Search This Blog

Sunday 22 May 2022

BARUA NDEFU KUTOKA BAGHDAD - 5

 







    Simulizi : Barua Ndefu Kutoka Baghdad

    Sehemu Ya Tano (5)





    Brian hakuonekana kuwa muelewa hata kidogo, bado alikuwa aking’ang’ania waelekee Karadah kwa ajili ya kuangalia sehemu ambazo wazungu walikuwa wamehifadhiwa.

    Hakukuwa na mtu aliyekuwa na nguvu za kumzuia kwani jambo lile ndilo ambalo alikuwa akilitaka litokee kwa wakati huo. Japokuwa Yasmin alikuwa aking’ang’ania zaidi na zadi kwamba sehemu ile ilikuwa ni ya hatari, mwisho wa siku akakubaliana nae na kisha kuanza kuelekea Karadah.

    Alichokifanya Yasmin ni kumbeba mdogo wake, Rahim na kuanza kuondoka ndani ya chumba kile na kutoka nje. Muda wote macho yao yalikuwa yakiangalia huku na kule, hawakuwa na amani kabisa, walikuwa wakifahamu fika kwamba kwa wakati huo walikuwa wakitafutwa sana na Waarabu ambao walikuwa wakitaka kuwaua.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mara baada ya kufika nje ya nyumba ile, wote wakaingia garini na Yasmin kushikilia usukani na kisha kuanza safari ya kuelekea Karadah. Watu waliokuwa pembeni ya eneo lile wakabaki wakiwashangaa tu, hawakuelewa mahali ambapo Yasmin alikuwa amewatoa watu wale ambao walionekana kuwa wageni machoni mwao.

    Vumbi jingi likatimka mahali hapo, Yasmin akalitoa gari katika eneo hilo kwa mwendo wa kasi ambao ulimshangaza kila mtu. Ndani ya gari, Yasmin alionekana kuwa na wasiwasi juu ya maisha yake, maisha ya Brian na Erick, aliitambua vizuri sana kambi iliyokuwa Karadah, ilikuwa moja ya kambi ambayo haikuhitaji kuletewa masihala hata kidogo.

    Mara baada ya dakika kadhaa wakawa wamekwishafika katika mji wa Karadah. Alichokifanya Yasmin ni kulipeleka gari lile katika eneo la nyumba moja na kisha kulipaki.

    Wote wakateremka garini huku Yasmin akimchukua mdogo wake na kumbeba. Brian na Erick walidhani kwamba ndani ya nyumba hiyo ndio ambayo walitakiwa kuingia, lakini kitu cha ajabu wakashangaa kumuona Yasmin akianza kuelekea sehemu nyingine.

    “Unakwenda wapi?” Brian alimuuliza Yasmin ambaye alikuwa akizidi kuondoka bila kujibu kitu chochote kile.

    Walichokifanya ni kuanza kumfuata Yasmin ambaye safari yake iliishia katika geti moja la hoteli ambayo wala haikuwa mbali kutoka katika nyumba ile waliyokuwa wamepanga. Moja kwa moja Yasmin akamfuata dada aliyekuwa mapokezini na kuanza kuongea nae, alipomaliza, akauingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi fulani cha fedha na kumkabidhi.

    Hawakutakiwa kubaki mahali hapo, wakaanza kuondoka kuelekea katika chumba ambacho Yasmin alikuwa amepewa. Dada wa pale mapokezini hakutakiwa kwenda pamoja nao, kwa sababu namba zilikuwa milangoni, wakaona ingekuwa vizuri kama wangekwenda wenyewe.

    Wakapandisha ghorofa ya kwanza mpaka ya pili na kisha kuanza kukitafuta chumba namba ishirini walichokuwa wamepangiwa, walipoingia ndani ya chumba hicho, Yasmin akamlaza Rahim kitandani na kuelekea dirishani. Macho yake akayapeleka katika gari lao ambalo walikuwa wameliacha upande wa pili katika nyumba ambayo wala haikuwa mbali kutoka pale walipokuwa.

    “Vipi” Brian aliuliza huku akimfuata.

    “Najaribu kuliangalia gari letu. Kama kweli tunatafutwa, wanaweza wakaja” Yasmin alimwambia Brian.

    Brian akasogea pale dirishani na kisha nae kuanza kuangalia nje, gari lile lilikuwa palepale huku kukiwa hakuna dalili za kuonyesha kama watu ambao walikuwa ndani ya nyumba ile walifahamu kama kulikuwa na gari ambalo lilikuwa limekiwa nje ya nyumba yao. Wala hazikupita dakika nyingi, magari mawili yakaonekana yakipita mahali hapo na kisha kusimamishwa na kuanza kurudishwa nyuma.

    Waarabu nane ambao walikuwa na bunduki mikononi mwao wakateremka na kuanza kulifuata gari lile na kuchungulia ndani, walipoona hakukuwa na mtu wakaanza kuingia ndani ya nyumba ile.

    Walikaa kwa sekunde kadhaa na kisha kutoka na mwanamke mmoja ambaye jamaa mmoja aliyeonekana kuwa kiongozi akionekana kumlazimisha mwanamke yule kusema kitu fulani.

    Waliendelea kumwangalia zaidi na zaidi, mwanamke yule alikuwa akilia kama mtoto hasa mara baada ya kuona amenyooshewa bunduki.

    Alichokifanya Yasmin, akachukua bunduki yake na kisha kuwaelekezea waarabu wale ambao walikuwa wakimwangalia mwanamke yule huku wakionekana kuwa na hasira.

    “Utaweza kumpiga risasi kweli?” Brian alimuuliza Yasmin.

    “Usijali. Shabaha niliyo nayo ni kubwa sana” Yasmin alijibu.

    Brian hakutaka kubaki hivi hivi, nae akachomoabunduki yake kutoka kiunoni na kuwalekezea vijana wale. Kila mmoja alikuwa amejiandaa kuwafyatulia risasi.

    Baada ya sekunde chache, wakaanza kuwafyatulia risasi waarabu wale. Hakukuwa na risasi yoyote ambayo ilimkosa mtu yeyote, zote ambazo zilizokuwa zimefyatuliwa zilikuwa zimeingia katika miili yao na kuanguka.

    Waarabu wote walikuwa chini, wengine walikuwa wakirusha rusha migu na mikono yao huku na kule na wengine wakiwa wametulia kabisa. Walipoona kwamba kazi yao imekamilika, wakatoka dirishani pale na kisha kushusha pazia.

    Watu wakaanza kujaa katika eneo lile na kisha kuanza kuiangalia miili ile ya watu wale, kila mmoja alishindwa kufahamu sehemu ambayo risasi zile zilikuwa zimetoka japokuwa kuna kipindi walikuwa wamesikia milio ya risasi.

    *****CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Waliendelea kukaa ndani ya chumba kile hotelini kwa takribani dakika kumi huku Brian akiwapigia simu wakuu wake wa kitengo cha upelelezi cha F.B.I na kuwaambia kuhusu kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea nchini Iraq hasa ndani ya jiji hilo la Baghdad.

    Kila taarifa ambayo alikuwa ameitoa mahali hapo ilikuwa ikilingana sawa sawa na kila kilichokuwa kikiendelea.

    Katika kipindi chote hicho Yasmin alikuwa akimwangalia mdogo wake, rahim ambaye alikuwa kimya kitandani, moyo wake ulikuwa ukimuuma sana, hakuamini kama mpaka katika kipindi hicho alikuwa amekosa fedha za kuweza kumtibia mdogo wake ili arudiwe katika hali ya kawaida kama ilivyokuwa zamani kabla ya ugonjwa ule kumshika.

    Waliendelea kukaa zaidi na ndipo miungurumo ya magari ikaanza kusikika nje, wakasimama na kisha kufungua kidogo pazia na kuanza kuangalia nje. Magari mawili ya polisi yalikuwa yamepaki katika eneo lile ambalo lilikuwa na miili ile na kisha kuanza kuipakiza ndani ya magari ambayo walikuwa wamekuja nayo mahali pale.

    Baada ya dakika kadhaa kuipakiza miili ile, wakaingia garini na kisha kuondoka mahali hapo huku wakiwa wamechukua maelezo ya kutosha kutoka kwa watu ambao walikuwa wakiishi ndani ya nyumba ile pamoja na majirani. Hali ilipoonekana kuwa kimya, Brian akaanza tena kulalamika kwamba iliwapasa kuelekea katika sehemu ambayo wazungu walikuwa wakitekwa na kuhifadhiwa hapo Karadah.

    “Ni lazima twende huko” Brian aliwaambia.

    “Lakini mbona unakuwa kama si muelewa?” Yasmin alimuuliza huku akionekana kukasirika.

    “Kama sehemu yenyewe ni ya hatari, haina budi ukabadilisha mawazo yako” Erick aliingilia na kumwambia Brian.

    Katika kila kitu ambacho kiliongelewa mahali hapo kikaonekana kutokueleweka kwa Brian, kitu ambacho alikuwa akikitaka kwa wakati huo ni kuelekea katika kambi ya mateka iliyokuwa hapo Karadah.

    Malumbano yakaendelea zaidi na zaidi lakini mwisho wa yote, Brian akaonekana kushinda na hivyo wote kujiandaa na safari hiyo ya hatari ya kwenda katika kambi hiyo.

    Hawakutaka kwenda huko pamoja na Rahim, walitakiwa kumuacha ndani ya chumba kile na kisha wao kutoka nje. Brian akachukua simu yake na kisha kuanza kupiga katika kitengo cha upelelezi cha F. B. I na kisha kuanza kuwaambia kwamba ilikuwa ni lazima wafike Karadah haraka iwezekanvyo.

    “Hivi kuna ulazima wa mimi kwenda huko? Naona kama ningebaki na mgonjwa” Erick aliuliza.

    “Umuhimu wako upo. Tena mkubwa sana hata zaidi ya Yasmin” Brian alijibu.

    “Kuna umuhimu gani sasa wa mimi kuwa huko?”

    “Kwa ajili ya kuandika habari. Itakupasa kuandika kila utakachokiona” Brian alimjibu Erick.

    Erick akabaki kimya, moyo wake haukujisikia amani kabisa, maisha ambayo alikuwa akipitia katika jiji la Baghdad yalionekana kuwa maisha ambayo yalijaa vitisho vikubwa sana. Alitamani kumkatalia Brian kwenda kule walipokuwa wakielekea lakini kwake likaonekana kuwa jambo gumu sana kwani angeonekana kuwa msaliti mkubwa.

    Walitembea kwa mwendo wa dakika arobaini na tano na ndipo kwa mbali mbele yao kukaonekana kuwa na jengo kubwa. Alichokifanya Brian ni kupiga tena simu na kisha kutoa maelekezo juu ya mahali ambapo walitakiwa kufika mara baada ya kuingia nchini Iraq. Wakaanza kupiga hatua kuelekea katika jengo lile huku wakijificha ficha.

    “Tutaingia salama na kutoka salama” Brian aliwaambia wenzake huku wakizianaa bunduki zake.

    “Ila lengo kubwa la kwenda mule ndani ni nini hasa?” Erick aliuliza.

    “Kuwaokoa wenzetu na kisha kuondoka nao” Brian alijibu.

    “Je tukishindwa kuwaokoa?”

    “Basi tutakufa” Brian alimjibu Erick ambaye woga aliokuwa nao ukizidi kuongezeka.

    Kwake, Brian alionekana kuwa mtu wa tofauti kabisa, mtu ambaye hakuwa akiogopa kufa hata mara moja. Muda wote Brian alikuwa akionekana kujiamini kupita kawaida, kwake kifo wala hakuonekana kukijali sana, moyoni aliamini kitu kimoja tu kwamba kila nafsi duniani ingeonja mauti.



    Taarifa zilikuwa zimetolewa ndani ya shirika la kipelelezi la kijasusi la F.B.I lililokuwa nchini Marekani. Taarifa ile ilionekana kumfurahisha kila mmoja, kujulikana kwa mahali ambapo wazungu walipokuwa wakipelekwa nchini Iraq ndani ya jiji la Baghdad zilionekana kuwafurahisha sana.

    Kwa haraka haraka maandalizi yakaanza kufanyika, hawakutakiwa watu kutoka nchini Marekani ndio waelekee huko bali Wamarekani ambao walikuwa nchini Iraq ndio ambao walitakiwa kwenda huko. Simu zikapigwa na kila kitu kuelezwa, hakukuwa na mtu wa kupinga na kwa sababu watekaji walikuwa wakitumia silaha, wanajeshi wa Marekani ndio ambao walitakiwa kutumia bunduki katika kufanya uvamizi ndani ya maeneo hayo na kisha kuanza kuua huku lengo kubwa likiwa ni kutaka kuwaokoa watu wao.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakukuwa na muda wa kuchelewa, simu ambazo zilikuwa zimepigwa kwa wanajeshi ambao walikuwa nchini Iraq ndizo ambazo ziliwafanya kufanya haraka haraka kwa ajili ya kwenda kufaya uvamizi katika sehemu hizo ambazo walikuwa wameelekezwa na Brian ambaye alikuwa huko.

    Wanajeshi wale wakatoka katika vituo vyao vilivyokuwa hapo Baghdad na kwenda katika mji wa Wassit ambao ulikuwa kaskazini mwa jiji hilo. Mwendo wa magari yao ulikuwa ni wa kasi kupita kawaida, hawakutaka kuchelewa hata mara moja. Kila kitu ambacho walikuwa wakitaka kukifanya mahali hapo walikuwa wakikifanya kwa haraka haraka.

    Raia wakajua kulikuwa na kitu ambacho kilitokea, haikuwa mara zote ambazo wanajeshi wa Marekani walikuwa wakiendesha gari kwa mwendo wa kasi namna ile. Watu wakajiweka pembeni na kisha kuyaangalia magari yale ambayo yalikuwa yakikimbia kupita kawaida.

    Mara baaba ya kufika katika mji mdogo wa Wassit, hapo hapo wakateremka na kuanza kuelekea katika nyumba ambayo walikuwa wameelekezwa Kwa kutumia darubini ambazo walikuwa nazo waliweza kuwaona baadhi ya waarabu wakitembea tembea ndani ya jumba lile huku wakiwa na bunduki mikononi mwao.

    Mkuu wa kikosi kile akanyoosha mkono wake juu na kisha kuvikunja vidole vyote na kuviacha viwili vikiwa vimesimama na kuvipeleka mbele na nyuma hali iliyomaanisha kwamba wanajeshi wawili tu ndio ambao walitakiwa kusogea mbele zaidi. Kama alivyotoa ishara ile na ndivyo ilivyokuwa, wanajeshi wawili wakaanza kusogea mbele zaidi kuifuata jengo lile na kisha wengine kufuata.

    Hawakuwa na muda wa kuchelewa, hapo hapo risasi zikaanza kusikika na waarabu wengi kuanguka chini. Kelele ziliendelea kusikika kutoka katika vyumba ambavyo mateka walipokuwa ndani ya jengo hilo. Waarabu wakaonekana kumalizika kupita kawaida, uvamizi ambao walikuwa wameutumia wamarekani katika kipindi hicho ulionekana kuwa uvamizi wa kushtukiza sana ambao uliwafanya waarabu wengi kuuawa kwa sababu ya kukosa maandalizi ya uvamizi ule.

    “Damu zilikuwa zimetapakaa katika jengo zima, moja kwa moja wanajeshi wale wa Kimarekani wakaanza kuingia ndani zaidi katika jengo lile. Bado walikuwa wakiendelea kuua zaidi na zaidi mpaka walipovifikia vyumba vile na kisha kuwatoa watu wao ambao walionekana kuwa katika hali isiyo ya kawaida, miili yao ilikuwa imeanza kukosa nguvu.

    “Kuna wengine?” Mwanajeshi mmoja aliuliza.

    “Ndio. Kuna jengo moja lipo Karadah”

    “Twendeni sasa hivi”

    “Hapana. Kuna wenzetu washakwenda huko”

    ****

    Bado Brian, Erick na Yasmin walikuwa wakiendelea kulisogelea lile jumba kwa tahadhari kubwa sana. Walikuwa makini kuliko katika kipindi chochote kile. Erick alikuwa akionekana kuwa na wasiwasi mkubwa lakini kwa Brian hali ilionekana kutokuwa ya wasiwasi kabisa. Kwake, aliamini kwamba roho ya binadamu ilikuwa ni lazima ionje mauti hata kama kuna kitu gani kitatokea.

    Waarabu waliokuwa na bunduki walikuwa wakionekana nje ya jengo lile, walichokifanya kwa wakati huo ni kuanza kuwalenga na risasi. Kila risasi ambayo ilikuwa ikitoka mahali hapo, haikupotea, ilikuwa ikimuingia mtu mmoja. Waliendelea kuwapiga risasi na ndipo kuanza kukimbia kwa kasi kulifuata geti la jumba lile na kuingia ndani.

    Hakukuwa na mtu yeyote katika eneo la nyumba ile jambo ambalo kila mmoja akabaki akishangaa, haikuwezekana kutokuwa na mtu yeyote yule, hiyo ilimaanisha kwamba wale walinzi ambao walikuwa wamewaua pale getini ndio walikuwa watu pekee ndani ya jengo lile? Kila walipokuwa wakijiuliza mahali hapo walikosa jibu.

    Hawakutaka kuendelea kujiuliza maswali ambayo hayakuwa na majibu, walichoamua kwa wakati huo ni kusonga mbele tu. Wakaanza kupandisha ngazi huku bunduki zao zikiwa tayari kwa kitu chochote kile ambacho kingetokea mahali hapo. Ukimya ulikuwa umetawala kupita kawaida, hakukuonekana kuwa na mtu yeyote yule jambo ambalo lilionekana kumshangaza hata Yasmin mwenyewe.

    Wakaufikia mlango wa chumba kimoja na kuufungua na kisha kuingia ndani. Chumba kilikuwa kikubwa sana ambacho kilikuwa na mateka wengi sana. Jambo la ajabu ambalo lilionekana kuwashangaza, mateka wote walikuwa kimya jambo ambalo halikuwa la kawaida. Huku wakiangalia kwa nyuso zilizojaa maswali, mara kundi la waaarabu ambalo lilikuwa limejificha katika kila kona ndani ya jumba lile likaibuka na kuwaweka chini ya ulinzi.

    Kwa kila tukio ambalo lilikuwa likionekana mahali hapo lilikuwa ni kama filamu ya maigizo ambazo mara kwa mara zilikuwa zikichezwa nchini Marekani. Idadi ya waarabu ilikuwa kubwa sana jambo ambalo likawafanya kuziachia bunduki zao na kisha kunyanyua mikono yao juu. Hawakuwa na jinsi, walifika mahali hapo kwa ajili ya kuokoa mateka lakini mwisho wa siku nao wakajikuta wakiwa mateka.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Bunduki zao zikachukuliwa na kisha kufungwa kamba na kutolewa nje katika uwanja mkubwa wa jumba lile. Kwa haraka sana bila kupoteza muda simu ikapigwa kwa Jabrouz ambaye ndani ya dakika tano akafika mahali hapo huku uso wake ukionekana kuwa na tabasamu. Akaanza kupiga hatua kuwafuata, alipowafikia, akaanza kumpiga vibao Yasmin kitendo ambacho kilimuuma sana Brian.

    “Nahitaji vichwa vyao wote watatu” Jabrouz huku akionekana kukasirika. Hakukuwa na sababu ya kusubiri, mkuu alikuwa amekwishaongea kitu kimoja ambacho kilitakiwa kufanyiwa kazi kwa haraka sana. Wote wakachukuliwa huku wakiwa wamefungwa kamba kwa nyuma. Muda wote Erick alikuwa akilia, hakuamini kama mwisho wake ungekuwa namna ile, kuchinjwa nchini Iraq ndani ya jiji kubwa la Baghdad.

    “Anza na Yasmin” Jabrouz alitoa amri.

    Kila klichoongelewa hapo ndicho ambacho kikafanyika, Yasmin akalazwa kifudifudi na kisha mwanaume aliyekuwa na kisu kikali kukaa juu ya mgongo wake. Yasmin alikuwa akipiga kelele za kuomba msamaha lakini hakukuwa na mtu yeyote ambaye alionekana kujali. Wanaume watatu ambao walikuwa wamemshika miguu yake walikuwa wamemshika vilivyo, kisu kikaanza kupitishwa shingoni mwake, damu zikaanza kutoa. Ndani ya sekunde ishirini tu, kichwa kilikuwa kipo mkononi mwa mchinjaji.

    Ile ilionekana kuwa kama ndoto moja kubwa na ya kutisha ambayo Erick hakudhani kama alikwishawahi kuiota. Kuliona tukio la mtu akichinjwa mbele ya macho yake lilionekana kumuogopesha kupita kawaida. Akabaki akitetemeka tu. Mwili wa Yasmin ulikuwa ukijirusha jirusha pale chini huku damu zikitapakaa mahali pale.

    Mtu ambaye alifuata kwa wakati huu alikuwa Brian. Brian alionekana kutokuhofia kitu chochote kile. Hata alipolazwa kifudifudi na kisha kukaliwa juu huku akishikwa na watu wawili kwa juu, hakuleta usumbufu wowote ule. Mwanaume yule ambaye alikuwa na kisu mkononi akamkalia kwa juu na kisha kukipeleka kisu kile shingoni mwa Brian.

    Kama kawaida yake, kisu kile kikaanza kuikata shingo yake, damu zilikwishaanza kuonekana. Mara ghafla katika hali ambayo hakukuwa na mtu ambaye aliifikiria, risasi zikaanza kusikika mahali hapo huku mchinjaji akiwa mtu wa kwanza kupigwa risasi ya kichwa. Kila mmoja akaonekana kuchanganyikiwa, hawakuwaona wapigaji, mapigano yakaanzia hapo.

    Ilikuwa ni vita kubwa, Erick alikuwa amelala chini huku akimwangalia Brian ambaye muda wote alikuwa akitabasamu huku akitokwa na damu shingoni mwake kutokana na kisu kumkata kidogo. Wamarekani ambao walikuwa wamevamia mahali hapo walionekana kujiandaa na vita.Risasi zilipigwa mfululizo na ndani ya nusu saa, hakukuwa na mwarabu yeyote ambaye alikuwa hai, wote walikuwa wamepigwa risasi na kufa akiwepo Jabrouz, mkuu wa jeshi la waasi nchini Iraq.

    “How do you feel? (Unajisikiaje?)” Mwanajeshi mmoja ambaye alikuwa akiongoza kikosi hicho cha uvamizi ailimuuliza Brian.

    “Take me to the hospital (Nipelekeni hospitalini)” Brian aliogea kwa shida.

    Kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea jijini Baghdad kikaonekana kuwa historia ndefu ambayo ilijaa vitisho vikubwa katika maisha yake. Mateka wote ambao walikuwa wametekwa wakaokolewa na yale majumba mawili kati ya lile la Wassit na Karadh kufungwa kabisa. Brian na Erick wakarudi nchini Marekani huku wakiwa pamoja na Rahim ambaye walimuona kutokuwa na msaada kabisa.

    Baada ya kufika nchini Marekani, matibabu ya ini la Rahim yakafanyika na uwekewa ini jingine kitu ambacho kilimrudishia afya njema maishani mwake na Brian kuamua kukaa nae kama shukrani kwa dada yake, Yasmin ambaye alikuwa amewaokoa jijini Baghdad.

    Baada ya kurudi nchini tanzania ambako alipokelewa kwa shangwe, Erick akaandika kitabu ambacho kilikuwa kimeelezea kwa kina maisha ambayo alipitia nchini Iraq ndani ya jiji la Baghdad na kukiita BARUA NDEFU KUTOKA BAGHDAD. Kitabu hicho kilichokuwa kimeandikwa kwa lugha tano kilikuwa kimedhaminiwa na mashirika makubwa na kuuzwa duniani kote.

    Kilikuwa kitabu ambacho kiliwafumbua macho watu wengi, kilikuwa ni kitabu ambacho kiliwaogopesha sana watu waliokuwa wamekisoma. Ndani ya mwezi mmoja tu, tayari Erick alikuwa ameuza zaidi ya kopi milioni tano duniani kote jambo ambalo lilimfanya kuingiza kiasi kikubwa maishani na kuwa mtu mwenye fedha nyingi ambazo aliamua kufungulia miladi mbalimbali.

    Kitabu kile hakikuishia hapo, bado kilikuwa kikizidi kununuliwa zaidi na zaidi na kumuingizia fedha sana ambazo nyingine aliamua kumgawia Brian pamoja na kuendeleza maisha ya Rahim aliyekuwa akiishi nchini Marekani.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya miezi kadhaa kupita, mke wake, Christina akajifungua mtoto wa kiume ambaye aliamua kumpa jina la Brian, kumbukumbu ya rafiki yake ambaye alikuwa amesaidiana nae kwa kila kitu nchini Iraq ndani ya jijila Baghdad.



    MWISHO.





0 comments:

Post a Comment

Blog