazil. “Bwana Scolleti, nilishakwambia kuwa mimi nimewekeza nje zaidi, hii ni nyumba yangu mwenyewe, na hawa wote ni wafanyakazi wangu wa kike kwa wa kiume nawalipa vizuri kuliko wanavyolipwa serikalini, ndani ya jumba hili nina wafanyakazi mia moja,” Muntazil alimwambia Scoleeti alieonekana kushtuka kwa maneno hayo.

    “Mbona hawa hata ishirini hawafiki? Au wanaingia kwa zamu?” Scolleti aliuliza.



    “Hapana bwana Scolleti, wote wanaingia muda sawa na wanakaa humu humu hawatoki, asilimia 90 kati yao ni yatima, nimewakusanya na kuwaweka hapa wakifanya kazi na kulipwa ujira mzuri sana,” Muntazil alimwambia Scolleti wakiwa mezani kwa chakula cha jioni. Scoletti alijiona mwenye bahati sana kujifunza hayo yote kwa rafiki yake huyo. Naye alitamani kuwa kama yeye, tamaa ya kujiwekea mali nyingi ikamfika, “Sasa bwana Muntazil, hapa Chile umewekeza katika nini?” akauliza Scolleti. “Hapa nimewekeza kwenye kilimo, nina heka za kutosha za mashamba makubwa ya mimea ambayo kwayo naingiza hela nyingi sana, usiku huu tutakwenda huko, tusubiri helkopta inakuja kutuchukua,” Muntazil alijibu.

    Majira ya saa tano usiku, helcopta kubwa ya kisasa ilitua katika uwanja wa jumba lile, Muntazil na mgeni wake waliondoka na kuingia katika helkopta hiyo na kuondoka zao. Safari ilikuwa ni kwenda katika mashamba ya Muntazil yaliyopo kusini mwa nchi ya Chile, katika jimbo la Temuco. Walifika usiku huohuo na kuingia mashambani, mataa makubwa ya umeme yaliangaza kiasi kwamba uliweza kuona kila kitu vizuri kabisa, mahindi manenen yaliyojaza vyema yalilijaza shamba zima. “Muntzail. Mahindi yiote haya unamuuzia nani au unatoa msaada?” Scolleti aliuliza.

    “Hapana, kaka, mahindi haya ni jalada tu kitabu chenyewe kipo ndani, twende kwa maana usiku huu huu inabidi turudi Santiago,” Muntazil alimwambia Scolleti kisha wote wakapanda ndani ya kigari maalumu na kuingia nshambani usiku huo wakiifuata njia ndogo inayopita katikati ya mahindi hayo.



    Uwanda mkubwa ulikuwa katikati ya shamba lile la mahidi, mimea iliyokuwa na rangi ya kijani iliyokolea ilionekana wazi kuwa katika udongo wenye rutuba nyingi, “Hii ni chai?” Scolleti aliuliza, “Hapana hii ni cocaine,” Muntazil alijibu huku akihamia upande wa pili wa eneo hilo walilosimama. “What? Umesema nini? Au sijasikia vyema?” Scolleti akuliza tena, “Hiyo ni cocaine, nikivuna hapa robo heka tu, nina uwezo wa kujenga mahoteli kama yako yote na zaidi, je unaonaje hii siyo biashara ya kujipatia kipato nawe uwe wa tisa kati ya wale G8?” Muntazil alimwambia Scolleti. Baada ya hapo alimpitisha sehemu mbalimbali na kumuaonesha jinsi wanavyovuna na kuifunga vizuri kabla ya kwenda kiwandani kwa usindikaji na usafirishaji katika maeneo mbalimbali. Walipomaliza ziara yao huko Temuco, usiku huohuo walirudi kwa helcopta mpaka Santiago kwenye jumba lilelile la Muntazil. “Vipi Scolleti mbona upo kimya sana?” Muntazil akamuuliza, “Nafikiria juu yah ii biashara ya kule Temuco, inakuwaje kama serikali ikigundua unachokifanya?” Scolleti akauliza. “Sikia Scolleti, serikali zote duniani zinaongozwa na mwanadamu, na huyo mwanadamu anaongozwa na pesa, na hiyo pesa tunayo sisi, unafikiri nini kinakuja hapa? Mkuu wan chi hii anajua kila ninachokifanya, wana usalama alikadhalika, hakuna lolote, mi nVuna nasindika, nauza kwa wafanyabiashara wengine kisha wao ndiyo wanasafirisha nje, mimi sisafirshi nje nauzia humuhumu ndani na baadhi ya wanunuzi wangu ndio haohao uliowataja, serikali,” Muntazil aliongea kwa kujiamini.





    Scolleti aliangalia saa yake ilikuwa ni saa 10:45 alfajiri, alijihisi uchovu sana, lakini ziara yao ilikuwa inakaribia mwisho, wakatoka tena na Muntazil ndani ya jumba hilohilo wakaingia milango kama mitano tofauti kisha wakatokea mahali ambapo wanafungia farasi, Muntazil akaingia na kumuamuru Scolleti kufanya hivyo, kisha akafunga ule mlango. Ndani ya banda hilo kulikuwa na farasi wawili weupe, “Usiku huu farasi wa nini Muntazil?” Scolleti aliuliza. “Hapana hatuchukui farasi, simama hapa,” Muntazil alimwambia Scolleti nae akasimama karibu kabisa na ukuta wa nyuma juu ya nyasi kavu, Muntazil akatoa mfukoni kitu kama rimoti na kubonyeza vitufe kadhaa mara lile eneo likaanza kushuka chini na kuacha wale farasi wakiwa kulekule juu. Mara wakasimama na kutoka kwenye kile kipande kilichowashusha chini na chenyewe kikarudi juu. Muntazil na Scolleti walitembea kwa mwendo wa wastani katika jumba lenye vyumba vingi sana humo ndani. “Scolleti, hapa ndio eneo la usindikaji, wanafanya kazi wanawake tu, kwa hiyo uwe mvumilivu ila kama utamtamani mmoja wao niambie nitampa taarifa atkuhudumia kabla hatujaondoka kisha mimi nitamlipa, usijali, upo tayari?”

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Muntazil akauliza. Moyo wa Scolleti ulianza kudunda maana hakujua nini maana ya kauli ya swahiba wake. Mlango ukafunguka, wakaingia na kukaribishwa na mwanadada mmoja mrembo sana mwenye kiuno kilichojigawanya sawia, kwa rijali yoyote hapo lazima apige goti na mwenyekiti wa kijiji hana budi kusimama. Scolleti alipigwa bumbuwazi baada ya kuona wasichana wengi sana takribani thelathini wakiwa wametingwa na kazi katika mashine zao, hakuna aliyeonekana kuongea na mwenzake, nyuso zao zilifichwa kwa barakoa maalum iliyofunika mdomo na pua na kuruhusu macho tu, zaidi ya hapo hawakuwa na vazi linguine, matiti yao yaliyopishana kwa umbo na ukubwa yalibaki nje, viuno vyao ambavyo kila mmoja alikuwa na shepu yake vilionekana wazi, cha namba nane, tano hata namba moja kilikuwepo. Kwa ujumla wasichana wale walikuwa wakifanya kazi bila nguo, uchi wa nyama na walikuwa wanawake tupu. Muntazil alimgeukia Scolleti na kumuona akiwa kachoka ghafla, eneo la chini ya kitovu lilikuwa limetuna kama mtu aliweka kipande cha muhindi. “Scolleti, pole sana, usijali, mmoja atakupoza munkali wako, hapa ndipo tunasindika madawa, hawa wadada hawavai nguo ili kuepusha wizi, maana akitoka na kete moja au tatu tayari anatengeneza pesa ndefu,” akamwambia. Baada ya hapo walitoka na kwenda upande wa wanaume nako ni hivohivo, walipomaliza wakapanda lifti sehemu nyingine na kuja juu katika lile jumba la bwana Muntazil. “Sasa, huyu mhudumua atakupeleka katika chumba, utapumzika na saa tano asubuhi tutaondoka kwenda Amazonia, Brazil ambapo tutakuwa na kikao cha dakika kumi na tano tu kisha tunarudi India.



    Scolleti akaondoka na Yule mhudumu mpaka chumba cha ghorofa ya juu, akakaribishwa na kuingia ndani kisha akajifungia mlango kwa ndani, alipogeuka nyuma kukielekea kitanda, lo, alibaki hana la kufanya kwa kile alichokiona kitandani. Msichana mmoja kati ya wale aliowakuta kule katika kitengo cha kusindika dawa za kulevya, Scolleti alikumbuka jinsi alivyokuwa akimtolea macho kwa umbo lake zuri la kuvutia, walitazamana, Scoletti hakuelewa la kufanya lakini alijikuta hali yake imekuwa mbaya huko chini, mapozi aliyokuwa akiweka Yule msichana pale kitandani yalimmaliza Scoletti, akiwa katika kutafakari hayo, yul;e binti alinyanyuka na kumfuata pale aliposimama huku kidole kimoja kikiwa kinywani kikibanwa kwa meno ya mbele ya taya la juu na la chini, Yule msichana akamkumbatia Scoletti huku mkono mmoja akianza kuchezea sehemu nyeti za bwanyenye huyo. Hali ikawa mbaya wakakokotana mpaka kitandani na kubwagana. Scoletti alitolewa nguo zote na kubaki kama alivyo kisha akapewa michezo ya ajabu iliyomtoa jasho na mara nyingine alijikuta akilia kama mtoto.



    §§§§§

    >>>>>RIO DE JENEIRO



    UPEPO MKALI ulikuwa ukipiga kutoka baharini na kuishia kwenye kuta za nyuma zilizojengwa katika ufukwe huo. Kwa wengine ilikuwa ni burudani lakini kwa wageni ambao hawakuizoea hali hiyo ilikuwa ni kero kubwa, kila mara walionekana kugeuza sura zao kule ambako upepo huo ulikuwa ukielekea.

    Katika moja ya nyumba zilizopo katika ufukwe huo, kulikuwa na kikao cha watu kumi na mbili kikiendelea katika ulinzi mkali, ulinzi wa siri ambao duru za usalama hazikuujua kama upo hapo.

    Muntazil na mgeni wake Scoletti walikuwa wamekutana na watu wengine kumi katika moja ya vyumba vya jengo hilo ambalo ukiliona kwa nje ni bovu kupita maelezo lakini kwa ndani lilikuwa linalingana na hoteli ya nyota tano. Meza kubwa yenye umbo la ovali iliwaunganisha wadau hao, kila mmoja akiwa na chombo maalum cha kuongelea na pia cha kusikilizia, hakuna mtu wa pembeni aliyeweza kusikia mazungumzo hayo isipokuwa tu Yule mwenye vyombo hivyo.



    Scoletti alitambulishwa kwa watu hao, nae akajua kuwa kumbe mbele yake amekutana na viongozi wa makundi hatari sana kama Tamil Tiger kikundi cha waasi cha Thailand, Hamas wa Palestina, Gorilla wa Peru na vikundi vingine asivyovijua. Scolleti alikuwa akifuatilia kila linalozungumzwa akagundua biashara haramu ya Muntazil ya kuwafadhili wapiganaji hao kwa pesa na silaha kali za kivita ili waendeleze mapigano katika nchi zao, wadhibiti sehemu nyeti kama zenye madini, mafuta na utajiri mwingine, wakati majeshi ya serikali yakipambana na vikundi hivyo wao upande mwingine wakivuna utajiri ule uliopo katika maeneo hayo. Scoletti alifuataili na kusikiliza, hakuongea lolote wala kushauri, alikuwa akisikiliza taarifa zinazowasilishwa na watu hao huku akisikiliza maelekezo na utekelezaji wa kikauli kutoka kwa Muntazil lakini hakuona hata wakati mmoja Muntazil akimkabidhi mmoja wao bastola au jiwe, alichosikia tu ‘nitawaongezea mabomu ya mkono tani moja,’ wengine akawaambi, ‘Nitawaletea jeep za kivita kumi na tano,’ engine wakaahidiwa kupewa RPG za kutosha na kupewa mafunzo maalumu ya kikombandoo ili kuutingisha utawala wan chi yao. Mara baada ya kujibu matakwa yao hayo sasa ikawa zamu ya wale watu kusema wanachotoa kwa msaada huo, wengine walisema ‘kilo kadhaa za dhahabu,’ wengine ‘makasha ya almasi,’ wengine wakamwambia ‘tutateka sehemu nyingine yenye mafuta ili uendelee kugema na hapo,’. Scolleti aligundua mzunguko mzima wa ulimwengu na matukio yake, akashusha pumzi nzito na kuzifiikiria roho za watu wanaopoteza maisha katika masakata hayo yasiyo na macho.



    Kilichomshangaza ni kuwa hakusikia hata sehemu moja wakisema ‘tutajenga shule’ au ‘hospitali,’ haikuwapo hiyo. Baada ya dakika kumi na tano tu kikao hiko kiliisha, na kila mtu akaondoka bila kumuaga mwenzio, hakuna kupeana mikono wala nini.

    “Muntazil, hii ni biashara gani?” Scoletti akamuuliza swahiba wake.

    “Hivi ndivyo dunia inavyoendeshwa, wewe ukijenga shule wenzio wanakuja kubomoa,” Muntazil alijibu, akakohoa kidogo na kuendelea, “mimi nikifadhili hawa kwa dola milioni thelethini, kwangu zinarudi na kuwa dola milioni sitini na ushehe, ni biashara nzuri sana naipenda sana, nina uwezo wa kuinunua ikulu ya Marekani na kuihamishia Afrika ya Mashariki bila kuivunja,” maneno hayo ya jeuri yalimtoka Muntazil na kumwendea Scoletti. Muntazil akamtazama Scolleti ambaye bado alikuwa ameketi kitini kama aliyepigwa shoti ya umeme, “Swahiba, dunia haina mwenyewe, kila mtu ataiacha, unafikiri matajiri wakubwa wanaojenga mahospitali, au mashule , au vyuo, pesa wanatoa wapi? Changamka kaka, mi nitakuongezea mtaji wa dola milioni kumi, kisha upate kikundi kimoja tu cha waasi ambacho utakifadhili kwa silaha na kila kitu chenyewe kitakupa mzigo wa maana, upo tayari?”



    Muntazil alimshawishi Scoletti, kimya kikatawala kati ya hao wawili, wakabaki wakitazamana. Scoletti alitamani kiloa kitu lakini alitakiwa aanze na kimoja. Baada ya mapatano, Scoletti aliamua kuanza na waasi. Kikundi chake cha kwanza kukifadhili kilikuwa ni kikundi cha waasi cha huko Mali, kilichofanya mauaji ya kutaka kuipindua serikalim akiwapa silaha na yeye kupata madini ya aina mbalimbali, pesa ikamnogea, akapata kikundi kingine cha huko Mexico cha kuuza na kusambaza madawa ya kulevya, akajitengenezea hela chafu. Baada ya hapo akajikita katika nchi mbalimbali, kila alipokuwa anajulikana hila zake alitimuliwa kwa masaa ishirini na nne, serikali ya India ikishutumiwa kwa ajili ya huyo raia wake, lakini walifumba macho. Baada ya malalamiko mengio yaliyotishia kuvunjika kwa uhusiano wa kidiplomasia ndipo walipoamua kumfungia kazi mtu huyo. Scoletti alijikuta Africa, Africa ya Mashariki na kubwa lililomleta ni ufadhili wa Freedom Fighter wanaotokea huko Mashariki ya kati wakija kutekeleza lile wanaloliita vita ya ukombozi, akawafadhili kwan kila kitu wakafanikiwa kulipua balozi za Marekani katika nchi ya Tanzania na Kenya. Bahati mbaya au nzuri wana usalama wa Tanzania walifanya kazi kubwa chini ya idara nyeti, idara ya juu inayoongozwa na mwanamama mahiri kwa kazi za kijasusi, Madam S, na kufanikiwa kumtia mbaroni mlipuaji huyo, Jegan Grashan ambaye amesumbua mataifa mengi na walishindwa kumpata. Kilichokuja kutokea ni kuwa vita ile ya ukombozi ikaamishiwa katika ardhi ya Tanzania, kumkomboa ndugu yao mwanamapinduzi mwenzao. Serikali ya India ikamtuma mwanadada ShaSha kufanya uchunguzi na kumjua kwa undani mtu huyo, kutokana na kuchoka na lawama, ShaSha alipewa kibali cha kuua, “Mkamate akibisha mlipue!” maneno aliyoambiwa na bosi wake wa idara nyeti ya usalama wa Taifa huko India.



    §§§§§



    SHASHA aliridhika na alichokisoma kwenye makabrasha hayo, akayatuma katika idara ya usalama wa Taifa huko India. Sasa kwake kazi ilikuwa ni moja tu, kumsaka popote alipo ili ikibidi ammalize, ShaSha hakuona haja ya kubishana na kiumbe huyo majinuni. Akanyanyuka na kuliendea kabati la chumba hicho na kutazama vifaa vyake kama vyote vipo katika hali nzuri, alipofungua kabati tu, pande la mtu likatoka ndanii ya kabati hilo na kisu kikubwa mkononi mwake, ShaSha akamuepa kisha akampiga karate hatari nyuma ya shingo yake, Yule mtu alikuwa imara, ijapokuwa aliyumba kidogo lakini alisimama na kurusha ngumi moja nzito ambayo ilikuta ShaSha bado yupo eneo lilelile ikatua shavuni na kumpeleka chini. Yule bwana akjirusha mzimamzima akitanguliza jisu lake lenye hasira ili kumchoma ShaSha lakini alibugi, ShaSha alijiviringa pembeni na kujiinua kwa ustadi kisha kumfumua teke moja kali lililopiga tumboni mpaka Yule bwana akatema damu na kujibwaga chini kama mzigo. ShaSha akasimama pembeni akiwa tayari kwa mashambulizi mengine lakini alichelewa, kutoka nyuma yake kitu kizito kilipiga kisogoni, akayumba na kupoteza fahamu, akaanguka chini juu ya lile jitu la mwanzoni. ShaSha akajaribu kupambana na giza lililokuwa likimfunika macho lakini ilikuwa ngumu, akajikuta akifunikwa na giza hilo kisha kuishiwa nguvu, kimya kikuu kikakijaza kichwa chake, akalala usingizi mzito, usingizi usio na ndoto.





    Kelele ya mapangaboi ya helkopta yalikuwa ykisikika katika masikio ya ShaSha, “Vipi ameamka?” alisiki kwa mbali watu wakiulizana, “Bado, lakini si muda mrefu atakuwa ameamka,” sauti nyingine ilijibu, “Akiamka tu, umpeleke kwa boss mambo yote yataishi huko,” ile sauti ya kwanza ilikuwa inaelekeza. ShaSha alihisi maumivu makali sana sehemu ya nyuma ya kichwa chake, alikumbuka kuwa hapo ndipo alipopigwa na kitu kile ambacho hakuwahi kukifahamu mara moja. Aliendelea kujifanya hajapata fahamu ili ajue kinachoendelea ndani hapo, alijaribu kufumbua macho kwa mbali, akagundua kuwa alichokuwa akifikira ni mapanga ya helkopta kumbe ni feni la juu lilikuwa likizunguka huku likipiga kelele kwa ubovu wake.



    8CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    HASIRA zilikuwa zimekitawala kichwa cha Kamanda Amata, aliamua kufanya maangamizi ambayo hayatasahaulika katika historia ya nchi hii, kwanza kwa kitendo cha kuua raia wale kwenye pantoni bila sababu maalumu, pili kwa kumteka Gina, kipenzi chake. Kamanda Amata aliapa lazima kisasi kifanyike na baya zaidi lilikuwa ni lile la kuachiwa huru Jegan Grashan, ilhali yeye alifanya kazi ngumu sana kumkamata mtu huyo aliyeshindikana kila kona ya dunia. ‘Lolote liwalo wacha liwe!’ alijiwazia mwenyewe huku akiendelea kutega saa za mabomu yake kadhaa aliyeokuwa nayo katika yadi ndogo ya freedom fighter pale Mabibo, mabomu kama matano aliyoyatega kiustadi kabisa akikumbuka alichofundishwa kule Cuba.



    Alipohakikisha yote kayaweka sehemu sahihi ambayo alijuwa hata yakilipuka hayatawadhuru raia wa pembezoni ila uharibifu utakaotokea katika jengo hilo utasababisha moto mkubwa, hilo alilifanya akihakikisha ndani ya jengo hilo hakuna Gina baada ya kusaka kila chumba na kuhakikisha hayupo, ‘Kesho saa nne’ alijisemea mwenyewe huku akisonya, kisha akatafuta njia ya kutoka katika yadi hiyo, ndipo aliposikia mtu akikohoa nyuma yake, aligeuka kwa haraka na kukutana na dhoruba kali ya mateke ya usoni, japokuwa alijitahidi kuyapangua lakini mawili ya kwanza yalimfikia. Kamanda Amata akarudi nyuma hatua kadhaa na kuepa teke moja kisha kupiga ngumi mbili maridadi zilizotua kwenye korodani za mtu huyo, nae bila kipingamizi alitua chini kama mzigo, Kamanda Amata akakanyaga shingo kwa nguvu zote na kusikia wazi mifupa iliyoshika shingo hiyo ikivunjika, akapiga goti kutaka kumuuliza kitu akakuta tayari mtu huyo hana uhai, akamvuta na kumuhifadhi kwenye jaba kubwa lilillokuwa tupu akalifunika juu yake.



    Akatembea kwa hadhari na kufanikiwa kutoka nje ya jengo hilo huku akiwaacha walinzi hawana habari yoyote juu ya lililoendelea ndani. Akatoka na kuiendea pikipiki yake aliyoiegesha kwenye moja ya club za usiku hapo mabibo, alipoitazama saa yake ilikuwa imetimu saa nane za usiku, akaliswasha pikipiki hilo na kuifuata Barabara ya Mandela kuelekea Ubungo, pale akanyoosha na kupita barabara ya Sam Nujoma mpaka Mwenge akapinga kushoto na kupiga gia kuelekea Bunju ambako kuna yadi kubwa kabisa ya jamaa hao, kichwani mwake alijua kwa vyovyote watu hao wamehifadhiwa katika moja ya yadi hizo ili watekeleze mauaji yao. Huku akiwa na mawazo mengi juu ya Gina, akiwa hajui ni wapi atakuwa amefichwa na mashetani hao. Mara saa yake ikaanza kumfinya usiku huo, huku akiwa mwendo wa kasi katika pikipiki lake hilo aliinua mkono na kuiruhusu saa hiyo kutoa ujumbe kwa kuibonyeza kitufe Fulani, saa ile ikaanza kutema mkanda wa maneno, ‘uelekeo wapi?’ ujumbe ulikuwa ni kutoka kwa Madam S, hakuufuatilia kujibu aliendelea kusonga na pikipiki lake, mpaka alipofika eneo husika na kuficha pikipiki lake sehemu kisha kurudi kwa mguu mpaka jengo hilo lililozungukwa na ukuta mkubwa sana. Akafanya analoweza na kuukwea ukuta ule ambao siku hiyo haikuwa mara ya kwanza kwake kuukwea, ilikuwa ni mara ya pili, lakini leo ni kwa shari kidogo.



    Alitua chini taratibu bila kushtua hata mbu, akatulia katika hali hiyo kwa sekunde kadhaa, kisha akaanza kutembea na kuuelekea mlango ule aliutumia siku ya kwanza, lo, haukuwa mlango tena bali ulizibwa wote kwa matofali na kupigwa plasta kabisa na rangi nyeupe juu. Sasa hakuwa na budi kutumia mlango wa mbele kuingia ambao ni mlango wa hatari zaidi kwani ulinzi wote uko huko, kwa kuwa alikwishajua kuwa jengo hilo lina camera za usalama kila kona alikuwa tayari amejiandaa kwa hilo. Akaendelea kuvuta hatua ndogo ndogo huku akiwa ndani ya mavazi meusi yaliyomficha kila kitu isipokuwa macho tu ambayo yalifunikwa kwa miwani maalumu yenye uwezo wa kuona gizani. Alitazama na kuwaona walinzi waliokuwa wakitembea huku na huku wakiwa katika doria ya ndani humo.



    Akiwa kama paka anayetaka kumkamata panya, Kamanda Amata alinyata taratibu sana kuuendea mlango uliokuwa jirani yake. Lakini kichwani aliona wazi kuwa hatoweza kufikia lengo lake bila ya kuonekana na walinzi hao ambao walikuwa wakiranda huku na huku. Akajibana kwenye tenka moja la mafuta na kumsubiri mlinzi aliyekuwa anakuja upande huo, alipofika tu, alimvuta na kumpatia kabali ya maana, Yule mlinzi hakutoa hata sauti, alilegea na kuwekwa chini kwa upole, kamanda akampigapiga kichwani kumpa salamu ya pumziko la milele, akajivuta tena kwa kupita chini ya tenka lile ambalo lilikuwa limewekwa juu ya vyuma virefu na kuweza kupita bila kuuinama. Mlango ulikuwa umbali wa mita kama mia moja hamsini hivi, lakini katikati ya eneo hilo hakukuwa na kitu hata kimoja, hivyo ingekuwa rahisi kwake kuonekana, hakuna ujanja, alichomoa bastola yake iliyofungwa kiwambo cha sauti na kasha akajaribu kupita kwa kasi katika eneo hilo, lakini kabla hajaufikia mlango, risasi kutoka upande wa walinzi zilisikika, Kamanda Amata alijitupa chini na kusota kwa mgongo huku bastola yake ikianza kazi, shabaha zisizokosa ziliwa maliza walinzi wale wane, ‘Sikutaka kuwaua lakini imebidi’ alijisemea moyoni, kisha Kamanda akanyanyuka na kujificha karibu kabisa na ua kubwa pembeni mwa mlango. Akasikia nyayo za watu wanaokimbia, akatulia na kiliskiliza nyayo hizo, kwa harakaharaka alishajua kuwa wapo watatu.



    Mara utulivu ukarejea, hakusikia tena zile nyanyo, nay eye akaendelea kutulia palepale ili kuona kitakacho endelea, akiwasubiri hao waliokuwa wakija upande huo. Kivuli cha mtu aliyekuwa akija kwa mwendo wa kunyata kilionekana kwenye mwanga wa taa kikiibuka kutoka nyuma ya ukuta, Kamanda Amata aliendelea kutulia palepale, akakitazama kivuli kile na kugundua mtu huyo alikuwa na bunduki mikononi mwake, akamsubiri ili ajitokeze waziwazi.

