Simulizi : The Last Summer In Tanzania
Sehemu Ya Pili (2)
Kamera ndogo za CCTV ziliendelea kufanya kazi kila siku, wanachuo waliendelea kufanya yao pasipo kugundua kwamba asilimia tisini ya mambo waliyokuwa wakiyafanya chuoni serikali ilikuwa ikiyafuatilia.
Gideon, kijana aliyekuwa na akili kushinda wanachuo wote chuoni hapo hakujua kitu chochote kilichokuwa kikiendelea, ndani ya jengo kubwa la TISS, walikuwa wameweka umakini katika kukifuatilia chuo hicho kila siku.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mmm!”
“Nini?”
“Hivi huyu jamaa ni kipofu kweli?’
“Kwa nini umeuliza hivyo?”
“Kuna jambo lmetokea, nahisi kuna kitu.”
“Jambo gani?”
“Alikuwa akishuka ngazi vizuri bila kuweka fimbo yake, watu walipotokea, ghafla akabadilika na kuitanguliza fimbo yake.”
“Hahaha! Acha masihara bwana, huyu jamaa ni kipofu toka mwaka jana alipokuja ndani ya chuo hicho, halafu kingine, vipofu wote duniani huwa na hisia, anaweza akasikia sauti yako tu, akajua kwamba wewe mzuri au mbaya,”
Hayo yalikuwa mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya jengo hilo kubwa la upelelezi Tanzania. Mfuatiliaji aliyekuwa mbele ya kompyuta alikuwa akimwambia mwenzake aliyekuwa naye ndani ya chumba hicho juu ya Gideon aliyeonekana kufanya kitu cha tofauti.
Ilikuwa ni usiku na chuoni hakukuwa na watu wengi na hata wale waliokuwepo chuoni hapo, walikuwa bwenini mwao wamelala. Huo ndiyo muda ambao Gideon alionekana kuwa tofauti, wakati alipokuwa akishuka ngazi, alishuka ngazi kadhaa bila kutanguliza fimbo yake lakini mara baada ya kusikia wanachuo fulani wakija kule alipokuwa, akaichukua fimbo yake na kuendelea na mchezo wa kupapapasa.
Hilo lilimtia shaka mfuatiliaji mmoja, akalichukua suala hilo na kuwafikishia viongozi wa juu ambao nao wakaungana naye na kuanza kumchunguza Gideon.
Kwa muda wa mwezi mzima, waliendelea kumfuatilia kwa kumrekodi na kisha baadae kumtazama kwenye mikanda yao, lakini hawakuambulia kitu, dalili zote zilionyesha kwamba kijana huyo alikuwa kipofu.
“Au uliona vibaya?”
“Hapana, sikuona vibaya, nilikuwa makini.”
“Ilikuwa tarehe ngapi vile?”
“25 mwezi uliopita.”
“Hebu tafuta mkanda wa siku hiyo.”
Agizo likatolewa na Materu, mkanda wa siku hiyo ukatafutwa kwa lengo la kuangalia tukio lililotokea siku hiyo usiku. Kama alivyosema kijana yule, kilionekana kitu kilekile kwamba Gideon alifanya kama maelezo ya kijana yule yalivyosema.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Inabidi tulichukulie suala hili kwa ukaribu zaidi,” alisema Materu.
Kumchunguza kwa mwezi mzima haukutosha, walichokifanya, wakawaandaa wanachuo wao na kuwapeleka chuoni hapo kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi wao juu ya upofu wa Gideon.
Wanachuo hao walijitahidi kuwa karibu naye huku wakiwa makini kutokuweza kugundulika lakini mwisho wa siku, nao wakachemka na ripoti zao zikaonyesha kwamba Gideon alikuwa kipofu kwa asilimia mia moja.
“Basi tuseme kwamba siku ile Mungu alitaka kufanya muujiza wake, tuendeleeni na mambo yetu,” alisema Materu na maisha kuendelea kama kawaida.
Miezi ikaendelea kukatika, chuoni kukawa na amani, siku ambayo tangazo lilitolewa kwamba mjasiriamali mkubwa duniani, bwana Potter Mickey angekuja chuoni hapo kwa ajili ya kufundisha masomo ya ujasiriamali, hakukuwa na mtu aliyekuwa na wasiwasi kabisa.
Siku ya tukio hilo la mauaji lilipokuwa likitokea, kamera zao za CCTV zilimuonyesha Gideon akaelekea porini huku akiwa amevaa begi lake kubwa, kofia na fulana yake na huku mkononi akiwa na fimbo.
Wafuatiliaji wale waliokuwa kwenye kompyuta ndani ya jengo la TISS walibaki wakimwangalia, hawakujua porini kule alikuwa akienda kufanya kitu gani. Wala haikuchukua dakika nyingi, ghafla ukasikika mlio wa risasi, watu wakaanza kukimbia, Gideon ambaye aliingia porini, naye akatoka na kuanza kukimbia huku akiwa na begi lake mgongoni na alionekana kuwa na wasiwasi mwingi mno.
Hapo ndipo ilipogundulika kwamba Gideon ndiye aliyefanya mauaji yale, hakukuwa na mtu aliyefahamu sababu ya mtu huyo kumuua bwana Mickey. Maswali mengi yakaanza kumiminika vichwani mwao juu ya sababu ya Gideon kumuua mjasiriamali yule lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa na jibu.
Mbali na kitu hicho, wakaanza kujiuliza maswali kuhusu upofu wa Gideon, waliwatuma watu wengi kumchunguza na majibu yakaonyesha kwamba alikuwa kipofu na hata wao walipojaribu kuchunguza kwa makini kupitia kamera zao, majibu yalikuwa yaleyale, Gideon alikuwa kipofu.
Kitu kilichobaki ambacho kilitakiwa kufanyika ni kumfuata Gideon chuoni, kumkamata kisha kumpeleka katika vyombo vya sheria ambapo huko, ukweli wote ungejulikana. Martin akatumwa kwa kazi hiyo.
****
Martin akafika chuoni hapo, moja kwa moja akaelekea katika ofisi ya Professa Mitimingi na kuomba kuzungumza naye kwani alikuwa na kitu muhimu alihitaji kukaa naye chini na kuongea.
Kwa sababu alikwishajitambulisha kipindi cha nyuma, hiyo wala haikuwa tatizo, akamkaribisha na kuanza kuzungumza. Alianzia mbali lakini mwisho wa siku akaamua kumwambia kile kilichokuwa kimemleta ofisini hapo.
“Ninataka kuonana na Gideon,” alisema Martin.
“Gideon yupi? Wapo wengi hapa,” aliuliza Professa.
“Gideon Mutinyama,” alisema Martin.
Hilo wala halikuwa tatizo, alichokifanya Professa ni kunyanyua simu yake na kisha kumpigia mtu wa upande wa pili na ndani ya dakika ishirini, mwanachuo mmoja akaanza kugonga mlango huo na kumruhusu kuingia.
“Gideon hayupo, hatujui amekwenda wapi,” alisema mwanachuo huyo.
“Mmejaribu kumwangalia sehemu zote?” aliuliza Martin.
“Ndiyo! Ila tumemkosa.”
“Hebu twende katika bweni lake,” alisema Martin.
Professa Mitimingi akahisi kwamba kulikuwa na tatizo limetokea japokuwa hakutaka kuwekwa wazi, alichokifanya, naye akainuka kutoka katika kiti chake na kuanza kuelekea huko pamoja nao.
Walikwenda mpaka katika bweni alilokuwa akiishi Gideon katika ghorofa ya tano, walipofika huko, waliangalia katika kila sehemu, hawakumuona. Hapo, Martin akapata uhakika kwamba kile kilichokuwa kimezungumziwa kilikuwa ukweli mtu kwamba Gideon alikuwa amehusika katika mauaji ya bwana Potter Mickey.
Wanachuo wengine wakabaki wakiwaangalia, halikuwa jambo rahisi kwa Professa mkuu kuingia katika mabweni kwa ajili ya kumtafuta mwanachuo fulani, walijua kulikuwa na tatizo.
Waliendelea kumtafuta ndani ya bweni hilo tena kwenye kila chumba lakini Gideon hakuwepo. Wakaamua kuwauliza wanafunzi wengine waliokuwa wakiishi ndani ya chumba hicho.
“Gideon yupo wapi?” aliuliza Professa Mitimingi.
“Sikumuona tangu jana, nahisi atakuwa amekwenda kuwatembelea ndugu zake,” alisema mwanachuo mmoja.
“Hakuna aliyemuona baada ya jana?”
“Mara ya mwisho kumuona ilikuwa juzi, baada ya hapo sikuona tena,” alisema mwanachuo mwingine.
Martin aliendelea kujipa uhakika kwamba ripoti iliyokuwa imetolewa kwamba Gideon alikuwa amehusika katika mauaji hayo ilikuwa sahihi kwani hakuwa akionekana katika kila kona, alipotea katika mazingira ya kutatanisha mno.
Hawakukata tamaa, waliendelea kumtafuta kwa kumuulizia lakini majibu yalikuwa ni yaleyale kwamba hakuonekana sehemu nyingine yoyote toka juzi.
“Mbona umekuja na kuanza kumtafuta Gideon, kuna nini?” aliuliza Professa Mitimingi.
“Hakuna kitu, subiri, tukimpata, utajua kila kitu,” alisema Martin, hakutaka kuendelea kubaki ofisini hapo, alichokifanya ni kuondoka.
Hapo kichwa chake kikaanza kugonga, hakuamini kama alikuwa ameshindwa kabisa kumpata Gideon, mwanafunzi aliyeaminika kuwa kipofu chuoni hapo. Aliingia ndani ya gari lake na kuanza kujifikiria, hakujua ni wapi alitakiwa kuanza, kitendo cha kumkosa mtu huyo kilimaanisha kwamba asingeweza kumpata tena.
Huku akiwa amekwishaliwasha gari lake kwa ajili ya kuondoka chuoni hapo, akaonekana kukumbuka kitu ambacho ilikuwa ni lazima kuulizia ili apate kujua ni wapi alitakiwa kuanzia.
Alichokifanya ni kuzima gari lake, akateremka na kuanza kurudi katika ofisi ya Professa Mitimingi, akagonga mlango, aliporuhusiwa, akaingia ndani.
“Ninataka kufahamu Gideon alitoka wapi,” alisema Martin.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Alitoka nchini Malawi.”
“Una uhakika?”
“Nahisi nina uhakika kwa sababu nyaraka zake zote zilionyesha kwamba alitokea nchini humo.”
“Kuna kitu kingine kinachoweza kukupa uhakika kwamba alitokea nchini humo?”
“Hapana zaidi ya hizo nyaraka.”
“Ni nani aliyekuwa rafiki yake wa karibu hapa chuoni?”
“Kuna msichana anaitwa Juliet, huyu ndiye niliyekuwa nikisikia kwamba alikuwa karibu na kipofu yule,” alisema Professa Mitimingi.
“Ninahitaji kumuona pia.”
“Sawa.”
Walichokifanya ni kuondoka ndani ya ofisi hiyo, japokuwa Professa Mitimingi alitaka kupiga simu, akazuiliwa na hivyo kutakiwa kumuona ana kwa ana kwa sababu Martin alikuwa na maswali mengi yaliyotakiwa kujibiwa na msichana huyo.
Walipofika katika bweni alilokuwa akiishi Juliet, wakaomba kuonana naye, hilo halikuwa tatizo, baada ya dakika mbili, msichana huyo alikuwa mbele yao ambapo wakamchukua na kuelekea naye chini.
“Unamfahamu vipi Gideon?”
“Alikuwa rafiki yangu,” alijibu Juliet.
“Hakuwahi kuwa mpenzi wako?”
“Hapana, alikataa hilo.”
“Unahisi kwa nini alikataa?”
“Hata mimi sifahamu.”
“Si kwa sababu alikwambia wewe siyo mzuri?”
“Hapana. Kila siku alikuwa akinisifia kwamba mimi ni mzuri lakini kila nilipotaka kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi, alikataa.”
“Unahisi kwa nini?”
“Sijajua kwa kweli.”
“Mara yako ya mwisho kumuona ilikuwa lini?”
“Toka juzi.”
“Ulijaribu kumtafuta simuni?”
“Nilifanya hivyo mara kadhaa lakini sikumpata.”
“Unaamini kwamba Gideon alikuwa kipofu?”
“Yaap! Naamini hilo.”
“Kipi kinachokufanya kuamini?”
“Macho yake, hakuna hii mboni nyeusi, jicho zima lilikuwa jeupe, pia matendo yake, alikuwa kipofu asilimia mia moja.”
“Sawa. Hivi ulishawahi kuishika hata simu yake?”
“Hapana! Alikuwa mgumu kukubali, na hata laptop yake alikuwa akiificha sana, hakutaka mtu mwingine yeyote aiwashe,” alisema Juliet.
“Sawa! Kwa hiyo unataka kuniambia haujui mahali alipo kwa sasa?”
“Ndiyo! Wala sifahamu!”
“Nashukuru!”
Siku hiyo, kila kitu alichokuwa akitaka kukifahamu, alikifahamu, alipoona kwamba ameridhika, akaondoka ofisini hapo huku akiwa na mipango mingi ya kufanya kuringana na maelezo yale aliyokuwa ameyasikia kutoka kwa watu wawili aliokuwa amezungumza nao.
Alipofika makao makuu, akaitwa katika chumba maalumu cha mikutano na kuulizwa kile kilichokuwa kimetokea, kwa maelezo waliyokuwa wameyatoa watu wale aliokwenda kuwahoji. Mbele yake kulikuwa na wakuu wake watano, akaanza kuelezea kila kitu kilichokuwa kimetokea.
“Kuna kitu hapa, nimeanza kuhisi kitu,” alisema Materu.
“Kitu gani?”
“Huyu mtu ametumwa!”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Nahisi tu, lakini subiri, ili hisia zetu zikamilike, nadhani tunatakiwa kumtafuta mpaka apatikane.”
“Atakuwa wapi sasa? Amerudi nchini kwake?”
“Inawezekana, lakini je, tunajua anapoishi? Tumesikia kwamba ni Malawi, kuna uhakika wowote kwamba nchini kwake ni Malawi?” aliuliza Ibrahim, mmoja wa wakuu katika Kitengo cha TISS.
“Hapo ndipo kwenye wakati mgumu, cha msingi tunapaswa kutuma watu wawili wa kufanya kazi hii, ni lazima wasafiri haraka iwezekanavyo kuelekea nchini Malawi, twende tukajaribu, nina uhakika tutampata tu,” alisema Ibrahim na kuendelea:
“Wa kwanza awe huyu Martin, wa pili nafikiri awe Mathias Jonathan, mnaonaje?” aliuliza Ibrahim.
“Haina tatizo. Tutawatuma waende huko, wahakikishe kwamba anapatikana,” alisema Materu.
“Na watakwenda kivipi?”
“Tutamfanya Martin awe kichaa, nafikiri ataweza hilo. Atakwenda katika Jiji la Lilongwe, huko atakuwa kichaa kwa muda wote mpaka Gideon atakapopatikana, wakati huohuo, Mathias atakuwa mfanyabaishara mkubwa wa madini, atakuwa akipenda sana starehe kuliko kitu kingine, kazi yake itakuwa ni kutumia fedha tu katika sehemu mbalimbali nchini humo.
“Kwa Martin, mara kwa mara tutakuwa tukimtuma mtu kwa ajili ya kumpelekea chakula pale alipokuwa, staili ya kumpa chakula ni kwamba kuna mfuko wa chakula utakuwa ukitupwa jalalani, atakuwa akiufuata na kukila chakula hicho, kila siku usiku itakuwa ni lazima kutoa ripoti amefikia wapi, kuna mengi yatajulikana, tuvuteni subira,” alisema Ibrahim, mmoja wa viongozi aliyekuwa na uwezo mkubwa wa kufikiria kuliko wengine.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Hilo wala halikuwa tatizo, taarifa zikasambazwa kwa watu wote ambao walitakiwa kujua ni kitu gani kilichokuwa kikitakiwa kufanyika, baada ya hapo, maandalizi yakawekwa tayari na watu waliotakiwa kufuatilia ishu hiyo, Martin na Mathias kuondoka nchini Tanzania kuelekea Malawi kwa ajili ya kuanza kazi yao mara moja. Japokuwa kwa mtazamo ilionekana kuwa kazi ngumu lakini kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba iwe isiwe ni lazima Gideon apatikane na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Kilikuwa ni kipindi cha baridi kali ndani ya Jiji la Lilongwe nchini Malawi, watu wote waliokuwa wakionekana mitaani, walikuwa na masweta au makoti makubwa kwa ajili ya kuzuia baridi hilo.
Hakikuwa kipindi kizuri kwa sababu wakazi wengi waliugua magonjwa mengi kama vichomi vilivyowapa wakati mgumu nyakati za usiku.
Wafanyabiashara ambao kwa Tanzania walijulikana kama Wamachinga, walikuwa wakiendelea na kutembeza bidhaa zao, kwa wakati huo hawakutembeza fulana nyepesinyepesi bali bidhaa kubwa waliyokuwa wakiitembeza ilikuwa ni makoti makubwa au masweta na huku wakati mwingine miamvuli, hasa pale walipoona kwa siku nzima manyunyu ya mvua yalikuwa yakidondoka.
Wakati wa mchana, hakukuwa na watu wengi mitaani, wengi walikuwa wakishinda ndani kutokana na baridi kali huku kwa nyakati za usiku, bila kuhofia kitu chochote kile, kila mtu alikuwa akiwasha moto nje ya nyumba yake na kisha kuanza kuota huku akiwa na shuka kubwa lililoufunika mwili wake.
Mishemishe ndani ya Jiji la Lilongwe zilipungua, si watu wengi waliokuwa wakizunguka huku na kule zaidi ya walevi waliokuwa wakirudi nyumbani kwao nyakati za usiku, walikuwa wakitembea kwa kuyumbayumba mpaka katika milango ya nyumba zao na kuingia ndani.
Katika kipindi hiki cha baridi kali, ndipo alipoanza kuonekana kichaa mmoja aliyekuwa akizurura hovyo ndani ya jiji hilo kiasi kwamba kila mtu akaanza kujiuliza juu ya kichaa huyo aliyeonekana kuwa na hasira kupita kawaida.
Kila wakati alikuwa na nguo zilizochakaa, mkononi alikuwa na fimbo huku nywele zake zikiwa timtim. Hakuonekana kuwa na masihara, kila mtu ambaye alipita karibu yake, alikuwa akimchapa kwa fimbo, na kama hakuwa na fimbo, alikuwa akikuvamia na kukupiga.
Watu wakaanza kumuogopa, hakuwa na makazi yoyote yale, kila siku alikuwa akilala barabarani huku muda wake mwingi wa mchana akitumia kushinda katika jalala kubwa lililokuwa pembezoni mwa Jiji la Lilongwe.
Kichaa huyo akaanza kupata umaarufu, alikuwa akizurura hovyo katika kila kona ya jiji hilo huku akiongea peke yake, kila wakati alikuwa akijikuna mwili wake uliokuwa ukiwasha mno na wakati mwingine kulala barabarani huku magari yakiendelea kupita.
Hakukuwa na mtu aliyejua historia kuhusu kichaa huyo ambaye kila siku alikuwa akikatiza huku na kule na makazi yake makubwa kuwa katika Jalala la Mabuya lililokuwa pembezoni kidogo mwa jiji hilo.
Upatikanaji wa kichaa huyo katika jiji hilo ikaonekana kuwa kero hivyo watu kuanza kuilalamikia Mamlaka ya Jiji kwa kuruhusu kichaa kama huyo kukaa mjini na wakati kulikuwa na wageni wengi waliokuwa wakifika kutoka nje ya nchi hasa Bara la Ulaya na Marekani.
Hapo ndipo mamlaka hiyo ilipoamua kuwakusanya vijana maalumu kwa ajili ya kazi moja ya kumkamata na kumpeleka katika hospitali iliyokuwa ikihifadhi vichaa wengine kama alivyokuwa yeye.
Kumkamata haikuwa kazi kubwa, japokuwa walikuwa vijana sita, lakini kila walipokuwa wakimsogelea, walichapwa fimbo na kupigwa ngumi. Alionekana kuwa kichaa lakini kwa jinsi alivyokuwa akipigana, ilionyesha kwamba kabla ya kuwa katika hali hiyo alipitia mafunzo ya mapigano.
Siku hiyo, wakashindwa kumkamata na hivyo kupanga siku nyingine. Siku iliyopangwa ilipofika, wakakusanyika tena, walikuwa zaidi ya watu kumi, walipomsogelea, kama kawaida walipokea mkong’oto na kuondoka.
Sifa za kichaa huyo zikaanza kutapakaa, asilimia kubwa ya wakazi waliokuwa wakikaa katika Jiji hilo lenye watu zaidi ya laki sita, walimfahamu kichaa huyo aliyekuwa na nguvu za ajabu zilizomuogopesha kila mtu.
Kila siku jioni, alikuwa akilisogelea jalala la Mabuya na kuokota chakula na kuanza kula. Hakukuwa na aliyejua kwamba yule kichaa waliyekuwa wakimwangalia, hakuwa kichaa kama walivyodhania bali alikuwa mpelelezi aliyekwenda kwa ajili ya kukamilisha kazi moja tu, kumkamata Gideon ambaye mara ya mwisho aliiona picha yake nchini Tanzania lakini bado aliendelea kumkumbuka vilivyo.
****
Bado watu hawakuwa wakiamini kile kilichokuwa kimetokea, hawakuamini kama mjasiriamali waliyekuwa wakimhusudu, Potter Mickey alikuwa ameuawa kwa kupigwa risasi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nchini Tanzania.
Watu waliokuwa wakiyafuatilia mafundisho yake na hata wale waliokuwa wamepiga hatua baada ya kufundishwa namna ya kujiingizia kipato, kuibadilisha dola moja kuwa bilioni, hawakuweza kuvumilia, walijikuta wakianza kububujikwa na machozi, kile kilichotokea, kwao ilionekana kama ndoto.
Mwili wake ukasafirishwa na kupelekwa nchini Marekani katika Jiji la Florida alipokuwa akiishi. Katika mazishi hayo, watu waliohudhuria walikuwa wale waliopewa mualiko maalumu kama ilivyokuwa kwa masupastaa wengi nchini humo.
Walikuja viongozi mbalimbali wa serikali, matajiri kutoka nchi mbalimbali zikiwemo za Uarabuni na watu wengine maarufu kama wanamuziki walikuwa walikusanyika katika mazishi ya bwana Mickey.
Saa 10:30 jioni, magari matano ya kifahari yakaanza kuelekea katika Makaburi ya St. Andrew Square na mwili wake kuzikwa katika makaburi hayo.
"Pumzika kwa amani baba" alijisemea Victor huku machozi yakimbubujika mashavuni mwake.
Msiba huo ulipomalizika, Victor hakutaka kuendelea kukaa nchini Marekani, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea nchini Uingereza katika Jiji la Liverpool kwa ajili ya kuonana na rafiki wa siku nyingi wa baba yake ambaye aliwahi kufanya kazi kama mpelelezi wa SIS (Secret Intelligence Service) kabla ya kustaafu, Edward Simpson.
Alipofika huko, kitu cha kwanza kabisa akataka kuonana naye faragha, hilo halikuwa tatizo, wakapanga siku ya kuonana na mahali, baada ya siku kadhaa, wakakutana katika Hoteli ya The Prince iliyokuwa katikati ya Jiji la Liverpool.
“Nikusaidie nini rafiki wangu wa siku nyingi?" aliuliza bwana Simpson.
“Baba yangu aliuawa wiki iliyopita" alisema Victor.
“Pole sana. Nilisoma magazetini, baba yako alikuwa mtu mwema, mcheshi, alikuwa baba mzuri na mtu wa karibu pia, polisi wamesemaje?" alisema na kuuliza bwana Simpson.
“Walituambia tusubiri, lakini huwa siziamini serikali za watu weusi, hasahasa serikali za kiafrika" alisema Victor.
“Kwa hiyo nikusaidie nini?"
“Nataka kufahamu ni nani aliyemuua baba yangu."
“Sawa! Nitakusaidia," alisema bwana Simpson.
Walizungumza mambo mengi siku hiyo, bwana Simpson alikuwa amestaafu kitambo kufanya kazi kama mpelelezi chini ya Shirika la Kijasusi la nchini Uingereza, SIS lakini kitendo cha Victor kumfuata na kumuomba msaada wa hali na mali, hakuwa na jinsi, alikubaliana naye.
Akamuahidi kwamba kila kitu kingefanyika na hata kama ilitakiwa kusafiri basi angesafiri na kwenda nchini Tanzania kwa ajili ya kuanza kazi yake na hatimae muuaji kupatikana ndani ya kipindi kifupi.
Victor akashukuru na hivyo kuagana naye na kumuahidi kwamba angemsaidia baada ya kumpa maelekezo ya kufika nchini humo kirahisi na pia kumwambia sehemu chuo hicho kilipo, kazi ingefanyika bila wasiwasi wowote ule.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Huyu jamaa ana hela za kufa mtu.”
“Jamaa gani?”
“Bilionea Kijana.”
“Ndiye nani.”
“Kuna jamaa alikuja jana usiku, alinunulia pombe klabu yote.”
“Acha utani!”
“Kweli tena, yaani ni balaa aisee! Jana aliingia hapo Sweat Garden, akawanunulia pombe watu wote waliokuwa ndani ya klabu ile, akawaambia wanywe mpaka wasaze, yaani kila mtu akapigwa na butwaa.”
“Mmmh!”
“Unashangaa! Kwanza umeiona hiyo gari anayotembelea?”
“Hapana! Ipo vipi?”
“Lamboghin!”
“Unasemaje?”
“Anatumia Lamboghin yenye rangi nyekundu! Ni balaa. Ukiachana na usafiri huo, jamaa anapiga pamba za kufa mtu, yaani ni hatari, wenye mademu zetu wakali wenye tamaa, hapana, huyu jamaa anaweza akawachukua!”
“Kwani huyo jamaa yupo vipi?”
“Kwa mtazamo ni wa kawaida tu.”
“Katokea wapi sasa?”
“Hata sisi wenyewe hatujui, jana tu alivamia ghafla klabu na kuanza kutupiga pombe, ukisema katokea wapi, wala hatufahamu.”
“Na gari lake ulilionaje?”
“Si unajua sisi wapambe bhana! Tulitoka kuangalia usafiri wake, ni noma sana,”
Mathias alikuwa ameharibu hali ya hewa ndani ya Klabu ya Sweat Garden iliyokuwa katikati ya Jiji la Lilongwe, kitendo chake cha kuingia ndani ya klabu hiyo huku akiwapa watu ofa ya kunywa pombe kadiri walivyotaka, kiliwapagawisha walevi wote kiasi kwamba akaanza kuonekana muhimu katika ukumbi huo.
Usiku huyo, walevi walipombeka kupita kawaida, wale waliotaka kubeba, walipewa nafasi hiyo japokuwa hawakuweza kufanya hivyo. Mbali na kugawa pombe kwa kila mtu aliyekuwepo ndani klabu hiyo, wakati alipokuwa akiondoka, wapambe walioamua kumsindikiza huku wakiimba ‘Young Bilionaire...Young Bilionaire...” walipigwa na mshtuko baada ya kuona gari la kisasa aina ya Lamboghin yenye thamani ya shilingi milioni mia nane ikiwa imepaki, Mathias akaingia na kuondoka zake.
Hiyo ndiyo ilikuwa stori ya jiji, kila aliyekuwa ameona tukio la siku hiyo, aliisambaza taarifa hiyo kwa watu ambao hawakuwepo katika klabu hiyo usiku huo. Jina la Young Bilionaire likaanza kuvuma, wale ambao hawakuwepo ndani ya klabu hiyo usiku huo wakatamani masaa yarudi nyuma ili waweze kuwepo.
Mitandaoni, alitawala Young Bilionaire, kila mtu alitaka kumuona, maelezo yaliyokuwa yakitolewa kwamba jamaa alikuwa na pesa chafu yalimpagawisha kila mmoja jijini Lilongwe.
Mathias hakutaka kuishia hapo, kwa sababu alikwishaambiwa kwamba angetumia kiasi chochote cha fedha, alizitumia huku malengo yake yakiwa kwenye kufanikisha kile alichokuwa ametumwa, kumpata Gideon na kumfikisha katika vyombo vya sheria.
Kila siku usiku Mathias alikuwa akifika katika klabu hiyohiyo na kuanza kuzitumia, watu wote waliokuwa wakikusanyika katika klabu hiyo wakaanza kumpatia jina la Young Bilionaire na kuwa jina lake rasmi.
Wanawake hawakutaka kupitwa, kwa kuwa mbele yao alionekana mwanaume aliyekuwa na fedha za kumwaga, nao wakaanza kujilengesha kwa kutaka kula naye maisha.
Sifa za Young Bilionaire ziliendelea kusikika kila kona, hakuwa mchoyo, kila aliyetaka fedha alipewa bila kinyongo chochote kile. Kila alipoingia baa au klabu, alikuwa na kipaza sauti kidogo ambacho hakikuweza kuonekana, hicho alikuwa akikificha sana kwa ajili ya kurekodia mawasiliano yoyote ambayo angefanya na mtu yeyote yule.
Fedha zake ‘zilitisha’ kiasi kwamba watu wakaanza kufanya uchunguzi ili kuona hizo fedha zilitokea wapi, alizipata wapi mpaka kuanza kuzitumia pasipo kuzionea huruma. Walipochunguza, tena kwa kina, wakagundua kwamba Young Bilionaire alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa madini, alikuwa akisafirisha madini ya Tanzanite kutoka Tanzania na kwenda sehemu nyingine barani Afrika.
“Utaendelea kujifanya mfanyabiashara wa madini, najua kuna mengi tutakuja kuyafahamu, wewe endelea kufuatilia,” ilisikika sauti ya bwana Materu simuni.
“Hakuna tatizo mkuu.”
“Na Martin unaonana naye?”
“Ndiyo! Huwa nipo naye karibu sana na ni mara chache ninapeana naye ishara za macho hasa mchana ambao watu hawagundui kwamba yule bilionea wa usiku ndiye mimi,” alisema Mathias.
“Safi sana! Acha nikuache upumzike, endeleeni kuchunguza, hata kama itawachukua miaka mitano, haina jinsi, pambaneni mpaka apatikane, na ninawahakikishia kwamba baada ya kufanikiwa, mtapata chochote mkitakacho,” alisema Materu.
“Hakuna tatizo bosi.”
Bado uchunguzi wa kimyakimya ulikuwa ukiendelea, hakukuwa na mtu yeyote aliyegundua kwamba yule kichaa aliyekuwa barabarani ambaye alishika sana hisia za watu na huyu mtumiaji mkubwa wa fedha katika klabu mbalimbali walikuwa watu wawili waliofahamiana ambao walifanya kazi kwa kificho huku wakiendelea kumtafuta mtu waliyetumwa kumtafuta.
Siku ziliendelea kukatika, jina la Young Bilionaire likawa kubwa katika Jiji lote la Lilongwe, matajiri waliokuwa wakitanua na fedha zao kwa kuchukua wanawake wazuri na kuwahonga wakawa wakimuogopa mno Mathias ambaye kama kawaida jina lake hilo la Young Bilionaire ndilo lililokuwa likijulikana zaidi.
“Unajua bosi mpaka sasa hivi sijajua unaitwa nani, mbali na hili la Young Bilionaire,” alisema jamaa mmoja, huyu aliitwa Oswald, kwa kipindi kirefu alijitahidi kujenga urafiki na Mathias, mwisho wa siku akafanikiwa na yeye kuanza kutumbua fedha ambazo hazikuwa na kikomo.
“Naitwa Kenneth Mutahaba, mimi ndiye mmiliki wa migodi zaidi ya mitano Tanzania,” alisema Mathias.
“Daaah! Unajua umewateka sana watu wa hapa mjini, kuna mtu nataka nikutambulishe kwake.”
“Mtu gani?”
“Dada mmoja hivi, hiyo ni mashine balaa, aliwahi kuwa Miss Malawi kabla ya kuanza kuwa muigizaji,” alisema Oswald.
“Yupo vipi?”
“Ni mkali sana, anaitwa Rebecca. Anavutia, wenye fedha wamejaribu kumfuata, mtoto kawakatalia.”
“Kweli?”
“Siwezi kukudanganya!”
“Basi sawa, wewe muite tu. Hela zipo ila watumiaji wamekosekana,” alisema Mathias.
Hilo halikuonekana kuwa tatizo hata mara moja, kwa kuwa yeye mwenyewe alijua kwamba angeweza kupata kitu chochote kile, akafanya mawasiliano na msichana huyo na kumuita katika nyumba aliyokuwa akiishi Mathias.
Baada ya masaa mawili, honi zilisikika nje ya nyumba hiyo na mlinzi alipofungua geti kuchungulia, macho yake yakatua katika gari la mrembo Rebecca. Kwa kuwa alikwishaambiwa kuhusu msichana huyo, akafungua geti na gari kuingizwa.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Maneno ya Oswald yalikuwa sahihi, muonekano wa msichana huyo ulikuwa balaa, alikuwa mrefu, hipsi zake zilionekana vema machoni mwa kila aliyemwangalia, alikuwa na mapaja manene huku ngozi yake nyeupe ikimpendezesha zaidi.
Mbali na umbo zuri alilokuwa nalo, Rebecca alikuwa amejaaliwa kuwa na sura nzuri, kila aliyemwangalia, sura yake ilimvutia kiasi kwamba akapewa jina la Barbie, ile midoli ya watoto inayoongoza kwa uzuri.
Kila alipokuwa, akitikisa, watu wengi walijaribu bahati zao kwa msichana huyo lakini hakukuwa na yeyote aliyepata bahati jambo lililomshangaza kila mtu. Hakuwa na fedha nyingi lakini aliwakataa watu wenye fedha hali iliyowafanya wasichana wengi kumshangaa.
Pamoja na uzuri wote aliokuwa nao, mvuto wote uliowapagawisha wanaume, aliposikia tu kuhusu Mtanzania aliyeitwa Young Billionaire, akaanza kuvutiwa naye, akahisi moyo wake ukianza kutekwa na mtu huyo hata kabla hajamuona.
Kitu pekee alichokuwa akikihitaji ni kuwa na mwanaume huyo huku kiu yake kubwa ikiwa ni kwenda nchini Tanzania na kukutana na msichana ambaye kila siku alimuona kuwa ‘Role Model’ wake, Wema Sepetu aliyekuwa akitikisa na filamu zake alizoigiza na Steven Kanumba ambazo zilitazamwa sana nchini Malawi.
Macho ya Mathias yalipotua kwa Rebecca akaonyesha mshtuko wa waziwazi, hakuamini kama hapa Afrika angeweza kukutana na msichana mrembo kama alivyokuwa Rebecca, alibaki akimwangalia kwa umakini kana kwamba alikuwa akimchunguza.
Msichana huyo akatoa tabasamu pana lilioonyesha kila kitu kwamba alikuwa tayari kwa lolote na ni Mathias ndiye aliyekuwa akisubiriwa kuzungumza kitu chochote alichotaka kuzungumza.
Hakutaka kueendelea kukaa kochini na wakati aliingia msichana mrembo kama alivyokuwa Rebecca, akajikuta akisimama, akianza kupiga hatua kumsogelea, alipomfikia, huku akijifanya kuwa na heshima kubwa, akamsalimia kiustaarabu na tabasamu pana akiliachia usoni mwake.
“You are welcome,” (Karibu) alisema Mathias huku akiachia tabasamu.
“Thank you.” (Nashukuru)
“Make yourself at home,” (Jisikie upo nyumbani)
“Thank you.” (Nashukuru)
Akili ya Mathias haikutulia hata kidogo, mara alikuwa akifanya hili mara lile, kila alipokuwa akimwangalia msichana huyo, alipagawa kupita kawaida. Alichokifanya ni kusimama na kulifuata friji, aliporudi, alikuwa na chupa ya pombe ya Amarula na kuiweka katika glasi.
“Wewe ndiye Amanda Posh?” aliuliza Mathias huku akichia tabasamu.
“Mmmh! Ndiye nani?”
“Yule msichana aliyekuwa akitembea na na muigizaji wa Marekani, Brad Pitt!”
“Hahaha! Hapana!”
“Mbona umefanna naye sana!”
“Kweli?”
“Ndiyo! Hakika Mungu anajua kuumba. Mara ya kwanza niliposikia kuhusu wewe, sikuamini hata kidogo, nikajua kwamba Oswald ananidanganya, ila sasa hivi, nimeamini, u mrembo sana!” alisema Mathias.
“Hahah! Acha utani wako bwana!”
“Kweli tena! Haki ya Mungu wewe mzuri!”
“Hivi ushawahi kwenda Keremeyi?”
“Hapana! Ndiyo wapi huko?” aliuliza Mathias, Rebecca akamgeukia Oswald.
“Hujawahi kumpeleka Young Bilionea Keremeyi?” aliuliza Rebecca.
“Hapana ila nilitaka kufanya hivyo. Uliponiambia kuhusu huyu jamaa, nikaona hakuna jinsi, hakukuwa na haja ya kwenda huko,” alisema Oswald.
“Jamani! Mbona mnanitenga! Huko Keremeyi ndiyo wapi?”
“Ni hapahapa Malawi, sehemu iliyokuwa na wanawake wengi wazuri, huko ndiyo watu wakubwa na wenye fedha kama nyie wanapokwenda. Kama unaniona mimi mrembo, hebu nenda huko, kaa hata kwa wiki moja, ukirudi, naomba uniambie tena kwamba mimi ni mzuri, sidhani kama utaweza,” alisema Rebecca.
“Hakuna kitu kama hicho, Rebecca, nimewahi kuona wanawake wengi warembo, nimewahi kutumia pesa na wanawake wengi warembo, ila ninakiri kwamba sikuwahi kuwa na msichana mzuri na mrembo kama ulivyo, niamini, wewe ni mrembo mno,” alisema Mathias.
Siku nzima alikuwa na kazi ya kuusifia uzuri wa msichana huyo, kila alipomwangalia, macho yake hayakuridhika, alitamani kumtazama zaidi na zaidi na hata kulala naye usiku huohuo ili aendelee kuwa karibu naye.
Alijijua kwamba ni mzuri, alijijua kwamba alikuwa na umbo zuri na mapaja yaliyovutia, kila wakati, alikuwa akibadilisha mikao, mara akae hivi, mara akae vile, mara mguu uje kwa juu staili ya kukunja nne, mara akae vile, yaani kila staili aliyokuwa akikaa kochini pale, Mathias alibaki hoi.
“Nilisikia kwamba unataka kuniona!” aliuliza Mathias.
“Ndiyo!”
“Kuna nini tena?”
“Nilihitaji ukaribu na wewe!”
“Ukaribu upi?”
“Wa urafiki tu.”
“Mmmh!”
“Nini tena?”
“Nitaweza kuwa rafiki na msichana mrembo kama wewe?”
“Kwa nini usiweze?”
“Hapana! Nafikiri naweza kushawishika kula tunda, haiwezekani simba kuwa rafiki wa swala, si unajua kuna kipindi cha ukame porini!” alisema Mathias.
Alijisahau kama alikwenda nchini Malawi kwa ajili ya kupeleleza mahali alipokuwa Gideon na kisha kumkamata na kumpeleka katika vyombo vya sheria, msichana aliyekuwa mbele yake, alimchanganya mno, alikuwa tayari kufanya kitu chochote lakini si kumkosa msichana huyo mrembo.
Hapo ndipo maneno ya Oswald yalipoanza kujirudia kwamba msichana huyo aliwakataa wanaume wengi, wale wenye fedha na hata wale waliokuwa maarufu, hakujua ni kwa sababu gani msichana huyo aliamua kumfuata yeye, kwa upande mwingine, alijiona kuokota embe chini ya mbuyu.
Siku hiyo ilikuwa ni ya kula bata tu, muonekano wa Mathias ulimpagawisha hata Rebecca mwenyewe. Ingawa alikuwa na sababu zake, lakini ukweli mwingine ni kwamba aliwapenda Watanzania, walikuwa wanaume wa tofauti kabisa na Wamalawi.
Wanaume wa kule, walikuwa wanywaji wa pombe wakubwa lakini pia hawakuwa walaji, walikuwa wakiishi tofauti na Watanzania ambao mara nyingi huwa wanakunywa na kula sana nyama, ila kwa Malawi, wanaume walikuwa tofauti na hivyo kupelekea ufanyaji wao wa tendo kitandani kuwa mdogo tofauti na Watanzania.
Kila alipokuwa akimwangalia Mathias, moyoni mwake alijihisi kumpenda kwa mapenzi ya dhati. Pasipo kutegemea wala kupanga, siku hiyo wakajikuta wakilala pamoja na kufanya mapenzi. Mathias alichukulia kila kitu kuwa kawaida, hakujua kwamba kukutana na msichana huyo, ilikuwa njiamojawapo ya kukamilisha upelelezi wake.
Usiku ukawa wa burudani!
**** CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Saa 6:15 usiku, ndege ya kubwa ya Shirika la KLM ilikuwa ikitua ndani ya Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere uliokuwa jijini Dar es Salaam. Mara baada ya ndege hiyo kusimama, abiria wakaanza kuteremka na miongoni mwa abiria hao alikuwepo bwana Simpson, mpelelezi aliyetumwa na Victor kwa ajili ya kumtafuta muuaji aliyemuua baba yake.
Alipoteremka, akaanza kuelekea katika sehemu ya kuchunguzia mizigo na kila kitu kilipokamilika, akachukua teksi ambayo ilimpeleka mpaka katika Hoteli ya Kilimanjaro.
Kichwa chake kilikuwa na mawazo, alijua fika kwamba mbele yake kulikuwa na kazi kubwa lakini pamoja na hayo yote, alihakikisha kwamba anaifanya kikamilifu kila hatua ili mwisho wa siku aje kufanikiwa kwani aliamini ilikuwa miongoni mwa kazi ngumu kuliko zote alizowahi kuzifanya maishani mwake.
Alipofika katika hoteli hiyo, akakabidhiwa chumba na maisha yake kuanza rasmi ndani ya hoteli hiyo. Japokuwa ilikuwa ni usiku sana, hakutaka kulala, alichokifanya ni kwenda kusimama dirishani na kisha kuanza kuangalia sehemu ya Jiji la Dar es Salaam.
Mandhari yake yalimfurahisha, aliporidhika, akaifuata brifukesi yake, akaifungua na kutoa laptop yake ndogo. Alichokuwa akitaka kukiona, ni baadhi ya kazi zake ambazo alizifanya katika kipindi cha nyuma.
Kompyuta ilikuwa na mafaili mengi, hasa ya kazi ambayo aliifanya kipindi cha nyuma alipotumwa nchini Iran, Syria na Libya, kote huko alikwenda kupeleleza na kazi yake ilipokamilika, alifanya mauaji yaliyomshangaza kila mtu pasipo kujua kwamba ni mpelelezi wa Uingereza ndiye aliyefanya hivyo.
Alijiamini kwa kila kitu, alijaribu kupitia faili moja baada ya jingine, alipomaliza, akachukua simu yake na kuanza kuyaingiza mafaili yake katika simu hiyo.
Alifika hapo huku akiwa hafahamu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kipo upande gani. Simu yake ndiyo ilikuwa msaada mkubwa kwa siku iliyofuata ndiyo ambayo ilimuongoza mpaka chuoni hapo ambapo akaomba kuonana na mkuu wa chuo, Professa Mitimingi.
“Who are you?” (Wewe ni nani?) aliuliza Professa Mitimingi huku akimwangalia Simpson kwa umakini.
“My name is Simpson from SIS” (Nitaitwa Simpson kutoka SIS) alijibu Simpson.
“What is it?” (Ndiyo nini hiyo?)
“Secret Intelligence Service.
“From United Kingdom, right?” (Kutoka Muungano wa Kingereza, sawa?)
“Yes!” (Ndiyo)
“What can I help you Simpson?” (Nikusaidie nini Simpson?)
Simpson akaanza kumuuliza kuhusu na mauaji yaliyokuwa yametokea wiki chache zilizopita, alihitaji kufahamu kila kitu kwani kulikuwa na kazi kubwa ambayo alitaka kuifanya, kazi ambayo aliamini hakukuwa na nchi yoyote ya Kiafrika ingeweza kuifanya.
Alichokifanya Professa Mitimingi ni kumpeleka katika eneo lililofanyika tukio hilo la mauaji. Simpson akasimama mahali pale, alianza kuangalia huku na kule, alionekana kama mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani.
“Mlisikia mlio wa risasi, si ndiyo?” aliuliza Simpson.
“Ndiyo!”
“Mlio wake ulifanana vipi?”
“Kama mlio fulani wa bomu, ulitoka kwa sauti kubwa.”
“Sawasawa. Muuaji alikuwa nani?”
“Wala sifahamu kwa kweli.”
“Umesema mlio wake ulisikika kama bomu?”
“Ndiyo!”
“Sawa, subiri.”
Alichokifanya bwana Simpson ni kuchukua simu yake na kuanza kuangalia vitu ambavyo hata Mitimingi hakuweza kuvifahamu, alibaki akimwangalia mpelelezi huyo, kwa muonekano alikuwa mtu makini sana ambaye hakuwa na masihala hata kidogo.
Kila alipokuwa akibonyeza simu yake, kuna kipindi alikuwa akikunja sura, kuna wakati mwingine alikuwa akiachia tabasamu, wakati mwingine alikuwa akihuzunika, kila hali ambayo binadamu wa kawaida alikuwa akiionyesha wakati anatazama tukio fulani.
“Hiyo ni bunduki ya kisasa, inaitwa Rifle, imetengenezwa nchini Urusi, ni bunduki hatari inayotumiwa na watu wenye mafunzo makubwa, ina uwezo wa kulenga umbali mrefu na hutoa mlio mkubwa endapo haikuwekwa kiwambo cha kuzuia mlio wa risasi.
“Ukiachana na AK-47 yaani Avtomat Kalashnikov iliyotengenzwa mwaka 1947 na mwanajeshi aitwaye Mikhail Kalashnikov, hii ni bunduki nyingine inayoongoza kwa kuua watu wengi duniani, ni bunduki hatari sana,” alisema bwana Simpson.
Siku hiyo ilikuwa kama darasa kwa Mitimingi, kila neno alilokuwa akilizungumza mpelelezi yule, lilikuwa somo kubwa kwake. Alizungumza mambo mengi huku akisisitiza kwamba alitaka kumfahamu mtu aliyefanya mauaji hayo.
Professa hakumwambia ila alichojaribu kukifafanua ni kwamba kuna watu walikuja na walimuulizia mtu mmoja aitwaye Gideon ambaye alisoma ndani ya chuo hicho na alikuwa mwanachuo kipofu mwenye uwezo mkubwa darasani.
“Basi! Ishia hapohapo!”
“Kwa nini?”
“Umesema ni kipofu na alikuwa na uwezo mkubwa darasani, si ndiyo?”
“Ndiyo!”
“Sawa, nashukuru! Bila shaka anatokea nchini Msumbiji!”
“Hapana! Alikuwa akitokea Malawi!”
“Usibishe, anatokea Msumbiji.”
“Wewe unajuaje na wakati haumfahamu?”
“Ni kipofu, mwenye uwezo mkubwa, inatosha, nishajua ni kitu gani kimetokea, kuna sababu kubwa ya bwana Mickey kuuawa, ni sababu ambayo hakuna mtu anayeweza kuifahamu. Sidhani kama natakiwa kukaa sana hapa, naomba niondoke,” alisema bwana Simpson.
“Mmmh! Sawa, hakuna tatizo.”
Bwana Simpson hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, alionekana kufahamu kila kitu kilichokuwa kimetokea, alichokifanya ni kuondoka chuoni hapo na kuelekea hotelini. Alionekana kuwa mtu mwenye mawazo lukuki, kila alipokuwa akikaa, alisonya kwa hasira huku wakati mwingine akijipigapiga mapajani.
Alipofika hotelini, kitu cha kwanza kabisa ni kuwasiliana na Victor kwani kulikuwa na mambo mengi ya kumwambia.
“Unajua baba yako alikuwa nani?” aliuliza Simpson.
“Kivipi?”
“Wasifu wake!”
“Alikuwa Mjasiriamali?”
“Hilo tu?”
“Ndiyo!”
“Basi haukuwa ukimfahamu baba yako. Usijisumbue kumtafuta muuaji, sijamfahamu muuaji ila sifa zake zinanifanya kugundua alitumwa na nani,” alisema Simpson.
“Naomba uniambie, baba yangu alikuwa nani.”
“Huwezi kujua, na hata mama yako hawezi kujua. Baba yako alikuwa mpelelezi wa CIA,” alisema Simpson.
“Unasemaje?”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Baba yako alikuwa CIA, alijifanya kuwa mjasiriamali kwa sababu alikuwa mpelelezi wa kimataifa, alisafiri nchi za Uarabuni si kwa sababu alikuwa mhamasishaji wa ujasiriamali, alisafiri kwenda huko kwa sababu alikuwa akifanya upelelezi kwani alikuwa chini ya CIA,” alisema Simpson.
“Mmmh!”
“Ndiyo hivyo! Na hata huyo mtu aliyemuua, alikuwa kama yeye.”
“Kivipi?”
“Na yeye ni mpelelezi kutoa CIA!”
“Unasemaje?”
“Ndiyo hivyo! Huyo jamaa anaitwa Jonathan Malumbu, mwanaume wa Kiafrika ambaye amekuwa akifanya oparesheni nyingi na kubwa, amekuwa akitumwa sehemu mbalimbali duniani, ni mwanaume mwerevu sana, mwenye nguvu na yupo makini katika utendaji wake.
“Kama upo nje ya kitengo, huwezi kumfahamu, ni mtu hatari sana. Alipokuja Tanzania, alikuwa akitumia jina la Gideon. Ni Mwafrika anayeishi Msumbiji, ila nilipoulizia hapa, niliambiwa kwamba ni kutoka Malawi, bila shaka hii kazi alipewa kwa kipindi kirefu, au kwa sababu baba yako pia alikuwa mtu makini kama alivyokuwa yeye na ndiyo maana kulikuwa na ugumu wa kumuua papo kwa papo, hivyo akaja huku kukaa kwa miaka kadhaa kwa ajili ya kumuua mzee wako,” alisema Simpson.
“Sasa kwa nini alimuua baba yangu?”
“Nitakuja kukwambia, hii ni siri kubwa ambayo hakuna anayeijua mbali na CIA, yote ni mambo ya kikazi, usijali, nitakwambia, na hili kukuthibitishia hili, nitakuletea ripoti kamili, nitakwenda Marekani na kuichukua.”
“Daaah! Sawa. Kwa hiyo hawezi kupatikana?”
“Anaweza, ila sitoweza kumuua, siwezi kumuua mtu ambaye sijapewa jukumu la kumuua.”
“Je kumkamata?”
“Naweza, ila kumfikisha kwako ni ngumu, ni mtu hatari mwenye uwezo wa kupambana na watu hata watano, mbali na hivyo, SIS kumkamata CIA ni jambo gumu na lisilokubalika kabisa, ni sawa na kumwandika mwandishi wa habari uovu alioufanya ukizingatia aandikwe na mwandishi mwenzake. Hii kazi haitowezekana,” alisema Simpson.
“Ooops! Haina tatizo!” alisema Victor.
Kila mmoja alitekwa na penzi la mwenzake, kila walipokuwa wakiangalia, walibaki wakitabasamu bila sababu yoyote ile. Usiku wa siku huyo ambao walilala pamoja, kila mmoja alichanganyikiwa na mwenzake, hakukuwa na mtu aliyeboreka au kumkwaza mwenzake.
Mathias akajionyesha kwamba alikuwa Mtanzania aliyekamilika asiyekunywa pombe wala kutumia viagra, nguvu alizopewa na Mungu ndizo zilizompeleka puta Rebecca kiasi kwamba akajutia kuchelewa kwake kuwa na mwanaume huyo.
Kuanzia siku hiyo, mapenzi ya wawili yao yakatengenezwa na hatimae kila walipokuwa, walikuwa pamoja hali iliyowafanya wanaume wengine ambao walijaribu kila njia kumpata Rebecca kuanza kumchukia Mathias aliyeonekana kuokota embe dodo chini ya mlimao.
“Kuna kitu nataka nikwambie mpenzi,” alisema Rebecca.
“Kitu gani?”
“Kuwa na mimi si jambo jepesi, kuna watu wengi watajiinua na kuanza kukuchukia,” alisema Rebecca.
“Watu gani?”
“Walionitaka na kuwakatalia.”
“Unahisi wataweza kuyaharibu mapenzi yetu?”
“Hapana! Hawawezi lakini ni wakorofi.”
“Kivipi?”
“Hawaoni hatari kumtoa mtu roho kwa ajili ya wanawake, kuna watu wengi walinusurika kuuawa na wengine kuuawa kisa wanawake,” alisema Rebecca.
“Achana nao, mimi hawaniwezi, kama fujo nazijua vizuri tu,” alisema Mathias.
“Sawa! Ila kuwa makini, siyo Tanzania hapa, hii inaitwa Malawi!”
“Usijali!’
Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Rebecca kuwa na mwanaume mwenye pesa, hakukuwa na tatizo lolote lile, kila siku alijisikia kuwa na amani huku akitumia fedha kadiri alivyotaka.
Mathias ambaye alijulikana kama Young Bilionaire aliendelea kusikika masikioni mwa watu, wale ambao hawakuweza kumfahamu kabla, wakatamani kumfahamu japo jina lake.
Hakikujulikana ni kitu gani kilitokea, baada ya wiki kadhaa, hakukuwa na picha yake yoyote ambayo ilisambazwa katika mitandao, na hata zile zilizokuwa zimeenea, haijulikani ni kitu gani kilitokea, zilipotea zote.
Kwa sababu alikuwa nchini Malawi kwa kazi maalumu, Mathias akakabidhiwa miwani maalumu iliyokuwa na uwezo wa kuzuia picha yoyote isitoke endapo angepigwa. Hilo ndilo lililosaidia, watu ambao waliahidi kwamba picha za Young Bilionaire zingeonekana ili kwa wale wasiomfahamu wamfahamu, walishangazwa na picha walizokuwa wakizipiga, hazikuwa zikionyesha sura, miwani ile ambayo iliwekwa kifaa kidogo sana cha kuzuia picha kutoka ilimsaidia.
Upepelezi wa kumtafuta Gideon ulikuwa ukiendelea kila siku, Martin akazoeleka kwamba alikuwa kichaa, katika mji wote wa Lilongwe ulimfahamu kama kichaa mkorofi hali iliyopelekea kila siku watu kufika kwenye mji huo kwa ajili ya kumpiga picha.
Muonekano wake ilikuwa ni vigumu mno kumgundua kwamba hakuwa kichaa kama alivyokuwa akionekana, alikuwa akishinda jalalani huku akiongea peke yake na kuvichapa fimbo vitu visivyokuwa vikionekana.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kila mtu alimpuuzia, hakukuwa na aliyejua kwamba yule kichaa mkorofi aliyekuwa akivuma hapo Malawi alikuwa mpelelezi mwenye ujuzi aliyetokea nchini Tanzania.
“Kuna chochote?” aliuliza Materu, ilikuwa saa sita usiku, alikuwa akizungumza na Martin usiku.
“Hapana! Ila bado tunaendelea. Hatujajua kama yule mtu yupo hapa Lilongwe au la!”
“Lakini kutakuwa na mafanikio? Miezi miwili ishapita!”
“Mafanikio yatakuwepo tu, subiri tuendelee. Hata kama nitakaa miaka kumi, nipo tayari lakini huyu mjinga apatikane tu.”
“Basi sawa, hakuna tatizo!”
Siku ziliendelea kuyoyoma kila siku lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale. Martin aliendelea kuwa chizi huku kila siku akiyaangalia mandhari ya jiji hilo huku akimtafuta Gideon lakini ilikuwa ngumu mno kumpata mwanaume huyo.
“Nitampata tu, au awe nchi nyingine, ila kama ni hapa, nitampata tu,” alijisemea Martin, hakuonekana kukata tamaa.
****
“Una samaki wazuri, huwa unawavua wapi?” ilisikika sauti ya msichana mrembo, mkononi alishika kapu huku mbele yake kukiwa na mwanaume aliyevaa nguo zilizolowana akiuza samaki.
“Nawavua ziwani hapahapa Malawi, umewapenda?” aliuliza muuzaji huyo.
“Yaaap! Ni wazuri, wakubwa na wanaonekana kuwa watamu sana,” alisema mwanamke huyo.
“Hahah! Huwa siuzi kitu kibaya, najua kuvua samaki wakubwa.”
“Sasa ukitoka hapa unakwenda kuwauza wapi?”
“Nitaanza kuuza kule Livingstone.”
“Mmmh! Mbona unakwenda kuuza kwa matajiri, kwa nini usije kuuza kwa walalahoi?”
“Sasa samaki kama hawa dada yangu ukienda kuuza uswahili utapata hela kweli?”
“Mmmh! Sawa, haina tatizo, nifungie wawili,” alisema mwanamke huyo huku akimkabidhi muuzaji huyo hela yake.
Mishemishe zilikuwa nyingi pembezoni mwa Ziwa Malawi, wauzaji wengi walikuwa wamejikusanya wakiuza samaki waliokuwa wakiwavua katika ziwa hilo. Kila mmoja alionekana kuwa bize mahali hapo ambapo kama ingekuwa Dar es Salaam basi tungepaita Feri.
Wauzaji kutoka sehemu nyingine, wote walikusanyika sehemu hiyo ambayo muda wote ilinuka shombo tu. Miongoni mwa wauzaji waliokuwa wakiuza samaki mahali hapo alikuwepo huyu kijana masikini ambaye kwa kumwangalia tu ungegundua kwamba alikuwa na maisha magumu, aliitwa Mutombo.
Mutombo alikuwa akitokea katika Mtaa wa Kipemalo uliokuwa hapohapo Lilongwe, huko, ndipo walipokuwa wakiishi watu masikini kama ilivyokuwa Tandale jijini Dar. Hakuwa na maisha mazuri, kila siku, alitegemea kujiingizia kipato kupitia biashara aliyokuwa akiifanya.
Samaki aliokuwa akiwavua, walikuwa wakubwa ambao kila siku walimfanya kuwavuta wateja wengi waliokuwa wakimiminika nyumbani kwake alipokuwa akiwakaanga.
Maisha yake hayo yalilowea uswahilini lakini baadae akaamua kuhama na kuhamia katika Mtaa wa Livingistone. Watu wengi wakalalamika kwamba ilikuwaje ahame na wakati walikuwa wakimhitaji.
Huko Livingstone alipata wateja wengi waliokuwa wakivutiwa na samaki wake, matajiri wa huko wakawa wakinunua samaki kwa bei kubwa kutoka kwake ambapo alitafuta kibanda kimoja na kuamua kuwauza mahali hapo.
Jina lake huko Livingstone likawa kubwa, akaendelea kufanya biashara hiyo huku akijiingizia kipato kikubwa. Hakuna aliyejua alipatwa na maswahibu gani, baada ya miezi miwili kufanya biashara yake, akatoweka.
Kila mmoja alisikitika, halikuwa jambo jepesi na rahisi kuamini kwamba Mutombo hakuwepo tena, waliokuwa wamemzoea walijaribu kumtafuta lakini walishindwa kumpata.
Baada ya kupotea kwa miaka miwili, akarudi tena na alipoulizwa alipokuwa, alisema kwamba alipotea ziwani na kwenda kwenye Kisiwa cha Abulegela kilichokuwa katikati ya Ziwa Malawi, huko, ndipo alipoishi kwa miaka hiyo na kuamua kurudi Jiji Lilongwe.
Biashara ikaanza upya katika mtaa wa kifahari wa Livingsone, bado watu waliendelea kumpenda na kununua samaki wake kama kawaida. Jina lake likarudi tena, watu wakaendelea kumiminika kiasi kwamba kuna wengine walikuwa radhi kusafiri umbali mrefu lakini mwisho wa siku wafike katika mtaa huo na kununua samaki wa Mutombo.
Siku zikaendelea kukatika, mbali na uuzaji huo wa samaki uliompa jina kubwa, hakukuwa na aliyejua kwamba muuzaji huyo samaki aliyeitwa Mutombo, alikuwa mpelelezi kutoka katika Shirika la Kipelelezi la nchini Msumbuji, na alikuwa Malawi kwa ajili ya kumpeleleza Bwana Timoth, tajiri mkubwa aliyemiliki fedha nyingi kupitia biashara ya madawa ya kulevya aliyokuwa akiifanya.
Kupotea kwake kwa miaka miwili, ni kwamba alitumwa na Shirika la Kijasusi la Marekani, CIA kwa ajili ya kumuua Mhamasishaji, Potter Mickey nchini Tanzania kwa kujifanya mwanachuo na kutumia jina la Gideon.
Mara baada ya kukamilisha kazi hiyo, akaamua kurudi Malawi kwa ajili ya kumalizia kazi aliyopewa na kisha kurudi Msumbiji na kuunganisha mpaka Marekani kwa ajili ya kuchukua pongezi zake.
Huku akiwa kwenye mipango ya kumkamata au kumuua Bwana Timoth, hakujua kama kulikuwa na Watanzania wawili ambao kila siku walikuwa wakimtafuta huku wakiwa na lengo la kumkamata au kumuua endapo akileta ubishi. CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Hakulijua hilo, aliendelea kupeleleza huku akitumia kivuli cha kuuzia samaki. Maisha yake yalikuwa hatarini bila kujijua, mbali na hiyo, kila siku aliendelea kujinyakulia wateja wengi wa samaki huku kila mmoja akijua kwamba kijana huyo alikuwa masikini wa kutupwa, kumbe nyuma ya pazia alikuwa mpelelezi mwenye fedha aliyetembea chini ya kivuli cha CIA, huku uwepo wake wa kuwepo Livingstone si kwamba alitaka kuuza samaki, alikuwa na kazi moja ya kuua mzizi mkubwa wa usafirishaji wa madawa ya kulevya, bwana Timoth.
Ilianza mwaka 1972, mwaka ambao biashara ya madawa ya kulevya ilishika kasi nchini Malawi. Vijana wengi walioonekana kuwa na nguvu ya kuliendesha taifa hilo wakajiingiza katika usafirishaji wa madawa ya kulevya na mwisho wa siku kuingia katika utumiaji wa madawa hayo.
Hawakuwa vijana wengi waliokuwa wamejiingiza katika biashara hiyo lakini kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele wakazidi kuongezeka hali ilionekana kuwa mbaya, wale watu waliokuwa wakiaminika ndiyo waliokumbwa na mkumbo wa utumiaji wa madawa hayo yaliyokuwa yakiwaharibu akili na miili yao kila siku.
Hapo ndipo kulipoanza kuwa na wafanyabiashara wakubwa ambao mbali na biashara nyingine walizokuwa wakizifanya, waliitegemea biashara hiyo ambayo iliendelea kukua kwa kasi kadiri siku zilivyoendelea kwenda mbele.
Hakukuwa na usafirishaji wa madawa hayo kwenda nje ya nchi, walikuwa wakiuziana ndani kwa ndani lakini ilipofika mwaka 1985, watu wakaanza kutoka na kwenda nchi za Kiarabu kama Qatar, Iran, Iraq, na nchi nyingine katika Bara la Asia kwa ajili ya kupeleka na kuchukua madawa ya kulevya, biashara ambayo ilianza kuwapatia fedha nyingi wale waliokuwa wakiifanya.
Ulipoingia mwaka 1992, wafanyabiashara wakubwa wakagundua kwamba mbali na ndege ambazo walikuwa wakizitumia, pia walikuwa na uwezo wa kutumia usafiri wa meli za mizigo kwa ajili ya kufikisha mizigo yao, hivyo mara moja usafirishaji wa madawa kwa kutumia usafiri huo ikaanza kufanyika.
Walifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuwa hakukuwa na polisi waliokuwa na uwezo wa kugundua ni meli gani ilikuwa imebeba mizigo ya madawa ya kulevya, na hata kama walikuwa wakigundua, kila walipoingia ndani ya meli hizo, walitafuta kila kona lakini mizigo haikuwa ikionekana.
Watu wakatajirika huku vijana wengi wakipotelea katika matumizi ya madawa hayo. Japokuwa nchini humo kulikuwa na wauzaji wengi wa madaya ya kulevya, lakini kulikuwa na mtu aliyekuwa akiifanya sana biashara hii, huyu alikuwa Timoth Makenzi.
Kwa kumwangalia, alikuwa kijana mdogo wa miaka thelathini lakini maisha aliyokuwa akiishi yalimshangaza kila mtu. Alimiliki kiasi kikubwa cha fedha kwa kuwa yeye ndiye alikuwa mzizi mkubwa wa kusafirisha madawa kutoka ndani ya nchi ya Malawi huku pia akiwa mpokeaji mkubwa wa madawa hayo ambayo mengi yalikuwa yakiletwa kutoka Pakistan.
Alitajirika, alikula raha, alitembelea fedha na kila alipokuwa, kichwa chake kilifikiria fedha tu. Alinunua magari mengi ya kifahari huku akijenga nyumba kubwa za thamani ambazo ziliwafanya watu wote kubaki midomo wazi.
Japokuwa tetesi zilisikika kwamba Timoth alikuwa akihusika na uuzaji wa madawa ya kulevya lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa na uhakika. Polisi hawakutaka kuwa nyuma, walichokifanya ni kuanza kumfuatilia hatua kwa hatua, lakini mwisho wa siku, hawakufanikiwa kupata kitu zaidi ya kuona kwamba fedha za mtu huyo zilikuwa zikiingia kutokana na biashara ya magari aliyokuwa akiifanya.
“I’m not dealing with coccain, I’m dealing with selling and buyying cars from Japan,” (Sijihusishi na madawa ya kulevya, najihusisha na uuzaji na ununuaji wa magari kutoka Japan) alisema Timoth.
“Are you sure?” (Una uhakika?)
“One hundred percent,” (Asilimia mia moja)
Polisi hawakuishia hapo, waliendelea kusikia tetesi kwamba Timoth alikuwa akijihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya lakini kila walipokuwa wakimfuata na kupekua nyumba nzima, hawakufanikiwa kuona madawa yoyote yale kitu kilichowashangaza sana na kubaki na maswali mengi.
Kitendo cha polisi hao kuja mara kwa mara nyumbani kwake kikamkosesha amani, alichokifanya ni kuanza kutumia fedha zake tu. Aliziamini fedha, aliamini kwamba hakukuwa na mtu aliyekuwa na nguvu ya kukataa fedha, hivyo akaanza kuzilamisha kufanya kazi aliyotaka zifanye.
Kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kuwakamata wakuu wa polisi, alimini hao ndiyo ambao walikuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba wanafika nyumbani kwake kwa ajili ya kumpekua.
Kwa kuwa alikuwa na fedha, kwa kila mkuu wa kituo cha polisi akampa ofa ya dola za kimarekani elfu tano ambazo ni zaidi ya kwacha milioni kumi na tano kwa ajili ya kuwafunga midomo. Hicho, kwao kilikuwa kiwango kikubwa cha fedha, wakajikuta wakiingia mkenge na kusahau kufanya majukumu yao ya kila siku.
Timoth akawa huru, akatanua soko lake na kuwaongeza wafanyakazi wake wa ndani. Madawa yaliendelea kusambazwa sehemu mbalimbali, kupitia yeye, wakaongezeka wauzaji wengine na kuufanya mnyororo kuwa mkubwa.
Ulipofika mwaka 2001 ambapo polisi walianza kuwatumia mbwa katika viwanja vya ndege kwa ajili ya kuchunguza watu waliokuwa wakibeba madawa, soko lake likaanza kuporomoka kwa kuwa vijana wake wengi walikuwa wakikamatwa.
“What should we do?” (Tufanye nini?) aliuliza mmoja wa vijana wake.
“I don’t know, can you just let me think about it?” (Sijui, unaweza kuniacha nifikirie juu ya hili?)
“No problem” (Hakuna tatizo)CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Usiku wa siku hiyo ulikuwa wa mawazo mengi, hakulala, hakupenda kuona biashara yake ikianguka kwa kiasi kikubwa kisa tu mbwa walikuwa wakimharibia shughuli uwanja wa ndege.
Alichukua masaa mengi kujifikiria na mwisho wa siku kuja na jibu kwamba ilikuwa ni lazima madawa yasafirishwe kupitia maiti. Hiyo ikawa njia nyepesi na rahisi, walichokifanya ni kuelekea hospitalini, wakaanza kuchukua maiti, wakazipasua na kuziwekea madawa na mwisho wa siku kuzisafirisha.
Njia hiyo aliyoigundua ikaonekana kuwa bora na ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana, akaanza kupanda juu kisoko kama kawaida.
Iliendelea kukatika miaka mingi huku utajiri wake ukiwa mkubwa. Polisi wote waliokuwa wakifuatilia, waliitwa chemba na kupewa kitu kidogo kilichowafanya kunyamaza. Tamaa za polisi hao zikawafanya vijana wengi kupotea, watumiaji wa madawa ya kulevya wakaongezeka kwa kiasi kikubwa mno.
Baada ya biashara hiyo kuendelea kwa siri, hapo ndipo serikali ikaamua kuungana na kitengo cha kipelelezi na kuanza kumpeleleza bwana Timoth aliyewafunga midomo polisi wengi hapo Malawi.
Ilikuwa ni siri kubwa, hakukuwa na mtu mwingine nje ya kitengo hicho ambaye alitakiwa kufahamu kilichokuwa kikiendelea, walichokifanya ni kumwambia kijana kutoka nchini Msumbiji mwenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi za kipelelezi, huyu aliitwa Jonathan Mulumbu.
Mara baada ya kuambiwa kile kilichokuwa kikiendelea, akapanda ndege na kwenda nchini Malawi na kisha kupewa maelekezo yote na kile alichotakiwa kukifanya, hapo ndipo alipoanza kujifanya kijana masikini aliyekuwa akifanya kazi ya uvuvi na kuuza samaki.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa amegundua, ilikuwa ni siri kubwa, polisi waliendelea kula hela kutoka kwa bwana Timoth bila kujua kwamba karibu na nyumba ya mzee huyo, kulikuwa na kijana maarufu kwa kuuza samaki ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kupeleleza kila kilichokuwa kikiendelea.
Chini ya meza yake alikuwa na bunduki ndogo iliyofungwa vilivyo, kiunoni mwake alikuwa na bunduki nyingine ambayo haikuweza kuonekana kwani muda wote shati lake lilikuwa likiificha bunduki hiyo, mbali na hayo yote, pembeni yake kulikuwa na miwani ya macho, ilionekana kuwa ya kawaida sana lakini kwa undani, miwani ile ilikuwa ni kamera iliyokuwa ikichukua kila kitu kilichokuwa kikiendelea ndani ya nyumba ile, ilikuwa na uwezo wa kuona hata kilichokuwa kikiendelea nyuma ya ukuta.
Aliona kila kitu, watu waliokuwa wakiingia na biashara kufanyika, picha zilizokuwa zikipigwa mahali hapo, zilipelekwa moja kwa moja mpaka mpaka katika makao makuu ya kipelelezi nchini hapo. Jonathan ambaye alitumia jina la Mutombo akaonekana kijana nuksi ambaye hakustahili hata kusogelewa.
Kila kilichofanyika, bado kiliendelea kuwa siri. Polisi wa Malawi waliendelea ‘kupiga mpunga’ bila kujua chochote kile.
Miongoni mwa watu waliowahi kuvutiwa Rebecca kutokana na uzuri aliokuwa nao alikuwa bwana Timoth, msichana huyo aliutikisa moyo wake, kila alipokuwa akimuona sehemu mbalimbali yakiwemo magazeti na televisheni, aliusikia moyo wake ukiingiwa na tamaa ya kutaka kulala na msichana huyo.
Alijiamini kwamba alikuwa na fedha, alijiamini kwamba hakukuwa na msichana yeyote ambaye angeweza kumkataa, hivyo akajipa uhakika kwamba hata kama angemfuata msichana huyo ilikuwa ni lazima amkubali.
Alichokiwaza ndicho alichokifanya, baada ya siku kadhaa, alisimama mbele ya msichana huyo katika Klabu ya Espanyol, klabu ya watu maarufu na matajiri hapo Lilongwe na kuanza kuzungumza na msichana huyo.
Kwa kuwa aliziamini sana fedha zake, alichokifanya siku hiyo ni kutumia fedha zake vilivyo, kila alipokuwa akiagiza kinywaji hiki na kile, vingine vilifuata huku akitumia muda wake mwingi kuwatuza wasichana waliokuwa wakicheza klabuni hapo.
Alikuwa na sifa, alijitengenezea CV iliyompa uhakika kwamba Rebecca asingeweza kumkataa. Mara baada ya kufanya vitu vingi klabuni hapo, akaamua kuanza kuzungumza na msichana huyo mrembo.
“Nimekuwa nikikutamani kwa muda mrefu sana, wewe ni msichana wa kipekee sana, najiona kuwa na bahati kukutana nawe,” alisema bwana Timoth huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Asante, nikusaidie nini?”
“Ninahitaji kuwa nawe usiku wa leo.”CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Unafikiri nipo hapa kwa ajili ya kujiuza?”
“Hapana, usinifikirie hivyo, nakuchukulia kuwa u miongoni mwa wasichana wanaojiheshimu na kujitambua,” alisema bwana Timoth.
“Sawa, naomba uniache,” alisema Rebecca na kutaka kuondoka mahali hapo, akashikwa mkono.
“Subiri kwanza,”
“Kuna nini?”
“Yaani unataka uniache kiholela kweli? Kweli umeamua kuniumiza namna hii? Subiri basi.”
“Hapana. Nimeamua tu, naomba uniache,” alisema Rebecca.
Bwana Timoth hakukubali kushindwa, alimhitaji sana msichana huyo kwa usiku wa siku hiyo, kitendo cha kumuona akiondoka hivihivi bila kufanya chochote kile kilimaanisha kwamba alishindwa, yaani fedha zake hazikusaidia kitu chochote kile.
“Rebecca!” alijikuta akiita.
Rebecca hakuitikia, akaanza kupiga hatua kuelekea nje ya klabu ile. Kitendo kile kilimaanisha kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho kwa mzee huyo kuzungumza na binti huyo kwa usiku huo.
Wasichana wengine waliokuwa wakiona kila kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, walimlaumu Rebecca kwani alikuwa akipoteza bahati waliyokuwa wakiililia usiku na mchana.
Rebecca akatoka ndani ya ile klabu na kuelekea nje, bwana Timoth hakutaka kubaki ndani, huku kitambi chake kikichezacheza akaamua kutoka nje. Bado alikuwa aking’ng’ania kuzungumza na mrembo huyo na mwisho wa siku kulala naye kwa usiku huo.
Hilo lilikuwa gumu, bado Rebecca aliendelea kuwa king’ang’anizi zaidi.
Alimbembeleza kadiri alivyoweza, hakujali fedha zake, alimsihi sana kuwa naye huku akimuahidi vitu vingi lakini bado msichana huyo alikuwa mbishi kukubaliana naye.
“Sawa, nashukuru kwa kila kitu, ila chukua hii,” alisema bwana Timoth huku akiwa amekishika kibunda cha fedha, kwacha milioni tano.
“Sikuhitaji wewe wala sihitaji fedha zako,” alisema Rebecca kwa dharau huku akimwangalia mzee huyo kuanzia chini mpaka juu, akalifuata gari lake na kuondoka zake.
Hilo lilikuwa moja ya matukio yaliyomuumiza mno moyoni mwake, hakuamini msichana kama Rebeca angeweza kufanya kitu kama kile, alisikia maumivu makali, kitendo cha kukataliwa penzi tena huku akiwa ametoa kiasi kikubwa cha fedha, ilimuumiza mno.
Baada ya miezi tisa, akapata tetesi kwamba kijana aliyekuja kwa kasi kwa kutumbua fedha, kijana aliyesadikiwa kwamba alikuwa na fedha zaidi yake, Young Bilionaire alikuwa ameingia nchini Malawi na mwisho wa siku kumchukua msichana huyo ambaye kila siku alilala usiku kucha akimuota.
Moyo ulimuuma zaidi, kila alipofikiria jinsi alivyokuwa amekataliwa na msichana huyo na mwisho wa siku kuja kuchukuliwa na mtu mwingine, alijisikia uchungu moyoni mwake. Hakutaka kuliona hilo likiendelea kutokea, kwa sababu alidhamiria kumchukua msichana huyo kwa nguvu zote basi akajiona kuwa na jukumu zito la kufanya mbele yake, hilo lilikuwa ni kumuua huyo mtu aliyejiita Young Bilionaire.
“Ni lazima nimuue,” alisema bwana Timoth huku akionekana kuwa na hasira.
“Nani bosi?”
“Mna risasi za kutosha?”
“Ndiyo!”
“Mna vijana wa kutosha?”
“Ndiyo mkuu! Kuna nini?” aliuliza kijana mmoja, alikuwa na mwili uliojengeka kimazoezi, muda wote alikuwa akivaa fulana.
“Kuna mnyama fulani nataka kummalizia, kanidhalilisha sana.”
“Yupi bosi?”
“Young Bilionaire.”
“Hakuna tatizo, bila shaka kitendo chake cha kumchukua Rebecca ndicho kilichosababisha, nipo nawe kiongozi, hata mimi nimekasirika sana, mbaya zaidi, nasikia ni Mtanzania, haiwezekani, lazima tummalize,” alisema jamaa huyo.
“Ninataka kazi ifanyike mara moja. Umesikia?”
“Ndiyo mkuu! Mpaka saa tisa usiku, atakuwa marehemu!”
Japokuwa alikuwa ametoa amri kwamba mtu huyo ilikuwa ni lazima kuuawa lakini bado moyo wake ulikuwa na hasira mno, kila wakati alikuwa akiyauma meno yake kwa hasira, hakutaka kumuona mwanaume huyo akiendelea kuwa na Rebecca, kisa tu ni kwa sababu alikataliwa.
Mipango ikapangwa, kijana yule aliyejulikana kwa jina la Matata akawaita vijana wake na kuwapanga tayari kwa kufanya mauaji hayo.
“Ila ni tajiri, hawezi kuwa na walinzi?” aliuliza jamaa mmoja, alikuwa miongoni mwa vijana waliokusanywa na Matata kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
“Hatujui, ila kwangu, sijawahi kumuona akiwa na walinzi, au awe ameanza wiki hii kuwa na nao,” alisema jamaa mwingine.
“Basi sawa, jipangeni, mpaka saa tisa nataka kazi iwe imekamilika.”
“Sawa mkuu. Tumuue kwa kifo gani sasa?”
“Apigwe risasi, ila isiwe ndani ya nyumba yake, hakikisheni mnamchukua na kumpeleka porini,” alisema Matata.
“Hakuna tatizo bosi.”
Sehemu nzuri ambayo walikuwa wamepanga kumkamata mtu wao ilikuwa ni katika klabu nyakati za usiku. Walijua fika kwamba hakuna kitu ambacho Young Bilionaire alikuwa akikipenda kama kwenda klabu usiku.
Usiku wa siku hiyo wakaanza kupeleleza ni mahali gani Young Bilionaire alipokuwa. Wakapewa taarifa kwamba alionekana katika Klabu ya Boniventure, klabu iliyokuwa na wacheza kamari wengi, hivyo wakaenda huko.
Walipofika, hawakutaka kuteremka, wakabaki garini huku wakianza kumsubiri. Gari lake la Lamboghin lilikuwa nje kitu kilichowafanya kuwa na uhakika kwamba mtu wao alikuwa ndani ya klabu ile.
Waliendelea kusubiri zaidi, ilipofika saa 9:14 usiku, Mathias akaanza kutoka ndani ya klabu ile huku akiwa ameongozana na Rebecca. Baadhi ya watu walikuwa wakimpongeza kwa kumpigapiga mgongoni kwani fedha alizozimwaga siku hiyo ndani ya ukumbi ule ilikuwa balaa.
Wote wawili wakaingia ndani ya gari lao la kifahari na kuondoka mahali hapo. Walichokifanya wale vijana ni kuanza kulifuatilia gari hilo lililokuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kawaida.
Walipofika katika katika makutano ya Barabara ya Ilukweza na St. Joseph, kwa mwendo wa kasi, dereva wa gari la vijana wale akalifuata pale lilipokuwa limesimama kwenye mataa na kwa haraka wakasimamisha gari lao kwa mbele na kuteremka garini.
Huku wakiwa na bunduki mikononi mwao, vijana wawili wakaanza kulifuata lile gari, walipolifikia, wakavunja kioo, wakatoa loki na kuufungua mlango.
Rebecca alikuwa akipiga kelele za kuomba msaada lakini vijana wale hawakutaka kuacha kufanya kile walichokuwa wamekikusudia, wakamtoa Mathias garini, hata kabla hajaongea kitu chochote kile, wakampiga vibao na mateke na kumpeleka katika gari lao na kuondoka naye.
Safari ya kwenda katika Msitu wa Mushibwara ikaanza huku kila mmoja akiwa na hamu ya kutekeleza kile walichokuwa wamekipanga.CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kwa Rebecca, hakunyamaza, bado alikuwa akiendelea kupiga kelele tu. Hakukuwa na mtu aliyetokea, ilikuwa ni usiku wa saa tisa, kila alipopiga kelele, zilionekana kuwa kazi bure.
Hakukuwa na gari upande wowote ule, baada ya dakika mbili kuona hakukuwa na msaada wowote aliokuwa ameupata, akakaa katika kiti cha dereva na kuliwasha gari lake, safari ya kuelekea kituo cha polisi ikianza, machozi yalikuwa yakimbubujika huku akionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
Hakuwafahamu watu waliomteka mpenzi wake, Mathias aliyemjua kwa jina la Kenneth, hakujua malengo yao yalikuwa nini na walitumwa na nani. Kila alipokuwa akilia zaidi, ni kama aliisikia sauti moyoni mwake ikimwambia kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha ya mpenzi wake, alitakiwa kumsalia sala ya mwisho.
Rebecca akazidi kulia!
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment