Search This Blog

Sunday 22 May 2022

MKONO WA JASUSI - 5

 







    Simulizi : Mkono Wa Jasusi

    Sehemu Ya Tano (5)





    KLINIKI YA KWAZULU NATAL – DURBAN

    LERETI KHUMALO ALIZINDUKA na kurudiwa na fahamu zake, alishangaa kuona jopo kubwa la madaktari na wauguzi wakiwa wamezunguka kitanda chake, aliwatazama bila kujua nini kinaendelea.

    “Dah! Asante Mungu,” Daktari wake ambaye daima ndiye anayemtibia alishukuru Mungua na kila mmoja mle ndani alikuwa akimpongeza.

    Mara baada ya Lereti kupata maswaibu yale hakukuwa na jinsi, daktari wake ambaye anafanya kazi katika kliniki hiyo akishikirikiana na madaktari kadhaa ilibisi wasimamishe shughuli nyingine na kuhakikisha wanarudisha maisha ya Lereti. Kwa kutumia dawa aina ya Methylethylglutarimide waliweza kufifisha nguvu ya dawa kali ya barbitulate paralytic na kumrejesha Lereti duniani.

    Akaendelea kuwatazama wote waliomzunguka, hakujua nini kimetokea.

    “Pumzika Lereti, hali yako ilibadilika ghafla sana,” Daktari wake alimwambia.

    “Hapana kuna daktari wenu alikuja na kuweka dawa Fulani kwenye drip mara nikaanza kuhisi usingizi na viungo v yangu kuwa havina nguvu, kutoka hapo sikujua kinachoendelea, yuko wapi Cinderella?” Lereti alieleza anachokumbuka na mwisho akmwulizia mfanyakazi wake anayempenda.

    “Lereti, Cinderella hatunaye duniani,” alijibiwa na hapo akaanza kulia kwa uchungu.

    “Aliyekuwekea ile dawa hakuwa daktari wetu Lereti, walidhamiria kukuua, lakini Mungu mkubwa umepona,” walizidi kumweleza na wakati huo bado Lereti alilia kwa uchungu sana. Hali yake ilipokuwa nazuri kwa siku hiyo alihamishwa chumba na kupelekwa chumba kingine ambacho alikaa na mwuguzi muda wote, hakuruhusiwa mtu kuingia hata mlinzi wake mpaka apewe ruhusa na daktari mkuu.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Lini nitaondoka humu ndani? Nina kazi ya kukamilisha huko nje,” alimwuliza daktari wake pindi tu alipokuja kumtembelea jioni ile.

    “Kwa hali ikiwa hivi, kesho utaruhusiwa kutoka, usiwe na wasiwasi,” akajibiwa na kisha Lereti akajilaza vyema kitandani akimwomboleza Cinderella. Kwa mapendo aliyokuwa nayo aliomba familia yake isifanye maazishi mpaka atakapotoka hospitalini.



    §§§§§

    Kama kawaida, kamanda Amata, akahifadhi ile hard disk kwenye safe box ndani ya gari yake kisha akaondoka eneo lile. Maisha ya Amata sasa yalikuwa hatarini zaidi kwani alikuwa akisakwa kila uchochoro na alijua wazi kuwa akirudi hotelini au kuingia mgahawa wowote basi ingekuwa ni hatari kwake. Aliamua kutoka nje ya mji kabisa, moja kwa moja akaelekea kwa Yule babu ambako alimuokoa Jesca, akaegesha gari mahala salama na kuteremka, mkononi akaibeba ile hard disk na kuingia katika mitaa hiyo ya watu weusi.

    Moja kwa moja akakuta bar moja kubwa iliyokuwa bado wazi, akaingia ndani. Mziki mkubwa ulikuwa ukipigwa, na vijana waliokwishapata kinywaji walikuwa wakicheza kurandana na midundo hiyo. Kamanda Amata akajiegesha katika moja ya viti virefu vya kaunta, akaagiza kinywaji na kuletewa, akanywa polepole huku akitazama vijana wale waliokuwa wakicheza kwa ufundi kabisa wimbo wa Chicco Twala, unaokwenda kwa jina la Money Pesa.

    Mara ule muziki ukazimwa na Yule mwanadada aliyekuwa pale kaunta akaongeza sauti ya luninga; ilikuwa ni taarifa ya dharula iliyoonesha jumba la kifahali lililokuwa likiteketea kwa moto.

    “Wacha waungue tu, hawana mana hao boers,” aliskika kijana mmoja akibwata kipombepombe.

    “Wewe weka muziki huko ni shayia time,” mwingine alidakia. Mara mdundo mkubwa ukaendelea, mara hii uliwekwa muziki wa Chaka Chaka, Im burning up na wale vijana wakaanza tena kulisakata ngoma.

    “Hey Man, ninunulie kinywaji kwanza ndio nikukaribishe,” sauti ya mwanadada ikifuatiwa na mguso wa kidole sehemu za mbavu za Amata ukamgutusha na kumlazimisha kugeuza sura yake kumtazama msichana huyo.

    “Ninunulie kinywaji leo utakuwa bebi wangu mpaka kucheee,” akaongeza na Kamanda Amata bila kujali akamwagizia Heineken mbili. Alipopiga mafundo matatu akazunguka na kusimama mbele ya Amata.

    “We sijawahi kukuona hapa Soweto, we mgeni wewe, maana mimi ni Stimela nabeba kila mtu, hivyo nawajua wote,” akaendelea kubwabwaja.

    “Hujakosea mpenzi,” kamanda akajibu.

    “Mambo si hayo bwana,” Yule mwanadada aliyeonekana kuchoka kwa pombe alizokunywa alijibu kilevilevi. Kamanda akatazama saa yake, tayari ilikuwa ni saa tisa za usiku, akateremka katika kiti chake.

    “Wapi tena bebi, hapa Soweto ndio kunakucha saa hii, ona watu ndo wanaingia,” Yule mwanadada akaendelea.

    “Sikiliza, unapenda kukaa hapa?” akamwuliza naye akajibu kwa kutikisa bega.

    “Sasa nataka unisaidie kitu kimoja, tukifanikiwa, utachagua wapi unataka nikupeleke nitakupeleka.”….







    wakatoka nje wakiwa wameshikana mikono, walipofika katikati ya giza nene ambapo hapakuwa na taa yoyote, kamanda akamsimamisha Yule mwanadada.

    “Sikia, nataka kompyuta, desktop kuna kazi nataka kufanya kama nusu saa hivi,” akamwambia Yule mwanadada.

    “Aaaa hilo tu? Twende kwa kaka yangu hapo mtaa wa pili atatusaidia”.

    Wakakokotana mpaka mtaa huo, Amata akaonana na yule kijana, kweli, akamkaribisha na kumpa kompyuta yake ya mezani aitumie. Akaibomoa mfuniko wake na kuipachika ile Hard Disk ili kupata vilivyomo. Wkati akiendelea na kazi hiyo Yule mwanadada akapitiwa na usingizi, alkadhalika Yule kijana.

    Ndani ya disk ile kulikuwa na mafaili mengi ya ajabu ambayo yalkimfanya Kamanda kusisimkwa na mwili, mipango michafu ya kuua na kupoteza, mipango ya ibada za kishetani za kundi hilo, mikataba ya ulaghai walioifanya na makampuni mbalimbali pale Afrika ya Kusini na kuwadhulumu kwa mtindo huohuo wa kuua na kubadilisha mikataba wakitoa vitisho na rushwa kwa watendaji wa serikali.



    Kulikuwamo na mafaili ya sauti ambayo yalirekodiwa ama katika mikutano Fulani au vikao vya siri, yaliyozungumzwa humo yalikuwa ni mazito, yanatisha, hayafai kusikiwa na mtu mwenye moyo wa nyama.

    Kamanda Amata akaendelea kupekuwa na katikati ya madokumenti hayo ndipo alipopambana na faili lililobebwa na kichwa habari ‘Top Secret’ yaani Siri Nzito, akaingia na kulisoma, ndani yake ndiko alikokuta mpango dhalimu wa ambao viongozi wa wengi wa Afrika wameingina mikataba na hawa jamaa bila kujijua, wakipeleka madini na mali mbalimbali ili kukingwa na kubaki katika nyadhifa zao. Katika faili hili ndiko alikokuta mazungumzo ya siri kwa njia ya sauti juu ya mgodi wa Tanzanite huko Mererani, akatikisa kichwa.

    Kurasa ya mwisho kabisa katika faili hilo akakuta mpangilio wa uongozi na picha za watu hao, Top Secret Service Hiarachy, jina la juu kabisa lilikuwa la Robinson Quebec kisha yakagawanywa majina kadiri ya kanda walizogawana, kanda ya Afika Kusini alikuwa ni Don Angelo, akawasoma wote watano yaani wa Kusini ambaye alikuwa akiishi Johanesburg, na mwingine alishika ukanda wa Mashariki huyu aliishi Antananarivo huko Madagascar, mwingine alishika ukanda wa Africa ya Kaskazini yeye aliishi Tunis katika nchi ya Tunisia na alisifiwa kwenye mkataba huo kwa kufanya kazi yake vyema kuwachonganisha watu wa huko na kuwafanya wapigane wenyewe kwa wenyewe.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Zaidi ya hao alikuwepo aliyeshika ukanda wa Afrika ya Maghalibi, huyu aliishi Abuja, Nigeria, yeye pia alifaulu kuanzisha vikundi mbalimbali vya ugaidi na kupora mali ya wananchi kama mafuta na gesi. Kulikuwapo na aliyeshika ukanda wa kati huyu aliishi Djamena, Mali, nay eye alikuwa na kazi hiyohiyo.

    Mipango ya kazi na siri nzito zilikuwa katika faili hilko, serikali zipi za kupinduliwa, marais wepi wa kuuawa na wepi wakuwekwa madarakani. Jamaa hawa walikuwa na ratiba ya chaguzi zote za Afrika hivyo waliyaweka mambo yao kisomi zaidi. Kamanda Amata alijikuta akizama katika kusoma hayo mambo na hasira ikizidi kupanda, akashtuliwa na jogoo lililowika kutoka katika nyumba ya pili.

    ‘Sasa nina watu wawili tu mkononi mwangu, Don Angelo na Robinson Quebec,’ akajiseme kisha akaing’oa ile disk na kurudisha iliyokuwepo. Akachomoa noti za dola hamsini hamsini, moja akaichomeka mfukoni mwa suruali ya Yule mwanadada na nyingine akaipachika kwenye vfulana mchinjo ya Yule kijan akisha yeye akatokomea zake.



    ONTARIO – CANADA



    SIR ROBINSON QUEBEC alifura kwa hasira, hakutaka kusikia la mhazini wala mnadi swala, kichwani mwake alijawa na jina moja tu la Amata Ric.

    “Ni nani huyu Amata sijui kamanda hata akisumbue kichwa changu namna hii?” alibwata hadi wasaidizi wake wakashtuka.

    “Hakuna mtu au kundi la watu la kutusumbua sisi hata serikali yoyote haiwezi kututikisa, huyu ni nani?”

    “Anaitikisa ngome yangu, ngome imara ya chuma, kaua vijana wetu karibu kumi na mbili, na kijana wangu mahiri Zebel, niliyemfundisha mwenyewe sanaa ya mapigano, shiiiit!” akang’aka.

    “Johnson, nataka uniitie viongozi wote wa kanda kuu ya Afrika, wafike hapa mara moja,” akamwagiza katibu wake naye akaondoka hapo mara moja. Robinson akavuta hatua na kuingia kwenye kiti chake maalumu kinachotembea kwenye reli na kumpeleka popote ndani ya kasri lake hilo, akaondoka zake na kuwaacha wasaidizi wake wakibaki kutazamana bila kujua la kufanya.

    Mpango dhalimu wa Robinson Quebec ulionekana kugonga ukuta kwa mara ya pili, mara ya kwanza ni pale alipotaka kupenyeza mbinu chafu kwa serikali makini ya Tanzania lakini kitengo maalumu cha kijasusi kilifanikiwa kuwaondoa watu wake Tracy Tasha na George McField. Na mara hii ni katika ukanda huohuo anakutana na kikwazo kingine katika mpango uleule aliouanza tangu miaka kumi iliyopita.



    ‘Kuna shida!’ aliwaza mwenyewe akiwa kajifungia ndani kwake. Mara simu yake ikaita alipotazama namba hizo moja kwa moja akajua inatoka kwa Don Angelus, akaiweka sikioni na kusikiliza huku akiwa ameikunja sura yake kwa hasira.

    “Huyu ni Kamanda Amata, kwenye rekodi yetu ni Yule aliyemuua Tracy Tasha, ni Mtanzania kitengo cha siri cha usalama wa Taifa,” aliyekuwa upande wa pili akahema.

    “Hebu, nataka taarifa kamili za kiumbe huyo, na natuma watu sasa waje kummaliza hapo hapo, hawezi kutufanya sisi wapumbavu kiasi hicho, tusumbuliwe na mtu mmoja!” aliongea kwa jazba huku akifuta jasho uso wake na ile simu ikakatika.

    ‘Huyu kijana anaonekana mahiri sana katika kazi yake, kama alimuua Tracy, George na sasa Zebel, mh! Ananipanda kichwani lazima hatua za haraka zichukuliwe,’ akajisemea kisha kwa kughafirika akapiga meza kwa ngumi nzito.



    DURBAN – AFRIKA YA KUSINI



    LERETI KHUMALO aliingia kwenye jumba lake saa tatu asubuhi mara tu baada ya kuruhusiwa kutoka kliniki, daktari nwake alichukua hatua hiyo mara baada ya kuona hali ya mtu huyo imeimarika lakini alimtaka kupata mapumziko zaidi, asifanye kazi walau wiki mbili. Wazo hilo kwa Lereti lilikuwa jema sana, alikubaliana nalo na akaamua kujipanga kwa safari hiyo ya dharula, mawazoni mwake aliona nchi bora kwake kwenda kupumzika ni Tanzania akiwa na lengo sasa akamtafute Amata mguu kwa mguu, aliwapa taarifa vijana wake nao walikubaliana naye na alikwishachagua vijana watatu wa kufuatana naye katika safari hiyo.

    Alipoingia nyumbani kwake moja kwa moja alikwenda katika ofisi yake ambayo ndani yake kuna simu inayohifadhi ujumbe wa kila simu iliyopigwa, alipoufungua mlango akapigwa na butwaa kuona koti la suti likwa limetundikwa kwenye kiti, akasogelea na kuliangalia bila kushika, alipotupa jicho katika meza yake yenye kompyuta akakutana na kijikaratasi chenye ujumbe; akakinyakua na kukisoma.



    ‘…usihofu ni mimi nilikuja, nimechukua kabrasha zako kwa kazi maalum nitakurudishia pindi tu kazi yangu ikitengemaa. Nakuomba kama utatoka usiliache koti langu kwani nimelisahau. Kamanda Amata.’



    Ule ujumbe ulikatika hapo. Hakukuwa na namba ya simu wala nini, Lereti akapigwa na mshangao, sura yake ikabadilika kutoka katika mshangao na kuanza kutoa machozi ya furaha. Moyoni mwake alijikuta amani na imani vijijenga pamoja. Lakini alihuzunika kuona Kamanda Amata hakumwachia mawasiliano yoyote.

    Akachukua lile koti na kuvaa kisha mikono yake akaifumbata kifuani huku tabasamu likichanua moyoni na usoni.

    Akatoka na kwenda chumbani kwake, akajibwaga kitandani na kukumbatia mto wa kulalia huku maneno ya mapenzi yakibwabwajika kinywani mwake akajisahau kama anaongea na mto. Nusu saa baadae akatoka na kuifuata simu yake. Akawasiliana na shirika la ndege la Afrika ya Kusini kuona kama kuna ndege itakayomwondoa katika nchi hiyo kwa muda mfupi ili akapate mapumziko.



    Akapewa jibu la kuwa ndege ipo siku hiyo hiyo usiku wa saa tatu; aliporidhika akatafuta na hoteli ya kufikia jijini Dar es salaam, ijapokuwa moyoni angependa sana kuonana na Amata lakini ilibidi atii maelekezo ya daktari wake. Siku hiyo aliitumia kupumzika kidogo na kujiandaa kwa safari.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    JOHANESBURG – AFRIKA YA KUSINI



    KENGELE YA SIMU YAKE ilimwamsha katika usingizi mzito usiokuwa na ndoto. Kamanda Amata akauvuta mkono wake na kuitazama saa iliyokuwa mkononi, saa ya kidigitali yenye kufanya kazi nyingi usizoeza kufikiri; akaitazama na kutabasamu, ilikuwa saa tatu na dakika hamsini asubuhi, akajua Lereti keshatoka hospitali na ameupata ujumbe wake, kwani ndani ya koti lile aliweka GPS button ili likihamishwa saa yake ingempigia kengele na kumjuza limeelekea upande upi, alifanya hivyo makusudi ili kama Lereti akiufuata ule ujumbe kuwa ahakikishe haliachi basi angejua kila alipo mwanamke huyo.

    Siku hiyo Kamanda alilala ndani ya gari yake kwani aliona ndiyo sehemu salama kuliko zote, akajinyanyua na kuketi sawia kitini, akashuka na kujinyoosha, kisha akachukua maji na kujiswafi japo usoni maana gari yake aliiegesha porini nje ya mji wa Johanesburg, alipoona yuko sawa aliingia barabarani na kuondoka eneo lile kuelekea mjini.



    HOTELI YA MICHELANGELO



    DON ANGELO alikuwa tayari kwa safari, aliwaita wasaidizi wake wa karibu.

    “Naondoka naenda Canada tuna kikao cha dharula na kikao chicho kimetokana na tatizo hili hapa kwetu, naomba huyo anyejiita Kamanda Amata muhakikishe mnammaliza leo hii, lakini mtafuteni kwa siri sana,” akawapa maagizo.

    “Sawa boss, tumeweka ulinzi hotelini kwake hawezi kutuponyoka, pia tumeimarisha uwanja wa ndege, hivyo hana njia ya kututoroka, tutakupa taarifa,” mmoja wasaidizi akajibu.

    “Ok, sawa lakini muwe waangalifu huyo jamaa ni mkorofi sana.” Akawajibu kisha akamtazama kijana mwingine mwenye misuli minene aliyesimama pembeni bila kuongea.

    “Jefferson, utakuwa mkuu wa idara ya usalama mpaka nitakaporudi, asanteni,” akatoa maagizo na kuondoka zake huku akifuatana na vijana wengine watatu ambao daima haacahani nao, walikuwa walinzi wake wa karibu.



    §§§§

    Kamanda Amata akashusha darubini yake ndogo iliyomuwezesha kuona wakati Don Angelo akitoka ndani ya hoteli ile na kufuatana na vijana wake, akaingia katika Mercides Benz new model na nyuma yake akafuatiwa na vijana wale latika gari nyingine, wakaondoka.

    ‘Unakimbia sio?’ kamanda alimuuliza mawazoni kisha akawasha gari na kuunga msafara uliokwenda kuishia Uwanja wa Ndege. Walipoteremka na yeye akateremka na kuendelea kuwatazama, alikuwa na nafasi kubwa na nzuri ya kufanya lolote lakini aliacha kwanza aone…







    DON ANGELO na vijana wake wawili waliingia katika jengo la uwanja huo na kupotelea ndani, Kamanda Amata kwa mwendo wa hadhari ili asionekane na wale wengine alitembea taratibu kuelekea kulekule ndani. Kwa mbali alimwona Don akifanya uhakiki wa tiketi zake, jicho la Kamanda likatua kwa mwanadada aliyekuwa akiifanya kazi ile, ‘Bingo!’ akajisemea kisha akasubiri Don na vijana wake waondoke katika eneo lile ili naye akafanye yake.

    Alipohakikisha Don keshaingia ndani kabisa, akavuta hatua na kuwapita baadhi ya wasafiri waliokuwa kwenye foleni huku akiwaomba samahani na moja kwa moja akafika kwenye kidawati cha Yule mwanadada.



    “Habari msichana! Mimi ni mwanausalama,” akamwonesha kitambulisho ‘feki’ cha upolisi wa Afrika Kusini.



    “Ndiyo nikusaidie nini?” Yule mwanadada akamwuliza, na kamanda akaeleza shida yake; bila hiyana akapatiwa maelezo yote kuwa Don anaelekea Canada katika jiji la Ontario kwa ndege ya shirika la USA, IATA Airlines. Akamshukuru na kauondoka eneo hilo.



    §§§§§



    “Yes! Madam S, mzigo wetu umeelekea Canada mchana huu,” kamanda akamwambia Madam kwa simu aliyompigia mara tu alipoingia ndani ya gari lake.



    “Ok, sawa, nitakupigia muda si mrefu, lakini jiandae kwa safari ya nyumbani kwani nitahitaji maelezo ya kina kutoka kinywani mwako wewe mwenyewe,” Madam S akamweleza na kisha akakata simu.

    Dakika ishirini baadae Kamanda Amata alifika Hoteli 77, akilini mwake alijua wazi kuwa lazima kuna wanaomsubiri hapo. Akaegesha gari mahali pa peke yake kisha akateremka. Hakupitia mlango wa siri wala njia za panya, moja kwa moja aliingia kupitia mlango wa mbele, kwa macho ya uchokozi aliweza kumuona kila mtu aliyekaa na aliyesimama, mara moja akajua nani mbaya na nani mwema kwake.

    Vijana wawili waliokuwa wakisoma magazeti kila mmoja kwa nafasi yake waliyateremsha kisha mmoja akanyanyuka na kumfuata Kamanda kule alikoelekea, lakini alipoingia kwenye lifti na kusuka hakumwona, akachanganyikiwa hakujua ni mlango upi kaingia.



    §§§§§

    Kamanda Amata alikagua chumba chake na kugundua kuwa kilipekuliwa kwa mara nyingine lakini hakujali, alikusanya kilicho chake na kutia katika begi kisha; alipohakikisha kila kitu kipo tayari akajipanga kuondoka lakini alikumbuka kuna mmoja aliyemfuata kuja huko hivyo alijua kama si mlangoni basi kuna mahali watakutana. Akafungua mlango na kuufunga nyuma yake, akimwona Yule kijana mwisho wa korido akijifanya kuangalia nje, akaachana naye na kuondoka.



    Yule kijana alimfuata kamanda na kuingia lifti ya upande mwingine huku kamanda akiwa tayari kateremka kwa lifti nyingine. Alipofika gorofa mbili kabla ya kufika chini, akateremka na kusubiri lifti ya upande ule alioingia Yule kijana, akaizuia kwa kubonyeza kitufe Fulani chenye mchoro wa pembetatu. Mlango ukafunguka, ndani ya lifti alikuwapo Yule kijana peke yake, akapigwa na butwaa na kutoa macho baada ya kumuona Kamanda akiingia mbele yake.

    “Unashangaa nini? Ulifikiri huwa nafuatwa kijinga hivyo?” kamanda akamwuliza na kisha akampa pigo moja la karate lililotua kwenye paji lake la uso, Yule jamaa akajibamiza kisogo na kupoteza fahamu huku damu kidogo zikitoka puani.



    §§§§§

    Vijana wapatao watano walilizunguka gari la Amata pale lilipoegeshwa. Alipotoka aliwaona vijana wale akaelewa lengo lao. ‘Bado wananiandama,’ akawaza na kuvuta hatua kuelekea maegesho ya tax.



    “Hii hapa mzee,” kijana mmoja alimkaribisha kwa ukarimu naye akaitikia kwa kichwa huku akiwa amesimama akiwaangalia wale vijana wa kizungu. ‘Nawahurumia sana, lakini kutokana na upumbavu wenu nitawaonesha maajabu ya Mlima Kolelo,’ akawaza na kutabasamu. Wale vijana walikuwa bado wamesimama kwa kuliegemea lile gari. Amata akatoa rimoti yake na kubofya hapa na pale. ‘Na hii ndiyo dawa yenu, pumbavu sana nyie!’ akajisemea moyoni mwake kisha akabonyeza tab iliyoandikwa OK.

    Mlipuko mkubwa ukatokea, ile gari ikalipuka na kufumuka vipande vipande, milango ikirushwa juu na magurudumu vilevile.

    Kamanda Amata akaingia ndani ya ile tax.



    “Twende!” akamwamuru dereva, wakaondoka eneo lile na kutokomea.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Tunaelekea wapi?” popote penye hoteli kubwa unayoona wewe inanifaa,” akamjibu na moja kwa moja akampeleka kwenye Hoteli ya Good Hope yenye hadhi ya nyota tatu. Akamlipoa na kisha akamwacha aondoke. Alipotokomea, akazunguka mtaa wa pili na kuchukua tax nyingine na kuelekea uwanja wa ndege.



    DAR ES SALAAM – saa 4:09 Usiku.

    MADAM S, CHIBA NA GINA walikuwa uwanja wa ndege, ndani ya gari yao bila kushuka, Chiba akiwa nyuma ya usukani. Kioo kikagongwa mara tatu na mlango ukafunguliwa na Gina.

    “Karibu Kamanda, tupo kwa ajili yako,” Gina akamwambia huku akimkumbatia.



    “Nashukuru, nimetoka kwenye midomo ya Mamba mwenye njaa au samba aliyejeruhiwa,” akajibu na kuketi sawia ndani ya gari hiyo kisha mlango ukafungwa.



    “Kamanda Amata!” Madam S akaita, “Ni hapahapa ambapo safari yako itakwisha na kuanza, nipe tafutishi zako harakaharaka,” Madam akamwambia na Amata akatoa yale makabrasha akampatia Madam na ile hard disk.



    “Ndani ya hiyo drive mtapata siri na mikakati mingi ya kishetani ya hao jamaa, zaidi ya ile tuliyokuwa tukiitarajia,” Kamanda akaeleleza.



    “Ok, Chiba atapitia na kuweka vizuri taarifa zote,” Madam S akaeleza.



    “Sasa Amata, ipo hivi; hauna muda wa kupoteza, kazi ipo kwenye wakati mzuri sana kwani imeonekana Robinson Quebec ndiyo kila kitu katika mpango huu kadiri ya maelekezo yako na taarifa fupi ulizonitumia. Hivyo basi, hauna budi kuondoka kwenda kumsabahi kule Canada ili hata nay eye akufahamu kwa ukaribu,” Madam aliongea huku akiwa ameivua miwani yake na kumtazama Amata kwa jicho pembe.

    Wakati huo Gina alimkabidhi Amata bahasha ambayo ndani yake ilikuwa na tiketi ya safari na hati nyingine ya kusafiria ambayo ilimtambulisha kwa jina jipya, tayari ikiwa na viza ya mwezi mzima.

    “Fika Ontario, kisha maelekezo utayakuta hukohuko,” Gina akamalizia na kuketi vizuri kitini.

    “Kamanda, naomba urudi salama, na likizo yako utaikuta ukirudi,” Madam akamalizia na wakati huo Amata tayari alikuwa nje ya gari hiyo.



    §§§§§

    DURBAN, AFRIKA YA KUSINI - Saa 4:00 usiku



    LERETI KHUMALO hakuamini kusoma barua pepe iliyoingia katika box lake mchana wa siku, hiyo, hii nayo ilimpa furaha ya ajabu ambayo hakuwahi kuihisi katika siku za karibuni.

    ‘Robinson anataka kujitoa katika ubia wa kampuni yetu, jambo jema sana, bora nijiendeshe mwenyewe,’ aliwaza mwenyewe huku akiwa kaikodolea macho laptop yake iliyokuwa mapajani wakati akisubiri kuondoka.

    Mwisho wa barua ile ilimtaka kufika Canada ili kutialiana saini katika hati ya kuvunja ushirikiano huo, alitakiwa kutaja tu ni siku gani ambayo ataweza kufika huko ili wanasheria wa pande mbili wajiandae kwa tukio hilo. Lereti muda huohuo akawasiliana na katibu wake naye akakiri kuipata barua hiyo isipokuwa alikuwa hajaifanyia kazi, akaandika barua pepe kwa mwanasheria wake na kuwaambia wajiandae kwa safari na siku ya tatu yake wakutane Ontario Canada.



    Lereti alivunja mapumziko ya Dar es salaam na kuona kuwa atakaa siku moja tu kwa kujiandaa kwa safari hiyo kisha aungane na watu wake huko Canada.

    Dakika chache baadae alikuwa ndani ya ndege kuelekea Tanzania ambako sasa si mapumzikoni tena bali ni kupita tu.

    Kichwa chake kilikuwa kikitawaliwa na wazo moja kubwa; jinsi ya kuendesha kampuni ile peke yake kwa manufaa ya familia yao, kuhakikisha jina kubwa la Khumalo linarudi katika hadhi yake. Akiwa katika wimbi la mawazo akapitiwa na usingizi na kuzama katika ndoto za moyoni, mara alicheka, mara alihuzunika ilimradi tu ndoto ilinoga.

    Alishtushwa tu mara chache alipotakiwa kuamka ili apate chochote naye akafanya hivyo, na saa tano baadae alishtuliwa na sauti ya mwanadada iliyomtaka kufunga mkanda kwani safari ilikuwa imefika mwisho wake; akafanya hivyo.



    ONTARIO – CANADA

    WAGENI wa Robinson Quebec waliwasiri katika jiji hilo ndani ya muda mchache tu tangu wapewe wito huo. Hawakuwa wengi, ni watu takriban kumi na sita hivi, kila mmoja alikuwa na ham,u ya kujua ni nini hasa mkuu wao amewaitia tena ghafla hivyo. Kila mmoja alifikia kwenye hoteli aitakayo kadiri ya matakwa yake isipokuwa tu walijua wazo kuwa usiku wa siku inayofuata ndio kikao hicho kitaanza kwa ibada maalumu na kutoa kafara ya damu mbichi ya mwanadamu kisha ndio wazungumze yaliyowapeleka. Daima mikutano yao ilifanywa usiku wa manane kwatika hali ya siri na ulinzi mkubwa.

    Siku hii tayari walinzi wao walitapakaa sehemu mbali mbali ya jiji la Ontario ili kujua kama kuna lolote linalozungumzwa na ikijulikana basi we uliyesema umekwenda na maji.

    Don Angelo moja kwa moja alifikia katika hoteli kubwa ya kifahari ambayo mara nyingi hufikia hapo, moyoni mwake alikuwa na wasiwasi sana, hakuwa na amani na kikao hicho. Mara tu alipoketi juu ya kitanda kikubwa na kujibwaga juuye ili kupata pumziko mara simu yake kubwa ikapokea ujumbe uliomuwacha kakodoa macho, akaitupa simu ile ukutani kwa nguvu na yeye kujitupa kitandani huku akitoa tusi la nguoni. ‘Tumekosea wapi? Na huyu jamaa anajiamini nini hata atufanye hivi?’ Don alijiuliza pasi na majibu.



    §§§§§

    “Mimi sio mjinga hata niuache mgodi ule uende hivihivi, kumbuka kati ya migodi inayoingiza hela kwetu ule unaongoza,” Robinson aliwaeleza watu wake wa karibu ambao alikuwa ameketi nao katika chumba cha siri ndani ya jingo lake kubwa lililobeba maofisi na mambo mbalimbali.

    “Hii ni janja yangu tu na najua kuwa atanasa, na ameshahakikisha anakuja, sasa kazi kwetu jinsi ya kumwondoa na kisha tunaanza michakato mipya, kule Afrika ya Kusini tayari kuna viongozi wa serikali wanasubiri tu wasikie juu ya hili,” Robinson aliendelea kunadi sera.

    “Sasa, kwani jaribio la kwanza lilishindikana vipi wakati kila kitu kilikuwa sawa na tulipeleka mtu mwenye taaluma hiyo?” Mjumbe mmoja mnene aliyekuwa akivujwa jasho mara kwa mara aliuliza swali hilo.



    “Aaaaa pale tumefeli, kuna mtu katumwa kutoka Tanzania huyu ndiye mwiba katika harakati zetu, ametuharibia kwa kumuua Tracy mwaka uleeee pamoja na McField, sasa sijajua kajipeyeza vipi katika hili, viongozi wa idara za usalama pale wamekiri kutokuwa na habari na mtu huyo,” akaendelea kujibu.

    Ukimya ukatawala kila mmoja akiwa anaangalia anakokujua, ‘Mkono wa Jasusi!’ mmoja wao akawaza, kisha akageuka kumtazama Robinson.

    “Huyu bwana nahisi atatuharibia kila upande, kwa nini hasimalizwe?” Yule bwana akaongea huku amekunja sura.

    “Tungemmaliza lakini sijajua anatuzidi vipi akili, kila tukipanga hili, yeye yupo sekunde kadhaa mbele,” Robinson akaeleza. Kikao hicho cha dharula kikaendelea kwa dakika kadhaa na kumalizika kisha kila mtu kurudi katika shughuli zake.



    §§§§§



    KAMANDA AMATA aliegesha gari yake nje ya jengo kubwa la ofisi za shirika moja la simu, katikati ya jiji la Ontario. Mbele yake alikuwa akiitazama gari iliyombeba Lereti na watu wake ambao waliingia Ontario kwa tofauti ya saa tatu tu na Amata. ‘Ni yeye!’ alijiwazia alipomwona Lereti akiingia ndani ya gari hiyo huku walinzi wake wakimlinda kama kawaida. Walipoondoka naye akawafuatia nyuma nyuma bila wao kujua mpaka pembezoni kidogo mwa jiji hilo ambapo kumesheheni mahoteli makubwa ya kifahari.

    Ontario Paradise, ilikuwa hoteli ya kisasa nje kidogo ya jiji hilo, Lereti alichagua eneo hilo kuweka makazi yake ya siku hizo chache huku mwanasheria na katibu wake nao wakiwa pamoja naye. Moja kwa moja aliongozwa chumbani kwake ambako pamoja na kila kilichomo alikabidhiwa bahasha moja kubwa na mwanadada mhudumu wa hoteli. Alipoisoma ilikuwa ni kadi maalumu ya mwaliko wa mkutano huo way eye na wadau wake ambao ungetukia saa nne tu baada ya hapo. Aliitazama saa yake, ilikuwa saa sita za mchana kwa saa za Canada. Akaamua kuingia maliwatoni ili kujiswafi kisha kupumzika kidogo.



    Ni wakati huo ambao alikuwa akioga na kujifungia mlango wa bafu hilo la ana yake lililojaa starehe za kila aina ndipo Kamanda Amata alipofungua taratibu mlango wa chumba hicho kwa kutumia kadi yake maalumu kwa kufungua vitasa kama hivyo.

    Alipojua Lereti kuwa anaoga, hakuwa na haja ya kunshtua au kumsubiri, alitembeza macho kwa haraka na kuiona ile bahasa, akainyakua na kuifuangua ndani haraka, akasoma na kuupata ujumbe hasa alioukusudia. Akatoka katika chumba hicho kabla ya Lereti kutoka bafuni mle.

    Ndani ya gari lake aliinua simu na kupiga namba Fulani.



    “Yeah ni leo saa 10:30 jioni katika jengo la Quebec High Tower namba 749,” akaongea katika simu ile.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Ok, maelekezo yanakuja dakika tatu zijazo,” ile sauti ikajibu, naye akatulia garini.

    Kama alivyoahidiwa, dakika tatu ile simu ikaita akainyakuwa na kuiweka sikioni.

    “Sikiliza kwa makini Kamanda, utatoka hapo ulipo na kuifuata barabara ya Hamingway, moja kwa moja kama unaelekea uwanja wa ndege lakini katika ile njia panda kubwa kunja kushoto, mbele yako mita kama 250 hivi egesha gari kulia, usubiri mtu atakayekuletea ujumbe, haongei na wala wewe usiongee,” ile sauti ikamaliza na Amata akaondo agari kufuata maelekezo kama alivyoambiwa.



    Akiwa kaegesha eneo lile aliloelekezwa, gari nyingine kubwa aina ya GMC ikasimama mbele yake, kulikuwa na vijawa wawili walioonekana wapo kisharishari, kijana mmoja akateremka akiwa kavalia kaptula ya jeans, shingoni mwake mikufu ya dhahabu ikimning’inia mkononi mwake alikuwa na kitu kama koba gumu lenye urefua kadiri ya mita moja hivi. Akasogelea gari ya Amata na kumkabidhi bila kuongea chochote, Amata akaingiza lile koba ndani katika siti ya pili naye akaketi nyuma ya usukani. Lakini kabla ya kuondoka akalifungua ndani yake na kuona kilichomo.



    “Shiiiiit” akajikuta akiongea peke yake.

    Bunduki kubwa la kudungulia, lenye uwezo wa kudungua umbali usiopungua mita 900 lilikuwa limelala ndani yake vipande vipande. Pembeni yake kulikuwa na darubini ya jicho moja na ile ya macho mawili, rimoti ya kuliongoza dude hilo kama hutaki kuwapo eneo la tukio, seti moja ya vifaa vya kusikilizia. Akavichukua na kuvipachika sikioni muda huohuo kuona kama kuna lolote.



    “…Saa kumi na dakika ishirini, katika ghorofa kubwa ya Stateway, chumba namba 740 ndipo utakapofanya mapenzi na msichana huyo, mara tu utakapokamilisha kazi sufanya haraka kuteremka utapata maelekezo yote kutoka kwenye hikihiki kifaa na watu wa kukuondosha watakuwa tayari eneo hilo…”



    Akawasha gari na kuondoka zake. Katikati ya mji wa Ontario kulikuwa na mgahawa mhubwa wa McDonald akaingia japo kupata chochote akisubiri muda kuwadia.



    §§§§§

    ONTARIO - Saa 9:45



    LERETI aliondoka kwa gari aliyoikodisha yeye na watu wake kuelekea eneo la tukio. Aliketi kwa utulivu katika kiti cha nyuma yeye na katibu wake huku kiti cha mbele akiwapo mwanasheria wake, gari ya pili nyuma kulikuwa na vijana wake makini wakiangalia usalama wa msafara huo.

    Moyoni mwake alikuwa akiwaza sana juu ya tukio hilo ambalo linategemewa kutokea dakika chache zijazo, alipatwa na furaha sana moyoni.



    §§§§§

    Majengo makubwa na marefu mawili yalimkaribisha Kamanda Amata eneo hilo, mojawapo la upande wa kulia lilikuwa na maandishi makubwa juu yake ‘QUEBEC HIGH TOWER’ na lile la kushoto liliandikwa ‘STATEWAY’ na katikati yake barabara kubwa ilikuwa imeyatenganisha, kwa muonekano hayakuwa na uhusiano kabisa . Amata akaegehsa gari yake na kuteremka na ule mkoba. Moja kwa moja akaingia mlango mkubwa na kutumia lifti akapanda mpaka ghorofa ya saba. Hakukuwa na maofisi mengi lakini mahala Fulani penye mlango mkubwa wa kioo palibeba kibao kidogo namba 740, akauendea na kuusukuma ulikuwa wazi. Kamanda Amata alikuwa ndani ya mavazi ya kazi, suruali ya jeans lakini iliyoweza kuvutika, fulana na jacketi lililobeba silaha mbalimbali na mgongoni mwake alikuwa na kijibegi kidogo, kofia ya mzula ilikifunika kichwa chake, gloves ziliificha mikono yake na viatu vyenye soli yenye vyuma vikali nyuma na mbele vilitulia miguuni mwake.



    Akatazama huku na kule hakuna mtu, alikuwa peke yake, akaanza shughuli ya kuliunganisha dude hilo kubwa, baada ya dakika sita tayari lilitokea bunduki kubwa lenye bomba refu na lililoonekana kuwa na nguvu ya ajabu, lilisimama kwa miguu yake miwili na kitako chake kujikita chini upande wa nyuma. Kiboksi chenye risasi mbili kubwa kilikuwa mkononi mwake.



    “…Unatakiwa kumuua Robinson bila kukosea, mara tu baada ya kumuua uondoke eneo hilo na gari ya kukuchukua itafika katika mlango ulioingilia nukta hiyohiyo…. On your mark,…” sauti ikasikika katika kile kisikilizio, Kamanda Amata akalala sakafuni na kulikamata lile bunduki kwa ustadi wa hali ya juu. ‘Sijazoea kuua kwa mtindo huu, ni nimezoea kupiga mkono kwa mkono, kusimama na windo langu mita zisizozidi kumi…’ aliwaza, mara ghafla sauti ikasikika katika ile mashine sikioni mwake.



    “…Katika jopo hilo lililoketi ni Yule mwenye suti nyeusi na miwani ya macho, aliyekamata makabrasha kadhaa mkononi mwake…”

    Kamanda Amata alikuwa bado hajapachika jicho katika lensi ya bunduki lile akafanya hivyo na kumwona bwana huyo kwa uzuri kabisa.



    §§§§§



    ONTARIO – Saa 10:30 jioni

    LERETI aliketi katika chumba cha mkutano na jopo la watu kadhaa akiwemo Don Angelo, yeye na mwanasheria wake walikuwa wameketi pamoja na upande ule Robinson na mwanasheria wake pia walikuwamo mashahidi kadhaa katika kikao hicho, kila mmoja upande wa Robinson alionekana kuwa na wasiwasi na maamuzi ambayo bwana huyo amechukua juu ya kampuni hiyo. Ukimya ulikuwa ni moja ya sehemu ya mkutano huo kwa wakati huo. Baada ya mazungumzo mafupi kati ya makundi hayo mawili, yale makabrasha yakatandazwa mezani na watu wa pande hizo wakayasoma kwa umakini, baada ya hapo wanasheria wa pande zote mbili wakasomeana tena kwa sauti na kupitia kipengele baada ya kipengele.

    Lereti alikuwa amsikilizaji tu, alipojiridhisha na hati ile akaridhia kuitia saini mbele ya mashahidi, karatasi zikawekwa mbele ya Lereti lakini mwanasheria wake akazuia boss wake kusaini akitaka Robinson asaini kwanza, kukatokea ubishano kati yao.



    §§§§§



    Saa 10:55



    “Natakiwa kumlipua wakati gani?” kamanda akauliza.

    “…Nataka umlipue sasa, usichelewe kwani tunaweza kugunduliwa kisha ikawa shida…” ile sauti ikamjibu kupitia katika vile visikilizio, Kamanda aliongea na mtu asiyemjua wala kumwona.

    “Subiri kidogo…”

    “…no! shoot now!” ile sauti ikang’aka.

    “Subiri, time bado bwana,” Amata naye akaonesha ukali.

    “…Amata, shoot now this is an order…” (Amata, lipua sasa hii ni amri) .

    Hata hivyo Amata alitulia tulia akiendele kuangalia mtu mmoja baada ya mwingine ndani ya chumba kile.

    “Yeeeessss! Do that,” (Ndiyo fanya hivyo) Amata alisema kwa sauti ndogo alipoona lile kabrasha likirudi kwa Robinson naye kuchomoa karamu kwenye kijaruba chake na kusaini ule mkataba.

    “Go, Lereti go!” (haya Lereti haya) . Lereti akaweka saini katika hati ile na jicho la Robinson lilikuwa baya waziwazi kwake, aliposaini na wale wanasheria wakasaini baada ya mashahidi wote kusaini ile hati ya kuvunja mkataba wa ubia kati ya zile kampuni mbili.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walipomaliza tu mlango ukafunguliwa na warembo wawili wakaingia na kitoroli kilichojaa vinywaji na kuanza kusambaza kwa kila mmoja. Chupa moja pekee alimiminiwa Lereti na wale watu wake na ikarudishwa.

    “Why?” (kwa nini?) Kamanda akajiuliza.

    “…umepoteza hesabu zote Amata, hutompata tena Robinson, na wewe kutoka ndani ya Ontario ni ndoto, wamekuona wanakufuata, kwaheri…”

    Ile sauti ikamwambia Amata na kisha kijisauti cha mawasiliano kukatika kikasikika kikibipu mara tano na kuzimika.

    “Shiiiit, Im out,” akajisemea kwa sauti ndogo, na kurudisha jicho kwenye lensi ya lile bunduki, moja kwa moja akapepesa jicho kumtafuta Robinson asimwone.

    “Come on! Where are you bastard?” ( uko wapi mwanaharamu?) alijiuliza mwenyewe kwa sauti na mara akamwona tena Robinson akiagana na wageni wake, akaweka shabaha yake vyema. Na wakati huohuo alimshuhudia Lereti akianguka chini sakafuni. Kamanda Amata akajikuta katikati hajui afanye nini, kitendo cha Lereti kuanguka kilimpa kigugumizi cha mikono, aliposhtuka alikutana uso kwa uso na Robinson aliyekuwa akiangalia kule aliko Amata tena kwa darubini.



    “Limeniona, goodbye,” akajisemea na kupachika dole la shahada kwenye kifyatulio kisha akavuta bila huruma.

    “Go baby go..” Amata alifyatua na lile bunduki bila kutoa mlio mkali likaachia risasi moja nzito iliyotawanya kifua cha Robinson na kumtupa ukutani kwa nguvu na kuacha doa kubwa jekundu katika ukuta ule.



    “Hapo hapo ulipo!” sauti ikatoka nyuma yake, Kamanda Amata hakujiuliza, aligeuka haraka na tayari bastola zake mbili zikiwa mikononi, kitendo cha sekunde tu alifyatua bastola zake na kuwapata vijana wawili waliokuwa nyuma yake, wakatupwa kando wakiwa wanaokoteza uhai wa mwisho. Kamanda Amata akasimama na kutazama huku na kule, tayari mtafaruku ulianza huko chini, na ndani ya chumba kile alichouawa Robinson kulikuwa ni heka heka.

    Akaondoka eneo lile na kuruka kwenye kikorido cha chini yake, akavua mkanda wake wa kiuno na kuupachika kwenye waya wa umeme akakamata huku na huku akazungusha miisho yake katika viganja vya mikono kisha akajiachia na kupita hewani kuelekea jingo lile walilokuwamo akina Lereti.

    Nyuma yake alisikia milio ya risasi ikimfuatia. Aliteremka kwa kasi na alipofika umbali wa mita mbili kutoka katika lile dirisha kubwa la kioo ambalo ndani yake kulikua na kile kikao, akajiachia na miguu yake ikatangulia kwenye kile kioo na kukitawanya vipande vipande kisha yeye akatua ndani yake na kuwatawanya watu walio karibu yake kwa mateke mawili makali.

    Alipotua sakafuni akakutana uso kwa uso na Don Angelo.

    “Zamu yako inakuja!” akamwambia kisha haraka akapiga risasi hewani na kumnyayua Lereti kutoka pale chini akiwa hajitambui. Akambeba kwa kumkumbati na kutoka naye pale dirishani kuelekea chini. Mkono mmoja akimshika Lereti kwa nguvu na ule mwingine akafytaua parachute lilikouwa ndani ya begi lake na kuteremka taratibu.

    Alipofika chini tu, gari moja aina ya GMC ilifunga breki ghafla.

    “Twendeeeee!!!!” Scoba akiwa nyuma ya usukani alimwita Amata naye bila kuchelewa, alimpakia Lereti kisha akajipakia nay eye na kuondoka kwa kasi eneo lile huku wakifuatiwa na ving’ora vya polisi. Scuba aliendesha gari ile kwa ustadi wa hali ya juu na kuwachenga polisi waliokuwwa na gari za kisasa. Baada ya kupita mitaa kadhaa, Scoba alitoka barabara ni na kuegesha pembeni. Kisha akabofya vidubwasha Fulani na sakafu ya chini ya gari ile ikafunguka. Chini barabarani kulikua na funiko kubwa la bomba la maji machafu, mara likafunuliwa, na Chiba akaonekana ndani yake, Amata akamshusha Lereti na kisha akaingia yeye mwisho akamalizia Scoba, wakajifungia na kupotelea ndani ya bomba hilo ambalo halikuwa na maji hata kidogo.

    Huko nje, polisi walipoliona lile gari limeegeshwa wakalikaribia na gari zao lakini wakasimama umbali kidogo na kuteremka wakiwa na bastola zao mikononi, wakitoa maonyo ya walio ndani kujisalimisha. Kabla amri hiyo haijatiiwa mlipuko mkubwa ulitokea na ile gari ikawaka moto na kuzua kizaazaa.



    §§§§§

    “Nilikutafuta sana Amata, nikashangaa pale nilipoandika mawasiliano yako kwenye kitabu changu, karatasi imechanwa na kuondolewa,” Lereti alilalamika akiwa chini ya pua ya Amata kwenye kitanda kikubwa cha sita kwa sita huku moto ukiendelea kuwaka kwenye chemba maalumu na kufanya kajoto ka wastani ili kupunguza baridi kali iliyolikumba jiji hilo.

    “Pole sana, nilikiondoa mimi mwenyewe pindi tu ulipokwenda kuoga na kukiacha ndani ya mkoba wako,” Amata akajibu.

    “Tabia mbaya, mi nateseka mpaka nataka kufa, nakutafuta nashindwa kukupata,”



    “Sasa mbona nimekuja kukusaidia? Tena kutoka Afrika Kusini mpaka Canada na ushindi umepata, mgodi wa baba yako umerudi mikononi mwako, hakuna utapeli tena, nilisubiri tu Yule bwege asaini na wewe usaini na wanasheria na mashahidi kisha nimmalize kama ilivyokuwa,” kamanda akamweleza.

    “Ha! Ni wewe uliyemuua?” Lereti akauliza na kujiinua huku akimsogeza Amata pembeni.

    “Ni nani mwingine mwenye mkono wa nguvu kama mimi? Huu ni mkono wa jasusi ukikuandikia kifo utakufa tu,” Amata akajibu.

    “Oh, asante, nikupe nini mpenzi zaidi ya hiki? Umenilipizia kisasi mara mbili, umenirudishia kitu kikubwa sana moyoni mwangu, amani, hata Mzee Khumalo huko aliko anafurahi hili,” akamtazama Amata usoni na kuvuta karibu akambusu kinywani kwa sekunde kadhaa.

    “Kamanda najua hauna motto, nataka kukupa motto,” Lereti akaongea huku chozi likimtoka.

    “Utanipa wangapi? Maana kazi hii bado haijaisha…”

    “What?”

    §§§§§



    Msafara wa maazishi uliojumuisha gari kama hamsini hivi za kifahari ulikuwa ukienda taratibu katika makaburi ya watu wazito yaliyojengwa nje ya jiji la Ontario. Ilikuwa ni safari ya mwisho ya kibopa Robinson Quebec.

    Vyombo vya habari zikiwamo redio, magazeti na televisheni vilikuwa vikirusha habari ya tajiri huyo aliyeuawa kwa kudunguliwa, vikisifu ulinzi aliokuwa nao na kuponda jinsi alivyokufa kizembe, lakini mpaka nukta hiyo hata wao walikuwa hawajui ni nani aliyetekeleza mauaji hayo walibaki kudhani tu, labda … labda.

    Kamanda Amata alishusha gazeti alilokuwa anasoma na kuyaruhusu macho yake kumwona Don Angelo aliyekuwa kati ya vijana watatu sambamba ah ii wakivuta hatua fupifupi kuingia katika uwanja wa makaburi yale.

    Idadi ya watu haikuwa kubwa kama misiba ya kwetu, takribani watu 100 walikuwapo na kila mmoja akiwa kwenye nguo nyeusi na kuketi kitini ibada ikiendelea.



    “Tangu lini unatembelea fimbo?” Lereti alimuuliza Amata.

    “Nimezeeka sasa, ah ii fimbo inanisaidia sana katika kutembea,” akamjibu huku akimwangalia usoni, kutoka pale walipoketi karibu kabisa na mlango wa kuingia katika yale makaburi, hakuna aliyewagundua kama kijana huyo ndiye aliyesababisha mauti ya huyo anayezikwa kwa jinsi alivyojibadili sura yake. Walipoona sasa watu wanatawanyika na maziko yamekamilika wao wa kwanza kutoka na kuingia kwenye gari yao yenye rangi kama za wale yaani nyeusi kisha wakatazama vizuri Don Angelo ataingia katika gari ipi.

    Scoba akageuza gari na kuendesha kwa mwendo mdogo mpaka usawa wa dirisha la gari aliyomo Don Angelo, Kamanda Amata akashusha kioo taratibu na kumtazama Don Angelo, wakakutana macho, akiinua fimbo yake na kuiweka dirishani ncha yake ikimtazama Don.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Na sasa ni zamu yako kama nilivyokuahidi,” akamwambia kwa sauti ambayo ilimfikia bila kikwazo.

    Don Angelo akakodoa macho, akahisi koo limemkauka ghafla, akameza fundo kubwa la mate huku macho yamemtoka kama anameza jiwe, kufumba na kufumbua kitu kama msumari kikatua katika paji la uso na kufanya jeraha dogo lililokuwa likichurizika damu. Don akabaki kakodoa macho uhai ukimwondoka bila hiyana.

    Scoba bakaondoa gari bila mtu yeyote kujua nini kimetokea.

    “Shiit, hiki ni nini Amata?”

    “Fimbo ya kutembelea,” akajibu.

    ‘Asante Bill Van Getgand kwa fimbo hii,’ akawaza na kutikisa kichwa huku kioo kikipanda juu taratibu.



    ††† MWISHO †††





0 comments:

Post a Comment

Blog