    Amakweli, subira huvuta heri, Yule mlinzi aliyekuwa akinyata akajitokeza, bado akiwa katika hali ya kujihami alitazama huku na kule bunduki ikiwa mkononi, Amata nae akajipanga kwa shambulizi la ghafla wakati huo akijua kuwa wengine watakuwa maeneo hayohayo, akaona ngoja asubiri kinachoendelea labda na wengine watajitokeza ili aone ni vipi ataanzisha shambulio lake. Yule mlinzi wa kwanza alipoona utulivu na hajkujua adui yake yuko wapi, akatoa ishara ya mkono kuwaita wengine, mara wale waliobaki wakajitokeza waziwazi tena wakitembea bila woga kuzielekea zile maiti mbili nza walinzi wenzao. “Wamekufa!” mmoja akawaambia wenzake, “Wamekufa?!” mwingine akauliza kwa sauti ya tashwishwi, baada ya hapo wote wakalundikana katika zile maiti wakijaribu kuangalia hiki na kile, “Wamepigwa risasi, unaona majeraha haya?” Yule wa kwanza aliwaambia wenzake. “Sasa mbona hatukusikia mjibishano wa risasi? Mi nimesikia risasi mbili tu za wao,” mwingine alionesa shaka.



    “Tumevamiwa,” Yule aliyesimama karibu na Amata, aliyekuwa wa kwanza kujitokeza aliewaeleza wenzake, kisha wakatawanyika kumsaka muuaji, “Hakikisheni mnampata, yumo humuhumu!” akawasisitiza kisha nay eye akachukua nafasi nyingine nzuri ya kumtafuta adui.

    Kamanda Amata akawa akicheka moyoni akiwasikiliza kwa kila walilokuwa wakiongea, akwasubiri watawanyike ili aanze kufanya vitu vyake. Alipohakikisha kuwa eneo lile kabaki Yule mlinzi wa kwanza tu, na wakati huo alikuwa ametoa simu akijiandaa kupiga mahali, Amata akaona kuwa hapo hapo ndio nafasi ya kufanya mambo yake, alichomoka kutoka pale alipojificha kwa kasi na kuruka hewani amako miguu yake ilitua mgongoni mwa Yule mtu, simu ikamponyoka nay eye mwenyewe kujikuta akisukumiwa mbele kwa kasi na kujibamiza kwenye gari ya mafuta iliyokuwa imeegeshwa eneo hilo. Kabla hajajiweka sawa Kamanda Amata alikuwa tayari amefika na kumsindikizia kichapo kikali kilichomzimisha jamaa huyo.



    Alipohakikisha ametulia, alimsogeza na kumuweka jirani na kichwa cha lori hilo, akamuinua na kumuegemeza kasha akamuashia sigara na kumpachika kinywani mwake kiasi kwamba ukija haraka haraka utasema mtu huyo amepumzika akivuta sigara. Kamanda Amata akauendea mlango na kuuchezea kwa namna ya ajabu, ilikuwa sekunde kadhaa tu alipojikuta ndani ya ujia mrefu, akarudisha mlango nyuma yake na kutulia akiangalia kama kuna kamera ya usalama eneo hilo, alitazama darini hakukuwa nayo wala pembezoni hakukuwa na kitu kama hicho, taa ya mwanga hafifu sana ilikuwa ikiwaka kumulika kijia hicho, ‘Usalama kwanza,’ akachomoa bastola yake na kufumua ile taa, giza likatawala katika ule ujia, Kamanda Amata akaona kijitaa chekundu kikiwakawaka palepale alipoipiga ile taa, akatikisa kichwa kuashiria kuwa ameng’amua kitu. Akasogea taratibu mpaka eneo lile, kwa akaichika ile kamera iliyokuwa ikining’inia, akakta nyaya zake kasha akaungania ule mweusi na mwekundu pamoja, akafasha shoti sakiti. Fuse inayolinda kamera hizo katika ‘distribution box’ ikaungua kwa kitendo kile na kufanya kamera zote kushindwa kufanya kazi. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Kamanda Amata akaendelea mbele huku akisoma milango iliyoandikwa majina na vyeo vya wahusika, alipofungua chumba kimoja baada ya kingine hakupata anachokitafuta. Katika chumba cha mwisho amako ndani yake kulikuwa na makorokoro mengi, pampu za mafuta na mambo kibao, ndipo alipopata hisia ya kuwepo kwa Gina eneo hilo. Baada ya kupekua na kukagua kila kilichomo, kwa kutumia kurunzi ndogo kama kalamu, aliweza kuiona heleni moja ikiwa chini, akaiokota na kuigeuzageuza, “Gina,” alijisemea kwa sauti ya chini. Akaichukua na kuitazama tena kwa makini, akatabasamu, ilikuwa ni heleni ya Gina, heleni ambayo mara kadhaa alimwambia akijikuta kwenye matatizo kama hayo aidondoshe chini kama ikibidi kuondolewa eneo hilo. Kamanda Amata akaichuku na kuibana sikioni mwake huku kitufe chake cha urembo akiwa amekipachika katika sikio lake kwa ndani, haikuwa heleni ya kawaida, bali mtu alipoivaa ni heleni ila kwenye kazi kama hizo unatakiwa kukifungua kitufe ca urembo na kukipachika kwenye tundu la sikio hapo utaweza kusikizana na Yule mwenye heleni ilobakia na mkfanya mawasiliano bila shida.





    SCOLLETI alikuwa katika hatua za mwisho za mazungumzo na watu wake, Shailan, Shakran, Tajan na wengine wawili wakiweka mambo sawa.

    “Jamani tayari julai saba imefika, tumejipanga vya kutosha?” Scolleti aliuliza.

    “Hapa tuko tayari, kila kitu kimepangwa kwa sababu kuna mambo makubwa mawili, kesho watamfungulia Jegan saa nne kamili asubuhi, hivyo sisi tutakuwa kule kwenye point yetu kama kawaida wakati wa tukio hilo, hawa jamaa nina wasiwasi nao sana, tukijitokeza pale kumchukua Jegan usishangae wote tukakamatika.” Shakran aliwaeleza wajumbe.

    “Sikilizeni, mpango upo hivi, Jegan atachukuliwa na watu wa ubalozi wa nchi yake kesho muda huo, sisi kama alivyosema Shakran tutakuwa tayari kwenye point husika kwa ajili ya kuwapa shukrani Watanzania, kikosi cha ukombozi kitakuwa tayari katika bahari ya hindi kwa kutumia boti iendayo kasi ambayo itatufikisha Mombasa kesho jioni,” Shailan alieleza.



    Kwa ufadhili alioutoa bwana Scolleti, boti ya kasi kutoka Ugiriki ilikuwa tayari katika pwani ya Pemba ikisubiri utekelezaji wa amri itakayofuata, ili iweze kusogea karibu na Bagamoyo kwa zoezi la kuwatorosha freedom fighters.

    Scolleti akatingisha kichwa kuonesha kuwa ameridhika na matumizi ya fedha nyingi alizokuwa amewekeza kwa jamaa hao kwa makubaliano ya yeye kupata mafuta kutoka visima vinavyomilikiwa nao huko Mashariki ya kati kwa muda wa miaka mitano zaidi. Aliendelea kukenua huku akiwatazama mmoja mmoja, “Kwa hiyo leo kuanzia saa nne asubuhi televisheni za Tanzania zitapendeza kwa maua mazuri mtakayorusha kumpokea Jegan uraiani?” Scolleti akawauliza.

    “Kabisa yaani kama ulikuwepo,” Shailan akajibu.

    “Na vipi kuhusu huyu mwanamke wao?” Scolleti aliuliza akimaanisha Gina.



    “Huyo nia yetu tumtumie kama chambo cha kumnasa Kamanda Amata, lakini sijajua mpaka sasa kinaendelea nini, hakuna taarifa katika yadi zote mbili,” Shailan akajibu. Shakrum akainua redio call yake na kuita.

    “Yadi moja, yadi moja, ova”.

    “Yadi moja tunakupata, ova,” akajibiwa.

    “Usalama tafadhali, nipe ripoti, ova”

    “Kila kitu salama, hakuna tatizo, ova” akajibiwa kwa kupewa taarifa hiyo ambayo kwa walinzi hao ilikuwa sawa, baada ya hapo aliita yadi ya pili ili kujua nako nini kinaendelea, majibu hayakuwa tofauti, lakini kumbe hakujua kama aliyejibu kutoka yadi mbili alikuwa kawekewa mtutu wa bastola kichwani akishinikizwa kujibu hivyo, shinikizo la Kamanda Amata. “Ok sasa twende kwenye point yetu na tusubiri muda ufike, Tajan utabaki yadi mbili kusubiri kama kutakuwa na lolote, ikiwa hakuna basi saa nne umuue Yule mwanamke kisha uje kwenye point yetu,” Shailan alikuwa akipanga kikosi, akamgeukia Yule mwingine, “Tashrini, wewe utakuwa gereza la Ukonga pale kutujulisha kila kinachoendelea, ukishahakikisha Jegan ameondolewa eneo lile ufuate msafara na uhakikishe amefika ubalozini bila kugundulika, baada ya hapo uje kwenye point, saa tano kamili tutaondoka wote kwenye point kuelekea Mombasa tukiwa na Jegan Grashan, Scolleti kama ulivyopewa maelekezo, ila kwa sasa tunakushukuru kwa msaada wako, asante,” Shailan alimaliza na kila mtu akawa katika hali ya kwenda kwenye kitengo alichopewa.



    §§§§§



    GINA akiwa amechoka sana, mwilini mwake akiwa na nguo ya kulalia tu, alikuwa chini ya ulinzi mkali, walinzi wanne walikuwa nje ya kibanda alichofungiwa wakizungukazunguka na bunduki zao zilizosheheni risasi zikiwa mikononi mwao huku vidole vyao vikiwa vimepachikwa katika kifyatulio tayari kwa amri yoyote itakayotolewa. Mara sikio la Gina likaanza kupata ukelele wa kitu kama mluzi, kwataabu kidogo akanyanyua mkono na kukifyatua kile kitufe cha heleni na kukipachika sikioni mwake.

    “Heyyy!!” akanong’ona, kisha akajibiwa vivyo hivyo.

    “Uko wapi Gina,?” Kamanda Amata aliuliza kwa kunong’ona maana huwezi kuongea kwa sauti eneo kama hilo.

    “Wamenifunga chini ya ardhi, tafuta mlango uliondikwa ‘Kisima’ ” Gina alitoa maelekezo. Mara Yule askari wa jirani yake akasikia mnong’ono ule.

    Akamuendea Gina mpaka pale alipo, akamtazama usoni akiwa kamuinamia.

    “We mwanamke, unaongea na nani au umepata kichaa?” Yule askari akamuuliza huku akiwa kamshika kichwani na bunduki yakeikiwa imeshikwa kwa mkono mmoja.

    “Naongea na shetani, unataka kumuona?” Gina akamuuliza Yule askari.



    “Unaleta upumbavu sio! Akarusha mkono ili amtandike kofi Gina, Gina akaepa lile kofi na kumpiga kichwa askari huyo, akaangukia upande wa pili, Ginaakajinyanyua na kumuwahi koromeo, alimkaba kwa nguvu zake zote,Yule askari alijitahidi kujikukurusha kutoka katikamikonoya Gina ambayoilisukumwa na nguvu za hasira. Yule askari akainua miguuyake na kuidaka shingo ya Gina kisha akamvuta nyuma kwa miguu yake. Gina aliiachia shingo ya askari huyo na kutaka kujinusuruna ile kabali ya miguu toka kwa askari Yule, alipoona kuwa njia hiyo anayotumia ni ya kizamani alijifayatua na kukubali uole mvutonwa ile miguu, akajirusha nyuma na kuchomoka bilatabu katika miguu hiyo, kwa haraka akasimama wima. Kelele za askari wengine wakiitana nakuja upande huo kutoa msaada zilimfikia Gina sawia kabisa, Yule askari pale chini alipotakakujiinua alizimishwa kwatekekali la usoni,akarudi chini na ile bunduki ikamtoka mikononi, Gina akaiwahi na kuimiliki mikononi mwake, akaiweka sawa na risasiya kwanza ikamteremsha askari aliyekuwa juu ya ngazi akiteremka kuja chini, akajibwaga kama mzigo. Gina alianzakufanya kazi ya kujinasua kutoka huko kisimani, akayapita mapipa kadhaa ya mafuta nakutoke upande mwingine.

    “Kamanda Amata!” aliita.

    “Nakusoma, Gina niko njiani kuelekea huko,” aliongeakwa kunong’ona kama awali.



    “Nimedhibiti kisima, usiwe na shaka,” Gina alimpa taarifa Kamanda Amata ambaye alikuwa mbioni kwenda kumuokoa.

    Majibizano ya risasi za Gina na wale askari yalisikika wazi kabisa. Gina alijikuta anaingia katika pambano la hatari na askari hao huku akitafuta njia ya kutokea ndani humo.

    “Tulia hivyo hivyo mwanamke hayawanimkubwa wewe!” sauti ilitokea kwa nyuma, Gina akageuka wakati akiamuriwa kuweka silaha yake chini na kunyoosha mikono yake hewani.

    “Unajifanya komandoo wa kike sio?” Yule askari aliongea huku akimfuata Gina na shotgun yake ikiwa tayari kwa lolote lakini kabla hajamfikia, alipaishwa juu na kujibwaga chini kama gunia jirani kabisa na miguu ya Gina, Gina akainua shingo uso kutazama kule risasi hiyo ya ukombozi ilikotokea maana alijua wazi kama Yule askari angemfikia basi ilikuwa ni kipigo cha mbwa mwizi, akamuona Kamanda Amata kama kawaida yake akirusha karanga moja moja kinywani mwake.

    “Kamandaaa!” akaita kwa furaha huku akimkimbilia.

    “Ginaaaa!” Naye alijibu wakakumbatiana kwa furaha, kisha wakaanza harakati za kutoka nje, Kamanda alitangulia mbele na Gina alifuata nyuma. Njia ilikuwa nyeupe ya kutokea nje kwani Kamanda alikuwa tayari kafanya kazi kubwa ya kuwateremsha wote waliokuwa hai ndani ya jengo hilo.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walitoka nje ya jengo hilo na kuuendea ukuta upande wa nyuma, akaikutanisha mikono yake kwa nyuma kwa kuifunganisha viganja.

    “Gina kanyaga hapo uruke nje!” akamwambia Gina. Baada ya Gina kuruka na kutua nje ya ukuta huo naye akapanda kiufundi zaidi kisha wote wawili wakatokomea na kuacha maafa katika yadi hiyo, akaenda alipoficha pikipiki yake na kuitoa, akakaa nyuma ya usukani na Gina akatulia nyuma yake.

    “Kamanda kabla hujaondoka sikiliza, kuna mpango mbaya sana hawa jamaa wameupanga dhidi ya Watanzania leo saa nne asubuhi, lakini sijajua ni wapi wanataka kutekeleza unyama huo,” Gina aliongea haraka harakakiasi kwamba ilikuwa ni ngumu kwa Kamanda kuipata vizuri sentensi hiyo. Gina akarudia alilolisema akisisistiza kuwa amewasikia wao wenyewe wakiongea katika kikao chao usiku huo. Kamandaa akaitazama saa yake, akaona jinsi ilivyopanga vishale vyake, kile kifupi kwenye namba nne juu kidogo na kile kishale kirefu kilikaribia namba sita, yaani saa kumi na dakika ishirini na kadhaa, akaishusha na kuwasha pikipiki lake kisha akaondoka kwa kasi.



    §§§§§





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog