Search This Blog

Sunday 22 May 2022

HATI FEKI - 2

 





    Simulizi : Hati Feki

    Sehemu Ya Pili (2)





    *****

    USIKU wa saa sita. Mosses ndula aliwaita watu wake wote kwa ajili ya kikao cha ghafla. Kikao ambacho ilikuwa ni lazima awahusishe wote. Hakumwacha hata dereva ambaye kazi yake ilikuwa ni kupewa amri ya nenda huku, simama hapo nisubiri au kamchukue Fulani. Wote walikuwepo usiku huo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akiwa na sura yenye furaha ya ushindi mkubwa mwezi mmoja baada ya kumaliza kushughulikia hati yake ya umiliki wa mgodi. Sasa alitaka kuwaeleza jambo watu wake.



    Alihisi kuna jambo la kuimarisha katika himaya yake ambayo sasa aliona inaimarika baada ya kumpindua mmiliki mkuu wa mgodi, mzee Amigolas na kuumiliki.



    “Nadhani imebaki kuanza kazi tu,” alisema Mosses Ndula akiwa na furaha baada ya kuwa amefanikisha kuipata hati ya umiliki ya mgodi. Alikuwa ameinyanyua juu huku akimwonyesha mmojammoja hati hiyo kumaanisha kwamba sasa kila kitu kilikwenda vizuri.



    “Mkuu, mi naona bado hatujafanikisha.” Alisema mmoja wa watu wake aliyekuwa amesimama pamoja na Mbashala aliyeitwa Nova, dereva wake wazamani.



    “Nisisikie tena….Wewe unasema kama nani? Minasema na wewe unasema?” Mosses Ndula alitoa bastola yake na kumpiga risasi ya kichwa na kufariki papo hapo. Hakutaka kusikia pingamizi lolote kutoka kwa mtu yeyote.



    “Sipingwi wala kushushwa, kila nikifanyacho ni zaidi ya mfikiriavyo…. Toa hiyo takataka hapo,” alifoka huku wasaidizi wake pamoja na walinzi wakiwa wanarudi nyuma kwa woga. Wawili kati yao waliutoa mwili wa Nova na kuupeleka kusikojulikana na kuutupa. Kikao kilikuwa kikiendelea ambapo tayari wote walikuwa wakisikiliza tu. Hakuna aliyejaribu kunyanyua mdomo wake kuongea kitu baada ya dakika chache zilizopita kushuhudia mwenzao akitolewa uhai. Wote walisimama kimya wakisubiri Mosses atakachokisema.



    Mosses Ndula hakutaka kubadili uamuzi wake juu ya kuachia mgodi. Kufanikiwa kwake kumsainisha kwa lazima Mzee Amigolas ilikuwa ni faraja kwake na kujiona tajiri mkubwa. Alihonga sana polisi na kuweza kujilimbukizia mali nyingi kwa muda mfupi. Alijuana na viongozi wengi na hata baadhi ya kesi zake zilizimwa kimya kimya kwani waliamini yeye ndo angeweza kuwafanikishia biashara zao haramu.



    Alipata kujiamini sana. Ni suala moja tu ambalo aliliwaza sana. Kumiliki mgodi. Mgodi uliokuwa ukitema madini kila kukicha. Mgodi wa mzee Amigolas. Na sasa hati anayo. Kicheko kiilimtoka kila alipofikiria kazi yake ilikuwa rahisi sana hasa baada ya kumtumia wakili wake na kufanikisha kubadilisha hati ya umiliki kwa madai ya kwamba mzee Amigolas alisaini wiki moja kabla hajafa baada ya kuuziana.



    Alijiamini kwa kuwa hati sasa iko mikononi mwake. Alijua ikitokea kesi yoyote basi angeonyesha hati hiyo kama kithibitisho. Alicheka. Alimkuwa haishi kumpigia wakili wake simu na kumpa shukrani tena na tena.



    Alikumbuka vitisho alivyovitoa kwa mzee Amigolas na familia yake.

    “Watoto wadogo sana wale…. Kazi tunajua sisi,” aliwaza na kucheka kwa kicheko cha ushindi. Sigara yake na glass ya wine vilikuwa mkononi vikisindikiza furaha yake. Pafu moja moja lilimkosha na kujiskia fahari.



    Siku hiyo kabla ya kumuua mzee Amigolas, alitoa hati ambayo alimpa mzee Amigolas aisaini. Mzee Amigolas alishangaa na kushtuka.



    Alikumbuka hati yake ilikuwa ndani ya nyumba yake, iweje Mosses yuko nayo. Alibaki akimwangalia Mosses. Alijua hati yake imechukuliwa. Aliona sehemu alizosaini kabla zikiwa tupu. Alijua kuna mchezo umechezwa. Alijua tayari kadhulumiwa.



    “Shika kalamu hii hapa,” Mosses alimkabidhi mzee Amigolas kalamu huku akimnyooshea bastola. Mzee Mosses alikuwa akitetemeka sana. Alijua atakufa. Alimwomba Mosses asimuue.



    “Kusaini nasaini. Tafadhali usiniue. Umeshawaua mke wangu na watoto. Naomba uniache. Tafadhali naomba usiniue,” mzee Mosses alimaliza kusaini ile hati na Mosses aliichukuwa na kuiweka mfukoni.



    “Mzee mpumbavu wewe, nikikuacha nitawezaje kuchukua hii mali? Lazima ufe.”



    “Tafadhaaa….” Kabla hajamalizia kusema alichotaka kusema Mosses alimfyatulia risasi Mzee Amigolas na kumuua. Damu iliruka na kuchafua kila mahali. Kisha Mosse na watu wake walitoka na kukimbia.



    *****

    Bodi inayosimamia mgodi ambayo iliwekwa na Mzee Amigolas hawakujua kinachoendelea. Hawakuwa na taarifa juu ya kuuzwa kwa mgodi hali iliyowachanganya wote. Wakiwa wanajitayarisha kuelekea nyumbani kwa Mzee Amigolas, walivamiwa na kundi la walinzi wa Mosses Ndula na kuuliwa.



    Habari zilifika kila mahali ikiwa ni pamoja na John na Antony waliokuwa wakijitayarisha kwa ajili ya kuanza kumsaka na kumjua aliyefanya mauaji nyumbani kwao.



    “Bodi nzima ilikuwa ikija huku John na wote walivamiwa na kuuliwa na majambazi,” Antony alimweleza John ambaye alikuwa amemwegemea Aminata asijue la kufanya.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mi nadhani kazi ianze, la sivyo hata sisi tutakuwa hatarini. Ni afadhali tuwe katika mapambano kuliko kuwasubiri waanze kutusaka sisi. Antony hakikisha unaidhibiti hiyo hati isipotee ikiwezekana uipeleke sehemu salama zaidi.”



    “Sawa mimi nitafanya hivyo. Nitaipeleka Nairobi kwa mtu ninayemwamini na kumkabidhi hadi itakapohitajika.” Wote walikubaliana na kuamua kuanza kazi.

    Kazi ambayo walikuwa wamejipanga vilivyo.



    ******

    Uzuri wa Aminata ulimchanganya sana John. Hakujua kwamba hata kwa upande wa Aminata alikuwa na swali na jibu sahihi kwamba inawezekana kama ikitokea wakiwa wapenzi. Walijikuta wakitoka kwa ajili ya mipango yao.



    Hiyo ilikuwa ni baada ya Antony kwenda Nairobi na hivyo katika kumsubiria waliamua kutumia muda huo kujuana na kuanza uhusiano wa kimapenzi.



    Walikuwa pamoja kila wakati. Walijikuta wakiingia kwenye penzi zito ndani ya wiki moja tu ambayo Antony aliitumia akiwa Nairobi.



    “John, tupo kwenye kipindi kigumu sana lakini siwezi kuuzuia moyo wangu juu yako,” sauti nyororo ya Aminata ilitooka ikiwa imelainishwa na juice baridi ambayo walikuwa wakiburudika ndani ya jumba kubwa na marehemu Mzee Amigolas.



    “Hata mi nakupenda sana Aminata, unansaidia sana. Namwomba Mungu tufanikiwe kwenye haya mapambano ili tuendelee kuwa pamoja,” John alisema huku akizishika nywele za Aminata ambaye nay eye alimruhusu John afanye analolitaka. Hali hiyo iliendelea huku mazungumzo nayo yakiendelea.



    “Ni wazi hadi sasa tumeshashinda.”



    “Ki vipi unasema hivyo mpenzi?” john alikuwa ameshaanza kumpapasa kifuani Aminata na kuyashika vizuri matiti yake yaliyokuwa yamesimama imara. Aminata hakuwa na la kusema. Alizungusha mikono yake nyuma ya mwili wa John na kuanza kumpapasa.



    “Nina uhakika na kile nkisemacho John. Kama nlivyokuambia….hee! nini hiko John?” ulikuwa ni mshindo mkubwa wa risasi ambao ulimwangusha chini mlinzi wa nyumba ya Mzee Amigolas. Kwa mara nyingine tena nyumba ya Mzee Amigolas inavamiwa na walinzi wa Mosses Ndula.



    “Nimewaona,” John alikuwa akichungulia kwa nje kuona ni kina nani. Walikuwa vijana watatu waliokuwa wamevalia kofia nyeusi za kufunika uso ili wasionekane. Haraka John na Aminata walijihami na kutoa bastola zao na kuzishika kikamilifu.



    Penzi liliwekwa pembeni na sasa ukawa ni mpambano kati yao na walinzi wa Mosses. Waliwajibu kwa risasi na kufanikiwa kumpiga mmoja na kudondoka chini. Risasi mfululizo ziliwafanya walinzi wa Mosses Ndula washindwe kuifikia nyumba ya Mzee Amigolas na kujikuta wakirudi nyuma na kutoka nje. Waliwasha gari lao na kukimbia.







    *****

    “John, wanaondoka,” Aminata alisema huku akiichukua nguo yake na kuvaa. John alichukua haraka funguo za gari ili kuwawahi.

    “Tusiwaruhusu wakaondoka John. Tuwafuatilie hadi mwisho wao ikiwezekana tuwamalize wote.” Aminata alisema huku akiufungua mlango na kutoka.



    “Sidhani kama watafika mbali. Kwa sababu watakuwa wameelekezwa, hapa wataishia njiani. Hafiki mtu.”



    John na Aminata walitoka nje na kuchukua gari na kuanza kuwafukuza. John alihimili usukani vilivyo na kukanyaga mafuta hadi alipowaona. Hawakutumia mwendo mrefu sana wakawa wamewakaribia kabisa. Waliwaona wakikata kona na hivyo waliongeza mwendo na kuikaribia kona huku John akiwa amezima taa za gari ili wasiwaone.



    “John usiwakaribie kwanza, watakimbia zaidi. Twende taratibu ili wasijue.”



    “Hawatakatiza.”



    Kila njia waliopita waliwafuata nyuma. Wakiwa Barabara ya Uhuru. Gari la walinzi wa Mosses Ndula lilikatiza na kuibukia Barabara ya Fire ambayo ilikuwa haina magari. walijua wamewapoteza na hivyo kupunguza mwendo. Hapo wakanza kutupiana lawama baada ya kushindwa kuvamia nyumbani kwa John.



    “Risasi imetuharibia kaka,” mmoja wao alianza kulalamika baada ya kuona kwamba mlio wa risasi uliwashtua John na Aminata.



    “Kwa nini usingefunga kizuizi sauti isitoke?”



    “Dah, askari yule tayari alikuwa ameshanielekezea mdomo wa bunduki aliyokuwa nayo. Hivyo sikuwa na muda wa kuitoa na ukikumbuka lengo letu ilikuwa ni kumteka na kumfunga kamba ndo tuingie kimyakimya.” Yule jamaa alijitetea huku akijilaumu mwenyewe.



    Jasho lilikuwa likiwatoka kwani walikimbiza gari sana kuhofia watu kuwakamata baada ya kusikika kwa mlio wa risasi. Sasa walikuwa wakiendesha kawaida baada ya kuona hali ni shwari na hakuna aliyewaona baada ya kukimbiza gari na kuiacha barabara ya Kijenge na kuibukia barabara ya Uhuru na kuingia barabara ya Fire.



    Zaidi ya mwendo wa kilomita moja wakawa wanajadiliana na kulaumiana juu ya kitendo kile. Wote wakwa wamenyamaza kimya bada y mmoja wao kuwatishia bastola na kuwaamuru wote wanyamaze.



    “Nimesema yaishe. Mnafanya ujinga alafu mnalaumiana. Tutarudi siku nyingine kama leo0 imeshindikana. Nisikie mtu analalamika. Tutamwambia bosi kwamba mambo mabaya. Hawakuwa wamelala na hivyo tulishindwa kulifikia geti.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “lakini akiuliza kwa nini askari amekufa baada ya kusikia taar4ifa. We unadhani itakuaje.”



    “Aaaaaah, na we tumia akili. Walipotuhisi sisi askari mmoja alitoka akaanza kurusha risasi ndo tukamuua. Ili mradi sisi wote tuko salama na hawakutujua. Kwa hiyo tusiogopeni. Bosi atatuelewa.”



    Ghafla walishangaa kuona gari mbele yao. Aminata na John walifika na haraka. Waliingia kwa mbele yao na kuwazuia wasiweze kukimbia. John alisimamisha gari na Aminata akatoa kichwa dirishani na kuanza kuwarushia risasi ambazo zote zilikuwa zikililenga gari. Aliendelea kuwarushia risasi. Risasi mfululizo zilifyatuliwa na Aminata huku John akiendelea kuwazuia wasiweze kupita.



    Wale watu walisikia sauti ya ving’ora vya polisi na hivyo waliona ni hatari zaidi. Waliongeza mwendo kurudisha gari nyuma ili wakimbie lakini risasi moja iliyofyetuliwa na Aminata ilimjeruhi dereva na kusababisha ashindwe kuhimili usukani na gari lao kupindukia ndani ya mtaro wa maji machafu.



    Hakuna aliyeweza kutoka kwani walifunga ilango. Mpaka walipoweza kufungua milango ili watoke, polisi walikuwa tayari wameshafika. Ilikuwa ni rahisi kwa John na Aminata kuwaweka chini ya ulinzi. Watu wengi walijazana kushuhudia watu hao wakikamatwa.



    Polisi nao walifika mara moja lakini walishindwa kuwachukua wakiwa hai kwani Aminata na John waliwamaliza palepale. Aminata aliwatambua watu wale. Mmoja wao alishangaa kumwona Aminata kabla ya kupigwa risasi.



    Askari waliwashangaa John na Aminata. Waliwatambua baada ya Aminata kuwaamrisha wawachukue maiti wale. P[olisi walitii amri ya Aminata. John alishangaa tukio lile la amri iliyotolewa na Aminata. Alitabasamu baada ya kuona akitolewa heshima na wale polisi.



    “Mkuu tumekuelewa,” alitania John huku akiingia kwenye gari na kumfungulia Aminata mlango.



    “Mwone kwanza.” Alijibu Aminata.



    “Mapambano sasa yameanza. Tusirudi nyumbani.” John alisema huku akiwasha gari tayari kuwafuata wengine eneo la Kambi ya Fisi.



    “Hapana mpenzi, tukamcheki kwanza mlinzi imekuaje, atakuwa amefariki au yu hai.” Aminata alimsihi John warudi kwanza nyumbani kwa ajili ya kucheki hali ya mlinzi ambaye alikuwa amelala chini baada ya kupigwa risasi ya kifuani.



    Walifika na kukuta umati wa watu wakiwa wameuzunguka mwili wa marehemu. Ulikuwa umefunikwa na polisi walikuwa wameshafika baada ya majirani kupiga simu na kutoa taarifa juu ya mauaji na baadaye magari mawili kutoka kwa kasi yakifukuzana. John alisikitika sana.



    Walifanya mipango na kuhakikisha askari wao anazikwa ndipo waendelee na mapambano. Alijua lazima wale watu wameshapata taarifa kuhusiana na kufa kwa watu wao wengine na hivyo mara tu baada ya mazishi ya yule askari, John na Aminata waliamua kuendelea kuwafatilia wale watu wa Mosses.



    “John, tuwawahi kabla hawajatuwahi, kwa sasa hawajui tulipo. Tumeanza na hao watatu. Tuhakikishe tunawamaliza wote,” Aminata alisema baada ya kuona mambo yamekwisha tulia.



    “Itabidi tusilale kwenye hii nyumba Aminata wala kwako tusiende, huenda wameshajua niko na wewe,” John alimsihi Aminata wasiendelee kuishi hapo badala yake wahamie hata hotelini ili wafanikishe kwanza mipango yao kisha watarudi.



    Walifunga nyumba na kisha kuondoka jioni na kwenda hotelini kuishi huko, waliamua wawe wanabadili hoteli mara kwa mara ili wasijulikane wako hoteli gani. Huko walikua wakifika usiku tu.



    Mchana kutwa walishinda barabarani wakiangalia baadhi ya watu wa Mosses ili kuwamaliza. Waliangalia pia njia ambayo wataitumia kuvamia ngome yao iliyokuwa kambi ya Fisi.



    “Antony,” Aminata alisema baada ya kumkumbuka Antony.



    “Amekuwa kimya sana huko Nairobi,” alisem John.

    Anarudi lini sasa?”



    “Alisema anarudi kesho. Nadhani tumtaarifu juu ya wapi tulipo ili asije akaenda Njiro.“



    “Kweli John,” John alitoa simu yake na kumpigia Antony.



    “Nadhani kila kitu kina kwenda swa. Mi nakuja kesho.”



    “Sawa lakini usifike nyumbani, ukishuka uwanja wa ndege nitakujulisha wapi utufuate.”



    “Sawa kaka, nitakufahamisha nikifika.”



    Antony alikuwa ndo anajitayarisha kwa ajili ya safari ya kurudi Tanzania.





    *****

    Mambo mawili kwa wakati mmoja. Huku mapambano huku mapenzi. Vyote vilimtawala Aminata. Hakuweza kutul;ia tu juu ya mwili wa John. Safari hii alivuka mipaka iliyomfanya John astaajabu. Hakuwa na la kujibu wala kuongea pale alipomwona Aminata akichojua nguo moja baada ya nyingine na kubakiwa na nguo za ndani. Mawazo ya kupambana aliyokuwa nayo yalikatika na kujikuta akimvamia Aminata kama vile Aminata alivyokuwa tayari kumpokea.



    Safari hii walifikia katika hoteli ya 7’7 iliyoko katikati ya mji wa Arusha. Walijivinjari taratibu kwa kipindi hicho amabacho walikuwa wakijiandaa kwenda kuendeleza tena mapambano.

    Mikono yao haikutulia katika kushambuliana wenyewe pale katika mbao za futi sita kila upande. Ofisa alizidisha utundu wake na kuhakikisha mtuhumiwa wake katika penzi hashindi kesi.



    Alimpagawisha John kwa kila aina ya vimbwenga ili mradi aiweke safi nafsi yake na kukata kiu aliyokuwa nayo kwa kipindi kirefu.



    Mpaka asubuhi ambapo walipata wazo. Wazo la kwenda Mererani. Hiyo ni baada ya kuwakosa pale Kambi ya Fisi na baada ya kujulishwa na Mbago ya kwamba mgodi ulikuwa ameshaanza kufanya kazi chini ya usimamizi wa mmiliki mwingine aitwaye Mosses ndula.



    Jambo hilo liliwashangaza sana na hivyo John aliona pasipokuchelewa ni bora wawafuate kulekule kwani endapo wangewashirikisha polisi hakuna ambacho kingefanyika. Walijiamini kwa kuwa hati miliki ya ukweli wanayo wao na kujua ya kwamba lazima ile aliyomiliki nayo Mosses Ndula ni feki.



    ****



    Ilipita wiki moja pasipo kufanya chochote. John na Aminata walikuwa bado wakiendelea kukaa hotelini. Huko walikula raha zote wakisubiri mambo yatulie ili Mosses Ndula asijue kama kuna mpango wa kufanya uvamizi. Pia Antony alichelewa kurudi na hivyo walikuwa wakimsubiri arudi ndipo waende pamoja.



    Ni baada ya kufahamishwa na Mbago ndipo walipoaamua kuwafata huko huko waliko na hivyo ilibidi zoezi la kufanya uvamizi kusimama baada ya kuwakosa eneo la Kambi ya fisi ambapo Mosses Ndula na genge lake walikimbia na kutelekeza kambi yao.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya kuzipata habari zile, John na Aminata waliondoka baada ya siku mbili. Waliamua kutangulia na kumwacha Antony. John alimweleza Aminata ya kwamba wangefika kwanza kisha wampigie simu na wamwelekeze ni wapi walipo.



    Alfajiri ya saa kumi na moja John na Aminata walikuwa njiani kuelekea Mji mdogo wa Mererani. Walitaka kwanza kujua hali ya mgodi. Walikwenda taratibu pasipo kuwa na haraka. Walifika ni kuchukua chumba katika moja ya nyumba za kulala wageni iliyokuwa maarufu na iliyotumiwa zaidi na wafanyabiashara wakubwa waliokuwa wakifika Mererani kwa ajili ya kununua madini au hata kukagua migodi yao.





    Ni usiku huohuo ambapo Aminata alijihisi mabadiliko. Mabadiliko ya kimwili na hivyo alijua bado yupo kazini na asingeweza kumwambia John kwani hajui ambalo angeamua na kushindwa kuendelea na kazi. Siku hiyo Aminata aliimwonyesha John hisia zake zote na kuficha hali yake hata pale alipohisi kichefuchefu.



    Mara kwa mara alimtoroka John ili asimgundue. Alirudi na kuendelea na raha zao na mipango yao ya uvamizi. Alihakkisha John hahisi jambo lolote kwake.



    Asubuhi waliamua kutoka kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa eneo zima la mgodi. John alikuwa amesahau sehemu nyingi na hivyo aliishia kuangaza tu macho. Waliamua kwenda moja kwa moja wakifuata njia ambayo aliikumbuka.



    Walifika na kushangaa mabadiliko makubwa ikiwemo kuzungushiwa kwa uzio mzito wa umeme ili kudhibiti watu kuingia. Ndiyo hukuhuku Mosses Ndula na genge lake waliweka makazi yao. Walijenga nyumba ndogondogo kwa ajili ya kambi yao. Uzio huo ulilindwa na walinzi waliokuwa wakisimama imara mlangoni na wengine walikuwa juu ya vibanda maalumu vya kuangalizia wezi na watu wanaokuja na kuondoka. John na Aminata waliwafuata baadhi ya wakazi wa huko na kuulizia kinachoendelea.



    “Samahani sana ndugu, habari yako,” walimsalimia mkazi mmoja aliyekuwa akizungukazunguka maeneo hayo.



    “Nzuri tu,” aliitikia salamu yule kijana.



    “Siye hatufahamu nani ameingia hapa maana hata sisi tuna hofu kubwa ingawa hawajawahi kutudhuru wala kutufanyia fujo. Hata mkuu wao anaonekana ni mtu mwema sana,” alikuwa ni mmoja wa wakazi wa mji huo ambaye alielezea ujio wa Mosses Ndula na kikosi chake ambao waliweka kambi hapo bila ya kuwadhuru wakazi wa eneo hilo.



    “Umeshazunguka na kuona mwisho wa uzio huu uliozungushiwa?” Aminata alimuuliza yule mkazi.



    “Njooni niwapeleke,” yule mkazi aliwachukua na kuwazungusha kila kona ili wauone uzio huo ulikopita na ulikoishia.



    Aliwaeleza ni namna gani wanapalinda pale na mtu yeyote akitaka kuingia lazima akaguliwe na kwamba unalindwa na askari wanaojiamini sana.



    Ilikuwa saa tatu asubuhi…pilikapilika katika eneo lile hazikuwepo kama awali. Ulinzi ulifanya watu kulikimbia lle eneo kwani lililindwa sana. baadhi ya viongozi wa serikalini walifika pale wakiongozana na Mosses Ndula.



    Viongozi hao ni wale waliojihusisha naye katika biashara za dawa za kulevya kabla hajaacha na kuamua kufanya umafia na kumiliki mgodi.



    Walifanikiwa kusimama katika moja ya nyumba ambazo zilikuwa karibu na uzio ule na uanza kuangalia ukubwa wa uzio. John alikuwa amemwona moja ya walinzi wakija. Aliwashtua Aminata na yule kijana nay eye kuzunguka kwa nyuma.



    Yule askari alifika na kuwaweka Aminata na yule kijana chini ya ulinzi lakini kabla hawajatii amri ile John alikuwa ameshafika na kumpiga kabala moja iliyomfanya ashindwe kujigeuza. Haraka Aminata alimnyang’anya silaha yake na kumficha kule ndani yule askari.



    Walimhoji juu ya Mosses na kuhusu mgodi. Yule askari alilazimishwa hadi akasema. Aminata alichukua kiwambo cha bastola yake na kukifunga kisha alimpiga risasi yule askari wa kuhofia akipata nafasi ataenda kuwaelezea wakuu wake.



    Waliamua kuondoka katika ile nyumba na kwenda pamoja na yule kijana hadi hotele waliyokuwa wakikaa. Walipanga waende tena jioni ili wapaone kwani kwenye giza wasingeweza kuonekana vizuri. Yule kijana alikuwa bado hajawaelewa John na Aminata pamoja na kwmba liongozana nao. Jua lilizama na wote waliamua kwenda tena.



    Ilikuwa ni saa mbili na nusu jioni. John, Aminata pamoja na yule kijana walianza kuzunguka uzio ule. Hakuna aliyemweleza yule kijana zaidi ya kumwomba tu waonyeshe kama alivyowaambia. Walikuwa bado wakizunguka ule uzio. Wao walichotaka kujua ni jinsi gani watakuja kuwavamia.



    Waliangaza kila walipopitishwa ili wajue wataingiaje. Hakuna aliyewaona kwani giza lilikuwa limekuwa kali kiasi katika eneo hilo. Yule mkazi aliwashangaa ni kwa nini wanapafatilia kiasi hicho wakati hawataweza kuingia kwani ni hatari.



    “Kwani kuna nini kati yenu na hawa jamaa?” alihoji yule mkazi.



    “Sikiliza….. hiyo siyo kazi yako…tunachotaka ni kuujua huu mgodi uzio wake unaishia wapi,” John alidakia kwa kumtaka yule mkazi asiingilie lakini ghafla Aminata aliingilia.



    “Hapana John, huyu jamaa anatusaidia. Inapasa tumweleze kwani bila yeye tusingeweza kufika hapa.”



    “Okey… ni kwamba huu mgodi ni mali yetu na hati tunayo….kwanza jina lako nani?” John alikatisha aliyokuwa akiyaelezea kuhusu mgodi na kutaka kujua jina la yule mkazi.



    “Mi naitwa, Francis. Ni mkazi wa huku na kuna kipindi nilishawahi kufanya kazi katika huu mgodi. Nakumbuka kipindi hicho ulikuwa ukimilikiwa na mzee mmoja ‘bonge’ hivi alikuwa akiitwa Amigolas. Yule mzee ndiye aliyetuajiri sisi na kipindi hicho ndiyo huu mgodi ulikuwa ukianza kukua kwani kabla ulikuwa hautambuliwi.



    Nasikia kwa sasa ni marehemu na kabla ya kifo chake aliamua kuuuza huu mgodi, alikuja akatutoa wachimbaji wote na kuamua kuajiri wachimbaji aliyewataka yeye na nadhani huyu jamaa ndiye aliyeununua. Inaonekana pia ni mtu mkubwa sana.



    “Hapana,” John alimkatisha…. “Huu mgodi haujauzwa. Mzee unayemsema ni baba yangu. Hakuuza mgodi huu ila umechukuliwa kwa nguvu na ndiyo chanzo cha kifo cha mzee wangu. Hivyo nataka kuurudisha huu mgodi kwani hata hati halali ninayo na hati wanayoitumia ni feki.



    Hapa tulipo tunataka tuwaangamize wote na kumaliza huu mtandao wao. Kama utaona hatari usijihusishe maana hapa haponi mtu.” John aliongea kwa hasira akimtaka Francis azingatie aliyosikia na awe tayari kwa lolote kama alivyoona kwa yule askari ambaye walimuua jana yake.



    Ghafla simu ya John iliita. Ilikuwa ni simu ya Antony. John aliwahi kuizima mlio ili wasije wakasikiwa. Aliipokea na kumtaarifu Antony kwamba atampigia baada ya dakika tano.

    Baada ya dakika tano, John, Aminata pamoja na Francis walikuwa wameshafika hotelini. John alimpigia simu Antony na kuongea naye.



    “Vipi kaka, uko poa?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Niko poa kaka, mko wapi?



    “Tuko Mererani. uje maana mgodi umeshavamiwa. Jamaa ameuchukua kweli. Njoo tuanze kazi mkuu.”



    “Dah, haiwezekani. Nakuja.”



    Antony alichukua gari yake na kuanza safari ya kuelekea Mererani kuungana na John na Aminata. Alijipanga vizuri kuhakikisha kweli anakwenda kwa kazi moja tu, kukomboa mali za baba yao.





    *****

    USALAMA katika ngome ya Mosses uliwatisha kidogo kina John. Walifika na gari karibu na uzio wa mgodi ule na kuangalia kwa mbali kidogo shughuli zilizokuw zikiendelea kule ndani.



    Mosses Ndula alifanikiwa kuweka ulinzi mkali. Si polisi wala mtu yeyote aliyeruhusiwa kuingia mle ndani. Hata viongozi nwa serikali na wateja wake wa madini waliofika pale walikaguliwa ipasavyo kuhakikisha hawaingii wala kutoka na chochote. Hakuamini mtu yeyote kwani alijua alifanyalo.



    Hata Mosses Ndula alikuwa akitoka kwa msafara wa gari tano hadi sita zikiwa zimebeba walinzi wake pamoja na wasaidizi wake. Gari zote zilikuwa nyeusi zenye vioo vyeusi ambapo ilikuwa ni nadra sana kwa mtu wa nje kuchungulia ndani. Pia mtu asingejua ni gari gani alilopanda Mosses Ndula kwani magari yote yalifanana.



    Hakupenda kujulikana japo alijulikana kwa taarifa zake tu kama mmiliki. Hakuna aliyemfahamu kwa sura. Alikuwa si mtu wa kukaa eneo moja. Aliwatumia zaidi wasaidizi wake. Ni katika dili kubwa tu ndipo yeye angetokea na kujihusisha nazo. Dili alizocheza na watu wakubwa ambazo zilihitaji awepo.



    Ni mara chache sana John na Aminata waliweza kuuona msafara huo ukipita wakati wa jioni. Hawakuweza kufanya chochote. Francis aliwaelezea juu ya mambo yanayoendelea.



    “Mkiona hivyo, mjue mida hii wanaenda sehemu. Na leo ni wiki endi wanaenda hoteli za kifahari na kumbi za starehe. Mosses alipenda sana kustarehe. Alifanya hivyo pasipo kujulikana.



    “Huu ndo mwanya wa kuingia ndani na kuwashambulia watakaobakia huko. Tuanzeni leoleo hakuna kusubiria tena,” Aminata alisema huku akiyaangalia yale magari ya Mosses yaliyokuwa kwenye msafara.



    Francis alikuwa ni kijana na hivyo alijua mambo mengi yaliyoendelea kwani tangu kuingia kwao alishuhudia ikiwa ni pamoja na kipindi walipoondolewa na kukaa bila kazi. Alikubali kushirikiana nao katika kazi.



    “Kwa kweli nna hamu ya kurudi kazini, nitasaidiana na nyie nihakikishe tunawaondoa hawa jamaa,” Francis aliwaambia John na Aminata.



    “Safi sana Francis. Na tunakuahidi makubwa endapo tutafanikisha huu mpango,” John alimwambia Francis ambaye alionekana kufurahia dili hilo.



    “Uwe makini lakini kwa sababu wanatumia silaha kali sana,” Aminata alimsihi Francis aliyejitolea kuwasaidia kuukomboa mgodi. Aliomba silaha ambayo itamsaidia.



    “Hutaweza kutumia silaha wewe, nadhani utafuata tu maelekezo. Pia muda wa kukufundisha hakuna,” Aminata alimwambia Francis.

    “Naweza dada angu. Nilishapitiaga jeshi.”



    “Acha utani,” John ambaye alikuwa akitazama eneo la uzio wa mgodi, alisema huku akionyesha kwamba hataki utani.



    “Kweli John. Naweza na nakuhakikishia nilimaliza mafunzo sema taabu za kule zilinishinda. Ila niko fiti sana.”



    John na Aminata walionyesha kupuuzia. John aliwasiliana na Antony ambaye alikuwa ameshawasili mjini Mererani. Alitaka kwenda hadi walipo.



    “Tayari tupo karibu na uzio. Na wameondoka hivyo tunataka kuingia.”



    “Basi nakuja hapo hapo mlipo tujue tutaingiaje.”



    Baada ya dakika kumi na tano, Alifika hadi walipokuwepo John na Aminata. Walikuwa pembeni ya hoteli ya kawaida ambayo ilikuwa ikitazamana kwa mbali kidogo na lango la kuingilia mgodini. Tayari walikuwa wametimia akiwa ameongezeka Francis ambaye alitambulishwa kwa Antony.



    "Karibu Antony,” alisema Aminata ambaye alikuwa akimwangalia Antony aliyekuwa ameshika bastola yake huku akiisafisha kwa kitambaa. Kutokana na baridi iliyokjuwepo mjini Mererani, wote walikuwa wamevalia makoti ya kuwakinga nayo.



    “Kazi inaanza sasa. Kama tulivyosema, Antony atabakia nje kwanza afu mi na John tutaingia pamoja na Francis. Francis atafika langoni na kuwahadaa kwa kuzungumza na askari kisha mi na John tutakata nyaya na kuingia ndani kisha wakimkatalia Francis kuingia atarudi na kutufata sehemu tuliyoingilia. Sawa?”



    “Nimewaza jambo,” Antony alisema.



    “Jambo gani tena?” Aminata aliuliza huku akiona kwamba kuna jambo linguine litaingilia uamuzi wao.



    “Yule jamaa aliyekuja home kutueleza kuhusu mgodi kuuzwa na aliyewajulisha kuwa jamaa wameanza kazi. Kwani si anafanya nay eye huku?”



    “Dah… kweli. Aminata,” aliita John aliyetaka kumweleza jambo Aminata.



    “Sema.”



    “Kwa nini hatukuwaza jambo kama hilo. Ingewezekana angetusaidia katika kujua kinachoendelea huko ndani ikiwa ni kuwaeleza na wenzake juu ya mpango wetu ili wawe tayari na tuingiapo waweze kutusaidia.”



    “Kweli, sasa kwa sasa tunaingia au?”



    “Subiri niwasiliane naye kama anapatikana tuweze kufanya naye hii ishu,” John alisema huku akitoa simu yake na kutafuta jina la Mbago. Alimpigia simu.



    Simu ya Mmbago iliita bila ya kupokewa. John alipiga tena na tena. Simu haikupokewa.



    “Ok, tusichoshane, nimepiga sana hapokei. Sijui kwamba ndo hawaruhusiwi simu huko?”



    “Kweli, ndo mlikuwa mnampigia mtu wa huko ndani?”

    “Ndiyo, inamaana hawaruhusiwi mawasiliano.”



    “Ndiyo hawaruhusiwi. Wanaacha simu zao ndo waingie. Pengine hakuzima yeye ila wanazima na kuingia wakitoka ndo wanazichukua. Na mara nyingi hutoka saa tano usiku,” Francis aliwaelezea kuhusu t5aratibu za mgodi ule. Yeye alifahamu kwani wapo rafiki zake ambao huwa anawatafuta na hawapati.



    Hivyo hugundua ya kwamba watakuwa wamezuiliwa simu. Ni hadi pale alipowauliza ndipo walipomwambia ya kwamba hawawezi kutumia simu hadi pale wanapotoka nje ya mgodi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa basi, haina haja ya kupoteza muda wale jamaa wakarudi tukashindwa kazi yetu.”



    “Ndiyo, tusichelewe basi. Tuanzeni mara moja kabla hawajarudi.”

    Mosses Ndula na walinzi wake walikuwa wametoka. Huo ulikuwa ni mwanya kwa kina John kuutumia kuingia ndani na kuwasubiria huko.





    ******

    Alikuwa ni Francis wa kwanza kutoka na kuelekea moja kwa moja hadi katika lango kuu la kuingilia mgodini. Alifika na kubonyeza kengele ambapo alifunguliwa na walinzi. Aliruhusiwa aingia ndani hadi sehemu ya mapokezi na kuanza kuhojiwa. Hakuonyesha wasiwasi wowote zaidi ya kuangalia kwa makini sehemu ambayo John na Aminata walikuwa wakipitia bila kuonwa na askari.



    Wakati huo John na Aminata walikuwa wameshatoka na kwenda moja kwa moja hadi kwenye uzio wakiwa wamesheheni kila aina ya silaha waliyoona itawafaa kwa mapambano. Francis hakwenda na silaha.



    “Umefuata nini hapa na unatoka wapi?”



    “Natokea mjini, nimesikia kuna kampuni mpya ya uchimbaji madini imeanzishwa hivyo nimekuja kuomba kazi ya kuchimba,” Francis alianza kuelezea huku akitazama kama John na Aminata wanaendelea kutafuta njia ya kuingilia.



    “Kazi hapa hakuna, wachimbaji wapo wengi, na kwa nini unakuja jioni yote hii karibia usiku unaingia? Ondoka haraka hapa. Uje kesho asubuhi,” mmoja wa wale askari alimfokea Francis ambaye taratibu alianza kurudi nyuma kuelekea mlango ulipo ili atoke aende zake.



    Francis hakuonyesha woga. Aliwaona kina John wakiwa wanaingia na yeye aliamua kutoka kiustaarabu ili wale askari wasije wakashtukiwa.



    John na Aminata walikuwa wamejificha nyuma ya gari kubwa la mizigo. Hakuna aliyewaona. Walishika silaha zao kikamilifu na kuanza kuelekea mahala nyumba zao zilipo.



    Waliwakuta askari wawili nje. Waliwafyatulia risasi. Walitumia bastola zao walizokuwa wamefunga viwambo ili sauti isisikike. Kisha waliingia kwenye zile nyumba na kuanza kuwashambulia askari waliokuwemo ndani.



    Walitoka na kuelekea katika nyumba nyingine wakifanya hivyohivyo. Askari wa lango la kuingilia hawakujua kilichoendelea kwani walikuwa wakiua bila ya watu kuwaona. Sasa walifikia eneo la machimbo. Waliwakuta askari wane wakiwa wanawaamrisha wachimbaji wakae chini.



    Mmoja wa wachimbaji wale alikuwa Mbago ambaye aliwaona kina John na Aminata. Aminata na John waliwavizi wale askari kwa nyuma na kuwapiga risasi na kuwaua.



    Baadhi ya askari waliona tukio lile na hivyo walikimbilia eneo lile ili kuwashambulia kina John. Mbago na wenzake walikuwa wameshachukua zile bunduki ambazo zilikuwa zikitumiwa na wale askari na kuanza kuwashambulia wale askari waliokuwa wakija.

    John na Aminata walitoka na kuwaacha pale wakiwamaliza.



    “Asibaki hata mmoja….ueni wote,” Aminata alisema kwa sauti kuwaambia wale wachimbaji baada ya kuona sasa mapambano yameanza. Nao walifanya hivyo kwani walichoka na dhuluma na mateso ya askari wale. Nia yao ilikuwa kuwamaliza na pia kumshikilia mkuu wao Mosses Ndula.





    *****

    Risasi mfululizo zilirushwa na kina John na Aminata kabla ya kuondoka. Walikuwa wakiwazuia wale askari wa Mosses kuwafikia kabla wale wachimbaji hawajasogea na kukaa sawa.

    Mbago na wachimbaji wenzake waliendelea kuwamiminia risasi wale askari wa Mosses ambao waliongezeka. Risasi zilirindima kiasi cha kuwafanya wakazi wa Mererani kukimbiakimbia wakihofia maisha yao.



    Aminata na John walikuwa wakiwafuata askari wa lango kuu. Walikuwa wote wameshauliwa. Hawakuona mtu yeyote zaidi ya milio ya risasi iliyosikika kutoka kwa wachimbaji waliokuwa wakiwashambulia askari wa Mosses.



    “Twendeni huku,” Antony ambaye alikuwa na Francis alitoka katika moja ya ofisi zilizokuwa karibu na lango kuu na kuwashtua kina John na Aminata ambao walikuwa amesimama kwa kujihami wakiangaza huku na kule kuangalia kama kuna adui anakuja.



    Antony aliwaelekeza John na Aminata wawafuate walikokua wanakwenda baada ya kuona taa za magari zikiwa zinakuja kuelekea lango kuu.



    “Tumeshawamaliza. Nimeona magari yanakuja kule. Njooni huku,” Antony alisema huku akizunguka nyuma ya gari kubwa la kubebea mchanga. Walisimama yeye pamoja na Francis huku kina Aminata John wakisimama ghafla.



    “Hapana, tusikae wote upande mmoja. Nyie nendeni na sisi twende huku,” Aminata aliamua kuwagawa na yeye na John walirudi kule ziliko ofisi za Mosses na kuwaacha Antony na Francis wakaenda kujificha nyuma ya magari huku wakiwasubiri Mosses na wenzake warudi. Hakutaka kumwachia John.



    Antony alimwangalia na kutabasamu. Aminata naye alitabasamu kama vile kila mmoja alielewa jambo. John hakuwa na la kusema. Alibaki akiangaza huku na kule. Aliyaona magari na hivyo alimshika mkono Aminata na kwenda kujificha kabla hawajaonwa.



    Magari yalikuwa yamerudi yote. Hawakuona mtu katika lango kuu zaidi ya miili ya wafu ambao ilikuwa imetapakaa damu. Askari waliokuwa wameongozana na Mosses waliteremka haraka kwenye gari na kuanza kuangalia huku na huko. Hawakuona lolote zaidi ya miili ya askari wenzao.



    Ghafla John aliwatokea na kuwamiminia risasi ambazo ziliwashtua Mosses na wenzake.



    “Wafuateni,” alifoka Mosses akiwaamuru askari waliobaki wawafuate wenzao. Huko yaliwakuta yaliyowakuta wenzao. Yeye pamoja na walinzi wenzake wligeuza gari na kuanza kuondoka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Antony alikutana na Mbago pamoja na wachimbaji wengine. Walivamia migodini na kuwatoa watu wote na kuhakikisha hakuna askari yeyote wa Mosses aliyesalia. Antonuy alitaka kuwajulisha juu ya kilichokuwa kikiendelea. Usiku huohuo ambapo hali ya mji wa Mererani haukuwa tena shwari ilisikika tu milio ya risasi.



    Msafara ulivurugika. hali ilizidi kuwa mbaya zaidi. Mashambulizi sasa yalihamia barabarani. Mosses na watu wake waligeuza na kuanza kukimbia wakielekea mjini. John na Aminata waliwaona na hivyo hawakuwaachia.



    “Wanaondoka. Tusiwaache,” John alisema huku akilikimbilia moja ya magari yaliyokuwa yamebaki. Alifyetua risasi iliyompata dereva na kumlenga ya kichwani. Aminata naye alifyatua na kuwalenga walinzi wengine wa Mosses. Hapo sasa wakawa wamepata gari. Mosses na mbashala pamoja na walinzi wawili na dereva walikuwa wakikimbia sasa. Waliwaacha umbali mdogo na hivyo walijua si rahisi wawafikie.



    Hakuna aliyejua aliyeamua kuvamia na kufanya mashambulizi katika mgodi wako. Mosses alikuwa amechanganyikiwa kwani hakuwa na taarifa ya kuwapo kwa John na Antony, mpacha wa mzee Amigolas.



    “Tembea na spidi zote,” alifoka kwa nguvu kumkaripia dereva aongeze kasi. Alizidi kuwaza.



    “Mbashala…. Nani wale? Unawajua?” alimuuliza Mbashala ambaye na yeye hakufahamu lolote.



    “Au ni serikali wamewatuma majasusi wao kufanya huu unyama. Nitaongea na kiongozi.”



    “Kiongozi gani?”



    “Mkuu wangu.. Haiwezekani hili. Mambo yanaharibika sasa…. Sijui ni kina nani hawa wanaharibu mipango yangu,” alisema Mosses ambaye alionekana kukasirika.



    John na Aminata walizidi kuwakaribia kwani Mosses alijua hakuna aliyekuwa akiwafuata nyuma. Dakika tano baadaye mlio wa risasi iliyofyetuliwa na Aminata ulilenga gari na kuwashtua kina Mosses.



    “Endesha, tuko kwenye hatari,” alifoka Mosses akimwamuru dereva wake. Dereva alipatwa na woga. Alitamani aruke aache gari lenyewe kwa kuhofia maisha yake. Alijua hila zote za Mosses zimefika mwisho na huo pia unaweza ukawa mwisho wake.



    Hakuwa na la kufanya. Kuona vile dereva alizidi kukimbiza gari. Alitafuta njia ambazo zilikuwa na kona nyingi ili kuwapoteza lakini hawakuwaacha mbali.



    Yule dereva aliogopa sana kwani Mosses alikuwa ameshikilia bastola yake na hivyo hakuweza kusimamisha gari ili kukimbia.

    Tayari walikuwa wameshaingia barabara kuu ya Moshi Arusha.





    *****

    Antony alifanikiwa kuipata ile hati ambayo alikuwa nayo Mosses Ndula. Alikuwa ameihifadhi ndani ya sanduku kulekule mgodini katika ofisi yake ambapo walifanya upekuzi pamoja na wale wachimbaji. Aliichukua kama ushahidi baada ya kupata taarifa juu ya kukamatwa kwake. Antony aliwaeleza wale wachimbaji kila kitu. Aliwataka sasa watulie.



    “Polisi walipata taarifa juu ya tukio hilo. Walituma baadhi ya askari kwenda kwa ajili ya kuangalia na kusaidia kule mgodini. Polisi walikuwa tayari wamefika katika mgodi huo na kuwaweka chini ya ulinzi wachimbaji wote pamoja na Antony.

    Polisi wengine walikuwa wakiwafuata John na Aminata waliokuwa wakiwakimbiza Mosses na watu wake.



    “Wekeni silaha zenu chini,” polisi mmoja alitoa amri. Antony aliwasihi wachimbaji waliokuwa na silaha waweke silaha chini na kuwasikiliza wale polisi.



    Mosses na watu wake walikuwa wakielekea eneo la Maji ya Chai. John na Aminata hawakuwa mbali nao. John alijitahidi sana kuwafikia. Walianza kuwarushia risasi ambapo na wao walikuwa wakizijibu kwa nyuma. Mosses alijua mambo yameshaharibika na hivyo aliamuru gari lisimamishwe ili waweze kuwashambulia kwa risasi na kuwamaliza kina John.



    Haikuwa rahisi kwani wakati wanarushiana risasi Aminata alifanikiwa kuwaua walinzi wawili. Alikuwa ni mlinzi pamoja na msaidizi wa Mosses ‘Mbashala’ na kufanya wabakie watatu. Dereva alikuwa tayari amekimbia na kuwaacha Mosses na walinzi wake wawili wakiendelea kurushiana Risasi.



    Polisi walifanikiwa kufika eneo la Maji ya chai na kukuta bado mapambano yakiendelea. Walisimama na kutoka nje ya magari yao na kuanza kuwafyetulia risasi kina Mosses ambao nao walijibu mapigo.



    “Acheni,’ Mosses aliwaamuru watu wake kuacha kushambulia kwani aliona ameshazidiwa na hivyo wangeuliwa. Hakuonekana mwenye kukata tama. Alijua atashinda huko mbele. Aliamua kuwazuia wenzake ambao mmoja wao alikuwa akivuja damu baada ya risasi ya John kumpata ya begani.



    Mosses Ndula na wenzake hawakuwa na ujanja tena zaidi ya kutii na kuweka silaha chini na kunyanyua mikono juu. John na Aminata walianza kusogea kuwafuata polisi waliko ili waweze kujitambulisha.



    “Heshima yako mkuu,” Polisi mmoja aliyekuwa amewafuata Aminata na John alitoa saluti kwa Aminata. Aminata alikuwa bado amewaelekezea Mosses na watu wake bastola hadi walipoweka silaha chini baada ya kugeuka na kuwaona polisi nao wakiwa wamewaelekezea mitutu ya bunduki na hivyo wasiweze kukimbia. Polisi waliwashangaa Mosses na watu wake wawili.



    “Huyu jamaa aliwahi kuja pale kituoni na wanasheria wake,” polisi mmoja alisema huku akistaajabu kulikoni mtu mkubwa vile akimbizwe na gari kama mhalifu.



    “Nyamaza… kila kitu kitajulikana huko huko. Waliwachukua Mosses Ndula pamoja na wenzake hadi Kituo cha Polisi. Mosses hakuonekana kutishika wala kujali. Dereva alikimbilia porini na hivyo hakuweza kutafutwa wala kujulikana.



    Aminata alimfuata kiongozi wa wale polisi na kumsihi wasikubali akatoroka hadi pale watakapofika mjini Arusha kesho yake.

    “Sawa mkuu,” tutawafikisha wote kama amri yako ilivyosema.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    KINA JOHN WANAFANIKIWA KUUVAMIA MGODI. WANASHAMBULUIA NA KUUA ASKARI WOTE.



    MOSSES ANAFANIKIWA KUKIMBIA PAMOJA NA WATU WAKE LAKINI NAYE ANATIWA NGUVUNI NA POLISI BAADA YA KUFUKUZWA NA JOHN NA AMINATA.



    SAFARI YA KUMPELEKA KITUONI MJINI ARUSHA NDIYO INAYOFUATIA.



    JE POLISI WATAFANIKIWA KUWAPELEKA KITUONI AU MOSSES KUTOROKA



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog